171
AHLUL BAYT NDANI YA TAFSIR ZA KISUNNI SEHEMU YA TATU KWA MUJIBU WA IBN KATHIR, SUYUTI, BURUSAWI, ALUSI NA QASIMI Kimeandikwa na: Sheikh Nizar al - Hasan Kimetarjumiwa na: Hemedi Lubumba (Abu Batul) Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:03 AM Page A

Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

Embed Size (px)

DESCRIPTION

Ahlul Bayt, yaani Watu wa Nyumba ya Mtume Muhammad SAW ni viongozi ambao Mtume alituusia tuwafuate. Katika hotuba yake ndefu na maarufu aliyoitoa pale Ghadir Khumm katika msafara wake wa kurejea kutoka Hija yake ya mwisho, Mtukufu Mtume SAW alisema haya mbele ya masahaba na mahujaji zaidi ya laki moja: “...Nakuachieni vitu viwili vizito: Qur’ani na Ahlul Bayt wangu. Viwili hivyo havitaachana mpaka vinifikie katika [hodhi ya] Kawthar. Nawausia juu ya Ahlul Bayt wangu! Angalieni jinsi mtakavyojihusisha nao. Kama mkishikamana na viwili hivi hamtapotea kamwe...” (kwa maelezo zaidi soma kitabu cha al-Ghadir)

Citation preview

Page 1: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

AHLUL BAYT NDANI YA

TAFSIR ZA KISUNNI

SEHEMU YA TATU

KWA MUJIBU WA IBN KATHIR, SUYUTI,BURUSAWI, ALUSI NA QASIMI

Kimeandikwa na:Sheikh Nizar al - Hasan

Kimetarjumiwa na:Hemedi Lubumba (Abu Batul)

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:03 AM Page A

Page 2: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

B

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:03 AM Page B

Page 3: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

©Haki ya kunakili imehifadhiwa na:AL-ITRAH FOUNDATION

ISBN: 978 - 9987 - 512 - 97 - 3

Kimeandikwa na:Sheikh Nizar al - Hasan

Kimetarjumiwa na:Hemedi Lubumba (Abu Batul)

]Kimehaririwa na:

Ustadh Abdalla Mohamed

Kimepangwa katika Kompyuta na:Hajat Pili Rajab

Toleo la kwanza: April, 2011Nakala: 1000

Kimetolewa na kuchapishwa na:Alitrah Foundation

S.L.P. 19701 Dar es Salaam, TanzaniaSimu: +255 22 2110640

Simu/Nukushi: +255 22 2127555Barua Pepe: [email protected]

Tovuti: www.alitrah.orgKatika mtandao: www.alitrah.info

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:03 AM Page C

Page 4: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

YALIYOMO

Utangulizi..........................................................................................2

Ahlul Bayt (a.s) ndani ya Tafsir ya Ibnu Kathir, Inayoitwa Tafsirul-Qur’an Al-Adhim..............................................................................9

Ahlul Bayt (a.s) ndani ya Tafsiri ya Suyuti, Inayoitwa Ad-Durul-Manthur Fit- Tafsir - U- Maathur ...................................................41

Ahlul Bayt (a.s) ndani ya Tafsir ya Burusawi, Inayoitwa TafsirRuhul-Bayan Fi Tafsiril-Qur’an .....................................................93

Ahlul Bayt (a.s) ndani ya Tafsir ya Alusi, inayoitwa Ruhul - Ma’aniyFittafsiril -Qur’an Al-Adhim Wasab’ul- Mathaniy.......................119

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:03 AM Page D

Page 5: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

E

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

NENO LA MCHAPISHAJI

Kitabu kilichoko mikononi mwako ni tarjuma ya kitabu cha Kiarabukiitwacho, Ahlu ‘l-Bayti Fi Tafasiri Ahli ‘s-Sunnah kilichoandikwa naSheikh Nazri Hasan. Sisi tumekiita, Ahlul Bayt Ndani ya Tafsiri zaKisunni. Hii ni sehemu ya tatu inayochambua tafsiri za wanavyuoniwakubwa wa Kisunni – Ibn Kathir, Suyuti, Burusawi, Alusi na Qasimi.

Ahlul Bayt, yaani Watu wa Nyumba ya Mtume Muhammad SAW ni vion-gozi ambao Mtume alituusia tuwafuate. Katika hotuba yake ndefu namaarufu aliyoitoa pale Ghadir Khumm katika msafara wake wa kurejeakutoka Hija yake ya mwisho, Mtukufu Mtume SAW alisema haya mbeleya masahaba na mahujaji zaidi ya laki moja: “...Nakuachieni vitu viwilivizito: Qur’ani na Ahlul Bayt wangu. Viwili hivyo havitaachana mpakavinifikie katika [hodhi ya] Kawthar. Nawausia juu ya Ahlul Bayt wangu!Angalieni jinsi mtakavyojihusisha nao. Kama mkishikamana na viwili hivihamtapotea kamwe...” (kwa maelezo zaidi soma kitabu cha al-Ghadir)

Lakini bahati mbaya sana sio Waislamu wote wanaowafuata Ahlul Bayt ASpamoja na kwamba wanavyuoni wa madhehebu zote wameandika habarizao katika vitabu vyao na kuonesha kwamba hawa ni viongozi wa Ummahuu wa Kiislamu.

Mwandishi wa kitabu hiki anajaribu kuthibitisha hilo kwa kutoa rejeambalimbali kutoka vitabu maarufu vya wanavyuoni wa Kisunni.

Ni muhimu kukubaliana na kuziheshimu tofauti za kila mmoja na kutam-bua msimamo na mtazamo wa kila mmoja. Matatizo huja pale mtu anapo-lazimisha tabia, imani na mila zake zitawale wengine au kuzifisha itikadina misimamo ya wengine. Ni muhimu kufikiria kila aina ya maoni katika

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:03 AM Page E

Page 6: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

F

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

kujaribu kuamua ukweli. Uislamu kimsingi uko dhidi ya kufuata kibubusa.

Wafuasi wa madhehebu nyingine wanaweza kuchambua uthibiti wa kitabuhiki ili kujenga maoni yao wenyewe kuhusu mtazamo mzuri wa mtumwenyewe. Ni muhimu mtu kuelewa hoja za wale ambao hakubaliani nao.Inaweza ikasemwa kwamba wale ambao hawaelewi kabisa mtazamo wamaoni tofauti, hawaelewi kwa ukamilifu mtazamo wa kwao wenyewe.

Tumekiona kitabu hiki ni chenye manufaa sana, hususan wakati huu wamaendeleo makubwa ya elimu katika nyanja zote, ambapo uwongo, nganoza kale na upotoshaji wa historia ni mambo ambayo hayana nafasi tenakatika akili za watu.

Kutokana na ukweli huo, Taasisi yetu ya Al-Itrah Foundation imeamuakuchapisha kitabu hiki kwa lugha ya Kiswahili kwa madhumuni yakeyaleyale ya kuwahudumia Waislamu, hususan wazungumzaji waKiswahili.

Tunamshukuru ndugu yetu, Hemedi Lubumba (Abu Batul) kwa kukubalijukumu hili la kukitarjumi kitabu hiki. Vilevile tunawashukuru wale wotewalioshiriki kwa njia moja au nyingine hadi kufanikisha kuchapishwakwake.

Ni matumaini yetu kwamba kitabu hiki kitakuwa ni changamoto kubwakwa wasomaji wetu.

Mchapishaji:Al-Itrah Foundation

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:03 AM Page F

Page 7: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

NENO LA JUMUIYA

Hakika mirathi ya Ahlul-Bait ambayo imehifadhiwa na kambi yao nawafuasi wao dhidi ya upotovu inaonyesha kambi iliyokusanya aina mbal-imbali za taaluma za kiislamu. Kambi hii imeweza kulea nafsi mbalimbalizilizo tayari kunywa kutoka kwenye chemchemu hiyo, na kuupa umma wakiislamu wanavyuoni wakubwa wenye kufuata nyayo za ujumbe wa Ahlul-Bait. Wanavyuoni waliokusanya vidodosa na maswali mbalimbali ya mad-hehebu na mitazamo tofauti ya kifikira kuanzia ndani ya desturi ya kiisla-mu hadi nje ya desturi hiyo, huku wao wakitoa majibu na utatuzi makinijuu ya maswali hayo ndani ya karne zote.

Jumuiya ya kimataifa ya Ahlul-Bait imefanya hima kutetea utukufu waujumbe wa Uislamu na ukweli wake ambao umechafuliwa na makundi,madhehebu na wanaharakati mbalimbali wenye chuki na Uislamu.Jumuiya imefuata nyayo za Ahlul-Bait na za wafuasi wa kambi yao njemaambayo imefanya hima kujibu madai yenye kuendelea na daima ikajaribukubaki ndani ya msitari wa mapambano kwa kiwango kinachohitajikandani ya kila zama.

Hakika uzoefu ambao umehifadhiwa ndani ya vitabu vya wanavyuoni wakambi ya Ahlul-Bait katika dhamira hii ni wa aina ya pekee, kwa sababuuna akiba ya kielimu inayotegemea akili na hoja, huku ukijiepusha namatamanio na upendeleo uliokatazwa. Unazungumza na wasomi nawanafikra wenye fani maalumu, mazungumzo ambayo yanakubalika kiak-ili na yanapokewa na maumbile yaliyo salama.

Jaribio hili la Jumuiya ya kimataifa ya Ahlul-Bait limekuja kuwapa watafu-ta ukweli hatua mpya ya uzoefu wa thamani katika ulingo wa mazungum-zo na maswali na kujibu hoja za utata zilizotolewa zama zilizopita au zina-zotolewa leo kwa njia ya Tovuti, na hasa kwa kupewa nguvu na baadhi ya

G

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:03 AM Page G

Page 8: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

duru zenye chuki dhidi ya Uislamu na Waislamu.Ikijiepusha na uchochezi uliyokatazwa, na ni yenye kuhangaikia kuzishau-ri akili zenye kufikiria na nafsi zenye kutafuta haki, ili ziweze kufikiakwenye haki ambayo inatolewa na Kambi ya Ahlul-Bayt ulimwengumzima, ndani ya zama ambazo akili inaerevuka na nafsi na roho zina-boreka kwa kasi ya pekee. Ni lazima tugusie kuwa mfululizo huu wa tafi-ti hizi umeandaliwa na Kamati maalumu toka jopo la wanachuoni watuku-fu, hivyo tunatoa shukurani njema kwa hawa wote na kwa wasomi nawahakiki kwa kila mmoja miongoni mwao kwa kupitia sehemu ya tafitihizi na kutoa mchango wao wa thamani kuhusu tafiti hizi.

Na sote tunategemea na kutaraji kuwa tutakuwa tumetoa kile tulichoki-weza katika juhudi za kutekeleza baadhi ya wajibu tulionao mbele yaujumbe wa Mtukufu Mola Wetu Mlezi ambaye alimtuma Mtume Wake nauongofu na dini ya haki ili aipe ushindi dhidi ya dini zote. Na MwenyeziMungu anatosha kuwa shahidi.

Jumuiya ya kimataifa ya Ahlu-BaitKitengo cha utamaduni

H

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:03 AM Page H

Page 9: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

I

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:03 AM Page I

Page 10: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:03 AM Page 1

Page 11: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

2

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

UTANGULIZIKila sifa njema ni ya Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa viumbe wote.Rehema na amani zimwendee Mtume Muhammad, yeye na aali zake wato-harifu. Na daima laana iwe juu ya wote walio maadui zao na wakanushajiwa fadhila zao.

Qur’ani iliteremkia katika nyumba tohara na safi, ambazo imeidhinishwazitukuzwe, katika nyumba za aali Muhammadi watoharifu, ambazoMwenyezi Mungu Mtukufu amezifanya makhsusi kwa ajili ya heshima nautukufu kuliko nyingine, na Mwenyezi Mungu akazitaja (nyumba hizo)kupitia Aya za Qur’ani tukufu ambazo zitaendelea kubaki muda wa dahariyote zikisomwa usiku na mchana, na si nyumba za viumbe wengine.

Kwa ajili hiyo tunawaona (a.s.) wao ndio watambuzi na wajuzi wa Kitabucha Mwenyezi Mungu Mtukufu kuliko wengine wote, na kwa ajili hiyotunamwona Amirul-Muuminina Ali bin Abu Talib (a.s.) akisema: “Launikitandikiwa mto kisha nikaketi juu yake nitahukumu baina ya wanatau-rati kwa Taurati yao na wanainjili kwa Injili yao, na baina ya wanazaburikwa Zaburi yao na wanafurqan kwa Furqani yao. Wallahi hakuna Aya yoy-ote iliyoteremshwa bara au baharini, katika tambarare au jabali, mbinguniau ardhini, usiku au mchana, ila mimi namjua ni nani wa iliteremka kwaajili yake, na iliteremka kuhusu nini.”1

Abu Naiim ameandika katika kitabu Hilyatul-Awliyai kutoka kwa ImamAli (a.s.) kwamba alisema: “Wallahi hakuna Aya iliyoteremka ila najuailiteremka kwa ajili ya nani, na wapi iliteremka, na hakika Mola WanguMlezi amenitunukia moyo wenye akili na ulimi wenye kudadisi.”

1 Matwalibus-Suul, cha Ibnu Talha as-Shafiiyu Juz. 1, Uk. 125, chapa ya Taasisiya Ummul-Qura.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:03 AM Page 2

Page 12: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

3

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

Na pia Abu Naiim ameandika katika kitabu Hilyatul-Awliyai kutoka kwaIbn Mas’ud, amesema: “Hakika Qur’ani iliteremshwa kwa herufi saba,hakuna herufi yoyote ila ina dhahiri na batini, na hakika Ali bin Abu Talibndiye mwenye dhahiri na batini.” Na kuna kauli moja inanasibishwa naAmirul-Muuminina (a.s.): “Lau nikitaka kuwapigisha magoti ngamiaarubaini kwa tafsiri ya Qur’ani ninaweza.”

Kisha wao ndio wafasiri wa wahyi wa Mwenyezi Mungu Mtukufu, wenzawa Kitabu chake na Kitabu kitamkacho, haya ndio yathibitishwayo naHadithi ya Vizito viwili: “Mimi ni mwenye kuacha kati yenu vizito viwili:Cha kwanza ni Kitabu cha Mwenyezi Mungu, humo mna uongofu nanuru…., na Ahlul-Baiti wangu, nawakumbusheni Mwenyezi Mungukuhusu Ahlul-Baiti wangu, nawakumbusheni Mwenyezi Mungu kuhusuAhlul-Baiti wangu.”2

Hivyo wao ndio wabainishaji, wafafanuzi na wafasiri wa misamiati yaQur’ani Adhimu. Kwa sababu Kitabu cha Mwenyezi Mungu kina haja yakupata mfasiri, mfafanuzi na mbainishaji, hivyo ni aula kifani chake namwenza wake ndiye mbainishaji, mfasiri, alimu na mjuzi wa Kitabu hichona si mwingine.

Kwa ibara nyingine tunaweza kusema: Hakika Ahlul-Baiti (a.s.) ndiowaliokusudiwa, kuainishwa na kuashiriwa katika semi zake (s.w.t.). Bali nikatika nyumba zao ndimo kilimoteremka Kitabu, na wenye nyumba ndiowajuzi zaidi wa yale yaliyomo ndani ya nyumba yao.

Kuanzia hapa tunawakuta Ahlul-Baiti (a.s.) siku zote wakiifasiri Qur’anina Maneno ya Mwenyezi Mungu vizuri zaidi na kwa ukamlifu mno. Nawatu wote wakirejea kwao bila kumtenga yoyote, na wala hatujaona tukiolililo kinyume na hali hiyo, hata Ibnu Abbas ambaye ni kinara na kiongoziwa wafasiri miongoni mwa sahaba yeye naye alikuwa ni mwanafunzi wa

2 Sahih Muslim, Juz. 4, Hadithi ya 1873.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:03 AM Page 3

Page 13: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

4

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

Ali (a.s.), yeye mwenyewe anasema: “Tafsiri ya Qur’ani niliyonayo nikutoka kwa Ali bin Abu Talib (a.s.)”.

Hapo hapo tunawaona ulamaa wa makundi mawili, Shia na Sunniwameifasiri Qur’ani Tukufu kupitia riwaya na nukuu, kama vile Tafsiri yaAli bin Ibrahim al-Qummiy, Tafsirul-Ayyashiy na Furatil-Kufiy, Kanzud-Daqaiq ya Ibnu al-Mash’hadiy, al-Burhan ya Sayyid Hashim al-Bahraniy,Nurut-Thaqalayn ya Sheikh Abdu Ali al-Hawiziy, na wengineo miongonimwa Maimamiya ambao wameifasiri Qur’ani kupitia Ahlul-Baiti (a.s.). Namiongoni mwa Masunni ni kama vile al-Haskaniy katika Shawahidut-Tanziil, Isfihaniy katika an-Nuru al-Mushtaalu na al-Wahidiy katikaAsbabun-Nuzuul.

Pia zipo tafsiri zilizozagaa huku na huko ambazo zinategemewa na Sunnikatika utafiti na mchakato wa kielimu. Tafsiri hizi zimefasiri baadhi ya Ayatukufu kwamba walengwa halisi wa Aya hizo ni aali Muhammad (a.s.),hivyo tumejaribu kuzikusanya na kuziweka pamoja Aya hizi toka katikakabati za vitabu vya tafsiri muhimu zenye kutegemewa kwao. Miongonimwazo ni:

1. Jamiul-Bayan Fii Tafsirul-Qur’ani ya Abu JafarMuhammad bin Jarir bin Yazid bin Kathiir bin Ghalib at-Tabari, aliyefariki mwaka 310 A.H. Nasi hapa tumetege-mea chapa ya Misri yenye juzuu 30.

2. Al-Kashfu wal-Bayan Anitafsiril-Qur’ani ya Abu Is’haqaAhmad ibnu Ibrahim at-Thaalabiy an-Nisaburiy al-Muqriu,aliyefariki mwaka 427 A.H.

3. Maalimut-Tanziil ya Abu Muhammad Husain bin Mas’udbin Muhammad, maarufu kwa jina la Farrau al-Baghawi as-Shafiy, aliyefariki mwaka 516 A.H. Nasi hapa tumetegemeachapa yake ya Beirut ambayo ina juzuu 4

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:03 AM Page 4

Page 14: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

5

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

4. Al-Kashaf Anihaqaiqit-Tanziil Wauyuunil-Aqawiil FiiWujuhit-Taawiil ya Abu Qasim Mahmudu bin Umar binMuhammad bin Umar al-Khawarazimiy al-Hanafiy al-Muutazaliy az-Zamakhshariy, mwenye lakabu ya Jarullah,aliyefariki mwaka 538 A.H. Nasi hapa tumetegemea chapaya Misri ya mwaka 1948 A.D.

5. Mafatihul-Ghaybi ya Abu Abdillah Muhammad bin Umarbin Husain bin Hasan bin Ali at-Tamimiy al-Bakriy at-Tarstaniy ar-Razi, mwenye lakabu ya Fakhrud-Din, maaru-fu kwa jina la Ibnul-Khatib as-Shafiy, aliyefariki mwaka606 A.H.

6. An’warut-Tanziil Waasrarut-Taawiil ya Kadhi MkuuNasrud-Din (Abul-Khayri), Abdullah bin Umar binMuhammad bin Ali al-Baydhawi as-Shafiy, aliyefarikimwaka 691 A.H. iliyo katika juzuu mbili, iliyochapishwaMisri mwaka 1968 A.D.

7. Al-Jamiu Liahkamil-Qur’an ya Abu Abdillah Muhammadbin Ahmad bin Abubakri al-Ansariy al-Khazrajiy al-Undlusiy al-Qurtubiy, aliyefariki mwaka 761 A.H. iliyokatika juzuu ishirini, iliyochapishwa Misri mwaka 1950A.D.

8. Tafsirul-Qur’ani al-Adhiim ya Hafidh Imadud-Din (Abul-Fidai), Ismail bin Amru bin Kathiir bin Dhaw’u bin Kathiirbin Zar’i al-Baswriy ad-Damashqiy, Ibnu Kathiir, aliyefari-ki mwaka 774 A.H. iliyo katika juzuu tano, iliyochapishwaBeirut.

9. Ad-Duru al-Manthur Fii Tafsiri Bil-Maathur ya HafidhJalalud-Din (Abul-Fadhli), Abdurahman bin Abubakri bin

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:03 AM Page 5

Page 15: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

6

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

Muhammad as-Suyuti, aliyefariki mwaka 911 A.H. iliyokatika juzuu nne, iliyochapishwa Misri.

10. Ruhul-Bayan ya Allamah Sheikh Ismail Haqiyyu al-Barusiyyu, aliyefariki mwaka 1137 A.H. iliyo katika juzuuthelathini, nasi hapa tumetegemea chapa ya Uthmaniya yamwaka 1330 A.H.

11. Ruhul-Maaniy ya Allamah Abul-Fadhli Shihabud-Din,Sayyid Muhammad Al-Alusiy, aliyefariki mwaka 1270A.H., iliyo katika juzuu thelathini, nasi hapa tumetegemeachapa ya Misri ambayo ilipigwa chapa na Al-Muniriyahmwaka 1345 A.H.

12. Tafsirul-Qummiy, maarufu kwa jina la Mahasinut-Taawiiliya Allamah as-Sham Muhammad bin Jamalud-Din al-Qasimiy, aliyefariki mwaka 1322 A.H., iliyo katika juzuukumi na saba, nasi hapa tumetegemea chapa ya Beirut yaIhyaut-Turathil-Arabiy ya mwaka 1415 AH.

Tafsiri hizi zimepangwa kulingana na kipaumbele na umuhimu.

Hivyo kutokana na wajibu wa kiitikadi na jukumu la kisheria, pia kutokanana kuwepo mapungufu ambayo ni lazima tuyazibe kwa kile kinachonasib-iana na ukubwa wa mahitaji ya upungufu huo, na ili kuitikia wito waMwenyezi Mungu Ambaye mara kwa mara ametangaza katika Qur’aniwito wa kuwapenda aali Muhammad (a.s.) aliposema: “Sema: Kwa hayasiombi malipo yoyote kwenu isipokuwa mapenzi katika kizazichangu” (Sura Shura: 23), tumefanya kazi hii iliyobarikiwa ambayoinamimina maji katika bahari ya aali Muhammad (a.s.) iliyojaa na yenyekububujika.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:03 AM Page 6

Page 16: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

7

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

Na ni kutokana pia na umuhimu wa kazi hii katika kuthibitisha maarifa nanafasi ya Ahlul-Baiti (a.s.), ili uthibitisho huo uwe hoja yenye nguvu, nahapo utimie msemo “Nafuata kinywa chako.” Pia ni ili kuthibitisha kwam-ba wao ndio walioainishwa na kukusudiwa na Kitabu cha MwenyeziMungu Mtukufu.

Kazi hii imeendelea toka siku ya kumi na nane ya mfunguo pili mwaka1420 A.H. mpaka siku ya ishirini na tatu ya mfunguo tatu mwaka 1426A.H., lakini kazi hii ilikumbwa na matatizo mengi ikiwa ni pamoja na halikutotulia, kutopatikana rejea, na nyudhuru nyingine mfano wa hizo.

Pamoja na hayo yote tulivumilia kwa kalamu ya mahaba na upendo wetukwa wateule Ahlul-Baiti (a.s.) nyudhuru zote zilizotukabili, tukazama kati-ka kina cha tafsiri na wafasiri ili tutoe humo johari na vito vya aaliMuhammad (a.s.) baada ya kuwa vimefichwa na kufunikwa na vumbi lahistoria kwa sababu za kisiasa na kidunia.

Pia katika ziara yetu ya kitafsiri tumezitambua nafsi za wafasiri, hivyotumegundua kwamba Ibnu Kathir ni ndiye mwenye maradhi makubwa yanafsi na ndiye mwenye chuki kubwa dhidi ya Ahlul-Baiti (a.s.) na wafuasiwao wema. At-Thaalabiy ndiye mwadilifu na mwenye insafu kulikowengine.

Utafiti huu tuliuwakilisha kwenye kongamano la mwaka la Sheikh Tusiyambalo lilifanyika katika Jamuhuri ya Kiislam ya Iran katika Jiji la QumTakatifu, mwaka 1426 A.H. hatimaye ukapata tuzo katika kongamano hiloadhimu.

Haya yote ni sehemu ya fadhila za Mola Wangu na neema kutoka Kwake(s.w.t.), na ni sehemu ya msaada toka katika roho toharifu (a.s.), kwasababu kazi hii ni kwa ajili yao na si kwa ajili ya mwingine.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:03 AM Page 7

Page 17: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

8

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

Mwisho tunainua mikono yote kutoa shukurani kwa Mwenyezi MunguMtukufu, tunamwomba maghufira dhidi ya utelezo na makosa yaliyotokakwetu, kwa sababu umaasumu ni wa wenye nao. Pia tunamtaka msamahamsomaji mpendwa kutokana na makosa yasiyo ya kukusudiwa atakayoy-akuta humu. Na kila sifa njema ni ya Mwenyezi Mungu Mola Mlezi waviumbe wote.

Nizar Hasan2 Mfunguo Nne 1427 A.H.Qum Takatifu

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:03 AM Page 8

Page 18: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

9

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

AHLUL-BAIT (A.S.) NDANI YA TAFSIRI YA IBNU KATHIR,INAYOITWA TAFSIRUL-QUR’AN AL-ÁDHIM

SURAT AL-BAQARAH

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Wale watoao mali zao usiku na mchana kwa siri na dhahiri, wanaujira wao kwa Mola wao Mlezi; wala haitakuwa hofu juu yao walawao hawatahuzunika.” (Sura Al-Baqarah: 274).

Ibnu Abi Hatim amesema: “Ametusimulia Abu Said al-Ashji kwamba:‘Alitupa habari Yahya bin Yaman kutoka kwa Abdul-Wahab bin Mujahidkutoka kwa Ibnu Jubayri kutoka kwa baba yake, amesema: ‘Ali alikuwa nadirhamu nne, akatoa sadaka dirhamu moja usiku na nyingine mchana,nyingine siri na nyingine dhahiri, ndipo ikatremka: “Wale watoao malizao…’”3

Lakini Ibnu Mardawayhi ameipokea kwa njia nyingine kutoka kwa IbnuAbbas kwamba iliteremka kwa ajili ya Ali bin Abutalib.4

3 Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 1, Uk. 281, Chapa ya Beirut ya D?rul-Qalam.4 Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 1, Uk. 281, Chapa ya Beirut ya D?rul-Qalam

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:03 AM Page 9

Page 19: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

10

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

SURAT A’ALI IMRAN

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“…Kila mara Zakariya alipoingia Mihrab hukuta vyakula. Akasema:“Ewe Maryam unatoa wapi hivi. “Akasema: Vinatoka kwa MwenyeziMungu. Hakika Mwenyezi Mungu humruzuku amtakaye bilahesabu.” (Sura Aali Imran: 37).

Al-Hafidh Abu Ya’la amesema: “Ametusimulia Sahlu bin Zanjila amese-ma: “Ametusimulia Abdullah bin Salih amesema: Ametusimulia Abdullahbin Lahi’ah kutoka kwa Muhammad bin al-Mukandir kutoka kwa Jabirkwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alikaa siku kadhaa bilakula chakula mpaka hali hiyo ikawa nzito juu yake. Akaenda kwenyenyumba za wakeze lakini hakupata kwa yeyote chochote, ndipo akaendakwa Fatima na kumwambia: “Ewe mwanangu mpendwa! Je una chochoteninachoweza kula kwani hakika mimi ni mwenye njaa?” Akamjibu:“Wallahi sina ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu kwa haki ya baba yanguna mama yangu.”

Mtume alipotoka, jirani wa Fatima alimletea Fatima vipande viwili vyamkate na finyango ya nyama, akavitwaa na kuviweka ndani ya bakuli lake,akasema: “Wallahi katika hiki nitampa kipaumbele Mtume wa MwenyeziMungu kabla ya nafsi yangu na kabla ya yule aliyopo kwangu.” Japokuwawote walikuwa wanahitajia chakula lakini Fatima alimtuma Hasan auHusein aende kumwita Mtume (s.a.w.w.) naye alikuja. Fatimaakamwambia: “Kwa haki yako na ya mama yangu, Mwenyezi Munguameleta kitu nami nimekihifadhi kwa ajili yako.” Akamwambia: “Kileteewe binti yangu mpendwa.”

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:03 AM Page 10

Page 20: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

11

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

Akamletea bakuli na alipolifunua ghafla akakuta limejaa mikate na nyama,akapatwa na mshangao na akatambua kuwa ni baraka toka kwa MwenyeziMungu. Akamuhimidi Mwenyezi Mungu, akamsalia Mtume na akamk-abidhi chakula hicho Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.).

Mtume (s.a.w.w.) alipokiona alimuhimidi Mwenyezi Mungu na akasema:“Umetoa wapi hivi ewe binti yangu mpendwa? “Akajibu: “Ni kutoka kwaMwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu humpa riziki amtakaye bilahesabu.”

Mtume akamuhimidi Mwenyezi Mungu na kusema: “Kila sifa njema ni yaMwenyezi Mungu Ambaye amekufanya ewe binti yangu mpendwa kifaniwa Seyida wa wana wa Israel (Mariam). Kwani hakika yeye alikuwaaruzukiwapo chochote na Mwenyezi Mungu kisha akiulizwa kakipatawapi husema: Hakika Mwenyezi Mungu humpa riziki amtakaye bilahesabu.”

Kisha Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akampelekea ujumbe Aliaje. Akala Mtume, Ali, Fatima, Hasan, Husein na wakeze wote na Ahlul-Baiti wake wote mpaka wakashiba. Fatima alisema: “Bakuli lilibaki kamalilivyokuwa likiwa limejaa. Hivyo nikawagawia majirani zangu wote naMwenyezi Mungu aliweka humo kheri nyingi na baraka tele. “5

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na Malaika waliposema: Ewe Maryam! Hakika Mwenyezi Munguamekuteua na akakutakasa na akakuteua juu ya wanawake waulimwenguni.” (Sura Aali Imran: 42).5 Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 1, Uk. 310.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:03 AM Page 11

Page 21: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

12

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

Tirmidhi amesema: “Ametusimulia Abu Bakr bin Zanjawihi amesema:Ametusimulia Abdur-Razzaq amesema: ‘Ametusimulia Ma’amar kutokakwa Qatadah kutoka kwa Anas kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w.) alisema: “Yakutosha katika wanawake wa ulimwenguni:Maryam binti Imran, Khadija binti Khuwaylid, Fatima binti Muhammadna Asia mke wa Firaun.” Ameipokea Tirmidhi peke yake na amesema niHadithi Sahihi.6

Na amesema Abdullah bin Abi Jafar Razi kutoka kwa baba yake amesema:“Thabit al-Banani alikuwa akisimulia kutoka kwa Anas kwamba Mtumewa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Wanawake bora ulimwenguni niwanne: Maryam binti Imran, Asia mke wa Firaun, Khadija bintiKhuwaylid na Fatima binti wa Mtume wa Mwenyezi Mungu.” AmeipokeaIbnu Mardawayhi.7

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na watakaokuhoji baada kukufikia elimu hii, waambie: Njoonituwaite watoto wetu na watoto wenu, na wanawake zetu na wanawakewenu, na nafsi zetu na nafsi zenu, kisha tuombe kwa unyenyekevututake laana ya Mwenyezi Mungu iwashukie waongo.” (Sura AaliImran: 61).

Abu Bakr bin Mardawayhi amesema: “Ametusimulia Sulayman binAhmad amesema: Ametusimulia Ahmad bin Daud al-Makkiy amesema:6 Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 1, Uk. 313.7 Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 1, Uk. 313.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:03 AM Page 12

Page 22: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

13

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

Ametusimulia Bashru bin Mahran amesema: Ametusimulia Muhammadbin Dinar kutoka kwa Daud bin Abi Hindi kutoka kwa as-Sha’biy kutokakwa Jabir amesema: “Aqib na Tayib walimwendea Mtume (s.a.w.w.) nayeakawaomba wafanye maapizano ya kuombeana laana, ndipo wakamwahi-di kwamba maapizano hayo yafanyike kesho yake. Mtume akatoka sikuiliyofuata akiwa na Ali, Fatima, Hasan na Husein, kisha akawatumiaujumbe waje kwenye maapizano, wakakataa lakini wakakubali kutoa kodi.Mtume wa Mwenyezi Mungu akasema: “Lau wangekataa (kulipa kodi yaJizya) basi bonde lao lingewaka moto toka mbinguni.” Jabir amesema: Na“Njooni tuwaite watoto wetu na watoto wenu….” iliteremka kwa ajiliyao. Jabir amesema: “…na nafsi zetu na nafsi zenu…” ni Mtume waMwenyezi Mungu na Ali. “…watoto wetu…” ni Hasan na Husein. Na“…. wanawake zetu….” ni Fatima.

Na hivyo ndivyo alivyoipokea al-Hakim kwa maana hiyo katika kitabuchake al-Mustadrak kutoka kwa Ali bin Isa kutoka kwa Ahmad binMuhammad al-Azhariy, kutoka kwa Ali bin Hajar kutoka kwa Ali binMus’har kutoka kwa Daud bin Abi Hindi. Kisha akasema: “Ni Hadithisahihi kwa mujibu wa sharti za Muslim ijapokuwa hajaiandika.8

SURAT NISAIKauli ya Mwenyezi Mungu:

“Enyi mlioamini! msikaribie Sala hali ya kuwa mmelewa mpaka mya-jue mnayoyasema, wala mkiwa na janaba isipokuwa mmo safarini,mpaka muoge.” (Sura Nisai: 43).

8 Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 1, Uk. 319

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 13

Page 23: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

14

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

Imepokewa kutoka kwa Ibnu Mas’ud kwamba baadhi ya Maansari milan-go yao ilikuwa ikitokea msikitini, hivyo baadhi ya nyakati walikuwawakipatwa na janaba na hali hawana maji na hivyo watokapo kutafuta majihuwa hawana njia ila msikitini, ndipo Mwenyezi Mungu akateremsha:“…wala mkiwa na janaba isipokuwa mmo safarini.”

Ama ile aliyoipokea Abu Isa Tirmidhi ambayo ni Hadithi ya Salim bin AbiHafsa kutoka kwa Atiya kutoka kwa Abu Said al-Khudriy ni kwamba ame-sema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Ewe Ali!Haruhusiwi yeyote asiyekuwa mimi na wewe kupatwa na janaba ndani yamsikiti huu.” Ibnu Kathir amesema: “Yenyewe ni Hadithi dhaifu.”9

SURAT AL-MAIDA

Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Enyi mlioamini! Tekelezeni wajibu...”(Surat al-Maida: 1).

Kutoka kwa Zayd bin Ismail as-Saighu al-Baghdadiy amesema:“Ametusimulia Muawiya, yaani Ibnu Hisham, kutoka kwa Isa bin Rashidkutoka kwa Ali bin Budhayma kutoka kwa Akrima kutoka kwa IbnuAbbas, amesema: “Katika Qur’ani hakuna Aya yenye ibara ‘Enyi mlioami-ni!’ isipokuwa Ali ndiye kinara wake na kiongozi wake. Na hakuna Sahabayeyote wa Mtume wa Mwenyezi Mungu ila alifokewa na Qur’ani ila Alibin Abu ??lib, yeye hakufokewa kwa sehemu yoyote ya Qur’ani.10

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Leo nimekukamilishieni dini yenu na kukutimizieni neema yangu na

9 Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 1, Uk. 430 na Uk. 431.10 Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2, Uk. 4, Chapa ya Beirut ya D?rul-Ma’rifa yaMwaka 1412 A.H.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 14

Page 24: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

15

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

nimekupendeleeni Uislamu uwe dini yenu..” (Surat Maida: 3).

Imesemekana kwamba ilimteremkia Mtume wa Mwenyezi Mungualipokuwa safarini kurudi toka Hija yake ya mwisho. Kisha imepokewakwa njia nyingine na Abu Jafar Razi kutoka kwa Rabiu kutoka kwa Anas.Na pia ameipokea Ibnu Mardawayhi kwa njia ya Abu Harun al-Abdiykutoka kwa Abu Said al-Khudriy kwamba ilimtremkia Mtume waMwenyezi Mungu Siku ya Ghadir Khum pale alipomwambia Ali: “Yuleambaye mimi nina mamlaka juu yake basi Ali ana mamlaka juu yake.”

Kisha ameipokea kutoka kwa Abu Huraira na katika maelezo yake nikwamba ilikuwa ni siku ya kumi na nane ya Mfunguo tatu, yaanialipokuwa akirejea kutoka Hija yake ya mwisho.11

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Hakika Walii wenu hasa ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake nawale walioamini ambao husimamisha Swala na hutoa Zaka wakiwawamerukui…..” (Surat al-Maida: 55).

Ametusimulia Abu Said al-Ashji amesema: “Ametusimulia al-Fadhlu binDakin Abu Naim al-Ahwal amesema: ‘Ametusimulia Musa bin Qaysi al-Hadhramiy kutoka kwa Salma bin Kahil amesema: Ali alitoa sadaka peteyake na hali akiwa amerukuu ndipo ikateremka: “Hakika Walii wenuhasa ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake na…..”

Ibnu Jariri amesema: al-Harith amenisimulia amesema: “Abdul-Aziz ame-tusimulia amesema: Ametusimulia Ghalib bin Ubaydullah amesema:

11 Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2, Uk. 15.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 15

Page 25: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

16

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

Nilimsikia Mujahid akisema kuhusu kauli yake (s.w.t.): “Hakika Waliiwenu hasa ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake..” kwamba iliteremkakwa ajili ya Ali bin Abu Talib alipotoa sadaka na hali akiwa amerukuu. NaAbdurazzaq amesema: Alitusimulia Abdul-Wahab bin Mujahid kutokakwa baba yake kutoka kwa Ibnu Abbas kuhusu kauli yake (s.w.t.):“Hakika Walii wenu hasa ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake..”kwamba iliteremka kwa ajili ya Ali bin Abu Talib.

Ibnu Mardawayhi amepokea kwa njia ya Sufyan Thawri kutoka kwa AbuSinan kutoka kwa Dhahak kutoka kwa Ibnu Abbas amesema: “Ali alikuwakatika Sala ndipo muombaji akapita na hali akiwa katika rukuu akampapete yake, ndipo ikateremka: “Hakika Walii wenu hasa ni MwenyeziMungu na Mtume wake…..”

Kutoka kwa Abi Salih kutoka kwa Ibnu Abbas amesema: “Mtume waMwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alikwenda msikitini akawakuta watu wak-isali, baadhi wapo katika rukuu na wengine katika sijda, wangine katikakisimamo na baadhi wameketi, na ghafla akamwona masikini akiomba,ndipo Mtume wa Mwenyezi Mungu akamuuliza: “Je kuna yeyote ameku-pa kitu?” Akasema: “Ndio.” Akamuuliza ni nani? Akasema ni yule aliyes-imama. Mtume akamuuliza: “Alikupa akiwa katika hali gani? “ Akasema:“Akiwa amerukuu.” Mtume akasema: “Yule ni Ali bin Abu Talib.” KishaMtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akatoa takbira huku akisema: “Naanayemtawalisha Mwenyezi Mungu, Mtume wake na wale walioamini,basi ajue hakika kundi la Mwenyezi Mungu ndilo lishindalo.”

Ibnu Kathir amesema: “Njia hii ya upokezi haikutwi na dosari.”12

12 Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2 Uk. 74.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 16

Page 26: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

17

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

SURAT AL-AN’AAM

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na Nuh tulimwongoza zamani na katika kizazi chake, Daud naSulaiman na Ayub na Yusuf na Musa na Harun. Na hivyo ndivyotuwalipavyo wafanya wema. Na Zakaria na Yahya na Isa na Ilyasa,wote walikuwa miongoni mwa watu wema.” (Surat An’aam:84 - 85).

Ibnu Abi Hatim amesema: “Ametusimulia ibnu Yahya al-Askari amesema:Ametusimulia Abdur-Rahman bin Salih amesema: Ametusimulia Ali bin‘?bis kutoka kwa Abdullah bin Atau al-Makkiy, kutoka kwa Abi Harbi binAbil-As’wad amesema: Hajjaj alituma ujumbe kwa Yahya bin Ya’murakasema: “Imenifikia habari kwamba wewe unadai kuwa Hasan na Huseinni kizazi cha Mtume (s.a.w.w.) kwa ushahidi wa Kitabu cha MwenyeziMungu, nami nimekisoma kuanzia mwanzo hadi mwisho na wala sijaupa-ta.” Akasema: Hujasoma Sura al-An’am: “Na Nuh tulimwongoza zamanina katika kizazi chake, Daud na Sulaiman na Ayub na Yusuf na Musana Harun. Na hivyo ndivyo tuwalipavyo wafanya wema. Na Zakariana Yahya na Isa na Ilyasa, wote walikuwa miongoni mwa watuwema.”? Akasema: “Nimesoma.” Yahya akasema: “Basi Isa si kutoka

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 17

Page 27: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

18

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

kizazi cha Ibrahim na hali hana baba.” Akasema: “Umesema kweli.”13

Na wengine wamesema: “Watoto wa binti wanaingia katika kizazi cha mtukutokana na riwaya iliyopo katika Sahih Bukhari kwamba Mtume waMwenyezi Mungu alimwambia Hasan bin Ali (a.s.): “Hakika mwananguhuyu ni Sayyidi…”14

SURAT AL-AN’FAL

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na walipokupangia njama wale waliokufuru ili wakufunge au waku-ue au wakutoe…” (Sura al-An’fal: 30).

Kutoka kwa Ibnu Abbas amesema: “Makuraishi walishauriana usikummoja huko Makka, baadhi yao wakasema: Akiamka mfungeni kwakizuizi. Wakimkusudia Mtume (s.a.w.w.). Na wengine wakasema:Muuweni huku wengine wakisema: Mfukuzeni. Ndipo Mwenyezi Munguakamjuza Nabii wake mkakati huo.

Ali bin Abu Talib akalala usiku huo juu ya kitanda cha Mtukufu Mtume naMtume akatoka mpaka pangoni, mushrikina wakakesha wakimlinda Aliwakidhani ndiye Mtume (s.a.w.w.), walipofika asubuhi walimvamia nawalimuona kuwa ni Ali, Mwenyezi Mungu alizuia njama yao.15

13 Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2 Uk. 160.14 Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2 Uk. 160.15 Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2 Uk. 316.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 18

Page 28: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

19

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

SURAT TAWBA

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“(Tangazo la) Kujitoa Mwenyezi Mungu na Mtume wake kwa walemlioahidiana nao miongoni mwa mushrikina.” (Sura Tawba: 1).

Imam Ahmad amesema: “Ametusimulia Affan amesema: AmetusimuliaHamad kutoka kwa Sammak kutoka kwa Anas bin Malik kwamba Mtumewa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alimtuma pamoja na Abu Bakr kuiba-lighisha Sura Baraa, walipofika Dhulhalifa akasema (s.a.w.w.): “Hapasikuibalighisha ila mimi au mtu atokanaye na Ahlul-Baiti wangu.” Ndipoakamtuma Ali bin Abu Talibi akaibalighishe. Ameipokea pia Tirmidhi kati-ka tafsiri yake.16

Abdullah bin Ahmad bin Hanbal amesema: “Ametusimulia Muhammadbin Sulayman amesema: Ametusimulia Muhammad bin Jabir kutoka kwaSammak kutoka kwa Hasan kutoka kwa Ali (a.s.) amesema: Zilipoteremkakwa Mtume Aya kumi za mwanzo wa Sura Baraa Mtume (s.a.w.w.)alimwita Abu Bakr na kumkabidhi ili akawasomee wakazi wa Makka.Kisha akaniita na kusema: “Mdiriki Abu Bakr na popote utakapomkutachukua Sura kutoka kwake na uende kuwasomea wewe wakazi wa Makka.Nikamkuta Juhfa na nikachukua Sura kutoka kwake. Abu Bakr akarejeakwa Mtume (s.a.w.w.) na kumwambia: “Ewe Mtume wa MweenyeziMungu! Kuna chochote kimeteremka kunikhusu?” Akasema: “Hapanalakini Jibril amenijia na kuniambia: Hapasi kufikisha kwa niaba yako ilawewe mwenyewe au mtu kutokana na wewe.”

16 Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2 Uk. 346.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 19

Page 29: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

20

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

Kutoka kwa Abu Is’haqa kutoka kwa Zayd bin Yathighu amesema: “Baraailipoteremka Mtume wa Mwenyezi Mungu alimtuma Abu Bakr kishabaadae akamtuma Ali akaichukua. Abu Bakr aliporejea alisema: “Je kunachochote kimeteremka kunihusu?” Akasema: “Hapana lakini nimeamrish-wa niibalighishe mimi mwenyewe au mtu kutoka katika Ahlul-Baitiwangu.” (Ali) Akaenda Makka na kuwatangazia watu wake mambomanne: Baada ya mwaka huu mushriku haruhusiwi kuingia Makka, walaharuhusiwi kutufu akiwa uchi, wala hatoingia peponi ila mwislamu, nayule ambaye baina yake na Mtume wa Mwenyezi Mungu kuna mkatababasi mkataba huo utaendelea mpaka mwisho wa muda wake.17

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Je, mnafanya kuwanywesha mahujaji na kuamirisha msikiti mtuku-fu ni sawa na yule aliyemwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwishona akapigana jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu? Hawawi sawambele ya Mwenyezi Mungu na Mwenyezi Mungu hawaongozi watumadhalimu.” (Sura Tawba: 19).

Abdu Razzaq amesema: “Ibnu Uyayna alitupa habari kutoka kwa Ismailkutoka kwa as-Sha’biy amesema: “Iliteremka kwa ajili ya Ali na Abbas.”

Ibnu Jariri amesema: “Talha bin Shayba toka kizazi cha Abdudar, Abbasbin Abdul-Muttalib na Ali bin Abu Talib kila mmoja alijigamba.

17 Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2 Uk. 346.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 20

Page 30: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

21

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

Talha akasema: ‘Mimi ndio mtunza Nyumba funguo zimo mikononimwangu na hata nikitaka nalala humo.’ Abbas akasema: ‘Mimi ndiyemgawa maji na msimamizi wake na hata nikitaka nalala msikitini.’ Aliakasema: ‘Sijui mtasema nini. Bila shaka nimeswali miezi sita kabla yamtu yeyote na mimi ndiye mwanajihadi.’ Ndipo Mwenyezi Munguakateremsha: “Je, mnafanya kuwanywesha mahujaji na kuamirisha msiki-ti mtukufu….”

Na hivyo ndivyo alivyoipokea as-Saddiy.18

SURAT HUD

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Wakasema: Unastaajabu amri ya Mwenyezi Mungu? Rehema yaMwenyezi Mungu na baraka zake iko juu yenu enyi watu wa nyumbahii. Hakika Yeye ndiye Mhimidiwa Mtukuzwa.” (Sura Hud: 73).

Amesema: “Imethibiti ndani ya Sahih mbili kwamba walisema:Tumeshajua namana ya kukusalimia basi ni vipi tutakavyokusalia eweMtume wa Mwenyezi Mungu? Akasema:Semeni:“Ewe Mwenyezi Mungu! Mrehemu Muhammad na aali Muhammad kamaulivyomrehemu Ibrahim na aali Ibrahim. Na mbariki Muhammad na aaliMuhammad kama ulivyombariki Ibrahim, hakika Wewe ni MhimidiwaMsifiwa).”19

18 Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2 Uk. 355.19 Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2 Uk. 468.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 21

Page 31: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

22

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

SURAT IBRAHIM

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Je hukuwaona wale waliobadilisha neema ya Mwenyezi Mungu kwakufuru na wakawafikisha watu wao katika nyumba ya maangamizo.”(Surat Ibrahim: 28).

Ibnu Abi Hatim amesema: “Alitusimulia baba yangu alisema:Ametusimulia Ibnu Nufayli alisema: Nilisoma mbele ya Ma’qal kutokakwa Ibnu Abi Husein kwamba: Ali bin Abu Talib alisimama na kusema:“Oh, yeyote aniulize kuhusu Qur’ani, na wallahi lau ningemjua leo yeyoteaijuaye kuliko mimi hata kama yupo ng’ambo ya bahari basi ningemfua-ta.” Abdullah bin al-Kawau akasimama na kusema: “Ni akina nani walewaliobadilisha neema ya Mwenyezi Mungu kwa kufuru na wakawafikishawatu wao katika nyumba ya maangamizo?” Akasema: “Ni mushrikina tokakwa makuraishi, walijiwa na neema ya Mwenyezi Mungu ambayo ni Imaniwakaibadili neema ya Mwenyezi Mungu kwa ukafiri na ndipo wakawafik-isha watu wao katika nyumba ya maangamizo.”20

SURAT AN-NAHLIKauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na hatukutuma kabla yako ila wanaume tuliowapa wahyi. Basiwaulizeni wenye ukumbusho ikiwa nyinyi hamjui.” (Surat an-Nahli:43).

20 Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2 Uk. 558

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 22

Page 32: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

23

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

Abu Jafar al-Baqir (a.s.) alisema: “Sisi ndio wenye ukumbusho.”21

Ibnu Kathir amesema: “Ulamaa wa nyumba tukufu ya Mtume waMwenyezi Mungu (s.a.w.w.) ndio maulamaa bora kwani wao ndiowaliokuwa katika Sunna ipasavyo, kama vile Ali, Ibnu Abbas, watoto waAli Hasan na Husein, Muhammad bin al-Hanafiyya, Ali bin HuseinZaynul-Abidin, Ali bin Abdullah bin Abbas, Abu Jafar al-Baqir ambaye niMuhammad bin Ali bin Husein, na Mwanae Ja’far na mfano wao miongo-ni mwa wale wenye kushikamana vilivyo na kamba imara ya MwenyeziMungu na njia Yake nyoofu…..”22

SURAT ISRAI

Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Na mpe jamaa wa karibu haki yake namaskini na mwana njia, wala usifanye ubadhirifu.” (Sura Israi: 26).

Al-Hafidh Abu Bakr al-Bazzar amesema: Ametusimulia Ibad bin Ya’kubamesema: Ametusimulia Abu Yahya at-Tamimiy amesema: AmetusimuliaFudhaylu bin Marzuq kutoka kwa Atiya kutoka kwa Abu Said amesema:Ilipoteremka: “Na mpe jamaa wa karibu haki…..” Mtume wa MwenyeziMungu (s.a.w.w.) alimwita Fatima na kumpa Fadak.23 Ibnu Kathir amese-ma: Na rai ya karibu zaidi ni kwamba yenyewe ni miongoni mwa uzushiwa marafidhi. Na Mwenyezi Mungu ndiye ajuaye.24

21 Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2 Uk. 591 na 592.22 Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2 Uk. 591 na 592.23 Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2, Uk. 34.24 Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2, Uk. 34. – Sielewi mpaka sasa ni kwa nini IbnuKathir umajununi wake unapanda pale anapoiona fadhila na heshima ya Ahlul-Baiti, na daima anajaribu kuidhoofisha ile iliyo mashuhuri, bila shaka si chochotebali ni uadui wake kwa Ahlul-Baiti (a.s.). Kisha riwaya hiyo wafasiri wakubwawameitaja kabla yetu kama vile al-Haskaniy katika kitabu chake Shawahidut-Tanziil.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 23

Page 33: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

24

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

SURAT MUUMINUNA

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Basi litakapopulizwa parapanda, hapo hautakuwapo ujamaa bainayao siku hiyo, wala hawataulizana.” (Sura Muuminuna: 101).

Imam Ahmad amesema: “Ametusimulia Abu Sa’id huria wa Bani Hashimamesema: Ametusimulia Abdullah bin Ja’far amesema: ‘AmetusimuliaUmmu Bakri binti ya al-Musawwar bin Makhrimah kutoka kwa Abdullahbin Abi R?fi’u kutoka kwa al-Musawwar amesema: Mtume wa MwenyeziMungu (s.a.w.w.) alisema:

“Fatima ni pande la nyama yangu hunisononesha yale yanay-omsononesha, na hunifurahisha yale yanayomfurahisha. Na haki-ka kila nasaba itakatika Siku ya Kiyama ila nasaba yangu nasababu yangu na ukwe wangu.”

Hadithi hii ina asili katika Sahih mbili (Muslim na Bukhari) kutoka kwa al-Musawwar kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema:“Fatima ni pande la nyama yangu, hunikarahisha lile linalomkarahisha nahuniudhi lile linalomuudhi.”25

25 Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 3 Uk. 222.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 24

Page 34: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

25

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

SURAT SHUA’RAUKauli ya Mwenyezi Mungu: “Na uwaonye jamaa zako wa karibu.”(Sura Shu’arau: 214).

Kutoka kwa Ibnu Abbas kutoka kwa Ali bin Abu Talib (a.s.), amesema:“Ilipoteremka Aya hii kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.): “Nauwaonye jamaa zako wa karibu,” Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.)alisema: ‘Nikatambua kwamba nitakapowadhihirishia jamaa zangu jambohili nitakumbana na nisiyoyapenda toka kwao. Nikanyamaza mpakaaliponiijia Jibril na kuniambia: ‘Ewe Muhammad! Hakika usipofanyaunayoamrishwa Mola wako Mlezi atakuadhibu. Ewe Ali! Tuandalie pishila chakula uweke mguu wa mbuzi na utujazie bilauri ya maziwa, kishanikusanyie watoto wa Abdul-Mu??alib.’ Nikatekeleza, wakakusanyikakwake na wakati huo walikuwa wanaume arobaini, amezidi mtu mmoja auamepungua mmoja, humo walikuwemo ami zake: Abu Talib, Hamza,Abbas na Abu Lahabi kafiri khabithi.

Nikawapelekea sinia la chakula, na ndipo Mtume wa Mwenyezi Munguakachukua kipande kidogo cha nyama akakikata kwa meno yake kishaakakitupia pembezoni mwa sinia, akasema: ‘Kuleni kwa Jina la MwenyeziMungu.’

Kaumu wakala mpaka wakatosheka na wala sikuona ila sehemu ambazomikono yao ilikuwa ikimega. Wallahi, chakula nilichowapa wote ni chakuweza kula mtu mmoja. Kisha Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.)akasema: ‘Wape watu kinywaji ewe Ali.’ Nikaja na ile bilauri wakanywampaka wakatosheka wote. Wallahi, kilikuwa ni kinywaji cha kutoshekamtu mmoja.

Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alipotaka kuwaeleza Abu Lahabialimtangulia kuongea, akasema: ‘Jamaa yenu amewaroga kwa karamu hii.’Ndipo kaumu wakatawanyika na wala Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w.) hakufanikiwa kuwaeleza. Ilipowadia siku iliyofuata Mtume waMwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: ‘Ewe Ali! tuandalie chakula na kiny-

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 25

Page 35: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

26

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

waji mfano wa kile ulichoandaa jana…..’ Nikatekeleza kisha nikawaku-sanya, naye Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akafanya kama alivy-ofanya jana, wakala mpaka wakatosheka, nikawaletea bilauri wakanywampaka wote wakatosheka. Wallahi, chakula na kinywaji nilichowapa woteni cha kuweza kutosheka mtu mmoja.

Kisha Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akaongea kwa kusema:‘Enyi wana wa Abdul-Mu??alib! Hakika mimi wallahi simjui kijana wakiarabu aliyewaletea jamaa zake kitu bora kuliko hiki nilichowaletea.Hakika mimi nimewaletea kheri ya dunia na akhera. Na hakika MwenyeziMungu ameniamuru niwalinganie kwayo, basi ni nani kati yenu atanisaidiakatika jambo hili, awe ndugu yangu na kadha wa kadha.’

Watu wote wakakaa kimya, nikasema na hali mimi nikiwa ndiye mdogokiumri kuliko wote, mwenye tongotongo machoni (mtoto) kuliko wote,mwenye tumbo kubwa kuliko wote na mwenye muundi wenye majerahamadogo kuliko wote: ‘Mimi ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu nakuwawaziri wako.’ Akaishika shingo yangu kisha akasema (s.a.w.w.): ‘Hakikahuyu ni ndugu yangu na kadha wa kadha, msikilizeni na mumtii.’ Kaumuwakaongea na hali wakicheka na wakimwambia Abu Taalib: ‘Bila shakaamekuamuru umsikilize na kumtii mwanao.’”26

26 Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2, Uk. 302. Ibnu Kathir anaielezea habari hiikwa kusema: “Kaipokea kwa mtiririko huu Abdul-Ghaffar bin al-Qasim bin AbiMariam pekee, naye ni muongo asiyefuatwa na ni Shia.” Maneno kama haya kuto-ka kwa Ibnu Kathir ni ya ajabu, na inashangaza kuona anajiita aalimu na hali yeyehajui bali anaharakia kuwahukumu wenzake. Hajui kwamba al-Hafidh al-Kunjiyas-Shafi’iyyu aliyefariki mwaka 658 A.H. ametaja tukio hili kwa njia mbili katikakitabu chake Kifayatut-Talib Uk. 304 mlango wa 51, na katika njia zote mbilihajataja jina la Abdul-Ghaffar bin al-Qasim bin Abi Layla, hii ni mosi. Pili: Tukiohili ni mashuhuri bali ni mutawatiri kwani limetajwa na wasimulizi wakubwa nawanahistoria wakubwa, miongoni mwao ni: Tabari katika kitabu chake cha histo-ria Juz. 2, Uk. 62, al-Muttaqiy al-Hindiy katika kitabu Kanzul-Ummal Juz. 6, Uk.392 na 397, Ahmad bin Hanbal katika al-Musnad Juz. 1, Uk. 195, al-Haythamiykatika Majmauz-Zawaid Juz. 8, Uk. 302, Tabari katika ar-Riyadhun-Nadhrah Juz.2, Uk. 167, na wengineo.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 26

Page 36: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

27

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

SURAT AHZAB

Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Na kama hamuwajui baba zao, basi nindugu zenu katika dini.” (Sura Ahzab: 5).

Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alimwambia Ali (a.s.): “Wewewatokana na mimi na mimi natokana na wewe.”27

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na akawarithisheni nchi yao na majumba yao na mali zao, na nchimsiyoikanyaga, na Mwenyezi Mungu ni Mwenye uwezo juu ya kilakitu.” (Surat Ahzab: 27).

Amesema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alimwacha IbnuUmmu Maktum Madina na akamkabidhi bendera Ali bin Abu Talib(a.s.).28

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea ucha-fu, enyi watu wa nyumba ya Mtume, na kuwatakasa kabisa kabisa.”(Sura Ahzab: 33).

27 Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2 Uk. 399.28 Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2 Uk. 408.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 27

Page 37: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

28

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

Kutoka kwa Anas bin Malik amesema kwamba: “Hakika Mtume waMwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alikuwa akipitia nyumbani kwa Ali muda wamiezi sita kila alipotoka kwenda kusali Sala ya alfajri, na alikuwa akisema:‘Swala enyi Ahlul-Baiti. Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anatakakuwaondolea uchafu, enyi watu wa nyumba ya Mtume, na kuwatakasakabisa kabisa.’” Ameipokea Tirmidhi kutoka kwa Abdu bin Hamid kutokakwa Affan, amesema: “Ni nzuri Gharib.”29

Ibnu Jarir amesema: “Ametusimulia Waki’u kutoka kwa Abu Is’haqa, ame-sema: Abu Daud amenipa habari kutoka kwa Abul-Hamrau, amesema:“Niliishi Madina miezi sita bila kutoka zama za Mtume wa MwenyeziMungu (s.a.w.w.), nilimwona Mtume kila ichomozapo alfajiri akiendakwenye mlango wa Ali na Fatima (a.s.) na kusema: ‘Sala Sala, Hakika simengineyo Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu enyi watu wanyumba ya Mtume, na kuwatakasa kabisa kabisa.”’30

Al-Awza’i amesema: “Ametusimulia Shaddad Abu Ammar amesema:“Niliingia kwa Wathila bin al-Asqau nikamkuta ameketi na baadhi yawatu, ndipo walipomtaja Ali na kumkashifu, nami nikamkashifu pamojanao, walipoondoka akasema (Wathila): ‘Hivi kweli umethubutukumkashifu huyu?’ Nikasema wamemkashifu ndipo nami nikamkashifupamoja nao. Akasema: ‘Nikupe habari za yale niliyoyaona toka kwaMtume wa Mwenyezi Mungu?’ Nikasema ndio. Akasema: Nilikwendakwa Fatima (a.s.) kumuulizia Ali (a.s.). Fatima akanijibu kwambaameelekea kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.), nikakaa namngo-jea mpaka Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alipokuja akiwa pamo-ja na Ali, Fatima, Hasan na Husain (a.s.) amemshika kila mmoja waomkono, akaingia kisha akawasogeza Ali na Fatima na kuwakalisha mbeleyake, na akamkalisha Hasan na Husein kila mmoja juu ya paja lake, kishaakawafunika nguo yake na kusoma Aya hii: “Hakika si mengineyo

29 Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2 Uk. 413.30 Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2 Uk. 413.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 28

Page 38: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

29

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu, enyi watu wa nyumba yaMtume, na kuwatakasa kabisa kabisa.” Na akasema: ‘Ewe MwenyeziMungu! Hawa ndio watu wa nyumba yangu, na watu wa nyumba yangundio wenye haki zaidi (kuliko mtu baki).’”31

Imam Ahmad amesema: Imepokewa kutoka kwa Ummu Salama kwambaalikuwa akitaja kuwa Mtume (s.a.w.w.) alikuwa nyumbani kwake ndipoakaja Fatima akiwa na chungu chenye uji na kuingia nacho kwa Mtume.Mtume akamwambia mwite mumeo na wanao. Alikuja Ali, Hasan naHusein wakaingia kwa Mtume na wakaketi wakinywa uji huo na haliMtume akiwa juu ya kitanda chake kilichotandikwa kishamia chaKhaibari. Nikiwa chumba kingine nasali ghafla Mwenyezi Mungualiteremsha Aya hii: “Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anatakakuwaondolea uchafu, enyi watu wa nyumba ya Mtume, na kuwatakasakabisa kabisa.” Mtume (s.a.w.w.) akashika pande za kishamia akawafuni-ka, kisha akatoa mkono wake akauelekeza mbinguni kisha akasema: ‘EweMwenyezi Mungu hawa ndio Ahlul-Baiti wangu na watu makhsusi kwan-gu. Waondolee uchafu na watakase kabisa kabisa.’ Nikaingiza kichwachumbani kwa Mtume na kumwambia: Je na mimi ni pamoja nanyi eweMtume wa Mwenyezi Mungu? Akasema: ‘Hakika wewe upo katika kheri.Bila shaka wewe upo katika kheri. ‘“32

Ibnu Jarir amesema: Imepokewa kutoka kwa A’mash kutoka kwa Hakimbin Sa’d amesema: Tulimtaja Ali bin Abu Talib (a.s.) mbele ya UmmuSalama, akasema: “Ndani ya nyumba yangu ndimo ilimoteremka: “Hakikasi mengineyo Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu, enyi watuwa nyumba ya Mtume, na kuwatakasa kabisa kabisa.”

“Ummu Salama akasema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alikujanyumbani kwangu, akaniambia usimpe yeyote idhini ya kuingia. Akaja

31 Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2 Uk. 413.32 Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2 Uk. 414.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 29

Page 39: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

30

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

Fatima sikuweza kumzuia na baba yake, kisha akaja Hasan sikuwezakumzuia asiingie kwa babu yake na mama yake. Akaja Husein sikuwezakumzuia asiingie kwa babu yake na mama yake. Kisha akaja Ali (a.s.)sikuweza naye kumzuia, walipokusanyika Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w.) akawafunika kwa kishamia alichokuwa amejitanda, kisha akase-ma: ‘Hawa ndio Ahlul-Baiti wangu. Waondolee uchafu na watakase kabisakabisa.’ Ndipo ikateremka Aya hii walipokusanyika juu ya busati.Nikasema ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Na mimi? Ummu Salamaanasema: Wallahi hakukubali bali alisema: Hakika wewe utaelekea katikakheri.”33

Ibnu Jarir amesema: Ametusimulia Abu Karib kutoka kwa Abdullah binWahab bin Zam’at, amesema: Ummu Salama alinipa habari kwamba:“Hakika Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) aliwakusanya Ali,Fatima, Hasan na Husein (a.s.) kisha akawafunika nguo yake, kishaakaelekea kwa Mwenyezi Mungu na kusema: ‘Hawa ndio Ahlul-Baitiwangu.’ Ummu Salama akasema: ‘Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu!(Allah) Amenijumuisha pamoja nao?’ akasema (s.a.w.w.): ‘Wewe nimiongini mwa wake zangu.”34

Imepokewa kutoka kwa Ummu Salama amesema: Siku moja Mtume akiwanyumbani kwangu nilimwambia mfanyakazi: “Hakika Ali na Fatima wakomlangoni.” Mtume wa Mwenyezi Mungu akaniambia: “Simama nawapishe Ahlul-Baiti wangu.” “Nikaketi kando kidogo pembezoni mwanyumba.” Wakaingia Ali na Fatima wakiwa na Hasan na Husein (a.s.)wakiwa bado watoto wadogo, akawachukua watoto na kuwaweka mapa-jani mwake na akawabusu, akamshika Ali kwa mkono wake mmoja naFatima kwa mkono wake mwingine, akambusu Fatima na kisha Ali,akawafunika shuka jeusi na kusema: “Ewe Mwenyezi Mungu tuleteKwako na si motoni, mimi na Ahlul-Baiti wangu.”35

33 Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2 Uk. 414.34 Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2 Uk. 414.35 Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2 Uk. 414.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 30

Page 40: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

31

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

Kutoka kwa Ibnu Abi Hatim kutoka kwa al-Awamu bin Hawshab, kutokakwa ami yake amesema: Niliingia na baba yangu kwa Aisha, nikamuulizakuhusu Ali (a.s.). Aisha akasema: “Umeniuliza kuhusu mtu aliyekuwaakipendwa sana na Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) kuliko watuwote, na alikuwa mume wa binti yake aliyekuwa akipendwa sana naMtume wa Mwenyezi Mungu. Nilimuona Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w.) akiwa amewaita Ali, Fatima, Hasan na Husein, akawafunikanguo na kisha akasema: ‘Ewe Mwenyezi Mungu! hawa ndio Ahlul-Baitiwangu, hivyo waondolee uchafu na uwatakase kabisa.’ Nikasogea na kuse-ma: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Je mimi ni miongoni mwa Ahlul-Baiti wako? Akasema: ‘Kaa pembeni, hakika wewe upo katika kheri.’”36

Ibnu Jarir amesema: Imepokewa kutoka kwa Atiyyah kutoka kwa Saidamesema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Aya hii“Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu,enyi watu wa nyumba ya Mtume, na kuwatakasa kabisa kabisa.” iliterem-ka kwa ajili ya watu watano: Mimi, Ali, Fatima, Hasan na Husein.”37

Ametusimulia Bakir bin Mismar amesema: Nilimsikia Amir bin Sa’dakisema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema pindi wahyiulipomshukia, akamchukua Ali na wanae wawili na Fatima, akawafunikanguo yake kisha akasema: “Ewe Mola Mlezi! hawa ndio ndugu zangu naAhlul-Baiti wangu.”38

Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Hakika Mwenyezi Mungu na malaika wakewanamswalia Nabii. Enyi ambao mmeamini! Mswalieni na mumsalimukwa salamu.” (Sura Ahzab: 56).

Bukhari katika kutafsiri Aya hii amesema: Imepokewa kutoka kwa Ka’abbin Ájrah amesema: Palisemwa: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu!

36 Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2 Uk. 414.37 Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2 Uk. 415.38 Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2 Uk. 415

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 31

Page 41: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

32

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

Kukutolea salamu tumeshajua basi ni ipi namna ya kukusalia? Akasema(s.a.w.w.): “Semeni:

?????? ???? ??? ????? ???? ?? ????? ??? ????? ??? ?? ??????????? ???? ????. ?????? ???? ??? ????? ???? ?? ????? ???

????? ??? ?? ??????? ???? ???? ????.

‘Ewe Mwenyezi Mungu! Mrehemu Muhammad na aaliMuhammad kama ulivyowarehemu aali Ibrahim, hakika Wewe niMhimidiwa Msifiwa. Na mbariki Muhammad na aali Muhammadkama ulivyowabariki aali Ibrahim, hakika Wewe ni MhimidiwaMsifiwa.’”39

Imam Ahmad amesema: Imepokewa kutoka kwa al-Hakam amesema:“Nilimsikia Ibnu Abi Layla akisema: Kaab bin Ajrah alikutana na mimi nakuniambia: Je nikupe zawadi? Siku moja alikuja Mtume wa MwenyeziMungu, nasi tukamuuliza, tukasema: Kukutolea salamu tumeshajua basi niipi namna ya kukusalia? Akasema (s.a.w.w.): “Semeni:

?????? ???? ??? ????? ???? ?? ????? ??? ????? ??? ?? ??????? ???? ????. ?????? ???? ??? ????? ???? ?? ????? ???

????? ??? ?? ??????? ???? ???? ????.

‘Ewe Mwenyezi Mungu! Mrehemu Muhammad na aaliMuhammad kama ulivyowarehemu aali Ibrahim, hakika Wewe niMhimidiwa Msifiwa. Na mbariki Muhammad na aali Muhammadkama ulivyowabariki aali Ibrahim, hakika Wewe ni MhimidiwaMsifiwa.’”40

39 Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2 Uk. 432.40Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2 Uk. 432.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 32

Page 42: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

Bukhari amesema: “Ametusimulia Abdullah bin Yunus kutoka kwa AbuSaid al-Khudriy amesema: Tulimwambia ewe Mtume wa MwenyeziMungu! Tumeshajua namna ya kukutolea salamu basi ni ipi namana yakukusalia? Akasema: “Semeni:

?????? ???? ??? ????? ???? ?????? ??? ????? ??? ?? ???????.? ???? ??? ????? ???? ?? ????? ??? ????? ??? ?? ??????? ????

???? ????.

‘Ewe Mwenyezi Mungu! Mrehemu Muhammad mja Wako naMtume Wako kama ulivyowarehemu aali Ibrahim. Na mbarikiMuhammad na aali Muhammad kama ulivyowabariki aaliIbrahim, hakika Wewe ni Mhimidiwa Msifiwa.’”41

Abdurahman bin Abu Layla, amesema: Kutoka kwa Ka’ab bin Ajrah, ame-sema: Ilipoteremka: “Hakika Mwenyezi Mungu na malaika wake wanam-swalia Nabii. Enyi ambao mmeamini! Mswalieni na mumsalimu kwa sala-mu.” Tulisema: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Tumeshajua namna yakukutolea salamu ni ipi namana ya kukusalia? Mtume akasema: ‘’Semeni:

?????? ???? ??? ????? ???? ?? ????? ??? ????? ??? ??????? ?????? ??????? ???? ???? ????. ? ???? ??? ????? ???? ?? ????? ???

????? ??? ??????? ???? ?? ??????? ???? ???? ????.

‘Ewe Mwenyezi Mungu! Mrehemu Muhammad na aaliMuhammad kama ulivyomrehemu Ibrahim na aali Ibrahim, haki-ka Wewe ni Mhimidiwa Msifiwa. Na mbariki Muhammad na aaliMuhammad kama ulivyombariki Ibrahim na aali Ibrahim, hakikaWewe ni Mhimidiwa Msifiwa.’’’42

33

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

41Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2 Uk. 432.42 Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2 Uk. 433.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 33

Page 43: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

Kutoka kwa Ibnu Mas’ud al-Ansariy alisema: “Mtume wa MwenyeziMungu alikwenda na kutukuta tumeketi katika baraza la Sa’d bin Ubada.Bushru bin Sa’d akamwambia: Mwenyezi Mungu ametuamuru tukutoleesalamu ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, basi ni vipi tutakavyokusalia?Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akakaa kimya mpaka tukatamanikwamba asingemuuliza. Kisha akasema (s.a.w.w.): “Semeni:

?????? ???? ??? ????? ???? ?? ????? ??? ????? ??? ?? ???????. ????? ??? ????? ???? ?? ????? ??? ????? ??? ?? ??????? ??

???????? ???? ???? ????.

‘Ewe Mwenyezi Mungu! Mrehemu Muhammad na aaliMuhammad kama ulivyowarehemu aali Ibrahim. Na mbarikiMuhammad na aali Muhammad kama ulivyowabariki aali Ibrahimkatika walimwengu, hakika Wewe ni Mhimidiwa Msifiwa.’’’

Pia ameipokea Abu Daud, Tirmidhi, Nasai na Ibnu Jariri kutoka katikahadithi ya Malik. Tirmidhi amesema: Ni nzuri na sahihi.43

SURAT YASIN

Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Ikasemwa: Ingia peponi! Akasema: Laitiwatu wangu wangejua. Jinsi Mola wangu alivyonighufuria na akani-fanya katika waheshimiwa.” (Sura Yasin: 26 - 27).

Al-Hafidh Abu Qasim Tabaraniy amepokea kwamba: “Alitusimulia Huseinbin Is’haq at-Tusturiy kutoka kwa Ibnu Abi Najihi kutoka kwa Mujahidkutoka kwa Ibnu Abbas (a.s.) kutoka kwa Mtume (s.a.w.w.) kwamba alise-ma: “Vinara ni watatu: Kinara kuelekea kwa Musa (a.s.) ni Yoshua binNun. Kinara kuelekea kwa Isa (a.s.) ni yule aliyezungumziwa na SuraYasin, na kinara kuelekea kwa Muhammad (s.a.w.w.) ni Ali bin Abu Talib(a.s.).”

34

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

43 Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2 Uk. 433.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 34

Page 44: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

Hakika yenyewe ni Hadithi isiyokubalika haijulikani ila kwa njia yaHusein al-As’haq naye ni Shia asiyefuatwa.44

SURAT AS-SSAFFAT

Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Amani kwa Ilyasin.” (Sura as-Saffat:130).Ibnu Mas’ud amesema: Yaani Aali Muhammad (s.a.w.w.).45

SURAT AS-SHURA

Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Sema: Kwa haya siwaombi malipo yoyotekwenu isipokuwa mapenzi kwa ndugu...” (Sura as-Shura: 23).

Kutoka kwa as-Sadiy, kutoka kwa Abu Daylam, amesema: “Alipoletwa Alibin Husein na hali ni mateka na kusimamishwa katika barabara kuu yaDamascus alisimama mzee mmoja kati ya watu wa Sham, akasema: “Kilasifa njema ni ya Mwenyezi Mungu ambaye amewauwa na kuwang’oeni nakung’oa mzizi wa fitina.” Ali bin Husein akasema: ‘Umewahi kusomaQur’ani?’ akajibu ndio. Akasema (a.s.): ‘Umewahi kusoma Aali HaaMiim?’ Akajibu nimewahi kusoma Qur’ani na sijawahi kusoma Aali HaaMiim. Akasema (a.s.): ‘Umewahi kusoma: “Sema: Kwa haya siwaombimalipo yoyote kwenu isipokuwa mapenzi kwa ndugu...”’ Mzee akasema:‘Nyinyi ndio hao?’ Akasema (a.s.): ‘Naam ndio sisi.’46

Ibnu Abi Hatim amesema: Ametusimulia Ali bin Husein amesema:“Ametusimulia mtu aliyemtaja jina: Ametusimulia Husein al-Ashqar kuto-ka kwa Qaysi kutoka kwa al-A’mash, kutoka kwa Said bin Jubair, kutokakwa Ibnu Abbas amesema: Ilipoteremka: “Sema: Kwa haya siwaombimalipo yoyote kwenu isipokuwa mapenzi kwa ndugu...” walimuuliza: Ewe

35

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

44 Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 2 Uk. 486.45 Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 4 Uk. 21.46 Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 4 Uk. 101.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 35

Page 45: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) ni akina nani hawa ndugu ambaoMwenyezi Mungu ameamuru kuwapenda? Akasema: “ Fatima na kizazichake.”47

Imepokewa kutoka kwa Zayd bin Arqam amesema: Mtume wa MwenyeziMungu (s.a.w.w.) alisema: “Hakika mimi ni mwenye kuwaachia kati yenukile ambacho lau mkishikamana nacho katu hamtapotea baada yangu,kimojawapo ni kitukufu kuliko kingine: Kitabu cha Mwenyezi Mungukamba iliyonyooka toka mbinguni hadi aridhini. Na kingine ni kizazichangu watu wa nyumba yangu, na havitoachana mpaka vinikute kwenyehodhi, basi angalieni ni jinsi gani mtakavyobaki navyo.”48

Kutoka kwa Jabir bin Abdillah amesema: “Nilimuona Mtume waMwenyezi Mungu Siku ya Arafa akiwa juu ya ngamia wake al-Qas’wauakiwahutubia watu, nikamsikia akisema: “Enyi watu! Hakika miminimeacha kati yenu kile ambacho lau mkishikamana nacho hamtapotea:Kitabu cha Mwenyezi Mungu na kizazi changu watu wa nyumbayangu.”49

Kutoka kwa Abu Dhari al-Ghaffariy alisema huku akiwa ameshikilia mlan-go: Enyi watu! Anayenitambua basi ameshanitambua na asiyenitambuabasi mimi ni Abu Dhari, nilimsikia Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.)akisema: “Hakika mfano wa Ahlul-Baiti wangu kwenu nyinyi ni sawa nasafina ya Nuh (a.s.) aliyeipanda aliokoka.”50

36

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

47 Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 4 Uk. 102.48 Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 4 Uk. 102.49 Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 4 Uk. 102.50 Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 4, Uk. 102. Lakushangaza sana ni kwamba IbnuKathir anaizingatia Hadithi mashuhuri kama hii kuwa ni dhaifu. Sijui amesahau auamejisahaulisha Hadithi ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.): “Ardhi hai-japata kumbeba wala mbingu haijapata kumfunika mtu mkweli kuliko Abu Dharial-Ghaffariy.”

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 36

Page 46: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

SURA AD-DUKHAN

Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Mbingu na ardhi hazikuwalilia; walahawakupewa muda.” (Sura ad-Dukhan: 29).

Ibnu Abi Hatim amesema: “Ametusimulia Ali bin Husein amesema:Ametusimulia Abdusalami bin Asim, amesema: Ametusimulia Ishaq binIsmail, amesema: Ametusimulia al-Mustawridu bin Sabiq kutoka kwaUbaydul-Maktabi kutoka kwa Ibrahim, amesema: “Dunia haijamlilia yey-ote tangu kuumbwa kwake ila wawili.” Nikamwambia vipi? Akasema:“Inapatwa na wekundu na kuwa kama ua waridi. Hakika Yahya binZakariya alipouawa mbingu ilipatwa na wekundu na ikadondosha mvua yadamu. Na hakika Husein bin Ali (a.s.) alipouwawa mbingu ilipatwa nawekundu.”51

Ametusimulia Jarir kutoka kwa Yazid bin Abi Ziyad amesema:“Alipouwawa Husein bin Ali (a.s.) pande zote za mbingu zilipatwa nawekundu muda wa miezi minne. Na wekundu wake ndio kulia kwake.”52

Na wametaja katika habari za mauaji ya Husein (a.s.) kwamba siku hiyohakuna jiwe lililoinuliwa au kugeuzwa ila chini yake kulikutwa damunzito, na kwamba jua lilipatwa, mbingu ikawa nyekundu na ikanyeshamvua ya mawe.53

37

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

51 Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 4 Uk. 127.52 Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 4 Uk. 127.53 Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 4 Uk. 127. Ibnu Kathir katika habari hii anase-ma: “Dhahiri ni kwamba habari hii ni miongoni mwa uzushi wa mashia na uongowao ili wakuze jambo….”. Nashangaa ni wepesi ulioje ulionao katika kuwatuhu-mu wengine? Na hilo tunakujibu nawe ndio wapasa zaidi kuwa muongo, kwasababu si sisi pekee tuliopokea hadithi hii, hiyo ni mosi. Pili: Wewe mwenyewekatika tafsiri yako umepokea kwamba: Mbingu humlilia muumini siku arubaini. Jewashakia Husein kuwa bwana wa waumini na kinara wao duniani na akhera baadaya babu yake, mama yake, baba yake na kaka yake? Tatu: Kwa nini wazikubalihabari hizi zihusishwapo na Yahya bin Zakariya lakini si pale zinapomhusu Huseinmtoto wa binti ya bwana wa Manabii na Mawasii?

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 37

Page 47: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

SURAT AL-AHQAF

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Enyi watu wetu muitikieni Mwitaji wa Mwenyezi Mungu namuaminini, atakusameheni madhambi yenye kuumiza.” (Sura al-Ahqaf: 31).

Imepokewa kutoka kwa Ibnu Mas’ud kwamba alisema: “Nilikuwa pamojana Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) usiku ndipo ukamfikia msafarawa majini, akavuta pumzi. Nikamwambia una nini ewe Mtume waMwenyezi Mungu? Akasema: “Ninajiomboleza mwenyewe ewe IbnuMas’ud.” Nikamwambia ainisha Khalifa. Akauliza nani? NikamwambiaAbu Bakr. Akakaa kimya, kisha ukapita muda kadhaa akavuta tena pumzi,nikamwambia kwa haki ya baba yangu na mama yangu, una nini eweMtume wa Mwenyezi Mungu? Akasema: “Ninajiomboleza mwenyeweewe Ibnu Mas’ud.” Nikamwambia ainisha Khalifa. Akauliza nani?Nikamwambia Umar. Akakaa kimya muda kadhaa, kisha akavuta tenapumzi, nikamwambia una nini? Akasema: “Ninajiomboleza mwenyewe.”Nikamwambia ainisha Khalifa. Akauliza nani? Nikamwambia Ali bin AbuTalib. Akasema: “Naapa kwa Yule Ambaye nafsi yangu imo mikononiMwake, lau wakimtii basi wote wataingia Peponi.”54

38

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

54 Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 4 Uk. 147.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 38

Page 48: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

SURAT MUJADILAH

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Enyi mlioamini! Mnaposema siri na Mtume, basi tangulizeni sadakakabla ya kumsemesha hayo ni bora kwenu na ni safi sana, na ikiwahamkupata basi Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe, Mwenyekurehemu.” (Surat Mujadilah: 12).

Imesemekana kwamba hakuna yeyote aliyeifanyia kazi Aya hii kabla yahukumu yake kufutwa ila Ali bin Abu Talib (a.s.).55

Ibnu Abi Najihu amesema: Kutoka kwa Mujahidu, amesema:“Walikatazwa kusema siri na Mtume (s.a.w.w.) mpaka watoe sadaka.Hakuna aliyeweza kusema naye siri ila Ali bin Abu Talib, alitoa sadaka yadinari kisha akasema siri na Mtume (s.a.w.w.) na alimuuliza mambo kumi,ndipo (baada ya sadaka hiyo) ikateremka ruhusa (iliyoondoa sharti la sada-ka.).”56

Kutoka kwa Mujahid amesema: Ali (a.s.) alisema: “Hakika katika Kitabucha Mwenyezi Mungu kuna Aya ambayo hakuna yeyote aliyeifanyia kazikabla yangu, wala hakuna yeyote atakayeifanyia kazi baada yangu,nilikuwa na dinari nikaibadili kwa dirhamu kumi, hivyo ikawa kila nina-

39

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

55 Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 4 Uk. 286.56 Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 4 Uk. 286.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 39

Page 49: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

posema siri na Mtume wa Mwenyezi Mungu natoa sadaka dirhamu moja,mpaka hukumu yake ikafutwa huku hakuna yeyote kabla yangualiyeifanyia kazi na wala hakuna baada yangu atakayeifanyia kazi, nayo ni:“Enyi mlioamini! Mnaposema siri na Mtume, basi tangulizeni sadakakabla ya kumsemesha hayo ni bora kwenu na ni safi sana…..””.57

SURA TAHRIM

Kauli ya Mwenyezi Mungu: “…..Basi Mwenyezi Mungu ni mlinzi wake,na Jibril na waumini wema na Malaika….” (Sura Tahrim: 4).

Laythu bin Abi Salim amesema kutoka kwa Mujahid kwamba: ‘’Na wau-mini wema’’ ni Ali bin Abu Talib.58

Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema kuhusu kauli yaMwenyezi Mungu: ‘’Na waumini wema’’ kuwa ni Ali bin Abu Talib.59

40

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

57 Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 4 Uk. 286.58 Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 4 Uk. 340.59 Tafsirul-Qur’an al-Adhim Juz. 4 Uk. 340. Mchakato toka katika tafsiri hii ume-timia siku ya ishirini na tatu ya Mfunguo tatu Mwaka 1426 A.H. katika Jiji la QumTakatifu.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 40

Page 50: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

AHLUL-BAIT (A.S.) NDANI YA TAFSIRI YA SUYU-TI,

INAYOITWA AD-DURUL-MANTHUR FIT-TAFSIR-IL-MAATHUR

SURAT AL-BAQARAH

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Basi Adam akapokea maneno kwa Mola wake Mlezi, na akamkubaliatoba yake, hakika yeye ndiye apokeaye toba, Mwenye kurehemu.”(Sura Al-Baqarah: 37).

Ad-Daylami ameiandika katika Musnadul-Firdawsi kwa riwaya aliy-oipokea kutoka kwa Ali, kwamba alisema: “Nilimuuliza Mtume (s.a.w.w.)kuhusu kauli yake (s.w.t.): “Basi Adam akapokea maneno kwa Mola wakeMlezi, na akamkubalia toba yake.” Akasema (s.a.w.w.): ‘Hakika MwenyeziMungu alimshusha Adam huko India, Hawa huko Jiddah, Ibilisi hukoBaysan, na nyoka huko Isfahani. Nyoka alikuwa na miguu kama yangamia, Adam akaishi huko India miaka mia moja huku akilia kwa kujutiakosa lake, mpaka Mwenyezi Mungu akampelekea Jibril na kumwambia:‘Ewe Adam! Hivi sijakuumba kwa mkono wangu! Hivi sijakupulizia rohoyangu! Hivi sikuwaamuru malaika wangu wakusujudie! Na hivi sijakuozaHawa, kijakazi wangu!’ Akasema: ‘Ndio umenifanyia hayo.’

Akamwambia: ‘Basi ni kwa nini walia kiasi hiki?’ Akajibu: ‘Na ni kipikitanizuia nisilie na hali nimetoka kwenye ujirani wa Rahman.’Akamwambia: ‘Shikamana na maneno haya, hakika Mwenyezi Munguataipokea toba yako na kukughufiria dhambi yako.’

41

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 41

Page 51: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

Akasema: ‘Ewe Mwenyezi Mungu! hakika mimi nakuomba kwa haki yaMuhammad na aali Muhammad, Subhanaka hakuna Mungu apasayekuabudiwa ila Wewe. Nimetenda uovu na nimeidhulumu nafsi yangu hivyonighufirie hakika Wewe ni Ghafuru Rahimu. Ewe Mwenyezi Mungu! haki-ka mimi nakuomba kwa haki ya Muhammad na aali Muhammad,Subhanaka hakuna Mungu apasaye kuabudiwa ila Wewe. Nimetenda uovuna nimeidhulumu nafsi yangu hivyo nisamehe hakika Wewe ni Mwenyekupokea toba na ni Rahimu.’ Haya ndio maneno aliyoyapokea Adam(a.s.).”’60

Ibnu an-Najjar ameandika kutoka kwa Ibnu Abbas kwamba alisema:Nilimuuliza Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) kuhusu manenoambayo aliyapokea Adam toka kwa Mola wake Mlezi na hatimayeakamkubalia toba yake. Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akasema:“Aliomba: Kwa haki ya Muhammad, Ali, Fatima, Hasan na Huseinnikubalie toba yangu. Akamkubalia toba yake.”61

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Wale watoao mali zao usiku na mchana kwa siri na dhahiri, wanaujira wao kwa Mola wao Mlezi; wala haitakuwa hofu juu yao walawao hawatahuzunika.” (Sura Al-Baqarah: 274).

Abdurazzaq, Abdu bin Hamid, Ibnu Jarir, Ibnu al-Mundhir, Ibnu AbiHatim, Tabarani na Ibnu Asakir wameandika kwa njia itokayo kwa Abdul-Wahab bin Mujahid kutoka kwa baba yake, kutoka kwa Ibnu Abbas, ame-

42

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

60 Kwa maelezo zaidi rejea Tafsirul-Burhan Juz. 1 Uk. 86, Chapa ya Ismailiyyan.61 Kwa uwazi kabisa inadhihiri kwamba Ahlul-Baiti ni Ali, Fatima, Hasan naHusein (a.s.) nao ndio Aali Muhammad na ndio waliokusudiwa katika Kisa chaKishamia na katika Aya ya Utakaso.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 42

Page 52: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

sema kuhusu kauli yake (s.w.t.): “Wale watoao mali zao usiku na mchanakwa siri na dhahiri..”: “Aya hii iliteremka kwa ajili ya Ali bin Abu Talibalikuwa na dirhamu nne, akatoa sadaka dirhamu moja usiku na nyinginemchana, nyingine siri na nyingine dhahiri.”62

SURA AALI IMRAN

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Hakika Mwenyezi Mungu alimchagua Adam na Nuh na kizazi chaIbrahim na kizazi cha Imran juu ya walimwengu wote.” (Sura AaliImran: 33).

Ibnu Jarir, Ibnu al-Mundhir na Ibnu Abi Hatim wameandika kupitia njia yaAli kutoka kwa Ibnu Abbas kuhusu kauli ya Mwenyezi Mungu: “na kizazicha Ibrahim na kizazi cha Imran” amesema: “Hao ni waumini kutoka kati-ka aali Imran, aali Ibrahim, aali Yasin na aali Muhammadi (s.a.w.w.).”63

43

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

62 Rejea Shawahidut-Tanziil cha al-Haskaniy Juz. 1, Uk. 109, Chapa ya Beirut yaKimataifa ya Mwaka 1974. Humo ameandika kutoka kwa al-Kalbiy kutoka kwaAbu Salih kutoka kwa Ibnu Abbas kuhusu kauli ya Mwenyezi Mungu: “”Walewatoao mali zao usiku na mchana kwa siri na dhahiri..” kwamba aliteremkakwa ajili ya Ali pekee, katika kisa cha dirhamu zake nne alizozitoa sadaka, mojamchana nyingine usiku, nyingine kwa siri na nyingine kwa dhahiri.

63 Nasema: Aali Yasin ndio aali Muhammad (s.a.w.w.) kwa sababu Yasin ni mojaya majina ya Mtume (s.a.w.w.) kama alivyotamka wazi hilo Suyuti katika tafsirihii Juz. 5, Uk. 258. Na al-Khazin ametaja hilo katika Juz. 4, Uk. 2 na Juz. 5, Uk.286. Na limetajwa katika Shawahidut-Tanziil Juz. 1, Uk. 118, Chapa ya Beirut.Kwa ziada rejea Tafsirul-’Ayyash Juz. 1, Uk. 191, Chapa ya Beirut ya mwaka1991.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 43

Page 53: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

Kauli ya Mwenyezi Mungu: “…Kila mara Zakariya alipoingia Mihrabhukuta vyakula. Akasema: Ewe Maryam unatoa wapi hivi. Akasema:Vinatoka kwa Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu hum-ruzuku amtakaye bila hesabu.” (Sura Aali Imran: 37).

Ameandika Abu Ya’la ameandika kutoka kwa Jabir kwamba Mtume waMwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alikaa siku kadhaa bila kula chakula mpakahali hiyo ikawa nzito juu yake. Akaenda kwenye nyumba za wakeze laki-ni hakupa kwa yeyote chochote, ndipo akaenda kwa Fatima nakumwambia: “Ewe mwanangu mpendwa! Je una chochote ninachowezakula kwani hakika mimi ni mwenye njaa?” Akamjibu: “Wallahi sina.”

Mtume alipotoka jirani wa Fatima alimletea Fatima vipande viwili vyamkate na finyango ya nyama, akavitwaa na kuviweka ndani ya bakuli lake,akasema: “Wallahi katika hiki nitampa kipaumbele Mtume wa MwenyeziMungu (s.a.w.w.) kabla ya nafsi yangu na kabla ya yule aliyopo kwangu.”Japokuwa wote walikuwa wanahitajia chakula lakini Fatima alimtumaHasan au Husein aende kumwita Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.)naye alikwenda. Fatima akamwambia: “Kwa haki yako na ya mama yangu,Mwenyezi Mungu ameleta kitu nami nimekihifadhi kwa ajili yako.”Akamwambia: “Kilete ewe binti yangu mpendwa.” Akamletea bakuli naalipolifunua ghafla akakuta limejaa mikate na nyama, alipokitazama akap-atwa na mshangao na akatambua kuwa ni baraka toka kwa MwenyeziMungu. Akamhimidi Mwenyezi Mungu na akamkabidhi chakula hichoMtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.).

Mtume (s.a.w.w.) alipokiona alimhimidi Mwenyezi Mungu na akasema:“Umetoa wapi hivi ewe binti yangu mpendwa?” Akajibu: “Ni kutoka kwaMwenyezi Mungu ewe baba yangu mpendwa. Hakika Mwenyezi Munguhumpa riziki amtakaye bila hesabu. “

Mtume akamhimidi Mwenyezi Mungu na kusema: “Kila sifa njema ni yaMwenyezi Mungu Ambaye amekufanya ewe binti yangu mpendwa kifani

44

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 44

Page 54: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

wa Seyida wa wana wa Israel (Mariam). Kwani hakika yeye alikuwaaruzukiwapo chochote na Mwenyezi Mungu kisha akiulizwa kakipatawapi husema: Hakika Mwenyezi Mungu humpa riziki amtakaye bilahesabu.”64

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na Malaika waliposema: Ewe Maryam! Hakika Mwenyezi Munguamekuteua na akakutakasa na akakuteua juu ya wanawake waulimwenguni.” (Sura Aali Imran: 42).

Al-Hakima ameandika kutoka kwa Ibnu Abbas kwamba Mtume waMwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Wanawake bora ulimwenguni ni:Khadija, Fatima, Maryam na Asia mke wa Firaun.”

Ibnu Mardawayhi ameandika kutoka kwa Ibnu Abbas kwamba Mtume waMwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: ‘’Hakika Mwenyezi Mungu aliwa-teua wanne kwa ubora kuliko wanawake wote wa ulimwenguni: Asia bintiMuzahim, Maryam binti Imran, Khadija binti Khuwaylid na Fatima bintiMuhammad (s.a.w.w.).”

Ahmad, Tirmidhi, Ibnu al-Mundhir, Ibnu Habban na al-Hakim wameandi-ka kutoka kwa Anas kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.)alisema: “Yakutosha toka katika wanawake wa ulimwenguni: Maryambinti Imran, Khadija binti Khuwaylid, Fatima binti Muhammad (s.a.w.w.)na Asia mke wa Firaun.”

45

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

64 Nasema: Hilo si zito kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu, ikiwa Mariam nimkweli wa Kizazi cha Israil na Fatima ni mkweli wa umma huu naye ni mbora wawanawake wote wa ulimwengu.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 45

Page 55: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

Ibnu Abi Shayba na Ibnu Jarir wameandika kutoka kwa Fatima (a.s.)kwamba alisema: “Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) aliniambia:Wewe ndiye mbora kuliko wanawake wote wa peponi na si Mariam al-Batul.”

Ibnu Asakir ameandika kutoka kwa Ibnu Abbas amesema: “Mtume waMwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Wanawake bora wa peponi niMaryam binti Imran, Fatima binti Muhammad (s.a.w.w.), Khadija bintiKhuwaylid na Asia mke wa Firaun.”

Ibnu Asakir ameandika kupitia njia ya Muqatil, kutoka kwa Dhahak kuto-ka kwa Ibnu Abbas kutoka kwa Mtume (s.a.w.w.) amesema: “Wanawakewanne ni wabora kuliko wanawake wote wa zama zao: Maryam bintiImran, Asia binti Muzahim, Khadija binti Khuwaylid na Fatima bintiMuhammad (s.a.w.w.) na yeye ndiye mbora wao kiulimwengu.”65

Ibnu Shayba ameandika kutoka kwa Abdurahman bin Abi Layla kwambaamesema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Fatima ndiyembora wa wanawake wa ulimwenguni baada ya Maryam binti Imran, Asiamke wa Firaun na Khadija binti Khuwaylid.”66

46

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

65 Allama al-Muttaqiy al-Hindiy amepokea katika kitabu Kanzul-Ummal hadithihii kutoka kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.): “Ewe Fatima! Hivi hau-ridhii wewe kuwa ndiye mwanamke bora kuliko wanawake wote wa ulimwengu-ni na mbora kuliko wake wote wote wa waumini na mbora kuliko wanawake wotewa umma huu.” Tazama Kanzul-Ummal Juz. 12 Uk. 12, Namba 34232.

66 Allama al-Bahraniy amepokea katika al-Burhani Juz. 1 Uk. 281, Chapa yaQum, kutoka kwa al-Mufadhal bin Umar kwamba amesema: Nilimwambia AbuAbdillah (a.s.): Nieleze kuhusu kauli ya Mtume wa Mwenyezi Mungu kwambaFatima ni mbora wa wanawake wa ulimwenguni. Je ni ulimwengu wa zama zake?Akasema (s.a.w.w.): “Hali hiyo ni kwa Mariam yeye ndiye aliyekuwa mbora kwawanawake wa ulimwengu wa zama zake. Ama Fatima yeye ni mbora wawanawake wa ulimwengu mzima kuanzia wale wa mwanzo mpaka wa mwisho.”

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 46

Page 56: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na watakaokuhoji baada kukufikia elimu hii, waambie: Njoonituwaite watoto wetu na watoto wenu, na wanawake zetu na wanawakewenu, na nafsi zetu na nafsi zenu, kisha tuombe kwa unyenyekevututake laana ya Mwenyezi Mungu iwashukie waongo.” (Sura AaliImran: 61).

Al-Hakim, Ibnu Mardawayhi na Abu Naiim katika ad-Dalail wameandikakutoka kwa Jabir kwamba alisema: al-Aqib na Seyyid walikwenda kwaMtume (s.a.w.w.) naye akawalingania waingie katika Uislamu, wakasema:“Tumesilimu ewe Muhammad.” Akawaambia: “Mmesema uongo, na mki-taka nitawaambieni ni kipi kinachowazuia kuingia katika Uislamu.”Wakamwambia: “Tueleze.” Akawaambia: “Kuupenda msalaba, kunywapombe na kula nyama ya nguruwe.”

Jabir anasema: Ndipo akawaomba wafanye maapizano, nao wakamwahidiiwe siku itakayofuata. Mtume wa Mwenyezi Mungu akatoka siku iliyofu-ata akiwa amemshika mkono Ali, Fatima, Hasan na Husein, kisha akawa-tumia ujumbe waje lakini wakakataa kuitikia wito na baadayewakamkubalia (kufanya suluhu). Mtume akasema: “Naapa kwa YuleAmbaye alituma kwa haki! Lau wangethubutu kufanya (maapizano) basibonde lingeteketea kwa moto.”

Jabir anasema: Na kwa ajili yao iliteremka Aya: “Njooni tuwaite watotowetu na watoto wenu.” Nafsi zetu na nafsi zenu ni Mtume wa MwenyeziMungu na Ali. Watoto zetu ni Hasan na Husein. Na wanawake zetu niFatima (a.s.).Al-Hakim ameandika kutoka kwa Jabir kwamba: Ujumbe wa Najran ulifi-

47

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 47

Page 57: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

ka kwa Mtume (s.a.w.w.) na kumwambia: “Unasemaje kuhusu Isa?”Akawaambia: “Yeye ni Roho wa Mwenyezi Mungu, Neno Lake, Mja waMwenyezi Mungu na Mtume Wake.” Wakasema: “Upo tayari kuapizananasi kwani ukweli si hivyo?”

Akasema: “Je hilo mwaliridhia?” Wakasema ndio. Akasema: “Kamamnataka basi hakuna kizuizi.” Ndipo akaenda kuwakusanya watoto wakeHasan an Husein. Kiongozi wao akasema: “Msifanye maapizano na mtuhuyu, Wallahi kama mtaapizana naye basi litaangamizwa moja kati yamakundi mawili.” Wakaja na kumwambia: “Ewe Abul-Q?sim! Hakikawaliotaka kufanya maapizano na wewe ni wale masafihi miongoni mwetu,nasi tunapenda utusamehe.” Akaesema: “Nimeshawasamehe.” Kishaakasema: “Hakika adhabu imeshatanda Najran.”

Muslim, Tirmidhi, Ibnu al-Mundhir, al-Hakim na al-Bayhaqiy katikaSunan yake wameandika kutoka kwa Sa’d ibnu Abi Waqqas kwamba alise-ma: Ilipoteremka Aya hii: “Njooni tuwaite watoto wetu na watoto wenu.”Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alimwita Ali, Fatima, Hasan naHusein, akasema: “Ewe Mwenyezi Mungu! Hawa ndio ndugu zangu.”

Ibnu Jarir ameandika kutoka kwa Aliyai bin Ahmar al-Yashkariy kwambaamesema: Ilipoteremka Aya hii: “Njooni tuwaite watoto wetu na watotowenu.” Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alimwita Ali, Fatima nawatoto wao Hasan na Husein. Akawaita mayahudi waje kwenyemaapizano na ndipo kijana toka kwa mayahudi akasema: “Ole wenu! Hivijana ndugu zenu waliogeuzwa manyani na nguruwe hawakuwakatazenikwamba msifanye maapizano.” Ndipo wakaacha.

Al-Bayhaqiy katika ad-Dalail ameandika kupitia njia ya Salmah bin AbduYushu’ kutoka kwa baba yake kutoka kwa babu yake, kwamba Mtume waMwenyezi Mungu (s.a.w.w.) aliwaandikia barua watu wa Najran kabla yakushushiwa Bismillahi ya Sulayman: “Kwa jina la Mungu wa Ibrahim,Is’haqa na Ya’qub. Kutoka kwa Muhammad Mtume wa Mwenyezi Mungukwenda kwa Askofu wa Najran na wakazi wa Najran. Ikiwa mtasilimu basi

48

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 48

Page 58: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

hakika mimi nitamhimidi Mwenyezi Mungu kwenu Mungu wa Ibrahim,Is’haqa na Ya’qub. Ama baad, hakika mimi nawaita kwenye ibada yaMwenyezi Mungu na mtoke kwenye ibada ya waja, na nawaita kwenyemamlaka ya Mwenyezi Mungu na mtoke kwenye mamlaka ya waja. Hivyomkikataa basi ni juu yenu kodi, na kama mkikataa nitaidhinisha vita dhidiyenu, wasalamu.”

Askofu aliposoma barua hii aliisadiki na akaingiwa na hofu kubwa, ndipoakatuma ujumbe aitwe mtu mmoja mkazi wa Najrani aliyejulikana kwajina la Sharhab?l bin Wid?’h, akampa barua ya Mtume (s.a.w.w.) nayeakaisoma. Askofu akamuuliza ni ipi rai yako? Sharhab?l akasema:“Nimeyajua yale ambayo Mwenyezi Mungu alimwahidi Ibrahim ambayoni unabii kutoka katika kizazi cha Ismail, hakuna kizuizi kinachozuia mtuhuyu kuwa ndiye, hivyo sina rai katika unabii. Lau ingekuwa ni kuhusumambo ya kidunia basi ningekupa rai na ningetoa juhudi zote kwako.”

Askofu akamwita moja baada ya mwingine katika wakazi wa Najran, nawote walisema mfano wa yale aliyosema Sharhab?l, ndipo wakaamua kwapamoja wamtume Sharhab?l bin Wid?’h, Abdullah bin Sharhab?l naJabbari bin Faydh waende kumdadisi Mtume wa Mwenyezi Mungu nahatimaye wawaletee habari zake. Ujumbe ukasafiri hadi kwa Mtume waMwenyezi Mungu (s.a.w.w.) wakamuhoji naye akawahoji, basi mahojianoyaliendelea mpaka wakamwambia: “Unasemaje kuhusu Isa bin Mariam?”Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akawaambia: “Leo hii sina kitucha kuwaambieni kuhusu Isa, subirini mpaka kesho asubuhi ndiponitawaelezeni yale nitakayoteremshiwa kuhusu Isa bin Mariam.”

Ndipo Mwenyezi Mungu akateremsha Aya hizi: “Hakika mfano wa Isambele ya Mwenyezi Mungu ni kama mfano wa Adam, alimuumbakutokana na udongo, kisha akamwambia kuwa, basi akawa. Ndiyohaki itokayo kwa Mola wako Mlezi, basi usiwe miongoni mwa wenyekutia shaka. Na watakaokuhoji baada kukufikia elimu hii, waambie:Njooni tuwaite watoto wetu na watoto wenu, na wanawake zetu nawanawake wenu, na nafsi zetu na nafsi zenu, kisha tuombe kwa

49

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 49

Page 59: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

unyenyekevu tutake laana ya Mwenyezi Mungu iwashukie waongo.”(Sura Aali Imran: 59 - 61).

Lakini wakakataa kuamini hilo. Siku iliyofuata baada ya kuwa tayari ame-shawapa habari, Mtume wa Mwenyezi Mungu alitoka kwa ajili yamaapizano akiwa na Hasan na Husain ndani ya joho lake na Fatima akiwanyuma ya mgongo wake, licha ya kwamba kipindi hicho tayari alikuwaameshakuwa na wanawake wengi.

Sharhab?l akawaambia marafiki zake: “Hakika kuna jambo ninalolionambele, ikiwa kweli huyu ni Nabii Mtume basi kitendo cha kuapizana nayehakitambakisha yeyote miongoni mwetu juu ya ardhi, hata unywele naukucha bali ni lazima ataangamia.” Wakamwambia: Ni ipi rai yako?Akasema: “Rai yangu ni kwamba tumuombe abadili maamuzi kwani haki-ka mimi namwona ni mtu asiyehamia kwenye maamuzi ya kiupuuzi katu.”Wakamwambia hilo ni juu yako. Ndipo Sharhab?l akamwendea Mtume waMwenyezi Mungu (s.a.w.w.) na kumwambia: “Hakika mimi nimeona kherinyingine kuliko kuapizana na wewe.” Akamuuliza ni ipi hiyo? Akasema:“Ubadili hatua yako ya leo mpaka kwenye ile ya usiku (wa jana), na tokakwenye ile ya usiku wako mpaka kwenye ile ya (jana) asubuhi, basi hatuayoyote utakayoichukua hapo kwa ajili yetu tutaipokea.” Ndipo Mtume waMwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akabadili maamuzi akarejea bila kuapizananao na akafanya nao suluhu kwa sharti walipe kodi.67

Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Na shikamaneni na kamba ya MwenyeziMungu nyote kwa pamoja wala msifarakane..” (Sura Aali Imran:103).

Ahmad ameandika kutoka kwa Zayd bin Thabit kwamba alisema: Mtumewa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Hakika mimi ni mwenye kuacha

50

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

67 Ameiandika al-Haskani katika kitabu Shawahidut-Tanziil Juz. 1, Uk. 120,chapa ya Beiruti. Na al-Manaqib cha Ibnu al-Mughazaliy, Hadithi ya 313. NaAhamad bin Hanbal katika kitabu Fadhailus-Sahaba, Hadithi ya 27, mlango wafadhila za Hasan na Husain (a.s.).

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 50

Page 60: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

kati yenu mirathi mbili: Kitabu cha Mwenyezi Mungu kamba iliyonyookabaina ya mbingu na ardhi, na kizazi changu watu wa nyumba yangu, nahakika hivyo viwili havitaachana mpaka vinikute kwenye hodhi.”68

Tabarani ameandika kutoka kwa Zayd bin Arqam kwamba alisema: Mtumewa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Mimi nawatangulia nanyimtanikuta katika hodhi, basi angalieni ni jinsi gani mtakavyoishi na vizitoviwili nyuma yangu.” Pakasemwa: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Nivipi hivyo vizito viwili? Akasema: “Kikubwa ni Kitabu cha MwenyeziMungu kamba ambayo ncha moja imo mikononi mwa Mwenyezi Munguna ncha nyingine mikononi mwenu, hivyo shikamaneni nacho hamtatelezawala kupotea. Na kidogo ni kizazi changu, na hakika hivyo viwili havi-taachana mpaka vinifikie kwenye hodhi. Na hilo nilimuomba Mola wanguMlezi hivyo msivitangulie mtaangamia na wala msivifundishe kwani haki-ka hivyo vina ujuzi kulikoni nyinyi.”

Ibnu Sa’d, Ahmad na Tabarani wameandika kutoka kwa Abu Said al-Khudri kwamba alisema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema:“Enyi watu! Hakika mimi ni mwenye kuacha kati yenu mambo mawiliambayo lau mkishikamana nayo hamtapotea baada yangu, kimoja nikikubwa kuliko kingine: Kitabu cha Mwenyezi Mungu kamba iliyonyookabaina ya mbingu na ardhi, na kizazi changu watu wa nyumba yangu, nahakika hayo mawili hayataachana mpaka yanikute kwenye hodhi.”69

51

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

68 Nasema: Baadhi ya wale ambao wana maradhi nyoyoni mwao miongoni mwawale wenye chuki na uadui na Ahlul-Baiti (a.s.) wameondoa maneno ‘Kizazichangu’ na kuweka badala yake neno ‘sunna yangu’, na hii ni batili ya wazi, kwasababu hata hiyo Sunna nayo inahitaji mfasiri na mfafanuzi, na hakuna ajuayehayo ila Ahlul-Bait (a.s.) kwa sababu wao ndio wajuzi zaidi wa yale yaliyomondani ya nyumba.69 Al-Haskani katika kitabu chake Shawahidut-Tanziil Juz. 1, Uk. 130 anapotafsiriAya hii, ameandika kutoka kwa Ali bin Musa Ridha (a.s.) kutoka kwa baba zakekutoka kwa Ali (a.s.) kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema:“Anayetaka kupanda safina ya uokovu na kushikamana na shikio imara nakushikamana na kamba ngumu ya Mwenyezi Mungu basi amtawalishe Ali na awa-fuate viongozi toka katika kizazi chake.”

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 51

Page 61: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

SURAT MAIDA

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Leo nimekukamilishieni dini yenu na kukutimizieni neema yangu nanimekupendeleeni Uislamu uwe dini yenu..” (Sura Maida: 3).

Ibnu Mardawayhi na Ibnu Asakir wameandika kwa sanad dhaifu kutokakwa Abu Said al-Khudri kwamba alisema: “Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w.) alipomsimika Ali Siku ya Ghadiri ya Mfunguo tatu alisema(s.a.w.w.): “Ambaye mimi nina mamlaka juu yake basi huyu Ali nimwenye mamlaka juu yake.” Ndipo Mwenyezi Mungu akateremsha: Leonimekukamilishieni dini yenu.70

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Hakika Walii wenu hasa ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake nawale walioamini ambao husimamisha Swala na hutoa Zaka wakiwawamerukui.” (Sura al-Maida: 55).

52

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

70 Hadithi hii imepokewa na sahaba wakubwa mia moja na kumi, na tabiinathamanini na nne. Pia zaidi ya watu mia nne miongoni mwa wasomi, wanahadithi,wafasiri, wanahistoria na wataalamu wa fani ya wapokezi, wameiandika hadithihii muhimu. Hivyo anayetaka maarifa zaidi ni juu yake kurejea Enklopedia yaGhadiri ya Allama al-Amin Juz. 1. Humo ameipokea toka kwa wanazuoni mia tatuna sitini na toka katika vitabu ishirini na sita wote wakiwa ni wanazuoni wa kisun-ni na ni vitabu vya kisunni.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 52

Page 62: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

Al-Khatib ameandika katika al-Muttafaq kutoka kwa Ibnu Abbas kwambaalisema: “Ali alitoa sadaka pete yake ndipo Mtume akamuuliza muombaji- ni nani aliyekupa pete hii? Akasema ni yule aliyomo kwenye rukuu,ndipo Mwenyezi Mungu akateremsha: “Hakika Walii wenu hasa niMwenyezi Mungu na Mtume wake na wale walioamini ambao husi-mamisha Swala na hutoa Zaka wakiwa wamerukui.”

Abdurazzaq, Abdu bin Hamid, Ibnu Jarir, Abu Shaykh na IbnuMardawayhi wameandika kutoka kwa Ibnu Abbas kwamba alisema:“Hakika Walii wenu hasa ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake na walewalioamini ambao husimamisha Swala na hutoa Zaka wakiwawamerukui,” iliteremka kwa ajili ya Ali bin Abu Talib.

Tabarani katika al-Awsat na Ibnu Mardawayhi wameandika kutoka kwaAmmar bin Yasir kwamba alisema: “Muombaji alisimama kwa Ali na haliakiwa katika rukuu ya Swala ya sunna, ndipo akavua pete yake na kumpamuombaji, naye akaenda kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu na kumjulishahilo, ndipo Aya hii ikateremka kwa Mtume (s.a.w.w.): “Hakika Waliiwenu hasa ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake na wale walioaminiambao husimamisha Swala na hutoa Zaka wakiwa wamerukui.”Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akawasomea sahaba zake kishaakasema: “Yule mbaye mimi nina mamlaka juu yake basi huyu Ali nimwenye mamlaka juu yake. Ewe Mwenyezi Mungu! Mpende ampendayena mfanyie uadui amfanyiaye uadui.”

Abu Shaikh na Ibnu Mardawayhi wameandika kutoka kwa Ali bin AbuTalib (a.s.) kwamba alisema: “Aya hii ilimteremkia Mtume wa MwenyeziMungu (s.a.w.w.) nyumbani kwake: “Hakika Walii wenu hasa niMwenyezi Mungu na Mtume wake na wale walioamini ambao husi-mamisha Swala na hutoa Zaka wakiwa wamerukui”, ndipo Mtume waMwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akatoka na kuingia msikitini akawakuta watuwakisali, wengine wamo katika rukuu, wengine katika sijda na wenginekatika kisimamo, ghafla akamwona muombaji, akamuuliza: Ewe muom-

53

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 53

Page 63: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

baji, je kuna yeyote aliyekupa kitu? Akajibu: ‘Hapana ila yule aliyemokatika rukuu naye ni Ali bin Abu Talib amenipa pete yake.”’

Ibnu Jarir ameandika kutoka kwa Mujahid kuhusu kauli ya MwenyeziMungu: “Hakika Walii wenu hasa ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake nawale walioamini ambao husimamisha Swala na hutoa Zaka wakiwawamerukui.” Kwamba iliteremka kwa ajili ya Ali bin Abu Talib, alitoasadaka na hali akiwa katika rukuu.

Ibnu Mardawayhi ameandika kupitia njia ya al-Kalbiy kutoka kwa AbuSalih kutoka kwa Ibnu Abbas kwamba alisema: Abdullah bin Salam aliku-ja na kundi lake kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) wakati waAdhuhuri, wakasema: ‘Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Hakika nyum-ba zetu ziko mbali na hatupati wa kuketi nasi na kujumuika nasi kinyumena msikiti huu, na hakika jamaa zetu walipoona tumemsadiki MwenyeziMungu na Mtume Wake na tumeiacha dini yao wametudhihirishia uadui nawameapa kwamba hawatajumuika nasi na wala hawatakula pamoja nasi,jambo hilo limekuwa zito juu yetu.’

Wakiwa bado wanaendelea kumlalamikia hali hiyo Mtume wa MwenyeziMungu (s.a.w.w.) ghafla ilimshukia Aya hii Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w.): “Hakika Walii wenu hasa ni Mwenyezi Mungu na Mtume wakena wale walioamini ambao husimamisha Swala na hutoa Zaka wakiwawamerukui.” Sala ya Dhuhri ikanadiwa na akatoka Mtume wa MwenyeziMungu (s.a.w.w.). akasema (kumuuliza muombaji): ‘Kuna yeyote aliyeku-pa kitu?’ Akajibu ndio. Akamuuliza: ‘Nani?’ Akajibu: Yule aliyesimama.Akamuuliza: ‘Alikupa akiwa katika hali gani?’ Akajibu: Akiwa katikarukuu. Akasema: ‘Yule ni Ali bin Abu Talib.’ Kisha Mtume wa MwenyeziMungu (s.a.w.w.) akatoa takbira huku akisema: ‘Na mwenye kumtawalishaMwenyezi Mungu na Mtume wake na wale walioamini, basi kwa hakikakundi la Mwenyezi Mungu ndilo lenye kushinda.’Ibnu Mardawayhi ameandika kutoka kwa Ibnu Abbas kwamba alisema:“Ali bin Abu Talib alikuwa amesimama akisali ndipo muombaji akapita,

54

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 54

Page 64: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

naye akiwa katika rukuu, akampa pete yake, ndipo ikateremka Aya hii:“Hakika Walii wenu hasa ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake na walewalioamini ambao husimamisha Swala na hutoa Zaka wakiwawamerukui.” Iliteremka kwa ajili ya wale walioamini na Ali ndio kinarawao.

Abdu bin Hamid, Ibnu Jarir na Ibnu al-Mundhir wameandika kutoka kwaAbu Ja’far kwamba aliulizwa kuhusu Aya hii kwamba ni akina naniwalioamini? Akasema: “Ni wale walioamini. Akaambiwa imetufikia habarikwamba iliteremka kwa ajili ya Ali bin Abu Talib. Akasema: Ali ni mion-goni mwa wale walioamini.”

Abu Naim ameandika katika al-Hilyah kutoka kwa Abdul-Malik bin AbuSulayman kwamba alisema: Nilimuuliza Abu Ja’far Muhammad bin Alikuhusu kauli ya Mwenyezi Mungu: “Hakika Walii wenu hasa ni MwenyeziMungu na Mtume wake na wale walioamini ambao husimamisha Swala nahutoa Zaka wakiwa wamerukui.” Nikasema hakika masahaba waMuhammad (s.a.w.w.) wanasema kwamba ni Ali. Akasema: “Ali ni mion-goni mwao.”71

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Ewe Mtume! Fikisha uliyoteremshiwa kutoka kwa Mola Wako; nakama hutafanya, basi hukufikisha ujumbe Wake. Na MwenyeziMungu atakulinda na watu. Hakika Mwenyezi Mungu hawaongoziwatu madhalim.” (Sura Maida: 67).Ibnu Abi Hatim, Ibnu Mardawayhi na Ibnu Asakir wameandika kutokakwa Said al-Khudriy kwamba alisema: Aya hii: “Ewe Mtume! Fikisha

55

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

71 Rejea pia Shawahidut-Tanziil Juz. 1, Uk. 161, Chapa ya Beirut.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 55

Page 65: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

uliyoteremshiwa kutoka kwa Mola Wako; na kama hutafanya, basi huku-fikisha ujumbe Wake. Na Mwenyezi Mungu atakulinda na watu. HakikaMwenyezi Mungu hawaongozi watu madhalim.” Iliteremka kwa Mtumewa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) Siku ya Ghadir Khum kwa ajili ya Ali binAbu Talib.

Ibnu Mardawayhi ameandika kutoka kwa Ibnu Mas’ud kwamba alisema:Zama za Mtume wa Mwenyezi Mungu tulikuwa tukisoma: “Ewe Mtume!Fikisha uliyoteremshiwa kutoka kwa Mola Wako; kwamba hakika Ali nimwenye mamlaka juu ya waumini, na kama hutafanya, basi hukufikishaujumbe Wake. Na Mwenyezi Mungu atakulinda na watu.”72

SURAT AL-AN’AAM

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na tukampa Is’haka na Yakub, wote tukawaongoza, na Nuh tulim-wongoza zamani na katika kizazi chake, Daud na Sulaiman na Ayubna Yusuf na Musa na Harun. Na hivyo ndivyo tuwalipavyo wafanyawema. Na Zakaria na Yahya na Isa na Ilyasa, wote walikuwa miongo-ni mwa watu wema.” (Sura An’aam:84 - 85).Ibnu Abi Hatim ameandika kutoka kwa Abu Harbi bin al-As’wad kwambaamesema: Hajjaj alituma ujumbe kwa Yahya bin Ya’mar kwamba:

56

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

72 Ad-Durul-Manthur Juz. 3, Uk. 28. Pia ameiandika Ibnu Asakir katika kitabuchake Tarikhud-Damashq katika wasifu wa Amirul-Muuminina (a.s.), Hadithi ya452.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 56

Page 66: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

‘Imenifikia habari kuwa wewe unadai kwamba Hasan na Husein ni katikakizazi cha Mtume (s.a.w.w.) kwa ushahidi wa Kitabu cha MwenyeziMungu, nami nimekisoma kuanzia mwanzo wake mpaka mwisho wakelakini sijauona.’ Akamjibu: Hivi unasoma Sura An’am: “Na katika kizazichake, Daud na Sulaiman na Ayub na Yusuf na Musa na Harun. Na hivyondivyo tuwalipavyo wafanya wema. Na Zakaria na Yahya na Isa?”Akasema ndio nimesoma. Akamuuliza: ‘Huoni Isa ni kizazi cha Ibrahim nahali hana baba?’ Akasema: Umesema kweli.

Abu Shaikh, al-Hakim na al-Bayhaqiy wameandika kutoka kwa Abdul-Malik bin Umayri kwamba alisema: Yahya bin Ya’mar aliingia kwa Hajjajna akamtaja Husein. Hajjaj akasema: “Hakuwa katika kizazi cha Mtume(s.a.w.w.).” Yahya akasema: “Umenena uongo.” Hajjaj akasema: “Nileteedalili juu ya hilo ulisemalo. “ Ndipo akamsomea: “…..na katika kizazichake, Daud na Sulaiman na Ayub na Yusuf na Musa na Harun. Na hivyondivyo tuwalipavyo wafanya wema. Na Zakaria na Yahya na Isa na Ilyasa”hivyo Mwenyezi Mungu akatoa habari kwamba Isa ni katika kizazi chaIbrahim. Hajjaj akasema: “Umesema kweli.”73

SURA AL-AA’RAF

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na semeni: Tufutie dhambi zetu, na ingieni mlangoni kwaunyenyekevu, tutakusameheni makosa yenu tutawazidishia watendaomema.” (Sura Aa’raf:161).

57

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

73 Rejea Tafsirul-Burhan ya Sayyid Hashim al-Bahraniy Juz. 1, Uk. 538, Chapaya Qum.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 57

Page 67: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

Ibnu Shayba ameandika kutoka kwa Ali bin Abu Talib kwamba alisema:Hakika mfano wetu katika umma huu ni kama mfano wa Safina ya Nuhuna mlango wa kufutiwa madhambi wa Kizazi cha Israil.

SURAT AL-AN’FALKauli ya Mwenyezi Mungu: “Na jueni kwamba chochote mlichopataghanima, basi khumsi yake ni ya Mwenyezi Mungu na Mtume najamaa na mayatima na masikini na msafiri……” (Sura al-An’fal: 41).

Ibnu Mardawayhi ameandika kutoka kwa Zayd bin Arqam kwamba alise-ma: Aali Muhammad waliopewa khumsi ni wale Aali Ali, Aali Abbas, AaliJa’far na Aali Aqil.

Ibnu Abi Shayba ameandika kutoka kwa Mujahid kwamba alisema: AaliMuhammad si halali kwao sadaka hivyo akawawekea Khumsi.74

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na kama wakitaka kukuhadaa, basi Mwenyezi Mungu ataku-tosheleza. Yeye ndiye aliyekusaidia kwa ushindi wake na kwa waumi-ni.” (Sura al-An’fal: 62).

Ibnu Asakir ameandika kutoka kwa Abu Huraira kwamba alisema: “Arshiimenakishiwa kwa “Hapana Mungu apasaye kuabudiwa kwa haki ila Mimipekee sina mshirika, Muhammad ni mja wangu na Mtume wangu, nimem-pa nguvu kupitia Ali.” Na hiyo ndio kauli ya Mwenyezi Mungu: “Yeyendiye aliyekusaidia kwa ushindi wake na kwa waumini.”

58

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

74 Ad-Durul-Manthur Juz. 3, Uk. 185.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 58

Page 68: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Hakika wale walioamini na wakahama, na wakapigania dini yaMwenyezi Mungu kwa mali zao na nafsi zao, na wale waliowapamahala pa kukaa na wakainusuru, hao ndio marafiki wao kwa wao.”(An’fal: 72).

Ibnu Mardawayhi ameandika kutoka kwa Ibnu Abbas kwamba amesema:Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alifunga udugu baina ya Ansari naMuhajirina, hivyo akaweka udugu baina ya Hamza bin Abdul-Muttalib naZayd bin Harith, baina ya Umar bin al-Khattab na Maadh bin Áfrau, bainaya Zubair bin al-Áwwam na Abdullah bin Mas’?d, baina ya Abu Bakr na?alha bin Abdullah, baina ya Abdurahman bin Awfi na Sa’d bin Rabi’u. naakawaambia masahaba zake wengine fungeni udugu, nami ndugu yangu nihuyu, yaani Ali bin Abu Talib. Waislamu wakaendelea katika hali hiyompaka ikateremka Aya hii.75

SURAT TAWBA

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“(Tangazo la) Kujitoa Mwenyezi Mungu na Mtume wake kwa walemlioahidiana nao miongoni mwa mushrikina.” (Sura Tawba: 1).

59

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

75 Ad-Durul-Manthur Juz. 3 Uk. 205.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 59

Page 69: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

Abdullah bin Ahmad bin Hanbal katika Zawaidul-Musnad, na Abu ShaikhIbnu Mardawayhi, wameandika kutoka kwa Ali (a.s.) kwamba alisema:Zilipoteremka kwa Mtume Aya kumi za mwanzo wa Sura Baraa alimwitaAbu Bakr ili akawasomee wakazi wa Makka. Kisha akaniita na kusema:“Mdiriki Abu Bakr na popote utakapomkuta chukua Sura kutoka kwake.Abu Bakr akarejea kwa Mtume (s.a.w.w.) na kumwambia: “Ewe Mtumewa Mwenyezi Mungu! Kuna chochote kimeteremka kunikhusu?”Akasema: “Hapana lakini Jibril amenijia na kuniambia: Hapasi kufikishakwa niaba yako ila wewe mwenyewe au mtu kutokana na wewe.”

Ibnu Abu Shayba, Ahmad, Tirmidhi, Abu Shaikh na Ibnu Mardawayhiwameandika kutoka kwa Anas kwamba alisema: Mtume wa MwenyeziMungu alimtuma Abu Bakr akiwa na Sura Baraa, kisha akamrejesha nakumwambia: “Haipasi yeyote yule kuibalighisha hii ila mtu kutoka katikandugu zangu.” Ndipo akamwita Ali na kumkabidhi Sura hiyo.

Ibnu Mardawayhi wameandika kutoka kwa Sa’d bin Abi Waqqas kwambaMtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alimtuma Abu Bakr aende na SuraBaraa kuwasomea wakazi wa Makka, kisha akamtuma Ali nyuma yakeakaichukue toka kwake, basi Abu Bakr akahisi hali fulani moyoni mwake.Mtume (s.a.w.w.) akasema: “Hafikishi kwa niaba yangu ila mimimwenyewe au mtu kutoka katika ndugu zangu.”

Ibnu Habban na Ibnu Mardawayhi wameandika kutoka kwa Said al-Khudrikwamba alisema: “Mtume wa Mwenyezi Mungu alimtuma Abu Bakrakaifikishe Sura Baraa kwa niaba yake, baada ya kumtuma alimpeleka Alibin Abu Talib (a.s.) akamwambia: “Ewe Ali! Hakika hafikishi kwa niabayangu ila mimi mwenyewe au wewe.” Kisha akamwambia amfuate akiwajuu ya ngamia wake al-Ádhb?u, akaenda mpaka akamkuta Abu Bakr naakaichukua Sura Baraa toka kwake. Abu Bakr akaja kwa Mtume (s.a.w.w.)na hali kaingiwa na khofu kutokana na hilo kwamba huenda kuna chochotekimeteremshwa kumhusu yeye. Alipofika kwa Mtume akasema:“Nimefanya nini ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu?” Akasema:

60

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 60

Page 70: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

“Hafikishi kwa niaba yangu asiyekuwa mimi au mtu kutokana na mimi.”76

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Je, mnafanya kuwanywesha mahujaji na kuamirisha msikiti mtuku-fu ni sawa na yule aliyemwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwishona akapigana jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu? Hawawi sawambele ya Mwenyezi Mungu na Mwenyezi Mungu hawaongozi watumadhalimu.” (Sura Tawba: 19).

Ibnu Mardawayhi ameandika kutoka kwa Ibnu Abbas kususu kauli yaMwenyezi Mungu: “Je, mnafanya kuwanywesha mahujaji na kuamirishamsikiti mtukufu” kwamba alisema: Iliteremka kwa ajili ya Ali bin AbuTalib (a.s.).

Ibnu Jariri ameandika kutoka kwa Muhammad Ka’b al-Qardhiy kwambaalisema: Talha bin Shayba, Abbas na Ali bin Abu Talib kila mmoja ali-jigamba. Talha akasema: ‘Mimi ndio mtunza Nyumba funguo zimomikononi mwangu.’ Abbas akasema: ‘Mimi ndiye mgawa maji na msi-mamizi wake.’ Ali akasema: ‘Sijui mtasema nini. Bila shaka nimeswalikabla ya mtu yeyote na mimi ndiye mwanajihadi.’ Ndipo MwenyeziMungu akateremsha: “Je, mnafanya kuwanywesha mahujaji na kuamirisha

61

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

76 Hii yenyewe ni dalili tosha kwamba Abu Bakr hastahiki kuwa mwakilishi waMtume (s.a.w.w.) katika jambo kama hili, lakini cha kushangaza yeye mwenyewealijitangaza kuwa ni Khalifa wa Mtume wa Mwenyezi Mungu bila dalili walatamko la Mtume au la Qur’ani. Na hali katika Umma yupo aliye mbora kushindayeye naye si mwingine ni Ali bin Abu Talib.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 61

Page 71: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

msikiti mtukufu ni sawa na yule aliyemwamini Mwenyezi Mungu na sikuya mwisho na akapigana jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu? Hawawisawa mbele ya Mwenyezi Mungu na Mwenyezi Mungu hawaongozi watumadhalimu.”

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Wameridhia kuwa pamoja na wanaobakia nyuma, na nyoyo zaozimepigwa muhuri, kwa hiyo hawafahamu.” (Sura tawaba: 87).

Ibnu Mardawayhi ameandika kutoka kwa Sa’d bin Abi Waqqas kwambaAli bin Abu Talib alitoka na Mtume (s.a.w.w.) mpaka wakafika Thaniyatul-Wida’u akikusudia kwenda Tabuk na hali Ali akilia na akisema:“Unaniacha pamoja na wanaobaki nyuma.” Mtume wa Mwenyezi Munguakasema: “Hivi huridhii kuwa wewe kwangu mimi una nafasi ya Harunkwa Musa ila ni kwamba hakuna unabii baada yangu.”77

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na wale waliotangulia wakawa wa kwanza katika Muhajiri naAnsari...” (Sura Tawba: 100).

Ibnu al-Mardawayhi ameandika kutoka kwa Ibnu Abbas kwamba alisema:“Wale waliotangulia wakawa wa kwanza katika Muhajiri ni: Ali, Salmanna Ammar bin Yasir.”

62

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

77 Ad-Durul-Manthur Juz. 3 Uk. 266.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 62

Page 72: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Enyi mlioamini! mcheni Mwenyezi Mungu na kuweni pamoja nawakweli.” (Sura Tawba: 119).

Ibnu al-Mardawayhi ameandika kutoka kwa Ibnu Abbas kuhusu kauli yake(s.w.t.): “Mcheni Mwenyezi Mungu na kuweni pamoja na wakweli.”Kwamba alisema: “Yaani kuweni pamoja na Ali bin Abu Talib.”

Ibnu Asakir ameandika kutoka kwa Abu Ja’far kuhusu kauli yake (s.w.t.):“Na kuweni pamoja na wakweli.” Kwamba alisema: “Yaani kuweni pamo-ja na Ali bin Abu Talib (a.s.).”

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Hayo ni kwa sababu haiwafikii kiu wala taabu wala njaa katika njiaya Mwenyezi Mungu, wala hawakanyagi njia iwachukizayo makafiri.”(Sura Tawba: 120).

Al-Hakim na Ibnu al-Mardawayhi wameandika kutoka kwa Ali (a.s.)kwamba alisema: Mtume wa Mwenyezi Mungu alitoka kwenda kwenyemoja ya vita na akamwacha Ali kama makamu wake kwa ndugu zake. Aliakasema: “Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Unaniacha Maquraishiwatasema nini, watasema amemtelekeza binamu yake mapema mno naamemwengua. Nami naona ni bora nitafute fadhila kutoka kwa MwenyeziMungu kwa sababu nimemsikia Mwenyezi Mungu akisema: “walahawakanyagi njia iwachukizayo makafiri.” Mtume akasema: “Ama kauliyako: Maquraishi watasema nini, watasema amemtelekeza binamu yake

63

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 63

Page 73: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

mapema mno na amemwengua. Bila shaka walishasema: Hakika mimimchawi na kuhani. Wakasema: Hakika mimi mwongo. Hivyo una kigezochema kwangu, huridhii kuwa wewe kwangu mimi una nafasi ya Harunkwa Musa ila ni kwamba hakuna Nabii baada yangu.”

SURAT YUNUSKauli ya Mwenyezi Mungu:

“Sema: Kwa fadhili za Mwenyezi Mungu na kwa rehema zake basiwafurahi, hiyo ni bora kuliko wanavyovikusanya.” (Yunus: 58).

Al-Khatib na Ibnu Asakir wameandika kutoka kwa Ibnu Abbas kwambaalisema: “Sema: Kwa fadhili za Mwenyezi Mungu” fadhila ni Nabii(s.a.w.w.). “na kwa rehema zake” rehema zake ni Ali bin Abu Talib.

SURAT HUD

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Basi je, aliye na dalili wazi itokayo kwa Mola wake na anaifuata nashahidi atokaye kwake..” (Sura Hud: 17).

Ibnu Mardawayhi na Ibnu Asakir wameandika kutoka kwa Ali kwambaalisema: “Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) ndiye aliye na daliliitokayo kwa Mola Wake, na mimi ndiye shahidi atokaye kwake.”

Ibnu Abi Hatim, Ibnu Mardawayhi na Abu Naim katika al-Ma’rifa wame-andika kutoka kwa Ali bin Abu Talibi kwamba: Alisema Ali (a.s.):

64

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 64

Page 74: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

“Hakuna mtu yeyote miongoni mwa makuraishi ila kuna sehemu yaQur’ani ilishuka kwa ajili yake.”

Ndipo mtu mmoja akamwambia: ‘’Ni ipi iliyoteremka kwa ajili yako?’’Aliakasema: “Hivi hausomi Sura Hud: “Basi je, aliye na dalili wazi itokayokwa Mola Wake na anaifuata na shahidi atokaye kwake..” Mtume waMwenyezi Mungu (s.a.w.w.) ndiye aliye na dalili itokayo kwa Mola Wake,na mimi ndiye shahidi atokaye kwake.”

Ibnu Mardawayhi ameiandika kwa njia nyingine kutoka kwa Ali (a.s.)kwamba alisema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Aliyena dalili itokayo kwa Mola Wake ni mimi, na shahidi atokaye kwake ni Ali(a.s.).”

SURAT AR-RAAD

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na katika ardhi mna vipande vilivyokaribiana. Na zipo bustani zamizabibu na mimea mingine na mitende ichipuayo kwenye shina naisiyochipua kwenye shina moja inayonyweshelezwa maji yaleyale.”(Raad: 4).

Al-Hakim ameiandika na Ibnu Mardawayhi amesema ni hadithi sahihi,kutoka kwa Jabir kwamba alisema: Nilimsikia Mtume wa MwenyeziMungu (s.a.w.w.) akisema: “Ewe Ali! Watu wanatokana na miti tofauti. Namimi na wewe tunatokana na mti mmoja.” Kisha Mtume (s.a.w.w.) akaso-ma: “Na katika ardhi mna vipande vilivyokaribiana. Na zipo bustani zamizabibu na mimea mingine na mitende ichipuayo kwenye shina na isiy-

65

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 65

Page 75: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

ochipua kwenye shina moja inayonyweshelezwa maji yaleyale.”78

Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Hakika wewe ni mwonyaji tu. Na kilakaumu ina wa kuwaongoza.” (Sura ar-Raad: 7).

Ibnu Jariri, Ibnu Mardawayhi, Abu Naim katika al-Ma’rifa, Daylamiy,Ibnu Asakir na Ibnu Najjar wameandika kwamba: Ilipoteremka: “Hakikawewe ni mwonyaji tu. Na kila kaumu ina wa kuwaongoza.” Mtume waMwenyezi Mungu (s.a.w.w.) aliweka mkono wake juu ya kifua chake nakusema: ‘Mimi ndiye mwonyaji.’ Kisha akaashiria mkono wake kwenyebega la Ali bin Abu Talib na kusema: ‘Ali wewe ndiye mwongozaji.Kupitia kwako wataongoka wenye kutaka kuongoka baada yangu.”

Ibnu Mardawayhi ameandika kutoka kwa Abi Barzati al-Aslamiy kwambaalisema: Nilimsikia Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akisema:“Hakika wewe ni mwonyaji tu.” Akaweka mkono wake juu ya kifua chake.Kisha akauweka juu ya kifua cha Ali huku akisema: “Kila kaumu ina wakuwaongoza.”

Ibnu Mardawayhi na al-Dhiyau katika al-Mukhtar wameandika kutokakwa ibnu Abbas kwamba alisema: Mtume wa Mwenyezi Mungu alisema:“Mwonyaji ni mimi na Mwongozaji ni Ali bin Abu Talib (a.s.).”

Abdullah bin Ahmad katika Zawaidul-Musnad, Ibnu Abi Hatim, Tabaraniykatika al-Awsat, al-Hakim na wamesema ni hadithi sahihi. IbnuMardawayhi na Ibnu Asakiri, hao wote wameiandika kutoka kwa Ali binAbu Talib kuhusu kauli ya Mwenyezi Mungu: “Hakika wewe ni mwonya-ji tu. Na kila kaumu ina wa kuwaongoza.” kwamba alisema: “Mtume waMwenyezi Mungu (s.a.w.w.) ndiye Mwonyaji, na mimi ndiyeMwongozaji.”79

66

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

78 Ad-Durul-Manthur Juz. 4, Uk. 44.79 Ad-Durul-Manthur Juz. 4, Uk. 45

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 66

Page 76: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

SURAT ISRAIKauli ya Mwenyezi Mungu:

“Utukufu ni wa yule ambaye alimpeleka mja wake usiku kutokaMsikiti Mtukufu mpaka msikiti wa mbali ambao tumevibarikivilivyoko pembezoni mwake, ili tumwonyeshe baadhi ya dalili zetu.Hakika yeye ni Mwenye kusikia, Mwenye kuona.” (Sura Israi: 1).

Tabarani ameandika kutoka kwa Aisha kwamba alisema: Mtume waMwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Nilipopelekwa mbinguni niliin-gizwa peponi, nikaona mti mmoja miongoni mwa miti ya peponi ambaosijaona peponi mzuri kushinda wenyewe, wala wenye majani yang’aayokushinda wenyewe, na wala wenye matunda matamu kushinda wenyewe,nikachuma moja ya matunda yake na nikala, ndipo mbegu za uzazi zikap-atikana katika uti wa mgongo wangu kutokana na tunda hilo, nilipoterem-ka ardhini nilimwingilia Khadija na ndipo akashika mimba ya Fatima(a.s.), hivyo niwapo na hamu ya kunusa harufu ya pepo hunusa harufu yaFatima.”80

Al-Hakim ameandika kutoka kwa Sa’d bin Waqqas kwamba alisema:Mtume wa Mwenyezi Mungu alisema: “Jibril (a.s.) aliniletea pera nikalilausiku ambao nilipelekwa miraji, na ndipo Khadija akashika mimba yaFatima, hivyo niwapo na hamu ya harufu ya peponi huinusa shingo yaFatima.”81

67

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

80Ad-Durul-Manthur Juz. 4, Uk. 153. Mtume wa Mwenyezi Mungu alisema:“Binti yangu Fatima ni Hurulaini wa kibinadamu, hajawahi kupata hedhi walanifasi. Na hakika Mwenyezi Mungu alimpa jina la Fatima (Mwachanishi) kwasababu Mwenyezi Mungu amemwepusha dhidi ya moto yeye na vipenzi vyake.”Tazama kitabu Kanzul-Ummal Juz. 12, Namba 3422.81Ad-Durul-Manthur Juz. 4 Uk. 153.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 67

Page 77: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

Ibnu Adiy na Ibnu Asakir wameandika kutoka kwa Anas kwamba alisema:Mtume wa Mwenyezi Mungu alisema: “Nilipopelekwa Miiraji nilionanguzo ya Arshi imeandikwa: Hapana Mungu apasaye kuabudiwa kwa hakiila Allah na Muhammad ni Mtume wa Allah nimempa nguvu kupitiaAli.”82

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na mpe jamaa wa karibu haki yake na maskini na mwana njia, walausifanye ubadhirifu.” (Sura Israi: 26).

Al-Bazzar, Abu Ya’la, Ibnu Abi Hatim na Ibnu Mardawayhi wameandikakutoka kwa Abu Said al-Khudriy kwamba alisema: Ilipoteremka Aya hii:“Na mpe jamaa wa karibu haki yake na maskini na mwana njia, wala usi-fanye ubadhirifu.” Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alimwitaFatima na kumkabidhi Fadak.

Ibnu Mardawayhi ameandika kutoka kwa Ibnu Abbas kwamba alisema:Ilipoteremka: “Na mpe jamaa wa karibu haki yake na maskini na mwananjia, wala usifanye ubadhirifu.” Mtume wa Mwenyezi Mungu alimpaFatima Fadak.83

SURAT MARYAM

Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Na amani iko juu yake siku aliyozaliwa nasiku atakayofariki, na siku atakayofufuliwa hai.” (Sura Maryam: 15).

Ahmad, Abu Ya’la, Ibnu Habban, Tabarani, al-Hakim na Dhayau wame-andika kutoka kwa Abu Said kwamba alisema: Mtume wa Mwenyezi

68

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

82 Ad-Durul-Manthur Juz. 4 Uk. 153.83 Ad-Durul-Manthur Juz. 4 Uk. 177.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 68

Page 78: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Hasan na Husain ni mabwana wawili wa vijanawa peponi, ila kwa wana wawili wa khalati: Isa bin Mariam na Yahya binZakariya.”84

Ibnu Asakir ameandika kutoka kwa Qurrat kwamba alisema: Mbinguhaikuwahi kumlilia yeyote ila Yahya bin Zakariya na Husain bin Ali, nawekundu wake ndio kulia kwake.85

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Hakika wale ambao wameamini na wakatenda mema Mwingi warehema atawajaalia mapenzi.” (Sura Maryam: 96).

Ibnu Mardawayhi na Daylamiy wameandika kutoka kwa al-Barau kwam-ba alisema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alimwambia Ali binAbu Talib: “Ewe Ali sema: Ewe Mwenyezi Mungu! Nipe hifadhi Kwakona niwekee mapenzi Kwako, na niwekee mapenzi katika nyoyo za waumi-ni.” Ndipo Mwenyezi Mungu akateremsha: “Hakika wale ambaowameamini na wakatenda mema Mwingi wa rehema atawajaalia mapen-zi.” iliteremka kwa ajili ya Ali (a.s.).86

Tabarani na Ibnu Mardawayhi wameandika kutoka kwa Ibnu Abbas kwam-ba alisema: “Iliteremka kwa ajili ya Ali bin Abu Talib (a.s.): “Hakika waleambao wameamini na wakatenda mema Mwingi wa rehema atawajaaliamapenzi.” yaani mahaba katika nyoyo za waumini.”

69

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

84 Ad-Durul-Manthur Juz. 4 Uk. 262.85 Ad-Durul-Manthur Juz. 4 Uk. 264.86 Ad-Durul-Manthur Juz. 4 Uk. 287.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 69

Page 79: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

SURAT TAHA

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Akasema: Ee Mola wangu! Nipanulie kifua changu. Na unifanyiewepesi kazi yangu. Na ufungue fundo katika ulimi wangu. Wapatekufahamu kauli yangu. Na uniwekee waziri katika jamaa zangu.Ndugu yangu Harun. “ (Sura Twaha: 25 – 30)

Salfiy ameandika katika Tuyuriyat kutoka kwa Abu Jafar Muhammad binAli kwamba alisema: “Ilipoteremka: “Na uniwekee waziri katika jamaazangu. Ndugu yangu Harun. Nitie nguvu kupitia yeye.” Mtume waMwenyezi Mungu alikuwa juu ya kilele cha mlima, kisha akamwombaMola wake kwa kusema: Ewe Mwenyezi Mungu! Nitie nguvu kupitiandugu yangu Ali. Mwenyezi Mungu akamkubalia ombi hilo.”87

70

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

87 Ad-Durul-Manthur Juz. 4, Uk. 295. Kauli hiyo inaungwa mkono na kauli yaMtume: “Wewe kwangu mimi una nafasi ya Harun kwa Musa ila ni kwamba haku-na Nabii baada yangu.” Ambayo inatamka wazi kwamba Ali ndiye Khalifa waMtume wa Mwenyezi Mungu na ndiye Wasii, Waziri na Mwenye mamlaka baadayake. Hivyo kila aliyemwondoa katika nafasi yake ni mnyang’anyi. Kwa rejeazaidi rejea kitabu al-Aqdu At-Thamin cha Imam Shawkaniy.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 70

Page 80: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

SURAT HAJJKauli ya Mwenyezi Mungu:

“Bila shaka Mwenyezi Mungu atawaingiza wale walioamini nakufanya vitendo vizuri katika Bustani zipitazo mito chini yake, kwahakika Mwenyezi Mungu hufanya atakavyo.” (Sura Hajj: 14).

Abdu bin Hamid ameandika kutoka kwa Lahiq bin Hamid kwamba alise-ma: Iliteremka: “Bila shaka Mwenyezi Mungu atawaingiza wale walioami-ni na kufanya vitendo vizuri……na kuongozwa kwenye njia ya Mwenyekuhimidiwa.” (Sura Twaha: 14 - 24) kwa ajili ya Ali bin Abu Talib, Hamza,na Ubaydah bin al-Harith.88

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Mwenyezi Mungu huchagua Wajumbe miongoni mwa Malaika namiongoni mwa watu, kwa hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenyekusikia, Mwenye kuona.” (Sura Hajj: 75).

Al-Baghawi ameandika katika Mu’jam, al-Barudiy, Ibnu Qaniu, Tabaranina Ibnu Asakir, wote wameandika kutoka kwa Zayd bin Abi Awfa kwam-ba alisema: “Niliingia kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu katika Msikiti waMadina, akaanza kusema yuko wapi bin fulani? Aliendelea kuwaita mpakawakakusanyika kwake, kisha akasema: “Mimi nataka kuwasimulienihadithi hivyo ihifadhini na muizingatie na mje kuwasimulia walewatakaokuja baada yenu: Hakika Mwenyezi Mungu aliteua kutoka mion-

71

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 71

Page 81: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

goni mwa viumbe Wake, viumbe maalumu: “Mwenyezi Mungu huchaguaWajumbe miongoni mwa Malaika na miongoni mwa watu,” viumbeatakaowaingiza peponi. Na mimi nachagua toka miongoni mwenu ambayenimependa kumchagua, na ninaweka udugu baina yenu kama MwenyeziMungu alivyoweka udugu baina ya Malaika.”

Kisha akamwita Sa’d bin Abi Waqqas na Ammar bin Yasir, akasema: “EweAmmar! Kundi ovu litakuuwa.” Kisha akaweka udugu baina yao. Ndipoakamwita Abu Dardau na Salman al-Farsiy na kusema: “Ewe Salman!Wewe ni katika watu wa nyumba.” Kisha akaweka udugu baina yao. kishaakatizama nyuso za masahaba zake akasema: “Furahini na tulieni.” Aliakasema: “Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Roho yangu imenitoka namgongo wangu umevunjika pale nilipokuona umewafanyia hayo sahabazako na kuniacha, basi ikiwa ni kutokana na ghadhabu yako juu yangu basionyo na heshima ni miliki yako.

Mtume akasema: “Naapa kwa yule Ambaye amenituma kwa haki,sikukuacha ila ili uwe kwa ajili yangu mwenyewe, kwani wewe kwangumimi una nafasi ya Harun kwa Musa, na ni mrithi wangu.” Ali akasema:Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Nitarithi nini toka kwako? Akasema:“Kile walichorithi warithi wa Manabii kabla yako: Kitabu cha MwenyeziMungu na Sunna ya Nabii wao, nawe pamoja na Fatima mtakuwa namikatika kasri la peponi, nawe ni ndugu yangu na rafiki89 yangu.” KishaMtume akasoma Aya hii: “Ndugu wakikaa juu ya viti kwa kuelekeana.”(Sura Hijri: 47).

72

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

88 Ad-Durul-Manthur Juz. 4, Uk. 349.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 72

Page 82: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

SURAT NURU

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Katika nyumba ambazo Mwenyezi Mungu ameruhusu ziinuliwe nakutajwa humo jina lake, wanamtakasa humo asubuhi na jioni.” (SuraNuru: 36).

Ibnu Mardawayhi ameandika kutoka kwa Anas bin Malik na Buraydakwamba walisema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisoma Ayahii: “Katika nyumba ambazo Mwenyezi Mungu ameruhusu ziinuliwe nakutajwa humo jina lake, wanamtakasa humo asubuhi na jioni.” Akasimamamtu mmoja na kumuuliza: “Ni nyumba zipi hizi ewe Mtume wa MwenyeziMungu?” Akasema: “Nyumba za Manabii.” Abu Bakr akasimama nakusema: “Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Nyumba hii ni miongonimwazo, nyumba ya Ali na Fatima? “ Akajibu: “Ndio ni miongoni mwazobali ndio iliyo bora kuliko nyingine.”

SURAT AS-SAJDA

Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Je, aliye muumini ni sawa na aliye fasiki?Hawawi sawa!” (Sura As-Sajda: 18).

Abu al-Faraj al-Asbahani ameandika katika kitabu al-Aghaniy, al-Wahidiy,Ibnu Adiy, Ibnu Mardawayhi, al-Khatib na Ibnu Asakir, wamepokea kwanjia tofauti kutoka kwa Ibnu Abbas kwamba alisema: Walid bin Uqbah binAbu Muit alimwambia Ali: ‘Mimi ni mfasaha kuliko wewe, mwenye menomakali kuliko wewe na shujaa kuliko wewe na hodari wa mapambanokuliko wewe.’ Ali akamjibu: ‘Nyamaza, bila shaka wewe ni fasiki.’ Ndipo

73

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 73

Page 83: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

Mwenyezi Mungu akateremsha: “Je, aliye muumini ni sawa na aliye fasi-ki? Hawawi sawa.” Yaani Muumini ni Ali na Fasiki ni Walid bin Uqbah binAbu Muit.90

Ibnu Is’haq na Ibnu Jariri wameandika kutoka kwa Atau bin Yasar kwam-ba alisema: Iliteremka Madina ikimuhusu Ali bin Abu Talib na Walid binUqbah. Kulikuwa na mzozo baina ya Walid na Ali, Walid bin Uqbahakamwambia Ali: ‘Mimi ni mfasaha kuliko wewe, mwenye meno makalikuliko wewe na shujaa kuliko wewe na hodari wa mapambano kulikowewe.’ Ali akamjibu: ‘Nyamaza, bila shaka wewe ni fasiki.’ NdipoMwenyezi Mungu akateremsha: “Je, aliye muumini ni sawa na aliye fasi-ki? Hawawi sawa!”91

Ibnu Abi Hatim ameandika kutoka kwa Abdurahman bin Abi Layla kuhusukauli ya Mwenyezi Mungu: “Je, aliye muumini ni sawa na aliye fasiki?Hawawi sawa,” kwamba alisema: Iliteremka ikimhusu Ali bin Abu Talib –yaani ndio Muumini, na Walid bin Uqbah – yaani Fasiki.92

Ibnu Mardawayhi, al-Khatib na Ibnu Asakir wameandika kutoka kwa IbnuAbbas kuhusu kauli ya Mwenyezi Mungu: “Je, aliye muumini ni sawa naaliye fasiki? Hawawi sawa,” kwamba alisema: Muumini ni Ali bin AbuTalib. Na Fasiki ni Walid bin Uqbah bin Abu Muit. Hiyo inatokana nasababu iliyokuwa baina yao, ndipo Mwenyezi Mungu akateremsha ayahiyo.93

74

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

89 Ad-Durul-Manthur Juz. 4, Uk. 371.90 Ad-Durul-Manthur Juz. 5 Uk. 178.91 Ad-Durul-Manthur Juz. 5 Uk. 178.92 Ad-Durul-Manthur Juz. 5 Uk. 178.93 Ad-Durul-Manthur Juz. 5 Uk. 178.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 74

Page 84: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

SURAT AHZAB

Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Nabii ana mamlaka zaidi kwa wauminikuliko nafsi zao…” (Sura Ahzab: 6).

Ibnu Abi Shayba, Ahmad na Nasai wameandika kutoka kwa Buraydakwamba alisema: “Nilishiriki vita pamoja na Ali huko Yaman, nikaonakwake ambalo sikupendezwa nalo, nilipofika kwa Mtume wa MwenyeziMungu (s.a.w.w.) nilimtaja Ali na nikaanza kumshusha hadhi, ghaflanikaona uso wa Mtume wa Mwenyezi Mungu umebadilika, akaniambia:“Ewe Buraydah! Mimi si mwenye mamlaka kwa waumini kuliko nafsizao?” nikasema ndio ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu. Akasema: “Basiyule ambaye mimi ni mwenye mamlaka juu yake Ali ni mwenye mamlakajuu yake.”94

Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Na Mwenyezi Mungu amewatoshelezaWaumini katika vita…” (Sura Ahzab: 25).

Ibnu Abi Hatim, Ibnu Mardawayhi na Ibnu Asakir wameandika kutokakwa Ibnu Masu’d kwamba alikuwa akisoma hivi: “Na Mwenyezi Munguamewatosheleza Waumini katika vita kupitia Ali bin Abu Talib.”95

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea ucha-fu, enyi watu wa nyumba ya Mtume, na kuwatakasa kabisa kabisa.”(Sura Ahzab:33).

Ibnu Jariri, Ibnu Mundhir, Ibnu Abi Hatim, Tabaraniy na Ibnu Mardawayhi

75

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

94 Ad-Durul-Manthur Juz. 5 Uk. 182.95 Ad-Durul-Manthur Juz. 5 Uk. 192.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 75

Page 85: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

wameandika kutoka kwa Ummu Salama mke wa Mtume (s.a.w.w.) kwam-ba: “Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alikuwa nyumbani kwakeameketi juu ya kitanda na hali kajifunika kishamia cha Khaibari, ndipoakaja Fatima akiwa na chungu chenye uji na kuingia nacho kwa Mtume.Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akamwambia mwite mumeo nawanao Hasan na Husain. Akawaita na ghafla walipokuwa wakila iliterem-ka kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.): “Hakika si mengineyoMwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu, enyi watu wa nyumba yaMtume, na kuwatakasa kabisa kabisa.” Mtume akachukua sehemu iliyozi-di ya kishamia chake na kuwafunika. Kisha akatoa mkono wake ndani yakishamia akaunyoosha mbinguni na kusema: “Ewe Mwenyezi Mungu!Hawa ndio Ahlul-Baiti wangu na watu makhsusi kwangu, hivyo waon-dolee uchafu na watakase kabisa kabisa.” Alisema hivyo mara tatu.Nikaingiza kichwa chumbani kwa Mtume na kumwambia: Je na mimi nipamoja nanyi ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu? Akasema: “Hakikawewe utaelekea katika kheri.” Alisema mara mbili.96

Tabarani ameandika kutoka kwa Ummu Salama kwamba alisema: Fatimaalikuja kwa baba yake akiwa amemletea uji uliokuwa ndani ya bakuli lake,akauweka mbele yake. Mtume akasema: “Yupo wapi mwana wa amiyako?” akasema yupo nyumbani. Akamwambia nenda ukamwite yeye nawanao. Akaja na wanae akiwa amemshika kila mmoja mkono na huku Aliakitembea nyuma yao, mpaka walipoingia kwa Mtume wa MwenyeziMungu (s.a.w.w.), akamkalisha kila mmoja kati yao (Hasan na Husein)katika paja lake, Ali akakaa kuliani kwake na Fatima kushotoni kwake.Kisha kikachukuliwa kishamia kilichokuwa kimetandikwa juu ya kitandachumbani kwangu.

Tabarani ameandika kutoka kwa Ummu Salama kwamba Mtume waMwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema kumwambia Fatima (a.s.): Niitiemumeo na wanao. Akawaita na ndipo Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w.) akawafunika kishamia cha Fadaki, kisha akaweka mkono wake

76

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

96 Ad-Durul-Manthur Juz. 5 Uk. 198.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 76

Page 86: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

juu yao na kusema: “Ewe Mwenyezi Mungu! Hawa ndio AaliMuhammadi, hivyo weka Sala zako na baraka zako juu ya AaliMuhammadi kama ulivyoziweka juu ya Aali Ibrahim, hakika Wewe niMhimidiwa Msifiwa.” Ummu Salama anasema: Nikainua kishamia iliniingie pamoja nao, lakini akakivuta toka mikononi mwangu na kuni-ambia: Hakika wewe uko kwenye kheri.97

Ibnu Mardawayhi ameandika kutoka kwa Ummu Salama kwamba alisema:Aya hii iliteremka nyumbani kwangu: “Hakika si mengineyo MwenyeziMungu anataka kuwaondolea uchafu, enyi watu wa nyumba ya Mtume, nakuwatakasa kabisa kabisa.” na nyumbani kulikuwa na watu saba: Jibril,Mikail, Ali, Fatima, Hasan na Husein, nami nikiwa nimesimama mlango-ni. Nikamwambia Mtume wa Mwenyezi Mungu je mimi sio katika Ahlul-Bait? Akasema: “Hakika wewe upo katika kheri, wewe ni miongoni mwawakeze Mtume.”

Ibnu Mardawayhi na Khatib wameandika kutoka kwa Said al-Khudriykwamba alisema: Ilikuwa ni siku ya Ummu Salama mama wa waumini,ndipo Jibril akateremka kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu akiwa na Ayahii: “Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea ucha-fu, enyi watu wa nyumba ya Mtume, na kuwatakasa kabisa kabisa.,”Mtume wa Mwenyezi Mungu akawaita Hasan, Husein, Fatima na Ali,akawakumbatia na kuwafunika nguo ilihali kukiwa na pazia kati yao naUmmu Salama, kisha akasema: “Ewe Mwenyezi Mungu! Hawa ndioAhlul-Baiti wangu, hivyo waondolee uchafu na watakase kabisa kabisa.”Ummu Salama akasema: Na mimi ni pamoja nao ewe Nabii wa MwenyeziMungu? Akasema: “Wewe una nafasi yako na bila shaka wewe upo katikakheri.”

Tirmidhiy ameandika na kusema kwamba ni sahihi, Ibnu Jariri, IbnuMundhir, al-Hakim, Mardawayhi na Bayhaqi katika Sunnani Yake, wotewameandika kwa njia tafauti kutoka kwa Ummu Salama kwamba alisema:

77

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

97 Ad-Durul-Manthur Juz. 5 Uk. 198.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 77

Page 87: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

“Nyumbani kwangu ndimo iliteremkia: “Hakika si mengineyo MwenyeziMungu anataka kuwaondolea uchafu, enyi watu wa nyumba ya Mtume, nakuwatakasa kabisa kabisa,” na hali ndani ya nyumba alikuwemo Fatima,Ali, Hasan na Husein, Mtume wa Mwenyezi Mungu akawafunikakishamia alichokuwa amejitanda, kisha akasema: “Hawa ndio Ahlul-Baitiwangu, hivyo waondolee uchafu na watakase kabisa kabisa.”98

Ibnu Jarir, Ibnu Abi Hatim na Tabarani wameiandika kutoka kwa Abu Saidal-Khudriy kwamba alisema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.)alisema: “Aya hii: “Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anatakakuwaondolea uchafu, enyi watu wa nyumba ya Mtume, na kuwatakasakabisa kabisa” imeteremka kwa ajili ya watano: Kwa ajili yangu, Ali,Fatima, Hasan na Husein.”

Ibnu Abi Shayba, Ahmad, Muslim, Ibnu Jarir, Ibnu Abi Hatim, na Hakimwameandika kutoka kwa Aisha kwamba alisema: “Siku moja Mtume ali-toka akajifunika shuka lililodariziwa na manyoya meusi. Wakaja Hasan naHusain akawafunika, kisha akaja Ali naye akamfunika, kisha akasema:“Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu,enyi watu wa nyumba ya Mtume, na kuwatakasa kabisa kabisa.’”

Ibnu Jarir, Hakim na Ibnu Mardawayhi wameandika kutoka kwa Sa’dkwamba alisema: Wahyi uliteremka na ndipo akawafunika Ali na Fatimashuka lake, kisha akasema: “Ewe Mwenyezi Mungu! Hawa ndio nduguzangu na Ahlul-Baiti wangu.”

Ibnu Abi Shayba, Ahmad, Ibnu Jarir, Ibnu Mundhir na Tabaraniy wame-andika kutoka kwa Wathila bin Asqaf kwamba alisema: Mtume waMwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alikuja kwa Fatima akiwa pamoja na Hasanna Husain na Ali, akaingia kisha akamsogeza Ali na Fatim na kuwakalishambele yake, na akawakalisha Hasan na Husein kila mmoja wao juu ya paja

78

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

98 Ad-Durul-Manthur Juz. 5 Uk. 198.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 78

Page 88: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

lake, kisha akawafunika shuka yake na hali mimi nikiwa nimewapa mgon-go, kisha akasoma Aya hii: “Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anata-ka kuwaondolea uchafu, enyi watu wa nyumba ya Mtume, na kuwatakasakabisa kabisa.”

Ibnu Abi Shayba, Ahmad, Tirmidhi na amesema ni hadithi hasan, IbnuJarir, Ibnu Mundhir, Tabaraniy, Hakim na amesema ni hadithi sahihi, naIbnu Mardawayhi, wote wameandika kutoka kwa Anas kwamba Mtumewa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alikuwa akipita mlangoni kwa Fatimaatokapo kwenda kuswali Sala ya Alfajri na husema: “Sala enyi Ahlul-Baiti,Sala enyi Ahlul-Baiti Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anatakakuwaondolea uchafu, enyi watu wa nyumba ya Mtume, na kuwatakasakabisa kabisa.”99

Ibnu Mardawayhi ameandika kutoka kwa Abu Said al-Khudriy kwambaalisema: “Ali alipomuoa Fatima, Mtume alikwenda mlangoni kwake sikuarobaini kila asubuhi, na alikuwa akisema: “Asalamu Alaykum Ahlul-BaitiWarahmatullah Wabarakatuhu. Mwenyezi Mungu akurehemuni. Hakika simengineyo Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu, enyi watu wanyumba ya Mtume, na kuwatakasa kabisa kabisa. Mimi ni mwenyekufanya vita na yule mwenye kuwapigeni vita nyinyi na ni mwenye amanina yule mwenye kufanya amani nanyi.”

Tabarani ameandika kutoka kwa Abu Hamrau kwamba alisema:“Nilimuona Mtume wa Mwenyezi Mungu muda wa miezi sita akijakwenye mlango wa Ali na Fatima na kusema: “Hakika si mengineyoMwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu, enyi watu wa nyumba yaMtume, na kuwatakasa kabisa kabisa.”

Ibnu Mardawayhi ameandika kutoka kwa Ibnu Abbas kwamba alisema:“Tulimshuhudia Mtume muda wa miezi tisa akija kila siku mlangoni kwaAli bin Abu Talib wakati wa kila Sala na kusema: “Asalamu Alaykum

79

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

99 Ad-Durul-Manthur Juz. 5, Uk. 199

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 79

Page 89: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

Ahlul-Baiti Warahmatullah Wabarakatuhu. Hakika si mengineyoMwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu, enyi watu wa nyumba yaMtume, na kuwatakasa kabisa kabisa. Mwenyezi Mungu akurehemuni.”Kila siku mara tano.

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na ulipomwambia yule ambaye Mwenyezi Mungu amemneemeshana wewe umemneemesha.” (Sura Ahzab: 37).

Bazzar, Ibnu Hatim, Hakim, na Ibnu Mardawayhi wameandika kutoka kwaUsama bin Zayd kwamba alisema: Abbas na Ali bin Abu Talib walikwen-da kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu na kumwambia: Tumekuja iliutueleze ni yupi umpendaye sana kati ya ndugu zako? Akasema:“Nimpendaye sana kati ya ndugu zangu ni Fatima.” Wakamwambia hatu-ulizi kuhusu Fatima. Akasema: “Ni Usama bin Zayd ambaye MwenyeziMungu amemneemesha nami nimemneemesha.” Ali bin Abu Talib akase-ma kisha nani ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu? Akasema: “Kisha wewekisha Abbas.” Abbas akasema: “Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Hiviumemuweka ami yako mwisho!” Mtume wa Mwenyezi Mungu akasema:“Hakika Ali alikutangulia kwa kuhama.”100

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Hakika Mwenyezi Mungu na malaika wake wanamswalia Nabii.Enyi ambao mmeamini! Mswalieni na mumsalimu kwa salamu.”(Sura Ahzab: 56).

80

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

100 Ad-Durul-Manthur Juz. 5, Uk. 201

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 80

Page 90: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

Said bin Mansur, Abdu bin Hamid, Ibnu Abi Hatim na Ibnu Mardawayhiwameandika kutoka kwa Ka’b bin Ajrah kwamba alisema: Ilipoteremka:“Hakika Mwenyezi Mungu na malaika wake wanamswalia Nabii. Enyiambao mmeamini! Mswalieni na mumsalimu kwa salamu,” tulisema: EweMtume wa Mwenyezi Mungu! Kukutolea salamu tumeshajua basi ni ipinamna ya kukusalia? Akasema (s.a.w.w.): “Semeni:

?????? ???? ??? ????? ???? ?? ????? ??? ????? ??? ??????? ???? ?????????

???? ???? ????. ? ???? ??? ????? ???? ?? ????? ??? ????? ??? ???????

‘Ewe Mwenyezi Mungu! Mrehemu Muhammad na aaliMuhammad kama ulivyomrehemu Ibrahim na aali Ibrahim, haki-ka Wewe ni Mhimidiwa Msifiwa. Na mbariki Muhammad na aaliMuhammad kama ulivyombariki Ibrahim na aali Ibrahim, hakikaWewe ni Mhimidiwa Msifiwa.’”101

Ibnu Jarir ameandika kutoka kwa Ka’b bin Ajrah kwamba alisema:Ilipoteremka Aya hii nilisimama na kumwambia: Ewe Mtume waMwenyezi Mungu! Kukutolea salamu tumeshajua basi ni ipi namna yakukusalia? Akasema (s.a.w.w.): “Semeni:

?????? ???? ??? ????? ???? ?? ????? ??? ????? ??? ??????? ???? ????????? ???? ???? ????.

‘Ewe Mwenyezi Mungu! Mrehemu Muhammad na aaliMuhammad kama ulivyomrehemu Ibrahim na aali Ibrahim, haki-ka Wewe ni Mhimidiwa Msifiwa. Na mbariki Muhammad na aaliMuhammad kama ulivyombariki Ibrahim na aali Ibrahim.’”

81

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

101 Ad-Durul-Manthur Juz. 5, Uk. 216

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 81

Page 91: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

Ibnu Jarir ameandika kutoka kwa Yunus bin Khabab kwamba alisema:“Faris alitutolea khutba akasema: “Hakika Mwenyezi Mungu na malaikawake wanamswalia Nabii. Enyi ambao mmeamini! Mswalieni na mumsal-imu kwa salamu.” Hakika amenipa habari yule aliyemsikia Ibnu Abbasakisema: Hivyo ndivyo ilivyoteremka, nao (masahaba) walisema: EweMtume wa Mwenyezi Mungu! Kukutolea salamu tumeshajua basi ni ipinamna ya kukusalia? Akasema (s.a.w.w.): “Semeni:

?????? ???? ??? ????? ???? ?? ????? ??? ????? ??? ??????? ??? ??????? ???? ???? ????. ????? ?????? ? ?? ????? ??? ?????? ??????? ???? ???? ????. ? ???? ??? ????? ? ?? ????? ???

????? ??? ??????? ???? ?? ??????? ???? ???? ????.

‘Ewe Mwenyezi Mungu! Msalie Muhammad na aali Muhammadkama ulivyomsalia Ibrahim na aali Ibrahim, hakika Wewe niMhimidiwa Msifiwa. Na mrehemu Muhammad na aaliMuhammad kama ulivyomrehemu Ibrahim na aali Ibrahim, haki-ka Wewe ni Mhimidiwa Msifiwa. Na mbariki Muhammad na aaliMuhammad kama ulivyombariki Ibrahim na aali Ibrahim, hakikaWewe ni Mhimidiwa Msifiwa.’”

Abu Daud, Ibnu Mardawayhi na al-Bayhaqiy katika Sunnan yake, wame-andika kutoka kwa Abu Huraira kwamba alisema: Mtume wa MwenyeziMungu (s.a.w.w.) alisema: “Anayependa alingane sawasawa na kipimokamili basi anapotusalia sisi Ahlul-Baiti aseme: Ewe Mwenyezi Mungumsalie Muhammad Nabii, yeye na dhuria wake na Ahlul-Baiti wake kamaulivyowasali Aali Ibrahim, hakika Wewe ni Mhimidiwa Msifiwa.”

Ibnu Abi Shayba, Ahmad, Abdu bin Hamid, Bukhari, Nasai, Ibnu Majah,na Ibnu Mardawayhi wameandika kutoka kwa Said al-Khudriy kwambaalisema: Tulisema: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Kukutolea salamu

82

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 82

Page 92: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

83

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

tumeshajua basi ni ipi namna ya kukusalia? Akasema (s.a.w.w.): “Semeni:

?????? ???? ??? ????? ???? ?????? ??? ????? ??? ?? ???????. ? ???? ??? ????? ???? ?? ????? ??? ????? ??? ?? ???????.

‘Ewe Mwenyezi Mungu! Msalie Muhammad mja Wako naMtume Wako kama ulivyowasalia aali Ibrahim. Na mbarikiMuhammad na aali Muhammad kama ulivyowabariki aaliIbrahim.’”102

Abdu bin Hamid, Nasai na Ibnu Mardawayhi wameandika kutoka kwa AbuHuraira kwamba alisema: Walimuuliza Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w.) ni jinsi gani tutakavyokusalia? Akasema: “Semeni:

?????? ???? ??? ????? ???? ?? ????? ? ???? ??? ????? ???? ?? ?????

‘Ewe Mwenyezi Mungu! Msalie Muhammad na aali Muhammad,na mbariki Muhammad na aali Muhammad kama ulivyomsalia nakumbariki Ibrahim na aali Ibrahim juu ya walimwengu, hakikaWewe ni Mhimidiwa Msifiwa.’”

Ibnu Mardawayhi ameandika kutoka kwa Abu Huraira kwamba alisema:“Tulisema ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Tumeshajua namna yakukutolea salamu, basi ni vipi tutakavyokusalia? Akasema: “Semeni: EweMwenyezi Mungu! Weka rehema na amani, na baraka Zako juu ya AaliMuhammad kama ulivyoziweka juu ya Aali Ibrahim, hakika Wewe niMhimidiwa Msifiwa.”

Ibnu Mardawayhi ameandika kutoka kwa Ali kwamba alisema: Nilisema:Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Ni namna gani tutakusalia? Akasema(s.a.w.w.): “Semeni: Ewe Mwenyezi Mungu msalie Muhammadi na Aali102 Ad-Durul-Manthur Juz. 5 Uk. 218

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:04 AM Page 83

Page 93: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

84

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

Muhammad kama ulivyomsalia Ibrahim na Aali Ibrahim, hakika Wewe niMhimidiwa Msifiwa.”

SURAT AS-SHURA

Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Sema: Kwa haya siwaombi malipo yoyotekwenu isipokuwa mapenzi kwa ndugu...” (Sura as-Shura: 23).

Abu Naim na Daylamiy wameandika kwa njia ya Mujahid kutoka kwaIbnu Abbas kwamba alisema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.)alisema: Kwa haya siwaombi malipo yoyote kwenu isipokuwa mapenzikwa ndugu, mnilindie heshima yangu kwa ndugu zangu na muwapendekwa ajili yangu.”103

Ibnu Mundhir, Ibnu Abi Hatim na Tabaraniy wameandika kwa njia ya Saidbin Jubair kutoka kwa Ibnu Abbas kwamba alisema: Ilipoteremka Aya hii:“Sema: Kwa haya siwaombi malipo yoyote kwenu isipokuwa mapenzikwa ndugu...” walisema: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Ni nani kara-ba zako hawa ambao tumewajibishwa kuwapenda? Akasema (s.a.w.w.):“Ali, Fatima na watoto wao.”

Ibnu Jarir ameandika kutoka kwa Abu Daylam kwamba alisema:Alipoletwa Ali bin Husein bin Ali bin Abu Talib (a.s.) na hali ni mateka nakusimamishwa katika barabara kuu ya Damascus alisimama mzee mmojakati ya watu wa Sham, akasema: “Kila sifa njema ni ya Mwenyezi Munguambaye amewauwa na kuwang’oeni na kung’oa mzizi wa fitina.” Ali binHusein akasema: ‘Umewahi kusoma Qur’ani?’ akajibu ndio. Akasema(a.s.): ‘Umewahi kusoma Aali Haa Miim?’ Akajibu hapana. Akasema(a.s.): ‘Umewahi kusoma: “Sema: Kwa haya siwaombi malipo yoyotekwenu isipokuwa mapenzi kwa ndugu...”’ Mzee akasema: ‘Nyinyi ndiohao?’ Akasema (a.s.): ‘Naam ndio sisi.’

103 Ad-Durul-Manthur Juz. 6 Uk. 7

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 84

Page 94: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

85

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

Muslim, Tirmidhiy na Nasai wameandika kutoka kwa Zayd bin Arqamkwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema:“Nawakumbusheni Mwenyezi Mungu kuhusu Ahlul-Baiti wangu, yaaniAli, Fatima, Hasan na Husein.”

Ibnu Adiy ameandika kutoka kwa Abu Said kwamba alisema: Mtume waMwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Atakayetuchukia sisi Ahlul-Baitibasi ni mnafiki.”

Tirmidhiy ameandika na kusema ni hadithi sahihi, na Ibnu al-Anbariy kati-ka al-Masahifu wameandika kutoka kwa Zayd bin Arqam kwamba alise-ma: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Hakika mimi nimwenye kuwaachia kati yenu vile ambavyo lau mkishikamana navyo katuhamtapotea baada yangu, kimojawapo ni kitukufu kuliko kingine: Kitabucha Mwenyezi Mungu kamba iliyonyooka toka mbinguni hadi ardhini. Nakingine ni kizazi changu watu wa nyumba yangu, na havitoachana mpakavinikute kwenye hodhi, basi angalieni ni jinsi gani mtakavyobaki navyo.”

Tabarani ameandika kutoka kwa Hasan bin Ali kwamba Mtume waMwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Hatatuchukia yeyote walakutuhusudu ila ataadhibiwa Siku ya Kiyama kwa mjeledi wa moto.

Ahmad bin Habban na al-Hakim wameandika kutoka kwa Abu Said kwam-ba alisema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: Naapa kwaYule Ambaye nafsi yangu imo mikononi mwake kwamba hakuna mtu yey-ote atakayetuchukia sisi Ahlul-Baiti ila ni lazima Mwenyezi Munguatamwingiza motoni.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 85

Page 95: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

86

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

SURAT MUHAMMAD

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na kama tungependa tungekuonyesha hao na ungewatambua kwaalama zao, na hasa utawafahamu kwa namna ya usemi wao, naMwenyezi Mungu anavijua vitendo vyenu.” (Sura Muhammad: 30).

Ibnu Mardawayhi na Ibnu Asakir wameandika kutoka kwa Abu Said al-Khudriy kwamba alisema kuhusu kauli ya Mwenyezi Mungu: “….na hasautawafahamu kwa namna ya usemi wao, na Mwenyezi Mungu anavijuavitendo vyao”: ni kwa kule kumchukia kwao Ali bin Abu Talib (a.s.).104

Ibnu Mardawayhi ameandika kutoka kwa Ibnu Mas’ud kwamba alisema:Hatukuwa tunawafahamu wanafiki zama za Mtume wa Mwenyezi Munguila kwa kule kumchukia kwao Ali bin Abu Talib (a.s.).105

SURAT RAHMAN

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Amezikutanisha bahari mbili. Baina yao kuna kizuizi haziingiliani.Basi nyinyi wawili mnakataa neema gani ya Mola wenu Mlezi? Katikahizo mbili hutoka lulu na marijani.” (Surat Rahman: 19 - 22).104Ad-Durul-Manthur Juz. 6 Uk. 66.105 Ad-Durul-Manthur Juz. 6 Uk. 66.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 86

Page 96: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

87

Ibnu Mardawayhi ameandika kutoka kwa Ibnu Abbas kwamba alisemakuhusu kauli ya Mwenyezi Mungu: “Amezikutanisha bahari mbili.” Ali naFatima kati yao kuna kizuizi hawaingiliani, kwani Mtume alisema:“Hutoka kwao hao wawili lulu na marijani, Hasan na Husein.”106

Ibnu Mardawayhi ameandika kutoka kwa Anas bin Malik kwamba alisemakuhusu kauli ya Mwenyezi Mungu: “Amezikutanisha bahari mbili”: “NiAli na Fatima, hutoka kwao hao wawili lulu na marijani, ambao ni Hasanna Husein.”

SURAT AL-WAQI’A

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na nyinyi mtakuwa namna tatu. Basi watu wenye kheri, watakuwanamna gani wenye kheri. Na watu wenye shari, watakuwa namna ganiwenye shari. Waliotangulia ndio waliotangulia.” (Sura al-Waqi’a: 7 -10).

Ibnu Mardawayhi ameandika kutoka kwa Ibnu Abbas kwamba alisemakuhusu kauli ya Mwenyezi Mungu: “Waliotangulia ndio waliotangulia”kuwa iliteremka kumuhusu Ali bin Abu Talib, na kila mtu miongoni mwaoni mtangulizi wa umma wake, na Ali ndiye mbora wao katika kutangu-lia.107

106 Ad-Durul-Manthur Juz. 6 Uk. 142107Ad-Durul-Manthur Juz. 6 Uk. 154.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 87

Page 97: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

88

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

Ibnu Abi Hatim na Ibnu Mardawayhi wameandika kutoka kwa Ibnu Abbaskwamba alisema kuhusu kauli ya Mwenyezi Mungu: “Waliotangulia ndiowaliotangulia”: Yoshua bin Nun ndiye aliyetangulia kumwamini Musa,Muumini wa Aali Yasin ndiye aliyetangulia kumwamini Isa, na Ali bin AbuTalib ndiye aliyetangulia Muhammad (s.a.w.w.).

SURAT MUJADILAH

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Enyi mlioamini! Mnaposema siri na Mtume, basi tangulizeni sadakakabla ya kumsemesha hayo ni bora kwenu na ni safi sana, na ikiwahamkupata basi Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe, Mwenyekurehemu.” (Sura Mujadilah: 12).

Abdu bin Hamid, Ibnu Mundhir na Ibnu Abi Hatim wameandika kutokakwa Mujahid kwamba alisema: “Walikatazwa kusema siri na Mtume(s.a.w.w.) mpaka watoe sadaka. Hakuna aliyeweza kusema naye siri ila Alibin Abu Talib, yeye alitoa sadaka ya dinari kisha akasema siri na Mtume(s.a.w.w.) na alimuuliza mambo kumi, ndipo (baada ya sadaka hiyo)ikateremka ruhusa (iliyoondoa sharti la sadaka.).”108

Said bin Mansur ameandika kutoka kwa Mujahid kwamba alisema:“Ilikuwa anayesema siri na Mtume ni lazima atoe sadaka ya dinari, na waawali aliyetekeleza hilo ni Ali bin Abu Talib, kisha ndipo ikateremkaruhusa: “…..na ikiwa hamkupata basi Mwenyezi Mungu ni Mwingi wakusamehe, Mwenye kurehemu.”

108 Ad-Durul-Manthur Juz. 6 Uk. 185.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 88

Page 98: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

Abdu bin Hamid ameandika kutoka kwa Salmah bin Kuhayli kuhusu kauliya Mwenyezi Mungu: “Enyi mlioamini! Mnaposema siri na Mtume, basitangulizeni sadaka kabla ya kumsemesha hayo ni bora kwenu na ni safisana, na ikiwa hamkupata basi Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusame-he, Mwenye kurehemu”: kuwa wa kwanza aliyeifanyia kazi ni Ali bin AbuTalib, kisha ikafutwa.

SURAT TAHRIM

Kauli ya Mwenyezi Mungu: “…..Basi Mwenyezi Mungu ni mlinzi wake,na Jibril na waumini wema na Malaika….” (Sura Tahrim: 4).

Ibnu Abi Hatim ameandika kutoka kwa Ali kwamba alisema: Mtume waMwenyezi Mungu alisema kuhusu ‘’Na waumini wema’’ kwamba ni Alibin Abu Talib.109

Ibnu Mardawayhi ameandika kutoka kwa Asmau binti Umaysi kwambaalisema: “Nilimsikia Mtume wa Mwenyezi Mungu akisema: ‘’Na waumi-ni wema’’ ni Ali bin Abu Talib.’”

Said bin Mansur, Abdu Hamid na Ibnu Mundhir wameandika kutoka kwaAlau bin Ziyad kuhusu kauli ya Mwenyezi Mungu: ‘’Na waumini wema’’ni Ali bin Abu Talib (a.s.).

SURAT AL-HAQQAH

Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Ili tuifanye ukumbusho kwenu, na sikiolisikialo lisikie.” (Sura al-Haqqah: 12).

Said bin Mansur, Ibnu Jarir, Ibnu Mundhir, Ibnu Abi Hatim na IbnuMardawayhi wameandika kutoka kwa Makhul kwamba alisema:

89

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

109 Ad-Durul-Manthur Juz. 6 Uk. 244.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 89

Page 99: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

Ilipoteremka Aya hii: “…..na sikio lisikialo lisikie,” Mtume wa MwenyeziMungu (s.a.w.w.) alisema: ‘’Nilimwomba Mwenyezi Mungu alifanyehivyo sikio la Ali.’’ Makhul anasema: Ali alikuwa akisema: “Sikusikia kituchochote toka kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu kisha nikakisahau.”110

Ibnu Jarir, Ibnu Abi Hatim, al-Wahidiy, Ibnu Mardawayhi, Ibnu Asakir naIbnu Najari wameandika kutoka kwa Burayda kwamba alisema: Mtumewa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alimwambia Ali: “Hakika MwenyeziMungu Mtukufu ameniamuru nikusogeze karibu nisikutenge mbali, nanikuelimishe nawe usikie vilivyo. Na Mwenyezi Mungu amehakikishaunasikia vilivyo.” Ndipo ikateremka Aya hii.

Abu Naim ameandika ndani ya al-Hilyah kutoka kwa Ali kwamba alisema:Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Ewe Ali! HakikaMwenyezi Mungu Mtukufu ameniamuru nikusogeze karibu na nikuelim-ishe nawe usikie vilivyo, ndipo ikateremka Aya hii: “…..na sikio lisikialolisikie.” hivyo wewe ndio sikio lisikialo vilivyo elimu yangu.”

SURAT AL-INSAN

Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Na huwalisha chakula masikini na yatima namfungwa hali ya kuwa wanakipenda. Tunakulisheni kwa ajili ya radhi zaMwenyezi Mungu tu, hatutaki kwenu malipo wala shukurani.” (Surat al-Insan: 8-9).

Ibnu Mardawayhi ameandika kutoka kwa Ibnu Abbas kuhusu kauli yaMwenyezi Mungu: “Na huwalisha chakula masikini na yatima na mfung-wa hali ya kuwa wanakipenda. Tunakulisheni kwa ajili ya radhi zaMwenyezi Mungu tu, hatutaki kwenu malipo wala shukurani.” Kwambailiteremka kwa ajili ya Ali bin Abu Talib na Fatima binti ya Mtume waMwenyezi Mungu (s.a.w.w.).111

90

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

110 Ad-Durul-Manthur Juz. 6 Uk. 360.111 Ad-Durul-Manthur Juz. 6 Uk. 299.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 90

Page 100: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

SURAT AL-BAYYINA

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Hakika wale walioamini na kutenda mema, hao ndio wema waviumbe.” (Surat al-Bayina: 7).

Ibnu Asakir ameandika kutoka kwa Jabir bin Abdillah kwamba alisema:Tulikuwa kwa Mtume na ndipo ghafla akaja Ali bin Abu Talib, Mtumeakasema: “Naapa kwa Yule Ambaye nafsi yangu imo mikononi mwake,hakika huyu na Shia wake ndio wenye kufuzu Siku ya Kiyama.” Ndipoikateremka: “Hakika wale walioamini na kutenda mema, hao ndio wemawa viumbe.” Basi masahaba wa Mtume wakawa atokeapo Ali husema:Amekuja kiumbe bora kushinda wote.112

Ibnu Adi ameandika kutoka kwa Ibnu Abbas kwamba alisema:“Ilipoteremka: “Hakika wale walioamini na kutenda mema, hao ndiowema wa viumbe.” Mtume wa Mwenyezi Mungu alisema kumwambia Ali:“Ni wewe na Mashia wako, Siku ya Kiyama mtakuja na hali mmeridhiananyi mmeridhiwa.”

Ibnu Mardawayhi ameandika kutoka kwa Ali kwamba alisema: Mtume waMwenyezi Mungu aliniambia: “Hivi hujasikia kauli ya Mwenyezi Mungu:“Hakika wale walioamini na kutenda mema, hao ndio wema wa viumbe.”Ni wewe na Mashia wako, ahadi yangu mimi na nyinyi ni kukutanakwenye Hodhi.

91

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

112 Ad-Durul-Manthur Juz. 6 Uk. 379.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 91

Page 101: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

SURAT NASRI

Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Utakapofika msaada wa MwenyeziMungu na ushindi.” (Sura Nasri: 1 ).

Ibnu Mardawayhi ameandika kutoka kwa Ibnu Abbas kwamba alisema:Mtume wa Mwenyezi Mungu alipofika kutoka Vita vya Hunayniilimteremkia Aya hii, ndipo Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akase-ma: “Ewe Ali bin Abu Talib! Na ewe Fatima binti Muhammad! Msaada waMwenyezi Mungu na ushindi vimefika, na nimeona watu wakiingia katikadini ya Mwenyezi Mungu makundi kwa makundi.”113

Tabarani ameandika kutoka kwa Ibnu Abbas kwamba alisema: Mtume waMwenyezi Mungu alipofika kutoka Vita vya Hunayni ilimteremkia Aya hii:“Utakapofika msaada wa Mwenyezi Mungu na ushindi.” ndipo Mtume waMwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akasema: “Ewe Ali bin Abu Talib! Na eweFatima binti Muhammad! Msaada wa Mwenyezi Mungu na ushindi vime-fika na nimeona watu wakiingia katika dini ya Mwenyezi Mungu makun-di kwa makundi. Ametakasika Mola wangu Mlezi na kila sifa njema niYake na ninamuomba sana maghufira, hakika Yeye ni Mwenye kupokeatoba. Ewe Ali! Lau ningekuwa namweka yeyote awe khalifa baada yangubasi yeyote asingekuwa na haki (ya ukhalifa huo) kuliko wewe,114 hiyo nikutokana na ukaribu wako na Uislamu, ukaribu wako na Mtume wa

92

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

113 Ad-Durul-Manthur Juz. 6, Uk. 407.114 Nasema: Ni wazi kwamba ziada hii ni nyongeza kutoka kwa wale wenyechuki na Ahlul-Baiti (a.s.), wale ambao kwa juhudi zao zote wamejitahidi kujaribukuuondoa ukhalifa na uwasii toka kwa Imam Ali na hivyo wakadai kwamba etiMtume hakuacha Wasii, alifariki bila kuusia. Lakini ukweli ni kama ulivyok-wishatambua hapo mwanzo kwamba Mtume (s.a.w.w.) aliusia ukhalifa kwa Ali naSiku ya Ghadir alimsimika rasmi mbele ya macho ya waumini, na kwa kinywa chakheri, ulimi wa ukweli na matamshi ya Wahyi akasema: “Yule ambaye mimi ninamamlaka juu yake basi huyu Ali ni mwenye mamlaka juu yake.”.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 92

Page 102: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.), ukwe wako, na kwako ndiko alikomwanamke bora kushinda wote wa ulimwenguni.”115

AHLUL-BAIT (A.S.) NDANI YA TAFSIRI YAAL-BARUSAWI, INAYOITWA TAFSIR RUHUL-BAYAN

FI TAFSIRIL-QUR’AN

BISMILAHI RAHMAN RAHIM

Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa Rehema Mwenye kurehemu

Ukisema: Kuna hekima gani Mwenyezi Mungu kufungua Kitabu chakekwa herufi Bau na si kwa herufi nyingine yeyote?

Jibu: Hakika kuna hikma kumi katika hilo la Mwenyezi Mungu kufunguaKitabu chake kwa herufi Bau.116

Ya Tisa: Hakika Bau ni herufi iliyokamilika kimaana yenyewe, kwani niherufi inayoonyesha, mwambatano, msaada na usaidizi. Inakamilishamaana ya tamko lingine pale inapolifanya jina la mbele liwe na Jari nalichukue sifa yake (Bau). Nayo ina hadhi na heshima ya juu kutokana nakule kulikamilisha tamko lingine kwa kutoa maana ya Tauhidi na mwon-gozo, kama alivyoashiria Sayiduna Ali kwa kusema: “Mimi ni nukta chiniya herufi Bau.” Hivyo Bau ina cheo cha kuongoza na kuelekeza katikaTauhidi.117

93

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

115 Nimemaliza mchakato wa tafsiri hii siku ya tano ya Mfunguo nne wa Mwaka1421 A.H. katika Jiji la Qum Takatifu.116 Tumeichagua ya kumi kwa kuwa ndio inayohusu mazungumzo yetu.117 Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 1 Uk. 7.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 93

Page 103: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

SURAT AL-BAQARAH

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na ambao huamini uliyoteremshiwa wewe, na yaliyoteremshwakabla yako, na Akhera wakiisadiki.” (Surat Al-Baqarah: 4).

Hakika mwenye kuvuka udhalili wa kizuizi cha dunia hupata utukufu wakusadikisha mambo ya Akhera na huwa anayaamini bila hata kuyashuhu-dia kwa macho, hivyo huwa ni mwenye yakini baada ya kuondoa kizuizi,kama alivyosema Amirul-Muuminina Ali (a.s.): “Lau kizuizi kikiondolewasintazidisha ila yakini.”118

Amesema: Tambua hakika sifa zinazomfanya mtu astahili kulaaniwa nitatu. Baadhi yao wamesema kwamba Yazid amelaaniwa kutokana naukafiri wake kuwa mashuhuri na kuenea kwa fedheha ya uovu wake palealipokufuru pale alipoamuru Husein auwawe. Na pale aliposema hukuakinywa pombe: “Ikiwa siku moja itaharamishwa na dini ya Muhammadbasi ichukue kupitia dini ya Masihi mwana wa Mariam.”

Wameafikiana kwamba inaruhusiwa kuwalaani wale waliomuuwa Husein,au aliyeamuru, au kuruhusu au kuridhia, kama alivyosema Taftazaniy:“Ukweli ni kwamba ridhaa ya Yazid juu ya kumuuwa Husein, furaha yakena kuwadhalilisha kwake Ahlul-Bait (a.s.) ni jambo mashuhuri kimaanaijapokuwa undani wake umetufikia kwa njia ya riwaya zisizokuwamutawatiri. Sisi hatuna shaka na mambo yake bali na imani yake, laana yaMwenyezi Mungu iwe juu yake na juu ya wasaidizi wake na wafuasi wake.Na Sahib bin Ubbad alipokuwa akinywa maji baridi husema: ‘Kiini cha

94

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

118 Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 1 Uk. 42.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 94

Page 104: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

ubaridi ni katika maji matamu, ambayo hutoa shukurani toka katika kinacha moyo.’ Kisha husema: ‘Ewe Mwenyezi Mungu! Anza upya kumlaaniYazidi.”119

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Wale wanaotoa mali zao katika njia ya Mwenyezi Mungu, kishahawafuatishii waliyoyatoa masimbulizi wala udhia, hao wana malipoyao kwa Mola wao Mlezi, wala haitakuwa hofu juu yao walahawatahuzunika.” (Sura Al-Baqarah: 262).

Imepokewa kwamba Hasan bin Ali (a.s.) alitamani chakula hivyo akauzakanzu ya Fatima kwa dirhamu sita, muombaji akamwomba naye akampa.Kisha akakutana na mtu anauza ngamia akamnunua kwa mali kauli, kishaakamuuza kwa mtu mwingine, na Hasan alipotaka kumpelekea thamaniyake yule aliyemuuzia kwa mali kauli hakumkuta. Ndipo akasimulia kisakwa Mtume (s.a.w.w.), Mtume akasema: “Ama muombaji alikuwa niRidh’wan, Muuzaji alikuwa ni Mikail, ama Mnunuzi alikuwa ni Jibril.”Ndipo ikateremka kauli ya Mwenyezi Mungu: “Wale wanaotoa mali zaokatika njia ya Mwenyezi Mungu, kisha hawafuatishii waliyoyatoa masim-bulizi wala udhia, hao wana malipo yao kwa Mola wao Mlezi, walahaitakuwa hofu juu yao wala hawatahuzunika.”120

95

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

119 Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 1 Uk. 179.120 Tafsiru Ruhul-Bayan Juz.3 Uk. 419

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 95

Page 105: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

SURAT AALI IMRAN

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“…Kila mara Zakariya alipoingia Mihrab hukuta vyakula. Akasema:Ewe Maryam unatoa wapi hivi. Akasema: Vinatoka kwa MwenyeziMungu. Hakika Mwenyezi Mungu humruzuku amtakaye bilahesabu.” (Sura Aali Imran: 37).

Mwandishi wa tafsiri hii anasema: “Katika Aya hii kuna dalili juu yaruhusa ya kuwakirimu mawalii, …….imepokewa kutoka kwa Mtumekwamba Mtume alizidiwa na njaa zama za ukame na ndipo Fatimaakamzawadia vipande viwili vya mkate na finyango ya nyama ambapoalimpa kipaumbele kabla ya nafsi yake mwenyewe, lakini Mtume alim-rudishia Fatima na kusema: “Chukua ewe mwanangu mpendwa.”Alipofunua bakuli alilikuta limejaa mikate na nyama, ndipo Fatima akapig-wa na butwaa na akatambua kuwa kimeteremka toka kwa MwenyeziMungu.

Mtume (s.a.w.w.) akasema: “Umetoa wapi hivi?” Akajibu: “Ni kutoka kwaMwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu humpa riziki amtakaye bilahesabu.”

Mtume akamhimidi Mwenyezi Mungu na kusema: “Kila sifa njema ni yaMwenyezi Mungu Ambaye amekufanya kifani wa seyida wa wana waIsrael (Mariam).”]

96

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 96

Page 106: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

Kisha Mtume (s.a.w.w.) akawakusanya Ali, Hasan na Husain. AkalaMtume na Ahlul-Baiti wake wote kwa pamoja mpaka wakashiba nachakula kikabaki kama kilivyokuwa kikiwa kimejaa. Ndipo Fatima akawa-gawia majirani zake wote.121

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na Malaika waliposema: Ewe Maryam! Hakika Mwenyezi Munguamekuteua na akakutakasa na akakuteua juu ya wanawake waulimwenguni.” (Sura Aali Imran: 42).

Kutoka kwa Ibnu Abbas amesema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.)alisema: “Wanawake bora ulimwenguni ni Maryam, Fatima, Khadija naAsia.” Ni Hadithi Hasan inaoana na Aya.

Na kutoka kwa Anas amesema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.)alisema: “Yakutosha kati ya wanawake wa ulimwenguni: Maryam bintiImran, Khadija binti Khuwaylid, Fatima binti Muhammad na Asia mke waFiraun.”122

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na watakaokuhoji baada kukufikia elimu hii, waambie: Njoonituwaite watoto wetu na watoto wenu, na wanawake zetu na wanawake

97

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

121 Tafsiru Ruhul-Bayan Juz.3 Uk. 29.122 Tafsiru Ruhul-Bayan Juz.3 Uk. 33

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 97

Page 107: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

wenu, na nafsi zetu na nafsi zenu, kisha tuombe kwa unyenyekevututake laana ya Mwenyezi Mungu iwashukie waongo.” (Sura AaliImran: 61).

Imepokewa kwamba wakristo wa Najran walipoitwa kwenye maapizanowalisema mpaka tutafakari. Walipoachana wakamwambia Aqib:“Unaonaje?” Akasema: Wallahi enyi wakristo mmeshaujua kwambaMuhammad ni Nabii aliyetumwa na bila shaka amewajieni na hoja yakini-fu kuhusu mtu wenu (Yesu), wallahi katu hakuna watu walioombeanalaana na Nabii kisha mkubwa wao akaendelea kuishi au mdogo wao kuza-liwa. Na kama mtafanya hivyo bila shaka mtaangamia, hivyo hakuna chakufanya ila ni nyinyi kuendelea kubakia katika imani yenu na dini yenu,nendeni mkamuage mtu huyu na mrejee nchini kwenu.

Ndipo kesho yake wakaja kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) naMtume akatoka akiwa amemkumbatia Husein na amemshika mkonoHasan huku Fatima akitembea nyuma yake na Ali akiwa nyuma ya Fatima.Akawaambia: “Mimi nitakapokuwa naomba nyinyi muwe mnaitikia.”

Askofu wao akasema: “Enyi wakristo! Mimi naziona nyuso hizi kama zita-muomba Mwenyezi Mungu auondoe mlima kutoka mahala pake, atauon-doa, msiapizane naye mtaangamia, na wala juu ya uso wa ardhi hatobakimkristo yeyote mpaka Siku ya Kiyama.”

Wakasema: Ewe Abul-Qasim! Tumeona tusiapizane na wewe natukuwache uendelee kuwa katika dini yako nasi tuendelee kubaki katikadini yetu. Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akasema: Mkikataakufanya maapizano basi msilimu mtapata haki waliyonayo waislamu namtawajibikiwa na yale yaliyo wajibu kwa waislamu. Wakakataa, ndipoMtume akawaambia: “Basi hakika mimi nitawapiga.” Wakasema:“Hatuna nguvu ya kupigana vita na waarabu, lakini sisi tunafanya suluhuna wewe usitushambulie kivita na wala usitufukuze na wala usitutoe kati-ka dini yetu…...”

98

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 98

Page 108: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Ambao hutoa katika raha na katika shida na wenye kujizuia naghadhabu na wenye kuwasamehe watu, na Mwenyezi Mungu hupen-da wafanyao wema.” (Sura Aali Imran:134).

Imesimuliwa kwamba mtumishi alikuwa amesimama juu ya kichwa chaHusain bin Ali (a.s.) naye (a.s.) akiwa pamoja na wageni wake katika mezaya chakula, ndipo bakuli lililokuwa mikononi mwa mtumishi likamdon-dokea Hasan (a.s.). mtumishi akasema: “na wenye kuwasamehe watu,”Hasan (a.s.) akasema: “Nimeshakusamehe.” Mtumishi akasema:“Mwenyezi Mungu hupenda wafanyao wema.” Hasan (a.s.) akasema:“Uko huru kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, na ninakuoza fulani.”123

SURAT AL-MAIDA

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na wale waliokufuru na kuzikadhibisha Aya zetu, hao ndio watu waMotoni.” (Sura al-Maida: 10).

Amesema: “Itakapofika Siku ya Kiyama bendera ya Mashuhadaa atak-abidhiwa Ali, na kila Shahidi atakuwa chini ya bendera yake, na kilaaliyeuawa pasi na haki atakuwa chini ya bendera ya Husain bin Ali, na hiyondio kauli ya Mwenyezi Mungu: “Siku tutakayowaita kila watu na Imamwao.”124

99

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

123 Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 4 Uk. 95.124 Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 6 Uk. 360.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 99

Page 109: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

SURAT AL-AN’AAM

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na tukampa Is’haka na Yakub, wote tukawaongoza, na Nuh tulim-wongoza zamani na katika kizazi chake, Daud na Sulaiman na Ayubna Yusuf na Musa na Harun. Na hivyo ndivyo tuwalipavyo wafanyawema. Na Zakaria na Yahya na Isa na Ilyasa, wote walikuwa miongo-ni mwa watu wema.” (Sura An’aam:84 - 85).

Na katika kumtaja Isa ni dalili ya kwamba kizazi kinapitia watoto wa binti,hivyo Hasan na Husain ni miongoni mwa kizazi cha Bwana wa MitumeMuhammad (s.a.w.w.) japokuwa ni kwa nasaba ya mama. Naatakayewaudhi hao wawili bila shaka amekiudhi kizazi chake (s.a.w.w.).

Fakiri125 anasema: “Ikiwa nasaba ya upande wa mama ni sahihi nainakubalika basi yule ambaye usharifu wake ni kupitia umamani nayeanakubalika, kama ilivyo kwa yule mwenye kupitia upande wa baba.Hivyo kigezo (katika usharifu) ni nasaba yake kukomea kwa ima Hasan auHusain, kwa upande wowote ule (sawa uwe mama au wa baba).”126

100

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

125 Mwandishi wa Tafsiru Ruhul-Bayan126 Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 7 Uk. 61.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 100

Page 110: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

SURAT AARAF

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na wakamuuwa yule ngamia na wakaasi amri ya Mola wao Mlezi nawakasema: Ewe Saleh! Tuletee unayotuahidi ikiwa wewe ni miongonimwa Mitume.” (Sura Aaraf: 77).

Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alimwambia Ali: “Ewe Ali hiviwajua ni nani muovu kuliko wote waliotangulia?” Akasema: “MwenyeziMungu na Mtume wake ndiye ajuaye.” Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w.) akasema: “Ni yule aliyemchinja ngamia.” Kisha akasema: “Hiviwajua ni nani muovu kuliko wote watakaokuja?” Akasema: “MwenyeziMungu na Mtume wake ndiye ajuaye.” Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w.) akasema: “Ni yule atakayekuuwa wewe.”127

SURAT TAWBA

Kauli ya Mwenyezi Mungu: “(Tangazo la) Kujitoa Mwenyezi Mungu naMtume wake kwa wale mlioahidiana nao miongoni mwa mushrikina.”(Sura Tawba: 1).

Kama ilivyopokewa ni kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.)alimpa uongozi wa Hija ya mwaka wa ukombozi wa Makka Itab binUsaydi, na katika msimu huo walihiji waislamu na mushrikina pamoja,hivyo ulipowadia mwaka wa tisa Mtume alimpeleka Abu Bakr awe kion-

101

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

127 Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 8 Uk. 195.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 101

Page 111: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

gozi wa msimu wa Hija. Alipotoka Abu Bakr kuelekea Makka Mtumealimtumia Ali akiwa amepanda Adhbau128 ili aende kuwasomea SuraBaraa mahujaji. Akaambiwa (s.a.w.w.): “Ewe Mtume wa MwenyeziMungu! ungemtumia Sura hiyo Abu Bakr.” Akasema: “Hafikishi kwaniaba yangu ila mtu atokanaye na mimi.”

Hiyo ni kwa sababu ada ya waarabu ni kwamba hawakilishi kabila katikauandishi au uvunjaji wa mkataba ila yule aliye chifu wa kabila hilo au mtuatokanaye na chifu wao au aliye ndugu wa chifu wao. Hivyo akamtuma Aliili kuondoa dhana hiyo….129

SURAT HUDKauli ya Mwenyezi Mungu:

“…na zitakuwako umma tutakazo zistarehesha, kisha zitawashikakutoka kwetu adhabu zenye kuumiza.” (Sura Hud: 48).

Amesema katika kitabu Uqad-Durar: “Ole wake muuwaji wa Husain vipiitakuwa hali yake pamoja na wazazi wake na babu yake.”Kisha akasoma shairi akisema:

Lazima Fatima atafika Siku ya Kiyama na hali gauni lake likiwalimetapakaa damu ya Husain.Ole wake yule ambaye waombezi wake ndio mahasimu wake, nabaragumu litapulizwa Siku ya Kiyama.Na katika Hadithi imesemwa: “Muuwaji wa Husain atakuwa kati-ka sanduku la Moto na atapata nusu ya adhabu ya watu wa duni-ani.”130

Imepokewa kutoka kwa Sha’abiy kwamba: Ali (a.s.) alipita huko Karbalaalipokuwa akielekea kwenye Vita vya Siffin, akasimama na akauliza jina

102

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

128 Jina la ngamia wa Mtume129 Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 10 Uk. 383.130 Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 12 Uk. 143.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 102

Page 112: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

la eneo hilo, wakamwambia linaitwa Karbala. Akalia sana mpaka ardhiikalowana kwa machozi yake, kisha akasema: “Niliingia kwa Mtume waMwenyezi Mungu (s.a.w.w.) nikamkuta akilia. Akaniambia: ‘Punde tuJibril alikuwa nami hapa na akanipa habari kwamba mwanangu Husainatauawa pembezoni mwa Mto Furati katika eneo linaloitwa Karbala. KishaJibril akatoa ukufi wa udongo na kuninusisha, ndipo sikuweza kuyazuiamacho yangu mpaka yalipotoa machozi.’”

Na imepokewa kwamba udongo huo Mtume wa Mwenyezi Mungu ali-uweka katika chupa na akamwambia Ummu Salama: “Hakika huu ni udon-go wa eneo la ardhi ambayo hapo atauawa Husain, hivyo pindiutakapouona umegeuka damu tambua kuwa ameuawa.” Ummu Salamaalisema: “Ulipofika usiku ambao aliuawa Husain nilimsikia msemaji aki-nadi: ‘Enyi mliomuuwa Husain kwa ujahili, jibashirieni adhabu naudhalili. Mmelaaniwa kwa ulimi wa mwana wa Daud, Musa na aliyekujana Injili.’131 Nikalia na nikatizama chupa nikakuta udongo umegeukadamu.”

Imeelezwa pia kwamba mbingu ilipatwa na wekundu kutokana na kuuawakwake.

Ibnu Sirin amesema: “Wekundu ambao huwa kwenye mawingu haukuwe-po hapo kabla mpaka pale alipouawa Husain, na hekima yake ni kamaalivyosema Ibnu al-Jawziy kwamba: Hakika ghadhabu zetu husababishawekundu usoni, na Haki (Mwenyezi Mungu) hana mwili, hivyo kupitiawekundu wa mawingu akadhihirisha ghadhabu yake juu ya yule aliye-muuwa Husain. Amefanya hivyo ili kudhihirisha ukubwa wa jinai. Na Sikuhiyo aliyouawa hakuna jiwe lililoinuliwa duniani ila chini yake kulikutwadamu nzito.”132

Abu Shaykhi ameandika kwamba: Hakika kuna kundi la watu lilikum-bushana kwamba hakuna yeyote aliyesaidia kuuawa Husain ila alisibiwa

103

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

131 Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 12 Uk. 144.132 Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 12 Uk. 144.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 103

Page 113: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

na balaa kabla ya kufariki kwake. Mzee mmoja akasema: ‘Mimi nilisaidiana sijapatwa na chochote.’ Ndipo aliposimama kwenda kutengeneza taa naghafla akaanza kuwaka moto huku akipiga kelele ‘moto moto moto’, aka-jidumbukiza katika Mto Furati, lakini pamoja na hilo aliendelea kuwakampaka akafariki.

Wengine walipatwa na kiu kali, ikawa wanakunywa wawezavyo lakini kiuhaitulii. Wengine waliadhibiwa kuuawa au upofu au kusawijika uso aukunyang’nywa utawala baada ya muda mchache tu, na mengineyo kamahayo. Hivyo baada ya kuyajua hayo jiepushe na wale wanaowafanyiauadui Ahlul-Baiti, na wala usiwe rafiki yao, kwani kufanya nao urafiki nikuwafanyia uadui Ahlul-Baiti na ni kuwachukia.133

SURAT AR-RAA’DKauli ya Mwenyezi Mungu: “Hakika wewe ni mwonyaji tu. Na kilakaumu ina wa kuwaongoza.” (Sura ar-Raad: 7).

Mwonyaji ni Muhammad, na kiongozi wa kuwaongoza ni Ali. Hoja juu yahilo ni kauli ya Mtume (s.a.w.w.): “Wallahi Mwenyezi Mungu kumuon-goza mtu mmoja kupitia wewe ni bora kwako kuliko kuwa na ngamiamwekundu.”134

Na Tabarani ameandika kwamba Ali alimwambia Fatima (a.s.): “Nabiiwetu ndio Nabii bora kushinda Manabii wote naye ni baba yako. Shahidiwetu ndiye shahidi bora kushinda mashahidi wote naye ni ami ya babayako Hamza. Na kutoka kwetu amepatikana aliye na mbawa mbili ana-zorukia peponi atakavyo, naye ni mwana wa ami ya baba yako Ja’far. Nakutoka kwetu wamepatikana watoto wa umma huu Hasan na Husain, naoni watoto wako. Na kutoka kwetu atapatikana al-Mahdi.”135

104

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

133 Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 12 Uk. 144.134 Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 13 Uk. 346.135 Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 13 Uk. 346.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 104

Page 114: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

SURAT ISRAI

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Sema: Kama mngezimiliki hazina za rehema ya Mola wangu Mlezi,hapo lazima nyinyi mngelizizuia kwa kuogopa kuzitumia, namwanadamu ni mchoyo sana.” (Surat Israi: 100).

Imepokewa kwamba Zainul-Abidin (a.s.) alikutana na mtu, ndipo mtu yuleakaanza kumtukana. Watumwa wake wakakasirika na kutaka kumwad-abisha, Zainul-Abidina akawaambia: “Mwacheni mtu huyu.” Kishaakamgeukia na kumwambia: “Yaliyositiriwa miongoni mwa mambo yetuni mengi, je una haja yoyote tukusaidie?” mtu yule akaona aibu, basiZainul-Abidina akamvulia kishamia chake na kumpa, na akaamrishaapewe dirhamu elfu moja.

Basi tangu siku ile mtu yule akawa akisema: “Nashahidilia kwamba haki-ka wewe ni miongoni mwa watoto wa mitume, wala aliyepotezwa hadhanikwamba wao walikuwa ni watu wa dunia wenye kuzalisha humo mali, balini kwamba walikuwa wakarimu na wenye muruwa, dunia ilikuwa ikiwa-fuata nao wanaitoa kwa ajili ya kesho, na kwao wao ndipo inaposadikikakauli ya msemaji: ‘Na wao hutoa mali mwanzo wa utajiri na wanatangulizasubira mwisho wa ufakiri. Mgeni afikapo mtaani humkirimu, hivyohutamjua ni yupi mkata kati yao na ni yupi tajiri.”’136

105

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

136 Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 15 Uk. 207.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 105

Page 115: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

SURAT KAHFIKauli ya Mwenyezi Mungu:

“Basi wakamkuta mja katika waja wetu, tuliyempa rehema kutokaKwetu, na tuliyemuelimisha elimu kutoka Kwetu.” (Surat Kahfi: 65).

Elimu ya siri ni sawa na mlango kwenye nyumba, na anayetaka kuingiandani ya nyumba ni wajibu juu yake kupita mlangoni, na Jumba la elimuna Jiji lake ni Mtukufu Nabii (s.a.w.w.), na lango la Jumba hili na la Jiji hilini Ali (a.s.) kama alivyosema Mtume (s.a.w.w.): “Mimi ni Jiji la elimu naAli ni lango lake.”137

SURAT TWAHAKauli ya Mwenyezi Mungu: “Twaha.” (Sura Twaha: 1).

Imam Ja’far as-Sadiq (a.s.) amesema: “Twaha ni kuapa kupitia utakaso waAhlul-Baiti na uongofu wao, kama alivyosema Mwenyezi Mungu: “Nakuwatakaseni kabisa.” (33:33)”138

SURAT HAJJKauli ya Mwenyezi Mungu:

“Anayedhani ya kwamba Mwenyezi Mungu hatamnusuru (Mtume)katika dunia na akhera, basi afunge kitanzi juu kisha ajinyonge, naaone je, hila yake yaweza kuyaondoa yale yaliyomghadhibisha?”(Sura Hajj: 15).

106

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

137 Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 15 Uk. 272.138 Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 16 Uk. 361.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 106

Page 116: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

Imepokewa kutoka kwa Anas bin Malik kwamba alisema: “Kuna myahudialikuja baada ya kufariki Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) na akain-gia msikitini na kusema: “Yuko wapi Wasii wa Muhammad?” hadhirinawakamwashiria kwa Abu Bakr, akasema: “Nakuuliza kuhusu mamboambayo hayajui ila Nabii au Wasii wa Nabii.” Abu Bakr akasema ulizautakalo.

Yahudi akasema: “Nieleze ni lipi asilolijua Mwenyezi Mungu, nalisilokuwa la Mwenyezi Mungu, na lisilokuwepo kwa Mwenyezi Mungu?”Abu Bakr akasema: “Akasema haya ni maneno ya wapagani.” Yeye nawaislamu waliyokuwepo hapo wakamjia juu. Ibnu Abbas akasema:“Hamjamtendea haki mtu huyu ikiwa mnalo jibu lake, na kama hamna lakumjibu basi nendeni kwa yule atakayemjibu, kwani hakika mimi nilim-sikia Mtume wa Mwenyezi Mungu akisema kumwambia Ali (a.s.): ‘EweMwenyezi Mungu upe nguvu moyo wake na uimarishe ulimi wake.’”Ndipo Abu Bakr na waliokuwa wamehudhuria hapo wakasimama nakumwendea Ali na wakamweleza hayo.

Ali akasema: “Ama asilolijua Mwenyezi Mungu ni ile kauli yenu enyiMayahudi ‘Hakika Uzayru ni mtoto wa Mwenyezi Mungu.’ MwenyeziMungu hajui kwamba ana mtoto. Ama lisilokuwa la Mwenyezi Mungu nikwamba Yeye hana mshirika. Na ama lisilokuwepo kwa Mwenyezi Munguni kwamba kwa Mwenyezi Mungu hakuna uonevu wala ajizi.” Yahudiakasema: “Nashahidilia kwamba hapana mungu ila Mwenyezi Mungu, nahakika wewe ni Wasii wa Mtume wa Mwenyezi Mungu.” Waislamu waka-furahi kwa hilo.139

SURAT AHZAB

Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Hakika si mengineyo Mwenyezi Munguanataka kuwaondolea uchafu, enyi watu wa nyumba ya Mtume, na

107

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

139 Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 17 Uk. 14.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 107

Page 117: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

kuwatakasa kabisa kabisa.” (Surat Ahzab: 33).

Siku moja Mtume alitoka akiwa amejifunika shuka lililodariziwa kwamanyoya meusi, kisha akaketi. Akaja Fatima akamwingiza katika shukahilo, kisha akaja Ali akamwingiza katika shuka hilo, kisha wakaja Hasanna Husain nao akawaingiza katika shuka hilo, kisha akasema:

“Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu,enyi watu wa nyumba ya Mtume. Watu wa kishamia ni Mtume waMwenyezi Mungu na binti yake na al-Murtadha (Ali), kisha ni watoto zakewawili pindi walipokusanyika.”140

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Hakika Mwenyezi Mungu na malaika wake wanamswalia Nabii.Enyi ambao mmeamini! Mswalieni na mumsalimu kwa salamu.”(Surat Ahzab: 56).

Ka’bi bin Ajrah, amesema: Ilipoteremka: “Enyi ambao mmeamini!Mswalieni na mumsalimu kwa salamu.” tulisimama na kumwambia: EweMtume wa Mwenyezi Mungu! Tumeshajua namna ya kukutolea salamu, niipi namna ya kukusalia? Mtume akasema: ‘’Semeni:

?????? ???? ??? ????? ???? ?? ????? ??? ????? ??? ??????? ???? ????????? ???? ???? ????.

“Ewe Mwenyezi Mungu! Mpe rehma na amani Muhammad na aaliMuhammad kama ulivyompa rehma na amani Ibrahim na aaliIbrahim. Hakika wewe ni Mhimidiwa Msifiwa.”141

108

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

140 Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 22 Uk. 171.141 Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 22 Uk. 225.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 108

Page 118: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

Na katika Hadithi Mtume alisema: “Hakuna dua yoyote ila kati yake naMwenyezi Mungu kuna kizuizi, mpaka pale atakapomsalia Muhammadi naAali Muhammad. Likitekelezwa hilo ndipo kizuizi huondoka na dua kupi-ta, na lisipotekelezwa hilo dua hurejea.”142

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Enyi mlioamini! Muogopeni Mwenyezi Mungu na semeni maneno yasawa.” (Surat Ahzab: 70).

Imeelezwa kwamba: “Hakika Yakub mtoto wa Is’haq aliyejulikana kwajina la Ibnu Sikit ambaye ni miongoni mwa ulamaa wakubwa wa lugha yaKiarabu, siku moja alikuwa ameketi na al-Mutawakil, ghafla akaja al-Muutazu na al-Muayad watoto wa al-Mutawakil, akasema al-Mutawakil:“Ni yupi umpendaye sana, ni wanangu wawili au Hasan na Husain?” IbnuSikit akasema: “Wallahi hakika Qanbar mtumishi wa Ali (a.s.) ni borakushinda wewe na kushinda watoto wako.” al-Mutawakil akasema:“Ng’oeni ulimi wake toka kinywani mwake.” Wakafanya hivyo na akawaamefariki usiku huohuo.143

SURAT ZUMARAKauli ya Mwenyezi Mungu:

“Mwenyezi Mungu amekupigieni mfano wa mtu mwenye washirikawanaogombana, na wa mtu mwingine aliyehusika na mtu mmoja, jewako sawa katika hali? Alhamdulillahi! Lakini wengine wao hawa-jui.” (Sura Zumar: 29).

109

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

142 Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 22 Uk. 230.143 Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 22 Uk. 248.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 109

Page 119: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

Hasan na Husain (a.s.) walikuwa wakicheza mikononi mwa Mtume(s.a.w.w.), naye akavutiwa nao. Jibril akamjia akiwa na chupa na karatasi,na ndani ya chupa mlikuwa na damu na ndani ya karatasi mkiwa na sumu.Akasema: “Ewe Muhammad je wawapenda hawa, basi tambua kuwammoja wao atauwawa kwa upanga na hii ndio damu yake, na mwingineatanyweshwa sumu na hii ndio sumu yake, ghafla akaondoa moyo wakekwa watoto na kuuelekeza moja kwa moja kwa Mwenyezi Mungu….”144

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Sema: Ewe Mola Mlezi! Muumba wa mbingu na ardhi, Mjuzi wayasiyoonekana na yanayoonekana, wewe utahukumu baina ya wajawako katika yale waliyokuwa wakikhitilafiana.” (Sura Zumar: 46).

Rabi’u alikuwa miongoni mwa wanahadithi, alikuwa hazungumzi ila lilelinalomhusu yeye, basi alipouawa Husain wakasema sasa atazungumza,ndipo akasoma: “Sema: Ewe Mola Mlezi! Muumba wa mbingu na ardhi,Mjuzi wa yasiyoonekana na yanayoonekana, wewe utahukumu baina yawaja wako katika yale waliyokuwa wakikhitilafiana.”

Na imepokewa kwamba alisema: “Ameuawa yule ambaye Mtume alikuwaakimkalisha mapajani mwake na akiweka ulimi wake ndani ya kinywachake.”145

110

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

144 Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 23 Uk. 104.145 Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 24 Uk. 120.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 110

Page 120: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

SURAT GHAFIR

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na akasema mtu muumini aliyekuwa mmoja wa watu wa Firaunanayeficha imani yake; je, mtamuuwa mtu kwa sababu tu anasemaMola wangu Mlezi ni Mwenyezi Mungu?” (Sura Ghafir: 28).

“Watatu hawajamkufuru Mwenyezi Mungu katu hata kidogo: EzekielMuumini toka aali Firaun, Habibu Najjari muumini toka aali Yasin, na Alibin Abu Talib naye ndiye mbora wao.”146

SURAT AS-SHURA

Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Sema: Kwa haya siwaombi malipo yoyotekwenu isipokuwa mapenzi kwa ndugu...” (Surat as-Shura: 23).

Imepokewa kwamba: Ilipoteremka palisemwa: Ewe Mtume wa MwenyeziMungu (s.a.w.w.) ni akina nani hawa ndugu ambao ni imewajibishwa juuyetu kuwapenda. Akasema: “Ali, Fatima na wanangu Hasan na Husain.”Na hilo linathibitishwa na ile riwaya iliyopokewa kutoka kwa Ali kwam-ba: “Nilimshitakia Mtume wa Mwenyezi Mungu kuhusu husuda za watudhidi yangu. Akasema: ‘Hivi huridhii kuwa wa kwanza kuingia Peponi.

111

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

146 Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 24 Uk. 176.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 111

Page 121: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

Mimi, Wewe, Hasan, Husein.”147

Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Ehe! atakayekufa na haliawapenda aali Muhammad basi amekufa na hali ni shahidi.

Ehe! atakayekufa na hali awapenda aali Muhammad basi amekufa na halini shahidi.

Ehe! atakayekufa na hali awapenda aali Muhammad basi amekufa na haliameghufuriwa.

Ehe! atakayekufa na hali awapenda aali Muhammad basi amekufa na haliametubia.

Ehe! atakayekufa na hali awapenda aali Muhammad basi amekufa na halini muumni aliyekamilika kiimani.

Ehe! atakayekufa na hali awapenda aali Muhammad basi amekufa na halimalaika ameshambashiria Pepo, kisha Munkar na Nakir.

Ehe! atakayekufa na hali awapenda aali Muhammad Mwenyezi Munguatawafanya malaika wa rehema wawe wenye kulizuru kaburi lake.

Ehe! atakayekufa na hali awapenda aali Muhammad atasindikizwa Peponikama biharusi asindikizwavyo kwenda nyumbani kwa mumewe. Ehe! atakayekufa na hali awapenda aali Muhammad Mwenyezi Munguatamfungulia milango miwili ya Pepo kaburini.

Ehe! atakayekufa na hali awapenda aali Muhammad Mwenyezi Munguatawafanya malaika wa rehema wawe wenye kulizuru kaburi lake.

112

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

147Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 25 Uk. 312.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 112

Page 122: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

Ehe! atakayekufa na hali awapenda aali Muhammad basi amefia ndani yaSunna.

Ehe! atakayekufa na hali awachukia aali Muhammad atakuja Siku yaKiyama na hali imeandikwa baina ya macho yake mawili: Amekata tamaana rehema za Mwenyezi Mungu.

Ehe! atakayekufa na hali awachukia aali Muhammad basi amekufa na halini kafiri.

Ehe! atakayekufa na hali awachukia aali Muhammad hatoipata harufu yaPepo.”148

SURAT AZ-ZUKHRUF

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na akalifanya neno hili liwe lenye kubaki katika kizazi chake iliwarejee.” (Sura az-Zukhruf: 28).

Baadhi wamesema kuhusu sababu ya kusema ‘Karamallahu Wajhahu’pindi atajwapo Ali bin Abu Talib (a.s.), ni kwamba imepatikana nukuukutoka kwa mama yake mzazi Fatima binti Asad bin Hashim kwamba kilaalipokuwa akitaka kulisujudia sanamu wakati akiwa na mimba yake, Alialikuwa akimzuia kufanya hivyo (akiwa angali tumboni).149

113

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

148 Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 25 Uk. 312.149 Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 25 Uk. 364.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 113

Page 123: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

SURAT AL-FAT’HU

Kauli ya Mwenyezi Mungu: “…Alama zao ni katika nyuso zao kwaathari ya kusujudu…..” (Sura al-Fat’hu: 29).

Imam Zaynul-Abidina ambaye ni Ali bin Husain bin Ali (a.s.) alikuwa aki-itwa: Mwenye sugu (sagamba). Na alikuwa na miti mia tano ya mizaituni,alikuwa akisali chini ya kila mti mmoja rakaa mbili kila siku. Mshairiakasema: “Nyumba za Ali, Husain, Ja’far, Hamza na Sajadi mwenyesugu”150

SURAT RAHMAN

Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Amezikutanisha bahari mbili. Baina yaokuna kizuizi haziingiliani.” (Sura Rahman: 19 - 20).

Imesemwa kwamba bahari mbili ni Ali na Fatima, na kizuizi ni Mtume(s.a.w.w.), na hutoka kwao hao wawili Hasan na Husein.151

SURAT MUJADILAH

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Enyi mlioamini! Mnaposema siri na Mtume, basi tangulizeni sadakakabla ya kumsemesha hayo ni bora kwenu na ni safi sana, na ikiwahamkupata basi Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe, Mwenyekurehemu.” (Sura Mujadilah: 12).

114

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

150Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 26 Uk. 58. Ubeti huu ni wa Da’bal al-Khaza’i(Mwenyezi Mungu amrehemu).151 Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 27 Uk. 296.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 114

Page 124: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

Imepokewa kutoka kwa Ali bin Abu Talib (a.s.) kwamba alisema: “Hakikakatika Kitabu cha Mwenyezi Mungu kuna Aya ambayo hakuna yeyotealiyeifanyia kazi kabla yangu, wala hakuna yeyote atakayeifanyia kazibaada yangu, nilikuwa nina dinari nikaichenji kwa dirhamu kumi, hivyoikawa kila nisemapo siri na Mtukufu Mtume natoa sadaka dirhamu moja.Yaani nilikuwa kila siku nasema siri na Mtume kwa dirhamu moja mpakasiku kumi, na nilikuwa namuuliza kuhusu sifa moja miongoni mwa sifanjema.”152

Ibnu Umar alisema: “Ali alikuwa na mambo matatu, kuwa nalo moja katiya hayo ni jambo nilipendalo mno kuliko kuwa na ngamia mwekundu:Kuozwa Fatima, kukabidhiwa bendera Siku ya Khaibar na Aya ya kuongeasiri na Mtume.”153

SURAT TAGHABUNKauli ya Mwenyezi Mungu:

“Bila shaka mali zenu na watoto wenu ni mtihani, na kwa MwenyeziMungu kuna malipo makubwa.” (Sura Taghabun: 15).

Katika kitabu Mishkatul-Maswabihi imeandikwa kwamba: “Mtume waMwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alikuwa akitoa hotuba na ghafla wakajaHasan na Husein wakiwa wamevaa kanzu mbili nyekundu na hali waki-dondoka na kuamka, akateremka toka mimbarini akawafuata nakuwachukua na kuwaweka mbele yake, kisha akasema: ‘Mwenyezi Munguamesema kweli. Bila shaka mali zenu na watoto wenu ni mtihani,nilipowaona hawa wawili wakitembea huku wakidondoka sikuweza kuvu-milia mpaka nimekatisha mazungumzo yangu na kuwanyanyua.’ Kishaakaendelea na hotuba yake….”154

115

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

152 Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 28 Uk. 405.153 Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 28 Uk. 40.154 Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 28 Uk. 18.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 115

Page 125: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

SURAT TAHRIM

Kauli ya Mwenyezi Mungu: “…..Basi Mwenyezi Mungu ni mlinzi wake,na Jibril na waumini wema na Malaika….” (Sura Tahrim: 4).

Imepokewa kutoka kwa Mujahid kwamba amesema: Waumini wema niAli bin Abu Talib.

Fakiri155 anasema: Hiyo inaungwa mkono na kauli ya Mtume (s.a.w.w.):“Ewe Ali! Wewe kwangu mimi una nafasi ya Harun kwa Musa.” Hivyoikiwa Ali ni sawa na Harun basi yeye ndio mwema mfano wake.156

SURAT NUH

Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Ili mtembee humo katika njia zilizopana.” (Sura Nuh: 20).

Amirul-Muuminina Ali (a.s.) alikuwa akisema: “Niulizeni kuhusu njia zambinguni kwani hakika mimi nazijua zaidi kushinda njia za ardhini.”157

SURAT AL-INSAN

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na huwalisha chakula masikini na yatima na mfungwa hali ya kuwawanakipenda. Tunakulisheni kwa ajili ya radhi za Mwenyezi Mungutu, hatutaki kwenu malipo wala shukurani.” (Surat al-Insan: 8 - 9).

116

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

155 Mwandishi wa tafsiri hii Tafsiru Ruhul-Bayan156 Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 28 Uk. 53.157Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 29 Uk. 180.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 116

Page 126: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

Kutoka kwa Ibnu Abbas amesema: Hasan na Husein walipatwa na marad-hi, babu yao Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alikwenda kuwaonaakiwa pamoja na baadhi ya watu. Wakamwambia Ali: “Ni vizuri lau uki-weka nadhiri kwa ajili ya wanao.”

Ali, Fatima na mtumishi wao Fidha wakaweka nadhiri kwamba ikiwa wat-apona watafunga siku tatu kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, kutafuta radhizake na kumshukuru.

Wakapona, na wao wakafunga na hali hawana chochote cha kufuturu. Aliakaenda kwa Simon Myahudi wa Khaibari, akakopa toka kwake pishi tatuza ngano. Fatima akachukua pishi moja akatwanga na kuoka mikatemitano kulingana na idadi yao. Chakula kikawekwa mbele yao wakati wakufuturu ili wafuturu, mara masikini akafika mlangoni kwao akasema:“Assalam Alaykum enyi watu wa nyumba ya Muhammad, mimi ni mask-ini miongoni mwa maskini wa kiislamu, nipeni chakula Mwenyezi Munguatakupeni chakula cha Peponi.” Wakampa chakula na wakashinda mchanakutwa na usiku kucha bila kuonja chochote ila maji.

Asubuhi wakaamka wakiwa wamefunga, waliposhinda mchana kutwa nakukiweka chakula mbele yao ili waftari, mara akafika mlangoni kwao yati-ma, akasema: “Assalam Alaykum enyi watu wa nyumba ya Muhammad,yatima toka katika watoto wa muhajirana, baba yangu amekufa kishahidiSiku ya Aqabah, nipeni chakula Mwenyezi Mungu atakupeni chakula chaPeponi.” Wakampa chakula.

Asubuhi wakaamka wakiwa wamefunga, waliposhinda mchana kutwa nakukiweka chakula mbele yao ili waftari, mara mfungwa wa kivita akafikamlangoni kwao, akasema: “Assalam Alaykum enyi watu wa nyumba yaunabii, mimi ni mfungwa miongoni mwa wafungwa, nipeni chakulaMwenyezi Mungu atakupeni chakula cha Peponi.” Wakampa chakula.

117

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 117

Page 127: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

Ilipofika siku ya nne wakiwa tayari wameshatimiza nadhiri yao Alialimshika Hasan mkono wa kulia na Husein mkono wa kushoto na kwen-da nao kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) na hali wao wawiliwakitetemeka kama vifaranga kutokana na ukali wa njaa. Mtume waMwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alipowatizama alisema: “Hali niionayo yani-umiza mno.” Akasimama na kwenda nao, wakamkuta Fatima akiwamihrabuni kwake na hali tumbo lake limeshikana na mgongo wake namacho yake yamebadilika, hilo likamuumiza sana. Ndipo Jibril (a.s.)akateremka na kusema:

“Ewe Muhammad pokea, Mwenyezi Mungu anakupa pongezi kwa kitendocha watu wa nyumba yako.” Na akamsomea Sura hii.158

Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Humo wataegemea viti vya enzi, humohawataona jua wala baridi.” (Sura Insan: 13).

Ibnu Abbas amesema: “Pindi watu wa Peponi watakapokuwa peponighafla wataona mwanga kama mwanga wa jua na Pepo imeangazwa kwamwanga huo. Watasema: Ewe Ridhwan! Mola wetu Mtukufu amesema:“Hawataona jua wala baridi.” hii ni nuru ya nini? Ridhwan atawaambia:“Hili si Jua wala si Mwezi, lakini huyu ni Fatima na Ali wamecheka, nakutokana na nuru ya kicheko chao Pepo imeangaziwa.”159

SURAT SHAMSI

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

118

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

158 Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 29 Uk. 268.159 Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 29 Uk. 270.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 118

Page 128: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

“Hapo Mtume wa Mwenyezi Mungu akawaambia: Ni ngamia waMwenyezi Mungu na kinywaji chake. Lakini walimkadhibisha nawakamchinja. Kwa hiyo Mola wao Mlezi aliwaangamiza kwa sababuya dhambi zao, na akifanya sawa.” (Sura Shamsi: 13 - 14).

Katika Hadithi ni kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.)alimwambia Ali: “Ewe Ali hivi wajua ni nani muovu kuliko wote waliotan-gulia?” Akasema: “Mwenyezi Mungu na Mtume wake ndiye ajuaye.”Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akasema: “Ni yule aliyemchinjangamia.” Kisha akasema: “Hivi wajua ni nani muovu kuliko wotewatakaokuja?” Akasema: “Mwenyezi Mungu na Mtume wake ndiyeajuaye.” Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akasema: “Ni yuleatakayekuuwa wewe.”160

AHLUL-BAIT (A.S.) NDANI YA TAFSIRI YAALUSIY, INAYOITWA RUHUL-MA’ANIY

FITTAFSIRIL-QUR’AN AL-‘ADHIM WASAB’UL-MATHANIY.

SURAT AL-BAQARAH

Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Na katika watu yuko auzaye nafsi yakekwa kutaka radhi ya Mwenyezi Mungu, na Mwenyezi Mungu niMpole kwa waja.” (Surat Al-Baqarah: 207).

Imamia na baadhi ya maulama wetu wamesema kwamba: Iliteremka kwaajili ya Ali (a.s.) pindi Mtume alipomwachia jukumu la kulala juu ya kitan-da chake huko Makka pale alipoondoka kwenda Pangoni.161

119

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

160 Imeshatangulia riwaya kama hii katika Sura Aaraf Aya ya 77.161 Tafsiru Ruhul-Bayan Juz. 2 Uk. 83.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 119

Page 129: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Wale watoao mali zao usiku na mchana kwa siri na dhahiri, wanaujira wao kwa Mola wao Mlezi; wala haitakuwa hofu juu yao walawao hawatahuzunika.” (Surat Al-Baqarah: 274).

Kutoka kwa Ibnu Abbas amesema: “Aya hii iliteremka kwa ajili ya Ali(a.s.) alikuwa na dirhamu nne, akatoa sadaka dirhamu moja usiku nanyingine mchana, nyingine siri na nyingine dhahiri.”162

SURAT AALI IMRAN

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Hakika Mwenyezi Mungu alimchagua Adam na Nuh na kizazi chaIbrahim na kizazi cha Imran juu ya walimwengu wote.” (Surat AaliImran: 33).

Imepokewa kutoka kwa Ahlul-Baiti (a.s.) kwamba wao husoma: “Na AaliMuhammad juu ya walimwengu wote.”163

120

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

162 Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 3 Uk. 41.163 Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 3 Uk. 116.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 120

Page 130: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

Kauli ya Mwenyezi Mungu: “…Kila mara Zakariya alipoingia Mihrabhukuta vyakula. Akasema: Ewe Maryam unatoa wapi hivi. Akasema:Vinatoka kwa Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu hum-ruzuku amtakaye bila hesabu.” (Surat Aali Imran: 37).

Abu Ya’la ameandika kutoka kwa Jabir bin Abdullah amesema kwambahakika Mtume (s.a.w.w.) alikaa siku kadhaa bila kula chakula mpaka halihiyo ikawa nzito juu yake. Akaenda kwenye nyumba za wakeze lakinihakukuta chochote kwao ndipo akaenda kwa Fatima na kumwambia: “Ewemwanangu mpendwa! Je una chochote ninachoweza kula kwani hakikamimi ni mwenye njaa?” Akamjibu: “Wallahi sina.”

Mtume alipotoka, jirani wa Fatima alimletea Fatima vipande viwili vyamkate na finyango ya nyama. Fatima akapokea na kuweka ndani ya bakulilake, akasema: “Wallahi katika hiki nitampa kipaumbele Mtume waMwenyezi Mungu (s.a.w.w.) kabla ya nafsi yangu na kabla ya yule aliyopokwangu.” Japokuwa wote walikuwa wanahitajia chakula lakini Fatimaalimtuma Hasna au Husein aende kumwita Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w.) naye alikuja. Fatima akamwambia: “Kwa haki yako na ya mamayangu, Mwenyezi Mungu ameleta kitu nami nimekihifadhi kwa ajiliyako.”

Akamwambia: “Kilete ewe binti yangu mpendwa.” Nikamletea bakuli nanilipolifunua ghafla nikakuta limejaa mikate na nyama, nilipolitazamanikapatwa na mshangao na nikatambua kuwa ni baraka toka kwaMwenyezi Mungu. Nikamhimidi Mwenyezi Mungu na nikamkabidhichakula hicho Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.). Alipokionaalimhimidi Mwenyezi Mungu na akasema: Umetoa wapi hivi ewe bintiyangu mpendwa? Akajibu: “Ni kutoka kwa Mwenyezi Mungu ewe babayangu mpendwa. Hakika Mwenyezi Mungu humpa riziki amtakaye bilahesabu. “

121

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 121

Page 131: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

Mtume akamhimidi Mwenyezi Mungu na kusema: “Kila sifa njema ni yaMwenyezi Mungu Ambaye amekufanya ewe binti yangu mpendwa kifaniwa seyida wa wana wa Israel (Mariam). Kwani hakika yeye alikuwaaruzukiwapo chochote na Mwenyezi Mungu kisha akiulizwa kakipatawapi husema: Hakika Mwenyezi Mungu humpa riziki amtakaye bilahesabu.”

Kisha akawakusanya Ali, Hasan na Husein na Ahlul-Baiti wake wotewakala mpaka wakatosheka na chakula kikabaki kama kilivyokuwa,Fatima akawagawia jirani zake.164

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na Malaika waliposema: Ewe Maryam! Hakika Mwenyezi Munguamekuteua na akakutakasa na akakuteua juu ya wanawake waulimwenguni.” (Surat Aali Imran: 42).

Ibnu Asakir ameandika kupitia moja ya njia zake kutoka kwa Ibnu Abbaskwamba alisema: “Wanawake bora wa peponi ni Maryam binti Imran,Fatima, Khadija na Asia mke wa Firaun.”

Ibnu Jarir ameandika kutoka kwa Fatima (a.s.) kwamba alisema: Mtumewa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Wewe ni Seyida wa wanawakewa peponi ila Bikira Maryam.” Makusudio ni kwamba Mariam ni mborakwa wanawake wa zama zake, na hiyo haipelekei yeye kuwa mbora kulikoFatima (a.s.). Hilo linaungwa mkono na ile riwaya aliyoiandika IbnuAsakir kwa njia ya Muqatil kutoka kwa Dhahak kutoka kwa Ibnu Abbas

122

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

164 Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 3 Uk. 124

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 122

Page 132: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

(a.s.) kutoka kwa Mtume (s.a.w.w.) kwamba alisema: “Wanawake wane niwabora kushinda wanawake wa zama zao: Mariam binti Imran, Asia bintiMuzahim, Khadija binti Khuwaylid na Fatima binti Muhammad, na mborawao kiulimwengu ni Fatima.”

Na ile aliyoipokea al-Harthi bin Usama katika Musnad yake kwa sanadisahihi ijapokuwa ni Hadithi ya Mursal: “Mariam ni mbora kwa wanawakewa zama zake.”

Na hii ndio rai ya Abu Ja’far (Imam al-Baqir) na ndio rai mashuhuri kuto-ka kwa Ahlul-Bait (a.s.). Rai ambayo naipa kipaumbele mimi ni kwambaFatima ni bora kushinda wanawake wote waliotangulia na watakaokuja,kwani yeye ni sehemu ya nyama ya Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w.), pili ni kutokana na wasifu mwingine ambao hauchafuliwi naHadithi hizo zilizotangulia hata tuseme kwamba mwingine asiyekuwayeye ni bora kumshinda……

Na kuanzia hapa ndipo unapojulikana ubora wake juu ya Aisha. Amawengi wanaokhalifu rai hiyo, hoja yao ni kauli ya Mtume (s.a.w.w.):“Chukueni theluthi ya dini yenu toka kwa Hamayrau (Aisha).” Na kauliyake (s.a.w.w.): “Ubora wa Aisha juu ya wanawake wengine ni sawa naubora wa mkate juu ya chakula.”

Lakini wewe wajua kilichopo katika dalili hizi na ni kwamba hazieleziubora wowote wa Aisha juu ya Fatima.

Kwanza: Cha maana sana kilichomo katika Hadithi hii iwapo tukisemaimethibiti ni kwamba yathibitisha kuwa yeye (Aisha) ni msomi hivyo the-luthi ya dini inachukuliwa toka kwake, na hii haikanushi uwepo wa elimumfano wa hiyo kwa kipande cha nyama ya Mtume (s.a.w.w.) (Fatima). Nakutokana na kujua kwake (s.a.w.w.) kwamba Fatima hatobaki muda mrefuambao watu wataweza kuchukua elimu toka kwake huenda ndio maanahakusema, na laiti angejua (anao muda wa kutosha) angesema: “Chukuenidini yenu yote kutoka kwa Zahra.”

123

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 123

Page 133: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

Na kutokutamka kauli hii kumhusu mtu ambaye akili na nukuu vyotevimethibitisha elimu yake haimaanishi kwamba yupo aliye bora zaidi yake,la sivyo Aisha angekuwa bora hata kushinda baba yake (Abu Bakr) kwanihakijapokewa chochote kutoka kwake kinachohusu dini ila kitu kichache.Zaidi ya hapo ni kwamba ile kauli ya Mtume (s.a.w.w.): “Hakika mimi nimwenye kuwaachia vizito viwili kati yenu: Kitabu cha Mwenyezi Munguna kizazi changu, havitoachana mpaka vinikute kwenye hodhi,” inachukuanafasi ya ile riwaya ya ubora wa Aisha ambayo kama ilivyo wazi ninyongeza (riwaya ya uwongo), kwani itawezekanaje iwe hivyo na haliFatima ndiye Seyida wa kizazi cha Mtume.

Pili: Kwa sababu Hadithi ya pili inapingana na zile zinazoonyesha kwam-ba wengine wasiyokuwa yeye (Aisha) ni bora kushinda yeye (Aisha). IbnuJarir ameandika kutoka kwa Ammar bin Sa’d kwamba alisema: “Mtumewa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Khadija amefanywa borakushinda wanawake wa umma wangu kama Mariam alivyofanywa borakushinda wanawake wa ulimwenguni.” Bali Hadithi hii ni dhahiri katikaubora, na inawasifu kamili kwa yule mwenye kutizama kwa akili yake naakajiepusha na ububusa na ulazimishaji.

Ama kauli ya mwenye kusema kwamba hakika mabinti wengine wa Nabiini bora kushinda Aisha, sioni kama ina tatizo. Na kwangu mimi mjadala wani nani aliye mbora kushinda wanawake wote wa ulimwenguni ni kati yaMariam na Fatima tu. Na kutokana na wasifu uliotangulia tayari umesha-jua rai yangu ninayoegemea. Imam as-Sabki aliulizwa kuhusu suala hiliakasema: “Tunalolichagua na kulifuata ni kwamba Fatima bintiMuhammadi ndiye bora kisha mama yake…”165

124

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

165 Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 3 Uk. 137 na Uk. 138.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 124

Page 134: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na watakaokuhoji baada kukufikia elimu hii, waambie: Njoonituwaite watoto wetu na watoto wenu, na wanawake zetu na wanawakewenu, na nafsi zetu na nafsi zenu, kisha tuombe kwa unyenyekevututake laana ya Mwenyezi Mungu iwashukie waongo.” (Surat AaliImran: 61).

Kutoka kwa Ibnu Abbas amesema: “Ujumbe wa Wakristo wa Najranulikuja kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu, nao walikuwa ni watu kumi nawane wakiongozwa na Sayid ambaye alikuwa ndio mkubwa wao, kishaAqib aliyekuwa akimfuatia kwa ukubwa na ndiye aliyekuwa mwenyeuamuzi wa mwisho kwao, Mtume wa Mwenyezi Mungu akawaambia:“Silimuni.” Wakasema tumeshasilimu. Mtume akawaambia: “Bado ham-jasilimu.” Wakasema tumeshasilimu kabla ya kufika kwako. Mtumeakawaambia: “Mnasema uongo, kuna mambo matatu yanawazuia kusil-imu: Kuabudu kwenu msalaba, kula kwenu nguruwe, na kudai kwenukuwa Mwenyezi Mungu ana mtoto.” Mwenyezi Mungu akateremsha:

“ “Hakika mfano wa Isa mbele ya Mwenyezi Mungu ni kama mfanowa Adam, alimuumba kutokana na udongo, kisha akamwambia kuwa,basi akawa. Ndiyo haki itokayo kwa Mola wako Mlezi, basi usiwemiongoni mwa wenye kutia shaka. (Surat Aali Imran: 59 - 60).

125

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 125

Page 135: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

Alipowasomea Aya hiyo wakasema hatujui uyasemayo, ndipo ikateremka:

“Na watakaokuhoji baada kukufikia elimu hii, waambie: Njoonituwaite watoto wetu na watoto wenu, na wanawake zetu na wanawakewenu, na nafsi zetu na nafsi zenu, kisha tuombe kwa unyenyekevututake laana ya Mwenyezi Mungu iwashukie waongo.” (Surat AaliImran: 61).

Mtume wa Mwenyezi Mungu akawaambia: “Hakika Mwenyezi Munguameniamuru ikiwa hamtakubali hili nifanye maapizano nanyi.”

Wakasema: “Ewe Abul-Qasim! mpaka turejee na tutafakari jambo hilikisha tutakuja.” Walipoachana na wakasadikishana wao kwa wao, Sayidalimwambia Aqib: “Wallahi mmeshajua kwamba hakika mtu huyu ni Nabiina Mtume, na lau mkifanya naye maapizano basi atawateketeza, wallahikatu hakuna watu walioombeana laana na Mtume kisha mkubwa waoakaendelea kuishi au mdogo wao kuzaliwa. Kama hamtomfuata namkikataa basi nyinyi endeleeni kubakia katika dini yenu, na nendeni mka-muage mtu huyu na mrejee nchini kwenu.

Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alikuwa ametoka akiwa pamoja naAli, Hasan, Husein na Fatima, akawaambia:

“Mimi nitakapokuwa naomba nyinyi muwe mnaitikia.” Ndipo wakakataakufanya naye maapizano na wakafanya suluhu kwa sharti la kutoa kodi.166

126

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

166 Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 3 Uk. 166 na Uk. 167.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 126

Page 136: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

Jabir amesema: Mtume alisema: “Naapa kwa Yule Ambaye aliyenitumakwa haki! Lau wangefanya maapizano bonde lao lingeteketea kwamoto.”167

Na imepokewa kwamba Askofu wa Najran alipomuona Mtume waMwenyezi Mungu akija akiwa na Ali, Fatima, Hasan na Husein alisema:“Enyi wakristo! Mimi naziona nyuso hizi kama zitamuomba MwenyeziMungu auondoe mlima kutoka mahala pake, atauondoa, msiapizane nayemtaangamia.”168

Na katika kadhia hii kuna dalili ya wazi juu ya unabii wake (s.a.w.w.), lasivyo wasingekataa kufanya naye maapizano, na kuna dalili juu ya uborawa mawalii wa Mwenyezi Mungu na Aali wa Mtume wa MwenyeziMungu, jambo ambalo hana shaka nalo yeyote aliye muumini.169

Muslim, Tirmidhi na weningineo wameandika kutoka kwa Sa’d binWaqqas kwamba alisema: Ilipoteremka Aya hii: “Na watakaokuhojibaada kukufikia elimu hii, waambie: Njooni tuwaite watoto wetu nawatoto wenu, na wanawake zetu na wanawake wenu, na nafsi zetu nanafsi zenu, kisha tuombe kwa unyenyekevu tutake laana ya MwenyeziMungu iwashukie waongo.” (Surat Aali Imran: 61), Mtume waMwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alimwita Ali, Fatima, Hasan na Husain,akasema: “Ewe Mwenyezi Mungu! Hawa ndio watu wa nyumbayangu.”170 Ibnu Abi ‘Allani ambaye ni Muutazila ametoa dalili kupitiakisa hiki kwamba Hasan na Husain (a.s.) walikuwa Mukalafu katika halihiyo, kwa sababu hairuhusiwi maapizano ila kwa waliobalehe.

Kupatikana hali hiyo hakutegemei balehe, kwani ukamilifu unawezakupatikana kabla yake, bali huenda ukashinda hata ule wa wale waliobale-

127

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

167 Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 3 Uk. 166 na Uk. 167.168 Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 3 Uk. 166 na Uk. 167.169 Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 3 Uk. 166 na Uk. 167.170 Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 3 Uk. 168.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 127

Page 137: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

he, hivyo hakuna kizuizi kinachozuia Hasan na Husain kutokuwa balehekipindi hicho, isipokuwa tu iwapo ni katika miaka ambayo haiwezekanikwa wao kuwa tayari ni wakamilifu wa akili. Zaidi ya hapo ni kwambainaewezekana Mwenyezi Mungu akavunja ada kwa hao mabwana hivyoakawapa lile ambalo hakuna mwingine yeyote atakayeshirikiana nao(yaani akawapa akili za utu uzima wangali watoto wadogo – kamailivyokuwa kwa Nabii Isa alivyoongea akiwa kwenye kitenga cha utotoni),hivyo lau ikisihi kwamba ukamilifu wa akili huwa hauwi katika miakahiyo, basi inajuzu kuwepo ukamilifu huo kwao kwa ajili ya kuwatofautishawao na watu wengine, na kwa ajili ya kuwa dalili juu ya nafasi yao kwaMwenyezi Mungu na umakhususi wao kwake, nao ni kaumu ambayo sifazilizo makhususi kwao hazihesabiki.171

Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Na shikamaneni na kamba ya MwenyeziMungu nyote wala msifarakane..” (Surat Aali Imran: 103).

Ahmad ameandika kutoka kwa Zayd bin Thabit kwamba alisema: “Mtumewa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Hakika mimi ni mwenye kuachakati yenu mirathi mbili: Kitabu cha Mwenyezi Mungu kamba iliyonyookabaina ya mbingu na ardhi, na kizazi changu watu wa nyumba yangu, nahakika hivyo viwili havitaachana mpaka vinikute kwenye hodhi.”172

SURAT NISAIKauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na wenye kumtii Mwenyezi Mungu na Mtume, basi hao watakuwapamoja na wale aliowaneemesha Mwenyezi Mungu, miongoni mwaManabii, na Masidiki, na Mashahidi na Watu wema, na hao ndiomarafiki wema.” (Sura Nisai: 69).

128

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

171 Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 3 Uk. 168.172Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 4 Uk. 17.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 128

Page 138: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

Amesema: “Pili: Nafasi ya Masidiki nao ni wale ambao wanaowafuataManabii (a.s.) katika maarifa, na mfano wao ni sawa na yule anayetazamakwa mbali kitu kilivyo, na hiyo ndiyo aliyomaanisha Ali (a.s.) palealipoambiwa: “Je umemuona Mwenyezi Mungu?” Akajibu: “Siwezikumwabudu Mola Mlezi nisiyemuona, macho hayamuoni kwa uono wamacho lakini nyoyo zinamuona kwa imani ya kweli.”173

SURAT MAIDA

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Leo nimekukamilishieni dini yenu na kukutimizieni neema yangu nanimekupendeleeni Uislamu uwe dini yenu..” (Sura Maida: 3).

Imethibiti kwetu kwamba alisema huko174 kuhusu haki ya Ali (a.s.): “Yuleambaye mimi nina mamlaka juu yake basi Ali ana mamlaka juu yake.” Naakaongeza zaidi ya hapo kama ilivyo katika baadhi ya riwaya.175

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Hakika walii wenu hasa ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake nawale walioamini ambao husimamisha Swala na hutoa Zaka wakiwawamerukui.” (Sura Maida: 55).

129

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

173 Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 5 Uk. 68.174 Yaani katika bonde la Ghadir Khum.175 Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 6 Uk. 55.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 129

Page 139: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

Wanahadithi wengi wamesema kwamba yenyewe iliteremka kwa ajili yaAli. al-Hakim, Ibnu Mardawayhi na wengineo wameandika kutoka kwaIbnu Abbas kwa sanad yenye kuungana kwamba alisema: Abdullah binSalam na kundi lake waliokuwa wamemwamini Mtume (s.a.w.w.) waliku-ja kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.), wakasema: ‘Ewe Mtumewa Mwenyezi Mungu! Hakika nyumba zetu ziko mbali na hatupati wakuketi nasi wala kuzungumza nasi kinyume na kikao hiki, na hakika jamaazetu walipoona tumemsadiki Mwenyezi Mungu na Mtume wake wame-tutenga na wameapa ndani ya nafsi zao kwamba hawataketi nasi,hawatatuozesha na wala hawatasema nasi, na jambo hilo limekuwa zito juuyetu.’ Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akawaambia: “Hakika Waliiwenu hasa ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake.”

Kisha (s.a.w.w.) akatoka na kuelekea msikitini na akawakuta watu wakiwawamesimama na wengine wakiwa katika rukuu, ndipo akamuona muom-baji, Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akamuuliza: ‘Kuna yeyotealiyekupa kitu?’ Akajibu ndio, amenipa pete ya fedha. Akamuuliza:‘Nani?’ Akajibu: Yule aliyesimama. Na akaashiria kwa Ali (a.s.). Mtumeakamuuliza: ‘Alikupa akiwa katika hali gani?’ Akajibu: Akiwa katikarukuu. Ndipo Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akatoa takbira kishaakasoma Aya hii.

Has?n akasimama na kusoma shairi:

“Abul Hasan nafsi yangu ni fidia kwako, roho yangu na kila kizito na chepesi chenye kuelekea katika uon-gofu. Hivi kweli sifa zako njema zitakwenda bure bila faida, hapana; sifa njema zitokazo kwa Mungu hazipotei bure. Kwani wewe ndiye uliyetoa sadaka ulipokuwa katika rukuu, nafsi yangu ni fidia kwako ewe mwenye rukuu bora kushinda zote. Ndipo Mwenyezi Mungu akateremsha kwako uwalii bora,na akauthibitisha ndani ya Kitabu cha sheria.”176

130

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 130

Page 140: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

SURAT AARAF

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na wakamuua yule ngamia na wakaasi amri ya Mola wao Mlezi nawakasema: Ewe Saleh! Tuletee unayotuahidi ikiwa wewe ni miongonimwa Mitume.” (Sura Aaraf: 77).

Imekuja katika Hadithi kwamba muovu kuliko wote waliotangulia ni yulealiyemchinja ngamia. Na muovu kuliko wote watakaokuja ni yule aliye-muua Ali (a.s.). Hilo ndilo Mtume alilomweleza Ali (a.s.). na kwa raiyangu mimi ni kwamba muovu kushinda wote watakaokuja ni muovu zaidikushinda yule muovu mwenye kuwashinda wote waliotangulia. Na tofautikati yao ni kama tofauti kati ya Ali na ngamia.

Habari zimegusia bali zimetamka kwamba muuwaji wa Amiril-Muumininaalikuwa amehalalisha mauwaji hayo, bali alikuwa akiamini kuwa kufanyahivyo ni thawabu kwake, na masahiba zake wamemsifu kwa tukio hilo,ndipo Amran bin Hatwan (Ghadhabu za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake),akatoa shairi:

“Pigo bora lilioje! Kutoka kwa mcha mungu, hakukusudia kwaloila kupata ridhaa kutoka kwa Mkuu wa Arshi (Mwenyezi Mungu).Hakika mimi namtaja leo na ninamzingatia kwamba ni kiumbechenye fungu kamili mbele ya Mwenyezi Mungu.”

Na Mwenyezi Mungu ana neema kwa yule aliyemjibu: “Pigo ovu lilioje! Kutoka kwa muovu aliyejirithisha Moto, atakutana na Rahman akiwa Amemghadhibikia.

131

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 131

Page 141: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

Kana kwamba kwa pigo lake hajapata kitu ila kuingia motoni kesho Siku ya mkusanyiko. Hakika mimi namtaja leo na ninamlaani, na pia namlaani Imran bin Hatwan.

Na kudai kwamba kitendo chake hicho ni shubha itakayomwokoa, ni kauli ambayo bila shaka ni sehemu ya kuweweseka. Kwani lau ikiwa mfano wa kitendo hicho ni chenye kumwokoa na adhabu ya dhambi hii, basi mtu afanye atakavyo! Umetakasika Mwenyezi Mungu na uzushi huu mkubwa.177

SURAT AL-AN’FAL

Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Na walipokupangia njama wale walioku-furu ili wakufunge au wakuue au wakutoe…” (Surat al-An’fal: 30).

Jibril (a.s.) alimjia Mtume wa Mwenyezi Mungu na kumwambia: “Usikuhuu usilale kitandani kwako ambapo huwa unalala.” Ulipowadia usikuwalijikusanya mlangoni kwake wakimvizia ni muda upi atalala iliwamvamie. Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alipoona nafasi yaoalimwambia Ali (a.s.): “Lala kitandani kwangu na jifunike shuka hili lakijani la kihadhramiy, hakika hakitakupata chochote chenye kukuudhi tokakwao.” Na ilikuwa ni kawaida ya Mtume wa Mwenyezi Mungu kujifunikashuka hiyo alalapo. Ali (a.s.) akasoma shairi kuashiria neema aliy-oneemeshwa na Mwenyezi Mungu, akasema:

Nimemkinga kupitia nafsi yangu yule mbora kushinda wotewaliowahi kukanyaga changarawe, na kuliko wote waliowahikutufu Nyumba ya kale na kugusa Jiwe. Mtume wa Mwenyezi Mungu amekhofia wasimfanyie hila, ndipoMungu Mwenye uwezo amemwokoa dhidi ya hila.

132

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

176 Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 6 Uk. 149.177 Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 8 Uk. 147.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 132

Page 142: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

Mtume wa Mwenyezi Mungu amelala kwa amani huko pangoni,akiwa chini ya ulinzi wa Mungu na sitara Yake.

Nimelala nikiwafuatilia wao na yale wanayonituhumu, na halinimeituliza nafsi yangu katika kuuawa na kufungwa.”178

SURAT TAWBA

Kauli ya Mwenyezi Mungu: “(Tangazo la) Kujitoa Mwenyezi Mungu naMtume wake kwa wale mlioahidiana nao miongoni mwa mushrikina.”(Sura Tawba: 1).

Alusiy amesema: “Riwaya zimetofautiana kuhusu je Abu Bakr alikuwakaamrishwa kuisoma au la? Nyingi zinaona alikuwa ameamriwa kuisoma,na kwamba Ali alipomfuata na kuichukua toka kwake aliamriwa kuisoma.Na imekuja katika riwaya kutoka kwa Ibnu Habban na Ibnu Mardawayhikutoka kwa Abu Said al-Khudri kwamba Abu Bakr aliponyang’anywa surahiyo alikuja kwa Mtume na hali akiwa ameingiwa na khofu kwamba huen-da kuna kitu kimeteremka kuhusu yeye. Alipofika kwa Mtume alisema:“Nina nini ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu?” Mtume akasema: “Ni kheritupu, wewe ni ndugu yangu na swahiba wangu pangoni, na wewe utakuwapamoja nami katika hodhi, isipokuwa ni kwamba hafikishi kwa niabayangu asiyekuwa mimi au mtu atokanaye na mimi.”179

Imekuja katika riwaya ya Ahmad na Tirmidhi, ambayo yeye Tirmidhi, AbuShaikh na wengineo wameizingatia kuwa ni Hasana, kwamba Anas ame-sema: “Mtume (s.a.w.w.) alimtuma Abu Bakr na Sura Baraa, kishaakamwita na kumwambia: “Haipasi yeyote kuifikisha hii ila mtu katikawatu wa nyumba yangu.” Ndipo akamwita Ali na kumkabidhi.180

133

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

178 Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 9 Uk. 176.179 Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 10 Uk. 40.180 Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 10 Uk. 40.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 133

Page 143: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Je, mnafanya kuwanywesha mahujaji na kuamirisha msikiti mtuku-fu ni sawa na yule aliyemwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwishona akapigana jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu? Hawawi sawambele ya Mwenyezi Mungu, na Mwenyezi Mungu hawaongozi watumadhalimu.” (Sura Tawba: 19).

Imepokewa kwa njia mbalimbali kwamba Aya hii iliteremka kwa ajili yaAli na Abbas, hiyo ni pale Amirul-Muuminina alimwambia Abbas: “EweAmi yangu, ungehamia Madina.” Akamjibu: “Hivi mimi siko katika kazibora kushinda kuhama, hivi mimi si ninatoa huduma ya maji kwa mahuja-ji na ninalinda Nyumba.”181

Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Bila shaka Mwenyezi Mungu amekusaidi-eni katika mapigano mengi na Siku ya Hunayni.” (Sura Tawba: 25).

Imepokewa kwamba al-Mutawakkil aliugua sana akaweka nadhiri iwapoMwenyezi Mungu atamponyesha basi atatoa sadaka mali nyingi.Alipopona aliwauliza ulamaa kipimo cha wingi, ndipo kauli zao zikatofau-tiana, wakamshauri amuulize Abu Hasan Ali bin Muhammad bin Ali binMusa al-Kadhim (a.s.), na alikuwa amemuweka kuzuizini huko nyumbani

134

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

181 Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 10 Uk. 60.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 134

Page 144: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

kwake, ndipo akaamuru aandikiwe barua. Akamrudishia jibu kwamba atoesadaka dirhamu themanini. Walipomuuliza sababu alisoma Aya hii nakusema: Tumehesabu maeneo hayo yakafikia themanini.182

SURAT HUD

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Basi je, aliye na dalili wazi itokayo kwa Mola wake na anaifuata nashahidi atokaye kwake..” (Sura Hud: 17).

Ibnu Mardawayhi ameandika kwa njia nyingine kutoka kwa Ali kwambaalisema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: “Basi je, aliyena dalili wazi itokayo kwa Mola wake ni mimi. Na na anaifuata na shahi-di atokaye kwake ni Ali.”183

SURAT AR-RAAD

Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Hakika wewe ni mwonyaji tu. Na kilakaumu ina wa kuwaongoza.” (Surat ar-Raad: 7).

Ibnu Jarir, Ibnu Mardawayhi, Daylamiy na Ibnu Asakir wameandika kuto-ka kwa Ibnu Abbas kwamba alisema: “Ilipoteremka Aya hii Mtume waMwenyezi Mungu (s.a.w.w.) aliweka mkono wake juu ya kifua chake nakusema: ‘Mimi ndiye mwonyaji.’ Akaashiria mkono wake kwenye bega laAli na kusema: ‘Ali wewe ndiye mwongozaji. Kupitia kwako wataongoka

135

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

182 Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 10 Uk. 65.183 Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 12 Uk. 26.184 Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 13 Uk. 97.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 135

Page 145: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

wenye kutaka kuongoka baada yangu.”184

Abdullah bin Ahmad ameandika katika Zawaidul-Musnad, Ibnu AbiHatim, Tabarani katika al-Awsat, al-Hakim katika Sahih yake, na IbnuAsakir pia, wote wameandika kutoka kwa Ali (a.s.) kwamba alisema:“Katika aya hii, Mtume wa Mwenyezi Mungu ndio Muonyaji, nami ndiyeMwongozaji.” Na katika kauli nyingine Mwongozaji ni mtu kutoka kizazicha Hashim, yaani yeye mwenyewe.185

SURAT IBRAHIM

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na mfano wa neno baya ni kama mti mbaya ambao umeng’olewaardhini hauna uimara.” (Surat Ibrahim: 25 - 26).

Imepokewa kutoka kwa Abu Ja’far katika tafsiri ya mti mbaya kwamba niBani Umaiya, na mti mzuri ni Mtume wa Mwenyezi Mungu, Ali, Fatimana watoto wao.186

SURAT AN-NAMLI

Kauli ya Mwenyezi Mungu: “ Basi waulizeni wenye ukumbusho ikiwanyinyi hamjui.” (Sura an-Namli: 43).Jabir amepokea na Muhammad bin Muslim kutoka kwa Abu Ja’far (a.s.)kwamba alisema: “Sisi ndio wenye ukumbusho.”187

136

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

185 Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 13 Uk. 97.186 Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 13 Uk. 193.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 136

Page 146: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

SURAT ISRAI

Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Na mpe jamaa wa karibu haki yake namaskini na mwana njia, wala usifanye ubadhirifu.” (Sura Israi: 26).

Kutoka kwa as-Asadiy, na ameandika Ibnu Jarir kutoka kwa Ali bin Husainkwamba (a.s.) alimwambia mzee mmoja wa Sham: “Hivi umewahi kuso-ma Qur’ani?” akajibu ndio. Ali akasema: “Hivi hujasoma katika SuratIsrai: “Na mpe jamaa wa karibu haki yake..”? Mzee akasema: ‘’Hivi nyinyindio jamaa wa karibu ambao Mwenyezi Mungu ameamuru wapewe hakiyao?!!” Ali akasema: “Ndio sisi.”188

SURAT MARYAM

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Hakika wale ambao wameamini na wakatenda mema Mwingi warehema atawajaalia mapenzi.” (Sura Maryam: 96).

Ibnu Mardawayhi na Daylamiy wameandika kutoka kwa al-Barau kwam-ba alisema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alimwambia Ali binAbu Talib: “Ewe Ali sema: Ewe Mwenyezi Mungu! Nipe hifadhi Kwakona niwekee mapenzi katika nyoyo za waumini.” Ndipo Mwenyezi Munguakateremsha Aya hii.

Na Muhammad bin al-Hanafiya alikuwa akisema: Hutampata muumini ilani yule anayempenda Ali na watu wa nyumba yake.189

137

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

187 Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 14 Uk. 134.188 Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 15 Uk. 58.189 Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 16 Uk. 130.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 137

Page 147: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

SURAT TWAHA

Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Hakika wewe unatuona.” (Surat Twaha:35).

Ibnu Mardawayhi, al-Khatib na Ibnu Asakir wameandika kutoka kwaAsmau binti Umaysi kwamba alisema: Nilimuona Mtume wa MwenyeziMungu mbele ya Mlima wa Thabir akisema: “Thabir amechomoza, Thabiramechomoza. Ewe Mwenyezi Mungu! Ninakuomba lile alilokuombandugu yangu Musa kwamba unipanulie kifua changu. Unifanyie wepesikazi yangu. Uniondolee fundo katika ulimi wangu. Ifahamike kauli yangu.Na uniwekee waziri katika jamaa zangu. Ndugu yangu Ali. Nitie nguvukupitia kwake. na umshirikishe katika kazi yangu. Ili tukutukuze sana.Hakika wewe unatuona.”190

Mfano wa hiyo ni ile kauli iliyosihi kutoka kwa Mtume (s.a.w.w.) kwam-ba alisema pindi alipompa umakamu juu ya watu wa nyumba yake sikualipokwenda katika Vita vya Tabuk: “Hivi huridhii kwamba wewe nafasiyako kwangu ni ile ya Harun kwa Musa ila ni kwamba hakuna Nabii baadayangu.”191

SURAT AHZABKauli ya Mwenyezi Mungu:

“Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea ucha-fu, enyi watu wa nyumba ya Mtume, na kuwatakasa kabisa kabisa.”(Surat Ahzab: 33).

138

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

190 Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 16 Uk. 169.191 Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 16 Uk. 169.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 138

Page 148: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

Tirmidhi na Hakim wameandika na kuizingatia kuwa ni riwaya sahihi, naIbnu Jarir, Ibnu Mundhir, Ibnu Mardawayhi na al-Bayhaqiy katika Sunanyake, wote wameandika kutoka kwa Ummu Salama kwamba alisema: Ayahii: “Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea ucha-fu, enyi watu wa nyumba ya Mtume, na kuwatakasa kabisa kabisa.” (SuraAhzab: 33) iliteremkia nyumbani kwangu, na humo alikuwemo Fatima,Ali, Hasan na Husain, ndipo Mtume wa Mwenyezi Mungu akawafunikakishamia alichokuwa amejifunika, kisha akasema: “Hawa ndio Ahlul-Baitiwangu, waondolee uchafu na watakase kabisa.”192

Imekuja katika baadhi ya riwaya kwamba Mtume (s.a.w.w.) alitoa mkonowake toka katika kishamiya na kuunyoonsha mbinguni, akasema: “EweMwenyezi Mungu! Hawa ndio Ahlul-Baiti na wasiri wangu hivyo waon-dolee uchafu na watakase kabisa.” Alisema hivyo mara tatu.193

Na katika riwaya nyingine ni kwamba Mtume (s.a.w.w.) aliwafunikakishamiya cha Khaibar, kisha akaweka mkono wake juu yao kisha akase-ma: “Ewe Mwenyezi Mungu! Hawa ndio Ahlul-Baiti wangu.”194

Na katika lafudhi nyingine: “Ewe Mola wangu, shusha rehma zako nabaraka zako juu ya aali Muhammad, kama ulivyoziweka juu ya aaliIbrahim, hakika wewe ni Mhimidiwa msifika.”195

“Na katika riwaya aliyoandika Tabarani kutoka kwa Ummu Salama nikwamba alisema: Nilifunua kishamiya ili niingie pamoja nao lakini Mtume(s.a.w.w) akakivuta toka mikononi mwangu, na akasema: “Hakika weweupo katika kheri.”196

139

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

192 Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 22 Uk. 14.193 Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 22 Uk. 14.194 Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 22 Uk. 14.195 Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 22 Uk. 14.196 Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 22 Uk. 14.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 139

Page 149: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

Na katika riwaya nyingine iliyopokewa na Ibnu Mardawayhi kutoka kwaUmmu Salama ni kwamba alisema: “Je mimi sio katika Ahlul-Baiti wako?Mtume akajibu: “Hakika wewe waelekea katika kheri, hakika wewe nimiongoni mwa wakeze Mtume.”197

Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Hakika Mwenyezi Mungu na malaikawake wanamswalia Nabii. Enyi ambao mmeamini! Mswalieni namumsalimu kwa salamu.” (Surat Ahzab: 56).

Abdu Razaq, Ibnu Abi Shayba, Imam Ahmad, Abdu bin Hamid, Bukhari,Muslim, Abu Daud, Tirmidhiy, Nasaiy, Ibnu Majah na Ibnu Mardawayhi,wameandika kutoka kwa Ka’bi bin Ajrah, kwamba amesema: ‘’Mtummoja alisema: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Tumeshajua namna yakukutolea salamu, ni ipi namna ya kukusalia?

Mtume akasema: ‘’Sema:

?????? ???? ??? ????? ???? ?? ????? ??? ????? ??? ?? ??????? ???? ????????.

?????? ???? ??? ????? ???? ?? ????? ??? ????? ??? ?? ??????? ???? ????????.

‘Ewe Mwenyezi Mungu! Mrehemu Muhammad na aaliMuhammad kama ulivyowarehemu aali Ibrahim, hakika wewe niMhimidiwa Msifika. Ewe Mwenyezi Mungu! mbariki Muhammadna aali Muhammad kama ulivyowabariki aali Ibrahim, hakikawewe ni Mhimidiwa Msifika.’”198

Imam Ahmad, Bukhari, Nasaiy, Ibnu Majah na wengineo, wameandikakutoka kwa Abu Said al-Khudriy kwamba alisema: Tulisema: Ewe Mtume

140

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

197 Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 22 Uk. 14.198 Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 22 Uk. 72.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 140

Page 150: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

wa Mwenyezi Mungu! Tumeshajua namna ya kukutolea salamu, ama salatutakusaliaje? Akasema: ‘Semeni: Ewe Mwenyezi Mungu! MrehemuMuhammad mja wako na Mtume wako kama ulivyomrehemu Ibrahim. Nambariki Muhammad na aali Muhammad kama ulivyombarikiIbrahim.”’199

Imam Ahmad, Abdu bin Hamid na Ibnu Mardawayhi, wameandika kutokakwa Ibnu Burayda kwamba alisema: “Tulisema: Ewe Mtume waMwenyezi Mungu! Tumeshajua namna ya kukutolea salamu, ama salatutakusaliaje? Akasema: ‘Semeni: Ewe Mwenyezi Mungu! Shusha rehemazako na baraka zako juu ya Muhammad na juu ya aali Muhammad, kamaulivyoziweka juu ya Ibrahim, hakika wewe ni Mhimidiwa Msifika.”’200

SURAT ZUMARA

Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Na aliyeleta ukweli na aliyeusadikisha,hao ndio wamchao (Mwenyezi Mungu)” (Sura 33).

Ibnu Jarir, al-Barudiy na Ibnu Asakir kwa njia ya Usayd bin Swaf’wan,wameandika kutoka kwa Ali (a.s.). Na Abu As’wad, Mujahid na jamaamiongoni mwa Ahlul-Baiti wamesema kwamba: Aliyeusadikisha ni Ali(a.s.).201

SURAT AS-SHURA

Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Sema: Kwa haya siwaombi malipo yoyotekwenu isipokuwa mapenzi kwa ndugu...” (Surat as-Shura: 23).

Makusudio ya ndugu zake (s.a.w.w.) hapa ni Ali, Fatima na watoto wake

141

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

199 Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 22 Uk. 72200 Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 22 Uk. 72.201 Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 24 Uk. 3.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 141

Page 151: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

(a.s.), na zimepokewa riwaya za kuvushwa kuhusu hilo. Ibnu al-Mundhir,Ibnu Abi Hatim, Tabarani na Ibnu Mardawayhi wameandika kupitia njia yaIbnu Jubair kutoka kwa Ibnu Abbas kwamba alisema: Ilipoteremka:“Sema: Kwa haya siwaombi malipo yoyote kwenu isipokuwa mapenzikwa ndugu...” walisema: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Ni akina nanihawa karaba zako ambao tunapasa kuwapenda? Akasema: “Ni Ali, Fatimana watoto wao wawili.”202

Ibnu Jarir ameandika kutoka kwa Abu Daylam kwamba alisema:Alipoletwa Ali bin Husein (a.s.) na hali ni mateka na kusimamishwa kati-ka barabara kuu ya Damascus alisimama mzee mmoja kati ya watu waSham, akasema: ‘Kila sifa njema ni ya Mwenyezi Mungu ambaye ame-wauwa na kuwang’oeni.’ Ali bin Husein radhi za Mwenyezi Munguzimwendee akasema: ‘Umewahi kusoma Qur’ani?’ akajibu ndio. Akasema(a.s.): ‘Umewahi kusoma Aali Haa Miim?’ Akajibu ndio nimewahi kuso-ma. Akasema (a.s.): ‘Hujawahi kusoma: “Sema: Kwa haya siwaombimalipo yoyote kwenu isipokuwa mapenzi kwa ndugu...”’ Mzee akasema:‘Nyinyi ndio hao?’ Akasema (a.s.): ‘Naam ndio sisi.’”203

Dhadhan alipokea kutoka kwa Ali (a.s.) kwamba alisema: “Katika AaliHamim (Sura Shura) kuna Aya inayotuhusu, hatupendi sisi ila muumini.”Kisha akasoma Aya hii: “Sema: Kwa haya siwaombi malipo yoyote kwenuisipokuwa mapenzi kwa ndugu...”

Na hili ndilo aliloashiria Kumayti katika shairi lake aliposema:“Tumewakuta mmo ndani ya Aya ya Aali Hamim, ameifasiri hivyo aliyemchamungu na mwarabu kati yetu.”204

Ibnu Habban na Hakim wameandika kutoka kwa Abu Said kwamba alise-

142

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

202 Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 25 Uk. 28.203 Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 25 Uk. 28.204 Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 25 Uk. 29.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 142

Page 152: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

ma: “Naapa kwa yule ambaye nafsi yangu imo mikononi mwake, hakunamtu atakayetuchukia sisi Ahlul-Baiti ila ni lazima Mwenyezi Munguatamwingiza motoni.”205

SURA MUHAMMAD

Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Na ndio Mwenyezi Mungu amewalaani na amewatia uziwi na ame-wapofusha macho yao.” (Sura Muhammad: 23).

Hakuna kizuizi katika kumlaani Yazid kutokana na wingi wa sifa zake

chafu na kutenda kwake madhambi makubwa muda wote wa utu uzimawake. Inakutosha lile alilowafanyia watu wa Madina na Makka, amepokeaTabarani kwa njia hasan kwamba Mtume alisema: “Ewe MwenyeziMungu! Atakayewadhulumu wakazi wa Madina na kuwasababishia khofu,laana za Mwenyezi Mungu, Malaika na watu wote zitakuwa juu yake,haitakubaliwa fidia wala badala kutoka kwake.”

Na msiba mkubwa ni kile kitendo alichowafanyia Ahlul-Baiti (a.s.) nakuridhia kuuawa Husain (a.s.) na kufurahia kitendo hicho, na kumdhalil-isha yeye na watu wa nyumba yake, kama maana hiyo ilivyo mutawatiri.

Jamaa miongoni mwa ulamaa wameamini na kutamka wazi kwamba inasi-hi kumlaani, miongoni mwao ni Hafidh Nasrus-Sunnah Ibnu al-Jawziy, nakabla yake ni al-Qadhiy Abu Ya’la. Allama Taftazaniy amesema: “Hatusitikuhusu jambo lake, bali ni kuhusu imani yake, laana ya Mwenyezi Munguiwe juu yake na juu ya watetezi wake na wasaidizi wake.”206

143

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

205 Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 25 Uk. 29.206 Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 26 Uk. 66. Anayetaka kwa undani suala la Yazidbin Muawiya kulaaniwa arejee kitabu Ar-Raddu ‘Alal-Muta’aswib al-‘Anid chaHafidh Abul Faraj aliye mashuhuri kwa jina la Ibnu al-Jawziy, aliyefarikimwaka 597 A.H.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 143

Page 153: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

SURAT RAHMAN

Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Amezikutanisha bahari mbili. Baina yao kuna kizuizi haziingiliani.Basi nyinyi wawili mnakataa neema gani ya Mola wenu Mlezi? Katikahizo mbili hutoka lulu na marijani.” (Sura Rahman: 19 - 22).

Ibnu Mardawayhi ameandika kutoka kwa Ibnu Asakir kwamba alisemakuhusu: “Amezikutanisha bahari mbili.” ni Ali na Fatima. “Baina yaokuna kizuizi haziingiliani.” ni Mtume (s.a.w.w.) “Katika hizo mbili hutokalulu na marijani.” Ni Hasan na Husein.”

Nionalo mimi207 ni kwamba kauli hiyo ikisihi basi si miongoni mwa tafsiribali ni taawili kama taawili nyingi za masufi katika Aya mbalimbali.Kwangu mimi wote Ali na Fatima ni watu adhimu mno kushinda baharikuu kielimu na kifadhila, na pia wote wawili Hasan na Husain ni wazuri nawenye kung’ara kushinda lulu na marijani kwa kiwango ambacho kimevu-ka kipimo cha hesabu.208

SURAT AL-WAQI’A

Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Waliotangulia ndio waliotangulia.” (Suratal-Waqi’a: 10).

144

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

207 Yaani mwandishi wa tafsiri hii.208 Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 27 Uk. 93.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 144

Page 154: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

Ibnu Mardawayhi ameandika kutoka kwa Ibnu Abbas kwamba:“Iliteremka kwa ajili ya Ezekiel muumini wa aali Firaun, Habib Najarambaye katajwa katika Sura Yasin, na Ali bin Abu Talib (a.s.)”209

SURAT MUJADILAH

Kauli ya Mwenyezi Mungu: S

“Enyi mlioamini! Mnaposema siri na Mtume, basi tangulizeni sadakakabla ya kumsemesha hayo ni bora kwenu na ni safi sana, na ikiwahamkupata basi Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe, Mwenyekurehemu.” (Sura Mujadilah: 12).

Al-Hakim ameiandika na kuizingatia kuwa ni sahihi, Ibnu al-Mundhir,Abdu bin Hamid na wengineo, wote wameandika kutoka kwa Amirul-Muuminina (a.s.) kwamba alisema: “Hakika katika Kitabu cha MwenyeziMungu kuna Aya ambayo hakuna yeyote aliyeifanyia kazi kabla yangu,wala hakuna yeyote atakayeifanyia kazi baada yangu, nayo ni Aya ya kuse-ma siri na Mtume: “Enyi mlioamini! Mnaposema siri na Mtume, basi tan-gulizeni sadaka kabla ya kumsemesha hayo ni bora kwenu na ni safisana…..” nilikuwa nina dinari nikazibadili kwa dirhamu, hivyo nikawakila nisemapo siri na Mtume natoa dirhamu moja kabla ya kusema nayesiri, kisha ikafutwa na hakuna yeyote aliyeifanyia kazi.”210

145

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

209 Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 27 Uk. 114.210 Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 27 Uk. 28.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 145

Page 155: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

SURAT TAGHABUN

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Bila shaka mali zenu na watoto wenu ni mtihani, na kwa MwenyeziMungu kuna malipo makubwa.” (Sura Taghabun: 15).

Imam Ahmad, Abu Daud, Tirmidhiy, Nasaiy, Ibnu Majah na Hakimambaye ameizingatia kuwa ni sahihi, wote wameandika kutoka kwaBuraida kwamba alisema: “Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.)alikuwa akitoa hotuba na ghafla wakaja Hasan na Husein wakiwawamevaa kanzu mbili nyekundu na hali wakidondoka na kuamka, Mtumewa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akateremka toka mimbarini akawafuata nakuwabeba kila mmoja katika bega lake, kisha akapanda juu ya mimbari nakusema: ‘Mwenyezi Mungu amesema kweli. Bila shaka mali zenu nawatoto wenu ni mtihani, hakika mimi nilipowaona hawa wawili wakitem-bea na wakidondoka sikuweza kuvumilia mpaka nikakatisha mazungumzoyangu na nikashuka kwenda kuwachukua.”211

Na katika riwaya ya Ibnu Mardawayhi kutoka kwa Abdullah bin Umar nikwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alipokuwa akiwahutubiawatu juu ya mimbari, Husain bin Ali alitokeza na kuanza kwenda kwaMtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w) ndipo akakanyaga nguo yakealiyokuwa amevaa na akawa amedondoka na kuanza kulia, basi Mtume waMwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akateremka toka juu ya mimbari, watuwalipomuona amefanya hivyo walimkimbilia Husain na kuanza kumbem-beleza mpaka akafika mikono mwa Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w.) na kusema: “Mwenyezi Mungu amuuwe shetani, hakika mtoto ni

146

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

211 Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 27 Uk. 111.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 146

Page 156: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

mtihani, naapa kwa yule ambaye nafsi yangu imo mikononi mwakesikuweza kujizuia212 hakika nimeteremka kutoka mimbarini kwangu.”213

SURAT AL-HAQQAH

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Ili tuifanye ukumbusho kwenu, na sikio lisikialo lisikie.” (Sura al-Haqqah: 12).

Katika habari ni kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.)alimwambia Ali (a.s.): ‘’Hakika mimi nilimwomba Mwenyezi Mungu ali-fanye hivyo sikio lako ewe Ali.’’ Amirul-Mu’minin Ali (a.s.) alisema:“Baada ya hapo sikuwahi kusahau chochote na wala sikupasa kusahau.”

SURAT AL-INSAN

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na huwalisha chakula masikini na yatima na mfungwa hali ya kuwawanakipenda. Tunakulisheni kwa ajili ya radhi za Mwenyezi Mungutu, hatutaki kwenu malipo wala shukurani.” (Surat al-Insan: 8 - 9).

147

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

212 Katika maelezo ya Juz. 27 Uk. 112 Alusiy amesema: “Sijui ingekuwaje lauMtume wa Mwenyezi Mungu angeiona hali ya Husain (a.s.) katika tukio laKarbala, sijui angefanya nini? Kwa kweli laana ya Mwenyezi Mungu, Malaikazake, Mitume wake na watu wote iwe juu ya yule aliyeamuru yale yaliyotokea,aliyerusha vimondo, kuwasha moto na akaridhia au kuongeza jeshi.213 Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 27 Uk. 111.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 147

Page 157: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

Riwaya ya Atau kutoka kwa Ibnu Abbas kwamba alisema: Hakika Hasanna Husein walipatwa na maradhi, babu yao Muhammad (s.a.w.w.) alik-wenda kuwaona, na masahaba nao pia walikwenda kuwaona. Wakasemakumwambia Ali: “Ewe Abu Hasan! Ni bora kama ungeweka nadhiri juu yawatoto wako.” Ali, Fatima na mtumishi wao Fidha wakaweka nadhirikwamba ikiwa watapona watafunga siku tatu kumshukuru MwenyeziMungu.

Vijana wawili wakapata afya njema na hali nyumbani kwa aali Muhammadhawana kitu si kichache wala kingi. Ndipo Ali akaenda kwa SimonMyahudi wa Khaibari, akakopa toka kwake pishi tatu za ngano. Akaja nazona Fatima akachukua pishi moja akatwanga na kuoka mikate mitano kulin-gana na idadi yao. Ali alipomaliza kuswali pamoja na Mtume Sala yaMagharibi alikuja nyumbani na kikawekwa chakula mbele yake, maramasikini akafika mlangoni kwao akagonga akisema: “Assalam Alaykumenyi watu wa nyumba ya Muhammad, mimi ni maskini katika watoto waumma wa kiislamu, nipeni chakula Mwenyezi Mungu atakupeni chakulacha Peponi.” Wakampa na wao wakalala bila kuonja kitu ila maji, na sikuya pili wakaamka wakiwa na funga.

Ilipofika siku ya pili Fatima akachukua pishi jingine akatwanga na kuokamikate. Ali alipomaliza kuswali pamoja na Mtume (s.a.w.w.) Sala yaMagharibi alikwenda nyumbani na kikawekwa chakula mbele yake, maraakafika mlangoni kwao yatima akagonga akisema: “Assalam Alaykumenyi watu wa nyumba ya Muhammad, yatima toka katika watoto wa muha-jirana, nipeni chakula Mwenyezi Mungu atakupeni chakula cha Peponi.”Wakampa chakula na wakashinda siku mbili mchana kutwa na usiku kuchabila kuonja chochote ila maji, na siku ya tatu wakaamka wakiwa na funga.

Ilipofika siku ya tatu Fatima akachukua pishi la tatu akatwanga na kuokamikate. Ali alipomaliza kuswali pamoja na Mtume (s.a.w.w.) Sala yaMagharibi alikuja nyumbani na kikawekwa chakula mbele yake, maramfungwa wa kivita akafika mlangoni kwao akagonga akisema: “Assalam

148

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 148

Page 158: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

Alaykum enyi watu wa nyumba ya Muhammad, mimi ni mateka waMuhammad, nipeni chakula Mwenyezi Mungu atakupeni chakula.”Wakampa chakula na wakashinda siku tatu mchana kutwa na usiku kuchabila kuonja chochote ila maji.

Ilipofika siku ya nne Ali alimshika mkono Hasan na Husein na kwenda naokwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.), alipowaona (s.a.w.w.)wakitetemeka kama vifaranga kutokana na ukali wa njaa, alisema: “EweAbal-Hasan! Hali niionayo kwenu yaniumiza mno.”

Akasimama na kwenda nao kwa Fatima (a.s.), wakamkuta akiwamihrabuni kwake na hali tumbo lake limeshikana na mgongo wake namacho yake yamebadilika kutokana na ukali wa njaa. Huruma ikamuingiMtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) na ikamuumiza hali hiyo, ndipoJibril (a.s.) akateremka na kusema: “Ewe Muhammad pokea, MwenyeziMungu anakupa pongezi kwa kitendo cha watu wa nyumba yako.” Mtumeakasema: “Nichukue nini ewe Jibril?” Jibril (a.s.) akamsomea SuratInsan.214

AHLUL-BAIT (A.S.) NDANI YA TAFSIRI YAAL-QASIMIY, INAYOITWA MAHASINUT-TAAWIL

SURAT AAL IMRAN

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

149

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

214 Tafsir Ruhul-Ma’aniy Juz. 29 Uk. 157.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 149

Page 159: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

“Na watakaokuhoji baada kukufikia elimu hii, waambie: Njoonituwaite watoto wetu na watoto wenu, na wanawake zetu na wanawakewenu, na nafsi zetu na nafsi zenu, kisha tuombe kwa unyenyekevututake laana ya Mwenyezi Mungu iwashukie waongo.” (Sura AaliImran: 61).

Hafidh Abu Bakr bin Mardawayhi amepokeakutoka kwa Sha’abiy kutokakwa Jabir kwamba amesema: Aqib na Tayib walikwenda kwa Mtume(s.a.w.w.), naye akawaomba wafanye maapizano, wakamwahidi wafanyemaapizano naye kesho yake, ndipo Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w.) akatoka na hali amewashika mkono Ali, Fatima, Hasan naHusain, kisha akawatumia ujumbe waje lakini wakakataa na hatimayewakakubali kutoa kodi. Mtume wa Mwenyezi Mungu akasema: “Naapakwa yule aliyenituma kwa haki! Lau wangesema la, basi bonde laolingeteketea kwa moto.”

Jabir anasema: Na kwa ajili ya hao iliteremka Aya hii: “Na watakaokuhojibaada kukufikia elimu hii, waambie: Njooni tuwaite watoto wetu na wato-to wenu, na wanawake zetu na wanawake wenu, na nafsi zetu na nafsizenu, kisha tuombe kwa unyenyekevu tutake laana ya Mwenyezi Munguiwashukie waongo.” (Sura Aali Imran: 61). “….. nafsi zetu na nafsi zenu”ni Mtume wa Mwenyezi Mungu na Ali. “…..watoto wetu” ni Hasan naHusein. “…..wanawake zetu” ni Fatima.

Hakim ameipokea kwa kuvushwa katika Mustadrak kutoka kwa Sha’bahkutoka kwa Mughira. Na hii ni sahihi zaidi.215

150

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

215 Tafsirul-Qasimiy inayoitwa Mahasinut-Taawil Juz. 2 Uk. 71.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 150

Page 160: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

SURAT MAIDA

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Leo nimekukamilishieni dini yenu na kukutimizieni neema yangu nanimekupendeleeni Uislamu uwe dini yenu..” (Sura Maida: 3).

Ibnu Mardawayhi amepokea kwa njia ya Abu Harun al-‘Abdiy kutoka kwaAbu Said al-Khudriy kwamba ilimteremkia Mtume wa Mwenyezi MunguSiku ya Ghadir Khum pale aliposema kuhusu Ali: “Yule ambaye mimi ninamamlaka juu yake basi Ali ana mamlaka juu yake.”

Kisha ameipokea kutoka kwa Abu Huraira na katika maelezo yake nikwamba ilikuwa ni siku ya kumi na nane ya Mfunguo tatu.216

SURAT MAIDAKauli ya Mwenyezi Mungu:

“Hakika walii wenu hasa ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake nawale walioamini ambao husimamisha Swala na hutoa Zaka wakiwawamerukui.” (Sura Maida: 55).

151

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

216 Tafsirul-Qasimiy inayoitwa Mahasinut-Taawil Juz. 7 Uk. 34.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 151

Page 161: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

Mpaka baadhi yao katika tendo hili wametaja athari inayomhusu Ali binAbu Talib kwamba: Hakika Aya hii iliteremka kwa ajili yake, muombajialipita kwake na hali akiwa katika rukuu yake ndipo akampa pete yake.217

SURAT TAWBA

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Na ni tangazo litokalo kwa Mwenyezi Mungu na Mtume wake, kwawatu Siku ya Hija kubwa.” (Sura Tawba: 3).

Ibnu Is’haqa amepokea kwa sanadi yake kutoka kwa Abu Ja’farMuhammad bin Ali (a.s.) kwamba ilipoteremka Sura Baraa kwa Mtume waMwenyezi Mungu (s.a.w.w.) na alikuwa tayari ameshamtuma Abu Bakrakaongoze Hija, ndipo akaambiwa: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu nivizuri lau ungemtuma nayo Abu Bakr. Akasema: “Hatekelezi kwa niabayangu ila mtu toka katika Ahlul-Baiti wangu.” Kisha akamwita Ali bin AbuTalib na kumwambia: “Nenda na kisa hiki kuanzia mwanzo wa Sura Baraa,na nenda kawatangazie watu siku ya kuchinja pindi watakapokusanyikahuko Mina, kwamba kafiri haingii peponi, baada ya mwaka huu haruhusi-wi Mushriku kuhiji, haruhusiwi kutufu akiwa uchi, na yule ambaye anamkataba na Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) utaendelea mpakamwisho wa muda wake.”218

152

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

217 Tafsirul-Qasimiy inayoitwa Mahasinut-Taawil Juz. 7 Uk. 156.218 Tafsirul-Qasimiy inayoitwa Mahasinut-Taawil Juz. 8 Uk. 85.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:05 AM Page 152

Page 162: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

Imenukuliwa kwamba Bani Umaiyya walikuwa wakimtukana Ali katikahotuba zao, na ukhalifa ulipoangukia mikononi mwa Umar bin Abdul-Azizaliondoa kipengele hicho (cha kumlaani Ali) na kuweka badala yake Ayahii.

Nasir amesema: “Huenda Aya hii kuwekwa badala ya kashfa hizo ilikuwani kutokana na kuoana kati ya maana yake ambayo ni kukataza uovu na ilehadithi inayosema kwamba kumfanyia uadui Ali ni uovu, kwani Mtume(s.a.w.w.) alimwambia Ammar aliyekuwa katika jeshi la Ali: “Litakuuwakundi ovu.” Naye akauawa akiwa pamoja na Ali (a.s.) Siku hiyo yaSiffin.219

SURAT AHZAB

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea ucha-fu, enyi watu wa nyumba ya Mtume, na kuwatakasa kabisa kabisa.”(Sura Ahzab; 33:33).

Mtume (s.a.w.w.) aliwakusanya Fatima, Ali, Hasan na Husain, kishaakawafunika kishamiya alichokuwa amejifunika, kisha akasema: “Hawandio Ahlul-Baiti wangu, waondolee uchafu.”220

153

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

219 Tafsirul-Qasimiy inayoitwa Mahasinut-Taawil Juz. 10 Uk. 543.220 Tafsirul-Qasimiy inayoitwa Mahasinut-Taawil Juz. 13 Uk. 506.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:06 AM Page 153

Page 163: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

SURAT AS-SHURA

Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Sema: Kwa haya siwaombi malipo yoyotekwenu isipokuwa mapenzi kwa ndugu...” (Sura as-Shura: 23).

Katika Sahih Bukhari imepokewa kutoka kwa Ibnu Abbas kwamba ali-ulizwa kuhusu “Sema: Kwa haya siwaombi malipo yoyote kwenuisipokuwa mapenzi kwa ndugu...” Said bin Jubair akasema: Ndugu ni aaliMuhammad.221

Na aliyoipokea Ibnu Abi Hatim ni kwamba ilipoteremka Aya hii walisema:“Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Ni akina nani hawa ambao MwenyeziMungu ameamuru tuwapende? Akasema: “Ni Fatima na kizazi chake.”222

SURAT MUJADILAH

Kauli ya Mwenyezi Mungu:

“Enyi mlioamini! Mnaposema siri na Mtume, basi tangulizeni sadakakabla ya kumsemesha hayo ni bora kwenu na ni safi sana, na ikiwahamkupata basi Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe, Mwenyekurehemu.” (Sura Mujadilah: 12).

154

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

221 Tafsirul-Qasimiy inayoitwa Mahasinut-Taawil Juz. 14 Uk. 172.222 Tafsirul-Qasimiy inayoitwa Mahasinut-Taawil Juz. 14 Uk. 172.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:06 AM Page 154

Page 164: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

Imepokewa kutoka kwa Mujahidu kwamba alisema: “Ali bin Abu Talib(radhi za Mwenyezi Mungu zimwendee) alisema: “Hakika katika Kitabucha Mwenyezi Mungu kuna Aya ambayo hakuna yeyote aliyeifanyia kazikabla yangu, wala hakuna yeyote atakayeifanyia kazi baada yangu.”223

Na imepokewa pia kutoka kwake (Mujahid) kwamba alisema:“Walikatazwa kusema siri na Mtume (s.a.w.w.) mpaka watoe sadaka.Hakuna aliyeweza kusema naye siri ila Ali bin Abu Talib (radhi zaMwenyezi Mungu zimwendee), alitoa sadaka ya dinari. Ndipo (baada yasadaka hiyo) ikateremka ruhusa (iliyoondoa sharti la sadaka). “224

Na mwisho wa maombi yetu ni kumshukuru MwenyeziMungu Mola Mlezi wa viumbe wote.

155

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

223 Tafsirul-Qasimiy inayoitwa Mahasinut-Taawil Juz. 16 Uk. 55.224 Tafsirul-Qasimiy inayoitwa Mahasinut-Taawil Juz. 16 Uk. 55.

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:06 AM Page 155

Page 165: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

ORODHA YA VITABU VILIVYO CHAPISHWA NAAL-ITRAH FOUNDATION

1. Qur'an Al-Kariim - Tafsir Al-Kashif Juzuu ya kwanza mpaka Thalathini

2. Uharamisho wa Riba3. Uharamisho wa uwongo Juzuu ya Kwanza 4. Uharamisho wa uwongo Juzuu ya Pili5. Hekaya za Bahlul6. Muhanga wa Imamu Husein (A.S.)7. Mikingamo iliyomzunguka Imamu Ali (A.S.)8. Hijab vazi Bora9. Ukweli wa Shia Ithnaashari10. Madhambi Makuu11. Mbingu imenikirimu12. Abdallah Ibn Saba13. Khadijatul Kubra14. Utumwa15. Umakini katika Swala16. Misingi ya Maarifa17. Kanuni za Ndoa na maadili ya Familia18. Bilal wa Afrika19. Abudharr20. Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu21. Salman Farsi22. Ammar Yasir23. Qur'an na Hadithi24. Elimu ya Nafsi25. Yajue Madhehebu ya Shia26. Ukusanyaji na Uhifadhi wa Qur'an Tukufu

156

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:06 AM Page 156

Page 166: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

27. Al-Wahda28. Ponyo kutoka katika Qur'an. 29. Uislamu mfumo kamili wa maisha ya kijamii30. Mashukio ya Akhera31. Al Amali32. Dua Indal Ahlul Bayt33. Udhuu kwa mujibu wa Kitabu na Sunna.34. Haki za wanawake katika Uislamu35. Mwenyeezi Mungu na sifa zake36. Amateka Na Aba'Khalifa37. Nafasi za Ahlul Bayt (a.s)38. Adhana.39 Upendo katika Ukristo na Uislamu40. Nyuma yaho naje kuyoboka41. Amavu n’amavuko by’ubushiya42. Kupaka juu ya khofu 43. Kukusanya swala mbili44. Bismillah ni sehemu ya Qur’ani na husomwa kwa Jahara45. Kuwaongoza vijana wa kizazi kipya46. Kusujudu juu ya udongo47. Kusheherekea Maulidi Ya Mtume (s)48. Tarawehe49. Malumbano baina ya Sunni na Shia50. Kupunguza Swala safarini51. Kufungua safarini52. Umaasumu wa Manabii53. Qur’an inatoa changamoto54. as-Salaatu Khayrun Mina -'n Nawm55. Uadilifu wa Masahaba 56. Dua e Kumayl57. Sauti Ya Uadilifu wa Binadamu

157

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:06 AM Page 157

Page 167: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

58. Umaasumu wa Mitume - Faida Zake Na Lengo Lake59. Umaasumu wa Mitume - Majibu Ya Aya Zenye Utata60. Umaasumu wa Mitume - Umaasumu wa Mitume

Muhammad (s)61. Nahju’l-Balaghah - Juzuu ya Kwanza62. Nahju’l-Balaghah - Juzuu ya Pili63. Kuzuru Makaburi64. Maswali Na Mishkili Elfu - Sehemu ya Kwanza65. Maswali Na Mishkili Elfu - Sehemu ya Pili66. Maswali Na Mishkili Elfu - Sehemu ya Tatu67. Maswali Na Mishkili Elfu - Sehemu ya Nne68. Maswali Na Mishkili Elfu - Sehemu ya Tano69. Maswali Na Mishkili Elfu - Sehemu ya Sita70. Tujifunze Misingi Ya Dini71. Sala ni Nguzo ya Dini72. Mikesha Ya Peshawar73. Malezi Ya Mtoto Katika Uislamu74. Ubora wa Imam 'Ali Juu ya Maswahaba Na Ushia ndio njia

iliyonyooka75. Hukumu za Kifikihi zinazowahusu Wanawake76. Liqaa-u-llaah77. Muhammad (s) Mtume wa Allah78. Amani na Jihadi Katika Uislamu 79. Uislamu Ulienea Vipi?80. Uadilifu, Amani na Mtume Muhammad (s) 81. Mitala na Ndoa za Mtume Muhammad (s) 82. Urejeo (al-Raja’a )83. Mazingira84. Utokezo (al - Badau) 85. Sadaka yenye kuendelea 86. Msahafu wa Imam Ali

158

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:06 AM Page 158

Page 168: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

87. Uislamu na dhana88. Mtoto mwema89. Adabu za Sokoni90. Johari za hekima kwa vijana91. Maalimul Madrasatain Sehemu ya Kwanza92. Maalimul Madrasatain Sehemu ya Pili93. Maalimul Madrasatain Sehemu ya Tatu94. Tawasali95. Imam Mahdi katika Usunni na Ushia96. Maana ya laana na kutukana katika Qur’ani Tukufu97. Hukumu ya kujenga juu ya makaburi98. Swala ya maiti na kumlilia maiti99. Shiya na Hadithi (kinyarwanda)100. Mariamu, Yesu na Ukristo kwa mtazamo wa Kiislamu101. Hadithi ya Thaqalain102 Fatima al-Zahra103. Tabaruku104. Sunan an-Nabii105. Historia na sera ya viongozi wema (Sehemu ya Kwanza)106. Historia na sera ya viongozi wema (Sehemu ya Pili)107. Mahdi katika sunna108. Kusalia Nabii (s.a.w)109. Ujumbe -Sehemu ya Kwanza110. Ujumbe - Sehemu ya Pili111. Ujumbe - Sehemu ya Tatu112. Ujumbe - Sehemu ya Nne113. Ngano ya kwamba Qur’ani imebadilishwa

159

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:06 AM Page 159

Page 169: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

114. Iduwa ya Kumayili115. Maarifa ya Kiislamu.116. Ukweli uliopotea sehemu ya Kwanza117. Ukweli uliopotea sehemu ya Pili118. Ukweli uliopotea sehemu ya Tatu119. Ukweli uliopotea sehmu ya Nne120. Ukweli uliopotea sehmu ya Tano121. Johari zenye hekima kwa vijana122. Safari ya kuifuata Nuru123. Idil Ghadiri124. Myahudi wa Kimataifa125. Kuanzia ndoa hadi kuwa Wazazi126. Visa vya kweli sehemu ya Kwanza127. Visa vya kweli sehemu ya Pili128. Muhadhara wa Maulamaa129. Mwanadamu na Mustakabali wake130. Imam Ali binamu ya Mtume Sehemu ya Kwanza131. Imam Ali binamu ya Mtume Sehemu ya Pili132. Khairul Bariyyah133. Uislamu na mafunzo ya kimalezi134. Vijana ni Hazina ya Uislamu.135. Yafaayo kijamii136. Kusoma sura zenye Sijda ya wajibu137. Taqiyya138. Vikao vya furaha 139. Shia asema haya Sunni asema haya Wewe wasemaje?

160

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:06 AM Page 160

Page 170: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

140. Uislamu na Mazingatio Sehemu ya Kwanza141. Uislamu na Mazingatio Sehemu ya Pili142. Azadari-Kuhuzunika na Kuomboleza143. Sunna katika Kitabu Fiqhi al-Sunnah144. Mtazamo Mpya - Wanawake katika Uislamu145. Kuonekana kwa Allah146. Tabia njema kwa Mujibu wa Ahlul-Bayt

(Sehemu ya Kwanza)147. Tabia njema kwa Mujibu wa Ahlul-Bayt (Sehemu ya Pili)148. Ndugu na Jirani149. Ushia ndani ya Usunni150. Maswali na Majibu151. Mafunzo ya hukmu za ibada 152 Ahlul Bayt ndani ya tafsiri za Kisunni Na 1153. Ahlul Bayt ndani ya tafsiri za Kisunni Na 2154. Ahlul Bayt ndani ya tafsir za Kisunnu Na.3155. Kati ya Alama kuu za dini ni Swala ya Jamaa na Adabu za

Msikiti na Taratibu zake156. Abu Huraira

157. Uadilifu katika Uislamu

161

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:06 AM Page 161

Page 171: Ahlulbayt ndani ya tafsiri za kisunni (sehemu ya tatu)

BACK COVER

Ahlul Bayt, yaani Watu wa Nyumba ya Mtume Muhammad SAW ni vion-gozi ambao Mtume alituusia tuwafuate. Katika hotuba yake ndefu namaarufu aliyoitoa pale Ghadir Khumm katika msafara wake wa kurejeakutoka Hija yake ya mwisho, Mtukufu Mtume SAW alisema haya mbeleya masahaba na mahujaji zaidi ya laki moja: “...Nakuachieni vitu viwilivizito: Qur’ani na Ahlul Bayt wangu. Viwili hivyo havitaachana mpakavinifikie katika [hodhi ya] Kawthar. Nawausia juu ya Ahlul Bayt wangu!Angalieni jinsi mtakavyojihusisha nao. Kama mkishikamana na viwili hivihamtapotea kamwe...” (kwa maelezo zaidi soma kitabu cha al-Ghadir)

Lakini bahati mbaya sana sio Waislamu wote wanaowafuata Ahlul Bayt ASpamoja na kwamba wanavyuoni wa madhehebu zote wameandika habarizao katika vitabu vyao na kuonesha kwamba hawa ni viongozi wa Ummahuu wa Kiislamu.

Mwandishi wa kitabu hiki anajaribu kuthibitisha hilo kwa kutoa rejeambalimbali kutoka vitabu maarufu vya wanavyuoni wa Kisunni.

Kimetolewa na kuchapishwa na:Alitrah FoundationS.L.P. 19701 Dar es Salaam, TanzaniaSimu: +255 22 2110640Simu/Nukushi: +255 22 2127555Barua Pepe: [email protected]: www.alitrah.orgKatika mtandao: www.alitrah.info

162

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No.3

Ahlul Bayt ndani ya Tafsir za Kisunni No 3 Check Lubumba.qxd 7/1/2011 11:06 AM Page 162