64
1 1. YUSUFU BABA WA KAMBO WA MWANA WA MUNGU (1:18-25) Kiongozi anaweza kuelezea kwa kifupi.Luka 1:26-38 Kwa mujibu wa sheria ya Musa, waliokiuka sheria za ndoa waliadhibiwa kwa kupigwa mawe.Uhusiano wa kingono haukuruhusiwa kabla ya ndoa.Kumb 22. HISTORIA: Swali katika mabano liulizwe tu kama hakuna mtu aliyekwisha kulijibu hapo kabla. 1.Nini kilichomfanya Yusufu ahisi kwamba Maria alimdanganya (18-19)? Unadhani ni nini ambacho kilikuwa kigumu zaidi kwa Yusufu? Je unahisi Maria alimwambia Yusufu kuhusu ujio wa malaika? Kama siyo, kwanini? kama ndiyo kwanini Yosefu alimwamini Maria? 2.Kwanini Yusufu hakupenda kulipiza kisasi kwa Maria pamoja na familia yake ingawa alikuwa na haki ya kufanya hivyo kisheria? Unafikiri kwa jinsi gani Yusufu alimuamini Maria kutokana na maelezo katika mistari (18-19) 3. Unadhani ni kwanini Mungu hakumtuma malaika kwa Yusufu siku ileile aliyomtuma kwa Maria(20) Kwanini upendo wa Yusufu ulipimwa kwa njia ngumu kiasi hicho? 4.Kuzaliwa na bikira ina maana manii yaliingia kwenye kizazi cha Maria kutoka nje ya ulimwengu huu.Ni katika misingi ipi inamfanya Yusufu kuamini uzazi bikira ingawaje hapo kabla katika historia haijawahi kutokea kitu kama hicho. Ni makala gani katika maandishi yetu inatuthibitishia kwamba kuzaliwa na bikira siyo habari ya kutunga? 5.Kwa nini unafikiria kuzaliwa na bikira ni kwa wengi(wanatheolojia pia) mafundisho magumu kuamini? Ni kwa jinsi gani imani katika kuzaliwa na bikira na dhana ya Mungu zinahusishwa pamoja? 6.Kwa nini haikuwa rahisi kwa Yesu kuokoa watu wake kutenda dhambi ilihali alikuwa mtoto wa Yusufu na Maria?

1. YUSUFU BABA WA KAMBO WA MWANA WA MUNGU (1:18-25

  • Upload
    lamphuc

  • View
    488

  • Download
    28

Embed Size (px)

Citation preview

1

1. YUSUFU BABA WA KAMBO WA MWANA WA MUNGU (1:18-25)

Kiongozi anaweza kuelezea kwa kifupi.Luka 1:26-38 Kwa mujibu wa sheria ya Musa, waliokiuka sheria za ndoa waliadhibiwa kwa kupigwa mawe.Uhusiano wa kingono haukuruhusiwa kabla ya ndoa.Kumb 22.

HISTORIA: Swali katika mabano liulizwe tu kama hakuna mtu aliyekwisha kulijibu hapo kabla.

1.Nini kilichomfanya Yusufu ahisi kwamba Maria alimdanganya (18-19)?

• Unadhani ni nini ambacho kilikuwa kigumu zaidi kwa Yusufu? • Je unahisi Maria alimwambia Yusufu kuhusu ujio wa malaika? Kama siyo,

kwanini? kama ndiyo kwanini Yosefu alimwamini Maria?

2.Kwanini Yusufu hakupenda kulipiza kisasi kwa Maria pamoja na familia yake ingawa alikuwa na haki ya kufanya hivyo kisheria?

• Unafikiri kwa jinsi gani Yusufu alimuamini Maria kutokana na maelezo katika mistari (18-19)

3. Unadhani ni kwanini Mungu hakumtuma malaika kwa Yusufu siku ileile aliyomtuma kwa Maria(20) Kwanini upendo wa Yusufu ulipimwa kwa njia ngumu kiasi hicho?

4.Kuzaliwa na bikira ina maana manii yaliingia kwenye kizazi cha Maria kutoka nje ya ulimwengu huu.Ni katika misingi ipi inamfanya Yusufu kuamini uzazi bikira ingawaje hapo kabla katika historia haijawahi kutokea kitu kama hicho.

• Ni makala gani katika maandishi yetu inatuthibitishia kwamba kuzaliwa na bikira siyo habari ya kutunga?

5.Kwa nini unafikiria kuzaliwa na bikira ni kwa wengi(wanatheolojia pia) mafundisho magumu kuamini?

• Ni kwa jinsi gani imani katika kuzaliwa na bikira na dhana ya Mungu zinahusishwa pamoja?

6.Kwa nini haikuwa rahisi kwa Yesu kuokoa watu wake kutenda dhambi ilihali alikuwa mtoto wa Yusufu na Maria?

2

• Kumbuka dhambi uliyoitenda ambayo dhamira yako inakusuta.Kisha soma mstari wa 21 tena.Weka jina lako mwenyewe sehemu yenye maneno ”watu wake” Je unapousoma huu mstari unaamini ni ya kwamba ni kweli?

7.Je Yusufu alivumiliaje kutokumgusa mkewe mpendwa Maria ilihali waliishi katika nyumba moja (25)?

8.Bila shaka kila mtu alidhani mtoto wa Maria alikuwa ni wa Yusufu.Je unafikiri Yusufu hakuieleza ukweli ili aonekane msafi kwa familia ya Maria?

• Kwanini Mungu hakumchagua mtu mwingine awe baba wa kambo wa mwanaye?

HABARI NJEMA: Hakika Yusufu alikufa kabla Yesu hajaanza huduma kwa uma, lakini alijua jambo muhimu kuhusu mwanawe huyo wa kambo:Angewaokoa watu wake akimjumuisha mwanaye wa kambo.

3

2. WATU WENYE BUSARA KUTOKA MASHARIKI 2:1-12

HISTORIA: Wayahudi wengi waliishi Uajemi(Zamani ilijulikana Babeli) hata baada ya uhamisho ulipomalizika mapema miaka 500.Watu wenye hekima walikuwa ni wachawi na wana anga na walikuwa na dini tofauti ya ile ya Wayahudi.Umbali kutoka Uajemi hadi Palestina ilikadiriwa kuwa kilometa 1000 hadi 1500.

1.Safari ya watu wenye busara ilichukua muda gani,iwapo ngamia alitembea kilometa 30 kwa siku?

• Je unadhani wakuu,wanawake na majirani waliichukuliaje safari hii?

2.Je unafikiria ni kwanini watu wenye busara walitaka kumwabudu Mfalme wa Wayahudi badala ya kumwabudu Mfalme wao ?

• Kwanini watu wenye busara walitaka kutoa zawadi za thamani kwa Mfalme mpya wa Wayahudi?

3.Wayahudi hawakuwa na Mfalme kwa muda wa miaka 600.Herode alikuwa tu ni kibaraka wa Warumi.Kwanini Herode na watu wote wa Yerusalemu walisikitika waliposikia habari ya kuzaliwa mfalme mpya(3)?

• Herode aliamini nini(4,16).(Aliamini nini kuhusiana na cheo chake -Biblia-masihi-mpango wa Mungu.

4.Ni kutokea hatua ipi hadi ipi nyota iliwaongoza watu wenye busara angalia mstari wa 2 na wa 9

• Kwanini Mungu hakuiruhusu nyota iwaongoze watu wenye busara moja kwa moja hadi Bethlehemu-kwanini wapitie Yerusalemu ? (Kwanini ilikuwa ni muhimu kwa watu wenye busara kuhusishwa na neno la Mungu?)

• Ni aina gani ya nyota Mungu ameituma kwenye maisha yako kukuongoza kumjua Yesu?

5.Wababeli walijenga mnara wa Babeli wakaiba safu ya agano na pia walibomoa hekalu.Watu wenye busara walikuwa wanao. Kwa nini Mugu aliwaongoza maadui kuwa wa kwanza kumwabudu mwanawe kama mfalme?

4

6.Wakati wakisikia uvumi wa kuzaliwa mfalme mpya Bethlehemu,umbali wa kilometa kumi na mbili,kwanini hakuna Myerusalemu yeyote kumwabudu kule?

7.Ni kwa njia gani mfalme mpya pengine alikuwa tofauti na waliyofikiria kabla?

• Ni nini kipo katika imani ya watu wenye busara kama mfano?

8.Watu wenye hekima walitoa zawadi kwa mtoto Yesu.Je wao walifaidika nini kutoka kwake?

• Kwanini zawadi hizo zilihitajika kwa familia ya Yusufu(13)? • Utampa nini Yesu kama zawadi ya kuzaliwa kwa mwaka huu?

9.Unafikiriaje maisha ya hawa watu wenye busara baada ya kurejea Uajemi katikati ya wapagani na dini za kipagani?

HABARI NJEMA: Mara nyingi katika maisha yake Yesu hakupewa heshima ya Kifalme.Watu wenye busara walimwabudu katika maisha yake na Pilato Gavana wa Kirumi aliandika cheo chake juu ya msalaba.Yesu alikuwa ni mfalme pekee aliyewaalika hata maadui zake waje kuabudu.

5

3. YESU ABATIZWA 3:13-17

HISTORIA: Wanaume wawili ambao umri wao ulikadiriwa miaka thelathini walikutana kando ya mto Yordani.Walikuwa ni binamu.Mmoja wao alikuwa amevaa mavazi ya ajabu.Kwa muda huo Yesu alikuwa anaishi Galilaya,John katika jangwa la Yuda.Haijaelezwa kama watu hao walishakutana hapo kabla.(Kiongozi anaweza kufafanua kwa ufupi kama ilivyoandikwa 3:13-17)

1. Kulikuwa na tofauti gani ukilinganisha maisha ya watu hawa wawili utotoni na ukubwani?

• Unafikiria ni lini Yohana alielewa kwamba Yesu ni mwana wa Mungu? • Kwa nini umaarufu haukumharibu Yohana?

2.Kulikuwa na tofauti gani kati ya Yesu na watu wengine waliotaka kubatizwa?

• Kwanini Yohana hakutaka kumbatiza Yesu? • Kwanini Yesu alitaka kubatizwa ijapokuwa ubatizo ulikuwa kwa wenye

dhambi?

3.Neno la Mungu katika mstari wa 15 unamaanisha nini?

• Msomaji anatkiwa kusoma Yohana 19.30.Yesu alitimizaje haki kwa wamwaminio?

4.Kifungu hiki kinatuambia nini kuhusu uhusiano kati ya Yesu na Mungu?

• Kifungu hiki kinatueleza nini kuhusu utatu? • Roho mtakatifu alikuwa katika Yesu wakati wote.Kwanini hakuonekana

baada ya Yesu akibatizwa?

5.Kwanini Mungu alitaka kuelezea watu wote mambo aliyoyasema katika mstari wa 17?

• Fikiria kilichokutokea mwezi uliopita.Je unafikiri Mungu angeweza kusema kitu gani kwako kama alivyosema kuhusu Yesu kwenye mstari wa 17?

6.Yohana alibatiza watu tu pale walipokiri kutenda dhambi,ndiyo maana ubatizo wake uliitwa ubatizo wa toba.Kuna tofauti gani kati ya ubatizo wa Kikristo na ubatizo wa Yuda? (Angalia pia Matendo 2:38)

6

7.Wakati wa ubatizo wa Kikristo Mungu aliwaambia waliobatizwa maneno yaleyale aliyomwambia mwanaye(17) Kwa misingi ipi anaweza kuyasema haya kwa wakosao?

8.Kiongozi anatakiwa kuelezea jinsi Ibrahimu alivyomtoa mwanawe kwa Mungu(Mwanzo 22).Maneno katika mstari wa 17 bila kufafanua yanakumbusha maneno ambayo Mungu alimwambia

Ibrahimu(Mwanzo 22:2) Kuna siri gani kati ya Mungu na Ibrahimu inayopelekea Ibrahimu kutoa sadaka wanawe?

7

4. YESU KUJARIBIWA KATIKA DHAMBI 4:1-11

HISTORIA: Shetani alimjaribu Hawa katika pepo hali iliyopelekea kuanguka dhambini.Kwa namna hiyo hiyo alimjaribu Mungu kipindi cha miaka 40 nyikani na kufanya kuanguka dhambini mara kwa mara.Shetani amejaribu kila mmoja wetu hali iliyopelekea kuanguka dhambini.yesu pia alijaribiwa kwa sababu alikuja kama binadamu na mwakilishi wa binadamu.

1.Fikiria unatakiwa kuwa jangwani kwa kipindi cha mwezi mmoja na nusu bila kuonana na mtu ,kula wala kunywa kitu chochote .Unafikiria ni hali gani itakuwa mbaya zaidi kwako?

• Je unafikiria Yesu alikuwaje kimwili na kiroho baada ya kufunga kwa siku 40?

• Ukijaribu majaribu yako na ya Yesu.Kuna tofauti gani?

2.Mara nyingi tunafikiri ya kwamba Roho Mtakatifu ni kiongozi wa waaminio katika ukamilifu wa maisha.Kwanini basi alimuongoza Yesu ajaribiwe na ibilisi kule jangwani? (1)

• Kwanni pia Roho Mtakatifu anatuongoza kwenye majaribu ambayo yanapelekea kujaribiwa na shetani?

3.Jaribu la kwanza linahusu matumizi yetu ya msingi:njaa,kiu,mahitaji ya ngono ,usalama n.k (3-4).Kwanini ingekuwa dhambi kwa Yesu kubadili mawe kuwa mikate?

4.Je unafikiria mwanadamu ataweza kuishi kwa neno la Mungu pekee bila mahitaji ya msingi kutimizwa? (4) Tafadhali jibu kwa uaminifu na kisha utoe sababu.

5.Jaribu la pili linahusu uhusiano wetu na Mungu(5-7) Mungu angeudhihirishia nini ulimwengu kama angejirusha?

• Ni kwa njia gani jaribu la pili linakuja maishani mwetu?

6.Jaribu la tatu inahusu kitu katika imani yetu.Je shetani alisema ukweli katika mstari wa 9? Toa sababu.

8

• Dunia ingepata nini kwa muda kama angefanya jinsi shetani alivyomwamuru?

• Ni faida gani ya muda mfupi twaweza kupata iwapo tutapiga magoti na kusujudu mabwana wengine zaidi ya Mungu aliye hai?

7.Ni nini ilikuwa silaha ya Yesu alipokuwa anapambana na Shetani?

• Ni nini silaha yako unapokuwa unapambana na majaribu pamoja na dhambi? •

8.Yesu alishinda vita dhidi ya shetani.Kwanini aliadhibiwa adhabu ya kifo ambayo ingewapasa tu wale walioshindwa vita?

• Angekuwa Mungu wa aina gani kama Yesu asingejaribiwa? • Ungekuwa ni aina gani ya mkristo kama usingejaribiwa?

HABARI NJEMA: Kiongozi asome Waebrania 2:18

9

5. MAHUBIRI KUTOKA MLIMA SINAI

HISTORIA: Kama Musa alivyowapa watu wake sheria ya Mungu kutoka mlima Sinai,ndivyo alivyofanya Yesu “Musa mpya ”.Katika amri ya zamani Yesu aliongeza ufahamu mpya.

1. Hasira inahusishwaje na mauaji? (21-22)

• Umewahi kuitwa “mwema kwa ajili ya kitu ” au “mjinga” Ulijisikiaje? • Je inamwathirije mtoto akiendelea kuitwa “asiyefaa” au“ mjinga”?

2. Je utajipa adhabu gani kwa dhambi iliyoongelewa katika mstari (21-22)

• Ungetoa adhabu gani kwa watu ambao wangetenda dhambi kwa ndugu zako?

3.Kwa nini ni lazima kupatana na watu wengine kabla ya kutekeleza wajibu wetu wa kidini? (23-24)

• Kwanini yesu hakupendelea makosa ya walalamikaji lakini aliwaamuru wamfuatao wachukue hatua za kuwezesha kupatikana kwa ndugu yao?(23 – 25)

• Nini kitatokea endapo kwenye familia/shule/eneo la kazi kama utafuata na kutekeleza maagizo ya Yesu katika mistari hii?

4. Mungu angesema “Kaka yako akikukosea sahau na usiweke moyoni kabisa! ”Je ni rahisi kwako kufuata maagizo zaidi ya yaliyotolewa?

• Nini kitatokea kwa mtu ambaye hasamehi wamkoseao? • Ni nani aliyemtenda dhambi Yesu unataka kusamehe leo? Unaweza kujibu

kwenye moyo wako

5. Kwa nini Yesu anafikiria dhambi iliyotendwa na mtu kifikra kwamba ni yakweli? (27-28)?

• Fikiria hali ambayo macho yako na mikono yako inakushawishi kutenda dhambi, ni kwa njia gani utaweza kuidhibiti hali hiyo? (29-30)?

6.Je ni nini hasa Yesu alifundisha kuhusu talaka(31-32)? Zingatia maandiko!

10

• Fikiria hali inavyokuwa pale mwanandoa anapopenda mtu mwingine.Yapaswa kufanya juhudi gani kama wakosaji wakiamua kufuata maagizo ya Yesu?

7. Kuna tofauti gani kati ya mafundisho ya Yesu kuhusu ndoa na jinsi watu wanavyofikiria katika ulimwengu wa kileo?

8. Ungeelezeaje kifungu hiki kwa mtu aliyekiri kuwa tayari kuishi kama amri zinavyoelekeza? Vipi kuhusu mtu aliyekata tamaa kwa kukosa uwezo wa kuishi kwa mujibu wao?

HABARI NJEMA: Yesu aiadhibiwa kwa adhabu zote zilizoorodheshwa kwenye kifungu hiki kutokana na hukumu ya moto wa Jehanamu.Alitakiwa kulipa hata senti yake ya mwisho ili kulipa madeni yetu-deni tunalodaiwa na Mungu ni kutokufuata amri zake.(Linganisha na mstari wa 26)

11

6.USIOGOPE 6 (25-34)

HISTORIA: Neno haki (33) maana yake ni usafi kamili wa maneno na matendo.Watu wema tu ndiyo watakaokwenda mbinguni.

1.Kwa kutumia maneno yako mwenyewe elezea mambo ambayo Yesu alitukataza katika kifungu hiki.

• Ni vitu gani kati ya vilivyoorodheshwa vinakupa hofu zaidi? • Maisha yako ya hofu yamebadilikaje baada ya kusoma kifungu hiki?

2.Je ni nini kitatokea katika familia yako iwapo mwanafamilia mmoja atakuwa na hofu ya pesa,afya na maisha ya baadaye?

• Je hofu inaifanyia nini miili yetu?

3.Je hofu na ukosefu wa imani vinashabihiana?

• Je tutapunguzaje kiwango cha hofu na ukosefu wa imani katika maisha yetu?

4.Tafuta ahadi zote Yeu alizowapa wanafunzi wake katika kifungu hiki.

• Ni ahadi gani ambayo ni rahisi kwako kuamini? Ni ipi ambayo ni ngumu kuamini?

5.Soma kifungu cha 31-35.Ni kitu gani unahitaji zaidi kwa leo(Unaweza kujibu moyoni)

• Je waamini ya kwamba Baba wa mbingunianajua mahitaji yako ya leo? Toa sababu.

6.Inamaanisha nini kwa vitendo kutafuta kwanza ufalme wa Mungu? (33)

• Kwa nini watu wanatafuta kwanza furaha zao badala ya kuanza na ufalme wa Mungu?

• Unatafuta nini kwanza? (Unaweza ukajibu moyoni)

7.Inamaanisha nini kivitendo kuutafuta wema wa Mungu ,na siyo wema wa mtu (33b)?

12

• Kama una uzoefu ambao umepelekea kutafuta haki yao mwenyewe kwa kutafuta haki ya Mungu,tafadhali badilishana uzoefu na wengine.

8. Mstari wa 34 una maana gani?

• Fikiria kipindi ambacho ulikuwa na wasiwasi kuhusu jambo fulani kwa siku zako zijazo.Ni nii unapaswa kufanya badala ya kuwa na hofu?

• Unaijua hali yako kwa sasa Yesu bado anaongea juu yako mistari 33-34.je utamjibu nini?

HABARI NJEMA: Daima Yesu aliuweka ufalme wa Mungu kuwa muhimu kuliko vitu vingine vyote.Na bado hakupewa moja ya mambo mema yaliyoahidiwa katika kifungu hiki lakini ni msalaba.Yesu alibeba adhabu ya msalaba na woga wa kutokumwamini Mungu.Ndiyo maana anaweza kupokea hata wenye imani haba.

13

7. MANABII WA UWONGO 7:15-25

HISTORIA: Manabii walikuwa ni watu ambao walitangaza neno la Mungu kwa watu wake.Tunaweza kutumia vigezo katika kifungu hiki kwa mtu yeyote ambaye anasimama mbele ya wengine kwa madai ya kutangaza neno la Mungu,bila kujali kama yeye ni mchungaji au msharika wa kawaida.

1.Jaribu kutafuta sababu nyingi kadiri iwezekanavyo kutokana na kifungu hiki kwanini ni vigumu kumwambia mtu kwamba wewe ni nabii wa uwongo.

• Kwa mujibu wa kifungu hiki,manabii wa uwongo hufanya kazi zao ndani au nje ya kanisa.

2. Unafikiriaje nabii wa uwongo,ambaye ni mbwa mwitu aliyevaa mavazi ya kondoo,kweli anafanya kazi ya kanisa?

• Je walimu wa uwongo wanajua wazi ya kwamba wao ni mbwa mwitu walio katika mavazi ya kondoo? Toa sababu.

• Ni matunda gani unaweza kuyaelezea endapo unabii ni ukweli au uwongo (16-20)? Toa baadhi ya mifano halisi.

3. Katika siku hizi umesikia wapi mambo haya yakitokea kama yalivyoelezewa katika mstari wa 22 (unabii,kutoa mapepo na miujiza)?

• Yesu anawakosolea nini hao watu, ambao hata wametenda miujiza mikubwa kwa jina lake?

• Ni kwa kigezo gani kinatumika kutathmini watu ambao wanafanya miujiza katika makanisa ya kikristo?

4. Je manabii wa uwongo wanachukuliwa kama lengo la dini?

• Fikiria mtu ambaye anatembelea mikutano hiyo ambapo miujiza hutokea.Nini kinakuwa kimepungua kwenye imani yake?

5. Ni nini tabia ya manabii wa uwongo dhidi ya dhambi (21,23)

• Kwa nini manabii wa uwongo walitambua wenyewe ya kwamba wao ni watenda maovu?

14

6. Fikiria jinsi manabii wa uwongo wanavyotumia jina la Yesu.Kwa makusudi gani hawatumii?

• Kiongozi anaweza kusoma Warumi 10:13.Kuna tofauti gani kati ya manabii wa uwongo na watu wa Paulo ilivyoainishwa katika mstari hapo juu,kuhusu jinsi jina a yesu lilivyotumika?

7. Ni kwa jinsi gani Yesu alijijua mwenyewe (23)?

• Kwanini Yesu hakugundua ya kwamba hawa watu walitumia jina lake katika kutenda miujiza mikubwa?

• Tunawezaje kujua leo kama Yesu atatukubali ama kutukataa siku ya mwisho?

8. Ni ujumbe gani ambao manabii wa ukweli wanao kwa wale wenye dhambi,wapotevu ambao wamepoteza furaha yao duniani na ambaowanakabiliwa na kifo?

• Ni kazi ya nani kwa ulimwengu wa leo kuwaonya Wakristo kuhusu manabii wa uwongo?

HABARI NJEMA: Shetani hawezi kuwa kama mwanakondoo wa Mungu,Yesu,kwa sababu yeye hana majeraha yeyote katika mwili wake.Tatizo la manabii wa uwongo hawakubali dhambi zao na kwa sababu hiyo hawahitaji msalaba.Ndiyo maana hawaoni umuhimu wa kumtambua Yesu kama mwokozi wao.

15

8.AFISA WA KIGENI

HISTORIA: Huyo alikuwa afisa wa Kirumi anayewakilisha majeshi ya utawala.Hakika watu waliuwawa kwa silaha.Dini ya askari wa Kirumi walifanya ibada ya Kaizari.kiongozi anatakiwa aelezee kwa ufupi mambo makuu kuhusu Abrahamu,Isaka na Yakobo.

1. Huyo afisa katika maandiko haya pengine alisikia mafundisho ya Mungu kutoka kwa mtumishi wake wa kiyahudi.Fikiria sababu nyingine ambazo kwanini afisa wa Kirumi amekuwa karibu na yeye(5-6)

2.Wayahudi hawakutembelea makazi ya wageni.kwa sababu iliwafanya najisi.Kulikuwa kuna sababu gani nyingine iliyokuwa katika akili ya Mroma kutokustahili kumpokea Yesu katika boma lale? (7-8)

3. Elezea imani ya huyo afisa wakati alipomsoggelea Yesu.

• Unaamini ya kwamba shida zako zitaweza kutatuliwa kwa neno moja kutoka kwa Yesu (8) ?

4. Ni kitu gani afisa alifikiria anacho kama Yesu?

• Afisa alilionaje jeshi la Yesu lisiloonekana iliahali hakuna mtu yeyote angeweza kuliona?

• Unaamini ya kwamba Yesu anaweza kuamuru malaika mmoja amsaidie mtu aliyemwomba kusaidiwa? Toa sababu.

5. Injili inataja matukio mawili tu ya Yesu yanayowafurahisha imani ya watu. Kulikuwa na nini maalum kuhusu imani ya mroma(8-10) (Kuna tofauti gani kuamini miujiza na kuamini neno la Yesu?)

6. Katika mstari wa 11 na 12 Yesu amesema inawezekana kuwa rahisi kwa mgeni,ambaye amekiri kutoka dini nyingine,amwamini zaidi ya hao ambayo wanaifahamu Biblia.Kwanini iwe hivyo?

• Kitatumika kigezo kipi ili kuweza kutambua watakaoingia kwenye ufalme wa Mungu (mbinguni) na ambao watatupwa kwenye giza(kuzimu)?

16

7. Mungu alikuwa amewapa ahadi zake kuhusu Masia na ardhi kwa Abrahamu,Isaka na Yakobo.Ni kwa jinsi gani imani ya hawa watu watatu inafanana na imani ya askari Mroma?

8. Afisa hakuwa amejua kilichomtokea mtumishi wake.Unafikiria alitegemea kukuta nini nyumbani? (13)?

• Yesu amesema maneno katika mstari wa 13 kwa ubinafi wa kileo..Utamjibu kitu gani?

HABARI NJEMA: Yesu alitupwa nje ya ufalme wa Mungu,kwenye giza,kulipokuwa na kilio na kusaga meno (12).Kwa njia hii aliandaa kibali cha kwenda mbinguni kwa askari wa Kirumi na kwetu ambao hata hatukustahili kuingia katika ufalme wa mbinguni.

17

9. WITO KWA MATHAYO 9:9-13

HISTORIA: Kwa Wayahudi wa wakati wa Yesu,kula pamoja ilikuwa ni ishara ya upendo.Watoza ushuru walikuwa wakionekana watu wenye imani haba kwa sababu hawakuwa waaminifu na masuala ya fedha.Mathayo alichukuliwa kama mtu ambaye aliandiak injili iliyozaa jina lake.

1.Fikiria maisha ya kila siku ya Mathayo,mtoza ushuru.Yapi aliyoyafanya yaliyokuwa mema na yapi yalikuwa mabaya?

• Unafikiria uhusiano wa Mathayo na Mungu ulikuwaje ingali alikuwa mtoza ushuru?

• Mathayo alitegemea Yesu aseme nini wakati alipoingia katika kibanda cha kukusanyia kodi?

2. Kwa nini Yesu hakumuuliza Mathayo : “Unataka kuwa mwanafunzi wangu”?

• Unadhani Mathayo alijisikiaje wakati mwalimu wake na mfanyakazi wa miujiza walivyomtaka kuwa mfuasi wake?

• Kwa nini Yesu alimtaka mtoza ushuru awe mwanafunzi wake ilihali alijua watu wangeweza kumkosoa?

• Kwa nini Yesu anataka wewe uwe mwanafunzi wake?

3.Wenzake Mathayo walifikiria nini baada ya yeye kuondoka pasipo kupanga dawati lake?

• Ni kwa jinsi gani Mathayo aliweza kuacha kazi yake ambayo ilikuwa inamuingizia kipato?

• Mathayo alipata faida gani baada ya kuacha kazi iliyokuwa inamuingizia kipato?

• Mungu anakwambia,labda ni mara yako ya kwanza,labda ni mara ya mia moja “Nifuate mimi!” Ungemjibu nini?

4. Pamoja na Mathayo,baba wa nyumba ya waamwaminio Yesu,Unafikiria maisha ya mke na watoto yalibadilika?

• Kwanini Mathayoalitaka kufanya sherehe kwa Yesu na wenzake(10)? •

18

5. Kuna makundi gani katika jamii yetu,watu wenye heshima ambao hawataki ushirikiano?

• Kwanii Mungu alitaka kushirikiana na watu wa aina zote?

6. Yesu anamaanisha nini katika mstari wa 12-13?

• Ni katika kundi gani ambalo unajiona uko kati ya hayo mawili:mwenye afya au ugonjwa,msafi au mwenye dhambi?(unaweza kujibu kimoymoyo.)

• Mwanga ulioupata katika maandiko haya,unafikiria umepata ugonjwa na dhambi maishani?

• Kwa nini mara nyingine ni rahisi kutoa sadaka kwa Mungu zaidi ya kuonyesha wema kwa majirani?

7.Kwa nini Yesu, “daktari”, alitakiwa awe na moyo uliopondeka? Kwanini yeye aliye mwema anatakiwa kuhesabiwa miongoni mwa wenye dhambi?(linganisha Isaya 53:10-12)

HABARI NJEMA: Yesu amekuwa sadaka kailifu kwa Mungu-ndiyo maana Yesu hakupendelea zawadi nyingine kutoka kwetu isipokuwa kutumia nguvu zetu kuokoa majirani zetu.

19

10.UVUMILIVU WA ADHA 10:16-31

1.Unadhani ni kwa kiasi gani Wakristo ni watu wa chini na hata kupata mateso katika jamii yetu?

• Wakristo wanashutumiwa zaidi kwa lipi katika jamii yetu?

2.Nini kitatokea kwa kondoo aliye katikati ya mbwa mwitu (16)?

• Yesu alimaanisha nini aliposema atawatuma wanafunzi wake kama kondoo waliozungukuwa na mbwa mwitu?

• Ni kwanini mtu anafananishwa na nyoka alivyo mjanja au mwerevu kama njiwa?

3. Ni kwa uhalifu gani wanafunzi wa Yesu walihusishwa walipoletwa kwenye majaribu (17-22)?

• Kama ungejua kwamba ungetiwa hatiani kwa sababu ya imani yako,unafikiria ungweza kuogopa la kusema? (19-20)

4. Ni katika aina gani ya jamii ambayo wanafamilia wanafanya mambo yalivyoelezwa katika mstari wa 21?

• Ni nini kinafanya mtu abaki katika imani hata watu wengine wasipokubaliana naye (22)?

• Unafikiria utaishije kama siku moja ungeteswa kwa sababu ya imani yako?

5. Tunaweza kuutumia mstari wa 23 katika ulimwengu wa kileo?

6. Nini maana ya mwanafunzi ambaye mwalimu wake alishavumilia mateso sawaa na yake (24-25)?

7. Fikiria watu wawili walioko katika mateso.Mmoja wao anajua uwongo utajulikana na ukweli utashinda mwishoni.Mwingine hana uhakika juu ya hilo.Itakuwa hali gani kati ya wawili hao (26)?

8. Tafuta sababu nyingi uwezavyo kwa nii Mkristo asiogope mateso(26-31).

• Mkristo anatakiwa afanye nini hata akiwa katika kipindi cha mateso(27)?

9. Katika mstari wa 28,Yesu alimtuma mungu kwa shetani?

20

• Jinsi gani mienendo ya Mkristo amnaye anahofia ya kwamba hakuna mwingine zaidi ya Mungu katika kipindi cha mateso?Vipi kuhusu Mkristo ambaye anamwogopa shetani?

• Kwa mujibu wa aya ya 28,ni janga gani katika maisha ya mwanadamu?

10.Yesu anaamini hata Mkristo anaweza kuuwawa na maadui zake(28).ni kwa jinsi gani tunaweza kutumia mstari wa 29-31 kwa maisha ya mashahidi kwa mfano Yohana mbatizaji?

• Kwa nini ni vigumu kuteketeza kanisa la Kikristo kwa kutumia mateso? • Katika mstari wa 30-31 Yesu anaongea na wewe.Wanamaanisha nini kwako

katika hali yako y amuda huu?

21

11. HABARI NJEMA KWA MASKINI

HISTORIA: Yohana mbatizaji, kwa sasa miaka 30 imepita alikuwa ni mwanaume aliyembatiza yesu na akashuhudia jinsi roho mtakatifu alishuka kutoka juu mbinguni.Katika jibu lake kwa Yohana,Yesu anamnukuu nabii Isaya(Isaya 35:5,6 na 61:1) Kiongozi anatakiwa kusoma aya hizi.

1. Yohana mbatizaji alifungwa kwa kumkosoa Mfalme Herode kwa uasherati wake.Ni nini kilimuumiza zaidi kwa kitendo cha kufungwa kwake?

• Yohana alipokutana na Yesu kwa mara ya kwanza,alisema ”Tazama mwanakondoo wa Mungu,aliyechukua dhambi za dunia”(Yohana 1:29). Ni nini kilichomfanya awe na mashaka imani yake ya awali?

2.Yohana atatoa hitimisho gani kuhusu maisha yake mwenyewe kama itakuwa wazi kuwa Yesu kwa wakati huo hakuwa kristo?

• Kama ulishawahi kuwa na wasiwasi kwamba Yesu ni Mungu au laa.Ni hali gani itakutokea?

3.Alipotuma wanafunzi wake kwa Yesu,Unafikiria Yohana alitegemea ujio wake wa kumtoa gerezanikiniujiza? (2-3) Toa sababu.

• Kwanini Yesu hakumtembelea Yohana alipokuwa gerezani?

4.Kwa nini Yesu hakujibu swali la Yohana:Ndiyo ni mimi.Hutakiwi kusubiri kwa mtu mwingine yeyote? (Kwanini yesu alitaka kujibu kwa kunakili katika maandiko kutoka katika agano la kale?)

• Utajisikiaje kama utapata mstari wa Biblia kutoka kwa rafiki yako wakati wa huzuni?

• Wakati wa kumnukuu isaya,kwanini yesu aliiruka ahadi kuhusu Masia kuwakomboa wafungwa?

5.Ni maneno gani ya Yesu ambayo Yohana angeweza kuyatumia?

• Habari njema maana yake ni msamaha wa dhambi(5). Kwa dhambi gani Yohana aliifanya iliyohitaji msamaha wa Mungu katika hali ile?

22

• Kwanini mara nyingi Mungu hufanya waumini wake kama maskini kama Yohana mbatizaji alipokuwa gerezani?

6.Maneno ya Mungu katika mstari wa 6 yanamaanisha nini?

• Kwa mujibu wa kifungu hiki,tunatakiwa tufanye nini tunapokuwa na mashaka kwa jinsi Yesu anavyowatendea wapendwa wetu na sisi wenyewe?

7.Je unafikiria Yohana alilipokeaje jibu kutoka kwa yesu? (Je alipata amani moyoni mwake kabla hajafa?)

• Yohana alikuwa muumini wa kwei katika maisha yake yote.Unadhani imani yake ilibadilikaje wakati akiwasiliana na Yesu kwa mara ya mwisho?

8.Yohana alifikiria nini kuhusu maisha na kifo pale ambapo Herode alipokuja kumkata kichwa?

HABARI NJEMA: Yesu alisema kwamba alikuja kuhubiri habari njema kwa maskini ili kuwaponya waliovunjika moyo,kuwatangazia uhuru mateka..kuwafariji wotewanaoomboleza.(Isaya 61:1-2) yesu anakuja pia kwako leo kufanya hayo yote –kupitia neno lake.

23

12.MZIGO MWEPESI 11:28-30

HISTORIA:Nira maana yake ni kipande cha mbao,ambacho kinaunganisha ngombe wawili ili waweze kuvuta kwa pamoja jembe,mzigo,n.k

1.Je ni nini baadhi ya mizigo ya kawaida ambayo watu wanabeba mabegani mwao siku hiizi?

• Jaribu kufikiria mateso yako ya sasa hivi kama mzigo wa saruji.Ni mzigo mzito unaokadiriwa kuwa kilo 100.Bila kuupima nafikiria mzigo wako ni kiasi gani?

2.Je ni jinsi gani mzigo wa mateso ni tofauti na mzigo wa dhambi(Mateso au dhamiri mbaya?)

3.Fikiria maisha yako bila mzigo wowote.Nini kitakuwa kizuri au kibaya katika pande hizi mbili za maisha?

4.Ni mtu wa aina gani unafikiria anaweza kukusaidia kubeba mzigo wako?

• Inamaanisha nini kwa vitendo ukienda kwa Yesu na kukiri dhambi zako kwake?

5.Yesu anamaanisha nini katika mstari wa 29?

• Umepata pumziko la moyo wako?(Unaweza kujibi kimoyomoyo.) • Kwanini mtu mnyenyekevu tu ndiyo anayeweza kuutua mzigo wake?

(Kwanini watu wengi wamekuwa na machungu wakati wa ubebaji mizigo yao?)

• Tutakuwaje wanyenyekevu na wapole kama Yesu alivyokuwa?

6.Maneno haya ya Jesus yanamaanisha nini: “Chukueni nira juu yenu”? (Nira ya Yesu ni nini? Inatofautianaje na mizigo yetu wenyewe?)

• Jinsi gani hali yetu inabadilika kama tutabeba nira pamoja na Yesu?

7.Yesu anamaanisha nini kwa kusema nira yake ni nyepesi na mzigo wake ni mwepesi(30)?

24

8.Je watu hao walifanya nini pamoja na mizigo yao ambao hawakutaka kupelekwa kwa Yesu?

• Kwanini hata Wakristo wengine daima hawapeleki mizigo yao kwa Yesu?

9.Unafikiria mzigo wako utakuwa mzito kiasi gani ukijua hakuna hatia na pia hutakiwi kufikiria kuhusu kosa ni la nani?

• Unafikiria mzigo wako utakuwa mzito kiasi gani iwapo utaamini ya kwamba Yesu atabadilisha matatizo yako yote yawe sawa bila wasiwasi?

HABARI NJEMA: Kiongozi asome Yohana 19:17.Msalaba wa Yesu umebeba mizigo yetu yote;mateso na dhambi zetu.

25

13.MANENO MATUPU 12:33-37

HISTORIA: Kabla ya majadiliano,jikumbushe niaina gani ya maneno uliyoyaongelea wiki iliyopita.

1.Ni wakati gani mgumu sana kuuzuia ulimi wako kunena mabaya?

• Kama unaweza kuishi maisha yako kwa mara nyingine tena,utaongea na nani vizuri zaidi ya ulivyofanya hapo awali? (Unaweza kujibu kimoyomoyo)

2.Kwa nini maneno yetu ni muhimu kwa Mungu zaidi ya matendo yetu?

• Heshima yamaneno yetu inafananje na matunda ya mti(33)? • Inawezekanaje mti mbaya kubadilika kuwa mti mzuri? • Inawezekanaje mtu mbaya kuwa mtu mwema?

3.Yesu anatumia mifano imara wakati akitoa wito kwa wamuelewao kizazi cha nyoka .Je nyoka mwenye sumu ana nini cha ziada na mtu anayezungumza maneno mabaya (34)?

• Yesu alimaanisha nini kwa maneno haya “ Yaujazayo moyo kinywa husema(34)?

• Tumia majaribu katika mstari wa 34 kwako mwenyewe.Moyo wako umejawa na nini? (Unaweza kujibu kimoyomoyo)

4.Katika mstari wa 35 Yesu ameonesha ya kwamba kila mtu ana ghala kwenye moyoni mwake.Ni kwa

mambo gani mambo hujaza maghala ya mioyo yao?

• Fikiria unazungumza nini kuhusu Yesu. Maneno yako yanaonesha nini uhusiano uliopo kati yako na Mungu?

5. “Maneno ya kutojali” yana maana gani (36)?

• Kinyume cha “maneno ya kutojali” ni nini? • Kwanini tunatakiwa kutoa hesabu siku ya hukumu kwa kila maneno ya

kutojali dhidi ya kila maneno mabaya? • Kutokana na kifungu hiki,unafikiria kitakutokea ninisiku ya hukumu?

26

6.Je unafikiria unaweza kuficha yaliyo moyoni mwako kwa wengine? Inawezekana kwa mfano kuongea maneno matamu wakati moyo wako una chuki na machungu?

• Je,unafikiriaje kuhusu mtu anajaribu kuongea maneno machache sana ili asitamke maneno yoyote ya kutojali?

7.Unadhani ya kwamba utakuwa unafuata mafundisho haya ya Yesu kuanzia sasa?

8.Yesu alisema yeye ni mzabibu na wanafunzi wake ni matawi(Yohana 15:11) Je tutawezaje kuzaa matunda mema wakati tumehifadhi mabaya mioyoni mwetu?

HABARI NJEMA: Moyo wa Yesu umehifadhi mambo mema na bado alihukumiwa kama kafiri kutokana na maneno yake.Msalaba wake ulikuwa wa mti unaozaa matunda machungu .

27

14.NGANO NA MAGUGU 13:24-30 na 36-43

HISTORIA: Magugu ni majani mabaya ambayo huota yenyewe mahali palipopandwa mazao.Magugu haya huonekana kama ngano inapokuwa changa.Kwa sababu magugu haya yana sumu hayatakiwi shambani.

1.MFANO (24-30)

• Kuna tofauti gani kati ya shamba lenye ngano pekee na lenye ngano na magugu?

• Mtu anayepanda magugu kwa jiran yake ana nia gani? • Utachukuiaje kama mtu ataiharibu kazi yako kwa namna hiyo? • Ni nini kinachoshangaza jinsi mhudumu wa shamba alivyokabiliana na

hujuma (28-30)? • Kwanini kila sehemu ya ngano ni muhimu kwa mkulima(29)? • Kuna uhusiano gani kati ya mbegu na tunda linalotokana na mbegu hiyo?

2.TAFSIRI YA MIFANO (36-43) Kumbuka ya kwamba neno shamba lina maana mbili;ulimwengu(38),ufalme wa mwana wa Adam(41) ambalo ni kanisa la Kristo.

• Mwanzoni Yesu aliita neno la Mungu mbegu.Kwanini sasa anawaita watu mbegu(38)?

• Nani anaotesha watu na ni kwa namna gani (37,39)? • Je mfano huu unatufundisha nini kuhusu shetani anavyofanya kazi? • Shetani alikuwa na malengo gani alipomweka mwanawe ndani ya kanisa

la Kikristo maeneo yote? • Muonekano wa usharika wa Mungu ukoje,kama hakuna matapeli ? • Kwanini hatuwezi daima kujua ambaye ni mwana wa Mungu na ambaye

ni shetani? • Kwa nini ni hawaruhusiwi kutupa "wana wa Ibilisi" nje ya kanisa kabla

ya hukumu ya mwisho? • Tumia ujumbe wa mfano huu katika ushirika wako mwenyewe Kikristo. • Unaweza kufikiria wewe ni mbegu ya aina gani;ngano au magugu?

(Unaweza kujibu kimoyomoyo) kimoyomoyo.)

28

• Kwa mujibu wa mfano huu, unafikiri inawezekana kwamba mtu ni nusu ngano, nusu magugu? Toa sababu.

• Mwisho wa dunia utakuwa kama nini(41-43)? • Je Mungu anategemea mavuno ya aina gani katika ulimwengu huu?

3. UADILIFU (43)

• Kwa nini mara nyingi Yesu hutumia neno "haki" katika tafsiri ya mfano wake?

• Kiongozi anapaswa kusoma Warumi 4: 5Tutakuwaje wenye haki?`

4.MUHTASARI WA MASWALI

• Tofauti ya msingi kati muumini wa kweli na mzushi ni ipi? • Unafikiri Yesu anataka kusema na wewe binafsi kupitia mfano huu?

HABARI NJEMA: Ingawa alikuwa ngano bora alikuwa milele katika dunia hii,Yesu alivutwa na kutupwa katika tanuru la moto kama gugu.Ndiyo maana sasa anaweza kubadili magugu kuwa ngano na kuyavuna katika ufalme wa Mungu.

29

15. PETRO ATEMBEA JUU YA MAJI 14: 22-34

HISTORIA: Ziwa la Galilaya lilikuwa na ukubwa wa 20x12km.Mara nyingine dhoruba hutokea katika ziwa hili.Zamu ya nne ilikuwa karibu saa tisa asubuhi(25).Wanafunzi walikuwa tayari ziwani kwa muda huo.

1. Kwa nini Yesu aliwatuma wanafunzi wake ziwani ingawa yeye shaka alijua ni nini kitakachotokea huko (22)?

• Kwa nini Yesu wakati mwingine hututuma katika "dhoruba"?

2. Fikiria jinsi wafuasi walivyoona na walichofanya wakati dhoruba ilipowazunguka saa baada ya saa (24)

• Je wanafunzi walimfikiriaje Yesu kwa kuwa hakuja nao kwenye mashua? • Unafikiria ni kwanini Yesu alikuwa akisali wakati rafiki zake walikuwa

katika hatari ya kifo (23)?

3. Wanafunzi hawakuweza kufikiria kwamba Yesu angekuwa na uwezo wa kutembea juu ya maji. Je, wao labda walifikiria angefanya nini katika hali hiyo?

• Ulitarajia Yesu angefanya nini katika hali ya kukatisha? • Kwa nini wanafunzi walifikiria Yesu ni mzimu (26)?

4. Ungejisikiaje jinsi Yesu mwenyewe alivyosimama katikati ya "dhoruba" unakabiliwa wewe na kusema: "Jipe moyo! Ni mimi Usiogope "(28)?

• Maneno "Ni mimi" ni kwa jina la Mungu (Bwana) katika Kiebrania. Kwa nini Yesu alitaka kutumia maneno haya katika hali hii?

5. Jaribu kupata sababu nyingi iwezekanavyo kwa nini Peter alitaka kutembea juu ya mawimbi makubwa na mashua kuruka juu na chini katika giza (27).

• Je, unafikiri ungethubutu kutembea juu ya mawimbi katika hali hiyo? • Kwa nini majaribio ya Petro hayakufanikiwa (30)?

6. Petro alikuwa anakosa nini katika imani yake kwa wakati huo (31)?

• Ungejibu nini kama Yesu angekwambia wewe maneno yaliyorekodiwa katika mstari wa 31?

30

• Kwa nini ni muhimu kujifunza kwa kuangalia ukweli katika imani yetu? • Tunafutwaje machozi katika kifungu hiki kwa wale wenye kujua ya kwamba

wana imani haba?

7. Kwa nini Yesu hakuja kuwasaidia rafiki zake mpaka saa tisa asubuhi? (Somo gani muhimu itakuwa wanafunzi watakuwa wamelikosa kama Yesu angalikuja kutoa msaada mapema? (Linganisha.31-33.)

• Kwa nini Yesu ame kuja kutusaidia kwa kuchelewa sana kuliko sisi tulivyotarajia aje?

HABARI NJEMA: Hakuna mtu yeyote aliyeweza kumfikia Yesu kwa mkono wakati alipokuwa katikati ya dhoruba (= hasira ya Mungu). Hiyo ilikuwa ni gharama ambayo Yesu alitakiwa aulipa kwa ajili ya ukosefu wetu wa imani. Lakini ndiyo maana yeye ana uwezo wa kufikia kuokoa hata kwa mtu ambaye ana imani haba.

31

16. HUZUNI KUBWA NA IMANIKUBWA 15: 21-28

HISTORIA: Wakanaani walikuwa maadui wakubwa wa Wayahudi. Tiro na Sidoni ni miji iliyojengwa katika umbali wa 45-60 km kutoka Galilaya. Yesu hakutaka mtu kujua kuhusu safari hii ya nje ya nchi (Mark 7:24). Kiongozi anatakiwa kuwaambia ukweli kuhusu Mfalme Daudi (22).

1. Fikiria maisha ya kila siku ya mama huyu, hasa mahusiano yake na watu wengine. (binti yake, mume, watoto wengine, majirani nk)

• Kwa nini mama labda alijishtaki mwenyewe? • Ni mama gani katika ulimwengu wa kileo mwenye huzuni kubwa moyoni

mwake kama mwanamke huyu alivyofanya?

2. Mwanamke Mkanaani tayari alijua kitu ambacho wengi wa Wayahudi hawakuwa na ufahamu wa: ya kwamba Yesu alikuwa Mwana wa Daudi (22). Jinsi gani unadhani alikuja kujua ukweli huu?

• Kwa nini mama aliomba kwa ajili yake (22)?

3. Yesu alichukua hatua gani tatu za mwanzo kumsaidia mam huyu? (23-26)?

• Kawaida Yesu huwakaribisha watu wote wanaosumbuliwa na matatizo. Kwa nini hakumsaidia mwanamke huyu?

• Ungefanya nini kama Yesu angetutendea sisi kama alivyomtendea huyu mwanamke?

4.Wanafunzi walijisikiaje kuhusu mwanamke Mkaanani katika hali nzima?

5.Jinsi gani mama Mkanaani alilalamika kwaYesu baada ya kukataliwa(23,25,27)?

6. Je, unafikiria ni nini kilichotokea katika moyo wa Yesu wakati alipokuwa kimya mama akiteseka?

• Kwa nini Yesu wakati mwingine huwa kimya wakati wakati tunapomlilia atusaidie?

• Kwa nini ni lazima imani ya kila mmoja wetu kupimwa?

7. Yesu alisifu imani ya watu wawili tu. Jaribu iwezekanavyo kutafuta sifa nyingi za imani kubwa katika mwanamke huyu (28).

32

8. Kwa ujumla ni jinsi gani inakisiwa ya kwamba mtu anapata imani kubwa katika moyo wa mtu?

• Kiongozi anapaswa kusoma Mark 7:30. Jinsi gani mama huyu mapagani alipata imani kubwa hata kabla ya kuona miujiza ikitokea?

• Katika hali ya aina gani hali tunahitaji imani kubwa?

9. Yesu alikuwa na madhumuni gani katika safari yake moja tuu nje ya nchi?

HABARI NJEMA: Juu ya msalaba Yesu alimwamini Mungu licha ya ukimya wake elezea Zaburi 22: 1-2,24. Imani ya Yesu ilikuwa sawa na ile ya mwanamke Mkanaani katika hatua hii. Tofauti kubwa kati ya hali zao ni kwamba katika kesi ya Yesu Mungu alikuwa kimya kwa sababu ya hasira yake, si kwa sababu ya upendo wake.

33

17. SIMIONI AWA MWAMBA 16: 13-23

HISTORIA: Jina la "Kristo" katika Agano Jipya lina maana sawa na "Masihi" katika la kale,. Wafalme na makuhani wakuu waliopakwa mafuta wakati wanachukua nafasi zao.

1. Katika mwanga wa kifungu hiki, unafikiri nini kuhusu zamani: "Kila mtu atakuwa ameokolewa kwa imani yake mwenyewe" (13-17)?

• Kwa nini ni sahihi na ni muhimu sana kukiri imani katika Ukristo?

2. Kati ya haya yapi ni rahisi kuamini: Kwamba Yesu alikuwa nabii Elia (ambaye alikufa miaka 800 iliyopita) au nabii Yeremia (ambaye alikufa miaka 600 iliyopita) au Yohana Mbatizaji (aliyeuawa miaka michache iliyopita) au kwamba yeye ndiye Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai (14-16)?

• Kwa maoni yako, watu ambao wanaweza kujibu swali la Yesu kama wale walio katika mstari wa 14 kuitwa Wakristo? Toa sababu.

3. Licha ya miujiza yote Yesu aliyoifanya, kwa nini wengi wa rika lake hawakutambua kwamba yeye ndiye Kristo, ambaye amekuwa nabii katika Agano la Kale?

4. Kwa mujibu wa kifungu hiki, ni jinsi gani tutaweza kuwa imani ya kweli (17)?

5. Ungejisikiaje kama mtu angekuita wewe "mwamba"?

• Unafikiria Petro alijisikiaje alivyoitwa "mwamba" na Yesu? • Baadhi ya watu wanadhani ya kwamba "mwamba" Yesu alimaanisha Peter

kama mtu binafsi. Wengine wanadhani kwamba Yesu alimaanisha petro kukiri katika mstari wa 16. Unafikiria nini?

6. Unafikiria aya 19 ina maana gani? (Je, funguo za ufalme wa mbinguni ni zipi? Nani anazo katika ulimwengu wa kisasa?)

7. Kwa nini Peter hakuamini chochote kama yaliyoandikwa katika mstari wa 21 yangemtokea Yesu?

• Linganisha mstari wa 17 na 23.Maneno ya Peter yalitoka katika vyanzo gani?

34

• Baada ya ungamo imani ya Peter ilikuwa na tatizo gani?

8. Yesu anawezaje kumwita mtu huyp huyo "mwamba" na "Shetani"?

• Ni nini kinachothibitisha kwamba Peter hakuwa mwendawazimu kwa wakati huu?

• Je, Shetani alijaribu kukamilisha nini kupitia Peter? • Katika hali gani hata Wakristo wanafanya kazi ya Shetani katika maisha ya

wale wanaowapenda?

9. Kuna tofauti gani kati ya njia mbili za kufikiria yaliyotajwa katika mstari wa 23?

• Katika kanisa la Kikristo ni njia ipi ya kawaida kufikiria? • Yesu anamhudumiaje mtu ambaye amekuwa akifanya kazi za shetani katika

maisha ya wengine?

HABARI NJEMA: Soma mstari wa 21 na uongeze maneno: “kwa sababu ya dhambi za Petro- na mimi ”.

35

18. MUONEKANO WA YESU KAMA MUNGU 17: 1-9

HISTORIA: Musa na Elia walitaka kuMUona Mungu miaka mia kabla ya tukio hili, lakini hawakuweza. Kwa mujibu wa OT, kama mwenye dhambi ataonekana mtakatifu katika uso wa Mungu atakufa.Kuhusiana na kifo cha wawili hawa,angalia kumb.34:1-6 na Wafalme 2:11.Mlima Hermoni unaweza kuwa mlima wa mabadiliko(2760).Angalia ramani.

MSTARI 1: Je, unadhani wafuasi hawa watatu waliona wakati Yesu aliuliza mwingine zaidi ya wao kwenda pamoja naye mlimani?

• Unafikiria ilikuwaje kupanda mlima hasa vifaa ya wakati huo?

MSTARI 2: Je, umewahi kutamani kumwona Mungu? Kama ulishawahi, ilikuwa katika hali gani?

• Uso wa Yesu ulimaanisha nini kwa ubadilishaji wa nguo kama ule? • Kwa nini Mungu anataka kuonesha kwa mara nyingine picha ya mwanawe

mbele ya wanadamu? • Kwa nini wafuasi walikufa ingawa walikutana na Mungu Mtakatifu uso kwa

uso?

MSTARI 3: Kwa nini pia wawakilishi wawili wa OT walitakiwa kuwepo katika tukio hili?

• Kwa nini Mungu hakuchagua mwingine zaidi ya Musa na Elia kuwa katika mlima huu?

• Unadhani wawili hawa walijisikiaje walipoona Masihi ambaye alikuja kama mtabiri?

MSTARI 4: Ni nini kilichowafanya wanafunzi kwajisikie vizuri hivyo nzuri katika hali hii?

• Kama wewe una uzoefu wa kidini na hutaki kurudi katika maisha yako ya kawaida, tuelezee kuhusu hilo.

• Unadhani Peter alipanga kuishi juu ya mlima mrefu katika hali hiyo?

36

MSTARI 5: Mawingu yanamaanisha nini katika hali hiyo?

• Kwa nini Mungu hakusema, "Mtiini yeye", akasema "msikilizeni yeye" • Linganisha hali hii kwa mmoja wakati Mungu alipotoa sheria yake kwa

watu wake iliyoandikwa juu ya jiwe kwenye Mlima Sinai. Kuna tofauti gani?

MSTARI 6: Peter ametoka tu kusema kwamba alijisikia vizuri sana. Alikuwa ana hofu ya nini?

• Je, ni kujisikia nzuri au mbaya wakati mmoja ni karibu Mungu Mtakatifu mwenyewe?

• Yesu yupi unafikiria ni rahisi kuwasiliana naye : mmoja wao aliyevalia nguo za kiseremala au yule ambaye anevaa vazi jeupe la wenye haki? Toa sababu.

MISTARI 7-9: Kulikuwa na umuhimu gani Yesu kugusa wanafunzi wake?

• Unadhani wanafunzi walijisikiaje baada ya Musa na Elia kutoweka? • Kwa nini Yesu hakutaka sura yake ijulikane kwa mtu mwingine, hata wale

wanafunzi wengine 9?

HABARI NJEMA: Kutoka mlima wa mabadiliko Yesu alianza safari yake kuelekea mlima mwingine, yaani Golgotha. Ili kutoa vazi jeupe la haki kwetu Yesu alitakiwa kufa akiwa uchi juu ya

msalaba, kutokana na aibu ya dhambi zetu.

37

19. MTUMISHI ASIYE NA REHEMA 18: 21-35

HISTORIA: Katika mfano huu, mfalme anamwakilisha Mungu, watumishi wanatuwakilisha sisi, madeni ya yanawakilisha dhambi zetu na gereza linawakilisha kuzimu. Kipawa ki moja ni sawa na ya mshahara wa miaka 17(24). Dinari 100 ni sawa na mshahara wa miezi 3 '(28).

1. Ni mara ngapi unafikiri inawezekana kumsamehe mtu mwingine ambaye anafanya mabaya dhidi yenu mara kwa mara (21)?

2. MIFANO

• Vipaji 10 000 ni sawa na thamani ya fedha zetu kiasi gani(23-24)? • Ni jinsi gani inawezekana a mtu mmoja apoteze kiasi kikubwa hivyo cha

pesa? • Kwa maoni yako, uamuzi wa Mfalme ulikuwa haki au la (25)? Toa sababu. • Kwa nini mtumishi hakumuuliza Mfalme wake amsamehe madeni (26)? • Unadhani mtumishi huyu angepata vipaji 10000 ajili ya ulipaji wa madeni

yake (26)? • Mtumishi hakufanya mgomo alishukuru kwa kusamehewa madeni (27-28).

Kwa nini? • Mtu anaweza kuokoa fedha kiasi gani ili kiew sawa na mshahara wa miezi

3 (29)? • Ni lazima kitokee nini kwa mtumishi wa kwanza ili aweze kumsamehe wa

pili (30)?

3.MAOMBI YA MFANO

• Madeni na dhambi yanashabihianaje? • Fikiria ukaribia kuwa na deni mbele ya Mungu kila kila utendapo dhambi:

uongo dola 50, mawazo machafu dola 100, kuchukiza mtu dola 1,000 nk, Unafikiri ni mzigo mkubwa kiasi gani wa madeni unao kwa sasa?

• Je, tunajilindaje sisi wenyewe pale tunaposhindwa kuwasamehe dhambi jirani zetu?

• Kuna ubaya gani kwa imani ya mtu ambaye amewasiliana na Mungu katika mstari wa 26?

38

4. MUHTASARI

• Je, mtumishi wa kwanza alikuwa Mkirsto au siyo Mkristo? Toa sababu. • Kuna tofauti gani kati ya kutotaka kusamehe na kutokuwa na uwezo wa

kusamehe? • Kwa mujibu wa mfano huu, tunapataje moyo wa kusamehe (32-33)? • Yesu aliwaombea wale ambao walimsupisha msalabani. Kwa nini basi yeye

aliadhibiwa kama mtumishi mwovu katika mfano huu (34-35)?

HABARI NJEMA: Yesu alibadili maeneo pamoja na sisi watumishi wasio na rehema. Alilipaa madeni yetu na madeni ya watu wote hadi senti ya mwisho. Fedha haikuwa dhahabu wala fedha lakini thamani ya damu yake (1 Pet.1: 18-19).

39

20. NDOA, TALAKA NA UOAJI TENA 19: 1-12

1. TALAKA 1-9

• Kwa nini Mafarisayo wamejawa maswali ya talaka (3) • Je, watu kwa wakati huu wanafikiria nini kuhusu talaka? • Kulingana na Yesu, ni nini kinatokea watu wawili wakioana (4-5a)? • Kiongozi anapaswa kusoma Kumb.24: 1. Nini hasa amri ya Musa na

aliruhusu nini katika kifungu hiki? Linganisha maneno yake pamoja na tafsiri ya Mafarisayo (7).

• Kulingana na Yesu, ni nini hoja ya maisha ya ndoa ya muda mrefu (4,5,6,8,9).

• Kwa nini unafikiri kutokuwa mwaminifu katika ndoa ni sababu pekee anayoikubali Yesu talaka (9)?

• Nini kitatokea katika jamii endapo talaka kitu cha kawaida au zaidi ya kawaida?

2. KUOA TENA 9-10

• Linganisha mistari 8-9 Mat.5: 32. Yesu anafundisha nini kuhusu kuoa tena wakati mke mtalaka bado yupo? Jikite kwenye maandishi!

• Kiongozi anapaswa kusoma 1 Kor.7: 10-11 na Rum 7: 2-3. Je, Paulo alifundisha nini kuhusu kuoa tena wakati mtalaka anaishi?

• Kwa nini wanafunzi waliguswa kama walivyofanya kwa mafundisho ya Yesu (10)?

• Kwa nini unafikiri mafundisho ya Yesu na Paulo kuhusu kuoa tena ni ni kitendo cha kukandamiza hata ndani ya makanisa ya kikristo ya siku hizi?

3. UPWEKE 11-12

• Ina maana gani ya kwamba mtu amezaliwa kama "towashi"? • Katika njia zipi watu wengine kufanya mtu asiweze kuoa? • Ina maana gani kivitendo mtu kujinyima ndoa kwa sababu ya ufalme wa

mbinguni?

40

4. MUHTASARI

• Je, unafikiri kwamba mtu anaweza kuishi maisha mema bila kutimiza ngono? Toa sababu.

• Kulingana na Yesu, ni kitu gani muhimu zaidi kwa Mkristo zaidi ya kujifurahisha binafsi?

• Yesu alikuwa na wasiwasi juu ya wakati wa kufanya sheria hizo kali za mahusiano kwa na jinsia nyingine?

• Je mtu ambaye hajatimiza amri,Yesu anaagiza afanye nini kwa maelekezo yaliyomo katika kifungu hiki?

• Je, unafikiri kitatokea nini kwa mtazamo wa kibiblia kama mtu anakanusha uhalali wa mafundisho ya Yesu katika kifungu hiki?

HABARI NJEMA: Kiongozi anatakiwa kusoma Yohana 8: 4-11

41

21. KAMWE KUCHELEWA 20: 1-16

HISTORIA: Katika wakati wa Yesu maisha ya wafanyakazi yalikuwa ya uhakika sana. Gawanya wastani wa mshahara wa mwaka kwa sasa katika sehemu 300 utapata thamani ya dinari moja. Masaa yalihesabiwa kuanzia saa 12 asubuhi. Mmiliki wa nyumba katika mfano huo amemwakilisha Mungu na shamba linawakilisha Ufalme wake.

1. MFANO

• Mwenye nyumba alikwenda kuwaajiri wafanyakazi katika shamba lake mara ngapi kwa siku (1-6)?

• Kwa nini mwenye nyumba alitoa taarifa kwa kundi la kwanza mshahara utakuwa kiasi gani (2,4)?

• Fikiria sababu mbalimbali kwa nini baadhi ya wafanyakazi hawakuwa katika soko saa kumi na mbili asubuhi.

• Kwa nini mwenye nyumba hakuwaajiri watu bora tuu bali mtu yeyote ambaye alikuwa anapatikana?

• Kwa nini hapakuwa na mtu yeyote aliyeajiriwa kutoka katika kundi la mwisho la wanaume (6-7)? Fikiria sababu mbalimbali.

• Linganisha utendaji kazi katika siku ya kwanza ya kundi la kwanza na kundi la mmwisho (7.12). Ni kundi lili lililovutia zaidi?

• Hebu tudhani kulikuwa na watu watano katika kundi la mwisho. Ni fedha kiasi gani (kwa fedha za yetu) mwenye nyumba angeweza "kuokoa" kama asingelikuwa ameajiri kundi lile?

42

• Kwa nini mwenye nyumba alianza kwa kulipa wale walioajiriwa mwisho (8)?

• Kwa nini kundi la kwanza lililalamika ingawa wao walipewa kile walichoahidiwa?

• Je kwa maoni yako mwenye nyumba aliwalipa mishahara kwa haki? Toa maoni yako

• Kwa nini mwenye nyumba alitaka kutoa kiasi sawa kwa kila mtu? Jaribu kutafuta maelezo mengi / sababu kama unavyoweza.

2. TAFSIRI YA MFANO

• Kwa nini Mungu anataka mtu yeyote na kila mtu afanye kazi katika utawala wake?

• Je, "mshahara" rejelea katika mfano huu? • Kwa nini mshahara ni sawa kwa kila mtu katika ufalme wa Mungu? • Ni katika muda gani "siku" umewahi kuitwa katika utawala wa Mungu? • Nani unadhani ana bahati: mtu ambaye amefanya kazi katika ufalme wa

Mungu kwa maisha yake yote, au mtu aliyeokolewa katika dakika ya mwisho? Toa sababu.

• Unajisikiaje kama mtu mwingine anasifiwa katika kanisa lako na unajua ya kwamba umefanya/unajua mengi zaidi yake ?

• Jinsi unafikirianini wewe kama siku ya mwisho Mungu atakupa mshahara sawa, tuseme, mtume Paulo?

• Je mstari wa 16 unatupa mwanga gani katika wa mfano huu?

Yesu anasema na wewe leo: "Wewe pia nenda mukafanye kazi katika shamba langu!" Utamjibu nini?

HABARI NJEMA: Yesu mwenyewe alifanya kazi Ngumu katika ufalme wa Mungu. Kwa kweli, katika siku ya mwisho alifanya kazi kwa bidii kubwa kila mtu mwanaume na mwanamke duniani aweze kulipwa mshahara wa denari moja kila mmoja kwa kile alichovuna.

43

22. MFALME APANDA MJINI KWAKE 21: 1-11

HISTORIA: Watu walikuwa wakisubiri ishara ambayo ingethibitisha kama Yesu alikuwa mfalme au la - na punda alikuwa ni ishara, walitoa unabii kwa Zakaria (9: 9). Kwa kweli, Yesu alikuwa mwana wa Mfalme Daudi katika kizazi cha 30.

1. KUINGIA KWA USHINDI

• Je, watu walitegemea nini mfalme baada ya kuingia kwa ushindi katika mji mkuu?

• Ingekuwaje kama kitu chochote kingekuwa tofauti na matarajo ya wanafunzi kwa Yesu katika kile umati ungefanya?

• Angalia kwa makini katika mwendelezo wa mtiririko, ilivyotokea wakati Yesu alipokuwa anakaribia Yerusalemu kwa mara ya mwisho. Ni nani aliyeandaa ukaribisho? Yote yalianzaje? Kwa nini watu walitandaza mavazi yao barabarani? Kwa nini mji mzima ulishtushwa?

2. MFALME

• Kwa nini Yesu alipokuwa anakwendaYerusalemu alipanda juu ya punda, na siyo juu ya farasi?

• Watu wangejuaje ya kwamba Yesu alikuwa ni mwana wa Daudi? (linganisha.20: 31)

• Yesu alikuwa na tabia gani ya Kifalme? • Kwa nini kwa ghafla watu wote hawakuwa na hofu ya kumwita Yesu

Mfalme, ingawa vikosi nya majeshi ya Warumi hawakutaka kusikia mambo kama hayo?

• Hadi hatua hii Yesu ameficha siri kwamba alikuwa mfalme. Kwa nini sasa aitumie kwa manufaa?

• Kuna tofauti gani kati ya wafalme wa dunia hii na Yesu katika hali hii? • Kwa nini Yesu alitakiwa afe kama mfalme?

44

3. WATU

• Je, unafikiri Yesu alikuwa na furaha umaarufu wake kufichwa ghafla? Toa sababu.

• Unadhani ilikuwa asilimia ngapi watu waliokuwa wakipiga kelele, "Msulubishe!" Baada ya siku tano?

• Kwa nini hakusimama mtu yeyote katika umati huu na kumtetea Yesu alipokuwa akinyanyaswa?

• Jinsi gani unaweza kuishi, kama utasimama peke yako na zako ambao wanakupinga?

4. HOSANNA (maana yake, " Bwana tuokoe / tusaidie!")

• Kilio cha watu katika mstari wa 9 kinaelezea nini? Cf. maana ya "Hosana". • Kwa nini ni sahihi zaidi kupiga kelele, "Nisaidie!" Kwa Mfalme Yesu

kuliko "Heko!" • Ni nini kinachoshangaza kuhusu mstari wa 11? • Tukio hili lina madhara gani juu ya mustakabali wa Yesu hapo baadaye?

5. WEWE NA MIMI

• Mambo gani yalikufanya ulie, "Hosanna, nisaidie!" Siku za hivi karibuni / wakati wa ujio huu?

• Kwa nini hii kilio maandalizi bora kwa ajili ya Krismasi?

HABARI NJEMA: Soma mstari wa 5 kwa mara nyingine tena na kuweka jina Lako mwenyewe katika nafasi ya "Binti Sayuni".

45

23. SHEREHE YA HARUSI YA MWANA WA MFALME 22: 1-14

HISTORIA: Harusi alikuwa moja ya mambo muhimu katika maisha ya kila siku ya watu wakati wa Yesu. Katika kitabu cha Ufunuo mbinguni wakati mwingine huitwa "harusi". Wageni waalikwa katika mfano huu awali walijulikana kuwa ni Wayahudi, lakini sasa maana yake ni mtu yeyote ambaye ana mawasiliano na kanisa la Kikristo, lakini hazingatii mwaliko wake kwa umakini.

1. Kumbuka harusi ya kifalme uliyowahi kuitazama kwenye TV. Walialikwa watu wa aina gani?

• Ni nani katika siku hizi unadhani angeweza kuishi katika njia ilivyoelezwa katika aya 3-5?

2. Je, wageni waalikwa labda walifikiria nini kuhusu mfalme?

• Kwa nini ilikuwa ni rahisi kwa wageni kukataa mwaliko? • Kwa nini wageni waalikwa hawakuwa na hofu ya matokeo ya tabia zao?

3. Mungu anatuita watu kwenye harusi ya kifalme mbinguni kupitia watumishi wake na Biblia. Kwa nini watu wengi kuishi kama wale walioalikwa katika mfano huu (3-5)?

4. Unajisikiaje ukialikwa katika kanisa, masomo ya Biblia nk wakati wewe unajishughulisha na mambo mengine?

• Kulingana na mtazamo wako kuelekea mwaliko wa Mungu (Biblia), ni kiasi gani unathamini harusi ya kifalme, k.v. mbinguni?

5. Kwa nini ni watumishi wa Mungu katika dunia hii wakati mwingine walihudumiwa kama wale katika mstari wa 6?

• Ni wakati gani mstari wa 7 ulitimia? / Lini hayo yatatimizwa?

6. Linganisha maisha ya kila siku ya kundi la kwanza na ya kundi la pili kwa walioalikwa harusini (5.10).

• Ni nani katika siku zetu ni wale waliokuja katika Ufalme wa mbinguni kutoka "kutoka mafichoni" (9-10)?

46

• Jinsi gani loiterers wamini ya kwamba mwaliko wa mfalme ulikuwa na maana ya kuchukuliwa kwa uzito?

• Ni kwa ajili ya nani mwaliko kwa harusi Mungu wa mbinguni furaha badala ya huzuni?

7. Kwakawaida walidhani kwamba mfalme alikuwa ameandaa tayari vazi kwa kila mmoja wa wageni waliotoka mitaani. Kwa nini unafikiria mmoja kati ya wageni alikataa kuvaa vazi hili (11-12)?

• Katika Biblia vazi la harusi mara nyingi linajulikana kwamba ni vazi la haki ambalo Mungu aliwavisha wenye dhambi. Ni aina gani ya imani mtu ambaye anadhani anaweza kwenda mbinguni anatakiwa avae "nguo" yake mwenyewe?

8. Je mstari wa 14 unatupa mwanga gani katika mfano huu?

• Je, ni nani ambaye bado hajapata mwaliko wa harusi ya kifalme ya Mungu?

• Ni nani waliochaguliwa? Jikite kwenye habari hii.

9. Kwa nini Yesu alikuwa na uzoefu sawa na mtumishi bila ya kuwa na vazi la harusi (13)?

HABARI NJEMA: Kiongozi anatakiwa kusoma Ufunuo.7: 13-14

47

24. NI NANI AMBAYE NI MNAFIKI? 23: 1-12

HISTORIA: Wakati Yesu anakosolewa hadharani Mafarisayo na walimu wa Sheria ilikuwa ni kashfa kubwa kama ilivyo katika siku za leo kuwaita viongozi maarufu wa dini wanafiki kwenye TV. "Akiwa ameketi katika kiti cha Musa" inmaanisha kuwa na sifa za kustahili kufundisha sheria ya Musa, Hiyo ni katika Agano la kale (2).

1. Wakati wa Yesu anafiki walikuwa na tabia gani (2-7)?

• Sema katika sentensi moja Yesu alikuwa na kitu gani dhidi ya Mafarisayo pamoja na walimu wa sheria.

2.Tabia ya mnafiki katika wakati wa sasa ni ipi?

• Katika wakati wa leo tutakutanaje na Mafarisayo? • Ni aina gani ya mafundisho inaongezeka kwa idadi ya Mafarisayo katika

ushirika wa Kikristo?

3. Ni kwa viwango gani Mafarisayo wa Yesu kwa wakati uliwalianisha watu?

• Ni kwa viwango gani wanafiki wa siku za leo unaainisha watu?

4.Kwanini watu huthamanisha viwango vya vyeo na shahada ? (7-10)?

• Kuna umuhimu gani kusema digrii na vyeo viko katika ushirika wa Kikristo?

• Kulingana na Yesu, ni nni kibaya kuhusu vyeo na shahada?

5. Kwa nini wakati mwingine ni vigumu hata kwa Wakristo kuwa watumishi wa wengine (11)?

• Kuna tofauti gani kati ya kuwa mtumishi (kwa maana jinsi Yesu alivyotumia neno katika mstari wa 11), na kuwa na udhalili?

• Elezea kiongozi wa Kikristo ambaye anatumia mstari wa 11 umakini.

6. Je mstari wa 12 maana katika kivitendo?

• Elezea uzoefu ulio nao kwa jinsi mstari wa 12 ulivyokuwa kweli katika maisha yako.

48

7. Yesu alikuwa na heshima gani tofauti viongozi wengine wa dini wa wakati wake?

• Kwa nini Yesu milele hakudai heshima na cheo kwa ajili yake mwenyewe, ingawa alistahili zaidi kuliko mtu mwingine katika dunia nzima?

8. Ni mafundisho gani katika kifungu hiki ni muhimu zaidi kwako binafsi? Vipi kuhusu kwa ushirika wenu wa Kikristo?

HABARI NJEMA: Yesu kamwe hakubebesha mizigo mizito kwa wengine. Kwa kinyume - yeye alichukua dhambi za wanadamu wote juu ya mabega yake msalabani.

49

25. MBINGU NA NCHI ZITAPITA 24: 29-44

HISTORIA: Kuna nadharia nyingi miongoni mwa Wakristo ya kwamba ni utaratibu upi mambo yatatokea wakati Yesu atakapokuja tena katika dunia hii. Katika utafiti huu wa Biblia hatujadili utaratibu wa mambo bali mambo yao wenyewe. Kiongozi anatakiwa kuelezea kwa ufupi kuhusu Nuhu na wakati wake. (37-39, linganisha.Mwanzo.6-7)

1.Kama ukisikia Yesu atarudi leo utajisikiaje?

• Kuna tofauti gani kati ya kumsubiri Yesu na kungoja kifo?

2. Ni aina gani ya mabadiliko yatatokea kabla ya kuja kwa Yesu? Jaribu kueleza mambo haya kwa maneno ya kisasa (29). (Nini kinaweza kusababisha giza duniani? Kumbuka pia wakati wa Nuhu.)

• Ni mategemeo gani yalitarajiwa ambayo hadi sasa hayajatokea?

3. Ni kwa jinsi gani ujio wa kwanza wa Yesu unatofautina na ule wa pili? Jaribu kupata tofauti kadiri iwezekanavyo (30).

• Mataifa yote yataomboleza kitu gani wakati Yesu akija tena (30)?

4. Nini kitatokea kwa Wakristo wakati Yesu atakapokuja tena (31)?

• Je, ungependa kuwa hai wakati matukio ya mstari wa 31 yatakapotokea? Toa sababu zako.

5. Je, Yesu alitaka kusema kuhusu nini wakati wa kuwapo kwake kupitia mfano mdogo wa mtini (32-34)? (Je, unafikiri mfano huu anaongea kuhusu Israel ya kileo? Kama ni hivyo, kwajinsi gani?)

6. Maneno ya Yesu yanamaanisha nini (= Biblia) kwa Wakristo wa kizazi kilichopita (35)

• Inamaanisha ninii kwako kwamba kuna mambo katika dunia hii ambayo hayatapita kamwe?

7. Kwanini siku ya kurudi tena ni siri hata kwa Yesu mwenyewe (36)?

• Maisha yako yatabadilikaje ukijua siku ambayo Yesu atakuja tena?

50

8. Jinsi gani rika la Nuhu linafanana na watu wa kileo (38-39)? (Walikuwa wanapendelea nini na hawakupendelea nini?)

9. Je mistari 40-41 ina maanisha nini? Linganisha wakati wa Nuhu na mstari 31.

• Fikiria jinsi dunia bila ingekuwa leo kama i mambo yaliyotabiriwa katika mistari hii yatatimia(40-41).

10. Ni kwa nani ujio wa Yesu unakuwa kama mwizi anavunja nyumba yake (43-44)? Kwa nani itakavyokuwa kama alitamani kukutana na rafiki mpendwa?

• Je mistari 42 na 44 unatushauri tufanye nini kivitendo? • Jinsi gani ujio wa mara ya pili wa Yesu kuwa faraja kwa ajili yetu,

badala ya mawazo ya kutisha?

51

26. WANAWALI KUMI 25: 1-13

HISTORIA: Maana ya "mafuta" katika mfano huu imefasiriwa kwa njia tatu tofauti: A) Ina maana Roho Mtakatifu. B) Ina maana imani katika Yesu. C) Ina maana Biblia. Bwana harusi inahusu Yesu na uwakilishi wa harusi mbinguni, ambayo ilitanguliwa na kuja kwake marna ujio wake wa mara ya pili.

1. Unafikiria " Mkristo mwaminifu" anakuwaje?

2. MFANO

• Kazi ya wasichana hawa katika harusi ilikuwa ni kwa ajili ya kuonesha mwanga kwa bwana harusi. Hakukuwa na lindo bado, ucheleweshwaji ulikuwa ni utawala badala ya ubaguzi. Kwa nini unafikiri wanawali wapumbavu hawakuwa kuona kwamba wangalikuwa mafuta ya kutosha katika kila hali?

• Fikiria sababu mbalimbali - fahamu kama vile unafahamu - kwa mtu asiyejali iwapo harusi ya rafiki yake itfanikiwa au la?

• Kuna uhusiano gani kati ya wanawali wenye busara na wale wapumbavu?

• Kwa nini hata wanawali wenye busara walikesha hadi usiku wa manane (5-7)?

• Je, unafikiri kuhusu wanawali wenye busara kutowagawia mafuta wale rafiki zao (8-10)?

• Bwana harusi lazima angewajua wasichana wote kumi kabla. Kwa nini alisema kwamba hakuwafahamu wale wapumbavu (11-12)?

3. TAFSIRI

• Yesu alimaanisha nani kutumia wanawali wenye busara? • Yesu alimaanisha nini kwa wajinga? • Tunapaswa kufanya maandalizi gani kwa ujio wa pili wa Yesu

kutegemeana tafsiri tatu tofauti tulizochagua? (Angalia "Muktadha") • Kuna tofauti gani kati ya imani ya mtu ambaye yuko tayari kwa ajili ya

ujio wa Yesu wa mara ya pili na ile ya wau wasiosubiria? • Je, unafikiria umefanya maandalizi ya kutosha kwa ajili ujio wa pili wa

Yesu?

52

• Je, Yesu alitaka kutufundisha nini kwa kuwafanya wanawali wote kumi wasinzie wakati wakisubiri (5.13)?

• Ni lini na nikwa jinsi gani yesu alijifunza kujijua mwenyewe (12)? • Ni katika hali gani tunatakiwa tujifunze kuamini harusi yambinguni? • Je mstari wa 13 unasema kwako binafsi?

HABARI NJEMA: Sisi kamwe hatutaweza kujifunza kumjua mtu mpaka yeye atutendee mabaya. Yesu hatoweza kutujua sisi katika hali halisi ya neno, kama hatuwezi kumwambia dhambi zetu na kumwomba msamaha.

53

27. KUWEKEZA KATIKA VIPAJI 25: 14-30

HISTORIA: Talanta moja ni sawa na mshahara wa miaka 17. Kuna njia tatu za kutafsiri upokeaji wa vipaji vya mfano huu: A. Wao wakilisha uwezo wetu na vipaji vya kiroho. B. Wao wakilisha neema ya Mungu (injili). (Linganisha.Eph.4: 7) C. Wao wakilisha njia ya neema, k.v. Biblia, ubatizo na Ushirika Mtakatifu.

1. Kiasi gani talanta moja ingekuwa na thamani kwa fedha zetu za leo? Kiasi gani kwa mbili? Je kuhusu tano (14-15)?

• Je, unafikiri ni ipi itakuwa njia bora ya kuwekeza kiasi sawa kwa talanta moja katika wakati wetu?

• Unadhani itachukua miaka mingapi ni kuongeza kiasi mara dufu? • Kwa nini mara nyingi sio rahisi kuwekeza kwa fedha za mtu mwingine?

2. Mtu tajiri alitumia kigezo gani kugawanywa fedha zake (15) ni nini?

• Inamaanisha nini kwa watumishi kupata kiasi tofauti cha vipaji kwa mujibu wa tafsiri A, B na C?

• Ni lini na ni kwa jinsi gani unaweza kupata kipaji chako kutoka kwa Mungu?

3. Jinsi gani hisia za watumishi kwa bwana wao kushawishi Jinsi tabia zao?

• Ni katika kile njia gani tofauti watumishi walishughulikia tatizo la bwana ambaye hakuwa wa kurudi haraka (19A)?

• Jinsi gani mtu "atawekeza" kipawa cha kiroho cha mtu mwingine (A)? Jinsi gani mtu "atawekeza" Neema ya Mungu (B)? Je kuhusu njia ya neema (C) (16)?

• Je inawezekanaje mtu kuzika zawadi ya mtu kiroho ardhini? Vipi kuhusu kuhusu injili? Na njia ya neema (18)?

• Ni ipi kati ya tafsiri hizi unadhani ni sahihi?

4. Je mstari wa 26 unatufundisha nini kuhusu Mungu?

• Ni katika hali gani unaamini ya kwamba Mungu ni mtu imara ambaye anahitaji kutatua yaliyoshindikana (24)?

54

• Kuna ubaya gani kwa imani ya mtu ambaye ni kama aliyekuwa mtumishi wa tatu katika mfano (24-27)?

5. Lini mtumishi mvivu atakuwa na kipaji tu cha kuchukuliwa (28)?

• Je mstari wa 29 una maana gani kwa mwanga tunaopata kutokana na tafsiri A, B na C?

6. Kwa nini adhabu ya mtumishi wa tatu ilikuwa kali hivyo hata ingawa yeye hakuhusika na fedha za bwana wake zilizoibiwa(30)? Fikiria kila moja ya hizi tafsiri tatu tena.

• Kwa nini Yesu mwenyewe aliadhibiwa kama waovu na mtumishi wavivu (30)?

7. Ni lazima tufanye nini, kama tunatambua ya kwamba sisi ni watumishi waovu na wavivu?

8. Nini kinatufanya sisi Wakristo "kuwekeza" katika vipaji yetu?

• Fikiria alichokisema Yesu katika mstari wa 21 juu yako katika siku ya hukumu. Ungemjibu nini?

55

28. KONDOO NA MBUZI 25: 31-46

HISTORIA: Mfano huu umekuwa kawaida kufasiriwa kwa njia tatu: ndugu mdogo wa Yesu maana A. mateso ya Wakristo, B. mateso ya Wayahudi, C. mateso yote ya watu duniani.

1. Je, umepata nini hasa cha kutisha katika mfano wa hukumu ya mwisho?

• Ni nini amani kitu, gani kinaweza kukupa faraja katika mfano huu? • Je, ungefikiria nini kuhusu Mungu kama asingeadhibiwa milele kwa

makosa yetu?

2. Je mfano huu unatufundisha nini kuhusu mbinguni na kuzimu (34, 41, 46)?

• Kulingana na akili ya kawaida, ni aina gani ya watu wanapaswa kwenda katika moto wa Jehanamu?

• Kwa mujibu wa mfano huu, ni dhambi gani "inammtupia" mtu jehanamu?

• Kwanini watu kwa wakati wetu wanazidi kutokuziamini habari za kuzimu?

3. Kuna makundi mangapi "ndugu wadogo" yameoneka katika mfano huu (35-36, 42-43)?

• Makundi mangapi yamekusaidia wewe? • Ni yapi kati ya makundi hayo sita umeona ni vigumu kusaidia?

4. Kwa nini ni vigumu sana kumwona Yesu katika hali ya njaa, kiu, kutokuwa na makazi, uchi, ugonjwa na (hata!) kufungwa jela?

• Je ushirika wako Mkristo unafanya nini kwa ajili ya kila mmoja katika makundi hayo sita?

5. Jinsi gani "mbuzi" labda wanatetea tabia zao: kwa nini wasingeyasaidia makundi haya sita?

• "Mbuzi" walikuwa na uaminifu wakati waliposikia hukumu yao. Kwa nini walitarajia iwe tofauti (44)?

6. Kwa nini "kondoo" pia walishangazwa na maneno ya mfalme (38-39)?

56

• "Kondoo" walipata wapi kupata nguvu ya kupenda hata wale ambao kwa kweli hawapendeki?

7. Ni yupi kati ya tafsiri zilizotajwa hapo juu unafikiria kuwa yuko sahihi?

• Ni matokeo gani ya kila moja ya tafsiri hizi yanadhihirisha tabia zetu ?

8.Mfano wa hukumu ya mwisho unaonekana tu kuhusika na matendo yetu. Imani inaingiaje katika hali hii? (Jinsi gani watu waligawanywa kwa mbuzi na kondoo katika nafasi ya kwanza?)

9. Lini Yesu mwenyewe angalau aligundua hatma ya ndugu zake: wakati alikuwa na njaa, kiu, kutokuwa na makazi, uchi, ugonjwa na kufungwa?

• Kwa nini hukumu hiyo alitamkwa kwa Yesu kama mbuzi katika mstari wa 41?

HABARI NJEMA: Katika historia nzima ya mwanadamu, kulikuwa na mambo mawili muhimu sana ya majaribio: Kesi ya Yesu, na hukumu ya mwisho. Kila mmoja wetu lazima kutoa mawazo, katika moja ya majaribio haya au mengine, kwa mapungufu yetu kuelekea ndugu zetu. Hakika kama wewe umeangukia katika dhambi zenu baada ya kuhukumiwa katika kesi ya Yesu, utakuwa huna hatia siku ya mwisho.

57

29. MAPAMBANO KULE GETHSEMANE 26: 36-46

HISTORIA: Katika Biblia kikombe kwa maana nyingine ni kikombe kilichojaa ghadhabu ya Mungu, ambayo mwenye dhambi ana gugumia chini (39).

1. Wakati ambao huna furaha, unataka watu wangapi wawe karibu na wewe? (Kwa nini Yesu hakutaka kwenda Gethsemane peke yake?)

• Wanafunzi hawa watatu wote walikuwa ni wavuvi ambao walikuwa wakifanya kazi mara nyingi wakati wa usiku. Kwa nini hawakuweza kukaa macho kwa saa moja?

2. Hii ni moja tu na ni wakati ambapo Yesu alizungumzia maumivu yake mwenyewe na huzuni (38). Nini hasa kilikuwa kichungu kwa ajili yake katika hali hii?

• Kama wewe mwenyewe ulishawahi kuzidiwa na huzuni kiasi cha kufa, ilikutokea katika hali gani?

3. Watu wengi wameshakutana na vifo vyao pasipo kuonyesha hofu yoyote. Kwanini siyo Yesu? (Iweje kama Yesu angekufa bila kuonyesha hofu yoyote, tabia yake gani imekuwa ishara kwetu?)

• Ni nini kiinachofanya mtu muongo kuinamisha kichwa chini (39)?

4. Kwanini Yesu hakuwaomba wanafunzi wake wamwombee (40-41)?

• Ni aina gani ya majaribu ambayo Yesu aliyazungumzia katika mstari wa 41?

5. Angalia maombi ya Yesu katika mstari wa 39. Je Yesu alikuwa na mapenzi sawa kama Baba yake wakati huo?

• Kwa nini sehemu ya kwanza ya sala hii ni muhimu? Kwa nini sehemu ya pili pia ni muhimu?

• Kitatokea kitu ganikwetu, kama tutaomba sehemu ya pili ya sala hiyo?

6. Jinsi gani maombi ya Yesu yalibadilika alipoomba kwa mara ya pili (39,42)?

58

• Kwa nini Yesu hakuacha baada ya kusali mara moja au mara mbili (39,42,44)?

7. Je ,atarajio ya Yesu yalibadilika alipokuwa anasali? Kama ni hivyo, kwa njia gani?

• Je, unafikiri unaweza kumuombeaa mtu unayempenda kuliko wote akuache, kama ni lazima? Toa sababu..

• Ingekuwaje kwetu kama Yesu angekataa kunywa kikombe cha hasira ya Mungu?

8. Unapata hisia gani kuhusu habari za Yesu katika mistari 45-46 ikilinganishwa na jinsi alivyokuwa hapo kabla? (Kwa mtulivu sana kutoka hatua hii juu ya hadi kifo chake?)

9. Ni nini kingetokea kama Yesu angeishia juu ya msalaba bila mapambano haya?

• Kwa nini ni muhimu kwamba sisi pia tuwe na Gethsemane yetu wenyewe kabla ya Golgotha?

HABARI NJEMA: Yesu alikuwa ametikiswa kwa sababu alijua kwamba uhusiano wake wa karibu na baba yake itakuwa ungesita wakati huo. Hatutakiwi kunywa kikombe cha ghadhabu ya Mungu kwa sababu Yesu alikunywa kwa ajili yetu.

59

30. KWA NINI WAMENIACHA 27: 33-54

HISTORIA: Ni vigumu kwa mtu kusulubiwa, wakati mwingine hata kupumua.Nabii Elia (49) akiishi miaka 800 iliyopita. Watu wa kawaida hawakuruhusiwa kuangalia Patakatifu nyuma ya pazia hekaluni (51).

1. Utekelezaji wa adhabu ya kifo uliachwa kwa wanaomiliki vikosi. Kulingana na aya 33-36, jinsi gani unadhani askari hawa wa Roma walijisikiaje wakati walipoamriwa kumgongea misumari mtu hai kwenye msalaba?

• Mvinyo ulikuwa kawaida kwa wale waliosulubiwa ili kupunguza maumivu. Kwa nini unafikiri askari alikuwa katika hali hii kuchanganya mvinyo na nyongo ili iwe kunywa (34)?

• Nini kinaweza kumfanya mtu kutumikia mateso ya binadamu mwingine na hata kuanza kufurahia hayo? (Unafikiri ni kwa kiasi gani vurugu katika sinema na michezo ya video inaweza kutushawishi?)

2.Ni nini kinachoshangaza kuhusu sababu zilizopelekea maadui wa Yesu kumdhihaki (39-44)?

• Kama wewe ungemwona Yesu wakati huo, unafikiri ungeweza kuamini ya kwamba alikuwa Mungu?

3. Je, maadui wa Yesu labda walitarajia kusema nini kwake kama maneno yake ya mwisho?

• Kwa nini Mungu alimwachaYesu (46)? • Kama wewe ungeona kwamba Mungu amewaacha ninyi, hali gani

ingetokea?

4. Je, unadhani wale waliokuwepo walipoona Yesu bado alimwita Mungu, Mungu wake mwenyewe?

• maneno katika mstari wa 46 ni nukuu kutoka Zaburi 22: 2. Kwa nini Yesu alitaka kueleza uchungu wake kwa njia ya maneno ya Biblia badala ya maneno yake mwenyewe?

• Ungependa kusema nini kama maneno yako ya mwisho katika dunia hii?

5. Kwa nini baadhi ya watu hupiga kelele wakati wakifa (50)?

60

• Kilio cha Yesu ykinatangaza nini kuhusu kifo chake?

6. Anga la Golgotha lilibadilika wakati wa mchana (51-54)?

7. Nini kilifanya afisa wa Kirumi (ambaye hakuijua Biblia) aamini ya kwamba mtu huyu ameachwa na Mungu na wanadamu kwa kweli walikuwa ni wana wa Mungu (54)?

• Kwa nini Wayahudi hawakuona kifo cha Yesu katika mwanga tofauti kuliko afisa wa Kirumi alivyofanya?

8. Mara nyingi tunafikiri kwamba mateso ya Yesu yalikuwa makubwa kwa sababu alikuwa amebeba dhambi zote za ulimwengu katika mabega yake. Unadhani ni kwa jinsi gani mateso yake kwa ukubwa ingekuwa kama angebeba dhambi zangu tu msalabani?

• Kama ungekuwa binadamu mmoja tu katika dunia hii, unafikiri Yesu angekuja angeteseka kwa sababu yako? Toa sababu.

HABARI NJEMA: Wakati ukiangalia fungu hili unaweza kuona wazi jambo moja, yaani kiasi gani Yesu anakupenda.

61

31. ULINZI MAKABURINI 27: 62-28: 15

HISTORIA: Maadui wa Yesu walikuwa wamepanga hatima ya jinai kwa ajili yake . Kwa kawaida mbwa walikula kile kilichoanguka chini kutoka msalabani. Hata hivyo, Yesu alizikwa vizuri (57-62). askari wa Kirumi kwa kawaida walichukuliwa kuwa jasiri sana.

1.Ni kwa jinsi gani makuhani wakuu na Mafarisayo humbuka Jinsi utabiri wa Yesu kuhusu ufufuo wake mwenyewe wakati wanafunzi walikuwa wamesahau kabisa (62-63)?

• Kwa nini makuhani wakuu waliamini kwamba wafuasi walikuwa jasiri zaidi kuliko wao (64)?

• Je, unafikiri makuhani wakuu kweli waliamini uwezekano wa Yesu kufufuka kutoka kifo?

2. Fungu la 65 ni kutaja mwisho kuhusu Pilato katika Biblia. Unapata hisia ya aina gani katika hatua hii?

• Je, Pilato labda alifikiria nini juu ya matukio ya siku hiyo? • Je, unafikiri Pilato ataweza kumsahau Yesu? Toa sababu.

3. Unadhani askari wa Kirumi walichukuliaje agizo la kulinda maiti?

• Angalia kwa makini kile walichokiona askari hao wenye uzoefu asubuhi ya Pasaka (2-4).

• Tutaelezeaje kwa lugha matibabu hali ya askari katika mstari wa 4?

4. Nini kiliwafanya askari wa Kirumi jasiri kuwa na hofu ya kupoteza ajira zao?

• Je, unafikiri askari waliangalia kaburini kabla ya kukimbia? Toa sababu.

5. Je, unadhani makuhani wakuu walitafsiri ripoti ya askari (11-14)?

• Nini kithibitisha ya kwamba makuhani wakuu hawakudai walinzi waadhibiwe, badala yake wakawapa kiasi kikubwa cha fedha (12-15)?

• Jinsi gani ubora wa Mungu ulibadilika kuwa bora kwa milki yake hata mambo yaliyofanywa na makuhani wakuu?

62

6. Orodhesha mambo yote ambayo yaliyowashawishi makuhani wakuu waamini yakwamba Yesu alifufuka kutoka wafu?

• Je, unafikiri ungeamini katika ufufuo kama wewe ungekuwa katika nafasi ya hao wakuu na Mafarisayo?

7. Nini matokeo gani makubwa yaliyo katika hadithi hii ya askari(13)?

• Unadhani huyo ofisa (kamanda wao) angetatuaje kama yeye angesikia habari hii (13)?

8. Kwa nini Yesu hakuonekana mbele ya makuhani wakuu?

• Punde baada ya haya, wanafunzi walibadilika na kuwa watu jasiri na kuanza kutangaza ufufuo bila kuogopa hata kifo. Kwa nini maadui wa Yesu walibadilika na kuwa Wakristo katika hatua hiyo? (elezea Luka 16:31)

• Je, unafikiri maisha waliyobakiza watu hawa yaikuwa kama nini?

9. Je ufufuo wa Yesu una maana gani kwako binafsi?

63

32. TUME KUU 28: 16-20

HISTORIA: Siku 40 zilikuwa zimepita tangu Pasaka. Yesu alikutana na wanafunzi wake kwa mara ya mwisho na kuweka yake kwao. Yeye alitaka kuwakumbusha Wakristo maneno yake ya mwisho kwa muda mrefu kama wao walivyokuwa wakiishi.

1. Unafikirije tabia ya wastani waikristo katika kazi za ujumbe katika kanisa lako? (Kiasi gani ni wastani Wakristo wako tayari kutumia muda wake, fedha na nishati kwa ajili ya kukuza ujumbe?)

• Ni kwa jinsi gani unaweza kukumbuka mitazamo ya jumbe ziliyopita ?

2. Wanafunzi labda walififikiria walikuwa wanakwenda kufanya nini juu ya mlima ambako Yesu alikuwa amewaalika (16)?

• Baadhi ya wanafunzi bado walitia shaka nini(17)? • Kwa nini Yesu alitaka kusema hasa maneno haya kama amri yake ya

mwisho kwa wanafunzi wake?

3. Yesu alitegemeaje watu 11wasiokuwa na elimu kuishinda dunia nzima kupitia yeye?

• Tayari Yesu alishawaita watu hawa kumfuata miaka mitatu ya nyuma. Ni kwa njia gani wito uko tofauti na tume kubwa katika kifungu hiki?

4. Unafikiri Jinsi Wanafunzi walijisikiaje baada ya kusikia maneno "mataifa yote", sio tu Israeli (19)?

• Ni kwa jinsi gani wafuasi walitaka kupinga utume wa Yesu? • Ni kwa jinsi gani unaweza kupinga wakati wewe hutaki kutoa muda wako

na pesa kwa kuimarisha utume kwa wageni?

5. Kwa nini hatuwezi kumwona Yesu kuwa na mamlaka yote mbinguni na duniani kwa sasa (18)?

• Je, unaamini kwamba Yesu ana mamlaka yote juu ya historia ya dunia kwa maisha ya wapendwa wako hata leo? Toa sababu.

64

6. Je, wafuasi walikuwa wanatakiwa kufanya nini katika ujumbe (19-20)?

• Kwa mujibu wa kifungu hiki, ni mambo gani mawili yanahitajika kwa ajili ya mtu kuwa mwanafunzi wa Yesu (19-20)?

7. Yesu aliwasaidiaje wanafunzi wake katika kufanikisha kazi hii kubwa (20)?

8. Kwa nini hakuna kanisa la Kikristo lenye uwezo wa kukamilisha kazi hii hata kwa miaka ya 2000?

• Katika ulimwengu wa kileo ni kero ipi kubwa katika kazi za misheni ? • ni nini kazi yako katika misheni za kigeni: unapaswa kwenda mwenyewe au

unaweza kumsaidia mtu mwingine kwenda? • Je, unafikiri ni nini kinzuri au kibaya katika maisha ya umishionari?

9.Unaelewaje kwamba Yesu yuko na wewe milele hata ukamilifu wa dahari, wakati una kutimiza kazi aliyokupa?