36
Je, Watoto Wetu Wanajifunza? Ujuzi wa Kusoma na Kuhesabu kaka Afrika Mashariki Agos 2012

Je, Watoto Wetu Wanajifunza? · 2013-04-18 · utafiti wa mwaka 2009/10 unazidi kuonyesha kwamba methodolojia na menejimenti ya Uwezo ni thabiti, imara na inaaminika. Uwezo inakaribisha

  • Upload
    others

  • View
    3

  • Download
    0

Embed Size (px)

Citation preview

Page 1: Je, Watoto Wetu Wanajifunza? · 2013-04-18 · utafiti wa mwaka 2009/10 unazidi kuonyesha kwamba methodolojia na menejimenti ya Uwezo ni thabiti, imara na inaaminika. Uwezo inakaribisha

iUwezo | Elimu bora, Jukumu langu!

Je, Watoto Wetu Wanajifunza?Ujuzi wa Kusoma na Kuhesabu katika Afrika Mashariki

Agosti 2012

Page 2: Je, Watoto Wetu Wanajifunza? · 2013-04-18 · utafiti wa mwaka 2009/10 unazidi kuonyesha kwamba methodolojia na menejimenti ya Uwezo ni thabiti, imara na inaaminika. Uwezo inakaribisha

ii Je, Watoto Wetu Wanajifunza? | Ujuzi wa Kusoma na Kuhesabu katika Afrika Mashariki | Agosti 2012

Hakimiliki: Uwezo & Hivos/Twaweza, 2012.

Sehemu yoyote ya chapisho hili inaweza

kunakiliwa kwa namna nyingine yoyote

kwa madhumuni yasiyo ya kibiashara kwa

kuzingatia kuwa chanzo kitatajwa na nakala

mbili zitumwe kwenda kwenye anwani iliyopo

hapa chini.

Uwezo Afrika Mashariki ilipo Twaweza

Barabara ya Lenana, ACS Plaza ghorofa ya 3,

S.L.P 19875 00200 Nairobi, Kenya

Simu: +254 203861372/3/4

Barua pepe: [email protected]

Page 3: Je, Watoto Wetu Wanajifunza? · 2013-04-18 · utafiti wa mwaka 2009/10 unazidi kuonyesha kwamba methodolojia na menejimenti ya Uwezo ni thabiti, imara na inaaminika. Uwezo inakaribisha

1Uwezo | Elimu bora, Jukumu langu!

Shukrani 2

Muhtasari 3

Utangulizi 4

Tafiti za Uwezo 6

Matokeo Muhimu 10

Hitimisho 21

VIAMBATISHO

KIAMBATISHO A 24

KIAMBATISHO B 25

KIAMBATISHO C 26

KIAMBATISHO D 27

KIAMBATISHO E 28

KIAMBATISHO F 29

YALIYOMO

Page 4: Je, Watoto Wetu Wanajifunza? · 2013-04-18 · utafiti wa mwaka 2009/10 unazidi kuonyesha kwamba methodolojia na menejimenti ya Uwezo ni thabiti, imara na inaaminika. Uwezo inakaribisha

2 Je, Watoto Wetu Wanajifunza? | Ujuzi wa Kusoma na Kuhesabu katika Afrika Mashariki | Agosti 2012

Uwezo ni sehemu ya Twaweza, ambayo ni asasi huru ya Afrika Mashariki inayokuza upatikanaji wa taarifa kwa watu, kuwawezesha wananchi kuchukua hatua pale walipo na kuboresha matokeo ya utoaji huduma katika eneo lote la Afrika Mashariki. Data kwa ajili ya ripoti hii zilikusanywa kwa ushirikiano na Asasi ya wanawake Watafiti

wa Elimu ijulikanayo kama “Women’s Education Reseachers of Kenya (WERK)” wakiongozwa na John Mugo, Mtandao wa Elimu Tanzania (TEN/MET) ukiongozwa na Suleman Sumra na Jukwaa la Taifa la Asasi zisizo za kiserikali la Uganda-the Uganda National NGO Forum (UNNGOF) likiongozwa na Richard Ssewakiryanga.

Ripoti hii imeandaliwa na kuwekwa pamoja na Sam Jones, ambaye pia ametumia umakini mkubwa katika kuhakiki usahihi wa data zilizotolewa humu. Youdi Schipper wa Uwazi-Twaweza alitoa msaada wa kiufundi na kiuchambuzi. John Mugo, Benjamin Piper and Njora Hungi walitoa ushauri wa kina ambao umezingatiwa sana kuboresha ripoti hii. Msaada wa uhariri ulitolewa na Hannah-May Wilson na Mtemi Gervas Zombwe. Kazi ya kutafsiri ripoti hii imefanywa Robert Sizya. Mwongozo wa jumla na kuhakiki ubora ulitolewa na Sara Ruto na Rakesh Rajani.

Kazi za Uwezo na Twaweza zinachangiwa na wafadhili makini na wapenda maendeleo, wakiwemo Mfuko wa Hewlett, DFID, Sida, SNV, Hivos na Banki ya Dunia. Matokeo na mapendekezo yaliyomo humu kimsingi hayawakilishi maoni ya yeyote kati ya washirika hawa.

Data zote zilizotumika katika ripoti hii zimechukuliwa kutoka kwenye ripoti ya Uwezo 2011 na tafiti za kitaifa zilizofanyika hapo awali na zinaweza kupatikana kwenye tovuti yetu ya www.uwezo.net.

Shukrani

Page 5: Je, Watoto Wetu Wanajifunza? · 2013-04-18 · utafiti wa mwaka 2009/10 unazidi kuonyesha kwamba methodolojia na menejimenti ya Uwezo ni thabiti, imara na inaaminika. Uwezo inakaribisha

3Uwezo | Elimu bora, Jukumu langu!

Muhtasari

Ripoti hii inajumuisha, inalinganisha na inawasilisha muhtasari wa taarifa za matokeo ya utafiti wa kitaifa wa Uwezo 2011 wa nchi za Kenya, Uganda na

Tanzania bara. Tafiti hizi ni tafiti kubwa zaidi za aina yake kuwahi kufanyika Afrika. Yapata watoto 350,000 katika kaya zaidi ya 150,000 katika maeneo ya nchi hizi tatu walipimwa uwezo wao katika stadi za msingi za kusoma, kuandika na kuhesabu kwa ngazi ya darasa la pili. Darasa la 2 linawakilisha ngazi ya chini ya umahiri unaotarajiwa baada ya mtoto kumaliza miaka miwili ya elimu ya msingi.

Jambo kubwa lililogundulika ni kwamba licha ya mafanikio makubwa katika kupanua wigo wa upatikanaji wa elimu ya msingi, ujuzi halisi katika kusoma na kuhesabu umebaki kuwa duni nchi zote za katika ukanda huu. Japokuwa watoto kwa sasa wameandikishwa shuleni kwa idadi kubwa mno kuliko awali, lakini hawajifunzi stadi za msingi zinazotarajiwa wajifunze katika ngazi za madarasa yao na katika umri wao. Kwa kubainisha, tathmini za Uwezo zimegundua kwamba:

(a) Zaidi ya watoto wawili kati ya kila watoto watatu walioandikishwa katika ngazi ya Darasa la 3 Afrika Mashariki walishindwa kufaulu majaribio ya kawaida ya Kiingereza, Kiswahili na Hesabu yaliyotungwa kwa kiwango cha ngazi ya Darasa la 2;

(b) Kuongezeka kwa ubora katika stadi za msingi za kusoma na kuhesabu kunaongezeka polepole sana wakati watoto wanapopanda madarasa katika mfumo wa elimu, ikimaanisha kwamba ubora wa kujifunza umebaki kuwa duni kwa ngazi zote za shule ya msingi;

(c) Ziko tofauti kubwa za wastani wa ufaulu wa majaribio miongoni mwa nchi za Afrika Mashariki. Ingawa matokeo ya jumla kwa ngazi zote ni duni, wanafunzi wa Kenya wanafanya vizuri zaidi katika kusoma na kuhesabu. Watoto wa Uganda wanafanya vibaya zaidi katika ngazi za chini lakini polepole wanashika kasi na kuwapita watoto Wakitanzania wanapofikia ngazi ya darasa la 6 na kuendelea;

(d) Kuna tofauti za msingi kwenye ufaulu wa majaribio miongoni mwa wilaya na wilaya katika nchi zote za Afrika Mashariki, huku kukiwa na tofauti kubwa katika nchi na nchi kwa nchi zote tatu;

(e) Kuna tofauti ndogo za ufaulu wa majaribio kati ya wavulana na wasichana: tofauti za kijinsi hazionekani kuwa kubwa katika miaka ya mwanzoni ya elimu;

(f) Maskini wanafanya vibaya kila mahali; watoto wanaotoka katika kaya zenye hali duni kiuchumi na kijamii hufanya vibaya katika majaribio yote na katika umri wa rika lolote; na

(g) Wanafunzi wanaosoma katika shule binafsi (zisizo za serikali) wanafanya vizuri zaidi kuliko wanafunzi wanaosoma shule za umma (za serikali) katika nchi zote tatu, tofauti hii imeonekana zaidi Tanzania.

Matokeo haya yanaonyesha picha ya kutisha ya hali ya elimu katika Afrika Mashariki, na yamekuwa yakikosolewa na baadhi ya watu eti yanaleta jina baya katika maendeleo ya elimu. Methodolojia ya Uwezo, muundo wa sampuli, zana zetu na mchakato mzima vimekuwa vikifanywa kwa mashauriano na wataalam wa kitaifa na kimataifa, na kuhakikiwa kwa umakini. Maelezo ya kina kuhusu methodolojia na mkusanyo kamili wa data pia vinapatikana kwa wote. Ukweli wa kwamba matokeo ya utafiti ya mwaka 2011 kwa sehemu kubwa yanaendana na yale ya utafiti wa mwaka 2009/10 unazidi kuonyesha kwamba methodolojia na menejimenti ya Uwezo ni thabiti, imara na inaaminika. Uwezo inakaribisha uchunguzi zaidi na changamoto zenye ushahidi wa msingi, kwa kuwa zitazidi kuimarisha utafiti.

Mwisho, japo matokeo ya utafiti yanatia wasiwasi, bado zipo sababu za kuwa na matumaini. Kwanza, sehemu zote Afrika Mashariki, Ziko baadhi ya shule na wilaya zinafanya vizuri licha ya kukabiliwa na vikwazo vya aina ileile sawa na sehemu zingine. Shule na jamii hizi zinajenga vyanzo muhimu vya ufumbuzi na majawabu ya jinsi ya kuboresha kujifunza kwa watoto. Pili, kuna dalili zinazoonesha wazi kuhama kwa mjadala wa umma na kuelekea kujikita kwenye ubora na matokeo ya kujifunza, na kuuliza maswali makini ambayo yanaweza kusaidia maamuzi ya kisera na kupata thamani kubwa kutoka katika uwekezaji uliopo sasa. Tatu, kidunia kunaongezeko la kufanyia majaribio uvumbuzi na ubunifu ili kuchochea kujifunza ambako kunaweza kuinufaisha Afrika Mashariki, tukichagua na kuamua kwa makini.

Fursa ya kumsaidia kila mtoto ili ajifunze ipo. Na ripoti hii ina lengo la kuwataarifu fursa hiyo.

Page 6: Je, Watoto Wetu Wanajifunza? · 2013-04-18 · utafiti wa mwaka 2009/10 unazidi kuonyesha kwamba methodolojia na menejimenti ya Uwezo ni thabiti, imara na inaaminika. Uwezo inakaribisha

4 Je, Watoto Wetu Wanajifunza? | Ujuzi wa Kusoma na Kuhesabu katika Afrika Mashariki | Agosti 2012

Utangulizi

Page 7: Je, Watoto Wetu Wanajifunza? · 2013-04-18 · utafiti wa mwaka 2009/10 unazidi kuonyesha kwamba methodolojia na menejimenti ya Uwezo ni thabiti, imara na inaaminika. Uwezo inakaribisha

5Uwezo | Elimu bora, Jukumu langu!

Mwanzoni mwa karne, mawaziri wa elimu kutoka katika nchi 100 duniani walionyesha dhamira ya dhati ya kutoa elimu bora ya msingi kwa watoto

wote, tena bure pasipo malipo kwenye Kongamano la Elimu la Dunia (World Education Forum) lililofanyika huko Dakar, Senegal.1

Hususan, wajumbe walikubaliana:“Kuhakikisha kwamba kufikia mwaka 2015 watoto wote, hasa wasichana, watoto walio mazingira magumu, na wale walioko katika makundi madogomadogo, wanaandikishwa bila malipo na kuhitimu elimu ya msingi yenye ubora.” (Lengo la 2)

Pia walidhamiria:“Kuboresha nyanja zote za ubora wa elimu na kuhakikisha masuala yote yahusuyo elimu yanaboreshwa ili matokeo ya kujifunza yanayotambulika na kupimika yafikiwe kwa wote, hasa katika kusoma na kuhesabu na stadi za msingi za maisha.” (Lengo la 6)

Maazimio haya yalipata mwitikio kote Afrika Mashariki, na kuleta ari mpya ya msisitizo kwenye elimu ya msingi. Kutokana na hayo, maendeleo makubwa yamefikiwa kwa kuongezeka uandikishwaji wa watoto katika shule za msingi katika ukanda mzima. Ushahidi kutoka katika tafiti mbalimbali za kaya, ikiwa ni pamoja na zilizoelezwa hapa, unaonesha kwamba hadi sasa hivi ongezeko la karibu 90% ya watoto wenye umri wa kwenda shule wameandikishwa katika shule za msingi nchini Kenya, Tanzania na Uganda (tazama kiambatisho A). Hata hivyo, licha ya mafanikio haya makubwa, kuna tatizo ambalo limeendelea kuongezeka, nalo ni kwamba watoto wako shuleni lakini hawajifunzi. Wakati upatikanaji wa elimu umeongezeka, ubora wa elimu inayotolewa umebaki kuwa palepale na kwa kweli unaweza ukawa umeshuka zaidi.

Tofauti na takwimu za uandikishwaji wa watoto shuleni, data zilizo wazi kwa wananchi kuhusu matokeo ya kujifunza kama vile stadi za msingi za kusoma, kuandika na kuhesabu zinapatikana kwa nadra sana. Kiini cha hamasa inayochochea jitihada za Uwezo ni kuziba pengo hili, na kusaidia kuhamisha mlengo wa umma na sera kutoka kwenye vitendeakazi/nyenzo za kielimu kwenda kwenye matokeo ya kujifunza.

1 Mawaziri husika wa Elimu kutoka Uganda na Tanzania walishiriki mkutano huu. Kujua orodha nzima ya uwakilishi kwenye mkutano huu huko Dakar angalia: www.unesco.org/education/efa/wef_2000/listpartwef.pdf

1. Utangulizi

Tangu mwaka 2009, Uwezo imefanya utafiti mpana wa kitaifa katika kaya kupima na kutathmini hali halisi ya ujuzi katika stadi za msingi za kusoma na kuhesabu kwa watoto wenye umri wa kwenda shule sehemu zote nchini Kenya, Tanzania na Uganda. Kwa kigezo cha kuyafikia maeneo kijiografia, tafiti hizi zinawakilisha tafiti huru kubwa zaidi zilizopo leo zinazopima matokeo ya elimu katika nchi zote tatu.2

Lengo la ripoti hii ni kulinganisha na kuwasilisha muhtasari wa matokeo ya utafiti wa Uwezo wa awamu ya pili wa kutathmini hali ya ujifunzaji ambao ulifanyika mwaka 2011 nchini Kenya, Tanzania (bara), na Uganda. Ripoti hii imepangiliwa kama ifuatavyo: Sehemu ya 2 inawasilisha tafiti za Uwezo kwa kifupi; Sehemu ya 3 inawasilisha matokeo muhimu ya utafiti; Sehemu ya 4 ni hitimisho kwa ufupi. Habari zaidi pia zinapatikana kwenye viambatisho kadhaa (tazama kisanduku hapa chini).

Kiambatisho A kinatoa data mahususi zaidi za Afrika Mashariki

Viambatisho B, C na D vinatoa matokeo maalum ya nchi kwa wastani wa alama zilizofikiwa katika majaribio, zikiwa zimetofautishwa kimadarasa (ngazi) wanayosoma, ki-makundi madogo madogo ya watu na ki-wilaya.

Kiambatisho E kinatoa mifano ya majaribio ya kusoma na hesabu yaliyotumika katika utafiti.

Kiambatisho F kinatoa matokeo kamili ya nafasi za ufaulu kwa wilaya za Afrika Mashariki.

Mwisho, matokeo yaliyowasilishwa katika ripoti hii yanatofautiana kidogo ukilinganisha na ripoti maalum za kila nchi kwa awamu zote mbili za tafiti wa Uwezo. Hii ni kwa sababu data zimechujwa kikamilifu, uzani mpya wa sampuli umekokotolewa ili kuakisi kwa ukaribu sifa za kiwango cha idadi ya watu, na masahihisho yamefanyika kwa uchunguzi uliokosekana ili kuimarisha ulinganifu kwa kipindi fulani. Wakati makadirio yako tofauti kidogo, bado hakuna tofauti kubwa kiasi cha kutufanya tubadilishe ripoti zetu za awali.

2 “Huru” ina maana kwamba utafiti haukufanywa au kuchambuliwa na taasisi/wakala wa serikali(umma)

Page 8: Je, Watoto Wetu Wanajifunza? · 2013-04-18 · utafiti wa mwaka 2009/10 unazidi kuonyesha kwamba methodolojia na menejimenti ya Uwezo ni thabiti, imara na inaaminika. Uwezo inakaribisha

6 Je, Watoto Wetu Wanajifunza? | Ujuzi wa Kusoma na Kuhesabu katika Afrika Mashariki | Agosti 2012

Taf iti za Uwezo

Page 9: Je, Watoto Wetu Wanajifunza? · 2013-04-18 · utafiti wa mwaka 2009/10 unazidi kuonyesha kwamba methodolojia na menejimenti ya Uwezo ni thabiti, imara na inaaminika. Uwezo inakaribisha

7Uwezo | Elimu bora, Jukumu langu!

Tafiti za Uwezo za kupima matokeo ya kujifunza zilianza kufanyika Kenya mwaka 2009, ikafuatiwa na Tanzania na Uganda mwaka 2010. Tafiti hizi ziliunda duru ya

kwanza ya tafiti za Uwezo (na hapa, inatajwa kama “Uwezo 1”). Tafiti zilifanyika tena katika nchi zote tatu mwaka 2011 na kuwakilisha duru ya pili ya zoezi hili (na hapa, inatajwa kama “Uwezo 2”).

2.1 Maeneo yaliyofikiwa na tafitiDuru zote mbili, Uwezo 1 na Uwezo 2 zilitumia mbinu ambazo zilitoa uwakilishi wa kitaifa wa sampuli za kinasibu kwa idadi ya watu waliokusudiwa (watoto wenye umri wa kusoma shule ya msingi na kuendelea, ikiwemo watoto wenye umri wa miaka 16.) Hii inamaanisha kwamba takwimu zilizohesabika kutoka kwenye tafiti hizi zinaweza kutumika katika kufuatilia kiwango cha ufaulu na matokeo ya kujifunza katika ngazi ya kitaifa, na pia zinaweza kutumika katika kulinganisha wakati mwingine tena inapohitajika. Sampuli pia zinauwakilishi wa ngazi ya wilaya, ambayo ina maana kwamba ulinganishi unaweza kufanywa kati ya wilaya na wilaya ndani ya nchi na kati ya nchi na nchi.

Tofauti kuu kati ya Uwezo 2 na Uwezo 1 ni kwamba awamu ya pili ilifikia idadi kubwa ya wilaya katika kila nchi, na kaya na watoto wengi zaidi kwa ujumla. Faida kuu ya kufikia eneo kubwa zaidi maana yake ni kuongeza usahihi kwenye matokeo, inatuwezesha sisi kuchunguza tofauti ya matokeo kati ya wilaya moja moja nyingi zaidi. Jedwali la 1 linatoa maelezo ya jumla ya maeneo yaliyofikiwa katika duru zote mbili katika kila nchi. Kuongezeka kwa maeneo yaliyofikiwa kati ya Uwezo 1 na Uwezo 2 ni kubwa; idadi ya wilaya zilizochaguliwa imepanda kutoka kwenye 38% hadi 90% ya wilaya zote katika ukanda (sasa inajumuisha wilaya zote za Tanzania bara na Uganda) na idadi ya watoto waliofikiwa imeongezeka maradufu (kwa kuchukua nchi zote tatu pamoja). Katika nchi zote mbili Tanzania na Uganda ambazo zilikuwa na idadi ndogo ya maeneo yaliyochaguliwa katika awamu ya kwanza ukilinganisha na maeneo yaliyochaguliwa Kenya, idadi ya watoto waliopimwa imekuwa karibu mara tatu zaidi. Hii inafanya tafiti za Uwezo kuwa moja ya tafiti zenye sampuli kubwa zaidi kuwahi kufanyika katika ukanda huu.

2. Taf iti za Uwezo

Nchi Duru Wilaya % Shule Vijiji Kaya Watoto

Kenya1 (Sept/Okt 2009) 70 44 2,029 2,029 33,760 79,693

2 (Feb/Mach 2010) 122 77 3,474 3,628 55,843 131,971

Tanzania1 (Mei 2010) 38 32 1,010 1,077 18,952 37,683

2 (Mach/Apr 2011) 119 100 3,709 3,825 59,992 114,761

Uganda1 (Aprili 2011) 27 34 748 792 12,412 32,882

2 (Apr/Mei 2011) 79 99 2,115 2,360 35,481 101,652

JumlaUwezo 1 135 38 3,787 3,898 65,124 150,258

Uwezo 2 320 90 9,298 9,813 151,316 348,384

Vidokezo: safu zote (ukiacha safu ya Nchi, Duru, ‘%’) zinataja idadi ya vitu vilivyofanyiwa sampuli na kubakia katika kundidata baada ya kuchujwa; safu ya ’%’ inahusu idadi ya wilaya katika sampuli kati ya wilaya zote katika nchi; idadi ya shule zilizofanyiwa sampuli mara nyingi ni pungufu kidogo kuliko idadi ya maeneo ya kuhesabia (vijiji) kwa kuwa si maeneo yote ya kuhesabia yanakuwa na shule ndani yake.

Chanzo: data zimekokotolewa kutoka kwenye data za Uwezo 1 na Uwezo 2.

Jedwali la 1: Maeneo yaliyofikiwa wakati tafiti za Uwezo 1 na Uwezo 2

Page 10: Je, Watoto Wetu Wanajifunza? · 2013-04-18 · utafiti wa mwaka 2009/10 unazidi kuonyesha kwamba methodolojia na menejimenti ya Uwezo ni thabiti, imara na inaaminika. Uwezo inakaribisha

8 Je, Watoto Wetu Wanajifunza? | Ujuzi wa Kusoma na Kuhesabu katika Afrika Mashariki | Agosti 2012

Mbinu ya utafiti wa Uwezo imechukuliwa kutoka katika shirika lijulikanalo kwa lugha ya kiingereza kama “the Annual Status of Education Report (ASER – tazama www.asercentre.org) ikimaanisha Ripoti ya Mwaka ya Hali ya Elimu. Kama ilivyo Uwezo, ASER ni tathmini ya mwaka ya kitaifa ya kupima uwezo wa watoto wenye umri kati ya miaka 6-16 katika kusoma na kuhesabu. Katika matokeo yaliyotolewa mwezi Januari 2012, ASER waliandika kuwa wamefanya tathmini katika wilaya 558 na kuzifikia shule 14,283, kaya 327,372 na kuwapima watoto 633,465 nchini India.

2.2 Muundo wa Utafiti wa UwezoManeno machache ya kitaalam yamewekwa katika mpangilio kuhusu muundo wa tafiti za Uwezo, pia jinsi gani matokeo yanapaswa kutafsiriwa (ufafanuzi wa kina zaidi wa masuala haya unaweza kupatikana katika ripoti yetu ya kitaalam). Kwanza, tafiti zote zimefuata ngazi tatu za hatua za uchaguzi sampuli kinasibu, kwa kufanya: (1) uchaguzi wa wilaya (sehemu) kwa uchaguzi sampuli rahisi wa kinasibu, huku kila wilaya imepewa welekeo sawa wa kuchaguliwa; (2) uchaguzi wa maeneo ya kuhesabia (vijiji) kuendana na uwiano wa ukubwa wa idadi ya watu; na (3) uchaguzi wa kaya katika kila eneo la kuhesabia kwa uchaguzi sampuli uliopangiliwa. Muundo huu unahakikisha kuwa utafiti ni kiwakilishi cha kitaifa na wilaya kwa watoto wote wenye umri kati ya miaka 6 na 16 (au miaka 7 na 16 kwa Tanzania) na watu gani ni wakazi katika kaya wakati wa utafiti (ukiacha wanaoishi katika taasisi). Uzani wa sampuli umekokotolewa kuendana na muundo wa sampuli na kujumuisha marekebisho yaliyokwishafanyika hapo mwanzo ili kuhakikisha uzani sahihi wa tofauti za umri uliofikiwa katika utafiti.

Pili, kwa kuzingatia mahesabu ya takwimu zilizowasilishwa hapa, uzani wa sampuli umetumika kote. Pale ambapo data zimekusanywa kutoka katika nchi zote tatu matokeo yanapimwa kwa ukubwa wa idadi kamili ya watu wa nchi hizi. Ukiweka kiutofauti, matokeo yaliyokusanywa yanaweza kusomwa kama wastani makadirio ya mtoto wa Afrika Mashariki (yaani, ambayo yamechaguliwa kinasibu kutoka Kenya, Tanzania au Uganda). Kutokana na ukubwa wa sampuli uliotumika katika duru zote za utafiti, hakika, tofauti zote katika makadirio kwa kila takwimu zilizotolewa katika makundi madogo madogo zina umuhimu kitakwimu katika ngazi za kawaida.

Mwisho, kumbuka kitu cha kuzingatia kuhusu jinsi ya kusoma matokeo kutoka kwenye majaribio ya kusoma na hesabu yaliyotumika katika tafiti za Uwezo. Kusema kwa dhati, alama za majaribio zilizofikiwa zinatoa makisio lakini haikosi kuwa huu ndiyo uthibitisho kamili wa ‘uwezo halisi’ wa watoto

au kiwango cha maendeleo yao katika kujifunza. Kama ilivyosemwa katika Uwezo mwaka 2010:33 “ili kutathmini kujifunza, kiwango cha mabadiliko, mtu atahitaji kudhibiti maarifa ya watoto tangu wanapoanza maisha ya kujifunza shuleni kwa Kenya, Uganda na Tanzania”. Katika uwasilishaji wa matokeo yetu kipekee tunajikita kwenye viwango vya ufaulu katika majaribio ya kusoma na kuhesabu.

Tunafanya hivyo kwa sababu kupima viwango hivi vya ufaulu kuna uhusiano wa moja kwa moja kuhusu matakwa ya mtaala na sera – watoto walioandikishwa katika ngazi ya darasa la tatu au zaidi wanapaswa kufaulu majaribio yaliyoandaliwa kwa ngazi ya darasa la 2. Sehemu ya watoto wanaoshindwa kufikia kiwango hiki wanaonesha pengo lililopo katika kujifunza. Kuongezeka kwa ukubwa wa pengo hili ndiyo msingi wa motisha wa tafiti za Uwezo, na tunaendeleza shabaha yetu dhahiri kwenye Nyanja hii katika ripoti yetu ya sasa.

2.3 Majaribio ya Kusoma na KuhesabuMaudhui ya tafiti za Uwezo yameelezwa katika ripoti maalumu ya kila nchi na kwenye tovuti ya Uwezo. 4Kwa kila kaya iliyotembelewa, vifungu vya maswali kadhaa viliulizwa kwa mkuu wa kaya ili kukusanya taarifa za msingi kuhusu kaya hiyo (kwa mfano, idadi ya wakazi na umiliki wa rasilimali kwa kila kaya). Pamoja na hayo, jaribio fupi la kusoma na kuhesabu lilitolewa kwa kila mtoto katika kaya hiyo mwenye umri wa kati ya miaka 6 na 16.

Wakusanya taarifa pia walijaza taarifa za kina zaidi kumhusu kila mtoto ikiwemo zinazoeleza kama anakwenda shule na anasoma darasa la ngapi. Jaribio la kusoma linalopima ujuzi wa kusoma na ufahamu katika lugha ya Kiingereza lilifanyika. Katika nchi zote tatu, lugha ya Kiingereza inafundishwa kama somo kuanzia darasa la 1 na hakika ni lugha inayotumika katika mitihani ya kuhitimu elimu ya msingi kwa Kenya na Uganda. Pamoja na hayo, kwa Tanzania na Kenya (lakini si kwa Uganda) jaribio jingine la kusoma lilifanyika katika Kiswahili. Katika majaribio haya ya stadi za kusoma, watoto waliulizwa kutambua herufi kutoka katika alfabeti, kusoma neno, kusoma aya, na kusoma na kuelewa hadithi fupi.

Katika majaribio ya hisabati, watoto waliulizwa kutambua namba na kuhesabu, na pia kufanya hesabu za msingi. Hapa chini ni mfano wa majaribio wakati Kiambatisho E kinaonyesha seti kamili ya majaribio kwa kila nchi ya kusoma (Kiingereza na Kiswahili) na majaribio ya hisabati yaliyotumika katika duru ya utafiti wa Uwezo 2011.

3 Uwezo 2011. Je, Watoto Wetu Wanajifunza? Kusoma na Kuhesabu katika Afrika Mashariki. www.uwezo.net

Page 11: Je, Watoto Wetu Wanajifunza? · 2013-04-18 · utafiti wa mwaka 2009/10 unazidi kuonyesha kwamba methodolojia na menejimenti ya Uwezo ni thabiti, imara na inaaminika. Uwezo inakaribisha

9Uwezo | Elimu bora, Jukumu langu!

Majaribio yote yaliandaliwa kwa kufuata mtaala wa ngazi ya Darasa la 2 kwa kila nchi, ambao ni kiwango kinachotarajiwa kufikiwa baada ya mtoto kutimiza miaka miwili ya elimu ya msingi. Hivyo basi, ili kuthibitisha kwamba viwango bora vya elimu vinazingatiwa, mtu angetarijia kwamba wanafunzi wote wanaosoma Darasa la 3 au zaidi waweze kujibu maswali yote kwa usahihi kabisa. Hii inatajwa kama ‘kufaulu’ katika uwasilishaji wa matokeo hapa chini. Majaribio yanaakisi mtaala wa taifa wa kila nchi. Kutokana na tofauti za msisitizo katika mitaala ya kitaifa, majaribio yaliyotumika katika tafiti siyo kwamba yanalingana kabisa.

Kwa hiyo, hayawezi kulinganishwa kwa usawa kabisa – kwa maana ya ngazi ya “kufaulu” kwa Kenya sio lazima iwe sawa na ngazi ya “kufaulu” kwa Tanzania. Hivyo ripoti hii inapaswa kutazamwa kama kipimo cha uwezo wa watoto wa ngazi ya Darasa la 2 kwa mujibu wa mtaala wa nchi yao. Hii haijalishi uchambuzi wa majaribio unaonesha kwamba yanafanana zaidi kuliko kutofautiana kwake. Ngazi katika jaribio la kusoma hazibadiliki, wakati tofauti chache tu zipo kwenye jaribio la hisabati katika nchi zote tatu. Ili kusaidia kuonesha ulinganifu katika nchi zote tatu, ni maswali yanayofanana tu katika tafiti zote ndiyo yamejumuishwa katika matokeo ya pamoja ya ujuzi wa kusoma na kuhesabu. Kwa mfano, kwa kuwa madaraja ya kufaulu hayatolewi kwa ngazi ya Darasa la 2 nchini Tanzania, data hizi hazijawasilishwa katika uchambuzi huu.

Jedwali la 2: Sampuli ya Majaribio ya Uwezo Afrika Mashariki mwaka 2011

Page 12: Je, Watoto Wetu Wanajifunza? · 2013-04-18 · utafiti wa mwaka 2009/10 unazidi kuonyesha kwamba methodolojia na menejimenti ya Uwezo ni thabiti, imara na inaaminika. Uwezo inakaribisha

10 Je, Watoto Wetu Wanajifunza? | Ujuzi wa Kusoma na Kuhesabu katika Afrika Mashariki | Agosti 2012

Matokeo Muhimu

Page 13: Je, Watoto Wetu Wanajifunza? · 2013-04-18 · utafiti wa mwaka 2009/10 unazidi kuonyesha kwamba methodolojia na menejimenti ya Uwezo ni thabiti, imara na inaaminika. Uwezo inakaribisha

11Uwezo | Elimu bora, Jukumu langu!

Kulingana na matokeo ya Uwezo 1 (angalia Ukweli namba 8), Uwezo 2 inathibitisha kwamba ujuzi wa stadi za kusoma na kuhesabu kwa watoto wa shule za msingi ni duni katika eneo lote la ukanda wa Afrika Mashariki. Kielelezo cha 1, ambacho kinabeba nchi zote tatu kwa pamoja, kinaonesha asilimia ya watoto wa shule ya msingi walioandikishwa katika ngazi ya Darasa la tatu ambao wanaweza kufaulu kila jaribio kati ya majaribio matatu yaliyoandaliwa kwa kiwango cha ngazi ya darasa la 2 yaliyojumuishwa katika dodoso la utafiti4. Pamoja na hayo, kielelezo pia kinaonyesha asilimia ya wanafunzi wa Darasa la 3 katika ukanda ambao walifaulu majaribio yote mawili, la maswali ya kusoma katika lugha yao ya taifa ya kufundishia (Kiingereza kwa Kenya na Uganda; Kiswahili kwa Tanzania) na maswali ya (kawaida) ya hisabati – maana yake, hii inapima uwiano wa walioweza kufaulu majaribio yote mawili kwa pamoja.5

4 Data maalum za kila nchi za viwango vya kufaulu majaribio zimetolewa kwenye Viambatisho B, C na D..

5 Maswali ya kawaida ya ujuzi wa kuhesabu ni yale yaliyojumuishwa kwenye majaribio katika kila nchi na kila duru ya utafiti. Yako (kwenye mpangilio wa kuongezeka kwa ugumu): Kutambua namba; Kujumlisha; Kutoa; na kuzidisha.

Kielelezo hiki kinaonyesha kwamba wanafunzi wachache sana walioandikishwa katika Darasa la 3 wanaweza kufaulu kila moja ya majaribio. Kiuhalisia, ni pungufu kidogo ya mmoja kati ya watoto watatu waliweza kufaulu jaribio la Kiswahili (31%) na majaribio ya hisabati (29%), lakini ni mmoja tu kati ya sita alifaulu jaribio la Kiingereza (16%). Vivyo hivyo, ni pungufu ya mmoja kati ya watoto sita aliweza kufaulu majaribio yote mawili ya kusoma na kuhesabu kwa pamoja (15%). Matokeo haya yanaonyesha kwamba kundi kubwa zaidi la wanafunzi hawapati ujuzi mahiri wakati wa kipindi cha miaka ya mwanzoni katika shule za msingi kama inavyotarajiwa katika mitaala ya kitaifa.

3. Matokeo Muhimu

Matokeo haya yanaonyesha kwamba kundi kubwa zaidi la wanafunzi hawapati ujuzi mahiri wakati wa kipindi cha miaka ya mwanzoni katika shule za msingi kama inavyotarajiwa katika mitaala ya kitaifa.

Kiswahili

Ukweli wa 1: Ni chini ya theluthi moja ya watoto Afrika Mashariki wana ujuzi wa kusoma na kuhesabu.

Kielelezo cha 1: Viwango vya kufaulu majaribio kwa watoto walioandikishwa katika Darasa la 3, Afrika Mashariki yote

Vidokezo: “Kwa pamoja” inamaanisha kufaulu maswali ya majaribio yote mawili, (ya kawaida) jaribio la hisabati na maswali ya jaribio la kusoma.

Chanzo: data zimekokotolewa kutoka kwenye data za Uwezo 2.

% y

a uf

aulu

wa

wan

afun

zi

Kiingereza Kwa pamojaHisabati

Page 14: Je, Watoto Wetu Wanajifunza? · 2013-04-18 · utafiti wa mwaka 2009/10 unazidi kuonyesha kwamba methodolojia na menejimenti ya Uwezo ni thabiti, imara na inaaminika. Uwezo inakaribisha

12 Je, Watoto Wetu Wanajifunza? | Ujuzi wa Kusoma na Kuhesabu katika Afrika Mashariki | Agosti 2012

Je, matokeo haya duni yanaendelea kuwepo katika ngazi zote za shule ya msingi? Kielelezo cha 2 kinaonyesha viwango vya kufaulu kwa kila jaribio kwa watoto walioandikishwa madarasa ya ngazi za juu zaidi ya Darasa la 3. Kielelezo kinaonyesha kwamba kadri watoto wanavyoendelea mbele katika mfumo wa shule kwenda madarasa ya juu zaidi, viwango vya kufaulu pia vinaendelea kuongezeka kwenye majaribio yote ya ngazi ya Darasa la 2. Hili linatuonyesha kwamba watoto wanajifunza na kupata baadhi ya stadi za msingi, japokuwa si katika wakati uliotarajiwa kama ulivyopangwa na mtaala. Kiwango kikubwa zaidi cha kujifunza kinatokea katika ngazi za juu za shule ya msingi kati ya Darasa la 4 hadi la 5, na Darasa la 5 hadi 6 ikionyesha kwamba watoto wengi wanapata ujuzi wa ngazi ya Darasa la 2 katika miaka ya mwishoni mwa elimu ya msingi.

Kutokana na ngazi ya chini ambayo majaribio yanaandaliwa, inaonyesha kwamba viwango vya kufaulu vinaongezeka polepole sana. Kwa mfano, katika Darasa la 4, yapata nusu tu ya wanafunzi wanaweza kufaulu jaribio la Kiswahili huku viwango vya kufaulu viko chini zaidi katika hisabati na Kiingereza. Ni katika Darasa la 7 tu ndiyo kuna zaidi ya theluthi mbili ya watoto waliofaulu kila jaribio. Hii inaonyesha kwamba ujuzi madhubuti wa watoto wengi katika kusoma na kuhesabu umebaki kuwa chini katika ngazi zote za shule ya msingi. Hofu nyingine ni kwamba idadi kubwa ya watoto wanaojiandaa kufanya mitihani yao ya mwisho ya kitaifa hawajawa na ujuzi katika stadi za msingi za kusoma na kuhesabu.

Kiwango kikubwa zaidi cha kujifunza kinatokea katika ngazi za juu za shule ya msingi kati ya Darasa la 4 hadi la 5, na Darasa la 5 hadi 6 ikionyesha kwamba watoto wengi wanapata ujuzi wa ngazi ya Darasa la 2 katika miaka ya mwishoni mwa elimu ya msingi.

Matokeo ya utafiti duru mbili za zilizopita yamerejewa kwenye matokeo ya ukanda mzima wa Afrika Mashariki. Hata hivyo, ziko tofauti ndogondogo kwa Kenya, Tanzania na Uganda kwa kuzingatia ujuzi katika stadi za kusoma na kuhesabu (matokeo ya majaribio) ya watoto wenye umri wa kwenda shule. Hii imeoneshwa katika kielelezo cha 3, kinachoonesha asilimia ya watoto wenye umri wa miaka kati ya 10 na 16 ambao wanaweza kufaulu kila jaribio (Kiingereza, Kiswahili

na Hisabati), pia majaribio yote ya kusoma na kuhesabu yakijumuishwa pamoja.

Kielelezo kinaonesha kwamba watoto wa Kenya wamefaulu zaidi kuliko watoto wengine wa nchi za Afrika Mashariki katika majaribio yote. Hii inaonekana wazi zaidi katika majaribio ya kusoma. Kiwango cha kufaulu cha watoto wa Kenya katika somo la Kiingereza ni zaidi ya mara mbili ya

Ukweli wa 2: Watoto wawili katika kila watoto 10 wa Darasa la 7 katika Afrika Mashariki hawana ujuzi wa ngazi ya Darasa la 2 katika kusoma na kuhesabu.

Ukweli wa 3: Kuna tofauti kubwa miongoni mwa nchi za Afrika Mashariki

Kielelezo cha 2: Viwango vya kufaulu majaribio kwa Madarasa kwa watoto walioandikishwa shule, Afrika Mashariki yote kwa pamoja

Vidokezo: namba zilizoko kwenye mhimili mlalo zinataja darasa la 4 na la 7 shule ya msingi. Pia kumbuka kwamba matokeo ya Kiswahili yamejumuisha Kenya na Tanzania tu.

Chanzo: imekokotolewa kutoka kwenye data za Uwezo 2.

% z

a uf

aulu

wa

wan

afun

zi

HisabatiKiingereza Kiswahili

Page 15: Je, Watoto Wetu Wanajifunza? · 2013-04-18 · utafiti wa mwaka 2009/10 unazidi kuonyesha kwamba methodolojia na menejimenti ya Uwezo ni thabiti, imara na inaaminika. Uwezo inakaribisha

13Uwezo | Elimu bora, Jukumu langu!

watoto wa Tanzania (ni asilimia 39 zaidi), na asilimia 29 zaidi ya watoto wa Uganda. Matokeo haya yanaweza kuonesha madhara ya lugha zinazotumika kufundishia kama Kiingereza kinatumika kwa mapana zaidi katika ngazi zote za shule ya msingi. Hata hivyo, hata katika jaribio la Kiswahili, ambacho kinazungumzwa sana Tanzania kuliko Kenya, Wakenya wamefanya vizuri -20% zaidi ya watoto wa Kenya wenye umri wa miaka 10-16 wanafaulu vizuri jaribio la Kiswahili kuliko watoto wa Tanzania. Tofauti iliyopo miongoni mwa nchi hizi tatu ni ndogo sana katika jaribio la hesabu ingawa hata huko nako wanafunzi wa Kenya wanafanya vizuri (kwa wastani) kuliko watoto wa nchi nyingine.

Pointi mbili za ziada zinaweza kusemwa. Kwanza, ikumbukwe kwamba kufaulu vizuri zaidi kwa wanafunzi wa Kenya kunaendana tu na wanafunzi wa nchi nyingine. Kwa ujumla, suala linabaki palepale kwamba katika ngazi ya Darasa la 3 karibu theluthi moja ya wanafunzi wa Kenya (na wanafunzi wachache zaidi wa Tanzania na Uganda) wanaweza kufaulu jaribio la ngazi ya Darasa la 2.

Pili, wakati Kielelezo cha 3 kinaonesha kwamba watoto wa Uganda wanafanya vibaya zaidi katika ukanda wa Afrika Mashariki (isipokuwa katika jaribio la Kiingereza), ziko tofauti ndogo sana kati ya Tanzania na Uganda kama mtu ataangalia ufaulu wa majaribio kwa kila Darasa (angalia Kiambatisho

B hadi D)6 Wanafunzi wa Uganda wanafanya vibaya kwa kulinganisha ngazi za madarasa ya chini, lakini wanaonesha kasi ya kuongeza ufaulu katika ngazi za juu. Kwa mfano, idadi ya watoto wa Uganda ambao wanafaulu katika kusoma na kuhesabu (kwa pamoja) iko chini kuliko Kenya na Tanzania kwa Darasa la 1 hadi la 5. Hata hivyo, kuanzia Darasa la 6 na kuendelea, wanafunzi wa Uganda wanawazidi kidogo katika kufaulu wanafunzi wa Tanzania.

Hivyo, katika Darasa la 7, karibu 90% ya wanafunzi wa Kenya wanafaulu katika kusoma na kuhesabu, majaribio yote mawili (kwa pamoja), ambayo inalinganishwa na 80% ya wanafunzi wa Uganda lakini ni theluthi mbili tu (66%) ya wanafunzi wa Tanzania.

Maelezo yanayoweza kutolewa kuhusu kasi ya kupanda kwa wanafunzi wa Uganda ni matumizi makubwa ya Kiingereza kama lugha ya kufundishia katika madarasa ya juu ya shule ya msingi (ambako kunaongeza kiwango cha kufaulu katika jaribio la kusoma Kiingereza Tanzania).7

6 Masuala haya pia yamejadiliwa kwa kina katika ripoti kubwa ya kiufundi (tazama www.uwezo.net)

7 High repetition rates in Uganda are indicated in external data sources, such as UNESCO (2011),Global Education Digest 2011: Comparing Educa-tion Statistics Across the World, Montreal: UNESCO Institute for Statistics

...kufaulu vizuri zaidi kwa wanafunzi wa Kenya kunaendana tu na wanafunzi wa nchi nyingine. Kwa ujumla, suala linabaki palepale kwamba katika ngazi ya Darasa la 3 karibu theluthi moja ya wanafunzi wa Kenya (na wanafunzi wachache zaidi wa Tanzania na Uganda) wanaweza kufaulu jaribio la ngazi ya Darasa la 2.

Kielelezo cha 3: Viwango vya kufaulu majaribio kwa watoto wenye umri wa miaka 10-16, kwa kila nchi

Vidokezo: mahesabu yanawahusu watoto wote (wawe wameandikishwa au hawajaandikishwa); “Kwa pamoja” inaonyesha ufaulu kwenye maswali ya aina zote mbili ya hesabu (za kawaida) na maswali ya kusoma katika lugha ya taifa ya kufundishia; jaribio la Kiswahili halikutumika kwa nchi ya Uganda.

Chanzo: imekokotolewa kutoka kwenye data za Uwezo 2.

% z

a uf

aulu

wa

wan

afun

zi

Kiswahili Kwa pamojaKiingereza Hisabati

Page 16: Je, Watoto Wetu Wanajifunza? · 2013-04-18 · utafiti wa mwaka 2009/10 unazidi kuonyesha kwamba methodolojia na menejimenti ya Uwezo ni thabiti, imara na inaaminika. Uwezo inakaribisha

14 Je, Watoto Wetu Wanajifunza? | Ujuzi wa Kusoma na Kuhesabu katika Afrika Mashariki | Agosti 2012

Ukweli wa 4: Ziko tofauti kubwa sana katika matokeo ya majaribio kati ya wilaya na wilaya ndani ya kila nchi

Tafiti za Uwezo zina uwakilishi katika ngazi ya wilaya katika kila nchi. Kwa hiyo, inafaa kujali kiwango ambacho ujuzi wa kusoma na kuhesabu unafautiana katika ngazi za wilaya. Hii inaweza kusaidia kubaini maeneo maalum (ya kijiografia) yanayofanya vizuri sana na yanayoshindwa kufanya vizuri ndani ya mfumo wa elimu, ambayo yana umuhimu mkubwa sana wa kuzingatiwa kisera kwa kuwa hali za ndani ya nchi zinatofautiana kati ya mikoa, kama inavyokuwa katika mgawo wa bajeti.

Ili kuchunguza kwa kina swali hili tulitafuta wastani wa kufaulu katika majaribio ya kusoma na kuhesabu kwa pamoja kwa watoto wenye umri wa miaka 10-16 katika kila wilaya. Baada ya hapo, katika kila nchi wastani huu wa viwango vya kufaulu ukapangwa kuanzia wa chini mpaka wa juu kabisa.

Jedwali la 3 limeorodhesha wilaya 10 bora zaidi na wilaya 10 dhaifu zaidi katika ukanda ambazo zinathibitisha kuwepo kwa tofauti kubwa sana kati ya wilaya na wilaya, na kati ya nchi na nchi. –wilaya kumi bora zote ziko Kenya (hasa ukanda wa Kati), wakati kumi dhaifu zaidi zote zinatoka Uganda (hasa ukanda wa Kaskazini).

Matokeo ya ngazi za wilaya pia yanafanya matokeo ya utafiti yawe na tofauti kubwa za ulinganifu katika kufaulu kati ya nchi hizi tatu. Kwa mfano, wilaya inayofanya vizuri zaidi nchini Uganda ilipata 72%, kiasi ambacho ni kikubwa kidogo tu ya kile cha kiwango cha kati cha kufaulu cha wilaya za Kenya.

Page 17: Je, Watoto Wetu Wanajifunza? · 2013-04-18 · utafiti wa mwaka 2009/10 unazidi kuonyesha kwamba methodolojia na menejimenti ya Uwezo ni thabiti, imara na inaaminika. Uwezo inakaribisha

15Uwezo | Elimu bora, Jukumu langu!

Jedwali la 3: Muhtasari wa Wilaya zinazofanya vizuri zaidi na Wilaya zinazofanya vibaya zaidi katika Afrika Mashariki

Nafasi Nchi Mkoa Wilaya% ya ufaulu kwa pamoja

% za Uandikishaji

1 Kenya Central Thika West 92.1 90.7

2 Kenya Central Kikuyu 89.9 97.2

3 Kenya Nairobi Nairobi East 89.4 91.5

4 Kenya Central Nyeri South 88.2 95.7

5 Kenya Central Gatanga 86.9 96.7

6 Kenya Central Kirinyaga 86.7 96.7

7 Kenya Rift Valley Kajiado North 86.4 85.4

8 Kenya Eastern Imenti South 85.6 92.9

9 Kenya Central Ruiru 85.2 86.0

10 Kenya Central Gatundu 85.1 92.6

311 Uganda Northern Amuru 25.3 95.0

312 Uganda Northern Dokolo 23.3 95.7

313 Uganda Western Bundibugyo 22.7 95.3

314 Uganda Eastern Bugiri 22.1 96.9

315 Uganda Eastern Kaliro 20.6 88.0

316 Uganda Northern Amolatar 20.3 94.5

317 Uganda Northern Nakapiripirit 19.4 60.7

318 Uganda Northern Moroto 19.1 61.0

319 Uganda Northern Kaabong 16.9 60.3

320 Uganda Northern Kotido 9.7 40.8Vidokezo: mpangilio wa ngazi umetafutwa kwa kukusanya alama kutoka kwenye alama za majaribio walizopata katika kila wilaya kwa kila nchi; uandikishwaji shule unahusu shule za msingi na sekondari; sampuli zinawahusu watoto wa umri wa miaka 10-16 tu; “Kwa pamoja” inahusu kufaulu katika maswali ya kawaida ya jaribio la hisabati na maswali ya jaribio la kusoma katika lugha ya taifa ya kufundishia shule ya msingi.

Chanzo: imekokotolewa kutoka kwenye data za Uwezo 2.

Jedwali la 3a: Muhtasari wa Wilaya zinazofanya vizuri zaidi na Wilaya zinazofanya vibaya zaidi nchini Kenya

Nafasi Mkoa Wilaya% ya ufaulu kwa pamoja

% za Uandikishaji

1 Central Thika West 92.1 90.7

2 Central Kikuyu 89.9 97.2

3 Nairobi Nairobi East 89.4 91.5

4 Central Nyeri South 88.2 95.7

5 Central Gatanga 86.9 96.7

6 Central Kirinyaga 86.7 96.7

7 Rift Valley Kajiado North 86.4 85.4

8 Eastern Imenti South 85.6 92.9

9 Central Ruiru 85.2 86.0

10 Central Gatundu 85.1 92.6

113 Rift Valley Samburu North 41.3 62.9

114 Coast Tana Delta 40.7 84.0

115 Rift Valley Turkana South 40.5 69.2

116 North Eastern Lagdera 40.5 63.4

117 North Eastern Wajir East 37.1 78.8

118 North Eastern Wajir West 36.0 71.6

119 North Eastern Wajir North 35.2 66.2

120 North Eastern Ijara 33.9 58.0

121 Rift Valley Turkana Central 30.8 61.4

122 Rift Valley Samburu East 26.5 47.9“Kwa pamoja” inaonesha wastani wa kiwango cha kufaulu (kwa wilaya) kwenye maswali ya majaribio yote mawili la hesabu (za kawaida) na maswali ya jaribio la ujuzi wa kusoma Kiingereza; mpangilio wa nafasi kwenye ufaulu “wa pamoja”unatokana na kiwango cha kufaulu; uandikishwaji unahusu shule za msingi na sekondari; sampuli zinawahusu watoto wa umri wa miaka 10-16 tu.

Chanzo: imekokotolewa kwa kutumia data za Uwezo 2.

Jedwali la 3b: Muhtasari wa Wilaya zinazofanya vizuri zaidi na Wilaya zinazofanya vibaya zaidi nchini Tanzania

Nafasi Mkoa Wilaya% ya ufaulu kwa pamoja

% za Uandikishaji

1 Arusha Arusha 80.2 96.7

2 Iringa IringaMjini 78.5 89.1

3 Kilimanjaro Moshi Mjini 72.5 86.0

4 Kagera Bukoba Mjini 71.1 90.9

5 Kilimanjaro Rombo 70.2 93.9

6 Morogoro Morogoro Mjini 69.7 86.9

7 Dar es Salaam Temeke 68.8 78.6

8 Mbeya Mbeya Mjini 68.4 95.9

9 Tanga Tanga 66.4 95.7

10 Dar es Salaam Ilala 66.3 90.1

110 Shinyanga Kishapu 31.8 84.3

111 Shinyanga Kahama 31.7 80.3

112 Mtwara Mtwara Vijijini 30.6 82.3

113 Mara Serengeti 29.8 63.9

114 Kigoma Kibondo 28.6 73.1

115 Tanga Kilindi 28.2 83.1

116 Shinyanga Meatu 28.0 87.0

117 Mwanza Ukerewe 27.7 87.9

118 Dodoma Mpwapwa 27.7 81.7

119 Shinyanga Bariadi 25.4 73.8“Pamoja” inaonesha wastani wa kiwango cha kufaulu (kwa wilaya) kwenye maswali ya majaribio yote mawili la hesabu (za kawaida) na maswali ya jaribio la ujuzi wa kusoma Kiswahili; mpangilio wa nafasi umezingatia kiwango cha “pamoja” cha ufaulu; uandikishwaji shule unahusu shule za msingi na sekondari; sampuli zinawahusu watoto wa umri wa miaka 10-16 tu.

Chanzo: imekokotolewa kwa kutumia data za Uwezo 2.

Jedwali la 3c: Muhtasari wa Wilaya zinazofanya vizuri zaidi na Wilaya zinazofanya vibaya zaidi nchini Uganda

Nafasi Mkoa Wilaya% ya ufaulu kwa pamoja

% za Uandikishaji

1 Central Kampala 69.3 94.3

2 Central Wakiso 64.5 92.6

3 Western Mbarara 54.9 93.1

4 Western Bushenyi 52.3 95.6

5 Central Mityana 50.4 96.1

6 Western Kiruhuura 50.0 95.3

7 Central Nakaseke 49.6 95.8

8 Central Luwero 47.7 94.7

9 Western Ibanda 47.4 92.9

10 Central Nakasongola 46.7 97.4

70 Northern Amuru 25.3 95.0

71 Northern Dokolo 23.3 95.7

72 Western Bundibugyo 22.7 95.3

73 Eastern Bugiri 22.1 96.9

74 Eastern Kaliro 20.6 88.0

75 Northern Amolatar 20.3 94.5

76 Northern Nakapiripirit 19.4 60.7

77 Northern Moroto 19.1 61.0

78 Northern Kaabong 16.9 60.3

79 Northern Kotido 9.7 40.8“Pamoja” inaonesha wastani wa kiwango cha kufaulu (kwa wilaya) kwenye maswali ya majaribio yote mawili la hesabu (za kawaida) na maswali ya jaribio la ujuzi wa kusoma Kiswahili; mpangilio wa nafasi unatoakana na kiwango cha ufaulu cha pamoja”; uandikishwaji unahusu shule za msingi na sekondari; sampuli zinawahusu watoto wa umri wa miaka 10-16 tu.

Chanzo: imekokotolewa kwa kutumia data za Uwezo 2.

Page 18: Je, Watoto Wetu Wanajifunza? · 2013-04-18 · utafiti wa mwaka 2009/10 unazidi kuonyesha kwamba methodolojia na menejimenti ya Uwezo ni thabiti, imara na inaaminika. Uwezo inakaribisha

16 Je, Watoto Wetu Wanajifunza? | Ujuzi wa Kusoma na Kuhesabu katika Afrika Mashariki | Agosti 2012

Katika baadhi ya wilaya zinazofanya vibaya, watoto wanahudhuria shuleni vizuri kwa uaminifu, hata ambapo hawana kitu kikubwa wanachoweza kuonesha kuwa wamejifunza shuleni.

Data zilizowasilishwa hapo juu zinaonesha mambo mawili zaidi. Katika baadhi ya wilaya, asilimia ya watoto waliofaulu jaribio la Uwezo iko juu kuliko idadi ya watoto walioandikishwa shule. Hii inaweza kumaanisha kwamba kuna idadi ya watoto ambao hawajaandikishwa shule, au wale ambao wanaweza kuwa wamemaliza elimu ya msingi lakini

hawakuendelea zaidi baada ya masomo shule ya msingi, wana ujuzi wa kusoma na kuhesabu katika wilaya zinazoonekana kufanya vizuri. Katika baadhi ya wilaya zinazofanya vibaya, watoto wanahudhuria shuleni vizuri kwa uaminifu, hata ambapo hawana kitu kikubwa wanachoweza kuonesha kuwa wamejifunza shuleni.

Jedwali la 4 linaonesha viwango vya kufaulu, asilimia kumi ya wilaya za mwisho kabisa (yaani ni viwango vya chini kabisa na vya juu kabisa vya asilimia kumi ya wilaya za mwisho), kiwango cha kati cha kufaulu, na kiwango kilichofikiwa cha viwango vya ufaulu cha asilimia kumi ya wilaya bora zaidi (maelezo ya kina zaidi yapo katika Kiambatisho cha 1). Data zinaonesha kwamba wilaya zenye ufaulu wa juu kabisa kwa Kenya zilipata kiwango cha ufaulu kati ya 84% na 92%; Tanzania wilaya za juu kabisa zilikuwa na wastani wa ufaulu cha kati ya 63% na 80%; ambapo Uganda, wilaya za juu kabisa zilipata wastani wa ufaulu kati ya 48% na 70%. Viwango vya kati vya ufaulu vinaonesha kwamba 50% ya wilaya zote za Kenya zilipata wastani wa ufaulu kuanzia 68%; hata hivyo, kwa Uganda, 50% ya wilaya (za kiwango cha kati) zilipata kiwango cha ufaulu cha 34% au pungufu yake.

Matokeo haya yana maanisha nini? Tofauti kubwa ya viwango vilivyofikiwa kwa wastani wa ngazi ya wilaya vinamaanisha kuwepo kwa utofauti wa kijiografia uliodhahiri katika kusoma na kuhesabu ndani ya kila nchi (ki-wilaya). Kwa maneno mengine, ujuzi tarajiwa wa kusoma na kuhesabu wa ‘wastani’ kwa wanafunzi katika kila wilaya unatofautiana kwa kutegemeana na maeneo wanakoishi. Kwa mfano, wilaya bora kabisa kwa ufaulu Tanzania, inapata wastani wa ufaulu waa 80% ukilinganisha na 25% katika wilaya inayofanya vibaya

zaidi, tofauti ya asilimia 55.8

Kwa nyongeza, matokeo haya yanaonesha maeneo kadhaa ya ubora na/au kushindwa katika kila nchi. Kwa Kenya, kiwango kilichofikiwa cha 10% ya wilaya za mwisho kinaonekana kiko juu, hii inaonesha kuwepo kwa idadi ndogo ya wilaya zinazofanya vibaya zaidi (nyingi ni wilaya za ukanda kame katika Bonde la Ufa na ukanda wa Kaskazini Mashariki, (tazama Jedwali 3a). Kiutofauti, japokuwa Tanzania na Uganda zote zina wilaya zenye alama za wastani wa chini sana, mtu atagundua kwamba kiwango kilichofikiwa cha 10% ya wilaya bora zaidi kinaonekana kikubwa.

Hii inaonesha kuwepo kwa idadi ndogo ya wilaya hasa zinazofanya vizuri katika nchi hizi, ambazo zinapatikana katika maeneo ya mijini yenye utajiri au wilaya zenye utajiri wa kilimo. Matokeo ya ngazi ya wilaya pia yanaonesha kuwepo kwa tofauti kubwa za kufaulu kati ya nchi na nchi. Kwa mfano, wilaya bora zaidi kwa kufanya vizuri Uganda ilipata wastani wa ufaulu wa 72%, ambayo ni mkubwa kidogo tu zcha wilaya zenye wastani wa kati nchini Kenya. Hii inamaanisha kwamba karibu nusu ya wilaya za Kenya zinazidi wastani wa ufaulu wa wilaya bora zaidi za Uganda.

8 Kama ilivyoelezwa kwa kina katika ripoti ya kiufundi kiwango cha ku-tokuwa sawa kijiografia kwenye matokeo ya kujifunza kiko juu Tanzania na chini zaidi Uganda, kikipimwa kwa kuangalia tofauti ya ufaulu kiwilaya

Jedwali la 4: Muhtasari wa wastani wa viwango vya kufaulu vya ngazi ya wilaya kwenye majaribio ya kusoma na kuhesabu kwa pamoja, kwa kila nchi

% y

a uf

aulu

wa

wan

afun

zi

Page 19: Je, Watoto Wetu Wanajifunza? · 2013-04-18 · utafiti wa mwaka 2009/10 unazidi kuonyesha kwamba methodolojia na menejimenti ya Uwezo ni thabiti, imara na inaaminika. Uwezo inakaribisha

17Uwezo | Elimu bora, Jukumu langu!

Sababu mbalimbali zinaweza kuhusishwa na uwepo wa tofauti hizi za ujuzi wa kusoma na kuhesabu miongoni mwa watoto wa Afrika Mashariki. Baadhi yake, ni hali ya maisha kijamii na kiuchumi inamchango mkubwa kuamua ujuzi wa mtoto. Mathalan, kaya zenye kipato cha juu zinaweza kumudu vizuri gharama za mahitaji ya vifaa vya ziada vya kujifunzia (kama vile vitabu na penseli) na pia haziwashirikishi sana watoto katika shughuli za kuzalisha kipato.

Katika kutafiti suala hili, kaya katika sampuli ziligawanywa katika makundi matatu ya hali za kiuchumi na kijamii kulingana na idadi ya maswali rahisi yaliyoulizwa – kama vile rasilimali za kudumu wanazomiliki, kama wana umeme na/au maji safi na salama, na kama mama katika kaya hiyo amepata elimu yoyote rasmi.9 Kwa hakika, huu pekee ndiyo uainishaji ghafi; hata hivyo, mtu ataona kuna tofauti kubwa kati ya makundi ya kiuchumi na kijamii katika matokeo ya kusoma na

9 Ili kuhakikisha kuna ulinganifu, aina tatu za makundi ya kiuchumi zimeta-jwa kwa namna ileile kwa kila nchi katika Ukanda wa Afrika Mashariki. Yaani, siyo makundi maalum ya ki-nchi.

kuhesabu. Hii imeonyeshwa katika kielelezo cha 5, ambacho kinaonesha asilimia ya watoto wenye umri wa miaka 10-16 katika kila kundi la kiuchumi na kijamii (kwa ukanda mzima), ambao wanaweza kufaulu majaribio yote mawili ya kusoma na kuhesabu (kwa pamoja). Kielelezo kinaonesha tofauti kati ya maskini na wasio maskini. Pengo kati ya maskini na wasio maskini ni pointi asilimia 18, wakati pengo kati ya fukara kabisa na wasio maskini ni alama asilimia 27. Hii ina maana kwamba watoto wengi kama mara mbili (karibu watoto 6 kati ya 10 wenye umri wa miaka 10-16) wanaotoka katika kaya zisizo maskini wanaweza kufaulu majaribio yote mawili ukilinganisha na watoto wanaotoka katika kaya fukara kabisa (karibu watoto 3 tu kati ya 10). Data hizi zinadhihirisha kwamba jitihada zinahitajika kwenye elimu ya umma kwa pande zote, ukweli ni kwamba fursa za kuendeleza ujuzi zinatofautiana sana katika Afrika Mashariki.

...jitihada zinahitajika kwenye elimu ya umma kwa pande zote, ukweli ni kwamba fursa za kuendeleza ujuzi zinatofautiana sana katika Afrika Mashariki.

Kielelezo cha 4 kinaonesha asilimia ya wavulana na wasichana wenye umri wa miaka 10-16 katika kila nchi ambao wanaweza kufaulu majaribio yote mawili kusoma na kuhesabu. Kwa nchi zote tatu, kielelezo kinathibitisha kuwepo kwa baadhi ya tofauti za kijinsia.

Kiuhalisi, kwa wastani, wasichana wanawazidi kidogo wavulana katika nchi zote tatu. Tofauti za viwango hivi ziko sawa katika alama za majaribio yote mawili ya kusoma na kuhesabu.

Ukweli wa 5: Kuna tofauti ndogo kati ya wavulana na wasichana katika ujuzi wao wa kusoma na kuhesabu

Ukweli wa 6: Watoto wanaotoka katika kaya maskini zaidi wanafanya vibaya kwenye majaribo katika umri wa rika zote.

Kielelezo cha 4: Viwango vya kufaulu katika majaribio ya kusoma na kuhesabu (kwa pamoja) kwa watoto wenye umri wa miaka 10-16, kwa vigezo vya kijinsia na ki-nchi

% z

a uf

aulu

wa

wan

afun

zi

Wavulana Wavulana WavulanaWasichana Wasichana Wasichana

Page 20: Je, Watoto Wetu Wanajifunza? · 2013-04-18 · utafiti wa mwaka 2009/10 unazidi kuonyesha kwamba methodolojia na menejimenti ya Uwezo ni thabiti, imara na inaaminika. Uwezo inakaribisha

18 Je, Watoto Wetu Wanajifunza? | Ujuzi wa Kusoma na Kuhesabu katika Afrika Mashariki | Agosti 2012

Pengo hili la kujifunza kati ya maskini na wasio maskini linaendelea pia kuonekana katika umri wa kila rika; yaani linaongezeka kwa kiwango cha juu sana. Hii inaonekana katika Kielelezo cha 6, ambacho kinaonyesha viwango vya kufaulu katika majiribio yote mawili pamoja kwa watoto wenye umri wa maalum (kuanzia umri wa miaka 7-16).

Mambo makubwa mawili yanajitokeza hapa. Kwanza, kiwango cha kufaulu cha wasio maskini kimeoneshwa na mstari wa juu (uliounganishwa na pembe tatu) mara zote huwa juu ya mistari mingine miwili, maana yake viwango vya ufaulu mara zote huwa viko juu kwa kundi hili. Katika umri wa miaka 10, kwa mfano, kiwango cha ufaulu miongoni mwa wasio maskini (33%) ni mara mbili ya kile cha maskini ambacho ni (16%) na ni mara tatu zaidi ya kile cha wale masikini zaidi kabisa ambacho ni (10%). Kwa wastani, uduni katika kujifunza utokanao na watoto kutoka katika kaya maskini, ukilinganisha

na watoto kutoka katika kaya zisizo maskini, ni unafanana kwa karibu miaka miwili (na hasa kwa kaya maskini zaidi). Hii ni kwa sababu katika umri wa miaka 12, karibu 34% ya watoto kutoka katika kaya zenye kipato kizuri wanafaulu majaribio yote mawili, ambayo ni sawa na kiwango cha ufaulu cha watoto wenye umri wa miaka 10 wanaotoka katika kaya zisizo maskini.

Pili, mtu atagundua kupanuka kwa pengo kati ya kundi maskini zaidi na makundi mengine kunaongezeka polepole kwa kuzingatia viwango vya kufaulu majaribio (kama ilivyooneshwa katika kielelezo), hasa baada ya umri wa miaka 14. Pamoja na sababu nyingine, hii kutokana na idadi kubwa ya watoto wanaokatisha masomo na idadi ndogo ya watoto wanaoendelea na masomo kwenda shule za sekondari kutoka familia maskini zaidi.10

10 Ni chini ya 4% ya watoto wote kutoka katika kaya maskini zaidi wenye umri wa miaka 10-16 ndio wameandikishwa katika shule za sekondari, ikilinganishwa na 15% ya watoto wanaotoka katika kaya zisizo maskini.

Katika umri wa miaka 10, kwa mfano, kiwango cha ufaulu miongoni mwa wasio maskini (33%) ni mara mbili ya kile cha maskini ambacho ni (16%) na ni mara tatu zaidi ya kile cha wale masikini zaidi kabisa ambacho ni (10%).

Kwa wastani, uduni katika kujifunza utokanao na watoto kutoka katika kaya maskini, ukilinganisha na watoto kutoka katika kaya zisizo maskini, ni unafanana kwa karibu miaka miwili (na hasa kwa kaya maskini zaidi).

Kielelezo cha 5: Kiwango cha ufaulu kwenye majaribio ya kusoma na kuhesabu (kwa pamoja) kwa watoto wenye umri wa miaka 10-16, kwa vigezo vya matabaka ya kiuchumi na kijamii, kote Afrika Mashariki

Kielelezo cha 6: Viwango vya ufaulu katika majaribio ya kusoma na kuhesabu (kwa pamoja), kwa vigezo vya kiuchumi na kijamii na umri, katika Afrika Mashariki yote

% y

a uf

aulu

wa

wan

afun

zi%

ya

ufau

lu w

a w

anaf

unzi

Wenye kipato kizuri

Wenye kipato kizuri

Umri wa mtoto

Maskini

Maskini

Masikini zaidi

Masikini zaidi

Page 21: Je, Watoto Wetu Wanajifunza? · 2013-04-18 · utafiti wa mwaka 2009/10 unazidi kuonyesha kwamba methodolojia na menejimenti ya Uwezo ni thabiti, imara na inaaminika. Uwezo inakaribisha

19Uwezo | Elimu bora, Jukumu langu!

Kwa kuongezea kwenye tofauti zilizopo katika matokeo ya majaribio ya kusoma na kuhesabu kutokana na maeneo na hali za kiuchumi na kijamii, pia ziko tofauti kubwa zinahusiana na aina ya shule wanazosoma. Hii imeoneshwa na Kielelezo cha 7, ambacho kinaonesha asilimia ya watoto wenye umri wa miaka 10-16 ambao wanaweza kufaulu majaribio yote mawili ya kusoma na kuhesabu (kwa pamoja) kwa kuzingatia iwapo wanasoma shule za serikali (umma) au shule binafsi. Grafu inaonesha kwamba shule binafsi zinatoa viwango vya juu vya ufaulu katika nchi zote. Kwa mfano, kiwango cha kufaulu katika shule za serikali za Tanzania ni ni 47% wakati katika shule binafsi ni 75%. Kwa sehemu, utofauti kati ya Tanzania na nchi nyingine ni kwamba kuna uwezekano unaletwa na idadi ndogo sana ya wanafunzi wanaosoma shule binafsi, hata miongoni mwa wanafunzi wenye kipato kizuri, ikiashiria kwamba huenda wanachagua kimaalum.

Mambo mawili zaidi yanajitokeza katika data hizi. Kwanza, pengo katika matokeo kati ya shule za umma na shule binafsi ni kubwa sana Tanzania kuliko Kenya au Uganda. Hili linaonekana kwenye umbali uliopo kwenye mihimili-grafu kati ya shule za umma na shule binafsi kwenye kielelezo. Kwa Tanzania, wanafunzi wa shule binafsi wanafanya vizuri kwa zaidi ya mara moja na nusu ya wale walioko shule za serikali. Kwa Kenya na Uganda umbali huu ni mdogo zaidi. Pili, bila kujali aina ya shule wanazosoma, tofauti kubwa miongoni mwa nchi za Afrika Mashariki zinabaki kuwa wazi. Kwa kila aina ya shule (ziwe za umma au binafsi), wanafunzi wa Kenya wanafanya vizuri zaidi kuliko wanafunzi wa Uganda na Tanzania. Zaidi ya yote, kwenye wastani, wanafunzi walioko kwenye shule zinazofanya vibaya za serikali za Kenya bado zinawazidi kwa kufanya vizuri wanafunzi wanaotoka katika shule zinazofanya vizuri zaidi kwa Uganda.

pengo katika matokeo kati ya shule za umma na shule binafsi ni kubwa sana Tanzania kuliko Kenya au Uganda.

Ukweli wa 7: Wanafunzi wanaosoma katika shule binafsi wanafanya vizuri zaidi kuliko wanafunzi wanaosoma katika shule za serikali (za umma)

Mwisho, ni muhimu kuangalia kama duru ya kwanza na ya pili ya tafiti za Uwezo zinatufikisha kwenye hitimisho lilelile, iwapo kumeendelea kuwepo ulinganifu na iwapo umakini wa kutosha umetumika ili kuruhusu ulinganishaji wakati mwingine. Kwa upande wa kwanza, mtu angetarajia matokeo yawe sawa kwa kuwa tafiti zote zilifanyika kwa uwakilishi wa kitaifa na kwa muda wa miaka miwili, (kwa upande wa Kenya) inatenga zile duru mbili, ambazo muundo ni wa muda mfupi kuweza kufikia mabadiliko ya kiwango kikubwa katika

matokeo ya elimu. Kwa upande mwingine, baadhi ya tofauti zinapaswa kutarajiwa, hasa kutokana na idadi kubwa ya wilaya zilizofikiwa katika duru ya pili. Hakika, ripoti ya Afrika Mashariki kwa duru ya kwanza ya tafiti za Uwezo (angalia www.uwezo.net) ilibainisha kwamba kunaweza kukawa na mkingamo kidogo katika matokeo kutokana na ukweli kwamba chini ya nusu ya wilaya zote zilijumuishwa katika sampuli. Kama ilivyobainishwa katika Sehemu ya 2, wasiwasi huu uliangaliwa katika Uwezo duru ya 2 ambayo ilifikia zaidi

Ukweli wa 8: Matokeo ya utafiti wa Uwezo mwaka 2011 kwa kiwango kikubwa yanaendana na yale ya awamu ya kwanza.

Kielelezo cha 7: Viwango vya ufaulu kwenye majaribio ya kusoma na kuhesabu (kwa pamoja) kwa watoto wenye umri wa miaka 10-16, kwa vigezo vya aina ya shule na nchi

% y

a uf

aulu

wa

wan

afun

zi

Binafsi Binafsi BinafsiUmma Umma Umma

Page 22: Je, Watoto Wetu Wanajifunza? · 2013-04-18 · utafiti wa mwaka 2009/10 unazidi kuonyesha kwamba methodolojia na menejimenti ya Uwezo ni thabiti, imara na inaaminika. Uwezo inakaribisha

20 Je, Watoto Wetu Wanajifunza? | Ujuzi wa Kusoma na Kuhesabu katika Afrika Mashariki | Agosti 2012

ya robo tatu ya wilaya zote katika kila nchi, ikimaanisha matokeo ya awamu ya pili ni ya uhakika zaidi.

Kwa kuangalia ukanda mzima (yaani, tukichukua Kenya, Uganda na Tanzania), kielelezo cha 8 kinalinganisha matokeo kati ya duru mbili za tafiti za Uwezo kwenye majaribio ya kusoma (Kiingereza na Kiswahili) na kuhesabu. Kielelezo kinaonesha asilimia ya watoto wenye umri wa miaka 10-16

katika ukanda ambao wanaweza kufaulu kila jaribio. Ni watoto wenye umri wa zaidi ya miaka 10 tu ndiyo wamejumuishwa, kwa kuwa katika umri huu, wanatarajiwa kuwa wametimiza angalau miaka 2 katika elimu ya msingi. Na hivyo, wanapaswa kuwa na uwezo wa kufaulu majaribio. Kielelezo kinaonesha bayana tofauti hizo katika viwango vya ufaulu kati ya duru hizi mbili kuwa ni ndogo.

Ni watoto wenye umri wa zaidi ya miaka 10 tu ndiyo wamejumuishwa, kwa kuwa katika umri huu, wanatarajiwa kuwa wametimiza angalau miaka 2 katika elimu ya msingi. Na hivyo, wanapaswa kuwa na uwezo wa kufaulu majaribio.

Matokeo kutoka katika duru mbili za utafiti kwa kila nchi yanalingana yakichukuliwa tofauti tofauti (Jedwali la 4). Data zinaonesha asilimia ya watoto wenye umri wa miaka 10-16 katika kila nchi ambao walijibu kwa usahihi majaribio ya kusoma na hisabati kwa pamoja. Tofauti ni ndogo, ikiashiria kiwango kikubwa cha ulinganifu kati ya awamu hizi mbili. Hii inaashiria kwamba methodolojia ya utafiti na uongozi inaonekana kuwa imara na ya kuaminika.

Jedwali la 4: Asilimia za wanafunzi waliofaulu majaribio yote mawili la kusoma na hisabati, kwa kila nchi

Duru ya 1 Duru ya 2

Kenya 65.6 69.7

Tanzania 44.3 45.4

Uganda 30.6 37.9

Afrika Mashariki 45.9 49.8

Vidokezo: Duru ya 1 ya tafiti ilifanyika mwaka 2009 (Kenya) na mwaka 2010 (Uganda na Tanzania); Duru ya 2 ya tafiti zote ilifanyika mwaka 2011.

Chanzo: imekokotolewa kutoka kwenye data za Uwezo 1 na Uwezo 2.

Matokeo ya majaribio ya kusoma na kuhesabu kwa watoto wenye umri wa miaka 10-16 kwa duru mbili za utafiti wa Uwezo

% y

a uf

aulu

wa

wan

afun

zi

Kiingereza Hisabati

Page 23: Je, Watoto Wetu Wanajifunza? · 2013-04-18 · utafiti wa mwaka 2009/10 unazidi kuonyesha kwamba methodolojia na menejimenti ya Uwezo ni thabiti, imara na inaaminika. Uwezo inakaribisha

21Uwezo | Elimu bora, Jukumu langu!

Hitimisho

Page 24: Je, Watoto Wetu Wanajifunza? · 2013-04-18 · utafiti wa mwaka 2009/10 unazidi kuonyesha kwamba methodolojia na menejimenti ya Uwezo ni thabiti, imara na inaaminika. Uwezo inakaribisha

22 Je, Watoto Wetu Wanajifunza? | Ujuzi wa Kusoma na Kuhesabu katika Afrika Mashariki | Agosti 2012

4. Hitimisho

Ripoti hii ni muhtasari wa matokeo muhimu ya utafiti Uwezo awamu ya pili (Uwezo 2) uliofanyika Kenya, Tanzania bara na Uganda mwaka 2011. Tafitihizi,

ambazo ni kati ya tafiti za kaya zenye sampuli kubwa zaidi kuwahi kufanyika Bara la Afrika, hutoa ushahidi makini kuhusu hali halisi ya ujuzi wa kusoma na kuhesabu wa watoto zaidi ya 100,000 (wenye umri miaka 6-16) katika kila nchi ndani ya nchi tatu, na kwenye wilaya zote katika nchi hizo. Tafiti hizi ni kiwakilishi cha kitaifa, kwa hiyo hutoa msingi mzuri wa kuchunguza viwango/ngazi ya ujuzi na mwenendo wa matokeo ya kujifunza.

Matokeo muhimu ya utafiti wa Uwezo awamu ya 2 yana akisi yale ya Uwezo awamu ya 1. Licha ya mafanikio muhimu katika upatikanaji wa elimu ya msingi eneo lote la Ukanda huu,kunakothibitishwa na kuongezeka kwa uwiano wa uandikishaji, idadi kubwa ya watoto bado hawajifunzi kikamilifu.Katika nchi zote tatu, zaidi ya theluthi mbili ya watoto wa darasa la 3 hawana ujuzi wa msingi wa kusoma na kuhesabu majaribio ya ngazi ya darasa la 2. Aidha, watoto wanapata stadi hizi polepole kadri wanavyopanga madarasa, na watoto wengi hupata ujuzi huo baada ya kukamilisha miaka mitano ya kujifunza au zaidi (badala ya miwili tu).

Tafiti hizi pia zimebainisha matokeo mengine kadha muhimu. Kuna tofauti kubwa kwenye wastani wa alama za ufaulu kati ya nchi na nchi Afrika ya Mashariki. Wanafunzi wa Kenya kufanya vibaya zaidi wakati wa miaka ya mwanzo ya elimu ya msingi, lakini wanaonesha maendeleo ya haraka na kuwazidi kidogo wanafunzi wa Tanzania wanapofikia mwisho wa elimu ya msingi. Pia kuna tofauti kubwa katika wastani wa ufaulu wa majaribio kati ya wilaya na wilaya ndani ya kila nchi. Nchini Kenya kuna idadi ndogo ya sana ya wilaya zinazofanya vibaya zaidi. Nchini Tanzania na Uganda kuna idadi kubwa ya wilaya zinazofanya vibaya sana na idadi ndogo ya wilaya zinazofanya vizuri zaidi.

Tofauti kwenye ufaulu wa majaribio (kati ya mwanafunzi mmoja mmoja na wilaya) ni kutokana na sababu kadhaa. Hata hivyo, jambo muhimu ni kwamba kuna tofauti chache katika alama za ufaulu wa majaribio kati ya wavulana na wasichana, na wasichana wanawazidi kidogo wavulana katika nchi zote tatu. Hata hivyo, watoto kutoka kaya duni kiuchumi na kijamii hufanya vibaya zaidi kwenye majaribio kwa umri wote, jambo linaloashiria kwamba kukosekana kwa usawa kwenye fursa

za elimu ni jambo linaloendelea kuwepo.Pia wanafunzi katika shule binafsi hufanya vizuri zaidi ya wanafunzi katika shule za serikali (umma) katika nchi zote tatu, tofauti ambayo ilionekana zaidi kwa watoto wa Tanzania.

Ripoti ya kiufundi yenye maelezo mengi inatoa uchambuzi wa kina zaidi ya utafiti wa Uwezo (inapatikana kutoka www.uwezo.net ). Pamoja na mambo mengine, utafiti wa siku zijazo utajaribu zaidi kuweka bayana vigezo vya matokeo ya kujifunza na tofauti zake katika ukanda wa Afrika Mashariki.

Pindi matokeo kama haya yanapotolewa, ni kawaida watu kuuliza ufumbuzi ni nini. Hakika, Uwezo yenyewe imeanzishwa si tukufanya utafiti lakini kuchochea maboresho katika stadi za kusoma na kuhesabu.Hata hivyo, bado tunasita kutoa orodha ya majibu yaliyo tayarishwa; kwa maana, uzoefu unatufundisha ufumbuzi unaonekana dhahiri unaweza usiwe na tija/ au manufaa. Katika mtazamo wetu swali la nini kifanyike linahitaji kuangaliwa kwa umakini mkubwa na uatayari wa kufikiri kitofauti. Katika mtazamo huo, tunapendekeza mambo matano ya kutilia maanani.

• Kutofanya zaidi kilekile tulichozoea kufanya. Katika uso wa matokeo duni, wanasiasa, mameneja elimu na Mashirika yasiyo ya Kiserikali (NGOs) mara nyingi hutoa wito wa kufanya zaidi, au rasilimali zaidi ziwekezwe kwenye shughuli au hatua zile zile za ufumbuzi, wakati tatizo la msingi kiuhalisia inaweza kuwa ni uchaguzi wa shughuli au hatua za ufumbuzi na wala siyo ukosefu wa rasilimali.

• Kusisitiza juu ya ushahidi huru na makini. Sera nyingi na bajeti huamriwa kwa kuzingatia matendo yaliyopita, upendeleo wa kiitikadi au matakwa ya kisiasa. Watunga sera na watawala wa shule wanaweza kufanya vyema kwa kuchunguza ushahidi ufanisi/tija inayoletwa na shughuli/hatua mbalimbali ili kuweka ufahamu mzuri zaidi wa nini kinafanyika na kuleta manufaa.

• Kuzingatia matokeo ya kujifunza badala ya vitendea kazi/vifaa vya elimu. Miongoni mwa wananchi watunga sera vilevile, elimu mara nyingi hutazamwa katika nyanja ya nyenzo/vifaa kama vile madarasa, madawati, vitabu, vilevile kama nyenzo za kibinadamu kama vile idadi ya walimu wenye sifa na wanafunzi waliojiunga. Wakati mambo haya pasipo shaka yanaweza kuchangia kipimo

Page 25: Je, Watoto Wetu Wanajifunza? · 2013-04-18 · utafiti wa mwaka 2009/10 unazidi kuonyesha kwamba methodolojia na menejimenti ya Uwezo ni thabiti, imara na inaaminika. Uwezo inakaribisha

23Uwezo | Elimu bora, Jukumu langu!

cha mwisho cha mafanikio , mawazo na akili zetu zote tunapaswa kuvielekeza kwenye uwezo wa anayejifunza/mwanafunzi, yaani; siyo kuangalia kuna madawati mangapi bali Juma anaweza kusoma.

• Kujifunza kutoka kile kinachoweza kufanyika na kuleta manufaa. Wakati matokeo kiujumla ni mabaya, baadhi ya shule na wilaya hufanya vizuri zaidi kuliko wengine licha ya kukabiliwa na vikwazo vinavyofanana na vya wengine. Mafanikio yao kwa sehemu yanaweza kutokana na fursa za kihistoria na kipato, lakini kunaweza kuwa na sababu nyingine za mafanikio kwa kuangalia menejimenti ya taasisi, jitihada za pamoja na ubunifu ambao wengine wanaweza kuiga.

• Kuchunguza na kufanyia majaribio mawazo mapya. Muundo wa msingi wa ualimu na ufundishaji katika shule nyingi leo haujabadilika sana kwa miongo kadhaa. Inaweza kuwa na maana kujenga utamaduni na nafasi kwa ajili ya mawazo “sumbufu” na teknolojia na kupima kama

uvumbuzi na mbinu tofauti, kama vile malipo unapofanya vizuri, vinaleta manufaa zaidi. Mambo haya matano ya kutilia maanani yako zaidi kwenye namna ya kufikiri na kulikabili tatizo kuliko kuendelea kutoa ufumbuzi kwenye masuala maalum. Na pengine hiyo inaweza kuwa hatua muhimu.

Hakika, wakati miundombinu ya shule imepanuliwa zaidi

na kuendelea kutumia moja ya tano ya bajeti ya taifa bado vinaendelea kutoa matokeo mabaya, changamoto yetu kuu inaweza kuwa iko kidogo kwenye kubainisha sera au kurekebisha utaalamu, kuanzisha mradi mpya au kupata fedha, lakini zaidi inatokana na kushindwa kwa ubunifu na mawazo yetu kuhusu kuboresha elimu. Kama matokeo ya utafiti wa Uwezo yanaweza kuchochea viongozi wa elimu na wananchi pia, wakiwemo walimu na wazazi, kutulia, na kujiuliza kwa kushangaa kama tunafanya kitu sahihi, na badala yake ni kufikiri juu kile kinachoweza kufanyika na kuleta manufaa na namna gani kukifanya, uwezo itakuwa imefanya sehemu kubwa ya kazi yake.

Page 26: Je, Watoto Wetu Wanajifunza? · 2013-04-18 · utafiti wa mwaka 2009/10 unazidi kuonyesha kwamba methodolojia na menejimenti ya Uwezo ni thabiti, imara na inaaminika. Uwezo inakaribisha

24 Je, Watoto Wetu Wanajifunza? | Ujuzi wa Kusoma na Kuhesabu katika Afrika Mashariki | Agosti 2012

KIAMBATISHO A: UWIANO WA UANDIKISHAJI SHULE YA MSINGI

Jedwali A1: Muhtasari wa wastani wa viwango vya kufaulu katika majaribio ya kuhesabu na kusoma kwa pamoja kwa ngazi ya wilaya, kinchi

10% Chini Kati 10% Juu

Kenya 26.5 - 50.0 67.6 84.3 - 92.1

Tanzania 25.4 - 33.3 42.8 63.1 - 80.2

Uganda 9.7 - 22.7 34.1 47.7 - 69.3

Vidokezo: 10% za Chini na za Juu zinaonesha wastani wa viwango vya kufaulu kwa wilaya za juu kabisa na za chini kabisa katika kufaulu kwa makundi ya 10% ya wilaya za juu na 10% ya wilaya za chini katika kila nchi.

Chanzo: imekokotolewa kutoka kwenye data za Uwezo 2.

Jedwali A2: Asilimia ya watoto wenye umri wa miaka 10-16 waliofaulu majaribio ya Uwezo, kijinsia na ki-nchi

Nchi Jaribio Wavulana Wasichana Tofauti

Kenya Kusoma 72.4 76.6 -4.2

Kuhesabu 70.0 72.9 -2.9

Kwa pamoja 67.7 71.8 -4.0

Tanzania Kusoma 55.2 59.0 -3.7

Kuhesabu 59.9 61.3 -1.4

Kwa pamoja 44.3 46.5 -2.2

Uganda Kusoma 42.9 46.2 -3.3

Kuhesabu 56.6 57.2 -0.5

Kwa pamoja 36.6 39.2 -2.6

Vidokezo: Majaribio ya ‘Kusoma’ yanahusu Kiingereza kwa Uganda na Kenya, na Kiswahili kwa Tanzania; majaribio “kwa pamoja’ ina maanisha wanafunzi ambao wanafaulu majaribio yote mawili ya kusoma na kuhesabu.

Chanzo: imekokotolewa kutoka kwenye data za Uwezo 2.

Kielelezo A.1: Uwiano wa watoto walioandikishwa shule za msingi, kwa umri

Vidokezo: kielelezo hiki kinaonesha uwiano wa watoto katika umri uliotajwa ambao wameandikishwa shule za msingi; kumbuka kwamba shule ya msingi kwa Tanzania wanaanza wakiwa na umri wa miaka 7, ambao ni mwaka mmoja baadaye kuliko Uganda na Kenya.

Chanzo: imekokotolewa kutoka kwenye data za Uwezo 2.

Page 27: Je, Watoto Wetu Wanajifunza? · 2013-04-18 · utafiti wa mwaka 2009/10 unazidi kuonyesha kwamba methodolojia na menejimenti ya Uwezo ni thabiti, imara na inaaminika. Uwezo inakaribisha

25Uwezo | Elimu bora, Jukumu langu!

KIAMBATISHO B: VIELELEZO NA MAJEDWALI YA NYONGEZA KWA KENYA

Kielelezo B.1: Viwango vya ufaulu majaribio Kimadarasa kwa watoto walioandikishwa shule, nchini Kenya

Kilelezo B.2: Viwango vya ufaulu majaribio ya kusoma na hisabati (kwa pamoja) kwa watoto wenye umri wa miaka 10-16, kwa vigezo vya hali ya kiuchumi na kijamii, nchini Kenya

Kielelezo B.3: Matokeo ya majaribio kwa watoto wenye miaka 10-16, kwa kila duru ya utafiti wa Uwezo, nchini Kenya

Vidokezo: duru za tafiti zimeoneshwa katika namba kwenye mihimili ulalo.

Chanzo: imekokotolewa kutoka kwenye data za Uwezo 1 na Uwezo 2.

Vidokezo: matabaka ya hali za kiuchumi na kijamii yamefafanuliwa kwenye maelezo.

Chanzo: imekokotolewa kutoka kwenye data za Uwezo 2.

Vidokezo: Namba zilizopo kwenye mihimili ya ulalo zinawakilisha Darasa la 3 hadi la 7 shule za Msingi; ‘Kwa pamoja’ inawakilisha ufaulu wa majaribio yote mawili kusoma kiingereza na kiswahili na hesabu.

Chanzo: imekokotolewa kutoka kwenye data za Uwezo 2.

Kiingereza Kiswahili

Hisabati Kwa pamoja

% y

a uf

aulu

wa

wan

afun

zi

% y

a uf

aulu

wa

wan

afun

zi

Wenye kipato kizuri Maskini Masikini zaidiKiingereza Kiswahili Hisabati

Page 28: Je, Watoto Wetu Wanajifunza? · 2013-04-18 · utafiti wa mwaka 2009/10 unazidi kuonyesha kwamba methodolojia na menejimenti ya Uwezo ni thabiti, imara na inaaminika. Uwezo inakaribisha

26 Je, Watoto Wetu Wanajifunza? | Ujuzi wa Kusoma na Kuhesabu katika Afrika Mashariki | Agosti 2012

KIAMBATISHO C: VIELELEZO NA MAJEDWALI YA NYONGEZA KWA TANZANIA (BARA)

Kiingereza Kiswahili

Hisabati Kwa pamoja

Kielelezo C.1: Viwango vya ufaulu majaribio Kimadarasa kwa watoto walioandikishwa shule, nchini Tanzania

Vidokezo: Namba zilizopo kwenye mihimili ya ulalo zinawakilisha Darasa la 3 hadi la 7 shule za Msingi; ‘Kwa pamoja’ inawakilisha ufaulu wa majaribio yote mawili, kusoma kiingereza na kiswahili na hesabu.

Chanzo: imekokotolewa kutoka kwenye data za Uwezo 2.

Kilelezo C.2: Viwango vya ufaulu majaribio ya kusoma na hisabati (kwa pamoja) kwa watoto wenye umri wa miaka 10-16, kwa vigezo vya hali ya kiuchumi na kijamii, nchini Tanzania

Vidokezo: matabaka ya hali za kiuchumi na kijamii yamefafanuliwa kwenye maelezo.

Chanzo: imekokotolewa kutoka kwenye data za Uwezo 2.

Vidokezo: duru za tafiti zimeoneshwa katika namba kwenye mihimili ulalo.

Chanzo: imekokotolewa kutoka kwenye data za Uwezo 1 na Uwezo 2

Kielelezo C.3: Matokeo ya majaribio kwa watoto wenye miaka 10-16, kwa kila duru ya tafiti wa Uwezo, nchini Tanzania

% y

a uf

aulu

wa

wan

afun

zi

% y

a uf

aulu

wa

wan

afun

zi

Wenye kipato kizuri Maskini Masikini zaidi

Kiingereza Kiswahili Hisabati

Page 29: Je, Watoto Wetu Wanajifunza? · 2013-04-18 · utafiti wa mwaka 2009/10 unazidi kuonyesha kwamba methodolojia na menejimenti ya Uwezo ni thabiti, imara na inaaminika. Uwezo inakaribisha

27Uwezo | Elimu bora, Jukumu langu!

KIAMBATISHO D: VIELELEZO NA MAJEDWALI YA NYONGEZA KWA UGANDA

Kielelezo D.1: Viwango vya kufaulu majaribio Kimadarasa kwa watoto walioandikishwa shule, nchini Uganda

Vidokezo: Namba zilizopo kwenye mihimili ya ulalo zinawakilisha Darasa la 3 hadi la 7 shule za Msingi; ‘Kwa pamoja’ inawakilisha ufaulu wa majaribio yote mawili Kusoma Kiswahili na Kiingereza na jaribio la hesabu.

Chanzo: imekokotolewa kutoka kwenye data za Uwezo 2.

Kilelezo D.2: Viwango vya kufaulu majaribio ya kusoma na hisabati (kwa pamoja) kwa watoto wenye umri wa miaka 10-16, kwa vigezo vya hali ya kiuchumi na kijamii, nchini Uganda

Kielelezo D.3: Matokeo ya majaribio kwa watoto wenye miaka 10-16, kwa kila duru ya tafiti wa Uwezo, nchini Uganda

Vidokezo: matabaka ya hali za kiuchumi na kijamii yamefafanuliwa kwenye maelezo.

Chanzo: imekokotolewa kutoka kwenye data za Uwezo 2.

Vidokezo: duru za tafiti zimeonyeshwa katika namba kwenye mihimili ulalo.

Chanzo: imekokotolewa kutoka kwenye data za Uwezo 1 na Uwezo 2.

% y

a uf

aulu

wa

wan

afun

zi

% y

a uf

aulu

wa

wan

afun

zi

Wenye kipato kizuri Maskini Masikini zaidi

Kiingereza

Hisabati Kwa pamoja

Kiingereza Hisabati

Page 30: Je, Watoto Wetu Wanajifunza? · 2013-04-18 · utafiti wa mwaka 2009/10 unazidi kuonyesha kwamba methodolojia na menejimenti ya Uwezo ni thabiti, imara na inaaminika. Uwezo inakaribisha

28 Je, Watoto Wetu Wanajifunza? | Ujuzi wa Kusoma na Kuhesabu katika Afrika Mashariki | Agosti 2012

KIAMBATISHO E: MIFANO YA MAJARIBIO YA UWEZO YA KUSOMA NA HESABU

Jaribio la Hisabati

Jaribio la Kiingereza

Jaribio la Kiswahili

Page 31: Je, Watoto Wetu Wanajifunza? · 2013-04-18 · utafiti wa mwaka 2009/10 unazidi kuonyesha kwamba methodolojia na menejimenti ya Uwezo ni thabiti, imara na inaaminika. Uwezo inakaribisha

29Uwezo | Elimu bora, Jukumu langu!

Kenya Thika West Central 1

Kenya Kikuyu Central 2

Kenya Nairobi East Nairobi 3

Kenya Nyeri South Central 4

Kenya Gatanga Central 5

Kenya Kirinyaga Central 6

Kenya Kajiado North Rift Valley 7

Kenya Imenti South Eastern 8

Kenya Ruiru Central 9

Kenya Gatundu Central 10

Kenya Githunguri Central 11

Kenya Kiambu Central 12

Kenya Muranga North Central 13

Kenya Nyandarua South Central 14

Kenya Lari Central 15

Kenya Masaba Nyanza 16

Kenya Mbooni Eastern 17

Kenya Nyandarua North Central 18

Kenya Manga Nyanza 19

Kenya Taita Coast 20

Kenya Laikipia East Rift Valley 21

Tanzania Arusha Arusha 22

Kenya Gucha Nyanza 23

Kenya Keiyo Rift Valley 24

Kenya Marakwet Rift Valley 25

Kenya Naivasha Rift Valley 26

Tanzania Iringa Mjini Iringa 27

Kenya Mombasa Coast 28

Kenya Nakuru Rift Valley 29

Kenya Baringo Central Rift Valley 30

Kenya Makueni Eastern 31

Kenya Nakuru North Rift Valley 32

Kenya Baringo North Rift Valley 33

Kenya Mwala Eastern 34

Kenya Buret Rift Valley 35

Kenya Eldoret East Rift Valley 36

Kenya Meru South Eastern 37

Kenya Wareng Rift Valley 38

Kenya Kisii Central Nyanza 39

Kenya Mandera West North Eastern 40

Kenya Sotik Rift Valley 41

Kenya Nandi North Rift Valley 42

Kenya Kangundo Eastern 43

Kenya Nandi Central Rift Valley 44

Kenya Emuhaya Western 45

Kenya Imenti North Eastern 46

Tanzania Moshi Mjini Kilimanjaro 47

Kenya Tharaka Eastern 48

Kenya Mbeere Eastern 49

Kenya Koibatek Rift Valley 50

Kenya Suba Nyanza 51

Kenya Kitui Eastern 52

Tanzania Bukoba Mjini Kagera 53

Kenya Kajiado Central Rift Valley 54

Kenya Nandi South Rift Valley 55

Tanzania Rombo Kilimanjaro 56

Kenya Hamisi Western 57

Kenya Trans Nzoia West Rift Valley 58

Tanzania Morogoro Mjini Morogoro 59

Kenya Yatta Eastern 60

Kenya Embu Eastern 61

Uganda Kampala Central 62

Kenya Kibwezi Eastern 63

Tanzania Temeke Dar Es Salaam 64

Kenya Mwingi Eastern 65

Kenya Butere Western 66

Kenya Rongo Nyanza 67

Tanzania Mbeya Mjini Mbeya 68

Kenya Bungoma North Western 69

Kenya Kisumu West Nyanza 70

Kenya Laikipia West Rift Valley 71

Kenya Marsabit Eastern 72

Kenya Molo Rift Valley 73

Kenya Nandi East Rift Valley 74

Kenya Mandera Central North Eastern 75

Kenya Tigania Eastern 76

Tanzania Tanga Tanga 77

Kenya Nyando Nyanza 78

KIAMBATISHO F: NAFASI ZA UFAULU WILAYA ZA AFRIKA MASHARIKII

Nchi Wilaya Mkoa Nafasi Nchi Wilaya Mkoa Nafasi

Page 32: Je, Watoto Wetu Wanajifunza? · 2013-04-18 · utafiti wa mwaka 2009/10 unazidi kuonyesha kwamba methodolojia na menejimenti ya Uwezo ni thabiti, imara na inaaminika. Uwezo inakaribisha

30 Je, Watoto Wetu Wanajifunza? | Ujuzi wa Kusoma na Kuhesabu katika Afrika Mashariki | Agosti 2012

Tanzania Ilala Dar Es Salaam 79

Kenya Rachuonyo Nyanza 80

Kenya Bomet Rift Valley 81

Kenya Kakamega Central Western 82

Kenya Lamu Coast 83

Kenya Teso North Western 84

Kenya Kericho Rift Valley 85

Tanzania Songea Mjini Ruvuma 86

Kenya Bondo Nyanza 87

Kenya Samia Western 88

Kenya Busia Western 89

Kenya Kakamega North Western 90

Uganda Wakiso Central 91

Kenya Trans Nzoia East Rift Valley 92

Kenya Rarieda Nyanza 93

Tanzania Mwanga Kilimanjaro 94

Kenya Taveta Coast 95

Kenya Malindi Coast 96

Tanzania Hai Kilimanjaro 97

Kenya Kyuso Eastern 98

Tanzania Kilolo Iringa 99

Kenya Mt Elgon Western 100

Tanzania Mufindi Iringa 101

Kenya Kakamega South Western 102

Kenya Bungoma East Western 103

Kenya Kuria East Nyanza 104

Tanzania Same Kilimanjaro 105

Kenya Migori Nyanza 106

Kenya Mutomo Eastern 107

Kenya Kilifi Coast 108

Kenya Kisii South Nyanza 109

Kenya Kwanza Rift Valley 110

Tanzania Shinyanga Mjini Shinyanga 111

Kenya Narok North Rift Valley 112

Kenya Igembe Eastern 113

Tanzania Njombe Iringa 114

Kenya Trans Mara Rift Valley 115

Kenya Bunyala Western 116

Tanzania Moshi Vijijini Kilimanjaro 117

Tanzania Ulanga Morogoro 118

Kenya Mandera East North Eastern 119

Kenya Gucha South Nyanza 120

Tanzania Ileje Mbeya 121

Tanzania Makete Iringa 122

Tanzania Pangani Tanga 123

Kenya Kaloleni Coast 124

Kenya Loitoktok Rift Valley 125

Tanzania Kinondoni Dar Es Salaam 126

Tanzania Iringa Vijijini Iringa 127

Kenya Moyale Eastern 128

Kenya West Pokot Rift Valley 129

Kenya Pokot Central Rift Valley 130

Tanzania Kibaha Coast 131

Tanzania Kyela Mbeya 132

Uganda Mbarara Western 133

Kenya Laikipia North Rift Valley 134

Tanzania Kigoma Mjini Kigoma 135

Kenya Teso South Western 136

Tanzania Newala Mtwara 137

Tanzania Dodoma Mjini Dodoma 138

Tanzania Ilemela Mwanza 139

Tanzania Mtwara Mjini Mtwara 140

Kenya Pokot North Rift Valley 141

Tanzania Simanjiro Manyara 142

Tanzania Songea Vijijini Ruvuma 143

Tanzania Lushoto Tanga 144

Tanzania Kisarawe Coast 145

Tanzania Manyoni Singida 146

Uganda Bushenyi Western 147

Kenya Samburu Central Rift Valley 148

Tanzania Tabora Mjini Tabora 149

Tanzania Chunya Mbeya 150

Tanzania Korogwe Tanga 151

Tanzania Musoma Mjini Mara 152

Uganda Mityana Central 153

Kenya Tana River Coast 154

Kenya Isiolo Eastern 155

Tanzania Singida Mjini Singida 156

Tanzania Babati Manyara 157

Kenya Msambweni Coast 158

Nchi Wilaya Mkoa Nafasi Nchi Wilaya Mkoa Nafasi

Page 33: Je, Watoto Wetu Wanajifunza? · 2013-04-18 · utafiti wa mwaka 2009/10 unazidi kuonyesha kwamba methodolojia na menejimenti ya Uwezo ni thabiti, imara na inaaminika. Uwezo inakaribisha

31Uwezo | Elimu bora, Jukumu langu!

Uganda Kiruhuura Western 159

Kenya Narok South Rift Valley 160

Uganda Nakaseke Central 161

Tanzania Nyamagana Mwanza 162

Tanzania Mbeya Vijijini Mbeya 163

Kenya Bungoma South Western 164

Tanzania Hanang Manyara 165

Tanzania Rungwe Mbeya 166

Tanzania Maswa Shinyanga 167

Uganda Luwero Central 168

Tanzania Mbinga Ruvuma 169

Uganda Ibanda Western 170

Uganda Nakasongola Central 171

Tanzania Mafia Coast 172

Tanzania Karatu Arusha 173

Tanzania Mvomero Morogoro 174

Uganda Hoima Western 175

Uganda Kabarole Western 176

Tanzania Mbarali Mbeya 177

Tanzania Kilombero Morogoro 178

Tanzania Arumeru Arusha 179

Uganda Rukungiri Western 180

Tanzania Kiteto Manyara 181

Tanzania Nachingwea Lindi 182

Tanzania Mbulu Manyara 183

Tanzania Kondoa Dodoma 184

Tanzania Ludewa Iringa 185

Uganda Masaka Central 186

Tanzania Kasulu Kigoma 187

Tanzania Mkuranga Coast 188

Uganda Mbale Eastern 189

Tanzania Mpanda Rukwa 190

Tanzania Singida Vijijini Singida 191

Tanzania Bukoba Vijijini Kagera 192

Tanzania Bukombe Shinyanga 193

Tanzania Bagamoyo Coast 194

Tanzania Bunda Mara 195

Uganda Ntungamo Western 196

Tanzania Liwale Lindi 197

Tanzania Namtumbo Ruvuma 198

Uganda Lyantonde Central 199

Kenya Samburu North Rift Valley 200

Uganda Kabale Western 201

Tanzania Lindi Mjini Lindi 202

Tanzania Masasi Mtwara 203

Kenya Tana Delta Coast 204

Kenya Turkana South Rift Valley 205

Kenya Lagdera North Eastern 206

Tanzania Kilwa Lindi 207

Uganda Mpigi Central 208

Tanzania Kwimba Mwanza 209

Tanzania Muheza Tanga 210

Tanzania Kigoma Vijijini Kigoma 211

Uganda Kalangala Central 212

Uganda Kanungu Western 213

Tanzania Misungwi Mwanza 214

Tanzania Urambo Tabora 215

Uganda Jinja Eastern 216

Tanzania Magu Mwanza 217

Uganda Gulu Northern 218

Uganda Mukono Central 219

Tanzania Igunga Tabora 220

Uganda Kasese Western 221

Tanzania Rufiji Coast 222

Tanzania Karagwe Kagera 223

Tanzania Biharamulo Kagera 224

Tanzania Morogoro Vijijini Morogoro 225

Uganda Rakai Central 226

Uganda Isingiro Western 227

Tanzania Kilosa Morogoro 228

Tanzania Uyui Tabora 229

Uganda Kitgum Northern 230

Uganda Busia Eastern 231

Tanzania Geita Mwanza 232

Tanzania Sikonge Tabora 233

Tanzania Lindi Vijijini Lindi 234

Tanzania Iramba Singida 235

Tanzania Handeni Tanga 236

Kenya Wajir East North Eastern 237

Tanzania Ngorongoro Arusha 238

Nchi Wilaya Mkoa Nafasi Nchi Wilaya Mkoa Nafasi

Page 34: Je, Watoto Wetu Wanajifunza? · 2013-04-18 · utafiti wa mwaka 2009/10 unazidi kuonyesha kwamba methodolojia na menejimenti ya Uwezo ni thabiti, imara na inaaminika. Uwezo inakaribisha

32 Je, Watoto Wetu Wanajifunza? | Ujuzi wa Kusoma na Kuhesabu katika Afrika Mashariki | Agosti 2012

Tanzania Ngara Kagera 239

Tanzania Ruangwa Lindi 240

Uganda Manafwa Eastern 241

Kenya Wajir West North Eastern 242

Tanzania Mbozi Mbeya 243

Tanzania Tandahimba Mtwara 244

Uganda Kisoro Western 245

Tanzania Dodoma Vijijini Dodoma 246

Uganda Moyo Northern 247

Uganda Kapchorwa Eastern 248

Tanzania Sumbawanga Mjini Rukwa 249

Tanzania Nzega Tabora 250

Uganda Kiboga Central 251

Tanzania Sengerema Mwanza 252

Tanzania Monduli Arusha 253

Kenya Wajir North North Eastern 254

Uganda Sironko Eastern 255

Uganda Bukwo Eastern 256

Tanzania Kongwa Dodoma 257

Tanzania Shinyanga Vijijini Shinyanga 258

Tanzania Muleba Kagera 259

Uganda Arua Northern 260

Uganda Kamwenge Western 261

Tanzania Sumbawanga Vijijini Rukwa 262

Uganda Kyenjojo Western 263

Uganda Pader Northern 264

Uganda Kumi Eastern 265

Kenya Ijara North Eastern 266

Tanzania Nkasi Rukwa 267

Uganda Masindi Western 268

Uganda Soroti Eastern 269

Tanzania Tunduru Ruvuma 270

Tanzania Musoma Vijijini Mara 271

Tanzania Tarime Mara 272

Uganda Lira Northern 273

Uganda Amuria Eastern 274

Uganda Kayunga Central 275

Tanzania Kishapu Shinyanga 276

Uganda Kibaale Western 277

Tanzania Kahama Shinyanga 278

Uganda Buliisa Western 279

Uganda Oyam Northern 280

Kenya Turkana Central Rift Valley 281

Tanzania Mtwara Vijijini Mtwara 282

Uganda Kaberamaido Eastern 283

Uganda Adjumani Northern 284

Tanzania Serengeti Mara 285

Uganda Abim Northern 286

Uganda Bukedea Eastern 287

Uganda Sembabule Central 288

Uganda Mubende Central 289

Uganda Nebbi Northern 290

Uganda Katakwi Eastern 291

Tanzania Kibondo Kigoma 292

Uganda Pallisa Eastern 293

Uganda Butaleja Eastern 294

Uganda Iganga Eastern 295

Uganda Bududa Central 296

Tanzania Kilindi Tanga 297

Uganda Mayuge Eastern 298

Tanzania Meatu Shinyanga 299

Tanzania Ukerewe Mwanza 300

Tanzania Mpwapwa Dodoma 301

Uganda Nyadri Northern 302

Uganda Apac Northern 303

Uganda Yumbe Northern 304

Uganda Koboko Northern 305

Uganda Tororo Eastern 306

Uganda Budaka Eastern 307

Kenya Samburu East Rift Valley 308

Uganda Kamuli Eastern 309

Tanzania Bariadi Shinyanga 310

Uganda Amuru Northern 311

Uganda Dokolo Northern 312

Uganda Bundibugyo Western 313

Uganda Bugiri Eastern 314

Uganda Kaliro Eastern 315

Uganda Amolatar Northern 316

Uganda Nakapiripirit Northern 317

Uganda Moroto Northern 318

Uganda Kaabong Northern 319

Uganda Kotido Northern 320

Nchi Wilaya Mkoa Nafasi Nchi Wilaya Mkoa Nafasi

Page 35: Je, Watoto Wetu Wanajifunza? · 2013-04-18 · utafiti wa mwaka 2009/10 unazidi kuonyesha kwamba methodolojia na menejimenti ya Uwezo ni thabiti, imara na inaaminika. Uwezo inakaribisha

33Uwezo | Elimu bora, Jukumu langu!

Page 36: Je, Watoto Wetu Wanajifunza? · 2013-04-18 · utafiti wa mwaka 2009/10 unazidi kuonyesha kwamba methodolojia na menejimenti ya Uwezo ni thabiti, imara na inaaminika. Uwezo inakaribisha

34 Je, Watoto Wetu Wanajifunza? | Ujuzi wa Kusoma na Kuhesabu katika Afrika Mashariki | Agosti 2012

Uwezo Afrika Mashariki ilipo Twaweza

Barabara ya Lenana, ACS Plaza ghorofa ya 3,S.L.P 19875 00200 Nairobi, Kenya

Simu: +254 203861372/3/4Barua pepe: [email protected]

www.uwezo.net

Ripoti hii inajumuisha, inalinganisha na inawasilisha muhtasari wa taarifa za matokeo ya utafiti wa kitaifa wa Uwezo 2011 wa nchi za Kenya, Uganda na Tanzania bara. Takriban watoto 350,000 katika maeneo ya nchi hizi tatu walipimwa uwezo wao katika stadi za msingi za kusoma, kuandika na

kuhesabu kwa ngazi ya Darasa la 2.

Methodolojia ya Uwezo, muundo wa sampuli, zana zetu na mchakato mzima vimekuwa vikifanywa kwa mashauriano na wataalam wa kitaifa na kimataifa, na kuhakikiwa kwa umakini. Maelezo ya kina kuhusu methodolojia na mkusanyo kamili wa data pia vinapatikana kwa wote.

Jambo kubwa lililogundulika ni kwamba licha ya mafanikio makubwa katika kupanua wigo wa upatikanaji wa elimu ya msingi, ujuzi halisi katika kusoma na kuhesabu umebaki kuwa duni katika nchi zote za ukanda huu. Japokuwa watoto kwa sasa wameandikishwa shuleni kwa idadi kubwa mno kuliko awali, lakini hawajifunzi stadi za msingi zinazotarajiwa wajifunze katika ngazi za madarasa waliyofikia na katika umri walionao.

Japokuwa matokeo haya yanaonesha picha ya kutisha ya hali ya elimu katika Afrika Mashariki, bado zipo sababu za kuwa na matumaini. Kwanza, sehemu zote Afrika Mashariki, Ziko baadhi ya shule na wilaya zinafanya vizuri licha ya kukabiliwa na vikwazo vya aina ileile sawa na sehemu zingine. Shule na jamii hizi zinajenga vyanzo muhimu vya ufumbuzi na majawabu ya jinsi ya kuboresha kujifunza kwa watoto. Pili, kuna dalili zinazoonesha wazi kuhama kwa mjadala wa umma na kuelekea kujikita kwenye ubora na matokeo ya kujifunza, na kuuliza maswali makini ambayo yanaweza kusaidia maamuzi ya kisera na kupata thamani kubwa kutoka katika uwekezaji uliopo sasa. Tatu, kidunia kunaongezeko la kufanyia majaribio uvumbuzi na ubunifu ili kuchochea kujifunza ambako kunaweza kuinufaisha Afrika Mashariki, tukichagua na kuamua kwa makini.

Fursa ya kumsaidia kila mtoto ili ajifunze ipo. Na ripoti hii inalengo la kuwataarifu fursa hiyo.