74
Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga 1 TANGAZO LA SERIKALI Na. 48 la tarehe 24/02/2017 SHERIA YA SERIKALI ZA MITAA (MAMLAKA ZA MIJI) (SURA YA 288) ______ KANUNI ZA KUDUMU ______ Zimetungwa chini ya kifungu cha 42 (1) ______ KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA MAFINGA ZA MWAKA 2017 YALIYOMO SEHEMU YA I MASHARTI YA MWANZO 1. Jina na tarehe ya kuanza kutumika 2. Tafsiri ya maneno yaliyotumika SEHEMU YA II MIKUTANO YA HALMASHAURI 3. Mikutano ya Kawaida ya Halmashauri 4. Utaratibu wa Uchaguzi 5. Mkutano Maalum wa Halmashauri 6. Mkutano wa Bajeti 7. Mkutano wa Mwaka 8. Taarifa za Mikutano 9. Akidi katika mikutano ya Halmashauri.

KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

  • Upload
    others

  • View
    31

  • Download
    0

Embed Size (px)

Citation preview

Page 1: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

1

TANGAZO LA SERIKALI Na. 48 la tarehe 24/02/2017

SHERIA YA SERIKALI ZA MITAA (MAMLAKA ZA MIJI)(SURA YA 288)

______

KANUNI ZA KUDUMU______

Zimetungwa chini ya kifungu cha 42 (1)______

KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA MAFINGA

ZA MWAKA 2017

YALIYOMO

SEHEMU YA IMASHARTI YA MWANZO

1. Jina na tarehe ya kuanza kutumika2. Tafsiri ya maneno yaliyotumika

SEHEMU YA IIMIKUTANO YA HALMASHAURI

3. Mikutano ya Kawaida ya Halmashauri4. Utaratibu wa Uchaguzi5. Mkutano Maalum wa Halmashauri6. Mkutano wa Bajeti7. Mkutano wa Mwaka8. Taarifa za Mikutano9. Akidi katika mikutano ya Halmashauri.

Page 2: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

2

SEHEMU YA IIITARATIBU ZA MIKUTANO

10. Uchaguzi wa Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri11. Uongozaji wa Mikutano ya Halmashauri12. Kumbukumbu ya mahudhurio13. Kuruhusu watu na Vyombo vya Habari kwenye Mikutano ya

Halmashauri14. Utaratibu wa shughuli za Mikutano15. Kuthibitisha muhtasari16. Hoja za Mwenyekiti17. Taratibu za Majadiliano18. Fujo zinazosababishwa na Wajumbe.19. Fujo zinazosababishwa na Umma20. Hoja za Marekebisho ya Hoja21. Hoja zinazoweza kutolewa bila taarifa.22. Haki ya kujibu23. Maswali24. Maswali ya papo kwa papo25. Taarifa za Kamati26. Taarifa kutoka kwenye Kata27. Uhuru wa Kutoa mawazo wakati wa majadiliano28. Kauli zenye kashfa29. Maamuzi ya Mikutano ya Halmashauri30. Mwaliko kwa wasiokuwa Wajumbe kushiriki na kuzungumza

kwenye vikao vya Halmashauri31. Mihtasari ya Kata na ya Vijiji/Mitaa32. Mihutasari kupelekwa kwa Mkuu wa Wilaya na Mkuu wa

Mkoa33. Hoja kuhusu matumizi34. Kupokelewa kwa taarifa ya Kamati35. Kuidhinishwa kwa taarifa ya Kamati36. Uhalali wa majadiliano ya Halmashauri37. Uwezo wa Halmashauri kujigeuza kuwa Kamati ya Halmashauri nzima.38. Hoja zinazohusu watumishi wa Halmashauri39. Kushiriki kwa Umma40. Uahirishaji wa Vikao

Page 3: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

3

SEHEMU YA IVKAMATI

41. Kamati za Kudumu42. Mwenyekiti kuwa Mjumbe wa Kamati zote.43. Uwezo wa Kamati44. Kamati za Pamoja45. Kukasimu madaraka kwenye Kamati46. Kamati Ndogo47. Mikutano ya Kamati48. Mwenyekiti wa Kamati49. Mkutano maalum wa Kamati50. Ajenda za Kamati51. Mahudhurio katika Mikutano ya Kamati52. Mtoa hoja kualikwa kwenye Mkutano wa Kamati53. Waalikwa wasiokuwa Wajumbe kuhudhuria na kushiriki katika

Mikutano ya Kamati54. Mahudhurio ya Umma na Vyombo vya Habari kwenye Mikutano ya

Kamati na Kamati Ndogo55. Athari za nafasi wazi kwenye Kamati56. Akidi kwenye Mikutano ya Kamati57. Kanuni za kudumu kutumika katika Mikutano ya Kamati58. Upigaji kura kwenye Mikutano ya Kamati59. Muhtasari wa Kamati60. Kufikiriwa upya maamuzi61. Kutunza siri za majadiliano ya Kamati na Kamati Ndogo62. Kujiuzulu wadhifa wa Mwenyekiti wa Kamati63. Kujiuzulu ujumbe wa Kamati na kujazwa kwa nafasi iliyoachwa wazi.

SEHEMU YA VUNUNUZI WA VIFAA, UPATIKANAJI WA HUDUMA NA UJENZI

64. Taratibu za uagizaji65. Kumbukumbu za majadiliano yanayohusu uagizaji66. Uzuiaji wa rushwa67. Usimamizi wa Mikataba68. Uvunjaji wa Mkataba69. Rejesta ya Mikataba70. Diwani au Afisa kutokuwa na maslahi kwenye Mikataba

Page 4: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

4

SEHEMU YA VIMASUALA MENGINE

71. Kiapo cha kukubali wadhifa72. Majukumu ya Diwani73. Nafasi wazi74. Kutokuwepo kwa Wajumbe75. Taratibu za kutunga Sheria Ndogo76. Ukaguzi wa nyaraka77. Uanzishaji wa Bodi ya Huduma78. Diwani kutembelea maeneo, shughuli mbalimbali za ujenzi79. Uhifadhi wa lakiri ya Halmashauri80. Utiaji muhuri kwenye nyaraka81. Uandikishaji wa anwani82. Uteuzi wa Wajumbe kwenye Taasisi za nje83. Kumwondoa Mwenyekiti madarakani

SEHEMU YA VIIPOSHO KWA WAJUMBE

84. Aina za posho85. Posho endapo Mkutano utaahirishwa

SEHEMU YA VIIIMABADILIKO KWENYE KANUNI ZA KUDUMU

86. Kusitisha utumiaji wa Kanuni za kudumu87. Marekebisho na mabadiliko ya Kanuni za Kudumu88. Kanuni za Kudumu kutolewa kwa Wajumbe89. Kutafsiri Kanuni za kudumu90. Ziara za Wajumbe91. Wimbo wa Taifa,Dua na sala ya kuiombea Halmashauri92. Kufuta Kanuni zilizopo

Page 5: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

5

SEHEMU YA IMASHARTI YA MWANZO.

KWA KUWA kauli-mbiu ya Halmashauri ni kuendesha shughulikwa namna inayozingatia demokrasia, ufanisi, tija,ushirikishwaji, uwazi na uwajibikaji;

NA KWA KUWA jukumu la Halmashauri ni kuimarishademokrasia katika ngazi zote na kutoa huduma kwa wananchikwa kuzingatia ufanisi, usawa, haki na kwa namna inayochocheamaendeleo ya maeneo yaliyo chini ya mamlaka ya Halmashaurikwa kuwashirikisha wananchi;

NA KWA KUWA madhumuni ya Kanuni hizi za kudumu nikuweka utaratibu wa namna Halmashauri itakavyoendeshaMikutano na shughuli zake kwa kuzingatia misingi ya utawalabora;

SASA BASI, Kanuni hizi za kudumu zinaelekeza ifuatavyo;

Jina na tareheyaKuanzakutumika

1. Kanuni hizi zitaitwa Kanuni za Kudumu za Halmashauri yaMji wa Mafinga za Mwaka 2017 na zitaanza kutumikamara baada ya kutangazwa kwenye Gazeti la Serikali;Katika Kanuni hizi, isipokuwa kama maelezo hayayatahitajika vinginevyo;

“Afisa wa Serikali za Mitaa” maana yake ni mtu ambayeameajiriwa na au ambaye yumo katika Utumishi waMamlaka ya Serikali za Mitaa na ambaye anashikaau anakaimu katika nafasi ya menejimenti;

“Akidi” ni idadi ya Madiwani itakayokamilika baada yakujiorodhesha katika rejesta ya Mahudhurio yaMkutano ambayo itaruhusu kufanya maamuzi yaMkutano kwa mujibu wa Kanuni za 9, 49 na 56;

“Chama” ni chama cha siasa chenye uwakilishi katikaBaraza la Madiwani;

Tafsiri 2.

Page 6: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

6

“Diwani” maana yake ni Mjumbe wa Halmashaurialiyetajwa kwa mujibu wa kifungu 24…… chaSheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Miji) Suraya 288;

“Fujo” maana yake ni kitendo chochote kinachowezakufanywa na Mjumbe au Mshiriki wa Vikao vyaHalmashauri au Kamati ya Kudumu ambacho nikinyume na taratibu za uendeshaji wa vikao,kinachoweza kuvuruga kikao. Mfano kuongea bilaruhusa ya Mwenyekiti, kutoa lugha isiyofaa, kutoakauli yenye maudhi, kuingia kwenye kikao akiwaumelewa, kuingia na silaha na kutoa lugha ya kashfa,kukaidi amri ya Mwenyekiti, kukaidi kutoka nje paleanapoamriwa kutoka kutokana na fujoalizosababisha;

“Halmashauri” maana yake ni Halmashauri ya Mji waMafinga;

“Kamati”(a) Inapotumika kuhusiana na Halmashauri ya Mji ina

maana ya Kamati iliyoanzishwa au iliyoteuliwa naHalmashauri ya Mji chini ya Sheria;

(b) Inapotumika kuhusiana na Kamati ya Maendeleoya Kata ina maana ya Kamati hiyo;

(c) Inapotumika kuhusiana na Kamati Ndogo maanayake ni Kamati Ndogo hiyo iliyoteuliwa na Kamati;

(d) Inapotumika kuhusiana na Kamati nyingine inamaana ya Kamati hiyo;

(e) Kwa maana ya Bodi ya Zabuni ni Katibu wa Bodiya Zabuni.

“Kura ya siri” Maana yake ni Kura itakayopigwa katikaeneo la faragha lililotengwa kwa madhumuni yakupiga kura, eneo ambalo halitapungua umbali wamita tano (5) kutoka kwa Msimamizi wa kura;

“Mkurugenzi” maana yake ni Mkurugenzi wa Halmashauriya Mji wa Mafinga na ni pamoja na Afisa yeyote

Page 7: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

7

aliyeteuliwa kutekeleza majukumu ya Mkurugenzi;

“Mjumbe” maana yake ni Mjumbe wa Halmashauri kamailivyoainishwa na kifungu cha 24(1) cha Sheria;

“Mwenyekiti”Kwa madhumuni ya Halmashauri maana yake niMwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Mafinga,na inajumuisha Makamu Mwenyekiti wakatianapotekeleza majukumu ya Mwenyekiti kwamujibu wa kanuni hizi.

“Sheria” maana yake ni Sheria ya Serikali za Mitaa(Mamlaka za Miji) Sura ya 288;

“Waziri” maana yake ni Waziri mwenye dhamana yaSerikali za Mitaa;

SEHEMU YA IIMIKUTANO YA HALMASHAURI

Mikutano yaKawaida yaHalmashauri

3. (1) Mikutano ya Kawaida ya Halmashauri itafanyikamara moja kila baada ya miezi mitatu, naitafanyika mahali, tarehe na katika muda kamautakavyokua umepangwa katika kalenda yaMikutano ya Halmashauri.

Mkutano waKwanza waHalmashauri.

(2) (a) Mkutano wa kwanza wa kawaida waHalmashauri utafanyika baada ya Tume yaUchaguzi kutangaza matokeo ya uchaguzi waMadiwani wa Kata na uteuzi wa Madiwaniwa Viti maalumu, na utafanyika mahali, sikuna katika muda utakaopangwa naMkurugenzi, ilimradi Mkurugenzi atapaswakuitisha Mkutano huo ndani ya siku thelathinikuanzia tarehe ya matokeo ya uchaguzi waMadiwani wa Kata na Uteuzi wa MadiwaniViti Maalum yanapotangazwa na Tume yaUchaguzi ambapo moja ya ajenda za Mkutanohuo ni kumchagua Mwenyekiti, Makamu

Page 8: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

8

Mwenyekiti na Wajumbe wa Kamati zaKudumu za Halmashauri.

(b) Katika Mkutano huo Mkurugenzi waHalmashauri atawasilisha Taarifa yakumbukumbu ya maamuzi ya utekelezaji washughuli za Halmashauri zilizofanyika katikakipindi ambacho Baraza la madiwanililivunjwa. Wajumbe wa baraza watapokea nakujadili bila kubatilisha maamuziyaliyokwishaamuliwa ili kujiridhisha uhalali.

Utaratibu wauchaguzi

4. Uchaguzi wa Mwenyekiti na Makamu Mwenyekitiutafanyika kwa kupiga Kura za siri na upigaji wakura utafanyikia sehemu ya faragha umbaliusiopungua mita (5) kutoka kwa Msimamizi waUchaguzi na mpiga kura atachukua karatasi yakupiga kura kutoka kwa Msimamizi wa Uchaguzi.

Mkutanomaalum waHalmashauri

5. (1) Mkutano Maalum wa Halmashauri unawezakuitishwa na Mwenyekiti ndani ya siku ishirini namoja baada ya kupokea maombi ya maandishiyaliyosainiwa na si pungufu ya theluthi moja yaWajumbe wote kutaka Mkutano huo ufanyike namaombi hayo yaeleze wazi madhumuni yakuitishwa kwa Mkutano Maalum huo.

(2) Endapo ajenda ya Mkutano huo itahusukumuondoa madarakani Mwenyekiti, Mkutano huoutaitishwa na Mkurugenzi baada ya kupokeamaombi yaliyosainiwa na Wajumbe waHalmashauri wasiopungua theluthi mbili yaWajumbe wote.

(3) Baada ya Mkurugenzi kupokea maombi kutakakufanyika kwa Mkutano wa kujadili ajenda ya

Page 9: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

9

kumuondoa madarakani Mwenyekiti, Mkurugenziatamtaarifu Mwenyekiti tuhuma na sababu zakutaka kuondolewa Uenyekiti na kumtaka aandaemajibu ya tuhuma ndani ya siku tano (5) baada yakupokea tuhuma hizo.

(4) Mkurugenzi katika muda wa siku Tatu (3) baada yakupokea maelezo ya utetezi kutoka kwaMwenyekiti, atawasilisha kwa Mkuu wa Mkoatuhuma pamoja na maelezo ya utetezi.

(5) Mkuu wa Mkoa baada ya kupokea taarifa yaMkurugenzi ndani ya muda wa siku tano (5)ataunda Timu ya Uchunguzi ambayo itakuwa nawajumbe wasiopungua watatu(3) na wasiozidiwatano(5).

(6) Timu ya Uchunguzi itatakiwa kukamilishaUchunguzi katika muda wa siku kumi na nne (14)na kuwasilisha taarifa hiyo kwa Mkuu wa Mkoa.

(7) Baada ya Mkuu wa Mkoa kupata taarifa ya Timuya Uchunguzi atairudisha Taarifa hiyo kwaMkurugenzi ambaye naye katika muda wa sikukumi na Nne (14) ataiwasilisha kwenye Kikao chaBaraza kwa uamuzi wa tuhuma hizo.

Kif.cha 25(5)Sura 288

(8) Endapo Mwenyekiti hataridhika na uamuzi waBaraza, atakata rufaa kwa Waziri kuhusu tuutaratibu uliotumika kumuondoa madarakani nasiyo vinginevyo.

Utaratibu wakuwasilisharufaa

(9) Utaratibu utakaotumika kuwasilisha nakushughulikia rufaa iliyowasilishwa na Mwenyekitini ule ulioelezwa kwenye Taratibu za KumuondoaMadarakani Mwenyekiti wa Halmashauri.

(10) Iwapo Mwenyekiti anakataa kuitisha Mkutanomaalum wa Halmashauri baada ya kupokeamaombi ya kutakiwa kufanya hivyo, maombi

Page 10: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

10

yaliyosainiwa na Wajumbe wa Halmashauriwasiopungua theluthi moja ya Wajumbe wotewakionyesha sababu ya kuitisha Mkutano huomaalum na kuwasilishwa kwake, au iwapo bilakukataa, Mwenyekiti, ndani ya kipindi cha sikusaba ataendelea kutoitisha Mkutano huo maalumbaada ya kupokea ombi la kuitisha Mkutano huomaalum, basi theluthi mbili ya Wajumbe waliotiasaini na kuwasilisha kwa Mkurugenzi wanawezakuitisha Mkutano huo maalum mara moja.

(11) Taarifa ya Mkutano maalum itatolewa angalau saaishirini na nne kabla ya Mkutano.

(12) Hakuna shughuli nyingine yoyote itakayojadiliwakatika Mkutano maalum wa Halmashauriisipokuwa ile tu iliyoelezwa kwenye taarifa yakuitishwa kwa Mkutano huo.

Mkutano waBajeti

6. Kutakuwepo na Mkutano wa Halmashauri waBajeti utakaofanyika kwa muda wa siku mbilimfululizo na utafanyika miezi miwili kabla yamwaka wa fedha kumalizika na utajadili mamboyafuatayo:-

(a) Utekelezaji wa Mipango na Bajeti yamwaka uliopita.

(b) Mipango na Bajeti ya mwaka unaofuata.

Mkutano waMwaka

7. (1) (a) Mkutano wa Mwaka wa Halmashauriutafanyika tarehe, mahali na muda utakaopangwana Halmashauri katika kalenda ya Mikutano nautaitishwa na Mkurugenzi baada ya kuwasiliana naMwenyekiti wa Halmashauri.

(b)Mikutano yote ya Baraza itapangwa na Baraza laMadiwani kwa kuzingatia ratiba ya Vikao vyaBunge ili kuwezesha Wabunge kuhudhuriaMikutano ya Baraza la Madiwani.

(c )Endapo italazimika kuitishwa kwa Mkutano wa

Page 11: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

11

Baraza wakati wa Vikao vya Bunge, Mkurugenziatamjulisha au atawajulisha Wabunge husikakuhusu kikao hicho ili wahudhurie.

(2) Mkutano wa Kwanza wa Uchaguzi wa Mwenyekiti,Makamu Mwenyekiti na Wajumbe wa Kamatiutaongozwa na Katibu Tawala wa Wilaya naMkurugenzi wa Halmashauri atakuwa Katibu.

(3) Katika Mkutano wa kawaida wa mwaka,Halmashauri itajadili mambo yafuatayo:-

(a) Kumchagua Makamu Mwenyekiti,(b) Kuteua Wajumbe wa Kamati za Kudumu;(c) Kujadili taarifa ya utendaji na uwajibikaji

wa Halmashauri kwa mwaka uliopita.(d) Kupitisha ratiba ya vikao vya Halmashauri

na Kamati za Halmashauri.

Taarifa zaMkutano

8. (1) Mkurugenzi atatoa taarifa ya Mkutano kwamaandishi kwa kila Mjumbe katika mudausiopungua siku saba akieleza mahali, siku na saaya Mkutano unaokusudiwa na mamboyatakayojadiliwa katika Mkutano huo.

(2) Taarifa ya Mkutano itaambatana na nyaraka aukumbukumbu muhimu zitakazotumika katikaMkutano huo.

(3) Isipokuwa kwa idhini ya Mwenyekiti na au ya idadiya Wajumbe isiyopungua robo tatu ya Wajumbewaliohudhuria Mkutano, hakuna shughuli yoyoteitakayofanywa katika Mkutano wa Halmashaurimbali na shughuli zilizotajwa katika mwaliko waMkutano huo.

Akidi katikaMikutano yaHalmashauri

9. (1) Hakuna Mkutano wa kawaida wa Halmashauriutakaofanyika isipokuwa kama kutakuwepo idadiya Wajumbe isiyopungua nusu ya Wajumbe wotewaliohudhuria na kujiandikisha kwenye daftari lamahudhurio.

Page 12: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

12

(2) Akidi katika Mikutano maalum ya Halmashauriitakuwa ni theluthi mbili ya Wajumbe wote waHalmashauri na itahesabiwa wakati wa ufunguzi waMkutano.

(3) Akidi katika Mkutano wa kawaida wa mwaka naMkutano wa kwanza wa Halmashauri itakuwatheluthi mbili ya Wajumbe wote wa Halmashauri.

(4) Endapo Wajumbe waliohudhuria Mkutanohawatafikia akidi ya Mkutano, Mkurugenziatauahirisha Mkutano huo na kuitisha tena ndani yasiku saba (7) na endapo akidi haitatimia tena, idadiyoyote ya Wajumbe waliohudhuria itatengenezaakidi ya Mkutano na Mkurugenzi atamjulishaWaziri kuwepo kwa hali hiyo.

(3) Akidi katika Mikutano maalum ya Halmashauriitakuwa ni theluthi mbili ya Wajumbe wote waHalmashauri na itahesabiwa wakati wa ufunguzi waMkutano.

(4) Akidi katika Mkutano wa kawaida wa mwaka naMkutano wa kwanza wa Halmashauri itakuwatheluthi mbili ya Wajumbe wote wa Halmashauri.

SEHEMU YA IIITARATIBU ZA MIKUTANO

Uchaguzi waMwekiti naMakamuMwenyekitiwaHalmashauri

10. (1) Mwenyekiti na Makamu Mwenyekitiwatachaguliwa na Wajumbe, kutokana na Wajumbewa Halmashauri kwa kura ya siri itakayopigwa naMjumbe mmoja mmoja kwenye eneo la faraghalitakalotengwa umbali usiopungua mita 5 kutokamahali alipoketi Msimamizi wa Uchaguzi.

Page 13: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

13

(2) Mjumbe kabla ya kwenda sehemu ya faragha kwaajili ya kupiga kura, atapatiwa na Msimamizi waUchaguzi karatasi ya kupigia kura kutoka kwenyechombo maalum kitakachowekwa mbele yaMsimamizi wa Uchaguzi, na atakwenda moja kwamoja kupiga kura yake kwenye sehemu ya faragha.

(3) Mtu atatangazwa kuchaguliwa kuwa Mwenyekitiau Makamu Mwenyekiti iwapo atapata zaidi yanusu ya kura zilizopigwa.

(4) Iwapo wakati wa kumchagua Mwenyekiti auMakamu Mwenyekiti jina moja tulimependekezwa, Wajumbe watapiga kura za siri za“ndiyo” au “hapana”na endapo kura za “ndiyo”zitazidi asilimia hamsini ya kura zote zilizopigwabasi mgombea atatangazwa kuwa Mwenyekiti auMakamu Mwenyekiti.

(5) Iwapo kura za “Hapana” zitazidi asilimia hamsiniya kura zote zilizopigwa, jina la mgombeamwingine litapendekezwa kwa njia na utaratibuuliotumika hapo awali.

(6) Iwapo kura zitafanana, uchaguzi utarudiwa kwamara ya pili na endapo hata baada ya kurudiauchaguzi kura zimefanana, Baraza litaamua kugawamuda wa kuwa madarakani kwa wagombea haoambao kura zao zimefanana.

(7) Kama itatokea nafasi wazi ya Mwenyekiti auMakamu Mwenyekiti, Halmashauri itamchaguaMwenyekiti au Makamu Mwenyekiti katika mudawa siku zisizozidi sitini tangu nafasi hiyo ilipotokeakuwa wazi.

Uongozaji waMikutano yaHalmashauri

11. (1) Mkutano wa Halmashauri utaongozwa na:-(a) Mwenyekiti; au(b) Kama Mwenyekiti hayupo, ; Makamu

Mwenyekiti au

Page 14: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

14

(c) Kama Mwenyekiti na Makamu Mwenyekitiwote hawapo, au kama Mwenyekiti naMakamu Mwenyekiti wote hawawezikuongoza Mkutano, Mjumbe yeyoteatachaguliwa na kutoka miongoni mwaWajumbe waliohudhuria kwa ajili yakuongoza Mkutano huo,

(d) Wajumbe wakiwa ndani ya ukumbi waMikutano wa Halmashauri watavaa mavazimaalum yaliyochaguliwa na kushonwamaalum kwa ajili hiyo,

(e) Endapo vazi maalum lililochaguliwa naHalmashauri ni joho basi litavaliwa juu yavazi la Mjumbe, na endapo Halmashaurihaina joho basi Mjumbe atavaa vazi laheshima,nguo za “jeans”, kofiazisizohusiana na dini na sare za Chamahazitaruhusiwa kuvaliwa wakati waMikutano ya Halmashauri na vikao vyaKamati za Kudumu za Halmashauri,

(f) Vazi rasmi la Mwenyekiti, Mkurugenzi naMakamu Mwenyekiti litakuwa lenyekuonyesha rangi za Bendera ya Taifa namazao yanayolimwa kwa wingi katikaeneo la Halmashauri kadri Halmashauriitakavyoona inafaa. Hata hivyo, Kanuni hiihaitaathiri majoho ambayo yanatumikakabla ya Kanuni hii,

(g) Endapo katika Mkutano huo Halmashauriitajigeuza kuwa Kamati, Wajumbe watavuamajoho.

(h) Endapo Baraza litajigeuza kuwa Kamatitaratibu za kuendesha Vikao vya Kamatizitatumika na kikao hicho kitakua cha siri.

(2) Madaraka au jukumu lolote la Mwenyekitikuhusiana na uendeshaji wa Mikutano yanawezakutekelezwa na mtu anayeongoza Mkutano huo.

(3) Halmashauri itatenga siku mbili kila wiki kwa ajili

Page 15: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

15

ya Mwenyekiti kufika ofisini na kutekelezamajukumu yafuatayo;

(a) Kusikiliza matatizo ya Wananchi;(b) Kupata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi

kuhusu uendeshaji wa shughuli zaHalmashauri ikiwa ni pamoja na masualaya manunuzi;

(c) Kusaini mikataba mbalimbali yaHalmashauri;

(d) Kushughulikia jambo ambalo Mkurugenziataona linahitaji kushughulikiwa aukutekelezwa na Mwenyekiti.

Kumbukumbuya mahudhurio

12. (1) Kila Mjumbe anayehudhuria Mkutano waHalmashauri au Kamati yoyote ya Halmashauriambamo yeye ni Mjumbe hatahudhuria Mkutanohuo mpaka awe ameweka saini yake kwenyeRejesta ya mahudhurio inayotunzwa naMkurugenzi kwa ajili hiyo.

(2) Isipokuwa siku ya kufanyika kwa Mikutano yaBaraza au Kamati ambayo Diwani ni Mjumbe aupale atakapoitwa kutekeleza majukumu ya Serikali,si ruhusa kwa Diwani kuwa katika Ofisi zaHalmashauri na kufanya shughuli ambazohazihusiani na Halmashauri au Serikali.

Kuruhusuwatu navyombo vyahabari kwenyeMikutano yaHalmashauri

13. (1) Mikutano ya Halmashauri itakuwa wazi kwa watuwote pamoja na vyombo vya habari.

(2) Halmashauri itapaswa kuutangazia Umma kuhusumuda, wakati na mahali pa Mkutano na italiwekatangazo hilo mahali panapoonekana kwa urahisikatika eneo la Halmashauri siku zisizopungua tatukabla ya Mkutano, na kama Mkutano umeitishwakatika muda mfupi zaidi basi wakati wa kuitishaMkutano huo.

Page 16: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

16

Utaratibu washughuli zaMikutano

14. (1) Isipokuwa kama Halmashauri, kutokana na sababuza dharura, itaamua kubadili utaratibu wa shughuliza Mikutano, utaratibu wa shughuli katika kilaMkutano wa kawaida wa Halmashauri utakuwakama ifuatavyo:-

(a) Mwenyekiti akiongozwa na Katibu ataingiaukumbini baada ya Mratibu wa vikaokutoa ishara maalum kuashiriaMwenyekiti kuingia ukumbini naWajumbe watasimama na kukaa kimyampaka pale Mwenyekiti atakaporuhusuWajumbe kukaa

(b) Mkutano utaanza kwa Sala au Duaitakayosomwa na Mwenyekiti ,

(c) Endapo Mwenyekiti au MakamuMwenyekiti hawatakuwepo, Wajumbewatachagua mtu wa kuongoza kikao,

(d) Baada ya Sala/Dua kusomwa Mkurugenzina Mwenyekiti wa Halmashauri watajibumaswali ya papo kwa papo kutoka kwaWajumbe wa Baraza la madiwani kwautaratibu na mpangilio kamailivyooneshwa kwenye Kanuni hizi,

(e) Kupokea na kujadili taarifa za kwenye Katakutoka kwa Madiwani wa Kata husika,

(f) Kujadili jambo lolote linalotakiwa kwamujibu wa Sheria kushughulikiwa kablaya shughuli nyingine yoyote,

(g) Kupokea taarifa yoyote inayopaswakupokelewa kisheria kabla ya shughulinyingine yoyote,

(h) Kusoma au kuthibitisha muhtasari waMkutano wa kawaida wa Halmashauriuliopita na Mikutano yoyote maalum yaHalmashauri iliyofanyika baada yaMkutano huo wa kawaida. Hata hivyoiwapo nakala za mihtasarizimesambazwa kwa kila Mjumbe kabla auwakati wa kupeleka taarifa ya kuhudhuria

Page 17: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

17

Mkutano, mihtasari hiyo itachukuliwakuwa imesomwa,

(i) kupokea taarifa yoyote ambayoMwenyekiti atapenda itolewe kwaHalmashauri,

(j) Kujibu maswali kufuatana na Kanuni ya 23ya Kanuni hizi,

(k) Kumalizia shughuli yoyote iliyobaki katikaMkutano wa kawaida uliopita,

(l) Kupokea na kufikiria taarifa za Kamati zaHalmashauri, kutoka kwa Wenyeviti waKamati ambao watahusika kujibu maswaliya Wajumbe kuhusiana na kazi za Kamatihusika,

(m) Kupokea na kujadili taarifa kutoka kwaMkurugenzi wa Halmashauri,

(n) Kuidhinisha utiaji lakiri katika hati,(o) Kufikiria hoja binafsi kufuatana na jinsi

zilivyopokelewa, na,(p) Kushughulikia mambo mengine

yaliyoonyeshwa katika taarifa yaMkutano.

(2) Halmashauri inaweza, katika Mkutano wowote wakawaida, kubadili utaratibu wa hoja zamazungumzo ili kutoa kipaumbele kwa shughuliyoyote ambayo kwa maoni ya Mwenyekiti nauharaka wa pekee, lakini mabadiliko hayohayatabadilisha mpangilio wa shughuli zilizotajwakatika aya (c), (f) na (g) za Kanuni ya 14(1) yaKanuni hii.

Kuthibitishamuhtasari

15. (1) Katibu ataandika muhtasari wa mazungumzo yakikao unaozingatia majina ya Wajumbewaliohudhuria na wasiohudhuria, jina la mtoa hoja,aliyeunga mkono hoja, mabadiliko ya hoja kwaufupi, ushauri uliotolewa na azimio lililofikiwa.Muhtasari huo utasomwa, kurekebishwa,kuthibitishwa na kusainiwa na Mwenyekiti waMkutano na kutunzwa katika rejesta maalum ya

Page 18: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

18

mihtasari.

(2) Mara baada ya kusoma Muhtasari, au kamaitachukuliwa kama umesomwa Mwenyekiti ataulizaswali “Je Muhtasari wa Mkutano wa Halmashauriwa tarehe…………… ya mwezi………….Mwaka……..utiwe saini kama kumbukumbusahihi?.”

(3) Hakuna hoja au majadiliano yatakayofanywakuhusiana na muhtasari isipokuwa kuhusiana nausahihi wa muhtasari, kama hakuna swalilililoulizwa, basi mara baada ya kuthibitishwaMwenyekiti atatia saini katika muhtasari huo.

(4) Muhtasari ambao utakuwa umesainiwa vilivyo nakama hakuna ushahidi wa kuwepo kwa makosautakuwa kumbukumbu sahihi na Mkutanoutahesabika kuwa umeitishwa na kufanyika vilivyona Wajumbe waliohudhuria watahesabika halali.

(5) Mihtasari ya Halmashauri itakuwa wazi kwaukaguzi na Wajumbe na kwa umma kwa wakatiunaofaa na kwa utaratibu utakaokubaliwa naHalmashauri na kwamba mtu yeyote anawezakupewa sehemu ya muhtasari huo kama akiombana baada ya kulipa ada kama itakavyoidhinishwa naHalmashauri.

Hoja zaMwenyekiti

16. Hoja zinazowasilishwa na Mwenyekiti hazitazidihoja tatu, bila kuathiri haki yake, kama Mjumbe yakuwasilisha hoja katika taratibu za kawaida.

Taratibu zamajadiliano

17. (1) Isipokuwa kwa idhini ya Halmashauri mtoa hojaatahutubia Mkutano wa Halmashauri kwa dakikazisizozidi kumi. Wajumbe wengine ikiwa nipamoja na mtoa hoja watazungumza kwa mudausiozidi dakika tano kila mmoja;

(2) Mjumbe anaruhusiwa kuzungumza mara moja

Page 19: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

19

katika hoja yoyote ile isipokuwa hojainayowasilishwa bila mjadala;

(3) Mtoa hoja atakuwa na haki ya kuzungumza kwamuda usiozidi dakika tano katika kujibumajadiliano na muda huo utaanza kuhesabika maraatakapoanza kuchangia au kujibu. Mratibu wavikao atatoa ishara maalum kumjulisha mtoa hojakuwa muda wake umeisha na mjadala juu ya hojahiyo utafungwa. Utaratibu huu wa kuhesabu mudautatumika pia kwa Mjumbe yeyote atakayepewamuda wa kuchangia hoja na mara tu baada yakujibu, mjadala juu ya hoja utafungwa;

(4) Mjumbe yeyote aliyekwishachangia kwenye hojahawezi kutoa au kuunga mkono marekebisho, ilamarekebisho yakitolewa na kuungwa mkono,Mjumbe aliyekwishazungumza katika hoja ya awalianaweza kuzungumza kwenye hoja iliyorekebishwakwa muda usiozidi dakika tatu;

(5) Iwapo Wajumbe wawili au zaidi watasimamawakati mmoja kuzungumza, Mjumbeatakayetamkwa na Mwenyekiti ndiye atakayepewanafasi kwanza;

(6) Bila kuathiri masharti ya Kanuni Ndogo ya (5) yaKanuni hii, Mwenyekiti atahakikisha kuwa, nafasiya kuchangia inatolewa kwa uwiano unaofaamiongoni mwa aina zote za uwakilishi waMadiwani walioomba kuchangia hoja hiyo;

(7) Mjumbe anapozungumza ataelekeza mazungumzoyake kwa Mwenyekiti tu na atapaswa kusimama;

(8) Mjumbe anapozungumza hatakatizwa, isipokuwakwa suala la utaratibu, lakini anaweza kutoa nafasikwa Mjumbe anayetaka kujieleza;

(9) Mjumbe anaposimama kutoa taarifa kuhusu

Page 20: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

20

utaratibu, Mjumbe anayezungumza ataketi naatabaki ameketi hadi hoja ya utaratibu itakapokuwaimeamuliwa na Mwenyekiti, isipokuwa kamaanasimama kumweleza Mwenyekiti kuhusu suala lautaratibu;

(10) Mwenyekiti ndiye pekee mwenye uamuzi kuhusuutaratibu katika Mikutano ya Halmashauri, naanayo madaraka ya kuzuia fujo na kuhakikishakuwa maamuzi yake katika kusimamia usalamayanatekelezwa mara moja. Wakati wa majadilianoMwenyekiti akisimama, Mjumbe anayezungumzaau aliyesimama ataketi na hakuna Mjumbeatakayesimama hadi Mwenyekiti aketi;

(11) Hakuna Mjumbe atakayebaki amesimama wakatiMjumbe mwingine anaelekeza mazungumzo yakekwa Mwenyekiti;

(12) Mkurugenzi wa Halmashauri atajibu swali loloteatakaloulizwa na Mwenyekiti kutokana na shughulizinazoendelea kwenye Mkutano isipokuwa kamaatadai haki ya kukataa kujibu swali kwa msingi yakwamba jibu linaweza kumweka hatiani au kuvunjauaminifu wake au linamhusisha yeye kama mtetezimahakamani;

(13) Hakuna mtu kwa niaba yake mwenyewe, au kwaniaba ya watu wengine walio kwenye ujumbe wawatu, atakayeruhusiwa kuzungumza katikaMkutano wa Halmashauri isipokuwa kwa idhini yaHalmashauri iliyotolewa kwa njia ya azimio. Idhiniya namna hiyo haitatolewa isipokuwa kama mtuhuyo au watu hao wanaotaka kuihutubiaHalmashauri watakuwa wamempatia Mkurugenziau Afisa aliyeruhusiwa naye, taarifa ya mudausiopungua siku tisa kabla ya Mkutano waHalmashauri ambamo wangetaka maombi yaoyafikiriwe kupewa idhini, maombi ya kimaandishiikieleza jambo linalotarajiwa kujadiliwa, na mpaka

Page 21: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

21

taarifa ya kupokelewa kwa maoni hayoitakapokuwa imebandikwa kwenye mbao zamatangazo za Halmashauri;

(14) Hakuna zaidi ya watu wawili watakaokuwa na hakiya kuhutubia Halmashauri kwa niaba ya uwakilishi;na wala hakuna ujumbe utakaozidi idadi ya watuwatano watakaoruhusiwa;

(15) Kiwango cha juu cha muda wa kuzungumza naHalmashauri ikiwa ni pamoja na muda wa kusomarisala hakitazidi dakika kumi;

Fujozinazosababishwa naWajumbe

18. (1) Katika Mkutano wowote wa Halmashauri kamaMjumbe wa Halmashauri ataonyesha kukosaheshima kwa madaraka aliyonayo Mwenyekiti aukudharau Kanuni za Kudumu za Halmashauri kwakuzuia kwa makusudi shughuli za Halmashaurizisiendelee au vinginevyo, Mwenyekiti ataelekezaMkutano kwa tukio hilo kwa kumtaja jina mtuanayehusika.

(2) Endapo baada ya kutajwa jina mjumbe ataendeleakudharau madaraka ya Mwenyekiti, basiMwenyekiti ataliomba Baraza kuahirisha shughuliza Mkutano na Mwenyekiti atatafakari jambo hilona kuagiza yafuatayo;

(a) Mjumbe atolewe nje ya Mkutano kama mjumbewa Halmashauri na kumzuia kuhudhuriavikao vitatu mfululizo pamoja na haki zakezote.

(b) Mjumbe kuzuiliwa kuhudhuria vikao vitatumfululizo na kupoteza haki zakezinazohusiana na vikao hivyo.

(3) Iwapo kutatokea fujo kubwa katika Mkutano

Page 22: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

22

wowote wa Halmashauri, Mwenyekiti anawezakama ataona ni muhimu kufanya hivyo, kuahirishaMkutano bila majadiliano au swali, aukusimamisha Mkutano kwa muda atakaoonaunafaa.

Fujozinazosababishwa na umma

19. (1) Iwapo mtu yeyote kati ya umma unaohudhuriaMkutano wa Halmashauri atavuruga Mkutanowa Halmashauri, Mmwenyekiti atamuonyamtu huyo aache kufanya hivyo. Endapo mtuhuyo ataendelea kuvuruga Mkutano,Mwenyekiti ataamuru mtu huyo atolewekwenye chumba cha Mkutano.

(2) Endapo kutakuwa na vurugu katika sehemuyoyote ya chumba cha Mkutanokinachotumika na umma, Mwenyekitiataamuru kuondolewa kwa watu wote waliokatika eneo hilo.

Hoja namarekebishoya hoja

20. (1) Taarifa ya kila hoja, isipokuwa hojailiyowasilishwa chini ya Kanuni ya 21,itawasilishwa kwa maandishi yaliyowekwa saini naDiwani au Madiwani waliotoa taarifa, naitapelekwa kwa Mkurugenzi angalau siku nne kablaya Mkutano wa Halmashauri unaofuata naakishaipokea, Mkurugenzi atagonga tarehe na kuipanamba na kuiingiza kwenye daftari kadri hojazilivyowasilishwa, na daftari hiyo itakuwa wazikukaguliwa na Mjumbe yeyote wa Halmashauri.

(2) Mkurugenzi ataonyesha katika taarifa ya kilaMkutano wa Halmashauri hoja zilizowasilishwa nakwa kadri zilivyopokelewa isipokuwa kama Diwanialiyetoa hoja hiyo ameeleza kwa maandishi wakatialipoleta hoja hiyo, kwamba anataka kuitoa katikaMkutano utakaofanyika baadaye, au baada yakuwasilisha ameifuta hoja hiyo kwa maandishi.

Page 23: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

23

(3) Iwapo hoja ambayo imeonyeshwa katika taarifa yaMkutano haiwezi kutolewa na Mjumbealiyewasilisha taarifa; au na Mjumbe mwingineyeyote kwa niaba yake, basi hoja hiyo, isipokuwakama imeahirishwa kwa idhini ya Halmashauri,itachukuliwa kama imeondolewa nahaitawasilishwa tena bila ya kutoa taarifa upya.

(4) Iwapo hoja itahusu jambo linalohusu Kamati auKamati mbalimbali baada ya kupendekezwa nakuungwa mkono, hoja hiyo itapelekwa bilamajadiliano kwenye Kamati ambayo Halmashauriitaelekeza ili iweze kufikiriwa na kutayarishiwataarifa.

(5) Ni lazima kila hoja ihusu jambo ambaloHalmashauri ina uwezo na wajibu nalo, au iweinahusu Halmashauri ya husika.

(6) Marekebisho ya hoja yaliyopendekezwa nakuungwa mkono yanaweza kuondolewa tu kwaridhaa ya Wajumbe wa Halmashauri walio wengiwaliopo katika Mkutano.

(7) Marekebisho ya hoja yanapokuwa yamethibitishwa,hoja ya msingi kama ilivyorekebishwa itatolewa naMwenyekiti kama ndiyo hoja ya msingi ambayonayo inaweza kufanyiwa marekebisho. Kamamarekebisho ya hoja hayakukubaliwa, rekebisholingine linaweza kupendekezwa.

(8) Kwa idhini ya Mwenyekiti, zaidi ya rekebisho mojalinaweza kutolewa kwa wakati mmoja mbele yaMkutano wa Halmashauri, lakini kila rekebisho lanamna hii litatolewa moja baada ya jinginekufuatana na jinsi mapendekezo hayoyalivyotolewa.

(9) Rekebisho halitachukuliwa kuwa sahihi kamalitakuwa sawa na kuikataa hoja moja kwa moja au

Page 24: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

24

kama si rekebisho la hoja ya msingi linalokusudiwakurekebisha.

(10) Rekebisho ambalo halikutolewa taarifa,halitapendekezwa baada ya mjadala wa hojainayozungumzwa kuendelea kwa nusu saa, ila kwamujibu wa sharti hili, taarifa ya idadi yoyote yamarekebisho inaweza kutolewa.

(11) Hoja ya kufuta azimio itapitishwa na Wajumbewasiopungua theluthi mbili ya Wajumbe wote.

(12) Hoja ya kuzingatia taarifa ya Kamati aukuidhinisha majadiliano au mapendekezo yaKamati inaweza kutolewa na Mwenyekiti waKamati husika, au na Mjumbe yeyote wa Kamatihusika kwa niaba yake.

(13) Mjumbe yeyote ambaye hajachangia katika mjadalawa hoja, au hajaitolea marekebisho, anawezakupendekeza “kwamba Halmashauri iendelee nashughuli inayofuata”. Hoja ya aina hiyo inaweza tukuzingatiwa baada ya hoja kupendekezwa nakuungwa mkono. Hoja inapotolewa, itaamuliwabila marekebisho au mjadala, na kama ikikubaliwa,shughuli iliyokatizwa na azimio hilo haitaendeleakujadiliwa katika kikao hicho. Hoja yakupendekeza kuendelea na shughuli inayofuatahaitatolewa zaidi ya mara moja katika mjadala wajambo lolote.

(14) Baada ya mjadala kuhusu hoja kuendelea kwamuda usiopungua nusu saa, Mjumbe ambayehajachangia katika majadiliano anaweza kuombaidhini ya kutoa hoja “kwamba suala lililo mbeleyetu sasa liamuliwe” na kama idhini hiyo itatolewakwa kukubaliwa na si chini ya Wajumbe watano,hoja “kwamba suala lililo mbele yetu sasaliamuliwe” itawasilishwa mara moja, na kamaikiafikiwa, mtoa hoja ya msingi anaweza

Page 25: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

25

kuzungumza kwa dakika zisizozidi tano, na baadaya hapo swali au maswali yaliyo mbele yaHalmashauri yatafanyiwa uamuzi.

(15) Hoja kwamba suala lililo mbele yetu sasaliamuliwe haitatolewa zaidi ya mara moja katikamjadala unaoendelea kuhusu jambo lolote mpakahapo mjadala utakapokuwa umeendelea kwaangalau nusu saa tangu kuwekwa mbele yaMkutano hoja ya aina hiyo ilipopendekezwa awali.

Hojazinazowezakutolewa bilataarifa

21. Hoja zifuatazo zinaweza kutolewa bila taarifa.(a) Kumchagua Mwenyekiti wa Mkutano

ambamo hoja imetolewa.(b) Hoja kuhusu usahihi wa muhtasari,

kufunga Mkutano, kuahirisha Mkutano,utaratibu wa Mkutano, au suala linalofuata.

(c) Kuteua Kamati au Wajumbe wa Kamati, auwawakilishi katika taasisi za nje,unaotokana na jambo lililotaarifiwa katikawito wa Mkutano.

(d) Kukubali taarifa na mapendekezo yaKamati na maazimio yote yanayotokana nataarifa au mapendekezo hayo;

(e) Kwamba idhini itatolewa kuiondoa hoja.(f) Kusahihisha hoja.(g) Kuongeza muda wa hotuba.(h) Kuwa, jambo lililotajwa katika taarifa ya

kuitisha Mkutano litangulie.(i) Kusimamisha Kanuni za kudumu;(j) Kwamba Mjumbe asisikilizwe tena au

aondoke katika Mkutano.(k) Kumwomba Mjumbe abakie Mkutanoni, na(l) Kutoa idhini ya Halmashauri pale ambapo

idhini inatakiwa kwa mujibu wa Kanuni zakudumu hizi.

Haki ya kujibu 22. (1) Mtoa hoja atakuwa na haki ya kujibu maswaliwakati wa kufunga mjadala juu ya hoja; kabla yahoja kupigiwa kura au kabla ya hoja kutolewa

Page 26: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

26

“kwamba kikao kiahirishwe,

(2) Mjumbe anayetumia haki yake ya kujibuhataanzisha hoja nyingine mpya,

(3) Baada ya kutolewa kwa jibu ambalo linahusiana naKanuni hizi, uamuzi utafikiwa bila majadilianozaidi.

Maswali 23. (1) Mjumbe anaweza kumuuliza Mwenyekiti waKamati swali lolote kuhusu muhtasari wa Kamatiuliofikishwa mbele ya Halmashauri,

(2) Kila swali litaulizwa na kujibiwa bila majadiliano,

(3) Swali au maswali yatajibiwa na Mwenyekiti waKamati mara moja, na Mjumbe anayeuliza maswalihayo hatanyimwa haki yake ya kujadili hojaambayo maswali hayo yanarejewa au kutoa hoja yamarekebisho,

(4) Pale ambapo swali la maandishi limeelekezwa kwaMwenyekiti wa Kamati, au Mkutano na taarifainayotakiwa imo katika mojawapo ya mihtasari yaHalmashauri, kuonyesha sehemu ya muhtasariambapo habari hiyo imeonyeshwa, kutachukuliwani jibu la kutosha.

Maswali yapapo kwapapo’

24. (1) Halmashauri itatenga muda wa angalau dakikathelathini katika kila Mkutano wa Kawaida waHalmashauri ambapo Mwenyekiti na Mkurugenziwa Halmashauri watajibu maswali ya papo kwapapo kutoka kwa Wajumbe kabla ya kuanza kwashughuli ya kawaida za Mkutano wa Halmashauri.

(2) Wajumbe ambao watataka kuuliza maswali ya papokwa papo kwa Mwenyekiti na Mkurugenziwatatakiwa kujiorodhesha kwanza kwa Mwenyekitiangalau masaa ishirini na nne(24) kabla yaMkutano wa Halmashauri kuanza.

Page 27: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

27

(3) Mjumbe yoyote ambae hatajiorodhesha kwaMwenyekiti ndani ya masaa ishirini na nneatahesabika kuwa amechelewa na hataruhusiwakumuuliza Mkurugenzi au Mwenyekiti swali lapapo kwa papo.

(4) Kabla ya kuanza kwa kipindi cha maswali ya papokwa papo Mwenyekiti atataja majina ya Wajumbewaliojiorodhesha kuuliza maswali ya papo kwapapo na idadi ya maswali,

(5) Mwenyekiti ataweka utaratibu ambao ataonaunafaa na kuridhiwa na Wajumbe wa namna boraya kuendesha kipindi cha swali la papo kwa papo.

(6) Mjumbe hataruhusiwa kuuliza zaidi ya swali mojala papo kwa papo.

(7) Maeneo ya muhimu ambayo Wajumbe watatakiwakuuliza maswali ya papo kwa papo:-

(a) Uendeshaji wa jumla wa Halmashauri;(b) Utekelezaji wa miradi ya Maendeleo;(c) Mipango ya kimkakati ya Halmashauri

kuwaondolea wananchi umaskini;(d) Mipango ya baadaye ya maendeleo ya

Halmashauri;(e) Usimamizi na utekelezaji wa Mipango na

Bajeti kwa mwaka husika;(f) Utoaji wa huduma za jamii kama vile

elimu, afya, maji, barabara na madaraja;(g) Hifadhi ya mazingira na utunzaji wa

vyanzo vya maji;(h) Usalama wa Chakula, Raia na Mali zao;(i) Utawala Bora na utatuzi wa kero za

wananchi.(8) Baada ya kujibiwa kwa swali, Mjumbe aliyeuliza

swali atapewa fursa ya kuuliza swali moja tu laufafanuzi na maswali yatajibiwa bila mjadala.

Page 28: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

28

(9) Mwenyekiti atakua na uwezo wa kuruhusu aukukataa swali lolote la papo kwa papo ambalolitaonekana linahitaji takwimu au utafiti zaidi auswali ambalo linalenga kumdhalilisha Mwenyekitiau mjumbe yeyote wa Baraza na uamuzi wakeutakuwa wa mwisho.

(10) Mara baada ya muda wa nusu saakumalizika,kipindi cha maswali ya papo kwa papokitamalizika na kuruhusu shughuli zingine za kikaokuendelea

Taarifa zaKamati

25. (1) Kila Kamati au Kamati ya pamoja iliyoteuliwachini ya Kanuni hizi itatoa, katika mojawapo yavikao viwili vya Halmashauri iliyoteua Kamati,Kamati ya pamoja au Kamati Ndogo, taarifa yamajadiliano yanayohusiana na utekelezajimajukumu iliyokasimiwa, kwa ujulisho waHalmashauri.

(2) Muhtasari wa Kamati unaohitaji idhini yaHalmashauri, na taarifa zozote zinazohusiana namuhtasari huo, na ambazo zinaonekana kwaKamati kuwa zinastahili, zitapelekwa kwa kilaMjumbe wa Halmashauri angalau siku saba kablaya Mkutano wa Halmashauri ambamo utafikiriwa.

(3) Mwenyekiti wa Kamati, au Mjumbe mwingine waKamati kwa niaba yake, wakati wa kupendekezakuidhinishwa kwa muhtasari wa Kamati, anawezakusema kuwa hakusudii kuwasilisha kipengele auvipengele fulani vya muhtasari huo kwa lengo lakupata idhini ya Halmashauri. Katika hali hiyoMjumbe yeyote hataweza kukizungumzia kipengeleau vipengele hivyo na muhtasari utawasilishwa bilavipengele hivyo. Kuondolewa kwa kipengele chaaina hiyo kutatolewa taarifa kwenye Mkutanounaofuata.

(4) Taarifa ya Kamati inapokuwa imepokelewa na

Page 29: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

29

Halmashauri itamaanisha kuwa hatuazilizochukuliwa na Kamati husika zimekubaliwa namapendekezo yaliyo kwenye taarifa hiyoyatatekelezwa na kwamba Mkurugenzi atakuwaameelekezwa ipasavyo.

Taarifa zakutokakwenye Kata

26. (1) Kila Kata itatakiwa kuwasilisha taarifa zautekelezaji katika Mkutano wa Halmashauriulioitishwa chini ya Kanuni ya 3(1) ya Kanuni hizi;

(2) Taarifa za utekelezaji kutoka katika Katazitawasilishwa na Diwani wa Kata husika, au kamadiwani hayupo, taarifa hiyo itawasilishwa naDiwani wa Viti Maalum anayeishi katika Kata hiyona kama Diwani Viti Maalum hayupo, Mwenyekitiatamtaarifu mapema Diwani yeyote ili ajiandaekuwasilisha taarifa hiyo;

(3) Kutakuwa na aina tatu za taarifazitakazowasilishwa:-

(a) Taarifa ya utekelezaji wa miradi ya maendeleokatika Kata ambayo itajumuisha ujenzi waMadarasa, Nyumba za Walimu, Matundu yaVyoo, Maabara, Viwanja vya Michezo, Vituovya Afya, Zahanati, Madaraja, Barabara,Mashamba darasa, Ofisi za Vijiji, Mitaa, Katana Tarafa; Idadi ya watu na vizazi

(b)Taarifa zinazohusu hali ya Kata ambazozitajumuisha-

(i) Maendeleo ya Elimu katika Katakuhusiana na uandikishaji wa watotowenye umri wa kwenda shule,ufundishaji, utoro, hali yamahudhurio, mimba mashuleni,ukaguzi na uratibu wa shule.

(ii) Hali ya majanga kama vile magonjwaya mlipuko, mafuriko, njaa, na hali

Page 30: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

30

ya uhalifu na vifo.

(iii) Maendeleo ya Kilimo, mifugo nauvuvi ambayo itajumuishaupatikanaji wa wataalamu, zana zakisasa na pembejeo za kilimo,mifugo na uvuvi.

(iv) Uimarishaji wa dhana ya uzalendo nautaifa kwa kuhamasisha vijanakuanzisha na kujiunga na vikundivya Vijana Wagani kazi na mafunzoya Jeshi la Mgambo, ulinzi shirikishina polisi jamii.

(c) Taarifa ya utekelezaji wa miradi yaMaendeleo na taarifa ya hali ya Kata shartiijumuishe pia taarifa za shughuli zakiuchumi, taarifa ya mavuno ya mazao yachakula na biashara pamoja na taarifa yautunzaji wa mazingira na vyanzo vya maji.

(4) Mkurugenzi wa Halmashauri atahakikisha taarifakutoka kwenye Kata, zinaandaliwa nakuwasilishwa na Diwani wa Kata hiyo kwenyeBaraza la Madiwani ili ipitiwe na kuchambuliwakwa nia ya kupata hoja zitakazowasilishwa katikaVikao vya Kamati husika na kutoa mrejesho.

Mafanikio nachangamoto

(5) Mwasilishaji wa taarifa atatakiwa kuelezeamafanikio yaliyopatikana, changamoto zilizojitokeza na mbinu za kukabiliana nazo.

(6) Mbinu za kukabiliana na changamoto shartiziwekewe malengo na muda maalum wa kuzitatua.

(7) Taarifa za mapokeo ya fedha na matumizi yakezitakazokuwa zimeandaliwa na Afisa Mtendaji waKata, zitawasilishwa sanjari na miradiiliyotekelezwa na gharama zake.

Page 31: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

31

(8) Baada ya taarifa kutoka kwenye Kata kupokelewana Halmashauri, itamaanisha kuwa taarifa hizozimeidhinishwa na mapendekezo yaliyomo kwenyetaarifa yatatekelezwa na Halmashauri, na Katakupewa taarifa ya utekelezaji wa majukumu hayo.

Uhuru wakutoa mawazowakati wamajadiliano

27. Kutakuwepo na uhuru wa kutoa mawazo wakati wamajadiliano katika Mikutano ya Halmashauri nauhuru huo hautaweza kuhojiwa katika mahakamayoyote au mahali popote nje ya Mkutano waHalmashauri.

Kauli zenyekashfa

28. (1) Inapotokea, kulingana na maoni ya Mwenyekiti aumtu yeyote anayeongoza Mkutano, kuwa kauliiliyotolewa na Mjumbe inakashifu mtu yeyote,Mwenyekiti atamtaka Mjumbe aliyetoa kauli hiyokufuta kauli yake na kumwomba msamaha mtualiyekashifiwa kwa maandishi ndani ya muda wasiku saba tangu kauli hiyo ya kashfa ilipotamkwa.

(2) Endapo Mjumbe aliyetoa kauli za kashfa atakataakufuta kauli yake na kuomba msamaha kwamaandishi kama inavyoelekezwa katika KanuniNdogo (1) ya Kanuni hii. Mwenyekiti wa Mkutano,atamsimamisha Mjumbe huyo kuhudhuria vikaovitatu mfululizo vya Halmashauri.

(3) Mjumbe aliyesimamishwa kwa mujibu wa kanuniNdogo(2) ya Kanuni hii atapoteza haki zake zoteikiwa ni pamoja na posho,nauli na upendeleo nakinga kwa muda wote wa kusimamishwa kwake;

Maamuzi yaMikutano yaHalmashauri

29. (1) Masuala yote yaliyojadiliwa na kupendekeza katikaMkutano wowote wa Halmashauri yataamuliwakulingana na wingi wa kura za Wajumbewaliohudhuria Mkutano huo, na ikitokea kura zaWajumbe zikalingana, basi Mwenyekiti au Mjumbeyeyote mwingine anayeongoza Mkutano, atapigakura ya turufu mbali ya kura ya kawaida.

Page 32: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

32

(2) Iwapo suala linalopigiwa kura linahusu kutokuwana imani au kumwondoa Mwenyekiti madarakani,au jambo lolote lingine kama itakavyoamuliwa naHalmashauri, kura zitapigwa kwa siri.

Mwaliko kwawasiokuwaWajumbekushiriki nakuzungumzakwenye vikaovyaHalmashauri

30. (1) Mwenyekiti, baada yakushauriana na Wajumbe,anaweza kumwalika mtu yeyote kuhudhuria nakuzungumzia jambo lolote, au kushiriki kwa njiayoyote, katika Mkutano wowote wa Halmashaurilakini mwalikwa huyo hatakuwa na haki yakupiga kura katika Mkutano huo.

(2) Wakuu wa Idara za Halmashauri na Maafisa Tarafawanapaswa kuhudhuria Mikutano yote yaHalmashauri lakini hawatakuwa na haki ya kupigakura katika Mikutano hiyo.

Mihtasari yaKamati yaMaendeleo yaKata,Mitaa/Vijiji

31. Mkurugenzi wa Halmashauri atahakikishamihtasari yote ya Kamati za Maendeleo za Kata, naMikutano Mikuu ya Mitaa inapitiwa nakuchambuliwa kwa nia ya kupata hojazitakazowasilishwa katika vikao vya Kamati husikana kutoa mrejesho inavyopaswa.

Mihtasari yaHalmashaurikupelekwakwa Mkuu waWilaya naMkuu waMkoa

32. (1) Mihtasari ya Halmashauri itatolewa na kupelekwakwa taarifa, kwa Mkuu wa Wilaya na Mkuu waMkoa ambamo Halmashauri imo katika muda wasiku 7 baada ya kuthibitishwa kwa mihutasari hiyo.

(2) Mkuu wa Wilaya na Mkuu wa Mkoa wanawezakupewa, wakiomba, nakala ya mihutasari ausehemu ya mihtasari ya Kamati za Kudumu naKamati nyingine.

(3) Wakuu wa Wilaya na Wakuu wa Mikoahawatabadilisha au kubatilisha au kuagizakubadilisha au kubatilisha uamuzi wa Halmashauri.

Page 33: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

33

Hoja kuhusumatumizi

33. Hoja yoyote isiyotokana na mapendekezo au taarifaya Kamati ya Fedha na Utawala, na ambayo, kamaikikubaliwa, itaongeza matumizi au kupunguzamapato yaliyo chini ya usimamizi wa Kamatiyoyote, au itasababisha matumizi ya Kamati yaKudumu, baada ya kupendekezwa au kuungwamkono, itaahirishwa bila majadiliano mpakaMkutano wa kawaida wa Halmashauri unaofuata,na Kamati yoyote inayohusika na hoja hiyoitafikiria iwapo ingependa kutoa taarifa kuhusuathari za kifedha za pendekezo hilo.

Kupokelewakwa taarifa zaKamati

34. (1) Taarifa ya Kamati inapowasilishwa kwenyeHalmashauri, hoja itakuwa “kwamba taarifaipokelewe”na baada ya kukubaliwa na Wajumbetaarifa itaanza kujadiliwa kipengele kimoja baadaya kingine.

(2) Mapendekezo yoyote yaliyomo katika taarifa hiyoyatapigiwa kura iwapo Mjumbe yeyote atapendaiwe hivyo. Baada ya hapo taarifa nzimaitawasilishwa mbele ya Mkutano kwa kupokelewaikiwa na au bila marekebisho.

Kuidhinishwakwa taarifa yaKamati

35. Taarifa ya Kamati inapokuwa imepokelewa naHalmashauri itamaanisha kuwa hatuazilizochukuliwa na Kamati iliyowasilisha taarifahiyo zimeidhinisha na mapendekezo yaliyo kwenyetaarifa yatatekelezwa na kwamba Mkurugenzi waHalmashauri atakuwa ameelekezwa kamainavyotakiwa.

Uhalali wamajadiliano yaHalmashauri

36. Uhalali wa majadiliano kwenye Halmashaurihautaathiriwa na nafasi yoyote wazi ya Mjumbe,dosari zozote zilizo katika uchaguzi au uteuzi waWajumbe wa Kamati au zile za maafisa wake.

Uwezo waHalmashaurikujigeuzakuwa Kamati

37. Halmashauri inaweza kujigeuza kuwa Kamati yaHalmashauri, na mara baada ya kujigeuza, taratibuza kuendesha vikao vya Kamati za Kudumu

Page 34: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

34

yaHalmashaurinzima

zitatumika.

HojazinazohusuWatumishi waHalmashauri

38. Kama litajitokeza jambo lolote katika kikao chaHalmashauri linalomhusu Mtumishi yeyote waHalmashauri kuhusu Uteuzi, kupandishwa cheo,kufukuzwa kazi, mishahara, mazingira ya kazi auutendaji kazi kwa jumla wake, jambo hilolitajadiliwa katika Kamati ya Halmashauri nzima.

Kushiriki kwaUmma

39. (1) Mtu yeyote ambaye ni mkazi katika eneo laHalmashauri anaweza kuhudhuria kikao chaHalmashauri kwa nia ya kuwasilisha hoja mbele yaHalmashauri, baada ya kutoa taarifa kwa maandishikwa Mkurugenzi, na Mkurugenzi akamkubalikufanya hivyo.

(2) Mtu yeyote ambaye ni mkazi katika eneo laHalmashauri anaweza kualikwa kuhudhuria kikaocha Kamati au Kamati Ndogo kabla uamuzihaujafanyika kuhusu masuala ambayo ana maonimahsusi.

Uahirishaji wavikao

40. (1) Kwa kuzingatia masharti ya Kanuni Ndogo ya (2)ya Kanuni 18 na Kanuni Ndogo ya 2 ya Kanuni hii,Halmashauri haitaahirisha Mkutano wake hadidondoo zote za agenda ya Mkutano huozitakapojadiliwa na kutolewa uamuzi.

(2) Pale ambapo katika Mkutano wowote waHalmashauri akidi haikutimia, Wajumbe waliopowataahirisha Mkutano na utaratibu wa kuitishaMkutano mwingine utafanyika kwa kuzingatiamaelekezo ya Kanuni hizi.

SEHEMU YA IVKAMATI

Page 35: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

35

Kamati zaKudumu

41. (1) Halmashauri katika Mkutano wake wa mwakaitateua Wajumbe wa Kamati za Kudumu zifuatazoambazo zitakuwa na idadi ya Wajumbe(ukimwondoa Mwenyekiti wa Halmashauriisipokuwa katika Kamati ya Fedha na Utawala)kama inavyoonyesha hapa chini au kamaitakavyorekebishwa na Halmashauri mara kwamara. Isipokuwa katika kuteua Wajumbe waKamati ya Fedha na Utawala, Mwenyekiti naMkurugenzi watazingatia uwiano wa uwakilishi wavyama katika Halmashauri.

Kamati Idadi yaWajumbe

Akidi

(a) Kamati ya Fedha naUtawala

7 4

(b) Kamati ya Uchumi,Afya na Elimu.

5 3

(c) Kamati ya MipangoMiji na Mazingira.

6 3

(d ) Kamati ya UKIMWI 5 3

(e) Kamati ya Maadili yaMadiwani

4 2

(2) Kila Mjumbe wa Halmashauri atakuwa Mjumbe waangalau Kamati moja ya Kudumu. Kamati ya Fedhana Utawala itakuwa na Wajumbe wafuatao;

(a) Mwenyekiti wa Halmashauri ambayeatakuwa Mwenyekiti.

(b) Makamu Mwenyekiti.(c) Mbunge au Wabunge wa Majimbo

wanaowakilisha Majimbo katika eneo laHalmashauri.

(d) Wenyeviti wa Kamati za Kudumu zaHalmashauri.

(e) Wajumbe wengine wasiozidi wawili (2)watakaopendekezwa na Mwenyekiti nakupigiwa kura na Baraza la Halmashaurimmoja kati yao awe mwanamke.

(3) Halmashauri yenye Madiwani wasiozidiishirini(20), idadi ya wajumbe wa Kamati wa Fedhaitakuwa kama ilivyoonyeshwa kwenye Kanuni ya

Page 36: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

36

41(2) ya Kanuni hizi

(4) Bila kuathiri masharti ya Kanuni Ndogo ya (2) yaKanuni hii, Halmashauri yenye idadi ya Madiwaniwanaozidi ishirini (20) na wasiozidi thelathini natano (35) Wajumbe wa Kamati ya Fedha watakuwakama ilivyoonyeshwa kwenye Kanuni ya 41(2)pamoja na wajumbe wengine wawili (2)watakaotokana na orodha itakayopendekezwa naMwenyekiti na kupigiwa kura na Baraza laHalmashauri mmoja kati yao awe wanawake.

(5) Bila kuathiri masharti ya Kanuni Ndogo ya (2)(3)na (4) ya Kanuni hii, Halmashauri yenye idadi yaMadiwani wanaozidi thelathini na tano(35) nazaidi Wajumbe wa Kamati ya Fedha watakuwakama ilivyoonyeshwa kwenye Kanuni ya 41(2)pamoja na wajumbe wengine wanne(4)watakaotokana na orodha itakayopendekezwa naMwenyekiti na kupigiwa kura na Baraza laHalmashauri wawili kati yao wawe wanawake.

(5) Wajumbe wa Kamati za Kudumu watashikanyadhifa zao kwa muda wa mwaka mmoja nawataendelea kushika nyadhifa hizo mpaka Mkutanowa mwaka wa Halmashauri unaofuata. IsipokuwaWajumbe waliochaguliwa kwenye Mkutano wakwanza baada Uchaguzi Mkuu watashika nyadhifazao kwa muda uliobaki kumaliza Mwaka wa Fedhaambapo Uchaguzi utafanyika tena.

(6) Halmashauri inaweza wakati wowote kuvunja nakuunda upya Kamati ya Kudumu iliyoteuliwa kwamujibu wa Kanuni hii ya kudumu, endapo kufanyahivyo kutakuwa ni kwa manufaa ya Halmashauri.

(7) Hakuna Halmashauri itakayounda Kamati yaKudumu mpya zaidi ya Kamati zilizotajwa kwenyeKanuni ya 41(1) hapo juu, isipokuwa baada yakuomba na kupata idhini ya maandishi kutoka kwa

Page 37: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

37

Waziri.

(8) Maombi ya Halmashauri ya kuanzisha Kamatimpya ya Kudumu lazima yakidhi na yawe namaelezo yafuatayo;

(a) Upekee wa majukumu yanayoombewakuundwa kwa Kamati ya Kudumu mpya namajukumu hayo yawe ambayo hayawezikutekelezwa na Kamati za Kudumuzilizopo na zilizotajwa kwenye Kanuni ya41(1) hapo juu,

(b) Gharama za uendeshaji wa Kamati hiyokwa mwaka,

(c) Kuundwa kwa Kamati ya Kudumu hiyompya ni hitaji la lazima na ni kipaumbelecha Halmashauri na jamii kwa ujumla.

(9) Kamati yoyote itakayoundwa na Halmashauri bilaidhini ya Waziri itakuwa batili na maamuzi yakeyote yatakua batili.

MwenyekitiwaHalmashaurikuwaMjumbe waKamati moja

42. Mwenyekiti wa Halmashauri atakuwa Mjumbe waKamati zote za kudumu za Halmashauri.

Uwezo waKamati

43. Kamati zote za Halmashauri zitawasilisha taarifazao kwa Halmashauri, na hakuna hatuaitakayochukuliwa kutekeleza uamuzi wowote waKamati yoyote mpaka hapo taarifa ya Kamatihusika itakapokuwa imekubaliwa na Halmashauri,isipokuwa pale ambapo idhini ya kuchukua hatuaimekasimiwa kwa Kamati.

Kamati zapamoja

44. (1) Halmashauri inaweza kukubaliana na Halmashaurinyingine kuteua Kamati ya pamoja kutokana naWajumbe wao kwa madhumuni yoyote yaleambayo wana maslahi ya pamoja, na Halmashaurihizo zinaweza kukasimu kwa Kamati hiyo ya

Page 38: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

38

pamoja, kutegemea na masharti na mipakazitakazoweka kama watakavyoona inafaa,madaraka au kazi ya Halmashauri zinazohusiana namadhumuni yaliyozifanya ziunde Kamati hiyo,isipokuwa shughuli zile ambazo Halmashaurihaziruhusiwi kukasimu.

(2) Muundo na muda wa kazi wa Wajumbe wake namipaka ya eneo ambamo Kamati hiyo ya pamojaitafanya kazi, itapangwa na Halmashaurizinazoiteua.

(3) Kamati ya pamoja haitaingia katika gharamazozote zaidi ya zile ambazo zimeidhishwa namamlaka iliyoteua Kamati hiyo.

KukasimumadarakakwenyeKamati

45. (1) Kufuatana na Kanuni Ndogo ya (2) ya Kanuni hiipamoja na masharti mengine ambayo Halmashauriitaona inafaa, Halmashauri inaweza kukasimu kwaKamati uwezo wa kutekeleza kazi yoyote kwaniaba yake.

(2) Halmashauri haitakasimu kwa Kamati yoyoteuwezo wa:-

(a) Kutunga Sheria Ndogo;(b) Kuweka na kutoza kodi;(c) Kuidhinisha makadirio ya mapato na

matumizi ya Halmashauri;(d) Kutoza ada na ushuru;(e) Kuidhinisha mpango na Bajeti ya

Halmashauri;(f) Kuingia mikataba mbalimbali ikiwa ni

pamoja na mikataba ya kukopa,(g) Kupitisha mpango wa utoaji huduma.

(3) Kazi za kila Kamati ya Kudumu ya Halmashauri nikama zilivyoonyeshwa katika jedwali la Kanuni zakudumu hizi.

(4) Halmashauri inaweza kusitisha au kurekebisha

Page 39: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

39

uamuzi wa kukasimu madaraka yoyote kwaKamati, lakini usitishaji au urekebishaji huohautaathiri jambo lolote lililofanywa kutokana nauamuzi wowote uliochukuliwa kihalali na Kamati.

(5) Shughuli yoyote iliyotekelezwa na Kamatikutokana na kukasimiwa kwa mujibu wa Kanunihii itatambuliwa kuwa imefanywa au kutekelezwana Halmashauri.

KamatiNdogo

46. (1) Kamati yoyote au Kamati ya pamoja inawezakuteua Kamati Ndogo kutokana na Wajumbe wakekadri itakavyoona inafaa kwa ajili ya kuchunguzana kutoa taarifa kuhusu jambo lolote, lakini Kamatihaitakasimu madaraka yake ya kiutendaji kwaKamati Ndogo yoyote.

(2) Idadi ya Wajumbe wa Kamati Ndogo pamoja namuda watakaotumikia vitaamuliwa na Kamatiiliyoteua Kamati Ndogo hiyo.

(3) Mwenyekiti wa Kamati atakuwa Mjumbe waKamati Ndogo yoyote kwa mujibu wa wadhifawake isipokuwa kama atamfahamisha Mkurugenzikwa maandishi kuwa hatakuwa Mjumbe waKamati hiyo.

(4) Kila Kamati Ndogo inaweza kumteua mmoja waWajumbe wake kuwa Mwenyekiti wa KamatiNdogo husika.

Mikutano yaKamati

47. (1) Mkutano wa kwanza wa Kamati utaitishwa naMkurugenzi ndani ya mwezi mmoja baada yaKamati kuteuliwa na baada ya hapo kulingana naratiba ya Mikutano kama itakavyoidhinishwa naHalmashauri.

(2) Taarifa ya angalau saa ishirini na nne yenye ajendaza kikao itabidi kutolewa kwa Wajumbe kabla yaMkutano wa Kamati.

Page 40: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

40

(3) Idadi ya Kamati haitazidi idadi ambayo itawekwana Waziri kutokana na uwezo aliopewa chini yakifungu cha 75(3) cha Sheria.

Mwenyekitiwa Kamati

48. (1) Katika kikao chake cha kwanza baada ya Mkutanowa mwaka wa Halmashauri na kabla ya kuendeleana shughuli yoyote nyingine, kila Kamatiitamchagua Mwenyekiti wa Kamati kwa mwakaunaohusika.

(2) Mwenyekiti wa Kamati, isipokuwa Kamati yaFedha na Utawala, atachaguliwa kwa kura ya siriya Wajumbe walio wengi kwa kupiga kura ya sirikwenye eneo la faragha litakalotengwa naMkurugenzi kwa ajili hiyo.

(3) Mwenyekiti wa Halmashauri atakuwa piaMwenyekiti wa Kamati ya Fedha na Utawala.

(4) Endapo nafasi ya Mwenyekiti wa Kamati itakuwawazi katika kipindi cha mwaka husika, Mkurugenziatatoa taarifa kwa Wajumbe wote wa Kamati kuwakatika kikao kijacho cha kawaida cha Kamatihusika dondoo ya kumchagua Mwenyekiti waKamati kwa kipindi cha mwaka kilichosaliaitakuwa ya kwanza katika agenda.

Mkutanomaalum waKamati

49. (1) Mkutano Maalum wa Kamati utaitishwa baada yatheluthi mbili ya Wajumbe wa Kamati kuombakwa maandishi kuwa Mkutano huo ufanyike nakueleza sababu.

(2) Taarifa ya Mkutano Maalum wa Kamati itaonyeshashughuli itakayofanyika katika Mkutano huoMaalum huo na hakuna jambo jingine lolotelitakalojadiliwa katika Mkutano huo.

Ajenda zaKamati

50. Mjumbe wa Kamati atakuwa na haki ya hoja zakekuwekwa katika ajenda ya Kamati kama atatoa taarifa ya

Page 41: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

41

angalau siku nne kabla ya tarehe ya kikao.

MahudhuriokatikaMikutano yaKamati

51. (1) Mjumbe wa Kamati ya Kudumu au Kamati Ndogo,ambaye ameshindwa kuhudhuria Mkutano waKamati Ndogo, hataruhusiwa kutuma mtumwingine kumwakilisha kwenye Mkutano waKamati au Kamati Ndogo.

(2) Mjumbe wa Halmashauri hatakuwa na haki yakuhudhuria kikao chochote cha Kamati au KamatiNdogo ambamo yeye si Mjumbe, isipokuwa kamaKamati au Kamati Ndogo inayohusika imemwalikakuhudhuria, na hata hivyo hatakuwa na haki yakupiga kura au kudai posho kwa kuhudhuriaMkutano huo wa Kamati au Kamati Ndogo.

Mjenga hojakualikwakwenyeMkutano waKamati

52. Mjumbe wa Halmashauri anayewasilisha hoja ambayoimepelekwa kwenye Kamati atapewa taarifa ya Mkutanowa Kamati ambamo hoja yake imepagwa kuzungumzwa nakama atahudhuria atapewa nafasi ya kuizungumzia.

WaalikwawasiokuwaWajumbekuhudhuria nakushirikikatikaMikutano yaKamati

53. Mwenyekiti wa Kamati, Kamati ya pamoja au KamatiNdogo baada ya kushauriana na Wajumbe wa Kamati,Kamati ya pamoja na Kamati Ndogo, anaweza kumwalikamtu yeyote kuhudhuria na kuzungumza kwenye Mkutanokuhusu suala lolote au kushiriki kwa namna yoyote kwenyekikao cha Kamati, lakini mtu huyo atakayealikwa hatakuwana haki ya kupiga kura kwenye Mkutano huo.

Mahudhurioya umma navyombo vyahabarikwenyeMikutano yaKamati naKamatiNdogo

54. Majadiliano katika Kamati, Kamati ya pamoja au KamatiNdogo hayatakuwa wazi kwa umma na vyombo vya habari,isipokuwa kwa kutokana na azimio la Halmashaurilinaloruhusu kuwa umma na vyombo vya habarivihudhurie.

Athari zanafasi wazikwenyeKamati

55. (1) Kunapotokea nafasi wazi kwenye Kamati, Kamatiya pamoja au Kamati Ndogo, Kamati itaendeleakutekeleza shughuli zake licha ya kuwepo kwanafasi wazi hiyo au hizo au mpaka nafasi hiyo au

Page 42: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

42

hizo zitakapojazwa kwa njia ya uchaguzi au uteuzi.Mjumbe atakayejaza nafasi hiyo atashika nafasiwazi hiyo kwa kipindi kilichosalia cha Mjumbeambaye nafasi yake imekuwa wazi.

(2) Uhalali wa tendo lolote au maamuzi ya Mkutanowowote wa Kamati hautaathiriwa kutokana nahitilafu katika uteuzi wa Mjumbe aliyeshika nafasihiyo au nafasi hizo kuachwa wazi na Mjumbe, auWajumbe au Mjumbe au Wajumbe kuamua kutokakwenye kikao kwa lengo la kukwamisha jambolinalotaka kutolewa maamuzi na Kamati hiyo.

Akidi kwenyeMikutano yaKamati

56. Endapo Wajumbe waliohudhuria Mkutano hawatafikiaakidi ya Mkutano, Mkurugenzi ataahirisha Mkutano huo nakuuitisha tena ndani ya siku saba (7) na endapo akidihaitatimia tena, idadi yoyote ya Wajumbe waliohudhuriaitatengeneza akidi ya Mkutano ambapo mkutano huoutaendelea na utakuwa halali na Mkurugenzi atamjulishaWaziri kuwepo kwa hali hiyo.

Kanuni zakudumukatikaMikutano yaKamati

57. (1) Kanuni ya 17 ya Kanuni hizi za Kudumuitatumika,baada ya kufanya marekebishoyanayostahili, kwenye Mikutano ya Kamati zaHalmashauri.

(2) Mjumbe anapozungumza katika Mkutano waKamati atakuwa ameketi na anaweza kuzungumzazaidi ya mara mbili juu ya jambo linalojadiliwa.

Upigaji kurakwenyeMikutano yaKamati

58. Masuala yote yanayoletwa mbele ya Kamati yataamuliwakwa wingi wa kura za Wajumbe waliohudhuria na kupigakura kwenye Mkutano husika. Endapo kunatokea kuramlingano mtu anayeongoza kikao hicho atakuwa na kura yaturufu.

Mihtasari yaKamati

59. (1) Muhtasari wa kila Kamati, Kamati ya pamoja naKamati Ndogo, utajumuisha majina ya Wajumbewaliohudhuria na wasiohudhuria, na utasainiwakwenye Mkutano unaofuata na mtu aliyeongozaMkutano na muhtasari uliosainiwa hivyo, kama

Page 43: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

43

hakuna ushahidi wa kuwa una makosa,utapokelewa kwa ushahidi bila uthibitisho zaidi.

(2) Hakuna hoja au mjadala utakaoendeshwakuhusiana na muhtasari wa Kamati isipokuwakuhusu usahihi wa suala lolote linalohusu usahihilitatolewa kwa hoja.

Kufikiriwaupyamaamuzi

60. Pale ambapo suala lililowasilishwa limeamuliwakwa mujibu wa Kanuni ya 58, suala hilo halitaanzakujadiliwa upya katika Mkutano huo wa Kamatiisipokuwa kama hoja hiyo inaungwa mkono natheluthi mbili ya Wajumbe waliohudhuria nakupiga kura.

Kutunza sirizamajadilianoya Kamati naKamatiNdogo

61. Mjumbe wa Kamati au Kamati Ndogo hatatoa njejambo lolote lililoletwa au kuzungumzwa kwenyeKamati au Kamati Ndogo bila ruhusa ya Kamatihiyo, au kuzungumza kwenye Kamati Ndogompaka hapo Kamati hiyo au Kamati Ndogo hiyoitakapokuwa imetoa taarifa kwenye Halmashauriau itakapokuwa imekamilisha utekelezaji wa jambohilo.

Kujiuzuluwadhifa waMwenyekitiwa Kamati

62. Mwenyekiti wa Kamati anaweza kujiuzulu wadhifawake kwa kutoa taarifa ya maandishi aliyoisaini nakutuma kwa Mkurugenzi.

Kujiuzuluujumbe waKamati nakujazwa kwanafasiiliyowazi

63. (1) Mjumbe yeyote wa Kamati anaweza kujiuzuluwadhifa wake kwa kutoa taarifa ya maandishialiyoisaini na kuituma kwa Mkurugenzi.

(2) Nafasi inayotokana na kujiuzulu kwa Mjumbeitajazwa na Halmashauri katika kikao chake chakawaida baada ya tarehe ya kujiuzulu kwaMjumbe.

Page 44: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

44

SEHEMU YA VUNUNUZI WA VIFAA, UPATIKANAJI WA

HUDUMA NA UJENZI

Taratibu zauagizaji Suraya 290

64. (1) Uagizaji wa mali, huduma na ujenzi katikaHalmashauri utazingatia Kanuni za Manunuzizilizotungwa chini ya kifungu cha 68 cha Sheria zaFedha za Serikali za Mitaa,Sura ya 290 na Sheriaya Manunuzi ya mwaka 2011.

(2) Kutakuwepo na Bodi ya Zabuni ambayoimeanzishwa kwa mujibu wa Kanuni za Bodi yaZabuni (Uanzishwaji na Mwenendo) za Serikali zaMitaa na ambayo itasimamia shughuli zote zauagizaji katika Halmashauri.

(3) Muhtasari wa Bodi ya Zabuni utapaswakuwasilishwa kwenye kikao kifuatacho chaHalmashauri baada ya muhtasari huo kujadiliwa nakupitishwa kwanza na Kamati ya Fedha naUtawala.

Kumbukumbu zamajadilianoyanayohusuuagizaji

65. Bodi ya Zabuni ya Halmashauri itawekakumbukumbu ya majadiliano yanayohusu taratibuza ununuzi zikiwa na angalau taarifa zifuatazo:-

(a) Maelezo mafupi kuhusu vitu, ujenzi auhuduma zinazotarajiwa kutolewa na hajailiyosababisha Bodi kuitisha zabuni.

(b) Majina na anuani ya Wazabuniwaliowasilisha zabuni, maelezo kuhususifa au ukosefu wa sifa za wazabuniwaliowasilisha zabuhi zao.

(c) Bei au msingi wa upangaji wa bei namuhtasari wa masharti mengine muhimuya kila zabuni na ya kila mkataba wauagizaji wa mali, huduma na ujenzi.

(d) Muhtasari wa tathmini na mlinganisho wazabuni pamoja na upendeleo uliokuwepokatika tathmini hiyo.

Page 45: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

45

(e) Kama zabuni zilikataliwa tamko kuhusuuamuzi huo na sababu za uamuzi huo.

(f) Kama utaratibu mwingine wa kupata vituau huduma mbalimbali ya utaratibu wazabuni ndio uliotumika, basi tamko kuhususababu zilizoifanya Bodi iamue kutumiautaratibu huo mwingine.

(g) Kama zabuni ilikataliwa kwa kuwamzabuni alitoa, alikubali kutoa moja kwamoja au kwa njia isiyo ya moja kwa moja,kwa mtumishi wa sasa au wa zamani waHalmashauri, bakshishi ya aina yoyote,ahadi ya kumwajiri au kitu chochotekinachohusiana na ajira au chenye thamani,kama hamasisho kwa utendaji au uamuziau utaratibu wa kutumia, tamko kuhusujambo hilo.

(h) Katika upataji wa huduma, sababu na haliiliyoifanya Bodi kuchagua utaratibu wakutumia katika upataji huo wa huduma.

(i) Katika upataji wa vitu au huduma ambaoBodi imeamua kudhibiti ushiriki kwamisingi ya Taifa, Mkoa au Wilaya, tamkokuhusu sababu na hali iliyofanya Bodikudhibiti ushiriki huo.

(j) Katika upataji wa vifaa na huduma kwakuwaomba watoaji kutoa mapendekezoyao moja kwa moja tamko la sababu nahali iliyofanya Bodi kuamua kutumiautaratibu huo, na

(k) Muhtasari wa maombi yoyote ya ufafanuzikuhusu mchujo wa zabuni au nyaraka zazabuni na majibu yaliyotolewa pamoja namuhtasari wa marekebisho yoyoteyaliyofanywa katika nyaraka hizo.

(2) Sehemu ya kumbukumbu zilizotajwa kwenyeKanuni Ndogo ya (1) (a) na (b) ya Kanuni hiizitatolewa, kama zikiombwa, kwa mtu yeyotebaada ya zabuni kutangazwa, kufunguliwa na

Page 46: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

46

kukubaliwa, au baada ya kusimamishwa kwataratibu za uagizaji bila ya kuingia katika mkatabawa uagizaji.

(3) Sehemu ya kumbukumbu zilizoelekezwa katikaKanuni Ndogo ya (1) (c) hadi (g) ya Kanuni hiikama itaombwa, itatolewa kwa wazabuniwaliowasilisha zabuni baada ya zabuni kukubaliwaau baada ya kusitishwa bila ya kuingia kwenyemkataba wa utoaji wa vitu au huduma.

(4) Isipokuwa kama itaelekezwa hivyo na mahakamayenye mamlaka na kutegemeana na masharti yamaelekezo hayo, Bodi haitatoa habari-

(a) kama utoaji huo wa habari utakuwakinyume cha Sheria; utazuia utekelezaji waSheria; hautakuwa na maslahi kwa umma;utahatarisha maslahi halali ya kibiashara yawahusika au utazuia ushindani halali; na;

(b) habari zinazohusu uchambuzi, tathmini naulinganisho wa zabuni pamoja na bei mbaliya muhtasari ulioelezwa kwenye KanuniNdogo ya (1) (e) ya Kanuni hizi.

(5) Mara baada ya zabuni kujadiliwa na Bodi, Katibuatamjulisha Mzabuni aliyefanikiwa ili makubalianoya nyaraka za mkataba yaweze kufikiwa.

(6) Nakala za muhtasari zitapelekwa kwa siri kwa kilaMjumbe wa Bodi, Mkurugenzi, Mweka Hazina,Mkaguzi wa Ndani na Mkuu wa Idara husika kwataarifa na kumbukumbu.

(7) Kila mzabuni ambaye hakufanikiwa atajulishwa naakiomba sababu za kutokubaliwa kwa zabuni yakeatapaswa kupewa sababu.

(8) Bodi ya Zabuni kwa kuzingatia masharti ya Kanuniza uagizaji itaandaa taarifa ya mwenendo na

Page 47: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

47

maamuzi ya zabuni zilizoitishwa na kuwasilishwakwenye Mkutano wa kawaida wa Halmashaurikupitia Kamati ya Kudumu husika.

Uzuiaji warushwa

66. Katika mkataba wowote wa kimaandishi,yatawekwa maneno ambayo yataonyesha kuwaHalmashauri itakuwa na haki kusitisha mkataba nakumdai Mkandarasi malipo ya fidia kutokana nakusimamishwa kwa mkataba huo endapoMkandarasi atabainika kuwa ameahidi kutoa auametoa, au amekubali kutoa kwa mtu yeyotezawadi yoyote au upendeleo wa aina yoyote kamakishawishi au zawadi kwa kufanya au kumpendeleaau kutomkubali mtu yeyote kuhusiana na mkatabana Halmashauri au kama vitendo hivyo vitakuwavimefanywa na mtumishi yeyote aliyeajiriwa nayeau kwa niaba yake iwe Mkandarasi anafahamu auhafahamu atakuwa ametenda kosa chini ya Sheriaya Kuzuia na Kudhibiti Rushwa ya mwaka 2007.

Usimamiajiwa mikataba

67. (1) Mkurugenzi wa Halmashauri atawajibika katikausimamiaji na ufuatiliaji mzuri wa Mikataba.

(2) Mkataba wa upataji vitu hautabadilishwa kwanamna yoyote ile baada ya kutiwa saini na pandezonazohusika isipokuwa kama mabadiliko hayo ni-

(a) kwa faida ya Halmashauri na hayaileteihasara Halmashauri;

(b) yamethibitishwa na Bodi ya zabuni yaHalmashauri; na

(c) Upande mwingine unaafiki.

(3) Malipo ya mwisho hayatafanywa mpaka mkatabamzima utakapokuwa umekamilika kutokana nakuridhika kwa Halmashauri na kulingana navipengele vya mkataba unaohusika.

(4) Malipo ya fedha za salio hayatalipwa mpaka upitemuda wa miezi sita na kazi iwe haina kasoro.

Page 48: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

48

Uvunjaji wamkataba

68. Pale ambapo mkataba uliotiwa lakiri/muhuri naHalmashauri haukufuatwa na mkandarasi, ikiwa nipamoja na ucheleweshaji usiokuwa wa kimsingi,Mkurugenzi atashauriana mapema iwezekanavyona Kamati ya Fedha na Utawala kwa kuzingatiataratibu zilizowekwa kwenye mkataba, itaamuahatua muafaka za kuchukua na kumfahamishaMkandarasi juu ya uamuzi.

Rejesta yamikataba

69. (1) Mkurugenzi atatunza maelezo yote ya mikatabakwenye rejesta ya mikataba na atafanya ulinganifuwa malipo halisi na yale yaliyoidhinishwa.

(2) Taarifa ya matumizi yote ya ziada lazimayapelekwe kwenye Bodi ya Zabuni yakiambatanana maelezo kutoka kwa Mkurugenzi.

Diwani/Afisakutokuwa namaslahikatikamikataba

70. (1) Endapo Diwani au Afisa wa Halmashauri anamaslahi ya kifedha ya moja kwa moja auvinginevyo katika mkataba wowote, mkatabaunaopendekezwa au jambo lolote, na yupo kwenyeMkutano wa Halmashauri au Kamati ambapomkataba huo, au mkataba unaopendekezwa aujambo lingine lolote linajadiliwa, atatangaza jambohilo mara Mkutano utakapokuwa umeanza nahatashiriki wala kuwepo katika majadiliano aukupiga kura kuhusu jambo linalohusu mkataba aumkataba unaopendekezwa au jambo lingine loloteambalo ana maslahi nalo.

(2) Kanuni hii haitatumika kuhusiana na maslahikatika mkataba au suala lingine ambalo Mjumbe auAfisa wa Halmashauri ana maslahi nalo kamamlipa kodi au mkazi katika eneo lililo katikahimaya ya Halmashauri.

(3) Diwani atahesabika kuwa na maslahi ya moja kwamoja katika mkataba au jambo jingine endapo-

(a) yeye au mtu aliyemchagua ni Mjumbe wa

Page 49: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

49

kampuni au chombo kingine au anayo hatiya hisa katika kampuni ambayo itaingia, auimependekezwa iingie katika mkataba, auanao uhusiano wa kifedha katika jambolinalojadiliwa; au

(b) yeye ni mbia au ameajiriwa na mtu ambayemkataba unafanywa naye, au utakuwachini yake, au anao uhusiano wa kifedhawa moja kwa moja katika sualalinalojadiliwa au kuzungumzwa.

(4) Katika Kanuni hii maslahi ya moja kwa moja nayasiyo ya moja kwa moja ya mwanandoa au nduguwa familia kama inafahamika kwa Mjumbe waHalmashauri itachukuliwa kuwa ni maslahi yamoja kwa moja au yasiyo ya moja kwa moja.

(5) Taarifa ya jumla itakayotolewa kwa Mkurugenzi naDiwani au Afisa wa Halmashauri kuhusiana nayeye, mkewe, mumewe au ndugu yake kwambaana maslahi ya moja kwa moja au yasiyo ya mojakwa moja katika mkataba unaokusudiwa au jambolingine na akieleza aina ya maslahi itachukuliwa,isipokuwa pale atakapoondoa taarifa hiyo, kuwaametoa taarifa ya kutosha ya maslahi yakekuhusiana na suala ambalo limo katika mjadala.

(6) Mkurugenzi ataandika taarifa za watu wenyemaslahi waliotoa taarifa chini ya Kanuni Ndogo ya(1) na taarifa yoyote iliyomo katika Kanuni Ndogoya (5) itakuwa wazi kwa ukaguzi wakati wa saa zakazi.

(7) Halmashauri inaweza baada ya kupata kibali chaWaziri, kuondoa kizuizi chini ya Kanuni hiikinachoifanya ishindwe wakati wowote kufanyaMkutano pale ambapo idadi ya Wajumbe wenyemaslahi ni kubwa mno kiasi cha kukwamishashughuli za Halmashauri au itakuwa ni kwa

Page 50: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

50

maslahi ya wakazi wa Halmashauri kuondoakikwazo hicho.

(8) Katika Kanuni za Kudumu hizi ,ndugu wa familiaitachukuliwa kuwa ni pamoja na baba, mama,mtoto, kaka, au dada na wanandoa wao.

SEHEMU YA VIMASUALA MENGINE

Kiapo nakukubaliwadhifa

71. Kila Diwani kabla ya kushika wadhifa wake kamaDiwani na kabla ya Mkutano wa kwanza waHalmashauri:-

(a) atakula kiapo kama kilivyoonyeshwakwenye nyongeza ya kwanza ya Kanunihizi za kudumu kitakachosimamiwa naHakimu Mkazi au Hakimu wa Wilaya; na

(b) atatoa tamko la kimaandishi lililoandikwakwa Mkurugenzi akiahidi kutekelezajambo linalohusiana na tamko la maslahikatika shughuli za kibiashara, mali, nakadhalika na kuzifuata Kanuni za Maadiliya Madiwani.

Majukumu yaDiwani

72. (1) Diwani atakuwa na majukumu yafuatayo:-(a) kuwa karibu na wapiga kura na kupata

ushauri wa Wananchi katika mamboyanayotarajiwa kujadiliwa kwenyeHalmashauri.

(b) kutoa maoni na mapendekezo ya wananchikwa Halmashauri.

(c) kuhudhuria Mikutano ya Halmashauri naya Kamati au Kamati Ndogo ambamo yeyeni Mjumbe.

(d) kutenga angalau siku moja kila mwezikukutana na wananchi katika eneo lake lauchaguzi.

(e) kutoa taarifa kwa wapiga kura kuhusu

Page 51: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

51

maamuzi ya jumla ya Halmashauri nahatua zilizochukuliwa na Halmashaurikuondoa matatizo yaliyowahi kuelezwa nawakazi wa eneo lake la uchaguzi.

(f) kuchangia ujuzi na uzoefu wake katikamajadiliano yanayofanyika katikaMikutano ya Halmashauri na Kamati zaHalmashauri, na

(g) kushiriki katika shughuli za pamoja zamaendeleo katika eneo lake la uchaguzi nakatika eneo zima la Halmashauri.

(2) Katika kutekeleza wajibu wake diwani atazingatia-

(a) Maslahi ya Taifa na maslahi ya Wananchikatika eneo la Halmashauri;

(b) Katiba, Sheria na Kanuni;

(c) Kanuni za Maadili ya Madiwani,Mwongozo juu ya mahusiano ya Madiwanina Watumishi na miiko mingine.

Nafasi wazi 73. (1) Kiti cha Mjumbe wa Halmashauri kitakuwa waziendapo Mjumbe-

(a) amefariki;(b) anakubali ajira kama mtumishi wa

Halmashauri;(c) kwa mujibu wa Sheria yoyote anatangazwa

kuwa hana akili timamu;(d) yuko chini ya hukumu ya kifo au kifungo

kinachozidi miezi sita kilichotolewa kwakena mahakama;

(e) kwa mujibu wa Sheria yoyote anatamkwakuwa anapoteza sifa za kuendelea kuwaMjumbe;

(f) atakoma kuwa mwanachama wa chama chasiasa kilichompendekeza kuwa mgombea

Page 52: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

52

wa kiti cha udiwani;(g) anapokuwa amepatikana na kosa kutokana

na Kanuni za Maadili ya Madiwani naadhabu ya kosa alilotenda ni pamoja nakumwondoa Mjumbe madarakani; na

(h) anapoteza ujumbe kwa mujibu wa Kanuniya 71 (2) ya Kanuni hizi za kudumu;

(i) anahukumiwa kwa kosa la kutotaja maslahiyake.

(j) amejiuzulu kutoka kiti chake;(k) Halmashauri imevunjwa na kuathiri

mipaka ya majimbo ya uchaguzi;(l) uchaguzi wa Mjumbe umetangazwa kuwa

batili;au(m) bila sababu ya kuridhisha au bila idhini au

kibali cha maandishi cha Mwenyekiti,Mjumbe anakosa kuhudhuria Mikutanomitatu ya kawaida inayofuatana yaHalmashauri au Kamati ambamo yeye niMjumbe.

(2) Waziri atatangaza kiti kuwa wazi paleatakapojulishwa na Mwenyekiti wa Halmashaurikwa maandishi kwamba kiti kiko wazi kwakuzingatia masharti ya kifungu cha 42 (1) chaSheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Miji) Suraya 288.

KutokuwepokwaWajumbe

74. (1) Halmashauri yaweza kutoa idhini ya kutokuwepokatika Mikutano yake kwa muda usiozidi miezikumi kwa Mjumbe yeyote anayetaka kwenda njeya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

(2) Pale ambapo Mjumbe kwa sababu yoyote ileamekuwa nje ya nchi kwa muda unaozidi miezikumi kiti chake cha udiwani kitachukuliwa kuwakipo wazi.

Page 53: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

53

Taratibu zakutungaSheria Ndogo

75. (1) Pale ambapo Halmashauri inakusudia kutungaSheria Ndogo itatoa tangazo kwa wakazi wa eneohusika kuhusu kusudio hilo katika namna ambayoitahakikisha kuwa watakaoathirika na SheriaNdogo inayokusudiwa kutungwa wanafahamuvilivyo na kuwaomba wanaopenda kutoa pingamizilolote au mapendekezo yao kwa maandishi katikamuda uliowekwa.

(2) Pale ambapo baada ya muda wa taarifa kumalizikahakuna pingamizi au malalamikoyaliyowasilishwa, au hakuna mtu yeyote aliyetoakipingamizi kinachokubalika mbele yaHalmashauri, Halmashauri itaendelea kutungaSheria Ndogo ikizingatia malalamiko na pingamizizilizotolewa.

(3) Sheria Ndogo zikishatungwa na Halmashaurizitapelekwa kwa Waziri ili aweze kuziidhinisha.

(4) Waziri anaweza kuidhinisha, kukubali au kukataakuidhinisha Sheria Ndogo au kutoa aukusimamisha kibali chake kwa kutoa mashartiatakayoyaeleza na anaweza baada ya kutoa idhiniyake, kupanga tarehe ya kuanza kutumika kwaSheria Ndogo hizo.

(5) Waziri anaweza, kabla ya kuidhinisha SheriaNdogo zenye athari kwenye maeneo yaliyotengwaau maeneo maalum au kwa Sheria nyingine yoyote,kushauriana na Waziri anayehusika na Sheriahusika au na jambo lililotungiwa Sheria Ndogokadri itakavyokuwa.

(6) Sheria Ndogo yoyote iliyotungwa na Halmashaurilazima itangazwe katika Gazeti la Serikali kabla yakuanza kutumika.

Page 54: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

54

Ukaguzi wanyaraka

76. (1) Mjumbe ataweza, kwa madhumuni ya kutekelezawajibu wake kama Mjumbe, na si vinginevyo,kukagua waraka wowote ambao umejadiliwa naKamati ya Halmashauri na kama nakalazinapatikana, anaweza kupewa, akiomba, nakalakwa madhumuni hayo hayo.

(2) Mjumbe hatakagua kwa makusudi au kutaka apewenakala ya waraka wowote unaohusu jambo ambaloyeye ana maslahi nalo kwa mujibu wa Sheria yaSerikali za Mitaa (Mamlaka za Miji), Sura ya 288.Hata hivyo Kanuni hii haitamzuia Mkurugenzikuzuia kukaguliwa kwa waraka wowote ambaoumezuiliwa kutolewa kwa mujibu wa Sheriayoyote au Kanuni zilizotungwa chini ya Sheriahizo.

Uanzishaji waBodi zaHuduma

77. (1) Halmashauri inaweza, kwa mujibu wa kifungu 88cha Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Miji),Sura ya 288 kwa madhumuni ya kutekeleza kazizake katika eneo lililo chini ya mamlaka yake,kuunda Bodi za Huduma kwa hati rasmiiliyotangazwa kwenye Gazeti la Serikali, kamaitakavyoona inafaa kufanya hivyo.

(2) Bodi ya Huduma iliyotajwa katika Kanuni Ndogoya (1) ya Kanuni hizi itawajibika moja kwa mojakwenye Halmashauri kupitia Kamati ya Kudumuhusika na itatekeleza kazi zake kamailivyofafanuliwa katika hati inayoianzisha.

Diwanikutembeleamaeneo,shughulimbalimbali zaujenzi n.k

78. (1) Mjumbe wa Halmashauri anaweza kutembeleaeneo, jengo au shughuli za ujenzi zinazotekelezwana au kwa niaba ya Halmashauri na anawezakutuma taarifa kwa Mkurugenzi akieleza sababu zamatembezi yake ili aweze kupangiwa Wataalam wamradi au shughuli husika kwa ajili kupatamaelekezo ya kitaalam.

Page 55: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

55

(2) Mjumbe wa Halmashauri anapotembelea shughuliau miradi ya maendeleo inayotekelezwa na au kwaniaba ya Halmashauri hataruhusiwa kutoamaelekezo au maagizo ya kitaalam awapo kwenyeeneo la mradi.

(3)

(4)

Baada ya diwani kutembelea maeneo au majengokama ilivyoainishwa kwenye Kanuni Ndogo ya (1)ya Kanuni hii anaona kuna umuhimu wa kutoamaoni au mang’amuzi yake juu ya matembezi hayoatafanya hivyo kwa kuwasilisha maoni aumang’amuzi yake kwa Mkurugenzi ambayeatafanyia kazi au kuyapeleka kwa afisaanayesimamia kazi husika kwa utekelezaji;

Endapo maoni au mang’amuzi ya Diwanihayawezi kufanyiwa kazi na Mkurugenzi au Afisamhusika, basi atamshauri diwani kupeleka maonina mang’amuzi yake kwa Kamati inayohusika iliyachunguzwe zaidi na kuamuliwa.

(5) Kamati za Kudumu za Halmashauri zinawezakutembelea miradi ya maendeleo au shughuliyoyote inayotekelezwa na au kwa niaba yaHalmashauri ili mradi katika kutembelea miradihiyo Kamati itaongozana na Wataalam wa mradiau shughuli husika ili kupata maelekezo yakitaalam.

(6) Kamati ya Kudumu itatembelea miradi au shughuliza maendeleo kabla ya Kikao cha Kamati ambachokitajadili mradi au shughuli hiyo.

Uhifadhi waLakiri yaHalmashauri

79. Lakiri ya Halmashauri itatunzwa kwa usalama nakufungiwa katika Kasiki kwenye Ofisi yaMkurugenzi mwenyewe.

Utiaji muhurikwenyenyaraka

80. (1) Lakiri ya Halmashauri haitabandikwa katika Hatiyoyote mpaka ubandikaji huo umeidhinishwa naazimio la Halmashauri likiidhinisha kukubaliwa

Page 56: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

56

kwa zabuni, ununuzi, uuzaji au upangishaji aukuchukua mali yoyote, utoaji wa Hati yoyote yaukopeshaji fedha, uwasilishaji wa madai yoyote,uwekaji wa viwango vya kodi, uingiaji kwenyemkataba, kutunga Sheria Ndogo, au hati yototeiliyo rasmi ambayo kwa mujibu wa Sheria auKanuni yoyote inahitaji kuwekwa lakiri yaHalmashauri.

(2) Lakiri itashuhudiwa au kuthibitishwa naMwenyekiti au MakamuMwenyekiti naMkurugenzi, na hati zilizowekwa lakiri zitasainiwana Mwenyekiti au MakamuMwenyekiti, kama haliitakavyokuwa.

Uandikishajiwa anuani

81. (1) Itakuwa wajibu wa kila Mjumbe katika kikao chakwanza cha Halmashauri, baada ya uchaguzi kutoataarifa ya maandishi kwa Mkurugenzi juu yaanuani yake ya kudumu ya kupokelea taarifa.Taarifa zilizopelekwa kwa kutumia anuaniiliyoandikishwa itachukuliwa kama ndiyo sahihi nainatosheleza kwa matumizi yote.

(2) Iwapo Mjumbe atatoa taarifa ya maandishi kwaMkurugenzi kuwa angependa taarifa ya Mikutanoya Halmashauri iwe inatumwa kwake kwa kutumiaanuani atakayoitaja kwenye taarifa hiyo ambayo nitofauti na ile katika Kanuni Ndogo ya (1), taarifayoyote itakayoachwa au itakayotumwa kwa njia yaposta kwa kutumia anwani hiyo itachukuliwa kuwainatosha kwa ajili ya kutoa taarifa inayotakiwa kwamujibu wa Kanuni za Kudumu hizi.

Uteuzi waWajumbekwenyetaasisi za nje

82. (1) Katika Mkutano wake wa kwanza, Halmashauriitateua wawakilishi wake kwenye Bodi na Taasisiza nje ambazo Halmashauri inastahilikuwakilishwa.

(2) Mjumbe au Wajumbe, wanaoiwakilishaHalmashauri kwenye Bodi na Taasisi za nje,

Page 57: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

57

watatakiwa kuwasilisha kwa Mkurugenzi taarifakuhusu shughuli za Bodi au Taasisi zinazogusaSera na maslahi ya Halmashauri na wakazi wakekijumla na Mkurugenzi atachukua hatua zifaazo.

KumwondoaMwenyekitimadarakani

83. (1) Halmashauri inaweza kumwondoa Mwenyekitimadarakani kwa azimio linaloungwa mkono natheluthi mbili ya Wajumbe kutokana na hoja ausababu yoyote kati ya sababu zifuatazo:-(a) Kutumia nafasi yake vibaya;(b) Kushiriki katika vitendo vya rushwa;(c) Kushindwa kutekeleza majukumu yake(d) Mwenendo mbaya au ukosefu wa adabu;

au(e) Ulemavu wa kimwili au kiakili kwa kiasi

cha kumfanya kushindwa kutekelezamajukumu yake kama Mwenyekiti.

(2) Hoja au sababu zitakazotolewa lazima iweimetimiza masharti yafuatayo:(i) Iwe na tuhuma mahsusi yenye ushahidi wa

kutosha(ii) Iwe imetolewa maelezo kamili na yenye

kueleweka kuhusu tuhuma zinazohusika.

(3) Kwa madhumuni ya kumwondoa Mwenyekitimadarakani, kwa sababu zozote zilizotamkwa chiniya Kanuni Ndogo ya (1) ya Kanuni hii,Halmashauri itatumia taratibu zilizotolewa katikaTaratibu za Kumwondoa Mwenyekitizilizotangazwa kwenye gazeti la Serikali na Wazirikwa mujibu wa Sheria.

SEHEMU YA VIIPOSHO KWA WAJUMBE

Aina za posho 84. (1) Wajumbe wa Halmashauri watalipwa poshombalimbali kama itakavyopendekezwa naHalmashauri na kuidhinishwa na Waziri.

Page 58: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

58

(2) Posho zitakazolipwa kwa Wajumbe waHalmashauri zitakuwa za aina zifuatazo-(a) Posho ya usafiri;(b) Posho ya kuhudhuria kikao;(c) Posho ya madaraka;(d) Posho ya kujikimu;(e) Posho ya mwezi.(f)Kiinua mgongo

(3) Endapo Mjumbe wa Halmashauri ataugua auataumia wakati akifanya kazi aliyotumwa naHalmashauri, gharama za matibabu yake zitalipwana Halmashauri.

Posho endapoMkutanoutaahirishwa

85. Endapo Mkutano wa Halmashauri au Kamatiutaahirishwa kwa sababu ya kukosekana kwa akidi,Mjumbe au Wajumbe waliofika kwa ajili yakuhudhuria Mkutano huo ulioahirishwa watastahilimalipo yaliyotajwa katika Kanuni ya 84 (2) (a) na(d) iwapo wamelazimika, bila kukusudia, kulalanjiani au kwenye Makao makuu ya Halmashauri.Hakuna malipo ya posho ya kuhudhuria kikaoyatakayofanywa katika hali ya namna hiyo.

SEHEMU YA VIIIMABADILIKO KWENYE KANUNI ZA

KUDUMU

Kusitishautumiaji waKanuni zaKudumu

86. (1) Kanuni yoyote inaweza kusitishwa kwa azimiolililoungwa mkono na theluthi mbili za Wajumbewaliohudhuria Mkutano wa Halmashauri kwa hojailiyopendekezwa bila taarifa kwa madhumuni yakuwezesha shughuli yoyote iliyofafanuliwa iliishughulikiwe na Halmashauri kama jambo ladharura au lenye manufaa.

(2) Halmashauri haitasitisha matumizi ya Kanuniyoyote kama kusitisha huko kutasababisha kufanyajambo ambalo limezuiliwa na Sheria au kutofanyajambo linalotakiwa kufanywa chini ya Sheria

Page 59: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

59

yoyote.

Marekebishona mabadilikoya Kanuni zaKudumu

87. Halmashauri inaweza kubadilisha, kuongeza,kurekebisha au kutengua Kanuni hizi za kudumukwa azimio lililoungwa mkono kwa wingiusiopungua theluthi mbili ya kura na baada yakupata idhini ya Waziri.

Kanuni zaKudumukutolewa kwaWajumbe

88. Nakala iliyochapishwa ya Kanuni za Kudumu hizizitatolewa na Mkurugenzi kwa kila Mjumbe.

KutafsiriKanuni zaKudumu

89. Uamuzi wa Mwenyekiti kuhusu maana yamatumizi ya Kanuni hizi au mwenendo waMkutano wa Halmashauri hautapingwa wakati waMkutano wowote wa Halmashauri.

SEHEMU YA IXZIARA ZA WAJUMBE

Ziara zaWajumbe

90. (1) Wajumbe wa Halmashauri wanaweza kwenda ziarambalimbali za mafunzo ili mradi ziara hizo ziwezimeainishwa kwenye mpango na Bajeti yaHalmashauri. Isipokuwa kwa ziara ambazogharama zake hazihusiani na Bajeti yaHalmashauri, Wajumbe watafanya ziara hizo kwamujibu wa ratiba ya mpango huo.

(2) Bila kuathiri masharti ya Kanuni Ndogo ya (1) yakanuni hii Halmashauri kabla ya kuruhusukufanyika kwa ziara itahaikikisha kwamba-

(a) shughuli ya ziara hiyo inafanana nashughuli zinazofanywa na Halmashauri;

(b) ziara hiyo inapata kwanza kibali cha Mkuuwa Mkoa;

(c) Wajumbe wanakitu cha kwenda kuonyeshakule wanakokwenda kujifunza;

(d) ziara zinazofanyika nje ya Mkoa zihusishe

Page 60: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

60

wadau mbalimbali wa Halmashaurikutegemeana na ziara husika.

(e) ziara iwe na matunda yanayoonekana;(f) Wajumbe walioshiriki kwenye ziara

warejeapo wanatakiwa kuandaa nakuwasilisha ripoti ya maandishi kwaHalmashauri kuhusu mambo mapya na yamsingi waliyojifunza na kuweka utaratibumzuri wa kuyatekeleza kwenye Kata zaona kwenye Halmashauri;

(g) Ziara zinafanywa kwa vikundi vyaWajumbe wachache kadriitakavyokubalika na Halmashauri.

Wimbo waTaifa,Dua/Sala yakuiombeaHalmashauri

91. Kabla ya kuanza kwa Mkutano wa Halmashauri,utaimbwawimbo wa Taifa na kufuatiwa na Dua au Sala ya kuiombeaHalmashauri ifuatayo;

“Ewe MWENYEZI MUNGU Mtukufu, Muumba waMbingu na Dunia umeweka katika Dunia Serikali zaWanadamu ili haki yako itendeke. Twakuomba,uibariki Halmashauri ya Mji wetu wa Mafingaidumishe uhuru, umoja, haki na amani. Uwajalieviongozi wetu wa Halmashauri ya Mji hekima, afyanjema na maisha marefu ili pamoja na wanaowashauriwadumishe utawala bora. Utuongezee hekima nabusara sisi Madiwani wa Halmashauri ya Mji waMafinga na utupe uwezo wa kujadili kwa dhati, mamboyatakayoletwa mbele yetu leo, ili tufanye maamuzisahihi yenye manufaa kwa watu wote na ustawi waHalmashauri ya Mji wetu. Amina”.

Page 61: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

61

JEDWALIChini ya Kanuni ya 42(3)

HADIDU ZA REJEA ZA KAMATI ZA KUDUMUZA HALMASHAURI ZA MIJI

Madhumuni ya jumla:

1. Kuishauri Halmashauri kutengeneza malengo yanayozingatia matakwaya Miji na kuchukua hatua ambazo zitaonekana zinafaa ili kufikiamalengo yaliyokusudiwa.

2. Kuishauri Halmashauri kufanya maamuzi juu ya Sera muhimu.3. Kuishauri Halmashauri kufanya maamuzi juu ya utoaji wa huduma

kulingana na rasilimali walizo nazo.4. Kuiwezesha Halmashauri kutengeneza taratibu zitakazoongoza utendaji

wa Kamati, Kamati Ndogo, na ule wa watumishi ili watimize wajibuwao.

5. Kufanya mapitio yatakayowezesha Halmashauri kuamua juu yakuongeza, kupunguza, kubinafsisha au kuwashirikisha wadau katikautoaji wa huduma.

6. Kuhakikisha kuwa miundo na taratibu za utendaji wa Halmashaurizinazingatia ufanisi, uthabiti na tija katika kufikia malengo yaHalmashauri.

7. Kuiwezesha Halmashauri kujenga mahusiano imara kati yake na Serikalikuu, Serikali zingine za Mitaa na Umma kwa ujumla.

A. Kamati ya Fedha na Utawala:

Majukumu ya jumla:Kamati hii inawashirikisha Wenyeviti wa Kamati zote za kudumu nainapaswa kukutana kila mwezi mara moja. Aidha, madaraka ya Kamatihii ni kama ya Kamati zingine za kudumu na hivyo hairuhusiwi kisheriakufanya kazi/majukumu ya Kamati zingine za kudumu. Kwa ujumla,majukumu yake ni pamoja na kusimamia na kudhibiti ukusanyaji wamapato na matumizi ya mali ya Halmashauri kwa kupitia vikao vyake.

Majukumu Maalum ya Kamati:

(i) Kuweka mikakati na kupendekeza uongezaji wa mapato(ii) Kuwasilisha mapendekezo ya Bajeti na mpango wa Maendeleo

kwenye Halmashauri ili kuidhinishwa na Halmashauri.(iii) Kusimamia utunzaji wa hesabu za fedha ikiwa ni pamoja na

uhakiki wa mali za Halmashauri, ukusanyaji wa mapato, kufutamadeni, na kuomba vibali maalum kwa matumizi yanayohitajikibali cha Waziri mwenye dhamana ya Serikali za Mitaa.

Page 62: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

62

(iv) Kufikiria na, pale inapowezekana, kupendekeza kwenyeHalmashauri masuala yanayohusu Sheria Ndogo nautendaji katika ngazi za chini za Halmashauri.

(v) Kupokea na kuzingatia mapendekezo ya kubadili matumiziya mafungu ya fedha (re-allocation) yaliyopo katikamakisio yaliyoidhinishwa na kuyapeleka kwa Halmashauri.

(vi) Kuratibu mapendekezo kutoka kwenye Kamati zinginekuhusu matumizi ya kawaida na miradi na kuyawasilishakwenye Halmashauri.

(vii) Kufikiria na kupendekeza kwenye Halmashauri mikopoyote ya Halmashauri.

(viii) Kutoa mapendekezo ya vitega uchumi kwa madhumuni yakuongeza mapato kwa mujibu wa Sheria ya Fedha zaSerikali za Mitaa, Sura ya 290.

(ix) Kupokea na kujadili taarifa za wakaguzi wa fedha na maliya Halmashauri na kupendekeza hatua za kuchukuliwakutokana na maelekezo na maoni ya wakaguzi kwa mujibuwa Sheria za Serikali za Mitaa, Sura ya 290.

(x) Kusimamia na kudhibiti matumizi ya fedha za Halmashauri,kwa kuzingatia taratibu zilizowekwa na Waziri na taratibunyingine zitakazowekwa na Halmashauri;

(xi) Kupitia marekebisho yote yaliyopendekezwa hususankuhusu taratibu za fedha, ikiwa ni pamoja na mapitio yamara kwa mara yanayohusu thamani ya fedha ambapoKanuni mbalimbali za manunuzi ya mali na vifaahutumika;

(xii) Kufikiria na kupendekeza mabadiliko ya viwango vya kodi,ada na ushuru mbalimbali, vinavyotolewa na Halmashauri;

(xiii) Kufikiria mapendekezo ya Bajeti na Mipango yaMaendeleo ya kila Kamati ya Kudumu na kuiwasilishakwenye Halmashauri ili kupata idhini;

(xiv) Kushughulikia tofauti ya mapato na matumizi katika bajetiyote na kupendekeza hatua stahiki ya kuchukua kuondoamapungufu katika mapato au ziada matumizi;

(xv) Kufikiria mapendekezo yote yanayohusu matumizimakubwa ya fedha kabla hayajawasilishwa kwenyeHalmashauri ili kupata idhini;

(xvi) Kupokea mahesabu ya mwaka ya Halmashauri nakuhakikisha taarifa ya mahesabu ya mwaka inawasilishwakwa wakati kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu zaSerikali;

(xvii) Kupitia na kuidhinisha mpango wa manunuzi waHalmashauri kwa kuzingatia mpango wa Bajetiuliopitishwa na Halmashauri;

(xviii) Kupitia taarifa ya kila robo mwaka kuhusu Manunuziiliyowasilishwa na Afisa Masuuli;

(xix) Kusimamia utekelezaji wa mikataba ya Halmashauri kwakukagua miradi inayotekelezwa na vifaa vilivyopokelewa;

Page 63: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

63

(xx) Kumwelekeza Mkurugenzi kufanya manunuzi au ukaguziwa huduma au vifaa vilivyonunuliwa ili kupata thamanihalisi, itafanyika hivyo endapo itadhihirika kwamba,maelezo yaliyotolewa kuhusu manunuzi ya vifaa auhuduma hayaridhishi;

(xxi) Kuidhinisha majina ya wajumbe wa Bodi ya zabuni na waBodi zingine kwa mujibu wa Sheria husika;

(xxii) Kushughulikia orodha ya wadaiwa woteitakayokayowasilishwa kwenye Kamati na kutoamapendekezo ya hatua za kuchukua;

(xxiii) Kupendekeza njia na taratibu za kuondosha vifaa chakavu.Uondoshaji wa vifaa unaweza kufanyika kwa njia ya kuuzaau kuviharibu;

(xxiv) Kujadili na kupitia taarifa za fedha za kila mwezi na kilarobo mwaka;

(xxv) Kupendekeza kwa Halmashauri hatua za kuchukua kuhusukufuta madeni ya Halmashauri;

(xxvi) Kushughulikia Sera kuhusu kukopa na uwekezaji,(xxvii) Kubuni na kupendekeza mpango wa kuanzisha na

kuendeleza uhusiano na Halmashauri nyingine.(xxviii) Kurekebisha na kusimamia makusanyo na matumizi ya

mapato ya vijiji na miji midogo kwa mujibu wa Sheria,(xxix) Kuteua wakaguzi wa fedha/mali za Serikali za Vijiji kwa

mujibu wa Sheria, Sura ya 290).(xxx) Kujadili na kutoa mapendekezo ya hatua za kuchukuliwa

kuhusu mambo yote ya yanayohusu masuala ya ajira nakinidhamu ya wafanyakazi na watumishi.

(xxxi) Kujadili na kutoa mapendekezo kuhusu masualayanayohusu nyumba za Halmashauri.

(xxxii) Kupokea na kutoa uamuzi juu ya mapendekezo yawatumishi wanaokwenda masomoni.

(xxxiii) Kujadili na kupendekeza masuala yote yanayohusu maslahiya jumla ya watumishi, ikiwa ni pamoja na mikopo,nyumba, usafiri, matibabu, rambirambi na motishanyinginezo.

(xxxiv) Kupitisha mapendekezo ya kuthibitisha watumishi kazinibaada ya kumaliza kipindi cha majaribio kulingana namiundo husika ya utumishi.

Page 64: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

64

B: Kamati ya Uchumi, Elimu na Afya:

Majukumu ya Jumla

Kushughulikia mambo yote yanayohusu afya ya jamii, elimu na huduma za maji.Kamati hii pia itashughulikia mambo yanayohusiana na jitihada za wanannchivijijini kujiletea maendeleo yao kwa kutumia mbinu mbalimbali ikiwa ni pamojana kushauri, kushawishi, kuzindua, kuelimisha na kushirikisha wananchi haohasa katika kutayarisha, kutekeleza, kusimamia na kutathmini mipango yao yamaendeleo.

Majukumu maalum ya Kamati:

(i) Kuandaa mipango madhubuti ya maendeleo ya upanuzi na ujenzi wahospitali, vituo vya afya na zahanati

(ii) Kuandaa mipago ya maendeleo ya upanuzi na ujenzi wa shule zaawali na msingi na elimu ya watu wazima kwa mujibu wa Sheria yaElimu ya 1978 kama ilivyorekebishwa mwaka 1995.

(iii) Kupendekeza mipango ya ujenzi au upanuzi wa vituo,viwanja,majengo na mazingira ya burudani, starehe, mapumziko namichezo.

(iv) Kuamua juu ya mambo yanayohusu uhifadhi wa mambo ya kale namandhari mbalimbali yenye sura nzuri.

(v) Kuandaa na kuratibu njia bora juu ya uhifadhi wa nyaraka muhimukwa ajili ya kumbukumbu hizo zitahifadhiwa kwa mujibu wa Sheriaya Serikali za Mitaa Sura ya 288

(vi) Kupendekeza njia bora juu ya uhifadhi wa sanaa mbalimbali zaufundi na za maonyesho kwa mujibu wa Sheria ya Serikali za MitaaSura ya 288

(vii) Kupendekeza matumizi mazuri ya lugha ya taifa.

(viii) Kupendekeza namna ya malezi ya vijana ili waweze kuwawazalishaji katika Taifa.

(ix) Kusimamia uanzishaji wa uendelezaji wa vikundi vya jamii na vyahiari vya wananchi katika Halmashauri kwa mujibu wa Sera wamaendelo ya jamii.

(x) Kusimamia na kuhakiki maeneo ya misitu, mapori, na mbugazilizotengwa kama hifadhi ya mamlaka ya Serikali za Mitaa.

Page 65: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

65

(xi) Kupendekeza na kufanya tathmini ya uendelezaji wa mabonde, mitona mabwawa.

(xii) Kubuni na kupendekeza namna ya kudhibiti moto

(xiii) Kubuni na kupendekeza mikakati ya utumiaji wa nishati mbadala,kuzuia ukataji miti ovyo, na kuhimiza upandaji miti kwa wingi.

(xiv) Kuhakikisha kwamba ukaguzi wa majengo unafanyika mara kwamara.

(xv) Kupendekeza mipango madhubuti ya ujenzi wa barabara vijijini nawilayani kwa ujumla.

(xvi) Kupendekeza Sheria Ndogo zinazohusu Kamati hizi.

C: Kamati ya Mipango Miji na Mazingira:

Majukumu ya jumla

Kamati hii itashughulikia masuala ya uzalishaji mali ikiwemo kilimo, mifugo,viwanda, madini, Biashara n.k. Aidha itashughulikia pia miundombinu na sualazima la mendeleo ya Ardhi na hifadhi ya mazingira.

Majukumu maalum ya Kamati;

(i) Kupendekeza kwa Halmashauri mipango ya kupanua biashara najinsi ya kukusanya mapato yatokanayo na upanuzi huo.

(ii) Kupendekeza mipango ya matumizi ya ardhi katika eneo laHalmashauri.

(iii) Kusimamia matumizi ya Sheria ya nguvu kazi.

(iv) Kuandaa mipango madhubuti ya maendeleo ya upanuzi wa kilimokatika Halmashauri

(v) Kusimamia na kuhakiki miradi ya ujenzi wa masoko, minada,majosho na vituo vya mifugo.

(vi) Kushughulikia uanzishaji na uendelezaji wa vyama vya ushirika kwamujibu wa Sheria ya Vyama vya Ushirika.

Page 66: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

66

D: Kamati ya Kudumu ya Kudhibiti Ukimwi

Majukumu ya Kamati:

1. Kushirikisha wadau tofauti katika maeneo husika ili kuongezauchangiaji wa mawazo na/au nyenzo, usimamizi, uratibu nautekelezaji wa kazi za Tume za kudhibiti UKIMWI;

2. Kusimamia uundaji wa Kamati zote za kudhibiti UKIMWI;3. Kupendekeza na kuchambua hali ya UKIMWI/Mipango na

utekelezaji wake na kufikisha katika ngazi husuka kwa hatua zaidi;4. Kutathmini hali ya UKIMWI katika eneo lake;

(i) Idadi ya waathirika: wagonjwa, yatima, wajane,

(ii) Kasi ya maambukizo.

(iii) Mazingira maalum yanayochangia maambukizo.

(iv) Uelewa wa wananchi juu ya janga hili.

(v) Serikali haitatoa fedha kwa Halmashauri isiyokuwa namipango madhubuti ya kudhibiti UKIMWI.

(vi) Kuweka mikakati madhubuti ya kuhakikisha kila mtotoaliyefikia umri wa kwenda shule anafanya hivyo.

(vii) Kuweka mikakati ya makusudi juu ya njia bora zakuchangia baadhi ya huduma za Elimu na Afya.

(viii) Kubuni na kupendekeza njia bora za kuzuia na kudhibitimagonjwa ya milipuko.

(ix) Kupendekeza Sheria Ndogo za Kamati hii.

Page 67: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

67

FAHARASA – HALMASHAURI ZA MIJI.

Kanuni Na. Kifungu cha SheriaAAjenda za KamatiAkidi katika Mikutano ya HalmashauriAkidi kwenye Mikutano ya KamatiAthari za nafasi wazi kwenye Kamati

BCDDiwani au Afisa kutokuwa na maslahi katikamikatabaDiwani kutembelea maeneo, shughulimbalimbali za ujenzi nk.Wimbo wa Taifa/Dua ya kuiombeaHalmashauriEFFujo zinazosababishwa na ummaFujo zinazosababishwa na Wajumbe

509

5655

70

78

91

1918

Sura ya 288 kif.36Sura ya 288 kif.51(2) na (3)Sura ya 288 kif.51(1);51(3)

Sura ya 288 kif.43

Page 68: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

68

GHHaki ya kujibuHoja kuhusu matumiziHoja na marekebisho ya hojaHoja za Mwenyekiti/MwenyekitiHoja zinazohusu watumishi wa HalmashauriHoja zinazoweza kutolewa bila taarifaIJKKamati za KudumuKamati za pamojaKanuni za kudumu kutumika katikaMikutano ya KamatiKanuni za kudumu kutolewa kwa WajumbeKauli zenye kashfaKiapo na kukubali wadhifaKuidhinishwa kwa Taarifa ya KamatiKufikiriwa upya maamuziKufutwa kwa Kanuni zilizopo

Kujiuzulu ujumbe wa Kamati na kujazwakwa nafasi iliyoachwa wazi.

Kujiuzulu wadhifa wa Mwenyekiti waKamatiKumbukumbu ya mahudhurio.

Kumwondoa Mwenyekiti madarakaniKupokelewa kwa taarifa za KamatiKuruhusu watu na vyombo vya Habarikwenye Mikutano ya Halmashauri.

2233201638

21

4144

57

88287135

6092

63

62

12

83

3413

Sura ya 288 kif.40 (2)

Sura ya 288 kif.25(5) ; GN263/95

Sura 288 kif.39(1)

Page 69: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

69

Kushiriki kwa UmmaKusitisha utumiaji wa Kanuni za kudumu.Kutafsiri Kanuni za kudumuKuthibitisha muhtasariKutokuwepo kwa WajumbeKutunza siri za Majadiliano ya Kamati naKamati Ndogo.LMMaamuzi ya Mikutano ya HalmashauriMahudhurio katika Mikutano ya KamatiMajukumu ya DiwaniMarekebisho na mabadiliko ya Kanuni zakudumuMaswaliMaswali ya papo kwa papoMihtasari ya Kamati za maendeleo za Katana vijiji/Mitaa.Mihtasari kupelekwa kwa Mkuu wa Wilayana Mkuu wa Mkoa.Mihtasari ya KamatiMikutano ya KamatiMikutano ya kawaida ya HalmashauriMtoa hoja kualikwa kwenye Mkutano waKamati.Mkutano wa BajetiMkutano wa MwakaMkutano maalum wa HalmashauriMkutano maalum wa KamatiMwaliko wa wasiokuwa WajumbeNNafasi wazi

3986

89157461

29

51

7287

232431

32

59473

52

6754930

73

Taz.pia Sura ya 290 kif.47Sura ya 288 kif.40(1)

Sura ya 288 kif.34(1)Sura ya 288 kif.34(3)

Sura ya 288 kif.45, 50

PAina za poshoPosho endapo Mkutano utaahirishwaQ

8485

Sura ya 288 kif. 42(2)

RRejesta ya mikatabaSTTaarifa za KamatiTaarifa kutoka kwenye kataTaarifa za Mikutano

69

25268 Sura ya 288 kif.35

Page 70: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

70

TafsiriTaratibu za kutunga Sheria NdogoTaratibu za MajadilianoTaratibu za UagizajiUUahirishaji wa vikaoUandikishaji wa AnwaniUandishaji wa Bodi za HudumaUchaguzi wa Mwenyekiti/ Mwenyekiti naMakamu Mwenyekiti wa HalmashauriUhalali wa majadiliano ya HalmashauriUhuru wa kutoa mawazo wakati wamajadilianoUkaguzi wa nyarakaAkidi kwenye Mikutano ya KamatiUpigaji kura kwenye Mikutano ya KamatiUsimamiaji wa mikatabaUtaratibu wa shughuli za MikutanoUteuzi wa Wajumbe kwenye Taasisi za njeUtiaji mhuri kwenye NyarakaUvunjaji wa mkatabaUwezo wa Halmashauri kujigeuza kuwaKamati ya Halmashauri nzima.Uwezo wa KamatiUzuiaji wa Rushwa

2751764

40817710

36

27

7656

58

6714

82

806837

4366

Sura ya 288 kif.38

VWWaalikwa wasiokuwa Wajumbe kuhudhuriana kushiriki katika Mikutano ya Kamati.XYZZiara za Wajumbe

53

90

Sura ya 288 kif.45(1)

Page 71: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

71

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

KIAPO CHA DIWANI

Mimi ……………………………… naapa/natamka kwa dhati kwamba

nitaitumikia Halmashauri ya………………….. kwa wadhifa wangu wa Udiwani na kwamba

nitahifadhi, nitalinda na kutetea, Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Sheria za Tanzania,

Maadili ya Madiwani na Kanuni za Kudumu za Halmashauri kama zilivyowekwa kwa mujibu wa

Sheria na kwamba nitaitumikia Halmashauri ya ………………………………………… kwa

uaminifu kwa uwezo na moyo wangu wote.

(Ewe Mwenyezi Mungu nisaidie)

Kiapo/Tamko hili limetolewa hapa; ………………………………………

Na……………………………………………………………………………..

Leo tarehe…………………… Mwezi wa…………………..20……….

Mbele ya:………………………………………..

Jina:………………………………………………

Cheo:…………………………………………….

Saini:……………………………………………

Anuani………………………………………….…………………………………..

Page 72: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

72

HAKIMU/WAKILI WA KUAPISHA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

TAMKO LA VIONGOZI WA UMMA KUHUSU

RASILIMALI NA MADENI

(Kwa mujibu wa kifungu cha 9 na cha 11 cha Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma)

Mimi……………………………………………………Anuani; …………………… baada ya kuchaguliwa/kuteuliwa na kuapishwa katika wadhifawa…….……...tarehe……………………….mwaka 20….Ninatamka rasmi nakwa moyo mnyofu kwamba hadi sasa nina rasilimali na madeni yafuatayo:-

(1) Fedha taslimu, Amana katika benki au taasisi ya fedha; taja namba ya akaunti, benki au taasisiya fedha na kiasi:……………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………….…………2) Hawala za Hazina (Treasury Bills) na dhamana nyingine maalum:-……………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………..……………………

3) Faida ya akiba, mafungu ya mgawanyo wa faida zinazotokana na hisa n.k.…………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………….……………………………

4) Nyumba au majengo ya kupangisha, taja mahali yalipo na ukubwa au eneo:……………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………..……………………………

* Rasilimali zinazotakiwa ni pamoja na zifuatazo, ambazo ni zako binafsi, za mume/mke au watotowadogo wasiooa au kuolewa wa kiongozi wa umma.

(a) Fedha taslimu na amana katika benki au taasisi nyingine ya fedha.

(b) Hawala za Hazina Treasury Bills) na nyinginezo za dhamana maalum zinazotolewa aukudhaminiwa na Serikali au vyombo vya Serikali.

(c) Faida itokanayo na fedha iliyowekwa akiba Benki, Chini ya Ujenzi au taasisi nyingine yafedha.

(d) Mgao wa fedha kutokana na fungu la rasilimali ya kampuni (stocks) au hisa za kiongozi waumma katika kampuni au shirika lolote.

(e) Maslahi katika chombo cha biashara kisichokuwa na mkataba na Serikali, na kisichokuwa naau kisichotawala amana zinazouzwa bayana na vyombo vya umma.

(f) Mashamba ya kibiashara.

Page 73: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

73

(g) Mali halisi zisizohamishika ambazo si rasilimali zisizotakiwa kutajwa; na

(h) Rasilimali zinazoleta faida, ambazo si rasilimali zisizotakiwa kutajwa na ambazo zinamilikiwakwa mbali.

(5) Mashamba ya kibiashara, mifugo, madini n.k.……………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………(6) Magari na aina nyingine za usafiri wa kibiashara;……………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………(7) Mashine za kusaga nafaka, viwanda na shughuli nyingine za kibiashara aumitambo:……………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………

(8) Rasilimali nyinginezo au maslahi ambayo kiongozi wa umma anapendakutaja:……………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………(9) Madeni;………………………………………………………………………Tamko hili linatolewa na kusainiwa mbele yangu………………………………………………………….na (mtoa tamko)………………………………………ninayemfahamu binafsi, au aliyetambulishwa kwangu na…………………………………………………………………

….…………..ambaye ninamfahamu leo tarehe ………………………… Mtoa tamkoMwezi wa ……………………………………………………saini……………………………………………………………Wadhifa:………………………………………………………Anuani:……………………………………………………….………………………………………………………………….(Tamko hili lazima litolewe mbele ya Kamishna wa Viapo)

KWA: KAMISHINA WA MAADILI, SEKRETARIETI YA MAADILI,S.L.P 13341,DAR ES SALAAM.

Page 74: KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MJI WA ......Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tangazo la Serikali Na. 48 (l inaendelea) 3 SEHEMU YA IV KAMATI 41. Kamati za Kudumu

Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Mji wa MafingaTangazo la Serikali Na. 48 (linaendelea)

74

Lakiri ya Halmashauri ya Mji wa Mafinga imebandikwa kwenyeSheria Ndogo hizi kwa kufuatia Azimio lililopitishwa kwenye Mkutanowa Halmashauri ulioitishwa na kufanyika vilivyo tarehe 19 Aprili 2016 nailibandikwa mbele ya:

SAADA S, MWARUKA,Mkurugenzi

Halmashauri ya Mji wa Mafinga

CHARLES JOHN MAKOGA,Mwenyekiti

Halmashauri ya Mji wa Mafinga

NAKUBALI,

Dodoma, GEORGE B. SIMBACHAWENE (MB.)9 Januari, 2017 Waziri wa Nchi-OR-TAMISEMI