162
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA ______________ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE ____________________ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Sura ya 2 ya Marejeo ya Sheria za Tanzania, Toleo la 2005] [TOLEO LA JANUARI, 2016]

KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

  • Upload
    others

  • View
    33

  • Download
    1

Embed Size (px)

Citation preview

Page 1: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA______________

BUNGE LA TANZANIA

KANUNI ZA KUDUMU ZABUNGE

____________________

[Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba yaJamhuri ya Muungano wa Tanzania,

Sura ya 2 ya Marejeo ya Sheria za Tanzania, Toleo la 2005]

[TOLEO LA JANUARI, 2016]

Page 2: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

BUNGE LA TANZANIA

KANUNI ZA KUDUMU ZABUNGE

____________________

[TOLEO LA JANUARI, 2016]

Page 3: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

[Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba yaJamhuri ya Muungano wa Tanzania,

Sura ya 2 ya Marejeo ya Sheria za Tanzania, Toleo la 2005]

Page 4: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

Zimepigwa Chapa naIdara ya Taarifa Rasmi za Bunge (Hansard),

OFISI YA BUNGE - DODOMA, TANZANIA.ISBN 978-9976-3-0001-7

Page 5: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

Kanuni za Kudumu za Bunge

KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE

TOLEO LA JANUARI, 2016

__________

YALIYOMO________

SEHEMU YA KWANZA

UTANGULIZI

Kanuni Kichwa cha Habari Ukurasa

1. Jina ......................................................................................................... 12. Matumizi ........................ .......................................................................... 13. Tafsiri ........................................................................................................ 1

SEHEMU YA PILI

UENDESHAJI WA SHUGHULI ZA BUNGE

4. Spika ....................................................... .......... ..................................... 45. Mamlaka ya Spika ................................ ............................................... 46. Majukumu ya Naibu Spika................................................................... 57. Majukumu ya Wenyeviti wa Bunge................................................... 68. Uadilifu kwa Kiongozi wa Bunge........................................................ 69. Uchaguzi wa Spika ................................................................................ 610. Uchaguzi wa Naibu Spika .................................................................. 911. Uchaguzi wa Wenyeviti wa Bunge .................................................1012. Uchaguzi wa Wabunge Wanaokwenda kwenye Vyombo Vingine vya Uwakilishi...........................................................1113. Kiongozi wa muda wa Shughuli za Serikali Bungeni .................... 1114. Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni ........................ 1115. Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni ........................ ...........................12

ii i

Page 6: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

Kanuni za Kudumu za Bunge

16. Uteuzi wa Wanadhimu wa Vyama Bungeni ................................. 1217. Majukumu ya Katibu wa Bunge .......................................................1318. Ofisi ya Bunge ...................................................................................... 1419. Mpambe wa Bunge ............................................................................1420. Majukumu ya Mpambe wa Bunge ..................................................1421. Mshauri Mkuu wa Bunge wa Mambo ya Sheria na majukumu yake...............................................................................15

SEHEMU YA TATU

MIKUTANO NA VIKAO VYA BUNGE

22. Mkutano wa Kwanza wa Bunge .....................................................1623. Shughuli za Mkutano wa Kwanza................................................... 1624. Kiapo cha Utii kwa Wabunge ........................................................ 1725. Kuthibitisha Uteuzi wa Waziri Mkuu .............................................. 1826. Ufunguzi Rasmi wa Bunge Jipya ................................................... ..1827. Mikutano ya kawaida ya Bunge ......................................................1828. Muda wa Vikao vya Bunge ..............................................................1929. Kuahirisha Bunge .................................................................................21

SEHEMU YA NNE

SHUGHULI ZA BUNGE

30. Mpangilio wa Shughuli za Bunge ................................................... 2131. Dua ya Kuiombea Nchi yetu na Kuliombea Bunge................... 2332. Taarifa ya Rais ..................................................................................... 2333. Taarifa ya Spika................................................................................... 2334. Kuwasilisha Maombi na Taarifa ya Ombi.................................... 2335. Masharti Kuhusu Maombi.................................................................. 2436. Nakala ya Maombi ............................................................................2437. Hati za kuwasilisha Bungeni ............................................................ 2438. Maswali kwa Waziri Mkuu................................................................. 2539. Maswali na Taarifa ya Maswali ...................................................... 2640. Masharti Kuhusu Maswali .................................................................. 2841. Kuondoa Maswali .............................................................................. 2842. Jinsi ya Kuuliza Maswali .....................................................................2943. Muda wa Maswali.............................................................................. 2944. Maswali ya Nyongeza....................................................................... 2945. Maswali ya Nyongeza Yasiyoruhusiwa .........................................2946. Maswali kujibiwa kikamilifu ............................................................ 3047. Kuahirisha shughuli za Bunge ili Kujadili Jambo la Dharura ...... 3048. Masharti ya jumla kuhusu Jambo la Dharura ...............................30

i v

Page 7: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

Kanuni za Kudumu za Bunge

49. Kauli za Mawaziri .................................................... ........................... 3250. Maelezo Binafsi ya Wabunge ...................................... .................. 3251. Masuala Yanayohusu Haki za Bunge .......................... .......................3252. Shughuli za Serikali .................................................. .......................... 3353. Hoja Zitakazotolewa Bungeni ................................... .......................3354. Jinsi ya Kuwasilisha Hoja ............................................. ......................3455. Taarifa ya Hoja........................................................ ............................3556. Utaratibu wa Kujadili Hoja ......................................... .......................3657. Kubadilisha Hoja......................................................... ......................... 3758. Mabadiliko ya Hoja na Kuondoa Hoja ........................ .......................38

SEHEMU YA TANO

KANUNI ZA MAJADILIANO

59. Nyakati za Mbunge kusema Bungeni ........................... .....................3960. Jinsi ya Kupata Nafasi ya kusema Bungeni ................. ................3961. Kutozungumzia jambo ambalo lina maslahi binafsi ya kifedha ............................................................... ............................4162. Muda wa kusema Bungeni .............................. .......... .......................4263. Kutosema uongo Bungeni .......................................... .......................4364. Mambo yasiyoruhusiwa Bungeni .................................. .......................4565. Kuzungumza zaidi ya mara moja ............................. .......................4666. Staha ndani ya Bunge ................................................ .......................4767. Mamlaka ya Spika kukatiza majadiliano .................... .....................4868. Taarifa kuhusu Utaratibu na Mwongozo......................... .............4869. Hoja ya Kuahirisha Mjadala ........................................ .......................4970. Hoja ya Kufunga Mjadala ................................. .......... .......................4971 Haki ya raia kujitetea na kujisafisha dhidi ya kauli zinazotolewa Bungeni .............................................. ....................... 50

SEHEMU YA SITA

AMANI NA UTULIVU BUNGENI

72. Mamlaka ya Spika kusimamia utaratibu ............................... .........5273. Adhabu zinazoweza kutolewa na Spika kwa ukiukaji wa Kanuni ..................................................................... 5274. Adhabu zinazoweza kutolewa na Bunge kwa ukiukaji wa Kanuni ......................................... ....................... 5375. Masharti kwa Mbunge aliyesimamishwa kazi ................ .................5476. Udhibiti wa fujo Bungeni ............................................ .......................54

v

Page 8: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

Kanuni za Kudumu za Bunge

SEHEMU YA SABA

UHALALI WA SHUGHULI

77. Akidi ya Vikao vya Bunge ............................................ ...................5478. Uhalali wa Maamuzi ya Bunge.......................... ............. ............... 5579. Uamuzi wa Bunge ....................................................... ....................... 55

SEHEMU YA NANE

KUTUNGA SHERIA – MASHARTI YA JUMLA

80. Utangazaji wa Miswada ya Serikali ..............................................5781. Utaratibu kuhusu Muswada Binafsi.......................... .......................5882. Uwasilishaji wa Muswada.......................................... .......................5883. Muswada Kusomwa Mara ya Kwanza ......................... ....................5884. Muswada kupelekwa kwenye Kamati......... .....................................5985. Taarifa ya Kamati .......................... ............... .......... .........................5986. Muswada Kusomwa Mara ya Pili................................ ...................5987. Kurejesha Muswada katika Kamati................................ ...............6188. Muswada katika Kamati ya Bunge Zima........................ ..............6289. Taarifa baada ya Muswada Kusomwa Mara ya Pili ..................................................................... .............................. 6390. Kuondoa Muswada Bungeni ...........................................................6491. Muswada Kusomwa Mara ya Tatu na kupitishwa na Bunge..................... ......................... ..........................6492. Ridhaa ya Rais na hifadhi ya Sheria........ ........................ ..............6493. Utaratibu wa Kusoma Miswada ya Sheria ..................................64

SEHEMU YA TISA

UTARATIBU WA KUTUNGA SHERIA KUHUSUMAMBO YA FEDHA

94. Bunge kukaa kama Kamati ya Mipango ....................... ...................6595. Masharti kuhusu Miswada, Hoja na Maombi ya Fedha........... 6696. Kuwasilisha dondoo na randama za vitabu vya Bajeti.........6797. Kuwasilisha mapendekezo ya mpango na Bajeti .........................6798. Kamati kukagua utekelezaji wa miradi .........................................6799. Kujadili utekelezaji wa Bajeti za Wizara .......................................68100. Kamati ya Matumizi............................................................................ 70

v i

Page 9: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

Kanuni za Kudumu za Bunge

101. Mjadala katika Kamati ya Matumizi ............................................70102. Kubadilisha Makadirio katika Kamati ya Matumizi...................70103. Hoja ya kuondoa shilingi kwenye Makadirio..................... .........71104. Kukamilika mjadala katika Kamati ya Matumizi .......................71105. Hotuba ya Bajeti ya Serikali Kusomwa Bungeni ........................72106. Mjadala kuhusu Hotuba ya Bajeti...................................................73107 Utaratibu wa kuidhinisha Makadirio ya Matumizi ya Serikali ...............................................................................................73108. Muswada wa Fedha za Matumizi...................................................74109. Muswada wa Sheria ya Fedha ........................................................74110. Makadirio ya Matumizi ya Nyongeza........................................... .74

SEHEMU YA KUMI

KAMATI ZA BUNGE

111. Mkutano wa Wabunge wote ........................................................ 75112. Kamati ya Vyama vya Siasa......................................................... 75113. Mikutano ya Kamati za Vyama vya Siasa................................ ..75114. Kamati ya Bunge Zima .................................................................... 76115. Akidi na Utaratibu katika Kamati ya Bunge Zima ....................76116. Muundo wa Kamati za Kudumu za Bunge................................. ..77117. Utaratibu katika Vikao vya Kamati za Kudumu za Bunge....... 79118. Kamati za Kudumu za Bunge .........................................................81119. Majukukumu ya jumla ya Kamati za Kudumu za Bunge ........81120. Utaratibu wa Kuunda Kamati Teule..............................................81121. Akidi na Utaratibu wa Vikao vya Kamati Teule........................82122. Taarifa ya Kamati Teule..................................................................82123. Muundo wa Taarifa za Kamati.......................................................83

SEHEMU YA KUMI NA MOJA

UTARATIBU WA KUMWONDOA RAIS MADARAKANI

124. Taarifa ya Hoja ya Kumwondoa Rais............................................83125. Masharti ya hoja ya kuunda Kamati Maalum ya Uchunguzi.......................................................................................... 84126. Wajumbe wa Kamati Maalum ya Uchunguzi ...........................84127. Utaratibu wa kazi ya Kamati Maalum ya Uchunguzi ..............85128. Utaratibu katika Kamati ya Bunge Zima kuhusu mashtaka dhidi ya Rais........................................................................................85129. Azimio la kumwondoa Rais..............................................................86

vi i

Page 10: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

Kanuni za Kudumu za Bunge

130. Utaratibu wa kumwondoa Makamu wa Rais Madarakani ...............................................................................86131 Masharti ya hoja ya kuunda Kamati Maalum ya Uchunguzi ...........................................................................................87132. Wajumbe wa Kamati .......................................................................87133. Utaratibu wa kazi ya Kamati Maalum ya Uchunguzi...... .......88134. Utaratibu katika Kamati za Bunge Zima kuhusu mashitaka dhidi ya Makamu wa Rais ........................................88135. Azimio la kumwondoa Makamu wa Rais madarakani............89

SEHEMU YA KUMI NA TATU

HOJA YA KUTOKUWA NA IMANI NA WAZIRI MKUU

136 Taarifa ya Hoja ya Kutokuwa na imani na Waziri Mkuu ........... 89

SEHEMU YA KUMI NA NNE

KUMWONDOA SPIKA AU NAIBU SPIKA MADARAKANI

137. Taarifa ya Hoja ya Kumwondoa Spika Madarakani............... 91138. Utaratibu wa Kumwondoa Naibu Spika Madarakani............ 91

SEHEMU YA KUMI NA TANO

WAGENI BUNGENI

139. Ruhusa kwa wageni Bungeni ...................................................... 92140. Ruhusa kwa Waandishi wa Habari ....................................... ... 93141. Mamlaka ya kuwaondoa wageni Bungeni .............................. 93142. Utambulisho wa Wageni ............................................................. 94

SEHEMU YA KUMI NA SITA

UKAAJI NDANI YA UKUMBI WA BUNGE

143. Utaratibu wa Kukaa kwa Wabunge, Watumishi na Wageni Bungeni ................................................. 94

vi i i

Page 11: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

Kanuni za Kudumu za Bunge

SEHEMU YA KUMI NA SABA

USALAMA WA MAENEO YA BUNGE

144. Utaratibu wa Kuingia Maeneo ya Bunge.................................. 95145. Ukaguzi ............................................................................... ............. 95

SEHEMU YA KUMI NA NANE

MENGINEYO

146. Wajibu wa Mbunge kuhudhuria Vikao vya Bunge .............. ...96147. Lugha Rasmi Bungeni .................................................................... 96148. Taarifa Rasmi za Bunge ........................................................ ....... 96149. Mavazi Rasmi ............................................................................... ... 97150. Bendera ya Bunge................................................................. ........ 99151. Utaratibu wa kupepeza Bendera .......................................... .... 99152. Utaratibu baada ya kifo cha Mbunge ...................................... 100153. Kutengua Kanuni za Bunge................................................... .........100154. Salamu za Pongezi na Pole ................................................... ..... 100155. Kufanya Mabadiliko katika Kanuni ...................................... ..... .101156. Kanuni kuanza kutumika .................................................................101157. Kufutwa kwa Toleo la Aprili, 2013 na Hifadhi ya mambo yaliyofanyika......................................... .......101

ix

Page 12: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

Kanuni za Kudumu za Bunge

___________NYONGEZA YA KWANZA

_________

KANUNI ZA UCHAGUZI WA SPIKA NA NAIBU SPIKA_____________

SEHEMU YA KWANZA

UTANGULIZI

Kifungu Kichwa cha Habari Ukurasa1. Jina ...................................................................................................... 1022. Matumizi ................................................................................................1023. Tafsiri ........................................................................................................102

SEHEMU YA PILI

MSIMAMIZI WA UCHAGUZI

4. Uendeshaji na Usimamizi wa Uchaguzi ....................................... 103

SEHEMU YA TATU

KUWASILISHA JINA LA MGOMBEA

5. Kuwasilisha majina ya Wagombea ..............................................103

SEHEMU YA NNE

MASHARTI YA MGOMBEA UCHAGUZI

6. Masharti kwa mgombea................................................................104

SEHEMU YA TANO

KUJITOKEZA MGOMBEA MMOJA

7. Kumpigia Kura Mgombea Mmoja...............................................104

x

Page 13: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

Kanuni za Kudumu za Bunge

__________NYONGEZA YA PILI

__________

KANUNI ZA UCHAGUZI WA WABUNGEWANAOKWENDA KWENYE VYOMBO VINGINE VYA

UWAKILISHI_________

SEHEMU YA KWANZA

UTANGULIZI

Kifungu Ukurasa

1. Jina ..................................................................................................... ...1052. Matumizi .................................................................................................1053. Tafsiri ..........................................................................................................105

SEHEMU YA PILI

UTEUZI WA WAGOMBEA

4 Uteuzi wa Wagombea............................................................ .........106

SEHEMU YA TATU

UTARATIBU WA UCHAGUZI

5. Uchaguzi wa Wagombea wa nafasi za Uwakilishi.................. 106

SEHEMU YA NNE

UCHAGUZI WA KUJAZA NAFASI ZA NASIBU

6. Uchaguzi wa nafasi za nasibu.........................................................107

xi

Page 14: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

Kanuni za Kudumu za Bunge

SEHEMU YA TANO

UTARATIBU WA KUPIGA KURA

7. Utaratibu wa kupiga kura ................................................................108

SEHEMU YA SITA

KUPIGA KURA

8. Kupiga kura........................................................................................108

SEHEMU YA SABA

KUHESABU KURA

9. Kuhesabu kura.....................................................................................109

SEHEMU YA NANE

KUTANGAZA MATOKEO YA KURA

10. Kutangaza matokeo ya kura.........................................................110

SEHEMU YA TISA

UTUNZAJI WA KUMBUKUMBU ZA KURA

11. Utunzaji wa kumbukumbu za kura...............................................111

SEHEMU YA KUMI

KUPINGA MATOKEO YA KURA

12. Kupinga Matokeo ya Kura.............................................................111

xii

Page 15: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

Kanuni za Kudumu za Bunge

PART IIINOMINATION OF CANDIDATE

4. Nomination of Candidates................................................................1135. Validity of nomination.........................................................................1136. Non-refundable deposit......................................................................1147. Rejection of nomination papers......................................................114

PART IVELECTION AND VOTING PROCEDURE

8. Election day...........................................................................................1159. Withdrawal of candidature...............................................................11510. Campaign by candidate.................................................................11511. Supervision of the Voting process..................................................11512. Votes Counting agents.....................................................................11613. Annoucement of election results...................................................11614. Custody of ballot papers...................................................................117

PART VANNULMENT AND AVOIDANCE OF ELECTION

15. Annulment and avoidance at election......................................11716. Grounds for annulment and avoidance of election.................117

PART VIMISCELLANEOUS

17. Matters not provided for..................................................................11718. Amendment of rules..........................................................................117

PART IIQUALIFICATION

3. Qualification of Candidate................................................................113

_________NYONGEZA YA TATU

_________

THE EAST AFRICAN LEGISLATIVE ASSEMBLY ELECTION RULES_________

PART IPRELIMARY RULES

1. Citation.....................................................................................................1122. Interpretation.........................................................................................112

xiii

Page 16: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

Kanuni za Kudumu za Bunge

___________

NYONGEZA YA NNE_________

THE SUBMISSION OF REGULAR REPORTS TO THE PARLIAMENT OFTANZANIA BY THE TANZANIA MEMBERS OF THE EAST AFRICAN

LEGISLATIVE ASSEMBLY_______________

1. Citation.....................................................................................................1182. Interpretation.........................................................................................1183. Presentation of annual report ......................................................... 1184. Time of presentation........................................................................... 1185. Presentation of special report and consultations.......................1186. Attendance and laying of reports on the table......................... 119

_______________

NYONGEZA YA TANO_______________

THE PAN-AFRICAN PARLIAMENTARY ELECTION RULESPART I

PRELIMINARY RULES

1. Citation.................................................................................................... 1202. Interpretation........................................................................................ 120

PART IIQUALIFICATION OF CANDIDATES

3. Qualification........................................................................................... 121

PART IIINOMINATION PROCEDURE

4. Appointment of nomination............................................................1215. Nomination procedure......................................................................126

xiv

Page 17: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

Kanuni za Kudumu za Bunge

5. Nomination procedure.......................................................................1216. Nomination of Candidates ...............................................................122

PART IVELECTION PROCEDURE

7. Election day ............................................................................................1238. Voting process....................................................................................... 1239. Candidates address voters ...............................................................12310. Voting procedures ............................................................................ 12311. Casting of votes ...................................................................................12412. Appointment of Counting Agents and counting of votes.... 12413. Place for counting of votes .............................................................12414. Declaration of election results .......................................................12415. Custody of ballot papers ..................................................................125

PART VMISCELLANEOUS

16. Matters not provided for...................................................................12517. Amendment..........................................................................................125

_____________

NYONGEZA YA SITA_______________

MWONGOZO KUHUSU MASWALI KWA WAZIRI MKUU

[Chini ya Kanuni ya 38(6)]____________

1. Maelezo ya Jumla............................. ....................................................1262. Utaratibu wa kupata fursa ya kumuuliza Waziri Mkuu ...............1263. Utaratibu wa kuuliza maswali kwa Waziri Mkuu.......................... 1264. Maswali na majibu kwa Waziri Mkuu.............................................. 127

xv

Page 18: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

Kanuni za Kudumu za Bunge

______________

NYONGEZA YA SABA_______________

MWONGOZO WA UPATIKANAJI WA HABARI KUTOKAKWENYE VIKAO VYA KAMATI ZA BUNGE

[Chini ya Kanuni ya 117(9) na (10)]

1. Maelezo ya jumla ................................................................................1282. Majukumu yatakayofanywa kwa uwazi........................................ 128

3. Majukumu yatakayofanywa kwa faragha............................... .... 129

4. Majukumu yenye uwazi wenye mipaka .........................................129

5. Mawaziri wanapotoa taarifa kwa waandishi wa habari baada ya kukutana na Kamati ........................................................ 130

xvi

Page 19: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

Kanuni za Kudumu za Bunge

1133. Ma

_______

NYONGEZA YA NANE________

KAMATI ZA KUDUMU ZA BUNGE

(Chini ya Kanuni ya 118)_________

SEHEMU YA KWANZA

KAMATI ZA KUDUMU ZISIZO ZA SEKTA

1. Kamati za Kudumu zisizo za Sekta .................................................132

2. Muundo na majukumu ya Kamati ya Uongozi..............................132

3. Muundo na majukumu ya Kamati ya Kanuni za Bunge ...............133

4. Majukumu ya Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge................................................................................................ 134

SEHEMU YA PILI

KAMATI ZA KUDUMU ZA BUNGE ZA SEKTA

5. Kamati za Kudumu za Sekta ............................................................134

6. Kamati na shughuli za Wizara .........................................................134

7. Majukumu ya Kamati za Sekta .......................................................136

SEHEMU YA TATU

KAMATI ZA SEKTA MTAMBUKA8. Kamati ya Sekta Mtambuka..............................................................137

9. Majukumu ya Kamati ya Bajeti.........................................................138

10. Majukumu ya Kamati ya Ukimwi .....................................................139

11. Majukumu ya Kamati ya Sheria Ndogo........................................139

xvii

Page 20: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

Kanuni za Kudumu za Bunge

Page 21: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

Kanuni za Kudumu za Bunge

12. Majukumu ya Kamati ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma .......139

SEHEMU YA NNE

KAMATI ZA KUDUMU ZA BUNGE ZINAZOSIMAMIA MATUMIZI YAFEDHA ZA UMMA

13. Kamati za Kudumu za Bunge zinazosimamia matumizi ya Fedha za Umma ................................................................................140

14. Majukumu ya Kamati ya Hesabu za Serikali .............................140

15. Majukumu ya Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa............140

16. Msingi wa Kamati ya Hesabu za Serikali na Kamati ya Serikali za Mitaa ...............................................................................141

xviii

Page 22: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

1

Kanuni za Kudumu za Bunge

KATIBA YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA YAMWAKA 1977

(SURA YA 2)________

KANUNI________

[Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1)]_______

KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE, TOLEO LA JANUARI, 2016_______

SEHEMU YA KWANZA

UTANGULIZI

1-. Kanuni hizi zitaitwa Kanuni za Kudumu za Bunge, Toleo laJanuari, 2016.

2-(1) Bila ya kuathiri masharti ya Katiba, Kanuni hizi zitatumika kwamambo yote yanayohusu utaratibu wa uendeshaji wa Shughuli zaBunge. (2) Iwapo jambo au shughuli yoyote haikuwekewa mashartikatika Kanuni hizi, Spika ataamua utaratibu wa kufuata katikajambo au shughuli hiyo, kwa kuzingatia Katiba, Sheria nyingine zanchi, Kanuni nyingine zilizopo, maamuzi ya awali ya Maspika waBunge pamoja na mila na desturi za uendeshaji bora wa Shughuliza Bunge na uamuzi huo utaingizwa katika Kitabu cha Maamuzi ilikuongoza mwenendo wa baadaye wa uendeshaji wa Shughuli zaBunge.

3.- Katika Kanuni hizi, isipokuwa kama maelezo yatahitajivinginevyo:-

“Akidi” ni idadi ya Wabunge inayoruhusu kufanya maamuzi yaBunge kwa mujibu wa Kanuni za 77, 78 na 79 za Kanuni hizi; “Bendera” ni Bendera rasmi ya Bunge la Jamhuri ya Muunganowa Tanzania ambayo ina rangi ya bluu iliyoiva iliyo katika umbo lamstatili na yenye umbo dogo la bendera ya Taifa ndani yake katika

Matumizi

Jina

Tafsiri

Page 23: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

2

Kanuni za Kudumu za Bunge

pembe juu ya upande wa kushoto na Siwa, chini kukiwa na utepewenye maneno “Bunge la Tanzania”; “Bunge” ni Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzanialililoanzishwa kwa mujibu wa Ibara ya 62 ya Katiba; “Bunge Jipya” ni Mkutano wa Kwanza wa Bunge ulioitishwa naRais kwa mujibu wa Ibara ya 90(1) baada ya kutangazwa matokeoya Uchaguzi Mkuu; “Chama” ni Chama cha Siasa chenye uwakilishi Bungeni; “Gazeti” ni Gazeti la Serikali ya Jamhuri ya Muungano; “Hoja ya Kamati” ni hoja iliyokubaliwa na Kamati ya Bunge baadaya majadiliano ya Kamati husika; “Hoja ya Mbunge” ni hoja inayotolewa na Mbunge asiyekuwaWaziri au Mwanasheria Mkuu wa Serikali; “Jamhuri ya Muungano” ni eneo lote lililokuwa ndani ya Mipakaya Jamhuri ya Tanganyika na eneo lote lililokuwa ndani ya Mipakaya Jamhuri ya Zanzibar kabla ya tarehe 26 Aprili, 1964; “Kamati” ni Kamati yoyote ya Bunge iliyoundwa kwa mujibu waKanuni hizi; “Kamati ya Bunge Zima” ni Kikao cha Wabunge wote wanapokaakama Kamati wakati wa:-

(a) kupitisha Muswada wa Sheria;(b) kujadili taarifa ya Kamati Maalumu ya Uchunguzi

kuhusu mashtaka dhidi ya Rais au Makamu waRais;

(c) kujadili hoja ya kutokuwa na imani na WaziriMkuu; au

(d) kujadili hoja ya kumwondoa madarakani Spikaau Naibu Spika.

“Kamati ya Matumizi” ni kikao cha Wabunge wote wanapokaakama Kamati kushughulikia Makadirio ya Matumizi ya Fedha zaSerikali; “Kamati ya Mipango” ni kikao cha Wabunge wote wanapokaakama Kamati katika Mkutano wa mwezi Oktoba-Novemba ilikujadili na kushauri kuhusu mapendekezo ya mpango wowote wamuda mrefu au wa muda mfupi unaokusudiwa kutekelezwa naSerikali katika Jamhuri ya Muungano; “Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni” ni Kambi ya Upinzaniiliyoundwa na Vyama vya Upinzani vinavyowakilishwa Bungeni, kwamujibu wa masharti ya fasili ya (2) ya Kanuni ya 14 ya Kanuni hizi; “Katiba” ni Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya mwaka 1977; “Katibu” ni Katibu wa Bunge aliyetajwa katika Ibara ya 87 yaKatiba na inajumuisha pia mtumishi mwingine yeyote wa Bungealiyeidhinishwa kutekeleza kazi yoyote ya Katibu;

Sura ya 2,Toleo la2002

Page 24: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

3

Kanuni za Kudumu za Bunge

“Kikao cha Bunge” ni kikao cha siku moja kinachoanza kwakusomwa Dua na kumalizika kwa kuahirisha Bunge hadi sikuitakayotajwa;“Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni” ni Mbungealiyeteuliwa au kuchaguliwa na Wabunge wanaounda Kambi Rasmiya Upinzani ili kuwa Kiongozi wa Kambi hiyo na inajumuisha NaibuKiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni; “Kiongozi wa Shughuli za Serikali Bungeni”ni Waziri Mkuu kamailivyoainishwa katika Ibara ya 52(2) ya Katiba; “Kitabu cha Maamuzi” ni kumbukumbu ya maamuzi mbalimbaliya Spika kuhusu suala lolote la utaratibu Bungeni; “Madaraka ya Bunge” ni haki na madaraka ya Bunge kamayalivyofafanuliwa katika Ibara ya 100 ya Katiba na katika Sheria yaKinga, Madaraka na Haki za Bunge; “Maisha ya Bunge” ni muda wote unaoanzia tarehe ambapoBunge Jipya limeitishwa na Rais kukutana kwa mara ya kwanzabaada ya Uchaguzi Mkuu na kuishia tarehe ya kuvunjwa kwa Bungekama ilivyoelekezwa na Ibara ya 65 ya Katiba; “Mbunge” ni mtu aliyechaguliwa au kuteuliwa kwa mujibu waIbara ya 66 ya Katiba kuwa mjumbe wa Bunge la Jamhuri yaMuungano; “Mkutano wa Bunge” ni mfululizo wa vikao vya Bunge, kuanziakikao cha kwanza hadi cha mwisho; “Mgeni” maana yake ni mtu yeyote ambaye si Rais, Mbunge,Katibu au mtumishi yeyote na ambaye hatekelezi kazi rasmizinazohusu Bunge; “Mpambe wa Bunge” ni mtumishi wa Ofisi ya Bungeanayetekeleza majukumu yaliyoainishwa katika Kanuni ya 20 yaKanuni hizi; “Mwenyekiti” ni Mbunge aliyechaguliwa kuongoza Shughuli zaBunge na pia lina maana ya Spika, Naibu Spika au Mbunge mwingineanapokuwa anaongoza Kamati ya Bunge Zima, Kamati ya Matumiziau Kamati ya Mipango na vilevile inajumuisha Mbunge yeyoteanayeongoza Kamati ya Kudumu, Kamati Ndogo ya Kamati yaKudumu, Kamati Teule au Mkutano wa Uchaguzi wa Spika; “Naibu Spika” ni Mbunge aliyetajwa kuwa Naibu Spika wa Bungekwa mujibu wa Ibara ya 85 ya Katiba na kuchaguliwa kwa mujibuwa Kanuni ya 10 ya Kanuni hizi; “Naibu Waziri” ni Mbunge aliyeteuliwa na Rais kwa mujibu waIbara ya 55(2) na (3) ya Katiba; “Orodha ya Shughuli” ni karatasi mahususi zinazooneshampangilio wa Shughuli za Bunge katika kila kikao cha Bunge;

Sura ya296,Toleola 2002

Page 25: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

4

Kanuni za Kudumu za Bunge

“Rais” ni mtu aliyechaguliwa kushika Kiti cha Rais wa Jamhuri yaMuungano wa Tanzania, kama ilivyoelekezwa katika Ibara ya 33 yaKatiba; “Shughuli za Serikali” ni shughuli zinazowasilishwa Bungeni naWaziri au na Mwanasheria Mkuu wa Serikali; “Shughuli Binafsi” ni shughuli zilizowasilishwa Bungeni na Kamatiya Kudumu ya Bunge au Mbunge; “Siwa” ni rungu la dhahabu linalotumika kama kielelezo chamamlaka ya Bunge ambalo hubebwa na Mpambe wa Bungeakimtangulia Spika wakati wa kuingia na kutoka kwenye Ukumbiwa Bunge kabla na baada ya kikao cha Bunge; “Spika” ni Spika wa Bunge aliyetajwa katika Ibara ya 84 yaKatiba na kuchaguliwa kwa mujibu wa Kanuni ya 9 ya Kanuni hizi; “Taarifa Rasmi” ni taarifa za majadiliano ya Bunge zilizotajwakatika Kanuni hizi; “Tume ” ni Tume ya Utumishi wa Bunge iliyoundwa kwa mujibuwa kifungu cha 12 cha Sheria ya Uendeshaji Bunge, Sura ya 115 yamarejeo ya Sheria za Tanzania; “Waziri” ni Mbunge aliyeteuliwa na Rais kwa mujibu wa Ibara ya55 ya Katiba; “Wimbo wa Taifa” ni Wimbo wa Taifa wa Jamhuri ya Muunganowa Tanzania.

SEHEMU YA PILI

UENDESHAJI WA SHUGHULI ZA BUNGE

Uongozi wa Bunge

4.- Spika atachaguliwa na Wabunge kwa mujibu wa Kanuni ya 9 nakushika madaraka yake kwa mujibu wa Katiba na Kanuni hizi.

5.-(1) Katika kutekeleza majukumu yake yaliyotajwa katika Ibaraya 84 ya Katiba, Spika ataongozwa na Kanuni hizi na pale ambapoKanuni hazikutoa mwongozo, basi Spika atafanya kazi kwakuzingatia Katiba, Sheria nyingine za nchi, Kanuni nyingine zilizopo,maamuzi ya awali ya Maspika wa Bunge pamoja na mila na desturiza Mabunge mengine yenye utaratibu wa kibunge unaofanana nautaratibu wa Bunge la Tanzania.

(2) Spika atawajibika kutilia nguvu Kanuni zote za Bunge, naMbunge yeyote anaweza kusimama mahali pake na kumwarifuSpika kuwa Mbunge fulani amekiuka Kanuni.

Spika

Mamlaka ya Spika

Page 26: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

5

Kanuni za Kudumu za Bunge

(3) Spika anaweza kumtaka Mbunge yeyote anayekiuka Kanunihizi kujirekebisha mara moja.

(4) Mbunge yeyote ambaye hataridhika na uamuzi wa Spikaanaweza kuwasilisha sababu za kutokuridhika kwake kwa Katibuwa Bunge ambaye atawasilisha malalamiko hayo kwa Spika.

(5) Spika atawajibika kuitisha kikao cha Kamati ya Kanuni zaBunge na kulijulisha Bunge kuhusu uamuzi utakaotolewa na Kamatihiyo.

(6) Spika au Naibu Spika hatakuwa Mwenyekiti wa Kamati yaKanuni za Bunge inapokaa kujadili uamuzi unaolalamikiwa, baliWajumbe watachagua Mwenyekiti wa muda kwa asilimia 50 yakura za siri.

(7) Bila ya kuathiri masharti ya Katiba na ya Kanuni hizi, wakatiwowote ambapo Spika hayupo Bungeni au kwa sababu nyingineyoyote hawezi kutekeleza madaraka au majukumu ya Spika, basimadaraka au majukumu ya Spika yatatekelezwa na Naibu Spika.

6.-(1) Naibu Spika aliyetajwa katika Ibara ya 85(1) ya Katiba,atachaguliwa kwa mujibu wa Kanuni ya 10 kutoka miongoni mwaWabunge na kushika madaraka yake kwa mujibu wa masharti yaKatiba na Kanuni hizi.

(2) Naibu Spika atakuwa msaidizi wa Spika katika kuliongozaBunge na atatekeleza majukumu yake kwa mujibu wa Kanuni hizi.

(3) Spika anaweza wakati wowote bila kutoa taarifa rasmi kwaBunge kumtaka Naibu Spika au Mwenyekiti kuongoza Shughuli zaBunge.

(4) Bila ya kuathiri masharti ya Katiba na ya Kanuni hizi, wakatiwowote ambapo Spika na Naibu Spika wote hawapo Bungeni aukwa sababu nyingine yoyote, hawawezi kutekeleza madaraka aumajukumu yao, basi madaraka au majukumu hayo yatatekelezwana Mwenyekiti wa Bunge.

(5) Naibu Spika anaweza wakati wowote, bila kutoa taarifarasmi kwa Bunge, kumtaka Mwenyekiti wa Bunge kuongoza Shughuliza Bunge.

MajukumuyaNaibuSpika

Page 27: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

6

Kanuni za Kudumu za Bunge

7.-(1) Kutakuwa na Wenyeviti watatu wa Bunge ambaowatachaguliwa na Wabunge kutoka miongoni mwao kwakuzingatia jinsia na pande za Muungano.

(2) Kamati ya Uongozi itapendekeza majina ya Wabunge sitaambayo yatawasilishwa Bungeni ili kupigiwa kura.

(3) Wenyeviti wa Bunge wanaweza kuongoza shughuli za Bungekwa utaratibu na maelekezo ya Spika au Naibu Spika kwa mujibuwa Kanuni hizi.

(4) Endapo Spika, Naibu Spika na Wenyeviti wa Bunge wotehawapo, Wabunge watamchagua mmoja wa Wenyeviti waKamati za Kudumu za Bunge kuendesha Shughuli za Bungekufuatana na utaratibu uliowekwa na Kanuni hizi.

8.- Kwa kuzingatia matakwa na masharti yaliyowekwa na kiapocha kazi zake na kwa madhumuni ya utoaji wa maamuzi nauendeshaji wa Shughuli za Bunge kwa haki na bila upendeleo, Spika:-

(a) ataendesha shughuli za Bunge na kutoamaamuzi kwa haki, uadilifu na bila chuki walaupendeleo wowote, kwa kuongozwa na Katiba,Sheria za nchi, Kanuni hizi, Kanuni nyinginezilizopo, maamuzi ya maspika wa Bungewaliotangulia na pia kwa kuzingatia uzoefupamoja na mila na desturi za mabunge mengineyanayofuata utaratibu wa kibunge unaofananana unaofuatwa na Bunge la Tanzania;

(b) hatafungwa na msimamo utakaowekwa aumakubaliano yatakayofikiwa na Kamati yoyoteya Chama cha Siasa kinachowakilishwa Bungeni.

Uchaguzi wa Viongozi wa Bunge

9.-(1) Kutakuwa na Uchaguzi wa Spika utakaofanyika kwa mujibuwa masharti ya Ibara ya 84 (1) ya Katiba pamoja na Kanuni hizi.

(2) Kila Chama cha Siasa kitakuwa na haki ya kupendekeza jinamoja la Mbunge wa Chama hicho ambaye atakuwa mgombea wanafasi ya Spika, kwa mujibu wa Katiba.

(3) Majina ya wagombea wasio Wabunge yatawasilishwa na

Uadilifu kwa Kiongozi wa Bunge

Uchaguzi wa Spika

MajukumuyaWenyeviti wa Bunge

Page 28: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

7

Kanuni za Kudumu za Bunge

vyama husika kwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi siku tano kabla yauchaguzi.

(4) Baada ya kupokea majina hayo, Tume itayachambua nakisha itawasilisha majina ya wagombea wenye sifa kwa Katibu sikumbili kabla ya uchaguzi.

(5) Endapo wamependekezwa wagombea wawili au zaidi,uchaguzi utafanyika kwa kufuata utaratibu ulioainishwa katika fasilizinazofuata za Kanuni hii.

(6) Mgombea yeyote anaweza kumtaarifu Katibu kwamaandishi kwamba anajitoa kugombea, kabla ya shughuli zakupiga kura kuanza Bungeni, na Katibu atalifuta jina la mgombeahuyo katika karatasi za kura.

(7) Mwanzoni mwa Kikao cha Kwanza cha Mkutano wa Kwanzawa Bunge Jipya, mara baada ya Katibu kusoma Tangazo la Rais naKikao kujigeuza kuwa Mkutano wa Uchaguzi wa Spika, Katibuatamwomba Mbunge asiye mgombea wa nafasi ya Spika kutokamiongoni mwa Wabunge ambao wamekuwa Wabunge kwamfululizo kwa muda mrefu, awe Mwenyekiti wa Mkutano huo waUchaguzi.

(8) Kabla ya kikao cha Bunge cha kumchagua Spika kuanza,Katibu ataandaa karatasi za kura zitakazoonesha majina yawagombea wote waliopendekezwa na wakati wa kupiga kuraatatoa karatasi moja tu ya kura kwa kila Mbunge.

(9) Mbunge ambaye kabla ya shughuli za uchaguzi kumalizikaatakosea katika kuweka alama kwenye karatasi ya kura ataruhusiwakumrudishia Katibu karatasi hiyo, na papo hapo Katibu ataifuta nakuiharibu kisha kumpa Mbunge huyo karatasi nyingine.

(10) Kila Mbunge atapiga kura ya siri kwa kuweka katika karatasiya kura alama ya “V” katika mraba pembeni mwa jina la Mgombeaanayemtaka awe Spika, na ataitumbukiza karatasi hiyo katikasanduku la kura.

(11) Baada ya Katibu kuridhika kwamba Wabunge wotewaliomo Bungeni wamepiga kura na kutumbukiza karatasi zao zakura kwenye masanduku ya kura, masanduku yote yatakusanywana kuwekwa mahali panapoonekana na baada ya hapo masandukuhayo ya kura yatapelekwa kwenye chumba maalumu na kura hizo

Page 29: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

8

Kanuni za Kudumu za Bunge

zitahesabiwa chini ya usimamizi wa wawakilishi walioteuliwa nawagombea, mmoja mmoja kwa kila mgombea.

(12) Endapo zoezi hili la uchaguzi litaendeshwa kwa mfumo waelektroniki wa upigaji kura basi upigaji na uhesabuji kura utakuwawa papo kwa papo na matokeo yake yatakuwa halali.

(13) Mgombea atakuwa amechaguliwa kuwa Spika kamaatapata zaidi ya nusu ya kura za Wabunge wote na iwapohakutakuwa na mgombea aliyepata zaidi ya nusu ya kura hizo,uchaguzi utarudiwa lakini ni wagombea wawili tu waliopata kuranyingi zaidi ndio watakaopigiwa kura, na katika hatua hiyo,mgombea atakayepata kura nyingi zaidi atatangazwa kuwamshindi.

(14) Endapo wagombea wawili au zaidi watapata kura sawakatika nafasi ya mwanzo, basi wagombea hao tu ndiyowatakaopigiwa kura na mgombea atakayepata kura nyingi zaidiatakuwa ndiye mshindi.

(15) Iwapo wagombea wawili au zaidi watapata kura sawakatika nafasi ya pili na yule wa kwanza hajapata zaidi ya nusu yakura zilizopigwa, basi wagombea hao wawili pamoja na yule wakwanza ndio watakaopigiwa kura na mgombea atakayepata kuranyingi zaidi atakuwa ndiye mshindi.

(16) Endapo awamu ya pili ya upigaji kura itashindwa kumpatamshindi, basi Mwenyekiti atapiga kura yake ya uamuzi ili mshindiapatikane.

(17) Endapo kutakuwa na mgombea mmoja tu basi mgombeahuyo atapigiwa kura ya “Ndiyo” au “Hapana” na atatangazwakuwa amechaguliwa kuwa Spika iwapo atapata kura za “Ndiyo”za idadi ya zaidi ya nusu ya kura za Wabunge wote.

(18) Mara baada ya mshindi kupatikana, Katibu atamtangazaSpika aliyechaguliwa na Spika huyo Mteule ataapa viapovilivyowekwa kwa mujibu wa Sheria na Kanuni hizi.

(19) Muda wa Spika Mteule kuapishwa utakapowadia,Mwenyekiti atamwita Spika Mteule ajongee mbele ya Bunge iliaape viapo vinavyohusika.

Page 30: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

9

Kanuni za Kudumu za Bunge

(20) Mtu au Mbunge yeyote aliyechaguliwa kuwa Spika, kablaya kushika madaraka yake, ataapa mbele ya Bunge Kiapo cha Utiina Kiapo cha Spika vitakavyokuwa na maneno yafuatayo:

Kiapo cha Utii:

“Mimi, …………..….. naapa kwamba, nitakuwa mwaminifu kwaJamhuri ya Muungano wa Tanzania na kuitumikia kwa moyo wanguwote na kwamba, nitaihifadhi, nitailinda na kuitetea Katiba yaTanzania kwa mujibu wa Sheria iliyowekwa. Ewe Mwenyezi Mungu,nisaidie.”

Kiapo cha Spika:

“Mimi, …………., naapa kwamba, nitaitumikia vyema na kwamoyo thabiti Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kazi zangukama Spika wa Bunge, na katika kutimiza wajibu wa cheo hichonitawatendea haki watu wote kwa mujibu wa Katiba, Kanuni zaBunge na Sheria, Mila na Desturi za Jamhuri ya Muungano na kwavyovyote vile sitatoa siri za Bunge. Ewe Mwenyezi Mungu, nisaidie.”

(21) Wakati wa kuapa, Spika anayeamini kuwa kuna Mungu,atalazimika kushika Biblia au Kuran au kitabu kingine kitakatifukinachotambuliwa na imani ya dini yake.

(22) Iwapo Spika haamini kuwa kuna Mungu, basi hatashikaBiblia au Kuran au kitabu chochote kitakatifu au kutamka maneno“Ewe Mwenyezi Mungu nisaidie,” bali atalazimika kuinua mkonowake wa kuume juu.

10.-(1) Kutakuwa na uchaguzi wa Naibu Spika wa Bunge katikanyakati zilizowekwa na Ibara ya 86(1) ya Katiba na utaratibuuliowekwa na Kanuni hizi.

(2) Uchaguzi wa Naibu Spika utafanyika katika Mkutano waKwanza wa Bunge Jipya, au mapema iwezekanavyo baada yawakati huo au katika kikao cha kwanza cha Bunge mara baada yanafasi ya Naibu Spika kuwa wazi, au mapema iwezekanavyo baadaya kikao hicho.

(3) Uchaguzi wa Naibu Spika utaendeshwa kwa utaratibu uleule unaotumika kumchagua Spika, isipokuwa kwamba, Mbunge

UchaguziwaNaibu Spika

Page 31: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

10

Kanuni za Kudumu za Bunge

hawezi kushiriki katika uchaguzi wa aibu Spika iwapo hajaapaKiapo cha Uamininifu.

(4) Mbunge yeyote atakayechaguliwa kuwa Naibu Spika, kablaya kushika madaraka yake, ataapishwa na Spika Kiapo cha NaibuSpika ambacho kitakuwa na maneno yafuatayo:

“Mimi, …………., naapa kwamba, nitaitumikia vyema na kwamoyo thabiti Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kazi zangukama Naibu Spika wa Bunge, na katika kutimiza wajibu wa cheohicho nitawatendea haki watu wote kwa mujibu wa Katiba, Kanuniza Bunge na Sheria, Mila na Desturi za Jamhuri ya Muungano nakwa vyovyote vile sitatoa siri za Bunge. Ewe Mwenyezi Mungu,nisaidie.”

(5) Wakati wa kuapa, Naibu Spika anayeamini kuwa kunaMungu, atalazimika kushika Biblia au Kuran au kitabu kinginekitakatifu kinachotambuliwa na imani yake ya dini.

(6) Iwapo Naibu Spika haamini kuwa kuna Mungu, hatashikaBiblia au Kuran au kitabu chochote kitakatifu au kutamkamaneno“Ewe Mwenyezi Mungu nisaidie,” bali atalazimika kuinuamkono wake wa kuume juu.

11.-(1) Uchaguzi wa Wenyeviti wa Bunge utafanyika kwa kuzingatiajinsia na pande za Muungano na kwa kufuata utaratibu kwamba:-

(a) karatasi ya kura itakuwa na majina ya Wabungesita ambao wamependekezwa na Kamati yaUongozi kupigiwa kura kutoka miongoni mwaWenyeviti na Makamu Wenyeviti wa Kamati zaKudumu za Bunge;

(b) kila Mbunge atapiga kura kwa kuchagua majinamatatu katika orodha hiyo; na

(c) wagombea watatu watakaopata kura nyingikuliko wenzao ndio watakuwa wamechaguliwakuwa Wenyeviti wa Bunge.

UchaguziwaWenyeviti wa Bunge

Page 32: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

11

Kanuni za Kudumu za Bunge

UchaguziwaWabungewanao-kwendakwenyevyombovinginevyauwakilishi

12.- Uchaguzi wa Wabunge wanaokwenda katika vyombo vingineambavyo kwa mujibu wa Sheria zilizounda vyombo hivyovinatakiwa viwe na wawakilishi wa Bunge na uchaguzi wakuwachagua Wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki utafanywakwa kuzingatia, kwa kadri iwezekanavyo, uwiano wa idadi yaWabunge wa Vyama mbalimbali vya Siasa vinavyowakilishwa

(2) Wenyeviti wa Bunge waliochaguliwa kwa mujibu wamasharti ya fasili ya (1) ya Kanuni hii watashika madaraka yao kwamuda ambao wataendelea kuwa Wenyeviti au Makamu Wenyevitiwa Kamati zao za Kudumu za Bunge mpaka mwisho wa Mkutanounaofuata mara baada ya Mkutano wa Kumi wa Bunge (ambaondio hukamilisha nusu ya kwanza ya maisha ya Bunge) utakaofanyikabaada ya kuchaguliwa kwao, lakini wanaweza kuchaguliwa tenakuwa Wenyeviti wa Bunge katika kipindi cha pili kilichobaki chamaisha ya Bunge la kipindi kinachohusika iwapo watachaguliwatena kuwa Wenyeviti wa Kamati za Kudumu za Bunge.

13.- Endapo Waziri Mkuu ambaye ndiye Kiongozi wa Shughuli zaSerikali Bungeni hatakuwepo Bungeni kwa kipindi kinachozidi sikumoja, basi atamteua Waziri mwingine kuwa Kiongozi wa muda waShughuli za Serikali Bungeni.

KiongoziwaKambiRasmiyaUpinzaniBungeni

14.-(1) Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni atachaguliwachini ya utaratibu ulioainishwa kwenye fasil i za Kanuni hiizinazofuata.

Kiongoziwa mudawaShughulizaSerikaliBungeni

(2) Wabunge wote wa Upinzani wanaweza kuunda KambiRasmi ya Upinzani iwapo idadi yao itakuwa si chini ya asilimia kumina mbili na nusu ya Wabunge wote.

(3) Chama cha Upinzani hakitakuwa na haki ya kuchaguaKiongozi wa Upinzani Bungeni, isipokuwa tu kama kina idadi yaWabunge wasiopungua asilimia kumi na mbili na nusu ya Wabungewote.

Page 33: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

12

Kanuni za Kudumu za Bunge

(4) Endapo kutakuwa na Vyama vya Upinzani zaidi ya kimojaambavyo kila kimoja kina Wabunge asilimia kumi na mbili na nusuau zaidi, basi Chama chenye idadi kubwa zaidi ya Wabunge kulikovingine ndicho kitakuwa na haki ya kuchagua Kiongozi wa KambiRasmi ya Upinzani Bungeni, lakini, ikiwa kutakuwa na vyama viwiliau zaidi vyenye idadi sawa ya Wabunge ambao ni zaidi ya asilimiakumi na mbili na nusu, Wabunge wa vyama vinavyohusikawatachagua Kiongozi wa Upinzani Bungeni chini ya utaratibuwatakaokubaliana wenyewe.

15.-(1) Chama chenye haki ya kumchagua Kiongozi wa Kambi Rasmiya Upinzani Bungeni kinaweza pia kuchagua Naibu Kiongozi waKambi Rasmi ya Upinzani Bungeni.

(2) Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni atateuaWabunge wa Chama chake au Wabunge wa Kambi Rasmi yaUpinzani Bungeni ambao watakuwa wasemaji wakuu wa Kambi yaUpinzani kwa Wizara zilizopo za Serikali.

16.-(1) Chama kinachounda Serikali na Chama chenye haki yakuchagua Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, vitateuaWanadhimu wa vyama hivyo Bungeni ambao watajulikana kwajina la Mnadhimu wa Serikali na Mnadhimu wa Kambi Rasmi yaUpinzani Bungeni.

UteuziwaWana-dhimuwa vyama Bungeni

KambiRasmiyaUpinzaniBungeni

(2) Vyama hivyo vitateua pia Wanadhimu Wasaidizi ambaoidadi yao itaamuliwa na Vyama vyenyewe.

(3) Mnadhimu wa Serikali atakuwa kiungo cha mawasilianokati ya Kiongozi wa Shughuli za Serikali Bungeni na Wabunge waChama kinachounda Serikali na Mnadhimu wa Kambi Rasmi yaUpinzani Bungeni atakuwa ni kiungo cha mawasiliano kati yaKiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni na Wabunge waUpinzani.

Page 34: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

13

Kanuni za Kudumu za Bunge

(4) Vyama vya Siasa vyenye uwakilishi Bungeni vinawezakutunga Kanuni za vyama kwa ajili ya uendeshaji bora wa shughuliza vyama hivyo Bungeni.

17.-(1) Katibu wa Bunge kama alivyotajwa kwenye Ibara ya 87(1)ya Katiba, atawajibika kuhakikisha utekelezaji bora wa Shughuli zaBunge na kwa madhumuni hayo:-

(a) atahudhuria au atawakilishwa katika vikao vyotevya Bunge na vya Kamati ya Bunge Zima na vikaovya Kamati nyingine yoyote ya Bunge;

(b) atawajibika kuweka kumbukumbu zinazotakiwaziwekwe kwa mujibu wa Kanuni hizi;

(c) atatayarisha Taarifa Rasmi za majadiliano yaBunge kwa mujibu wa Kanuni hizi;

(d) atatayarisha siku hadi siku, Kitabu chaShughuli za Bunge na kukihifadhi Ofisini kwake,kikiwa kinaonesha:

(i) maagizo yote yaliyotolewa na Bunge;

(ii) shughuli zote zilizopangwa kufanywasiku yoyote ya baadaye;

(iii) taarifa zote za maswali na hojazilizokubaliwa na Spika.

(2) Katibu atawajibika kutunza Kitabu cha Maamuzi ya Spika,Kitabu cha Shughuli, Taarifa Rasmi, Miswada ya Sheria na Hatinyingine zilizowasilishwa Bungeni, na Mbunge au mtu yeyoteanaweza kukagua kumbukumbu hizo wakati wowote unaofaa kwakufuata utaratibu utakaowekwa na Spika.

MajukumuyaKatibuwaBunge

(3) Katibu ataweka kumbukumbu za maamuzi ya mara kwamara ya Spika kuhusu masuala ya utaratibu Bungeni.

Page 35: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

14

Kanuni za Kudumu za Bunge

(4) Katibu atawajibika kuhakikisha kuwa, Ukumbi wa Mikutanoya Bunge na mazingira yake, huduma kwa Wabunge na vifaavingine vinavyohusika na Shughuli za Bunge, viko katika haliinayofaa kuliwezesha Bunge kutekeleza wajibu wake ipasavyo.

18.-(1) Bila ya kuathiri masharti ya Katiba na ya Kanuni hizi kuhusuuwekaji wa nafasi na ngazi za utumishi katika Ofisi ya Bunge, Ofisihiyo itakuwa na Idara, Sehemu na Vitengo mbalimbali kwa namnana idadi ambayo itaiwezesha kutoa huduma bora na kamilifu kwaBunge, Wabunge na Kamati za Bunge.

(2) Bila ya kuathiri masharti yaliyotangulia ya Kanuni hii,kutakuwa na Makatibu Wasaidizi wa Bunge, kwa idadi na ngazimbalimbali kadri itakavyoamuliwa na Tume ya Huduma za Bungeiliyoundwa kwa mujibu wa Sheria ya Uendeshaji wa Bunge.

(3) Kutakuwepo na watumishi wengine wa Bunge ambaonyadhifa, kazi na idadi yao vitaamuliwa na Tume ya Huduma zaBunge.

19.- Kutakuwa na Mpambe wa Bunge ambaye atatekeleza shughulimbalimbali za Bunge kwa kufuata maagizo atakayopewa na Spika,Naibu Spika, Mwenyekiti au Katibu, kwa kadri itakavyokuwa.

20.- (1) Pamoja na kutekeleza shughuli mbalimbali kwa mujibu wamasharti ya Kanuni ya 19, Mpambe wa Bunge:-

(a) atasimamia masuala yote ya ulinzi na usalama waofisi, mali, vifaa na majengo yote ya Bunge;

(b) atahakikisha utulivu na amani katika sehemuwanayokaa wageni na atawawekea utaratibumaalum wa kuingia na kutoka Bungeni; na

(c) atamtangulia Spika, akiwa amebeba Siwa, wakatiSpika anapoingia na anapotoka kwenye Ukumbiwa Mikutano ya Bunge.

(2) Kwa madhumuni ya utekelezaji bora wa majukumu yakewakati wa vikao vya Bunge, Mpambe wa Bunge anaweza kutoamaagizo anayoona yanastahili kutolewa kwa wahudumu wa Bunge,na wahudumu hao watawajibika kutekeleza maagizo hayo.

OfisiyaBunge

MpambewaBunge

MajukumuyaMpambewaBunge

Page 36: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

15

Kanuni za Kudumu za Bunge

(3) Mpambe wa Bunge atawajibika kuratibu na kushauri juuya usalama wa Ukumbi, majengo na vyumba vyote vya Bunge napia sehemu zote za majengo yote yanayotumiwa na Bunge auKamati za Bunge au Wabunge au watumishi wa Bunge.

(4) Mpambe wa Bunge atakuwa na uwezo wa kutoa maagizokwa askari mwingine yeyote aliyekabidhiwa kutekeleza majukumukwenye Ukumbi wa Bunge na mazingira yake au kwenye majengo,vyumba au sehemu nyingine zinazotumiwa kwa ajili ya kutekelezashughuli za Bunge kwa mujibu wa Kanuni hizi.

21.-(1) Kutakuwa na Mshauri Mkuu wa Bunge wa Mambo ya Sheriaambaye atakuwa Msaidizi Mkuu wa Katibu wa Bunge kwa masualayote yanayohusu Sheria. Pamoja na kazi nyingine, Mshauri wa Bungewa Mambo ya Sheria atashughulikia mambo yafuatayo:-

(a) kutoa ushauri wa kisheria kuhusu Miswadayote ya Sheria inayowasilishwa Bungeni;

(b) kuchambua Miswada ya Sheria inayowasilishwaBungeni na kuwasaidia Wabunge kupatauelewa sahihi wa Miswada hiyo;

(c) kutoa ushauri kwa Bunge kupitia Kamati yaKanuni za Bunge kuhusu marekebisho yoyoteyanayohitajika kufanyika katika Kanuni zaKudumu za Bunge;

(d) kutoa huduma za ushauri wa kisheria kwa Kamatiza Bunge na Wabunge kila atakapohitajikakufanya hivyo;

(e) kuandaa Miswada ya Sheria ya Kamati, MiswadaBinafsi ya Sheria na Hoja Binafsi za Wabunge;

(f) kusaidia Wabunge kutayarisha marekebisho yaMuswada wa Sheria unaowasilishwa Bungeni;

(g) kuwa ndiye mwakilishi rasmi wa Bunge katikamasula yote ya kisheria na kwa madhumunihayo, anaweza kushirikiana na wanasheriawengine kuliwakilisha Bunge au Tume ya Hudumaza Bunge endapo Bunge au Tume ya Huduma zaBunge itashtaki au itashtakiwa;

MshauriMkuuwaBungewaMamboyaSherianamajukumuyake

Page 37: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

16

Kanuni za Kudumu za Bunge

(h) kuhakikisha kuwa Muswada wowote wa Sheriauliopitishwa na Bunge unachapishwa kamaulivyopitishwa na Bunge na kuwasilishwa kwaRais kwa ajili ya kupata kibali cha Rais na nakalamoja kupelekwa kwa Spika; na

(i) kushughulikia masuala yote ya Sheriayatakayopelekwa kwake na uongozi waBunge.

(2) Masuala ya Sheria yanayotoka kwa Mbunge mmojammoja au Kamati yoyote ya Bunge yatapelekwa kwa Katibu waBunge ambaye atayakabidhi kwa Mshauri Mkuu wa Bunge waMambo ya Sheria i l i kuyafanyia kazi katika kipindiatakachoelekezwa.

(3) Mshauri Mkuu wa Bunge wa Mambo ya Sheria atateuliwana Tume ya Huduma za Bunge kutoka miongoni mwa wanasheriawaandamizi.

SEHEMU YA TATUMIKUTANO NA VIKAO VYA BUNGE

22.-(1) Mkutano wa Kwanza wa Bunge Jipya utafanyika mahali,tarehe na saa ambayo Rais atatamka wakati akiitisha Mkutano waBunge Jipya.

(2) Bila ya kuathiri Masharti ya Kanuni hizi kuhusu kuanza na kufungwakwa vikao vya Bunge, Mkutano wa Kwanza wa Bunge utaendeleakwa muda wowote ambao utahitajika kwa ajili ya kutekeleza nakukamilisha shughuli zote za Mkutano wa Kwanza wa Bunge Jipya.

23.-(1) Shughuli za Mkutano wa Kwanza wa Bunge Jipya zitakuwakama ifuatavyo:-

(a) Kusomwa Tangazo la Rais la kuitisha Bunge;(b) Uchaguzi wa Spika;(c) Kiapo cha Spika;(d) Wimbo wa Taifa na Dua;(e) Kiapo cha Uaminifu kwa Wabunge wote;(f) Hoja ya kuthibitisha uteuzi wa Waziri Mkuu;

(g) Uchaguzi wa Naibu Spika; (h) Ufunguzi rasmi wa Bunge Jipya utakaofanywa na Rais;

MkutanowakwanzawaBunge

ShughulizaMkutanowaKwanzawaBunge

Page 38: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

17

Kanuni za Kudumu za Bunge

(i) Hoja ya kujadili Hotuba ya Rais; na (j) Shughuli yoyote ambayo Bunge litaona inafaa

kushughulikiwa kwa wakati huo.

(2) Mwanzoni mwa Kikao cha Kwanza cha Mkutano waKwanza wa Bunge Jipya, Katibu atasoma Tangazo la Rais lakuitisha Bunge Jipya.

(3) Mara baada ya Tangazo la Rais kusomwa, Kikao kitajigeuzakuwa Mkutano wa Uchaguzi wa Spika.

(4) Katibu atamwomba Mbunge asiye mgombea wa nafasihiyo ya Spika kutoka miongoni mwa Wabunge ambao wamekuwaWabunge kwa mfululizo kwa muda mrefu awe Mwenyekiti waMkutano huo wa Uchaguzi.

(5) Katibu wa Bunge atagawa karatasi za kura kwa Wabunge,na uchaguzi wa Spika utafanywa kwa kuzingatia utaratibu na Kanunihizi.

(6) Baada ya Uchaguzi wa Spika kumalizika na mshindikutangazwa, Mwenyekiti atasitisha Mkutano wa Uchaguzi wa Spikana kutaja muda ambao Spika Mteule ataapishwa.

(7) Baada ya Spika Mteule kuapishwa atakalia kiti chake nakutoa hotuba fupi ya shukrani kwa Bunge na kisha ataliahirishaBunge hadi wakati mwingine atakaoutaja ambapo shughuli zakuapisha Wabunge wote Kiapo cha Utii zitaanza.

24.-(1) Kila Mbunge ataapa Kiapo cha Utii kitakachokuwa namaneno yafuatayo:

“Mimi,…………….., naapa kwamba, nitakuwa mwaminifu kwaJamhuri ya Muungano wa Tanzania na kuitumikia kwa moyo wanguwote na kwamba, nitaihifadhi, nitailinda na kuitetea Katiba yaJamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa mujibu wa Sheriailiyowekwa. Ewe Mwenyezi Mungu, nisaidie.”

(2) Wakati wa kuapa, Mbunge anayeamini kuwa kuna Mungu,atalazimika kushika Biblia au Kuran au kitabu kingine kitakatifukinachotambuliwa na imani ya dini yake.

KiapochaU t i ikwaWabunge

Page 39: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

18

Kanuni za Kudumu za Bunge

(2) Baada ya Spika kutaja jina la Mbunge anayependekezwa,Mwanasheria Mkuu wa Serikali atatoa hoja ya kuliomba Bungelithibitishe uteuzi wa Mbunge husika kuwa Waziri Mkuu.

(3) Baada ya kuthibitisha uteuzi wa Waziri Mkuu, Bungelitamchagua Naibu Spika.

(4) Iwapo Bunge litakataa kumthibitisha Waziri Mkuu, Spikaatamjulisha Rais kuhusu uamuzi huo wa Bunge.

26.-(1) Baada ya uchaguzi wa Naibu Spika, Spika atalitangaziaBunge mahali, siku na muda ambao Rais atalihutubia na kulifunguarasmi Bunge Jipya na baada ya Tangazo hilo, Spika anaweza:-

(a) kuahirisha Shughuli za Bunge hadi wakati huo; au

(b) kuahirisha Kikao cha Bunge hadi siku na mudaatakaoutaja.

(2) Rais atakapowasili katika viwanja vya Bunge, atapokelewana Spika akifuatana na Waziri Mkuu na kisha atakaribishwa ilialihutubie na kisha kulifungua Rasmi Bunge Jipya.

(3) Baada ya hotuba ya Rais, Waziri Mkuu atatoa hoja yakuahirisha Bunge hadi mahali, siku na muda atakaoutaja.

27.-(1) Isipokuwa kama itaelekezwa vinginevyo, kila Mkutano waBunge utafanyika katika ukumbi wa Bunge Dodoma.

(2) Wimbo wa Taifa utapigwa na kuimbwa katika kila kikaocha kwanza na cha mwisho kwa Mikutano yote ya Bunge kufuatanana utaratibu utakaowekwa na Bunge.

25.-(1) Baada ya shughuli ya kuwaapisha Wabunge kukamilika,Spika atasoma Taarifa ya Rais inayotaja j ina la Mbungeanayempendekeza kuwa Waziri Mkuu ili aweze kuthibitishwa naBunge.

Kuthibiti-shaUteuziwaWaziriMkuu

UfunguziRasmiwaBungejipya

MikutanoyakawaidayaBunge

Page 40: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

19

Kanuni za Kudumu za Bunge

(3) Bila ya kuathiri masharti yanayofuata ya Kanuni hii, kilaMkutano isipokuwa Mkutano wa Kwanza wa Bunge Jipya, utaanzatarehe itakayowekwa na Bunge.

(4) Endapo manufaa ya Taifa yatahitaji kuwa Bunge lisikutanetarehe ile iliyowekwa kwa Mkutano utakaofuata, bali likutanetarehe ya mbele zaidi au ya nyuma zaidi, basi Spika anaweza, baadaya kushauriana na Kamati ya Uongozi, kuliita Bunge likutane tarehehiyo ya mbele zaidi au nyuma zaidi.

(5) Iwapo Bunge litatakiwa kukutana tarehe ya mbele zaidikuliko tarehe iliyotangazwa awali, basi tarehe hiyo mpya haitakuwambele zaidi ya siku kumi na nne kutoka tarehe iliyotangazwa hapoawali.

28.-(1) Vikao vya Mikutano ya Bunge, isipokuwa Kikao cha Kwanzacha Mkutano wa Kwanza wa Bunge Jipya, vitaanza saa 3.00 asubuhi,ila tu, kama Bunge litaamua vinginevyo.

(2) Bunge litakutana hadi saa 7.00 mchana ambapo Spikaataahirisha shughuli yoyote itakayokuwa inafanyika hadi saa 11.00jioni, isipokuwa kama Spika akiona inafaa, Bunge linawezakuendelea kukutana kwa muda usiozidi dakika 30 au kusitishwawakati wowote kabla ya saa 7.00 mchana baada ya kuwahojiWabunge.

(3) Hoja ya kubadilisha nyakati za vikao itatolewa na Wazirina itaamuliwa kama hoja nyingine yoyote na haitahitaji kutolewataarifa.

(4) Bunge litaendelea kukaa hadi saa 1.45 usiku wakatiambapo Spika atasitisha shughuli na kuliahirisha hadi kesho yakeau siku nyingine atakayoitaja.

(5) Iwapo shughuli zilizopangwa kwa siku hiyo zimemalizikakabla ya saa 1.45, Spika ataliahirisha Bunge bila kuhoji, lakini iwapozimesalia dakika kumi kabla ya kufikia muda wa kuahirisha kikao, naBunge au Kamati ya Bunge Zima au Kamati ya Matumizi badohaijamaliza shughuli zake, Spika anaweza kuongeza muda usiozididakika thelathini, bila kulihoji Bunge au Kamati ya Bunge Zima auKamati ya Matumizi ili kukamilisha shughuli zilizobaki.

MudawaVikaovyaBunge

Page 41: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

20

Kanuni za Kudumu za Bunge

(6) Iwapo wakati wa kusitisha shughuli umefika na Spikaatakuwa analihoji au yupo karibu kulihoji Bunge, basi hatasitishashughuli mpaka hoja iwe imeamuliwa.

(7) Baada ya hoja kuamuliwa, Waziri atatoa hoja ya kuahirishaKikao cha Bunge hadi kesho yake au siku nyingine itakayotajwa.

(8) Endapo Spika atakuwa amepokea taarifa ya Mbungeyeyote anayetaka kutoa maelezo binafsi, basi Spika hataliahirishaBunge bali ataongeza muda usiozidi dakika thelathini bila ya kulihojiBunge ili kutoa nafasi kwa Mbunge huyo aweze kutoa maelezoyake, isipokuwa kwamba, maelezo hayo sharti yawe yameandikwana kuwasilishwa kwa Spika angalau siku moja kabla hayajatolewana Mbunge anayehusika atalazimika kuyasoma kamayalivyowasilishwa.

(9) Baada ya kusitisha Shughuli za Bunge, hakuna shughulinyingine yoyote itakayofanywa katika kikao hicho na Spikaataliahirisha Bunge hadi kesho yake au siku nyingine itakayotajwa.

(10) Endapo majadiliano yoyote katika Bunge au katika Kamatiya Bunge Zima yatasitishwa na Spika kwa mujibu wa masharti yaKanuni hii, wakati yatakaporudiwa katika Bunge au katika Kamati,yataendelezwa kuanzia hapo yalipositishwa na Mbunge yeyoteambaye hotuba yake ilikatizwa na Spika atakuwa na haki yakuendelea na maelezo yake katika marudio ya mjadala huo naendapo Mbunge hakuitumia haki yake hiyo, basi atahesabiwa kuwaalikuwa amemaliza hotuba yake.

(11) Bila ya kuathiri masharti ya Kanuni hii, wakati Spikaanapotaka kuliahirisha Bunge, wakati huo unaweza kutumiwa kamafursa kwa Mbunge yeyote kutaka ufafanuzi utolewe na Waziri juuya jambo lolote lililo chini ya madaraka ya Waziri huyo au kuanzishamjadala juu ya jambo lolote la dharura kwa idhini ya Spika,isipokuwa kwa jambo ambalo haliwezi kujadiliwa bila hoja maalumukutolewa kwanza kwa ajili hiyo.

(12) Jambo lolote haliwezi kuwasilishwa na kujadiliwa kwamujibu wa Kanuni hii, isipokuwa tu kama Mbunge amewasilisha kwaSpika Taarifa ya maandishi siyo chini ya saa ishirini na nne kabla yakutolewa kwa jambo hilo Bungeni akieleza kwa ufupi msingi wajambo analotaka kuzungumzia.

Page 42: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

21

Kanuni za Kudumu za Bunge

hawezi hawezi kushiriki katika uchaguzi wa Naibu Spika iwapohajaapa Kiapo cha Uaminifu.

(13) Jumla ya dakika zisizozidi thelathini zitatumika kwa mtoahoja kuwasilisha Bungeni hoja yake pamoja na majadiliano namaamuzi ya Bunge kwa hoja husika.

(14) Iwapo dakika thelathini zitapita tangu Spika alipotakakuliahirisha Bunge chini ya fasili ya (7) na (10) ya Kanuni hii, basiSpika atasitisha majadiliano yanayoendelea.

(15) Iwapo shughuli zote zilizopangwa kwa ajili ya kikaohazijamalizika, Spika atalihoji Bunge kuhusu hoja ya kuahirisha kikaocha Bunge na baada ya hoja hiyo kuafikiwa, atakiahirisha kikaohicho hadi kikao kinachofuata ambacho, kama Bunge halikuamuavinginevyo, kitakuwa ni siku itakayofuata, isipokuwa tu kamaitakuwa ni siku ya Jumamosi, Jumapili au siku ya mapumziko.

29.-(1) Kila Mkutano wa Bunge utafungwa kwa kuliahirisha Bungehadi Mkutano utakaofuata.

(2) Endapo shughuli zote zilizowekwa kwenye Orodha yaShughuli kwa ajili ya Mkutano huo zimemalizika, hoja ya kuahirishaBunge itakayotolewa na Kiongozi wa Shughuli za Serikali Bungeniitataja siku, mahali na saa ambapo Mkutano unaofuata utaanza.

(3) Mara tu baada ya Bunge kupitisha hoja ya kuahirishaMkutano wa Bunge, Wimbo wa Taifa utapigwa na kuimbwa kwamujibu wa utaratibu uliowekwa na Bunge.

SEHEMU YA NNE

SHUGHULI ZA BUNGE

30.-(1) Rais anaweza kulihutubia Bunge siku yoyote ambayo Bungelinakutana na wakati mwingine wowote kwa mujibu wa Ibara ya 91ya Katiba.

(2) Wakati wa kuanza Kikao cha Kwanza cha Mkutanowowote wa Bunge baada ya Wimbo wa Taifa kupigwa na kuimbwana Dua kusomwa au kwa vikao vinavyofuata, Dua pekee kusomwana Spika kukalia kiti chake:-

KuahirishaBunge

MpangiliowaShughulizaBunge

Page 43: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

22

Kanuni za Kudumu za Bunge

(a) kama Spika amepata taarifa kuwa Raisanakusudia kulihutubia Bunge siku hiyo, Spikaatalitangazia Bunge ni wakati gani Rais atafanyahivyo;

(b) wakati uliopangwa kwa ajili ya Rais kulihutubiaBunge utakapofika, Spika atampokea Rais nakumkaribisha alihutubie Bunge; na

(c) baada ya hotuba ya Rais, Spika anaweza amakusitisha kikao kwa muda ili amsindikize Rais aukuliahirisha Bunge hadi siku nyingine itakayotajwa.

(3) Baada ya kushauriana na Kamati ya Uongozi, Spikaatatenga muda kwa ajili ya kujadili hotuba ya Rais.

(4) Shughuli za Bunge zitaendeshwa kwa mpangilio ufuatao:-

(a) kuwaapisha Wabunge wapya Kiapocha Uaminifu;

(b) taarifa ya Rais;(c) taarifa ya Spika;(d) kuwasilisha Maombi;(e) hati za kuwasilisha Bungeni;(f) maswali kwa Waziri Mkuu;

(g) maswali ambayo taarifa zake zimetolewa;(h) hoja za kuahirisha shughuli ili kujadili mambo

muhimu ya dharura;(i) kauli za Mawaziri;(j) maelezo binafsi ya Mbunge;(k) mambo yahusuyo haki za Bunge, ikiwa ni pamoja

na kuzifanyia mabadiliko Kanuni za Bunge;(l) shughuli za Serikali;(m) hoja au taarifa za Kamati;(n) hoja binafsi za Wabunge; na(o) shughuli yoyote ambayo Bunge litaona

inafaa kushughulikiwa kwa wakati huo.

Page 44: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

23

Kanuni za Kudumu za Bunge

(5) Bila ya kuathiri masharti mengine ya Kanuni hii na baadaya kushauriana na Kamati ya Uongozi, katika kila Mkutano wa BungeSpika atatenga muda mahususi kwa ajili ya Bunge kushughulikiaHoja Binafsi na Miswada ya Kamati na Miswada Binafsi ya Wabungekama itakuwepo.

(6) Shughuli za Bunge katika kila kikao zitatekelezwa kwakufuata Orodha ya Shughuli za siku hiyo au kwa kufuata utaratibumwingine ambao Spika ataagiza ufuatwe kwa ajili ya uendeshajibora wa shughuli za Bunge.

31.- Dua ya kuiombea nchi yetu na kuliombea Bunge itasomwa naSpika, itakuwa na maneno yafuatayo:-

“Ewe MWENYEZI MUNGU Mtukufu, Muumba Mbingu na Dunia,Umeweka katika Dunia Serikali za Wanadamu na Mabunge yaMataifa ili haki yako itendeke. Twakuomba, uibariki nchi yetuidumishe uhuru, umoja, haki na amani, Umjalie Rais wetu hekima,afya njema na maisha marefu ili pamoja na wanaomshauri,wadumishe utawala bora. Utuongezee hekima na busara, sisiWabunge wa Bunge hili la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nautupe uwezo wa kujadili kwa dhati, mambo yatakayoletwa mbeleyetu leo, ili tufanye maamuzi sahihi yenye manufaa kwa watu wotena ustawi wa nchi yetu. Amina.”

32.-(1) Taarifa ya Rais, kama ipo, itasomwa na Spika.

(2) Kila inapowezekana, taarifa ya Rais itasomwa Bungeni kwakufuata mpangilio wa Shughuli za Bunge, lakini Spika anaweza,wakati wowote, kusitisha shughuli za Bunge kwa madhumuni yakuwezesha taarifa hiyo isomwe.

33.-(1) Spika atatoa taarifa Bungeni kuhusu Miswada yoteiliyopitishwa na Bunge katika Mkutano wake uliotangulia, yaanikama imekubaliwa na Rais au kama Rais ametoa uamuzi mwingine.

(2) Wakati wa kikao, Spika anaweza kutoa taarifa nyinginezokadri atakavyoona inafaa.

34.-(1) Mbunge yeyote anaweza kuwasilisha Bungeni maombikuhusu jambo lolote kwa niaba ya watu wanaotoa ombi hilo, naombi hilo halitawasilishwa Bungeni mpaka kwanza taarifa ya ombihilo iwe imetolewa kwa maandishi na kupokelewa na Katibu si chiniya siku mbili za kazi kabla ya Mkutano ambapo ombi hilolinakusudiwa kuwasilishwa.

TaarifayaRais

TaarifayaSpika

Dua yakuiombeanchi yetunakuliombeaBunge

Kuwasil i-shamaombina taarifaya ombi

Page 45: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

24

Kanuni za Kudumu za Bunge

(2) Ombi lolote linaweza kuwasilishwa Bungeni na Mbunge,likionesha jina la Mbunge anayeliwasilisha.

(3) Mbunge anayewasilisha ombi atatoa maelezo mafupi yakutambulisha watu wanaotoa ombi hilo, idadi yao, sainizilizoambatanishwa kwenye ombi hilo, madai ya msingi yaliyomo,na madhumuni ya ombi hilo.

(4) Baada ya kutimiza masharti ya fasili ya (3) ya Kanuni hii,Mbunge anayewasilisha ombi anaweza kutoa hoja kwamba, Bungelijadili ombi hilo, isipokuwa kwamba hoja hiyo haitahitaji kutolewataarifa na inaweza kuamuliwa bila mjadala wowote.

(5) Mbunge yeyote hataruhusiwa kuwasilisha ombi linalomhusuyeye mwenyewe au ambalo yeye amelitia saini yake au ambalolinakiuka masharti yanayohusiana na utaratibu wa kutunga Sheriakuhusu mambo ya fedha.

35.- Ombi lolote halitawasilishwa Bungeni isipokuwa tu kama Spikaataridhika kuwa limezingatia masharti yafuatayo:-

(a) limeandikwa katika lugha ya Kiswahili auKiingereza; na

(b) limeandikwa kwa lugha fasaha, ya heshima nalinahitimishwa kwa maelezo ya jumla kuhusumadhumuni ya ombi hilo.

36.- Nakala ya kila ombi itawasilishwa kwa Katibu si chini ya sikuzisizopungua mbili za kazi kabla ya siku ya kuwasilishwa Bungeni.

37.-(1) Hati inaweza kuwasilishwa Bungeni wakati wa vikao vyaBunge na:-

(a) Waziri; au (b) Mwanasheria Mkuu wa Serikali; au(c) Kamati yoyote ya Bunge; au(d) Mbunge yeyote.

(2) Nakala za matoleo yote ya Gazeti pamoja na Nyongezazake zilizochapishwa tangu kikao cha mwisho cha Mkutano waBunge uliopita, zitawasilishwa Bungeni na Waziri na kugawiwa kwaWabunge.

MashartikuhusuMaombi

NakalayaMaombi

Hatizakuwasili-shaBungeni

Page 46: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

25

Kanuni za Kudumu za Bunge

(3) Hati zote zitawasilishwa Bungeni bila kutolewa hojayoyote kwa ajili hiyo.

(4) Baada ya hati kuwasilishwa Bungeni, Waziri, MwanasheriaMkuu wa Serikali au Mbunge, anaweza kutoa hoja kwamba Bungelijadili hati hiyo.

(5) Hoja inayotolewa kwa mujibu wa Kanuni hii haitahitajikutolewa taarifa na itaamuliwa bila ya mabadiliko au mjadalawowote.

(6) Hoja ya kujadili hati iliyowasilishwa Bungeni ikikubaliwa,itashughulikiwa kwa kufuata Mpangilio wa Shughuli za Bunge.

(7) Taarifa zinazowasilishwa Bungeni na Kamati yoyote yaKudumu, Kamati Teule, Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu waHesabu za Serikali pamoja na Mapendekezo ya Matumizi yaNyongeza ya Fedha zitatengewa muda wa kujadiliwa Bungeni bilahoja kutolewa.

(8) Taarifa ambazo Sheria inaelekeza ziwasilishwe Bungenizitajadiliwa na Kamati husika za Kudumu za Bunge.(9) Mjadala unaweza kuzingatia kila jambo lililomo katika hati,isipokuwa kama Spika, kwa kuzingatia uendeshaji bora wa shughuliza Bunge, ataamua vinginevyo.

38.- (1) Waziri Mkuu anaweza kuulizwa maswali na Mbunge yeyoteambayo yatazingatia masharti kuhusu maswali ya Bunge pamojana Mwongozo uliowekwa na Nyongeza ya Sita ya Kanuni hizi.

(2) Maswali atakayoulizwa Waziri Mkuu hayatakuwa na taarifaya awali kama maswali mengine.

(3) Kipindi cha Maswali kwa Waziri Mkuu kitakuwa kila siku yaAlhamisi na hakitazidi dakika thelathini.

(4) Waziri Mkuu anaweza kutumia Kipindi cha Maswali kwaWaziri Mkuu kutoa taarifa au ufafanuzi kuhusu suala lolotelinalohusiana na shughuli za Serikali na lenye maslahi kwa ummakwa muda usiozidi dakika kumi, ikifuatiwa na maswali ya Wabungekwa dakika ishirini kuhusu taarifa yake au masuala mengine yoyoteya Serikali.

Maswal ikwaWaziriMkuu

Page 47: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

26

Kanuni za Kudumu za Bunge

(5) Iwapo siku hiyo, kwa sababu maalum, Waziri Mkuuhatakuwepo Bungeni hakutakuwa na maswali kwa Waziri Mkuu.

(6) Pamoja na kutawaliwa na masharti kuhusu maswali yaBunge yaliyowekwa na Kanuni hizi, maswali kwa Waziri Mkuuyatatawaliwa pia na Mwongozo uliowekwa na Nyongeza ya Sitaya Kanuni hizi.

(7) Maswali kwa Waziri Mkuu yatafuatiwa na maswali menginekwa Mawaziri kwa dakika sitini wakati wa Vikao vya Kawaida vyaBunge na kwa dakika thelathini wakati wa Mkutano wa Bunge laBajeti, kama yatakavyokuwa yamepangwa kwenye Orodha yaShughuli ya siku hiyo.

39.-(1) Waziri anaweza kuulizwa maswali kuhusu masuala yoyoteya umma au jambo lingine lolote ambalo linasimamiwa na Ofisiyake, na vilevile Mbunge yeyote anaweza kuulizwa maswali kuhusumambo yoyote anayohusika nayo kutokana na kuteuliwa na Bungekushughulikia mambo hayo.

(2) Maswali yanayoulizwa kwa mujibu wa Kanuni hii yatakuwamafupi kwa kadri inavyowezekana na kila swali litahusu jambo mojatu mahususi.

(3) Madhumuni halali ya swali lolote yatakuwa kutekelezaIbara ya 63(2) na (3)(a) ya Katiba.

(4) Taarifa ya swali itatolewa kwa maandishi na itapelekwana kumfikia Katibu si chini ya siku ishirini na moja kabla ya tareheambayo jibu linahitajiwa kutolewa.

(5) Taarifa haitatolewa Bungeni kwa mdomo, isipokuwakwamba, taarifa zote za maswali zitaingizwa kwenye Kitabu chaShughuli za Bunge kuonesha kuwa zimepokelewa na maswali yoteyaliyopangwa kujibiwa yatawekwa kwenye Orodha ya Shughuli zasiku inayohusika.

(6) Waziri aliyeulizwa swali atatoa jibu lake papohapo wakatiwa kipindi cha Maswali.

(7) Endapo swali halikuwahi kujibiwa siku hiyo kwa sababu yamuda wa maswali kumalizika, litapangiwa nafasi ya kujibiwabaadaye katika Mkutano huo unaoendelea. Kama siku inayohusika

Maswalinat a a r i f ayaMaswali

Page 48: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

27

Kanuni za Kudumu za Bunge

ndiyo siku ambapo Mkutano wa Bunge unafungwa, swali hilolitajibiwa katika Mkutano unaofuata.

(8) Bunge linapovunjwa, maswali yote ambayo hayakuwahikujibiwa yatajibiwa kwa maandishi.

(9) Kwa madhumuni ya fasili ya (1), endapo swali lililoulizwalimeelekezwa kwa Mbunge, basi kwa idhini ya Spika, Mbungeambaye swali limeelekezwa kwake atapewa fursa ya kujibu swalihilo.

(10) Maswali yatajibiwa Bungeni kwa mdomo. Lakini endapoMbunge mwenye swali hayupo Bungeni kuuliza swali lake, na Spikahakutoa ruhusa kwa swali hilo kuulizwa na Mbunge mwingine, basiWaziri aliyeulizwa swali atapeleka kwa Katibu jibu la maandishinaye Katibu ataliingiza jibu hilo kwenye Taarifa Rasmi.

(11) Katika hali ya kawaida, Mbunge haruhusiwi kuuliza zaidiya maswali manne yanayohitaji majibu ya mdomo katika Mkutanommoja wa Bunge.

(12) Endapo kwa maoni ya Spika, swali lililoulizwa na Mbungesiyo la sera na majibu yake ni marefu au linahitaji takwimu, basiswali hilo litajibiwa kwa maandishi na litaorodheshwa kwenyeOrodha ya Shughuli na kuonyesha kwamba limejibiwa kwamaandishi na Wabunge wote watagawiwa nakala.

(13) Bila ya kuathiri masharti ya fasili ya (11) ya Kanuni hii, swalialiloulizwa Waziri mmoja laweza kujibiwa na Waziri mwingine auMwanasheria Mkuu wa Serikali.

(14) Maswali yote katika Mkutano mmoja yatapewa nambazinazofuatana kwa mfululizo na namba zilizotolewa kwa kila swalizitaingizwa kwenye Kitabu cha Shughuli za Bunge.

(15) Maswali yote ambayo yamepangwa kujibiwa katika Kikaokimoja, yanaweza kuwekwa pamoja kwenye Orodha ya Shughulina kujibiwa kwa zamu kadri itakavyooneshwa kwenye Orodha yaShughuli.

Page 49: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

28

Kanuni za Kudumu za Bunge

40.- Swali lolote la Bunge halitaruhusiwa kuulizwa Bungeni kama:-

(a) linakiuka Kanuni yoyote ya Bunge;

(b) linashutumu tabia au mwenendo wa mtuyeyote ambaye mwenendo wake unaweza tukujadiliwa kwa hoja maalumu;

(c) linahitaji habari ambazo zinapatikana katika hatiambazo Mbunge anaweza kujisomeamwenyewe kama vile nakala za Sheria aumaandiko ya kumbukumbu za kawaida.

(d) limekusudiwa kupata maoni ya kisheria yakinadharia au kutoa mapendekezo juu ya jambola kubahatisha tu;

(e) lina maelezo ya dhihaka, uongo, sifazisizolazimu, au linatokana na habari zakubahatisha tu;

(f) lina madhumuni ya kutoa habari, au linaulizwakwa njia inayoonesha jibu lake au kutambulishamkondo fulani wa maoni;

(g) linahusu jambo zaidi ya moja na ni refu kupitakiasi; au

(h) linamtaja mtu yeyote kwa jina au kutoa maelezomahususi juu yake ila tu kama ni lazima ilikulifanya lieleweke.

41.- Mbunge anayeuliza swali anaweza kuliondoa swali lake wakatiwowote kabla halijajibiwa-

(a) kwa kuwasilisha barua ya kufanya hivyo kwaKatibu iwapo siku iliyopangwa kwa swali hilokujibiwa haijafika; au

(b) iwapo swali husika tayari limewekwa kwenyeOrodha ya Shughuli, kwa kusimama mahali pakejina lake linapoitwa wakati wa maswali nakutamka kuwa analiondoa swali lake nakueleza kwa kifupi sababu za kufanya hivyo.

Kuondoa Maswali

Masharti kuhusu Maswal iyaBunge

Page 50: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

29

Kanuni za Kudumu za Bunge

42.-(1) Wakati swali linalohusika litakapofikiwa katika Orodha yaShughuli, Spika atamwita Mbunge mwenye swali hilo au kamahayupo, Spika atamwita Mbunge mwingine yeyote aulize swali hilokwa niaba ya Mbunge mwenye swali.

(2) Mbunge atakayeitwa atasimama na kuuliza swali, pamojana masahihisho (kama yapo), kwa kutamka maneno yafuatayo bilaya kuongeza jambo lingine lolote:-

“Naomba swali langu (atataja namba ya swali lake lililopokwenye Orodha ya Shughuli) sasa lijibiwe.”

43.-(1) Muda wa Maswali Bungeni utakuwa dakika tisini, isipokuwakatika Mkutano wa Bunge la Bajeti, ambapo muda utakuwa dakikasitini.

(2) Spika anaweza kuweka kiwango cha juu cha maswaliyatakayowekwa katika Orodha ya Shughuli ambayo anaonayanaweza kujibiwa katika muda uliowekwa.

44.-(1) Maswali ya nyongeza yanaweza kuulizwa na Mbunge yeyotekwa madhumuni ya kupata ufafanuzi zaidi juu ya jambo lolotelililotajwa katika jibu lililotolewa.

(2) Mbunge anayeuliza swali la msingi ataruhusiwa kuulizamaswali ya nyongeza yasiyozidi mawili na Mbunge mwingine yeyoteatakayepewa nafasi ataruhusiwa kuuliza swali moja tu la nyongeza.

(3) Kwa madhumuni ya Kanuni hii, swali ambalo litawekwakatika vifungu vya (a) na (b) litahesabiwa kuwa ni maswali mawili.

(4) Isipokuwa kama Spika ataelekeza vinginevyo, Wabungewatakaouliza maswali ya nyongeza hawatazidi watatu kwa swalimoja la msingi, na Mbunge hataruhusiwa kusoma swali lake.

45.-(1) Swali lolote la nyongeza ambalo linaleta mamboyasiyotokana au kuhusiana na swali la msingi au linakiuka mashartiyanayohusiana na taratibu za kuulizwa maswali litakataliwa.

(2) Endapo Spika atakataa swali la nyongeza kwa kukiukamasharti ya Kanuni hizi, swali hilo halitajibiwa wala halitaoneshwakwenye Taarifa Rasmi.

JinsiyaKuulizaMaswal i

Maswaliyanyongezayasiyo-ruhusiwa

MaswaliyaNyongeza

MudawaMaswal i

Page 51: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

30

Kanuni za Kudumu za Bunge

(3) Iwapo Spika ataridhika kuwa, swali la msingi aul nyongezahalijapata majibu ya kuridhisha, ataaiza lijibiwe kwa ufasaha zaidikatika kikao kingine cha Bunge.

46.-(1) Waziri anayeulizwa swali atakuwa na wajibu wa kulijibuswali hilo kwa ukamilifu kama lilivyoulizwa , isipokuwa kwamba,kama jibu linalohusika ni refu au lina takwimu nyingi, Waziri atampaMbunge muuliza swali nakala ya jibu mapema baada ya kikaokuanza, kabla ya muda wa kmujibu swali hilo haujafikiwa.

(2) Endapo Mbunge muuliza swali atamwomba Waziri ampatienakala ya jibu la swali lake kabla ya muda wa kujibu swali hilihaujafikiwa basi Waziri anaweza kumpa Mbunge muuliza swalinakala ya jibu kama lilivyoombwa.

(3) Waziri Mkuu au Waziri mwingine yeyote au MwanasheriaMkuu wa Serikali anaweza kutoa majibu ya nyongeza kwa majibuyaliyotolewa na Waziri.

47.-(1) Baada ya Muda wa Maswali kwisha, Mbunge yeyote anawezakutoa hoja kuwa Shughuli za Bunge kama zilivyooneshwa kwenyeOrodha ya Shughuli ziahirishwe ili Bunge lijadili jambo halisi ladharura na muhimu kwa umma.

(2) Hoja ya namna hiyo itakuwa ni maalumu na inawezakutolewa wakati wowote hata kama majadiliano yatakuwayanaendelea.

(3) Hoja itatolewa na Mbunge kwa kusimama mahali pakena kuomba idhini ya Spika kutoa hoja ya kuahirisha Shughuli zaBunge kwa madhumuni ya kujadili jambo halisi la dharura na muhimukwa umma.

(4) Iwapo Spika ataridhika kwamba jambo hilo ni la dharura,halisi na lina maslahi kwa umma, basi ataruhusu hoja hiyo itolewekwa muda usiozidi dakika tano na mjadala juu ya hoja hiyoutaendelea kwa muda ambao Spika ataona unafaa kwa kuzingatiamazingira ya suala linalojadiliwa.

48.-(1) Masharti ya jumla yafuatayo yatatumika vilevile kuhusuhoja ya kujadili suala la dharura:-

(a) hoja hiyo haitaruhusiwa iwapo inahusu jamboambalo kwalo taarifa ya hoja imekwisha

KuahirishaShughuliza BungeiliKujadiliJambo laDharura

M a s w a l ikujibiwaKikamilifu

MashartiyajumlakuhusuJambolaDharura

Page 52: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

31

Kanuni za Kudumu za Bunge

kutolewa au jambo ambalo limekwisha kuwekwakwenye Orodha ya Shughuli;

(c) jambo ambalo litakuw alimejadiliwa katika hojaya kuahirisha Shughuli za Bunge iliyotolewa kwamujibu wa Kanuni hii, halitletwa tena Bungeni katika Mkutnao ule ule kwa kutumia Kanuni hii.

(2) Jambo linaloletwa kwa hoja chini ya Kanuni hiilitahesabiwa tu kuwa ni jambo halisi, iwapo:-

(a) ni jambo mahususi;

(b) halikuwekwa katika lugha ya jumla mno au linamambo mengine mchanganyiko;

(c) halikutolewa kwa kutegemea habari zisizo za uhakika au habari halisi juu ya jamo hilo hazipatikani; au

(d) halihusu mambo ya kinadharia.

(3) Jambo linaloletwa kwa hoja chini ya Kanuni hiilitahesabiwa kuwa ni jambo la dharura, iwapo:-

(a) athari zake ni dhahiri na linaweza kutokea wakati wowote;

(b) limetokea siku hiyo au siku za karibuni na limetwa bila kuchelewa; au

(c) hakutatokea fursa ya kulijadili siku za karibuni kwa njia ya kawaida ya kushghulikia mambo ya Bunge.

(4) Jambo lolote litahesabiswa kuwa ni lenye maslahikwa umma iwapo utatuzi wake unategemea hatua zaidi kuliko zileza utekelezaji wa kawaida wa sheria peke yake.

Page 53: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

32

Kanuni za Kudumu za Bunge

49.-(1) Waziri anaweza kutoa kauli Bungeni kuhusu jambo lolotelinaloihusu Serikali.

(2) Kauli za aina hiyo zinaweza kutolewa kwa idhini ya Spikakatika wakati unaofaa kufuatana na mpangilio wa Shughuli zaBunge na zitahusu jambo mahususi, halisi na zisizozua mjadala namuda wa kusema utakuwa ni dakika zisizozidi thelathini.

(3) Waziri mwenye kutoa kauli atawajibika kutoa nakala yakauli yake kwa Wabunge wote wakati anapoiwasilisha Bungeni.

50.-(1) Mbunge yeyote anaweza, kwa idhini ya Spika kutoa maelezobinafsi Bungeni yanayolenga kufafanua kuhusu jambo lolotelinalomhusu na lililoifikia jamii.

MaelezoBinafsiyaWabunge

KaulizaMawaziri

(2) Mbunge anayekusudia kutoa maelezo binafsi atapaswakuwasilisha maelezo hayo mapema kwa Spika na muda wa kusemautakuwa ni dakika zisizozidi kumi na tano, na maelezo hayohayatakuwa na mjadala kuhusu jambo hilo.

51.-(1) Mbunge anayetaka kuwasilisha jambo ambalo anaaminilinahusiana na haki za Bunge atafanya hivyo wakati unaofaakufuatana na mpangilio wa Shughuli za Bunge uliowekwa na Kanunihizi na atakuwa amemwarifu Spika mapema kuhusu kusudio lakehilo na jambo ambalo anataka kuliwasilisha.

(2) Spika akimwita Mbunge anayetaka kuwasilisha jamboambalo anaamini linahusiana na haki za Bunge, Mbunge huyoataeleza kwa kifupi sababu zinazofanya aamini kwamba jamboanaloliwasilisha linahusu haki za Bunge zilizotajwa kwenye Sheriaya Kinga, Madaraka na Haki za Bunge.

(3) Endapo Spika ataamua kwamba jambo hilo linahusu haki zaBunge, basi atampa nafasi Mbunge mhusika kutoa hoja yake kishahoja hiyo itapewa kipaumbele katika kupanga shughuli nyinginezote za kikao kinachohusika.

(4) Mambo yanayohusu haki za Bunge yatawasilishwa kwakufuata utaratibu uliowekwa katika Kanuni hizi na endapo wakatiwa kikao chochote cha Bunge jambo lolote litazuka ghafla ambalolitaonekana linahusu haki za Bunge, shughuli zitasitishwa kwamadhumuni ya kuliwezesha jambo hili kuwasilishwa na kuamuliwa,isipokuwa tu kama wakati huo kura inapigwa.

Masualayanayo-husuHaki zaBunge

Sura ya296,Toleola 2002

Page 54: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

33

Kanuni za Kudumu za Bunge

52.-(1) Shughuli za Serikali zitaanza wakati Spika atakapomwitaWaziri au Mwanasheria Mkuu wa Serikali aliyetoa taarifa yakuwasilisha Muswada au ya kutoa hoja Bungeni baada ya Katibukusoma jambo linalohusika kwenye Orodha ya Shughuli.

(2) Baada ya Spika kutoa wito huo, Mbunge yeyote binafsihataruhusiwa kutoa hoja ya kuahirisha Shughuli za Bunge walakuuliza swali.

53.-(1) Isipokuwa kama Kanuni hizi zimeagiza vinginevyo, hakunamjadala wowote utakaoendeshwa Bungeni ila tu kuhusu shughuliiliyoingizwa kwenye Kitabu cha Orodha ya Shughuli za Bunge nakuwekwa kwenye Orodha ya Shughuli za kikao hicho.

(2) Bila ya kuathiri masharti ya Katiba na ya Kanuni hizi, Waziriau Mbunge mwingine anaweza, kwa kutoa hoja, kupendekezakwamba, suala lolote lijadiliwe Bungeni na hoja hiyo itaamuliwakwa mujibu wa masharti ya Kanuni hizi.

(3) Isipokuwa kama Spika ataamua vinginevyo, kila hojaambayo taarifa yake imekubaliwa itapelekwa kwanza kwenyeKamati inayohusika.

(4) Endapo hoja itapelekwa kwenye Kamati inayohusika,Kamati hiyo itaanza kuifanyia kazi hoja hiyo mapema iwezekanavyo,na haitatolewa Bungeni mpaka Mwenyekiti wa Kamati hiyoatakapokuwa amemtaarifu Spika kwamba, Kamati imemalizakuifanyia kazi hoja hiyo.

(5) Kamati iliyopelekewa hoja kwa mujibu wa Kanuni hiiinaweza kufanya mabadiliko katika hoja hiyo kwa kushauriana namtoa hoja husika.

(6) Endapo hoja haikupelekwa kwenye Kamati na imewekwakwenye Orodha ya Shughuli au kama ilipelekwa kwenye Kamati naKamati hiyo imemaliza kuishughulikia na imewekwa kwenye Orodhaya Shughuli, hoja itawasilishwa na kuamuliwa Bungeni kwa kufuatamasharti yafuatayo:-

Shughuli zaSerikali

Hojazitakazo-tolewaBungeni

Page 55: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

34

Kanuni za Kudumu za Bunge

(a) baada ya hoja kutolewa na inapobidi kuungwamkono Spika ataomba hoja hiyo ijadiliwe;

(b) mara baada ya mtoa hoja kuwasilisha hojayake, Mwenyekiti wa Kamati iliyopelekewa hojahiyo atatoa maoni ya Kamati; na

(c) kama hoja inayohusika ni hoja ya Serikali,msemaji wa Kambi ya Upinzani atapewa nafasiya kutoa maoni juu ya hoja hiyo na kama hojainayohusika siyo ya Serikali, msemaji wa Serikaliatapewa nafasi ya kutoa maoni ya Shughuli zaSerikali juu ya hoja hiyo. Isipokuwa masharti yafasili hii hayatahusu hoja za Kamati.

(7) Baada ya mjadala kumalizika, Spika atawahoji Wabungeili kupata uamuzi wa Bunge.

(8) Mbunge yeyote hataruhusiwa kufufua jambo lolote ambaloBunge lilikwisha kuliamua ama katika Mkutano huo uliopo au uleuliotangulia, wala kuwahisha shughuli ya Mkutano huounaoendelea, isipokuwa kwa kufuata masharti ya Kanuni hizi aukuwahisha shughuli ambayo itazingatiwa katika Mkutanounaoendelea.

54.-(1) Bila ya kuathiri masharti ya Katiba au ya Kanuni hizi, Mbungeyeyote anaweza kupendekeza jambo lolote lijadiliwe Bungeni kwakuwasilisha hoja, yaani kwa kutoa pendekezo lililokamilika ili lipateuamuzi wa Bunge.

(2) Jambo lolote litakalowasilishwa kwa mujibu wa Kanuni hiilitawekwa katika lugha ambayo italiwezesha Bunge kufanyauamuzi ambao ni bayana.

(3) Isipokuwa kama itaelekezwa vinginevyo katika Kanuni hizi,mfumo wa maneno ya hoja inayowasilishwa Bungeni utakuwa kamaifuatavyo:- “KWA KUWA, ..................................................

NA KWA KUWA, ............................................ KWA HIYO BASI, Bunge linaazimia kwamba ...”

JinsiyaKuwasi-lishaHoja

Page 56: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

35

Kanuni za Kudumu za Bunge

(4) Hoja ambayo, kwa maoni ya Spika ina lengo la kutakajambo ambalo lilikwisha amuliwa na Bunge katika kipindi cha miezikumi na miwili iliyopita kabla ya kikao kinachoendelea lifikiriwetena, haitakubaliwa na Spika, isipokuwa tu kama ni hoja ya kutakauamuzi wa Bunge uliokwisha fanyika ubadilishwe.

(5) Taarifa yoyote ya hoja ambayo inakiuka masharti yaKatiba au ya Kanuni hizi haitakubaliwa.

55.-(1) Isipokuwa kama Kanuni hizi zitaruhusu vinginevyo au kamaSpika atatoa idhini yake kwa kutilia maanani udharura wa jambolenyewe, hoja yoyote haitatolewa Bungeni mpaka taarifa ya hojahiyo iwe imewasilishwa na kupokelewa na Katibu angalau siku mojaya kazi kabla ya Mkutano ambapo hoja hiyo inakusudiwa kutolewa.

(2) Taarifa ya hoja yoyote itatolewa kwa maandishi naitawekwa saini na Mbunge anayeitoa kabla ya kupokelewa naKatibu kufuatana na masharti ya Kanuni hizi.

(3) Hoja zifuatazo zinaweza kutolewa bila taarifa:-

(a) kutengua Kanuni yoyote kati ya Kanuni hizi;

(b) kuahirisha Bunge au kuahirisha mjadala;

(c) kutaka wageni waondoke Bungeni;

(d) kutaka ombi lililowasilishwa Bungeni lijadiliwe;

(e) kuahirisha Shughuli za Bunge zinazoendelea ilikujadili jambo la dharura;

(f) kuhusu jambo lolote linalohusiana na haki zaBunge; na

(g) kutaka Hati iliyowasilishwa Bungeni ijadiliwe.

(4) Bila ya kujali masharti ya fasili ya (2) ya Kanuni hii, iwapoanayetoa taarifa ni Waziri au Mwanasheria Mkuu wa Serikali, taarifahiyo itawekwa saini na Waziri anayehusika au Mwanasheria Mkuuwa Serikali, lakini hoja hiyo inaweza kuwasilishwa na Waziri mwingineyeyote au Naibu Waziri au Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

TaarifayaHoja

Page 57: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

36

Kanuni za Kudumu za Bunge

UtaratibuwakujadiliHoja

(5) Endapo hoja ambayo kwayo taarifa iliyotolewahaitajadiliwa katika Mkutano alioutaja mtoa hoja, basi taarifaya hoja hiyo itatenguka lakini inaweza kutolewa tena katikaMkutano mwingine.

(6) Isipokuwa tu kwa idhini maalumu ya Spika, taarifakuhusu jambo lolote linalohitaji taarifa itolewe kwa mujibu waKanuni hizi, lazima taarifa hiyo itolewe.

(7) Hoja zitaingizwa kwenye Kitabu cha Shughuli mapemabaada ya kupokelewa na Katibu, na zitawekwa kwenye Orodha yaShughuli ya kikao cha Bunge kulingana na maelekezo ya Spika.

(8) Kila hoja itawekwa kwenye Orodha ya Shughuli ikiwakama ilivyowasilishwa au kama ilivyofanyiwa marekebisho aumabadiliko ambayo Spika ataagiza yafanyike.

(9) Spika hataruhusu hoja yoyote inayokiuka Katiba au Sheriaau Kanuni za Bunge na Katibu atairudisha hoja hiyo pamoja navielelezo vyake vyote kwa Mbunge mhusika na maelezo ya sababuza kukataliwa kwa hoja hiyo.

(10) Iwapo Mbunge anapenda kufanya mabadiliko ya manenoaliyoyatumia katika hoja anayokusudia kuitoa, anaweza kufanyahivyo kwa kutoa taarifa ya kutaka kufanya mabadiliko angalausiku moja kabla ya siku ile ambapo hoja hiyo imewekwa kwenyeOrodha ya Shughuli ili ijadiliwe.

(11) Mbunge ambaye hakutoa taarifa ya kutaka kufanyamarekebisho au mabadiliko katika hoja yake, anaweza kumwombaSpika afanye marekebisho au mabadiliko katika hoja hiyo wakatianawasilisha hoja yake bila ya kutoa taarifa.

(12) Pamoja na kuwa taarifa ya kutaka kufanya marekebishoau mabadiliko itakuwa imetolewa, marekebisho au mabadilikoyoyote hayatakubaliwa kama, kwa maoni ya Spika, mabadiliko hayoyanabadilisha mambo ya msingi yaliyomo katika hoja auyanabadilisha makusudio au upeo wa hoja hiyo.

56.-(1) Mbunge atakapoitwa na Spika kutoa hoja, atasimamamahali pake na kutoa hoja yake.

(2) Hoja au marekebisho au mabadiliko ya hoja yoyote,yatahitaji kuungwa mkono na Wabunge wasiopungua kumi na

Page 58: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

37

Kanuni za Kudumu za Bunge

endapo hayataungwa mkono hoja au marekebisho au mabadilikohayo yatatenguka na Katibu ataweka kumbukumbu kwenye TaarifaRasmi kwamba, kwa kuwa hoja au marekebisho au mabadiliko hayohayakuungwa mkono, basi hayakujadiliwa.

(3) Mbunge anaweza kuunga mkono hoja kwa kusimama tumahali pake bila kusema lolote kuhusu hoja hiyo, kisha akakaa;lakini Mbunge aliyefanya hivyo bado atakuwa na haki yakuizungumzia hoja hiyo hapo baadaye.

(4) Iwapo hoja imewekwa katika Orodha ya Shughuli naMbunge mtoa hoja anapoitwa na Spika anashindwa kuitoa, hojahiyo itatenguka, isipokuwa kama kuna Mbunge mwinginealiyeidhinishwa na mtoa hoja, anaweza kuitoa kwa niaba yake aukama mtoa hoja ametoa taarifa ya kutaka kuiahirisha, hoja hiyoitaahirishwa.

(5) Hoja inayohusu shughuli za Serikali inaweza kutolewa naWaziri au Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

(6) Hoja iliyotenguka yaweza kutolewa tena baadaye, baadaya taarifa mpya kutolewa kwa mujibu wa Kanuni hizi.

(7) Endapo hakuna Mbunge zaidi anayependa kuzungumziahoja iliyotolewa, Spika atampa mtoa hoja nafasi ya kuhitimishahoja yake.

(8) Ikiwa muda uliotengwa umekwisha wakati Bunge likokwenye Kamati ya Bunge Zima kujadili vifungu vya Muswada waSheria au katika Kamati ya Matumizi kujadili Makadirio ya Matumiziya Serikali, basi Mwenyekiti, bila kulihoji Bunge, ataongeza mudausiozidi dakika thelathini kwa ajili ya kukamilisha kazi ya kupitishaIbara za Muswada wa Sheria au mafungu ya fedha yaliyobaki.

57.-(1) Hoja ikishatolewa ili iamuliwe inaweza kubadilishwa kwa:-(a) kuondoa maneno fulani kwa ajili ya kuingiza

maneno mengine;

(b) kuondoa maneno fulani bila kuongeza mengine;au

(c) kuingiza au kuongeza maneno mapya.

Kubadili-shaHoja

Page 59: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

38

Kanuni za Kudumu za Bunge

Mabadi-likoyaHojanaKuondoaHoja

(2) Kabla ya kutoa hoja hiyo, mtoa hoja atamkabidhiKatibu maandishi yenye saini yake na yanayoonesha mabadilikoanayotaka yafanywe.

(3) Kila badiliko linalopendekezwa sharti liwiane na hojainayokusudiwa kufanyiwa mabadiliko na pia liungwe mkono nalisiingize jambo lolote ambalo, kwa maoni ya Spika, linawezakuwasilishwa kwa hoja maalumu.

(4) Badiliko lolote halitaruhusiwa kama, kwa maoni ya Spika,linapingana moja kwa moja na hoja ya msingi iliyotolewa.

(5) Iwapo hoja ya mabadiliko inapendekeza kuondoamaneno fulani na kuingiza maneno mengine, basi mjadala juu yasuala la kufanya mabadiliko unaweza kuangalia kwa pamoja yalemaneno yanayopendekezwa yaondolewe na maneno ambayoyanapendekezwa yaingizwe.

(6) Iwapo hoja inapendekeza kuondoa au kuingiza maneno,mjadala utahusu tu uondoaji au uingizaji wa maneno mapya, kadriitakavyokuwa.

(7) Hoja ya kufanya mabadiliko katika hoja nyingine yamabadiliko sharti ihusiane na hoja ya kwanza ya mabadiliko naitatolewa, itajadiliwa na kuamuliwa kabla ya ile hoja ya kwanza yamabadiliko kufanyiwa uamuzi.

58.-(1) Endapo Mbunge anapenda kupendekeza mabadilikoyafanywe katika hoja kwa kufuata masharti ya Kanuni hizi, anawezakutoa hoja yake ya kufanya mabadiliko wakati wowote baada yahoja anayotaka kuibadilisha kutolewa, lakini kabla Bungehalijahojiwa liifanyie uamuzi.

(2) Endapo kuna mapendekezo mawili au zaidi ya kubadilishahoja moja, Spika atawaita watoa hoja hizo kwa kufuata mpangilioatakaoamua.

(3) Iwapo mapendekezo yote ya mabadiliko yameamuliwa,Spika ataitoa tena hoja ya awali ili ijadiliwe kama itakavyokuwaimebadilishwa.

(4) Hoja yoyote inaweza kuondolewa wakati wowote kablahoja hiyo haijafikishwa Bungeni iwapo Mbunge mtoa hoja atatoakwa Katibu, taarifa ya maandishi ya kuiondoa hoja hiyo.

Page 60: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

39

Kanuni za Kudumu za Bunge

(5) Endapo hoja imefikishwa Bungeni, mtoa hoja anaweza tukuiondoa hoja yake kwa kusimama mahali pake na kusema “Ninaomba ruhusa kuondoa hoja” na papo hapo Spika ataliulizaBunge kama linaafiki hoja hiyo kuondolewa na inapotokeaWabunge walio wengi watakubali, Spika atasema “Hojainaondolewa kwa idhini ya Bunge” na hoja hiyo itakuwaimeondolewa na Bunge litaendelea na shughuli inayofuata.

SEHEMU YA TANO

KANUNI ZA MAJADILIANO

59.- Kwa idhini ya Spika, Mbunge yeyote anaweza kusimama nakuchangia Bungeni katika nyakati zifuatazo:-

(a) wakati wa kuchangia mjadala wa hoja yoyoteiliyowasilishwa Bungeni ambayo Kanunizinaruhusu ijadiliwe;

(b) wakati anatoa hoja ili ijadiliwe;

(c) wakati anawasilisha mabadiliko yoyote ya hoja;

(d) wakati amesimama kutaka kuzungumzia jambololote linalohusu utaratibu;

(e) wakati amesimama kuzungumzia jambo linalohusuhaki za Bunge;

(f) wakati wa kutoa hoja ya kuahirisha shughuli zaBunge kwa madhumuni ya kujadili jambo ladharura na muhimu kwa Umma;

(g) wakati wa kutoa Maelezo Binafsi;

(h) wakati wa kuuliza au kujibu swali;

(i) wakati wa kutoa taarifa baada ya kupewa idhiniya Spika kufanya hivyo.

60.-(1) Mbunge akitaka kusema anaweza:-

(a) kumpelekea Spika ombi la maandishi;(b) kusimama kimya mahali pake; au(c) kutumbukiza kadi ya elektroniki.

NyakatizaMbungekusemaBungeni

JinsiyakupatanafasiyakusemaBungeni

Page 61: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

40

Kanuni za Kudumu za Bunge

(2) Isipokuwa kwamba, Mbunge yeyote hataanzakuzungumza hadi aitwe na Spika ama kwa jina au wadhifa wake nakumruhusu kusema na wakati wa kusema ataelekeza maneno yakekwa Spika.

(3) Mbunge akimaliza kutoa maelezo yake atakaa kwenyenafasi yake na hapo Spika atamwita Mbunge mwinginealiyempelekea ombi la maandishi au kama Spika hakupata ombilolote la maandishi, basi Mbunge mwingine yeyote anayetakakujadili hoja anaweza kusimama mahali pake na kusubiri Spikaamwone.

(4) Iwapo Wabunge wawili au zaidi watasimama wakatimmoja, Spika atamwita Mbunge atakayemwona kwanza.

(5) Endapo maombi ya kuchangia hoja fulani yatakuwamengi zaidi ya muda uliotengwa kwa hoja hiyo, Spika atatoa nafasiya kwanza kwa Wabunge ambao:-

(a) hawajachangia katika hoja zilizotanguliakujadiliwa katika Mkutano unaoendelea; au

(b) wamechangia mara chache.

(6) Bila ya kuathiri masharti ya fasili ya (5) ya Kanuni hii, Spikaatahakikisha kuwa, nafasi za kuchangia zinatolewa kwa uwianounaofaa baina ya aina zote za Wabunge walioomba kuchangiahoja hiyo.

(7) Masharti yaliyotangulia katika Kanuni hii, hayatamzuiaSpika kutoa nafasi ya kuchangia kwa Mbunge mwingine yeyoteiwapo ataona kuwa, taaluma au uzoefu fulani wa Mbunge huyoutaboresha hoja inayojadiliwa.

(8) Mbunge hatasoma maelezo, isipokuwa, kwa madhumuniya kutilia nguvu maelezo yake, anaweza kusoma dondoo kutokakwenye kumbukumbu zilizoandikwa au kuchapishwa na anawezapia kujikumbusha kwa kuangalia kwenye kumbukumbu alizoziandika.

(9) Kila Mbunge atalisemea jambo ambalo liko katika mjadalatu na hatarudiarudia maneno yake au yale yaliyokwisha kusemwana Wabunge wengine na iwapo itatolewa hoja ya kufanyamabadiliko katika hoja inayojadiliwa, mjadala sharti uwe juu yahoja hiyo ya mabadiliko mpaka imalizike ndipo mjadala urudiekwenye hoja ya msingi.

Page 62: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

41

Kanuni za Kudumu za Bunge

(10) Kila Mbunge atasema akiwa amesimama na atatoamaelezo yake kwa kutumia vyombo vilivyowekwa kwa madhumuniya kutafsiri, kukuza na kurekodi sauti.

(11) Kwa ruhusa ya Spika, Mbunge yeyote aliye na ulemavuau ugonjwa anaweza kuzungumza akiwa ameketi.

(12) Endapo Spika atasimama wakati Waziri au Mbungeanatoa hotuba Bungeni au atakuwa amesimama mahali pakeakisubiri kuanza kuzungumza, Waziri au Mbunge huyo ataketi mahalipake na Bunge litabaki kimya ili Spika aweze kutoa maelekezo autaarifa yake.

(13) Mbunge hataruhusiwa kuzungumzia suala lililokuwalikijadiliwa baada ya Spika kuwahoji Wabunge na hoja hiyokutolewa maamuzi.

(14) Mbunge yeyote anaweza pia kutoa maoni yake kwamaandishi na kumpelekea Waziri au Mbunge mtoa hojainayohusika, wakati ambapo hoja inaendelea kujadiliwa.

(15) Mtoa hoja atayakabidhi maoni hayo kwa Katibu iliyaweze kuingizwa katika Taarifa Rasmi za Bunge.

(16) Katika mjadala wowote, Mawaziri watatajwa kwamajina ya nyadhifa zao na Wabunge watatajwa kwa kutumia neno“Mheshimiwa” kabla ya majina yao.

61.-(1) Wakati wa majadiliano Bungeni au kwenye Kamati yoyoteya Bunge, Mbunge hataruhusiwa kuzungumzia jambo lolote ambaloyeye mwenyewe ana maslahi binafsi nalo ya kifedha, isipokuwabaada ya kusema jinsi anavyohusika nalo na kutaja kiwango chamaslahi hayo, na kwa sababu hiyo, itakuwa ni lazima kwa Mbungeyeyote anayetaka kuzungumzia jambo hilo Bungeni au kwenyeKamati yoyote ya Bunge, kusema kwanza jinsi anavyohusika najambo hilo na kutaja kiwango cha maslahi ya kifedha aliyonayokuhusiana na jambo hilo kabla ya kuanza kulizungumzia.

(2) Kwa madhumuni ya Kanuni hii, Mbunge au mwananchiyeyote anaweza kumwarifu Spika, kwa maandishi, akitoa naushahidi kuwa, Mbunge amezungumzia jambo ambalo ana maslahi

Kuto-zungumziajamboambalolinamaslahibinafsiyakifedha

Page 63: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

42

Kanuni za Kudumu za Bunge

MudawakusemaBungeni

binafsi nalo ya kifedha bila kusema jinsi anavyohusika nalo walakutaja kiwango cha maslahi hayo.

(3) Baada ya kupokea taarifa iliyowasilishwa kwake kwamujibu wa fasili ya (2) ya Kanuni hii, Spika ataipeleka taarifa hiyokwenye Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge.

(4) Baada ya kupokea taarifa iliyopelekewa na Spika chiniya fasili ya (3) ya Kanuni hii, Kamati ya Haki, Maadili na Madarakaya Bunge itaichunguza taarifa hiyo na endapo itadhihirika kwambani kweli Mbunge amezungumzia jambo ambalo ana maslahi binafsinalo ya kifedha bila kusema jinsi anavyohusika nalo wala kutajakiwango cha maslahi hayo, Kamati hiyo ya Bunge inaweza kulishauriBunge kwamba, Mbunge huyo aadhibiwe kwa ukiukwaji wa Kanunihii kama ifuatavyo:-

(a) ikiwa hilo ni kosa lake la kwanza, asihudhurievikao vya Bunge visivyozidi kumi;

(b) ikiwa hilo ni kosa lake la pili au zaidi, asihudhurievikao vya Bunge visivyozidi ishirini;

(5) Bunge linaweza kuzingatia ushauri mwingine wowoteuliotolewa na Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kuhusuadhabu anayostahili kupewa Mbunge aliyekiuka masharti ya Kanunihii.

(6) Kabla ya Bunge kupitisha Azimio la kumwadhibu Mbungekwa kuzingatia ushauri wa Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka yaBunge utakaotolewa chini ya fasili ya (4) na (5) ya Kanuni hii, Mbungemhusika atapewa nafasi ya kutoa utetezi wake mbele ya Bunge.

62.-(1) Isipokuwa kama imeelezwa vinginevyo kwenye Kanuni hizi:- (a) kila Mbunge anayejadili hoja, ataruhusiwa kusema kwa muda usiozidi dakika kumi na tano;

(b) Waziri anayetoa hoja ataiwasilisha hoja yakekwa muda usiozidi dakika thelathini nawakati anahitimisha hoja yake atasema kwamuda usiozidi dakika sitini;

(c) Mwenyekiti anayewasilisha maoni ya Kamatiatayawasilisha kwa muda usiozidi dakikathelathini;

Page 64: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

43

Kanuni za Kudumu za Bunge

(d) Msemaji wa Upinzani anayewasilisha maoni yaKambi ya Upinzani atayawasilisha maonihayo kwa muda usiozidi dakika thelathini; na

(e) Mbunge anayetoa hoja binafsi ataiwasilisha hojayake kwa muda usiozidi dakika thelathini nawakati wa kuhitimisha hoja yake atasema kwamuda usiozidi dakika sitini.

(2) Bila ya kuathiri masharti mengine ya Kanuni hii, Mbungeanayejadili hoja ataruhusiwa kusema kwa muda unaoruhusiwa naKanuni hizi.

63.-(1) Bila ya kuathiri masharti ya Ibara ya 100 ya Katibayanayolinda na kuhifadhi uhuru wa mawazo na majadiliano katikaBunge, ni marufuku kabisa kusema uongo Bungeni na kwa sababuhiyo, Mbunge yeyote anapokuwa akisema Bungeni ana wajibu wakuhakikisha kwamba anatoa kauli au maelezo kuhusu jambo ausuala ambalo yeye mwenyewe anaamini kuwa ni la kweli na siyojambo la kubuni au la kubahatisha tu.

(2) Mbunge yeyote anapokuwa akisema Bungenihatachukuliwa kuwa anasema uongo iwapo anafanya rejea yahabari kuhusu jambo fulani lililotangazwa au lililoandikwa navyombo vya habari.

(3) Mbunge mwingine yeyote anaweza kusimama mahalipake na kutamka “kuhusu utaratibu” na baada ya kuruhusiwa naSpika, kudai kwamba, Mbunge aliyekuwa anasema kabla yakeametoa maelezo ya uongo kuhusu jambo au suala alilokuwaanalisema Bungeni.

(4) Mbunge anayetoa madai kwa mujibu wa fasili ya (3) yaKanuni hii atakuwa na wajibu wa kutoa na kuthibitisha ukweli kuhusujambo au suala hilo kwa kiwango cha kuliridhisha Bunge.

(5) Bila ya kuathiri masharti ya fasili zilizotangulia za Kanunihii, Spika au Mbunge mwingine yeyote, baada ya kutoa maelezomafupi ya ushahidi unaotilia mashaka ya dhahiri kuhusu ukweli wakauli au usemi au maelezo juu ya jambo au suala ambalo Mbungeamelisema Bungeni, anaweza kumdai Mbunge huyo atoeuthibitisho wa ukweli wa kauli au usemi au maelezo yake na kama

KutosemauongoBungeni

Page 65: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

44

Kanuni za Kudumu za Bunge

atashindwa kufanya hivyo, afute kauli au usemi au maelezo yakehayo.

(6) Mbunge aliyetakiwa kuthibitisha ukweli wa kauli au usemiau maelezo yake aliyoyatoa Bungeni, atawajibika kutoa uthibitishohuo kwa kiwango cha kuliridhisha Bunge, papo hapo au katika mudaatakaopewa na Spika kwa ajili ya kufanya hivyo.

(7) Endapo Mbunge aliyetakiwa kuthibitisha kauli au usemiau maelezo yake aliyoyatoa Bungeni atashindwa kufanya hivyo,anaweza kujirekebisha kwa kufuta kauli au usemi au maelezo yakehayo, papo hapo au katika muda atakaokuwa amepewa na Spikakwa ajili ya kuthibitisha kauli au usemi au maelezo yake.

(8) Endapo hadi kufikia mwisho wa muda aliopewa, Mbungealiyetakiwa kutoa uthibitisho wa ukweli wa kauli au usemi aumaelezo yake aliyoyatoa Bungeni atakataa au atashindwa kutoauthibitisho huo kwa kiwango cha kuliridhisha Bunge na kamaatakataa kujirekebisha kwa kufuta kauli au usemi au maelezo yake,basi Spika atamwadhibu kwa kumsimamisha Mbunge huyoasihudhurie vikao vya Bunge visivyozidi vitano.

(9) Endapo Mbunge mwingine yeyote ataona kwamba uongouliosemwa na Mbunge huyo Bungeni ni mkubwa kiasi cha kuathiriheshima ya Bunge, anaweza kutoa hoja kwamba, Mbunge huyo: -

(a) ikiwa ni kosa lake la kwanza, asihudhurievikao vya Bunge visivyozidi kumi;

(b) ikiwa ni kosa lake la pili au zaidi, asihudhurievikao vya Bunge visivyozidi ishirini;

(c) achukuliwe hatua nyingine za kinidhamuzitakazotajwa katika hoja yake.

(10) Hoja ya aina hiyo inaweza kutolewa bila taarifa naitajadiliwa na kuamuliwa kwa utaratibu ufuatao:-

(a) Mtoa hoja atatoa hoja yake;

(b) Mbunge anayetuhumiwa kusema uongo Bungenichini ya fasili ya (9) ya Kanuni hii atapewa nafasiya kujitetea;

Page 66: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

45

Kanuni za Kudumu za Bunge

(c) Wabunge, kwa idadi itakayoamuliwa na Spikakulingana na muda uliopo, watachangia hojahiyo kwa dakika zitakazopangwa;

(d) Mtoa hoja atahitimisha hoja yake;

(e) Mbunge anayetuhumiwa kusema uongoBungeni au Mbunge mwingine yeyote anawezakutoa maombi ya adhabu iliyopendekezwa kwakosa la kusema uongo Bungeni ipunguzwe kwakiwango au namna atakayoipendekeza;

(f) Spika atawahoji Wabunge ili kupata uamuziwa Bunge kuhusu ombi la kupunguziwa adhabukama litatolewa na Mbunge anayetuhumiwa auMbunge mwingine yeyote;

(g) Iwapo pendekezo la kupunguziwa adhabulitakataliwa, basi Spika atalihoji Bunge ili kupatauamuzi kuhusu adhabu iliyopendekezwa na Mtoahoja.

64.-(1) Bila ya kuathiri masharti ya Ibara ya 100 ya Katiba yanayolindana kuhifadhi uhuru wa mawazo na majadiliano katika Bunge,Mbunge:-

(a) hatatoa ndani ya Bunge taarifa ambazo hazinaukweli;

(b) hatazungumzia jambo ambalo haliko kwenyemjadala;

(c) hatazungumzia jambo lolote ambalo linasubiriuamuzi wa Mahakama au jambo lolote ambalolilijadiliwa na kutolewa maamuzi kwenyeMkutano uliopo au uliotangulia na ambalohalikuletwa rasmi kwa njia ya hoja mahususi navilevile hatapinga uamuzi wowote uliofanywana Bunge, isipokuwa tu kwa kutoa hojamahususi inayopendekeza kuwa uamuzi huouangaliwe upya;

(d) hatatumia jina la Rais kwa dhihaka katikamjadala, au kwa madhumuni ya kutaka

Mamboyasiyo-ruhusiwaBungeni

Page 67: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

46

Kanuni za Kudumu za Bunge

kulishawishi Bunge kuamua jambo lolote kwanamna fulani;

(e) hatazungumzia mwenendo wa Rais, Spika,Mbunge, Jaji, Hakimu au mtu mwingine yeyoteanayeshughulikia utoaji wa haki, isipokuwa tukama kumetolewa hoja mahususi kuhusu jambohusika;

(f) hatamsema vibaya au kutoa lugha ya matusikwa Mbunge au mtu mwingine yeyote;

(g) hatatumia lugha ya kuudhi au inayodhalilishawatu wengine.

(2) Mbunge yeyote anayeamini kuwa Mbunge mwingineamevunja au amekiuka masharti ya fasili ya (1) ya Kanuni hii,atasimama mahala pake na kumwambia Spika wa Bunge “Kuhusuutaratibu” na atakaporuhusiwa na Spika kusema, atalazimika kutajamasharti ya Kanuni hii yaliyovunjwa au kukiukwa na Mbunge huyomwingine, na kama Mbunge huyo mwingine atakuwa anasemawakati huo, atakaa chini kusubiri maelekezo na mwongozo wa Spikakuhusu jambo hilo.

65.-(1) Isipokuwa tu kwa idhini ya Spika, Mbunge yeyotehataruhusiwa kusema zaidi ya mara moja juu ya hoja, ila tu kama:-

(a) wakati huo Bunge liko kwenye Kamati ya BungeZima au Kamati ya Matumizi;

(b) anatumia haki yake ya kujibu; au

(c) anasema kuhusu utaratibu.

(2) Mbunge ambaye amezungumza juu ya hoja anawezakuzungumza tena juu ya hoja ya kufanya mabadiliko katika hojaaliyoisemea; na Mbunge ambaye amependekeza kufanyamabadiliko katika hoja ya awali, anaweza kuzungumza tena juu yahoja ya awali baada ya mabadiliko kufanyika.

(3) Mbunge mtoa hoja ya msingi au mtoa hoja ya kutakakufanya mabadiliko katika hoja iliyokwisha kutolewa, atakuwa nahaki ya kujibu kabla uamuzi juu ya hoja hiyo haujatolewa.

Kuzungu-mzazaidi yamaramoja

Page 68: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

47

Kanuni za Kudumu za Bunge

(4) Wakati wa kujibu, mtoa hoja atapaswa kujibu mamboyale tu yaliyozungumzwa na Wabunge waliochangia hoja yake nahataruhusiwa kutoa maelezo yoyote mapya, isipokuwa kamamaelezo hayo ni ya lazima kwa madhumuni ya kufafanua jambolililochangiwa na Wabunge.

(5) Mbunge yeyote hataruhusiwa kusema Bungeni baadaya Spika kuwahoji Wabunge na kura ya sauti ama ya elektroniki auya siri ya “ndiyo” au “siyo” au ya “kutokukubaliana” au kura yauamuzi ya aina nyingine yoyote kupigwa, isipokuwa pale ambapoitaonekana kuwa kuna mashaka kuhusu matokeo ya kura kwakufuata wingi wa sauti kwa mujibu wa fasili ya 5 ya Kanuni ya 79 yaKanuni hizi.

66.-(1) Wakati wa Vikao vya Bunge, Spika anapokuwa anaingiaau kutoka katika Ukumbi wa Bunge, Wabunge na wageni wotewaliopo kwenye Ukumbi huo watasimama kwa utulivu mahali paona kubaki kimya hadi Spika atakapokuwa ameketi katika Kiti chakeau atakapokuwa ametoka kwenye Ukumbi wa Bunge.

(2) Wakati Bunge linaingia kwenye Kamati ya Bunge Zima aukatika Kamati ya Matumizi, Wabunge na wageni wote waliopokwenye Ukumbi wa Bunge watasimama kwa utulivu mahali pao nakubaki kimya ili kutoa heshima kwa mchakato wa Bunge kuingiakwenye Kamati ya Bunge Zima au kwenye Kamati ya Matumizi nabaadaye Bunge kurejea.

(3) Mbunge aliyepo Bungeni wakati wa mjadala atatakiwa:-

(a) kuingia au kutoka kwenye Ukumbi wa Bunge kwastaha na atainamisha kichwa kuelekea kwaSpika au kufanya mkunjo wa magoti kwaheshima, kila mara Mbunge huyo atakapokuwaakienda au kutoka mahali pake;

(b) kutulia na kukaa kwa heshima mahali pake, nahatatangatanga kwenye ukumbi wa Mikutanobila sababu;

(c) kutopita kati ya Kiti cha Spika na Mbungeanayesema;

Stahandani ya Bunge

Page 69: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

48

Kanuni za Kudumu za Bunge

(d) kutosoma kitabu chochote, gazeti au barua,isipokuwa kama vitu hivyo vinahusu shughuli zamjadala unaoendelea wakati huo; na

(e) kuzima simu ya mkononi na kwa namna yoyotekutotumia simu.

67.-(1) Spika anaweza kulihutubia Bunge wakati wowote na kwaajili hiyo, anaweza kumkatiza Mbunge yeyote anayezungumza.

(2) Endapo Spika atasimama wakati wa mjadala, na kuanzakuzungumza, Mbunge yeyote ambaye atakuwa anazungumzawakati huo au ambaye atakuwa amesimama mahali pake akisubirikuanza kuzungumza, ataketi mahali pake, na Bunge litabaki kimyaili Spika aweze kutoa maelekezo au taarifa yake.

68.-(1) Mbunge anaweza kusimama wakati wowote na kusemamaneno “kuhusu utaratibu”, ambapo Mbunge yeyote ambayewakati huo atakuwa anasema atanyamaza na kukaa chini na Spikaatamtaka Mbunge aliyedai utaratibu ataje Kanuni au sehemu yaKanuni iliyokiukwa.

(2) Mbunge aliyedai utaratibu atalazimika kutaja Kanuni ausehemu ya Kanuni ya Bunge iliyokiukwa.

(3) Baada ya kutaja Kanuni au sehemu ya Kanuni ya Bungeiliyokiukwa Mbunge aliyesimama kuhusu utaratibu, ataketi mahalipake kusubiri maelekezo na uamuzi wa Spika.

(4) Spika anaweza, ama papo hapo kutoa uamuzi wake juuya jambo la utaratibu lililotajwa au kuahirisha uamuzi ili alifikiriezaidi jambo hilo na kutoa uamuzi baadaye au kutoa uamuzi nabaadaye kutoa sababu za uamuzi huo, vyovyote atakavyoamua.

(5) Katika kufikia uamuzi wake, Spika anaweza kuitaka Kamatiya Kudumu ya Kanuni za Bunge au Kamati nyingine yoyote ya Bungeimpe ushauri kuhusu jambo husika.

(6) Mbunge aliyekuwa anazungumza wakati jambo la utaratibulilipohojiwa anaweza kuendelea na hotuba yake baada ya Spikakutoa uamuzi juu ya jambo hilo.

(7) Hali kadhalika, Mbunge anaweza kusimama wakatiwowote ambapo hakuna Mbunge mwingine anayesema na

MamlakayaSpikakukatizamajadiliano

Taarifa kuhusuutaratibunaMwongozo

Page 70: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

49

Kanuni za Kudumu za Bunge

kuomba “Mwongozo wa Spika” kuhusu jambo ambalo limetokeaBungeni mapema, ili Spika atoe ufafanuzi kama jambo hilolinaruhusiwa au haliruhusiwi kwa mujibu wa Kanuni na taratibu zaBunge na majibu ya Spika yatatolewa papo hapo au baadaye,kadri atakavyoona inafaa.

(8) Vilevile, Mbunge yeyote anaweza kusimama mahali pakena kusema “taarifa” na kwa ruhusa ya Spika, atatoa taarifa auufafanuzi kwa Mbunge anayesema, ambapo Spika atamtakaMbunge anayesema aketi kusikiliza taarifa hiyo.

(9) Mtoa taarifa atakapomaliza na kuketi, Spika atamuulizaMbunge aliyekuwa akisema mwanzo kama anaikubali au haikubalitaarifa hiyo kabla ya kumruhusu kuendelea kuchangia hoja.

(10) Uamuzi wa Spika kuhusu suala lolote la utaratibu utakuwani wa mwisho.

69.- (1) Mbunge anayependa mjadala unaoendelea juu ya hojayoyote uahirishwe hadi wakati wa baadaye, anaweza kutoa hoja“Kwamba mjadala sasa uahirishwe” na atataja mjadala huouahirishwe hadi wakati gani na pia atalazimika kutoa sababu kwanini anataka mjadala uahirishwe.

(2) Kama Spika atakuwa na maoni kwamba kuwasilishwa kwahoja hiyo ni kinyume cha uendeshaji bora wa shughuli za Bunge,atakataa kuitoa ili iamuliwe; vinginevyo, papo hapo atawahojiWabunge juu ya hoja hiyo kadri atakavyoona inafaa.

(3) Endapo hoja iliyowasilishwa haitapata kibali cha Bunge,mjadala kuhusu hoja iliyoko mbele ya Bunge utaendelea.

(4) Mbunge yeyote hataruhusiwa kutoa hoja ya kufanyamabadiliko katika hoja iliyotolewa kwa mujibu wa Kanuni hii.

70.-(1) Utaratibu utakaotumika kufunga mjadala ni kutoa hoja yakufunga mjadala endapo bado kuna Wabunge wanaopendakuzungumza juu ya jambo lililoko katika mjadala lakini mudauliotengwa umekwisha au endapo Bunge limewekewa kiwangocha juu cha muda wa kujadili hoja inayohusika na muda huo badohaujaisha.

(2) Hoja ya kufunga mjadala inaweza kutolewa baada yahotuba yoyote kukamilika au ikiwa Spika ataruhusu hoja ya kufanya

HojayakuahirishaMjadala

Hojaya KufungaMjadala

Page 71: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

50

Kanuni za Kudumu za Bunge

mjadala, mara tu au muda mfupi baada ya hoja hiyo kutolewa iliiamuliwe.

(3) Mbunge anayetoa hoja ya kufunga mjadala, anawezakusimama mahali pake na kutoa hoja “Kwamba mtoa hoja sasaapewe nafasi ya kujibu”.

(4) Endapo Spika ataona kuwa hoja ya kufunga mjadalainakiuka mwenendo bora wa Shughuli za Bunge au inavunja haki zaWabunge, basi ataikataa.

(5) Endapo hoja “Kwamba mtoa hoja sasa apewe nafasiya kujibu” itakubaliwa, mtoa hoja atajibu kama akipenda na baadaya hotubaya kujibu kukamilika au kama mtoa hoja hapendi kujibu basi Spikaatawahoji Wabunge ili kuamua hoja hiyo.

71.-(1) Bila ya kuathiri masharti ya Ibara ya 100 na 101 ya Katiba,mtu yeyote asiye Mbunge ambaye atajisikia kuwa amepata atharihasi kutokana na kauli au maneno au shutuma zilizotolewa Bungenikumhusu yeye binafsi, anaweza kupeleka malalamiko pamoja namaelezo yake ya kujitetea kwa Spika:-

(a) yawe yameandikwa kwa lugha fasaha na yaheshima na yanahitimishwa kwa maelezo yajumla kuhusu madhumuni yake;

(b) yawe yamewasilishwa katika kipindi cha sikukumi na nne baada ya kauli au manenoyanayolalamikiwa kutolewa;

(c) yawe yamewasilishwa na mtu binafsi ambaye niraia wa Tanzania na hayajawasilishwa na aukwa niaba ya Kampuni, Shirika au Taasisi;

(d) yaonyeshe wazi kuwa, kwa dhahiri mhusikaaliathirika yeye binafsi kutokana na kauli aumaneno au shutuma zilizotolewa Bungeni;

(e) yaeleze kwa ufasaha ni jinsi gani mhusikaamepata athari hasi, kama vile kuchafuliwajina lake na heshima yake katika jamii aukuharibu sifa, mahusiano na ushirikiano wakena wengine au kazi yake anayoifanya katikajamii au kuingilia uhuru na maisha yake binafsi

Haki yaraiakujiteteanakujisafishadhidi yakaulizinazo-tolewaBungeni

Page 72: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

51

Kanuni za Kudumu za Bunge

na familia yake isivyo halali kutokana na kauli aushutuma zilizotolewa Bungeni;

(f) yatoe ombi kwamba, endapo kwa utaratibuuliowekwa na Kanuni hizi yatakubalika, basimaelezo ya utetezi au ufafanuzi yaliyotolewa namhusika kwa ajili ya kusafisha jina nakurejesha heshima yake yachukuliwe na Bungekuwa ndiyo majibu sahihi ya kauli au shutumazilizotolewa Bungeni.

(2) Mara baada ya kupokea malalamiko yaliyowasilishwakwake kwa mujibu wa fasili ya (1) ya Kanuni hii na kujiridhisha kuwamalalamiko hayo yameandikwa katika lugha ya heshima na yakistaarabu na yanatoa hoja mahususi na ambayo si ya uzushi, uongo,uchochezi au chuki binafsi; na kwamba yanastahili kufikiriwa aukufanyiwa kazi na Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge,Spika atayapeleka malalamiko hayo kwenye Kamati ya Haki,Maadili na Madaraka ya Bunge ili kuyatafakari na kulishauri Bunge.

(3) Katika kuyafanyia kazi malalamiko yaliyopelekwa kwakena Spika kwa mujibu wa fasili ya (3) ya Kanuni hii, Kamati ya Haki,Maadili na Madaraka ya Bunge:-

(a) itakutana katika kikao cha faragha;

(b) inaweza kumhoji mtu aliyewasilisha malalamikoyake kwa Spika au Mbunge au Waziri aliyetoaBungeni kauli au shutuma zinazolalamikiwa;

(c) haitajadili wala kutoa uamuzi kuhusu ukweli wakauli au shutuma zilizotolewa Bungeni au ukweliwa maelezo yaliyotolewa kwenye malalamikohusika;

(d) haitatangaza maelezo yaliyomo kwenyemalalamiko husika wala mwenendo wamajadiliano yake kuhusiana na malalamikohusika.

(4) Baada ya kukamilisha kazi yake, Kamati ya Haki, Maadilina Madaraka ya Bunge itawasilisha Bungeni, taarifa ya uamuzi wakekuhusu malalamiko husika, pamoja na maelezo yote au sehemu yamaelezo ya malalamiko husika, kwa ajili ya kuridhiwa na Bunge.

Page 73: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

52

Kanuni za Kudumu za Bunge

Adhabuzinazowezakuto-lewa naSpikakwaukiukaj iwaKanuni

(5) Taarifa itakayowasilishwa Bungeni na Kamati ya Haki,Maadili na a Madaraka ya Bunge inaweza kupendekeza mojawapoya yafuatayo:-

(a) maelezo ya utetezi au ufafanuzi wa mlalamikaji,kama yalivyoelezwa kwenye taarifa hiyo,yaingizwe kwenye Taarifa Rasmi za Bunge; au

(b) Bunge lisichukue hatua yoyote nyingine.

SEHEMU YA SITA

AMANI NA UTULIVU BUNGENI

72.-(1) Spika atakuwa na wajibu wa kuhakikisha kuwa, utaratibubora unafuatwa Bungeni, na uamuzi wa Spika kuhusu jambo lolotela utaratibu utakuwa ni wa mwisho.

(2) Mbunge atakayekiuka utaratibu uliowekwa na Kanunihizi anaweza papo hapo kutakiwa na Spika afuate utaratibu navilevile Mbunge mwingine yeyote anaweza kusimama nakumfahamisha Spika kuhusu ukiukwaji wa utaratibu huo na katikakufanya hivyo, atalazimika kutaja Kanuni ya Bunge iliyowekautaratibu uliokiukwa.

(3) Endapo Mbunge yeyote atatakiwa kuthibitisha ukweli wajambo au suala alilolisema Bungeni na hadi kufikia mwisho wa mudaaliopewa amekataa au ameshindwa kutoa uthibitisho huo, Spikaanaweza kumsimamisha Mbunge huyo kuhudhuria vikao vya Bungevisivyozidi vitano.

(4) Endapo Mbunge atafanya kosa ambalo alikwishawahikuadhibiwa kwa mujibu wa fasili ya (2) na (3) ya Kanuni hii, Spikaatalipeleka suala lake kwenye Kamati ya Haki, Maadili na Madarakaya Bunge kwa mujibu wa masharti ya Kanuni ya 71 ya Kanuni hizi iliKamati hiyo ilishauri Bunge kuhusu hatua za kinidhamu zinazostahilikuchukuliwa dhidi ya Mbunge huyo.

73.-(1) Mbunge au Waziri atakayezungumzia jambo au mamboambayo hayaruhusiwi na Kanuni hizi, anaweza kuamriwa na Spikaau Naibu Spika au Mwenyekiti akatishe hotuba yake na kukaa mahalipake.

MamlakayaSpikakusimamiautaratibu

Page 74: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

53

Kanuni za Kudumu za Bunge

(2) Endapo Mbunge au Waziri atatumia maneno au lughaisiyotakiwa Bungeni, yaani lugha ya matusi, usafihi, uchokozi aulugha ya maudhi na akitakiwa na Spika ajirekebishe kwa kufutamaneno au lugha hiyo atakataa kufanya hivyo, Spika anawezakumwamuru Mbunge huyo atoke mara moja nje ya Ukumbi waBunge na abaki huko nje kwa muda wote uliosalia wa kikao chasiku hiyo.

(3) Endapo Mbunge yeyote atatakiwa kuthibitisha ukweliwa maneno aliyoyasema na hadi kufikia mwisho wa muda aliopewa,amekataa au ameshindwa kutoa uthibitisho huo, Spika anawezakumsimamisha Mbunge huyo asihudhurie vikao vya Bungevisivyozidi vitano.

(4) Endapo Mbunge atafanya kosa ambalo alikwishawahikuadhibiwa kwa mujibu wa fasili ya (2) na (3) ya Kanuni hii, Spikaatalipeleka suala lake kwenye Kamati ya Haki, Maadili na Madarakaya Bunge ili Kamati hiyo ilishauri Bunge kuhusu adhabu inayostahilikutolewa kwa Mbunge mhusika.

74.-(1) Spika anaweza kutaja jina la Mbunge kwamba amedharauMamlaka ya Spika na kisha kupeleka jina hilo kwenye Kamati yaHaki, Maadili na Madaraka ya Bunge ikiwa:-

(a) kwa maneno au vitendo, Mbunge huyoanaonesha dharau kwa mamlaka ya Spika; au

(b) Mbunge huyo atafanya kitendo chochote chamakusudi cha kudharau Shughuli ya Bunge auMbunge yeyote anayeongoza shughuli hiyo.

(2) Ikiwa maneno au vitendo vya Mbunge vilivyoainishwakatika fasili ya (1) ya Kanuni hii vimetokea wakati Bunge likiwa katikaKamati ya Bunge Zima, basi Mwenyekiti atasimamisha shughuli zaKamati na ataagiza Bunge kurudia ili kumpatia Spika fursa ya kutoataarifa kwa Bunge kuhusu mwenendo wa Mbunge huyo nakuwasilisha suala hilo kwenye Kamati ya Haki, Maadili na Madarakaya Bunge.

(3) Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge itajadilisuala hilo na ikithibitika kuwa Mbunge husika ametenda kosainaweza kushauri kwamba:-

Adhabuzinazo-wezakutolewanaBungekwaukiukajiwaKanuni

Page 75: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

54

Kanuni za Kudumu za Bunge

AkidiyaVikaovyaBunge

(a) ikiwa ni kosa lake la kwanza Mbunge huyoasihudhurie vikao vya Bunge visivyozidi kumi; au

(b) ikiwa ni kosa lake la pili au zaidi Mbunge huyoasihudhurie vikao vya Bunge visivyozidi ishirini;

(4) Bunge linaweza kuzingatia ushauri mwingine wowoteutakaotolewa na Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bungekuhusu adhabu anayostahili kupewa Mbunge aliyekiuka mashartiya Kanuni hii.

(5) Bila ya kujali masharti ya fasili ya (4) ya Kanuni hii, Bungelinaweza kumchukulia hatua nyinginezo za kinidhamu, ikiwa nipamoja na kumsimamisha kazi Mbunge yeyote aliyetenda kosachini ya Kanuni hii.

(6) Adhabu yoyote itakayotolewa kwa Mbunge aliyekiukamasharti ya Kanuni hii itatolewa kupitia Azimio la Bunge ambalolitataja adhabu hiyo pamoja na sababu zake.

75.- Mbunge aliyesimamishwa kazi atatoka katika Bunge nahataingia tena katika sehemu yoyote ya Ukumbi wa Bunge namaeneo ya Bunge kwa muda wote atakapokuwa amesimamishwa,na atalipwa nusu mshahara na nusu posho zinazoambatana namshahara huo.

76.-(1) Kwa madhumuni ya kudhibiti fujo endapo itatokea ndani yaUkumbi wa Bunge na Spika ataona kuwa kuna haja ya kutumianguvu, basi anaweza kuahirisha Shughuli za Bunge bila ya hojayoyote kutolewa au kusitisha kikao kwa muda atakaoutaja ili fujohiyo iweze kudhibitiwa na Mpambe wa Bunge.

(2) Baada ya utulivu kurudia, Spika atalipeleka kwenye Kamatiya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge suala ambalo lilisababishakutokea kwa fujo ikiwa ni pamoja na jina la Mbunge au majina yaWabunge waliohusika na fujo hiyo ili Kamati hiyo iweze kulishauriBunge kuhusu adhabu inayostahili kutolewa.

SEHEMU YA SABA

UHALALI WA SHUGHULI

77.-(1) Akidi kwa kila kikao cha Bunge wakati wa kufanya maamuzi

MashartikwaMbungealiyesima-mishwakazi

Udhibitiwa fujoBungeni

Page 76: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

55

Kanuni za Kudumu za Bunge

itakuwa ni nusu ya Wabunge wote, kama ilivyofafanuliwa katikaIbara ya 94 ya Katiba, isipokuwa kwamba, idadi hiyo haitahusu hojakuhusu uamuzi wa kubadilisha masharti yoyote ya Katiba kwa mujibuwa Ibara ya 98 ya Katiba.

(2) Mbunge yeyote aliyehudhuria anaweza kumjulisha Spikakwamba, Wabunge waliopo ni pungufu ya akidi inayohitajika kwaajili ya shughuli inayoendelea.

(3) Endapo Spika ataridhika kwamba ni kweli idadi yaWabunge walio ndani ya Ukumbi wa Bunge ni pungufu ya akidiinayohitajika, basi atasimamisha Shughuli za Bunge kwa mudaatakaoutaja na atamwagiza Katibu kupiga kengele.

(4) Bunge litakaporudia baada ya wakati uliotajwakukamilika, Spika atahakikisha kama idadi ya Wabunge waliopoinafikia akidi inayohitajika ili kuruhusu uamuzi kufanyika.

(5) Endapo Spika ataridhika kwamba bado idadi yaWabunge waliomo ndani ya Ukumbi wa Bunge haifikii akidiinayohitajika basi ataahirisha Shughuli za Bunge hadi mudamwingine atakaoutaja.

78.- Shughuli za Bunge hazitakuwa batili kwa sababu tu kwambanafasi yoyote ya Mbunge ipo wazi.

79.-(1) Bila ya kuathiri masharti ya Ibara za 46A, 50(3), 53A na 98 zaKatiba, mambo yote yanayohitaji kuamuliwa na Bunge yataamuliwakwa kufuata maoni ya Wabunge walio wengi waliohudhuria nakupiga kura Bungeni.

(2) Spika, wakati amekalia kiti cha Spika, hatakuwa na kuraya kawaida bali atakuwa na kura ya uamuzi endapo kura za “Ndiyo”na “Siyo” zitalingana.

(3) Wakati mjadala juu ya hoja unapomalizika, Spikaatawahoji Wabunge ili kupata uamuzi juu ya hoja hiyo kama ilivyoau baada ya kufanyiwa marekebisho au mabadiliko, Spika kwanzaatataka uamuzi wa wale wanaoafiki kwa kusema: “Wale wanaoafikiwaseme Ndiyo” na baadaye atataka uamuzi wa Wabungewasioafiki kwa kusema: “Wale wasioafiki waseme Siyo.”

Uhalali wa maamuzi ya Bunge

UamuziwaBunge

Page 77: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

56

Kanuni za Kudumu za Bunge

(4) Isipokuwa kama imeelekezwa vinginevyo katika Kanunihizi, uamuzi juu ya mambo yote utapatikana kwa kufuata wingi wasauti za Wabunge za “Ndiyo” au “Siyo” na Spika atatangazamatokeo ya kura kwa kusema “Naamini Walioafiki Wameshinda”au “Naamini Wasioafiki Wameshinda.”

(5) Endapo itaonekana kuwa kuna mashaka kuhusu matokeoya kura kwa kufuata wingi wa sauti kwa mujibu wa fasili ya (4) yaKanuni hii, Spika ataruhusu muda upite ili kutoa nafasi kuhakikishauamuzi wa Bunge juu ya jambo hilo na kwa muda huo, ikiwainaonekana kuwa kuna mashaka kuhusu matokeo ya kura, Mbungeyeyote anaweza kusimama na kusema “Kura zihesabiwe.”

(6) Endapo hakuna Mbunge aliyeomba kura zihesabiwe, Spikaatatoa kauli ya uamuzi wa mwisho kwa kusema “WalioafikiWameshinda” au “Wasioafiki Wameshinda”, kulingana na haliitakavyokuwa.

(7) Endapo Mbunge yeyote ataomba kura zihesabiwe, basiSpika ataamuru kura zihesabiwe ikiwa Wabunge wengine kumi auzaidi watasimama mara moja kuunga mkono maombi ya kurakuhesabiwa.

(8) Endapo Spika ataamuru kura zihesabiwe, Katibu atapigakengele ya kuwaita Wabunge kwa muda wa dakika moja na baadaya muda huo, Spika atamwagiza Katibu kumwita Mbunge mmojammoja kwa jina lake na kumuuliza anapiga kura yake upande ganina kurekodi kura hiyo.

(9) Bila ya kuathiri masharti ya fasili zilizotangulia za Kanunihii, Mbunge yeyote atakayepiga kura juu ya jambo lolote ambaloyeye binafsi ana maslahi nalo ya kifedha atahesabiwa kuwahakupiga kura.

(10) Baada ya Katibu kukamilisha shughuli ya kuhesabu kura,atamjulisha Spika kuhusu kura zote za wanaoafiki, wasioafiki nawasiokuwa na upande wowote na Spika atatangaza matokeo yahesabu hiyo ya kura.

(11) Orodha kamili itaandaliwa ikionyesha namna kurazilivyopigwa na itarekodiwa katika Taarifa Rasmi kwa ajili ya kuwekakumbukumbu ya uamuzi wa Bunge.

Page 78: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

57

Kanuni za Kudumu za Bunge

SEHEMU YA NANE

KUTUNGA SHERIA – MASHARTI YA JUMLA

80.-(1) Kila Muswada wa Sheria utatangazwa kwenye Gazeti katikamatoleo angalau mawili, kukiwa na kitambo kisichopungua sikusaba kamili kati ya toleo la kwanza na la pili.

(2) Tangazo la Kwanza la Muswada wa Sheria litatolewa nakumfikia Katibu katika muda usiopungua siku 21 kabla ya Muswadahuo kusomwa Bungeni kwa Mara ya Kwanza, na litaoneshaMuswada mzima, ikiwa ni pamoja na maelezo kuhusu madhumuniya Muswada husika yaliyotiwa saini na Waziri au Mwanasheria Mkuuwa Serikali.

(3) Muswada wa Serikali utahesabiwa kuwa umetangazwamara ya pili endapo itatolewa taarifa katika Gazeti inayotaja jinala Muswada, nambari na tarehe ya Gazeti ambapo Muswadaulitangazwa mara ya kwanza.

(4) Muswada wowote wa Sheria wa Serikali wa dharurahautaingizwa kwenye shughuli za Bunge bila ya kuwa na hatiiliyowekwa saini na Rais inayoeleza kuwa Muswada uliotajwa katikahati hiyo ni wa dharura.

(5) Muswada huo utawasilishwa kwanza kwenye Kamati yaUongozi ukiwa umeambatishwa na hati ya dharura ili Kamati hiyoiweze kujiridhisha iwapo Muswada husika wa sheria unastahilikuwasilishwa kwa dharura au la.

(6) Iwapo Kamati ya Uongozi itaona kuwa Muswada waSheria wa Serikali uliowasilishwa kwa hati ya dharura haustahilikuwasilishwa kwa dharura, Kamati hiyo itaishauri Serikali ipasavyo.

(7) Haitakuwa lazima kwa Waziri au Mwanasheria Mkuu waSerikali kutoa taarifa ya Muswada wa Serikali ambao unakusudiwakuwasilishwa Bungeni iwapo Muswada huo umekwisha kutangazwakwenye Gazeti.

(8) Katibu atagawa kwa kila Mbunge nakala ya kila Muswadawa Sheria kama ulivyochapishwa na kutangazwa kwenye Gazeti.

Utanga-zajiwaMiswadayaSerikali

Page 79: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

58

Kanuni za Kudumu za Bunge

MuswadaKusomwaMara yaKwanza

81.-(1) Bila ya kuathiri masharti ya Ibara ya 99 ya Katiba, Kamatiyoyote ya Kudumu ya Bunge au Mbunge yeyote anawezakuwasilisha Bungeni Muswada Binafsi wa Sheria.

(2) Taarifa ya kuwasilisha Muswada Binafsi wa Sheria naMuswada wa Sheria wa Kamati itapelekwa kwa Katibu na taarifahiyo itaeleza jina la Muswada unaopendekezwa pamoja namadhumuni na sababu zake.

(3) Baada ya taarifa kutolewa, Muswada Binafsi wa Sheriaau Muswada wa Sheria wa Kamati utatangazwa katika Gazeti kamailivyo kwa Miswada ya Sheria ya Serikali, isipokuwa kwamba,madhumuni na sababu yatawekwa saini na Mwenyekiti wa Kamatiya Kudumu ya Bunge au Mbunge anayehusika.

(4) Muswada Binafsi wa Sheria utahesabiwa kuwaumetangazwa mara ya pili endapo itawekwa taarifa kwenye Gazetiinayotaja jina la Muswada, nambari na tarehe ya Gazeti ambapoMuswada ulitangazwa Mara ya Kwanza.

(5) Masharti kuhusu muda wa utangazaji wa Miswada yaSheria yanaweza kuwekwa kando na kutenguliwa kwa hojakutolewa na kuamuliwa kama kutawasilishwa Bungeni hatiiliyowekwa saini na theluthi mbili ya Wajumbe wote wa Kamatikama ni Muswada wa Kamati na kwa Muswada wa Mbunge hatiiliyowekwa saini na Wabunge wasiopungua kumi inayoeleza kuwaMuswada Binafsi uliotajwa katika hati hiyo ni wa dharura.

(6) Masharti ya kujadili hoja hii yatakuwa kama yalivyo kwaupande wa Miswada ya Sheria ya Serikali.

82.-(1) Muswada wa Sheria wa Serikali utawasilishwa Bungeni naWaziri au Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

(2) Muswada Binafsi wa Sheria unaweza kuwasilishwa Bungenina Mwenyekiti wa Kamati yoyote ya Kudumu ya Bunge au Mbungeyeyote ambaye si Waziri.

83.-(1) Muswada wowote wa Sheria ambao umetangazwa kwenyeGazeti, unaweza kuwasilishwa Bungeni kufuatana na Orodha yaShughuli ili Kusomwa Mara ya Kwanza na katika hatua hiyo Katibuatasoma jina refu la Muswada wa Sheria unaohusika bila hojayoyote kutolewa kwa ajili hiyo.

Utaratibu kuhusu Miswada Binafsi

Uwasi l i -shaji waMuswada

Page 80: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

59

Kanuni za Kudumu za Bunge

(2) Hakutakuwa na mjadala wowote wakati wa Muswadawa Sheria Kusomwa Mara ya Kwanza.

84.-(1) Spika atapeleka Muswada wa Sheria kwenye Kamatiinayohusika na Kamati itaanza kuujadili Muswada huo mapemaiwezekanavyo.

(2) Kamati iliyopelekewa Muswada itatoa matangazo auitatoa barua ya mwaliko kumwalika mtu yeyote afike kutoa maoniyake mbele ya Kamati hiyo kwa lengo la kuisaidia katika uchambuziwa Muswada huo.

(3) Bila ya kuathiri masharti ya Ibara ya 99 ya Katiba, Kamatii l iyopelekewa Muswada itakuwa na uwezo wa kufanyamarekebisho katika Muswada wa Sheria kwa kumshauri Waziri auMbunge anayehusika na Muswada huo kufanya mabadiliko, vilevileSerikali itakuwa na uwezo wa kuishauri Kamati ya Kudumu ya Bungekuhusu kufanya marekebisho au mabadiliko juu ya Muswada Binafsi.

(4) Kabla Muswada wa Sheria uliofanyiwa mabadilikohaujawasilishwa Bungeni kwa ajili ya Kusomwa Mara ya Pili,utapelekwa kwenye Kamati inayohusika kwa madhumuni yakuzingatia mabadiliko hayo.

85.-(1) Kamati iliyopelekewa Muswada wa Sheria itakapokamilishakuujadili Muswada huo Mwenyekiti wa Kamati atamjulisha Spikakwa maandishi kwamba, Kamati imemaliza kujadili Muswada husika.

(2) Spika ataagiza Muswada huo uwekwe kwenye Orodha yaShughuli kwa ajili ya kusomwa Mara ya Pili.

86.-(1) Siku ambayo Muswada wa Sheria uliokwisha kujadiliwa naKamati umepangwa kwenye Orodha ya Shughuli, Waziri,Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mwenyekiti wa Kamati au Mbungemwenye Muswada husika atawasilisha hoja kwamba Muswada waSheria ambao atautaja kwa jina Kusomwa Mara ya Pili.

(2) Hoja ya Muswada wa Sheria Kusomwa Mara ya Pili itakuwakama ifuatavyo:-

“Kwamba, Muswada wa Sheria uitwao….. sasa usomwemara ya pili.”

Au kadri itakavyokuwa;“Kwamba, Muswada uitwao ……………… kama

Muswadakupele-kwakwenyeKamati

Taarifa ya Kamati

MuswadaKusomwaMarayaPili

Page 81: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

60

Kanuni za Kudumu za Bunge

ulivyorekebishwa kwa mujibu wa jedwali la marekebisho au kamaulivyochapishwa upya sasa usomwe mara ya pili.”

(3) Haitakuwa halali katika hatua hii kuleta hoja ya kufanyamabadiliko katika hoja isipokuwa tu kwamba:-

(a) mabadiliko bila kutoa sababu yanaweza kutolewakwa kusema:

“Kwamba, Muswada huu usisomwe mara ya Pilisasa na badala yake usomwe baada ya …..kuanzia …..”, na hapo muda ambao Muswadahuo unaokusudiwa kusomwa utatajwa.

(b) mabadiliko yenye kutoa sababu yanawezakutolewa kwa kusema:

“Kwamba, Bunge hili likatae Muswada huuKusomwa Mara ya Pili kwa sababu zifuatazo... ”,

na hapo sababu za kupinga Muswada Kusomwa Mara ya Pili zitatajwa kwa ukamilifu.

(4) Iwapo hoja itatolewa chini ya fasili ya 3(a) na (b) yaKanuni hii, Spika atalihoji Bunge ili kufikia uamuzi.

(5) Mwenyekiti wa Kamati iliyopelekewa Muswada waSheria au Mjumbe mwingine wa Kamati aliyeteuliwa kwa ajili hiyo,atatoa maoni ya Kamati kuhusu Muswada husika.

(6) Ikiwa Muswada wa Sheria unaohusika ni Muswada waSerikali, basi Msemaji wa Kambi ya Upinzani atatoa maoni yake juuya Muswada husika na endapo ni Muswada Binafsi au Muswada waKamati, basi msemaji wa Serikali atatoa maoni yake.

(7) Mjadala wakati wa Muswada wa Sheria Kusomwa Maraya Pili utahusu ubora na misingi ya Muswada huo tu.

(8) Majadiliano juu ya hoja kuhusu Muswada kama yapoyatahusu maneno yanayohusiana na hoja tu.

(9) Mbunge yeyote au Waziri anaweza, wakati wa mjadalahuo, kumshauri Mtoa hoja afanye mabadiliko katika Muswada, amamabadiliko ya jumla au yale atakayoyataja Mbunge.

Page 82: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

61

Kanuni za Kudumu za Bunge

(10) Katika hatua hii iwapo mtoa hoja anataka kufanyamarekebisho au mabadiliko katika Muswada wa Sheria kutokanana ushauri uliotolewa ama katika Kamati au wakati wa Muswadawa Sheria Kusomwa Mara ya Pili au kwa sababu nyingine yoyote,iwapo Muswada huo ni wa Serikali atamjulisha Mwandishi Mkuu waSheria na iwapo Muswada husika ni wa Kamati au Binafsiatamjulisha Mshauri Mkuu wa Bunge wa Mambo ya Sheria iliatayarishe na kumkabidhi Katibu ambaye atagawa kwa kilaMbunge nakala ya:-

(a) Muswada wa Sheria uliochapishwa upya ukiwana marekebisho au mabadiliko yanayokusudiwakufanyika; au

(b) Jedwali la Marekebisho au mabadilikoyanayokusudiwa kufanyika.

(11) Kamati au Mbunge anaweza kuwasilisha kwa Katibu,kwa maandishi, mabadiliko anayokusudia kuyafanya katikaMuswada huo wakati wa Kamati ya Bunge Zima akionesha bayanamabadiliko yanayokusudiwa kufanyika katika kila Ibara inayohusika.

87.-(1) Endapo Muswada ulikwishasomwa mara ya Pili na haukuwana mabadiliko, lakini kuna jambo au suala jipya limetokea nalinahitaji kuzingatiwa, Mtoa hoja anaweza kumwomba Spika wakatiwowote kabla Muswada haujapelekwa katika Kamati ya BungeZima kwamba, Muswada huo urejeshwe tena kwenye Kamatiinayohusika.

(2) Endapo Muswada wa Sheria utapelekwa tena kwenyeKamati inayohusika, Mbunge yeyote ambaye wakati wa Muswadawa Sheria Kusomwa Mara ya Pili alimwomba mtoa hoja kufanyamabadiliko katika Muswada huo, anaweza kuhudhuria mkutano waKamati na kushiriki katika majadiliano, isipokuwa kwamba, Mbungehuyo hatakuwa na haki ya kupiga kura kuhusu uamuzi wowote waKamati hiyo.

(3) Kamati itakutana mapema iwezekanavyo ili kujadilimabadiliko yaliyopendekezwa.

(4) Bila ya kuathiri masharti ya Ibara ya 99 ya Katiba,Kamati inayohusika itakuwa na mamlaka ya kufanya mabadilikokatika Muswada uliopelekwa kwake kwa mujibu wa Kanuni hii kwa:-

Kureje-shaMuswadakatika Kamati

Page 83: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

62

Kanuni za Kudumu za Bunge

(a) kumshauri Waziri, Kamati au Mbunge anayehusikana Muswada kufanya mabadiliko katika Muswadahuo; au

(b) kupitisha Azimio la kutoa Bungeni, taarifa maalumukuhusu Muswada huo.

(5) Baada ya Kamati kukamilisha kuujadili Muswada kwamara ya pili, Muswada huo utapelekwa katika Kamati ya BungeZima.

(6) Endapo Kamati iliyojadili Muswada kwa mara ya piliitaazimia kuwa taarifa maalumu juu ya Muswada huo itoleweBungeni, basi Mwenyekiti wa Kamati atamjulisha Spika na taarifahiyo itatolewa na Mwenyekiti au Mjumbe mwingine wa Kamati kwaniaba ya Mwenyekiti, kabla Muswada huo haujawasilishwa katikaKamati ya Bunge Zima.

88.-(1) Mtoa hoja au Mbunge mwingine anayekusudia kuwasilishamabadiliko katika Muswada unaojadiliwa, anaweza kumwombaSpika kwamba, hatua ya kuingia katika Kamati ya Bunge Zimaiahirishwe hadi wakati atakaoutaja katika ombi lake na Spikaatatoa uamuzi wake kadri atakavyoona inafaa.

(2) Mabadiliko yote yaliyopendekezwa kufanyika katikaMuswada wa Sheria sharti yawekwe katika Jedwali la Mabadilikolitakaloandaliwa kwa ajili hiyo na kugawiwa kwa Wabunge nakatika kujadili na ama kuyapitisha au kutoyapitisha, vyovyoteitakavyokuwa, mabadiliko hayo yatashughulikiwa kwa mpangilioutakaofuata na kwa kuzingatia mtiririko wa Ibara za Muswada waSheria unaohusika.

(3) Kwa madhumuni ya Bunge kujadili na ama kupitisha aukutopitisha, mabadiliko yaliyopendekezwa, Mtoa hoja atapewafursa ya kwanza kueleza mapendekezo yake kabla ya mabadilikomengine yatakayokuwa yamependekezwa na Wabunge wengine.

(4) Mabadiliko yoyote yaliyopendekezwa kufanyika katikaMuswada wa Sheria na kuwekwa katika Jedwali la Mabadilikohayataondolewa na Mtoa hoja, isipokuwa tu kwa idhini ya Spika.

(5) Mtoa hoja anayependekeza mabadiliko kufanywa katikaMuswada wa Sheria atawasilisha hoja yake ya mabadiliko hayokwa muda wa dakika tano.

Muswadakatika KamatiyaBunge Zima

Page 84: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

63

Kanuni za Kudumu za Bunge

(6) Endapo kuna mabadiliko mengine yamependekezwakufanyika katika Jedwali la Mabadiliko, basi mabadiliko hayoyaliyopendekezwa awali na ambayo yamo katika Jedwali laMabadiliko hayatahesabiwa kwamba yameondolewa hadimajadiliano juu ya mabadiliko hayo yatakapokuwa yamefikiamwisho au Waziri, Kamati ya Bunge au Mbunge aliyetoamapendekezo yaliyomo katika Jedwali la Mabadilikoatakapoomba kwa Spika mapendekezo yake yaondolewe.

(7) Mtoa hoja aliyependekeza mabadiliko yoyote kufanyikakatika Muswada wa Sheria na mapendekezo hayo kuwekwa katikaJedwali la mabadiliko atapewa nafasi ya kuwasilisha na kufungahoja yake ya mabadiliko.

(8) Baada ya Mtoa hoja kuhitimisha hoja yake ya mabadiliko,Spika atalihoji Bunge ili kupata uamuzi kuhusu hoja hiyo yamabadiliko.

(9) Muda wa kusema katika Kamati ya Bunge Zima kwawachangiaji mbalimbali wanaounga mkono hoja ya kufanyamabadiliko utakuwa dakika tatu.

(10) Kamati ya Bunge Zima itajadili na kupitisha au kufanyamabadiliko na kupitisha Muswada wa Sheria Ibara moja baada ya Ibara nyingine, isipokuwa kwamba, Mwenyekiti, akiona inafaa,anaweza kuihoji Kamati itoe uamuzi wake kwa sehemu moja yenyeIbara kadhaa au Ibara zote zilizomo katika sehemu moja yaMuswada.

89.-(1) Baada ya Kamati ya Bunge Zima kukamilisha kazi ya kupitiaMuswada wa Sheria, Bunge litarejea na Mtoa hoja atatoa taarifaBungeni kwa maneno yafuatayo:-

“Kamati ya Bunge Zima imeupitia Muswada wa Sheria, Ibarakwa Ibara na kuukubali bila mabadiliko, naomba kutoa hoja.” au kama kuna mabadiliko yaliyofanywa kwa manenoyafuatayo:- “Kamati ya Bunge Zima imeupitia Muswada wa Sheria,Ibara kwa Ibara na imeukubali pamoja na marekebishoyaliyofanyika, naomba kutoa hoja” na kisha atatoa hoja:

“Kwamba, Muswada wa Sheria wa …………sasa ukubaliwe”. au kama kuna mabadiliko yaliyofanywa katika Muswada kwa maneno yafuatayo:-

Taarifa baada ya Muswada Kusomwa Mara ya Pili

Page 85: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

64

Kanuni za Kudumu za Bunge

“Kwamba, Muswada wa Sheria wa …. Kama ulivyorekebishwaau kubadilishwa katika Kamati ya Bunge zima, sasa ukubaliwe.”

(2) Hoja ya kupitisha Muswada wa Sheria wa mabadilikoya Katiba itaamuliwa kwa mujibu wa Ibara ya 98 ya Katiba. Kwasababu hiyo, kura zitapigwa kwa kuita jina la Mbunge mmoja mmojakatika hatua ya Muswada huo Kusomwa Mara ya Pili.

90.- Mtoa hoja anayewasilisha Muswada wa Sheria anawezakuuondoa Muswada wakati wowote kabla ya Bunge kuhojiwakutoa uamuzi wake, baada ya kutoa taarifa kwa Spika.

91.- Baada ya Muswada wa Sheria Kusomwa Mara ya Tatu,utahesabika kuwa umepitishwa na Bunge.

92.-(1) Muswada kama ulivyopitishwa na Bunge, utatayarishwachini ya uangalizi na usimamizi wa Katibu kwa kuingiza mabadilikoyote yaliyofanyika na atawasilisha nakala moja ya Muswada huokwa Rais mapema ili Rais atoe kibali chake kwa mujibu wa Ibara ya97 (1) ya Katiba na pia nakala moja kwa Spika kwa taarifa.

(2) Nakala halisi ya Sheria iliyopata kibali cha Rais itahifadhiwana Katibu.

93.-(1) Bunge halitashughulikia hatua zaidi ya moja kwa Muswadawowote wa Sheria katika Mkutano mmoja wa Bunge.

(2) Bila ya kuathiri masharti ya fasili ya (1) ya Kanuni hii, Bungelinaweza kushughulikia Muswada wa Sheria katika hatua zaidi yamoja endapo:-

(a) hoja mahususi itatolewa kwamba Muswadahuo ushughulikiwe katika hatua zaidi ya moja;

(b) Spika ataridhika na hoja hiyo; na

(c) Bunge litaafiki hoja hiyo kwa kupiga kura.

KuondoaMuswadaBungeni

MuswadaKusomwaMaraya TatunakupitishwanaBunge

Ridhaaya Rais na hifadhiya Sheria

UtaratibuwaKusomaMiswadayaSheria

Page 86: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

65

Kanuni za Kudumu za Bunge

BungekukaakamaKamati yaMipango

(3) Masharti ya Fasili ya (1) ya Kanuni hii hayatatumika kwaMuswada wa Sheria ya Fedha, Muswada wa Matumizi ya Fedha naMuswada wowote unaowasilishwa kwa hati ya dharura.

SEHEMU YA TISA

UTARATIBU WA KUTUNGA SHERIAKUHUSU MAMBO YA FEDHA

94. (1) Katika Mkutano wake wa mwezi Oktoba – Novemba kwakila mwaka, Bunge kwa siku zisizopungua tano, litakaa kama Kamatiya Mipango ili kukidhi matakwa ya Ibara ya 63(3)(c) ya Katiba, kwakujadili na kuishauri Serikali kuhusu mapendekezo ya utekelezajiwa Mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali katikamwaka wa fedha unaofuata.

(2) Katika Mkutano huo, Bunge pamoja na mambo mengine,litafanya shughuli zifuatazo:-

(a) kupokea, kujadili na kutoa maoni na ushauri kuhusu mwongozo wa kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali;

(b) kupokea, kujadili na kutoa maoni na ushauri kuhusu vyanzo vya mapato ya Serikali; na

(c) kupokea, kujadili na kutoa maoni na ushauri kuhusu mapendekezo ya utekelezaji wa Mpango wa Serikali na vipaumbele kuhusu Mpango huo.

(3) Kwa madhumuni ya utekelezaji wa masharti ya fasili ya(1), Serikali itawasilisha kwa Katibu mapendekezo ya Mpango waTaifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali na nakala zitapelekwana kumfikia kila Mbunge siku saba kabla ya tarehe iliyopangwakujadili mapendekezo hayo.

Page 87: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

66

Kanuni za Kudumu za Bunge

(4) Kabla ya mapendekezo ya Mpango wa Taifaunaokusudiwa kutekelezwa na Serikali kuwasilisha Bungeni,mapendekezo hayo yatajadiliwa na Kamati ya Bajeti.

(5) Mjadala kuhusu mapendekezo ya mpango wa Taifa:

(a) utatanguliwa na maoni ya Mwenyekiti wa Kamati ya Bajeti iliyochambua mapendekezo hayo, na maoni ya Kambi ya Upinzani Bungeni;

(b) utaendelea kwa siku zisizopungua tano;

(c) utahitimishwa na Serikali kwa kutoa maelezo ya ufafanuzi katika maeneo mbalimbali yaliyotolewa maoni na ushauri na Wabunge.

(6) Mjadala wa mapendekezo ya Mpango wa Taifa utahusumambo ya jumla na Wabunge watachangia na kuishauri Serikalikuhusu utekelezaji wa sera za kiuchumi, za kifedha, za kodi navipaumbele katika mpango wa Bajeti ya Serikali ya mwaka wafedha unaofuata.

95.- Bunge halitashughulikia Muswada, hoja au ombi lolotelililotolewa na Mbunge au Kamati ya Kudumu ya Bunge endapoMwanasheria Mkuu wa Serikali atathibitisha kwamba, matokeo yaMuswada, hoja au ombi hilo yatakuwa ni:-

(a) kuweka masharti yanayoanzisha au kuongeza kodi yoyoteyanayoweza kuongeza kiwango cha matumizi ya fedhazitakazotolewa kutoka katika Mfuko Mkuu wa Hazina yaJamhuri ya Muungano au yanayofuta au kupunguza denilolote linalodaiwa kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano;au

(b) kubadilisha mishahara, marupurupu au masharti ya utumishi, ikiwa ni pamoja na likizo, usafiri na kupandishwa cheo kwa mtumishi yeyote wa umma au kufanya mabadiliko katika Sheria, Kanuni au taratibu zinazohusu pensheni, kiinua mgongo au marupurupu mengineyo ya mtumishi wa umma au ya mjane, watoto wanaomtegemea au wawakilishi wake.

M a s h a r t ikuhusu Miswada,Hoja na Maombi ya Fedha

Page 88: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

67

Kanuni za Kudumu za Bunge

96.(1) Kila ifikapo tarehe kumi ya mwezi Machi kila mwaka, kilaWizara itawasilisha kwa Katibu nakala za dondoo za vitabu vyaMakadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara kwa mwaka wa fedhaunaofuata, pamoja na nakala za randama za Makadirio hayokulingana na idadi ya Wajumbe wa Kamati, kwa ajili ya kuziwezeshaKamati za Bunge kufanya uchambuzi wa makadirio hayo.

(2) Kwa mujibu wa wa fasili (1), iwapo tarehe kumi ya mweziMachi itakuwa si siku ya kazi, uwasilishwaji huo utafanywa tareheinayofuata ya siku ya kazi.

97.- (1) Tarehe kumi na moja ya mwezi Machi ya kila mwaka autarehe ya siku nyingine ya kazi inayofuata iwapo tarehe hiyoitakuwa si siku ya kazi, Waziri anayehusika na masuala ya mipangoatawasilisha kwa Wabunge, mapendekezo ya Serikali ya mpangokwa mwaka wa fedha unaofuata.

(2) Kwa mujibu wa fasili (1), siku hiyo pia, Waziri anayehusikana masuala ya fedha, atawasilisha kwa Wabunge, mapendekezoya Serikali ya kiwango na ukomo wa Bajeti ya Serikali kwa mwakawa fedha unaofuata.

(3) Katika hatua ya uwasilishwaji wa mujibu wa fasili ya (1)na ya (2), hakutakuwa na mjadala wowote kuhusu mapendekezoya mpango na kiwango cha ukomo wa Bajeti ya Serikali kwa mwakawa fedha unaofuata.

(4) Baada ya mapendekezo ya mpango na kiwango chaukomo wa Bajeti ya Serikali kuwasilishwa kwa mujibu wa fasili ya (1)na (2) Spika atawasilisha mapendekezo hayo kwenye Kamati yaBajeti ili yafanyiwe uchambuzi na Kamati hiyo itazishauri Kamati zaBunge za Kisekta pamoja na Serikali kuhusu mapendekezo hayo.

98.-(1) Baada ya kuwasilishwa kwa mapendekezo ya mpango nakiwango na ukomo wa Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedhaunaofuata kwa Wabunge, Kamati za Bunge za Kisektazitatembelea na kukagua utekelezaji wa miradi iliyotengewa fedhakwa mwaka wa fedha unaoisha, kwa siku zisizozidi saba.

(2) Baada ya kutembelea miradi, Kamati za Bunge zaKisekta, kwa kipindi kisichozidi siku tisa, zitafanya vikao vyakuchambua taarifa

Kuwasi l i -shadondoonarandamaza vitabuvya Bajeti

Kuwasi l i -shamapende-kezoyampangona Bajeti

Kamatikukaguautekelezajiwamiradi

Page 89: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

68

Kanuni za Kudumu za Bunge

za utekelezaji wa Bajeti za Wizara inazozisimamia kwa mwaka wafedha unaoisha, kwa ajili ya kufanya ulinganisho kuhusu Makadirioya Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa fedha unaofuata.

(3) Siku moja kabla ya kufanya majumuisho kwa mujibu wafasili ya (4), Kamati ya Uongozi itafanya kikao cha mashauriano naKamati ya Bajeti kuhusu mambo muhimu yaliyojitokeza kwenyeKamati za Kisekta wakati wa kujadili utekelezaji wa Bajeti za Wizarakwa mwaka wa fedha unaoisha na Makadirio ya Matumizi yaSerikali kwa mwaka wa fedha unaofuata.

(4) Katika kipindi cha siku tatu kabla ya Mkutano wa Bajetikuanza, na wakati Kamati za Bunge za Kisekta zikiendelea na shughulizake, Serikali kwa kushauriana na Kamati ya Bajeti, itafanyamajumuisho kuzingatia ushauri wa Kamati za Bunge za Kisektakuhusu utekelezaji wa Bajeti za Wizara kwa mwaka wa fedhaunaoisha, na maombi ya fedha kwa mwaka wa fedha unaofuata.

(5) Baada ya Kamati ya Bajeti kushauriana na Serikali kwamujibu wa fasili (4), Kamati ya Uongozi itafanya kikao na Kamati yaBajeti kwa ajili ya kupata taarifa ya matokeo ya mashauriano katiya Kamati hiyo na Serikali.

99.-(1) Katika Mkutano wa Bunge wa Bajeti utakaonza mapemamwezi Aprili kwa kila mwaka, jumla ya siku zisizozidi hamsini na nanezitatengwa kwa ajili ya Bunge kujadili utekelezaji wa Wizara zotewa Bajeti kwa mwaka wa fedha unaoisha, pamoja na Makadirio yaMatumizi ya Serikali kwa mwaka wa fedha unaofuata.

(2) Mjadala katika Bunge la Bajeti kwa kila mwaka utaanzana Hotuba ya Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu, na kufuatiwa na Hotubaza Bajeti za Wizara nyingine zote, kwa utaratibu utakaopangwa naSpika, baada ya kushauriana na Kamati ya Uongozi.

(3) Shughuli za Bajeti zitapewa nafasi ya kwanza kabla yaShughuli nyingine yoyote, na zitawekwa kwanza kwenye Orodhaya Shughuli za kikao kila siku hadi pale zitakapokuwa zimemalizika,isipokuwa kama Bunge litaamua vinginevyo.

(4) Kabla ya taarifa za utekelezaji na Makadirio ya Matumiziya Wizara kujadiliwa Bungeni, zitachambuliwa na Kamati za Bungeza Kisekta, kwa utaratibu uliowekwa na fasili ya 98(2) ya Kanuni hii,na pia katika Nyongeza ya Nane ya Kanuni hizi.

Kujadiliutekele-zaji waBajeti zaWizara

Page 90: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

69

Kanuni za Kudumu za Bunge

(5) Asubuhi ya siku ambayo Waziri amepangiwa kuwasilisha hojaya Makadirio ya Wizara yake, Waziri, Mwenyekiti wa Kamatiinayohusika au mjumbe yeyote atakayeteuliwa kwa niaba yake,na Msemaji wa Kambi ya Upinzani kwa Wizara husika WatawekaMezani nakala ya taarifa zao kwa kuzingatia mpangilio wa Shughuliza Bunge.

(6) Pamoja na kuwasilisha mezani nakala ya Hotuba ya hoja yaMakadirio ya Wizara, Waziri atawasilisha pia nakala 10 za randamaya makadirio hayo, siku moja kabla ya siku ambayo Hotuba yakeimepangwa Kusomwa Bungeni.

(7) Wakati utakapofika wa kuwasilisha Hotuba ya Bajeti yaWizara inayohusika, hoja itatolewa kwa maneno yafuatayo:-

“Kwamba sasa Bunge likubali kujadili na kupitisha Makadirioya Matumizi ya Wizara yangu.”

(8) Isipokuwa kwa Hotuba ya Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu,muda wa Waziri anayewasilisha Hotuba ya Bajeti utakuwa ni dakikazisizozidi sitini.

(9) Baada ya Waziri kuwasilisha Hotuba ya Bajeti kwa mujibu wafasili (1), Mwenyekiti wa Kamati iliyopitia Makadirio husika naMsemaji wa Kambi ya Upinzani watatoa maoni yao kwa mudausiozidi dakika thelathini kila mmoja.

(10) Wakati wa kujadili Makadirio ya Matumizi ya Wizara, mudawa Wabunge kuchangia utatolewa kulingana na uwiano wa idadiya Wabunge kutoka katika kila Chama.

(11) Idadi ya Wabunge watakaopewa nafasi ya kuchangiaMakadirio ya Matumizi ya Wizara kwa mujibu wa fasili (10)utaamauliwa na Spika.

(12) Mbunge anayejadili Makadirio ya Matumizi ya Wizaraataruhusiwa kusema kwa muda usiozidi dakika kumi:

Isipokuwa kwamba, Kambi za Vyama zinaweza kupendekeza kwa Spika kugawa muda huo kwa Wabunge wasiozidi wawili, mapema kabla ya mjadala huo kuanza.

Page 91: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

70

Kanuni za Kudumu za Bunge

(13) Endapo Spika ataona kuwa muda uliotengwa kwa ajili yakujadili Bajeti ya Wizara inayohusika umekaribia kwisha, atafungamjadala ili kumpatia Waziri mtoa hoja nafasi ya kujibu ndani yamuda wa dakika sitini.

(14) Bila ya kuathiri masharti ya Kanuni ya 154, maneno yoyoteya utangulizi, utambulisho, salamu za pole, pongezi au shukrani,pamoja na kutaja majina ya Wabunge waliochangia hojahavitaruhusiwa kwa Mbunge au Waziri wakati wa kujadili Hotubaya Bajeti.

100.- Mjadala wa jumla kuhusu Makadirio ya Matumizi kwa Wizarautakapomalizika, Bunge litaingia katika Kamati ya Matumizi ilikupitisha Makadirio ya Wizara husika kifungu kwa kifungu.

101.-(1) Katika Kamati ya Matumizi, Mwenyekiti atawahoji Wajumbekuhusu kifungu kimoja kimoja cha Makadirio ya Matumizi, na kilakifungu kitaafikiwa peke yake.

(2) Mbunge yeyote anaweza kuomba ufafanuzi au maelezozaidi katika Kifungu chochote cha Fungu linalohusika, wakatiKifungu hicho kitakapofikiwa na Kamati ya Matumizi.

(3) Mbunge atakayeamua kutumia kifungu chenye mshaharawa Waziri, ataruhusiwa tu iwapo ataomba ufafanuzi wa sualamahsusi la sera na hatazungumzia zaidi ya jambo moja.

(4) Kwa kuzingatia masharti ya fasili ya (3), Kamati za Vyamazitawasilisha kwa Spika majina ya Wabunge watakaoomba kupataufafanuzi wa suala mahsusi la sera, na Spika atatoa nafasi kwaWabunge kwa kuzingatia uwiano.

(5) Muda wa kusema katika Kamati ya Matumizi kwa ajili yakuomba au kutoa ufafanuzi hautazidi dakika tano.

102.-(1) Katika Kamati ya Matumizi, Mbunge yeyote anaweza kutoahoja ya kutaka kufanya mabadiliko katika Makadirio ya Matumiziya Serikali iwapo mabadiliko hayo hayatabadili madhumuni yaFungu.

(2) Endapo hoja iliyotolewa kwa ajili ya kupunguza kifungu fulanikatika Fungu lolote haijapitishwa, hoja nyingine bado inawezakutolewa kwa madhumuni ya kupunguza kifungu kingine cha Funguhilo hilo.

KamatiyaMatumizi

MjadalakatikaKamatiyaMatumizi

KubadilishaMakadiriokatikaKamati yaMatumizi

Page 92: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

71

Kanuni za Kudumu za Bunge

103.-(1) Kwa kuzingatia utaratibu wa majadiliano uliowekwa naKanuni hizi, Mbunge yeyote anaweza kuomba ufafanuzi aumaelezo zaidi katika kifungu chochote cha Fungu linalohusika,wakati kifungu hicho kitakapofikiwa na Kamati ya Matumizi.

(2) Vilevile Mbunge yeyote anaweza kutoa hoja ya kuondoashilingi moja katika kifungu chochote cha Fungu hilo.

(3) Madhumuni ya hoja ya aina hiyo ni kumwezesha Mbungealiyeitoa aweze kueleza kutoridhika kwake na utekelezaji wajambo fulani mahsusi ambalo dhahiri linahusika na kifungu hicho.

(4) Hoja ya aina hiyo itatolewa kwa muda usiozidi dakika tano.

(5) Wabunge wanaweza kuchangia hoja ya kuondoa shilingimoja iliyoanzishwa kwa mujibu wa fasili ya (2) kwa muda usiozididakika tatu kila mmoja.

(6) Waziri anayehusika atapewa nafasi ya kutoa majibu ya hojahiyo.

(7) Mbunge aliyetoa hoja ya kuondoa shil ingi ndiyeatakayefunga mjadala wa hoja hiyo.

(8) Muda utakaotumiwa na Waziri na Mbunge kwa mujibu wafasili ya (6) na (7) utaamuliwa na Spika.

(9) Endapo Mbunge atashikilia hoja ya kuondoa shilingi mojakatika kifungu hicho, basi kura itapigwa kwa kuhoji wanaoafiki nawasioafiki hoja hiyo.

(10) Endapo hoja ya kuondoa shilingi moja katika kifunguchochote itakubalika, basi kifungu hicho kitakuwa kimepitishwakikiwa pungufu ya hiyo shilingi moja.

(11) Endapo hoja iliyotolewa kwa ajili ya kuondoa shilingi mojakatika kifungu chochote cha Fungu linalohusika imekataliwa, hojanyingine yenye madhumuni ya kuondoa shilingi moja katika kifungukingine cha Fungu hilo hilo bado inaweza kutolewa.

104.-(1) Iwapo zimesalia dakika kumi kabla ya kufikia muda wakuahirisha kikao cha Bunge na Kamati ya Matumizi bado haijamaliza

KukamilikamjadalakatikakamatiyaMatumizi

Hoja yakuondoashilingikwenyeMakadirio

Page 93: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

72

Kanuni za Kudumu za Bunge

HotubayaBajetiyaSerikaliKusomwaBungeni

kupitisha mafungu, Mwenyekiti anaweza kuongeza mudausiozidi dakika thelathini bila kuihoji Kamati ili kukamilisha Shughuliya kupitisha mafungu yaliyobaki.

(2) Iwapo zimesalia dakika kumi kabla ya kumalizika mudaulioongezwa chini ya fasili ya (1) na Kamati bado haijamalizakupitisha mafungu yote, Mwenyekiti atafunga mazungumzoyanayoendelea na papo hapo atawahoji Wajumbe kuhusumafungu yaliyosalia, kama yapo.

(3) Baada ya Kamati ya Matumizi kumaliza kazi ya kupitishaMakadirio ya Matumizi ya Wizara na Bunge kurudia, waziri mtoahoja atatoa taarifa kwamba:-

(a) “Mheshimiwa Spika, Bunge lako likikaa kama Kamatiya Matumizi limekamilisha kazi zake”; na kuombakwamba:

(b) “Taarifa ya Kamati ya Matumizi ikubaliwe na Bunge”; naatahitimisha kwa kusema: “Naomba kutoa hoja”.

(4) Spika atawahoji Wabunge kwa kuuliza, “Wanaoafikiwaseme Ndiyo”, na “Wasioafiki waseme Siyo”.

105.-(1) Baada ya Bunge kukamilisha mjadala wa Makadirio yaWizara zote, ndani ya siku sita kabla ya Hotuba ya Bajeti KusomwaBungeni, Serikali kwa kushauriana na Kamati ya Bajeti itafanyamajumuisho kwa ajili ya kuzingatia hoja zilizojitokeza wakati wakujadili utekelezaji wa Bajeti za Wizara kwa mwaka wa fedhaunaoisha, na Makadirio ya Matumizi ya Wizara hizo kwa mwaka wafedha unaofuata.

(2) Katika kipindi cha kufanya majumuisho kwa mujibu wa fasiliya (1), Bunge litaendelea na shughuli zake nyingine kamazitakavyokuwa zimepangwa na Spika baada ya kushauriana naKamati ya Uongozi.

(3) Wakati Serikali ikifanya majumuisho kwa mujibu wa fasili ya(1), wajumbe wa Kamati ya Uongozi kwa nafasi zao, watakuwawajumbe wa Kamati ya Bajeti.

Page 94: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

73

Kanuni za Kudumu za Bunge

(4) Makadirio ya Fedha za Matumizi ya Serikali yatawasilishwaBungeni na Waziri anayehusika na masuala ya fedha kwa Hotubakuhusu Makadirio hayo itakayoitwa “Hotuba ya Bajeti ya Serikali:ambayo itasomwa Bungeni kabla ya tarehe ishirini ya mwezi Junikila mwaka.

(5) Muda wa kusoma Hotuba ya Bajeti ya Serikali utaamuliwa naSpika kadri atakavyoona inafaa.

(6) Hoja ya kuwasilisha Makadirio hayo itakuwa katika manenoyafuatayo:

“Kwamba Bunge likubali kupitisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha wa ...”

(7) Siku ya kuwasilisha Bungeni Hotuba ya Bajeti ya Serikali, nafasipia itatolewa kwanza kwa Waziri anayehusika na mipango auuchumi kutoa maelezo kuhusu hali ya uchumi kwa ujumla.

(8) Hotuba ya Bajeti ya Serikali na ya Waziri anayehusika namipango, zitafuatiwa na hotuba za Mwenyekiti wa Kamati ya Bajeti,na Msemaji wa Kambi ya Upinzani.

(9) Muda wa kusoma maoni ya Kamati na ya Kambi ya Upinzani,utakuwa dakika zisizozidi thelathini kwa kila hotuba.

106.-(1) Mjadala kuhusu Hotuba ya Bajeti ya Serikali utaendeleakwa siku zisizozidi saba, ambapo dakika zisizozidi kumi zitatolewakwa kila Mbunge anayetaka kuchangia Hotuba hiyo.

(2) Katika hatua hii, majadiliano yatahusu mambo ya jumlakuhusiana na hali ya uchumi, na Mbunge yeyote hataruhusiwakupendekeza mabadiliko katika Makadirio ya Mapato na Matumiziya Serikali.

107.(1) Mjadala kuhusu Hotuba ya Bajeti ya Serikali utakapomalizika,Spika atalihoji Bunge litoe Uamuzi wake wa kupitisha aukutokupitisha Bajeti ya Serikali ili kukidhi matakwa ya Ibara ya90(2)(b) ya Katiba.

(2) Uamuzi wa Bunge wa kupitisha au kutokupitisha Bajeti yaSerikali utafanywa kwa kupiga kura ya wazi kwa kuita jina la Mbungemmoja mmoja.

UtaratibuwakuidhinishaMakadirioyaMatumiziya Serikali

MjadalakuhusuHotubaya Bajeti

Page 95: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

74

Kanuni za Kudumu za Bunge

108.-(1) Kabla ya tarehe 30 ya mwezi Juni kwa kila mwaka, baadaya Bunge kukamilisha kazi ya kujadili na kupitisha Bajeti ya Serikalikwa mwaka unaohusika, Muswada wa Sheria ya Fedha zaMatumiziutawasilishwa Bungeni na kupitishwa mfululizo katikahatua zake zote.

(2) Kwa madhumuni ya Kanuni hii, “Muswada wa Fedha zaMatumizi” maana yake ni Muswada wa Sheria ya Fedha za Matumiziya Serikali kwa mwaka wa fedha unaofuata.

(3) Muswada wa Fedha za Matumizi hautapelekwa kwenyeKamati yoyote ya Kudumu wala Kamati ya Bunge Zima, na mashartikuhusu Miswada Kusomwa Mara ya Kwanza hayatatumika.

(4) Muswada wa Fedha za Matumizi hautatangazwa kwenyeGazeti kabla haujawasilishwa Bungeni.

109.-(1) Baada ya Bunge kukamilisha kazi ya kupitisha Muswadawa Fedha za Matumizi, Muswada wa Sheria ya Fedha utajadiliwana kupitishwa kwa kuzingatia masharti yaliyowekwa na Sehemu yaNane ya Kanuni hizi.

(2) Marekebisho au mabadiliko ya kupunguza kiwango cha kodikatika Ibara yoyote ya Muswada wa Sheria ya Fedhayatakayopendekezwa na Mbunge yeyote hayatakubaliwa iwapohayatatoa mapendekekezo mbadala yanayoziba pengolinalotokana na punguzo linalopendekezwa.

110.- Mapendekezo yoyote kwa ajili ya Matumizi ya Nyongezaya Fedha za Serikali au kwa ajili ya kuto fedha yoyote ya nyongezazaidiya Fedha za Matumiziya Mwaka huo:-

(a) yataitwa Makadirio ya Nyongeza ya Matumizi;

(b) yatapelekwa kwenye Kamati ya Matumizi kufuatana na masharti ya Ibara ya 99 ya Katiba; na

(c) yatafuata masharti ya Kanuni zote zinazohusu Makadirio ya Mwaka ya Matumizi ya Serikali.

MuswadawaSheriaya Fedha

M a k a d i r i oyamatumiziyaNyongeza

MuswadawaFedhazaMatumizi

Page 96: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

75

Kanuni za Kudumu za Bunge

SEHEMU YA KUMI

KAMATI ZA BUNGE

111.-(1) Kutakuwa na Mkutano wa Wabunge wote ambao unawezakuitishwa na Spika siku moja kabla au wakati wa Mkutano wowotewa Bunge.

(2) Mkutano wa Wabunge wote utajadili masuala yote yenyemaslahi kwa Wabunge na utaipa Serikali fursa ya kutoa taarifambalimbali kwa Wabunge kuhusu hali ya nchi kwa ujumla.

(3) Mwenyekiti wa Kikao cha Mkutano wa Wabunge wote atakuwaKiongozi wa Shughuli za Serikali Bungeni.

112.-(1) Wabunge wa kila Chama cha Siasa kinachowakilishwaBungeni wanaweza kuunda Kamati ya Wabunge wa Chama kwakuzingatia Katiba, Kanuni na Taratibu za Chama kinachohusika.

(2) Endapo makubaliano yamefikiwa baina ya Vyama viwili auzaidi vya Upinzani vyenye idadi sawa ya Wabunge ambao ni zaidiya asilimia kumi na mbili na nusu basi Wabunge wa Kambi yaUpinzani wanaweza kuunda Kamati ya Wabunge wote wa Kambiya Upinzani.

113.-(1) Kamati za Vyama vya Siasa Bungeni zitajiwekea utaratibukwa ajili ya uendeshaji wa shughuli.

(2) Majadiliano yote kwenye mikutano ya Kamati pamoja namambo mengine yote yanayohusu Kamati hizo yatakuwa na hadhi,kinga na nafuu zote zinazotolewa kwa mujibu wa Sheria kuhusumajadiliano, kumbukumbu na mambo mengineyo ya Bunge navikao vyake kwa mujibu wa masharti ya Ibara ya 100 (1) na (2) yaKatiba na Sheria ya Kinga, Madaraka na Haki za Bunge.

` `

MkutanowaWabungewote

MikutanoyaKamatiza VyamavyaSiasa

KamatizaVyamavyaSiasa

Page 97: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

76

Kanuni za Kudumu za Bunge

(3) Mjumbe yeyote anaweza kuchangia katika hoja yakutaka ufafanuzi iliyoanzishwa kwa mujibu wa fasili ya (2) (b).

(4) Muda wa kusema katika kuchangia hoja ya ufafanuzihautazidi dakika tano.

(5) Mjumbe yeyote anayetaka kutoa hoja kwambamajadiliano ya Kamati ya Bunge Zima yaahirishwe mpaka wakatimwingine, anaweza kutoa hoja hiyo wakati wowote, kwa manenoyafuatayo:

“Kwamba Waziri au Mbunge atoe taarifa kwa Bunge juu yamaendeleo ya kazi ya Kamati hii na kuomba ruhusa Kamati hiiikutane tena baadae.”

(6) Bunge litakaporudia, Waziri au Mbunge aliyehusika nashughuli zilizokuwa zikifanywa na Kamati atasimama mahali pakena kuliarifu Bunge kwamba Kamati imeshughulikia maendeleo lakinihaikukamilisha kazi yake.

114.- Kwa kufuata yaliyomo kwenye Orodha ya Shughuli au kwamujibu wa Kanuni hizi, ukifika wakati wa Bunge au Bunge likihitajiwa kuingia katika Kamati ya Bunge Zima, Spika ataondoka kwenyeKiti chake bila hoja yoyote kutolewa.

Akidi naUtaratibukatikaKamatiyaBungeZima

KamatiyaBungeZima

115.-(1) Masharti ya Kanuni ya 77 yatatumika kuhusu Kamati yaBunge Zima, ila tu kama idadi ya Wabunge waliohudhuria itakuwabado haifikii nusu ya Wabunge wote baada ya kipindi kilichowekwana Kanuni ya 77(3), Mwenyekiti ataondoka kwenye Kiti, Bungelitarudia na Katibu atahesabu idadi ya Wabunge waliohudhuria nakama idadi yao itakuwa bado haifikii nusu ya Wabunge wote, basiSpika ataahirisha Bunge.

(2) Kanuni za Bunge zinazohusu mwenendo wa Bungezitatumika katika Kamati ya Bunge Zima isipokuwa kwamba katikaKamati hiyo:-

(a) hoja ikitolewa haitahitaji kuungwa mkono;

(b) Kwa idhini ya Mwenyekiti, Mjumbe anayetakaufafanuzi anaweza kuzungumza mara mbili juu yasuala hilo.

Page 98: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

77

Kanuni za Kudumu za Bunge

(7) Mara tu baada ya Waziri au Mbunge aliyehusika nashughuli zilizokuwa zikifanywa na Kamati kuliarifu Bunge kuhusukutokamilika kwa kazi yake, Spika atalitaarifu Bunge siku na wakatiambapo Kamati itaendelea na kazi yake.

(8) Kamati ya Bunge Zima itafikiria mambo yale tuyatakayopelekwa na Bunge kwenye Kamati hiyo.

(9) Kamati ya Bunge Zima inaweza kuamua, baada ya hojakutolewa, kwamba shughuli iliyo mbele yake wakati huo irudishweau ipelekwe kwenye Kamati ya Kudumu inayohusika.

(10) Baada ya Kamati ya Bunge Zima kukamilisha shughulizake, Mwenyekiti ataondoka kwenye Kiti na kurejea kwenye Kiticha Spika ambapo Bunge litarudia.

116.-(1) Mbunge yeyote ambaye si Waziri au Mwanasheria Mkuuwa Serikali anaweza kuteuliwa kuwa Mjumbe wa Kamati ya Kudumuya Bunge yoyote ambayo inahusika na Kanuni hii na Waziri mwenyedhamana ya jambo lolote linalopelekwa au kujadiliwa na Kamati,pamoja na Naibu Waziri aliyeteuliwa kumsaidia Waziri huyo,watakuwa wajumbe wa Kamati wakati Kamati itakapokuwainashughulikia jambo hilo.

(2) Bila ya kujali masharti ya fasili ya (1) ya Kanuni hii, Mbungeyeyote ambaye ni Mkuu wa Mkoa au Mkuu wa Wilayahatachaguliwa kuwa Mjumbe wa Kamati ya Hesabu za Serikali naKamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa.

(3) Wajumbe wa Kamati zote watateuliwa na Spika kwanamna ambayo itawezesha kila Mbunge kuwekwa kwenye Kamatimojawapo.

(4) Wajumbe walioteuliwa kwenye Kamati ya Kanuni za Bungena Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge wanaweza piakuteuliwa kwenye Kamati nyingine.

(5) Wakati wa kuteua Wabunge kuwa Wajumbe wa Kamatimbalimbali, Spika:-

MuundowaKamatizaKudumuzaBunge

Page 99: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

78

Kanuni za Kudumu za Bunge

(a) atateua idadi ya Wabunge inayolingana kwakila Kamati, isipokuwa kama imeelekezwavinginevyo katika Kanuni hizi;

(b) atazingatia aina zote za Wabunge na kuwateuaWabunge wa aina mbalimbali kwa kila Kamati,akiongozwa na kigezo cha asilimia ya kila ainaya Wabunge hao ilivyo Bungeni;

(c) kwa kadri inavyowezekana, atayapa kipaumbelematakwa ya Wabunge wenyewe, lakinihatalazimika kutosheleza kila takwa au ombi;

(d) atazingatia haja kwa kila Kamati kuwa naWabunge wenye uzoefu au ujuzi maalumu kuhusukazi za Kamati hiyo.

(6) Katibu atahakikisha kuwa Wabunge wote wanapewaorodha inayoonesha jinsi walivyoteuliwa katika Kamati mbalimbali.

(7) Ujumbe katika Kamati za Kudumu za Bunge utadumumpaka mwisho wa Mkutano wa Kumi wa Bunge ambao ni nusu yakwanza ya maisha ya Bunge.

(8) Bila ya kuathiri masharti ya fasili ya (7) ya Kanuni hii,Mbunge yeyote anaweza kuteuliwa tena katika Kamati aliyokuwaanaitumikia katika nusu ya kwanza ya maisha ya Bunge.

(9) Bila ya kuathiri masharti ya fasili ya (7) ya Kanuni hii,Mbunge atakoma kuwa Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bungeendapo atateuliwa kuwa Waziri au kuchaguliwa kuwa Spika auNaibu Spika.

(10) Wajumbe wa kila Kamati watawachagua Mwenyekitina Makamu Mwenyekiti kutoka miongoni mwao ambao kwa mudawote watakaokuwa Wabunge, wataendelea kushika nafasi hizompaka mwisho wa kipindi kilichotajwa katika fasili ya (7) ya Kanunihii, lakini wanaweza kuchaguliwa tena.

11) Wenyeviti wa Kamati za Bunge zinazosimamia matumiziya fedha za Umma ambazo ni Kamati ya Hesabu za Serikali naKamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa watachaguliwa kutokamiongoni mwa Wajumbe wa Kamati hizo ambao wanatoka katikaKambi Rasmi ya Upinzani Bungeni.

Page 100: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

79

Kanuni za Kudumu za Bunge

117.-(1) Masharti ya Kanuni hii yatatumika kwa Kamati zote zakudumu.

(2) Mwenyekiti ataongoza vikao vyote vya Kamati naendapo Mwenyekiti hayupo kwenye kikao, Makamu Mwenyekitiataongoza shughuli za kikao hicho na ikiwa Mwenyekiti na Makamuwake wote hawapo, wajumbe waliohudhuria watamchaguammojawapo miongoni mwao kuongoza kikao hicho.

(3) Kamati ya Kudumu itakutana kila inapoitwa na Spika,Naibu Spika au na Mwenyekiti wake baada ya kupata idhini yaSpika.

(4) Mikutano ya kawaida ya Kamati za Kudumu itafanyikaDodoma, Dar es Salaam au Zanzibar.

(5) Kila Kamati itafanya vikao vyake kwa kuzingatia bajetiya Kamati husika ambayo imeidhinishwa kwa mwaka huo wa fedha.

(6) Akidi ya mkutano wowote wa Kamati ya Kudumuitakuwa theluthi moja ya Wajumbe wote wa Kamati.

(7) Mambo yote yatakayojadiliwa na Kamatiyataamuliwa kwa kufuata maoni ya walio wengi kati ya Wajumbewa Kamati waliohudhuria na kupiga kura.

(8) Bila ya kuathiri masharti yaliyotangulia ya Kanuni hii, kila Kamatiitajiwekea utaratibu wake, na Kamati inaweza kuwaruhusuWabunge ambao si Wajumbe wa Kamati au watu ambao siWabunge kuhudhuria na kushiriki katika shughuli za Kamati, lakinihawatakuwa na haki ya kupiga kura.

(9) Shughuli za kawaida za Kamati zitaendeshwa kwa uwaziambapo Kamati itaalika wadau ili kupata maoni na ushauri waokwa ajili ya kuboresha Muswada au jambo ambalo litakuwalinashughulikiwa na Kamati hiyo.

(10) Bila ya kujali masharti ya fasili ya (9) ya Kanuni hii, shughulizote za Kamati zinazohusu kuandaa na kutoa mapendekezo yakuwasilishwa Bungeni zitafanywa kwa faragha.

UtaratibukatikaKamatizakudumuzaBunge

Page 101: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

80

Kanuni za Kudumu za Bunge

(11) Maoni ya Kamati yatakuwa ni yale yaliyokubaliwa nawajumbe walio wengi na kuwasilishwa Bungeni na Mwenyekiti auMjumbe mwingine.

(12) Mjumbe yeyote wa Kamati hataruhusiwa kuzungumziahadharani maoni ya Kamati kuhusu Muswada au jambo lolotelitakalokuwa linashughulikiwa na Kamati kabla maoni hayohayajawasilishwa rasmi Bungeni.

(13) Mwanasheria Mkuu wa Serikali na au mwakilishi wake,atahudhuria kila mkutano wa kila Kamati ya Kudumu inapokuwainachambua Muswada wa Sheria.

(14) Kamati yoyote ambayo Spika atapeleka kwake kwanzaMuswada au jambo lingine lolote, itahesabiwa kuwa ndiyo Kamatiinayohusika kushughulikia Muswada huo au jambo hilo.

(15) Itakuwa ni lazima kwa kila Kamati ya Kudumu ya Bungekuwasilisha Bungeni taarifa ya mwaka ya shughuli zake kwamadhumuni ya kujadiliwa katika Mkutano wa mwisho kabla yaMkutano wa Bajeti.

(16) Taarifa ya Kamati inapowasilishwa Bungeni, itashughulikiwakwa kufuata mpangilio wa Shughuli za Bunge.

(17) Spika ataweka utaratibu wa kujadili taarifa za Kamati naendapo Kamati yoyote katika kutekeleza majukumu yake, itaonakuwa kuna mambo ya utekelezaji ambayo yanahitaji kurekebishwa,inaweza kutoa taarifa maalumu ya ushauri kwa Waziri mwenyedhamana juu ya mambo hayo ili Waziri aweze kuchukua hatuazinazostahili.

(18) Kamati yoyote inaweza kuunda Kamati Ndogo kwa ajiliya utekelezaji bora wa Shughuli zake, kadri itakavyoona inafaa nakila Kamati Ndogo itapangiwa kazi zake na Kamati ya Kudumuinayohusika.

(19) Mjumbe wa Kamati yoyote hataruhusiwa kuzungumzia aukushughulikia jambo lolote lililofikishwa katika Kamati iwapo anamaslahi binafsi katika jambo hilo au idara hiyo isipokuwa anawezakufanya hivyo baada ya kutaja jinsi anavyohusika na kiwango chamaslahi hayo.

Page 102: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

81

Kanuni za Kudumu za Bunge

118.-(1) Kutakuwa na Kamati za Kudumu za Bunge kamazilivyoainishwa kwenye Nyongeza ya Nane ya Kanuni hizi.

(2) Muundo na majukumu ya Kamati za Kudumu za Bungeyameainishwa kwenye Nyongeza ya Nane ya Kanuni hizi.

119. Mbali na majukumu ya msingi ambayo yameorodheshwa kwakila Kamati ya Kudumu, Kamati yoyote inaweza kupendekeza kwaSpika ipewe majukumu ya nyongeza ambayo yatatajwa katikapendekezo hilo, na vilevile Spika anaweza kukabidhi jambo linginelolote kwa Kamati yoyote kadri atakavyoona inafaa, kwa ajili yakufanyiwa kazi na Kamati hiyo.

120.-(1) Kamati Teule inaweza kuundwa na Bunge kwa madhumunimaalumu kwa hoja mahsusi itakayotolewa na kuafikiwa.

(2) Bila ya kuathiri masharti ya fasili ya (1) ya Kanuni hii,baada ya kujadili hoja yoyote, Bunge linaweza kuunda Kamati Teulekwa madhumuni ya kushughulikia jambo lolote lililotokana na hojahiyo kwa utaratibu ufuatao:-

(a) Baada ya hoja iliyokuwa ikijadiliwa kuamuliwa,Mbunge yeyote mwenye nia ya kutoa hoja chiniya Kanuni hii anaweza kusimama mahali pake nakutoa taarifa ya mdomo kwamba anakusudiakutoa hoja ya kuunda Kamati Teule;

(b) Mbunge ambaye anakusudia kutoa hoja yakuunda Kamati Teule atawasilisha taarifa ya hojayake kwa maandishi kwa Katibu na hoja hiyoitashughulikiwa wakati unaofaa kwa kuzingatiampangilio wa shughuli kama ulivyoainishwa chiniya Kanuni ya 30 (4).

(3) Bunge litapeleka jambo linalotokana na hoja iliyokuwaikijadiliwa Bungeni kwenye Kamati Teule.

(4) Wajumbe wa Kamati Teule watateuliwa na Spika nawatamchagua Mwenyekiti wa Kamati hiyo kutoka miongoni mwao.

KamatizaKudumuzaBunge

Majukumuya jumlayaKamatizaKudumuza Bunge

UtaratibuwaKuundaKamatiTeule

Page 103: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

82

Kanuni za Kudumu za Bunge

TaarifayaKamatiTeule

121.- (1) Kila Kamati Teule itakuwa na Wajumbe wasiozidi watano.

(2) Akidi ya vikao vya Kamati Teule itakuwa ni theluthi mbiliya wajumbe wake.

(3) Kamati Teule itafanya kikao chake cha kwanza mahalina saa atakayoamua Mwenyekiti na vikao vinginevyo vitafanyikakwa wakati na mahali popote itakapoamua.

(4) Mwenyekiti ataongoza vikao vyote vya Kamati Teule, naiwapo Mwenyekiti hayupo katika kikao chochote, Wajumbewaliohudhuria watamteua mmoja wao kuwa Mwenyekiti wa kikaohicho.

(5) Endapo kwa sababu yoyote Mjumbe yeyote wa KamatiTeule atashindwa kufanya kazi yake, Spika atamteua Mbungemwingine kushika nafasi yake.

(6) Majadiliano ya Kamati Teule yatahusu tu mamboyaliyopelekwa kwake na Bunge na yatakuwa ya wazi au sirikufuatana na Kamati itakavyoamua kulingana na masuala husika.

122.-(1) Kamati Teule itatoa taarifa Bungeni kuhusu maoni nauchunguzi wake pamoja na kumbukumbu za ushahidi uliopokelewana vilevile inaweza kutoa taarifa maalumu juu ya mambo yoyoteambayo itaona yanafaa kuwasilishwa Bungeni.

(2) Taarifa ya Kamati Teule itawasilishwa Bungeni naMwenyekiti. (3) Iwapo baada ya hoja kutolewa, Bunge litaamua kujadilitaarifa hiyo, hoja itakayotolewa Bungeni itakuwa ni kwa madhumuniya kuliomba Bunge likubali mapendekezo yaliyomo katika taarifahiyo.

(4) Bunge linaweza kuamua vinginevyo kwa kutumiautaratibu wa kubadilisha hoja ambao umeelezwa katika Kanuni ya57 ya Kanuni hizi.

(5) Katibu wa Kamati Teule ataweka kumbukumbuzinazoonesha majina ya Wajumbe waliohudhuria mikutano yaKamati na maamuzi yaliyofanyika.

AkidinautaratibuwaVikaovyaKamatiTeule

Page 104: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

83

Kanuni za Kudumu za Bunge

(6) Kumbukumbu zitakazowekwa kwa mujibu wa mashartiya fasili ya (5) ya Kanuni hii zitawekwa saini na Mwenyekiti naWajumbe wa Kamati na zitaambatishwa kwenye Taarifa ya Kamatina kuwasilishwa Bungeni pamoja na taarifa hiyo.

123.- Taarifa yoyote ya Kamati inayowasilishwa Bungeni itakuwakatika muundo ufuatao:-

(a) Sehemu ya Utangulizi, ambayo itaoneshahadidu za rejea ambazo Kamati ilipewa;maelekezo yoyote yaliyotolewa kwa Kamati,njia au mbinu zilizotumika na Kamati katikakutekeleza majukumu yake, pamoja na mambomengine, kama yapo, ambayo yalijitokezawakati wa uchunguzi;

(b) Sehemu ya Katikati, ambayo itatoa maelezokamili kuhusu jambo au mambo yoteyaliyofanyiwa Uchunguzi na Kamati; na

(c) Sehemu ya Mwisho, ambayo itatoa maoni namapendekezo ya Kamati ya Bunge.

SEHEMU YA KUMI NA MOJA

UTARATIBU WA KUMWONDOA RAIS MADARAKANI

124.- Mbunge yeyote anaweza kuwasilisha kwa Spika taarifa yaHoja ya kumshtaki Rais kwa madhumuni ya kumwondoa Raismadarakani kupitia Azimio la Bunge kwa mujibu wa Ibara ya 46A yaKatiba ikiwa inadaiwa kwamba Rais -

(a) ametenda vitendo ambavyo kwa ujumlavinavunja Katiba au Sheria ya Maadili ya Viongoziwa Umma;

(b) ametenda vitendo ambavyo vinakiuka maadiliyanayohusu uandikishwaji wa Vyama vya Siasayaliyotajwa katika Ibara ya 20(2) ya Katiba; au

(c) amekuwa na mwenendo unaodhalilisha Kiti chaRais wa Jamhuri ya Muungano. Isipokuwakwamba, hoja ya namna hiyo haitatolewa, ndani

MuundowaTaarifazaKamati

Taarifa yaHoja yaKumwo-ndoaRais,

Sura ya 2,Toleola 2002

Sura ya398,Toleola 2002

Page 105: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

84

Kanuni za Kudumu za Bunge

WajumbewaKamati MaalumuyaUchunguzi,

Sura ya 2,Toleo la2002

ya miezi kumi na miwili tangu ilipotolewa nakukataliwa na Bunge.

125.-(1) Bunge halitajadili wala kushughulikia hoja ya kumshtakiRais, isipokuwa tu kama: –

(a) taarifa ya maandishi, iliyowekwa saini nakuungwa mkono na Wabunge wasiopunguaasilimia ishirini ya Wabunge wote itatolewa;

(b) taarifa hiyo itawasilishwa kwa Spika, sikuthelathini kabla ya kikao ambapo hoja hiyoinakusudiwa kutolewa Bungeni;

(c) taarifa hiyo pia itafafanua makosa aliyoyatendaRais; na

(d) taarifa hiyo vile vile itapendekeza kuwa, KamatiMaalumu ya Uchunguzi iundwe ili ichunguzemashtaka yaliyowasilishwa dhidi ya Rais.

(2) Wakati wowote baada ya kupokea taarifa iliyowekwasaini na Wabunge na kujiridhisha kuwa masharti ya Katiba kwa ajiliya kuwasilisha hoja hiyo Bungeni yametimizwa, Spika atamruhusumtoa hoja kuiwasilisha hoja hiyo Bungeni.

(3) Hoja hiyo itakapowasilishwa Bungeni, Spika atalitakaBunge, bila ya kufanya majadiliano yoyote, lipige kura ya siri ilikupata uamuzi juu ya hoja hiyo.

126.-(1) Endapo hoja ya kumshtaki Rais itaungwa mkono naWabunge wasiopungua theluthi mbili ya Wabunge wote, Spikaatatangaza majina ya wajumbe wa Kamati Maalumu ya Uchunguzi,kwa kuzingatia masharti ya Ibara ya 46A(4) ya Katiba.

(2) Kamati Maalumu ya Uchunguzi itakuwa na wajumbewafuatao:-

(a) Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano, ambayeatakuwa ndiye Mwenyekiti wa Kamati hiyo;

(b) Jaji Mkuu wa Tanzania Zanzibar; na

Mashartiyahojayakuunda KamatiMaalumuyaUchunguzi

Page 106: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

85

Kanuni za Kudumu za Bunge

(c) Wajumbe saba walioteuliwa na Spika kwakuzingatia uwiano wa uwakilishi baina ya Vyamavya Siasa vinavyowakilishwa Bungeni.

(3) Endapo Bunge litapitisha hoja ya kuunda KamatiMaalumu ya Uchunguzi, Rais atahesabiwa kuwa hayupo kazini, nakwa sababu hiyo, kazi na madaraka ya Rais yatatekelezwa kwamujibu wa masharti ya Ibara ya 37(3) ya Katiba hadi Spikaatakapomfahamisha Rais juu ya Azimio la Bunge kuhusiana namashtaka yaliyotolewa dhidi yake.

127.-(1) Ndani ya siku saba baada ya Kamati Maalumu ya Uchunguzikuundwa, itakaa ichunguze na kuchambua mashtaka dhidi ya Raisna itampatia Rais fursa ya kujieleza na kujitetea kuhusu mashtakayaliyotolewa dhidi yake kwa mujibu wa masharti na utaratibuuliowekwa na Sheria ya Kinga, Madaraka na Haki za Bunge naKanuni hizi.

(2) Mapema iwezekanavyo na kwa vyovyote vile katikamuda usiozidi siku tisini, Kamati Maalumu ya Uchunguzi itatoa taarifayake kwa Spika.

(3) Akidi ya mkutano wowote wa Kamati Maalumu yaUchunguzi itakuwa ni Mwenyekiti, Jaji Mkuu wa Tanzania Zanzibarna Wajumbe wengine wanne kutoka Bungeni.

(4) Baada ya Spika kupokea taarifa ya Kamati Maalumu yaUchunguzi, taarifa hiyo itawasilishwa Bungeni kwa kufuata utaratibuuliowekwa na Kanuni hizi.

128.-(1) Endapo kwa mujibu wa Orodha ya Shughuli za Bunge utafikawakati wa Bunge kujadili taarifa ya Kamati hiyo Maalumu yaUchunguzi, basi Bunge litaingia kwenye Kamati ya Bunge Zima ilikushughulikia taarifa hiyo na Bunge linaweza kumruhusu Mwenyekitina mjumbe mwingine ambaye siyo Mbunge wa Kamati Maalumuya Uchunguzi kuwasilisha na kuelezea uamuzi wa Kamati yakekwenye Kamati ya Bunge Zima.

(2) Baada ya taarifa ya Kamati Maalumu ya Uchunguzikuwasilishwa Bungeni, Bunge litaijadili taarifa hiyo na litampa Raisfursa ya kujieleza na kujitetea kuhusu mashtaka yaliyotolewa dhidiyake.

Utaratibuwakaziya KamatiMaalumuyaUchunguzi,

Sura ya296, Toleola 2002

UtaratibukatikaKamatiyaBungeZimakuhusumashtakadhidi yaRaismashtakadhidi yaRais

Page 107: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

86

Kanuni za Kudumu za Bunge

Utaratibu wakumwo-ndoaMakamuwaRaisMadarakani,

Sura ya 2,Toleo la2002

Suraya 398,

Suraya 2,Toleola 2002

129.-(1) Baada ya kusikiliza utetezi wa Rais, Wabunge watapigakura ya siri ili kupata uamuzi wa Bunge iwapo mashtaka dhidi yaRais yamethibitika au mashtaka hayo hayakuthibitika.

(2) Baada ya Kamati ya Bunge Zima kukamilisha kazi zake naBunge kurudia, Mbunge aliyetoa hoja ya kumshtaki Rais atatoataarifa ya kukamilika kwa shughuli za Kamati ya Bunge Zima naendapo mashtaka dhidi ya Rais yatakuwa yamethibitika, kwakuungwa mkono na kura za Wabunge wasiopungua theluthi mbiliya Wabunge wote, papo hapo atatoa hoja kwamba, Bunge lipitisheAzimio la kumwondoa Rais madarakani, kwa mujibu wa mashartiya Ibara ya 46A(5) ya Katiba.

(3) Endapo Bunge litapitisha Azimio la kumwondoa Raismadarakani, Spika atawafahamisha Rais na Mwenyekiti wa Tumeya Uchunguzi juu ya Azimio hilo la Bunge na Rais atawajibika kujiuzulukatika kipindi cha siku tatu tangu Bunge lilipopitisha Azimio hilo.

(4) Endapo Rais ataacha kushika kiti cha Rais kutokana namashtaka dhidi yake kuthibitika na Bunge kupitisha Azimio lakumwondoa madarakani, Rais hatakuwa na haki ya kupata malipoyoyote ya pensheni.

SEHEMU YA KUMI NA MBILI

UTARATIBU WA KUMWONDOA MAKAMUWA RAIS MADARAKANI

130.-(1) Rais anaweza kuwasilisha Bungeni hati ya kuliomba Bungelipitishe Azimio la kumwondoa Makamu wa Rais madarakani ikiwaMakamu wa Rais ameacha au ameshindwa kutekeleza kazi zaMakamu wa Rais kwa mujibu wa Ibara ya 50(3) ya Katiba.

(2) Bila ya kuathiri masharti ya fasili ya (1) ya Kanuni hii, Mbungeyeyote anaweza kuwasilisha Bungeni hoja ya kutaka kumwondoaMakamu wa Rais madarakani ikiwa Makamu wa Rais:-

(a) ametenda vitendo ambavyo kwa ujumlavinavunja Katiba au Sheria ya Maadili yaViongozi wa Umma;

(b) ametenda vitendo vinavyokiuka maadiliyanayohusu uandikishaji wa Vyama vya Siasavilivyotajwa kutoka Ibara ya 20 (2) ya Katiba; au

Sura ya 2,Toleola 2002

Azimiolakumwo-ndoaRais

Page 108: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

87

Kanuni za Kudumu za Bunge

(c) amekuwa na mwenendo unaodhalilisha Kiti chaRais wa Jamhuri ya Muungano au Kiti chaMakamu wa Rais. Isipokuwa kwamba, hoja yanamna hiyo haitatolewa ndani ya miezi kumi namiwili tangu hoja ya namna hiyo ilipotolewa nakukataliwa na Bunge.

131.-(1) Bunge halitajadili wala kushughulikia hoja ya kumshtakiMakamu wa Rais isipokuwa tu kama: -

(a) taarifa ya maandishi, iliyowekwa saini nakuungwa mkono na Wabunge wasiopunguaasilimia ishirini ya Wabunge wote imetolewa;

(b) taarifa hiyo itawasilishwa kwa Spika, sikuthelathini kabla ya kikao ambapo hoja hiyoinakusudiwa kutolewa Bungeni;

(c) taarifa hiyo pia itafafanua makosa aliyoyatendaMakamu wa Rais; na

(d) taarifa hiyo pia itapendekeza kuwa, KamatiMaalumu ya Uchunguzi iundwe ili ichunguzemashtaka yaliyowasilishwa dhidi ya Makamu waRais.

(2) Wakati wowote baada ya kupokea taarifa iliyowekwasaini na Wabunge na kujiridhisha kuwa masharti ya Katiba kwa ajiliya kuwasilisha hoja hiyo Bungeni yametimizwa, Spika atamruhusumtoa hoja kuiwasilisha hoja hiyo Bungeni.

(3) Hoja hiyo itakapowasilishwa Bungeni, Spika atalitakaBunge, bila ya kufanya majadiliano yoyote, lipige kura ya siri ilikupata uamuzi juu ya hoja hiyo.

132.-(1) Endapo hoja ya kumshtaki Makamu wa Rais itaungwa mkonona Wabunge wasiopungua theluthi mbili ya Wabunge wote, Spikaatatangaza majina ya wajumbe wa Kamati Maalumu ya Uchunguzi,kwa kuzingatia masharti ya Ibara ya 46A(4) ya Katiba:-

(2) Kamati Maalumu ya Uchunguzi itakuwa na wajumbewafuatao:-

Mashartiyahojayak u u n d aKamatiMaalumyaUchunguzi

WajumbewaKamatiMaalumuyaUchunguzi

Sura ya 2,Toleo la2002

Page 109: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

88

Kanuni za Kudumu za Bunge

Sura ya 2,Toleo la2002

(a) Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano ambayeatakuwa ndiye Mwenyekiti wa Kamati hiyo;

(b) Jaji Mkuu wa Tanzania Zanzibar; na

(c) Wajumbe saba walioteuliwa na Spika kwakuzingatia uwiano wa Uwakilishi baina ya vyamavya siasa vinavyowakilishwa Bungeni.

(3) Endapo Bunge litapitisha hoja ya kuunda KamatiMaalumu ya Uchunguzi, Makamu wa Rais atahesabiwa kuwahayupo kazini, na kwa sababu hiyo, kazi na madaraka ya Makamuwa Rais yatatekelezwa kwa mujibu wa masharti ya Ibara ya 37(3)ya Katiba hadi Spika atakapomfahamisha Makamu wa Rais juu yaAzimio la Bunge kuhusiana na mashtaka yaliyotolewa dhidi yake.

133.-(1) Ndani ya siku saba baada ya Kamati Maalumu ya Uchunguzikuundwa, itakaa ichunguze na kuchambua mashtaka dhidi yaMakamu wa Rais na itampatia Makamu wa Rais fursa ya kujielezana kujitetea kuhusu mashtaka yaliyotolewa dhidi yake kwa mujibuwa masharti na utaratibu uliowekwa na Sheria ya Kinga, Madarakana Haki za Bunge na Kanuni hizi.

(2) Mapema iwezekanavyo na kwa vyovyote vile katikamuda usiozidi siku tisini, Kamati Maalumu ya Uchunguzi itatoa taarifayake kwa Spika.

(3) Akidi ya mkutano wowote wa Kamati Maalumu yaUchunguzi itakuwa ni Mwenyekiti, Jaji Mkuu wa Tanzania Zanzibarna Wajumbe wengine wanne kutoka Bungeni.

(4) Baada ya Spika kupokea taarifa ya Kamati Maalumu yaUchunguzi, taarifa hiyo itawasilishwa Bungeni kwa kufuata utaratibuuliowekwa na Kanuni hizi.

134.-(1) Endapo kwa mujibu wa Orodha ya Shughuli za Bunge utafikawakati wa Bunge kujadili taarifa ya Kamati hiyo Maalumu yaUchunguzi, basi Bunge litaingia kwenye Kamati ya Bunge Zima ilikushughulikia taarifa hiyo na Bunge linaweza kumruhusu Mwenyekitina mjumbe mwingine ambaye siyo Mbunge wa Kamati Maalumuya Uchunguzi kuwasilisha na kuelezea uamuzi wa Kamati yakekwenye Kamati ya Bunge Zima.

Utaratibuwakaziya KamatiMaalumuyaUchunguzi,

Sura ya296, Toleola 2002

UtaratibuKatikaKamatiyaBungeZimakuhusumashtakadhidi yaMakamuwa Rais

Page 110: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

89

Kanuni za Kudumu za Bunge

(2) Baada ya taarifa ya Kamati Maalumu ya Uchunguzikuwasilishwa Bungeni, Bunge litaijadili taarifa hiyo na litampaMakamu wa Rais fursa ya kujieleza na kujitetea kuhusu mashtakayaliyotolewa dhidi yake.

135.-(1) Baada ya kusikiliza utetezi wa Makamu wa Rais, Wabungewatapiga kura ya siri ili kupata uamuzi wa Bunge iwapo mashtakadhidi ya Makamu wa Rais yamethibitika au mashitaka hayohayakuthibitika.

(2) Baada ya Kamati ya Bunge Zima kukamilisha kazi zake naBunge kurudia, Mbunge aliyetoa hoja ya kumshtaki Makamu waRais atatoa taarifa ya kukamilika kwa shughuli za Kamati ya BungeZima na endapo mashtaka dhidi ya Makamu wa Rais yatakuwayamethibitika, kwa kuungwa mkono na kura za Wabungewasiopungua theluthi mbili ya Wabunge wote, papo hapo atatoahoja kwamba, Bunge lipitishe Azimio la kumwondoa Makamu waRais madarakani, kwa mujibu wa masharti ya Ibara ya 46A(5) yaKatiba.

(3) Endapo Bunge litapitisha Azimio la kumwondoa Makamuwa Rais madarakani, Spika atawafahamisha Rais, Makamu wa Raisna Mwenyekiti wa Tume ya Uchunguzi juu ya Azimio hilo la Bunge naMakamu wa Rais atawajibika kujiuzulu katika kipindi cha siku tatutangu Bunge lilipopitisha Azimio hilo.

(4) Endapo Makamu wa Rais ataacha kushika kiti cha Makamuwa Rais kutokana na mashtaka dhidi yake kuthibitika na Bungekupitisha Azimio la kumwondoa madarakani, Makamu wa Rais,hatakuwa na haki ya kupata malipo yoyote ya pensheni.

SEHEMU YA KUMI NA TATU

HOJA YA KUTOKUWA NA IMANI NA WAZIRI MKUU

136.-(1) Mbunge yeyote anaweza kutoa taarifa ya maandishi kwaSpika ya kutaka kuleta hoja ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuukwa mujibu wa Ibara ya 53A ya Katiba.

(2) Hoja yoyote ya kutaka kupitisha Azimio la kura ya kutokuwana imani na Waziri Mkuu haitatolewa Bungeni endapo:-

Sura ya2, Toleola 2002

Taarifa yaHoja yakutokuwa na imanina WaziriMkuuSuraya 2,Toleola 2002

Azimio lakumwo-ndoaMakamu wa Raismadarakani

Page 111: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

90

Kanuni za Kudumu za Bunge

(a) haina uhusiano na utekelezaji wa majukumu yaWaziri Mkuu yaliyoainishwa katika Ibara ya 52 yaKatiba;

(b) hakuna madai kwamba Waziri Mkuu amevunjaSheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma;

(c) haijapita miezi sita tangu alipoteuliwa; au

(d) haijapita miezi tisa tangu hoja ya namna hiyoilipotolewa Bungeni na Bunge likakataakuipitisha.

(3) Hoja ya kura ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu haitajadiliwana Bunge isipokuwa tu kama:-

(a) taarifa ya maandishi iliyowekwa saini nakuungwa mkono na Wabunge wasiopunguaasilimia ishirini ya Wabunge wote itatolewakwa Spika, siku zisizopungua kumi na nne kabla ya siku inayokusudiwa kuwasilishwa Bungeni;

(b) Spika ataridhika kuwa masharti ya Katiba kwaajili ya kuleta hoja hiyo yametimizwa.

(4) Hoja inayotolewa chini ya Kanuni hii na iliyotimiza masharti yaKatiba, itawasil ishwa Bungeni mapema iwezekanavyo naitaamuliwa kwa kura za siri.

(5) Hoja ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu itapitishwa tu iwapoinaungwa mkono na Wabunge walio wengi.

(6) Endapo hoja ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu itapitishwana Bunge kwa kupigiwa kura na Wabunge walio wengi, Spikaatawasilisha Azimio hilo kwa Rais na mapema iwezekanavyo nakwa vyovyote vile ndani ya siku mbili tangu Bunge lilipopitishaAzimio hilo, Waziri mkuu atajiuzulu na Rais atamteua Mbungemwingine kuwa Waziri Mkuu.

Suraya 398 Toleola 2002

Sura ya 2,Toleo la2002

Page 112: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

91

Kanuni za Kudumu za Bunge

SEHEMU YA KUMI NA NNE

KUMWONDOA SPIKA AU NAIBU SPIKA MADARAKANI

137.-(1) Mbunge yeyote anayetaka kuwasilisha hoja ya kumwondoaSpika madarakani chini ya Ibara ya 84(7)(d) ya Katiba, atawasilishataarifa ya maandishi ya kusudio hilo kwa Katibu akieleza sababukamili ya kutaka kuleta hoja hiyo.

(2) Mara tu baada ya kupokea taarifa ya maandishi ya kusudiola kumwondoa Spika kwenye madaraka, Katibu ataipeleka taarifahiyo kwenye Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kwaajili ya kuijadili.

(3) Endapo Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bungeitaridhika kuwa zipo tuhuma mahususi dhidi ya Spika zinazohusuuvunjaji wa masharti ya Ibara ya 84(7)(a), (b), (e), (f), (g) na (h) yaKatiba, Sheria au Kanuni zinazoongoza shughuli za Bunge, basiKamati hiyo itaidhinisha kuwa hoja hiyo ipelekwe Bungeni iliiamuliwe.

(4) Naibu Spika, atakalia Kiti cha Spika wakati wa kujadilihoja ya kutaka kumwondoa Spika madarakani na Spika atakuwana haki ya kujitetea wakati wa mjadala.

(5) Spika atakuwa ameondolewa kwenye madaraka endapozitapigwa kura zisizopungua theluthi mbili ya idadi ya Wabungewote za kuunga mkono hoja hiyo na uamuzi wa Bunge utafanywakwa kuzingatia kura za siri.

(6) Spika anayetuhumiwa anaweza kujiuzulu nafasi yake kwakutoa maelezo ya kujiuzulu kwake Bungeni kabla ya uamuzi juu yahoja ya kumwondoa madarakani.

138.-(1) Utaratibu wa kumwondoa Naibu Spika madarakani chiniya Ibara ya 85(4)(c) ya Katiba utakuwa kama ule wa kumwondoaSpika, isipokuwa tu taarifa ya kusudio la kumwondoa Naibu Spikamadarakani inayoeleza sababu kamili za kuleta hoja hiyo,itapelekwa kwa Spika ambaye ataiwasilisha kwenye Kamati ya Haki,Maadili na Madaraka ya Bunge kwa ajili ya kuijadili.

(2) Endapo Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bungeitaridhika kuwa zipo tuhuma mahususi dhidi ya Naibu Spikazinazohusu uvunjaji wa Katiba, Sheria au Kanuni zinazoongoza

Taarifaya HojayakumwondoaSpikamadarakani

Sura ya 2,Toleo la2002

Sura ya 2, Toleola 2002

Sura ya 2,Toleo la 2002

Utaratibuwakumwo-ndoaNaibu SpikaMadarakani

Page 113: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

92

Kanuni za Kudumu za Bunge

Ruhusa kwa wageniBungeni

Shughuli za Bunge, basi Kamati hiyo itaidhinisha kuwa hoja hiyoipelekwe Bungeni ili iamuliwe.

(3) Spika atakalia Kiti wakati wa kujadili hoja ya kutakakumwondoa Naibu Spika madarakani na Naibu Spika atakuwa nahaki ya kujitetea wakati wa mjadala.

(4) Naibu Spika atakuwa ameondolewa kwenye madarakaendapo zitapigwa kura zisizopungua theluthi mbili ya idadi yaWabunge wote za kuunga mkono hoja hiyo na uamuzi wa Bungeutafanywa kwa kuzingatia kura za siri.

(5) Naibu Spika anayetuhumiwa anaweza kujiuzulu nafasiyake kwa kutoa maelezo ya kujiuzulu kwake Bungeni kabla ya uamuzijuu ya hoja ya kumwondoa madarakani.

SEHEMU YA KUMI NA TANO

WAGENI BUNGENI

139.-(1) Wageni wanaweza kuruhusiwa kuingia kwenye Ukumbi waMikutano ya Bunge katika sehemu yoyote ya Ukumbi huo ambayoitatengwa kwa ajili hiyo.

(2) Wageni wakiwa ndani ya Ukumbi wa Mikutano ya Bungewatalazimika kufuata na kuzingatia masharti yafuatayo:-

(a) Watakaa kimya na kwa heshima inayostahilihadi watakapotoka nje ya Ukumbi huo;

(b) Wanapaswa wawe wamevaa mavazi yaheshima;

(c) Wataingia na kutoka Ukumbini kwa staha;

(d) Wasisome kitabu chochote, gazeti, baruaau hati nyingineyo ambayo si Orodha yaShughuli za Bunge;

(e) Wasiandike wala kurekodi jambo lolotelinalozungumzwa, isipokuwa tu kama niwawakilishi wa vyombo vya habari;

Page 114: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

93

Kanuni za Kudumu za Bunge

(f) Inapolazimu kuzungumza, wasizungumze kwasauti ya juu;

(g) Wasivute sigara au kiko wakati wowote wakiwandani ya Ukumbi wa Mikutano ya Bunge aumahali popote nje ya Ukumbi huo ambapo kunamahali pa kukaa wageni;

(h) Wazime simu zao za mikononi;

(i) Wasiingie na kamera wala kupiga picha;

(j) Wasishangilie wala kuzomea wakiwa ndani yaukumbi wa Bunge; na

(k) Wasifanye jambo au kitendo chochote ambachokinaweza kuvuruga amani na utulivu Bungeni.

(3) Spika anaweza kumwamuru mgeni yeyote aondokekwenye Ukumbi wa Bunge endapo atavunja lolote kati ya mashartiyaliyotajwa katika fasili ya (2) ya Kanuni hii.

140.-(1) Katibu anaweza kutoa ruhusa maalumu au ya jumla kwamwakilishi wa chombo chochote cha habari kuhudhuria vikao vyaBunge katika sehemu ya Ukumbi wa Mikutano ya Bunge iliyotengwakwa ajili hiyo.

(2) Ruhusa yoyote itakayotolewa na Katibu inawezakuwekewa masharti yafuatayo:-

(a) Chombo husika kitoe maombi rasmi;

(b) Chombo husika kiteue Waandishi wenye sifa namaadili ya kuweza kuandika habari za Bunge.

(3) Katibu anaweza wakati wowote kuondoa ruhusa aliyotoakwa mwakilishi wa chombo chochote cha habari, iwapo chombohicho kitatoa taarifa yoyote kuhusu Shughuli za Bunge ambayo,kwa maoni ya Bunge, inapotosha ukweli au vinginevyo inakiukaKanuni, taratibu au haki za Bunge.

141.-(1) Spika anaweza kuamuru wageni watoke nje ya sehemuyoyote ya Ukumbi na maeneo yake na anaweza kuamuru milangoya Ukumbi wa Mikutano ya Bunge ifungwe.

RuhusaKwaWaandishi waHabari

MamlakayakuwaondoawageniBungeni

Page 115: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

94

Kanuni za Kudumu za Bunge

Utambu-lishowaWageni

UtaratibuwakukaakwaWabunge,WatumishinaWageni Bungeni

(2) Endapo wakati wa kikao chochote Mbunge atatoa hojakuwa wageni watoke nje, Spika atalihoji Bunge papo hapo na hojaitaamuliwa bila ya mjadala au mabadiliko yoyote, wakati wowoteatakapoona inafaa kufanya hivyo.

(3) Mtumishi yeyote wa Bunge hataruhusiwa kumtoa njemgeni au kuagiza mgeni atolewe nje ya Ukumbi wa Bunge endapoKatibu atakuwa amemruhusu mgeni huyo kuwa ndani ya Ukumbiwa Bunge.

142.- (1) Spika anaweza kuwatambulisha wageni wote wa kitaifana kimataifa waliomo katika Ukumbi wa Bunge.

(2) Spika vilevile anaweza kuwatambulisha wageni wenginewaliomo katika Ukumbi wa Bunge ambao:-

(a) wanahusika moja kwa moja na shughuli zaMajimbo;

(b) wanatembelea Bunge kwa ajili ya ziara zamafunzo; na

(c) wametoa mchango wa kitaifa unaohitajikuenziwa.

SEHEMU YA KUMI NA SITA

UKAAJI NDANI YA BUNGE

143.- Spika ataweka utaratibu maalumu wa ukaaji wa Wabungendani ya Bunge, bila ya kuathiri mpangilio ufuatao:-

(a) Kiongozi wa Shughuli za Serikali Bungeni atakaakiti cha kwanza akifuatiwa na Mwanasheria Mkuuwa Serikali na Mawaziri, upande wa kulia waSpika.

(b) Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni atakaakiti cha kwanza akifuatiwa na Wasemaji Wakuuwa Upinzani upande wa kushoto wa Spika.

(c) Endapo hakuna Kiongozi wa Upinzanialiyechaguliwa na chama chenye haki ya

Page 116: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

95

Kanuni za Kudumu za Bunge

kuchagua Kiongozi wa Upinzani Bungeni lakiniWabunge wa Upinzani wapo, basi Wabunge haowatakaa upande wa kushoto wa Spika.

(d) Wapambe wa Bunge, watumishi wa Ofisi yaBunge, wahudumu wa Bunge, Watumishi waSerikali wenye shughuli maalumu Bungeni,waandishi wa vyombo vya habari na wageniwengine watakaa sehemu ambazo zimetengwakwa ajili yao.

(e) Wageni wa Wabunge na wageni wenginewanaweza kutengewa sehemu maalumu yakukaa.

(f) Wageni mashuhuri, Mabalozi na Viongoziwengine watakaa sehemu maalumu ya Spika.

SEHEMU YA KUMI NA SABA

USALAMA WA MAENEO YA BUNGE

144.-(1) Spika ataweka utaratibu wa kutoa vitambulisho kwaWabunge, watumishi wa Bunge, watumishi wa Serikali na kwa mtumwingine yeyote anayeingia kwenye Ukumbi wa Bunge au maeneomengine ya Bunge.

(2) Katibu atatoa vitambulisho vya aina tofauti kwa ajili yaWabunge, watumishi wa Bunge, watumishi wa Serikali na wageniwanaokaribishwa katika Ukumbi wa Bunge au maeneo mengineya Bunge.

145.-(1) Kutakuwa na utaratibu wa kumkagua mtu yeyoteanayeingia katika maeneo ya Bunge kwa kuzingatia:-

(a) staha na heshima; na

(b) tofauti ya jinsia.

(2) Endapo katika kufanya ukaguzi mtu yeyote atapatikana

UtaratibuwakuingiaMaeneoyaBunge

Ukaguzi

Page 117: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

96

Kanuni za Kudumu za Bunge

WajibuwaMbungekuhudhuriaVikaovyaBungeSura ya 2,Toleola2002

LughaRasmiBungeni

TaarifaRasmizaBunge

na kifaa ambacho kwa asili yake ni cha hatari, kifaa hicho atakiachakwa walinzi waliopo mlangoni.

(3) Mbunge, mtumishi au mgeni yeyote atakayekataakukaguliwa au kukabidhi kitu chochote ambacho walinzi wataonakwamba ni cha hatari, hataruhusiwa kuingia ndani ya Ukumbi waBunge au maeneo ya Bunge.

SEHEMU YA KUMI NA NANE

MENGINEYO

146.-(1) Kuhudhuria vikao vya Bunge na Kamati zake ni wajibu wakwanza wa kila Mbunge.

(2) Mbunge yeyote atakayeshindwa kuhudhuria Mikutano yaBunge mitatu mfululizo bila ruhusa ya Spika iliyotolewa kwamaandishi, atapoteza Ubunge wake kwa mujibu wa Ibara ya71(1)(c) ya Katiba na Spika ataiarifu Tume ya Uchaguzi.

(3) Mbunge atakapokosa kuhudhuria nusu ya vikao vyaMkutano mmoja bila ya sababu ya msingi atapewa onyo.

(4) Mbunge yeyote atakayeshindwa kuhudhuria vikao vyaBunge na Kamati zake kwa sababu maalumu atatakiwa kupatakibali cha Spika.

(5) Kwa madhumuni ya fasili ya (4) ya Kanuni hii, kibalikitatolewa katika Ofisi za Bunge za Dodoma au Dar es Salaam auZanzibar.

147.-(1) Shughuli za Bunge zitaendeshwa katika lugha ya Kiswahiliau Kiingereza, bila tafsiri ya lugha hizo kutolewa.

(2) Kwa kadri itakavyowezekana, Mbunge atajitahidikutochanganya lugha zote mbili wakati anasema Bungeni,isipokuwa tu pale anaponukuu.

148.-(1) Taarifa Rasmi ya Majadiliano Bungeni, ikiwa katika lughailiyotumiwa na msemaji, yakiwa ni maneno halisi aliyoyatamka,itatayarishwa chini ya usimamizi wa Katibu wa Bunge kwa kufuatamaagizo yatakayotolewa na Spika kwa ajili hiyo.

Page 118: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

97

Kanuni za Kudumu za Bunge

(2) Kila Mbunge aliyetoa hotuba Bungeni atapewa nakalaya hotuba yake mapema iwezekanavyo, ili aweze kusahihishamakosa ya uchapaji, kama yatakuwepo ila hataruhusiwakubadilisha maana halisi ya maneno aliyoyasema Bungeni.

149.-(1) Mbunge anayeingia kwenye Ukumbi wa Bunge atawajibikakuvaa mavazi ambayo ni safi na yenye kuhifadhi heshima yake,hadhi ya Bunge na utamaduni wa nchi, kama ilivyoainishwa katikaKanuni hii.

(2) Vazi Rasmi la Spika na Naibu Spika litakuwa ni joho lenyekuonesha rangi za Bendera ya Taifa, Nembo ya Taifa na baadhi yamazao makuu nchini, lililoshonwa maalumu kwa ajili hiyo, ambalolitavaliwa juu ya vazi lolote ambalo ni vazi rasmi kwa Wabunge.

(3) Vazi rasmi kwa Wabunge litakuwa lolote kati ya yafuatayo:-

(a) Kwa Wabunge Wanawake:-(i) vazi lolote la heshima yaani ambalo si la

kubana mwili, lisiloonesha maungoambayo kwa mila na desturi za Kitanzaniahayapaswi kuoneshwa na ni refu kuvukamagotini;

(ii) gauni la kitenge au blauzi inayovaliwana kitenge au sketi ya rangi yoyote;

(iii) kilemba cha kadiri au mtandio;

(iv) suti ya kike; au

(v) vazi linalovaliwa wakati wa eda.

(b) Kwa Wabunge Wanaume:-(i) suti ya Kiafrika au safari ya mikono mirefu

au mifupi yenye ukosi au shingo yamviringo na yenye fulana au bila fulanandani, ya rangi moja, isiyokuwa na nakshi,pamoja au bila baragashia;

(ii) vazi la kimwambao yaani kanzu rasmi nanadhifu, koti, baraghashia na makubadhiau viatu;

Mavazi Rasmi

Page 119: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

98

Kanuni za Kudumu za Bunge

(iii) suti kamili ya kimagharibi ya rangi kadiriisiyomeremeta;

(iv) koti aina ya blazer na tai, pamoja na surualiyoyote ya heshima; au

(v) tarbushi na kilemba cha Singasinga, aukilemba chochote kinachovaliwa kwa mujibu wamasharti ya imani au mila.

(4) Vazi Rasmi la Katibu na Wasaidizi wake Bungeni litakuwakama ifuatavyo:-

(a) Kwa Makatibu Wanaume:

(i) suti kamili ya kiafrika au safari, yenye ukosiau shingo ya mviringo na mikono mirefuau mifupi ya rangi nyeusi au bluu; au

(ii) suti kamili ya kimagharibi ya rangi nyeusiau bluu na shati jeupe na tai.

(b) Kwa Makatibu Wanawake:

Suti ya rangi nyeusi au ya bluu na shati jeupe natai.

(c) Makatibu na Wahudumu watavaa mavazimaalumu wakati wa shughuli maalumu za Bunge.

(5) Mpambe wa Bunge na Wasaidizi wake ndani ya Ukumbiwa Bunge watavaa mavazi rasmi ambayo yataamuliwa na Spika.

(6) Spika anaweza kwa sababu maalumu, kumruhusu mtumwingine anayehusika na shughuli za Bunge kuvaa viatu ambavyosio rasmi.

(7) Mbunge yeyote anaweza kutoa taarifa Bungeni iwapoMbunge mwingine ataingia kwenye Ukumbi wa Bunge akiwa namavazi yasiyoruhusiwa kwa mujibu wa Kanuni hii.

(8) Spika atakaporidhika kuwa Mbunge aliyetolewa taarifakwa mujibu wa fasili ya (7) ya Kanuni hii hajavaa mavazi rasmiataamuru Mbunge huyo atoke nje ya Ukumbi wa Bunge.

Page 120: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

99

Kanuni za Kudumu za Bunge

(9) Mbunge aliyetolewa nje kwa mujibu wa fasili ya (8) yaKanuni hii hataingia ndani ya Ukumbi wa Bunge hadi paleatakapokuwa amevaa mavazi rasmi.

150. - Kutakuwa na Bendera rasmi ya Bunge la Jamhuri ya Muunganowa Tanzania itakayoitwa Bendera ya Bunge, ambayo:-

(a) itakuwa katika umbo la mstatiri na rangi ya bluuiliyoiva na pembeni itakuwa na umbo dogo labendera ya Taifa ndani yake katika pembe ya juuupande wa kushoto.

(b) itakuwa pia na Siwa ya Bunge yenye rangi yadhahabu, chini kukiwa na utepe wenye maneno“Bunge la Tanzania.”

151.-(1) Bendera ya Bunge itapepezwa kwenye maeneoyafuatayo:-

(a) Katika Ofisi za Bunge Dodoma, Dar es Salaam naZanzibar.

(b) Nje ya Ofisi za Wabunge zilizopo Makao Makuuya Mkoa, Wilaya na katika Majimbo ya Uchaguzi.

(c) Ndani ya Ofisi ya Mbunge juu ya mezaanayofanyia kazi.

(d) Katika magari binafsi ya Wabunge ambapoBendera hiyo itapepezwa ikiwa mbele upandewa kushoto wa gari la Mbunge wakati Mbungemwenyewe anapokuwa ndani ya gari hilo, naakiwa anaendeshwa na dereva mwingine, siyoanapokuwa anaendesha mwenyewe.

(2) Mbunge hatapepeza Bendera kwenye gari lake awapokatika Miji ya Dodoma, Dar es Salaam na Zanzibar, na anapokuwaanatumia gari la kukodi au la kuazima.

(3) Bila ya kuathiri masharti yaliyotangulia ya Kanuni hii,Bendera ya Bunge itapepezwa kuanzia saa 12.00 asubuhi nakuteremshwa mara ifikapo saa 12.00 jioni kila siku.

Utaratibuwa kupepezaBendera

BenderayaBunge

Page 121: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

100

Kanuni za Kudumu za Bunge

(4) Bendera ya Bunge itaendelea kupepezwa katika gari laMbunge baada ya saa 12.00 jioni endapo anayepepeza Benderahiyo atakuwa safarini hadi pale atakapomaliza safari yake.

152.- Endapo Mbunge atafariki wakati Bunge likiwa katika shughulizake, Spika ataahirisha shughuli za Bunge kwa siku hiyo kwa ajili yamaombolezo.

153.-(1) Kwa idhini ya Spika, Kanuni yoyote inaweza kutenguliwakwa madhumuni mahususi baada ya Waziri, Mwanasheria Mkuu waSerikali au Mbunge yeyote kutoa hoja kwa ajili hiyo.

(2) Hoja ya kutengua Kanuni za Bunge haitahitaji kutolewataarifa.

(3) Maelezo ya hoja ya kutaka kutengua Kanuni yoyoteitakuwa ni pamoja na maelezo kuhusu madhumuni ya kutaka Kanunihiyo itenguliwe.

(4) Kanuni hiyo itatenguliwa kwa madhumuni yaliyokusudiwatu na siyo kwa madhumuni mengine yoyote.

154.-(1) Endapo litatokea jambo lolote ambalo muhusika wake aumwathirika wa jambo hilo anastahili kupewa pongezi au pole naWabunge basi Spika atatoa pongezi au pole kwa mhusika aumwathirika wa jambo hilo kwa niaba ya Wabunge wote.

(2) Baada ya Spika kutoa pongezi au pole kwa muhusika aumwathirika wa jambo lolote, kwa ajili ya kuokoa muda wamajadiliano, Mbunge yeyote hataruhusiwa kutoa pongezi au polekwa muhusika au mwathirika wa jambo hilo wakati wowote wamajadiliano Bungeni.

(3) Kwa upande wa Serikali, Kiongozi wa shughuli za SerikaliBungeni atatoa pongezi au pole kwa muhusika au mwathirika wajambo lolote kwa niaba ya Serikali.

(4) Baada ya Kiongozi wa shughuli za Serikali Bungeni kutoapongezi au pole kwa muhusika au mwathirika wa jambo lolote,kwa aji l i ya kuokoa muda wa majadil iano, Waziri yeyotehataruhusiwa kutoa pongezi au pole kwa muhusika au mwathirikawa jambo hilo wakati wowote wa majadiliano Bungeni.

Salamu zaPongezi naPole

Utaratibu baada yakifo cha Mbunge

KutenguaKanuni zaBunge

Page 122: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

101

Kanuni za Kudumu za Bunge

155.-(1) Bunge linaweza kupitisha Azimio la kufanya mabadilikokatika Kanuni yoyote kutokana na mapendekezo ya Kamati yaKanuni za Bunge.

(2) Mabadiliko yoyote ya Kanuni za Bunge yatawasilishwaBungeni na Naibu Spika.

(3) Spika, kwa kushauriana na Kamati ya Kanuni za Bunge,atakuwa na madaraka ya kuzifanyia marekebisho au mabadilikoNyongeza za Kanuni hizi, kulingana na mahitaji ya wakati, kadriatakavyoona inafaa.

156.-(1) Mabadiliko yaliyopitishwa hayataanza kutumika mpakayatakapochapishwa na kuingizwa katika Toleo la Kanuni za Bungelitakalofuata.

(2) Endapo Kanuni za Bunge zitafanyiwa mabadiliko, Spikaataagiza zichapishwe upya kwenye Gazeti kwa madhumuni yakuingiza mabadiliko yaliyofanyika.

(3) Nakala za Kanuni za Bunge zilizochapishwa kwa kufuatautaratibu uliofafanuliwa katika Kanuni hii itahesabiwa kuwa nakalahalisi za Kanuni za Kudumu za Bunge zilizofanyiwa mabadiliko.

157.-(1) Kanuni za Kudumu za Bunge, Toleo la Aprili, 2013 zinafutwa.

(2) Bila kujali masharti ya fasili ya (1) ya Kanuni hii jambo lolote,amri yoyote, uteuzi wowote, agizo au suala jingine lolote lililofanyikakwa mujibu wa Kanuni za Kudumu za Bunge, Toleo la Aprili, 2013halitakuwa batil i na l itaendelea kuwa halali hadilitakapobadilishwa, kufutwa au kuagizwa vinginevyo kwa mujibuwa Kanuni hizi.

Kanunikuanzakutumika

KufanyaMabadi-likokatikaKanuni

KufutwakwaToleola Aprili 2013nahifadhiyamamboyaliyo-fanyika

Page 123: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

102

Kanuni za Kudumu za Bunge

Jina

Tafsiri

Matumizii

________

NYONGEZA_________

NYONGEZA YA KWANZA________________

KANUNI ZA UCHAGUZI WA SPIKA NA NAIBU SPIKA_________

(Chini ya Kanuni ya 9 na 10)_________

SEHEMU YA KWANZAUTANGULIZI

1. Kanuni hizi zitaitwa Kanuni za Uchaguzi wa Spika na Naibu Spika.

2. Kanuni hizi zitatumika katika mchakato wa Uchaguzi wa Spikana Naibu Spika.

3. Katika Kanuni hizi, isipokuwa pale maelezo yatakapohitajivinginevyo:- “Chama” ni Chama cha Siasa chenye usajili wa kudumu; “Chombo cha Uteuzi” ni Chama kinachopendekeza mgombeaau wagombea wake; “Katibu” ni Katibu wa Bunge; “ Mbunge” ni mtu aliyechaguliwa au kuteuliwa kwa mujibu waIbara ya 66 ya Katiba kuwa mjumbe wa Bunge la Jamhuri yaMuungano; “Mgombea” ni mtu aliyejitokeza au aliyependekezwa naChama cha Siasa kuwa mgombea wa uchaguzi; “Msimamizi wa Uchaguzi” ni mtu ambaye kwa mujibu wa Kanunihizi amepewa mamlaka ya kuendesha na kusimamia Uchaguzi; “Nafasi” ni nafasi wazi ya Spika au Naibu Spika, iliyotokea amakutokana na kuvunjwa kwa Bunge au kutokana na nafasi itokeayokwa nasibu;

Page 124: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

103

Kanuni za Kudumu za Bunge

“Nafasi ya nasibu” ni nafasi wazi ya uwakilishi wa Wabungeisiyotokana na kuvunjwa kwa Bunge; “Naibu Spika” ni Naibu Spika wa Bunge aliyetajwa katika Ibaraya 85 ya Katiba; “Siku ya uteuzi” ni siku ambayo imetangazwa na msimamizi wauchaguzi kwamba ndiyo siku ya mwisho ya kupokea majina yawagombea; “Spika” ni Spika wa Bunge aliyetajwa katika Ibara ya 84 yaKatiba; “Uchaguzi” ni Uchaguzi wa Spika au Naibu Spika.

SEHEMU YA PILIMSIMAMIZI WA UCHAGUZI

4. Isipokuwa kama imeelezwa vinginevyo, uchaguzi wa Spika naNaibu Spika utaendeshwa na kusimamiwa na Katibu wa Bunge,kwa mujibu wa utaratibu uliowekwa na Kanuni za Bunge pamojana Kanuni hizi.

SEHEMU YA TATUKUWASILISHA JINA LA MGOMBEA

5.-(1) Inapofika wakati wa uchaguzi wa Spika au Naibu Spika,Chama chochote cha Siasa chenye kusudio la kushiriki kwenyeuchaguzi huo kitawasilisha kwa Katibu wa Bunge jina moja tu laama Mbunge wa Chama hicho au la mtu mwingine yeyote waChama hicho mwenye sifa za kuwa Mbunge kuwa mgombea wake.

(2) Mgombea mhusika au Ofisa wa ngazi ya kitaifa wa Chamakilichompendekeza, atawasilisha jina la mgombea huyo kwa Katibuambaye ndiye Msimamizi wa Uchaguzi.

(3) Jina la mgombea huyo linatakiwa limfikie Katibu Ofisini kwakeDodoma, kabla ya saa kumi jioni ya siku ya uteuzi.

Uende-shajinausimamiziwauchaguzi

Kuwasilishamajinayawagombea

Page 125: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

104

Kanuni za Kudumu za Bunge

SEHEMU YA NNEMASHARTI YA MGOMBEA UCHAGUZI

6. Mtu yeyote anaweza kuteuliwa kugombea kuchaguliwa kuwaSpika au Naibu Spika iwapo tu atakuwa ametimiza masharti yoteya kuwa mgombea wa nafasi hizo, kama yalivyotajwa katikaKifungu cha 38 cha Sheria ya Uchaguzi, Sura 343, Toleo la 2010.

SEHEMU YA TANOKUJITOKEZA MGOMBEA MMOJA

7. Endapo hadi kufikia saa kumi jioni ya siku ya uteuzi kutakuwa najina moja tu lililowasilishwa kwa Msimamizi wa Uchaguzi, mgombeahuyo atapigiwa kura ya “Ndiyo” au “Hapana”, na iwapo atapatakura za “Ndiyo” za idadi ya zaidi ya nusu ya kura za Wabunge woteatatangazwa na Msimamizi wa Uchaguzi kuwa amechaguliwa kuwaSpika au Naibu Spika.

Kumpigiakuramgombeammoja

Mashartikwamgombea

Page 126: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

105

Kanuni za Kudumu za Bunge

_________NYONGEZA YA PILI

_________

KANUNI ZA UCHAGUZI WA WABUNGE WANAOKWENDAKWENYE VYOMBO VINGINE VYA UWAKILISHI

_________(Chini ya Kanuni ya 12)

_________

SEHEMU YA KWANZAUTANGULIZI

1. Kanuni hizi zitaitwa Kanuni za Uchaguzi wa Wabungewanaokwenda katika vyombo vingine vya uwakilishi au kuwaWajumbe wa Tume ya Bunge.

2. Kanuni hizi zitatumika kwa uchaguzi wa Wabunge wanaokwendakatika vyombo vingine kuliwakilisha Bunge na pia kwa uchaguziwa Wabunge wanaogombea kuwa wajumbe wa Tume ya Bunge.

3. Katika Kanuni hizi, isipokuwa pale maelezo yanapohitajivinginevyo:- “Chama” ni Chama cha Siasa chenye uwakilishi Bungeni; “Chombo cha Uteuzi” ni chama kinachopendekeza mgombeaau wagombea wake; “Katibu” ni Katibu wa Bunge; “Idadi inayotakiwa” ni idadi ya kura zinazotakiwa kupatikanaau idadi ya nafasi zinazotakiwa zijazwe kwenye Uchaguzi; “Mbunge” ni mtu aliyechaguliwa au kuteuliwa kwa mujibu waIbara ya 66 ya Katiba kuwa mjumbe wa Bunge la Jamhuri yaMuungano;

Jina

Matumizi

Tafsiri

“Mgombea” ni mtu aliyejitokeza au aliyependekezwa na Chamacha Siasa kuwa mgombea wa uchaguzi; “Msimamizi wa Uchaguzi” ni mtu ambaye kwa mujibu wa Kanunihizi amepewa mamlaka ya kuendesha na kusimamia Uchaguzi; “Nafasi” ni nafasi wazi ya uwakilishi wa Wabunge kutoka miongonimwa Wabunge iliyotokana na kuvunjwa kwa Bunge au na nafasiitokeayo kwa nasibu;

Page 127: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

106

Kanuni za Kudumu za Bunge

“Nafasi ya nasibu” ni nafasi wazi ya uwakilishi wa Wabungeisiyotokana na kuvunjwa kwa Bunge; “Siku ya uteuzi” ni siku ambayo imetangazwa na Msimamizi wauchaguzi kwamba ndiyo siku ya mwisho ya kupokea majina yaWagombea; “Spika” ni Spika wa Bunge aliyechaguliwa kwa mujibu wa Ibaraya 84 ya Katiba; “Uchaguzi” ni uchaguzi wa Wabunge wanaokwenda katikavyombo vingine kuliwakilisha Bunge au kuwa Wajumbe wa Tumeya Bunge.

SEHEMU YA PILIUTEUZI WA WAGOMBEA

4. Uteuzi wa Wagombea utafuata utaratibu ufuatao:-

(a) Unapofika wakati wa Uchaguzi, kila Mbungeanayetaka kushiriki atawasilisha jina lake kwaKatibu ambaye atakuwa ndiye Msimamizi waUchaguzi huo.

(b) Majina ya Wagombea wote yatatakiwa kumfikiaKatibu Ofisini kwake Dodoma, siku moja kabla yasiku ya uteuzi.

SEHEMU YA TATUUTARATIBU WA UCHAGUZI

5.-(1) Uchaguzi wa wagombea wa nafasi za Uwakilishi utaendeshwana kusimamiwa na Katibu kwa utaratibu ufuatao:-

(a) Wakati wa Uchaguzi wa kwanza katika maisha yaBunge wa nafasi zilizotangazwa, mara tu baadaya Wagombea kuwasilisha majina yao, Spika:-

(i) Ataagiza majina ya wagombea wotewaliojitokeza yasambazwe kwa Wabunge;

(ii) Atatangaza Bungeni siku na mudaambapo kura zitapigwa;

UteuziwaWago-mbea

UchaguziwaWagombeawanafasi zaUwakilishi

Page 128: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

107

Kanuni za Kudumu za Bunge

(b) Katibu atatoa Taarifa ya maandishi kuhusu saa yakupiga kura ambayo itatolewa si chini ya saaishirini na nne kabla ya muda wa kupiga kura.

(c) Endapo itatokea nafasi miongoni mwa Wabungewaliochaguliwa kwa kufuata Kanuni hizi kutokanana sababu isiyohusiana na kuvunjwa kwa Bungeau kama nafasi ya namna hiyo haikujazwa, Spikaatatoa taarifa ya kutokea kwa nafasi hiyo kwaWabunge wote Bungeni.

(2) Utaratibu wa kujaza nafasi ambazo zimetengwa maalumu kwaajili ya ama kundi la Wabunge Wanawake au kundi la Wabungewa Kambi ya Upinzani, utakuwa kama ifuatavyo:-

(a) Katibu atatangaza siku ya uteuzi ambayoitakuwa si zaidi ya siku tano baada ya tangazola Spika kutolewa Bungeni kwa mujibu wa fasiliya (1)(c) ya Kanuni hii.

(b) Mbunge yeyote wa kundi linalohusika anayetakakuwa mgombea wa nafasi hiyo atawasilishajina lake kwa Katibu, angalau siku moja kablaya siku ya uteuzi iliyowekwa.

(c) Endapo atajitokeza mgombea mmoja wa nafasiinayohusika, Wabunge watampigia kura za“Ndiyo” au “Hapana”

(3) Baada ya kupata majina ya wagombea wote, Katibu atatoamatangazo kuhusiana na idadi ya wagombea, siku na muda wauchaguzi.

(4) Endapo kunatokea nafasi mbili au zaidi za nasibu kwa wakatimmoja, uchaguzi na upigaji kura utaendeshwa kama uchaguzimmoja.

SEHEMU YA NNEUCHAGUZI WA KUJAZA NAFASI ZA NASIBU

6. Kwa madhumuni ya uchaguzi wa kujaza nafasi yoyote ya nasibu,kutakuwa na karatasi moja tu ya kura ambayo itakuwa na orodhaya majina ya wagombea wote waliojitokeza, inayofuata mfululizowa alfabeti pamoja na jina la Chama cha mgombea na kutakuwa

Uchaguziwakujazanafasizanasibu

Page 129: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

108

Kanuni za Kudumu za Bunge

Utaratibuwakupigakura

Kupigakura

na nafasi tupu pembeni ya jina la kila mgombea kwa ajili ya kuwekaalama ya kupiga kura.

SEHEMU YA TANOUTARATIBU WA KUPIGA KURA

7.-(1) Kila Mbunge atakayekuwepo ukumbini wakati wa kupigakura anaweza, katika uchaguzi wa kwanza katika maisha ya Bungeau katika uchaguzi wa kujaza nafasi ya nasibu moja au zaidi:-

(a) kupiga kura moja moja au zaidi kulingana namaelekezo yaliyomo kwenye karatasi ya kurakwa ajili ya wagombea uchaguzi wa nafasiinayoshindaniwa kutoka miongoni mwa walewaliopendekezwa; au

(b) kupiga kura moja kwa kila mgombea Uchaguzimmoja kwa kufuata idadi ya nafasi za nasibuzilizopo katika Uchaguzi huo.

(2) Mbunge atapiga kura yake kwa kuweka alama ya “V” katikanafasi wazi ya karatasi ya kura pembeni ya jina la mgombeaanayetaka kumpigia.

SEHEMU YA SITAKUPIGA KURA

8.-(1) Utakapofika wakati wa kupiga kura, Spika atasitishamajadiliano ya Bunge na kuelekeza kwamba, kura ipigwe.

(2) Wakati huo huo mambo yafuatayo yatafanyika:-

(a) Katibu atatangaza idadi au aina ya Chaguzizitakazofanyika au nafasi zitakazojazwa;

(b) Kila mgombea atapewa muda wa kujieleza nakuomba kura.

(3) Kabla ya kupiga kura, sanduku la kura litaoneshwa kwenyeukumbi kuwa ni tupu, baada ya hapo kila Mbungeatakayekuwepo ukumbini atapewa karatasi moja ya kupiga kura.

(4) Sanduku la kura litawekwa chini ya usimamizi wa Katibu pamoja

Page 130: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

109

Kanuni za Kudumu za Bunge

na Wabunge waliochaguliwa kusimamia kuhesabiwa kwa kurampaka wakati wa kuhesabiwa kwa kura, na Katibu pamoja na haoWabunge watakuwa na madaraka kuhakikisha kwamba, sandukuhilo halifunguliwi mpaka wakati wa kuanza kuhesabu kura nakwamba, hakuna kitu kitakachowekwa ndani ya sanduku hilobaada ya karatasi za kura kukusanywa kwa mujibu wa fasili ya (3).

(5) Baada ya Wabunge kupiga kura, karatasi zitakusanywa nakutumbukizwa kwenye sanduku la kura.

(6) Baada ya zoezi la kupiga kura kukamilika na karatasi za kurakukusanywa, Spika atachagua Wabunge wawili wasimamie kaziya kuhesabu kura na majadiliano ya Bunge yatarudia kuanzia paleyalipositishwa.

SEHEMU YA SABAKUHESABU KURA

9.-(1) Mapema itakavyowezekana baada ya kupiga kura na kablaya kumaliza Kikao kilichopo cha Bunge, Katibu, mbele ya Wabungewawili waliochaguliwa kusimamia zoezi la kuhesabu kura,atalifungua sanduku la kura, kuzihesabu na kuziandika kura alizopatakila mgombea.

(2) Karatasi ya kura itakataliwa na kura hazitahesabiwa katikakaratasi hiyo:-

(a) ikiwa karatasi hiyo siyo rangi rasmi yakaratasi ya kupigia kura iliyotolewa na Katibu;

(b) ikiwa mpiga kura amepiga kura zaidi au pungufuya zile zinazotakiwa kupigwa;

(c) ikiwa kutaonekana kwenye karatasi hiyomaandishi yoyote au alama yoyoteiliyowekwa na mpiga kura isiyokuwa ya ile ya“V”;

(d) ikiwa haikuwekwa alama au imewekwa alamaisiyoonesha dhahiri ni mgombea yupi ambayempiga kura amempigia; isipokuwa kwamba,ikiwa baadhi ya kura kwenye karatasi ya kurani dhahiri na nyingine si dhahiri, karatasi ya kura

Kuhesabu kura

Page 131: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

110

Kanuni za Kudumu za Bunge

Kutangazamatokeoya kura

hiyo itakataliwa kuhusu tu zile kura zisizokuwadhahiri na kura zilizo dhahiri zitahesabiwa.

(3) Uamuzi wa Spika juu ya kuwa karatasi ya kura ikataliwe yote ausehemu tu utakuwa ni wa mwisho.

SEHEMU YA NANEKUTANGAZA MATOKEO YA KURA

10.-(1) Baada ya kura kuhesabiwa, Katibu atatangaza matokeo yakura zote zilizopigwa kisha atatamka majina ya wagombeawaliochaguliwa ambao wamepata idadi kubwa zaidi ya kura nakuwatangaza kwamba wamechaguliwa.

(2) Endapo baada ya kuhesabu kura kutakuwa na sababu ya kurudiaUchaguzi kutokana na kutokupatikana mshindi katika nafasi yoyoteinayohusika katika uchaguzi huo, Spika ataeleza sababu zakutokupatikana mshindi, kisha ataagiza kura ipigwe tena ili kupatamshindi kwa nafasi hiyo.

(3) Kura ya uamuzi haitatumika kwenye uchaguzi.

(4) Iwapo imeamuliwa ipigwe kura tena kwa mujibu wa fasili ya(2), basi wagombea wanaopigiwa kura watakuwa ni wale tu ambaowalipata kura sawa.

(5) Iwapo Spika hawezi kutangaza idadi inayotakiwa yawagombea waliochaguliwa kwa sababu ya kukosekana kura, basi:-

(a) atatangaza kadri ya wingi wa wagombeawaliochaguliwaambao wamepata kura kuwawamechaguliwa; na

(b) atawaarifu Wabunge wote kuhusu nafasiiliyobakia au zilizobakia na utaratibu wa uchaguziutaanza upya kwa ajili ya nafasi hiyo au nafasi hizo.

(6) Kila tamko na agizo linalotolewa na Spika kwa mujibu wa Kanunihii litatolewa Bungeni.

Page 132: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

111

Kanuni za Kudumu za Bunge

SEHEMU YA TISAUTUNZAJI WA KUMBUKUMBU ZA KURA

11.-(1) Katibu ataandika maneno “imekataliwa” na “kurailiyokataliwa” kwenye karatasi za kura zilizokataliwa na ataziwekakaratasi hizo pamoja na zile zilizokuwa safi kwa muda wa miezi sitabaada ya kutangazwa matokeo ya uchaguzi.

(2) Baada ya hapo, isipokuwa kama Bunge litaamuru vinginevyo,Katibu ataziharibu karatasi hizo.

(3) Karatasi za kura zilizokwishatumika hazitaonyeshwa kwa mtuyeyote na Katibu, isipokuwa kwa mujibu wa azimio la Bunge baadaya hoja ya kutaka zionyeshwe kupitishwa.

SEHEMU YA KUMIKUPINGA MATOKEO YA KURA

12.- Iwapo mgombea yeyote hataridhika na matokeo ya Uchaguziau jinsi uchaguzi ulivyofanywa, atakuwa na haki ya kupeleka madaiyake mahakamani na madai hayo yatashughulikiwa kwa mujibuwa Sheria il iyowekwa na Bunge kwa ajil i ya kushughulikiamalalamiko ya uchaguzi wa Wabunge.

Utunzajiwakumbu-kumbuza kura

KupingaMatokeo ya kura

Page 133: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

112

Kanuni za Kudumu za Bunge

Citation

Interpre-tation

__________

NYONGEZA YA TATU__________

THE EAST AFRICAN LEGISLATIVE ASSEMBLYELECTION RULES

______(Made under Standing Order 12 and Article 50

of the Treaty for the Establishment ofEast African Community)

_______

ARRANGEMENT OF RULES____________

PART IPRELIMINARY RULES

1. These Rules may be cited as the East African Legislative AssemblyElection Rules.

2. In these rules, all the parliamentary words and expressions usedshall have the same meaning assigned to them in the ParliamentaryStanding Orders and, unless the context requires otherwise:-

“Candidate” means a person who is nominated to stand forelection to the East African Legislative Assembly as provided forin rule 5 of these rules; “Election” means an election to the East African LegislativeAssembly; “Nomination” means nomination as a candidate to stand forelection to the East African Legislative Assembly;

Page 134: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

113

Kanuni za Kudumu za Bunge

“Returning Officer” means the Clerk of the National Assembly; “Treaty” means the Treaty for the Establishment of the EastAfrican Community, 1999; “Voter” means a Member of Parliament present and votingduring the election;

PART IIQUALIFICATION OF CANDIDATES

3. A person shall be qualified to be a candidate for election to theEast African Legislative Assembly who he is qualified to be electedin accordance with Article 50(2) of the Treaty.

PART IIINOMINATION OF CANDIDATES

4. -(1) Where an election is to be held, the Returning Officer shallby notice published in the Gazette, appoint a nomination day forthat election.

(2) The Returning Officer shall give at least fourteen days notice ofsuch nomination day.

5.-(1) In order to be validly nominated as a candidate for the EastAfrican Legislative Assembly elections, a person must benominated in a transparent and democratic manner by the politicalparty which is sponsoring him.

(2) The nomination shall be in the prescribed form, signed by thecandidate and by the Secretary General of the party nominatinghim, and shall contain the following particulars:-

(a) The name, educational qualifications, addressand occupation of the candidate;

(b) A certificate by the candidate that he is willingand otherwise qualified to stand for election.

(3) Every nomination paper shall be accompanied by the followingdocuments:-

NominationofCandidates

Validity ofnomina-tion

Qualifi-cationofcandidates

Page 135: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

114

Kanuni za Kudumu za Bunge

Cap.258

Non-refunda-bledeposit

Rejectionofnomina-tionpapers

(a) Proof of citizenship of the United Republic ofTanzania, provided by the ImmigrationDepartment;

(b) Detailed biographical information relating tothe candidate signed by the candidate himself,which shall enable the Returning Officer todetermine whether or not the candidate hasproven experience or interest in consolidatingand furthering the aims and objectives of theCommunity in terms of Article 50(2)(e) of theTreaty; and

(c) An extract of the nomination proceedings of theparty organ which approved the finalnomination of the candidate, signed by theChairman and Secretary of that Organ whichshall enable the Returning Officer to determinewhether or not the relevant political party’sproceedings were democratic and transparent interms of the Political Parties Act.

(4) The candidate or an official of the Party nominating him, shalldeliver the nomination papers to the Returning Officer at his officein Dodoma, not later than four o’clock in the afternoon of thenomination day.

(5) Any political party which is entitled to sponsor candidates maysubmit to the Returning Officer, the names of three candidates foreach vacant seat in the following relevant groups:-

Group A: Women Candidates;Group B: Zanzibar Candidates;Group C: Opposition Parties Candidates;Group D: Mainland Candidates.

6. A candidate, or an official of the party nominating him shall, atthe time of delivering the nomination paper, deposit a non-refundable deposit of fifty thousand shillings, to cover for the costof election expenses.

7. Objections may be made by the Returning Officer to thenomination of a candidate, if it is apparent to him from the contentsof the nomination papers that the candidate is not qualified to

Page 136: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

115

Kanuni za Kudumu za Bunge

stand for election. In which case the Returning Officer shallforthwith reject the nomination papers of that candidate.

PART IVELECTION AND VOTING PROCEDURE

8. The Returning Officer shall by notice published in the Gazette,appoint an election day which shall be not more than seven daysafter nomination day, provided that, such election day shall be aday when the National Assembly is sitting in ordinary session.

9.-(1) A candidate may withdraw his candidature by notice inwriting, signed and delivered by him to the Returning Officer and acopy to the Secretary General of the Party sponsoring him, notlater than four o’clock in the afternoon of the day followingnomination day, thereafter no withdraws shall be accepted.

(2) Where any candidate dies after four o’clock in the afternoonof nomination day and before election day, the election processwill continue undisturbed.

10.-(1) An aspiring candidate may introduce himself to the votersand seek their support even before nomination day and maycontinue to do so after nomination day.

(2) Before the votes are cast on election day, each candidate willbe permitted to appear before the voters, duly assembled in anordinary sitting of the House and address them in English for suchlength of time and answer such number of questions, if any, as maybe determined by the Speaker for that purpose.

11.-(1) The voting shall be conducted under the general supervisionof the Returning Officer.

(2) The Returning Officer shall issue only one ballot paper to eachvoter.

(3) The ballot paper shall contain the names of all candidates,arranged alphabetically in the following groups:-

Election day

Withdrawalofcandida-ture

Campaign bycandidates

Supervisionof theVotingprocess

Page 137: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

116

Kanuni za Kudumu za Bunge

Announcementofelectionresults

Group A: Women Candidates;Group B: Zanzibar Candidates;Group C: Opposition Parties Candidates;Group D: Mainland Candidates.

(4) A voter shall be required to cast a specified number of votes,to be announced by the Speaker in each of the groups.

(5) On receiving a ballot paper, each voter shall secretly recordhis votes by putting a mark against the names of the ninecandidates he wishes to vote for.

(6) Each voter shall be required to cast as many votes as there arevacancies, otherwise his whole ballot paper will be regarded asspoilt.

(7) A voter who has accidentally spoiled his ballot paper whilethe voting is still in progress may surrender the spoilt ballot paperto the Returning Officer and obtain a replacement thereof.

12.-(1) When all the voters have casted their votes, the Speakershall appoint two counting agents, one from the ruling party andthe other from the opposition benches, to act as counting agentsfor all the candidates.

(2) Immediately after all the ballots have votes been collected,the Returning Officer, with the assistance of Clerk Assistants andbefore the two counting agents as witnesses, shall count the votesso casted.

(3) In order to enable the National Assembly to proceed with otherbusiness, the counting of votes shall take place outside theAssembly Chamber, in a room designated by the Clerk for thatpurpose within the precincts of the Assembly.

13. When the votes have already been counted and the results ofthe election has been ascertained, the Returning Officer shall:-

(a) Report to the Assembly the election results,together with the number of votes recorded foreach candidate in each group.

(b) Announce to the Assembly the names of ninepersons receiving the majority number ofvotes in each group and shall declare those

VotesCountingagents

Page 138: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

117

Kanuni za Kudumu za Bunge

persons to have been elected as members ofthe East African Legislative Assembly.

14.-(1) The Returning Officer shall ensure the safe custody of allballot papers and other documents relating and pertaining to theconduct of the election.

(2) The Returning Officer shall cause all documents to which thisparagraph applies to be destroyed after the expiration of sixmonths from the election day, unless otherwise directed by anorder of the High Court arising from any proceedings of a petitionrelating to the election.

PART VANNULMENT AND AVOIDANCE OF ELECTION

15. Pursuant to the provisions of Article 52(1) of the Treaty, theelection of a candidate as a member of the East African LegislativeAssembly may be declared null and void only on an Election Petition.

16. The procedure, jurisdiction and grounds for declaring theelection of such member null and void shall be the same as thoseprovided by law for election petitions in respect of Members ofthe Parliament of the United Republic of Tanzania.

Custodyof ballotpapers

Groundsforannulmentandavaoid-anceof election

Annulmentand avoida-nce ofelection

PART VIMISCELLANEOUS

17. (1) If any matter or thing arises which is not specifically providedfor in these rules, the Speaker shall make a ruling directing what isto be done in respect of that matter or thing.

(2) In making such a ruling, the Speaker shall be guided by thepractices and procedures normally followed in similar situationswith regard to Parliamentary elections.

18. These rules may be amended at any time by a resolution of theNational Assembly on a proposal submitted to it by the StandingOrders Committee.

Mattersnotprovidedfor

Amend-mentofrules

Page 139: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

118

Kanuni za Kudumu za Bunge

Citation

Interpretation

Presentationofannualreport

Timeofpresentation

__________NYONGEZA YA NNE

__________

THE SUBMISSION OF REGULAR REPORTS TO THEPARLIAMENT OF TANZANIA BY THE TANZANIA MEMBERS

OF THE EAST AFRICAN LEGISLATIVE ASSEMBLY___________

[Made under Article 65 of the Treaty for theEstablishment of the East African Community]

_________

1. These Regulations may be cited as the Submission of RegularReports to the Parliament of the United Republic of Tanzania bythe Members of the East African Legislative Assembly Regulations.

2.-(1) These Regulations are made to provide for a procedure forthe Members of the East African Legislative Assembly hailing fromTanzania to submit regular reports to the Parliament of the UnitedRepublic of Tanzania.

(2) These Regulations shall apply to members of East AfricanLegislative Assembly hailing from the United Republic of Tanzania.

3. The Members of the East African Legislative Assembly shallpresent an annual report of the activities of the East AfricanLegislative Assembly for the relevant year, to the Parliament ofthe United Republic of Tanzania through its Standing Committeeresponsible for Foreign Affairs and International Co-operation.

4. The annual reports shall be presented at a regular meeting ofthat Committee at a time to be determined by the Chairman ofthe Committee.

5. The Tanzania members of the East African Legislative Assemblymay, if they consider it desirable to do so, present any specialreport, or make any appropriate consultations with the Committee,on any matter which is relevant to the work of the East AfricanLegislative Assembly at any other scheduled meeting of theCommittee.

Presenta-tionofspecialreportandconsultations

Page 140: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

119

Kanuni za Kudumu za Bunge

6.-(1) All Tanzania Members of the East African Legislative Assemblyshall be present at the time of presentation of any such report.

(2) All such reports shall subsequently be laid on the Table of theHouse and shall be debated upon.

Attenda-nceandlayingofreportson theTable

Page 141: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

120

Kanuni za Kudumu za Bunge

Citation

Interpre-tation

__________NYONGEZA YA TANO

__________THE PAN-AFRICAN PARLIAMENTARY ELECTION RULES

[Made under Standing Order 12 and Article 2 of the Protocolto the Treaty for Establishing of the African EconomicCommunity Relating to the Pan-African Parliament]

_______________

PART IPRELIMINARY RULES

1. These Rules may be cited as the Pan-African ParliamentaryElection Rules, and shall come into operation on the day of theiradoption by resolution of the National Assembly.

2. In these Rules, unless the context requires otherwise- “Candidate” means a Member of Parliament who is dulynominated to stand for election to the Pan-African Parliament asprovided for in rule 5 of these Rules; “Election” means the election to membership of the Pan-AfricanParliament; “Election day” means the day on which the election of Membersof the Pan-African Parliament is set to be conducted; “Nomination” means nomination as a Candidate to stand forelection to the Pan-African Parliament; “Nomination day” means the day which shall by notice publishedby the Returning Officer, be set to be the last day for receivingapplication forms from Candidates; “Nominator” means a Member of Parliament of the Parliamentof the United Republic of Tanzania entitled to vote, who nominatesand supports a Candidate who aspires to stand and contest forelection to the Pan-African Parliament; “Qualification” means the qualification which entitles a personto stand and contest for election to the Pan-African Parliament; “Returning Officer” means the Clerk of the National Assembly; “Speaker” means the Speaker of the National Assembly; “Voter” means a Member of Parliament of the United Republicof Tanzania present and voting during the election.

Page 142: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

121

Kanuni za Kudumu za Bunge

PART IIQUALIFICATION OF CANDIDATES

3. No person shall be qualified to be a Candidate for election tothe Pan-African Parliament unless he or she is a Member ofParliament of the United Republic of Tanzania, and is fluent in anyof the languages approved for use in the proceedings of the Pan-African Parliament.

PART IIINOMINATION PROCEDURE

4.-(1) Where election of Members of the Pan-African Parliament isto be held, the Returning Officer shall, by written notice circulatedto all members of the Parliament of the United Republic of Tanzania,appoint a nomination day for that election, which must be a dayduring any period when the National Assembly is in ordinary session.

(2) The Returning Officer shall give at least seven days notice ofsuch nomination day.

5. The following shall be the procedure for the nomination ofcandidates that:-

(a) in the case of a General Election of all the fivemembers of the Pan-African Parliamentrepresenting Tanzania, the candidates will benominated in accordance with thefollowing groups:-

Group A: Women Candidates;Group B: Zanzibar Candidates;Group C: Mainland Candidates;Group D: Opposition Parties Candidates;

Provided that, whereas Group A shall be reserved forWomen Candidates only, the remaining Groups shall beopen to both men and women Candidates.

(b) the number of candidates to be elected ineach group shall be as follows:-

Qualifica-tionofCandidates

Appointmentofnominationday

Nominationprocedure

Page 143: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

122

Kanuni za Kudumu za Bunge

Group A: One Candidate;Group B: One Candidate;Group C: Two Candidates;Group D: One Candidate;

(c) in the case of a by-election to fill a casualvacancy, candidates will be nominated only inrespect of the group in which the vacancy hasoccurred;

(d) no candidate may be nominated for more thanone specified group.

6.-(1) In order to be validly nominated to stand as a candidate forelection to Pan-African Parliament, a person shall be nominatedand supported in writing by not less than ten nominators who areentitled to vote at that election. A nominator may nominate up tofour candidates, one for each of the four groups.

(2) The nomination shall be in the prescribed form obtainable fromthe Returning Officer, and shall contain working experience of thecandidate.

(3) The time for receipt by the Returning Officer of nomination formsduly completed by the aspiring Candidates shall expire at fouro’clock in the afternoon of the nomination day and soon thereafter,the Returning Officer shall give written notification to all Membersof Parliament, of the complete list of the all Candidates who havebeen validly nominated for the election in respect of each of thefour groups.

(4) After being validly nominated, a Candidate may withdraw hiscandidature by notice in writing signed and delivered by him tothe Returning Officer, not later than four o’clock in the afternoonof the day following the nomination day, thereafter, no withdrawalsshall be accepted.

(5) Where any Candidate dies at any time after nomination dayand before election day, the election process shall continueundisturbed.

(6) After being validly nominated, a Candidate may conduct his orher election campaign.

Nominationofcandidate

Page 144: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

123

Kanuni za Kudumu za Bunge

PART IVELECTION PROCEDURE

7. The Returning Officer shall, by written notice circulated to allMembers of Parliament, appoint an election day, which must be aday on which the National Assembly is sitting in ordinary session,and shall be not more than five days after nomination day.

8. The voting process shall be conducted under the generalsupervision of the Speaker, provided that, if the Speaker himself orherself is a Candidate, he or she shall vacate the chair before thecommencement of the election proceedings.

9. Before the voting exercise takes place on election day, eachCandidate shall be given an opportunity to appear before thevoters assembled in an ordinary sitting of the National Assemblyand address them in English for such length of time and answersuch number of questions, if any, as may be determined by theSpeaker for that purpose.

10. Immediately after address of the candidates, voting shallcommence and proceed as follows:-

(a) Only one ballot paper shall be issued to eachvoter.

(b) The ballot paper shall contain all names of theCandidates arranged in alphabetical order foreach of the groups.

(c) Each voter shall be required to cast the exactnumber of votes equal to the number ofpersons to be elected in each group. Any ballotbe treated as spoilt and will not be counted.

Votingprocess

Electionday

Votingprocedure

Candidatestoaddressvoters

Page 145: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

124

Kanuni za Kudumu za Bunge

(2) A voter who has accidentally spoiled his or her ballot paperwhile voting is still in progress may surrender the spoilt ballot paperto Returning Officer and obtain a replacement thereof.

12.-(1) Immediately after all the votes have been placed in theballot boxes and before the ballot boxes are removed from theAssembly Chamber for counting the votes, the Speaker shallappoint one counting agent for the Candidates in each of thegroups. Provided that, any candidate who wishes to appoint his or herown counting agent may do so by submitting the name of thatagent to the Speaker immediately after the appointments by theSpeaker have been announced.

(2) The counting of Votes shall be done by such number of Officersof the Assembly as may be appointed by the Returning Officer, andshall be witnessed by the counting agents.

13. In order to enable the National Assembly to proceed withother business scheduled for that day, the counting of votes shalltake place in a room designated by the Speaker for thatpurpose within the precincts of the Assembly.

14. After the counting of votes is complete and the resultsascertained and certified by the Returning Officer and the countingagents, the Returning Officer shall immediately submit the resultsto the Speaker who shall:-

(a) Report to the Assembly the results of the electiontogether with the number of votes recorded foreach candidate in each of the Groups.

(b) Announce to the Assembly the names of fiveCandidtes receiving the highest number of votesin each Group, and shall declare those candidatesto have been elected as Members of the Pan-African Parliament.

Appoint-mentofCountingAgentsandcountingofvotes

Decla-rationofelec-tionresults

Placeforcount-ing ofvotes

11.-(1) On receiving a ballot paper each voter shall secretly recordhis or her five votes by placing a tick in the space provide againstthe name of each Candidate, and thereafter shall place the ballotpaper in the ballot box.

Casting of votes

Page 146: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

125

Kanuni za Kudumu za Bunge

15.-(1) The Returning Officer shall ensure the safe custody of allballot papers and other documents pertaining to the election.

(2) The Returning Officer shall cause all documents to which thisrule applies to be destroyed after the expiration of six months fromthe election day.

PART VMISCELLANEOUS

16. Where anything arises which is not specifically provided for inthese Rules, the Speaker shall make a ruling directing what is to bedone. In making such a ruling, the Speaker shall be guided by theprocedures and practices normally followed in similar situationswith regard to Parliamentary elections.

17. These Rules may be amended at any time by a resolution of theNational Assembly on a proposal submitted to it by the StandingOrders Committee.

Custodyofballotpapers

Mattersnotprovidedfor

Amend-ment

Page 147: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

126

Kanuni za Kudumu za Bunge

_____________NYONGEZA YA SITA

_____________

MWONGOZO KUHUSU MASWALI KWA WAZIRI MKUU______________________________

[Chini ya Kanuni ya 38(6)]____________

1. (1) Kipindi cha Maswali kwa Waziri Mkuu kikishaanza Bungeni,hakitakatishwa wala kusitishwa, isipokuwa kutokana na sababumaalum ya dharura.

(2) Maswali yatakayoulizwa kwa Waziri Mkuu wakati wa Kipindicha Maswali kwa Waziri Mkuu yatakuwa ni yale yanayohusu Seraza Serikali au jambo lolote lenye manufaa na maslahi kwa jamiina Taifa lililo chini ya madaraka na mamlaka ya kazi ya WaziriMkuu.

(3) Maswali kwa Waziri Mkuu yatakuwa ni ya papo kwa papo;yaani yataulizwa bila kutolewa taarifa na yatajibiwa kwa mdomopapo kwa papo.

(4) Waziri Mkuu hatalazimika kujibu swali lolote linalohitajitakwimu au majibu yanayohitaji utafiti.

2. Bila ya kuathiri masharti ya fasili ya 3(1) ya Mwongozo huu,Wabunge wanaotaka kumuuliza Waziri Mkuu swali wakati waKipindi cha Maswali kwa Waziri Mkuu, watawasilisha majina yaokwa Katibu, kabla ya saa 2.30 Asubuhi, siku hiyo ya Maswali kwaWaziri Mkuu.

3. (1) Kipindi cha Maswali kwa Waziri Mkuu kinapoanza Bungeni,Spika atamwita Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni nakumpa fursa ya kwanza ya kumuuliza Waziri Mkuu swali.

(2) Baada ya kuuliza na kujibiwa swali lake la kwanza, Kiongozi waKambi Rasmi ya Upinzani Bungeni anaweza kumuuliza Waziri Mkuuswali moja la ziada la kudai ufafanuzi.

MaelezoyaJumla

UtaratibuwakupatafursayakumuulizaWaziriMkuuSwali

UtaratibuwakuulizamaswalikwaWaziriMkuu

Page 148: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

127

Kanuni za Kudumu za Bunge

(3) Mbunge yeyote atakayepata fursa ya kumuuliza Waziri Mkuuswali na kujibiwa, anaweza kumuuliza Waziri Mkuu swali linginemoja la ufafanuzi.

(4) Endapo orodha ya majina ya wauliza maswali kwa Waziri Mkuukwa siku hiyo itafikia mwisho lakini muda wa Kipindi cha Maswalikwa Waziri Mkuu bado haujamalizika, Spika anaweza kutoa fursakwa Mbunge yeyote ambaye hakupangwa katika orodha hiyokumuuliza Waziri Mkuu swali.

(5) Mbunge anayetaka kupewa fursa na Spika kwa mujibu wa fasiliya (4), atasimama mahala pake ili Spika amwone na kumwita.

(6) Mbunge yeyote aliyepata fursa ya kumuuliza Waziri Mkuu swaliwakati wa Kipindi cha Maswali kwa Waziri Mkuu, atakuwana haki pia ya kuuliza swali lake lililowekwa kwenye Orodha yaShughuli za siku hiyo, wakati wa Kipindi cha Maswali ya Bungekitakapowadia.

4. Maswali na majibu katika kipindi cha Maswali kwa Waziri Mkuuyawe mafupi.

MaswalinamajibukwamaswalikwaWaziriMkuu

Page 149: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

128

Kanuni za Kudumu za Bunge

________NYONGEZA YA SABA

________MWONGOZO WA UPATIKANAJI WA HABARI KUTOKA

KWENYE VIKAO VYA KAMATI ZA BUNGE_________

[Chini ya Kanuni ya 117(9) na (10)]_________

1. Mwongozo wa upatikanaji wa habari kutoka kwenye Vikao vyaKamati, ikiwa ni mojawapo ya njia za kukuza demokrasia za uwazikwa shughuli za Kamati za Bunge na kudumisha mahusiano nawananchi kupitia Vyombo vya Habari utatambua aina yamajukumu ambayo yanatekelezwa na Kamati.

2. Majukumu yatakayofanywa kwa uwazi na ambayo yanawezakutolewa kwa Waandishi wa Habari bila kuleta athari kwenyemaamuzi ya Kamati ni yafuatayo:-

(a) mambo ya kawaida ya kuisimamia na kuishauri Serikali,kama vile kutathmini utekelezaji wa miradi mbalimbaliya maendeleo;

(b) mambo yatolewayo na wadau walioalikwa na Kamatikulingana na utaratibu wa ‘Public Hearing’ uliowekwana Bunge;

(c) majukumu ambayo yanalenga kuwapatia Wabungeelimu, Semina, Makongomano na ziara za mafunzo;

(d) maelezo yanayotolewa na Serikali kwenye Kamati zaBunge kwa lengo la kuwaelimisha Waheshimiwa Wajumbewa Kamati kabla ya kufanya kazi ya uchambuzi wa Hojaau jambo lolote na ambayo Waziri ataona hayatakuwana athari kwa upande wa Serikali, mfano mmojawapoukiwa ni pale Waziri wa Fedha na Mipango, anapotoataarifa ya Hali ya Uchumi wa nchi.

Maelezoyajumla

Majukumuyatakayo-fanywakwauwazi

Page 150: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

129

Kanuni za Kudumu za Bunge

3.-(1) Majukumu yatakayofanywa kwa faragha yatahusu mamboyote ambayo habari zake zikitolewa kwa Waandishi wa Habarikabla ya wakati wake yanaweza kuathiri maamuzi ya Kamati napia kusababisha ukiukwaji wa Kanuni za Bunge ni yafuatayo:-

(a) kazi zote zinazopelekwa kwenye Kamati naMheshimiwa Spika ili baadaye apelekewetaarifa ya mapendekezo ya hatua zakuchukuliwa na Bunge au kuyatolea maamuzi.

(b) shughuli zote za uchambuzi wa Hoja mbalimbalizilizoko mbele ya Kamati.

(c) Shughuli zote zinazofanywa kwa utaratibu wauchunguzi.

(d) shughuli zote za kiuchunguzi zenye utaratibuuliowekewa masharti zinazofanywa na Kamati.

(e) shughuli zote zinazofanywa na Kamati Ndogozilizoundwa na Mheshimiwa Spika au Kamatihusika ili kufanya kazi maalumu.

(f) Kamati zinapofanya ziara za kiuchunguzi.

(2) Kamati zitakazofanya kazi zake kwa faragha ni Kamati ya Haki,Maadili na Madaraka ya Bunge, Kamati ya Mambo ya Nje , Ulinzi naUsalama, Kamati ya Hesabu za Serikali na Kamati ya Hesabu yaSerikali za Mitaa.

4.-(1) Majukumu yenye uwazi wenye mipaka ni yaleyanayotekelezwa na Kamati za kiuchunguzi zifuatazo zenyeutaratibu uliowekewa masharti :-

(a) Kamati ya Hesabu za Serikali;

(b) Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa;

(c) Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge;

(d) Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama.

Majukumuyatakayo-fanywakwafaragha

Majukumuyenye uwaziwenyemipaka

Page 151: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

130

Kanuni za Kudumu za Bunge

(2) Mfano wa uwazi wenye mpaka ni ufuatao:-(a) taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu

za Serikali inapowasilishwa Bungeni inakuwa wazikwa Vyombo vya Habari; na

(b) mchakato wa Kamati hizi kuanza kuwahojiMaafisa Masuhuli kuhusiana na taarifa ya Mdhibitina Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali utakuwawazi hadi hatua ambayo Kamati inataka kufanyamaamuzi ya kutoa mapendekezo ya hatua zakuchukuliwa na Bunge, ambapo Kamati itafanya

kazi zake kwa faragha.

(3) Iwapo mchakato wa kuhoji Maafisa Masuhuli utakuwa ni wakiuchunguzi, mchakato utafanyika kwa faragha.

(4) Kamati zinapofanya ziara kwa lengo la kujifunza au kujielimisha,shughuli zake zitafanywa kwa uwazi na Wajumbe wa Kamatiwatakuwa na uhuru wa kutoa maoni yao ya jumla kwenye vyombovya habari. (5) Maoni ya Kamati yatakuwa ni yale ambayo hayaathiri maamuziyatakayotolewa kwa faragha na Kamati baada ya ziara yake.

(6) Waandishi wa Habari katika kutoa taarifa za namna hii waelezewazi kwamba, maoni hayo ni ya Mbunge binafsi na siyo ya Bungewala Kamati ya Bunge au Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni.

5.-(1) Kwa kuwa Mawaziri wanapokutana na Kamati kwenye Vikaovilivyopangwa wanakuwa Wajumbe, na kwa kuwa inapotokeawamekutana na Waandishi wa Habari mara baada ya Kikaokuzungumzia suala lolote lililojadiliwa kwenye Kamati; Mwenyekitiwa Kamati au Mwakilishi wake au Msemaji wa Kambi Rasmi yaUpinzani Bungeni watakuwa huru kulitolea maoni jambo hilo, ilimradi maelezo yao hayatahusu maamuzi yaliyotolewa na Kamatiambayo yanatakiwa kuwasilishwa Bungeni.

Mawaziriwanapo-toataarifakwawaandishiwahabaribaadayakukutananakamati

Page 152: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

131

Kanuni za Kudumu za Bunge

(2) Wenyeviti wa Kamati zote wataandaliwa utaratibu wa kawaidawa kukutana na Waandishi wa Habari kuzungumzia shughuliitakayofanywa au iliyofanywa na Kamati na maelezo hayoyanayotolewa kwenye Vyombo vya Habari, kwa namna yoyote,yasiwe ni mapendekezo ambayo Kamati imeazimia kuyawasilishaBungeni na ambayo yanaweza kuathiri maamuzi hayo.

(3) Kama kuna jambo ambalo lina maslahi kwa umma na wananchiwanataka maelezo, Mwenyekiti wa Kamati au Mwakilishi wakeatakuwa na uhuru wa kulitolea maelezo ya jumla ili mradi maelezohayo hayatahusiana na maamuzi ya Kamati ambayo yanatakiwakuwasilishwa Bungeni.

Page 153: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

132

Kanuni za Kudumu za Bunge

_______

NYONGEZA YA NANE________

KAMATI ZA KUDUMU ZA BUNGE

[Chini ya Kanuni ya 118]_________

SEHEMU YA KWANZAKAMATI ZA KUDUMU ZISIZO ZA SEKTA

1.- Kamati za Kudumu zisizo za Sekta zitakuwa zifuatazo:

(a) Kamati ya Uongozi;(b) Kamati ya Kanuni za Bunge; na(c) Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge.

2.-(1) Kamati ya Uongozi itakuwa na Wajumbe wafuatao:

(a) Spika, ambaye atakuwa Mwenyekiti;(b) Naibu Spika ambaye atakuwa Makamu Mwenyekiti;(c) Kiongozi wa Shughuli za Serikali Bungeni au

Mwakilishi wake;(d) Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni

au Mwakilishi wake; (e) Mwanasheria Mkuu wa Serikali; na

(f) Wenyeviti wa Kamati za Kudumu au Makamuwao.

(2) Katibu atakuwa Katibu wa Kamati.

(3) Majukumu ya Kamati ya Uongozi yatakuwa ni kujadili nakumshauri Spika kuhusu mambo yote yanayohusu uendeshajibora wa Shughuli za Bunge, na utaratibu wa kurahisisha maendeleoya Shughuli za Bunge au za Kamati yoyote.

KamatizaKudumuzisizo zaSekta

Muundonamajuku-muyaKamatiyaUongozi

Page 154: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

133

Kanuni za Kudumu za Bunge

MuundonamajukumuyaKamatiyaKanuniza Bunge

(4) Katika kutekeleza kazi zilizotajwa katika fasili ya (3), Kamati yaUongozi itakuwa na uwezo wa kuweka muda ambao shughuli yoyoteiliyopelekwa katika Kamati inayohusika sharti ikamilike, na iwaposhughuli iliyopelekwa imewekewa muda kama huo, basi baada yakwisha muda huo au baada ya kwisha muda wowote ulioongezwa,Kamati inayohusika itahesabiwa kuwa imemaliza shughuli hiyo, nashughuli hiyo itaendelea kwenye hatua nyingine kama kwambaMwenyekiti wa Kamati hiyo amemuarifu Spika kumalizika kwashughuli hiyo.

3.- (1) Kamati ya Kanuni za Bunge itakuwa na Wajumbe wafuatao:(a) Spika ambaye atakuwa Mwenyekiti;

(b) Naibu Spika ambaye atakuwa Makamu Mwenyekiti;

(c) Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni au Mwakilishi wake;(d) Mwanasheria Mkuu wa Serikali; na

(e) Wajumbe watakaoteuliwa na Spika.

(2) Vikao vya Kamati ya Kanuni za Bunge vitaongozwa na Spika,na kama Spika hayupo, vitaongozwa na Naibu Spika.

(3) Majukumu ya Kamati ya Kanuni za Bunge yatakuwa ni:

(a) kujadili na kutoa mapendekezo juu ya kufanyamarekebisho au mabadiliko katika Kanuni za

Bunge;

(b) kuchunguza na kutoa taarifa juu ya pendekezololote la mabadiliko katika Kanuni za Kudumu za

Bunge ambalo limepelekwa kwa Kamati hiyo na Spika au na Mbunge yeyote;

(c) kuchunguza na kutoa taarifa kuhusu malalamiko yoyote dhidi ya Uamuzi wa Spika ambayo yamewasilishwa kwa Kamati hiyo na Spika au na Mbunge yeyote; na

(d) kwa kushauriana na Spika, kuzifanyia marekebisho au mabadiliko Nyongeza za Kanuni za Kudumu za Bunge.

Page 155: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

134

Kanuni za Kudumu za Bunge

(4) Akidi ya kila Kikao cha Kamati ya Kanuni za Bunge itakuwa ninusu ya Wajumbe waliotajwa katika kifungu cha 3(1)(c), (d) na(e).

4.-(1) Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge itatekelezamajukumu yafuatayo:

(a) kuchunguza na kutoa mapendekezo kuhusumasuala yote ya haki, kinga na madaraka ya Bunge yatakayopelekwa na Spika;

(b) kushughulikia mambo yanayohusu maadili yaWabunge yatakayopelekwa na Spika.

(2) Kamati itakapokamilisha kushughulikia jambo husika,Mwenyekiti wa Kamati atamjulisha Spika kwa maandishikwamba, Kamati imemaliza kujadili jambo husika.

(3) Spika baada ya kupokea taarifa hiyo, ataagiza iwekwekwenye Orodha ya Shughuli za Bunge kwa ajili ya kuwasilishwa nakujadiliwa Bungeni.

SEHEMU YA PILIKAMATI ZA KUDUMU ZA BUNGE ZA SEKTA

5.-(1) Kamati za Kudumu za Bunge za sekta zitakuwa zifuatazo:

(a) Kamati ya Viwanda, Biashara na Mazingira;(b) Kamati ya Katiba na Sheria;(c) Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama;(d) Kamati ya Utawala na Serikali za Mitaa;(e) Kamati ya Huduma na Maendeleo ya Jamii;(f) Kamati ya Ardhi, Maliasili na Utalii;(g) Kamati ya Kilimo, Mifugo na Maji;(h) Kamati ya Miundombinu; na(i) Kamati ya Nishati na Madini.

K a m a t izaKudumuzaSekta

MajukumuyaKamatiya Haki, MaadilinaMadarakayaBunge

6.-(1) Kamati ya Viwanda, Biashara na Mazingira itasimamia Wizarazifuatazo:

KamatinashughulizaWizara

Page 156: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

135

Kanuni za Kudumu za Bunge

(2) Kamati ya Katiba na Sheria itasimamia shughuli za Wizarazifuatazo:

(a) Ofisi ya Waziri Mkuu - Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Walemavu; (b) Wizara ya Katiba na Sheria; na

(c) Ofisi ya Makamu wa Rais - Muungano.

(3) Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama itasimamiashughuli za Wizara zifuatazo:

(a) Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Ushirikiano wa Kikanda na Kimataifa;

(b) Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa; na (c) Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

(4) Kamati ya Utawala na Serikali za Mitaa itasimamia shughuliza Ofisi ya Rais:

(i) Utawala Bora na Menejimenti ya Utumishi wa Umma; na (ii) Tawala za Mikao na Serikali za Mitaa.

(5) Kamati ya Huduma na Maendeleo ya Jamii itasimamiashughuli za Wizara zifuatazo:

(a) Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto; (b) Wizara ya Habari, Utamaduni, Wasanii na Michezo; na (c) Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi.

(6) Kamati ya Ardhi, Maliasili na Utalii itasimamia shughuli zaWizara zifuatazo:

(a) Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi; na

(b) Ofisi ya Makamu wa Rais - Mazingira. (a) Wizara ya Viwanda Biashara na Uwekezaji; na

(b) Wizara ya Maliasili na Utalii.

Page 157: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

136

Kanuni za Kudumu za Bunge

Majukumuya jumlayaKamatizaSekta

(7) Kamati ya Kilimo, Mifungo na Maji itasimamia shughuli zawizara zifuatazo:

(a) Wizara ya Maji na Umwagiliaji; na(b) Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi.

(8) Kamati ya Miundombinu itasimamia shughuli za Wizara yaUjenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.

(9) Kamati ya Nishati na Madini itasimamia shughuli za Wizaraya Nishati na Madini.

7.-(1) Majukumu ya Kamati za Kudumu za Bunge za sekta yatakuwayafuatayo:-

(a) kushughulikia bajeti ya Wizara inazozisimamia;(b) kushughulikia Miswada ya Sheria na Mikataba

inayopendekezwa kuridhiwa na Bunge iliyo chiniya Wizara inazozisimamia;

(c) kushughulikia Taarifa za utendaji za kila mwaka zaWizara hizo; na

(d) Kufuatilia utekelezaji wa majukumu ya Wizara hizo

(2) Bila ya kuathiri majukumu ya jumla ya Kamati za sekta kamayalivyoainishwa katika fasili ya (1), Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzina Usalama itatekeleza pia majukumu yafuatayo:

(i) kuimarisha ushirikiano kati ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mabunge ya nchi nyingine;

(ii) kufuatilia mwenendo na hali yamtangamamo wa Afrika Mashariki na Jumuiya ya Maendeleoya nchi za Kusini mwa Afrika;

(iii) kushughulikia taarifa za wawakilishi waTanzania katika Bunge la Afrika Mashariki,

SADC na Bunge la Afrika;

(iv) kushughulikia Taarifa zote za wawakilishikatika Vyama mbalimbali vya kibunge

Page 158: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

137

Kanuni za Kudumu za Bunge

ambapo Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni mwanachama; na

(v) Kushughulikia Taarifa za hali ya Ulinzi na Usalamawa Mipaka ya Nchi, na Usalama wa Raia na Malizao.

(4) Kamati iliyoundwa kwa mujibu wa masharti ya fasili ya (3)itafanya kazi zake kwa kuzingatia hadidu za rejea zitakazotolewana Spika, na itaongozwa na Mwenyekiti atakayeteuliwa na Spika.

(5) Akidi ya Mkutano wa Kamati ya Pamoja itakuwa ni theluthimoja ya Wajumbe wa kila Kamati ya Bunge inayounda Kamati hiyo.

(3) Bila ya kuathiri masharti mengine kuhusu muundo namajukumu ya Kamati, Spika anaweza kuunda Kamati ya Pamojaitakayojumuisha Kamati za Bunge mbili au zaidi, kwa ajili ya kulifanyiakazi jambo ambalo, kwa busara zake, ataona linahitaji kufanyiwakazi na Kamati zote.

SEHEMU YA TATUKAMATI ZA SEKTA MTAMBUKA

8.- Kamati za Sekta Mtambuka zitakuwa zifuatazo:

(a) Kamati ya Bajeti;

(b) Kamati ya Masuala ya Ukimwi;

(c) Kamati ya Sheria Ndogo; na

(d) Kamati ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma.

KamatizaSektaMtambuka

Page 159: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

138

Kanuni za Kudumu za Bunge

MajukumuyaKamatiyaBajeti

9. Kamati ya Bajeti itatekeleza majukumu yafuatayo:

(a) Kusimamia Shughuli za Wizara ya Fedha na Mipango;

(b) kujadili na kutoa maoni na ushauri kuhusu uandaaji wa mwongozo wa kutayarisha Mpango na Bajeti ya Serikali kwa kila mwaka;

(c) kutathmini na kuchambua Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali ya kila mwaka yatokanayo na vyanzo vya kodi na vyanzo vingine visivyo vya kodi;

(d) kufuatilia na kusimamia utekelezaji wa Bajeti ya Serikali;

(e) kuchambua na kushauri kuhusu Miswada ya Sheria inayowasilishwa Bungeni yenye madhumuni ya kuongeza au kupunguza mapato na Bajeti ya Serikali;

(f) kufanya utafiti na uchambuzi kuhusu sera za kodi, sera za fedha, na sera za kiuhasibu zilizopendekezwa na Serikali;

(g) kujadili na kutoa maoni na ushauri kuhusu vyanzo vya mapato ya Serikali, na mapendekezo ya hatua za kupunguza utegemezi wa kibajeti;

(h) kutoa ushauri wa jumla kuhusu Bajeti ya Serikali kwa Bunge na Kamati za Kudumu za Bunge;

(i) kuchambua na kutoa maoni na ushauri kuhusu Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaopendekezwa na Serikali; na

(j) kuchambua hoja zitakazojitokeza kwenye Kamati za Bunge za Kisekta wakati wa kujadili Bajeti za Wizara kwa ajili ya kuishauri Serikali.

Page 160: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

139

Kanuni za Kudumu za Bunge

10. Kamati ya masuala ya UKIMWI itatekeleza majukumu yafuatayo:

(a) kuratibu masuala yanayohusu Ukimwi katika sektazote;

(b) kufuatilia utekelezaji wa sera na mipango yaSerikali kuhusu UKIMWI na udhibiti wa Madawa yaKulevya;

(c) kujadili na kutoa mapendekezo na ushauri kuhusuhatua za kudhibiti madawa ya kulevya; na

(d) kushughulikia Bajeti za Tume ya Kudhibiti UKIMWITanzania na Tume ya Kuratibu Udhibiti wa Madawaya Kulevya.

11. Kamati ya Sheria Ndogo itakuwa na Majukumu ya KuchambuaSheria Ndogo ili kujiridhisha iwapo zimekidhi Matakwa na Mashartiya Katiba, Sheria Mama na Sheria nyingine za Nchi.

12. Majukumu ya Kamati ya Uwekezaji wa Mitaji ya Ummayatakuwa kama ifuatavyo:

(a) Kuchambua na kubaini iwapo utekelezaji miradi yauwekezaji wa umma una ufanisi na kuwa umezingatiataratibu na Sheria na miongozo mujarabu ya biashara;na

(b) Kuchambua na kujadili Taarifa ya Mwaka ya Msajili waHazina na Mashirika ya Umma na Kampuni ambazoSerikali ina hisa.

MajukumuyaKamati ya Masualaya UKIMWI

MajukumuyaKamatiyaUwekezaji waMitaji yaUmma

MajukumuyaKamatiyaSheriaNdogo

Page 161: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

140

Kanuni za Kudumu za Bunge

MajukumuyaKamatiyaH e s a b uza Serikaliza Mitaa

Kamati zaKudumu zaBungezinazosimamiamatumizi yafedha zaUmma

MajukumuyaKamatiyaHesabuza Serikali

SEHEMU YA NNE

KAMATI ZA KUDUMU ZA BUNGE ZINAZOSIMAMIA MATUMIZI YAFEDHA ZA UMMA

13. Kamati za Kudumu za Bunge zinazosimamia matumizi ya fedhaza Umma zitakuwa zifuatazo:

(a) Kamati ya Hesabu za Serikali; na

(b) Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa.

14.- Majukumu ya Kamati za Hesabu za Serikali yatakuwa yafuatayo:

(a) kushughulikia maeneo yenye matatizo sugu yamatumizi mabaya ya fedha za Umma katika Wizaraza Serikali yaliyoainishwa katika taarifa ya Mkaguzina Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali;

(b) kufuatil ia utekelezaji wa mapendekezoyaliyokwishatolewa na Kamati hiyo yenye lengo lakuondoa matatizo hayo; na

(c) kutoa mapendekezo na ushauri kwa wizara zaSerikali kuhusu matumizi mazuri ya fedha za Ummaili kupunguza matumizi mabaya ya fedha za Umma.

15. Majukumu ya Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaayatakuwa kama ifuatavyo:

(a) kushughulikia maeneo yenye matatizo sugu ya matumizi mabaya ya fedha za Serikali za Mitaa yaliyoainishwa katika Taarifa ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali;

Page 162: KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE...JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA _____ BUNGE LA TANZANIA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE _____ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

141

Kanuni za Kudumu za Bunge

(b) Kufuatilia utekelezaji wa mapendekezo yaliyokwisha- tolewa na Kamati hiyo ili kuondoa matatizo hayo; na

(c) kutoa mapendekezo na ushauri kwa Serikali za Mitaa kuhusu matumizi mazuri ya fedha ili kupunguza matumizi mabaya ya fedha za Umma.

16. Msingi wa kazi za Kamati ya Hesabu za Serikali na Kamati yaHesabu za Serikali za Mitaa utatokana na Taarifa ya Hesabuzilizokaguliwa ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali.

Zimepitishwa kwa mujibu wa Azimio la Bunge la tarehe 10 Aprili,2013 na marekebisho yaliyofanywa tarehe 15 Januari, 2016 kwamujibu wa Kanuni ya 155(3).

Dodoma Dkt. Thomas D. Kashililah Katibu wa Bunge

MsingiwaKamatiiyaHesabuza SerikalinaKamatiyaHesabuzaSerikali zaMitaa