44
Haki na Wajibu Wa Mtumiaji Katika Sekta ya Usafirishaji Oscar Kikoyo Katibu Mtendaji, Baraza la Ushauri la Watumiaji wa Huduma zinazothibitiwa na SUMATRA NSSF Waterfront Building, 7 th Floor, P.O BOX 14154, Dar es Salaam Simu +255 22 2127410, Fax +255 22 2127410 Barua Pepe: [email protected] Tofuti: www.sumatraccc.go.tz

Haki na Wajibu Wa Mtumiaji wa Huduma za Usafiri wa Anga.Ibara ya 44(1)(c) ya Rasimu ya Katiba Mpya inaweka wazi zaidi haki ya watu ... Kwa usafiri wa majini ndani ya Tanzania, sheria

  • Upload
    others

  • View
    44

  • Download
    0

Embed Size (px)

Citation preview

Page 1: Haki na Wajibu Wa Mtumiaji wa Huduma za Usafiri wa Anga.Ibara ya 44(1)(c) ya Rasimu ya Katiba Mpya inaweka wazi zaidi haki ya watu ... Kwa usafiri wa majini ndani ya Tanzania, sheria

Haki na Wajibu Wa Mtumiaji

Katika Sekta ya Usafirishaji

Oscar Kikoyo

Katibu Mtendaji,

Baraza la Ushauri la Watumiaji wa Huduma zinazothibitiwa na

SUMATRA

NSSF Waterfront Building, 7th Floor,

P.O BOX 14154, Dar es Salaam

Simu +255 22 2127410, Fax +255 22 2127410

Barua Pepe: [email protected]

Tofuti: www.sumatraccc.go.tz

Page 2: Haki na Wajibu Wa Mtumiaji wa Huduma za Usafiri wa Anga.Ibara ya 44(1)(c) ya Rasimu ya Katiba Mpya inaweka wazi zaidi haki ya watu ... Kwa usafiri wa majini ndani ya Tanzania, sheria

Nukuu ya Mada hii.

“Haki isiyodaiwa ni Haki iliyopotea

kwenye upeo lakini Wajibu usiotimizwa ni

adui wa Haki iliyo usoni”.

James Earl “Jimmy” Carter Jr. (Sources of

Strength)

Page 3: Haki na Wajibu Wa Mtumiaji wa Huduma za Usafiri wa Anga.Ibara ya 44(1)(c) ya Rasimu ya Katiba Mpya inaweka wazi zaidi haki ya watu ... Kwa usafiri wa majini ndani ya Tanzania, sheria

Wajumbe wa Baraza –Kituo cha DART Ferry

Page 4: Haki na Wajibu Wa Mtumiaji wa Huduma za Usafiri wa Anga.Ibara ya 44(1)(c) ya Rasimu ya Katiba Mpya inaweka wazi zaidi haki ya watu ... Kwa usafiri wa majini ndani ya Tanzania, sheria

Utangulizi

Chimbuko la dhana ya haki za Mtumiaji ni

mfumo wa uchumi wa soko

Sekta binafsi huendesha uzalishaji mali na

usambazaji kwa ajili ya kutengeneza faida.

Watumiaji hubaki waangaliaji kwa kukosa mbinu

za kukabiliana na watoa huduma.

Soko kukosa uwiano baina ya ubora wa huduma

zitolewazo na gharama za huduma hizo

Page 5: Haki na Wajibu Wa Mtumiaji wa Huduma za Usafiri wa Anga.Ibara ya 44(1)(c) ya Rasimu ya Katiba Mpya inaweka wazi zaidi haki ya watu ... Kwa usafiri wa majini ndani ya Tanzania, sheria

Utangulizi unae.

Wadau wakuu katika uchumi wa soko ni Watoa

Huduma, Watumiaji na Serikali

Kila kundi lina maslahi binafsi yanayokinzana

kimtazamo.

Mtoa huduma – HUDUMA HAFIFU, FAIDA

KUBWA.

Mtumiaji – HUDUMA BORA, GHARAMA NAFUU.

Serikali - KODI

Page 6: Haki na Wajibu Wa Mtumiaji wa Huduma za Usafiri wa Anga.Ibara ya 44(1)(c) ya Rasimu ya Katiba Mpya inaweka wazi zaidi haki ya watu ... Kwa usafiri wa majini ndani ya Tanzania, sheria

Utangulizi unae.

Maslahi ya Mtoa huduma yanarandana na

maslahi ya Serikali katika Uchumi wa

soko.

Faida kubwa kwa mtoa huduma - huzaa

Kodi Kubwa kwa Serikali.

Page 7: Haki na Wajibu Wa Mtumiaji wa Huduma za Usafiri wa Anga.Ibara ya 44(1)(c) ya Rasimu ya Katiba Mpya inaweka wazi zaidi haki ya watu ... Kwa usafiri wa majini ndani ya Tanzania, sheria

Dira ya sera ya Uchukuzi

Dira ya uchukuzi ni kuwa na huduma

bora, nafuu, za uhakika, zenye kukidhi

mahitaji ya kila nyanja ya jamii kiuchumi,

na zinazozingatia usalama na pia

kuhifadhi mazingira

Page 8: Haki na Wajibu Wa Mtumiaji wa Huduma za Usafiri wa Anga.Ibara ya 44(1)(c) ya Rasimu ya Katiba Mpya inaweka wazi zaidi haki ya watu ... Kwa usafiri wa majini ndani ya Tanzania, sheria

Dhamira ya Sera ya Taifa

Kuendeleza miundombinu na huduma za

uchukuzi zenye kuzingatia usalama,

uhakika wa upatikanaji, kukidhi mahitaji

ya uchukuzi kwa gharama nafuu

kulingana na mikakati ya Serikali kwa

maendeleo ya jamii kiuchumi na

mazingira endelevu

Page 9: Haki na Wajibu Wa Mtumiaji wa Huduma za Usafiri wa Anga.Ibara ya 44(1)(c) ya Rasimu ya Katiba Mpya inaweka wazi zaidi haki ya watu ... Kwa usafiri wa majini ndani ya Tanzania, sheria

Taswira ya Sekta ya Uchukuzi

Gharama za juu (Value for Money

Concept)

Huduma zisizokidhi mahitaji

(Demand/Supply ratio)

Uchakavu wa vyombo vya

usafiri/miundombinu

Ukiukwaji wa haki za watumiaji

Page 10: Haki na Wajibu Wa Mtumiaji wa Huduma za Usafiri wa Anga.Ibara ya 44(1)(c) ya Rasimu ya Katiba Mpya inaweka wazi zaidi haki ya watu ... Kwa usafiri wa majini ndani ya Tanzania, sheria

HAKI ZA MTUMIAJI

Watumiaji wote bila kujali hali zao za

kimaumbile wana haki sawa.

Page 11: Haki na Wajibu Wa Mtumiaji wa Huduma za Usafiri wa Anga.Ibara ya 44(1)(c) ya Rasimu ya Katiba Mpya inaweka wazi zaidi haki ya watu ... Kwa usafiri wa majini ndani ya Tanzania, sheria

Kanuni za John F. Kennedy

Maendeleo ya utetezi wa haki za watumiaji

yalianza katika miaka ya 1960 huko

marekani. Aliyekuwa Rais wa Marekani

kwa wakati huo bwana John F. Kennedy

ndiye aliyekuwa chachu ya vuguvugu la

kutetea maslahi ya Watumiaji katika soko.

Page 12: Haki na Wajibu Wa Mtumiaji wa Huduma za Usafiri wa Anga.Ibara ya 44(1)(c) ya Rasimu ya Katiba Mpya inaweka wazi zaidi haki ya watu ... Kwa usafiri wa majini ndani ya Tanzania, sheria

Kanuni za John F. Kennedy

Watoa huduma na wazalishaji walionekana

kuwa na nguvu na hila nyingi katika

kuhakikisha kuwa wanachokiuza

kinakubalika kwa watumiaji bila kujali

ubora wa huduma au bidhaa hiyo.

Page 13: Haki na Wajibu Wa Mtumiaji wa Huduma za Usafiri wa Anga.Ibara ya 44(1)(c) ya Rasimu ya Katiba Mpya inaweka wazi zaidi haki ya watu ... Kwa usafiri wa majini ndani ya Tanzania, sheria

Kanuni za John F. Kennedy

Kutokana na hali hiyo, J.F.Kennedy alikuja

na Haki nne za mtumiaji katika suala zima

la kumkomboa mtumiaji kutokana na hila

za soko. Haki hizo zilikuwa haki ya

usalama, haki ya kupewa taarifa, haki ya

kuchagua na haki ya kusikilizwa. Haki hizi

nne zilijulikana kama Kanuni za Kennedy.

Mwaka 1970 raisi Gerald Ford aliongeza

haki ya kuelimishwa

Page 14: Haki na Wajibu Wa Mtumiaji wa Huduma za Usafiri wa Anga.Ibara ya 44(1)(c) ya Rasimu ya Katiba Mpya inaweka wazi zaidi haki ya watu ... Kwa usafiri wa majini ndani ya Tanzania, sheria

Kanuni za CI

Tarehe 23/03/1978 Consumer

International, katika mkutano wake mkuu

uliofanyika Kyoto, Japan, uliongeza haki

nyingine tatu ambazo ni haki ya kupata

mahitaji muhimu, haki ya kulipwa fidia na

haki ya mazingira salama.

Tarehe 09/04/1985 Umoja wa Mataifa

uliridhia na kuzipitisha rasmi kama Haki

nane za kimataifa za Mtumiaji.

Page 15: Haki na Wajibu Wa Mtumiaji wa Huduma za Usafiri wa Anga.Ibara ya 44(1)(c) ya Rasimu ya Katiba Mpya inaweka wazi zaidi haki ya watu ... Kwa usafiri wa majini ndani ya Tanzania, sheria

Haki za Watumiaji katika sekta

ya usafirishaji Haki ya kupata mahitaji muhimu

Haki ya Usalama

Haki ya kupewa taarifa

Haki ya kuchagua

Haki ya kusikilizwa

Haki ya kulipwa fidia

Haki ya kuelimishwa

Haki ya mazingira salama

Page 16: Haki na Wajibu Wa Mtumiaji wa Huduma za Usafiri wa Anga.Ibara ya 44(1)(c) ya Rasimu ya Katiba Mpya inaweka wazi zaidi haki ya watu ... Kwa usafiri wa majini ndani ya Tanzania, sheria

Haki ya kupata mahitaji muhimu

Mwananchi yeyote kwa ujumla anayo haki ya

kupata mahitaji muhimu katika maisha ya

kila siku.

Miundombinu ya usafiri na uchukuzi ni moja

ya mahitaji muhimu kwa watumiaji katika

sekta hiyo. Bara bara nzuri, vyombo vya

uchukuzi vilivyo bora, viwanja vya ndege,

njia za reli, bandari, vivuko vya majini, meli

nk ni mfano wa mahitaji muhimu.

Page 17: Haki na Wajibu Wa Mtumiaji wa Huduma za Usafiri wa Anga.Ibara ya 44(1)(c) ya Rasimu ya Katiba Mpya inaweka wazi zaidi haki ya watu ... Kwa usafiri wa majini ndani ya Tanzania, sheria

Haki ya kupata mahitaji muhimu

Ibara ya 11 ya Katiba ya nchi yetu ya 1977

pamoja na mambo mengine inasisitiza juu ya

hali bora na maendeleo kwa wananchi.

Sheria mbali mbali zimetungwa ili kukidhi

haja ya ibara hii.

Mifano ya sheria hizi katika sekta ya

usafirishaji ni ile inayoanzisha Tanroads,

Mamlaka ya Bandari (TPA) na Mamlaka ya

viwanja vya ndege (TAA) na RAHCO.

Page 18: Haki na Wajibu Wa Mtumiaji wa Huduma za Usafiri wa Anga.Ibara ya 44(1)(c) ya Rasimu ya Katiba Mpya inaweka wazi zaidi haki ya watu ... Kwa usafiri wa majini ndani ya Tanzania, sheria

Haki ya Watu wenye ulemavu

kupata Usafiri Watu wenye ulemavu wanalindwa na Sheria ya Watu

wenye ulemavu ya Mwaka 2010 na Kanuni za SUMATRA.

Kifungu cha 50(b) inatamka bayana kuwa ni kosa la jinai kumkatalia mtu kupata usafiri kwa kisingizio cha ulemavu wake.

Kanuni za SUMATRA za (usalama na viwango vya ubora wa huduma) kwa magari ya abiria, 2008 kupitia kanuni 5 (1) (g) inatamka bayana kwamba kila gari la abiri mjini liwe na sehemu yenye upana wa sentimita 90 x 140 kwa ajili ya “wheel chair”

Page 19: Haki na Wajibu Wa Mtumiaji wa Huduma za Usafiri wa Anga.Ibara ya 44(1)(c) ya Rasimu ya Katiba Mpya inaweka wazi zaidi haki ya watu ... Kwa usafiri wa majini ndani ya Tanzania, sheria

Haki ya Watu wenye ulemavu

kupata Usafiri

Kanuni ya 5(1)(h) inamtaka kila mtoa

huduma kuweka vifaa vya kumsaidia

mtu mwenye ulemavu.

Ibara ya 44(1)(c) ya Rasimu ya Katiba

Mpya inaweka wazi zaidi haki ya watu

wenye ulemavu kupata usafiri.

Page 20: Haki na Wajibu Wa Mtumiaji wa Huduma za Usafiri wa Anga.Ibara ya 44(1)(c) ya Rasimu ya Katiba Mpya inaweka wazi zaidi haki ya watu ... Kwa usafiri wa majini ndani ya Tanzania, sheria

Haki ya Watu wenye ulemavu

kupata Usafiri

Ibara ya 44(1)(c) ya Rasimu ya Katiba

inasomeka hivi:-

Mtu mwenye ulemavu anastahiki

kuwekewa miundombinu na mazingira

yatakayowezesha kwenda anapotaka,

kutumia vyombo vya usafiri na kupata

habari

Page 21: Haki na Wajibu Wa Mtumiaji wa Huduma za Usafiri wa Anga.Ibara ya 44(1)(c) ya Rasimu ya Katiba Mpya inaweka wazi zaidi haki ya watu ... Kwa usafiri wa majini ndani ya Tanzania, sheria
Page 22: Haki na Wajibu Wa Mtumiaji wa Huduma za Usafiri wa Anga.Ibara ya 44(1)(c) ya Rasimu ya Katiba Mpya inaweka wazi zaidi haki ya watu ... Kwa usafiri wa majini ndani ya Tanzania, sheria
Page 23: Haki na Wajibu Wa Mtumiaji wa Huduma za Usafiri wa Anga.Ibara ya 44(1)(c) ya Rasimu ya Katiba Mpya inaweka wazi zaidi haki ya watu ... Kwa usafiri wa majini ndani ya Tanzania, sheria

Haki ya Usalama

Mtumiaji wa bidhaa na huduma anayo haki ya kupata bidhaa au huduma iliyo salama isiyokuwa hatarishi kwa maisha yake.

Ibara ya 14 ya katiba inamhakikishia kila raia haki ya kuishi. Sheria mbali mbali zimetungwa ili kukidhi haja ya ibara hii. Mifano ya sheria hizi katika sekta ya usafirishaji ni :

Sheria ya SUMATRA, 2001

Sheria ya leseni za usafirishaji Cap 317

Sheria ya Reli, 2002

Sheria ya meli za biashara, 2003

Sheria ya Usafiri wa anga Cap 80

Sheria ya ushindani, 2003

Factory ordinance cap 297

Page 24: Haki na Wajibu Wa Mtumiaji wa Huduma za Usafiri wa Anga.Ibara ya 44(1)(c) ya Rasimu ya Katiba Mpya inaweka wazi zaidi haki ya watu ... Kwa usafiri wa majini ndani ya Tanzania, sheria

Haki ya usalama

Kwa mfano Kanuni za SUMATRA za (usalama na viwango vya ubora wa huduma) kwa magari ya abiria, 2008 kupitia kanuni 5 (1) (a) inatamka kuwa ujenzi wa bodi ya basi ni lazima uendane na viwango maalumu vilivyowekwa na TBS (TZS 598:1999).

Page 25: Haki na Wajibu Wa Mtumiaji wa Huduma za Usafiri wa Anga.Ibara ya 44(1)(c) ya Rasimu ya Katiba Mpya inaweka wazi zaidi haki ya watu ... Kwa usafiri wa majini ndani ya Tanzania, sheria

Haki ya usalama

Kanuni 5 (1) b inatamka kuwa ubora au

uimara wa basi ni lazima uwe umekidhi

viwango vya TBS (TZS 608:2003)

Kanuni 5 (1) c inatamka matairi ni lazima

yakidhi matakwa ya TBS (TZS 617:1999)

Kanuni 5 (2) inataka vitu vifuatavyo visiwe na

nyufa

Chasis frame, leaf spring, axles na rim za

matairi

Page 26: Haki na Wajibu Wa Mtumiaji wa Huduma za Usafiri wa Anga.Ibara ya 44(1)(c) ya Rasimu ya Katiba Mpya inaweka wazi zaidi haki ya watu ... Kwa usafiri wa majini ndani ya Tanzania, sheria

Haki ya usalama

Kanuni 6 (1) inataka “modifikesheni” ya gari isifanywe ispokuwa kwa kufuata maelekezo ya mtengenezaji.

Mwenye gari anayetaka kufanya modifikesheni nje ya maelekezo ya mtengenezaji ni lazima apate kibali kutoka TBS (Kanuni 6 (2))

Sehemu ya IV ya sheria ya Reli kwa ujumla wake inazungumzia usalama.

Kanuni ya 5 (1) ya Kanuni za usalama wa reli, 2006 inawataka watoa huduma kuandaa mpango wa usalama (safety plan) kama sharti la kupewa leseni.

Page 27: Haki na Wajibu Wa Mtumiaji wa Huduma za Usafiri wa Anga.Ibara ya 44(1)(c) ya Rasimu ya Katiba Mpya inaweka wazi zaidi haki ya watu ... Kwa usafiri wa majini ndani ya Tanzania, sheria

Haki ya kupewa taarifa Mtumiaji wa huduma na bidhaa anayo haki ya

kupewa taarifa muhimu zinazo husu bidhaa au huduma inayotarajiwa kuuzwa kwake.

Ibara ya 18 ya katiba inazungumzia juu ya haki ya kupata taarifa na uhuru wa kujieleza. Sheria mbali mbali zimetungwa zinazokidhi haja ya ibara hii. Katika sekta ya usafirishaji kuna Kanuni za SUMATRA za (usalama na viwango vya ubora wa huduma) kwa magari ya abiria, 2008, sheria ya meli za biashara ya 2003, sheria ya reli ya 2002, sheria ya usafiri wa anga cap 80, Sheria ya ushindani, 2003 nk.

Page 28: Haki na Wajibu Wa Mtumiaji wa Huduma za Usafiri wa Anga.Ibara ya 44(1)(c) ya Rasimu ya Katiba Mpya inaweka wazi zaidi haki ya watu ... Kwa usafiri wa majini ndani ya Tanzania, sheria

Tiketi ya abiria

Kanuni ya 14 (2) ya Kanuni za SUMATRA za

(usalama na viwango vya ubora wa huduma)

kwa magari ya abiria, 2008, imeweka mambo

yafuatayo juu ya tiketi ya abiria:

Jina la abiria na namba ya seat

Muda wa kuripoti na kuondoka

Mahali chombo kinapoondoka na mwisho wa safari

Nauli ya safari

Anuani, namba za simu za mtoa huduma

Namba ya chombo

Jina la njia

Page 29: Haki na Wajibu Wa Mtumiaji wa Huduma za Usafiri wa Anga.Ibara ya 44(1)(c) ya Rasimu ya Katiba Mpya inaweka wazi zaidi haki ya watu ... Kwa usafiri wa majini ndani ya Tanzania, sheria

Haki ya kuchagua

Mtumiaji wa huduma na bidhaa anayo haki ya kuchagua bidhaa au huduma aitakayo kulingana na viwango vinavyoweza kukidhi mahitaji yake. Mzalishaji haruhusiwi kumlaghai mtumiaji ili achague bidhaa au huduma inayokusudiwa kutolewa.

Sheria ya ushindani ya mwaka 2003, sheria ya SUMATRA 2003, TCAA 2003 nk zimemhakikishia mtumiaji juu ya haki hii.

Page 30: Haki na Wajibu Wa Mtumiaji wa Huduma za Usafiri wa Anga.Ibara ya 44(1)(c) ya Rasimu ya Katiba Mpya inaweka wazi zaidi haki ya watu ... Kwa usafiri wa majini ndani ya Tanzania, sheria

Haki ya kuchagua

Kifungu cha 15 (1) cha Sheria ya Ushindani,

2003 kinakataza kabisa tabia zozote zile za

ufanyaji biashara ambazo zinamuelekeo wa

kudangaya au kupotosha.

Kifungu 16 (a) mpaka (k) cha Sheria hiyo hiyo

kinakataza kabisa tabia au vitendo vyovyote vile

ambavyo vinaweza kumfanya mtumiaji achague

bidhaa au huduma kutokana na hila au

udanganyifu. Ubora wa bidhaa/huduma ndio

kigezo cha kuchagua.

Page 31: Haki na Wajibu Wa Mtumiaji wa Huduma za Usafiri wa Anga.Ibara ya 44(1)(c) ya Rasimu ya Katiba Mpya inaweka wazi zaidi haki ya watu ... Kwa usafiri wa majini ndani ya Tanzania, sheria

Haki ya kusikilizwa(Kuwakilishwa)

Mtumiaji wa huduma na bidhaa anayo haki ya kusikilizwa katika masuala yote yanayogusa maslahi yake katika soko kupitia njia ya uwakilishi.

Sheria zinazoanzisha mabaraza ya watumiaji za mamlaka za udhibiti zinakidhi haja ya haki hii.

Kazi kuu ya mabaraza haya ni kuwasilisha maoni ya watumiaji kwa Serikali na mamlaka za udhibiti.

Page 32: Haki na Wajibu Wa Mtumiaji wa Huduma za Usafiri wa Anga.Ibara ya 44(1)(c) ya Rasimu ya Katiba Mpya inaweka wazi zaidi haki ya watu ... Kwa usafiri wa majini ndani ya Tanzania, sheria

Haki ya kulipwa fidia

Mtumiaji wa huduma na bidhaa anayo haki ya kulipwa fidia kutokana na madhara atakayoyapata yanayotokana na huduma au bidhaa aliyoitumia.

Sheria ya leseni za usafirishaji (Transport Licensing Act cap 317) imeweka sharti la kila muombaji wa leseni hiyo kuwa na bima ambayo itawawezesha kuwalipa fidia abiria wao zinapotokea ajali. Sheria nyingine ni kama Sheria ya meli za biashara (merchant shipping Act, 2003), Sheria ya Reli 2002 na Sheria ya uchukuzi wa anga 2006.

Page 33: Haki na Wajibu Wa Mtumiaji wa Huduma za Usafiri wa Anga.Ibara ya 44(1)(c) ya Rasimu ya Katiba Mpya inaweka wazi zaidi haki ya watu ... Kwa usafiri wa majini ndani ya Tanzania, sheria

Haki ya kulipwa fidia

Sheria za kimataifa ni kama Sheria ya Athens

ya usafirishaji wa abiria na mizigo yao kwa njia

ya majini ya 1974(Athens Convention relating

to the carriage of Passengers and their

Luggage by Sea), Sheria ya Montreal ya

usafirishaji wa anga ya 1999.

Page 34: Haki na Wajibu Wa Mtumiaji wa Huduma za Usafiri wa Anga.Ibara ya 44(1)(c) ya Rasimu ya Katiba Mpya inaweka wazi zaidi haki ya watu ... Kwa usafiri wa majini ndani ya Tanzania, sheria

Haki ya kulipwa fidia

Kulingana na Sheria za kimataifa na safari za kimataifa Mtoa huduma anawajibika kuwalipa fidia abiria wanapopata madhara yafuatayo:

Kuchelewa kuanza safari, Kuchelewa kwa mizigo au shehena, kuharibika kwa mizigo au shehena, kuumia au kupoteza maisha kunakotokana na ajali.

Page 35: Haki na Wajibu Wa Mtumiaji wa Huduma za Usafiri wa Anga.Ibara ya 44(1)(c) ya Rasimu ya Katiba Mpya inaweka wazi zaidi haki ya watu ... Kwa usafiri wa majini ndani ya Tanzania, sheria

Haki ya kulipwa fidia

Kulingana na sheria ya Athens fidia kwa majeruhi

na vifo safari za majini ni kiwango kisichozidi

700,000 francs kwa kila abiria, mizigo ya ndani ni

kiwango kisichozidi 12,500 francs kwa kila abiria.

Fidia kwa uchelewaji wa safari za ndege ni

kiwango kisichozidi dola za kimarekani 5000 kwa

kila abiria, madhara kwa mizigo ni kiwango

kisichozidi dola za kimarekani 1200 kwa kila

abiria, na majeraha au vifo vya ajali ni kiwango

kisichozidi dola za kimarekani 120,000 kwa kila

abiria

Page 36: Haki na Wajibu Wa Mtumiaji wa Huduma za Usafiri wa Anga.Ibara ya 44(1)(c) ya Rasimu ya Katiba Mpya inaweka wazi zaidi haki ya watu ... Kwa usafiri wa majini ndani ya Tanzania, sheria

Haki ya Kulipwa fidia

Kwa usafiri wa majini ndani ya Tanzania,

sheria ya meli za biashara, 2003, imeweka

kiwango cha hesabu cha 333,000 kwa meli

zisizozidi tani 500. tani 501 mpaka 3000

kiwango cha hesabu 500. Tani 3001 mpaka

30,000 kiwango cha hesabu 333.Tani 30,001

mpaka 70,000 kiwango cha hesabu 250. Meli

zinazozidi tani 70,000 ni kiwango cha hesabu

167.

Page 37: Haki na Wajibu Wa Mtumiaji wa Huduma za Usafiri wa Anga.Ibara ya 44(1)(c) ya Rasimu ya Katiba Mpya inaweka wazi zaidi haki ya watu ... Kwa usafiri wa majini ndani ya Tanzania, sheria

Haki ya kulipwa Fidia

Kurudishiwa nauli pindi safari iliyopangwa inapovunjika.

Kanuni ya 11 (1) a ya Kanuni za SUMATRA za (usalama na viwango vya ubora wa huduma) kwa magari ya abiria, 2008, inasema kuwa endapo Basi litaharibika kwa safari za mijini, mtoa huduma anatakiwa atoe usafiri mbadala ndani ya dakika 15 au arudishe nauli kwa abiria inayofanana na nauli ya sehemu iliyobakia ya safari.

Page 38: Haki na Wajibu Wa Mtumiaji wa Huduma za Usafiri wa Anga.Ibara ya 44(1)(c) ya Rasimu ya Katiba Mpya inaweka wazi zaidi haki ya watu ... Kwa usafiri wa majini ndani ya Tanzania, sheria

Haki ya kulipwa Fidia

Kanuni ya 11 (1) b ya kanuni hizo hizo, Kwa

safari za kutoka mkoa hadi mkoa, basi

likiharibika njiani litengenezwe ndani ya

masaa mawili au mtoa huduma atoe usafiri

mbadala ndani ya masaa hayo.

Abiria akiamua arudishiwe nauli, basi mtoa

huduma atarudisha nauli kwa abiria ya

sehemu iliyobaki ya safari yake ndani ya siku

saba. Kanuni ya 11 (2) a

Page 39: Haki na Wajibu Wa Mtumiaji wa Huduma za Usafiri wa Anga.Ibara ya 44(1)(c) ya Rasimu ya Katiba Mpya inaweka wazi zaidi haki ya watu ... Kwa usafiri wa majini ndani ya Tanzania, sheria

Haki ya kuelimishwa

Mtumiaji wa huduma na bidhaa anayo haki ya

kupewa elimu juu ya huduma au bidhaa anayo

tarajiwa kuitumia.

Hii ni haki ya Elimu kwa ujumla wake. Kazi ya

kuwaelimisha watumiaji wa huduma za usafiri

inafanywa na mabaraza ya watumiaji ya

Mamlaka za Udhibiti. SUMATRA CCC, TCAA

CCC, SUMATRA na TCAA.

Page 40: Haki na Wajibu Wa Mtumiaji wa Huduma za Usafiri wa Anga.Ibara ya 44(1)(c) ya Rasimu ya Katiba Mpya inaweka wazi zaidi haki ya watu ... Kwa usafiri wa majini ndani ya Tanzania, sheria

Haki ya mazingira salama

Mtumiaji ana haki ya kusafiri na kutumia huduma au bidhaa za usafiri katika mazingira yaliyo salama.

Sheria mbali mbali zimemhakikishia mtumiaji juu ya haki hii. Sheria hizo ni kama Sheria ya Mazingira ya mwaka 2004, Sheria ya leseni za usafirishaji cap 317, Kanuni za SUMATRA za (usalama na viwango vya ubora wa huduma) kwa magari ya abiria, 2008, sheria ya mamlaka ya usafiri wa anga cap 80, Kanuni ya 18 juu ya mazingira katika usafirishaji wa anga nk

Page 41: Haki na Wajibu Wa Mtumiaji wa Huduma za Usafiri wa Anga.Ibara ya 44(1)(c) ya Rasimu ya Katiba Mpya inaweka wazi zaidi haki ya watu ... Kwa usafiri wa majini ndani ya Tanzania, sheria

Haki ya mazingira salama

Kwa mfano Kanuni za SUMATRA za

(usalama na viwango vya ubora wa

huduma) kwa magari ya abiria, 2008,

watoa huduma wanatakiwa kuhakikisha

kuwa kuna huduma ya vyoo vilivyo safi

katika vituo vya kungojelea abiria (Kanuni

18 (1) a. Kanuni 18 (2) inawataka watoa

huduma kuwa na huduma hiyo katika

vituo vyote vya njiani.

Page 42: Haki na Wajibu Wa Mtumiaji wa Huduma za Usafiri wa Anga.Ibara ya 44(1)(c) ya Rasimu ya Katiba Mpya inaweka wazi zaidi haki ya watu ... Kwa usafiri wa majini ndani ya Tanzania, sheria

Wajibu wa Mtumiaji

Wajibu wa kudai mahitaji muhimu

Wajibu wa kusoma na kufuata maelekezo ya

usalama

Wajibu wa kutafuta taarifa muhimu

Wajibu wa kuchagua na kufanya maamuzi sahihi

Wajibu wa kuwasilisha maoni na kero

Wajibu wa kudai fidia

Wajibu wa kujielimisha

Wajibu wa kutetea mazingira salama na

kuyatunza

Page 43: Haki na Wajibu Wa Mtumiaji wa Huduma za Usafiri wa Anga.Ibara ya 44(1)(c) ya Rasimu ya Katiba Mpya inaweka wazi zaidi haki ya watu ... Kwa usafiri wa majini ndani ya Tanzania, sheria

Hitimisho

Katika uchumi wa soko, watumiaji wanaulazima mkubwa sana wa kujua haki zao na masuala mengine yanayo husu soko. Serikali iliamua kuunda mabaraza ya watumiaji katika sekta mbali mbali ili kukidhi haja hiyo. Watumiaji wanapaswa kuyatumia mabaraza haya ili kupata ufahamu wa haki zao na uwezo wa kusimama imara katika soko.

Mabaraza kupitia kamati zake za mikoa na kanda yana wajubu mkubwa wa kuwafikishia elimu hiyo watumiaji wote waishio vijijini, wilayani na mijini ili kumkomboa mtumiaji.

Page 44: Haki na Wajibu Wa Mtumiaji wa Huduma za Usafiri wa Anga.Ibara ya 44(1)(c) ya Rasimu ya Katiba Mpya inaweka wazi zaidi haki ya watu ... Kwa usafiri wa majini ndani ya Tanzania, sheria

Asanteni sana

Timiza wajibu wako,

utapata haki yako.