28
JULAI - DESEMBA 2014 /Nyumba Newsletter www.nhctz.com 1 NYUMBA NEWSLETTER JARIDA LA SHIRIKA LA NYUMBA LA TAIFA JULAI - DESEMBA 2014 TUNAJENGA TAIFA LETU >> Rais Kikwete afungua nyumba za gharama nafuu >> Waziri Mkuu Pinda apongeza mpango wa NHC >> Waziri Tibaijuka azindua Bodi mpya ya NHC >> NHC yaimarisha utendaji, Uendeshaji na udhibiti

National Housing Corporation (NHC) Newsletter

Embed Size (px)

DESCRIPTION

 

Citation preview

JULAI - DESEMBA 2014 /Nyumba Newsletterwww.nhctz.com1

NYUMBA NEWSLETTERJA R I DA L A S H I R I K A L A N Y U M B A L A TA I FA

JULAI - DESEMBA 2014TUNAJENGA TAIFA LETU

>> Rais Kikwete afungua nyumba za gharama nafuu

>> Waziri Mkuu Pinda apongeza mpango wa NHC

>> Waziri Tibaijuka azindua Bodi mpya ya NHC

>> NHC yaimarisha utendaji, Uendeshaji na udhibiti

Nyumba Newsletter/JULAI - DESEMBA 2014 www.nhctz.com2

JULAI - DESEMBA 2014 /Nyumba Newsletterwww.nhctz.com1

NYUMBA NEWSLETTER

Jarida hili hutolewa na Shirika la

Nyumba la Taifa mara mbili kwa mwaka

Julai - Desemba 2014

ISSN NA. 0856-8510

BODI YA UHARIRI

Mwenyekiti

Nehemiah Kyando Mchechu

Mhariri Mkuu

Susan Omari

Mhariri Habari

Muungano K. Saguya

Yahya Charahani

Msanifu Kurasa

Arnold Njuki

Mchapishaji

Iprint Ltd

ANUANI

S.L.P 2977, Dar es Salaam.

Simu: +255 22 2105002,

Baruapepe: [email protected],

Tovuti: www.nhctz.com.

WATAYARISHAJI

Limesanifiwa na Kutayarisha na:

SHIRIKA LA NYUMBA LA TAIFA

Tahariri 2

Rais Kikwete afungua nyumba za gharama nafuu 3

Waziri Mkuu Pinda apongeza mpango wa NHC 4

Waziri Tibaijuka aizindua Bodi mpya ya NHC 5

Serikali yawahakikishia wawekezaji mazingira bora 7

NHC yaajiri wafanyakazi wapya 100 9

Wabunge watembelea Uturuki 10

Viongozi wa Shirika na Wizara wazuru Singapore 12

NHC yavutia wawekezaji nchini Dubai 12

Habari katika picha 17

NHC yafanikiwa katika utekelezaji mpango mkakati 17

Wastaafu utumishi NHC 20

Karibu NHC YALIYOMO

Page 3

Page 6Page 16

Nyumba Newsletter/JULAI - DESEMBA 2014 www.nhctz.com2

TUNAUNGA MKONO AGIZO LARAIS KIKWETE KWA HALMASHAURI

TAHARIRI

Katika nyakati tofauti wakati akifungua

nyumba za gharama nafuu zilizojengwa

na NHC katika Halmashauri mbalimbali

za Wilaya nchini, Rais wa Jamhuri ya

Muungano wa Tanzania, Dk.Jakaya Mrisho

Kikwete aliziagiza halmashauri zote nchini

kutenga maeneo ya ardhi kwa ajili ya

kulipatia Shirika la Nyumba la Taifa na taasisi

zingine zinazojishughulisha na uendelezaji

miliki, ili kuwezesha ujenzi wa nyumba za

gharama nafuu.

Rais Kikwete alitoa agizo hilo baada ya

kufungua miradi ya nyumba za gharama

nafuu zilizojengwa na NHC katika maeneo

ya Mkinga- Tanga, Mkuzo-Ruvuma na

Mnyakongo Kongwa. NHC inayo miradi

ya aina hii katika Halmashauri kadhaa

katika mikoa 19 hivi sasa. “jukumu la kila

halmashauri sasa ni kuhakikisha inatenga

ardhi ya kutosha na kulipatia shirika bila

gharama yoyote kwa ajili ya kukamilisha

azma yake hii njema ya kujenga nyumba za

gharama nafuu”.

Sisi Nyumba Newsletter, tunaunga mkono

na kupongeza kwa dhati agizo hilo la Rais

Kikwete kwani limeangalia hali halisi na

kuona umuhimu wa halmashauri kutenga

maeneo kwa ajili ya kujenga nyumba za

gharama nafuu. Kwa kufanya hivyo siyo

tu kutasaidia wananchi wengi kupata

makazi bora kwa gharama nafuu, bali

kutaboresha pia mandhari ya miji yetu na

kupunguza kasi ya makazi holela ambayo

inakuwa siku hadi siku kutokana na idadi

ya watu wanaohamia mijini kuongezeka

kwa kasi. Aidha, ni Halmashauri hizi hizi

zitakazonufaika na kupata kodi mbalimbali

kutokana na uwekezaji utakaofanywa

katika Halmashauri zao na waendelezaji

Miliki. Kadhalika, kuwepo kwa nyumba

katika Halmashauri hizo kutawawezesha

watumishi wa Halmashauri hizo kupata

nyumba na hivyo kupunguza hali ya

watumishi kukimbia baadhi ya maeneo ya

nchi kutokana na kukosa nyumba za kuishi.

Pamoja na kuunga mkono na kupongeza

uamuzi huo wa Rais, tunaamini kuwa

watendaji wa Halmashauri hizo

watatekeleza agizo hilo la Mheshimiwa

Rais kwa kuwa lina maslahi mapana

kwa watanzania na Halmashauri husika.

Utekelezaji wa agizo hilo kwa wakati

utaondoa changamoto nyingi zinazozikabili

Halmashauri zetu na kuziondolea

Halmashauri jukumu la kujenga nyumba za

watumishi wake kwa kuacha jukumu hilo

kwa NHC yenye dhamana ya kuwezesha

wananchi kupata nyumba.

Kwa kuzingatia yote hayo, tunaona uwe

ni utaratibu wa serikali za Miji na Wilaya

kuanzia sasa wa kutenga ardhi kwa ajili

ya waendelezaji wote wa miliki nchini ili

kuboresha mandhari ya miji, kuondoa

makazi holela na kupisha miradi mingine ya

maendeleo.

Tunaamini kuwa Halmashauri zitachukulia

uamuzi huu kama fursa ya kuongeza siyo tu

makazi bora kwa watu wake bali pia ajira na

ustawi wa maisha kwa wakazi wake.

Rais Dr. Jakaya Kikwete na aliyekuwa Mkuu wa mkoa wa Tanga Mh. Chiku Galawa pamoja na Kaimu Mkurugenzi wa shirika la Nyumba NHC Bw. Felix Maagi wakikata utepe kwa pamoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa nyumba za gharama nafuu Mkinga Tanga.

JULAI - DESEMBA 2014 /Nyumba Newsletterwww.nhctz.com3

RAIS KIKWETE AFUNGUA NYUMBA ZA GHARAMA NAFUU

UZINDUZI GHARAMA NAFUU

Na Mwandishi Wetu,

RAIS Jakaya Kikwete ameziagiza

Halmashauri za Miji na Wilaya nchini

kutenga maeneo kwa ajili ya kuwezesha

NHC na waendelezaji wengine wa nyumba

kujenga nyumba za gharama nafuu. Rais

Kikwete aliyasema hayo alipofungua kwa

nyakati tofauti miradi ya ujenzi ya nyumba

za gharama nafuu iliyojengwa na NHC

katika Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga

–Tanga, Mkuzo-Ruvuma na Mnyakongo –

Kongwa. Katika hafla hiyo, Rais alilazimika

kutoa agizo hilo baada ya kuelezwa kuwa

NHC inalazimika kulipa fidia ya ardhi jambo

linaloongeza gharama ya ujenzi wa nyumba

zinazojengwa. Hivyo, Rais aliziagiza

halmashauri zote nchini kutenga maeneo ya

ardhi kwa ajili ya kulipatia Shirika la Nyumba

la Taifa (NHC) bila gharama yoyote ili

liweze kutekeleza mradi wake wa ujenzi wa

nyumba bora za gharama nafuu. “Nachukua

nafasi hii kuwapongeza NHC kwa kujenga

nyumba hizi za bei nafuu ambazo sisi

serikali tunazihitaji sana ili kuwawezesha

wananchi wetu kuishi kwenye makazi bora…

wito wangu kwa kila halmashauri sasa ni

kuhakikisha inatenga ardhi ya kutosha na

kulipatia shirika bila gharama yoyote kwa

ajili ya kukamilisha azma yake hii”, alisema.

Akiwa Mkuzo Songea Rais Kikwete alirejea

kauli yake aliyoitoa Kasera, Mkinga Tanga

kwamba Halmashauri zizipatie taasisi

zingine zinazojishughulisha na uendelezaji

miliki kama NSSF, PPF, GEPF, PSPF na LAPF

maeneo bila ya masharti ili ziweze kujenga

nyumba za gharama nafuu.

Akijibu maombi mbalimbali ya Shirika, Rais

alisema kuwa Serikali itafanyia kazi suala la

kupunguza kodi ya VAT katika nyumba mpya

kwa kuangalia uwezekano wa kuondolea

kodi hiyo ili kuwarahisishia wananchi

kuzinunua nyumba hizo.

Awali, akitoa taarifa ya Shirika katika mradi

wa Mnyakongo ulioko Kongwa, Mkurugenzi

Mkuu wa NHC Bw. Nehemia Kyando

Mchechu alisema kuwa lengo la kubuniwa

kwa mradi wa nyumba za gharama nafuu

ni kupunguza tatizo la uhaba wa nyumba

hususan za watu wa kipato cha kati na chini

linalowakabili wananchi katika maeneo

mbalimbali nchini. Alisema kuwa mradi huu

utasaidia juhudi za serikali za kuwaletea

wananchi maisha bora kwa kuwezesha

watumishi wa umma kuishi karibu na vituo

vyao vya kazi na kuwaondolea gharama za

usafiri.

“Ni ukweli ulio wazi kwamba hapa nchini

kuna mahitaji makubwa ya nyumba

yanayokadiriwa kufikia zaidi ya nyumba

milioni tatu hivi sasa na yanaongezeka kwa

idadi ya nyumba 200,000 kila mwaka wakati

uzalishaji wa nyumba ni kiasi cha asilimia 10

ya mahitaji ya mwaka mzima,” alisema

Bw. Mchechu alisema kuwa ujenzi wa

mradi huu unahitaji ardhi ya kutosha

ambapo alibainisha kuwa kwa sasa Shirika

linakabiliwa na changamoto kadhaa ikiwemo

halmashauri nyingi kutokuwa na mpango

mahususi wa maendeleo ya ardhi na hivyo

kusababisha NHC kulazimika kununua

ardhi kwa fedha ya mikopo ya benki ili

kulipa fidia. Alisema hatua hiyo inaongeza

gharama ya nyumba hizo zinazoendelea

kujengwa katika halmashauri mbalimbali.

Alisema kuwa ujenzi wa nyumba za gharama

nafuu utaongeza ajira katika

Halmashauri.

Mradi huo wa nyumba za gharama nafuu

una nyumba zenye vyumba viwili na vyumba

vitatu na imewekewa huduma muhimu za

kijamii kama zahanati, shule ya chekechea

na maduka ya bidhaa za aina mbalimbali.

• Afurahishwanakasiyaujenziwa

nyumbahizokatikahalmashauri

• AziagizaHalmashaurikutengamaeneo

yaujenziwanyumbazagharamanafuu

• NHCkujenganyumbazagharama

nafuukatikaHalmashaurizote

Rais Jakaya Kikwete na Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Mh. Saidi Mwambungu (kulia), Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. Profesa Anna Tibaijuka (kushoto) na Kaimu Mkurugenzi wa shirika la Nyumba NHC Bw. David Shambwe wakikata utepe kwa uzinduzi wa Mradi wa Nyumba za gharama nafuu, Mkuzo Songea Mjini

Nyumba Newsletter/JULAI - DESEMBA 2014 www.nhctz.com4

Na Mwandishi Wetu,

WAZIRI Mkuu wa Jamhuri ya

Muungano wa Tanzania, Mh.

Mizengo Kayanza Peter Pinda amezitaka

Halmashauri zote za Miji na Wilaya zilizoko

nchini kuhakikisha zinaunga mkono juhudi

za NHC za kuwapatia ajira vijana. Alizitaka

Halmashauri hizo kuhakikisha kuwa vikundi

vya vijana vya ujenzi wa nyumba nafuu

(building brigades) vilivyoundwa visaidiwe

kwa hali na mali kwa kuvifanya viwe sehemu

ya miradi ya kila Halmashauri.

Mh. Waziri Mkuu alitoa agizo hilo wakati

akizungumza na wakufunzi wanafunzi

kutoka VETA waliohitimu mafunzo

yaliyotolewa na Wakala wa Serikali wa

Utafiti wa Vifaa bora vya ujenzi (NHBRA) ya

namna ya kutumia mashine za kufungamana

kutengeneza matofali. Waziri Mkuu

alifunga mafunzo hayo yaliyotolewa Jijini

Dar es salaam kwa wakufunzi wataalam hao

waliotoka katika kila Mkoa wa Tanzania Bara

ambao sasa wanaendelea kutoa mafunzo

kwa vikundi vya vijana vilivyoko katika

Mikoa yao. Zaidi ya mashine 700 zimetolewa

na NHC kwa ajili ya kuwezesha makundi ya

vijana yaliyoundwa katika kila Halmashauri

nchini kujiajiri kwa kutengeneza matofali

kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za gharama

nafuu.

Halmashauri hizo zimetakiwa kusaidia

mpango huu wenye nia njema kwa kutoa

maeneo kwa ajili ya vijana kuendeshea

shughuli za mpango huo. Maeneo hayo

yanapaswa kuwa na udongo unaofaa

kutengenezea matofali na kuwa karibu na

maeneo ya mjini ili kurahisisha masoko ya

matofali watakayotengeneza.

Waziri Mkuu alisema kuwa yeye binafsi

alimshawishi Mkurugenzi Mkuu wa NHC,

Bw. Nehemia Kyando Mchechu kuwa

katika ujenzi wa nyumba za gharama nafuu

nchini, ahakikishe kuwa anatafuta mbinu

za kutumia teknolojia rafiki wa mazingira

ili kuepuka janga la uharibifu wa mazingira

unaosababishwa na matumizi makubwa ya

kuni mbichi ili kuchoma matofali.

“Licha ya kuwa utengenezaji wa matofali

ya kuchoma unatekeleza azma ya Serikali

ya kutaka wananchi wake wawe na nyumba

bora, kwa kweli roho huwa inaniuma

hasa ukizingatia kiasi kikubwa cha miti

inayokatwa kuyachoma hayo matofali hadi

yawe imara, tena ikiwa mibichi,” alisema Mh.

Pinda.

Aliupongeza Wakala wa Serikali wa Utafiti

wa Vifaa Bora vya Ujenzi (NHBRA) kwa

kubuni mashine hizo ambazo alisema

zinauzwa kwa bei ambayo Halmashauri zote

zinaweza kuzimudu kuwanunulia vijana

wengine ili kupanua ajira.

“Mkurugenzi Mkuu ameniambia kila

mashine inauzwa shilingi 450,000/- na

inaweza kutengeneza matofali 700 kwa siku

moja, hayo matofali yanatumia mifuko saba

tu ya saruji. Hili ni jambo linalowezekana!”

alisisitiza. Hivyo, akawataka Wakurugenzi

wa Miji na Wilaya kushiriki kikamilifu katika

kuhakikisha kuwa mpango huu unakuwa

endelevu ili vijana wanufaike na mpango

huu. Alisema anataka Wakurugenzi hao

wachangamkie haraka kuzinunua hizo

mashine kwa sababu zinasaidia uhifadhi

wa mazingira, zinachochea ufanisi wa

teknolojia, zinapunguza gharama za

ujenzi na zinasaidia kutoa ajira kwa

vijana. Hata hivyo, Waziri Mkuu aliwasihi

watakaoendesha miradi hiyo wasitoze bei

kubwa kwa matofali watakayotengeneza

ili wananchi wengi waweze kumudu bei na

wabadili hadhi za makazi yao. Waziri Mkuu

alimtaka Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw.

Mchechu aweke mpango wa kuendeleza

kampeni hiyo aliyoianzisha angalau kwa

miaka mitano mfululizo ili mpango huo

WAZIRI MKUU AUPONGEZA MPANGO WA NHC WA KUTOA AJIRA

WAZIRI MKUU PINDA

• Niwakusaidiavijanamashineza

kufyatuamatofali

• Unalengakutoaajirazipatazo7000

• Zaidiyamashine700zasambazwa

katikaHalmashauri

• AzitakaHalmashaurinchini

kusaidiampangohuo

Waziri Mkuu Mizengo Pinda akikabidhi cheti kwa mmoja wa wahitimu wa mafunzo ya wataalam wa mashine za kutengeneza matofali kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za gharama nafuu Mafunzo hayo yaliyoanza Januari 6 mwaka huu, yaliendeshwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) pamoja na Mamlaka ya Elimu ya Ufundi Stadi (VETA) kwa kushirikiana na Wakala wa Utafiti wa Vifaa Bora vya Ujenzi (NHBRA) iliyo chini ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi. Kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa Nehemia Mchechu na kushoto kwa Waziri Mkuu ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadick na kulia kwa Waziri Mkuu ni Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt Fenella Mukangara.

Continued page 10 >>

JULAI - DESEMBA 2014 /Nyumba Newsletterwww.nhctz.com5

BODI MPYA

Na Mwandishi Wetu,

WAZIRI wa Ardhi, Nyumba na

Maendeleo ya Makazi, Profesa

Anna Kajumulo Tibaijuka, ameagiza Bodi

ya Wakurugenzi wa Shirika la Nyumba la

Taifa (NHC) kuendelea na ujenzi wa nyumba

za gharama nafuu ili kuendeleza falsafa

iliyolianzisha Shirika hilo mwaka 1962 ya

kuboresha makazi ya watu wa kipato cha

chini na kati. “Ninachotaka kuwasisitizieni

Bodi mpya na Menejimenti ya NHC, Shirika

lisisahau lilipotoka liendelee na dhima

ya kuanzishwa kwake mwaka 1962 kwa

kuwajali pia wananchi kwa kujenga nyumba

za gharama nafuu, suala la nyumba lilikuwa

ni kampeni ya chama cha TANU,” alisema.

Agizo hilo alilitoa Waziri Anna Tibaijuka

Makao Makuu ya NHC, wakati alipokuwa

akizindua Bodi mpya ya Wakurugenzi

ya NHC yenye wajumbe saba hafla

iliyohudhuriwa pia na Watendaji wa

Shirika. Akizungumza katika hafla hiyo,

Waziri Tibaijuka aliagiza Shirika kuendelea

kutekeleza mabadiliko ya kuboresha

huduma za Shirika ili kuongeza tija

kubwa.“Nina imani kuwa mtaendelea na

utaratibu huu mzuri wa kujenga nyumba za

gharama nafuu ili kuwezesha Watanzania

wengi zaidi kunufaika na mipango yenu

mizuri mliyoianzisha,” alisema Tibaijuka.

Waziri Tibaijuka alisema kuwa pamoja na

kuwa hadi hivi sasa hakuna sera ya nyumba,

aliiagiza Bodi na Menejimenti ya NHC

kuhakikisha kuwa Shirika linajiendesha

kwa kufuata misingi ya ushindani, lakini

lisipoteze roho yake ya kujenga nyumba

za gharama nafuu na kuwe na vigezo

vitakavyowawezesha wenye sifa za kupata

nyumba za gharama nafuu wanufaike na

siyo wengine.

Waziri Tibaijuka alilipongeza Shirika la

Nyumba la Taifa na kubainisha kuwa hivi

sasa Shirika hilo limeimarika licha ya

kupitia katika changamoto nyingi sana huko

nyuma na kwamba Shirika linaongozwa

na Menejimenti yake huru, huku Serikali

kupitia Wizara yake ikifanya jukumu lake la

usimamizi.

Akizungumzia mabadiliko ya Sheria,

Waziri huyo alisema kuwa Serikali

ilijitahidi kubadilisha sheria mbalimbali

zilizokwamisha uwekezaji katika sekta ya

nyumba. Alizitaja sheria hizo zilizofanyiwa

marekebisho kuwa ni pamoja na sheria ya

ardhi namba 4 ya mwaka 1999, sheria ya

mikopo ya nyumba ya mwaka 2008 na sheria

ya hati pacha katika majengo ya ghorofa ya

mwaka 2008. Aidha, alisema kuwa mwaka

2010, Serikali iliagiza Shirika hili lifanyiwe

mabadiliko makubwa na lisukwe upya kwa

kulipatia uongozi mpya.

Aliiambia Bodi kuwa Wizara yake imekuwa

ikifanya mengi kuboresha sekta ya

nyumba ikiwemo kuboresha sera na sheria

mbalimbali kwa kuwa hatuwezi kuwa na

nyumba bora bila ya kuwa na mazingira bora

ya uwekezaji na sheria bora.

Alisema kuwa Bodi ambayo ameizindua

imelikuta Shirika na sekta ya uendelezaji

miliki vikiwa katika hali nzuri, hivyo akaiagiza

Bodi hiyo kuendeleza moto ule ule iliyokuwa

nayo Bodi iliyomaliza muda wake.

Alilitaka Shirika hilo kuweka uwiano

mzuri kati ya nyumba za kupangisha na

zile za kuuza ili kuweza kujilinda pindi

kunapotokea kuporomoka kwa soko la

nyumba. “Ninaomba kabisa Bodi yetu mpya

tuangalie “sustainability” ya tunayoyafanya,

washaurini hawa vijana wanunue nyumba

zinazowazunguka humu mijini ili kuwa na

vitega uchumi vilivyo katika mandhari nzuri,

siyo mbananishe maghorofa kama ilivyo

Kariakoo,”alisema.

Naye, Mkurugenzi wa NHC Bw. Nehemia

Kyando Mchechu, alisema kuwa Shirika la

Nyumba la Taifa lina mali zenye thamani

isiyopungua shilingi trilion 1.5 hivyo

changamoto kubwa iliyopo kwa sasa ni

kuhakikisha wanatumia fursa zilizopo

kuwapatia Watanzania makazi bora.

Alisema kuwa Watanzania wana matumaini

makubwa na Shirika hilo ambalo hivi sasa

limedhamiria kufanya mabadiliko makubwa

hasa yenye lengo la kujiimarisha kibiashara

ikiwemo kujenga nyumba nyingi zaidi ili

kukuza uchumi wa Taifa na wa mtu mmoja

mmoja.

Alisema pamoja na jitihada hizo, Shirika

linakabiliwa na changamoto mbalimbali

kama kulazimika kununua ardhi kwa

gharama kubwa kwenye halmashauri za

Wilaya hapa nchini. Pia alisema kuwa Shirika

linalazimika kutengeneza miundombinu ya

umeme, maji na barabara katika maeneo

ya miradi na kuongeza gharama kubwa

jukumu ambalo alisema linapaswa kufanywa

na mamlaka zingine zinazohusika. Aliiomba

Serikali kuondoa kodi kwenye mauzo ya

nyumba mpya ambazo hazizidi shilingi

milioni 100 hatua itakayosaidia watu wengi

kuweza kununua nyumba kwa gharama

ndogo.

Wakizungumza katika hafla hiyo,

Wakurugenzi hao wa Bodi waliipongeza

Bodi iliyopita kwa kazi yao nzuri ya kuiongoza

Menejimenti ya Shirika. Walimshukuru Rais

Jakaya Mrisho Kikwete na Waziri Tibaijuka

kwa kuwapa jukumu zito la kulisimamia

Shirika na wakaahidi kuendeleza mambo

makubwa yaliyofanywa na Bodi iliyomaliza

muda wake.

Bodi hiyo inaundwa na Mwenyekiti

Mheshimiwa Zakhia Hamdani Meghji,

Bw. Diotrephes Mmari (aliyewahi kuwa

Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba

na Maendeleo ya Makazi)ambaye ndiye

Makamu Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Bibi

Subira Mchumo, Bw. Patrick Rutabanzibwa

(aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi,

Nyumba na Maendeleo ya Makazi), Bw.

Samson Kasalla (aliyekuwa Kamishna wa

Jeshi la Polisi), Bibi Irene Isaka (Mkurugenzi

Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mifuko ya

Jamii(SSRA), Bw. Bedason Shallanda kutoka

Benki Kuu ya Tanzania na Bw.Charles

Mafuru (Mkurugenzi wa Nyumba -Wizara

ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi).

WAZIRI TIBAIJUKA AIZINDUA BODI MPYA YA NHC • AlipongezaShirikakwakazinzuri

• Alitakaliongezekasiyakujenganyumbazagharamanafuu

• Atakavigezovyakuuzanyumbahizokwawananchistahiliviwekwe

• Wenyewewamshukuru,waahidikufanyamakubwa

• SerikaliyaombwakuondoakodiyaVATkatikanyumbazagharamanafuu

BODI MPYA KATIKA PICHA

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Kajumulo Tibaijuka akizungumza na watendaji wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) (hawapo pichani) kwenye uzinduzi rasmi wa Bodi mpya ya Shirika hilo uliofanyika kwenye Makao Makuu ya Shirika hilo jijini Dar es Salaam jana. (Picha zote kwa hisani ya kitengo cha Mawasiliano na Huduma kwa Jamii cha NHC)

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Anna Kajumulo Tibaijuka akimkabidhi mkoba Mjumbe mpya wa Bodi ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) , Diotrepes Mmari.

Wajumbe wapya wa Bodi ya Shirika la Nyumba la Taifa wakiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Anna Kajumulo Tibaijuka.

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Anna Kajumulo Tibaijuka akimkabidhi mikoba Mwenyekiti mpya wa Bodi ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) , Mama Zakhia Hamdani Meghji.

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Anna Kajumulo Tibaijukakatika picha ya pamoja na Mjumbe wa Bodi ya NHC, Irene Isaka.

Mjumbe mpya wa Bodi ya NHC, Charles Mafuru, ambaye pia ni Kaimu Mkurugenzi wa Nyumba wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi akiwaelekeza jambo watendaji wakuu wa Shirika la Nyumba (NHC) (hawapo pichani)

JULAI - DESEMBA 2014 /Nyumba Newsletterwww.nhctz.com7

MAZINGIRA BORA

Na Mwandishi Wetu,

WADAU wa sekta ya uendelezaji miliki

nchini wamehakikishiwa mazingira

bora na salama kwa ajili ya uwekezaji katika

sekta hiyo inayokuwa kwa kasi nchini katika

siku za hivi karibuni.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Ardhi,

Nyumba na Maendeleo ya Makazi Profesa

Anna Tibaijuka jijini Dar es Salaam,

alipozungumza na wadau mbalimbali

waliohudhuria kwenye jukwaa la

wawekezaji wa ndani lililoandaliwa na

Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) ambalo pia

lilishirikisha baadhi ya Wakuu wa Mikoa.

Profesa Tibaijuka alisema kuwa mazingira

bora ya uwekezaji katika sekta ya uendelezaji

miliki yameshawekwa na Serikali kwa

kuunda sheria rafiki za uwekezaji ambapo

ongezeko la uwekezaji wa moja kwa moja

kutoka nje ya nchi umekuwa na mageuzi

ya kiuchumi yamefanywa na yamewezesha

kuboreka kwa uchumi wa soko.

Alisema programu mbalimbali za mabadiliko

ya kisheria na kitaasisi yamefanywa na

serikali ambayo yana lengo la kuboresha

mazingira ya soko na uwekezaji binafsi

katika sekta binafsi.

Alisema pia kwamba maboresho ya

kitaasisi kwa kutoa vipaumbele kwa miradi

mbalimbali tayari yameshafanywa na

Kituo cha Uwekezaji nchini (TIC) na taasisi

nyingine za umma hali inayowarahisishia

wawekezaji kuamua mahali sahihi pa

kuwekeza.

“Ninachukua fursa hii kuwakaribisheni

wawekezaji ambao mmeshiriki kwenye

jukwaa hili, mchukue fursa hii kupata

taarifa muhimu mnazozihitaji na hatimaye

kuchukua fursa zilizopo tayari katika

uwekezaji kwenye miradi ya Usa River na

Safari Satellite City kule Arusha, na Salama

Creek Satellite City-Dar es Salaam,” alisema

Prof. Anna Tibaijuka.

Mkurugenzi Mkuu wa NHC, Bw. Nehemia

Kyando Mchechu, alisema kuwa fursa

zilizopo katika sekta ya uendelezaji miliki

ni za kuvutia na hazina ushindani mkubwa

na ndiyo maana NHC imepanga kujenga

nyumba nyingi zaidi kwa ajili ya biashara na

makazi nchini kote.

Katika kipindi cha miaka mitano iliyopita,

sekta ya uendelezaji miliki imechukua

nafasi ya tano kati ya vivutio kumi vikuu vya

uwekezaji wa moja kwa moja kutoka nje ya

nchi yaani Foreign Direct Investment (FDI).

Bw. Mchechu alisema kuwa Shirika la

Nyumba la Taifa (NHC), limedhamiria

kuyabadilisha maeneo ya jiji la Dar es Salaam

na mikoa mingine nchini baada ya kuzindua

ujenzi wa miji midogo inayojitegemea ndani

ya miji ya sasa. Alisema kuwa miradi hiyo

itakapokamilika itabadilisha mandhari ya

maeneo mbalimbali nchini na kuyafanya

kuwa ya kisasa.

Bw.Mchechu alisema ujenzi wa miradi

mitatu utaanza hivi karibuni ikiwemo ya

miji midogo katika majiji ya Dar es Salaam

na Arusha pamoja na kuendeleza nyumba

zilizobomolewa ili kupisha uendelezaji

mpya.

Alisema katika jiji la Dar es Salaam,

kutakuwa na mradi wa Salama Creek

ulioko Kigamboni na Up Town Kawe ulioko

ilipokuwa Tanganyika Packers ambayo

italifanya jiji hilo kubadilika na kuwa la kisasa

zaidi tofauti na linavyoonekana sasa.

Bw. Mchechu alisema katika miradi hiyo,

kutajengwa nyumba nyingi za kuishi,

biashara na sehemu za huduma muhimu

na kwamba itakapokamilika itabadili

muonekano wa maeneo hayo.

Alisema miradi mingine itakayotekelezwa ni

ya Usa River na Safari City itakayojengwa

Jijini Arusha na kwamba inalenga

kulibadilisha jiji hilo ili kuwa la kisasa.

Mkurugenzi Mkuu alisema kuwa mradi

mwingine ambao utatekelezwa katika Jiji

la Dar es Salaam, ni mradi wa ujenzi wa miji

mdogo wa Luguruni.

Mchechu alisema kuwa kila mradi

utagharimu dola za Marekani milioni mbili

(zaidi ya shilingi bilioni 3.4) na itakamilika

kati ya kipindi cha miaka 7 mpaka 12.

Alisema miradi mingine ambayo

itatekelezwa ni pamoja na Bagamoyo,

Dodoma, Mbeya, Mtwara, Lindi, Mwanza na

maeneo mengine nchini.

Mchechu alisema jukwaa hilo limetokana

na mkutano mkubwa wa wawekezaji

waliofanya hivi karibuni nchini Dubai

ambalo liliwahusisha wawekezaji wa nje

ili wawekeze katika sekta ya miliki nchini

Tanzania.

SERIKALI YAWAHAKIKISHIA WAWEKEZAJI MAZINGIRA BORA

• Niwawekezajiwandaniwasektayamiliki

• Sherianavivutiovingikatikasektahiyovyaboreshwa

• NHCyadhamiriakubadilishamandhariyamijinchini.

“Profesa Tibaijuka alisema

kuwa mazingira bora ya

uwekezaji katika sekta

ya uendelezaji miliki

yameshawekwa na Serikali

kwa kuunda sheria rafiki za

uwekezaji ambapo ongezeko

la uwekezaji wa moja kwa

moja kutoka nje ya nchi

umekuwa na mageuzi ya

kiuchumi yamefanywa na

yamewezesha kuboreka kwa

uchumi wa soko.

Nyumba Newsletter/JULAI - DESEMBA 2014 www.nhctz.com8

KAMATI POAC

• Afurahishwanakasiyaujenziwanyumbahizokatikahalmashauri

• AziagizaHalmashaurikutengamaeneoyaujenziwanyumbazagharamanafuu

• NHCkujenganyumbazagharamanafuukatikaHalmashaurizote

serikali tunazihitaji sana ili kuwawezesha

wananchi wetu kuishi kwenye makazi bora…

wito wangu kwa kila halmashauri sasa ni

kuhakikisha inatenga ardhi ya kutosha na

kulipatia shirika bila gharama yoyote kwa

ajili ya kukamilisha azma yake hii”, alisema.

Akiwa Mkuzo Songea Rais Kikwete alirejea

kauli yake aliyoitoa Kasera, Mkinga Tanga

kwamba Halmashauri zizipatie taasisi

zingine zinazojishughulisha na uendelezaji

miliki kama NSSF, PPF, GEPF, PSPF na LAPF

maeneo bila ya masharti ili ziweze kujenga

nyumba za gharama nafuu.

Akijibu maombi mbalimbali ya Shirika, Rais

alisema kuwa Serikali itafanyia kazi suala la

kupunguza kodi ya VAT katika nyumba mpya

kwa kuangalia uwezekano wa kuondolea

kodi hiyo ili kuwarahisishia wananchi

kuzinunua nyumba hizo.

Awali, akitoa taarifa ya Shirika katika mradi

wa Mnyakongo ulioko Kongwa, Mkurugenzi

Mkuu wa NHC Bw. Nehemia Kyando

Mchechu alisema kuwa lengo la kubuniwa

kwa mradi wa nyumba za gharama nafuu

ni kupunguza tatizo la uhaba wa nyumba

hususan za watu wa kipato cha kati na chini

linalowakabili wananchi katika maeneo

mbalimbali nchini. Alisema kuwa mradi huu

utasaidia juhudi za serikali za kuwaletea

wananchi maisha bora kwa kuwezesha

watumishi wa umma kuishi karibu na vituo

vyao vya kazi na kuwaondolea gharama za

usafiri.

“Ni ukweli ulio wazi kwamba hapa nchini

kuna mahitaji makubwa ya nyumba

yanayokadiriwa kufikia zaidi ya nyumba

milioni tatu hivi sasa na yanaongezeka kwa

idadi ya nyumba 200,000 kila mwaka wakati

uzalishaji wa nyumba ni kiasi cha asilimia 10

ya mahitaji ya mwaka mzima,” alisema

Bw. Mchechu alisema kuwa ujenzi wa

mradi huu unahitaji ardhi ya kutosha

ambapo alibainisha kuwa kwa sasa Shirika

linakabiliwa na changamoto kadhaa ikiwemo

halmashauri nyingi kutokuwa na mpango

mahususi wa maendeleo ya ardhi na hivyo

kusababisha NHC kulazimika kununua

ardhi kwa fedha ya mikopo ya benki ili

kulipa fidia. Alisema hatua hiyo inaongeza

gharama ya nyumba hizo zinazoendelea

kujengwa katika halmashauri mbalimbali.

Alisema kuwa ujenzi wa nyumba za gharama

nafuu utaongeza ajira katika Halmashauri.

Mradi huo wa nyumba za gharama nafuu

una nyumba zenye vyumba viwili na vyumba

vitatu na imewekewa huduma muhimu za

kijamii kama zahanati, shule ya chekechea

na maduka ya bidhaa za aina mbalimbali.

RAIS KIKWETE AFUNGUA NYUMBA ZA GHARAMA NAFUU

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Huduma kwa Jamii Cha Shirika la Nyumba la Taifa (National Housing) Susan Omari (kushoto) akitoa maelezo na kisha kukabidhi kwa Rais Dk. Jakaya Mrisho Kikwete mashine za kutengeneza matofali ya kufungamana ambazo zimekwishagawanywa kwenye wilaya zote za Mkoa wa Tanga ili kuwawezesha kuanzisha vikundi vya ujenzi vya vijana. Kulia ni aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Tanga Luteni Mstaafu Chiku Galawa. Mashine hizo zilitolewa wakati wa Uzinduzi wa nyumba za bei nafuu Wilayani Mkinga

Na Mwandishi Wetu,

RAIS Jakaya Kikwete ameziagiza

Halmashauri za Miji na Wilaya nchini

kutenga maeneo kwa ajili ya kuwezesha

NHC na waendelezaji wengine wa nyumba

kujenga nyumba za gharama nafuu. Rais

Kikwete aliyasema hayo alipofungua kwa

nyakati tofauti miradi ya ujenzi ya nyumba

za gharama nafuu iliyojengwa na NHC

katika Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga

–Tanga, Mkuzo-Ruvuma na Mnyakongo –

Kongwa. Katika hafla hiyo, Rais alilazimika

kutoa agizo hilo baada ya kuelezwa kuwa

NHC inalazimika kulipa fidia ya ardhi jambo

linaloongeza gharama ya ujenzi wa nyumba

zinazojengwa. Hivyo, Rais aliziagiza

halmashauri zote nchini kutenga maeneo ya

ardhi kwa ajili ya kulipatia Shirika la Nyumba

la Taifa (NHC) bila gharama yoyote ili

liweze kutekeleza mradi wake wa ujenzi wa

nyumba bora za gharama nafuu. “Nachukua

nafasi hii kuwapongeza NHC kwa kujenga

nyumba hizi za bei nafuu ambazo sisi

“Ni ukweli ulio wazi kwamba hapa nchini kuna mahitaji makubwa ya nyumba yanayokadiriwa kufikia zaidi ya nyumba milioni tatu hivi sasa na yanaongezeka kwa idadi ya nyumba 200,000 kila mwaka wakati uzalishaji wa nyumba ni kiasi cha asilimia 10 ya mahitaji ya mwaka mzima,”

JULAI - DESEMBA 2014 /Nyumba Newsletterwww.nhctz.com9

WAAJIRIWA WAPYA

Na Mwandishi Wetu,

SHIRIKA la Nyumba la Taifa (NHC)

limeajiri wafanyakazi wapya 100 kutoka

wa kada mbalimbali ikiwa ni jitihada za

kuimarisha ikama na kuboresha huduma

zake kwa umma.

Taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya

Uendelezaji Rasilimali watu imeeleza kuwa

wafanyakazi hao walioajiriwa kuanzia

Januari 2013 mpaka Oktoba 2014.

Wfanyakazi hao ni wa taaluma za Usimamizi

na Uendelezaji Miliki, Biashara, Utawala,

Manunuzi, Sheria na Ugavi.

Wafanyakazi hao ni pamoja na Mameneja

miradi ambao ni Bw. Etheldreder Koppa,

Bw. George Magembe, Bw. Samwel Metili,

Bw. Cliford Hungu na Bw. Subira Gudadi.

Maafisa Miliki walioajiriwa ni Mwasiti

Jimmy, Amon Mazanda, Dastani Mgouya,

Songoro Saidi, Lwitiko Ndigha, Emenick

Sanga, Victor Lawrence Sheushi, Edward

Haule, Amos Manyama, Costantine Yuda,

Keneth Ntulo, Fadhili Anyegile, Augustino

Sanga, Elizabeth Michael Maro, Wambura

Jafari Chege. Maafisa Miliki wengine

walioajiriwa ni Thomas Msambwa,

Mukakaro Mukakaro, Humphrey Tarimo,

Zenna Nyange, Goodluck Thomas,

Ramadhani Sadicki na Philip Gawa.

Katika kundi la Maafisa Manunuzi

waliajiriwa wamo Aman Sehaiya, Rukia

Kidasi, Fransisca Francis Michael, Kaiza

Straton, Paskalina Monko, Devina Msechu,

Victor Christopher, Evarista Mallya,

Castro Nzaye, Jimmy Mbogela, Anitha

Aloyce, Ritha Mokimirya na Olga William.

Wahasibu Wasaidizi walioajiriwa ni pamoja

Mkurugenzi wa Rasilimali Watu, James Rhombo akiwasilisha mada kwenye semina ya mafunzo kwa waajiriwa wapya inayofanyika kwa siku mbili kwenye hoteli ya JB Belmonte iliyoko Golden Jubilee Tower, Jijini Dar es Salaam.

Pichani baadhi ya Waajiriwa wapya kutoka kushoto Fatima Rajabu, wa tatu Clara Lumbanga, Felichism Mtenga na Lister Nyabilinyi wakisikiliza mada kutoka kwa Mkurugenzi wa Rasilimali Watu, James Rhombo wakati akiwasilisha mada kwenye semina ya mafunzo kwa waajiriwa wapya inayofanyika kwa siku mbili kwenye hoteli ya JB Belmonte iliyoko Golden Jubilee Tower, Jijini Dar es Salaam.

na Seleki Apolinary, Mussa Efata, Gloria

Otto Ringia, Lilian Reuben, Nimo William,

Salim Mbwana Salum, Benson Shabani,

Repson Yosia, Nancy Joseph na Baha j.

Nkhangaa.

Katika kada ya madereva wamo Nicholaus

Lyimo, George Kyamba, Raphael Maliva,

Anderson Fungo, Aquiline Mushi, Elias

Polepole, Aidin Stafford, Mohamed

Swanga na Abdulkher Abdallahtif.

Wafanyakazi wengine na vyeo vikiwa

kwenye mabano ni Grayson Godfrey

(Facility Manager), Rashid Omar

Amani (Msaidizi Masjala), Iddi Khalifa

Kitete (Msaidizi Masjala), Edna Lucas

Chogo (Afisa Utumishi Mwandamizi) na

Emmanuel Kabeya (Mwanasheria).

Wengine ni Godlove Godwin (Afisa

Utumishi), Gema Guerino Gamanywa

(Afisa Utumishi), Telesphori Focus (Injinia

wa Umeme), Nikundiwe Mmakasa

(Mkaguzi wa Ndani Mwandamizi) Bulla

Boma (Meneja Ofisi ya Mkurugenzi Mkuu)

Tuntufye Mwambusi (Meneja Mauzo),

Emmanuel Kyarwenda (Mhasibu Kodi),

Sixtus Kilenga (Afisa Utawala Mwandamizi),

John Laswai (Mwanasheria Mwandamizi)

na Elias Mwashiuya (Meneja Huduma za

Sheria.

Pia wamo Clara Matern Lumbanga (Afisa

Mwandamizi Uendelezaji Biashara),

Fatima Adadi Rajabu (Afisa Mwandamizi

Uendelezaji Biashara), Salvatory Venant

Hinju (Afisa Mwandamizi Uendelezaji

Biashara), Getrude E. Mallya (Afisa

Utawala), Gloria E. Staki (Mapokezi),

John Temu(Mhasibu Msaidizi), Rose

Erasimus Uisso (Mhasibu Msaidizi),

Rose Michael Mwandemani (Mhasibu

Msaidizi), Khalid Maulid Mvungi(Mhasibu

Msaidizi), Felichism S. Mtenga(Mhasibu

Msaidizi),Hilda Anderson Temu(Mhasibu

Msaidizi), Lister Joseph Nyabinyili

(Mhasibu Msaidizi) na Mwita Bernard

Megabe(Mhasibu Msaidizi).

Wengine ni Domina Willbard Rwemanyila

(Afisa Huduma kwa wateja)Dyana Hatuey

Mwamba ((Afisa Huduma kwa wateja),

Jackline Kilawe (Afisa Mapokezi), Edwin

Martin Pesha (Dereva), Shija Samuel

Shimbi(Dereva), John Gustav Masika

(Dereva), Selemani A. Mashaka(Dereva),

Sadiki Muhamed Mneka(Dereva), Simon

Mhiliwa(Mhasibu Msaidizi) na Malima

Mukama(Mhasibu Msaidizi).

Menejimenti ya Shirika inawatakia

wafanyakazi hao wapya kazi njema yenye

kuliletea Shirika mafanikio zaidi hususan

wakati huu ambapo Shirika linatekeleza

mpango mkakati wake ambao unalenga

kujenga nyumba 15,000 katika kipindi cha

miaka mitano ijayo, idadi ambayo haijawahi

kufikiwa na Shirika tangu kuundwa kwake

Agosti 1, 1962.

• Niwakadambalimbalizautumishi

• Nimkakakatiwakuimarishaikamanaufanisi

NHC YAAJIRI WAFANYAKAZI WAPYA 100

Nyumba Newsletter/JULAI - DESEMBA 2014 www.nhctz.com10

Na Mwandishi Wetu,

JUMLA ya wafanyakazi arobaini

wamestaafu rasmi utumishi wao

kwa umma kwa mujibu wa sheria kwa

nyakati tofauti kati ya Januari hadi

Julai mwaka huu.

Taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya

Uendelezaji Rasilimali watu imeeleza

kuwa wafanyakazi hao waliostaafu

katika kipindi hicho ni wa kada

mbalimbali hususan za Uendelezaji

Miliki, Utawala, Usimamizi Miliki na

Ubunifu Majengo.

Wafanyakazi hao na vyeo vyao

walivyotumikia vikiwa kwenye

mabano ni Joseph Mganga (Meneja

Uendeshaji Miliki), Verynice J. Nassary

(Accounts Technician), Simon Samo

(Mhandisi), Jumanne Mtuli (Fundi

Mchundo) Lusagana B. M. Lusagana

(Meneja wa Miradi ya Ubia), Dekusura

Kimaro (Karani wa Mahesabu) na

Telly Swebe (Msaidizi Mwandamizi

Utawala).

Wengine ni Traiphon Ndunguru

(Fundi Mwandamizi) , Khalfani Mhina

Juma (Dereva), Lazaro Lwanyakasura

(Fundi Mchundo), Omari Abbasi(Fundi

Mwandamizi), Alexander Nicolaus

(Msaidizi wa Ofisi) na Rajabu M.

Ngubureni(Dereva).

Pia katika orodha hiyo wamo Laurensia

Justinian (Msaidizi Mahesabu) ,

Goodnes Meresi (Msaidizi wa Ofisi),

Bakari Mnkande (Fundi Mchundo),

Augustino Joseph (Mlinzi), Cecilia

Sentala (Msaidizi masuala ya nyumba),

Leonard C. Maganga (Mkusanya

Madeni Mwandamizi).

Wastaafu wengine ni Bakari

Gumbo (Dereva), Michael Masudi

(Mlinzi), Monica Mlay (Mhudumu

Arusha), Modesta Gervas (Mhudumu

Kinondoni), Anastazia Togoro (Mpiga

chapa Shinyanga), Jane Nkwama

(Mpiga chapa Arusha), Simon

Shekigenda (Msaidizi masuala ya

nyumba), Loyce Petro (Mkadiriaji

Majengo Mwandamizi), Catherine

Fumbuka (Mhasibu), Said Mnongane

(Fundi Mchundo), Herman Kaseka

(Afisa Nyumba Kilimanjaro), Marcus

Mdugala, Sarah Mhanga (Mpiga chapa),

Twahir Chamulume (Afisa Masjala),

Allan Kabogo (Daktari wa Shirika),

Damian Hugho (Mhasibu), Seleman

Said (Afisa Stoo), Mathew Kabunga

(Mwanasheria), Ally Nangwanda

(Mhasibu Msaidizi), Alexander

Nicholaus (Mhudumu), Omari Abbasi

(Fundi) , Asubi Mwaigwisya (Fundi

Mchundo) na Mathias Chilemba (Fundi

Mchundo).

Wengine ni Ng’aranga Magai (Meneja

Mkoa –Kagera), Paul Mokimirya

(Meneja Mkoa –Ruvuma), Suresh

Dhrona – Meneja Ukaguzi wa Ndani,

Mariam Kambi- (Meneja Mkoa

Singida),Amina Salum(Mhudumu wa

Ofisi- Ilala) na Yassin Simtitu(Mhandisi

– Ruvuma).

Katika hatua nyingine wafanyakazi

watatu wa Shirika waliamua kuacha

kazi wenyewe kwa hiyari yao na

wengine kuachishwa kazi kwa sababu

mbalimbali .

Menejimenti ya Shirika inawatakia

wafanyakazi hao wastaafu maisha

mema na yenye mafanikio hasa

baada ya kushiriki vilivyo kuliletea

Shirika mafanikio makubwa hususan

wakati huu ambapo Shirika limekuwa

likitekeleza mpango mkakati wake

ambao unalenga kujenga nyumba

15,000, idadi ambayo haijawahi

kufikiwa na Shirika tangu kuundwa

kwake Agosti 1, 1962.

WASTAAFU

WASTAAFU UTUMISHI NHC•Niwakadambalimbalizautumishi

•WalilitumikiaShirikakwamafanikiomakubwa

uweze kuwa na matokeo chanya na maslahi

mapana kwa jamii.

Naye, Mkurugenzi Mkuu wa NHC, Bw.

Nehemia Kyando Mchechu alisema kuwa

chini ya sera ya NHC ya kusaidia miradi

ya maendeleo inayofanywa na jamii (CSR),

Shirika limekuwa linachangia pia sekta

za afya na elimu na hivi sasa limelenga

vijana hasa ili kutoa ajira katika sekta ya

ujenzi. Aliwasihi Wakuu wa Wilaya na

Wakurugenzi wa Halmashauri watoe

ushirikiano kwa Shirika ili mpango huo wa

kutoa ajira kwa vijana uweze kufanikiwa.

Aidha, alivitaka vikundi vya vijana vilivyoko

katika Halmashauri hizo kuunda SACCOS

zao ili kupanua shughuli zao za kiuchumi.

Katika mpango huo, kila Halmashauri

imepewa mashine nne, na kila mashine

inahudumiwa na vijana 10 kwa hiyo

itachangia ajira ya moja kwa moja kwa

vijana zaidi ya 7000. Pamoja na msaada

wa mashine, Shirika limetoa Shilingi laki

tano (500,000/=) kwa kila Halmashauri

kama kianzio cha vijana hao kununua

vifaa muhimu vya kuwezesha kazi ya

kufyatua matofali kuanza. Aidha, Shirika

limegharamia utoaji wa mafunzo kwa

vijana katika kila Halmashauri. Mpango huo

umeligharimu Shirika zaidi ya shilingi milioni

700 hadi kukamilika.

Akizungumza katika Mkutano wa Maafisa

Vijana kutoka Mikoa yote ya Tanzania

uliofanyika mjini Tabora Oktoba 16 mwaka

huu, Mkuu wa Mawasiliano na Huduma kwa

Jamii, Bibi Susan Omari aliwaomba wasaidie

kufuatilia utekelezaji wa mpango huu.

Maafisa Vijana hao walilishukuru Shirika

kwa uamuzi huo wa kizalendo ambao

umesaidia sana kutoa ajira kwa vijana na

waliahidi kuunga mkono

Baadhi ya wahitimu wa mafunzo ya Ufundi wa utengenezaji Natofali kwakutumia teknolojia ya kisasa na kwa gharama nafuu wakimsikiliza Waziri Mkuu (hayupo pichana) wakati akiwahutubia kwenye hafla ya kufunga mafunzo yao na kuwakabidhi vyeti.

WAZIRI MKUU AUPONGEZA MPANGO WA NHC WA KUTOA AJIRA

<< Continued page 4

JULAI - DESEMBA 2014 /Nyumba Newsletterwww.nhctz.com11

Na Mwandishi Wetu,

Hatua iliyopigwa na Serikali ya Uturuki

katika kupanga upya na kuyaendeleza

makazi yaliyokuwa na msongamano

mkubwa wa watu, imeonekana kuwaduwaza

wabunge wa Tanzania waliokuwapo kwenye

ziara ya mafunzo katika miji ya Ankara na

Istanbul iliyodhaminiwa na NHC.

Katika ziara hiyo, Wabunge hao walielezwa

kuwa Uturuki kupitia Mamlaka yake ya

Usimamizi na Maendeleo ya Nyumba,

iliyopo chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu

(TOKI), iliwahamisha wakazi zaidi ya 6,500

waliokuwa wakiishi kwenye maeneo ya

ujenzi holela na sasa eneo hilo katika Mji wa

Ankara limepangwa na kuendelezwa upya

na baada ya kukamilika litakuwa na uwezo

wa kukaliwa na watu zaidi ya 18,000.

Ujumbe wa wabunge hao, wengi wakiwa

wajumbe wa Kamati ya Ardhi, Maliasili

na Mazingira ulioongozwa na Mbunge

wa Kuteuliwa, Zakia Meghji (CCM) (sasa

Mwenyekiti wa Bodi wa Shirika la Nyumba

la Taifa), huku kwa upande wa Serikali

ukiongozwa na aliyekuwa Naibu Waziri wa

Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi,

Goodlucky Ole Medeye.

Aliyekuwa Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Goodlucky Ole Medeye (katikati), akiwa na wabunge wa Tanzania wakitembelea nyumba zilizojengwa na Serikali nchini Singapore na kuuzwa wananchi

ZIARA UTURUKI

Wengine katika ziara hiyo iliyoandaliwa

na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) ni

wawakilishi kutoka Kamati za Bunge za

Bajeti na ile ya Tawala za Mikoa na Serikali

za Mitaa, pamoja na viongozi wakuu kutoka

Halmashauri ya Wilaya za Arusha na

Arumeru pamoja na Jiji la Arusha.

Katika ziara hiyo ya siku sita, ilibainika

kuwa tatizo linalokwaza uendelezaji wa

makazi Tanzania ni gharama kubwa za

ujenzi ambazo zinachangiwa na bei kubwa

ya ardhi, riba ya mikopo ya benki na kodi

ya ongezeko la thamani (VAT) baada ya

nyumba kujengwa.

Nchini Uturuki, TOKI hupewa ardhi na

Serikali kwa gharama ndogo na nyumba

zinazojengwa huuzwa pasipo kuongeza

faida wala kutozwa kodi kutokana na

Serikali kuwekeza fedha nyingi katika sekta

hiyo, huku wale wanaouziwa wakilipa fedha

hizo kwa miaka 20 bila kutozwa riba.

Meneja wa Tawi la Uhusiano wa Kimataifa

katika Idara ya Mipango miji ya TOKI, Sule

Karabey alisema gharama za nyumba kwa

ajili ya makazi yanayojengwa kwa ajili ya

watu wenye kipato cha kati na cha chini,

huuzwa kwa fedha ambazo ni sawa na

Shilingi 19.2 milioni za Tanzania.

Kiasi hicho ni zaidi ya mara mbili ya gharama

za nyumba za bei nafuu zinazojengwa na

NHC na kuuzwa kwa wananchi.

Mkurugenzi Mkuu wa NHC, Bw. Nehemia

Mchechu mara kadhaa amekuwa akieleza

kuwa gharama kubwa ya ardhi, kodi kwenye

vifaa vya ujenzi na kwenye mauzo ya

nyumba kuwa ni kikwazo kwa shirika hilo

kujenga nyumba za gharama nafuu.

Mchechu aliwaambia wabunge hao kuwa,

kikwazo kingine ni kutokuwapo kwa

huduma za jamii kama maji, umeme na

barabara katika maeneo ambayo shirika

lake linayaendeleza na kwamba wakati

mwingine NHC hugharamia huduma hizo

hivyo kusababisha gharama za nyumba

kuongezeka.

Mbunge wa Ubungo, John Mnyika

(Chadema), alisema tatizo lililopo ni

kukosekana kwa mawasiliano na uratibu

miongoni mwa taasisi za Serikali na kwamba

kama yangekuwapo hilo lisingekuwa tatizo.

WABUNGE WATEMBELEA UTURUKI

Nyumba Newsletter/JULAI - DESEMBA 2014 www.nhctz.com12

ZIARA SINGAPORE

• Watanzaniawatakiwakufuata

sheriazamipangomiji

• BodiyaNHCyatakiwakuitisha

mkutanowawadauwamipangomiji

• MipangomijiSingapore

imefanikiwakutokananaraiawake

namamlakazotekuzingatiasheria

zamipangomiji.

Na Mwandishi Wetu,

NAIBU Waziri wa Ardhi, Nyumba na

Maendeleo ya Makazi, Mh. George

Simbachawene, amezitaka mamlaka

zinazosimamia mipango miji nchini

kuhakikisha kuwa sheria na taratibu zote za

mipango miji zinafuatwa na kusimamiwa.

Simbachawene alitoa kauli hiyo Jijini

Singapore alipokuwa akifanya majumuisho

ya ziara ya siku nne nchini humo mwezi

Julai,2014.

Akiwa ameandamana na watendaji wa NHC

na wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya

Shirika, Naibu Waziri huyo alisema kuwa

Tanzania ina sheria na taratibu zinazoongoza

mipango miji kama ilivyo kwa Singapore,

lakini kinachokosekana nchini mwetu ni

usimamizi wa sheria na taratibu hizo.

Akasema kuwa ili kuleta mwafaka katika

usimamizi wa mipango miji nchini Tanzania,

ni vema Bodi ya NHC na Menejimenti ya

Shirika wakaangalia namna wanavyoweza

kuwakutanisha wadau wa mipango miji ili

kuona namna watakavyoweza kuibadili

VIONGOZI WA SHIRIKA NA WIZARA

WAZURU SINGAPORE

miji ya Tanzania kwa kuwa na mpango

kabambe wa kupanga miji hiyo. Mkutano

huo wa wadau utaweza kujadili changamoto

zilizopo katika usimamizi wa mipango

miji ya Tanzania na kupata ufumbuzi wa

changamoto hizo.

Kwa mujibu wa Naibu Waziri huyo, katika

nchi ya Singapore miji ikishapangwa

kulingana na matumizi husika hakuna mtu

au taasisi yoyote inayoweza kubadilisha

kiholela mpango uliopitishwa tofauti na

ilivyo kwa Tanzania.

Hata hivyo, alisema changamoto kubwa

iliyopo nchini ili kuyafikia hayo ni kutokana

na kukosekana kwa uadilifu, nidhamu na utii

wa sheria zinazoongoza mipango miji.

Ujumbe wa NHC ukiangalia ramani ya Singapore inayoonyesha ujenzi wa miundombinu na makazi mbalimbali ya watu.

JULAI - DESEMBA 2014 /Nyumba Newsletterwww.nhctz.com13

Ujumbe wa NHC ukisikiliza maelezo kutoka kwa watendaji wakuu wa Halmashauri ya jiji la Holland Bukit Panjang Singapore wanaotumia mfumo wa Kampuni Surbana katika kufanikisha na kudhibiti matengenezo ya nyumba.

Ujumbe wa NHC ukiwa katika picha ya pamoja (kutoka kushoto) ni Meneja Uendelezaji Biashara Willliam Genya, Meneja Biashara, Richard Ndeona, Meneja Huduma Miliki za Nyumba Grayson Godfrey, Meneja Fedha, Adolf Kasegenya, Mkurugenzi wa Uendelezaji Miliki, Hamad Abdallah, Jaffar Chege Wambura Ofisa Miliki Arusha, Meneja Mifumo ya Taarifa Suzanne Kyaruzi, Meneja Ofisi ya Mkurugenzi Mkuu Bulla Boma na Emson Kabwogi Afisa wa Ukaguzi wa Ndani NHC. Walikuwa katika ofisi za Mamlaka ya Uendelezaji Miji nchini Singapore.

Ujumbe wa NHC ukisikiliza maelezo kutoka kwa watendaji wakuu wa Surbana ya Singapore.

Naye, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni

inayosimamia upangaji wa mji wa Singapore

ya Surbana, Tay Hang Hock Luois, alitaja

mambo mbalimbali yaliyosaidia upangaji wa

mji huo kuanzia ilipopata uhuru wake mwaka

1963, kuwa ni utii wa sheria za mipango miji,

usimamizi madhubuti wa serikali wa sheria

na taratibu za mipango miji.

Ziara hiyo ya mafunzo iliuwezesha ujumbe

huo wa Tanzania kutembelea Mamlaka ya

Mipango Miji ya Singapore na kampuni

inayosambaza majisafi na salama katika

mji wa Singapore ya Hyflux ambayo

imeonyesha nia ya kupunguza tatizo la maji

nchini Tanzania hasa maeneo zinakojengwa

nyumba mpya na NHC.

Ujumbe huo wa Tanzania ulipata pia fursa

ya kutembelea Makao Makuu ya Shirika

linalohusika na upangaji na uendelezaji miji

(Surbana); Mamlaka ya Uendelezaji upya

miji - Urban Redevelopment Authority

(URA); Housing & Development Board

(HDB na Mji mpya wa makazi eneo la

Punggol.

Shirika la Nyumba liliandaa ziara hiyo ya

mafunzo ili kuweza kuwapatia watendaji hao

uzoefu na kujifunza toka nchi zilizofanya

vizuri duniani katika masuala ya Upangaji

wa Miji, Viwango vya Majengo na Mikakati

ya Uendelezaji wa Miji Mipya (Satellite

Cities) kwa kushirikiana na Sekta binafsi.

Nyumba Newsletter/JULAI - DESEMBA 2014 www.nhctz.com14

• Niwasektayanyumba

• Wawekezajiwengiwaonyeshania

yakuwekezaTanzania

Na Mwandishi Wetu,

Katika jitihada kubwa zinazofanywa

na NHC katika kutengeneza fursa

nyingi kwenye sekta ya uendelezaji wa

makazi, Shirika limeweka historia kwenye

medani ya kimataifa kwa kufanikiwa kwa

mara ya kwanza kufanya kongamano la

uwekezaji nchini Dubai. Katika kongamano

hilo, Shirika lilifanikiwa kuonyesha fursa

zilizopo kwenye sekta ya ujenzi wa nyumba

nchini Tanzania, kwa makampuni makubwa

ya ujenzi yaliyopo Mashariki ya Kati na

kwingineko duniani ambayo yalihudhuria

katika kongamano hilo.

Tukio hili la kipekee na la kihistoria kwa

Tanzania lilizinduliwa na Makamu wa Rais

wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,

Mheshimiwa Dk. Mohamed Gharib Bilal

na lilihudhuriwa na makampuni makubwa

ya ujenzi Dubai kama Damac, Nahkeel,

Jumeirah na Emaar, ambayo yamehusika

na ujenzi wa majengo makubwa na maarufu

Dubai kama Burj Khalifa, Hoteli za Jumeira

na Dubai Mall.

Makampuni mengine yaliyohudhuria

yalitoka ukanda wa Guba kama Qatar na

Bahrain pamoja na nchi nyingine za Korea,

Sweden na Romania na yameonyesha

nia ya makampuni makubwa ya nchi hizo

kuwekeza kwenye sekta ya makazi Tanzania.

Akizungumzia kongamano hilo, Mkurugenzi

Mkuu wa NHC, Bw. Nehemia Kyando

Mchechu, alisema kuwa kongamano la

Wawekezaji Wa Sekta ya Makazi Tanzania ni

sehemu ya lengo kuu la NHC lenye dhamira

ya kupanua ukuaji wa sekta ya nyumba

nchini. Mchechu alisema kuwa kongamano

hilo lilikuwa ni mkakati wa kuionyesha

dunia kuwa Tanzania ni sehemu pekee yenye

mazingira mazuri ya uwekezaji na urudishaji

wa faida kwenye sekta ya makazi.

‘Tanzania inatoa fursa ya pekee linapokuja

suala la uwekezaji kwenye sekta ya makazi

barani Afrika na hii ni kutokana na uwazi

pamoja na utulivu wa kisiasa na amani

inayopatikana nchini, uchumi unaokua

pamoja na ushirikiano mkubwa unaotolewa

na serikali” ‘Tukio hili la kihistoria ni sehemu

tu ya mpango kamili wa kuifahamisha dunia

kuhusu fursa za uwekezaji kwenye sekta

ya makazi zinazopatikana nchini” alisema

Mchechu.

Mchechu anaamini kuwa huu ni muda

mwafaka kwa wawekezaji kuitazama

Tanzania na Afrika kwa ujumla. Alibainisha

kuwa hapo zamani ilikuwa ni vigumu kwa

wawekezaji kuwekeza Afrika na Tanzania,

lakini akasema kuwa kwa uchumi wa leo ni

hatari nchi kuwazia kutowekeza Tanzania.

Mchechu anasema kongamano hili

linalenga kupata wawekezaji wenye uwezo

wa kuanzia dola milioni 20 hadi dola nusu

bilioni. ‘Tunajua uwezo wa uwekezaji

unaotakiwa hauwezi kufikiwa kwa usiku

mmoja na ndio maana miradi yetu mingi ni

zaidi ya miaka 5 hadi 7, lakini tuna miradi

ambayo inaanzia dola milioni kumi hadi

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal (wa nne kutoka kulia) akijumuika na baadhi ya viongozi wakati alipohudhuria Mkutano wa GBF, uliofanyika kwenye Hoteli ya Atlantis jijini Dubai.

NHC YAVUTIA WAWEKEZAJI NCHINI DUBAI

“Hatujawasahau dada na kaka zetu nyumbani Tanzania, wengi wao wana nafasi kubwa ya kuwekeza katika miradi ya uendelezaji wa sekta ya makazi nchini na tunataka kuhakikisha wanapata fursa hiyo pia”.

WAWEKEZAJI

JULAI - DESEMBA 2014 /Nyumba Newsletterwww.nhctz.com15

Baadhi ya wajumbe waliofika kwenye kongamano la uwekezaji Dubai ambalo lilihudhuriwa na kampuni kubwa za ujenzi Dubai kama Damac, Nahkeel, Jumeirah na Emaar, ambazo zimehusika na ujenzi wa majengo makubwa na maarufu Dubai kama Burj Khalifa, Hoteli za Jumeira na Dubai Mall. Tukio hili la kipekee na kihistoria kwa Tanzania lilizinduliwa na Makamu wa Rais, Dk. MohammedGharib Bilal .

dola milioni mia, kwahiyo kiasi chochote

ambacho mwekezaji atakuwa nacho kati ya

kiwango hicho tuna fursa za kuwekeza naye’

anasema Mchechu.

Kati ya miradi ya NHC iliyoonyeshwa kwa

wawekezaji ni pamoja na miradi mitatu

ambayo itaendelezwa kwa kipindi cha miaka

5 hadi 10. Hii inajumuisha miradi miwili

ya kuendeleza Arusha inayoitwa Safari

City na USA River ambayo kwa pamoja

itakuwa na jumla ya nyumba 8000, pamoja

na mradi wa kuendeleza makazi Dar es

Salaam utakaofahamika kama Salama Creek

Satellite City ambao utakuwa na jumla ya

nyumba 9,500.

Miradi hii yote iko tayari kwa maana ya

ya kupata uwekezaji unaotakiwa.

Akizungumza katika kongamano hilo,

Makamu wa Rais, Mheshimiwa Dk

Mohamed Gharib Bilal alielezea kuwa

serikali ya Tanzania imefanya kazi kubwa ya

kutengeneza fursa katika sekta ya makazi

ikiwemo kuzifanyia mabadiliko sheria

mbalimbali zinazohusu sekta hiyo. Sheria

hizo ni pamoja na sheria ya hati pacha, sheria

ya mikopo ya nyumba na uanzishwaji wa

kampuni ya kuwezesha mikopo ya nyumba

(TMRC) ambazo kwa hakika zimechangia

mabadiliko makubwa kwenye sekta ya

makazi.

‘Tanzania kwa sasa inashuhudia mafanikio

makubwa kwenye sekta ya makazi, huku

kukiwa kuna upungufu wa jumla ya nyumba

milioni 3.8 na upungufu huo unakua kwa

kiasi cha makazi 200,000 kwa mwaka,

ambayo kwa hakika inatoa changamoto

kubwa kwa Tanzania lakini ni fursa kubwa

kwa wawekezaji’ alisema Makamu wa Rais.

Naye, Balozi wa Tanzania kwenye nchi

za Falme za Kiarabu, Mheshimiwa Balozi

Mbarouk Nassor Mbarouk akizungumza

na wageni waalikwa alisisitiza namna sekta

ya makazi ilivyoimarika nchini Tanzania.

“Sekta ya makazi ndio sekta inayokua kwa

kasi zaidi nchini Tanzania na tunakaribisha

wawekezaji kutoka nchi za falme za Kiarabu”

alisema Mbarouk.

Kadhalika, Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba

na Maendeleo ya Makazi, Mheshimiwa

George B. Simbachawene, alisema kuwa

msingi mkuu wa kukua kwa sekta ya makazi

Tanzania umetokana na ushirikiano uliopo

baina ya serikali na sekta binafsi ambao

unaruhusu uwekezaji na ukuaji mzima wa

sekta.

Bw. Mchechu alisema kuwa wawekezaji

wa ndani ya Tanzania hawataachwa nyuma

na akabainisha kuwa nao watashirikishwa

katika kuekeza katika miradi ya ujenzi.

“Hatujawasahau dada na kaka zetu

nyumbani Tanzania, wengi wao wana

nafasi kubwa ya kuwekeza katika miradi ya

uendelezaji wa sekta ya makazi nchini na

tunataka kuhakikisha wanapata fursa hiyo

pia”.

Kongamano hili lilifanyika kwa ushirikiano

kati ya Balozi Mdogo wa Tanzania Dubai,

Mheshimiwa Omary Mjenga pamoja na

Balozi Maalumu wa Mambo ya Kiuchumi,

Bwana Cleophas Ruhumbika, ambao

walishughulikia taratibu za kongamano

pamoja na kualika makampuni ya uwekezaji

ya Dubai.

“Tuna furaha kubwa kufanya kazi bega kwa

bega na Shirika la Nyumba la Taifa kwenye

tukio hili la kihistoria’ anasema Mjenga. ‘

Sehemu kubwa ya kazi yetu hapa Dubai

ni kuwezesha fursa kwa Tanzania ambayo

inaendana na wajibu wetu hapa. Pia tuna

furaha kubwa kuwa tukio limekuwa la

mafanikio makubwa na nina hakika kuwa

fursa zaidi za wawekezaji kuja Tanzania

zitazidi kufunguka’ anamalizia Mjenga.

NHC YAVUTIA WAWEKEZAJI NCHINI DUBAIkuwa vibali vyote vya mradi vimepatikana

na kinachotakiwa ni kuwekeza tu na

kongamano hili lilikuwa muhimu kwa ajili

Nyumba Newsletter/JULAI - DESEMBA 2014 www.nhctz.com16

Baadhi ya maafisa wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) waliohudhuria mafunzo kazini kuhusiana na masuala ya kisheria ‘Dispute adjudication (Module 3)’ chini ya mkataba wa Shirikisho la Ushauri wa kitaalamu wa kihandisi (FIDIC). Mafunzo hayo yaliratibiwa na Chama cha Wahandisi Washauri Tanzania (ACET).

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Anna Kajumulo Tibaijuka katika picha ya pamoja na Wajumbe mpya ya Bodi ya NHC na wakurugenzi wa NHC

Mkurugenzi wa shirika la nyumba la taifa Nehemia Mchechu akiwa na mkuu wa wilaya ya Mbeya Norman Sigalla katika maandamano ya Jubilee ya miaka 50 ya shule ya sekondari Mbeya Day. Shirika la Nyumba la Taifa lilichangia kiasi cha shilingi milioni 20.

HABARI KATIKA PICHA

JULAI - DESEMBA 2014 /Nyumba Newsletterwww.nhctz.com17

Mkurugenzi wa Fedha wa NHC Felix Maagi akikabidhi hati ya umiliki wa nyumba za makazi za Medeli, Dodoma kwa Mkurugenzi wa Utawala na Raslimali watu wa BOT Bw Leonard Kisarika. BOT imenunua nyumba katika mradi huo kwa ajili ya wafanyakazi wake.

Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Bi.Zakhia Meghji akizungumzakwa ufupi mbele ya wageni waalikwa mbalimbali wakiwemo baadhi ya Wakuu wa Mikoa na Wadau mbalimbali kwenye jukwaa la Uwekezaji wa sekta ya nyumba.

HABARI KATIKA PICHA

Wabunge na watendaji wa Shirika la Nyumba la Taifa wakiwasili katika eneo la Kunduchi Range (Tanganyika Packers) kilichokabidhiwa kwa Shirika la Nyumba na Jeshi la Wananchi wa Tanzania JWTZ) na baadaye kuelekea mradi wa Kawe City

www.nhctz.com18

SAFARI CITY - ARUSHA

Nyumba Newsletter/JULAI - DESEMBA 2014

www.nhctz.com19

UPTOWN - KAWE

JULAI - DESEMBA 2014 /Nyumba Newsletter

Nyumba Newsletter/JULAI - DESEMBA 2014 www.nhctz.com20

Mwandishi Wetu,

Moja ya vigezo muhimu kwa taasisi yoyote

yenye nia ya kusonga mbele kwa kasi ya

kuridhisha ni kuwa na utawala bora kwa

maana ya utendaji, uendeshaji na uthibiti

wa rasilimali zake unaozingatia viwango

vya ubora wa hali ya juu katika kutekeleza

majukumu yake ya siku hadi siku.

Si ajabu ndio maana hata Shirika la ubora wa

viwango la kimataifa au the International

Standards Organisation (ISO) limeingiza

viwango vya utendaji kazi au utoaji huduma

kwa taasisi zisizo na majukumu ya moja kwa

moja ya uzalishaji kama ilivyo kwa NHC au

taasisi kama Shirika la Posta, Kampuni za

uchukuzi nk.

Ni kwa msingi huo Shirika la Nyumba la

Taifa limeweza kuanzisha utaratibu wa

kudhibiti matumizi ili yasizidi makadirio

ya bajeti. Mambo kadhaa yaliyoainishwa

katika mpango mkakati wa miaka mitano

yamepata mafanikio kadhaa na sasa Shirika

la Nyumba linaaminika sana katika utoaji wa

huduma zake.

Kadhalika, Shirika lilikuwa miongoni mwa

mashirika ya umma yaliyofuata taratibu

za manunuzi kwa kupata alama asilimia 86

kwa mwaka 2012/2013 zikilinganishwa na

asilimia 37 za mwaka 2009/2010. Vilevile,

Shirika limeanzisha mifumo ya mawasiliano

ya teknolojia ambayo imeongeza ufanisi

katika uendeshaji wa shughuli zake. Mifumo

hii ni pamoja na Mansoft, Document

Management System, Asset Management

System, Geographical Information System

na Fleet Management System.

Serazatayarishwakuongezaufanisi

Shirika limeanzisha sera mbalimbali ambazo

zinaliongoza katika utendaji wa shughuli

zake na zinalenga kuongeza ufanisi katika

utekelezaji wa majukumu yake. Baadhi ya

sera zilizoanzishwa ni pamoja na Sera ya

Mafunzo, Sera ya Fedha, Sera ya Uwekezaji,

Sera ya Ukaguzi, Sera ya Mawasiliano

ya Teknolojia, Sera ya Manunuzi, Sera ya

Usimamizi wa Nyumba, Sera ya Huduma

kwa Jamii, Sera ya Mawasiliano na vyombo

vya habari na Sera ya Afya.

Mfumowaudhibitinatahadhariyamajanganamatukiohasiwaanzishwa

Shirika liliweza kuanzisha mfumo wa

kutambua mapema tahadhari ya majanga

na matukio hasi na hivyo kuepukana na

gharama kubwa zinazotokana na majanga

hayo.

Lafanikiwakatikakutumiarasilimaliwatukikamilifu

Kuongeza ufanisi katika kutumia rasilimali

watu ni moja ya mikakati mipya ya NHC

katika kuhakikisha linatimiza majukumu

yake kwa ufanisi mkubwa na hivyo kukidhi

mahitaji ya wateja na matarajio ya serikali

juu ya huduma bora katika sekta ya nyumba

hapa nchini.

Ili kuweza kutumia vema rasilimali watu

iliyo nayo, Shirika liliboresha muundo wake

ili uendane na mpango mkakati pamoja na

majukumu yake yanayoendelea kupanuka.

Vilevile, Shirika linawapatia wafanyakazi

wa ngazi za chini mafunzo ya kuwaongezea

ujuzi na kuwapangia majukumu mengine

yenye tija kwa Shirika.

Pamoja na mafanikio haya, Shirika limeweza

kuajiri wataalamu wa fani mbalimbali kwa

ajili ya kuongeza tija katika utendaji. Ajira

hizi mpya, zimeweza kupandisha uwiano

kati ya wafanyakazi wenye taaluma na

wasiokuwa na taaluma kutoka asilimia 22

kwa 78 mnamo mwaka 2010 na kufikia

asilimia 51 kwa 49 hivi sasa. Lengo ni kuwa

na uwiano wa wafanyakazi wenye taaluma

asilimia 70 dhidi ya wale wasiokuwa na

taaluma asilimia 30 ifikapo Juni, 2015.

Mfumowaupimajiutendajikaziwaanzishwailikuongezaufanisi

Ili kuboresha utendaji wa kazi, Shirika

limeanzisha mfumo wa kupima utendaji wa

wafanyakazi wake (balance score card) na

kuwatambua wafanyakazi bora kila mwaka

kwa ajili ya kuwabakiza (retention) na

kuwandaa kuchukua nafasi za walio juu yao

(succession plan).

Mikatabambalimbaliyaboreshwakuletatija

Kuanzia mwaka 2010 Shirika liliweza

kupitia mikataba kati yake na wadau. Kati ya

mikataba 186 ya ubia iliyokuwepo, Shirika

lilifuta mikataba 59 ambayo haikuwa na

tija kwa NHC na Taifa. Vilevile, Shirika

lilirekebisha mikataba mingine 311. Shirika

linaendelea na marekebisho ya mikataba ya

upangaji kwa ajili ya kuiboresha ili ilete tija

kwa Shirika na wapangaji.

Marekebishoyasherianamba2yamwaka1990

Shirika kwa kushirikiana na Wizara ya

Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi,

linaendelea na mchakato wa kurekebisha

Sheria Na. 2 ya mwaka 1990 iliyoliunda

upya.

Lengo la marekebisho haya ni kuliwezesha

kupanua wigo wa shughuli zake za

kuwa mwendelezaji mkuu; kuliwezesha

kuendesha shughuli zake katika mazingira

shindani; kuoanisha sheria ya Shirika na

sheria zingine na kuliwezesha kujitafutia

mitaji kwenye soko la fedha.

Lafanikiwakupunguzamashaurimahakamani

Tangu mwaka 2010 Shirika limeweza

kupunguza kesi zilizokuwa mahakamani kwa

zaidi ya asilimia 50. Aidha, Shirika lilishinda

kesi 185 kati ya kesi 190 ambazo ni sawa

na asilimia 97. Vilevile, Shirika limeweza

kubuni mikakati ya kuzuia kuibuka kwa kesi

mpya. Kwa sasa Shirika lina kesi 121 zilizopo

mahakamani katika masuala mbalimbali

na nyingi zina muelekeo wa kumalizika hivi

karibuni.

YAIMARISHA UTENDAJI

NHCYAFANIKIWAKATIKAUTEKELEZAJI MPANGO MKAKATI

• Yaimarishaudhibitiwarasilimalizake

• Serazakuongezaufanisizaanzishwa

• TaswirayaShirikayaboreshwakwakuwajaliwateja

JULAI - DESEMBA 2014 /Nyumba Newsletterwww.nhctz.com21

KuboreshaTaswirayaShirika

Shirika limekuwa likitekeleza mkakati wa

kubadili mtazamo hasi juu ya shirika kwa

kuanzisha utaratibu wa kuuelimisha umma

kuhusu shughuli zake kupitia vipindi vya

televisini na redio vya Maisha ni Nyumba.

Pamoja na juhudi nyingine za kuboresha

utendaji wa Shirika, vipindi hivi vimesaidia

kuondoa mtazamo hasi wa jamii na wadau

wake na hivyo kupunguza malalamiko

dhidi ya Shirika. Mtazamo chanya wa

Shirika umeongezeka kutoka asilimia 40

mwaka 2010 na kufikia asilimia 76 mnamo

Desemba, 2013.

KuboreshamwonekanowaShirika(rebranding)

Shirika limekamilisha mchakato wa

kubadilisha mwonekano wake ili kupanua

fursa za biashara, kuondoa mtazamo hasi

wa wateja wake na kukuza soka la nyumba

za Shirika, ili kwenda sambamba na malengo

yake ya sasa.

Kuboreshaserayauwajibikajikwajamii

Kupitia sera yake ya huduma kwa jamii,

Shirika limedhamiria kuchangia katika

kupunguza tatizo la ajira kwa vijana. Kwa

kushirikiana na Chuo Cha Mafunzo ya

Ufundi (VETA) cha Dar es Salaam; Wakala

wa Utafiti wa Vifaa bora vya Ujenzi na

Majengo (NHBRA); na Halmashauri za

Wilaya, Shirika linaendelea na mpango wa

mafunzo kwa vijana yanayoambatana na

kuwapatia vijana mashine za kutengeneza

matofali yanayofungamana (soil-cement

stabilized interlocking bricks) na mtaji.

Chini ya mpango huu, Shirika limetoa

mashine nne kwa kila Halmashauri nchini

kwa ajili ya kuwajengea vijana uwezo

wa kujiajiri wenyewe kupitia miradi ya

kutengeneza matofali. Katika utaratibu huu

zaidi ya mashine 700 zimetolewa katika

Halmashauri mbalimbali nchini na gharama

ya mradi huu inakadiriwa kufikia zaidi ya

shilingi milioni 700.

Mpango huu utakapokamilika utaweza

kuwapatia ajira ya moja kwa moja vijana

7000 kwa awamu ya kwanza. Lengo ni

kuendelea na mpango huu mpaka uweze

kufikisha ajira za vijana 200,000 kwa nchi

nzima.

TANZIA

Na Mwandishi Wetu,

MKURUGENZIMkuuwaShirikalaNyumbalaTaifa(NHC)anasikitikakutangaza

vifovyawafanyakaziwakewatano,vilivyotokeakwanyakatitofauti.

AkizungumziavifohivyoMkurugenziMkuu,Bw.NehemiahMchechualiwapapole

wafanyakazi wote kwa kuondokewa na wafanyakazi Fatuma Kibiki aliyefariki

mwishonimwamwaka jananaRashidJakulagizaaliyefariki usikuwakuamkia

AlhamisiyaJanuari10mwakahuu,nyumbanikwakeGongolamboto.

KifokinginenichamfanyakaziOmariIssaMalibichealiyekuwaderevaaliyefariki

dunia nyumbani kwake usiku wa kuamkia Februari 14, mwaka jana. Alizikwa

kwaoLindi.

MfanyakazimwinginewaNHCaliyeiagaDunianiAdamMwinyekulealiyekuwa

akifanyia kazi bohari yaMkoawaUpanga aliyefarikiMachi 17mwaka janana

kuzikwakwaoMbeya.

Mwaka huu Machi 25, Jeremiah Mchome aliyekuwa Mhasibu Idara ya Fedha

KinondonialifarikidunianamazishiyakeyakafanyikahukoSame,Kilimanjaro.

Mfanyakazimwingine LuanganoKikoti alifariki dunia asubuhi ya Jumamosi ya

Aprili5mwakahuukatikahospitaliyaTumaini,DaresSalaam.

Shirika pia lilimpoteza Batholomeo Brashi aliyekuwa AfisaNyumba Msaidizi

Mkoa wa Iringa aliyefariki mchana wa Oktoba 9 katika Hospitali ya Taifa

Muhimbili na ambaye alizikwa kwaoMpanda. Mwingine ni Melesiana Casturi

aliyekuwamhudumuwaofisiBukoba aliyefariki tarehe21 Septemba, 2014na

Joseph Lyapula aliyekuwa Boharia Mkoani Mwanza ambaye alifariki tarehe 1

Novemba,2014katikaHospitaliyaMwananchiJijiniMwanza.Alizikwanyumbani

kwaoHekaManyoniSingidaNovemba4mwakahuu.

“Mungu amewapenda zaidi na imempendeza yeye kuwachukua wenzetu

kutanguliakatikasafariambayosotetutapitanakilamtukwawakatiwakeaujuao

MolaMaulana,”alisemaMchechu.

Amewashukuru wale wote ambao waliweza kwenda kutoa pole na kuwaona

ndugu na familia ya Marehemu katika kipindi kigumu cha maombolezo na

kwambauwepowaoulikuwaniuwakilishiwaShirikanaWafanyakaziwote.

Amewapapolewafanyakaziwote,marafikiwakaribuwaMarehemu,nduguna

jamaawote,MunguazilazerohozaMarehemumahalapemaPeponi.

AMINA!

Nyumba Newsletter/JULAI - DESEMBA 2014 www.nhctz.com22

Na Mwandishi Wetu,

Pato la ndani la Taifa lolote duniani

hutokana na mchango wa sekta

mbalimbali za uzalishaji na huduma. Katika

sekta hizi aghalabu sekta ya nyumba

imejitokeza kuwa na mchango mkubwa

katika kila nchi kutokana na ukweli kuwa

imejichukulia umuhimu wa pekee katika

maisha ya kila siku ya binadamu duniani

kote.

Ukweli huu upo dhahiri kwa kuwa huwezi

kukuta mji wowote mkubwa au mdogo

duniani kote usio na nyumba za makazi,

majengo ya biashara kama hoteli, kumbi za

mikutano, shule na vyuo. Majengo mengine

yanatumika kwa uzalishaji kama viwanda na

sehemu za kutolea huduma mbalimbali.

Ni ukweli usiopingika kuwa sekta ya

nyumba inayazunguka maisha ya kila siku ya

binadamu. Sekta hii kwa kiasi kikubwa ndio

inayomtambulisha binadamu na maendeleo

yake au ustaarabu wake kwani kama mji

au Jiji limepangwa vema na kujengeka

kikamilifu basi taswira inayojengwa kwa

watu wa Jiji lile na nchi lililopo huwa ni

chanya kwamba nchi hiyo imeendelea na

watu wake wana uchumi mzuri.

Hii ndio sababu iliyolifanya Shirika la

Nyumba la Taifa (NHC) kuandaa mpango

mkakati wa miaka mitano 2010/11-

2014/15 wa kuleta mapinduzi katika

sekta ya nyumba hapa nchini. Mkakati huo

umelenga kuhakikisha kuwa sekta hii inatoa

mchango mkubwa katika kukuza pato la

Taifa na uchumi wa nchi kwa ujumla.

Taarifa za kitaalamu juu ya mchango wa

sekta ya nyumba kwa pato na uchumi wa

Taifa hapa nchini zinaonyesha kuwa sekta

hiyo inatoa mchango wa asilimia 1.0 tu huku

sekta hiyo hiyo katika nchi zilizoendelea

huchangia kati ya asilimia 50 mpaka 70 ya

pato la Taifa kwa mwaka.

Katika kuhakikisha sekta ya nyumba

inachangia kwa kiasi kikubwa pato la

Taifa mpango mkakati wa NHC unalenga

kuhakikisha kuwa sekta hii inakuza pato na

uchumi wa Taifa hadi kufikia asilimia 11.

Kwa sasa Tanzania inakabiliwa na

changamoto ya uhaba mkubwa wa nyumba

bora ambao unakadiriwa kuwa zaidi ya

nyumba 3,000,000 huku pengo hilo likikua

kwa takriban nyumba 200,000 kwa mwaka.

Upungufu wa nyumba ni mkubwa zaidi

sehemu za mijini ambako asilimia 37.5 ya

Watanzania ndiko wanakoishi. Shirika la

Nyumba la Taifa likiwa chombo cha Serikali,

linatarajiwa kukabiliana na changomoto hii.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, kutokana na

kuongezeka kwa mahitaji ya nyumba nchini

na mchango wa nyumba katika kukuza

ustawi wa wananchi, Serikali ililiagiza

Shirika kujielekekeza zaidi kwenye ujenzi

wa nyumba badala ya usimamizi wa miliki

zake pekee. Kwa kupitia ujenzi wa nyumba

na hasa zile za gharama nafuu, Shirika

linatakiwa kuwawezesha wananchi kumiliki

nyumba kupitia fursa ya Sheria za Hati

Pacha na Mikopo ya Nyumba za mwaka

2008.

Ili kufanikiwa katika kukidhi matarajio

ya serikali kwa upande mmoja na yale

ya wananchi kwa upande wa pili, serikali

iliagiza NHC kutumia miliki zake kwa ajili

ya maendeleo na kuweza kujiendesha

kibiashara.

Shirika la Nyumba la Taifa limekuwa katika

safari ndefu ya kuleta mageuzi katika sekta

ya miliki nchini tangu Serikali ilipoamua

kufanya mageuzi katika utendaji kazi na

uendeshaji kazi wake. Katika safari hii,

Shirika limepewa jukumu la kutatua uhaba

wa nyumba pamoja na kukuza mchango wa

MCHANGO WA NYUMBA

NHC YADHAMIRIA KUONGEZA MCHANGO WA

NYUMBA KATIKA PATO LA TAIFA

Mchoro wa namna litakavyokuwa jengo la Eco Residence litakaloanza kujengwa katika kitalu namba 67 kwenye makutano ya mitaa ya Ngano na Wakulima, Dar es Salaam litakapokamilika litakuwa na ghorofa 16, sehemu za makazi 118 na kuwa makazi ya watu zaidi ya 840 wakati kabla lilikuwa makazi ya familia moja

JULAI - DESEMBA 2014 /Nyumba Newsletterwww.nhctz.com23

1. Naanzakuwasalimu,wafanyakaziwanyumba

Nyoteninawaheshimu,awaongozemuumba,

Tuyashikeyamuhimu,ilitusijekuyumba

Shirikasasalapaahebutufungemikanda

2. Leonasemaukweli,siyokamanajigamba

Mamboyameshamiri,uwanjanitunatamba

Tuwesotestamili,mafanikiokuchimba

Shirikasasalapaa,hebutufungemikanda

3. Mikakatitulopanga,neemayajitokeza

Hakunawakutupinga,kwapamojatumeweza

Tumetengezamizinga,tuachanenakucheza

Shirikasasalapaa,hebutufungemikanda

4. TulipokuwaSingida,malengotumeyaweka

Tukamilishekwamuda,tusijetukabweteka

Kilamjumbeshuhuda,malengokukamilika

Shirikasasalapaa,hebutufungemikanda

5. Kwapamojatunaweza,kujenganyumbakwa

wingi

Tuwezekutekeleza,hiyoserayamsingi

Butitumeshalikaza,kujenganyumbakwawingi

Shirikasasalapaahebutufungemikanda

6. KwaspiditumeanzaMindu,UbungoKibada

KatavinakuleMwanza,MchikichiniSingida

Zakuuzanakutunza,hiyondiyoyetumada

Shirikasasalapaa,hebutufungemikanda

7. Natoamsisitizo,bidiiiwekazini

Iliujepatatuzo,kaskedikusaini

Ukiletamatatizoutajatozwafaini

Shirikasasalapaa,hebutufungemikanda

MALENGA WETU

8. Tulikotokazamanitulikuwanaaibu

Viongozinajiranihatawalemaswaibu

Tulisemahadharani,rushwaimetuaribu

Shirikasasalapaahebutufunge

mikanda

9. TumshukuruRabuki,Mchechu

katuletea

KajanusuruShirika,leotunaendelea

Rushwahaitasikika,mabaya

kutokomea

Shirikasasalapaahebutukazemikanda

10. Ewekipenzichawatu,juhudizo

endeleza

Angaliakilamtu,kipatochekuongezeka

Tupamojakilakitu,Jahazikuliongoza

Shirikasasalapaa,hebutufunge

mikanda

11. Viongoziwaridhika,ubingwa

tumeshapewa

Tusijetukapotoka,kwasifa

tunazopewa

Jahazilikitobokatutakujalaumiwa

Shirikasasalapaa,hebufungeni

mikanda

12. Tamatinimeshafika,kalamunaweka

chini

Niwaachewahusika,waingia

mitamboni

Manenohayakushikatukiwepovituoni

Shirikasasalapaa,hebutufungeni

mikanda

sekta hii ambayo mchango wake kwenye

pato la Taifa bado upo chini, ukilinganisha

na uwezo wa sekta nzima ya ujenzi wa

nyumba nchini.

Kutokana na umuhimu wa sekta ya

nyumba katika kuchangia maendeleo

ya jamii na ukuaji wa uchumi, Shirika

lilitayarisha mpango mkakati wa miaka

mitano ambao umekuwa dira ya kuleta

msukumo mpya wa sekta ya nyumba

nchini.

Kutokana na kufanikiwa kwa kiasi

kikubwa kutekelezwa kwa mpango

mkakati wa 2010/11-2014/15 thamani

ya mali za shirika ambazo kwa asilimia

kubwa ni nyumba na majengo mbalimbali

inaonyesha kukua hadi kumiliki majengo

2,389 yenye sehemu ya nyumba 17,111

yenye thamani ya shilingi trilioni 2.911

Juhudi zilizofanywa za mabadiliko

ya sekta ya nyumba zilianza Machi

2010, ambapo Serikali iliteua uongozi

mpya wa Shirika kwa maana ya Bodi

ya Wakurugenzi na Menejimenti kwa

nia ya kuimarisha utendaji na ufanisi

wa Shirika ili liweze kuwa na mchango

mkubwa katika kutatua tatizo la uhaba

wa nyumba nchini.

Jukumu la kwanza la uongozi huu,

lilikuwa ni kutayarisha mpango mkakati

wa ambao umeainisha mwelekeo mpya

na malengo mapya ya Shirika.

Kwa kiasi kikubwa uongozi wa NHC

ulioteuliwa mwaka 2010 unahusika

na kuongezeka kwa kasi ya ujenzi wa

nyumba za Shirika ambazo ama zinauzwa

au kupangishwa. Ni uongozi huu ambao

umeleta chachu ya kuona kuwa sekta

ya nyumba kupitia NHC inachangia

kwa kiwango cha juu zaidi katika ukuaji

wa pato la ndani kwa kujiwekea lengo

la kuchangia asilimia 11 ya pato la Taifa

kwa kushirikisha wadau wa sekta hii

zikiwemo benki. Hivi sasa nyumba za

gharama nafuu zimejengwa katika mikoa

takriban 19 huku nyumba za vitega

uchumi na za makazi kwa ajili ya watu wa

kipato cha kati na juu zikiwa zimeshamiri

kujengwa na kuuzwa katika maeneo

mbalimbali nchini.

HEBU TUFUNGE MIKANDA

(Doctor)MOHAMMEDMNEKA

BOX2977,DARESSALAAM.

Nyumba Newsletter/JULAI - DESEMBA 2014 www.nhctz.com24

• Asisitizauadilifukatikautendaji

kaziilikuletatija

• Atakakasiyaujenziwanyumbaza

gharamanafuuiendelezwe

• Wafanyakaziwaazimiakuongeza

tijakatikautendaji

Na Mwandishi Wetu,

Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba

na Maendeleo ya Makazi, Alfayo Japan

Kidata amefungua kikao cha Baraza Kuu

la Wafanyakazi wa Shirika la Nyumba la

Taifa (NHC), akisisitiza uadilifu mkubwa

miongoni mwa wafanyakazi ili kuliwezesha

Shirika kutoa huduma za makazi zilizo bora

kwa wananchi.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa

kikao hicho kilichofanyika kwenye Hoteli

ya Tanga Beach Resort, jijini Tanga, Bw.

Kidata alisema kuwa uadilifu ndiyo

utakaowawezesha wafanyakazi wa Shirika

kutenda kazi zao kwa ufanisi mkubwa.

Alisema kuwa wafanyakazi hao wakitenda

kazi zao kwa juhudi na maarifa huku

wakitambua umuhimu mkubwa wa sekta

ya nyumba waliyopewa dhamana ya

kuisimamia, kutalifanya Shirika hilo kuweza

kutekeleza malengo yake ya kuwajengea

Watanzania nyumba bora.

Alisema utendaji kazi wenye uwazi,

uadilifu na weledi wa hali ya juu ndiyo

utakaowaongezea heshima kubwa

wafanyakazi hao na kujenga taswira nzuri

ya Shirika katika jamii ya watanzania.

Akizungumzia kasi ya ujenzi wa nyumba

za gharama nafuu katika miji mbalimbali

ya Halmashauri za Miji na Wilaya nchini,

Katibu Mkuu huyo alilipongeza Shirika

kwa kurejesha utaratibu huo wa kizalendo

aliouanzisha Baba wa Taifa.

“ Nafahamu kuwa hivi sasa mmeshaifikia

mikoa 19 na mnayo matumaini makubwa

ya kufikia mikoa yote kufikia Desemba

mwaka huu. Utaratibu huu unaolenga

kuwawezesha wananchi wa kipato cha kati

na chini kumiliki nyumba, umepongezwa

sana na Serikali Kuu na viongozi mbalimbali

wakiwemo Waheshimiwa Wabunge.

Hivyo, mnayo dhima na jukumu kubwa la

kuusimamia mpango huu ili ndoto hiyo ya

kuwawezesha watu wengi kumiliki nyumba

iweze kutimizwa,”alisema.

Alisema kwa kufanya hivyo Shirika litakuwa

limeweka msingi mkubwa wa kukumbukwa

katika Taifa letu na vizazi vijavyo kama

tunavyomkumbuka Baba wa Taifa wa

kueneza ujenzi wa nyumba za gharama

nafuu katika miji mingi baada ya Uhuru wa

Taifa letu.

“ Ili kuzifanya nyumba hizo zinazojengwa

kuwa nafuu, narudia kusisitiza agizo

alilolitoa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri

ya Muungano wa Tanzania Dk. Jakaya

Mrisho Kikwete kuwa Halmashauri za Miji

na Wilaya zilipatie Shirika la Nyumba na

waendelezaji wengine wa Miliki maeneo

ya kujenga nyumba hizo bila kuhitaji fidia

kubwa,” alisema.

Alisema pamoja na juhudi na ubunifu

mbalimbali uliofanywa na NHC uliosaidia

kuongeza kasi ya ujenzi wa nyumba za kada

zote, Serikali inaamini kuwa kasi ikiongezeka

zaidi katika ujenzi wa nyumba, licha ya

kuwa Shirika litakuwa limetekeleza ilani

ya uchaguzi ya chama tawala na litakuwa

limeisaidia pia Serikali katika juhudi zake za

kuondoa umaskini nchini.

Likiwasilisha maazimio ya Mkutano huo wa

Baraza Kuu, yaliyowasilishwa na Meneja

wa Mkoa wa Tabora Bw. Erasto Chilambo,

wajumbe wa Baraza hilo wamemshukuru

Katibu Mkuu kwa kuwa mstari wa

mbele katika kufanikisha uandaaji wa

Mpango Mkakati wa Shirika wa miaka

kumi unaoanzia 2015. Aidha, Baraza

linamshukuru kwa kufanikisha upatikanaji

wa hati miliki ya eneo la Kawe, Tanganyika

Packers.

Kadhalika, Baraza hilo limeazimia kila

mkoa uhakikishe unaongeza mapato yake

ili kupata uwezo wa kujiendesha kibiashara.

Ili kufanikisha hilo, jitihada zitafanyika

kwa kila mkoa kuwezeshwa kupata walau

mradi mmoja wa jengo la biashara ambalo

litaongeza mapato ya mkoa husika.

Aidha, alisema kwa kuwa ujenzi wa

nyumba za gharama nafuu ni kioo cha

Shirika la Nyumba mbele ya Jamii, jitihada

zote zichukuliwe kuhakikisha kwamba

miradi yote inajengwa na kusimamiwa

BARAZA LA WAFANYAKAZI

KATIBU MKUU ARDHI AFUNGUA BARAZA KUU LA WAFANYAKAZI

Picha ya pamoja ya Wajumbe wa kikao cha Baraza Kuu la Wafanyakazi wa Shirika la Nyumba la Taifa kilichofanyika hoteli ya Tanga Beach Resort, Tanga

JULAI - DESEMBA 2014 /Nyumba Newsletterwww.nhctz.com25

MILIKI NYUMBA

kwa kuzingatia ubora, muda na gharama

iliyokusudiwa.

Baraza hilo liliazimia pia kuwa makusanyo

ya kodi ni uti wa mgongo wa uendeshaji

wa majukumu mbalimbali ya Shirika,

hivyo mikoa yote inawajibika kukusanya

mapato yote kwa wakati. Azimio jingine ni

kuhakikisha kuwa mikoa yote iwezeshwe

kufanya matengenezo yote ya lazima kwa

majengo ya Shirika ili kuboresha huduma

kwa wapangaji.

Azimio jingine la Baraza lililotolewa ni

kuongeza jitihada za kuuza na nyumba na

kukusanya mapato ya mauzo ya nyumba

hizo zifanyike siyo tu na kitengo cha mauzo

bali liwe jukumu nambari moja kwa kila

mfanyakazi na hasa katika kipindi hiki

ambapo Shirika limepanua wigo wa ujenzi

wa nyumba za makazi na biashara nchi

nzima.

Naye, Mkukurugenzi Mkuu wa NHC, Bw.

Nehemia Kyando Mchechu, alisema licha

ya Shirika kupata mafanikio kadhaa,, zipo

changamoto zinazoikabili sekta ya nyumba

ikiwemo gharama kubwa ya vifaa vya ujenzi

na upatikanaji wa mikopo ya nyumba ya

muda mrefu yenye riba nafuu.

Bw. Mchechu alisema kuwa, ikiwa Serikali

itapunguza kodi gharama ya nyumba

inaweza kupungua, jambo ambalo

linaweza kuwasaidia wananchi wa kawaida

kuzinunua.

“Tunaiomba Serikali kuangalia upya kodi

zilizoongezeka, kwa sababu zimechangia

kupanda kwa gharama za nyumba,”alisema

Mchechu.

Alisema, mkakati uliopo ni kuhakikisha

kuwa, miradi iliyoanzishwa inakwisha katika

kipindi kilichopangwa ili iweze kusaidia

wananchi.

1 Chukua fomu ya kununua Nyumba kutoka ofisi yoyote ya mkoa popote nchini au kwenye tovuti ya shirika.

2 Rudisha fomu iliyojazwa ikiwa na uthibitisho wa kulipiwa na malipo ya 10% (ikiwa na VAT) ya thamani ya Nyumba husika.

3 Maombi yako yatapitiwa kwa umakini ili kuhakikisha kunakuwa na usawa katika uchaguaji wa watu wanaostahili kulingana na Vigezo na masharti ya NHC na taratibu za Jamhuri ya Tanzania.

4 Kama umefanikiwa, utatumiwa barua za kuthibitishiwa kukubaliwa maombi yako. Barua zitatolewa kwa wote waliokidhi Vigezo vilivyowekwa.

5 Utatakiwa kulipa 90% iliyobaki kulingana na thamani ya nyumba husika

ndani ya siku 90 tangu umepewa.

6 Endapo ukishindwa kulipa ndani ya siku 90, NHC itatoa nyumba kwa Waombaji waliopo kwenye orodha ya wanao subiri.

7 Orodha ya wanaosubiri itakuwa na majina ya waombaji waliolipia malipo ya

mwanzo lakini wakakosa nafasi kwa kuwa nyumba zote zilishapata watu.

8 Kama ukishindwa kulipia kiasi kilichobakia, au ukakosa nafasi ukiwa kwenye orodha ya wanaosubiri, kiasi cha 10% kilicholipwa kinaweza kutumiwa kulipia kwenye miradi mingine ya NHC na waliopo kwenye orodha ya wanaosubiri au kurudishiwa pesa zao.

9 Mauzo ya nyumba za mradi husika yatatangazwa yamefungwa pindi Waombaji waliofanikiwa kupata nyumba wamemaliza kufanya malipo yao yote.

10 NHC itafanya utaratibu wa kutafuta hati za nyumba na kisha kuwapatia wanunuzi walioweza kulipia pesa zote taslimu au kupitia taratibu za mkopo. Miliki nyumba yako sasa. Kumiliki nyumba

Utaratibu huu unaolenga kuwawezesha wananchi wa kipato cha kati na chini kumiliki nyumba, umepongezwa sana na Serikali Kuu na viongozi mbalimbali wakiwemo Waheshimiwa Wabunge

HATUA RAHISI ZA KUMILIKI

NYUMBA YAKO LEO

Nyumba Newsletter/JULAI - DESEMBA 2014 www.nhctz.com26

SHIRIKA LA NYUMBA LA TAIFAMAKAO MAKUU S.L.P 2977 SIMU: +255 22 2105002

NUKUSHI: +255 22 2105000 BARUA PEPE: [email protected]

TOVUTI: www.nhctz.com

1. MKOA WA UPANGA S.L.P 9634, Dar es Salaam SIMU: 022 2128314 022 2128305 / 022 2128306

2 . MKOA WA KINONDONI S.L.P 23200, Dar es Salaam SIMU: 022 2667150

3 . MKOA WA ILALA S.L.P 25110 Dar es Salaam SIMU: 022 2863126

4. MKOA WA TEMEKE S.L.P 45674 Dar es Salaam SIMU: 022 2866829 022 2863121

5. MKOA WA MWANZA /GEITA /SIMIYU S.L.P 1683, Mwanza SIMU: 028 2503047 028 2503048

6. MKOA WA MTWARA S.L.P 67, Mtwara SIMU: 023 23333

7. MKOA WA TABORA S.L.P 166, Tabora SIMU: 026 2604530 026 2604752

8. MKOA WA MBEYA/NJOMBE S.L.P 541, Mbeya SIMU: 025 2502482 025 2500699

9. MKOA WA ARUSHA S.L.P 883, Arusha SIMU: 027 2755052 027 2502995

10. MKOA WA KILIMANJARO S.L.P 1458, Moshi SIMU: 027 2755052 027 2754080

11. MKOA WA TANGA S.L.P 5041, Tanga SIMU: 027 2644479 027 2644480

12. MKOA WA MOROGORO S.L.P 892 Morogoro SIMU: 023 2603268 023 2604535

13. MKOA WA IRINGA S.L.P 206, Iringa SIMU: 026 2702603

14. MKOA WA MARA S.L.P 257 Musoma SIMU: 028 2622032

15. MKOA WA DODOMA S.L.P 391, Dodoma SIMU: 026 2323151

16. MKOA WA SHINYANGA S.L.P 478, Shinyanga SIMU: 028 2762045

17. MKOA WA KAGERA S.L.P 369, Bukoba SIMU: 028 2220035/36

18. MKOA WA SINGIDA S.L.P 254, Singida SIMU: 026 2502332

19. MKOA WA KIGOMA S.L.P 271, Kigoma SIMU: 028 2802844

20. MKOA WA LINDI S.L.P 206, Lindi SIMU: 023 2202054

21. MKOA WA RUVUMA S.L.P 65, Songea Ruvuma

22. MKOA WA KATAVI S.L. P 375 MPANDA,KATAVI.

TUNAJENGA TAIFA LETU