19
JAMHURI YA KENYA WIZARA YA KILIMO, MIFUGO, UVUVI NA UNYUNYIZAJI (MoALFI) IDARA YA KITAIFA YA UVUVI, KILIMO CHA MAJINI NA UCHUMI WA BAHARINI (SDFA-BE) RASIMU YA MWISHO MFUMO WA MAKUNDI YALIYOTENGWA NA KUTELEKEZWA (VMGF) MRADI WA MAENDELEO YA KIJAMII NA KIUCHUMI WA UVUVI WA BAHARINI KENYA (KEMFSED) WARSHA YA KUHALALISHA MOMBASA JUNI 19 - 20, 2019

WIZARA YA KILIMO, MIFUGO, UVUVI NA UNYUNYIZAJI (MoALFI) · 4. Mfumo wa VMGF utatumiwa na Idara ya Kitaifa ya Uvuvi na Uchumi wa Baharini, mashirika ya kutekeleza mradi wa KEMFSED

  • Upload
    others

  • View
    11

  • Download
    0

Embed Size (px)

Citation preview

Page 1: WIZARA YA KILIMO, MIFUGO, UVUVI NA UNYUNYIZAJI (MoALFI) · 4. Mfumo wa VMGF utatumiwa na Idara ya Kitaifa ya Uvuvi na Uchumi wa Baharini, mashirika ya kutekeleza mradi wa KEMFSED

JAMHURI YA KENYA

WIZARA YA KILIMO, MIFUGO, UVUVI NA UNYUNYIZAJI

(MoALFI)

IDARA YA KITAIFA YA UVUVI, KILIMO CHA MAJINI NA UCHUMI

WA BAHARINI (SDFA-BE)

RASIMU YA MWISHO MFUMO WA MAKUNDI

YALIYOTENGWA NA KUTELEKEZWA (VMGF)

MRADI WA MAENDELEO YA KIJAMII NA KIUCHUMI WA

UVUVI WA BAHARINI KENYA (KEMFSED) WARSHA YA KUHALALISHA

MOMBASA

JUNI 19 - 20, 2019

Page 2: WIZARA YA KILIMO, MIFUGO, UVUVI NA UNYUNYIZAJI (MoALFI) · 4. Mfumo wa VMGF utatumiwa na Idara ya Kitaifa ya Uvuvi na Uchumi wa Baharini, mashirika ya kutekeleza mradi wa KEMFSED

Utangulizi

1. Mfumo huu wa Makundi ya Waliotengwa na Kutelekezwa (VMGF) umeandaliwa kwa ajili ya

Maendeleo ya Uchumi wa Jamii katika Uvuvi wa Baharini nchini Kenya (KEMFSED) na

utafadhiliwa na Benki ya Dunia. Umebuniwa kutokana na matokeo na mapendekezo ya utafiti

wa Kuchunguza Jamii ambao ulifanywa kwa ajili ya mradi huu katika Makundi ya

Waliotengwa na Kutelekezwa wanaoishi katika maeneo yaliyo karibu na kingo za maji katika

Pwani ya Kenya. Kwa sababu mikakati ya mradi unaopendekeza itatekelezwa katika maeneo

ambapo kuna Wenyeji (IP) ambao wanarejelewa kuwa Makundi ya Waliotengwa na

Kutelekezwa (VMG)1 nchini Kenya, sera ya ulinzi ya Benki ya Dunia (WB) ya OP/BP 4.10

imerejelewa na mfumo wa VMGF umetayarishwa ili kuongoza utekelezaji wa mradi huu.

2. Mradi wa KEMFSED unalenga kuimarisha uchumi na maisha ya wapwani kutokana na uvuvi

wa baharini na kilimo cha maji huku ikidumisha ubora wa mfumo husika wa ekolojia kupitia

utaratibu unaoshirikisha jamii. Imebuniwa kutokana mafunzo tuliyopata kupitia utekelezaji wa

Mradi wa Maendeleo ya Pwani ya Kenya (KCDP) ambao pia ulifadhiliwa na Benki ya Dunia

na mikakati mbalimbali iliyotekelezwa na jamii ambayo ililenga kuboresha maisha ya makundi

ya VMG katika kaunti za pwani ya Kenya.

Malengo ya Mfumo wa Makundi ya Waliotengwa na Kutelekezwa (VMGF)

3. Lengo la mfumo wa VMGF ni kuongoza muundo, mpangilio na utekelezaji wa mikakati ya

KEMFSED ambayo huenda ikaathiri makundi ya VMG katika maeneo yaliyopendekezwa

kwenye mradi. Mfumo wa VMGF unatokana na kifungu cha OP 4.10 cha Benki ya Dunia

pamoja na kanuni na sheria husika za Serikali ya Kenya. Kifungu cha OP 4.10 hurejelewa

wakati ambapo kuna uwezekano wa makundi ambayo yanatimiza vigezo vya kifungu cha

Benki ya Dunia cha OP 4.10 “yanayoishi au yana uhusiano wa pamoja na eneo ambako mradi

utafanyika.” Mfumo wa VMGF inajumuisha aina za shughuli na mikakati iliyopendekezwa;

athari nzuri na mbaya kwenye makundi ya VMG; mbinu za kuhakikisha mashauriano

yanayoeleweka, ya wazi na yanayopangwa mapema; mipango ya taasisi ya kukagua shughuli

zinazoendelezwa katika mradi na kukagua na kubaini uwepo wa makundi yaVMG katika eneo

la mradi; mbinu za kufuatilia na kuripoti, na kufahamisha makundi yaVMG kuhusu mbinu

hizo.

4. Mfumo wa VMGF utatumiwa na Idara ya Kitaifa ya Uvuvi na Uchumi wa Baharini, mashirika

ya kutekeleza mradi wa KEMFSED na Benki ya Dunia ili kuhakikisha kuwa vifungu vya Sera

ya Utendaji wa Benki ya Dunia (OP) 4.10 vinazingatiwa katika utekelezaji na usimamizi wa

mradi huu. Hatua hii itahakikisha kuwa athari mbaya zinatambuliwa kikamilifu na

kushughulikiwa, ilhali athari nzuri zinaendelezwa kwenye makundi ya VMG.

Vipengee vya Mradi

1 VMG ni jamii ambazo zinalengwa na mradi wa KEMFSED na zinatimiza masharti na vigezo vya Benki ya Dunia kwa mujibu wa kifungu cha OP 4.10 na vigezo vya Serikali ya Kenya (GoK) vya “jamii zilizotengwa” na za “wachache” kwa mujibu wa Katiba ya Kenya.

Page 3: WIZARA YA KILIMO, MIFUGO, UVUVI NA UNYUNYIZAJI (MoALFI) · 4. Mfumo wa VMGF utatumiwa na Idara ya Kitaifa ya Uvuvi na Uchumi wa Baharini, mashirika ya kutekeleza mradi wa KEMFSED

5. Vipengee vya Mradi vimebuniwa ili kuafikiana na Mfumo mpana wa Uchumi wa Baharini

nchini Kenya na mchakato unaoendelea wa ugatuzi. Vipengee vikuu na vidogo vilibainishwa

na kupangwa ili kuboresha malengo, utaratibu, ujumuishaji na usawazishaji wa dhana za

miundombinu pamoja na usaidizi wa kiufundi/programu, mafunzo na kukuza uwezo

wafanyakazi.

Mchoro 1: Nadharia ya Mabadiliko ya Mradi wa KEMFSED

Kipengee cha 1 – Kuboresha Uongozi na Usimamizi wa Uvuvi wa Baharini.

6. Hatua hi italenga kuboresha usimamizi wa uvuvi wa baharini katika maeneo yanayokaribia

kingo za maji nchini Kenya.

a) Kipengee kidogo cha 1.1: Kuboresha uongozi wa uvuvi na uchumi wa baharini. Kipengee

hiki kidogo kitalenga kuboresha uongozi na usimamizi wa uvuvi, kukagua sera za uvuvi

na sheria husika na kuimarisha mbinu za ufuatiliaji na uchunguzi wa mradi. Kipengee hiki

kidogo pia kitalenga utafiti unaotakikana ili kuimarisha usimamizi wa uvuvi baharini,

ikiwa ni pamoja na kutengenezwa kwa Mfumo wa Ufuatiliaji na Habari za Uvuvi (FIMS)

ambao ni thabiti na utarahisisha hatua ya kufikia habari ili kuboresha usimamizi wa

shughuli za uvuvi. Katika maeneo yakayobainishwa, uvuvi maalum utalengwa kupitia

mikakati mahususi kulingana na Mipango ya Kuboresha Uvuvi (FIP), ikiwa na nia ya

kubadilisha uvuvi huu ili uweze kusimamiwa vizuri kwa nia ya kuhakikisha manufaa ya

kudumu katika jamii husika. Mradi huu pia utasaidia kuendeleza Hatua ya Mipango za

Kitaifa za kukabili uvuvi wa papa, ndege na Uvuvi Haramu, Usioripotiwa na Usiodhibitiwa

(IUU).

b) Kipengee kidogo cha 1.2: Kuboresha usimamizi wa uvuvi unaokaribia ufuko. Kipengee

hiki kitaimarisha usimamizi wa shughuli za uvuvi zinazofanyika karibu na ufuko na

Page 4: WIZARA YA KILIMO, MIFUGO, UVUVI NA UNYUNYIZAJI (MoALFI) · 4. Mfumo wa VMGF utatumiwa na Idara ya Kitaifa ya Uvuvi na Uchumi wa Baharini, mashirika ya kutekeleza mradi wa KEMFSED

utekeleza wa Mipango ya Usimamizi wa Uvuvi (FMP). Kwa kushirikiana na FMP za

kitaifa kwa ajili ya uvuvi maalum, maeneo mapya Yaliyounganishwa na Kusimamiwa kwa

Pamoja (JCMA) yatabuniwa. Usimamizi wa maeneo yaliyopo utaimarishwa. Mradi huu

pia utaendeleza utekelezaji wa Maeneo Yanayosimamiwa kwa Pamoja (CMA) ikiwa ni

pamoja na utekelezaji wa mikakati ya Ufuatiliaji, Udhibiti na Uchunguzi (MCS) na utoaji

wa vifaa vinavyotakikana na usaidizi wa kiufundi kwa ajili ya MCS.

c) Kipengee kidogo cha 1.3: Uendelezaji wa miundombinu kwa ajili ya usimamizi wa uvuvi.

Kipengee hiki kidogo kinajumuisha uendelezaji wa miundombinu ambayo inalenga

kusaidia usimamizi wa uvuvi katika viwango vya kitaifa na kaunti. Hususan, inajumuisha

jengo la ofisi ya Huduma za Uvuvi Kenya (KeFS) mjini Nairobi na Kituo cha Kitaifa cha

Mafunzo na Rasilimali za Baharini katika Kaunti ya Kwale. Mifano ya miundombinu ya

uvuvi inajumuisha kuboresha viwango vya ofisi za uvuvi za kaunti na kupanua chuo cha

Mombasa Bandari Maritime Training College.

Kipengee cha 2 – Kuwezesha Uwekezaji wa Kudumu katika sekta ya Uvuvi wa Baharini na Kilimo

cha Majini

7. Hatua hii itabuni Huduma ya Maendeleo ya Biashara Ndogo Ndogo na za Wastani

(SME/SME-DS), zinazotoa huduma za kitaalamu kwa wajasiriamali, SME na makundi ya

serikali katika kaunti za pwani,. Pia itawezesha kuongezeka kwa faida inayotokana na uvuvi

na kilimo cha baharini kwa kuwekeza katika miundombinu ya umma kama vile barabara,

umeme na maji, inayohusiana na utaratibu wa kuboresha bidhaa na uwekezaji wa binafsi.

a) Kipengee Kidogo cha 2.1: SME-DS Katika Jamii za Pwani. Tutahusisha SME-DS

itakayojumuisha timu ya wataalamu wa SME wanaoshughulikia maendeleo,

watakaopatikana katika jamii za wavuvi zinazoishi katika pwani ya Kenya. Wataalamu

hawa wataendeleza huduma zao kwa Vitengo vya Usimamizi wa Fuo (BMU) na wenyeji

wa pwani wanaotaka kuanzisha au kukuza biashara inayohusiana na uvuvi. Pia, watatoa

usaidizi wa kiufundi unapotakikana, huduma za uchanganuzi, mafunzo kwa wafanyakazi

na kutoa ushauri mbalimbali. SME-DS itabaini pia matatizo au hatari za kimfumo ambazo

zinazuia kutelelezwa kwa miradi inayotarajiwa na itapendekeza hatua za kusuluhisha

zinazotakikana ili kuondoa au kupunguza athari za hatari hizo. Itajumuisha pia mafunzo na

maelekezo ya kufikia njia mpya na zilizopo za kupata mikopo. Kipengee hiki kidogo pia

kitasaidia SME ambazo zinataka kuanzisha huduma ili kuboresha na kufanya utaratibu wa

kutengeneza vyakula vya baharini uwe wazi zaidi. Zaidi ya hayo, mradi utatoa usaidizi wa

kiufundi ili kuongoza mchakato wa kuanzisha na kuendeshwa kwa Mamlaka ya Kenya ya

Soko la Samaki.

b) Kipengee Kidogo cha 2.2: Kuboresha Miundombinu Inayohusiana na Uvuvi na Kilimo

cha Majini kwa ajili ya kuendeleza Utaratibu wa Kutayarisha Bidhaa. Kipengee hiki kidogo

kitalenga mapengo yanayobainishwa na kaunti katika miundombinu ya umma (maji,

umeme, usafiri) ambayo inazuia nafasi za uwekezaji wa binafsi katika uvuvi wa mabahari

na Kilimo cha Baharini. Ili kuhakikisha kuwa uwekezaji wote utathibitishwa vizuri,

kuendeleza uwekezaji wa binafsi na kupunguza uwezo wa kuvua samaki kupita kiasi,

miundombinu yote ya umma inayohusiana na utaratibu wa kutayarisha bidhaa

inayopendekezwa na kaunti itatokana na mpangilio na ramani ya maendeleo ya

miundombinu ya Kilimo cha Baharini na uvuvi katika kaunti. Mabadiliko ya anga

Page 5: WIZARA YA KILIMO, MIFUGO, UVUVI NA UNYUNYIZAJI (MoALFI) · 4. Mfumo wa VMGF utatumiwa na Idara ya Kitaifa ya Uvuvi na Uchumi wa Baharini, mashirika ya kutekeleza mradi wa KEMFSED

yanayohusiana na hatari yatazingatiwa wakati wa kuanzisha uwekezaji wote wa

miundombinu.

Kipengee cha 3 – Riziki na Uimarishaji wa Jamii za Pwani. (Dola za Marekani milioni 30)

8. Kipengele hiki kitalenga kuimarisha maisha ya familia maskini katika jamii za pwani, kama

njia ya kijitegemea na pia kuwasaidia wavuvi kutii masharti ya usimamizi wa uvuvi. Mbinu ya

jumla inayolenga njia za ziada za kuendeleza maisha itafuatwa, kwa kiasi fulani kupitia

kuanzisha ushirikiano wa kimkakati na biashara za kifedha zilizopo au biashara mpya

zinazotumia mifumo ya kilimo ya kandarasi katika kilimo cha majini au kilimo cha kawaida

ili kuwasaidia watu wanaokuza bidhaa ndogo ndogo. Kwa njia ya jumla zaidi, miradi midogo

ya kujipatia riziki, inayotekelezwa na watu mahususi au makundi ya biashara ndogo ndogo,

itafadhiliwa kupitia utoaji wa ruzuku, usaidizi wa kiufundi na mafunzo ya ujuzi na ya biashara.

a) Kipengee Kidogo cha 3.1: Kuimarisha Hali ya Maisha ya Jamii za Pwani. Kipengee hiki

kidogo kinajumuisha ufadhili wa ruzuku unaosaidia watu wanaotimiza masharti kupitia

njia tatu zilizobainishwa: i) Ruzuku za kujipatia riziki kwa wakulima wa kiwango cha chini

wanaofanya miradi midogo, ambao wametimiza masharti; ii) Ruzuku kwa ajili ya miradi

midogo ya jamii na mazingira (mtaji asili); na iii) Ruzuku za kuongeza mtaji kwa makundi

ya akiba na mikopo vijijini (VSL).

b) Kipengee Kidogo cha 3.2: Huduma za Usaidizi katika Kuendeleza Uwezo wa

Wafanyakazi na Kuboresha Riziki. Vipengee hivi vidogo ambavyo vitatekelezwa na

kaunti mahususi, vitatoa aina mbalimbali za huduma za usaidizi na kukuza uwezo wa

wafanyakazi katika makundi yanayolengwa ambayo yanatarajiwa kuanzisha shughuli

zinazotekelezwa chini ya kipengee kidogo cha 3.1 ikiwa ni pamoja na: i) Kutoa Huduma

na Usaidizi wa Kiufundi (TA) ili kutambua na huduma ili kubaini watakaopokea ruzuku

na kusaidia katika maandalizi, usimamizi na uchunguzi wa miradi midogo; ii) Kutoa

mafunzo ya ujuzi na biashara kwa watakaopokea ruzuku na wafanyabiashara wengine

wadogo wadogo; iii) Mpango wa Akiba na Mikopo Vijijini (VSL); na iv) Ufadhili wa

masomo rasmi, mafunzo ya kiufundi na elimu ya shule.

Kipengee cha 4 – Usimamizi wa Mradi.

9. Kipengee hiki cha 4 kitatoa usaidizi waziada wa kifedha katika usimamizi wa miradi katika

viwango vya kitaifa na kaunti ili kuhakikisha usimamizi na utekelezaji unaofaa wa shughuli za

miradi. Hususan, itasaidia kuchunguza na kusimamia mradi ikiwa ni pamoja na kuwezesha

Kamati ya Kitaifa ya Kuendeleza Miradi (NPSC) na Kamati ya Kutoa Ushauri wa Kiufundi

kwenye Mradi (PTAC); kuanzisha na kuendeleza Kitengo cha Usimamizi wa Mradi (PCU)

katika kiwango cha kitaifa na Vitengo vya Kutekeleza Mradi (PIU) katika kiwango cha kaunti,

ikiwa ni pamoja na kutoa vifaa, usimamizi udhamini, ikijumuisha uhasibu na ukaguzi wa

hesabu za ndani/nje; mifumo ya kuhakikisha na kudhibiti ubora, usimamizi wa ulinzi wa jamii

na mazingira; na ukaguzi wa kiufundi kadri inavyotakikana. Kipengee hiki pia kitatoa ufadhili

wa kutayarisha na kutekeleza mikakati ya mawasiliano na utekelezaji wa mfumo wa

Kutathmini na Kufuatilia. Mfumo wa Kutathmini na Kufuatilia (M&E), ambao unahitaji

kutekelezwa ili kurekodi data kuhusu hatua za kifedha na hali halisi, utendaji wa shirika la

utekelezaji na mashirika mengine ya kutoa huduma, na matokeo yatakayopatikana kwa njia za

Page 6: WIZARA YA KILIMO, MIFUGO, UVUVI NA UNYUNYIZAJI (MoALFI) · 4. Mfumo wa VMGF utatumiwa na Idara ya Kitaifa ya Uvuvi na Uchumi wa Baharini, mashirika ya kutekeleza mradi wa KEMFSED

matumizi na mafanikio. Vile vile, itasaidia ubunifu wa Mbinu za Kushughulikia Malamiko na

kuhakikisha kuwa wananchi wanashirikishwa.

Eneo la Mradi

10. Mradi huu utatekelezwa katika sehemu tano zinazokaribia kingo za maji katika kaunti za

Kwale, Mombasa, Kilifi, Lamu na Tana River; kwenye kaunti ndogo za Matuga, Kinango,

Msambweni, Lunga Lunga, Kilifi Kusini, Kilifi Kaskazini, Malindi, Magarini, Lamu

Magharibi, Lamu Mashariki, Tana Delta/Garsen, Changamwe, Nyali, Kisauni, Jomvu, Likoni,

Mvita.

11. Mahali kwenye mradi ambapo jamii ya VMG inaishi na ambapo kifungu cha sera ya Benki ya

Dunia cha OP.4.10 kitarejelewa wakati wa mradi ikijumuisha; Wadi ya Pongwe/Kikokeni

(Visiwa vya mukwiro na wasini na kijiji cha Tswaka) katika kaunti ndogo ya Lunga Lunga,

wadi ya Ramisi katika kaunti ndogo ya Msambweni na Samburu/Chengoni, Kasemeni, wadi

za Mackinon Road katika kaunti ndogo ya Kinango zote zinapatikana katika kaunti ya Kwale;

Dabaso na wadi ya Watamu katika kaunti ya ndogo ya Kilifi Kaskazini, Maarafa, wadi za

Gongoni na Adu katika kaunti ndogo ya Magarini zote zinapatikana katika kaunti ya Kilifi;

wadi za Kiunga na Basuba katika kaunti ndogo ya Lamu Mashariki na wadi za Hindi,

Mkunumbi, Witu na Mkomani katika kaunti ndogo ya Lamu Magharibi katika kaunti la Lamu

na Kipini katika kaunri ndogo ya Garsen/Tana Delta, kaunti ya Tana River. Vikundi vya VMG

ambavyo vilijumuishwa katika uchunguzi huu vilikuwa; Wakifundi, Wavumba, Watshwaka,

Washiratzi, Watha katika Kwale (kaunti ndogo ya Kinango) na kaunti ya Kilifi; Aweer/Boni

na Saanye katika kaunti ya Lamu na Wasaanye wanaoishi katika wadi ya Kipini katika kaunti

ndogo ya Tana Delta, kaunti ya Tana River.

Miradi Midogo ambayo inaweza kufadhiliwa chini ya mradi wa KEMFSED kulingana na vipengele

vya Mradi

12. Kipengee cha 1 – Usimamizi na udhibiti wa uvuvi wa baharini na rasilimali za majini ambao

unalenga kuimarisha udhibiti wa kilimo cha majini na uvuvi wa baharini ili kuzuia matukio ya

kuvua samaki kupitia kiasi na kudumisha au kuboresha ongezeko la bidhaa na kukuza hadhi

ya mfumo wa ekolojia husika. Kipengee kidogo cha 1 kitalenga kusimamia na kuimarisha

taasisi ili kuhakikisha kuwa rasilimali za kilimo cha majini na uvuvi zinalindwa katika

muktadha wa kutekeleza mfumo wa uchumi wa baharini. kipengee kidogo cha 2 kitalenga

uimarishaji wa Mifumo ya Mawasiliano ya Uvuvi (FIS) ili kuhakikisha upatikanaji wa habari

za sekta zote kwa ajili ya kuwasiliana kuhusu umuhimu wa sekta ya kilimo cha majini na uvuvi

katika kuleta maendeleo kwenye maeneo yote ya pwani. Kipengee kidogo cha 3 kitalenga

kuboresha usimamizi wa uvuvi wa kiwango kidogo kidogo unaofanyika ufuoni. Kipengee

kidogo cha 4 kitalenga kuboresha usimamizi wa uvuvi unaofanyika maeneo yaliyo mbali na

ufuo. Utekelezaji wa Mipango ya Kuboresha Uvuvi (FIP) na usaidizi wa kubadilisha sekta ya

uvuvi ili kuboresha usimamizi, utazingatia jinsi makundi ya VMG yatakavyoathiriwa na

mabadiliko katika usimamizi ambayo yanaweza kujumuisha uanzishaji wa kanuni, masharti

na miundo mipya ambayo znaweza kuathiri kabisa kushiriki kwa makundi ya VMG katika

Page 7: WIZARA YA KILIMO, MIFUGO, UVUVI NA UNYUNYIZAJI (MoALFI) · 4. Mfumo wa VMGF utatumiwa na Idara ya Kitaifa ya Uvuvi na Uchumi wa Baharini, mashirika ya kutekeleza mradi wa KEMFSED

shughuli za uvuvi kutokana na kiwango cha chini cha elimu, matatizo ya hesabu na kiwango

kidogo cha kujishirikisha katika shughuli za uchumi wa uvuvi, ingawa kuna uwezo wa

kuboresha jinsi wanavyoweza kushirikishwa katika uvuvi karibu na ufuo unaofanywa na

wanaume wa VMG na shughuli za kuboresha hatua za wanawake kutayarisha samaki, kama

vile biashara za mama karanga, kung'oa mwani na shughuli za burudani kwenye ufuo.

Mojawapo ya miundo hii ya usimamizi ni Kuanzisha Maeneo Yaliyounganishwa na

Kusimamiwa kwa Pamoja (JCMA) ambayo yanajumuisha wenyeji kupitia mpango wa

kupendelea wenyeji. Mashauriano yatafanyika ili kutathmini uwezekano wa athari ya miundo

mipya iliyotekelezwa ya udhibiti wa uvuvi kwenye jamii za VMG. Mbinu za kujumuisha

makundi ya VMG pamoja na wenyeji katika miundo ya udhibiti zitajadiliwa kupitia mikutano

ya mashauriano na kukubaliwa na pande zote kabla ya kutekeleza miundo mipya au kuimarisha

miundo iliyopo ya udhibiti ambayo inafaa ili kutimiza malengo ya mradi wa KEMFSED. Zaidi

ya hayo, tutaangazia zaidi miundo iliyopendekezwa ambayo inalenga kuboresha usimamizi wa

uvuvi wa kiwango kidogo au unaofanyika karibu na ufuo kwa sababu hii ndiyo shughuli ya

uvuvi inayofanywa na makundi ya VMG katika pwani ya Kenya.

13. Kipengee cha 2 – Kuendeleza uwekezaji katika uvuvi wa baharini na kilimo cha majini ili

kuwezesha utumiaji bora na kuongeza thamani kwa rasilimali kwa kuongeza kiasi cha

uwekezaji katika sekta ya kilimo cha majini na uvuvi wa baharini. Kipengee kidogo cha 1

kitalenga kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji wa sekta ya binafsi katika uvuvi na

kilimo cha majini kupitia Huduma za Maendeleo ya Biashara za Wastani na Ndogo Ndogo

(SME/SME-DS). SME-DS zitatoa huduma za kitaalamu kwa wajasiriamali, SME na makundi

ya serikali katika kaunti za pwani. Kutakuwepo na wataalam wa kuendeleza huduma za

Vitengo vya Usimamizi wa Ufuo (BMU) na wenyeji wa pwani wanaotaka kuendeleza au

kukuza biashara zinazohusiana na uvuvi. Pia, watatoa usaidizi wa kiufundi unapotakikana

kupitia juhudi za kuboresha ujuzi wa wafanyakazi, ambazo zitajumuisha huduma za mafunzo.

Utekelezaji wa shughuli katika kipengee hiki kidogo utaanza kwa kutathmini kiwango cha

uwakilishaji wa makundi ya VMG, kwa wanaume au wanawake katika BMU. Uendelezaji wa

uwekezaji katika uvuvi wa baharini utahitaji pia juhudi za kuboresha ujuzi wa wafanyakazi

kwa lengo la kubadilisha mitazamo ya jamii za VMG ili kuchukulia shughuli za uvuvi kama

uwekezaji huku wakitarajia kupata faida ikilinganishwa na mtazamo wa sasa wa jamii ambapo

shughuli za uvuvi katika fuo za pwani zinafanywa na jamii za VMG kama njia ya kupata riziki

tu. SME-DS itabaini pia matatizo au hatari za kimfumo ambazo zinazuia kutelelezwa kwa

miradi inayotarajiwa na itapendekeza hatua za kusuluhisha zinazotakikana ili kuondoa au

kupunguza athari za hatari hizo. Tutachukua tahadhari ili kuhakikisha kuwa tathmini za

matatizo au hatari za kimfumo za kuzuia utekelezaji wa mradi inafanyika katika njia inayofaa

tamaduni ya wanajamii wa VMG bila kupoteza utambulisho wao wa kitamaduni. Itajumuisha

pia mafunzo na maelekezo ya kufikia njia mpya na zilizopo za kupata mikopo. Kipengee hiki

kidogo pia kitasaidia SME ambazo zinataka kuanzisha huduma ili kuboresha na kufanya

utaratibu wa kutengeneza vyakula vya baharini uwe wazi zaidi. Zaidi ya hayo, mradi utatoa

usaidizi wa kiufundi ili kuongoza mchakato wa kuanzisha na kuendeshwa kwa Mamlaka ya

Kenya ya Soko la Samaki. Ufikiaji wa soko la samaki chini ya Mamlaka ya Soko la Samaki

Page 8: WIZARA YA KILIMO, MIFUGO, UVUVI NA UNYUNYIZAJI (MoALFI) · 4. Mfumo wa VMGF utatumiwa na Idara ya Kitaifa ya Uvuvi na Uchumi wa Baharini, mashirika ya kutekeleza mradi wa KEMFSED

nchini Kenya na masharti ya utaratubu wa utayarishaji katika ufikiaji kama huo yatakuwa

sehemu ya kanuni chini ya hatua ya kupendelea wenyeji ili kuwezesha jamii za VMG kufikia

huduma. Shughuli za SME-DS zitategemea SME zilizobainishwa, ambazo jamii za VMG

zinafanya jinsi itakavyobainishwa katika utafiti wa Kuchunguza Jamii za VMG kama vile

kujihusisha katika biashara za kiwango kidogo katika maeneo kuweka samaki na maeneo

yenye samaki wengi, shughuli za watalii kutokana na vijana, biashara ya korosho na nazi na

shughuli za kilimo cha mwani.

14. Kipengee kidogo cha 2 kitaboresha miundombinu inayohusiana na uvuvi na Kilimo cha

Baharini ili kuwezesha uongezaji wa thamani ya bidhaa. Kaunti hii ndogo italenga mapengo

yaliyobainishwa na kaunti katika miundombinu ya msingi ya umma kama vile maji, umeme

na usafirishaji, ambayo inazuia nafasi za uwekezaji wa binafsi katika uvuvi na Kilimo cha

Baharini. Miundombinu yote ya umma inayohusiana na michakato ya kuongeza thamani ya

bidhaa, itakayopendekezwa na kaunti itatokana na mpango na ramani ya maendeleo ya

miundombinu ya uvuvi na Kilimo cha Baharini katika kaunti. Hii itaunganishwa na Mipango

ya Maendeleo Iliyojumuishwa katika Kaunti (CIDP) maeneo ya kaunti zinazolengwa

yanayokaribia kingo za maji. Juhudi zitatekelezwa ili kuhakikisha mipango na mipangilio ya

maendeleo ya uvuvi na Kilimo cha Baharini inajumuisha kwa njia ya wazi maeneo/wadi

ambazo VMG wanaishi. La muhimu pia ni kuendeleza miundombinu ya maji ili iwafae kwa

njia ya wazi wanajamii wa VMG, katika mpango uliojumuishwa kupitia hatua za kupendelea

wenyeji. Jamii za VMG zililalamika wakati wa utafiti wa kuchunguza jamii, kwamba kulikuwa

na miradi ya maji ambayo ilipitia maeneo yao lakini hawakufaidika kutokana na miradi hiyo

kwa kufungua maeneo ya kuuza maji ili kuhudumia jamii za VMG jinsi ilivyofanyika katika

jamii jirani za Mijikenda.

15. Kipengee cha 3 – Kuboresha Riziki inayotokana na Kilimo cha Majini na Uvuvi wa Baharini

kwa jamii zinazoishi pwani, ambayo inalenga kupitia mbinu ya jumla, kuleta manufaa ya

kiuchumi na kijamii ambayo jamii za pwani zitapata kupitia utumiaji wa kudumu wa rasilimali

za baharini. Uendelezaji wa njia za ziada za kupata riziki kupitia mchakato wa kubuni ushirika

wa kimkakati na biashara mpya za kifedha au au zilizopo, kwa kutumia mifumo ya kilimo cha

kandarasi cha majini au kilimo cha kawaida ambacho kinawafaidi wakulima wadogo wadogo,

itakuwa sehemu ya shughuli za kipengee hiki. Juhudi za wazi zitafanyika ili kuwezesha jamii

za VMG zishiriki na zipate manufaa kutokana na miradi midogo ya kupata riziki inayofanywa

na makundi mahususi ya VMG au makundi madogo ya biashara kupitia uanachama kwenye

VMG. Katika hali ambapo usaidizi kama huo unatolewa kwa vikundi vya biashara kupitia

uanachama kwenye VMG pamoja na wanachama wa kikundi kikubwa cha wenyeji, mbinu za

ndani zitabainishwa katika uanachama wa kikundi uliojumuishwa ili kuhakikisha kuwa VMG

zilizo ndani ya vikundi zinanufaika kupitia utoaji wa ruzuku, usaidizi wa kiufundi na mafunzo

ya ujuzi na biashara, pamoja na wanachama wengine wa kundi. Hatua muhimu ya utekelezaji

katika kipengee hiki itakuwa kurekodi kwa njia ya wazi kuwepo kwa mpango wa Akiba na

Mikopo Vijijini (VSL) miongoni mwa VMG na ufaafu wa kupata manufaa kutokana na

shughuli za kipengee cha tatu cha mradi wa KEMFSED. Ili kufanikisha mbinu inayojumuisha

jamii kupata maendeleo yanayotarajiwa chini ya mradi wa KEMFSED, tutabuni kigezo

Page 9: WIZARA YA KILIMO, MIFUGO, UVUVI NA UNYUNYIZAJI (MoALFI) · 4. Mfumo wa VMGF utatumiwa na Idara ya Kitaifa ya Uvuvi na Uchumi wa Baharini, mashirika ya kutekeleza mradi wa KEMFSED

ambapo VSL au makundi ya Jamii yanayotuma ombi, yanapaswa kuonyesha kuwepo kwa

wanachama wa VMG miongoni mwa wanachama wengine wa jamii. Tunastahili kuwa makini

kuzuia ujumuishaji wa wanachama wa jamii jirani wanaojifanya kuwa wawakilishi wa VMG

na kutenga wawakilishi halisi wa VMG kwenye vikundi vinavyozingatiwa kupata ruzuku na

kuboresha uwezo wa wafanyakazi. Kigezo cha kuchagua VMG katika mashirika makubwa ya

jamii kitabuniwa kupitia mchakato wa mashauriano wakati wa kubuni VMGP na kujumuisha

VMGP katika mpango wa utekelezaji wa miradi mikubwa ya KEMFSED.

16. Kipengele cha 4 –Kipengee hiki kinalenga usimamizi wa mradi ambao unajumuisha uzinduzi

na utekelezaji wa kamati ya mradi, wadhamini na ulinzi wa jamii na mazingira na ufuatiliaji

na kutathmini mradi. Utekelezaji unaofaa wa ulinzi wa kijamii na kimazingira unaobuniwa na

KEMFSED utahakikisha kushirikishwa na kujumuishwa kwa jamii ya VMG katika shughuli

za mradi.

17. Kutokana na matokeo ya utafiti wa kuchunguza jamii na ukaguzi wa mpango wa utekelezaji

wa mradi wa KEMFSED, kuna uwezekano wa kupendekeza miradi kadhaa midogo. Kuna

uwezekano kuwa miradi hii midogo inaweza kupendekezwa ili kufathiliwa chini ya vipengee

vitatu vya mradi wa KEMFSED ambavyo vinajumuisha; Udhibiti Bora wa Uvuvi na Uchumi

wa Baharini, Kuboresha Usimamizi wa Uvuvi Karibu na Fuo, Kuendeleza Miundombinu ya

Usimamizi wa Uvuvi chini ya kipengee cha kwanza. Miradi midogo inayoweza kubuniwa

chini ya kipengee hiki italenga kuzuia matendo ya kuvua samaki kupita kiasi, uvuvi haramu

na shughuli za uvuvi ambazo haziripotiwi katika Fuo za Bahari ya Hindi.

18. Baadhi ya shughuli za miradi midogo ambazo zitapendekezwa chini ya kipengee hiki kidogo

zinaweza kujumuisha; kuzuia matendo ya kuvua samaki kupita kiasi, kudumisha uzalishaji wa

samaki na kuboresha mfumo husika wa ekolojia. VMG zinaweza kunufaika kutokana shughuli

za kuvua samaki kupita kiasi kupita shughuli za ‘mama karanga’. Kuna jamii za VMG ambazo

zinahusika na uhifadhi wa msitu wa mikoko ambayo inatambulika kuwa maeneo muhimu ya

kudumisha ukuzaji wa samaki na mfumo wa ekolojia ya bahari. Juhudi za kuboresha uwezo

wa wafanyakazi zinazolenga kuimarisha shughuli za miradi midogo chini ya kipengee hiki

kidogo zinaweza kufanywa katika lugha ya Kiswahili ambayo inaeleweka na jamii zote za

VMG. Zaidi ya hayo, shughuli nyingine za miradi iliyo chini ya kipengee hiki zinaweza

kujumuisha kuimarisha usimamizi wa uvuvi unaodumu na utumiaji wa rasilimali za baharini

na inaweza kuhusisha uimarishaji wa taasisi za usimamizi na kubuni masharti mapya au

kuendeleza masharti yaliyopo yanayohusu shughuli za uvuvi ambayo hayawezi kuathiri riziki

ya watu mahususi wanaotumia boti za kuvuta nyavu, neti au mikuki na pia jamii nzima ambayo

inategemea uvuvi kwa jumla. Hii itajumuisha shughuli za jamii za VMG ambao ni mama

karanga wanaofanya biashara ya samaki katika maeneo ya kuweka samaki, zinazotegemea

kiwango cha samaki waliovuliwa. Kuna uwezekano kuwa shughuli za mradi mdogo

zitajumuisha kuboresha/kupanua miundombinu ili kuboresha usimamizi wa uvuvi kando na

maeneo ya kuweka samaki, maeneo yenye samaki wengi kama vile Shimoni, kupanua na

kuwezesha BMU ili kuboresha shughuli za usimamizi wa uvuvi. Kuna BMU ambazo

zinajumuisha VMG wengi ambako watu wa VMG hizo ndio wengi katika jamii. Hii ni hali

Page 10: WIZARA YA KILIMO, MIFUGO, UVUVI NA UNYUNYIZAJI (MoALFI) · 4. Mfumo wa VMGF utatumiwa na Idara ya Kitaifa ya Uvuvi na Uchumi wa Baharini, mashirika ya kutekeleza mradi wa KEMFSED

halisi katika BMU walio katika Visiwa vya Mukwiro na Wasini pia BMU wa Bodo na Munje

katika kaunti ya Kwale ambazo zina Washiratzi wengi. Hata hivyo, kuna ubaguzi na utengaji

wa jamii za VMG katika maeneo mengine kama vile BMU ya Kilifi ambapo jamii za VMG

zinaishi pamoja na jamii za Mijikenda, Wabajuni na Wapemba.

19. Utafiti wa kuchunguza jamii ya VMG ulionyesha kuwa kutokana na hali ya utengaji, jamii za

VMG hazifikii taasisi za mikopo, hazina makundi ya kujitegemea yaliyosajiliwa au Mashirika

ya Jamii (CBO) na kuwa baadhi ya mashirika ya jamii ambayo yalianzishwa hapo awali

yalianguka kutokana na usimamizi mbaya na ukosefu wa soko kwa bidhaa zao kama vile

mwani. Vijana katika jamii za VMG ambao wanajihusisha katika shughuli za utalii wamesajili

makundi ya vijana ambayo yanajumuisha wahudumu wa mashua (aghalabu ni wanaume) na

wanawake kufanya shughuli za burudani kwenye ufuo. Utafiti wa kuchunguza jamii

ulionyesha kuwa wanapata changamoto za kufikia huduma za mikopo na kuna umuhimu wa

kuboresha uwezo wa wafanyakazi ili waweze kushindana na watu wengine wanaojihusisha na

shughuli za kuendeleza utalii, zinazowapa riziki.

20. Baadhi ya miradi midogo katika kipengee cha 2 inaweza kujumuisha kuendeleza shughuli za

kilimo cha majini na Kilimo cha Baharini kupitia miundombinu bora, kuendeleza biashara

Ndogo Ndogo na za Wastani (SME) kwa kutoa mikopo, ushauri au kuboresha uwezo wa

wafanyakazi watakaopata mikopo. Jamii za VMG zitalengwa na shughuli hizi katika mradi.

21. Kipengee cha 3 cha KEMFSED kinalenga kuwezesha jamii za pwani na kuwapa njia za

kudumu za kupata riziki kupitia huduma za usaidizi na riziki kwa Jamii za Pwani zinazolenga

kuimarisha riziki na kuboresha uwezo wa wafanyakazi. Baadhi ya shughuli za miradi

zitakazofanyika chini ya kipengele hiki ni pamoja na; kutoa ufadhili wa elimu, kutoa zawadi

za kifedha na za kiufundi kama njia za ziada za kupata riziki na kupanua nyenzo za mapato na

kuendeleza utalii wa Baharini na Pwani. Hizi zinaweza kujumuisha kuendeleza shughuli za

kilimo, kuwapa vijana mafunzo ili kupata riziki kupitia shughuli za kitalii na kufufua baadhi

ya viwanda vilivyokuwa vimeanguka kama vile kiwanda cha korosho na kuboresha njia za

mapato yanayotokana na ukulima wa nazi. Pia itasaidia makundi ya jamii ili yapande miti kama

njia mbadala ya kukuza mikoko. Kwa mfano, miongoni mwa Washiratzi, kuna Shirika la Jamii

la Misitu (CFA) ambalo linahifadhi misitu na juhudi hizi zinastahili kuigwa katika jamii

nyingine za VMG ili zihifadhi mikoko. Wakifundi na Wavumba tayari wanajihusisha katika

shughuli za kitalii licha ya kupata changamoto kadhaa ambazo zinawazuia kutekeleza uwezo

wao kikamilifu. Kutakuwepo na juhudi za kusaidia njia hizi mbadala za kupata riziki kupitia

ubunifu wa mipango ya hatua kujumuishwa kwa jamii za VMG ambazo zinategemea mipango

ya jumla ya utekelezaji wa mradi wa KEMFSED.

Mipango ya Utekelezaji

22. Mradi wa KEMFSED utatekelezwa na Idara ya Taifa ya Uvuvi na Uchumi wa Baharini kama

shirika kuu, kwa ushirikiano na idara mbalimbali za serikali kama vile za mimea, Mifugo,

usimamizi wa uvuvi, Hazina ya Kitaifa, Idara ya Kitaifa ya Mazingira na Misitu, mwenyekiti

wa kamati ya idara za serikali katika Sekta ya Kilimo, Kitengo cha Mfumo wa Usimamizi wa

Page 11: WIZARA YA KILIMO, MIFUGO, UVUVI NA UNYUNYIZAJI (MoALFI) · 4. Mfumo wa VMGF utatumiwa na Idara ya Kitaifa ya Uvuvi na Uchumi wa Baharini, mashirika ya kutekeleza mradi wa KEMFSED

Fuo za Bahari ya Pwani, Shirika la Pwani la Wakulima wa Samaki na Shirika la Kenya la

Watayarishaji na Wauzaji wa Samaki katika Nchi za Kigeni (AFIPEK) katika ngazi ya kitaifa;

Serikali za kaunti husika katika fuo za pwani zitakuwa mashirika ya utekelezaji wa mradi

katika kiwango cha serikali za kaunti. Zitatoa mbinu za ufuatiliaji na utekelezaji katika

kiwango cha kaunti. Chini ya viwango vya kaunti vya utekelezaji na viwango vya usimamizi,

kutakuwa na viwango vya jamii vya miundo ya utekelezaji ambavyo vitajumuisha hasa

Mashirika ya Maendeleo Yanayosimamiwa na Jamii. Miundo ya utekelezaji katika kiwango

cha jamii itakuwa na kamati ndogo. Kutakuwepo na mashauriano mengine baada ya

Mashauriano yanayoeleweka, ya wazi na yanayopangwa mapema (FPIC) yanayofanywa

katika jamii za VMG kuhusu mipango ya utekelezaji WA mradi wa KEMFSED na kutambua

mikakati ya kutekeleza mradi jumuishi ambao unazingatia sifa za kipekee za uchumi na jamii

za VMG kabla ya kufanya mikutano ya mashauriano ya utekelezaji wa jamii yote.

Methodolojia

23. Data ilikusanywa kwa wakati mmoja ili kufahamisha SA na VMGF kwa kutumia njia za

msingi na za upili. Data ya upili ilipatikana kupitia kusoma vitabu, ilhali data ya msingi

ilikusanywa kupitia mashauriano na wadau, kuhoji wataalamu (KII), majadiliano

yanayoangazia makundi (FGD) na kutembea nyanjani.

Mifumo ya Sheria, Sera na Taasisi

24. Katiba ya Kenya (CoK) 2010 inatambua haki za tamaduni uchumi na uchumi wa jamii za

wananchi wote jinsi ilivyoashiriwa katika Kifungu cha 56 kinachohusu Makundi ya

waliotengwa na ya wachache. Kifungu hiki kinabainisha kuwa “taifa litaanzisha mipango ya

kupendelea wenyeji ambayo itahakikisha kuwa makundi ya waliotengwa na ya wachache

yanashiriki na kuwakilishwa katika uongozi na sehemu nyingine za maisha, b) yanapewa

nafasi maalum katika nyanja za uchumi na elimu, c) yanapewa nafasi maalum za kazi, d)

yanaendeleza matendo, lugha na shughuli za kitamaduni, na e) yanapata huduma nzuri za maji,

matibabu na miundombinu. Kifungu cha 260 kinatambua makundi yaliyotengwa na

yaliyotelekezwa. Kinatambua jamii za VMG kuwa jamii za wachache ambao wametengwa

kupitia matendo ya kihistoria. Inakataza ubaguzi wa makundi yaliyotengwa kupitia dhana

kuwa jamii hizo zina watu wachache au sababu nyinginezo, haijaweza kushiriki kikamilifu

katika shughuli za uchumi na jamii nchini Kenya kwa jumla. Pia, inatambua jamii ambazo

zimedumisha utambulisho na tamaduni zao za kipekee, hatua inayozizuia kushiriki katika

shughuli za maendeleo ya kiuchumi katika nchi ikiwa ni pamoja na usasi na utafutaji wa

vyakula mwituni, miongoni mwa nyingine. Utambuaji wa makundi haya ya VMG unapaswa

kuchangia katika uhifadhi wa utambulisho wao na kuwawezesha washirikishwe katika

maendeleo na makundi mengine, ikiwa ni pamoja na shughuli za kisiasa.

Hali za Uchumi wa Jamii za Kaunti za KEMFSED

25. VMG ilibaini ukosefu wa zana za uvuvi unaofanyika katikati mwa bahari, ukosefu wa ujuzi

wa uvuvi, kukosa kuwakilishwa katika miradi ya jamii ikiwa ni pamoja na uanachama katika

Vitengo vya Usimamizi wa Fuo kwa sababu zinashindwa katika kura na makundi yenye watu

Page 12: WIZARA YA KILIMO, MIFUGO, UVUVI NA UNYUNYIZAJI (MoALFI) · 4. Mfumo wa VMGF utatumiwa na Idara ya Kitaifa ya Uvuvi na Uchumi wa Baharini, mashirika ya kutekeleza mradi wa KEMFSED

wengi. Makundi ya Waliotengwa na Waliotelekezwa (VMG) yana matatizo ya mashamba na

wanaishi kama maskwota.

26. Vijana katika makundi ya VMG wameanzisha njia za kutengeneza mapato kupitia miradi

ambayo inajumuisha uhifadhi wa mazingira (upanzi wa miti na kuhifadhi mikoko), kuosha

magari, huduma za burudani kwenye ufuo na shughuli za mashua zinazolenga watalii.

27. Wanawake miongoni mwa makundi ya VMG wamejikita katika shughuli za ukulima wa

mwani, ushonaji na ‘mama karanga’ (kukaanga samaki) kuwa njia ya kutengeneza mapato

pamoja na ukulima wa vyakula ambao unategemea mvua.

28. SA ilitambua kuwa makundi mengi ya VMG yanapungua katika idadi au yanaacha tamaduni

zao ili kufuata tamaduni za wengi; kwa mfano, lugha ya Kisaanye inapotea na inajumuishwa

katika tamaduni na lugha ya Kibajuni. Watha wamejipanga ili kulinda utamaduni wao, kutetea

haki zao na kuhamasisha jamii zao ili kuendeleza mipango ya maendeleo.

29. Kuna kiwango cha chini cha elimu miongoni mwa jamii za VMG katika Pwani ya Kenya.

Kiwango cha chini cha elimu kinatokana na ukosefu wa pesa za kulipa karo ya watoto kwa

sababu ya viwango vikubwa vya umaskini. Ukosefu wa elimu rasmi unaoendeleza hali ya

kutengwa na jamii jirani.

Athari Zinazoweza Kutokea Kulingana na Vipengee

Kipengee cha 1: Kuboresha Udhibiti na Usimamizi wa Uvuvi wa Baharini.

30. Makundi ya VMG yatafaidika haswa kutokana na uimarishaji wa taasisi kama vile BMU

kupitia kuboresha uwakilishaji wake katika miundo ya usimamizi wa uvuvi kwenye maeneo

ya pwani. Kuzuia shughuli za kuvua samaki kupita kiasi na kudumisha uzalishaji wa samaki

pamoja na mfumo wa ekolojia ulioimairishwa utachangia kuongezeka kwa idadi ya samaki

wanaovuliwa na kuongezeka kwa mapato ya makundi ya VMG.

31. Nafasi za kazi zitaongezeka kupitia watu kujiari au kuajiriwa iwapo shughuli za uvuvi

zitasimamiwa vizuri.

Kipengee cha 2: Kuwezesha Uwekezaji wa Kudumu katika sekata ya Uvuvi wa Baharini na Kilimo cha

Majini

32. VMG zitanufaika kutokana na mipango ya kuendeleza kilimo cha majini kama njia mbadala

za kutengeneza pesa kupitia mpango wa mradi wa KEMFSED wa kujadili vikwazo

vinavyozuia uwekezaji katika shughuli za kudumu za uvuvi.

33. Baadhi ya VMG katika utafiti wa kuchunguza jamii walisema kuwa waliacha kujihusisha

katika kilimo cha mwani kwa sababu walikosa soko la bidhaa zao. Uboreshaji wa mazingira

ya biashara kupitia shughuli za mradi wa KEMFSED utaimarisha ufikiaji wa soko kwa

wakulima wa mwani na kuendeleza shughuli za kilimo cha majini katika jamii za VMG.

Kipengee cha 3: Riziki na Uimarishaji wa Jamii za Pwani

Page 13: WIZARA YA KILIMO, MIFUGO, UVUVI NA UNYUNYIZAJI (MoALFI) · 4. Mfumo wa VMGF utatumiwa na Idara ya Kitaifa ya Uvuvi na Uchumi wa Baharini, mashirika ya kutekeleza mradi wa KEMFSED

34. Utafiti wa kuchunguza jamii uliofanywa na KEMFSED umeonyesha kuwa jamii za VMG

zilizo katika eneo la mradi zinakosa uwezo wa kiufundi (ujuzi unaotakikana katika shughuli

za uvuvi bora) na uwezo wa kifedha (vifaa vya uvuvi) ambazo zinaweza kuwasaidia wapate

riziki ya kudumu kutokana na rasilimali za baharini. Zaidi ya hayo, utafiti wa kuchunguza

jamii umeonyesha umuhimu wa kuwa na mabadiliko ya mitazamo ya jamii za VMG kuwa

uvuvi unaweza kutumika kama shughuli za kibiashara lakini si kwa matumizi ya nyumbani

pekee. Pia VMG walielezea kuwa watoto wao hawawezi kupata ufadhili wa kielimu au pesa

zilizotengewa jamii ambako wanaishi kutokana na ubaguzi. Watanufaika kutokana na shughuli

za mradi wa KEMFSED zinazolenga kuimarisha uwezo wa jamii kupata ujuzi wa biashara na

kupata usaidizi wa ruzuku na kifedha. Mipango kama hiyo ya kuboresha uwezo wa

wafanyakazi itakuza ujuzi wao katika uvuvi na biashara ikiwa ni pamoja na kubadilisha

mitazamo kuhusu shughuli za uvuvi.

35. Utoaji wa huduma za mikopo na ufadhili wa elimu utaboresha viwango vya elimu kwa watoto

katika jamii za VMG kwa kuwafanya kuendelea na masomo.

36. Utafiti wa kuchunguza jamii ulionyesha kuwa kuna mashirika yaliyopo ya Jamii ambayo

yamesajiliwa ama hayajasajiliwa ambayo yanatoa mikopo kwa jamii za VMG. Pia kuna

ushahidi wa mashirika ya jamii ambayo yalianguka katika maeneo ya jamii za VMG. Makundi

ya VMG yatapata fursa ya kufufua mashirika yaliyoanguka au kuimarisha mashirika ya jamii

yaliyopo kupitia njia za kupata fedha na mikopo.

37. Kuboresha shughuli za uchumi na utumiaji wa kudumu wa rasilimali za bahari kupitia mpango

jumuishi utaendeleza utangamano katika jamii miongoni mwa makundi ya VMG na jamii

kubwa jirani ili yaishi kwa amani.

Athari Mbaya Zinazoweza Kutokea

38. Utafiti wa kuchunguza jamii ulionyesha kuwa kuna wanawake – ‘mama karanga’ ambao

wanapata samaki kutoka kwa wavuvi wa kiume wanaotoka baharini ili wazikarange na

wawauzie wenyeji katika maeneo ambayo samaki zinaletwa kutoka Bahari ya Hindi ya pwani

mwa Kenya. Hiki ni kitega uchumi kikuu ambacho ni maarufu kwa wanawake maskini na

wanaoweza kutelekezwa ambao pia wanatafuta riziki kwa familia zao katika Pwani mwa

Kenya. Usasishaji na uboreshaji wa maeneo ya kuwekwa samaki, unaweza kuanzisha kodi na

masharti mapya ya usafi. Hali hii inaweza kuwafurusha mama karanga kwenye biashara zao

na kuathiri riziki ya jamii za VMG ambazo tayari ni maskini. Kama njia ya kuzuia hili, kupitia

mpango wa makazi mapya, njia za ziada za kupata riziki zitaanzishwa katika mradi huu kuwa

njia za kufidia hasara yoyote inayotokana na uchumi.

39. Utafiti huu ulionyesha zaidi kuwa kuna vijana ambao wanabeba wasafiri kwa mashua kati ya

visiwa kama vile jamii za Wakifundi na Wavumba katika Visiwa vya Mukwiro na Wasini

katika bandari ya kuweka samaki ya Shimoni. Vijana hawa wanaoendesha mashua

wanasafirisha watu kutoka na kuenda barani na kituo cha afya ambacho wenyeji wanategemea

kiko Msambweni –Msambweni Sub-District Hospital. Vijana walihofia kuwa uboreshaji wa

bandari ya Shimoni, uwezekano wa kuzuia usafiri na uanzishaji wa vyombo vikubwa vya

Page 14: WIZARA YA KILIMO, MIFUGO, UVUVI NA UNYUNYIZAJI (MoALFI) · 4. Mfumo wa VMGF utatumiwa na Idara ya Kitaifa ya Uvuvi na Uchumi wa Baharini, mashirika ya kutekeleza mradi wa KEMFSED

majini, zinaweza kufanya wakose kazi. Pia kulikuwa na hofu kuwa njia ya kufikia kituo cha

afya cha Msambweni itakuwa vigumu iwapo bandari itaboreshwa na mashua ndogo kuzuiliwa

kufanya kazi kwenye visiwa. Pia, usasishaji wa bandari ya Shimoni unaweza kusababisha

uhamiaji wa wahudumu wengi walioelimika wanaoendesha mashua, ambao wanajimudu

katika lugha za kigeni kama vile Kihispani, Kifansa na Kijerumani, walio na vyeti vya

Mawasiliano ya Kompyuta ambao unatakikana ili kuhudumu katika sekta ya utalii, hali

ambayo itawaathiri wenyeji Wavumba na Wakifundi wanaoendesha mashua na hawajui lugha

hizi za kigeni.

40. Shughuli za mradi wa KEMFSED zitaathiri vibaya Makundi ya Waliotengwa na Kutelekezwa

(VMG) iwapo shughuli za mradi zitasababisha uharibifu wa miti au maeneo ya kidini kama

vile makaburi au maeneo ya kuabudu. Jamii za VMG ziliteta kwamba hakutakuwa na

mashauriano iwapo shughuli za mradi zitaharibu misitu na maeneo ya kidini.

Mipango ya Kufuatilia na Kuripoti

41. Ripoti za maendeleo ya kila robo ya mwaka zitaandaliwa na mashirika yanayotekeleza mradi

kuanzia mifumo ya kiwango cha jamii, kaunti na mifumo ya kiwango cha kitaifa, kama

masharti ya ripoti ya jumla ya Ufuatiliaji na Tathmini ili kufafanua maandalizi na utekelezaji

wa VMGP na malalamiko yaliyopatikana na kusuluhishwa. Ripoti hii itawasilishwa kwa Benki

ya Dunia kupitia shirika linaloongoza utekelezaji – idara ya Uvuvi na Uchumi wa Baharini.

Mifumo ya Kufuatilia na Kutathmini Mradi

42. Hatua zifuatazo zimependekezwa kuwa mbinu za kubuni mfumo bora wa kutathmini na

kufuatilia mradi:

Kuhamasisha na kufunza jamii kuhusu usanifu, uandalizi na utekelezaji wa mradi.

Mafunzo haya yanayolenga jamii yanapaswa kushirikisha wadau wote katika viwango vya

jamii na vinajumuisha; viongozi wa jamii, viongozi wa madini na utamaduni, vijana

(wakibainishwa kulingana na jinsia), wanawake na makundi mengine husika katika jamii

Kubuni mbinu ya kuhakikisha kuwa kuna mfumo wa kutoa maoni kwa wakati unaofaa,

ambao unaweza kudumisha kuangaziwa kwa shughuli za mradi. Mbinu hii itakayobuniwa

wakati wa mashauriano ya jamii inapaswa kuwa na mbinu ya kindani ya kuwawezesha

wawakilishi wa jamii kutoa ripoti maendeleo kwa jamii pana. Aidha, njia zinazofaa na

zilizokubaliwa za mawasiliano katika jamii zinatakiwa kubuniwa ili kuimarisha shughuli

za kutathmini na kufuatilia mradi.

Timu inayofaa ya kufuatilia na kutathmini mradi inapaswa kuwepo na itajumuisha

wawakilishi waliochaguliwa wa jamii ya VMG kuwa miongoni mwa wawakilisha kutoka

kwa jamii jirani, wawakilishi wa serikali ya kaunti na wawakilishi wa kamati ya utekelezaji

wa mradi wa KEMFSED.

Mbinu inapaswa kubuniwa ili kujumuisha wawakilishi waliochaguliwa wa vijana,

walemavu na wanawake katika timu ya kutathmini na kufuatilia mradi.

Viashiria vya Kutathmini na Kufuatilia Mradi wa KEMFSED/VMGF

43. Jedwali lililo hapa chini linaonyesha viashiria vya kufuatilia na kutathmini jinsi KEMFSED

itakavyoathiri jamii ya VMG.

Page 15: WIZARA YA KILIMO, MIFUGO, UVUVI NA UNYUNYIZAJI (MoALFI) · 4. Mfumo wa VMGF utatumiwa na Idara ya Kitaifa ya Uvuvi na Uchumi wa Baharini, mashirika ya kutekeleza mradi wa KEMFSED

Ufuatiliaji na Tathmini

Viashiria vya KEMFSED

Mradi

Kiashiria Wajibu Vyanzo vya Data

Juhudi za kuboresha

uwezo wa wafanyakazi

katika SME, ujuzi wa

uvuvi,

Kuendesha mashua,

usalama baharini na

shughuli za utalii

zinazohusika, Kilimo cha

Baharini

Na kilimo cha majini

Idadi ya wanachama wa

VMG waliopata mafunzo

ya biashara, kuvua,

kuendesha mashua

Na ujuzi wa usalama wa

baharini, Kilimo cha

Baharini na kilimo cha

majini.

Usimamizi wa

Uvuvi na Idara

ya Kitaifa ya

Uvuvi na

Uchumi wa

Baharini

Warsha za mafunzo

Kuipa jamii mapema

Vifaa vya uvuvi vya kisasa

(neti, boti n.k)

Idadi ya wanachama wa

VMG ambao wamepata

boti na neti bora za uvuvi,

nk

Usimamizi wa

Uvuvi na Idara

ya Kitaifa ya

Uvuvi na

Uchumi wa

Baharini

Fomu za maombi ya

bidhaa

zinazonunuliwa

Kuimarisha ufikiaji wa

huduma za ufadhili wa

kifedha na usaidizi wa

ruzuku

Idadi ya wanachama wa

VMG ambao wamenufaika

kutokana na usaidizi wa

ruzuku/kifedha

Usimamizi wa

Uvuvi na Idara

ya Kitaifa ya

Uvuvi na

Uchumi wa

Baharini

Rekodi ya

walionufaika kupata

usaidizi wa kifedha

na ruzuku

Ushauri kwa walionufaika

kutokana na usaidizi wa

ruzuku na fedha

Usaidizi

Idadi ya VMG

walionufaika kutokana na

usaidizi wa ruzuku na

fedha ambao wamefunzwa

kuhusu SME

Usimamizi wa

Uvuvi na Idara

ya Kitaifa ya

Uvuvi na

Uchumi wa

Baharini

Orodha za

mahudhurio na ripoti

za mafunzo

Ufadhili wa elimu Idadi ya wanajamii wa

VMG ambao wamenufaika

kutokana na ufadhili wa

elimu katika viwango

mbalimbali

Usimamizi wa

Uvuvi na Idara

ya Kitaifa ya

Uvuvi na

Uchumi wa

Baharini

Rekodi za

walionufaika

kutokana na ufadhili

wa elimu katika

vikundi mbalimbali

Ufuatiliaji wa utendaji wa

BMU

Wawakilishi wa wanajamii

wa VMG katika BMU

ambapo BMU hiyo

inapatikana katika

jamii/mfumo wa

wanajamii wa VMG

Usimamizi wa

Uvuvi na Idara

ya Kitaifa ya

Uvuvi na

Uchumi wa

Baharini

Ripoti za Kufuatilia

na Kutathmini Mradi

Kuboresha uwezo wa

Wafanyakazi katika BMU

Idadi ya wawakilishi wa

VMG ambao

wameshiriki/kuhudhuria

vipindi vya kuboresha

uwezo wa wafanyakazi

katika BMU

Usimamizi wa

Uvuvi na Idara

ya Kitaifa ya

Uvuvi na

Uchumi wa

Baharini

Orodha za

mahudhurio na ripoti

za mafunzo

Usajili na utoaji leseni wa

mashua za uvuvi

Idadi ya mashua za uvuvi

zinazomilikiwa na VMG

ambazo zimesajiliwa na

Usimamizi wa

Uvuvi na Idara

ya Kitaifa ya

Ripoti za Kufuatilia

na Kutathmini Mradi

Page 16: WIZARA YA KILIMO, MIFUGO, UVUVI NA UNYUNYIZAJI (MoALFI) · 4. Mfumo wa VMGF utatumiwa na Idara ya Kitaifa ya Uvuvi na Uchumi wa Baharini, mashirika ya kutekeleza mradi wa KEMFSED

kupewa leseni ili

zihudumu katika BMU

Uvuvi na

Uchumi wa

Baharini

Uwezeshaji wa jinsia ili

kupata riziki ya ziada

Shughuli

Ulinganishaji wa idadi ya

wanawake na wanaume

katika VMG ambao

wamewezeshwa kuendesha

SME, wamesaidiwa

kufanya kilimo,

Usimamizi wa

Uvuvi na Idara

ya Kitaifa ya

Uvuvi na

Uchumi wa

Baharini

Ripoti za Kufuatilia

na Kutathmini Mradi

Uendelezaji wa shughuli za

kudumu za mfumo wa

ekolojia

Idadi ya shughuli za

kuhifadhi mazingira katika

jamii (mikoko, njia

mbadala ya kupanda miti

nk) ambazo zimeanzishwa

na kujumuisha uongozi wa

VMG miongoni mwa

wanachama wengine

katika jamii pana

Usimamizi wa

Uvuvi na Idara

ya Kitaifa ya

Uvuvi na

Uchumi wa

Baharini

Ripoti za Kufuatilia

na Kutathmini Mradi

Mikutano ya uhamasishaji

wa jamii ya kusaidia jamii

pana ya VMG

Idadi ya mikutanao ya

uhamasishaji ya kusaidia

jamii pana iliyofanywa

miongoni

mwa/kuhudhuriwa na

jamii za VMG

Usimamizi wa

Uvuvi na Idara

ya Kitaifa ya

Uvuvi na

Uchumi wa

Baharini

Rekodi za mikutano

za jamii

Mbinu ya Kushughulikia Malalamiko

44. Kila mwanachama wa VMG katika eneo la mradi alikuwa na mbinu thabiti za zinazoongozwa

na tamaduni/mila kulingana na mfumo wa Baraza la Wazee ambao waliashiria kuwa njia

waliyopendelea kusuluhisha mizozo wakati wa kutekeleza VMGP. Kulingana na jamii nyingi,

mwanajamii yeyote ambaye anakataa kukubali unamuzi wa “mahakama” za kimataduni

amelaaniwa na wazee na jamii na yuko tayari kusuluhisha mzozo kupitia njia za mahakama na

kisheria. Kanuni hii itatumika kama njia ya kusuluhisha mizozo katika mradi huu.

45. Wakati wa mashauriano, wanachama mbalimbali wa VMG walielezea kuwa wangependa

kusuluhisha mizozo na malalamiko kupitia miundo ambayo wamewakilishwa kikamilifu na

isiyoathiriwa zaidi na jamii kuu. Walipendekeza kiwango cha chini zaidi, yaani kiwango cha

jamii, kwa kutumia mifumo ya kiusimamizi na ya kitamaduni ya wazee wa vijiji kadri

iwezekanavyo. Walitilia shaka viwango vya juu vya Kusuluhisha Mizozo kwa kuwa

hawajawakilishwa na hawakuamini mifumo ambayo inasimamiwa na watu waliosoma sana.

Mipango ya Kuidhinisha na Kuvumbua

Kuidhinisha

46. Rasimu hii ya VMGF itapitia hatua mbalimbali za uidhinishaji katika Idara ya Kitaifa ya

Uvuvi, Kilimo cha Majini na Kilimo cha Baharini, timu ya utekelezaji wa mradi wa

KEMFSED na timu ya Ulinzi wa Benki ya Dunia katika nchi na kanda.

Uvumbuzi

Page 17: WIZARA YA KILIMO, MIFUGO, UVUVI NA UNYUNYIZAJI (MoALFI) · 4. Mfumo wa VMGF utatumiwa na Idara ya Kitaifa ya Uvuvi na Uchumi wa Baharini, mashirika ya kutekeleza mradi wa KEMFSED

47. Kwa mujibu wa Katiba ya Kenya ya CoK, 2010 na sera ya Benki ya Dunia ya Kuvumbua kwa

Umma, 2011, uwazi na uwajibikaji ni mambo muhimu katika mchakato wa maendeleo

yanayolenga kupunguza umaskini. Kwa hivyo, uvumbuzi katika umma wa VMGF utachukua

mtindo wa: (i) shughuli ambazo mradi unafadhili; (ii) jinsi rasilimali zimegawanywa na

kutumiwa; (iii) maendeleo katika utekelezaji wa mradi; na mwisho, (iv) mafunzo ambayo

yametokana na mradi ili yashirikiwe miongoni mwa wadau na wahusika wa mradi.

48. Njia inayofaa ya kuvumbua maelezo haya itabainishwa mara kwa mara, japo kupitia

mashauriano tulifahamu kuwa mabaraza ya umma (mikutano ya jumla ya jamii), wadi, utawala

wa eneo, miundo inayofaa ya kiwango cha kaunti na kaunti ndogo na ofisi za chifu

ingependelewa kwa VMG. Uvumbuzi hasa katika kiwango cha jamii, hasa kupitia mabaraza

ya jumla utafanyika katika Kiswahili, lugha ambayo inatumiwa zaidi na jamii ya VMG.

Muhtasari utafaa katika hali hii. Ripoti kamili inapaswa kuvumbuliwa kwenye makao makuu

ya Kaunti na Kaunti ndogo. Mwisho, VMGF imechapishwa kwenye tovuti za washirika

wanaotekeleza mradi, haswa zile za idara ya Kitaifa ya Uvuvi na Uchumi wa Baharini na pia

Tovuti za Nje za Kimataifa.

Muhtasari wa Mapendekezo, Majukumu na Wajibu wa KEMFSED

Mapendekezo

49. Ili kushirikisha VMG zaidi, kuna umuhimu wa kujumuisha jamii katika hatua zote za mradi.

Wakati wa utekelezaji, ujumuishaji wa VMG na uhusiano wao na jamii nyingine, pamoja na

athari za mradi katika masilahi yao yanapaswa kufuatiliwa kikamilifu.

a) Shughuli zinazofaa za uhamasishaji na uwasilishaji zinapaswa kuratibiwa kupitia hatua

mbalimbali zinazotumika za mawasiliano, kuwa sehemu ya mbinu za utoaji huduma (yaani

ulengaji, malipo, G&CM nk.). Inatarajiwa kuwa hali hii itaendelea katika awamu zote za

huduma ya KEMFSED, na kutekelezwa zaidi wakati wa KEMFSED.

b) Mikakati na zana za mawasiliano itajumuisha mabaraza ya jumla ya jamii, redio, SMS,

vipeperushi, matangazo kupitia megafoni nk. Hususan, Mikakati ya Uhamasishaji kwa

Wanaonufaika kupitia ujumbe maalum wa VMG itatumika ili kuhakikisha ujumuishaji wa

VMG na itatoa mbinu zinazofaa za kuhakikisha kuwa VMG wamefikiwa na kuwa habari

inatolewa kwa njia ambazo zinaeleweka kwa urahisi. Huenda hatua hii itahitaji kulenga

makundi mbalimbali ya VMG, kulingana na mahali waliko, lugha, kiwango cha elimu,

kujumuishwa katika jamii pana na elimu ya uraia.

c) Kuandika idadi na aina ya malalamiko ambayo yamewasilishwa kuhusu mradi na hatua

ambazo zimechukuliwa na kuhakikisha kuwa njia zinazofaa zimebuniwa na kutekelezwa.

d) Kukusanya data ya malalamiko na maoni ya wanaonufaika mara kwa mara ili kuhakikisha

kuwa maeneo yanayolengwa ambayo jamii ya wachache ipo yanafikiwa na malalamiko

yanayojirudia yanapelelezwa ili kupata njia za kuyasuluhisha.

e) Kuhakikisha kuwa vizuizi vya ujumuishaji (kama vile ugumu wa kupata Vitambulisho na

Huduma Namba) vinashughulikiwa kwa wanajamii husika, ikiwa ni pamoja na VMG.

f) Ufahamu na rekodi bora za lugha, tamaduni na kizazi cha Wasaanye itatakikana ili

kuchunguza Wasaanye ambao watanufaika kutokana na mradi wa KEMFSED na miradi

ya baadaye ya Benki ya Dunia inayolenga jamii Zilizotengwa na Zinazotelekezwa

Page 18: WIZARA YA KILIMO, MIFUGO, UVUVI NA UNYUNYIZAJI (MoALFI) · 4. Mfumo wa VMGF utatumiwa na Idara ya Kitaifa ya Uvuvi na Uchumi wa Baharini, mashirika ya kutekeleza mradi wa KEMFSED

g) Kuna umuhimu wa mawasiliano ya ziada katika jamii ili kubainisha maeneo mengine

ambako inatarajiwa kuwa shughuli za mradi wa KEMFSED zinaweza kuathiri misitu ya

kidini na sehemu za VMG.

50. Kuna umuhimu wa kuhamasisha na kuwapa mafunzo wadau wote kuhusu utambulisho na

ujumuishaji unaofaa wa aina mbalimbali za VMG. Kwa hivyo, mashirika yanayotekeleza

KEMFSED yanapaswa kukagua hifadhidata iliyopo ya VMG kwa kila kaunti ya KEMFSED.

Zaidi ya hayo, maafisa wa mpango wanapaswa kuhamasishwa kuhusu hali za ukasumba, na

jinsi ya kujumuisha makundi kama hayo katika KEMFSED. Hatua hii itasaidia kuelewa sifa

na maeneo ya VMG na kuwahamasisha maafisa kuhusu VMG ili waweze kuwasiliana nao na

kuwalenga vizuri. Ili kuongeza uhusiano na VMG, kuna haja ya kuhimiza ushirikiano kati ya

idara za serikali za uvuvi na uchumi wa baharini na washirika wa utekelezaji na mashirika

mengine ya jamii na ya serikali ambayo yanafanya kazi na VMG.

51. Elimu ya uraia na mafunzo kwa jamii yanapaswa kufanywa ili kuimarisha weledi na haki za

kila mtu, ikiwa ni pamoja na VMG. Mafunzo kuhusu haki yanaweza kufanywa kama sehemu

ya mpango wa kuhamasiaha wanaonufaika katika jamii na wote wanaonufaishwa na

KEMFSED.

52. Wakati wa kuwasiliana na VMG, hakikisha kuwa njia na mbinu zinazofaa za mawasiliano

zinatumiwa na kutambuliwa na wanajamii wa VMG wenyewe. Huenda vituo vya redio vya

FM visifikiwe au kueleweka na kila mtu. Kwa hivyo, unaweza kupiga simu, kutuma ujumbe

kwa wawakilishi na viongozi na kufanya mikutano ya mabaraza ya moja kwa moja.

53. Wakati unalenga makundi ya wachache, jumuisha makundi ya wachache wakati wa kupanga

ili wakuunge mkono na uendeleze utangamano unaofaa. Hakikisha kuwa makundi ya

wanawake na vijana yanashauriwa vizuri kuhusu njia bora ya kuyahusisha na mapendekezo

yao ili mradi utimize malengo yake.

54. Mashirika ya utekelezaji yanapaswa kuandaa VMGP kwa kila shughuli ya KEMFSED iwapo

VMG watatambuliwa kuwepo katika eneo la shughuli na kuchukuliwa kuwa wameathiriwa na

shughuli na itaongozwa na sheria ya Benki ya Dunia ya OP4.10, Annex B. Hususan, VMGP

itatayarishwa kwa ajili ya jaribio la mikakati ya kiuchumi, kwa kuwa athari kwenye VMG

inatarajiwa iwe kubwa zaidi katika shughuli hizi. Hata hivyo, VMGP pia itaandaliwa katika

shughuli hizo nyingine mbili (utoaji wa pesa na upanuaji wa neti za usalama), panapofaa,

kutokana na utambuaji wa VMG katika maeneo ya mradi. Idhini ya Benki ya Dunia kwa

VMGP itatakikana kabla ya utekelezaji.

Majukumu na Wajibu

Mashirika ya Utekelezaji wa KEMFSED

55. Mashirika ya utekelezaji wa KEMFSED katika Kaunti yatakuwa na wajibu wa:

i. Kubaini makundi ya VMG katika kaunti zao, ikiwa ni pamoja na mahali waliko na jinsi ya

kuwafikia;

ii. Kuendeleza VMGP ili kutambua athari kubwa, kubuni njia za kusuluhisha na kutoa mwelekeo

kuhusu jinsi njia hizo za kusuluhisha zitafadhiliwa na kufuatiliwa.

Page 19: WIZARA YA KILIMO, MIFUGO, UVUVI NA UNYUNYIZAJI (MoALFI) · 4. Mfumo wa VMGF utatumiwa na Idara ya Kitaifa ya Uvuvi na Uchumi wa Baharini, mashirika ya kutekeleza mradi wa KEMFSED

iii. Kuchunguza athari za mradi na ufanisi wa njia zilizopendekezwa za kusuluhisha matatizo

yanayotokana na VMG husika. Wakati wa kutekeleza shughuli za mradi, athari na hatari za jamii,

hali za makundi ya VMG yaliyoathiriwa na uwezo wa mashirika ya utekelezaji kutoka kiwango

cha kitaifa na kaunti, unapaswa kuchunguzwa.

iv. Kuchunguza utoshelezaji wa utaratibu wa mashauriano na usaidizi mpana wa VMG zilizoathiriwa

katika mradi. Hii itajumuisha utekelezaji wa VMGP, kushughulikia matatizo ya utekelezaji na

kurekodi mambo waliyojifunza yanayohusu VMG na utumiaji wa VMGF/VMGP.

Benki ya Dunia

i. Kuidhinisha VMGF kwa KEMFSED.

ii. Kupokea VMGP zote zilizoandaliwa, kuzikagua na Kuziidhinisha au vinginevyo, kabla ya

kutekeleza shughuli za KEMFSED.

iii. Wakati wa kutekeleza, itathmini na kufuatilia nyanjani, inavyohitajika.

iv. Kusaidia katika kuboresha uwezo wa wafanyakazi kadri inavyotakikana.