Rais Magufuli Ahudhuria Ibada Ya Pasaka Azania Front

Embed Size (px)

Citation preview

  • 8/19/2019 Rais Magufuli Ahudhuria Ibada Ya Pasaka Azania Front

    1/2

    JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

    KURUGENZI YA MAWASILIANO YA RAIS IKULU

    Simu: 255-22-2114512, 2116898

     E-mail: [email protected]

    Tovuti : www.ikulu.go.tz 

     Faksi: 255-22-2113425

    OFISI YA RAIS,

    IKULU,

    1 BARABARA YA BARACK OBAMA,

    11400 DAR ES SALAAM.

    Tanzania. 

    T RIF KW VYOMBO VY H B RI

    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amewasihi

     watanzania kuendelea kuwa wamoja na kushirikiana kuijenga nchi yao, badala ya

    kubaguana.

    Rais Magufuli ametoa wito huo leo katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania

    (KKKT), Usharika wa Azania Front Jijini Dar es salaam, ambako amesali ibada ya

    Pasaka pamoja na waumini wa kanisa hilo.

     Amesema Mwenyezi Mungu alimtoa mwanae wa pekee Yesu Kristo kuja

    kuikomboa dunia bila kuwabagua wanadamu, vivyo hivyo nasi binadamu tunapaswa

    kutobaguana, iwe kwa dini zetu, makabila yetu, mitazamo ya kisiasa na hata rangi

    zetu.

     Aidha, Rais Magufuli amewakumbusha watanzania kufanya kazi kama ambavyo

     vitabu vitakatifu vinasisitiza umuhimu wa kufanya kazi, na amebainisha kuwa

    Tanzania yenye neema inawezekana endapo kila mtu atazingatia kufanya kazi.

    “Tukifanya kazi hatuhitaji hata misaada kutoka nje nchi hii ina neema nyingi. Kwa

    kweli tukifanya kazi kwa bidi nchi yetu inapaswa kuwa inatoa misaada kwa nchi

    nyingine n sio kuomb mis d kutok nchi nyingine” Amesisitiza Dkt. Magufuli.

    Rais Magufuli ambaye amesali kwenye kanisa hilo kwa mara ya kwanza tangu

    achaguliwe kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, lakini ikiwa ni mara

     yake ya nne kusali katika kanisa hilo hata kabla ya kuwa Rais, amewaomba

     watanzania kuendelea kuliombea Taifa lao na pia kumuombea yeye ili afanikiwe

    kutekeleza jukumu kubwa na zito la kuiongoza nchi.

    http://www.ikulu.go.tz/http://www.ikulu.go.tz/http://www.ikulu.go.tz/http://www.ikulu.go.tz/

  • 8/19/2019 Rais Magufuli Ahudhuria Ibada Ya Pasaka Azania Front

    2/2

    Pamoja na kuongoza maombi ya kumuombea Rais Magufuli na Mkewe Mama

     Janeth Magufuli waliohudhuria ibada hiyo, Askofu Mkuu wa KKKT Dayosisi ya

    Mashariki na Pwani, Dkt. Alex Malasusa amempongeza Rais Magufuli kwa tabia

     yake ya kupenda kuhudhuria ibada na kuwasihi viongozi wengine kupenda ibada.

     Askofu Malasusa ameuelezea ufufuo wa Yesu Kristo kuwa jambo la kuleta

    matumaini, na hivyo amepongeza mwelekeo wa nchi kwa sasa, huku akisema Kanisa

    linaona matumaini kwa Taifa.

    Gerson Msigwa

    Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU

    Dar es salaam

    27 Machi, 2016