20
DIBAJI Ndugu wanajumuiya, Assalam alaikum Naomba nianze kwanza kwa kumshukuru ALLAH (SW) mwingi wa rehema kwa kutujalia afya kwa mwaka 2012, kuweza kutekeleza kazi mbalimbali za Jumuiya. Pili napenda kuwapa pole wanajumuiya mbalimbali ambao kwa mwaka 2012, walifiwa na wawapendao, kama wazazi, waume, wake au watoto Pia nichukue fursa hii kuwapongeza wale wote waliofanikiwa kufunga ndoa, na wale waliojaliwa kupata watoto. Mwenyezi Mungu awape Baraka tele na afya. Ndugu Wanajumuiya kwa mujibu wa katiba yetu ibara ya 10: 7;3 na 13, Jumuiya inapaswa kuandaa taarifa ya utekelezaji wa shughuli za mwaka mmoja na kufanya mkutano mkuu wa mwaka kati ya Januari/ Februari. Mkutano mkuu utapokea taarifa za Jumuiya kwa kipindi cha mwaka mmoja na kujadili, kutoa maoni na mapendekezo. Nichukue pia fursa hii kuwashukuru nyinyi wanajumuiya kwa ushiriki wenu mzuri kwa mwaka 2012, pia niwashukuru viongozi wote wa ngazi mbalimbali kwa kufanikisha utendaji wa kazi mbalimbali za Jumuiya kwa mwaka 2012. 1

Taarifa Ya Mwaka

Embed Size (px)

Citation preview

Page 1: Taarifa Ya Mwaka

DIBAJI

Ndugu wanajumuiya,

Assalam alaikum

Naomba nianze kwanza kwa kumshukuru ALLAH (SW) mwingi wa rehema kwa kutujalia afya

kwa mwaka 2012, kuweza kutekeleza kazi mbalimbali za Jumuiya.

Pili napenda kuwapa pole wanajumuiya mbalimbali ambao kwa mwaka 2012, walifiwa na

wawapendao, kama wazazi, waume, wake au watoto

Pia nichukue fursa hii kuwapongeza wale wote waliofanikiwa kufunga ndoa, na wale

waliojaliwa kupata watoto. Mwenyezi Mungu awape Baraka tele na afya.

Ndugu Wanajumuiya kwa mujibu wa katiba yetu ibara ya 10: 7;3 na 13, Jumuiya inapaswa

kuandaa taarifa ya utekelezaji wa shughuli za mwaka mmoja na kufanya mkutano mkuu wa

mwaka kati ya Januari/ Februari. Mkutano mkuu utapokea taarifa za Jumuiya kwa kipindi cha

mwaka mmoja na kujadili, kutoa maoni na mapendekezo.

Nichukue pia fursa hii kuwashukuru nyinyi wanajumuiya kwa ushiriki wenu mzuri kwa mwaka

2012, pia niwashukuru viongozi wote wa ngazi mbalimbali kwa kufanikisha utendaji wa kazi

mbalimbali za Jumuiya kwa mwaka 2012.

Baada ya utangulizi huo naomba sasa nihudhurishe mbele yenu taarifa ya Jumuiya ya mwaka

2012, nanyi muijadili ,mtoe maoni au mapendekezo

Wenu

Abdallah Bihoga

Amir

1

Page 2: Taarifa Ya Mwaka

SURA YA KWANZA

UTANGULIZI

Jumuiya ya waislam KCMC (KMA) ni jumuiya huru ya Kiislamu iliyopo Moshi- Kilimanjaro.

Jumuiya hii wanachama wake ni wanafunzi wanaosoma vyuo mbalimbali vya KCMC,

Wataalamu wa afya mafunzoni( Interns) na wafanyakazi wa taasisi mbalimbali za KCMC.

Pia Jumuiya hii hutoa nafasi ya Uanachama wa heshima kwa Muislamu yeyote mwenye mapenzi

na jumuiya na kwa wale waliowahi kuwa wanachama wa Jumuiya (wale waliomaliza mafunzo

au kuacha/ kustaafu kazi KCMC).

Madhumuni ya Jumuiya hii ni kuwaunganisha na kuwaweka pamoja waislamu wote waliopo

kwenye jamii ya KCMC ili kukuza moyo wa kidugu wa kiislamu na ushirikiano baina yao; pia

kuhakikisha wanajumuiya wanaishi kwa kufuata miongozo, mila na hulka za dini ya kiislamu.

2

Page 3: Taarifa Ya Mwaka

SURA YA PILI

UONGOZI

Kwa mwaka 2012, Jumuiya ya Kislamu ya KCMC (KMA) imekuwa na viongozi kwa awamu

mbili (2) kutokana na kufanya uchaguzi katikati ya mwaka.

Kwa mwaka 2012, Viongozi wakuu wa Jumuiya walikuwa ni:_

Awamu ya kwanza Awamu ya pili

Abdallah Bihoga- Amir Abdallah Bihoga- Amir

Amour Shaaban- Naibu Amir Mwalimu Khalid- Naibu Amir

Fani Musa- Katibu Mkuu Fani Musa- Katibu Mkuu

Pia katika kuhakikisha kuwa kuna kuwa na ufanisi katika utendaji wa kazi za Jumuiya. Jumuiya

ina kamati tano (5) za utendaji na katika mwaka 2012, wafuatao ndio walikuwa viongozi wa

kamati

KAMATI YA HUDUMA ZA JAMII

Awamu ya kwanza Awamu ya pili

Othman Wamala- Amir Shamiru Ismail- Amir

Shamiru Ismail- Katibu Abubakar Sudi- Katibu

Nyanza Simba- Mjumbe Heri Nyamvi- Mjumbe

Mary Kawiche- Mjumbe Shaban Yusuf- Mjumbe

Maimuna Mohamed- Mjumbe Husna Muna- Mjumbe

Nazmin Nazir- Mjumbe Hamisi Matula- Mjumbe

Warda Baltazar- Mjumbe Juma B.Juma- Mjumbe

Ziad Abdul- Mjumbe Salama Omar Mahawi- Mjumbe

Heri Nyamvi- Mjumbe

3

Page 4: Taarifa Ya Mwaka

KAMATI YA DA’AWA

Awamu ya kwanza Awamu ya pili

Mwalimu Khalid- Amir Abdallah Mwinyihaji- Amir

Yahaya Ali- Katibu Ramadhani Y.Ramadhani- Katibu

Athumani Mwedi- Mjumbe Musa Makame- Mjumbe

Fatma Msemo- Mjumbe Ramadhani Hamis- Mjumbe

Hussein Mwangi’mba- Mjumbe Salum Ally- Mjumbe

Masoud Rashid- Mjumbe Salma Jafari- Mjumbe

Abdallah Mwinyihaji- Mjumbe Fatma Miraji- Mjumbe

Arafat S.Suleiman- Mjumbe Uwesu Muki-Mjumbe

KAMATI YA FEDHA NA UCHUMI

Awamu ya kwanza Awamu ya pili

Hamisi Mvugalo- Amir Shabani Massawe- Amir

Asha Kumpuni- Katibu Lulu Mushi- Katibu

Mwanaid Mwinjuma- Mjumbe Faudhia Hadith- Mjumbe

Shabani Massawe-Mjumbe Arafat Massawe- Mjumbe

Daudi Katwana- Mjumbe Ismail A.Chuwa- Mjumbe

Samiha A. Juma- Mjumbe Hamisi Sembe- Mjumbe

Mohamed Mbalazi- Mjumbe Amri Kyaruzi- Mjumbe

Mwanaid Mwinjuma- Mjumbe

4

Page 5: Taarifa Ya Mwaka

KAMATI YA HABARI, MAWASILIANO NA TAKWIMU

Awamu ya kwanza Awamu ya pili

Hassan Kabange- Amir Othman Wamala- Amir

Daudi A. Joho- Katibu Daudi A. Joho- Katibu

Mubashir Jusabani- Mjumbe Ibrahim Sassilo- Mjumbe

Nuru Mwaluwinga- Mjumbe Maulid Abdallah- Mjumbe

Ashraf Hamza- Mjumbe Yusuf Abdulrahman- Mjumbe

Ibrahim Sassilo- Mjumbe Dawani Ngomelo- Mjumbe

Maulid Abdallah- Mjumbe Thabit K- Ramadhani- Mjumbe

Asha Mswahili- Mjumbe

KAMATI YA WANAWAKE

Awamu ya kwanza Awamu ya pili

Zubeda Amir- Amira Ashura Kazema- Amira

Salma Sued- Naibu Amira Samiha Abdallah- Naibu Amira

Salma Mwamba- Katibu Nuru Mwaluwinga- Katibu

Orpar E Msuya- Mjumbe Aisha Abubakar-Mjumbe

Mwema Ndekio- Mjumbe Rabia Mmanga-Mjumbe

Sabra Yahya- Mjumbe Asha Kumpuni-Mjumbe

Dr. Hudaa Akabi-Mjumbe Nabila F. Ally-Mjumbe

Dr. Fatma Makuka-Mjumbe Maimuna Ally-Mjumbe

Samiha Abdallah-Mjumbe

Salha M. Sheikh-Mjumbe

5

Page 6: Taarifa Ya Mwaka

Pia kulingana na mahitaji ya jumuiya iliunda kamati ndogo, ya nusra na viongozi wake walikuwa

ni:-

Othman Wamala - Amir

Mwalimu Khalid - Naibu Amir

Mussa Makame - Katibu

Salha Ally Omari - Mjumbe

Rashida Ismail - Mjumbe

Zuwena Gwotta - Mjumbe

6

Page 7: Taarifa Ya Mwaka

SURA YA TATU

UTEKELEZAJI WA KAZI MBALIMBALI ZA JUMUIYA

A: MAFANIKIO;

Mafanikio ya jumla

(i) Umoja

jumuiya ya kiislamu, inajivunia kwa kuimarisha umoja na mshikamano miongoni mwa

wanajumuiya, bila kujali tofauti baina yetu. kwa kipindi chote cha 2012, tumekuwa wamoja,

na tumekuwa na mshikamano thabiti.

(ii) Ushirikishwaji wanajumuiya

Wanajumuiya wote , wamekuwa wakishirikishwa na kushiriki kikamilifu katika kazi za

utendaji za kila siku, na pia katika majukumu ya uongozi katika ngazi zote. Na maamuzi

yote yamekuwa yakitolewa na wote na wala sio watu au kikundi mahususi

(iii) Katiba

Mwaka 2012, wanajumuiya walifanikiwa kutoa maoni yao na hatimaye tumekamilisha

uandishi wa katiba ya jumuiya yetu na tunategemea mwaka 2013 kusajiliwa rasmi

(iv) Kufungua sanduku la barua

Mwaka 2012, jumuiya imefanikiwa kufungua sanduku la barua rasmi S.L.P 287 Moshi,

kwa jili ya mawasiliano, kupokea barua na vifurushi

(v) Seminaelekezi

Jumuiya ilifanikisha kuendesha semina elekezi mbili (2) kwa mwaka 2012.

Semina ya kwanza ilikuwa ni kwa ajili ya kuItambulisha jumuiya na semina ya pili ilikuwa

ni kuwapa mafunzo viongozi wa kamati mbalimbali juu ya utekelezaji wa kazi zao za kila

siku.

(vi) Ujenzi wa sehemu ya kuchukua udhu

Jumuiya na kupitia wahisani tumefanikiwa kutengeneza sehemu nzuri ya kuchukulia udhu

katika msikiti wetu na hivyo kuupa msikiti mandhari ya kupendeza

7

Page 8: Taarifa Ya Mwaka

(vii) Ununuzi wa vitabu mbalimbali

Jumuiya yetu imefanikiwa kununua vitabu mbalimbali kwa ajili ya kuimarisha maktaba

yetu pia tulipokea msaada wa vitabu kutoka taasisi ya African Muslims Agency

(viii) Kuchapisha vitabu vya stakabadhi

Jumuiya ilichapisha vitabu vya stakabadhi, ambavyo vimetumika kuweka kumbukumbu

sahihi za mapato ya jumuiya

(ix) Ununuzi wa viandiko na muhuri,

Jumuiya imenunua viandiko (stationaries) mbalimbali na pia ilichonga mihuri ya jumuiya

ili kufanikisha kazi za kiofisi za jumuiya

(x) Vikao vya jumuiya

Jumuiya imekuwa ikifanya kazi kwa vikao vyake rasmi, kama vikao vya ngazi za

mashina na Shura ili kuleta ufanisi zaidi

(xi) Uchaguzi mkuu

Jumuiya ilifanya uchaguzi wake mkuu juni 2012 na kuchagua viongozi wa kuendesha

jumuiya mpaka Februari 2013

(xii) Kusimamia utendaji wa kazi za jumuiya na uelekezi

Jumuiya imekuwa ikifanya kazi za usimamiaji wa utendaji wa kamati ( supervision) na

mashina na kutoa uelekezi ili kuboresha utendaji kazi

8

Page 9: Taarifa Ya Mwaka

Mafanikio mahsusi:-

Masuala ya huduma ya jamii;

i. Kusimamia matukio ya msiba

kamati ilifanya kazi ya kuarifu wanajumuiya juu ya misiba iliyowafika wanajumuiya

wenzetu na kuwashirikisha wanajumuiya katika kuwafariji wenzetu.Mwaka 2012 Dr. Mtagi

Kibatala, Neema Massawe na Fatma Ahmed na Mwanaidi Mwinjuma walifikwa na misiba

ya wapendwa wao.

ii. Kusimamia masuala ya maradhi

Kamati pia imekuwa ikiwaarifu wanajumuiya juu ya wanaofikwa na maradhi na

kuhamasisha kuwahudumia.Wanajumuiya mbalimbali walifikwa na maradhi na mwenzetu

mmoja,Amani Kapinga (MD4) alipatwa na ajali ya kupigwa na risasi.

iii. Kusimamia masuala ya harusi

Kamati pia imekua ikitoa taarifa za wanajumuiya wanaofunga ndoa na kuhamasisha ushiriki

wa wanajumuiya katika harusi hizo kwa hali na mali.Mwaka 2012 wanajumuiya wafuatao

walifunga ndoa Dr. Adnan Juma na Dr. Rehema, Asma Bakari

iv. Michezo

Kamati iliandaa tamasha la michezo la ndani kwa ajili ya wanajumuiya pia tulishiriki katika

tamasha la michezo nje ya jumuiya kwa madhumuni ya kuimarisha udugu na umoja wetu wa

kiislamu

v. Kuratibu mfungo wa mwezi wa Ramadhani

Kamati iliandaa utaratibu mzuri wa mfungo wa mwezi wa Ramadhani,kwa kuhakikisha

wanajumuiya tunafuturu pamoja na pia kuandaa daku kwa wote

vi. Kutoa msaada na kutembelea watoto yatima

Kamati iliandaa siku maalum ya kutembelea watoto yatima kuwafariji na kuwapa msaada

vii. Kutoa elimu ya Afya

Kamati kwa kushirikia na kamati ya Da’awa walitoa elimu ya Afya ya magonjwa ya zinaa

kwa vijana wa sekondari

viii. Kuandaa sherehe mbalimbali

Mwaka 2012, kamati iliratibu na kuandaa sherehe za Idd El fitri & Eid El Haji, sherehe ya

kuwakaribisha mwaka wa kwanza na mahafali.

9

Page 10: Taarifa Ya Mwaka

Masuala ya kamati ya Da’awa

i. Uendeshaji wa madarasa ya Ijumaa , Jumamosi na Jumapili

Kamati iliandaa madarasa ya Ijumaa, kwa ufanisi mkubwa

Pia iliendesha kwa wastani madarasa ya Jumamosi na Jumapili

Kamati pia ilitafuta watoa mada katika madarasa na sherehe mbalimbali za jumuiya

ii. Uangalizi wa Msikiti

Kamati ilihakikisha usafi wa msikiti wa kila wiki mwisho wa mwezi unafanyika, pia

kuuweka msikiti katika mandhari nzuri.Kamati pia ilisimamia ibada mbali kama sala

tano(5), tarawehe, hadithi ya siku vinasimamishwa katika msikiti

iii. Jaula

Kamati ilifanya ziara za kuwatembelea wanajumuiya katika hosteli na pia wanafunzi wa

sekondari nje ya jumuiya kwa lengo la kubadilishana mawazo,kuamrishana mema na

kukatazana mabaya

Masuala ya Kamati ya fedha na uchumi

i. Kukusanya michango na kuendesha miradi

Kamati ilikusanya michango mbalimbali kama ada za wanajumuiya,zaka/ sadaka na

michango ya ngazi ya kifamilia. Pia iliweza kukusanya fedha kutoka katika miradi ya

jumuiya.Kamati lifanikiwa kukusanya jumla ya Tsh 2, 948,985/=

ii. Kuandaa bajeti na taarifa za fedha

Kamati ilikuwa ikiandaa taarifa za fedha (mapato na matumizi) za mwezi, miezi 3,6, na

ya mwaka na pia kuandaa bajeti ya mwaka ya jumuiya.

iii. Kuweka Akiba

Kamati pia imeendeleza kuweka akiba, kuhakikisha hazina ya jumuiya haitetereki.Kwa

mwaka 2012, Kamati iliweka akiba ya Tsh. 627,123.91 na mpaka mwisho wa mwaka

2012, Jumuiya imebaki na salio la Tsh 1, 267, 591.51 benki.

10

Page 11: Taarifa Ya Mwaka

Masuala ya Kamati ya habari, takwimu na mawasiliano

i. Kusimamia vyombo vya habari vya jumuiya

Kamati ilisimamia sanduku la barua, blogu, barua pepe na mitandao ya kijamii ya

facebook ili kurahisisha mawasiliano na uenezaji wa habari.

ii. Utunzaji wa kumbukumbu takwimu na uchambuzi wa taarifa za usajili za uanachama

Kamati imekuwa ikikusanya taarifa za wanajumuiya katika faili la usajili, pia imekuwa

ikitunza taarifa za uanachama na takwimu za mahudhurio katika semina na sherehe

mbalimbali.

iii. Kusaidia mitambo ya kompyuta katika sherehe na madarasa mbalimbali.

Kamati imekuwa ikisimamia mitambo ya kompyuta au projekta kwenye madarasa au

sherehe mbalimbali za jumuiya na pia kuandaa waendeshaji wa sherehe (MCs)

iv. Kuendesha mradi wa kuuza DVD za mahafali

Kamati ilizalisha na kuuza DVD za mahafali ya jumuiya yetu, ambazo zilisaidia kuingiza

mapato katika jumuiya.

Masuala ya kamati ya wanawake

i. Kuendesha darasa la wanawake la kila jumapili na kutafuta wahadhiri

Kamati iliendesha darasa la wanawake la kila jumapili ili kuwainua kiimani wanawake na

pia ilitafuta wahadhiri kutoka nje, kufanikisha uendeshaji wa darasa hilo.

ii. Kushiriki kongamano la wanawake

Kamati ilishirikiana na kamati ya wanawake wa Mkoa, katika kuandaa na kushiriki

katika kongamano la wanawake la mkoa lililofanyika January 2012

iii. Siku ya Hijabu

Kwa mara ya kwanza, kamati yetu iliweka historia kuasisi siku ya Hijabu kwa wanawake

wa KCMC. Siku hiyo ilifana na wanawake waliweza kubadilishana

mawazo,kuelimishana na kupeana mawaidha yenye manufaa

iv. Kuimarisha Umoja wa wanawake

Kamati umefanya juhudi kubwa katika kuhimiza na kufanikisha umoja wa wanawake

waliopo KCMC na nje ya Jumuiya.

11

Page 12: Taarifa Ya Mwaka

B: CHANGAMOTO / MATATIZO

1. Simu ya Jumuiya

Jumuiya licha ya kufanikiwa kufungua sanduku la barua,bado haijafanikiwa kuwa na

simu ya jumuiya kwa kuwa usajili wa jumuiya haujakamilika.Ni matazamio yetu kwa

mwaka 2013 huenda tukafanikiwa kuwa na simu ya jumuiya.

2. Mahudhurio hafifu ya vikao

Vikao vya ngazi zote vimekuwa na mahudhurio ya wastani kwa wajumbe, hivyo

kumekuwa na ukosefu wa ufanisi katika baadhi ya maamuzi

3. Ukosefu wa mfuko maalum wa harusi, msiba na majanga

- Jumuiya bado haina mfuko maalum wa harusi, misiba na majanga

- Jumuiya iko mbioni kuandaa mfuko huo na kupendekeza kiwango maalum cha

mfuko huo.

4. Ushiriki wa michezo

- Kumekuwa na ushiriki hafifu wa michezo katika matamasha mbalimbali

yaliyofanyika mwaka 2012.

5. Usafi wa msikiti na utunzaji wa mazingira yake.

- Wanajumuiya wachache hushiriki katika usafi wa kila wiki na mwezi wa msikiti na

pia baadhi ya wanajumuiya wanaharibu mandhari ya msikiti mathalani kugeuza

sehemu ya malazi, kuweka mizigo yao pasipo na utaratibu au kugeuza sehemu ya

kutilia udhu kuwa sehemu kufulia nguo.

6. Kutokutoa michango kwa wakati au kutokutoa kabisa.

- Wanajumuiya wengi hawatoi ada ya uanachana kwa wakati na wengine hawatoi

kabisa. Mathalani kwa mwaka 2012, ni wanajumuiya 123 tu kati ya 269 ndio walitoa

ada ya uanachama.Michango hafifu au kutokutoa michango kunaathiri

kutokutimizwa au kutokidhi bajeti ya jumuiya.

7. Ukosefu wa miradi ya kutosha

- Jumuiya kwa mwaka 2012 ilikuwa na miradi miwili (2 )tu ya kuuza vocha na kuuza

DVD za mahafali miradi hiyo bado inaingiza kiasi kidogo cha mapato na pia

kuibiwa kwa simu moja kuliathiri kushuka kwa mapato

12

Page 13: Taarifa Ya Mwaka

8. Ukosefu wa kompyuta na tovuti

Jumuiya inakosa kompyuta kwa ajili ya kurahisisha utendaji kazi, pia bado haina tovuti

ya kuweza kujitangaza na kutoa habari zake

9. Tatizo la usajili wa wanajumuiya

- Jumuiya kwa sasa haina daftari la kudumu la wanachama, pia kumekuwa na udhaifu

katika kuwaingiza wanajumuiya katika parua pepe za jumuiya.

Jumuiya ipo mbioni kuakikisha tunaanzisha daftari la kudumu la wanachama na pia

kuhakikisha wanajumuiya wanaingiza taarifa zao katika barua pepe yetu na pia

tutakapokuwa na tovuti yetu, itakuwa ni rahisi kwa wanajumuiya kuweka taarifa zao.

10. Uvaaji wa hijabu na darasa la wanawake

- Kumekuwa na mahudhurio hafifu ya darasa la wanawake na pia wanawake wengi

hawajitokezi kuwa wahadhiri sambamba na hilo bado uvaaji wa hijabu haukidhi

matarajio na pia baadhi ya hijabu hazikidhi viwango vilivyoanishwa katika Quran na

Hadith za Mtume(SAW).

C: MAPENDEKEZO/ MIPANGO YA BAADAYE

1. Jumuiya ina malengo/ mipango ya kuhakikisha

(i) Tunakuwa na simu ya jumuiya na tovuti ili kurahisisha mawasiliano

(ii) Kununua kompyuta ya jumuiya

(iii) Kuongeza na kubuni miradi ili kuiongezea jumuiya mapato, tunafikiri kuanzisha

mradi ya kuuza T-shirt, kalenda na mitandio na majuba

(iv) Kukuhakisha tunaweka akiba zaidi katika akaunti yetu ili kutunisha hazina yetu.

13

Page 14: Taarifa Ya Mwaka

SURA YA NNE

4.0 SHUKRANI

Jumuiya inapenda kutoa shukrani kwa wanajumuiya na wadau mbalimbali kwa kufanikisha

utekelezaji wa shughuli za jumuiya.

Jumuiya inawashukuru Afrika Muslims Agency kwa msaada wa vitabu, pia inawashukuru

Friends of KMA kwa kusaidia baadhi ya shughuli za jumuiya

Jumuiya inawashukuru wanajumuiya waliokuwa na nafasi za uongozi, katika ngazi mbalimbali

kwa michango yao ambayo imesaidia jumuiya kupiga hatua.

Na mwisho tunawashukuru tena wanajumuiya wote kwa ushiriki wao wa hali na mali katika

kuhakikisha jumuiya inadumu na kusonga mbele.

4.1 MWISHO

Taarifa hii imeandikwa na viongozi wa kamati zote za jumuiya na kukusanywa katika taarifa

moja na Katibu Mkuu wa jumuiya kwa mujibu wa utaratibu uliowekwa

4.2 MAWASILIANO

KCMC Muslims Association

P.O.Box 287 Moshi

Blogu: kcmcmuslimsassociation.blogspot.com

Facebook group: kcmc muslims association

Email: [email protected]

14