3
1 TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI 01 – 06 2014 TATHMINI KUHUSU UFINYU WA BAJETI INAYOTENGWA KWA AJILI YA DAWA MUHIMU, VIFAA TIBA NA VITENDANISHI Ukosefu wa mara kwa mara wa dawa muhimu na vifaa tiba katika vituo vya huduma za afya vya umma bado ni tatizo Tanzania. Tatizo hili linachangia kutolewa kwa huduma duni za afya zinazopelekea athari kwa afya za wananchi. Tathmini mbalimbali zimeonesha kuwa upatikanaji wa dawa muhimu na vifaa tiba ni mdogo katika vituo vya huduma za afya vya umma. Kwa mfano, utafiti uliofanywa na Sikika mwaka 2012 umeonesha kuwa asilimia 52 ya hospitali [N=52] hazikuwa na dawa muhimu na vifaa tiba kwa zaidi ya wiki nne. 1 Moja ya sababu kuu za kukosekana kwa dawa muhimu na vifaa tiba ni bajeti ndogo inayotengwa na serikali. Mwenendo wa mgao wa fedha za dawa muhimu na vifaa tiba kutoka Bajeti ya WAUJ kutoka 2008/09 hadi 2014/15 1 Sikika: Report on Availability of Essential Medicines, Medical Supplies and Bed Capacity in Hospitals in Tanzania mainland, March 2013 Mwaka Bajeti ya WAUJ (Tsh Bilioni) Bajeti ya dawa muhimu na vifaa tiba (Tsh Bilioni) Mabadiliko ya asilimia ya bajeti ya dawa muhimu na vifaa tiba 2008/09 440.2 53.4 2009/10 478.9 49.6 7.1 2010/11 676.3 61.4 23.8 2011/12 584.2 78.7 28.2 2012/13 576.1 80.5 2.3 2013/14 753.9 64 20.5 2014/15 622.9 45.8 28.4

Press Release on Budget Allocation for Medicines & Medical Supplies

Embed Size (px)

DESCRIPTION

TATHMINI KUHUSU UFINYU WA BAJETI INAYOTENGWA KWA AJILI YA DAWA MUHIMU, VIFAA TIBA NA VITENDANISHI

Citation preview

Page 1: Press Release on Budget Allocation for Medicines & Medical Supplies

  1  

   

 

 

TAARIFA  KWA  VYOMBO  VYA  HABARI  

01  –  06  -­‐  2014  

TATHMINI  KUHUSU  UFINYU  WA  BAJETI  INAYOTENGWA  KWA  AJILI  YA  

DAWA  MUHIMU,  VIFAA  TIBA  NA  VITENDANISHI  

 

Ukosefu   wa   mara   kwa   mara   wa   dawa   muhimu   na   vifaa   tiba   katika   vituo   vya  

huduma   za   afya   vya   umma   bado   ni   tatizo   Tanzania.   Tatizo   hili   linachangia  

kutolewa  kwa  huduma  duni  za  afya  zinazopelekea  athari  kwa  afya  za  wananchi.    

 

Tathmini  mbalimbali   zimeonesha   kuwa   upatikanaji  wa   dawa  muhimu   na   vifaa  

tiba   ni  mdogo   katika   vituo   vya   huduma   za   afya   vya   umma.   Kwa  mfano,   utafiti  

uliofanywa   na   Sikika   mwaka   2012   umeonesha   kuwa   asilimia   52   ya   hospitali  

[N=52]  hazikuwa  na  dawa  muhimu  na  vifaa  tiba  kwa  zaidi  ya  wiki  nne.1  

Moja  ya  sababu  kuu  za  kukosekana  kwa  dawa  muhimu  na  vifaa  tiba  ni  bajeti  ndogo  inayotengwa  na  serikali.    

Mwenendo  wa  mgao  wa  fedha  za  dawa  muhimu  na  vifaa  tiba  kutoka  Bajeti  

ya  WAUJ  kutoka  2008/09  hadi  2014/15  

 

                                                                                                               1  Sikika:  Report  on  Availability  of  Essential  Medicines,  Medical  Supplies  and  Bed  Capacity  in  Hospitals  in  Tanzania  mainland,  March  2013  

Mwaka    Bajeti  ya  WAUJ  (Tsh  Bilioni)  

Bajeti  ya  dawa  muhimu  na  vifaa  tiba  (Tsh  Bilioni)    

Mabadiliko  ya  asilimia  ya  bajeti  ya  dawa  muhimu  na  vifaa  tiba  

2008/09   440.2   53.4      2009/10   478.9   49.6     -­‐7.1  2010/11   676.3   61.4     23.8  2011/12   584.2   78.7     28.2  2012/13   576.1   80.5     2.3  2013/14   753.9   64     -­‐20.5  2014/15   622.9   45.8     -­‐28.4  

Page 2: Press Release on Budget Allocation for Medicines & Medical Supplies

  2  

Chanzo:  Sikika 2010/2011 Health Sector Budget Analysis, Sikika  Budget  Analysis  of  the  MoHSW  for  

fiscal  year  2013/14.  

 Mahitaji  ya  dawa  muhimu  na  vifaa  tiba    Ingawa  mojawapo  ya  vipaumbele  vya  Wizara  ya  Afya  ni  kuboresha  upatikanaji  

wa   dawa  muhimu,  mgao  wa   fedha   kwa   dawa  muhimu   na   vifaa   tiba   umekuwa  

hauendani  na  mahitaji  yake.  Kwa  mfano  kwa  mujibu  wa    makadirio  ya  Wizara  ya  

Afya  zitahitajika  kiasi  cha  Tsh  250  bilioni  kukidhi  mahitaji  ya  dawa  muhimu  kwa  

mwaka  wa  fedha  2014/15.  Hata  hivyo,  mgao  unaotarajiwa  kupangwa  ni  shilingi  

bilioni  45  tu.  Mgao  huu  ni  sawa  na  asilimia  7.7  ya  mahitaji.  

 

Pamoja  na  hivyo,   ingawa  kipaumbele  cha  Wizara  ya  Afya  ni  kupungunguza  vifo  

vya   kina   mama   vitokanavyo   na   kujifungua,   bajeti   ya   vifaa   vya   kujifungulia  

(delivery   kits)   inapungua   mwaka   hadi   mwaka.   Mfano,   kwa   mwaka   wa   fedha  

2012/13  zilitengwa  jumla  ya  Tsh  bilioni  nne  kwa  ajili  ya  vifaa  vya  kujifungulia.  

Bajeti  hii  ilipungua  kufikia  bilioni  tatu  mwaka  2013/14,  na  kama  hakutakuwepo  

mabadiliko  itapungua  hadi  kufikia  shilingi  bilioni  moja  na  nusu  mwaka  ujao  wa  

fedha  2014/15    

 

Pia,   pamoja   na   serikali   kuahidi   bunge   mwaka   jana   kulipa   deni   ambalo   MSD  

inaidai  serikali,  deni  hilo  limeongezeka  toka  shilingi  bilioni  76  mwaka  2013  hadi  

bilioni  89  mwaka  2014  

 Mjadala  wa  Bunge  juu  ya  Bajeti  ya  WAUJ    Mapitio  ya  hansards  (2008/09  –  2012/13)  yamebaini  kuwa  takribani  asilimia  35  

ya   wabunge   ambao   huchangia   katika   mjadala   wa   bajeti   ya   Afya   hulalamika  

kuhusu  uhaba  wa  dawa  vituoni  na  huitaka  serikali,  pamoja  na  mambo  mengine  

kuongeza   bajeti.   Tunawapongeza   Wabunge   kwa   kazi   hii   nzuri.   Lakini   kama  

ilivyoainishwa  hapo   juu,  bajeti  ya  dawa  imekuwa  ikipungua  na  uhaba  wa  dawa  

muhimu   umeendelea   kuwepo.   Pia   akina   mama   wanaojifungua   wameendelea  

kulalamika  ukosefu  wa  vifaa  vya  kujifungulia  

 Mapendekezo    

Page 3: Press Release on Budget Allocation for Medicines & Medical Supplies

  3  

1. Serikali   itafute   fedha   za   ziada   kutoka   katika   sekta   nyingine   (kuhamisha)   ili  

kuongeza   bajeti   ya   dawa  muhimu   inayotarajiwa   kutengwa   kwa  mwaka  wa  

fedha  2014/15  kutoka  bilioni  45  hadi  bilioni  250  (kwa  mujibu  wa  makadirio  

ya  Wizara  ya  Afya)  

2. Wizara   ya   Afya   na   ustawi   wa   Jamii   ihamishe   fedha   kutoka   kwenye   idara  

nyingine   kwenda   kwenye   dawa   muhimu   na   vifaa   tiba   ili   kuweza   kuwa   na  

bajeti  inayolingana  na  mahitaji.  

3. Serikali  ijadiliane  na  wafadhili  ili  waweze  kuongeza  fedha  katika  bajeti  hii  ya  

mwaka   2014/15   (kama   suluhisho   la   muda   mfupi)   wakati   ikiendelea  

kubainisha    suluhisho  la  kudumu  kama  kuboresha  na  kusimamia  ukusanyaji  

wa   kodi,   kupunguza   au   kuondoa   misamaha   ya   kodi   pia   kuboresha  

makusanyo   yannayokana   na   mifuko   ya   afya   kama   Mfuko   wa   Afya   wa  

jamii(CHF)   na   Mfuko   wa   Bima   ya   Afya   wa   Taifa.(NHIF).   Serikali   inapaswa  

kuwa   Mchangiaji   mkuu   wa   dawa   muhimu   na   vifaa   tiba   na   sio   kuwaachia  

jukumu  hili  wafadhili.  

4. Mipango  na  mgao  wa  bajeti  unapaswa  kuzingatia    mapendekezo  yaliyotolewa  

na  bunge  kupitia  kamati  ya  kudumu  ya  huduma  za  jamii.    

   

 

   

Mr. Irenei Kiria Executive Director of Sikika, P.O. Box 12183 Dar es Salaam,

Tel: +255 222 666355/57, Fax: 2668015, Email: [email protected], Website: www.sikika.or.tz