27
i MUHTASARI Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ilifanya utafiti kwa lengo la kutoa ushauri sahihi juu ya njia na namna ya kuziba mianya ya rushwa katika huduma zinazotolewa na Hospitali ya Mkoa wa Morogoro. Aidha, utafiti ulikuwa na madhumuni yafuatayo: (a) kubaini mianya ya rushwa katika mlolongo wa utoaji huduma; (b) kubaini na kuainisha vikwazo vya utoaji huduma; (c) kupendekeza namna bora ya kuziba mianya ya rushwa; na (d) kudhibiti kutorudiwa kwa mbinu na taratibu zinazoonekana kuwa ni vyanzo vya rushwa. Ukusanyaji wa taarifa ulifanyika kwa kipindi cha majuma mawili kuanzia tarehe 02 Oktoba hadi 16 Oktoba 2010. Utafiti huu ulitokana na ombi rasmi la Ofisi ya Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro na uongozi wa Hospitali, kutokana na kutambua athari mbaya za rushwa katika maboresho ya Hospitali ya Mkoa wa Morogoro na wajibu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kisheria. Hospitali ya Mkoa wa Morogoro ipo kwenye maboresho makubwa ya huduma na miundombinu ya Hospitali. Maboresho ya huduma yanahusu upatikanaji wa dawa muhimu, vifaa na vitendea kazi. Aidha, maboresho ya miundombinu yanahusu ujenzi wa majengo mapya, ukarabati wa majengo ya zamani, kuboresha Teknolojia ya Mawasiliano na Habari (ICT), na kuboresha mfumo wa umeme, maji safi na maji taka. Kwa upande wa fedha, Hospitali inalenga kuongeza mapato yake kupitia uchangiaji. Hospitali hiyo inakabiliwa na malalamiko ya wateja kuhusu vitendo vya rushwa dhidi ya watumishi wake. Mbinu zilizotumika katika ukusanyaji wa taarifa zilihusisha: taarifa za msingi (primary data), taarifa za upili (secondary data) na Utambuzi wa Mtafiti (Non-Participant Observation). Taarifa za msingi zilitokana na mahojiano rasmi kwa njia ya madodoso, mjadala (kikao na Menejimenti ya Hospitali) na mahojiano yasiyo rasmi. Taarifa za upili zilipatikana kwenye sera, sheria, miongozo ya utendaji kazi na nyaraka nyingine muhimu. Kuhusu utambuzi wa mtafiti, watafiti walihusika na kuangalia mazingira ya kazi, vitendea kazi, utendaji kazi, na mwenendo wa wadau. Matokeo ya utafiti yanabainisha mianya ya rushwa katika makundi matatu: uwajibikaji mdogo wa watumishi, uwazi mdogo wa huduma na upungufu wa maadili . Uwajibikaji mdogo unasababishwa na udhaifu wa udhibiti wa ndani hasa katika unaibishaji, mawasiliano ya ndani, mbinu za uongozi, tathmini za utendaji, ufanyaji maamuzi, na udhibiti wa rasilimaliwatu. Uwazi mdogo wa huduma za Hospitali umesababisha mambo yafuatayo: kutojulikana kwa haki za wagonjwa; kutojulikana kwa taratibu za huduma; kutojulikana na kutoimarika kwa Kitengo cha kupokelea na kushughulikia malalamiko; na kuwepo kwa mawasiliano duni kati ya Hospitali na wadau. Upungufu wa maadili, pamoja na mambo

MUHTASARI - pccb.go.tz · ya Hospitali. Mawasiliano duni yanasababisha kutokuwepo maelewano kati ya wafanyakazi na uongozi na hivyo kusababisha wafanyakazi kukata tamaa na kujihusisha

Embed Size (px)

Citation preview

Page 1: MUHTASARI - pccb.go.tz · ya Hospitali. Mawasiliano duni yanasababisha kutokuwepo maelewano kati ya wafanyakazi na uongozi na hivyo kusababisha wafanyakazi kukata tamaa na kujihusisha

i

MUHTASARI

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ilifanya utafiti kwa lengo la kutoa ushauri

sahihi juu ya njia na namna ya kuziba mianya ya rushwa katika huduma zinazotolewa na Hospitali ya

Mkoa wa Morogoro. Aidha, utafiti ulikuwa na madhumuni yafuatayo: (a) kubaini mianya ya rushwa

katika mlolongo wa utoaji huduma; (b) kubaini na kuainisha vikwazo vya utoaji huduma; (c)

kupendekeza namna bora ya kuziba mianya ya rushwa; na (d) kudhibiti kutorudiwa kwa mbinu na

taratibu zinazoonekana kuwa ni vyanzo vya rushwa. Ukusanyaji wa taarifa ulifanyika kwa kipindi cha

majuma mawili kuanzia tarehe 02 Oktoba hadi 16 Oktoba 2010.

Utafiti huu ulitokana na ombi rasmi la Ofisi ya Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro na uongozi wa

Hospitali, kutokana na kutambua athari mbaya za rushwa katika maboresho ya Hospitali ya Mkoa wa

Morogoro na wajibu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kisheria. Hospitali

ya Mkoa wa Morogoro ipo kwenye maboresho makubwa ya huduma na miundombinu ya Hospitali.

Maboresho ya huduma yanahusu upatikanaji wa dawa muhimu, vifaa na vitendea kazi. Aidha, maboresho

ya miundombinu yanahusu ujenzi wa majengo mapya, ukarabati wa majengo ya zamani, kuboresha

Teknolojia ya Mawasiliano na Habari (ICT), na kuboresha mfumo wa umeme, maji safi na maji taka.

Kwa upande wa fedha, Hospitali inalenga kuongeza mapato yake kupitia uchangiaji. Hospitali hiyo

inakabiliwa na malalamiko ya wateja kuhusu vitendo vya rushwa dhidi ya watumishi wake.

Mbinu zilizotumika katika ukusanyaji wa taarifa zilihusisha: taarifa za msingi (primary data), taarifa za

upili (secondary data) na Utambuzi wa Mtafiti (Non-Participant Observation). Taarifa za msingi

zilitokana na mahojiano rasmi kwa njia ya madodoso, mjadala (kikao na Menejimenti ya Hospitali) na

mahojiano yasiyo rasmi. Taarifa za upili zilipatikana kwenye sera, sheria, miongozo ya utendaji kazi na

nyaraka nyingine muhimu. Kuhusu utambuzi wa mtafiti, watafiti walihusika na kuangalia mazingira ya

kazi, vitendea kazi, utendaji kazi, na mwenendo wa wadau.

Matokeo ya utafiti yanabainisha mianya ya rushwa katika makundi matatu: uwajibikaji mdogo wa

watumishi, uwazi mdogo wa huduma na upungufu wa maadili. Uwajibikaji mdogo unasababishwa na

udhaifu wa udhibiti wa ndani hasa katika unaibishaji, mawasiliano ya ndani, mbinu za uongozi, tathmini

za utendaji, ufanyaji maamuzi, na udhibiti wa rasilimaliwatu. Uwazi mdogo wa huduma za Hospitali

umesababisha mambo yafuatayo: kutojulikana kwa haki za wagonjwa; kutojulikana kwa taratibu za

huduma; kutojulikana na kutoimarika kwa Kitengo cha kupokelea na kushughulikia malalamiko; na

kuwepo kwa mawasiliano duni kati ya Hospitali na wadau. Upungufu wa maadili, pamoja na mambo

Page 2: MUHTASARI - pccb.go.tz · ya Hospitali. Mawasiliano duni yanasababisha kutokuwepo maelewano kati ya wafanyakazi na uongozi na hivyo kusababisha wafanyakazi kukata tamaa na kujihusisha

ii

mengine, umesababishwa na ufahamu mdogo wa rushwa na madhara yake, na maana na namna ya

kukabiliana na mtanziko wa maadili.

Aidha, upungufu wa maadili umesababisha mahusiano mabovu kati ya wagonjwa na watumishi ambayo

yanasababishwa na lugha mbaya ya watumishi kwa wagonjwa, wizi wa dawa walizopewa wagonjwa, na

watumishi kutovaa vitambulisho na kutia ugumu wa kutambuliwa na wagonjwa. Vilevile, upungufu wa

maadili unasababishwa na kutokuwepo au udhaifu wa vyombo vinavyosimamia maadili (yaani Kamati ya

Nidhamu na kamati ya Maadili). Aidha, wahojiwa walitoa maoni yaliyoonyesha kuwa sehemu ya

upasuaji inaongoza kwa rushwa ikifuatiwa na mapokezi na wodi ya wazazi.

Utafiti uliainisha mbinu za kudhibiti rushwa katika Hospitali ya Mkoa wa Morogoro kuwa ni kuboresha

maslahi, kuhakikisha utoshelevu wa rasilimali, elimu ya maadili kwa watumishi, mafunzo kazini, na

kuimarisha uwazi na uwajibikaji.

Page 3: MUHTASARI - pccb.go.tz · ya Hospitali. Mawasiliano duni yanasababisha kutokuwepo maelewano kati ya wafanyakazi na uongozi na hivyo kusababisha wafanyakazi kukata tamaa na kujihusisha

iii

YALIYOMO

MUHTASARI ................................................................................................................................................ i

YALIYOMO ................................................................................................................................................ iii

Orodha ya majedwali ................................................................................................................................... iv

Orodha ya Viambatanisho ............................................................................................................................. v

Orodha ya vifupisho ..................................................................................................................................... vi

1. UTANGULIZI ..................................................................................................................................... 1

2. MATOKEO YA UTAFITI ................................................................................................................... 2

2.1 Vikwazo vya utendaji katika hospitali ...................................................................................... 2

2.2 Uwajibikaji hospitalini .............................................................................................................. 4

2.3 Uwazi wa huduma katika hospitali ........................................................................................... 8

2.4 Vitendo vya Rushwa hospitalini ............................................................................................... 9

2.5 Maoni ya wahojiwa ................................................................................................................. 10

3. MAPENDEKEZO .............................................................................................................................. 12

3.1.1 Mapendekezo kwa hospitali ................................................................................................ 12

4. MKAKATI WA KUDHIBITI MIANYA YA RUSHWA ................................................................. 15

5. HITIMISHO ....................................................................................................................................... 18

Page 4: MUHTASARI - pccb.go.tz · ya Hospitali. Mawasiliano duni yanasababisha kutokuwepo maelewano kati ya wafanyakazi na uongozi na hivyo kusababisha wafanyakazi kukata tamaa na kujihusisha

iv

Orodha ya majedwali

Jedwali 1: Maoni ya wahojiwa kuhusu maeneo ya hospitali yanayohitaji udhibiti wa rushwa

Jedwali 2: Maoni ya wahojiwa kuhusu mbinu za kudhibiti rushwa hospitalini

Jedwali 3: Mapendekezo kwa hospitali ya mkoa wa Morogoro

Jedwali 4: Mkakati wa kuboresha huduma Hospitali ya mkoa wa Morogoro

Page 5: MUHTASARI - pccb.go.tz · ya Hospitali. Mawasiliano duni yanasababisha kutokuwepo maelewano kati ya wafanyakazi na uongozi na hivyo kusababisha wafanyakazi kukata tamaa na kujihusisha

v

Orodha ya Viambatanisho

Kiambatanisho I: Muundo wa Hospitali ya Mkoa wa Morogoro

Kiambatanisho II: Thamani ya vifaa na dawa-Hospitali ya Mkoa wa Morogoro 2009/10

Kiambatanisho III: Makusanyo na matumizi ya fedha za uchangiaji huduma za afya 2009/10

Page 6: MUHTASARI - pccb.go.tz · ya Hospitali. Mawasiliano duni yanasababisha kutokuwepo maelewano kati ya wafanyakazi na uongozi na hivyo kusababisha wafanyakazi kukata tamaa na kujihusisha

vi

Orodha ya vifupisho

HMT - Hospital Management Team

ICT - Information and Communication Technology

IPD - In-Patient Department

KRAs - Key Result Areas

MKUKUTA

MOI/C

- Mkakati wa Kuondoa Umasikini na Kukuza Uchumi

Medical Officer Incharge

MSD - Medical Stores Department

OPD - Out Patient Department

OPRAS - Open Performance Review and Appraisal System

RAS

RHMT

-

Regional Administrative Secretary

Regional Health Management Team

TAKUKURU - Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa

TUGHE - Trade Union for Government Health Employee

Page 7: MUHTASARI - pccb.go.tz · ya Hospitali. Mawasiliano duni yanasababisha kutokuwepo maelewano kati ya wafanyakazi na uongozi na hivyo kusababisha wafanyakazi kukata tamaa na kujihusisha

1

1. UTANGULIZI

Mapambano dhidi ya rushwa katika sekta ya afya ni muhimu katika kufanikisha mpango wa maboresho

wa sekta hiyo unaotekelezwa na serikali. Mpango huo unalenga kuziwezesha Hospitali za Mikoa kuwa za

rufaa ili kuongeza ubora wa huduma kwa maana ya kupanua upatikanaji wake, na kuongeza dawa na

watumishi wenye sifa katika ngazi ya mkoa. Maboresho haya yanafanyika kwa kuzingatia Sera ya Taifa

ya Afya ya mwaka 2003 inayohimiza, pamoja na mambo mengine, kuongeza usambazaji wa dawa na

vifaa ili kukidhi mahitaji ya vituo vya afya (health facilities) na kutoa mafunzo kazini kwa watumishi

ambao utendaji wao wa kazi hauridhishi kutokana na kukosa mafunzo ya kutosha.

Hospitali ya Mkoa wa Morogoro ipo kwenye maboresho makubwa ya huduma na miundombinu ya

Hospitali. Maboresho ya huduma yanahusu upatikanaji wa dawa muhimu, vifaa na vitendea kazi. Aidha,

maboresho ya miundombinu yanahusu ujenzi wa majengo mapya, ukarabati wa majengo ya zamani,

kuboresha Teknolojia ya Mawasiliano na Habari (ICT), na kuboresha mfumo wa umeme, maji safi na

maji taka. Kwa upande wa fedha, Hospitali inalenga kuongeza mapato yake kupitia uchangiaji. Hospitali

inakabiliwa na msongamano wa wagonjwa kwa sababu kuu mbili: moja, inategemewa kwa rufaa na

wilaya zote tano za mkoa wa Morogoro. Mbili, hutumiwa kila siku na wilaya za Morogoro na Mvomero

kwa kuwa katika wilaya hizo hakuna hospitali za wilaya. Vilevile, Hospitali inakabiliwa na malalamiko

ya wateja kuhusu vitendo vya rushwa dhidi ya watumishi wake.

Kwa kutambua athari za rushwa katika maboresho ya Hospitali na wajibu wa Taasisi ya Kuzuia na

Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kisheria, Ofisi ya Katibu Tawala Mkoa na uongozi wa Hospitali

waliiomba TAKUKURU kufanya utafiti kwa lengo la kutoa ushauri sahihi juu ya njia na namna ya kuziba

mianya ya rushwa katika huduma zinazotolewa na Hospitali ya Mkoa wa Morogoro. Aidha, utafiti

ulikuwa na madhumuni yafuatayo: (a) kubaini mianya ya rushwa katika mlolongo wa utoaji huduma; (b)

kubaini na kuainisha vikwazo vya utoaji huduma; (c) kupendekeza namna bora ya kuziba mianya ya

rushwa; na (d) kudhibiti kutorudiwa kwa mbinu na taratibu zinazoonekana kuwa ni vyanzo vya rushwa.

Page 8: MUHTASARI - pccb.go.tz · ya Hospitali. Mawasiliano duni yanasababisha kutokuwepo maelewano kati ya wafanyakazi na uongozi na hivyo kusababisha wafanyakazi kukata tamaa na kujihusisha

2

2. MATOKEO YA UTAFITI

Matokeo ya utafiti yanaonesha kuwepo vikwazo vya kimuundo na kiutendaji, uwajibikaji na

uwazi mdogo wa huduma, na vitendo vya rushwa katika Hospitali hiyo ya Mkoa kama ifuatavyo:

2.1 Vikwazo vya Utendaji Katika Hospitali

a) Vikwazo vya kimuundo na kiutendaji katika Hospitali ya Mkoa wa Morogoro

Matokeo yanaonyesha kuwepo vikwazo vya kimuundo na kiutendaji katika Hospitali ya Mkoa wa

Morogoro. Kwa wastani wahojiwa walieleza kuwepo udhibiti mdogo wa uwajibikaji (43%), mawasiliano

duni kati ya viongozi na wafanyakazi (53%), mawasiliano duni kati ya idara (40%), mawasiliano duni

baina ya Hospitali na wadau wengine (43%), mishahara midogo (30%), na upungufu wa vitendea kazi

(21%) na wafanyakazi (11%). Upungufu wa vitendea kazi unatajwa kuwa, pamoja na mambo mengine,

unatokana na ubora mdogo wa vifaa vinavyotolewa na MSD. Vifaa vya MSD vinadaiwa kuwa havidumu

muda mrefu kwa kuwa aghalabu havitimizi hata mwaka mmoja baada ya kuanza kutumika.

Aidha, matokeo yanabainisha kuwa kikwazo kikubwa ni mawasiliano duni kati ya uongozi na

wafanyakazi na baina ya Hospitali na wadau wengine, haya yamejipambanua zaidi kwa wauguzi na

watumishi wengine. Hata hivyo, TUGHE wao wameeleza kuwa wana ushirikiano mzuri na menejimenti

ya Hospitali. Mawasiliano duni yanasababisha kutokuwepo maelewano kati ya wafanyakazi na uongozi

na hivyo kusababisha wafanyakazi kukata tamaa na kujihusisha na vitendo kinyume na maadili ya

utumishi wa umma. Vilevile, mwanya mwingine unatokana na Hospitali kutokuwa na Bodi ya Hospitali

(Kiambatanisho I) na hivyo kukwaza ushiriki wa jamii katika usimamizi wa Hospitali. Kwa mfano,

kutokana na umuhimu wa Bodi katika kudhibiti ukusanyaji na kuidhinisha matumizi ya mapato ya

Hospitali, kutokuwepo kwake kunasababisha majukumu ya Bodi kufanywa na Kamati ya Uendeshaji ya

Hospitali au Mganga Mfawidhi wa Hospitali.

Hali hii inaonesha kuwa kazi za utendaji na usimamizi zinafanywa na mtu yuleyule (ukiritimba –

monopoly) na hivyo kutoa mwanya wa wafanyakazi kujihusisha na vitendo vinavyokwenda kinyume na

taratibu na sheria zinazoongoza huduma za afya. Kwa upande wa unaibishaji mamlaka (delegation),

umebainika udhaifu wa baadhi ya watumishi kuingiliwa kazi zao na walio juu yao, na hatimaye kuathiri

mlolongo wa uwajibikaji (accountability chain) katika Hospitali. Kamati ya Uendeshaji ya Hospitali ya

Mkoa (RHMT) inatajwa kuingilia kazi za utendaji za Kamati ya Uendeshaji ya Hospitali (HMT)

kiutawala (administratively), kifedha (financially) na kitaaluma (technically). Hali hii inatajwa kuwa

inatokana na viongozi na watumishi kukosa mbinu za uongozi (managerial skills) na kutokuwa na

Page 9: MUHTASARI - pccb.go.tz · ya Hospitali. Mawasiliano duni yanasababisha kutokuwepo maelewano kati ya wafanyakazi na uongozi na hivyo kusababisha wafanyakazi kukata tamaa na kujihusisha

3

maelezo ya kazi zao (job description). Muundo unawapa watumishi nafasi za uongozi wa Hospitali kwa

taaluma zao (technical skills), lakini wanakosa mbinu za uongozi. Hivyo, ili kuondoa muingiliano wa kazi

na kuongeza uwajibikaji, watumishi wa Hospitali wanapaswa kuwa na maelezo ya kazi zao na pia

kupatiwa mafunzo ya mbinu za uongozi.

Kwa upande wake tofauti ya kimtazamo kati ya viongozi, madaktari na wauguzi kuhusu uchache wa

watumishi kuwa chanzo cha rushwa, inaonesha haja ya kufanyika mjadala zaidi katika hili. Tofauti na

viongozi, wauguzi na madaktari, watumishi wengine wote walieleza kuwa uchache wa watumishi si

kikwazo cha utendaji. Hali hii inaweza kuelezeka kuwa huenda kundi hili likawa na sababu nyingine zaidi

ya hii ambazo kwao ndiyo kikwazo cha utendaji. Lakini kwa mujibu wa matokeo, watumishi wengine

wanaona kuwa udhibiti mdogo wa uwajibikaji na mawasiliano duni baina ya Hospitali na wadau kuwa

ndiyo vikwazo vya utendaji.

Jitihada za kudhibiti vikwazo hivyo zinatajwa kufanyika katika Hospitali, lakini ni wastani wa asilimia 38

tu ya wahojiwa ambao walieleza kuwepo jitihada za kuimarishwa kwa mawasiliano baina ya Hospitali na

wadau wengine. Matokeo yanaonesha kusigana kwa makundi mbalimbali ya watumishi kuhusu jitihada

zinazofanywa kudhibiti vikwazo vilivyobainika. Viongozi, takribani wote, wanaeleza kuwepo kwa

jitihada za kudhibiti vikwazo, kinyume na maoni ya watumishi waliobaki ambao wengi hawaoni kama

jitihada zinafanywa kukabili vikwazo hivyo. Kusigana kwa makundi haya ya watumishi kunaashiria

kuwepo mkwamo wa utiririkaji wa taarifa kimuundo kutoka juu kwenda chini. Hatua madhubuti na za

makusudi zinapaswa kufanywa ili kuondoa vikwazo na kuboresha mtiririko wa taarifa (information flow).

b) Uwepo wa Mkataba wa Huduma kwa Mteja na Kamati ya Kudhibiti Maadili

Matokeo yanaonyesha kuwa Hospitali ya Mkoa wa Morogoro bado haijatayarisha Mkataba wa Huduma

kwa Mteja, na vilevile haijaunda Kamati ya Kudhibiti Maadili Hospitalini hapo (hii ni kwa mujibu wa

kikao cha Menejimenti cha tarehe 02/10/2010). Ukweli huu unakinzana na majibu ya wahojiwa wengi

ambao wanaeleza kuwepo kwa Kamati ya maadili (70%) na Mkataba wa Huduma kwa Mteja (52%).

Wahojiwa hawa wanashindwa kutofautisha kati ya Kamati ya Maadili na Kamati ya Nidhamu, na kati ya

Mkataba wa Huduma kwa Mteja na miongozo na matangazo mbalimbali ya Hospitali yanayoelekeza

kuhusu huduma kwa wagonjwa. Mkanganyiko huo unaimarisha dhana kuwa uongozi na watumishi wengi

wa Hospitali hawaifahamu miongozo muhimu ya kitaifa ya kudhibiti maadili na kuongeza uwajibikaji wa

watumishi. Kutofahamu huko kunatoa mwanya mkubwa wa vitendo vya rushwa na mkengeuko wa

maadili.

Page 10: MUHTASARI - pccb.go.tz · ya Hospitali. Mawasiliano duni yanasababisha kutokuwepo maelewano kati ya wafanyakazi na uongozi na hivyo kusababisha wafanyakazi kukata tamaa na kujihusisha

4

c) Muda ambao mtumishi amefanya kazi katika Hospitali ya mkoa wa Morogoro

Matokeo yanaonesha kuwa, kwa wastani, asilimia 46 ya watumishi waliohojiwa wamekwishakaa kwenye

eneo moja la kazi kwa muda unaozidi miaka mitano, wengi wao wakiwa ni wauguzi na watumishi

wengine. Hali hii inatoa mwanya mkubwa wa vitendo vya rushwa na ukiukwaji wa maadili kwa

watumishi hasa wauguzi ambao wamekuwa wakilalamikiwa kwa vitendo hivyo.

2.2 Uwajibikaji Hospitalini

a) Jinsi uwajibikaji wa watumishi wa Hospitali unavyopimwa

Matokeo ya utafiti yanaonesha kuwa wastani wa asilimia 67 ya wahojiwa walieleza kuwa utendaji

hospitalini hapo hupimwa kwa Utaratibu wa Wazi wa Tathmini za Utendaji (Open Performance Review

and Appraisal System – OPRAS). Hata hivyo, baadhi ya wahojiwa wakiwemo TUGHE wanaeleza kuwa

OPRAS haijaanza kwa kuwa upimaji bado unafanywa kwa siri kupitia miundo ya utumishi - ‘scheme of

service’. Aidha, wastani wa asilimia 52 ya wahojiwa walieleza kuwa uwajibikaji unapimwa kwa

kuzingatia uandishi wa taarifa za uwajibikaji zenye kuzingatia maadili ya kitaalamu na viwango bora vya

utendaji na zenye kuonesha kilichofanyika, kilichotumika na kwa nini. Hata hivyo, wahojiwa wachache

(wastani wa asilimia 34 tu) walieleza kuwa upimaji wa uwajibikaji katika Hospitali ya Mkoa wa

Morogoro hufanywa kwa kuzingatia matumizi bora ya rasilimali.

Matokeo haya yanabainisha tashwishi ya kutokuwepo udhibiti imara wa uwajibikaji hasa kwa kuzingatia

kuwa ni nusu tu ya viongozi waliohojiwa ambao walieleza kuwepo kwa uandishi wa taarifa za uwajibikaji

na matumizi sahihi ya rasilimali. Viongozi wote waliohojiwa walieleza kuwa OPRAS inatumika kupima

uwajibikaji kinyume na maelezo ya makundi mengine ya watumishi yaliyohojiwa. Hali hiyo huenda

inasababishwa na OPRAS kuwa ndiyo kwanza imeanza kutumika katika mwaka huu wa fedha wa

2010/11 Hospitalini hapo na inawezekana kuwa watumishi bado hawajaelimishwa vya kutosha kuhusu

lengo na faida za OPRAS.

Mbinu nyingine inayoweza kudhibiti uwajibikaji ni kukagua mahudhurio ya watumishi na kuchukua

hatua zifaazo kwa wachelewaji, watoro na wasiohudhuria kazini. Matokeo ya ukaguzi wa daftari la

mahudhurio yanaonesha kuwa daftari hilo hukaguliwa kila siku, lakini halina sehemu kwa ajili ya kusaini

watumishi wanaokwenda nje ya Hospitali ndani ya muda wa kazi. Kwa upande wa wachelewaji kazini,

uongozi unaeleza kuwa wachelewaji hujadiliwa katika vitengo vyao na wanapozidi wanapelekwa kwenye

Kamati ya Nidhamu ya Hospitali. Aidha, kumbukumbu za vikao vya Kamati ya Uendeshaji ya Hospitali

zinaonesha kuwa suala la utoro limekuwa likijadiliwa mara kwa mara.

Page 11: MUHTASARI - pccb.go.tz · ya Hospitali. Mawasiliano duni yanasababisha kutokuwepo maelewano kati ya wafanyakazi na uongozi na hivyo kusababisha wafanyakazi kukata tamaa na kujihusisha

5

b) Uwepo wa kitengo cha kupokelea na kushughulikia malalamiko ya wagonjwa katika hospitali

Matokeo yanaonesha kuwa wastani wa asilimia 54 ya wahojiwa walieleza kuwepo kwa Kitengo cha

Kupokelea na Kushughulikia Malalamiko Hospitalini hapo. Hata hivyo, muhtasari wa kikao cha Kamati

ya Uendeshaji ya Hospitali cha tarehe 02/08/2010 na mahojiano na baadhi ya viongozi yanabainisha kuwa

kitengo hicho hakikuwa na ofisi na kwamba uongozi ulikuwa katika maandalizi ya ofisi na kuajiri afisa

mwenye taaluma ya ustawi wa jamii kwa ajili hiyo. Aidha, Hospitali inayo masanduku ya maoni ambayo

kwa idadi, kama yalivyohesabiwa na watafiti, masanduku hayo hayazidi kumi, na kuna baadhi ya wodi

masanduku hayo hayapo. Kwa mujibu wa maelezo ya wahojiwa na kuthibitishwa na kumbukumbu za

vikao vya HMT, inaonekana kuwa malalamiko yanapokelewa kupitia masanduku au taarifa ya moja kwa

moja kwenye ofisi ya Mganga Mfawidhi wa Hospitali na hatimaye kwenye Kamati ya Nidhamu ya

Hospitali. Masanduku ya Maoni hufunguliwa na Sekretarieti ya Mkoa (Afisa Utumishi wa Mkoa) kila

baada ya miezi mitatu (3). Utafiti ulipitia mihtasari ya vikao vya HMT na kubaini kuwepo mashauri ya

nidhamu ya baadhi ya watumishi wa Hospitali. Hata hivyo, baadhi ya wahojiwa walieleza kuwa kamati

haichukui hatua zipasazo kutokana na woga walionao wajumbe wa kamati hiyo.

Vilevile, matokeo yanaonesha kuwa Kitengo cha Kupokelea na Kushughulikia malalamiko hakifahamiki

kwa watumishi wengine wengi (56%), na wagonjwa wa ndani wote (100%) na wagonjwa wa nje wote

(100%). Hali hii inatokana na kutowekwa wazi kwa kitengo hicho muhimu. Uwazi huu mdogo

unasababishwa na kutokuwepo kwa mbao za matangazo za kutosha na kutokuwepo kwa bango

linalowaelekeza wagonjwa kuhusu kutoa maoni au malalamiko yao kwenye kitengo hicho. Hali hii

inaashiria kuwepo udhaifu katika Hospitali wa kushughulikia malalamiko ya wagonjwa hasa ikizingatiwa

kuwa baadhi ya Wakuu wa Idara (22%) walieleza kutokuwepo Kitengo cha Kupokelea na Kushughulikia

Malalamiko.

Kuhusu namna ambavyo malalamiko yanapokelewa Hospitalini hapo, wastani wa asilimia 74 ya

wahojiwa walieleza kuwa malalamiko yanapokelewa kwa njia ya sunduku la maoni. Njia nyingine za

kupokelea malalamiko zilitajwa kuwa ni ofisi ya kitengo cha malalamiko (63%), vyombo vya habari

(17%), viongozi wa Hospitali (16%) na kuwahoji wagonjwa baada ya hatua yao ya mwisho ya huduma

(Exit Interview) (4%).

Hata hivyo, maelezo ya kupokelewa malalamiko kupitia ofisi ya Kitengo cha Kupokelea Malalamiko,

yanakosa mashiko kwa kuwa Kitengo hicho hakikuwa na ofisi Hospitalini hapo. Vilevile, ilifahamika

kwenye kikao na Menejimenti ya Hospitali cha tarehe 02/10/2010 kuwa pamekuwepo na utaratibu wa

kuwahoji wateja wanapoondoka hospitalini baada ya kupata huduma (Exit Interview); kwa lengo la

kutathmini utendaji na kufahamu malalamiko na maoni ya wagonjwa, lakini matokeo ya utafiti huu

Page 12: MUHTASARI - pccb.go.tz · ya Hospitali. Mawasiliano duni yanasababisha kutokuwepo maelewano kati ya wafanyakazi na uongozi na hivyo kusababisha wafanyakazi kukata tamaa na kujihusisha

6

yanaonesha kuwa Madaktari, wauguzi na watumishi wengine hawafahamu kama ‘Exit Interview’

hutumika kukusanyia malalamiko ya wagonjwa. Muhtasari wa kikao cha Kamati ya Uendeshaji ya Mkoa

na Kamati ya Uendeshaji ya Hospitali cha tarehe 14/07/2010 unatoa taarifa ya matokeo ya ‘Exit

Interview’ iliyofanyika hospitalini hapo na hivyo kuonesha kuwa inafanyika, hali inayoashiria kuwa

huenda taarifa sahihi kuhusu kinachojiri kwenye vikao hivyo huwa haziwafikii watumishi wengi.

c) Muda ambao mgonjwa umetumia kupata huduma

Matokeo yanaonesha kuwa wastani wa asilimia 71 ya wahojiwa walieleza kusubiri muda mrefu (masaa

mawili hadi matano) kabla ya kumwona daktari na aghalabu hucheleweshewa majibu ya vipimo.

Aidha, wamezitaja huduma zinazotolewa kwa muda wa chini ya masaa mawili kuwa ni kumwona daktari

(73%) na x-ray (54%). Huduma ambayo imeelezwa kutumia muda mrefu ni kupata majibu ya maabara.

Uchelewaji wa majibu ya maabara (saa 2 na zaidi) umetajwa na nusu ya wagonjwa wa nje kuliko

wagonjwa wa ndani (19%), hali ambayo huenda inatokana na wagonjwa wa ndani kutohusika moja kwa

moja na ufuatiliaji wa vipimo vyao. Aidha, hali hii inaweza kuwa inatokana na uchache wa madaktari na

watumishi wa maabara, na upungufu wa vifaa.

Hata hivyo, kwa ujumla wastani wa asilimia 28 ya wahojiwa walieleza kuwa muda wa huduma ulikuwa

bora, wakati asilimia 36 ya wahojiwa walieleza kuwa muda wa huduma Hospitalini hapo haufai.

Matokeo haya yanatofautiana na matokeo ya ‘Exit Interview’ yaliyotolewa kwenye Kikao cha

RHMT/HMT cha tarehe 14/07/2010 ambapo ilibainishwa kuwa asilimia 80 (wagonjwa 16 kati ya 20) ya

wagonjwa waliridhika na huduma za Hospitali. Hali hii inaonesha umuhimu wa kufanya tathmini za mara

kwa mara kuhusu kuridhika kwa wagonjwa juu ya huduma za Hospitali, badala ya kuegemea kwenye

tathmini moja tu.

d) Vikwazo ambavyo mgonjwa amepata wakati wa kupata huduma

Matokeo yanaonesha kuwa wastani wa asilimia 38 ya wahojiwa, hasa wagonjwa wa nje, walieleza

kuwahi kukwazwa na madaktari na wauguzi wakati wa huduma katika Hospitali ya Mkoa wa Morogoro.

Aidha, wastani wa asilimia 56 ya waliokwazwa, hasa wagonjwa wa ndani, waliwahi kukaripiwa na

wauguzi wa Hospitali ya Mkoa wa Morogoro. Kuwepo kwa lugha mbaya katika Hospitali

kunadhihirishwa pia na azimio la wajumbe wa kikao cha RHMT/HMT cha tarehe 14/07/2010 la kutaka

jitihada zifanyike kuondoa lugha mbaya ya watumishi.

Page 13: MUHTASARI - pccb.go.tz · ya Hospitali. Mawasiliano duni yanasababisha kutokuwepo maelewano kati ya wafanyakazi na uongozi na hivyo kusababisha wafanyakazi kukata tamaa na kujihusisha

7

Kwa upande wa wagonjwa kupewa nafasi ya kujieleza, asilimia 33 ya wagonjwa wa ndani walieleza

kutopewa muda wa kujieleza na daktari. Vilevile, wastani wa asilimia 62 ya wagonjwa walieleza

kutopatiwa dawa zote walizoandikiwa na daktari kutokana na upungufu wa dawa ikilinganishwa na

mahitaji. Kumbukumbu za Hospitali zinaonesha kuwa thamani ya dawa na vifaa kwa mwaka wa fedha wa

2009/10 ilikuwa ni shilingi 156,367,021.18 (Kiambatanisho II) ambazo utolewaji wake haukufanywa

kwa wakati na kusababisha Hospitali kukabiliwa na madeni. Aidha, kuna tatizo la udhibiti mdogo wa

fedha za Hospitali zinazopelekwa MSD kwa kuwa Hospitali haijulishwi na Wizara ya Afya kuhusu

mgawo huo. Vilevile, tatizo la wizi wa dawa za wagonjwa nalo linapunguza upatikanaji wake; mara

nyingine baadhi ya watumishi wa Hospitali walilalamikiwa kuwa walichukua dawa za wagonjwa wa

ndani kwa manufaa yao. Hata hivyo, katika maelezo yao wagonjwa wote waliohojiwa walieleza kuwa

hawajawahi kupeleka malalamiko yao kwa uongozi wa Hospitali.

Matokeo haya yanaashiria uwezekano wa kufanyika vitendo vya rushwa kutokana na hofu inayojengwa

kwa mgonjwa kiasi cha mgonjwa kushindwa kuomba usaidizi au kuhoji mambo anayofanyiwa kinyume

na haki zake kama mgonjwa. Hali inaweza kupelekea baadhi ya wagonjwa au ndugu/jamaa wa wagonjwa

kutumia pesa kama nyenzo ya kupunguza ukali wa wauguzi. Vilevile, hali hii inaweza kupunguza ufanisi

wa utendaji katika Hospitali. Ukali wa watoa huduma unaweza pia kuwakimbiza wagonjwa kutoka

Hospitali ya Mkoa wa Morogoro na kwenda kutafuta huduma kwingine na hata kwenye tiba za kienyeji,

na hivyo kukwaza jitihada za serikali za kuhakikisha wananchi wake wote wanapata huduma bora za

afya.

e) Mgonjwa kupatiwa stakabadhi kwa malipo ya huduma aliyoyafanya

Matokeo ya dodoso kwa wagonjwa yanaonesha kuwa wastani wa asilimia 52 ya wagonjwa walikuwa

wamelipia huduma, wengi wao ni wagonjwa wa nje (79%), wastani wa asilimia 90 ya wagonjwa

waliolipia huduma walipatiwa stakabadhi kwa malipo waliyoyafanya. Hata hivyo, wastani wa asilimia 10

ya wagonjwa walieleza kutopatiwa stakabadhi kwa malipo waliyoyafanya ambapo baadhi walieleza

kutolipia huduma kwa kuwa walikuwa kwenye utaratibu wa msamaha.

Wagonjwa waliohojiwa wanaeleza kuwa walifahamu gharama za huduma kupitia mbao za matangazo

(24%), kuelezwa mapokezi (37%), na kwa kuelezwa na daktari (33%).

Hospitali imeweka wazi na kuheshimu utaratibu wa kutoa msamaha kwa wagonjwa kwa maana ya

kuhakikisha ujazwaji sahihi wa fomu maalumu ya msamaha na vibali kwa wagonjwa wa ndani na wa nje.

Hata hivyo, Hospitali bado haina Afisa Ustawi wa Jamii ambaye ni mtu muhimu sana katika usimamizi

wa misamaha. Kwa upande wa wagonjwa wa ndani, hasa nyakati za usiku, Muuguzi Mfawidhi wa zamu

Page 14: MUHTASARI - pccb.go.tz · ya Hospitali. Mawasiliano duni yanasababisha kutokuwepo maelewano kati ya wafanyakazi na uongozi na hivyo kusababisha wafanyakazi kukata tamaa na kujihusisha

8

ndiye anayeidhinisha msamaha wa muda kwa wagonjwa wenye sifa za kupewa msamaha. Uidhinishaji

wa msamaha katika Hospitali ya Mkoa wa Morogoro inafanywa na Mganga Mfawidhi. Kwa upande wa

baadhi ya wagonjwa kutopewa stakabadhi, kunaashiria pamoja na mambo mengine, uwezekano wa

kuwepo upotevu wa mapato ya Hospitali yatokanayo na uchangiaji wa gharama za matibabu. Kwa mfano

katika mwaka wa fedha 2009/10 Hospitali ililenga kukusanya shilingi 200,000,000.00 lakini ikakusanya

shilingi 134,468,418.00 (67%) (Kiambatanisho III). Sababu nyingine zinazotajwa kupunguza mapato ni

mpangilio mbaya wa majengo ya Hospitali kwa ajili ya wagonjwa wa nje (OPD) na wagonjwa wa ndani

(IPD), rushwa na upendeleo katika misamaha. Muhtasari wa kikao cha HMT cha tarehe 16/07/2010

unabainisha kuwa misamaha ya wagonjwa ina harufu ya rushwa kutokana na shinikizo za watumishi wa

ngazi mbalimbali wa Hospitali kutaka watu wao wapewe misamaha. Aidha, kikao cha HMT cha tarehe

02/08/2010 kilionesha kutoridhishwa na ukusanyaji wa mapato na kuwataka watumishi wote kuwajibika

ipasavyo.

Kuhusu mpangilio wa OPD na IPD, Hospitali kihistoria ilikuwa ni kambi ya jeshi, hivyo haina mpangilio

wa kihospitali kiasi cha OPD na IPD kutojipambanua vyema. Hali hii inarahisisha kutoroka kwa

wagonjwa wanaopewa msamaha wa muda – yaani msamaha unaolazimisha kulipia huduma zinazofuata.

Kwa hali ilivyo sasa katika Hospitali, ni vigumu kumdhibiti mgonjwa iwapo ataamua kutoroka.

2.3 Uwazi wa Huduma katika Hospitali

a) Wagonjwa kufahamu haki zako wakati wa kupata huduma na njia waliyotumia kuzifahamu

Matokeo yanaonesha kuwa wastani wa asilimia 48 tu ya wagonjwa ndiyo walikuwa wanafahamu haki

zao; wengi wao (52%) walikuwa hawazifahamu haki zao hasa wagonjwa wa ndani (69%).

Aidha, wagonjwa walieleza kuzifahamu haki zao kupitia kuelezwa na wafanyakazi wa Hospitali (20%),

mbao za matangazo za Hospitali (30%), kuelezwa na jirani (41%), na vyombo vya habari (57%).

Haki ambazo wagonjwa wengi walieleza kuzifahamu ni pamoja na: haki ya kuhudumiwa kwa muda

sahihi (94%), haki ya kusikilizwa (90%), haki ya kutotamkiwa lugha ya ukali (79%), na haki ya

kujulishwa taratibu za huduma (53%).

Ufahamu mdogo wa wagonjwa kuhusu haki zao ni mwanya wa rushwa hasa kwa wagonjwa wa ndani

ambao pia walieleza kuchukuliwa dawa zao na watumishi wa Hospitali. Huenda kutofahamu haki kwao

huko ndiko kulikosababisha wao kuchelea kutoa taarifa za vitendo vya wizi wa dawa zao. Vilevile,

matokeo yanaashiria kuwa huenda wagonjwa wengi hawasomi mbao za matangazo za Hospitali na hivyo

kuwepo haja ya kubuni utaratibu mzuri wa kuwaelekeza wagonjwa na kuwapa elimu wananchi na

Page 15: MUHTASARI - pccb.go.tz · ya Hospitali. Mawasiliano duni yanasababisha kutokuwepo maelewano kati ya wafanyakazi na uongozi na hivyo kusababisha wafanyakazi kukata tamaa na kujihusisha

9

wagonjwa kuhusu haki na wajibu wao katika huduma za afya. Kwa kuanzia Hospitali inapaswa

kutekeleza utaratibu uliotajwa katika kikao cha HMT cha tarehe 02/08/2010 kuhusu kuwepo mtu maalum

wa kuwaelekeza wagonjwa (mfano; mtu aliyevaa nguo iliyoandikwa “NIULIZE MIMI”).

b) Uwazi katika mlolongo wa huduma

Taratibu za huduma za Hospitali zinapaswa kuwa wazi kwa wagonjwa ili kudhibiti mianya ya rushwa na

hatimaye kuongeza ufanisi wa utoaji huduma. Matokeo yanaonesha kuwa wastani wa asilimia 61 ya

wagonjwa walieleza kuwa mlolongo wa kupata huduma umewekwa wazi.

Hata hivyo, kuwepo kwa idadi kubwa ya wagonjwa wa ndani (63%), kwa maana ya jumla ya walioeleza

kutowekwa wazi kwa mlolongo wa huduma (19%) na wasiojua kama mlolongo wa huduma upo wazi

(44%), kunaashiria kuwa taratibu za huduma kwa wagonjwa wa ndani hazifahamiki kwa wagonjwa.

Kutofahamika huko kunatoa mwanya wa vitendo vya rushwa katika wodi za Hospitali.

2.4 Vitendo vya Rushwa Hospitalini

a) Wagonjwa walioshuhudia vitendo vyovyote vinavyoashiria rushwa Hospitalini

Matokeo yanaonesha kuwa wastani wa asilimia 38 ya wagonjwa walishuhudia vitendo vinavyoashiria

rushwa kutendeka Hospitalini hapo. Walivitaja vitendo vinavyoashiria rushwa kuwa ni: mgonjwa kupata

kitanda wakati wodi imefurika, mgonjwa kuombwa fedha ya soda na wauguzi, upendeleo kwa baadhi ya

wagonjwa, na kutopewa risiti ya malipo.

Kwa upande wao, watafiti wanakubaliana na maelezo ya wagonjwa ya kuwepo vitendo vya rushwa

Hospitalini hapo kwa sababu zifuatazo: Kwanza, mahojiano na viongozi yanadhihirisha kupokelewa kwa

malalamiko kumi (10) ya rushwa dhidi ya watumishi wa Hospitali katika kipindi cha kuanzia mwishoni

mwa 2009 hadi Oktoba 2010. Pili, waliokataa kushuhudia vitendo vya rushwa, walifanya hivyo kutokana

na woga waliokuwa nao wakati wa mahojiano. Wastani wa asilimia 62 ya wagonjwa waliokataa

kushuhudia vitendo vya rushwa, wengi wao wakiwa ni wagonjwa wa ndani (67%) walionekana kuwa na

hofu, kwa kuangalia maeneo mbalimbali ya wodi, pale walipoulizwa swali la kama wameshuhudia

vitendo vinavyoashiria rushwa. Hofu ya wagonjwa ilionekana kuzidi pale wauguzi walipopita karibu yao

wakati wa mahojiano. Hali hiyo ilimfanya mgonjwa mmoja kusita kujibu kwa sauti na badala yake

kuendelea kuitikia kwa ishara ya kichwa. Hofu yao inatia shaka ya kama walichokuwa wanaeleza ndicho

walichomaanisha. Hofu hiyo, ilisababisha wengi wao kudai kusikia zaidi kuliko kushuhudia moja kwa

moja na hivyo kukwepa ingawa si moja kwa moja. Hofu na woga wa wananchi umekuwa unakwaza

jitihada za serikali za kupambana na rushwa nchini Tanzania.

Page 16: MUHTASARI - pccb.go.tz · ya Hospitali. Mawasiliano duni yanasababisha kutokuwepo maelewano kati ya wafanyakazi na uongozi na hivyo kusababisha wafanyakazi kukata tamaa na kujihusisha

10

Sababu nyingine ya wagonjwa kukwepa kueleza kama walishuhudia vitendo vya rushwa inaweza

kutokana na kuogopa kuwa mashahidi dhidi ya watumishi husika hasa katika utambuzi wa watumishi

husika. Woga huu unaweza kuwa unachangiwa na baadhi ya watumishi kutokuwa na vitambulisho vya

kuvaa, na hata walionavyo, vitambulisho vyao havifanani kwa ubora kwa watumishi wote kiasi cha

kuwachanganya wagonjwa. Hali hii inakwaza utoaji wa malalamiko ya rushwa dhidi ya watumishi kwa

kuwa inakuwa vigumu kumtambua mtumishi husika.

b) Mafunzo ya utawala bora na mapambano dhidi ya rushwa kwa watumishi

Matokeo yanaonesha kuwa wastani wa asilimia 56 ya wahojiwa walieleza kupatiwa mafunzo ya utawala

bora na mapambano dhidi ya rushwa. Hata hivyo, madaktari wengi (78%), watumishi wengine (44%),

wauguzi (25%) na Wakuu wa Idara (22%) hawajapata mafunzo ya utawala bora na mapambano dhidi ya

rushwa ikilinganishwa na Menejimenti ambao wote walieleza kupatiwa mafunzo hayo. Matokeo haya

yanarandana na uadilifu mdogo wa baadhi ya watumishi waliotajwa kwenye kikao cha HMT cha tarehe

30/09/2010. Vilevile, Mpango Mkakati wa Hospitali wa 2009/10 hauzungumzii mapambano dhidi ya

rushwa katika ‘Key Result Areas’ (KRAs) zote hasa ‘KRA1’ inayohusika na rasilimaliwatu, ingawa zana

zilizotumika kama mwongozo wa kuweka vipaumbele vya kukabiliana na matatizo ya afya ya msingi

zinatajwa kuwa ni pamoja na MKUKUTA na Malengo ya Maendeleo ya Milenia. Mojawapo ya malengo

ya MKUKUTA ni kujenga utawala bora yakiwamo mapambano dhidi ya rushwa. Hali hii inaashiria

uwezekano wa ukiukwaji wa maadili kwa makundi hayo ya watumishi wa Hospitali ya Mkoa wa

Morogoro, hasa kwa kuzingatia kuwa Hospitali haijaunda Kamati ya Maadili.

2.5 Maoni ya Wahojiwa

Katika kutafuta mbinu za kudhibiti mianya ya rushwa katika Hospitali ya Mkoa wa Morogoro,

watumishi wa Hospitali, wagonjwa, CSOs na TUGHE waliombwa kuainisha sehemu za Hospitali

zenye rushwa na namna ya kuidhibiti Hospitalini hapo. Maoni ya wahojiwa yanaonesha kuwa sehemu

ya upasuaji inaongoza kwa rushwa ikifuatiwa na mapokezi na wodi ya wazazi (jedwali 1).

Page 17: MUHTASARI - pccb.go.tz · ya Hospitali. Mawasiliano duni yanasababisha kutokuwepo maelewano kati ya wafanyakazi na uongozi na hivyo kusababisha wafanyakazi kukata tamaa na kujihusisha

11

Jedwali 1; Maoni ya wahojiwa kuhusu maeneo ya Hospitali yanayohitaji udhibiti wa

rushwa

Eneo Alama

(%)

Upasuaji 21.6

Mapokezi 20.3

Wazazi (Labour) 14.9

Uhasibu 13.5

Maabara 12.2

Manunuzi 9.4

Utawala 8.1

JUMLA 100.0

Vilevile, waliainisha mbinu za kudhibiti rushwa katika Hospitali ya Mkoa wa Morogoro kuwa ni

kuboresha maslahi, kuhakikisha utoshelevu wa rasilimali, elimu ya maadili kwa watumishi, mafunzo

kazini, na kuimarisha uwazi na uwajibikaji. Uboreshaji wa maslahi ya watumishi umepata alama za juu,

ukifauatiwa na elimu ya maadili na rushwa kwa watumishi wa Hospitali na kusimamia uwajibikaji

(Jedwali 2).

Jedwali 2; Maoni ya wahojiwa kuhusu mbinu za kudhibiti rushwa Hospitalini

Mbinu Alama

(%)

Kuboresha maslahi ya watumishi 15.5

Kutoa elimu kwa watumishi kuhusu maadili na rushwa 14.7

Kusimamia uwajibikaji 13.2

Kuongeza na kuboresha vitendea kazi 11.6

Kuchukua hatua dhidi ya wala rushwa 10.8

Kutoa elimu kwa wananchi kuhusu taratibu za huduma 8.5

Kuongeza watumishi 5.4

Kuhakikisha uwiano mzuri wa mafunzo kwa watumishi 4.6

Kuondoa matabaka na upendeleo sehemu ya kazi 3.1

Kujenga hospitali za wilaya 3.1

Kuchunguza stakabadhi 3.1

Nyingine (kuongeza uwazi katika idara, kutoa fedha kulingana na bajeti, watumishi

wasikae eneo moja muda mrefu, na kuanzisha rejesta ya wagonjwa wa upasuaji)

6.4

JUMLA 100.0

Page 18: MUHTASARI - pccb.go.tz · ya Hospitali. Mawasiliano duni yanasababisha kutokuwepo maelewano kati ya wafanyakazi na uongozi na hivyo kusababisha wafanyakazi kukata tamaa na kujihusisha

12

3. MAPENDEKEZO

3.1.1 Mapendekezo kwa hospitali

Jedwali 3: Mapendekezo kwa Hospitali ya Mkoa wa Morogoro

Na. MIANYA YA

RUSHWA

MAPENDEKEZO YA KUZIBA MIANYA YA RUSHWA

1.0 UWAJIBIKAJI

MDOGO WA

WATUMISHI

WA

HOSPITALI

1.1 Kuboresha udhibiti wa ndani kwa kuzingatia yafuatayo:

Kuzingatia matakwa ya muundo ya unaibishaji wa mamlaka (yaani

majukumu na maamuzi);

Kuweka wazi mlolongo wa uwajibikaji;

Kuimarisha mawasiliano ya ndani;

Kuwapatia watumishi maelezo ya kazi zao (job description);

Kuwepo, kutambulika na kutumika kwa Mkataba wa Huduma kwa

Mteja;

Kufanywa kwa tathmini za utendaji (OPRAS na Exit Interview);na

Kufanya ukaguzi wa kushtukiza mara kwa mara; na uwazi katika

maamuzi kwa kuzingatia sheria.

1.2 Kuondoa ucheleweshaji wa huduma kwa kufanya yafuatayo:

Kusimamia mahudhurio na kudhibiti utoro wa watumishi;

Kuhamisha watumishi waliokaa sehemu moja ya kazi kwa muda

mrefu; na

Kufanya kazi kulingana na sheria, kanuni na taratibu.

1.3 Kuongeza tija ya watumishi kwa kufanya yafuatayo:

Kuboresha maslahi, mishahara na motisha kwa watumishi;

Kudhibiti manunuzi na usambazaji wa dawa na vifaa unaofanywa na

MSD;

Kuimarisha usimamizi wa rasilimaliwatu, dawa, na vifaa-tiba;

Kusimamia mapato na matumizi ya fedha; na

Kulipa stahili za watumishi ipasavyo.

Page 19: MUHTASARI - pccb.go.tz · ya Hospitali. Mawasiliano duni yanasababisha kutokuwepo maelewano kati ya wafanyakazi na uongozi na hivyo kusababisha wafanyakazi kukata tamaa na kujihusisha

13

2.0 UWAZI

MDOGO WA

HUDUMA

1.1 Kuimarisha mawasiliano ya Hospitali na wadau.

1.2 Kuweka wazi HAKI za WAGONJWA na taratibu za huduma kwa wadau

wote kwa njia mbalimbali ikiwa ni pamoja na vipeperushi na vyombo vya

habari.

1.3 Kukiimarisha na kukiweka wazi Kitengo cha Kupokelea na

Kushughulikia Malalamiko kwa maana ya:

Kuongeza masanduku ya maoni;

Kuwa na vhumba kinachokidhi kupokea malalamiko;

Kuwepo watumishi maalum wa Kitengo;

Kukitangaza kitengo cha kushughulikia malalamiko kwa wadau;

Kuwepo Kamati Maalum ya kufungua masanduku ya maoni na

kupitia maoni. Aidha, mihtasari ya vikao vya kamati iwe inaandikwa;

na

Masanduku ya Maoni yafunguliwe kila baada ya wiki 2.

1.4 Kuimarisha mawasiliano ya Hospitali na wadau.

3.0 UPUNGUFU

WA MAADILI

3.1 Kuongeza ufahamu wa watumishi na wananchi kuhusu rushwa kwa

kufanya yafuatayo:

Kutoa elimu ya mtanziko wa maadili (ethical dilemma) na jinsi ya

kukabiliana nao;

Kutoa elimu ya huduma bora kwa mteja;

Mafunzo kwa watumishi kuhusu suala la maadili;

Kutilia mkazo elimu ya madhara ya rushwa; na

Kuuingiza mkakati wa Hospitali wa kupambana na rushwa katika

Mpango Mkakati wa mwaka wa Hospitali.

3.2 Kuboresha mahusiano kazini kati ya mgonjwa/mdau na mtumishi kwa

kufanya yafuatayo:

Kuondoa lugha mbaya na wizi wa dawa za wagonjwa; na

Kuwapatia watumishi wote vitambulisho vya kuvaa.

3.3 Kuendeleza maadili, nidhamu na uwajibikaji wa watumishi kwa kufanya

yafuatayo:

Kuboresha Kamati ya Nidhamu kwa kuzingatia matakwa ya Sheria ya

Mahusiano ya Kazi ya mwaka 2004;

Kuundwa, kutambulika na kufanya kazi kwa Kamati ya Maadili;

Kuweka wazi majukumu ya Kamati ya Nidhamu, na makosa, adhabu

Page 20: MUHTASARI - pccb.go.tz · ya Hospitali. Mawasiliano duni yanasababisha kutokuwepo maelewano kati ya wafanyakazi na uongozi na hivyo kusababisha wafanyakazi kukata tamaa na kujihusisha

14

na haki ya kukata rufaa;

Kutoa zawadi kwa watendaji bora na kuwaadabisha wakosaji;

Kuimarisha usimamizi wa misamaha ya wagonjwa;

Kuondoa aina yoyote ya ubaguzi kazini; na

Kulipa stahili za watumishi.

3.1.2 Mapendekezo Kwa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii

Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii inashauriwa kuboresha uwajibikaji wa watumishi wa Sekta ya Afya

nchini kwa kufanya yafuatayo:

(i) Madaktari waliopewa madaraka wapatiwe mafunzo ya Uongozi na Utawala. Chuo cha Utumishi wa

Umma kinaweza kuendesha mafunzo hayo (TAKUKURU inaweza kusaidia);

(ii) Kusimamia uundwaji wa Bodi za Hospitali nchini;

(iii) Kujenga Hospitali za Wilaya za Morogoro na Mvomero;

(iv) Kuendelea na uboreshaji wa miundombinu ili kutenganisha OPD na IPD; na

(v) Kuongeza tija ya watumishi kwa kufanya yafuatayo:

Kuongeza mishahara na motisha kwa watumishi;

Kudhibiti manunuzi na usambazaji wa dawa na vifaa unaofanywa na MSD; na

Kuongeza watumishi na vifaa.

Page 21: MUHTASARI - pccb.go.tz · ya Hospitali. Mawasiliano duni yanasababisha kutokuwepo maelewano kati ya wafanyakazi na uongozi na hivyo kusababisha wafanyakazi kukata tamaa na kujihusisha

15

4. MKAKATI WA KUDHIBITI MIANYA YA RUSHWA

Baada ya kukamilika utafiti, TAKUKURU kwa kushirikiana na uongozi wa Mkoa na Hospitali ya

Morogoro iliandaa warsha ya kujadili matokeo. Warsha hii ilifanyika tarehe 10 Desemba, 2010 mjini

Morogoro na kuweka maazimio ya utekelezaji katika kudhibiti mianya ya rushwa iliyobainika katika

utafiti. Baada kuweka maazimio washiriki waliweka mkakati wa kudhibiti mianya ya rushwa ili

kuboresha huduma katika Hospitali ya Mkoa wa Mororgoro (Jedwali 4).

Jedwali 4: Mkakati wa Kuboresha Huduma za Hospitali ya Mkoa Morogoro.

Na

.

MAPUNGUFU

/MIANYA YA

RUSHWA

MAAZIMIO/MAPENDEKEZO

1.0 Uwajibikaji

mdogo wa

watumishi wa

Hospitali.

Kuboresha udhibiti wa ndani kwa kuzingatia yafuatayo:-

Kuzingatia matakwa ya muundo ya unaibishaji wa mamlaka (yaani

majukumu na maamuzi),

Kuweka wazi mlolongo wa uwajibikaji

Kuimarisha mawasiliano ya ndani

Kuwapatia watumishi maelezo ya kazi zao (job description)

Kuwepo, kutambulika na kutumikak wa Mkataba wa Huduma kwa

Mteja

Kufanywa kwa tathmini za utendaji (OPRAS na Exit Interview)

Kufanya ukaguzi wa kushtukiza mara kwa mara, na uwazi katika

maamuzi kwa kuzingatia sheria.

Kuondoa ucheleweshaji wahuduma kwa kufanya yafuatayo:-

- Kusimamia mahudhurio na kudhibiti utoro wa watumishi na

Kuhamisha watumishi waliokaa sehemu moja ya kazi kwa muda

mrefu.

Kufanya kazi kulingana na sheria, kanuni na taratibu

Kuongeza tija ya watumishi kwa kufanya yafuatayo:

- Kuboresha maslahi, mishahara na motisha kwa watumishi.

Kudhibiti manunuzi na usambazaji wa dawa na vifaa unaofanywa na

MSD.

Page 22: MUHTASARI - pccb.go.tz · ya Hospitali. Mawasiliano duni yanasababisha kutokuwepo maelewano kati ya wafanyakazi na uongozi na hivyo kusababisha wafanyakazi kukata tamaa na kujihusisha

16

Kuimarisha usimamizi wa rasilimali watu, dawa, na vifaa-tiba; na

Kusimamia mapato na matumizi ya fedha.

Kulipa stahili za watumishi ipasavyo

2.0 Uwazi mdogo

wa Huduma

Kuimarisha mawasiliano ya Hospitali na wadau

Kuweka wazi HAKI za WAGONJWA na taratibu za huduma kwa

wadau woe kwa njia mbalimbali ikiwa ni pamoja na vipeperushi na

vyombo vya habari

Kukiimarisha na kukiweka wazi Kitengo cha kupokelea na

kushughulikia malalamiko kwa maana ya:-

- Kuongeza masanduku ya maoni

Kuwa na chumba kinachokidhi kupokea malalamiko

Kuwepo watumishi maalum wa kitengo

Kukitangaza kitengo cha kushughulikia malalamiko kwa wadau

Kuwepo Kamati Maalum ya kufungua masanduku ya maoni na

kupitia maoni. Aidha, mihtasari ya vikao vya Kamati iwe

inaandikwa.

Masanduku ya maoni yafunguliwe kila baada ya wiki 2

3.0 Upungufu wa

maadili

Kuongeza ufahamu wa watumishi na wananchi kuhusu rushwa kwa

kufanya yafuatayo:-

- Kutoa elimu ya mtanziko wa maadili (Ethical dilemma) na jinsi

ya kukabiliana nao.

Kutoa elimu ya huduma bora kwa mteja

Mafunzo kwa watumishi kuhusu suala la maadili.

Kutilia mkazi elimu ya madhara ya rushwa, na kuingiza mkakati wa

Hospitali wa kupambana na rushwa katika Mpango Mkakati wa

mwaka wa Hospitali.

Kuboresha mahusiano kazini kati ya mgonjwa/mdau na mtumishi

kwa kufanya yafuatayo:-

- Kuondoa lugha mbaya na wizi wa dawa za wagonjwa

Kuwapatia watumishi wote vitambulisho vya kuvaa

Kuendeleza maadili, nidhamu na uwajibikaji wa watumishi kwa

kufanya yafuatayo:-

- Kuboresha Kamati ya Nidhamu kwa kuzingatia matakwa ya

Page 23: MUHTASARI - pccb.go.tz · ya Hospitali. Mawasiliano duni yanasababisha kutokuwepo maelewano kati ya wafanyakazi na uongozi na hivyo kusababisha wafanyakazi kukata tamaa na kujihusisha

17

Sheria ya Mahusiano ya Kazi ya mwaka 2004.

Kuundwa, kutambulika na kufanya kazi kwa Kamati ya Maadili.

Kuweka wazi majukumu ya Kamati ya Nidhamu, na makosa ,

adhabu na haki ya kukata rufaa.

Kutoa zawadi kwa watendaji bora na kuwaadabisha wakosaji.

Kuondoa aina yoyote ya ubaguzi kazini

4.0 Mapendekezo

kwa Wizara ya

Afya na Ustawi

wa jamii

Madaktari waliopewa madaraka wapatiwe mafunzo ya Uongozi na

Utawala, Chuo cha Utumishi wa Umma kinaweza kuendesha

mafunzo hayo. Aidha, TAKUKURU inaweza kusaidia.

Kusimamia uundwaji wa Bodi za Hospitali nchini

Kujenga Hospitali za halmashauri ya Wilaya za Manispaa,

Morogoro na Mvomero

Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii waendelee kusapoti

utenganishaji wa OPD na IPD

Kuongeza tija ya watumishi kwa kufanya yafuatayo:-

- Kuongeza mishahara na motisha kwa watumishi

- Kudhibiti manunuzi na usambazaji wa dwa na vifaa unaofanywa

na MSD, na

- Kuongeza watumishi na vifaa

Page 24: MUHTASARI - pccb.go.tz · ya Hospitali. Mawasiliano duni yanasababisha kutokuwepo maelewano kati ya wafanyakazi na uongozi na hivyo kusababisha wafanyakazi kukata tamaa na kujihusisha

18

5. HITIMISHO

Mianya ya rushwa iliyobainika katika huduma za Hospitali ya Mkoa wa Morogoro imeainishwa katika

makundi matatu ambayo ni: uwajibikaji mdogo wa watumishi, uwazi mdogo wa huduma za Hospitali, na

upungufu wa maadili.

Uwajibikaji mdogo unasababishwa na udhaifu wa udhibiti wa ndani hasa katika unaibishaji, mawasiliano

ya ndani, mbinu za uongozi, tathmini za utendaji, ufanyaji maamuzi, na udhibiti wa rasilimaliwatu.

Uwazi mdogo wa huduma za Hospitali umesababisha mambo yafuatayo: kutojulikana kwa haki za

wagonjwa; kutojulikana kwa taratibu za huduma; kutojulikana na kutoimarika kwa Kitengo cha

Kupokelea na Kushughulikia Malalamiko; na kuwepo kwa mawasiliano duni kati ya Hospitali na wadau.

Upungufu wa maadili pamoja na mambo mengine umesababishwa na ufahamu mdogo wa rushwa na

madhara yake, na maana na namna ya kukabiliana na mtanziko wa maadili. Aidha, upungufu wa maadili

umesababisha mahusiano mabovu kati ya wagonjwa na watumishi ambayo yanasababishwa na lugha

mbaya ya watumishi kwa wagonjwa, wizi wa dawa walizopewa wagonjwa, na watumishi kutovaa

vitambulisho na kutia ugumu wa kutambuliwa na wagonjwa. Vilevile, upungufu wa maadili

unasababishwa na kutokuwepo au udhaifu wa vyombo vinavyosimamia maadili (yaani Kamati ya

Nidhamu na kamati ya Maadili). Kamati ya Nidhamu iliyopo imelalamikiwa kuwa ni dhaifu kutokana na

kutochukua hatua zifaazo dhidi ya wakosaji. Udumavu wa kamati hiyo unatajwa kuwa unasababishwa na

woga wa wanakamati, na kutowekwa wazi kwa: kanuni zinazoongoza kazi za kamati; majukumu ya

kamati; makosa; adhabu; na haki ya kukata rufaa. Hata hivyo, Hospitali haina Kamati ya Maadili na hivyo

kusababisha mwanya wa ukiukwaji wa maadili. Utafiti unaamini kuwa iwapo serikali na uongozi wa

hospitali utayatafutia ufumbuzi mambo haya kama ambavyo imependekezwa, vitendo vya rushwa

vitadhibitiwa na huduma itaboreka zaidi hospitalini hapo.

Page 25: MUHTASARI - pccb.go.tz · ya Hospitali. Mawasiliano duni yanasababisha kutokuwepo maelewano kati ya wafanyakazi na uongozi na hivyo kusababisha wafanyakazi kukata tamaa na kujihusisha

19

VIAMBATANISHO

Kiambatanisho I: Organization Structure of Morogoro Regional Hospital

RDO RR RHET RLT RNO

HAB RMCHC

C

MOI/C

HHS HMT

HEAD PARTMENTS NOI/C HO OS

NO

ET ANAE STHE

T IST

PAEDIA

TRICIAN PATHO

LOGIST

SURG

EON

PHYSI

CIAN OBSGYN

PHAR

MACI ST

PHYS IOTH

MED.

SOC. W CASUALITY

AND OPD

OFFICER

OPTHAL

MOLOGIST DENTAL

OFFICER

RADIO

LOGIST

RMO

RPHCC

RHMT RHS

RE RHO RO

OCC

THER

ORTH

TECH

Page 26: MUHTASARI - pccb.go.tz · ya Hospitali. Mawasiliano duni yanasababisha kutokuwepo maelewano kati ya wafanyakazi na uongozi na hivyo kusababisha wafanyakazi kukata tamaa na kujihusisha

20

RMO – Regional Medical Officer RPHCC – Regional Primary Health Care

Coordinator/Committee

RHS – Regional Health Secretary RHMT – Regional Health Management Team

RNO – Regional Nursing Officer RMCH-CO – Regional Maternal & Child Health Coordinator

RE – Regional Epidemiologist RHO – Regional Health Officer

RP – Regional Pharmacist RO – Regional Ophthalmologist

RR – Regional Radiographer RDO – Regional Dental Officer

RLT – Regional Laboratory Tech. RHET – Regional Hospital Engineering Technician

HAB – Hospital Advisory Board MOI/C – Medical Officer In charge

HHS – Hospital Health Secretary HMT – Hospital Management Team

NOI/C – Nursing Officer In charge HO – Health Officer

OS – Office Supervisor ET – Engineering Technician

OBSGYN – Obstetrician &

Gynecologist

MED.SOC.W – Medical Social Worker

PHYSIOTH - Physiotherapist OCC.THER – Occupational Therapist

ORTH-TECH – Orthopaedic

Technician

CHANZO:Hospitali ya Mkoa wa Morogoro

Kiambatanisho II: Thamani ya vifaa na dawa-Hospitali ya Mkoa wa Morogoro 2009/10

TAREHE FEDHA

17/07/2009 27,364,018.09

08/09/2009 8,630,759.25

14/10/2009 16,312,739.10

14/10/2009 9,272,898.00

18/12/2009 15,188,558.00

17/03/2010 16,078,336.56

17/03/2010 5,383,061.40

10/05/2010 9,493,835.70

25/05/2010 3,432,000.00

15/06/2010 34,167,620.89

15/06/2010 7,531,194.19

JUMLA 156,367,021.18

CHANZO:Hospitali ya Mkoa wa Morogoro

Page 27: MUHTASARI - pccb.go.tz · ya Hospitali. Mawasiliano duni yanasababisha kutokuwepo maelewano kati ya wafanyakazi na uongozi na hivyo kusababisha wafanyakazi kukata tamaa na kujihusisha

21

Kiambatanisho III: Makusanyo na matumizi ya fedha za uchangiaji huduma za afya 2009/10

MWEZI MAKUSANYO MATUMIZI

Agosti……………………………………………………. 10,525,600/= 7,647,105/=

Septemba………………………………………………… 12,631,600/= 14,306,458/=

Oktoba……………………………………………………. 9,533,200/= 13,226,780/=

Novemba………………………………………………… 8,649,200/= 11,611,250/=

Desemba…………………………………………………. 14,517,200/= 8,088,400/=

Januari……………………………………………………. 13,831,600/= 8,293,361/=

Februari…………………………………………………… 12,191,200/= 5,798,200/=

Machi……………………………………………………… 12,653,618/= 15,154,200/=

Aprili……………………………………………………… 12,688,900/= 16,012,630/=

Mei………………………………………………………… 13,875,100/= 11,288,600/=

Juni………………………………………………………… 13,371,200/= 9,153,000/=

JUMLA 134,468,418/= 120,579,984/=

CHANZO:Hospitali ya Mkoa wa Morogoro