29
Kitabu kuhusu ´Aqiydah Imaam na Haafidhw Abul-Husayn Muhammad bin Abiy Ya´laa al-Hanbaliy www.firqatunnajia.com 1 عتقادب ا كتاKitabu kuhusu ´Aqiydah Mwandishi: Imaam na Haafidhw Abul-Husayn Muhammad bin Abiy Ya´laa al- Hanbaliy Tarjama: Firqatunnajia.com

ì¬ß ¦§¢¬ï - firqatunnajia.comfirqatunnajia.com/wp-content/uploads/2019/02/ab_2.pdf · Bukhaariy, Muslim, Abu ´Iysaa at -Tirmid hiy, Abu D aawuud, Ibn Khuzaymah, ad -Daa raqut

  • Upload
    others

  • View
    1

  • Download
    0

Embed Size (px)

Citation preview

Kitabu kuhusu ´Aqiydah Imaam na Haafidhw Abul-Husayn Muhammad bin Abiy Ya´laa al-Hanbaliy

www.firqatunnajia.com 1

كتاب اإلعتقادKitabu kuhusu ´Aqiydah

Mwandishi: Imaam na Haafidhw Abul-Husayn Muhammad bin Abiy Ya´laa al-

Hanbaliy

Tarjama: Firqatunnajia.com

Kitabu kuhusu ´Aqiydah Imaam na Haafidhw Abul-Husayn Muhammad bin Abiy Ya´laa al-Hanbaliy

www.firqatunnajia.com 2

YALIYOMO

[1] Tunaanza kwa kutaja yale ambayo Allaah (Ta´ala) ameyafaradhisha kwa waja Wake, ............................ 4

[2] Imani inathibitishwa kwa kutamka kwa ulimi, kuamini na matendo ya viungo ...................................... 4

[3] Imani na Uislamu ni maneno mawili yenye maana mbili tofauti ........................................................... 4

[4] Qur-aan ni maneno ya Allaah yaliyoteremshwa na haikuumbwa ........................................................... 5

[5] Hakuacha na bado ni mwenye kuendelea kuzungumza ........................................................................ 5

[6] Allaah ni Mmoja asiyefanana na chochote ............................................................................................ 6

[7] Yule mwenye kuitakidi juu ya sifa hizi na mapokezi Swahiyh mfano wake kufanana ........................... 10

[8] Kuzikanusha sifa ni madhehebu ya Jahmiyyah ................................................................................... 10

[9] Yule mwenye kuzipitisha kama zilivyokuja ......................................................................................... 10

[10] Ni wajibu kuamini Qadar ................................................................................................................. 11

[11] Inatakiwa kuamini adhabu ya ndani ya kaburi na Munkar na Nakiyr ................................................. 12

[12] Inatakiwa kuamini ufufuliwaji na Njia .............................................................................................. 14

[13] Kuamini Mizani ............................................................................................................................... 14

[14] Inatakiwa kuamini Hodhi na Uombezi ............................................................................................. 14

[15] Mtu anatakiwa kuamini pia mahojiano ............................................................................................. 15

[16] Kuamini kwamba Allaah aliumba Pepo na Moto kabla ya kuumba viumbe ...................................... 16

[17] Kuhusiana na wapwekeshaji watenda madhambi .............................................................................. 16

[18] Inatakiwa kuamini vilevile kwamba Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ndiye Mtume wetu

............................................................................................................................................................... 17

[19] Miongoni mwa hayo ni kitabu chake ambacho kinavihukumu vitabu vyengine vyote ....................... 18

[20] Ana (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alama kubwa za ardhini na mbinguni ................................... 20

[21] Yule mwenye kunyanyua sauti yake mbele ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) .................. 23

[22] Kiumbe bora baada ya Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) .................................... 28

[23] Ni wajibu kuwakata Ahl-ul-Bid´ah na wapotevu ............................................................................... 29

[24] Hii ndio ´Aqiydah yangu na yale ninayomwabudu kwayo Mola wangu ............................................. 29

Kitabu kuhusu ´Aqiydah Imaam na Haafidhw Abul-Husayn Muhammad bin Abiy Ya´laa al-Hanbaliy

www.firqatunnajia.com 3

Siku ya ijumaa tarehe 13 Shawwaal mwaka wa 573 alinikhabarisha

muheshimiwa Shaykh Abu Sa´iyd ´Abdul-Jabbaar bin Yahyaa bin ´Aliy bin

Hilaal al-A´rabiy kwa njia ya kunisomea na mimi nasikiliza. Amesema:

Muheshimiwa Abul-Husayn Muhammad bin Muhammad bin al-Farraa´

amsema:

Himdi zote anastahiki Allaah mpaka aridhie. Hapana mwabudiwa wa haki

isipokuwa Allaah, Aliyetukuka, Aliye juu kabisa. Himdi zote ni za Allaah

ambaye anastahiki kushukuriwa pasi na kikomo. Himdi zote anastahiki Allaah

ambaye ametuumba baada ya kutokuwepo, akatujaalia kuwa katika Ummah

bora na akatuteulia kiumbe Chake bora na Mtume Wake mtukufu zaidi

kutuongoza. Amemfanya kuwa mtu wa kwanza aliyetangulia inapokuja katika

manzilah na Mtume bora kabisa inapokuja katika ujumbe –Allaah amsifu na

familia yake wazuri swalah ambayo itawakusanya wote pamoja.

Allaah atukinge sisi na nyinyi juu ya kujikafilisha mambo tusiyoyaweza wala

kudai tusiyoyamairi. Allaah atulinde sisi na nyinyi kutokamana na Bid´ah na

uongo ambavyo ndio uovu na uchafu mkubwa zaidi ambavyo mtu anaweza

kuwa navyo.

Hakika umeniuliza kuhusu ´Aqiydah yangu na yale ninayomwabudu Mola

wangu (´Azza wa Jall) ili uweze kuyafuata na matokeo yake ufuzu kutokamana

na Bid´ah na matamanio yenye kupotosha na utunukiwe na Allaah (´Azza wa

Jall) ngazi za juu. Hivyo nakujibu yale uliyoniuliza hali ya kutaraji thawabu

kubwa kutoka kwa Allaah na kuogopa adhabu Yake kali na namtegemea juu

ya kuzungumza maneno yaliyo ya sawa.

Kitabu kuhusu ´Aqiydah Imaam na Haafidhw Abul-Husayn Muhammad bin Abiy Ya´laa al-Hanbaliy

www.firqatunnajia.com 4

[1] Tunaanza kwa kutaja yale ambayo Allaah (Ta´ala) ameyafaradhisha kwa waja Wake,

akamtumiliza Mtume Wake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na akateremsha

vitabu Vyake; nako ni kule kumwamini Allaah (´Azza wa Jall). Maana yake ni

kusadikisha yale (Tabaarak wa Ta´ala) aliyosema, akayaamrisha,

akayafaradhisha na akayakataza kupitia yale yote yaliyofikishwa na Mitume

kutoka Kwake na yakateremshwa na vitabu. Mitume wametumwa kwa hayo.

Amesema (Ta´ala):

و وا و ر و ر وا م قو ر م و م ر س ول م ر س وم م و ر م و ر س و م وقـ و م ر و و واعر س س وم

“Hatukutuma kabla yako Mtume yeyote isipokuwa Tulimfunulia Wahy ya kwamba: “Hakika hapana Muabudiwa wa haki ila Mimi; basi Niabuduni.”1

[2] Imani inathibitishwa kwa kutamka kwa ulimi, kuamini na matendo ya

viungo. Inazidi kwa kufanya matendo [mema] mengi na kuzungumza na

inashuka kwa maasi.

Hakuna neno kwa mtu kufanya uvuaji katika imani yake. Kufanya uvuaji ni

jambo halina shaka yoyote kwani ni njia iliyotumiwa na wanachuoni. Mtu

akiulizwa kama ni muumini basi anatakiwa kusema:

”Mimi ni muumini Allaah akitaka.”

Vilevile anaweza kusema:

”Nataraji kuwa ni muumini.”

Pia anaweza kusema:

”Nimemwamini Allaah, Malaika Wake, Vitabu Vyake na Mitume Wake.”

[3] Imani na Uislamu ni maneno mawili yenye maana mbili tofauti. Uislamu

kwa upande wa Shari´ah ni zile shahaadah mbili pamoja na kusadikisha ndani

ya moyo ilihali imani ni ule utiifu wote.

1 21:25

Kitabu kuhusu ´Aqiydah Imaam na Haafidhw Abul-Husayn Muhammad bin Abiy Ya´laa al-Hanbaliy

www.firqatunnajia.com 5

[4] Qur-aan ni maneno ya Allaah yaliyoteremshwa na haikuumbwa pasi na

kujali namna itakavyosomwa na namna itakavyoandikwa na popote pale

itakaponakiliwa. Kitabu ni yale yaliyoandikwa, kisomo ni yale yanayosomwa.

Maneno ya Allaah ni ya kale [milele] na hayakuumbwa katika hali zote. Ni

maneno ya Allaah ambayo hayakuumbwa, hayakuzuliwa wala kutengenezwa

kwa hali yoyote ile. Wala sio mwili, kiungo, jauhari wala aradhi, Bali ni sifa

moja katika sifa za kidhati zinazotofautiana na viumbe vyote.

[5] Hakuacha na bado ni mwenye kuendelea kuzungumza. Maneno Yake

hayawezi kutengana na dhati Yake. Wakati fulani yanasikika kutoka Kwake

(´Azza wa Jall) na wakati mwingine yanasisika kutoka kwa msomaji. Yule

mwenye kuyasikia moja kwa moja kutoka kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala)

ndiye aliyepokea uzungumzishwaji mwenyewe pasi na mkatikati wala

mkalimani. Kwa mfano Allaah alimzungumzisha Mtume wetu Muhammad

(Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) usiku wa kupandishwa mbinguni. Kadhalika

aliongea na Muusa kwenye mlima wa Sinai. Vivyo hivyo Malaika

wanaozungumzishwa Naye. Vinginevyo, maneno ya Allaah ya kale yanasikika

kikweli kutoka kwa msomaji na yana herufi zenye kufahamika na sauti yenye

kusikika.

Kitabu kuhusu ´Aqiydah Imaam na Haafidhw Abul-Husayn Muhammad bin Abiy Ya´laa al-Hanbaliy

www.firqatunnajia.com 6

[6] Allaah ni Mmoja asiyefanana na chochote. Hatuzifananishi sifa Zake za

sifa za viumbe na wala hatuzifanyii namna sifa Zake. Allaah yuko kinyume

kabisa na vile ambavyo akili ya mtu inavofikiria.

Yuko hai kwa uhai, ni mjuzi kwa ujuzi, ni muweza kwa uwezo, ni misikivu

kwa usikizi, ni muoni kwa uoni, ni mwenye kuzungumza kwa maneno,

mwenye kutaka kwa utashi, mwenye kuamrisha kwa amri, mwenye kukataza

kwa makatazo.

Tunathibitisha kwamba amemuumba Aadam kwa mkono Wake kutokana na

maneno Yake (Ta´ala):

وا و قو و و وو و ر س و م وا و وقر س م و و ر

”Kipi kilichokuzuia usimsujudie Niliyemuumba kwa mikono Yangu?”2

ااس و ر س ووتواوم و ر و و

”Bali mikono Yake imefumbuliwa.”3

Kwamba ana mkono wa kuume, kutokana na maneno Yake (Subhaanah):

تت م و م م م وا ر وا واتس و ر م ر

”Mbingu zitakunjwa mkononi mwake mwa kuume.”4

Kwamba ana uso kutokana na maneno Yake:

كس ل و ر ل وا م ت م ر و ر و س

“Kila kitu ni chenye kuhiliki isipokuwa uso Wake.”5

وم واإلرمكر واام و قو قرقو ـ و ر س و م و س اارو و

2 38:75 3 05:64 4 39:67 5 28:88

Kitabu kuhusu ´Aqiydah Imaam na Haafidhw Abul-Husayn Muhammad bin Abiy Ya´laa al-Hanbaliy

www.firqatunnajia.com 7

”Utabakia uso wa Mola Wako wenye utukufu na ukarimu.”6

Kwamba ana unyayo kutokana na maneno ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi

wa sallam):

”Mpaka pale Mola wako ataweka unyayo Wake juu yake ambapo utasema:

”Tosha, tosha.”7

Bi maana juu ya Moto. Ameipokea Ahmad, al-Bukhaariy, Muslim, Abu ´Iysaa

at-Tirmidhiy na wengineo.

Kila usiku Anashuka katika mbingu ya chini ya dunia kutokana na maneno ya

Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):

“Mola wetu anashuka katika mbingu ya chini ya dunia pale kunapobaki

theluthi ya mwisho ya usiku.”

Tamko hili ni la al-Bukhaariy. Hadiyth hii imepokelewa na Ahmad, Maalik, al-

Bukhaariy, Muslim, Abu ´Iysaa at-Tirmidhiy, Abu Daawuud, Ibn Khuzaymah,

ad-Daaraqutwniyna maimamu wengine wa Kiislamu.

Anamcheka mja Wake muumini kutokana na maneno ya Mtume wa Allaah

(Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):

”Allaah (Ta´ala) anawacheka watu wawili. Mmoja amemuua mwengine na

wote wawili wanaingia Peponi.” Wakasema: “Vipi?” Akasema: “Mmoja

amepigana katika njia ya Allaah (´Azza wa Jall) ambapo akauawa shahidi.

Kisha Allaah akamsamehe yule muuaji ambaye aliingia katika Uislamu. Halafu

akapigana katika njia ya Allaah (´Azza wa Jall) ambapo akauawa shahidi.”8

Ameipokea al-Bukhaariy na wengineo.

Tunathibitisha kuwa Allaah ana nafsi isiyofanana na nafsi zengine. Amesema:

و سو م سكس س ا رق س قو ر و س

“Allaah anakutahadharisheni na nafsi Yake.”9

6 55:27 7 al-Bukhaariy (4848) na Muslim (2846) 8al-Bukhaariy (2826) na Muslim (1890). 9 03:28

Kitabu kuhusu ´Aqiydah Imaam na Haafidhw Abul-Husayn Muhammad bin Abiy Ya´laa al-Hanbaliy

www.firqatunnajia.com 8

واصر و قو رتس و م قو ر م

“Nimekuchagua kwa ajili Yangu.”10

Abu Hurayrah amesimulia kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi

wa sallam) amesema:

“Allaah (´Azza wa Jall) anasema: “Mimi ni vile anavyonidhania mja Wangu na

mimi niko pamoja naye pindi anaponitaja. Akinitaja ndani ya nafsi yake, basi

Namtaja ndani ya nafsi Yangu.”11

Tunathibitisha kwamba Allaah yuko juu ya ´Arshi Yake amelingana. Hivi

ndivyo ilivyokuja katika Qur-aan katika Suurah saba: al-A´raaf, Yuunus, ar-

Ra´d, Twaa Haa, al-Furqaan, as-Sajdah na al-Hadiyd.

Tunathibitisha kuwa:

“Mwingi wa huruma amemuumba Aadam kwa sura Yake.”

Ameipokea Ahmad bin Hanbal, Ibn Khuzaymah na wengineo. Vilevile

imepokelewa:

“… kwa sura ya Mwingi wa huruma.”

Ameipokea ad-Daaraqutwniy, Abu Bakr an-Najjaad, Abu ´Abdillaah bin

Battwah na wengineo.

Tunathibitisha kuwa Allaah ana vidole. Ibn Mas´uud (Radhiya Allaahu ´anh)

amesema:

“Kuna mwanachuoni mmoja wa kiyahudi alikuja kwa Mtume (Swalla Allaahu

´alayhi wa sallam) na akamwambia: “Ee Muhammad! Sisi tunakuta kuwa

Allaah ataziweka mbingu juu ya kidole, ardhi juu ya kidole, miti juu ya kidole,

maji juu ya kidole na viumbe vyengine vilivyobaki juu ya kidole. Halafu

atasema: “Mimi ndiye Mfalme.” Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)

akacheka mpaka magego yake yakaonekana kwa kusadikisha maneno ya

mwanachuoni huyu wa kiyahudi. Kisha akasoma maneno ya Allaah (Swalla

Allaahu ´alayhi wa sallam):

10 20:41 11 al-Bukhaariy (7405) na Muslim (2675).

Kitabu kuhusu ´Aqiydah Imaam na Haafidhw Abul-Husayn Muhammad bin Abiy Ya´laa al-Hanbaliy

www.firqatunnajia.com 9

تت م و م م م و ر س وم عا قو ر وتس س قو راو ا رقم وا و م وا ر ا واتس و ر م ر و وا و و س ا اارو وو ر و ر مام واار”Hawakumkadiria Allaah inavyostahiki kukadiriwa! Ardhi yote itakamatwa

mkononi Mwake wa kuume siku ya Qiyaamah.”1213

Ameipokea Hibatullaah at-Twabariy, al-Bukhaariy, Muslim na Abu ´Iysaa at-

Tirmidhiy ambaye tamko yeye limekuja ifuatavyo: Amenikhabarisha al-

Mubaarak bin ´Abdil-Jabbaar as-Sayrafiy kwenye kikao cha baba yangu

(Rahimahu Allaah) kwenye msikiti wa Mansuur kwa cheni ya wapokezi wake

kutoka kwa ´Abdullaah ambaye amesema:

”Kuna myahudi alikuja kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na

kusema: ”Ee Muhammad! Allaah ataziweka mbingu juu ya kidole, ardhi juu ya

kidole na viumbe wengine juu ya kidole. Kisha atasema: ”Mimi ndiye

Mfalme.” Ndipo Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akaanza

kucheka mpaka magego yake yakaonekana. Kisha akasoma:

تت م و م م م و ر س وم عا قو ر وتس س قو راو ا رقم وا و م وا ر ا واتس و ر م ر و وا و و س ا اارو وو ر و ر مام واار”Hawakumkadiria Allaah inavyostahiki kukadiriwa! Ardhi yote itakamatwa

mkononi Mwake wa kuume siku ya Qiyaamah.”

Abu ´Iysaa amesema:

”Hadiyth hii ni nzuri na Swahiyh.”

Katika upokezi mwingine imekuja:

”Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akacheka kwa

kupendekezwa na kumsadikisha.”

Abu Sa´iyd amesimulia kwamba amemsikia Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa

sallam) akisema:

”Mola wetu atafunua muundi Wake ambapo atamsujudia kila muumini

mwanaume na muumini mwanamke na watabaki [hali ya kusimama] wale

ambao walikuwa wakisujudu duniani kwa kujionyesha na kutaka kusikika. Pale

12 39:67 13 al-Bukhaariy (4811) na Muslim (2786).

Kitabu kuhusu ´Aqiydah Imaam na Haafidhw Abul-Husayn Muhammad bin Abiy Ya´laa al-Hanbaliy

www.firqatunnajia.com 10

atapoenda ili kusujudu, tahamaki mgongo wake utarudi na kuwa talaka

moja.”14

Anas ameeleza kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)

amesema:

”Allaah hufurahishwa na tawbah ya mja wake zaidi kuliko vile anavyofurahi

mmoja wenu pale anapomkosa ngamia wake ambaye yuko na chakula na

kinywaji chake juu yake. Kisha akamtafuta na asimpate. Baada ya hapo akalala

chini ya mti na huku akisubiria kifo. Tahamaki ngamia yule amesimama juu

yake. Akamshika khatamu na kwa furaha nyingi akasema: ”Ee Allaah! Wewe

ni mja wangu na mimi ndiye Mola Wako.”15

´Abdullaah amesimulia kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)

alimtaja ad-Dajjaal kisha akasema:

”Hakika ana chongo, lakini Mola wenu (´Azza wa Jall) hana chongo.”16

[7] Yule mwenye kuitakidi juu ya sifa hizi na mapokezi Swahiyh mfano wake

kufanana inapokuja katika miili, aina, shakili na urefu, ni kafiri.

[8] Kuzikanusha sifa ni madhehebu ya Jahmiyyah. Yule mwenye kuzifasiri

kutokana na lugha na majazi ni Jahmiy.

[9] Yule mwenye kuzipitisha kama zilivyokuja bila kuzipindisha maana,

kuzifasiri, kuzifanya mwili wala kuzifananisha, kama walivyofanya

Maswahabah na Taabi´uun, amefanya jambo la wajibu kwake.

14 al-Bukhârî (4919) na Muslim (183). 15 al-Bukhaariy (6308) na Muslim (2747). 16 al-Bukhaariy (7131) na Muslim (2933).

Kitabu kuhusu ´Aqiydah Imaam na Haafidhw Abul-Husayn Muhammad bin Abiy Ya´laa al-Hanbaliy

www.firqatunnajia.com 11

[10] Ni wajibu kuamini Qadar, kheri na shari yake, matamu yake na machungu

yake, makubwa yake na machache yake, yenye kuonekana na yenye kujificha,

yale yenye kupendwa na yale yenye kuchukiwa na mazuri yake na yasiyokuwa

mazuri.

Mwanzo na mwisho wake ni kutoka kwa Allaah. Amepanga mipango Yake

juu ya waja Wake na akakadiria makadirio juu yao. Hakuna yeyote awezaye

kushinda matakwa ya Allaah (´Azza wa Jall) na wala hakuna yeyote awezaye

kushinda mipango Yake, bali wote hawana ujanja ni wenye kupita chini ya yale

aliyowaumba kwayo. Huu ni uadilifu kutoka kwa Mola wetu (´Azza wa Jall).

Anataka utiifu utendeka, yuko radhi nao, anaupenda na ameuamrisha. Hata

hivyo hakuamrisha maasi na wala hayapendi na kuyaridhia. Upande mwingine

ameyahukumu, akayakadiria na akataka yatendeke. Muuliwaji anauawa pindi

muda wake unapofika.

Kitabu kuhusu ´Aqiydah Imaam na Haafidhw Abul-Husayn Muhammad bin Abiy Ya´laa al-Hanbaliy

www.firqatunnajia.com 12

[11] Inatakiwa kuamini adhabu ya ndani ya kaburi na Munkar na Nakiyr.

Allaah (Ta´ala) amesema:

وإمور و س و م شو ع ضو كعا

“Basi hakika atapata maisha ya dhiki kabisa.”17

Wafasiri wa Qur-aan wamesema:

”Bi maana adhabu ya ndani ya kaburi.”

Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alisema kumwambia ´Umar bin al-

Khattwaab (Radhiya Allaahu ´anh):

”Ee ´Umar! Hali ingelikuwa vipi endapo ungeliona fitina za Malaika wawili wa

kaburi? Ni weusi na wana macho ya bluu na kama umeme na sauti yao ni

kama radi. Wanaingia kwenye nywele zao na wanachimba kwa meno yao ya

kuchimba. Mikononi mwao wana nyundo za vyuma. Lau wangeliwapiga watu

na majini, basi wangelikufa.” ´Umar (Radhiya Allaahu ´anh) akasema: ”Siku

hiyo nitakuwa na hali gani?” Akasema: ”Katika hali yako hiyohiyo ulionayo.”

Akasema: ”Basi nitakutosheleza nao, ee Mtume wa Allaah!”18

Umm Khaalid (Radhiya Allaahu ´anhaa) amesimulia:

”Nilimsikia Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akiomba kinga dhidi ya

adhabu ya kaburi.”19

Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

”Lau angelikuweko yoyote atakayeokoka na mbano wa kaburi, basi

angeliokoka Sa´d bin Mu´aadh ambaye ´Arshi ya Mwingi wa rehema ilitikisika

kwa ajili yake.”20

Halafu baada ya hapo mtu anatakiwa kuamini sauti ya parapanda kutoka kwa

Israafiyl kwa ajili ya kufufuka kutoka ndani ya makaburi. Ulazimishe moyo

kwamba utakufa na utabanwa ndani ya kaburi. Ni wajibu pia kuamini kuwa

mtu atahojiwa ndani ya kaburi na atafufuliwa baada ya kufa. Mwenye

kuyakanusha haya ni kafiri.

17 20:124 18 al-Bayhaqiy katika ”Ithbaat ´Adhaab-il-Qabr” (116–117) na Ibn Abiy Daawuud katika ”al-Ba´th” (7). 19 al-Bukhaariy (6364) na Muslim (584). 20 Ahmad (6/55).

Kitabu kuhusu ´Aqiydah Imaam na Haafidhw Abul-Husayn Muhammad bin Abiy Ya´laa al-Hanbaliy

www.firqatunnajia.com 13

Kitabu kuhusu ´Aqiydah Imaam na Haafidhw Abul-Husayn Muhammad bin Abiy Ya´laa al-Hanbaliy

www.firqatunnajia.com 14

[12] Inatakiwa kuamini ufufuliwaji na Njia. Nembo ya waumini siku hiyo

itakuwa:

”Salimisha, salimisha.”

Imekuja katika Hadiyth kwamba Njia itakuwa yenye makali zaidi kuliko

upanga na nyembamba zaidi kuliko unywele21.

[13] Kuamini Mizani. Amesema (Ta´ala):

ئعا ثقرقواوو وو ر ل م ر و ردوول و و وعس ا ر و وازم و ا رقم رطو م قو رام ا رقم وا و م و و سظر و س قو رست و قر و مو كواوو م وكو و ـ م وا ووا م م و و قو قر وا بموا

“Tutaweka mizani ya uadilifu siku ya Qiyaamah, basi hakuna nafsi itakayodhulumiwa chochote japo ikiwa uzito wa mbegu ya haradali Tutaileta. Inatosheleza Kwetu kuwa wenye kuhesabu.”22

´Abdullaah bin Mas´uud amesema:

”Siku ya Qiyaamah watu wataletwa kwenye Mizani na hapo watabishana

ubishi mkubwa kabisa.”

Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

”Mkono wa kuume wa Allaah (´Azza wa Jall) umejaa. Haupungui kwa kutoa

mchana na usiku. Kwenye mkono Wake mwingine kuna mizani ambayo

hushusha na hupandisha.”23

[14] Inatakiwa kuamini Hodhi na Uombezi. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa

sallam) amesema:

21 Muslim (195). 22 21:47 23 al-Bukhaariy (4684), Muslim (993), Ahmad (2/242) na at-Tirmidhiy (3045) ambaye amesema: “Hdiyth hii ni nuri na Swahiyh na akaifasiri Aayah:

ااس و ر س ووتواوم س م س كو ر و وشوا س غس ر ر و ر م م ر و س م س ا بموا وا س ا و وا و م ا ر قو س دس و س اارم وغر س و ت و ر و و

“Mayahudi wakasema: “Mkono wa Allaah umefumbwa.” Mikono yao ndio iliyofumbwa na wamelaaniwa kwa yale

waliyoyasema. Bali mikono Yake imefumbuliwa hutoa atakavyo.” (05:64)

Hadiyth imepolewa na maimamu. Tunaiamini kwa udhahiri wake pasi na kuifasiri wala kuifanyia namna. Hivyo ndivo

walivosema maimamu akiwemo Sufyaan ath-Thawriy, Maalik bin Anas, Ibn ´Uyaynah na Ibn-ul-Mubaarak;

zinatakiwa kupitishwa na kuziamini pasi na kuzifanyia namna.”

Kitabu kuhusu ´Aqiydah Imaam na Haafidhw Abul-Husayn Muhammad bin Abiy Ya´laa al-Hanbaliy

www.firqatunnajia.com 15

”Mimi nina Hodhi inayoanzia Ayla kwenda mpaka Adeni na vikombe vyake

ni sawa na idadi ya nyota mbinguni.”24

Bi maana ni kubwa sana.

Anas bin Maalik amesema:

”Mwenye kukadhibisha Hodhi basi hatokunywa humo.”

[15] Mtu anatakiwa kuamini pia mahojiano. Allaah (Ta´ala) atamuhoji mja kwa

yale yote aliyoyafanya, madogo na makubwa.

24al-Bukhaariy (6591) na Muslim (2298).

Kitabu kuhusu ´Aqiydah Imaam na Haafidhw Abul-Husayn Muhammad bin Abiy Ya´laa al-Hanbaliy

www.firqatunnajia.com 16

[16] Kuamini kwamba Allaah aliumba Pepo na Moto kabla ya kuumba

viumbe. Neema za Peponi zitaendelea kuwepo milele na kamwe wanawake wa

Peponi hawakutokufa.

Adhabu ya Motoni ni yenye kudumu na watu wake ambao walitengana na

dunia hii hali ya kuwa si wenye kumwabudu Allaah pekee na si wenye kufuata

Sunnah, watadumishwa humo.

[17] Kuhusiana na wapwekeshaji watenda madhambi, watatolewa humo ndani

kwa uombezi. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

”Uombezi wangu ni kwa ajili ya watenda madhambi makubwa kutoka katika

Ummah wangu.”25

Watoto wa washirikina watakuwa Motoni.

25 Ahmad (3/213), Abu Daawuud (4739) na at-Tirmidhiy (2345).

Kitabu kuhusu ´Aqiydah Imaam na Haafidhw Abul-Husayn Muhammad bin Abiy Ya´laa al-Hanbaliy

www.firqatunnajia.com 17

[18] Inatakiwa kuamini vilevile kwamba Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi

wa sallam) ndiye Mtume wetu, Nabii wa mwisho, bwana wa Mitume, kiongozi

wa wachaji na mjumbe wa Mola wa walimwengu.

Amemtumiliza kwetu na kwa viumbe wengine wote. Yeye ndiye bwana wa

wana wa Aadam na ndiye wa kwanza atakayefufuliwa na ardhi. Aadam na

walioko chini yake watakuwa chini ya bendera yake. Yeye ndiye shahidi wa

kila Mtume na ndiye shahidi wa kila Ummah. Allaah (Ta´ala) amechukua

mkataba kwa Mitume kumwamini, kutoa bishara njema juu yake, kumwelezea

na kumbainisha katika vitabu vyao pamoja na zile alama na miujiza yenye

kugonga ambayo Allaah alimtunuku kabla na baada ya kupewa utume.

Kitabu kuhusu ´Aqiydah Imaam na Haafidhw Abul-Husayn Muhammad bin Abiy Ya´laa al-Hanbaliy

www.firqatunnajia.com 18

[19] Miongoni mwa hayo ni kitabu chake ambacho kinavihukumu vitabu

vyengine vyote na kinachovitolea khabari, kinachovitolea ushahidi na

kuvisadikisha. Hakifanani na mashairi wala barua. Kimetakasika na maneno

mengine yote. Kimefazaisha usikizi na uelewa. Hakiingiliwi na batili mbele

yake wala nyuma yake. Ni Uteremsho kutoka kwa Mwingi wa hekima,

Mwenye kustahiki kuhimidiwa. Watu na majini wameshindwa kuleta mfano

wake, japokuwa watakuwa ni wenye kusaidizana wao kwa wao. Ni kitabu

kilichokusanya mifumo, miujiza, ufafanuzi, ufaswaha, balagha,

matahadharisho, mawaidha, maamrisho kuhusu kila utiifu, karama, adabu,

makatazo kuhusu kila uovu na aina zote kubwa za ´ibaadah kama twahara,

swalah, swawm, zakaah, hajj, jihaad, kuunga udugu, kujitolea, zawadi,

swadaqah, utimizaji, kuogopa, kutaraji na aina nyenginezo zisizohesabika.

Wakati watu wake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) walipomwambia:

ا و ر و م ر س قـ و اار م مقس ر ول غو رم و

“Lete Qur-aan nyingine badala ya hii au ibadilishe.”

akasema:

مور و ر معس م ر وا س وو ـ ملور وا وكس وس لم وور س و م و س م م رقوا م قو ر م

“Hainipasii mimi kuibadilisha kwa khiyari ya nafsi yangu. Mimi sifuati isipokuwa tu yale nilofunuliwa Wahy.”26

Bi maana kutoka kwa Mola wangu. Halafu akawaambia:

و و و قوقو ر و مثر س م كس ر عس س عا م قو ر م م ر ر وا و ا رق س وا قو و ر س س عو و ركس ر و و ودر واكس م م قو رقم س وو

“Kama angetaka Allaah nisingelikusomeeni na wala asingelikujulisheni nayo. Kwani nimekwishaishi nanyi umri wote kabla yake. Je, basi hamfahamu?”27

26 10:15 27 10:16

Kitabu kuhusu ´Aqiydah Imaam na Haafidhw Abul-Husayn Muhammad bin Abiy Ya´laa al-Hanbaliy

www.firqatunnajia.com 19

Bi maana kwa miaka arubaini mimi ni yatima, fakiri, si mwenye kujua kusoma

wala kuandika, sikuwa naenda kwa mwalimu wowote, mchawi, kuhani wala

mshairi. Je, hivi si mzingatie hayo? Mnajua fika ya kwamba Aayah mfano wa

hizi hakuna aziwezaye isipokuwa Allaah – hamkuweza kufanya hivo na wala

hamtoweza kufanya hivo.

Akafanya Aayah hizi ni zenye kushinda katika uhai wake na baada ya kufa

kwake pasi na yeyote kuja na mfano wake. Hakuna yeyote aliyefanikiwa kuja

na mfano wa Qur-aan kwa upande wa Aayah zake, mpangilio wake, ukweli

wake, usahihi wa maana yake na elimu zake kubwa. Kadhalika viumbe

hawakuweza kuzunguka uelewa wake wala kufikia kilele cha elimu yake.

Isitoshe yeye (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amekhabarisha kuhusu watu

wa kale na wataokuja nyuma:

و ر م و س م قو ر م غو و م م ر و قوغر م س وو م م رعم م م و غس م و م ا ل اس م ودر و اار

“Warumi wameshindwa. Katika nchi iliyo karibu, nao baada ya kushindwa kwao watashinda hivi karibuni. Katika miaka michache.”28

عس و قس و ل وو ا ل قس و و قس ر واس اارو ر

“Utashindwa mjumuiko wao na watageuza migongo.”29

Ameelezea hayo kabla ya kutokea kwake. Amesema (Ta´ala):

ا م و ر و ا م ر و م ر و وا م ا رغو ر م س وم و قـ و ا و و و و قو ر س و م قو ر م و وا كس و قو ر و س و

“Hizo ni katika khabari zilizofichikana Tunazokufunulia Wahy. Hukuwa unazijua wewe na wala watu wako kabla ya hii [Qur-aan].”30

28 30:02-04 29 54:45 30 11:49

Kitabu kuhusu ´Aqiydah Imaam na Haafidhw Abul-Husayn Muhammad bin Abiy Ya´laa al-Hanbaliy

www.firqatunnajia.com 20

[20] Ana (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alama kubwa za ardhini na

mbinguni. Hakuna mtu mwingine anayeshirikiana naye kwazo wala kuzifikia.

Mtu mwenye busara na mwenye uoni wa mbali akizizingatia, basi atatambua

kuwa Allaah amemtunuku nafasi na ngazi tukufu na akamfadhilisha kwazo juu

ya walimwengu wengine wote. Alama hiyo ni kwamba usiku mmoja

alimpanda mnyama al-Buraq kumpeleka Yerusalemu. Halafu akanyanyuliwa

juu mbinguni ambapo akawasalimia Malaika na Mitume ambao pia

aliwaswalisha. Aliingia Peponi na akauona Moto. Katika usiku huo

akafaradhishiwa swalah na akamuona Mola Wake. Akasogea karibu Naye na

akazungumza Naye na akamtukuza. Akaona karama na alama. Akamsogelea

Mola Wake na akawa kiasi cha umbali wa mipinde miwili au karibu zaidi.

Allaah aliuweka mkono Wake juu ya mabega yake na akahisi ubaridi kati ya

matiti yake na akapata elimu za wale wa mwanzo na wa mwisho. Amesema

(´Azza wa Jall):

و وا و و ر وا ا ل ر و ا ر م و و قر وااو م ر متقر و ع م راام

“Hatukuijaalia ndoto ambayo tulikuonyesha isipokuwa ni [kutaka kuwatia] mtihani kwa watu.”31

Uonaji huu ulitokea katika hali ya umacho na haikuwa ndoto. Usiku huohuo

akarudi kwa mwili wake kwenda Makkah. Akaeleza kwamba yeye (Swalla

Allaahu ´alayhi wa sallam) huko Aakhirah atapewa fadhilah na utukufu zaidi

kuliko alivyopewa hapa duniani na akasema:

و و و ر و قس ر م و و ل و قوتقو رضو ـ

“Bila shaka Mola wako atakupa na utaridhika.”32

Miongoni mwa yale atakayopewa huko Aakhirah ni kile Cheo chenye kusifiwa

ambacho hakuna yeyote ambaye atakisogelea. Abu Bakr Ahmad bin Abiy

Khaythamah amesimulia kwa cheni ya wapokezi wake kutoka kwa Mujaahid

ambaye amesema kuhusu maneno Yake:

31 17:60 32 93:05

Kitabu kuhusu ´Aqiydah Imaam na Haafidhw Abul-Husayn Muhammad bin Abiy Ya´laa al-Hanbaliy

www.firqatunnajia.com 21

عو و ـ وو قو قر وثو و و ل و وقوا عا مرر س دعا

“Hakika Mola wako akakuinua cheo kinachosifika.”33

”Atamkaza juu ya ´Arshi.”34

Abu Bakr bin Abiy Shaybah na ´Uthmaan bin Abiy Shaybah wamepokea kwa

cheni za wapokezi wao kutoka kwa Mujaahid ambaye amesema kuhusiana na

Aayah hiyohiyo:

”Atamkaza juu ya ´Arshi.”

Kadhalika ´Abdullaah bin Ahmad amepokea kwa cheni ya wapokezi wake

kutoka kwa Mujaahid. Vivyo hivyo amepokea Ishaaq bin Raahuuyah kutoka

kwa Ibn Fudhwayl kutoka kwa Layth kutoka kwa Mujaahid ambaye amesema

kuhusiana na Aayah hiyohiyo:

”Atakaa pamoja naye juu ya ´Arshi.”

Ibn ´Umayr amesema:

”Nimemsikia Abu ´Abdillaah Ahmad bin Hanbal akiulizwa kuhusu Hadiyth

ya Mujaahid ambapo akasema: ”Wanachuoni wameinukuu kwa kuikubali na

hivyo tunaipitisha kama ilivyokuja.”

Ibn-ul-Haarith amesema:

”Ndio, Muhammad atakazwa juu ya ´Arshi.”

´Abdullaah bin Ahmad amesema:

”Mimi namkemea kila yule ambaye anairudisha Hadiyth hii.”

Ibn ´Abbaas amesema kuhusiana na Aayah hiyohiyo:

”Atamkaza juu ya ´Arshi.”

Mapokezi haya yamepokelewa na Shaykh wetu Abu Bakr al-Marwaziy na

akatunga kitabu kikubwa juu ya maudhui hayo. Kadhalika ameeleza baba

yangu kutoka kwake kwa cheni ya wapokezi wake kutoka kwa Ibn ´Umar

kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kuhusiana na Aayah

hiyohiyo:

33 17:79 34Taariykh Ibn Abiy Khaythamah.

Kitabu kuhusu ´Aqiydah Imaam na Haafidhw Abul-Husayn Muhammad bin Abiy Ya´laa al-Hanbaliy

www.firqatunnajia.com 22

”Atakaa pamoja naye juu ya kiti.”

Kadhalika kwa cheni ya wapokezi kutoka kwa ´Aaishah (Radhiya Allaahu

´anhaa) ambaye amesema:

”Nilimuuliza Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kuhusu

Cheo chenye kusifiwa. Akasema: ”Mola wangu ameniahidi kukaa juu ya

´Arshi.”

Vivyo hivyo kwa cheni ya wapokezi kutoka kwa Ibn ´Umar ambaye amesema:

”´Umar bin al-Khattwaab alisema kunambia: ”Nilimuuliza Mtume (Swalla

Allaahu ´alayhi wa sallam) kile alichomuahidi Mola wake Akasema:

”Ameniahidi Cheo chenye kusifiwa ambacho ni kukaa juu ya ´Arshi.”

Vilevile ana Hodhi hiyo siku ya Qiyaamah.

Kitabu kuhusu ´Aqiydah Imaam na Haafidhw Abul-Husayn Muhammad bin Abiy Ya´laa al-Hanbaliy

www.firqatunnajia.com 23

[21] Yule mwenye kunyanyua sauti yake mbele ya Mtume (Swalla Allaahu

´alayhi wa sallam) kunachelea juu yake kuporomoka matendo yake. Amesema

(´Azza wa Jall):

م و و تور و س ا و س بم رقو روم كو و ر م و و قل وا ا ر م و و س ا و قو ر قو س ا وصر وا وكس ر قو رقو صو رتم ا ربم قو ر مكس ر م قو ر ل وو ور وطو وعر وا سكس ر و و تس ر و وشر س س وو

“Enyi walioamini! Msizinyanyue sauti zenu juu ya sauti ya Mtume na wala msiseme naye kwa sauti ya juu kama mnavyosemezana wenyewe kwa wenyewe kwa sauti za juu, yasije yakaporomoka matendo yenu nanyi hamhisi.”35

Akawafunza adabu namna wanavyotakiwa kuwa pindi wanapomzungumzisha

na kuzungumza na Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Akasema:

ر تور و س ا دسعوا و ا ر س وم قو قر وكس ر كو سعوا م قو ر مكس قو ر عا

“Msifanye wito wa Mtume baina yenu kama wito wa nyinyi kwa nyinyi.”36

Msisemi: ”Ee Ahmad! Ee Muhammad! Ee Abul-Qaasim!” Badala yake

semeni: “Ee Mtume wa Allaah! Ee Nabii wa Allaah!” Allaah (´Azza wa Jall)

amesema:

م تقس ر م س ا بم رق م و و س م م و قس و م س اس و قس و م س اس و س و م س اس سكر وةع و وصم ع

“Ili mumwamini Allaah na Mtume Wake na mumtukuze na mumheshimu na mumsabihi asubuhi na jioni.”37

Amewaamrisha kumuadhimisha yeye (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kama

ambavyo Yeye kamuadhimisha na kumtukuza mbele ya Mitume wengine wote

kwa vile anamsemesha:

و و قل وا ا ر س وس و م ر وا س موو م و ر و م ر م و

35 49:02 36 24:63 37 48:09

Kitabu kuhusu ´Aqiydah Imaam na Haafidhw Abul-Husayn Muhammad bin Abiy Ya´laa al-Hanbaliy

www.firqatunnajia.com 24

“Ee Mtume! Fikisha yale yaliyoteremshwa kwako kutoka kwa Mola wako.”38

Sambamba na hilo amewasemesha Mitume kwa majina yao: “Ee Aadam!”,

“Ee Nuuh!”, “Ee Ibraahiym!”, “Ee Muusa!” na “Ee ´Iysaa!” Amesema:

كس س ا ر س وس وخس س اس و وا قو واكس ر عو ر س وا تقو س ا و وا تو

“Kile anachokupeni Mtume basi kichukueni na anachokukatazeni basi kiacheni.”39

Amefanya maamrisho na makatazo yake kuwa na nafasi kama ya Qur-aan.

Kadhalika akamkusanyia sifa mbili miongoni mwa sifa Zake na akasema:

كس ر عو م ت عو و ر م وا عو متل ر وو م يت عو و ركس بم ر س ر م م و و س ت روم ت وقو ر وا وكس ر و س وت م ر و س م

“Hakika amekujieni Mtume anayetokana na jinsia yenu nyinyi wenyewe. Yanamuhuzunisha yanayokutaabisheni, anakuhangaikieni na kwa waliomuamini ni mpole na mwenye huruma.”40

Hakuwahi kuapa kwamba yeyote ni Mtume isipokuwa yeye. Amesema:

توقم ل وا رقس ر وم ااروكم م م ر و و م و ا ر س ر و م و عو و ـ صم واال ل ر

“Naapa kwa Qur-aan yenye hekima. Hakika wewe ni miongoni mwa Mitume. Uko juu ya njia iliyonyooka.”41

Vilevile amesema:

م ر قو ر و س وو و و ر ساو م قر س ر و م وكر و م

“Naapa kwa umri wako hakika wao walikuwa katika ulevi wao wanatangatanga kwa upofu.”42

Ameeleza kwamba Ibraahiym amesema: 38 05:67 39 59:07 40 09:128 41 36:02-04 42 15:72

Kitabu kuhusu ´Aqiydah Imaam na Haafidhw Abul-Husayn Muhammad bin Abiy Ya´laa al-Hanbaliy

www.firqatunnajia.com 25

و و سر م م قو راو قس قر وثس وو

“Usinihizi siku watakayofufuliwa.”43

Halafu akamjibu juu ya hilo. Hata hivyo ameyasema haya juu ya Mtume wetu

(Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) pasi na yeye kuanza kumuomba:

ر وا ر م و و س ا و و س قو راو و سر م ا رق س ا ربم

“Siku ambayo Allaah hatomfedhehesha Nabii na wale walioamini pamoja naye.”44

Muusa amesema:

واوو وبم ا ر وحر لم صو ر م

“Akasema: “Mola wangu nikunjulie kifua changu.”45

Allaah akamjibu juu ya hilo na akasema:

و ر س م و س ر و و و س و ـ

“Umekwishapewa ombi lako, ee Muusa.”46

Hata hivyo alisema kumwambia Mtume wetu (Swalla Allaahu ´alayhi wa

sallam):

و ور وشر وحر و و صو ر واو

“Je, kwani hatukukupanulia kifua chako kukubainishia?”47

Amemsamehe madhambi yake pamoja na kuyaficha na wakati huohuo

amesamehe madhambi ya wengine pamoja na kuyaweka wazi. Amesema:

43 26:87 44 66:08 45 20:25 46 20:36 47 94:01

Kitabu kuhusu ´Aqiydah Imaam na Haafidhw Abul-Husayn Muhammad bin Abiy Ya´laa al-Hanbaliy

www.firqatunnajia.com 26

تقو وااس و ل س قوتوابو عو و ر م و و و ـ وعو و ـ دواس و ر س قوغو و ـ سر ا ر

“Aadam akamuasi Mola wake akapotoka kisha Mola wake akamteua akapokea tawbah yake na akamwongoza.”48

Amesema kumwambia Daawuud:

تقوغر و و و ر س و و ر واكم عا و و وبو قوغو و ر و و س وـ م و و مور و س عم و و و س ر و ـ و و ر دوا س دس و روا قوتقو رااس وا ر ووس ر و و بل

“Daawuud akahisi kwamba Tulimpa mtihani, basi akamuomba Mola wake msamaha na akaanguka chini kusujudu na akatubia. Hivyo tukamsamehe hayo na hakika yeye bila shaka ana Kwetu makurubisho na marejeo mazuri.”49

Vilevile amesema:

ا سر و وبو و وقو ر قوتقو را س و ر واوو و و رقو قر وا عو و ـ كس ر م م م و و ع

“Hakika Tulimpa mtihani Sulaymaan na tukamtupia juu ya kiti chake mwili kisha akarejea.”50

Pia amesema:

و وا ا ل وم م ر و و سغواضم عا وظو ر وو ر قرقر م و عو و ر م قو وادو ـ م ا ظل س واتم وو ر م وقـ و م ر و و س ر وا و و م م كس س م و ا ظرا م م و

“Dhan-Nuun alipoondoka hali ya kuwa ameghadhibika akadhani kwamba hatutamdhikisha, akaita katika kiza kwamba: “Hapana mwabudiwa wa haki isipokuwa Wewe, kutakasika kutokamana na mapungufu ni Kwako! Hakika mimi nilikuwa miongoni mwa madhalimu.”51

Amesema kumwambia Mtume wetu (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):

48 20:121-122 49 38:24-25 50 38:34 51 21:87

Kitabu kuhusu ´Aqiydah Imaam na Haafidhw Abul-Husayn Muhammad bin Abiy Ya´laa al-Hanbaliy

www.firqatunnajia.com 27

م قوغر م و و و ا رق س وا قوقو راو م و م و و وا وو ر و

“Ili Allaah akusamehe yale yaliyotangulia katika madhambi yako na yale yanayofuatia.”52

Hakuyataja madhambi hayo. Kadhalika amesema:

و ور وشر وحر و و صو ر واو و وضو ر وا عو و مزر واو ا ر م و قو و و ر واو

“Je, kwani hatukukupanulia kifua chako kukubainishia na Tukakuondolea mzigo [madhambi] wako ambao ulithakilisha mgongo wako?”53

Hata hivyo hakutaja mzigo huo.

52 48:02 53 94:01-03

Kitabu kuhusu ´Aqiydah Imaam na Haafidhw Abul-Husayn Muhammad bin Abiy Ya´laa al-Hanbaliy

www.firqatunnajia.com 28

[22] Kiumbe bora baada ya Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa

sallam) na ambaye ana manzilah ya juu kabisa baada ya Manabii na Mitume na

ambaye ana haki zaidi ya ukhaliyfah baada ya Mtume wa Allaah (Swalla

Allaahu ´alayhi wa sallam) ni Abu Bakr as-Swiddiyq (Radhiya Allaahu ´anh).

Baada ya hapo anafuatia ´Umar bin al-Khattwaab (Radhiya Allaahu ´anh).

Halafu anafuatia Dhun-Nuurayn ´Uthmaan bin ´Affaan (Radhiya Allaahu

´anh). Kisha anafuatia Abul-Hasan ´Aliy bin Abiy Twaalib (Radhiya Allaahu

´anh).

Tunawashuhudilia wale kumi Pepo ambao ni Abu Bakr, ´Umar, ´Uthmaan,

´Aliy, Twalhah, az-Zubayr, Sa´d, Sa´iyd, ´Abdur-Rahmaan bin ´Awf na Abu

´Ubaydah bin al-Jarraah. Mtu anatakiwa kumuomba Allaah awarehemu

Maswahabah wote wa Mtume wa Allaah, kuanzia wa mwanzo wao mpaka wa

mwisho wao, na pia kuyataja mazuri yao.

Mu´aawiyah ndiye mjomba wa Waumini na alikuwa ni mwandishi wa Wahy

wa Mola wa walimwengu.

Kitabu kuhusu ´Aqiydah Imaam na Haafidhw Abul-Husayn Muhammad bin Abiy Ya´laa al-Hanbaliy

www.firqatunnajia.com 29

[23] Ni wajibu kuwakata Ahl-ul-Bid´ah na wapotevu. Kama mfano wa

Mushabbihah, Mujassimah, Ash´ariyyah, Mu´tazilah, Raafidhwah, Murji-ah,

Qadariyyah, Jahmiyyah, Khawaarij, Saalimiyyah, Karraamiyyah na mapote

mengine yaliyobaki yenye kusemwa vibaya.

[24] Hii ndio ´Aqiydah yangu na yale ninayomwabudu kwayo Mola wangu na

ndio ambayo baba yangu amekufa juu yake – Allaah amrehemu.