79
YALIYOMO Jamsii ya Wasangu ukurasa 1. Utangulizi ........................................................................................................................ 1 2. Wasangu wanapokaa ......................................................................................................... 1 3. Mito Mikuu ya Bonde la Usangu......................................................................................... 2 4. Bonde la Usangu ................................................................................................................ 3 5. Ramani ionyeshayo Eneo la Usangu ................................................................................. 3 6. Udongo wa Bonde la Usangu............................................................................................. 4 7. Magonjwa ........................................................................................................................... 4 8. Historia .............................................................................................................................. 5 9. Misafara ya kwanza ya Kiarabu .......................................................................................... 6 10. Kuja kwa Wangoni .............................................................................................................. 6 11. Wasangu wapigana na Amrani Masudi ........................................................... :................ 6 12. Kindumbwe ndumbwena Wahehe ................................................................................... 8 13. Merere akiwa Ukimbu ......................................................................................................... 9 14. Merere akiwa Mfumbi ........................................................................................................ 9 15. Merere atawala nchi ya Wasafwa........................................................................................ 10 16. Wajerumani waja mwaka wa 1892 ..................................................................................... 10 17. Kilimo katika Bonde la Usangu ......................................................................................... 11 18. Historia ya kilimo cha mpunga ...................................................................................... 11 19. Ndoa za Wabaluchi .......................................................................................................... 12 20. Kilimo kinachoendeshwa sasa Usangu .............................................................................. 13 21. Sehemu zihazopandwa mpunga katika Bonde la Usangu .................................................. 14 22. Kilimo kwa jumla ............................................................................................................. 17 23. Kilimo cha mpunga .............................................................................................................. 17 24. Matatizo ya kilimo cha mpunga ................................................................................... 18 25. Mifugo katika Bonde la Usangu........................................................................................ 19 26. Magonjwa ya Mifugo ......................................................................................................... 19 27. Matatizo kuhusu Mifugo .................................................................................................... 19 28. Kilimo cha Wasangu ......................................................................................................... 20 29. Ghala za Chakula ............................................................................................................... 21 30. Ufugaji wa ng'ombe .......................................................................................................... 22 31. Shabaha ya kufuga ng'ombe.............................................................................................. 22 32. Utawala wa Wasangu ......................................................................................................... 22 33. Sifa kuu za Mwene ........................................................................................................ 23 34. Familiana ndoa ya Kisangu ........................................................................................... 23 35. Imani na Dini ....................................................................................................................... 24 36. Uchawi ................................................................................................................................ 24 37. Nyumba za Wasangu .......................................................................................................... 24 38. Mavazi yao ya jadi .............................................................................................................. 25 39. Michezo ya Wasangu ........................................................................................................ 25 40. Miiko ya Ngoma ................................................................................................................. ..25 41. Mapendekezo ..................................................................................................................... .25 Jamii ya Wasafwa 42. Utangulizi ..................................................................................……………………………..29 43. Jamii ya Wasafwa ilipo ...................................................................................................... 30 44. Historia fupi ya Wasafwa .................................................................................................. 31 45. Kipindi cha majilio ya Wageni na Vita.......................................................................... 33 46. Kuja kwa Wamishonari ...................................................................................................... 34

YALIYOMO Jamsii ya Wasangu ukurasa - Safarilandsmbuga za Usangu ni nzuri sana kwa hiyo mkulima halazimiki kutia mbolea hata kidogo katika mashamba yake. Mbolea ya asili ni nyingi mno

  • Upload
    others

  • View
    30

  • Download
    0

Embed Size (px)

Citation preview

YALIYOMO

Jamsii ya Wasangu ukurasa

1. Utangulizi ........................................................................................................................ 1 2. Wasangu wanapokaa......................................................................................................... 1 3. Mito Mikuu ya Bonde la Usangu......................................................................................... 2 4. Bonde la Usangu................................................................................................................ 3 5. Ramani ionyeshayo Eneo la Usangu ................................................................................. 3 6. Udongo wa Bonde la Usangu............................................................................................. 4 7. Magonjwa ........................................................................................................................... 4 8. Historia .............................................................................................................................. 5 9. Misafara ya kwanza ya Kiarabu .......................................................................................... 6

10. Kuja kwa Wangoni.............................................................................................................. 6 11. Wasangu wapigana na Amrani Masudi ........................................................... :................ 6 12. Kindumbwe ndumbwena Wahehe ................................................................................... 8 13. Merere akiwa Ukimbu......................................................................................................... 9 14. Merere akiwa Mfumbi ........................................................................................................ 9 15. Merere atawala nchi ya Wasafwa........................................................................................ 10 16. Wajerumani waja mwaka wa 1892 ..................................................................................... 10 17. Kilimo katika Bonde la Usangu ......................................................................................... 11 18. Historia ya kilimo cha mpunga ...................................................................................... 11 19. Ndoa za Wabaluchi .......................................................................................................... 12 20. Kilimo kinachoendeshwa sasa Usangu.............................................................................. 13 21. Sehemu zihazopandwa mpunga katika Bonde la Usangu.................................................. 14 22. Kilimo kwa jumla ............................................................................................................. 17 23. Kilimo cha mpunga.............................................................................................................. 17 24. Matatizo ya kilimo cha mpunga ................................................................................... 18 25. Mifugo katika Bonde la Usangu........................................................................................ 19 26. Magonjwa ya Mifugo......................................................................................................... 19 27. Matatizo kuhusu Mifugo .................................................................................................... 19 28. Kilimo cha Wasangu ......................................................................................................... 20 29. Ghala za Chakula ............................................................................................................... 21 30. Ufugaji wa ng'ombe .......................................................................................................... 22 31. Shabaha ya kufuga ng'ombe.............................................................................................. 22 32. Utawala wa Wasangu......................................................................................................... 22 33. Sifa kuu za Mwene ........................................................................................................ 23 34. Familiana ndoa ya Kisangu ........................................................................................... 23 35. Imani na Dini ....................................................................................................................... 24 36. Uchawi ................................................................................................................................ 24 37. Nyumba za Wasangu.......................................................................................................... 24 38. Mavazi yao ya jadi .............................................................................................................. 25 39. Michezo ya Wasangu ........................................................................................................ 25 40. Miiko ya Ngoma ................................................................................................................. ..25 41. Mapendekezo..................................................................................................................... .25

Jamii ya Wasafwa 42. Utangulizi..................................................................................……………………………..29 43. Jamii ya Wasafwa ilipo...................................................................................................... 30 44. Historia fupi ya Wasafwa .................................................................................................. 31 45. Kipindi cha majilio ya Wageni na Vita.......................................................................... 33 46. Kuja kwa Wamishonari ...................................................................................................... 34

47. Serikali ya Kijerumani .......................................................................................................... 34 48. Kilimo .................................................................................................................................... 35 49. Mgawanyo wa kazi ............................................................................................................... 36 50. Kuvuna .................................................................................................................................. 36 51. Ghala ya mazao .................................................................................................................... 36 52. Kuhama hama kwa watu ....................................................................................................... 37 53. Wanyama Waf ugwao ........................................................................................................... 37 54. Umbo la familia ya Kisafwa ................................................................................................. 38 55. Ndoa ..................................................................................................................................... 39 56. Ndoa ya siku hizi .................................................................................................................. 40 57. Sifa za wachumba................................................................................................................ 41 58. Talaka................................................................................................................................... 41 59. Desturi za kula chakula ........................................................................................................ 42 60. Mama anayezaa Mapacha ................................................................................................... 42 61. Mama aliyefiwa na bwana yake ........................................................................................... 43 62. Mama kupata mimba bila kupitia hali yake ......................................................................... 43 63. Kuotesha meno ya juu kwanza ............................................................................................ 43 64. Utawala................................................................................................................................. 44 65. Kifo .............................. , ....................................................................................................... 44 66. Kuzika................................................................................................................................... 45 67. Mavazi................................................................................................................................... 45 68. Miiko..................................................................................................................................... 45 69. Imani ..................................................................................................................................... 46 70. Kutambikia Mvua ................................................................................................................. 46 71. Maana ....................................................................................................................................... 47 72. Maji ....................................................................................................................................... 48 73. Elimu yaWatoto ................................................................................................................... 74. Kumpeleka mtoto shuleni .................................................................................................... 49 75. Nyumba za Wasafwa............................................................................................................ 49 76. Orodha ya vitabu vya kumbukumbu..................................................................................... 50

Jamii ya Wasagara

77. Historia ya Wasagara........................................................................................................... 51 78. Imani ..................................................................................................................................... 53 79. Tambiko la Mvua.................................................................................................................. 54 80. Uchawi .................................................................................................................................. 55 81. Desturi za Wasagara ............................................................................................................ 55 82. Chakula cha Wasagara ........................................................................................................ 56 83. Mwanamke mwenye mimba ............................................................................................... 56 84. Mtoto .................................................................................................................................... 56 85. Jando.................................................................................................................................... 57 86. Siku ya kutoka...................................................................................................................... 57 87. Wakati wa Posa...................................................................................................................58 88. Kuvunjika ndoa ................................................................................................................... 59 89. Mahari ................................................................................................................................. 59 90. Msichana .............................................................................................................................. 59 91. Kifo ....................................................................................................................................... 60 92. Ufundi ............................................................................................................................... 61 93. Utani wa Wakaguru na Wasagara .......................................................................................61 94. M ichezo ya Wasagara ........................................................................................................ 62 95. Kilimo chajadi cha Wasagara .............................................................................................62

96. Mgawanyo wa kazi ............................................................................................................... 65 97. Plani ya ghala ...................................................................................................................... 66 98. Chama cha Ushirika cha wilaya ya Kilosa............................................................................ 67 99. Hudumaza chama cha ushirikakwa wakulimawa Kilosa .................................................. 68 100. Wanyama............................................................................................................................. 69 101. Familia ............................................................................................................................... 69 102. Nyumba za Wasagara.......................................................................................................... 69 103. Milango-aina ya mbila ..................................................................................................... 70 104. Ndoa .................................................................................................................................... 70 105. Desturi za kuamkiana .. ..................................................................................................... 72 106. Utawala ............................................................................................................................... 72 107. Kiapo.................................................................................................................................... 73 108. Mali ................................................................................................................................... 73 109. Mavazi ya Wasagara ............................................................................................................ 74 110. Mapambo............................................................................................................................. 74 111. Mwisho . ........................................................................ 74

Sura ya Kwanza

JAMII YA WASANGU

UTANGULIZI

Makala haya yanazungumzia habari za Wasangu waishio katika bonde la Usangu katika Wilaya ya Mbeya. Kama inavyojulikana Utafiti huu, ambao unaendelea, wafanywa kwa shida nyingi za usafiri kutoka mahali fulani hadi pengine ambapo utafiti watakiwa ufanyike. Magari hatuna ambayo yangalituwezesha kufika mahali pa utafiti kwa urahisi zaidi. Safari zotezafanywa kwa miguu na watu ambao pengine wangesaidia kutoa habari wanashindwa kutembea au sisi wenyewe watafiti tunashindwa kuwafikia kwa wakati unaofaa.

Zaidi ya hayo, habari nyingi zimesahauliwa sana kwa sababu hakuna mtu aliyejishughulisha kuzitafuta na kuzihifadhi kwa sababu Wazungu walipofika huku kwetu waliziita hizo habari ni za kishenzi. Basi watu wakaziacha na habari zake zikapotea kabisa.

Shukurani nyingi ziwaendee wazee wote wa Jamii ya Wasangu ambao walijitahidi sana kukumbuka habari kiasi walichoweza na kupoteza muda wao mwingi ambao wangeliutumia kwa shughuli zao za kuinua maisha yao. Shukurani nyingi zaidi zimwendee Mzee Merere — ambaye ni Katibu Tarafa wa Chimala na ambaye alikuwa Chifu wa jadi wa Wasangu kabla ya kupata Uhuru 1961, kwa msaada wake mwingi sana katika kutoa habari nyingi za Wasangu, katika kuwa mkalimani wetu kati yetu na Wazee wa Kisangu, pia katika uwezo wake wa kuweza kuwakusanya watu wanaofahamu habari nyingi za Jamii ya Wasangu. Bila ya msaada wa Mzee Merere pengine sehemu kubwa ya kazi yangu kuhusu utafiti juu ya Mila za Wasangu isingeliweza kufanyika.

MITO MIKUU YA BONDE LA USANGU

BONDE LA USANGU

Jumla ya Wakaaji wa bonde la Usangu ni zaidi ya watu 74,000 Kama ilivyohesabiwa mwaka 1972. Lakini jumla ya watu kamaSerikali ilivyohesabu mwaka 1967 ni watu 56,743, kwahiyo jumlaya watu katika bonde la Wasangu yaongezeka kwa haraka sana kuliko jumla ya watu inavyoongezeka katika sehemu zingine za Tanzania. Sababu zinazofanya watu waongezeke upesi sana katika bonde hili ni nyingi sana; na baadhi yasababu zenyewe ni kama hizi hapachini:-

Sababu ya kwanza ni kwamba bonde hili la Usangu tangu zamani lilikuwa halijulikani sawasawa na watu wengi jinsi lilivyo na manufaa kwa shughuli mbali mbali za uzalishaji mali kwa sababu Wasangu walikuwa wapiganaji hodari wa vita kwa hiyo ilikuwa ni vigumu sana kwa jatnii zingine kwenda kufanya mastaakimu yao huko. Hata baada ya Wakoloni kukomesha vita vya jamii mbalimbali za Nyanda za juu za Kusini, jamii zilikuwa hazijui habari kamili kuhusu bonde hili. Baada ya Uhuru tu, mawasiliano katika bonde hili na nje ya mbugaza Usangu yakabadilika sana na kuwa bora zaidi yaliyoletwa na Chama chaTANU katika kuhudumia watu wake sawasawa. Pili, udongo wa mbuga za Usangu ni nzuri sana kwa hiyo mkulima halazimiki kutia mbolea hata kidogo katika mashamba yake. Mbolea ya asili ni nyingi mno katika udongo na mimea ikipandwa hustawi sana. Tatu, kuna mito mingi yenye maji kwa matumizi ya watu na mifugo pia, kwa hiyo watu wamevutiwa sana na mali ya asili ya namna hii. Nne, Mbuga za Usangu zinafaa sana kwa ufugaji wa mifugo — hasa ng'ombe, mbuzi na kondoo. Manyasi yanapatikana kwa urahisi na maji kwa ajili ya mifugo kwa hiyo wafugaji wamevutiwa sana na mbuga hizi kutoka wilaya za jirani na za mbali pia. Tano, mbuga za Usangu ni kubwa sana na zina nafasi kubwa za kustawisha malisho ya mifugo na ulimaji wa mazao mbalimbali. Mvua zanyesha kiasi cha kutosha bali kuna jua kali sana wakati wa kiangazi. Hali kadhalika ziko sababu zingine nyingi zilizowavutia watu kuja kukaa katika mbuga za Usangu

toka Mikoa mingine.

3

Jamii zinazoishi katika bonde la Usangu ni Wasangu ambao ni wenyeji wa mbugaza Usangu Wanyakyusa ambao wamehamia mbuga za Usangu toka Rungwe kuja kulima mashamba ya mpunga na mimea mingine; Wabena ambao wamehamia mbuga hizo toka Wilaya ya Njombe na hushughulika zaidi na kilimo cha mpunga na mazao mengineyo. Wakinga toka Wilaya ya Njombe, nao hujishughulisha sana na biashara — hasa biashara ya samaki; Wahehe toka Wilaya ya Iringa — hujishughulisha na kilimo pamoja na ufugaji; Wahehe wanafanana sana na Wasangu katika mila na desturi; Wamasai na Wasukuma, ambao hasa walianza kuhamia katika mbuga za Usangu tangu mwaka1973, mwezi Septemba. Jamii hizi mbili zimehamia mbugaza Usangu juzi juzi tu, lakini jamii zingine zilihamia mbuga za Usangu miaka mingi kidogo iliyokwisha pita. Wamasai hujishughulisha zaidi na ufugaji na Wasukuma hujishughulisha na mambo yote mawili, ufugaji na ukulima. Jamii nyingine ambayo imekaa sana katika bonde la Usangu ni jamii ya Wabaluchi ambao wanaitwa kama "Maburushi". Jamii hii imekaa katika mbuga za Usangu tangu karne ya 19 na tangu wakati huo jamii hii imejishughulisha sana na kilimo cha mpunga na pia mazao mengine. Walikuwa watu wa kwanza katika bonde ia Usangu Kutumia kilimo cha kumwagilia maji katika mashamba kwa njia ya mifereji iliyochimbwatoka mto Mbarali. Angalia habari zao hapa chini.

UDONGO WA BONDE LA USANGU Bonde la Usangu lilikuwa na mi to ambayo maji yake yalikuwa yanatiririkia kuelekea katika

bonde la Ziwa Rukwa naZiwa Nyasa. Milipuko ya Volkano ya mlima Rungwe ikaizuia mito hiyo kwa mwinuko wa ardhi halafu mito ikatiririka katika bonde la Usangu na kulifanya bonde la Usangu kuwa ziwa. Katika mabadiliko ya ardhi, udongo, changarawe na michanga ikaletwachini yaziwa lenyewe. Mito ambayo ilikuwa inatiririkia katika bonde la ziwa Rukwa na ziwa Nyasa, sasaziwa lililokuwapo katika bonde la Usangu (mahali ambapo mbuga za Usangu zipo sasa) likapata nafasi ya kuyamwaga maji yote kwa njia ya mito upande wa Kaskazini — Mashariki, na mbuga zikatokea toka kwenye mchanga wa ziwa lenyewe. Na udongo na matope na udongo wa mfinyanzi unaopatikana katika mbuga za Usangu umeletwa na mito mbali mbali inayotiririkia katike. bonde hili la Usangu.

Udongo wa mbuga za Usangu ni wa aina nyingi na unafaa sana kwa mazao. Kuna udongo wa mfinyanzi, udongo wa mbuga, na udongo mweusi wenye rutuba sana. Udongo waainazote hizi una rutuba nyingi sana kwa mazao.

Mazao yapandwayo katika bonde hili ni mpunga, mahindi, viazi vitamu, viazi ulaya, ulezi, migomba, maharage, karanga, miwa, mihogo na maboga mbalimbali.

MAGONJWA Mbuga za Usangu zina maradhi mengi sana, magonjwa ambayo yanawasumbua sana watu ni

homa, kichocho, safura, surua, homa ya papasi, ugonjwa wa kuhara na magonjwa ya minyoo ya aina mbalimbali. Walakini magonjwa mabaya sana ambayo yanammalizia mkulima wakati wake mwingi sana ni kichocho, homa, safura na ugonjwa wa kuhara. Sababu ya kupatikana kichocho kwa wingi sana katika mbuga za Usangu ni kwamba mbuga za Usangu zina matopematope mengi sana na pia kuna majimaji mengi ambayo yamekwama hayatembei. Konokono ambao ndio hueneza vidudu vya ugonjwa wa kichocho hupenda sana kuogelea katika maji ambayo yamekwama na kwa jinsi hii vidudu vya kichocho huachwa humohumo majini vikingojea mwanadamu yeyote kupitia katika maji hayo au kuogelea katika maji hayo na wakati huo vidudu vya kichocho vyamrukia mtu na kupenyeza katika mwili wake hadi kibofuni na kwenye matumbo ambako vyazaliana sana na kuanza kula sehemu ya ngozi ya sehemu hizo. Kuutibu ugonjwa wa kichocho ni kazi ngumu sana lakini waweza kuzuiliwa kwa urahisi sana kwa kutumia njia zilizo rahisi sana za kiafya.

Ugonjwa mwingine unaowasumbua sana watu waishio katika mbuga hizi ni homa ya mbu. Mbu nao huzaliana kwa wingi sana kwa sababu ya unyevunyevu mwingi unaopatikana katika mbuga hizi — hasa katika mashamba ya mpunga ambayo yana maji ya kumwagilia mashamba yakaayo kwa

4

muda mrefu hata kuwawezesha mbu kuzaliana kwa muda mrefu sana. Penye maji yaliyosimama ndipo mbu huzaliana haraka sana na kwa urahisi mno. Kama nilivyosema hapo juu, mbuga za Usangu zina matopematope mengi na madimbwimadimbwi mengi yaliyokwama ambayo yanafaa sana kwa mbu kuzaliana.

Ugonjwa mwingine wa watu wa Usangu unaowasumbua sana ni ugonjwa wa kuhara. Ugonjwa huu watokana na kunywa maji machafu, na mbuga za Usangu nyingi zina maji yaliyo machafu na hayafai kunywa binadamu.

Lakini watu hawana njia nyingine ya kupatia maji yaliyo safi isipokuwa hiyo tu. Maji ya mto ambayo ni maji safi kidogo kuliko maji yaliyotuama yanapitia kwa mbali sana na ni watu wachache tu wanaonufaika na maji haya ambazo wanaishi karibu ya hiyo mito.

Kwa sasa hivi Wizara ya Afya inatoa mafunzo ya afya kwa akina mama walio karibu na kituo cha afya cha Rujewa na vijiji vingine. Pia kituo hicho kinatoa dawa za kukinga maradhi ya surua, kifaduro, ndui, polio na kifua kikuu. Tatizo kubwa kwa upande wa utumishi ni kwamba wafanyakazi ni wachache sana.

HISTORIA Wasangu ni watu ambao wametokana na jamii za Kihehe, Kisafwa, Kibena, Kinyakyusa na

kidogo jamii ya Kingoni. Jamii zote hizi, isipokuwa Wangoni, ni jirani za Wasangu, na kwa jumla Wasangu walikuwa ni watu ambao walijulikana sana katika nyanda za juu za Kusini katika karne ya 18 na karne ya 19. Mali kadhalika walikuwa ni jamii iliyokuwa na nguvu nyingi sana ya utawala na kivita. Hawa watu walikuwa wanaishi sehemu ya llamba iliyo karibu maili 60 Kaskazini ya Utengule kabla ya kuja Waarabu na Wajerumani, na kila mahali walipofanya maskani yao walipaita "Utengule", mahali paamani.

Waarabu walipokuwa wanaingia katika nchi ya Usangu waliingia kufanya biashara. Hawa Waarabu walikuwa wanauza nguo, magobole, baruti na shanga. Kutoka kwa Wasangu, Waarabu walipata meno ya tembo. Hapo awali mbuga zote za Usangu zilikuwa na wanyama wa kila aina na ndovu walienea kila mahali katika mbuga hizi za Usangu, kwa hiyo ilikuwa rahisi sana kwa Wasangu kuwaua tembo na kupata meno yao ill wayauze kwa Waarabu.

Biashara nyingine kubwa ambayo ilikuwa inafanywa na Waarabu katika mbuga hizi za Usangu ilikuwa biashara ya utumwa. Wasangu walikuwa ni watu ambao walijua namna ya kupigana vita sawasawa na kwa kuwa walikuwa na chifu wao mmoja tu ilikuwa rahisi kwao kuungana pamoja na kufanya jeshi moja kali na lenye nguvu sana kuliko jamii zingine walizopakana nazo ambazo zilikuwa hazina utawala mmoja kama vile Wanyakyusa, Wasafwa na kadhalika. Lakini Wahehe na Wakimbu walikuwa na utawala mmoja sawa kama Wasangu walivyokuwa.

Kwa kuwa utawala wa Wasangu ulikuwa na nguvu na umoja mkubwa, waliweza kupigana vita kwa nguvu moja na jamii zingine zilizokuwa jirani nao. Chifu Merere, ambaye ndiye aliyekuwa mtawala wa Wasangu, alikuwa mtawala shupavu na mpenda raia wake. Kwa kuwa alikuwa anapata silaha bora toka kwa Waarabu alipowauzia meno ya tembo, aliweza kuwashinda maadui zake bila taabu kubwa na mateka waliuzwa kwa Waarabu wafanya biashara ya utumwa. Hasa Merere aliwauza utumwani watoto wa Kisafwa na Kihehe ambao aliwateka wakati wa vita. Uwezo wake Merere katika kupigana na jirani zake ulisaidiwa sana na ushauri aliokuwa anaupata toka kwa wazee wa Kisangu na pia toka Mbaluchi ambaye alikwenda Usangu na kuwa Mshauri Mkuu wa Vita wa Chifu Merere I ambaye yaaminiwaaliingia nchi ya Usangu kati yamwaka1878 na mwaka1880. Mbaluchi (Mburushi) huyu aliitwa Jemadariambaye kufika kwake Utengule/Usangu kulisababisha Wabaluchi (Maburushi) wengine kuja Usangu na kuanza shughuli za kilimocha mpunga (angaliachini ya kilimo hapachini). Wasangu wenyewe wanasimulia kuwa Waarabu walianza kuingia nchi ya Usangu wakati wa utawala wa Chifu Njali aliyewazaa akina Merere.

5

siri na kupita huko. Si njia ya kutoka pwani tu iliyohatarishwa na Wasangu ball hata njia ya kuelekea nchi ya Wabemba kuelekea Zambia ilitiwa msukosuko.

Mara kwa mara Wasangu waliuteka utawala wa Kiwele uliokuwa sehemu ya kati ya Ukimbu ambao ulikuwa njiani Kusini ya Tabora. Mara baada ya Chifu Kilanga kutawala katika nchi ya Ubungu, Wasangu walimshambulia katika mwaka wa 1856 — 1857 wakimsaidia ndugu yake Kaf-wimbi, na ingawa Wasangu walishindwa, Kafwimbi alitorokea nchi ya Usangu tena.

Kati ya mwaka 1859 wakati Bwana Burton alipoondoka Afrika ya Mashariki na mwaka 1866 Tippu Tip alipotembelea reli ya Usangu chifu Muigumba akafariki wakati akipigana na Wahehe. Binini, ndugu ya Mihwela alikuwa amejifunza sana maarifa ya kupigana vita, na kwa kuwa alikuwa na ari kubwa ya kutaka kutawala Uhehe nzima. Wakati fulani karibu ya miaka ya 1860 alifanya vita na Wasangu na alifanikiwa kuviteka vijiji vingi sana na kuwateka wanawake na mifugo yao. Binini mwenyewe alimwua kiongozi wao Muigumba na akachukua jina lake na kujiita yeye mwenyewe Munyigumba kama ukumbusho wa ushindi wa kuwatawala Wahehe wote. Huyu Binini (Munyigumba) ndiye aliyekuwa baba wa chifu Mkwawa na ndiye chifu mkuu wa kwanza wa Wahehe wote.

Baada ya kifo cha Muigumba vita vikali sana vya urithi wa utawala vikatokea na mjukuu wake Muigumba kwa jina Merere Towelamahamba akatokea kuwa mshindi na akawaua jamaa zake wengi sana ambao alishindana nao katika kurithi utawala. Ugomvi wa urithi wa utawala uliwadhoofisha sana Wasangu katika kupigana vita na majirani zao.

Kati ya mwaka wa 1866 na mwaka wa 1872 Wasangu wakatokea jamii yenye nguvu sana chini ya chifu Merere wa kwanza kuliko hapo awali, na wakawashambulia majirani zao na kuziteka nchi zao zote hasa upande wa Mashariki Kusini na upande wa katikati wa nchi ya Wakimbu. Wak&ti huu Wasangu walikuwa wamefikia kilele cha nguvu zao na hakuna jamii nyingine yoyote iliyoweza kuikabili jamii ya Kisangu katika pande hizo za Tanzania.

Katika mwaka wa 1867 Bwana Livingstone aliambiwa na Waarabu katika nchi ya Ubungu kwamba Wasangu walikuwa ni wapole kwa wageni wowote, na kwamba Merere mara nyingi alifanya mashambulizi kwa machifu wa jirani ili ateke mifugo na watumwa na kuwauza kwa wafanya biashara wa Kiarabu. Katika mwezi wa Agosti Bwana Livingstone alisikia habari nyingi zaidi za kupendeza kuhusu chifu Merere na alichelea kuwa huenda akaharibiwa na Waarabu. Walakini katika mwaka wa 1871 habari zikafika Mayema kwamba Merere kisha kosana na Waarabu akiwatuhumu kwamba walikuwa wanafanya njama ya kumshambulia ili Goambari, mmojawapo wa Wajukuu wa Muigumba aweze kutawala. Kwa ajili ya sababu hii Merere akawashambulia Waarabu na marafiki zao wote. Akamwua Mwarabu mmoja naakawanyang'anya Waarabu wenginemali yote waliyokuwa nayo.

Wakati huu Amrani Masudi akajitokeza kwenye uwanja wa vita. Amrani alikuwa ni Mwaarabu toka Zanzibar wakati Zanzibar ilipotawaliwa na Waarabu. Tanzania Bara ilikuwa inatawaliwa na machifu mbalimbali wa jamii mbali mbali na Waarabu waliokuwa wakiishi Tanzania Bara walikuwa wafanya biashara tu sio watawala. Kwa jinsi hii Amrani hakupendelea utaratibu huu, kwa hiyo akaamua kuwafanyia vita machifu wote wa Tanzania Bara na kuwafanya watu wote wawe chini yake ili baadaye waweze kumleteamenoyatembo bilaya kuyalipiachochote.

Wakati Amrani Masudi alipofika Tabora akaambiwa kuwa kuna machifu wawili wenye nguvu sana ambao walihatarisha misafara yote ya biashara ya Waarabu na kuwatoza kodi kubwa kabla ya kuwaruhusu kupita katika nchi zao. Machifu wenyewe ni Nyungu-ya-Mawe wa Kiwele katika nchi ya Ukimbu na Merere wa Usangu. Lakini chifu wa hatari kabisa na mwenye nguvu zaidi kuliko mwen-zake alikuwa Merere. Baada ya kupata habari hizo, Amrani akalichukuwa jeshi lake na akaomba kuongezewa askari toka kwa machifu waliomwogopa kupigana naye ili aende na jeshi kubwa la kuweza kumshambulia Merere vilivyo. Alipoondoka Tabora, alipita Ngulu, Unyangwila, Itumba, Kipembawe na Igunda mpaka akafika Usangu. Maluteni wake walipita Ukonongo, Isamba, Wikangulu, Ubungu na Uguruke. Wengine walipitia Ugogo. Kila chifu wa sehemu za Magharibi na kati na Kusini ya Tanzania alitoa kwa Amrani askari wa kumsaidia katika vita kati yake na Wasangu. Lakini Nyungu-ya-Mawe hakutoa hata askari mmoja wa kumpa Bwana Amrani.

7

^

MISAFARA YA KWANZA YA KIARABU 1850 - 1929

Njia ya kwanza ya biashara ya Waarabu kutoka Pwani hadi Unyamwezi ilipita Ukimbu karibu na mpaka wa Wasangu, na mpaka katikati ya miaka 1830 Waarabu wafanya biashara walifika katika utawala wa Isenge na Isange upande wa Mashariki wa nchi ya Ukimbu. Huko waliweza kukutana na Wanyamwezi ambao walibadilishana nao bidhaa — hasa Waarabu wakabadilishana nao bunduki na bidhaa na meno ya tembo. Baada ya mwaka 1835 waliendelea na safari yao hadi Unyamwezi yenyewe. Mahali paitwapo Isenga na Isange ndipo njia ya kuelekea Pwani ilipogawanyika: njia ya Kaskazini iliyokwenda Mbwamaji na njiaya Kusini ikipita Usangu kwenda Kilwa.

Wakati huo kulikuwapo Chifu mmoja maarufu sana aliyeitwa Munyugumba aliyewashinda majirani zake wote waliokuwa wakiishi katika bonde la Ruaha na akaifanya jamii ya Kisangu kama jamii ya kivitaambayo iliogopwa sana na majirani na misafara ya biashara hali kadhalika.

Ari ya kivita ya Wasangu ilisababishwa na silaha zenye nguvu zaidi walizopata toka kwa Waarabu na pia mshawasha walioupata katika vita vya kijamii ambamo waliwateka watu wengi na kuwauza utumwani. Angalia maelezo zaidi hapo juu. Utawala wa Wakimbu wa Isange na Isenga ambapo palikuwa kituo cha mwisho cha njia ya biashara ya Waarabu ulikuwa sasa katika hatari kubwa ya kuvamiwa na Wasangu na Waarabu wakalazimika kutafuta njia nyingine ya kufanyia biashara yao ambayo baadaye ikasababisha kuanzisha kituo cha Tabora na mji wa Tabora ukaan-zishwa wakati huo kama kituo kipya cha kufanyia biashara yao.

KUJA KWA WANGONI Baada ya Wangoni kuondoka Ufipa, kundi moja likaenda upande wa Kusini hadi Songea ambako

walifanya maskani yao katika miaka 1850, Wakiwa katika safari yao kuelekea Kusini wakapitia nchi ya Usangu na kuwashambulia vikali sana Wasangu na Wasangu wakakimbilia Usavila Magharibi ya Uhehe. Wasangu wakiwa Usavila wakayaunganisha majeshi yao pamoja na majeshi ya Wasavila ili waweze kumpiga vita Chifu wa Wahehe aliyeitwa Mihwela aliyeishi sehemu za Udongwe. Kwa bahati nzuri chifu Mihwela akasikia habari hizi na akafanya mpango wa kuhamisha ng'ombe wote na kuwaweka mahali pa salama ili wasije wakatekwa na Wasangu. Wasangu wakafanya kambi yao Ipagala sehemu iliyo kati ya Tosamaganga na Kalenga. Walakini asubuhi na mapema chifu Mihwela, ambaye alikuwa chifu wa kwanza wa Wahehe aliwakomoa sana hawa Wasangu kwa kuwatandika barabara.

Wangoni walipoondoka nchi ya Usangu basi nao Wasangu wakarudi nchini mwao na chifu Muyugumba akajenga ngome mpya upande wa Mashariki wa llamba mahali ambapo Mto Ruaha waingia penye bwawa. Sasa Wasangu wakaanza kulijenga jeshi lao upya kwa kufuata utaratibu wa majeshi ya Wangoni kwa' kutumia mikuki mikubwa na ngao kubwa za ngozi za wanyama. Wasangu walijifunza maarifa mengi ya kupigana vita na maarifa hayo yakawafanya Wasangu waweze kuwa watu wenye jeshi la nguvu sana kupita majeshi yote katika nyandaza juu za Kusini.

WASANGU WAPIGANA NA AMRANI MASUDI NA KILANGA WA KWANZA 1855—1875

Wasangu walikuwa wamenyamazishwa kidogo na Wangoni katika kuishambulia misafara iliyopitia katika nchi walizozitawala. Walakini Wangoni walipocndoka tu toka nchi ya Usangu basi Wasangu wakavifufua vita upya na katika mwaka wa 1855 waliweza kuwaua wafanya biashara wa Kiarabu kutoka Mbwamaji. Wakati Bwana Burton alipoweza kutembelea pande hizi za Tanzania katika mwaka wa 1857 Waarabu hawakuthubutu kupitia karibu na nchi ya Usangu wakichukuwa bidhaa zao za kibiashara toka pwani ingawa misafara michache michache iliweza kujipenyeza kwa

6

Habari za kuja kwa jeshi la Amrani zikamfikia chifu Merere, kwa hiyo Merere akawaambia watu waliokuwa mipakani mwake kuwa wasiwashambulie maadui hao mara tu wawaonapo, ball wao waende Makao Makuu llamba (Utengule Usangu) alipokuwa anaishi chifu. Ujanja huu ulikuwa wa kumlazimisha Amrani Masudi aondoke sehemu za milimani na zenye misitu ill ateremke katika Mbuga za Usangu ambazo zilikuwa hazina misitu. Baada ya kuambiwa hivyo, watu wa Merere walipowaona maadui wanakuja wakakimbilia Utenguie Makao Makuu ya Wasangu. Amrani Masudi aliingia ndani ya nyumba za Wasangu na kuchukuwa chakula na mifugo ya kuwalisha askari wake. Wakazidi kuwafuata Wasangu ambao kwa sasa walikuwa wanakimbilia Utengule mpaka jeshi lake Amrani likafika Utengule Makao Makuu ya Merere. Wakati majeshi ya Amrani yalipokaribia Utengule, Merere akawaamuru watu wake waanze kuwashambulia watu wa Amrani.

Yasemekana kuwa vita ilipiganwa toka asubuhi hadi jioni. Kesho yake vita ikaanza asubuhi mpaka jioni tena. Siku ya tatu ya vita, Amrani akauawa na Wasangu na vita ikasimama kwa mara ya kwanza tangu ianze. Chifu Kilanga ambaye alikuwa anaongozaria na Amrani akimsaidia, akaamua kuendelea kupigana na Wasangu, ambapo machifu wengine wakaamua kukimbia kwa sababu kiongozi wao wa vita Amrani alikuwa ameuawa. Walakini Kilanga peke yake asingeweza kumshinda Merere kwa hiyo akauawa hapo hapo vitani. Baada ya hapo maadui walipoona mambo yamewaelemea vibaya wakaanza kukimbia na huku Wasangu wakiwafukuza nyuma na kumwua mtu yeyote wanayemkamata.

Amrani alitaka kupigana kwanza na Merere kwa sababu Merere alikuwa ni chifu mwenye nguvu zaidi kuwashinda machifu wote. Kama angalimshinda Merere^basi Amrani angalikwenda kupigana na chifu Nyungu-ya-Mawe ambaye alikuwa anatawala Ukimbu wakati huo. Tangu wakati huo, wakati Amrani Masudi alipopata cha mtema kuni na kunyolewa kikavu na chifu Merere, hakuna Mwaarabu yeyote aliyejaribu kuitawala Tanzania Bara na kuanzisha serikali yao wenyewe. Vita hii kubwa yawezekana ilipiganwa mwanzoni mwa mwezi Oktoba, 1873.

KINDUMBWENDUMBWE NA WAHEHE1875 Kushindwa kwa Amrani Masudi kulisaidia kuongeza na kueneza umaarufu wa chifu Merere

ingawa baadaye kidogo alikiona kindumbwendumbwe akichezeshwa na Wahehe. Kati ya mwaka 1860 na 1880 Wahehe nao walitokea kuwa watu wenye nguvu sawa na nguvu za Merere. Wakati wa miaka ya 1860 Munyigumba aliziteka tawala za Kihehe na aliweza kuanzisha utawala wake katika nchi ya Uhehe. Kufaulu kwake kulisababishwa na mambo mawili, wasifu mzuri na watu wengi walikuwa tayari kuukubali utawala wake kwa sababu aliweza mara nyingi sana kuyazuia mashambulizi ya Wasangu ya mara kwa mara na baadaye mashambulizi ya Wangoni. Pili alikuwa amejifunza maarifamengi ya kivitatoka kwa Wasangu ambao nao waliigatoka kwa Wangoni.

Wahehe waliiga sana utawala wa Wasangu na utaratibu wa majeshi yao. Wahehe walijifunza toka kwa Wasangu namna ya kuwatia ari wapiganaji vita kama ilivyotumiwa na Wasangu wakati wa vita na kwa kuwa Wahehe walikuwa wamejifunza Kisangu kwa hiyo wakajivunia sana lugha hii mpya ya Kisangu. Wasangu na Wahehe waliyagawanya majeshi yao katika makundi makundi ya askari ambayo yalikuwa na majina maalum. Mikuki mikubwa na matumizi ya ngao za ngozi za wanyama ziliigwa toka kwa Wangoni. Wasangu na Wahehe wanafanana sana katika desturi zao.

Mmoja wa mabinti wa chifu Munyigumba alikuwa ametolewa na wakampa Chifu Merere Towalahamba ill awe mkewe. Yasemekana kwamba chifu Merere alikuwa na zaidi ya wake 300, kwa sababu chifu aliyeshindwa na Merere vitani alilazimishwa kumtoa binti yake mmoja au zaidi na kumpa Merere. Na zaidi ya hayo, Merere mwenyewe alijigawia wanawake wengine aliowateka wakati wa vita na jirani zake. Wakati binti huyo wa Munyigumba ambaye alikuwa mke wa Merere alipopofushwa macho na ndui akamuudhi Munyigumba kwa kumrudishia binti yake akiwa katika hali ya upofu. Kwa hiyo naye Munyigumba akamrudishia tusi hili kwa kumshambulia Merere katika mwaka 1875. Merere alitwangwa vizuri sana na ikambidi akimbie kuokoa maisha yake. Kuanzia wakati huo Wahehe ndio wakawa jeshi lenye nguvu kushinda majeshi ya jirani zao na wakati Merere aliposhambuliwa akakimbilia Kiloli katika nchi ya Ukimbu pamoja na wafuasi wake ambako akawa mgeni wa Nyungu-ya-Mawe.

8

MERERE AKIWA IIKJMBU MWAKA 1875

Nyungu-ya-Mawe alikuwa rafiki mkubwa wa Merere na wakati Amrani alipofunga safari ya kwenda kumshambulia Merere, Nyungu-ya-Mawe alikataa kutoa msaada kwa Amrani kwa kujua yeye mwenyewe angalishambuliwa na Waarabu baadaye. Nyungu ya Mawe alikuwa ameziteka tawala za Ukimbu kati ya mwaka wa 1871 na mwaka wa 1881.

Merere na Wasangu hawakuwa wageni sana katika nchi ya Ukimbu. Babu yake Merere kwa jina Mui'gumbi alikuwa ametembelea tawala za Ukimbu kabla ya Merere kufika huko na alikuwa amek-wisha pigana na Kilanga katika nchi yaWabungu. Kabla ya Nyungu-ya-Mawe kuwa mtawala mwenye nguvu Wasangu walikuwa wameshinda machifu wote wa Ukimbu ya kati na kusini na mashariki mwa nchi na machifu wa Kikimbu wa Kipembawe, Igunda, na Hume (Chunya) walikuwa wanatawala nchi hizo kwa ruhusa ya Wasangu. Katika nchi ya Kiwele machifu llaasi na Kupumpa walikuwa marafiki wakubwa wa Merere na kwa msaada wake Merere hawa machifu waliweza kuwatia wasiwasi machifu wa Wakimbu kwa upande wa kaskazini.

Kati ya mwaka wa 1871 na mwaka wa 1875, Nyungu-ya-Mawe aliupanua utawala katika tawaia za Wakimbu. Alivanya mpango wa kuishambulia Kiwele lakini kabla ya kufanya hivyo akanuia kuwaomba Wasangu ambao kwa wakati huo walikuwa wanapigana na Wahehe na kusema kweli walikuwa tayari kuupokea msaada wake Nyungu-ya-Mawe, tena mmojawapo wa mabinti wa Nyungu-ya-Mawe alikuwa ametolewa na kumpa Merere awe mke wake.

Merere alipopigwa na Wahehe katika mwaka wa 1875, aliweza kutoroka na wapiganaji wake wachache. Baada ya kukaa kwa muda mfupi katika nchi ya Ubungu ambako watu wa Ubungu walikuwa wanamchukia, Merere akaenda kujificha chini ya ulinzi wa Nyungu-ya-Mawe Kiwele. Huko alikaa kwa muda wa mwaka mmoja na akaweza kuanzisha jeshi jingine jipya kabla ya kurudi kwake Usangu. Wakati alipokuwa akiishi Ukimbu, aliweza kumsaidia Nyungu-ya-Mawe katika kuishinda nchi nzima ya Wakimbu. Kijiji alichokijenga Merere sehemu ya Kiwele bado kinaitwa Kiloli mpaka sasa likiwa na maana ya "WALOLI". Katika mwaka wa 1877 Merere alirudi nchini kwake naakajenga ngome nyingine mpya chini ya Milima ya Mporoto pahala paitwapo MFUMBI.

MERERE AKIWA MFUMBI Wakati Merere aliporejeshewa mamlaka yake, Wavumbuzi wa Kiingereza Elton na Cotteril!

walifika Mfumbi mwezi wa Oktoba 1877. Na kuweza kuishi kwa muda wa wiki mbili katika ngome yake hiyo. Mara tu baada ya kuondoka Mfumbi. Elton naCotterill wakasikia ya kuwa Wangoni walik-wishapatana na Wasangu kuwaponda Wahehe na kuiteka mifugo yao iliyokwishaibiwa na Wahehe hapo awalj kitendo ambacho kiliwaudhi sana Wahehe na kuwafanya wawashambulie Wangoni. Wahehe walifanikiwa katika kuwaponda Wangoni kwa sababu chifu wa Wangoni alikuwa hajawa tayari kwa vita. Wangoni nao wakaazimu kulipiza kisasi na kuwashambulia Wahehe na kumlazimisha chifu Munyigumba kwenda kujificha katika mapango yaliyokuwa upande wa kaskazini wa Uhehe ambako alikufa baada ya kuugua.

Kwa wakati huu utawala wa Wahehe ulikuwa umebadilika sana; badala ya nchi nzima kutawaliwa na machifu wengi sana Uhehe nzima ilikuwa inatawaliwa na chifu mmoja tu ambaye kwa sasa watu wake walikuwa wamejifunza sana mambo ya vita na kuwashinda majirani zao vibaya sana Kama vile watu wa Utemikwila, Wangoni na Wahehe. Chifu mpya wa Uhehe akafanya mapatano na Wangoni katika mwaka 1881 Hi wasishambuliane mpaka watoto wakue na kwa jinsi hii Wahehe na Wangoni wakawa watani wao, uhusiano ambao mpaka sasa upo kati ya jamii hizi mbili. Lakini watu waiiokuwa wamebakia kuwa wa hatari sana kwa Wahehe ni Wasangu.

Baada ya kufa chifu Munyigumba mwaka 1878 watoto wakashindania urithi, na baadaye Mkwawa akatokea kuwa chifu mwenye nguvu kubwa katika mwaka wa 1883 na vita ya mara kwa mara ilitokea kati ya Merere na Mkwawa na Mkwawa mara nyingi aliweza kumshinda Merere.

9

MERERE ATAWALA NCHI YA WASAFWA TOKA 1883 - 1898

Mara nyingi sana Mkwawa aliweza kumshambulia Merere na mwishowe Merere akalazimika kukimbilia nchi ya Wasafwa. Mkwawa akatawala nchi ya Usangu na Merere alishindwa kumwondoa kutoka katika nchi yake. Baada ya Merere kufanya misafara yake ya vita katika nchi ya Ukukwe, Umalila, Uhehe na Usafwa mwishowe akajenga ngome yake mpya sehemu ya Mpedjere chini ya mlima Mbeya na kuiita Utengule mpya. Merere alishindwa kabisa na Mkwawa na ingawa Merere aliweza kumpa chifu Mkwawa binti zake wawili lakini hawakufanya amani hata siku moja. Akiwa katika nchi ya Usafwa Merere aliendelea na vitendo vyake vya kuwashambulia majirani zake pande zote Kusini, Mashariki Kaskazini na Magharibi huku akiwatia katika utawala wake mkali, kama vile Wanyakyusa wa Kaskazini, Wanyiha na Wasafwa, na mara nyingi alikuwa na wazo akilini mwake la kumwondoa chifu Mkwawa kutoka katika nchi yake ya Usangu.

WAJERUMANI WAJA MWAKA WA 1892

Katika mwezi wa Januari mwaka wa 1892, Wamishonari wa kwanza walifika Utengule, nao ni Merensky na Nauhaus wa misheni ya Berlin. Baada ya mwaka mmoja kupita Wamishonari wengine wa Moravian walifika Utengule, hao ni Meyer na Richard na Kootz. Katika mwaka huo huo alifika MejaVon Wissman na DK. Bumiller nakamanda wakampuni Meja Von Prince.

Wajerumani walikuwa wamepata habari za kuhusu vita vya Merere vya kuwashambulia Wahehe mara kwa mara. Ingawa Merere alisababisha matata mengi kwa jamii za jirani lakini chifu Mkwawa alid.haniwa na Wajerumani ni mtu wa hatari kubwa kwa utawala wao, nao kwa jinsi hii, Wajerumani walikuwa tayari kumsaidia Merere katika kila hali. Wajerumani walikuwa na matumaini kupata msaada wa Wasangu katika kumtia adabu chifu Mkwawa, naye Merere alitumaini kuwatumia Wajerumani ili aweze kumfukuza adui yake mkubwa kutoka katika nchi yake. Katika mwaka huo huo wa 1893 Merere wa kwanza akafariki nakurithiwa na mtoto wake Merere wa pili Mgandilwa.

Von Wissman akaanzisha uhusiano mzuri na chifu Merere wa pili ambaye alikuwa bado mmoja wapo wa machifu wenye nguvu sana pande hizo za Tanzania kabla ya kumshambulia chifu Mkwawa. Von Wissman akaona afadhali aende ziwa Rukwa na kumwadhibu Bwana KIMALAUNGA ambaye alikuwa ni mnyanganyi na ambaye alijiimarisha mwenyewe kama mtawala wa bonde la Ziwa Rukwa. Von Wissman akamtuma msaidizi wake DK. Bumiller kwa Merere ili akamwombe msaada wa askari 100 wa Kisangu. Kusikia haya, Merere akafurahi sana na kuona ndiyo nafasi yake naye ya kujiimarisha katika utawala wake. Kwa hiyo Merere akamshauri DK. Bumiller awashambulie Wanyiha chini ya chifu NZUNDA. Wakamshambulia chifu Nzunda na kumshinda lakini gharama ya kumshinda ilikuwa kubwa mno na ikawalazimu waahirishe safari yao ya kwenda kumtwanga Kimalaunga. Vita waliyomfanyia Nzunda ilimtingisha sana chifu Merere kwa sababu ya kuwapoteza askari wengi waliokufa wakati huo, lakini hata hivyo chifu Merere aliwahitaji sana Wajerumani ili waweze kuwashambulia Wahehe.

Mwishowe matumaini ya Merere yakadhihirika wakati Wajerumani walipoanza kufanya mipango ya kumshambulia chifu Mkwawa. Von Schele akawa ndio kamanda wa msafara wa vita hii na Dk. Bumiller akawa mkuu wa sehemu nyingine ya jeshi. Wakati wa kiangazi cha mwaka wa 1894 Von Schele akaanza mashambulizi yake juu ya chifu Mkwawa na akaiharibu kabisa ngome ya Mkwawa ya Kalenga: kuharibiwa kwa ngome ya Kalenga kulimaanisha kuwa mwisho wa nguvu za utawala umefika ingawa chifu Mkwawa aliendelea kuitawala nchi ya Uhehe kwa muda wa miaka mingine minne baadaye na ilikuwa mwaka wa 1898 Mkwawa alipojiua yeye mwenyewe wakati Wajeruman walipokuwa wakimtafuta.

Kifo cha Mkwawa kilimaanisha mwisho wa vipingamizi vya Wahehe kwaserikali ya Wajeruman na hii ikasababisha Wahehe kuondoka katika nchi ya Usangu ambayo ikarudishwa kwa chifu Merere ambaye akafanya maskani yake au makao yake Makuu Utengule (Usangu). Utawala wa Usafwa na Makao yake Makuu Utengule (Usongwe) ukarudishwa kwa Wasafwa chini ya chifu wao Mwalyego.

10

Wakati wa vita vya Uhuru vya Maji maji Wajerumani walitiwa wasiwasi mkubwa na chifu Merere kwa sababu yeye ndiye aliyekuwa chifu mwenye nguvu zaidi katika Wilaya ya Iringa ambaye alikuwa amejijengea ngome ya makao yake Makuu. Mara mbili chifu Merere alilazimishwa na Wajerumani kutoa askari. "Hi waende kuwasaidia Wajerumani katika shughuli zao za Vita na jamii zingine za Tanzania. Hata baada ya kufariki Merere wa nne katika mwaka wa 1906 kutokana na sumu wasiwasi wa Wajerumani ulizidi kuongezeka hata Katibu Mkuu wa Serikali ya Kijerumani alisema", ili kuhakikisha utii wa Wasangu ni lazima ngome ya askari ianzishwe ama sivyo utii wa Wasangu hautajulikana sawasawa". Ingawa ngome ya askari ilianzishwa lakini hata hivyo mambo yakazidi kuwa mabaya zaidi mpaka mwisho wa mwaka wa 1909 ambapo Wasangu wakafikiriwa kuwa ni wa hatari sana kwa utawala wa Wajerumani. Merere wa tano alikuwa ni mtu mvivu, na ambaye hakuwa mwangalifu na kawatawala watu wake katika njia mbaya sana. Alichukiwa sana na Wajerumani kuliko mtu yeyote katika nchi nzima na Wajerumani wakamwondoa kutoka katika nchi yake na kumpeleka katika kisiwa cha Mafia mwezi wa Oktoba 1910 kwa sababu ya utawala wake mbaya, na badala yake ndugu yake Mtengela akatawala.

KILIMO KATIKA BONDE LA USANGU

Katika kueleza kilimo kinachoendeshwa katika bonde la Usangu nitajaribu kueleza hictoria ya kilimo cha mpunga ambacho ndicho kilimo kikubwa kushinda vilimo vyote vinavyoendeshwa katika bonde hili na halafu nitajaribu kuelezea jinsi kinavyoendeshwa kwa sasa hivi na hapo baadaye nitaelezea kilimo cha jadi cha Wasangu wenyewe ambao ndio wenyeji wa Mbuga za Usangu.

HISTORIA YA KILIMO CHA MPUNGA Yaaminiwa kuwa mpunga ulipandwa katika bonde la Usangu kwa mara ya kwanza na mfanya

biashara ya utumwa Mwaarabu kwa jina TIPP TIP ambaye katika mwaka wa 1968 aliwaacha watu katika bonde la Usangu ili wapande mpunga; na kilimo hiki cha mpunga kikaweza kuendelezwa zaidi na jamii ya Wabaluchi (Maburushi)ambapo Mbaluchi wa kwanza kufika Utengule/Usangu alikuwa bwana Jemadari ambaye alifika Utengule kuwa mshauri Mkuu wa vita wa chifu Merere wa kwanza. Baada ya miaka kumi baadaye, kuja kwake Mbaluchi (Mburushi) huyu katika nchi ya Wasangu kuliwavutia Wabaluchi (Maburushi) wengine kuja kukaa katika Usangu, na mwisho wa karne ya19 familia za Kibaluchi zikaingia katika bonde la Usangu na kuanza kulima kilimo cha mpunga.

Mbaluchi (Mburushi) aliyeacha historia nzuri ya kilimo cha mpunga cha kumwagilia maji alikuwa Bwana MOOLAR ABDALLAHIM PREMOHAMED, ambaye mpaka sasa kizazi chake yaani wajukuu zake, bado wanaishi Rujewa wakishughulikia kilimo cha kumwagilia maji.

Bwana Moolar Abdballahim Premohamed alifika nchini Tanzania mwaka wa 1920, na baadaye akaamua kwenda kukaa Usangu katika bonde la Usangu na kuanza kulima kilimo cha mpunga katika mwaka wa 1928. Katika mwaka wa 1940 akaomba ruhusa kutoka kwa serikali ya kikoloni ya Kiingereza ili aweze kuchimba mfereji wa maji kwa ajili ya kilimo cha kiangazi cha mpunga. Bwana Moolar alipewa masharti na Serikali ya Kiingereza kwamba kwa kuwa kaomba kuchimba mfereji wa maji ni lazima aumalize mfereji huo katika muda wa miezi kumi na mbili tu, si zaidi ya hapo. Baada ya kupata ruhusa akaanza kuuchimba mfereji huo na kuumaliza katika mwaka wa 1941 na alitumia miezi kumi na moja tu katika kuumaliza mfereji wenyewe. Zana alizozitumia katika kuuchimba mfereji huo ni sululu, majembe, nyundo na maji ambayo yalitumiwa kumwagia miamba ya mawe ili iweze kupasuka kwa urahisi huku wakiipasha moto tena. Mfereji huo ambao mpaka sasa unatumika una urefu wa maili saba.

Serikali ya Kiingereza ilitoa sheria kuwa si ruhusa kwa mtu ambaye si Mzungu kulima eka zaidi ya kumi. Kwa hiyo, bwana Moolar aliruhusiwa kulima eka 10 tu kwa sababu hakuwa Mzungu. Lakini Mbaluchi (Mburushi) huyo aliweza kupata eka 40 badala ya eka 10 kwa kutumia majina ya shemeji na watoto wake; na aina za mpunga zilizopandwa wakati huo ni Kahogo na faya. Na katika mwaka wa 1945 bwana Moolar aliruhusiwa na serikali ya Kiingereza kupata shamba lake mwenyewe baada ya kuona juhudi zake kubwa katika kuuchimba huo mfereji wa maji ambao bado unatumika wakati huu.

11

Tabia ya Wabaluchi (Maburushi) ni kwamba huweka chakula cha akiba cha kutosha miaka miwili inayokuja ill kuepukana na maafa ya vita, njaa, nzige na majira mabaya ya hali ya hewa. Wenyeji wa Usangu wameiga mambo mengi — hasa ufundi na ujuzi mwingi sana wa kuchimba mifereji ya maji ya kumwagilia mashamba yao ya mpunga. Hali kadhalika utaalam wa kutumia trakta na jembe ulaya la kukokotwa na ng'ombe umeigwa na wenyeji fulani fulani wanaolima kilimo cha kisasa waishio Usangu.

Hapo awali hawa Wabaluchi (Maburushi) walikuwa wanakodisha plau za Wabena ambazo ndizo zilizolima mashamba yao ya mpunga. Wabena walikuwa na maplau na ng'ombe wa kuyakokota maplau, halafu waliwalimia mashamba yao hawa Wabaluchi (Maburushi) kwa kulipwa fedha. Baadaye, katika mwaka wa 1958 Wabaluchi (Maburushi) wa Rujewa walinunua trakta lao la kulimia na mpaka wakati wa kuandika habari hizi, Februari, 1975. Wabaluchi (Maburushi) wana matrakta matano ya kulimia ambayo pia yanatumiwa kulimia mashamba ya wenyeji kwa kuyakodi.

Hawa Wabaluchi (Maburushi) walitoka nchi iliyo kati ya Pakistan na Iran iitwayo Baluchistani ambayo sehemu moja iko Iran na sehemu nyingine iko Pakistan. Huko walikotoka hawa Wabaluchi (Maburushi) hulima mashamba yao kwa kutumia maplau ya miti yaliyochongwa vizuri na kutiwa chuma nchani na kukokotwa na ng'ombe. Na mazao yao yalimwayo huko walikotoka ni choroko, mtama, mpunga na ngano mazao ambayo yanapandwa kwa kufuatana na hali ya nchi. Chakula chao' kikuu huko walikotoka ni wali, zao ambalo ni zao kuu la watu hawa. Hata huko Usangu kwenyewe Wabaluchi hawa hupanda sana mpunga na ndilo zao na chakula chao kikuu. Shughuli yao kuu ni kilimo cha mpunga ingawa mazao mengine pia yanapandwa na watu hawa. Pia wanafuga ng'ombe, mbuzi na kondoo huko Rujewa na wanakunywa sana maziwa ya ng'ombe. Dini yao kubwani Uislamu na wanatumia dakika 75 kila siku za kusali na saa za shambani ni saba kwa siku. Halafu wakati unaobakia unatumiwa katika shughuli zingine kama vile kula chakula, kukamua maziwa, kuongea, kuuza duka na kuyatengeneza matrakta yao ili yawe katika hali timamu tayari kwa kazi ya kesho yake. Zana zingine za kilimo chao ni vyombo vya kupandia mbegu, matrakta, na maplau. Vifaa vinapoharibika vyatengenezwa na wao wenyewe kwani kila Mbaluchi ni makanika mwenyewe wa trakta lake hapeleki trakta lake kwa mtu mwingine yeyote kumtengenezea, bali hulitengeneza yeye mwenyewe kama limeharibika.

Kazi ya shambani ni ya wanaume tu na wanawake wa Kibaluchi (Kiburushi) hujishughulisha na kazi za kinyumbani tu.

NDOA ZA WABALUCHI (MABURUSHI)

Wabaluchi (Maburushi) huoana kwa kufuatana na ubinamu. Kama jamii nyingi za Kiarabu zinavyofanya. Makusudi ya kufuata ndoa za namna ni kudumisha ukoo wao, pili kuepukana na talaka nyingi ambazo si za lazima, tatu kupanua ukoo wao; na kadhalika. Wakati wa kuoa, fedha iliyopangwa na baba ya msichana yatolewa ikiwa kama mahari. Mali hiyo yatumiwa na msichana katika kununulia vitu vya kwenda navyo kwa bwana yake. Na iwapo kumetokea talaka, basi bwana hutoa kiasi fulani cha fedha na kumpa mkewe ambaye anatalikiwa naye ili ikamsaidie kule anakokwenda. Kama ni bibi anataka kumwacha bwana, basi naye bibi hufanya hivyo hivyo kumpa bwana yake fedha naye ikamsaidie kule anakokwenda. Walakini inatokea mara nyingi sana kwa bwana kumsamehe bibi asimpe mahari yoyote wakati bibi ataka kuachika na bwana yake. Jamii ya Wabaluchi (Maburushi) iliyoko Rujewa ni ya ukoo mmoja kwa sababu wamekuwa wakioana wao kwa wao kwa kufuata ubinamu na hawaoani nje ya utaratibu huu labda itokee kwa bahati mbaya.

12

KILIMO KINACHOENDESHWA SASA USANGU

Jamii zote za Usangu zimegawanyika katika shughuli za uzalishaji mali kama ifuatavyo hapa chini—

1. Wavuvi wa samaki Usangu na wafanya biashara ya samaki ni WAKINGA. 2. Wakulima ni WANYAKYUSA, WABENA, WABALUCHI (Maburushi) na WASUKUMA. 3. Wafugaji ni WASANGU, WAMASAI na WASUKUMA.

Ufuatao hapa chini ndio utaratibu wa shughuli za kilimo katika Wilaya ya Mbeya:-

MWEZI MAZAO MIPANGOYA KAZI

JUNI Kahawa Kuendelea kuvuna na kuchimba mashimo

JULAI Ulezi Mahindi Maharage

Kuvuna Kuvuna Kuvuna

JULAI /AGOSTI SEPTEMBA

— Kazi za maendeleo Kuuza mazao.

OKTOBA Ulezi Mahindi

Kutayarisha mashamba Kutayarisha mashamba

NOVEMBA Kahawa Kufukia mashimo, kutia dawa na kazi za maendeleo

SEHEMU YA MASHARIKI

NOVEMBA Mahindi Pamba Mpunga Karanga

Kulima na kupanda Kulima na kupanda

DESEMBA / JANUARI

FEBRUARI / MACHI Mahindi Pamba Mpunga Karanga

Kupalilia Kupalilia

MACHI / APRILI /MEI Vitunguu Viazi Vitamu Mihogo

Kulima na kupanda Kulima na kupanda Kulima na kupanda

JUNI / JULAI / AGOSTI Mpunga Mahindi Karanga Pamba

Kuvuna Kuvuna Kuvuna Kuvuna

SEPTEMBA / OKTOBA Vitunguu Mpunga Pamba Mahindi

Kuchimba mifereji na kupanda Kutayarisha mashamba Kutayarisha mashamba Kutayarisha mashamba

13

Kama nilivyoeleza hapo juu, kilimo cha mpunga kiliwachwa na Waarabu wafanya biashara ya utumwa na baadaye kilimo hiki kikaendelezwa zaidi na Wanyakyusa, Wabena, Wahehe, Wasangu na kufikia kima cha kilimo hiki killchopo sasa. Miche ya mpunga hupandikizwa na kupandwa wakati mvua zimeanza kunyesha na baadaye umwagiliaji maji watumika sana. Mbolea ya aina yoyote haitumiwi ili kurutubisha ardhi yake kwa sababu udongo wake una rutuba nyingi mno. Jembe la mkono ndilo zana kubwa sana ya kulimia ingawa jembe la kukokotwa na ng'ombe na trakta yanazidi kutumiwa sana siku hizi. Kulima kwa trakta au plau huanza mwezi wa Desemba na katika kutengeneza majaruba majembe ya mikono yatumiwa kati ya Januari na Machi. Kupandikiza miche kwafanyika mara tu baada ya kuyasawazisha na kuyatengeneza majaruba. Mpunga wavunwa na huondolewa kwenye masuke kati ya mwezi wa Juni na mwezi wa Agosti. Mavuno yote ya mpunga tukiacha shamba la Taifa yaweza kukadiriwa kuwa Tani 24,000 kwa wastani, ambayo asilimia 50 yanauzwa.

Mkulima hutumia familia yake katika kazi za shamba. Wakati wa shughuli nyingi za shamba, mkulima hupata msaada katika kazi za shambani kwa kuwaalika watu wengine na wakulima wengine wanaojiweza huwaajiri watu wengine na kuwalipa ujira wao. Umwagiliaji maji wa mashamba ya mpunga huwa wa lazima kwa sababu aina za mpunga zinazopandwa Usangu zinahitaji maji mengi mno. Milima ya Mporoto, Kipengere na Milima ya Chunya ndiyo inayotoa mito ambayo maji yake yanatumika sana katika kumwagilia mashamba ya mpunga kwa kuchlmba mifereji midogo midogo ambayo inapeleka maji kwenye kila shamba la mkulima wa mpunga.

SEHEMU ZINAZOPANDWA MPUNGA KATIKA BONDE LA USANGU

14

Hizi hapa chini ni takwimu za mpunga ulionunuliwa kutoka bonde la Usangu kufikia Desemba 31,1972.

MWAKA WA KUPANDA MPUNGA WAISHIA 31 MEI

TAN I ZILIZONUNULIWA

1964 — 1965 37,780

1965 — 1966 20,580

1966 — 1967 37,550

1967 — 1968 30,160

1968 — 1969 44,440

1969 — 1970 63,353

1970 — 1971 92,240

1971 —1972 69,445

*1972 — 1973 55,121

Toka: Bodi ya Taifa ya

Mazao. * : Mpaka

Desemba, 1972.

15

Takwimu hizi hapa chini zaonyesha ununuzi wa Mpunga na Bodi ya Mazao ya kilimo kwa kufuata Mkoa katika Tanzania Baratoka mwaka wa 1969 — 1973 katikaTani.

MKOA 1969 — 1970 1970 — 1971 1971 — 1972 1972 — 1973

Mbeya 20,238.6 19,553.9 22,264.8 17,539.2

Tabora 20,437.2 26,812.2 15,291.0 9,352.1

Mwanza 9,296.2 17,870.0 2,723.9 1 ,323.0

Morogoro 2,162.0 4,890.4 10,868.3 9,732.6

Mara 4,344.3 8,992.3 3,811.1 1 ,534.4

Shinyanga 1,975.2 5,820.3 2,820.2 5,732.4

Kilimanjaro 2,196.2 3,623.0 3,630.6 5,224.4

Pwani 235.9 175.8 4,978.9 3,969.0

Iringa 893.0 2,011.4 1,180.9 222.0

Kigoma 812.7 1,327.7 707.7 14.0

Tanga 187.5 903.3 368.8 351.2

Mtwara 447.4 233.0 515.0 —

Ruvuma 126.7 — 234.2 71.9

Arusha — 24.3 22.5 —

Dodoma — 2.0 15.9 —

Jumla 63,352.9 92,239.6 69,444.8 55,125.2

Toka: Bodi ya Mazao ya kilimo.

Takwimu hizo hapo juu zaonyesha kuwa Mikoa 15 tu ndio inayotoa mpunga kati ya Mikoa 18 ya Tanzania Bara na Mikoa yote imepangwa kiasi cha tani zilizouzwa katika miaka 4 iliyopita ya kupanda mpunga. Mkoa wa Mbeya umekuwa wa kwanza kwa kutoa mpunga mwingi uliokwisha uzwa ukifuatiwa na Mkoa wa Morogoro na Tabora.

Mvua zinapokuwa haba katika mwaka, basi mito yote hii inayopeleka maji katjka bonde la Usangu hupungua sana kima chake hata husababisha upungufu wa maji kwa ajili ya Wakulima na wafugaji wa mifugo. Hata hivyo maji huwa hayatoshi kabisa kwa mifugo wakati wa kiangazi kwa sababu wakulima ambao wana mashamba yao sehemu za upande wa juu wa bonde la Usangu, ambao wamezibaziba maji mengi kwa ajili ya kunyweshea mashamba yao. Kwa hiyo maji mengi yanaelekea katika sehemu hizi za mashamba na wafugaji ambao wana mifugo mikubwa sana ya wanyama wanashindwa kupata maji ya kutosha,kwa ajili ya mifugo; yao. Kuna haja ya kurekebisha tena utaratibu wa kugawanya maji ili wafugaji, ambao ndio wenyeji bonde-hili la Usangu pamoja na wakulima wengine, wasipate taabu

KILIMO KWA JUMLA

Wakulima huanza kulima mashamba ya mahindi mara mvua zinyeshapo katika miezi ya Novemba na Desemba. Katika mashamba haya, maharage na wakati mwingine karanga zapandwa pamoja na mahindi.katika shamba moja. Wakati huo huo viunga vya kutayarishia miche ya mpunga yaanzishwa katika majaruba au kati ya matuta mawili ya mihindi kwa kutegemea kiasi cha maji kinachopatikana wakati huo.

Kilimo cha mpunga chaanza mara tu baada ya ardhi ya shamba kulainika vizuri na pia baada ya kufanyika kazi ya kulima mashamba ya mahindi. Wakulima wengine hufanya matayarisho ya kilimo cha kwanza katika mwezi wa Agosti na Septemba wakati ardhi ikiwa bado laini. Jembe la Plau na wakati mwingine matrekta yaweza kutumiwa wakati wa kilimo hiki cha kwanza. Kilimo cha pili chafanyika pamoja na kusawazisha udongo katika mwezi wa Januari na Februari hadi katikati ya mwezi wa Machi na hii ni kazi ya jembe la mkono; kila jaruba lajazwa maji na majani sasa yamek-wisha kuwa marefu sana. Majani haya yalimwa na kulundikwa katika mafungu mafungu, na udongo chini ya mizizi yake watolewa na maji na kisha majani hayo yalundikwa katika matuta yakifanya majaruba. Kisha kusawazisha kwa-fanyika kwa kulima udongo pamoja na maji na hufanya matope ambayo huchanganywa vizuri sana mpaka usawa wa maji umefikiwa. Baada ya hapo miche ya mpunga yapandikizwa.

Wakati wa kupandikiza miche ambayo ni kazi inayofanywa na wanaume halikadhalika wanawake, vile vile kilimo cha viazi vitamu chafanyika wakati wa miezi hii hii pamoja na kuanzisha kwa mashamba ya maharage. Wakati wa kusawazisha majaruba kazi hii yaendelea hadi kupalilia majaruba yaliyotangulia kupandikizwa miche ya mpunga. Wakati wa miezi ya Aprili na Mei, kazi ya kuamia ndege yaanza na kazi ya kukata miti kwa ajili ya ulezi, na karibu na mwisho wa Juni hadi Agosti kazi ya kuvuna mpunga huwa imeshamiri barabara. Na kazi ya kupepeta mpunga vile vile yafanyika wakati wa miezi hii hii. Pia mahindi yanavunwa na kuwekwa katika vihenge. Wakati wa kiangazi shughuli za kilimo huwa zimepungua sana isipokuwa" kwa wale wakulima ambao wanayo maji ya akiba ndio huendelea na shughuli za kilimo. Wakati huu wa kiangazi vitunguu vyalimwa na mwezi wa Novemba, matawi makavu na majani yalfyokauka katika mashamba ya ulezi huchomwa moto.

KILIMO CHA MPUNGA

Kilimo cha mpunga kama nilivyoeleza hapo mwanzoni ni kikubwa zaidi kuliko kilimo chochote cha mazao katika bonde la Usangu, lakini kilimo chenyewe kina dosari zake. Kwa mfano, mashamba yote ya mpunga hayatiwi mbolea ambayo inapatikana kwa wingi sana katika bonde hili. Ingawa' udongo wa bonde la Usangu una rutuba sana, lakini upo uwezekano mkubwa wa rutuba kupungua baada ya kupanda mpunga kwa muda wa miaka minne au mitano mfululizo. Mpunga unapovunwa, wakati, mwingine mpunga wavunwa kabla mabua yake hayajakauka vizuri, kwa hiyo joto na unyevunyevu waweza kuharibu mpunga wenyewe.

Kuondoa punje za mpunga toka kwenye masuke hufanyiwa ardhini. Wakati mwingine fimbo zatumiwa ili kuondolea punje za mpunga toka kwenye masuke na kitendo hiki chaufanya mpunga utakaopepetwa kuchanganyikana na changarawe ndogo ambazo ni za hatari kwa meno na matumbo pia. Yafaa njia nyingine nzuri itumiwe. Mali kadhalika mpunga wachukuwa wakati mwingi sana wa mkulima kuliko yanavyomchukuwa mazao mengine katika kuyalima; na pia magonjwa yachukuwa muda mrefu wa mkulima. Kuna haja ya kufanya kampeni ya magonjwa yanayopatikana katika bonde hili ili yaweze kushambuliwa au kuzuiwa.

17

MATATIZO YA KILIMO CHA MPUNGA

Wakulima wengi sana wanatumia majembe ya mikono. Hili ni tatizo kwa sababu jembe la mkono lamchukuwa mkulima wa kawaida saa nyingi kumaliza eka moja na pia anatumia nguvu nyingi zaidi wakati wa kulima kuliko ambavyo angalitumia kama angalitumia plau au trekta. Kuna haja vile vile ya kubadili mila na desturi za Wasangu ambao kwa kweli wafuga ng'ombe kwa wingi sana kwa ajili ya ufahari tu bila ya kuwatumia ipasavyo. Na jamii zingine zilizo katika bonde la Usangu zatumia zaidi kilimo cha jadi badala ya kilimo cha kisasa. Vijiji vya ujamaa ndivyo ambavyo vimeendelea mbele kidogo katika kutumia njia za kisasa za kilimo. Lakini watu waishio katika vijiji vya ujamaa, wengi wao hawana matrekta wala plau.

Tatizo jingine linasababishwa na jua. Kipinrdi cha jua kali ni kirefu zaidi kuliko majira ya mvua. Kwa kawaida mvua zaanza mwezi Novemba hadi Desemba halafu kuna kipindi cha jua kali na ukame mwezi Januari hadi Februari. Halafu kuanzia mwezi wa Machi hadi Aprili mvua zanyesha. Baada ya hapo kipupwe na ukame wafuata ukiambatana na jua kali katika miezi ya Juni hadi Oktoba.

Wengi wa Wasangu na jamii zingine waajiriwa na Wabaluchi katika kulima mashamba ya watu hawa. Waacha kazi za mashambani mwao na kufanya kazi za kulipwa, kumbe katika kufanya hivyo kazi zao za mashamba yao zinalala na kazi katika mashamba ya Wabaluchi hazilali hata kidogo. Kwa hiyo, Waafrika wengi hubakia nyuma siku zote kwa kufanya kazi za kulipwa katika mashamba ya watu wengine. Si Wabaluchi tu wanaoajiri vibarua bali hata mtu yeyote yule anayejiweza huajiri vibarua wakumsaidia kazi shambani. Angalia hapo juu chini ya kilimo katika bonde la Usangu.

Tatizo jingine lililo kubwa sana katika bonde hili ni mgawanyo wa maji ya kunyweshea mashamba mbali mbali ya mpunga na mazao mengine. Kusema kweli watu wengi hawana maji bali hutegemea sana maji ya mvua. Mvua zisiponyesha, basi wakulima hawa hawawezi kulima na wakapata mazao mazuri. Pia wale wakulima wachache ambao wanategemea maji ya mito katika kunyweshea mashamba yao ya mpunga wana matatizo yao, yaani jinsi ya kuwa na utaratibu mzuri wa kugawana maji ya mito sawa sawa ili wakulima wengine wasipunjike. Mpaka wakati huu kuna kupunjana sana katika kuyatumia maji ya mito iliyomo katika bonde hili. Kadri nilivyoona na kuyaangalia mashamba ya mpunga niliona kuwa watu wengine walikuwa na maji ya kutosha katika mashamba yao yanayoletwa na mifereji ya kuchimbwa kutoka kwenye mito wakati watu wengine walikuwa hawana tone la maji ingawa nao walichimba mifereji ya kiasi chao. Wakati huo huo wafugaji wa mifugo walikuwa na shida kubwa ya kukosa maji kwa ajili ya mifugo yao. Maji ya mito yatakuja leta mzozo mkubwa kati ya wakulima iwapo utaratibu mzuri wa kuyagawanya maji kwa watu wote waishio katika bonde hili la Usangu hautapatikana. Maji ya mito katika bonde la Usangu yanathaminiwa sana na watu wote waishio huko kwa sababu ndio mtaji mkubwa sana kwa watu wote. Kwa jinsi hii, utaratibu mzuri wa kuyagawanya maji wafaa uanzishwe upesi.

Tatizo jingine la wakulima wa Usangu ni kwamba yasemekana wakulima wengine wa Kiafrika wanafanya magendo ya kuuza mazao yao kwa Wabaluchi bila ya kuyapeleka mazao kwenye chama. Lakini hili sina hakika nalo iwapo ni kweli kitendo hiki kinafanyika. Iwapo ni kweli jambo hili linafanyika basi kuna haja kubwa ya kulipiga vita kabisa kwa kutumia njia safi na maarifa mengi. Tatizo jingine ni kwamba wakulima wengi wanaweka fedha zao kwa Wabaluchi (Maburushi) badala ya kuziweka katika benki ya biashara. Tabia hii ni mbaya sana kwani inamletea matatizo mengi yule mtu anayeweka fedha zake kwa Mbaiuchi badala ya kuziweka fedha zake katika benki. Mtu huyo anayeweka fedha zake kwa Mbaiuchi, anapozitaka hachukuwi fedha taslim bali huambiwa kuchukuwa vitu kidogo kidogo toka duka la huyo Mbaiuchi mpaka kima chote cha fedha alizoweka zimekwisha. Bei ya vitu anavyochukuwa toka dukani huandlkwa na mwenye duka na ndiye peke yake anayejua ni kiasi gani kimebakia katika jumla ya fedha zote zilizowekwa dukani mwake na mkulima. Sikupata nafasi ya kulithibitisha jambo hili lakini pengine safari ijayo nitaweza kuthibitisha iwapo jambo hili ni la kweli.

18

MIFUGO KATIKA BONDE LA USANGU

Ifuatayo hapo chini ndiyo idadi ya Mifugo yotekatika Wilaya yote ya Mbeya iliyohesabiwakabla ya mwaka 1973: —

1. Ng'ombe walikuwa 250,600 2. Mbuzi walikuwa 39,080 3. Kondoo walikuwa 25,069 4. Nguruwe walikuwa 1,889 5. Punda walikuwa 293 6. Kuku walikuwa 42,552

Idadi ya mifugo katika bonde la Usangu peke yake kabla ya Wamasai na Wasukuma kuingia katika bonde hili mwaka wa 1973.

1. Ng'ombe walikuwa 149,528 2. Mbuzi walikuwa 10,490 3. Kondoo walikuwa 7,543

Takwimu hizi hazina idadi ya ng'ombe wa Wamasai na Wasukuma ambao walianza kuingia katika bonde la Usangu kuanzia mwezi wa Agosti mwaka 1973 baada ya kuhesabu mifugo yote katika bonde hili mwaka 1972.

MAGONJWA YA MIFUGO

Magonjwa makubwa yanayoisumbua mifugo katika bonde la Usangu ni haya: — 1. Chambevu (Blackquarter) 2. Kimeta(Anthiax) 3. Ndigana (East Coast Fever) 4. Ndigana Baridi (Anaplasmosis) 5. Ugonjwa wa midomo na miguu (Foot and Mouth) 6. Ndorobo.

MATATIZO KUHUSU MIFUGO

Baada ya Wamasai na Wasukuma kuingia katika bonde hili matatizo mengi yamezuka hasa kuhusiana na mifugo yao ambayo imesababisha mgongano kidogo na Wasangu ambao pia ni wafugaji stadi. Wamasai na Wasukuma walianza kuingia bonde la Usangu mwezi wa Agosti mwaka 1973 huku wakiandamana na mifugo yao mikubwa. Walipokuwa wakiingia bonde hili la Usangu waliweza kueneza ugonjwa wa ng'ombe wa miguu na midomo (Foot and Mouth disease) ugonjwa ambao ulikuwa haujulikani kabisa katika bonde la Usangu. Ugonjwa huu uliua mifugo mingi ya Wasangu na jambo hili liliwaudhi wafugaji wa Kisangu. Pia mifugo ya Wamasai na Wasukuma ilisababisha ukosefu wa malisho ya kutosha kwa Wasangu jambo ambalo hawakulizoea tangu zamani.

Halikadhalika Wamasai ambao ndio waliotangulia kuingia bonde la Usangu kabla ya Wasukuma walianza kugongana na Wasukuma wakati Wasukuma wakiingia katika bonde hilo na kuwakuta tayari Wamasai wamejiimarisha.

Kuyadhibiti maradhi ya ng'ombe huwa ni vigumu sana kwa maafisa wa mifugo kwa sababu hawa wahamiaji Wamasai na Wasukuma huingia katika bonde hili bila ya utaratibu wowote, na hueneza magonjwa mengi ya mifugo kwa urahisi sana. Vile vile wafugaji wengine hawanunui dawa za kutibia na kuzuia magonjwa ya mifugo kwa sababu husema kuwa dawa hizo ni aghali sana ambapo wafugaji wengine hukubali kununua dawa hizo na kuwatibu wanyama wao.

19

Idara ya mifugo inapatataabu sana katika kutoa huduma safi kwa wafugaji katika bonde hili kwa sababu wafugaji wenyewe wametawanyika huko na huko pamoja na mifugo yao. Hawakai pamoja. Kwa jinsi hii, ni vigumu sana kutoa huduma nzuri kwa wafugaji wote pamoja. Hili ni tatizo linaloikabili Idara ya Mifugo. Halikadhalika barabara hazipitiki wakati wa majira ya mvua. Kwa hiyo huwa ni vigumu kwa Idara ya Mifugo kuwahudumia wafugaji kwa sababu wanashindwa kusafiri hadi mahali walipo hao wafugaji.

Zaidi ya hayo kuhamahama kwa wafugaji ambao huhamia bonde la Usangu na mifugo yao na pia kutoka katika bonde hilo kwafanya kazi ya Idara ya Mifugo kuwa ngumu sana pia kuidhibiti sawasawa tabia hii ya kuhamia bonde hili bila taarifa yoyote kwa idara ya mifugo katika Wilaya ya Mbeya huwa ni kazi ngumu. Pia hawa wafugaji ni wagumu sana kuwasikiliza mabwana mifugo wanapotoa mashauri yao kwa hawa wafugaji. Tatizo jingine ni kwamba wafugaji wenyewe hawana chama chao cha ushirika kitakachoweza kuwasaidia wafugaji katika shughuli zao za ununuzi na uuzaji wa wanyama wao. Mpaka wakati wa kuandika habari hizi, Mbaluchi mmoja ndiye aliyeruhusiwa kununua na kuuza ng'ombe katika Mikoa mingine inayotaka kununua ng'ombe na kadhalika. Ingawa chama cha wakulima wa Usangu wanajaribu kununua ng'ombe wachache lakini hakitoshi.

Kwa upande wa utumishi kuna tatizo la upungufu wa watumishi wa Idara ya Mifugo. Wengine waliopo sasa hivi katika Wilaya ya Mbeya hawajapata nafasi ya kuwaongezea ujuzi wao kama idara zingine zinavyofanya. Kuna haja ya kuongezea mafunzo watumishi wa mifugo waliopo sasa. Hii itasaidia kuinua ujuzi wao na kufanya uchumi wa mifugo uweze kuongezeka zaidi. Labda itafaa kuongeza nafasi kwa watumishi hawa katika vyuo vya Mpwapwa na Morogoro ambavyo hasa ndio vyuo vyataifa vinavyotegemewa sana kwa kutoa watumishi wa mifugo hapa nchini.

Kwa sasa hivi, Idara ya Mifugo inazo zahanati nne za mifugo katika bonde la Usangu na Idara hii inao mpango wa kuanzisha kituo cha mafahali wa nyama na kuanzisha kiwanda cha kutengeneza samli. Vile vile wanatarajia kuanzisha shamba la kufugia ng'ombe (Ranch).

KILIMO CHA WASANGU

Baada ya kusimulia shughuli za uchumi kwa jumla katika bonde hili la Usangu sasa nitasimulia shughuli za uchumi za Wasangu kama jamii pekee ya asili kabisa katika bonde hili. Kama ilivyoelezwa katika historia ya Wasangu hapo juu, Wasangu wametokana na jamii za Wasafwa, Wahehe, Wabena, Wanyakyusa ambao jadi yao ni ukulima wala sio ufugaji. Wasangu tangu awali walikuwa wanalima na kufuga ng'ombe wachache sana kama jamii zinazowazunguka zilivyokuwa zinafuga. Utamaduni wa Wasangu wa kufuga ng'ombe wengi na kuacha utamaduni wao wa kwanza wa kilimo ulianza kutokea wakati wa vita mbalimbali vilivyopiganwa kati ya wao na majirani zao. Angalia hapa chini. Kilimo chao kilikuwacha majembe ya mikono. Majembe haya yalitengenezwa na Wakinga kutoka Ukinga na wakayaleta kwa Wasangu ili wayauze. Wakinga walibadilishana majembe yao na ng'ombe; huyu ng'ombe alichukuliwa na Mkinga aliyeleta majembe, na akakaa naye huyu ng'ombe mpaka wakati wa kuzaa. Baada ya kuzaa mara moja tu kwa Mkinga, ng'ombe huyo alirudishwa kwa Msangu maana bei ya jembe au majembe ilikadiriwa kwa mtamba au mitamba. Na iwapo ng'ombe huyo aliyechukuliwa na Mkinga alifia kwa Mkinga kwa bahati mbaya, basi Mkinga alilazimika kumchuna ngozi na kuirudisha kwa mwenye ng'ombe pamoja na majembe mawili au matatu kama malipo.

Mpini wa jembe ulitengenezwa kwa mti uitwao "mshala" na wakati wa kuchomeka jembe lenyewe katika mpini mlunda, kitu kama msumari mrefu, ambao ulichomwa sana moto, ulitumika kutobolea shimo kwenye mpini kwa kuuchoma mpini wenyewe. Baada ya hapo jembe nalo lilichomwa sana na kutiwa kwenye shimo la mpini uliokwisha tobolewa na msumari halafu majani fulani yaliyochanganywa na mavi ya ng'ombe yalitiwa pamoja kwenye jembe na kutiwa katika shimo ili jembe liweze kusaki barabara. Kazi hii ilifanywa na mafundi maalum ambao walikuwa wanaishi kijijini.

20

Wakati wa kuanza shamba jipya, miti na majani hufyekwa kwa kutumia shoka na miundu. Baada ya hapo miti iliyofyekwa shambani huachwa ili iweze kukauka kwa jua. Wakati majira ya mvua yanakaribia, majani na matawi yote ya miti huchomwa moto. Shamba hulimwa kwa sesa na kupandwa ulezi. Katika mwaka wa pili shamba hulimwa matuta na kupandwa mahindi. Kilimo chao kilifanyika kati ya mwezi wa Januari na Februari katika kila mwaka. Kulima kwao kulikuwa kwa njia ya kualikana. Pombe ilipikwa ili iweze kunywewa baada ya kazi ya kulima. Siku hizi utaratibu wa kualikana wakati wa kulima umetoweka na ubinafsi umekuwa mwingi mno.

Wakati wa kuvuna Wasangu hawakualikana; kila familia ya Kisangu ilivuna mavuno yake. Mashamba ya familia ya Kisangu yaligawanyika sehemu mbili; sehemu ya mke na sehemu ya bwana, na mavuno pia yalitenganishwa. Mavuno kutoka shamba la mwanamke yaliwekwa katika kihenge chake na mavuno toka shamba la bwana yaliwekwa katika kihenge cha bwana. Wakati wageni walipotembelea ndugu zao, waliweza kupewa chakula kwa kufuatana walikuwa ni wageni wa nani — wageni wa bwana au wageni wa mwanamke. Kama walikuwa wageni wa bwana basi walipewa chakula toka kwenye ghala ya bwana na kama walikuwa wa mwanamke basi wageni walipewa chakula toka ghala ya mwanamke.

Watoto hawakushughulika sana na kilimo bali walijishughulisha na kuchunga ndama au mitamba. Mpaka wakati huu kilimo cha Wasangu hakijabadilika sana yaani matumizi ya jembe la mkono ni yale yale yaliyokuwapo zamani kabla ya Wasangu hawajaanza kufuga ng'ombe kwa wingi. Labda kitu kilichobadilika katika kilimo cha Wasangu, ni kuacha kujishughulisha na kilimo zaidi kama hapo awali na kuanza kujishughulisha na mifugo zaidi katika karne ya 18 na karne ya 19.

GHALA

Ghala za vyakula zajengwa kwa kutumia miti ya MIPEREHEME na huezekwa kwa manyasi yaitwayo LIPEPETE au LIKUHI. Kamba za kufungia fito ni za MAHANGO na mayota. Ghala hujengwa kwa kuinuliwa juu ya ardhi kwa kuogopa mchwa. Ghala zenyewe si madhubuti sana kwa kuzuia panya.

21

UFUGAJI WA NG'OMBE

Kama ilivyoelezwa hapo mwanzoni, Wasangu walikuwasi wafugaji maarufu wa ng'ombe Kama walivyo sasa, bali walifuga ng'ombe wachache na kwa wastani kila familia iliweza kufuga ng'ombe wawili au watatu hivi. Lakini kazi yao kubwa sana ilikuwa kilimo. Ufugaji wa mifugo mingi ulianza Wasangu walipokuwa wanafanya vita na majirani zao katika karne ya 18 na karne ya 19. Shabaha mojawapo kubwa ya Wasangu kufanya vita na majirani zao ni kuteka mifugo ya maadui. Pia walikuwa na shabaha ya kuteka wanawake wa maadui na baada ya kuletwa utumwa katika nchi za jirani, basi wakaanza kuwateka watoto wa maadui ili wakawauze utumwani. Basi ilikuwa wakati huu wa vita ambapo walijiongezea mifugo kwa wingi sana na kila Msangu aliyeshiriki katika vita aligawiwa ng'ombe waliowateka vitani. Chifu wao aliwagawia ng'ombe watu wake wote walioshiriki vitani. Kwa jinsi hii Wasangu waliacha utamaduni wao wa kwanza wa kulima na kuanza kufuga na kutegemea sana mifugo yao badala ya kulima.

SHABAHA YA KUFUGA NG'OMBE

( i ) Nguo za Wasangu zilitengenezwa kwa kutumia ngozi za ng'ombe, na pia matandiko ya kitanda yalikuwa ni ngozi.

(ii) Maziwaya ng'ombe ni mboga kubwa sana kwa Wasangu. (iii) Ng'ombe wanatumiwa kama mahari ya kuolea wanawake. (iv) Ng'ombe huchinjwa kilioni na matambikoni na nyama kuliwa na watu. ( v ) Kwa siku hizi Wasangu wanauza ng'ombe ili wapate fedha lakini ng'ombe wanaouzwa ni

wachache sana. (vi) Kuonyesha ufahari wa utajiri kuliko Wasangu wasiokuwa na ng'ombe wa kutosha. (vii) Kwa kawaida ng'ombe wa Wasangu hawachinjwi kwa ajili ya nyama, bali ng'ombe wafugwa

ili kuonyesha ufahari wa utajiri katika jamii ya Wasangu na hapo zamani matajiri wa Kisangu waliweza kutoa ng'ombe mmoja au wawili kwa chifu wao ili wamwonyeshe utajiri wao. Halafu chifu wao aliwateua hao matajiri kuwa viongozi wa vijiji na kuweza kutawala baadhi ya vijiji fulani. ( v i i i ) Kwa wastani familia moja ya Kisangu hufuga kati ya 200 — 300; na

wanaogopa kupanua Kilimo chao kwa sababu ya kuogopa kumaliza malisho ya mifugo.

Dawa a kutibia magonjwa mbalimbali ya ng'ombe ni (i) Limulimuli. (ii) Lirungurugu (iii) na dawa ya kutibia ugonjwa wa mlguu na midomo ilikuwa ni kuwapa wanawake shughuli ya kuwachunga ng'ombe ambayo haikuwa kazi yao hasa. Wanaume hawakuruhusiwa kupitia sehemu ambako wanawake walikuwa wakichunga hao ng'ombe waliposhik-wa na ugonjwa huu. Wakati wa kuchunga ng'ombe, wanawake walivaa nguo za wanaume wakati ambapo wanaume nao walivaa nguo za kike na walibakia nyumbani na kupika badala ya wanawake kupika. Yaaminiwa kuwa kwa kufanya hivyo, ng'ombe wa ugonjwa huu walipona kabisa bila ya dawa yoyote. Kitendo hiki cha kubadilishana kazi ya kuwachunga ng'ombe kati ya wanaume na wanawake kilitosha kabisa kuwatibu ng'ombe walioshikwa na ugonjwa huu wa miguu na midomo.

UTAWALA WA WASANGU

Kabla ya kuja Waarabu katika bonde hili, Wasangu walikuwa na mtawala mmoja mkuu ambaye alitawala nchi nzima ya Usangu. Chini ya Mwene alikuwapo jumbe mkuu ambaye ndiye alikuwa Waziri Mkuu wa serikali ya Kisangu, naye alisaidiwa na wajumbe wadogo walioitwa Watambuli. Baada ya hawa Watambuli walikuja raia. Wakati wa kumtafuta chifu wa kutawala nchi ya Usangu, Watambuli (wazee) ndio waliomchagua Mwene wao.

Kwa kawaida chifu katika uhai wake kabla hajafa aliwachagua watoto wake wawili kuwa kati yao mmoja atatawala, ndipo Watambuli (wazee) humchagua mmoja kati yao aliye na busara.

22

SIFA KUU ZA MWENE

Lazima mtu yule atakayechaguliwa kuwa chifu awe na utii kwa wazee; lazima aweze kuyakubali yanayosemwa na wazee; lazima huyo chifu awe kiongozi bora katika vita. Kabla yakutawazwa chifu mteule akae na wazee (Watambuli) kwa muda ili apigwe msasa safi. Siku ya kutawazwa ikiwadia, Mjumbe Mkuu humchukuwa yule chifu mteule na kumkalisha kitini cha ufalme. Sasa kiapo chasemwa na wazee wenyewe huku chifu mteule amekaa kimya pale kitini. Baada ya hapo, wazee wanamwondoa huyo chifu na kumpeleka nyumbani kwake. Shughuli huambatana na sherehe. kubwa ambapo pombe nyingi hupikwa na vyakula vingi vyaandaliwa. Ng'ombe hao walichinjwa kwa wingi.

Mambo ya uhalifu yalishughulikiwa zaidi na majumbe na wahalifu walikamatwa na kupelekwa kwa chifu. Adhabu zilitolewa kwa kufuatana na uzito wa makosa. Aliyeua alipewa adhabu ya kuwapa ndugu wa marehemu ng'ombe. Katika makosa ya kupigana majembe kutoka Ukinga yalitumika sana katika kulipia adhabu. Mtu aliyeshikwa ugoni, ng'ombe wake wote walikatwa mishipa ya miguu kama adhabu. Wakati mwingine vita ilizuka kati ya kijiji na kijiji kwa sababu ya kuzuia watu wenye mkealiyeshikwa ugoni na bwana mwingine asije akafyeka miguu ya ng'ombe wao.

Kodi ya nchi ililipwa kwa mwene kwa kulima shamba la mwene. Kila kijiji kilikuwa na zamu ya kwenda kulima shamba la mwene — kila jumbe alileta watu wake kuja kulima shamba la mwene.

FAMILIA NA NDOA YA KISANGU

Kwa kawaida Msangu wa kawaida alikuwa anaoa mke mmoja tu na mtindo wa kuoa mwanamke zaidi ya mmoja kwa Msangu wa kawaida ni mtindo ulioigwa siku hizi. Wajumbe wa Kisangu katika vijiji ndiyo walioweza kuoa wake zaidi ya mmoja kwa sababu hawa walikuwa na nafasi ya kuweza kupata majembe ya kuolea wake. Hii ilikuwa ni tabaka ya kijamii ya Wasangu ambayo ilifuatana na utajiri wa kuwa na majembe ya kutosha. Wakati wa kuoa mke, ilimbidi ahamie mji au kijiji cha bwana. Kwa hiyo familia moja ya Kisangu ilikuwa ni ya namna mbili: familia ndogo na familia kubwa. Familia ndogo yenye kuwa na mume na mke na watoto wao. Familia kubwa ilikuwa na baba, mama, watoto — pia kulikuwapo familia alikotoka baba na familia walikotoka mama. Mahari iliyotolewa wakati huo ilikuwa jembe na ushanga, nakadhalika. Hii ndiyo ilikuwa mahari kubwa ya Wasangu. Ng'ombe hawakutumika kama mahari. Siku hizi mahari ya jembe na shanga havitumiki tena ball ng'ombe (mitamba) wawili na kambaku mmoja hutumika badala ya jembe na shanga.

Hapo zamani wavulana ambao walikuwa tayari kuoa waliambiwa na wajumbe wa vijiji kwenda porini ili kila mmoja akatayarishe mwenge na kuupeleka kwa mwene. Yule mvulana aliyefaulu kuwasha mwenge na kuufikisha kwa mwene huyo alikuwa anajipatia sifa mojawapo ya kuweza kumpata mke wa kuoa. Lakini yule aliyeshindwa kuufikisha mwenge kwa mwene, basi alibakia mgane siku zote. Hali kadhalika wasichana kuolewa walikamatwa na jumbe wa kijiji na kupelekwa kwa Mwene (chifu) ili waweze kugawiwa mume wa kumwoa.

Baada ya wavulana kupeleka mienge kwa chifu kila jumbe wa kijijini aliulizwa na mwene ana wavulana wangapi kijijini mwake wa makamo ya kuoa na waliofaulu kupeleka mwenge kwa Mwene. Baada ya kupata majibu toka kwa wajumbe wa vijiji, kila jumbe aligawiwa wasichana ili akawagawie wavulana walio na sifa zinazotakiwa. Mahari ya jembe na ushanga ilitoka kwa Mwene na kuwapa wavulana hao waliopata wake wa kuoa — hao walipeleka mahari kwa wazazi wa wasichana. Vile vile wavulana hao waliopewa mahari walilazimika kwenda kwa Mwene kulima shamba la chifu kwa muda wa siku kama mbili hivi kila mmoja. Wakati huo pombe ya kunywa na chakula viliandaliwa kwa ajili ya walimaji hao. Baada ya hapo, wavulana hao waliwapeleka wake zao katika nyumba ambamo walikuwa wanalala mitamba mpaka wavulana watakapojenga nyumba zao. Kwa hiyo, binti hao waliweza kukaa pamoja na wazazi wao kwa muda ili waweze kupevuka zaidi, na wakati huu mvulana (mme wa msichana) ilimpasa apate mahitaji yake ya chakula toka kwa wazazi wa msichana (mkewe) na vile vile ilimbidi huyo mvulana awasaidie wakweze katika shughuli za kilimo.

23

Wakati wa arusi watu walicheza zeze (Gombo) ill kufurahia arusi hizo na nyimbo nyingi ziliimbwa kwa mfano wimbo huu hapa ulitumika sana katika kuimbwa wakati wa arusi: —

Towene mandu lyamlamba lya menda lyahanjika lyagwaa, shoo — shoo. Maana yake:- Tumecheza mno, mpaka jua limetua na kupumzika (Huu ni wimbo wa kumsifu mtwa wao).

Talaka hazikuwapo wakati huo katika jamii ya Wasangu kwa sababu chifu alikataza kitendo hiki kisitokee. Lakini siku hizi mambo ya talaka katika jamii ya Wasangu imekuwa ni jambo la kawaida. Mila ya kudumisha ndoa ya zamani imepotea kabisa. Iwapo mama fulani alipatikana na jambo la kufiwa na watoto basi huyo mama aliruhusiwa na chifu Hi aende akaolewe mahali pengine na bwana mwingine. Ilionekana kuwa bwana aliyemwoa huyo mama alikuwa na mkosi wa kuwapoteza watoto wake. Kwa hiyo mama huyo aliruhusiwa kujaribu bahati yake mahali pengine kwa bwana mwingine. Bwana mwenye bibi huyo aliyetaka kumwacha bwana yake alikwenda kwa chifu wake kulia hali ill aweze kupatiwa mke mwingine.

Iwapo bwana ya mke alifariki dunia, basi ndugu wa kwanza wa marehemu aliweza kumrithi mke wa ndugu marehemu na mwanamke alikuwa hana uchaguzi.

IMANI NA DINI Dini ya asili ya Wasangu hufanyika mahali watemi wanapozikwa. Kwanza kabla ya kuanza

shughuli za sala ulezi huchangwa na raia halafu ng'ombe wa kuchinjwa wakati wa shughuli hizo hutolewa kwa kufuata zamu. Kuna vikundi hivi hapa chini vinavyoshughulika na utoaji wa ng'ombe wa kuchinjwa wakati wa kuomba sala; vikundi hivyo vyaitwa FIPUGA. Navyo viko vinane:-

1. Kikundi cha Wanyangamana 5. Kikundi cha Wanyakongwe 2. Kikundi cha Wanyakulwa 6. Kikundi cha Wanyawami 3. Kikundi cha Wasagarua 7. Kikundi cha Wayegenza 4. Kikundi cha Wanamwani 8. Kikundi cha Wanyibanga.

Kasisi Mkuu ni mzee Mfumbulwa. Baada ya kazi ya sala pombe hunywewa na nyama wanagawana. Hapo zamani mavazi maalum yalitumiwa wakati wa kazi hii. Kasisi alivaa joho jeusi na ushanga na hujipaka chokaa iitwayo NKENJI. Viatu na vitambaa vilivyovaliwa kichwani hutolewa halafu ndipo sala zasemwa. Nyimbo fulani zaimbwa na akina mama. Baada ya hapo watu hupata kile kitu wanachokiomba.

UCHAWI UHABI Kwa kawaida ramli hupigwa kumtambua mchawi. Baada ya kumtambua mchawi, basi huyo

mchawi alikabiliwa na adhabu ya kifo na mtu maalum aliwekwa kwa ajili ya kutoa adhabu. Mtu alipokufa alifungwa ndani ya ngozi au kirago na kutupwa porini. Hii ndiyo iliyokuwa njia yao ya kuzika maiti. Desturi ya kuzika maiti katika makaburi imeanza wakati Wajerumani walipoingia nchi ya Usangu.

NYUMBA ZA WASANGU Nyumba za Wasangu ni za aina ya tembe, nazo zajengwa kwa kutumia miti ya "mipecheme"

na huezekwa kwa majani yaitwayo "lipepete" au "likuhi". Kamba za kufungia miti ya kujengea nyumba za fito ni za mahango na mayota. Mwamba wa nyumba ni "mganga", sakafuni husiliba udongo uliochanganywa na mavi ya ng'ombe. Ukutani udongo huu huu hutumika kwa kusilibwa. Mlango wake huwa ni wa matete yaliyosukwa pamoja kwa kutumia kamba. Kwa kawaida mlango huwa ni mmoja na chumba huwa ni kimoja. Siku hizi Wasangu wengine wamebadili mtindo wa kujenga nyumba zao kwa kufuatana na nyakati za kisasa na pia kufuatana na utamaduni mpya wa jamii mbalimbali zilizoingia katika bonde la Usangu.

24

MAVAZI YAO YA JADI Vazi liitwalo MAJIHU, ainaya usinga, lilivaliwa na Wasangu kuficha sehemu zasiri nachifu wao

ndiye aliweza kununua usinga huu na raia zake wakapewa bure. Chifu alivaanguo na kichwani alivaa vazi lililoitwa NJORA Akina mama walivaa ngozi za mbuzi.

MICHEZO YA WASANGU

Ngomaza Wasangu zilizo maarufu sana ni:-(i) Malenjelana, (ii) Ligombo

MALENJELA ni ngoma ambayo ngoma tano ndogo zapigwa pamoja na kubwa moja, jumla ni ngoma sita. Ngoma ndogo zapigwa kwa kutumia kijiti kimoja na ngoma kubwa yapigwa kwa kutumia vijiti viwili. Katika kucheza wanawake hujipanga upande na wanaume hujipanga upande mwingine halafu ndipo huanza kucheza kwa kutamba.

MIIKO YA NGOMA

Wakati wa kutengeneza ngoma mtu haruhusiwi kupitia mahali hapo ama sivyo atanyang'anywa nguo zake. Wapiga ngoma hawana ruhusa kutoroka wakati ngoma zinapigwa ama sivyo nguo zao zitanyang'anywa. Wakati unaofaa kucheza ngoma hizi ni ule baada ya kuvuna mtama halafu ndipo habari zipelekwe kwa mtemi. Baada ya kufikisha habari kwa mteni na kupata kibali chake ndipo mpango hutayarishwa ili ngoma ichezwe.

MAPENDEKEZO

Lingalikuwa jambo zuri kama wafugaji wote wanaoishi Usangu wangehimizwa na serikali ili waunde chama cha Ushirika cha mifugo yao ili kuendeleza shughuli ya ufugaji wa ng'ombe iwe nzuri na yenye kuwaletea manufaa zaidi kuliko ilivyo sasa. Umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu. Wanyama wote ambao kwa sasa hivi wananunuliwa na kuuzwa na mtu mmoja wangaliuzwa kwa chama na chama kingalikuwa na jukumu la kutafuta masoko ya kuuzia hao, wanyama nje ya Mkoa wa Mbeya. Chama hiki kingalisaidia sana katika kutoa mashauri mema kwa wanachama wake jinsi ya kuwatunza wanyama walio bora zaidi. Pia madawa mbalimbali ya kutibia maradhi mbalimbali ya mifugo yangaliweza kutolewa na chama chao huku wakishirikiana na Idara ya Mifugo katika Mkoa. Vile vile Idara ya Mifugo ifanye kampeni ya kuwaelimisha wafugaji umuhimu wa kutumia madawa mbalimbali ya maradhi ya ng'ombe. Kwa sasa hivi wafugaji wengi wanakataa kuzinunua dawa zinazoletwa na Idara ya Mifugo kwa kuogopa bei za madawa hayo. Kwa jinsi hii maradhi mengi ya ng'ombe yanabakia pale pale ingawa kuna wafugaji wachache sasa ambao huzinunua dawa hizo na kuzitumia katika kutibu maradhi ya ng'ombe. Lakini wafugaji wachache hawa hupoteza nguvu zao bure kwa sababu jirani zao wengine wanakataa kuzinunua hizo dawa.

Pendekezo jingine ni kwamba ingalikuwa jambo zuri iwapo Serikali ingefanya kampeni ya kutosha kwa wafugaji, ili waweze kuwatumia wanyama wao vizuri. Mpaka sasa wafugaji wote hawa hawatumii ng'ombe wao kama inavyopasa — yaani, ng'ombe wanafugwa kwa ajili ya ufahari tu na pengine kuuzwa wachache mara shida zinapowatopea. Ingalifaa hawa ng'ombe wafanywe njia mojawapo kuu ya kuchuma mali. Kama wafugaji wakifanya hivyo, basi ng'ombe hawa watakuwa wa manufaa sana kwa wananchi hao.

25

Maziwa ya ng'ombe hao hayatumiwi Kama ipasavyo. Lingekuwa jambo zuri iwapo maziwa yangalikamuliwa ya kutosha ili yauzwe kwa watu wengine kama njia moja wapo ya kujipatia fedha kwa wafugaji, na pengine hata kiwanda cha kutengenezea Siagi, Jibini, na Samli kingejengwa katika bonde hili. Kuna uwezekano wa kupata maziwa mengi sana iwapo ng'ombe watafugwa vizuri zaidi kuliko ilivyo sasa. Vile vile idadi ya hao ng'ombe ingepunguzwa kwa kuwauza ng'ombe wengine mnadani, na katika kufanya hivyo hao wafugaji wangaliweza kujipatia fedha ambayo ingalitumika katika kununulia vifaa vingine vya kusaidia katika kuzalisha mali kwa njia nyingine. Kwa mfano, matrekta na majembe ya kukokotwa na ng'ombe yangalipatikana, na wafugaji hawa wangeweza pia kulima mashamba ya vyakula na mimea mingine kuliko ilivyo sasa. Kwa sasa hivi wafugaji wengi hawapendi kulima, au kama wanapenda, hawalimi sana wakati ambapo ardhi yao ni nzuri sana kwa kilimo cha mimea mbalimbali. Kwa mfano, Wasangu wameacha utamaduni wao wa kulima na wakaiga utamaduni wa kufuga ng'ombe na kulima kidogo sana. Nchi ya Wasangu ni nzuri sana kwa kilimo na ingalifaa sana kama wangalijishughulisha na mambo yote mawili — kilimo na ufugaji kuliko kujishughulisha sana na mifugo kama wafanyavyo kwa sasa hivi: hufuga zaidi na kulima kidogo.

Uhamiaji wa wafugaji kuingia katika bonde hili wafaa uthibitishwe sana na Idara ya mifugo ili waweze kujua idadi ya mifugo inayoingia katika bonde hili na kuweza kujua ni maradhi ya namna gani yanayoweza kuletwa na mifugo kutoka Mikoa mingine. Lakini iwapo mtindo uliopo sasa wa kuihamishia mifugo sehemu za Usangu kutoka nje ya Mkoa wa Mbeya bila ya wataalam kujua utaendelea, itawawia vigumu sana kwa watumishi wa Idara ya Mifugo kuweza kutoa huduma zilizo bora kwa wafugaji. Mpaka wakati wa kuandika habari hizi mwezi wa Februari 1975, Idara ya Mifugo ya Mkoa wa Mbeya ilikuwa haijui idadi ya mifugo iliyomo katika bonde la Usangu kwa sababu imekuwa ni vigumu sana kujua ni lini wafugaji wengine watahamia katika bonde hilo.

Wakati wa kiangazi, maji ya mito inayotiririkia katika bonde la Usangu hupungua sana kima chake. Kwa hiyo huwa ni vigumu kwa watu wote waishio katika bonde hili kupata sehemu yao ya maji kwa ajili ya shughuli za uzalishaji mali. Utaratibu uliopo sasa wa kugawanya maji si mzuri kwa sababu ni watu wachache sana ambao hupata maji kwa ajili ya shughuli ya kilimo na mifugo ambapo wako upande wa chini wa bonde hili wanapata shida kubwa katika kuyatafuta maji kwa ajili ya mifugo yao na hali kadhalika kwa ajili ya matumizi yao wenyewe. Pia wakulima ambao mashamba yao yako upande wa chini ambako wafugaji wako hukosa kabisa maji kwa ajili ya shughuli ya kilimo chao. Kwa jinsi hii, utaratibu mzuri wa kugawanya maji kwa ajili ya wakulima na wafugaji wote unafaa uanzishwe upesi na utaratibu uliopo sasa uachwe kwa sababu unawanufaisha watu wachache sana. Katika kufanya hivyo. wakulima na wafugaji wangeshauriwa ili wakae pamoja na kuamua jinsi ya kuanzisha sehemu za kilimo na sehemu za kufugia mifugo. Baada ya kufanya hivyo mifereji ingalichimbwa ambayo itayapeleka maji toka mitoni hadi sehemu hizi za uzalishaji mali na vile vile habari kamili ziwekwe kuhusu kiasi cha maji yanayotakiwa kwa shughuli hizi — shughuli hii wataalam wa kilimo na mifugo wangeweza kuandika kila habari katika vitabu ambavyo baadaye vitasaidia sana kuwa vitabu vya kumbukumbu kwa mtu yeyote yule anayetaka kujua jinsi maji yanavyotumika kwa kilimo na ufugaji, na iwapo mtu anataka kuanzisha mradi mpya wa uchumi katika bonde hili. Vile vile utaalam wa kutengeneza mifereji ya maji iliyo bora uweze kutolewa na wataalam wanaohusika lakini kazi ya kuchimba mifereji iwe ndiyo kazi ya kujitolea kwa wakulima na wafugaji wenyewe. Kama utaratibu mzuri wa kugawanya maji ukianzishwa matatizo mengi ambayo yangeweza kutokea au yanayotokea sasa hivi yataepukika.

Zaidi ya hayo, mbolea ya ng'ombe ingalifaa itumiwe ingawa udongo una rutuba sana, mkulima aweza kulima shamba lake kwa muda wa miaka minne mfululizo, lakini mazao hayawezi kuwa ni yale yale. Mara nyingi hupungua sana kwa hiyo kama jamaa hawa wakijif unza namna ya kutumia mbolea ya ng'ombe, basi itakuwa ni rahisi sana kwao kulima shamba mfululizo bila ya kupata mazao hafifu katika miaka mingine.

Vile vile kampeni ingalifaa sana kuwaelimisha wafugaji wa mifugo ili waweze kutumia madawa yanayotolewa na idara ya mifugo na kuweza kutibu na kuzuia magonjwa mbalimbali ya mifugo.

26

Mpaka sasa wafugaji wengi wanaogopa kununua dawa hizo eti zauzwa aghali. Siku hizi ni siku za kupanda kwa bei za vitu mbalimbali hapa duniani, bei zenyewe zapanda kila mwezi. Kwa hiyo bei ya madawa lazima ipande kwa sababu inatengenezwa na watu ambao hulipwa mishahara. Kwa hiyo si dawa za ng'ombe tu zinazouzwa aghali ball kila kitu hapa duniani chauzwa aghali.

Zaidi ya hayo, wananchi wa Usangu ambao wanashindwa kutunza fedha zao katika benki na kuzipeleka kwa tajiri Hi amtunzie, wanayo shida kubwa. Kwa sababu fedha zinazowekwa kwa Mbaluchi zaleta matatizo mengi ya Uchumi wa mtu. Mtu anayehusika anaweza kuvutiwa na vitu vilivyomo katika duka la huyo mfanya biashara na kuanza kuvichukuwa vitu hivyo kidogo kidogo mpaka fedha zake zote zimekwisha. Kwa jinsi hii mtu anayehusika hubakia maskini siku zote. Pia tatizo jingine linalomkabili huyo mtu anayeweka fedha kwa Mbaluchi ni kwamba bei za vitu-anavyovichukuwa zapangwa na Mbaluchi mwenyewe bila ya mwenye fedha kushirikishwa. Kwa hiyo. kuna uwezekano wa ujanja kwa upande wa yule mwenye duka kuweza kuutumia ili zile fedha ziishe upesi. Pia kuna uwezekano wa kuibiwa huyo Mbaluchi siku yoyote au kuunguliwa duka na moto. Kwa jinsi hii hasara ni kwa yule mwenye kuziweka fedha kwa huyo Mbaluchi. Kwa hiyo kuna haja kubwa sana kwa viongozi wa TANU wa pande za Usangu kuwaelimisha wananchi faida ya kuzitunza fedha zao katika benki kuliko kuzipeleka kwa Mbaluchi ambako zaweza kumletea matatizo mengi ya kiuchumi. Vile vile watu wanaofanya magendo ya mazao na kuyauza nje ya chama cha Ushirika cha Chimala na Rujewa yafaa wapigwe vita kwa kutumia maarifa na ujuzi mwingi. Kwenda pupa katika kukipiga vita kitendo hiki kunaweza kusifanikiwe na nguvu zikapotea bure. Vile vile chama cha Ushirika pamoja na wazee wa TANU wa pande hizo wapewe semina au njia yoyote ile inayofaa ili wapewe elimu juu ya manufaaya chama cha Ushirika na hasara za kufanya magendo nchini.

Jam bo hili litawasaidia wananchi wenyewe, chama chao cha Ushirika na nchi nzima kwa jumla.

27

Wazee waliojitolea kutoa habari nyingi sana na misaada mbalimbali kuhusu utafiti wetu ni hawa:-

1. Mzee L. Mwandangala — Utengule — Usangu

2. Mzee F. Malisa — Utengule — Usangu

3. Mzee J. Mfumbulwa — Utengule — Usangu

4. Mzee W. Mfumbulwa — Utengule — Usangu

5. Mzee G. Makela — Utengule — Usangu

6. Mzee S. Mbeda — Utengule — Usangu

7. Mzee Yotichuma — Ruiwa — Usangu

8. Mzee Fundi Nasoro — Malanda — Rujewa — Usangu

9. Mzee Mwankili — Rujewa — Zahanati — Usangu

10. Mzee W.K. Simtengo — Bwana Afya — Rujewa

11. Katibu Tarafa — Rujewa — Usangu

12. Bwana Gulam — Mbaluchi — Rujewa

13. Afisa utamaduni — Mkoa wa Mbeya

14. Afisa Kilimo — Wilayani Mbeya

15. Afisa Mifugo—Wilayani Mbeya

I

28

JAMII YA WASAFWA

UTANGULIZI

Makala haya kuhusu jamii ya Wasafwa inayokaa katika Wilaya ya Mbeya ni mojawapo ya mfululizo wa makala mbalimbali yanayokusanywa na Idara ya Utafiti ya Wizara ya Utamaduni wa Taifa na Vijana kuhusu jamii mbalimbali za Watanzania.

Makala haya, ambayo ni matokeo ya utafiti uliofanywa na Ndugu J.S. Mwakipesile, yaonyesha kuwa kuna jamii fulani iitwayo WALUGURU inayopakana na WAWANJI. Jamii hii vile vile imeonyeshwa katika jarida la Utamaduni la Mkoa wa Mbeya Uk. 28 - 29. Mali kadhalika, Bwana S.R. Charsley katika kitabu chake, THE PRINCES OF NYAKYUSA, amewaonyesha Waluguru hawa katika picha inayoelekea ukurasa 48 kama WABUNDUGULU. Kusema kweli, kuna jamii ndogo sana sehemu za Mporoto na sehemu za mlima Rungwe ambayo inajiita Waluguru tofauti kabisa na jamii ya WALUGURU wanaoishi katika Wilaya ya Morogoro. Tunaposoma habari za Waluguru wa Wilaya ya Njombe na Rungwe, tusiwe na mawazo ya Waluguru wa Morogoro. Utafiti zaidi utafanywa kuhusu jamii hii na historia yake.

Zaidi ya hayo, kuna mam bo mengine katika makala haya hayakukamilika kwa sababu ya ukosefu wa ukweli safi kwa sababu mambo yamekuwapo au yametokea kila mara na kwamba imekuwa vigumu sana kujishughulisha ili kutaka kujua maana yake kwa nini mambo yamekuwa hivyo.

Watu waliotoa msaada mkubwa wa kutoa habari hizi, kuhusu jamii ya Wasafwa — mila na desturi zao, ambao wanapewa shukurani nyingi sana ni kama ifuatavyo hapa chini: —

1. Andrea Mwanjonga — Mwalimu washule ya watu wa Inshinshi, Mbeya.

2. MzeeY. Mpayo — Uyole, Iganjo, Mbeya.

3. A. Lyoba — Afisa utamaduni, Mbeya.

4. J.Kimamula — Majengo, Mbeya.

5. Ndugu Sleet — Kanisa katoliki, Mbeya.

6. Ndugu M. Lehner — Mbalizi Mission.

29

Sura ya Pili JAMII

YA WASAFWA

HALI YA NCHI Wilaya ya Mbeya ni Wilaya yenye milima na vilima vingi sana vinavyozungukwa na mabonde

pande zote. Nchi hii ni ya rutuba nyingi sana na udongo wake umetokana na milipuko ya volkano -kitu ambacho kinatoa rutuba nyingi sana. Juu ya milima hii kuna baridi nyingi sana na mvua zinapoanza kunyesha, kupanda milima kwa kutumia magari huwa ni taabu kubwa kwa sababu magari huteleza. Kwa jinsi hii huwa ni hatari kwa msafiri kwenda huko nyakati za mvua kwa kutumia gari bali huwa ni salama kwenda katika sehemu hizo kwa njia ya miguu ingawa kuna shida ya kuweza kuchoka katika kupanda milima yenyewe.

Mji wa Mbeya umekaa katika kitako (Saddle) cha milima ya Mbeya na unaelekea upande wa Kusini. Mtu anapotaka kuufikia mji wa Mbeya kutoka nje ya sehemu ya Mbeya, yampasa kwanza apande milima; baada ya kupanda hiyo milima ndipo aweze kuteremka milima hiyo na kuufikia mji wenyewe. Mji wa Mbeya unapendeza sana usiku na mchana kwa sababu unaonekana wazi wazi wakati wa kuteremka milima yake.

Jina hili Mbeya limetokana na mlima uitwao "Mlima Mbeya" ambao umebonyezwa na kufanya kitako ulipojengwa mji wa Mbeya. Asili ya jina hili la "Mbeya" ni kwamba mlima huu ulikuwa na magadi mengi yanayofaa kwa chumvi na pia mlima huu ulikuwa na panya wengi sana zama hizo, basi wenyeji wanasema mlima huo uliitwa mlima wa Mbewa (Mlima wa Mapanya) na wenyeji wengine wanasema kuwa mlima huu uliitwa hivyo kwa sababu ya chumvi nyingi iliyopatikana huko (Mbeye) (Chumvi). Sasa wakoloni walipofika wenyewe sehemu za Mbeya walishindwa kutamka sawa sawa jina hili "Mbeye" au "Mbewa" na wakatamka "Mbeya" kama walivyoshindwa kutamka "Nzovwe" badala yake wakatamka "Nsofe", "Nzombe" wakatamka "Njombe" "Ntwara" wakatamka "Mtwara", "Riringa" wakatamka "Iringa" (Ngome) Sumbuwanga (tupa uchawi) wakatamka Sum-bawanga, nakadhalika.

Wilaya ya Mbeya kwa upande wa Mashariki inapakana na wilaya ya Njombe, Kusini Mashariki inapakana na wilaya ya Rungwe, Kusini Magharibi inapakana na Wilaya ya Mbozi, Kaskazini' Magharibi inapakana na Wilaya ya Chunya, na Kaskazini inapakana na Wilaya ya Iringa.

30

Mvua zanyesha kwa wingi katika senemu yote ya Usatwa na zaanza kunyesha mwezi Oktoba na zinaendelea hadi mwezi wa Mei. Baada ya mwezi wa Mei kipupwe chatokea kikiambatana na baridi kali sana kwa sababu ya mwiriuko wa nchi yenyewe. Barafu huanguka na kufunika sehemu ya ardhi kama unga mweupe uliotandazwa, na mimea mingi yaunguzwa sana wakati huu. Milima ya Mporoto ndiyo inayotia fora kabisa kwa kuwa na baridi kali. Milima hii ina baridi kali karibu wakati wote wa mwaka. Lakini bonde la Usangu huwa na kipindi kirefu cha ukame na ni joto sana wakati wa kiangazi kwa sababu sehemu yenyewe ya Usangu iko chini katika Bonde Kuu la Ufa la Afrika Mashariki linalotoka Ziwa Rudolf. Bonde hili halina rutuba kama ile iliyoko kwenye milima, lakini linaweza kufaa kabisa iwapo kilimo cha kiangazi kitastawishwa vizuri kwa kutumia utaalamu wa kisasa kwa kutumia mfano wa mradi wa kilimo cha Mbalari. Katika Bonde hili la Ufa iiitwalo bonde la Usangu linafaa sana kwa kulima mahindi, mpunga, mtama na kadhalika. Katika sehemu za milimani, mazao yalimwayo huko ni kahawa, ngano, viazi ulaya au viazi mviringo, njegere, pareto, maharagwe, mahindi, viazi vitamu, migomba, ulezi, choroko, na kadhalika. Miti mbali mbali ya matunda inapandwa. Mali kadhalika udongo wa sehemu za milimani unafaa sana kupanda miti mbali mbali kama vile mikaratusi, miti ya kutengenezea karatasi, miti ya mbao na mingine mingi. Katika sehemu za Mporoto, kuna mianzi ambayo haikupandwa na mtu, na mianzi hii wenyeji wa huko hutumia kwa kutengenezea mabomba ya kusafirishia maji toka sehemu yenye kijito au chemchemi. Hutoboa mianzi hiyo katikati halafu huunganisha pamoja na kutega kwenye chemchemi au kijito halafu maji husafiri ndani ya mianzi hii mpaka kwenye kila nyumba ya mtu anayetaka maji yafikie nyur.iba yake ili asipate taabu ya kuyafuata maji huko kuliko na chemchemi au kijito chenyewe. Watu wa sehemu hizo za Mporoto wameweza kutatua shida ya maji kwa kutumia utaalamu wao huu wa asili.

Mifugo hufugwa lakini si kwa wingi. Ng'ombe, Kondoo, Mbuzi hufugwa na watu wa Mbeya. Bonde la Usangu linafaa sana kwa ufugaji wa ng'ombe labda shida ya maji ndiyo yaweza kuzuia ufugaji safi wa ng'ombe kwa sababu ng'ombe wanahitaji maji ya kutosha ili waweze kuwa wanyama bora wenye manufaa kwa wafugaji. Pia sehemu za milima ya Mporoto zafaa kwa ufugaji wa Kondoo wa manyoya au wa nyama.

Kilimo cha kiangazi kinaweza kutumiwa wakati wote kwa sababu Mbeya ni nchi yenye bahati ya kuwa na vijito vingi vinavyotiririka kwenye milima hiyo kila wakati bila kukauka. Wenyeji wengi hutumia sana vijito hivi kwa kazi mbali mbali zenye manufaa. Kwa mfano, wenyeji hutumia maji hayo kwa kufyatulia matofali, kufulia nguo, kumwagilia bustani za mboga, na mashamba mengine. Kwa hiyo mpango huu ungalitiliwa maanani sana katika sehemu zile za Mbeya ambako matumizi ya maji kwa kumwagilia mashamba hayajaanza bado kama vile sehemu za Utengule, Songwe na Njerenje.

Kuna barabara madhubuti zinazopitika wakati wote. Barabara moja kuu itokayo Dar es Salaam kwenda Lusaka, Zambia imetiwa lami, na pia barabara itokayo Mbeya kwenda Kyela imetiwa lami. Barabara zingine hazijatiwa lami lakini ziko imara na zapitika wakati wote.

HISTORIA

Jamii kubwa kuliko jamii zote katika wilaya ya Mbeya ni Wasafwa. Wasafwa huishi katika milima ya Mporoto Kaskazini ya mlima Rungwe na katika bonde ambalo laenea kati ya milima ya Mbeya upande wa Kaskazini na milima ya Umalila na Unyiha kwa upande wa Kusini na Kusini Magharibi. Mali kadhalika, Wasafwa huishi upande wa Kaskazini wa mlima Mbeya na katika sehemu ya uwanda wajuu unaopakana na Wilaya ya Chunya.

Wasafwa wanazungukwa na jamii hizi:- Wasangu upande wa Kaskazini, Wanyiha upande wa Magharibi, Wamalila upande wa Kusini-Magharibi, na Wanyakyusa kwa upande wa Kusini.

Wasafwa hawajapata kuwa chini ya Utawala wa namna moja, bali walikuwa wametawaliwa na machifu mbali mbali. Machifu wa Kisafwa waliokuwa wanajulikana sana tokea karne ya 19 ni

31

Mwalyego ambaye alijenga nyumba yake kwenye miteremko ya milima ya Mbeya karibu na Utengule, Chifu Lyoto alitawala sehemu ya mteremko wa mlima Mbeya upande wa Usafwa ya Kaskazini kuelekea bonde la Usangu, Zambi alitawala sehemu ya upande wa Kaskazini - Mashariki za miteremko ya milima ya Umalila, Malema alitawala sehemu za Kaskazini - Mashariki za miteremko ya milima ya Unyiha.

Ingawa ni vigumu sana kujua chimbuko la Wasafwa lakini koo mbali mbali za Wasafwa zakumbuka wapi zilitoka. Chimbuko la Wasafwa limo katika sehemu tatu. Sehemu ya kwanza ni ile inayowahusu Wasafwa ambao asili yao ni Ugogo. Ziko sababu nyingi ambazo zilisababisha kwa Wagogo fulani kwenda kuishi sehemu za Usafwa na kuoana na Wasafwa. Nchi ya Mbeya ilikuwa na rutuba nyingi kwa kupanda mazao ya chakula, biashara ya utumwa ambayo iliendeshwa zaidi na Waarabu, na kadhalika. Msafara wa watumwa ulifuata bonde la Usangu kuelekea sehemu za pwani ambako ndiko yalikuwako masoko ya kuwauzia hao watumwa. Njia hii ya watumwa ilifuatwa wakati njia ya kupitia Ugogoni ilipoonekana ni ya gharama kubwa sana kwa wafanya biashara hii na wakati mwingine ilifungwa na jamii za Kigogo kwa sababu mbali mbali za kutoelewana na Waarabu, Wafanya biashara. Na kama tunavyoelewa machifu wa Kiafrika nao walijitupa barabara katika biashara hii na kuwauza wenzao. Kwa hiyo, Wagogo waliokwenda sehemu za Mbeya yawezekana walifuata biashara halafu baadaye wakafanya mastaakimu yao pande hizi za Mbeya na kuweza kuoana na Wasafwa wa huko na baadaye watoto wao wakafuata malezi ya Kisafwa na kuwa Wasafwa Kamili. Pengine hao Wagogo walikwenda sehemu hizo za Usafwa kwa sababu ya kukimbia taabu ya kutiwa utumwani na Waarabu kwa sababu njia kuu ya biashara ya utumwa ilipitia katika nchi yao.

Chimbuko jingine la Wasafwa ni Ukinga. Hasa hili ndilo chimbuko kubwa la Wasafwa ambao kwa mila na desturi wanafanana nao sana. Wasafwa wanatoa sababu kubwa iliyowafanya waje sehemu hizi za Mbeya nayo ni sababu ya kupata moto. Kama inavyosimuliwa na wazee wengi wa Kisafwa, watu wa asili waliokuwa wanakaa pande za Mbeya, walijua jinsi ya kutengeneza moto, na Wasafwa wengi wakafuata utaalam huo toka pande za Ukinga na baadaye wakafanya maskani yao huko pengine baada ya kuwafanyia vita wenyeji wa huko halafu wao Wasafwa ndio wakawa watawala wa nchi yote ya Mbeya. Kwa kawaida Wasafwa wana desturi ya kukoka moto mmoja halafu huo moto huenea nchi nzima ya Usafwa. Moto huu ulikokwa kwa kufuata sherehe maalum.

Chimbuko la tatu la Wasafwa ni Unyakyusa na pande za Kaskazini za Malawi - Karonga. Kwa mfano, chifu Mwalyego ambaye baadaye alifanywa na Wajerumani kuwa chifu mkuu wa Wasafwa katika mwaka wa 1898 yeye husimulia kuwa asili yao ni Karonga na baba mkubwa wa Mwalyego (great grand father) Bwana Shyungu aliishi Karonga na utawala wake ulienea sehemu yote ya nchi ya Ukonde. Mtoto wake Mwamwondo alifanya maskani yake Nshorongo sehemu iliyo karibu na milima ya Igale. Mtu huyu alioa wanawake wengi na pia alioa binti ya Chifu Lyoto ambaye alitawala Usafwa wakati huo. Baadaye Mwamwondo akaasi na kumpindua mkwewe na yeye akawa ndiyo mtawala wa sehemu hii ya Usafwa. Mwamwondo alizaa wavulana wengi. Mwamparandje, Mwenipyana na Nsewe. Mtoto huyu Nsewe alizaliwa na mke wa Mwamwondo ambaye alikuwa binti ya Lyoto. Mwamwondo alifariki dunia mara baada ya Nsewe kuzaliwa. Mwamparandje akatawala nchi ya Nshorongo badala ya baba yake. Walakini ndugu yake Mwenipyana alipigana na Mwamparandje na akamshinda. Kwa hiyo Mwenipyana akatawala sehemu ya Nshorongo na Mwamparandje akakimbilia katika milima ya Igale.

Wasafwa walimkataa Mwenipyana kwa sababu mama yake hakuwa Msafwa na pia tabia yake mbaya ilimfanya asikubaliwe kutawaia. Wakati Wangoni walipoingia Mwenipyana aliwasaidia Wangoni kwa kuwapa chakula ambacho raia wake walikihifadhi. Tabia hii iliwaudhi sana Wasafwa, kwa hiyo wakamkataa kuwatawala.

Mwamwondo alipofariki mke wake, binti Lyoto alirudi kwa baba yake pamoja na mtoto wake Nsewe. Nsewe alipokua, babu yake Lyoto alimteua Nsewe kuwa chifu badala ya baba yake -Mwamwondo. Baadaye Nsewe akamwasi babu yake na akapigana naye kalazimika kukimbilia milimani alikofia wakati wa majilio ya Wangoni. Nsewe alizaa watoto wengi:- Mwalyambi, Zambi, Milambo, Ngaja, Nswila, Mpoli, Mwansonswe, Mwembe, Sidjodjo, Djedjo na Mudjenda. Nsewe aligawanya sehemu ya Utawala wake na kuwagawia watoto wake hawa.

32

Wasangu chini ya chifu Merere walipoingia katika nchi ya Nsewe, Nsewe alikufa wakati wa vita na watoto wake wakatoroka. Nswila allkwenda Ukonde, Zambi akakimbilia Unyamwanga na watoto wengine wakajificha chini ya machifu wengine. Nswila hakukata tamaa na kwa msaada wa machifu wa Unyamwanga na Unyiha, akawashambulia Wasangu na akawashinda na kuwatoa toka nchini mwake. Nswila alipotuliza nchi yake, ndugu zake wote wakarudi toka walikokimbilia na wakamheshimu sana kwa kitendo alichokifanya cha kuwafukuza Wasangu toka Usafwani, lakini hawakumkubali kama yeye ndiye chifu mkuu wa Usafwani. Badala yake kila mmoja wao alitawala sehemu aliyopewa na baba yao Nsewe.

KIPINDI CHA MAJILIO YA WAGENI NA VITA 1845 — 1893

Katika mwaka 1845 Wangoni kutoka Ufipa ambako waligawanyika baada ya kufa kiongozi wao, waliingia katika nchi ya Usafwa na kuishambulia kikatili sana wakiua wanaume na kuwatia utumwani wanawake na watoto, na huku wakichoma vijiji na kuharibu mimea. Njaa ikatokea na Wasafwa walilazimika kula mizizi na matunda ya porini. Njaa ilikuwa kali sana hata Wangoni wakalazimika kuiacha nchi ya Usafwa na kwenda mahaii pengine. Wasafwa ambao walikuwa wamekimbilia milima ya Igale, Umalila na Mporoto, wakaanza kurudi Usafwani pole pole tena mmoja mmoja. Wakajenga nyumba, wakalima mashamba na wakawa na amani kwa muda mfupi.

Katika sehemu ya Mashariki ya Usafwa bonde la Ufa lapitia na ndio iliyokuwa njia kuu ya wafanya biashara ya utumwa na mara nyingi sana Wasangu na Wahehe walipitia katika bonde hili kuja kuwashambulia Wasafwa. Bonde lenyewe latokea sehemu za Dodoma kuja Iringa - na kuungana na bonde la Usangu - Laendelea hadi Uyole - Mbalizi - Utengule - hadi Tunduma mpakani mwa Zambia na Tanzania. Hii ndio iliyokuwa njia yao kubwa na sehemu zingine hazikuwezekana kupitia kwa sababu ya milima mirefu. Wahehe waliwashambulia Wasangu na walisukumwa mpaka Usafwani ambako chifu Lyoto alijaribu kuwazuia Wasangu na vita ikapiganwa sana mahaii paitwapo llomba -sehemu iliyo karibu sana na mji wa Mbeya. Chifu Lyoto alishindwa na kuuawa. Merere akapeleka mifugo, wanawake na watu fulani katika uwanda wa Usafwa. Yeye mwenyewe Merere aliendelea kupigana vita katika milima ya Ukimbu na kumfukuza Chifu Zumba ambaye alikuwa mtawala wa milima ya Chalangwa, na akapiga kambi yake katika nchi ya Ubungu. Wabungu walipojaribu kumwua, Merere akaenda Kiwele Kaskazini - Mashariki. Watu wa Merere hawakuipenda hali ya nchi kwa hiyo Merere akalazimika kurudi Usangu.

Baadaye Mkwawa akaanza tena kutaka kupigana na Merere, lakini safari hii Merere akakimbilia katika milima ya Mporoto halafu akaingia katika nchi ya Ukukwe ya chifu Mwakalinga ambako aliwaua Wanyakyusa wengi na kuteka mifugo mingi na kuipeleka Uporoto. Hali ya hewa ya unyevu unyevu ya milima ya Mporoto haikumpendeza Merere, kwa hiyo akalazimika kwenda katika milima ya Unyiha katika nchi ya chifu Mwashambwa akipitia milima ya Umalila. Chifu Merere alikaa huko mpaka alipomshinda chifu Mwashambwa, na baadaye akapigana na chifu Zambi upande wa Kaskazini Mashariki wa milima ya Umalila. Baadaye akaenda kufanya kambi yake Mpedjere chini ya mlima Mbeya. Wakati machifu wa Kisafwa waliposhambulia walifikiria kuwa jeshi lake Merere limedhoofika kwa vita vingi lilivyopigana, lakini chifu Malema ambaye alikuwa mtawala wa Wasafwa ya Magharibi karibu na milima ya Unyiha aliwahaini watu wake na hakushiriki katika kumshambulia Merere kama machifu wengine wa Kisafwa walivyoamua kumzunguka. Kwa hiyo Merere akapata mwanya wa kuweza kuwashinda machifu wa Kisafwa.

Mpedjere, ngome mpya ya Merere, ikaanza kujengwa na kutoka hapo aliweza kuwashambulia machifu wote wa Kisafwa mpaka wote wakamsujudu. Wakati wavita kule Mpedjere, chifu Mwalyego alishindwa vita na akakimbilia kwenye utawala wa chifu Zumba Kaskazini ya Mlima Mbeya. Wakati huu Merere alijijenga sana sana na kuimarisha utawala wake katika nchi ya Wasafwa na akajenga ngome kubwa sana ya mawe yenye kuta ndefu naakaiita ngome hii mpya "Utengule" ikiwa na maana "Mahaii pa amani", jina lile lile la mji wake mkuu sehemu za Usangu ulioitwa "Utengule", Kwa jinsi hii Merere aliuimarisha utawala wake. Katika nchi ya Usafwa na machifu wote wa Kisafwa wakaacha uchifu wao na kumtambua Merere kama ndiye chifu wa Usafwa ingawa hawakumpenda hata kidogo.

33

Chifu Zambi peke yake, akiwa mtawala wa sehemu ya milima, ya Umalila, alikataa kumtambua Merere kuwa kama chifu wa Usafwa na akakataa kufanya kazi chini yake. Chifu Zambi alikuwa na chuki nyingi na kwa ajili ya ujasiri wake akamwomba chifu Mkwawa wa Wahehe ili amsaidie katika kumshambulia Merere, na kwa bahati chifu Mkwawa akakubali ombi lake. Wahehe, machifu wa Kisafwa Mwalyego, Zumba, Mbuvi, wakaunganisha majeshi yao nawakauzunguka mji wa Utengule. Walijaribu kuzuia njia za kupatia chakula cha Wasangu waliokuwa wanaishi katika ngome ya Utengule na mpango huu uliwachukua miezi minne, na baadaye wakaushambulia mji wa Utengule lakini jeshi la Merere liliyarudisha nyuma majeshi yote ya Mkwawa. Pengine safari hii majeshi ya Mkwawa yangeweza kuwashinda majeshi ya Merere kama chifu Malema asingaliwapa chakula Wasangu wakati majeshi ya Mkwawa na Wasafwa yalipowazunguka. Mwishowe Mkwawa akaamua kuiacha vita hii na kurudi katika nchi yake. Baada tu Mkwawa kurudi kwake, Merere akaamua kulipiza kisasi kwa kuwaua Wasafwa wengi sana walioshiriki katika kumshambulia. Wale machifu wa Kisafwa ambao walishiriki katika kumshambulia Mwalyego, Mbuvi, Zumba, Mpyila na Zambi, kila mmoja alilazimika kumpa Merere binti yake mmoja ikiwa kama adhabu yao. Malema vile vile alitoa mabinti wake wawili na kumpa chifu Merere. Pia kila chifu ilimbidi atoe mazao yake ya mwaka na kumpa Merere. Lakini Merere alikuwa hataki amani, shida yake ilikuwa vita na akaviharibu sana vijiji vingi sana na kuwauza watu wengi utumwani. Mali hii ya wasi wasi iliendelea mpaka walipofika Wajerumani.

KUJA KWA WAMISIONARI 1892

Wamisionari wa kwanza walifika katika nchi ya Usafwa mwaka 1892 Januari, wakiwa Merensky na Nauhaus, ambao walikuwa wa madhehebu ya Misheni ya Berlin. Wamisionari wa Moravian walikuja baadaye. Mkurugenzi wa Misheni ya Moravian alimwomba Bwana Kootz na mkewe Kret-schmer kuja kwenye koloni za Kijerumani za Afrika ya Mashariki mwaka 1894, kuja kufanya kazi kama Wamisionari kwenye pwani ya Kaskazini ya Ziwa Nyasa. Miaka mitatu ya nyuma kazi ya Misheni ilikuwa imeanza katika nchi ya Unyakyusa - mahali paitwapo Ipyana. Walianza kazi yao katika mwaka wa 1894 mwezi wa Julai.

Baada ya kufanya kazi nusu mwaka na Bwana Th.Richard ambaye alikuwa amewasili huko mwaka wa 1891, waliombwa kwenda kufanya kazi ya kimisheni katika nchi ya Usangu. Wakati huo chifu Merere alikuwa amefanya urafiki na Wajerumani. Richard alifuatana na Bwana Kootz na Kretschmer katika safari hii na Misheni ikafunguliwa Utengule makao makuu ya chifu Merere na mahali ambapo Wasangu walikuwa wanaishi baadaya wao kufukuzwa Usangu na Wahehe. Utengule ikawa ndio makao makuu ya Misheni ya Moravian katika Usafwa na Usangu.

SERIKALI YA KIJERUMANI Serikali ya kikoloni ya Kijerumani ilianza kuleta amani katika nchi ya Usafwa kati ya mwaka wa

1895 na 1900. Serikali hiyo ilikomesha vita vya machifu na biashara ya utumwa, na baada ya kuwashinda Wahehe, serikali hiyo iliwafukuza Wahehe wote kutoka nchi ya Usangu, na pia Wasangu waliokuwa wanatawala nchi ya Usafwa waliambiwa warudi kwao Usangu, na chifu Mwaiyego akapewa utawala wake juu ya Wasafwa. Walakini Wasafwa hawakupata kuwa chini ya utawala wa chifu mmoja, kwa hiyo chifu Mwalyego alipotawazwa na Wajerumani kama chifu mkuu wa Wasafwa, machifu wengine wa Usafwa walikataa kumtambua.

Basi kwa kufuatana na masimulizi hayo hapo juu utaonaya kuwa jamii ya Kisafwa inachimbuko lake sehemu tatu, ya kwanza ni kwamba ukoo mmoja wa Kisafwa ulitoka Ugogo, ya pili ni kwamba ukoo mwingine wa Kisafwa ulitoka Ukinga, na ya tatu ni kwamba ukoo ule ule ulitoka Unyakyusa sababu nyingi za kihistoria na za Kiutamaduni zimeelezwa kuhusu kufika kwa Wasafwa katika nchi ya Mbeya na kukaa huko. Lakini sababu zingine zinazohusu jiografia hazikuelezwa kikamilifu - hasa kuhusu ukoo uliotoka Ukinga. Sababu moja kubwa ya kijiografia ambayo ilisababisha kuondoka kwa

34

Wasafwa kutoka sehemu za Ukinga ni kwamba nchi ya Ukinga imeinuka sana na mwinuko huu huwagawanya watu kuwa katika pande mbili zilizo tofauti ya hali ya Kijiografia, hata baadaye watu ambao pengine asili yao ni moja kuwa katika jamii mbili zilizo tofauti kabisa, ambazo lugha zao zatofautiana. Mambo yanapotokea hivi, basi kutoelewana kwaweza kutokea na kuchukiana pia kukatokea. Ngazi hii ikifikiwa basi kundi lisilotaka ugomvi huhamia mahali pengine ambapo kuna usalama zaidi na hali hii yawezekana kabisa iliwapata Wasafwa na kuamua kuhamia sehemu za Mbeya ambako maskani yao ya kudumu yalifanyika.

Jamii ya Wasafwa yagawanyika katika jamii hizi kubwa:-

(i) Wasongwe ambao huishi sehemu za mto Songwe; (ii) Wamalila ambao wanaishi katika milima ya Umalila. (iii) Wamporoto ambao huishi kwenye milima ya Mporoto. (iv) Wambwila ambao huishi kati ya Wasongwe na Wasangu. (v) Waguluhaambao huishi sehemu za lleya.

KILIMO Wasafwa walitumia majembe yao ya kwanza ambayo yalikuwa ya miti, yaani miti ilichongwa

vizuri kabisa mithili ya jembe halafu wakayatumia kwa kulimia. Katika kuchonga majembe ya miti, tezo na mashoka yalitumiwa, zana ambazo zilikuwa za chuma kilichotengenezwa toka Ukinga. Pia zana hizi hizi, mashoka na tezo, zilitumika katika kuchongea mizinga ya nyuki. Miti iitwayo 'Magambo' na miyombo ilifaa sana kutengenezea majembe. Mizinga ya nyuki ilichongwa kutokana na mti wowote ule. Baadaye sana, majembe ya miti yakaonekana hayafai ndipo majembe ya chuma kutoka Ukinga yakatumiwa zaidi na kuonekana bora zaidi.

Katika shughuli za kulima, kwanza walianza kulima mashamba ya chifu wao, yaani "Kwila", maana yake "Shamba la Chifu". Baada ya hapo kila raia alikwenda kulima shamba lake. Walakini kualikana katika shughuli za kilimo lilikuwa jambo la kawaida ili mashamba yamalizike upesi. Mtu alipotaka kualika wenziwe wamsaidie kulima mashamba yake, alipika pombe na chakula cha kutosha ili baada ya kulima watu waweze kula na kunywa pombe. Wale walioalikwa siku hiyo waliimba nyimbo wakati wa kula chakula na pia ngoma zilichezwa ili kuonyesha furaha kubwa ya chakula walichopewa. Iwapo jamaa mmoja alitokea kutokuwa na chochote, yaani hana pombe wala chakula cha kuwapa watu watakaolima shamba lake, aliweza pia kuwaalika wenziwe hapo kijijini ili wam-saidie kulima na kumaliza shamba lake. Wanakijiji waliweza kulima shamba la mwenzao bure. Baada ya mavuno kupatikana basi huyo jamaa aliyelimiwa shamba lake bure aliweza sasa kupika pombe na chakula na kuwakaribisha wale wale jamaa waliomlimia shamba lake hapo awali ili kuonyesha shukrani zake kwa msaada aliopewa alipokuwa yeye hana kitu cha kuwapa. Ilikuwa ni desturi kwa kila mwanakijiji kukubali kualikwa na mwanakijiji yeyote, na kukataa kumsaidia mwanakijiji katika kulima ilikuwa ni mwiko. kitendo hiki cha kulimiwa shamba bure mtu anapokuwa hana pombe wala chakula kiliitwa "Alimishumiwa", maana yake wanalima bure bila kuwapa chochote cha kula wanaolima shamba la mtu siku hiyo. Siku hizi Wasafwa wanaalikana katika shughuli za kilimo lakini si sana kama ilivyokuwa hapo zamani.

Katika nchi ya Usafwa shughuli za kilimo zaendelea wakati wowote katika mwaka kwa sababu hali ya hewa na ya ardhi yaruhusu sana shughuli ya kilimo iweze kuendelea mwaka mzima, ingawa sehemu zingine za usafwa hazina bahati ya kuwa na hali hii ya hewa na rnanufaa mengine mengine ya kuendeleza hali ya kilimo. Kuna mazao ya aina nyingi sana ambayo hulimwa nyakati mbali mbali tofauti na mazao hayo hupandwa kwa kutegemea ardhi na jiografia ya mahali penyewe kwa sababu jiografia ya nchi ya Usafwa yahitilafiana toka mahali hadi pengine. Kilimo chao maalum ni cha sesa, lakini pia wanalima matuta, ufundi ambao wameigatoka kwa Wanyakyusa. Watu wa Mporoto hulima matuta ya terrace ili kuzuia mmomonyoko wa udongo kando kando ya milima. Karibu robo moja ya. Wakulima wa Kisafwa hutumia trekta au plau lakini matumizi ya zana hizi mbili hutegemea jiografia ya mahali shamba lilipo.

35

MGAWANYO WA KAZI Katika jamii ya Kisafwa, baba huwa na shamba lake na mama huwa na shamba lake pia. Iwapo

baba ametangulia kumaliza shamba lake huenda kumsaidia mkewe. Kufanya hivi hakumfanyi bwana adai sehemu yoyote juu ya umilikaji wa shamba na mali iliyomo katika shamba hilo. Bali husaidia tu kwa imani, lakini shamba labakia kuwa ni la mwanamke. Kila mtu alikuwa na mamlaka juu ya shamba lake hata mavuno yake pia. Mavuno kutoka shamba la baba ndilo lilifanya ghala ya chakula cha familia nzima. Kama mke mmoja hakuvuna kiasi cha kutosha, basi mwanamke huyo aliweza kupata chakula toka ghala ya bwana yake. Lakini iwapo kila mwanamke ana chakula cha kutosha toka shambani mwake, basi bwana aliweza kuuza baadhi ya chakula toka kwenye ghala yake, ill kupata fedha za kununulia ng'ombe au mbuzi. Pia mwanamke alikuwa haingiliwi na bwana wake katika umilikaji wa chakula. Alikuwa na uhuru kabisa wa kuweza kuuza chakula chake kama alipenda. Watoto walikitumia chakula toka kwa mama zao katika 'Ibanza' yao bila wasi wasi bila kujali mama ya nani kapika chakula hicho. Lakini siku hizi ni vigumu kwa akina mama kulisha watoto wote sawa. Hujali sana watoto wao tu; wamekuwa wachoyo na hawawezi kuwalisha watoto wa mwingine kama ambavyo wangaliwalisha watoto wao wenyewe. Ubinafsi umewaingia sana kitu ambacho hakikujulikana hapo zamani.

Kabla ya kwenda kulima au kuvuna, mama hupika chakula asubuhi Hi waje wale mchana baada ya kazi. Umwagiliaji wa mashamba ulitumika kama Wasafwa wanavyotumia utaalamu huo kwa sasa. Mama, baba na watoto hulima pamoja.

KUVUNA Wakati wa kuvuna, ngano hukatwa shina zima na kisu halafu hulundikwa pamoja. Baada ya

kumaliza kuvuna, ngano yote hupigwa pigwa na mti (threshing) ili itoke kwenye masuke yake. Ulezi hukatwa vichwa vyake na kisu halafu huwekwa pamoja na baadaye huzitengeneza kwa kutenganisha punje zake toka kwenye masuke. Mahindi huvunwa kwa kukwanyua vigunzi vyake toka kwenye shina lake na kuwekwa pamoja. Kazi yote hii hufanywa kwa kualikana. Mtu mmoja peke yake alikuwa hawezi. Nyimbo ziliimbwa wakati wa kazi ya kuvuna na vyombo hivi, "Indili, Izeze, na Marimba" yalitumika katika kuwatumbuiza wafanyakazi.

GHALA

Chakula kilihifadhiwa katika ghala maalum zilizotengenezwa kwa kazi hiyo. Ulezi na ngano vilihifadhiwa katika vilindo vikubwa vilivyotengenezwa kwa kusuka matete pamoja kwa kutumia kamba za miyombo ambayo zama hizo zilipatikana kwa wingi karibu karibu na vijiji vyao. Mpaka sasa njia hii ya kuhifadhi mazao yatumika Usafwani kote.

Picha hii yaonyesha kilindo cha matete

36

Mahindi yalivunwa na kuanikwa penye uchanja kwanza ili yapate kukauka sawasawa. Baada ya hapo, mahindi yaliwekwa ndani ya kihenge kilichojengwa nje ya nyumba ya kulala. Hii ndiyo iliyokuwa ghala ya mahindi. Zamani hakukuwa na wizi na iwapo mtu fulani alionekana kuwa yu mwizi mtu huyo alizomewa sana na pia wanakijiji walimnyima mwizi huyu haki yake ya kuoa mke (Social Control). Kwa hiyo watu waliogopa kuiba ili wasije wakaambiwa ni wezi na kukosa mwanamke wa kuoa. Siku hizi wezi ni wengi mno hata wananchi huwa na wasiwasi sana katika kujenga ghala zao mbali na majumba yao. Sababu kubwa zinazofanya wizi uongezeke ni kwamba viongozi wengi wavijijini huogopa kuwafichua wezi na pia huhongwa pombe na wale ambao ni wezi. Basi jamaa hawa hushindwa kutekeleza wajibu wao sawasawa. Wakati mwingine mwizi aweza kukamatwa na wanakijiji na kumpeleka mwizi huyo kwa bwana hakimu. Wanapofika huko naye, hao wanakijiji wanaulizwa maswali kama wanao ukweli kwamba mtu waliyemleta ni mwizi. Basi wanakijiji wengi hukata tamaa na mara nyingi wanakijiji wengine hujichukulia madaraka mikononi mwao na kumwadhibu yule mwizi vibaya sana.

KUHAMA KWA WATU (MIGRATION)

Zamani watu walikuwa wachache sana na kuhamahama kwao kulikuwa kuchache. Kuhamahama kulitokea tu wakati njaa ilipoingia katika nchi fulani au vita kutokea, basi jamaa walihama. Kuhamahama kwa Wasafwa twaweza kusema kuwa walihama mara yao ya mwisho walipoingia nchi ya Usafwa miaka mingi iliyokwishapita. Shida zao zilikuwa ni hizo hapo juu zilizo wafanya watu wahamehame na kwa jumla kuhamahama kulisababishwa na maafa hayo. Siku hizi Wasafwa wengi, hasa vijana huhamia sehemu zile zilizo na nafasi ya kazi kama vile mji wa Dar es Salaam, sehemu zenye mikonge mingi - Tanga - Kilosa - Morogoro na kadhalika. Pia Wasafwa wengi walio vijana wamehamia nchi za Zambia ambako kazi nyingi zapatikana katika migodi na viwanda. Wasafwa wazee ndio hubakia nyumbani kwa sababu ya jukumu walilo nalo juu ya familia zao, na pia wao hawapendi zaidi kuhamia nchi za kigeni ambazo zina watu walio na desturi na mila tofauti na za kwao. Zaidi na zaidi wazee wa Kisafwa hubakia nyumbani wakilima mashamba yao. Kundi lingine lililo na uhuru wa kuhamia sehemu zilizo na nafasi za kazi ni wale Wasafwa ambao hawajaoa.' Hawa huhamia sehemu zilizo na kazi bila taabu kwa sababu hawana matatizo ya familia. Lakini kwa jumla vijana wa Kisafwa wanaotaka kujaribu bahati yao katika maisha yao ndio wengi huhama kila mwaka.

WANYAMA WAFUGWAO

Wasafwa si wafugaji hodari kama jamii zingine za Watanzania zilivyo. Wamasai, Wambulu, Wagogo, Wahehe, Wanyiha ni wafugaji wakubwa wa ng'ombe. Lakini Wasafwa walifuga wanyama wachache sana na mpaka sasa wanafuga wanyama wachache sana katika vijiji vyao. Walifuga.mbuzi na ng'ombe wachache sana kwa ajili ya kutambika au kuwachinja wakati wa kilioni kwa ajili ya mboga, kwa wale waliopo kilioni. Siku hizi ng'ombe, mbuzi, kondoo, wanafugwa kwa ajili ya maziwa na nyama. Pia kuku na nguruwe wafugwa kwa sababu ya mayai na nyama.

37

Familia ya Kisafwa inaweza kuwa na baba mmoja, mama mmoja pamoja nawatoto, au inaweza kuwa na baba mmoja, mama wawili au watatu pamoja na watoto wao. Hapo zamani familia zilikaa katika vijiji kwa kufuata ukoo. Kwa hiyo kila kijiji kilikuwa na ukoo fulani. Mtu alipoposa msichana basi alihamia katika kijiji cha msichana na kukaa huko na kuongeza jumla ya familia. Kwa hiyo familia iliyokuwa na mabinti wengi iliweza kupanuka sana na kufanya kijiji chao wao wenyewe cha wakwe na baba na mama mkwe na watoto na wajukuu, na kadhalika. Utaratibu huu wa kuishi pamoja namna hii kwa kufuata undugu bado unafuatwa na watu wengi katika nchi ya Usafwa. Jamii ya Wasafwa ni jamii inayofuata urithi kwa upande wa baba. Katika kurithi baba akifa ni lazima mtoto wa kwanza wa kiume arithi mali ya baba yake. Lakini katika kurithi mall ya baba, yampasa mtoto huyo aonyeshe busara safi, bila hivyo hawezi kurithi mali ya baba yake kwa sababu ya kukosa busara. Mtoto wa pili aweza kuchaguliwa na ukoo wa baba ili aweze kurithi iwapo alionyesha busara safi, zaidi kuliko kaka yake mkubwa. Kwa kawaida warithi walitoka kwa mke mkubwa, na iwapo mke mkubwa alikosa kuzaa watoto wa kiume na akazaa watoto wa kike, basi mtoto wa kiume wa mke wa pili aliweza kurithi.

Mirathi iligawanywa kwa ndugu zake wote, lakini yeye mrithi alizidishiwa mirathi zaidi kwa sababu yeye ndiye aliyebadili nafasi ya baba yake na alipaswa kuwatunza ndugu zake sawa sawa kama baba yao alivyokuwa akiwatunza alipokuwa bado yu hai. Siku ya kurithi, pombe nyingi ilipikwa na kutengenezwa na chakula kwa wingi kilipikwa ill watu wale na kunywa na kufurahi sana. Watu walicheza na kuimba nyimbo za furaha. Utaratibu huu wa kurithi mali ya baba bado unafuatwa na Wasafwa wengi ingawa yapo mabadiliko mengi.

NDOA Kwa kawaida mvulana aliweza kusikilizana na msichana anayetaka kumchumbia. Baada ya

hapo, mvulana alikwenda kwa baba yake na kumwambia ya kwamba anamtaka binti ya fulani am-chumbie. Basi babake aliweza kumwambia mzee mwenzie pale kijijini kuwa aende akamwambie baba ya binti kuwa wanamtaka kumchumbia binti yake. Iwapo mzee wa binti huyo anakubali ombi la wazee wenzie, basi posa inapelekwa.

Njia ya pili ya kumposa msichana ni kwamba mvulana na msichana wanakubaliana waoane. Baada ya kufanya hivyo, wanaamua wote wawili kutoroshana bila ya wazee kujua, isipokuwa wazee wanaambiwa baada ya kutoroshana hao vijana. Kwa kawaida msichana hutoroshwa na mvulana ambaye atakuwa mumewe wa maisha. Mvulana humpeleka msichana huyo aliyetoroshwa kwa baba yake mvulana. Mzee wa mvulana akishaona mambo yamefikia kiwango hicho, huondoka haraka kwenda kwa mzee pale kijijini na kumwomba aende mara moja kwa baba ya msichana aliyetoroshwa na kumwambia ya kuwa wanataka kumuoa binti yake na kwamba kwa sasa binti huyo wamem-chukuwa tayari yuko nyumbani kwao hao jamaa. Basi baba ya binti hukubali na kuwaambia ya kuwa wakalete mahari.

Kwa kawaida mahari ilikuwa kuku au ng'ombe au mbuzi mmoja au jembe lapelekwa kama posa au mahari. Zamani mahari yalikuwa si mengi na tena yalikuwa hayadaiwi sana kama siku hizi iwapo mtu aliyehusika alikuwa hana chochote bali alitaka kuoa mwanamke. Vijana wa Kisafwa walikuwa hawana taabu katika kuoa mke kwa sababu mahari yalikuwa rahisi sana. Lakini siku hizi mahari yamekuwa makubwa; Ng'ombe sita au zaidi hudaiwa kama mahari na hii yasababisha kushindwa kwa vijana wengi wa Kisafwa kuoa wanawake na wanawake kushindwa kuolewa. Kwa hiyo namba ya wanawake wasioolewa huzidi na ya wanaume yaongezeka, na mwishowe umalaya waongezeka nchini. Kwa jinsi hii, ile mila ya zamani ya Wasafwa ya kuukataa umalaya kabisa katika nchi yao umeanza kupungua. Yasemekana ya kuwa mtindo huu wa kutoza mahari mengi sana umeigwa na Wasafwa toka kwa Wanyakyusa ambao wana desturi ya kutoza mahari mengi watoto wao wanapoolewa. Tabia hii ya kutoza mahari mengi ilianza kuigwa tangu mwaka 1919.

Baada ya mahari kupelekwa kwa baba ya msichana, basi yule kijana huanza kumsaidia kazi nyingi baba mkwe wake. Wakati mwingine aweza kulima shamba la mkwewe nyumbani kwake. Iwapo watoto hawakutoroshana, basi baada ya posa kupelekwa kwa baba mkwe, wazazi wa

39

msichana wanaweza kumleta binti yao kwa bwana yake wakati wowote ule na wala hakuna sherehe kubwa katika kufanya hivi. Baada ya ndoa, mvulana pamoja na msichana (mkewe) huhamia kwa baba mkwe na kujenga nyumba yao huko. Ilikuwani lazima msichana avunje ungo ndipo aweze kuposwa. Inampasa mtoto wa kiume amsaidie baba wa msichana kama posa au mahari ilirudishwa kwa mwenyewe baadae kama alishazaa mara moja kwa baba mkwe. Mtamba alibakia kwa baba mkwe.

NDOA YA SIKU HIZI Mvulana baada ya kupatana na msichana anayetarajia kumwoa humpa msichana huyo shillngi

ishirini, na msichana huchukua hizo shilingi ishirini na kununua nguo yoyote ile inayompendeza, bila ya kuwaeleza wazazi wake. Kama wazazi wake wakimwuliza kapata wapi nguo aliyovaa, huwaambia kauza kuni ndizo zilizomletea fedha za kununulia nguo. Baada ya hapo, mchumba wake aweza kumchukua mchumba wake bila ya wazazi wa msichana kujua na kumpeleka mchumba wake hadi kwa mama yake mvulana ambaye naye hutoa shilingi ishirini na kumpa huyo mchumba wa mtoto wake. Baada ya kufanya hivyo, habari zinaietwa kwa wazazi wa msichana kuwa mtoto wao wanaye nyumbani kwao na kwamba wanataka kumuoa. Wazazi wa msichana hukubali na baada ya siku nne hivi, msichana hurudishwa kwa wazazi wake. Siku ya kwanza ambayo msichana huchukuliwa na mchumba wake, anapofika mlangoni kwa nyumba ya mama ya mchumba lazima apewe shilingi 150/- na mchumba wake. Safari ya pill, msichana huyo huchukuliwa na mchumba wake baada ya kukaa kwao msichana miezi mitatu au sita, na sasa msichana hupelekwa moja kwa moja hadi nyumbani kwa mvulana, ambako hulala siku mbili hivi, halafu baba ya mvulana huwaambia wazazi wa msichana kuwa binti yao yuko hyumbani kwake. Wazazi wa msichana humwambia baba ya mvulana kuwa warudishiwe binti yao siku ya pill. Basi msichana hurudishwa saa za jioni siku hiyo ya pill na msichana hupewa shilingi tatu au nne hivi kama kuku wa kuwapa wazee wake ikiwa kama ni adhabu. Msichana hukaa kwa wazazi wake kiasi cha miezi miwili au sita kwa kutegemea mahari aliyonayo mchumba wake. Kama mahari ipo, basi msichana hatakaa miezi mingi kwao bila kwenda kwa mchumba wake ambayo hupelekwa kidogo kidogo kwa wazazi wake. Safari ya tatu, msichana huchukuliwa tena na mchumba wake na kupelekwa nyumbani kwa mchumba wake. Mpaka wakati huu msichana hawezi kupika chakula cha mume wake sababu bado hajawa ni mke. Wakati wote huu wanapata chakula chao toka kwa mama ya mvulana. Msichana hukaa siku mbili kwa mchumba wake na siku ya tatu baba ya mvulana hutoa habari kijijini kwao kuwa waanze kutayarisha pombe na vyakula vichache. Baada ya kuona kuwa pombe imekuwa tayari, baba wa msichana huwaambia wazazi wa mvulana ya kuwa wawarudishie binti yao. Wakati huu baba wa mvulana hujitayarisha sawa sawa na huvunja fedha kiasi cha shilingi mia nne ambazo huwa katika mahela mahela au vikoroti.

Siku hiyo wazazi wa msichana hunywa pombe sana na huwachagua wazee fulani ambao hutumwa kwa baba ya mvulana na kusema kuwa wanamtaka binti yao. Halafu baba wa mvulana humchagua mtu mmoja wa kumpeleka msichana kwa wazazi wake. Mtu huyo aneyempeleka msichana kwa wazazi wake ndiye anayeshika helazote hizi zilizovunjwa na mzazi wa mvulana, na pia jamaa huyu hufuatana na ndugu wa mvulana wakati wa kumpeleka msichana nyumbani kwao. Msichana hutembea tembea kidogo kidogo ili aweze kupewa fedha nyingi sana, na hujaribu kutafuta sababu nyingi na visingizio vingi ill aweze kusimama, na akisimama hupewa fedha ili aweze kutembea. Kwa njia hii msichana huyo aweza kuchuma fedha nyingi sana kiasi cha shilingi mia tatu au zaidi kabla hajafika nyumbani kwao. Wafikapo nyumbani kwa wazazi wa msichana, wale waliokuja kumsindikiza msichana hupewa pombe kiasi cha madebe thelathini hivi na kuyapeleka nyumbani kwa baba ya mvulana. Huko nyumbani kwa wazazi wa mvulana hunywa pombe waliyopewa na wazazi wa msichana. Lakini wazazi wengine wa mvulana wanaweza kutoa kila mmoja shilingi tatu halafu kila mmoja akichukua debe moja la pombe na kwenda nayo nyumbani kwake na kuinywa. Kila ndugu ya baba ya mvulana aweza kutoa shilingi tatu na kuchukua debe moja la pombe.

Msichana hulala siku moja nyumbani kwao. Baada ya siku hiyo, baba ya mvulana huenda nyumbani kwa wazazi wa msichana kwenda kumpa baba ya msichana shilingi kumi na tano. Katika

40

safari hii, baba wa mvulana hufuatana na wenzie watatu au watano hivi. Baada ya kupokea zile shilingi kumi natano, baba wa msichana huwapa binti yake wazazi wa mvulana. Kesho yake, baada ya msichana kufika nyumbani kwa bwana yake, huanza kutayarisha mafiga na kupika chakula cha bwana yake kwa mara ya kwanza katika maisha yake ya kuwa mwanamke aliyeolewa.

Bwana yake hawezi kula chakula hicho kilichopikwa na mke wake mpaka kwanza mke ampe bwana yake shilingi sitini ndipo ale chakula chake. Chakula kingine kilichopikwa na huyo mke kinapelekwa kwa baba mkwe. Mali kadhalika baba mkwe hawezi kula chakula cha mkwe wake mpaka naye apewe na huyo mkwe wake (mke wa mtoto wake) shilingi ishirini na tano ndipo ale chakula chake. Bila ya kupewa hizi shilingi ishirini na tano baba mkwe hawezi kula chakula cha mkwe wake. Hizo shilingi ishirini na tano zatiwa pembeni mwa sahani za chakula wakati wa kupeleka chakula kwa baba mkwe. Baada ya hapo, msichana huyo huendelea kuwapelekea chakula baba na mama ya bwana yake, mpaka watakapomkataza asiwapelekee chakula tena. Sasa atakuwa mwanamke kamili nyumbani.

SIFA ZA WACHUMBA

Wachumba wanatakiwa wawe na sifa nzuri kabla ya kuoana, yaani wanatakiwa wasiwe wezi au wasitoke katika ukoo wa watu walio wezi wasiwe malaya. Wanatakiwa wawe wema na wasiwe wachoyo bali wawe wakarimu. Inawabidi watoke kwenye koo zilizo nzuri na bora. Magonjwa kama ukoma yalitiliwa mashaka makubwa katika posa. Iwapo mchumba mmojawapo anatoka katika ukoo ulio na ugonjwa wa ukoma basi mchumba huyo itamwia vigumu sana kumpata mchumba mwenzie. Kwa kawaida mkoma hutengwa mbali sana na watu wengine na kujengewa nyumba yake ya pekee chini ya mti wa mlagalila, na anapokufa mkoma huzikwa chini ya huo huo mti halafu mti wenyewe hukatwa ili uangukie nyumba yake na vyombo vyake vyote vifunikwe kabisa. Makusudi ya kufanya hivi ni kwamba Wasafwa wanajaribu sana kuepusha watu wasio na ugonjwa huu wasikamatwe nao. Walakini sifa zote hizi zilizoelezwa hapo juu kuhusu wachumbazimeanza kusahauliwa, na sasa watu wengi wa Usafwa hawaangalii sana sifa hizi kwa sababu ya elimu nyingi na pia mwingiliano wa utamaduni mbali mbali wa kigeni.

Sherehe haikuwa kubwa sana bali kitu kikubwa sana katika ndoa yao kilikuwa kudumisha ndoa yao kwa wale waliohusika. Ndoa za Kisafwa zilidumu sana bila kuvunjika, lakini siku hizi ndoa nyingi zinazofungwa hazidumu sana kwa sababu ya mabadiliko ya maendeleo yaliyokwisha tokea yakiambatana na utamaduni wa kigeni. Ingawa kuna sherehe kubwa zinazofanyika siku hizi wakati wa arusi, lakini ndoa nyingi hazidumu sana kama zamani. Ingawa kuna mabadiliko mengi ya utamaduni katika jamii ya Wasafwa lakini Wasafwa ni watu ambao hawakupoteza sana utamaduni wao kama jamii zingine za mkoa wa Mbeya zilivyopoteza utamaduni wao.

Kila msichana alipimwa bikira yake kabla ya kupelekwa kwa bwana yake. Hii ilikuwa ni desturi ya jamii nyingi za Mkoa wa Mbeya. Kwa kawaida wasichana wote wa Kisafwa walitunza bikira zao vizuri sana mpaka siku ya kuolewa. Lakini siku hizi nidhamu hii imeanza kupungua uzito wake kwa sababu ya mwingiliano wa ustaarabu mbali mbali.

TALAKA

Hapo zamani talaka katika jamii ya Kisafwa zilikuwa nadra sana kupatikana. Mwanamke kutoka kwa bwana yake na kwenda kwa bwana mwingine ilikuwa shida. Pia bibi kumtoroka bwana na kutorokea kwa bwana mwingine ilikuwa vigumu sana. Iwapo mwanamke alifanikiwa kufanya hivyo, vita kati ya kijiji alikotoka na kijiji anakotorokea ilizuka. Ng'ombe na wanawake wa kijiji alikotorokea walitekwa kwa hiyo kumtorosha mke wa mtu au kumghilibu akili zake, watu waliogopa sana matokeo yake. Kwa hiyo upuuzi huu wa kutoroshana au kumtaliki mwanamke ovyo ulikuwa nadra sana. Kwa hiyo vita ilipiganwa na kusababisha hasara kubwa kwa pande zote, hasa kwa wanakijiji waliom-

41

torosha mwanamke wa kijiji kingine. Kwa jinsi hii, wanawake waliogopa sana kuwatoroka mabwana zao kwa sababu ya kuepuka vita kati ya kijiji na kijiji, na pia wanaume waliogopa kufanya kitendo hiki kwasababu hii hii ya kuepukana na vita baina ya kijiji na kijiji. Lakini siku hizi za mamboleo, mtindo huu wa kuwatorosha wanawake au wanawake kuwatoroka mabwana zao umeenea sana katika jamii ya Kisafwa. Sababu zilizowafanya baadhi ya Wasafwa kuiacha nidhamu yao ya bwana kubakia na mke au mke kubakia na bwana yake ni kwamba Elimu ya kikoloni, mchanganyiko wa jamii mbali mbali; vimedhoofisha nidhamu hii. Na yasemekana kuwa mtindo huu wa kuachana achana kwingi kati ya bwana na mke hasa kumeanza kwenye miaka 1930. Iwapo bwana na bibi walichoshana kwa amani, basi mahari yote ilirudishwa kwa bwana. Siku hizi kuna utaratibu mwingine uliowekwa na serikali ya TANU.

DESTURI ZA KULA CHAKULA

Zamani Wasafwa walikuwa wanakula pamoja kijijini. Nyumba ilijengwa katikati ya kijiji na iliitwa Ibanza, yaani nyumba ya kulia chakula na pia kulala wanaume wote. Ilikuwa vigumu kwa mwanaume yeyote kwenda kulala katika nyumba ya mkewe. Hii haikuwa desturi yao. Nyumba zao zilijengwa pamoja. Siku hizi 'Ibanza' imetoweka- bali kila familia inaweza ikawa na Ibanza' yake kwa ajili ya watoto wake ili waweze kula pamoja. Mtu mkubwa hawezi kula katika Ibanza kwa sababu utaratibu wa zamani haupo tena.

Maji ya kunawa yaliletwa katika kata na kila mtu alinawa maji, yaliyokuwa safi na maji machafu yalimwagikia chini halafu kila mtu alikata kipande cha ugali na akakiweka juu ya kiganja cha mkono wake ndipo akala. Hata kunywa pombe kila mtu alimiminiwa pombe mkononi pake, ndipo anywe. Lakini siku hizi watu hutia maji ndani ya bakuli na watu wote hunawa maji hayo hayo ambayo kila mtu ametumbukiza mkono wake na kunawa. Maji hayo huwa ni machafu sana. Ni rahisi kueneza magonjwa kwa kunawa maji ya namna moja. Watu wanapokunywa pombe hutumia mkenge mmoja unaotumiwa na kila mmoja.

Wakati wa kula ilikuwa lazima aanze mkubwa ndipo hufuata mtoto. Wakati wa kumaliza kula ilikuwa lazima mtoto awe wa mwisho kumalizia kula, na ilikuwa ni lazima mtoto aondoe vyombo vya chakula. Nyama iligawanywa na mkubwa. Watoto wa kike walikula pamoja na mama zao. Lakini siku hizi desturi hizi zimeanza kusahauliwa kabisa na watu wameiga desturi za kigeni ambazo baadhi yake si desturi nzuri.

MAMA ANAYEZAA MAPACHA

Mama wa Kisafwa anapozaa mapacha hutengwa na bwana yake na kulala nje ya nyumba yake, yaani upenuni pamoja na mapacha yake. Kesho yake mbiu yapigwa kijijini kuwa kwa fulani kuna mapacha na kwa hiyo watu wasiende kulima kwa muda wa siku tatu, kwasababu mtu akienda kulima wakati mapacha yamezaliwa, yaaminiwa kuwa chakula hakitastawi shambani, kwa sababu yaonekana kuwa ni mkosi kuzaa mapacha. Wakati wa siku tatu hizo wanakijiji huwajengea kijumba chao hao jamaa waliozaa mapacha (bwana na bibi) mbali kidogo na kijiji chenyewe. Halafu bwana na bibi wenye mapacha hukaa katika kijumba chao kwa muda wa miezi miwili bila kuja kijijini. Chakula wanaletewa na mashamba yao yanalimwa na ndugu zao. Baada ya hiyo miezi miwili jamaa za hao ndugu hukoroga pombe na huwatangazia wanakijiji kuwa wanakwenda kuwatoa ndugu zao kule walikowekwa. Halafu siku hiyo nguo za wenye mapacha zavuliwa na kutupwa huko huko waliko na huvaa nguo mpya au nguo zingine ambazo hazijatumiwa wakati hao jamaa walipokuwa katika shughuli ya kutengwa. Nywele zao zanyolewa na ndipo wanapelekwa nyumbani kwao kwa zamani. Baada ya hapo huanza kuishi maisha ya kawaida na kufanya kazi kama kawaida. Desturi hii yaanza kufa katika sehemu zingine za Usafwa kwa sababu ya elimu ya siku hizi.

42

MAMA ALIYEFIWA NA BWANA YAKE

Mama aliyefiwa na bwana hutengwa na kujengewa kijumba chake cha muda mbali kidogo na nyumba yake ya kawaida. Mama huishi katika nyumba hiyo kwa muda wa mwezi mmoja. Wakati anapokoka moto wake hapulizii na pumzi yake bali hupepea moto huo na kipande cha bati au debe. Hali kadhalika mama mzaa mapacha hutumia kipande cha bati au debe kupulizia moto upate kuwaka; baada ya mwezi mmoja, mama mjane hutolewa nje baada ya ndugu zake kukoroga pombe kwa ajili ya sherehe hii. Mama mjane hunyolewa nywele, nguo zake alizokuwa akizitumia katika kijumba cha kutengwa zatupwa. Hupewa dawa fulani na mganga ili anywe ili kuondoa balaa jingine toka mwilini mwake. Baada ya kukaa mwaka mjane anaweza kurithiwa na ndugu ya marehemu pamoja na watoto wake na watoto watakaozaliwa wataitwa kwa jina la mrithi. Katika kufanya hivyo lazima pombe ya marehemu ikorogwe na kunywewa.

Iwapo mtoto wa kwanza katika familia amefariki, basi maiti yake itazikwa kwa baba ya mama yake kwa sababu kwa mila mtoto wa kwanza katika familia ni mtoto wa baba ya mama. Kwa hiyo anapokufa anazikwa kwa baba ya mama. Mtoto wa pili akifa huzikwa kwa baba ya baba ya marehemui kwa sababu ndiye mtoto wake kamili. Mtoto wa tatu na kuendelea huwa ndio mtoto wao, yaani wazazi wa mtoto.

MAMA KUPATA MIMBA BILA KUPITIA HALI YAKE

Mama akipata mimba bila ya kupitia hali hii, watu huwa na mashaka na wasi was! mwingi sana, kwa sababu hii yaonyesha ni balaa kubwa sana kwa nchi. Ili kuthibitisha kitendo hiki cha kushika mimba bila kupitia hali yake ya kawaida jamaa huenda kwa mganga kupiga ramli na baada ya kuthibitishwa na mganga, wananchi waliotumwa kwa ajili ya shughuli hii hurudi kijijini kwao na kumuuliza mama huyo kama yaliyokwisha semwa na mganga ni kweli na mama, huitika kuwa yaliyosemwa ni ukweli mtupu. Baada ya mama kukubali hayo, bwana yake hutoa mbuzi mmoja kwa chifu na kusema maneno haya:—

Chifu tumeharibu nchi yako kwa hiyo tunatubu". Chifu hupokea mbuzi na kuwaita wazee anaoshirikiana nao katika ibada mbali mbali, halafu mbuzi huyo huchinjwa huku mtawala huyo akisema maneno machache ya sala kama: —

"Mtu huyu anasema ameharibu nchi na ametoa mbuzi huyu na kutubu.

Kwa hiyo msifanyie lolote baya!"

Basi mbuzi huchinjwa halafu nyama yachomwa na kuliwa na wazee wenyewe. Basi bwana na bibi wanaohusika wanatengwa, mahali mbali mpaka bibi amejifungua. Baada ya kujifungua wananyweshwa dawa wote wawili pamoja na mtoto ili wasije wakapatikana tena na janga hili siku nyingine. Halafu wanarudishwa nyumbani kwao na kuishi maisha ya kawaida.

KUOTESHA MEMO YA JUU KWANZA

Iwapo mtoto mdogo wa mtu fulani ameotesha meno ya juu kwanza, hii huonekana kama ni mkosi mkubwa katika nchi yote. Mganga hutafutwa ili awanyweshe dawa hao jamaa na kuwatenga wasichanganyikane na watoto wengine katika nyumba yao wenyewe. Pia vyombo vyao wanavyotumia huwa ni maalum na hawawezi kutumia vyombo vingine vyo vyote katika nyumba. Hao jamaa wanaohusika wanakaa katika hali hii kwa muda wa wiki mbili au tatu hivi. Halafu mganga huwatoa na kuwapa dawa ya kuendelea kumpa mtoto.

43

UTAWALA

Zamani Wasafwa walikuwa na machifu wengi sana kama nilivyoeleza katika historia yao hapo kwanza. Kila chifu alikuwa na watu wa kumsaidia katika utawala na hasa wazee ambao wengi wao walishirikiana na chifu wao katika matambiko mbali mbali. Wasafwa hawajapata kuwa chini ya mtawala mmoja kabla ya kuja wakoloni. Kila sehemu ya Usafwa ilikuwa na mtawala wake na mtawala alipofariki, jamii yote katika utawala wake huyo chifu ilimchagua mtu na kutawala. Kwa kawaida Wasafwa walimchagua chifu wa kuwatawala kwa kufuatana na busara aliyokuwa nayo huyo mtu anayechaguliwa. Uchaguzi haukufuata mtoto mkubwa tu wa chifu la, ball busara yake aliyoonyesha kwa watu ndiyo ilikuwa sifa kubwa sana.

Mtu ye yote aliyevunja sheria alihukumiwa kutubu na baadaye kulipa ng'ombe mmoja kwa wazee (mafumu). Bila ya kulipa ng'ombe, mvunja sheria alilaaniwa. Kodi zama hizo ilikuwa kila raia kwenda kulima shamba la Mwene (Mtawala), na shamba hili lilikuwa kama shamba la ushirika hivi. Kama mtu hakuenda kulima shamba la Mwene, kuku wake alikamatwa kama adhabu yake ya kutofika kulima shamba la Mwene.

Raia walipeleka shida zao kwa mafumu wadogo halafu toka hapo shida zilipelekwa kwa wafumu wakubwa na kuendelea mpaka kumfikia Mwene mwenyewe.

KIFO

Mtu akifa watu hukusanyika pale kilioni. Watu wengine huleta kuku, wengine huleta nguo na wengine huleta chakula. Mtu anapokufa sababu inatafutwa kwa nini kwa kupiga ramli. Kitendo hiki cha kupiga ramli kimeigwa toka kwa Wanyiha, Wakinga na Wanyakyusa. Zamani kabla ya kuiga, kupiga ramli watu kijijini waliwauliza familia yake kama wametenda jambo moja ovu ambalo limesababisha kifo cha marehemu. Iwapo mtu mmoja mbaya aliingia ndani kumtazama mgonjwa na mgonjwa akafa baadaye, mtu huyo mbaya alilaumiwa sana na kijiji. Ilikuwa ni mwiko kwa mtu anayefahamika kuwa ni mbaya kwenda kuwaangalia wagonjwa, walimokuwa wanauguzwa kwa kuogopa kuwa hao watu waovu wangeweza kusababisha vifo vya wagonjwa. Mgonjwa alitunzwa vizuri na watu wabaya

walizuiliwa wasifike kumtazama mgonjwa. Mtu akifa lazima wamzike siku ya pili yake ili kuwapa nafasi wanaohusika kupashwa habari kuhusu kifo hiki. Iwapo ramli imemtaja mtu fulani kijijini ndiye kamchawia marehemu basi huyo mchawi hukamatwa na kuzikwa karibuni akiwa yu hai. Kwa hiyo utaona yakuwa uchawi ulikuwa hautakiwi kabisa katika jumuia ya Wasafwa. Kumzika mchawi angali hai ni desturi ya zamani ambayo haifuatwi siku hizi.

Siku hizi mtu anapokufa ghafla wanakijiji huchimba kaburi na mganga huja kupasua maiti ili kutaka kujua ni nini kilichosababisha kifo cha huyo marehemu. Kama ni uchawi uliosababisha kifo,

44

wanakijiji huenda kwa mganga kupiga ramli na mganga mwenyewe, kwa kufuatana na ufundi wake, humtaja yupi ni mchawi ambaye kafanya kitendo hicho. Habari zinazomtaja mchawi zinaletwa kijijini, na mchawi anayetajwa katika ramli kuhusu kifo cha marehemu huulizwa mbele yahadhara kama kweli katenda hivi. Mtu huyo akikubali kuhusu jambo hili, basi yeye pamoja na wale wpte alioshirikiana nao wanafukuzwa kijijini pale kwenda kijiji kingine. Iwapo huyo mchawi anayedhaniwa katenda jambo hili anataka kuhamatoka kijiji chake alimofanya kitendo cha uchawi, basi, wanakijiji wanamwambia kuwa wanakijiji wote watamuua kama mpango wao ukifaulu.

KUZIKA Kwa kawaida Wasafwa hutumia nguo za kawaida kuzikia hasa nguo zilizokwisha tumiwa. Kama

mtu aliyekufa ni mtu mkubwa, kaburi lake huchimbwa ndani ya nyumbayake halafu maiti huzikwa humo, kama ni Mwene, basi huyu huzikwa mahali.patakatifu na nyumba hujengwa juu yake. Iwapo mtu amezikwa katika nyumba, nyumba hiyo itaendelea kukaliwa na familia yake.

Iwapo maiti ilipasuliwa, vitu fulani vyatolewa toka kwenye maiti. Baada ya kaburi kumalizika kuchimbwa maiti inazikwa na inazikwa kiasi cha robo tatu ya kaburi halafu hushindilia sawasawa. Baada ya hapo wale watu waliokuwa wakipasua maiti huchukuwa sehemu zile zilizotolewa kwenye maiti ambazo zilikuwa bado kufukiwa kaburini na wanazitia kaburi ni nakuendelea kufukia. Baada ya hapo waganga huenda kwenye kaburi wakati wa usiku, na kabla ya hapo tangazo latolewa kuwa mtu yeyote asiwepo mahali karibu na kaburi na hao waganga hutia dawa fulani kwenye kaburi.

Hapo awali mtu aliyeugua ugonjwa unaoponyeka, aliweza kuuguzwa bure bila malipo. Walakini baada ya kupona ugonjwa wake ndipo mgonjwa, kwa hisani yake kwa msaada alioupata toka kwa mganga wake, aliweza kutoa mbuzi au chochote kama ndiyo shukrani yake. Mgonjwa wa safura alipokufa alizikwa pamoja na vyombo vyake vyote asije akawaambukiza watu wengine ugonjwa huo. Mgonjwa wa ugonjwa wa kawaida alitumia vyombo vyake maalum peke yake wakati wa kuugua ugonjwa huu.

Siku hizi mambo mengi yameanza kusahauliwa kabisa. Kwa mfano, mchawi hawezi kuzikwa na wanakijiji akiwa yu hai, wala mtu mwenye safura hatengwi na watu wengine katika familia na kadhalika.

MAVAZI Hapo awali mavazi ya wanaume na wanawake wa Kisafwa yalihitilafiana kidogo. Wanawake

nguo zilitengenezwa kwa ngozi ya mbuzi ambazo zilivaliwa mbele na nyuma. Ngozi ililainishwa sana na baadaye ikapambwa na shanga mbalimbali. Wanaume walivaa adumbwi. Hii ilitengenezwa kwa kutumia kamba za mti fulani fulani ambazo zililainishwa vizuri kiasi cha kuifanya nguo inayotengenezwa iweze kuvaliwa, na zaidi vazi hili lilivaliwa kiunoni. Katika kuyalainisha mavazi, mawe na miti ilitumika na mavazi yakatengenezwa vizuri.

Kichwani wanawake walitumia pambo walilolitengeneza kwa kutumia vijiti walivyovipaka rangi na halafu wakavaa kichwani. Miguuni walivaa viatu vilivyotengenezwa kwa kutumia ngozi za mbuzi -na vazi hili lilitumiwa zaidi na wanaume kwa sababu wao walivitumia kwa kutembeatembea porini wakati wa kuwinda wanyama ili miguu yao isichomwe na miiba au kuumizwa na mawe. Na wanawake hawakushiriki hasa katika kazi za uwindaji wa wanyama wa porini, kwa hiyo viatu hivyo havikuhitajiwa sana nao.

MIIKO

Kama jamii zingine za Watanzania, Wasafwa waliiogopa miiko fulani fulani. Kwa mfano, wanawake walikataa kula kuku na mayai yake kwa kuogopa kuwa kama wakila, wangegeuka kuwa wapumbavu. Labda kuku alionekana kuwa ni ndege mpumbavu, kwa jinsi hii wanawake waliogopa

45

kuwa wangalikuwa wapumbavu kama wangalikula nyama na mayai yake. Ajabu yake ni kwamba katika utafiti wangu sikuambiwa kuwa wanaume nao walikatazwa kula huku. Ukisoma maelezo yangu hapo juu utaona kuwa kuku alitumiwa sana katika shughuli mbali mbali kama vile kutambikia mvua na kadhalika, na kuomba sala mbalimbali zilizohusu maafa yao. Lakini sikuona mahali popote palipoonyesha kuwa hao makasisi waligeuka kuwa wapumbavu baada ya kula nyama ya kuku. Labda mwiko huu huu uliwapendelea wanaume na kuwatisha wanawake wasifaidi hiyo nyama ya kuku. Hali kadhalika hata katika shughuli kubwa kubwa za kutambikia mvua au kutakasa nchi wanawake hawakushirikishwa kikamilifu ball walikujashiriki katika ngazi ya mwisho ya shughuli yote kama vile kushiriki katika kucheza baada ya sala za mwisho kumalizika. Hii yaonyesha nafasi ya mwanaume na mwanamke ilikuwa namna gani katika jamii ya Kisafwa. Mwanamke alipokuwa katika hedhi, ilikuwa ni mwiko kwake kumpikia chakula bwana yake wala hata mwanaume ye yote hakuruhusiwa kuingia katika nyumba ya mwanamke aliyekuwa katika hali hii mpaka siku saba zimepita, ambapo mwanamke aliyehusika ilimbidi kusafisha nyumba na kuisiliba upya ndipo bwana au mwanaume yeyote aruhusiwe kuingia katika nyumba yake. Pia ilikuwako miiko mingine mingi, lakini miiko yote hii imetoweka kabisa au miiko yote imo katika kutoweka kwa sababu ya elimu nyingi mpya inayoleta fikra mpya kabisa na kuyakataa yale ya zamani yasiofaa.

IMANI Hapo zamani kabla ya kuathiriwa na utamaduni wa kikoloni Wasafwa walikuwa ni watu wenye

imani kubwa sana kuliko ilivyo sasa. Kwa mfano, iwapo mtoto aliugua nyumbani, wazazi iliwapasa waungane kama wamepata kugombana nyumbani ambako huenda ndiko kumesababisha kuugua kwa mtoto, na walipofanya hivyo, yaani walipoungana, kijiji kizima kiliungana na wazazi hao waliokuwa wakiuguliwa mtoto katika kuungana na kuomba kwa Mungu mtoto aweze kupona. Kijiji kilipofanya hivyo, mtoto aliendelea kupona maradhi yake. Hata magonjwa makubwa makubwa kama vile ndui ambao ni ugonjwa wa hatari sana, haukuweza kumuuwa mgonjwa baada ya kijiji chote kuungana na kuomba kwa Mungu ugonjwa huo uondoke mara moja. Simba alipokamata ng'ombe kijijini, wanakijiji waliwachagua vijana wawili wamwendee simba ili wakamuue na kweli wale vijana wawili waliweza kumuua bila taabu. Hali kadhalika mwanaume aliweza kulala nyumba moja na mke wa mtu mwingine bila kumtamani. Ilikuwa ni mwiko kwa Msafwa yeyote kufanya hivyo. Mtu aliyevunja mahindi ya shamba la mtu, aliweza kuvunja hayo mahindi vizuri na kuyalaza mabua yake pale pale karibu na shamba hilo vizuri ili kuonyesha ya kuwa mtu huyo hakuwa mwizi bali alikuwa na njaa yake. Wakati wa kuposa msichana, kulikuwa hakuna haja ya kuwepo shahidi kwa sababu Wasafwa waliaminiana sana, na iwapo ndoa ilivunjika hapo baadaye, mahari ilirudishwa bila ya kuwapo mashahidi wo wote. Mvua iliposhindwa kunyesha, Wasafwa waliomba na mvua ikanyesha siku hiyo hiyo. Lakini mpaka sasa sehemu zingine za Usafwa bado watu wanaomba mvua na mvua inanyesha. Kwa mfano, sehemu za Iganjo na kwa Inshinshi, ni sehemu mojawapo ambako Wasafwa wanaomba mvua kama imeshindwa kunyesha na mvua hunyesha siku hiyo hiyo.

KUTAMBIKA MVUA

Miaka mingine hutokea kwamba mvua hazinyeshi au zakawia kunyesha. Kama tunavyoelewa, mvua ni kitu cha lazima kwa binadamu, wanyama, wadudu na mimea kadhalika. Kwa hiyo mvua zinaposhindwa kunyesha, zasababisha maafa ya kila namna kwa viumbe nilivyovitaja hapo juu. Kwa jinsi hii, mvua zinaposhindwa kunyesha viumbe mbali mbali na wanyama mbali mbali hustushwa sana na ukosefu huu wa mvua. Duniani pote hupata pigd kubwa sana iwapo mvua zinashindwa kunyesha na binadamu hufanya juu chini ili kupigana na mazingira ya namna hii waepukane na maafa yanayoambatana na ukosefu wa mvua.

Wasafwa wana njia yao ya kupigana na mazingira ya mvua. Mvua zinapokosekana au zinapochelewa kunyesha, Wazee fulani wa Kisafwa huenda mahali patakatifu na kuomba kwa Mungu

46

mvua iweze kunyesha. Mfano wa sehemu mojawapo zilizo maarufu sana kuomba (kutambikia) mvua ni Iganjo, sehemu za Uyole karibu na mlima Mbeya. Kwa kawaida chifu wa jadi, ambaye watu wa sehemu hizo humwita Mfalme, huwa ndio kasisi Mkuu wa matambiko, lakini sehemu zingine za Usafwa Mzee fulani anayeaminika na kufuatana na chifu wao, ndiye huwa Kasisi Mkuu wa kuomba mvua. Yeye hutafuta ulezi wa kukorogea pombe na baada ya pombe hii kukorogwa na kuwa tayari pombe hiyo yatiwa ndani ya vibuyu vitano au sita. Kisha kasisi huwatangazia wazee wanaohusika na salaza kuombea mvua na sifku huchaguliwa ili kufanya shughuli zote hizi.

Sasa kuku mweusi hutafutwa (sehemu zingine mbuzi au kondoo hutafutwa kwaajili ya shughuli hizi). Mambo yote yakiwa tayari watu wote wanaohusika hjuenda mahali palipo patakatifu na kuanza kuomba mvua inyeshe. Kasisi mkuu huanza kusema maneno haya. "Uposhele inguku ini tuhanzaje hwunzi hwilwipei invula itonye, iviyabo vihwone. Ingukuinj mulyarrje mwendi mwik-wizyanajei abantu balalamiha baiga, "Tukosile yenu? Invulayinyu Mhutima?"Tulaba twalamba sana ngatukosile shimo vyanje. Ngazilipo zimo uvitilwe utuwozye we wewe dada pipo nahumo uhwinyi washimbilile. Tusubila wenewe ungulubi uwinji numo."

MAANA "Pokea kuku huyu tunataka nchini kuwe kweupe, Mvua inyeshe vyakuia vinakauka. Watu wanalalamika wanasema,Tumekosa nini? Kwa nini unatunyima mvua? Tunakuomba sana kama tumekosa lolote useme. Kama kuna jambo lolote lililokukasirisha

utuambie wewe baba. Kwa sababu hakuna mahali pengine pa kukimbilia. Tunakutegemea wewe mwenyewe, Mungu mwingine hakuna."

Wakati sala hizi zinaposemwa, pombe iliyo katika vibuyu viwili yamwagwa chini mahali patakatifu na huku kuku atiwa ndani ya pombe iliyomwagwa chini na hushikiliwa hivyo hivyo mpaka kuku huyu kukosa hewa kabisa na kufa kwa kushindwa kuvuta hewa. Baada ya kuku kufa manyoya yake yananyonyolewa na nyama yake huchomwa. Baada ya kumchoma kuku huyo, kasisi huchukua nyama kidogo na maini yake na kukatakata vipande vidogo vidogo vya nyama ambavyo vyatiwa pembeni mwa mahali pale pombe imemwagwa. Nyama inayobaki inaliwa na makasisi wado-go waliopo hapo pamoja na kasisi Mkuu, Makasisi hao wadogo huwa watano au kumi hivi kwa kutegemea na mahali penyewe na watu walivyo na shida zao, na jinsi wanavyotaka kuomba mvua yenyewe. Lakini kabla ya kusema sala zao, wale makasisi, wengine hucheza cheza kwanza hapo hapo mahali patakatifu isipokuwa kasisi mkuu na kusema, "Tumefika sisi watoto wenu msije mkasema ni watoto wengine". Ndipo kasisi mkuu huwaambia makasisi wake wakae chini halafu huendelea na sala kama ilivyoelezwa hapo juu na mvua hunyesha mara baada ya sala hizo. Wakati mahindi yamekomaa mashambani hakuna mtu wa kuanza kuvunja mahindi hayo kutoka shambani mwake na kuanza kula mpaka kwanza sherehe maalum imefanyika. Sherehe ya namna hii hufanyika sehemu zingine zingine katika nchi ya Usafwa. Mwezi wa tatu ambapo ndiyo wakati mahindi yaanza kukomaa kiasi cha kuweza kuliwa, Kasisi mkuu huwakusanya watu wote wa sehemu yake na kuwaambia siku ya kukutana pamoja kwa ajili ya shughuli ya ufunguzi rasmi wa kuanza kula mahindi mapya. Siku hiyo ikifika watu wote huondoka na kwenda mahali pa kukusanyikiana huku wakichukuwa mapembe na fimbo na miilini mwao na usoni hujipamba kwa rangi mbali mbaii. Siku hiyo wanakijiji hao hucheza sana kuanzia saa saba adhuhuri hadi saa moja jioni. Wakati wa kucheza, watu huwa katika safu - wanaume upande mmoja na wanawake upande mwingine, na wale walio na mapembe hufanya safu, ya katikati. Wakati wa kucheza watu hawavai mavazi rasmi balil huvaa mavazi ya kawaida tu. Kasisi Mkuu huvaa shuka na kaptura hukamata mikuki mitatu, halafu hupanda juu ya mti na huko mtini huchomeka mikuki miwili. Baada ya kufanya hivyo, kasisi hushuka chini na mkuki mmoja. Saa za jioni huwakusanya watu wote halafu humwaga unga wa malezi chini na kusema.

"Baba Inshinshi tuongene apa usanyono, Tuhwanza aje iviyabo vimelaye ishinza mwatulima Idondoma tumanyile aje linanganya, Tulawa ugazije amalondoma gasinanganaye iviyabo Nantele baba pahandinealine amagonda gao, Iviyabo vyao vyamelile ishi bahwande aje balyanje. Ovisaye abantu basinanganye, Tumanyile aje balipo abitunga, Tulaba aje ngoshele balipo abitunga bawoneshe, Utuvuzye aje abitunga babana nganya, balipo abantu bafumu nutali,

47

Bahwanza aje bananganya insi yitu. Abitunga balogaje abantu babahwinza ananganye insi itu, Ishi bagosi tumalile ivlyabo vyetu visayirwe".

MAANA: "Baba Inshinshi tumekusanyika hapa leo, Tunataka vyakula vyote vizurl tunamolima. Tunajua kwamba viwavi vinaharibu, Tunaomba uwazuie viwavi wasiharibu vyakula. Na tena waliowahi kulima mashamba yao, Vyakula vyao vimekomaa wanataka wale, Uvlbarlki vyakula wachawi wasijarlbu kuchukua chakula. Tunaomba kama wako wachawl utuombee kwamba kama kuna watu waliotoka mbali kuja nchini kama wapo wachawi wawaloge hao wageni. Wachawi wawaloge watu wanaokuja kuharibu nchi yetu." Sasa wakuu tumemaliza kwa hiyo vyakula vyetu vimebarikiwa. Baada ya kumallza haya, watu wote huondoka na kukimbia kwenda nyumbani kwao, bila ya kugeuka nyuma. Kaslsl mkuu hubakla mahali pale pale penye shughuli hii ya sala kwa muda mrefu kldogo. Iwapo mtu aklgeuka nyuma wakatl wa kukimbllia nyumbani yaaminiwa kuwa mtu huyo hupotea yaani hawezl kujua nyumbani kwake ni wapi mpaka atakapotafutwa na jamaa zake. Basi baada ya kurudi nyumbani watu wote wanaweza kuanza kuja chakula chao toka mashambani. Lakini iwapo mvua ni nyingi sana nazinazidi kunyeshazaidi ya kawaida ya kusaidia mimea,

vile vile lazima tambiko lifanywe. Kasisi mkuu humchagua mfuasi wake mkuu ili akatafute kuku mweupe kabisa toka kwa wanakijiji na humnunua na kumpeleka kwa kasisi mkuu (ambaye kwa kawaida huwa ndiyo chifu mwenyewe) na kuku akishapokelewa, kasisi naye humpeleka huyo kuku mahali patakatifu na kuwaomba mababu, kuwa nchini kuwe kweupe ili jua lije, na mara nyingi huenda huko mahali patakatifu na wazee 5 na pia pombe lazima itolewe. Kasisi mkuu huanza sala zake kama hivi:

Kasisi: "ini kuku" (kuku huyu) Msaidizi: "Mumvwaje" (Msikie) Kasisi: "Tuhwanzaje isanye lihole" (tunatakajua liwake) Msaidizi: "Mumvwaje" (Msikie). Kasisi: "Imvula inanganya ivi yabo" (mvua inaharibu mazao) Msaidizi: "Mumvwaje" (Msikie) Kasisi: 'Twalamba sana" (Tunaomba sana) Msaidizi: "Mumvwaje" (Msikie) Kasisi: "Twalamba sana" (Tunaomba sana) Msaidizi: "Mumvwaje" (Msikie) Kasisi: "Inzagatwenzile izinji" (hatujaja kwa mambo mengine) Msaidizi: "Mumvwaje" (Msikie) Kasisi: "Basi atwe twamala" (Basi sisi tumemaliza) Msaidizi: "Mumvwaje" (Msikie).

Basi baada ya hapo kuku anachinjwa na kuchomwa nyama yake kuliwa hapo hapo. Kesho yake jua linawaka sana na linaendelea kuwaka na iwapo lazidi kuwaka na kuwatia wasiwasi wanakijiji, sala nyingine itafanyika ili kuomba mvua zianze kunyesha. Huu hapo juu ni mfano wa sala za kuombea mvua uliochukuliwa toka kwa Inshinshi juu ya mlima Mbeya (nyuma yake).

MAJI Nchi ya Usafwa ilikuwa haina shida ya maji. Maji yalipatikana tele kila mahali katika nchi ya

Usafwa na misitu ilikuwapo mingi iliyohifadhi maji yasikaushwe na jua. Lakini watu walipoanza kulima karibu na kingo za chemchemi za maji, basi maji yakaanza kupungua kabisa katika sehe-mu zingine za Usafwa. Mpaka sasa ziko sehemu zingine zenye ukame wa maji kama vile sehemu zinazopakana na bonde la Usangu na sehemu za Njerenje na za Songwe ambazo ziko mbali na mto Songwe. Walakini sehemu zingine za Usafwa zina maji chungu mbovu, na maji haya hutumika kwa matumizi mbali mbali kama vile kumwagilia mashamba wakati wakiangazi hasa sehemu za Uyolena sehemu za Mporoto. Maji ya sehemu hizi yanatumiwa sana kumwagilia mashamba ya mboga mbali mbali kama vile kabichi, vitunguu, na kadhalika. Mashamba ya mihindi yamwagiliwa maji hasa nyakati za kiangazi wakati mvua zimepungua na kuna ukame ukame. Shughuli hii yapaswa kuen-delezwa vizuri zaidi na wataalamu wa kilimo hasa katika sehemu zile ambazo mpango huu wa kum-

48

wagilia mashamba haujaanza bado katika mkoa wa Mbeya. Kwa matumizi ya nyumbani, maji yanatumiwa kwa kunywa, kunyweshea mifugo, kufulia, kuoga na kadhalika. Kama nilivyosema hapo 'iuu sehemu zingine za Usafwa zina bahati ya kuwa na chemchemi na vijito vingi vinavyo tiririka miteremko ya milima hudumu daima kwa hiyo, Wasafwa hutumia mianzi na kuitoboa katikati halafu inaunganishwa na kufanya bomba la maji linalopeleka maji sehemu zile zinazotakiwa - hasa sehemu zilizo na nyumba za kukaa watu.

Watu wengi wanaoishi sehemu za Mporoto wametatua tatizo la kuyafuata maji yaliko kwa kuyaleta maji karibu na nyumba zao kwa kutumia mabomba yaliyotengenezwa kwa kutumia mianzi ambayo inapatikana pande hizi za Usafwa. Matumizi mengine makubwa ya maji ni kujengea nyumba za kisasa. Watu wengi wa Usafwa, karibu robo tatu ya wakazi wote wa wilaya ya Mbeya wanajenga nyumba zao kwa kutumia matofali mabichi au yaliyochomwa, na juu ya mapaa ya nyumba zao huezekea mabati. Kwa kweli watu wa wilaya ya Mbeya wamepiga hatua kubwa katika kujenga nyumba za kisasa zilizo na nafasi ya kutosha. Maji mengi yanatumiwa katika njia hii kwa sababu karibu kila mkazi wa Wilaya amejaribu kujenga nyumba ya matofali ya kumtosha yeye na familia yake.

ELIMU YA WATOTO Mtoto anapozaliwa hupewa maziwa - yaani mtoto huanza kujifunza kunyonya maziwa toka kwa

mama yake, na huendelea kunyonya mpaka baada ya siku nyingi kidogo ambapo huanza kupewa uji wa ulezi. Huendelea hivyo hivyo mpaka baadaye atakapoanza kupewa chakula laini laini.

Elimu kubwa kabisa wanayofunzwa watoto wa Kisafwa ni kujifunza kazi zote zinazofanywa na wazazi. Elimu hii inaanza mapema kabisa tena ni elimu ya kujitegemea. Ni elimu ya kuona na kufanya, haina nadharia yoyote ndani yake. Kazi kubwa ambayo lazima watoto wajifunze ni kulima. Hii ni kazi ya kwanza kabisa ambayo mtoto wa Kisafwa anapaswa kujifunza upesi sana ili aweze kuwasaidia wazazi wake na pia aweze kuwa na kijishamba chake mwenyewe cha mahindi ya kuchoma. Mvulana na Msichana wote hufundishwa kazi hii mapema sana. Watoto wanaanza kujifunza kazi hii tokea umri wa miaka mitano na kuenuelea. Watoto wanatengenezewa vijembe vidogo sana vilivyo na ukubwa wa kiganja cha mkono na mipini yake ni mifupi sana ambayo ina urefu wa kiasi cha mkono mmoja au mkono na nusu hivi kwa kutegemea kimo na umri wa mtoto anayetengenezewa kijembe hicho. Jembe ni maisha kwa mtoto yeyote wa Kisafwa.

Mtoto, baada ya kufahamu kazi ya jembe, huanza kujifunza elimu nyingine. Pia, hasa kwa kufuatana na maisha yake na baadaye atakapokuwa mtu mzima. Elimu yenyewe ni kama vi le kujifunza kupika, kusafisha vyombo, kuteka maji, kukandika nyumba, na kadhalika. Elimu hii hasa yatolewa kwa msichana. Mvulana hujifunza elimu ya kujenga nyumba, kuchonga mizinga ya nyuki, kukamua maziwa, kuchunga ng'ombe, mbuzi, kondoo, na kadhalika. Elimu yake yote hutolewa kwa kufuatana na kazi atakayofanya baadaye katika maisha yake. Kwa mfano, mtoto wa kiume anafunzwa elimu ambayo itamsaidia kuishi na mke na watoto wake, na mtoto wa kike hufunzwa elimu itakayomsaidia kuishi na bwana yake na jinsi ya kuwalea watoto wake.

Katika jamii ya Kisafwa hamna utaratibu wa marika, bali watoto hula pamoja, hucheza pamoja, na kulala pamoja na watoto wenzao pale kijijini.

KUMPELEKA MTOTO SHULENI Siku hizi Wasafwa wengi huwapeleka watoto wao katika shule za serikali kujifunza elimu

nyingine ya kisasa. Lakini hapo nyuma kidogo watu wengine walikuwa wanaogopa kuwapeleka watoto wao shuleni kwa sababu eti wangelogwa na watu wasiopenda watoto wa watu fulani waendelee. Wasiwasi huu ulikuwapo sana, lakini siku hizi jambo hili limekufa kabisa kwa sababu watoto wengi sana wanasoma shule za serikali na hakuna kinachotendeka.

NYUMBA ZA WASAFWA Nyumba za asili ni za mviringo ingawa siku hizi nyumba za aina nyingine zinajengwa na

Wasafwa. Nyumba za asili zinajengwa mviringo yaani "msonge", na vifaa vitumikavyo katika kujengea nyumba hizi ni miti, magugu, matete na kamba za miyombo kwa kufungia fito pamoja na

49

miti ya kujengea. Kwa kawaida ndani ya nyumba za asili hazigawanywi vyumba, bali huachwa hivi hivi na kutumiwa hivyo hivyo. Nyumba zenyewe zakandikwa kwa kutumia matope kwanza halafu Mpu iliyochanganywa na mavi ya ng'ombe hufuata juu ya matope. Lipu ya namna hii hulainisha sana ukuta na kuufanya ukae sawasawa. Mlango wa nyumba hizi huwa ni mmoja. Juu ya nyumba manyasi maalum yaitwayo "Isonze" huezekwa. Manyasi haya ni laini sana na yanadumu hata miaka sita bila kuharibika. Kutengenezea kenchi na paa hutumia miti au mianzi nasakafu yake hutengenezwa vizuri kwa kusiriba matope na kuifanya sakafu iwe sawasawa na kuonekana maridadi na imara.

Siku hizi watu hujenga nyumba za namna nyingine hasa nyumba zenye kuta nne. Kwa kawaida watu wa wilaya ya Mbeya wanajenga nyumba zao kwa kutumia matofali mabichi au matofali ya kuchomwa. Maji mengi yanatumika kutengenezea na kufyatulia matofali. Nyumba za miti zimeach-wa isipokuwa wale watu wanaoishi karibu na mianzi. Hawa hutumia mianzi au matofali katika kujengea nyumba zao. Kitu kinachowasumbua wakazi wa Mbeya ni saruji ya kujengea na bati za kuezekea nyumba zao. Shida inayowatokea hawa jamaa ni kwamba vitu vinapatikana kwa msimu. Ni shida kupatikana wakati wote. Shida ya pili ni ile ambayo kila mtu anaelewa yaani ya kupanda kwa bei ya vifaa vya kujengea nyumba. Kwa hiyo utaona kwamba nyumba nyingi zinachelewa kumalizika kujengwa kwa sababu ya shida hizi mbili zilizotajwa hapo juu.

ORODHA YA KUMBUKUMBU YA VITABU

1. E.Kootz Kretschmer: ABRISS EINER LANDESGESCHIEHTE VON USAFWA IN OSTAFRIKA, 1929.

2. E.Kootz-Kretschmer: DIE SAFWA. 3 BANDE, 1933.

3. TH.SIaats: PEOPLES OF MBEYA DIOCESE, 1972.

4. Afisautamaduni: JARIDA LA UTAMADUNI LA MKOA WA MBEYA, 1970.

5. Charsley, S.R. THE PRINCES OF NYAKYUSA, 1969.

50

Sura ya Tatu

JAMII YA WASAGARA

UTAFITI ULIOFANYWA KUHUSU ELIMU YA JADI YA WASAGARA

Wasagara ni jamii inayoishi Wilaya ya Kilosa wakipakana na Wakaguru upande wa Kaskazini na Wavidunda upande wa Kusini, ha Waluguru upande wa Mashariki na Wagogo upande wa Magharibi. Nchi yao ni ya rutuba sana tena ni ya tambarare. Udongo wake ni mzuri sana, mimea mbali mbali hupandwa. Katani kama zao la kuwaletea fedha iimekuwa likipandwa na Makampuni ya kizungu kwa muda mrefu sana. Wasagara wenyewe wamekuwa hawalishughulikii zaidi zao hili kwa sababu ya kazi ngumu inayotakiwa katika kulishughulikia zao hili kikamilifu. Kwa hiyo Wasagara wenyewe wamekuwa wakipanda mazao kama vile mtama, bwembwela, maboga, kunde (safe), mlenda (hombomgunda), Derega, mwage, tele, kikundembala (mwamizi Mulungu), sunga, mpunga na pamba, na kadhalika. Mpunga na pamba ni mazao yanayowaletea fedha.

Kwa upande wa Kaskazini, nchi ya Kilosa imeinuka na mwinuko huu huendelea katika milima ya Kilosa ambayo inaungana na milima ya Mpwapwa na ya Ukaguru. Mvua zanyesha kwa wingi sana wakati wa masika na maji ya mvua yanatuama sana juu ya udongo na kuifanya ardhi ya nchi ya Kilosa, ionekane kama yenye matope matope. Wakati wa kiangazi, jua linawaka sana. Reli Kuu ya Kati imepita hapa na barabara za magari ya kwenda Mpwapwa, Gairo, Morogoro na Mikumi zapitia katika mji wa Kilosa.

Nchi ya Kilosa ni maarufu sana kwa mashamba ya mkonge ambayo yametapakaa karibu kila upande wa nchi hiyo. Mashamba ya mkonge kama yale ya Msowero, Kimamba na Kilosa ndiyo yaliyoifanya nchi ya Kilosa ijulikane sana katika nchi ya Tanzania. Mali kadhalika Reli Kuu ya Kati imeongezea umaarufu wa nchi hii. Reli iendayo Kilombero kupitia Mikumi, yaanzia Kilosa. Pia llonga ambacho ni kituo cha kilimo, elimu na mawasiliano, kimeongezea umaarufu wa nchi ya Kilosa.

Kama inavyofahamika, Wasagara ni watu wapole sana na wema! Watu hawa hawajui vita hata kidogo na hawataki kumwudhi mtu. Wako tayari kumwachia mali yao adui yeyote anayetaka kupigana nao. Ni watu wapole sana na waoga kwa vita. Wasagara wengi wanaishi sehemu za mashambani na wageni karibu wote wanakaa mjini Kilosa. Wasagara ni watu wanaojishughulisha sana na kilimo. Kwa sasa hivi Wasagara wengi sana wamepiga hatua kubwa ya kuhamia katika vijiji vya maendeleo ambamo shughuli nyingi za pamoja zafanyika, na Wasagara wengi sana kwa sasa wananufaika sana kwa kuitikia mwito wa kukaa pamoja katika vijiji hivi.

HISTORIA

Jina hili "Wasagara" lina maana ya "Wachokozi". Asili ya Wasagara yasemekana kuwa ni Palaulanga. Huko Palaulanga walifanya kambi kubwa kwa sababu walikuwa katika makundi makubwa makubwa, na kama inavyoeleweka kila mahali penye kundi au makundi makubwa ya watu hapakosi mgawanyiko wa watu. Kwa sababu kufanya kazi kwa pamoja huwa ni vigumu sana. Basi hayo makundi yakiwa bado Palaulanga yaligawanyika, na kundi lililoitwa Wasagara lilikaa penye majani yaliyoitwa mazaganza. Wasagara wengine walikaa mahali palipoitwa Peupe (Nzelu) watu wenyewe wakaitwa Wanzelu (Weupe). Huu ni ukoo wa Wasagara uliokaa mahali hapa. Watu hawa wakiwa katika hali ya makundi haya mawili, kundi moja ambalo lilikaa juu ya Mazaganza likaenda kuwachokoza Wanzelu walipokwenda kuomba moto, tumbaku na vitu vingine vingi. Kuomba kwao

51

vitu hivi kulikuwa ni kwa mara nyingi mno hata Wanzelu wakachoshwa na tabia hii ya kusumbuliwa na hawa watu. Basi Wanzelu wakaanza kulalamika na kusema kuwa watu hawa ni "Wasagara" - yaani ni "Wachokozi". Wakubwa wa Wanzelu walipouliza kwa nini watu wao wanalalamika, Wanzelu wakaelezea kisa chote toka mwanzo hadi mwisho. Basi mkuu wa Wanzelu na mkuu wa Wasagara wakasikiliza kisa chote na wakaangua kicheko, kuonyesha kuwa basi yote yale yaliyowaudhi Wanzelu yamekwisha. Tangu hapo wale waliokaa juu ya majani ya mazaganza wakaitwa wachokozi yaani Wasagara.

Basi makundi ya watu hawa yakazidi kuendelea na safari zao, na walipofika mto Mdukwi wakatengeneza daraja la kuvukia. Watu wengi walivuka mto Mdukwi kwa kutumia daraja hilo. Makundi mengine ya watu yakiwa katika kuvuka huo mto, daraja likavunjika. Lite kundi la Wasagara lililovunja daraja la kuvukia likaitwa Wabenadiloko — yaani Wavunja daraja". Basi watu wote hawa waliokuwa katika kundi hili wakaitwa "Wabenadiloko" na ukafanywa kuwa ukoo maalum. Daraja lenyewe lilivunjwa wakati wa safari za hawa Wasagara.

Walipokuwa katika safari zao, njaa ikawashika, nao walikuwa hawana moto wa kupikia ingawa chakula walikuwa nacho. Kwa hiyo, baadhi ya watu wakafikiria njia ya kupatia moto wa kupikia. Wakatafuta mti mkavu na mti wa kupekechea na wakaanza kupekecha moto. Baadaya kupata moto, wakashindwa kuutumia moto huo kwa sababu hawakujua jinsi gani wapike hicho chakula. Mtu mmoja toka kundi mojawapo ya makundi ya Wasagara akatafuta mawe na kuyapasua na kuyafanya yaonekane kuwa mafiga ya kutelekea chungu cha chakula, na kweli hayo mawe yakafaa kuwa maf iga na wakapika chakula chao na baadaye wakashibisha njaa yao. Jambo hili liliwafurahistia na kuwastaajabisha watu wengi sana. Wakubwa wao wakauliza, "Ni nani kaleta elimu ya kutumia mafiga"? Watu wakaeleza jinsi watu wa kundi moja kati yao, lilivyoweza kupasua mawe na kufanya maf iga ya kupikia. Basi kundi lote la yule mtaalamu aliyetafuta hayo mafiga likaitwa ukoo wa Mahafigwa. watu wenyewe wanaitwa Wahafigwa.

Walipozidi kuendelea na safari yao, makundi fulani ya watu yalishindwa kutwanga unga wa kutengenezea ugali, basi ikawabidi waende kuomba unga kwa watu wengine waliokuwa katika misafara hiyo. Hao watu walioombwa unga wakatoa chengachenga za unga badala ya kutoa na kuwapa unga. Zile chenga zikapikwa na wakala. Baada ya kula zile chenga, wazee wa makundi yaliyoomba unga wa kupikia ugali wakawauliza watu wao ni nani aliyewapa zile chenga, nao wakajibiwa na akina mama ya kwamba waliowapa hizo chenga ni wale pale. Wazee wakaonyeshwa wale watu waliozitoa hizo chenga. Basi wazee wakaamua na kusema kuwa hao watu ni "Wanyasenga". Basi baadhi ya Wasagara wakaitwa hivyo — Wanyasenga , yaani watu waliotoa chenga.

Kama tunavyoelewa sote, misafara yoyote huandamwa sana na magonjwa mbali mbali. Wasagara hawakuepuka maafa hayo. Maradhi mengi yaliwasumbua sana, na mwishowe jamaa fulani kutoka katika mojawapo ya makundi ya Wasagara wenyewe, akagundua mizizi ya dawa ya kuponyeshea magonjwa fulani fulani. Basi watu wote waliougua magonjwa fulani fulani walipewa

mizizi kama dawa ya kuponyeshea na wengi walisaidiwa sana. Jamaa wote wakamheshimu sana na wakakata shauri kuwa kundi lake huyo mganga alimotoka liitwe Wazizimiza. Basi huo ukawa ni ukoo mmojawapo maarufu sana katika jamii ya Kisagara. Pia palitokea mzee mmoja aliyekwenda kuwatembelea wenziwe saa za jioni. Alipofika katikati ya safari yake, akasikia harufu mbaya ya chpo. Jamaa huyo akauliza, "Nani huyo"? Kumbe kulikuwa na mtu ambaye alikuwa anajisaidia vichakani. Yule mtu kule kichakani akaitikia, "Ni mimi". Akamwuliza, "Unafanya nini?" Yule mtu kule kichakani akajibu, "Ninakwenda chooni". Basi jamaa akaendelea na safari yake hadi alikokusudia kwenda. Kumbe alipokuwa anazungumza na yule mtu aliyekuwa anajisaidia vichakani, watu walimsikia. Alipofika tu wakamwuliza, "Ulikuwa unazungumza na nani huko porini usiku huu?" Akajibu, "Nimemkuta mtu anajisaidia pale porini usiku huu". Basi wale wenzie wakamwambia kuwa hao ni "Wanyakilo", yaani watu waendao choo usiku.

52

Katika hizo safari zao, walifika kwenye mto wa Matete, watu walishindwa namna ya kuvuka mto huo. Basi jamaa mmoja kutoka katika kundi moja akawaonyesha wenzie namna ya kuvuka mto ule kwa kutumia kushika matete yaliyoota pembeni mwa mto wenyewe. Basi watu wengine walipouliza ni nani kaleta maarifa haya; jamaa wakamtaja huyo mtu mwenyewe. Basi kundi lake lote yule jamaa mwenyewe kuleta maarifa haya likaitwa "Wadete". Wakati wakizidi kusafiri katika safari zao jamaa mmoja alisahau kitu chake nyuma alikotoka. Alipokumbuka ikambidi arudi nyuma akakitafute. Alipofika mahali penyewe walipotoka, akaanza kukitafuta kitu chenyewe huko na huko huku wenzie wakimngojea. Walipoona anachelewa kurudi, wakaamua wamfuate ili wamsaidie. Kumbe katika kufanya hivyo, yale makundi mengine yakawaita watu hao "Wasemwa", yaani "Waliosahau". Basi ukoo wa "Wasemwa" ukawa umetokea tayari katika jamii ya Wasagara. Wakati huu walikuwa wamefika kambi ya Kwiva, na sasa wakaanza kusambaasambaa wakikaa pamoja katika makundi makundi ya watu watano au kumi au zaidi. Basi hivyo ndivyo koo mbali mbali za jamii ya Wasagara zilivyotokea.

IMANI Wasagara ni watu ambao hapo awali walikuwa na imani kubwa sana na wenye kushika sana

dini yao ya jadi tena walikuwa waoga wa vitendo viovu. Baadhi za imani za watu hawa zimeelezwa hapa chini. Mama anapokuwa katika hali mbaya (mwezini) ilikuwa ni mwiko kwake kumpikia chakula bwana yake, ilikuwa lazima mtu mwingine ampikie chakula bwana yake. Hali kadhalika mwiko mwingine kuhusu hali hii ulikuwa mwanamke hawezi kumzunguka bwana iwapo alitaka kupita. Ilimbidi mama apite mbele ya bwana. Iwapo mgonjwa alikuwapo, ilimbidi apakatwe na Mzelu yaani mtu wa ukoo wa Wanzelu, halafu unga ulinyunyizwa kuzunguka mgonjwa na baadaye "Mulungu" (Mungu) akaombwa ill amsaidie huyo mgonjwa. Yasemekana kuwa kweli huyo mgonjwa alipona. Katika kila kijiji alimokuwamo mgonjwa ilipitishwa amri ya kuwa hakuna mtu wa kuongea na bwana yake au mke wake mpaka mgonjwa amepona na watu wote walishika sana amri hii. Vile vile iwapo palitokea simba kijijini aliyetaka kukamata mtu, watu wote pale kijijini walitoka nje ya nyumba zao nakupiga magoti nakumwomba Mungu (Mlungu) amsaidie ndugu huyo ambaye alikabiliwana janga la kukamatwa na simba na kumwepusha hilo janga. Basi simba hakuweza kumkamata huyo mtu na akaondoka kijijini bila ya kufanya ghasia zingine tena.

Jamii ya Wasagara ilikuwa inafuata urithi kwa mjomba. Mjomba alikuwa na mamlaka makubwa na aliogopwa na kuheshimiwa sana na watoto wa dada zake. Mjomba aliweza hata kumchukua 1 mwipwaye na kumtia rehani na hakuna ambaye angalimwuliza kisa cha kufanya hivyo. Baba ya mtoto hakuwa na la kufanya bali kazi yake huyo baba ilikuwa ni kuzaatu nakusaidia kuwalea watoto wake, lakini mamlaka juu ya watoto hao alikuwa hana kabisa.

Wasagara walikuwa na imani kubwa sana katika dini yao ya asili na kumwamini Mlungu (Mungu) ilikuwa kwa njia ya tambiko kuelekea kwa Mwenyezi Mungu. Kuongopa ilikuwa ni mwiko kwa Msagara yeyote. Iwapo ugonjwa ulitokea kijijini, waiimchukuwa mgonjwa na kumweka chini ya mti waliouchagua na kumwomba Mungu amsaidie mgonjwa apone haraka, Unga wa mtama, machicha ya pombe, viazi vikuu, majani ya hozavilinyunyizwa mahali pa tambiko. Muwa mwekundu uliomenywa, tumbaku ya mkate, viliwekwa mahali pa tambiko. Vitu vyote hivi viliwekwa juu ya majani ya mgomba yaliyotandikwa chini. Kondoo wa tambiko alichinjwa na kuku mweupe aliweza kuletwa mahali hapo na kuchinjwa. Lakini shughuli kubwa za tambiko lolote lile ilikuwa lazima kondoo achinjwe. Zaidi ya hayo bao lilipigwa na mganga kutafuta sababu ill atoe kiini cha ugonjwa wenyewe, halafu mtani wa mgonjwa alitafutwa ambaye alitakiwa kutafuta unga na kutambikia Mungu ili mgonjwa apone. Maneno aliyoyasema huyo mtani wa kutambikia ni kama hivi:

"Mulungu mkawage" maana yake, "Mungu mwachilie mgonjwa huyu ili aweze kupona" na huku baba yake yule mgonjwa hutajwa. Matambiko yalifanywa wakati wowote shida zilipowatopea.

Wakati wa tambiko kubwa, kasisi wa shughuli hizi huvaa ngozi, ushanga na mgobole ulipigwa. Kondoo huchinjwa kwanza hata kama wanyama wengine wa kuchinjwa wapo. Baada ya tambiko watu hurudi kijijini kwao na kula chakula pamoja na kunywa pombe.

53

Kabla ya kondoo kuchinjwa, kondoo huyo huzungushwa mahali patakatifu na mtani mara nne au tano hivi na wakati huo huo manyoya ya kuku mweupe na kuku mweusi hunyonyolewa moja baada ya moja na huku wimbo ukiimbwa kama hivi:

"Mgole kwega uleke mgole, Kwega uleke mgole".

Kabla kuku hajachinjwa huzungushwa mahali patakatifu mara saba na mwimbo ukiendelea tu. Na wakati wa kuwachinja hao kuku mweupe na kuku mweusi, wanachinjwa kidogo tu ili muradi damu zinamtoka huyo kuku, na huachiliwa ili ajipigepige wakati anapotapatapa halafu ubawa watakaoangukia basi ndio itakuwa tafsiri ya tambiko lenyewe - kama ni upande wa kuume au upande wa kushoto. Basi yule mgonjwa, ataambiwa kama ni babu zake ndio waliochukia na kuleta baa hili la ugonjwa, basi sala zitaelekezwa huko.

TAMBIKO LA MVUA

Iwapo mvua hazikunyesha kama kawaida yake, basi wazee wa sehemu fulani za Usagara ambao ndio waliohusika waliwaambia vijana wa Kisagara shida iliyokuwa inawakabili katika nchi yao. Basi vijana wakaamua kuchanga fedha ili wanunue chumvi na kaniki halafu wawakabidhi wazee vitu hivyo viwili. Basi wazee walimtafuta mtani wao na mtu mwingine kutoka kijijini pao. Hawa watu walitumwa kwa Mundo ambaye maskani yake yalikuwa Ukaguruni. Yasemekana huyu Mundo alikuwa mchafu sana kwa kuleta mvua nyingi kila siku. Jamaa hawa wawili walikwenda mpaka kwa Mundo, mtani "tu ndiye aliyeruhusiwa kuingia mahali alipokuwa anaishi Mundo, na yule mwanakijiji aliachwa mbali na mahali hapo. Yule mtani alipoingia mahali anapoishi Mundo, alitoa zawadi hizo kwa Mundo huku akitukana matusi chungu mbovu. Baada ya kumtukana na kumkabidhi zile zawadi - chumvi, kaniki na tumbaku ya mkate, Mundo alimkabidhi yule mtani Mzimu wa mvua na kuuwambia, "Haya sasa nenda maombi yenu yamesikilizwa". Basi huyo mtani kabla hajafika nyumbani mvua zaanza kunyesha nyuma alikotoka na mbele anakokwenda. Basi mtani akifika nyumbani humkabidhi Mkuu wa sehemu hiyo ulikotoka mzimu wa mvua, wakati huo mvua zinazidi kunyesha. Lakini lazima Mzee Kutukutu, ambaye ndiye aliyekuwa mtawala wa nchi yote ya Kilosa, ajulishwe kuhusu shughuli zote hizi, kwamba watu wake wa mahali fulani wanatambikia mvua.

Pia mvua ilitambikiwa kutoka kwa Kingo ambaye maskani yake yalikuwa Morogoro. Kwanza baada ya kuona kuwa mvua haijapiga kwa muda mrefu, mzee Muhongola ambaye alikuwa waziri wa Kutukutu, alimwendea na kumwambia kuwa watu watakufa na njaa kwa sababu mvua hazinyeshi na kwamba ingalifaa atambikie. Basi Muhongola alitumwa Morogoro na Mzee Kutukutu kupeleka zawadi za mganga Kingo anayeishi Morogoro. Zawadi zenyewe zilikuwa shoka au jembe halafu na kitambi. Baada ya kuzifikisha hizo zawadi na Bwana Muhongola Kingo mganga wa mvua, alim-wambia Muhongola ale kwanza chakula. Lakini Muhongola alikataa kabisa kula chakula kwanza mpaka apate mvua iliyompeleka huko ndipo ale chakula. Basi baada ya kupokea zawadi zake, mganga Kingo alitoa dawa yake ya mizimu ya mvua na kumwambia Muhongola aende nayp na akampe Kutukutu ili ikalale ndani ya maji, na siku ya pili yake mzee Kutukutu aitishe mkutano wa kupiga gumba, yaani kuchoma sindano kwenye sikio la kila mmoja na iwapo kuna mtu ambaye sikio lake halipitishi sindano, yaani sindano haipenyi sikio lake, basi mtu huyo atashikwa kuwa ana mzimu wa mvua atakuwa ndiyo mtu aliyeshika mvua. Sasa Mzee Muhongola hurudi kwa Kutukutu na kumwelezea yote yale aliyoambiwa. Basi Kutukutu aliitisha mkutano baada ya dawa aliyopewa na mganga kulala ndani ya maji. Watu wote walikusanyika pamoja na kila mtu alipigwa gumba (sin-dano) ili kumtafuta nani sindano hiyo ilikataa kuingia ndani ya sikio lake. Kwa kawaida katika nchi ya Wasagara lilikuwapo jitu moja ambalo lilikuwa haliogi halichani na jitu la kutisha na baya kwa sura. Hili jitu hasa ndilo lilikuwa na mizimu ya mvua katika nchi hiyo. Jitu hili vile vile lilikuwepo wakati wa kupiga gumba na siku zote zamu yake ilipofikajitu hili sindano ilikataa kupenya sikio lake. Baada ya kuona hivyo mtawala Kutukutu alimwambia yule mtu wa kutisha. "Basi nenda kafungue mvua! jioni yake siku hiyo tambiko la mvua lilifanywa na kesho yake lile jitu lilifunga safari kwenda porini kufungua mvua. Baada tu ya jitu hili kufungua mvua ilinyesha mfululizo siku saba na ardhi ikajaa

54

maji kila mahali. Baada ya kuona hivi raia wakapatwa na wasi wasi. Basi mzee Muhongola alikwenda kwa Kutukutu na kumwambia kuwa mvua sasa zinaharibu mashamba ya watu. Kutukutu akaliambia hili jitu likafunge ile mvua ili ipungue watu wapate nafasi ya kulima na kupanda. Mvua ilifungwatena na jitu hilo hilo na watu wakapata nafasi ya kupanda mbegu shambani mwao.

UCHAWI Uchawi ni imani ambayo binadamu huwa nayo kuhusu utaalam wa kufanya mambo kwa njia ya

siri. Katika nchi ya Wasagara uchawi uliogopwa sana na mtu yeyote aliyeonekana na uchawi alikuwa ni adui mkubwa sana. Kwa jumla wachawi katika vijiji walikuwa wanatafuta visa ili waweze kuwadhuru watu. Na zaidi ya hayo uchawi ulikuwa mara kwa mara ni wa biashara, yaani watu waliofanya uchawi walifaidika kwa kupata vipesa kidogo au kupata mbuzi.

Kwa kawaida mtu alipofariki, sababu ya kifo chake ilitafutwa na iwapo kulikuwa na mtu aliyeshukiwa kuwa katenda kitendo hiki kibaya basi mnong'ono uliweza kusikika wakati wa kilio na habari zilienea upesi sana kuwa mtu aliyetenda kitendo kile ni fulani. Siku ya kuondoa matanga wanakijiji walifika matangani na kusema kwa watu wote waliohudhuria matanga hayo kuwa ingawa walikuwa wanamaliza matanga, lakini mtu fulani ndiye kafanya kitendo kile kibaya. Na sasa wazee waliamua hapo hapo kumwuuliza jamaa anayeshukiwa kumtendea marehemu uchawi. Lakini huyo jamaa mtenda mabaya alikataa kabisa kuhusu sababu ya kufariki kwa marehemu. Alisema kuwa hana habari yoyote kuhusu uchawi, wanakijiji waliwachagua wajumbe wawili waende kwa mganga wakapige ramli. Waganga mafundi wa kupiga ramli walikuwapo na kusema kweli walikuwa mafundi sana wa kupiga ramli. Kama Wasagara wenyewe wanavyoelewa hao waganga walikuwa hawakosei sana katika kazi zao hizo. Mganga alitazama ramli yake na kumtaja mchawi aliyemwua marehemu. Wajumbe baada ya kusikia hivi hurudi nyumbani kijijini kwao na kutoa taarifa ya ujumbe wao na kuwaeleza wazee wote kuhusu ramli ya mganga. Mchawi adhaniwaye kuwa ndiye aliyefanya tendo la kuua huwapo wakati habari hizi zikielezwa. Basi kila anapoulizwa na mchawi hukataa kabisa kuhusu kitendo hiki. Ujumbe hutumwa kwa mganga na katika msafara huu huwamo yule mchawi ili akajionee yeye mwenyewe kuhusu ubaya wake. Na iwapo bado mchawi anakataa mbele ya yule mganga, basi mganga hutafuta dawa ambayo huchemshwa sana na chungu hicho chenye dawa inayochemka hutiwa kipande cha chuma au kengele na kuchemshwa sana. Baada ya kuchemsha sana vitu hivi dawa na kengele ya chuma, kila mtu huambiwa kuopoa kile chuma kwa kutumia mikono mitupu bila chombo cha kuopolea na kitendo hiki hufanywa kwa zamu. Inasemekana kuwa yule mtu ambaye hana hatia ya uchawi huopoa kile chuma kilichochemshwa bila kuungua, lakini mtu ambaye ndiye mchawi aliyetenda maovu, hudhurika sana kwa kuunguzwa mkono, na hapo hapo kukubali kuwa ndiye aliyefanya kitendo cha uchawi na kwamba kamwua marehemu. Baada ya kuthibitisha yote hayo, ujumbe hurudi kijijini kutoa habari kuwa mchawi kapatikana. Kablaya kurudi nyumbani kwao mchawi hunyweshwa dawa pamoja na wenziwe walio katika ujumbe huo na wote kunyolewa hywele zote na kupakwa dawa utosini pao iii wasifanye uchawi tena - hasa yule mchawi.

Basi mashauri hufanywa pale kijijini, yule mchawi huambiwa na wanakijiji kuwalipa jamaa za marehemu mbuzi kumi au kumi na tano. Baada ya kufanya hivi, yule mchawi hushikana mikono na jamaa za marehemu kuonyesha kuwa sasa uadui hakuna tena na kwamba hapatakuwepo na uhasama wowote tena kati ya huyo mchawi na jamaa za marehemu.

DESTURI ZA WASAGARA

1. Wasagara walikuwa na desturi ya kula ugali kuanzia chini na kuendelea. Si desturi kwa Msagara kula ugali kutoka juu yake. Mtu akifanya hivyo atakuwa amekiuka desturi yao.

2. Kama chakula kimefunikwa, bwana hana ruhusa kukifunua mpaka mama au watoto wake ndio wanaweza kufunua chakula.

55

3. Mtu akipiga hodi mara mbili hivi na Kama hakuna jibu, hana ruhusa kuingia ndani. 4. Bwana yeyote wa Kisagara hana ruhusa kufunua funua kitanda chake anacholala na mkewe.

Mkewe tu ndiye anayeweza kufunua funua kitanda hicho.

5. Wakati wa kula ni mwiko kuvuta sahani ya chakula. 6. Kwa Msagara ni mwiko kwake kumfyonya mtu yeyote yule.

7. Wakati wa kula chakula, wanaume wote walikuwa wanakula pamoja na wanawake wote pale kijijini walikuwa wanakula pamoja.

CHAKULA CHA WASAGARA

Chakula cha Wasagara ni kama hiki hapa chini: — ( i ) Ugali wa mtama na Bwembwembela. nn Maboga. ( i i i ) Safe (kunde). ( i v ) Mlenda(hombomgunda). ( v ) Derega. ( v i ) Mwage. ( v i i ) Tele. (viii) Kikundambala - Mwamizi Mulungu. Maana yake mboga hii yajiotea yenyewe na Mungu tu

ndiye anayeiotesha. (ix) Sunga - ambacho kiungo chake uf uta.

MWANAMKE MWENYE MIMBA

(i) Mwanamke mwenye mimba alikula chochote kile ambacho roho yake ilitaka. (ii) Bwana alikatazwa kumpiga mkewe wakati kama huu. ( i i i ) Mama mja mzito alitembea kwa tahadhari kubwa kwa kuogopa watu waliokuwa wamechanja

dawa mbaya zinazodhuru mimba za watu. (iv) Mikuwa ni mwiko kwa mama mja mzito kutembea na wanaume wengine. ( v ) Mali kadhalika ilikuwa ni mwiko kwa bwana ambaye mkewe ni mja mzito kutembea na

wanawake wengine.

MTOTO

Mtoto anapozaliwa hunyweshwa maji ndipo uji ufuate baadaye. Kama maji hayapiti kwenye koo-la mtoto, basi yaaminiwa kuwa mtoto huyo labda ni wa kufa au hakukomaa sawasawa. Mtoto anafunzwa kuanza kutembea na mafunzo hayo yaambatana Sana na nyimbo maalum ambazo zilitungwa kwa madhumuni hayo. Mfano wa nyimbo hizo ni kama wimbo huu hapa chini: —

"—Do yaya do, Maikoka do, na kadhalika."

Maana yake ni:— "Pengine mimi nitaondoka, Afadhali ujisaidie." Katika kufunza mtoto namna ya kusema na kutamka maneno, wazazi wa Kisagara hutumia zaidi

maneno haya hapa: Wize mwisukulu, Wize mzangazanga, Wize mbena, na kadhalika.

Jukumu kubwa la mama mzazi ni kumwelekeza mtoto wake ill mtoto huyo afanye matendo kama anavyoelekezwa na mama. Iwapo mtoto katika kuchezacheza mchangani kazingirwa na Nyoka ait-waye "Moma", katika lugha ya Kisagara ikiwa na maana ya "Kifutu", kama mzazi kaona kuwa mtoto

56

wake kazlngirwa hivyo na huyo nyoka, hana ruhusa ya kupiga kelele kuwa mtoto wake labda ..amekufa. Kitu anachotakiwa huyo mzazi kukifanya ni kunyamaza kimya halafu huyonyoka ataandoka mwenyewe bila ya kumdhuru mtoto. Lakini kama mzazi kapatwa na woga na kupiga kelele "Mtoto wangu amekufa jamani" anapoona mtoto wake kazingirwa na "Moma", basi huyo "Moma" atam-wuma huyo mtoto na kwa vyo vyote vile yule mtoto atakufa. Kwa hiyo Wasagara hawapigi kelele iwapo mtoto wao kazingirwa na huyo "Moma" na "Moma" hawezi kumwuma mtoto kama mzazi wake hakupiga kelele.

JANDO

Watoto walikwenda jandoni kuanzia umri wa miaka kumi na kuendelea. Wazazi wa kila mtoto walikaa chini na kuamua lini mtoto wao aende jandoni. Baada ya wazazi wa kila mtoto kuamua lini mtoto wao aende jandoni, ndipo walipofanya mkutano na wazazi wa watoto wengine ili kuamua kwa pamoja lini watoto wao katika kijiji chao waende kuhudhuria mafunzo ya jando. Jumla ya watoto wanaotakiwa kwenda jandoni itategemea wako watoto wangapi pale kijijini ambao wamefikia sifa hii ya kwenda jandoni. Watoto zaidi ya hamsini wanaweza kwenda jandoni mradi wanazo sifa zinazotakiwa. Muda wa kukaa jandoni ni kutoka mwezi mmoja au zaidi, na mara nyingi mahali pa kuendeshea mafunzo ya jando huwa ni mbali kidogo na mji wao au kijiji chao. Wakiwa jandoni hufundishwa elimu ya kuwatayarisha ill waje waishi katika jamii ya Kisagara bila taabu na wasiweze kuishi maisha kinyume cha maisha ya Wasagara. Baadhi ya mafunzo yanayotolewa wakiwa jandoni ni: Watoto wanafundishwa kuwa kutukana watu ni makosa, kutukana wakubwa ni mwiko, kupita mahali anapoogea mama au mtu yeyote mkubwa ni marufuku. Mtoto hatakiwi tena kupita au kupitia mahali hapo. Mtoto anapoamkia wakubwa lazima kwanza apige magoti, akishapiga magoti yake, aondoe kofia yake, halafu ndipo aseme "shikamoo". Anapotaka kuingia ndani ya nyumba ya mama yake lazima abishe hodi naakiambiwa "karibu", yampasa asimame ukumbini tu. Haruhusiwi kuingia ndani ya chumba wazazi wake walimo sababu yake kubwa ya kufanya hivi ni kwamba hawezi kujua hao wazazi wake wanafanya nini ndani. Kwa jinsi hii, mtoto yampasa kusimama ukumbini tu, na wazazi watamwambia la kufanya au yeye atasema shida yake iliyomleta.

Endapo mtoto kavunja sheria au kanuni yamafunzo yake baada ya kumaliza mafunzo, basi baba anaweza kumchukulia hatua kali mtoto wake ya kumrudisha tena kwa mwalimu wake wa zamani (mwalimu wa jando). Yule mwalimu akishaona hivi, basi atasema hivi: "Lusimbi nitamwona tena," huku akitia alama vumbini kwa kutumia kidole kimoja cha mkono wake wa kulia - hasa kidole cha shahada, halafu hufanya alama kuzunguka shingo yake na kuapa. Neno "Lusimbi" maana yake ni dawa ya vidonda iliyotumika kuponyeshea vidonda baada ya kutahiriwa. Dawa yenyewe ilikuwa vumbi la udongo ambalo ndiyo ilikuwa dawa ambalo lilipakwa kwenye vidonda vya mtoto aliyetahiriwa. Basi yule mtoto ambaye alimaliza mafunzo yake siku nyingi na kufaulu masomo yake, akivunja au kufanya makosa katika maisha yake ya kawaida, basi anaweza kurudishwa na baba yake kwa mwalimu wake tena. Yule mwalimu humtia yule mtoto katika kundi la wanafunzi wajifunzao upya na huyo mtoto mkosaji huanza upya tena kujifunza masomo ambayo alikuwa ameyamaliza.

Watoto wanapokuwa jandoni wanalala uchi bila chochote cha kujifunika na hupelekwa mtoni saa kumi na moja kuoga maji ya baridi. Kusudi kubwa la kufanya hivi ni kutaka kuwakomaza watoto Hi waweze kuwa wakakamavu wa maungo na waweze kujitegemea katika maisha yao ya baadaye. Zaidi ya hayo, watoto hutandikwa viboko kama wamefanya makosa.

SIKU YA KUTOKA

Siku ya kutoka inapowadia, habari hupelekwa majumbani ikieleza ni lini watoto watatoka jandoni na hasa siku ambayo ilifaa sana kwa sherehe ya kutoka jandoni ilikuwa siku ya Jumapili. Baada ya kufahamika siku hiyo, wazazi wote kijijini walitayarisha mtama kwa wingi na uwanja mkubwa ulitengenezwa kwa ajili ya sherehe hiyo na watoto wanaotoka jandoni hukaa kwa pamoja hapo uwanjani na wazazi wao (akina mama tu) watafika mahali hapo na kukutana nao. Uwanja wa shughuli hii waitwa uwanja wa "Mbilu" hapo hapo ndipo ngoma itakapochezwa. Wakati huo watoto huvaa nguo rasmi iitwayo "Usambo" wa mbuyu, nayo huvaliwa kiunoni na kuzungushwa kichwani.

57

Siku ya Jumamosi akina mama hutayarisha unga wa mtama na nyama na kupikwa ili kuwa chakula cha sherehe. Siku hiyo hiyo ya Jumamosi akina mama ambao watoto wao ndio wanatoka, kila mmoja atamwita mtoto wake kwa zamu na kuita huko ni kama hivi: —

"Mwanangu longalonga nhulike", maana yake, "Mwanangu sema nikusikie". Mtoto wake anapaswa kuitikia hivi: —

"Nabaha mai nabaha, maana yake "Niko hapa mama, niko hapa." Mama yake akisikia sauti ya mtoto wake, basi hupiga kigelegele cha furaha kubwa kwa sababu

mtoto yupo na pili kamaliza mafunzo yake. Mtoto anaweza kufia huko huko jandoni, lakini mama yake haambiwi kama mtoto wako amefariki, bali baba yake tu anaambiwa na mazishi yanafanyika kimya kimya bila ya mama yake kujua. Mkewe haambiwi hata kidogo. Mama anaweza kupeleka chakula cha mtoto wake huko jandoni hata kama mtoto amefariki kwa sababu hajui wala haambiwi. Ataendelea kupeleka chakula mpaka siku ya kutoka watoto wote. Siku mama atakapojua kuwa mtoto wake hayupo ni siku ya kutoka ambapo akina mama wanakusanyika na watoto pia hukusanyika, halafu akina mama huita jina la mtoto wake. Iwapo mtoto wake haitikii, basi mama huondoka akifahamu kuwa mtoto wake hayupo na kwamba mtoto wake kafariki. Basi mama ataondoka mahali hapo walipo watoto na kurudi nyumbani bila ya kuonyesha huzuni yoyote. Pia siku ya Jumapili inayofuata ambayo ndiyo siku kuu kubwa ya watoto wote atakuwapo kusherehekea na atawapikia chakula watoto wa wenzie - kwa sababu katika mila za Wasagara watoto wa familia zingine kijijini wanafikiriwa kama ni watoto wa kila mmoja pale kijijini wala si watoto wa yule tu aliyezaa. Ni watoto wa kijiji kizima na mama yeyote au mzazi yeyote kijijini anaweza kuwatuma watoto wowote wam-fanyie kazi na watoto hawawezi kukataa. Mtoto yeyote anayetumwa kazi na mzazi yeyote ambaye hakumzaa akikataa, anaweza kupewa adhabu kali kabisa na yule anayemtuma. Kwa hiyo kwa desturi ya Wasagara mtoto yeyote kijijini ni mtoto wa mzazi yeyote kijijini pake.

Nyama na unga vinavyoletwa pale vyapikwa pamoja ili watoto wale kwa pamoja siku hiyo ya sherehe. Siku hiyo ya Jumapili kunakuwa na ngoma kubwa sana na watu hucheza sana ngoma hiyo. Akina baba hali kadhalika akina mama hushiriki katika kucheza ngoma hiyo. Zama hizo ngoma hii ilichezwa toka saa kumi na mbili ya jioni ya Jumamosi hadi saa kumi na mbili ya Jumapili bila kupumzika. Baada ya hiyo Jumapili, wazee fulani waliamua kuwapeleka watoto wao kama kumi hivi, kwa mzee mmoja hivi kwa ajili ya kuonyesha furaha waliyonayo wale wazazi wa watoto hao. Basi mzee huyo aliyepelekewa watoto hao alishinda nao siku moja na kulala nao usiku mmoja halafu asubuhi yake aliwarudisha hao watoto kwa wazazi wao. Lakini watoto wengine walirudi kwa wazazi wao siku hiyo hiyo ya Jumapili.

Baada ya kumaliza mafunzo ya Jandoni mtoto lazima aandamane na baba yake katika kila shughuli anayofanya, ili naye ajifunze ije imsaidie katika maisha yake ya baadaye. Shughuli hizi ni kama kujenga nyumba, kulima mashamba na kadhalika.

WAKATI WA POSA Mtoto akikua na kubalehe, basi baba ya mtoto huzungumza na mkewe na kumwambia kuwa

mtoto wao amekua afadhali achumbiwe msichana. Basi baba yake huchukua jukumu la kuangazaangaza macho huku na huko kutafuta mtoto wa kike ambaye anafaa na mwenye ukoo wa heshima. Baada ya kumpata msichana anayefaa, baba mtoto huenda kwa baba ya msichana na kumwambia kuwa anataka amchumbie mtoto wake binti yake. Basi baba ya binti akikubali, akina mama - mama ya mvulana na mama ya msichana hukutana peke yao na kuzungumza juu ya jambo hili na kukubaliana. Baada ya hapo, wazazi wa msichana humwambia binti yao mchumba wake ni nani, na pia wazazi wa mvulana humwambia mchumba wake ni nani. Baada ya hayo, msichana anapelekewa mkufu wa kuvaa mkononi na mama ya mvulana kuonyesha kuwa msichana huyo kafungwa ni wa mtu, hayuko huru. Baada ya msichana kuvikwa mkufu huo na mama ya mvulana, hupelekwa "Mbopa mkoa" yaani kitambi, kwa mama ya msichana ikiwa ni zawadi yake - shukrani kwa taabu aliyopata wakati wa kumbeba na kumchafua. Baada ya "mbopa mkoa" kupelekwa, ndipo posa yenyewe yapelekwa kwa wazazi wa msichana. Mbuzi hupelekwa na kima cha juu sana cha posa

58

ni mbuzi watano. Baada ya hapo, msichana hupelekwa moja kwa moja kwa wazazi wa mvulana kufunga ndoa na kufanya arusi.

Siku hizi, baada ya kupelekwa posa, Sheikh anaitwa na baba ya binti anatoa idhini kama amekubali. Basi Sheikh hufukiza ubani na kitezo huku baba ya mtoto hupiga magoti - na ndoa hufungwa kwa kufuata desturi za Kiisiamu au Kikristo.

Iwapo mvulana hana nyumba siku ya arusi, mvulana atakaa na mkewe katika nyumba ya babu yake, na kama nyumba ya babu yake haipo, basi nyumba yoyote ya jirani ambaye wanaelewana naye itafaa mpaka wakati huo mvulana atakapojenga nyumba yake mwenyewe. Na iwapo haiwezekani kuipata nyumba hiyo basi baba ya mvulana humwachia mtoto wake, chumba kimoja ill waweze kukaa mpaka watakapojenga nyumba yao.

KUVUNJIKA NDOA

Iwapo ndoa ilivunjika, bibi hampendi bwana, na bwana hampendi bibi, basi kilitafutwa kibua chochote na kibua chenyewe kilikeketwa vizuri na baba ya mvulana halafu akawapelekea wazazi wa msichana mbele ya watu na kusema, "Haya chukua kibua, binti yenu simpendi tena". Kama kibua hakikukeketwa vizuri (ambayo ndiyo talaka hasa ya jadi) basi kibua kilikataliwa kwa sababu ilionyesha kuwa bado binti yao anapendwa na bwana. Lakini kama kilikeketwa vizuri basi talaka ilikubaliwa. Basi matumizi ya kibua kwa jamii ya Wasagara yalikuwa ya maana sana. Talaka zote ziliwekewa msingi na kibua.

MAHARI Wakati wa kuvunjika ndoa mahari ingaliweza kuachwa yote kwa wazazi wa msichana bila ya

kurudishwa iwapo msichana alikaa vizuri na bwana yake. Mahari hayo huwekwa kama akiba ya heshima ili watakapotaka kuposa mahali pengine waweze kukubaliwa upesi kama watu wenye heshima na wasiokuwa na matata yoyote. Kuiacha mahari kwa wazazi wa msichana ilikuwa ni mojawapo ya sifa maalum kwa ukoo wa mvulana. Wakati mwingine mahari inaachwa nusu tu na nusu inarudishwa kwa sababu ya utumishi aliotumika kwa bwana yake. Basi baba ya mvulana huamua kuwa nusu ya mahari irudishwe na nusu yake ibakie. Lakini iwapo wazazi wa mvulana wamesikia kuwa huyo binti amemwacha mtoto wao kwa sababu kampata bwana mwingine, wazazi wa mvulana huamua kurudisha mahari yote.

MSICHANA

Wakati msichana alipovunja ungo, wazazi wake walitangaza mji mzima kuwa binti yao kavunja ungo. Sherehe ilifanyika kufurahia jambo hili. Mara baada ya hiyo sherehe, msichana aliwekwa ndani kwa mafunzo maalum jinsi ya kuishi na bwana, heshima kwa watu, kazi za nyumbani, na mambo mengine mengine mengi yanayohusu maisha yake ya baadaye na jinsi ya kuishi na bwana yake. Wakati anapokuwa "ndani" msichana hufunzwa na waalimu wawili - mama yake na bibi yake. Akiwa ndani, msichana hujipaka pumba ya mahindi iliyochanganywa na maji na kujisugua sana mpaka ameiva vizuri kabisa.

Muda wa kukaa ndani ulitegemea nyakati au majira. Iwapo alivunja ungo wakati wa masika, basi msichana aliwekwa ndani mpaka wakati wa kiangazi kwa sababu watu wote walikuwa na shughuli nyingi za kilimo mashambani. Lakini iwapo alivunja ungo wakati wa kiangazi basi aliwekwa ndani mpaka kiangazi kingine. Walakini muda wa kuwekwa ndani ulitegemea zaidi shughuli za wakazi wa kijiji cha msichana huyo. Iwapo watu walikuwa na shughuli nyingi, basi msichana huyo aliwekwa ndani kwa muda mrefu zaidi kuliko wakati ambapo shughuli zawanakijiji zilikuwa chache. Shughuli za kilimo ndizo zilizotawala muda wa msichana kuwekwa ndani.

Wakati wa kutoka msichana huyo alikoshwa vizuri na alivikwa nguo nzuri nzuri, na alipambwa kwa shanga na nguo mpya mpya alipewa na kuvalishwa siku hiyo. Ngoma zilichezwa sana ikiwa sherehe kubwa sana kwa siku hiyo wakati msichana akitoka. Wachezaji wa ngoma hii hasa ni akina mama ambao hushangilia mtoto wao kwa kutoka ndani. Akina mama walikuwa katika hali ya kucheza kumzunguka mtoto wao na kumzingira kabisa hata akina baba huwa ni vigumu kumwona

59

huyo mwali mwenyewe alipokaa. Iwapo huyo mwali alikuwa ameposwa tayari, basi baadaya sherehe hiyo yule mwali hupelekwa kwa bwana yake moja kwa moja. Siku ya kutoka msichana huyo, ndugu za mchumba wake wa klume huwapo kusherehekea kutoka kwa huyo mchumba wao wa kike.

Baada ya ngoma hiyo kubwa, siku ya pill yake msichana huchezewa ngoma ya ndani ya nyumba tu, ngoma hiyo yaitwa "Goko" au Koko", yaani ngoma ya mafunda. Wanawake wengi huwapo wakati wa ngoma hii ya ndani ya nyumba, na kila mwanamke wa maana hutoa mafunzo yake ya kumfunda na kumfunza yule mwali kwa mara ya mwisho. Pia mama ya msichana huwapo wakati huo ill kutoa mafunzo ya siri kwa mwali. Kwa mfano, mama mmoja hutoa mafunzo namna ya kupika, mama mwingine hutoa mafunzo namna ya kucheza, mama mwingine hutoa mafunzo jinsi ya kutambua shida ya bwana yake, nakadhalika. Hii ndiyo ngoma ya mwisho katikaelimu yake yote yule binti. Hli ndiyo elimu yake ya kumfanya afaulu na kushinda mtihani wake wote. Siku hii ndiyo (graduation day) siku ya kutoka.

Wakati msichana yumo ndani akihudhuria mafunzo mbali mbali kabla ya kutoka, wakati wa kulala hujifunika mgololi na nguo moja ya kushindia. Chakula chake wakati wote huo wa kukaa ndani ni nyama, kuku, maharagwe na chakula kinglne kllicho kizuri klzuri. Baada ya kutoka, na iwapo huko aliko hafuati yale aliyojifunza wakati akiwa mwali, basi mwalimu wake huambiwa habari hizi - hata kama ni mke wa mtu sasa. Basi mwalimu wake anangojea siku ambayo kuna mwali mwingine ambaye ndiyo kwanza anahitimu mafunzo yake, humwita yule mwanafunzi wake wa zamani ambaye hafuati na kutoitumia elimu yake vizuri na kumwambia aanze kufanya mazoezi upya tena kama vile mwali anavyofanya ili ajifunze upya kabisa kwa maana elimu yake aliyopata zamani haikumfaa. Basi huyo mwanamke huyarudia mafunzo yote siku hiyo ya sherehe ya mwali mwingine, basi siku hiyo wanafunzi wanakuwa wawili. Baada ya kumaliza mafunzo hayo siku hiyo, basi mwanamke huyo huruhusiwa kurudi kwa bwana yake ili akayatekeleze yale aliyokuwa hayafuati. Kwa kuwa ni aibu sana kwa mwanamke aliyeolewa kurudi tena kujifunza elimu ya wasichana wanaotayarishwa, basi hujitahidi sana ili aitumie elimu yake hiyo vizuri.

KIFO

Mtu mara anapokufa huzikwa mara moja - hata kama mtu kafa saa nne za usiku, lazima azikwe mara moja wakati huo huo, tena huzikwa kimya kimya bila maneno yoyote. Baadaya kuzika, mtama hutafutwa. Kuku au mbuzi huchinjwa. Iwapo marehemu alikuwa ameoa na kumwacha mke, na kama huyo mama anataka kurithiwa na ndugu za marehemu basi atarithiwa la kama hataki atarudishwa kwao. Na iwapo wapo ndugu za marehemu ambao wangependa kurithi mwanamke huyu mfiwa, basi pale kilioni wakati wakitoa sadaka mtani humwambia mfiwa kuwa kuna mnong'ono wa maneno wa kutaka kumrithi na kuambiwa kuwa anapewa uchaguzi wa kumchagua yupi ndugu ya marehemu atafaa kumrithi yule mjane, na wakati wote huu yule mjane hasemi neno ila huitikia tu kwa kutumia kichwa. Basi baada ya kutolewa taarifa hii mtani huchukuwa kijiti nakukikata vipande kwa kufuatana na jumla ya ndugu za marehemu. Mjane huletwa mbele ya wanakijiji huku akiwa amefunikwa nguo mwili mzima. Mtani huanza kusema, "Bwana Juma kijiti chake ni hiki". Yule mama huchukuwa kijiti cha Juma na kukitupa chini iwapo hampendi huyo Juma, Halafu kinatolewa kijiti kingine cha Hamisi, na mjane huchukuwa kile kijiti na kukitia kifuani mwake iwapo yule mama anampenda Hamisi awe ndiye mume wake mpya baada ya marehemu. Mara akifanya hivyo, basi vigelegele vyapigwa, na yule ndugu ambaye kijiti chake kimekubaliwa, hushikwa mkono na kupelekwa mahali pale mama amekaa na kukatishwa hapo. Mwenye shughuli ya kuongoza sherehe hii ni yule mtani wake. Sherehe ya arusi hufanyika, na yule jamaa huonywa na kukemewa sana ili aweze kuwatunza vizuri watoto wa ndugu yake marehemu.

Wasagara walipozika maiti walitumia magome ya miti ambayo yalitengenezwa vizuri kama nguo, na yakatumika kuzikia maiti. Wakati huo ngoma za kuomboleza kifo zilichezwa sana.

60

UFUNDI

Wasagara wanao ufundi wa aina mbali mbali, kwa mfano, Wasagara wana ufundi wa kuchonga vitanda, wana ufundi wa kuchonga vigoda, mipini ya mashoka na visu, wana ufundi wa kuchonga vinu, miiko, na kadhalika. Pia Wasagara wana ufundi wa kuvua samaki kwa kutumia migono, nyavu na ndoano. Vile vile Wasagara wana ufundi wa kutengeneza vilindo vya kuhifadhia nafaka mbali mbali, wanachonga mizinga na wanafinyanga vyungu wanasuka virago na kufua vyuma na kutengeneza mashoka na miundu (sengo).

UTANI WA WAKAGURU NA WASAGARA

BABA NA WANA

Baadhi ya Baba na wana kuna wakati wa kutaniana na wakati huo ni baada ya baba kufurahishwa na kitendo cha mwanawe. Kama kupatiwa pombe, nguo, nyama au tumbaku. Baba huyo anaweza kumtania mwanawe kwa kumfanya kama rafiki yake. Anamtania kwa kumpa majina ya kiutani utani kuwa yu Sultani "Mndewa" au Mkombozi - "Muonyi". Majina hayo anayomwita mwanawe ni kwa wakati ule ule wa ukarimu wake aliyomtendea. Majina hayo ijapokuwa ni ya utani yaani kilemba cha ukoka, lakini yanampa mtoto moyo mkuu wa kumsaidia baba yake kwa ajili ya ule utani wa kumtaja kwa majina ya vyeo.

Vile vile mwana anaweza kumtania baba yake iwapo baba huyo amemkaribisha kunywa pombe au kumpa tumbaku wakati huo huo tu mwana anaweza kumtania baba yake kwa maneno ya kiutani utani kumwita yu rafiki yake.

Wakati fulani utani unatumika sana jandoni kati ya baba na mtoto iwapo mtoto wake katahiriwa. Anaambiwa kuwa baba yake ni rafiki yake au ni mtani wake kwani umefanana naye kwa viungo vyenu vya kiume. Kwa hiyo kutoka katika rika hilo mvulana anajiona ana uhusiano na baba yake kwa utani hasa wawapo ni wawili tu.

Kwa jumla watoto na wazazi wao wanataniana wakati wa kutendeana matendo mema ya kiukarimu. Wanaambiana ni marafiki au ni watani. Wasichana vile vile wanataniana na mama zao kwa ajili ya mambo ya kuvunja ungo. Wakati huo msichana huwa amefanana na mama yake kwa mawaidha yakimaisha kwa kuvunja ungo, matukio ya miezi na mbinu za kushika mimba na malezi ya watoto. Vile vile wanaweza kuvaa sare na kufanya kazi za namna moja wakawa ni wa namna moja kwa kikazi na kwa utani.

MABABU, MABIBI NA WAJUKUU

Kwa kawaida hao ni watani hasa. Majina ya mababu na mabibi ndiyo majina wanayopewa wajukuu wao. Wavulana hupewa majina ya mababu zao. Wasichana wanapewa majina ya bibi zao. Wajukuu wana uhuru wa kuwatania babu na bibi zao. Ikiwa wana mapengo watawaita ni vibogoyo bila ya kuambiwa wanafanya kosa kwa mababu na mabibi zao. Waona hiyo? Wajukuu wanaweza kulalia vitanda vyao bila ya kukatazwa kwani wao ni watani wao.

VILEMBWE NA BIBI ZAO

Kwa kawaida vilembwe hawana utani na bibi au babu za wazazi wao isipokuwa babu zao ndiyo waliyo na utani nao, kwa ajili ya cheo cha ubabu na ubibi. Vilembwe ni tabaka la nne kwa hiyo wao hawana utani na mababu na mabibi wa wazazi wao, ila tu wanaweza kuwatania ikiwa kuna sherehe za pombe na furaha za ngoma.

61

SIKU ZA UTANI Kwa kawaida siku ya kwisha kilio na siku ya kuzika ndizo siku maalum za mambo ya

utani. Siku hizo utani hauwi baadhi ya watu wa familia yao ila utani unafanywa na watu wa ng'ambo ya ukoo. Kwa mfano waliyofiwa kama wana ukoo wa Wampene huwa wenye ukoo wa mpakani mwao waitwao Wasongo ndiyo watani wa kifo. Ikiwa hakuna mtani wa ukoo wa Kingambungambu kama akiwapo Mnyamwezi au Msukuma anaweza kuwa ni mtani wa kifo hicho.

UTANI KIFONI Mtani kazi yake kifoni ni kutoa maneno yenye porojo ili wenye huzuni ya kifo wasisimke

kusahau huzuni ya kifo. Wakati mwingine anamwambia marehemu analima au anawinda au ameonana na huyo mtani na kumwagizia mambo fulani fulani. Hizo ni baadhi tu za porojo za watani ili watu wacheke.

MSHAHARAWA MTANI Watani wanapewa mshahara wa kuku au vichwa vya mbuzi waliochinjwa pale kifoni

iwapo wenye kifo watawatania. Watani watasomba kuku, mbuzi, vyakula na nguo hata vitanda bila ya kuambiwa wamefanya kosa.

Kwa kawaida Wasagara na Wakaguru wanathamini sana utani kwa shughuli za vifo. Kwa hiyo Wasagara na Wakaguru wanafurahia sana maneno yenye kuwachekesha na ikiwa yamewakolea, basi yanatekelezwa vyema.

MICHEZO YA WASAGARA

Kwa jumla michezo yote ya kijijini walishirikiana vijana na wasichana. Michezo ilichezwa mara baada ya kukusanya mavuno mashambani. Michezo hiyo ilihusu ujengaji wa vibanda vidogo vidogo vya majani ambavyo wenyewe huviita (vibunda). Vibanda vilijengwa kwa manyasi, majani na mabua. Wavulana walishiriki sana katika ujenzi na wasichana walishugnulika na utayarishaji wa vyakula katika vijumba hivyo. Michezo kama vile kasimbago; michezo ya kujificha na kutafutana, michezo ya mbio na michezo ya "mafulugwa" - mchezo unaohusu kupanga miguu mmoja juu ya mmoja na kuupangua - sehemu nyembamba ndipo kamba hupitishwa na mchezaji huinua kamba juu na kupishana kati ya mkono na mkono - ikianza kuzunguka vizuri hutupwa juu na kudakwa tena.

Michezo mingine ya kuimba hufanywa wakati wa mbalamwezi. Vifaa vilivyotumika ni miti; mabua ya mahindi, mtama- udongo, mawe na kadhalika.

KILIMO CHA JADI CHA WASAGARA

Kilimo cha jadi cha Wasagara kilikuwa na faida sana kama wanavyoona Wasagara wenyewe. Zamani baada ya mvua kunguruma, mkuu wa mji alitoka nje na kukitangazia kijiji kizima kuwa ni juu ya kila mwanakijiji kutayarisha mashamba mapema kabisa kabla ya mvua kuanza kunyesha. Kila mtu aliambiwa kutayarisha mashamba mapema kabisa ili mvua zinyeshapo, wakulima wapande tu kwa sababu mashamba yametayarishwa kabisa kwa hiyo ilikuwa ni jukumu la mkuu wa Kijiji kuhakikisha kuwa kila mtu katika kijiji alikuwa ametayarisha shamba lake mapema kabla ya mvua kunyesha. Mkuu wa Kijiji huyo alisema "Humbusa", yaani "Tuanze kulima wakulima." Katika kuanza kulima kwenyewe kulianzwa kama hivi:— Kwanza mtani alitafutwa kama vile Mnzelu au Mnyakilo ambaye alichukua jembe, na kwenda mahali ambapo wanakijiji waliamua kulima mashamba yao, huko huyo mtani alianza kukwatua nyasi mahali ambapo ni njia panda au kama huko kwenye mashamba hakukuwa na njia panda, lakini palitafutwa mahali popote penye njia panda na huyo mtani wao.

62

akafanya sherehe ya kukwatua nyasi ikiwa ndiyo sherehe ya kuanzisha rasmi kulima mashamba yao hao wanakijiji waliohusika. Kila kijiji cha Wasagara kilifanya hivyo. Sherehe hiyo ya kufungua kulima ilihudhuriwa na kila mwanakijiji wa kijiji kilichohusika. Baada yasherehe hiyo ya uanzishaji rasmi wa kulima mashamba katika kijiji basi watu wote, wake kwa waume waliyavamia mashamba yao na kuyalima kwa pamoja.

Wasagara walikuwa hawalimi mtu mmoja mmoja, bali walilima pamoja kama kijiji. Kila familia ilikuwa na mashamba yake, lakini kulima kulifanywa kwa pamoja kwa kufuata zamu. Sababu ya kufanya hivi ilikuwa kwamba kwao Wasagara mvua ilikuwa kama mgeni ambaye siku ya kuja kwake nyumbani haikujulikana hata kidogo bali hutokea wakati wowote. Kwa jinsi hii, iliwalazimu Wasagara waweze kulima pamoja kwa kufuata zamu mpaka kila shamba la kila mwanakijiji limelimwa. Mvua ni kitu ambacho hutokea ghafla tu bila kutazamiwa kwa hiyo kwa kulima pamoja, Wasagara waliweza kumwahi huyo mgeni wao "Mvua."

Walianza kulima shamba la Mkuu wa Kijiji na baada ya kumaliza kulima shamba la mkuu wa Kijiji ndipo walipoanza sasa kulima shamba moja baada ya moja la kila mwanakijiji. Natunaposema shamba la mwanakijiji, hatuna maana ya eka moja au mbili hivi, bali ni zaidi ya eka 14 au 15 hivi, ndiyo shamba la mtu mmoja. Na zama hizo Wasagara walikuwa na ardhi kubwa na safi yenye rutuba nyingi sana. Kande zilipikwa ill ziliwe wakati wanakijiji wakilima. Kande hizi zilikuwa za kuwapotezea njaa tu lakini hazikuwa ndiyo chakula chao maalum kilicholiwa baada ya kazi ya shamba. Pia pombe ilinywewa baada ya kazi ya shamba na mara kwa mara mwanakijiji mwenye zamu ya kulimiwa shamba siku hiyo ndiye alikuwa na jukumu la kupika chakula cha wafanyakazi.

Wakati wa kulima wanakijiji waliberega kwanza (kukwatua). Wakati huo huo watu wengine hufuata nyuma wakitapanya (broadcasting) mihindi pamoja na udongo. Mihindi hii ni ya kuota upesi upesi kabla hawajaanza kupanda rasmi mbegu za mahindi zingine hapo baadaye. Makusudi ya kufanya hivyo ni kwamba mihindi hii inayotapanywa wakati wa kukwatua ardhi ni kutaka kupona njaa maana itaota upesi sana na wanakijiji wataepukana na baa la njaa iwapo mihindi mingine inayopandwa baadaye itakuwa bado kukomaa. Kulima kwa ushirika ndiyo kilimo cha jadi cha Wasagara. Walikuwa hawajapata kulima kila mtu mmoja mmoja, bali jadi yao kulima kwa ushirika, na tena mtu yeyote aliye na afya yake timamu ni lazima atoke kwenda kulima labda awe mgonjwa hapo husamehewa. Pia mtu mvivu hupimiwa ngwe yake mwenyewe ambapo wanakijiji wengine hulima pamoja kwa furaha na vifijo. Ikiwa yule mvivu hakumaliza ngwe yake aliyopimiwa kwa sababu ya uvivu wake, wanawake wote wa kijiji chake humcheka na kusema hafai kuwa mwanaume kwa sababu ya uvivu. Basi Wasagara waliogopa sana kuchekwa na wanawake kwa hiyo walijitahidi sana waweze kufanya kazi kwa bidii ili wasichekwe na wanawake jambo ambalo linashusha hadhi kwa wanaume wa Kisagara. Pia Wasagara walikuwa wanalima pamoja, wanaume na wanawake. Kwa jinsi hii, wanaume kuonekana mvivu na kupimiwa ngwe yake ambapo wanawake walionekana ni wenye bidii ilikuwa ni adhabu kali kabisa isiyopimika. Kwa hiyo, wanaume wengi wa Kisagara walijitahidi sana wasionekane wavivu mbele ya wake zao.

Wakati wa kulima, Wasagara waliimba nyimbo za kuwatia nguvu wakulima (work songs). Mfano wa wimbo wa kulimia ni kama huu hapa: —

"Wakulu mulimile hoi, Manye

wao walimile hoi, Manye wao

walimile kutalitali".

63

Maana yake, "Simameni mbali msije mkakatana mnapolima." Mali kadhalika waliweza kuutumia wimbo huu wakati wa kuvuna mazao yao na nyimbo nyingine nyingi. Wimbo mwingine wenye mafunzo mazuri ni kama huu hapa chini. "Kuliga kolojo uhwilehi?" Maana yake, "Unamtukana mjomba wako unamtumaini nani?" Kwa sababu, mjomba ndiye aliyekuwa anathaminiwa sana kwa sababu ya urithi, wapwazake walimwogopa na kumheshimu sana mjomba.

Zana walizozitumia katika kutayarishia mashamba yao ni Sengo (Mundu), mashoka na majembe. Mashoka na Miundi ilitumika kwa kufyekea vichaka na miti lakini majembe ndiyo yaliyotumiwa kwa kulimia. Majembe yao ya "Msuka" yalikuwa kama plena inavyoonyesha hapa chini: —

Mti ulichongwa vizuri sana kwa urefu uhaotakiwa halafu, jembe lililotengenezwa na mhunzi baada ya kuchimba chuma na kukiyeyusha motoni, lilichomekwa katika mpini kwa kutoboa tundu sehemu ya mviringo ya mpini - hasa kwa kutumia chuma kilichochomwa motoni kwanza.

Katika kutengeneza majembe, kwanza chuma chenyewe kilichimbwa toka ardhini na udongo wenye chuma ulipatikana huko Mdukwi sehemu ambayo iko katika Wilaya ya Kiiosa na mpaka sasa udongo hup wa chuma unapatikana huko. Wasagara walipogundua udongo huu wa chuma, wakaanza kuchimba na kuukusanya na halafu kuyeyusha. Vifaa vilivyotumika katika kuyeyushia hicho chuma ilikuwa ni kuni nyingi ambazo zilipatikana kwa wingi sana katika nchi ya Usagara zama hizo. Baada ya kukichoma chuma hicho basi chuma safi kikatoka, na chuma kisichofaa kikatupwa. Kile chuma safi kikatengenezwa tena katika zana mbalimbali kama vile majembe, mundu na mashoka na kadhalika. Mipini safi ya kutengenezea majembe yao ilitengenezwa toka miti ya mipingo ambayo ilipatikana kwa wingi nyakati hizo.

Wasagara waliweza kugundua udongo wenye chuma kwa kuangalia chembechembe zake ambazo zinametameta kama vile chembechembe za Ulanga (Mica). Basi baada ya kuziona chem-bechembe hizo, Wasagara waliamua kuchimba chuma hicho ili kiwafaidie katika shughuli zao za ufundi mbalimbali.

Vifaa walivyotumia katika kuchimbia chuma ni mawe yalichongwa kama majembe. Kabla ya kuanza kuchimba chuma chao, walichukua majani yaitwayo "Hoza" na wakayafikicha, na baada ya kuyafikicha, walinyunyiza maji yake juu ya mahali pale walipotaka kuchimba chuma chenyewe ili kupapooza pasitokee shari yoyote wakati wa uchimbuzi wa chuma. "Hoza" ni dawa ambayo inatumika kwa mambo mengi ili pasitokee shari au mkosi wowote. Dawa hii yatumika kunyunyizia mtu anapokuwa amefariki dunia.

64

Kilimo cha Wasagara kilifanyika wakati wa kiangazi na wakati wa masika. Wakati wa kiangazi, mto wao maarufu sana Mkondoa uliwaletea manufaa mengi sana Wasagara. Mto huu ulikuwa bado kuchimba sana bonde lake na ulikuwa na matete na magugu mengi sana katika kingo zake. Wakati ulipofurika maji yake yalisambaa na yalipindukia kingo zake na baadaye yakarudi tena katika njia yake wakati wa kiangazi huku yakiacha unyevu unyevu na mbolea nyingi sana katika sehemu za mashamba yaliyokuwa yakilimwa kandokando ya mto huu. Basi Wasagara walilima sana mazao rnengi wakati huu na kuweza kupata mazao bora licha ya kupata mazao ya wakati wa masika. Kwa hiyo, baa la njaa katika nchi ya Usagara ilikuwa shida kuwakabili.

Kupanda mbegu shambani Wasagara walipanda pamoja wake kwa waume, kama walivyofanya katika shughuli za kulima mashamba yao na kilimo chao maarufu sana kilikuwa ni Sesa. Na kupanda mbegu walianzia shamba la Mkuu wa mji au Mkuu wa kijiji halafu na kuendelea kupanda mbegu katika mashamba ya wanakijiji wote. Wakati wa kupanda, walichanganya mbegu za mihindi na mbegu za mtama katika shimo moja. Mtama uliota na mhindi ukatoka katika shimo hilo hilo moja na walitumia majembe katika kupanda mbegu mashambani. Njia hii ya kupanda mbegu za aina mbili tofauti katika shimo moja ilikuwa na manufaa sana. Kwanza mbegu zina uwezo unaotofautiana katika kupambana na wadudu waharibifu, kwa hiyo iwapo mbegu za aina fulani zitashambuliwa na wadudu mbegu za aina nyingine zitabakia, kwa hiyo mkulima hatapata hasara ya jumla, atapata mimea kutokana na aina nyingine ya mbegu. Pili, faida nyingine za mbegu zachukuwa muda mfupi sana kuzaa mazao kuliko mbegu za mimea mingine. Kwa hiyo mkulima atazidi kupata mazao fulani wakati mazao mengine yanaendelea kukomaa pole pole. Tatu mimea mingine yahitaji mvua nyingi na mingine yahitaji mvua chache, kwa hiyo iwapo mvua zitakuwa chache mwaka huo, mkulima atapata mavuno ya mimea yenye kutaka mvua chache tu. Nne, mkulima anapopalilia shamba lake, anapaiilia shamba lenye aina mbili za mimea. Kwa hiyo mkulima akipalilia shamba moja, kusema kweli atakuwa amepalilia mashamba mawili yenye mimea ya aina mbili tofauti. Tano, kwa kufanya hivyo mkulima anaweza kuwa na ardhi nyingi zaidi kwa ajili ya mimea mingine. Sita, wakati wa kuvuna mkulima anavuna mazao ya aina mbili tofauti.

Mashamba yaliyokuwa karibu na nyumba, Wasagara walipanda mbegu kwa kutumia "Mwokambiko" au "Mandu". Hiki ni kijiti cha kuchimbia mashimo ya kupandia mbegu ili kuku waweze kushindwa kuparuaparua mashimo yenye mbegu na kuzila.

MGAWANYO WA KAZI

Kulima na kupanda ilikuwa kazi ya wanaume na wanawake isipokuwa kuchimba mashimo ilikuwa kazi ya wanaume tu. Kuvuna walivuna pamoja ili chakula kisiharibikie shambani kama kawaida ya Wasagara, kazi zote zilizofanywa pamoja zilianzia kwa Mkuu wa Kijiji. Kwa kuvuna walianza shamba la Mkuu wa Kijiji halafu baada ya kumaliza shamba la mkuu wa kijiji, ndipo wakaendelea kuvuna mashamba ya wanakijiji kwa zamu, wakati wa kuvuna nyimbo nyingi ziliimbwa shambani.

Baada ya kuvuna chakula chote, kingine kiliwekwa katika maghala ya kila mwanakijiji na kuhifadhiwa humo. Chakula cha kutumia hakikuwekwa katika ghala hizo bali kiliwekwa katika ghala tofauti ili kurahisisha kazi ya kukichukua na kukitumia. Chakula kilichowekwa katika ghala, kilihifadhiwa vizuri sana tena kwa ufundi maalum. Maghala yenyewe yalikuwa ya Msonge na kila mwanakijiji alikuwa-na ghala yake, hata mkuu wa mji au mkuu wa kijiji alikuwa na ghala yake. Muundo wa maghaia wenyewe ulikuwa kama inavyoonyesha picha hapa chini.

65

Na hii ndiyo sehemu inayozungushiwa

nje ya ghala yenyewe nayo yaitwa Herengo. Halafu moto ulikokwa chini ili kuyakausha mazao yaliyomo ndani ya ghala ili mazao yasishambuliwe na wadudu. Kilichokuwa katika ghala hakikuliwa mpaka wakati wa shida. Iwapo shida ya chakula ilimkabiii jamaa fulani, basi Wasagara wenziwe walimgawia chakula bure - hasa mkuu wa mji alitoa chakula toka kwenye ghala yake na kuwagawia watu wake waliopatwa na shida hiyo. Hakuna aliyeweza kununua chakula katika k i j i j i . Shida ya chakula ya mtu mmoja ilikuwa ni shida ya kijiji kizima.

Iwapo kijiji kingine kiliingiwa na baa la njaa mtu mmoja kutoka kijiji hicho alitumwa na mkuu wa mji ili aende katika kijiji cha pili chenye neema na kuwaomba wawagawie chakula.

Basi mkuu wa kij i j i chenye chakula humwambia mjumbe huyo kuwa arudi kwao na kwamba watapata habari kesho yake. Baada ya huyo mjumbe kurudi kwao, mkuu wa kijiji huitisha mkutano wa watu wote kijijini na kuelezea shida ya wanakijiji wa kijiji cha pili. Basi katika mkutano huo wote kwa pamoja hutoa uamuzi wa kiasi cha chakula kitakachotolewa. Baada ya hapo Mkuu wa Kijiji wenye shida huwa na wazo kwamba baadaye watakapopata neema basi chakula walichogawiwa, ambacho ni mali ya kijiji, watawarudishia. Lakini kama baa hili linahusu wanakijiji wenyewe kwa wenyewe, chakula chatolewa bure na Mkuu wa kijiji na wala hakuna kulipa hapo baadaye hata kama neema itapatikana namna gani - kwa sababu wao ndio wenye chakula ndio wenye ghala na mkuu wa kijiji hutunza hiyo ghala kwa niaba ya wanakijiji.

66

PLANI YA GHALA

UAABO LA GHALA YENYEWE

Ghala za kijiji zilijengwa imara kabisa Hi kuzuia panya na wanyama waharibifu. Walitumia miti na majani ya kuezekea katika kuzijenga ghala zenyewe na zilikandikwa ili zisiweze kuingiliwa na wanyama waharibifu. Mlango wake ulikuwa imara kabisa na uliweza kutosha barabara katika nafasi ya tundu lake. Iwapo ilionekana kuwa panya waliingia ndani ya ghala kwa bahati mbaya, basi wanakijiji wote walialikana siku hiyo na kuzifumua ghala zote na kuwaua panya wote kwa kuwapiga fimbo. Pombe ilipikwa ili iweze kunywewa baada ya kazi ya kuua mapanya. Wizi ulikuwa hamna kabisa zama hizo. Mali kadhalika chakula hakikuuzwa kwa mtu yeyote kwa sababu kila mtu alikuwa nacho, na mtu mwenye njaa aliweza kupewa chakula bure.

CHAMA CHA USHIRIKA CHA WILAYA YA KILOSA

Katika Wilaya ya Kilosa kuna Chama cha Ushirika ambacho ndicho kinachotoa huduma za kiushirika kwa upande wa watu wa Kilosa. Chama hiki kinaonyesha mfano bora wa ushirikiano wa kisasa tofauti na ule ushirikiano wa kijadi uliokwisha elezwa hapo juu. Chini ya chama hiki kuna vyama vingine vidogo vidogo vya wakulima ambavyo vinashughulikia mazao yao moja kwa moja. Chama cha Ushirika cha Wilaya ya Kilosa kina shughulikia mazao haya: —

(i) Mpunga; (ii) Nyonyo;

(irl) Mahindi; (iv) Alizeti, n.k.

Kutoka kwenye vyama vidogo vidogo vya ushirika vya wakulima chama cha Ushirika cha Kilosa hununua mazao haya na kuyasafirisha hadi mjini Kilosa na kutunzwa katika maghala ya Chama mpaka siku yatakaposafirishwa tena kwenda kule yanakotakiwa kama ilivyoelezwa hapo chini. Chama hutuma magari yao ambayo hukodishwa na kuyasomba mazao yote mpaka kwenye maghala yao. Gharama zote za uchukuzi hulipwa na mkulima mwenyewe, ndiyo kusema kwamba katika ile bei ya kununulia ni lazima gharama ya usafirishaji itiwe. Hivyo basi mkulima hulipa kiasi fulani cha fedha za usafirishaji kwa kilo itakayopimwa. Na vile vile mlaji wa kila zao linaloshughulikiwa na chama cha Ushirika yampasa kulipia gharama zote hizo.

Maghala yao yako imara kwa kuweza kuhifadhi mazao kuzuia wanyama waharibifu wasipate nafasi ya kuyaharibu mazao hayo yanapokuwa ghalani. Mali kadhalika mazao hayo yakiwa bado ghalani hutiwa madawa ya kuzuia wadudu wasiyashambulie. Wakati msimu ni mzito, yaani wakati mavuno mengi yamepatikana, maghala yao hujaa sana na kusababisha kutunza mazao mengine nje ya maghala. Lakini wakati mazao mengine yanapotunzwa nje namna hii, tahadhari huchukuliwa ili mazao hayo yasije yakaharibiwa na mvua, wanyama, wadudu au kuibiwa na watu.

Chama hiki kinapata magari ya kusafirishia mazao toka kwa wakulima kwa kuyakodi. Magari hayo yapatikana toka kwa: —

(a) UMITA (b) Chama cha Ushirika cha Mkoa. (c) Bwana Aziz Kassam, n.k.

Barabara za Kilosa sio imara sana tena ni nyembamba mno. Kwa jinsi hii malori yenye tani nyingi hayawezi kupita kwa usalama katika barabara hizi; labdatu hayo malori yasipakie hayo mazao kiasi cha uzito wake. Wakati wa majira ya mvua, kazi ya kusafirisha hayo mazao huwa ni ngumu zaidi kwa sababu zilizokwisha elezwa hapo juu. Kwa hiyo chama chajitahidi sana kuyasafirisha mazao hayo wakati wa kiangazi tu kutoka kwa wakulima. Na chama chenyewe sasa huyasafirisha mazao hayo toka Kilosa hadi Dar es Salaam kwa kutumia reli zaidi. Mazao hayo husafirishwa toka Kilosa hadi kwenye Mashirika ya Gapex na Usagaji (National Milling) kwa sababu chama cha ushirika cha Kilosa ni ajenti tu wa mashirika hayo, na gharama zote za usafirishaji wa mazao haya ni juu ya mashirika hayo.

67

HUDUMA ZA CHAMA CHA USHIRIKA KWA WAKULIMA WA KILOSA

Kama nilivyosema hapo juu chama cha Ushirika ni namna mpya ya ushirikiano katika shughuli za uzalishaji mali (Angalia ushirika wa jadi wa Wasagara hapo juu). Ingawa ushirika wa namna hii ni mpya, lakini si kitu kigeni kwa Wasagara kwa sababu wakulima walikuwa na ushirika wa asili tangu zamani ushirika ambao uliwaletea manufaa mengi sana kimaisha. Huduma wazipatazo wakulima kutoka kwenye chama hiki ni kama ilivyoonyesha hapo juu. Kwanza chama kinawasaidia wakulima kwa kusafirisha mazao yao toka kwenye maghala yao hadi makao makuu ya chama ambako mazao hayo yanahifadhiwa vizuri mpaka pale yatakapotakiwa kusafirishwa tena hadi Usagaji na Gapex Dar es Salaam. Pili chama vile vile kinawauzia wanachama wake mbolea kwa bei nafuu, tatu chama kinawasaidia wanachama wake kwa kuwatafutia madawa bora ya kuulia wadudu waharibifu wa mimea mbali mbali. Kwa ajili ya huduma hizo, chama cha ushirika kinafanya kazi ya kuwa kama karakana ya utaalamu wa kutawanya maarifa mbali mbali kwa wakulima na wanachama (As a workshop of technology for the diffusion of innovations).

Picha hii hapa chini yaonyesha jinsi zao hilo hilo linalolimwa na mkulima linavyoweza kumfikia mkulima tena. Kwa hiyo gharama huzidi kuongezeka mpaka kumfikia mkulima tena.

Tabia za watu fulani fulani za kuhamahama kutafuta kazi (Labour Migration) hazikujulikana zama hizo za Wasagara mpaka ukoloni ulipoingizwa na Wazungu. Kila mtu katika Kijiji alikuwa na kazi yake na kufanya uvivu hakukuwepo, na iwapo kulitokea kwamba watu fulani walikuwa wavivu hao walipewa adhabu ya kupimiwa ngwe zao na halafu kuchekwa na kudharauliwa na wanawake. Hizi ndizo namna za adhabu walizopewa kijijini. Lakini baada ya ukoloni kuingia nchini Wasagara wengi walihamia sehemu za mashamba ya mikonge, wengine wakahamia mijini kutafuta kazi, na kwa jinsi hii utaratibu wa maisha ukaharibiwa sana na ukoloni na nidhamu waliyokuwa nayo Wasagara katika Mila na Desturi zao ikaathiriwa kabisa na kuweza kupoteza heshima ya Wasagara ya Zamani.

68

WANYAMA Wanyama waliofugwa na Wasagara ni Mbuzi, Kondoo, Bata, Kuku na kadhalika. Ng'ombe

hawajapata kufugwa na jamii ya Wasagara. Mbwa hawakuwapo tangu awali lakini walikuja fugwa baadaye sana tena watu wachache sana waliwafuga wanyama hawa. Matumizi ya mbwa yalikuwa kuwafukuzia wanyama waharibifu kama vile nyani. Mbuzi hawakufugwa kwa ajili ya maziwa bali twaweza kusema wanyama hawa walifugwa kwa ajili ya ufahari tu (Social Prestige) kwa sababu kufugwa kwa mbuzi hakukuwasaidia sana Wasagara. Tena wanyama hawa hawakuchinjwa ill kupata nyama yake ambayo ilikuwa ni kitu cha muhimu kwa afya yao. Lakini zaidi mbuzi walitumika kama mahari kwa kuolea wanawake. Wahindi walipokuja kuishi na kufanya biashara katika nchi ya Kilosa, basi Wasagara wakaanza kuwakamua mbuzi wao na kuwauzia maziwa Wahindi.

Kondoo walifugwa tu bila ya kuchinjwa ili kupata nyama wala maziwa yao hayakukamuliwa. Matumizi makubwa ya Kondoo yalikuwa kwa ajili ya tambiko na kufanyia dawa ya kuponyeshea safura.

FAMILIA Kwa kawaida kila familia ya Wasagara ilikuwa na Baba, Mama, Wana, na Mabinti. Hii ndiyo

familia maalum ya Kisagara. Lakini kwa sababu za maradhi au uzee mama wa familia fulani, baada ya kuona kuwa nguvu zake zilipungua sana, na kazi nyingi kumzidi, hasa kazi na mashamba ambayo yalikuwa ni makubwa sana kuliko mashamba ya siku hizi, aliweza kumwomba bwana yake aoe mwanamke wa pili aweze kumsaidia katika kazi za kuhudumia familia yao. Basi bwana anayehusika aliweza kuoa mwanamke wa pili baada ya kupata ruhusa toka kwa mke wake. Iwapo bwana huyo alioa mwanamke wa pili alilazimika kumjengea nyumba yake huyo mwanamke wa pili mbali kidogo na nyumba ya mke mkubwa. Ilikuwa ni desturi ya Wasagara waliooa mitara namna hii kuwajengea nyumba za peke yao. Haikuwa ni desturi kwao kuwaweka wanawake wote katika nyumba moja. Lakini kwa jumla, mitara ilikuwa nadra sana kupatikana katika majumba ya jamii ya Wasagara kwa sababu haikuwa jadi yao.

Iwapo mitara ilikaa karibu na ikatokea kwamba bwana wa mitara hiyo kafariki dunia, na iwapo mama wote wawili walizaa watoto, basi wanakijiji walikusanyika na kuigawanya mali sawa sawa -marehemu aligawiwa 6/10 ya mali yote iliyokuwa katika nyumba ya kila mwanamke, na kila mwanamke alipata 4/10 ya mali iliyokuwa katika nyumba yake aliyochuma pamoja na bwana yake. Sasa mali yote ya marehemu toka mitara yote miwili ilikuwa 6/10 + 6/10 na ikawekwa pamoja, na baada ya kufanya hivi watoto wote wa mama wote wawili waligawiwa sehemu ya marehemu. Lakini iwapo wake zake walikaa mbali mbali sana, yaani kila mtara umbali wa maili kumi au zaidi hivi toka nyumba ya mtara mmoja hadi mwingine, basi kila mtara ulibakia huko huko pamoja na watoto na kurithi mali ya nyumba yake.

Katika jamii ya Kisagara, familia - koo - milango au jamii walikuwa hawabaguani wala kuogopana wala kugombana bali walipendana, hata kati ya jamii na jamii nyingine walikuwa hawagombani wala kuogopana. Waliweza kusaidiana katika shida mbali mbali zilizowatopea katika maisha yao. Ingawa walisaidiana namna hirna kutoogopana. Lakini ulinzi wa kabila lao ulikuwa mkali kabisa. Kwa mfano, mgeni yeyote aliyefika katika mji wa watu ambao si wa kwao ilimlazimu afikie kwa mkuu wa mji huo ama sivyo alifukuzwa saa ile ile anapogunduliwa kuwa kaingia na kukaa katika mji wa watu bila idhini ya mkuu wa mji. Pia kila mwanakijiji alikuwa na jukumu la kuhakikisha kwamba hakuna mtu yeyote mgeni aliyekaa kijijini bila kwanza kukutana na Mkuu wa Kijiji na kupata ruhusa ya kukaa humo. Kila mgeni aliripotiwa kwa mkuu wa Kijiji. Hii ilikuwa ni kwa ajili ya usalama wakijiji kizima.

NYUMBA ZA WASAGARA

Nyumba zao zilikuwa za msonge, na zilijengwa kuzunguka nyumba moja ya msonge iliyojengwa katikati ya kijiji. Nyumba hii ilikuwa ndipo mahali pakulia chakula pamoja kwa wanakijiji. Chakula chote kutoka kila nyumba kililetwa hapo na wanaume wote wakakaa hapo saa za chakula na kula chakula chao hapo. Pia hapo hapo katikati, nyumba ya Mkuu wakijiji ilijengwa, pengine madhumuni

69

ya kufanya hivyo ni kumlinda Mkuu wa kijiji asije akadhuriwa na watu wabaya. Vifaa vilivyotumika kujengea nyumba ni miti, mikambaa, misani, na kamba zake ni gamba la miombo - hasa kamba hizi zilitoka vizuri sana wakati wa masika ambapo miti mingi ilikuwa imefyonza maji mengi toka ardhini. Pia kamba za mibungo zilitumika sana katika kujengea nyumba. Fito zilizotumika ni mianzi ambayo ilipasuliwa katikati na kufanya fito nzuri sana za kujengea nyumba.

Fito za mkole vile vile zilitumiwa kwa kujengea nyumba. Mwamba wa nyumba ulikuwa ni miti, na kenchi ya paa ilifungwa na mibungo. Vifaa vyote hivi vilipatikana karibu na kijiji. Majani ya kuezekea yalikuwa majani ya sanje, majani ya motomoto, na kadhalika, ambayo yalifungwa katika mafungu mafungu wakati wa kuezeka. Majani ya kuezekea yalipofungwa mafungu mafungu kwa kamba na halafu kuezekwa, yaliweza kudumu muda mrefu sana, hata zaidi ya miaka mitatu.

MILANGO - AINA YA MBILA

Milango hii ilikuwa inasukwa vizuri kabisa na kufanya mlango. Miti ilitafutwa na kupangwa chini katika safu halafu fito zilitafutwa na kusukwa nje ya hiyo miti pande zote mbili - na baadaye miti hiyo ikazibwa kabisa na kusukwa kwa fito pande zote mbili - nje na ndani. Kamba za mibungo zilitumika katika kusukia hizo fito zenyewe juu ya miti iliyokwisha tandikwa chini katika safu moja.

PICHAYAAALANGO

NDOA

Kwa kawaida mwanaume alioa mke kufuatana na maelezo yaliyotolewa katika elimu ya jadi ya Wasagara. Lakini iwapo mtu aliyekwisha oa anataka kuoa tena mke mwingine, hasa hii ilitokea wakati mke wa kwanza alionekana mkali kwa bwana wake, alikwenda kwa rafiki yake na kumwelezea shida yake inayosababishwa na ukali wa mke. Basi yule mshenga wake humwambia rafiki yupi mwanamke mgani ana sifa safi za kuolewa na bwana. Basi kama rafiki yake akikubaliana na sifa hizo, mshenga wake huenda kumwita huyo mwanamke mgani wanayemtaka. Baada ya huyo mwanamke kuambiwa na mshenga kuwa bwana mwenyewe ni huyu anayemtaka kumwoa, humuuliza mshenga swali huku mama huyu ameinama bila kuwaangalia wale wanaozungumza nao kuwa, "Je ninyi mwanijuaje?" Basi hao wanaume humwelezea jinsi wanavyomfahamu. Anayetaka kumposa huyo

70

mwanamke hasemi neno lolote ila tu yule mshenga wake ndiyo mwenye kukabili maswali yote yatokayo kwa mwanamke. Basi mama akisha kubali huvikwa "Kikomo" cha chuma mkononi mwake na anayefanya kazi ya kumvika mwanamke huyo hicho kikomo ni yule mshenga. Kikomo hicho ndicho kifunga uchumba.

Basi yule bwana lazima aende nyumbani kwa yule mwanamke mgani na kabla hajaenda anapatana na yule mwanamke anayetaka kumwoa juu ya alama atakazozitumia wakati wa kubisha nodi nyumbani kwake. Yule mwanaume maana anatakiwa kwenda huko saa nne za usiku na kulala huko huko kwa mwanamke mgani. Basi baada ya kupatana juu ya alama atakazozitumia yule bwana, mwanamke huondoka na kurudi nyumbani kwake. Basi. bwana siku ya kuondoka kwenda kwa yule mwanamke anayetaka kumwoa, huchukua jembe, mundu na shoka kama ndio alama za kuonyesha uanaume. Huondoka saa za usiku kama saa nne hivi usiku na kwenda kwa yule bibi anayemtaka. Anapofika kwa huyo mchumba wake, hubisha mlango kwa kutumia alama alizomwelezea mchumba wake. Basi yule mwanamke huamka baada ya kusikia kubisha kwa mtu, anajua kabisa zile alama alizoelezewa. Kabla hajafungua mlango, ni lazima kwanza achungulie kupitia pembeni mwa mlango wake au kupitia kijidirisha cha nyumba yake. Anapofanya hivyo anahakikisha kama kweli yule mtu ndiye mchumba wake, lakini kama si yeye basi hawezi kuufungua mlango. Baada ya kufunguliwa mlango, yule bwana huingia ndani na kulala humo humo pamoja na mchumba wake. Kabla ya yule bwana kwenda nyumbani kwa yule mwanamke, yule mwanamke huwa ametoa taarifa kwa Mkuu wa kijiji chake kuwa atapata mgeni usiku huo, na habari hii huzagaa kijiji chote cha yule mwanamke. Kwa hiyo yule bwana atakapofika kwa yule mwanamke huwa kila mtu anafahamu nini kinatendeka nyumbani kwake huyo mama.

Bwana huyo hulala kwa mwanamke huyo mpaka asubuhi, na asubuhi hiyo bwana huyo huchelewa kuamka. Asubuhi na mapema, yule mwanamke huenda kwa Mkuu wa mji na kutoa taarifa ya kwamba mgeni alilala nyumbani kwake. Basi Mkuu wa kijiji humwambia huyo bibi kuwa aende akamwambie mgeni wake ya kuwa aende akamwamkie huyo mkuu wa kijiji. Wakati huo watu wote kijijini hawaendi shambani bali hukaa nje ya nyumba zao ili waweze kumwona huyo bwana. Basi yule bwana hutoka nje ya nyumba ya mchumba wake huku akichukuwa mundu, shoka, jembe lake na kwenda kwa Mkuu wa kijiji au mji. Wakati akitoka watu humwangalia na kumpima kama huyo kweli ni mwanaume au la. Jambo kubwa lililomfanya mwanaume aonekane kama ni mwanaume kweli ni zile zana anazokuja nazo kwa yule mwanamke, yaani mundu, jembe, na shoka.

Basi yule bwana huondoka pale nyumbani pa mwanamke na kwenda kumwamkia Mkuu wa mji. Baada ya kumwamkia Mkuu wa mji, huambiwa aje siku ya pili yake ili aonyeshwe kishamba cha kumlimia yule Mkuu wa mji. Kiasi cha kijishamba chenyewe ni zaidi ya eka mbili hivi. Yule bwana huenda kwa Mkuu wa mji na kuonyeshwa shamba lenyewe. Basi yule jamaa hushinda huko shambani akifyeka na kulima. Kazi yenyewe ilimchukuwa siku saba au zaidi, si kazi rahisi. Baada ya kumaliza kulima lile shamba yule bwana humwambia mchumba wake kuwa amemaliza kulima shamba na kwamba aende akamwarifu Mkuu wa mji kwenda kuangalia na yeye hurudi nyumbani kwake na kwamba yeye Mkuu wa mji sasa aende akaliangalie lile shamba lililolimwa na yule mchumba wake. Mkuu wa mji huenda kuliangalia lile shamba baada ya kuliangalia shamba lenyewe, humwambia yule bibi kuwa yule ndio bwana wa kumwoa - anafaa kabisa. Basi yule bwana huambiwa alete mbuzi mmoja iwe ndio posa na mahari ya kwanza. Mahari huendelea na kufikia mbuzi watano. Mahari haikuthaminiwa sana bali nguvu za mtu katika kufanya kazi ndizo zilizothaminiwa sana kuliko mahari yenyewe. Siku ya arusi palipikwa pombe nyingi na chakula kwa wingi. Siku hiyo kuku walichinjwa sana ili kusherehekea arusi hiyo, karibu kila nyumba ilipika pombe ya arusi. Ngoma na nyimbo kwa wingi ziliimbwa na bibi arusi alipewa kitambi kimoja kama zawadi. Sherehe ilichezwa kwa kufuatana na wingi wa pombe zilizopikwa siku hiyo.

Nyimbo na ngoma zilichezwa. Mfano wa ngoma zenyewe ni hizi:

Kombe, Kisembe, Ndomole, Segesela na Mbilu. Hizo ndizo ngoma za wanaume. Wanawake hucheza sana ngoma ya Gubi.

71

Kazi za akina mama katika jamii ya Kisagara ni kusaidia wanaume kujenga nyumba - kutwanga mahindi - kusuka mikeka - vitunga - majamvi, ufinyanzi - kulima - kupika nakadhalika. Wanaume wana kazi ya kulima - kujenga nyumba na zinginezo nyingi.

DESTURI ZA KUAMKIANA

Desturi za Wasagara za kuamkiana zilikuwa zinatiliwa maanani kama ni sehemu ya adabu na nidhamu kwa Wasagara wote. Kwa hiyo kuamkiana ilikuwa ni jambo la lazima na mpaka sasa Wasagara huamkiana sana kuonyesha adabu, nidhamu na upole. Mwanamke wa Kisagara anapotaka kuwaamkia wanaume, huenda karibu na nyumba au karibu na mti wowote ulio karibu na hapo kujificha nusu ya sehemu ya mwili wake kwa kutumia mti huo au ukuta wa nyumba halafu huchuchumaa chini na kuwaamkia huku jicho moja tu huwaangalia wanaume anaowaamkia na kusema "Amsindile" - habari za kutwa kama ni asubuhi huamkia "Hamwasile" Mmeamkaje.

Iwapo mwanamke amekutana na mwanaume njiani, basi mwanamke huacha njia - humwachia njia mwanaume halafu hupiga magoti bila kumtazama na humwamkia huyo bwana. Mwanaume anapomwamkia mwanaume mwenziwe zaidi itategemea yupi kati yao yu mkubwa kwa umri. Kwa kawaida mdogo hupiga magoti kumwamkia mkubwa huku akitoa kofia iwapo anayo. Mali kadhalika mtawala wa nchi ya Wasagara aliamkiwa hivi hivi kama ilivyoelezwa hapo juu.

UTAWALA

Umbo la utawala wa nchi ya Wasagara - Chifu Mzee Kutukutu - Waziri wake - Wandewa wadogo - wazee - mabaraza ya usuluhisho na kila tarafa ilikuwa na mkuu wake - na mashauri yalipelekwa moja kwa moja kwa Kutukutu mwenyewe. Adhabu zilitolewa kwa kufuatana na makosa yenyewe. Makosa makubwa yalipelekwa kwa Kutukutu mwenyewe.

Kodi iliyotolewa haikutolewa kwa kutumia fedha, bali chakula kilichochangwa kwenda kwa chifu. Kila mtu alifanya hivyo. Mali kadhalika wakati wa kulima kila mtu ilimbidi akalime shamba la mkuu wa kijiji au chifu. Chakula kilichovunwa katika shamba la chifu kiliwekwa katika ghala ya nchi au ghala ya kijiji, na wakati wa dhiki, chakula hiki kiligawiwa kwa wananchi wote bure.

Mundewa alitawazwa na mtani wa Wasagara. Mara nyingi Mundewa anayetawazwa lazima awe ni mtu anayekubalika na wananchi. Kwanza kabla ya kutawazwa mtani anayefanya kazi ya kum-tawaza Mundewa huwauliza watu ni mtu wa ukoo gani huyo anayetaka kutawazwa. Basi ndugu za huyo Mundewa anayetaka kutawala husimulia hadithi yote kuhusu Mundewa huyo na kutoa sifa zote alizonazo. Halafu mtani huwauliza watu, "Je! Mundewa huyu ni mtumwa, Suria au vipi?"

Basi mtani huyo anahakikishiwa kuwa Mundewa huyo ni Mwuungwana. Katika nchi ya Wasagara mtu Suria alikubaliwa kutawala nchi hiyo. Sababu kubwa ya kufanya hivi ni kwamba, Wasagara ni jamii ambayo ilikuwa inafuata urithi kwa upande wa mama (Matrilineal Society) na waliogopa kuwa iwapo mtu ambaye hakuwa Suria alitawala, utawala huo wakati wa kurithi kwa mjomba wake ambayo ndiyo iliyokuwa ada yao, angepeleka utawala wote wa Wasagara kwa wajomba zake, halafu wajomba zake tu ndio wangeweza kurithi utawala huo. Pia Wasagara waliogopa kumpa utawala mtu ambaye hakuwa Suria kwa sababu baada ya kuupeleka utawala wa Wasagara kwa wajomba zake, basi wasingeweza kumnyang'anya huyo Mundewa utawala iwapo alifanya makosa au kukiuka miiko ya utawala wao. Lakini Suria ni mtu asiyekuwa na wajomba ambako angepeleka ufalme wa Wasagara, pili ilikuwa ni rahisi kwa Wasagara kumnyang'anya utawala wao iwapo huyo Suria alikiuka miiko ya utawala wa Wasagara.

72

Wakati wa kutawazwa, huyo Mundewa au chifu hukalishwa juu ya kigoda huku amefunikwa nguo. Shughuli hii hufanywa na mtani - ndiye kasisi wa sherehe zote hizi. Halafu Mundewa huvikwa kikomo mkononi. Baada ya hapo huyo jamaa anayetawazwa hupewa shoka, mundu, zana za kufyekea miti na majani shambani. Mkuki - alama ya kuonyesha iwapo vita itatokea aweze kulinda Taifa lake. Akiwa bado kigodani, mfalme huyo hutemewa pombe kinywani mwake toka kinywani mwa mtani anayefanya kazi ya kumtawaza siku hiyo na anaimeza pombe hiyo.

KIAPO

Mfalme huyo hula kiapo cha kutawala nchi kama hivi:-

Uleke ukobo - acha kuwanyima watu. Uleke ugoni

ugoni - acha mambo ya uzinifu. Uleke upekeupeke -

acha uwongo.

Wewe jina lako liwe "Nifenazo" - yaani "Wewe uwe mtunza siri, cheka na kila mtu". "Mhasemwe wadala" - usisahau wazee. Halafu mfalme anatiwa mafuta ya nyonyo kichwani pake, halafu mafuta

yale hutiririka kuja usoni - puani mpaka mdomoni; halafu mtani wake wa kike huja na kuyalamba mafuta yale yaliyotiririka karibu na mdomo wa mfalme na kuyameza.

Mtani anayefanya kazi hii ya kumtawaza mfalme hupewa mbuzi kama zawadi yake kwa kazi aliyoifanya siku hiyo. Halafu huyo mtani huingia ndani ya nyumba ya mfalme na kulala juu ya kitanda cha mfalme na kumwita mke wake mtani na kulala naye juu ya hicho kitanda cha mfalme ila hawatendi jambo lolote. Nyumba ya mfalme hunyunyiziwa hoza ill kuipooza.

MAJI

Maji ya kunywa ilikuwa lazima yatoke kisimani ambacho kilichimbwa katika kila kijiji cha Wasagara - hasa kisima kilichimbwa chini ya mti mbali kidogo na kijiji kuhakikisha kuwa maji hayakuchafuliwa na chochote. Maji ya mto Mkondoa hayakutumika kwa kunywa ila kwa kumwagilia mashamba tu. Kisima chenyewe kilifunikwa na magome ya miti. Maji ya kufulia nguo na kuoga yalitoka kisimani, na yalitekwa na kutiwa katika chungu kikubwa kilichotengenezwa kilichoitwa "Ponda".

73

Wasagara walikuwa wanatengeneza mavazi ya wao wenyewe kabla ya kuletwa mavazi mapya na wakoloni. Walitengeneza mavazi yao toka kwenye magome ya miti ya "Mlenye". Gome la mti huu liliondolewa vizuri sana kwa kutumia shoka na tezo, halafu likalainishwa vizuri sana kwa kulipon-daponda na jiwe au kipande cha mti na kisha likavaliwa kiunoni. Kofia vile vile zilitengenezwa kutokana na magome ya miti hii ya "Mlenye". Mbeleko ya kubebea mtoto na viatu vyote vilitengenezwa kutokana na hayo hayo magome ya miti. Wakati mwingine viatu vilitengenezwa kutokana na ngozi ya mbuzi.

MAPAMBO

Mwanamke alijipaka mafuta ya nyonyo ambazo zilikuwa zikipandwa sana wakati huo na ambazo mpaka wakati huu zapandwa sana kama zao la kuwaletea fedha. Masikio ya wanawake yalitobolewa na kutiwa mpingo. Nywele zao zilikatwa halafu zikatiwa mafuta.

MWISHO

Kama nilivyojaribu kuonyesha mila na desturi za Wasagara katika makala hayo na makala yaliyokwisha tolewa mwezi wa Oktoba, 1974, ni kwamba watu hawa wana asili ya kushirikiana sana katika shughuli za kuzalisha mali karibu kila kazi walioifanya walishirikiana pamoja kama kijiji na kazi zao za kulima mashamba ziliisha mara moja kabla ya mvua kunyesha. Mkuu wa kijiji, baada ya kusikia ngurumo ya mvua alipiga mbiu ya mgambo na kuwatahadharisha wanakijiji wote kuanza kulima mashamba yao. Na kazi hii walifanya kwa zamu hata ikatokea kwamba mashamba yao mengi yalilimwa mapema. Umoja ni nguvu na Utengano ni udhaifu. Kuna haja kubwa ya kufufua desturi hii ya kufanya kazi pamoja ili wananchi waweze kushirikiana kama zamani katika kutekeleza kazi zao barabara na upesi zaidi.

Zaidi ya hayo, zamani Wasagara walikuwa hawana shida yachakula-yaani chakula kilipatikana kwa urahisi wakati wo wote wa kiangazi au wa masika. Wasagara walilima na kupanda mazao ya chakula mara mbili kwa mwaka. Wakati wa masika mimea yao mashambani ilitumia maji ya mvua na wakati wa kiangazi mimea yao ilitumia maji yakumwagilia ya mto Mkondoa. Mboga nyingi za majani zilipandwa wakati huu kwa kutumia maji ya mto lakini jambo hiii sasa halifanyiki hata kidogo kwa sababu utaalamu ule wa zamani umepotea na pia mto wa Mkondoa sasa uko chini kidogo kuliko ilivyokuwa hapo zamani. Manufaa yote ya kutumia maji ya kumwagilia ya mto Mkondoa kwa kum-wagilia mashamba hamna sasa isipokuwa mto huu unatumika tu kwa kuogelea, kufulia na kuvua samaki. Mto wenyewe haukauki na tena ni mkubwa, kwa hiyo ingalikuwa vyema zaidi kama mifereji midogo midogo ingalitengenezwa ili ipeleke maji katika mashamba au bustani wakati wa kiangazi. Na wakati wa masika mifereji hii ingaliweza kuzibwa kwa sababu wakati huu hakuna haja ya kutumia maji ya mto wakati ipo mvua. Isipokuwa kama mvua imeshindwa kunyesha. Kitendo hiki kingekuwa cha manufaa sana kwa Taifa zima kwa kutumia utaalamu wa kisasa.

Jambo jingine la kulifufua ni ulinzi wa Taifa. Wasagara walikuwa na ulinzi mkubwa wa vijiji vyao kila mwananchi alikuwa najukumu hilo. Tukifanya Kama walivyolinda Taifa lao hawa jamaa tutaweza kwenda mbali zaidi katika kulilinda Taifa la Watanzania lisiingiliwe na maadui wowote.

74

MAVAZI YA WASAGARA

Katika kufanya kazi, kila mtu katika nchi ya Wasagara alikuwa na wajibu wa kufanya kazi, kila mtu alipewa kazi ya kufanya na jamii. Mvivu aliadhibiwa na kuzomewa na pia alipewa kazi ya kufanya kwa kupimiwa ngwe yake Mwenyewe ili aimalize Mgonjwa na mtoto ndio hawakupewa kazi kwa sababu walikuwa hawajiwezi. Lakini mtu mzima yeyote mwanamke kwa mwanaume, wote walifanya kazi pamoja bila kutegeana. Desturi hii ilikuwa nzuri sana kwa maoni yangu naona kama ingalifufuliwa na kuenezwa kila mahali nchini ili kila mtu awe na kazi ya kufanya.

Heshima na adabu vilitiliwa mkazo sana katika jamii ya Wasagara, hasa heshima kwa wakubwa na viongozi wa Wasagara. Huu ni mfano wa kuiga sana toka kwa watu hao. Heshima na adabu kwa viongozi wetu ni wajibu wetu. Ni lazima tuwape heshima wanaostahili kupewa na waliochini yao. Kwa sababu vijana wengi wameanza kupoteza heshima na adabu kwa viongozi wetu, ingalifaa kama jambo hili lingefufuliwa upesi sana kwa sababu heshima hainunuliwi.

MWISHO

Wafuatao ndio hasa waliotoa habari zilizoandikwa hapo juu:

1. Mzee Enzi Muhongola- Mwenyekiti waTANU na Diwani. 2. Mzee Mganga Salum Mjumbe wa Halmashauri yaTANU

na mjumbe wa nyumba kumi kumi.

3. Mzee Maiko Paulo - Mjumbe wa Halmashauri yaTANU, na mjumbe wa nyumba kumi kumi.

4. Mzee Kibwana Mohamed Mkulungwe - Mzee. 5. Mzee AM Issa-Mzee. 6. Bwana Saidi Madege - mjumbe wa nyumba kumi kumi. 7. MzeeMuya-Mtafiti.

ORODHA YA KUMBUKUMBU YA VITABU 1. Wizara ya Utamaduni : Historia fupi ya Utamaduni wa Mtanzania. 1974. 2. CharsleyS.R.: The Princes of Nyakyusa, 1969. 3. Mwakipesile J.S.: Utamaduni wa Wasagara, 1974. 4. A.M.T. Mabeleand Bjarne F.K. Gorm P.. Strategies and methods of the Development of museal Activities on local Level in Tanzania; 1974. 5. MwakipesileJ.S.: Jamii ya Wasafwa, 1974. 6. Dr. S.A. Lucas & A. F. Masao: The Present State of Research on cultural Development in Tanzania, 1974. 7. Dr. I.K. Katokeand Dr. S.A. Lucas: Cultural Development as a factor in social charge, 1975.

75