Upload
nathan-komba
View
404
Download
10
Tags:
Embed Size (px)
DESCRIPTION
Iwe Elimu Kwanza
Citation preview
i
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI
MKAKATI WA UTEKELEZAJI WA SERA YA ELIMU NA MAFUNZO
YA MWAKA 2012 KWA KIPINDI CHA MWAKA 2014-2024
RASIMU YA KWANZA
MACHI, 2013
ii
YALIYOMO
FASIRI ..................................................................................................................................................... v SURA YA KWANZA .............................................................................................................................. 1 MAUDHUI YA MIKAKATI KUTEKELEZA SERA YA ELIMU NA MAFUNZO ............................ 1
1.0 Utangulizi ....................................................................................................................................... 1 SURA YA PILI ........................................................................................................................................ 8 DIRA, DHIMA NA MALENGO KATIKA MKAKATI WA UTEKELEZAJI WA SERA ................... 8 2.0. Utangulizi ....................................................................................................................................... 8 SURA YA TATU ..................................................................................................................................... 9
MIFUMO, MIUNDO NA TARATIBU NYUMBUFU KUMWEZESHA MTANZANIA
KUJIENDELEZA KWA NJIA MBALIMBALI KATIKA MIKONDO YA
KITAALUMA NA KITAALAMU. .............................................................................................. 9 3.0. Utangulizi ....................................................................................................................................... 9
3.1. LENGO Na.1: Kuweka mfumo, miundo na taratibu nyumbufu katika elimu na mafunzo
ili kuleta ulinganifu, muunganiko na ufanisi katika ngazi na fani mbalimbali za
kitaaluma na kitaalamu ili kumwezesha mwanafunzi kutoka mkondo mmoja kwenda
mwingine........................................................................................................................................ 9
3.2. LENGO Na. 2: Elimu ya Awali kuwa ya lazima na kutolewa kwa watoto wenye umri
kati ya miaka mitatu hadi mitano kwa kipindi kisichopungua mwaka mmoja. ........................... 10 3.3 LENGO Na. 3: Elimu-Msingi kuwa ya lazima kuanzia darasa la kwanza hadi kidato
cha nne; na kutolewa kwa miaka kumi na umri wa kuanza darasa la kwanza kuwa kati
ya miaka minne hadi sita kulingana na maendeleo na uwezo wa mtoto kumudu masomo
katika ngazi husika. ...................................................................................................................... 10 3.4 LENGO Na. 4:Kuweka utaratibu ili kuhakikisha muda wa kukamilisha elimu na
mafunzo katika ngazi mbalimbali za elimu baada ya Elimu - Msingi unakuwa na tija na
ufanisi. .......................................................................................................................................... 11
SURA YA NNE ..................................................................................................................................... 13 ELIMU NA MAFUNZO YENYE VIWANGO VYA UBORA UNAOTAMBULIKA
KIKANDA NA KIMATAIFA NA YANAYOKIDHI MAHITAJI YA SASA NA YA
BAADAYE YA TAIFA. ............................................................................................................. 13 4.0 Utangulizi ..................................................................................................................................... 13
4.1 LENGO Na.1: Kuimarisha ithibati na uthibiti wa ubora wa elimu na mafunzo katika
ngazi zote yakiwemo masuala ya ushauri. ................................................................................... 13
4.2 LENGO Na. 2: Kuimarisha ukuzaji, utayarishaji na utekelezaji wa mitaala kwa
kuzingatia mahitaji ya taifa na ya walengwa katika ngazi zote za elimu na mafunzo. ................ 14 4.3 LENGO Na.3: Kuimarisha usimamiaji na upimaji wa utekelezaji wa mitaala katika
taasisi za elimu na mafunzo katika ngazi zote ili kuleta ufanisi wa elimu na mafunzo
yatolewayo. .................................................................................................................................. 16
4.4 LENGO Na 4: Kuimarisha ufundishaji na ujifunzaji wa lugha ili kuwa na wanafunzi
mahiri wenye uwezo wa kuwasiliana kwa Kiswahili, Kiingereza na lugha nyingine za
kigeni katika mfumo wa elimu na mafunzo. ................................................................................ 16 4.5 LENGO Na. 5: Kuwezesha lugha ya alama kutumika katika ngazi zote za elimu na
mafunzo........................................................................................................................................ 17 4.6 LENGO Na. 6: Kuimarisha uthibiti wa programu, mitihani na tuzo za nje zinazotolewa
nchini katika ngazi zote za elimu na mafunzo. ............................................................................ 17 SURA YA TANO .................................................................................................................................. 19
iii
UPATIKANAJI WA FURSA MBALIMBALI ZA ELIMU NA MAFUNZO NCHINI ....................... 19
5.0 UTANGULIZI ............................................................................................................................. 19 5.1 LENGO Na.1: Kuongeza fursa anuwai za elimu na mafunzo kwa usawa kwa makundi
yote ya kijamii katika ngazi zote. ................................................................................................ 19
5.2 LENGO Na. 2: Kuondoa vikwazo vinavyozuia fursa ya wanafunzi kuendelea na
masomo na kukamilisha mzunguko wa elimu na mafunzo katika ngazi husika. ........................ 20 5.3 LENGO Na.3: Kuweka utaratibu utakaowezesha maendeleo ya wanafunzi wenye
vipaji, vipawa na kasi tofauti katika kujifunza kwa ngazi zote za elimu na mafunzo. ................ 21 5.4 LENGO Na. 4: Kuweka utaratibu na kuimarisha utambuzi wa viwango vya Elimu na
mafunzo ili kutoa fursa ya kila Mtanzania kujiendeleza kielimu, kupata maarifa na stadi
za kazi kwa kuzingatia kwamba elimu au mafunzo hayana mwisho........................................... 21 SURA YA SITA ..................................................................................................................................... 23 ONGEZEKO LA RASILIMALI MBALIMBALI KULINGANA NA MAHITAJI KATIKA
NGAZI ZOTE ZA ELIMU NA MAFUNZO .............................................................................. 23 6.0 UTANGULIZI ............................................................................................................................. 23
6.1 LENGO Na.1: Kuimarisha mfumo wa ajira katika sekta ya elimu na mafunzo ili uwe
mahsusi na kukidhi mahitaji, upatikanaji na usimamizi wa rasilimaliwatu kwa ajili ya
maendeleo ya sekta ya elimu na mafunzo.................................................................................... 23 6.2 LENGO Na. 2: Kuweka mazingira bora na kuhakikisha kuwa sekta ya elimu na
mafunzo inatoa rasilimaliwatu wa kutosha na mahiri kukidhi mahitaji ya sekta
mbalimbali kwa maendeleo ya Taifa. .......................................................................................... 24 6.3 LENGO Na. 3: Kuweka utaratibu wa kuhakikisha uwepo wa miundombinu bora na
stahiki ya kutosheleza mahitaji ya elimu na mafunzo katika ngazi zote. .................................... 25 6.4 LENGO Na. 4: Kuweka utaratibu wa kuhakikisha vifaa, nyenzo na zana stahiki za
kufundishia na kujifunzia katika elimu na mafunzo zinatosheleza kulingana na mahitaji
na maendeleo ya sayansi, teknolojia na mbinu za kufundishia na kujifunzia katika ngazi
zote. .............................................................................................................................................. 26 6.5 LENGO Na 5: Kuweka utaratibu wa kuwezesha lugha ya Kiswahili na Kiingereza
kuwa lugha za kufundishia na kujifunzia katika ngazi zote za elimu na mafunzo ...................... 27
6.6 LENGO Na. 6:Kuweka utaratibu na mazingira wezeshi ya kuhakikisha elimu na
mafunzo katika ngazi zote inatolewa kwa ufanisi kwa njia huria na masafa. ............................. 28
6.7 LENGO Na. 7: Kuhakikisha kila taasisi ya elimu na mafunzo inakuwa na hatimiliki ya
ardhi mahali ilipo taasisi hiyo kwa ngazi zote. ............................................................................ 29
SURA YA SABA ................................................................................................................................... 30 MFUMO ENDELEVU WA UGHARIMIAJI WA ELIMU NA MAFUNZO NCHINI ........................ 30 7.0 UTANGULIZI ............................................................................................................................. 30 7.1 LENGO Na. 1: Kuimarisha mfumo wa ugharimiaji wa elimu na mafunzo kwa ngazi
zote kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa sekta ya elimu na mafunzo. ............................ 30
SURA YA NANE .................................................................................................................................. 32 UONGOZI, USIMAMIZI NA UENDESHAJI WA ELIMU NA MAFUNZO NCHINI ...................... 32
8.0 UTANGULIZI ............................................................................................................................. 32 8.1 LENGO Na. 1: Kuongeza ufanisi, tija uwajibikaji na uongozi bora, usimamizi na
uendeshaji wa elimu na mafunzo nchini ...................................................................................... 32 8.2 LENGO Na. 2: Kuimarisha mfumo wa menejimenti ya data na taarifa za elimu na
mafunzo kwa ngazi zote za elimu na mafunzo. ........................................................................... 32 SURA YA TISA ..................................................................................................................................... 34
iv
MASUALA MTAMBUKA KATIKA ELIMU NA MAFUNZO KUZINGATIWA ............................ 34
9.0 UTANGULIZI ............................................................................................................................. 34 9.1 LENGO Na.1: Elimu na Mafunzo yenye maudhui ya masuala mtambuka kwa ajili ya
maendeleo endelevu ya Taifa....................................................................................................... 34
9.2 LENGO Na. 2: Kuweka utaratibu wa kuimarisha utoaji wa huduma ya ushauri na
unasihi katika ngazi zote za elimu na mafunzo. .......................................................................... 34 9.3 LENGO Na. 3: Kuweka utaratibu utakao hakikisha kuwa haki za binadamu zinalindwa
na hawapewi adhabu za kutesa au kudhalilisha wakati wakipatiwa elimu au mafunzo
katika ngazi mbalimbali. .............................................................................................................. 35
9.4 LENGO Na.4: Kuweka utaratibu wa kuhakikisha maadili ya walimu na watumishi
wengine yanazingatiwa katika ngazi zote za elimu na mafunzo. ................................................ 36 9.5 LENGO Na.5: Kuimarisha muundo wa kutekeleza maazimio na itifaki za ushirikiano
baina ya Tanzania na nchi nyingine, kikanda na kimataifa katika elimu na mafunzo ................. 36
9.6 LENGO Na. 6: Kuimarisha utaratibu wa kuwezesha wanafunzi kujifunza kwa ufanisi
masomo ya hisabati, sayansi na tekinolojia katika ngazi zote za elimu na mafunzo. .................. 37
9.7 LENGO Na. 7: Kuweka utaratibu wa kuhakikisha matumizi zaidi ya sayansi na
tekinolojia katika utoaji wa elimu na mafunzo katika ngazi zote. ............................................... 37
9.8 LENGO Na. 8: Kuweka utaratibu na kuimarisha ushiriki fanisi wa wadau mbalimbali
katika sekta ya elimu na mafunzo katika ngazi zote .................................................................... 38 SURA YA KUMI ................................................................................................................................... 40
MGAWANYO WA MAJUKUMU NA WAJIBU KWA WADAU MBALIMBALI ........................... 40 10.0 UTANGULIZI ............................................................................................................................. 40
10.1 Ngazi ya Taifa .............................................................................................................................. 40 10.2 Ngazi ya Mkoa ............................................................................................................................. 45 10.3 Halmashauri za Wilaya, Mji, Manispaa na Jiji ............................................................................ 46
10.4 Ngazi ya Kata ............................................................................................................................... 46
10.5 Ngazi ya Shule na Chuo ............................................................................................................... 46 SURA YA KUMI NA MOJA ................................................................................................................ 47 UFUATILIAJI NA TATHMINI ............................................................................................................ 47
v
FASIRI
NENO FASIRI
MKUKUTA Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kuondoa Umasikini Tanzania MMEJ Mpango wa Maendeleo ya Elimu Ya Juu
MMEM Mpango wa Maendeleo ya Elimu Ya Msingi
MMES Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Sekondari
OWM Ofisi ya Waziri Mkuu
OWM-TAMISEMI Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
PMSE Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Elimu
SADC Southern African Development Community (Nchi Wanachama wa
Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi Kusini mwa Afrika VETA Vocational Education and Training Authority (Mamlaka ya Elimu na
Mafunzo ya Ufundi Stadi) WEMU Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
1
SURA YA KWANZA
MAUDHUI YA MKAKATI WA KUTEKELEZA SERA YA ELIMU NA MAFUNZO
1.0 Utangulizi
Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi (WEMU) imeandaa Sera ya Elimu na Mafunzo ya
mwaka 2013 ikiwa na madhumuni ya kuhakikisha taifa linapata wananchi walioelimika, wenye
ujuzi, stadi na maarifa stahiki ili kuchangia kikamilifu katika kutekeleza malengo ya taifa ya
maendeleo; na kuboresha maisha ya wananchi kama ilivyoainishwa katika Dira ya Taifa ya
Maendeleo ya mwaka 2025 na Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kuondoa Umaskini Tanzania
(MKUKUTA). Mikakati iliyotamkwa hapa itatekelezwa kwa kipindi cha miaka kumi, yaani
kuanzia 2014 hadi 2024. Mkakati unaonyesha kikamilifu maeneo ya utekelezaji, vipaumbele
vyake, shabaha zake, mgawanyo wa majukumu katika kufikia shabaha hizo, mahitaji ya
kirasilimali ili kutekeleza majukumu hayo, muda wa utekelezaji wa majukumu hayo, taratibu za
kupima utekelezaji na viashiria vya kupima ufanisi wa utendaji kazi katika kufanikisha
majukumu hayo.
1.1 Sababu ya kuwa na Mikakati
Ufanisi katika utekelezaji wa Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2013 unahitaji uwepo wa
mikakati mbalimbali katika kila eneo ambalo Sera imelilenga kuliimarisha. Mikakati hii
itawezesha:
a) Wadau mbalimbali kutekeleza matamko mbalimbali yaliyomo katika Sera;
b) Asasi na taasisi za elimu na mafunzo kuandaa mipango mkakati yake ya muda mfupi na
mrefu;
c) Kubaini vipaumbele vya utekelezaji wa sera ya elimu na mafunzo;
d) Kubaini rasilimali zitakazowezesha utekelezaji wa vipaumbele vya sera ya elimu na
mafunzo; na
e) Wizara inayohusika na elimu na mafunzo kusimamia, kuratibu utekelezaji na kufanya
tathmini;
1.2 Mambo yanayotarajiwa kutekelezwa
Muktadha wa Sera ya Elimu na Mafunzo ya Mwaka 2013 unahitaji mabadiliko makubwa katika
miundo, mfumo na taratibu za utoaji elimu na mafunzo yatakayogusa shule, vyuo, taasisi
mbalimbali, watendaji, viongozi, asasi na wadau mbalimbali wa elimu na mafunzo kwa ujumla.
Kwa mantiki hii mikakati iliyopo hapa inatarajiwa kutekeleza mambo muhimu yafuatayo:
a) Kuhuisha muundo na taratibu mpya za elimu na mafunzo kwa kuhakikisha kuwa kila
mtoto mwenye umri kati ya miaka mitatu na mitano anapitia elimu ya awali kwa
kipindi kisichopungua mwaka mmoja kabla ya kujiunga na elimu - msingi; na
kuunganisha elimu ya msingi na elimu ya sekondari ya kawaida ya sasa ili kuunda elimu
- msingi itakayotolewa kwa kipindi cha miaka kumi.
2
b) Kuhuisha mitaala ya sasa ya elimu ili iweze kukidhi muundo mpya wa elimu na
mafunzo nchini.
c) Kuhuisha sheria na taratibu mbalimbali za utoaji elimu nchini ili ziendane na muundo
mpya wa elimu – msingi.
d) Kuimarisha mfumo wa usimamizi, ithibati na uthibiti wa ubora wa elimu na mafunzo
katika ngazi zote ili uweze kukidhi malengo na muundo mpya wa elimu – msingi.
e) Kuongeza ubora wa miundombinu katika shule za sasa za msingi ili kukidhi mahitaji na
malengo ya elimu - msingi ikiwa ni pamoja na kuongeza madarasa ya elimu- msingi
katika kila shule ya msingi ya sasa; kujenga maabara za sayansi na maktaba katika kila
shule ya elimu – msingi.
f) Kutenga rasilimali fedha za kutosha kwa ajili ya nyenzo, vifaa na zana za kufundishia
na kujifunzia, vitabu vya kiada na ziada, maandiko, machapisho ya maktaba pamoja na
vifaa vya maabara.
g) Kuimarisha matumizi ya lugha za Kiswahili na Kiingereza katika ngazi ya elimu msingi
kama lugha za kujifunzia na kuwasiliana
h) Kuweka utaratibu utakaohakikisha kuwa wanafunzi wanaomaliza elimu na mafunzo ya
ngazi husika kwa ufanisi na wale wanaokatisha masomo au mafunzo yao kwa sababu
mbalimbali wanaendelea na kuhitimu masomo au mafunzo yao katika mfumo rasmi wa
elimu na mafunzo.
i) Kutoa elimu kwa umma kuhusu madhumuni, malengo na matarajio ya sera mpya ya
elimu na mafunzo.
1.3 Mgawanyo wa majukumu ya Utekelezaji
Ili kutekeleza mkakati huu, inatarajiwa kuwa wadau wote muhimu wa elimu na mafunzo nchini
watashiriki kikamilifu katika utekelezaji wa malengo, shabaha na kazi mbalimbali
zilizoainishwa katika mkakati huu. Watekelezaji muhimu wa mkakati huu ni pamoja na hawa
wafuatao:
a. Wizara yenye dhamana ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi pamoja na taasisi zake.
b. Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na taasisi zake.
c. Wizara ya Fedha, Wizara ya yenye dhamana ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Watoto na,
na wizara za sekta nyingine pamoja na taaisi zake.
d. Halmashauri za Majiji, Manispaa, Miji na Wilaya.
e. Mashirika na taasisi za dini.
f. Mashirika, asasi na taasisi zisizo za serikali.
g. Shule na vyuo vya umma na binafsi.
h. Washirika wa maendeleo.
1.4 Matokeo chanya yanayotarajiwa kupatikana baada ya mkakati kutekelezwa
Katika kipindi cha utekelezaji wa mkakati huu, matokeo yanayotarajiwa kupatikana ni pamoja
na haya yafutayo:
a) Kuwepo kwa elimu ya awali ya lazima kwa kipindi kisichopungua mwaka mmoja kabla
ya kujiunga na elimu - msingi.
b) Kuwepo kwa elimu - msingi ya miaka kumi kuanzia darasa la kwanza hadi kidato cha
nne cha sasa kwa watoto wote wenye rika lengwa la kwenda shule.
3
c) Kuwepo kwa mfumo nyumbufu, miundo na taratibu za kujiendeleza katika mikondo
anuai ya kitaalamu na kitaaluma.
d) Kuwepo kwa elimu na mafunzo yenye viwango, ubora na sifa zinazotambulika kitaifa,
kikanda na kimataifa.
e) Kuwepo kwa fursa mbalimbali za elimu na mafunzo zinazokidhi mahitaji ya wananchi
na ya nchi kiuchumi, kijamii, kisayansi na kitekinolojia.
f) Kuwepo kwa ugharimiaji endelevu wa elimu na mafunzo.
g) Kuwepo kwa mfumo wa elimu na mafunzo unaozingatia masuala mtambuka.
1.5 Hali ilivyo
Katika kutekeleza malengo yaliyowekwa katika Dira ya Maendeleo ya Taifa 2025, sekta ya
elimu imepewa kipaumbele cha pekee. Elimu katika dira hii inatazamwa si tu kama nyenzo
muhimu ya kufikia malengo ya dira, bali na elimu yenyewe ni sehemu ya malengo mahsusi ya
dira hii. Dira ya Maendeleo ya Taifa inalenga, pamoja na mambo mengine, kuiwezesha Tanzania
kufikia uchumi wa kati. Ili kukamilisha ‘ndoto’ hii, limewekwa lengo mahsusi la kuhakikisha
kuwa ifikapo mwaka 2025 Tanzania inakuwa jamii iliyoelimika na inayopenda kujielimisha
zaidi.
Ni kwa kutambua umuhimu wa elimu katika kufikia malengo yaliyomo katika Dira ya
Maendeleo ya Taifa ya mwaka 2025, sekta ya elimu imepewa kipaumbele cha pekee. Kwa
mfano, katika Bajeti ya Taifa ya mwaka 2012/2013, sekta ya elimu ilitengewa jumla ya shilingi
trilioni 3.6, ikiwa ni sawa na asilimia 24 ya bajeti nzima ya Taifa, ikiwa ni bajeti kubwa zaidi
kuliko sekta zingine katika Bajeti ya Mwaka 2012/2013.
Katika kufanikisha malengo ya kielimu, serikali imekuwa ikitekeleza mipango mbalimbali.
Mipango hii ni pamoja na Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM), Mpango wa
Maendeleo ya Elimu ya Sekondari (MMES) na Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Juu
(MMEJ).
Mafanikio mbalimbali yamepatikana katika utekelezaji wa mipango hii. Mafanikio haya ni
pamoja na kupanuka kwa fursa za kujiunga na elimu kuanzia ngazi ya elimu ya msingi hadi
elimu ya juu. Kwa mfano, kumekuwa na ongezeko la idadi ya shule za msingi kutoka shule 14,
257 mwaka 2005 hadi shule 16,331 mwaka 2012. Idadi hii imeongeza uandikishaji wa
wanafunzi wa shule za msingi kutoka 7,541,208 (Wavulana 3,855,712 na wasichana 3,685,496)
mwaka 2005 hadi 8,247,172 (wavulana 4,086,280 na wasichana 4,160,892) mwaka 2012.
Ongezeko la idadi ya shule za msingi na mkazo katika uandikishaji umeiwezesha Tanzania
4
kufikia kiwango cha asilimia zaidi ya 90 ya uandikishaji wa rika lengwa, na kuifanya Tanzania
kuwa moja ya nchi duniani zinazoelekea kufanikiwa kutekeleza kikamilifu lengo la pili (2) la
Maendeleo ya Milenia, linalotaka watoto wote wenye umri wa kujiunga na elimu ya msingi
wawe wamejiunga ifikapo mwaka 2015.
Kwa upande wa elimu ya sekondari, takwimu zinaonyesha kuwa kumekuwa na ongezeko la
shule za sekondari kutoka shule 1,745 mwaka 2005 hadi shule 4,528 kwa mwaka 2012.
Kupanuka kwa fursa za kujiunga na shule za msingi na sekondari kumewezesha ongezeko la
wanafunzi wa elimu ya sekondari ngazi ya kawaida kutoka 489,942 (wavulana 258,134 na
wasichana 231,808) mwaka 2005 hadi wanafunzi1,802,810 (wavulana 954,961 na wasichana
447,849) mwaka 2012. Aidha, Idadi ya wanafunzi katika elimu ya sekondari ngazi ya juu
imeongezeka kutoka 34,383 (wavulana 21,620 na wasichana 12,763) mwaka 2005 hadi
wanafunzi 81,462 wavulana 55,512 na wasichana 25,950) mwaka 2012. Katika Elimu na
Mafunzo ya Ufundi Stadi kumekuwa na ongezeko la vyuo kutoka 695 mwaka 2005 hadi 750
mwaka 2011 na kuwezesha ongezeko la wanachuo kutoka 78,586 (wanaume 43,022 na
wanawake 35,564) mwaka 2005 hadi wanachuo 104,840 (Wanaume 54,350 wanawake 50,190)
mwaka 2011.
Aidha, vyuo vya elimu ya ufundi na mafunzo viliongezeka kutoka Vyuo 195 mwaka 2005 hadi
kufikia vyuo 260 mwaka 2011 na kuongeza udahili wa wanachuo kutoka 40,059 (Wanaume
30,123 na wanawake 9,636) mwaka 2005 hadi 85,040 (wanaume 46,342 na wanawake 38,698)
mwaka 2011. Hali kadhalika katika vyuo vya ualimu kumekuwa na ongezeko la vyuo kutoka 52
mwaka 2005 hadi vyuo 103 mwaka 2011 na kuwezesha ongezeko la wanachuo kutoka 26,224
(Wanaume 13,484 na wanawake 12,740) mwaka 2005 hadi 43,258 (wanaume 24,360 na
wanawake 18,898) mwaka 2012. Upande wa Vyuo vya Elimu ya juu kumekuwa na ongezeko la
vyuo vikuu na Vyuo vikuu vishiriki kutoka 23 mwaka 2005 hadi Vyuo Vikuu na Vyuo Vikuu
vishiriki 46 mwaka 2011 na kuongeza udahili wa wanachuo kutoka 37,667 (Wanaume 25,061na
wanawake 12,606) mwaka 2005 hadi 166,484 (wanaume 105,892 na wanawake 60,592) mwaka
2012.
Pamoja na mafanikio yaliyopatikana katika kupanua fursa za kujiunga na taasisi za elimu katika
ngazi mbalimbali, mafanikio haya bado ni madogo ukilinganisha na takwimu kama hizo katika
5
bara la Afrika na duniani kwa ujumla. Kwa mfano, ni asilimia kumi (10) tu ya wahitimu wa
elimu ya msingi na ambao hawaendelei na elimu ya sekondari ndio wanaojiunga na mafunzo ya
ufundi stadi na wanaobaki hujiunga na ulimwengu wa kazi bila kuwa na stadi stahiki. Pamoja na
kwamba karibu asilimia hamsini (50) ya wanafunzi wanaomaliza elimu ya msingi hupata fursa
ya kujiunga na elimu ya sekondari, ni asilimia 12.1 pekee ya wanafunzi wanaomaliza elimu ya
sekondari ndio hupata fursa ya kujiunga na elimu ya juu ya sekondari ya kidato cha tano. Aidha,
Tanzania ipo nyuma katika udahili wa wanafunzi katika elimu ya juu ambapo ni aislimia 1.5
pekee ya wanafunzi wanaomaliza elimu ya sekondari ndio hupata fursa ya kujiunga na vyuo
mbalimbali vya elimu ya juu nchini, ukilinganisha na wastani wa asilimia 13 kwa nchi zilizo na
uchumi wa kati. Kiwango hiki pia ni kidogo zaidi katika nchi zilizopo ukanda wa kusini mwa
Jangwa la Sahara. Viwango hivi duni vya udahili katika ngazi ya sekondari na elimu ya juu
vinatishia utekelezwaji wa malengo ya Taifa kama yalivyoanishwa katika Dira ya Taifa ya
Mwaka 2025 na mipango mingine ya maendeleo.
Aidha, kupanuka kwa kiwango cha uandikishaji katika ngazi ya elimu ya msingi na sekondari
kumeambatana na changamoto katika ubora wa elimu inayotolewa. Kwa mfano, miaka kumi ya
upanuzi wa elimu ya sekondari imeshuhudia vilevile kuendelea kushuka kwa kiwango cha ufaulu
katika mitihani ya Taifa, hasa ya mitihani ya Kidato cha Nne. Takwimu zinaonyesha kuwa
kiwango cha ufaulu wa wanafunzi wanaofanya mitihani ya Kidato cha Nne kimekuwa kikishuka
tangu miaka ya 2000, ambapo kiwango cha ufaulu kilishuka kutoka asilimia 90.3 mwaka 2007,
hadi asilimia 72.5 mwaka 2009, na hadi 53.6 mwaka 2011. Kiwango cha ufaulu kiliporomoka
hadi kufikia asilimia 34.5 mwaka 2012 (Tazama umbo Na. 1 hapo chini).
6
Umbo Na. 1: Kiwango cha ufaulu kidato cha nne 2001-2012
Changamoto mbalimbali zimechangia katika kushuka kwa kiwango cha ubora wa elimu, ambazo
sera mpya na mkakati wa utekelezaji zitajikita kuzikabili. Changamoto hizi ni pamoja na
kutokuwa na:
a) Mfumo nyumbufu unaoruhusu elimu na mafunzo kupatikana na kutambulika kwa njia
mbalimbali mbadala.
b) Mitaala inayokidhi mahitaji halisi ya rasilimaliwatu katika kuleta maendeleo ya Taifa.
c) Miundo mbinu, Vifaa na nyenzo bora na za kutosha kwa ajili ya kufundishia, utafiti na
kujifunzia kwa kuzingatia mabadiliko ya sayansi na teknolojia.
d) Walimu wa kutosha katika shule zote, na hasa shule za maeneo ya vijijini
e) Mfumo unaotoa motisha ya kutosha kwa wahitimu waliofaulu vizuri katika ngazi za
elimu ya sekondari kujiunga na kubaki katika taaluma ya ualimu
f) Mfumo wa ajira unaowezesha upatikanaji wa wataalam wa kada mbalimbali
wanaohitajika katika sekta elimu na mafunzo nchini.
7
g) Uwezo wa kuhakikisha fursa kwa usawa inatolewa kwa kila Mtanzania kulingana na
mahitaji yake na sehemu na mazingira aliyopo.
8
SURA YA PILI
DIRA, DHIMA NA MALENGO KATIKA MKAKATI WA UTEKELEZAJI WA SERA
2.0. Utangulizi
Mkakati huu unalenga kutekeleza Dira, Dhima na malengo ya Sera ya Elimu na Mafunzo ya
mwaka 2012 kama inavyoelezwa katika sura hii.
2.1. Dira
Kuwa na mtanzania aliyeelimika na mwenye maarifa, stadi, umahiri, uwezo na mtazamo
chanya ili kuweza kuchangia katika kuleta maendeleo ya Taifa.
2.2. Dhima
Kuweka na kuboresha mifumo na taratibu zitakazowezesha kupata watanzania walioelimika na
wanaopenda kujielimisha ili waweze kuchangia katika maendeleo ya Taifa.
2.3. Malengo ya Mkakati wa utekelezaji wa Sera
2.4. Lengo la Jumla:
Mtanzania aliyeelimika na mwenye maarifa na ujuzi anayeweza kuchangia kwa haraka katika
kuleta maendeleo ya taifa ili kuhimili ushindani wa kikanda na kimataifa.
2.4.1. Malengo Mahsusi
Malengo mahsusi ya Mkakati wa Sera ni kuwa na:
(a) Mfumo,miundo na taratibu nyumbufu kumwezesha Mtanzania kujiendeleza kwa njia
mbalimbali katika mikondo ya kitaaluma na kitaalamu.
(b) Elimu na mafunzo yenye viwango vya ubora unaotambulika kitaifa, kikanda na
kimataifa.
(c) Upatikanaji wa fursa mbalimbali za elimu na mafunzo katika ngazi zote nchini.
(d) Ongezeko la rasilimali mbalimbali kulingana na mitaala katika ngazi husika.
(e) Mfumo endelevu wa ugharimiaji wa elimu na mafunzo nchini.
(f) Mfumo wa elimu na mafunzo unaozingatia masuala mtambuka
9
SURA YA TATU
MIFUMO, MIUNDO NA TARATIBU NYUMBUFU ZA KUMWEZESHA MTANZANIA
KUJIENDELEZA KWA NJIA MBALIMBALI KATIKA MIKONDO YA KITAALUMA
NA KITAALAMU
3.0. Utangulizi
Mfumo wa sasa wa elimu na mafunzo una miundo ya kitaaluma na kitaalamu ambayo
haiingiliani kwa ufanisi katika masuala ya mitaala, upimaji, tuzo, ithibati na uthibiti. Hali hii
imechangia elimu na mafunzo kutokuwa na tija na ufanisi wa kutosha katika ngazi mbalimbali
za elimu na mafunzo na hivyo kusababisha baadhi ya wahitimu kukosa mwendelezo katika
ngazi mbalimbali za elimu na mafunzo na wengine kutokuwa na mwelekeo kabisa.
Serikali inakusudia kuweka mfumo wa elimu na mafunzo wenye tija na ufanisi ambao utakuwa
na miundo anuai na taratibu nyumbufu zenye kuleta ulinganifu, muunganiko na ufanisi wa ngazi
na fani mbalimbali za kitaaluma na kitaalamu ili kumwezesha mwanafunzi kutoka mkondo
mmoja kwenda mwingine baada ya kuhitimu Elimu-Msingi.
Ili kufanikisha azma hiyo, Serikali imedhamiria kurekebisha muda wa elimu na mafunzo katika
ngazi mbalimbali ili kuleta tija, ufanisi. Kupitia Sera, muda wa elimu ya awali umerekebishwa
kuwa mwaka mmoja badala ya miaka miwili. Aidha, muda wa elimu ya lazima umerekebishwa
kuwa miaka kumi ya elimu-msingi badala ya miaka saba ya elimu ya msingi. Pia, mikakati na
shabaha zinalenga kuwa na elimu-msingi ambayo inajumuisha elimu ya msingi na elimu ya
sekondari ngazi ya kawaida. Marekebisho haya yanalenga kuwa na mhitimu wa elimu – msingi
mwenye maarifa, stadi na mwelekeo utakaomwezesha kuendelea kwa ufanisi na elimu ya
sekondari au elimu ya ufundi na mafunzo ya ufundi stadi. Muda wa elimu baada elimu - msingi
utarekebishwa kulingana na fani, maudhui na umahiri unaotambulika katika ulimwengu wa kazi
3.1. LENGO Na.1: Kuweka mfumo, miundo na taratibu nyumbufu katika elimu na
mafunzo ili kuleta ulinganifu, muunganiko na ufanisi katika ngazi na fani mbalimbali za
kitaaluma na kitaalamu ili kumwezesha mwanafunzi kutoka mkondo mmoja kwenda
mwingine.
3.1.1 MIKAKATI
1. Kuhuisha mfumo wa elimu na mafunzo uliopo sasa na kuweka mfumo mpya ulio nyumbufu
utakaomwezesha mtanzania kujiendeleza kwa njia mbalimbali ili kukidhi mahitaji ya
maendeleo ya kitaifa, kikanda na kimataifa.
10
2. Kuweka Mfumo wa Tuzo wa Taifa unaozingatia vigezo na viwango vya ubora wenye kuleta
ulinganifu, muunganiko katika ngazi zote za elimu na mafunzo ya kitaaluma na kitaalamu.
3.1.2 SHABAHA
1. Mfumo wa elimu na mafunzo nchini kuwa nyumbufu ili kumwezesha mtanzania
kujiendeleza kwa njia mbalimbali katika mikondo ya kitaaluma na kitaalamu ifikapo mwaka
2018.
2. Mfumo wa tuzo wa Elimu na mafunzo wenye kuleta ulinganifu, muunganiko unaomwezesha
mtanzania kujiendeleza kutoka mkondo mmoja kwenda mwingine kuwepo na kuanza
kutumika ifikapo mwaka 2018.
3.1.3 VIASHIRIA
a) Mfumo wa elimu na mafunzo uliohuishwa;
b) Sheria ya elimu na mafunzo iliyohuishwa;
c) Muundo wa tuzo wa kitaifa ambao ni nyumbufu wenye kuleta ulinganifu na muunganiko;
d) Idadi ya programu za kuelimisha umma zilizoendeshwa kwa njia mbalimbali kote nchini;
e) Idadi ya watekelezaji katika ngazi mbalimbali za elimu na mafunzo waliyohudhuria mafunzo
kuhusu muundo mpya wa tuzo.
3.2. LENGO Na. 2: Elimu ya Awali kuwa ya lazima na kutolewa kwa watoto wenye
umri kati ya miaka mitatu hadi mitano kwa kipindi kisichopungua mwaka mmoja.
3.2.1. MKAKATI
Kuweka vigezo, viwango na utaratibu ili elimu ya awali iwe ya lazima na itolewe katika kila
shule ya Elimu –Msingi.
3.2.2. SHABAHA
1. Sheria, miongozo na taratibu kuruhusu elimu ya awali kuwa ya lazima kuwekwa na
kutekelezwa ifikapo mwaka 2018;
2. Elimu ya awali kwa watoto wote wa rika lengwa kutolewa ifikapo mwaka 2018.
3.2.3 VIASHIRIA
a) Sheria na miongozo iliyohuishwa kuhusu elimu ya awali kutumika katika shule zote za
elimu-msingi;
b) Idadi ya watoto wa rika lengwa waliojiunga na elimu ya awali.
3.3 LENGO Na. 3: Elimu-Msingi kuwa ya lazima kuanzia darasa la kwanza hadi kidato
11
cha nne; na kutolewa kwa miaka kumi na umri wa kuanza darasa la kwanza kuwa kati ya
miaka minne hadi sita kulingana na maendeleo na uwezo wa mtoto kumudu masomo
katika ngazi husika.
3.3.1 MKAKATI.
Kuhuisha sheria na taratibu ili elimu - msingi iwe ya lazima na itolewe hadi kidato cha nne.
3.3.2 SHABAHA
1. Sheria na Miongozo kuhusu elimu - msingi kuwekwa na kutekelezwa ifikapo mwaka 2016.
2. Mpango wa utekelezaji wa utoaji wa elimu – msingi kuwepo ifikapo mwaka 2018.
3. Elimu – msingi kutolewa ifikapo mwaka 2018.
3.3.3 VIASHIRIA
a) Sheria na miongozo kuhusu elimu-msingi iliyohuishwa.
b) Idadi ya wanafunzi wa rika lengwa waliojiunga na elimu-msingi.
c) Idadi ya shule za elimu-msingi
3.4 LENGO Na. 4:Kuweka utaratibu ili kuhakikisha muda wa kukamilisha elimu na
mafunzo katika ngazi mbalimbali za elimu baada ya Elimu - Msingi unakuwa na tija
na ufanisi.
3.4.1 MIKAKATI
1. Kuhuisha sheria na utaratibu wa utoaji wa elimu ya sekondari ngazi ya juu
2. Kuimarisha vyuo vya elimu ya juu na mafunzo ya ufundi stadi, mafunzo ya ualimu, elimu ya
ufundi na mafunzo ya kitaalamu ili viweze kutoa elimu na mafunzo mbalimbali kulingana na
mahitaji ya maendeleo ya taifa na soko la ajira.
3. Kuweka utaratibu wa kuhakikisha mafunzo yanakamilika kwa muda stahiki katika ngazi zote
za elimu na mafunzo.
3.4.2 SHABAHA
1. Sheria na taratibu za utoaji wa elimu ya sekondari ngazi ya juu kuhuishwa ifikapo mwaka
2017.
12
2. Utaratibu wa kuwaendeleza wanafunzi wanaofaulu elimu - msingi kuendelea na elimu ya
sekondari ngazi ya juu, elimu ya ufundi na elimu na mafunzo ya ufundi stadi kuwekwa
ifikapo mwaka 2015.
3. Udahili wa wanafunzi wa sekondari ngazi ya juu kuongezeka kutoka asilimia 5.2 mwaka
2012 hadi asilimia 40 ifikapo mwaka 2019.
4. Sheria na kanuni za matumizi ya vyuo vya elimu ya juu, mafunzo ya ualimu, mafunzo ya
ufundi stadi, elimu ya ufundi na mafunzo ya kitaaluma elimu na mafunzo kuhuishwa ifikapo
mwaka 2017.
5. Utaratibu wa kuwaendeleza wanafunzi wanaofaulu elimu ya sekondari ngazi ya juu
kuendelea na Elimu ya juu, mafunzo ya ualimu, mafunzo ya ufundi stadi, elimu ya ufundi na
mafunzo ya kitaalam kuwekwa ifikapo mwaka 2016.
6. Utaratibu wa matumizi fanisi ya vyuo vya elimu na mafunzo kulingana na miundo ya mitaala
mipya kuandaliwa ifikapo mwaka 2016.
7. Fursa anuwai za kuendelea na masomo katika ngazi mbalimbali za elimu na mafunzo
kuongezwa ifikapo mwaka 2020.
8. Idadi ya wahitimu katika ngazi mbalimbali kuongezeka ifikapo mwaka 2020.
9. Ujuzi mhitimu alioupata katika ngazi ya elimu au programu ya mafunzo kutambuliwa kwa
ajili ya kujiunga na ngazi ya elimu au programu nyingine ifikapo mwaka 2018.
10. Ujuzi ambao mtu ameupata katika ulimwengu wa kazi na ujasiriamali kubainishwa na
kutambuliwa kwa ajili ya kujiendeleza kielimu na kiujuzi ifikapo mwaka 2018.
3.4.3 VIASHIRIA
a) Miongozo ya utekelezaji wa elimu ya sekondari ngazi ya juu;
b) michepuo yakinifu;
c) Idadi ya wanafunzi wanoendelea na elimu ya sekondari ngazi ya juu;
d) Sheria na kanuni za matumizi ya vyuo vya elimu ya juu, mafunzo ya ualimu, mafunzo ya
ufundi stadi, elimu ya ufundi na mafunzo ya kitaaluma zilizohuishwa;
e) Idadi ya wanafunzi wanoendelea na elimu ya juu, mafunzo ya ualimu, mafunzo ya ufundi
stadi, elimu ya ufundi na mafunzo;
f) Idadi ya fursa anuwai za kuendelea na masomo katika ngazi mbalimbali za elimu na
mafunzo;
g) Idadi ya wahitimu katika ngazi mbalimbali kuongezeka;
h) Muda wa elimu na mafunzo wenye ufanisi na tija; na
i) Mfumo wa kutambua ujuzi uliopatikana katika ngazi nyingine ya mafunzo, nje ya mfumo
rasmi na kazini.
13
SURA YA NNE
ELIMU NA MAFUNZO YENYE VIWANGO VYA UBORA UNAOTAMBULIKA
KIKANDA NA KIMATAIFA NA YANAYOKIDHI MAHITAJI YA SASA NA YA
BAADAYE YA TAIFA
4.0 Utangulizi
Ubora wa elimu ya Tanzania unatambuliwa kimataifa kunakodhihirishwa na kukubalika kwa
vijana wanaohitimu katika mfumo wa elimu wa Tanzania kujiunga na taasisi za elimu
mbalimbali duniani. Aidha, wahitimu mbalimbali waliomaliza katika mfumo wa elimu wa
Tanzania wamekuwa wakiajiriwa katika nafasi za kitaalamu na uongozi katika nchi mbalimbali
duniani. Hata hivyo, katika miaka ya karibuni, kiwango cha ubora wa elimu Tanzania
kinaonekana kushuka, kunakothibitishwa na vigezo mbalimbali, kama vile: kushuka kwa
kiwango cha ufaulu katika ngazi ya shule ya msingi na sekondari. Kwa mfano, kiwango cha
ufaulu katika mitihani ya kidato cha nne kimeshuka kutoka asilimia zaidi ya 70 mwaka 2000
hadi asilimia 35 mwaka 2012.
Changamoto mbalimbali zimechangia hali ya kushuka kwa kiwango cha ubora wa elimu,
zikiwemo: upatikanaji wa nyenzo; vifaa na zana nyingine stahiki za kujifunzia na kufundishia;
miundombinu kama majengo, mifumo ya maji, umeme na barabara kuwa duni. Pia kuna
viashiria vya udhaifu katika mitaala ya elimu na mafunzo na utekelezaji wake.
Ili kuhakikisha Viwango na vigezo vya ubora wa elimu na mafunzo vinavyotambulika kikanda
na kimataifa Serikali itaendesha zoezi la kupitia upya mitaala ya elimu na mafunzo katika
ngazi zote ili iendane na maendeleo na mabadiliko ya sayansi na teknolojia kitaifa, kikanda na
kimataifa. Sheria za vyombo vya ithibati na uthibiti elimu na mafunzo pia vitaimarishwa ikiwa
ni pamoja na kuimarisha muundo wa kitaasisi, ithibati na uthibiti wa program mbalimbali za
elimu na mafunzo za ndani na program za nje pamoja na masuala ya upimaji na tathmini ya
maendeleo ya mwanafunzi.
Katika yote haya mikakati ifuatayo itatumika.
4.1 LENGO Na.1: Kuimarisha ithibati na uthibiti wa ubora wa elimu na mafunzo
katika ngazi zote yakiwemo masuala ya ushauri.
4.1.1 MKAKATI
Kuimarisha muundo wa kitaasisi wa ithibati na uthibiti wa elimu na mafunzo katika ngazi zote.
4.1.2 SHABAHA
1. Chombo madhubuti cha ithibati na uthibiti wa elimu - msingi na sekondari ngazi ya juu
kuwepo ifikapo mwaka 2018.
14
2. Chombo madhubuti cha ithibati na uthibiti wa elimu na mafunzo ya ufundi stadi na
ujasiriamali kuimarishwa ifikapo mwaka 2019.
3. Chombo madhubuti cha ithibati na uthibiti wa elimu ya ufundi kuimarishwa ifikapo mwaka
2019.
4. Chombo madhubuti cha ithibati na uthibiti wa elimu ya juu Tanzania kuimarishwa ifikapo
mwaka 2019.
5. Chombo madhubuti cha uratibu, ithibati na uthibiti wa maendeleo ya sayansi, tekinolojia,
utafiti na ubunifu Tanzania kuimarishwa ifikapo mwaka 2019.
6. Viwango na vigezo vya ubora wa elimu na mafunzo vinavyotambulika kikanda na kimataifa
kuwepo ifikapo mwaka 2019.
7. Tekinolojia za kisasa na za kisayansi kutumika katika usimamizi, ithibati na uthibiti katika
ngazi zote za elimu na mafunzo ifikapo mwaka 2019
4.1.3 VIASHIRIA
a) Sheria za vyombo vya ithibati na uthibiti elimu na mafunzo zilizohuishwa;
b) Viwango na vigezo vya ubora wa elimu na mafunzo katika ngazi zote vilivyohuishwa; na
c) Mbinu za kisasa zinazotumika katika uthibiti na ithibati.
4.2 LENGO Na. 2: Kuimarisha ukuzaji, uboreshaji na utekelezaji wa mitaala kwa
kuzingatia mahitaji ya taifa na ya walengwa katika ngazi zote za elimu na mafunzo.
4.2.1 MIKAKATI
1. Kuhuisha miundo ya mitaala ya kitaifa katika ngazi zote za elimu na mafunzo kwa kuzingatia
umahiri unaotarajiwa katika kila ngazi ya elimu na mafunzo kulingana na mahitaji ya
maendeleo ya taifa na soko la ajira.
2. Kuhuisha na kuimarisha miongozo ya ukuzaji, utayarishaji, utekelezaji na uhuishaji wa
mitaala kwa kuzingatia mahitaji ya taifa na ya walengwa katika ngazi zote za elimu na
mafunzo kulingana na muundo wa tuzo wa taifa.
3. Kuhuisha mitaala katika ngazi zote za elimu na mafunzo ili iendane na miundo mipya ya
mitaala ya kitaifa.
4. Kuimarisha mpango wa upatikanaji wa vitabu vya kiada na ziada kwa ngazi zote za elimu na
mafunzo.
5. Kuhuisha na kuimarisha au kuweka muundo wa upimaji wa kitaifa wa maendeleo ya
mwanafunzi katika kila ngazi ya elimu na mafunzo.
6. Kujenga miundo ya ulinganifu wa programu mbalimbali kulingana na mitaala kwa mahitaji
ya taifa pamoja na yale ya ulimwengu wa kazi, utandawazi na sehemu nyingine.
15
4.2.2 SHABAHA
1. Muundo wa mtaala wa kitaifa wa elimu ya awali kulingana na muundo na tuzo za elimu na
mafunzo kuhuishwa ifikapo mwaka 2016.
2. Miongozo ya ukuzaji, utayarishaji, utekelezaji na uhuishaji wa mitaala kuhuishwa na
kutekelezwa ifikapo mwaka 2016.
3. Muundo wa mtaala wa kitaifa wa elimu – msingi na elimu ya sekondari ngazi ya juu
kuhuishwa kulingana na muundo wa tuzo kuwepo ifikapo mwaka 2016.
4. Miundo ya mitaala ya kitaifa katika ngazi nyingine kuhuishwa ili iendane na mabadiliko ya
muundo katika elimu-msingi, sekondari ngazi ya juu na soko la ajira kuwepo ifikapo mwaka
2016.
5. Miongozo ya ukuzaji, utayarishaji, utekelezaji na uhuishaji wa mitaala kuimarishwa na
kutekelezwa ifikapo mwaka 2016.
6. Mitaala kusambazwa nchini na kutoa elimu kwa umma, watekelezaji na walengwa wa
mitaala kufanyika na kutekelezwa ifikapo mwaka 2016
7. Kuwa na mitaala nyumbufu yenye viwango vinavyokubalika kitaifa kikanda na kimataifa
ifikapo mwaka 2016.
8. Muundo wa upimaji wa kitaifa wa maendeleo ya mwanafunzi kwa kuzingatia umahiri
kuandaliwa kwa kila ngazi ya elimu na mafunzo ifikapo mwaka 2016.
9. Programu rekebishi itakayowezesha kubaini uwezo, utayari na kuwasaidia wanafunzi
kuendelea na masomo ngazi za juu kuandaliwa ifikapo mwaka 2016.
10. Ulinganifu wa masomo, programu na fani mbalimbali za elimu na mafunzo baada ya elimu
ya sekondari kuandaliwa ifikapo mwaka 2016.
11. Vitabu vya kutosha vya kiada na ziada kwa ngazi zote za elimu na mafunzo kuwepo katika
shule na vyuo ifikapo mwaka 2020.
4.2.3 VIASHIRIA
a) Miundo ya mitaala ya kitaifa ya elimu ya awali, elimu- msingi na sekondari ngazi ya juu
iliyohuishwa;
b) Idadi ya wataalamu waliojengewa uwezo wa kukuza na kutekeleza mitaala ;
c) Idadi ya programu za kuelimisha umma kupitia njia mbalimbali za mawasiliano kuhusu
miundo mipya ya mitaala ya kitaifa ya elimu ya awali, elimu-msingi na sekondari ngazi ya
juu na idadi ya waliohudhuria;
d) Muundo mpya wa mitaala ya elimu na mafunzo katika ngazi nyingine za elimu na mafunzo
zilizohuishwa;
e) Idadi ya programu ya kuelimisha umma kupitia njia mbalimbali za mawasiliano, semina
elekezi kwa watekelezaji kuhusu miundo mipya ya mitaala baada ya elimu msingi na idadi ya
waliohudhuria;
f) Miongozo ya ukuzaji, utayarishaji na utekelezaji wa mitaala iliyopitishwa kwa muda
uliopangwa na kwa kuzingatia mahitaji ya wakati;
g) Idadi ya watekelezaji na walengwa waliosambaziwa mitaala;
16
h) Mitaala iliyohuishwa na kuandaliwa kulingana na mahitaji ya taifa;
i) Muundo wa upimaji wa kitaifa wa maendeleo ya mwanafunzi kwa kuzingatia umahiri wa
stadi kwa kila ngazi ya elimu na mafunzo ulioandaliwa;
j) Idadi ya wanafunzi wenye kasi kubwa ya kujifunza, vipawa na vipaji walioendelezwa;
k) Idadi ya wanafunzi wenye kasi ndogo ya kujifunza walioendelezwa ;
l) Miongozo ya ulinganifu wa programu kulingana na mahitaji ya kitaifa na kimataifa;
m) Idadi na aina za programu zilizofanyiwa ulinganifu; na
n) Upatikanaji endelevu wa vitabu vya kiada na ziada vilivyobainishwa kwa ajili ya ngazi zote
za elimu na mafunzo.
4.3 LENGO Na.3: Kuimarisha usimamiaji na upimaji wa utekelezaji wa mitaala katika
taasisi za elimu na mafunzo katika ngazi zote ili kuleta ufanisi wa elimu na mafunzo
yatolewayo.
4.3.1 MKAKATI
Kuhuisha na kuimarisha vigezo, misingi na utaratibu yakinifu wa kuhakiki, kusimamia na
kupima utekelezaji wa mitaala katika asasi za elimu na mafunzo katika ngazi zote.
4.3.2 SHABAHA
1. Miongozo ya kuhakiki, kusimamia na kupima utekelezaji wa mitaala katika asasi za elimu na
mafunzo katika ngazi zote kuandaliwa na kutumika ifikapo mwaka 2016.
2. Usimamizi fanisi wa utekelezaji wa mitaala kwa kuhusisha ngazi mbalimbali za usimamizi
wa elimu na mafunzo ifikapo mwaka 2015.
3. Wasimamizi na watekelezaji mahiri wa mitaala katika taasisi za elimu na mafunzo
kuandaliwa ifikapo mwaka 2016.
4.3.3 VIASHIRIA
a. Miundo na miongozo ya kuhakiki, kusimamia na kupima utekelezaji wa mitaala katika
taasisi za elimu na mafunzo.
b. Idadi ya wasimamizi na watekelezaji mahiri wa mitaala katika ngazi zote.
c. Idadi ya taasisi za elimu na mafunzo zilizofanyiwa tathmini ya utendaji kazi.
4.4 LENGO Na 4: Kuimarisha ufundishaji na ujifunzaji wa lugha ili kuwa na wanafunzi
mahiri wenye uwezo wa kuwasiliana kwa Kiswahili, Kiingereza na lugha nyingine za
kigeni katika mfumo wa elimu na mafunzo.
17
4.4.1 MIKAKATI
1. Kuweka, kuendeleza na kuimarisha mbinu za kufundisha na kujifunza kwa umahiri na
kuwasiliana kwa ufasaha kwa Kiswahili na Kiingereza kwa kutumia wataalamu na walimu
mahiri.
2. Kuweka mazingira na utaratibu utakaowezesha wanafunzi walengwa kujifunza lugha
nyingine za kigeni na kuwasiliana kwa ufasaha.
4.4.2 SHABAHA
1. Kuwa na wanafunzi mahiri katika kujifunza na kuwasiliana kwa Kiswahili na Kiingereza
ifikapo mwaka 2016.
2. Kuwa na wanafunzi wenye uwezo wa kujifunza na kuwasiliana kwa ufasaha lugha nyingine
za kigeni zilizoidhinishwa kutumika katika Jumuiya ya Afrika Mashariki, SADC na Umoja
wa Afrika ifikapo mwaka 2016.
4.4.3 VIASHIRIA
a) Wanafunzi mahiri katika lugha za Kiswahili na Kiingereza.
b) Sheria na Miongozo inayowezesha kufundisha na kujifunza lugha nyingine za kigeni.
c) Idadi ya walimu mahiri wa kufundisha lugha mbalimbali za kigeni kwa ufasaha pamoja na
stadi za kuwasiliana.
4.5 LENGO Na. 5: Kuwezesha lugha ya alama kutumika katika ngazi zote za elimu na
mafunzo
4.5.1 MKAKATI
Kuweka mazingira na utaratibu utakaowezesha kujifunza, kufundishia na kuwasiliana kwa
kutumia lugha za alama katika ngazi zote za elimu na mafunzo.
4.5.2 SHABAHA
Kuwa na wanafunzi mahiri katika kujifunza na kuwasiliana kwa lugha za alama kwa ufasaha
ifikapo mwaka 2016.
4.5.3 VIASHIRIA
a) Miongozo inayowezesha kufundisha na kujifunza kwa lugha za alama
b) Idadi ya wanafunzi mahiri katika kutumia lugha za alama
c) Idadi ya walimu mahiri katika kufundisha na kutumia lugha za alama
4.6 LENGO Na. 6: Kuimarisha uthibiti wa programu, mitihani na tuzo za nje
18
zinazotolewa nchini katika ngazi zote za elimu na mafunzo.
4.6.1 MKAKATI
Kuhuisha sheria, kanuni na miongozo ya ithibati na uthibiti wa programu na mitihani ya nje
inayoendeshwa nchini.
4.6.2 SHABAHA
Uratibu na uthibiti wa tuzo na vyeti vinavyotolewa na vyuo vya ndani na nje ya nchi kukidhi
mahitaji ya mfumo wa tuzo wa taifa ifikapo mwaka 2016.
4.6.3 VIASHIRIA
Sheria, kanuni na miongozo ya ithibati na uthibiti wa programu na mitihani ya nje
inayoendeshwa nchini
19
SURA YA TANO
UPATIKANAJI WA FURSA MBALIMBALI ZA ELIMU NA MAFUNZO
NCHINI
5.0 UTANGULIZI
Utoaji wa elimu na mafunzo unazingatia upatikanaji wa fursa za elimu na mafunzo bila ubaguzi
wa jinsi, rangi, kabila, dini hali ya kijamii au kipato. Pamoja na juhudi za Serikali, sekta binafsi
na washirika wa maendeleo kuongeza fursa za elimu kwa makundi yote, baadhi ya makundi
bado hayajafikiwa kikamilifu kutokana na sababu za kijamii, kiuchumi na kijiografia.
Ili kutimiza lengo la kuwa na mtanzania aliyeelimika na anayependa kujielimisha, serikali
imedhamiria kuondoa vikwazo vyote vinavyoweza kuzuia mwanafunzi kupata elimu na mafunzo
madhalan, sababu za ujauzito, ndoa za utotoni, ajira za watoto na utoro.
5.1 LENGO Na.1: Kuongeza fursa anuwai za elimu na mafunzo kwa usawa kwa
makundi yote ya kijamii katika ngazi zote.
5.1.1 MIKAKATI
1. Kuhuisha sheria, kanuni na miongozo ya kuhakikisha upatikanaji wa fursa za elimu na
mafunzo kwa usawa kwa makundi yote ya kijamii katika ngazi zote.
2. Kuimarisha na kuweka utaratibu wa kuongeza, na kutumia fursa za elimu na mafunzo ya
ndani na nje ya nchi kwa makundi yote ya kijamii kwa usawa katika ngazi zote
3. Kuimarisha elimu na mafunzo yanayoshirikisha vyuo vya elimu ya ufundi stadi, viwanda vya
umma na sekta binafsi (uanagenzi) ili kuongeza fursa na ubora wa elimu na mafunzo ya
ufundi stadi kwa usawa kwa makundi yote ya kijamii.
4. Kuimarisha ushiriki wa wadau mbalimbali katika utoaji wa mafunzo tarajali na mazoezi kwa
vitendo sehemu za kazi kwa wanachuo.
5. Kuimarisha utoaji wa elimu na mafunzo kwa njia huria na masafa kuhakikisha inawafikia
watu wa rika na mahitaji mbalimbali.
5.1.2 SHABAHA
1. Sheria, kanuni na miongozo ya kuhakikisha upatikanaji wa fursa za elimu na mafunzo kwa
usawa kwa makundi yote ya kijamii kwa ngazi zote kuhuishwa na kutumika ifikapo mwaka
2016.
2. Fursa za elimu na mafunzo zinapatikana na kutumika kwa usawa kwa makundi yote ya
kijamii katika ngazi zote ifikapo mwaka 2016.
3. Programu za Maendeleo ya sekta ya elimu na mafunzo zinazoongeza fursa kutekelezwa kwa
ufanisi na tija ifikapo mwaka 2016.
20
5.1.3 VIASHIRIA
a) Sheria, kanuni na miongozo inayohusu upatikanaji wa fursa za elimu na mafunzo kwa
usawa kwa makundi yote iliyoandaliwa.
b) Miundombinu nyenzo, vifaa na zana rafiki kwa makundi yote ya kijamii
c) Idadi ya programu za maendeleo zinazoongeza fursa sawa kwa makundi yote ya jamii
d) Idadi ya shule na vyuo
e) Idadi ya sekta binafsi zinazoshiriki kikamilifu katika kuongeza fursa
f) Sheria na miongozo ya uanagenzi iliyohuishwa
g) Wanachuo kupata mafunzo tarajali na mazoezi kwa vitendo sehemu za kazi
h) Elimu na mafunzo yanayotolewa kwa njia huria na masafa yanayokidhi viwango
i) Idadi ya programu zilizofanyika kuhamasisha umma kuhusu elimu na mafunzo kwa njia
huria na masafa.
j) idadi ya washiriki katika programu za elimu na mafunzo kwa njia huria na masafa
5.2 LENGO Na. 2: Kuondoa vikwazo vinavyozuia fursa ya wanafunzi kuendelea na
masomo na kukamilisha mzunguko wa elimu na mafunzo katika ngazi husika.
5.2.1 MIKAKATI
1. Kuhuisha miongozo kuhusu wanafunzi kukamilisha mzunguko wa elimu – msingi.
2. Kuweka mpango maalumu na taratibu zitakazowezesha wanafunzi waliokatiza masomo
kutokana na vikwazo na sababu mbalimbali kuendelea na masomo na/au kukamilisha
mzunguko husika.
5.2.2 SHABAHA
1. Taratibu na miongozo ya kuwezesha mwanafunzi kukamilisha mzunguko wa elimu msingi
kuhuishwa katika ngazi zote ifikapo mwaka 2016
2. Wanafunzi wanaokamilisha mzunguko wa elimu msingi kuongezeka ifikapo mwaka 2016
3. Miongozo na taratibu za wanafunzi waliokatiza masomo kutokana na vikwazo mbalimbali
kuendelea na masomo na/au kukamilisha mzunguko wa elimu na mafunzo husika kuwepo
ifikapo mwaka 2016.
4. Utambuzi wa masomo aliyofaulu mwanafunzi ili kumwezesha kuendelea na masomo kwa
ngazi husika au ngazi nyingine ifikapo mwaka 2016
5.2.3 VIASHIRIA
a. Miongozo na mipango ya kuwarudisha katika mfumo wa elimu na mafunzo wanafunzi
walioacha masomo kutokana na sababu mbalimbali
b. Idadi ya wanafunzi waliorejea katika mfumo wa elimu na mafunzo
c. Idadi ya wanafunzi waliokatiza masomo kukamilisha mzunguko wa elimu na mafunzo
husika.
21
d. Mwanafunzi kuendelea na kumaliza mzunguko wake kwa kutambua limbikizo alama za
ufaulu
5.3 LENGO Na.3: Kuweka utaratibu utakaowezesha maendeleo ya wanafunzi wenye
vipaji, vipawa na kasi tofauti katika kujifunza kwa ngazi zote za elimu na mafunzo.
5.3.1 MKAKATI
Kuweka utaratibu na vigezo vya kuwatambua mapema wanafunzi wenye vipaji, vipawa na
wenye kasi ya kujifunza na wengine wenye mahitaji maalumu katika ngazi mbalimbali za elimu
na mafunzo.
5.3.2 SHABAHA
Vipaji, vipawa na kasi ya kujifunza ya wanafunzi katika ngazi mbalimbali za elimu na mafunzo
kutambuliwa na kukuzwa ifikapo mwaka 2016.
5.3.3 KIASHIRIA
Idadi ya wanafunzi wenye vipaji, vipawa na wenye kasi ya kujifunza katika ngazi mbalimbali za
elimu na mafunzo kuongezeka.
5.4 LENGO Na. 4: Kuweka utaratibu na kuimarisha utambuzi wa viwango vya Elimu
na mafunzo ili kutoa fursa ya kila Mtanzania kujiendeleza kielimu, kupata maarifa na
stadi za kazi kwa kuzingatia kwamba elimu au mafunzo hayana mwisho.
5.4.1 MKAKATI
Kuimarisha utaratibu wa kuwa na vigezo vya utambuzi wa uwezo na umahiri wa mtu alioupata
akiwa nje ya mfumo wa shule au chuo na kumpa tuzo itakayomwezesha kujiendeleza katika
ngazi mbalimbali za elimu na mafunzo kulingana na mahitaji yake au kupata sifa ya kujiunga na
fani husika.
5.4.2 SHABAHA
1. Vigezo vya utambuzi wa uwezo na umahiri wa mtu alioupata nje ya mfumo wa shule au chuo
kuwekwa ifikapo mwaka 2016.
2. Tuzo kwa watu wenye ujuzi na uzoefu mbalimbali walioupata nje ya mfumo wa elimu
kutolewa ifikapo mwaka 2016.
3. Tuzo na umahiri alioupata mtu akiwa nje ya mfumo wa shule au chuo kutambulika ili
kumwezesha kujiunga na kujiendeleza katika ngazi mbalimbali za elimu na mafunzo ifikapo
mwaka 2016
22
5.4.3 VIASHIRIA
a. Idadi ya watu waliopata tuzo nje ya mfumo wa elimu
b. Idadi ya watu waliojiendeleza katika ngazi mbalimbali za elimu baada ya kutambuliwa ujuzi
wao na kupata tuzo
23
SURA YA SITA
ONGEZEKO LA RASILIMALI MBALIMBALI KULINGANA NA MAHITAJI KATIKA
NGAZI ZOTE ZA ELIMU NA MAFUNZO
6.0 UTANGULIZI
Uwezo wa utoaji wa elimu na mafunzo unaathiriwa na uhitaji mkubwa wa rasilimali
mbalimbali ikiwa ni pamoja na rasilimaliwatu hususan walimu, wahadhiri, wakufunzi na
watendaji wengine katika shule na vyuo; upungufu wa vifaa, nyenzo na zana za kujifunzia na
kufundishia hususan vitabu, vifaa vya maabara na karakana katika shule na vyuo pamoja na
miundombinu. Rasilimali watu pia imekuwa haitoshi na hivyo kusababisha baadhi ya shule na
vyuo kuwa na upungufu wa waalimu na watumishi wenginge muhimu katika utoaji wa elimu
bora.
Hali hii inachangiwa na changamoto katika mfumo na miundo ya kuwatambua na
kuwatayarisha, ajira, usimamizi, kuwavutia na kuwabakisha kazini na kuwaendeleza watumishi
katika sekta ya elimu na mafunzo katika fani husika.
6.1 LENGO Na.1: Kuimarisha mfumo wa ajira katika sekta ya elimu na mafunzo ili
uwe mahsusi na kukidhi mahitaji, upatikanaji na usimamizi wa rasilimaliwatu kwa ajili ya
maendeleo ya sekta ya elimu na mafunzo.
6.1.1 MIKAKATI
1. Kuhuisha miundo ya utumishi na utayarishaji, ajira na maendeleo ya walimu na wasimamizi
wa elimu na mafunzo kwa ajili ya elimu ya awali, elimu- msingi na sekondari ngazi ya juu.
2. Kuhuisha miundo ya utumishi na utayarishaji, ajira na maendeleo ya walimu na wasimamizi
wa elimu na mafunzo katika Vyuo vya ufundi stadi, vyuo vya ufundi, vyuo vya ualimu na
vyuo vikuu (ngazi mbalimbali baada ya elimu – msingi).
3. Kuandaa utaratibu wa kuongeza nafasi za mafunzo ya ualimu, mafunzo ya ukufunzi, uhadhiri
kukidhi ongezeko la wanafunzi katika ngazi zote za elimu na mafunzo.
6.1.2 SHABAHA
1. Miundo ya utumishi katika sekta ya elimu na mafunzo ngazi ya elimu ya awali, elimu msingi
na sekondari ngazi ya juu kuhuishwa ifikapo mwaka 2016.
2. Miongozo, vigezo na viwango vya elimu na ujuzi wa walimu na wasimamizi wa elimu ya
awali, elimu - msingi na sekondari ngazi ya juu kuhuishwa ifikapo mwaka 2016.
3. Uwiano wa mwalimu kwa wanafunzi katika elimu ya awali kupungua kutoka 1:124 mwaka
2012 hadi kufikia 1:25 ifikapo mwaka 2025.
24
4. Walimu mahiri wenye uwezo wa kufundisha elimu ya awali kwa ufanisi na ufasaha
kupatikana ifikapo mwaka 2018.
5. Wasimamizi wa utekelezaji wa elimu ya awali na elimu – msingi katika ngazi mbalimbali za
uongozi kuwepo ifikapo mwaka 2016.
6. Uwiano wa mwalimu kwa wanafunzi katika elimu –msingi kuimarika ifikapo mwaka 2025.
7. Walimu mahiri na wenye uwezo wa kufundisha elimu –msingi kwa ufanisi na ufasaha
kupatikana ifikapo mwaka 2016.
8. Mpango wa kuandaa mipango ya kuongeza nafasi za mafunzo ya ualimu, wakufunzi,
wahadhiri katika ngazi zote za elimu na mafunzo ifikapo mwaka 2017.
6.1.3 VIASHIRIA
a) Miundo ya utumishi wenye ufanisi na tija katika sekta ya elimu na mafunzo ngazi ya elimu
ya awali, elimu msingi na sekondari ngazi ya juu;
b) Miongozo, vigezo na viwango vya elimu na ujuzi wa walimu na wasimamizi wa elimu ya
awali elimu msingi na sekondari ngazi ya juu;
c) Idadi ya walimu wa shule za awali ili kuwa na uwiano wa mwalimu na wanafunzi katika
elimu ya awali kupungua kuwa 1:25;
d) Idadi ya walimu wa shule za awali waliopata mafunzo;
e) Idadi ya wasimamizi wa shule za awali waliopata mafunzo;
f) Idadi ya walimu wa shule za elimu –msingi ili kuwa na uwiano wa mwalimu na wanafunzi
katika elimu –msingi kuwa 1:40;
g) Idadi ya walimu wa shule za elimu –msingi waliopata mafunzo;
h) Idadi ya wasimamizi wa shule za elimu –msingi waliopata mafunzo;
i) Miundo ya utumishi wenye ufanisi na tija katika sekta ya elimu na mafunzo katika ngazi
mbalimbali baada ya elimu – msingi;
j) Muundo na mfumo wa ajira ya walimu, wakufunzi, wahadhiri na wasimamizi;
k) Ongezeko la Idadi ya walimu, wakufunzi, wahadhiri, waendeshaji na wasaidizi wengine;
l) Idadi ya walimu, wakufunzi wahadhiri, waendeshaji na wasaidizi wengine walioendelezwa
kitaaluma na kitaalamu; na
m) Nafasi za mafunzo ya ualimu, wakufunzi na wahadhiri zilizoongezeka.
6.2 LENGO Na. 2: Kuweka mazingira bora na kuhakikisha kuwa sekta ya elimu na
mafunzo inatoa rasilimaliwatu wa kutosha na mahiri kukidhi mahitaji ya sekta
mbalimbali kwa maendeleo ya Taifa.
6.2.1 MIKAKATI
1. Kuweka utaratibu wa sekta ya elimu na mafunzo kuandaa rasilimaliwatu ya kutosha yenye
ujuzi na umahiri unaotakiwa kwenye sekta mbalimbali za uchumi.
2. Kuweka utaratibu wa elimu na mafunzo kutoa kipaumbele kwenye sekta zinazokuwa haraka
na zinazojitokeza mfano mafuta, gesi na madini ili kuongeza rasilimaliwatu wenye ujuzi na
umahiri unaotakiwa katika sekta hizi kwa ngazi mbalimbali za ajira.
3. Kuweka utaratibu wa kutoa elimu na mafunzo kwa ajili ya sekta zisizo rasmi na kilimo ili
kulifanya taifa kukua kutoka uchumi wa chini kwenda wa kati
25
6.2.2 SHABAHA
1. Elimu na mafunzo inayotolewa kuendana na mahitaji ya soko la ajira ifikapo mwaka
2018.
2. Kuwa na vyuo maalumu vinavyotoa elimu na mafunzo yanayokidhi mahitaji ya sekta
zinazokua haraka na zinazoibuka ifikapo mwaka 2018.
3. Vyuo vya ufundi stadi vya Wilaya pamoja na vyuo vya maendeleo ya wananchi
kuongezwa na kuimarishwa ifikapo mwaka 2019.
4. Vituo atamizi kwa ajili ya kuandaa wahitimu kujiajiri kuanzishwa ifikapo mwaka 2017.
5. Idadi ya vijana, na watu wazima wasiojua kusoma, kuandika na kuhesabukupungua
ifikapo 2018.
6.2.3 VIASHIRIA
a) Ongezeko la ajira kwa wahitimu wa elimu na mafunzo katika sekta rasmi na isiyo rasmi;
b) Idadi ya wataalamu katika sekta zinazokuwa haraka na zinazoibuka;
c) Idadi ya vyuo vyenye ubora vinavyotoa elimu na mafunzo kwa ajili ya sekta isiyo rasmi;
na
d) Kuwepo kwa idadi ya vituo atamizi.
e) Ongezeko la vijana, na watu wazima wanaojua kusoma, kuandika na kuhesabu.
6.3 LENGO Na. 3: Kuweka utaratibu wa kuhakikisha uwepo wa miundombinu bora na
stahiki ya kutosheleza mahitaji ya elimu na mafunzo katika ngazi zote.
6.3.1 MIKAKATI
1. Kuweka vigezo na viwango vya miundombinu ya shule za elimu-msingi ili kukidhi mahitaji
ya elimu ya awali na elimu - msingi.
2. Kuimarisha na kujenga miundombinu inayokidhi mahitaji ya elimu ya awali na elimu-
msingi.
3. Kuimarisha na kujenga miundombinu inayokidhi mahitaji ya elimu ya sekondari ngazi ya juu
4. Kuweka vigezo na viwango vya miundombinu inayokidhi mahitaji ya Vyuo vya ufundi stadi,
vyuo vya ufundi, vyuo vya ualimu na vyuo vikuu (ngazi mbalimbali baada ya elimu –
msingi)
5. Kuimarisha na kujenga miundombinu inayokidhi mahitaji ya Vyuo vya ufundi stadi, vyuo
vya ufundi, vyuo vya ualimu na vyuo vikuu (ngazi mbalimbali baada ya elimu – msingi)
6. Kujenga utamaduni wa utunzaji, usimamizi, ukarabati na ukarafati wa miundombinu ya asasi
za elimu na mafunzo.
6.3.2 SHABAHA
1. Vigezo na viwango vya miundombinu ya shule za elimu-msingi kuwepo ifikapo mwaka
2016.
2. Miundombinu, inayokidhi mahitaji ya elimu ya awali na elimu -msingi ifikapo mwaka 2019.
26
3. Shule za elimu ya sekondari ngazi ya juu za kutosha zenye miundombinu inayokidhi mahitaji
kuwepo ifikapo mwaka 2019.
4. Vigezo na viwango vya miundombinu ya asasi za elimu na mafunzo katika ngazi mbalimbali
baada ya elimu – msingi kuwepo ifikapo mwaka 2016.
5. Vyuo vya ufundi stadi, vyuo vya ufundi, vyuo vya ualimu na vyuo vikuu kuwa na
miundombinu inayokidhi mahitaji na ongezeko la udahili kuwepo ifikapo mwaka 2019.
6. Miongozo ya usimamizi, utunzaji, ukarabati na ukarafati wa miundombinu kuwepo ifikapo
mwaka 2016.
6.3.3 VIASHIRIA
a. Miongozo, vigezo na viwango vya miundombinu katika ngazi ya elimu ya awali, elimu
msingi na sekondari ngazi ya juu;
b. Mfumo mpya wa elimu msingi kutekelezwa katika viwango vilivyowekwa;
c. Idadi ya shule za elimu – msingi;
d. Idadi ya shule za sekondari ngazi ya kawaida zinazotoa masomo ya elimu ya sekondari ngazi
ya juu;
e. Miongozo, vigezo na viwango vya miundombinu baada ya elimu msingi;
f. Idadi ya vyuo vyenye miundombinu bora;
g. Sheria, kanuni na miongozo ya utunzaji, ukarabati na ukarafati wa miundombinu; na
h. Miundombinu yenye ubora stahiki.
6.4 LENGO Na. 4: Kuweka utaratibu wa kuhakikisha vifaa, nyenzo na zana stahiki za
kufundishia na kujifunzia katika elimu na mafunzo zinatosheleza kulingana na
mahitaji na maendeleo ya sayansi, teknolojia na mbinu za kufundishia na kujifunzia
katika ngazi zote.
6.4.1 MIKAKATI
1. Kuhuisha viwango vya ubora wa nyenzo, vifaa na zana za kufundishia na kujifunzia ili kuleta
usawa katika upatikanaji wa Elimu na mafunzo katika shule na vyuo ngazi zote.
2. Kuweka utaratibu yakinifu wa upatikanaji wa vifaa, nyenzo,na zana za kufundishia na
kujifunzia katika shule na vyuo vya Elimu na mafunzo katika ngazi zote.
3. Kujenga utamaduni wa utunzaji, usimamizi, ukarabati wa vifaa, nyenzo,na zana za
kufundishia na kujifunzia mafunzo.
6.4.2 SHABAHA
1. Miongozo ya ubora wa nyenzo, vifaa na zana katika shule na vyuo vya elimu na mafunzo
katika ngazi zote kutolewa na kusambazwa ifikapo mwaka 2016.
2. Shule na vyuo vya elimu na mafunzo katika ngazi zote vyenye vifaa, nyenzo,na zana za
kufundishia na kujifunzia kulingana na viwango vilivyowekwa ifikapo mwaka 2025
3. Miongozo ya usimamizi, utunzaji, ukarabati wa vifaa, nyenzo na zana kuwepo ifikapo
mwaka 2016.
27
6.4.3 VIASHIRIA
a. Miongozo ya viwango vya msingi vya ubora kati ya shule na vyuo vya elimu na mafunzo vya
serikali na vya binafsi katika ngazi zote;
b. Idadi ya vifaa,nyenzo, na zana za kufundishia na kujifunzia katika shule na vyuo vya elimu
na mafunzo katika ngazi zote; na
c. Sheria, kanuni na miongozo ya utunzaji, ukarabati wa nyenzo,na zana za kufundishia na
kujifunzia.
6.5 LENGO Na 5: Kuweka utaratibu wa kuwezesha lugha ya Kiswahili na Kiingereza
kuwa lugha za kufundishia na kujifunzia katika ngazi zote za elimu na mafunzo
6.5.1 MIKAKATI
1. Kuweka utaratibu utakaowezesha lugha ya Kiswahili kutumika kufundishia katika ngazi zote
za elimu na mafunzo.
2. Kuweka utaratibu utakaowezesha lugha ya Kiingereza kama lugha ya mawasiliano kikanda
na kimataifa kufundishwa kwa ufasaha katika ngazi zote za elimu na mafunzo.
3. Kuimarisha kujifunza na kufundisha lugha mbalimbali za kigeni katika ngazi mbalimbali za
elimu na mafunzo
6.5.2 SHABAHA
1. Vifaa, nyenzo na zana za kufundishia na kujifunzia kwa umahiri kwa kutumia lugha ya
Kiswahili kuwepo ifikapo mwaka 2025.
2. Vitabu kutafsiriwa au kuandikwa kwa lugha ya Kiswahili kwa masomo mbalimbali ifikapo
mwaka 2018.
3. Maktaba kuimarishwa kuwa na vitabu na maandiko mengine kiswahili ifikapo mwaka 2019.
4. Maabara zenye kuwezesha ufundishaji na ujifunzaji wa lugha ya Kiswahili kuwepo kwenye
shule na vyuo nchini ifikapo mwaka 2019.
5. Vifaa, nyenzo na zana za kufundisha na kujifunza kwa umahiri kwa kutumia lugha ya
Kiswahili kuwepo ifikapo mwaka 2018.
6. Maktaba kuimarishwa kwa vitabu na maandiko mengine ya Kiingereza ifikapo mwaka 2017.
7. Maabara za lugha ya Kiingereza kuwepo kwenye shule na vyuo nchini ifikapo mwaka 2016.
8. Vifaa, nyenzo na zana za kufundishia na kujifunzia kwa umahiri lugha za kigeni kuwepo
ifikapo mwaka 2016.
6.5.3 VIASHIRIA
a. Sheria, kanuni na miongozo ya lugha ya Kiswahili kutumika kufundishia;
b. Lugha ya Kiswahili kutumika kufundishia;
c. Vitabu kutafsiriwa au kuandikwa kwa lugha ya Kiswahili;
28
d. Andiko la programu ya kuwezesha ujenzi wa maabara za lugha katika shule na vyuo
lililoidhinishwa na Serikali;
e. Miongozo ya kujifunza lugha ya Kiingereza;
f. Andiko la mpango wa kufundisha lugha ya Kiingereza lililoidhinishwa na serikali ;
g. Andiko la mpango wa kuwezesha upatikanaji wa vifaa vya maabara za lugha katika shule na
vyuo lililoidhinishwa na serikali;
h. Idadi ya walimu wa lugha za kigeni, nyenzo, vifaa na zana zinazotumika kujifunza lugha za
kigeni; na
i. Andiko la programu ya kufundisha lugha zingine za kigeni lililoidhinishwa na serikali.
6.6 LENGO Na. 6:Kuweka utaratibu na mazingira wezeshi ya kuhakikisha elimu na
mafunzo katika ngazi zote inatolewa kwa ufanisi kwa njia huria na masafa.
6.6.1 MIKAKATI
1. Kuimarisha njia za utoaji wa elimu na mafunzo zikiwemo huria na masafa ili kuwawezesha
watanzania wengi kujiendeleza kielimu bila vikwazo.
2. Kuhakikisha taasisi zote zinazotoa elimu na mafunzo kwa njia huria na masafa
zimeunganishwa katika mkongo wa taifa na kwa njia nyingine za kisasa.
3. Kuimarisha uhusiano kati ya sekta ya umma na binafsi ili kuleta tija na ufanisi katika utoaji
wa elimu kwa njia huria na masafa.
6.6.2 SHABAHA
1. Rasilimaliwatu wanaosimamia na wanaotekeleza elimu na mafunzo huria na masafa kuwa
wamejengewa uwezo ifikapo mwaka 2025.
2. Miundombinu, vifaa, nyenzo na zana kwa ajili ya elimu na mafunzo kwa njia huria na
masafa kuwepo ifikapo mwaka 2020.
3. Kuhakikisha taasisi zote zinazotoa elimu na mafunzo kwa njia huria na masafa
zimeunganishwa katika mkongo wa taifa na kwa njia nyingine za kisasa ifikapo mwaka
2019.
4. Huduma bora kupitia elimu kwa njia huria na masafa kupatikana nchi nzima ifikapo mwaka
2020.
6.6.3 VIASHIRIA
a) Idadi na aina ya programu za elimu na mafunzo kwa njia huria na masafa;
b) Programu rekebishi za kuimarisha utoaji wa elimu na mafunzo kwa njia huria na masafa;
c) Idadi ya taasisi za elimu na mafunzo zilizounganishwa kwenye mkongo wa taifa;
d) Idadi ya mikataba ya ushirikiano baina ya sekta binafsi zinazoshiriki kutoa elimu kwa njia na
huria na masafa.
29
6.7 LENGO Na. 7: Kuhakikisha kila taasisi ya elimu na mafunzo inakuwa na hatimiliki
ya ardhi mahali ilipo taasisi hiyo kwa ngazi zote.
6.7.1 MKAKATI
Kuwezesha upatikanaji wa Ardhi na hatimiliki ya ardhi kwa taasisi za elimu na mafunzo kwa
ngazi zote.
6.7.2 SHABAHA
1. Taasisi za elimu na mafunzo kuwa na ardhi na hatimiliki kuanzia mwaka 2014.
2. Ardhi kwa ajili ya matumizi ya shughuli za elimu na mafunzo kutambulika na kutengwa
kuanzia mwaka 2014.
6.7.3 VIASHIRIA
a. Idadi ya taasisi zilizo na ardhi ya kutosha yenye hatimiliki.
b. Mpango wa kuwezesha taasisi zote kupata ardhi.
30
SURA YA SABA
MFUMO ENDELEVU WA UGHARIMIAJI WA ELIMU NA MAFUNZO NCHINI
7.0 UTANGULIZI
Pamoja na serikali kutoa kipaumbele katika sekta ya elimu, ongezeko la mahitaji ya elimu na
mafunzo ni changamoto kwa serikali katika ugawaji wa bajeti ambayo ni endelevu katika
ugharimiaji wa elimu na mafunzo. Kwa kutambua hili, serikali imekuwa ikitenga kati ya asilimia
3.6 hadi 6.3 ya pato la taifa kugharimia elimu na mafunzo.Pamoja na jitihada hizi bado
ugharamiaji wa elimu na mafunzo umeendelea kuwa changamoto kubwa na hivyo kuhitaji
mikakati endelevu katika kutatua changamoto hizo. Aidha, serikali imenuaia kuendeleza ubia
na sekta binafsi na kuimarisha ushiriki wa wadau mbalimbali katika ugharimiaji wa elimu na
mafunzo katika ngazi mbalimbali za elimu na mafunzo.
7.1 LENGO Na. 1: Kuimarisha mfumo wa ugharimiaji wa elimu na mafunzo kwa ngazi
zote kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa sekta ya elimu na mafunzo.
7.1.1 MIKAKATI
1. Kuimarisha muundo wa ugharimiaji endelevu wa elimu na mafunzo nchini.
2. Kujenga na kuendeleza ubia kati ya sekta ya umma na binafsi katika kufanikisha miradi ya
elimu na mafunzo kwa ngazi zote.
3. Kuimarisha ushiriki wa wadau katika sekta mbalimbali katika ugharimiaji wa mafunzo
tarajali na mazoezi kwa vitendo sehemu za kazi kwa wanachuo.
7.1.2 SHABAHA
1. Gharama halisi ya kuelimisha mwanafunzi kwa ngazi zote ikiwemo elimu na mafunzo kwa
njia huria na masafa kubainishwa ifikapo mwaka 2014.
2. Vyanzo vya kugharimia elimu na mafunzo katika ngazi mbalimbali kubainishwa na
kutumika ifikapo mwaka 2016.
3. Utaratibu utakaohusisha sekta mbalimbali na jamii katika kugharimia elimu kwa ngazi zote
kuainishwa na kutumika ifikapo mwaka 2016.
4. Tengeo la bajeti ya serikali ya kugharimia elimu na mafunzo lisipungue asilimia 25 ya bajeti
ya serikali ifikapo mwaka 2015.
5. Huduma ya elimu na mafunzo yanayotolewa na sekta binafsi kuwa ya gharama nafuu kwa
kadri iwezekanavyo ifikapo mwaka 2016.
6. Utaratibu endelevu wa kuwawezesha wanafunzi wanaoshindwa kuchangia gharama za elimu
na mafunzo kuwepo ifikapo mwaka 2016.
31
7. Mazingira ya kufanya taasisi za fedha kushiriki katika ugharimiaji wa elimu na mafunzo
kujengwa ifikapo mwaka 2015.
8. Wahitimu wa elimu na mafunzo katika ngazi mbalimbali na jamii kushiriki kugharimia elimu
na mafunzo ifikapo mwaka 2016.
9. Wadau mbalimbali kushiriki katika kugharimia mafunzo tarajali na mazoezi kwa vitendo
katika sehemu mbalimbali za kazi ifikapo mwaka 2016.
7.1.3 VIASHIRIA
a. Gharama halisi ya kumsomesha mwanafunzi kwa ngazi zote za elimu na mafunzo;
b. Idadi ya vyanzo mahsusi vya fedha za kugharimia elimu na mafunzo;
c. Asilimia 25 ya tengeo la bajeti ya serikali kugharimia elimu na mafunzo;
d. Sheria, kanuni na miongozo ya ugharimiaji wa elimu iliyohuishwa;
e. Gharama nafuu za huduma katika taasisi za elimu na mafunzo;
f. Mwongozo wa utaratibu yakinifu wa kuwawezesha wanafunzi wanaoshindwa kuchangia
gharama za elimu na mafunzo;
g. Taasisi za fedha kushiriki katika ugharimiaji wa elimu na mafunzo;
h. Idadi ya miradi ya elimu na mafunzo baina ya sekta binafsi na sekta ya elimu na mafunzo;
i. Muundo wa ugharimiaji wa elimu na mafunzo tarajali na kwa vitendo ; na
j. Ushiriki wa wadau katika ugharimiaji wa mafunzo tarajali na mafunzo kwa vitendo katika
sehemu mbambali za kazi.
32
SURA YA NANE
UONGOZI, USIMAMIZI NA UENDESHAJI WA ELIMU NA MAFUNZO NCHINI
8.0 UTANGULIZI
Uongozi na utawala bora ni muhimu kwa ufanisi wa mfumo wa elimu na mafunzo. Watekelezaji
na wasimamizi wa elimu na mafunzo katika ngazi mbalimbali hawana budi kuwa na sifa stahiki
za kitaalam na kitaaluma, uzoefu na ujuzi kulingana na nafasi zao. Mikakati iliyoandaliwa
imelenga kuongeza ufanisi katika uongozi na utawala katika ngazi zote za elimu na mafunzo kwa
kuweka mfumo madhubuti wa utendaji, usimamiaji na uwajibikaji.
8.1 LENGO Na. 1: Kuongeza ufanisi, tija uwajibikaji na uongozi bora katika usimamizi
na uendeshaji wa elimu na mafunzo nchini
8.1.1 MIKAKATI
1. Kuhuisha mfumo wa uongozi, usimamizi na uendeshaji wa elimu na mafunzo katika ngazi
zote za elimu na mafunzo ikiwa ni pamoja na ugatuaji wa madaraka.
2. Kuweka mpango wa utambuzi, usajili, kuendeleza na kusimamia taaluma ya ualimu, weledi
na maadili.
8.1.2 SHABAHA
1. Miongozo kuhusu vigezo, viwango na taratibu za uongozi, usimamiaji na upimaji wa
maendeleo ya elimu na mafunzo ifikapo mwaka 2016.
2. Mgawanyo wa majukumu, usimamizi na uwajibikaji wenye tija na ufanisi katika elimu na
mafunzo kuwepo ifikapo mwaka 2016.
3. Majukumu na umahiri wa watendaji katika masuala mbalimbali kwa ngazi zote za elimu na
mafunzo kuhuishwa na kuboreshwa mara kwa mara kuanzia mwaka 2014.
4. Utambuzi na usajili wa walimu katika sekta ya elimu na mafunzo kuwepo ifikapo mwaka
2016.
8.1.3 VIASHIRIA
a) Sheria na miongozo kuhusu uongozi, usimamizi na uendeshaji wa elimu na mafunzo
Iliyohuishwa;
b) Miundo ya uongozi, usimamizi na uendeshaji; na
c) Sheria, kanuni na miongozo kuhusu utambuzi na usajili wa walimu.
8.2 LENGO Na. 2: Kuimarisha mfumo wa menejimenti ya data na taarifa za elimu na
mafunzo kwa ngazi zote za elimu na mafunzo.
33
8.2.1 MKAKATI
Kuimarisha mfumo wa menejimenti ya taarifa za elimu ili kuleta tija na ufanisi katika kuweka
mipango na maamuzi kuhusu utoaji wa elimu na mafunzo katika ngazi zote za elimu na
mafunzo.
8.2.2 SHABAHA
1. Data na taarifa zinazoaminika kupatikana ifikapo mwaka 2016.
2. Data na taarifa kutumika katika mipango na maamuzi katika sekta ya elimu na mafunzo
ifikapo mwaka 2016.
8.2.3 VIASHIRIA
a. Miongozo ya kuimarisha Mfumo wa Menejimenti ya taarifa za Elimu.
b. Matumizi stahiki ya taarifa za elimu.
34
SURA YA TISA
MASUALA MTAMBUKA KATIKA ELIMU NA MAFUNZO KUZINGATIWA
9.0 UTANGULIZI
Umuhimu wa masuala mtambuka katika elimu na mafunzo haukwepeki. Mikakati iliyoandaliwa
inakusudia kuingiza maudhui ya masuala mtambuka katika mitaala na programu kwa ngazi zote
za elimu na mafunzo ili kuleta maendeleo endelevu
9.1 LENGO Na.1: Elimu na Mafunzo yenye maudhui ya masuala mtambuka kwa ajili
ya maendeleo endelevu ya Taifa.
9.1.1 MKAKATI
Kuingiza katika mitaala maudhui ya masuala ya stadi za maisha na mabadiliko ya tabianchi na
stadi nyinginezo muhimu katika maendeleo ya nchi.
9.1.2 SHABAHA
1. Mitaala na programu yenye maudhui ya stadi za maisha na mabadiliko ya tabianchi
kuwepo ifikapo mwaka 2016.
2. Walimu mahiri katika kuwawezesha wanafunzi kujifunza masomo mbalimbali yenye
maudhui mtambuka ifikapo mwaka 2016.
3. Wanafunzi wenye uelewa wa stadi za maisha na mabadiliko ya tabianchi ifikapo mwaka
2018.
9.1.3 KIASHIRIA
Programu na mihtasari inayojumuisha maudhui ya masuala mtambuka.
9.2 LENGO Na. 2: Kuweka utaratibu wa kuimarisha utoaji wa huduma ya ushauri na
unasihi katika ngazi zote za elimu na mafunzo.
9.2.1 MKAKATI
Kuimarisha muundo wa ushauri na unasihi katika ngazi zote za elimu na mafunzo nchini.
35
9.2.2 SHABAHA
1. Miongozo na utaratibu wa utoaji wa ushauri na unasihi katika elimu na mafunzo kuandaliwa
ifikapo mwaka 2015.
2. Miundombinu na nyenzo za kutolea ushauri nasaha na unasihi katika elimu na mafunzo
kuwepo ifikapo mwaka 2018.
3. Kuwepo na wataalamu mahiri wa ushauri na unasihi wa kutosha katika ngazi zote elimu na
mafunzo ifikapo mwaka 2020.
4. Wanafunzi kupata huduma za ushauri na unasihi kwa kutumia wataalamu mahiri katika shule
na vyuo ifikapo mwaka 2020.
9.2.3 VIASHIRIA
a. Miongozo ya ushauri na unasihi;
b. Huduma za ushauri na unasihi katika elimu na mafunzo; na
c. Idadi ya wataalamu mahiri wa huduma za ushauri na unasihi katika ngazi zote za elimu na
mafunzo.
9.3 LENGO Na. 3: Kuweka utaratibu utakao hakikisha kuwa haki za binadamu
zinalindwa na hawapewi adhabu za kutesa au kudhalilisha wakati wakipatiwa elimu au
mafunzo katika ngazi mbalimbali.
9.3.1 MKAKATI
Kuweka muundo, miongozo, kanuni na taratibu za kurekebisha tabia na mienendo ya wanafunzi
wanaokiuka taratibu mbalimbali za shule na vyuo bila kuwadhalilisha au kukiuka haki za
binadamu.
9.3.2 SHABAHA
1. Adhabu za kutesa au kudhalilisha zinazuiliwa katika mfumo wa elimu na mafunzo ifikapo
mwaka 2016.
2. Wanafunzi wanaokiuka taratibu za shule au za vyuo kurekebishwa kwa njia endelevu na za
kitaalamu ifikapo mwaka 2016.
3. Taratibu za kuwafukuza shule wanafunzi wa elimu - msingi kutokana na sababu mbalimbali
kuhuishwa ifikapo mwaka 2016.
4. Walimu na jamii kuelewa taratibu za kutatua matatizo ya kinidhamu ya wanafunzi shuleni na
vyuoni ifikapo mwaka 2016.
36
9.3.3 KIASHIRIA
Sheria, kanuni na miongozo inayohusu haki za binadamu katika mfumo wa elimu na
mafunzo iliyohuishwa
9.4 LENGO Na.4: Kuweka utaratibu wa kuhakikisha maadili ya walimu na watumishi
wengine yanazingatiwa katika ngazi zote za elimu na mafunzo.
9.4.1 MKAKATI
Kuweka muundo na utaratibu wa kuhakikisha kwamba maadili ya walimu na watumishi wengine
yanazingatiwa katika ngazi zote za elimu na mafunzo kwa kuzingatia sheria za kazi na haki za
binadamu.
9.4.2 SHABAHA
1. Sheria, miongozo, kanuni na taratibu kuhusu maadili ya walimu na watumishi wengine
kuhuishwa ifikapo mwaka 2016.
2. Nidhamu, uwajibikaji na uadilifu kuimarika katika ngazi zote za elimu na mafunzo ifikapo
mwaka 2017.
3. Mazingira bora ya kazi na ya kuishi mwalimu kuwepo ifikapo mwaka 2020.
9.4.3 VIASHIRIA
a. Muundo na utaratibu wa nidhamu na maadili ya kazi na uwajibikaji wa walimu uliohuishwa
na kutumika;
b. Sheria na kanuni kuhusu maadili ya walimu na watumishi wengine katika ngazi zote za elimu
na mafunzo zilizohuishwa na kutumika; na
c. Mazingira ya kazi na ya kuishi mwalimu kwa kuzingatia haki za binadamu
9.5 LENGO Na.5: Kuimarisha muundo wa kutekeleza maazimio na itifaki za
ushirikiano baina ya Tanzania na nchi nyingine, kikanda na kimataifa katika elimu na
mafunzo
9.5.1 MKAKATI
Utaratibu wa kushughulikia makubaliano ya utekelezaji wa maazimio mbalimbali yanayogusa
elimu na mafunzo kikanda na kimataifa.
9.5.2 SHABAHA
Miongozo na utaratibu wa kushughulikia na kutekeleza maazimio na itifaki yanayohusu elimu na
mafunzo kuwepo ifikapo mwaka 2016.
37
9.5.3 KIASHIRIA
Muundo wa kutekeleza maazimio na itifaki za ushirikiano na nchi nyingine.
9.6 LENGO Na. 6: Kuimarisha utaratibu wa kuwezesha wanafunzi kujifunza kwa
ufanisi masomo ya hisabati, sayansi na tekinolojia katika ngazi zote za elimu na mafunzo.
9.6.1 MKAKATI
Kuimarisha na kuweka utaratibu utakaowezesha masomo ya hisabati, sayansi na tekinolojia
kufundishwa kwa ufanisi zaidi.
9.6.2 SHABAHA
1. Hisabati, sayansi, na tekinolojia, kufundishwa kwa ufanisi ifikapo mwaka 2018.
2. Rasilimaliwatu mahiri na wakutosha kuwezesha wanafunzi kujifunza masomo ya hisabati,
sayansi na tekinolojia katika ngazi zote za elimu na mafunzo kuwepo ifikapo mwaka 2018.
3. Umahiri wa wanafunzi katika nyanja za hisabati, sayansi na tekinolojia kuongezeka ifikapo
mwaka 2018.
9.6.3 VIASHIRIA
a. Viwango vya ufaulu wa wanafunzi katika masomo ya hisabati, sayansi, na tekinolojia.
b. Idadi ya wataalamu wenye uwezo na umahiri katika kufundisha masomo ya hisabati, sayansi
na tekinolojia.
c. Idadi ya wahitimu wenye umahiri katika masomo ya hisabati, sayansi na tekinolojia.
9.7 LENGO Na. 7: Kuweka utaratibu wa kuhakikisha matumizi zaidi ya sayansi na
tekinolojia katika utoaji wa elimu na mafunzo katika ngazi zote.
9.7.1 MIKAKATI
1. Kuweka mpango wa kutumia vifaa bandia (Simulators) katika kufundisha masomo kwa
vitendo katika maabara na karakana ili kupunguza gharama za elimu na mafunzo
2. Kuimarisha ubia baina ya sekta ya elimu na mafunzo na viwanda ili kuwezesha upatikanaji
wa vifaa, zana na nyenzo za kufundishia na kujifunzia hisabati, sayansi na tekinolojia
3. Kuwezesha kila taasisi ya elimu na mafunzo kuwa kitovu cha sayansi na tekinolojia katika
jamii.
38
9.7.2 SHABAHA
a) Vifaa bandia (Simulators) kutumika katika kufundisha na kujifunza kwa ngazi zote za elimu
na mafunzo ifikapo mwaka 2020.
b) Maabara za shule na vyuo kubuni na kutengeneza vifaa, zana na nyenzo za kufundishia na
kujifunzia hisabati, sayansi na teknolojia katika ngazi husika ifikapo mwaka 2020.
c) Walimu na Wanafunzi wenye uwezo wa kubuni na kutengeneza vifaa, zana na nyenzo za
kufundishia na kujifunzia kuwepo ifikapo mwaka 2025.
d) Ushiriki wa viwanda na sekta binafsi kuwezesha upatikanaji wa vifaa, zana na nyenzo za
kufundishia na kujifunzia hisabati, sayansi na tekinolojia ifikapo mwaka 2016.
e) Mpango wa taifa wa kushirikisha sekta binafsi katika upatikanaji wa vifaa, zana na nyenzo za
kufundishia na kujifunzia hisabati, sayansi na tekinolojia kuwepo na kutumika ifikapo
mwaka 2016.
f) Taasisi za elimu na mafunzo kuwa kitovu cha matumizi ya sayansi na tekinolojia katika jamii
ifikapo mwaka 2018.
g) Taasisi za elimu na mafunzo kuwa ni vituo vya elimu (Resource centers) katika jamii ifikapo
mwaka 2016.
h) Taasisi za elimu na mafunzo kuwa vituo atamizi ili kujenga uwezo wa wahitimu katika jamii
ifikapo mwaka 2017.
9.7.3 VIASHIRIA
a. Matumizi ya vyombo bandia (Simulators) katika karakana na maabara za shule na vyuo;
b. Idadi ya vifaa, zana na nyenzo zilizotengenezwa shuleni na vyuoni;
c. Idadi ya wanafunzi na walimu wenye uwezo wa kubuni na kutengeneza vifaa, zana na
nyenzo;
d. Sheria na miongozo ya ubia baina ya sekta ya elimu na mafunzo na sekta binafsi;
e. Idadi ya miradi ya ubia ya sekta binafsi katika upatikanaji wa vifaa, zana na nyenzo za
kufundishia na kujifunzia hisabati, sayansi na tekinolojia;
f. Sheria na miongozo kuwezesha taasisi za elimu kuwa kitovu cha sayansi na tekinolojia;
g. Idadi ya taasisi za elimu na mafunzo ambazo ni vitovu vya sayansi na teknolojia; na
h. Idadi ya taasisi zenye vituo atamizi.
9.8 LENGO Na. 8: Kuweka utaratibu na kuimarisha ushiriki fanisi wa wadau
mbalimbali katika sekta ya elimu na mafunzo katika ngazi zote
9.8.1 MIKAKATI
1. Kupanua wigo wa ushiriki wa wadau katika mipango, uendeshaji, ugharimiaji, ufuatiliaji na
tathmini katika ngazi zote za elimu na mafunzo.
2. Kuongeza ushiriki wa wadau katika utoaji wa huduma mbalimbali mfano chakula na malazi
katika elimu na mafunzo.
39
9.8.2 SHABAHA
1. Wigo wa ugharimiaji wa elimu na mafunzo katika ngazi zote za elimu kwa kushirikisha
wadau mbalimbali kupanuka ifikapo mwaka 2016.
2. Ushiriki wa wadau katika mipango, uendeshaji na tathmini ya elimu na mafunzo katika ngazi
zote kuongezeka ifikapo mwaka 2016.
3. Utaratibu wa kushirikisha wadau katika utoaji wa huduma mbalimbali mfano chakula na
malazi katika elimu na mafunzo kuwekwa ifikapo mwaka 2016.
4. Huduma mbalimbali katika shule na vyuo kutolewa kwa kushirikisha wadau ifikapo mwaka
2016.
9.8.3 VIASHIRIA
a. Wigo wa ushiriki wa wadau katika ugharimiaji wa elimu na mafunzo;
b. Idadi ya wadau wanaoshiriki katika uendeshaji, ugharimiaji na ufuatiliaji wa elimu na
mafunzo;
c. Utaratibu wa huduma mbalimbali zinazotolewa na wadau; na
d. Aina za huduma mbalimbali zinazotolewa na wadau.
40
SURA YA KUMI
MGAWANYO WA MAJUKUMU NA WAJIBU KWA WADAU MBALIMBALI
10.0 UTANGULIZI
Utekelezaji wa sera ya elimu na mafunzo, unategemea ushirikishwaji wa wadau mbalimbali
katika kufikia malengo yaliyokusudiwa. Wadau hao ni pamoja na Wizara yenye dhamana ya
Elimu na Mafunzo, Wizara yenye dhamana ya masuala ya Fedha, Wizara yenye dhamana ya
Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto; Wizara yenye dhamana ya Ardhi na Maendeleo ya
Makazi, Wizara yenye dhamana ya Afya na Ustawi wa Jamii; Wizara yenye dhamana ya
Mawasiliano, Sayansi na Tekinolojia; Wizara yenye dhamana ya Kilimo, Chakula na Ushirika;
Wizara yenye dhamana ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi; Wizara yenye dhamana ya Ujenzi;
Wizara yenye dhamana ya Maliasili na Utalii; Wizara yenye dhamana ya Viwanda na Biashara;
Wizara yenye dhamana ya Nishati na Madini; Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa Serikali
za Mitaa (OWM – TAMISEMI), mashirika na taasisi za Serikali na zisizo za Serikali, shule na
vyuo, washirika wa maendeleo wa ndani na nje, jamii na wadau wengine wa elimu na mafunzo.
Aidha, kiutawala, Mkakati wa kutekeleza Sera ya Elimu na Mafunzo utatekelezwa katika ngazi
za Taifa, Mkoa, Mamlaka za Halmashauri, Kata, Shule na Vyuo.
10.1 Ngazi ya Taifa
Mkakati wa Kutekeleza Sera ya Elimu na Mafunzo utaelekeza utekelezaji wa Sera ya Elimu na
Mafunzo katika Wizara mbalimbali pamoja na taasisi zake kulingana na majukumu
yaliyokasimiwa kwa wizara na taasisi hizo. Wizara, idara na taasisi hizo zitatekeleza majukumu
na wajibu huo katika sekta ya elimu kwa kushirikiana na wizara yenye dhamana ya elimu na
mafunzo ya ufundi. Majukumu hayo ni kama ifuatavyo:
10.1.1. Wizara yenye dhamana ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
Jukumu kuu la wizara ni kuandaa, kusimamia na kuratibu utekelezaji wa sera kwa kuhuisha
sheria, kanuni, miongozo na viwango vya utekelezaji wa sera. Majukumu mengine ni haya
yafuatayo:
a) kulinda uhuru na kujenga uwezo wa vyombo vya ithibati na uthibiti wa ubora wa elimu
nchini;
b) Kujenga uwezo wa idara za makao makuu, taasisi na vyombo vilivyo chini ya wizara
kwa ajili ya kutekeleza majukumu yake kama yanavyoainishwa na mkakati wa
utekelezaji wa sera; Kufanya ufuatiliaji na tathmini ya utekelezaji wa sera na kutumia
matokeo ya tathmini, tafiti na taarifa mbalimbali zinazohusu hali halisi ya utoaji elimu
na mafunzo ili Wizara iweze kutoa maamuzi yenye tija na yatakayoongeza ufanisi
katika utekelezaji wa mkakati wa sera;
c) Kuhuisha utekelezaji wa mkakati wa sera ya elimu na mafunzo kwa kushirikiana na
wadau wengine wa elimu; na
d) Kuelimisha jamii kuhusu sera, mkakati wa utekelezaji wa sera na majukumu ya WEMU,
41
wizara nyingine za serikali na wadau wa elimu na mafunzo katika utekelezaji wa
mkakati wa sera ya elimu na mafunzo.
10.1.2. Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM –
TAMISEMI),
Wizara hii inajukumu la kuhakikisha uwepo wa shule katika maeneo mbalimbali ya nchi. Hivyo
basi, katika ngazi ya mkoa sera za serikali zinasimamiwa na Sekretarieti ya Mkoa
inayoongozwa na Afisa Tawala wa Mkoa. Afisa elimu wa mkoa ni mtaalamu wa elimu katika
Sekretarieti na ana jukumu la kusimamia mkakati wa utekelezaji wa Sera ya Elimu na Mafunzo
katika katika ngazi ya mkoa. Hakuna muunganiko mzuri wa mgawanyo wa majukumu na
uwajibikaji kati ya Afisaelimu wa Mkoa na Ma-Afisa elimu katika ngazi ya Halmashauri. Hali
hii inasababisha udhaifu katika utekelezaji wa sera.
Katika ngazi ya halmashauri, utendaji wa idara ya elimu unasimamiwa na Afisa elimu Elimu
Sekondari na Afisa elimu Msingi. Hawa wanateuliwa na Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na
Mafunzo ya Ufundi na wanapata maelekezo miongozo na taratibu za utekelezaji kutoka kwa
Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi; katika utendaji wao wa kazi wa kila siku
wanawajibika moja kwa moja kwa Mkurugenzi wa Halmashauri. Mkaguzi Mkuu wa Shule wa
wilaya anawajibika moja kwa moja kiutendaji kwa Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na mafunzo
kupitia kwa Mkaguzi Mkuu wa Kanda. Ili kusimamia utekelezaji wa mkakati wa sera kwa
ufanisi katika ngazi mbalimbali mambo yafuatayo yanapendekezwa:
a) Pawepo na mgawanyo wa majukumu uliobayana na taratibu za uwajibikaji kati ya Afisa
elimu wa Mkoa na Afisa elimu wa Halmashauri. Uwekwe utaratibu wa mgawanyo wa
majukumu katika ngazi zote za Wilaya, Tarafa, Kata na Kijijini/Mtaa. Ofisi ya Mratibu
wa Elimu Kata iimarishwe kiutendaji na kujengewa uwezo wa kumudu jukumu la
kuratibu shule na vyuo katika eneo husika. Kamati /bodi za shule na vyuo ziwajibike
kwa wananchi katika kusimamia shule za msingi na sekondari kupitia ofisi za Waratibu
Elimu Kata; na
b) Kuweka utaratibu utakaowezesha Halmashauri na jamii kushiriki kikamilifu katika
ugharimiaji wa elimu – msingi kwa wote. Halmashauri zitawajibika kuratibu na
kuunganisha nguvu za wananchi na wadau wengine katika eneo husika katika
kuwezesha upatikanaji wa miundombinu, vifaa, nyenzo na zana na kuhakikisha shule
zote na vyuo vinakuwa na vitabu, vifaa, nyenzo na zana za kujifunzia na kufundishia za
kutosha kulingana na mahitaji.
10.1.3. Kamati Maalum ya Kisekta na Wadau
Wizara yenye dhamana ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi na OWM-TAMISEMI zitashirikiana
kuunda kamati maalumu itakayo jumuisha wawakilishi kisekta toka Wizara ya Fedha, Wizara
ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto; Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi, Wizara
ya Afya na Ustawi wa Jamii; Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika; Wizara ya Maendeleo ya
Mifugo na Uvuvi; Wizara ya Miundombinu; Wizara ya Viwanda na Biashara; Wizara ya
Nishati na Madini; na wadau kutoka mashirika na taasisi za Serikali na zisizo za Serikali,
washirika wa maendeleo wa ndani na nje, jamii na wadau wengine wa elimu na mafunzo.
42
10.1.4. Wizara yenye dhamana ya masuala ya Fedha
Wajibu wa wizara hii ni kuhakikisha kuwa fedha za kugharimia elimu katika ngazi mbalimbali
zinapatikana kama ifuatavyo:
a) Kuwezesha mifuko mbalimbali ya kugharimia elimu kuanzishwa na wakala
mbalimbali wanahusishwa katika kuchangia mifuko ya elimu;
b) Kuweka sheria au taratibu za kutenga asilimia ya pato la taifa na bajeti ya
serikali ili kuelekezwa katika kuchangia gharama za elimu katika ngazi zote za
elimu na mafunzo;
c) Kutumia vyuo vilivyo chini ya wizara katika kupata wataalamu, vifaa na zana za
kufundishia na kujifunzia;
d) Kuhamasisha uwekezaji katika sekta ya elimu kwa kutumia kituo cha uwekezaji;
na
e) Kuhusisha kituo cha uwekezaji katika kutafuta fedha kwa ajili ya kugharimia
elimu na mafunzo.
10.1.5. Wizara yenye dhamana ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
Wizara yenye dhamana ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto itahusika moja kwa moja na
uandaaji wa mitaala ya watoto kwa ajili ya vituo vya kulelea watoto wadogo. Majukumu
mengine ni kama ifuatavyo:
a) Kuratibu na kusimamia elimu ya makuzi katika vituo vya kulelea watoto wadogo;
b) Kuandaa walezi wa watoto wadogo watakaofanya kazi katika vituo vya kulelea watoto
wadogo; na
c) Kusimamia na kuratibu mafunzo katika vyuo vya Maendeleo ya Jamii.
10.1.6. Wizara yenye dhamana ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi
Jukumu kubwa la wizara hii ni kuandaa mpango wa matumizi ya ardhi kwa ajili ya shule, vyuo
na taasisi nyingine za elimu na mafunzo. Majukumu mengine mahsusi ni kama ifuatavyo:
a) Kuandaa na kuwezesha upatikanaji wa hati miliki za ardhi kwa shule, vyuo na taasisi
nyingine za elimu na mafunzo;
b) Kuanzisha uhusiano kati ya vyuo vya elimu na mafunzo ya ardhi na shule za elimu
msingi katika kuleta ufanisi wa ufundishaji shuleni na vyuoni; na
c) Kusimamia vyuo vilivyo chini ya wizara viandae mitaala kulingana na maelekezo ya
mkakati wa kutekeleza sera ili wahitimu wawe mahiri na waweze kushiriki kikamilifu
katika soko la ajira na ulimwengu wa kazi.
10.1.7. Wizara yenye dhamana ya Afya na Ustawi wa Jamii
Wizara hii itakuwa na jukumu la kuandaa, kusimamia na kuratibu upatikanaji wa huduma za
afya katika ngazi zote za elimu na mafunzo. Katika kufanya hivyo wizara itawajibika kufanya
yafuatayo:
a) Kuhakikisha kuna mpango mahsusi wa upatikanaji wa huduma za afya katika shule na
vyuo;
43
b) Kuandaa wataalamu wa afya watakao hitajika shuleni na vyuoni na kuhakikisha afya za
watoto zinaimarishwa kwa kupatiwa chanjo na mafunzo ya huduma ya kwanza;
c) Kuandaa Kliniki za afya katika shule na vyuo kwa kushirikiana na wataalamu
mbalimbali wa tiba na afya ya binadamu pamoja na taasisi za utafiti wa masuala ya
magonjwa na afya ya binadamu;
d) Kuleta ushirikiano baina ya vyuo na viwanda vya kutengeneza madawa mbalimbali ili
kuwezesha upatikanaji wa nafasi za wanafunzi kupata fursa ya kujifunza kwa vitendo
katika viwanda hivyo;
e) Kuleta ushirikiano baina ya shule, vyuo na viwanda vya kutengeneza madawa
mbalimbali ili kuwezesha upatikanaji wa madawa ya maabara za shule na vyuo kwa njia
ya msaada au kwa bei nafuu; na
f) Kusimamia vyuo vilivyo chini ya wizara viandae mitaala kulingana na maelekezo ya
mkakati wa kutekeleza sera ili wahitimu wawe mahiri na waweze kushiriki kikamilifu
katika soko la ajira na ulimwengu wa kazi.
10.1.8. Wizara yenye dhamana ya Kilimo, Chakula na Ushirika
Jukumu la wizara hii litakuwa ni kuandaa, kusimamia na kuratibu upatikanaji wa chakula kwa
ajili ya elimu- msingi na ngazi nyingine za elimu na mafunzo. Majukumu mengine ni:
a) Kuanzisha miradi ya lishe shuleni na vyuoni
b) Kusimamia vyuo vya kilimo na vya ushirika viandae mitaala kulingana na maelekezo ya
mkakati wa kutekeleza sera ili wahitimu wawe mahiri na wanaohitajika katika soko la
ajira na ulimwengu wa kazi; na
c) Kusimamia vyuo vya kilimo na vyuo vya ushirika katika kupanua nafasi za mafunzo.
10.1. 9. Wizara yenye dhamana ya Viwanda na Biashara
Jukumu kubwa la wizara hii litakuwa kusimamia na kuratibu ushiriki wa viwanda katika
uandaaji wa vifaa vya shule na vyuo. Majukumu mengine ni:
a) Kushirikiana na Wizara husika katika kuandaa mpango wa ushirikishaji wa
wanafunzi katika mafunzo ya vitendo viwandani,
b) Kuweka mazingira ya uanagenzi (apprenticeship) kwa wanavyuo wa vyuo vya
ufundi stadi ili wapate mafunzo viwandani; na
c) Kusimamia vyuo vilivyo chini ya wizara ili viandae mitaala kulingana na maelekezo
ya mkakati wa kutekeleza sera ili wahitimu wawe mahiri na wanaohitajika katika
soko la ajira na ulimwengu wa kazi.
10.1.10. Wizara yenye dhamana ya Nishati na Madini
Jukumu la wizara hii litakuwa ni kuandaa, kusimamia na kuratibu upatikanaji wa nishati ya
umeme wa uhakika kwa ajili ya shule na taasisi za elimu na mafunzo. Majukumu mengine ni:
a) Kuandaa mpango wa kuwezesha shule, vyuo na taasisi nyingine za elimu na mafunzo
kuwa na miundombinu bora ya nishati.
b) Kuwezesha wanafunzi kujifunza kwa vitendo katika kampuni mbalimbali zinazohusika
na nishati na madini.
c) Kusimamia vyuo vilivyo chini ya wizara ili viandae mitaala kulingana na maelekezo ya
mkakati wa kutekeleza sera ili wahitimu wawe mahiri na wanaohitajika katika soko la
ajira na ulimwengu wa kazi.
44
10.1.11. Wizara yenye dhamana ya masuala ya Maji
Jukumu la wizara hii litakuwa ni kuandaa, kusimamia na kuratibu upatikanaji wa maji safi na
salama ya kutosha kwa ajili ya shule na taasisi za elimu na mafunzo. Majukumu mengine ni:
a) Kuhakikisha shule zote na vyuo vinakuwa na vyanzo salama vya maji safi na salama;
b) Kuhakikisha shule, vyuo na taasisi nyingine za elimu na mafunzo zina miundombinu
bora ya kusambaza maji safi na salama;
c) Kuhakikisha shule, vyuo na taasisi nyingine za elimu na mafunzo zina miundombinu
bora ya maji taka; na
d) Kusimamia vyuo vilivyo chini ya wizara ili viandae mitaala kulingana na maelekezo ya
mkakati wa kutekeleza sera ili wahitimu wawe mahiri na wanaohitajika katika soko la
ajira na ulimwengu wa kazi.
10.1.12. Wizara yenye dhamana ya masuala ya Ujenzi
Jukumu la wizara hii litakuwa ni kuandaa, kusimamia na kuratibu upatikanaji wa miundombinu
bora kwa ajili ya shule na taasisi za elimu na mafunzo. Majukumu mengine ni:
a) Kuhakikisha kwa kushirikiana na halmashauri zote nchini kunakuwa na mpango wa
ujenzi wa nyumba za walimu na vyumba vya madarasa vinavyokidhi mahitaji ya shule
na vyuo;
b) Kuandaa mpango wa kuwezesha shule, vyuo na taasisi nyingine za elimu na mafunzo
zinakuwa na miundombinu stahiki na ya kutosha;
c) Kuwezesha wanafunzi kujifunza kwa vitendo katika kampuni mbalimbali zinazohusika
na miundombinu na katika sekta ya ujenzi; na
d) Kusimamia vyuo vilivyo chini ya wizara ili viandae mitaala kulingana na maelekezo ya
mkakati wa kutekeleza sera ili wahitimu wawe mahiri na wanaohitajika katika soko la
ajira na ulimwengu wa kazi.
10.1.14. Wizara yenye dhamana ya Mawasiliano, Sayansi na Tekinolojia
Jukumu la wizara hii litakuwa ni kuandaa, kusimamia na kuratibu mpango wa kufanya shule na
vyuo kuwa vitovu vya sayansi na tekinolojia. Majukumu mengine ni:
a) Kuwezesha tekinolojia ya mawasiliano kutumika shuleni na vyuoni ili kutimiza
azma ya shule na vyuo kuwa vitovu vya sayansi na tekinolojia; na
b) Kusimamia vyuo vilivyo chini ya wizara ili viandae mitaala kulingana na maelekezo
ya mkakati wa kutekeleza sera ili wahitimu wawe mahiri na wanaohitajika katika
soko la ajira na ulimwengu wa kazi.
10.1.15. Wizara yenye dhamana ya masuala ya Kazi na Ajira
Jukumu la wizara hii ni kuwezesha waajiri kutoa nafasi za mafunzo ya uanagenzi, mafunzo
tarajali na mazoezi ya vitendo sehemu za kazi kwa wanafunzi wa vyuo. Aidha, kama
msimamizi wa ajira, wizara hii itakuwa na jukumu la kutoa taarifa za ajira ili kuandaa
programu za elimu na mafunzo stahiki kulingana na mahitaji ya rasilimaliwatu.
45
10.1.16. Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma
Jukumu la Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa umma litakuwa kuhuisha muundo wa
utumishi wa walimu na watumishi wengine katika sekta ya elimu ili kuongeza tija na ufanisi.
Majukumu mengine ni pamoja na:-
a) Kuandaa mpango wa kuajiri na kubakiza idadi ya kutosha ya walimu katika shule na
vyuo;
b) Kuandaa mpango wa ajira kwa watendaji wa elimu katika shule na vyuo ambao siyo
walimu; na
c) Kutoa posho kwa ajili ya walimu na watendaji wengine wa sekta ya elimu kuwezesha
kufanya kazi katika mazingira magumu.
10.1.17. Vyombo vinavyosimamia Ubora wa Elimu na Mafunzo
Vyombo hivi vikiwa mkono wa kitaalamu wa wa serikali katika elimu na mafunzo, vitakuwa na
wajibu wa kuandaa vigezo na viwango vya ubora wa elimu na mafunzo na kuhakikisha
vinazingatiwa. Aidha, vyombo hivi vitahakikisha kuwa shule na vyuo vinafanyiwa usajili,
ithibati na uthibiti.
10.1.18. Sekta Binafsi, Mashirika yasiyo ya Kiserikali na Vyama vya Jamii
Sekta binafsi inajukumu la:
a) Kushirikiana na Wizara mbalimbali, Halmashauri na vyama vya kijamii kuwezesha
utoaji wa elimu katika ngazi zote za elimu na mafunzo;
b) Kushiriki katika mipango mbalimbali ya uendeshaji wa elimu na mafunzo;
c) Kutoa huduma mbalimbali za elimu na mafunzo katika shule na vyuo;
d) Kuhamasisha wananchi katika kuchangia maendeleo ya elimu na mafunzo katika nyanja
mbalimbali; na
e) Kushiriki katika kupanua fursa za elimu na mafunzo kwa kumiliki shule na vyuo,
kuchangia fedha au kusaidia wanafunzi katika mazingira magumu.
10.1.19. Washirika wa Maendeleo
a) Kushiriki katika kusaidia miradi ya elimu na mafunzo katika ngazi mbalimbali za elimu
na mafunzo; na
b) Kushiriki katika ujenzi wa miundombinu ya shule na vyuo.
10.2 Ngazi ya Mkoa
Jukumu la mkoa ni kupokea, kusimamia na kuratibu utekelezaji wa sheria, kanuni na miongozo
ya elimu na mafunzo katika ngazi ya halmashauri ikiwa ni pamoja kuelimisha watekelezaji
kuhusu miongozo hiyo kwenye ngazi ya Halmashauri za Wilaya, Mji, Manispaa na Jiji. Aidha,
mkoa utawajibika katika kuratibu utekelezaji wa mipango ya elimu na mafunzo ya halmashauri,
kutathmini na kutoa taarifa ya utekelezaji wa sera kwa ngazi ya taifa. Katika kutekeleza
majukumu yake ngazi ya mkoa itahitaji kuwa na timu ya uongozi wa elimu na mafunzo yenye
nyenzo muhimu na wataalamu wa elimu katika kutekeleza majukumu yake.
46
10.3 Halmashauri za Wilaya, Mji, Manispaa na Jiji
a) Halmashauri zitapokea miongozo mbalimbali ya uendeshaji na usimamizi wa elimu-
msingi, elimu ya sekondari ngazi ya juu na vyuo na kutoa elimu kwa watekelezaji
kuhusu miongozo hiyo;
b) Halmashauri zitahusika katika usimamizi na uendeshaji wa elimu na mafunzo wa
siku kwa siku katika shule za elimu-msingi, sekondari na vyuo na programu
nyingine katika eneo lake;
c) Ngazi hii itasimamia moja kwa moja uendeshaji wa shule za elimu - msingi na
sekondari ngazi ya juu zilizoko katika halmashauri hiyo na utoaji wa elimu katika
njia mbalimbali ikiwemo njia huria na masafa kwa watu wa rika mbalimbali;
d) Halmashauri itawajibika katika kupanga, kuratibu, kutekeleza, kutathmini na kutoa
taarifa ya utekelezaji wa sera kwa ngazi za mkoa na taifa; na
e) Halmashauri kuajiri watalamu mahiri wa elimu na mafunzo wenye uwezo na nyenzo
za kutekeleza majukumu hayo.
10.4 Ngazi ya Kata
a) Ngazi ya Kata itahusika na uratibu wa utekelezaji wa Sera ya Elimu na Mafunzo katika
ngazi hiyo;
b) Kata itawajibika katika kuratibu utekelezaji wa mipango ya shule za elimu- msingi,
sekondari ngazi ya juu na elimu kwa njia mbalimbali ikiwemo masafa na huria;
c) Utekelezaji wa majukumu ya elimu katika ngazi hii kufuatana na mfumo mpya wa
elimu utahitaji rasilimaliwatu iliyo elimika na yenye uwezo stahiki; na
d) Kupokea miongozo mbalimbali ya uendeshaji na utekelezaji wa sera ya elimu na
mafunzo na kuisambaza kwa walengwa ikiwemo mitaala.
10.5 Ngazi ya Shule na Chuo
a) Wakuu wa shule na vyuo watahusika katika usimamizi wa utekelezaji wa utoaji wa
elimu wa siku kwa siku katika taasisi zao;
b) Mkuu wa shule ya elimu - msingi na wa shule ya sekondari ngazi ya juu atasimamia na
kutekeleza Sera ya Elimu na Mafunzo katika shule na atawajibika kupanga, kusimamia
utekelezaji kwa kushirikiana na mamlaka ya kijiji/ mtaa na kutoa taarifa za utekelezaji
kwa Kata na Halmashauri; na
c) Mkuu wa chuo cha ualimu, chuo cha elimu ya ufundi, chuo cha mafunzo ya ufundi stadi
na chuo kikuu atapanga, atasimamia utekelezaji wa Sera ya Elimu na Mafunzo katika
chuo na kutoa taarifa za utekelezaji kwa mamlaka zilizo juu yake.
d) Wakuu wa shule na vyuo watakuwa na wajibu wa kuelimisha walimu na watendaji
wengine katika ngazi ya shule na vyuo kuhusu miongozo mbalimbali inayotolewa na
wizara ya elimu na mafunzo ikiwemo mitaala na mihtasari ya masomo.Aidha,
watatakiwa kuhakikisha wakati wote mitaala na mihtasari inafahamika kwa walimu na
walengwa wote kwenye shule na chuo husika.
47
SURA YA KUMI NA MOJA
11.0. UFUATILIAJI NA TATHMINI
Mkakati wa Ufuatiliaji na Tathmini ni nyenzo muhimu katika kuweka mfumo wa kujenga msingi
wa kutambua ufanisi katika utekelezaji wa Mkakati wa Sera ya Elimu na Mafunzo ambao ni wa
kipindi cha miaka 15. Mkakati huo unalenga kupata taarifa za utendaji na ufanisi katika maeneo
yote yaliyoainishwa kwenye Mkakati wa Sera kulingana na hatua mbalimbali za utekelezaji wa
malengo yaliyowekwa kwa ajili ya kufanya maamuzi muhimu kwa wakati muafaka
yatakayofanikisha malengo yaliyokusudiwa na Sera.
Serikali inatambua michango ya wadau mbalimbali katika ufuatiliaji na tathmini ya utekelezaji
wa malengo ya Sera zilizopo ingawa hakukuwa na uratibu rasmi wa ufuatiliaji na tathmini.
Wadau waliweza kutoa taarifa mbalimbali kuhusu hali ya elimu na mafunzo na taarifa hizo
zimesaidia sana katika mchakato wa kuandaa Sera mpya ya Elimu na Mafunzo na Mkakati wake.
Mafanikio na tija ya utekelezaji wa Sera inategemea kwa kiasi kikubwa jinsi Mkakati
utavyooanishwa na mifumo na taratibu mbalimbali zilizopo ndani ya taasisi zitakazotekeleza
Mkakati wa utekelezaji wa Sera kwa kutumia viashiria vinavyokubalika na wadau ambao ndio
watekelezaji. Kila mdau ataandaa Mpango wa Ufuatiliaji na Tathmini katika eneo lake kwa
kutumia Viashiria vinavyohusu upatikanaji wa mahitaji au rasilimali (Input Indicators);
mchakato wa utekelezaji (Process Indicators); kufanikisha utekelezaji (Output Indicators);
kuonekana kwa matokeo ya awali (Effects/Results Indicators) na kufikiwa kwa matokeo
yaliyokusudiwa (Impact Indicators). Mkakati huu unatambua na kuainisha Nafasi, majukumu na
wajibu wa kila mdau kuanzia ngazi ya Serikali Kuu hadi Mamlaka za Serikali za Mitaa, Sekta
Binafsi na Washirika wa Maendeleo.
48
Mfumo, miundo na taratibu nyumbufu za kumwezesha mtanzania kujiendeleza kwa njia mbalimbali katika mikondo ya kitaaluma na
kitaalamu.
MIKAKATI SHABAHA
KAZI/ SHUGHULI
VIASHIRIA VYA UFANISI NJIA YA KUHAKIKI WAHUSIKA
Lengo 1: Kuweka mfumo, miundo na taratibu nyumbufu katika elimu na mafunzo ilikuleta ulinganifu, muunganiko na ufanisi wa ngazi na fani
mbalimbali za kitaaluma na kitaalamu ili kumwezesha mwanafunzi kutoka mkondo mmoja kwenda mwingine.
1. Kuhuisha
mfumo wa elimu
na mafunzo
uliyopo sasa na
kuweka mfumo
mpya na
nyumbufu
utaomwezesha
mtanzania
kujiendeleza kwa
njia mbalimbali ili
kukidhi mahitaji
ya maendeleo ya
kitaifa, kikanda na
kimataifa.
1.1. Mfumo wa elimu
na mafunzo
nchini kuwa
nyumbufu ili
kumwezesha
mtanzania
kujiendeleza kwa
njia mbalimbali
katika mikondo
ya kitaaluma na
kitaalamu ifikapo
2018.
1.1.1. Kuhuisha
mfumo wa
elimu na
mafunzo.
1.1.2. Kuhuisha Sheria
na kanuni za
elimu na
mafunzo
a) Mfumo wa elimu na
mafunzo uliohuishwa.
b) Sheria ya elimu na
mafunzo iliyohuishwa
i. Waraka wa mfumo
wa elimu
ulioidhinishwa na
serikali.
ii. Sheria ya elimu na
mafunzo
iliyoidhinishwa na
Serikali.
Wizara zenye
dhamana na Elimu
na Mafunzo; Afya
na Ustawi wa
Jamii; Maendeleo
ya Jamii, Jinsia na
Watoto; Sheria na
Katiba;OWM-
TAMISEMI; Asasi
Zisizo za
Kiserikali; Ofisi
ya Mwanasheria
Mkuu
2. Kuweka Muundo
wa Tuzo wa
Taifa
unaozingatia
vigezo na
viwango vya
ubora wenye
kuleta
ulinganifu,
muunganiko
katika ngazi
zote za elimu na
mafunzo ya
kitaaluma na
2.1. Muundo wa tuzo
wa Elimu na
mafunzo wenye
kuleta ulinganifu,
muunganiko
unaomwezesha
mtanzania
kujiendeleza
kutoka mkondo
mmoja kwenda
mwingine kuwepo
na kuanza
kutumika ifikapo
2018.
2.1.1. Kuandaa muundo
tuzo wa kitaifa
wenye
muunganiko,
mchanganuo wa
vigezo na
viwango vya
ubora kuanzia
elimu ya awali
hadi elimu ya juu
pamoja na elimu
na mafunzo ya
kitaalamu.
a) Muundo wa tuzo wa
kitaifa ambao ni nyumbufu
wenye kuleta ulinganifu na
muunganiko.
i. Waraka wa
muundo wa Tuzo
wa kitaifa
ulioidhinishwa na
Serikali
Wizara zenye
dhamana na Elimu
na Mafunzo;
Viwanda na
Biashara; Vyombo
vya ithibati na
uthibiti wa ubora;
OWM-
TAMISEMI; Asasi
Zisizo za
Kiserikali; na
Wizara zote.
49
MIKAKATI SHABAHA
KAZI/ SHUGHULI
VIASHIRIA VYA UFANISI NJIA YA KUHAKIKI WAHUSIKA
kitaalamu. 2.1.2. Kutoa elimu kwa
umma kuhusu
muundo wa tuzo
wa taifa
a) Idadi ya programu za
kuelimisha umma
zilizoendeshwa kwa njia
mbalimbali kote nchini
i. Taarifa za
utekelezaji
2.1.3. Kutoa elimu na
mafunzo kwa
watekelezaji
kuhusu matumizi
ya muundo wa
tuzo wa taifa
a) Idadi ya watekelezaji
kutoka ngazi mbalimbali
za elimu na mafunzo
waliohudhuria za mafunzo
kuhusu muundo mpya wa
tuzo.
i. Taarifa ya
utekelezaji
Lengo Na. 2: Elimu ya Awali kuwa ya lazima na kutolewa kwa watoto wenye umri kati ya miaka mitatu hadi mitano kwa kipindi kisichopungua
mwaka mmoja.
1. Kuweka vigezo,
viwango na
utaratibu ili
elimu ya awali
iwe ya lazima
na itolewe
katika kila shule
ya Elimu –
Msingi.
1.1. Sheria, miongozo
na taratibu
kuruhusu elimu
ya awali kuwa ya
lazima kuwekwa
na kutekelezwa
ifikapo 2018
1.1.1. Kupitia na
kuweka sheria,
miongozo ili
kuruhusu elimu
ya awali kuwa ya
lazima na
kutolewa katika
shule zote za
Elimu-Msingi
a) Sheria na miongozo
iliyohuishwa kuhusu
elimu ya awali kutolewa
katika shule zote za
Elimu-Msingi
i. Nyaraka za Sheria
na miongozo
iliyopitishwa na
Serikali.
Wizara zenye
dhamana ya Elimu
na Mafunzo; OWM-
TAMISEMI; Wizara
yenye dhamana ya
Sheria na Katiba
1.2. Elimu ya Awali
kuanza kutolewa
kwa watoto wote
wa rika lengwa
ifikapo mwaka
2018
1.2.1. Kujenga na/ au
kuimarisha
miundombinu
inayokidhi elimu
ya awali katika
shule zote za
elimu – msingi
b) Idadi ya watoto wa rika
lengwa waliojiunga na
elimu ya awali
i. Takwimu za
udahili na
maendeleo
Wizara zenye
dhamana ya Elimu
na Mafunzo; Afya
na Ustawi wa Jamii;
Maendeleo ya Jamii,
Jinsia na Watoto;
Sheria na Katiba;
OWM-TAMISEMI;
Asasi Zisizo za
50
MIKAKATI SHABAHA
KAZI/ SHUGHULI
VIASHIRIA VYA UFANISI NJIA YA KUHAKIKI WAHUSIKA
Kiserikali; Ofisi ya
Mwanasheria Mkuu
Lengo Na 3: Elimu-Msingi kuwa ya lazima kuanzia darasa la kwanza hadi kidato cha nne; na kutolewa kwa miaka kumi na umri wa kuanza darasa
la kwanza kuwa kati ya miaka minne hadi sita kulingana na maendeleo na uwezo wa mtoto kumudu masomo katika ngazi husika.
1. Kuhuisha sheria
na taratibu ili
elimu - msingi
itolewe hadi
kidato cha nne.
1.1. Sheria na
Miongozo kuhusu
elimu - msingi
kuwekwa na
kutekelezwa
ifikapo 2016
1.1.1. Kuandaa sheria,
miongozo ya
uendeshaji wa
elimu-msingi
a) Sheria na miongozo
kuhusu elimu – msingi
iliyohuishwa
i. Nyaraka za sheria
na miongozo
Wizara zenye
dhamana ya Elimu
na Mafunzo; Afya
na Ustawi wa
Jamii; Maendeleo
ya Jamii, Jinsia na
Watoto; Sheria na
Katiba;
TAMISEMI; Asasi
Zisizo za
Kiserikali; Ofisi
ya Mwanasheria
Mkuu
1.2. Mpango wa
utekelezaji wa
utoaji wa elimu –
msingi kuwepo
ifikapo mwaka
2018
1.2.1. Kuandaa mpango
wa kuwezesha
utoaji wa elimu -
msingi
b) Idadi ya wanafunzi wa
rika lengwa waliojiunga na
elimu-msingi.
ii. Takwimu za udahili
na maendeleo
1.3. Elimu – msingi
kutolewa ifikapo
mwaka 2018
c) Idadi ya shule za elimu-
msingi
iii. Takwimu za elimu
Lengo Na 4 : Kuweka utaratibu ili kuhakikisha muda wa kukamilisha elimu na mafunzo katika ngazi mbalimbali za elimu baada ya Elimu - Msingi
unakuwa na tija na ufanisi.
1. Kuhuisha Sheria
na utaratibu wa
utoaji wa elimu
ya sekondari
ngazi ya juu
1.1. Sheria na taratibu
utoaji wa elimu
ya sekondari
ngazi ya juu
ifikapo mwaka
2017
1.1.1. Kuandaa
miongozo ya
utekelezaji wa
elimu ya
sekondari ngazi
ya juu
a) Miongozo ya utekelezaji
wa elimu ya sekondari
ngazi ya juu
i. Nyaraka za
miongozo
iliyoidhinishwa
Wizara zenye
dhamana ya Elimu
na Mafunzo; Afya
na Ustawi wa
Jamii; Maendeleo
ya Jamii, Jinsia na
Watoto; Viwanda
na Biashara; Sheria
na Katiba; OWM-
TAMISEMI; Asasi
Zisizo za
Kiserikali; Ofisi ya
1.2. Utaratibu wa
kuwaendeleza
wanafunzi
wanaofaulu elimu
msingi kuendelea
na Elimu ya
1.2.1. Kuandaa utaratibu
wa kuwezesha
wanaofaulu elimu
msingi kuendelea
na elimu ya
sekondari ngazi ya
b) Idadi ya wanafunzi
wanoendelea na elimu ya
sekondari ngazi ya juu
ii. Waraka kuhusu
utaratibu wa
kuendelea na
masomo katika
ngazi ya sekondari
51
MIKAKATI SHABAHA
KAZI/ SHUGHULI
VIASHIRIA VYA UFANISI NJIA YA KUHAKIKI WAHUSIKA
sekondari ngazi ya
juu au elimu ya
ufundi na mafunzo
ya ufundi stadi
ifikapo mwaka
2015
juu kwa miaka
miwili.
ya juu
uliyoidhinishwa na
Serikali
Mwanasheria
Mkuu, WAAJIRI
1.3. Udahili wa
wanafunzi wa
sekondari ngazi ya
juu kuongezeka
kutoka asilimia
5.2 mwaka 2012
hadi asilimia 40
ifikapo mwaka
2019
1.3.1. Kuandaa mpango
wa kuongeza
udahili wa
wanafunzi wa
elimu ya sekondari
ngazi ya juu
iii. Takwimu za elimu
na mafunzo
2. Kuimarisha vyuo
vya elimu ya juu
na mafunzo ya
ufundi stadi,
mafunzo ya
ualimu, elimu ya
ufundi, mafunzo
ya kitaalamu ili
viweze kutoa
elimu na
mafunzo
mbalimbali
kulingana na
mahitaji ya
maendeleo ya
taifa na soko la
ajira.
2.1 Sheria na kanuni
za matumizi ya
vyuo vya elimu ya
juu, mafunzo ya
ualimu, mafunzo
ya ufundi stadi,
elimu ya ufundi na
mafunzo ya
kitaaluma elimu na
mafunzo
kuhuishwa ifikapo
mwaka 2017
2.1.1 Kuhuisha sheria
na kanuni za
matumizi ya
vyuo vya elimu
ya juu, mafunzo
ya ualimu,
mafunzo ya
ufundi stadi,
elimu ya ufundi
na mafunzo ya
kitaaluma.
a) Sheria na kanuni za
matumizi ya vyuo vya
elimu ya juu, mafunzo ya
ualimu, mafunzo ya ufundi
stadi, elimu ya ufundi na
mafunzo ya kitaaluma vya
elimu na mafunzo
zilizohuishwa
i. Nyaraka za Sheria
na kanuni za
matumizi ya vyuo
vya elimu na
mafunzo
zilizoidhinishwa na
vyombo husika.
Wizara zenye
dhamana ya Elimu
na Mafunzo;
OWM-
TAMISEMI; Asasi
Zisizo za
Kiserikali; Ofisi ya
Mwanasheria
Mkuu; na
WIZARA ZOTE.
2.2 Utaratibu wa
kuwaendeleza
wanafunzi
wanaofaulu elimu
ya sekondari ngazi
ya juu kuendelea
na Elimu ya juu,
2.2.1 Kuandaa
utaratibu wa
kuwezesha
wahitimu elimu
ya sekondari
ngazi ya juu
kuendelea na
b) Idadi ya wanafunzi
wanoendelea na elimu ya
juu, mafunzo ya ualimu,
mafunzo ya ufundi stadi,
elimu ya ufundi na
mafunzo.
ii. Takwimu za
udahiliwa
wanafunzi katika
vyuo
52
MIKAKATI SHABAHA
KAZI/ SHUGHULI
VIASHIRIA VYA UFANISI NJIA YA KUHAKIKI WAHUSIKA
mafunzo ya
ualimu, mafunzo
ya ufundi stadi,
elimu ya ufundi na
mafunzo ya
kitaalam ifikapo
mwaka 2016
elimu ya juu,
mafunzo ya
ualimu mafunzo
ya ufundi stadi,
elimu ya ufundi
na mafunzo ya
kitaalam.
2.3 Utaratibu wa
matumizi fanisi
ya vyuo vya elimu
na mafunzo
kulingana na
miundo ya
mitaala mipya
kuandaliwa
ifikapo mwaka
2016
2.3.1 Kuandaa
utaratibu wa
matumizi fanisi
ya vyuo vya
elimu na mafunzo
kulingana na
miundo ya
mitaala mipya.
3. Kuweka
utaratibu wa
kuhakikisha
mafunzo
yanakamilika
kwa muda
stahiki katika
ngazi zote za
elimu na
mafunzo.
3.1 Fursa anuwai za
kuendelea na
masomo katika
ngazi mbalimbali
za elimu na
mafunzo
kuongezwa
ifikapo mwaka
2016.
3.1.1 Kuweka
mazingira
stahiki
kuwezesha
utekelezaji wa
miundo ya
mitaala
nyumbufu.
a) Idadi ya fursa anuwai za
kuendelea na masomo
katika ngazi mbalimbali
za elimu na mafunzo
i. Taarifa ya
utekelezaji
1.1. Idadi ya
wahitimu wa
katika ngazi
mbalimbali
kuongezeka
ifikapo mwaka
2020
1.1.1. Kuandaa
utaratibu wa
kuongeza fursa
za kuendelea na
masomo katika
ngazi
mbalimbali za
elimu na
b) Idadi ya wahitimu wa
katika ngazi mbalimbali
kuongezeka
ii. Taarifa ya
utelezaji
Wizara zenye
dhamana ya Elimu
na Mafunzo; OWM-
TAMISEMI; Asasi
Zisizo za Kiserikali;
Ofisi ya
Mwanasheria Mkuu;
na WIZARA ZOTE.
53
MIKAKATI SHABAHA
KAZI/ SHUGHULI
VIASHIRIA VYA UFANISI NJIA YA KUHAKIKI WAHUSIKA
mafunzo
1.2. Ujuzi mhitimu
alioupata katika
ngazi ya elimu
au programu ya
mafunzo
kutambuliwa
kwa ajili ya
kujiunga na
ngazi ya elimu
au programu
nyingine ifikapo
mwaka 2018
1.2.1. Kuandaa
utaratibu wa
kutambua ujuzi
wa mtu
alioupata katika
ulimwengu wa
kazi au sehemu
nyingine kwa
ajili ya
maendeleo yake
ya elimu na
mafunzo
c) Muda wa elimu na
mafunzo wenye ufanisi na
tija
iii. Nyaraka
zinazoonyesha
muda wa elimu
na mafunzo
1.3. Ujuzi ambao
mtu ameupata
katika
ulimwengu wa
kazi na
ujasiriamali
kubainishwa na
kutambuliwa
kwa ajili ya
kujiendeleza
kielimu na
kiujuzi ifikapo
mwaka 2018
1.3.1. Ujuzi mtu
alioupata katika
ulimwengu wa
kazi au sehemu
nyingine
kubainishwa na
kutambuliwa
kwa ajili ya
maendeleo yake
kielimu ifikapo
2016
d) Mfumo wa kutambua
ujuzi uliopatikana katika
ngazi nyingine ya
mafunzo, nje ya mfumo
rasmi na kazini
iv. Nyaraka
zinazoonyesha
mfumo wa
utambuzi
Wizara zenye
dhamana ya Elimu
na Mafunzo;
OWM-
TAMISEMI; Asasi
Zisizo za
Kiserikali; Ofisi
ya Mwanasheria
Mkuu; na
WIZARA ZOTE.
54
Elimu na mafunzo bora yenye viwango vinavyotambulika kikanda na kimataifa na yanayokidhi mahitaji ya sasa na ya baadaye ya taifa.
MIKAKATI SHABAHA KAZI/ SHUGHULI VIASHIRIA VYA UFANISI NJIA YA
KUHAKIKI
WAHUSIKA
Lengo Na 1: Kuimarisha ithibati na uthibiti wa ubora wa elimu na mafunzo katika ngazi zote ikiwemo masuala ya ushauri.
1. Kuimarisha
muundo wa
kitaasisi wa
ithibati na
uthibiti wa elimu
na mafunzo
katika ngazi
zote.
1.1. Chombo cha
ithibati na uthibiti
wa Elimu -
Msingi na
Sekondari ngazi
ya juu kuwepo
ifikapo mwaka
2018
1.1.1. Kupitia na kuhuisha
sheria, kanuni na
miongozo
inayosimamia ithibati
na uthibiti Elimu -
Msingi na Sekondari
ngazi ya juu
1.1.2. Kuunda chombo cha
ithibati na uthibiti wa
Elimu – Msingi na
Sekondari ngazi ya
juu
a) Sheria za vyombo vya
ithibati na uthibiti elimu
na mafunzo
zilizohuishwa.
i. Nyaraka za
Sheria za
chombo cha
ithibati na
uthibiti wa
elimu – msingi
na sekondari
ngazi ya juu
zilizoidhinishw
a na serikali.
Wizara zenye
dhamana ya Elimu
na Mafunzo, na
Sheria na Katiba.
1.2. Chombo cha
ithibati na uthibiti
wa Elimu na
Mafunzo ya
Ufundi Stadi na
Ujasiriamali
kuimarishwa
ifikapo mwaka
2019.
1.2.1. Kuhuisha sheria,
kanuni na
miongozo
inayosimamia
ithibati na uthibiti
wa elimu ya ufundi
stadi na
ujasiriamali
b) Viwango na vigezo vya
ubora wa elimu na
mafunzo katika ngazi zote
vilivyohuishwa
ii. Nyaraka za
Sheria za
vyombo vya
ithibati na
uthibiti
zilizoidhinishw
a na serikali.
Wizara yenye
dhamana ya Elimu
na Mafunzo;
Vyombo vya
Ithibati na Uthibiti.
1.3. Chombo cha
ithibati na uthibiti
wa Elimu ya
Ufundi
kuimarishwa
ifikapo mwaka
2019
1.3.1. Kupitia na
kuhuisha sheria,
kanuni na
miongozo
inayosimamia
ithibati na uthibiti
wa elimu ya ufundi
55
MIKAKATI SHABAHA KAZI/ SHUGHULI VIASHIRIA VYA UFANISI NJIA YA
KUHAKIKI
WAHUSIKA
1.4. Chombo cha
ithibati na uthibiti
wa Elimu ya Juu
Tanzania
kuimarishwa
ifikapo mwaka
2019
1.4.1. Kupitia na kuhuisha
sheria, kanuni na
miongozo
inayosimamia
ithibati na uthibiti
wa elimu ya juu
1.5. Chombo cha
uratibu, ithibati na
uthibiti wa
maendeleo ya
Sayansi,
Tekinolojia,
Utafiti na Ubunifu
Tanzania
kuimarishwa
ifikapo mwaka
2019
1.5.1. Kupitia na kuhuisha
sheria, kanuni na
miongozo
inayosimamia
ithibati na uthibiti
wa maendeleo ya
Sayansi,
Tekinolojia, Utafiti
na Ubunifu
1.6. Viwango na vigezo
vya ubora wa
elimu na mafunzo
vinavyotambulika
kikanda na
kimataifa kuwepo
ifikapo mwaka
2019.
1.6.1. Kuandaa viwango
na vigezo vya
ubora wa elimu na
mafunzo katika
ngazi zote
a) viwango na vigezo vya
ubora wa elimu na
mafunzo katika ngazi
zote
i. Nyaraka za
viwango na
vigezo vya
ubora wa elimu
na mafunzo
katika ngazi
zote
vilivyoidhinish
wa
1.7. Tekinolojia za
kisasa na za
kisayansi
kutumika katika
usimamizi, ithibati
na uthibiti kwa
ngazi zote za
elimu na mafunzo
1.7.1. Kubuni na kutumia
mbinu za kisasa za
ithibati na uthibiti
wa elimu na
mafunzo
b) Mbinu za kisasa
zinazotumika katika
ithibati na uthibiti
ii. Taarifa za
utekelezaji
56
MIKAKATI SHABAHA KAZI/ SHUGHULI VIASHIRIA VYA UFANISI NJIA YA
KUHAKIKI
WAHUSIKA
ifikapo mwaka
2019.
Lengo Na. 2: Kuimarisha ukuzaji, uboreshaji na utekelezaji wa mitaala kwa kuzingatia mahitaji ya taifa na ya walengwa katika ngazi zote za elimu
na mafunzo.
1. Kuhuisha
miundo ya
mitaala ya kitaifa
(National
Curriculum
Framework)
katika ngazi zote
za elimu na
mafunzo kwa
kuzingatia
umahiri
unaotarajiwa
katika kila ngazi
ya elimu na
mafunzo.
1.1. Muundo wa mtaala
wa kitaifa wa
elimu ya awali
kulingana na
muundo na tuzo
za elimu na
mafunzo
kuhuishwa ifikapo
mwaka 2016
1.2. Miongozo ya
ukuzaji,
utayarishaji,
utekelezaji na
uhuishaji wa
mitaala
kuimarishwa na
kutekelezwa
ifikapo mwaka
2016
1.2.1. Kuhuisha muundo
wa mtaala wa
kitaifa wa elimu ya
awali ili uendane na
muundo mpya na
tuzo za elimu na
mafunzo
1.2.2. Kutoa elimu kwa
umma na
watekelezaji
kuhusu muundo
mpya wa mtaala
wa elimu ya awali
a) Miundo ya mtaala ya
kitaifa ya elimu ya awali,
elimu- msingi na sekondari
ngazi ya juu iliyohuishwa
b) Idadi ya wataalamu
waliojengewa uwezo wa
kukuza na kutekeleza
mitaala.
i. Muhtasari na
nyaraka
mbalimbali
zinazoakisi
muundo mpya
wa mtaala wa
kitaifa wa
elimu ya awali
ulioidhinishwa
na chombo
husika
ii. Taarifa za
utekelezaji za
kila robo
mwaka na
mwaka.
Wizara yenye
dhamana ya
Elimu na
Mafunzo
pamoja na
WIZARA
ZOTE.
1.3. Muundo wa mtaala
wa kitaifa wa
elimu – msingi na
elimu ya
sekondari ngazi ya
juu kuhuishwa
kulingana na
muundo wa tuzo
ifikapo mwaka
2016
1.3.1. Kuhuisha muundo
na mitaala ya
kitaifa ya elimu-
msingi na
sekondari ngazi ya
juu
1.3.2. Kujenga uwezo wa
wakuza mitaala na
watekelezaji wa
mitaala kuhusu
muundo mpya wa
c) Idadi ya Programu za
kuelimisha umma kupitia
njia mbalimbali za
mawasiliano kuhusu
miundo mipya ya mitaala
ya kitaifa ya elimu ya
awali, elimu-msingi na
sekondari ngazi ya juu na
idadi ya waliohudhuria
iii. Mihtasari na
nyaraka
mbalimbali
zinazoakisi
miundo mipya
ya mitaala wa
kitaifa ya
elimu msingi
na sekondari
57
MIKAKATI SHABAHA KAZI/ SHUGHULI VIASHIRIA VYA UFANISI NJIA YA
KUHAKIKI
WAHUSIKA
mtaala wa kitaifa
wa elimu -msingi
na sekondari ngazi
ya juu
1.3.3. Kuelimisha umma
na watekelezaji wa
mitaala kuhusu
muundo mpya wa
mtaala wa kitaifa
wa elimu -msingi
na sekondari ngazi
ya juu
ngazi ya juu.
iv. Taarifa za
utekelezaji
1.4. Miundo ya mitaala
ya kitaifa katika
ngazi nyingine
kuhuishwa ili
iendane na
mabadiliko ya
muundo katika
elimu-msingi,
sekondari ngazi ya
juu na soko la
ajira ifikapo
mwaka 2016.
1.4.1. Kuhuisha miundo ya
mitaala ya kitaifa
katika ngazi nyingine
ili iendane na
mabadiliko ya
muundo katika
elimu-msingi,
sekondari na soko la
ajira
1.4.2. Kuelimisha umma
na kujenga uwezo
kwa watekelezaji wa
elimu na mafunzo
kuhusu misingi na
utekelezaji wa
muundo mpya wa
mitaala.
d) Miundo mipya ya mitaala
ya elimu na mafunzo
katika ngazi nyingine za
elimu na mafunzo
iliyohuishwa
e) Idadi ya programu ya
kuelimisha umma kupitia
njia mbalimbali za
mawasiliano, semina
elekezi kwa watekelezaji
na idadi ya waliohudhuria
v. Miundo ya
mitaala ya
elimu na
mafunzo
katika ngazi
nyingine
iliyoidhinishw
a na vyombo
husika.
vi. Taarifa ya
utekelezaji
kuhusu
programu za
elimu kwa
umma
i.
2. Kuhuisha na
kuimarisha
miongozo ya
ukuzaji,
utayarishaji,
2.1. Miongozo ya
ukuzaji,
utayarishaji,
utekelezaji na
uhuishaji wa
2.1.1. Kuandaa miongozo
ya ukuzaji
utayarishaji,
utekelezaji na
uhuishaji wa mitaala
a) Miongozo ya ukuzaji,
utayarishaji na utekelezaji
wa mitaala iliyopitishwa
kwa muda uliopangwa na
kwa kuzingatia mahitaji
i. Nyaraka za
ukuzaji,
utayarishaji na
utekelezaji wa
mitaala
58
MIKAKATI SHABAHA KAZI/ SHUGHULI VIASHIRIA VYA UFANISI NJIA YA
KUHAKIKI
WAHUSIKA
utekelezaji na
uhuishaji wa
mitaala kwa
kuzingatia
mahitaji ya taifa
na ya walengwa
katika ngazi zote
za elimu na
mafunzo
kulingana na
muundo wa tuzo
wa Taifa.
mitaala
kuimarishwa na
kutekelezwa
ifikapo mwaka
2016
kwa kuzingatia
mahitaji ya taifa na
ya walengwa katika
ngazi zote za elimu
na mafunzo
kulingana na
Muundo wa Tuzo wa
Taifa.
ya wakati. iliyoidhinishwa
na vyombo
husika.
ii. Nyaraka za
mitaala kuwepo
katika ngazi
zote za asasi za
elimu na
mafunzo
2.2. Mitaala kuhuishwa
kila baada ya
kipindi cha miaka
mitano au pale
uhuishaji huo
utakapohitajika
kwa sababu ya
mabadiliko
yanayosababisha
uhuishaji wa
mtaala ufanyike
ifikapo mwaka
2016.
2.2.1. Kuhuisha mitaala
itakayokuwa
imetumika kipindi
cha miaka 5
b) Idadi ya watekelezaji na
walengwa
waliosambaziwa mitaala.
Nyaraka za mitaala
iliyoidhinishwa.
2.3. Mitaala
kusambazwa
nchini na kutoa
elimu kwa umma,
watekelezaji na
walengwa wa
mitaala kufanyika
na kutekelezwa
ifikapo mwaka
2016
2.3.1. Kuandaa utaratibu
yakinifu wa
kusambaza Mitaala
ya kitaifa kwa ngazi
ya elimu msingi na
sekondari kwa
kuhusisha ofisi za
elimu mkoa, wilaya
na kata kwa umma
na watekelezaji.
i. Taarifa za
utekelezaji
katika ngazi
zote.
3. Kuhuisha
mitaala katika
ngazi zote za
3.1. Kuwa na mitaala
nyumbufu yenye
viwango
3.1.1. Kuhuisha mitaala
iliyopo na kuandaa
mitaala mipya
a) Mitaala iliyohuishwa na
kuandaliwa kulingana na
i. Nyaraka za
mitaala
zilizoidhinish
Wizara yenye
dhamana ya Elimu
na Mafunzo pamoja
59
MIKAKATI SHABAHA KAZI/ SHUGHULI VIASHIRIA VYA UFANISI NJIA YA
KUHAKIKI
WAHUSIKA
elimu na
mafunzo ili
iendane na
miundo mipya
ya mitaala ya
kitaifa
vinavyokubalika
kitaifa kikanda na
kimataifa ifikapo
mwaka 2016.
kulingana na mahitaji
ya taifa
mahitaji ya taifa wa na WIZARA ZOTE
4. Kuimarisha
mpango wa
upatikanaji wa
vitabu vya kiada
na ziada kwa
ngazi zote za
elimu na
mafunzo.
4.1. Vitabu vya
kutosha vya kiada
na ziada kwa ngazi
zote za elimu na
mafunzo kuwepo
katika shule na
vyuo ifikapo
mwaka 2020.
4.1.1. Kuhuisha mpango
wa upatikanaji wa
vitabu vya kiada na
ziada kwa ajili ya
ngazi zote za elimu
na mafunzo
4.1.2. Kuhamasisha
uandishi wa vitabu
kwa ngazi ya kitaifa
kwa ajili ya shule na
vyuo
a) Upatikanaji endelevu
wa Vitabu vya kiada
na ziada
vilivyobainishwa kwa
ajili ya ngazi zote za
elimu na mafunzo
i. Taarifa ya
uhakiki wa
vitabu kila
mwaka
katika
shule na
vyuo
5. Kuhuisha na
kuimarisha au
kuweka muundo
wa upimaji wa
kitaifa wa
maendeleo ya
mwanafunzi
katika kila ngazi
ya elimu na
mafunzo.
5.1. Muundo wa
upimaji wa
kitaifa wa
maendeleo ya
mwanafunzi kwa
kuzingatia
umahiri
kuandaliwa kwa
kila ngazi ya
elimu na
mafunzo ifikapo
mwaka 2016
5.1.1. Kuandaa muundo wa
upimaji wa kitaifa
wa maendeleo ya
mwanafunzi kwa
kuzingatia umahiri
wa stadi kwa kila
ngazi ya elimu na
mafunzo
a) Muundo wa upimaji wa
kitaifa wa maendeleo ya
mwanafunzi kwa
kuzingatia umahiri wa
stadi kwa kila ngazi ya
elimu na mafunzo
ulioandaliwa
i. Nyaraka za
muundo wa
upimaji wa
kitaifa wa
maendeleo ya
mwanafunzi
kwa kuzingatia
umahiri wa
stadi kwa kila
ngazi ya elimu
na mafunzo
ulioidhinishwa
na vyombo
husika.
5.2. Programu
rekebishi
itakayowezesha
kubaini uwezo,
5.2.1. Kuwabaini
wanafunzi wenye
uwezo na
kuwaendeleza, ngazi
b) Idadi ya wanafunzi wenye
kasi kubwa ya kujifunza,
vipawa na vipaji
walioendelezwa.
ii. Taarifa za
utekelezaji na
takwimu za
wanafunzi
60
MIKAKATI SHABAHA KAZI/ SHUGHULI VIASHIRIA VYA UFANISI NJIA YA
KUHAKIKI
WAHUSIKA
utayari na
kuwasaidia
wanafunzi
kuendelea na
masomo ngazi za
juu kuandaliwa
ifikapo mwaka
2016.
za juu za elimu na
mafunzo.
5.2.2. Kuwabaini
wanafunzi wenye
uwezo mdogo na
kuwaendeleza, ngazi
za juu kulingana na
uwezo wao.
c) Idadi ya wanafunzi wenye
kasi ndogo ya kujifunza
walioendelezwa.
walioendelezw
a.
6. Kujenga miundo
ya ulinganifu wa
programu
(benchmarking
of programs)
mbalimbali
kulingana na
mitaala kwa
mahitaji ya Taifa
pamoja na yale
ya ulimwengu
wa kazi,
utandawazi na
sehemu
nyingine.
6.1. Ulinganifu wa
masomo,
programu na
fani mbalimbali
za elimu na
mafunzo baada
ya elimu ya
sekondari
kuandaliwa
ifikapo mwaka
2016.
6.1.1. Kuandaa miongozo
ya ulinganifu wa
programu katika
ngazi zote baada ya
elimu ya sekondari
a) Miongozo ya ulinganifu
wa programu kulingana na
mahitaji ya kitaifa na
kimataifa
i. Nyaraka za
miongozo ya
ulinganifu
6.1.2. .Kufanya ulinganifu
wa programu katika
fani na ngazi
mbalimbali za
elimu na mafunzo
baada ya elimu ya
sekondari
b) Idadi ya programu
zilizofanyiwa ulinganifu.
ii. Taarifa ya
utekelezaji na
mihtasari ya
programu
zilizofanyiwa
ulinganifu.
Lengo Na 3: Kuimarisha usimamiaji na upimaji wa utekelezaji wa mitaala katika taasisi za elimu na mafunzo katika ngazi zote ili kuleta ufanisi wa
elimu na mafunzo yatolewayo.
1. Kuhuisha na
kuimarisha
vigezo, misingi
na utaratibu
yakinifu wa
kuhakiki,
kusimamia na
kupima
utekelezaji wa
mitaala katika
1.1. Miongozo ya
kuhakiki,
kusimamia na
kupima utekelezaji
wa mitaala katika
asasi za elimu na
mafunzo katika
ngazi zote
kuandaliwa na
kutumika ifikapo
1.1.1. Kuandaa miongozo
ya kuhakiki,
kusimamia na
kupima utekelezaji
wa mitaala katika
asasi za elimu na
mafunzo
a) Miundo na Miongozo ya
kuhakiki, kusimamia na
kupima utekelezaji wa
mitaala katika taasisi za
elimu na mafunzo
i. Nyaraka
zilizoidhinishw
a
Wizara yenye
dhamana ya Elimu
na Mafunzo;
OWM-
TAMISEMI;Vyom
bo vya Ithibati na
Uthibiti wa ubora
wa elimu; pamoja
na WIZARA
ZOTE
61
MIKAKATI SHABAHA KAZI/ SHUGHULI VIASHIRIA VYA UFANISI NJIA YA
KUHAKIKI
WAHUSIKA
taasisi za elimu
na mafunzo
katika ngazi
zote.
mwaka 2016.
1.2. Usimamizi fanisi
wa utekelezaji wa
mitaala kwa
kuhusisha ngazi
mbalimbali za
usimamizi wa
elimu na mafunzo
ifikapo mwaka
2015
1.2.1. Kuandaa utaratibu
utakaowezesha
usimamizi fanisi wa
utekelezaji wa
mitaala katika elimu
na mafunzo kwa
ngazi zote
b) Idadi ya wasimamizi na
watekelezaji mahiri wa
mitaala katika ngazi zote.
ii. Taarifa za
utendaji wa
wasimamizi
1.3. Wasimamizi na
watekelezaji
mahiri wa mitaala
katika asasi za
elimu na mafunzo
kuandaliwa
ifikapo mwaka
2016.
1.3.1. Kuajiri idadi ya
kutosha ya watendaji
katika ngazi zote za
elimu na mafunzo
kulingana na
miongozo
c) Idadi ya taasisi za elimu
na mafunzo zilizofanyiwa
tathmini ya utendaji kazi
iii. Takwimu
zinazoonyesha
idadi ya
wasimamizi na
watendaji
iv. Taarifa ya
utendaji kazi
Lengo Na 4: Kuimarisha ufundishaji, ujifunzaji wa lugha ili kuwa na wanafunzi mahiri wenye uwezo wa kuwasiliana kwa Kiswahili, Kiingereza na
lugha nyingine za kigeni katika mfumo wa elimu na mafunzo.
1. Kuweka,
kuendeleza na
kuimarisha
mbinu za
kufundisha na
kujifunza kwa
umahiri na
kuwasiliana kwa
ufasaha kwa
Kiswahili na
Kiingereza kwa
kutumia
wataalamu na
1.1. Kuwa na
wanafunzi
mahiri katika
kujifunza na
kuwasiliana kwa
Kiswahili na
Kiingereza
ifikapo mwaka
2016.
1.1.1. Kuandaa walimu
mahiri
watakaofundisha
Kiswahili na
kiingereza katika
ngazi mbalimbali
kulingana na
miongozo
1.1.2. Kuandaa utaratibu
wa kupata walimu
wa lugha ya
kiingereza kutoka
sehemu mbalimbali
a) Wanafunzi wenye umahiri
katika lugha za Kiswahili
na kiingereza
i. Taarifa za
ufuatiliaji wa
umahiri wa
wanafunzi na
wahitimu kila
miaka mitatu
Wizara zenye
dhamana ya Elimu
na Mafunzo; Habari,
Vijana, Utamaduni
na Michezo; na
Asasi zisizo za
Kiserikali;
62
MIKAKATI SHABAHA KAZI/ SHUGHULI VIASHIRIA VYA UFANISI NJIA YA
KUHAKIKI
WAHUSIKA
walimu mahiri. duniani
2. Kuweka
mazingira na
utaratibu
utakaowezesha
wanafunzi
walengwa
kujifunza lugha
nyingine za
kigeni na
kuwasiliana kwa
ufasaha.
2.1. Kuwa na
wanafunzi wenye
uwezo wa
kujifunza na
kuwasiliana kwa
lugha nyingine za
kigeni
zilizoidhinishwa
kutumika katika
Jumuiya ya Afrika
Mashariki, SADC
na Umoja wa
Afrika kwa
ufasaha ifikapo
mwaka 2016
2.1.1. Kuandaa walimu
mahiri
watakaofundisha
lugha za kigeni
zilizoidhinishwa
katika ngazi
mbalimbali za elimu
na mafunzo.
a) Sheria na Miongozo
inayowezesha kufundisha
na kujifunza lugha za
kigeni
ii. Taarifa za
utekelezaji wa
miongozo na
sheria
2.1.2. Kuandaa utaratibu
wa kupata walimu
wa lugha nyingine
kutoka sehemu
mbalimbali duniani
b) Idadi Walimu mahiri wa
kufundisha lugha
mbalimbali za kigeni kwa
ufasaha pamoja na stadi
za kuwasiliana.
iii. Takwimu za
walimu mahiri
wa lugha
2.1.3. Kuandaa mihtasari
ya lugha
zitakazofundishwa.
Lengo Na. 5
Kuwezesha lugha ya alama kutumika katika ngazi zote za elimu na mafunzo
1. Kuweka
mazingira na
utaratibu
utakaowezesha
kujifunza,
kufundishia na
1.1. Kuwa na
wanafunzi mahiri
katika kujifunza
na kuwasiliana
kwa lugha za
alama kwa
1.1.1. Kuweka miongozo
ambayo itawezesha
lugha za alama kuwa
ya lazima katika
elimu msingi
.
a) Miongozo inayowezesha
kufundisha na kujifunza
kwa lugha za alama
i. Taarifa za
utekelezaji wa
sheria miongozo
Wizara yenye
dhamana ya
Elimu na
Mafunzo;
Habari, Vijana,
Utamaduni na
63
MIKAKATI SHABAHA KAZI/ SHUGHULI VIASHIRIA VYA UFANISI NJIA YA
KUHAKIKI
WAHUSIKA
kuwasiliana kwa
kutumia lugha za
alama katika
ngazi zote za
elimu na
mafunzo.
ufasaha ifikapo
mwaka 2016.
1.1.2. Kuandaa walimu
mahiri
watakaofundisha za
lugha ya alama
katika ngazi
mbalimbali
kulingana na
miongozo
b) Idadi ya wanafunzi mahiri
katika kutumia lugha za
alama
ii. Taarifa za
ufuatiliaji wa
umahiri wa
wanafunzi na
wahitimu kila
miaka mitatu
Michezo; Asazi
za Lugha za
Kigeni;
1.1.3. Kuandaa utaratibu
wa kupata walimu
wa lugha za alama
kutoka sehemu
mbalimbali duniani
c) Idadi ya walimu mahiri
katika kufundisha na
kutumia lugha za alama
1.1.4. Kuandaa mihtasari
ya kufundushia lugha
za alama.
Lengo Na 3: Kuimarisha uthibiti wa programu, mitihani na tuzo za nje zinazotolewa nchini katika ngazi zote za elimu na mafunzo.
1. Kuhuisha sheria,
kanuni na
miongozo ya
ithibati na
uthibiti wa
programu na
mitihani ya nje
inayoendeshwa
nchini
1.1. Uratibu na uthibiti
wa Tuzo na Vyeti
vinavyotolewa na
vyuo vya ndani na
nje ya nchi kukidhi
mahitaji ya Mfumo
wa Tuzo wa Taifa
ifikapo mwaka
2016.
1.1.1. Kuandaa sheria,
kanuni na miongozo
ya ithibati na uthibiti
wa programu na
mitihani ya nje
inayoendeshwa
nchini
a) sheria, kanuni na
miongozo ya ithibati na
uthibiti wa programu na
mitihani ya nje
inayoendeshwa nchini
i. Nyaraka za
sheria, kanuni
na miongozo
ya ithibati na
uthibiti
iliyoidhinishwa
na vyombo
husika
Wizara zenye dhamana ya Elimu na Mafunzo; Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
64
Upatikanaji wa fursa mbalimbali za elimu na mafunzo nchini
MIKAKATI SHABAHA KAZI/ SHUGHULI VIASHIRIA VYA
UFANISI
NJIA YA
KUHAKIKI
WAHUSIKA
Lengo Na 1: Kuongeza fursa anuwai za elimu na mafunzo kwa usawa kwa makundi yote ya kijamii kwa ngazi zote.
1. Kuhuisha sheria, kanuni na
miongozo ya kuhakikisha
upatikanaji wa fursa za
elimu na mafunzo kwa
usawa kwa makundi yote
ya kijamii kwa ngazi zote.
1.1 Sheria, kanuni na
miongozo ya
kuhakikisha
upatikanaji wa fursa
za elimu na mafunzo
kwa usawa kwa
makundi yote ya
kijamii kwa ngazi
zote kuhuishwa na
kutumika ifikapo
mwaka 2016.
1.1.1. Kurekebisha na
kutunga sheria, kanuni
na miongozo ya
kuhakikisha
upatikanaji wa fursa za
elimu na mafunzo kwa
usawa kwa makundi
yote ya kijamii kwa
ngazi zote.
a) Sheria, kanuni na
miongozo ya
kuhakikisha
upatikanaji wa
fursa za elimu na
mafunzo kwa
usawa kwa
makundi yote ya
kijamii kwa ngazi
zote iliyoandaliwa.
Nyaraka za Sheria,
kanuni na miongozo
iliyoidhinishwa na
vyombo husika.
Wizara zenye
dhamana ya Elimu
na Mafunzo; Fedha;
OWM-TAMISEMI;
Asasi Zisizo za
Kiserikali;
WMM,WIZARA
NYINGINE
2. Kuimarisha na kuweka
utaratibu wa kuongeza, na
kutumia fursa za elimu na
mafunzo ya ndani na nje
ya nchi kwa makundi yote
ya kijamii kwa usawa
katika ngazi zote
2.1. Fursa za elimu na
mafunzo
zinapatikana na
kutumika kwa
usawa kwa makundi
yote ya kijamii
katika ngazi zote
ifikapo mwaka 2016
2.1.1. Kujenga na
kuongeza
miundombinu,
nyenzo, vifaa na
zana rafiki makundi
yote ya kijamii
katika ngazi
mbalimbali za elimu
na mafunzo
a) Miundombinu,
nyenzo, vifaa na
zana rafiki kwa
makundi yote ya
kijamii
Kuhakiki uwepo wa
miundo mbinu.
2.2. Programu za
maendeleo ya sekta
ya elimu na
mafunzo
zinazoongeza fursa
kutekelezwa kwa
ufanisi na tija
ifikapo mwaka 2016
2.2.1. Kutathmini programu
ya maendeleo ya
sekta ya elimu na
mafunzo ili kubaini
fursa zilizopo
zinazotumika kwa
usawa na maeneo
yanayohitaji
kuimarishwa
b) Idadi ya programu
za maendeleo
zinazoongeza fursa
sawa kwa makundi
yote ya jamii
Kuhakiki kuwepo
kwa programu na
taarifa za utekelezaji
65
MIKAKATI SHABAHA KAZI/ SHUGHULI VIASHIRIA VYA
UFANISI
NJIA YA
KUHAKIKI
WAHUSIKA
2.2.2. Kutumia fursa na
nafasi zilizopo kwa
ufanisi.
Wizara zenye
dhamana ya Elimu
na Mafunzo; Afya
na Ustawi wa
Jamii; Maendeleo
ya Jamii, Jinsia na
Watoto; na
WAUJ
2.2.3. Kuandaa mpango wa
kuongeza shule na
vyuo katika ngazi
mbalimbali za elimu
na mafunzo kwa
kuzingatia upatikanaji
fursa sawa kwa
makundi yote ya
kijamii.
c) Idadi ya shule na
vyuo
Taarifa za
utekelezaji na
kufanya uhakiki
2.2.4. Sekta binafsi
kushiriki
kikamilifu katika
kuongeza fursa
sawa za elimu na
mafunzo ifikapo
2016.
2.2.5. Kuandaa mpango wa
ushirikishaji wa sekta
binafsi katika
kuongeza fursa sawa
za elimu na mafunzo.
d) Idadi ya sekta
binafsi
zinazoshiriki
kikamilifu katika
kuongeza fursa
Taarifa za
utekelezaji na
kufanya uhakiki
Wizara yenye
dhamana ya Elimu
na Mafunzo; Ofisi
yenye Dhamana ya
Utumishi wa
Umma;Kazi na
Maendeleo ya
Vijana, Asasi Zisizo
za Kiserikali;
WIZARA
NYINGINE
3. Kuimarisha elimu na
mafunzo yanayoshirikisha
vyuo vya elimu ya ufundi
stadi, viwanda vya umma
na sekta binafsi
(Apprenticeship/uanagenzi
) ili kuongeza fursa na
ubora wa elimu na
mafunzo ya ufundi stadi
kwa usawa kwa makundi
yote ya kijamii.
3.1. Wanafunzi wa
uanagenzi wa fani
mbalimbali za
ufundi stadi
kupokelewa
viwandani ifikapo
2016.
3.1.1. Kuhuisha sheria na
miongozo ya
uanagenzi
(Apprenticeship) ili
kuongeza fursa na
ubora wa elimu na
mafunzo ya ufundi
stadi kwa usawa kwa
makundi yote.
a) Sheria na miongozo
ya uanagenzi
iliyohuishwa
i. Nyaraka na
miongozo ya
uanagenzi
iliyoidhinishwa
na chombo husika
Wizara yenye
dhamana ya Elimu ,
na Mafunzo; OWM-
TAMISEMI; Asasi
Zisizo za Kiserikali;
66
MIKAKATI SHABAHA KAZI/ SHUGHULI VIASHIRIA VYA
UFANISI
NJIA YA
KUHAKIKI
WAHUSIKA
3.1.2. Kuandaa utaratibu wa
kuwezesha viwanda
katika sekta za
uchumi kutoa fursa za
uanagenzi katika fani
mbalimbali kutoka
vyuo vya elimu ya
ufundi stadi
Wizara yenye
dhamana ya Elimu
na Mafunzo, AZAKI
4. Kuimarisha ushiriki wa
wadau mbalimbali katika
utoaji wa mafunzo tarajali
na mazoezi kwa vitendo
sehemu za kazi kwa
wanachuo
4.1. Wanachuo wanapata
fursa za mafunzo
tarajali na mazoezi
kwa vitendo katika
sehemu mbalimbali
za kazi ifikapo 2016
4.1.1. Kupitia na Kuandaa
sheria, kanuni na
miongozo kuhusu
ushiriki katika kutoa
mafunzo tarajali na
mazoezi kwa vitendo
kwa wanachuo
a) Wanachuo kupata
mafunzo tarajali
na mazoezi kwa
vitendo sehemu
za kazi.
i. Taarifa za
uhakiki kuhusu
mafunzo hayo
Wizara yenye
dhamana ya Elimu
na Mafunzo; Afya
na Ustawi wa Jamii;
Maendeleo ya Jamii,
Jinsia na
Watoto;OWM-
TAMISEMI
5. Kuimarisha utoaji wa
elimu na mafunzo kwa njia
huria na masafa
kuhakikisha inawafikia
watu wa rika na mahitaji
mbalimbali.
5.1. Elimu na mafunzo
yanayotolewa kwa
wanafunzi katika
ngazi mbalimbali
kwa njia Huria na
Masafa kulingana
viwango vya tuzo
husika yanapatikana
ifikapo 2016.
5.1.1. Kuandaa utaratibu na
kuhakikisha mfumo
wa kufundisha na
kujifunza kwa masafa
unatumika katika
ngazi zote za elimu
na mafunzo
a) Elimu na mafunzo
yanayotolewa kwa
njia huria na
masafa
yanayokidhi
viwango
b) Idadi ya programu
zilizofanyika
kuhamasisha umma
kuhusu elimu kwa
njia huria na
masafa
c) Idadi ya washiriki
katika programu za
elimu kwa njia
i. Taarifa za
ufuatiliaji wa
wanafunzi na
wahitimu kila
baada ya miaka 3.
ii. Taarifa ya
utekelezaji
Wizara yenye
dhamana ya Elimu
na Mafunzo;
Viwanda na
Biashara;
67
MIKAKATI SHABAHA KAZI/ SHUGHULI VIASHIRIA VYA
UFANISI
NJIA YA
KUHAKIKI
WAHUSIKA
huria na masafa
5.1.2. kuandaa na kuweka
teknolojia na
miundombinu stahiki
kwa ajili ya
kufundisha na
kujifunza kwa njia ya
masafa katika ngazi
zote za elimu na
mafunzo
Wizara yenye
dhamana ya Elimu
na Mafunzo; Afya
na Ustawi wa Jamii,
Maendeleo ya Jamii,
Jinsia na Watoto;
Mawasiliano
Sayansi na
Teknolojia; Habari,
Utamaduni na
Michezo, OWM-
TAMISEMI
NA WIZARA
NYINGINE
5.1.3. Kuandaa na kujenga
uwezo wa
rasilimaliwatu mahiri
kwa ajili ya
utekelezaji na
matumizi ya njia ya
masafa katika elimu
na mafunzo nchini
5.1.4. Kuhamasisha
ushirikiano baina ya
sekta ya umma na
binafsi katika kutoa
elimu na mafunzo
kwa njia masafa
5.1.5. Kuhamasisha jamii
kuhusu elimu na
mafunzo kwa njia
68
MIKAKATI SHABAHA KAZI/ SHUGHULI VIASHIRIA VYA
UFANISI
NJIA YA
KUHAKIKI
WAHUSIKA
masafa
5.1.6. Kuandaa na kuweka
huduma stahiki kwa
ajili ya walimu na
wanafunzi kuwezesha
utoaji fanisi wa elimu
na mafunzo kwa njia
masafa
Lengo Na. 2: Kuondoa vikwazo vinavyozuia fursa ya wanafunzi kuendelea na masomo na kukamilisha mzunguko wa elimu na mafunzo katika ngazi
husika.
1. Kuhuisha miongozo
kuhusu wanafunzi
kukamilisha mzunguko wa
elimu – msingi
1.1.Taratibu na
miongozo ya
kuwezesha
mwanafunzi
kukamilisha
mzunguko wa elimu
-msingi kuhuishwa
katika ngazi zote
ifikapo mwaka 2016
1.1.1. Kuandaa miongozo
itakayowezesha
wanafunzi
kukamilisha
mzunguko wa
elimu -msingi
a) Miongozo na
mipango ya
kuwarudisha katika
mfumo wa elimu
wanafunzi waliacha
masomo kutokana
na sababu
mbalimbali
i. Nyaraka za
miongozo
iliyopitishwa na
Serikali
Wizara yenye
dhamana ya Elimu
na Mafunzo;
1.2.Wanafunzi
wanaokamilisha
mzunguko wa elimu
msingi kuongezeka
ifikapo mwaka 2016
1.2.1. Kuweka utaratibu
wa wanafunzi
wanaokatisha
masomo yao ya
elimu msingi kwa
sababu mbalimbali
kupimwa ujuzi
walioupata na
kuwawezesha
kuendelea na elimu
na mafunzo katika
ngazi nyingine.
b) Idadi ya wanafunzi
waliorejea katika
mfumo wa elimu
i. Machapisho na
Takwimu
Wizara yenye
dhamana ya Elimu
na Mafunzo; Asasi
Za Kiraia.
2. Kuweka mpango maalumu
na taratibu
zitakazowezesha
2.1. Miongozo na
taratibu za
wanafunzi
2.1.1. Kuandaa miongozo
itakayowezesha
a) Idadi ya wanafunzi
waliokatiza
masomo
i. Takwimu za
wanafunzi
waliokatiza
Wizara yenye
dhamana ya Elimu
na Mafunzo; Asasi
69
MIKAKATI SHABAHA KAZI/ SHUGHULI VIASHIRIA VYA
UFANISI
NJIA YA
KUHAKIKI
WAHUSIKA
wanafunzi waliokatiza
masomo kutokana na
vikwazo na sababu
mbalimbali kuendelea na
masomo na/au kukamilisha
mzunguko husika.
waliokatiza
masomo kutokana
na vikwazo
mbalimbali
kuendelea na
masomo na/au
kukamilisha
mzunguko wa
elimu na mafunzo
husika kuwepo
ifikapo mwaka
2016.
wanafunzi
waliokatiza masomo
kutokana na vikwazo
na sababu
mbalimbali
kuendelea na
masomo na/au
kukamilisha
mzunguko wa elimu
na mafunzo husika.
kukamilisha
mzunguko wa
elimu na mafunzo
husika.
masomo na
baadae
kukamilisha
mzunguko wa
elimu na
mafunzo husika.
Za Kiraia.
2.2. Utambuzi wa
masomo aliyofaulu
mwanafunzi ili
kumwezesha
kuendelea na
masomo kwa ngazi
husika au ngazi
nyingine ifikapo
mwaka 2016
2.2.1. Kuandaa miongozo ya
kulimbikiza na
kutumia alama za
ufaulu katika masomo
ili kumwezesha
mwanafunzi
kukamilisha
mzunguko wa elimu
na mafunzo katika
ngazi husika au ngazi
nyingine
b) Mwanafunzi
kuendelea na
kumaliza
mzunguko wake
kwa kutambua
limbikizo alama za
ufaulu
ii. Takwimu za
wahitimu
waliokamilisha
mafunzo kwa
utaratibu wa
limbikizo la alama
za ufaulu.
Lengo Na.3
Kuweka utaratibu utakaowezesha maendeleo ya wanafunzi wenye vipaji, vipawa na kasi tofauti katika kujifunza kwa ngazi zote za elimu na mafunzo.
1. Kuweka utaratibu na
vigezo vya kuwatambua
mapema wanafunzi wenye
vipaji, vipawa na wenye
kasi ya kujifunza na
wengine wenye mahitaji
maalumu katika ngazi
mbalimbali za elimu na
1.1. Vipaji, vipawa na
kasi kujifunza ya
wanafunzi katika
ngazi mbalimbali za
elimu na mafunzo
kutambuliwa na
kukuzwa ifikapo
1.1.1. Kuandaa vigezo vya
kuwatambua
wanafunzi wenye
vipaji, vipawa na kasi
ya kujifunza
a) Idadi ya wanafunzi
wenye vipaji,
vipawa na wenye
kasi ya kujifunza
katika ngazi
mbalimbali za elimu
na mafunzo
kuongezeka.
i. Takwimu za
wanafunzi wenye
vipaji na kazi ya
kujifunza.
Wizara yenye
dhamana ya Elimu
na Mafunzo; Asasi
Za Kiraia; Afya na
Ustawi wa Jamii,
Maendeleo ya Jamii,
Jinsia na Watoto;
SHULE, VYUO
70
MIKAKATI SHABAHA KAZI/ SHUGHULI VIASHIRIA VYA
UFANISI
NJIA YA
KUHAKIKI
WAHUSIKA
mafunzo. mwaka 2016.
1.1.2. Kuwatambua na
kuwaendeleza
wanafunzi wenye
vipaji, vipawa na
wenye kasi ya
kujifunza katika ngazi
mbalimbali za elimu
na mafunzo
1.1.3. Kuandaa utaratibu
mahsusi wa
kuwahudumia na
kuwaendeleza
kielimu wanafunzi
wenye vipaji, vipawa
na wenye kasi ya
kujifunza na wenye
mahitaji maalumu
kulingana na mahitaji
yao.
1.1.4. Kuelimisha jamii
kuhusu utambuzi wa
wanafunzi wenye
vipaji na kasi
yakujifunza na
utaratibu wa
kuwaendeleza
Lengo Na. 4: Kuweka utaratibu na kuimarisha utambuzi wa viwango vya Elimu na mafunzo ili kutoa fursa ya kila Mtanzania kujiendeleza kielimu, WEMU,AZAKI,
71
MIKAKATI SHABAHA KAZI/ SHUGHULI VIASHIRIA VYA
UFANISI
NJIA YA
KUHAKIKI
WAHUSIKA
kupata maarifa na stadi za kazi kwa kuzingatia kwamba elimu au mafunzo hayana mwisho. WAMJ,WMJJW,SHUL
E, VYUO
4. Kuimarisha utaratibu wa
kuwa na vigezo vya
utambuzi wa uwezo na
umahiri wa mtu alioupata
akiwa nje ya mfumo wa
shule au chuo na kumpa
tuzo itakayomwezesha
kujiendeleza katika ngazi
mbalimbali za elimu na
mafunzo kulingana na
mahitaji yake au kupata
sifa ya kujiunga na fani
husika.
4.1. Vigezo vya utambuzi
wa uwezo na
umahuru wa mtu
alioupata nje ya
mfumo wa shule au
chuo kuwekwa
ifikapo mwaka 2016
4.2. Tuzo kwa watu
wenye ujuzi na
uzoefu mbalimbali
walioupata nje ya
mfumo wa shule au
chuo kutolewa
ifikapo 2016.
4.2.1. Kuandaa mpango wa
kutoa tuzo kwa watu
wenye ujuzi na
uzoefu mbalimbali
walioupata nje ya
mfumo wa elimu
a) Idadi ya watu
waliopata tuzo nje
ya mfumo wa elimu
i. Machapisho na
Takwimu.
Wizara yenye
dhamana ya Elimu
na Mafunzo;
Viwanda na
Biashara; SHULE,
VYUO;
4.3. Tuzo na umahiri
alioupata mtu akiwa
nje ya mfumo wa
shule au chuo
kutambulika ili
kumwezesha
kujiunga na
kujiendeleza katika
ngazi mbalimbali za
elimu na mafunzo
ifikapo mwaka 2016
4.3.1. Kuandaa utaratibu wa
kutambua umahiri na
kupima uwezo
kulingana na tuzo
kwa mtu mwenye
ujuzi na uzoefu
mbalimbali alioupata
nje ya mfumo rasmi
wa elimu ili
kumwezesha kujiunga
na kujiendeleza
katika ngazi
mbalimbali za elimu
na mafunzo
b) Idadi ya watu
waliojiendeleza
katika ngazi
mbalimbali za
elimu baada ya
kutambuliwa ujuzi
wao na kupata tuzo.
ii. Takwimu za
watu
waliojiendeleza
baada ya kupata
tuzo ya
kutambua
umahiri
uliopatikana nje
ya mfumo wa
elimu na
mafunzo.
Ongezeko la rasilimali mbalimbali kulingana na mahitaji katika ngazi zote za elimu na mafunzo.
72
MIKAKATI SHABAHA KAZI/ SHUGHULI VIASHIRIA VYA
UFANISI
NJIA YA
KUHAKIKI
WAHUSIKA
Lengo Na.1 :Kuimarisha mfumo wa ajira katika sekta ya elimu na mafunzo ili uwe mahsusi na kukidhi mahitaji, upatikanaji na usimamizi wa
rasilimaliwatu kwa ajili ya maendeleo ya sekta ya elimu na mafunzo.
1. Kuhuisha miundo ya
utumishi na utayarishaji,
ajira na maendeleo ya
walimu na wasimamizi
wa elimu na mafunzo kwa
ajili ya elimu ya awali,
elimu msingi na sekondari
ngazi ya juu.
1.1.Miundo ya utumishi
katika sekta ya elimu
na mafunzo ngazi ya
elimu ya awali, elimu
- msingi na sekondari
ngazi ya juu
kuhuishwa ifikapo
mwaka 2016.
1.1.1. Kuhuisha miundo
ya utumishi ya
walimu,
wasimamizi na
watendaji wengine
wa elimu na
mafunzo katika
ngazi ya elimu ya
awali, elimu
msingi na
sekondari ngazi ya
juu.
a) Miundo ya utumishi
wenye ufanisi na
tija katika sekta ya
elimu na mafunzo
ngazi ya elimu ya
awali, elimu
msingi na
sekondari ngazi ya
juu
i. Nyaraka za
miundo wa ajira
katika sekta ya
elimu na mafunzo
ngazi ya elimu ya
awali, elimu
msingi na
sekondari ngazi
ya juu
zilizoidhinishwa
ii. Tathimini ya
ufanisi na tija ya
miundo
Wizara yenye dhamana ya Elimu
na Mafunzo na
Maendeleo ya
Jamii, Jinsia na
Watoto, Ofisi
yenye Dhamana ya
Utumishi wa
Umma na Wizara
ya Fedha.
1.2.Miongozo, vigezo na
viwango vya elimu
na ujuzi wa walimu
na wasimamizi wa
elimu ya awali elimu
msingi na sekondari
ngazi ya juu
kuhuishwa ifikapo
mwaka 2016.
1.2.1. Kuandaa
miongozo, vigezo
na viwango vya
elimu na ujuzi wa
walimu na
wasimamizi wa
elimu ya awali
elimu msingi na
sekondari ngazi ya
juu
a) Miongozo, vigezo
na viwango vya
elimu na ujuzi wa
walimu na
wasimamizi wa
elimu ya awali elimu
msingi na sekondari
ngazi ya juu
Nyaraka za viwango
vya elimu
1.3.Uwiano wa mwalimu
kwa wanafunzi
katika elimu ya
awali kupungua
kutoka 1:124
mwaka 2012
kufikia 1:25 ifikapo
mwaka 2025.
1.3.1. Kuajiri walimu,
wasimamizi na
watendaji wengine
kwa kuzingatia
miongozo na
uwiano wa
mwalimu na
wanafunzi katika
elimu ya awali
b) Idadi ya walimu wa
shule za awali ili
kuwa na uwiano wa
mwalimu na
wanafunzi katika
elimu ya awali
kupungua kuwa
1:25.
Nyaraka
zinazoonyesha
takwimu za idadi ya
walimu na
wanafunzi.
73
MIKAKATI SHABAHA KAZI/ SHUGHULI VIASHIRIA VYA
UFANISI
NJIA YA
KUHAKIKI
WAHUSIKA
1.4.Walimu mahiri na
wenye uwezo wa
kufundisha elimu ya
awali kwa ufanisi na
ufasaha kupatikana
ifikapo mwaka 2018
1.4.1. Kuandaa mpango
wa kupima na
kuendeleza
walimu wa elimu
ya awali
c) Idadi ya walimu wa
shule za awali
waliopata mafunzo.
Taarifa za
utekelezaji
1.5.Wasimamizi wa
utekelezaji wa elimu
ya awali katika ngazi
mbalimbali za
uongozi katika elimu
ya awali kuwepo
ifikapo mwaka 2016
1.5.1. Kuandaa mpango
wa kupima na
kuendeleza
wasimamizi wa
elimu ya awali
d) Idadi ya wasimamizi
wa shule za awali
waliopata mafunzo.
Taarifa za
utekelezaji
Wizara yenye
dhamana ya Elimu
na Mafunzo, Ofisi
yenye Dhamana ya
Utumishi wa
Umma, Wizara ya
Fedha.
2. Kuhuisha miundo ya
utumishi na utayarishaji,
ajira na maendeleo ya
walimu na wasimamizi
wa Elimu na mafunzo
katika vyuo vya ufundi
stadi, vyuo vya ufundi,
vyuo vya ualimu na vyuo
vikuu (Ngazi mbalimbali
baada ya elimu –msingi).
2.1.Uwiano wa mwalimu
kwa wanafunzi
katika elimu –
msingi kuimarika
ifikapo mwaka
2025.
2.1.1. Kuajiri walimu,
wasimamizi na
watendaji wengine
kwa kuzingatia
miongozo na
uwiano wa
mwalimu na
wanafunzi katika
elimu –msingi
a) Idadi ya walimu wa
shule za elimu –
msingi ili kuwa na
uwiano wa
mwalimu na
wanafunzi katika
elimu –msingi
kupungua kuwa
1:25.
i. Nyaraka
zinazoonyesha
takwimu za
idadi ya walimu
na wanafunzi.
2.2.Walimu mahiri na
wenye uwezo wa
kufundisha elimu –
msingi kwa ufanisi na
ufasaha kupatikana
ifikapo mwaka 2018
2.2.1. Kuandaa mpango
wa kupima na
kuendeleza
walimu wa elimu –
msingi
b) Idadi ya walimu wa
shule za elimu –
msingi waliopata
mafunzo.
ii. Taarifa za
utekelezaji
2.3.Wasimamizi wa
utekelezaji wa elimu
ya awali na elimu-
msingi katika ngazi
mbalimbali za
uongozi kuwepo
2.3.1. Kuandaa mpango
wa kupima na
kuendeleza
wasimamizi wa
elimu –msingi
c) Idadi ya wasimamizi
wa shule za elimu –
msingi waliopata
mafunzo.
iii. Taarifa za
utekelezaji
Wizara yenye
dhamana ya Elimu
na Mafunzo;
OWM-
TAMISEMI; Asasi
Za Kiraia
74
MIKAKATI SHABAHA KAZI/ SHUGHULI VIASHIRIA VYA
UFANISI
NJIA YA
KUHAKIKI
WAHUSIKA
ifikapo mwaka 2016 ,
3. Kuhuisha miundo ya
utumishi na utayarishaji,
ajira na maendeleo ya
walimu na wasimamizi
wa elimu na mafunzo
katika vyuo vya ufundi
stadi, vyuo vya ufundi,
vyuo vya ualimu na vyuo
vikuu (ngazi mbalimbali
za elimu baada ya elimu
msingi)
3.1.Miundo ya utumishi
katika sekta ya
elimu na mafunzo
katika ngazi
mbalimbali baada
ya elimu – msingi
kuhuishwa ifikapo
mwaka 2016.
3.1.1. Kuhuisha miundo
ya utumishi ya
walimu/wakufunzi
/wahadhiri,
wasimamizi na
watendaji wengine
wa elimu na
mafunzo katika
ngazi mbalimbali
baada ya elimu –
msingi
a) Miundo ya utumishi
wenye ufanisi na
tija katika sekta ya
elimu na mafunzo
katika ngazi
mbalimbali baada
ya elimu – msingi
i. Nyaraka za
miundo wa ajira
katika sekta ya
elimu na
mafunzo katika
ngazi
mbalimbali
baada ya elimu –
msingi
zilizoidhinishwa
ii. Tathimini ya
ufanisi na tija ya
miundo
3.2.Miongozo, vigezo na
viwango vya elimu
na ujuzi wa
walimu/wakufunzi/w
ahadhiri na
wasimamizi wa
baada ya elimu-
msingi kuandaliwa
ifikapo 2016.
3.2.1. Kuandaa miongozo
ya viwango vya
elimu na ujuzi
stahiki wa
mwalimu/wakufunzi
/wahadhiri na
wasimamizi katika
elimu na mafunzo
baada ya elimu -
msingi
b) Muundo na mfumo
wa ajira ya walimu,
wakufunzi,
wahadhiri na
wasimamizi.
iii. Nyaraka za
muundo wa ajira
ya walimu,
wakufunzi,
wahadhiri na
wasimamizi
3.3. Idadi ya walimu,
wakufunzi
wahadhiri,
waendeshaji na
wasaidizi wengine
kuongezeka ifikapo
2025.
3.3.1. Kuajiri walimu
wakufunzi
wahadhiri,
waendeshaji na
wasaidizi wengine
kwa kuzingatia
miongozo na
mahitaji katika
ngazi mbalimbali
baada ya elimu –
c) Ongezeko la Idadi
ya walimu,
wakufunzi,
wahadhiri,
waendeshaji na
wasaidizi wengine.
iv. Nyaraka
zinazoonyesha
takwimu za idadi
ya walimu,
wakufunzi
wahadhiri,
waendeshaji na
wasaidizi
wengine.
Wizara zenye
dhamana ya Elimu
na Mafunzo;
Fedha; Maendeleo
ya Jamii, Jinsia na
Watoto; Mambo ya
Nje na Ushirikiano
wa Kimataifa;
Asasi Za Kiraia;
OWM-
TAMISEMI.
75
MIKAKATI SHABAHA KAZI/ SHUGHULI VIASHIRIA VYA
UFANISI
NJIA YA
KUHAKIKI
WAHUSIKA
msingi
3.4.Idadi ya walimu,
wakufunzi
wahadhiri,
waendeshaji na
wasaidizi wengine
kuendelezwa
kitaaluma na
kitaalamu ifikapo
2025
3.4.1. Kuandaa mpango wa
kupima na
kuendeleza walimu,
wakufunzi,
wahadhiri,
waendeshaji na
wasaidizi wengine
katika ngazi zote za
elimu na mafunzo
baada ya elimu –
msingi.
d) Idadi ya walimu,
wakufunzi
wahadhiri,
waendeshaji na
wasaidizi wengine
walioendelezwa
kitaaluma na
kitaalamu.
Wizara yenye
dhamana ya Elimu
na Mafunzo;
OWM-
TAMISEMI, Asasi
Za Kiraia;
4. Kuandaa utaratibu wa
kuongeza nafasi za
mafunzo ya ualimu,
mafunzo ya ukufunzi,
uhadhiri kukidhi
ongezeko la wanafunzi
katika ngazi zote za elimu
na mafunzo.
4.1.Mipango ya kuongeza
idadi ya walimu,
ukufunzi na
wahadhiri kukidhi
ongezeko la
wanafunzi katika
ngazi zote za elimu na
mafunzo kuandaliwa
ifikapo mwaka 2017.
4.1.1. Kuandaa mipango
ya kuongeza nafasi
za mafunzo ya
ualimu, ukufunzi na
uhadhiri katika
ngazi zote za elimu
na mafunzo
a) Ongezeko la nafasi
za mafunzo ya
ualimu, ukufunzi
na uhadhiri katika
ngazi zote za elimu
na mafunzo
i. Takwimu na
taarifa za
tathmini
Ofisi yenye
Dhamana ya
Utumishi wa
Umma;
Wizara yenye
dhamana ya Elimu
na Mafunzo.
LENGO 2: Kuweka mazingira bora na kuhakikisha kuwa sekta ya elimu na mafunzo inatoa rasilimaliwatu wa kutosha na mahiri kukidhi mahitaji ya
sekta mbalimbali kwa maendeleo ya Taifa.
1. Kuweka utaratibu wa
sekta ya elimu na
mafunzo kuandaa
rasilimaliwatu ya kutosha
yenye ujuzi na umahiri
unaotakiwa kwenye sekta
mbalimbali za uchumi.
1.1. Elimu na mafunzo
inayotolewa
kuendana na
mahitaji ya soko la
ajira
1.1.1. Kuandaa utaratibu
mahsusi wa kupata
taarifa kutoka
kwenye soko la ajira
Ongezeko la ajira kwa
wahitimu wa elimu na
mafunzo katika sekta
rasmi na isiyo rasmi
Taarifa za tathmini
za ufuatiliaji wa
wahitimu
2. Kuweka utaratibu wa 2.1. Kuwa na vyuo
maalumu
2.1.1. Kuandaa utaratibu
wa kuwa na vyuo
Idadi ya wataalamu Taarifa za tathmini
za ufuatiliaji wa
Wizara yenye
dhamana ya Elimu
76
MIKAKATI SHABAHA KAZI/ SHUGHULI VIASHIRIA VYA
UFANISI
NJIA YA
KUHAKIKI
WAHUSIKA
elimu na mafunzo kutoa
kipaumbele kwenye sekta
zinazokuwa haraka na
zinazojitokeza mfano
mafuta, gesi na madini ili
kuongeza rasilimaliwatu
wenye ujuzi na umahiri
unaotakiwa katika sekta
hizi kwa ngazi mbalimbali
za ajira.
vinavyotoa elimu na
mafunzo
yanayokidhi
mahitaji ya sekta
zinazokua haraka na
zinazoibuka ifikapo
2018
maalumu vinavyotoa
elimu na mafunzo
yanayokidhi mahitaji
ya sekta zinazokua
haraka na
zinazoibuka
katika sekta
zinazokuwa haraka na
zinazoibuka
wahitimu na Mafunzo; na
WIZARA ZOTE
3. Kuweka utaratibu wa
kutoa elimu na mafunzo
kwa ajili ya sekta zisizo
rasmi na kilimo ili
kulifanya taifa kukua
kutoka uchumi wa chini
kwenda wa kati
3.2 Vyuo vya ufundi stadi
vya Wilaya pamoja na
vyuo vya maendeleo
ya wananchi
kuongezwa na
kuimarishwa ifikapo
2019
3.2.1 Kutekeleza mpango
wa kuimarisha na
kuongeza vyuo vya
ufundi vya Wilaya
na vile vya
maendeleo ya
wananchi
a) Idadi ya vyuo
vyenye ubora
vinavyotoa elimu
na mafunzo kwa
ajili ya sekta isiyo
rasmi
i. Takwimu za
vyuo vinavyotoa
mafunzo kwa
ajili ya sekta
maalumu (sector
specific training
centres and
colleges)
Wizara yenye
dhamana ya Elimu
na Mafunzo;
Kilimo,chakula na
Ushirika; na
Utumishi wa
Umma
3.3 Vituo atamizi kwa ajili
ya kuandaa wahitimu
kujiajiri kuanzishwa
ifikapo 2017
3.3.1 Kuandaa utaratibu
wa kuwa na vituo
atamizi
vitakavyosaidia
kuandaa wahitimu
wa elimu na
mafunzo kujiajiri.
b) Idadi ya vituo
atamizi
ii. Takwimu za
vituo atamizi
Wizara yenye
dhamana ya Elimu
na Mafunzo;
Kilimo, Chakula na
Ushirika; na
Utumishi wa
Umma
Lengo Na.3: Kuweka utaratibu wa kuhakikisha uwepo wa miundombinu bora na stahiki ya kutosheleza mahitaji ya elimu na mafunzo katika ngazi zote WEMU, OWM-
TAMISEMI, OR-
MUU
1. Kuweka vigezo na
viwango vya
miundombinu ya shule za
elimu-msingi ili zikidhi
mahitaji ya elimu ya awali
1.1. Vigezo na viwango
vya miundombinu ya
shule za elimu-
msingi kuwepo
1.1.1. Kuandaa miongozo,
vigezo na viwango
vya miundombinu
kwa ajili ya shule za
a) Miongozo, vigezo
na viwango vya
miundombinu
katika ngazi ya
elimu ya awali,
Nyaraka za
miongozo, vigezo na
viwango vya
miundombinu
Wizara yenye
dhamana ya Elimu
na Mafunzo; Afya
na Ustawi wa
Jamii; Maendeleo
77
MIKAKATI SHABAHA KAZI/ SHUGHULI VIASHIRIA VYA
UFANISI
NJIA YA
KUHAKIKI
WAHUSIKA
na elimu - msingi. ifikapo mwaka 2016 elimu - msingi. elimu –msingi na
sekondari ngazi ya
juu
zilizoidhinishwa ya Jamii, Jinsia na
Watoto; Sheria na
Katiba;
TAMISEMI, Asasi
Za Kiraia; Ofisi
ya Mwanasheria
Mkuu
2. Kuimarisha na kujenga
miundombinu inayokidhi
mahitaji ya elimu ya awali
na elimu- msingi.
2.1 Miundombinu,
inayokidhi mahitaji
ya elimu ya awali na
elimu -msingi
ifikapo mwaka
2016.
2.1.1 Kubadilisha shule
16,331za elimu ya
msingi ili kutoa
elimu ya awali na
elimu – msingi.
2.1.2 Kujenga shule
mpya kwa ajili ya
elimu ya awali
elimu - msingi
ikijumuisha
a) Mfumo mpya wa
elimu- msingi
kutekelezwa katika
viwango
vilivyowekwa
b) Idadi ya shule za
elimu - msingi.
Taarifa na uhakiki
wa utekelezaji wa
elimu msingi
Wizara yenye
dhamana ya Elimu
na Mafunzo , Afya
na Ustawi wa
Jamii; Maendeleo
ya Jamii, Jinsia na
Watoto, Ujenzi,
Mawasiliano
Sayansi na
Teknolojia,
Mawasiliano na
uchukuzi, Mambo
ya Nje, Nishati na
Madini OWM-
TAMISEMI, Asasi
Za Kiraia,
3. Kuimarisha na kujenga
miundombinu inayokidhi
mahitaji ya elimu ya
sekondari ngazi ya juu
3.4 Shule za elimu ya
sekondari ngazi ya
juu za kutosha zenye
miundombinu
inayokidhi mahitaji
kuwepo ifikapo
mwaka 2019.
3.5 Kuandaa utaratibu wa
kutumia baadhi ya
shule za Sekondari
ngazi ya kawaida
kutoa masomo ya
sekondari ngazi ya
juu
a) Idadi ya shule za
sekondari ngazi ya
kawaida zinazotoa
masomo ya elimu
ya sekondari ngazi
ya juu
Takwimu za elimu
msingi na elimu ya
sekondari ngazi ya
juu
Wizara yenye
dhamana ya
Elimu, Ujenzi,
Asasi Za Kiraia
4. Kuweka vigezo na
viwango vya
miundombinu inayokidhi
mahitaji ya Vyuo vya
ufundi stadi, vyuo vya
ufundi, vyuo vya ualimu
4.1 Vigezo na viwango
vya miundombinu ya
asasi za elimu na
mafunzo katika
ngazi mbalimbali
baada ya elimu –
4.1.1 Kuhuisha miongozo,
vigezo na viwango vya
miundombinu kwa ajili ya
asasi za elimu na mafunzo
katika ngazi mbalimbali
baada ya elimu – msingi
a) Miongozo, vigezo na
viwango vya
miundombinu
baada ya elimu -
msingi
Nyaraka za
miongozo, vigezo na
viwango vya
miundombinu
zilizoidhinishwa
Wizara yenye
dhamana ya Elimu
na
Mafunzo,Ujenzi,
TAMISEMI,
Fedha.
78
MIKAKATI SHABAHA KAZI/ SHUGHULI VIASHIRIA VYA
UFANISI
NJIA YA
KUHAKIKI
WAHUSIKA
na vyuo vikuu (ngazi
mbalimbali baada ya
elimu – msingi)
msingi kuwepo
ifikapo mwaka 2016
5. Kuimarisha na kujenga
miundombinu inayokidhi
mahitaji ya Vyuo vya
ufundi stadi, vyuo vya
ufundi, vyuo vya ualimu
na vyuo vikuu (ngazi
mbalimbali baada ya
elimu – msingi)
1.1. Vyuo vya ufundi stadi,
vyuo vya ufundi,
vyuo vya ualimu na
vyuo vikuu kuwa na
miundombinu
inayokidhi mahitaji
na ongezeko la
udahili kuwepo
ifikapo mwaka 2019.
1.1.1. Kujenga na
kuimarisha
miundombinu katika
vyuo vya ufundi
stadi, vyuo vya
ufundi, vyuo vya
ualimu na vyuo
vikuu
a) Idadi ya vyuo
vyenye
miundombinu bora
Takwimu
zinazoonyesha idadi
ya vyuo vyenye
miundombinu bora
Wizara yenye
dhamana ya Elimu
na Mafunzo,
TAMISEMI, WUJ,
WF
1.1.2. Kuandaa mpango wa
kitaifa wa kujenga
vyuo vipya katika
maeneo mbalimbali
nchini
Wizara yenye
dhamana ya Elimu
na Mafunzo,
WIZARA ZOTE
6. Kujenga utamaduni wa
utunzaji, usimamizi,
ukarabati na ukarafati wa
miundombinu ya asasi za
elimu na mafunzo.
3.6 .Miongozo ya
usimamizi, utunzaji,
ukarabati na
ukarafati wa
miundombinu
kuwepo ifikapo
mwaka 2016
3.6.1 Kuandaa miongozo
ya utunzaji,
usimamizi, ukarabati
na ukarafati wa
miundombinu.
a) Sheria, kanuni na
miongozo ya
utunzaji, ukarabati
na ukarafati wa
miundombinu.
b) Miundombinu
yenye ubora stahiki
i. Nyaraka za
sheria, kanuni
na miongozo
iloyoidhinishwa
ii. Taarifa ya
tathmini ya
utekelezaji
Wizara yenye
dhamana ya
Elimu na
Mafunzo , OWM-
TAMISEMI na
Asasi Za Kiraia,
3.6.2 Kuhamasisha
uongozi na jamii
inayozunguka shule,
wazazi na wadau
wengine kuhusu
utunzaji, usimamizi,
ukarabati, ukafati wa
miundombinu.
Lengo Na 4:
Kuweka utaratibu wa kuhakikisha vifaa, nyenzo na zana stahiki za kufundishia na kujifunzia katika elimu na mafunzo
79
MIKAKATI SHABAHA KAZI/ SHUGHULI VIASHIRIA VYA
UFANISI
NJIA YA
KUHAKIKI
WAHUSIKA
zinatosheleza kulingana na mahitaji na maendeleo ya sayansi, tekinolojia na mbinu za kufundishia na kujifunzia katika ngazi zote.
1. Kuhuisha viwango vya
ubora wa nyenzo, vifaa na
zana za kufundishia na
kujifunzia ili kuleta usawa
katika upatikanaji wa
elimu na mafunzo katika
shule na vyuo ngazi zote.
1.1. Miongozo ya ubora
wa nyenzo, vifaa na
zana katika shule na
vyuo vya elimu na
mafunzo katika ngazi
zote kutolewa na
kusambazwa ifikapo
mwaka 2016.
1.1.1. Kuandaa miongozo
ya ubora wa nyenzo,
vifaa na zana katika
shule na vyuo vya
Elimu na mafunzo
katika ngazi zote
a) Miongozo ya
viwango vya
msingi vya ubora
kati ya shule na
vyuo vya elimu na
mafunzo vya
serikali na vya
binafsi.katika ngazi
zote.
i. Nyaraka za
miongozo
iliyoidhinishwa
Wizara yenye
dhamana ya
Elimu na
Mafunzo, OWM-
TAMISEMI, na
Asasi Za Kiraia,
2. Kuweka utaratibu yakinifu
wa upatikanaji wa vifaa,
nyenzo,na zana za
kufundishia na kujifunzia
katika shule na vyuo vya
elimu na mafunzo katika
ngazi zote
2.1 Shule na vyuo vya
elimu na mafunzo
katika ngazi zote
zenye vifaa,
nyenzo,na zana za
kufundishia na
kujifunzia kulingana
na viwango
vilivyowekwa ifikapo
mwaka 2025
2.2 Kuandaa mpango
mahsusi wa
kuhakikisha shule na
vyuo vya elimu na
mafunzo katika ngazi
zote zina vifaa,
nyenzo,na zana
kufundishia na
kujifunzia kulingana
na viwango
vilivyowekwa.
a) Idadi ya
vifaa,nyenzo, na
zana za
kufundishia na
kujifunzia katika
shule na vyuo vya
elimu na mafunzo
katika ngazi zote
Wizara yenye
dhamana ya
Elimu na
Mafunzo, OWM-
TAMISEMI,
Asasi Za Kiraia.
3. Kujenga utamaduni wa
utunzaji, usimamizi,
ukarabati wa vifaa,
nyenzo,na zana za
kufundishia na kujifunzia.
Mafunzo.
2.1. Miongozo ya
usimamizi, utunzaji,
ukarabati wa vifaa,
nyenzo na zana
kuwepo ifikapo
mwaka 2016
2.1.1. Kuandaa miongozo
ya utunzaji,
usimamizi, ukarabati
wa vifaa, nyenzo,na
zana za kufundishia
na kujifunzia.
a) Sheria, kanuni na
miongozo ya
utunzaji, ukarabati
wa nyenzo,na zana
za kufundishia na
kujifunzia.
i. Nyaraka za
sheria, kanuni
na miongozo
iloyoidhinishwa
ii. Taarifa ya
tathmini ya
utekelezaji
Wizara yenye
dhamana ya Elimu
na Mafunzo,
OWM-
TAMISEMI, Asasi
Za Kiraia,
Lengo Na 5:
Kuweka utaratibu wa kuwezesha lugha ya Kiswahili na Kiingereza kuwa lugha za kufundishia na kujifunzia katika ngazi zote za elimu na mafunzo
1. Kuweka utaratibu
utakaowezesha lugha ya
1.1.Vifaa, nyenzo na zana
za kufundisha na
1.1.1. Kufanya tathmini ya
kitaifa ya hali
a) Sheria, kanuni na
Miongozo ya lugha
Nyaraka za
miongozo inayohusu
Wizara yenye
dhamana ya Elimu
80
MIKAKATI SHABAHA KAZI/ SHUGHULI VIASHIRIA VYA
UFANISI
NJIA YA
KUHAKIKI
WAHUSIKA
Kiswahili kutumika
kufundishia katika ngazi
zote za elimu na mafunzo.
kujifunza kwa
umahiri kwa
kutumia lugha ya
Kiswahili kuwepo
ifikapo mwaka
2025
halisi ya mahitaji
ya miundombinu,
nyenzo, vifaa na
zana za
kufundishia na
kujifunzia lugha ya
Kiswahili.
ya kiswahili
kutumika
kufundishia.
matumizi ya
Kiswahili
na Mafunzo,
OWM-
TAMISEMI,
1.2.Vitabu kutafsiriwa au
kuandikwa kwa
lugha ya Kiswahili
kwa masomo
mbalimbali ifikapo
mwaka 2018
1.2.1. Kuandaa programu
ya lugha ya
Kiswahili
kutumika katika
kufundishia kwa
ngazi zote za
elimu na mafunzo
b) Lugha ya Kiswahili
kutumika
kufundishia
Taarifa ya tathmini
ya matumizi ya
lugha ya Kiswahili
katika shule na vyuo
Wizara yenye
dhamana ya
Elimu na
Mafunzo, OWM-
TAMISEMI,
Utamaduni Asasi
Za Kiraia,
1.3.Maktaba kuimarishwa
kwa vitabu na
maandiko mengine
ya kiswahili ifikapo
mwaka 2019
1.3.1. Kuweka mpango wa
upatikanaji wa
vitabu na
maandiko mengine
kwa lugha ya
kiswahili
c) Vitabu kutafsiriwa
au kuandikwa kwa
lugha ya Kiswahili
Vitabu na nyenzo
nyingine za
kufundishia kwa
lugha ya Kiswahili.
Wizara yenye
dhamana ya Elimu
na Mafunzo,
TAMISEMI,
WAANDISHI
WA VITABU
1.4. Maabara zenye
kuwezesha
ufundishaji na
ujifunzaji wa lugha
ya Kiswahili
kuwepo kwenye
shule na vyuo
nchini ifikapo
mwaka 2019
Kuandaa mpango wa
kuwezesha ujenzi wa
maabara za lugha katika
shule na vyuo
d) Andiko la programu
ya kuwezesha
ujenzi wa maabara
za lugha katika
shule na vyuo
vilivyoidhinishwa
na Serikali
Waraka wa
Programu na taarifa
za utekelezaji
Wizara yenye
dhamana ya Elimu
na Mafunzo,
OWM-
TAMISEMI na
Utamaduni
2. Kuweka utaratibu
utakaowezesha lugha ya
Kiingereza kama lugha ya
mawasiliano kikanda na
kimataifa kufundishwa
2.1. Vifaa, nyenzo na zana
za kufundishia na
kujifunzia kwa
umahiri kwa kutumia
lugha ya Kiswahili
2.1.1. Kufanya tathmini
ya kitaifa ya hali
halisi ya mahitaji
ya miundombinu,
nyenzo, vifaa na
a) Miongozo ya
kujifunza lugha ya
Kiingereza.
Nyaraka za
miongozo
Wizara yenye
dhamana ya
Elimu na
Mafunzo, OWM-
81
MIKAKATI SHABAHA KAZI/ SHUGHULI VIASHIRIA VYA
UFANISI
NJIA YA
KUHAKIKI
WAHUSIKA
kwa ufasaha katika ngazi
zote za elimu na mafunzo.
kuwepo ifikapo
mwaka 2018
zana za kujifunzia
lugha ya
Kiingereza.
TAMISEMI,
2.2. Maktaba kuimarishwa
kwa vitabu na
maandiko mengine ya
kiingereza ifikapo
mwaka 2017
2.2.1. .Kuandaa Mpango
wa kufundisha
lugha ya
Kiingereza
b) Andiko la Mpango
wa kufundisha
lugha ya kiingereza
lililoidhinishwa na
na Serikali
Waraka wa mpango
na taarifa za
utekelezaji
Wizara yenye
dhamana ya
Elimu na
Mafunzo, OWM-
TAMISEMI,
2.3. Maabara za lugha ya
kiingereza kuwepo
kwenye shule na vyuo
nchini ifikapo mwaka
2016
Kuandaa mpango wa
kuwezesha upatikanaji
wa vifaa vya maabara za
lugha katika shule na
vyuo
e) Andiko la mpango
wa kuwezesha
upatikanaji wa
vifaa vya maabara
za lugha katika
shule na vyuo
lililoidhinishwa na
Serikali
Waraka wa
Programu na taarifa
za utekelezaji
Wizara yenye
dhamana ya
Elimu na
Mafunzo, OWM-
TAMISEMI,
Utamaduni
3. Kuimarisha kujifunza na
kufundisha lugha
mbalimbali za kigeni
katika ngazi mbalimbali
za elimu na mafunzo
3.1. Vifaa, nyenzo na zana
za kufundishia na
kujifunzia kwa
umahiri lugha za
kigeni kuwepo ifikapo
mwaka 2016
3.1.1. Kufanya tathmini ya
kitaifa ya hali halisi
ya miundombinu,
nyenzo, vifaa na
zana kwa ajili ya
kujifunza na
kufundisha lugha
nyingine za kigeni
a) Idadi ya walimu wa
lugha za kigeni,
nyenzo, vifaa na
zana zinazotumika
kujifunza lugha za
kigeni
Nyaraka za takwimu Wizara yenye
dhamana ya
Elimu na
Mafunzo, OWM-
TAMISEMI,
Utamaduni
3.1.2. .Kuandaa programu
za kufundisha lugha
za kigeni katika
elimu na mafunzo
b) Andiko la programu
za kufundisha lugha
zingine za kigeni
lililoidhinishwa na
Serikali
Waraka wa
Programu na taarifa
za utekelezaji
Wizara yenye
dhamana ya
Elimu na
Mafunzo, OWM-
TAMISEMI,
Utamaduni Asasi
za Kiraia.
Lengo Na.6: Kuweka utaratibu na mazingira wezeshi ya kuhakikisha elimu na mafunzo katika ngazi zote inatolewa kwa ufanisi kwa njia huria na
masafa.
82
MIKAKATI SHABAHA KAZI/ SHUGHULI VIASHIRIA VYA
UFANISI
NJIA YA
KUHAKIKI
WAHUSIKA
1. Kuimarisha njia za utoaji
wa elimu na mafunzo
zikiwemo huria na masafa
ili kuwawezesha
Watanzania wengi
kujiendeleza kielimu bila
vikwazo.
1.1.Rasilimaliwatu
wanaosimamia na
wanaotekeleza Elimu
na mafunzo huria na
masafa kuea
wamejengewa uwezo
ifikapo mwaka 20125
1.1.1. Kufanya tathmini ya
kitaifa ya hali halisi
ya mahitaji
rasilimaliwatu,
miundombinu,
nyenzo, vifaa na
zana kwa ajili ya
kutoa elimu na
mafunzo kwa njia
huria na masafa
katika ngazi
mbalimbali za elimu
na mafunzo
a) Idadi na aina ya
programu za elimu
na mafunzo kwa
njia huria na
masafa
Nyaraka za taarifa
na takwimu
Wizara yenye
dhamana ya Elimu
na Mafunzo,
Menejimenti ya
Utumishi wa
Umma.
1.2.Miundombinu, vifaa,
nyenzo na zana kwa
ajili ya elimu na
mafunzo kwa njia
huria na masafa
kuwepo ifikapo
mwaka 2020
1.2.1. Kuweka programu
rekebishi ili
kuimarisha
rasilimaliwatu,
miundombinu,
nyenzo, vifaa na
zana kwa ajili ya
kujifunza na
kufundisha kwa njia
huria na masafa
b) Programu rekebishi
za kuimarisha
utoaji wa elimu na
mafunzo kwa njia
huria na masafa
Nyaraka za
programu na taarifa
ya utekelezaji wa
programu
Wizara yenye
dhamana ya
Elimu na
Mafunzo, OWM-
TAMISEMI,
Asasi zisizo za
Serikali
2. Kuhakikisha taasisi zote
zinazotoa elimu na
mafunzo kwa njia huria
na masafa
zimeunganishwa katika
mkongo wa taifa na kwa
njia nyingine za kisasa.
2.1. Kuhakikisha taasisi
zote zinazotoa elimu
na mafunzo kwa njia
ya huria na masafa
zimeunganishwa
katika mkongo wa
Taifa na kwa njia
nyingine za kisasa
ifikapo mwaka 2019
2.1.1. Kuweka programu
ya kitaifa ya
kuunganisha asasi
zinazotoa elimu na
mafunzo katika
mkongo wa Taifa.
a) Idadi ya Taasisi za
elimu na mafunzo
zilizounganishwa
kwenye mkongo
wa taifa
Orodha ya taasisi za
elimu zenye mkongo
wa taifa
Wizara yenye
dhamana ya
Elimu na
Mafunzo, OWM-
TAMISEMI,
Asasi zisizo za
Serikali
3. Kuimarisha uhusiano kati
ya sekta ya umma na
binafsi ili kuleta tija na
3.1. Huduma bora kupitia
elimu kwa njia huria
na masafa
3.1.1. Kuandaa mpango wa
ushirikiano baina ya
sekta ya umma na
a) Idadi ya mikataba ya
ushirikiano baina
ya sekta binafsi
Taarifa, Miakataba
na takwimu za
ushiriki wa sekta
Wizara yenye
dhamana ya
Elimu na
83
MIKAKATI SHABAHA KAZI/ SHUGHULI VIASHIRIA VYA
UFANISI
NJIA YA
KUHAKIKI
WAHUSIKA
ufanisi katika utoaji wa
elimu kwa njia huria na
masafa
kupatikana nchi
nzima ifikapo
mwaka 2020
binafsi katika
masuala ya
Rasilimaliwatu,
Miundombinu, vifaa,
nyenzo na zana za
kujifunzia na
kufundishia katika
ngazi mbalimbali za
elimu na mafunzo
zinazoshiriki kutoa
wa elimu kwa njia
huria na masafa
binafsi Mafunzo, OWM-
TAMISEMI,
Asasi zisizo za
Serikali
Lengo Na.7: Kuhakikisha kila taasisi ya elimu na mafunzo inakuwa na hatimiliki ya ardhi mahali ilipo taasisi hiyo kwa ngazi zote.
1. Kuwezesha upatikanaji
wa ardhi na hati miliki ya
ardhi kwa taasisi za elimu
na mafunzo kwa ngazi
zote
1.1. Taasisi za elimu na
mafunzo kuwa na
ardhi na hati miliki
kuanza mwaka 2014
1.1.1. Kuandaa miongozo
ya upatikanaji wa
Ardhi na hati miliki
kwa asasi za elimu na
mafunzo kwa ngazi
zote
a) Idadi ya taasisi
zilizo na ardhi ya
kutosha yenye
hatimiliki
Taarifa ya asasi
zilizo na ardhi na
hatimiliki
Wizara yenye
dhamana ya Elimu
na Mafunzo,
OWM-
TAMISEMI,
Ardhi na
maendeleo ya
makazi
1.2. Ardhi kwa ajili ya
matumizi ya shughuli
za elimu na mafunzo
kutambulika na
kutengwa kuanzia
mwaka 2014
1.2.1. Kuandaa mpango wa
kitaifa utakaowezesha
upatikanaji wa ardhi
kwa ajili ya matumizi
ya asasi za elimu na
mafunzo
b) Mpango wa
kuwezesha taasisi
zote kupata ardhi
Taarifa ya
utekelezaji wa
Mpango
Wizara yenye
dhamana ya Elimu
na Mafunzo ,
OWM-
TAMISEMI, Ardhi
na maendeleo ya
makazi
84
Mfumo endelevu wa ugharimiaji wa elimu na mafunzo nchini
MIKAKATI SHABAHA KAZI/ SHUGHULI VIASHIRIA VYA
UFANISI
NJIA YA
KUHAKIKI
WAHUSIKA
Lengo Na. 1: Kuimarisha mfumo wa ugharimiaji wa elimu na mafunzo kwa ngazi zote kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa sekta ya elimu na
mafunzo.
1. Kuimarisha muundo wa
ugharimiaji endelevu wa
elimu na mafunzo nchini.
1.1.Gharama halisi ya
kuelimisha
mwanafunzi kwa
ngazi zote
ikiwemo elimu na
mafunzo kwa njia
huria na masafa
kubainishwa
ifikapo mwaka
2014
1.1.1. kufanya tathmini ya
hali halisi ya
ugharimiaji wa elimu
na mafunzo nchini
a) Gharama halisi ya
kumsomesha
mwanafunzi kwa
ngazi zote za
elimu na mafunzo
Nyaraka za
gharama na taarifa
za tathmini
Wizara yenye
dhamana ya Elimu
na Mafunzo, Fedha,
viwanda, Taasisi za
Fedha, Asasi za
Kiraia na OWM-
TAMISEMI
1.2.Vyanzo vya
kugharimia elimu
na mafunzo katika
ngazi mbalimbali
kubainishwa na
kutumika ifikapo
mwaka 2016.
1.2.1. Kubainisha vyanzo
mbalimbali vya
rasilimali fedha kwa
ajili ya kugharimia
elimu na mafunzo
katika ngazi zote.
b) Idadi ya vyanzo
mahsusi vya
fedha za
kugharimia elimu
na mafunzo
Taarifa yenye
orodha ya vyanzo
vya fedha
Wizara yenye
dhamana ya Elimu
na Mafunzo, Fedha,
viwanda, Taasisi za
Fedha, Viwanda,
Asasi za Kiraia na
OWM-TAMISEMI
1.3.Utaratibu
utakaohusisha
sekta mbalimbali
na jamii katika
kugharimia elimu
kwa ngazi zote
kuainishwa na
kutumika ifikapo
mwaka 2016
1.3.1. Kuweka utaratibu wa
kubaini gharama halisi
za kumsomesha
mwanafunzi katika
kila ngazi
c) Asilimia 25 ya
tengeo la bajeti ya
Serikali
kugharimia elimu
na mafunzo
Bajeti ya Serikali
1.4.Tengeo la bajeti ya
serikali ya
kugharimia elimu
1.4.1. Kuweka utaratibu wa
kushirikisha sekta
binafsi katika
d) Sheria, kanuni na
miongozo ya
ugharamiaji wa
i. Sheria na
kanuni
zilizopitishwa
85
MIKAKATI SHABAHA KAZI/ SHUGHULI VIASHIRIA VYA
UFANISI
NJIA YA
KUHAKIKI
WAHUSIKA
na mafunzo
lisipungue asilimia
25 ya bajeti ya
serikali ifikapo
mwaka 2018.
kugharimia elimu na
mafunzo katika ngazi
zote
1.4.2. Kuandaa muundo wa
utekelezaji wa
ugharimiaji kwa
kuzingatia matokeo ya
utendaji wa asasi za
elimu na mafunzo
elimu
iliyohuishwa
na Serikali
1.5.Huduma ya elimu
na mafunzo
yanayotolewa na
sekta binafsi kuwa
ya gharama nafuu
kwa kadri
iwezekanavyo
ifikapo mwaka
2016
1.5.1. Kuandaa utaratibu wa
kuwezesha asasi za
elimu na mafunzo za
binafsi kutoa huduma
kwa gharama nafuu
e) Gharama nafuu za
huduma katika
taasisi za elimu
na mafunzo
ii. Taarifa ya
tathmini kuhusu
gharama
Wizara yenye
dhamana ya Elimu
na Mafunzo, Fedha,
viwanda, Taasisi za
Fedha, Viwanda,
Asasi za Kiraia na
OWM-TAMISEMI
1.6.Utaratibu endelevu
wa kuwawezesha
wanafunzi
wanaoshindwa
kuchangia
gharama za elimu
na mafunzo
kuwepo ifikapo
mwaka 2016
1.6.1. Kuandaa Utaratibu
endelevu wa
kuwawezesha
wanafunzi
wanaoshindwa
kuchangia gharama za
elimu na mafunzo
f) Mwongozo wa
utaratibu yakinifu
wa kuwawezesha
wanafunzi
wanaoshindwa
kuchangia
gharama za elimu
na mafunzo
iii. Mwongozo
ulioidhinishwa
2. Kujenga na kuendeleza
ubia kati ya sekta ya
umma na binafsi katika
kufanikisha miradi ya
2.1.Mazingira ya
kufanya taasisi
za fedha
kushiriki katika
ugharamiaji wa
2.1.1. Kufanya tathmini ya
maeneo ya ubia kati
ya sekta ya elimu na
mafunzo na sekta
a) Taasisi za fedha
kushiriki katika
ugharimiaji wa
elimu na
mafunzo.
i. Nyaraka za
sheria na
kanuni
zilizopitishwa
Wizara yenye
dhamana ya Elimu
na Mafunzo, Fedha,
viwanda, Taasisi za
Fedha, Viwanda,
86
MIKAKATI SHABAHA KAZI/ SHUGHULI VIASHIRIA VYA
UFANISI
NJIA YA
KUHAKIKI
WAHUSIKA
elimu na mafunzo kwa
ngazi zote
elimu na
mafunzo
kujengwa ifikapo
mwaka 2015.
binafsi Asasi za Kiraia na
OWM-TAMISEMI
2.2.Wahitimu wa elimu
na mafunzo katika
ngazi mbalimbali
na jamii kushiriki
kugharimia elimu
na mafunzo ifikapo
mwaka 2016.
2.2.1. Kubuni miradi ya ubia
ubia kati ya sekta ya
elimu na mafunzo na
sekta binafsi
b) Idadi ya miradi ya
elimu na mafunzo
baina ya sekta
binafsi na sekta
ya elimu na
mafunzo
ii. Taarifa ya miradi
na takwimu za
ushiriki wa
sekta binafsi
Wizara yenye
dhamana ya Elimu
na Mafunzo, Fedha,
viwanda, Taasisi za
Fedha, Viwanda,
Asasi za Kiraia na
OWM-TAMISEMI
3. Kuimarisha ushiriki wa
wadau mbalimbali katika
ugharimiaji wa mafunzo
tarajali na mazoezi kwa
vitendo sehemu za kazi
kwa wanachuo
3.1.Wadau mbalimbali
kushiriki katika
kugharimia
mafunzo tarajali
na mazoezi kwa
vitendo katika
sehemu
mbalimbali za
kazi ifikapo
mwaka 2016
3.1.1. Kuandaa utaratibu wa
kugharimia mafunzo
tarajali na mazoezi kwa
vitendo kwa
kushirikisha wadau
mbalimbali sehemu za
kazi
a) Muundo wa
ugharimiaji wa
elimu na mafunzo
tarajali na mazoezi
ya vitendo
sehemu za kazi
i. Nyaraka za
muundo
ulioidhinishwa
na Taarifa za
tathmini za
ushiriki
Wizara yenye
dhamana ya Elimu
na Mafunzo, Fedha,
viwanda, Taasisi za
Fedha, Viwanda,
Asasi za Kiraia na
OWM-TAMISEMI
87
Uongozi, usimamizi na uendeshaji wa elimu na mafunzo nchini
MIKAKATI SHABAHA KAZI/ SHUGHULI VIASHIRIA VYA
UFANISI
NJIA YA
KUHAKIKI
WAHUSIKA
Lengo Na.1: Kuongeza ufanisi, tija, uwajibikaji na uongozi bora katika usimamizi na uendeshaji wa elimu na mafunzo nchini
1. Kuhuisha mfumo wa
uongozi, usimamizi na
uendeshaji wa elimu na
mafunzo katika ngazi
zote za elimu na
mafunzo ikiwa ni
pamoja na ugatuaji wa
madaraka
1.1 Miongozo kuhusu
vigezo, viwango na
taratibu za uongozi,
usimamiaji na
upimaji wa
maendeleo ya elimu
na mafunzo ifikapo
mwaka 2016.
1.1.1 Kuweka miongozo
kuhusu uongozi,
usimamiaji na
upimaji wa
maendeleo katika
masuala mbalimbali
ya elimu na mafunzo
a) Sheria na
miongozo kuhusu
uongozi,
usimamiaji na
upimaji wa
maendeleo ya
elimu na mafunzo
iliyohuishwa
i. Nyaraka
zilizoidhinishwa
Wizara yenye
dhamana ya Elimu
na Mafunzo,
TAMISEMI, Ofisi
yenye Dhamana ya
Utumishi wa
Umma
1.2 Mgawanyo wa
majukumu,
Usimamizi na
uwajibikaji wenye tija
na ufanisi katika
elimu na mafunzo
kuwepo ifikapo
mwaka 2016
1.2.1 Kuhuisha
mgawanyo wa
majukumu,
utekelezaji na
uwajibikaji katika
ngazi mbalimbali
za uongozi,
usimamizi na
uendeshaji wa
elimu na mafunzo.
b) Miundo ya
uongozi,
usimamizi na
uendeshaji
ii. Nyaraka
zilizoidhinishwa
Wizara yenye
dhamana ya Elimu
na Mafunzo,
TAMISEMI, Ofisi
yenye Dhamana ya
Utumishi wa
Umma
1.3 Majukumu na umahiri
wa watendaji katika
masuala mbalimbali
kwa ngazi zote za
elimu na mafunzo
kuhuishwa na
kuboreshwa mara
kwa mara kuanzia
2014
1.3.1 Kuandaa utaratibu
endelevu wa kujenga
uwezo kwa
viongozi,
wasimamizi na
watekelezaji katika
elimu na mafunzo
1.3.2 Kuhuisha na
kuandaa mpango wa
kurithishana
majukumu ya
88
MIKAKATI SHABAHA KAZI/ SHUGHULI VIASHIRIA VYA
UFANISI
NJIA YA
KUHAKIKI
WAHUSIKA
uongozi, usimamizi
na utekelezaji katika
elimu na mafunzo
kwa kuzingatia
vigezo na viwango
stahiki.
2. Kuweka mpango wa
utambuzi, usajili,
kuendeleza na
kusimamia maadili ya
mwalimu.
2.1. Utambuzi na usajili
wa walimu katika
sekta ya elimu na
mafunzo kuwepo
ifikapo mwaka 2016
2.1.1. Kuhuisha na
kuandaa Sheria,
kanuni na miongozo
kuhusu utambuzi na
usajili wa walimu
wa ngazi zote.
a) Sheria, kanuni na
miongozo kuhusu
utambuzi na
usajili wa walimu.
i. Nyaraka
zilizoidhinishwa
Wizara yenye
dhamana ya Elimu,
TAMISEMI, Ofisi
yenye Dhamana ya
Utumishi wa
Umma
Lengo Na.2 : Kuimarisha mfumo wa menejimenti ya data na taarifa za elimu na mafunzo kwa ngazi zote za elimu na mafunzo.
1. Kuimarisha mfumo wa
menejimenti ya taarifa
za elimu ili kuleta tija na
ufanisi katika kuweka
mipango na maamuzi
kuhusu utoaji wa elimu
na mafunzo katika ngazi
zote za elimu na
mafunzo
1.1.Data na taarifa
zinazoaminika
kupatikana ifikapo
mwaka 2016
1.1.1. Kuandaa miongozo
ya kuimarisha
EMIS ili kuleta tija
na ufanisi katika
kuandaa mipango
na kufanya
maamuzi.
a) Miongozo ya
kuimarisha
Mfumo wa
Menejimenti ya
taarifa za elimu
i. Nyaraka za
miongozo ya
Mfumo wa
Menejimenti ya
taarifa za Elimu
(EMIS)
iliyoidhinishwa na
vyombo husika.
Wizara yenye
dhamana ya Elimu
na Mafunzo,
OWM-TAMISEMI,
Wizara zote, , Ofisi
ya Rais, NIDA
1.2.Data na taarifa
kutumika katika
mipango na
maamuzi katika
sekta ya elimu na
mafunzo ifikapo
mwaka 2016
1.2.1. Kuandaa mfumo
unganifu na wa kisasa
wa ukusanyaji,
utunzaji, uchambuzi
na upatikanaji wa
data katika ngazi zote
za elimu na mafunzo.
b) Matumizi stahiki
ya taarifa za
elimu
89
Masuala mtambuka katika elimu na mafunzo kuzingatiwa
MIKAKATI SHABAHA KAZI/ SHUGHULI VIASHIRIA VYA
UFANISI
NJIA YA
KUHAKIKI
WAHUSIKA
Lengo Na.1 : Elimu na Mafunzo yenye maudhui ya masuala mtambuka kwa ajili ya maendeleo endelevu ya Taifa.
1. Kuingiza katika
mitaala maudhui ya
masuala ya stadi za
maisha na
mabadiliko ya
tabianchi na stadi
nyinginezo
muhimu katika
maendeleo ya nchi.
1.1.Mitaala na programu
yenye maudhui stadi
za maisha na
mabadiliko ya
tabianchi kuwepo
ifikapo mwaka
2016
1.1.1. Kuhuisha mitaala na
programu kuingiza
dhana ya stadi za maisha
na mabadiliko ya
tabianchi na stadi
nyinginezo muhimu
katika maendeleo ya
nchi.
Programu, mihtasari
inayojumuisha maudhui
ya masuala mtambuka
Programu za masomo
na mitasari
iliyoidhinishwa
Wizara yenye
dhamana ya
Elimu na
Mafunzo,
MAZINGIRA,
Maji, Asasi za
Kiraia, OWM-
TAMISEMI,
OMR.
1.2.Walimu mahiri katika
kuwawezesha
wanafunzi kujifunza
masomo mbalimbali
yenye maudhui
matambuka ifikapo
mwaka 2016
1.2.1. Kuandaa miongozo
itakayowezesha
wanafunzi kujifunza
masuala ya stadi za
maisha na mabadiliko
ya tabianchi.
1.3.Wanafunzi wenye
uelewa wa stadi za
maisha na
mabadiliko ya
tabianchi ifikapo
mwaka 2018
1.3.1. Kuandaa walimu
mahiri
watakaowezesha
wanafunzi kujifunza
masuala ya stadi za
maisha na mabadiliko
ya tabianchi
Lengo Na.2 : Kuweka utaratibu wa kuimarisha utoaji wa huduma ya ushauri na unasihi katika ngazi zote za elimu na mafunzo.
1. Kuimarisha
muundo wa
ushauri na unasihi
katika ngazi zote
za elimu na
1.1.Miongozo na
utaratibu wa utoaji
wa ushauri na
unasihi katika elimu
na mafunzo
1.1.1. Kuandaa taratibu na
miongozo ya utoaji wa
ushauri na unasihi
katika elimu na
a) Miongozo ya
ushauri na unasihi
Nyaraka za miongozo
ya ushauri na unasihi
Wizara yenye
dhamana ya
Elimu na
Mafunzo, Afya
na Ustawi wa
90
MIKAKATI SHABAHA KAZI/ SHUGHULI VIASHIRIA VYA
UFANISI
NJIA YA
KUHAKIKI
WAHUSIKA
mafunzo nchini kuandaliwa ifikapo
mwaka 2015
mafunzo Jamii, Asasi za
Kiraia na OWM-
TAMISEMI. 1.2.Miundombinu na
nyenzo za kutolea
ushauri nasaha na
unasihi katika elimu
na mafunzo kuwepo
ifikapo mwaka 2018
1.2.1. Kuandaa miundombinu
na nyenzo muhimu za
kutolea ushauri na
unasihi katika elimu na
mafunzo
b) Huduma za ushauri
na unasihi katika
elimu na mafunzo
Taarifa za utekelezaji
1.3.Kuwepo na
wataalamu mahiri
wa ushauri na
unasihi wa kutosha
katika ngazi zote
elimu na mafunzo
ifikapo mwaka
2020.
1.3.1. Kuandaa utaratibu wa
kupata wataalamu
mahiri wa ushauri na
unasihi katika ngazi
zote elimu na mafunzo.
c) Idadi ya wataalamu
mahiri wa huduma
za ushauri na unasihi
katika ngazi zote
elimu na mafunzo.
Nyaraka za takwimu
za washauri nasihi
1.4.Wanafunzi kupata
huduma za ushauri
na unasihi kwa
kutumia wataalamu
mahiri katika shule
na vyuo ifikapo
mwaka 2020
Lengo Na. 3: Kuweka utaratibu utakao hakikisha kuwa haki za binadamu zinalindwa na hawapewi adhabu za kutesa au kudhalilisha wakati
akipatiwa elimu au mafunzo katika ngazi mbalimbali.
1. Kuweka muundo,
miongozo, kanuni
na taratibu za
kurekebisha tabia
na mienendo ya
wanafunzi
1.1.Adhabu za kutesa au
kudhalilisha
zinazuiliwa katika
mfumo wa elimu na
mafunzo ifikapo
mwaka 2016
1.1.1. Kuhuisha sheria,
miongozo, kanuni na
taratibu kuhusu
kurekebisha tabia na
mienendo ya
wanafunzi wanaokiuka
a) Sheria, kanuni na
miongozo inayohusu
haki za binadamu
iliyohuishwa
Nyaraka na taarifa za
utekelezaji
Wizara yenye
dhamana ya
Elimu na
Mafunzo,
OWM-
TAMISEMI,
91
MIKAKATI SHABAHA KAZI/ SHUGHULI VIASHIRIA VYA
UFANISI
NJIA YA
KUHAKIKI
WAHUSIKA
wanaokiuka
taratibu
mbalimbali za
shule na vyuo bila
kuwadhalilisha au
kukiuka haki za
binadamu.
taratibu mbalimbali za
shule na vyuo.
Katiba na
Sheria,
Maendeleo ya
Jamii, Jinsia na
Watoto na Afya
na Ustawi wa
Jamii.
1.2.Wanafunzi
wanaokiuka taratibu
za shule au za vyuo
kurekebishwa kwa
njia endelevu na za
kitaalamu ifikapo
mwaka 2016.
1.2.1 Kuweka utaratibu wa
kuelimisha walimu,
wazazi na jamii na
wamiliki wa shule na
vyuo kwa ujumla juu
ya taratibu za
kurekebisha tabia na
mienendo ya
wanafunzi katika
ngazi mbalimbali za
elimu na mafunzo
Idadi ya wanafunzi wa
shule na vyuo
waliorekebishwa
1.3.Utaratibu wa
kuwafukuza shule
wanafunzi wa elimu
- msingi kutokana
na sababu
mbalimbali
kuhuishwa ifikapo
mwaka 2016
1.3.1 Kuandaa mwongozo
utakaowezesha
wanafunzi
waliofukuzwa shule
na vyuo kuendelea na
masomo
Miongozo iliyoandaliwa Miongozo iliyopo
1.4.Walimu na jamii
kuelewa taratibu za
kutatua matatizo ya
kinidhamu ya
wanafunzi shuleni
na vyuoni ifikapo
mwaka 2016
1.4.1 Kuhamasisha walimu
na jamii kuhusu
utatuzi wa masuala ya
kinidhamu
Kupungua matatizo ya
kinidhamu katika shule
na vyuo
Nyaraka za Taarifa
ya utekelezaji
Lengo Na.4: Kuweka utaratibu wa kuhakikisha maadili ya walimu na watumishi wengine yanazingatiwa katika ngazi zote za elimu na mafunzo.
1. Kuweka muundo
na utaratibu wa
kuhakikisha
1.1.Sheria, miongozo,
kanuni na taratibu
kuhusu maadili ya
1.1.1. Kuhuisha muundo na
utaratibu wa
a) Muundo na utaratibu
wa nidhamu na
i. Nyaraka za
miundo na
Wizara yenye
dhamana ya
Elimu na
92
MIKAKATI SHABAHA KAZI/ SHUGHULI VIASHIRIA VYA
UFANISI
NJIA YA
KUHAKIKI
WAHUSIKA
kwamba maadili
ya walimu na
watumishi
wengine
yanazingatiwa
katika ngazi zote
za ellimu na
mafunzo kwa
kuzingatia sheria
za kazi na haki za
binadamu.
walimu na watumishi
wengine kuhuishwa
ifikapo mwaka 2016
kuhakikisha kuwa
nidhamu na maadili ya
kazi na uwajibikaji wa
walimu
maadili ya kazi na
uwajibikaji wa
walimu uliohuishwa
na kutumika
taratibu. Mafunzo,
Utumishi wa
Umma, OWM-
TAMISEMI,
OMR,
TAKUKURU 1.2.Nidhamu, uwajibikaji
na uadilifu kuimarika
katika ngazi zote za
elimu na mafunzo
ifikapo mwaka 2017.
1.2.1. Kuhuisha sheria,
miongozo, kanuni na
taratibu kuhusu maadili
ya walimu na
watumishi wengine
katika ngazi zote za
ellimu na mafunzo.
b) Sheria na kanuni
kuhusu maadili ya
walimu na
watumishi wengine
katika ngazi zote za
elimu na mafunzo
zilizohuishwa na
kutumika
ii. Nyaraka za sheria
na kanuni
zilizopitishwa
1.3.Mazingira ya bora
ya kazi na ya kuishi
mwalimu kuwepo
ifikapo mwaka 2020
1.3.1. Kuweka mazingira ya
kufanyia kazi na ya
kuishi mwalimu
yanayozingatia afya na
haki za binadamu
c) Mazingira ya kazi na
ya kuishi mwalimu
kwa kuzingatia haki
za binadamu
Lengo .5: Kuimarisha muundo wa kutekeleza maazimio na itifaki za ushirikiano baina ya Tanzania na nchi nyingine, kikanda na kimataifa katika
elimu na mafunzo
1. Utaratibu wa
kushughulikia
makubaliano ya
utekelezaji wa
maazimio
mbalimbali
yanayogusa elimu
na mafunzo
kikanda na
kimataifa
1.1. Miongozo na
taratibu wa
kushughulikia na
kutekeleza
maazimio na itifaki
yanayohusu elimu
na mafunzo kuwepo
ifikapo mwaka 2016
1.1.1. Kuandaa miongozo na
utaratibu wa
kutekeleza maazimio
na itifaki mbalimbali
yanayohusu elimu na
mafunzo kikanda na
kimataifa
a) Muundo wa
kutekeleza
maazimio na itifaki
za ushirikiano na
nchi nyingine.
Nyaraka za muundo
wa kutekeleza
maazimio na itifaki
Wizara yenye
dhamana ya
Elimu na
Mafunzo, Mambo
ya Nje na
Ushirikiano wa
kimataifa,
Ushirikiano wa
Afrika Mashariki,
Katiba na Sheria
Lengo Na. 6
93
MIKAKATI SHABAHA KAZI/ SHUGHULI VIASHIRIA VYA
UFANISI
NJIA YA
KUHAKIKI
WAHUSIKA
Kuimarisha utaratibu wa kuwezesha wanafunzi kujifunza kwa ufanisi masomo ya hisabati, sayansi na tekinolojia katika ngazi zote za elimu na
mafunzo.
1. Kuimarisha na
kuweka utaratibu
utakaowezesha
masomo ya
hisabati, sayansi
na tekinolojia
kufundishwa kwa
ufanisi zaidi.
1.1. Hisabati, sayansi,
na tekinolojia,
kufundishwa kwa
ufanisi ifikapo
mwaka 2018.
1.1.1. Kuhuisha mbinu za
ufundishaji na
ujifunzaji wa Hisabati,
Sayansi, na tekinolojia,
a) Viwango vya
ufaulu wa
wanafunzi katika
masomo ya
hisabati, sayansi, na
tekinolojia.
Taarifa za maendeleo
ya kitaaluma za
wanafunzi katika
masomo hayo
Wizara yenye
dhamana ya
Elimu na
Mafunzo, OWM-
TAMISEMI
WIZARA ZOTE
1.2. Rasilimaliwatu
mahiri na
wakutosha
kuwezesha
wanafunzi
kujifunza
masomo ya
hisabati, sayansi
na tekinolojia
katika ngazi zote
za elimu na
mafunzo kuwepo
ifikapo mwaka
2018.
1.2.1. Kuandaa mpango wa
kitaifa utakaowezesha
hisabati, sayansi na
teknolojia kufundisha
na kujifunza kwa
ufanisi katika ngazi
zote za elimu na
mafunzo
1.2.2. Kuandaa na kuajiri
rasilimaliwatu mahiri
kwa ajili ya kuwezesha
wanafunzi kujifunza
masomo ya hisabati,
sayansi na teknolojia
katika ngazi zote za
elimu na mafunzo.
b) Idadi ya wataalamu
wenye uwezo na
umahiri katika
kufundisha masomo
ya hisabati, sayansi
na tekinolojia.
Takwimu za
wataalamu
wanaofundisha
masomo hayo katika
ngazi zote za elimu
na mafunzo
Wizara yenye
dhamana ya
Elimu na
Mafunzo,
OWM-
TAMISEMI
WIZARA ZOTE
1.3. Umahiri wa
wanafunzi katika
nyanja za hisabati,
sayansi na tekinolojia
kuongezeka ifikapo
mwaka 2018.
1.3.1. Kuhamasisha na
kumotisha ufundishaji
na ujifunzaji wa
masomo ya hisabati,
sayansi na teknolojia
c) Idadi ya wahitimu
wenye umahiri
katika masomo ya
hisabati, sayansi na
tekinolojia.
Takwimu za
wataalamu wa
hisabati, sayansi na
teknolojia.
Wizara yenye
dhamana ya
Elimu na
Mafunzo, OWM-
TAMISEMI
WIZARA ZOTE
Lengo .7: Kuweka utaratibu wa kuhakikisha matumizi zaidi ya sayansi na tekinolojia katika utoaji wa elimu na mafunzo katika ngazi zote.
94
MIKAKATI SHABAHA KAZI/ SHUGHULI VIASHIRIA VYA
UFANISI
NJIA YA
KUHAKIKI
WAHUSIKA
1. Kuweka mpango
wa kutumia vifaa
bandia
(Simulators)
katika kufundisha
masomo kwa
vitendo katika
maabara na
karakana ili
kupunguza
gharama za elimu
na mafunzo
1.1. Vifaa bandia
(Simulators)
kutumika katika
kufundisha na
kujifunza kwa ngazi
zote za elimu na
mafunzo ifikapo
mwaka 2020
1.1.1. Kuandaa utaratibu wa
utakaowezesha
matumizi ya vyombo
bandia (Simulators)
katika kufundisha
masomo kwa vitendo
darasani, kwenye
maabara na karakana
a) Matumizi ya
vyombo bandia
(Simulators) katika
karakana na
maabara za shule
na vyuo
i. Vyombo bandia
katika karakana
na maabara
Wizara yenye
dhamana ya
Elimu na
Mafunzo, OWM-
TAMISEMI,
Wizara zote,
Ofisi yenye
Dhamana ya
Utumishi wa
Umma
1.2. Maabara za shule na
vyuo kubuni na
kutengeneza vifaa,
zana na nyenzo za
kufundishia na
kujifunzia hisabati,
sayansi na
tekinolojia katika
ngazi husika ifikapo
mwaka 2020
1.2.1. Kuandaa utaratibu wa
kutumia karakana na
maabara za vyuo kubuni
na kutengeneza vifaa,
zana na nyenzo za
kufundishia hisabati,
sayansi na teknolojia.
b) Idadi ya vifaa,
zana na nyenzo
zilizotengenezwa
shuleni na vyuoni
ii. Taarifa
zinazoonyesha
idadi ya vifaa
vifaa, zana na
nyenzo
Wizara yenye
dhamana ya
Elimu na
Mafunzo, Fedha,
OWM-
TAMISEMI,
Wizara zote,
Taasisi za
uwekezaji.
1.3. Walimu na
Wanafunzi wenye
uwezo wa kubuni na
kutengeneza vifaa,
zana na nyenzo za
kufundishia na
kujifunzia kuwepo
ifikapo mwaka 2025
1.3.1. Kuwajengea walimu
na wanafunzi uwezo wa
kubuni na kutengeneza
vifaa, zana na nyenzo za
kufundishia na
kujifunzia
c) Idadi ya wanafunzi
na walimu wenye
uwezo wa kubuni
na kutengeneza
vifaa, zana na
nyenzo
iii. Taarifa za
walimu na
wanafunzi
wabunifu
2. Kuimarisha ubia
baina ya sekta ya
elimu na mafunzo
na viwanda ili
kuwezesha
upatikanaji wa
vifaa, zana na
nyenzo za
2.1. Ushiriki wa viwanda
na sekta binafsi
kuwezesha
upatikanaji wa vifaa,
zana na nyenzo za
kufundishia na
kujifunzia hisabati,
sayansi na
2.1.1. Kuandaa sheria na
miongozo ya ubia baina
ya sekta ya elimu na
mafunzo na sekta
binafsi
a) Sheria na
miongozo ya ubia
baina ya sekta ya
elimu na mafunzo
na sekta binafsi
i. Taarifa ya
utekelezaji
95
MIKAKATI SHABAHA KAZI/ SHUGHULI VIASHIRIA VYA
UFANISI
NJIA YA
KUHAKIKI
WAHUSIKA
kufundishia na
kujifunzia
hisabati, sayansi
na tekinolojia
tekinolojia ifikapo
mwaka 2016
2.2. Mpango wa taifa wa
kushirikisha sekta
binafsi katika
upatikanaji wa vifaa,
zana na nyenzo za
kufundishia na
kujifunzia hisabati,
sayansi na tekinolojia
kuwepo na kutumika
ifikapo mwaka 2016.
2.2.1. Kuabuni miradi ya Ubia
baina ya sekta ya umma
na binafsi katika
masuala ya upatikanaji
wa vifaa, zana na
nyenzo za kufundishia
na kujifunzia hisabati,
sayansi na teknolojia.
b) Idadi ya miradi ya
ubia ya sekta
binafsi katika
upatikanaji wa
vifaa, zana na
nyenzo za
kufundishia na
kujifunzia hisabati,
sayansi na
tekinolojia
ii. Taarifa, za
utekelezaji wa
miradi takwimu
za ushiriki wa
sekta binafsi
Wizara yenye
dhamana ya
Elimu na
Mafunzo, OWM-
TAMISEMI,
Taasisi za
uwekezaji,
Fedha,Mawasilia
no, Sayansi na
Teknolojia, na
Wizara zote
2.2.2. Kuandaa mpango wa
taifa wa kushirikisha
sekta binafsi katika
upatikanaji wa vifaa,
zana na nyenzo za
kufundishia na
kujifunzia hisabati,
sayansi na teknolojia.
3. Kuwezesha kila
taasisi ya elimu na
mafunzo kuwa
kitovu cha sayansi
na tekinolojia
katika jamii.
3.1. Taasisi za elimu na
mafunzo kuwa
kitovu cha matumizi
ya sayansi na
tekinolojia katika
jamii ifikapo mwaka
2018
3.1.1. Kuandaa sheria na
miongozo kuwezesha
kila asasi ya elimu na
mafunzo kuwa kitovu
cha sayansi na
teknolojia.
a) Sheria na miongozo
kuwezesha taasisi za
elimu kuwa kitovu
cha sayansi na
tekinolojia
i. Nyaraka za sheria
na miongozo
3.2. Taasisi za elimu
na mafunzo kuwa ni
vituo vya elimu
(Resource centers)
katika jamii ifikapo
3.2.1. Kuandaa mpango wa
taifa wa kuwezesha kila
asasi ya elimu na
mafunzo nchini kuwa
kitovu cha sayansi na
b) Idadi ya taasisi za
elimu na mafunzo
ambazo ni vitovu
vya sayansi na
ii. Orodha ya Asasi
ambazo vituo vya
sayansi na
teknolojia
96
MIKAKATI SHABAHA KAZI/ SHUGHULI VIASHIRIA VYA
UFANISI
NJIA YA
KUHAKIKI
WAHUSIKA
mwaka 2016 teknolojia katika jamii tekinolojia
3.3. Taasisi za elimu na
mafunzo kuwa vituo
atamizi ili kujenga
uwezo wa wahitimu
katika jamii ifikapo
mwaka 2017
3.3.1. Kuwezesha asasi za
elimu na mafunzo kuwa
vituo atamizi vya
kujenga uwezo wa
wahitimu katika jamii
c) Idadi ya taasisi
zenye vituo
atamizi
iii. Orodha ya Asasi
ambazo vituo
atamizi
Lengo Na.8: Kuweka utaratibu na kuimarisha ushiriki fanisi wa wadau mbalimbali katika sekta ya elimu na mafunzo katika ngazi zote.
1. Kupanua wigo wa
ushiriki wa wadau
katika mipango,
uendeshaji,
ugharimiaji,
ufuatiliaji na
tathmini katika
ngazi zote za
elimu na
mafunzo.
1.1. Wigo wa ugharimiaji
wa elimu na
mafunzo katika
ngazi zote za elimu
kwa kushirikisha
wadau mbalimbali
kupanuka ifikapo
mwaka 2016.
1.1.1. Kuandaa miongozo ya
ushiriki wa wadau
katika mipango,
uendeshaji,
ugharimiaji, ufuatiliaji
na tathmini katika
ngazi zote
a) Wigo wa ushiriki
wa wadau katika
ugharimiaji wa
elimu na mafunzo
i. Nyaraka za
tathmini na
miongozo ya
ushiriki
Wizara yenye
dhamana ya
Elimu na
Mafunzo,OWM-
TAMISEMI,
Wizara zote
1.2. Ushiriki wa wadau
katika mipango,
uendeshaji na
tathmini ya elimu na
mafunzo katika ngazi
zote kuongezeka
ifikapo mwaka 2016.
1.2.1. Kuandaa utaratibu wa
kuhamasisha ushiriki
wa wadau katika
mipango, uendeshaji,
ugharimiaji na
ufuatiliaji wa
utekelezaji wa elimu na
mafunzo
b) Idadi ya wadau
wanaoshiriki
katika uendeshaji,
ugharimiaji na
ufuatiliaji wa
elimu na mafunzo
ii. Taarifa ya idadi
ya wadau
wanaoshiriki
katika elimu na
mafunzo
2. Kuongeza ushiriki
wa wadau katika
utoaji wa huduma
mbalimbali mfano
chakula na malazi
2.1. Utaratibu wa
kushirikisha wadau
katika utoaji wa
huduma mbalimbali
mfano chakula na
2.1.1. Kuandaa miongozo na
taratibu wa
kuhamasisha ushiriki
wa wadau katika utoaji
c) Utaratibu wa
huduma
mbalimbali
zinazotolewa na
i. Taarifa ya idadi
ya wadau
wanaoshiriki
katika kutoa
Wizara yenye
dhamana ya
Elimu na
Mafunzo, Fedha,
OWM-
97
MIKAKATI SHABAHA KAZI/ SHUGHULI VIASHIRIA VYA
UFANISI
NJIA YA
KUHAKIKI
WAHUSIKA
katika elimu na
mafunzo
malazi katika elimu
na mafunzo
kuwekwa ifikapo
mwaka 2016
wa huduma
mbalimbali1
wadau huduma
mbalimbali
TAMISEMI, na
Wizara ZOTE
2.2. Huduma mbalimbali
katika shule na vyuo
kutolewa kwa
kushirikisha wadau
ifikapo mwaka 2016
d) Aina za huduma
mbalimbali
zinazotolewa na
wadau
1 Chakula, Maji safi na salama, Afya na usafiri na nyinginezo katika asasi za elimu na mafunzo