146
1 ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI ZANZIBAR MHE. PANDU AMEIR KIFICHO - SPIKA 1.Mhe. Balozi Seif Ali Iddi MBM/Makamo wa Pili wa Rais/Kuteuliwa na Rais 2.Mhe. Dr. Mwinyihaji Makame Mwadini MBM/Waziri wa Nchi, Afisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi/Jimbo la Dimani. 3.Mhe. Omar Yussuf Mzee MBM/Waziri wa Nchi, Afisi ya Rais, Fedha, Uchumi na Mipango ya Maendeleo/ Kuteuliwa na Rais 4.Mhe. Haji Omar Kheri MBM/Waziri wa Nchi, Afisi ya Rais, Utumishi wa Umma na Utawala Bora/Jimbo la Tumbatu 5.Mhe. Fatma Abdulhabib Fereji MBM/Waziri wa Nchi, Afisi ya Makamo wa Kwanza wa Rais/Kuteuliwa 6.Mhe. Mohammed Aboud Mohammed MBM/Waziri wa Nchi, Afisi ya Makamo wa Pili wa Rais/Kuteuliwa 7.Mhe. Abubakar Khamis Bakary MBM/Waziri wa Katiba na Sheria/Jimbo la Mgogoni. 8.Mhe. Rashid Seif Suleiman MBM/Waziri wa Miundombinu na Mawasiliano/Jimbo la Ziwani. 9.Mhe. Ali Juma Shamuhuna MBM/Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali/Jimbo la Donge 10.Mhe. Juma Duni Haji MBM/Waziri wa Afya/Kuteuliwa

ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

  • Upload
    others

  • View
    59

  • Download
    0

Embed Size (px)

Citation preview

Page 1: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

1

ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI

ZANZIBAR

MHE. PANDU AMEIR KIFICHO - SPIKA

1.Mhe. Balozi Seif Ali Iddi MBM/Makamo wa Pili wa

Rais/Kuteuliwa na Rais

2.Mhe. Dr. Mwinyihaji Makame Mwadini MBM/Waziri wa Nchi, Afisi

ya Rais na Mwenyekiti wa

Baraza la Mapinduzi/Jimbo la

Dimani.

3.Mhe. Omar Yussuf Mzee MBM/Waziri wa Nchi, Afisi

ya Rais, Fedha, Uchumi na

Mipango ya Maendeleo/

Kuteuliwa na Rais

4.Mhe. Haji Omar Kheri MBM/Waziri wa Nchi, Afisi

ya Rais, Utumishi wa Umma

na Utawala Bora/Jimbo la

Tumbatu

5.Mhe. Fatma Abdulhabib Fereji MBM/Waziri wa Nchi, Afisi

ya Makamo wa Kwanza wa

Rais/Kuteuliwa

6.Mhe. Mohammed Aboud Mohammed MBM/Waziri wa Nchi, Afisi

ya Makamo wa Pili wa

Rais/Kuteuliwa

7.Mhe. Abubakar Khamis Bakary MBM/Waziri wa Katiba na

Sheria/Jimbo la Mgogoni.

8.Mhe. Rashid Seif Suleiman MBM/Waziri wa

Miundombinu na

Mawasiliano/Jimbo la Ziwani.

9.Mhe. Ali Juma Shamuhuna MBM/Waziri wa Elimu na

Mafunzo ya Amali/Jimbo la

Donge

10.Mhe. Juma Duni Haji MBM/Waziri wa

Afya/Kuteuliwa

Page 2: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

2

11.Mhe. Zainab Omar Mohammed MBM/Waziri wa Ustawi wa

Jamii na Maendeleo ya Vijana,

Wanawake na

Watoto/Kuteuliwa

12.Mhe. Said Ali Mbarouk MBM/Waziri wa Habari,

Utamaduni, Utalii na

Michezo/Jimbo la Gando

13.Mhe. Ramadhan Abdalla Shaaban MBM/Waziri wa Ardhi,

Makaazi, Maji na

Nishati/Kuteuliwa.

14.Mhe. Suleiman Othman Nyanga MBM/Waziri wa Kilimo na

Maliasili/Jimbo la Jang‟ombe

15.Mhe. Nassor Ahmed Mazrui MBM/Waziri wa Biashara,

Viwanda na Masoko/Jimbo la

Mtoni

16.Mhe. Abdillah Jihad Hassan MBM/Waziri wa Mifugo na

Uvuvi/Jimbo la Magogoni

17.Mhe. Haroun Ali Suleiman MBM/Waziri wa Kazi,

Uwezeshaji Wananchi

Kiuchumi na Ushirika/Jimbo la

Makunduchi

18. Mhe. Shawana Bukheti Hassan MBM/Waziri Asiyekuwa na

Wizara Maalum/ Jimbo la Dole

19. Mhe. Haji Faki Shaali MBM/ Waziri Asiyekuwa na

Wizara Maalum/Jimbo la

Mkanyageni

20.Mhe. Machano Othman Said MBM/Waziri Asiyekuwa na

Wizara Maalum/Jimbo la

Chumbuni.

21.Mhe. Othman Masoud Othman Mwanasheria Mkuu

Page 3: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

3

22.Mhe. Issa Haji Ussi Naibu Waziri wa

Miundombinu na

Mawasiliano/Jimbo la Chwaka

23.Mhe. Zahra Ali Hamad Naibu Waziri wa Elimu na

Mafunzo ya Amali/Nafasi za

Wanawake

24.Mhe. Dr. Sira Ubwa Mamboya Naibu Waziri wa

Afya/Kuteuliwa na Rais

25.Mhe. Bihindi Hamad Khamis Naibu Waziri wa

Habari,Utamaduni,Utalii na

Michezo/ Nafasi za Wanawake

26.Mhe. Haji Mwadini Makame Naibu Waziri wa Ardhi,

Makaazi, Maji na

Nishati/Jimbo la Nungwi

27.Mhe. Thuwaybah Edington Kissasi Naibu Waziri wa Biashara,

Viwanda na Masoko/Jimbo la

Fuoni

28.Mhe. Mtumwa Kheir Mbarak Naibu Waziri wa Kilimo na

Maliasili/Nafasi za Wanawake

29. Mhe. Mohammed Said Mohammed Naibu Waziri wa Mifugo na

Uvuvi/ Jimbo la Mpendae

30.Mhe. Abdalla Juma Abdalla Jimbo la Chonga

31.Mhe. Abdalla Moh‟d Ali Jimbo la Mkoani

32. Mhe. Ali Mzee Ali Kuteuliwa

33.Mhe. Abdi Mosi Kombo Jimbo la Matemwe

34.Mhe. Ali Abdalla Ali Jimbo la Mfenesini

35. Mhe. Ali Salum Haji Jimbo la Kwahani

36.Mhe. Amina Iddi Mabrouk Nafasi za Wanawake

Page 4: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

4

37. Mhe. Asaa Othman Hamad Jimbo la Wete

38.Mhe. Asha Abdu Haji Nafasi za Wanawake

39.Mhe. Asha Bakari Makame Nafasi za Wanawake

40.Mhe. Ashura Sharif Ali Nafasi za Wanawake

41.Mhe. Bikame Yussuf Hamad Nafasi za Wanawake

42.Mhe. Farida Amour Mohammed Nafasi za Wanawake

43.Mhe. Fatma Mbarouk Said Jimbo la Amani

44.Mhe. Hamad Masoud Hamad Jimbo la Ole

45.Mhe. Hamza Hassan Juma Jimbo la Kwamtipura

46.Mhe. Hassan Hamad Omar Jimbo la Kojani

47.Mhe. Hija Hassan Hija Jimbo la Kiwani

48.Mhe. Hussein Ibrahim Makungu Jimbo la Bububu

49.Mhe. Ismail Jussa Ladhu Jimbo la Mji Mkongwe

50.Mhe. Jaku Hashim Ayoub Jimbo la Muyuni

51.Mhe. Kazija Khamis Kona Nafasi za Wanawake

52.Mhe. Mahmoud Muhammed Mussa Jimbo la Kikwajuni

53.Mhe. Makame Mshimba Mbarouk Jimbo la Kitope

54.Mhe. Mansoor Yussuf Himid Jimbo la Kiembesamaki

55.Mhe. Marina Joel Thomas Kateuliwa na Rais

56.Mhe. Mbarouk Wadi Mussa Jimbo la Mkwajuni

57.Mhe. Mgeni Hassan Juma Nafasi za Wanawake

58.Mhe. Mlinde Mbarouk Juma Jimbo la Bumbwini

Page 5: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

5

59.Mhe. Mohammed Haji Khalid Jimbo la Mtambile

60.Mhe. Mohammed Mbwana Hamad Jimbo la Chambani

61.Mhe. Mussa Ali Hassan Jimbo la Koani

62.Mhe. Mohamedraza Hassanali Mohamedali Jimbo la Uzini

63.Mhe. Mwanaidi Kassim Mussa Nafasi za Wanawake

64.Mhe. Mwanajuma Faki Mdachi Nafasi za Wanawake

65.Mhe. Nassor Salim Ali Jimbo la Rahaleo

66.Mhe. Omar Ali Shehe Jimbo la Chake-Chake

67.Mhe. Panya Ali Abdalla Nafasi za Wanawake

68.Mhe. Raya Suleiman Hamad Nafasi za Wanawake

69.Mhe. Rufai Said Rufai Jimbo la Tumbe

70.Mhe. Saleh Nassor Juma Jimbo la Wawi

71.Mhe. Salim Abdalla Hamad Jimbo la Mtambwe

72.Mhe. Salma Mohammed Ali Nafasi za Wanawake

73.Mhe. Salma Mussa Bilali Nafasi za Wanawake

74.Mhe. Salmin Awadh Salmin Jimbo la Magomeni

75.Mhe. Shadya Mohamed Suleiman Nafasi za Wanawake

76.Mhe. Shamsi Vuai Nahodha Jimbo la Mwanakwerekwe

77.Mhe. Subeit Khamis Faki Jimbo la Micheweni

78.Mhe. Suleiman Hemed Khamis Jimbo la Konde

79.Mhe. Ussi Jecha Simai Jimbo la Chaani

80.Mhe. Viwe Khamis Abdalla Nafasi za Wanawake

81.Mhe. Wanu Hafidh Ameir Nafasi za Wanawake

Ndugu Yahya Khamis Hamad Katibu wa Baraza la Wawakilishi

Page 6: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

6

Kikao cha Kumi na Saba – Tarehe 8 Julai, 2013

(Kikao kilianza saa 3:00 asubuhi)

DUA

Mhe. Naibu Spika, (Ali Abdalla Ali) alisoma Dua

TAARIFA

Mhe. Naibu Spika: Waheshimiwa Wajumbe, kabla ya kuanza shughuli zetu

asubuhi kuna taarifa ya mechi iliyochezwa jana baina ya Timu ya Baraza la

Wawakilishi Sport Club na wenzetu wa Uhamiaji. Matokeo ni kwamba Timu

ya Baraza Sport Club imeshinda mabao mawili na Uhamiaji hawakupata kitu.

Wafungaji wetu wa mabao hayo ni moja amefunga Mhe. Ussi Jecha Simai na

goli la pili amefunga mtendaji wetu Fuad Rashid Omar. (Makofi)

Kwa matokeo hayo, sasa tumeingia nusu final na tunampongeza kocha wetu

Sumbu na anasema yako matumaini ya kuchukua kombe timu yetu. (Makofi)

MASWALI NA MAJIBU

Nam. 131

Wafungwa na Mahabusu Kunyimwa Haki ya Kutoa Maoni na Habari

Mhe. Jaku Hashim Ayoub – Aliuliza:-

Mhe. Naibu Spika, kabla kujibiwa swali langu Nam. 131 naomba kwa

heshima na taadhima nitoe utangulizi kwa ruhusu yako Mhe. Naibu Spika.

Kesho au kesho kutwa tunategemea kuwa na mwezi mtukufu wa Ramadhani

na serikali kwa kuwathamini wananchi wake katika mwezi huo Mtukufu wa

Ramadhani imeondoa msamaha wa kodi zote ikiwemo mchele, sukari na unga

wa ngano. Kwa hivyo, ombi langu kwa serikali kwamba isimamie vizuri zoezi

hili ili wananchi waweze kufaidika.

Vile vile katika mwezi Mtukufu wa Ramadhani tumeshuhudia mavazi ya

rusha roho katika mwezi huu Mtukufu wa Ramadhani. Kutokana na hali hiyo,

naiomba serikali kupitia kwako Mhe. Naibu Spika, kwamba itoe tamko rasmi

kabisa kwa mavazi hayo kwa muda huu wa mwezi Mtukufu wa Ramadhani

yawe basi.

Page 7: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

7

Kifungu cha 18(1) cha Katiba za Zanzibar ya mwaka 1984 kinatoa haki kwa

kila mtu yuko huru kuwa na maoni yoyote na kutoa nje mawazo yake na

kutafuta kupokea na kutoa habari kupitia chombo chochote, bila ya kujali

mipaka ya nchi na pia ana uhuru wa mawasiliano yake kutoingiliwa kati.

(a) Je, kwa nini wafungwa na mahabusu wananyimwa haki ya

kuzungumza na vyombo vya habari visiwani Zanzibar.

(b) Wizara ina mpango gani wa kuhakikisha haki za wafungwa na

mahabusu za kutoa maoni inazingatiwa kwa mujibu wa Katiba ya

nchi.

(c) Wafungwa wangapi na mahabusu Zanzibar ambao walipata haki ya

kutoa maoni kuhusu mabadiliko ya Katiba mpya ya Jamhuri ya

Muungano wa Tanzania.

Mhe. Waziri wa Nchi, (OR) na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi –

Alijibu:-

Mhe. Naibu Spika, kabla sijajibu swali la Mhe. Mwakilishi naomba ku-

respond au kuzungumza kidogo kuhusu mambo aliyoyazungumza. Mhe.

Naibu Spika, ni kawaida kwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inapokaribia

mwezi Mtukufu wa Ramadhani huwa inatoa msamaha wa vyakula muhimu

kama vile unga wa ngano, mchele na sukari kila mwaka tunasamehe kodi.

(Makofi)

Sasa namuomba sana Mhe. Mjumbe kupitia kwako Mhe. Naibu Spika, akiwa

mfanyabiashara, basi tuitumie vizuri fursa hiyo ili wananchi wetu waweze

kuona unafuu wa punguzo hilo linalotolewa na serikali kwa makusudi.

Kuhusu ombi lake la pili sote tunafahamu kwamba nchi yetu ni ya Kiislamu

kwa taratibu zetu pamoja na mila zetu. Vile vile huwa tunakumbushana tu kila

mwaka inapokaribia mwezi Mtukufu wa Ramadhani huwa tunarekebisha

mpaka wakati ule wa kuondoka kazini.

Pia nyumba zote za starehe, mikahawa pamoja na restaurants zinafungwa na

hali hiyo ni kawaida, isipokuwa nazidi kuwakumbusha tu wananchi wenzangu

na hayo ni ya kawaida na tunazidi kukumbusha na sote tutekeleze wajibu

wetu kwa mwezi Mtukufu wa Ramadhani.

Mhe. Naibu Spika, baada ya utangulizi huo kwa niaba ya serikali. Sasa

naomba kumjibu swali lake Nam. 131 lenye vifungu (a), (b) na (c) kama

ifuatavyo:-

Page 8: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

8

(a) Mhe. Naibu Spika, fursa ya kuwasiliana baina ya wanafunzi ama

mahabusu na jamaa zao na watu wengine wowote ikiwamo hawa

aliowataja waandishi wa habari, zilizokuwepo kwa mujibu wa sheria

Chuo cha Mafunzo ni ya kuandika barua, ambazo hutuma kwa ndugu

na jamaa na ile ya kuonana uso kwa uso na watu ambao yeye

mwenyewe ameomba kuwaona au jamaa na ndugu watakaofika

kumuona.

(b) Serikali huwa inatoa ruhusa maalum pale inapotokea haja ya

wanafunzi wa mahasubu kutoa maoni kwa mujibu wa Katiba. Kwa

mfano, serikali ilipokea maombi kutoka Tume ya Mabadiliko ya

Katiba ya kutaka kupokea maoni kutoka kwa wanafunzi na

mahabusu ambao wamo katika Vyuo vya Mafunzo vilioko Kisiwani

Pemba. Kwa hivyo, maombi hayo yalikubaliwa na wanafunzi na

mahabusu walipata fursa ya kutoa maoni yao.

(c) Jumla ya wanafunzi watano na mahabusu saba wa Chuo cha

Mafunzo Zanzibar walipata haki ya kutoa maoni yao katika

mchakato wa kuandaa Rasimu ya Mabadiliko ya Katiba mpya ya

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Mhe. Jaku Hashim Ayoub:Mhe. Naibu Spika, ahsante pamoja na majibu

ambayo ametoa Mhe. Waziri kutokidhi swali la msingi.

(a) Je, gereza la Kiinua Miguu lina wanafunzi ama mahabusu wangapi,

mpaka wakapewa nafasi watu wawili kutoa maoni.

(b) Katika swali langu la msingi nimeuliza kwa nini wafungwa na

mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari

wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya

Zanzibar.

Mhe. Waziri wa Nchi, (OR) na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi:

Mhe. Naibu Spika, nafikiri nilisema kwenye majibu ya swali mama (a),

kwamba fursa ya kuwasiliana baina ya wanafunzi ama mahabusu na jamaa

zao na watu wengine pamoja na waandishi wa habari ni kwamba wao

wenyewe kwa mujibu wa Sheria ya Chuo cha Mafunzo wao waandike barua

ambazo huduma kwa ndugu na jamaa zao kuonana uso kwa uso na watu

ambao yeye mwenyewe ameomba.

Sasa wanafunzi wa Chuo cha Mafunzo (Kiinua Miguu) hawakuitumia fursa

hiyo, yaani hawajawahi kwa taarifa nilizonazo, isipokuwa walioomba ni

wanafunzi watano na mahabusu saba wa Chuo cha Mafunzo cha Wete Pemba,

Page 9: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

9

ambao hao ndio waliomba na fursa hiyo wakapatiwa. Kwa hiyo, hakuna tatizo

isipokuwa wafuate zile taratibu za kuomba tu.

Mhe. Makame Mshimba Mbarouk: Mhe. Naibu Spika, ahsante kwa kunipa

fursa hii ya kuuliza swali la nyongeza pamoja na majibu mazuri ya Mhe.

Waziri. Kwa hivyo, nadhani huko nyuma kulikuwa na serikali inawapelekea

mahabusu magazeti pamoja na redio kwa ajili ya kusikiliza mambo ya

ulimwengu yanavyokwenda.

Je, utaratibu huu upo unaendelea na kama hauendelei, basi kwa nini

tusiendeleze kuwapatia vitu kama hivyo ili kuweza kujua ulimwenguni kuna

nini.

Mhe. Waziri wa Nchi, (OR) na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi:

Mhe. Naibu Spika, ni kweli na hasa kutokana na haki za binadamu

zilivyoashiria siku hizi ulimwenguni watu kama hawa mahabusu

aliozungumza wanapaswa wapewe fursa za magazeti. Kwa kweli nina hakika

fursa ya redio na televisheni wanayo na sina hakina na magazeti, basi

nitafuatilia na nione kama hawapewi basi na hiyo tunaiingiza.

Mhe. Shadya Mohammed Suleiman:Mhe. Naibu Spika, ahsante sana kwa

kunipatia nafasi ya kuweza kumuuliza Mhe. Waziri swali moja la nyongeza.

Mhe. Waziri nataka kufahamu wastani wa wanafunzi na mahabusu.

Mhe. Waziri wa Nchi, (OR) na Mwenyekiti wa Baraza la

Mapinduzi:Mhe. Naibu Spika, ni kawaida kwenye Vyuo vyetu vyote vya

Mafunzo huwa tunao mahabusu wengi zaidi ya wanafunzi na hiyo ndio trend

ya wastani kwa jumla tuliyonayo siku zote. Kwa kweli haijawahi kutokea

tukawa na wanafunzi na mahabusu idadi sawa.

Hali hii zaidi inatokana na kwamba kesi zile huwa zinachelewa kukamilika,

kwa hiyo mahabusu wale wanakwenda na kurudi na uchungu bado

haujakamilika. Sasa mpaka tarehe ya leo 08 Julai, 2013 kuna mahabusu

wapatao 223 na wanafunzi 98 na utaona uwiano na mara nyingi trend

inakwenda hivyo.

Page 10: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

10

Nam. 36

Upatikanaji wa Ving’amuzi

Mhe. Hassan Hamad Omar – Aliuliza:-

Tulipata kusikia ndani ya vyombo vya habari kwamba Serikali ya Mapinduzi

ya Zanzibar itapata msaada wa ving‟amuzi laki mbili na kuvigawa kwa

wananchi kwa thamani ndogo sana, kisha tukasikia vitauzwa kwa thamani ya

shilingi 50,000/= sasa shilingi 75,000/= na malipo yaende katika taasisi za

AGAPE badala ya wizarani.

(a) Je, hali hii ya kutatanisha imesababishwa na nini na ukweli ni upi.

(b) Je, huoni kuweka thamani kubwa ya bei ya king‟amuzi kutapelekea

wananchi wengi ambao idadi kubwa ni wanyonge washindwe

kufaidi haki ya kupata habari kupitia televisheni.

(c) Je, kuna ubaya gani kuendelea kubakia na analogue na king‟amuzi

ikabaki kuwa ni hiari.

Mhe. Waziri wa Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo – Alijibu:-

Mhe. Naibu Spika, nakushukuru na naomba nimjibu Mhe. Mwakilishi swali

lake Nam. 36 kama ifuatavyo:-

(a) Mhe. Naibu Spika, serikali kupitia Wizara ya habari, Utamaduni,

Utalii na Michezo haijawahi kutangaza kwamba itapata msaada wa

wa ving‟amuzi laki mbili na kuvigawa kwa wananchi kwa thamani

ndogo sana au bure.

Kwa kweli tulichokitangaza ni kwamba ving‟amuzi vitakavyoletwa

vitaanza kuuzwa kwa bei ya shilingi 50,000/= kwa king‟amuzi

kimoja, na kwamba hadi leo king‟amuzi kinachorushwa matangazo

ya digital Zanzibar kinauzwa kwa shilingi 50,000/= kila kimoja,

labda hapo baadaye kitakapopanda kwenye kiwanda basi na sisi

tutalazimika kupandisha na kuwaarifu wananchi.

Mhe. Naibu Spika, isipokuwa gharama za ziada za matumizi ya

king‟amuzi chenyewe baada ya kukinunua ndio kimefanya jumla

yake gharama hizo zifikie shingi 73,000/= kama ifuatavyo:-

(i) Bei ya ununuzi wa king‟amuzi ni shilingi 50,000/=

Page 11: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

11

(ii) Gharama ya kutanguliza malipo ya muda wa

mwezi mmoja ni shilingi 8,000/=

(iii) Gharama ya usajili na uunganishaji kwenye

mtambo mkuu head hand ni shilingi 15,000/=.

Kwa hivyo, hiyo ndio inayofanya jumla iwe

shilingi 73,000/=

Mhe. Naibu Spika, baada ya ujenzi wa miundombinu ya digital ya

Serikali kukamilika pamoja na kupata maarifa ya uendeshaji wa

miundombinu hiyo. Kwa kweli wizara yangu imetiliana mkataba wa

uendeshaji wa miundombinu hiyo ya digital ya Serikali na mjenzi wa

miundombinu hiyo Kampuni ya AGAPE kwa muda wa miaka

miwili.

Moja ya masharti ya mkataba huo ni kuwa Kampuni ya AGAPE

itafute yenyewe mkopo wa ununuzi na uuzaji wa ving‟amuzi hivyo

na ndio maana malipo ya ununuzi wa king‟amuzi yanakwenda kwa

taasisi ya AGAPE badala ya wizara.

(b) Mhe. Naibu Spika, si kweli kwamba bei ya king‟amuzi hicho ni

kubwa kuliko ving‟amuzi nyengine na zaidi ukitilia maanani

kwamba kiwango cha king‟amuzi chetu kina fursa za matumizi ya

internet kuweza kurikodi vipindi na kutumika katika matangazo ya

High Definition Digital hapo baadae kutoka Standard Digital kwa

hivi sasa.

Mhe. Naibu Spika, naomba niwaambie Waheshimiwa Wajumbe wa

Baraza lako hili tukufu, kwamba king‟amuzi hichi kwa hapa nchini

hivi sasa basi ndio pekee chenye hadhi ya kurusha matandao wa

Standard Digital na pia High Definition Digital. Vile vile kwa hali

ya king‟amuzi hicho popote Tanzania king‟amuzi hicho basi

hakiuzwi chini ya shilingi 110.

(c) Ubaya wa kubakia katika mfumo wa matangazo ya Analogue ni

kwamba,

(i) Moja tutakuwa tunavunja makubaliano ya nchi hizi

za Afrika ya Mashariki kwamba ikifika mwezi wa

Januari 2013 zianze kurusha matangazo ya digital

katika nchi zetu.

(ii) Ikiwa sisi Zanzibar tutabakia katika mfumo wa

matangazo ya Analoue na nchi za jirani ziingie

Page 12: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

12

katika mfumo wa matangazo ya digital, kuna

uwezekano wa mawingi yetu ya matangazo ya

analogue yakaingiliwa na kuchafuliwa na

matangazo ya digital ya nchi jirani na hivyo

kukosa kabisa matangazo ya televisheni katika

nchi yetu.

Mhe. Hassan Hamad Omar: Ahsante sana Mhe. Naibu Spika, kwa kunipa

fursa ya kumuuliza waziri swali la nyongeza. Mhe. Naibu Spika, pamoja na

majibu mazuri ya Mhe. Waziri naomba nimuulize swali lenye (a) na (b).

Mhe. Naibu Spika, ni kweli kwamba siku hizi hali ya upatikanaji wa

matangazo katika king‟amuzi cha ZBC umeimarika.

(a) Mhe. Waziri alisema kutakuwa na channel 36, mbona kuna channel

20 tu.

(b) Nasikia kuna utaratibu wa kutumia satellite, kwani kuna njia ngapi

za digital na kwa nini sisi tukatumia hii ya ving‟amuzi.

Mhe. Waziri wa Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo: Mhe. Naibu

Spika, swali lake la (b) ni la kiufundi sana, lakini nitajaribu kulifafanua.

Kwanza ni kweli kwamba tulitangaza tutatoa channel 36 na hivi sasa tunatoa

channel 20.

Sababu yake ni kwamba tumeweka transmitter mbili kwa kila kituo katika

vituo vyetu sita, lakini kwa sababu ya uzoefu wa nchi jirani, Kenya na

Tanzania walipoingia digital moja kwa moja mwezi wa Januari mwaka huu

wananchi wa nchi hizo walizua vurugu kubwa Kenya walienda Mahkamani

wakazuwia utaratibu huo, kwa sababu nchi ya Kenya ilifunga matangazo ya

analogue moja kwa moja wakarusha matangazo ya digital. Kwa hivyo,

wananchi kwa kweli walipata usumbufu mkubwa na Mahkama ikaingilia kati.

Kwa upande wa Bara mpaka leo kuna tatizo kubwa. Sasa sisi kuzuia hilo

tukaamua twende kwa pamoja digital na analogue kwa mpigo. Katika hili

channel moja ya digital inaweza kurusha matangazo mpaka channel 20,

frequency moja mpaka 20, transmitter moja ya digital inarusha mpaka

channel 20. Kwa hivyo, transmitter moja tumeiweka kwa ajili ya digital na

moja tumeiweka kwa ajili ya analogue. Sasa tunatumia transmitter moja

tunarusha channel 20.

Hii transmitter nyengine tumeiacha kwa ajili ya wananchi ambao hawajapata

ving‟amuzi ili waweze kufaidi Mhe. Naibu Spika, fursa za matangazo, ndio

maana yake hatujazima ile ya analogue tukizima tutafika channel zile zile 36-

Page 13: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

13

40. Kwa hivyo, tumefanya hivyo makusudi kwa ajili ya kuhakikisha kwamba

wananchi wetu ambao hawajapata ving‟amuzi bado wanaendelea kufaidi

matunda ya kupata matangazo kwa sababu ni haki ya Kikatiba.

Suala la pili Mhe. Naibu Spika, kama nilivyosema ni suala la kiufundi kidogo

lakini ni kwamba kuna njia tatu za kurusha matangazo ya digital. Njia ya

kwanza ni ya kutumia satellite, tatizo lake hii capital cost yake ni kubwa sana,

kwa hiyo kwa hali yetu tukaona tusianze huko. Gharama yake ni kubwa lakini

pia matangazo yake yana tendency ya kuingiliwa na hali ya hewa, wale watu

wenye madishi kama Arabic Set na watu wengine wanaona wakati mwengine

hali ya hewa. Kwa hivyo, gharama yake ni kubwa kidogo hii ya pili.

Aina ya pili ni ya kutumia cable kama Zanzibar Cable lakini tatizo lake ni

kwamba itumike kwa eneo dogo. Sasa tabu sana kwa Zanzibar Cable kutoa

cable hapa mpaka Makunduchi, kwa hivyo inatumika kwa njia ndogo. Mhe.

Naibu Spika, sisi tumekusudia kwamba digital yetu itumike nchi nzima

ikiwemo Micheweni na Makunduchi. Kwa hivyo, hii isingetufaa.

Aina ya tatu ni hii terrestrial ambayo inatumia kwa minara tofauti, ndiyo

ambayo sisi tumeamua kutumia hiyo lakini zote zinatumia ving‟amuzi Mhe.

Naibu Spika.

Mhe. Mbarouk Wadi Mussa: Mhe. Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa

nafasi na mimi nimuulize Mhe. Waziri swali la nyongeza. Mhe. Waziri, azma

ya mapinduzi ya Zanzibar ilikuwa ni moja kuwaletea wananchi wake

maendeleo na moja kati ya maendeleo ni kuanzisha ile television ya rangi

kuweza kupata habari nchi mbali mbali na kuona badala ya ile redio kwa

kusikia. (Makofi)

Sasa wananchi wetu wa Zanzibar wengi wao ni maskini na hili linajulikana

kabisa. Mhe. Naibu Spika, unapoanzisha kitu kama hichi inabidi wanunue,

haoni kwamba atakuwa anakwenda kinyume na ile azma ya mapinduzi ya

kuwapatia habari wale wananchi ya television kwa sababu watakuwa hawana

uwezo kwa kununua kile king‟amuzi.

Mhe. Waziri wa Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo: Mhe. Naibu

Spika, kwamba ni kweli azma ya serikali ni kuwapatia wananchi matunda ya

mapinduzi na shughuli ya television, yaani mtandao ni moja katika shahaba

hiyo.

Lakini sio kweli kwamba wananchi wa Zanzibar hawawezi kumiliki

king‟amuzi. Mhe. Naibu Spika, wananchi wa Zanzibar wanaweza kumiliki

Page 14: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

14

television shilingi 200,000/= sasa king‟amuzi cha shilingi 50,000/= kwa nini

wasiweze, kwa kweli itakuwa haiwezekani.

Vile vile ni mfumo kwamba haiwezekani tuendelee kubakia analogue ni

lazima twende katika digital, kwa sababu dunia nzima inaelekea huko, kwa

hivyo hatuwezi kuwaambia Wazanzibari bakieni analogue, tutapitwa na

itakuwa hata hayo matangazo hatuyaoni, yaani technology imetulazimisha

kwenda huko Mhe. Naibu Spika, na wala hakuna njia nyengine.

Kwa hivyo, hatuwezi vyenginevyo na sisi hizo serikali kwa uwezo wake wa

kibajeti hatuwezi kugawa ving‟amuzi kila nyumba bure na hiyo

haitawezekana. Lakini ninachosema kwamba tunajitahidi kuona kwamba

wananchi wetu tunajaribu kufidia kama nilivyosema king‟amuzi hichi katika

soko la kawaida ni shilingi 120,000/= na zaidi. Mhe. Naibu Spika, sisi

tumejaribu kuhakikisha kwamba wananchi wetu wanapata ving‟amuzi katika

bei hiyo.

Mhe. Salma Moh’d Ali:Mhe. Naibu Spika, nakushukuru pamoja na majibu

mazuri ya Mhe. Waziri naomba nimuulize swali la nyongeza. Mhe. Naibu

Spika, ni kweli kuna taarifa ya uhakika kwamba digital hapa Unguja imeanza

vizuri, lakini kwa upande wa Pemba hata pale Chake Chake kwenye mnara

wa television basi matangazo yake huwa ni ya kukatakata na baadhi ya siku

hayapatikani kabisa.

(a) Kutokana na hali hiyo, namuomba Mhe. Waziri anifahamishe je nini

sababu ya tatizo hili.

(b) Wananchi wa Pemba wategemee tatizo hili litatatuka lini.

Mhe. Waziri wa Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo: Mhe. Naibu

Spika, ni kweli kwamba digital Pemba haijatulia nakiri hilo na niombe radhi

kwa wananchi wa Pemba kwamba tunaendelea na jitihada zetu na zitafika

pahala.

Kwa kweli sababu kubwa ni kwamba tulipo-design huu mtandao tuli-design

mawimbi yapeperushwe kwa kutumia mkonga na kwamba microwave link

zibakie kama akiba endapo mkonga utaharibika. Mhe. Naibu Spika, kwa

bahati mbaya mkonga haujawa tayari na kwa hivyo tunatumia ule utaratibu

wa akiba wa microwave link.

Kwa hivyo, Pemba inapata signal kutoka mnara wa Nungwi kwenda mnara

uliopo Kichunjuu, ili signal ionekane vizuri lazima makawa yaliyo juu ya

minara yaonane line of site yaonane, na kukiwa na upepo kidogo ikinyumba

Page 15: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

15

basi digital nayo inayumba na hiyo ndio tendency iliopo Nungwi kwamba

kuna upepo mkubwa na kwa hiyo digital ikiyumba kidogo basi na hali ya

matangazo inayumba Pemba.

Mhe. Naibu Spika, hiyo ndio hali halisi na tunajitahidi mpaka juzi Jumapili

mimi mwenyewe nilikwenda Nungwi kwenye mnara kuona namna gani

wahandisi wanajaribu kuweka hali sawa, lakini wamejaribu kidogo na

nimeambiwa kwamba hali kidogo imetengemaa na hiyo ndio hali halisi.

Vile vile mategemeo yetu ni kwamba itakapofanyakazi mkonga wa taifa basi

hali hii itatengemaa vizuri na kwa mujibu wa Mhe. Waziri wa Nchi, (OR),

Utumishi wa Umma na Utawala Bora juzi katika bajeti yake alitwambia

kwamba baada ya muda mfupi wametia mkataba na Kampuni ya ZANTEL, ili

mkonga wa taifa ufanye kazi na hali hiyo ikiwa tayari basi na wananchi

Pemba watapata matangazo bila ya kukatika hata kidogo.

Nam. 123

Ujenzi wa Nyumba ya Daktari katika Hospitali ya Chake Chake – Pemba

Mhe. Rufai Said Rufai – Aliuliza:-

Kwa kuwa kuna taarifa kwamba Hospitali ya Chake Chake ina tatizo la

daktari wa tiba (Doctor of Medicine MD) na kwa kuwa kuna taarifa kuwa

wizara iko tayari kupeleka daktari wa fani hiyo, lakini kikwazo kikubwa

kilichopo ni nyumba ya kuishi daktari.

Je, ni lini serikali italipatia ufumbuzi tatizo hilo.

Mhe. Naibu Waziri wa Afya – Alijibu:-

Mhe. Naibu Spika, kwa ruhusa yako naomba kumjibu Mhe. Mwakilishi swali

Nam. 23 kama ifuatavyo:-

Ni kweli kwamba Hospitali ya Chake Chake kuna madaktari bingwa wa

maradhi ya kawaida (physician), daktari wa magonjwa ya wanawake

(Obstretics and Gynecologist), daktari wa watoto (Pediatrition) na daktari

bingwa wa upasuaji (Surgeon). Lakini hao ni wageni na mzalendo ni wa

mkataba. Kwa taratibu za ugawaji wa wafanya kazi kwa mahitaji (minimum

requirement) katika mahospitali yetu, kila hospitali inatakiwa iwe na daktari

mzalendo ili kuwa dhamana wa hospitali husika.

Page 16: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

16

Daktari aliyekubalika ni daktari wa kawaida MD (General Doctor of

Medicine). Mhe. Naibu Spika, sio kweli kwamba kukosekana kwa nyumba

kumekwamisha kupatikana kwa MD ila hawapo kwa sasa wa kupangiwa

huko, pindipo wakipatikana watapangiwa na pa kukaa patapatikana.

Mhe. Rufai Said Rufai: Mhe. Naibu Spika, nashukuru na naomba nimuulize

swali moja la nyongeza Mhe. Naibu Waziri. Mhe. Naibu Spika, kuna taarifa

kwamba nyumba ya kukaa daktari ipo ambayo aliyokuwa akikaa daktari

dhamana wa Hospitali ya Chake Chake. Lakini sasa imewekwa mtumishi wa

serikali wa kawaida. Je, kwa kufanya hivyo ni kuboresha huduma ya afya au

ni kurudisha nyuma huduma hiyo.

Mhe. Naibu Waziri wa Afya: Mhe. Naibu Spika, kwa uwelewa wangu mimi

kuhusu nyumba iliyopo Chake-Chake anayekaa ni clinical officer kwa level

yake lakini kwa vile ndio daktari aliyopo, kwa hivyo tumempa hiyo nyumba

pindi akitokea daktari akipatikana tutamuondosha yule tutampa yule

anayestahiki.

Mhe. Saleh Nassor Juma: Ahsante Mhe. Naibu Spika, pamoja na majibu

mazuri ya Mhe. Naibu Waziri wa Afya naomba niulize swali moja dogo sana

la nyongeza. Kwa kuwa malengo ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa

kiasi kikubwa ni kupunguza vifo vya mama na mtoto. Na kwa kuwa umekiri

hapa kwamba daktari bingwa pale Chake-Chake hayupo, hospitali ambayo

inahudumia asilimia kubwa ya wakaazi wa kisiwa cha Pemba.

a) Je. Mhe. Naibu Spika, kuendelea kuiacha hospitali ile kukosa daktari

bingwa ni pia lengo la Melennium goals kufikia kupunguza vifo vya

mama na watoto katika Zanzibar.

b) Kwa kuwa kila siku wanafunzi wa Zanzibar wana graduate katika

vyuo Vikuu vya Mambo ya Afya na Wazanzibari katika graduation

hizo wamo. Je ni lini kwa sababu ulisema akipatikana daktari

utapelekwa kule, sasa ni lini utampeleka daktari katika hospitali ya

Chake-Chake kwa vile wana graduate siku hadi siku katika vyuo

vikuu vya nchi hii.

Mhe. Naibu Waziri Afya: Mhe. Naibu Spika, naomba kujibu swali la

a) Ni kweli vifo vya mama na watoto vinatakiwa vikingwe na hilo ndio

lengo la serikali.

Chake Chake nimesema pana madaktari wengi akiwemo daktari wa

wanawake akiwemo na daktrari wa watoto. Kwa hiyo suala hilo hata

Page 17: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

17

wananchi wengi wameshakwenda madaktari hao wapo, isipokuwa ni

hao wa kigeni, lakini wote ni mabingwa.

b) Mhe. Naibu Spika, tunasomesha madaktari wengi, nje na ndani ya

nchi, wanakuja na kuondoka wengine wanakaa. Kuna utaratibu

tumeupanga kwamba kila hospitali pawe na daktari wa aina fulani.

Tunayemtaka na tunayemzungumza hapa ni daktari atakayekuwa

dhamana kwenye hospitali husika. Hospitali za Wilaya zote

zinatakiwa ziwe na daktari dhamana mzalendo. Sasa

watakapokuwepo tutapanga, Hospitali ya Micheweni, Chake-Chake,

Vitongoji, Mkoani na Hospitali ya Wete, wakija tutapanga lakini

tunategemea labda mwaka huu watakuja madaktari wengi, kwa

sababu wapo wanaomaliza Muhimbili, tutahakikisha tunafanya hivyo

na kwa Unguja tutapeleka Kivunge na Makunduchi.

Nam. 23

Upatikanaji wa Maji Safi na Salama Kijiji cha Jitenge, Kojani

Mhe. Hassan Hamad Omar - Aliuliza:-

Kwa kuwa kumekuwa na kero na usumbufu mkubwa sana kwa wananchi wa

Kijiji cha Jitenge Maziwani Jimbo la Kojani kwa kukosa maji safi na salama

kwa muda mrefu. Pamoja na juhudi zinazochukuliwa na Mwakilishi na

Mbunge wa jimbo hilo na Halmashauri ya Wilaya ya Wete bado huduma hiyo

ni kikwazo kupatikana.

a) Je, Mhe. Waziri nini kinachokwamisha juhudi hizi.

b) Je, ni lini wananchi wa kijiji cha Jitenge Maziwani watarajie

kupata huduma hii muhimu ya maji safi na salama.

Mhe. Naibu Waziri wa Ardhi, Makaazi, Maji na Nishati - Alijibu:-

Mhe. Naibu Spika, naomba kumjibu Mhe. Waziri swali lake Nam. 23 kama

hivi ifuatavyo:-

(a) Mhe. Naibu Spika, kijiji cha Jitenge awali kiasi kama miaka

sita iliyopita kilikuwa kinatumia huduma ya maji kwa kutumia hand

pump kwa msaada wa UNICEF. Huduma hii ilikuwa inapatikana bila

ya usumbufu wowote. Halmashauri ya Wilaya ya Wete, Mbunge na

Mwakilishi walichangia mipira nchi tatu kasorobo kupitia maziwani

ambapo pia kulikuwa na matatizo ya maji. Kwa bahati mbaya mipira

Page 18: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

18

hiyo ilikuwa ni midogo kwa Kijiji cha Jitenge, namuomba Mhe.

Mwakilishi na Halmashauri wawe na moyo wa kuchangia huduma

hiyo ya maji ili kupatikana mipira yenye kiwango kama ushauri wa

Mamlaka utakavyotolewa.

(b) Mhe. Naibu Spika, kwa kijiji cha Ziwani najua mipira

iliyotolewa na Mhe. Mwakilishi iko chini ya kiwango Class C

ambapo husababisha kupasuka mara kwa mara. Ningemuomba Mhe.

Mwakilishi ashirikiane na Mamlaka yetu ya maji tawi la Pemba ili

kuhakikisha kwamba mipira inayotafutwa ni mipira yenye kiwango

na kuzuia uvujaji huo wa mara kwa mara.

Mhe. Hassan Hamad Omar: Ahsante sana Mhe. Naibu Spika, pamoja na

majibu mazuri ya Mhe. Naibu Waziri wa Ardhi, Makaazi na Nishati, naomba

nimuulize swali la nyongeza kama hivi ifuatavyo.

Mhe. Naibu Waziri utakubaliana na mimi kama juhudi ya Mbunge wangu wa

Jimbo la Kojani pamoja na Halmashauri ya Wilaya tumefanya juhudi kubwa

sana. Lakini mpaka hivi ninavyozungumza maji Jitenge hayapatikani.

Wananchi hawa wa kijiji cha Jitenge walishakusudia kwamba wamekwenda

sambamba na jina lao kwamba jitenge kweli wametengwa. Ndio maana

tukapeleka nguvu kubwa wakataka kujitoa katika jimbo hili na kuomba

sehemu nyengine wakajiunge. Tukawashajihisha wabaki katika jimbo na

Inshallah kwa uwezo wa Mwenyezi Mungu na jitihadi ya serikali watapata

huduma.

Nataka uniahidi ni lini kero lile litamalizika na wananchi wa jitenge watapata

maji.

Mhe. Naibu Waziri wa Ardhi, Makaazi, Maji na Nishati: Mhe. Naibu

Spika, nimshukuru tena kwa mara nyengine kwa msaada wao yeye pamoja na

Mhe. Mbunge kwa kushirikiana nasi katika kuchangia huduma hii. Kwa hivyo

wananchi hawa wa Jitenge sitaki niseme lini, lakini namuomba tushirikiane

tena mimi na yeye pamoja na Mamlaka yangu ili kwenda kushughulikia hili

tatizo. Namuhakikishia kwamba tutakaposhirikiana basi wananchi hao

wataipata huduma hii na tatizo hilo litawaondokea.

Mhe. Subeit Khamis Faki:Nakushukuru sana Mhe. Naibu Spika, kwa kunipa

fursa nimuulize Mhe. Naibu Waziri swali la nyongeza.

Mhe. Naibu Spika, katika kuwatatulia wananchi kero ya maji serikali

imefanya jitihada ya kila aina ili kupunguza kero la maji katika nchi yetu ya

Zanzibar. Kwa kuwa mwezi huu Mtukufu wa Ramadhani tunaoingia kesho

Page 19: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

19

kutwa, ni vyena wananchi kuwapunguzia kero zaidi hasa katika huduma hii

ya maji, kwa sababu watu wanakuwa wana thaumu na kwenda mabondeni

kujitwika ndoo kwenye mabonde na kupandisha kwenye milima inakuwa ni

tatizo zaidi. Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imeanzisha huduma ya kusaidia

wananchi pale ambapo wananchi hawapati maji kwa upande wa Unguja kuna

magari maalum ya maji yanawapelekea wananchi kuwasaidia ili

kuwapunguzia usumbufu.

(a) Je, namuuliza Mhe. Waziri katika kipindi hichi cha Mwezi

Mtukufu wa Ramadhani wamejipanga vipi na kule kuona katika

sehemu za vijiji ambavyo hawapati maji kuna magari maalum

yanawapelekea wananchi ili kuwapunguzia usumbufu katika mwezi

huu mtukufu wa Ramadhani.

(b) Je, na kama hivyo sivyo ni lini watajipanga zaidi ili

wananchi waepukane na matatizo hayo.

Mhe. Naibu Waziri wa Ardhi, Makaazi, Maji na Nishati: Ahsante Mhe.

Spika, kama alivyozungumza Mhe. Mwakilishi kwamba tunao utaratibu wa

kuwasaidia wananchi wale ambao huduma ya maji safi na salama

haijawafikia katika vijiji vyao, hususan katika kipindi hichi cha mwezi wa

Ramadhani. Namuomba Mhe. Mwakilishi aelewe kwamba huduma hii sio

kwa Unguja tu nilisema Zanzibar. Kwa hiyo tunafanya Unguja na Pemba.

Bado Wizara yangu kupitia Mamlaka ya Maji itaangalia vile vijiji ambavyo

huduma hiyo haipo hasa kwa mwezi huu Mtukufu wa Ramadhani basi

itaendelea kuwasaidia kama ilivyowasaidia katika miaka mengine.

Mhe. Saleh Nassor Juma: Ahsante sana Mhe. Naibu Spika, kunipatia fursa

ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Pamoja na majibu mazuri ya Mhe. Naibu

Waziri naomba niulize swali hilo kama ifuatavyo.

Kwa kuwa wananchi wa Jitenge katika jimbo la Kojani wameendelea na

wataendelea kukosa maji pale. Kwa sababu juzi tu Mhe. Waziri wakati

anajibu swali pale alisema tunategemea maji ya visima virefu ambavyo sasa

hivi maji yanakosekana kutokana na mabadiliko ya tabia nchi na yataendelea

kukosekana. Kwa hivyo hili tatizo linaonekana litaendelea.

Kwa kuwa tatizo hili litaendelea kuwepo sio Jitenge tu lakini Vitongoji, Wawi

na hata hapa maskini hapa Mji Mkongwe nao maji ni tatizo. Sasa vipi pale

Jitenge Mhe. Waziri kwa sababu serikali inaonekana haina uwezo wa

kupeleka maji.

Page 20: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

20

(a) Je, ni lini mtakwenda kuwafundisha kupeleka elimu ya

kuvuna maji ya mvua ili kama wenzao Bara wanavyovuna

maji ya mvua. Hii elimu ya kuvuna maji ya mvua ni lini

mtaipeleka Jitenge ili watu waweze kufaidika na hii taaluma

ya kupata maji ya kuvuna ya mvua.

(b) Kwa kuwa kila kukicha serikali yetu inashindwa kufanya

ubunifu wa kupata maji. Maana juzi tuliambiwa vile vile hamuwezi

kuyageuza maji ya bahari na kuwa maji safi ya kutumia. Je, ni lini

Mhe. Naibu Waziri mtajenga mitambo hii kutibu maji (Water

treatment plans) ambazo zitatusaidia haya maji taka kuyageuza

kuwa maji mazuri ya kutumia kama wanavyofanya wenzetu katika

nchi za Ghuba na hata hizi nchi nyengine katika Jangwa la Sahara.

Ni lini mtajenga mitambo ya kutibu maji ili na sisi tuondokana na

hili tatizo.

Mhe. Naibu Waziri wa Ardhi, Makaazi, Maji na Nishati: Mhe. Naibu

Spika, kuhusu kujenga mitambo hiyo aliyoizungumza basi inategemea hali ya

fedha ambayo itaingia katika mamlaka yangu. Ni suala ambalo linahitaji

gharama, kwa hivyo serikali iko tayari kulishughulikia hili lakini vile vile

inaangalia hali ya fedha itakavyowezesha kufanya mitambo hiyo.

Vile vile suala la Jitenge, bado narejesha kauli kwamba Wizara yangu

itaangalia zaidi jinsi gani ya kuwasaidia wananchi wa Jitenge. Lakini bado

nimesema naomba sana mashirikiano mimi pamoja na Mhe. Mwakilishi

tushirikiane kisha tuangalie njia gani ya kuliondosha tatizo la wananchi wa

Jitenge kuhusiana na suala la maji.

Mhe. Waziri wa Ardhi, Makaazi, Maji na Nishati: Mhe. Naibu Spika,

pamoja na majibu mazuri ya Mhe. Naibu Waziri naomba kuongezea majibu

ya ziada kutokana swali la Mhe. Saleh Nassor Juma kama hivi ifuatavyo.

Mhe. Naibu Spika, katika suala la maji Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar

imefanya jitihada kubwa kabisa na ndio maana imebuni miradi mingi mipya

hivi sasa ambayo tayari ili katika kiwango cha kutekelezwa ambacho

tunategemea tukifika mwakani kwenye mwezi wa Septemba na Oktoba hali

ya maji katika Zanzibar itakuwa ni nzuri, tuna matumaini makubwa sana.

Kwa hivyo, hasa haya maeneo ambayo kweli yana matatizo maji tunategemea

kwamba tukifika mwakani hali ya maji katika maeneo hayo pia itakuwa

imeshakuwa nzuri kabisa kuliko ilivyo hivi sasa.

Anapozungumzia suala la water treatment plans nadhani kwa Zanzibar

hatujafika kiwango hicho kwa sababu tatizo letu kubwa ni kuwa na pampu au

Page 21: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

21

vyanzo vya maji vya kutosheleza. Hivi sasa hivi kuna miradi ya kuongeza

vyanzo vya maji vingi sana, kwa sababu bado ardhini inaonesha dalili

kwamba kuna maji mengi, maji yaliopo hapa juu ndiyo yameathirika sana na

tabia ya nchi, lakini ardhini inaonesha kuna maji mengi. Kwa sababu kila

kisima kinachochimbwa kinatoa maji ya kutosha kabisa.

Kwa hivyo napenda kumwambia kwamba haijafikia kiwango hicho cha

kufanya water treatment plans hapa Zanzibar, lakini tutegemee miradi yetu

hii inayoendelea sasa hivi italeta mafanikio. Kuna mradi mkubwa sasa hivi wa

Ras al Khaimah ambapo wanachimba visima katika maeneo mbali mbali na

wanapata mafanikio makubwa sana kwamba maji wanayakuta mengi sana.

Tukitoka hapo labda angetwambia Mhe. Mwakilishi kwamba bado tuna

reserve ya maji kubwa katika upande wa Magharibi wa Kisiwa cha Unguja

kuelekea Mainland, huko kuna reserve kubwa sana ya maji ambayo nayo

tukifanya maarifa na tukipata wahisani pamoja na sisi wenyewe tunaweza

tukayapata maji hayo tukayatumia kwa matumizi. Zanzibar ina bahati ya

kuwa ni kisiwa chenye maji matamu sana na tunaweza tukayaendeleza ikiwa

uwezo utakuwepo. Ahsante sana.

HOJA ZA SERIKALI

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya kwa

Mwaka wa Fedha 2013/2014

Mhe. Waziri wa Afya: Kabla sijaanza naomba nieleze kwamba kutokana na

ukubwa wa hotuba yangu nimeruhusika kwa mujibu wa Kanuni kifungu cha

96 (2) kuweza kusoma muhtasari angalau nisizidi masaa mawili. Kwa hivyo

nitakaposoma nitakuwa kila mara nawaejesha Wajumbe kwenye hichi kitabu

chengine, kwa hivyo naomba nisome muhtasari tu ili ninusuru wakati.

Bismillahi Rahmani Rahim.

Utangulizi

Mhe. Naibu Spika, naomba kutoa hoja kwamba sasa Baraza lako tukufu likae

kama Kamati ya Matumizi ili liweze kupokea, kujadili, kuchangia na

mwishoe liidhinishe makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Afya

kwa kazi za kawaida na kazi za maendeleo, kwa mwaka wa fedha 2013/2014.

Mhe. Naibu Spika, kwanza sina budi kumshukuru Mwenyezi Mungu muumba

wa vyote viliomo nchi kavu, baharini na angani kwa kutupa afya njema

ambayo imetuwezesha kukutana mara nyengine tena katika kikao hiki

muhimu cha bajeti.

Page 22: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

22

Mhe. Naibu Spika, sasa naomba kumpongeza Mhe. Dr. Ali Mohamedd Shein,

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pamoja na

Makamu wa Kwanza na Makamu wa Pili wa Rais kwa uongozi wao wa

busara na wenye kutumia hekma nyingi kuiongoza nchi hii, hivyo kuendelea

kuwa ya amani na utulivu. Aidha, nawashukuru kwa mara nyengine tena

kutokana na maelekezo yao wanayoyatoa kupitia vikao vya kila robo mwaka,

mikutano ya kawaida au ziara za kikazi ambayo huwa na lengo la kuimarisha

utoaji wa huduma bora za afya kwa wananchi wa nchi hii.

Mhe. Naibu Spika, wewe mwenyewe pamoja na wajumbe wako wa Baraza

hili, mmekuwa na mchango mkubwa kwenye vita vya kupambana na maradhi

visiwani mwetu. Fikra na mawazo yenu na hata nguvu mnazozitoa majimboni

mwenu kiujumla au kwa mtu mmoja mmoja zimechangia kwa kiasi kikubwa

kwenye mapambano dhidi ya maradhi mbali mbali yanayowaathiri wananchi.

Kwa niaba ya uongozi na watendaji wote wa Wizara ya Afya tunawashukuru

kwa kujumuika nasi kwenye shughuli hii pevu na muhimu. Haya yote

mnayoyafanya yanatuongezea ujasiri wa kutekeleza majukumu yetu kwa

ufanisi bila ya kuchoka. Tunakuombeni muendelee kuwa nasi bila ya kurudi

nyuma au kukata tamaa, kwani mpiganaji mzuri ni yule asiyevunjika moyo au

kukata tamaa.

Mhe. Naibu Spika, kazi zinazofanywa na Kamati za Baraza la Wawakilishi

zinazisaidia sana sekta katika kutekeleza majukumu yake. Hivyo napenda

kuishukuru Kamati ya Maendeleo na Ustawi wa Jamii ya Baraza la

Wawakilishi iliyomaliza muda wake chini ya Mwenyekiti Mhe. Amina Iddi

Mabrouk, kwa kipindi chote cha kazi zake Kamati ilikuwa ikitoa maelekezo

na ushauri kwa Wizara ambao ulisaidia kwa kiasi kikubwa kutekeleza

majukumu yake ya utoaji wa huduma za afya ikiwemo kinga na tiba kwa

wananchi wa Zanzibar. Vile vile napenda kuchukua nafasi hii kumpongeza

Mwenyekiti mpya wa Kamati Mhe. Mgeni Hassan Juma kwa kuteuliwa

kuiongoza kamati hii muhimu, ni matumaini yangu tutashirikiana kwa pamoja

katika kuwatumikia wananchi kwa kuhakikisha wanapata huduma stahiki za

afya kwa shughuli zake za kila siku pamoja na zile iliyojipangia kutekelezwa.

Majukumu ya Wizara

Mhe. Naibu Spika, majukumu makuu ya Wizara ya Afya ni haya yafutayo:

a) Kuandaa na kusimamia utekelezaji wa sera, sheria, mikakati,

mipango na miongozo ya utoaji wa huduma za afya,

Page 23: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

23

b) Kutoa huduma za kinga, tiba na marekebisho ya tabia kwa

jamii,

c) Kusimamia maendeleo ya taaluma kwa wafanyakazi wa ngazi

mbali mbali wa sekta ya afya,

d) Kusimamia upatikanaji wa raslimali (fedha, nguvu kazi, vifaa

na madawa) katika kufanikisha utoaji wa huduma,

e) Kutoa ushauri wa kitaalamu kwa taasisi na wizara juu ya

umuhimu wa afya ya jamii,

f) Kusimamia na kudhibiti ubora na usalama wa chakula, dawa

na vipodozi,

g) Kufanya uchambuzi na kutoa ushauri kwa jamii juu ya

matumizi bora ya kemikali,

h) Kusajili wataalam wa kada mbali mbali za afya,

i) Kusimamia uendeshaji wa hospitali za binafsi, maduka ya

madawa pamoja na kuratibu shughuli za matibabu ya asili,

j) Kuchukua tahadhari za haraka kukabiliana na maradhi ya

miripuko.

Muhtasari wa Mafanikio ya Wizara

Mhe. Naibu Spika, katika kipindi cha mwaka 2012/2013 wizara imepata

mafanikio mazuri katika utendaji kutokana na kazi zake za maendeleo, baadhi

ya mafanikio hayo ni pamoja na:

a) Kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi kutoka 285 kwa kila

vizazi hai 100,000 mwaka 2011 kufikia 221 kwa kila vizazi

hai 100,000 mwaka 2012,

b) Kuanzisha chanjo mpya dhidi ya maradhi ya kuharisha

(Rotavirus) na chanjo dhidi ya homa ya uti wa mgongo

(Pneumococcal),

c) Kupungua kwa maambukizi ya virusi vya UKIMWI kwa

makundi maalumu.

Page 24: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

24

i. Wanaume wanaojamiiana kutoka 12.3% mwaka 2008 na

kufikia 2.6% mwaka 2012,

ii. Watumiaji wa madawa ya kulevya kwa njia ya kujidunga

sindano kutoka 16% mwaka 2008 hadi 11.3% mwaka

2012.

d) Kuendelea kwa kasi kubwa ya ujenzi wa jengo la Mradi

Shirikishi wa Mama na Mtoto liliopo Kidongo Chekundu.

e) Kupitishwa sheria za afya ya jamii na wataalamu wa afya ya

mazingira katika Baraza la Wawakilishi. Sheria hii itakuwa

kichocheo katika kuimarisha afya ya jamii na kuepusha

maradhi yanayosababishwa na mazingira yasio salama.

f) Kuanzisha mfuko maalumu wa fedha kwa ajili ya huduma za

afya wilayani (District Health Services Basket Fund), ili

kuimarisha utoaji wa huduma katika vituo vya afya.

g) Kumalizika ujenzi wa jengo la Bohari Kuu ya Dawa

Maruhubi,

h) Kuanzisha utaratibu wa kufuatilia majumbani wagonjwa

wanaogundulika na malaria ndani ya siku tatu,

i) Kukamilika ujenzi wa majengo mapya ya maabara katika

hospitali za Wete, Chake-Chake na Micheweni,

j) Kupunguza msongamano wa jamaa wa wagonjwa

wanaolazwa katika hospitali ya Mnazi Mmoja,

k) Kuongezeka kwa asilimia ya mama wajawazito

wanaojifungua chini ya uangalizi wa wataalamu wa afya

kutoka asilimia 47.1 mwaka 2011 kufikia 51.3 mwaka 2012,

l) Kukamilika kwa matengenezo makubwa ya nyumba tisa za

wafanyakazi zilizoko Kivunge.

Utekelezaji Kifedha

Mhe. Naibu Spika, kwa mwaka wa fedha 2012/2013, Wizara ilipangiwa

kuchangia jumla ya Tsh. 805,500,000 kwenye Mfuko Mkuu wa Serikali.

Kufikia mwezi wa Machi 2013, kiasi cha Tsh. 366,020,263 (45.4%)

Page 25: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

25

zilikusanywa. Aidha wizara iliidhinishiwa jumla ya Tsh. 18,234,000,000 kwa

ajili ya kazi za kawaida, mishahara, maposho na ruzuku. Kati ya hizo Tsh.

3,946,000,000 kwa Kazi za Kawaida. Hadi kufikia Machi 2013, jumla ya Tsh.

2,385,944,437 (60.46) zilikwishatolewa, kwa upande wa mishahara na posho

Tsh. 13,731,080,000 ziliidhinishwa na hadi kufikia Machi, 2013 jumla ya

Tsh. 10,475, 486,742 (76.29) zilitolewa na Tsh. 556,920,000 ziliidhinishwa

kama Ruzuku kwa Chuo cha Taaluma za Afya – Mbweni ambapo kufikia

Machi Tsh. 172,956,000 (31.06) tayari zilikwishatolewa. Miradi ya

Maendeleo ilitengewa jumla ya Tsh. 2,731,600,000, kufikia Machi 2013

jumla ya Tsh. 724,251,400 (26.5%) zilitolewa.

Mhe. Naibu Spika, naomba uniruhusu nieleze utekelezaji kwa mchanganuo

wa kila Idara, fedha zilizotengwa na kuingizwa hadi kufikia Machi kwa

mwaka 2012/2013 na zilizotengwa kwa mwaka 2013/2014. Ufafanuzi wake

unaonekana kiambatisho namba 17.

Utekelezaji wa Bajeti ya Mwaka 2012/2013

Mhe. Naibu Spika, katika mwaka 2012/13, Wizara ilitekeleza majukumu yake

kwa kuzingatia Malengo ya Milenia, Dira ya Maendeleo (2020), Mkakati wa

Kukuza Uchumi na Kupunguza Umaskini II (2010), Sera ya Afya (2011)

pamoja na maazimio mengine ya kitaifa na kimataifa. Maeneo

yaliyotekelezwa ni haya yafuatayo kwa ufupi:

Magonjwa Yasiyo ya Kuambukiza (NCD)

Mhe. Naibu Spika, magonjwa yasio ya kuambukiza yanaonekana kuongezeka

kwa kasi katika visiwa vya Zanzibar kwa miaka ya karibuni. Magonjwa hayo

ni pamoja na shindikizo la damu, kisukari, saratani na magonjwa mengine

sugu ya mapafu ikiwemo pumu n.k. Kwa kuona umuhimu wa kukabiliana na

hali hiyo, Wizara imeanzisha Kitengo cha kupambana na magonjwa hayo

ikiwa na lengo la kupunguza kasi ya ongezeko la magonjwa yasiyo ya

kuambukiza na kusimamia utekelezaji wa mikakati yenye lengo la

kukabiliana na magonjwa hayo.

Mhe. Naibu Spika, utafiti wa kuweza kubaini hali halisi ya kutambua

mahitaji ya taaluma, vitendea kazi pamoja na raslimali umefanyika kwa vituo

vya afya 34 vya daraja la pili vinavyotarajiwa kuanzisha huduma za maradhi

yasioambukiza, hospitali 4 za vijiji na hospitali 3 za wilaya. Pia matayarisho

ya mpango mkakati wa kupunguza kasi ya maradhi hayo yameanza

sambamba na urushaji wa vipindi mbali mbali vya televisheni na redio na

kuandikwa makala ya magazeti kuhusiana na maradhi hayo.

Page 26: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

26

Mhe. Naibu Spika, kwa ufafanuzi na kwa urefu na wa-refer wajumbe kuanzia

kifungu namba 2.1.0 hadi 2.1.3 ya hotuba yangu iliyomo ndani ya kitabu.

KITENGO CHA KUFUATILIA MWENENDO WA MARADHI

Mhe. Naibu Spika, wizara kwa mwaka wa fedha 2012/2013 imeweza

kufuatilia mienendo ya maradhi mbali mbali ikiwemo magonjwa ya miripuko

kama vile kuharisha damu, ugonjwa wa kutafunwa na mbwa, ugonjwa wa

surua, ugonjwa wa tetekuanga, ugonjwa wa kuharisha kwa kawaida na

ugonjwa wa neoanatal tetanus. Kazi hii imefanywa baada ya kupokea taarifa

za kila wiki juu ya hali ya maradhi maalum kutoka vituo vyote vya Serikali.

Aidha katika kuimarisha mfumo huo wakuu wa vituo hivyo na wataalamu

wanaoshughulika na ukusanyaji wa taarifa „Infectious Diseases Weekly

Ending‟ (IDWE) katika ngazi ya wilaya walipatiwa mafunzo juu ya ufuatiliaji

wa maradhi kwa kila wiki.

Mhe. Naibu Spika, katika mwaka 2012/2013 kulitokea mripuko wa maradhi

ya kuharisha huko Bumbwini, ufuatiliaji ulifanywa ili kujua ukubwa wa tatizo

kwa kufanya utafiti wa kina (Operational Research). Matokeo ya utafiti

yalibainisha kwamba asilimia 33.3 ya waliougua walitumia maji yasiyokuwa

safi na salama na asilimia 66.7 walikula dagaa lisilokuwa salama. Mbali na

hayo kwa kushirikiana na Timu ya Afya ya Wilaya sampuli ya choo (Stool

Sample) ilichukuliwa kwa wagonjwa watatu na matokeo yake yalionesha

kuwa kuna vijidudu vijulikanavyo „Vibrio Parahaemolytica‟, ambavyo

vinapatikana kwa njia ya kula vyakula vya pwani (Sea food). Sambamba na

hilo ufuatiliaji pia ulifanyika katika sehemu mbali mbali, matokeo ya maradhi

yaliyogundulika kwa mgawanyo wa umri na kwa Wilaya yanaonekana katika

kiambatisho namba 1 na 2 ya hotuba yangu na maelezo zaidi kuhusu

ufuatiliaji wa maradhi yanapatikana kifungu namba 2.2.0 hadi namba 2.2.6.

MARADHI YASIYOPEWA KIPAUMBELE

Mhe. Naibu Spika, uchunguzi juu ya maradhi yasiyopewa kipaumbele

yakiwemo kichocho, minyoo matende na mabusha ulifanyika. Kwa upande

wa kichocho jumla ya watu 1,299 kutoka sehemu mbali mbali

walichunguzwa. Kati yao watu 928 waligunduliwa kuwa na ugonjwa sawa na

asilimia 71 na kwa wale waliogunduliwa na maradhi walipatiwa tiba. Aidha

tafiti kwa ajili ya kuimarisha njia za mapambano dhidi ya kichocho, minyoo

na matende zilifanyika ikiwa pamoja na kufanya tathmini za mwenendo wa

maradhi ya kichocho katika skuli 48. Aidha katika mzunguko wa pili wa

ulishaji dawa za kichocho na minyoo, jumla ya wananchi 1,183,154

waliorodheshwa kula dawa hizo, kati ya hao wananchi 976,122 walikula dawa

sawa na asilimia 83.

Page 27: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

27

Mhe. Naibu Spika, ugonjwa wa matende ni moja ya ugonjwa unaowasumbua

wananchi hasa wa Wilaya ya Kusini. Kwa mantiki hii uchunguzi mdogo kwa

watu 32 ulifanyika ambapo ni mtu mmoja tu ndiye alionekana kuwa na

vimelea. Vile vile huduma za maradhi haya zinaendelea kwa kupokea

wagonjwa walioathirika zamani na kupatiwa mbinu za kuweka uvimbe katika

hali ya usafi (home based care).

Mhe. Naibu Spika, ufafanuzi kamili wa kitengo hiki unapatikana katika

kifungu 2.3.0 hadi 2.3.6 cha hotuba yangu.

KITENGO CHA AFYA BANDARINI

Mhe. Naibu Spika, katika kuzuia kusambaa kwa maradhi kutoka nchi hadi

nchi, ukaguzi kwa vyombo vya usafiri na abiria (uwanja wa ndege na

bandarini) ulifanyika. Jumla ya vyombo vya usafiri (meli kubwa, boti na

majahazi) 2,063 vilipangwa kukaguliwa, kati ya hivyo, vyombo 2,066 (102%)

vilikaguliwa Unguja na kwa Pemba ni 29. Ukaguzi ulibainisha kuwa vyombo

31 havikuwa katika hali ya usafi hivyo vilifanyiwa ufukizwaji (fumigation) na

vyombo 30 vimefanyiwa hatua za usafi (upuliziaji/mitego). Aidha abiria

450,704 wa kawaida na 188,622 wa kigeni walikaguliwa. Maelezo zaidi

kuhusu kazi zilizofanywa na Kitengo cha Afya bandarini yanapatikana katika

kifungu 2.4.0 hadi 2.4.7 ya hotuba yangu.

KITENGO CHA HUDUMA ZA MATIBABU YA MACHO

Mhe. Naibu Spika, uchunguzi na utibabu wa macho ulifanyika kwa wanafunzi

2,665 wa Skuli za Jambiani, Kizimkazi Mkunguni, Matemwe, Kidutani

Maandalizi, Kisiwandui na Skuli ya Kidongo Chekundu. Kati yao wanafunzi

587 walipatiwa matibabu na kupewa miwani. Pia askari polisi 69 wa

Hanyegwa Mchana walichunguzwa, kati yao askari 51 walipatiwa miwani na

18 walitibiwa macho. Jumla ya miwani 445 za kusomea ilitolewa kupitia

huduma za masafa katika sehemu mbali mbali. Kiambatisho namba 3 cha

hotuba kinajieleza zaidi.

Mhe. Naibu Spika, kutokana na ukosefu wa daktari bingwa wa macho kwa

watoto hapa nchini, kwa mashirikiano makubwa na Kitengo cha Matibabu ya

Macho kwa watoto cha Muhimbili (MCBI). Kitengo kimeweka utaratibu wa

kuwapeleka watoto wenye matatizo makubwa ya macho huko Muhimbili au

madaktari hao bingwa wa Muhimbili kuja hapa nchini na kutoa huduma

zinazostahili. Kupitia mpango huu kwa kipindi cha Julai hadi Machi, 2013

jumla ya watoto 131 walipatiwa matibabu na madaktari hawa kati ya hao 32

walifanyiwa upasuaji wa mtoto wa jicho na presha ya macho.

Page 28: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

28

Mhe. Naibu Spika, ufafanuzi kamili wa kitengo hiki unapatikana katika

kifungu 2.6.0 hadi 2.6.6 cha hotuba yangu.

KITENGO CHA AFYA YA WAFANYAKAZI

Mhe. Naibu Spika, katika kuhakikisha afya ya wafanyakazi, jumla ya

wafanyakazi 2,364 (Unguja 2,030 na Pemba 334) kutoka taasisi mbali mbali

zinazohusisha chakula walichunguzwa afya zao na kubainika maradhi mbali

mbali ikiwemo pumu, UKIMWI, homa ya tumbo (typhoid), homa ya ini kwa

wafanyakazi 108. Wafanyakazi hawa walifanyiwa utaratibu wa kupatiwa

matibabu. Kiambatisho namba 4 kinatoa ufafanuzi na maelezo zaidi

yanapatikana kifungu namba 2.7.0 hadi namba 2.7.3.

Mhe. Naibu Spika, maelezo zaidi ya utekelezajii wa kitengo hiki yanapatikana

katika kifungu 2.7.0 hadi 2.7.3 cha hotuba yangu.

KITENGO CHA LISHE

Mhe. Naibu Spika, katika kukabiliana na tatizo la ugonjwa wa tezi shingo

(Goitre) yanayosababishwa na ukosefu wa madini joto ambayo hupatikana

kwenye chumvi maalumu, wizara imechapisha na kusambaza vitabu 1,000

vya kanuni ya chumvi kwa maafisa wa ngazi mbali mbali. Halikadhalika

ulishaji wa matone ya vitamin A na dawa za minyoo kwa watoto walio na

umri wa miaka mitano ulifanyika na kubainika kushuka kwa ulaji wa matone

hayo kutoka asilimia 95% hadi 61.5% kitaifa. Sababu kubwa iliyopelekea

kushuka kwa kiwango hiki ni pamoja na kubadilisha mikakati ya utekelezaji

wa kazi hii ambapo kwa sasa kazi inafanywa kwa kupitia huduma za kawaida

(routine services) badala ya kutolewa kwa mfumo wa kampeni kama

ilivyokuwa hapo zamani.

Mhe. Naibu Spika, ufafanuzi kamili wa kitengo hiki unapatikana katika

kifungu 2.8.0 hadi 2.8.4 cha hotuba yangu.

Mhe. Naibu Spika, kwa ujumla Idara ya Kinga na Elimu ya Afya imeelezwa

kwa urefu kuanzia ukurasa wa 5 mpaka ukurasa wa 18 wa hotuba yangu.

HUDUMA ZA TIBA

HOSPITALI ZA WILAYA

Mhe. Naibu Spika, huduma za tiba kwa hospitali tatu za Wilaya na nne za

Vijiji, ziliendelea kutolewa kama kawaida. Hospitali hizi zimefanyiwa

matengenezo na kupatiwa vifaa mbali mbali. Kwa upande wa matengenezo;

Page 29: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

29

Hospitali ya Abdalla Mzee ilitengenezewa mfumo wa maji safi, Hospitali ya

Chake-Chake imefanyiwa matengenezo makubwa katika sehemu inayotoa

huduma za viungo; Hospitali ya Wete wodi ya wanaume na kliniki ya watoto;

ukarabati mkubwa wa nyumba tisa za daktari na ujenzi wa ukuta umefanyika

katika hospital ya Kivunge. Katika Hospitali ya Micheweni kumetengenezwa

chumba cha kuhifadhia dawa na mfumo wa maji safi umetengenezwa katika

Hospitali ya Vitongoji. Aidha kwa upande wa vifaa kama X-ray, mashine ya

Ultra Sound na ECG pamoja na vitanda na magodoro vilinunuliwa kwa

baadhi ya hospitali.

Mhe. Naibu Spika, napenda kuliarifu Baraza lako tukufu kwamba maabara ya

hospitali ya Chake-Chake imechaguliwa kuwemo kwenye maabara 18

zilizomo nchini Tanzania ambazo ziko kwenye ubora (quality), jambo hili

linatia matumaini makubwa katika utoaji wa huduma za maabara katika

hospitali hii. Sambamba na hili wafanyakazi wa maabara hiyo wamepatiwa

mafunzo ili waweze kutoa huduma kwa kiwango kinachostahili.

Mhe. Naibu Spika, ufafanuzi kamili wa Hospitali za Wilaya unapatikana

katika kifungu 3.1.0 hadi 3.9.1 cha hotuba yangu.

HUDUMA ZA UZAZI KATIKA HOSPITALI ZA IDARA YA TIBA

Mhe. Naibu Spika, akinamama kujifungulia katika hospitali ni moja kati ya

mikakati inayochangia kupunguza vifo vya akinamama vitokanavyo na uzazi.

Kwa kipindi cha Julai 2012 hadi Machi 2013, jumla ya wajawazito 9,176

walilazwa katika hospitali hizo. Kati ya hao wajawazito 7,782 walijifungua

kwa njia ya kawaida na akinamama 522 walijifungua kwa njia ya upasuaji.

Akinamama 20 walifariki dunia kutokana na sababu mbali mbali kama kifafa

cha mimba, kutokwa na damu kwa wingi na mengineyo. Ufafanuzi wa hali ya

uzazi unaonekana katika kiambatisho namba 6.

MPANGO WA DAMU SALAMA

Mhe. Naibu Spika, kwa kipindi cha mwaka 2012/2013, jumla ya unit za damu

6,127 (77%) zilikusanywa ambapo lengo lilikuwa kukusanya unit 8,000.

Aidha, wizara kwa kushirikiana na wadau mbali mbali itaendelea na jitihada

za kuwahamasiha wananchi juu ya umuhimu wa kuchangia damu. Kwa

maelezo zaidi naomba watu wasome ukurasa namba 24 hadi 25.

MATIBABU NJE YA NCHI

Mhe. Naibu Spika, shughuli ya kusimamia matayarisho ya usafirishaji

wagonjwa nje ya nchi baada ya kushindikana kimatibabu ndani ya nchi nalo

Page 30: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

30

ni jukumu la Idara ya Tiba. Kwa mwaka wa fedha 2012/2013 jumla ya

wagonjwa 223 walitathminiwa na Bodi (Medical Board), Hadi kufikia Machi

2013 jumla ya wagonjwa 144 ndio waliosafirishwa nje ya nchi. Vile vile

wagonjwa 45 walipelekwa Tanzania Bara. Jumla ya Tsh. 990,248,168

zilitumika kwa huduma hiyo ambazo zimepita kiwango cha fedha

zilizotengwa kwa mwaka 2012/2013 ambazo jumla zilikuwa ni Tshs.

335,000,000. Hali hii inaathiri kwa kiasi kikubwa utekelezaji wa kazi

nyengine za wizara.

Mhe. Naibu Spika, maelezo zaidi ya utekelezaji wa Idara yaTiba yameelezwa

kuanzia kifungu 3.0 mpaka 3.13.3 ambavyo vinavyopatikana ukurasa wa 19

mpaka ukurasa wa 25 wa hotuba yangu.

IDARA YA HOSPITALI YA MNAZI MMOJA

Mhe. Naibu Spika, jukumu muhimu la idara ya Hospitali ya Mnazi Mmoja ni

kutoa huduma za uchunguzi na matibabu kwa wagonjwa ikiwemo huduma za

rufaa, pamoja na mambo mengine, Idara hii kupitia hospitali zake za Mnazi

Mmoja, Mwembeladu na Hospitali ya Wagonjwa wa Akili K/Chekundu hutoa

mafunzo kwa vitendo kwa wanafunzi wa kada mbali mbali za afya wanaotoka

katika Chuo cha Taaluma za Sayansi za Afya na vyuo vya afya vya binafsi na

skuli ya madaktari ya Zanzibar inayoendeshwa kwa msaada wa Cuba.

Mhe. Naibu Spika, nia ya Serikali ni kuifanya Idara hii kuwa taasisi yenye

kujitegemea (Semi Autonomous) ili kuongeza ufanisi katika utoaji wa

huduma. Katika kufanikisha hilo rasimu ya sheria ya kuanzisha taasisi hiyo

imeshaandaliwa na imo katika mchakato wa kujadiliwa katika vikao husika.

HOSPITALI YA MNAZI MMOJA

Mhe. Naibu Spika, kwa mwaka wa fedha 2012/2013 hospitali imeweza

kuendesha huduma za afya kupitia kambi maalum kwa kushirikiana na

madaktari bingwa kutoka nchi ya Spain na Ujerumani. Hadi kufikia Machi

2013 jumla ya wagonjwa 296 waliohndumiwa na madaktari bingwa kutoka

Spain na Ujerumani, kati yao 60 walifanyiwa upasuaji. Wagonjwa 47

walionwa na madaktari kutoka Ujerumani na wagonjwa 19 walifanyiwa

upasuaji ukiwemo wa hyrocephulus, spinal bifida repair yaani uti wa

mgongo, lamine ctomy pamoja na maradhi mengine. Aidha huduma za

wagonjwa wa nje na wa kulazwa zinapatikana katika kiambatisho namba 8 za

kliniki maalum ikiwemo macho, masikio, koo namba 9 na uzazi namba 10.

Mhe. Naibu Spika, mbali na utoaji wa huduma hospitali pia imefanikiwa

kutekeleza mambo yafuatayo:

Page 31: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

31

a) Kuweka mtambo wa oxygen kwenye chumba cha upasuaji

(theatre), wodi ya wagonjwa mahututi (ICU), wodi ya wazazi (maternity)

na chumba cha dharura;

b) Mashine ya kisasa ya kufanyia operesheni (minimal access

surgery) imewekwa kwenye chumba cha upasuaji;

c) Kufungua kituo cha meno cha tabasamu (smiling center) kwa

mashirikiano na wataalamu kutoka China na madaktari wazalendo

wa Zanzibar kwa kufanya marekebisho kwa midomo yenye kasoro;

d) Mfumo wa kuweka kumbukumbu za wagonjwa kwa kutumia

kompyuta (Electronic medical Record System) umeanzishwa

hospitalini hapo;

e) Kuifanyia ukarabati mdogo wodi ya wazazi na chumba cha

wagonjwa wa dharura.

Mhe. Naibu Spika, huduma za kujifungua ni moja ya huduma inayopewa

kipaumbele katika hospitali hii, kwa mwaka 2012/13 Wizara imekuwa

ikitekeleza agizo la Mhe Rais la kutoa huduma hizo bila ya malipo wakati

wote vifaa vya kutolea huduma hiyo vilipopatikana. Katika kipindi cha Julai

2012 – Machi 2013, jumla ya wajawazito 5,503 walijifungua kwa njia ya

kawaida (normal delivery), wajawazito 1,042 walijifungua kwa njia ya

upasuaji na wajawazito 24 walifariki dunia kutokana na sababu mbali mbali,

takwimu zinaonesha kuwa idadi ya wajawazito waliofariki imepanda kutoka

20 kwa mwaka 2011/2012. Kwa ufafanuzi zaidi angalia kiambatisho namba

10. Maelezo ya kina kwa hospitali hii yanapatikana ukurasa 26 hadi 30 katika

hotuba.

HOSPITALI YA WAGONJWA WA AKILI (Kidongo Chekundu)

Mhe. Naibu Spika, kuanzia Julai 2012 hadi Machi 2013, jumla ya wagonjwa

wa nje 4,522 walipatiwa matibabu (2,314 ni wanaume na 2208 ni wanawake).

Aidha, wagonjwa waliolazwa ni 230 (152 ni wanaume na 78 ni wanawake),

mgonjwa mmoja alifariki dunia. Idadi ya wagonjwa waliolazwa imeongezeka

kwa wagonjwa 54

.

Mhe. Naibu Spika, moja kati ya changamoto niliyoieleza katika Baraza hili

katika hotuba ya Wizara ya mwaka 2012/13 ni msongomano wa ndugu na

jamaa wa wagonjwa waliolazwa katika hospitali hii. Tatizo hili limekuwa ni

la muda mrefu na hatua kadhaa zimekuwa zikichukuliwa ili kutoa fursa kwa

madaktari kupata muda na wasaa mzuri wa kuwahudumia wagonjwa. Kwa

Page 32: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

32

sasa wizara imeajiri kampuni ya ulinzi ili kudhibiti uingiaji ovyo wa watu

hospitalini. Napenda kutumia fursa hii kuwaomba wananchi kushirikiana na

uongozi wa hospitali ili utaratibu huu mpya uliowekwa kwa manufaa yetu

pamoja na wagonjwa waliolazwa ufanikiwe.

Mhe. Naibu Spika, Idara ya Hospitali ya Mnazi Mmoja imeelezwa kwa urefu

kuanzia vifungu 4.0 mpaka 4.3.3 kwenye ukurasa wa 25 mpaka 32 wa hotuba

yangu.

OFISI YA MFAMASIA MKUU

Mhe. Naibu Spika, upatikanaji wa dawa muhimu na vifaa tiba ni moja ya eneo

muhimu kwa sekta ya afya ingawa bado upatikanaji wake haukidhi mahitaji

halisi, kwa mwaka wa fedha 2012/2013,wizara imepokea jumla ya Tsh.

271,441,649 kwa ununuzi wa dawa na zana za tiba kutoka mfuko mkuu wa

serikali kati ya Tsh. 1,500,000,000 zilizotengwa. Kwa upande wa washirika

wa maendeleo jumla ya dawa zenye thamani ya Tsh. 3,550,857,320

zilipatikana. Kiambatisho Namba 12 kinatoa ufafanuzi.

Mhe. Naibu Spika, ili kuondokana na kutokuwa na uhakika wa upatikanaji wa

dawa, Wizara imekubaliana na Shirika la Maendeleo la Denmark

(DANIDA), kuanzisha Mfuko maalum wa dawa muhimu (Essential Medicine

Fund) ambao utaruhusu washirika wengine wa maendeleo kuweza kujiunga

na mfuko huo na kuwa na „Account‟ maalum ambayo itafunguliwa. Katika

mchakato huo Shirika la DANIDA limekubali kuchangia Shilingi za

Kitanzania bilioni mbili (bilioni 2) Katika kufanikisha azma hii Serikali ya

Mapinduzi ya Zanzibar inatakiwa kuchangia Shilingi milioni mia tano (500,

000,000). Fedha hizo ni kwa ajili ya dawa muhimu (100 items) ambazo

zinatumika kuanzia ngazi ya vituo vya afya hadi katika Hospitali za Wilaya,

vijiji na hospitali ya Mnazi Mmoja.

Mhe. Naibu Spika, utaratibu maalum wa kuzinunua dawa muhimu

„Framework contract‟ utatumika kutoka mfuko wa dawa. Tayari mtaalam

elekezi yupo nchini katika kusaidiana na wataalamu wetu ili kufanikisha azma

hii. Kwa upande wa dawa za ziada ambazo zinatumika zaidi Hospitali kubwa

za wilaya na Mnazi Mmoja hizi zitanunuliwa kwa kutumia bajeti ya Serikali

ya bilioni 1.5 ambazo ni kati ya bilioni 2.1 zilizotengwa kwa ajili ya ununuzi

wa dawa kwa bajeti ya mwaka 2013/14, pia utaratibu wa Framework

Contract utatumika.

Mhe. Naibu Spika, mbali na mafanikio niliyoyaeleza, Ofisi ya Mfamasia

Mkuu wa Serikali ilikabiliwa na changamoto zifuatazo katika utekelezaji wa

kazi zake zikiwemo:

Page 33: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

33

a) Fedha za ununuzi wa dawa zinazotolewa na Serikali huwa hazitoshi na

upatikanaji wake huwa chini ya kiwango kilichopangwa kwenye bajeti

kwa wakati zinapotakiwa.

b) Kuwepo kwa ucheleweshaji wa dawa kutoka Bohari ya Dawa ya Dar es

Salaam (Medical Store Department). Kwa kipindi cha mwaka uliopita

2012/2013, dawa za miezi mitatu ambazo zilitakiwa zifike Januari 2013,

dawa hizo zilifika mwezi wa Mei 2013, na dawa zilizopatikana zilikuwa

ni asilimia 40 tu ya dawa zote zilizoagizwa, hivyo kufanya dawa nyingi

kukosekana katika vituo vya afya. Hili ni moja kati ya tatizo sugu kwa

uagizaji wa dawa za wizara yetu. Mfumo huu ndio uliotulazimisha

kutafuta mfumo mbadala niliouelekeza katika maelezo yaliyotangulia

hapo juu.

Mhe. Naibu Spika, Idara ya Mfamasia imeelezwa kwa ukamilifu kuanzia

kifungu 5.0 mpaka 5.0.8 vilivyo kwenye ukurasa wa 32 mpaka 35 wa hotuba.

BOHARI KUU YA DAWA

Mhe. Naibu Spika, katika kuhakikisha ubora na uimara wa huduma za

usambazaji dawa na vifaa tiba, Idara inaendelea kuimarisha mfumo wa

usambazaji kulingana na mahitaji (Pull System) kutoka vituo vya afya 19 hadi

kufikia 98 (Unguja 56 na Pemba 42) ambayo sawa na asilimia 71 ya vituo

vyote vya afya. Kupitia mfumo huu mahitaji halisi ya dawa na vifaa tiba

hubainishwa na kituo cha afya husika kwa mashirikiano na Timu ya Afya ya

Wilaya.

Mhe. Naibu Spika, mafunzo yanayolenga usimamizi mzuri wa dawa

yalitolewa kwa wasimamizi wa dawa kutoka Timu za Afya za Wilaya. Katika

mwaka wa fedha 2013/2014, Bohari Kuu ya Dawa inatarajia kuongeza idadi

ya vituo vya afya vinavyoagiza dawa kulingana na mahitaji (Pull System)

kutoka 98 hadi kufikia vituo vyote (144).

Mhe. Naibu Spika, Idara ya Bohari Kuu ya Dawa imeelezwa kwa ukamilifu

kuanzia kifungu 6.0 mpaka 6.0.4 vinavyopatikana kwenye ukurasa wa 35

mpaka 37 wa hotuba.

MKEMIA MKUU WA SERIKALI

Mhe. Naibu Spika, Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali imefanya

uchunguzi wa vielelezo 405 vinavyotoka katika taasisi mbali mbali zikiwemo

Jeshi la Polisi, Vikosi vya SMZ na watu binafsi. Mbali ya uchunguzi wa

vielelezo, Ofisi ya Mkemia Mkuu imefanikiwa kufanya ununuzi wa kemikali

na vifaa vya maabara kwa ajili ya kazi za uchunguzi. Kiambatisho namba 13

Page 34: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

34

kinatoa ufafanuzi wa idadi ya sampuli zilizochunguzwa na Idara ya Mkemia

Mkuu wa Serikali.

Mhe. Naibu Spika, katika kipindi cha mwaka wa fedha 2013/2014 ili kufikia

kuwa na maabara ya kisasa na yenye vifaa vya uhakika na kupata ufanisi

mkubwa wa kufanikisha kazi zake ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali

imejipangia kuongeza ujuzi wa wafanyakazi wa maabara kwa kuwapatia

mafunzo ya ziada ya nadharia na vitendo, vile vile ofisi inategemea kuandaa

rasimu ya sheria ya kemikali pamoja na kuanzisha utafiti wa kisayansi ili

kudhibiti uharibifu wa mazingira unaohusiana na matumizi ya kemikali.

Mhe. Naibu Spika, Idara ya Mkemia Mkuu imeelezwa kwa ukamilifu kuanzia

kifungu 7.0 mpaka 7.0.3 ndani ukurasa wa 37 mpaka 38 wa hotuba yangu.

IDARA YA SERA, MIPANGO NA UTAFITI

Mhe. Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2012/2013, wizara imekuwa

ikiendelea na mchakato wa kuangalia njia mbadala za kugharamia huduma za

afya. Timu ya wataalamu kutoka taasisi za SMZ zimekuwa zikishirikiana kwa

pamoja katika mchakato huu, moja kati ya mapendekezo yaliyoridhiwa ni

kuendelea na taratibu za kuanzisha bima ya afya. Hatua zilizofikwa hadi sasa

tayari uchambuzi yakinifu umeshafanyika juu ya utayari wa wananchi

kuhusiana na bima ya afya na mafunzo kwa timu ya wataalamu yamefanyika

kwa msaada wa mtaalamu kutoka Shirika la Afya Duniani.

Mhe. Naibu Spika, mapitio ya Mpango Mkakati wa tatu wa Wizara

yamefanyika, mapitio haya yameenda sambamba na kufanya tathmini ya kina

(Situation Analysis and Response) ya utekelezaji wa mpango mkakati wa II

wa miaka mitano iliyopita (2006/07-2010/11). Katika kuimarisha utayarishaji

mipango kazi na upatikanaji wa ripoti kwa wakati na kwa urahisi, wizara

imeanzisha programu maalumu ya mtandao (Web Based Planning and

Reporting Tool).

Mhe. Naibu Spika, Idara ya Sera, Mipango na Utafiti imeelezwa kwa

ukamilifu kuanzia kifungu 8.0 mpaka 8.0.6 kwenye ukurasa wa 38 mpaka 41

wa hotuba.

IDARA YA UTUMISHI NA UENDESHAJI

Mhe. Naibu Spika, uhaba wa wafanyakazi hasa wenye fani za kitaalamu

umekuwa ni tatizo la muda mrefu kwa wizara. Napenda kueleza kwamba kwa

mwaka 2012/13, wizara iliidhinishiwa nafasi mpya za ajira 816 hadi sasa ni

nafasi 366 tu ndizo zilizokwisha jazwa (asilimia 45). Hali hii pia

Page 35: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

35

imechangiwa na kutokuwepo kwa wataalam wa afya wenye kiwango

kinachotakiwa waliomaliza na kuomba ajira.

Mhe. Naibu Spika, jumla ya wafanyakazi 101 wameweza kustaafishwa

kutokana na kufikia umri wa kustaafu (Unguja 62 na Pemba 39), na

wafanyakazi 28 walifariki dunia. Aidha wizara imefanikiwa kuziomba na

kupewa kibali cha kuzijaza nafasi hizo, na hatua za kuajiri wafanyakazi

wengine zinaendelea. Sambamba na hilo wizara imeimarisha mfumo wa

takwimu za rasilimali watu (HRIS), mfumo ambao umeiwezesha wizara

kupitia kamati ya mgawanyo wa wafanyakazi kuweza kuweka uwiano wa

wafanyakazi katika ngazi zote za huduma.

Mhe. Naibu Spika, wizara imeandaa mapendekezo ya rasimu ya maposho ya

kufanya kazi katika mazingira hatarishi na maposho ya dhamana kwa

wafanyakazi wanaostahiki kupatiwa maposho hayo na rasimu hizo

zimeshawasilishwa Wizara ya Utumishi na Utawala Bora kwa hatua za

utekelezaji.

Mhe. Naibu Spika, kupitia Idara hii mpango mkuu wa mafunzo kwa

wafanyakazi utakaokuwa ni kiongozi katika kupeleka wafanyakazi

masomoni umekamilika. Pia Idara imefanikiwa kupeleka masomoni

wafanyakazi na wanafunzi katika vyuo mbali mbali kwa mafunzo ya muda

mrefu na muda mfupi, ndani na nje ya nchi ambapo jumla ya wafanyakazi

226 kati yao 115 wanawake na 111 wanaume wamepatiwa mafunzo ya

muda mrefu. Wafanyakazi 14 walipatiwa mafunzo ya muda mfupi. Aidha

Jumla ya Wafanyakazi 82 wamerudi masomoni wakiwemo madaktari

bingwa wa fani ya moyo, upasuaji na usingizi.

Mhe. Naibu Spika, utekelezaji wa Idara ya Utumishi na Uendeshaji

umeelezwa kwa ukamilifu kuanzia kifungu 9.0 mpaka 9.2.5 kwenye ukurasa

wa 41 mpaka 44 wa hotuba yangu.

TAASISI MAALUM ZA WIZARA YA AFYA

CHUO CHA TAALUMA ZA SAYANSI ZA AFYA

Mhe. Naibu Spika, Chuo hiki kina jumla ya wanafunzi 588 wa kada mbali

mbali ambao wanaendelea na masomo, kati ya hao wanaume ni 315 na

wanawake ni 273. Aidha wanafunzi 408 (wanawake 242 na wanaume 166)

wanatarajiwa kumaliza masomo yao ifikapo Juni 2013. Katika juhudi za

kukuza viwango vya elimu inayotolewa, chuo kimeweza kupitia mitaala

miwili ya fani za Afisa Tabibu na Afisa Afya ya Jamii na Mazingira. Sanjari

Page 36: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

36

na hilo walimu 11 wamepelekwa masomoni ili kukidhi mahitaji ya elimu

inayotolewa.

Mhe. Naibu Spika, maelezo zaidi juu ya taaluma ya sayansi ya

afya yanapatikana kifungu kumi moja mpaka kumi

moja tano.

Bodi ya Ushauri wa Hospitali Binafsi

Mhe. Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2012/2013 bodi ilifanya ukaguzi

katika hospitali na vituo vya afya 68, kati ya hivyo, vituo vya afya 10

vilisimamishwa kutoa huduma kutokana na uchakavu wa majengo, madaktari

dhamana kutokwenda kikawaida vituoni huko na uhaba wa wafanyakazi

wenye sifa, vituo hivyo vilivyozuiliwa ni Hundi Clinic, Almanac Dispensary,

Mahonda Medical Centre, Mwembemakumbi Dispensary, Huduma

Dispensary, Salama M. Centre,Maryam Clinic, Bububu Dispensary, Kiponda

Medical Clinic na Magogoni Dispensary yaani Huruma, kati ya hizo hospitali

tisa ziliruhusiwa kuendelea kutoa huduma baada ya kurekebisha mapungufu

yaliobainika na kuridhiwa na Bodi.

Mhe. Naibu Spika, kwa mwaka wa fedha uliopita Bodi iliweza kutekeleza

majukumu yake ya kusimamia ubora na usalama wa chakula

a) Kuendelea kufanya mikutano ya pamoja na wamiliki wa

hospitali binafsi ili kuimarisha huduma zinazotolewa na

hospital hizo;

b) Kufanya marekebisho ya sheria na miongozo ya kuendesha

hospitali binafsi;

c) Kuendelea kufanya ukaguzi katika Hospitali na vituo vya afya

binafsi.

Bodi ya Chakula Dawa na Vipodozi

Mhe.Naibu Spika, Bodi imefanya ukaguzi wa maduka 637 ya chakula ya

jumla na rejareja, kati ya 600 yaliyopangwa, maghala saba ya kuhifadhia

chakula, hoteli 129, mikahawa 67, viwanda sita vya chakula, supermarket 6

maduka ya kuuzia nyama 146, maduka 84 ya dawa na 21 ya vipodozi, ghala

moja la kuhifadhia dawa, machinjio tisa, mazao ya baharini kilogram 15.5 na

jumla ya lita 136,243 za maziwa ya ng‟ombe, katika ukaguzi huo, hatua

zilichukuliwa katika kuondoa matatizo yaliyogundulika

Page 37: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

37

Mhe. Naibu Spika, Maabara ya Bodi ya Chakula, Dawa na Vipodozi

ilichunguza jumla ya sampuli 1,045 za Chakula, kati ya sampuli hizo, 1,035

zilikua salama na Sampuli 10 hazikufaa kwa matumizi ya binadamu. Aidha,

Sampuli 25 za dawa zilichunguzwa, Sampuli 16 zilipasi na sampuli tisa

zilifeli. Sampuli 31 za dawa za mitishamba ambazo zote zilionekana zinafaa

kwa matumizi ya binaadamu pia zilichunguzwa.

Mhe. Naibu Spika, hatua mbali mbali zilichukuliwa kwa waliobainika na

kasoro baada ya ukaguzi huo uliofanyika ikiwemo kupewa maelekezo ya kuja

kusajili biashara zao, kupewa muda wa kuweka bidhaa katika mpangilio

mzuri ndani ya maduka, kuhamasisha wafanyakazi kuchunguza afya zao

kutenganisha bidhaa za chakula na vipodozi.

Mhe. Naibu Spika, kwa mwaka wa fedha 2013/2014 Bodi imeanzisha rasmi

ofisi inayoshughulikia Mfumo wa Utoaji wa Huduma Bora (Quality

Management System). Aidha, Bodi imedhamiria kufuata na kutekeleza

miongozo ya kimataifa ya utoaji wa huduma bora kama ilivyoainishwa

kwenye “IS0 900I:2008 na Muongozo wa Huduma kwa wateja (ZFDB

Service Client Charter).

Mhe. Naibu Spika, pamoja na mafanikio hayo lakini Bodi bado inakabiliwa

na changamoto ya kuwepo kwa bandari na njia zisizo rasmi, jambo ambalo

linapelekea kuingizwa kwa bidhaa nchini zilizo chini ya kiwango. Naomba

mamlaka husika na serikali kwa ujumla kulitatua suala hili kwa manufaa ya

wananchi. Kutokana na tabia ya baadhi ya wafanya biashara kuleta bidhaa

zenye kiwango pungufu, bodi imeagizwa kupitia upya sheria ya bodi na

kuleta marekebisho ya mabadiliko yake katika Baraza lako kabla ya

kumalizika kikao hiki cha bajeti.

Mhe. Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2013/2014, Bodi imejipangia

kutekeleza kazi kuu zifuatazo:-

a) Kuendelea kushiriki kikamilifu katika Mpango wa Uwiano wa

Usajili wa Dawa kwa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki;

b) Kujenga Ofisi mpya za Bodi katika eneo la Mombasa Zanzibar;

c) Kusimamia marekebisho ya Sheria ili kuifanya Bodi kuwa

Mamlaka kamili.

Baraza la Wauguzi

Mhe. Naibu Spika, jumla ya wauguzi na wauguzi wasaidizi 71 walisajiliwa

hadi kufikia mwezi Machi 2013 na kupewa leseni za utendaji kazi. Wauguzi

watano waliokwenda kinyume na maadili ya kiuguzi walichukuliwa hatua za

Page 38: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

38

kinidhamu kutokana na makosa mbalimbali ikiwemo kutohudhuria kazini bila

ya kuwa na sababu maalum.

Mhe. Naibu Spika, kwa mwaka 2012/13, Baraza limeifanyia marekebisho

sheria ya Baraza la Wauguzi na Wakunga ya mwaka 1986 baada ya kubainika

mapungufu katika sheria hiyo. Kwa sasa sheria imo katika mchakato wa

kujadiliwa katika vikao mbalimbali.

Mhe. Naibu Spika, katika kipindi cha mwaka 2013/2014 Baraza limejipangia

kutekeleza yafuatayo:-

a) Kutayarisha miongozo mbali mbali ya utoaji wa huduma za

uuguzi na ukunga;

b) Kukamilisha marekebisho ya sheria ya Baraza la Wauguzi na

Wakunga;

c) Kusaidia katika mchakato wa kuanzisha Jumuiya ya Wakunga

Zanzibar.

Baraza la Tiba Asili na Tiba Mbadala

Mhe. Naibu Spika, kazi zilizofanyika kwa kipindi cha mwaka 2012/2013 ni

usajili na ukaguzi wa maduka 30 ya dawa za tiba asili na mbadala Pia

waganga 153, kliniki 10, (nane kwa Unguja na mbili Pemba), wasaidizi

waganga 38 na vilinge 92 vilifanyiwa usajili.

Mhe. Naibu Spika, wizara imekuwa ikifanya ufuatiliaji wa karibu katika

kuona sekta hii haiendi kinyume na matakwa ya sheria. Hivyo waganga wa

jadi na ambao sio waganga na wale ambao hawakufuata sheria za uuzaji wa

dawa za asili walidhibitiwa kwa kushirikiana na askari polisi pamoja na

vyombo vya habari ili kubainisha taarifa zao. Hatua nyengine zilizochukuliwa

ni kuziteketeza dawa hizo na kudhibiti matangazo ambayo yapo kinyume na

taratibu za Baraza. Aidha, hatua pia zilichukuliwa kwa wale walioonekana

kuuza dawa katika sehemu za miskiti, barabarani na sehemu ambazo

hazikubaliki na baraza hivyo ukaguzi wa mara kwa mara ulifanyika.

Mhe. Naibu Spika, kwa mwaka wa fedha 2013/2014 kazi kuu zifuatazo

zitatekelezwa na Baraza.

a) Kuendelea kuelimisha jamii juu ya umuhimu wa tiba asili na

utumiaji mbaya wa dawa za tiba asili na tiba mbadala kwa baadhi ya

waganga kupitia vyombo vya habari na vipeperushi;

b) Kujenga uhusiano mzuri kati ya madaktari wakisasa

(Biomedical Practitioners) na waganga wa asili (Traditional healers);

c) Kuendelea kusajili waganga wa tiba asili pamoja, maduka na

vituo vya afya vya tiba asili na mbadala;

Page 39: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

39

d) kuendelea kufanya ukaguzi wa waganga wa tiba asili na

wauzaji wa dawa misikitini.

Maabara ya Afya ya Jamii – Pemba

Mhe. Naibu Spika, maabara ya Afya ya Jamii (P H L – I d C) ni Taasisi

inayohusika na kufanya tafiti pamoja na kufanya uchunguzi yakinifu wa

sampuli kutoka maabara mbali mbali za hapa nchini. Pia, maabara hii

huangalia nyendo za maradhi mbali mbali yanayoathiri afya ya jamii na

kubuni mbinu za kuyadhibiti. Katika mwaka 2012-13 maabara ilipokea

sampuli 156 (101 Unguja na 55 Pemba) za makohozi na kuzifanyia uhakiki.

Kati ya hizo sampuli 30 (23 kutoka Unguja na 7 Pemba) zilionekana

kuambukizwa na kifua kikuu.

Mhe. Naibu Spika, mafanikio mengine yaliyopatikana ni kuanza kufanya

kipimo cha kuotesha vidudu na kuangalia dawa mjarabu kwa vidudu (Culture

and Sensitivity) kwa sampuli za hospitali kama vile choo kikubwa, mkojo,

damu, CSF, HVS na nyenginezo.

Mhe. Naibu Spika, kwa upande wa hudumia za akinamama wajawazito na

watoto wachanga (Cord care and Pregnant Study), jumla ya watoto wachanga

23,202 wamepatiwa huduma stahiki. Vile vile jumla ya akina mama

wajawazito 2,064 walitambuliwa. Kati ya hao 1,767 wameshaorodheshwa

tayari kwa kupatiwa huduma zikiwemo kupima mapigo ya moyo (BP) na

mkojo mara tatu kabla ya kujifungua na mara mbili baada ya kujifungua.

Mhe. Naibu Spika, napenda kuliarifu baraza lako tukufu kuwa maabara hii pia

inasaidia kutoa mchango mkubwa katika kuwapatia ajira vijana wetu kwani

mbali ya kada muhimu zilizomo ndani ya maabara hii ambao ni wafanyakazi

waliomo ndani ya wizara ya afya maabara pia hutoa ajira za muda mfupi na

muda mrefu. hadi sasa jumla ya wafanyakazi tisini 90 wanafanya kazi katika

mabara hii. Halikadhalika zaidi ya wanawake 80 kutoka shehia zote za Pemba

wameshafanyiwa usaili.

Mhe. Naibu Spika, kwa mwaka ujao wa fedha maabara itaendelea kufanya

utafiti kuhusiana na kichocho utakaohusiana na DNA, kuenedelea na utafiti

wa minyoo ikiwemo kupima ubora wa dawa mbali mbali zitakazoweza kuwa

bora zaidi kwa kutibu maradhi hayo.

MIRADI YA MAENDELEO

Mradi wa Kusaidia Kupunguza Vifo Vitokanavyo na Uzazi

Page 40: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

40

Mhe. Naibu Spika, mafanikio yaliyopatikana kwa mradi huu kwa mwaka

2012/2013 ni pamoja na kukamilika kwa matengenezo ya Kituo cha Afya cha

Bogoa na kuanza matengenezo ya Kituo cha Afya Wesha.

Mheshimiwa Spika, mradi umewapatia mafunzo ya muda mfupi hapa nchini

wafanyakazi 95 juu ya “Community Participation in Health” na wafanyakazi

50 kwa mafunzo ya “Emerging Health Problems and Medical Procedures”.

Mafunzo haya yaliwashirikisha wafanyakazi kutoka vituo vya afya na

hospitali za vijiji.

Mhe. Naibu Spika, katika baraza lako la mwaka 2012/2013 wizara yangu

ilitoa taarifa ya maendeleo mazuri yanayoendelea kwenye ujenzi wa jengo la

wagonjwa wa Akili liliopo Hospitali ya Wete Pemba na kujenga matumaini

ya kukabidhiwa jengo baada ya miezi mitatu. Bahati nzuri wakati ujenzi

ukiendelea ilionekana kasoro ya kutokuwepo eneo la kutolea huduma za kazi

za “Occupational Therapy”, hali hii ilisababisha hatua za haraka kuchukuliwa

kwa kufanya marekebisho yanayostahiki. Kwa hivi sasa ujenzi unaendelea

na unatarajiwa kumalizika wakati wowote kuanzia hivi sasa.

Mheshimiwa Spika, kwa kipindi cha mwaka 2013/2014 mradi utakamilisha

majukumu yafuatayo:-

a) Kufanya matengenezo makubwa ya jengo la huduma za uzazi

na watoto katika hospitali ya Wete pamoja na kulipatia vifaa na

samani;

b) Kulipatia vifaa na samani jengo la huduma za magonjwa ya

Akili Pemba baada ya ujenzi kukamilika;

c) Kujenga vituo vya afya na nyumba za wafanyakazi

Mzambarauni Pemba na Mwera Unguja pamoja na kuvipatia

vifaa;

d) Kufanya matengenezo ya vituo vya afya Wingwi na Tundaua;

e) Kugharamia mafunzo ya muda mfupi kwa wafanyakazi sita wa

mradi;

f) Kufanya tathmini ya mwisho na kufunga mradi.

Mradi Shirikishi wa Afya ya Uzazi na Mtoto

Mheshimiwa Spika, kwa mwaka wa fedha 2012/ 2013, mradi uliweza kufanya

utafiti mdogo juu ya upatikanaji wa huduma za dharura za uzazi (EmONC

assessment) katika vituo 79 Unguja na Pemba. Lengo ni kuziimarisha huduma

katika vituo vyote vya afya ili mama wajawazito waweze kuzifikia huduma

hizo kiurahisi. Utafiti huo utasaidia katika kuwa na mipango madhubuti yenye

muelekeo katika kuimarisha huduma za uzazi.

Page 41: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

41

Mhe. Naibu Spika, jumla ya watoa huduma 80 Unguja na Pemba wamepatiwa

mafunzo ya utoaji wa huduma za uzazi wa mpangilio ya nadharia na vitendo,

jumla ya vipandikizi 2,752 vimenunuliwa na kusambazwa kwenye vituo na

hospitali kwa lengo la kurahisisha watendaji kuyatumia mafunzo hayo

kivitendo. Mafunzo mengine yaliyotolewa yalihusu namna ya kutoa huduma

za haraka kwa mtoto mchanga (Neonatal Resuscitation), kwa wafanyakazi 25

kwa kila wilaya. Mafunzo haya yalikwenda sambamba na ununuaji wa vifaa

(newborn resuscitation kits & suction machines) kwa ajili ya huduma hizo.

Mhe. Naibu Spika, mapitio ya mpango wa kuharakisha kupunguza vifo

vitokanavyo na uzazi na watoto (Road Map Review) ulifanyika. Ripoti ya

mapitio inaonesha kwamba kuna mafanikio na changamoto. Miongoni mwa

mafaniko yaliopatikana ni kupungua kwa vifo vitokanavyo na uzazi kutoka

vifo 285 kwa kila vizazi hai 100,000 mwaka 2011 hadi kufikia vifo 221 kwa

kila vizazi hai 100,000 mwaka 2012.

Mhe. Naibu Spika, kwa upande wa changamoto zilizojitokeza katika mapitio

hayo imegundulika kwamba mkakati huu haukusambazwa ipasavyo hasa

katika ngazi za chini; ikiwemo ngazi ya wilaya, vituo vya afya na ngazi ya

jamii, na hata usimamizi wake haukufikia kiwango kilichokusudiwa ingawa

jitihada zilitumika kuhakikisha utekelezaji wake unakuwa mzuri.

Mhe. Naibu Spika, Ujenzi wa Jengo la ofisi ya kitengo shirikishi unaendelea

kwa kasi, na linatarajiwa kumalizika mwanzoni mwa mwaka wa fedha

2013/2014. Jengo hili linategemewa kufunguliwa Rasmi wakati wa

maadhimisho ya miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar. Aidha, gari mbili za

kubebea wagonjwa (Ambulances) zilinunuliwa kwa ajili ya hospitali ya Wete

na Makunduchi.

Mhe. Naibu Spika, mafunzo ya matibabu ya magonjwa ya watoto kwa njia ya

uwiano “Integrated Management of Childhood Ilnesses (IMCI)” kwa njia ya

elimu masafa kwa wahudumu kumi na tisa kutoka vituo mbali mbali vya

Unguja na Pemba yametolewa. Ufuatiliaji baada ya mafunzo hayo ulifanyika

katika vituo 17 kwa Unguja na 11 kwa Pemba. Vile vile mafunzo ya IMCI

kwa njia ya elimu masafa (e- Learning) yalitolewa kwa walimu (Training Of

Trainers) 15 wa Chuo cha Sayansi za Afya pia mafunzo msasa ya IMCI

yalitolewa kwa watendaji 33 kutoka wilaya ya kati.

Mhe. Naibu Spika, hadi kufikia sasa jumla ya vituo 137 vinatoa huduma za

kuzuia maambukizi ya VVU kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto, kati ya

hivyo, vituo 64 vipo Pemba na 73 Unguja. Katika mwaka 2012, akina mama

wajawazito 46,221 walipatiwa ushauri nasaha na kupimwa afya zao. Kati ya

hao kina mama 281 sawa na asilimia 0.6 waligunduliwa kuwa na

Page 42: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

42

maambukizo ya VVU. Halikadhalika kati ya watoto 148 waliochunguzwa

watoto saba waligunduliwa na maambukizo ya VVU sawa na asilimia 4.7%.

Huduma za Chanjo

Mhe. Naibu Spika, kwa mwaka 2012/2013 kiwango cha chanjo kitaifa

kimeshuka kutoka asilimia 96 ya mwaka 2011 hadi kufikia asilimia 90 ya

mwaka 2012. Kupungua kwa kiwango hiki kitaifa kumechangiwa sana na

kushuka kwa kiwango cha chanjo katika Wilaya za Mkoani, Chake Chake,

Micheweni, Kaskazini “A‟ na Kaskazini “B”, wilaya ambazo zilichanja chini

ya asilimia 80. Pia ufinyu wa fedha za kuendeshea kazi za chanjo, ufuatiliaji

mdogo wa kazi za chanjo na matatizo ya upatikanaji wa umeme (TUKUZA)

kwa vituo vya Afya vya Pemba ni sehemu ya changamoto iliyoshusha chanjo.

Ufafanuzi unaonekana katika kiambatanisho namba 15.

Mhe. Naibu Spika, napenda kuliarifu Baraza lako tukufu kwamba, katika

kukabiliana na maradhi yanayozuilika kwa chanjo, wizara imefanikiwa

kuanzisha chanjo mbili mpya za “Rotavirus” ambayo inakinga maradhi ya

kuharisha na „Pneumococcal‟ yenye kukinga maradhi ya homa ya kichomi na

ya uti wa mgongo. Hivyo katika kufanikisha utowaji wa chanjo hizo, jamii

pamoja na watoa huduma wa afya walihamasishwa ili kuzielewa na hatimae

kuzikubali chanjo hizo.

Mhe. Naibu Spika, katika kuhakikisha kuwepo kwa uhifadhi mzuri wa chanjo

unaokubalika, wizara imeanza kufanya matayarisho ya ujenzi wa chumba cha

mtambo wa baridi huko Pemba. Mchoro na ramani ya ujenzi huo tayari

imeshaandaliwa, zabuni imeshatangazwa, kutathiminiwa na mkandarasi

ameshachaguliwa. Ujenzi huu utagharamiwa kwa mashirikiano baina ya

Serikali na Shirika la kimataifa la kuhudumia watoto (UNICEF).

Mhe. Naibu Spika, kwa mwaka wa fedha 2013/2014 mradi huu unalenga

kutekeleza kazi kuu zifuatazo:

a) Kufanya uhamasishaji na kujenga uwezo juu ya huduma za uzazi,

maambukizi ya virusi vya UKIMWI kwa mama wajawazito, uzazi wa

mpangilio na huduma rafiki kwa vijana Unguja na Pemba;

b) Kuimarisha mfumo wa mawasiliano wa huduma za afya ya uzazi kwa

kina mama wajawazito na watendaji wa afya kwavituo vyote vya afya;

c) Kufanya mafunzo kwa wahudumu wa afya juu ya huduma za afya ya

uzazi na mtoto ikiwa ni pamoja na huduma za uzazi za dharura (EmOC)

na huduma za chanjo;

Page 43: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

43

d) Kununua dawa za uzazi wa mpangilio pamoja na ununuzi wa chanjo na

vifaa vyake. Kutoa chanjo ya pepopunda katika skuli za Sekondari

Unguja na Pemba;

e) Kufanya tafiti zinazohusiana na masuala ya chanjo (Operational

research);

f) Kufanya Uhakiki wa takwimu za chanjo (DQS);

g) Kukamilisha kuchapisha na kusambaza muongozo wa utoaji huduma za

chajo kwa wachanjaji;

h) Kuanzisha dozi ya pili ya chanjo ya surua (measles second dose) na

kutoa chanjo nyengine za kawaida.

i) Kutoa mafunzo juu ya Matibabu ya Watoto wachanga na maradhi ya

kuharisha kwa watoa huduma za watoto kwa Pemba.

j) Kuanzisha mikakati ya kuondoa kabisa maambukizi ya VVU kwenda

kwa mtoto.

Mradi Shirikishi wa Ukimwi, Kifua Kikuu na Ukoma

Mhe. Naibu Spika, Mradi Shirikishi wa UKIMWI, Kifua Kikuu na Ukoma ni

muunganisho wa miradi miwili yote yenye lengo la kusimamia, kuratibu na

kutoa huduma za tiba na kinga dhidi ya maambukizo ya UKIMWI, kifua

kikuu na Ukoma.

Mhe. Naibu Spika, kwa mwaka wa fedha 2012/2013, wizara ilifanya utafiti

wa kutathmini mwenendo wa maambukizo ya VVU kwa makundi matatu

hatarishi; wanaume wanaojamiiana (MSM), wanawake wanaofanya biashara

ya ngono (FSW) na watumiaji wa dawa za kulevya kwa kujidunga sindano

(IDUs) pamoja na kujua idadi yao kwa kila kundi (size estimation). Matokeo

ya awali ukilinganisha na mwaka 2007 yanaonyesha kwamba hali ya

maambukizo ya VVU kwa wanaume wanaojamiiana yamepungua kutoka

asilimia 12.3 (2007) hadi asilimia 2.6 (2012), wanaojidunga sindano za

madawa ya kulevya yamepungua kutoka asilimia16 (2007) hadi asilimia 11.3

(2012). Aidha, wanawake wanaofanya biashara ya ngono maambukizi

yameonekana kupanda kutoka 10.8 (2007) hadi asilimia 19.3 (2012).

Mhe. Naibu Spika, katika kufikia lengo la kuwapatia dawa za kupunguza

makali ya VVU (ARV) bila malipo kwa watu wanaoishi na VVU, hadi kufikia

Machi 2013 jumla ya watu 6,906 wanaoishi na VVU walikuwa tayari

wameshasajiliwa kwenye kliniki 10 (6 Unguja na 4 Pemba), miongoni mwao,

watu 4,090 (59.2%) wanatumia dawa za ARVs, kati yao watoto ni

392(9.6%).

Mhe. Naibu Spika, ili kuimarisha huduma za tiba katika maabara zinazotoa

huduma za uchunguzi wa UKIMWI, mradi ulipokea mashine tatu mpya za

Page 44: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

44

CD4 ambazo zimepelekwa katika Hospitali ya Mnazi Mmoja, Mwembeladu

na Kivunge. Aidha mashine aina mbili za “Haematology na Chemistry”

zilipokelewa na kupelekwa katika hospitali za Micheweni, Makunduchi na

Mwembeladu.

Mhe. Naibu Spika, kwa mwaka wa fedha 2012/13, mradi huu ulifanya

ufuatiliaji na kubaini kasoro mbali mbali za kiutendaji katika baadhi ya

hospitali zinazotoa huduma ya tiba ya UKIMWI. Hali hiyo ilipelekea mradi

kufanya mafunzo maalum ya vitendo ya siku mbili yaliyohusu Ushauri juu ya

ufuasi wa dawa na Ujazwaji wa Madaftari na ripoti za robo mwaka. Kliniki

ambazo watendaji wake walipata mafunzo haya ni Al – Rahma, Kivunge,

Makunduchi kwa Unguja, na Micheweni na Mkoani kwa Pemba.

Mhe. Naibu Spika, moja ya lengo la mradi huu kwa mwaka wa fedha

2012/2013 ilikuwa ni kuanzisha huduma ya chanjo ya kujikinga na

maambukizi ya homa ya ini aina ya “B” (Hepatitis B Vaccine) kwa watu

wanaoishi na VVU. Azma hii imeanza kutekelezwa kwa kutoa chanjo hiyo

kwa kundi la wanaotumia madawa ya kulevya kwa njia ya kujidunga sindano

na wale walioko katika utafiti wa maradhi hayo katika kliniki ya Mnazi

Mmoja.

Mhe. Naibu Spika, chanjo hizo zimetolewa katika nyumba sita (6) kati ya

saba (7) maalum za kurekebisha tabia (sober houses) zilizopo Unguja.

Takwimu zinaonyesha kuwa jumla ya watu 233 waliopimwa katika nyumba

hizo 221 (95%) hawakugundulika na virusi vya homa ya ini “B”na hivyo

wanastahiki kupatiwa chanjo ya homa hiyo, miongoni mwao watu 59 (27%)

walipata angalau dozi moja, 40 (18%) walikamilisha dozi mbili na watu 30

(14%) tu ndio walioweza kukamilisha dozi tatu za chanjo hiyo. Hii ni

kutokana na ugumu uliojitokeza wa kuwafikia watu hao.

Mhe. Naibu Spika, kwa wale wanaofanyiwa utafiti katika kliniki ya huduma

na Tiba ya UKIMWI katika hospitali ya Mnazi Mmoja, jumla ya wagonjwa

1,571 wameshaorodheshwa katika utafiti huo. Kati yao watu 558

wameshapata chanjo ya kujikinga na ugonjwa huo na 56 ambao

wamegunduliwa na ugonjwa wa homa ya Ini B walianzishiwa dawa.

Mhe. Naibu Spika, moja ya mkakati wa kupambana na maradhi haya thakili

ni kuhimiza utumiaji wa mipira ya baba wakati wa kujamiiana. Katika

kuhakikisha kuwa wahitaji wanapata mipira hiyo bila malipo, mradi

umesambaza jumla ya mipira ya baba 34,700 katika vituo vya Afya,

waelimishaji rika, hotelini, majumba ya starehe pamoja na jumuiya zisizo za

Serikali (NGOs).

Page 45: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

45

Mhe. Naibu Spika, kwa upande wa huduma za Kifua Kikuu, jumla ya watu

280 waligunduliwa kuwa na maradhi hayo, kati yao 243 (86.8%) walitibiwa

na kupona. Wanaume 172 (61.43%) na Wanawake 108 (38.57%). Vile vile

huduma za ufuatiliaji majumbani zilifanyika kwa wagonjwa 18. Aidha watu

169 ambao ni jamaa wa wagonjwa hao pia walipatiwa elimu juu ya namna ya

kujikinga. Katika nyumba hizo 18 kumepatikana watoto 21 ambao

wameanzishwa dawa za kuwakinga dhidi ya ugonjwa wa kifua kikuu kwa

kipindi cha miezi sita. Pia wakati wa zoezi hili vipeperushi 367 vimegawiwa

kwa watu waliopatiwa elimu.

Mhe. Naibu Spika, kwa upande wa huduma za maradhi ya ukoma jumla ya

watu 97 waligundulika na maradhi haya (wanawake 32 na wanaume 65), kati

yao wagonjwa sita walikuwa na ulemavu grade 2. Aidha, ununuzi wa vifaa

vya kutengenezea miguu bandia na kiatu chake ulifanyika kwa walioathirika

na Ukoma. Aidha jumla ya watu 169 ambao ni jamaa wa wagonjwa

walipatiwa elimu ya afya juu ya maradhi hayo.

Mhe. Naibu Spika, mkakati mwengine unaotumika katika kupambana dhidi

ya maradhi haya ni kuelimisha jamii namna ya magonjwa haya

yanavyoambukizika na njia za kujikinga. Kwa mwaka 2012/13, jumla ya

vipeperushi 32,531 vimechapishwa kwa ajili ya kuelimisha jamii, kati ya

hivyo, 10,000 – vinalenga katika kushajiisha jamii juu ya umuhimu wa

kupima kabla ya ndoa na vipeperushi 20,000 vinahusu Huduma ya ushauri

nasaha na upimaji kwa wagonjwa wanaofika vituo vya afya na hospitali na

vipeperushi 2,531 vilihusu kujinga na maradhi ya kifua kikuu na ukoma. Pia

vipindi saba vya Televisheni na redio vilirushwa heweani.

Mhe. Naibu Spika, licha ya juhudi zinazoendelea kuchukuliwa na Wizara ya

Afya, bado suala la UKIMWI ni tatizo, hivyo juhudi makhsusi za pamoja

zinahitajika katika kupambana na maradhi haya thakili. Mkazo zaidi

unatakiwa katika kuondosha unyanyapaa kwa wanaoishi na VVU/UKIMWI,

kupiga vita imani potofu juu ya mipira ya baba au mama (kondomu),

kuongezeka kwa waganga wanaowashawishi wagonjwa kutumia dawa za

kienyeji badala ya ARVs na changamoto za kutoa huduma za tiba kwa

makundi maalum.

Mhe. Naibu Spika, kwa mwaka wa fedha 2013/14 mradi huu umeazimia

kutekeleza kazi kuu zifuatazo:

a) Kuendelea kuimarisha tiba na ushauri kwa kuwapatia dawa za kupunguza

makali ya VVU (ARV) kwa watu wanaoishi na VVU bila malipo kwa

wananchi wote wanaostahiki kutoka asilimia 60% mwaka 2013 kufikia

asilimia 65 mwaka 2014;

Page 46: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

46

b) Kuimarisha na kuongeza huduma za ushauri nasaha na upimaji kutoka

vituo 87 mwaka 2013 kufikia 100 mwaka 2014 na kuhakikisha nyenzo

na vifaa vinapatikana kwa wakati;

c) Kuendelea kuimarisha tiba na ushauri kwa kuwapatia dawa za

kupunguza makali ya VVU (ARV) kwa watu wanaoishi na VVU bila

malipo kwa wananchi wote wanaostahiki kutoka asilimia asilimia 60%

2013 kufikia asilimia 65% mwaka 2014;

d) Kuendelea kutoa taaluma zaidi ya maradhi ya UKIMWI kwa watendaji

wa afya wa Unguja na Pemba katika sehemu zao za kazi (mentor

couching) kuhusiana na tiba kwa kutumia dawa za ARV, uzuiaji wa

maambukizo ya mama kwenda kwa mtoto (PMTCT) na ushauri nasaha wa

kujikubalisha matumizi ya dawa (adherence counseling) na kuwahudumia

makundi maalum;

e) Kupanua huduma na tiba kwa makundi maalum ili kuwapatia huduma za

karibu na bora makundi hatarishi ya kuambukizwa na VVU;

f) Kuendelea kushirikiana na Idara ya madawa ya Kulevya na kurekebisha

tabia kuanzisha utoaji wa huduma na tiba na kuwapatia dawa kwa

watumiaji 200 wa madawa ya kulevya;

g) Kutekeleza mpango wa tiba kama kinga kwa baadhi ya makundi ya watu

watakaogundulika na VVU (watu wa makundi maalum, mama wajawazito,

watakaogundulika ya kuwa na VVU na homa ya ini pamoja na wenza);

h) Kufanya ukaguzi wa huduma za ushauri na upimaji wa VVU na kwa kwa

huduma za wagonjwa wanaolazwa na wanaotibiwa katika hospitali ( PITC na

VCT).

Mradi wa Kuipandisha Hadhi Hospitali ya Mnazi Mmoja kuwa ya Rufaa

Mhe. Naibu Spika, mradi huu unalenga katika kuipandisha hadhi hospitali hii

kuwa ya Rufaa kwa Zanzibar, ambapo itatoa huduma za rufaa zitakazo

kwenda sambamba na mpango mkakati wa hospitali hii. Huduma hizo ni

pamoja na kuongeza miundo mbinu, wataalamu (specialist) na huduma za

kitalaamu kama vile upasuaji wa moyo (cardioverscular surgery), upasuaji

wa maradhi ya mgongo na ubongo (neurosurgical services), na huduma za

maradhi ya figo (Dialysis).

Mhe. Naibu Spika, katika mwaka wa bajeti 2012/13, wizara iliazimia kuanza

matayarisho ya zabuni kwa ajili ya kuanza kutekeleza mradi wa kuipanua

hospitali hii kwa mashirikiano na Uholanzi. Napenda kuliarifu Baraza lako

tukufu kuwa siku ya tarehe 18/2/2013 Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na

Serikali ya Uholanzi ziliwekeana saini mkataba wa makubaliano wa kuanza

kuutekeleza mpango kazi wa mradi huo. Aidha hatua za awali za matayarisho

ya utekelezaji wa mpango mkakati huo umeshaanza.

Page 47: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

47

Mhe. Naibu Spika, miongoni mwa mambo muhimu yaliomo katika mradi huu

ni ujenzi wa kliniki za maradhi maalumu zitakazo endeshwa na madaktari

bingwa, wodi ya kina mama ya kujifungulia na baada ya kujifungua na

chumba cha huduma za dharura (Emergency Units/casuality). Eneo

lilotengwa kwa ajili ya ujenzi huu ni katika majengo ya zamani ya kiwanda

cha dawa. Sambamba na hilo ukarabati wa jengo la Mapinduzi mpya

unaendelea na uko katika hatua za mwisho.

Mhe. Naibu Spika, uchache wa upatikanaji wa fedha za maendeleo umeathiri

zaidi utekelezaji wa shughuli za mradi huo, ambapo hadi sasa idara

imeshindwa kununua tanuri la kuchomea takataka kifaa ambacho ni muhimu

sana katika kufanikisha usafi na ubora wa huduma. Hata hivyo, wizara

imepata fedha kutoka mfuko wa msamaha wa madeni wa Kimataifa (MDRI)

fedha ambazo zitatumika kwa ajili ya ununuzi wa tanuri la kuchomea taka

(incinarator), mobile X-ray,na vifaa vya uchunguzi wa saratani. Zabuni kwa

ajili ya ununuzi huo imeshatangazwa.

Mhe. Naibu Spika, kwa mwaka wa fedha 2013/2014, mradi huu umejipangia

kutekeleza kazi kuu zifuatazo:-

a) Kutekeleza mradi wa ORIO;

b) Kujenga jengo litakalotoa huduma za maradhi ya figo (Dialysis);

c) Kujenga jengo la wodi ya watoto;

d) Kujenga jengo litakalotoa huduma za upasuaji wa maradhi ya mgongo na

ubongo (neurosurgical services) ambalo litajumuisha chumba cha upasuaji

(theatre), chumba cha wagonjwa mahututi (ICU), klinik pamoja na wodi;

e) Kuendelea kuwapatia wafanyakazi mafunzo ya matibabu kwa huduma

mpya zinazotaka kuanzishwa kama vile kansa na mafigo (Dialysis);

f) Kufanya matengenezo ya miundo mbinu na ununuzi wa vifaa tiba.

Mradi wa Kudhibiti Malaria Zanzibar

Mhe. Naibu Spika, mradi huu unalenga katika kutoa huduma za kinga na tiba

dhidi ya ugonjwa wa malaria. Juhudi mbali mbali zinazotumika katika

kutokomeza ugonjwa huu ni pamoja na kuanzisha kampeni ya Maliza Malaria

Zanzibar ambayo imepelekea mafanikio makubwa katika nchi yetu.

Mhe. Naibu Spika, kazi za ufuatiliaji na ukaguzi zilifanyika katika vituo vya

afya 142 Unguja na Pemba kati ya 202 vilivyopangwa kukaguliwa,

(vikiwemo vya serikali na binafsi) kwa lengo la ukaguzi huu ni kuangalia

zaidi namna ya uchunguzi na matibabu ya malaria yanavyotolewa kwa

kuzingatia miongozo iliyokubalika.

Page 48: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

48

Mhe. Naibu Spika, napenda kuliarifu baraza lako tukufu kuwa katika kipindi

cha Julai 2012 hadi Machi 2013, hali ya upatikanaji wa dawa za malaria kwa

wagonjwa waliogundulika kuwa na malaria ulikuwa ni mzuri na hakukuwa na

upungufu wa dawa hizo. Wagonjwa wengi waliopatiwa huduma hiyo

waliweza kutumia dawa hizo bila ya kuwaletea madhara ya aina yoyote

isipokuwa wagonjwa 17 tu waliripotiwa kupata matatizo madogo madogo

kama vile matatizo ya ngozi, kuhara na kutapika, matatizo ambayo hayakuwa

na uhusiano na dawa za malaria.

Mhe. Naibu Spika, upigaji wa dawa ya majumbani kwa maeneo maalum ya

wilaya za Magharibi, Kati, Kusini, Chake Chake, Wete, Mkoani na

Micheweni, ambayo yalibainika kuwa na maambukizi ya ugonjwa wa

malaria. Katika zoezi hili jumla ya nyumba 28,463 zilipangiwa kupigwa

dawa, kati ya hizo nyumba 26,900 sawa na asilimia 94.5 zilifanikiwa kupigwa

dawa. Haya ni mafanikio makubwa ya zoezi hili, ambapo Shirika la Afya

duniani linasisisitiza angalau asilimia 80 ya nyumba zote ziwe zimepigwa

dawa.

Mhe.Naibu Spika, katika kuangalia uimara wa dawa za majumbani dhidi ya

mbu wanaoambukiza malaria, aina tano za dawa za majumbani zilifanyiwa

uchunguzi, ili kubaini uwezo wake wa kuuwa mbu wa malaria. Dawa

zenyewe ni Bendiocarb, permethrine, deltamethrine, DDT, na labda

cyhalothrine. Aidha dawa aina ya Bendiocarb, pyrethroids na DDT

zimeonesha kuwa na nguvu kubwa kabisa ya kuangamiza mbu wa malaria,

hata hivyo tahadhari zinahitajika ili kuweza kulinda nguvu ya dawa hizo.

Dawa za permethrine na deltamethrine zilionesha kuwa na nguvu ndogo ya

kuuwa mbu wa malaria. Kwa sasa dawa inayoendelea kutumiwa ni aina ya

Bendiocarb.

Mhe. Naibu Spika, shughuli za uchunguzi wa malaria ziliendelea kama

kawaida ambapo jumla ya watu 71,584 walichunguzwa damu kwa njia ya

darubini miongoni mwao, 213 sawa na asilimia 0.31 waligunduliwa kuwa na

vimelea vya malaria. Kwa upande wa uchunguzi kwa njia ya haraka (mRDT),

jumla ya wagonjwa 72,591 walichunguzwa malaria kwenye vituo tofauti

Unguja na Pemba, kati ya hao wagonjwa 321 (0.44%) waligundulika kuwa na

vimelea vya maradhi hayo.

Mhe. Naibu Spika, mfumo wa ukusanyaji wa taarifa za malaria, kupitia simu

za mkononi umesaidia kuweza kuwafuata wagonjwa wa malaria katika

sehemu wanazoishi mara tu taarifa hizo zinapofika sehemu husika. Kwa

kipindi cha bajeti hii jumla ya wagonjwa 370 waliripotiwa. Ufuatiliaji

ulibainisha kuwa asilimia 38 walikuwa na kumbukumbu za kusafiri nje ya

Zanzibar katika kipindi cha mwezi uliopita. Hali hii inaonesha kuwepo

Page 49: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

49

umuhimu wa kuwachunguza wageni wanaoingia Zanzibar kupitia baharini na

angani. Ufuatiliaji pia ulifanyika kwa familia zilizoripotiwa kuwa na

wagonjwa, hivyo watu 1,385 walichunguzwa, kati yao 69 walionekana kuwa

na vimelea sawa na asilimia tano na kupatiwa tiba sahihi kwa wakati.

Mhe. Naibu Spika, kazi za kufuatilia mwenendo wa mbu waenezao ugonjwa

wa malaria katika maeneo teule (sentinel sites) Unguja na Pemba ilifanyika.

Kwa upande wa Unguja maeneo yaliyo husika ni Mwera Chaani Bumbwini

na Malindi. Kwa Pemba ni Bopwe, Vitongoji Uwandani na Tumbe.

Mhe. Naibu Spika, matokeo kwa ujumla yanaonesha kuwa idadi ya mbu wa

malaria wamepungua ukilinganisha na miaka ya nyuma kabla ya upigaji dawa

wa majumbani na ugawaji vyandarua. Hata hivyo tabia ya mbu inaonekana

kubadilika ambapo inakisiwa asilimia 70 ya mbu hao wanauma nje usiku wa

mapema kuanzia saa moja mpaka saa tano, kipindi ambacho wananchi wengi

wanakuwa nje wakiongea au kujipumzisha, Kutokana na changamoto hii njia

za ziada za kumaliza malaria zinahitajika zikiwemo za kuangamiza viluilui

katika maeneo yenye madimbwi na mabonde ya maji.

Mhe. Naibu Spika, kwa mwaka 2013/2014, mradi umejipangia kutekeleza

kazi kuu zituatazo:-

a) Kuchunguza uimara wa dawa za safu ya kwanza ya kutibu

malaria (dawa za mchanganyiko);

b) Kuendelea kufuatilia mwenendo wa maradhi ya malaria kwa

kufanya tafiti zitakazojitokeza ambazo zitakazopelekea kuleta maamuzi

yatakayosaidia kuendeleza mbele kampeni ya maliza malaria Zanzibar;

c) Ugawaji wa vyandarua katika mpango endelevu;

d) Kuangalia uimara wa viuwatilifu (Chemicals) dhidi ya mbu

wanaoneza malaria.

Mradi wa Ujenzi wa Bohari Kuu ya Dawa

Mhe. Naibu Spika, mradi wa Ujenzi wa Bohari Kuu ya Dawa una lengo la

kuwa na ghala kubwa na la kisasa ambalo litakuwa na uwezo mkubwa wa

kuhifadhi dawa kwa ajili ya hospitali na vituo vya afya Unguja na Pemba.

Mhe. Naibu Spika, kama nilivyoeleza katika hotuba ya mwaka wa fedha

2012/2013 kuwa wizara ilikuwa inajenga jengo kwa ajili ya Bohari kuu ya

Dawa. Napenda kuliarifu Baraza lako tukufu kwamba jengo hilo limemalizika

na kufunguliwa rasmi na Mhe. Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la

Mapinduzi Dr. Ali Mohamed Shein siku ya tarehe 6/01/2013. Kupatikana kwa

ghala hii kumewezesha uhifadhi wa dawa na vifaa tiba kuwa ni wa uhakika na

Page 50: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

50

salama, kwani ghala hili limewekewa mitambo maalum wa kutambua

ubadhirifu wowote ambao unaweza kutokea.

Mhe. Naibu Spika, mambo mengine yaliyofanywa katika kuimarisha ghala hii

ni pamoja na ununuzi wa samani za ofisi, kompyuta, folk-lift pamoja na

jenereta kubwa na jipya la kusambazia umeme wakati wa dharura. Sambamba

na hilo, ujenzi wa kantini kwa huduma za vyakula utakamilika wakati wowote

kuanzia hivi sasa.

Mhe. Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2013/2014 mradi umejipangia

kutekeleza kazi kuu zifuatazo:-

a) Kujenga Bohari Kuu ya Dawa Pemba;

b) Kununua gari kwa ajili ya usambazaji wa dawa na ukaguzi;

c) Kuongezwa kwa folk-lift, kwani mpaka sasa ipo moja tu.

Mradi wa Kustawisha Siha za Wazanzibari

Mhe. Naibu Spika, mradi huu unalenga kuhamasisha jamii juu ya masuala

yanayohusu afya ili waweze kujikinga na maradhi yakiwemo ya kuambukiza

na yasiyo ya kuambukiza pamoja na mambo hatarishi.

Mhe. Naibu Spika, kwa mwaka wa fedha 2012/2013, jumla ya vipindi 81

vimetangazwa kupitia redio na televisheni vyenye nia ya kuhamasisha jamii

katika masuala mbali ya afya ikiwemo uchangiaji wa damu kwa hiari,

umuhimu wa matone ya Vitamin A kwa watoto chini ya umri wa miaka

mitano, matumizi ya chumvi yenye madini joto, uanzishwaji wa chanjo mpya

ya kuzuia maradhi ya kuharisha na chanjo ya kukinga maradhi ya uti wa

mgongo na namna ya kujikinga na maradhi yasiyo ya kuambukiza.elimu ya

afya kuhusiana na usafi wa mazingira ilitolewa katika skuli 120 Unguja na

Pemba.

Mhe. Naibu Spika, vikundi 10 vya mazoezi vilipatiwa elimu juu ya umuhimu

wa kufanya mazoezi na wanavikundi walipata fursa ya kupimwa afya zao na

kufahamishwa uwiano wa urefu na uzito ili waweze kujua maendeleo ya afya

zao. Kwa mantiki hiyo hiyo ya kujikinga na maradhi yasiyo ya kuambukiza,

wananchi walihamasishwa kuepukana na matumizi ya pombe na tumbaku

pamoja na kuzingatia ulaji bora ambao una lishe kamili. Zoezi hili lilifanyika

kwa kubandika matangazo na mabango 3,000 kwenye mitaa, maskuli na

masokoni. Pia gari za abiria 40 zilibandikwa stika kwa kuhamasisha juu ya

athari zitokanazo na matumizi ya sigara na tumbaku.

Mhe. Naibu Spika, kwa mwaka wa fedha 2013/2014 mradi huu umejipangia

kutekeleza kazi zifuatazo:

Page 51: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

51

a) Kufundisha waganga 30 wa kienyeji waliosajiliwa kwa siku

mbili juu ya sababu hatarishi na ugunduzi wa mapema wa maradhi

yasioambukiza;

b) Kufanya uchunguzi wa afya ya kinywa kwa shule za msingi za

Unguja na Pemba;

c) Kuendelea kutoa elimu ya afya juu ya maradhi ya kuambukiza

na yasiyo ya kuambukiza kwa kutumia vyombo vya habari;

d) Kubuni na kusambaza vipeperushi mbali mbali vinavytoa elimu

ya afya juu ya kujua dalili na kujiepusha na maradhi ya kuambukiza na

yasiyoambukiza;

e) Kuhamasisha jamii juu ya uchangiaji wa damu salama ili iweze

kusaidia kwa haraka kwa wagonjwa watakaohitaji kusaidiwa damu;

f) Kundelea kufuatilia mienendo ya taarifa mbalimbali ya

magonjwa katika jamii;

g) Kununua mitambo ya uchapishaji wa vielimishaji jamii.

Mradi wa Kupandisha Hadhi Hospitali za Vijiji na Wilaya

Mhe.Naibu Spika, mradi huu una jukumu kubwa la kuongeza majengo,

kuongeza vifaa na kukarabati majengo yaliyopo pamoja na vitendea kazi ili

kuzipandisha hadhi hospitali za vijiji kuwa za Wilaya na Wilaya kuwa za

Mikoa.

Mhe. Naibu Spika, hospitali ya Abdalla Mzee imo katika mpango wa

kujengwa upya na kuwa na hadhi ya hospitali ya Mkoa wa Kusini Pemba na

kuwa na hadhi ya rufaa kwa Pemba na yenye uwezo wa kulaza wagonjwa

160. Hospitali hii itajengwa kwa msaada mkubwa kutoka Jamhuri ya Watu

wa China na itakuwa ni ya kisasa yenye uwezo wa kutoa huduma za

wagonjwa mahututi (ICU), huduma za dharura (accident and emergency) na

huduma za uchunguzi wa CT Scan.

Mhe. Naibu Spika, hadi hivi sasa wizara imeshafanya makisio ya gharama za

nyumba zitakazovunjwa ili kutoa nafasi kwa ujenzi huo kuendelea. Jumla ya

Tsh. 1.2 bn zitatumika kwa ajili ya kazi ya kuwalipa fidia watu

watakaobomolewa nyumba zao. Hadi kumalizika kwake ujenzi huo

utagharimu jumla ya RMB 70, 000,000 ya Jamhuri ya Watu wa China sawa

na Tsh. 18.6 bn. Kazi inayoendelea hivi sasa ni kukamilisha ramani pamoja

kufanya gharama ya vifaa vya hospitali na mradi huu unatarajiwa kuanza

rasmi mwaka ujao wa fedha unaoanza July 2013.

Mhe. Naibu Spika, katika kufanikisha malengo yake kwa mwaka 2013/2014

mradi umejipangia kutekeleza kazi kuu zifuatazo:-

a) Kuanza ujenzi wa hospitali ya Abdalla Mzee;

Page 52: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

52

b) Kutengeneza chumba cha upasuaji katika hospitali ya Kivunge;

c) Kufanya matengenezo ya wodi ya wanawake na wanaume

katika hospitali ya Micheweni.

Mradi wa Mabadiliko ya Sekta ya Afya

Mhe. Naibu Spika, mkutano wa Saba wa mwaka wa Mapitio ya Sekta ya Afya

(7th AJHSRM) ambao uliwashirikisha wadau mbali mbali wakiwemo

washiriki wa maendeleo umefanyika. Mkutano huu uliibua mafanikio

yaliyopatikana pamoja na changamoto kwa mwaka uliopita. Mambo

yaliyoibuliwa yanajumuisha kubadilisha muelekeo wa sera kwa kuyapa

kipaumbele maeneo ambayo yamekuwa ni changamoto kwa jamii mfano

maradhi yasio ya kuambukiza na kuweka nguvu zaidi katika huduma za

watoto wachanga (neonatal care).

Mhe. Naibu Spika, ziara ya Kimasomo kwa viongozi wa Wizara ya Afya

pamoja na wataalamu mbali mbali nchini Rwanda yenye lengo la kujifunza

namna ya utekelezaji wa mfumo wa kutathmini ufanisi wa utendaji wa kazi

katika vituo vya afya na Hospitali (Performance Based Finance) imefanyika.

Ziara hii itasaidia sana katika kuanzisha mfumo huu hapa kwetu kwa kutumia

uzoefu uliopatikana.

Mhe. Naibu Spika, kujitathmini katika kazi yeyote ni jambo la msingi ili

kuona huduma zinazotolewa zinakidhi kiwango. Kufanikisha azma hii

muongozo wa kufanya tathmini ya utekelezaji wa kazi (Performance

Assessment Tool) katika Wilaya na Vituo vya Afya ulitayarishwa, sambamba

na kupatiwa mafunzo kwa madaktari dhamana wa Wilaya na wakuu wa vituo

vya afya. Baada ya mafunzo hayo zoezi la ufuatiliaji linaendelea kufanyika ili

kubaini kama, muongozo huo unafuatwa na huduma zinazotolewa zimefikia

viwango.

Mradi wa Ujenzi wa Maabara ya Mkemia Mkuu

Mhe. Naibu Spika, lengo kuu la mradi huu ni kujenga maabara kubwa na ya

kisasa pamoja na kuipatia vifaa ambavyo vitaipelekea maabara hii kuweza

kutoa huduma za uchunguzi wa kitaalamu kwa sampuli mbali mbali

zinazowasilishwa.

Mhe. Naibu Spika, kwa mwaka wa fedha 2012/2013, wizara imekamilisha

ukarabati mkubwa wa jengo la Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali liliopo

Maruhubi, kuipatia samani pamoja na vifaa vya kisasa vya kufanyia

uchunguzi ili kuongeza ufanisi wa kazi zake.

Page 53: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

53

Mhe. Naibu Spika, katika kuongeza ufanisi wa watendaji wafanyakazi

wawili wa maabara hii wamekwenda nchini Uturuki kwa kubadilishana

uzoefu wa kitaalamu wa uendeshaji wa maabara.

Mhe. Naibu Spika, kwa mwaka wa fedha 2013/2014 mradi umejipangia

kujenga majengo mapya ya Maabara za kisasa Unguja na Pemba.

Mradi wa Chuo cha Madaktari Zanzibar (Zanzibar Medical School)

Mhe. Naibu Spika, chuo cha Madaktari kinatoa mafunzo ya udaktari kwa

mashirikiano makubwa na Chuo Kikuu cha Matansas, Cuba. Kwa sasa chuo

kana jumla ya wanafunzi 50 (38 kwa Unguja na 12 Pemba).

Mhe. Naibu Spika, katika mwaka 2012/2013, niliahidi kushirikisha madaktari

wazalendo katika kutoa taaluma ya afya katika chuo hiki. Napenda kuliarifu

Baraza hili tayari madaktari wawili wazalendo wanasaidiana na madaktari wa

Cuba katika kutoa taaluma chuoni hapo.

Mhe. Naibu Spika, katika mwaka 2013/2014 chuo kitaendelea kutoa taaluma

ya udaktari kwa wanafunzi wote wanaosoma katika chuo hiki.

Mradi wa Kuimarisha Huduma za Afya Wilayani

Mhe. Naibu Spika, Timu za afya za wilaya ni kiungo kikuu cha utekelezaji wa

shughuli za utoaji wa huduma za afya kati ya wizara ya afya, program na

vitengo vya wizara, vituo vya afya, wadau wengine na jamii kwa ujumla.

Timu hizi zina jukumu la kusimamia utekelezaji wa huduma mbali mbali za

afya zinazotolewa katika vituo vya afya ikiwemo wafanyakazi, majengo na

vifaa. Kwa mwaka wa fedha 2012/2013 wizara iliamua kuanzisha mfumo

maalum wa kuendesha kazi za timu hizi ambapo mfuko maalum wa pamoja

wa fedha (District Health Servises Basket Fund) uliazishwa.

Mhe. Naibu Spika, utumiaji wa huduma za afya wilayani ni kiashiria muhimu

katika kupima utumiaji wa huduma hizo. Katika mwaka 2012 kwa wastani

Wilaya sita (Chake-Chake na Wete kwa Pemba: Kati, Kaskazini A, Kusini na

Mjini kwa Unguja) zilionekana kuwa na utumiaji mzuri wa huduma za afya

ambapo kila mtu mmoja alitembelea mara moja au zaidi. Kiwango hiki ni

zaidi ya kiwango kinachopendekezwa na Shirika la Afya Ulimwenguni

ambapo inakadiriwa kwamba mwanadamu yeyote anatakiwa kwenda kituo

cha afya kwa ajili ya kupata huudma angalau mara moja kwa mwaka. Hali hii

inaamaanisha kwamba wananchi wengi wanapatiwa huduma za afya katika

vituo vya afya vilivyopo.

Page 54: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

54

Mhe. Naibu Spika, utekelezaji wa shughuli katika wilaya hizi unatofautiana

kutegemeana na mazingira na mahitaji halisi ya wilaya husika. Kwa mwaka

wa fedha 2012/2013, Siku za Afya za Vijiji zilifanyika katika Shehia 50 za

Unguja na Pemba. Katika Siku hizo huduma mchanganyiko za afya zilitolewa

kwa wanavijiji, wananchi waliweza kuchunguzwa afya zao kwa kupimwa

maradhi ya Shinikizo la damu, Kisukari, Saratani ya Shingo ya kizazi na

matiti, VVU, Kifua Kikuu, Macho na meno. Tiba ilitolewa kwa wale

waliostahiki na kwa wale waliokuwa na hali mbaya walipatiwa rufaa.

Mhe. Naibu Spika, katika kuimarisha elimu ya afya mashuleni, mafunzo ya

ukufunzi (TOT) juu ya uhusiano wa ugonjwa wa kifua kikuu na VVU kwa

walimu kupitia vituo vya walimu (Teacher‟s Centre) yalitolewa. Walimu

hawa walitakiwa kutoa taaluma kwa klabu za wanafunzi (School Clubs)

pamoja na wanafunzi wa madarasa) na hatimae klabu hizo hutakiwa

kuwaelemisha wenzao (elimu rika). Vile vile, elimu kuhusu umuhimu wa

chanjo ya Pepo Punda imetolewa kwa wanafunzi wa sekondari shamba na

mijini wengi wao waliitikia wito na kupatiwa chanjo hiyo mara tu baada ya

mafunzo hayo kutolewa.

Mhe. Naibu Spika, ukaguzi wa majengo kama vile mikahawa na skuli

umefanyika na imeonekana kuwa hali ya mazingira ni mbaya hususan maeneo

ya vyoo. Pia, wahudumu walikaguliwa afya zao na kupewa ushauri wa kiafya.

Aidha, akina mama lishe na wauza mikahawa wamepewa elimu ya usafi

binafsi (personal hygiene) na utaratibu wa kutayarisha chakula pamoja na

usafi wa mazingira. Hali ambayo itasaidia katika kupunguza kasi ya maradhi

mbali mbali.

Mhe. Naibu Spika, uhamasishaji kwa wakunga wa Jadi, wahudumu wa uzazi

wa mpango na watu maarufu umefanyika kwa kupewa elimu juu ya umuhimu

wa kuhudhuria kliniki za mama waja wazito ndani ya wiki 16. Wadau hao

walielezwa huduma mbali mbali zinazotolewa katika hudhurio la mwanzo na

za marudio pia walitakiwa kuwashajihisha kina mama kujifungua katika

Vituo vya Afya na kufata utaratibu uliowekwa wa kuhudhuria kliniki mara tu

baada ya kujifungua kwa kuchunguza afya zao na kupewa matone ya Vit-A

pamoja na watoto kuanza chanjo.

Mhe. Naibu Spika, kwa mwaka 2013/14 kazi zifuatazo zitatekelezwa:-

a) Kuendelea kufanya ufuatiliaji katika vituo vya afya;

b) Kuendelea na kusimamia matengenezo madogo madogo ya

vituo vya afya na hospitali za vijiji;

c) Kuendela kutoa mafunzo ya afya kwa wafanyakazi wa vituo na

hospitali za vijijii (mafunzo juu ya kumhudumia mtoto

Page 55: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

55

kulingana na muongozo wa IMCI, Afya ya mama na mtoto) ili

waweze kutoa huduma zinazoendana na miongozo ya utoaji

wahuduma za afya ya kitaifa na kimataifa;

d) Kuendelea kutoa huduma ya afya ya jamii kupitia njia mbali

mbali ikiwemo huduma za mkoba katika maeneo ya Tumbatu,

Kijini, Kinuni, Kisiwa Panza, Fundo).

CHANGAMOTO

Mhe. Naibu Spika, kama nilivyoeleza kuwa, mafanikio makubwa

yamepatikana katika utekelezaji wa majukumu ya wizara kwa kipindi cha

mwaka 2012/2013. Hata hivyo, Wizara ya Afya bado inakabiliwa na

changamoto nyingi ambazo zinahitaji mashirikiano yetu sote kuweza

kuzitatua.

Mhe. Naibu Spika, miongoni mwa changamoto hizi ni bajeti iliyopangwa na

kuidhinishwa huwa haiendani na utoaji wa fedha kutoka Serikali Kuu, hivyo

huathiri utekelezaji wa kazi za kawaida na za maendeleo. Matumizi baada ya

kumalizika kikao cha bajeti kama hiki huombwa Ofisi ya Rais Fedha na

Mipango ya Maendeleo kwa mfumo wa kila robo mwaka na wizara hujiwekea

vipaumbele kwa mujibu wa mahitaji tuliyonayo, lakini bado maombi hayo

hayapatikani kwa wakati na huwa hayalingani na kile kilichoombwa kwa kazi

za kawaida na maendeleo. Hiyo changamoto moja Mhe. Naibu Spika,

inayotusumbua.

Mhe. Naibu Spika, moja katika mkakati wa Wizara ya Afya ni kuimarisha

huduma za afya wilayani na vijijini. Hata hivyo, utekelezaji wa mkakati huu

hauendani na kasi ndogo ya serikali ya kuimarisha madaraka wilayani ya

Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, tunaiomba serikali

kukamilisha taratibu zilizobakia ili tuende sambamba na utoaji bora wa

huduma za afya wilayani na vijijini.

Mhe. Naibu Spika, ujenzi wa vituo vya afya vinavyoanzishwa na wananchi

bila ya kufuata utaratibu bado ni tatizo kutokana na ufinyu wa bajeti ya afya

na ukosefu mkubwa wa wafanyakazi wanohitajika kuvihudumia vituo hivyo

wakati vinapomalizika. Taarifa tuliyonayo hivi sasa kuna vituo 28

vilivyoanzishwa ambavyo vinahitaji wataalamu, dawa na vifaa mambo

ambayo ni changamoto kubwa kwa wizara yetu. Kama nilivyosisitiza katika

hotuba ya bajeti ya Wizara ya Afya ya mwaka 2012/2013, kwa mara nyengine

tena, naomba kutoa wito kwa viongozi na wananchi kujihusisha zaidi katika

kujenga nyumba za wafanyakazi na kununua dawa, vifaa na tiba mbadala ya

kufikiria kujenga vituo vipya vya afya ambapo tulivyonavyo vinatosha.

Page 56: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

56

Mhe. Naibu Spika, kutokamilika kwa mfumo madhubuti unaowalazimisha

wafanyakazi kubakia makazini hasa wale ambao wanaopelekwa masomoni

wa kada za kitaalamu, kunapelekea wafanyakazi kutorudi au hata wale

waliokuwepo kukimbia. Kwa mfano, katika kipindi hiki jumla ya

wafanyakazi 32 wa kada tofauti hawajarejea katika sehemu zao za kazi wakati

serikali imelipia gharama kubwa za kuwasomesha.

Mhe. Naibu Spika, gharama kubwa za huduma za maji na umeme imekuwa ni

tatizo kwa uendeshaji wa vituo vya afya vijijini na hata kwa hospiatali zetu za

wilaya na rufaa. Ukubwa wa tatizo hili unatokana na Shirika la Umeme na

Mamlaka ya Maji kulipisha vituo vya afya na hospitali kama ni kampuni za

kibiashara, jambo ambalo linapelekea kutumia fedha chache tulizonazo kwa

kazi za kawaida na maendeleo kulipia umeme, ambazo zingetumika kwa

shughuli nyengine. Nachukua fursa hii kuzitaka taasisi husika kulizingatia

suala hili na kulipatia ufumbuzi.

Mhe. Naibu Spika, kushuka kwa kiwango cha chanjo kitaifa ni moja katika

tatizo sugu linalotusumbuaWizaraya Afya. Kushuka kwa kiwango cha chanjo

kitaifa ni tatizo lililojitokeza hasa katika wilaya ambazo zilichanja chini ya

kiwango cha asilimia 80. Hali hii imepelekea kuibuka kwa maradhi ya surua

ambayo yalikuwa hayapo kwa watoto, maradhi ambayo ni tishio kwa taifa.

Hivyo nawaomba wananchi wenzangu kupitia hotuba hii kwa pamoja

tushirikiane kuwashajihisha akinamama na baba kuwapeleka watoto wao

kuchanjwa kwani janga la maradhi yakitokea huwa hayachagui sura wala

kabila wala kijiji.

MALENGO YA WIZARA YA AFYA KWA MWAKA 2013/2014

Mhe. Naibu Spika, Wizara ya Afya kwa mwaka wa fedha 2013/2014

imejipangia kutekeleza mambo makuu yafuatayo:-

a) Kuhakikisha upatikanaji wa dawa, vifaa, tiba na vitenganishi

vyenye ubora na usalama katika ngazi zote;

b) Kuimarisha utoaji wa elimu ya afya kwa jamii ili kupunguza

kiwango cha maradhi ya kuambukiza na yasiyokuwa ya

kuambukiza;

c) Kuendeleza mashirikiano na Wizara ya Utumishi wa Umma ili

kupata ufumbuzi wa motisha za wafanyakazi wa afya na

wafanyakazi wanaofanya kazi katika mazingira magumu;

d) Kuendelea kutoa mafunzo ya kada mbali mbali za afya kwa

wafanyakazi;

e) Kuanzisha mkakati wa muda mrefu wa vyanzo mbadala vya

rasilimali fedha kwa ajili ya kutolea huduma za afya;

Page 57: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

57

f) Kuimarisha na kusimamia shughuli za utafiti, tathmini na

ufuatiliaji wa taarifa za afya katika ngazi zote;

g) Kuimarisha miundombinu ya afya ikiwemo ujenzi wa Hospitali

ya Abdalla Mzee na upanuzi wa Hospitali ya Mnazi Mmoja;

h) Kukamilisha mpango mkakati wa afya wa III na kuufanyia

mahitaji yake kifedha;

i) Kuimarisha utoaji wa huduma za afya katika ngazi za wilaya

kupitia mfuko wa fedha wa pamoja wa wilaya (District Health

Services Basket Fund) ikijumuisha Hospitali za Wilaya,

Hospitali za Vijiji na Vituo vya Afya.

HITIMISHO

Mhe. Naibu Spika, mafanikio yaliyopatikana ya kutoa huduma bora za afya

kwa wananchi kulitegemea mashirikiano makubwa yaliyokuwepo ndani ya

wizara hii. Hili halikuwa jukumu la mtu mmoja, kwa mustakbala huo, sina

budi kuwapongeza viongozi wote ndani ya wizara ikiwa ni pamoja na Naibu

Waziri wangu Dr. Sira Ubwa Mamboya, Katibu Mkuu, Wakurugenzi na

Wakuu wote wa vitengo/sehemu zilizomo ndani ya wizara, kwa mashirikiano

makubwa waliyonipa na tuliyofanya pamoja.

Mhe. Naibu Spika, nathamini mchango mkubwa wa wafanyakazi wa ngazi

zote za ndani ya wizara kwa kufanya kazi bila ya kuchoka kwani

wanakabiliwa na changamoto nyingi katika utoaji wa huduma kwa wananchi.

Hali hii imeniwezesha kufanikisha utekelezaji wa majukumu yangu kwa kiasi

fulani kwa urahisi sana. Aidha, nathamini mchango na mashirikiano kutoka

kwa taasisi nyengine za serikali katika kusaidia upatikanaji wa huduma za

afya visiwani mwetu.

Mhe. Naibu Spika, huduma za afya zimekuwa zikitolewa kwa mashirikiano

na sekta binafsi (Private Sector), pamoja na jamii ya Wazanzibari na

wananchi wote. Wizara yangu itakuwa mchoyo wa fadhila pindipo

haitaipongeza sekta hii kwa mchango wao katika kutoa huduma. Hali hii

imesaidia wizara yangu katika kufanikisha utekelezaji wa jukumu lake la

kuipatia jamii huduma inayostahiki. Aidha, wizara inaishukuru jamii ya

Wazanzibari na wananchi wote kwa ujumla kwa mashirikiano na michango

yao katika utoaji na upokeaji wa huduma za afya.

Katika kipindi chote cha utoaji wa huduma za afya, serikali za nchi marafiki,

mashirika ya kitaifa na kimataifa pamoja na watu binafsi yalikuwa sambamba

na wizara yangu, hivyo kutoa mashirikiano makubwa pamoja na misaada ya

hali na mali ili kuhakikisha afya za jamii za watu wetu zinaimarika.

Page 58: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

58

Mhe. Naibu Spika, nitakuwa sikuzitendea haki taasisi zote hizo pindipo

sikutoa shukurani zangu za dhati kwao, nawaomba wasichoke kwa vile safari

ya kutoa huduma bora za afya kwa wananchi wetu ingali ndefu na inahitaji

mashirikiano yetu sote. Nachukua fursa hii adhimu kuwashukuru wote hasa

WHO, UNICEF, UNFPA, UNDP, WORLD BANK, ADB, JHIEPIGO,

GLOBAL FUND, USAID, DANIDA, ICAP, HIPZ, CLINTON FOUNDATION,

SAVE THE CHILDREN, IVODE CANERI na ITALIAN FOUNDATION. Pia

shukurani ziende kwa nchi marafiki za Cuba, Italy, Marekani, Oman, China,

Israel, Turky, Misri, France, India, Netherland, Uingereza na wote ambao

sikuwataja katika orodha huu.

Mhe. Naibu Spika, kwa mwaka wa fedha 2013/2014 Wizara ya Afya

imepangiwa kuchangia jumla ya Shilingi 924,000,000 kwenye Mfuko Mkuu

wa Serikalii kiambatisho namba 16 kinaonesha ufafanuzi. Pia wizara

imepangiwa kutumia Shilingi 5,764,000,000 kwa kazi za kawaida, Shilingi

1,368,000,000 ikiwa ni ruzuku na Shilingi 14,186,000,000 kwa mishahara na

maposho. Kiambatisho namba 17 kinaonesha ufafanuzi. Kwa kazi za

Maendeleo wizara imepangiwa kutumia jumla ya Shilingi 6,333,000,000

kutoka Mfuko Mkuu wa Serikali, Shilingi 37,257,128,000 misaada na Shilingi

5,078,489,000 ikiwa ni Mikopo kutoka nje. Kiambatisho namba 18

kinaonesha ufafanuzi.

Mhe. Naibu Spika, utekelezaji wa majukumu ya wizara yangu yanategemea

kwa kiasi kikubwa kupitishwa kwa hotuba yangu hii ya bajeti. Kwa mintarafu

hiyo nategemea Baraza lako tukufu limeipokea, litaijadili, kuichangia na

mwishoe litapitisha bila ya mashaka ili wizara yangu iweze kuwapatia

wananchi huduma bora za afya na hatimae kuimarisha afya zao. Naomba

Mhe. Naibu Spika, Baraza hili liidhinishe jumla ya Shilingi 21,318,000,000

kwa Kazi za Kawaida, Ruzuku, Mishahara na Maposho. Pia naomba Baraza

liidhinishe jumla ya Shilingi 6,333,000,000 kwa Kazi za Maendeleo kutoka

serikalini na Shilingi 37,257,128,000 ikiwa ni ruzuku kwa washirika wa

maendeleo, Shilingi 5,078,489,000 mkopo kutoka kwa washirika wa

maendeleo.

Mhe. Naibu Spika, kwa heshima kubwa na taadhima na kwa idhini yako

naomba kutoa hoja.

(Hoja ilitolewa iamuliwe)

Page 59: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

59

Kiambatisho Nam 1: Mwenendo wa Maradhi kwa Mgawanyo wa

Umri 2012/13

Kiambatisho Nam 2: Mwenendo wa Maradhi kwa Mgawanyo wa

Wilaya

Page 60: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

60

Kiambatisho Nam 3: Takwimu za Wagonjwa Walioonekana kupitia

Uchunguzi wa Vijijini kwa mwaka 2012/13

Page 61: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

61

Kiambatisho Nam 4: Matatizo yaliyogunduliwa Wakati wa Uchuguzi wa

Afya za Wafanyakazi

Page 62: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

62

Kiambatisho Nam 5: Wagonjwa wa Nje na Ndani Katika Hospitali za

Idara ya Tiba Julai, 2012 - Machi, 2013

Page 63: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

63

Kiambatisho Nam 6: Taarifa ya Hali ya Uzazi Katika Hospitali za

Idara ya Tiba, Julai, 2012 – Machi, 2013

Kiambatisho Nam 7: MAHUDHURIO YA WAGONJWA KATIKA

KLINIKI ZA MARADHI MAALUM KWA HOSPITALI ZA IDARA YA

TIBA, July 2012 - March 2013

Page 64: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

64

Kiambatisho Nam 8: Mahudhurio ya Wagonjwa wa Nje, Waliolazwa

na Waliofariki Katika Idara ya Hospitali ya Mnazi Mmoja, Julai 2012 -

Machi 2013

Page 65: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

65

Kiambatisho Nam 9: Mahudhurio ya Wagonjwa Katika Kliniki za

Maradhi Maalum Katika Hospitali ya Mnazi Mmoja Julai 2012, - Machi,

2013

Kiambatisho Nam 10: Taarifa ya Hali ya Uzazi Katika Wodi ya

Wazazi kwa Hospitali za Mnazi Mmoja na Mwembeladu Julai, 2012 –

Machi, 2013

Page 66: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

66

Kiambatisho Nam 11: Kambi zilizofanywa na ZOP kuanzia Julai

2012- Machi 2013

Kiambatisho Nam 12: Thamani ya Dawa na Zana za Tiba

Zilizopatikana (Julai, 2012 – Machi, 2013)

Page 67: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

67

Kiambatisho Nam 13: Idadi ya Sampuli Zilizochunguzwa Julai 2012 -

Machi 2013

Page 68: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

68

Page 69: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

69

Kiambatisho Nam 14: Wanafunzi waliorudi Masomoni,

Julai 2012 – Machi 2023

Cadre

Level

Grand

Total

Certificate

Diploma

Advanced

Diploma

Degree

Post

Grade

Diploma

Masters

pHd

Accounting 1 1

AMO 2 2

Anaethetic

Nurse

6 6

Biomedical

Technician

8 8

Chemist 1 1

DDS 2 2

Dental

Surgery

1 1

Economic &

Nutrition

1 1

ENT 2 2

Entomology

& Vector

Control

1 1

Guidence &

Councelling

1 2 3

Internal

Medicine

1 1

M.B.B.S 4 4

Medical

Imaging

4 4

Medical

Laboratory

2 2

Nursing 16 1 17

Oncology 1 1

Paediatrics 1 1

Procurement 1 1

Psychology

&

Counseling

2 2

Public

Health

4 4

Page 70: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

70

Reproductive

Health

1 1

Social Work 1 1

Vector

Control

1 1

Grand Total 14 4 6 38 1 4 1 68

Kiambatisho Nam 15: Taarifa ya Huduma ya Chanjo kwa Watoto

chini ya Mwaka mmoja Julai 2012 - Mach 2013

Page 71: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

71

Kiambatisho Nam 16: Fedha Zilizotengwa na Kukusanywa kwa

Kipindi cha Julai 2012- Machi 2013 na Mapendekezo ya Makusanyo

2013-2014

Kasma Maelezo ya

Mapato

Makadirio

2012/2013

Makusanyo

Julai-Machi

2012/2013

Asilimia

Mapendekezo

ya Makadirio

ya Mapato

2013/2014

4 IDARA YA MIPANGO NA UENDESHAJI

142126

Huduma za

Maabara ya

Mkemia

Mkuu

1,000,000.00 - -

-

JUMLA

NDOGO

1,000,000.00 - -

-

6 IDARA YA KINGA

142238

Shahada ya

maradhi ya

kuambukiza

15,000,000.00

7,249,000.00 48.33

16,000,000.00

142260

Huduma za

daktari na

orodha wa

wafanyakazi

na abiria

14,000,000.00

8,416,000.00 60.11

15,000,000.00

JUMLA

NDOGO

29,000,000.00

15,665,000.00 54.02

31,000,000.00

7 IDARA YA TIBA UNGUJA

142261

Malipo ya

X-Ray na

uchunguzi

wa damu

20,000,000.00

11,597,000.00 57.99

20,000,000.00

JUMLA

NDOGO

20,000,000.00

11,597,000.00 57.99

20,000,000.00

0801- IDARA YA TIBA PEMBA

Page 72: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

72

142261

Malipo ya

X-Ray na

uchunguzi

wa damu

10,000,000.00

1,511,000.00 15.11

3,000,000.00

JUMLA

NDOGO

10,000,000.00

1,511,000.00 15.11

3,000,000.00

145000 MICELLANIOUS REVENUES

145002 Mapato

mengineyo

35,000,000.00

45,072,800.00 128.78

70,000,000.00

JUMLA

NDOGO

35,000,000.00

45,072,800.00 128.78

70,000,000.00

145000 1501 M/MMOJA HOSPITAL

145001 Mapato

mengineyo

710,500,000.00

292,174,463.00 41.12

384,000,000.00

Huduma za

haraka -

-

-

416,000,000.00

JUMLA

NDOGO

710,500,000.00

292,174,463.00 41.12

800,000,000.00

JUMLA

KUU

805,500,000.00

366,020,263.00 45.44

924,000,000.00

Kiambatisho Nam 17: Fedha Zilizotengwa na Kuingizwa kwa Kazi za

Kawaida kwa kipindi cha julai 2012- machi 2013 na makadirio 2013-2014

Page 73: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

73

Page 74: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

74

Kiambatisho Nam 18: Fedha Zilizotengwa na Kuingizwa kwa Kazi za

Maendeleo kwa Kipindi cha Julai 2012-Machi 2013 na Makadirio 2013-

2014

Mhe. Hassan Hamad Omar (Makamo Mwenyekiti wa Kamati ya

Maendeleo ya Wanawake na Ustawi wa Jamii): Mhe. Naibu Spika, kwa

ruhusa yako naomba kusoma hotuba ya maoni ya Kamati ya Maendeleo ya

Wanawake na Ustawi wa Jamii kuhusiana na bajeti ya Wizara ya Afya kwa

mwaka wa fedha 2013/2014.

Mhe. Naibu Spika, awali ya yote hatuna budi kumshukuru Mwenyezi Mungu

kwa kuturuzuku uhai na afya njema na kutuwezesha kukutana tena leo hii

kwa madhumuni ya kuwatumikia wananchi wetu na manufaa ya taifa letu kwa

ujumla.

Page 75: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

75

Pili napenda nikushukuru wewe binafsi kwa kuniruhusu kusimama mbele ya

Baraza lako tukufu kwa niaba ya Kamati ya Maendeleo ya Wanawake na

Ustawi wa Jamii, kuwasilisha maoni ya Kamati kuhusiana na makadirio ya

mapato na matumizi ya kazi za kawaida na maendeleo kwa mwaka wa fedha

2013/2014.

Mhe. Naibu Spika, napenda kuchukua nafasi hii kumshukuru Waziri wa Afya,

Naibu Waziri, pamoja na watendaji wote wa wizara kwa mashirikiano yao

waliyotupa wakati wa kupitia na kuichambua bajeti ya wizara, kwa kweli

mashirikiano yao yamefanikisha kumaliza kazi hii kwa wakati na kwa ufanisi

mkubwa.

Sitokuwa nimetenda haki hata kidogo iwapo nitakosa kuwashukuru na

kuwapongeza Wajumbe wa Kamati ya Maendeleo ya Wanawake na Ustawi

wa Jamii kwa kazi nzuri waliyoifanya hadi kuniwezesha leo hii kusimama

mbele ya Baraza lako tukufu kuwasilisha maoni ya Kamati juu ya Makadirio

ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2013/2014. Naomba

niwatambue kwa kuwataja majina wajumbe wa Kamati kama hivi ifuatavyo:-

1. Mhe. Mgeni Hassan Juma Mwenyekiti

2. Mhe. Hassan Hamad Omar M/Menyekiti

3. Mhe. Abdi Mosi Kombo Mjumbe

4. Mhe. Ali Salum Haji Mjumbe

5. Mhe. Farida Amour Moh'd Mjumbe

6. Mhe. Mwanaid Kassim Mussa Mjumbe

7. Mhe. Mohamed Mbwana Hamad Mjumbe

8. Ndg. Maryam Rashid Ali Katibu

9. Ndg. Asha Said Mohamed Katibu

Mhe. Naibu Spika, baada ya utangulizi huo, naomba kutoa maoni ya Kamati

kuhusiana na Bajeti ya Wizara ya Afya.

Jengo la Ofisi Kuu – Pemba

Mhe. Naibu Spika, Kamati yetu imesikitishwa na hali ya Wizara ya Afya

Pemba kukosa ofisi yake. Ofisi Kuu Pemba imekuwa haina jengo kwa muda

mrefu na inatumia chumba kimoja kidogo kilichopo katika hospitali ya Wete;

hali ambayo hairidhishi kwani chumba hicho kinakuwa hakikidhi haja kwa

matumizi ya wizara nzima. Afisa Mdhamini anashindwa kuwa karibu na

wasaidizi wake mbali mbali kutokana na ufinyu wa ofisi.

Page 76: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

76

Mhe. Naibu Spika, Kamati inaiomba serikali kutatua tatizo la ofisi ya wizara

Pemba. Kiukweli Kamati haikuridhika na hali ya ufinyu wa ofisi kwa sababu

utekelezaji wa majukumu ya wizara unakuwa ni mgumu.

Upatikanaji wa Dawa na Vifaa Tiba katika Hospitali na Vituo vya Afya

Pemba

Mhe. Naibu Spika, upatikanaji wa dawa na vifaa tiba ni muhimu katika

hospitali na vituo vya afya, lakini Kamati ilipotembelea vituo vya afya na

hospitali mbali mbali ilibaini upungufu mkubwa wa dawa na vifaa tiba.

Sambamba na hilo, Kamati ilifanya mahojiano na timu nne za afya Pemba

zilizopo katika Wilaya ya Micheweni, Wilaya ya Wete, Wilaya ya Chake

Chake na Wilaya ya Mkoani; nazo zilikiri kuwa upatikanaji wa dawa na vifaa

tiba ni tatizo katika wilaya zao.

Mhe. Naibu Spika, kutokana na umuhimu wa huduma za afya na dawa,

Kamati inaishauri Wizara kutafuta kampuni nyingine ya kuagiza na kuingiza

dawa nchini badala ya kutegemea ghala kuu ya dawa ya Dar es Salaam pekee

MSD (Medical Store of Dar es Saalam) ambao nao huchangia uhaba wa

upatikanaji wa dawa katika hospitali na vituo vyetu vya afya katika muda

unaotakiwa.

Kuhusu Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo

Kamati haikuridhishwa na utekelezaji wa miradi unaondeshwa na wizara.

Katika bajeti ya wizara ya mwaka wa fedha 2012/2013, wizara ilijipangia

kutekeleza miradi mbali mbali ya maendeleo. Kamati imebaini utekelezaji

usio wa ufanisi katika programu shirikishi ya afya ya mama na mtoto, mradi

wa kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi na mradi wa kuvipandisha hadhi

vituo vya huduma za afya. Malengo ya miradi hiyo hayakuweza kufikiwa

kikamilifu.

Mhe. Naibu Spika, katika utekelezaji wa programu shirikishi ya afya ya mama

na mtoto ambayo ilikusudia kujenga vyumba vya baridi na kufanya ukarabati

wa ofisi ya chanjo Pemba. Kamati ilisikitishwa sana kuwa utekelezaji wake

haukuweza kufanyika na hakukuwa na sababu za msingi kwani fedha za

wahisani ziliingizwa na kushindwa kufanyiwa kazi katika muda

uliokusudiwa. Kitendo hichi ni kuwavunja moyo wahisani wetu na Kamati

inamtaka waziri atoe maelezo juu ya jambo hili.

Pia Kamati inaiagiza wizara katika utekelezaji wa bajeti ya mwaka 2013/2014

kuhakikisha kuwa wanafanya ujenzi wa haraka wa vyumba vya baridi pamoja

na ukarabati wa Ofisi ya Chanjo, kwani chanjo zote kwa upande wa Pemba

Page 77: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

77

zinahifadhiwa katika ofisi hiyo, kuendelea kuchelewa kufanya ujenzi

kutapelekea kutokuwa na uhakika wa usalama wa chanjo zetu pamoja na

wafanyakazi wanaohudumia ofisi hiyo.

Mhe. Naibu Spika, katika mradi wa kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi,

Wizara ilikusudia kufanya matengenezo katika vituo vya afya vya

Mzambarauni na Wesha kwa upande wa Pemba na kwa Unguja Kituo cha

Afya Mwera. Vituo vyote hivyo vilikosa kukarabatiwa katika kipindi husika,

ukarabati uliofanyika ni wa Kituo cha Afya cha Bogoa pekee ambacho

utekelezaji wake ulikuwa wa tangu bajeti ya mwaka wa fedha 2011/2012.

Aidha, katika mradi wa kuvipandisha hadhi vituo vya huduma za afya, lengo

lake lilikuwa ni kufanya utanuzi wa majengo ya Hospitali ya Kivunge na

Micheweni pamoja na ununuzi wa vifaa mbali mbali kwa ajili ya utoaji mzuri

wa huduma za afya katika hospitali hizo. Utekelezaji wake haukuwa wa

kuridhisha.

Mhe. Naibu Spika, Kamati inaitaka serikali kuingizia fedha wizara kwa

wakati ili iweze kutekeleza mipango yake iliyojipangia ikiwemo utekelezaji

wa miradi kwa lengo la kuimarisha huduma za afya nchini na kuinua sekta hii

muhimu.

Idara ya Utumishi na uendeshaji

Mhe. Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2012/2013, idara ilikamilisha

mpango mkuu wa mafunzo kwa wafanyakazi ambao utekelezaji wake utaanza

kutumika rasmi katika mwaka huu wa fedha. Kamati inaipongeza wizara kwa

kuweza kukamilisha mpango huo muhimu ambao utasaidia katika kupunguza

upungufu mkubwa wa wafanyakazi wa afya katika kada mbali mbali kwa

hospitali na vituo vya afya.

Katika nchi yetu tumekuwa na upungufu mkubwa wa madaktari wa

magonjwa ya akili, madaktari wa X-ray, madaktari wa magojwa ya damu na

madaktari wa kensa. Kamati inaishauri wizara katika mpango mkuu wa

mafunzo kwa mwaka wa fedha 2013/2014 kuwahimiza wafanyakazi

watakaoenda masomoni kuchukua fani zilizokuwa pungufu katika nchi yetu

na pia kuwepo na motisha maalumu kwa watakaokubali kuchukua fani hizo.

Mhe. Naibu Spika, pia Kamati inaisisitiza wizara kusimamia vyema mfumo

wa takwimu za rasilimali watu, mfumo ambao husaidia katika kupangia

wafanyakazi sehemu za kazi kwa mujibu wa mahitaji. Wizara imekuwa

inakabiliana na changamoto ya wafanyakazi wengi wa afya kutopendelea

kufanya kazi vijijini na badala yake kupendelea zaidi kubakia mijini pekee.

Page 78: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

78

Mhe. Naibu Spika, Kamati inaiomba wizara ijitahidi kusimamia maslahi ya

wafanyakazi na ihakikishe inasimamia ipasavyo mapendekezo ya rasimu ya

maposho kwa wafanyakazi wanaofanya kazi katika mazingira ya hatarishi na

pia kuwazingatia wale wanaofanya kazi katika mazingira ya vijijini

yaliyokosa huduma muhimu. Kufanya hivyo, kunaweza kuwavutia

wafanyakazi wetu kubakia katika ajira na kupunguza idadi kubwa ya

wafanyakazi wanaokimbia kufanya kazi vijijini na katika nchi yetu kwa

ujumla.

Idara ya Sera, Mipango na Utafiti

Mhe. Naibu Spika, Kamati inapongeza jitihada zinazoendelea kufanywa na

idara katika mchakato mzima wa kuanzisha bima ya afya kwa wananchi.

Kiukweli bima hiyo ni muhimu na itawasaidia wananchi kuwa na uhakika wa

kupata huduma za afya kila watakapokuwa wanasumbuliwa na maradhi mbali

mbali.

Mhe. Naibu Spika, kumekuwa na wananchi ambao hushindwa kuhudhuria

katika hospitali na vituo vya afya kutokana na kushindwa kumudu gharama za

afya. Kamati ina matumaini makubwa kwamba kuanzishwa kwa bima ya afya

kutawawezesha wananchi walio wanyonge kufaidika na huduma za afya kwa

kadri watakavyokuwa wanazihitajia.

Kamati inaisisitiza wizara kuendelea na hatua mbali mbali zinazohusiana na

kukamilika kwa bima hiyo na pia kuandaa utaratibu mzuri ambao utapelekea

kupatikana kwa huduma kwa wepesi na kunufaisha wananchi wote.

Idara ya Kinga na Elimu ya Afya

Mhe. Naibu Spika, miongoni mwa majukumu ya idara ni kukinga na

kukabiliana na maradhi ya kuambukiza na yasiyo ya kuambukiza. Katika

miaka ya hivi karibuni, katika visiwa vya Zanzibar kumekuwa na ongezeko

kubwa la magonjwa yasio ya kuambukiza ikiwemo shindikizo la damu,

kisukari, saratani na magojwa mengine sugu ya mapafu kama vile pumu.

Kamati inaipongeza wizara kwa kuweza kufanya utafiti katika hospitali nne

za vijiji na hospitali tatu za wilaya na kuweza kubaini hali halisi ya magonjwa

na kutambua mahitaji ya taaluma, vitendea kazi na rasilimali watu.

Mhe. Naibu Spika, kitengo cha kupambana na magonjwa yasio ya

kuambukiza kinaendelea kusimamia utekelezaji wa mikakati ya kukabiliana

na magonjwa hayo na Kamati inasisitiza wizara, pamoja na kuwepo kwa

Page 79: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

79

kitengo, kuendelea kuusimamia muongozo wa matibabu ya magonjwa

yasioambukiza ili uweze kukamilika na kuanza kutumika.

Aidha, kwa upande wa maradhi ya malaria, Kamati inapenda kuipongeza

wizara kwa jitihada wanayoendelea kuchukua ya kudhibiti maradhi hayo.

Kamati iliweza kujionea wenyewe kisiwani Pemba, Shehia ya Tumbe kuwa

ugonjwa wa malaria katika kijiji hicho umeweza kutokomezwa. Kamati

inaiomba wizara kuendelea na juhudi ya kudhibiti maradhi ya malaria ili

yasije yakaibuka tena kwa kuendela kutoa elimu ya kinga ya maradhi hayo.

Kamati ina matumaini makubwa kuwa idara itaendelea kufanya vizuri katika

majukumu yake mbali mbali kutokana na ongezeko la bajeti kutoka shilingi

milioni mia mbili thalathini na moja (231,000,000) katika mwaka wa fedha

2012/2013 mpaka kufikia milioni mia tatu hamsini (350,000,000) katika

mwaka huu wa fedha.

Idara ya Tiba

Mhe. Naibu Spika, idara hii inajumuisha Hospitali za Wilaya na Vijiji na pia

inasimamia mradi wa kupandisha Hospitali za Vijiji na Wilaya. Kiujumla

hospitali zetu zinakabiliana na changamoto za msingi ikiwemo hali mbaya ya

upatikanaji wa dawa na vifaa, uchakavu wa majengo, uchache wa

wafanyakazi, kuwepo kwa madeni makubwa ya maji na umeme, kukosekana

kwa uzio katika vituo vya afya, walinzi na kadhalika.

Mhe. Naibu Spika, Kamati inaitaka serikali kuisadia wizara katika

kukabiliana na changamoto hizi. Kamati imeweza kushuhudia uchakavu na

ufinyu wa majengo katika hospitali zetu za vijiji na wilaya. Kwa upande wa

Hospitali ya Vitongoji Pemba, maabara, wodi na nyumba za madaktari

zimekuwa ni chakavu na hali ya upatikanaji wa dawa na vifaa sio mzuri.

Mhe. Naibu Spika, Kamati inaona kama kweli ile azma ya serikali ya

kuzipandisha hospitali za vijiji kuwa za wilaya na zile za wilaya kuwa za

mkoa inafikiwa, lazima serikali ihakikishe inaongeza fedha, majengo, vifaa na

vitendea kazi katika hospitali hizo.

Mradi wa Kuimarisha Huduma za Afya Wilayani.

Mhe. Naibu Spika, utekelezaji wa mradi huu unategemea ufanisi mkubwa wa

Timu za Afya za Wilaya pamoja na mfumo ulioanzishwa na wizara wa

kuendesha kazi za timu za wilaya ambapo Mfuko maalum wa pamoja wa

fedha (District Health Services Basket Fund) hutumika katika kuwapatia

fedha timu hizo.

Page 80: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

80

Kamati imegundua kuwa utaratibu unaotumika wa kuwapatia fedha Timu za

Afya za Wilaya bado haujafahamika kwa timu zewenyewe na hivyo

kupelekea timu hizo kukosa fedha kwa wakati. Kamati inaiomba wizara

kuendelea kutoa elimu juu ya mfumo uliyoanzishwa ili maafisa wa timu za

afya za wilaya wapate fedha kwa wakati na pia wapewe madaraka ya

kuzitumia fedha kwa kufanikisha kazi zao.

Mhe. Naibu Spika, timu za afya za wilaya zimeweza kufikia vituo mbali

mbali vya afya na kuona utekelezaji wa huduma zinazotolewa katika vituo.

Mbali na jitihada za kufikia vituo hivyo, timu hizo ziliweza kugundua

changamoto zilizopo kama ufinyu wa vituo, upungufu wa wafanyakazi,

kukosekana kwa uzio katika vituo, madeni makubwa ya umeme na maji,

matokeo ya uvamizi na wizi na ukosefu wa vifaa tiba.

Mhe. Naibu Spika, Kamati inaiomba Serikali kuisaidia wizara katika

kuzitafutia ufumbuzi changamoto hizo ili hatimae huduma za afya za wilayani

ziweze kuimarika.

Hitimisho

Mhe. Naibu Spika, Wizara ya Afya kwa bajeti ya mwaka 2012/2013 imepata

mafanikio katika baadhi ya maeneo huku ikiwa bado baadhi ya maeneo

yanahitaji kufanyiwa kazi. Kamati yetu kiujumla haijaridhika kabisa na

uingizwaji wa fedha katika Wizara ya Afya kwa matumizi ya kazi za kawaida

na kazi za maendeleo. Uingizwaji wa fedha usioridhisha unaendelea

kuikwamisha wizara katika kutekeleza majukumu yake. Hivyo Kamati

inaiomba Serikali kuipa kipaumbele wizara kwa kuingizia fedha ipasavyo ili

iweze kutekeleza majukumu yake.

Mhe. Naibu Spika, baada ya maelezo hayo, nawaomba Wajumbe wenzangu

wa Baraza lako Tukufu, kuidhinisha makadirio ya mapato na matumizi ya

mwaka wa fedha 2013/2014 jumla ya Tshs 21,318,000,000 kwa kazi za

kawaida, ruzuku, mishahara na maposho na Tshs 6,333,000,000 kwa kazi za

maendeleo.

Mhe. Naibu Spika, nawashukuru sana kwa kunisikiliza na kwa niaba ya

Kamati naunga mkono hoja na naomba kuwasilisha. Ahsante sana. (Makofi).

Mhe. Jaku Hashim Ayoub: Mhe. Naibu Spika, kabla ya yote sina budi

kumshukuru Mwenyezi Mungu aliyeniwezesha kusimama hapa na kuweza

kutumia pumzi zake alizoweza kuniazima.

Page 81: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

81

Baada ya hapo Mhe. Naibu Spika, nataka nimshukuru Mhe. Rais wa Zanzibar

Dr Ali Moh'd Shein kwa kuwajalia wananchi wake wa visiwa vyake Unguja

na Pemba kwa kuthibitisha hilo Mhe. Naibu Spika, hata katika uteuzi wake

wa Mawizira sijui karibu nane au kumi Wizara ya mwanzo alianzia ni Wizara

ya Afya si kama herufi imeanzia (A), hii ni muhimu kwa wananchi wake wa

Zanzibar.

Ushahidi wa hilo Wajumbe wako humu katika Baraza hasa mimi mmoja

ambaye nilikuwa sipati jibu kwa muda mrefu suala la ada ya uzazi. Nilikuwa

nikizungumza kwa muda mrefu na nikathubutu kusema ndani ya Baraza hili

kuna watu wanaweka vitu vyao rehani ikiwemo bangili, simu zao za mkononi,

vyombo vya dhahabu hospitali chini pale ili kupata vitu vya kwenda

kujifungua. Lakini majibu nikayapata hapa mbele kwa Naibu Waziri

hayaridhishi lakini namshukuru Mhe. Dr Ali Moh'd Shein kulipitai hilo na

akaliona suala la ukweli kwa kujali wanancchi wake na kuweza kuliondoa.

Namshukuru sana.

Mhe. Naibu Spika, itakuwa si mwingi wa fadhila kama sijakushukuru wewe

kwa kunipa nafasi hii kuwa wa mwanzo kuchangia kwa siku ya leo.

Mhe. Naibu Spika, kabla ya kuanza mchango wangu kwanza nitataka maelezo

katika sehemu karibu 15.

(1) Ni lini kitengo cha X-ray kitakuwepo huduma muda wa massa 24, ni

kitengo muhimu. Mimi binafsi nimeshakupigiwa simu karibu mara tatu

mpaka nne karibu saa nne usiku mpaka tano nakwenda pale hapana mtu na

kitengo hichi kinalipiwa hivyo mwanzo nitahitaji maelezo.

(2) Sehemu ya Theater ni sehemu muhimu sana, sehemu ya operesheni

nitahitaji maelezo vile vile ni lini mtaweka madaktari masaa 24

kuhudumia kitengo kile. Kunatokea ajali mara nyingi usiku na watu

wanapoteza maisha yao Mhe. Naibu Spika.

(3) Sehemu ya Uzazi bado ni kitendawili mpaka juzi mimi naondoka

pale Mhe. Naibu Spika, pana matatizo, baadhi ya vifaa kuna upungufu. Kuna

nyuzi hizi hata juzi nilizungumza aina ya viclen, mimi ningeomba

zingetengwa pesa kama milioni moja zikanunuliwa, wizara kama haina pesa

akija kujifungua yule mtu atalipia zile ada ndogo ndogo. Lakini inakuwa

usumbufu mgonjwa kenda pale kaingia saa tisa za usiku mtu kishabeba

mimba miezi tisa kufika pale kitu kile hakipo, ni hatari kubwa hii.

(4) Hii inanisikitisha mpaka hivi sasa asubuhi natoka huku Hospitali ya

Mental. Mimi nataka nielewe ile Hospital au ward, milioni mbili

kwa mwezi wanazopewa Mhe. Naibu Spika, ni ndogo sana. Hizi

milioni mbili zigawe kwa mia si zitakuwa sh. 700/= tu kwa siku

atakula kweli mgonjwa yule, si tunawaumiza sisi wenyewe hizo

Page 82: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

82

shilingi milioni mbili Mhe. Naibu Spika, hazifiki kwa wakati.

Nitahitaji maelezo hapo Mhe. Waziri.

(5) Kuna upungufu wa walinzi na hicho kimekuwa kilio cha muda mrefu

hata kwenye kamati iliyoongozwa na Mhe. Mwenyekiti mtetezi wa

wanyonge Mhe. Hija Hassan Hija tulitembelea na suala hilo

tukalikuta na tukatoa maagizo.

(6) Risk Allowance za madaktri Hospitali ya Mnazi Mmoja tumepiga

kelele muda mrefu nazo hatujapata taarifa hadi muda huu. Wale watu

wanafanyakazi katika hali hatarishi.

(7) Kuna course za madaktari leo mwezi wa nne mpaka sasa hivi Mhe.

Naibu pika, bado hawajatiliwa kweli ndio wataweza kufanyakazi wale kwa

moyo mkunjufu wala sibahatishi atakapokuja hapa atanieleza Mhe. Waziri.

(8) Jengo la Kitengo cha Macho ni bovu Mhe. Hija Hassan Hija alipiga

kelele sana hapa na hivi sasa kunahatarisha usalama wa lile jengo lenyewe

lilivyo, na hili nitahitaji maelezo.

(9) Mhe. Naibu Spika, mgonjwa anapofika pale kunako sehemu ya

kupokea mgonjwa panakuwa na vigari vya kupakiwa mgonjwa na kupelekwa

juu, leo kuna kigari kimoja tu na hakiendi. Mhe. Naibu Spika, shilingi ngapi

kigari kile kinahitaji au tuwaajiri watu wenye nguvu wachukue wagonjwa

kwa mikono yao wawapeleke juu kule. Nitahitaji maelezo hapo.

(10) Hospitali ya Mnazi Mmoja tangu ilipojengwa mwanzo wake mpaka

leo yale madirisha yanatia huruma yanahitaji bajeti ya shilingi ngapi

ukapita pale chini unamuona mgonjwa anachungulia.

(11) Lini Hospitali ile ya Mnazi Mmoja itakuwa inategemewa kuitwa

hospitali ya Rufaa lakini mimi naona kama ni ndoto.

(12) Ningeomba watendaji wakuu wa Hospitali ya Mnazi Mmoja

wakiongozana na Waziri mwenyewe na Mhe. Naibu Waziri, Katibu

hebu wafanye siku wawapitie wale wagonjwa wakawakague mle

wakaona tatizo ni nini. Aibu Mhe. Naibu Spika, utakaa tu na ma-files

yako juu ya meza yako huwezi kufanya kazi namna hiyo ulifuate file

machozi. Pahali panatia huruma Mhe. Waziri, Naibu Waziri, Katibu

Mkuu na majuzi magharibi saa moja au hivi mbili taa moja

wanatumia madaktari wawili, daktari anatoka pake anakwenda kwa

mweziwe kukaa kufuata taa, bulb imeungua kiza, utendaji kwa kweli

mbovu wa Wizara ya Afya haya mengine hayahitaji bajeti ni

kujituma tu na kujitolea.

(13) Kamati imepita Mhe. Naibu Spika, niliagiza watafutiwe usafiri wa

basi wale mpaka leo hakuna.

Sasa sehemu yangu itahitaji maelezo Mhe. Waziri sasa nitakwenda kwenye

mchango wangu.

Mhe. Naibu Spika, utaratibu unaofanywa katika Hospitali ya Mnazi Mmoja,

utaratibu huu ni mzuri unasaidia kupunguza msongamano katika hospitali.

Tatizo linakuja katika Vituo vya Afya, hivi zitatoa huduma vipi wakati

Page 83: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

83

vitendea kazi havina. Vituo havina mahitaji ya huduma za saa 24 si kutiana

changa la macho Mhe. Naibu Spika, huku. Tufanye jambo tuambizane

wananchi wanatusikia huku usije kufika hapaliwi tukadanganyana. Mtu

anatoka kwenda Mnazi Mmoja anafuata daktari na akifika hayupo kenda kula

mbatata za urojo nje.

Jambo jengine hawa wanafunzi wa Chuo cha Afya kufanya majaribio kwenye

miili ya wagonjwa kama ni majaribio hichi kitu ni hatari, kufanya mazoezi ya

vitendo kwa wagonjwa hii hatari Mhe. Naibu Spika.

Mhe. Naibu Spika, nije kwenye Kitengo cha Dharura. Mpaka sasa Hospitali

ya Mnazi Mmoja haina kitengo cha haraka na dharura. Hili ni tatizo Mhe.

Naibu Spika, wagonjwa wanapopata ajali mshituko wa moyo wakiletwa hapo

wanasubiri masaa kadhaa bila ya kutokea daktari, hayo hayataki hata tochi

Mhe. Naibu Spika, hii inatokana na kutokuwepo kitengo maalumu cha

kushughulikia wagonjwa wa dhahura. Mhe. Waziri atueleze ni lini hospitali

itakuwa na kitengo cha huduma ya dharura.

Nije katika utaratibu wa ulinzi katika Hospitali ya Mnazi Mmoja huu ni wa

kupongezwa na wa kupigiwa mfano. Lakini kampuni gani iliyopewa jukumu

lile na utaratibu wa kupewa kazi ya ulinzi inakuwaje pale. Leo tuna vikosi

vyetu vingeweza kulinda ili kupunguza gharama. Bajeti yenyewe iliyoko

Wizara ya Afya ni ya kusikitisha na kutia huruma na ningeomba sana

Wajumbe wenzangu mimi nimechangia mwazo nina sababu zangu.

Lakini kwa kweli haikidhi tusiwalaumu tu watendaji hawa ndio ukweli

usiofichika, tutamsukumia makombora Mhe. Waziri, Naibu Waziri, Katibu

Mkuu lakini Serikali haiko makini kwa suala hili. Tutapiga makelele mpaka

tutachoka. Hawawezi kulaumika Wizara ya Afya tunawabebesha mzigo

ulikokuwa si wao lakini wapewe nyenzo. Leo kweli zimekatwa pesa za meli

haielekei hasa. Nilipiga kelele sana hapa lakini na Mwanyezi Mungu

alipitisha rehema zake yakajakuonekana ukweli wake, Mwenyezi Mungu

amrehemu Mhe. Hassan Mtondoo amlaze mahali pema peponi naye alipiga

kelele sana hapa.

Mhe. Naibu Spika, ukurasa wa 87 Kazi za kawaida Ruzuku bilioni 6.3 ni kazi

za maendeleo. Hii kweli Wizara ya Afya ni Wizara nyeti kwa nchi hii.

Waheshimiwa Wajumbe tusiwalaumu sana wafanyakazi wa wizara hii, hoja

mimi naomba tuirudishe Wizara ya Afya wakajipange tena.

Mimi si mgeni wa suala hilo nimeshapata majukumu na nishatukanywa kwa

wizara hii. Mwaka juzi kuingia tu mwanzo Wizara ya Afya ilirejeshwa

akataka kushitakiwa muandishi wa habari nikawaambia msimshitaki yeye,

nishitakini mimi ndio niliyezungumza shilingi milioni mia tatu wameshindwa

kutenga miaka miwili mitatu, ulitokea mtihani mzito. Kilitokea ugonjwa wa

kipindupindu tumefadhiliwa na watu wawili tu na mmoja ameshatangulia

mbele ya haki na mmoja yupo, hatuwezi kuchukua rehani maisha ya watu na

kuna magonjwa mengine Mhe. Naibu Spika, huwezi kujua wakati gani

yatakuja kuonekana.

Page 84: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

84

Mfano huu Mhe. Naibu Spika, Wizara ilipanga kutumia shilingi bilioni 5.7

kwa kazi za kawaida na bilioni 14.1 kwa mishahara na posho ni bilioni 6.3

kwa kazi za maendeleo, katika Mfuko Mkuu wa Serikali. Wakati ruzuku za

wahisani ni bilioni 1.3 Mhe. Naibu Spika, ukiangalia fedha zilizotengwa za

bajeti kwa mwaka 2012/2013 kiwango cha fedha kilichoingizwa utaona

Wizara ya Afya ina tatizo kubwa la Fedha wanazoomba katika makisio ni

ndogo.

Mfano kiambatanisho namba 17 Idara ya Mfamasia Mkuu wa Serikali,

makadirio ni bilioni 1.5 hadi Machi imeingiziwa milioni 271.4 sawa na

asilimia 17.55. Idara ya Utumishi na Uendeshaji Pemba makadirio shilingi

mia moja sitini na tano milioni, hadi Machi wameingiziwa shilingi milioni 64,

hebu nambie Mhe. Naibu Spika. Mkemia Mkuu Pemba milioni 20 makadirio

hadi Machi kaingiziwa shilingi nne laki tisa. Tutakwenda kweli, sawa na

asilimia 24.6.

Idara ya Mipango Unguja makadirio ni milioni mmoja thalathini na mbili hadi

Machi wamepewa shilingi milioni 41.3. Bajeti hii tunapitisha na posho na

vikao lakini matumizi ya kuwezesha kuondoa kero katika huduma ya afya

bado ufumbuzi haujapatikana.

Mhe. Naibu Spika, ripoti ya Utelezaji wa Malengo ya Wizara katika kipindi

cha Oktoba mwaka jana inaonesha wahisani wameanza kuondoka na hili ni

tatizo kubwa, litaloweza kutu-cost sisi. Sasa hivi wahisani wameshaza

kufunga virago ambao walikuwa wachangiaji wakubwa wa madawa.

Mhe. Naibu Spika kuna ripoti hii ambayo ni ya kusikitisha Ripoti ya

Utekelezaji wa Malengo Wizara ya Afya katika kipindi cha Oktoba mpaka

Disemba katika mwaka uliopita jumla bilioni 1.2 zilihitajiwa hazikupatikana

katika mfuko, badala yake zilipatikana shilingi mia 530 milioni sawa na

asilimia 25, kiwango ambacho Mhe. Naibu Spika, ni kidogo sana. UNICEF

walikuwa wachangie shilingi milioni mia moja na sitini milioni hawakutoa

kitu, Global Fund hawakutoa kitu, DANIDA walikuwa watoe shilingi bilioni

1.1 wametoa shilingi milioni mia 500 na DANIDA nasikia wako njiani mwaka

2014 wanaondoka.

Wizara hapa lazima iongeze pesa katika kitengo cha madawa. Kama

hatukuwa makini tutapiga makofi tu hapa tutakuwa tunabeba jukumu.

Kitengo hichi kiongezwe mara mbili kutokana na bajeti iliokuwepo hivi sasa

lazima iongezwe mara mbili. Vyenginevyo narudia tena yale yale

tutawalaumu watendaji wa Wizara ya Afya, Waziri, Naibu Waziri, Katibu

Kuu na Wakurugenzi bila ya kuwa na nyenzo za kazi hawawezi kufanyakazi

hawa.

Lakini jambo la kusikitisha Mhe. Naibu Spika, kama wanavyosema

Waswahili kuwa anayebebwa na yeye mwenyewe hujikaza. Serikali nao hapa

ilitakiwa ichangie hadi Disemba shilingi milioni 150 lakini kwa mshangao

imetoa milioni 30 tu. Ndipo niliposema kwamba anayebebwa naye hujikaza.

Serikali ilikuwa inatakiwa itoe mfano na anayekuja naye aone haya.

Page 85: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

85

Mhe. Naibu Spika, mfuko huu ndio unaotoa huduma muhimu za tiba hasa za

Chanjo za Mama Wajawazito na Watoto. Kama fedha hazipatikani kutoka wa

wahisani mfumko wa dawa safari hii ukutakuwa mkubwa, upangiwe dawa za

kutosha iwekwe mara mbili bajeti yake.

Mhe. Naibu Spika, ukurasa wa 49 chombo hiki kina umuhimu sana kwa

sababu bila ya wauguzi hospitali inakuwa haijakamilika. Lakini jambo la

kusikitisha wauguzi wetu wamekuwa wakivunjwa moyo na viongozi wetu.

Hivi majuzi tu wauguzi hawa walifanya sherehe lakini cha kusikitisha na cha

kutia aibu hakuna kiongozi hata mmoja wa Wizara ya Afya aliyekwenda

kujumuika nao, si Waziri, si Naibu Waziri wala si Katibu Mkuu si

Wakurugenzi ilikuwa ni siku wa wauguzi duninai. Kwa unyonge mkubwa

sana kwa sababu Mhe. Waziri na Naibu Waziri hawakushirikishwa

hawakupewa taarifa katika maazimisho hayo na kusababisha mgeni rasmi

kugoma kusoma hotuba yake, ilikuwa Maisara juzi hapa Mhe. Naibu Spika.

Nije katika Bodi ya Chakula na Vipodozi ukurasa wa 47. Mhe. Naibu Spika,

nazungumza ukaguzi wa maduka, maghala na chakula, hoteli na mikahawa.

Lakini cha kusikitisha Zanzibar hivi sasa kuna tatizo kubwa la kuanza kuuza

vyakula vilivyokwisha muda wake hasa vya makopo, utakuta pale Darajani

soda tatu za kibati zinauzwa elfu moja badala ya soda ile moja shilingi elfu

moja.

Mhe. Naibu Spika, nije katika hii hospitali yetu inayotaka kuitwa ya Rufaa.

Narudia tena itakuwa ni ndoto. Nije katika sehemu ya watoto. Mhe. Naibu

Spika, hivi sasa kitanda kimoja wanalala watoto watatu, mabomba ya vyoo

hayafanyi kazi sehemu ya watoto hiyo viti vya madaktari hazisemeki. Mhe.

Naibu Spika, kuna dawa hii ya vidonda inaitwa Povidon haipo, kuna dawa ya

mtoto inaitwa Ventolin haipo na muhimu sana mtoto anapopata ajali au

kaletwa mtu pale inaitwa manitol drop haipo katika ward ya watoto. Nirudi

katika sehemu ya ICU pale kuna vein machine ni mbili tu katika sehemu hiyo

ambapo vitanda sita vilivyokuwepo. Ndio nikasema bado ICU haijakamilika

na hiki kitengo ni muhimu mashine hizi za mapigo ya moyo mbili tu ndio

zinazofanyakazi na vitanda ni sita.

Mhe. Naibu Spika: Zimebaki dakika tano.

Mhe. Jaku Hashim Ayoub:Mhe. Naibu Spika, kuna kitengo hiki cha EEG,

hichi kinatoa huduma kwa masaa matatu tu na siku zenyewe ni Jumatatu,

Jumanne na Jumatano, saa 2 mpaka saa 5 hichi kitengo ni muhimu na kazi

zake ni kubwa.

La mwisho Mhe. Naibu Spika, wagonjwa wetu wanapokwenda pale wanapata

tabu kuingia hospitali ya Mnazi Mmoja. Wale wana haki yao hospitali au

wizara iandae utaratibu maalum wa kuwatafutia pahali wakajifiche wale watu

wanapata mvua, jua. Kwa hivyo na hapa nitahitaji maelezo. Mhe. Waziri pale

wasifukuzwe tu wale watu wana wagonjwa wao hawakutaka kuja kutembea

pale shida ndio iliyowaleta pale na matatizo.

Page 86: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

86

Kuna kitengo cha Chanjo, hivi majuzi kimefanya kazi mwaka jana

wafanyakazi hawa walilipwa mshahara huko mashamba walinipa salamu

niwaulizie watapata chochote au hawapati au wamejitolea fisabilillahi. Kwa

hayo, Mhe. Naibu Spika, sitounga mkono hoja hii na Wajumbe wenzangu

nakunasihini sana kila anayeinuka hapa aitizame bajeti hii ni ndogo sana.

Narudia tena tusiwategemee wahisani, wahisani wameshaanza kukunja virago

bajeti hii naomba kila anayekuja hapa tuirudishe mpaka ijipange tena Serikali.

Vyenginevyo tutakuwa tunawatesa wananchi tu tunawalaumu tena watendaji

hawa bila ya kupewa nyenzo hawawezi kufanya kitu. Kila anayeinuka hapa

nasaha zangu asiunge mkono bajeti hii mpaka ikajipange tena Serikali, fedha

ni ndogo walizopewa hizi hazifanyi kitu, tutawalaumu bure na tutaendelea

kulaumu. Ahsante sana Mhe. Naibu Spika. (Makofi).

Mhe. Makame Mshimba Mbarouk: Mhe. Naibu Spika, ahsante sana na

mimi kuweza kunipa nafasi hii niwe mtu wa pili kwa kuweza kuichangia

bajeti hii ya Wizara ya Afya.

Mhe. Naibu Spika, mimi siku zote napenda panapo zuri niseme zuri na

panapo baya niseme ubaya.

Lakini nimshukuru sana Mhe. Waziri wangu leo kwa mara ya kwanza na

kukiri kusema kwamba bado hatujawa na Hospitali ya Rufaa tutapokamilika

ndipo tutakuwa na Hospitali ya Rufaa. Hapo Mhe. Waziri nakushukuru sana

kuwa zile kauli zetu tunazosema kumbe mnakuwa mnaziona lakini

mnatupinga kwa kuwa mawaziri tu ndio wenye uwezo wa kusema.

Mhe. Naibu Spika, mara nyingi sana husema kuna wizara haiko makini katika

utendaji wake kuwatekelezea kwenye bajeti. Hilo ni kweli sio siri wizara hizi

ambazo ni muhimu sana na tuwaongozee sana wizara zile zinazoshughulika

na jamii, kutowaingizia bajeti kamili bila ya kuwapunguzia Mhe. Naibu

Spika, ni kweli inakuwa hitilafu kubwa na kasoro zinajitokeza katika utendaji.

Mhe. Naibu Spika, hilo mimi nakiri na naiomba sana na mtu ambaye

aliyechukua nafasi ya Waziri wa Fedha alione hilo suala, ili waweze

kuwakamilishia hawa watu. Kwa kusema tu Mhe. Naibu Spika, ukweli ulivyo

nimesikitika sana na fungu hili la kasma hii ya likizo. Kifungu 21104 kama

kweli macho yangu naona kama kuna milioni moja ya likizo. Sasa sijui vipi

hiyo Mhe. Naibu Spika, hapa ni kuwachezea na kuwafanyia utani

wafanyakazi wa Wizara hii ya Afya.

Lakini la kusikitisha zaidi labda inawezekana hii ni mia moja lakini kwa

niliovyoona hii ni milioni moja ya likizo amepewa Mhe. Waziri kwa wizara

yake. Sasa hili mimi naomba sana liangaliwe ndio maana nikasema kuwa

tunawatania au tunawachezea hawa wenzetu katika wizara hii. Sasa Mhe.

Waziri utakuja kunisahihisha kama ni milioni mia moja au milioni moja,

mimi binadamu leo sikuvaa miwani, kwa hiyo baadae kifungu hicho cha

kasma cha likizo.

Mhe. Naibu Spika, niende ukurasa wa 11 Kitengo cha Afya Bandarini. Mimi

naomba sana Mhe. Waziri tuwe serious na kitengo hichi kwa kukisaidia vifaa

Page 87: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

87

vyote vinavyohusika vinavyokwenda na wakati vya uchunguzi na upembuzi.

Tunaomba sana hichi tukipe kipaumbele nacho kwa kuwa walinzi wa

kuangalia matatizo ya mwanzo yanayoingia nchini. Sasa kama leo

hatutokuwa na vifaa vya kisasa itakuwa kazi yetu bure na tutasema kuwa

haina maana kitengo hicho kuwepo hapo.

Lakini Mhe. Naibu Spika, ukurasa wa 14 sehemu ya huduma Kitengo cha

Macho. Mhe. Naibu Spika, hawa

Nam.607

IMESAHIHISHWA

Mhe. Makame Mshimba Mbarouk: (Anaendelea) ukurasa wa 14 sehemu ya

huduma ya kitengo cha macho. Mhe. Naibu Spika, niwashukuru sana hawa

kuanzia ma-experts wetu wa hapa Zanzibar pamoja na wataalamu wa Kichina.

Mhe. Naibu Spika, ni mahodari sana na wanajitahidi sana kuwaokoa wenye

matatizo ya macho ambayo yanatuingia mara kwa mara kutokana na vyakula

tunavyokula ni vibovu.

Mhe. Naibu Spika, kwa kweli wanajitahidi sana na wanajaribu kuokoa macho

yetu ili kuweza kuona, lakini ukiiangalia ile sehemu yao ni ya hatari zaidi na

niliisemea sana mwaka jana katika bajeti yao. Hivi sasa nimeambiwa

wameshahamishwa wanapelekwa sijui Kibweni kule. Mhe. Naibu Spika, lile

jengo linakwenda na maji. Pamoja na hayo naomba sana Mhe. Waziri

tuwaangalie kwa ufanisi zaidi na kuweza kuwatekelezea mahitaji yao.

Mhe. Naibu Spika, hiki kitengo ni muhimu na kina zana za kisasa na

hazitakiwi kutembezwa huku na huku, ukizipeleka huku na huku mwisho

zitakuwa na matatizo katika ufanyajikazi wake, hazitakiwi ziondolewe mara

kwa mara, zinatakiwa zikikaa pahali iwe zimekaa pale pale. Hili ni moja

ambalo tuliangalie kwa uangalifu na kwa umakini kabisa jengo hili tufanye

kila hila na ikiwezekana, kuna mafungu mengine makubwa humu

tuyapunguze ili tuwarudishie watu wa Hazina watusaidie kutuwekea fungu

jengine kwa kufuata pale marekebisho ya haraka sana katika kitengo hiki.

Mhe. Naibu Spika, nikiendelea na huduma ambazo zina umuhimu sana hasa

katika hospitali yetu hii, niingie katika ukurasa wa 25 kuhusu Idara ya

Hospitali ya Mnazi Mmoja. Mhe. Naibu Spika, kuna mambo mengi sana

yametajwa humu kwenye kifungu hiki, hospitali ya Mnazi Mmoja yenyewe,

huku kuna Idara ya Hospitali ya Mnazi Mmoja yenyewe.

Page 88: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

88

Nakwenda huku na huku Mhe. Naibu Spika, kote nitachangia, litakalokuwa la

huku wataligawa wenyewe na litakalokuwa la huku wataligawa wao. Mhe.

Naibu Spika, hapa ndipo nilipokuwa nataka kusema, naomba sana niseme

kwa unyonge sana na kutokana na hali yetu. Mimi siendi kule Hospitali ya

Mnazi Mmoja kwa umbea, wala si sehemu ya kusema kuna disko, wala sio

sehemu ya kusema kuna swimming pool, niende nikakoge na wala sisemi kule

niende nikaangalie rusha roho. Mhe. Naibu Spika, nakwenda kule kwa

matatizo ya wananchi wetu, naomba sana nieleweke. Kuna mambo nayaona

mimi mwenyewe kabisa.

Mhe. Naibu Spika, mimi nina uzoefu mmoja, hili nasema Mwenyezi Mungu

kanijaalia. Sikusoma kama walivyosoma watu lakini mtu niletewe wa PhD na

mimi elimu yangu niliyoipata kwenye vibanda vya Baja, basi nitamshinda wa

PhD. Kwa sababu kitu chochote Mhe. Naibu Spika, ukikikubali ndani ya nafsi

yako tayari wewe unapata kujua. Kitu chochote tu Mhe. Naibu Spika,

ukishakikubali basi na kile kitu kinakukubali ndani ya nafsi yako kwa nini

usijue, neno dogo utaweza kulijua kubwa.

Mhe. Naibu Spika, mimi siku moja nilisema hivi, naomba sana nimnukuu

babu yangu Mhe. Juma Duni, alikasirika tu lakini hakutaka kupata ukweli,

pamoja na mimi aliniambia sikutaka ukweli, lakini nakubaliana nayo hiyo ni

sawa. Mimi ni kama wakili namchokoza mtu wangu ili nione points zake

atakuja kunijibu vipi.

Katika Hansard hii nimshukuru sana babu Juma Duni, nilifikiria atanitia

makosani. Amejibu vizuri sana na kwa uangalifu, kumbe yale yote

niliyoyasema yako juu ya alama na yako sahihi. Kwa nini nikasema hivyo.

Mhe. Naibu Spika, Mhe. Waziri alisema humu kuhusu shuka la kuwawekea

wagonjwa kwenye theatre, aliniambia kuwa hivyo vitu vipo na Babu Juma

usidanganywe, nina ushahidi tosha. Nilikuwa na mgonjwa wangu alikuwa na

matatizo ya mkojo, nilikwenda kusikiliza kwa nini leo huyu hakufanyiwa

upasuaji. Jibu likatoka unamuona huyu tunamtoa, imekosekana nguo ya

kufunikiwa. Sasa niseme uongo kwa kutaka nini Babu Juma, wananiambia

hivi na nimeona. Mimi nilifikiria kwa sababu kuna mambo mawili katika

upasuaji, inawezekana presha imepanda labda kwa kitu hicho mgonjwa

anaweza akarejeshwa. Lakini jambo la pili nguo zikikosekana sio kanzu ya

kuchukua nyumbani ukaipeleka pale ukamfunika. Kuna taratibu zake, haiwi

viatu tu katika eneo lile unaambiwa uvuwe, je nguo uichukuwe nyumbani

ulete pale, utaongeza virus.

Kwa hivyo, Mhe. Naibu Spika, naomba sana tunapowaambia hawa mawaziri,

hebu wakae wafikiri huyu mtu kaniambia ni kweli hili jambo au basi tu. Mhe.

Page 89: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

89

Waziri mimi sitaki nafasi yako ya Uwaziri wa Afya, siutaki hata siku moja

nikuambie, wala sitaki nafasi ya Naibu Waziri wa Afya siitaki. Leo babu

Juma ukisema unajiuzulu na naibu wako jiuzuluni, lakini mimi siitaki nafasi

hiyo, si mchezo. Mhe. Naibu Spika, nakuomba sana kwamba watufahamu.

Mhe. Naibu Spika, Hospitali yetu ya Mnazi Mmoja ina mapungufu sana tena

makubwa sana. Mwenzangu alipitia, sasa na mimi naingia ndani. Mhe. Naibu

Spika, kulikuwa na kitanda cha upasuaji kimoja kilikuwa kibovu na

waniambie, nimekiona kitanda kinakokotwa kinaletwa juu. Haya niambieni,

sisi leo tunakusaidieni. Sio vibaya ukiniambia kweli mheshimiwa kitanda

kibovu lakini Wizara ya Fedha, Uchumi na Mipango ya Maendeleo

haikunitilia pesa nikakamilisha, nitakuwa mimi nampigia debe nani?

nakupigia debe wewe kuikamata serikali, kwa nini isikutilie fedha kwenye

jambo hilo. Hamtaki kukubali hivyo.

Mhe. Naibu Spika, leo humu kuna ukurasa ambao Mhe. Waziri anasema

kuwa bado anatafuta fedha za kutaka kununua vifaa vya uchunguzi wa

cancer, hapa ndipo ninapokuja, hili suala linanisikitisha sana. Babu Juma

ukubali na picha ninazo mpaka leo zile mashine naomba bora mkazipeleke

kwenye ma-scrape kule mkauze, nakubaliana hilo kuwa mpaka leo mashine

zile hazina catalogue, catalogue iliyoletwa hailingani na mashine. Babu Juma

unaogopa nini?

Juzi mama Waziri pale Bi. Fatma Mjasiri alikubali nilipomchokoza suala

kama hili kwa walemavu dawa zao zimechakachuliwa. Akakubali, akawa

wazi pale. Kwa hivyo, leo nataka uwe wazi na wewe. Amekwenda Makamu

wa Kwanza wamempiga changa la macho, amekwenda Makamu wa Pili

mmemdanganya, bado mpaka leo mashine zile Mhe. Waziri kubali kosa

liseme na likubali kuwa kweli alipewa mtu tender siye ambaye ni maalum

kwa masuala kama yale, haya ndio yanayotuuma sisi. Unaambiwa mashine

zimechunika, mashine zikachunike mpaka leo zisifanye kazi, tia rangi kama

zimechunika ili zifanyekazi.

Mhe. Naibu Spika, nataka nikuambia sasa hivi sijui ni mara ya ngapi mimi

nalipa fedha ya kwenda kuchunguzwa wananchi wangu wa Jimbo la Kitope.

Mimi naomba sana Mhe. Waziri kama hamtaki mimi nije kule hospitali basi

nendeni Jimbo la Kitope, kawaambieni huyu mtu hatumtaki asije hospitali

kuwauguzeni, tutakutibuni sisi, basi mimi sitofika hospitali. Lakini

haiwezekani nione fedha za wafadhili zinaletwa kwa makusudio ya

kuwasaidia wananchi wetu waliokuwa katika hali ngumu, halafu baadae watu

tu wakajichumie matumboni wakila, mimi sikubaliani na Babu Juma.

Page 90: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

90

Babu Juma mimi hili silikubali kabisa tena munipe sababu maalum kubwa

sana, pamoja na kuwa wewe umeniambia kuwa nithibitishe rushwa. Hapa

automatically sio lazima rushwa useme fulani, mpaka leo hii mwaka jana

naisema hadithi hiyo hiyo na wewe unaniahidi kuwa utachukua tume kutoka

Dar es Salaam na mimi utaniita pale niangalie. Je, umeniita, hujaniita. Sasa

mimi nitasema nini, nitasema rushwa ipo, kwa nadharia hiyo nitasema rushwa

ipo. Lakini kwa nini Mhe. Waziri asiitwe yule mtu aliyeleta vile vifaa

tukamwambia hivi, bwana wee! vifaa havijakamilika, kuna visu hamna na

kuna kitu fulani hamna katukamilishie, kwani mnaona tabu gani kama sio

nadharia ya rushwa, kwa sababu atawaambia wale nipeni na mimi

nilichokupeni asilimia 10, ndio ugumu na mvutano wenyewe uko hapa. Babu

Juma usione tabu njoo niambie Mwenyezi Mungu atakupa fungu lako, usione

tabu usiwaweke hawa watu wabaya.

Sasa hayo ndio tunayolalamika sisi wananchi tumeshika msahafu pale na

tukasema kuwa tutawatendea wananchi kwa kila haki yote, Ewe Mwenyezi

Mungu nisaidie, ogopa hiyo na leo ulianza kwa Bismillah. Sasa nitaomba

ulianza kwa kutaja jina la Mwenyezi Mungu kuwa ulisema ripoti yako ni ya

uhakika na utajibu maneno ambayo ni ya uhakika moja hilo. Naomba sana

Mhe. Naibu Spika, tuweke kanuni kando kama itawezekana zile mashine

ziletwe na zikiletwa hapa kama zikiwa complete mimi naomba Mhe.Naibu

Spika, nitajiuzulu niko tayari kuliachia jimbo, ziletwe hapa mashine,

wanasheria kama wapo, hiyo sheria kanuni kuweka kando mashine ziletwe,

sasa naomba Baraza lako tukufu Mhe. Naibu Spika, mashine ziletwe ndani ya

ukumbi huu ili tuone nasema kweli au fitna tu, utaniangalia Mhe.Naibu Spika,

angalia hilo suala.

Mhe. Naibu Spika, sasa niende katika insulin. Leo nimekuja na quality za

insulin ninazitoa kwa heshima yako. Hii insulin ambayo waliyoizoea

wagonjwa na hii insulin ambayo tumeipigia kelele, hebu iangalieni sample

nyie wenyewe mtaona ipi big quality, materials na vitu viliomo humu

automatical utaona, leo nasema hii hapa. Mimi nauliza kitu kimoja

Mheshimiwa wangu hapa nakwenda kidogo kidogo sasa hivi. Mhe. Naibu

Spika, kule kuna kitengo maalumu, mimi juzi nilivyosema sikimtaja daktari

gani anayehusika sikusema katika Hansard yangu tafuteni lakini nilisema kwa

uchungu tu. Mimi naamini sababu zipi Mhe. Waziri, ukaitisha tenda bila ya

kumuona daktari muhusika na wagonjwa wako ukawaambia jamani eeeh!

tunatoa tenda ya insulin ambayo sasa hivi na ile ya zamani hatuitaki tena, ni

sababu zipi uje unipe sababu.

Mhe. Naibu Spika, mimi nashangaa sana, utakuta mtu engineer wa nyumba,

engineer wa kutengeneza barabara za reli, wewe unataka kutengeneza

barabara, unafikiria unakwenda kuwauliza wale engineers wa nyumba na

Page 91: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

91

engineer wa reli utapata jibu, hupati jibu hata siku moja, kwa sababu kuwa

wale sio specialist wa mambo kama yale. Naomba sana Babu Juma

wasikuchanganye nisikilize mimi. Unajua sasa hivi hii dawa imeshaathiri

watu na tena nakwambia sikwambii kwa uficho na watafute hawa wazee

wako tayari hata ukiwapigia simu, hii dawa imeshawaathiri watu na pale kwa

nini nyinyi mnataka mtu akenda kuchukua dawa aandike namba ya simu kwa

sababu gani, haidhuru ndio utaratibu wa kuchukua dawa, lakini kwa nini?

Mhe. Naibu Spika, naomba sana Mhe. Waziri Babu Juma sikupingi sana

lakini naomba sasa nisome Hansard yako kama hivi;

"Mhe. Spika, naomba niwaeleze na nimueleze Mhe. Mshimba

kwamba hao aliowaeleza hawa kwamba ni mabingwa wa tiba hii ya Dr.

Kaushid na Professor Sawi niliwaita mimi"

Mhe. Naibu Spika, naomba unisikilize kwa makini hapo. Narudia tena hii ni

Hansard ya Mhe. Waziri wa Afya alipokuja kunijibu. Mhe. Waziri alikubali

kwa maana hiyo kuwa kweli kikao cha tarehe 12 kilikuwepo, nimshukuru

kwa hilo. Anasema aliwaita yeye mwenyewe kutafuta ushauri wa kitabibu,

hawakuitwa na daktari wa kisukari kama ilivyoelezwa. Mimi sikusema hivyo.

Lakini sawa na iwe hivyo hivyo, nilipofanya kikao hicho na wataalamu wa

wizara ambao nao ni madaktari kama huyo wa kisukari akiwemo Katibu

Mkuu mwenyewe na Mkurugenzi wa Hospitali ya Mnazi Mmoja na daktari

wetu huyo wa kisukari wote walikuwepo wakati wa mjadala wa Dk. Kaushid,

aliulizwa swali la moja kwa moja. Je, wewe mtaalamu wa tiba dawa hii inafaa

au haifai. Dk. Kaushid alishindwa kutupa jibu la moja kwa moja kwamba

haifai. Hakutoa jibu la moja kwa moja kuwa haifai au inafaa. Lakini sasa

sikiliza kitu chengine kinakuja.

Isipokuwa alisema kwa baadhi ya nchi kama USA, Uingereza na WHO

hawajathibitisha. Sasa si ndio walimwengu hao, si ndio wenye nchi hao WHO

nani asiyewajua, USA nani asiyeijua, Uingereza nani asiyeijua. Amekiri yeye

mwenyewe babu yangu namshukuru sana kwa maelezo yake ya Hasarnd hii

humu. Lakini naendelea na kikao baada ya kikao tulimuomba atuletee ushauri

wake kwa maandishi. Alikaa kimya hata baadae kumuhimiza mara mbili.

Namshukuru sana Babu Juma Duni, alimuhimiza huyo Professor anasema

kuwa baada ya mkutano wake na mimi nilimuomba aniletee ripoti yake,

mwishowe aliniletea ripoti hiyo kwa mtandao na wala hakuitia saini na ndio

maana Mhe. Mshimba aliyopewa na anaitumia kwamba ndicho kielelezo cha

udhaifu wetu wa kukataa ushauri wa bingwa.

Babu Juma umefanya haraka Mhe. Waziri, ungesubiri ile barua ya mtaalamu

alete

Page 92: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

92

Mhe. Naibu Spika: Umwite Mhe. Waziri.

Mhe. Makame Mshimba Mbarouk: Aaah! Babu Juma, samahani.

Mhe. Naibu Spika: Babu Juma mwite mitaani huko.

Mhe. Makame Mshimba Mbarouk: Ahsante. Mhe. Waziri nakushukuru

sana kumbe hujahamaki, naendelea na maelezo yangu.

Mhe. Naibu Spika, mimi namuambia Mhe. Waziri ilikuwa yeye asubiri

kwanza.

Kifungu chengine,

"Mhe. Spika, baada ya kupata maelezo ya kitabibu ya wizara iliomba

tena ushauri kwa wasimamizi wa kujadili dawa ya Serikali ya Muungano

hapa kwetu Zanzibar, wao kwa pamoja walijibu kwamba dawa hii

imesajiliwa".

Hee! huyu msimamizi ndio professor. Kumbe kapata ushauri kwa

wasimamizi sio kwa wale wataalamu aliowaita yeye mwenyewe kwa mujibu

wa kupata jibu. Hapa namuomba sana Mhe. Waziri sina nia mbaya na yeye,

sitaki nikuzuilie fungu lakini hapa nakuzuilia fungu na mshahara wako

nauzuia kutokana na maelezo haya yameniudhi sana Mhe. Waziri Babu Juma.

Samahani nimekuzoea babu yangu.

Mhe. Naibu Spika, hapa ndipo nitakapoweza kuzuia fungu ili kuweza kupata

ufafanuzi wa kutosha. Mhe. Naibu Spika, nina wagonjwa ambao tayari dawa

hiyo imewadhuru, nikisema Bwana Juma Ame Juma wa Chukwani na yeye

dawa hii imemdhuru, Bibi Safia Mohamed miaka 40 wa Kikwajuni na yeye

dawa hii imemdhuru na amesema kuwa dawa hii hatoweza kuitumia kuntum.

Naomba sana Mhe. Waziri usiambiwe jambo ukalikubali moja kwa moja bila

ya kupata ushauri, nakuomba sana ukae na washauri wako husika wataalamu

wetu kabla hawajatukimbia ili ukae nao kuliko watu wengine.

Kwa sababu Mhe. Waziri tulichokifanya kimoja serikali ambacho ni kibaya

sana Mhe. Naibu Spika, Mkurugenzi wa Mnazi Mmoja ni specialist wa

mambo ya usingizi, tuna Surgery ambapo yeye ni Mkurugenzi, tuna Katibu

Mkuu ni professor, ni daktari anajulikana wapi na wapi. Leo tunakwenda

kumpa Ukatibu Mkuu, hapa tumefanya kosa moja kubwa sana serikali, lakini

ndio mambo tumefanya tu na ukiangalia hospitalini hatuna tena wengine

baada ya hao, sio kama hatuna hatuna. Unafikiria watakalia wapi, watakalia

juu kwenda kwa serikali wale wenzao watawakandamiza.

Page 93: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

93

Mhe. Naibu Spika, kuhusu mafao ya madaktari wetu. Wenzetu Bara sasa hivi

wanapata mishahara mizuri, naomba sana Mhe. Waziri aangalie mafao yao.

Mhe. Naibu Spika, kuna matatizo ya orderlies na nurses. Hawa huduma ya

kwanza wanaanza wao, halafu baadae ndio anaitwa daktari muhusika.

Mhe. Naibu Spika, kuhusu risk allowance yao hawa, mwenzangu kishaisema

sitaki niirejee. Kuna watu wanapata matatizo na wengine wanapata TB katika

utibabu mpaka leo haki zao wanashindwa kupewa. Mhe. Waziri tunaomba

sana hilo suala lazima Mhe. Naibu Spika

Mhe. Naibu Spika: Bado dakika tano.

Mhe. Makame Mshimba Mbarouk:Namalizia. Mhe. Naibu Spika, nilisema

kuwa ma-nurses, ma-ordelies bado na madaktari wenyewe tugeuke, hizi

scheme of services bado hazijakidhi haja kwa wao wana kazi kubwa,

wanafanyakazi masaa 24 na wanajitahidi kadri ya umaskini wao pamoja na

kuwa hawana vitendea kazi. Naomba sana Mhe. Naibu Spika, kwamba hili

suala liongezwe fungu ili Mhe. Waziri aweze kuwasaidia hawa watu ili

wapate kufanyakazi kwa uangalifu sana.

Mhe. Naibu Spika, inasikitisha sana kama hamtowaangalia hawa watu wetu.

Sasa hivi niwashukuru sana kuwa kuna baadhi ya nguo zimeoneshwa kuwa

zimerudishwa kwenye makontena. Lakini Mhe. Waziri vyakula bado, sijui

kama ule unga mpaka leo kama umesharejeshwa? Mimi siogopi kusema

bwana, kama ule unga haujaondoshwa bandarini kauondoweni bwana, mimi

siogopi kusema kwa sababu nawatetea wananchi, wananchi ndio wamenileta

hapa ili niwatetee wao, tena mwenye kununa, asiyenuna shauri yake. Lakini

nitasema jambo la ukweli, kama ule unga haujaondoshwa basi uondoweni,

kwa nini mmeweza kurudisha mitumba ya nguo na mitumba ya friji kwa

sababu haiko katika quality, mshindwe kuuondoa unga, uondoweni bwana,

mimi siogopi kabisa, nasema uondoweni mara moja tusije tukafa

Wazanzibari. Wazanzibari tunapata maradhi kutokana na vitu sio standard,

ndio maana cancer zinakuwa nyingi, mnatafuta nini, msitafute kitu hamna

utafiti wa kutafuta. Vyakula vibovu vimekwisha muda wake, mnatuleta tule

hapa Wazanzibari tufe. Sasa unafikiria vipi, ni lazima hiyo tunasema kwamba

ishirikishwe.

Mhe. Naibu Spika, kwa kukidhi muda wako, mimi naomba sana kuwa

wananchi wangu waangalie wale member wa sukari, hii ndio tunaitaka, hii

chukuweni wenyewe, tunaitaka hii dawa, hii dawa ndio quality, dawa

iliyomzowea mwenyewe mgonjwa anaitaka hii, msimlazimishe mwachieni

Page 94: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

94

huru, waachieni wenyewe watumie, Usiitishe tender bila ya kuwaita wenyewe

wanaohusika, hilo ndio kosa lenyewe Mhe. Waziri.

Mhe. Naibu Spika, kwa hayo machache naizuia bajeti hii, sitomruhusu Mhe.

Waziri atumie. Mhe. Waziri sitomruhusu atumie mpaka anipe maneno

mazuri, asikubali kufuata maneno ya wataalamu ajiangalie mwenyewe katika

qualification zake. Maana yake wakati mmoja Mhe. Naibu Spika, ngoja

kidogo alikuwa akipenda kusema zamani madudu, kumbe madudu yamo

kwenye wizara yake. Lugha hii akipenda sana kuitumia Mhe. Waziri na mimi

nilikuwa nikiwapenda zamani watu wangu hawa watatu. Mhe. Haji Faki

Shaali wakati ule tukishirikiana naye katika kujibu maneno yake, Mhe.

Abubakar Khamis walikuwa wakijibu vizuri wakati ule.

Sasa na sisi Mhe. Waziri zamu yako kuwa madudu yamo ndani ya wizara

yako. Mhe. Naibu Spika, naondoa shilingi yangu, ahsante.

Mhe. Suleiman Hemed Khamis: Mhe. Naibu Spika, nakushukuru kwa

kunipatia nafasi na mimi kuweza kutoa mchango wangu katika wizara hii

kubwa sana ambayo imepewa majukumu makubwa sana ya utekelezaji.

Mhe. Naibu Spika, niseme kwa ufupi kwamba Wizara hii ya Afya ina

majukumu ya kusimamia utoaji wa huduma za afya, ikiwemo kutoa ushauri

wa wagonjwa, kutoa elimu ya afya na kutoa matibabu. Haya ni moja katika

majukumu ya Wizara hii ya Afya na ni majukumu makubwa.

Mhe. Naibu Spika, mimi nilitegemea kwamba wizara hii kubwa iliyo na

majukumu mazito, nilitegemea kwamba Mhe. Waziri wa Fedha, Uchumi na

Mipango ya Maendeleo tutakuwa naye hapa, kwa sababu kuizungumza

wizara hii, bila ya kuwepo Waziri wa Fedha, Uchumi na Mipango ya

Maendeleo sio jambo zuri, kwa hapa pana matatizo makubwa katika

kuyatekeleza majukumu haya. Kwa hivyo, nasikitika kwamba Waziri wa

Fedha hayupo ili asikie kilio cha watu waliokuwemo humu ndani. Kwa hivyo,

pamoja na kutoa ushauri, pamoja na elimu na utibabu. Pia utakuta kwamba

utibabu huu umo ndani ya nchi lakini pia wizara inahusika na utoaji wa

utibabu wa nje na inaonesha kwamba wizara hii haina ubaguzi, inafanyakazi

zake vizuri bila ya kuwa wanaotaka kuhudumiwa wana ubaguzi wa aina

yoyote, watu wanatolewa huduma sawa kwa sawa, haki sawa kwa

wote.(Makofi)

Mhe. Naibu Spika, inatoa huduma za kinga vile vile na maradhi ya

kuambukiza ambayo ni majukumu makubwa sana, inaangalia pia vifo vya

watoto wachanga ambao haya yanatokana na mama zao wakati wa

kujifungua, wanakabiliwa na matatizo makubwa sana hasa watoto wachanga.

Page 95: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

95

Vile vile wanahitaji katika fedha hii kuwa iwe nyingi lazima kuwe na vifaa

vya kutosha na inavyoonesha baada ya kuisoma hii kwamba katika kupewa

kiwango cha fedha ni kidogo sana hakitoshi kabisa. Hii ni wizara kubwa na

inahitaji fedha nyingi ili kuweza kufanikisha malengo ya wizara hii.

Mhe. Naibu Spika, katika mambo mengine ambayo nahisi yana jukumu

kutokana na maradhi mbali mbali ya homa kali sana, pamoja na hayo mengine

ambayo tumepata taarifa hapa kwamba kesi za Ukimwi katika nchi hii

zimekuwa ni nyingi bado zinaendelea, pamoja na wao kusema kwamba

zinapungua, lakini wakati huo huo bado kesi zinaendelea kwa wingi, pamoja

na kusema kwamba kesi za wagonjwa 6,906 wamesajiliwa kwenye clinic 10,

ambazo sita zikiwa hapa Unguja na nne zikiwa Pemba. Wagonjwa 4,000

wanatumia dawa za ARV na watoto ambao ni wengi sio chini ya watoto 392,

bado wanaendelea kupata matibabu kutokana na mama zao.

Mhe. Waziri hili suala ni zito na ni gumu kabisa. Je, hawa watoto ambao

tayari wamekwishaonekana wanahifadhiwa vipi watoto hawa katika suala hili

zima, maana watoto sio kidogo ambao tayari wamezaliwa 392 ni watoto

wengi sana, ni juhudi gani ambazo zinachukuliwa kuwasaidia watoto hawa

katika maisha yao ya baadae.

Mhe. Naibu Spika, kwa sababu inaonekana kutokana na suala hili ni lazima

wizara isaidie kwa vyovyote vile kutokana na hali hii watoto ambao tayari

wamezaliwa na maradhi haya ya Ukimwi.

Jambo jengine Mhe. Naibu Spika, ambalo nataka nilizungumzie na Mhe.

Waziri kalisema kwenye ripoti yake kuhusu masuala haya ya madawa ya

kulevya, ambayo bado vijana wetu wengi sana wanajiingiza katika mambo

haya na bado inaonesha kwamba vijana hawajaamua kuwacha suala hili.

Suala la madawa ya kulevya linaendelea kwa wingi sana na maambukizo

yanakuwa ni mengi sana. Hapa inaonesha kwa upande wa wanaume ni

asilimia 2.6 wanaendelea na mambo haya na kwa upande wa wanawake

ambao ndio wengi zaidi sio chini ya asilimia 19.3. Hii inaonesha kuwa suala

hili bado siku baada ya siku maradhi haya yanaendelea, au wale vijana

ambao ni injection drug user na hawa pia wako wengi sio chini ya asilimia

11.3.

Mhe. Waziri katika masuala haya kuna mpango gani wa kuweza kuwasaidia

hawa vijana au hamasa gani mnachukua katika kuwasaidia vijana wazidi

kuacha tabia hii ya madawa ya kulevya na kujidunga sindano ambapo

maambukizo yanakuwa kwa wingi.

Page 96: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

96

Mhe. Naibu Spika, tumeambiwa katika ripoti yako kwamba maradhi haya ya

madawa ya kulevya ambapo vijana wanaojidunga sindano wanapata homa

kali sana ya ini. Je, Mhe. Waziri katika masuala haya ni vijana wangapi

ambao wamejitokeza wenye masuala haya ya homa hizi kali za ini.

Mhe. Naibu Spika, suala jengine ambalo nataka kulizungumzia ni maradhi

haya ya ukoma ambayo mara nyingi tunaambiwa bado yako na yanaendelea.

Lakini siku za nyuma katika uchunguzi imeonekana kwamba watu hawa

hawana mambo ya kuambukiza na wameachiwa huru kutembea wanakotaka

na

Nam.908

IMESAHIHISHWA

Mhe. Suleiman Hemed Khamis: (anaendelea) hawana mambo ya

kuambukiza na wameachiwa huru kutembea wanakotaka.

Lakini hapa kwa taarifa zake Mhe. Waziri maradhi ya ukoma inaonekana

bado wapo wamechunguzwa si chini ya watu 97, ambao wamechunguzwa na

kuonekana na maradhi hayo, watu hao kiasi 65 ni wanaume na 32 ni

wanawake. Kwa kweli zamani tuliambiwa maradhi haya hayapo na wala

hayaambukizi.

Mhe. Naibu Spika, namuomba Mhe. Waziri wakati atakapokuja hapa atupe

maelezo kwamba ni kweli kuwa haya maradhi kwa sababu watu hawa

wameachiwa huru kama kule Pemba sehemu za Kinyasini, hawa watu

wanatembea wanachanganyika na wananchi, wanakula vyakula pamoja na

zamani tuliambiwa hawana maambukizo na ndio maana katika haki za

binadamu wameachiliwa wawe huru. Lakini je, hii hali inayojitokeza baada

ya uchunguzi na utafiti inaonekana kwamba watu hawa ni wengi sana.

Kwa hivyo, ni hatua gani ambazo atazichukua Mhe. Waziri juu ya watu kama

hawa ili kupunguza matatizo ya ugonjwa kama huu wa kuambukiza ambao

tuko nao bega kwa bega.

Page 97: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

97

Vile vile ninataka kujua kutoka kwa Mhe. Waziri kupitia kwako Mhe. Naibu

Spika, kwa hapa Unguja tunao pharmacist wengi sana na pharmacies ziko

nyingi sana hapa Unguja na kule Pemba ziko pharmacies pia. Lakini jambo la

kustaajabisha ni kwamba hatuna pharmacist, ambapo sisi watu wa Pemba

hatuhitaji kuwa na pharmacist kule, kwa sababu pharmacies ziko nyingi

lakini wao hawako. Kwa hivyo, hilo Mhe. Naibu Spika, naomba kuelewa na

kupata maelezo japo kidogo.

Mhe. Naibu Spika, kuna maradhi ambayo Mhe. Waziri aliyazungumza hapa.

Kwa mfano, maradhi ya kichocho, minyoo na matende. Sasa hapa katika

ripoti yake Mhe. Waziri alizungumzia kwamba maradhi hayapewi

kipaumbele, yaani hayamo kwenye priority amekusudia nini kusema kwamba

maradhi haya hayamo kwenye priority. Kwa kweli maradhi haya tunayo sisi

binadamu, kama vile maradhi ya matende, minyoo kwa watoto wetu pamoja

na kichocho kwa wale wanaokoga kwenye mito. Mhe. Naibu Spika, kila moja

katika hili ukiliangalia ni zito ambalo linatuhusu sisi na wala sijui taaluma

gani ambayo inayotoka.

Mhe. Naibu Spika, mimi nilitaka kwenye mambo mengi haya ya maradhi

nisingependelea kama pale anapotoa taarifa si vibaya kusema kwamba

television na redio zipo zinatoa maelezo. Lakini mimi naona kuna kitu

ambacho ni cha msingi zaidi ambapo itaweza kutoa elimu ya kutosha kwa

wananchi ili ambayo tuliyokuwa tukitumia zamani kwa njia ya mobile. Njia

hii ndio ya pekee kijiji hadi kijiji kuweza kuwaelezea wananchi kujua nini

tatizo liliopo kwa maradhi ambayo husika. Kwa hivyo, nadhani kuondoka

kwa Mobile Cinema na hili ni suala ni zito na hivi sasa ndio maradhi yanazidi.

Kwa mfano, tunajua hii kichocho ni life cycle and where to break it na

kukatika kwake ni kuondosha makonokono.

Lakini kwenye taarifa zake hakutuambia Shehia ngapi ambazo

zimetembelewa, yaani katika kila jimbo imeelekeza watu wangapi, kwa

sababu kila mahala kuna mito ya kutosha na kuzaliwa kwa makonokono kwa

sababu makonokono wapo wengi na hawa ndio wanaosababisha maradhi ya

kichocho. Kwa maana hiyo, hatujui ni maeneo gani ambayo tayari

yameshatembelewa na watu wamepewa elimu ya kutosha.

Mhe. Naibu Spika, suala la minyoo ni jambo muhimu sana kwa wananchi na

bado taarifa zake kwa wazazi bado halijapewa kipaumbele, namna ya kuwa

na usafi wa vyakula, mazingira na watoto kuweza kuhifadhiwa vizuri.

Mhe. Naibu Spika, nataka kumwambia Mhe. Waziri kwamba suala la

matende kwa kule Pemba halikuonekana upande wa Kaskazini na zamani

tuliambiwa matende yako sana upande wa Kusini Pemba. Je, kwa nchi nzima

Page 98: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

98

hasa imeonekana maeneo gani maradhi haya kwa sababu zamani maradhi

haya yalikuwa yakijulikana kwa maeneo maalum. Kwa hivyo, inawezekana

kutokana labda infection ya mazingira ndio iliyochangia kwamba watu sasa

wanaendelea kupata maradhi haya.

Mhe. Naibu Spika, prevention is better than cure, kuhifadhi ni bora kuliko

kutibu, kwani kutibu ni gharama kubwa sana. Sasa kama tutakuwa na njia ya

kuhifadhi maambukizo ya matende basi itakuwa ni bora zaidi kwa sababu

binadamu yeyote anapopata matende inakuwa hata mwendo unabadilika,

maisha yanabadilika, uwezo wa kufanyakazi hana.

Kwa hivyo, hili ni suala muhimu na Mhe. Waziri ameeleza hapa kwamba

hayakupewa kipaumbele. Mhe. Naibu Spika, namuomba Mhe. Waziri wakati

atakapokuja hapa basi alizungumzie suala hili kwa nini akazungumzia

maradhi haya hayakupewa kipaumbele.

Nikiendelea na mchango wangu sasa naomba nizungumzie kuhusu suala zima

la Kitengo cha Bandarini. Mhe. Naibu Spika, ameelezea Mhe. Waziri

kwamba amefanya ukaguzi wa baadhi ya meli kuhakikisha kwamba mnafika

kwa ajili ya kutoa huduma kwa meli tofauti hapa Unguja. Lakini suala

amelizungumza vizuri sana na wala hakuficha ule ukweli katika kuangalia

suala hili, pia bado linaonekana kwamba kuna baadhi ya vyombo vyengine

hawafuati utaratibu wa kuweka usafi wa meli zao, ambapo inabidi nyinyi

mukafanye fumigations kwenye meli hizi.

Mhe. Naibu Spika, nataka kumuuliza Mhe. Waziri kwamba kwa nini hawa

watu hawataki kufanya usafi wa meli zao na kwa nini watu hawa iwe kuna

ulazima wa kuangaliwa usafi wao, kwani usafi ni wao na wao ndio

wanaolazimika kufanya hivyo. Sasa kama watu hawataki je, upande wake ni

hatua gani ambazo wanachukua kuhakikisha kwamba usafi wa meli zao upo.

Vile vile naomba kushauri kitu kimoja kama inawezekana, kwa sababu wizara

yako ina kazi nyingi za kufanya na hana muda wa kutosha, kwa nini hatoi

mafunzo kwa wale na wao wakapewa namna ya kufanya fumigations katika

meli zao, badala ya watu wake kuondoka na kwenda kuifanyakazi ile,

napenda kutoa ushauri huo kama unafaa.

Katika mambo yaliyozungumzwa hapa kwa Zanzibar matatizo bado

yanaendelea kuibuka kwa wingi, yaani matatizo ya maradhi ya macho. Mhe.

Naibu Spika, suala la ugonjwa wa macho linakuwa ni tatizo kubwa sana na

zamani tulikuwa tunategemea matatizo ya macho ni kwa watu wazima. Lakini

hivi sasa inaonekana kwamba maradhi ya macho kwa watoto yamekuwa ni

Page 99: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

99

mengi sana na suala hili limekuwa ni gumu katika utekelezaji wake, kwa

sababu lina gharama.

Mhe. Naibu Spika, hivi sasa naomba anieleze Mhe. Waziri kwamba hana

daktari bingwa wa macho, je hii ni kweli. Kwa hivyo, namuomba Mhe.

Waziri wakati atakapokuja hapa kufanya majumuisho, basi anieleze hivi ni

kweli hana daktari bingwa wa macho. Hali hii ina maana kusema kwamba

madaktari wa macho mpaka tukapate kutoka Muhimbili, sasa kama hatuna

basi wizara ijitayarishe kwa kuweka madaktari bingwa wa masuala ya macho.

Kwa kweli mara nyingi inaonesha tunasafiria madaktari kutoka Muhimbili au

nchi za nje. Sasa nataka kujua kutoka katika wizara yake ni lini hasa

atajipanga kuona na yeye badala ya kupata watu kutoka nje katika utibabu wa

macho, basi Serikali ya Zanzibar au Wizara ya Afya inahudumia suala hili

kwa watoto na watu wazima.

Jambo la mwisho pia nataka kujua angalau ile kupanda kwa ugonjwa huu wa

macho. Je, unapungua huu ugonjwa wa macho au unazidi kuendelea. Sasa

kama ugonjwa wa macho unazidi kuendelea ni hatua gani ambayo atachukua

zaidi ya kutoa mafunzo kwa watu ambao wanaoathirika na ugonjwa wa

macho, kwa sababu hivi sasa operations za macho wenye watoto wa macho

zimekuwa nyingi sana kuanzia watu wa zima mpaka watoto wadogo.

Mhe. Naibu Spika, pia ninalo suala jengine ambalo nataka kumueleza Mhe.

Waziri kwamba suala la lishe, ambalo hili ni suala la utapiamlo, hali hii

inatokana kwetu sisi ngazi ya jamii. Kwa hivyo, tunataka kujua suala hili la

utapiamlo ambapo lishe haipatikani ya kutosha amechunguza nini katika suala

hili na utafiti gani mkubwa ambao ameufanya na nini anaweza kuwasaidia

wananchi katika suala lenyewe, yaani atawaambia nini wananchi na

amegundua kitu gani, kwa sababu ni lazima katika suala hili la utapiamlo kwa

watoto wetu ni jambo muhimu, kwa sababu hawa ndio nguvu kazi wa kesho.

Sasa ikiwa jamii yetu kubwa ina suala zima la utapiamlo, basi nafikiri suala

hili ni vyema likachukuliwa hatua. (Makofi)

Katika suala la huduma za uzazi na kupunguza vifo kwa akinamama

linaendelea. Lakini inaonesha kwamba huduma hizi kwa kweli ni nyingi sana,

yaani kutokana na idadi ya hospitali zetu tulizonazo nchi nzima, basi hospitali

ni nyingi na kila hospitali hata ndogo unayoifikia wewe tuache hii ambayo

hivi sasa ni kubwa sana, lakini hata hospitali ndogo basi huduma hii

inahitajika. Kwa mfano, katika vijiji vyetu kutokana na kila masafa ya meli

tano hivi sasa kuna hospitali na tunatarajia wazazi watakuwa wanakwenda

katika hospitali hizi.

Page 100: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

100

Je, Mhe. Waziri kupitia kwako Mhe. Naibu Spika, kiasi gani atatusaidia

kuweza kupunguza vifo hivi vya wazazi ambao wanatoka katika maeneo ya

mbali na kuweza kufika katika hospitali ambapo mara nyingi kesi kama hizi

na wala sina haja ya kumficha kwamba zinafanyiwa refer kutoka hospitali

ndogo kwenye hospitali kubwa. Kwa mfano, wazazi waliopo Konde

wanategemea labda Hospitali ya Micheweni lakini mara nyingi wanafanyiwa

refer Mkoani.

Kwa hivyo, ninachotaka kuzungumzia Mhe. Waziri kwa Hospitali ya

Micheweni ni kubwa na mara nyingi sisi tunapata kesi pale Konde ambapo

wazazi wanataka kupelekwa Hospitali ya Chake-Chake. Sasa nadhani ni

vyema na ile Hospitali ya Konde nayo ifikiriwe, kwa sababu akichunguza

yeye mwenyewe basi anajua kwa idadi ya watu tulionao pale Konde, basi

wanahitaji kuwa na gari yao ya kuwasaidia kuwapeleka Chake-Chake. Je, ni

lini Mhe. Waziri atafikiria na Hospitali ya Konde kuwawekea gari ya kuweza

kuwafanyia kesi za rufaa badala ya kupeleka mbali.

Mhe. Naibu Spika, katika suala hili linakuja swali kwa wazazi kuhusu

upasuajia. Kwa kweli mimi nataka kujua tu Mhe. Naibu Spika, kwamba nini

na sababu au chanzo cha kufanyika operation namna hizi kwa wazazi, tuulize

labda ni ukosefu wa damu. Vile vile kama suala hili linajulikana hawa

wanawake mara nyingi wanafika katika Clinic, yaani kila baada ya kipindi

fulani wanaambiwa waje.

Sasa kama kulikuwa na matatizo ya wanawake kwa nini ifikie hadi kufanyiwa

operation sababu hasa huwa nini. Mhe. Naibu Spika, ikiwa kama kulikuwa na

sababu kabla kwa nini mzazi au watu wake waliokuja na mzazi hawaambiwi

wajitayarishe kwa namna kadha mpaka inafika hadi wanawake kufanyiwa

operation. Mhe. Naibu Spika, namuomba Mhe. Waziri wakati atakapokuja

kufanya majumuisho basi anisaidie kunielezea kama ni suala la damu au

linatokana na matatizo mengine.

Vile vile tunataka kujua kuhusu suala zima la maradhi ya kifafa cha mimba

kwa wazazi. Kwa kweli maradhi haya yanakuwa vipi na hayana matibabu na

kwa nini yanatokezea wakati mwanamke anapotaka kujifungua na precaution

gani ambazo mwanamke anatakiwa azichukue kabla hajajifungua na hilo pia

tunataka kulijua.

Mhe. Naibu Spika, katika mambo mengine ambayo nataka nitoe mchango

wangu ambapo linatukumba Zanzibar na nikisema Zanzibar ninamaanisha ni

Unguja na Pemba maradhi ya kisukari. Maradhi haya yamechukua namba

kwa Zanzibar, hivi sasa hata watoto wadogo wanaozaliwa wengi wanakuwa

Page 101: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

101

labda kwa sababu ya urithi kutokana na wazazi wao wenye ugonjwa wa

kisukari, lakini maradhi ya kisukari ni mengi sana hapa Zanzibar.

Je, Mhe. Waziri kupitia kwako Mhe. Naibu Spika, katika utafiti wa wizara

yake ni kitu gani ambacho amegundua hasa na tatizo liko na ikiwa lipo tatizo

tufanye nini. Sasa hii advise kama hii najua labda pengine mara nyengine

unaipeleka kwenye kutoa huduma katika redio au television. Kwa hivyo,

tuelewe kisiwa cha pili kilichopo kule suala la redio na television usilipe uzito

mkubwa sana, kwa sababu hakuna kinachoonekana wala hakuna taarifa na

hiyo television yenyewe haifanyikazi sawa sawa, yaani mara inaonekana na

wakati mwengine haionekani. (Makofi)

Mhe. Naibu Spika, pamoja na kujinasua kwamba huduma nyingi anazipeleka

kwenye redio na television na hizo hazitufiki. Kwa hivyo, je kwa upande

wake kwenye suala hili la kisukari ambalo ni common disease kwa Zanzibar,

je tunafanya nini au tunakwenda wapi Wazanzibari. Kwa kweli hivi sasa ni

wagonjwa wa kisukari pamoja na ugonjwa wa macho yote haya ni matatizo

makubwa sana.

Hata hivyo, sasa naomba nizungumzie kuhusu vyakula ambavyo tunategemea

hawa wagonjwa hasa hasa kwa wagonjwa kuweza kupatiwa hizi dawa

ambazo ni dawa zao wa ugonjwa wa kisukari zinapatikana hapa, lakini wakati

mwengine hazipatikani, maana tunasikia hapa kuna watu wanayo Society au

Chama cha Wagonjwa wa Kisukari, je, suala hili liko vipi.

Maradhi mengine ni kuhusu pressure ambalo pia linahangaisha watu.

Matatizo ya Wazanzibari hivi sasa kila unayemsikia anasema ana ugonjwa wa

miguu, yaani kila wakati watu wanazungumza habari ya ugonjwa wa miguu

inauma na haitembei sawa sawa na hapa tatizo nini.

Mhe. Naibu Spika, tumuombe Mhe. Waziri aina ya nyakula tunavyotumia

pengine inawezekana tayari contaminated au vimeshapitiwa na wakati ama

kuna matatizo ambapo vyakula hivi si vizuri kwetu sisi, basi aweze kutushauri

kwamba vyakula fulani si vizuri na tuweze kutumia zaidi natural foods, yaani

vyakula ambavyo vinatoka katika mashamba.

Suala jengine ambalo nataka kulizungumzia ni mental case, yaani wagonjwa

wa akili. Mhe. Naibu Spika, katika nchi yetu hivi sasa ya Zanzibar, ukitembea

katika miji utawaona vijana wengi sana wamepungua akili, yaani akili

imeharibika na idadi ya vijana hivi sasa inaongezeka barabarani na ni wengi

sana. Kutokana na hali hiyo, tunategemea labda serikali itakuwa na mpango

maalum wa kuwadhibiti hawa vijana ambao wanazurura barabarani ambao

akili zao kidogo si barabara.

Page 102: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

102

Hata hivyo, kwa hapa Unguja namuomba Mhe. Waziri kupitia kwako Mhe.

Naibu Spika, aweze kuitembelea Hospitali yake ya Wagonjwa wa Akili

upande wa wanaume na ule wa wanawake. Kwa kweli hali si ya kuridhisha

hata katika chakula hali sio nzuri. Vile vile vijana wanakuwa ni wengi zaidi

kuliko watu wengine. Kwa hivyo, namuomba Mhe. Waziri suala hili alifanyie

utafiti wa kutosha, kwa sababu naona kama hii Hospitali ya Wagonjwa wa

Akili ni wengi sana kwa pande zote mbili, yaani wanawake na wanaume. Sasa

Mhe. Waziri tupe hasa nini matatizo ya hospitali hii ambapo huduma kidogo

haziridhishi.

Mhe. Spika, tunataka kujua kwa nini Pemba mpaka leo hospitali hii

haijamalizika ni miaka mingi imeombwa hospitali hii na bado hospitali hii

haijapatikana. Kwa kweli suala hili linanishangaza hii huduma kutoka Pemba

kuja hapa Unguja ni nzito sana, huduma kama hii ya mgonjwa wa akili

kumchukua mtu binafsi na kuja naye hapa kwa gharama zake yeye

mwenyewe ni nzito sana.

Lakini zamani ninavyojua mimi Mhe. Naibu Spika, huduma hii ilikuwa kuna

mashirikiano baina ya mzazi mwenye mtoto mgonjwa pamoja na wizara yake

hushirikiana bega kwa bega kumsafirisha kutoka Pemba na kumleta Unguja,

na hivi sasa anaachiwa mzee peke yake.

Suala hili ni zito tena ni gumu sana na linahitaji gharama kubwa sana

kuwasafirisha, kwa sababu huwezi kumsafirisha mgonjwa wa akili mtu

mwenyewe peke yake lazima awepo mtu kama askari wa kuweza kumu-ascot

mpaka hapa. Kwa kweli jambo hili wizara hii kwa upande wa Pemba

haifanyiki kazi hiyo, unapokwenda kudai masuala haya wanakwambia

jitegemee wewe mwenyewe. Hii Mhe. Waziri ndio hali halisi ilivyo.

Mhe. Naibu Spika: Mhe. Mjumbe malizia dakika 20 zimekwisha.

Mhe. Suleiman Hemed Khamis: Mhe. Naibu Spika, ahsante. Masuala

mengine ni kuhusu maslahi ya wafanyakazi.

Mhe. Naibu Spika, kuhusu maslahi ya wafanyakazi bado mpaka hivi sasa

mishahara midogo na ndio maana katika wizara yake wafanyakazi aliowataja

kiasi 32 wameondoka katika wizara yake. Kwa kweli suala hili ni gumu tena

ni zito sana. Kwa hivyo, ni vyema alichunguze suala hili kwa nini watu

wanaacha kazi wanaondoka vijana baada ya kuingia kazini, nadhani

inaonekana kwamba ni maslahi ni madogo. (Makofi).

Page 103: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

103

Mwisho Mhe. Naibu Spika, naomba hili linimalizie kwenye jimbo langu

kwamba nataka nimwambie Mhe. Waziri kupitia kwako kwamba mimi ninao

upungufu wa wazalishaji, kwa sababu wazalishaji waliopo ni kidogo

hawatoshi na huduma zinakuwa ni nzito.

Pili Mhe. Naibu Spika, kuhusu call allowance. Kwa hiyo, hapa zaidi ya miezi

mitatu au minne hawa wakunga au wazalishaji hawapati haki zao. Kwa hivyo,

ninamuomba Mhe. Waziri kupitia kwako Mhe. Naibu Spika, kwamba suala

hili la call allowance waweze kulipwa kwa wakati. (Makofi)

Jambo jengine laboratory hatuna mtu ambaye anashughulikia mambo ya

ndani, pia hatuna mlinzi wa kuweza kulinda Hospitali yetu ya Konde ambayo

inahitaji mlinzi tuwe naye.

Mhe. Naibu Spika, nakushukuru na mimi kwa kunipa nafasi ya kuweza kutoa

mchango wangu katika suala hili.

Mhe. Naibu Spika: Waheshimiwa Wajumbe, sasa tunamalizia dakika kumi

na nyengine kumi kipindi cha jioni. Mhe. Asaa Othman Hamad.

Mhe. Asaa Othman Hamad: Mhe. Naibu Spika, nikushukuru na mimi

kunipa muda huu uliobaki na kukubali kwamba itakuwa nakudai.

Nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kuniwezesha mimi na wenzangu

siku hii kufika kwenye jengo lako hili tukufu tukiwa wazima wa afya.

Mhe. Naibu Spika, bajeti ya mwaka huu tulisema ni ya huduma ya wananchi

wa Zanzibar. Sasa kama hivyo ndivyo basi tulitarajia bajeti zinazofuata

zinakwenda kwenye mtiririko wa kauli hiyo iliyotangulia mwanzo.

Mhe. Naibu Spika, leo tunajadili Wizara ya Afya ambayo ina umuhimu kwa

maisha ya watu wetu, pia kwa taifa hili kuwa na watu wenye afya bora. Mhe.

Naibu Spika, fedha zilizotengwa kwa wizara hii hazikidhi mahitaji ya

kuendesha wizara lakini pia kuyafikia malengo waliyojiwekea. Kwa hivyo,

nianze kwa kumshukuru Mhe. Waziri pamoja na watendaji wake, pia

niishukuru Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa dawa za watoto, chanjo na

kuharisha na huko tumeona mambo yamekwenda vizuri. Hata hivyo, kuna

mapungufu Mhe. Naibu Spika yanayokatisha tamaa.

Vile vile na mimi niungane na waliotangulia kwanza Mhe. Naibu Spika,

serikali haitutendei haki Baraza lako, kwamba leo tunajadili wizara kama hii

na hata nyengine isiyokuwa hii Mtendaji Mkuu wa Shughuli za Serikali ndani

ya Baraza hili halipo, Waziri wake Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais hayupo

Page 104: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

104

na Waziri wa Nchi, (OR), Fedha, Uchumi na Mipango ya Maendeleo naye

hayupo. (Makofi)

Mhe. Naibu Spika, angalau basi kwa taratibu za Mabunge haya ya

Commonwealth mtu kama huyo anapokuwa hayupo basi Wabunge

wanaarifiwa nani anachukua nafasi ile, lakini tunasimama ni sisi na waziri na

naibu wake. Kwa hivyo, Mhe. Naibu Spika, katika hili tunaomba sana serikali

ione umuhimu wa watu hawa kuwemo kwenye chombo hichi.

Mhe. Naibu Spika, nitakuwa na maswali kwa Mhe. Waziri na nitamuomba

anisikilize kwa makini kwa sababu ninataka majibu sahihi. Kwanza nimuulize

Mhe. Waziri katika wizara yake hii kuna mpaka wa utendaji kwa watendaji

wenyewe pia kwa maslahi ya watendaji baina ya Unguja na Pemba.

Kwa kweli tunalalamika na kupiga kelele madaktari wetu wazalendo

wanaondoka na mwenzake waziri aliyeondoka wa wizara hii alikuwa

anatuambia wala serikali ihatomzuia mtu anayetaka kuondoka. Lakini

chochote kinachotendeka kina sababu. Mhe. Naibu Spika, Hospitali ya Jimbo

langu ya Wete tunao upungufu mkubwa wa wafanyakazi.

Katika hili Mhe. Waziri asijekuja na jibu la nyumba, hospitali inazo nyumba

zake, isipokuwa wamewagaiya watu ambao si wa hospitali waliokuja pale

kusaidia wakakosa makaazi na badala yake tukaambiwa sisi tuwape nyumba

kwa ajili ya kukaa madaktari waliokuja mwaka jana. Kwa maana hiyo,

nyumba ya Hospitali ya Wete ipo wamewapa wasiokuwa wafanyakazi wa

hospitali na matokeo yake wanaokuja kusaidia watu pale wanakosa makaazi.

Kwa hivyo suala la nyumba lisijekuwa ni jibu. (Makofi)

Mhe. Naibu Spika, tunao upungufu mkubwa wa wafanyakazi wetu na hata

yale maeneo nyeti kama vile theater. Kwa hivyo, kunahitajika kikosi

kikamilike kwa wakati unaohitajiwa na hapa kuna tatizo.

Mhe. Naibu Spika, kama muda umefika basi naomba nisite na Inshaallah nije

nianze Hospitali ya Wete kwa wakati muafaka.

Mhe. Naibu Spika: Waheshimiwa Wajumbe, ninawashukuru na sasa

tunaakhirisha kikao chetu hadi saa 11:00 za jioni.

(Saa 7:00 mchana Baraza liliakhirishwa mpaka saa 11:00 jioni)

Page 105: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

105

(Saa 11:00 jioni Baraza lilirudia)

(Majadiliano Yanaendelea)

Mhe. Asaa Othman Said: Nakushukuru kwa mara nyengine Mhe. Naibu

Spika, baada ya kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutufikisha jioni hii

tukiwa wazima wa afya. Mhe. Naibu Spika, tulifikia Wete Hospitali. Hospitali

hii ina wafanyakazi kidogo sana. Ni kidogo sana kwa idadi yao na ni kidogo

hasa kwa yale maeneo ambayo yana umuhimu mkubwa siku hadi siku. Mfano

wa hilo ni ile theatre, ina nurses watatu na daktari wao mmoja wa akina

mama kwa magonjwa haya ya akina mama. Hawa anayekwenda likizo ni

mtihani, lakini hawa wao wasihudhurie misiba wala furaha. Hawa wanaingia

saa 1:30 asubuhi lakini ni masaa 24.

Kazi za theatre, zinaeleweka. Mhe. Naibu Spika, kilio cha wafanyakazi wa

sekta hii Pemba ni wao kutengwa kutopewa hizi allowances na hizi wanazoita

call. Lakini kilichofanyika hapa hapa kuzingatiwa mazingira ya kule Pemba.

Pemba wao ni kidogo kwa idadi yao na ndio hao hao wanaoingia call, hawana

shift, hawana chochote. Sasa palipotajwa malipo ya call wakatajwa madaktari

na specially kule hakuna na huyo aliyekuwepo hapewi kitu.

Nilianza mchango wangu kwa kuuliza Mhe. Waziri, watendaji wako ndani ya

Wizara yako Unguja na Pemba umeweka mpaka wa stahili. Mhe. Naibu

Spika, huyu gyner ambaye ni mzalendo, muungwana huyu, huyu ni mchaji wa

Mungu, hapewi zaidi ya mshahara wake lakini ni usiku na mchana anatumika.

Mhe. Naibu Spika, nilisema na naendelea kusema kwamba wafanyakazi ni

kidogo. Mhe. Waziri kilio hichi alikisikia akawaleta wengi, tatizo aliloliona

yeye akataja nyumba. Nasema nyumba ni tatizo nalikubali, lakini sikubaliani

naye kwa nini zile ziliopo zao wao wenyewe Wizara ya Afya mbona

wamezigawa kwa watu waliokuwa sio wa sekta ya Afya. Mhe. Waziri

angeleta kilio hichi baada ya kuishiwa na kile alichonacho. Lakini tumekuja

kuliona kumbe kuna tatizo kubwa zaidi kuliko nyumba na ndio maana

wafanyakazi Pemba hawakai. Mfanyakazi aliyehitimu siku moja, kada moja,

chuo kimoja na mwenzake aliyekuwepo Unguja lakini hawalingani mishahara

yao. Kuna upendeleo, kuna ubaguzi katika hili na hili ndilo linalowahamisha

wafanyakazi.

Mhe. Naibu Spika, tulikuwa na daktari wa watoto alikuwa anasoma na

mwenzake nchi moja Afrika Mashariki, akaja Pemba, alipokuwa anasafiri

kuja Unguja kutizama mazingira ya kazi na wenzake na malipo, akaligundua

hili. Alipolalamika akaambiwa Nabii Muhammad alizaliwa Makka na alihajj

Page 106: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

106

na weye kama unayataka haya hapa na wewe hajj na kweli aliondoka Pemba

hayupo, yuko wapi? Mhe. Waziri akitaka nitamwambia yuko wapi.

Sasa mimi nauliza hivi kumbe ni kwa makusudi yanafanywa haya ili kusudi

kule wahame? Wakikuwepo kule hawalipi kodi ya Serikali? Wananchi wa

kule Pemba hawalipi kodi ya serikali hii? Kwa nini wafanyiwe hivi?

Kuwasumbua watendaji hawa si wao tu lakini pia wanawasumbua na

wananchi wa Kisiwa kile cha Pemba.

Mhe. Naibu Spika, madaktari wa magonjwa mbali mbali ukiacha huyu wa

magojwa ya akina mama, hatuna Wete, kuna hawa ma - VSO wanatajwa

wapo, wanatusaidia, lakini bado tatizo ni kubwa, hakuna daktari wa mifupa

hapa, kwa watoto ndio huyu Mcuba yupo anasaidia, na wengine wengi

hawapo, kumbe kuna tatizo. Mhe. Waziri nitakuomba miye uje utufafanulie

tatizo ni nini hasa linalokwamisha kwa nini kule Pemba wasipelekwe

madaktari wa fani tofauti kuwasaidia wananchi wa kisiwa kile.

Mhe. Naibu Spika, Mhe. Waziri alikuwa na kikao na Makamu wa Kwanza wa

Rais wa Zanzibar. Wafanyakazi wakapeleka kilio chao hichi, Mhe. Waziri na

watendaji wake alibeba ahadi, akazitaja wiki mbili kulishughulikia.

Namuomba leo kutoka siku hiyo hadi leo ni wiki ngapi sasa? Waliotajwa na

Wizara kwamba hao ndio wanaostahiki kulipwa hizi call ni madaktari na hao

mabingwa, lakini narudia kusema kuna haja ya kuyatizama mazingira halisi

ya kule Pemba. Hawa watu hawana shift, hawana likizo, kwa sababu ni lazima

aende akaokoe maisha ya mtu.

Mhe. Spika, kuna mwenzetu sijui kama nikimtaja na yeye hatohamishwa

huko aliko, ndiye anayetusaidia kwa nguvu zake zote Kamanda wa Chuo cha

Mafunzo. Karibuni hii gyner huyu mzalendo alikuwa likizo, kazi yote ya pale

ilikuwa inamuangukia bwana huyu, Mwenyezi Mungu atamlipa malipo

anayoyajua yeye mwenyewe. Huyu hana mapumziko, wakati wake wa

mapumziko tunauchukua sisi, hajui matembezi anakuja kutoa msaada pale,

mbali ya wale anaowaokoa jamaa zangu wanapoletwa na vitanda kutoka

kwao wanapovuka pale jirani.

Mhe. Naibu Spika, hali halisi na hivyo vitendea kazi vya dharura navyo

hapana. Kuna tatizo pia la uingizwaji na ucheleweshwaji wa pesa. Magonjwa

ya sukari sasa hivi ni tatizo kubwa, hawa wanatakiwa wachangiwe lakini

wanatofautiana uzito wa ugonjwa wenyewe. Anaambiwa na daktari wake kwa

wiki aripoti mara tatu ama zaidi ya hapo. Hali ya maisha kiuchumi ya kwetu

ni mbaya sana. Hili ndio pale niliposema kutowepo mtendaji Mkuu wa

shughuli za serikali humu ndani hatutendewi haki na serikali. Kwa sababu

hapa nilikuwa na lugha zaidi ya kuizungumza, serikali itoe jibu.

Page 107: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

107

Suala la mama waja wazito. Mhe. Naibu Spika, pamoja na kauli ya Mhe. Rais

bado tatizo lipo. Kinachopelekwa hakikidhi haja na bado tunaendelea kuzaa.

Anapofika mama kutaka kujifungua saa ile wanamdai vifaa vya kujifungulia

hili ni tatizo. Mhe. Naibu Spika, labda utayabeba wewe mwenyewe leo.

Nadhani niwaombe Waheshimiwa Wajumbe wa Baraza lako Tukufu kwanza

tuzuie bajeti hii kutoipitisha, tena tuizuie kwa nia njema kabisa, hadi pale

serikali itakapotoa jibu juu ya masuala tunayoyauliza. Hatuna nia ya

kuikomoa wizara wala mtu mwengine yoyote. Nia yetu ni kuwatendea haki na

mema Wazanzibari wote.

Mhe. Naibu Spika, mpaka kitabu hiki cha bajeti jaduweli la 17 limenipa picha

ya haya ninayoyasema kuna mpaka mkubwa utolewaji wa fedha baina ya

Unguja na Pemba. Hii siyo haki, sijui wanakomolewa Wapemba wenyewe

ama anakomolewa Waziri wa Wizara hii, nashindwa kupata jibu sahihi. Ndio

maana nikasema ningefurahi zaidi kama angekuwepo Mtendaji mkuu wa

shughuli za serikali akatusaidia katika haya.

Mhe. Naibu Spika, scheme za wafanyakazi za wenzao Pemba zimekama,

wanaambiwa wao ni wengi sana. Za wenzao Unguja zimetekelezwa,

kitendawili hichi Mhe. Waziri hebu njoo utusaidie utakaposimama, kwa nini

iwe hivi? Wale mabingwa na madaktari hawapo, lakini hata simu nayo

haithaminiwi. Wote hawa ni wafanyakazi wa wizara hii hii.

Mhe. Spika, kuna jengo Wete pale la magonjwa ya akili limetelekezwa, Mhe.

Waziri tunaomba utupe ufafanuzi kulikoni. Wanaokuja kutizama ndugu zao

waliolazwa hospitali hawana sehemu ya kukaa. Hospitali yenyewe haina uzio,

tatizo linalowapata watendaji sasa ni kutoa huduma huku watu waliokuja

kutizama wagonjwa wakishuhudia kinachoendelea, matokeo yake

wanabebeshwa lawama wafanyakazi wa hospitali kumbe lawama sio yao

wao. Hili nalo ni tatizo lipo, tunakuomba utupe muhtasari wa majibu, naomba

sana. La kwanza ni lile la mpaka nililouliza, upo haupo? Na kama upo kwa

nini? Ushahidi kwamba kuna mpaka vielelezo vya bajeti ya kitabu chako,

lakini na maelezo niliyonayo.

Mhe. Naibu Spika, la mwisho orodha aliyoiomba Mhe. Rais, baada ya

kulalamika wenzetu hawa hawana pesa za kulipa call nina majina 86, majina

haya hayana hata jina moja kutoka Pemba, kwa sababu nilizozitaja. Lakini

namuomba sana Mhe. Waziri wale kule wanafanya kazi zaidi ya hawa hapa.

Hawa waliyokuwemo kwenye orodha hii kwa maana hawana muda wa

mapumziko wao. Theatre ina watu watatu, daktari ni mmoja, akitoka saa 9:30

anarudi tena saa 12, saa 12 anatoka tena baada ya sala ya Alfajiri. Huyu mtu

unasema humlipi call kwa sababu yeye sio specialist, hivi tukueleweje,

Page 108: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

108

haiwezekani! Hapa ni lazima serikali huko mlikopeleka orodha hii mpeleke

nyengine kwa maelezo stahiki kusudi na wao waweze kupata taasisi zao kama

wenziwao wanavyopata.

Mhe. Naibu Spika, nakushukuru kwa muda wangu uliopungua lakini angalau

umeu - consider baada ya hayo nasema siipitishi miye bajeti hii na nawaomba

Waheshimiwa Wawakilishi bajeti hii isipite kwanza hadi pale serikali

itakapotoa kauli thabiti kuhusu kauli ya mwanzo bajeti hii ni kwa ajli ya

huduma kwa wananchi wa Zanzibar. Nakushukuru.

Mhe. Abdalla Juma Abdalla: Nakushukuru Mhe. Naibu Spika, kwa kupata

nafasi hii niweze kueleza machache katika makadirio na mapato katika sekta

hii muhimu sana katika jamii yetu. Nitajitahidi kadiri inavyowezekana

kufuata maelekezo yako Mhe. Naibu Spika, nisitumie muda mwingi. Kwa

sababu hiyo basi sitaki nipongeze ila nataka niende kwenye mada moja kwa

moja.

Nitakachokianzia Mhe. Naibu Spika masikitiko, nasikitika kidogo na sisikitiki

na Wizara hii, lakini nasikitika na mwenendo wa Wizara ya Fedha katika

kuingiza fedha hizi ambazo fedha chache tulizozikadiria kutoziruhusu

zipelekwe katika sekta ya afya. Lakini mwenendo wa kuzipeleka unakuwa ni

wa kusuasua sana. Ukifunua ukurasa wa 32 kuna Ofisi ya Mfamasia Mkuu,

imeelezwa hapa katika nukta, paragrafu 502 kwamba fedha iliyoidhinishwa

katika bajeti ya mwaka huu tunayomaliza ilikuwa ni bilioni moja mia tano na

arubaini na saba milioni kwa ajili ya dawa, hiyo ni portion ya serikali, maana

na wafadhili na wao wanachangia.

Mhe. Naibu Spika, kilichotiwa hadi kufikia mwezi wa Machi ni shilingi mia

mbili na sabini na moja milioni, hiyo ni asilimia ndogo sana ni kama asilimia

nafikiri 18. Lakini kwa kifupi Mwanasheria Mkuu huwa anasema tukamcheka

hapa kwamba hatuko serious. Lakini hii inaonesha kweli hatupo serious,

maana hakuna sekta muhimu, hata ukisoma MKUZA moja katika malengo ni

kuimarisha afya na siha za watu, lakini kwenye MKUZA tunaandika vile

wakati wa ku - practise sasa unafanya kitu kama hichi.

Mhe. Naibu Spika, na mimi nataka niungane na Mhe. Asaa kwamba kwa

kweli kuna haja ya bajeti hii kwanza kuirudisha ili tuone wenzetu Wizara ya

Fedha wanatoa umuhimu wa kutosha kwa sekta muhimu kama hii. Hatuwezi

kujenga nchi tukiwa na watu wagonjwa. Watu wanaumwa, Wazanzibari

tunaumwa kwa asilimia kubwa, leo serikali yenyewe haipeleki pesa kwa ajili

ya tiba. Mimi nadhani si jambo zuri hata kidogo. Kuna haja ya kuwa wakali

kidogo Waheshimiwa katika hili. Kwa sababu jamii yetu ina watu wanyonge

hakuna mmoja anayeweza kujihudumia mwenyewa kwa afya. Lazima huu

Page 109: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

109

msaada wa serikali upatikane 100%. Kwa hivyo mimi kwanza nataka nitoe

lawama zangu hizo kali sana.

Pili nijaribu kuangalia hichi kitabu cha bajeti ya programu, nikaenda kwenye

programu Nam. 3 ambayo inahusu Sera ya Afya, Utawala na Uendeshaji.

Lakini hiyo ina programu mbili ndogo ndogo. Ile programu ya 3(b) inasema

ni Sera, Mipango na Utafiti, sasa haja yangu hapa ni huu utafiti.

Mhe. Naibu Spika, jamii yetu imeelemewa sana na maradhi ambayo

yanaongezeka kila siku, yamekuwa maradhi maarufu sana tena maradhi sugu

sana. Kwa mfano maradhi ya Kisukari, ni tatizo kubwa sana sasa hivi,

utafikiri ni vile maleria zamani. Ukienda kwenye clinic ya wagonjwa wa

kisukari ni kubwa sasa kuliko maradhi mengine, kuna maradhi ya moyo, kuna

maradhi ya Kiharusi. Imekuwa ni jambo la kawaida sasa hivi, maradhi ya

figo, saratani na maradhi ya miguu. Ni maradhi ambayo yanatusumbua sana

Wazanzibari.

Mhe. Naibu Spika, nadhani kitengo cha utafiti sasa watwambie Wazanzibari

tuna tatizo gani? Maana kama tunakula vyakula visivyofaa watwambie

kwamba ukila chakula hiki ndio maana ya tatizo hili, lakini tukiendelea

kunyamazia hili basi siku moja tutakuja kujikuta hapa sote ni walemavu.

Maana yake sasa hivi nusu ya watu ni karibu walemavu, kila mtu anakwenda

tata kama anajifundisha kutembea sasa hivi kwa matatizo ya miguu na

wengine wamekondeana kwa sukari. Sasa nadhani ni vyema kitengo hiki

kifanye kazi kwa bidii sana, haya matatizo tujue sababu ni kitu gani,

yanatuvamia sana maradhi haya.

Nikiacha hilo Mhe. Naibu Spika, sasa niende kwenye tatizo jengine kubwa na

sugu sana, kama tunavyojua jamii yetu ina watu wanyonge sana, haya

matatizo niliyoyataja mengi yao kwa mfano kama maradhi ya moyo, saratani,

kiharusi ni maradhi ambayo hayatibiki ndani ya nchi, hata maradhi ya miguu

waliyo na mbawa zao huruka kidogo kwenda nje ya nchi kwa ajili ya kutibu

miguu. Tatizo tulilonalo jamii yetu ni wanyonge sana.

Mhe. Naibu Spika, katwambia Mhe. Waziri kwa mwaka uliopita katumia

karibu milioni 900 kwa ajili ya kusafirisha watu kupeleka nje kwa matibabu.

Hiyo ukiangalia wale wagonjwa wanaohitaji kwenda nje haifiki hata asilimia

3% wanaopelekwa. Watu ni wengi, uwezo wa serikali wa kusafirisha watu

kupeleka nje ni mdogo sana, kwa hivyo wanabakia masikini za Mungu kufa

hivi hivi wakijiona. Masikini ya Mungu huwezi kumwambia aende kwa fedha

zake akatibiwe India hata siku moja, kama hajapata msaada wa serikali

hawezi kwenda. Tunawaona humu wanapita miskitini wakiombaomba pesa,

wana matatizo na unamuhisi kwamba huyu sasa anaelekea kwenye kaburi

Page 110: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

110

hana vya kufanya. Pengine maisha yake yangeokolewa kama angekuwa na

pesa za kupelekwa nje.

Tatizo ni kubwa na nilikuwa naiomba serikali ikae iumize vichwa sana, tena

tuwe na nia ya makusudi kabisa, kwamba zile huduma zinazofuatwa kule nje

kwa nini hatufanyi utaratibu tukazipata hapa ndani ya nchi. Kwa mfano

tunaweza kusomesha kama wale mabingwa wanaotibu kule India tukawa na

mabingwa wenye taaluma zile wakatusaidia hapa. Kama kuna vifaa

wanavyovitumia kule India vikanunuliwa vikawepo hapa, japo ni ghali lakini

tukiwa na nia na tukaweza kutoa taaluma kwa wananchi wakatufahamu wao

wenyewe watachangia. Lakini kwa hivi tunavyokwenda tutapoteza watu kila

siku.

Nikiacha hilo Mhe. Naibu Spika, sasa niendelee na lawama zangu. Lawama

nyengine ni tatizo la wataalamu wetu kuondoka katika nchi. Nakumbuka

ukisoma kitabu cha Mhe. Waziri kaiweka hii kama changamoto. Kweli

tunawasomesha watu kwa pesa za wanyonge, masikini za Mungu wagonjwa

hohe hahe, lakini mtu akishapata taaluma unamkuta yuko karibu basi yupo

Dar-es-Salaam, lakini mara nyingi utawakuta wapo nje kabisa. Kwa upande

mmoja mimi nawalaumu sana kwa sababu waliowafikisha pale au

zilizowafikisha pale ni pesa za wanyonge za masikini. Walipaswa kwa

vyovyote vile kuwa wazalendo kusaidia jamaa zao. Lakini maslahi ya

kibinafsi yanawachukua wanaisaliti jamii yao. Mimi nawanasihi sana, tamaa

za kibinafsi hazitotufikisha mbali katika kujenga jamii yetu, kwa hivyo

wabakie kwanza watusaidie katika nchi.

Kwa upande wa pili lawama zangu nazilenga serikalini. Serikali kuna haja ya

kuangalia kwa makusudi hawa wataalamu ni mali sana. Ukitaka kujua kama

ni mali wao aondoke leo tu hapa kesho utamtafuta Dar-es-Salaam

keshaajiriwa zamani, watu wanatafuta. Sasa kile kinachotafutwa na wenzetu

na sisi tukitunze. Kwa hivyo nadhani wataalamu si watu wengi sana katika

jamii, hebu serikali ijipange kuhakikisha kwamba wataalamu hawa

hawaondoki wanabakia. Wanaweza wakalinganisha hivi kwani Dar-es-

Salaam wanawalipa shilingi ngapi, basi kile anacholipwa Dar-es-Salaam hebu

na sisi tumlipe hapa asiondoke. Mimi nadhani hilo tukilifanya tunaweza

kubakisha wataalamu wengi sana hapa.

Mhe. Naibu Spika, mimi mara nyingi huwa napenda kutoa mfano mmoja.

Mimi nilikuwa na mgonjwa wangu binafsi akawa na tatizo la moyo.

Nikampeleka Abdalla Mzee, wakanambia huyu mpeleke Unguja tatizo lake ni

kubwa. Nikaja naye Mnazi Mmoja wakanambia huenda ukawa na safari ya

India kwa tatizo lake. Nikaanza kushtuka kweli kweli maana pesa za

kumpeleka India mgonjwa wangu sina. Lakini wakanambia kwa kuanzia hebu

Page 111: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

111

nenda kwa dokta mmoja pale Dar-es-Salaam anaitwa Lowakatare. Mimi

nikamfuata Lowakatare, kabla ya kufika kwa yule dokta Lowakatare yule

karani wake tu, alimpima yule mgonjwa kwanza akanambia huyu mtoto tatizo

analo kweli, lakini kwa ninavyoliona ni dogo na halihitaji kwenda nje ya nchi,

lakini nenda kwa daktari.

Basi nikampeleka kwa daktari akamfanyia vipimo akanambia sikupi hata

panadoli, tatizo hili ni dogo sana kaa nae baada ya mwaka mmoja niletee tena

nimpime. Moja kwa moja lile tatizo likaondoka. Sasa nikasema basi Zanzibar

nzima wameshindwa kugundua hili tatizo kuwa si kubwa wananipeleka India,

kama sikupita huku ningesema nakwenda India moja kwa moja ingekuwaje.

Yule karani aliyenambia hivyo ni mtoto wa Kizanzibari alivyonisikia nasema

tu akaniuliza wewe ni Mpemba wa wapi. Nikamwambia Chake-chake, na

yeye akaniambia anatoka huko huko Chake Chake. Huyu tungekuwa naye

hapa angetusaidia mangapi, hatukuwatunza wanatukimbia Mhe. Naibu Spika.

Sasa mimi naihusia sana Serikali tusione gharama ya kuwatunza hawa

wataalamu, hebu tuwapeni pesa wakae hapa watusaidie.

Jambo jengine Mhe. Naibu Spika, ni tatizo hili ambalo Mhe. Naibu Waziri,

amelieleza kwa sababu sekta ya afya ni sekta ya huduma haizalishi, hii sekta

inatoa tu huduma, sasa kuna haja ya kusaidiwa na sekta nyengine.

Amelalamika sana Mhe. Waziri kwamba analipishwa umeme katika kiwango

kile ambacho wanalipishwa wafanyabiashara na yeye hafanyi biashara, yeye

anatoa huduma. Shirika la Umeme ni Shirika la Serikali, hata Mamlaka ya

Maji ni Mamlaka ya Serikali, walipaswa kufanya huruma fulani kutoa offer

kwa hospitali, wasilete bili kama wanam-charge mtu mwengine anayefanya

biashara. Hii nadhani kuna haja kwa Serikali kulifanyia kazi vile vile tukaona

kama Shirika la Umeme basi angalau ile bili inakwenda nusu nusu kule sio

kamili, na hata Mamlaka ya Maji vile vile iwasaidie hawa wenzetu waweze

ku-save pesa kidogo za kusaidia hizi huduma za wananchi wetu.

Jambo jengine ambalo nilisema niliseme kidogo Mhe. Naibu Spika, ni kuhusu

Baraza la Tiba Asili na Tiba Mbadala. Hii sekta inakuwa sasa katika nchi

yetu na nadhani kuna mambo mawili muhimu ya kufanya, na nakumbuka

niliwahi kusema mwaka hivi kwamba kuna haja sasa Wizara ya Afya ikaweka

kitengo maalumu na ikiwezekana kukawa na mtaala maalumu wa kusomesha

madaktari wetu mambo haya ya tiba asilia au tiba mbadala, kwa sababu

visiwa vyetu vimezungukwa na miti, na wataalamu walionusanusa kidogo

wanasema miti yote iliyotuzunguka hapa ni dawa ya maradhi mamoja au

mengine, tatizo letu hatuwezi kugundua mjiti ni dawa ya kitu gani na uzuri wa

dawa hizi sio chemical, ni miti shamba haileti athari kubwa ndani ya miili

yetu, lakini bahati mbaya wengi wetu hatujui.

Page 112: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

112

Mhe. Naibu Spika, nilikuwa nadhani kuna haja ya hili kulipa umuhimu, lakini

kwa upande wa pili hizi tiba asilia zinaanza kutumika hapa katika nchi na ni

sekta inayokuwa, maduka ya madawa ya asili yako mengi sasa, sasa khofu

yangu inakuja kuna miti mengine kwa mfano kama muarubaini; muarubaini

wanasema asili ya kuitwa hivyo ni kwa sababu unatibu maradhi arubaini,

lakini ule mjiti wenyewe una sumu na ukiikosea kipimo sumu yake badala ya

kutibu inaweza kukuletea madhara.

Sasa ndio inakuja ule umuhimu wa kupata wataalamu wanaoweza kuchuja ile

dozi hasa iwe kiasi gani ili akiweza kutumia ule mjiti basi uweze kumtibu

badala ya kumdhuru. Nafikiri tungefanya hivyo tukaweza kuitumia miti yetu

iliyotuzunguka hapa pengine hata hili tatizo la kuhangaika madawa ya

hospitali lingepungua kwa kiwango kikubwa, kuna haja ya kuelimisha

madaktari wetu na wao watoe taaluma kwa wananchi, maana yake sifa ya

mjini huu kama umeshaujua wewe ah! Si lazima uende kwa daktari,

ukishikwa na tumbo unazunguka nyuma kachimbe mti fulani unakunywa

mambo yamekwisha, umeshapunguza gharama za kwenda hospitali,

ushampunguzia daktari adha ya kwenda kutatua maradhi yako. Sasa na hili

nafikiri ni jambo muhimu sana kwa sababu mazingira yetu yanaruhusu hii

miti tunayo mengi sana.

Mhe.Naibu Spika, kama nilivyokwambia kwamba nitajitahidi kuutumia muda

wako vizuri sitatumia muda mwingi sana naomba niseme jambo la mwisho.

Hili nataka ni-quote kiambatanisho nambari kumi na saba, sikufurahi sana na

mgao wa fedha unavyokwenda kati ya Unguja na Pemba. Nilikuwa nasoma

hapa kwa mfano kitengo cha tiba Unguja ukiangalia kiambatanisho nambari

kumi na saba kiko ukurasa wa 104, kitengo cha tiba kiko Unguja na Pemba,

sasa Unguja makadirio ya fedha ilikuwa ni 435,000,000/= hapa ziliingizwa

zaidi ya hizo, paliingizwa 1,093,699,000/= ni sawa sawa na asilimia 250,

lakini kitengo hicho hicho Pemba kilikadiriwa 213,000,000/= lakini

zilizoingizwa 96,000,000/= sawa sawa na asilimia 45 hayalingani, kule kuna

asilimia 250 pengine kulikuwa na sababu ya msingi naomba ufafanuzi, lakini

hapa ukitizama utaona kama kule Pemba kumeachwa nyuma kidogo.

Mhe. Naibu spika, ukiangalia Mkemia Mkuu Unguja, makadirio yalikuwa ni

99,000,000/= zikapatikana 38,848,000/= ni sawa na asilimia 39, lakini

Mkemia Mkuu Pemba ilikadiriwa 20,000,000/= zikapatikana 4,000,000/=

sawa sawa na asilimia 24, sijui kuna tatizo gani mpaka mtiririko unakuwa

hivi? Na ukiangalia Idara ya Utumishi na Uendeshaji kwa hapa Unguja ni

347 zikapatikana 223 sawa na asilimia 64, lakini Idara hiyo hiyo Pemba

ilikadiriwa 165 zikapatikana 64 sawa na asilimia 39 yaani iko nyuma, na

ukiangalia hizi ni huduma ambazo bila ya shaka ziwe sawa, sasa kwa graph

Page 113: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

113

hii inaonekana kama kule Pemba inawezekana kama Waziri ana sababu za

msingi labda.

Baada ya kusema haya nMhe. Naibu Spika, nataka nisisitize kwamba kwa

kweli sisi Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi tukijipanga vizuri tunaweza

kuilazimisha Serikali ikaweza kutia fedha za kutosha katika Wizara hii

muhimu. Sasa mimi nawaomba wenzangu kwa hili tuwe serious kwa

kumtegemea babu Juma tu na Dkt. Sira wanaweza wakashindwa kuishawishi

Wizara ya Fedha ikatia fedha za kutosha. Kwa hiyo kazi kwetu. Ahsante

Mhe. Naibu Spika.

TAARIFA

Mhe. Naibu Spika: Kabla sijaendelea na wachangiaji niliowataja, naomba

nitoe taarifa kwamba kuna ndugu yetu anaitwa Keith R. Weghorst ambae ni

raia wa Marekani amepata kibali cha serikali kufanya utafiti hapa Zanzibar,

na kwa sababu utafiti wanaoufanya unahusu mambo ya Bunge, Ndugu Keith

ameruhusiwa na uongozi wa Baraza kukusanya taarifa anazozihitaji kutoka

kwa Waheshimiwa Wajumbe. Kwa maana hiyo Waheshimiwa Wajumbe

tunapewa taarifa kwamba ndugu huyu atakuwepo hapa kwa ajili ya kufanya

mahojiano na baadhi yetu, mahojiano hayo yanaweza kufanywa ama na yeye

mwenyewe au anatumia watafiti wasaidizi ambao mmoja ni Ndugu Abdalla

Ali Abeid na wa pili ni Ndugu Riziki Pembe Juma, ambao wapo hapa katika

ukumbi huu leo hapa juu.

Kwa hivyo Waheshimiwa tunaomba tutoe ushirikiano kipindi tutakapohitajika

kufanya mahojiano hayo. Halkadhalika naomba muwatambue watafiti

wasaidizi hao ambao ni Ndugu Abdalla Ali na Ndugu Riziki naomba

wasimame, hao ndio wanaomsaidia utafiti kwa hivyo tuwape mashirikiano.

Waheshimiwa Wajumbe niendelee na uchangiaji ninamshukuru Mhe. Abdalla

katumia muda mzuri, Waheshimiwa Wajumbe tuko nyuma siku 4 katika

bajeti yetu hii, kwa hivyo naomba leo twendeni vizuri ili kesho asubuhi

tuimalize hii tuingie bajeti nyengine.

Mhe. Ismail Jussa Ladhu: Mhe. Naibu Spika, awali ya yote naomba nianze

kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu subhanahu wataala kwa kunijaalia mimi

na sisi sote uhai na uzima tukaweza kuendelea na shughuli zetu hapa, Mhe.

Naibu Spika, ninakushukuru na wewe kwa kunipa nafasi hii na mimi

kuichangia bajeti hii ya Wizara ya Afya. Tatu naomba nimpongeze Mhe.

Waziri wa Afya Mhe. Juma Duni Haji kwa uwasilishaji mzuri wa hotuba yake

asubuhi hii ya leo.

Page 114: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

114

Mhe. Naibu Spika, mimi naomba nianze kuwa kusema kwamba mimi binafsi

na kwa niaba ya wananchi ninaowawakilishi hapa wa Jimbo la Mji Mkongwe

ninaikataa na siiungi mkono bajeti hii ya Wizara ya Afya. Mhe. Naibu Spika,

tofauti na zile Wizara nyengine ambazo nilizikataa kwa sababu ya matatizo

mbali mbali. Hii naikataa ili kupeleka ujumbe kwa serikali ya Mapinduzi ya

Zanzibar kwamba haturidhiki na jinsi wanavyocheza na afya za wananchi

wetu.

Mhe. Naibu Spika, tunajadili bajeti muhimu sana hapa na yule ambaye

tungepaswa kumpa ujumbe wetu hasa Mhe. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais

Fedha Uchumi na Mipango ya Maendeleo hayupo lakini hata Kiongozi wa

Shughuli za Serikali katika Baraza hatunaye hapa na sisi hatuna taarifa ni nani

Kaimu Kiongozi wa Shughuli za Serikali katika Baraza hili. Kwa sababu ni

kawaida katika mabunge ya Jumuiya ya Madola anapoondoka kiongozi wa

serikali anakuwepo kaimu wake. Sasa Mheshimiwa nasikitika sijui kama

tutakayoyasema yatakuwa yanafika ndiko na yatapata ufumbuzi au itakuwa

ndio kama kawaida yetu, business as usual; tunafanya kazi kama tulivyozoea.

Mhe. Naibu Spika, tuliposomewa bajeti kuu ya serikali katika ukurasa wa 31

wa kitabu cha hotuba ya bajeti ya serikali tuliambiwa kwamba bajeti ya

mwaka ujao wa fedha ni bajeti ya huduma za jamii kwa wananchi wa

Zanzibar. Mimi Mheshimiwa mimi naona haya ni maneno ya kisiasa tu,

maneno ya kisiasa kutaka kuwafurahisha wananchi na kutucheza shere sisi

Wawakilishi wao katika Baraza hili. Kwa sababu hali halisi Mhe. Naibu

Spika, haioneshi hivyo na si tu haioneshi hivyo kwa makisio au makadirio ya

bajeti hii, maana makadirio yanaweza kuwa ni mazuri sana na nakumbuka

alipokuwa akiichangia bajeti kuu Mhe. Naibu Waziri wa Afya aliipongeza

kwamba Wizara ya Afya mara hii imetengewa zuri. Lakini fungu hili

lilikuwemo katika nambari likiwa halitokezi katika uhalisia lina faida gani

kwa wananchi wa Zanzibar na afya zao.

Mhe. Naibu Spika, katika mtiririko wa uingizwaji fedha katika kitabu hiki cha

bajeti ya Waziri wa Afya. Wizara ya Afya ni katika Wizara iliyopewa

vipaumbele vya chini kabisa na serikali hii. Kwenye afya za wananchi wetu

kwenye maisha yao halafu tunakuja hapa tunawadanganya kwamba ni

huduma za jamii. Na hili Mheshimiwa si kwa mwaka huu tu mwaka huu

limetafutiwa lugha ya kisiasa kwamba ni bajeti ya huduma za jamii. Lakini

mwaka jana, mwaka juzi, tunaendelea kuambiwa hivyo hivyo kwamba

kipaumbele cha bajeti zetu moja ni afya, na kama utakumbuka Mhe. Naibu

Spika, tulipokuwa katika semina kule tuliambiwa kwamba uwekezaji katika

sekta moja inabidi ufanyike kwa muda mrefu ili tija ionekane. Sasa tija katika

Wizara ya Afya na sekta ya Afya hatuioni.

Page 115: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

115

Mhe. Naibu Spika, wenzangu wamesoma hapa kiambatanisho namba 17

kilichoko ukurasa wa 104 wa hotuba ya Waziri, ukitizama Ofisi Kuu Pemba

bajeti imeingizwa asilimia 35.52, mipango Unguja asilimia 31.29, Kinga

Unguja asilimia 37.37, Tiba Unguja asilimia 251.43 ndio pahala pekee

palipovunja rekodi hapo. Tiba Pemba hiyo hiyo tiba tizama huyu ndumila

kuwili. Pemba asilimia 45.19 Unguja ni 251.43 Pemba asilimia 45.19.

Mkemia Mkuu Pemba asilimia 39.24, hospitali ya Mnazi Mmoja asilimia

63.89, Mkemia Mkuu Pemba asilimia 24.90, Utumishi na Uendeshaji Unguja

asilimia 64.04, Utumishi na Uendeshaji Pemba asilimia 39.90, Mfamasia

Mkuu wa serikali asilimia 17.55.

Mhe. Naibu Spika, tunacheza shere na maisha ya watu ukitizama kama

ingelikuwa Wizara ya Afya yenyewe inatoa msukumo chini ya mwenye bajeti

hii ambaye ni Katibu Mkuu wizara kwamba kipaumbele chake ni Utumishi na

Uendeshaji sio afya za wananchi, na ndio maana bajeti imejitokeza vizuri

sana katika Utumishi na Uendeshaji tena Unguja sio Utumishi na Uendeshaji

Unguja na Pemba, Unguja. Mhe. Naibu Spika, hali hii inasikitisha sana. Sasa

ninajiuliza mimi kwamba katika uhalisia huu bajeti hii tunampitishia Waziri

wa Afya tunampitishia nambari, zikamsaidie nini nambari hizi?

Mhe. Naibu Spika, bajeti hii ina matatizo mengi sana kwa upande wa fedha za

kawaida ni hivyo. Ukija katika fungu la maendeleo ukurasa 105 wameandika

hapa vichekecho vikubwa Mhe. Naibu Spika, kwenye jumla huku chini

asilimia fedha walizopata ni 332, hii inakuonesha jinsi gani katika Wizara ya

Afya kwenye utawala kumefeli, Katibu na timu yake wamefeli kazi. Yaani

jumla ya bajeti yake asilimia kajumlisha zile asilimia 13, 54, halafu jumla

kapata asilimia 332 tungekuwa tunaogelea kwa maisha mazuri ya afya katika

Zanzibar tungekuwa tunapata bajeti ya maendeleo asilimia 332. Yaani

utawala wa Wizara ya Afya umeshindwa hata kufanya hesabu ukatupa

asilimia halisi.

Mhe. Naibu Spika, mimi nimefanya hesabu, bajeti halisi ambayo pesa

iliyopatikana ni 724,251,400 kati zilizokadiriwa bilioni 2,731,600,000 ni sawa

na asilimia 26.5 basi. Hapa wanatuandikia ati asilimia 332, mtawala huyu ana

timu yake ya wataalamu, wameandaa kitabu sijui kwa miezi mingapi pale

katika Baraza la Wawakilishi tena kilikosewa ukabandikwa ukurasa juu yake

kwamba hii ndio sahihi isharekebishwa marekebisho yale ndio haya Mhe.

Naibu Spika, tuliyoletewa hapa, are we serious? Yuko wapi Mhe. Rashid Seif

ilikuwa nimuulize leo.

Mhe. Naibu Spika, nasema tena hatuko tayari kuhudumia afya za wananchi

wetu. Mhe. Naibu Spika, inanisikitisha sana huu muda ulionipa leo ni mdogo

sana kwa madudu yaliyokuwemo katika Wizara hii. Mhe. Naibu Spika, ili

Page 116: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

116

kuonesha hali halisi ya uingizaji wa fedha nimeazima hapa kutoka katika

kamati iliyopita ya Ustawi wa Jamii makadirio ya matumizi ya fedha na

uingizwaji wake kwa mwezi wa Oktoba/Disemba kwa kazi za kawaida, kwa

kazi za kawaida iko hapa Mhe. Naibu Spika, na kwa kazi za maendeleo iko

hapa ukitizama ni aibu Mheshimiwa sina haja ya kusoma kifungu kimoja

kimoja, kwa sababu nitakuwa ninawapotezea watu muda na mimi nitapoteza

muda wangu. Lakini suala la jumla tu Mheshimiwa kwa Oktoba mpaka

Disemba kuonesha kwamba serikali hii haijali afya za wananchi wake katika

uingizwaji wa fedha.

Makadirio ya kazi za kawaida ilikuwa ni 18,234,000,000, lakini matumizi

halisi 2012, 2013 Oktoba mpaka Disemba ni 3,918,867651, wapi bilioni 18,

wapi bilioni 3 walizoingiziwa.

Mhe. Naibu Spika, katika fedha za maendeleo zilikuwa jumla yake kwa

miradi tofauti kwa kipindi hiki cha Oktoba/Disemba mwaka 2012 zilikuwa

ziwe 2,731,600000, lakini kilichoingizwa ni 192,251400. Kweli tunawajali

wananchi wetu Mheshimiwa, hiyo ndio uchambuzi wa bajeti. Tunaambiwa ati

bajeti ya huduma za jamii kwa wananchi wa Zanzibar tunachezwa shere na

wanachezwa shere wananchi wa Zanzibar Mhe. Naibu Spika.

Mhe. Naibu Spika, nikitoka hapo hilo nimetoa picha halisi tuone kwamba

tunadanganyana humu ndani ya Baraza. Niseme jengine Mheshimiwa kabisa

nimwambie Mhe. Waziri wa Afya kabla sijaingia katika nukta zangu hasa

akakae na watendaji wake wa Wizara ya Afya waliotoka Pemba waliokuja

katika hiki kikao cha bajeti, kuonesha hii aliyoizungumza Mhe. Asaa na

akaigusia Mhe. Abdalla Juma kwamba kuna double standard katika utendaji

wa Wizara hii, watendaji wamekuja hata posho katika kikao hiki cha Baraza

la Wawakilishi kinachoendelea wapo juu hapo Mhe. Naibu Spika, wao

hawakufikiriwa. Halafu tunasema kwamba tunajali usawa wa wananchi,

tunajali huduma zao.

Mhe. Naibu Spika, nikitoka hapo katika kitabu chake cha hotuba Mhe. Waziri

kataja changamoto, na mimi ninampongeza katika hili Mhe. Waziri wa Afya

ndio Waziri pekee ambaye tangu nimeingia Baraza hili katika hotuba yake

siku zote kunakuwa na sehemu ya changamoto, yeye mwenyewe anatwambia

changamoto ambazo anazikabili. Mhe. Naibu Spika, katika changamoto hizi

kazungumzia suala la madaktari na wafanyakazi au watumishi wa sekta ya

afya kuondoka nchini, liko katika ukurasa wa 81.

Mhe. Naibu Spika, madaktari wataendelea kutukimbia na watumishi wengine

wa serikali kwa sababu hatujali maslahi yao. Mimi najiuliza kila siku Mhe.

Spika, na juzi nilipochangia hapa nilisema katika Wizara ya Utumishi wa

Page 117: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

117

Umma, hivi Zanzibar kuna madaktari wangapi hao waliokuwa wana sifa

zilizotimia za udaktari tukawa tunashindwa kuyafanya maslahi yao yakawa

bora wakabakia wakatumika kilillahi katika nchi hii? Tuna Wakurugenzi

mamia tunajua kulinda maslahi yao, tuna mameneja chungu nzima tunalinda

maslahi yao, tuna Makatibu Wakuu sijui kumi na ngapi sasa tunalinda

maslahi yao, tuko Wawakilishi, tuko Mawaziri tunalindana maslahi yetu,

lakini huyu ambaye tunampa dhamana ya kutetea afya zetu, wangapi

Mheshimiwa hivyo serikali ingeweza kufanya maamuzi leo ikasema daktari

inamlipa mshahara na stahiki kama anazolipwa Mkurugenzi wa Idara

tungepoteza nini sisi? Leo katika bajeti hii kumetengwa bilioni 17.5 ili

kwenda kurekebisha mishahara, niliuliza hapa tunashindwa kuchangia Mhe.

Naibu Spika, tunapouliza tupeni basi mchanganuo wa marekebisho yenu ya

mishahara tuchangie vizuri tunaambiwa aa tunajiandaa, tunapanga

tutakwambieni, hakuna maelezo kwa Wawakilishi wa wananchi.

Mhe. Naibu Spika, leo tunamlipa daktari wetu sisi hapa MD unamlipa shilingi

laki sita kwa mwezi anapoanza huyu baada ya makato ya kodi anabakia laki

nne tisiini elfu. Assistance Medical Officer analipwa kama laki tano

akishakatwa kodi anabakia kama na laki nne. Lakini hata specialist wenye

ma-PHD hao tunamlipa laki nane Mhe. Naibu Spika, hivyo tunategemea

kweli hawa watakuwa na moyo kujituma wakati wanaona huku kuna

watendaji wengine tunakumba tu? Tunajenga matabaka katika nchi hii. Kuna

tabaka la wala nchi ambao wananchi wanatuona ni sisi wanasiasa na kuna

tabala la wavuja jasho wananchi huko wanaoteseka wakiwemo madaktari

wetu kama hawa Mhe. Naibu Spika.

Mhe. Naibu Spika, leo tunapenda kulinganisha mambo na Tanganyika mbona

katika hili hatulinganishi. Mhe. Naibu Spika, wenzetu katika bajeti hii kuanzia

tarehe 1 Julai, daktari anayeanza kazi na nnayo pay slip hii hapa atakuwa

analipwa milioni moja laki moja na elfu mbili, baada ya kukatwa PSPF, Kodi

ya Mapato, na makato mengine anabakia na laki nane elfu moja mia tano na

hamsini na nane hii hapa Mhe. Naibu Spika. Wameongezewa ndani ya bajeti

hii kwa asilimia 65 ili kukimbia watu wasiondoke ndani ya nchi. Sisi

tunaimba tu siasa kila siku wanaondoka, wanaondoka, sasa tunachukua hatua

gani kuwalinda wako wangapi nilisahau kusema Mheshimiwa. Mhe. Waziri

wa Afya anakuwa muungwana sana atwambie ukweli humu ndani, kwamba

yeye kafika pahala kagonga mwamba katika Wizara ya Fedha na Wizara ya

Utumishi wa Umma, kwamba alifika kusema kwamba nitagoma nao

madaktari wakifika kugoma kwa sababu hamuwalindii maslahi yao.

La kusikitisha Mhe. Naibu Spika, kwamba ilifika pahala katika kikao cha

Makatibu Wakuu kulijadili hili, Katibu Mkuu wao wa Wizara ya Afya badala

ya kuwatetea madaktari wake anakasirika kwamba kwa nini kunafikiriwa

Page 118: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

118

maslahi ya madaktari wake. Mimi naona jambo la ajabu Mhe. Naibu Spika,

nilitegemea yeye awe mstari wa mbele maana wengine wanakuja kwetu

wakitu-lobby wakitushawishi tuwajengee hoja hapa mambo yao yawe mazuri.

Huyu naambiwa katika Kikao cha Makatibu Wakuu kakasirika. Mheshimiwa

tunawapenda na yeye anatoka katika fani hii hii anayajua mambo yalivyo

halisi.

Mhe. Naibu Spika, nimetaja hapa kwamba specialist tunamlipa laki nane,

hapo Tanganyika tu specialist analipwa zaidi ya milioni mbili halafu atabakia

hapa afanye kazi gani. Lakini kuna mambo yao ya posho zao Mhe. Naibu

Spika. Kuna call allowance posho ya wito mfanyakazi yoyote wa serikali

taratibu tulizoziweka mwisho kazini saa tisa na nusu akifanya kazi zaidi ya

hapo akiitwa maana yake alipwe posho. Leo mna maposho maalum chungu

nzima katika mabuku haya, lakini madaktari yao hatuyatambui, wanafanya

kazi katika mazingira ya hatari, kuna risk allowance haipo wanafanya kazi

hawana usafiri wanataka wapewe posho la usafiri transport allowance haipo.

Nyumba za madaktari mfano tunagawana sisi kwa sisi wao sasa inabidi

wapewe posho ya nyumba, posho ya nyumba hawapewi, zimetoka baada ya

kelele zetu fedha mwaka jana zimetoka toka kufika mwaka huu zimekwama.

Imekuwa kila kitu cha kusukuma tu mpaka watishwe, mbona yetu sisi

hatungoji tukatisha tukapewa maslahi yetu?

Mhe. Naibu Spika, naambiwa katika bajeti hii hakuna kifungu cha kuwalipia

ndio maana inabidi wanakamatia kamatia ndani ya bajeti kwa nini? Uongozi

wa Wizara ya Afya katika ngazi watendaji Katibu Mkuu na wenzake kwa nini

hawalifikirii hili, tumeona bajeti ya Utumishi na Uendeshaji imenona, kwa

Unguja asilimia 65 wamefika wao lakini nyengine asilimia 17. Ndio maana

ukakuta kipaumbele chao siku zote kwenye kutaka kusafiri kwenda katika

mikutano ya kimataifa, hakuna kukosekana bajeti siku zote bajeti ipo

wanakwenda tu safari, lakini pesa kulipwa daktari hakuna Mhe. Naibu Spika.

Mhe. Naibu Spika, wako ma-orderly, wako wauguzi leo mshahara huu mkia

wa mbuzi tunaomlipa halafu hata kumuwekea chakula wengine wanaweza

kufanya kazi masaa 24 pale anaingia mtu leo anatoka kesho hata chakula

haikewi posho, hata kuwekea chakula haekewi. Huo mshahara mkia mbuzi

tunaomlipa huo atoe akatafute chakula ajilishe mwenyewe anaihudumia nchi,

anaihudumia serikali pale. Mbona sisi katika masemina yetu tunaweka

maposho na viburudishaji kwa nini tunajenga matabaka katika nchi hii,

kwamba ukiwa mwanasiasa tu wewe au mtendaji mkubwa katika serikali

wewe maslahi yako mazuri lakini hawa wanaotumika kuijenga hiyo nchi

tunawasahau maslahi yao? Watwambie watendaji.

Page 119: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

119

Mhe. Naibu Spika, zilipendekezwa hizo allowance au posho na marekebisho

ya mishahara namalizia ninayo mengi lakini nitajitahidi kufupisha.

Wamepeleka mapendekezo yao ninazo nyaraka zao hapa zote zimekaa juu ya

meza ya Katibu Mkuu hazisongi mbele, kuna Wizara ya Nchi Ofisi ya Rais

Utumishi wa Umma na Utawala Bora, tukiwauliza hapa hakuna majibu,

halafu tunalalamika wanakimbia, watakimbia wote Mhe. Naibu Spika, hao.

Mhe. Naibu Spika, jengine ninasikitika sana na muda leo ni mazingira yao ya

kufanyia kazi; leo Rais Mhe. Naibu Spika, katangaza kama huduma za

kujifungua ni bila ya malipo, lakini hali halisi haiko hivyo kwa sababu bajeti

yenyewe haipo. Leo hawa wamesema wanahatarisha maisha yao

unawafungua watu wanatwambia leo wanafunguliwa wengi wengine unakuta

kwa mfano wanaathirika na ukimwi, anakwenda pale anacheza na mgonjwa

kama yule yeye hana kinga ya aina yoyote hata ile posho ya kumkinga

hawana. Lakini tunawalaumu wao na huko nje mtu hajui anatukana daktari tu,

anatukana wauguzi kumbe hatujawapelekea huduma. Wanakuja watu wa

shamba pale hawana pa kupata vitu, anakwenda kufanya nini? Ndio hayo

aliyosema Mhe. Jaku wanaishia kuweka rehani vitu vyao, kwa sababu

unamwambia kwamba huduma bure na ameshasikia katika tangazo la redio na

televisheni, lakini hali halisi akienda pale unaambiwa kuna post operation

dawa hakuna, hakuna sindano hakuna chochote zote anaambiwa kanunue hizi,

kama suala la Ambulance hakuna mafuta mradi hakuna chochote Mhe. Naibu

Spika, leo unaambiwa ukifika pale kuna machupa ya JIK kama unataka

kufanya biashara ya machupa ya JIK ukayachukue hospitali yalivyojaa, kwa

sababu wanaambiwa wakayatafute wao, hakuna chochote kilichokuwa pale,

nini kipaumbele chetu?

Mhe. Naibu Spika, hivi ninavyozungumza oxygen hakuna hospitali, kuna

mgonjwa naambiwa tangu Jumamosi anataka kufanyiwa upasuaji mpaka

dakika hii tunazungumza hajafanyiwa kwa sababu hakuna oxygen theatre

chumba cha upasuaji. Mhe. Naibu Spika, kisa nini bajeti imekwisha

wanaambiwa wasubiri mpaka bajeti mpya, maisha ya watu, hivyo Serikali

imeshindwa na mpango wa vipi kuhudumia hichi kipindi cha mpito baina ya

bajeti iliyopita na bajeti mpya.

Mhe. Naibu Spika, matatizo yako mengi muda huu hata ungenipa saa nzima

mimi siyamalizi yaliyokuwepo katika Wizara ya Afya.

Niseme haraka haraka Mhe. Naibu Spika, nizungumzie suala la matibabu ya

nje ya Zanzibar, tunaambiwa bajeti yake imezidi mno iliyokisiwa, iko katika

ukurasa wa 24 wa kitabu cha Mhe. Waziri. Mhe. Naibu Spika, wanatuambia

bajeti hiyo awali ilipangwa kutumia 335,000,000/= lakini imetumia

990,244,168/=. Mhe.Naibu Spika, ilipokuja Serikali hii tuliambiwa maneno

Page 120: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

120

mengi katika kuongeza vitengo pale katika hospitali ya Mnazi Mmoja

kuifanya hospitali ya rufaa, yangelikuwa haya yanashughulikiwa, haya

mabilioni yanayokwenda kila siku kusafirisha wagonjwa nje yangelikuwa

yanatumika kuimarisha huduma tukanunua vifaa, tukawalipa madaktari,

ingelikuwa hizi shughuli zinafanyika hapa hapa Zanzibar, lakini tutaendelea

kila siku kutumia mabilioni kupeleka watu nje, na huko mpaka pengine

ujuane na mtu upate kupenya kwenda huko mbele lakini ndani ya nchi

yenyewe huduma mbovu kabisa.

Mhe. Naibu Spika, nimalizie kwa sababu ya muda ni suala la miradi hii.

Mimi nataka kutoa pendekezo kwamba ukitizama orodha ya miradi ya

maendeleo ni mingi sana, sasa mimi najiuliza mwisho wa mwaka huu fedha

zinazoingizwa ndio kama nilivyoeleza hapa tunategemea wahisani ambao

wenyewe wanaondoshwa, kwa hiyo matokeo yake yote imepata hichi asilimia

10 asilimia 15 hakuna moja linalofika popote, kwa nini Wizara ya Afya

isichague miradi kwa mfano michache ikaingiziwa fedha kikamilifu

ikaonekana tofauti yake, ikakamilishwa ikaonekana tofauti yake, lakini kuna

orodha tele, si kuonesha uhodari Mhe. Naibu Spika, kuja hapa kuonesha

miradi ya maendeleo 10 sijui nini, lakini mwisho wa mwaka hakuna hata

moja iliyofika hata asilimia 10 ya hatua yake, huo si utaratibu.

Kwa hivyo Mhe. Naibu Spika, niseme nimesikitika sana na hali hii, nasikitika

sana hatuwajali madaktari wetu wauguzi wetu, leo mmeacha kuzungumzia

hali ya wananchi wetu kwa sababu kama haya hatuyahudumii, hao wananchi

wetu wataendelea kuimba kila siku na sisi tutapiga kelele kila siku hapa lakini

mwisho itakuwa hakuna kinachopatikana kwa sababu hatuwatunzi

tunawadhalilisha, tunadharau maslahi yapo kwetu sisi tu watendaji na

wakubwa wa Wizara ya Afya. Mhe. Naibu Spika, naomba sana hilo moja la

pili la Serikali ije kujibu kuhusu uingizaji wa fedha kama hatukulipatia

jawabu hili Mhe. Naibu Spika, mimi bajeti hii siipitishi na naomba wenzangu

hii tusiipitishe tupeleke ujumbe Serikalini kwamba sisi tunajali afya za

wananchi kuliko wanavyojijali wao ambao zaidi wanajali safari zao za

kwenda nje kila siku, kazi yao wakubwa kusafiri, haijawahi kukosekana bajeti

ya kusafiri Mhe. Naibu Spika, hata siku moja kwa hiyo bajeti hii hatuipitishi

mpaka tupate jibu la Serikali, si Waziri wa Afya, maana yeye ndiye aliyekuwa

haingiziwi fedha, ila Serikali Kuu ije itujibu hapa.

Mhe. Naibu Spika, narejea kusema siipitishi bajeti hii, siiungi mkono hata

siku moja itarudi kwao. Ahsante.

Mhe. Kazija Khamis Kona: Ahsante Mhe. Naibu Spika, kwa kunipa nafasi

na mimi ya kusimama hapa kuchangia machache. Kwanza kabisa

nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujaalia afya njema tukakutana hapa

Page 121: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

121

tena leo jioni hii kuendelea na ujenzi wa taifa letu. Vile vile nimpongeze

Mhe. Waziri, kwa juhudi anazozichukua katika Wizara yake. Mhe. Naibu

Spika, kwa kuanzia mimi nitaanzia ukurasa wa 5 Kitengo cha Kupambana na

Magonjwa yasiyoambukiza.

Mhe. Naibu Spika, kitabu chake kilieleza magonjwa ambayo yasiyoambukiza

ni sukari, saratani na shinikizo la damu na pumu. Sasa nimuombe Mhe.

Waziri, maradhi haya sijui Wizara yake imefanya utafiti wa kugundua chanzo

kinachosababisha maradhi haya na nimuombe vile vile kama utafiti

haujafanyika basi Wizara yake ichukue jitihada ya kufanya utafiti ili

wananchi wetu wapewe kuwa maradhi haya yanasababishwa na nini?

Mhe. Naibu Spika, kwa kuendelea naenda na hospitali ya Kivunge. Mhe.

Naibu Spika, kabla ya hapo kwanza ninataka ninukuu ukurasa wa kumi na tisa

kifungu cha tatu zero moja kinasema:

"Idara hii inajumuisha hospitali tatu za Wilaya, hospitali ya Chake

Chake, Hospitali ya Abdalla Mzee, Hospitali ya Wete na hospitali nne

za vijiji ambazo ni hospitali ya Makunduchi na Kivunge".

Hapa nadhani Mhe. Waziri, naomba anifafanulie, kwa sababu hospitali ya

Kivunge mara tunaambiwa ya Wilaya na leo hapa naona tunaambiwa wa

vijiji. Kwa hiyo Mhe. Waziri, hapa mimi nataka aje anifafanulie aniwekee

wazi kuwa hospitali ya Kivunge na ya Makunduchi hospitali ya vijijini au za

Wilaya. Halafu Mhe. Naibu Spika, niende hospitali ya Kivunge kwanza

nimshukuru Waziri hospitali ile kwa kutujengea ukuta mzuri uliozuia

kuingiza wanyama, lakini Mhe. Waziri, jengo lile ukuta ule umeujenga mpaka

leo hii bado halijawekwa lango la geti pale, jambo ambalo ni sawa sawa na

kuwa hujafanya kitu kwa sababu pale pako wazi kama wadudu wanaingia,

wanyama wanaingia, hivyo nimuombe Mhe. Waziri, alikamilishe hili ili

tuondokane na usumbufu wa wanyama.

Mhe. Naibu Spika, hapo hapo hospitali ya Kivunge Mhe. Waziri, naomba aje

anihakikishie kwa sababu tumesikia fununu ya kwamba hospitali ya Kivunge

baadhi ya huduma zinafanywa na walinzi, sasa Mhe. Waziri, naomba uje

unihakikishie suala hili ni kweli au laa? Halafu Mhe.Naibu Spika, suala hili

kama lipo basi nimuombe Mhe. Waziri, ya kwamba siku yoyote suala la

kupewa watu ambao taaluma hawana, kwa hiyo suala hili ni tatizo, itakuja

kutokea athari kwa wananchi wetu pamoja na Serikali yetu. Naomba Mhe.

Waziri, suala hili alifanyie kazi kwa kina kama alijue namna gani ya kutatua

na kama hawa walinzi wanafanya hivyo basi awaambie waache mara moja na

kama hospitali ina upungufu wa wataalamu hao basi Mhe. Waziri, awapeleke

wataalamu hao katika hospitali hiyo.

Page 122: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

122

Mhe. Naibu Spika, niendelee na hospitali ya Mnazi Mmoja, kwanza leo hapa

nimelisikia tamko ya kwamba Hospitali ya Mnazi Mmoja haijawa kuwa

hospitali ya rufaa, lakini huko nyuma Mhe. Naibu Spika, tuliambiwa hospitali

ya Mnazi Mmoja ni hospitali ya rufaa, sasa jee tulikubali sisi lipi? Hospitali

bado haijawa ya rufaa au vipi?

Mhe. Naibu Spika, hospitali hii tunayosema ambayo Mhe. Waziri, leo

maelezo yake alisema haijakamilika ya kuwa ni hospitali ya Rufaa ina

mashaka mengi au matatizo mengi na ndio maana nadhani akaogopa kutoa

uthibitisho kamili kama hospitali ya rufaa kwa sababu haijakamilika kiurufaa

ndio akachelea kulisema hilo.

Sasa Mhe, Naibu Spika, hospitali hii ya Mnazi Mmoja ina matatizo kiasi

fulani au tuseme madaktari wetu wana matatizo kiasi fulani, sio wote baadhi

ya madaktari. Kwa sababu nikasema hilo Mhe. Naibu Spika, mgonjwa

anatolewa hospitali ya Wilaya au ya Vijiji ntakuja kufafanuliwa, analetwa

hospitali ya Mnazi Mmoja ya Rufaa. Lakini mgonjwa yule Mhe. Naibu

Spika, akishafika hospitali ya Mnazi Mmoja anapewa transfer ya hospitali

binafsi, suala hili lipo si kwa mgonjwa mmoja wala wawili. Kwa hiyo Mhe.

Naibu Spika, aje atuambia Mhe. Waziri, hivi kweli ni haki mgonjwa

kuondolewa hospitali ile hospitali yao ambayo wanachangia kadi na

imewekwa kuwahudumia wao wananchi leo atolewe hospitali ile apelekwe

hospitali ya binafsi, hii kweli ni haki?

Mhe. Naibu Spika, Mhe. Waziri hapa aje anifafanulie na anieleze vizuri ili

nifahamu na kama kweli suala hili lipo na mimi naona lipo haswa kwa sababu

mimi mwenyewe nimelishuhudia achukue hatua zinazostahiki ili madaktari

hawa maana sawa sawa na kusema wanawaiba wagonjwa kwa kwenda

kuwatibu hospitali zao, sasa huu wizi wanaoufanya madaktari wetu Mhe.

Waziri, aufanyie utafiti, upo mimi nishaufanya utafiti upo, sasa na yeye

afanye utafiti ili athibitishe ikisha na hatua achukue.

Halafu Mhe. Naibu Spika, Mhe. Waziri, kitabu chake hapa alieleza namba 5

ya kwamba wana tatizo na daktari bingwa wa macho, kwa sasa hivi daktari

bingwa anatoka Bara hospitali ya Muhimbili. Sasa hapa nimuombe Mhe.

Waziri, afanye jitihada zake na sisi tuwe hawa madaktari bingwa wa matatizo

haya ya macho ili tuondokane na usumbufu wa kuwapeleka wagonjwa wetu

Bara au kumtoa daktari kumtoa Bara.

Mhe. Naibu Spika, Mhe. Waziri alisema ya kwamba hospitali ya Mnazi

Mmoja bado msongomano upo kutokana na watu wanakaa kuwasikiliza

wagonjwa wao au kuwasubiri. Suala hili Mhe. Naibu Spika, halitaondoka

Page 123: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

123

hasa kwa wale wenye waja wazito, kwa sababu mtu akiwa na mja mzito huwa

roho yake inampaparika anataka awe karibu nae, sasa nimuombe tu Mhe.

Waziri, hawa wenye kukaa kuwasubiria wagonjwa wao awatafutie sehemu

maalumu ili wakae kwa kusubiri wagonjwa wao au kusikiliza taarifa za

wagonjwa, maana saa nyengine utaambiwa mgonjwa wako fulani jamaa yake

yuko wapi, sasa akiwa hayupo pale itakuwa tatizo.

Sasa nije Wodi ya Wazazi Mhe. Naibu Spika. Wodi ya Wazazi nayo ina

matatizo yake, ina matatizo tena makubwa, halafu katika Wodi hii ya Wazazi

nimuombe au niiombe Serikali au Wizara, Wodi hii kusiwe na Wakunga wa

kiume, kwa sababu nimewashuhudia mimi mwenyewe mle muna Wakunga

wanaume, wasafishaji wanaume na wanawake walivyo jamani wakaumwa

tunajijua wenyewe, kila mtu anakaa anavyojaaliwa na Mungu, sasa kwa kweli

tunakashifika na hayafai kuyasema niliyoyaona hospitali, lakini ninamuomba

Mhe. Waziri, hili alifanyie kazi, hivi jamani ndio tuseme kweli hawapo

Wakunga wanawake ambao waliosomea fani hii. Mhe. Waziri, hili kwa

wanawake wanatukashifu wanaume, kwa hiyo tuiombe Serikali au Wizara

suala hili lishughulikiwe tuwe na Wakunga wanawake, wasafishaji mle ndani

wanawake, halafu pia niwaombe madaktari wetu watumie lugha iliyokuwa

laini wakati wanapowashughulikia wagonjwa hasa waja wazito

wanapokwenda kujifungua, waondokane na lugha za kuwakemea na lugha

zilizokuwa chafu.

Ahsante sana Mhe. Naibu Spika, baada ya kusema hayo naunga mkono hoja.

Mhe. Abdalla Mohamed Ali: Ahsante Mhe. Naibu Spika, na mimi kunipa

fursa alasiri hii kuzungumza machache kuhusiana na mpango huu wa

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya.

Mhe. Naibu Spika, kidogo baada ya kupitiapitia mpango huu ningependa

nipate maelezo kidogo kwa sababu kuna vifungu hasa katika Idara ya Kinga,

vote 220101 ya gharama za simu. Mwaka jana kitengo hichi kilikuwa na

kama 1,000,000/=, lakini mwaka huu nikiangalia gharama zake zimefikia

karibu 14,000,000/=, sasa najiuliza kulikoni katika Idara hii ya Kinga kiasi

kwamba kwa mwezi wastani wa 1, 000, 00/= na kitu. Lakini pia kuna vote

220202 ununuzi wa zawadi, pia naona kifungu hichi nacho kimenona sana,

kwa sababu mwaka uliopita kilikuwa kina 500,000/= lakini mwaka huu kuna

11,000,000/= sasa sijui zawadi hizi wanapewa wageni wanapoondoka wale

wenzetu kutoka Cuba au vipi nataka nipate maelezo zaidi.

Jengine Mhe. Naibu Spika, katika hilo ni kwamba Idara ya Tiba Unguja. Idara

hii katika Vote 211120 kuna medical allowance, sasa kwa hapa Unguja

medical allowance, destination yake ni 21,000,000/=, lakini Idara hii ya Tiba

Page 124: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

124

Pemba, destination yake ni 96,000,000/= sasa mawazo yangu mimi ni

kwamba kama ni wafanyakazi imani yangu Unguja wapo wengi zaidi kuliko

Pemba, je ni vipi huku Pemba iwe hii vote inachukua fedha nyingi zaidi

kuliko hapa Unguja.

Mhe. Naibu Spika, niendelee kidogo kutoa mchango wangu katika Wizara hii.

Ukiangalia kitabu hiki Mhe. Naibu Spika, utaona kuna jengo zuri sana ambalo

tunalitarajia kuwa ni Hospitali ya Rufaa ya Abdalla Mzee, Mkoani Kisiwani

Pemba. Hili ni jambo zuri sana na labda tungeipongeza Serikali kuona sasa

upo umuhimu wa kuwa na Hospitali kama hizi. Isipokuwa Mhe. Naibu Spika,

ni kwamba hivi sasa huwa mara nyingi bajeti zetu zinakwenda kwa programu

na matatizo yetu makubwa ni madaktari, na tunapokuwa na maendeleo kama

haya bila ya shaka huwa tunayakamilisha kwa kupata zana zote na moja kati

ya zana hizo ni madaktari. Sasa labda niulize katika programu zetu

tunazozifanya je tumeandaa utaratibu wa kupata madaktari ambao labda

baada ya kukamilika kwa ujenzi wa Hospitali hii wataweza kuhudumia

hospitali ile.

Mhe. Naibu Spika, kwa nini ninasema hivyo, ni vizuri kwamba Makomredi

wenzetu toka mwaka 1969 wanatusaidia katika kuiendesha hospitali hii ya

Abdalla Mzee Mkoani, lakini hivi sasa Mhe. Naibu Spika, ni kuwa hospitali

hii haina daktari mzalendo, kwa maana hiyo wenzetu wamebadilika kiuchumi,

sasa inapofika wakati wa likizo huwa kipindi kirefu madaktari hawa hawapo

inawezekana siku nyengine mwezi mmoja na ziada. Ikifikia kipindi hicho

Mhe. Naibu Spika, huwa tunapata tabu sana, sasa sijui Mhe. Waziri, hilo

tunalijua kwamba hawa wenzetu wanaotusaidia kwa hali na mali, kuna wakati

huwa wanaondoka na kuiacha hospitali bila ya madaktari, ingawaje siku

nyengine huwa tunaelezwa huwa tunapata madaktari kutoka sehemu

nyengine, lakini hii mimi kwa mawazo yangu haitoshelezi.

Hivyo ningeomba katika utaratibu utakaokuja hivi sasa basi tuhakikishe

kwamba daktari mzalendo anakuwepo akasaidiana na wale wenzetu au

watakapokuwa hawapo basi yeye atafanya kazi yake kama kawaida.

Lakini Mhe. Naibu Spika, pia niseme kwamba tunapokuwa na miradi ya

maendeleo kama hii bila ya shaka kutakuwa na negative au positive aspect na

negative zake. Mhe. Naibu Spika, katika utanuzi wa hospitali hii bila ya

shaka kutatokea watu ambao wataathirika, na kwa ujumla ni wale watu ambao

wanakuwa wapo karibu na eneo la hospitali hii. Mara nyingi watu kama

hawa huwa wanafanyiwa malipo compensation ya vijumba vyao, lakini la

kushangaza kwamba tunapofanya tathmini ya majumba haya huwa Mhe.

Naibu Spika, tunaangalia ile bati aidha na yale matofali tu hatuangalii

mengine.

Page 125: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

125

Hivi sasa hata kama mtu utamlipa pengine thamani ya nyumba yake

10,000,000/= itakuwa ni thamani ya kile kijumba, bado hatujazingatia

kwamba mtu yule anahitaji kiwanja akiondoka pale ili apata kujijengea hiyo

nyumba nyengine. Sasa kinachotokea ni kwamba malipo tunayowapa

wananchi wetu yanakuwa ni kidogo hayawasaidii kuweza kupata kujenga, ku-

replace zile nyumba zao ambazo zimevunjwa.

Kwa hiyo ningeomba wakati wa kufanya tathmini kama hii na wao wenyewe

tukawashirikisha, tusiwaache wakawa wapo pale tukawapalekea tu wewe

tathmini ya nyumba yako ni kiasi fulani, lazima tukae pamoja tufanye

tathmini na tukubaliane tuone kwamba na hawa wameridhika na sio tu

kwamba Serikali inataka kufanya jambo fulani kwa hiyo unawajibika

uondoke japo kwa shingo upande. Nafikiri wote ni raia wa nchi hii na

wanahitaji na wao kupewa haki zao ili wajione wanatunzwa na kuthaminiwa

katika nchi yao.

Mhe. Naibu Spika, labda niende kidogo katika kitengo cha huduma za damu

salama. Ninachokijua ni kwamba hichi ni kitengo kimoja muhimu sana kwa

hivi sasa, kwa sababu hakuna mtu yeyote ambaye anakwenda hospitali

akaambiwa wewe unatakiwa utoe damu au unatakiwa usaidie damu kwa njia

moja au nyengine, isipokuwa kitengo hiki ndicho kinachosimamia kusambaza

damu kwa hospitali zote zilizopo. Lakini kila nikiangalia nahisi kwamba

labda kitengo hichi sisi kama ni Serikali hatujakipa umuhimu wa kipekee,

kwa sababu sioni fungu ambalo limeingizwa au ruzuku yoyote na

tumewaachia wahisani tu watu ambao tunajua fika kwamba mchango wao

umeanza kupungua. Sasa nafikiri kulikuwa na haja kubwa sana hivi sasa

kuona kwamba kitengo hichi kina umuhimu wa pekee, na hivyo kupatiwa

fedha ili kuweza kujiendesha, tusiwaachie peke yao hawa Wahisani, siku

ambayo watasimama basi na sisi angalau tuwe tushaanza kutembea japo

kupiga mbio hatujaweza lakini kutembea tumeshaanza.

Mhe. Naibu Spika, sasa niendelee kidogo katika kitengo cha Mkemia Mkuu

wa Serikali. Mimi nafikiri kama Wizara ingelikuwa ina umakini basi hapa

ndio ingelianzia ile prevention kwa sababu utumiaji wa vyakula na vipodozi

na mambo mengine ndio unasababisha mengi katika matatizo tuliyonayo.

Lakini kitengo hichi bado hatujakipa umuhimu wake, nafikiri tungeangalia

kwa kina sasa tukajua kwamba tukikiendeleza kitengo hichi basi ni moja kati

ya kinga, tutakuwa tumeanza njia moja ya kuwakinga wananchi wetu na

maradhi, kwa hiyo zile fedha ambazo labda tunazitenga katika kununulia

madawa zingelipungua.

Page 126: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

126

Kama sijakosea Mhe. Naibu Spika, jana nilipitia gazeti moja linalotoka

Tanzania Bara na nikaona kwamba kuna kitengo kinachoshughulika na

mambo kama haya, wao wamepiga marukufu au wameona kwamba kuna

matatizo katika utumiaji wa mafuta ya OKI, nikawa najiuliza kwa nini watoe

ripoti kama ile, wakati kwetu sisi hapa hakuna ripoti yoyote inayoeleza.

Imani yangu ni kwamba tajiri aliyekwenda kununua mafuta yale basi na tajiri

mwengine alitokea katika kisiwa cha Zanzibar na yeye akaleta mafuta kama

yale. Lakikni matokeo hapa sisi tunaendelea na hakuna taarifa yoyote lakini

kule kwa wenzetu taarifa imeshatoka kwamba mafuta haya hayana ubora wa

kutumia mwanaadamu. Sasa labda kuna ushirikiano wowote kati ya vitengo

vyetu hivi viwili vinavyoshughulika na mambo haya ya vyakula na vipodozi

na mengineyo ili linapotokea suala kama hili upande mmoja ikawa taarifa, na

sehemu nyengine imefika na labda taarifa sio kufika tu lakini ikawa

imekubalika itumike ipasavyo.

Mhe. Naibu Spika, labda niende tena kidogo katika Vituo vya Afya. Mimi

nafikiri hapa tumesahau kwamba mpango wa Serikali ni kueneza vituo vya

afya vijijini. Tunashukuru kwamba kila kona unayopita unavikutia vituo hivi,

lakini la kushangaza baada ya kukutia kile kikapu wanachopimiwa watoto

basi hukutii chengine, dawa hakuna, vifaa vyengine hamna, na sehemu

nyengine hata huyo daktari pengine anakaa meli sita ndio anafika au hayupo

kabisa.

Kwa hiyo hapa nahisi Wizara ingeangalia kwa kina kwamba hivi sasa kuna

umuhimu wa vituo hivi kwa vile tuna Bohari Kuu ya Madawa basi navyo

vikapata mgao wa kutosha, ili tukajua kweli ile thamani ya kuvijenga vituo

hivi ipo.

Mhe. Naibu Spika, vituo vyengine tulivyonavyo vinafikia hata milioni mia

mbili, mia tatu thamani yake lakini ni jambo la aibu kuona unakwenda katika

kituo kile huduma unazozipata ni chache mno, sasa Wizara hilo ilione na

tukijaaliwa mwaka unaofuata basi tuone sehemu hizi nazo zinapatiwa huduma

zinazostahili. Lakini baada ya kusoma ripoti hii nimegundua kwamba kuna

ongezeko kubwa la kutoona yaani wananchi wanapungua nuru ya macho hasa

nilipoisoma ile ripoti ya Hanyengwa Mchana, katika askari 59 waliofanyiwa

kuna waliopewa miwani na kuna waliopewa dawa, hii inamaanisha kwamba

hivi sasa hili ni moja katika matatizo makubwa yanayowasumbua wananchi

wetu, sasa labda Wizara imeshaandaa utafiti wowote ikaweza kutusaidia

wananchi tuepukane na mambo haya angalau ukatwambia ongezeko hili

limesababishwa na tatizo moja, mbili, tatu, pengine nina imani kwamba labda

vyakula tunavyokula inawezekana ikawa ndio sababau, kama bado basi

ningeishauri Wizara kama ilivyofanya tafiti katika kitengo katika mradi wa

malaria, basi na hapa ukaanza utafiti mapema, kwa sababu moja katika

Page 127: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

127

matatizo sugu yanayokuwa kwa wingi hivi sasa ni wananchi kutoona, hasa hii

iliyotueleza kwamba kuna watoto maskulini, sasa sijui watakuwa wanasoma

vipi. Ingawaje njia za kisasa zipo lakini kinga ni bora kuliko tiba. Mhe. Naibu

Spika, nakushukuru.

Mhe. Salma Mohammed Ali: Mhe. Naibu Spika, nakushukuru sana kwa

kunipa nafasi, lakini kwanza nataka nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa

kuniwezesha kusimama hapa na kuchangia hotuba hii. Mhe. Naibu Spika,

sasa nitarudia kukushukuru wewe sana kwa kunipa nafasi, tena nasema ni

nafasi ya upendeleo. Kwa sababu Mhe. Naibu Spika, kisa cha kusema hivyo

leo mimi sijaleta karatasi ya kutaka kuchangia, kwa hivyo naamini huo ni

upendeleo au kuna mmoja humu aliyenipendelea nichangie basi akaniandikia

kikaratasi. Nakushukuru sana Mhe. Naibu Spika. (Kicheko)

Mhe. Naibu Spika, sasa naomba nitumie nafasi hii kumpongeza sana Mhe.

Waziri kwa jinsi alivyoisoma hotuba yake, na vile vile nampongeza zaidi kwa

pale alipotueleza kuwa kaweza kupunguza msongamano wa jamaa wa

wagonjwa wanaolazwa katika Hospitali ya Mnazi Mmoja.

Mhe. Naibu Spika, hili ni jambo zuri kwa sababu haipendezi kwenda wodini

muda wote ikawa mmejaa watu, hata daktari anashindwa kufanya kazi ya

kuhudumia wale wagonjwa. Lakini Mhe. Naibu Spika, hapa naomba

nimuulize Mhe. Waziri tayari keshajitayarisha? Kwa sababu naamini watu

wengine wanaokaa mle huwa wanaingia kwa kuwahudumia wale wagonjwa

wao, hakuna hata mmoja anayependa mgonjwa wake aidha akae na kinyesi

kwa muda mkubwa au adhalilike. Sasa ikiwa Mhe. Waziri keshajipanga basi

mimi nitamshukuru sana kwa sababu tunaona hospitali za wenzetu tukienda,

mgonjwa unaingia kwa masaa kumtizama lakini unamkuta hali yake

inaridhisha. Kwa sababu zile huduma za usafi na kila kitu anafanyiwa.

Kwa hivyo, namuomba Mhe. Waziri aliangalie hili kwanza, tayari anao

wafanyakazi wa kutosha wa kufanya hizo kazi? Asije akawazuia watu kuingia

kuwasaidia wagonjwa wao wakati yeye hana uwezo wa kuwahudumia.

Mhe. Naibu Spika, sasa nataka niende ukurasa wa 32, hapa pana Ofisi ya

Mfamasia Mkuu naomba ninukuu Mhe. Naibu Spika. “Ofisi ya Mfamasia

Mkuu wa Serikali ina jukumu la kuhakikisha upatikanaji wa dawa muhimu,

vifaa, tiba pamoja na kusimamia matumizi sahihi ya dawa. Katika kulifikia

lengo hili, Ofisi ya Mfamasia Mkuu imepewa dhamana ya kufanya makisio na

kuratibu ununuzi wa dawa na vifaa, kufanya ukaguzi kwenye Hospitali na

Vituo vya Afya ili kuhakikisha utumiaji sahihi wa dawa”.

Page 128: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

128

Sasa Mhe. Naibu Spika, katika kiambatanisho nambari 17 ukurasa wa 104,

Makadirio yaliyopangwa ni shilingi 1,547,000,000/-, zilizopatikana ni shilingi

271,000,000 tu sawa na asilimia 17. Sasa namuomba Mhe. Waziri

atakapokuja atwambie hizi asilimia 17 kweli zinaweza kutekeleza haya

majukumu yaliyopangwa ya Mfamasia Mkuu.

Mhe. Naibu Spika, nataka niende kwenye kiambatanisho hicho hicho, fungu

0701 Tiba Unguja, fedha zilizopatikana ni asilimia 251.43. Lakini

kiambatanisho hicho hicho fungu 0801 Tiba Pemba fedha zilizopatikana ni

asilimia 45. Sasa namuomba Mhe. Waziri hapa akijasimama anambie ni

sababu zipi na kwa nini Idara ni moja ya Tiba Unguja ipate asilimia 251 na ya

Tiba Pemba ipate asilimia 45? Namuomba akija anipe sababu, kwa sababu

ingelikuwa angalau ni idara mbali mbali tungelisema vyengine, lakini idara

moja Tiba Unguja na Tiba Pemba, hapa asilimia 251 kule asilimia 45.

Namuomba Mhe. Waziri atwambie hili. Kwa sababu hapa ni kuwavunja

moyo wananchi wataona upande mmoja wanabaguliwa.

Sasa Mhe. Naibu Spika, nataka niende kwenye kiambatanisho Nam. 18

kifungu 60008. Mhe. Naibu Spika, hapa pana programu ya kudhibiti malaria.

Mhe. Naibu Spika, hapa tumeelezwa kwamba imepata asilimia 19 tu hiyo

programu ya kudhibiti malaria.

Mhe. Naibu Spika, hili ni tatizo kwa sababu malaria yalikuwa yamepungua

kwa asilimia kubwa, lakini hivi sasa Mhe. Naibu Spika, malaria yashaanza

kurudi, ingawa ukienda hospitali ukiangaliwa damu unaambiwa huna malaria,

lakini ukiondoka tayari dose ya malaria unapewa. Kwa nini upewe dose ya

malaria kama huna malaria, ni kwa kuwa tayari yameshaanza kurudi. Sasa

namuomba Mhe. Waziri anambie hapa hivi kweli wakiondoka tu hawa

wafadhili haya malaria ndio yanarudi, inaonesha serikali haiko tayari kwa

sababu ukisaidiwa lazima kile ulichosaidiwa ukithamini. Leo wanaondoka

wafadhili hawajafika kwao wanasikia Zanzibar malaria tayari.

Mhe. Naibu Spika, hili linasikitisha tena naiomba serikali ijizoweshe hasa

ikifadhiliwa ikubali ule ufadhili. Serikali yetu haijajiweza, sasa

ikishafadhiliwa ule ufadhili waupokee si kwa kuwa akishaondoka mtu tena

basi. Hivyo kweli wewe umejengewa nyumba yule aliyekujengea mpaka

kufagia aje akufagilie? Mhe. Naibu Spika, serikali ijizoweshe hasa, ifanye

makusudi kujizowesha kuthamini nguvu za wenzetu, si kwa kuwa

wameshatusaidia tuache zipotee, hivyo kweli sisi kila siku tutasaidiwa jambo

lile lile tu, keshokutwa wanakuja wafadhili wengine ati wanakuja kupambana

na malaria, haipendezi, waje watusaidie kwa mengine.

Page 129: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

129

Mhe. Naibu Spika, sasa nataka niende kwenye Maabara ya Jamii Pemba. Kwa

kweli mimi hapa nasikitika sana, hii ni bajeti ya tatu nimo katika Baraza hili,

katika hotuba hatujaona hata pesa ndogo inayotengwa kwa maabara hii. Mhe.

Naibu Spika, hilo ni tatizo, ndio hapo hapo tulipozowea kufadhiliwa

tukajiachaacha na wakishaondoka waliotufadhili hatujui kuendeleza.

Mhe. Naibu Spika, mimi Wafanyakazi wa Wizara ya Afya huwasikia sana

kuwa maabara hii haitengewi fedha na kazi zake Mhe. Waziri katueleza, wana

kazi kubwa wanazofanya tena nzuri, lakini leo serikali haiwafikirii hata

kidogo ikiwa hawajajizowesha leo hao wafadhili wakiondoka hawa wataweza

kweli. Mhe. Naibu Spika, yote hayo niliyosema namuomba Mhe. Waziri

akinyanyuka anijibu.

Sasa nataka niende kwenye ukaguzi wa abiria Bandarini na Airport. Mhe.

Naibu Spika, mimi hapa nina masikitiko makubwa, kwa sababu katika airport

ya Pemba katika ziara ya Kamati tulikwenda hicho kijumba kilichoandikwa

pale mlangoni „Afya‟; Mhe. Naibu Spika, mimi mwenyewe kama ni choo basi

ningelitafuta vya kukaa, nikae vipi niweze kujisaidia hicho chumba kilivyo,

maana ile kujisaidia ningeliona wasi wasi nikatafuta vya kukaa. Chumba

kibovu, madirisha hakina, hapana madaktari na hata ile panadol haipo. Sasa

namuomba Mhe. Waziri akija na hili anambie pale kweli ni Kituo cha Afya au

pana maandishi tu ya afya.

Vile vile nataka nije katika tatizo kubwa linalotukabili wanawake na

wanaume, lakini wanawake tumezidi ugonjwa wa kensa. Mhe. Naibu Spika,

hili ni tatizo ni ugonjwa mgumu, ugonjwa uliokuwa matibabu yake ni ghali na

wananchi wetu tunawajua hali zao. Matibabu yake hayapatikani hapa petu

mpaka uende kwa wenzetu. Sasa namuomba Mhe. Waziri anambie ana

mpango gani wa kutusaidia? Tunateketea! Kwa sababu uwe unaumwa malaria

tu peke yake basi utakuwa wewe tayari unaangamia huna kitu je, leo ugonjwa

kama ule unaoambiwa mpaka upate mamilioni ya kutibiwa, shilingi elfu mbili

mtu hanayo, lazima Wizara ya Afya hili walitizame tunateketea!

Sasa hivi wanawake wengi kila mmoja utamsikia nina kensa ya kizazi. Kwa

hivyo, namuomba Mhe. Waziri walitizame hili kila mmoja na uwezo wake au

aliyekuwa hana uwezo akishaumwa ndio basi.

Halafu katika ukurasa wa 69. Mhe. Naibu Spika, hapa nimekuta mfumo wa

ukusanyaji wa taarifa za malaria kupitia simu za mkononi. Namuomba Mhe.

Waziri anifahamishe vizuri kwa sababu mimi sijaisikia hii, sijui humu vijijini

wana watu wao mtu akishaumwa anatoa zile taarifa au ni mgonjwa

mwenyewe. Namuomba hapa akija anifahamishe ili tujue huu utaratibu na sisi

Page 130: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

130

tuweze kuutumia. Kwa sababu pengine kuna watu walio na malaria wengi

lakini hawajajua huu utaratibu.

Suala jengine ambalo nataka nilizungumzie Mhe. Spika, ni kwamba pale

Wawi pana Hospitali hii ama nawapongeza sana Mhe. Waziri kwa huduma

wanazozitoa hasa za mama na watoto. Lakini Mhe. Naibu Spika, aliyepo pale

sijui ni daktari au ni nesi lakini ni mmoja, akiumwa yule basi ile kazi

haifanyiki pale. Hii miezi ya nyuma Mhe. Naibu Spika, alikuwa yuko likizo

kama miezi mitatu alikuwa anatoka daktari aidha kutoka Gombani au Jeshini

na akija pale kwa siku moja kwa wiki, ukienda wanawake na watoto pale

wanasokoteana. Hebu Mhe. Waziri pale atuongezee mtu, mtu mmoja huyu

atakayefanya kazi kuanzia asubuhi mpaka saa tisa hapumziki na maslahi ndio

kama hayo yanayosemwa kila siku hayapo; hivyo Mhe. Naibu Spika, si

kuwarejesha nyuma wafanyakazi?

Namuomba Mhe. Waziri apatizame pale kile kituo ni cha jeshi na huyo

aliyepo wamempeleka wao kutoka Wizara ya Afya, lakini watuongezee mtu,

wanawake na watoto wanahangaika sana kufika toka alfajiri. Mtu akishasali

tu anatoka kwake kukimbilia kuweka foleni na atarudi saa saba au nane. Kwa

hiyo Mhe. Waziri, nakuomba na hapo utusaidie.

Mhe. Naibu Spika, jengine ambalo nataka niliseme kidogo ni kuhusu

madaktari. Naomba Mhe. Naibu Spika, madaktari wajijue kama ni madaktari

na kazi zao ni tofauti na wafanyakazi wengine. Kwa sababu wao wanafanya

kazi na wagonjwa, na mgonjwa vile ukimpokea vizuri au ukizungumza nae

vizuri basi peke yake ile huwa keshapata faraja, yale maradhi yanaanza

kupungua. Lakini ikiwa mgonjwa utampokea vibaya na kumpa maneno

mabaya basi hata kama utampa ile dawa yeye atajisikia ni mnyonge tu. Kwa

hivyo, namuomba Mhe. Waziri awape semina madaktari, wajue kama kazi

wanazofanya wao ni tofauti na wafanyakazi wengine, wao wana kazi nzito

kukaa na wagonjwa, na si semina tu hata maslahi yao yaboreshwe kwa sababu

ndio wameshatajwa wana kazi nzito.

Lakini pia Mhe. Naibu Spika, katika hizo kazi tunawaomba wale waliokuwa

wanatusaidia kule katika kujifungua wasitumie maneno yaliyokuwa sio. Mhe.

Naibu Spika, hata kutoka roho kila mmoja na vile anavyotoka, na kujifungua

kila mmoja na anavyojifungua, ikiwa mtu atapiga makelele sema naye

umwambie huo si utaratibu mzuri ni aibu hiyo, lakini kumkaripia

ukamwambia hizo starehe zako uliniita haipendezi, hakuna asiyejua kama

jambo lile ni la starehe, lakini kwa nini umwambie mtu pale maneno ya

kashfa.

Page 131: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

131

Mhe. Naibu Spika, namuomba Mhe. Waziri atoe semina sana kwa

wafanyakazi wake kwa kweli wana kazi ngumu na wanahitaji wafikiriwe hata

kwa maposho, lakini pia na kauli zao ziwe nzuri kwa wagonjwa.

Mhe. Naibu Spika, jambo moja linalowavunja moyo wanawake na

wakajifungulia nyumbani na wakahatarisha maisha yao ni hili. Wakati

mwengine Mhe. Naibu Spika, unakuta watoto waliokuwa hata hawajaolewa

wanakujibu maneno hayo, wewe mwenyewe unaona aibu kuwatizama

anakwambia haya ilikuwaje uliniita hiyo siku hiyo, haya kwani lazima

nikuite.

Mhe. Naibu Spika, nakushukuru sana, namuomba Mhe. Waziri anijibu hoja

zangu.

Mhe. Nassor Salim Ali: Ahsante Mhe. Naibu Spika, na mimi kunipa nafasi

hii ya kuchangia kidogo Hotuba ya Bajeti ya Wizara hii ya Afya. Mhe. Naibu

Spika, kwanza nichukue fursa hii kukupongeza wewe kwa kunipa nafasi hii.

Aidha, pia nimpongeze Mhe. Waziri pamoja na Katibu Mkuu na watendaji

wote wa Wizara ya Afya kwa kuweza kufanya kazi ngumu na ndefu na nzito

ya afya ambayo inagusa jamii yote ya Wazanzibari.

Aidha, pia nimpongeze sana kwa dhati kabisa Rais Dr. Ali Mohamed Shein

kwa kuweza kusimamia vyema serikali yetu au serikali yake inayoongoza

kwa kuwapa miongozo mawaziri wake na watendaji katika kuleta huduma

zilizo bora. Vile vile nimpongeze kwa jana kutangaza kwamba ataleta

mishahara mipya kwa wafanyakazi wa serikali na nina imani kwamba

wafanyakazi wa Wizara hii ya Afya basi na wao watakuwa wamefurahia suala

hili. Nampongeza sana Mhe. Rais.

Mhe. Naibu Spika, nije katika ukurasa wa 31 wa kitabu cha Mhe. Waziri

Hospitali ya Wagonjwa wa Akili, Kidongochekundu. Mhe. Naibu Spika,

mbali na uboreshaji wa majengo mbali mbali katika hospitali ile bado kuna

matatizo makubwa ambayo yapo katika hospitali ile. Mhe. Naibu Spika, kwa

kweli kuna jambo la kusikitisha sana kuona kwamba hospitali ile ambayo

inawagusa jamii yetu, ndugu zetu kuona kwamba bado ina matatizo ya

masuala ya usafi na kuna matatizo ya wadudu ambao wakiwemo kunguni na

wadudu wengine ambao wanaleta matatizo katika hospitali ile. Hili lalamiko

limetujia sisi na vile vile kuthibitisha kuwa kuna tatizo hili.

Lakini cha kusikitisha sana Mhe. Naibu Spika, kuona kwamba kuondoa

matatizo ya kunguni ambapo karatasi ninayo ya bajeti ya kuweza kuja

kufanya utibabu wa kuondoa kunguni katika hospitali ile ni takriban kama

shilingi laki tatu na nusu. Hii ni aibu na ni jambo la kusikitisha sana,

Page 132: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

132

ningemuomba sana Mhe. Waziri kufuatilia suala hili kuhakikisha kwamba

ndugu zetu, jamaa zetu, wanaondokana na matatizo ya wadudu kama vile

kunguni katika Hospitali ile ya Wagonjwa wa Akili pale Kidongochekundu.

Mhe. Naibu Spika, nije katika ukurasa wa 30 Hospitali ya Wazazi

Mwembeladu. Nitoe pongezi kubwa sana kwa Waziri pamoja na watendaji

wake katika kusimamia vyema na kufuata miongozo na ushauri tuliokuwa

tukiutoa hapa katika Baraza lako tukufu. Mhe. Naibu Spika, katika vikao

mbali mbali vilivyopita tulizungumzia suala la matatizo ya madaktari, lakini

tunashukuru kwamba kumepelekwa madaktari wawili na Waziri ametueleza

hapa ambao wamepelekwa pale na ambao wamesaidia kuondoa matatizo

makubwa yaliyokuwa yanaikabili hospitali ile.

Mhe. Naibu Spika, katika kitabu hiki naomba uniruhusu kusoma, “Kufikia

Machi 2013, jumla ya kinamama 4,067 walilazwa na akinamama 3,498

walijifungua kwa njia ya kawaida na hakuna mzazi aliyefariki dunia. Aidha,

hospitali hii hushughulikia huduma ya mama na mtoto pamoja na kutoa

huduma za VVU na UKIMWI.

Mhe. Naibu Spika, kuweza kuwazalisha akinamama takriban elfu nne na

kuweza kutotokea kifo hata cha mtu mmoja hii ni hatua kubwa na ni hatua ya

kupongezwa. Kwa kweli mimi kwa dhati kabisa nampongeza Mhe. Waziri

pamoja na watendaji wake na madaktari wetu kwa kusimamia vyema na

kuweza kutoa huduma zilizo bora katika hospitali ile. Lakini bado pia ipo haja

ya kuweza kuongeza bidii na kuongeza huduma zilizo bora zaidi katika

hospitali ile.

Mhe. Naibu Spika, nije Idara ya Mipango, Sera na Utafiti ukurasa wa 246

katika kitabu kikuu. Ukifungua katika kifungu cha 2000201 Chakula na

Vinywaji. Mhe. Naibu Spika, nataka maelezo wakati Waziri atakapokuja,

atupe maelezo sahihi kuona kwamba katika fungu hili kwa mwaka 2012/2013

kulikuwa na jumla ya shilingi 3,475,000/-, lakini katika bajeti ya mwaka huu

2013/2014 kuna jumla ya shilingi 15,266,000/-. Sasa ukitoka katika mwaka

jana shilingi 3.4 milioni na hivi sasa ni 15.2 milioni kweli ni kiongezeko

kikubwa. Kwa hivyo, akija atupe maelezo sahihi Mhe. Waziri.

Vile vile ukija katika kitabu kikubwa kile cha kurasa 247 kifungu 220517

Utayarishaji wa Mpango wa mwaka wa Bajeti. Mhe. Naibu Spika, katika

bajeti ya 2012/2013 kulikuwa na shilingi 6,900,000; lakini ukija katika bajeti

ya mwaka huu 2013/2014 kuna shilingi 20,000,000/-. Ni vyema Mhe. Waziri

akija atufafanulie atupe maelezo kutoka shilingi 6,900,000 mpaka shilingi

20,000,000.

Page 133: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

133

Mhe. Naibu Spika, baada ya kusema hayo nije katika Kituo cha Afya cha

Rahaleo. Kituo cha Afya cha Rahaleo ni kituo ambacho kimekuwa kikitoa

huduma na kuweza kusaidia jamii katika masuala mbali mbali yakiwemo pia

ya UKIMWI. Na kituo kile hapo zamani kilikuwa kikisaidiwa sana na

Agakhan Foundation. Lakini taarifa tulizonazo kwamba tayari Agakhan

Foundation wanataka kuondoa mkono wao katika kusaidia kituo kile. Sasa

nilikuwa nataka maelezo kwamba hili ni kweli? Na kama ni kweli basi

wamejipanga vipi ili kuweza kukiendeleza kituo kile ambacho kinasaidia sana

jamii ambayo imo katika Wilaya hii ya Mjini.

Lakini vile vile kituo kile kinahitajika kufanyiwa ukarabati na kuweza

kukiendeleza na kukiweka katika hali nzuri na kuweza kusaidia jamii.

Lakini Mhe. Naibu Spika, nije katika kitabu cha Mhe. Waziri ukurasa wa 50,

Baraza la Tiba Asili na Tiba Mbadala.

Mheshimiwa katika Baraza lako hili tukufu kupitia Kamati ya Maendeleo ya

Wanawake na Ustawi wa Jamii katika kipindi kilichopita kilitoa maelekezo

haya ili kuweza kupata taarifa ya waganga asilia au waganga wa tiba wa

Kichina. Kama Mhe. Waziri unakumbuka Makamo Mwenyekiti Mhe. Hija

Hassan alitamka hapa Barazani na kusema tupate taarifa sahihi za tukio

ambalo lilitokea pale kwa waganga wa jadi hawa wa Kichina kwamba kuna

mama mmoja au mzalendo Mzanzibari alipoteza maisha yake katika kipindi

kile ambacho tulizungumza kwenye Baraza lililopita. Lakini mpaka leo

hatujapata taarifa au maelezo yoyote kuhusiana na uchunguzi au taarifa za

wenzetu hawa ambao wanashughulika na tiba asilia za Kichina. Kwa hivyo, ni

vyema atakapokuja atupe taarifa ya uchunguzi umefikia wapi kuhusiana na

suala lile.

Mhe. Naibu Spika, baada ya kusema hayo naunga mkono kwa asilimia mia

moja, lakini vile vile namuomba Mhe. Waziri atupe yale ambayo nimetaka

kuyajua. Baada ya kusema hayo Mheshimiwa nakushukuru sana.

Mhe. Subeit Khamis Faki: Nakushukuru sana Mhe. Naibu Spika, usiku huu

kunipa na mimi fursa nichangie hotuba hii ya bajeti ya Wizara ya Afya

ambayo ni wizara muhimu sana.

Mhe. Naibu Spika, kwanza napenda nishukuru na kumpongeza Mhe. Makamu

wa Pili wa Rais kwa kuweza kusaidia Hospitali ya Micheweni vitanda pamoja

na magodoro 40. Nampongeza sana kwa uzalendo wake na kuona kwamba

kuna haja ya kuisaidia Hospitali hiyo na akafanya hivyo, namuomba

Mwenyezi Mungu amjaalie awe na moyo pale anapoona kunastahiki kusaidia

atusaidie tena.

Page 134: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

134

Jambo la pili, pia napenda niipongeze Wizara ya Afya kwa kushirikiana na

wafadhili kwa kujenga maabara nzuri ya Micheweni kwa ajili ya kusaidia

Hospitali ya Micheweni pamoja na wananchi wa Wilaya ya Micheweni kwa

ujumla. Lakini pamoja na pongezi hizo muhimu, sasa napenda niwaambie

Wizara ya Afya kama pamoja na kutujengea maabara nzuri sana lakini

maabara ile inahitaji kupata madaktari wazuri ili iweze kufanya kazi vizuri.

Kwa sababu kujenga maabara ni kitu kimoja kimekamilika lakini kuweka

madaktari wakaweza kufanya kazi vizuri ni kitu chengine. Kwa hivyo,

namuomba Mhe. Waziri aone kwamba kuna haja ya kuweka madaktari wazuri

ili ile maabara iliyopo pale iweze kufanya kazi vizuri.

Pia niwaombe watendaji wa hii Hospitali ya Micheweni kuitunza sana ile

maabara, kufanya kazi kwa kuitunza na kuishughulikia vizuri ili iweze

kudumu na kufanya kazi kwa muda mrefu zaidi.

Mhe. Naibu Spika, suala jengine ninalotaka kuzungumza nafikiri kipindi

kilichopita nilizungumza sana katika bajeti mbili zilizopita; na bajeti hii

nitazungumza tena. Mhe. Naibu Spika, Hospitali ya Micheweni kabla ya

kuazimia kuwa ifanywe kama Hospitali ya Wilaya, basi ilikuwa inafanya kazi

kama Hospitali ya Wilaya. Kwa hivyo, kipindi kilichopita nilisema kwamba

hospitali yetu ni ndogo haitoshi na leo napenda nikumbushe tena.

Namuomba Mhe. Waziri afanye kila jitihada anazozijua lakini hospitali yetu

ya Micheweni haitoshi ni ndogo mno. Kwa sababu ni dhahiri anaona kwamba

kuna kipindi inakuwa mpaka vile vyumba vya madaktari vinakuwa ni

hospitali.

Sasa namuomba Mheshimiwa kuwa kuna kila haja ya kuboreshwa zaidi

kuongezwa wodi za kulazwa wagonjwa hasa ukizingatia kwamba wodi za

kulazwa watoto pamoja na watu wazima ziko pamoja. Kwa hivyo, kuna haja

ya kutenganisha wodi za watoto zikawa ziko mbali na zile za wazee ziwe

mbali. Sasa namuomba Mhe. Waziri aone kwamba hospitali yetu ni ndogo na

ni ndogo sana na haitoshi. Namuomba Mhe. Waziri hili alione na alifanyie

kazi.

Mhe. Naibu Spika, suala jengine ni kwamba kule Micheweni kulitayarishwa

chumba cha upasuaji kwa ajili ya kuwasaidia watu wa Micheweni, kwa

sababu hospitali zilizopo za upasuaji kwa Pemba ziko mbali mno na

Micheweni. Kwa hivyo, kwa makusudi kukatengenezwa chumba kizuri kwa

ajili ya upasuaji. Sasa chumba kile kipo lakini sasa matatizo tuliyonayo ni

kwamba chumba kile kifanye kazi basi, ile sehemu ya upasuaji ifanye kazi

hasa ukizingatia kwamba kumtoa mzazi Micheweni mpaka ukimfikisha

Mkoani au Chake Chake basi kwa kweli hali inakuwa ni taabani sana au

Page 135: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

135

pengine anaweza akakata roho njiani kwa sababu ya umbali zaidi wa

kumsafirisha kumpeleka kule.

Sasa azma ile ya kuona kama kuna haja ya kufanyiwa upasuaji kule

Micheweni basi ikamilike madaktari tayari wapo wanasoma. Lakini sasa zile

zana za kupasulia hakuna kwa mfano hakuna mashine ya ganzi na vifaa

vyengine vya upasuaji havipo. Kwa hiyo, namuomba Mhe. Waziri kupitia

wizara yake waone kwamba sasa kuna haja ya ile azma ikamilike.

Mhe. Naibu Spika, suala jengine nitakalolizungumza ni suala la madereva wa

hospitali. Mhe. Naibu Spika, madereva wetu nao wana kazi ngumu sana. Kwa

hiyo, naomba na wao wafikiriwe. Aidha watengewe hata maposho ya ziada

kwa sababu wanafanya kazi mpaka usiku, mtu anakuwa saa nyengine

keshakuwa nyumbani kwake anapigiwa simu kuna mgonjwa anataka

kupelekwa hospitali, kama kwetu sie anataka kupelekwa Chake Chake au

Mkoani inabidi atoke usiku kwa ajili ya kumuwahisha ngonjwa hospitali.

Kwa hiyo, Mhe. Naibu Spika, naomba na hawa madereva waangalie kwa

jicho la huruma kabisa, kwa sababu na wao wana kazi ngumu sana. Aidha

watengewe maposho ya ziada ya kupewa na wao ili waweze kufanya kazi

zetu vizuri zaidi.

Mhe. Naibu Spika, suala jengine nitakalolizungumza ni suala la aidha

wanapotokea wagonjwa wa dharura wa ghafla yaani kwa mfano kama wale

waliopata ajali. Mhe . Naibu Spika, hawa wagonjwa wakipata ajali

wanachukua muda mkubwa kupata matibabu. Sasa mgonjwa keshapata ajali

na akawa bado anakaa muda hajapata matibabu inakuwa wale wenye

wagonjwa hawaridhiki na wanapiga kelele sana na wanailaumu Serikali.

Kwa hiyo, naomba Mhe. Waziri aone kama kuna haja ya kuweka kitengo

maalum inapotokea dharura ili waweze kutibu watu kwa haraka haraka sana,

ikiwa kipo basi kitayarishwe zaidi kiimarishwe zaidi, kama hakipo basi aone

kama kuna haja ya kukiweka ili wagonjwa wetu wakipata matatizo ya ghafla

waweze kutibiwa mara moja ili waweze kuwahiwa na kupata nafuu. Maana

mgonjwa siku nyengine damu zinatoka nyingi lakini anakaa muda mkubwa

hajapa matibabu, kwa hiyo yule mgonjwa anaona kama ni dharau. Kwa hiyo

naomba Mhe. Waziri kama hakipo kitengo hichi basi kiwekwe na kama kipo

basi kiimarishwe ziadi ili kiweze kufanya kazi zaidi.

Mhe. Naibu Spika, suala hili ni suala jengine nimeona humu la Mkemia Mkuu

kwa upande wa Pemba. Basi sijui kama Pemba kuna Mkemia Mkuu, lakini

nimeangalia nimeona kama yuko Mkemia Mkuu Pemba. Lakini nilipoangalia

kwenye Mkemia Mkuu Pemba nimeona vifungu vyote vya fedha

Page 136: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

136

ninavyoviangalia ni ziro mpaka mwisho kabisa nimeona kuna total ya milioni

20. Sasa sijui yeye huku Pemba hana kazi za kufanya mpaka ikawa mote ni

ziro tu au kwa nini iwe hivi. Kwa hiyo, naomba hili labda atakapokuja Mhe.

Waziri anitolee ufafanuzi ili nifahamu zaidi.

Suala jengine nimeona huku kwenye kifungu 1501 Hospitali ya Mnazi

Mmoja. Nimeangalia sasa kwenye kifungu hichi 263185 kuna mfumo wa

pamoja wa usimamizi wa Kitaifa, kuna milioni hamsini laki tisa na thalathini

na mbili. Sasa mimi huu mfumo wa pamoja wa kitaifa mimi sijaujua ni

mfumo gani na fedha ni nyingi sana na bahati nzuri au bahati mbaya

2011/2012 hamna 2012/2013 hamna. Lakini 2013/2014 ndio ipo hiyo milioni

hamsini kwenye huo mfumo wa pamoja wa usimamizi wa kitaifa. Kwa hiyo,

naomba Waziri labda atakapokuja kufanya majuisho anifahamishe ili na mimi

niujue huu usimamizi wa kitaifa ni upi.

Mhe. Naibu Spika, kwa hayo machache nakushukuru sana. (Makofi).

Mhe. Naibu Spika: Ahsante nakushukuru na wewe Mheshimiwa kwa kujali

muda.

Mhe. Mussa Ali Hassan: Ahsante Mhe. Naibu Spika, kwa kuweza kunipa

nafasi ya kuweza kuchangia Bajeti hii ya Wizara ya Afya.

Vile vile namshukuru Mhe. Waziri pamoja na watendaji wake kuhusu

shughuli nzuri za wizara hii.

Mhe. Naibu Spika, nataka nimuhakikishie kwamba kazi zake ni nzuri tena ni

nzuri sana. Isipokuwa kwa leo nachangia katika kifungu namba 3 ukurasa wa

21 kuhusu Hospitali ya Mkoa wa Kusini Unguja.

Mhe. Naibu Spika, kwa kweli Mkoa wa Kusini hivi sasa una matatizo

makubwa sana kuhusu upatikanaji wa madawa kwa wagonjwa wetu wa Mkoa

mzima kwa hivi sasa. Hospitali nyingi za Mkoa wetu zina matatizo ya

madawa. Kwa hivyo, namshauri Mhe. Waziri ajitahidi sana kuipa kipaumbele

Mkoa wa Kusini kuweza kupata madawa hasa yale muhimu ambayo yana

ugumu kupatikana katika Mkoa wetu ni madawa ya Ukimwi pamoja na

Sukari.

Kwa hivi sasa akiweko mgonjwa wa Ukimwi inabidi afuatilie masafa ya

mbali sana ili kuweza kupata dawa, au mgonjwa wa sukari inabidi afuate

mafasa makubwa sana ili apate madawa kwa ajili ya maradhi ya sukari, na

ukitizama magonjwa haya ni magonjwa sugu ambayo kutibika kwake ni

kugumu. Kwa hivyo, namshauri Mhe. Waziri aipe kipaumbele Mkoa wa

Kusini Unguja ili iwe na madawa hasa zile hospitali zake ziko mbali sana.

Page 137: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

137

Vile vile namshauri Mhe. Waziri Mkoa wa Kusini ina Wilaya zake kubwa

sana kwa hivyo, atusaidie tuweze kuwa na hospitali ya Wilaya ili rufaa

zipatikane katika Wilaya hasa katika maeneo nyeti kuweza kujengwa

Hospitali ya kisasa tukavijivunia katika Mkoa wa Kusini hasa Wilaya ya Kati

na sehemu nzuri tunazo kwa kumsaidia angelifanikisha katika maeneo mapya

ya mji mpya Tunguu na akaweza kuweka Hospitali ya Wilaya ya Mkoa wa

Kusini Unguja.

Vile vile namshauri Mhe. Waziri kwa kweli katika Mkoa wa Kusini kuna

hospitali ziko mbali mbali sana hasa ukitizama ukivuka kabisa ambayo iko

katika kijiji cha Uzi Ng‟ambwa. Kwa kweli Uzi Ng‟ambwa kuna matatizo

hasa kwa vile ni kisiwa kuvuka kwake ni shida wananchi wanapata tabu sana

kuweza kufuatia hospitali masafa makubwa ili kuhami afya zao.

Kwa kweli Uzi Ngambwa hivi sasa kuna aibu sana kwa Wizara ya Afya. Hivi

sasa hospitali ipo lakini kwa kweli haina daktari hata mmoja, sielewi hii

inakuja kwa nini au Mhe. Waziri amesahau kupeleka madaktari kule na kama

amesahau kwa kweli namkumbusha, na kama amepeleka aelewe kwamba

madaktari Uzi Ng‟ambwa hawaendi kufanya kazi kwa sababu ni kisiwa na

kiko mbali.

Kwa kweli inasikitisha sana kwa sababu tunayo nyumba nzuri ya madaktari

lakini ukienda kwa hivi sasa wanalala mbuzi na kondoo hamna daktari sielewi

hili suala lina faida gani kupoteza pesa za Serikali kuweza kujenga nyumba

kama ile ni nzuri hata mimi sina, na yeye Waziri na hakika hana kama ile ya

Uzi lakini utakuta hivi sasa inalala wanyama kama hao sijui kuna faida gani?

Na kama amepeleka daktari na kama haendi namuomba Mhe. Waziri achukue

hatua ya kumfungulia mashtaka daktari huyo kwa sababu amepoteza pesa za

Serikali kuweza kujengwa nyumba ile kwa ajili ya madaktari, lakini hivi sasa

hakuna daktari hata mmoja.

Kwa kweli ukienda kunasikitisha sana madaktari wake ni wale wa huduma ya

mwanzo peke yake utakuta watu wa Uzi Ng‟ambwa hivi sasa wana kilio

kikubwa sana hata kama daktari anataka kwenda gari ile inayogeuza tu Uzi

Ng‟ambwa ndio ile ile ndio anakwenda na ile ile anarudia ile ile, sielewi kama

yupo kwa kweli kama ndivyo alivyoweka mkataba. Kwa kweli Mhe. Waziri

akija anieleze sababu gani zilizosababisha kwamba Uzi Ng‟ambwa hakuna

daktari hadi hivi leo.

Mhe Naibu Spika, kwa kweli hivi sasa sina zaidi ya kuchangia isipokuwa

nachangia kifungu 4.3 ukurasa wa 31 kuhusu Hospitali ya wagonjwa wa akili.

Kwa kweli namshukuru sana Mhe. Waziri kwa hesabu yake na kitabu chake

kuanza kukisoma nimeona kwamba ametibu wagonjwa wa akili katika

Page 138: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

138

Hospitali ya Mental ya Kidongochekundu wagonjwa 4522. Kwa kweli nampa

hongera sana. Kwa kweli watu wa Unguja sasa hivi kama walivyokuwa

wagonjwa wa Malaria karibu kutakuwa hakuna wagonjwa wa akili.

Lakini nasikitika sana Mhe. Waziri katika kitabu chake sikuona kwamba

ametibu mgonjwa hata mmoja katika Hospitali ya Pemba. Sasa nataka

nimuulize Pemba hakuna wagojwa wa akili? Na kwa nini Pemba sikuona

kwamba iko Hospitali ya wagonjwa wa akili nimekwenda sana Pemba lakini

sijaiona hospitali ambayo imewekwa kwamba hii ina jina la wagonjwa wa

akili.

Mhe. Waziri naomba akija anisaidie kunijuilisha kwamba wagonjwa wa akili

wa Pemba wanatibiwa wapi ama kule Pemba hakuna mgonjwa wa akili hata

mmoja? Lakini nikitembea njiani nawakuta tuseme wale wote ni wala unga tu

wale. Kwa hivyo, Mhe. Waziri akija nataka anieleze kwamba wagonjwa wa

akili Pemba wanatiwa wapi na katika kitabu chake naona amesahau hakutia

hata mgonjwa mmoja ambaye ametoka Pemba ametibiwa wapi au wote

wanakwenda nchi za nje. Mhe. Waziri ukija naomba unisadie suala hili kama

si hivyo mimi nitaondoa shilingi yangu katika bajeti yako.

Mhe. Naibu Spika, kwa kweli mchango mkubwa kwa hivi sasa unakwenda

katika Hospitali zetu za Rufaa za hapa Mjini Zanzibar. Namshukuru Mhe.

Rais wa Zanzibar kuweza kutoa wagonjwa wote wanaozaa pale kwamba

wasitoe chochote. Hili nalipongeza sana lakini tu tuhuma zinazokwenda hivi

sasa kama ni za kweli Mhe. Waziri katika hospitali yako, kwa kweli hivi sasa

inavyosemekana kwamba wazazi wetu wanapokwenda kujifungua

wakimaliza kujifungua wanaambiwa wachangie chupa ya Jik sijui Mhe.

Waziri kama hili suala unalifahamu na kama hulifahamu basi ujue wazazi

wetu wanatoa chupa ya Jik sijui hii Jik inafuliwa mashuka au Jik hii

inakwenda wapi.

Kwa kweli, Mhe. Waziri nisikupe muda mgumu sana isipokuwa tu

nakupongeza sana katika shughuli zao lakini naomba utakapofika hapa yote

niliyoyasema nataka uhakikishe kwamba unayajibu si hivyo naondoa shilingi

katika bajeti yako.

Kwa kweli mimi na wananchi wangu wa Jimbo la Koani naunga mkono hoja

hii mia kwa mia ahsante sana.

Mhe. Viwe Khamis Abdalla: Ahsante sana Mhe. Naibu Spika, kwa kunipa

fursa hii usiku huu nikaweza kuchangia Hotuba ya Mhe. Waziri wa Afya.

Page 139: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

139

Mhe. Naibu Spika, nichukue nafasi hii nimpongeze Mhe. Waziri kwa

uwasilishaji wake mzuri wa hotuba yake. Mhe. Naibu Spika, pia nataka

nimpongeze Mhe. Afisa Mdhamini kwa kutekeleza vizuri majukumu yake.

Mhe Naibu Spika, naomba nichangie katika Hospitali ya Mnazi Mmoja.

Hospitali ya Mnazi Mmoja ni Hospitali ya Rufaa. Lakini hospitali ile haina

usafi. Kwa hivyo, naomba nimwambie Mhe. Waziri alisimamie vizuri suala

hili la usafi. Kwa sababu usafi ni muhimu katika mazingira yote anayoishi

binaadamu.

Mhe. Naibu Spika, nikitoka hapo niende kwenye hospitali ya Vitongoji. Mhe.

Naibu Spika, Hospitali ya Vitongoji ni hospitali inayotumiwa na wananchi

ambao wako kwenye vijiji; tukiangalia kijiji cha Ole, Kiuyu Minungwini,

Vitongoji yenyewe. Lakini Mhe. Naibu Spika, hospitali hii ina uchunguzi wa

damu ya Malaria tu haina vifaa vyovyote vile mgonjwa akiwa anapokuwa

anashindikana na tatizo lolote lazima apelekwe Chake Chake, na huko Chake

Chake unaweza ukaenda pale ushapelekwa kama umepelekwa usiku

unawekwa mpaka asubuhi ili kwa kuweza kupatiwa vipimo. Mhe. Naibu

Spika, nimuombe Mhe. Waziri suala hili alishughulikie ili hospitali ya

Vitongoji iweze kupatiwa vifaa.

Mhe. Naibu Spika, nikitoka hapo niende katika Hospitali ya kijiji cha Kiuyu

Minungwini kituo cha Afya. Mhe. Naibu Spika, kituo hichi cha Afya kwa

kweli ni kituo cha miaka mingi sana tayari kimeshaanza kufanya ufa hakiwezi

kutekeleza huduma yake, namuomba Mhe. Waziri aje anieleze ni lini kituo

kile kitajengwa kipya au kitafanyiwa ukarabati.

Mhe. Naibu Spika, nikitoka hapo niende kwenye ukurasa wa 57 Huduma za

Chanjo. Mhe. Naibu Spika, katika kitabu hichi kimeeleza kama katika

huduma za chanjo za kupunguza maradhi Pemba haikufanikisha kutokana na

umeme wa Tukuza. Sasa namuomba Mhe. Waziri aje anieleze hivi kweli

Wizara nzima ya Afya inashindwa na pesa ya kununua umeme wa Tukuza.

Mhe. Naibu Spika, nikitoka hapo niende kwenye Ajira za Madaktari ambao

wana utaalamu wa kusafisha matatizo ya kibofu cha Mkojo. Kutokana na

tatizo linalowasumbua wananchi kisiwani Pemba tatizo hili limeenea sana

katika Wilaya ya Chake Chake. Unapokwenda pale hospitali ya Chake Chake

ukifika tu ukiwa na matatizo haya ya kibofu cha mkojo wanakuingiza mpira

na baadae kukusababishia matatizo makubwa sana, namuomba Mhe. Waziri

katika ajira atakazoajiri mwaka huu watafute daktari ambaye atakuwa na

utaalamu wa kuweza kuliondoa tatizo hili na linawasumbua zaidi kina baba.

Page 140: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

140

Mhe. Naibu Spika, kwa kuwa muda wako nauthamini sana naomba niunge

mkono hotuba ya Mhe. Waziri, lakini nikimuachia suala langu la Kituo cha

Afya cha Kiuyu Minungwini.

Mhe. Salmin Awadh Salmin: Ahsante sana Mhe. Naibu Spika, kunipa nafasi

hii na mimi nikaweza kuchangia mawili matatu katika Hotuba hii ya Mhe.

Waziri wa Afya Mhe. Juma Duni Haji kuhusu Makadirio ya Mapato na

Matumizi kwa mwaka 2013/2014.

Mhe. Naibu Spika, Wizara hii ya Afya ni Wizara muhimu sana kwa ajili ya

maendeleo ya Afya ya wananchi wa Zanzibar. Kama tunavyofahamu Mhe.

Naibu Spika, kipindi hiki au katika zama hizi kumekuwa na maradhi mengi

yanayowakabili wananchi, na hii inatokana na mambo mbali mbali ambayo

wataalamu wetu wamekuwa wakitueleza ikiwemo masuala mazima ya

vyakula vyetu hivi tunavyovila. Kwa hivyo, wizara hii ni muhimu na kwa

sababu inabeba uhai wa wananchi wa Zanzibar.

Mhe. Naibu Spika, wenzetu hawa wamekuwa wakijitahidi kuhudumia

wananchi wa Zanzibar na kuhakikisha kwamba Afya zao zinaimarika kila

siku. Lakini tatizo tuliloliona ambalo tatizo hili mimi nashindwa kuelewa sijui

nimlaumu nani na kwa sababu mambo haya yanategemeana na hali halisi ya

uchumi wetu. Sote tunafahamu Wajumbe wa Baraza hili kwamba hali ya

Uchumi wa nchi yetu kwa kweli si nzuri na hii mimi nadhani inapelekea

kutupa tabu namna ya kugawana hii rasilimali fedha tuliyo nayo. Kwa sababu

mapato yetu ni madogo lakini mahitaji yetu ni makubwa. Lakini hata hichi

kidogo ambacho tunakipata nacho kinaonekana hatukitumii uzuri.

Kwa hivyo, Mhe. Naibu Spika, mimi nathubutu kusema kwamba sijui

nimlaumu nani, na kwa sababu ukiangalia migawanyo tunayogawana katika

wizara mbali mbali basi utakuta fedha zinazotolewa au mgao unaotolewa basi

haufikii yale malengo ambayo tumelenga. Sasa nasema Mhe. Naibu Spika,

kwamba sijui nimlaumu nani sijui niilaumu Wizara ya Fedha? sijui nimlaumu

Waziri wa Afya au Mawaziri wengine, sijui nimlaumu Katibu Mkuu wa

Wizara ya Afya, kwa sababu huwezi kutekeleza malengo kama rasilimali

fedha ulizopewa ni chache. Tunabakia hapa kulaumiana.

Lakini Mhe. Naibu Spika, mimi ninaloliona kwetu sisi wana siasa na wenzetu

watendaji tuisimamie Serikali tuhakikishe kwamba uchumi wetu unakua,

mapato yetu yanakuwa vianzio vyetu vya mapato vinaongezeka ili tuweze

kupata fedha za kuweza kutekeleza mahitaji yetu, vyenginevyo kila siku

tutakuwa tunalaumiana bure hapa.

Page 141: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

141

Mhe. Naibu Spika, katika Bajeti ya mwaka uliopita na katika bajeti hii ya

mwaka huu Mhe. Waziri wa Fedha pia alituambia katika mambo yaliyoekewa

kipaumbele ni masuala ya Afya. Lakini ukiangalia mimi nimeangalia fedha za

maendeleo zilizotengwa na zilizopatikana. Lakini nimeangalia fedha za

matumizi ya usoni zilizotengwa hadi kupatikana hadi kufikia mwezi wa

Machi nafikia pahala sijui nimlaumu nani.

Kwa hivyo, Mhe. Naibu Spika, mambo haya yanahitaji kuangaliwa kwa

umakini sana, tutakuja kufika pahala tutalaumiana wengine wanataonekana

wabaya, lakini kumbe tatizo upatikanaji wa fedha, waswahili wamesema

"Maskini hapendi mwana". Msemo huu una umuhimu mkubwa sana, kwa

sababu wewe unapokuwa masikini huna huwezi kufanya mambo mengine

yoyote yale hata nyumbani kwako Mhe. Naibu Spika, ukiwa huna fedha basi

matumizi yako yataoana na kipato chako. Pengine ungependa kila siku ule

biriani nyumbani kwako, lakini fedha huna utafanyaje. Kwa hivyo, masikini

hapendi mwana pengine ungependa mtoto wako kila anapokwenda skuli

aondoke na shilingi elfu kumi. Lakini unampa shilingi mia tano si kwa sababu

humpendi lakini fedha ulizokuwa nazo ndio kwa kiasi kile ulichokuwa nacho.

Kwa hivyo, Waheshimiwa Wajumbe wenzangu wa Baraza hili lazima tufike

pahala hili tulizingatie kwa umakini, vyenginevyo tutakuwa tunanyosheana

vidole, Waziri mbaya, Katibu Mkuu mbaya, kumbe rasilimali fedha tuliokuwa

nayo ni chache.

Mjumbe mwenzangu hapa Mhe. Ismail Jussa Ladhu alisema kwamba katika

kikao cha Makatibu wakuu anapinga kuwaongeza madakatari mimi sifikirii

kama jambo hili linaweza likawa sifikirii, kwamba Katibu Mkuu asifanye

mbinu zozote za kuona madaktari wake wanapata maslahi makubwa, mimi

sidhani kama kuna Katibu Mkuu wa aina hiyo pengine ni dhana tu. Kwa

sababu maslahi yote ya wafanyakazi wa Serikali yapo katika Idara ya

Utumishi, na juzi tulikuwa tunasema hapa tunaitaka Serikali kupitia Wizara

ya Utumishi ijaribu kuangalia na kuboresha maslahi ya wafanyakazi wa

Serikali wakiwemo madaktari.

Sasa tunapofika pahala tukalaumiana mimi naogopa sana tusije kufika pahala

tukamgombanisha Katibu Mkuu na madaktari wake. Mimi leo ukinambia

kuwa Spika, anazuia maslahi yangu sina urafiki na Mhe. Spika, halkadhalika

binaadamu yoyote atakaposikia fulani anazuia maslahi ya mtu mwengine

urafiki huo utakuwa haupo.

Kwa hivyo, tusije kujenga dhana kwa madaktari wetu kwamba Katibu Mkuu

anazuia maslahi ya madaktari, kwa kweli tutakujamfikisha pahala pabaya na

si jambo zuri. Suala la maslahi ya wafanyakazi yako chini ya Wizara ya

Page 142: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

142

Utumishi, na mara zote wenzetu watumishi wanatwambia hata Mhe. Rais

anasema mara zote kwamba ataongeza maslahi ya wafanyakazi pale hali

itakaporuhusu. Safari hii ametenga fedha bilioni 17 kwa ajili ya maslahi ya

wafanyakazi.

Hata jana Mhe. Rais kwenye mkutano uliofanyika Kibanda Maiti alisema na

alirudia kwamba atajitahidi kadiri ya uwezo wake kuhakisha maslahi ya

wafanyakazi yanaboreshwa kila hali itakaporuhusu. Sasa nadhani tuzingatie

haya maelezo yanayotolewa na Viongozi wetu tusije kufika pahala tukaona

kuna mtu anajaribu kumzuia mwengine.

Mimi nakubaliana sana na Wahehimiwa Wajumbe wenzangu kwamba bado

maslahi ya madaktari yanahitaji kuboreshwa, na hapa walipo Mhe. Naibu

Spika siko wanakotoka, sote mashahidi, madaktari wanatoka hali mbaya ziadi

huko nyuma kabla wakati wa Mhe. Dr. Ali Mohamed Shein na wameweza

kurekebishiwa maslahi yao katika hatua hii waliopo, haidhuru hawawafikii

wenzao wa Tanzania Bara, lakini maslahi ya madaktari yameboreshwa.

Siwezi kutaja takwimu hapa, lakini sote tunafahamu kwamba maslahi ya

madaktari yameboreshwa na serikali itakapopata uwezo itaboresha zaidi ili

yawe bora zaidi, na mimi nakubaliana sana na Waheshimiwa Wajumbe

wanaosema madaktari ni muhimu, pamoja na umuhimu wa wafanyakazi

wengine lakini madaktari ni muhimili muhimu sana.

Mhe. Naibu Spika, nakubaliana na wazo la Mhe. Ismail Jussa Ladhu kwamba

madaktari wanastahiki kulipwa mishahara yao, ili angalau ioane na

Wakurugenzi na huu ni juu ya umuhimu wa kada hii waliyonayo. Kwa hivyo,

Mhe. Naibu Spika, hali yetu kwa kweli ya kifedha isije ikafika pahala

tukaanza kuzozona wenyewe kwa wenyewe, sote keki ya taifa tunaijua, keki

yetu tunayoipata hapa tunaijua, namna tunavyogawana tunajua.

Takwimu hizi ambazo wenzetu wa Wizara ya Afya wametuletea asilimia 30,

35, 17 sijui asilimia ngapi, hakuna hata eneo moja lililokiuka zaidi ya asilimia

hizi za namna ya utekelezaji. Kwa hivyo, tusije tukafika pahala tukalaumiana

katika hili, lakini pia tusije tukawalaumu zaidi wenzetu wa Wizara ya Fedha,

Uchumi na Mipango ya Maendeleo kwa sababu ndio keki tuliyokuwa nayo,

fedha tulizokuwanazo hatuwezi zote tukaielekeza eneo moja, lazima

tugawane kidogo kidogo. Hata mzee wetu muasisi Marehemu Mzee Abeid

Aman Karume alisema kwamba bora tugawane kidogo kidogo kuliko kuja

kugombania kilichopo. Kwa hivyo, hiyo ni misemo ambayo ni sahihi waasisi

wetu wametueleza kwamba kidogo tulichokuwanacho basi tugawane kidogo

kidogo, kuliko kuja kuwa na kingi tukaanza kugombania.

Page 143: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

143

Mhe. Naibu Spika, kuhusu utaratibu unaofanywa wa kuwapeleka wagonjwa

katika maeneo katika hospitali ya Mnazi Mmoja. Kwa kweli Mhe. Naibu

Spika, wenzetu wamekuwa na utaratibu kwa upande mmoja naweza kusema

ni mzuri, lakini kinachoonekana bado Hospitali ya Mnazi Mmoja

hawajajipanga katika hili. Kumekuwa na utaratibu ambao sasa hivi

unalalamikiwa na wananchi walio wengi. Wagonjwa wanapofika katika

Hospitali ya Mnazi Mmoja wanaulizwa, wewe umetokea wapi. Anajibu mimi

natokea Magomeni, anaambiwa nenda Kidongo Chekundu au nenda Nyumba

za Wazee. Ni sawa, lakini je Wizara ya Afya wamekiandaa vipi kitu kile

kidogo kilichopo. Unapomwambia mgonjwa aende kituo cha Mental pale au

mgonjwa wa Magomeni aende kituo cha Fuoni, au unapomwambia nenda

katika kituo cha Sebleni, hicho kituo umekiandaaje, au yule mgonjwa

unayempeleka kule kile kituo umekiandaaje? Kwa sababu sio suala la kwenda

tu ni suala la huduma ambayo ataipata kule. Kwa hivyo, wananchi wetu

wamekuwa wakitulalamikia sana juu ya utaratibu huu, wamesema utaratibu

huu hauwapi faraja.

Mimi nadhani Hospitali ya Mnazi Mmoja isipunguze msongomano wa eneo

lile kwa utaratibu huu, maana yake wananchi wetu watakuja kuonekana

kwamba tunawatelekeza na ni jambo ambalo sio zuri. Unamtoa katika

hospitali ya Mnazi Mmoja ambapo mwenyewe alitegemea kwamba atapata

matibabu, halafu unamwambia nenda katika kituo cha Sebleni, Sebleni

hakuna daktari, hakuna huduma nyengine yoyote. Kwa kweli utaratibu huu

nadhani ni mapema mno. Ni vyema Wizara ya Afya ikaviandaa hivi vituo

kwa ajili ya kupokea wagonjwa, ikiwemo kuwa na madaktari na vifaa vya

kutosha.

Mhe. Naibu Spika, sidhani kama vituo hivi vya karibu vingekuwa na huduma

ya kutosha, kama mwananchi angetoka Magomeni akaenda zake Mnazi

Mmoja, sidhani. Lakini wananchi wanatoka katika maeneo haya wakitegemea

kwamba Mnazi Mmoja ndiko kwenye huduma ambayo wanaweza kuipata.

Kwa hivyo, suala hili Mhe. Waziri nasema kwamba bado linahitaji uliangalie

kwa makini zoezi hili, ni zuri linaweza likapunguza msongomano katika

Hospitali yetu ya Mnazi Mmoja, hospitali ya rufaa. Lakini hivi vituo ambavyo

tunawapeleka wagonjwa wetu vimeandaliwa.

Leo Mhe. Naibu Spika, ukienda katika kituo cha Fuoni ambacho kinahudumia

maeneo yote yale, sijui utafikiria pana kitu gani. Ni kituo kinachobeba

wagonjwa wengi, kituo ambacho kimechukua eneo kubwa. Kwa hivyo, Mhe.

Waziri jambo hili linalalamikiwa sana na ninaamini utaliona na utachukua

hatua zinazostahiki juu ya jambo hili.

Page 144: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

144

Jengine Mhe. Naibu Spika, ni suala hili ambalo wenzangu pia wamelisema ni

juu ya utaratibu huu wa kwenda kuwaangalia wagonjwa. Mimi ninaongeza

nyama katika hili, maana kichwani mwangu lilikuwepo, japokuwa hupendi

Mhe. Naibu Spika, lakini najaribu kuongeza nyama.

Mhe. Naibu Spika, kwa kweli katika Hospitali ya Mnazi Mmoja hakuhitaji

vurugu ambazo zinasababisha mambo mengi. Lakini sasa vurugu zile badala

ya kuwemo mule ndani, sasa vurugu zinakuja barabarani, kwa sababu wale

wanaokwenda kuwaangalia wagonjwa wao hawapati nafasi ya kuingia ndani,

matokeo yake wanazagaa huko barabarani. Hii inatokana na nini Mhe. Naibu

Spika, kwa sababu bado hawajaamini kuwa wagonjwa wao wanaweza

kuhudumiwa ipasavyo. Sote tunajua kwamba tuna upungufu wa dawa, wakati

mwengine mgonjwa anaandikiwa dawa yuko kitandani, lakini wale wa

kwenda kununua ile dawa wako nje, matokeo yake mgonjwa yule anakua

hapati huduma ya kutosha, hiyo ndio hofu yao. Laiti wagonjwa wale

wangekuwa wanapata huduma ya kutosha mule ndani ya ward, mna

wahudumu wa kutosha, mgonjwa anapotaka kwenda chooni anasaidiwa, basi

sidhani kama watu wangekuwa wanakwenda kurundikana, kwa sababu

wangekuwa na matumaini makubwa juu ya huduma inayotolewa mule katika

Hospitali yetu ya Mnazi Mmoja.

Kwa hivyo, ni suala zuri, lakini kama nilivyotangulia kusema lile la mwanzo,

tunatakiwa kwanza tujipanga vizuri sana ili tuone kwamba mambo haya

yanayotuletea matatizo katika jamii yetu yanaondoka.

Mhe. Naibu Spika, Mhe. Waziri wa Fedha, Uchumi na Mipango ya

Maendeleo hayupo, na Mkuu wa Shughuli za Serikali pia hayupo, kama

alivyosema Mhe. Ismail Jussa. Lakini ombi langu Mhe. Naibu Spika, katika

bajeti hii ya mwaka 2013/2014 waiangalie sana Wizara ya Afya, pamoja na

ufinyu wa bajeti au pamoja na keki ndogo tuliyonayo, lakini waiangalie sana

Wizara ya Afya na kwa sababu Wizara ya Afya ndio kwenye uhai. Ukiwa na

nguvu kazi ambayo haiwezi kufanya kazi kutokana na maradhi basi huwezi

kupata maendeleo na sote Wazanzibari ni wagonjwa, asiyeugua hiki ana hiki,

hakuna hata mmoja ambaye yuko mzima kwa asilimia 100 sote tuna maradhi

na sote tunahitaji kukimbilia hospitalini.

Kwa hivyo, Mhe. Waziri wa Fedha, Uchumi na Mipango ya Maendeleo kama

Kaimu yupo, namuona Kaimu yupo wa Wizara ya Fedha, Uchumi na

Mipango ya Maendeleo Dk. Mwinyihaji tunakuomba sana takwimu hizi

zilizojitokeza katika bajeti hii, basi mwakani kuonekana mabadiliko.

Tusizungumzie suala la asilimia 17 au asilimia 20. Kama tunakusudia

kwamba Wizara ya Afya ni kipaumbele, basi kwa kadiri tunavyoweza ile sura

ya kipaumbele iweze kuonekana. Sio lazima kwamba kwa asilimia 100, lakini

Page 145: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

145

angalau Wajumbe wako wa Baraza la Wawakilishi waone kwamba kweli

hapa kipaumbele kimewekwa, lakini kilishindikana kutekelezwa kwa asilimia

100 kwa sababu ya ufinyu wa bajeti, lakini kwa hivi takwimu zilivyo

inaonesha dhahiri kwamba hakuna kipaumbele ni haya mambo ya

kubabaishana babaishana tu, lakini hakuna kipaumbele katika bajeti hii.

Kwa hivyo, kipaumbele lazima kionekane Mhe. Naibu Spika, Wizara ya

Fedha, Uchumi na Mipango ya Maendeleo ni lazima iweke fedha za kutosha

kwa ajili ya huduma za wananchi. Tunasubiri bajeti ya mwakani, mimi

niwaombe Waheshimiwa Wajumbe wenzangu, pamoja na kwamba Mhe.

Ismail Jussa rafiki yangu anasema haiungi mkono kwa asilimia 100. Lakini

mimi nadhani tuiunge mkono hii bajeti ya Mhe. Juma Duni, kwa sababu

tutakuja kumalizika, kama hatutoipitisha bajeti hii, maana yake tutawamaliza

wananchi wetu.

Tuiunge mkono bajeti hii ili angalau japo hizo panadol waweze kuzipata.

Sasa kama hatutoipitisha bajeti hii ya Wizara ya Afya, maana yake hakuna

huduma yoyote itakayotolewa. Kwa hivyo, tuiunge mkono bajeti hii ipite,

lakini lazima serikali iangalie sana eneo hili ni muhimu, eneo la madaktari,

maslahi ya madaktari ni muhimu, eneo la madawa ni muhimu, eneo la

huduma za afya ni muhimu.

Kwa hivyo, Mhe. Naibu Spika, kwa kuwa muda wako unamalizika na mimi

maelezo yangu yanamalizika kwamba naunga mkono bajeti hii ya Wizara ya

Afya kwa masharti kwamba mambo haya ambayo yanaonekana ni kasoro,

basi serikali iyaangalie na sisi Inshaallah Mwenyezi Mungu akitujaalia bajeti

mwakani tupo, tutaiangalia.

Lakini kubwa zaidi Mhe. Juma Duni uelewe kwamba wewe ndio dhamana wa

wizara hii, wewe ndiye mas-ul na hili huwezi ukalikwepa, kwa sababu

matatizo yaliopo hapa hawezi kuteremka kule Katibu Mkuu na Mkurugenzi

kuja kujibu, utakayejibu ni wewe. Kwa hivyo, wewe ndiye mas-ul wa Wizara

ya Afya, wewe ndiye dhamana wa Wizara ya Afya. Matatizo yote

yanayojitokeza wewe ndiye utakayejibu kwa niaba ya serikali. Kwa hivyo,

hili nalo Mhe. Waziri ulijue. Sisi hatumkamati mtu mwengine hapa,

tutakukamata wewe, tukitaka kuwawajibisha basi tutakuwajibisha kwanza

wewe katika hili. Kwa hivyo, huwezi ukakwepa lawama yoyote itakayotokea

katika wizara hii, wewe ndiye mas-ul.

Baada ya maelezo haya Mhe. Naibu Spika, naunga mkono hoja na niwaombe

Waheshimiwa Wajumbe wenzangu waunge mkono, ili tuendeleze mbele

mambo yetu, ahsante sana Mhe. Naibu Spika.

Page 146: ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI … · mahabusu wananyimwa haki ya kuzungumza na vyombo vya habari wakati haki yao kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar

146

Mhe. Naibu Spika: Mhe. Salmin Awadh Salmin tunakushukuru.

Waheshimiwa Wajumbe, nilizungumza katika kipindi cha jioni kwamba hivi

sasa tuko nyuma kwa siku nne ya bajeti yetu, na nikazungumza wanaotaka

kuchangia walete mapema ili tujipange. Kwa bahati mbaya sasa hivi

nimepokea majina sita kwa mfululizo na tumeshasema kwamba kesho

asubuhi Mhe. Waziri anajumuisha.

Kwa hivyo, niwaombe Waheshimiwa Wajumbe wafuatao walete michango

yao asubuhi kwa maandishi ili Waziri wakati wa maswali aweze kutafuta

majawabu, hivyo tunawataka radhi sana, nao ni;

1. Mhe. Mohamed Mbwana Hamad

2. Mhe. Salma Mussa Bilali

3. Mhe. Mohamed Haji Khalid

4. Mhe. Farida Amour Mohamed

5. Mhe. Mahmoud Muhammed Mussa

Waheshimiwa Wajumbe, kesho asubuhi tukijaaliwa tukimaliza maswali,

wamebakia wachangiaji wawili. Mhe. Bi Panya Ali Abdalla na Mhe.

Mwanajuma Faki Mdachi. Wao walileta majina tangu asubuhi.

Baada ya hapo tutamwita Mhe. Naibu Waziri na baadae tuwaite mawaziri

wanaotaka kumsaidia. Baada ya maelezo hayo nawashukuru kwa

mashirikiano yenu. Naakhirisha kikao chetu mpaka kesho siku ya Jumanne

tarehe 09/07/2013 saa 3:00 barabara za asubuhi.

(Saa 1: 45 usiku Baraza liliakhirishwa hadi tarehe 09/07/2013 saa 3:00

asubuhi)