4
1 HALMASHAURI YA MANISPAA YA ILALA TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI Ndugu wananchi Halmashauri ya Manispaa ya Ilala katika kutekeleza jukumu la kuweka mazingira safi ya eneo lake imekuwa ikikabiliana na changamoto mbalimbali za uchafuzi wa Mazingira. Changamoto hizo zimesababisha kuwepo kwa magonjwa ya mlipuko kama kipindupindu na kuharisha. Pamoja na changamoto hizo shughuli za usafi wa Mazingira katika Manispaa ya Ilala zinaendelea kutekelezwa kulingana na sheria na taratibu. Hivyo kila mwananchi anapaswa kuzingatia sheria na taratibu hizo za kutunza Mazingira. Kama nilivyoeleza kuwa zipo changamoto zinazozuia jitihada za kuiweka Manispaa katika hali ya usafi miongoni mwa hizo ni hizi zifuatazo; uchafuzi wa Mazingira unaotokana na vyombo vya usafiri, uoshaji holela wa magari, utupaji ovyo wa taka,

Taarifa Kwa Vyombo Vya Habari Usafi PDF

  • Upload
    ilala

  • View
    337

  • Download
    6

Embed Size (px)

DESCRIPTION

Manispaa ya Ilala yazindua kampeni ya usafi

Citation preview

Page 1: Taarifa Kwa Vyombo Vya Habari Usafi PDF

1

HALMASHAURI YA MANISPAA YA ILALA

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Ndugu wananchi

Halmashauri ya Manispaa ya Ilala katika kutekeleza jukumu la

kuweka mazingira safi ya eneo lake imekuwa ikikabiliana na

changamoto mbalimbali za uchafuzi wa Mazingira. Changamoto

hizo zimesababisha kuwepo kwa magonjwa ya mlipuko kama

kipindupindu na kuharisha. Pamoja na changamoto hizo shughuli

za usafi wa Mazingira katika Manispaa ya Ilala zinaendelea

kutekelezwa kulingana na sheria na taratibu. Hivyo kila

mwananchi anapaswa kuzingatia sheria na taratibu hizo za

kutunza Mazingira.

Kama nilivyoeleza kuwa zipo changamoto zinazozuia jitihada za

kuiweka Manispaa katika hali ya usafi miongoni mwa hizo ni hizi

zifuatazo; uchafuzi wa Mazingira unaotokana na vyombo vya

usafiri, uoshaji holela wa magari, utupaji ovyo wa taka,

Page 2: Taarifa Kwa Vyombo Vya Habari Usafi PDF

2

uunganishaji wa maji taka katika mifereji ya wazi, magari mabovu

yaliyoegeshwa kwa muda mrefu, ujenzi usiofuata taratibu ambao

husababisha miundombinu ya maji ya maji ya mvua kushindwa

kufanya kazi. Maelekezo yanatolewa kuwa kila chombo cha

Usafiri wa Umma na watu binafsi kinatakiwa kuwa chombo cha

kutupia taka na abiria yeyote katika chombo cha usafiri haruhusiwi

kutupa taka nje. Atakayebainika kutupa taka nje atachukuliwa

hatua yeye binafsi na chombo chake cha usafiri.

Kwa wamiliki wa magari wote wanashauriwa kupeleka magari

yao katika maeneo yaliyoruhusiwa (Washing bay). Adhabu

itatolewa kwa yeyote atakayebainika kuosha gari katika

sehemu isiyoruhusiwa. Muda wa siku saba (7) unatolewa

kuanzia tarehe 1/12/2015 kwamba wenye wagari mabovu

wawe wameondosha magari hayo.

Nachukua fursa hii kuwafahamisha kuwa, atayekiuka taratibu za

usafi na kusababisha uchafuzi wa Mazingira atachukuliwa hatua za

kisheria ikiwemo kulipa faini ya papo kwa papo. Kwa mara

nyingine Manispaa inasisitiza kuwa, mwananchi yeyote

atakayesadia kumkamata mchafuzi wa Mazingira atalipwa asilimia

hamsini ya faini iliyotozwa kutoka kwa mchafuzi huyo.

Page 3: Taarifa Kwa Vyombo Vya Habari Usafi PDF

3

Jitihada za kujenga uelewa wa masuala ya usafi wa mazingira kwa

wananchi zinaendelea ambapo Manispaa imeanzisha utaratibu wa

matangazo ya mtaani kwa kutumia gari maalum la matangazo.

Vilevile kwa kutumia vipindi vya television na redio ambapo

makosa ambayo yanayosababisha mtu kupewa adhabu ya uchafuzi

yamekuwa yakibainishwa na inaaminika kuwa elimu inayotolewa

inajenga uelewa kwa kila mwananchi kulinda na kutunza

mazingira yanayomzunguka.

Halmashauri ya Manispaa ya Ilala inao mkakati endelevu wa usafi

na Mazingira. Mkakati huu unalenga kubadili sura ya Jiji la Dar es

Salaama ili liwe lenye mazingira safi na salama, pia unalenga kwa

kila mwananchi kujiona kuwa anawajibika moja kwa moja katika

Mkakati huu. Aidha mkakati unahimiza kuwa na wakandarasi

walio na uwezo wa kutoa huduma iliyo bora ya kusafisha na

kuzoa taka inayozingatia viwango.

Kutokana na siku ya maadhimisho ya siku ya uhuru tarehe 9

Disemba, kuelekezwa itumike kwa shughuli za usafi na utunzaji

wa Mazingira maandalizi yamefanyika na shughuli za kusafisha

mazingira zimeanza katika kata zote za Manispaa ya Ilala. Kila

mtendaji wa mtaa, na kata kwa kushirikiana na kamati zao za usafi

na Mazingira, wametakiwa kuandaa utaratibu wa kusafisha

Page 4: Taarifa Kwa Vyombo Vya Habari Usafi PDF

4

maeneo yao. Kila mkazi wa Manispaa hii anaelekezwa

kushirikiana na wananchi wenzake kuhakikisha anasafisha

mazingira yanayo mzunguka na kwamba zoezi hili ni endelevu.

Manispaa ya Ilala inaendelea kuwakumbusha wananchi wake

kuwa, kwakuwa tayari tumetangaziwa kuwepo mvua za El nino na

Wataalamu wa hali ya Hewa, ambazo zitanyesha maeneo

mbalimbali ya nchi hii ikiwemo na maeneo ya Jiji la Dar es

salaam Tunawahimiza wananchi wote wa Manispaa hii kusafisha

mifereji na mitaro ya maji ya mvua inayowazunguka. Halmashauri

kwa kushirikiana na taasisi mbali mbali imeanza kusafisha

mifereji na mitaro yote ya maji ili kuepuka mafuriko yasiyokuwa

ya lazima. Shime Wanachi mnasisitizwa kutotupa taka ovyo katika

mifereji ya wazi ili kuepusha kuziba kwa mifereji hiyo.

Asanteni kunisikiliza

Isaya M. Mngurumi

Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala