Upload
massawe-michael-baraka
View
221
Download
25
Embed Size (px)
DESCRIPTION
ECONOMICS
Citation preview
Somo la uchumi ni sayansi ya kijamii ambalo hutafiti uzalishaji, usambazaji, na matumizi ya bidhaa
na huduma. Nenouchumi linatokana na neno la Kigiriki cha Kale oikonomia [3]
(oikonomia "usimamizi wa kaya, utawala") kutoka [5] oikos"nyumba") + [7] (nomos , "desturi" au
"Sheria"), kwa hivyo "sheria za nyumba (kaya)".[1] Aina za masomo ya kiuchumi ya kisasa
zilizotokana na somo pana la uchumi wa kisiasa katika miaka ya mwisho ya karne ya 19, kutokana
na matamanio ya kuchukua mwelekeo jarabati unaofaa zaidi sayansi za kiasilia.[2]
Ufafanuzi unaojumuisha mengi ya masomo ya kiuchumi ya kisasa ni ule wa Lionel Robbins katika
insha yake: “sayansi inayotafiti tabia ya binadamu kama uhusiano baina ya hatima na njia haba
ambazo zina matumizi badala."[3] Uhaba unamaanisha kuwa rasilimali zinazopatikana hazitoshi
kutosheleza matamanio na mahitaji yote. Ikiwa hakuna uhaba na kuna matumizi badala ya rasilimali
zinazopatikana, basi hakuna shida ya kiuchumi. Hivyo somo lililofafanuliwa linahusu utafiti wa
chaguzi kama vile zinavyobadilishwa na vishawishi na rasilimali.
Somo la kiuchumi linalenga kufafanua vile chumi hufanya kazi na vile viungo vya kiuchumi hufanya
kazi pamoja. Uchambuzi wa kiuchumi huhusisha sehemu zote za jamii, katika biashara, fedha na
serikali, na hata katika uhalifu,[4] elimu,[5]familia, afya,sheria, siasa, dini,[6] taasisi za kijamii, vita,[7] na sayansi.[8] Hoja inayoendelea kukua ya somo la kiuchumi katika sayansi ya kijamii imeelezwa
kuwa ubeberu wa kiuchumi.[9][10]
Tofauti za kawaida huelezwa baina ya jinsi mbalimbali za somo la kiuchumi: baina ya uchumi
chanya (kueleza “kile kilichoko”) na uchumi unaozidi kuongezeka (kueleza “kile linachostahili kuwa”)
au baina ya uchumi nadharia na uchumi wa utenzi au baina ya uchumi uliotanda (ulio “halisi”
unaojihusisha na “wiano wa fikira-ubinafsi-msawazo”) na uchumi usio wa kiasilia (“badilishi” zaidi
unaoshughulika na “wiano wa taasisi-historia-muundo wa kijamii"[11]). Hata hivyo tofauti ya kimsingi
ya kiada baina ya “uchumi wa kiwango cha chini” (microeconomics), ambao unaotafiti tabia ya
kiuchumi ya viungo (pamoja na watu binafsi na makampuni) na “uchumi wa kiwango cha juu”
(macroeconomics), ambao hushughulikia maswala ya ukosefu wa ajira, mfumuko wa bei, sera ya
fedha na hazina kwa uchumi wote.
Historia juu ya mawazo ya kiuchumi[hariri | hariri chanzo]
A stele depicting mtu ameketi chini
Makala kuu ya: History of economic thought
Majimbo ya mijini ya Sumer yalianzisha uchumi wa biashara na soko uliohusika hapo awali na
sarafu ya Shekel ambayo ilikuwa ni uzito wa kipimo fulani cha shayiri, huku Wababeli na
majirani wao wa majimbo ya mijini wakianzisha hapo baadaye mfumo wa mwanzo wa uchumi
kwa kutumia kipimo cha bidhaa mbalimbali, ambao uliwekwa katika kanuni ya kisheria.[12] Kanuni
za mapema za kisheria kutoka Sumer zinaweza kuchukuliwa kuwa utaratibu wa kwanza
(ulioandikwa) wa kiuchumi, na zilikuwa na jinsi ambazo zinazotumika katika mfumo wa bei wa
kisasa …kama vile kanuni za kiasi cha fedha za mikataba ya biashara (riba), faini za pesa kwa
‘dhuluma’, sheria za urithi, sheria za kushughulikia kutuzwa kwa kodi au kugawanywa kwa mali
binafsi, na kadhalika.[13][14] Kwa muhtasari wa sheria, tazama sheria za Babeli na Sheria ya kale
ya kiuchumi.
Dhana ya kiuchumi ina mwanzo wake kutoka kwa utamaduni wa mapema wa Kimesopotamia,
Kigiriki, Kirumi, Kihindi, Kichina, Kiajemi na Kiarabu. Waandishi wa kutajika ni pamoja na
Aristotle, Chanakya (aliyejulikana vilevile kama Kautilya), Qin Shi Huang, Thomas Aquinas na
Ibn Khaldun hadi karne ya 14. Joseph Schumpeter hapo awali alikadiria usomi wa karne ya 14
hadi ile ya 17 kuwa “karibu zaidi kuliko kikundi kingine chochote kuwa ‘waanzilishi’ wa uchumi
wa kisayansi” kwa kifedha, riba, na nadharia ya thamani katika mtazamo wa sheria-asili.[15] Hata
hivyo, baadaye, baada ya kugundua kitabu cha Ibn Khaldun cha Muqaddimah, Schumpeter
alianza kumwona Ibn Khaldun kama mwanzilishi wa kwanza wa uchumi wa kisasa,[16] kwa vile
nyingi za nadharia zake hazikuwa zinajulikana Ulaya hadi nyakati za hivi karibuni.[17]
Licha ya hayo, utafiti wa karibuni unaonyesha kuwa mwanachuo-mwanafalsafa wa Kihindi
Chanakya ( 340-293 BCE) alitangulia Ibn Khaldun kwa milenia moja na nusu kama mwanzilishi
wa uchumi wa kisasa,[18][19][20][21] na ameandika kwa upana zaidi juu ya mada hii, hasa juu ya
uchumi wa kisiasa. Maandishi yake maarufu zaidi, Arthashastra (The Science of Wealth and
Welfare), [22] ni mwanzo wa dhana za kiuchumi ambazo ni pamoja na gharama ya fursa
(opportunity cost), muundo wa mahitaji na ugavi, kushuka kwa mapato, uchambuzi wa
mabadiliko katika viungo vya mfumo, bidhaa za umma, tofauti kati ya muda mfupi na muda
mrefu, habari za kupendelea upande mmoja wa shughuli za biashara na faida ya muuzaji.[23] Katika cheo chake kama mshauri wa mfalme wa Himaya ya Maurya ya India ya kale,
alishauri pia juu ya vyanzo na masharti ya ukuaji wa uchumi, vikwazo kwake na motisha ya
ushuru ili kuhimiza ukuaji wa kiuchumi.[24]
Bandarini meli ikiwasili
Makundi mengine mawili, ambayo baadaye yalijulikana kama ‘mercantilists’ na ‘physiocrats’,
ambayo yalikuwa na ushawishi wa moja kwa moja wa baadaye wa ustawi wa mada. Makundi
yote mawili yalihusishwa na mwanzo wa utaifa wa kiuchumi na ukapitalisti wa kisasa barani
Ulaya. Umekantili ulikuwa ni mafundisho ya kiuchumi yaliyostawi kutoka karne ya 16 hadi ile ya
18 katika juzuu maridhawa ya fasihi, iwe ya wachuuzi au watawala. Nadharia hii ilishikilia kuwa
utajiri wa taifa ulitegemea ulimbikizaji wa dhahabu na fedha. Mataifa ambayo hayakuwa na
migodi yangeweza kupata dhahabu na fedha kutoka kwa biashara tu kwa kuuza bidhaa katika
nchi za ng’ambo na kuzuia ununuzi wa bidhaa kuingia kwa nchi ambavyo havikuwa dhahabu
wala fedha. Dhana hii ilihitaji kuagiza kwa malighafi ya kutumika katika utengenezaji wa bidhaa,
ambazo zingeweza kuuzwa, na kwa usimamizi wa nchi kwa kutoza ushuru wa uhifadhi kwa
bidhaa zilizotengenezewa nje ya nchi na kuzuia utengenezaji wa bidhaa katika makoloni.[25][26]
Physiocrats, kikundi cha karne ya 18 cha wanafalsafa na waandishi, walibuni wazo la uchumi
kama mkondo wa mzunguko wa mapato na matumizi. Adam Smith alieleza mfumo wao “ukiwa
na kutokamilika kwake kwote” kama “pengine kisio la ufasaha zaidi wa ukweli ambalo limewahi
kuchapishwa” juu ya mada hii. Watu wa kikundi cha Physiocrats waliamini kuwa ni mapato ya
kilimo tu ambayo yalizalisha faida juu ya gharama iliyo wazi, na hivyo kuonyesha kuwa kilimo
ndicho kilikuwa msingi wa mali yote.
Kwa hivyo walipinga sera ya wamekantilisti ya kukuza viwanda na biashara kwa gharama ya
kilimo, pamoja na ushuru wa kuagiza. Kikundi cha Physiocrats walishauri kutoa mkusanyo wa
ushuru ulio ghali kwa usimamizi na kuweka mahali pake ushuru wa aina moja kwa mapato ya
wamiliki wa ardhi. Jinsi tofauti za ushuru huo wa ardhi zilichukuliwa na wanauchumi wa baadaye
(akiwemo Henry George karne moja baadaye) kama chimbuko la ushuru ambalo kwa kiwango
kikubwa halikuwa la kupotosha. Kama mmenyuko dhidi ya masharti mengi mno ya biashara ya
kimekantili, kikundi cha physiocrats kilitetea sera ya uholela (laissez-faire), ambayo ilihitaji
mwingilio wa serikali wa kiwango cha chini katika uchumi.[27][28]
Uchumi wa kisiasa wa kirasimi[hariri | hariri chanzo]
Makala kuu ya: Classical economics
Machapisho ya Adam Smith ya The Wealth of Nations ya mwaka wa 1776, yameelezwa
kuwa “zao fanisi la uchumi kama somo tofauti."[29] Kitabu hicho kilibainisha ardhi, ufanyakazi,
na mtaji kama vipengele vitatu vya uzalishaji na michango mikubwa kwa utajiri wa taifa.
mtu yanayowakabili haki
Kwa maoni ya Smith, uchumi kamili ni mfumo wa soko la kujidhibiti ambao hutosheleza bila
kubadilika mahitaji ya kiuchumi ya wakazi. Alieleza mfumo wa soko kuwa “mkono
usiionekana” ambao unaongoza watu wote, katika harakati zao za kutafuta maslahi yao
wenyewe, kuzalisha faida kubwa kwa jamii kwa ujumla. Smith alijumuisha baadhi ya dhana
za kikundi cha physiocrats, ikiwemo ile ya kutohusika kwa serikali katika maswala ya
uchumi, yaani uholela, katika nadharia zake mwenyewe za kiuchumi, lakini alikataa dhana
kuwa ni kilimo tu kilichozalisha mapato.
Katika mfano wake maarufu wa mkono usioonekana, Smith alitoa hoja kwa wazo
lililoonekana kuwa kinyume kuwa soko lilionekana kujongeza maslahi ya kijamii, ingawa
yaliongozwa na maslahi nyimivu zaidi ya kibinafsi. Mtazamo wa kawaida ambao Smith
alisaidia kuanzisha ulijulikana kama uchumi wa kisiasa na baadaye kama uchumi wa
kirasimi. Ulijumuisha watu maarufu kama vile Thomas Malthus, David Ricardo, na John
Stuart Mill walioandika kutoka karibu mwaka wa 1770 hadi 1870.[30]
Huku Adam Smith akisisitiza uzalishaji wa mapato, David Ricardo alilenga ugavi wa mapato
baina ya wamiliki wa ardhi, wafanyakazi, na wenye mtaji. Ricardo aliona mgogoro wa ndani
baina ya wamiliki wa ardhi kwa upande mmoja na utenda kazi na mtaji kwa upande
mwingine. Alisisitiza kuwa ukuaji wa idadi ya watu na mtaji, ukisonga ardhi isiyoongezeka,
uliongeza gharama ya kodi na kuzuia kuongezeka kwa marupurupu na faida.
mtu zinazoikabili Viewer
Maltus alitumia dhana ya mapato yanayopungua kueleza viwango vya chini vya maisha.
Idadi ya watu, alisisitiza, ilionekana kuongezeka katika muundo wa kijiometria, kuzidi
uzalishaji wa chakula, ambao uliongezeka kihisabati. Shinikizo la idadi ya watu iliyokuwa
inaongezeka kwa haraka dhidi ya kiasi kidogo cha ardhi lilimaanisha mapato yaliyokuwa
yanapungua kwa wafanyakazi. Matokeo, alidai, yalikuwa ni marupurupu ya kiwango cha
chini daima, ambayo yalizuia hali ya maisha kwa wengi ya wakazi kupanda kupita kiwango
cha chini.
Vilevile, Malthus alihoji mwelekeo wa uchumi wa soko wa kutoa ajira kwa wote. Alilaumu
ukosefu wa ajira kwa mwelekeo wa uchumi wa kuzuia matumizi ya pesa kwa kuweka akiba
sana, hoja iliyosahaulika hadi pale John Maynard Keynes alipoifufua katika miaka ya 1930.
Akija mwishoni mwa utamaduni wa Urasimi, John Stuart Mill alitofautiana na wanauchumi
wa kirasimi wa awali katika swala la kutoepukika kwa ugavi wa mapato yaliyozalishwa na
mfumo wa soko. Mill alionyesha tofauti ya wazi baina ya majukumu mawili ya soko: mgao
wa rasilimali na utoaji wa mapato. Soko linaweza kuwa na ufanisi katika ugavi wa rasilimali
lakini si kwa utoaji wa mapato, aliandika, hivyo kushurutisha kuingilia kati kwa jamii.
Nadharia ya thamani ilikuwa muhimu katika nadharia ya urasimi. Smith aliandika kuwa “bei
halisi ya kila kitu … ni mahangaiko na matatizo ya kukipata kitu hicho” huku ikishawishika na
uhaba wake. Smith alisisitiza kuwa, pamoja na kodi na faida, gharama zingine zaidi ya
marupurupu pia huchangia katika bei ya bidhaa.[31] Wanauchumi wengine wa kirasimi
walionyesha aina tofauti za dhana ya Smith, ambayo ilijulikana kama ‘nadharia ya thamani
ya ajira’ (labour theory of value). Wanauchumi wa kirasimi walizingatia mwelekeo wa soko
wa kusonga katika msawazo wa muda mrefu.
Umaksi[hariri | hariri chanzo]
Makala kuu ya: Marxian economics
Mwanamme akimwangali mtazamaji
Uchumi wa Kimaksi (ambao baadaye ulijulikana kama Markian economics) unatokana
na uchumi wa kirasimi. Unachimbuka kutoka kwa maandishi ya Karl Marx. Sehemu ya
kwanza ya maandishi makuu ya Marx, Das Kapital, yalichapishwa kwa Kijerumani
mnamo 1867. Katika kitabu hiki, Marx alizingatia nadharia ya thamani ya ajira na kile
alichokichukulia kuwa udhalilishaji wa wafanyakazi na waajiri.[32][33]Nadharia ya thamani
ya ajira ilishikilia kuwa thamani ya kitu iliamuliwa na kazi iliyotekelezwa ili kukizalisha.
Hii inatofautiana na ufahamu wa kisasa kuwa thamani ya kitu inaamuliwa na gharama
ambayo mtu yu tayari kulipa ili kukipata.
Uchumi wa aina ya urasimi mpya[hariri | hariri chanzo]
Makala kuu ya: Neoclassical economics
Unahusu nadharia zilizojulikana baadaye kama ‘uchumi wa urasimimpya’ au
‘uchumi wa kutumia viungo vya pambizoni’ (marginalism) uliobuniwa kutoka karibu
mwaka wa 1870 hadi 1910. Neno ‘uchumi’ lilipewa umaarufu na wanauchumi wa
urasimimpya kama vile Alfred Marshall kama neno fupi lenye maana sawa na
‘sayansi ya kiuchumi’ na neno badala kwa jina la awali, lililo na maana pana ya
‘uchumi wa kiasiasa".[34][35] Hii iliwiana na mvuto wa mbinu za hisabati zinazotumika
katika sayansi asilia.[2]
Uchumi wa aina ya urasimimpya uliratibisha ugavi na mahitaji kama vipengele vya
pamoja vya kuamua bei na kiasi katika msawazo wa soko, hivyo kuadhiri ugavi wa
mazao na utoaji wa mapato. Uliacha nadharia ya thamani ya ajira iliyorithiwa kutoka
kwa uchumi wa urasimi na kupendelea nadharia ya ajira ya matumizi ya pambizoni
(marginal utility theory) katika upande wa mahitaji na nadharia ya gharama ya
ujumla zaidi katika upande wa ugavi. Cite error: Closing </ref> missing
for <ref> tag[36]
Uchumi wa urasimimpya huitwa mara kwa mara uchumi halisi (orthodox
economics) na wakosoaji wake na vilevile wafuasi wake. Uchumi wa kisasa
uliokubalika na wengi unatokana na uchumi wa urasimimpya ingawa una umakini
mwingi ambao unautimiliza au unaujumuisha uchambuzi wa awali, kama vile
uchumikihisabati, nadharia ya bahati, uchambuzi wa kuanguka kwa soko na
ushindani usiokamilika, na mfumo wa urasimimpya wa ukuaji wa uchumi wa
kuchambua viungo vya muda mrefu vinavyoathiri mapato ya kitaifa.
Uchumi wa Keneshia[hariri | hariri chanzo]
Makala kuu yas: Keynesian economics and Post-Keynesian economics
Wanaume wawili wakiwa wamevalia suti wakizungumza
Uchumi wa Keneshia unatokana na John Maynard Keynes, hasa kitabu
chake The General Theory of Employment, Interest and Money (Nadharia ya
Jumla ya Ajira, Riba na Pesa) (1936), ambacho kilianzisha uchumi wa kiwango
cha juu wa kisasa kama kitengo tofauti.[37][38]Kitabu hicho kililenga mambo
yanayoamua mapato ya taifa katika muda mfupi wakati bei hazibadiliki. Keynes
alijaribu kueleza kinaganaga katika upana wa kinadharia ni kwa nini ukosefu
mkuu wa ajira katika soko la wafanyakazi hauwezi kujirekebisha wenyewe kwa
sababu ya “mahitaji fanisi” ya chini na kwa nini hata ugeukaji wa bei na sera za
kifedha vinaweza kuwa visivyo na maana. Maneno kama “mapinduzi”
yametumiwa kuzungumzia kitabu hicho katika athari zake juu ya uchambuzi wa
kiuchumi.[39][40][41]
Uchumi wa Keneshia una waandamizi wawili. Uchumi wa baada ya Keneshia
pia unachunguza sana ugumu wa uchumi wa kiwango cha juu na michakato ya
kuratibisha. Utafiti juu ya wakfu za kiwango cha chini kuhusu mifano yao
unaonyeshwa kama ule unaohusu uhalisi wa maisha kuliko mifano tu ya ufanisi.
Unahusishwa na Chuo Kikuu cha Cambridge na maandishi ya Joan Robinson.[42]
Uchumi mpya wa Kineshia pia huhusishwa na maendeleo katika muundo wa
Keneshia. Katika kikundi hiki, watafiti hushiriki na wanauchumi wengine katika
msisitizo juu ya mifano inayotumia misingi ya kiwango cha chini na tabia ya
ufanisi lakini ukilenga kwa kiwango kidogo zaidi mada za kawaida za Keneshia
kama vile kutobadilika kwa bei na marupurupu. Hivi huchukuliwa kuwa
vipengele vya ndani vya mifano hiyo, na wala havijumuishwi tu kama katika
miundo mingine ya zamani ya Keneshia.
Taasisi ya Chicago School of economics[hariri | hariri chanzo]
Makala kuu ya: Chicago school (economics)
Taasisi ya Chicago school of economics inajulikana vyema zaidi kwa
utetezi wake wa soko huru na mawazo yake ya kifedha (monetarist ideas).
Kwa mujibu wa Milton Friedman na wamonetaristi, chumi za kisoko ni za
imara kwa jinsi yao ikiwa zitaachwa bila kuingiliwa na unyogofu huingia tu
kwa sababu ya mwingilio wa serikali.[43] Friedman, kwa mfano, alitoa hoja
kuwa Unyogofu Mkuu ulisababishwa na kupungua kwa utoaji wa pesa
ambazo zilithibitiwa na Benki Kuu ya Shirikisho, na wala si kwa ukosefu wa
uwekezaji kama vile Keynes alikuwa amedai. Ben Bernanke, Mwenyekiti
wa sasa wa Benki Kuu, ni pamoja na wanauchumi wa leo ambao
wanakubali uchambuzi wa Friedman juu ya vyanzo vya Unyogofu Mkuu.[44]
Milton Friedman aliiga kwa ufanisi nyingi za kanuni za kimsingi zilizobuniwa
na Adam Smith na wanauchumi wa urasimi na kuzipa sura mpya. Mfano
mmoja wa jambo hili ni makala yake katika toleo la Septemba 1970 la The
New York Times Magazine, ambapo alidai kuwa wajibu wa kijamii wa
biashara unafaa kuwa “kutumia machumo yake na kushiriki katika shughuli
ambazo zimekusudiwa kuongeza faida zake…(kupitia kwa) ushindani wa
wazi na huru bila udanaganyifu wala hila." [45]
Mifumo na mielekeo mingine[hariri | hariri chanzo]
Makala kuu ya: Schools of economics
Mifumo mingine maarufu au mielekeo ya mawazo ambayo huashiria
jinsi fulani ya uchumi unaofuatwa na kusambazwa ni kutoka kwa
makundi ya wasomi yanayodhihirika vyema ambayo ni maarufu
ulimwenguni kote, ni pamoja na the Austrian School, the Freiburg
School, the School of Lausanne, post-Keynesian economics na the
Stockholm school. Uchumi wa kisasa uliotanda kwa sasa huwekwa
wakati mwingine kwa makundi ya mwelekeo wa Saltwater wa vile vyuo
vikuu vilivyo katika pwani za Mashariki na Magharibi za Marekani, na
mwelekeo wa Freshwater, au mwelekeo wa Chicago-school.
Katika jinsi ya uchumi wa kiwango cha juu kunao, katika utaratibu wa
orodha ya kuzuka kwao katika fasihi: uchumi wa urasimi, uchumi wa
Keneshia, muungano wa urasimimpya, uchumi wa enzi ya baada ya
Keneshia, umonetaristi, uchumi wa urasimi mpya, uchumi wa upande
wa ugavi. Mifumo badala ni pamoja na uchumi wa kiikolojia, uchumi wa
taasisi, uchumi wa mageuzi, nadharia ya kutegemea, uchumi wa
kimaumbile (structuralist economics), nadharia ya mifumo ya dunia,
ekonofizikia (econophysiscs) na uchumi wa bayofozikia (biophysical
economics).[46]
Uchumi wa kiwango cha chini[hariri | hariri chanzo]
Makala kuu ya: Microeconomics
Uchumi wa kiwango cha chini hutazama mwingiliano kupitia
masoko binafsi, huku kukiwa na uhaba na uthibiti wa serikali. Soko
linaweza kuwa la bidhaa, kama vile mahindi mabichi, au huduma
za kipengele fulani za uzalishaji, kwa mfano upangaji wa matofali.
Nadharia hii huzingatia jumla ya kiwango kinachohitajika na
wanunuzi na kiwango kinachohitajika na wanunuzi na kiwango
kinachotolewa na wauzaji kwa kila bei iwezekanayo kwa kitu
kimoja. Inaunganisha mambo haya pamoja ili kueleza vile soko
linaweza kufikia usawazishaji kulingana na bei na kiwango au
kukabiliana na mabadiliko ya soko baada ya muda.
Huu huitwa kwa kawaida uchambuzi wa ugavi na mahitaji. Miundo
ya soko, kama vile ushindani kamilifu na umiliki, huchunguzwa kwa
mtazamo wa athari kwa tabia na ufanisi wa kiuchumi. Uchambuzi
wa mabadiliko katika soko moja huendelea kutoka kwa fikira ya
urahisi kuwa mahusiano ya tabia katika masoko hubaki bila
kubadilika, yaani, uchambuzi wa sehemu ya usawazishaji.
Nadharia ya usawazishaji wa jumla inaruhusu mabadiliko katika
masoko tofauti na ujumla katika masoko yote, zikiwemo harakati
zao na miingiliano yao kuelekea msawazo.|Nadharia ya
usawazishaji wa jumla inaruhusu mabadiliko katika masoko tofauti
na ujumla katika masoko yote, zikiwemo harakati zao na
miingiliano yao kuelekea msawazo.[47][48]
Masoko[hariri | hariri chanzo]
Makala kuu yas: Production-possibility frontier, Opportunity cost, and Production theory
basics
Katika uchumi wa hali ya chini, uzalishaji ni ubadilishaji wa pembejeo kuwa
mazao. Huu ni mchakato wa kiuchumi unaotumia rasilimali kutengeneza
bidhaa ambayo inafaa kubadilishwa. Michakato hii inaweza kuwa pamoja na
utengenezaji, uwekaji kwa bohari, usafirishaji kwa meli, na kufungasha.
Baadhi ya wanauchumi hueleza uzalishaji kwa upana kuwa shughuli zote za
kiuchumi ila tu matumizi. Wao huona kila shughuli ya uchumi ila ununuzi wa
mwisho kama aina ya uzalishaji. Uzalishaji ni utaratibu, na kwa hivyo hutokea
katika wakati na mahali. Kwa sababu ni dhana ya kufuatana, uzalishaji
hupimwa kama “kiwango cha mazao kwa kipindi cha muda".
Kuna vipengele vitatu katika michakato ya uzalishaji, vikiwemo kiwango cha
bidhaa iliyozalishwa, aina ya bidhaa iliyotengenezwa na usambazaji wa
bidhaa iliyozalishwa kwa mithili ya wakati na mahali. Gharama ya fursa hutoa
pendekezo kuwa kwa kila chaguo, bei ya kweli ya kiuchumi ni fursa bora
zaidi inayofuata. Uchaguzi ni lazima ufanywe baina ya matendo mawili
yanayotamanika lakini ambayo hayawezi kutekelezwa yote kwa pamoja.
Imeelezwa kuwa inayoeleza “uhusiano wa kimsingi baina ya uhaba na
chaguo.".[49]Wazo la gharama ya fursa huwa na jukumu muhimu katika
kuhakikisha kuwa rasilimali hutumika kwa ufanisi.[50] Kwa hivyo, gharama ya
fursa haihusu tu gharama za kihazina au kifedha tu: gharama halisi ya zao la
kutotwaliwa, wakati uliopotezwa, radhi au faida yoyote nyingine ya matumizi
inapaswa kuzingatiwa.
Pembejeo na rasilimali zinazotumiwa katika uzalishaji huitwa vipengele vya
uzalishaji. Pembejeo zinazoweza kutumika huwa kwa kawaida zimewekwa
katika makundi sita. Vipengele hivi ni malighafi, mashine, huduma za kazi,
vifaa vya mtaji, ardhi na kampuni. Kwa muda mfupi, kinyume na muda mrefu,
kwa uchache kimoja kati ya vipengele hivi vya uzalishaji huwa hakibadiliki.
Mifano ni pamoja na vifaa, nafasi ya viwanda inayofaa, na wafanya kazi
muhimu.
Kipengele kinachobadilika katika uzalishaji ni kile ambacho kiwango cha
matumizi yake kinaweza kubadilishwa kwa urahisi. Mifano ni pamoja na
matumizi ya nguvu za umeme, huduma za usafirishaji, na nyingi za
pembejeo za malighafi. Katika hali ya “muda mrefu”, vipengele hivi vyote vya
uzalishaji vinaweza kuratibishwa na wasimamizi. Katika hali ya muda mfupi,
“kadiri ya utendakazi” ya kampuni huamua idadi ya juu zaidi cha mazao
ambao yanaweza kuzalishwa, lakini katika hali ya muda mrefu, hakuna
mpaka wa idadi. Mabadiliko ya jail ya muda mrefu na muda mfupi huwa na
nafasi muhimu katika miundo ya kiuchumi.
Ufanisi wa kiuchumi hueleza ni vipi mfumo unaweza kuzalisha mazao ya
kiwango cha juu zaidi yanayohitajika kwa kutumia utaratibu fulani wa
pembejeo na teknolojia iliyoko. Ufanisi huboreshwa ikiwa mazao mengi
yanazaliswa pasi na kubadili pembejeo, au kwa usemi mwingine, kiwango
cha “msuguano” au “upotevu” kinapunguzwa. Wanauchumi hutafuta ufanisi
wa Pareto, ambao hufikiwa pale mabadiliko hayawezi kumfaidi mtu bila
kumdhuru mtu mwingine.
Ufanisi wa kiuchumi hutumika kuashiria idadi ya dhana ambazo zinahusiana.
Mfumo unaweza kusemwa kuwa na ufanisi wa kiuchumi iwapo: hakuna
atakayefaidika bila kumdhuru mwingine, mazao mengi zaidi hayawezi
kupatikana bila kuongeza kiwango cha pembejeo, na uzalishaji huhakikisha
gharama ya chini zaidi iwezekanavyo kwa kitengo. Fafanuzi hizi za ufanisi
hazina maana inayofanana barabara. Hata hivyo, zimezungukwa zote na
dhana kuwa hakuna kitu zaidi kinachoweza kupatikana kwa kutumia
rasilimali zilizoko.
Umaalumu[hariri | hariri chanzo]
Makala kuu yas: Division of labour, Comparative advantage, and Gains from trade
Umaalumu huchukuliwa kuwa kipengele muhimu kwa ufanisi wa kiuchumi kwa sababu watu au nchi
tofauti huwa na manufaa linganifu. Huku nchi moja inaweza kuwa na manufaa kamili katika sehemu
zote juu ya nchi zingine, inaweza hata hivyo kuwa na umaalumu katika sehemu ambayo kwa
kiwango fulani ina manufaa linganifu, na hivyo kufaidikika kwa kufanya biashara na nchi ambazo
hazina manufaa kamili. Kwa mfano, nchi inaweza kuwa na umaalumu katika uzalishaji wa bidhaa za
kiteknolojia za hali ya juu, kama vile nchi zilizostawi hufanya, na kufanya biashara na mataifa
yanayostawi kwa bidhaa zinazozalishwa katika viwanda, ambapo wafanyakazi hupatikana kwa bei
rahisi na kwa wingi.
Kwa mujibu wa nadharia, katika njia hii bidhaa jumla na utumizi zaidi vinaweza kupatikana kuliko
ikiwa nchi zinazalisha bidhaa zao zenyewe za kiwango cha juu na zile za kiwango cha chini.
Nadharia ya manufaa linganifu huwa san asana ndiyo kigezo cha imani ya mwanauchumi wa
kawaida katika faida ya biashara huru. Dhana hii huhusisha watu binafsi, mashamba,
watengenezaji, watoaji wa huduma, na chumi. Baina kila mojawapo ya mifumo hii ya uzalishaji, kuna
uwezekano wa kuwa na ugavi wa ajira unaohusiana ambapo kila mfanyakazi huwa na kazi tofauti au
hufanya kazi maalumu kama sehemu ya juhudi za uzalishaji, au kwa uhusiano aina tofauti za vifaa
vya mtaji na matumizi tofauti ya ardhi.[51][52][53]
Kitabu cha Wealth of Nations (1776) cha Adam Smith huzungumzia faida za ugavi wa ajira. Smith
alinena kuwa mtu anafaa kuwekeza rasilimali, kwa mfano, ardhi au kazi, ili kuchuma mapato ya juu
yawezekanayo kutokana na uwekezaji huo. Hivyo, matumizi yote ya rasilimali yanafaa kuzalisha
kiwango sawa cha mapato (ambacho kimeratibishwa na athari za kila biashara). La sivyo
ubadilishaji hutokea. Wazo hili, aliandika George Stigler, ndilo shauri kuu la dhana ya kiuchumi, na
kwa sasa huitwa nadharia ya pembezoni ya uzalishaji ya ugavi wa mapato. Mwanauchumi wa
Kifaransa Turgot alikuwa amelizungumzia swala hilo hilo mnamo 1766.[54]
Katika maneno ya kawaida zaidi, kuna nadharia kuwa motisha za soko, ikiwemo bei ya mazao na
pembejeo za uzalishaji, huchagua mgawo wa vipengele vya uzalishaji kwamanufaa linganifu , yaani,
ili kwamba pembejeo za bei ya chini (kwa kiwango fulani) zinatumika ili kumudu chini gharama ya
fursa ya aina fulani ya mazao. Katika mchakato huu, jumla ya mazao huongezeka kama matokeo ya
kutopanga au kwa kukusudia.[55] Umaalumu kama huo wa uzalishaji hubuni fursa kwa faida kutoka
kwa biashara ambapo wenye rasilimali hufaidika kwa biashara kutokana na uuzaji wa aina moja ya
mazao kwa bidhaa zingine, zilizo na thamani kubwa zaidi. Kipimo cha faida kutokana na biashara ni
ongezeko la mazao (rasmi, jumla ya ongezeko la mabaki ya mtumiaji na faida za mzalishaji) kutoka
kwa umaalumu wa uzalishaji na biashara inayofuatia.[56][57][58]
Ugavi na mahitaji[hariri | hariri chanzo]
Supply and demand
alt = A depicting Quantity graph ya X-axis na Price juu ya Y-axis
Nadharia ya mahitaji na ugavi ni kanuni andalizi ya kueleza bei na viwango vya bidhaa ambavyo
vimeuzwa na mabadiliko yanayofuatia katika uchumi wa soko. Katika nadharia ya uchumi wa
kiwango cha chini, huashiria uamuzi wa bei na mazao katika soko lililo na ushindani kamili. Hii
imekuwa ni kigezo muhimu kwa uundaji wa mifumo mingine ya masoko na kwa mielekeo
mingine ya kinadharia.
Kwa soko fulani ya bidhaa, mahitaji huonyesha kiwango ambacho wanunuzi wanaotazamiwa
watakuwa tayari kununua kwa kila kitengo cha bidhaa. Mahitaji mara nyingi huonyeshwa
kwa kutumia jedwali au mchoro unaohusisha bei na kiwango kinachohitajika (tazama
mchoro ulio katika kijisanduku). Nadharia ya mahitaji hueleza wanunuzi wa kibinafsi kama
ambao huchagua kwa kufikiria kiwango ambacho kinatamanika cha kila bidhaa, kulingana
na mapato, bei, mapendeleo, na kadhalika. Maneno yanayotumika kuelezea hali hii ni
‘utumiaji uliozuiwa wa hali ya juu’ (huku mapato yakiwa ndiyo kizuizi kwa mahitaji). Hapa,
utumiaji huashiria (kwa makisio) mapendeleo ya watumiaji wa kibinafsi. Utumiaji na mapato
hutumiwa basi kubuni mali ya kukisia kuhusu athari ya mabadiliko ya bei kwa kiwango
kinachohitajika.
Sheria ya mahitaji husema kuwa, kwa ujumla, bei na kiwango kinachohitajika katika soko
fulani huhusiana kwa kinyume. Yaani, ikiwa bei ya bidhaa ni ya juu, basi watu wachache
zaidi huwa na uwezo au utashi wa kuinunua (ikiwa vitu vingine havibadiliki). Jinsi bei ya
bidhaa inavyoongezeka, ndivyo uwezo wa kununua hupungua (matokeo ya mapato) na
watumiaji huelekea katika bidhaa zenye bei ya chini zaidi (matokeo ya ubadala). Vipengele
vingine vinaweza pia kuathiri mahitaji; kwa mfano kuongezeka kwa mapato kutasogeza
mchirizo wa mahitaji kuelekea upande wa nje kulingana na chanzo, ilivyo katika mchoro.
Ugavi ni uhusiano baina ya bei ya bidhaa ya kiwango kilichopo kwa kuuza kutoka kwa
wasambazaji (kama vile wazalishaji) katika bei hiyo. Ugavi mara nyingi huelezwa kwa
kutumia jedwali au mchoro unaohusisha bei na kiwango kinachosambazwa. Wazalishaji
wanakisiwa kuwa wanaotaka kuzalisha faida ya kiwango cha juu zaidi, kumaanisha
wanajaribu kuzalisha kiwango cha bidhaa ambacho kitawaletea faida ya juu zaidi. Ugavi kwa
kawaida huashiriwa kama uhusiano wa moja kwa moja baina ya bei na kiwango
kilichosambazwa (ikiwa vitu vingine havibadiliki).
Hivi ni kusema kuwa, ikiwa bei ambayo bidhaa inaweza kuuzwa ni ya juu, basi wengi wa
wazalishaji wataisambaza. Bei hii ya juu zaidi hufaidisha kuongezeka kwa uzalishaji. Katika
bei iliyo chini ya msawazo, kuna uhaba wa kiwango kinachosambazwa ikilinganishwa na
kiwango kinachohitajika. Hii inasogeza bei chini. Muundo wa ugavi na mahitaji hutabiri kuwa
kwa kila mchirizo wa ugavi na mahitaji, bei na kiwango vitaimarika kwa bei ambayo itafanya
kiwango kinachosambazwa kuwa sawa na kiwango kinachohitajika. Hii inasogeza bei chini.
[[]]Muundo wa ugavi na mahitaji hutabiri kuwa kwa kila mchirizo wa ugavi na mahitaji, bei na
kiwango vitaimarika kwa bei ambayo itafanya kiwango kinachosambazwa kuwa sawa na
kiwango kinachohitajika. Hii ni katika mkingamo wa michirizo miwili katika mchoro ulio hapa
juu, msawazo wa soko.
Kwa kiwango fulani cha bidhaa, mahali halisi pa bei katika mchirizo wa mahitaji huonyesha
thamani, au utumiaji wa pembezoni kwa watumiaji[59] kwa kitengo hicho cha cha mazao.
Inapima bei ambayo mtumiaji anaweza kuwa tayari kulingana na kitengo cha bidhaa. Mahali
halisi pa bei katika mchirizo wa ugavi hupima gharama ya pembezoni, ongezeko la gharama
ya jumla kwa msambazaji kulingana na kitengo cha bidhaa. Bei katika msawazo huamuliwa
na ugavi na mahitaji. Katika soko lililo na ushindani halisi, ugavi na mahitaji hulinganisha
gharama na thamani katika msawazo.|Katika soko lililo na ushindani halisi, ugavi na mahitaji
hulinganisha gharama na thamani katika msawazo.[60]
Mahitaji na ugavi vinaweza pia kutumika kulinganisha usambazaji wa mapato kwa vipengele
vya uzalishaji, vikiwemo kazi na mtaji, kupitia masoko husika. Katika soko la wafanyakazi,
kwa mfano, idadi ya wafanyakazi walioajiriwa na bei ya kuwalipa (kiwango cha marupurupu)
huonyeshwa kama yaliyowekwa na mahitaji ya kupata wafanyakazi (mahitaji ya makampuni
ya biashara na kadhalika kwa uzalishaji) na utoaji wa ufanyakazi (kutokwa kwa
wafanyakazi).
Mahitaji na ugavi hutumika kueleza tabia ya soko lililo na ushindani kamili. Mahitaji na ugavi
vinaweza kujumuishwa ili kueleza vigezo vinavyobadilika katika uchumi woue, kwa mfano,
kiwango cha mazao yote na hali ya kawaida ya bei, vinavyotafitiwa katika somo la uchumi
wa kiwango cha juu.
Katika uchambuzi wa ugavi na mahitaji, bei ya bidhaa huratibu viwango vya uzalishaji na
utumiaji. Bei na kiwango vimeelezwa kama jinsi zinazoonekana zaidi moja kwa moja katika
bidhaa iliyozalishwa kwa soko.|Bei na kiwango vimeelezwa kama jinsi zinazoonekana zaidi
moja kwa moja katika bidhaa iliyozalishwa kwa soko.[61] Ugavi, mahitaji na msawazo wa soko
ni vigezo vya kinadharia vinavyounganisha bei na kiwango. Lakini kufuatilia athari za
vipengele vinavyotabiriwa kugeuza ugavi na mahitaji – na kupitia kwao, bei na kiwango – ni
zoezi la kawaida katika masomo tendaji ya uchumi wa kiwango cha chini na uchumi wa
kiwango cha juu. Nadharia ya uchumi inaweza kubainisha ni katika mazingira yapi bei huwa
kifaa mwafaka cha mawasiliano cha kuratibu kiwango.[62] Utumiaji katika hali halisi duniani
unaweza kujaribu kupima ni kwa kiwango kipi vigezo vinavyobadilika na vinavyoongeza
ugavi na mahitaji hubadilisha bei na kiwango.
Upembezoni ni matumizi ya dhana za pembezoni katika somo la kiuchumi. Dhana za
pembezoni huhusishwa na badiliko fulani katika kiwango kilichotumika cha bidhaa au
huduma, na wala si wazo la umuhimu unaopita kiasi wa hiyo aina ya bidhaa au huduma, au
wa ujumla wa aina yoyote ile. Dhana kuu ya upembezoni halisi ni ile ya utumiaji wa
pembezoni, lakini wasomi wa dhana hii waliofuata mwongozo wa Alfred Marshall walizidi
kutegemea sana dhana ya uzalishaji wa unaoonekana wa pembezoni katika maelezo yao ya
bei; na mapokeo ya urasimimpya ambao yalitokana na upembezoni wa Uingereza yaliasi
dhana ya utumiaji na kuyapa mabadiliko ya viwango vya pembezoni umuhimu zaidi katika
uchambuzi wao.
Kuanguka kwa soko[hariri | hariri chanzo]
Makala kuu yas: Market failure, Government failure, Information economics, Environmental economics,
and Agricultural economics
alt = A smokestack ikitoa moshi
Maneno “kuanguka kwa soko” hujumuisha matatizo kadha wa kadha ambayo hudhoofisha
fikira za kawaida za kiuchumi. Ingawa wanauchumi huorodhesha kuanguka kwa soko katika
makundi tofauti,[63] makundi yafuatayo hupatikana kutokana na nakala kuu.[64]
Makundi asili yanayotawala shughuli za soko, au dhana zinazoambatana za kundi tawala
“tendaji” au “la ustadi”, huhusisha ulegevu wa ushindani katika kuthibiti wazalishaji. Tatizo hili
huelezwa kama hali ambapo ikiwa bidhaa itaendelea kuzalishwa zaidi, basi mapato
yanakuwa ya kiwango cha juu. Hii humaanishwa kuwa hali hii humfaidi tu mzalishaji mmoja.
Kutolingana kwa habari hutokea pale kikundi kimoja kina maelezo zaidi au bora zaidi kuliko
kingine. Kuwepo kwa kutolingana kwa habari huzua matatizo kama shida za kimaadili, na
uteuzi mbaya, ambayo hutafitiwa katika nadharia ya mkataba. Uchumi wa habari
hufungamana na maswala mengi, ambayo ni pamoja na fedha, bima na sheria ya mkataba,
na maamuzi chini ya hali za hatari na ukosefu wa uhakika.[65]
Masoko yasiyokamilika ni jina ambalo hutumika katika hali ambapo wanunuzi na wauzi
hawana habari ya kutosha kuhusu hali ya mwingine ilikuweza kuweka bei ya bidhaa au
kutoa huduma ipasavyo. Huku kikitokana na makala ya George Akerlof ya Market for
Lemons, kiolezo cha kutoa mfano ni kile cha soko yenye hila ya magari yaliyotumika. Wateja
wasiokuwa na uwezo wa kujua iwapo wananunua “limau” watasukuma bei ya wastani chini
zaidi kuliko ile bei inayostahili kwa ya gari nzuri iliyotumika. Kwa njia hii, bei inaweza
kutoonyesha thamani ya kweli.
Bidhaa za umma ni bidhaa ambazo zina uhaba katika soko la kawaida. Jinsi za kutambua
hali hii ni kuwa watu wanaweza kutumia bidhaa hizi pasi na kuzilipia na kuwa zaidi ya mtu
mmoja anaweza kutumia bidhaa hii kwa wakati mmoja.
Vipengele vya nje huzuka pale ambapo kuna gharama au faida za juu za kijamii kutoka kwa
uzalishaji au utumiaji ambavyo havidhihiriki katika bei za soko. Kwa mfano, uchafuzi wa
hewa unaweza kuzua kipengele cha nje kisichofaa, na elimu inaweza kuzua kipengele cha
nje kilicho na manufaa (kupungua kwa uhalifu, na kadhalika.). Serikali mara nyingi hulipisha
kodi kwa na kuweka vizuizi kwa bidhaa zilizo na vepengele vya nje visivyofaa katika jitihada
za kurekebisha upotovu wa bei unaosababishwa na vipengel hivi vya nje.[66]Nadharia ya
kimsingi ya mahitaji-na-ugavi hutabiri msawazo lakini si kasi ya urekebishaji wa mabadiliko
ya msawazo kutokana na mabadiliko katika mahitaji na ugavi.[67]
Katika sehemu nyingi, aina fulani ya utobadilikaji wa bei hukubalika ili kueleza sababu ya
viwango, na wala si bei, na kurekebisha kwa muda mfupi mabadiliko katika upande wa
mahitaji au ule wa ugavi. Hii hujumuisha uchambuzi wa kawaida wa maisha ya biashara
katika somo la uchumi wa kiwango cha juu. Uchambuzi mara nyingi huhusisha sababu za
kutobadilika huku kwa bei na athari zake katika kufikia msawazo unaokisiwa kwa muda
mrefu. Mifano ya kutobadilika kwa bei katika masoko fulani ni pamoja na viwango vya
marupurupu katika soko la ajira na bei zilizowekwa katika masoko ambayo hayana ushindani
kamili.
Ukosefu wa kuimarika kwa uchumi wa kiwango cha juu, unaozungumziwa hapa chini, ni
chanzo muhimu cha kuanguka kwa soko, ambapo kupotea kwa uthabiti wa biashara kwa
ujumla au mshtuko wan je unaweza kusitisha uzalishaji na usambazaji, na hivyo kudhoofisha
masoko ambayo yalikuwa yameimarika hapo awali.
Baadhi ya masomo yaliyochanganuliwa ya kiuchumi hushughulika na kuanguka kwa masoko
kuliko mengine. Uchumi wa sekta ya umma ni mfano mmoja, kwani iwapo masoko
huanguka, basi aina fulani ya uthibiti au mpango wa serikali ndilo jibu. [[]]Nyingi za chumi za
kimazingira huhusisha vipengele vya nje au “mabaya ya umma".
Aina za sera hujumuisha vithibiti ambavyo huonyesha uchambuzi wa gharama-faida au
ufumbuzi wa masoko ambao hubadili motisha, kama vile ada za uchafuzi wa mazingira au
udhihirishaji upya wa haki za kumiliki mali.[68][69]
Makampuni[hariri | hariri chanzo]
Makala kuu yas: Theory of the firm, Industrial organization, Labour economics, Financial
economics, Business economics, and Managerial economics
alt = watu wawili kukaa saa kompyuta wachunguzi na taarifa
ya fedha
Mojawapo ya fikira kuhusu masoko yaliyo na ushindani kamili ni kuwa kunao wazalishaji
wengi, hamna baina yao anayeweza kushawishi mabadiliko ya bei wala kufanya kazi pasi na
kuzingatia masharti ya soko. Hata hivyo, katika hali halisi, watu hawafanyi biashara tu kwa
soko, huwa wanafanya kazi na kuzalisha katika makampuni. Aina za wazi kabisa za
makampuni ni mashirika, ubia na amana. Kwa mujibu wa Ronald Coase, watu huanza
kupanga uzalishaji wao katika makampuni wakati gharama za kufanya biashara huwa za
chini kuliko wakati wafanyapo shughuli hizi sokoni.[70] Makampuni hujumuisha kazi na mtaji,
na zinaweza kupata faida nyingi zaidi za upanuzi ( wakati kuzalisha vitu viwili zaidi ni nafuu
zaidi kuliko kuzalisha kitu kimoja) kuliko kufanya biashara ya kitu kimoja katika soko.
Uchumi wa ajira hutafuta kuelewa utendakazi wa soko na mienendo ya ajira. Masoko ya ajira
hufanya kazi kupitia kwa mwingiliano wa wafanyakazi na waajiri. Uchumi wa ajira huangalia
watoaji wa huduma za kazi (wafanyakazi), wanaohitaji huduma za kazi (waajiri), na juhudi za
kuelewa mifumo inayotokea ya marupurupu na mapato mengine kutokana na kazi na ya
ajira na ukosefu wa ajira. Matumizi halisi ni pamoja na kusaidia katika ubuni wa utumizi
kamili wa sera.[71]
Mpagilio wa viwanda hutafiti tabia za mikakati ya makampuni, miundo ya soko na
maingiliano yao. Miundo ya kawaida ya masoko iliyotafitiwa ni pamoja na ushindani kamili,
ushindani ulio na kundi moja lililo na sehemu kubwa ya shughuli za sokp, na aina nyingi ya
makundi kadhaa yanayomiliki sehemu kubwa ya soko, na kundi moja linalomiliki sehemu
kubwa ya soko.[72]
Uchumi wa kifedha, huitwao mara nyingi fedha, hushughulika na ugavi wa rasilimali za kifedha
katika mazingira ambayo hayana uhakika (au yaliyo na hatari fulani). Kwa hivyo, zingatio lake ni
katika utendakazi wa masoko ya kifedha, uwekaji wa gharama katika vifaa vya kiuchumi, na miundo
ya kifedha ya makampuni.[73]
Uchumi wa usimamizi hulinganisha uchambuzi wa uchumi wa kiwango cha chini na maamuzi
maalumu katika makampuni ya biashara au vitengo vya usimamizi. Uchumi huu hutegemea sana
sana na mbinu za kujumuisha wingi kama vile utafiti wa utendakazi na utaratibishaji na kutoka kwa
mbinu za takwimu kama vile uchambuzi wa kuridi nyuma katika hali ya ukosefu wa uhakika na
habari kamilifu. Hoja ya kuunganisha ni jaribio la kuimarisha ufanisi wa maamuzi ya kibiashara,
ikiwemo kupunguza iwezekanavyo kwa bei ya kitengo na kuongeza iwezekanavyo kwa faida,
kulingana na malengo ya kampuni na vikwazo vinavyotokana na teknolojia na hali ya soko.[74][75]
Sekta ya umma[hariri | hariri chanzo]
Economics of the public sector and Public finance
Tazama pia: Welfare economics
Fedha za umma ni sehemu ya uchumi ambayo hushughulika na ubuni wa bajeti ya mapato na
matumizi ya kitengo cha sekta ya umma, kwa kawaida serikali. Mada hii hushughulikia maswala
kama vile malipo ya ushuru (ni nani hasa analipa ushuru fulani), uchambuzi wa gharama-faida
wa mipango ya serikali, athari juu ya ufanisi wa kiuchumi na ugavi wa mapato katika aina tofauti
za matumizi na ushuru, na siasa za kifedha. Jambo hili la mwisho, ambalo ni kipengele cha
nadharia ya chaguo ya umma, hubuni tabia ya sekta ya umma kama mfano wa uchumi wa
kiwango cha chini, unaohusisha maingiliano ya wapiga kura wanaojali maslahi yao wenyewe,
wanasiasa, na wafanyakazi wa serikali au mashirika mengine.[76]
Wingi wa uchumi ni wa manufaa, kwani hutafuta kueleza na kutabiri matukio ya kiuchumi.
Uchumi wa kuamua thamani (normative economics) hujihusisha na kubaini lililo zuri au baya
kiuchumi.
Uchumi wa ustawi ni tawi la uchumi wa kuamua thamani unaotumia ustadi wa uchumi wa
kiwango cha chini ili kubainisha kwa wakati huo huo ufanisi wa ugavi katika uchumi na ugavi wa
mapato unaohusishwa nao. Huwa unajaribu kupima ustawi wa jamii kwa kuchunguza shughuli
za kiuchumi za watu wanaobuni jamii.[77]
Uchumi wa kiwango cha juu[hariri | hariri chanzo]
alt = A graph depicting "Mzunguko katika Microeconomics"
Makala kuu ya: Macroeconomics
Uchumi wa kiwango cha juu huchunguza uchumi mzima ilikueleza mikusanyiko mipana na
mwingiliano wao “kutoka juu hadi chini,” yaani, kwa kutumia aina iliyorahisishwa ya nadharia ya
msawazo wa ujumla.[78] Mikusanyiko kama hiyo ni pamoja na mapato na mazao ya kitaifa, kiwango
cha ukosefu wa ajira, na mfumuko wa bei na mikusanyiko midogo kama jumla ya matumizi na
matumizi ya uwekezaji na vipengele vyake. Somo hili hutafiti pia athari za sera ya hazina na sera ya
kifedha.
Tangu angalau miaka ya 1960, uchumi wa kiwango cha juu umekuwa na ujumuishaji zaidi na hivyo
kuwa na sekta za aina ya uchumi wa kiwango cha chini, ikiwemo uwiano wa akili wa washikadau,
utumiaji wa ufanisi wa habari ya soko, na ushindani usio kamilifu.[79]Jambo hili huzungumzia
wasiwasi wa muda mrefu juu ya ukosefu wa uthabiti katika maendeleo ya mada hiyo hiyo.[80]
Uchambuzi wa uchumi wa kiwango cha juu huzingatia vipengele vinavyoathiri kiwango cha muda
mrefu na ukuaji wa mapato ya kitaifa. Vipengele kama hivyo ni pamoja na ukusanyaji wa mtaji,
mabadiliko ya kiteknolojia na ukuaji idadi ya wafanyakazi.[81][82]
Ukuaji[hariri | hariri chanzo]
alt = A dunia ramani na nchi mwekundu katika vivuli
tofauti ya machungwa
Makala kuu yas: Economic growth and General equilibrium
Uchumi wa ukuaji hutafiti vipengele vinavyoeleza ukuaji wa kiuchumi – ongezeko la pembejeo kwa
kila mkazo wa nchi katika muda mrefu. Vipengele hivyo hivyo hutumika kueleza tofauti
katika kiwango cha mapato kwa mtu baina ya nchi, hasa kwa nini baadhi ya nchi hukua kwa kasi
kuliko zingine, na ikiwa nchi hukutana katika viwango sawa vya ukuaji.
Vipengele vilivyochunguzwa zaidi ni pamoja na viwango cha uwekezaji, ukuaji wa idadi ya watu, na
mabadiliko ya kiteknolojia. Vipengele hivi huwakilishwa katika namna ya nadharia au ujarabati
(kama ilivyo katika miundo ya urasimimpya na ukuaji wa kindani) na katika ukuaji wa uhasibu.[83][84]
Mzunguko wa Biashara[hariri | hariri chanzo]
Makala kuu ya: Business cycle
Tazama pia: Circular flow of income, Aggregate supply, Aggregate
demand, Unemployment, na Great Depression
Uchumi wa unyogofu ndio ulikuwa kichocheo cha ubuni wa “uchumi wa kiwango cha juu” kama
kitengo tofauti cha somo la uchumi. Wakati wa Unyogofu Mkuu wa miaka ya 1930, John Maynard
Keynes aliandika kitabu kiitwacho The General Theory of Employment, Interest and
Money ambacho kiliorodhesha nadharia muhumu za uchumi wa Keneshia. Keynes alishikilia kuwa
mahitaji ya jumla kwa bidhaa yanaweza kutotosha katika nyakati za kurudi nyuma katika ukuaji wa
kiuchumi, huku matokeo yake yakiwa ni ukosefu wa ajira wa kiwango cha juu sana na ukosefu wa
mapato yaliyokisiwa.
Kwa hivyo alitetea kuwekwa kwa sera tendaji na sekta ya umma, kukiwemo kuwekwa kwa sera ya
hazina na benki kuu na kuwekwa kwa sera ya kifedha na serikali ili kuimarisha mapato katika muda
wa mzunguko wa biashara.[85] Kwa hivyo, hitimisho muhimu la uchumi wa Keneshia ni kuwa, katika
hali fulani, hakuna ustadi wa moja kwa moja unaosogeza mapato na ajira kuelekea viwango vya
uwepo wa ajira kwa wafanyakazi wote. Muundo wa John Hicks wa IS/LM umekuwa ndiyo tafsiri
yenye ushawishi mkuu zaidi wa Nadharia ya Kiujumla.
Jinsi miaka imeendelea kupita, ndivyo kueleweka kwa mzunguko wa biashara kumegawika katika
matawi mbalimbali ya mawazo, yanayohusika na au kutofautiana na Ukeneshia. [[]]Muhtasari wa
urasimimpya huashiria mapatano ya uchumi wa Keneshia na ule wa urasimimpya, huku ukisema
kuwa Ukeneshia unafaa katika muda mfupi, huku uchumi ukifuata nadharia ya urasimimpya katika
muda mrefu.
[[]]Mfumo wa Mpya wa urasimi hukosoa maoni ya Keneshia juu ya mzunguko wa kibiashara.
Unahitimisha kuwa dhana ya Friedman ya mapato ya kudumu juu ya matumizi, “mageuzi ya
matarajio yaendayo na mawazo"[86] yaliyoongozwa na Robert Lucas, na nadharia ya mzunguko halisi
wa biashara.
Kwa kinyume, mfumo Mpya wa Keneshia hushikilia matarajio ya kimawazo, ingawa hushikilia aina
mbalimbali za kuanguka kwa masoko. Ukeneshia Mpya hasa hushikilia kuwa bei na marupurupu
“havibadiliki”, kumaanisha kuwa havibadiliki moja kwa moja kulingana na hali ya kiuchumi.
Kwa hivyo, urasimi mpya hushikilia kuwa bei na marupurupu hufikia ajira kwa kila mtu moja kwa
moja, huku Wakeneshia wapya huona ajira kwa watu wote ikifikiwa tu baada ya muda mrefu, na
hivyo kuhitaji sera za serikali na benki kuu kwa sababu “muda mrefu” haupo mbali sana.
Mfumuko wa bei na sera ya kifedha[hariri | hariri chanzo]
Makala kuu yas: Inflation and Monetary policy
Tazama pia: Money, Quantity theory of money, Monetary policy, History of money, na Milton
Friedman
alt = mbele na nyuma ya sarafu. A kiumbe's kichwa ni juu ya mbele.
Pesa ni njia ya malipo ya mwisho ya bidhaa katika mingi ya mifumo ya bei na kitengo cha akaunti
ambacho hutumika kwa kawaida kwa kuweka bei. Hujumuisha sarafu ambazo zinashukiliwa na
umma usio benki na amana ambazo zinaweza kulipwa na pesa. Mfumo huu umeelezwa kuwa
mkataba wa kijamii, kama lugha, inayofaa mmoja kwa sababu inawafaa wengine.
Kama chombo cha ubadilishanaji, pesa huwezesha biashara. Kazi yake ya kiuchumi inaweza
kutofautishwa na ubadilishanaji wa bidhaa (ubadilishanaji ambao hauhusishi pesa). Huku kukiwa na
aina tofauti tofauti za bidhaa zilizozalishwa na wazalishaji maalum, ubadilishanaji wa bidhaa
unaweza kuhitaji bahati mara dufu ambayo ni ngumu kupata kulingana na vitu vya kubadilisha, kwa
mfano tufaha na kitabu. Pesa inaweza kupunguza gharama ya ubadilishanaji kwa sababu ya
kukubalika kwake kwa urahisi. Hivyo, huwa ni nafuu zaidi kwa muuzaji kukubali pesa katika
ubadilishanaji, kuliko mazao ambayo mnunuzi huzalisha.[87]
Katika kiwango cha uchumi, nadharia na ushahidi vinalingana sawa sawa na uhusiano wa manufaa
unaotoka kwa jumla ya usambazaji wa pesa kelekea kwa bei ya siku hiyo na jumla ya mapato na
kiwango cha bei ya kawaida. Kwa sababu hii, usimamizi wa usambazaji wa pesa ni kipengele
muhimu cha sera ya kifedha.[88][89]
Sera ya hazina na uratibishaji[hariri | hariri chanzo]
Makala kuu yas: Fiscal policy, Government spending, Regulation, and National accounts
Uhasibu wa kitaifa ni mbinu ya kujumlisha mkusanyiko wa shughuli za kibiashara katika taifa.
Akaunti za taifa ni mifumo ya uhasibu ya ncha mbili za kuweka hesabu ambayo hutoa hatua za
kiundani zilizo na maelezo bayana kama hayo. Akaunti hizi ni pamoja na akaunti za kitaifa za
mapato na bidhaa (NIPA), ambazo hutoa makadirio ya thamani ya pesa ya mazao na mapato kwa
mwaka au robo.
NIPA huruhusu kufuatilia kwa utendakazi wa uchumi na vipengele vyake kupitia kwa mizunguko ya
kibiashara au katika vipindi virefu zaidi. Takwimu za bei zinaweza kuruhusu kutofautisha kwa bei ya
siku kutoka kwa bei halisi, yaani, kurekebisha jumla ya pesa kwa mabadiliko ya bei kupitia vipindi
vya nyakati.[90][91] Akaunti za kitaifa hujumuisha pia kipimo cha mitaji ya hisa, utajiri wa taifa, na
mtiririko wa mtaji wa kimataifa.[92]
Uchumi wa kimataifa[hariri | hariri chanzo]
Makala kuu yas: International economics and Economic system
Biashara ya kimataifa hutafiti vigezo vya mtiririko wa bidhaa-na-huduma kupitia mipaka ya kimataifa.
Hushughulika pia ukubwa na usambazaji wa faida kutoka kwa biashara. Utendakazi wa sera
hujumuisha kukisiwa kwa kubadilika kwa viwango vya ushuru na sehemu ya haki ya kibiashara.
Fedha ya kimataifa ni kitengo cha uchumi wa kiwango cha juu kinachodadisi mtiririko wa mtaji
kupitia mipaka ya kimataifa, na athari za mabadiliko katika viwango vya ubadilishaji. Kuongezeka
biashara ya bidhaa, huduma na mtaji baina ya nchi ni athari kuu ya utandawazi wa leo.[93][94][95]
alt = A dunia ramani na nchi mbalimbali colored colors.
Kitengo tofauti cha uchumi wa ustawi huchunguza vipengele vya uchumi vilivyo katika mchakato wa
ustawi katika nchi zilizo na mapato ya chini huku kikizingatia kwa ubadilishaji wa mifumo, ufukara,
na ukuaji wa uchumi. Mielekeo katika uchumi wa ustawi mara nyingi hujumuisha vipengele vya
kijamii na vya kisiasa.[96][97]
Mifumo ya kiuchumi ni tawi la uchumi linalotafiti mbinu na taasisi ambazo jamii hutumia kubaini
umiliki, usimamizi, na ugavi wa rasilimali za kiuchumi. Mfumo wa kiuchumi wa jamii ni kitengo cha
utafiti.
Katika mifumo ya kisasa katika nchi tofauti za upindi wa uratibishaji ni mifumo ya kisoshialisti na
kikapitalisti, ambako wingi wa uzalishaji hutokea katika mashirika yanayosimamiwa na serikali na
yale ya kibinafsi mtawalia. Baina ya makundi haya mawili kunao chumi zilizochanganyika. Jambo
linalotokea katika makundi haya yote ni mwingiliano vishawishi vya kiuchumi na kisiasa, ambavyo
huelezwa kwa upana kuwa uchumi wa kisiasa. Mifumo linganifu ya kiuchumi hutafiti utendakazi na
tabia ya chumi au mifumo tofauti.[98][99]
Uchumi katika utekelezi[hariri | hariri chanzo]
Makala kuu yas: Mathematical economics, Economic methodology, and Schools of economics
Uchumi wa sasa uliotanda, kama kitengo rasmi cha mifano cha hisabati, unaweza pia kuitwa uchumi
wa kihisabati.[100] Uchumi huu hutegemea vifaa vya masomo ya kihisabati ya calculus, linear algebra,
takwimu, nadharia ya bahati, na sayansi ya kompyuta.[101] Wanauchumi wa kitaalamu hutarajiwa
kujua vifaa hivi, ingawa wanauchumi wote huwa na utaalamu, na baadhi yao huwa wataalamu wa
uchumikihisabati na mbinu za kihisabati huku wengine wakiwa wataalamu katika vitengo vingine
ambavyo havina hesabu nyingi.
Wanauchumi wa mfumo wa heterodox hutilia hisabati msisitizo mchache, na baadhi ya wanauchumi
wa kihistoria, wakiwemo Adam Smith na Joseph Schumpeter, hawajakuwa wanahisabati. Mawazo
ya kiuchumi huhusisha ujuzi wa akili kuhusu dhana za kiuchumi, na wanauchumi hujaribu
kuchambua hadi pale wanagundua matokeo ambayo hayakutarajiwa.
Nadharia[hariri | hariri chanzo]
Nadharia ya uchumi iliyotanda hutegemea mifumo ya kiuchumi ya kihisabati ambayo haitegemei
uzoevu, ambayo hutumia dhana kadha wa kadha. Nadharia huendelea mbele na wazo la vipengele
vingine vikibaki vilivyo, ambalo humaanisha kumudu vipengele vingine jinsi vilivyo ila kile kimoja
kinachozingatiwa. Katika kubuni nadharia, lengo ni kupata zile ambazo kwa uchache ni rahisi kwa
matakwa ya habari, sahihi zaidi katika utabiri wake, na za faida kubwa katika uzalishaji wa utafiti
zaidi kuliko nadharia zilizokuwepo awali.[102]
Katika uchumi wa kiwango cha chini, dhana kuu ni pamoja na ugavi na mahitaji, upembezoni,
nadharia ya chaguo la kutokana na mawazo, gharama ya fursa, vikwazo vya kibajeti, utumiaji na
nadharia ya kampuni.[103][104] Mifumo ya mapema ya uchumi wa kiwango cha juu ilizinhatia kubuni
uhusiano baina ya vipengele jumuishi, lakini kwa vile uhusiano ulionekana kubadilika katika wakati
wanauchumi walishurutishwa kutumia wakfu za kiwango cha chini kama msingi wa mifumo yao.
Dhana za uchumi wa kiwango cha chini ambazo zimekwishatajwa huwa na nafasi muhimu katika
mifumo ya uchumi wa kiwango cha juu – kwa mfano, katika nadharia ya kifedha, nadharia ya
viwango ya pesa hutabiri kuwa kuongezeka katika usambazaji wa pesa huongeza mfumuko wa bei,
na mfumuko wa bei hufikiriwa kushawishika na matarajio ya kifikira. Katika uchumi wa ustawi, ukuaji
wa polepole katika mataifa yanayostawi unetabiriwa mara nyingine kwa sababu ya kupungua kwa
mapato ya pembezoni kutoka kwa uwekezaji na mtaji, na hali hii imeonekana katika mataifa manne
ya Kiasia yajulikanayo kama Four Asian Tigers. Mara nyingine dhana ya kiuchumi huwa tu ni
ya kueleza jinsi ya kitu na wala si ya kihisabati. [105]
Maonyesho ya kubainisha fikira za kiuchumi mara nyingi hutumia michoro ya pande mbili ili
kuonyesha husiano za kinadharia. Katika kiwango cha juu cha ujumuishaji, maandishi ya Paul
Samuelson Foundations of Economic Analysis (1947) yalitumia mbinu za kihisabati kueleza
nadharia, hasa jinsi ya kuweka kwa kiwango cha juu zaidi uhusiano wa kitabia wa vipengele tekelezi
ili kufikia msawazo. Kitabu hicho kilizingatia kuchunguza kundi la taarifa lijulikanalo kama semi za
kinadharia zenye maana katika utekelezi katika uchumi, ambazo ni semi za kinadharia ambazo
zinaweza kupingwa na takwimu za ujarabati.[106]
Utafiti wa ujarabati[hariri | hariri chanzo]
Makala kuu yas: Econometrics and Experimental economics
Nadharia za kiuchumi mara nyingi huchunguzwa kijarabati, sanasana kwa kutumia uchumukihisabati
kutumia takwimu za kiuchumi.[107] Majaribio ya kuthibitiwa yanayopatikana sanasana katika sayansi
za kiasili ni magumu na hayapatikana sana katika somo la kiuchumi[108],na badala yake takwimu za
upana hutafitiwa kwa kufanyiwa uchunguzi; aina hii ya uchunguzi huonekana na wengi kuwa rahisi
kuliko ile ya majaribio ya kuthibitiwa, na mahitimisho huwa kwa kawaida yasiyo na uhakika kamili.
Idadi ya sheria zilizovumbuliwa na somo la kiuchumi ni ya chini ikilinganishwa na ile ya sayansi
asilia.[onesha uthibitisho]
[[]]Mbinu za kutumia takwimu kama vile uchambuzi wa kurudi nyuma ni za kawaida. Watekelezaji
hutumia mbinu kama hizo kukisia ukubwa, umuhimu wa kiuchumi, na umuhimu wa takwimu (“nguvu
za ishara”) za mahusiano yaliyokisiwa na kuratibisha kelele kutoka kwa vipengele vingine. Kwa njia
hiyo, dhana inaweza kukubaliwa, ingawa kwa jinsi ya makisio na wala si uhakika. Kukubalika
hutegemea dhana zinazoweza kuwekewa uongo ambazo zilimudu majaribio. Utumiaji wa mbinu
zinazokubalika kwa kawaida hauna haja ya kutoa hitimisho la mwisho. Au hata makubaliano juu ya
swala fulani, ikiwa lilikuwa na majaribio tofauti, takwimu tofauti , na imani za awali.
Ukosoaji unaolenga viwango vya kitaalamu na ukosefu wa kufanana katika matokeo huwa ni
masharti zaidi dhidi ya uonevu, upotovu, na ujumuisha wa kiwango cha juu mno,[104][109] ingawa wingi
wa utafiti wa kiuchumi umekosolewa kwa ukosefu wa kufanana katika matokeo, na nakala za
kifahari zimekosolewa kwa kutowezesha urudiaji wa matokeo yaliyofanana kwa kutoa nambari za
kificho na takwimu.[110] Kama ilivyo katika nadharia, matumizi ya takwimu za majaribio huwa
yamefunguka yenyewe kwa uchambuzi wa kukosolewa,[111][112][113] ingawa ufafanuzi muhimu wa
nakala juu ya uchumi katika jedwali za kifahari kama vile American Economic Review umepungua
kwa kiwango kikubwa katika miaka 40 iliyopita.[114] .[116] Jambo hili limehusishwa na motisha ya
majedwali ya kutaka kuongeza nukuu ili kuorodheshwa katika nafasi nzuri kwenye Fahirisi ya Nukuu
za Sayansi ya Kijamii - Social Science Citation Index (SSCI).[115]
Katika uchumi tekelezi, mifumo ya pembejeo na mapato itumiayo mbinu za utaratibishaji wa
kunyooka (linear programming) ni ya kawaida mno. Viwango vikubwa vya takwimu hupitishwa katika
mipangilio ya kompyuta ili kuchambua matokeo ya sera fulani; IMPLAN ni mfano mmoja maarufu.
Uchumi wa majaribio umeimarisha utumiaji wa majaribio ya kuthibitiwa ya kisayansi. Hali hii
imepunguza tofauti ya kutoka jadi baina ya uchumi na sayansi asili wa kukubalia majaribio ya
vipengele vilivyofikiriwa hapo awali kuwa dhana.[116][117] Katika visa kadhaa majaribio haya
yamegundua kuwa dhana huwa si sahihi hasa; kwa mfano mchezo wa hatima ulionyesha kuwa watu
hukataa matoleo ambayo hayatoshani.
Katika uchumi wa kitabia, wanasaikolojia Daniel Kahneman na Amos Tversky wameshinda Matuzo
ya Nobel ya kiuchumi kwa kazi ya uvumbuzi wa kijarabati wa uonevu wa kimawazo na jibu lililo
karibu zaidi na jibu halisi (heuristics). Majaribio ya ujarabati yanayofanana na hayo hufanywa katika
somo la uchumi wa kiubongo (neuroeconomics). Mfano mwingine ni wazo la chaguzi za kibinafsi
dhidi ya mfumo ambao huchunguza chaguzi binafsi, za kutaka ustawi wa wengine na za ushirikiano.[118][119] Ustadi huu umesababisha wengine kusema kuwa uchumi ni “sayansi halisi.".[9]
Nadharia ya bahati[hariri | hariri chanzo]
Makala kuu ya: Game theory
Nadharia ya bahati ni tawi la hisabati tekelezi ambalo hutafiti mwingiliano wa mbinu baina ya
vipengele tekelezi. Katika mbinu za bahati, vipengele tekelezi huchagua mbinu ambazo zitaongeza
mapato yao, ukilinganisha na mbini ambazo vipengele vingine huchagua. Nadhari hii hutoa mfumo
rasmi wa mwelekeo kwa hali za kijamii ambapo wafanya maamuzi huingiliana na watendaji wengine.
Nadharia ya bahati hujumuishwa mielekeo ya kuongeza yaliyobuniwa ili kutafiti soko kama vile
mfumo wa ugavi na mahitaji. Somo hili lilitokana na kitabu cha urasimi cha 1944 kiitwacho Theory of
Games and Economic Behavior kilichoandikwa na John von Neumann na Oskar Morgenstern. Somo
hili limepata utekelezi wa kiwango kikubwa kiasi katika sehemu nyingi nje ya uchumi vile
inavyofikiriwa, ambayo ni pamoja na ubuni wa ustadi wa kinyuklia, maadili, sayanzi ya kisiasa na
nadharia ya mageuzi.[120]
Taaluma[hariri | hariri chanzo]
Makala kuu ya: Economist
Kufanywa taaluma kwa uchumi, jinsi inavyoonekana katika ongezeko la masomo ya daraja ya pili ya
vyuo vikuu katika somo hilo, kumeelezwa kuwa “badiliko kuu katika somo la uchumi tangu miaka ya
1900".[121] Idadi kubwa ya vyuo vikuu vya kutajika na taasisi nyingi huwa na somo kuu, kitivo, au
idara kuu ambapo shahada za kielimu hutolewa katika somo hili, iwe ni kwa masomo ya sanaa
huria, biashara, au kwa masomo ya taaluma.
Tuzo la Bank of Sweden Prize in Economic Sciences in Memory of Alfred Nobel (kwa usemi, Tuzo la
Nobel katika Uchumi) ni tuzo ambalo hutolewa kwa mwanauchumi kila mwaka kwa mchango mkuu
wa kimawazo katika somo hili. Katika sekta ya kibinafsi, wanauchumi wataalamu huajiriwa kama
washauri na katika sekta, inayojumuisha uhifadhi katika benki na maswala ya kifedha. Wanauchumi
pia hufanya kazi katika idara na mashirika ya serikali, kama vile Hazina ya kitaifa, Benki Kuu au Afisi
ya Takwimu.
Somo la uchumi na masomo mengine[hariri | hariri chanzo]
Makala kuu yas: Philosophy of economics, Law and Economics, Political economy, and Natural
resource economics
Uchumi ni mojawapo ya sayansi za kijamii baina ya zingine kadhaa na huwa na matawi
yanayopakana na masomo mengine, yakiwemo jiografia ya kiuchumi, historia ya kiuchumi, uchaguzi
wa umma, uchumi na nisharti, uchumi wa utamaduni, na uchumi wa taasisi.
Sheria na uchumi au utafiti wa kiuchumi wa sheria, ni mwelekeo wa nadharia ya kisheria ambao
hutumia mbinu za kiuchumia katika sheria. Somo hili hujumuisha utumizi wa dhana za kiuchumi ili
kueleza athari za kanuni za kisheria, kubainisha ni kanuni zipi za kisheria zilizo na ufanisi wa
kiuchumi, na kutabiri ni kanuni za kisheria zinazweza kuwa.[122][123] Makala ya mafundisho
yaliyoandikwa na Ronald Coase na kuchapishwa mnamo 1961 yalipendekeza kuwa sheria za umiliki
wa mali zilizodhihirishwa vyema hushinda matatizo yanayotokana na vipengele vua nje.[124]
Uchumi wa kiasiasa ni utafiti unaojumuisha masomo mengi kwa kuchanganya uchumi, sheria, na
sayansi ya kisiasa ili kueleza jinsi taasisi za kisiasa , mazingira ya kisiasa, ma mfumo wa kiuchumi
(ukapitalisti, usoshialisti, mchanganyiko) hushawishiana. Unatafiti maswali kama vile jinsi makundi
yanayotawala shughuli za soko, tabia ya kutafuta manufaa ya kibinafsi kwa madhara ya wengine, na
vipengele vya nje vinafaa kuathiri sera ya serikali.[125][126] Wanahistoria wametumia uchumi wa
kisiasa kutafiti njia za wakati uliopita ambazo watu na makundi yaliyo na maslahi yanayofanana ya
kiuchumi wametumia siasa ili kuleta mabadiliko ambayo yanafaidi maslahi
yao. UNIQc30d0a039b59f51f-nowiki-00000188-QINU127UNIQc30d0a039b59f51f-nowiki-00000189-� � �
QINU �
Uchumi wa nishati ni sehemu pana ya somo la kisayansi inayojumuisha mada zinazohusiana na
ugavi wa nishati na mahitaji ya nishati. [[]]Georgescu-Roegen alianzisha upya dhana ya entropy
aliyoihusisha na uchumi na nishati kutoka kwa somo la ubadilishaji wa nishati la thermodynamics,
huku akiitofautisha na kile alichoona kuwa msingi wa kiufundi wa uchumi wa urasimimpya
unaotokana na fizkia ya Newton. Kazi yake ilichangia kwa kiwango kikubwa kwa somo la uchumi wa
kubadilisha nishati kuwa kazi na joto na kwa uchumi wa kiikolojia. Vilevile alifanya kazi ya kimsingi
ambayo iliendelea na kuwa uchumi wa mageuzi.[128][129][130][131][132]
Ukosoaji wa somo la kiuchumi[hariri | hariri chanzo]
[[]]"Sayansi duni” ni jina badala lililo la kudharau litumikalo kwa uchumi na lililobuniwa na
mwanahistoria wa enzi ya Victoria Thomas Carlyle katika karne ya 19. Mara nyingi, husemekana
kuwa Carlyle aliupatia uchumi jina la utani la “sayansi duni” kama jibu kwa maandishi karne ya 18 ya
Reverend Thomas Robert Malthus, ambaye alitabiri kwa hofu kuwa njaa ingetokea, vile matarajio ya
ukuaji wa idadi ya watu yangezidi ongezeko la usambazaji wa chakula. Mafundisho ya Malthus
hatimaye yalijulikana chini ya mwavuli wa maneno “Dhana Duni ya Malthus". Utabiri wake ulisitishwa
na uboreshaji mkubwa ambao haukuwa umetarajiwa katika ufanisi wa uzalishaji wa vyakula katika
karne ya 20; ilhali mwisho wa hatari ambao aliutabiri unabaki kuwa uwezekano ambao haukubaliki
na wengine, ikiwa uzuli wa binadamu utashindwa kumudu ongezeko la idadi ya watu.[133]
Baadhi ya wanauchumi kama vile John Stuart Mill au Leon Walras, wamedumisha fikira kuwa
uzalishaji wa mali haufai kuunganishwa na usambazaji wake. Uzalishaji ni kitengo cha “uchumi
tekelezi” huku usambazaji ukiwa ni aina ya “uchumi wa kijamii” na sana sana huwa ni swala la
mamlaka na siasa.[134]
Katika The Wealth of Nations, [[]]Adam Smith anazungumzia maswala mengi ambayo kwa sasa ni
mada ya mjadala na mabishano. Smith alishambuliwa mara kadhaa makundi ya watu waliojihusisha
na siasa ambao hujaribu kutukia ushawishi wao kuishurutisha serikali kufanya vile watakavyo.
Katika enzi ya Smith, haya yaliitwa makundi ya wafitini, lakini kwa sasa hujulikana sana kama
maslahi maalum, jina ambalo linaweza kujumuisha wafanyakazi wa mabenki, mashirika ya
makampuni, makundi yanayotawala kwa wazi shughuli za soko, kikundi kimoja kinachotawala
shughuli za soko, vyama vya wafanyakazi na makundi mengine.[135]
Uchumihalisi, kama sayansi ya kijamii, huwa huru kutoka kwa vitendo vya kisiasa vya serikali yoyote
au mashirika mengine yanayofanya uamuzi, hata hivyo, wabuni wengi wa sera au watu binafsi walio
na vyeo vikubwa sana ambavyo vinaweza kuwa na ushawishi katika maisha ya watu wengine wana
sifa ya kutumia bila mpangilio wowote dhana nyingi sana za kiuchumi na maneno matupu kama
chombo cha kuhalalisha ajenda na mifumo ya maadili, na huwa hawakomeshi usemi wao kwa
maswala yanayohusu majukumu waliyo nayo.[onesha uthibitisho] wa karibu wa nadharia na utekelezi wa
kiuchumi na siasa [136] [138] ni swala la utata ambalo linaweza kuingilia au kupotosha hata yale
malengo ya kiuchumi yasiyo na madai hata kidogo, na huchanganyishwa mara nyingi na ajenda
maalum za kijamii na mifumo ya maadili.[137]
Katika Steady State Economics 1977, Herman Daly alisema kuwa kunao maswala ambayo
hayawiani kimantiki baina ya msisitizo unaowekwa kwa ongezeko la idadi ya watu na upatikanaji
mdogo wa maliasilia. UNIQc30d0a039b59f51f-nowiki-000001A9-QINU138UNIQc30d0a039b59f51f-� � �
nowiki-000001AA-QINU �
Maswala kama uhuru wa benki kuu, sera za benki kuu na ufasaha wa kunena katika usemi wa
magavana wa benki kuu au nguzo za sera za uchumi wa kiwango cha juu[139] (fedha na sera ya
fedha) ya Marekani, ni mwelekeo wa msuguano na kukosolewa. [140] [141] [142] [143]
Deirdre McCloskey amesema kuwa utafiti mwingi wa kijarabati wa kiuchumi huripotiwa visivyofaa,
na ingawa ukosoaju wake umepokelewa vyema, yeye na Stephen Ziliak wamedai kuwa utekelezaji
haujaboreshwa. UNIQc30d0a039b59f51f-nowiki-000001BB-QINU144UNIQc30d0a039b59f51f-� � �
nowiki-000001BC-QINU � Madai haya ya nyuma ni ya utata.[145]
Utafiti wa shirika la International Monetary Fund wa mwaka wa 2002 ulizingatia “utabiri wa
makubaliano” (utabiri wa makundi makubwa ya wanauchumi) ambao ulifanywa awali kabla ya kurudi
nyuma kwa uchumi kwa mataifa 60 tofauti katika miaka ya 90; katika 97% ya visa wanauchumia
hawakutabiri mpunguo kwa mwaka mmoja kabla ya tukio. Katika visa vile vya nadra ambako
wanauchumi walitabiri kwa mafanikio kurudi nyuma kwa uchumi, walikadiria makali yake kwa
kiwango cha chini mno.[146].
Ukosoaji wa dhana[hariri | hariri chanzo]
Uchumi umekuwa mada ya ukosoaji hadi hutegemea dhana ambazo hazina uhakika, haziwezi
kuthibitishwa na zimerahisishwa visivyofaaa, kwa wakati mwingine kwa sababu dhana hizi hutumia
hisabati zinazovutia. Mifano ni pamoja na habari kamilifu, uimarishaji wa faida kwa kiwango cha juu
zaidi na chaguzi za kimawazo.[147] [148][149] Baadhi ya nadharia za kisasa za kiuchumi zimezingatia
kuzungumzia matatizo haya kupitia kwa matawi madogo ya somo hili yanayoibuka kama vile uchumi
wa taarifa, uchumi wa tabia, na uchumi wa utata, huku Geoffrey Hodgson akitabiri mabadiliko
makubwa katika mwelekeo uliotanda wa kiuchumi.[150] Hata hivyo, wanauchumi maarufu wa uchumi
uliotanda kama vile Keynes[151]na Joskow, pamoja na wanauchumi wa kiheteredoksi, wametoa
maoni kuwa kiwango kikubwa cha uchumi huwa ni cha kidhana na wala si cha kihisabati, na huwa ni
vigumu kuweka mifumo na kuurasmisha kwa kutumia mbinu za kihisabati. Katika majadiliano juu ya
utafiti wa makundi ya kutawal shughuli za soko, Paul Joskow alionyesha mnamo 1975 kuwa katika
utekelezi, wanafunzi wenye bidii wa uchumi halisi, huwa na mazoea ya kutumia “mifumo isiyo rasmi”
inayotokana na vipengele vya maelezo ambavyo hutumiwa katika sekta maalum. Joskow aliamini
sana kuwa kazi muhimu ya kutafiti makundi yanayotawala shughuli za soko ilifanya kupitia
uchunguzi usio rasmi huku mifumo rasmi ilikuwa “ikionyeshwa kwa madaha baada
yakazi kumalizika ". Alidai kuwa mifumo rasmi kwa kiasi kikubwa haikuwa na maana katika kazi ya
ujarabati, vilevile, na kuwa kipengele muhimu kilicho msingi wa nadharia ya kampuni, tabia,
kilipuuzwa.[152]
Licha ya wasiwasi huu, masomo ya daraja ya pili ya vyuo vikuu yameendelea kuwa ya kiufundi na
kihisabati.[153] Ingawa nyingi ya kazi ya kimsingi ya utafiti wa kiuchumi katika historia ulihusu dhana
na wala si hisabati, kwa sasa huwa ni vigumu zaidi kupata uwezekano wa kuchapisha nakala isiyo
ya kihisabati katika jedwali mashuhuri.[154] Kuona ukweli kwa upande wa baadhi ya wanafunzi
kuhusu kuzingatia kwa uchumi kwa vitu ambavyo haviwezi kushikika na vya ufundi kumesababisha
kuzuka kwa kundi la uchumi wa baada ya hali ya autism, ambao ulianza Ufaransa mnamo 2000.
[[]]David Colander, mtetezi wa uchumi tata, amezungumzia vilevile kwa kukosoa mbinu za kihisabati
za kiuchumi, ambazo anahusisha na mfumo wa chuo cha MIT kwa uchumi, kinyume cha ule wa
Chicago (ingawa anasema pia kuwa mfumo wa Chicago hauwezi tena kuitwa ulio na maono ya
kiakili). Anaamini kuwa mapendekezo ya sera kutokana na mfumo wa maono ya kiakili ya Chicago
yalichangia kushuka kwa uchumi wa maono ya kiakili. Anasema pia kuwa amewahi kukutana na
wanauchumi wenza ambao wamekataa katakata kujadiliana kuhusu uchumi wa kusisimua pasipo na
mfumo rasmi, na anaamini kuwa mifumo mara nyingine huzuia maono ya mawazo.[155] Hivi karibuni
zaidi, hata hivyo, ameandikwa kuwa uchumi wa kiheterodoksi, ambao mara nyingi huchukua zaidi
mwelekeo wa maono ya kimawazo, unafaa kushirikiana na wanahisabati na kuwa wa kihisabati
zaidi.[100] "Uchumi uliotanda ni mfumo wa kirasmi”, anaandika, na kinachohitajika si kupungua kwa
hisabati wala ni kuongezeka kwa viwango vya hisabati. Anaeleza kuwa baadhi ya mada
zinazozingatiwa na wanauchumi wa kiheterodoksi, kama vile umuhimu wa taasisi au ukosefu wa
uhakika, zinatafitiwa kwa sasa kupitia mifumo ya kihisabati bila kutaja kazi iliyofanya na wanauchumi
wa kiheterodoksi. Uchumi mpya wa taasisi, kwa mfano, huchunguza taasisi kihisababti bila
kuhusisha sana somo linatokana kwa kiasi kikubwa na kiheterodoksi la uchumi wa taasisi.
Katika hotuba yake ya Tuzo la Nobel ya 1974, Friedrich Hayek, anayejulikana kwa uhusiano wake
wa karibu na mfumo wa kiheterodoksi wa uchumi wa Kiaustria, alilaumu kutofaulu kwa sera za
ushauri wa kiuchumi kwa maelekeo ya kuiga utaratibu wa kihisabati unaotumika kwa sayansi asilia
bila kupambanua au kutumia mbinu za kisayansi. Anatoa hoja kuwa hata matukio ya kiuchumi
ambayo yametafitiwa kwa kiwango kikubwa, kama vile ukosefu wa ajir akatika soko, huwa kwa
kindani na utata mkubwa kuliko matukio kama hayo katika somo la sayansi asilia ambako mbinu
zilibuniwa hapo awali. Vilevile, nadharia na takwimu huwa mara nyingi havidhihiriki na
hushughulikwa kulingana na mwelekeo wa mabadiliko yanayohitajika, na wala si ukubwa wake.[156] Kwa upande mmoja kwa sababu ya ukosoaji, uchumi umepatwa na uratibishaji wa hali ya juu na
ufafanuzi wa dhana na mbinu tangu miaka ya 1940, ambao baadhi yake imeelekea katika
utekelezaji wa mbinu ya kidhana na kimawazo (hypothetico-deductive method) katika kueleza
matokeo ya dunia halisi.[157]