127
The University of Dodoma University of Dodoma Institutional Repository http://repository.udom.ac.tz Humanities Master Dissertations 2014 Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando George, Grace Chuo Kikuu cha Dodoma George, G. (2014). Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando (Tasnifu). Chuo Kikuu cha Dodoma, Dodoma. http://hdl.handle.net/20.500.12661/1990 Downloaded from UDOM Institutional Repository at The University of Dodoma, an open access institutional repository.

Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

  • Upload
    others

  • View
    12

  • Download
    1

Embed Size (px)

Citation preview

Page 1: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

The University of Dodoma

University of Dodoma Institutional Repository http://repository.udom.ac.tz

Humanities Master Dissertations

2014

Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya

teule za Penina Muhando

George, Grace

Chuo Kikuu cha Dodoma

George, G. (2014). Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando (Tasnifu).

Chuo Kikuu cha Dodoma, Dodoma.

http://hdl.handle.net/20.500.12661/1990

Downloaded from UDOM Institutional Repository at The University of Dodoma, an open access institutional repository.

Page 2: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

USAWIRI WA MWANAMKE KATIKA TAMTHILIYA TEULE ZA

PENINA MUHANDO

Na

Grace George

Tasnifu Iliyowasilishwa kwa Ajili ya Kukamilisha Masharti ya Shahada ya Uzamili

ya Sayansi ya Jamii katika Fasihi ya Kiswahili Chuo Kikuu cha Dodoma

Chuo Kikuu cha Dodoma

Oktoba, 2014

Page 3: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

i

ITHIBATI

Aliyetia sahihi hapa chini anathibitisha kuwa amesoma na hapa anapendekeza kwa Chuo

Kikuu cha Dodoma, kukubali kupokea tasnifu hii: Usawiri wa Mwanamke katika

Tamthiliya Teule za Penina Muhando katika kukamilisha matakwa ya shahada ya uzamili

katika fasihi (MA Kiswahili) ya Chuo Kikuu cha Dodoma.

……………………………………………………..

Prof. Frowin Paul Nyoni

(MSIMAMIZI)

Tarehe……………………………………

Page 4: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

ii

IKIRARI NA HAKIMILIKI

Mimi, Grace Martin George, ninathibitisha kwamba tasnifu hii ni kazi yangu mwenyewe

halisi na haijawasilishwa wala haitawasilishwa katika Chuo Kikuu kingine chohote kwa ajili

ya kutunukiwa Shahada nyingine yoyote.

Sahihi………………………………………..

Haki zote zimehifadhiwa. Hairuhusiwi kuzalisha, kunakili, wala kusambaza sehemu

yoyote ya tasnifu hii kwa namna yoyote bila kibali cha maandishi kutoka kwa

Mwandishi au Chuo Kikuu cha Dodoma.

Page 5: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

iii

SHUKURANI

Kwanza kabisa napenda kumshukuru Mungu kwa kunipa uhai, uzima na afya njema

hata nikaweza kufanikisha kazi hii, bila matatizo yoyote yale ya kiafya. Pia aliyenipa

akili na ufahamu wa kufanikisha kazi hii na kufikia hapa nilipofikia.

Pili, namshukuru msimamizi wangu Profesa Frowin Paul Nyoni ambaye ni Mkuu

wa Skuli ya Sanaa na Lugha katika Chuo Kikuu cha Dodoma kwani yeye ndiye

aliyekuwa mhimili mkuu katika kufanikisha kazi hii, amekuwa nami bega kwa bega

ili kuhakikisha kazi hii inafikia kiwango hiki. Licha ya shughuli nyingi lakini

alijitolea muda wake mwingi katika kunisahihisha na kunikosoa pale nilipokwama.

Nauthamini sana mchango wake, Mungu ambariki.

Tatu naishukuru sana familia yangu akiwemo mama yangu mzazi Bi Maria na baba

yangu kwa kukubali kunipeleka shule bila kujali umri na uwezo wako kifedha.

Mungu awaongezee siku za kuishi duniani. Pia nawashukuru kaka zangu na dada

zangu wote ambao hawakusita kunishauri na hasa kunisikiliza na kunitimizia

mahitaji yangu ya shule. Mungu awabariki sana.

Nne nawashukuru sana Profesa Penina Mhando, Profesa Imani Sanga, Daktari

Vicensia Shule, Daktari Mona Mwakalinga na Mwalimu Mtiro wa Chuo Kikuu cha

Dar es Salaam kwa kunipa mchango na maarifa pamoja na kunihimiza kukamilisha

tasnifu hii maana haikuwa kazi rahisi. Nauthamini sana mchango wao na

ninawaombea heri na fanaka katika siku za maisha yao yote.

Page 6: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

iv

Mtu mwingine muhimu sana ni Daktari Elias Manandi Songoyi. Shukrani zangu za

dhati zimfikie kwani aliweza kunielekeza namna ya kutafuta mada ya kufanyia

utafiti. Akiwa darasani alisisitiza kutofautisha mambo yanayohusu jamii, yaani

sosholojia na yale ya fasihi, akahimiza kuwa tusichanganye vitu hivyo viwili. Hii

ilinisaidia kupata mada ambayo ndiyo iliyofanyiwa utafiti huu.

Zaidi ya hao nitumie nafasi hii kumshukuru Daktari Rafiki Sebonde. Huyu ni

mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Dodoma. Wakati wa mafunzo ya darasani

alinifundisha namna ya kuandika utafiti kwa kunipa mwongozo wa kuchanganua

mambo muhimu yanayotakiwa kuwemo katika utafiti kwa kufuata mpangilio

unaokubalika, pia jinsi mtafiti anavyotakiwa kuwa wakati wa kukusanya data hasa za

uwandani. Daktari alinifanya nijiamini na hii ilinisaidia sana katika kufanikisha

utafiti wangu. Mungu ambariki sana.

Pia, ninamshukuru sana Prof. V. Lakshmanan kwa kunifundisha kuhusu nadharia za

fasihi. Katika utafiti huu sikupata mahangaiko yoyote kwani tayari nilishamakinika

katika uchaguzi na upembuzi wa nadharia ambazo zimeniongoza kufanya utafiti huu.

Siwezi kuwasahau wanafunzi wenzangu wa Shahada ya Uzamili wa mwaka (2014)

kwa ushirikiano wao katika majadiliano mbalimbali ya kitaaluma. Fidelis

Kyarwenda, Steven Jeremia, Ally Azizi kwa kutaja baadhi tu.

Shukrani zangu za pekee ni kwa wahadhiri wote walionifundisha katika Chuo Kikuu

cha Dodoma, Shahada ya uzamili, hata kunifanya kuwa mahiri katika lugha yangu ya

Kiswahili niipendayo sana. Mungu awabariki wote kwa pamoja.

Page 7: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

v

Nichukue nafasi hii kumshukuru mume wangu mpenzi kwa dhati kabisa, Bwana

Colman Temba kwa kunitia moyo na kunifadhili kwa hali na mali wakati wote wa

masomo yangu tangu Shahada ya Awali na sasa Shahada ya Uzamili. Na hiki ni

kithibitisho tosha kuwa tasnifu hii si mali yangu binafsi bali ni yetu sote na Mungu

ambariki sana.

Pia, ninawashukuru sana watoto wangu Gift Colman na Ian Colman kwa

kunivumilia wakati wote wa masomo kwani muda mwingi niliutumia katika kazi

zangu na kushindwa kutekeleza kikamilifu jukumu la kuwaangalia wao. Pia watoto

hawa walikuwa msaada mkubwa kwangu hasa katika kuchapa kazi zangu

mbalimbali za kimasomo katika ngamizi.

Page 8: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

vi

TABARUKU

Kazi hii ninaitabaruku kwa mama yangu mpenzi na baba yangu Bibi na Bwana

Msacky na ndugu zangu wote, Lucy, Devotha, Agatha, Simon, Veronica, Emanuel,

Flora na Joachim, kwani walijitoa bila kuchoka ili nisome kadri nitakavyo. Pia kwa

kunipa muda mzuri wa kujisomea, kunipa ushauri pale nilipochoka, kuniamini na

kuniombea hata nilipokuwa mbali na nyumbani. Asanteni na Mungu awabariki na

kuwapa afya na maisha marefu.

Page 9: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

vii

IKISIRI

Utafiti huu umejadili kuhusu Usawiri wa Mwanamke katika Tamthiliya Teule za

Penina Mhando. Tatizo lililojenga utafiti huu ni kutokana na hali ya kila siku ya

waandishi wa tamthiliya za Kiswahili wakiwemo wanaume, kumkweza mwanaume

kinafasi na kimajukumu na kumshusha mwanamke, hivyo utafiti huu ulijikita

kuchunguza nafasi ya mwanamke katika tamthilia teule za Penina Muhando.

Utafiti huu ulitumia mbinu ya maktabani kwa kuchunguza kazi mbalimbali ili kupata

ruwaza ya jumla kuhusu nafasi ya mwanamke na mgawanyo wa majukumu kijinsia,

pia vitabu teule ambavyo ni Hatia (1972) na Nguzo Mama (1982) vimesomwa na

kuchunguzwa kwa makini na kuona jinsi mwanamke alivyochorwa. Mahojiano

yalifanyika ili kupata mawazo mbalimbali kuhusu mada ya utafiti. Pia umeongozwa

na nadharia ya Ufeministi. Hivyo utafiti huu umebaini kuwa kuna tofauti kubwa za

kimajukumu kati ya mwanaume na mwanamke. Kwa upande mmoja mwanamke

amechorwa kwa mtazamo hasi na chanya yaani ameonekana ni kiumbe duni,

mnyonge, na hivyo kuendelea kumdharau, kumkejeli na kumdhihaki. Kwa upande

mwingine mwanamke amechorwa kama mshauri, mlezi, mbunifu, mvumilivu na mtu

mwenye huruma na ushirikiano katika jamii. Pia utafiti huu umebaini kuwa zipo

athari mbalimbali zinazosababishwa na uchorwaji wa mwanamke katika tamthilia.

Athari mojawapo ni kuigwa kwa matendo machafu ambayo yanasababisha

kudharaulika na kuendelea kukandamizwa kwa wanawake. Hivyo basi kutokana na

matokeo ya utafiti huu tumefikia mahitimisho kuwa katika jamii nafasi ya

mwanamke na mgawawanyo wa majukumu huwa tofauti na mwanaume kwa sababu

ya mila na tamaduni mbovu ambazo humchukulia mwanamke kama kiumbe duni

wakati wote ingawa uhalisia wa sasa hauko hivyo.

Page 10: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

viii

YALIYOMO

ITHIBATI ....................................................................................................................................... i

IKIRARI NA HAKIMILIKI ................................................................................................ ii

SHUKURANI ............................................................................................................................... iii

TABARUKU ................................................................................................................................ vi

IKISIRI.. ....................................................................................................................................... vii

YALIYOMO .............................................................................................................................. viii

ISTILAHI ZILIZOTUMIKA KATIKA UTAFITI HUU .......................................... xi

ORODHA YA VIFUPISHO VILIVYOTUMIKA ....................................................... xii

SURA YA KWANZA: UTANGULIZI WA UTAFITI ................................................. 1

1.1 Usuli wa Tatizo la Utafiti ..................................................................................................... 3

1.2 Tamko la Tatizo la Utafiti .................................................................................................... 7

1.3 Malengo ya Utafiti ................................................................................................................. 9

1.3.1 Lengo Kuu ............................................................................................................................ 9

1.3.2 Malengo Mahsusi ................................................................................................................ 9

1.4 Maswali ya Utafiti ............................................................................................................. 10

1.5 Umuhimu wa Utafiti ............................................................................................................ 10

1.6 Nadharia ya Utafiti .............................................................................................................. 11

1.6.1 Nadharia ya Kifeministi .................................................................................................. 11

1.7 Mipaka ya Utafiti .................................................................................................................. 19

1.8 Hitimisho................................................................................................................................. 19

SURA YA PILI: MAPITIO YA MACHAPISHO MBALIMBALI KUHUSU

MWANAMKE ............................................................................................................................ 20

2.0 Utangulizi ............................................................................................................................... 20

2.1 Mwanamke katika Fasihi ya Kiswahili .......................................................................... 20

2.1.1 Mwanamke Wakati wa Umwinyi/ Ukoloni............................................................... 25

2.1.2 Mwanamke Baada ya Uhuru ......................................................................................... 26

2.2 Mapitio ya Machapisho Mbalimbali kuhusu Mwanamke ....................................... 28

2.3 Hitimisho................................................................................................................................. 35

SURA YA TATU : MBINU ZA UTAFITI ...................................................................... 36

3.0 Utangulizi .............................................................................................................................. 36

3.1 Eneo la Utafiti........................................................................................................................ 36

3.2 Mbinu za Ukusanyaji wa Data .......................................................................................... 36

Page 11: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

ix

3.2.1 Uchambuzi wa Matini ..................................................................................................... 37

3.2. 2 Mahojiano / Usaili ........................................................................................................... 37

3.3 Usampulishaji na Njia za Usampulishaji ....................................................................... 38

3.4 Vyanzo vya Data................................................................................................................... 39

3.4.1 Vyanzo vya Data za Msingi ........................................................................................... 39

3.4.2 Vyanzo vya Data Fuatizi................................................................................................. 39

3.5 Vifaa katika Ukusanyaji wa Data ................................................................................... 40

3.5.1 Kalamu na Shajara ............................................................................................................ 40

3.5.2 Dodoso ................................................................................................................................. 40

3.5.3 Ngamizi (Kompyuta) ....................................................................................................... 41

3.5.4 Kinyonyi .............................................................................................................................. 41

3.5.5 Tepurikoda .......................................................................................................................... 41

3.5.6 Kamera ................................................................................................................................. 42

3.6 Mbinu ya Uchanganuzi wa Data ..................................................................................... 42

3.7 Hitimisho................................................................................................................................. 42

SURA YA NNE: UWASILISHAJI, UCHAMBUZI NA MJADALA WA

MATOKEO YA UTAFITI .................................................................................................... 43

4.0 Utangulizi .............................................................................................................................. 43

4.1 Historia ya Penina Muhando ............................................................................................. 44

4.2 Hatia (1972) ........................................................................................................................... 46

4.2.1 Utangulizi ............................................................................................................................ 46

4.2.2 Uwasilishaji na Uchambuzi wa Data .......................................................................... 49

4.2.2.1 Mwandishi Alivyomsawiri Mwanamke katika Tamthilia ya Hatia (1972)

kwa upande Chanya katika Nafasi na Kimajukumu .......................................................... 49

4.2.2.2 Mwandishi Alivyomchora Mwanamke katika Tamthilia ya Hatia (1972)

kwa upande Hasi katika Nafasi na Kimajukumu ............................................................... 54

4.2.3 Mjadala na Dhamira Zilizoibuka Kutokana na Uchorwaji wa Mwanamke

katika Tamthiliya ya Hatia (1972) ......................................................................................... 60

4.3 Nguzo Mama (1982) ............................................................................................................ 70

4.3.1Utangulizi ............................................................................................................................. 70

4.3.2Data na uchambuzi wake ................................................................................................. 73

4.3.3Mwanamke Alivyochorwa katika Tamthiliya ya Nguzo Mama (1982) kwa

Upande Chanya ............................................................................................................................ 73

Page 12: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

x

4.3.4 Mwanamke Alivyochorwa katika Tamthiliya ya Nguzo Mama (1982) kwa

Upande Hasi ................................................................................................................................ 81

4.3.5 Mjadala wa Dhamira Zilizojitokeza Kutokana na Uchorwaji wa Mwanamke

katika Tamthiliya ya Nguzo Mama (1982) ........................................................................... 87

4.4 Athari za Uchorwaji wa Wahusika Wanawake katika Kazi za Fasihi ................. 92

4.6 Hitimisho................................................................................................................................. 96

SURA YA TANO: MUHTASARI WA MATOKEO YA UTAFITI ,

MAPENDEKEZO, NA HITIMISHO ............................................................................... 98

5 .0 Utangulizi .............................................................................................................................. 98

5.1 Muhtasari wa Mpangilio wa Tasnifu .............................................................................. 98

5.2 Muhtasari wa Matokeo ya Utafiti ...................................................................................... 100

5.4 Mapendekezo ....................................................................................................................... 102

5.4.1Mapendekezo kwa Watafiti........................................................................................... 102

5.4.2Mapendekezo kwa Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) ................................... 102

5.4.4Mapendekezo kwa Jamii ................................................................................................ 103

5.4.5 Mapendekezo kwa Waaandishi wa Tamthiliya ...................................................... 103

5.5 Hitimisho............................................................................................................................... 104

MAREJELEO ........................................................................................................................... 105

VIAMBATANISHO ............................................................................................................... 109

Page 13: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

xi

ISTILAHI ZILIZOTUMIKA KATIKA UTAFITI HUU

Athari: Ni matokeo yanayotarajiwa, mawazo au hisia anazopata mtangazaji

au msikilizaji

Dhamira: Ni kiini cha jambo au habari iliyosimuliwa au kuandikwa, hasa katika

fasihi.

Jinsia: Ni mahusiano ya kijamii kati ya mwanaume na mwanamke. Pia

jinsia ni ile hali ya kuwa na maumbile ya kike au ya kiume. Katuli

(2002) anaelezea kwamba jinsia ni tabia za kijamii, kiutamaduni na

kisaikolojia ambazo zinamtambulisha mtu kama mwanaume au

mwanamke.

Taswira: Picha ya mwanamke inayojitokeza baada ya matumizi mbalimbali ya

semi, ishara, lugha katika kazi za kifasihi.

Tamthiliya: Ni mchezo wa kuigiza au kazi ya kisanaa iliyoandikwa kwa lengo la

kuigizwa jukwaani ili kufikisha ujumbe Fulani kwa hadhira.

Usawiri wa mwanamke: Ni wahusika wanaotumika kueleza jambo katika kazi za

kifasihi, wasifu wao, tabia zao, lugha zao, itikadi zao, vionjo vyao,

na hata mitazamo yao.

Ni hali ya kuonyesha matendo na mienendo ya wahusika katika kazi

ya kifasihi.

Page 14: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

xii

ORODHA YA VIFUPISHO VILIVYOTUMIKA

Dkt: Daktari wa Falsafa

EAJA: Equal Access to Justice Act

FPA: Kitengo cha Sanaa za Maonyesho ( Fine Perfoming Art)

M.A: Masters of Arts (Shahada ya Uzamili katika Sanaa)

Prof: Profesa

TATAKI: Taasisi ya Taaluma za Kiswahili

TGNP: Tanzania Gender Networking Program ( mtandao wa jinsia Tanzania)

TUKI: Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili

uk: Ukurasa

Page 15: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

1

SURA YA KWANZA

UTANGULIZI WA UTAFITI

1.0 Utangulizi

Utafiti huu unahusu Usawiri wa Mwanamke katika Tamthiliya Teule za Penina

Muhando. Utafiti umechunguza kazi mbili za Penina Muhando ambazo ni Hatia

(1972) na Nguzo Mama (1982), na kuona namna zinavyomsawiri mwanamke na

kuweka wazi mgawanyo wa majukumu.

Sura hii imepitia vipengele mbalimbali ambavyo vinatoa maelezo ya utangulizi wa

mwelekeo wa utafiti huu. Vipengele hivyo ni pamoja na usuli wa tatizo, tamko la

tatizo la utafiti, malengo ya utafiti. Vipengele vingine katika sura hii ni maswali na

umuhimu wa utafiti huu, pamoja na nadharia iliyotumika.

Tamthiliya ni moja kati ya tanzu kubwa muhimu za fasihi andishi. Tanzu nyingine za

fasihi andishi ni ushairi na riwaya. Mtunzi wa tamthiliya husawiri mawazo kwa

maongezi ya wahusika na kwa kujenga migongano na mijadala baina ya wahusika

hao. Tamthiliya hutungwa kwa ajili ya kuigizwa, hivyo mawazo huwekwa katika

matendo na mazungumzo.

Tamthiliya ina historia ndefu sana. Ilianza katika mataifa ya nje, hususani huko

Ulaya ambayo ndiyo imeathiri sana tamthiliya ya Kiswahili. Kihistoria ilichipuka

kutokana na mambo matatu ambayo ni miviga na viviga vya kijamii na kidini

pamoja na tendi na misahafu ya kidini, umathilishaji wa maisha ya kawaida kwa ajili

ya burudani, maonyo au michezo na sanaa za maonyesho za kijadi kama vile ngoma

na dansa.

Page 16: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

2

Tamthiliya kama utanzu wa fasihi andishi katika lugha ya Kiswahili ililetwa Afrika

Mashariki na wakoloni (Bertoncini, 1989). Mgeni kutoka Uingereza aliyejihusisha

na uigizaji hapo mwanzo mwaka (1957) alikuwa Graham Hyslop aliyetunga michezo

ya kuigiza kama Akilimali (1945), Afadhali Mchawi (1957) na Mgeni Karibu (1957).

Mmojawapo wa wanafunzi wake ni Henry Kuria aliyetunga tamthiliya ya

Nakupenda Lakini (1957). Baadaye waandishi wengine walifuata kama vile

Gerishon Ngugi aliyetunga tamthiliya ya Nimelogwa Nisiwe na Mpenzi (1961).

Wafula (1999) anasema kuwa baadhi ya tamthiliya zilitungwa moja kwa moja

katika lugha ya Kiswahili ilhali nyingine zilitafsiriwa kutoka lugha ya Kiingereza na

lugha nyingine za kigeni. Kwa mfano, Morrison (1966) alitafsiri mchezo wa kuigiza

ulioitwa “Mchuuzi Muungwana”.

Waandishi wengi wa tamthiliya wamekuwa wakiandika maudhui ya kazi zao

kulingana na matukio yaliyotendeka na yanayotendeka katika jamii. Hivyo hutumia

mbinu mbalimbali za kisanii ili kufikisha ujmbe kwa jamii.

Miongoni mwa waandishi wa tamthiliya za Kiswahili ni Amandina Lihamba,

Ebrahim Hussein, Emanuel Mbogo, Balisidya Ndyianao na Penina Muhando ambao

wametumia mbinu hizo ili kuweka sawa maudhui yao katika jamii na kueleza

matatizo mbalimbali na uozo uliopo katika jamii. Maudhui katika tamthiliya nyingi

yanamsawiri mwanamke kama kiumbe duni hata katika majukumu ilionekana

kwamba kuna kazi ambazo hawezi kuzifanya kwamba ni za mwanaume tu.

Kutokana na kudunishwa huko ilisababisha mwanamke ajisikie vibaya na kujiona

kwamba kuna mambo ambayo hawezi kuyafanya katika jamii. Hii ndiyo sababu

Page 17: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

3

mtafiti amekuwa na hamasa za kufanya utafiti kuhusu Usawiri wa mwanamke

katika tamthiliya Teule za Penina Muhando.

1.1 Usuli wa Tatizo la Utafiti

Mwanamke katika kazi mbalimbali za fasihi amechorwa kwa mtazamo tofautitofauti.

Katika riwaya za Kezilahabi Rosamistika (1971) tunaona kuwa mwandishi

anamtumia mhusika Rosa kama mhusika mkuu wa riwaya yake. Mwandishi

amemchora Rosa katika picha ya kusikitisha, kwani amechorwa katika hali ya

kunyanyaswa, kama Malaya, kama chombo cha starehe na biashara. Hivyohivyo

katika riwaya za Mohamed (1976) Nyota ya Rehema mwandishi pia kaonyesha jinsi

mhusika wake huyo ambaye ndiye mhusika mkuu katika riwaya hiyo jinsi

anavyonyanyaswa yeye na mama yake.

Pia uchorwaji wa mwanamke katika magazeti kipengele cha hadithi fupi kimekuwa

mstari wa mbele kumchora mwanamke katika mtazamo hasi. Haya aliyaona Nkya

(2004) alipofanya uchunguzi katika magazeti ya Mzalendo na Sunday News ya

nchini Tanzania. Aliona kuwa magazeti haya yalimchora mwanamke kama malaya,

chombo cha starehe, mdhaifu na chanzo cha dhambi katika jamii. Katika miaka ya

sabini, Besha (1976) alitafiti hadithi hizo zinazoandikwa kwenye magazeti mengine

na kupitia baadhi ya nyimbo zilizoimbwa katika vituo vyetu vya redio. Alihitimisha

kwa kutoa picha kwamba, mwanamke anachorwa kama mwovu, mshawishi,

anayewapotosha wanaume. Katika baadhi ya hadithi alipata dhana nyingine ya kuwa,

mwanaume alionekana kama mtu bora, anayetawala mkewe hasa katika ndoa.

Page 18: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

4

Chaligha (2011) amefanya utafiti kuhusu jinsi mwanamke alivyosawiriwa katika

katuni mnato. Katika utafiti wake naye ameonyesha jinsi mwanamke

anavyodhalilishwa kwa kuchorwa akiwa amevaa nusu uchi, mwanamke kama mtu

asiyekuwa na haki ya kupata elimu, mwanamke kama chombo cha starehe kwa

mwanaume. Hivyo basi yeye amegundua kuwa wasanii wengi wanaojihusisha na

sanaa ya katuni mnato ikiwa kama mojawapo ya kazi za kifasihi wanapochora katuni

mwanamke anachorwa kwa mtazamo hasi tu na mwanaume huchorwa kama mtu

mstaarabu, aliyeelimika na mwenye kuvaa mavazi mazuri ya heshima.

Senkoro (1982:84) anaeleza kuwa, historia ya kunyanyaswa na kugandamizwa kwa

mwanamke katika jamii ni ndefu. Inarudi nyuma hadi wakati jamii ilipogawanyika

katika matabaka mbalimbali. Hata hivyo ufuatiliaji huo wa kihistoria haujaweka

kando ukweli kuwa katika baadhi ya jamii kulikuwepo vipindi vya kihistoria

ambavyo wanawake walitawala kisiasa, kiuchumi na kimadaraka kwa jumla. Mara

nyingi katika jamii, mgawanyiko kati ya jinsia ya kiume uligeuka kuwa mgawanyiko

kati ya matabaka mara jamii ilipogawanyika kati ya wale waliomiliki nyenzo na njia

zote za uchumi, ambao walikuwa wanaume, na wale ambao hawakuwa na chochote

isipokuwa jasho lao na wengi wao wakiwa wanawake. Anaendelea kueleza kuwa

kuanzia wakati huo basi, mwanamke alilazimika kumtegemea mwanaume

aliyezitumia nguvu hizo kufanya lolote juu ya mwanamke.

Pia usawiri wa mwanamke katika kazi za fasihi, sanaa na katika jamii umeelezwa na

wataalamu mbalimbali wa fasihi kwa namna tofauti tofauti. Profesa Penina Muhando

kwa maelezo yake mwenyewe mbele ya mtafiti tarehe 11.11.2013, anaeleza kuwa,

kihistoria mwanamke amenyanyasika sana na alionekana kuwa hana sauti kwa

Page 19: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

5

mwanaume, yeye ni wa kusikiliza kila kitu anachosema na anachotaka mwanaume.

Anaendelea kusema kuwa, wakati wao wanashughulikia suala la jinsia (gender)

mwanamke alikuwa hana sauti, hata wakati wa kuajiriwa mwanamke alikuwa

hapewi nyumba lakini mwanaume alipewa nyumba. Nanukuu maelezo yake, “hata

wakati tunaajiriwa sisi mwanamke alikuwa hapewi nyumba lakini kwa kazi hiyohiyo

na elimu hiyohiyo kwa mwanaume alikuwa akipewa nyumba”.

Muhando anaona kuwa, katika taasisi mbalimbali mwanamke hata akiwa ana elimu

kiasi gani au ana kiwango cha elimu sawa na mwanaume bado anadharaulika na

kuonekana kuwa hawezi. Anasema kuwa huo ndio unyanyasaji wenyewe. Muhando

anamalizia kwa kusema kuwa, mwanamke katika jamii athaminiwe na kuonekana

kuwa na yeye ni mtu anayeweza kuleta mabadiliko na sio wanaume tu. Pamoja na

mwanaume kuonekana kuwa yeye ndiye mleta maendeleo lakini bila mwanamke pia

bado hayo maendeleo hayajakamilika.

Fasihi ya Kiswahili tangu zamani imewasawiri wanawake kama watumwa. Katika

tenzi za awali mathalani Utendi wa Mwanakupona na hata Mashairi ya Muyaka, sura

tunayoipata ni ile inayomfanya mwanamke chombo cha kutumiwa na mwanaume ili

kijifurahisha. Taswira hii iliathiriwa kwa kiasi kikubwa na mfumo wa kimwinyi.

Wosia ulio katika Utendi wa Mwanakupona ni wa kuwadunisha na kuwahubiria

wanawake wakubali kuwatumikia na kuwaabudu wanaume. (Ndungo 19850).

Balisidya (1982:8) anaeleza kuwa, Mwanamke katika jamii ya watanzania

anatazamwa kama chombo cha starehe kwa wanaume. Anaendelae kueleza kuwa

Page 20: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

6

mtazamo huu haumpi heshima mwanamke kama mzazi bali chombo muhimu kwa

mwanaume cha kujitosheleza haja zake za kimwili.

Baada ya nchi za Afrika Mashariki kujipatia uhuru wake waandishi wa fasihi ya

Kiswahili waliibua, kutumia na kufuata mtindo wao wa uandishi wa kazi zao

uliotofautiana na ule uliozoeleka katika kuwelezea wanawake. Pia chambuzi,

tahakiki na tafiti mbalimbali zilizofanywa na baadhi ya wataalam zimezidi

kumkandamiza mwanamke kwa kumchora kama kiumbe dhaifu. Kwa kupitia

Momanyi (2000) tumeona kuwa uchorwaji wa mwanamke katika kazi za Shaaban

Robert, amegundua kuwa mwanamke amechorwa katika mtazamo hasi yaani kiumbe

tegemezi kwa mwanaume.

Utafiti huu umelenga kuchambua “Usawiri wa Mwanamke katika Tamthiliya Teule

za Penina Muhando”. Mwandishi huyu amechaguliwa kwa kigezo cha umahiri wake

katika kumchora mwanamke kwa namna tofautitofauti kulingana na jinsi au matendo

wanayofanyiwa katika jamii zetu. Pia mwandishi huyu ni mwanafasihi ambaye

anashughulikia maswala ya harakati za ukombozi wa mwanamke ulimwenguni. Pia

tamthilia hizo teule zimechaguliwa kwa sababu ni kati ya kazi zake nyingi ambazo

maudhui yake yanaonyesha mambo maovu na mema anayofanyiwa mwanamke

katika jamii zetu. Pia tamthiliya hizo ni kazi yake ya kwanza yaani Hatia (1972)

ambayo aliandika kabla ya kujiingiza katika maswala ya jinsia na Nguzo Mama

(1982) ni kazi yake ya zama hizi za harakati za ukombozi wa mwanamke duniani.

Tamthiliya zote hizo zimezungumzia maswala ya mwanamke na wahusika wake

wakuu ni wanawake.

Page 21: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

7

Katika kipindi cha 1971-1984 jamii ilikuwa katika mhemko wa utekelezaji wa

Azimio la Arusha hivyo basi ni kwa kupitia kipindi hiki waandishi wengi waliweza

kutoa dukuduku zao kuhusu mwanamke. Hivyo, ni muktadha wa kipindi pia ndio

uliotusaidia au uliotusababisha tukachagua tamthilia hizo. Hata hivyo utafiti huu

ulitegemea sana kumwona mwandishi huyu wa kike alivyomchora mwanamke

katika kipindi cha nyuma na alivyomchora mwanamke katika kipindi hiki.

Kwa upande mwingine katika kazi nyingi za fasihi ya Kiswahili mhusika wa kike

anaonekana kuwa kivutio kwa waandishi wengi wa riwaya, tamthilia, mashairi na

hata kwa wasanii wanaojihusisha na uchoraji wa katuni na magazeti kwani

humtumia mwanamke kama chombo cha starehe. Haya yameonekana wazi kwa

kupitia utafiti huu na tafiti mbalimbali kuwa picha ya mwanamke katika fasihi ni

hasi wakati inapolinganishwa na mwanaume. Hii sio sahihi, kwani pamoja na

mwanamke kuwa na wajibu wa kuzaa, kunyonyesha nakadhalika pia anao wajibu wa

kufanya kazi nyingine ambazo zinaingiza kipato katika familia, jamii na taifa kwa

ujumla.

1.2 Tamko la Tatizo la Utafiti

Tamthiliya ni fasihi pana na inayoitazama jamii na kuielezea kwa namna ya utofauti.

Hutumia lugha ya kuigiza ikiambatana na matendo ili kufikisha ujumbe kwa jamii.

Kumekuwa na harakati nyingi zinazoendelea kuhusu kumkomboa mwanamke, siyo

Tanzania pekee bali ulimwenguni kote. Tangu Umoja wa Mataifa utangaze kwamba,

mwaka 1975 ni mwaka wa wanawake duniani, juhudi mbalimbali zimekuwa

zikifanywa kuwakomboa wanawake kutokana na ukandamizwaji na udhalilishwaji.

Harakati zinazofanywa ni pamoja na kuwepo kwa mikutano ya hadhara, mikutano ya

Page 22: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

8

kimataifa kama vile Beijing, kampeni za kitaifa, kuwepo kwa siku ya wanawake

duniani ambayo huadhimishwa kila mwaka ifikapo tarehe nne Machi.

Watafiti pamoja na wahakiki wachache wamezungumzia kidogo suala la usawiri wa

mwanamke katika tamthiliya. Mfano Wegesa (1994) alitafiti kuhusu “mwanamke

katika tamthiliya za Ebrahimu Hussein” ambazo ni Alikiona, Wakati Ukuta,

Kinjekitile, Mashetani, Arusi na Kwenye Ukingo wa Thim. Wegesa aligundua kuwa,

tamthiliya zote kwa pamoja zimemsawiri mwanamke kama mnyonge, muasherati,

chipukizi wa kisiasa, mdhaifu na tegemezi kwa mwanaume.

Mtiro (2005) alitafiti kuhusu “Taswira ya mwanamke katika tamthilyia mbili za

Kitanzania ambazo ni: Alikiona na Machozi ya Mwanamke, katika utafiti wake

akagundua kuwa, katika tamthiliya ya machozi ya mwanamke, mwanamke

amesawiriwa kama mzazi na mlezi katika jamii na familia kwa jumla, asiye na haki

ya kuwatembelea wazazi wake, kiumbe kinachodhulumiwa na kugandamizwa,

mwanamke kama mtu asiyepinga suala la wanawake kutopigania haki zao. Wakati

katika tamthiliya ya Alikiona, mwanamke amesawiriwa kama mzinzi na asiye

mwaminifu katika ndoa yake, mwongo, kiumbe duni na mwenye tamaa.

Mwakalinga (2003) amezungumzia nafasi ya mwanamke katika filamu za

Kitanzania. Yeye anaeleza kuwa, mwanamke lazima ajiamini kwa kile

anachokifanya na kuonyesha juhudi zake katika kazi mbalimbali za kisanaa, kijamii

na kiuchumi ili aweze kupata thamani katika jamii kama ilivyo kwa wanaume.

Shule (2004) amefanya utafiti juu ya mchango wa filamu katika harakati za

kupunguza unyanyasaji wa kijinsia na hatari zinazoweza kusababisha UKIMWI.

Page 23: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

9

Katika utafiti wake ameonyesha jinsi filamu zinavyoweza kusaidia kuwaelimisha

vijana wa kiume katika kuzuia unyanyasaji wa kijinsia ambao ni mojawapo ya

mambo yanayoweza kusababisha kuenea kwa maambukizi ya UKIMWI.

Senkoro (2009) ameeleza kwa ufupi jinsi mwanamke alivyosawiriwa katika

vipengele vichache tu kama vile kejeli na dhamira. Aidha, wataalamu hao

hawajamchambua mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando kama

mhusika mkuu katika tamthiliya hizo. Tatizo lililojenga utafiti huu ni kutokana na

hali ya kila siku waandishi wa kiume wa tamthiliya za Kiswahili kumkweza

mwanaume kinafasi na kimajukumu na kumshusha mwanamke. Aidha wataalam hao

hawajamchambua mhusika mwanamke jinsi alivyosawiriwa na mwandishi

mwanamke katika kazi za kifasihi. Hivyo utafiti huu unakusudia kuchunguza usawiri

wa mwanamke katika tamthiliya za Hatia na Nguzo Mama za Penina Muhando.

1.3 Malengo ya Utafiti

Malengo katika utafiti yako ya aina mbili yaani lengo kuu na malengo mahususi.

1.3.1 Lengo Kuu

Kuchunguza usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando.

1.3.2 Malengo Mahsusi

Malengo mahsusi katika utafiti ni haya yafuatayo;

i. Kubainisha nafasi ya mwanamke katika tamthiliya za

Hatia na Nguzo Mama kwa jumla.

Page 24: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

10

ii. Kuchambua namna wahusika wa kike

walivyochorwa kwa mujibu wa mgawanyo wa

majukumu katika tamthiliya hizo.

iii. Kuchunguza athari zinazotokana na usawiri wa

mwanamke katika tamthiliya za Hatia na Nguzo

Mama.

1.4 Maswali ya Utafiti

i. Nini nafasi ya mwanamke katika tamthiliya za

Hatia na Nguzo Mama.?

ii. Je, wahusika wa kike wamechorwaje kwa mujibu

wa majukumu katika tamthiliya hizo?

iii. Ni athari gani zinazopatikana kutokana na usawiri

wa mwanamke katika tamthiliya za Hatia na Nguzo

Mama?

1.5 Umuhimu wa Utafiti

Kazi yoyote ile ya fasihi hubeba ujumbe ndani yake. Hata kama ujumbe huo

haujaelezwa kinagaubaga lakini bado hubaki kuwa ujumbe. Asiyeelewa akiuliza

haitwi mjinga bali hupatiwa jibu. Tamthiliya kama kazi ya fasihi kwa vyovyote vile

imesheheni ujumbe uliokusudiwa kufikishwa kwa jamii. Inatarajiwa kuwa kazi hii

itawasaidia watafiti wengine kutafiti zaidi juu ya tamthiliya na hasa katika vipengele

ambavyo havijaguswa kwa undani, kama vile migogoro, dhamira, falsafa za

wanatamthiliya, mtindo, muundo, mandhari na matumizi ya lugha. Kwa kufanya

hivyo, uwanja mpana utaachwa kwa watafiti wengine kutafiti suala hili kiundani na

kuandika ikiwezekana hata vitabu. Hili litasaidia kuwa na marejeo mengi. Utafiti

huu unategemewa kuleta matumaini mapya kwa waandishi hasa wanawake katika

Page 25: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

11

tamthiliya. Waandishi hao wataandika zaidi na zaidi kwa kuwa watajiona wako sawa

na waandishi wengine wa kazi za kifasihi, na hivyo watafanya vizuri zaidi hasa

baada ya kugundua kwamba kazi zao ni za thamani kwa wanazuoni na watafiti.

Wasomaji nao wanatarajiwa kugeuzwa mtazamo wao wa awali kuhusu uchorwaji

wa mwanamke katika tamthiliya kwa kuwa wengi huzisoma na kuziacha tu bila

kufuatilia ujumbe uliomo ndani yake, bila kuchukua hatua za makusudi za

kubadilisha mwenendo ikiwa ni mbaya.

1.6 Nadharia ya Utafiti

Wamitila (2008) anaeleza kuwa, “nadharia ni maarifa ya kitaaluma ambayo msomaji

au mhakiki anapaswa kuyajua na kuyafahamu kabla ya kuianza kazi yake”. Pamoja

na hivyo nadharia pia ni maarifa ambayo inatupasa kuwa nayo kabla ya kujihusisha

na kazi yoyote ile ya uhakiki. Pia nadharia ni maarifa ambayo yanamwezesha

msomaji kupanua uelewa wake na kwa njia hiyo, kuboresha usomaji wake na

kuifanya kazi ya fasihi.

Sehemu hii inafafanua uteuzi wa nadharia inayoongoza utafiti huu katika ukusanyaji

na uchambuzi wa data. Uchanganuzi wa nadharia unatokana na jinsi nadharia

yenyewe inavyobainisha mahusiano baina ya mwanamke na mwanaume katika

jamii. Utafiti huu unaongozwa na nadharia ya Ufeministi kwa kuona kuwa inaweza

kujibu na kuongezea upungufu uliojitokeza katika tahakiki zilizotangulia.

1.6.1 Nadharia ya Kifeministi

Ufeministi ni nadharia na mtazamo wa dunia. Kama nadharia, Ufeministi ni mfumo

wa mawazo yanayofasili, na yanayoelezea mambo yanayohusiana na uhusiano wa

Page 26: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

12

kijinsia na uwepo wa mwanamke. Felluger (1998) anaeleza kwamba nadharia ya

Ufeministi inatafuta kuondoa nadharia za utawala wa mwanaume ili kuweka bayana

dosari za asili, na upofu wa jinsia.

Mafeministi wanaendeleza mikabala mipya, kutoa fasili ya mwanamke na ukweli

kuhusu mwanamke.

Naye Tsikataa (1991) anafafanua zaidi kwamba, Ufeministi ni utambuzi wa ubaguzi

wa kimfumo dhidi ya wanawake katika uwanja wa jinsia na katika kujitoa kufanya

kazi kuyakabili mabadiliko yaliyopo katika jamii. Anazidi kueleza kwamba, baada

ya wanawake kuona kwamba wamewekwa katika daraja la mwisho kwenye ngazi

zote za maaamuzi, kama vile siasa, uchumi na katika ngazi ya jamii, ndipo

walipoamua kupambana ili waweze kujikomboa wenyewe.

Mwanzoni mapambano hayo yalipigwa vita, lakini kuanzia miaka ya 1800 mpaka

1900 madai yao mengi, kama vile haki ya kupiga kura, na kupata nafasi katika ngazi

ya uchumi na jamii yalipitishwa. Walionekana kwamba wana haki kubwa kushiriki

katika kuzalisha maarifa kama walivyo na haki ya kuwa sehemu ya maarifa hayo.

Nadharia ya Kifeministi ilianza mwanzoni mwa miaka ya 1792 huko Ulaya. Kwa

mujibu wa Ma Humm na Walker (1992), historia ya nadharia ya ufeministi inaweza

kugawanywa katika vipindi vitatu. Kipindi cha kwanza kilikuwa kati ya karne ya 19

na mwanzoni mwa karne ya 20, kipindi cha pili kilitokea katika miaka ya 1960 na

1970. Kipindi cha tatu kilianzia miaka ya 1990 mpaka sasa. Wanazidi kueleza

Page 27: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

13

kwamba nadharia ya Ufeministi ilianzia kwenye harakati za mafeministi za

kujikomboa.

Licha ya Humm na Walker kuelezea chimbuko au mwanzo wa kuibuka kwa

nadharia ya ufeministi lakini Mackinnon (1991) anafafanua zaidi na kueleza

kwamba, Ufeministi ni nadharia ya kwanza kuibuika kutokana na watu ambao

walivutiwa nayo. Yaani ni nadharia iliyoibuliwa na kundi la watu waliovutiwa na

mustakabali wake. Anazidi kueleza kwamba zipo sababu nne zilizofanya suala la

ukombozi wa mwanamke liwe la kisiasa. Kwanza kabisa ni wanawake kama kundi,

wanatawaliwa na wanaume kama kundi, na mwanamke mmoja anatawaliwa na

mwamaume mmoja. Pili, wanawake wamefanywa kuwa tegemezi katika jamii na sio

kwa sababu za asili ya mtu au za kibaolojia. Tatu mgawanyo wa majukumu, ambao

unahusisha jinsia unamuweka mwanamke katika kiwango cha juu cha kazi zisizo na

hadhi. Hali ya kutokuthamini kazi azifanyazo mwanamke imetawala katika jamii

nyingi na jamii humwona mwanamke hata hisia zake binafsi ni za kiegemezi. Nne,

tangu matatizo ya mwanamke yalipojulikana kuwa sio ya mtu mmoja bali ya

wanawake wote, na hayawezi kutatuliwa na mtu binafsi, ndipo suala hili likawa la

kisiasa zaidi.

Hata hivyo Cox (1965) anaeleza kwa kuweka wazi jinsi nadhaharia ya Ufeministi

ilivyoibuka kwa kusema kwamba, nadharia ya Kifeministi ilianzishwa kama njia ya

kujadili matatizo ya wanawake ambao hudhaniwa kuwa na hadhi ya chini, katika

jamii nyingi duniani.

Page 28: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

14

Katuli (2002) ni mtaalamu mwingine anayeelezea mgawanyiko wa mafeministi, na

kueleza kwamba mafeministi wamegawanyika katika makundi manne ambayo ni

mafeministi wa Kiradikali (wenye siasa kali), Mafeministi wa Kiliberali (wenye

kutaka mabadiliko), mafeministi wa Ki-Marx na mafeministi wa nchi za dunia ya

tatu. Ijapokuwa kila kundi lina msimamo na kanuni zake, lakini lengo la makundi

hayo bado ni moja tu la kumkomboa mwanamke.

Pamoja na maelezo hayo ya wataalamu hao hapo juu hata hivyo katika miaka ya

1900, wanawake wengi walianza kuandika vitabu akiwemo Mary Wollstencecraft,

aliyeandika Vindication of the Right of Women (1792) na A Room of One’s Owns,

kilichoandikwa na Virginia Woolf (1929). Mwingine ni Sarah Gremke aliyeandika

Anti Slavery Leader na makala yake ya “Letters on the Equality of Sexes and the

Condition of Woman” (1938). Gremke aliandika kuhusu asasi za dini zenye sheria

ngumu zinazomnyayasa na kumkandamiza mwanamke.

Naye Simone de Beauvoir katika kitabu chake cha Second Sex (1949) anashambulia

asasi kongwe ambazo zinaonekana kuwa mhimili mkubwa wa udhalilishaji wa

wanawake ambazo ni ndoa, dini, na utamaduni. Anazidi kueleza kuwa asasi ya ndoa

inampa mwanaume nafasi kubwa ya kupanga na kuamua juu ya familia na

kumwacha mwanamke kama chombo tu. Dini nayo anaieleza kuwa ni asasi ambayo

ina maagizo na amri ambazo ni ngumu na zinazomkandamiza mwanamke kwani

zinamtaka kunyenyekea.

Pia Bond (2000) anashadidia asasi ya utamaduni na kusema kwamba kipengele cha

utamaduni ni kipengele pekee kinachotengeneza mazingira ya kumkandamiza

Page 29: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

15

mwanamke asifikie ngazi za juu za uongozi. Anazidi kueleza kwamba katika suala la

uongozi wanaume wengi hawaamini kwamba mwanamke ataweza kuongoza vizuri

kabisa na kufanya maamuzi sahihi na yanayostahili.

Sanjari na maelezo ya Bond na de Beauvoir kuhusu asasi zinazomkandamiza

mwanamke, York na wenzake (1991) katika moja ya kanuni zao wanafafanua

kwamba, watu wanaokandamizwa tu ndio wanaoweza kusema juu ya ukandamizwaji

wao, ni wao tu wanaoweza kuelezea tajiriba zao na kutoa mchanganuo ambao

hautapinga jitihada zao, na sio wakandamizaji. Ina maana kwamba mwanaume

hawezi kutetea haki za mwanamke isipokuwa kama na yeye anajua kwamba

mwanamke anaonewa na mifumo iliyopo katika jamii.

Wamitila (2002:157) anasema, utamaduni anaokulia mwanamke unachangia katika

kumdidimiza katika hali ya unyonge. Utamaduni huo unamfanya mwanamke

ajichukulie kuwa ni kiumbe duni. Baada ya kukubali hali hiyo mwanamke anaishia

kuwa chombo cha kutumikishwa na kuendeleza utamaduni huo hasi katika jamii.

Ndoa nia taasisi mojawapo ya kitamaduni inayoendeleza ukandamizaji wa

mwanamke. Asasi hiyo imejengwa kwenye imani kuwa mwanaume ana uwezo

mkubwa katika nyanja mbalimbali na kuishia kumwangalia mwanamke kama

chombo tu.

Katika kufafanua nadharia ya ufeministi Wamitila anasema kuwa tamaduni jamii

yenye mfumo dume huegemea upande wa kiumeni, yaani mwanaume anatukuzwa

huku mwanamke akikandamizwa. Utamaduni huo unawapitishia wanajamii wake

mila ambazo zinajitokeza kwenye sanaa ya lugha yake. Utamaduni umeumbwa kwa

Page 30: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

16

namna ya kumkandamiza mwanamke katika nyanja zote za maisha. Wanawake

katika jamii zao hususani za Kiafrika, wanachukua mitazamo inayoendeleza itikadi

hii ambayo ni hasi. Kwa jinsi hii huweza kudharau jinsia zao wenyewe na kukosa

moyo wa kujiamini kwa wandishi wa kike, hii ni mojawapo ya jinsia iliyoathirika na

mfumo dume. Nadharia hii ya Ufeministi wa Kiafrika ni muafaka katika kuchambua

na kubainisha ukweli wa mtazamo ya Kifeministi.

Palmer (1983) anasema kuwa jamii ya kitamaduni inamuumba mwanamke ambaye

anataka kujikomboa na kujijua lakini ambaye bado anaamini misingi ya mila na

desturi kuhusu nguvu aliyonayo mwanamke katika jamiii. Hivyo kutokana na

maelezo haya tumetumia mkabala huu wa Kifeministi kuonyesha namna mwanamke

anavyochorwa katika fasihi ya Kiswahili huku tukiangalia mwandishi mwanamke.

Kama ilivyo mitazamo mingine ya kijamii, Ufeministi una mizizi yake katika siasa

ya ukombozi kwa hivyo nadharia hii iliongoza katika harakati za ukombozi wa

mwanamke zilipopamba moto kunako miaka ya sitini ( hasa Marekani). Baadhi ya

mambo yaliyozingatiwa na muungano huu ni kuunda upya uhalisia wa mwanamke

kwa kupunguza na kudhihirisha miundo ya kijadi ambayo inamtukuza mwanaume

na kumkandamiza mwanamke.

Kwa kuelewa hayo hapo juu, Scott (1986:1053) anasema:

wananadharia wamefanya busara sana kubadilisha msimamo

wao kwa kuanza kutumia jinsia pahala ukike hasa

wanaporejelea mahusiano ya jinsia hizi mbili katika utaratibu

wa jamii. Bila shaka wamegundua kuwa wanawake na

wanaume hufafanuliwa kwa kurejeanana basi hapana ufafanuzi

Page 31: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

17

wa upande wowote ule utakaofuzu iwapo watatenganishwa.

(tafsiri yetu)

Mawazo ya Scott yanaelekea kufafanua ukweli uliopo kuwa wanaume na wanawake

ni viumbe walio na uwezo sawa na ambao husaidiana katika majukumu yao ya

kijamii japokuwa kimaumbile ni tofauti.

Donnely (2009), yeye anadai kwamba wanawake wahusika katika katuni inatakiwa

wachorwe kwa kuonesha kuwa wanaweza. Donnely alivutiwa na wanakatuni na

wachoraji wanawake wa zamani ambao walichora katuni zilizopinga mfumo dume.

Ijapokuwa katuni hizo ziko kwa namna ya kuchekesha lakini ndani yake zina ujumbe

mzito uhusuo mgawanyo wa majukumu kati ya wanawake na wanaume, na jinsi

mwanamke anavyochorwa katika jamii. Donnely ameonesha vizazi viwili tofauti

ambapo mwanamke alitazamwa kwa namna tofauti. Mwanzoni kabisa alionekana

kama mtu asiye na vigezo vya kupata kazi ila anafaa kuwa mama wa nyumbani tu na

chombo cha starehe kwa mwanaume. Lakini kilifika kipindi ambacho mwanamke

naye alitoka na kwenda kutafuta kazi huku akijiamini kwamba anaweza. Mwaka

1977 alimuona mwanamke akihesabiwa kama mama wa nyumbani asiyeweza

kufanya kazi ya kuingiza kipato bali alionekana kama mfanyakazi mkuu nyumbani.

Naye Kiango (1992) anasema kwamba mkanganyo kuhusu nafasi ya mwanamke

husababishwa na ukosefu wa itikadi murua za uchambuzi. Anasema:

Kulegalega na kukanganyikiwa kwa waandishi kuhusu

nafasi ya mwanamke kunatokana na kukosekana kwa

itikadi murua ya uchambuzi. Kukosekana kwa itikadi

hiyo ndiko kunakomfanya mwanamke apewe picha

isiyo nzuri na iliyo potofu. (uk 84-89).

Page 32: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

18

Kutokana na tamthilia alizozichambua yaani ya Uasi, Mke Mwenza, Nakupenda

Lakini, Nimelogwa Nisiwe na Mpenzi, na Jirani Kanyolewa, Kiango anaeleza

kwamba maendeleo katika teknolojia yanategemewa vile vile kuathiri nafasi ya

mwanamke katika jamii. Anafafanua zaidi kwamba katika kazi kadha wa kadha za

kifasihi mwanamke anachorwa kama kitega uchumi au chombo cha kuleta faida kwa

mwanaume. Hii inatokana na kukosekana kwa itikadi murua za kichambuzi ambazo

zitamweka mwanamke katika mtazamo chanya. Nadharia ya Ufeministi itatumika na

itamsaidia mtafiti kuchambua na kuelezea nafasi ya mwanamke katika fasihi ya

tamthiliya na mwitikio wa mafeministi juu ya uchorwaji wa wanawake.

Manufaa muhimu ya nadharia ya Ufeministi ni kule kuzungumzia masuala ya

wanawake na kupigania usawa miongoni mwa wanadamu na kuonyesha udhaifu wa

mfumo dume.

Nadharia inayoongoza utafiti huu ni kitengo kimoja cha Ufeministi ambao ni

Ufeministi wa Kiafrika. Hii ni nadharia inayojaribu kuelezea matatizo

yanayowakabili Waafrika, kisababishi cha matatizo yao na jinsi wanavyoweza

kujiepusha nayo. Kwa mfano Chukwuma (1994) anasema kuwa utambuzi wa

mapambano ya mwanamume wa Kiafrika, utambuzi wa kutokuwa na usawa na

matatizo ya mafundisho ya mila za ukoloni, kuwepo kwa Ufeministi kumeangalia

utamaduni wa Mwafrika na uasili wake katika kumchunguza mwanamume na

mwanamke. Davies na Grave (1986) wametoa mchango wao kuwa wameshikilia

utambuzi wowote wa mwanamke wa kiafrika, jamii yake na ukweli wa kihistoria

lazima vizingatiwe.

Page 33: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

19

Kwa hivyo azma kuu ya Ufeministi hasa Ufeministi wa Kiafrika ni kusoma upya

kazi za fasihi ili kusisitiza umuhimu wa vipengele vilivyopuuzwa na wahakiki wengi

au ambavyo hawangeviona kwa sababu walikuwa wanafanya kazi katika nadharia za

kijadi zinazomtukuza mwanaume. Hivyo nadharia hii ndiyo iliyoongoza utafiti huu

kwa kuwa inazungumzia masuala yanayohusu wanawake na namna ya kutatua

matatizo yanayowakwamisha. Pia imetupa mbinu mbadala inayotumika katika

kumkuza mhusika wa kike. Hivyo utafiti huu ni njia mojawapo ya kumnusuru

mwanake na kumpa nyenzo na njia ya kupigana nayo katika nyanja mbalimbali iwe

matatizo yake kijijini, mjini, katika ndoa na hata kazini.

1.7 Mipaka ya Utafiti

Utafiti huu umejikita katika kuchunguza usawiri wa mwanamke katika kazi teule za

Penina Muhando. Kazi hizo ni Hatia (1972) na Nguzo Mama (1982). Uteuzi wa

tamthiliya hizi umefanywa kwa sababu ni kazi ambazo wahusika wake wakuu ni

wanawake, pia zimeandikwa na mwandishi wa jinsia ya kike na pia kigezo cha

wakati kimezingatiwa. Hivyo mtafiti ameangalia ni jinsi gani mwandishi mwanamke

alivyomsawiri mhusika mwanamke.

1.8 Hitimisho

Katika sura hii tumeeleza utangulizi kwa jumla kuhusu utafiti, usuli wa tatizo la

utafiti, tamko la tatizo la utafiti. Pia kiunzi cha nadharia kinachoongoza utafiti huu

kimebainishwa katika sura hii. Aidha malengo ya utafiti, maswali ya utafiti na

umuhimu pamoja na mipaka ya utafiti vimejadiliwa. Kwa hiyo sura ya pili inajadili

kwa kina mapitio ya machapisho mbalimbali yanayohusiana na mwanamke.

Page 34: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

20

SURA YA PILI

MAPITIO YA MACHAPISHO MBALIMBALI KUHUSU MWANAMKE

2.0 Utangulizi

Katika sura hii mtafiti amefanya mapitio ya machapisho mbalimbali yanayohusiana

na utafiti huu. Mtafiti amegundua kuwa machapisho haya ni muhimu kwani

yamemwongoza kubaini pengo la utafiti ambalo halijafanyiwa kikamilifu na watafiti

wengine. Mwishoni mwa sehemu hii limeoneshwa pengo hilo lililoshughulikiwa na

mtafiti wa utafiti huu.

2.1 Mwanamke katika Fasihi ya Kiswahili

Katika fasihi ya Kiswahili, taswira ya mwanamke imejitokeza katika namna

mbalimbali, katika kufanya hivi tunajaribu kudhihirisha ni kwa kiasi gani nafasi na

wajibu wa mwanamke wanaopewa na waandishi hawa unaambatana na itikadi na

imani kuhusu nafasi ya mwanamke katika jamii za Kiafrika.

Katika Nimelogwa Nisiwe na Mpenzi (1961) na Nakupenda Lakini (1957),

mwanamke amesawiriwa kama bidhaa ya kuchuma pesa. Wazee wanadai kiasi

kikubwa sana cha mali kama mahari. Kama bidhaa wanawake huuzwa na

kununuliwa. Katika Nimelogwa Nisiwe na Mpenzi, Muriithu anamweleza Ronaldo:

MURIITHI: nilipokuwa kijana nilimpenda mama yako, alafu

nikamnunua. Sasa mimi ni mzee ndipo sasa naenda

kumuuza Wangare ambaye ni mali yangu. Nawe

utakapokuwa mzee utakuwa ukila nyama kama zile

tunazokwenda kula, heri mungu akujalie upate kununua mke

(uk 80).

Page 35: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

21

Maneno hayo yanatudhihirishia kuwa mwanamke hakuwa na heshima yoyote katika

jamii hii. Hivyo mwanaume aliyekuwa na hela aliweza kununua mwanamke yoyote

anayempenda katika utamaduni wa kijadi, msichana hakupewa uhuru wa

kujichagulia mchumba aliyempenda. Mbaabu (1985:28-29) katika Uasi (1989) baba

yake Riziki alitaka kumchagulia binti yake mchumba. Nyamawi wa rika lake

anamuona Riziki kama bidhaa ya kuuzwa kwa wenye pesa wala si kwa John, kijana

maskini asiyeweza kulipa mahari.

Chande anasema

(Kwa John)------ Nisingekukataza kutembea na binti yangu kijana

lakini kama ujuavyo wazee wako maskini hawana cha kunipa ,ikiwa

nia yako ni kumuoa Riziki. Riziki sitaki madeni na wasiokua na

kitu.Watanipa nini? (uk 13).

Vivyo hivyo Sita wa Zabibu Chungu (1985) hakubali kuolewa na Shekh Zabibu,

mzee ambaye walimchagulia, Sita anatoroka siku ya harusi na kuolewa na Makuu,

kijana ambaye walipendana kama Chande wa Uasi, Bi Radhia wa Zabibu Chungu,

hajali hisia za binti yake cha muhimu sana kwake ni ile mali watakayoipata baada

ya mahari kulipwa.

Hapa tunaona jinsi mahari katika jamii za Kiafrika ilivyotumiwa kumkandamiza

mwanamke. Mtoto wa kike hakuwa na hadhi yoyote katika jamii. Hakuthaminiwa

na watu kwa sababu atakapoolewa angebadilishwa na mifugo au pesa. Hali hii

alimdhalilisha sana mtoto wa kike na kumtoa utu. Ilimfanya aonekane kama mali ya

mumewe ambaye alimnunua na anamtunza na anamtumia anavyopenda.

Page 36: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

22

Kwa mujibu wa tamaduni za Kiafrika wa kijadi dhima na nafasi ya mwanamke ni

jikoni. Nafasi hii ya mwanamke inajidhihirisha wazi katika tamthiliya, mfano

Mulwa katika Bunami (1984), Rehema na Eda wanapika na kukamua ng‟ombe tu.

Katika Ukame (1983), Mosi na Bintiye Nawo humkamua ng‟ombe na kumpikia

Mzee Heri tu. Utamaduni wa jamii hizi ulimnyima mwanamke nafasi ya kushiriki

katika mambo mengine ya nje ya mazingira ya nyumba.

Maonevu ya kitamaduni yanawafanya wazee wasione faida yoyote katika

kumuelimisha mtoto wa kike. Katika Jirani Kanyolewa (1975) msichana Chadi

licha ya kufaulu mtihani wake vizuri hana matumaini ya kuendelea na masomo

kwani wazazi hawaoni haja ya kumwelimisha. Katika Ukame, Nema alikoseshwa

nafasi ya kusoma ili kaka yake Mambo asome. Kwa maoni ya mzee Heri, Nema

ambaye ni mwanamke hangeisaidia familia yake. Hali hii inamfanya mwanamke

kuoneka kama mtu duni, asiye na usawa na mwanaume. Imani hii imetokana na

hali kwamba mtoto wa kike anapoolewa hufaa jamii ya mumewe kuliko jamii yake

mwenyewe. Katika riwaya za Euphrase Kezilahabi, kama Rosa Mstika (1971),

Kichwa Maji( 1974), Dunia Uwanja wa Fujo (1975) na Gamba la Nyoka (1978)

anaendeleza falsafa ya jamii yake kongwe kuhusu mwanamke. Falsafa hii

inamchukulia mwanamke kuwa kiumbe duni aliye chini ya utawala wa mwanaume.

Katika Rosa Mistika, Regina anapatwa na mateso mengi lakini hawezi kumwacha

mumewe Zakaria kwa sababu ya watoto. Katika utamaduni na mila za Kiafrika

mwanamke akishaolewa anapaswa kuyakabili yote yanayompata kwa unyenyekevu

(Ngocbo 1986:149), katika uhusiano wao Regina hathubutu kumuuliza Zakaria

chochote. Zakaria anapoziiba pesa za karo ya mtoto ya

Page 37: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

23

shule alizozipata Regina kwa kumuuza ng‟ombe wake na kuzinywa pombe, Regina

anaogopa kumuuliza, bali anasononeka tu kwa mawazo. Katika maelezo yake

Kezilahabi anasema,:

Katika kijiji cha Namagondo hapakuwa na mwanamke aliyekuwa

akipigwa karibu kila juma kama Regina. Wanawake wengi kijijini

walijiuliza kwanini hakutaka kumwacha bwana wake. Wengi walimwona

mjinga.(uk 7)

Kutokana na hali hii tunamwona Regina kama mfano wa mwanamke aliyekubali hali

yake kama mjaaliwa. Mungere wa Dunia Uwanja wa Fujo, anaonyesha

unyenyekevu kwa mumewe kwa kila hali. Bintiye anapopata mimba na kuadhibiwa

na baba yake, Mungere hamtetei anabaki analia tu pembeni. Wahusika hawa

wanachorwa katika hali ya kuridhika na hali na nafasi zao. Ni taswira za aina hii

huzua maoni kuwa, Kezilahabi ni mwandishi anakatisha tama ukombozi wa

mwanamke.

Hizi ni taswira ambazo hazimsaidii mwanamke aliyedunishwa kujifahamu na

kujitafakari juu ya hali yake. Badala yake zinazomfanya kuamini kuwa nafasi duni

anayoishikilia katika jamii ni majaaliwa.

Taasisi nyingine ya kitamaduni inayomkandamiza mwanamke ni utawala. Baadhi ya

jamii huwatawisha wasichana wao, kwa kuwafungia ndani ya nyumba ili wasitoke

nje na wasionekane na wavulana mpaka siku ya ndoa. Katika Utengano (1980 ) Said

A Mohamed anatuonyesha jinsi hali ya utawa inavyomtesa mwanamke Maimuna

aliyenyimwa uhuru wa kutoka nje na alimtii baba yake bila kupinga. Kwa kuzidiwa

na kero na kushindwa kuvumilia, aliasi utawa huu na kuingilia ukahaba. Katika

Page 38: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

24

Buriani, Eda na Rehema wametawishwa nyumbani. Rehema analalamika kuwa baba

yao hawapeleki katika mikutano ya sherehe ili wakapate kubadilisha mazingira. Hali

hii ya utawa ilimnyima mwanamke fursa ya kwenda nje na kukabiliana na hali halisi

ilivyo. Kama ilivyodhihirika katika Utengano, mwanamke anapoasi utawa huu

hujikuta katika maovu yanayomdhalilisha sana.

Katika Machozi ya Mwanamke (1977) Madahiro anamchukulia mwanamke kuwa

chombo cha kuzalisha mali. Hii ndio sababu inayomfanya aamue kuoa wake wengi.

Pesa anazozipata kutokana na mauzo ya tumbaku anazitumia kwa manufaa yake

binafsi. Mwanamke hana haki ya kumiliki mali anayoizalisha. Hapa tunaona jinsi

ndoa inavyotumiwa kuwanyonya na kuwanyanyasa wanawake. Katika muktadha

huu wanawake huonekana kama wanyama wa huduma, kwa jinsi ambavyo

wanatumikishwa na waume zao mashambani.

Mbali na kazi za shamba, mwanamke anafanya kazi zote za nyumbani kama kutafuta

kuni, kufua nguo, kupika, kuteka maji, kumpashia mumewe maji na kumwandalia

chakula. Hapa tunaona kuwa Madahiro hana huruma wala utu, anawafanya wake

zake kama watumwa. Mume akishamnunua mke kwa mahari, anakuwa mali yake na

hivyo anamtumia apendavyo.

Katika Mke Mwenza, Gange ameoa wasichana ambao wakishirikiana na watoto

wanatosha kuhudumia mashamba yake. Badala ya kuajiri wafanyakazi anaoa wake

wengi ili apate watu wa kufanya kazi, faida inayotokana na kazi yao yeye huitia

mfukoni.

Page 39: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

25

Hivyo basi tunatarajia kwamba picha ya mwanamke katika kazi za fasihi, kama

inavyojadiliwa hapo juu japokuwa hizo ni baadhi tu ya kazi chache za fasihi

zilizomsawiri mwanamke kwa namna hiyo zinatuangazia kuhusu picha ya

mwanamke. Taswira tulizozipata zinaambatana na nafasi na majukumu waliyopewa

wanawake katika utamaduni wa jadi katika kazi hizo. Baadhi ya picha hizo

zinajitokeza katika kazi nyingine za kifasihi za sasa na katika jamii zetu kwa jumla.

Hapo tumetumia mifano michache tu na hivyo inatupa misingi ya kuangalia Penina

Muhando ambaye naye ni mwandishi wa kike jinsi alivyowachora wahusika wake

wa kike katika tamthiliya za Hatia na Nguzo Mama.

2.1.1 Mwanamke Wakati wa Umwinyi/ Ukoloni

Katika kipindi hiki, tabaka tawala la kimwinyi lilitawala njia zote za kiuchumi na

kitamaduni. Hali ya mwanamke haikubadilika. Wanawake waliokuwa katika tabaka

la watwana walifanyishwa kazi nyingi kwa masaa marefu, bila malipo yoyote mbali

na kutumiwa kama vyombo vya kukidhi haja na uchu wa wanaume. Wanawake

waliokuwa katika tabaka la mamwinyi vilevile, walikandamizwa na waume zao

ambao waliwachukulia tu kama chombo cha kuzaa na kifaa kilichopenda mapambo

ya kuvutia wanaume (Nzomo 1987:114).

Hali hii ilimfanya mwanamke abaki kwenye nafasi duni sana katika jamii, nafasi ya

chini ya kuonekana, kujiona na kujikubali kuwa pambo la kuufurahisha moyo na

jicho la mwanaume (Senkoro 1987:24).

Mfumo wa urithi kwa upande wa baba ambao ulitokana na ugawaji wa kazi kwa

misingi ya ujinsia, uliwafanya wanaume kuwa bora zaidi na waliokua warithi wa

Page 40: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

26

mali yote katika jamii, katika hali hii mwanamke alipewa nafasi ya pili, nyuma ya

mwanaume kazi zake za kushona zilidunishwa kwa vile hazikuleta faida kubwa

kama vile kazi za wanaume za kufuga na kuwinda (Reed 1983:70). Mabadiliko haya

ya kijamii, ambayo yaliletwa na mabadiliko katika utaratibu wa mfumo wa

kiuchumi, yalikuwa na athari kubwa kwa upande wa wanawake. Sifa yake katika

jamii kuanza kupungua. Alianza kudunisha na kupuuzwa (Reed 1970:240) na katika

kipindi hiki mifumo mbalimbali ya kiuchumi, kisiasa, kijamii na kiutamaduni

ilimnyima mwanamke haki yake. Mwanaume aliyekuwa na wanawake wengi

alipewa hadhi ya juu, kwani wanawake walichukuliwa kama mali. Mwanamke

alitarajiwa kufanya kazi zote za shambani na nyumbani. Kwa upande mwingine

mwanaume alipewa wajibu wa kulinda usalama, kujenga nyumba, kuchunga mifugo,

kuwinda na kutayarisha konde. Ingawa mwanamke alifanya kazi nzito shambani

mazao yalipopatikana alinyimwa haki ya kuyamiliki na faida iliyopatikana pia

alinyimwa. Mumba (1990:2) anasema kuwa, katika jamii zilizoendelea urithi

ulikuwa kwa upande wa baba, mwanamke alipewa nafasi duni, nafasi ya kurithi

mali yoyote ilikuwa kwa baba. Wakati huo mwanamke hakuruhusiwa kurithi

chochote mumewe alipofariki. Mwanaume aliyekuwa ameoa alipofariki mali yake

iligawiwa watoto wa kiume. Mjane naye na mali yake yote na watoto alirithiwa na

ndugu wa kiume wa mumewe. Ikiwa ndoa ililazimika kuvunjika mwanamke

aliondoka na watoto walibaki kwa baba yao (Reed 1970:24) na (Ngcobo 1986:144).

2.1.2 Mwanamke Baada ya Uhuru

Wanawake kama wanajamii walipigania uhuru wakitarajia kwamba

utakapopatikana hali yao hii ya maisha ingekuwa bora zaidi. Matarajio haya

hayakutimia, kwani baada ya mkoloni kuondoka, ukoloni uliendelea kwa sura

Page 41: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

27

nyingine na mwanamke aliendelea kunyanyaswa. Waafrika waliochukua mamlaka

walijinyakulia mashamba yaliyokuwa mikononi mwa wakoloni, viongozi

waliwatumia wanyonge kulima katika mashamba hayo ili na wao waweze

kujitajirisha hivyo wanyonge wakiwemo wanawake waliendelea kunyanyaswa hata

baada ya uhuru. Hatamu za uongozi zilichukuliwa na wanaume, wanawake

walisahauliwa. Wanawake waligundua kuwa kupatikana kwa uhuru hakukuleta

mabadiliko yoyote kwa kundi lao hili. Hawakushirikishwa katika kutoa maamuzi

kwa maswala ya kisiasa, kijamii na kiuchumi na hata maswala yanayowahusu wao

wenyewe. Madaraka makubwa nyumbani au serikalini yalipewa mwanaume.

Mipango yote ya maendeleo haikumuhusisha mwanamke. Baada ya muda

wanawake waliona haja ya kunyanyuka na kupigania haki zao (Wipper 1970:4-6).

Kufika miaka ya sabini, harakati za kujikomboa mwanamke zilipamba moto.

Umoja wa mataifa ukiongoza shughuli hizi za ukombozi ulitangazwa mwaka 1975

kuwa mwaka wa kina mama ulimwenguni. Kulionekana haja ya kupigania uhuru wa

kiuana, usawa katika malezi ya watoto, uhuru wa kiuchumi na kisiasa pamoja na

kisheria. Hapa usawa utakuwa na maana kuwa mwanamke atakuwa na uhuru wa

kuyaendeleza maisha yake na kujiendeleza bila vikwazo vyovyote (West

1975:9).Vyama na makundi mbalimbali ya kina mama viliundwa ili kupigania usawa

huu. Mengi yamefanywa na makundi haya kuangazia umuhimu wa mwanamke

kama jamii. Mikutano mingi imewahi kufanywa na mapendekezo mengi yakatolewa

kuhusiana na swala la kuyaboresha maisha ya mwanamke. Kufikia sasa baadhi ya

mapendekezo haya yametekelezwa kwa kiasi fulani, kama vile kuwapo wanawake

wa nafasi katika elimu, siasa na hata sheria. Hata hivyo mengi bado yanatarajiwa

kutoka kwa serikali za Kiafrika (Wipper 1970:8).

Page 42: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

28

2.2 Mapitio ya Machapisho Mbalimbali kuhusu Mwanamke

Chaligha (2011) alitafiti kuhusu, “Usawiri wa mwanamke na mgawanyo wa

majukumu kujinsia katika fasihi picha ya katuni mnato za Kiswahili”. Alibaini kuwa,

mwanamke katika sanaa ya katuni anakandamizwa kwa kiasi kikubwa. Mwanamke

bado hajapewa muonekano chanya japo zipo katuni chache ambazo zimemuonyesha

kwa mtazamo chanya. Katika asasi nyingi mwanamke hukandamizwa na

kudunishwa na vyombo mbalimbali hususani katika suala la utoaji mahari, elimu

duni, uhuru wa kuchagua na kuchaguliwa. Chanzo cha hayo ni mfumo dume uliopo

katika jamii. Pia mwanamke ameonekana hana maadili mema ila ni mtu wa

kugeuzwa na tamaduni wa kigeni ulioingia nchini. Yote haya yamesababishwa na

mwanamke kukosa urazini kuhusu haki zake.

Sanga (2011) naye katika tasnifu yake amechunguza usawiri wa mwanamke katika

utanzu wa nyimbo za kizazi kipya Tanzania. Muziki huo hutawala sana matangazo

ya redio na vyombo vingine vya habari ambavyo vina nguvu katika kujenga

mtazamo wa kijamii juu ya mambo mbalimbali. Ameonyesha kuwa taswira ya

mwanamke katika nyimbo za kisasa anachorwa kwa udhalili na zaidi mwanamke

anachorwa kama mwenye kuwa na tamaa ya starehe na mwenye kukosa uaminifu.

Hivyo basi, kazi ya Sanga itatoa mwanga mkubwa katika utafiti huu katika kupata

usawiri wa mwanamke na mgawanyo wa majukumu katika tamthiliya kwa kuangalia

kwa jicho la kipekee na kihistoria katika kazi nyingine.

Naye Rosalind (2010), mwanamama mcheshi katika makala ya “Ack! Cartoonists

and Feminsts Quarrel Over Demise of Cathy” (yaliyochapwa tarehe 20/8/2010)

anafafanua kwamba, katika magazeti ya katuni ya miaka ya 1975, wanaume tu ndio

Page 43: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

29

waliochorwa kwa mtazamo chanya lakini wanawake walichorwa kama akina mama

wa nyumbani au wasichana wauza baa au hoteli. Anamsifu Cathy na kusema ni

mwanakatuni mfeministi aliyefungua ukurasa mpya kwa kuanza kumchora

mwanamke kwa mtazamo chanya. Anaeleza kwamba wanawake waandishi

walipewa nafasi ya pili katika kuhariri katuni lakini wanawake hawakujali ndipo

wakaamua kuandika na kuchora kupitia wavuti na tovuti. Kwa hakika Rosalind

hakujadili nafasi ya mwanamke kiundani ila aliandika tu makala kuhusiana na nafasi

ya mwanamke mwanakatuni katika fani ya uandishi na uchoraji. Hakuchambua

nafasi ya mwanamke mhusika kama alivyochorwa katika tamthiliya. Hata hivyo kazi

ya Rosalind ni muhimu katika kupata ufafanuzi wa nafasi ya mwanamke katika

uhariri na pia itatoa mwanga wa kuwaelewa wanawake na jinsi wanavyoielezea

nadharia ya Kifeministi ambayo ndiyo itakayotumika katika kuongoza tasnifu.

Soko na Senkoro (2009) wameeleza kwa kifupi nafasi ya mwanamke katika katuni

za michezo. Wanadhihirisha hilo kwa kueleza kwamba nafasi ya mwanamke katika

fasihi picha ya katuni mnato za michezo ni ndogo sana na hata hivyo wamechorwa

kikejeli na kwa mabezo. Hawa wamemwangalia mwanamke katika kipengele kimoja

tu cha michezo, lakini si katika vipengele vingine vya kijamii. Hata hivyo makala

yao itatoa mchango mkubwa sana katika utafiti huu kwani kejeli, sitiari na dhihaka

ndivyo vipengele vinavyobeba ujumbe ambao unaelezea nafasi ya mwanamke katika

fasihi tamthiliya.

Omari (2008) “Katika Makala ya Fasihi Simulizi na Jinsia” ametafiti nyimbo za

watoto na kuona jinsi mwanamke na mwanaume wanavyosawiriwa. Baadhi ya

Page 44: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

30

nyimbo alizofanyia utafiti ni Kula Mbakishie Baba, Nitakusemea kwa Baba, Gari la

Baba, Namsaka Mke Wangu, Tumenye Machungwa na Watoto Wangu eh.

Usawiri wa mwanamke katika nyimbo za watoto ni kwamba baba ni mtu wa

kutoshinda nyumbani na ni mpiganaji. Nyimbo nyingi za watoto zinaonyesha kuwa

baba au mwanaume ni mtu ambaye mara nyingi hakai nyumbani kwani mwanamke

ndiye anayepaswa kukaa nyumbani na kufanya kazi za kifamilia ikiwa ni pamoja na

kumwandalia mwanaume na watoto.

Omari (2008) anaendelea kueleza kuwa, nyimbo nyingi za watoto zinaonyesha kuwa

baba ni mtu wa kuogopwa na ni mkali. Dhana hii inatumika sana katika kuwatisha

watoto pindi wakifanya kosa kwa kuambiwa, “Nitakusemea kwa Baba”. Watoto

wanaposikia hivyo huwa wanaogopa sana. Pia katika utafiti wake anatuonyesha

kuwa, baba ndiye mmiliki wa mali na mwanamke ni mtu ambaye hawezi kujimudu

kimaisha.

Utafiti uliofanywa na Omari kuhusu usawiri wa mwanamke na mwanaume katika

nyimbo za watoto umeonyesha kumdhalilisha mwanamke na kumpa sifa chanya

mwanaume. Hii inatoa taswira kwamba hata watoto wamejengewa imani kwamba

wanawake siku zote ni wanyonge. Utafiti wa Omari umempa mtafiti mchango

mkubwa sana katika utafiti huu.

McCabe (2007), alifanya mahojiano kwa njia ya baruapepe na Jacky Fleming,

mwanakatuni wa Uingereza ambaye alianza kuchora katuni kuhusiana na ufeministi

mwaka 1978. Fleming katika mahojiano hayo, anaeleza kwamba wakati wote

Page 45: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

31

wanawake walichorwa vibaya katika vyombo vya habari. Anasema kwamba, kwa

wanawake hazikuwa habari za kuvutia kabisa kama mwanaume anavyoona vibaya

kwa mwanamke kumfanya asiwe na uwezo wa kuzalisha watoto. Hata hivyo

madhumuni ya mahojiano hayakuchambua nafasi ya mwanamke katika jamii kama

mhusika katika kazi ya katuni, bali kutaka kujua nafasi ya mwanamke mwandishi na

mtazamo wa kifeministi. Ijapokuwa mahojiano hayo hayakuchambua nafasi ya

mwanamke katika fasihi ya tamthiliya lakini yamemsaidia mtafiti kuelewa kwa

haraka nafasi ya mwanamke na jinsia katika tamthiliya za Hatia na Nguzo Mama

zilivyochorwa na wasanii wa kike au wa kiume.

Shule (2004) amefanya utafiti juu ya mchango wa filamu katika harakati za

kupunguza unyanyasaji wa kijinsia na hatari zinazoweza kusababisha UKIMWI.

Katika utafiti wake ameonyesha jinsi filamu zinavyoweza kusaidia kuwaelimisha

vijana wa kiume katika kuzuia unyanyasaji wa kijinsia ambao ni mojawapo ya

mambo yanayoweza kusababisha kuenea kwa maambukizi ya UKIMWI. Stadi hii

inatoa mwanga juu ya mambo au majanga ya jamii yanavyoweza kuingizwa kwenye

tamthiliya na kutumika kama njia ya kuifundisha au kuikanya jamii.

Mwakalinga (2003) amezungumzia nafasi ya mwanamke katika filamu za

Kitanzania. Anaeleza kwamba wanawake wanastahili kusawiriwa katika mtazamo

chanya ili kuwasilisha picha sahihi ya wanawake wa Kiafrika. Wanawake pia

wanatakiwa kuandika hadithi zao wenyewe, na kutengeneza na kusimamia filamu

zao wenyewe. Utafiti wa Mwakalinga unasaidia kuonyesha jinsi ambavyo kazi za

kifasihi zimekuwa zikiwasawiri wanawake na mambo yanayotokea kwenye jamii.

Page 46: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

32

Unasaidia pia katika kutuongoza kuona nafasi mbalimbali za mwanamke katika

tamthiliya za Hatia na Nguzo mama.

Ndungo (1998) alitafiti suala la kiuana katika methali za Gikuyu na Kiswahili.

Utafiti huo ulitilia mkazo matumizi ya lugha ya kitamathali katika methali na

misemo. Ingawa maoni ya Ndungo kuhusu uchorwaji wa mwanamke katika fasihi

simulizi siyo tofauti na wale waliomtangulia, ameonyesha kuwa utamaduni na

malezi huchukua nafasi muhimu katika kuunda na kuimarisha itikadi na mielekeo ya

jamii kuhusu wanawake. Hivyo hata jamii nayo inahusika katika kumkandamiza

mwanamke katika fasihi, tukiangalia jamii aliyokulia mwandishi kama ilikuwa ya

kumdunisha mwanamke basi hata katika kazi zake aghalabu atamdunisha

mwanamke. Hivyo basi Ndungo ametoa mchango maridhawa kwa watafiti wapya.

Pia utafiti wake umetuwezesha kuziba baadhi ya mapengo yaliyokuwepo hapo

awali, kwa kutuangazia picha ya mwanamke kama ilivyo katika fasihi na matumizi

ya lugha ya Kiswahili kwa jumla. Kufika sasa kulingana na tafiti hizo imebainika

kuwa mwanamke anaonewa na kuchukua nafasi ya pili baada ya mwanaume. Hivyo

mwanamke ni kiumbe duni anapolinganishwa na mwanaume, hata hivyo tafiti hizi

hazikumchambua mwandishi mwanamke jinsi alivyomchora mhusika mwanamke

kitu ambacho kimemsukuma mtafiti kufanya utafiti huu.

Lughano (1989) amehakiki usawiri wa mwanamke katika riwaya nne za Euphraise

Kezilahabi. Kulingana naye ni mwandishi wa kiume ambaye anakatisha tama

ukombozi wa mwanamke. Maoni ya Lughano ni kwamba Kezilahabi anaendeleza

falsafa ya jamii yake kongwe kuhusu mwanamke, falsafa ambayo inamchukulia

mwanamke kuwa kiumbe duni aliye chini ya utawala wa mwanaume. Utafiti huu pia

Page 47: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

33

umetusaidia sana katika utafiti wetu kwani maoni yake yameweza kuendeleza

mawazo yetu kuhusa usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina

Muhando.

Chesaina (1987) amehakiki jukumu na usawiri wa wahusika wa kike katika

tamthiliya zilizoandikwa katika lugha ya kiingereza, Kifaransa na Kiswahili.

Amewachukua waandishi wa kike na wa kiume na kuwalinganisha, huku akitoa hoja

kwamba waandishi wa kike wanatofautiana kwa kiasi kikubwa jinsi

wanavyowasawiri wahusika wa kike. Hoja yake kuu ni kuwa wanaume

wanapoandika juu ya masuala ya kike wanakumbana na vikwazo kutokana na hali

kwamba wao wenyewe hawajakumbana na dhuluma hizi binafsi kwa hivyo

hawawezi kuipenya nafsi ya mwanamke. Hoja zake zimetufaa katika utafiti wetu,

kwani zimetusaidia katika kubainisha jinsi Penina Muhando alivyoweza kumchora

mwanamke.

Senkoro (1982), amehakiki wahusika wa kike katika riwaya ya Kezilahabi, Dunia

Uwanja wa Fujo (1975). Pia Senkoro (1987) anagusia kwa ufupi uchorwaji wa

wahusika wa kike katika fasihi ipatikanayo katika mfumo wa kibepari. Maoni yake

ni kwamba katika fasihi inayopatikana katika mfumo huu, mwanamke huonyeshwa

kama pambo la kutamaniwa na mwanaume au kama kiumbe duni ambaye jukumu

lake kuu liko kitandani. Uhakiki wake unatofautiana na wa kwetu kwani

hakuchambua kazi yoyote maalum ya kifasihi. Hata hivyo baadhi ya maoni

anayotoa yametufaa katika utafiti huu.

Page 48: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

34

Mbughuni (1982) ameandika makala kuhusu taswira ya mwanamke katika riwaya za

Tanzania. Anatoa hoja kuwa taswira inayoendeleza kuhusu mwanamke katika

riwaya za Tanzania ni za aina mbili. Ya kwanza ni ile ya Hawa wa biblia ambaye

anawakilisha uovu wote katika jamii, mchoyo, shetani na mlaghai. Taswira ya pili

inamweka mwanamke jikoni, akiwa anatawaliwa na mwanaume. Wakati Mbughuni

amejifunga kwenye riwaya za Kitanzania sisi tumeshughulikia tamthilia za

mwandishi wa Kitanzania vilevile. Hivyo basi kazi yake hiyo imetusaidia sana katika

utafiti wetu.

Siyo hao tu waliomjadili mwanamke bali hata waandishi wengine ambao

wameandika riwaya, tamthilia na ushari. Waandishi hao ni pamoja na Mwanakupona

binti Mshamu aliyeandika Utenzi wa Mwanakupona uliochapwa na kuhaririwa na

Nabahany (1972). Mshamu katika utenzi wake anasisitiza maadili mema na jinsi

mwanamke anavyotakiwa kuishi na mumewe. Anatakiwa awe mnyenyekevu,

mwelekevu na msikivu pale mwanamume anaposema au kutoa amri fulani.

Utendi huu umeleta mwanga katika utafiti huu hasa katika vipengele vya maadili,

utamaduni na dini. Kazi hii kubwa ya Mshamu imeleta mwanga hasa katika

utamaduni na dini, ambazo ni asasi kongwe zilizomuonea, zilizomtweza na

kumnyanyasa mwanamke.

Waandishi wengine ni pamoja na Nawal El Saadawi aliyeandika riwaya ya Woman

at Point Zero (1983), Elieshi Lema aliyeandika riwaya ya Parched Earth (2001), na

Ama Ata Aidoo aliyeandika riwaya ya Changes (1991). Hawa ni waandishi

wanawake waliomchora mwanamke

Page 49: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

35

kama jamii ilivyomhesabu. Hata hivyo mwanamke katika riwaya hizo anaonesha

harakati za kujikomboa na kujitoa katika kunyanyaswa, kuonewa na kuwa tegemezi

kwa mwanaume,anaondoka na kujitafutia maisha ya uhuru wake yeye mwenyewe.

Kazi za wanawake wanafasihi hawa, zitajenga utafiti huu katika kushadidia data za

msingi ambazo zitachunguza usawiri wa mwanamke katika fasihi ya tamthiliya za

Hatia na Nguzo Mama.

2.3 Hitimisho

Mapitio haya yametoa mwanga kwa mtafiti kuhusu usawiri wa mwanamke katika

tamthiliya za Hatia, na Nguzo Mama kwani usawiri wake haukuelezewa kiasi cha

kueleweka vizuri katika jamii, na hivyo imempa mtafiti uwanja mpana wa kujadili

usawiri huo katika tamthiliya na kuchambua mgawanyo wa majukumu kijinsia

katika jamii kama tamthiliya hizo zilivyobainisha.

Sura inayofuata inahusu mbinu mbalimbali za utafiti zilizotumika katika utafiti huu

pamoja na mbinu zilizotumika kuchambua na kuwasilisha data za utafiti.

Page 50: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

36

SURA YA TATU

MBINU ZA UTAFITI

3.0 Utangulizi

Sehemu hii inahusika na mbinu mbalimbali za utafiti zilizotumiwa na mtafiti ili

kupata data na mbinu ambazo zilitumiwa kuzichambua na kuziwasilisha data hizo

kulingana na mada ya utafiti.

3.1 Eneo la Utafiti

Utafiti huu ulifanyikia uwandani na maktabani. Mtafiti alikwenda Chuo Kikuu cha

Dar es salaam, katika kitengo cha sanaa za maonyesho (FPA) kuwahoji wahadhiri

watano ambao ni Profesa Penina Muhando, Daktari Imani Sanga, Daktari Vicensia

Shule, Daktari Mona Mwakalinga na Bw Mtiro. Maktaba zilizotumika ni Maktaba

Kuu ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Chuo Kikuu cha Dodoma, Taasisi ya

Taaluma za Kiswahili (TATAKI), Mtandao wa Jinsia, Taasisi ya Taaluma ya

Maendeleo Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Mapitio ya vitabu pia yalifanywa katika

Makavazi ya Taasisi ya Taaluma za Kiswahili, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Pia,

mtafiti alitumia njia za kielektroniki kwa ajili ya kupata makala mbalimbali na

baadhi ya data za upili ambazo zilisaidia kukamilisha utafiti huu.

3.2 Mbinu za Ukusanyaji wa Data

Data za msingi zilipatikana katika tamthiliya teule za Penina Muhando ambazo ni:

Hatia (1972) na Nguzo Mama (1982). Mtafiti kachagua tamthiliya hizo kwa sababu

ni mojawapo ya tamthiliya ambazo hazijafanyiwa tafiti za kina kuhusu taswira

zinazojitokeza kuhusu mwanamke. Pia, tamthiliya hizo wahusika wake wakuu ni

wanawake. Pia, data fuatizi zilipatikana katika majarida, tasnifu, vitabu, makala na

Page 51: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

37

machapisho mbalimbali yaliyogusia suala la tamthiliya kwa jumla, ikiwa ni pamoja

na yale yaliyogusia usawiri wa mwanamke katika fasihi na katika kazi ambazo si za

kifasihi pamoja na mahojiano yaliyofanyika kwa mwandishi mwenyewe na

wataalamu wa fasihi.

3.2.1 Uchambuzi wa Matini

Uchambuzi wa matini ni mbinu inayojumuisha uchambuzi wa majarida, magazeti

pamoja na matini za mazungumzo ambazo hazijaandikwa (Kothari 2008). Katika

utafiti huu mbinu hii ilitumika kupata data za msingi pamoja na za upili. Mtafiti

alisoma kazi teule, machapisho na nyaraka mbalimbali ambazo zilimpatia data za

msingi na data za upili zilizomsaidia mtafiti katika utafiti huu.

3.2. 2 Mahojiano / Usaili

Mahojiano ni njia ya kupata data inayohusisha maswali na majibu yanayofanywa

kwa mazungumzo kati ya mtafiti na mtafitiwa (Kothari 2008). Kwa mujibu wa

King‟ei na Kisovu (1987) wanaeleza kuwa, mahojiano ni mbinu inayotumika katika

utafiti wa Fasihi Simulizi ambapo mtafiti huweza kukutana ana kwa ana na

watafitiwa kwa njia zingine na kuuliza maswali kuhusu habari anayoitafiti. Pia

mtafiti anaweza kufafanuliwa jambo fulani lenye utata ili aweze kulifahamu vizuri.

Mbinu hii ilimsaidia mtafiti kupata taarifa za msingi zinazohusiana na mada ya

utafiti. Kwa upande wa uwandani njia ya mahojiano huru ilitumika, na katika

mahojiano hayo nyenzo iliyotumika ni dodoso. Faida ya kutumia mahojiano ni

kupata taarifa za msingi kwa haraka. Pia ilimsaidia mtafiti kupata data nyingi na

thabiti zilizosaidia kufanikisha utafiti huu. Kazi ya mahojiano ilifanywa na mtafiti

Page 52: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

38

katika maeneo ya utafiti yaliyopendekezwa.Wahojiwa walitakiwa kujibu maswali

yaliyoandaliwa na mtafiti kwa maelezo au kwa kuandika.

3.3 Usampulishaji na Njia za Usampulishaji

Sampuli ni sehemu ya populesheni ambayo mtafiti alitumia katika ukusanyaji wa

taarifa zilizomsaidia kufikia malengo ya utafiti. Mtafiti alitumia mbinu ya

usampulishaji nasibu, lengwa na holela, ambapo kila mhusika anapewa nafasi sawa

ya kuchaguliwa na kujumuishwa katika sampuli. Katika utafiti huu mtafiti

aliwachagua wawakilishi hao kulingana na jinsi wanavyokidhi haja na malengo ya

utafiti bila kuzingatia jinsi zao. Sampuli hiyo ilichaguliwa kiholela kutoka katika

makundi yote yaundayo jamii tafitiwa ili kutoa fursa kwa kila mlengwa kutafitiwa.

Sampuli hiyo ilihusisha tamthiliya mbili ambazo ni Hatia na Nguzo Mama.

Wahadhiri watano kutoka katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam waliobobea katika

taaluma ya Fasihi ya Kiswahili walihojiwa ili kupata taarifa zaidi zilizomsaidia

kukamilisha utafiti huu. Mtafiti alitumia tamthiliya za Hatia na Nguzo Mama na

sababu hasa ya kuteua tamthiliya hizo imetokana na malengo ya tasnifu yenyewe

ambapo tamthiliya hizo wahusika wake wakuu ni wanawake. Pia mwandishi huyu

amechaguliwa kwa kigezo cha umahiri wake katika kumchora mwanamke kwa

namna tofautitofauti kulingana na jinsi au matendo wanayofanyiwa katika jamii zetu

za kila siku. Pia mwandishi huyu ni mwandishi mwanamke ambaye ni

mwanaharakati katika maswala ya jinsia kuhusu ukombozi wa mwanamke na

amewahi kufanya kazi katika mashirika yanayoshughulikia maswala ya mwanamke.

Page 53: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

39

3.4 Vyanzo vya Data

Data zilizochambuliwa zilitoka katika vyanzo mbalimbali, hata hivyo, data za msingi

zilitoka katika tamthiliya za Hatia na Nguzo Mama za Penina Muhando. Data fuatizi

zimetoka katika machapisho mbalimbali yaliyosomwa maktabani na mahojiano

yaliyofanywa na mtafiti kwa wataalamu na waandishi wa tamthilia. Vifuatavyo ni

vyazo vya data za msingi na vyanzo vya data fuatizi.

3.4.1 Vyanzo vya Data za Msingi

Data zilizokusanywa na kutumika katika utafiti huu ni data za msingi na data za

upili. Data za msingi ni data zilizokusanywa na mtafiti kutoka uwandani kwa lengo

la kujibu maswali ya utafiti. Data hizi huwa ni taarifa ambazo ni mpya na za awali

katika tarehe ya kuchapishwa (Kamuzora, 2008). Data za msingi katika tasnifu hii

zilipatikana kwa kusoma tamthiliya ya Hatia na Nguzo mama ili kuchunguza usawiri

wa mwanamke katika tamthilia hizo.

Vitabu vya tamthiliya za Hatia na Nguzo Mama vilinunuliwa ili kupata data za

msingi. Vyanzo hivi vimesaidia katika upatikanaji wa data za msingi ambazo

zimejenga usuli wa tatizo la utafiti.

3.4.2 Vyanzo vya Data Fuatizi

Data za upili zinafafanuliwa na Kamuzora (2008:143) kuwa, ni data zipatikanazo

kutoka katika data zilizokusanywa na watu wengine kwa madhumuni mengine na

katika vyanzo vya kifasihi. Data hizi humilikiwa na mtu mwingine na si mwandishi

wa sasa. Huwa zimekwishatokea katika nyaraka zingine. Maandiko na machapisho

Page 54: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

40

mengine kutoka kwa wataalamu na wachambuzi wa kazi za fasihi zihusuzo

tamthiliya lengwa zilisomwa na data za upili kupatikana.

Vyanzo vya data fuatizi ni vile vilivyotokana na makala mbalimbali zilizosomwa,

kama vile tasnifu, vitabu, majarida na katika makala zilizopatikana katika tovuti na

wavuti na maktabani pamoja na mahojiano na mwandishi na wataalamu wa fasihi.

Data hizi zimesaidia kushadidia data za msingi zilizotumika katika tasnifu hii, na

kusaidia kutimiza malengo ya utafiti na kujibu maswali ya utafiti. Uchambuzi wa

matini ni njia iliyotumika katika vyanzo fuatizi.

3.5 Vifaa katika Ukusanyaji wa Data

Ili kukamilisha utafiti huu, vifaa au nyenzo mbalimbali zilitumika kukusanya data

uwandani na maktabani kama vile kalamu za wino, shajara, ngamizi (kompyuta)

kinyonyi, dodoso, hojaji, kamera na kinasa sauti. Nyenzo hizi zilimsaidia mtafiti

kupata data zisizo za kiidadi, yaani data zilizochambuliwa kwa maelezo kuhusu

Penina Muhando. Ufafanuzi wa vifaa hivyo ni:

3.5.1 Kalamu na Shajara

Ni vifaa vilivyotumika maktabani na uwandani, mtafiti alichukua nukuu muhimu

wakati wote alipokusanya data katika maeneo mbalimbali na kuziandika kwenye

shajara kwa kutumia kalamu.

3.5.2 Dodoso

Ni orodha ya maswali yaliyotumika katika kuwasaili watafitiwa. Mtafiti anakuwa na

maswali ambayo yanamwongoza wakati wa kufanya utafiti (Kothari 2008). Katika

utafiti huu, mtafiti alitumia dodoso katika mahojiano aliyoyafanya na watafitiwa

Page 55: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

41

waliopo katika maeneo yaliyopendekezwa. Watafitiwa hao walishiriki kwa moyo wa

ukarimu katika kujibu maswali ya dodoso hizo na baadaye alizifanyia uchambuzi ili

kuona kama zimejibu maswali ya utafiti na hatimaye kukidhi malengo ya utafiti huu.

3.5.3 Ngamizi (Kompyuta)

Hiki ni kifaa muhimu katika kufanya utafiti kwani licha ya kuwa data za maktabani

na uwandani zimehifadhiwa humo, pia kilitumika kama sehemu ya maktaba tembezi

au maktaba ya kidijitali ambapo mtafiti aliweza kupata fursa ya kusoma nyaraka

zinazohusiana na utafiti wake pamoja na kupata maelezo kuhusu nadharia

iliyotumika. Hivyo basi, ngamizi imetumika katika kipindi chote cha utafiti yaani

kuanzia wakati wa maandalizi ya utafiti, wakati wa kuchanganua data na wakati wa

kuandaa ripoti ya utafiti huu.

3.5.4 Kinyonyi

Ni kifaa ambacho kilitumika kutunza nakala tepe (soft copy) zilizohusiana na utafiti

huu. Kifaa hiki ni muhimu katika zoezi zima la utafiti kwani kilitumika tangu

mwanzo wa utafiti huu mpaka sasa kazi imekamilika. Hata baada ya kukamilika kwa

utafiti, kinyonyi kimetumika kuhifadhi ripoti nzima ya utafiti huu. Matumizi ya kifaa

hiki huenda sambamba na matumizi ya ngamizi. Hivyo, ngamizi na kinyonyi

hutegemeana.

3.5.5 Tepurikoda

Ni kifaa kinachotumika katika kunasa na kurekodi sauti wakati wowote katika

muktadha wote ule. Katika utafiti huu, tepurikoda ilitumika uwandani ambako

Page 56: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

42

mtafiti alirekodi mahojiano baina yake na watafitiwa. Taarifa zilizorekodiwa katika

tepurikoda zilitumika katika uchambuzi wa data katika utafiti huu.

3.5.6 Kamera

Ni kifaa kilichotumika katika kupata taarifa mbalimbali ambazo haziko katika

maandishi kwa mfano picha za wahojiwa na maeneo mbalimbali ambayo

yanahusiana na mada husika.

3.6 Mbinu ya Uchanganuzi wa Data

Data zote zimechanganuliwa kwa mkabala usio wa kiidadi yaani ule wa maelezo. Hii

ni kwa sababu utafiti huu haukuhusisha takwimu. Pia, data zimepangwa kulingana

na malengo na maswali ya utafiti, hii ni kwa sababu mtafiti alitaka uchanganuzi wa

data hizo ulandane na malengo ya utafiti, sambamba na kujibu maswali ya utafiti. Ili

kurahisisha zoezi la upangaji kulingana na malengo na maswali, data zote zimepewa

msimbo ili kuiweka tasnifu katika mtiririko na mpangilio mzuri. Data zote

zilizoambatanishwa kama vielelezo zimechambuliwa kila moja kwa nafasi yake, ili

kurahisisha uchakataji. Pia, data fuatizi zimenukuliwa pale ilipobidi ili kuthibitisha

uchambuzi wa data za msingi.

3.7 Hitimisho

Mbinu hizo ndizo zilizotumika katika kupata data zilizochambuliwa katika utafiti

huu. Data hizo zimejibu maswali ya utafiti na matokeo yake ndiyo yametimiza

malengo ya utafiti na hivyo tatizo la utafiti limetatuliwa na pengo la mapungufu

limezibwa japo kwa sehemu au kutoa mwanga juu ya tafiti zijazo. Sura inayofuata

inahusu uwasilishaji na uchambuzi wa data.

Page 57: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

43

SURA YA NNE

UWASILISHAJI, UCHAMBUZI NA MJADALA WA MATOKEO YA

UTAFITI

4.0 Utangulizi

Sura hii inahusu uwasilishaji na uchambuzi wa data. Tromp na Kombo (2006:110)

wanasema, uchambuzi wa data ni kuchunguza kwa undani data na kuzitolea

hitimisho. Uwasilishwaji wa data kwa mujibu wa waandishi hawa ni namna ya

kupangilia data ili ziweze kueleweka vizuri. Uwasilishwaji umefanywa kwa mbinu

ya ufafanuzi kulingana na malengo mahsusi ya utafiti. Sura hii imeshughulikia

mambo matatu yanayoakisi malengo yetu, kila jambo tumejadili kwa kina kuakisi

data zilizokusanywa uwandani kwa kutumia mbinu za mahojiano na mapitio ya

maandiko. Pia nadharia ya Ufeministi wa Kiafrika imetumika.

Kuna mitazamo miwili katika tasnifu hii, mtazamo hasi na mtazamo chanya, kwa

maana kwamba, Penina Muhando katika tamthiliya zake za Hatia na Nguzo Mama

kamchora mwanamke kama mtu anayeweza yeye mwenyewe hata asipowezeshwa.

Lakini pia kwa upande mwingine ameonyesha jinsi gani wanaume wanavyomtazama

mwanamke kama kiumbe dhaifu kinachomtegemea mwanaume kwa kila kitu hata

kimawazo. Pia ameonyesha jinsi mwanamke alivyobebeshwa mambo yote maovu

katika jamii.

Pia utafiti huu umebainisha majukumu anayopewa mwanamke katika jamii na jambo

la tatu tumejadili athari zinazotokana na usawiri wa mwanamke katika kazi za

kifasihi. Sehemu hii imejadili tamthiliya mbili za Penina Muhando ambazo ni Hatia

Page 58: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

44

(1972) na Nguzo Mama (1982). Mwisho ni sura ya tano ambayo ina muhtasari wa

tasnifu nzima, matokeo ya utafiti, mapendekezo na hitimisho.

4.1 Historia ya Penina Muhando

Penina Muhando alizaliwa 03/03/1948 wilayani Kilosa katika mkoa wa Morogoro

nchini Tanzania. Kwa upande wa kabila, anasema kuwa mama yake alikuwa Mnguu

kutoka Tanga na baba yake ni Mkaguru kutoka Morogoro. Penina Muhando,

alisoma katika shule mbalimbali za Tanzania na mwaka 1971 akapata shahada ya

kwanza. Baada ya kumaliza masomo hapo Chuo Kikuu cha Dar es salaam, aliajiriwa

hapo hapo chuoni kusomesha Sanaa za Maonesho. Mwaka 1973 alitunukiwa

Shahada ya Uzamili ya Sanaa za Maonyesho na mwaka 1983, Muhando alipata

Shahada ya Uzamivu ya Falsafa ya Sanaa za Maonyesho hapo hapo Dar es Salaam

na kupanda madaraja hadi kufikia hadhi ya Profesa. Penina Muhando pia ni

mwanamke wa kwanza Tanzania kushika wadhifa wa Afisa Taaluma katika Chuo

Kikuu cha Dar es Salaam.

Licha ya kuwa mhadhiri hapo chuoni, Penina alitumia muda wake mwingine

kuandika tamthiliya na kumfanya kuwa mmoja kati ya waandishi waliofanikiwa sana

katika uandishi wa sanaa za maonesho. Aidha, baada ya kuolewa na Bwana Mlama,

Penina alibadili jina la ubini wake na kwenda kwenye jina la mumewe hivyo kuitwa

Penina Mlama. Hata hivyo, kwenye kazi zake mbalimbali bado ameendelea

kulitumia jina lake la Penina Muhando. Katika maisha yake na mumewe Penina

amebahatika kupata watoto wawili. Kwa sasa ni mjane.

Page 59: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

45

Mwandishi huyu kwa sasa amerudi tena katika Chuo Kikuu cha Dar es Salam

kusomesha, baada ya kupumzika kwa muda kutokana na kutingwa na majukumu ya

ukurugenzi katika asasi zinazojishughulisha na masuala ya wanawake. Baadhi ya

asasi hizo na mashirika hayo yasiyokuwa ya kiserikali aliyoyafanyia kazi ni

Foundation for African Women Educationalist (FAWE), shirika lenye makao makuu

jijini Nairobi Kenya, na pia asasi isiyo ya kiserikali iitwayo Campaign for Female

Education (CAMFED) Tanzania, yenye makao yake makuu huko Cambridge,

Uingereza.

Penina Muhando ni mojawapo wa wasomi wa kujivunia kutoka katika Chuo Kikuu

cha Dar es salaam na Tanzania kwa jumla, kwa maana ni msomi aliyesomea nchini

Tanzania, kuanzia shule ya msingi, sekondari mpaka Chuo Kikuu aliposomeshwa

Shahada ya Kwanza, ya Pili mpaka Shahada ya Udaktari wa Falsafa katika Sanaa za

Maonesho.

Penina Muhando ameandika kazi mbalimbali kwa lugha ya Kiswahili na Kiingereza

zote zikiwa na mchango mkubwa kwenye Fasihi Andishi hususani kwenye utanzu

wa tamthiliya. Baadhi ya kazi hizo ni: Hatia (1972), Tambuaeni Haki Zetu (1973),

Heshima Yangu (1974), Pambo (1975), Modern African Theatre with Special

Emphasis on East Africa (1975), Nguzo Mama (1982), Lina Ubani (1984), The

Challenge to the African Writers Today (1990), Culture and Development: The

Popular Theatre in Africa (1991), Gender Responsive Pedagogy: a Teacher’s

Handbook (2005). Kati ya kazi zilizotajwa hapo juu za kitamthiliya ni: Hatia

(1972), Tambueni Haki Zetu (1973), Heshima Yangu (1974), Pambo (1975), Talaka

si Mke Wangu (1976), Nguzo Mama (1982) na Lina Ubani (1984).

Page 60: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

46

Profesa Penina Muhando mwandishi wa Hatia na Nguzo Mama akiwa katika

mahojiano na mtafiti ofisini kwake Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam tarehe

11/11/2013.

4.2 Hatia (1972)

4.2.1 Utangulizi

Katika utangulizi, tunaona kuwa, Hatia ni mchezo unaotuonyesha matatizo

yanayowakabili wanawake wanapoishi kwenye mazingira yenye msingi tofauti na ile

waliyolelewa nayo. Cheja ni mfano wa wasichana wengi Tanzania ya leo ambao

waendapo kuishi mjini na hali wamelelewa kijijini hutumbukia katika udanganyifu

wa kimjini ambao baadaye huwaletea matatizo wao pamoja na jamii zao.

Tamthiliya hii ya Hatia inaweza kumfaa mtu wa kiwango chochote kwa kuwa

inahusu maisha ya watu wengi katika jamii na hasa vijana. Mwandishi amedhihirisha

umahiri wake kwa kuonyesha jinsi jamii zetu zinavyowakandamiza wanawake na

kuwaweka katika nafasi duni.

Page 61: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

47

Ni dhahiri kuwa mambo yanayozungumzwa katika tamthiliya hii, kwa hakika ni

mambo ambayo wanafanyiwa wanawake wengi katika jamii tunazoishi.

Tamthiliya ya Hatia (1972) ina jumla ya maonesho sita yenye kurasa 41. Onesho la

kwanza lina kurasa tisa. Ni onesho lililoonesha jinsi wasichana wanaotoka kijijini

wanavyokubali kudanganywa na wanaume wa mjini. Mwanamke anakubali

kushawishiwa na vijana wa mjini bila kujua kuwa kuna madhara, na bila kufanya

uchunguzi wa kina kwa vijana hao. Mfano mzuri ni mhusika Cheja ambaye

alidanganywa na Juma muuza samaki na kisha kukubali kufanya naye mapenzi.

Onesho la pili lina kurasa chache zaidi ya onesho la kwanza. Lina jumla ya kurasa

sita tu. Linaonesha juhudi za akina mama katika kushirikiana katika kazi mbalimbali

ili waweze kuyamudu maisha. Licha ya hayo, pia linaonesha jinsi mwanamke

anavyoweza kumshauri au kutoa ushauri katika mambo mbalimbali katika jamii. Hii

inaonesha kuwa, ushauri wa mwanamke katika familia au jamii ukifuatwa basi ni

wazi kuwa unaweza kuleta mafanikio. Mfano mzuri ni Mwanamke II

anavyomshauri Bw Chowe kuchukulia mambo taratibu, kutafakari na kufuata

utaratibu wa jamii zao.

Katika onesho hili la pili ndipo tunaonyeshwa jinsi mwanamke alivyo na ushirikiano

katika jamii na mshauri wa mambo mbalimbali katika jamii. Hapa mwanamke

amepewa nafasi ya kumshauri mwanaume, amesawiriwa kama mtu mwenye busara

hata katika kuamua na kufanya maamuzi mbalimbali.

Page 62: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

48

Onesho la tatu lina jumla ya kurasa nane. Katika onesho hili ndipo tunaoneshwa

jinsi mila na desturi za jadi zinavyotenga mwanamke katika maamuzi. Mfano mzuri

ni Bi Chowe na mwanae Cheja kutokushirikishwa katika kikao cha wazee ambacho

kililenga kuzungumzia matatizo yaliyotokea katika familia yao. Pia, hapa

mwanamke anaonekana kama kitega uchumi kwa kuwa wazee wamekaa na kupanga

malipo ya Cheja bila kumshirikisha yeye mwenyewe.

Onesho la nne lina jumla ya kurasa sita. Katika onesho hili tunaoneshwa jinsi mila

na desturi za jadi zinavyotumika katika kuamua mambo. Waapishaji wanajiandaa

kwa ajili ya shughuli ya uapishaji. Kutokana na hali ya usasa na kuelimika, Sembuli

anakataa kuapishwa kwa kuwa haamini mambo hayo. Japokuwa alisingiziwa, lakini

haamini kama mila zao zinaweza kuhakikisha hilo. Hapa tunaoneshwa pia shughuli

hii ya uapishaji inafanywa na wanaume tu.

Onesho la tano lina kurasa tatu. Ndilo onesho lenye kurasa chache kuliko yote.

Katika onesho hili, tunaonyeshwa udhaifu wa mwanamke, pia tunaonyeshwa jinsi

mwanamke anavyoweza kukata tama na kufanya maamuzi ya kujiua. Mfano mzuri

ni mhusika cheja baada ya kuona vita imepamba moto kijijini anataka kujinyonga.

Pia katika onesho hili tunooneshwa jinsi mwanamke alivyosawiriwa kama mlezi.

Mfano ni Bi chowe kumtafuta mwanae kwa bidii zote ili aweze kumwokoa na mauti

kwani atamtunza yeye na mtoto wake atakayezaliwa.

Onesho la sita lina kurasa tisa sawa na onesho la kwanza. Onesho linapoanza,

wanaonekana familia zote mbili zilivyoumizwa. Vita hivi vilikuwa vita vikubwa

sana maana watu waliumia sana. Hapa ndipo mwanamke amesawiriwa kama mtu

Page 63: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

49

mwongo katika jamii, kwa kuwa kasababisha vita kutokea kwa kusema uongo.

Mfano mzuri ni mhusika Cheja ambaye kutokana na ujinga wake wa kuyavamia

maisha ya mjini kusababisha kupata ujauzito na kisha kumtaja mtu asiyehusika kuwa

ndiye aliyehusika na ujauzito huo.

4.2.2 Uwasilishaji na Uchambuzi wa Data

4.2.2.1 Mwandishi Alivyomsawiri Mwanamke katika Tamthilia ya Hatia (1972)

kwa upande Chanya katika Nafasi na Kimajukumu

Ushirikiano

Mwanamke amechorwa kama mtu mwenye ushirikiano katika jamii. Mwandishi

amedhihirisha hili kwa kumtumia mwanamke wa I, mwanamke wa II na mwanamke

wa III pamoja na Bi. Chowe katika uk. wa 10, wanaposema kuwa:

MSIMULIZI: Kijiji kimoja katika wilaya ya Kilosa. Saa za mchana. Nje ya

nyumba ya Bwana Chowe, wanawake watatu wanatwanga

mahindi huku wakiimba wimbo wa kutwanga. Mmoja wao

Bi Chowe na wengine majirani.

Bi. Chowe: Jamani tayari yameiva. Tupepete sasa. Hivyo basi Muhando

anatuonyesha namna wanawake wanavyoshirikiana katika

jamii. Ili kurahisisha kazi wanakutana kwa pamoja na

kufanya kazi kwa kushirikiana ili waweze kumaliza mapema.

Mtafiti ameona kuwa, wanawake hupenda sana kushirikiana katika kazi mbalimbali

ambazo zinaleta maendeleo yao kiuchumi. Kama alivyoeleza Daktari Vicensia Shule

kuwa, wanawake wengi wa miaka hii ya karibuni wamekuwa na ushirikiano

mkubwa sana kiasi kwamba maisha yao yanabadilika kutoka katika hali ya

unyanyaswaji na waume zao. Anaendelea kusema kuwa, kutokana na ushirikiano

huu wa akina mama wameweza kuanzisha vikundi mbalimbali vya uwekezaji na pia

Page 64: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

50

kujiunga na vyama mbalimbali katika ujasiriamali. Anaeleza kuwa kutokana na

ushirikiano wanaoonyesha wanawake, na manufaa ya kushirikiana kwao, wanaume

nao wameshawishika nao kujiunga na vyama mbalimbali kitu ambacho kinafanya

vyama hivyo viwe vya watu wote. Bila kuchagua wanawake na wanaume.

Anamalizia kwa kusema kuwa, ushirikiano katika jamii ni kitu muhimu sana. Umoja

ni nguvu utengano ni dhaifu

Uvumilivu

Mwanamke amechorwa kama kiumbe mvumilivu katika maisha na hata katika ndoa

yake. Hii inajidhihirisha katika uk. wa 13, anaposema kwamba:

Bw. Chowe: Acha kuniletea upuuzi hapa. Alikwambia atakuja? (Bi. Chowe

anatingisha kichwa). (Anafoka.) kwanini hukumuuliza. Vipi

yeye anafanya kutoroka na kuwasumbua akina Sembuli? Jambo

la aibu na wewe unalichekelea kama mpumbavu. Mwite hapa

Cheja sasa hivi aeleze nini kimemtorosha. Wanawake wengine

kumbe wajinga. (Bi Chowe bado amesimama ameshangazwa na

hasira za mume wake). Upesi kamlete mtoto wako kabla

ghadhabu yangu haijavuka kiwango. Shenzi kabisa.

Bw. Chowe: Hivyo wewe unajua maana ya kwenda kuleta kitu. Nimesema

nenda kamlete hapa. Punda wee! Kama kuna mambo

mmeyapanga na mtoto wako leo mtanieleza au mtaniona.

Katika uk. wa 14, mwandishi anaendelea kusema kuwa:

Bw. Chowe: hapana mama yangu. Nilifahamu hili litoto lijinga sana. Lakini

limeharibiwa na limama Lake. Sisi kwenye ukoo wetu

hatuko namna hii. Haya yanataka mpaka yapigwe ndipo

yaseme. Lakini kama ni kupiga tu kwangu si kazi hasa kwa

jambo kama hili. (Anawatishia) leo nyie, nyie! (kwa

mwanamke wa II) mama yangu; mimi na Sembuli

tunaaminiana halafu leo hili litoto linatoroka hata bila

kuaga. Kwani wamekufanyia uovu nao. ( kwa sauti) sema!

Sema! Au nitakukong‟ota sasa hivi (anainua fimbo).

Page 65: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

51

Pamoja na kuwa Cheja kweli kafanya makosa, lakini lawama zote pamoja na matusi

anabebeshwa mama yake. Licha ya kutukanwa, Bi Chowe amevumilia na kufuata

kila analoambiwa na mume wake.

Mtafiti amegundua kuwa, wanawake wana asili ya uvumilivu katika mioyo yao.

Kwani pamoja na mateso yote ayapatayo mwanamke katika ndoa, mara nyingi

huyavumilia wala hakimbii mateso hayo. Profesa Imani Sanga na Bw Mtiro kwa

pamoja mawazo yao yanafanana. Wote waliona kuwa mwanamke ni kiumbe

mvumilivu sana katika maisha kuliko mwanaume. Wanasema kuwa, pamoja na

mateso yote ayapatayo mwanamke ikiwa ni pamoja na kupigwa, kutukanwa,

kudhalilishwa pamoja na kusalitiwa hasa katika ndoa wanavumilia. Mtiro alitoa

mfano jinsi mwanamke katika jamii za Kikurya anavyopigwa na mume wake lakini

sio rahisi mwanamke akimbie bali huvumilia ili aweze kuwalea watoto wake.

Mshauri

Pia mwanamke kachorwa kama mshauri mzuri katika jamii. Hili linajidhihirisha

dhahiri katika uk. wa 13-14, mwandishi anaeleza kuwa:

Mwanamke II: Baba mkimchukulia polepole atasema. Mbona

nyumbani ndiko alikokimbilia.

Mwanamke II : Hapana, baba, hapana. Usiyachukulie mambo kwa

ghadhabu. Usijihangaishe kumtafuta unaweza

usimwone. Na nani ajuae, kwenye jiji kubwa kama

Dalisalama lolote linaweza likutokee. Baraza letu la

wazee mbona lipo na wewe ukiwa mmoja wao.

Yafanyeni mashtaka haya kimila tu.

Page 66: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

52

Mwanamke II: Isiwe mambo harakaharaka. Hata hao wazee wenyewe

si ajabu wengine wako wako makazini kwao kama

mkutano ni leo hawataweza.

Mwanamke II: Vumilia tu baba. Yote yategemea baraza litakapokutana.

Kutokana na maelezo hayo ni wazi kabisa kuwa mwanamke ni mshauri mzuri sana

katika jamii. Bwana Chowe alitaka kuchukulia mambo kwa pupa lakini kutokana na

ushauri wa mwanamke wa pili alipunguza hasira na kisha kufuata utaratibu

unaotakiwa.

Mlezi

Mwanamke amechorwa kama mlezi na mtu mwenye huruma. Mfano mzuri ni Bi

Chowe alivyokuwa analia kuhusu ujauzito wa mwanae na kuhangaika kumwokoa

alivyotaka kujinyonga. Haya yanajidhihirisha katika uk. wa 31 kuwa:

Bi. Chowe: Uuuuuuuuuuuu! Uuuuuuuuuuuuuuuu! Mie, ooooooooo

maskini mie (mara hiyo mzee wa 1 na 2 wanafika tena

wanakimbia kutoka upande walioelekea mwanzo

wanashtuka kumwana Bi. Chowe.)

Mzee 2: Nini tena jamani?

Mzee 1: Kuna jambo lolote lililotokea?

Bi. Chowe: Eee wazee wangu, mimi leo sijui Mungu kanionaje.

Namtafuta Cheja kapotea.Watoto wamesema wamemwona

ametoka ameshika kamba. Uuuuuu! Labda anataka kwenda

kujinyonga.

Mzee 2 : Jamani huyu mtoto vipi lakini?

Bi. Chowe: Cheja mwanangu angekaa tu hata huyo mototo nitalea

mimi. Niacheni nimtafute upesi kabla hajajiua. (Anatoka

mbio)

Page 67: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

53

Licha ya mwanamke kuonekana kama mshauri pia mwanamke amechorwa kama

mtu mwepesi kuomba msamaha. Hii inajidhihirisha katika uk. wa 38, Cheja

anaposema kuwa:

Cheja: Nimesema mwacheni. Iliyobaki naomba mnisamehe.

Mnisamehe wazee wangu, hasa mzee Sembuli, mnisamehe.

Hivyo basi, mwandishi amemwonyesha mhusika Cheja kama mfano mzuri wa

mwanamke baada ya kugundua kuwa amekosa amejirudi na kuomba msamaha.

Mbunifu

Mwanamke kachorwa kama mtu mbunifu na mwenye uwezo wa kujitegemea bila

msaada wa mwanaume. Mwandishi anadhibitisha haya katika uk. wa 39, anaposema

kuwa:

Cheja: Juu ya maisha yangu niachieni mimi mwenyewe. Nitakwenda

Majogo.

Bi. Chowe: Uende wapi tena? Utulie nyumbani sasa. Unaanza kusema nini

tena?

Cheja: Ndio mama. Nitakwenda majogo nijiunge na hao walioanzisha

kijiji kipya.

Nitashirikiana nao katika kazi nijitegemee.

Kutokana na maelezo hayo basi, ni dhahiri kuwa mwanamke anaweza kujitegemea

mwenyewe hata bila kumsubiri mwanaume amletee.

Mtafiti amegundua kuwa, mwanamke pia akidhamiria jambo anaweza. Sio kwamba

mwanamke humtegemea mwanaume kwa kila kitu, bali wanawake nao wana juhudi

mbalimbali ambazo zinachangia au zinatoa mchango mkubwa katika familia.

Page 68: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

54

4.2.2.2 Mwandishi Alivyomchora Mwanamke katika Tamthilia ya Hatia (1972)

kwa upande Hasi katika Nafasi na Kimajukumu

Rahisi kushawishika

Mwanamke amechorwa kama mtu ambaye ni rahisi kushawishika. Mfano mzuri ni

Cheja. Hii inaonekana wazi katika uk. wa 8 asema kuwa:

Juma: Lahaula! Unafanya nini mahali kama hapa peke yako?

Unatoka wapi na unakwenda wapi?

Cheja: Popote. Juma nimekuwa nikikutafuta hii wiki ya pili.

Nimefika nyumbani kwako lakini nimeambiwa

ulishahama. Nimejaribu sana kukupata ulipo bila

mafanikio.

Juma: (Anahamaki) Vipi nini? Kitu gani kinakufanya unitafute hivyo?

Cheja: Haa, Juma mpenzi. Ni wewe kweli unauliza kwa nini

ninakutafuta! Hayo yote tuyaachilie mbali. Nina jambo

kubwa la kukuambia, Juma.

Juma: (Akimkodolea macho) jambo gani?

Cheja: (polepole) Juma yale mambo ya siku ile. Nina mimba.

Kutokana na hayo, mwandishi anaonyesha kuwa, Cheja kashawishiwa na Juma na

kisha kufanya naye mapenzi na hatma yake ni ujauzito ambao Juma hataki hata

kusikia. Anamkataa, anasema kuwa yeye hahusiki. Cheja alitoka kijijini na kuvamia

maisha ya mjini. Matokeo yake kashawishiwa na Juma naye akakubali kwa haraka

bila kuwaza kuwa wanaume wengi wa mjini ni matapeli na ni waongo. Yeye alitaka

tu kutimiza haja zake na kisha kumwacha.

Kitega Uchumi

Mwanamke amechorwa kama kitega uchumi katika jamii. Haya yanadhihirika wazi

katika uk. wa 11 pale mwandishi anaposema kuwa:

Page 69: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

55

Bi. Chowe: Ndugu yangu wee! huyo mkami kwani ni mtu wa kuoa hivi

karibuni? Anangojea mali ya dada yake ndio aoe nayo.

Hapa mwandishi anatuonyesha kuwa, mtoto wa kike katika jamii ni kama

kitegauchumi kinachotegemewa na familia. Endapo mtoto wa kike akiolewa,

watapata fedha na vitu ambavyo vitawasaidia katika familia. Kama ilivyoonekana

kwa mhusika Cheja ambaye ni binti, na Mkami ni kijana ambaye anategemea kuoa

endapo dada yake ataolewa na kutolewa mahari na ndipo sehemu ya mahari hayo

itolewe kwa ajili ya Mkami.

Daktari Vicensia Shule, Daktari Mona Mwakalinga na Profesa Imani Sanga kwa

pamoja mawazo yao kuhusu mwanamke kama kitega uchumi yanafanana.

Wameeleza kuwa suala la mwanamke kuonekana kama kitega uchumi ni la muda

mrefu hasa katika kipengele cha mahari.

Wazazi wengi wanawaozesha watoto wao wakiwa katika umri mdogo lengo lao ni ili

wapate mali kupitia mtoto huyo. Imeonekana kuwa ni tatizo kubwa kwa jamii

nyingi za Kiafrika kumbadilisha mtoto wa kike na vitu kwa lengo la kujinufaisha

kimaisha. Wao wameona kuwa kutokana na mila na desturi za jamii zetu

zinasababisha mwanamke kuwa kitega uchumi katika familia

Chombo cha Starehe

Mwanamke amechorwa kama chombo cha starehe katika jamii. Katika uk. wa 1-9

mwandishi anaonyesha haya anapoeleza kuwa:

Cheja: Haa, Juma mpenzi. Ni wewe kweli unaniuliza kwa nini

ninakutafuta! Haya yote tuyaachilie mbali, nina jambo

kubwa la kukuambia Juma.

Page 70: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

56

Juma: Una mimba? Yangu mimi.

Juma: Unasema upange na nani? Kama una maana upange na mimi,

tafadhali sana dada tusiingiliane. Yanakuhusu wewe

mwenyewe.

Kwa maelezo hayo, mwandishi anaonyesha kuwa, Juma hakuwa anampenda Cheja

bali haja yake ni kupata starehe yake aliyokuwa anaihitaji. Alihitaji kuburudika tu na

kuondoka, lakini ujauzito ulipotokea hakutaka hata kusikia, anadai yeye hahusiki.

Mtafiti amegundua kuwa, mwanamke anakuwa kama chombo cha starehe kwa

mwanaume kwa sababu mwanaume akishafanya anachokitaka mambo

yatakayotokea baadaye kama ujauzito hujidai hahusiki. Lakini wakati anamtaka ili

kukamilisha haja zake hujidai anampenda kumbe lengo lake ni kumchezea tu ili

akamilishe haja na starehe yake. Wanawake wengi wakishaambiwa na mwanaume

kuwa anampenda, basi hujikuta akisahau kila kitu na kumwona huyo mwanaume

kuwa ndiye wa maana kwake. Mara nyingi wanawake husahau yatakayotokea

baadaye. Majuto huja baadaye na kukumbuka mapenzi aliyokuwa akipewa na ndipo

huanza kuiona dunia ni mbaya.

Mwongo

Mwanamke amechorwa kama mtu mwongo, tapeli na asiyekuwa mwaminifu ambaye

anadanganyika. Kwa kudhihrisha hili, katika uk. wa 8 na 14 mwandishi anasema

kuwa:

Cheja: Sasa nyumbani nitasema nini ikiwa wewe hapa unanikana?

Juma: Aaa (kwa uovu) hivyo ndiyo shida yako? Waambie kosa hilo

limetendwa na mwajiri wako.

Juma: Tena basi. Wewe tazama. Yule bwana Sembuli mnatoka naye

kijiji kimoja kwa hiyo wazazi wako wanamfahamu. Licha

ya hayo unaishi nyumbani kwake.

Page 71: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

57

Mwandishi anaonyesha jinsi Cheja alivyo mjinga anashawishiwa kwenda kusema

uongo naye anakubali bila kufikiria juu ya kumsemea uongo mtu ambaye hajatenda

kosa hilo. Mwandishi anaendelea kudhihirisha hili kwa kueleza kuwa:

Cheja: (kwa kusita hali akiwa bado katazama chini) Bwana Se….

Bwana Sembuli alinikosea kwa nguvu na sasa mimi ni

mjamzito.

Hivyo basi, mhusika Cheja anakubali kusema uongo ili mtoto atakayemzaa apate

matunzo na yeye mwenyewe kutunzwa, kitu ambacho si haki yake.

Mwanamke kama Chombo cha Biashara

Mwanamke amesawiriwa kama chombo cha biashara katika jamii. Hii

imejidhihirisha pale ambapo wazee wanapanga mali wanazotakiwa kulipwa na

Sembuli, uk. wa 18, anasema kuwa:

Mzee Chimaisi: Haya sasa basi kama alivyokuwa akisema mzee mwenzetu

hapo mwanzo, adhabu ya Sembuli ni malipo. Na kama

ilivyo jadi yetu malipo yenyewe ni sehemu tatu kwa vile

ametumia nguvu. Kwanza malipo ya wazazi, pili, malipo

ya msichana mwenyewe, na tatu malipo ya kumtunza

mtoto atakapozaliwa. Sasa basi tuanze malipo ya wazazi.

Kwa muktadha huu, tunaona kuwa mwanamke anafanywa kama chombo cha

biashara katika jamii, hasa wanafamilia kujipatia kipato kikubwa kwa kupitia ya

mtoto wa kike.

Page 72: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

58

Mwanamke hana Maamuzi

Mwanamke amesawiriwa kama mtu ambaye hana maamuzi na asiyeweza

kushirikishwa katika vikao vya kufanya maamuzi. Mwandishi ameonyesha haya

katika uk. wa 21, anasema kuwa:

Mzee 1: Wazee sasa mnataka kujidharau wenyewe pamoja na jadi yetu.

Mna maana kusema kuwa sisi wazee wote hapa na mvi zetu

tumeshindwa na jambo hili hata tumwite mwanamke, tena

msichana mdogo, aje aseme? Mliona wapi mambo kama haya

jamani?

Kwa maana hiyo, tunaona wazi kabisa jinsi tamaduni zinavyozidi kumkandamiza

mwanamke na kumnyima haki ya kutoa mawazo.

Mwanamke Kama Mtu wa Kukata Tamaa

Mwanamke amechorwa kama mtu ambaye hukata tamaa kwa haraka. Hii

imejidhihirisha kaitka uk. wa 30-31, mwandishi anaposema kuwa:

Cheja: (anatoka mafichoni pake na kukimbilia upande wa pili)

lazima nijinyonge wasije wakanikuta wakaniuliza.

Nitasemaje?

Hii inaonyesha kuwa ni rahisi sana mwanamke kukata tamaa anapopatwa na

matatizo makubwa, kama mhusika Cheja anavyotaka kujiua kutokana na matatizo

yaliyompata.

Utafiti huu umeona kuwa, mwanamke ni mtu ambaye hawezi kukabiliana na

vikwazo katika maisha bali ni rahisi sana kukata tamaa kutokana na mambo

anayoyapata katika jamii. Na mara nyingi maamuzi huwa ni kujinyonga au kujiua

kwa njia yoyote ile.

Page 73: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

59

Mwanamke kama Mtegemezi

Mwanamke amechorwa kama kiumbe dhaifu, bila mwanaume hawezi. Mwandishi

ameonyesha haya katika uk. wa 36, anaposema kuwa:

Cheja: (kwa uchungu) yaani kweli, Juma. Imekuwa si kitu kwako

litakalonipata baadaye.

Hunifikirii nitamfanyaje mtoto. Uk. wa 9.

Mwandishi anaedelea kusema kuwa:

Cheja: …..lakini nilidhani kwa kufanya vile mtoto wangu atapata

matunzo kama watoto wengine. Mimi mwenyewe ningepata

matunzo kama wengine. Uk. wa 38.

Hii ni wazi kabisa kuwa, mwanamke bila mwanaume hawezi kuyakabili maisha.

Ndio maana mhusika Cheja akaamua kukubali kumsingizia Bwana Sembuli ule

ujauzito ili aweze kupata matunzo.

Mwanamke kama Kiumbe Kinachonyanyasika

Mwanamke amesawiriwa kama kiumbe kinachonyanyasika na kunyanyaswa na

mwanaume. Hii imejidhihirisha katika uk. wa 13, anaposema kuwa:

Bw. Chowe: Hivyo wewe unajua maana ya kwenda kuleta kitu.

Nimesema kamlete hapa. Punda wee! Kama kuna mambo

mmeyapanga na mtoto wako leo mtanieleza au mtaniona.

Hapa mwanamke ananyanyasika kwa kutukanwa matusi na mumewe, jambo ambalo

linasikitisha kwa kuwa anatukanwa wakati kosa katenda mwingine. Mwanamke

ameonekana kama chanzo cha matatizo yaliyotokea katika familia ya bwana Chowe.

Page 74: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

60

4.2.3 Mjadala na Dhamira Zilizoibuka Kutokana na Uchorwaji wa Mwanamke

katika Tamthiliya ya Hatia (1972)

Ukombozi wa Mwanamke

Suala la ukombozi wa mwanamke limekuwa likijadiliwa na waandashi wa kazi za

fasihi toka zama za kale, kuwa mwanamke anakabiliwa na matatizo ya

kukandamizwa, kunyanyaswa na kunyimwa haki zake. Muhando katika tamthiliya

ya Hatia amejadili matatizo yanayomkabili mwanamke na mbinu za kukabiliana na

matatizo hayo. Kwa mfano, Cheja anapewa mimba kisha anakanwa na kutelekezwa

na Juma kijana anayeishi mjini. Katika kutatua matatizo kama haya, Muhando

anaamini kuwa jamii iungane kuwaelimisha vijana wanaofanya uhalifu kama huo.

Ijapokuwa zoezi hilo ni endelevu kwani halitafanyika kwa siku moja. Zingatia

maongezi yafuatayo:

Sembuli: Cheja akishanieleza juu ya kijana huyu nitafanya chini juu

impate. Halafu nitajaribu kwa njia zozote kumwelewesha

ubaya wa maisha anayoendesha…

Mzee 3: Lakini kama kijana mwenyewe ni muhuni tu wa mjini

atayasikiliza maneno yako?

Sembuli: Itachukua siku nyingi na njia nyingi pia kubadilisha

mwenendo huu… uk. 40

Utafiti huu umegundua na kuona kuwa, suala la ukombozi wa mwanamke ni suala la

kimchakato. Mwanamke pekee ndiye anayeweza kujikomboa mwenyewe na sio

kusubiri mwanaume kumkomboa. Mtafiti amegundua kuwa, mwanamke anapaswa

kujishughulisha katika kazi mbalimbali na sio kuchagua kazi ndipo aweze

kujikomboa katika nyanja mbalimbali za maisha.

Page 75: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

61

Profesa Imani Sanga katika mahojiano na mtafiti yaliyofanyika tarerhe 08/11/2013,

anasema kuwa, mwanamke ili aweze kujikomboa asijione kuwa ana tofauti na

mwanaume kimajukumu katika jamii, anapaswa kufanya shughuli zote zilizopo

katika jamii ili aweze kuchangia katika kuinua uchumi pamoja na shughuli zote za

kimaendeleo. Mwanamke anapaswa apate elimu sawa na wanaume, ajishughulishe

katika kazi mbalimbali. Anaendelea kusema kuwa, hata siku hizi wanawake hupiga

vinanda makanisani au sehemu za ibada, pia ni waweka hazina pamoja na

waongozaji wa kwaya au nyimbo. Kwa upande mwingine anasema kuwa kampeni

hizi za ukombozi wa mwanamke, zimesaidia sana kuwafanya wanawake wajitambue

na kujinasua katika unyanyaswaji. Vilevile anadai kuwa, ni kwa kiasi kidogo sana

kwa sasa zile kazi ngumu na za kutumia nguvu zinaonekana kuwa za wanaume, ila

kwa kiasi kikubwa wanawake wameweza kujikomboa hata kiuchumi.

Hata hivyo mafeministi wa Kimarx wanasema kwamba kinachotakiwa ni kuwaweka

wanaume na wanawake katika daraja au tabaka moja yaani asiwepo aliye mkuu au

bwana kwa mwenzake. Kwa mtazamo wao ni kwamba kazi zinazomhusu

mwanamke zinabaki kuwa zile zile lakini ikitokea anataka nafasi katika ngazi ya

jamii basi kusiwepo na matabaka.

Mwanamke katika Kufanya Maamuzi

Uwakilishi wa Wanamke ni mdogo sana popote pale maamuzi yanapofanyika bila

kujali ngazi au taasisi inayohusika. Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) (2001;44-

45), wanaeleza kwamba, tofauti ni kubwa kati ya wanawake na wanaume katika

masuala ya jamii yanayojitokeza serikalini katika ngazi ya uongozi na ufanyaji wa

maamuzi. Licha ya ukweli kwamba, katiba ya mwaka 1977 pamoja na kufanyiwa

Page 76: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

62

marekebisho mwaka 1984 inatoa haki sawa kwa wanawake na wanaume, kupiga

kura na kutumikia umma, bado uwakilishi wa wanawake ni mdogo sana.

Ufanyaji wa maamuzi katika ngazi ya kaya bado sio wa kidemokrasia, kwani

wanawake na watoto hawahusishwi.

Umasikini

Suala la umasikini na hali ngumu ya maisha ni tatizo ambalo huwakumba watu

mijini na vijijini. Katika tamthiliya ya Hatia, Muhando amejadili suala la umaskini

na jinsi linavyowakatisha tamaa watu na kujiona wanyonge siku zote. Kwa upande

mwingine, watu wa vijijini huamua kwenda mijini kutafuta kazi ili kupambana na

umasikini lakini kuna msemo usemao „mjini kisomo‟ kwani watu wengi

wanaokimbilia mijini hukumbana na masaibu na kushindwa kukabiliana nayo. Kwa

mfano Cheja kapewa ujauzito na kutelekezwa hivyo kuongeza umaskini katika

familia. Rejea maongezi ya Bi Chowe; „…Kwanza hii yote shauri ya umaskini tu.

Mwanangu asingekwenda kufanya kazi Dalisalama…‟ Uk 10.

Mwanamke Kama Mlezi

Muhando amemchora mwanamke katika nafasi mbalimbali, katika Hatia amemchora

mwanamke katika nafasi mbalimbali kama mzazi, mlezi wa watoto, msimamizi wa

masuala ya familia ikiwemo kuandaa chakula, kwa mfano Bi. Chowe, Mwanamke I

na II ni wazazi na walezi wa familia.

Mtafiti amegundua kuwa, katika tamthiliya kinamama ni watu wenye bidii katika

kulea watoto na watu wenye huruma. Mfano mzuri ni Bi Chowe alivyokuwa akilia

Page 77: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

63

baada ya kuambiwa kuwa Cheja ni mjamzito. Pia alijitoa katika kumlea yeye

mwenyewe pamoja na mtoto atakayezaliwa.

Dkt Vicensia Shule katika mahojiano yaliyofanywa tarehe 08/11/2013 pamoja na

mtafiti anasema kuwa, katika jamii zetu, wanawake ndio wenye jukumu kubwa la

kuwalea watoto iwe wa kike au wa kiume. Anaendelea kusema kuwa, iwapo mtoto

wa kike akiharibikiwa au akipata matatizo kama vile mimba na kuacha shule au

kufeli, basi lawama zote hupewa mama. Baba anaona kuwa mwenye makosa ni

mama na hivyo lawama zote hupewa mama. Licha ya akina mama wengi kuwa pia

na jukumu la kuleta kipato katika jamii au familia, lazima ahakikishe kuwa anawapa

watoto malezi bora.

Hivyo basi utafiti huu umeona kuwa, mwanamke anajukumu kubwa la kulea familia

licha ya kuwa na shughuli nyingine mbalimbali za kuleta kipato katika jamii.

Mwanamke ameonekana kuwa, muda mwingi huwa na watoto tofauti na baba.

Unyanyaswaji

Kwa upande wa pili mwanamke amechorwa kama kiumbe duni asiyejitambua,

anakandamizwa na ananyimwa haki. Hivyo wanaume hutumia mwanya huo

kumchukulia mwanamke kama mtu asiyekuwa na msaada wowote katika familia na

jamii kwa jumla. Kwa mfano, Juma anampa ujauzito Cheja baadaye anamkana na

kumtelekeza. Halikadhalika, Bw. Chowe anamdhalilisha mwanamke kwa maneno

yafuatayo:

Mimi kila siku nawaambia watoto wa kike ovyo sana

mnabisha…Acha kuniletea upuuzi hapa … Jambo la aibu na

Page 78: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

64

wewe unalichekea kama mpumbavu…Jamani wanawake

wengine kumbe wajinga…shenzi kabisa…punda wee! uk. 12

na 13

York na wenzake (1991) wanaeleza kwamba, tofauti kubwa kati ya mwanamke na

mwanaume mbali na jinsi, ni ile ya mwanamke kunyanyaswa, na mwanaume ndiye

mnyanyasaji. Wanazidi kueleza kwamba, mwanaume hashiriki kabisa katika

kunyanyaswa ila yeye ndiye anayefaidika. Hiyo ndiyo sababu wanawake walitaka

kujikomboa wenyewe bila kuwashirikisha wanaume, kwani walijiona wao ndio

waathirika wakubwa wa unyanyasaji.

Unyanyasaji na usaliti wa kimahusiano umechorwa kimzaha ili kuishambulia asasi

ya ndoa ambayo imepoteza heshima yake. Kuhusu suala hili, mafeministi Leathwood

Carole na Hay Valeria (2006), wanasema kwamba sababu sio kukandamizwa bali

kuelewa kuwa maisha ya kiukandamizwaji aishiyo mwanamke hayasababishwi na

ujinsia tu bali pia na ubaguzi, umri, na utabaka. Urazini huo ndio uliomuinua Bi

Chowe kuamua kuvumilia matusi aliyokuwa anatukanwa na mume wake mbele ya

wanawake wenzake.

Msanii yeyote yule hufanya sanaa yake kulingana na mazingira yaliyomzunguka

kama asemavyo Kezilahabi (1983:230) katika Makala ya Semina za Kimataifa ya

Waandishi wa Kiswahili III, anasema kwamba:

Waandishi wengi waliofanikiwa ni wale waliowaweka

wahusika wao chini ya misingi ya mazingira

wanayoyaelewa na hasa yale ya kabila lao, ili kuweka

hadharani tatizo la kitaifa.

Page 79: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

65

Waandishi wanavyomchora mwanamke katika hali ya kunyanyaswa na kuumizwa

kila mara hutokana na hali halisi waionayo katika mazingira halisi

yanayowazunguka. Na hili linathibitishwa na mafeministi wanaosema kwamba,

wanawake wote wanaishi katika hali ya kunyanyasika lakini ni wajibu wa kila

anayenyanyasika kujikomboa (York na wenzake 1991).

Mwanamke kama Chombo cha Starehe

Pia mwanamke anaonekana kuwa mwili wake ni chombo cha starehe kwa

mwanaume. Free Encyclopedia inaeleza jinsi mwili wa mwanamke unavyohusishwa

na udunishwaji kwamba mwanamke ni kama kitu/kifaa, mali, na hata bidhaa

inayoweza kubadilishwa miongoni mwa wanaume. Tamaa ya mapenzi inamfanya

mwanaume kutokuridhika na mke wake, hivyo miili ya wanawake anaifanya kama

bidhaa ambayo inaweza kubadilishwa tu na kwa wakati wowote.

Katika tamthiliya ya Hatia, mhusika Juma ameonekana kumdanganya Cheja kuwa

anampenda na hatima yake Cheja kukubali kufanya naye mapenzi, kumbe lengo la

Juma ni kujifurahisha na kutimiza haja zake na sio kuwa anampenda Cheja. Mtafiti

amegundua kuwa, wanawake wengi hutumiwa kama chombo cha kumstarehesha

mwanaume na kutimiza haja za wanaume kwa kufanya nao mapenzi wakijua kuwa

wanapendwa kweli. Jambo hili limezungumziwa pia na Dkt Vacensia Shule katika

mahojiana na mtafiti tarehe 08/11/2013. Anaeleza kuwa wanawake wengi

wanadanganyika kuwa wanapendwa bila kufanya utafiti kuwa kama ni upendo wa

ukweli. Hivyo hujikuta tayari wameshamkubalia mwanaume, lakini lengo la

wanaume ni kutaka kutimiza haja zao au hamu yao ya mapenzi na baada ya hapo

hawana tena habari na mwanamke huyo bali huishia kumtafuta tena mwanamke

Page 80: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

66

mwingine. Anaendelea kusema kuwa, wanaume huwachezea wanawake kwa kufanya

nao mapenzi ili tu kutimiza haja zao na kutaka kujua mwili wa kila mwanamke

wanayemwona ili kupata tu starehe.

Mwanamke kama Kitega Uchumi

Tamthilia hii pia inatuonyesha kuwa, hadhi ya wasichana katika jamii imejikita

katika uwezekano wa kuwatumia kupata mali. Hivyo mabinti ni vitega uchumi

miongoni mwa jamii nyingi za kiafrika. Binti hathaminiwi kwa kuwa ni binadamu

mwenye uwezo na nguvu. Katika jamii nyingi za Kiafrika, wanawake wanaishi kwa

ajili ya watu wengine hususani mwanaume. Kama si baba basi kaka au ndugu wa

kiume. Mfano mzuri Mkami, ni mwakilishi bora wa imani kuwa mwanamke ni

kitega uchumi kwa manufaa ya mwanaume.

Katika tamthiliya hii Mkami anathibitisha imani inayowafanya wanawake

wadunishwe katika jamii. Maneno yafuatayo yanathibitisha:

Mkami : (kwa haraka) Ng‟ombe saba, mbuzi tisa na kuku watatu.

Mzee Chimaisi: (huku akicheka) Babu vipi? Unataka ujipatie ng‟ombe

wa kuolea hapohapo?

Mkami: Ndio, kwanza huyu dada yangu angeolewa vizuri angepata

zaidi ya hizo. Uk. wa 18

Mtafiti amegundua kuwa, wanawake wamepewa hadhi ya chini kwa kuwa,

wanadhalilishwa mno. Wanadhalilishwa kwa kuwa miili yao na utu wao unatumiwa

katika kuipatia familia kipato. Pia mwanamke anaweza kutumia mwili wake ili

kuweza kupata mahitaji mbalimbali ya kijamii na kujikimu kimaisha. Hii

inasababisha kushusha utu wake na thamani yake katika jamii.

Page 81: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

67

Mwanamke katika Utamaduni

Katika utamaduni mwanamke amechorwa pia kwa hali ya kudhalilishwa, kuaibishwa

kuonewa, kunyanyaswa na kukandamizwa. Kwa kuwa mwanamke tangu kale

utamaduni ulimtaka awe mtu mnyenyekevu, mtiifu kwa mumewe, basi ameendelea

kunyanyasika na kudhalilishwa. Simone de Beauvoir (1972) ni miongoni mwa

wanawake wanaoipiga vita mitazamo ya kitamaduni inayomuona mwanamke kama

kiumbe dhaifu.

Utamaduni ndio unaoweka alama zinazoonesha nafasi na majukumu ya mwanamke

na mwanaume. Kipengele cha utamaduni kinatengeneza mazingira ya

kumkandamiza mwanamke asifikie ngazi za juu za uongozi kwani wanaume

hawaamini kama wanawake wanaweza kuwaongoza vizuri kabisa na kuyatimiza

maamuzi ya wanaume na wanawake kwa usawa. Siku zote wanaume wanapata

mashaka juu ya uongozi wa mwanamke katika suala la uongozi (Bond, 2000). Pia

huweka alama ambazo hulingana na uthamani wa kijinsia. Hapa basi, wanaume ni

wanajamii walio katika tabaka la juu na wanawake katika tabaka la chini. Kwa

mfano kazi zinazofanywa na wanawake hazionekani kuwa ni muhimu wala kuwa ni

kazi za kimaendeleo. Hata kama zikionekana kuwa muhimu, muonekano huo

hauelezewi katika ngazi ya jamii isipokuwa katika ngazi ya familia tu. Rosaldo

(1974), anaona kuwa mwanamke wakati wote anachorwa katika mtazamo hasi na

haoni kama kweli kuna ukumbozi wa jinsia ya kike kutokana na mfumo wa utawala

wa kiutamaduni ambao unamilikiwa na wanaume.

Mtafiti amegundua kuwa, kutokana na utamaduni au jadi ya Mwafrika, mwanamke

inambidi avumilie yote yanayotokea akiwa kwa mume wake. Mfano mzuri ni Bi

Page 82: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

68

Chowe ambaye anavumilia manyanyaso yote ya mumewe kwa sababu ya matatizo

yaliyompata Cheja. Kutokana na utafiti huu tumeona kuwa, ni vigumu mwanamke

aliyekulia katika utamaduni au jadi ya kiafrika kuyakimbia matatizo yatakayompata

akiwa kwa mumewe. Yampasa ayakabili na kuvumilia kwa kuwa hawezi kuondoka

tena.

Mwanamke kutolewa mahari wakati anaolewa ni jambo la kiutamaduni katika jamii

nyingi za Tanzania na labda Afrika. Mahari inaweza kuonekana kama ishara ya

umoja kati ya familia mbili na wengine wanadai kuwa ni ishara ya kuaminiana na

haina tofauti na mila za Kimagharibi za kuvishana pete (FEMA, 2010). Lakini suala

hili la kiutamaduni linamfanya mwanamke kuwa mfungwa au mtumwa wa

mwanaume hivyo kushusha hadhi ya mwanamke na kumfanya awe mali ya

mwanaume. Kama asemavyo Balisidya (1982), fasihi simulizi inadhihirisha kwamba

mwanamke alifundishwa tangu kale. Tena anajua kwamba akiisha kutolewa mahari

hawezi kumkimbia mume wake wala familia ya mume wake hata kama ataonewa,

atanyanyaswa na kukandamizwa. Lakini hata hivyo inampasa kuvumilia tu pale pale

kwani yuko kwenye kifungo cha mahari ambayo wazazi wake hawawezi kuilipa

tena.

Utafiti uliofanywa na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania

(TAMWA), kama walivyonukuliwa na timu ya FEMA (2010), umehusisha ulipaji

mahari na unyanyasaji wa wanawake. Utafiti huo umeonesha kuwa unyanyasaji huo

unaohusishwa na mahari ni kama vile wasichana kukatishwa masomo ili waolewe,

kuvumilia vipigo na kupoteza haki ya kumiliki mali.

Page 83: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

69

FEMA (2010) wanasema kuwa, ijapokuwa ni utamaduni wa Watanzania na

Waafrika kwa ujumla kwamba, wanawake baada ya kuolewa wanatarajiwa

kuhudumiwa na kulindwa na waume zao, lakini matokeo yake wanawake sasa

wanakuwa hawana mamlaka katika jamii, wamebakia majumbani, na kuzaa watoto.

Pia utamaduni unamnyanyasa mwanamke kwa sababu mwanaume katika jamii

nyingi habebi wala kufanya kazi yoyote ile ambayo inaonekana kuwa ni ya akina

mama. Wengine wanahofia kuchekwa na wengine ni ujeuri tu na kukosa huruma.

York na wenzake (1991) wanaelezea ukombozi wa mwanamke katika mojawapo za

kanuni za ukombozi wa mwanamke kwamba:

Wanawake wote wanashiriki katika unyanyaswaji

mmoja tofauti kubwa kati ya wanawake na wanaume

(mbali na ujinsia) ni kwamba unyanyasikaji wa

wanawake ni maalumu kwa faida ya wanaume ambapo

wanaume ndio wanyanyasaji. [Tafsiri yangu]

Umoja na Ushirikiano

Katika tamhiliya ya Hatia (1972) mwandishi anaonyesha jinsi wanawake walivyo na

umoja na ushirikiano katika mambo mbalimbali. Mfano ni katika wanawake wa kijiji

cha Bi Chowe wanavoshirikiana katika kutwanga mahindi. Hii imejidhirisha katika

uk. wa 10 anaposema

MSIMULIZI: kijiji kimoja katika wilaya ya Kilosa. Saa za mchana.

Nje ya nyumba ya Bana Chowe. Wanawake watatu

wanatwanga mahindi huku wakiimba wimbo wa

kutwanga. Mmoja wao ni Bi. Chgowe na wengine ni

majirani.

Page 84: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

70

Mwandishi huyu amemchora mwanamke kama mtu anayependa ushirikiano katika

jamii. Hii ni wazi kabisa kuwa wanawake hujibidiisha katika kazi mbalimbali ili

kuweza kuondoa umaskini na pia ili waweze kujikomboa wao wenyewe. Mtafiti

amegundua kuwa, akina mama katika tamthilia hii wamechorwa kama watu wenye

umoja katika kufanya mambo mmbalimbali katika jamii.

4.3 Nguzo Mama (1982)

4.3.1 Utangulizi

Katika tamthiliya hii mwandishi anasema kuwa, toka Umoja wa Mataifa kutangaza

kwamba mwaka 1975 ni mwaka wa wanawake duniani, juhudi mbalimbali

zimekuwa zikifanywa kuwakomboa wanawake kutokana na ukandamizwaji na

udhalilishwaji. Je harakati hizi ambazo zimeendelea toka wakati huo mpaka sasa

zimepata mafanikio na matatizo gani? Nguzo Mama ni tamthiliya inayochambua

matatizo yanayowakabili kina mama katika juhudi zao za kuendesha harakati hizi za

kujikomboa. Kwa kupitia tamthiliya hii ndipo tutagundua au tutaona kama harakati

hizi zimeleta manufaa au la.

Tamthiliya ya Nguzo Mama (1982) ina maonesho manne yenye jumla ya kurasa 59.

Tamthiliya hii imeundwa hivi kwamba, onesho linalobeba dhamira kuu limepewe

nafasi zaidi. Katika kuhakikisha hilli, onesho la kwanza lina kurasa kumi tu ndilo

onesho fupi kuliko yote. Ni onesho linaloelezea juhudi mbalimbali zinazofanywa

na akina mama wa Patata katika kujaribu kusimamisha Nguzo Mama. Kila

mwanamke kuwa na wazo tofauti na mwenzake akiamini moja kwa moja kuwa,

ndilo litakalofaa kuinua Nguzo Mama. Mfano, Bi. Moja anapendekeza dhahabu,

fedha, uturi na maua. Bi. Pili kwa upande wake anaonelea jembe lenye mpini mrefu

Page 85: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

71

au mfupi, chungu mdomo mdogo au kikapu cha gogo. Bi. Tatu, lake ni mabenzi,

mavolvo, ST au SU yote hayo ni mawazo tu ya akinamama katika kukabiliana na

kuinua Nguzo Mama. Pamoja na kuwepo kwa mawazo mazuri ya akina mama

wanakwamishwa na baadhi yao kama akina Bi. Nane. Pia katika onesho hili wapo

wawakilishi wa wanawake wenye fikra pevu mfano mzuri uk wa 7 pale Bi Nne

anaposema: “Bora tufanye mikutano, badala ya maandamano, maazimio tutoe na

sana tuyatangaze”.

Onesho la pili lina kurasa zaidi ya kwanza lina kurasa 19. Ndilo onesho refu kuliko

mengine. linaonesha visa na vituko zaidi katika kumwandaa msomaji kufahamu

matatizo wanayokutana nayo wanawake, katika juhudi za kusimamisha Nguzo

Mama. Ni onesho linaloelezea juhudi mbalimbali zinazofanywa na wanawake

katika kuinua Nguzo Mama. Mfano, uk. wa 12 Bi. Nane anasema: “Mnajua

NGUZO MAMA haiwezi kusimama mpaka tuivute kwa kamba”. Bi. Nane

anajaribu kutoa maarifa ambayo yatasaidia kuinua Nguzo Mama. Mwandishi

anatuonesha kuwa, wakati akina mama wanajaribu kuinua Nguzo Mama kuna

wengine wanajaribu kukwamisha zoezi hili kutokana na chuki zao. Kwa mfano,

katika uk. wa 13 tunaoneshwa Bi. Nne akisema: “Aaa! Kaanza Bi. Nane mambo

yake. Alikaa wapi? NGUZO MAMA ilipoletwa hatukumwona hapa, wala kwenye

maandamano hakuja. Sasa watu wanapanga mambo vizuri ndio anajidai. Alikuwa

wapi siku zote, acheni! tupeni kwamba hizo”.

Katika onesho hili la pili ndipo tunapooneshwa kuwa, wanawake wamechorwa

kama wajasiriamali wanaojishungulisha na miradi midogomidogo itakayoweza

kuleta maendeleo. Mfano tunaoneshwa Bi. Pili akipika na kuuza pombe katika

Page 86: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

72

kilabu. Pamoja na kufanikiwa kwa Bi. Pili kupata pesa kidogo nyumbani

anakumbana na kikwazo cha maendeleo ambaye ni mume wake. Wanawake

wanaonesha hili kwa kusema kuwa, “Si Sudi mume wa Bi. Pili aliyetaka pesa zote

za pombe apewe”. Wanawake wengine katika ujasiriamali ni Bi. Moja na wenzake

wanafuma vitambaa, wengine mikeka na wengine mapambo ya meza. Licha ya

kufuma na kwenda kuviuza sehemu mbalimbali anatokea Bi. Tano ambaye, ni

mvivu wa kuuza vitambaa kwa madai eti hawezi kuwabembeleza wateja. Pia

mwanamke amechorwa kama mtu anayeona umuhimu wa elimu Bi. Nne

anatambua umuhimu wa elimu hasa pale anaposema: “pia somo la ushonaji

litatiliwa mkazo mashuleni.”

Mwanamke amechorwa kama kiongozi mbaya, mfano mzuri tunaupata kutoka

kwa Mwenyekiti ambaye baada ya kuletewa mashtaka na Bi. Nne kuhusu Bi Nane

yeye aliyachukua kama yalivyo, kwa kuamua kesi yeye na Bi. Nne pasipo

kuwashirikisha wajumbe wengine. Vilevile mwanamke amechorwa kama mtu

mwenye chuki kwa mfano, Bi nne ambaye alipeleka mashtaka ya uongo kwa

Mwenyekiti kwa lengo la kutaka kumgandamiza Bi. Nane.

Onesho la tatu lina jumla ya kurasa 16 ni onesho linalofuata kwa urefu baada la

onesho la pili. Limepewa urefu huu ili kujenga na kusisitiza umuhimu wa ukombozi

kwa mwanamke. Tangu mwanzo tunaandaliwa kumuona mwanamke Bi. Msimulizi

akisimulia yale matukio yote yanayotokea katika harakati za ukombozi wa

mwanamke. Bi. Msimulizi anaonekana kukerwa na vikwazo mbalimbali

vinavyokwamisha kusimama kwa Nguzo Mama kama vile tamaa ya Bi. Moja

kutamani kanga na hivyo kuacha kuvuta Nguzo Mama, kukosekana kwa

Page 87: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

73

ushirikiano, kutumikishwa kwa wanawake, ukahaba unaofanywa na Bi. Sita,

dhuluma zinazofanywa na Kiando na Makande dhidi ya shemeji yao. Kuwa kuna

kila sababu ya kuteketeza vikwazo hivyo kwani, vinachangia kurudisha nyuma

maendeleo ya wanawake na kamwe hayatawezekana mpaka vigingi hivi vyote

vitokomezwe.

Onesho la nne lina jumla ya kurasa 15 tu. Limepewa urefu huu ili kuendeleza

kusisitiza ukombozi wa wanawake. Onesho linapoanza tunakutana na Bi. Msimulizi

ambaye anasema: “sana walifadhaika hasa yeye Bi Nane wakarudi majumbani

roho zinasononeka. Asubuhi na mapema vitandani bado wamo la mgambo likalia”.

Moja kwa moja tunapatanishwa kuwa, katika onesho lilopita kuwa, Bi. Nane

amewashinda kesi akina Mwenyekiti na Bi. Nne katika onesho hili tunaoneshwa

kuwa, juhudi za kuinua Nguzo Mama bado zinaendelea na zimeshika kasi. Ndipo

wanawake wanapogundua kuwa, juhudi hizi zinahitaji ushirikishwaji wa jamii

nzima wakiwemo wanaume na watoto wote. Kujitenga kwa akinababu, nako

kunakwamisha maendeleo na kuwepo kwa wasaliti katika jamii zetu

kunakwamisha kusimama kwa Nguzo Mama

4.3.2 Data na uchambuzi wake

4.3.3 Mwanamke Alivyochorwa katika Tamthiliya ya Nguzo Mama (1982)

kwa Upande Chanya

Mwanamke kama Mbunifu

Mwanamke amechorwa kama mtu anayetafuta njia na mbinu mbadala zitakazosaidia

katika kufanikisha kupata ukombozi wa mwanamke. Mwandishi amedhihirisha hili

kwa kuwatumia Bi. Moja na Bi.Tatu. Mfano, Bi. Moja anaposema ( uk. wa 1):

Page 88: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

74

BI. MOJA : “Tukupambe kwa dhahabu

Au tukupambe kwa fedha

Wanja hina na uturi

Tukupambeje maua”

Naye Bi Pili anasema katika uk. wa 2

BI. PILI: “Jembe gani unataka

Mpini mrefu au mfupi

Chungu mdomo mdogo

Au kikapu cha kigogo

Tukupambeje maua”

Hivyo basi, Muhando anatuonesha namna wanawake wanavyohamasika na

ukombozi wao, kila mmoja akijaribu kutoa wazo lake, akiamini kuwa ndilo

litakalosaidia kusimama kwa Nguzo Mama.

Mwanamke kama Mlezi

Mwanamke amechorwa kama mzazi na mlezi. Mfano dhahiri ni Bi. Saba, alikuwa na

watoto watano, aliowazaa na kuwalea yeye mwenyewe. Baadaye alikuja

kunyang‟anywa watoto hao na ndugu wa marehemu mumewe. Hili linajihidhirisha

pale, Bi. Msimulizi anaposimulia (uk. wa 44):

Bi. MSIMULIZI: “Alipoona wanawe wote watano

Mdogo miaka mitatu

Wanaswagwa kama mbuzi”.

Pia, Bi. Pili naye ni kiwakilishi cha mazazi na mlezi bora. Aliwalea watoto wake

pamoja na mumewe vizuri. Mpaka jamii yote ikawa inampongeza kwa malezi yake.

Mfano ni Chizi, ambaye alitambua juhudi za Bi. Pili katika kuilea familia yake kwa

kuwapikia chakula, kufua nguo na kulima. Pia, alijihusisha na upikaji wa pombe

uliomuwezesha kupata kipato kidogo cha familia. Tazama uk. wa 59 pale Chizi

anaposema:

Page 89: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

75

CHIZI: “Mke kujipatia awe kama Bi. Pili

Nguo anifulie na pombe anipatie

Ambaye taabu yote atakubali

Watoto anizalie na pia anilelee

Chakula anilimie na pia anipikie”

Mwanamke katika Kujikomboa

Mwanamke amechorwa kama mtu anayeona na kutambua umuhimu wa ukombozi

wa wanawake.

Hivyo anahimiza jamii nzima kushirikiana kwa pamoja katika kutafuta ukombozi

wa mwanamke. Hili linajihidhirisha uk. wa 59 pale Bi. Nane anaposema:

Bi. NANE: “Tushirikishe wanaume pia

NGUZO MAMA ina faida kwa wote”.

Bi . Nane anawataka wanawake wenzake wawashirikishe wanaume katika harakati

zao. Hii ina maana kwamba, jamii nzima inahitajika kushiriki katika ukombozi wa

wanawake. Pasipo kujali jinsia, umri wala watoto, wote kwa pamoja wanahitajika

ndipo Nguzo Mama itasimama.

Mwanamke pia amechorwa kama mwanaharakati katika kutafuta ukombozi wa

mwanamke. Mfano Bi. Msimulizi anaposema (uk. wa 5)

BI. MSIMULIZI: “Haraka wakaivamia hao wabeba wana

Nguzo kutaka kusimamisha”

Kutokana na maneno hayo tunaonyeshwa kuwa, kila mwanamke anaguswa na

harakati zinazofanywa ili kuweza kuwakomboa wanawake isipokuwa Nguzo

Mama ni nzito inahitaji jamii nzima ishiriki ndipo mafanikio yatakapopatikana.

Page 90: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

76

Mwanamke amechorwa kama mtu anayejitegemea na anayeweza kujimudu

kimaisha pasipo kuwa tegemezi kwa mtu mwingine. Hili linajidhihirisha katika uk.

wa 42 pale Bi.Tatu anapomwambia Bi. Nne:

Bi NNE: “Unasemaje hivyo kwa kuwa wewe una kazi ya mshahara

Hata ukiachwa unajitegemea”.

Muhando amemsawiri mhusika Bi. Nane kuwa, ni mwanamke msomi na aliyepata

bahati ya kuajiriwa. Anapokea mshahara unaomuwezesha kujikimu kimaisha na

kuondokana na utegemezi katika jamii.

Mwanamke ni Msomi

Mwanamke amechorwa kama msomi, anayetambua umuhimu wa elimu aliyonayo na

kisha anajaribu kuitumia vizuri, kwa kuwaelimisha wanawake wenzake namna ya

kuweza kuinua Nguzo Mama. Kwa mfano, Muhando amemtumia mhusika Bi. Nane

kwa kumuonesha kuwa, ndiye mwanamke msomi aliyemudu kuitumia elimu yake

ipasavyo. Hili linajihidhihirisha katika uk. wa 10 pale mwandishi anaposema

MWANDISHI: “Anaingia Bi Nane, haimbi. Amevaa nguo za kisasa.

Ameshika vitabu vipatavyo sita hivi. Anakwenda kwa

mwendo wa kikazi. Anafika pale kwenye NGUZO MAMA

anaimba, anafunua vitabu vyake na kusoma hapa na pale

Katika kufunua vitabu vyake Bi. Nane, mwandishi anataka kutupa taswira ya kuwa

Bi. Nane pamoja na kugundua umuhimu wa elimu aliyonayo alipenda kurejelea

vitabuni ili kupata maarifa zaidi yatakayosaidia kusimamisha Nguzo Mama.

Page 91: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

77

Vilevile, mhusika msichana naye ni kiwakilishi cha wasomi. Msichana huyo

amevaa sare za shule na anakwenda shule ili kutafuta elimu anayoamini kuwa

itakuwa ni ufunguo wa maisha yake.

Hay (2006) kama alivyonukuliwa na Pullen anaeleza kwamba elimu hasa elimu ya

juu katika hisia au mawazo ya vijana wanawake haipo, kwani hufikiri kwamba

haiwahusu. Anaona ni vema utamaduni huo uvunjwe miongoni mwa mabinti

wadogo kwani wote wanastahili elimu sawa na vijana wa kiume. Hata kama mtoto

huyo wa kike alipenda kusoma sana lakini ataishia kupenda na kutamani tu bila

kutimiza tamaa yake ya kutaka kusoma.

Mwanamke kama Mshauri

Mwanamke amechorwa kama mtu anayetoa ushauri na kuwatia wenzake moyo

kuwa, wasikate tamaa katika kusimamisha Nguzo Mama badala yake watafute

mbinu sahihi itakayo wawezesha kuinua Nguzo Mama. Hili linajidhiirisha uk. wa

11 Bi. Msimulizi anaposema:

BI. MSIMULIZI : “Tamaa tusikate tutafute maarifa”.

Bi. Msimulizi anawataka wanawake wenzake kuwa, wasikate tamaa katika

kusimamisha Nguzo Mama isipokuwa inawabidi wakae chini washauriane nini cha

kufanya.

Bi. Nane naye ni mhusika mwanamke aliyesawiriwa kama mtu anayetoa maarifa

kwa wenzake akiamini kuwa, maarifa hayo huenda yakasaidia kusimamisha Nguzo

Mama. Hili linajidhihirisha uk wa 12 pale Bi Nane anaposema

BI. NANE: “Basi, tusikilizane, mnajua NGUZO MAMA

Page 92: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

78

haiwezi kusimama mpaka tuivute kwa kamba.

Hebu njooni mchukue hizi kamba tuzifunge

kwenye NGUZO MAMA halafu kila mmoja avute”.

Bi. Nane anaamini kuwa, kamba ikitumika katika kuvuta Nguzo Mama basi

itasimama. Hayo ni baadhi tu ya maarifa aliyojaribu kuyatoa Bi. Nane kwa

wanawake wenzake.

Mwanamke amesawiriwa kama mtu anayesikitishwa na kusononeshwa kwa

kukosekana kwa ushirikiano miongoni mwa wanawake wenzake. Kwani kuwepo

kwa jambo hili kunachelewesha kusimama kwa Nguzo Mama. Hili

linajidhihirisha uk. wa 13 pale Bi. Nane anaposema

BI. NANE: “Jamani vipi tena mbona mnaondoka?

(Ameshangaa na kamba zake mikononi.)

NGUZO MAMA hii haitasimama”.

Hivyo basi, Bi. Nane anaonesha kuwa, ni dhahiri Nguzo Mama haitaweza

kusimama mpaka vigingi vyote vitokomezwe, ikiwemo kutokuwepo kwa umoja

na ushirikiano miongani mwa wanawake wenzake. Kwani Waswahili wanasema,

kidole kimoja hakivunji chawa. Pia umoja ni nguvu utengano ni dhaifu.

Mwanamke kama Mjasiriamali

Mwanamke amechorwa kama mjasiriamali. Kwa mfano, Bi. Pili ambaye ni

mhusika mwanamke anajishunghulisha na upikaji wa pombe ili kuweza kujipati

maendeleo ya familia yake. Hili linajihidhirisha uk. wa 14 pale Bi. Msimulizi

anaposema:

BI. MSIMULIZI: “kaamua Bi. Pili

Pombe kujipikia na kilabuni kuiuza

Page 93: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

79

Pesa akipata, pesa msema kweli

na NGUZO MAMA itasimama”.

Mwandishi anatuonesha kuwa, Bi. Pili anajishughulisha na upikaji wa pombe

unaomwezesha kupata pesa kidogo zinazosaidia kulea familia yake vyema. Licha

ya pesa anazopata mumewe anamlazimisha ampe.

Baadhi ya wanawake wa Patata kama vile Bi. Moja na wanawake wengine nao

walikuwa ni wajasiriamali wanaojishughulisha na miradi midogomidogo kama

vile ufumaji wa vitambaa, mapambo ya nyumba na usukaji mikeka. Baada ya

kufuma na kusuka mikeka walikwenda kuviuza sehemu mbalimbali. Kutokana na

juhudi hizo walijipatia pesa kidogo ambayo waliamini kuwa, ingewasaidia katika

harakati za kuinua NGUZO Mama. Mfano katika uk. wa 17 unatudhihirisha

miradi hiyo ya kina mama, mfano mzuri ni pale Bi Msimulizi anaposema:

BI. MSIMULIZI: “Anaingia Bi. Moja na akina mama wengine

wanatandika mikeka na kukaa. Kila mmoja

anafuma kitu fulani wengine vitamba vya meza,

wengine mapambo ya nyumba wengine wanasuka

mikeka”.

Mwanamke kama Mpiga Vita Suala la Uvivu

Mwanamke amechorwa kama mtu anayepiga vita vikali suala la uvivu, kwani

linarudisha nyumba maendeleo ya wanawake na jamii kwa ujumla. Hili

linajihidhirisha uk. wa 18 pale Bi. Moja anaposema:

BI. MOJA : “Hata haiwezekani! Sema tu hukwenda

Nakwambia uvivu unaturudisha nyuma sisi”.

Page 94: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

80

Bi. Moja ni kielelezo cha wanawake wanaopiga vita suala nzima la uvivu,

kwa kumwambia Bi. Tano kuwa, biashara inahitaji kubembeleza. Hivyo basi, ili

ukombozi wa wanawake upatikane hatuna budi kutupilia mbali tabia ya uvivu.

Mwanamke kama Mvumilivu

Mwanamke amechorwa kama mtu anayeweza kukabiliana na vikwazo pamoja

na matatizo mbalimbali yanayoweza kumpata katika jamii. Kwa mfano Bi.

Nane aliweza kuwakabili vyema mwenyekiti pamoja na Bi. Nne, kwa mashtaka

ya uongo ambayo Bi. Nne aliyapeleka kwa mwenyekiti. Mfano katika uk. wa

23 unatudhihirisha Bi. Nane alivyoweza kuyakabili matatizo yaliyompata;

anasema:

BI. MSIMULIZI: “Hasira zikampanda Bi Nane

lakini vyema akizitawala

mdomo akauma neno lisije mtoka”

Hivyo basi, tunaonyeshwa kuwa, Bi. Nane aliwasikiliza mwenyekiti na Bi. Nne

na mwisho akagundua kuwa, wote wawili walikuwa na hila juu yake. Na ndipo

alipowajibu kwa busara namna mambo yanavyopaswa kuendeshwa. Kisha

mwenyekiti na Bi. Nane wakabaki midomo wazi wasijue la kufanya.

Mwanamke kama Mchapakazi

Mwanamke amechorwa kama mchapakazi anayejibidisha katika kufanya kazi ili

kuweza kulea familia yake vyema. Hili linajihidhihirisha katika uk. wa 36, pale

Bi. Pili anaposema:

BI. PILI: “Nimefua mchana huu. Asubuhi si nilidamkia

shambani. Kurudi shambani kwanza nikapikia

Page 95: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

81

watoto, maji hakuna, nikaenda kuyachukua”

Muhando anatuonyesha kuwa, aghalabu mwanamke amekuwa akichapa kazi za

nyumbani peke yake tena bila ya kupumzikia. Akitoka shambani anawapikia

watoto wake chakula. Anapaswa pia kwenda kuchota maji. Bila shaka alikuta

nyumba na vyombo ni vichafu ataanza kusafisha nyumba na kuosha vyombo.

4.3.4 Mwanamke Alivyochorwa katika Tamthiliya ya Nguzo Mama (1982) kwa

Upande Hasi

Kiumbe anayenyanyaswa

Mwanamke kama kiumbe kinachonyanyasika katika jamii. Kutokana na kuwepo

kwa mfumo dume unaowagandamiza kwa kuwafanya ni wazazi tu na mambo

muhimu hawawahusishi. Mfano uk wa 4 ni pale Bi Msimulizi anaposimulia:

BI. MSIMULIZI: “Wabeba wana vibaya walinyanyasika

wakaonekana si watu ingawa jamii waliikuza”

Inaonekana katika jamii ya Patata, wanawake walidharauliwa na kunyanyaswa.

Walikuwepo tu kwa sababu ya kuzaa. Hawakutambua umuhumi mwingine wa

kuwepo kwa wanawake katika jamii yao.

Mwanamke amechorwa kama mtu anayefanyiwa vitendo vya kikatili ikiwemo

kunyang‟anywa pesa pamoja na kupigwa na mumewe. Hili linajidhihirisha uk.

wa16 pale Sudi anapomwambia Bi. Pili:

SUDI: “Wee! Hawara zako ndiyo wanakutia jeuri unaninyima

pesa toa pesa sasa hivi (Anampiga Bi. Pili anakimbia

huku analia)”

Page 96: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

82

Bi. Pili alipata pesa kidogo kutokana na pombe aliyokuwa anaipika na kuiuza.

Lakini bado dume hilo lilizoea kulelewa na halikuridhika, likataka kuzitawala pia

pesa za Bi Pili. Huu ni uonevu uliokithiri katika jamii nyingi za kiafrika.

Pia, mwanamke amechorwa kama mtu anayefanyiwa dhuluma kwa

kunyang‟anywa vitu vyote alivyoachiwa na marehemu mumewe, wakiwemo na

watoto wake watano. Hili linajidhihirisha uk. wa 43 pale Bi Saba anaposema:

BI. SABA: “Nitawaambia mara ngapi

ndugu yenu amekufa hela zote mmechukua,

watoto wote mmeninyang‟anya, vitu vyote

mmechukua, bado mnaniambia nimechukua hela”.

Bi. Saba mara baada ya kufiwa na mumewe, ndugu wenye uchu na tamaa ya

kumiliki mali walijitokeza na kumnyang‟anya kila kitu. Hii ni dhuluma kubwa

aliyofanyiwa Bi. Saba ambapo haina budi kukomeshwa na kutokomezwa kabisa

katika jamii tuliyo nayo sasa. Ili kwamba wajane wanaoachwa waweze kujua kuwa

wataendelea vipi na maisha na sio kuanza kuwaza watakavyoanza maisha upya.

Tuangalie mfano kutoka katika uk. wa 43 jinsi BI SABA anavyoshangaa baada ya

kuwaona shemeji zake wamerudi tena kuchukua mali:

BI SABA: “Haa! Shemeji mmerudi kuchukua hata kitanda!

Hata sufuria! Nitalala wapi na nitapikia wapi jamani!”.

Mwanamke kama Mtegemezi

Mwanamke amechorwa kama kiumbe duni, kisichoweza kujitegemea chenyewe bila

nguvu ya mwanaume. Na hivyo kuwa tegemezi kwa mume wake kwa kila kitu. Hili

linajidhihirisha katika uk wa 41 pale Bi. Tatu anaposema:

BI TATU: “ Siyo utani ndugu yangu. Tunakwenda kwenye pati na

mume

Page 97: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

83

wangu leo saa moja. Lazima nipalilie unga kwa baba

watoto wangu ati. Nitakula nini”.

Hapa tunapata picha kuwa, Bi Tatu siyo kwamba amekwenda kwenye pati na

mumewe kwa kupenda, isipokuwa asingekwenda angenyimwa pesa kwa ajili ya

mahitaji ya watoto pamoja na mahitaji yake binafsi. Kwa maana kwamba mumewe

angekataa kutoa huduma za nyumbani. Hivyo mwanamke anafuata kila kitu

anachotaka mumewe kutokana na kuwa yeye ndiye ameshikilia maisha yake, na

kuwa akikataa kufuata anayoyataka mumewe basi huduma hizo asingezipata. Wakati

umefika kwa wanawake kizinduka kutoka usingizini na kukataa kuwa tegemezi kwa

mume.

Utamaduni unavyomkandamiza Mwanamke

Mwanamke amechorwa kama mtu anayegandamizwa na mila potofu zinazoruhusu

mwanamke kunyang‟anywa mali alizoachiwa na mumewe. Kuwa mwanamke

anapofiwa na mumewe anapaswa kutaja mali zote walizokuwa wamechuma na

marehemu kwa ndugu wa marehemu. Hii sio haki kwa kuwa mali hizo wametafuta

mke na mume, na sio vizuri ndugu wa mwanaume kwenda kuzidai. Hili

linajidhihirisha uk. wa 43, Makange anapomwambia Bi. Saba kuwa:

BI. SABA: “Umeficha mali ya ndugu yetu

mwanamke wewe. Huogopi hata waliokufa!”

Kutokana na tamaa na uchu wa mali waliyonayo ndugu wa mume wa Bi Saba

wanaamini kuwa, kuna mali nyingine zimefichwa. Wanataka mali ambazo

hawajazitolea jasho. Hivyo basi umefika wakati ambapo sheria inafaa ichukue

mkondo wake na sio kuogopa waliokufa. Wanajaribu kumpa Bi Saba imani potofu

ya kuogopa waliokufa. Kama kufa kafa mmoja na mali ilichumwa na wote wawili

Page 98: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

84

hivyo inapaswa mali zilizosalia kumilikiwa na kuendelezwa na aliyebaki ambaye

naye ameshiriki kuchuma mali hizo.

Mwanamke kama Msaliti

Mwanamke amechorwa kama msaliti. Pale ambapo, licha ya kutambua kuwa

mhusika Chizi ni mtoto wa kaka yake lakini kwa makusudi anaamua kusema kuwa,

hamfahamu na anamkataza asimuite shangazi. Hili linajidhihirisha uk. wa 50, Bi

Tatu anapomwambia Chizi kuwa:

BI. TATU: “Usiniite shangazi, toa balaa lako hapa

ukirudi nitakuitia mbwa akuume”.

Bi Tatu amemkataza Chizi asimwite shangazi na isitoshe anamtishia kuwa,

atamwitia mbwa, hii ni hali ya kukataa majukumu ya kifamilia ambayo inapaswa

kupigwa vita vikali katika jamii zetu kwani inarudisha nyuma maendeleo katika

jamii.

Mwanamke kama Chombo cha Starehe

Mwanamke amechorwa kama chombo cha starehe. Ambaye anajihusisha na biashara

ya ukahaba, ambapo amegeuza mwili wake kuwa kama bidhaa iuzwayo sokoni

inayosubiri mnunuzi aje ili anunue. Mfano mzuri ni mwanamke kahaba ambaye ni

Bi Sita. Hili linajidhihirisha katika uk wa 8 pale mwandishi anaposema kuwa:

MWANDISHI: “Wakati wimbo unaendelea anaingia Bi. Sita haimbi.

Anaingia kwa miondoko ya kikahaba na amevaa

kikahaba”.

Kuvaa kikahaba kwa Bi Sita kunatudhihirishia kuwa yuko sokoni. Ameamua

kuanika biashara yake ili wanunuzi wafike na kuinunua. Hapa mwandishi

anatuonyesha kuwa wanawake wanategemewa kupata maendeleo kwa kujiuza.

Page 99: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

85

Vile vile mwanamke amechorwa kama chombo cha starehe, kilichopo kwa ajili ya

kumstarehesha mwanaume. Mfano mzuri ni pale Bi Sita anapomwambia Bi Tano

katika uk wa 39:

BI. SITA: “ Mwambie mumeo ashike yake kwanza

alinifuta yeye mwenyewe. Wewe ulikuwa wapi?”

Licha ya Bi. Sita kutambua kuwa ana uhusiano wa kimapenzi na mume wa Bi. Tano,

kamwe hakujali. Kwani amekubali kufanywa kama chombo cha starehe kwa

kuchezewa na kisha kuachwa, kwani alijua kabisa kuwa mumewe Bi. Tano ana mke

na sio kwamba anataka kumwooa ila ni tamaa tu za kutimiza haja zake za kimwili.

Mwenye Wivu

Mwanamke pia, amechorwa kama mtu mwenye wivu, fitina na chuki binafsi. Na

hivyo kuchangia kukwamisha juhudi za ukombozi wa mwanamke. Mfano mzuri ni

mwanamke mwenye fitina, wivu na chuki binafsi ambaye ni Bi. Nne, ambaye mara

kwa mara anaonekana kutokukubaliana na mawazo ya Bi. Nane hata kama

anafahamu kuwa yana manufaa huyapinga. Hili linajidhihirisha katika uk. wa 13, Bi.

Nne anaposema kuwa:

BI. NNE: “Ha! Mnafanya nini

nani kawaambia mfanye hivi? Ndio nini hii?”

Kila juhudi inayopigwa na wanawake anatokea Bi. Nne na kuwarudisha nyuma.

Hivyo basi, ili ukombozi wa mwanamke uweze kupatikana kuna kila sababu ya

kupiga vita wivu, fitina na chuki.

Page 100: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

86

Mvivu

Mwanamke amechorwa kama mvivu, asiyewajibika ipasavyo katika kufanya kazi

inayoweza kuleta maendeleo ya mwanamke. Hili linajidhihirisha katika uk. wa

19 pale Bi. Tano anaposema:

BI. TANO: “Kila nilipokwenda wananiambia wameshanunua vya

kutosha.sasa mimi ningewalazimisha!”

Bi. Tano ni mwanamke mzembe na mvivu asiyependa kuwajibika katika kufanya

kazi. Haoni tatizo hata kidogo kwa kukosa wateja wa kununua vitambaa vyake.

Wanawake kama Bi. Tano ndiyo wanaokwamisha upatikaji wa maendeleo ya

wanawake kwani hawapendi kujishungulisha.

Mwanamke kama Mtu mwenye Tamaa

Mwanamke amechorwa kama mtu mwenye tamaa ya vitu vidogo vidogo kama

vile kanga. Hili linajihidhirisha uk. wa 35 pale Bi. Moja anapomwambia Shabani:

BI. MOJA: “Kama ulijua kufika sasa hivi nipe hela za kanga bwana.

Meli hii hainikosi leo utanipa hela hizo kanga nikakate.

Mwezi wa tatu huu kanga sizijui”.

Muhando anatuonesha kuwa, Bi. Moja ni kiwakilishi cha wanawake wenye tamaa

ya vitu vidogovidogo kama kanga. Inavyoonekana Shabani hana hela hizo za

kununulia kanga.

Lakini Bi. Moja anamlazimisha mwisho wake ni kutokea kutokuelewana. Hivyo

basi mwandishi anaitaka jamii kuacha kuwa na tamaa ya vitu visivyo vya lazima

kwa sababu ndivyo vyanzo vya kukwamisha maendeleo ya jamii kwa ujumla.

Page 101: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

87

Mwanamke Kama Mpinga Maendeleo

Mwanamke amechorwa kama mtu asiye na ushirikiano na wenzake na ndiye

chanzo cha kukwamisha maendeleo. Hili linajidhihirisha katika uk. wa 41 pale Bi.

Tatu anaposema

BI. TATU: “Jamani mie naondoka. Mnaiona volvo hiyo

imenifuata mie”

Bi. Tatu hana ushirikiano na wanawake wenzake wakati wa kuinua Nguzo Mama

yeye Volvo inamfuata na hivyo anaamua kuiacha Nguzo Mama na kwenda

kupata Volvo.

Mfano mwingine wa mwanamke asiye na ushirikiano na wenzake ni Bi Sita

ambaye yeye mikononi yake ati ni laini hivyo hawezi kuinulia Nguzo Mama.

Hili linajidhihirisha uk. wa 41 pale Bi. Msimulizi anaposimulia:

BI. MSIMULIZI : “Naye yule Bi. Sita alienda zake kimoja.

Kamwe hakurudi kuigusa Nguzo Mama sikuzoea

kazi Ngumu Mama mie mikono yangu laini

mwenyewe nategemea. Leo nitashika kamba

mikononi kutwaniza.

Halafu hicho chakula nitategemea nini?”

4.3.5 Mjadala wa Dhamira Zilizojitokeza Kutokana na Uchorwaji wa

Mwanamke katika Tamthiliya ya Nguzo Mama (1982)

Ukombozi wa Mwanamke

Usawiri wa mhusika mwanamke katika tamthiliya ya Nguzo Mama (1982) umeweza

kujenga dhamira ya ukombozi wa mwanamke. Tumeoneshwa kuwa, mwanamke

amekuwa akitafuta ukombozi wake kwa kutafuta maarifa zaidi juu ya kuinua

Nguzo Mama. Vilevile mwanamke kama Bi. Pili amekuwa akijishungulisha na

Page 102: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

88

kupika pombe na wanawake wengine wakisuka mikeka, vitambaa vya meza pamoja

na mapambo ya ndani. Juhudi zote hizi zimekuwa zikifanywa ili kuhakikisha kuwa,

Nguzo Mama inasimama.

Umoja na Ushirikiano

Kama Waswahili wasemavyo, umoja ni nguvu, utengano ni dhahifu. Hivyo basi,

usawiri wa muhusika mwanamke umeweza kujenga dhamira ya umoja na

ushirikiano. Mwandishi anatuonesha kuwa, ili Nguzo Mama iweze kusimama

hakuna budi jamii yote kushirikiana katika suala nzima la kuinua Nguzo Mama. Hili

linajihidhirisha wazi pale mwandishi anaposema uk. wa 58. “Bila umoja

hatutafanikiwa kitu”.

Muhando anaitaka jamii kushirikiana kwa pamoja katika suala la kuinua Nguzo

Mama kwani wakiachiwa wanawake wenyewe kamwe hawataweza kuinua Nguzo

Mama bali anachokitaka ni watu wote kuona umuhimu wa kuinua Nguzo Mama.

Udunishwaji, Unyanyaswaji na Ugandamizaji wa Wanawake katika Jamii

Usawiri wa mhusika mwanamke umeweza pia kujenga dhamira hii, kwa maana

kwamba, wanawake wameoneshwa kama wahusika wanaogandamizwa na

kudunishwa katika jamii wanamoishi. Kwa mfano, mwanamke kama Bi. Saba

alinyang‟anywa mali zake zote alizoachiwa na marehemu mumewe ikiwa ni pamoja

na watoto wake wote watano. Tena mwandishi anatueleza kuwa, watoto wake

aliwalea Bi. Saba kwa shida sana huku baba yao akiwa analewa pombe.

Unyanyasaji pia tunauona kwa Bi. Pili ambaye alikuwa anauza pombe lakini pesa

yote aliyoipata kwenye pombe hiyo alinyang‟anywa na mumewe Sudi tena kwa

Page 103: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

89

kupigwa kipigo kikali. Udunishwaji wa wanawake, tunauona pia kwa Bi. Pili

ambaye licha ya kujishughulisha na upikaji pombe wanaume kama Totolo

walionekana kumdharau kwa kutoamini kuwa, Bi Pili naye anaweza kupika pombe.

Mfano dhahiri unajihidhirisha katika onesho la pili uk. wa 14 pale Totolo

anapomwambia Bi. Pili:

TOTOLO: “Lo! Hata na wewe Bi. Pili siku hizi unapika pombe

kwa maana hiyo,

Totolo alitegemea kazi hiyo ifanywe na mwanaume na siyo mwanamke. Ndiyo

maana hata kushangaa kwake kunaonesha ni kumdharau Bi. Pili.

Uongozi Mbaya

Udikteta unaoneshwa kuwa ni zao la uongozi mbovu uliopo kwenye jamii ya wana

Patata. Viongozi kama mwenyekiti wa kamati ya mashauri wamesawiriwa kama

madikteta. Wanafanya wajisikiavyo au vile waambiwavyo na watu wao wa karibu,

bila kufuata misingi na miongozo waliyowekewa na katiba za jamii zao.

Mwenyekiti wa kamati ya mashauri anatumia vitisho kumlazimisha Bi. Nane

kusema asichokijua ili mradi tu yeye ni kiongozi. Pia, mwenyekiti anaonesha

udikteta wake pale alipotaka kuamua kesi aliyosikiliza upande mmoja tu wa

mashtaka, tena maelezo hayo kapewa wakati mshtakiwa hayupo.

BI. MSIMULIZI: “……Vipi mtu atakubali kutoa ushauri kutumia vitisho!

kufuata maelezoya mshtaki peke yake tena yaliyoelezwa

wakati mshtakiwa hakuwepo vipi mtu atamshauri

mshtakiwa bila kujua mawazo yake” …uk. wa 24.

Pia Muhando anaonesha jinsi udikteta uliokithiri unavyitawala jamii ya Patata, yaani

mtu mmoja anaweza kuamua maamuzi yanayotakiwa kufanywa na kamati nzima.

Mfano ni pale Mwenyekiti wa kamati ya mashauri alipounda kamati ya watu wawili

Page 104: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

90

ili wamshtaki Bi. Nane. Uongozi mmbaya pia umewakilishwa na Bi Saba ambaye

licha ya kuwa kiongozi hajui hata nini maana ya Nguzo Mama, mpaka Chizi

anamshangaa.

Uvivu na Uzembe

Utafiti huu umegundua kuwa mwanamke amesawiriwa kama mvivu na mzembe.

Mfano ni pale wanawake wa Patata waliposhindwa kuinua nguzo mama. Wakati

walipokuwa wanafanya kazi hiyo, wanawake wengine wakawa wanategeana na

kusababisha kushindwa kuinuka kwa Nguzo Mama. Bi. Moja anaacha kuvuta kamba

na kuanza kuongea na Bi Tano kuhusu kanga ambazo kwa muktadha waliokuwepo

wasingepaswa kuzungumzia mambo hayo. Anauliza wapi wamenunua kanga naye

B. Tano anaanza kumweleza kuwa, ni kwa Mwarabu na pia anamtahadharisha

kuwa, anapaswa kuwahi la si hivyo zitakwisha. Mara B.i Moja anaacha kuvuta

kamba na kuondoka ili kuziwahi kanga. Mara Bi Nane anashtuka na kuuliza,

BI. NANE: “sasa jamani Bi. Moja anakwenda wapi tena!! Bi. moja

akiwa mbali anajibu, Aaa !! jamani nitarudi lakini,

kanga hizi sizikosi” uk. wa 34.

Bi. Sita naye amesawiriwa kama mwanamke asiyewajibika na asiyejali umuhimu wa

kazi za maendeleo, kwani naye baadaye anaacha kuvuta kamba na kumfuata

mwanaume eti kwa sababu tu alimkonyeza ili amfuate licha ya umuhimu uliopo

kwenye kuinua Nguzo Mama.

Bi. Tatu naye kwake Nguzo Mama si mali kitu zaidi ya mume na sherehe, hivyo

anawasusia wenzake kamba na kukimbilia kwenye Volvo lililomfuata na kuelekea

kwenye pati ambayo kwake ni muhimu zaidi kuliko Nguzo Mama.

BI. TATU: jamani mie naondoka mnaiona Volvo hiyo imenifuata mie.

Page 105: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

91

Sio utani ndugu yangu. Tunakwenda kwenye pati na

mume wangu leo saa moja lazima nipalilie unga kwa

watoto wangu ati. Nitakula nini” uk. wa 14.

Hata viongozi nao wanaonekana wababaishaji na waliojaa maneno matamu

mdomoni pasipo uwajibikaji kwa vitendo. Bi. Nne kama kiongozi naye anaondoka

kwenye kazi muhimu itakayowezesha maendeleo ya wanawake kupatikana na

kwenda kwenye vikao na kupiga soga bila utekelezaji. Mtafiti amegundua kuwa,

wanawake wenyewe ndio wanaokwamisha maendeleo yao wenyewe kutokana na

wivu, uvivu na uzembe kama ilivyobainika katika tamthiliya ya Nguzo Mama.

Utegemezi wa Mwanamke

Utafiti huuu umeliangalia suala la utegemezi wa wahusika wanawake kwa wanaume

kwa mawanda mapana. Mtafiti amegundua kuwa, tamthiliya ya Nguzo Mama

(1982) imemsawiri mwanamke kama kiumbe kisichokamilika katika mazingira ya

kipekee kijinsia. Mwanamke anamtegemea mwanaume katika masuala mbalimbali,

hususani kiuchumi na katika masuala yakifamilia na kijamii kwa jumla. Mfano ni

katika uk. wa 14 pale Bi. Tatu anaposema:

Bi. Tatu: Siyo utani ndugu yangu tunakwenda kwenye pati na

mume wangu leo saa moja.Lazima nipalilie unga kwa

baba watoto wangu.

Mwanamke amedunishwa kwa kuonekana kuwa tegemezi kwa mwanaume kwa

kuwa, mwanaume anamlisha yeye na watoto. Siyo kuwa Bi. Tatu anakwenda

kwenye pati na mume wake kwa kupenda au kwa ridhaa yake mwenyewe bali kwa

kumpendezesha mume wake na kumridhisha ili atoe pesa za matumizi. Hii ni kwa

lengo la kumbembeleza ili apate unga, maana asipokwenda unga atapata wapi!

Page 106: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

92

4.4 Athari za Uchorwaji wa Wahusika Wanawake katika Kazi za Fasihi

Utafiti huu umebaini athari mbalimbali zinazopatikana kutokana na usawiri wa

wahusika wanawake katika tamthiliya za Hatia na Nguzo Mama. Athari zenyewe

zaweza kuwa mbaya au nzuri. Usawiri wa wahusika hawa katika kazi za kifasihi

unaweza kuleta athari kubwa kwa kizazi kijacho kwani wanajenga hisia kuwa huo

ndio mtindo bora wa maisha. Kazi hizi zinaposomwa na vijana wa siku hizi

zinaweza kuwavutia kuiga tabia na mwenendo wa wahusika hao.

Dkt Vicensia Shule alisema kuwa, athari mojawapo itokanayo na usawiri chanya wa

wahusika wanawake katika kazi za kifasihi ni kuwa wanapozisoma kazi hizi

wanaona kuwa wanawake nao wanapewa kipaumbele na wanathaminiwa katika

jamii. Hata hivyo ameendelea kusema kuwa, mwanamke anapothaminiwa na

kupewa nafasi katika hizi kazi za kifasihi, msomaji anapoisoma kazi hiyo huwa na

hamasa ya kutaka kuonyesha juhudi zaidi katika jamii ili wapate nafasi ya kuendelea

kuthaminiwa zaidi. Ameendelea kueleza kuwa, mwanamke anaposoma kazi ya

kifasihi iliyoandikwa na mwanamke na kuona nafasi na majukumu waliyopewa

wanawake hususani katika tamthiliya moja kwa moja husababisha wanawake wengi

kuanza kuandika kazi mbalimbali za kifasihi au kujiunga na vyama mbalimbali vya

wanawake ili nao kujiunga katika kupinga hali ya unyanyasaji wa wanaume kwa

wake zao. Pia, anasema kuwa, nafasi na majukumu wanayopewa wakina mama

katika kazi za kifasihi husaidia kutoa hamasa zaidi katika jamii na kwa wanawake

kwa jumla katika kutetea harakati za ukombozi wa mwanamke.

Hivyo basi utafiti huu umegundua kuwa, athari mojawapo ya kutumia taswira

chanya kuhusu mwanamke katika kazi za kifasihi hususani tamthiliya, inasaidia sana

Page 107: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

93

katika kuwafanya watazamaji au wasomaji hasa wanawake kujitambua na kuweza

kuongeza juhudi zaidi katika kupigania haki na ukombozi wa mwanamke kifikra na

hata kiuchumi.

Profesa Penina Muhando katika mahojiano na mtafiti yaliyofanyika tarehe

11/11/2013, naye amesema kuwa usawiri chanya wa mhusika mwanamke katika kazi

yoyote ya kifasihi husababisha au huleta matokeo chanya kwa msomaji au kwa

mtazamaji kama ni tamthiliya. Anaendelea kueleza kuwa, wanawake wengi hasa wa

vijijini hawajatambua haki zao kama vile suala la elimu na mambo mengine ya

kijamii na kifamilia kwa jumla. Katika suala la elimu amesema kuwa, asilimia

kubwa ya wanawake wa vijijini hawajui kuwa elimu ni haki yao, ila wanapotazama

tamthiliya au kusoma tamthiliya kwa wale wanaojua kusoma, hasa kipindi hiki cha

utawandazi ulioenea hadi vijijini kwa sasa, wamegundua kuwa wao wana haki ya

kupata elimu kama ilivyokuwa kwa wanaume. Alitoa mfano kuwa, kwa sasa

wasichana wengi wanakataa kuolewa au kuachishwa masomo na pia wengine

hudiriki hata kutoroka kwa kupinga suala zima la unyanyasaji wa wanawake katika

nyanja mbalimbali katika jamii zao. Ameendelea kusema kuwa, wanawake wengi

wamejitambua na kuchukua hatua za kukataa manyanyaso ya wanaume kama vile

kulazimishwa kuolewa wakiwa na umri mdogo, kukeketwa nakadhalika.

Tumeona kuwa kwa kiasi kikubwa kazi hizi za kifasihi zimesaidia sana katika

kuzindua akili za wanawake katika jamii na kujitambua, pia wanawake wengi

wamejikita katika kujishughulisha na kazi mbalimbali katika jamii ilimradi tu na

wao wainue kipato chao pamoja n kuilea familia kwa jumla.

Page 108: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

94

Mtafiti amegundua kuwa, mwanamke anaweza kubadilisha mwenendo na

kujithamini pale anaposoma kazi ambazo zina mtazamo chanya juu yake.

Kutokakana na utafiti huu tumeona kuwa kuna funzo kubwa sana kwa wasichana na

akina mama kwa jumla. Suala la elimu ni jambo ambalo limeonekana kuwasisimua

watu wengi kwa kuona kuwa elimu ndicho chombo pekee kinachoweza kuleta

ukombozi wa mwanamke. Katika tamthiliya ya Nguzo Mama mwanafunzi amewatia

hamasa akina mama kwa kumwona amebeba vitabu na amevalia sare za shule. Licha

ya mwanafunzi, pia mwalimu naye amekuwa kishawishi kizuri kwa wakina mama

wa Patata. Msomaji au mtazamaji wa tamthiliya hiii hupata msukumo na hamasa za

kuona umuhimu wa elimu katika jamii.

Pia usawiri au uchorwaji wa mwanamke kwa upande chanya katika kazi za kifasihi

husaidia kuhamasisha wasomi kufanya utafiti. Hivi sasa baada ya utafiti mwingi

kufanyika umeweza kuamsha hamu ya watu kuandika kazi mbalimbali zinazohusu

mwanamke katika kazi za kifasihi.

Kwa kufanya utafiti jamii itafahamu mambo yaliyomo katika tamthiliya hizo na

matatizo yote yaliyomo katika jamii na jinsi ya kutatua.

Pia athari mbaya zinazotokana na usawiri au taswira hasi za wanawake katika kazi

za fasihi zimejitokeza kama ifuatavyo:

Utafiti huu umegundua kuwa, mwanamke anaposawiriwa katika hali ya uhasi,

matokeo yake ni kusababisha matatizo makubwa katika jamii kama vile vita

nakadhalika. Mfano mzuri ni mhusika Cheja katika tamthiliya ya Hatia (1972) jinsi

Page 109: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

95

alivyozua vita kwenye kijiji kizima, watu wamepigana, wameumizana na hata

kusababisha hela nyingi kupotea katika matibabu.

Dkt Mona Mwakalinga ameeleza kuwa, athari zinazoweza kujitokeza kutokana na

usawiri hasi katika kazi za kifasihi hususani katika tamthiliya ni wasomaji kuiga

matendo mabaya yanayoigizwa au wanayosoma katika kazi hizo. Aliendelea kueleza

kuwa, mwanamke hupenda kuiga mambo si kawaida yake kufanya kwa wengine.

Alitoa mfano kuwa, hasa kwa kipindi hichi tulichonacho cha utandawazi.

Mwanamke katika kazi ya kifasihi amechorwa kavaa mavazi mafupi au

yanayomwacha wazi sehemu zake za mwili. Msomaji au mtazamaji wa tamthiliya

huweza kuiga matendo machafu ambayo yameonyeshwa kuwa mwanamke ndiye

anayefanya ili kuvutia wanaume.

Bw Mtiro naye ameeleza athari mojawapo ni kuwa msomaji au mtazamaji wa

tamthiliya hujenga dhana potofu kuwa mwanamke ni mtu wa kujiremba tu, ni mtu

wa kumtegemea mwanaume tu, ni mtu wa kumfurahisha mwanaume tu, ni mtu wa

kukandamizwa tu, ni mtu ambaye hawezi kufanya maamuzi katika jamii au katika

familia yake na ni mtu malaya tu. Anaendelea kueleza kuwa, watu wengi hasa

wanaume wanaposoma kazi hizi au kuzitazama hujaribu au kuwapeleka wake zao

kama walivyoona au kama walivyosoma katika kazi hizo. Hata katika majukumu

msomaji au mtazamaji hutoka na dhana potofu kuwa majukumu ya mwanamke ni

kupika, kufua na kulea familia ikiwa ni pamoja na mume.

Utafiti huu umeona kuwa, uchorwaji hasi wa mwanamke katika tamthiliya

husababisha kukata tamaa kwa wanawake na madhara yake anaishia kujinyonga au

Page 110: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

96

kujiona kuwa hana thamani katika jamii. Mwanamke mara nyingi ameonekana ni

mtu wa kukata tamaa katika maisha. Uchorwaji huu wa mwanamke kama kiumbe

dhaifu cha kukata tamaa haraka husababisha mtazamo hasi kwa wasomaji na

watazamaji kuona kuwa mwanamke ni kiumbe dhaifu na mara nyingi mwisho wake

wanaonekana sio wa mafanikio tofauti na wanaume.

Hivyo basi, waandishi wengi wa kazi za kifasihi husana kazi zao kulingana na jamii

au matendo yanayofanyika katika jamii zao. Hivyo husababisha watu wa utamaduni

mwingine au wa jamii nyingine wanaposoma kazi hizo kuiga matendo

yanayofanywa na jamii nyingine bila kujua madhara yake.

4.6 Hitimisho

Sura hii ya nne imefanya jitihada ya kuyajibu maswali ya utafiti. Katika sura hii

mtafiti ameelezea jinsi mwandishi anavyoweza kumsawiri mwanamke kutokana na

vitendo mbalimbali wanavyofanyiwa wanawake katika jamii na jitihada

wanazofanya wanawake katika jamii mbalimbali, na kwa kadri atakavyotaka ujumbe

uifikie jamii kuhusu mwanamke. Hii inatokana na kwamba mwanamke kutumiwa

kueleza mambo hasi na wakati mwingine katika upande wa chanya na hivi ndivyo

ilivyojitokeza kati tamthiliya tulizozijadili. Ambapo mwandishi wa tamthiliya ya

Hatia (1972) na Nguzo Mama (1982) ametumia taswira mbalimbali kuelezea maovu

yanayotendwa na wanaume juu ya wanawake pamoja na harakati zinazofanywa na

mwanamke katika kujikomboa. Katika tamthiliya hizi taswira ya mwanamke

imetumika katika pande zote mbili yaani hasi na chanya. Pia katika sura hii mtafiti

amebainisha dhamira mbalimbali zilizojitokeza katika tamthiliya teule zilizojadiliwa

kwa lengo la kuonyesha uhusiano wa moja kwa moja na usawiri wa mwanamke.

Page 111: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

97

Katika uchambuzi wa data uhusiano huo umeshadidiwa na nadharia ya Ufeministi

ambayo imekuwa mhimili mkubwa katika kuchakata data zilizopatikana. Sura

ifuatayo itaelezea muhtasari wa kazi zima, ikiwa ni pamoja na maoni na

mapendekezo ya mtafiti kwa mwandishi, jamii na waandishi wachanga wa kazi za

fasihi.

Page 112: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

98

SURA YA TANO

MUHTASARI WA MATOKEO YA UTAFITI , MAPENDEKEZO, NA

HITIMISHO

5 .0 Utangulizi

Utafiti huu ulikuwa na lengo la kuchunguza jinsi mwanamke alivyochorwa katika

tamthiliya teule za Penina Muhando. Katika sura hii, muhtasari wa sura

zilizotangulia umetolewa. Kila sura imeelezwa kwa kifupi ili kuweka wazi kile

kilichofanyika katika utafiti. Vilevile, sura hii inatoa maoni na mapendekezo

yanayoweza kufanyiwa utafiti na wanazuoni wengine kwa kina zaidi na kuhusu

tamthiliya. Nadharia iliyotumika ni nadharia ya Ufeministi wa Kiafrika. Muhtasari

wa matokeo ya Utafiti uliongozwa na maswali matatu ya utafiti ambayo ni:

i. Nafasi ya mwanamke imesawiriwa vipi katika

tamthiliya za Hatia na Nguzo Mama?

ii. Je, wahusika wa kike wamechorwaje kwa mujibu wa

majukumu katika tamthiliya hizo?

iii. Ni athari gani zinazopatikana kutokana na usawiri wa

mwanamke katika kazi za kifasihi?

5.1 Muhtasari wa Mpangilio wa Tasnifu

Tasnifu hii ilihusu jinsi mwanamke alivyochorwa katika tamthiliya teule za Penina

Muhando. Tasnifu hii ina sura tano, ambapo sura ya kwanza inahusu utangulizi wa

jumla wa tasnifu zima, usuli wa tatizo ambao kwa kifupi, historia ya tamthiliya kwa

ujumla katika dunia na Tanzania. Usuli huo unafafanua maendeleo ya tamthiliya na

jinsi wanawake walivyozungumziwa. Tatizo la utafiti limeelezewa sanjari na

malengo ya utafiti ambayo yamegawanyika katika sehemu kuu mbili ambazo ni

lengo kuu na malengo mahususi ambayo yako matatu. Malengo hayo matatu

Page 113: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

99

yamezalisha maswali ya utafiti ambayo nayo yako matatu. Maswali hayo

yamejibiwa katika uchanganuzi wa data na hivyo malengo ya utafiti yakatimizwa.

Katika sura hii pia nadharia iliyotumika imefafanuliwa, ambayo ni nadharia ya

Kifeministi. Katika sura hii pia umuhimu wa utafiti umeoneshwa na kuelezea jinsi

wataalamu mbalimbali, wasomaji na watafiti Watakavyofaidika. Mwishoni mwa

sura hii ya kwanza kuna mpangilio mzima wa utafiti. Katika kurasa za kwanza

istilahi na msamiati mbalimbali umefafanuliwa ili kutoa utata kwa wasomaji na

watafiti wengine. Pia vifupisho vya maneno yaliyotumika vimeandikwa kwa kirefu

katika sura hii.

Sura ya pili inatoa historia za waandishi wa kazi zilizoteuliwa na mtafiti katika

utafiti huu, wanawake katika fasihi na wanawake katika jamii. Pia mtafiti ametalii

maandiko mbalimbali yaliyotumika kujenga hoja madhubuti iliyofanya utafiti uwe

muhimu. Kigezo kilichotumika katika maandiko haya ni cha kutalii tafiti zilizohusu

waandishi na jinsi kazi zao zilivyofanyiwa utafiti na hii imemsaidia mtafiti kubaini

pengo ambalo watafiti wengine hawajalifanyia kwa kina.

Sura ya tatu ya tasnifu hii inaelezea mbinu mbalimbali za utafiti zilizotumika

kukamilisha tasnifu hii. Mbinu hizo ni pamoja na eneo la utafiti, usampulishaji, vifaa

vya utafiti sambamba na vyanzo vya data za msingi na vyanzo vya fuatizi. Utafiti

huu ulifanyikia katika maktaba ya Chuo Kikuu cha Dodoma, Chuo Kikuu cha Dar es

Salaam kuwahoji baadhi ya wataalam wa Fasihi ya Kiswahili, Makavazi ya Taasisi

ya Taaluma ya Kiswahili (TATAKI) na Maktaba ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Maandiko mbalimbali yalisomwa. Uchambuzi wa data za utafiti huu ulizingatia

nadharia ya Ufeministi.

Page 114: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

100

Katika sura ya nne ya tasnifu ndipo data zilipochanganuliwa. Uchanganuzi wa data

hizi ndio uliojibu maswali ya utafiti sambamba na kutimiza malengo ya utafiti

yaliyokusudiwa. Data zote zilizopatikana katika kazi teule za Penina Muhando,

maktabani na kwa wataalam wa fasihi ya Kiswahili zilichambuliwa na kuweka

bayana usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Hatia (1972) na Nguzo

Mama (1982). Mgawanyo wa majukumu kijinsia pia umeelezewa kwa uwazi kwa

kushadidiwa na hoja mathubuti na faafu za wataalamu mbalimbali waliofanya

kuhusu mwanamke. Sura hii imeongozwa na nadharia moja yaani ya ufeministi.

Mwisho tasnifu hii imejengwa na sura ya tano ambayo inatoa muhtasari wa tasnifu

nzima, inahitimisha na kutoa mapendekezo kwa watafiti, wataalamu, wasomaji/jamii

na waandishi wa tamthiliya.

5.2 Muhtasari wa Matokeo ya Utafiti

Lengo kuu la kazi hii lilikuwa kuchunguza jinsi mwanamke alivyochorwa katika

tamthiliya teule za Penina Muhando. Kutokana na uchambuzi wa data, matokeo ya

utafiti yanaonyesha kuwa tamthiliya zote mbili, Hatia na Nguzo Mama zimeonyesha

taswira mbalimbali ambazo zinaakisi masuala mbalimbali ya maisha kuhusu

mwanamke katika jamii na jinsi au mtazamo na muonekano wa mwanamke katika

jamii.

Katika utafiti huu, imegundulika kwamba nafasi ya mwanamke katika tamthiliya,

mwanamke anakandamizwa kwa kiasi kikubwa. Mwanamke bado hajapewa

muonekano chanya japo zipo taswira chache ambazo zimemuonesha mwanamke

kwa mtazamo chanya ambapo mwanamke ameonekana kama mtu mwenye

ushirikiano, mlezi na mwenye jitihada za kujikomboa pamoja na mwenye ushauri na

Page 115: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

101

busara katika jamii. Katika baadhi ya asasi mbalimbali mwanamke ameonekana

kukandamizwa na kudunishwa na vyombo vya sheria, suala la utoaji mahari, elimu

ndogo kuhusu uhuru wa kuchagua na kuchaguliwa na mfumo dume uliopo katika

jamii. Pia mwanamke ameonekana hana maadili mema ila ni mtu wa kugeuzwa na

utamaduni wa kigeni uliongia nchini. Yote haya yamesababishwa na mwanamke

kukosa urazini kuhusu haki zake. Hali hiyo ndiyo iliyowaamsha wanawake

mafeministi kuanza harakati za kujikomboa ili waweze kutokana na hali ya

kugandamizwa.

Katika swali la kwanza tumegundua kuwa, mwanamke kapewa nafasi mbalimbali za

uzuri na ubaya katika tamthilia za Hatia (1972) na Nguzo Mama (1982).

Katika upande wa mgawanyo wa majukumu, mwanamke ameonekana kuwa hawezi

kufanya kazi ambayo ni ya mshahara sawa na mwanamume. Pia mwanamke

anaonekana kuachiwa kazi zote za nyumbani ambazo hazina ujira wowote. Kazi hizo

hazithaminiwi kuanzia ngazi ya familia mpaka ngazi ya jamii, kama zilivyo za

wanaume. Hata ikiwa mwanamke amepata kazi lakini mshahara wake hauwezi

kulingana na wa mwanaume, mwanamke analipwa mshahara mdogo zaidi kwa kuwa

anaonekana kuwa hawezi.

Utafiti huu umetoa mchango ambao umeleta changamoto mpya katika fasihi

tamthiliya na katika jamii kwa ujumla. Pia umetoa changamoto katika tafiti nyingine

za kifasihi hasa katika usawiri wa mwanamke katika kazi nyingine za kifasihi.

Kwa upande mwingine, utafiti huu umetoa mwanga kwa wanawake waandishi wa

fasihi na wale wasio wa fasihi ila wanaandika kuhusiana na wanawake, kwani

Page 116: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

102

tasnifu imeweza kugusa pande zote za kifasihi. Pia umewasaidia wanawake kujua

uthamani wa kazi zao katika jamii kwani wanafikisha ujumbe waliokusudia katika

jamii kwa njia ya fasihi kwa kuandika na kuigiza majukwaani kama ilivyo kwa

waandishi wengine wanavyofikisha ujumbe kwa njia ya maandishi.

5.4 Mapendekezo

Tasnifu hii ilihusu usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina

Muhando, ambazo ni Hatia (1972) na Nguzo Mama (1982). Kazi za kifasihi zipo

nyingi na zote zinatumia wahusika katika kufikisha ujumbe wake kwa jamii.

5.4.1 Mapendekezo kwa Watafiti

Kwa kuwa tasnifu ilijikita katika kuangalia wahusika wanawake katika tamthiliya,

itakuwa vema kwa watafiti wengine kuchunguza tamthiliya na kuandika makala,

majarida, na vitabu vingi kabisa ili marejeo yawe mengi. Pia ni muhimu watafiti

wengine wakafanya uchunguzi wa tamthilia kuangalia wahusika wa kiume ili kuona

kama kuna wanaume waliosawiriwa kama wanawake.

Vilevile wahusika wanawake katika tamthiliya wamechorwa kwa namna tofauti na

wasanii tofauti. Ni vema kuwachunguza wanatamthiliya na kuchunguza ujumbe wao

kisha tuweze kupata falsafa, mtazamo na msimamo wao ili kuona mchango wake

katika jamii.

5.4.2 Mapendekezo kwa Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP)

Wanawake ni watu walio duni mbele ya wanaume kwani jamii ndivyo inavyowaona.

Uduni wao ndio unaowafanya wasipate kazi za kuajiriwa kwa wingi kama walivyo

Page 117: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

103

wanaume. Ingawa jamii imeanza kufunguka na kuona umuhimu wa mwanamke

katika ngazi zote lakini hata katika ajira walio wengi hawapati haki, malipo na nafasi

sawa na wanaume. Hii ni kwa sababu wanaume hawaamini kama wanawake

wanaweza kama wanaume wanavyoweza. Kutokana na tatizo hili, Mtandao wa

Jinsia nchini Tanzania unapaswa utambue kwamba hata wanawake wanaweza hata

kama wasipowezeshwa. Mtandao unapewa changamoto ya kuhimiza mabadiliko ili

mwanamke naye apate fursa sawa na mwanaume.

5.4.4 Mapendekezo kwa Jamii

Katika tamthiliya zilizotafitiwa imegundulika kwamba wanawake kwa sehemu

kubwa wamekejeliwa kutokana na jinsi walivyo, na jinsi jamii inavyowatazama na

inavyowachukulia. Pengine kejeli juu ya mwanamke inasababishwa na muonekano

wa matendo yake ndani ya jamii kuwa si mazuri. Hivyo inapaswa waelewe kwamba

fasihi au sanaa nyingine ni kioo cha jamii kinachoonesha mwenendo mzima wa watu

ndani ya jamii. Aidha wanatakiwa kubadilika na kuwa na mwenendo mzuri ili

maadili mema yaweze kuonekana kwao na wawe mfano wa kuigwa. Hata hivyo

jamii inatakiwa ipambane na suala la umalaya kwa kuwapatia wanawake kazi zenye

malipo mazuri kwani inaonekana kuwa machangudoa wengi wanafanya biashara

hiyo kwa sababu hawana kazi zinazoweza kuendesha maisha yao.

5.4.5 Mapendekezo kwa Waaandishi wa Tamthiliya

Tasnia ya uandishi wa tamthiliya imepanuka kwa kiasi kikubwa ikilinganishwa na

kipindi cha nyuma mara baada ya Tanganyika kupata uhuru. Waaandishi wengi wa

tamthiliya aghalabu wanamchora mwanamke kama kichekesho, mtu aliyekosa

ustaarabu, kahaba na aliyekosa maadili, duni, mnyonge, tegemezi asiyeweza

Page 118: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

104

kujitegemea mwenyewe, mtawaliwa na mjinga asiye na elimu. Aidha waandishi wa

tamthiliya inatakiwa wabadilike kulingana na wakati kwani wanawake walio wengi

wamestaarabika na wamesoma. Idadi ya wanawake waliosoma kwa sasa sio sawa na

ya miaka ya nyuma ambapo ilihitajika wapate elimu ya ngumbaro ndipo waonekane

wamesoma. Waandishi wa tamthiliya wanapaswa kumchora mwanamke katika

taswira ambazo zitamkweza mwanamke hasa tukizingatia wakati na majira

tuliyonayo kuhusu suala la ukombozi wa mwanamke. Hilo litawasaidia wanawake

kujitambua zaidi na kujua wajibu wao katika jamii, tofauti na sasa ambapo kila siku

wanakutana na tamthiliya au kazi zinazoudhalilisha utu wao. Hivyo basi mwanamke

asionekana kwa mabaya zaidi bali kwa mema pia maana yapo mengi yanayofanywa

na wanawake yanaweza hata kuzidi yale ya wanaume.

5.5 Hitimisho

Wanawake wanaweza ikiwa watawezeshwa na hata bila kuwezeshwa ikiwa

watapewa nafasi ya kuweza. Kama jamii itaona umuhimu wa kuwapa madaraka na

mamlaka ya kuongoza na kusimamia kazi katika sehemu nyeti pia. Maendeleo

yanaweza kutokea katika nchi ikiwa wanawake watapewa nafasi sawa na wanaume

katika sekta zote za uongozi yaani kuanzia nafasi ya Urais, Uwaziri, Ubunge, Jeshi,

na Uongozi wa sehemu nyingine mbalimbali, na sio kama sasa wanavyopewa tu

katika baadhi ya sekta.

Page 119: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

105

MAREJELEO

Bader Z. (1974), “Social Condition of the Peasant Women in Zanzibar and Pemba.”

Paper No, 18 iliyowasilishwa katika semina ya Wanawake Brulap, Chuo

Kikuu cha Dar es Salaam.

Balisidya, M.L (1982), “The Image of Woman in Tanzania Oral Literature: A

Survey” Katika. Mulokozi (mh), Jarida la Taasisi ya Uchunguzi wa

Kiswahili, Juzuu 49/2. Uk. 08.

Birkett, J na Elizabeth H. (1991) (wah), Determined Women: Studies in the

Construction of Female subject 1900-90, London, The Macmillan Press

Ltd.

Bond, S (2000), “Culture and Feminine Leadership”, katika Women Power and the

Academic From Rhetoric to Reality. New York, Berghahn Books.

Davenport(1900),www.sanseverrting.wordpress.com/2008/01/30/guy_davenport_the

_writer_as_cartoonist. 12/04/2013, Saa 12:00 Jioni

Eckman, F. na O‟Sullivan (1988)

http://www.ncbi.nlm.nihgox/pmc/articles/PMC.2223159#bhan

05/04/2013 saa 6:35 Mchana

El Saadawi (1983), Woman at Point Zero. Egypt, Zed Books.

Felluger, D.F (1998), “Undegraduate Introduction to Critical Theory” http://

scout.cs.wisc.edu/scout/report/socsci/ 11/05/2013, Saa 8:12 Mchana.

Hughes, D.M (2000), Men Create the Demand; Women Are the Supply. Lecture on

Sexual Exploitation Queen Sofia Center, Valencia, Spain November 2000

Universit of Rhodes Island.

Ilumoka A.O (1994), African Women’s Economic, Social and Cultural Rights.

Philadelphia, University of Pennsylvania Press.

Kayoka, C.M (200), The Woman in Kiswahili Literature: A Feminist Approach. Dar

es Salaam, The Open University of Tanzania.

Kezilahabi, E (2003), “Mandhari na Wahusika”, katika Makala za Semina ya

Kimataifa ya Waandishi wa Kiswahili 111 Fasihi. Dar es Salaam, Taasisi

ya Uchunguzi wa Kiswahili, Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam. Uk.84-89

Kiango, S.D (1982), “Tamthilia za Kiswahili: Dhamira Chapwa na Usuli katika

Uchapwa” katika Mulokozi (Mh) Jarida la Taasisi ya Uchunguzi wa

Kiswahili Juzuu 49/2.

Kiango S.D (1992), “Taswira ya Mwanamke katika Tamthilia za Kiswahili za

Kenya” katika Ibrahim, S. (Mh) Baragumu, Jarida la Kiswahili Juzuu

Namba 1.

Page 120: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

106

King‟ei, K. na C.N.M Kisovi (2005), Msingi wa Fasihi Simulizi. Nairobi, Kenya

Literature Bureau.

Mackinnon, C.A (1991), Toward A Feminist Theory of the State. London, Havard

University Press.

Mbilinyi, M na Ophelia M (1980), Women and Development in Tanzania: An

Annotated Bibliography. Addis Ababa EtiopiaECA/ Ford Foundation.

Morris, P (1993), Literature and Feminism. Oxford Black.

Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) (2001), Kuelekea Kwenye Usawa: Taswira ya

Mwanamke Tanzania. Dar es Salaam, SARDC.

Mulokozi, M. M (1996), Utangulizi wa Fasihi ya Kiswahili. Dar es Salaam, Chuo

Kikuu Huria Tanzania.

Mulokozi, M.M. na Kahigi, K.K (1979), Kunga za Ushairi na Diwani Yetu.

Dar es Salaam, Tanzania Publishing House.

Mlama, P .(1976), Hatia, . Dar es Salaam: East African Publishing House.

Mlama, P. (1982), Nguzo Mama. Dar es Salaam: Dar es Salaam University Press.

Mtiro, C (2005), The Image of Women in two Tanzanian Plays, A case of Alikiona

and Machozi ya Mwanamke, Unpublished M.A Dissertation, Universty

of Dar es Salaaam,

Nabahany, A. (1972), (mh) Utenzi wa Mwanakupona. Nairobi, Heinemann

Ndomba, R.G.S (2001), “A Study on Cartoons Language in Tanzanian Newspapers:

A Sociolinguistic Stylistic Perspective.” B. A Desertation paper LL 300,

University of Dar es Salaam.

Nicholas, J. (2005), A Shelf of Our Own; Creative Writing and Australian Literature.

Australia, Australian Book Review.

Noordin M.M (2008), “Nadharia ya Ufeministi wa Kiislamu katika Fasihi ya

Kiswahili” katika Ogechi N.O, na wenzake Nadharia katika Taaluma ya

Kiswahili na Lugha za Kiafrika. Eldoret Kenya, Moi University Press.

Nyerere, Mwalimu JK (1967),”Socialism and Rural Development” Dar es Salaam.

Ngugi, G. (1961), Nimelogwa Nisiwe na Mpenzi. Nairobi: East Africa Publishing

House.

Okin, S.M (1995), “Inequality between the Sex in Different Cultural Context” katika

Women Culture and Development: A Study of Human Capabilities.

Nussbaum, M na Jonathan, G. (wah) Clarendon Press Oxford

Pullen, C. (2006), Marxist against Feminists on Education. London

Page 121: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

107

Rasaldo, M.Z (1974), “Women Culture and society: A Theoretical Overview in

Michelle Zambalist”. katika Rosaldo and Liuise L. (wah) katika Women

Culture and Society, Stanford University Press.

Sanga, Imani. (2001), Construction of Gender and Gender Roles in Religious Choirs

in Dar es Salaam. Unpublished MA Dissertation. University of Dar es

Salaam.

Sen, A. (1995), “Gender Inequality and Theories of Justice” katika Women Cultural

and Development: A Study of Human Capabilities. Nussbaum, M, C na

Jonathan G (wah). Clarendon Press-Oxford.

Senkoro F.E.M.K (1987), Fasihi. Dar es Salaam, Press and Publicity Centre.

Senkoro, F.E.M.K (2008), “English is not our Mother Land; Anecedotal Discussions

and Views on the Language Question in Tanzania”, katika LOITASA

Reflecting on Phase I and Entering Phase II. E&D Vision Publishing

Limited. Dar es Salaam.

Soko, N na Senkoro, F.E.M.K (2009), “Engendered Sports Coverage in Zambia and

Tanzania”. Paper for Presentation in the Forthcoming CODESRIA

Gender Symposium. Cairo Egypty

Shule,V. (2004), “Effective Video Film Reducing Young Mens Gender Violence

and Other .H.I.V Risk Behaviours”, (Unpublished M.A Theatre Arts

Dissertation) University of DSM.

Taib A.H (2008), “Mkabala wa Kiislamu katika Uchanganuzi na Uhakiki wa Fasihi

ya Kiswahili”, katika Ogechi N.O na wenzake (wah) Nadharia katika

Taaluma ya Kiswahili na Lugha za Kiafrika. Eldoret Kenya, Moi

University Press.

UNDP (1996), Womeni in Africa Profile of Leadership A Mandate For Change.

UNDP Regional Bureau for Africa UNDP 1 UN Plaza New York.

UNESCO.(1988)http://portal.unesco.org/ci/en/ev,php_URL_ID=14786&URL_DO=

TOPIC&URL_SECON=201.html. 25/04/2013

Wamitila, K.W (2002), Uhakiki wa Fasihi, Misingi na Vipengele vyake, Nairobi,

Phoenix Publishers.

Wegesa B. B. N. (1994). Mwanamke Katika Tamthiliya za Ebrahim Hussein:

Shahada ya Uzamili ya Falsafa katika Idara ya Kiswahili Chuo Kikuu cha

Moi (Haijachapwa).

York, J. na wenzake (1991), “We are the Feminists That Women Have Warned Us

About” katika Gunew, S (mh) A Reade in Feminists Knowledge

Zerbisias A. (2010), “Ack! Cartoonists and Feminists Quarrel Over Demise of

Cathy.”

Page 122: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

108

http://www.thester.com/living/columnists/94657_zeerbisias_antonia. Published on

Friday August, 20 ,2010.. 18/04/2013, Saa 1:10 Jioni.

Page 123: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

109

VIAMBATANISHO

KIAMBATANISHO (a)

Hojaji kwa mwandishi

1. Je, unaitwa nani? Taja majina yako kamili.

2. Umezaliwa mwaka gani?

3. Umeolewa?

4. Je wewe ni kabila gani?

5. Je, mmebahatika kuwa na watoto wangapi?

6. Je, ni kazi zipi umewahi kufanya za kijamii tofauti na kazi za kifasihi?

7. Kwa sasa unafanya kazi gani?

KIAMBATANISHO (b)

Hojaji kwa wataalamu wa Fasihi ya Kiswahili na Sanaa

1. Mwanamke amezungumziwa vipi katika kazi za kifasihi ulizowakuzisoma?

2. Umewahi kusoma kitabu chochote cha Profesa Penina Muhando?.

3. Wanawake wametumika vipi katika matukio mbalimbali ya kijamii?

4. Ni kwanini waandishi wengi huwatumia wanawake katika matukio mabaya?

5. Mwanamke kasawiriwa vipi katika kazi za Penina Muhando?

6. Unajisikiaje unaposoma kazi ya kifasihi na kuona taswira zinazomdhalilisha

mwanamke?

7. Ni athari gani zinazotokana na usawiri wa mwanamke katika kazi za kifasihi?

8. Kwa sasa mwanamke anaonekana vipi katika kazi za kifasihi na katika jamii

ukilinganisha na kipindi cha nyuma?

Page 124: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

110

ORODHA YA PICHA

Picha mbalimbali kuonyesha wataalamu waliohojiwa na mtafiti

Pichani ni Mtafiti pamoja na Profesa Penina Muhando mwandishi wa

tamthilia za Kiswahili wakiwa katika mahojiano katika Chuo Kikuu cha Dar

es salaam tarehe11/11/2013.

Profesa Penina muhando akiwa ofisini kwake wakati wa mahojiano mnamo tarehe

11/11/2013 katika ofisi za Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Page 125: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

111

Pichani ni Profesa Penina Muhando mwandishi wa tamthiliya ya Hatia na

Nguzo Mama akimkaribisha mtafiti ofisini kwake siku ya mahojiano tarehe

11/11/2013.

Profesa Imani Sanga akiwa ofini kwake na mtafiti siku ya mahojiano tarehe

08/11/2013, akimpatia mtafiti baadhi ya makala zake alizoandika kuhusu

mwanamke.

Page 126: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

112

Daktari Mona Mwakalinga akiwa pamoja na mtafiti ofisini kwake baada ya

mahojiano katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam tarehe 05 /11/2013.

Pichani ni daktari Vicensia Shule akishukuriwa na mtafiti ofisini kwake

tarehe 08/11/2013 baada ya mahojiano.

Page 127: Usawiri wa mwanamke katika tamthiliya teule za Penina Muhando

113

Pichani ni Mwalimu Mtiro akimdadavulia kwa kina mtafiti kuhusu usawiri

wa mwanamke katika kazi za kifasihi tarehe 18/11/2013.

Pichani ni Mwalimu Mtiro akiwa katika mahojiano na mtafiti ofisini kwake

tarehe 18/11/2013.