2
Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania- TCU Yah: Wanafunzi Wanaoomba Kudahiliwa Upya (Re-application for Admission) Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania inapenda kuwaarifu wanafunzi waliokuwa wamedahiliwa miaka ya nyuma na kwa sababu moja au nyingine wakashindwa kuendelea na masomo yao wanatakiwa wafanye yafuatayo; 1. Kwa wale ambao walichaguliwa na hawakuripoti kwenye vyuo walivyodahiliwa wanatakiwa waandike barua Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania wakitoa maelezo na sababu zilizopelekea wao kushindwa kuanza masomo yao na kwamba wanaomba kuruhusiwa kufanya maombi upya. Barua hizi zinatakiwa ziambatanishwe na taarifa ya uthibitisho wa kutokuripoti (confirmation letters) kutoka vyuo walivyokuwa wamedahiliwa 2. Kwa wale wanafunzi ambao walidahiliwa na kusajiliwa kwenye vyuo husika, wanatakiwa waandikie barua Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania, wakieleza vyuo na programu walizokuwa wamedahiliwa pamoja na sababu zilizopelekea wao kushindwa kuendelea na masomo yao na kwamba wanaomba kuruhusiwa kuomba upya. Barua hizi zinatakiwa ziambatanishwe na taarifa ya kuacha masomo (clearance letters) kutoka vyuo walivyokuwa wamesajiliwa NB: 1.Barua za waombaji wa aina zote mbili lazima ziwe na taarifa za msingi ikiwa ni pamoja na majina halisi ya mwombaji, Index namba ya Kidato cha Nne na

Wanafunzi Wanaoomba Kudahiliwa Upya

Embed Size (px)

DESCRIPTION

Wanafunzi Wanaoomba Kudahiliwa Upya(Re-application for Admission)

Citation preview

  • Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania- TCU

    Yah: Wanafunzi Wanaoomba Kudahiliwa Upya (Re-application for Admission) Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania inapenda kuwaarifu wanafunzi waliokuwa wamedahiliwa miaka ya nyuma na kwa sababu moja au nyingine wakashindwa kuendelea na masomo yao wanatakiwa wafanye yafuatayo; 1. Kwa wale ambao walichaguliwa na hawakuripoti kwenye vyuo

    walivyodahiliwa wanatakiwa waandike barua Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania wakitoa maelezo na sababu zilizopelekea wao kushindwa kuanza masomo yao na kwamba wanaomba kuruhusiwa kufanya maombi upya. Barua hizi zinatakiwa ziambatanishwe na taarifa ya uthibitisho wa kutokuripoti (confirmation letters) kutoka vyuo walivyokuwa wamedahiliwa

    2. Kwa wale wanafunzi ambao walidahiliwa na kusajiliwa kwenye vyuo husika, wanatakiwa waandikie barua Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania, wakieleza vyuo na programu walizokuwa wamedahiliwa pamoja na sababu zilizopelekea wao kushindwa kuendelea na masomo yao na kwamba wanaomba kuruhusiwa kuomba upya. Barua hizi zinatakiwa ziambatanishwe na taarifa ya kuacha masomo (clearance letters) kutoka vyuo walivyokuwa wamesajiliwa

    NB: 1.Barua za waombaji wa aina zote mbili lazima ziwe na taarifa za msingi ikiwa ni pamoja na majina halisi ya mwombaji, Index namba ya Kidato cha Nne na

  • mwaka aliomaliza, barua pepe (email address) pamoja na namba ya simu ya mhusika ili kurahisisha mawasiliano 2. Majina ya waombaji yaliyokwishafanyiwa kazi na kupatiwa kibali cha kuruhusiwa kuomba upya yatatangazwa kwenye tovuti ya Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania. Pia watapata taarifa kupitia namba zao za simu na barua pepe. MUHIMU. Kusoma ama kupakua orodha ya walioruhusiwa kuomba upya udahili kwa mwaka wa masomo 2015/16 bonyeza hapa chini.

    1. Batch One.