Upload
cathbert-angelo
View
11.368
Download
7
Embed Size (px)
DESCRIPTION
Ziara Za Rais JK
Citation preview
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIAWIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA
Simu: 255-22-2114615, 211906-12
Barua pepe: [email protected] pepe: [email protected] : www.foreign.go.tzNukushi: 255-22-2116600
20 KIVUKONI FRONT, P.O. BOX 9000,
11466 DAR ES SALAAM, Tanzania.
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Safari za Mhe. Rais Jakaya Mrisho Kikwete Nje ya Nchi
Wizara imesikitishwa na taarifa za uongo zilitolewa katika vyombo
vya habari kuwa Mhe. Jakaya Kikwete, Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania katika uongozi wake wa miaka 10
ametumia Shilingi trilioni 4 kwa ajili ya safari za kikazi nje ya nchi,
ambazo ni wastani wa bajeti nzima ya wizara kwa miaka mitano
(5).
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa inapenda
kutoa ufafanuzi kuwa tangu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete aingie madarakani mwaka
2005, kiasi kikubwa kabisa cha bajeti kuwahi kutengwa kwa ajili
ya safari za Viongozi Wakuu yaani Rais, Makamu wa Rais na
Waziri Mkuu ni shilingi bilioni 50 ambazo zilitengwa kwa Mwaka
wa Fedha 2014/2015 kwa ajili ya Idara ya Itifaki. Kwa miaka
mingine yote wastani umekuwa ni kati ya shilingi bilioni tano hadi
25 kulingana na mahitaji ya idara hiyo.
Ifahamike kuwa kiasi hicho cha shilingi bilioni 50 ni bajeti nzima
ya Idara ya Itifaki, ambapo kuna fungu maalum kwa ajili ya ziara
za viongozi. Fungu hilo linagharamia makundi makuu matano
kama ifuatavyo:
1. Kundi la Rais wakiwemo Wasaidizi, Mawaziri au Wakuu wa
Taasisi na Walinzi;
2. Kundi la Makamu wa Rais wakiwemo Wasaidizi, Mawaziri au
Wakuu wa Taasisi na Walinzi;
3. Kundi la Waziri Mkuu wakiwemo Wasaidizi, Mawaziri au
Wakuu wa Taasisi na Walinzi;
4. Kundi la Wakuu wa Nchi na Serikali kutoka nje ya nchi
wanapotembelea Tanzania; na
5. Kundi la Wajumbe Maalum wanaokuja nchini kuleta taarifa
muhimu kwa Rais.
Makundi yote haya hugaramiwa na Serikali kupitia Wizara ya
Mambo ya Nje ndani ya bajeti ya Idara ya Itifaki kifungu cha Ziara
za Viongozi.
Aidha uandaaji wa bajeti ya Wizara chini ya Idara ya Sera na
Mipango unahusisha wadau wengine nje ya Wizara kama vile
Kamati ya Bunge ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na
hupitishwa kila mwaka na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania.
Tunapenda kuwaatahadharisha wananchi juu ya watu wanaotoa
taarifa za uongo kwa madhumuni ya kujenga chuki dhidi ya
Serikali. Ikumbukwe kuwa ziara za viongozi zinazoratibiwa na
Wizara ya Mambo ya Nje zina mafanikio makubwa kwa nchi na
Watanzania kwa ujumla.
Wizara inaandaa taarifa ya ndefu ya utekelezaji wa majukumu ya
Wizara, changamoto na mafanikio yaliyopatikana ndani ya kipindi
cha miaka kumi ya uongozi wa Rais Jakaya Mrisho Kikwete
ambayo itatolewa kwa umma kwa lengo la kutoa elimu zaidi.
MWISHO.
Imetolewa na:Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali kwa Umma,Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,17 Septemba 2015