72
HALMASHAURI YA KIJIJI CHA KASANGANTONGWE MPANGO WA USIMAMIZI WA MSITU WA HIFADHI WA KANKOSYA KIJIJI CHA KASANGANTONGWE HALMASHAURI YA KIJIJI CHA KASANGANTONGWE S. L. P. 1 MPANDA.

HALMASHAURI YA KIJIJI CHA KASANGANTONGWE · Shughuli za kiuchumi za wakazi wa kijiji cha Kasangantongwe zinategemea sana Uvuvi na kilimo. Kwa upande wa kilimo wananchi wa kijiji hiki

  • Upload
    others

  • View
    29

  • Download
    0

Embed Size (px)

Citation preview

HALMASHAURI YA KIJIJI CHA

KASANGANTONGWE

MPANGO WA USIMAMIZI WA

MSITU WA HIFADHI WA KANKOSYA KIJIJI

CHA KASANGANTONGWE

HALMASHAURI YA KIJIJI CHA KASANGANTONGWE S. L. P. 1 MPANDA.

i

SEHEMU YA KWANZA - UTANGULIZI ....................................................................... 1

MAELEZO YA JUMLA YA MPANGO ........................................................................... 1

MAELEZO...................................................................................................................... 2

Msitu wa Hifadhi ya Kijiji cha Kasangantongwe ........................................................... 2

MSITU WA HIFADHI WA KIJIJI CHA KASANGANTONGWE; .................................... 3

MATUMIZI YA MSITU WA HIFADHI YA KIJIJI CHA KASANGANTONGWE ............. 4

KIJIJI CHA KASANGANTONGWE ............................................................................... 6

Sehemu ya tatu: ............................................................................................................ 7

Madhumuni ya mpango wa usimamizi wa msitu wa kijiji cha Kasangantongwe........ 7

ENEO DOGO LA USIMAMIZI LA MPAPA. .................................................................. 8

ENEO DOGO LA USIMAMIZI LA KABHUKINDU. ..................................................... 10

ENEO DOGO LA USIMAMIZI LA ZIWA TANGANYIKA ............................................ 11

SEHEMU YA PILI ........................................................................................................ 12

MPANGOWA UTEKELEZAJI ..................................................................................... 12

Meneja Mteule ............................................................................................................. 12

Uwezo na Majukumu ya Kamati ya Mazingira ........................................................... 13

Majukumu ya Mwenyekiti wa kamati ya Maliasili ya Kijiji ......................................... 15

Majukumu ya Katibu wa kamati ya mazingira: ........................................................... 15

Majukumu ya Mtunza hazina: .................................................................................... 17

Msimamizi wa Doria: ................................................................................................... 17

ii

Majukumu ya Wahusika Wengine .............................................................................. 18

Halmashauri ya Kijiji: ................................................................................................... 18

Wanakijiji...................................................................................................................... 18

Wataalamu wa Misitu katika ngazi mbalimbali ........................................................... 19

Viongozi wa Kata, Tarafa, Wilaya na Mkoa,............................................................... 19

UTENDAJI KAZI WA KAMATI YA MALIASILI YA KIJIJI. .......................................... 20

MAELEZO MENGINEYO ............................................................................................ 20

UTOAJI TAARIFA ....................................................................................................... 20

UWEKAJI WA KUMBUKUMBU .................................................................................. 21

MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA ZA KAMATI YA MAZINGIRA ......................... 21

MATARAJIO YA UFANISI WA UTEKELEZAJI WA MPANGO WA USIMAMIZI WA

MSITU.......................................................................................................................... 22

UTUNZAJI KUMBUKUMBU ........................................................................................ 23

VITABU VYA KUMBUKUMBU .................................................................................... 23

KITABU CHA MAKOSA NA FAINI.............................................................................. 23

KITABU CHA STAKABADHI...................................................................................... 24

VITABU VYA VIBALI ................................................................................................... 24

KITABU CHA DORIA .................................................................................................. 24

KITABU CHA AKAUNTI .............................................................................................. 25

KITABU CHA MAPATO NA MATUMIZI ..................................................................... 26

USIMAMIZI WA FEDHA.............................................................................................. 26

iii

WAHUSIKA WAKUU; .................................................................................................. 26

AFISA MUWAJIBIKAJI WA MASUALA YA FEDHA ................................................. 26

MATUMIZI YANAYOIDHINISHWA; ............................................................................ 28

Mipaka ya Msitu wa hifadhi wa kijiji cha Kasangantongwe ........................................ 29

MAELEKEZO MAALUM .............................................................................................. 29

ULINZI NA UKAGUZI WA ENEO LA MSITU WA KIJIJI CHA

KASANGANTONGWE ................................................................................................ 29

Sifa za Walinzi wa Msitu. ............................................................................................ 30

Wajibu, Majukumu na Mafao ya Walinzi wa Msitu wa Hifadhi ya Kijiji ...................... 31

OPERESHENI ............................................................................................................. 31

ZAWADI YA PONGEZI KWA MWANA DORIA ........................................................ 32

Kanuni za Kutumia Msitu wa Hifadhi ya kijiji .............................................................. 32

Kanuni za matumizi ya msitu: ..................................................................................... 33

Matumizi ya Msitu yanayohusu Ukataji wa Miti .......................................................... 33

TARATIBU NA SHERIA NYINGINEZO ...................................................................... 34

Adhabu ........................................................................................................................ 34

MCHAKATO WA KUMSHUGHULIKIA MKOSAJI NA KOSA ................................... 34

FAINI NA ADHABU KWA KILA KOSA ....................................................................... 36

FAINI ZA KUTOWAJIBIKA ......................................................................................... 37

KUUENDELEZA MSITU ............................................................................................. 37

UTANGULIZI: .............................................................................................................. 38

iv

UVUNAJI WA MITI ...................................................................................................... 38

HATUA ZA HARAKA ................................................................................................... 39

UFUATILIAJI ............................................................................................................... 40

Vigezo vya Mafanikio: ................................................................................................. 40

Wafuatiliaji ................................................................................................................... 41

Taarifa ya Ufuatiliaji Itatolewa kwa: ............................................................................ 41

Muda wa Kufanya Ufuatiliaji ........................................................................................ 41

Wataalam wa Misitu & ngazi za Eneo, (W)/ (M): ........................................................ 42

RATIBA YA UTEKELEZAJI ........................................................................................ 42

Hatua za Awali za Utekelezaji: ................................................................................... 42

Hatua Zitakazofuata .................................................................................................... 43

MUDA WA MPANGO, MAREKEBISHO NA MAPITIO YAKE: .................................. 43

1

MPANGO WA USIMAMIZI SHIRIKISHI WA MSITU WA HIFADHI YA KIJIJI CHA

KASANGANTONGWE

SEHEMU YA KWANZA - UTANGULIZI

MAELEZO YA JUMLA YA MPANGO

Mpango huu wa usimamizi umeandaliwa na Timu ya Tathimini Shirikishi ya Rasilimali

za Msitu kwa kushiriana na wataalamu wa misitu wa halmashauri ya wilaya ya

Mpanda.

Maandalizi ya mpango huu wa usimamizi wa msitu wa kijiji cha Kasangantongwe

umefanyika kwa niaba ya wananchi wa Kijiji cha Kasangantongwe ambao ndio

wamiliki wa msitu huu.

Mpango huu umepitishwa na Halmashauri ya kijiji na Mkutano Mkuu wa kijiji cha

Kasangantongwe na kuidhinishwa na Halmashauri ya Wilaya Mpanda.

Uamuzi wa kutenga na kuuhifadhi msitu huu wa kijiji cha Kasangantongwe kuwa

msitu wa Hifadhi wa kijiji umetokana na wanakijiji wenyewe kuona umuhimu wa

uhifadhi. Pia kuweka taratibu za kisheria ili kuwezesha kijiji kupata manufaa

yatokanayo na mazao na huduma za msitu na kuepusha vizazi vijavyo kukosa kabisa

rasilimali za msitu huu.

Malengo makuu ya mpango huu wa usimamizi wa msitu wa kijiji cha

Kasangantongwe ni kuhifadhi, Kuuendeleza na Kutumia kwa namna endelevu kwa

manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho cha Tanzania na dunia kwa ujumla.

2

MAELEZO

Msitu wa Hifadhi ya Kijiji cha Kasangantongwe

Msitu wa Hifadhi ya kijiji cha Kasangantongwe unahifadhiwa na kumilikiwa na

halmashauri ya Kijiji cha Kasangantongwe. Madhumuni ya msingi ya kuhifadhi msitu

huu ni kutunza na kuhifadhi uoto wa asili uliopo kwa wingi kwenye msitu huu, kutoa

mazao ya msitu na huduma ya/za misitu kwa kuzingatia misingi ya matumizi endelevu

na kuhifadhi bioanuai muhimu zinazopatikana ndani yake kwa manufaa ya vizazi vya

sasa na vijavyo vya Tanzania na ulimwengu kwa jumla.

Msitu huu wa hifadhi ya kijiji ni matokeo ya zoezi la Mpango wa Matumizi Bora ya

Ardhi ya kijiji lililofanyika mwaka 2015 na kuridhiwa na wananchi wote wa

Kasangantongwe.

Msitu huu umeenea eneo la Milima Kankosya, mto Lwega hadi mlima Mbamba

kufuata mito Itoto, Kamkindo, Kamnyovu, Mkangasi kuvuka mto Kakese pembezoni

mwa ghuba za Bundola, Kakese, Mbamba Mkangasi hadi Ziwa Tanganyika.kwa

upande wa mashariki, unapakana na barabara ya zamani ya watafiti wa madini wa

kampuni ya Anglo. Ukubwa wa msitu huu una eneo la hekta 5859.

Msitu huu una uoto wa miti ambao kwa kadiri sehemu kubwa una umri mkubwa na

sehemu nyingi vilevile ambazo zina uoto mchanga. Kwa juu msitu umefunga kwa

viwango tofauti tofauti toka sehemu moja hadi nyingine. Kuna sehemu ambazo msitu

umefunga sana kwa juu hasa kando kando ya mito Mkangasi, Kamkindo na Itoto,

sehemu zilizofunga wastani, na sehemu zilizo wazi hasa kutokana na uvamizi wa

msitu kwa ajili ya kilimo, sehemu zenye uoto wa mianzi na miti mtawanyiko na zile

sehemu za mabonde ambayo ni vyanzo vya maji na mbuga. Ndani ya msitu huu kuna

njia za miguu zinazounganisha kijiji cha Kasangantongwe na baadhi ya vitongoji vyake

3

na pia vijiji jirani vya Lufubu.Pia kuna njia nyingi zisizo halali za miguu ambazo

hutumiwa na wavamizi wa msitu kwa ajili ya kilimo, wapasua mbao na wategaji wa

wanyamapori. Mipaka ya msitu huu imewekwa alama za kudumu za maboya ya zege

(bikoni) na kwa upande wa Kaskazini msitu huu unapakana na Mto Lwega.

MSITU WA HIFADHI WA KIJIJI CHA KASANGANTONGWE;

Msitu huu upo kaskazini mwa Kijiji cha Kasangantongwe. Msitu huu una ukubwa wa

hekta 5859 wenye bioanuai nyingi muhimu kwa kijiji na taifa kwa ujumla. Msitu huu

umeathiriwa kwa kiasi na shughuli za kibinadamu kama vile uchungiaji wa mifugo,

uchomaji moto, uvunaji holela, Kilimo na makazi holela msituni.

Hali ya msitu huu sio nzuri sana kutokana na uharibifu mkubwa unaofanyika kutokana

na upasuaji mbao haramu wa miti ya Myovu. Wapasuaji mbao walio wengi wanatoka

nje ya kijiji cha Kasangantongwe. Pia uvamizi wa msitu kwa ajili ya kilimo, hasa kando

kando ya Mto Lwega, hufanyika. Wavamizi wengi wa msitu kwa ajili ya kilimo ni

wasukuma wanatoka nje ya kijiji na wachache toka vijiji jirani hasa kando kando na

ndani ya Mto Lwega wanatoka nje ya kijiji upande wa mkoa wa Kigoma.

(Wilaya ya Uvinza).

Moto ni tishio la msitu wote wa hifadhi ya kijiji cha Kasangantongwe. Vyanzo vya moto

ndani msitu wa hifadhi ya kijiji cha Kasangantongwe ni wawindaji wa wanyamapori,

wawindaji wa asali, wavuvi, wasafiri na wavuta sigara. Madhara ya moto ndani ya

msitu wa hifadhi ya kijiji cha Kasangantongwe ni kuwa umebadilisha ukuaji wa uoto

wa msitu huu.

4

Msitu huu pia una vivutio vingine vya utalii kama vile safu za Milima ya Kankosya,

Mbamba kandokando ya ziwa Tanganyika, maeneo mengi yanayopendelewa na

Sokwe kwa ajili ya malazi na chakula na maporomoko ya maji ya Mto Lwega

unapoingia ziwa Tanganyika,

Mmiliki mkuu wa msitu huu ni Halmashauri ya Kijiji Cha Kasangantongwe, ambacho

kutokana na utaratibu wa muundo wa serikali za mitaa, usimamizi wa msitu huu

utafanywa kupitia ‘kamati ya Maliasili ya Kijiji kwa niaba ya wana kijiji wote wa kijiji cha

Kasangantongwe kwa kuwa hii ndiyo kamati katika muundo wa utawala wa vijiji

ambayo inahusika na usimamizi wa masuala ya mazingira ya kijiji kwa ujumla.

MATUMIZI YA MSITU WA HIFADHI YA KIJIJI CHA KASANGANTONGWE

Kabla, msitu huu hapo awali haukuwa na utaratibu wowote wa jinsi ya kutumia au

kuvuna rasilimali zake, bali kila mtu aliingia kwa wakati wake na kuvuna chochote

alichohitaji kwa manufaa yake na kutoka bila ya kuhojiwa na mtu. Hali kadhalika,

ndani ya msitu huu kuna wafugaji wa jamii ya Kisukuma toka Shinyanga na Bariadi

ambao huchangia miti midogo kupotea kabisa.

Ukataji wa miti usiofuata mpango wa Uvunaji kulingana na uwezo wa msitu hupelekea

kutoweka kwa miti muhimmu kama Mninga, Mkora na Msawala katika msitu huu. Hali

kadhalika uchomaji moto unaofanywa na wafugaji ili kupata nyasi mpya na wawindaji

ili kurahisisha kazi yao ya kuwinda Pia imani potofu kwa baadhi ya wanakijiji kuwa

ukianzisha moto na ukawaka muda mrefu maana yake ni utaishi miaka mingi. Vitendo

hivi huua kabisa makuzi ya machipukizi na hivyo msitu hubaki na kizazi cha miti

mikubwa tu ambayo ndiyo ilikuwa ikivunwa.

5

Kwa upande wa matumizi ya rasilimali za msitu huu; zipo rasilimali zipatikanazo katika

msitu huu ambazo zina manufaa kwa uchumi wa kila mwananchi na kijiji kwa ujumla,

hizi ni pamoja na; -

• Msitu huu ni makazi ya wanyamapori ambao ni faida kwa kijiji na taifa kwa

ujumla.

• Ipo miti yenye manufaa kiuchumi kwa wananchi mfano miti ya mbao kama

Milembela, Mitundu, Mininga, Mibanga, Mikurungu, Kasanda, Mfulu, Mpilipili,

ambayo ina umuhimu kiuchumi na kwamba itakinufaisha kijiji endapo utaratibu

wa uvunaji utasimamiwa ipasavyo na kwa uaminifu, ndani ya msitu huu kuna

makorongo ambyayo ni mito ya msimu hasa wakati wa masika ila hunyauka

wakati wa kiangazi mfano Mkangasi Kamkindo na Mto Kakese, pia pembezoni

mwa msitu huu kuna mto Lwega unaotiririsha maji mwaka mzima.

Kuni ni moja wapo ya matumizi muhimu kiuchumi toka katika msitu huu.

• Aidha, watumiaji wakuu wa rasilimali za msitu huu wa kijiji cha

Kasangantongwe, ni wanakijiji wenyewe wa Kasangantongwe, pili ni wananchi

toka vijiji jirani kama Ikola, Isengule na Lufubu kwa upande wa Mkoa wa

Kigoma. Watumiaji wengine ni wale wakutoka nje ya kijiji na kata hii ya Isengule

na wafanyabiashara wa mazao ya misitu toka Mpanda mjini. Pamoja na taratibu

za kulipia zatakazo wekwa lakini yapo mahitaji mengine ambayo wanakijiji wa

Kasangantongwe pekee wataruhusiwa kuingia na kuvuna bila malipo bali kwa

utaratibu maalum.

6

KIJIJI CHA KASANGANTONGWE

Kijiji cha Kasangantongwe ni miongoni mwa vijiji vinne vilivyomo katika kata ya

Isengule Tarafa ya Karema wilayani Mpanda. Vijiji vingine vilivyomo kwenye kata hii

ya Isengule ni pamoja na Isengule, Maana ya Neno Kasangantongwe imetokana na

lugha ya kitongwe maana yake "amekutwa Mtongwe" Kijiji hiki kina jumla ya wakazi

1319 wanaoishi katika jumla ya kaya 412.

Kihistoria Kasangantongwe kilikua kijiji kamili na kusajiliwa mwaka 1999 baada ya

kukidhi vigezo vya usajili wa kijiji. Kijiji hiki kina vitongoji vinne (4) ambavyo ni

Isimwa, Kapondogoro, Keselamuyaga, na Kasangantongwe. Kijiji cha

Kasangantongwe kinapakana na vijiji vifuatavyo, upande wa kaskazini kinapakana na

kijiji cha Lufubu, kusini ni kijiji cha Isengule na shukula. Kwa upande wa magharibi

kinapakana na ziwa Tanganyika.

Kijiji hiki kina mchanganyiko wa makabila kadhaa. Makabila yanayotawala katika kijiji

hiki ni Watongwe, Wabende, Wafipa Wasukuma, na waha.

Shughuli za kiuchumi za wakazi wa kijiji cha Kasangantongwe zinategemea sana

Uvuvi na kilimo. Kwa upande wa kilimo wananchi wa kijiji hiki hulima sana zao la

Mihogo, Ufuta, Mahindi, Maharage na Mtama. Mazao haya huuzwa hapa kijijini na na

mengine kwa wingi huuzwa kwa wafanyabiashara toka Ikola na kwingineko.

Aidha, shughuli ya ufugaji hufanywa na kabila la wasukuma, wanyamwezi na wafipa

kwa kiasi kikubwa japo makabila mengine hufuga mifugo midogo midogo kama mbuzi,

kondoo bata na kuku.

7

SEHEMU YA TATU:

Madhumuni ya mpango wa usimamizi wa msitu wa kijiji cha Kasangantongwe

Msitu wa hifadhi ya kijiji cha Kasangantongwe ni msitu wa kijiji unaohifadhiwa kwa

lengo la kutunza vyanzo vya maji, udongo na upatikanaji wa mazao na huduma za

msitu kwa njia endelevu. Kutokana na uharibifu wa msitu unaoendelea kufanyika

madhumuni hayo ya msingi yameathirika sana. Hivyo dhumuni kuu la mpango huu ni

kuimarisha utumiaji, ulinzi na uendelezaji wa eneo hilo la msitu kwa kushirikisha

wananchi ili kurejesha hali nzuri ya msitu iliyokuwepo. Hii itafanikiwa kwa kufanya

yafuatayo:

• Kuweka taratibu / kanuni za kutumia, kulinda, na kuendeleza msitu na Ziwa

Tanganyika kwa njia endelevu.

• Kuboresha ushiriki wa wadau wote katika usimamizi msitu.

• Kuongeza ushirikiano kati ya wananchi, Halmashauri ya Kijiji, Halmashauri ya

Wilaya na wakala wa huduma za misitu Tanzania.

• Kuwaelimisha wanakijiji wa Kasangantongwe juu ya umuhimu wa msitu kwao,

Taifa na Ulimwengu na jukumu lao la kufuata taratibu za utunzaji na matumizi

zilizowekwa na kukubalika.

• Kuuweka msitu wetu katika udhibiti madhubuti unaokubalika na wanakijiji wote

ili kwamba kusiwe na uvunaji holela, uvamizi wa mifugo, na ujenzi wa makazi

holela au kupanua mashamba kuingia katika msitu huu. Kwa kufanya hivi,

tutasaidia msitu huu kuwa chini ya umiliki wa kijiji chote kwa manufaa yetu wote

bila kudhulumiana na kwamba rasilimali zilizopo zitumike katika misingi

endelevu kwa faida ya kizazi hiki na kijacho.

Msitu huu umegawanyika katika maeneo makuu Matatu ya usimamizi (3) yaitwayo

8

“maeneo madogo ya usimamizi” (EDU) kama ifuatavyo; -

1) ENEO DOGO LA USIMAMIZI LA Mpapa (2113 ha)

2) ENEO DOGO LA USIMAMIZI LA Kabhukindu (2611 ha)

3) ENEO DOGO LA USIMAMIZI LA Ziwa Tanganyika (1135ha)

RAMANI YA MSITU WA HIFADHI WA KIJIJI CHA KASANGANTONGWE

ENEO DOGO LA USIMAMIZI LA MPAPA.

Eneo hili dogo la usimamizi (EDU) la Mpapa lina ukubwa wa hekta 2113 ambalo liko

Mashariki mwa msitu wa kijiji cha Kasangantongwe. Lina anzia pembezoni mwa mto

Lwega Usawa wa bikoni namba 3 na 4 (VF3 na VF4) kuelekea kusini kuvuka mto Itoto

9

na Kamuyovu, lina ambaa na barabara ya Anglo kulekea kusini kuvuka mto Mkangasi

na kuishia kwenye bikoni namba 8 na 9 (VF8 na VF9). Kwa upande wa magharibi

inapakana na EDU ya Kabhukindu. Lengo kuu la uhifadhi wa EDU hii ni “MATUMIZI”.

Kutokana na hali halisi ya EDU hii na uwiano wa ukubwa wa miti, uvunaji unaweza

kufanyika baada ya miaka mitano toka sasa, ili kuipa nafasi ya ukuaji wa miti muhimu

ifikie kwenye kiwango cha kuweza kuvunwa. EDU hii ina jumla ya miti 1,019,522 kwa

ujumla wakati jumla ya miti 247 tu ni miti inayofaa kuvunwa kwa ajili ya mbao kwa

miaka mitano ijayo, ambayo ni sawa na miti 49 tu kwa mwaka. Miti hiyo ni; -

• Msawala

• Mpilipili

• Mlembela

• Mbanga

• Mninga

• Msindwi

• Kabamba

• Kasanda

• Mkurungu

Hivo basi kwa kuwa uvunaji hautokuwepo kwenye EDU hii kwa wakati huu, yapo

matumizi mengine yanayoruhusiwa nayo ni kama yafuatayo; -

• Urinaji wa asali

• Uchimbaji wa dawa za asili (miti shamba)

10

• Kusenya kuni kavu (si miti mibichi)

• Ukataji wa nyasi za kuezekea nyumba

• Uvunaji wa miti ya boriti (pau), fito na nguzo

ENEO DOGO LA USIMAMIZI LA KABHUKINDU.

Eneo hili dogo la usimamizi la Kabhukindu lina ukubwa wa hekta 2611. Kaskazini

linaanzia mto Lwega pembezoni mwa jiwe namba 3 (VF3) kuelekea kusini kuvuka

mlima Kankosya, mto kamkindo, mlima Mbamba na kuishia mbele kidogo ya mto

Kakese. Kwa upande wa mashariki linapakana na EDU ya Mpapakaskazini kuna mto

Lwega unaotenganisha kijiji cha Kasangantongwe na Lufubu, na upande wa

Magharibi inapakana na EDU ya Uhifadhi ya Ziwa Tanganyika. Lengo kuu la uhifadhi

wa EDU hii ni “MATUMIZI”

Kwakuwa uvunaji unaruhusiwa (matumizi) kwa ujumla EDU hii ina jumla ya miti

2,347,861 kwa ujumla wakati jumla ya miti ni miti inayofaa kuvunwa kwaajili ya mbao,

ambayo ni sawa na miti 544 kwa mwaka. Miti hiyo haina tofauti na ile ya EDU ya

Mpapa kwa kuwa ni msitu mmoja na wenye uoto wa aina moja ya Miombo nayo ni; -

• Msawala

• Mpilipili

• Mlembela

• Mbanga

• Mninga

11

• Msindwi

• Msolankanga

• Kasanda

• Mkurungu

Matumizi mengine yatakayoruhusiwa katika EDU hii ni pamoja na:

• Urinaji wa asali

• Uchimbaji wa dawa za asili (miti shamba)

• Kusenya kuni zilizojikaukia

• Ukataji wa nyasi za kuezekea nyumba

• Uvunaji wa miti ya boriti (pau) na fito na nguzo

• Shughuli za Utalii

ENEO DOGO LA USIMAMIZI LA ZIWA TANGANYIKA

Eneo hili linapakana na ziwa Tanganyika kwa upande wa magharibi. linaazia kusini

kwenye ghuba ya Kakese kwenye jiwe namba VF1, kuelekea kaskazini kuvuka mto

mkangasi na matawi yake, milimba ya Mbamba na kuishia ukingoni mwa mto Lwega.

Ukubwa wa eneo hili ni hekta 1135. Kwa upande wa mashariki eneo hili linapakana

na eneo la Kabhukindu.

12

SEHEMU YA PILI

MPANGOWA UTEKELEZAJI

Meneja Mteule

Katika mpango huu wa usimamizi wa msitu wa hifadhi wa Kijiji cha Kasangantongwe,

meneja atakuwa ni KAMATI YA MALIASILI YA KIJIJI ambayo hufupishwa kama

VNRC (kwa kiingereza ni Village Natural Resources Committee). Kamati hii ni ile

inayoelekezwa katika muundo wa uongozi wa vijiji. Kamati hii itakuwa na wajumbe 14

kwa mchanganuo ufuatao;

• Wawakilisha toka kila kitongoji cha kijiji

• Skauti wa kijiji wasiopungua wawili kama hawapo basi hata askari mgambo

wanaweza kutumika badala ya Skauti wa kijiji

• Mtu/watu maarufu katika kijiji wanaoweza kuchangia katika suala zima la

uhifadhi. mfano wazee maarufu na wakongwe wa kijiji n.k.

• Wanawake (Theluthi moja au 30% ya wajumbe wote) maalumu kwa nafasi ya

upendeleo kwa wanawake.

Kamati hii itapatikana kwa kufuata utaratibu ufuatao; -

• Wajumbe hawa watachaguliwa na mkutano mkuu wa kijiji

• Baada ya majina hayo kupatikana Halmashauri kuu ya Kijiji huketi na

kuyathibitisha majina hayo.

• Kamati hii itakuwa madarakani kwa muda wa miaka mitatu (3) baada ya hapo

uchaguzi unafanyika tena. mjumbe anaweza kuchaguliwa tena kulingana na

imani ya wananchi kwake.

13

• Mwenyekiti, katibu na mweka hazina watachaguliwa miongoni mwa wajumbe

waliochaguliwa na mkutano mkuu na kuthibitishwa na Halmashauri ya kijiji.

• Kamati hii itapewa nguvu ya kisheria ya kusimamia sheria ya kijiji na itawajibika

kwa Halmashauri kuu ya Kijiji.

• Itaandika taarifa ya utekelezaji kwa Halmashauri ya kijiji mara moja kila mwezi,

yenye nakala kwa Afisa Misitu (W)

• Itafanya vikao vyake mara moja kila mwezi na vya dharura pale inapobidi.

• Itapokea, kujadili na kufuatilia taarifa za walinzi wa msitu (Kamati ya doria) na

vikundi vingine vitakazoundwa kuisaidia Kamati ya Mazingira katika kutekeleza

majukumu yake.

Uwezo na Majukumu ya Kamati ya Mazingira

• Kuhakikisha kuwa mipaka yote ya msitu wa hifadhi ya kijiji cha Kasangantongwe

inaeleweka waziwazi kwa wanakijiji wote wa Kasangantongwe.

• Kusimamia utekelezaji wa mipango yote inayohusu utumiaji, ulinzi na uendelezaji

wa kijiji cha Kasangantongwe.

• Kutunza kumbukumbu zote zinazohusu shughuli za utumiaji, ulinzi, na uendelezaji

wa msitu wa hifadhi ya kijiji. Kumbukumbu hizo ni: -

▪ Mihtasari ya mikutano

▪ Doria

▪ Uhalifu na faini

▪ Vibali vilivyotolewa

▪ Mapato na matumizi ya fedha za msitu

14

▪ Uoteshaji na upandaji miti, pia shughuli zote za uhifadhi mazingira

ndani ya maeneo ya kijiji

• Kuhakikisha kuwa walinzi wa msitu (timu ya doria) wanatekeleza kazi yao

kikamilifu na kuchukua hatua zinazopasa kuondoa dosari zinazojitokeza katika

kazi ya ulinzi.

• Kufanya ukaguzi wa msitu wa hifadhi ya kijiji angalau mara mbili kwa mwezi.

• Kuhakikisha matumizi endelevu ya msitu yanazingatiwa kulingana na kanuni za

matumizi zilizowekwa na kukubaliwa.

• Kuwashughulikia wahalifu wa msitu kwa mujibu wa kanuni za adhabu zilizowekwa

na kukubalika kwa ushirikiano na Halmasahauri ya kijiji.

• Kwa ushirikiano na Halmashauri ya kijiji, kuwahamasisha wanakiiji kushiriki katika

suala zima la uhifadhi wa msitu na mazingira ya kijiji kwa ujumla.

• Kutumia na kutunza vitabu vya stakabadhi vilivyoidhinishwa na Halmashauri ya

Wilaya ya Mpanda.

• Kufungua Akaunti Benki ya Kamati ya Mazingira ya kijiji kwa ajili ya kuweka fedha

za mapato ya msitu (ushuru na faini).

• Kuhakikisha kuwa fedha za Akaunti ya Kamati ya Mazingira zinatumika kama

zilivyokusudiwa na kuidhinishwa na Halmashauri ya kijiji cha Kasangantongwe.

• Kuweka utaratibu wa utoaji wa vibali ili kuhakikisha kuwa vibali vinavyotolewa ni

vile vilivyoko katika mamlaka ya Kamati ya Mazingira na kwamba utoaji wa vibali

unakwenda sambamba na mahitaji yaliyopo na sio vinginevyo.

15

Majukumu ya Mwenyekiti wa kamati ya Maliasili ya Kijiji

• Kuhakikisha kuwa mikutano ya Kamati ya Mazingira inafanyika ipasavyo kwa

kufuata ratiba iliyopangwa. (angalau mara moja kila mwezi)

• Kuhakikisha kuwa Mhasibu na Katibu wa Kamati ya Mazingira wanafanya kazi

zao ipasavyo kwa kuweka kumbukumbu zote za vibali, doria, faini, idadi ya

wahalifu, fedha zilizopo, matumizi n.k.

• Kuhakikisha kuwa Kamati ya doria ya msitu wa hifadhi ya kijiji wanafanya kazi

yao ipasavyo na wanapewa haki zao kama zilizoainishwa kwenye Mpango huu.

• Atakuwa mmoja wa watia sahihi wa Akaunti ya Kamati ya Mazingira wakati wa

kutoa fedha Benki kwa matumizi yaliyoidhinishwa na Halmashauri ya kijiji kwa

ajili ya uendelezaji wa msituna shughuli zingine za maendeleo kijijini.

• Atawajibika kuhudhuria vikao vyote vya Halmashauri kuu ya kijiji na kutoa

taarifa ya utendaji kazi wa kamati.

Majukumu ya Katibu wa kamati ya mazingira:

• Atawajibika Kuweka na kutunza kumbukumbu zifuatazo: - Kumbukumbu za

mikutano yote (Kitabu cha kumbukumbu za mikutano)

o Doria zilizofanyika, uhalifu/uharibifu ulioonekana kwenye kitabu cha

Doria.

o Uhalifu ulioonekana, wahalifu waliohusika, faini zilizotozwa, tarehe ya

uhalifu na faini zilizolipwa kwenye kitabu cha “Uhalifu na faini”

o Vibali ilivyotolewa, kwa nani, kwa ajili gani, fedha zilizolipwa, tarehe,

namba ya risiti, n.k kwenye kitabu cha Vibali

16

o Fedha zilizotolewa, tarehe, kwa ajili gani, namba ya risiti kwenye kitabu

cha Risiti na fedha.

• Atahakikisha kuwa Akaunti ya Mazingira inafunguliwa na mara kwa mara baada

ya kupokea fedha na kuziingiza kwenye vitabu vinavyohusika zinapelekwa

Benki na Mweka Hazina.

• Atakuwa mmoja wa watia sahihi wa Akaunti ya Kamati ya Mazingira wakati wa

kutoa fedha Benki kwa matumizi yaliyoidhinishwa na Halmashauri ya kijiji kwa

ajili ya uendelezaji wa msitu na shughuli zingine za maendeleo kijijini.

• Atawajibika kusimamia utekelezaji wa maagizo ya Serikali ya Kijiji na

Halmashauri kuu ya kijiji

• Atawajibika kuandaa taarifa ya utendaji kazi wa kamati na maendeleo ya msitu

kila mwezi, robo mwaka, nusu mwaka na mwaka na kuwasilisha katika mkutano

mkuu wa kijiji wa robo mwaka baada ya kupitiwa na Halmashauri kuu ya kijiji.

• Ataidhinisha doria kufanyika kwa maandishi maalumu ambayo mwenyekiti wa

kijiji pia atapaswa kujulishwa kwa wakati utakaoonekana unafaa kulingana na

mazingira.

• Atapokea taarifa ya doria mara baada ya kumalizika na kukagua daftari la doria.

• Atatunza kumbukumbu za kesi zote za wavunaji haramu wa mazao ya msitu

wa hifadhi ya kijiji cha Kasangantongwe.

• Atawajibika kutunza orodha ya wavunaji wote wa rasilimali za msitu wa hifadhi

ya kijiji cha Kasangantongwe pamoja na kiasi walichovuna na kuwasilisha kwa

DFO/DED kila mwezi.

• Atawajibika kusimamia mapato na matumizi kwa umakini na kutoa taarifa kwa

Halmashauri ya kijiji kila inapoonekana inafaa

17

Majukumu ya Mtunza hazina:

• Atawajibika kutunza kumbukumbu zote za mapato yatokanayo na leseni za

uvunaji wa mazao ya misitu na vibali mbalimbali.

• Atawajibika kutunza kumbukumbu za matumizi yote ya fedha zitokanazo na

maduhuli ya mazao ya msitu wa hifadhi ya kijiji cha Kasangantongwe kama

ilivyoidhinishwa na vikao husika vya kijiji cha Kasangantongwe na siyo

vinginevyo.

• Ataandaa taarifa ya Mapato na Matumizi ya fedha ya Kamati ya Mazingira na

kuiwasilisha kwenye vikao vya Kamati ya Mazingira.

• Atakuwa mmoja wa watia sahihi wa Akaunti ya Kamati ya Mazingira wakati wa

kutoa fedha Benki kwa matumizi yaliyoidhinishwa na Halmashauri ya kijiji kwa

ajili ya uendelezaji wa msitu na shughuli zingine za maendeleo kijijini.

Msimamizi wa Doria:

• Atatakiwa kusimamia doria zote na kuziongoza

• Atatunza daftari la kila mtu atakayekamatwa katika msitu wa kijiji akivuna

mazao ya misitu bila idhini (kibali) cha kijiji.

• Atawajibika kumuweka chini ya ulinzi mtu yeyote pamoja na maliasili

aliyokamatwa nayo (kama ipo) na kumkabidhisha kwa mtendaji wa Kijiji kwa

hatua zaidi za kisheria.

• Atawajibika kuhakikisha ulinzi wa mipaka ya msitu unadumu na kuwa imara ili

msitu usivamiwe kwa kilimo, makazi au kuchungia.

18

Majukumu ya Wahusika Wengine

Halmashauri ya Kijiji:

Itakuwa mhusika mkuu katika utekelezaji wa mpango huu kwa upande wa kijiji na

itakuwa na wajibu na majukumu yafuatayo: -

• Kusimamia utekelezaji wa mpango

• Kutunga na kusimamia Sheria ndogo

• Kuhakikisha kuwa Kamati ya Mazingira inafanya kazi yake ipasavyo.

• Kushirikiana na wataalamu wa Misitu wa ngazi zote katika kuandaa mikakati

mipya ya uhifadhi misitu na mazingira kwa jumla.

• Kufanya ufuatiliaji na tathimini ya utekelezaji wa mpango huu, kwa kuwa na

agenda ya kudumu katika vikao vyake vya kila mwezi pia kutembelea msitu wa

hifadhi angalau mara moja kila mwezi.

Wanakijiji

Watashiriki katika shughuli za utumiaji, ulinzi na uendelezaji wa msitu wa hifadhi kama

ifuatavyo: -

• Kuzuia na kuzima moto katika maeneo yao ya makazi, mashamba na misitu

inayowazunguka.

• Kusafisha mipaka ya nje ya msitu wa hifadhi ya kijiji na kuhakikisha kuwa iko

wazi wakati wote wa mwaka.

• Kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu.

• Kuotesha na kupanda miti kwa lengo la kupunguza utegemezi wa misitu ya asili

kwa kila zao au huduma ya msitu.

19

• Kushiriki katika mikutano na kuchangia katika kuandaa mikakati mipya ya

kutumia, kulinda na kuendeleza msitu wa hifadhi ya kijiji cha Kasangantongwe.

• Kubuni na kutekeleza shughuli mbadala za kuongeza kipato ili kupunguza

umaskini kwa kutumia rasilimali zilizo ndani ya msitu wa hifadhi ya kijiji, zilizo

katika maeneo ya makazi. Baadhi ya mbinu hizo ni ufugaji wa nyuki kwa njia za

kisasa, usukaji wa mikeka kwa kutumia ukindu kwa ajili ya soko, Kuzingatia

matumizi ya majiko banifu, nishati mbadala na matumizi sahihi ya mazao ya

misitu.

Wataalamu wa Misitu katika ngazi mbalimbali

• Kutoa msaada wa kitaalam katika kubuni mikakati mipya ya kuhifadhi msitu wa

hifadhi ya kijiji cha Kasangantongwe

• Kusaidia shughuli za uoteshaji na upandaji miti.

• Kusimamia Sera ya Misitu na Sheria ya Misitu 14, 2002.

• Kufanya ufuatiliaji na tathimini ya utekelezaji wa mpango huu wa usimamizi.

• Kusaidia utekelezaji wa mpango.

Viongozi wa Kata, Tarafa, Wilaya na Mkoa,

• Kutoa msukumo katika utekelezaji wa mpango

• Kuhakikisha kuwa Polisi na Mahakama zinatekeleza wajibu wao ipasavyo

katika utekelezaji wa Sheria ya Misitu No. 14, 2002 na Sheria zinazosimamia

rasilimali za majini.

• Kushirikiana na Idara ya Misitu na Nyuki.

20

• Kutoa msukumo katika utekelezaji wa Sera, Sheria na Kanuni za kutunza na

kulinda misitu.

• Kusaidia utatuzi wa migogoro inapotokea.

UTENDAJI KAZI WA KAMATI YA MALIASILI YA KIJIJI.

• Itafanya kazi zile zile zilizoainishwa katika majukumu ya kamati ya maliasili ya

kijiji

• Itakutana mara moja kila mwezi

• Itatunza mihutasari ya mikutano yake

• Mkutano utafanyika iwapo tu idadi ya wajumbe imefika nusu ya wajumbe wote.

• Katika kila mkutano watapaswa kupokea taarifa ya doria na mwenendo wa

uvunaji wa mazao ya msitu wa hifadhi ya kijiji cha Kasangantongwe kutoka kwa

kiongozi wa doria.

• Watatakiwa kujua idadi ya leseni zilizotolewa katika mwezi husika, kiasi cha

maliasili kilichovunwa na mapato yaliyopatikana

• Watapokea na kujadili maombi ya leseni za kuvuna mbao kwa kuwasilisha kwa

Serikali ya Kijiji.

• MAELEZO MENGINEYO

UTOAJI TAARIFA

• Kamati ya Mazingira ya kijiji itatoa taarifa ya utekelezaji kwa Halmashauri ya

kijiji mara moja kwa mwezi yenye nakala kwa Afisa Misitu wa Wilaya Mpanda.

21

• Afisa Mtendaji wa Kijiji (VEO) atatoa taarifa ya maendeleo ya shughuli za msitu

wa hifadhi ya kijiji na kwa Mkutano Mkuu mara nne (4) kwa mwaka yenye

nakala kwa Afisa Mtendaji Kata (WEO) na Afisa Misitu (W).

UWEKAJI WA KUMBUKUMBU

Kumbukumbu zifuatazo zitawekwa na kuhifadhiwa na Kamati ya Mazingira ya Kijiji:

• Mihutasari ya vikao vya kamati

• Uhalifu na faini zilizotozwa

• Doria zilizofanyika

• Stakabadhi ya fedha na Hati ya malipo.

• Vibali vilivyotolewa

• Akaunti ya Kamati ya Mazingira

• Mapato na matumizi ya fedha za msitu.

MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA ZA KAMATI YA MAZINGIRA

Mapato ya Kamati ya Mazingira yatatokana na:

• Faini zitakazotozwa wahalifu wa msitu wa hifadhi ya kijiji.

• Malipo ya mazao na huduma ya msitu yaliyoruhusiwa kwa kulipia katika

Mpango huu.

• Mauzo ya mazao ya msitu yaliyokamatwa na zana zilizokamatwa katika ulinzi.

• Wafadhili na wasamaria wema watakaotoa fedha/ msaada kwa ajili ya

22

Usimamizi wa msitu wa hifadhi ya kijiji.

Mapato yatokanayo na mazao na huduma za msitu wa kijiji cha Kasangantongwe

yatakua ni mali ya kijiji cha Kasangantongwe kwa asilimia 100% na hayatagawanywa

yatagawanywa kati ya Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda.

MATARAJIO YA UFANISI WA UTEKELEZAJI WA MPANGO WA USIMAMIZI WA

MSITU

Katika matembezi ya kukatiza msitu vikwazo Matatizo yafuatavyo vilibainika msituni:

• Moto kichaa

• Uvunaji haramu wa mbao

• Uchungiaji wa mifugo

• Kilimo msituni

• Ukaaji wa miti

Mpango wa usimamizi ukitekelezwa vilivyo kwa msitu huu hifadhi wa kijiji cha

Kasangantongwe kwa kuzingatia vikwazo vilivyobainika katika matembezi ya kukatiza

msitu kama yalivyofupishwa hapo juu yafuatayo yanatarajiwa kuonekana;

• Kupungua au kutoweka kabisa kwa matukio ya moto

• Kuwepo kwa watuhumiwa wa kesi za uchomaji moto hovyo msituni kwa

utaratibu wa kukubalika/kwa kufuata taratibu za nchi

23

UTUNZAJI KUMBUKUMBU

Mpango huu wa usimamizi unaainisha bayana ni kumbukumbu zipi zitatunzwa,

zitatunzwa katika vitabu gani na vitabu hivyo vitatunzwa na nani kwa utaratibu gani.

Ufuatao ni ufafanuzi; -

VITABU VYA KUMBUKUMBU

Hiki ni kitabu kitakachohusika na kutunza kumbukumbu zifuatazo,

• Kumbukumbu za mihutasari ya vikao vya kamati

• Kumbukumbu za maamuzi mbalimbali ya kamati

• Tukio lolote linalofanywa na kamati au watu wachache waliotumwa na kamati

• Matokeo ya shughuli yoyote iliyofanywa na kamati au watu wachache

walioteuliwa na kamati

• Kumbukumbu za ukaguzi wowote uliofanywa na kamati au baadhi ya

wanakamati waliotumwa na kamati

KITABU CHA MAKOSA NA FAINI

Kumbukumbu za makosa yoyote yaliyofanywa na mhalifu dhidi ya sheria ndogo za

Kijiji cha Kasangantongwe ya Kuhifadhi Msitu wa Kijiji cha Kasangantongwe.

• Jina la mkosaji na kosa alilokosa Kiasi alichotozwa, tarehe aliyotozwa na

namba ya stakabadhi aliyopewa kwa faini aliyotozwa

• Ionyeshwe ni katika akaunti gani pesa hiyo imeingizwa

24

• kama idhini ya kutumika nimetolewa na mamlaka husika, onyesha hapa

imetumika kufanyia nini?

KITABU CHA STAKABADHI

Hivi ni vitabu ambavyo Mtunza hazina wa Halmashauri ya Wilaya atatoa kwa kijiji,

lakini ionyeshwe nani kapewa vitabu vingapi kuvitumia ndani ya kamati.

VITABU VYA VIBALI

Kazi ya kitabu hiki ni kutunza kumbukumbu za vibali vyote vilivyoidhinishwa na kamati

ya Maliasili ya Kijiji. Kitabu hiki kionyeshe mambo yafuatayo; -

• Kuainisha lengo la kibali, jina la aliyepewa kibali hicho,

• kiasi cha malipo aliyolipa,

• Namba ya stakabadhi iliyotolewa kwa mteja na

• tarehe ya kutolewa kibali na ya kuisha kutumika kibali hicho.

• Pia kitabu kionyeshe jina la mjumbe atakayekagua kibali hicho na la mjumbe

atakayesimamia matumizi ya kibali hicho.

Kimsingi, leseni na vibali vitasainiwa na katibu/ Mhasibu wa Kamati ya Maliasili ya Kijiji

kugongwa muhuri wa Kamati ya Maliasili ya Kijiji.

KITABU CHA DORIA

Hiki ni kitabu kitakachokuwa kinatunzwa na msimamizi wa doria. kinapaswa

kuandikwa mambo yafuatayo;

25

• Tarehe,

• Majiina ya wanaofanya doria siku hiyo,

• eneo ambalo watu hao watafanya doria,

• ni uharibifu gani umefanyika katika eneo hilo la msitu ambalo watu hao

wamepangiwa kufanya doria.

• Pia katika taarifa ya hao waliopangiwa kufanya doria katika eneo husika

wakiona kitu mfano, wanyamapori. wanapaswa kutoa taarifa kwa kamati ya

maliasili ya Kijiji.

KITABU CHA AKAUNTI

Baada ya muda kijiji kitakuwa na fedha nyingi kutokana na mapato ya msitu, hivyo

kutakuwa na kitabu cha benki kwa ajili ya kumbukumbu za kibenki. Katika kitabu hiki

kutakuwa na majina ya watia saini. watia saini watakuwa kama ifuatavyo;

• mtia saini kundi ‘A’ – toka Serikali ya Kijiji,

• Mtia saini kundi ‘A’ – toka Kamati ya Maliasili ya Kijiji,

• Mtia saini kundi ‘B’ – toka Serikali ya Kijiji

• Mtia saini kundi ‘B’ – toka Kamati ya Maliasili ya Kijiji.

N: B: Izingatiwe kuwa hakuna fedha itakayo chukuliwa benki bila ya kuwa na saini za

watia saini wawili toka makundi mawili tofauti pamoja na muhtasari wa kikao cha

mkutano mkuu wa kijiji ulioidhinisha matumizi ya fedha hizo.

26

KITABU CHA MAPATO NA MATUMIZI

Hiki ni kitabu kitakachukuwa kinatunza kumbukumbu za fedha zote zinazoingia kutoka

katika faini na ada za vibali au leseni mbalimbali. Pia kitakuwa na kumbukumbu za

matumizi yote ya fedha zinazotumika ikionyesha saini ya aliyechukuwa na

viambatanisho vya uthibitisho kuwa malipo hayo yameidhinishwa na mamlaka husika.

Mfano wa malipo ni pamoja na zawadi ya pongezi kwa wafanya doria kwa kazi nzuri

itakayokuwa imethibitishwa na kuidhinishwa kuwa wapewe kiasi kadhaa kwa

maandishi. Hapa ni lazima mpokeaji athibitishe kuwa amepokea pesa hiyo.

USIMAMIZI WA FEDHA

Katika kifungu hiki sisi wanakijiji cha Kasangantongwe tunaainisha mfumo

utakaotumika kusimamia fedha hususani katika matumizi yake.

WAHUSIKA WAKUU;

Mtu atakaye husika kushika vitabu vya risiti na kupokea fedha toka kwa mlipaji

atakuwa ni mtunza fedha. Fedha hizo zitahifadhiwa benki kwenye akaunti ambayo

itafunguliwa kwaajili ya fedha zitokanazo na msitu wa hifadhi ya kijiji cha

Kasangantongwe.

AFISA MUWAJIBIKAJI WA MASUALA YA FEDHA

Afisa muwajibikaji wa fedha za Msitu wa Kijiji atakuwa AFISA MTENDAJI WA KIJIJI

kwa kuwa huyu ndiye anayewajibika kwa masuala yote yahusuyo fedha hapa kijijini.

Anaweza kumhoji mtunza fedha na kukagua vitabu vya fedha wakati wowote

atakapoona inafaa. Hata hivyo mtunza hazina anapaswa kutoa taarifa ya mwenendo

wa makusanyo ya fedha kila wiki.

27

Hata hivyo, kwa kuzingatia misingi ya uhuru wa habari na taratibu za utawala bora

mwananchi yeyote anaweza kuomba kukagua kitabu cha makusanyo. pamoja na

taratibu hizi za pekee, Mamlaka inayowajibika ya juu kabisa katika kijiji ni Mkutano

mkuu, hivyo , taarifa ya mapato na matumizi yatasomwa kila baada ya miezi mitatu

katika mikutano mkutano mkuu wa kijiji kama ilivyo desturi ya mikutano hiyo hapa

kijijini.

Kwa upande wa ukiukwaji wa taratibu au tuhuma dhidi ya mtunza hazina taratibu

zifuatazo zitatumika;

Endapo mtunza hazina /fedha atahisiwa kuwa katumia fedha tofauti na utaratibu au

ridhaa ya wananchi hatua zifuatazo zitumike; -

• Mwenyekiti wa Kamati ya Maliasili ya Kijiji ataitisha kikao cha kamati yake na

kumhoji juu ya tuhuma husika

• Ikiwa ameshindwa kutoa maelezo ya kujitosheleza na kushindwa kuondoa

mashaka hayo, Taarifa hiyo itapelekwa kwa mwenyekiti wa kijiji ambaye

anapaswa kuitisha kikao cha Serikali ya Kijiji kumhoji juu ya tuhuma husika,

kama maelezo yake hayajajitosheleza kiasi cha kuuongezea uongozi wa kijiji

mashaka, Atapewa barua ya kujieleza ikiwa ni nafasi ya kujieleza kufuatia

tuhuma au mashaka dhidi ya matumizi mbaya ya fedha ya kijiji.

• Endapo maelezo yake katika barua hayataondoa utata, mwenyekiti ataitisha

Halmashauri ya kijiji iliyomchagua na kuwasilisha hoja ya kumsimamisha kazi

ili hatua za kisheria zichukue mkondo wake. Hoja ikipitishwa VEO ataandika

barua ya kumsimamisha kazi hadi hapo mahakama/baraza la kata itakapo

amua kuwa ana hatia ama la,

28

• Baada ya kusimamishwa kazi VEO atamfikisha mtuhumiwa

polisi/mahakamani/baraza la kata. moja ya vyombo hivyo ndicho kitakachotoa

tamko la mwisho.

• Akipatikana na hatia atafukuzwa kazi hiyo na kutekeleza adhabu zilizoamriwa,

na mara moja Mwenyekiti wa kijiji kufanya taratibu za kuziba pengo la mtunza

hazina aliyepita.

MATUMIZI YANAYOIDHINISHWA;

Kwanza ifahamike kuwa matumizi makuu ya fedha itokanayo na uhifadhi wa msitu

wetu yatagawanyika katika makundi makuu matatu kama ifuatavyo; -

• 50% itatumika katika shughuli za maendeleo ya kijiji kwaajili ya wananchi wote

• 30% pesa hii itatumika kwaajili ya kuboresha kamati ya maliasili ya Kijiji.

• 20% itatumika kwaajili ya kufanya shughuli za uhifadhi wa msitu wa kijiji cha

Kasangantongwe kuwa endelevu kama vile:

▪ Ununuzi wa vitabu vya kumbukumbu kama vilivyoainishwa katika

“Kugharamia marekebisho ya mipaka".

▪ Kugharamia tathimini ya Rasilimali na kuboresha Mpango huu wa

Usimamizi

▪ Kugharamia uendeshaji wa kesi.

▪ Kutoa motisha kwa kikosi cha doria na Kamati ya Maliasili ya Kijiji katika

kutekeleza majukumu yao.

29

▪ Kununua zana za doria mfano sare, mahema, tochi, makoti ya mvua n.k.

▪ Kugharamia mahitaji wakati wa doria kama chakula n.k.

Mipaka ya Msitu wa hifadhi wa kijiji cha Kasangantongwe

Msitu huu wa hifadhi ya kijiji cha Kasangantongwe una jumla ya mawe (beacons}

saba (7) tu zinazozunguka mipaka ya nje ya msitu huu.

MAELEKEZO MAALUM

Katika maelekezo haya inasisitizwa kwamba maamuzi yote kuhusu usimamizi wa

msitu wetu turejee vipengele vilivyoelekezwa na kukubaliwa na sisi wenyewe katika

mpango huu. Hatutegemei tena wataalamu toka wilayani kuja kufanya maamuzi

kwaajili yetu bali kuwaomba ushauri katika kupambanua mkwamo fulani ili baadaye

sisi tufanye maamuzi.

ULINZI NA UKAGUZI WA ENEO LA MSITU WA KIJIJI CHA

KASANGANTONGWE

Kila mwanakijiji wa Kasangantongwe ana jukumu la kulinda na kutunza hifadhi ya ziwa

na msitu wa kijiji. Hili jukumu litafanyika kwa kutekeleza yafuatayo:

• Kutoa taarifa za uhalifu

• Kutambua na kutoa taarifa za wahalifu wa msitu wa hifadhi ya kijiji na zana za

uvunaji haramu ndani na hifadhi ya msitu wa kijiji.

• Kuzuia moto usitokee na kuzima unapotokea.

30

• Kushiriki katika shughuli za uoteshaji miche ya miti na upandaji wa miti katika

maeneo ya makazi na mashambani.

• Ni wajibu wa wakazi wote wa kijiji cha Kasangantongwe kushirikiana katika

ulinzi wa msitu wa hifadhi ya kijiji.

• Doria za ukaguzi katika msitu wa hifadhi ya kijiji zitafanywa na kamati ya doria

angalau mara mbili kwa mwezi.

• Walinzi wa msitu na hifadhi watachaguliwa na Halmashauri ya kijiji na

kuthibitishwa na Mkutano Mkuu wa kijiji kutoka katika vitongoji vyote vya kijiji

kwa uwakilishi wa Vitongoji vya Kaselamuyaga, Isimwa, Kasangantongwe na

Kapondogoro.

Sifa za Walinzi wa Msitu.

Zifuatazo ni miongni mwa sifa ambazo inabidi mlinzi wa msitu sharti awe nazo:

• Awe na tabia na mwenendo mzuri.

• Wenye kujituma na mwaminifu.

• Mkakamavu na mwenye afya nzuri.

• Asiwe mlevi

• Awe mkazi wa kijiji cha Kashagulu na raia wa Tanzania.

• Awe na umri wa miaka kumi na nane (18) na kuendelea.

• Ajue kusoma na kuandika.

31

Wajibu, Majukumu na Mafao ya Walinzi wa Msitu wa Hifadhi ya Kijiji

• Walinzi watachagua kiongizi wao (Kamanda) kutoka miongoni mwao ambaye

atawajibika kupanga utaratibu kwa kushirikiana na walinzi wenzake wa doria

na utoaji taarifa kwa Kamati ya Mazingira.

• Walinzi wa msitu hawatalipwa mishahara lakini watapata motisha kama

itakavyoamuliwa na Serikali ya kijiji. Aidha walinzi husika wanaweza kupewa

25% ya faini anayotozwa mhalifu.

• Walinzi wa msitu wanaweza kusamehewa kazi nyingine za maendeleo kijijini.

• Walinzi watakaokwenda kinyume na maadili yao ya kazi wataadhibiwa kwa

kuonywa, kutozwa faini na kufukuzwa au kushitakiwa Mahakamani kutokana

na ukubwa wa kosa lililotendeka.

• Walinzi watatoa taarifa yao ya doria kila wanapofanya doria kwa Kamanda wao

ambaye atapaswa kutoa taarifa kwa Kamati ya Mazingira haraka iwezekanavyo

(isizidi siku moja).

• Walinzi waliofanya kazi nzuri watazawadiwa kila mwisho wa mwaka na

Halmashaurii ya Kijiji. Walinzi hao watapendekezwa na Kamati ya Mazingira na

kuthibitishwa na Halmashauri ya kijiji. Zawadi/ motisha kwa walinzi waliofanya

vizuri itakuwa kama ilivyopendekezwa hapo juu.

OPERESHENI

Yapo mazingira ya pekee ambapo kikosi pekee hakitoweza kukabiliana na uhalifu

fulani wa mpito, hivyo operesheni maalumu itaandaliwa kwa idhini ya mwenyekiti wa

32

kijiji kupitia kamati yake ya serikali ya kijiji kwa ushauri wa kamati kuu mbili;- Kamati

ya Ulinzi ya Kijiji na

Kamati ya Maliasili ya Kijiji.

N:B. Maandalizi haya lazima yawe ya siri sana.

ZAWADI YA PONGEZI KWA MWANA DORIA

Kutakuwa na utaratibu wa kutoa zawadi ya pongezi au motisha kwa mwana kikosi cha

doria ambaye atafanya kazi kwa ujasiri, ushujaa na uadilifu mkubwa utakao thibitishwa

na wajumbe wa mkutano wa Halmashauri kuu ya Kijiji na Kuungwa mkono na Mkutano

Mkuu wa Kijiji. Kiasi cha pongezi au motisha kitapangwa na Halmashauri kuu ya kijiji.

zawadi hii itatolewa hadharani na kuwekwa katika kumbukumbu za vitabu husika.

Kanuni za Kutumia Msitu wa Hifadhi ya kijiji

• Mkazi yeyote wa kijiji cha Kasangantongwe, Afisa Misitu au mtu yeyote

aliyeruhusiwa wanaweza kuingia ndani ya msitu wa hifadhi ya kijiji kwa idhini

ya Kamati ya Mazingira.

• Afisa Misitu yeyote wa Idara ya Misitu na Nyuki wakati wowote anaweza kuingia

ndani ya msitu wa hifadhi ya kijiji aidha akiwa peke yake au kwa kushirikiana

na Kamati ya Mazingira ya kijiji kwa lengo la kufanya ukaguzi na kutoa ushauri

kwa Kamati ya Mazingira ambao unapaswa kupokelewa na kufanyiwa kazi kwa

lengo la kuboresha uendelezaji wa eneo hilo la msitu.

Kifungu Cha Kumi Taratibu

33

• Sio ruksa kwa mtu yeyote kuingia msitu wa hifadhi ya kijiji bila kibali kutoka kwa

Kamati ya Mazingira isipokuwa Walinzi wa msitu, Halmashauri ya kijiji, Kamati

ya Mazingira na Afisa Misitu wanaweza kufanya hivyo bila kibali.

• Wageni wote wenye vibali toka Wizarani, Wilayani au wafadhili ni sharti wapite

kijijini na kuonyesha vibali vyao kwa Kamati ya Mazingira ya kijiji kabla ya

kuanza kufanya kazi yoyote ndani ya msitu wa hifadhi ya kijiji.

Kanuni za matumizi ya msitu:

Mahitaji yaliyoruhusiwa yatapaswa kupatikana kutoka maeneo ya matumizi ndani ya

msitu wa hifadhi ya kijiji cha Kasangantongwe. Maeneo yaliyohifadhiwa

hayataruhusiwa kupata mahitaji ya mbao, miti ya nguzo/miamba ya nyumba na

mengineyo yasiyoruhusiwa.

Matumizi ya Msitu yanayohusu Ukataji wa Miti

Mahitaji yote yanayohusu ukataji miti aina fulani kwa ajili ya mbao, nguzo na miamba

ya nyumba ndani ya msitu wa hifadhi ya kijiji cha Kasangantongwe yanaruhusiwa

katika EDU za Mpapa na Kabhukindu kwa kibali kitakachotolewa na Kamati ya

Mazingira na kuwekwa alama kwa kutumia nyundo maalum ya Idara ya Misitu ya

Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda. Miti husika itavunwa kwa kiwango ambacho

hakitaathiri lengo la msingi la kuhifadhi msitu ambalo ni kuhifadhi vyanzo vya maji na

upatikanaji endelevu wa rasilimali na huduma ya msitu kwa vizazi vya sasa na vijavyo.

34

TARATIBU NA SHERIA NYINGINEZO

Adhabu

Uwezo na haki ya kupiga faini kwa Kamati ya Mazingira ya kijiji cha Kashagulu

umetolewa kwake na Halmashauri ya kijiji cha Kasangantongwe kufuatana na Sheria

za Serikali za Mitaa (Serikali za Vijiji) 1982 No. 7 zilizoundwa chini ya kifungu cha

120 (i) na 167.

Mtu yeyote atakayekiuka masharti ya matumizi ya msitu wa hifadhi ya kijiji cha

Kasangantongwe yaliyowekwa na kukubaliwa atatozwa faini kwa mujibu wa Sheria

Ndogo ya kijiji cha Kasangantongwe ya kulinda na kutunza msitu wa hifadhi ya kijiji.

Kifungu Cha Kumi na Moja Adhabu

MCHAKATO WA KUMSHUGHULIKIA MKOSAJI NA KOSA

• Hairuhusiwi kwa mwanakijiji, mwanakamati, mlinzi au kiongozi yeyote kumtoza

faini mhalifu akiwa peke yake.

• Mazao ya misitu yaliyovunwa kinyume cha utaratibu pamoja na zana

zilizotumika katika uhalifu huo yakikamatwa ni lazima yafikishwe kwenye ofisi

ya kijiji ambapo hatua zaidi itachuliwa na Kamati ya Mazingira ya kijiji.

• Iwapo itabainika kuwa mtu au watu wamekiuka taratibu za matumizi ya msitu

wa hifadhi ya kijiji, mtu huyo au watu hao watafikishwa mbele ya Kamati ya

Mazingira ya kijiji na suala lao litashughulikiwa kwa utaratuibu ufuatao hapa

chini:

35

▪ Mhalifu/wahalifu watafikishwa katika ofisi ya kijiji ambapo Afisa Mtendaji

wa Kijiji atamuweka/atawaweka chini ya ulinzi. Afisa Mtendaji wa Kijiji

atawaarifu viongozi wa kamati/wajumbe wa Kamati ya Mazingira

angalau wawili ili kuwatoza faini wahalifu iwapo watakiri/atakiri kosa kwa

kuweka sahihi katika daftari la “makosa na faini”

▪ Iwapo mhalifu/mtuhumiwa atakataa kukiri kutenda kosa kwa kukataa

kuweka sahihi katika daftari, mtu huyo atatakiwa kupelekwa

mahakamani.

▪ Endapo mhalifu/wahalifu watakiri kutenda kosa, faini yote lazima iwe

imelipwa katika muda wa siku tatu (3) toka siku ya kukiri kutenda kosa

hilo. Hata hivyo mhalifu atalazimika kuwekewa dhamana na mtu

anayekubalika katika kijiji cha Kasangantongwe.

• Katibu atapokea malipo ya faini iliyolipwa kwa kuandika stakabadhi ambayo

atampatia mhalifu. Namba ya stakabadhi iliyotolewa itaandikwa kwenye daftari

la “Makosa na Faini” na kumkabidhi Mweka Hazina azipeleke kwenye akaunti

ya Kamati ya Mazingira ya kijiji.

• Iwapo mtu anayetuhumiwa kutenda kosa atakataa kukiri kosa mbele ya

Kamati ya Mazingira na mbele ya Mwenyekiti wa Kijiji au Afisa Mtendji wa Kijiji

basi itabidi vyombo hivyo vya utendaji vifikishe shauri hili mahakamani kwa

uamuzi zaidi.

• Iwapo mhalifu atashindwa kulipa faini katika kipindi kilichokubaliwa basi Kamati

ya Mazingira au Afisa Mtendaji wa Kijiji atafikisha suala hilo mahakamani.

36

FAINI NA ADHABU KWA KILA KOSA

Mtu yoyote atakayetiwa hatiani kwa kutenda kosa lolote lililoidhinishwa katika kifungu

cha 10 cha sheria ndogoza kulinda msitu wa hifadhi ya kijiji cha Kasangantongwe

ataadhibiwa kama ifuatavyo:

• Kosa la kuingiza/kupitisha/kuchunga mifugo atatozwa Tshs 10,000/= kwa kila

mbwa, ng’ombe na Punda na Tsh 5000/= kwa mbuzi na kondoo.

Atakayeshindwa kulipa mifugo yake itaifishwe kulingana na gharama ya faini.

• Kosa la kuingia msituni bila kibali adhabu yake itakuwa ni faini isiyopungua Tsh

10,000/= na isiyozidi Tsh 20,000/=

• Kosa la Kuchoma mkaa faini shilingi Tsh 50,000/= na kutaifisha mkaa huo.

• Kosa la Kukata miti bila kibali adhabu itatolewa kulingana na thamani ya mti

uliokatwa na faini isiyopungua Tsh 10,000/= na isizidi Tsh 50,000/= pamoja na

kutaifisha miti hiyo.

• Kosa la Kufanya shughuli za kilimo faini shilingi elfu hamsini (50,000/=) kwa

hekari moja, kutaifisha mazao na kupelekwa mahakamani.

• Kosa la Kuchoma moto faini ya isiyopungua Tsh 5,000/= na isiyozidi Tsh

50,000/= na atashitakiwa kwa mujibu wa sheria ya kosa husika.

• Kosa la Kufanya shughuli nyingine yoyote isiyohusika katika msitu huo

atatozwa faini Tsh 5,000/=

• Kosa la kufanya shughuli za uvuvi itakuwa ni faini ya Tsh. 10,000 kwa kila

chombo cha mwanakijiji na Tsh. 50,000/=kwa kila mgeni.

37

FAINI ZA KUTOWAJIBIKA

Iwapo mjumbe yeyote katika Halmashauri ya Kijiji, Kamati ya Mazingira au walinzi wa

msitu atakiuka taratibu za kiutendaji kuhusiana na uhifadhi wa msitu wa hifadhi ya kijiji

cha Kasanagntongwe, atakuwa ametenda kosa kwa mujibu wa Sheria hii na atatozwa

faini itakayojulikana kama faini ya wenye dhamana/madaraka. Faini hiyo itakuwa mara

mbili ya faini zitakazotozwa kwa watu wasiokuwa na madaraka kijijini/ zilizoainishwa

hapo juu.

• Pamoja na faini hizo, makosa ya viongozi hao lazima yajadiliwe kwenye vikao

vya juu katika kijiji na kuwachukulia hatua kali kama vile barua za onyo la

maandishi, kusimamishwa na kuwaondoa kwenye nafasi zao baada ya

kuidhinishwa na Mkutano Mkuu wa Kijiji.

• Kwa wajumbe wa Halmashauri ya Kijiji, Afisa Mtendaji Kata ataitisha Kikao

kujadili hatima ya kiongozi aliyefanya uhalifu huo.

Kifungu Cha Kumi na Mbili Kuboresha msitu na Ukarabati wake

KUUENDELEZA MSITU

Kwa bahati nzuri utengaji wa msitu ulizingatia maeneo ya kulima kuchungia mifugo,

makazi n.k. hivyo hakuna mvutano wa mgogoro wa hitaji la shughuli hizi katika eneo

la msitu huu. Shughuli kama hizi zitafanyika nje ya msitu kwa kujitosheleza. Hapa

Mpango huu wa Usimamizi wa Msitu unapiga marufuku kufanyika shughuli za aina

hii ndani ya msitu.

38

Aidha, ni marufuku mtu au kikundi cha watu kupanda mti wowote wa kigeni ndani ya

msitu huu.

Aina pekee za miti zinazoruhusiwa kuvunwa na kiasi chake zimeorodheshwa katika

majedwali ya viambat . Hairuhusiwi kutumia msumeno wa mnyororo katika msitu huu.

Kifungu Cha Kumi na Tatu Matumizi

UTANGULIZI:

Msitu huu ni msitu wa matumizi na Uhifadhi yaani uvunaji wa miti ya mbao

unaruhusiwa kwa kiwango kilicho ainishwa katika mpango huu, uvunaji wa rasilimali

nyinginezo za misitu unaruhusiwa katika EDU ya Mpapa na Kabhukindu. Lakini

jambo la kuzingatia ni kiasi, wakati na utaratibu wa uvunaji. EDU ya Uhifadhi ya Ziwa

Tanganyika haitaruhusiwa kufanyika shughuli zozote za uvunaji kwani ni kwa ajili ya

Uhifadhi tu kutokana na kuwa maeneo yanayopendelewa na sokwe pia makorongo

marefu, vyanzo vya maji na bioanuai mbalimbali muhimu na ni ukingoni mwa ziwa

Tanganyika. Hivyo basi, Mahitaji yaliyoruhusiwa yatapaswa kupatikana kutoka

maeneo ya matumizi ndani ya msitu wa hifadhi ya kijiji cha Kasangantongwe. Maeneo

yaliyozuiliwa / hifadhiwa hayataruhusiwa kupata mahitaji ya mbao, miti ya

nguzo/miamba ya nyumba na mengineyo yasiyoruhusiwa.

UVUNAJI WA MITI

Uvunaji wa miti unaoruhusiwa ni kwa miti ya aina zilizoorodheshwa katika Jedwali Na1

39

EDU hii ina jumla ya miti kama inavyoonyeshwa katika Jedwali Na 3 na 10 kwa EDU

zote mbili. Tazama katika viambata. Wakati aina ya miti ya kuvunwa imeainishwa

katika jedwali namba .. na .. ikiwa ni pamoja na matumizi mengineyo ya EDU hii

Kiasi kamili cha miti ya kuvunwa kwa kila aina ya mti vimeonyeshwa katika jedwali

namba 7 na 12 kwa EDU zote. Katika majedwali haya imeonyeshwa bayana kiasi gani

cha kuvunwa kwa kila mwaka na ni aina gani ya miti. Inapaswa kuzingatiwa bila

kuongeza hata kidogo.

Kifungu Cha Kumi na Nne Ratiba

HATUA ZA HARAKA

• KAMATI YA MALIASILI KIJIJI na Timu ya Doria zinapaswa kuchaguliwa

katika mkutano mkuu wa kijiji

• Kamati ya Maliasili ya Kijiji inapaswa kufanya mkutano wake wa kwanza

• Taratibu za ununuzi wa vitabu vya kumbukumbu zinatakiwa zifanyike mwanzoni

mwa mwezi December, 2016 ili Kamati ikutane na Mtunza Hazina wa WIlaya

kabla ya mwisho wa mwezi wa Novemba,2016. zoezi hili litakamilishwa na

Hafla au mkutano utakaohudhuriwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya kwa

uzinduzi rasmi.

• Mwezi January 2017 ni mwezi wa kuanza kazi rasmi kwa utekelezaji wa

Mpango wa Usimamizi wa Msitu huu wa hifadhi ya kijiji cha Kasangantongwe.

40

UFUATILIAJI

Vigezo vya Mafanikio:

Vifuatavyo ni Vigezo vya mafanikio vitatumika katika ufuatiliaji wa utekelezaji wa

Mpango huu wa Usimamizi wa msitu wa hifadhi ya kijiji:

• Wanakijiji kuunga mkono juhudi za uhifadhi kwa:

▪ Kutoa ushirikiano kwa Kamati ya Mazingira na walinzi wa msitu na

hifadhi.

▪ Kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu.

▪ Kuotesha na kupanda miti katika maeneo ya kaya na mashamba.

▪ Kuheshimu na kutekeleza taratibu za ulinzi na utunzaji Misitu.

• Kupungua kwa matukio ya upasuaji mbao, moto, uwindaji wa wanyama pori,

uvamizi wa msitu kwa ajili ya kilimo na ufugaji.

• Kupungua na kufunga kwa njia zisizoruhusiwa msituni.

• Kuongezeka kwa uoto wa asili na hivyo msitu kufunga hasa katika maeneo

yaliyoharibiwa.

• Kurejea au kuongezeka kwa wanyama pori, ndege na viumbe vingine hai katika

msitu wa kijiji.

• Kuongezeka kwa kiwango cha maji kwenye mito, chemchem au kufufuka kwa

chemechem zilizokufa kutokana na uharibifu.

• Kuongezeka kwa makundi ya nyuki ndani ya msitu wa hifadhi ya kijiji.

• Mipaka ya nje ya msitu wa hifadhi kuwa wazi, safi na kuonekana bila ugumu

wowote.

41

Wafuatiliaji

Wafuatao watahusika kufanya ufuatiliaji kwa kukusanya taarifa kuhusu vigezo vya

mafanikio:

• Wataalamu wa Misitu wa ngazi zote.

• Halmashauri ya kijiji

• Kamati ya Mazingira ya kijiji.

Taarifa ya Ufuatiliaji Itatolewa kwa:

• Afisa Misitu (W)/ Afisa Misitu (M) Mkutano Mkuu wa kijiji.

• Mkuu wa Wilaya/Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya.

• Halmashauri ya kijiji.

Muda wa Kufanya Ufuatiliaji

Kamati ya Mazingira: Itafanya ufuatiliaji wa utekelezaji wa Mpango huu mara mbili

(2) kila mwezi na kuandaa taarifa kwa Halmashauri ya kijiji mara moja kwa mwezi

yenye nakala kwa Afisa Misitu (W).

Halmasahauri ya kijiji: Itafuatilia mpango huu mara moja (1) kila mwezi

• kwa kutembelea msitu wa hifadhi ya kijiji angalau mara moja kila mwezi

• kuwa na agenda ya kudumu katika vikao vyake Kwa kutumia taarifa ya

Kamati ya Mazingira.

42

Wataalam wa Misitu & ngazi za Eneo, (W)/ (M):

• Wataalam wa ngazi ya Eneo (Kata/Tarafa) watafanya ufuatiliaji wa mpango huu

mara moja kila mwezi.

• Wataalam wa ngazi ya Wilaya & Mkoa watafuatilia utekelezaji wa mpango huu

mara moja kila baada ya miezi mitatu (3) yaani robo mwaka

IKUMBUKWE: Taarifa ya matokeo ya ufuatailiaji itajadiliwa mara baada ya kazi ya

ufuatiliaji kukamilika.

Mpango huu unaweza kufanyiwa marekekebisho baada ya miaka mitano (5) ya

utekelezaji kwa kuzingatia taarifa za ufuatiliaji na uamuzi uliofikiwa wakati wa kujadili

taarifa hiyo.

RATIBA YA UTEKELEZAJI

Hatua za Awali za Utekelezaji:

• Kuchagua Kamati ya Mazingira na walinzi wa msitu (Kamati ya doria) itafanyika

mara baada ya mpango wa utekelezaji kupitishwa na Mkutano

Mkuu wa kijiji.

• Kikao cha kwanza cha Kamati ya Mazingira na walinzi kitafanyika siku moja

baada ya uchaguzi wao kufanyika.

• Kununua vitabu vya kumbukumbu itafanyika baada ya Kamati ya Mazingira

kufanya kikao chake cha kwanza.

43

Hatua Zitakazofuata

Kuweka mabango ya matangazo.

MUDA WA MPANGO, MAREKEBISHO NA MAPITIO YAKE:

Mpango huu wa utekelezaji utatumika kwa miaka mitano (5) kuanzia mwaka 2016 –

2021. Marekebisho ya mpango yatafanyika kwa kuzingatia mahitaji yatakayojitokeza

kwa lengo la kuuboresha 2021 na Kamati ya Mazingira ya kijiji itahusika kwa

ushirikiano na Afisa Misitu (W) Mpanda.

44

45

46

VIAMBATA

MPANGO WA UVUNAJI KWA AINA MBALIMBALI ZA MITI KATIKA EDU ZA

MPAPA NA KABHUKINDU

JEDWALI Na 1: ORODHA YA MITI YA INAYORUHUSIWA KUVUNWA - EDU YA

MPAPA.

MITI

MUHIMU

MITI

MINGINEYO

MATUMIZI MENGINEYO

Mkalya

Mbanga Mhongolo Urinaji wa asali

Kabhamba Mpandepande Uvunaji wa miti ya mbao

Muyovu Mhama Uchimbaji wa dawa za kienyeji

Mninga Mkundye Kukata nyasi

Mkurungu Munsa Kukusanya kuni

Msawala Mubha

Mbombo Ukatajiwa boriti, nguzo na fito

Maji

Matambiko

Kukusanya uyoga

Kuwinda wanyamapori

Ukataji wa milala

47

48

JEDWALI Na . 2 MAJUMUISHO YA TAKWIMU KUTOKA KATIKA PLOTI ZA SAMPULI

MSITU WA HIFADHI WA KANKOSYA EDU YA MPAPA UCHAMBUZI WA TAKWIMU ZA VIPIMO VYA MITI TOKA

KATIKA PLOTI ZA SAMPULI

Forest assessment form C

Village Kasangantongwe Forest Name Kankosya No. of sample plots (N) 30

FMU Name Mpapa FMU area (ha) (A) 2113 Plot area (ha) (P) 0.04

Diameter class <4 4 - 7 8 - 14 15 - 29 30 - 49 50+

Important spp

Mninga 0 - 0 0 1 1,761 1 1,761 0 0 0

0

Mkurungu 2 3,522 17 29,934 24 42,260 12 21,130 11 19,369 0

0

49

Mbanga 0 0 1 1,761 4 7,043 8 14,087 2 3,522 0

0

Kabamba 18 31,695 90 158,475 171 301,103 84 147,910 16 28,173 9

15,848

Mfuru 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0

0

Msawala 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0

0

Mkora 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0

0

Mlembela 0 0 1 1,761 0 0 1 1,761 4 7,043 1

1,761

Mtundu 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0

0

Myovu 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0

0

FMU total 20 35,217 109 191,931 200 352,167 106 186,648 33 58,108 10

17,608

Average

17 91

167 88

28

8

Other spp

Msongati 5 8,804 62 109,172 84 147,910 27 47,543 0 0 0

0

Mkoma 3 5,283 1 1,761 5 8,804 0 0 0 0 0 0

50

mkole 2 3,522 5 8,804 11 19,369 3 5,283 0 0 0 0

Kolwe 0 0 5 8,804 19 33,456 6 10,565 0 0 0 0

Sifunfwe 51 89,803 96 169,040 91 160,236 27 47,543 3 5,283 0 0

Mhongolo 0 0 0 0 3 5,283 2 3,522 0 0 0 0

Mhunsa 5 8,804 14 24,652 23 40,499 9 15,848 0 0 0 0

Mtopetope 0 0 4 7,043 16 28,173 6 10,565 0 0 0 0

Mpapa 3 5,283 2 3,522 5 8,804 1 1,761 0 0 0 0

Mpogopogo 2 3,522 0 0 0 0 1 1,761 0 0 0 0

Kasemele 11 19,369 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0

Kaselenge 0 0 1 1,761 2 3,522 0 0 0 0 0 0

Mkarakata 0 0 0 0 1 1,761 4 7,043 0 0 0 0

Tola 8 14,087 19 33,456 14 24,652 7 12,326 2 3,522 0 0

Msubhu 1 1,761 5 8,804 2 3,522 2 3,522 0 0 0 0

Mla Mbuzi 0 0 0 0 1 1,761 1 1,761 0 0 0 0

Ngawera 0 0 0 0 1 1,761 1 1,761 1 1,761 0 0

51

Mbeko 0 0 1 1,761 4 7,043 2 3,522 0 0 0 0

Mlama 0 0 1 1,761 3 5,283 1 1,761 0 0 0 0

Chinga 0 0 0 0 4 7,043 2 3,522 0 0 0 0

Mgoigoi 0 0 1 1,761 3 5,283 2 3,522 1 1,761 0 0

Bhuka 1 1,761 1 1,761 1 1,761 0 0 0 0 0 0

Mvundo 0 0 0 0 1 1,761 0 0 0 0 0 0

Mvinje 0 0 0 0 2 3,522 0 0 0 0 0 0

Msele 0 0 0 0 5 8,804 0 0 1 1,761 0 0

Kamshange 0 0 2 3,522 5 8,804 2 3,522 0 0 0 0

Mketya 0 0 0 0 2 3,522 0 0 0 0 0 0

Mbangalela 0 0 0 0 2 3,522 1 1,761 0 0 0 0

Msansamale 0 0 0 0 0 0 1 1,761 0 0 0 0

Mlabhuka 0 0 0 0 0 0 1 1,761 0 0 0 0

Kikarekare 0 0 0 0 2 3,522 0 0 0 0 0 0

Kacheko 0 0 2 3,522 6 10,565 2 3,522 0 0 1 1,761

52

Mpinipini 9 15,848 1 1,761 0 0 0 0 0 0 0 0

Mbarebare 1 1,761 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0

Kabumbu 0 0 0 0 0 0 1 1,761 2 3,522 0 0

Mpakakofi 0 0 4 7,043 0 0 0 0 0 0 0 0

Total in FMU Iother

spp 102 179,605 223 116,215 89 147,910 1 47,543 0 17,608 0 1,761

Average other spp 85 0 55 0 70 0 23 0 8 0 1

Important spp

20

35,217 109 191,931 229 352,167 106 186,648 33 58,108 10 1,761

Average important

spp 17 0 91 0 167 0 88 0 28 0 1

All spp combined 122 214,907 332.1055372 308,201 318.0421202 500,077 107.0004733 234,191 33 75,724 10

3,523

Average 102

146 0 237 111

36 2

JEDWALI Na 3 FOMU ‘C’ YA TATHIMINI

ASSESSMENT FORM C

Village Forest name No. of plots (N)

53

FMU Name FMU area (ha) (A) Plot area (ha) (P)

Diameter

classes

< 4 cm

4 – 7 cm

8 – 14 cm

15 – 29 cm

30 – 49 cm

50+

Important

Species

Measure

d total (T)

FMU total

(F)

Measure

d total

(T)

FMU total

(F)

Measure

d total

(T)

FMU

Total (F)

Measure

d total

(T)

FMU

Total (F)

Measure

d total (T)

FMU total

(F)

Measure

d total

(T)

FMU

Total (F)

Other

species

Total

For each dbh/size class, Total (F) = A/P * T/N Where A = FMU area (ha); N = No. of sample plots; T = No. of measured trees (in all sample plots

combined); P = Sample plot area (ha)

54

JEDWALI Na 4: MIHIMILI YA MSINGI KUONYESHA UWINGI WA MITI KATIKA EDU YA MPAPA.

Miti Muhimu - EDU YA MPAPA

Miti Mingineyo - EDU YA

MPAPA

Stems/ha

< 4 4-7 8-14 15-29 30-49 50+

DBH classes (cm)

85

55

70

23 8 1

0

20

40

60

80

100

< 4 4 - 7 8 - 14 15 - 29 30 - 49 50+ DBH classes

Stems/ha

17

91

167

88

28

8

0

20

40

60

80

100

120

140

160

180

55

MTI MUHIMU NA MINGINEYO

- EDU YA MPAPA

JEDWALI Na. 5 ; MIHIMILI YA IDADI YA KILA AINA YA MTI (MITI MUHIMU NA

102

146

237

111

36 9

0

50

100

150

200

250

4 < 4 - 7 8 - 14 15 - 29 30 - 49 50+ Diameter classes (Cm)

Stems/ha

56

Miti muhimu - EDU ya

Kabukindu 2611ha

MITI MUHIMU NA MINGINEYO-

EDU YA KABUKINDU, 2611ha

< 4 4-7 8-14 15-29 30-49 50+

DBH classes (cm)

MINGINEYO) - EDU YA KABUKINDU

Mingineyo - EDU ua Kabukindu

2611ha

20

136

226

102

37 18

0

50

100

150

200

250

< 4 4 - 7 8 - 14 15 - 29 30 - 49 50+ DBH classes

Stems/ha

42

234

413

163

42 19 0

100

200

300

400

500 stems/ha

57

22

98

187

61

5 1 0

50

100

150

200

4 < 4 - 7 8 - 14 15 - 29 30 - 49 50+ DBH classes

stems/ha

58

JEDWALI Na 7. UFUPISHO WA MPANGO WA UVUNAJI KATIKA EDU YA Kabukindu KWA MWAKA 2016/2017 HADI

2020/2021

Na

JINA LA MTI

IDADI YA MITI

KATIKA EDU

IDADI YA MITI VUNWA KWA

MIAKA 5

2009/2010-2014/2015

IDADI YA MITI

VUNWA KILA

MWAKA

1 Msawala 172,616 227 44

2 Mkola 111,083 323 63

3 Mninga 104,548 454 91

4 Kabamba 16,764 421 84

5 Masaka 135,586 258 51

6 Myovu 157,366 669 134

7 Mkurungu 104,003 322 64

JUMLA KUU 1,301,966 2,674 531

JEDWALI Na 8: ORODHA YA MITI YA INAYORUHUSIWA KUVUNWA - EDU YA KABUKINDU

MITI MUHIMU MITI MINGINEYO MATUMIZI MENGINEYO

Msawala Mbarebare Uvuvi wa samaki

59

Kabamba Mhongolo Urinaji wa asali

Myovu Mvinje Uvunaji wa miti ya mbao

Mkola Mhama Uchimbaji wa dawa za kienyeji

Mninga Mkoma Kukata nyasi

Mkurungu Mhunsa Kukusanya kuni

Masaka Mubha Kamba za miti

Mbombo Ukatajiwa boliti,nguzo na fito

Matambiko

JEDWALI Na 9 MAJUMUISHO YA TAKWIMU TOKA KATIKA PLOTI ZA SAMPULI

UCHAMBUZI WA TAKWIMU TOKA KATIKA PLOTI ZA SAMPULI KATIKA EDU YA KABHUKINDU (2611ha)

Forest assessment form C

Village Kasangantongw

e

Forest Name

Kankosya No. of sample plots (N)

65

60

FMU Name Kabukindu FMU area (ha) (A) 2611 Plot area (ha)

(P)

0.04

Diameter class <4 4 - 7 8 - 14 15 - 29 30 - 49 50+

Important spp

Mninga 0 - 2 2,008 4 4,017 5 5,021 4 4,017 3 3013

Mkurungu 3 3,013 20 20,085 33 33,140 33 33,140 21 21,089 17 17,072

Mbanga 0 0 0 0 2 2,008 1 1,004 3 3,013 0 0

mpilipili 6 6,025 1 1,004 1 1,004 1 1,004 2 2,008 3 3,013

Msawala 0 0 1 1,004 0 0 0 0 0 0 2 2,008

Kabamba 27 27,114 226 226,956 376 377,591 147 147,622 38 38,161 16 16,068

Mnyovu 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 7 7,030

Total important

spp 36 36,152 250 251,058 416 417,760 187 187,791 68 68,288 46 48,203

Stems/ha 14 0 96 0 160 0 72 0 26 0 18

61

Other spp

Mlama 0 0 3 3,013 7 7,030 1 1,004 0 0 0 0

Tola 1 1,004 5 5,021 2 2,008 2 2,008 1 1,004 0 0

Msongati 7 7,030 57 57,241 147 147,622 40 40,169 0 0 0 0

Kaselenge 0 0 1 1,004 5 5,021 8 8,034 1 1,004 0 0

Kalongolola 0 0 0 0 2 2,008 6 6,025 1 1,004 0 0

Msigisigi 1 1,004 7 7,030 11 11,047 1 1,004 0 0 0 0

Kamshange 0 0 10 10,042 12 12,051 0 0 0 0 0 0

Buka 1 1,004 7 7,030 15 15,063 0 0 0 0 0 0

Mbeko 0 0 6 6,025 9 9,038 9 9,038 0 0 0 0

Mvinje 2 2,008 2 2,008 3 3,013 1 1,004 0 0 0 0

Mgunga 1 1,004 0 0 0 0 4 4,017 1 1,004 0 0

Msubhu 1 1,004 4 4,017 0 0 1 1,004 0 0 0 0

Mbarebare 0 0 0 0 2 2,008 0 0 3 3,013 0 0

Mtopetope 3 3,013 4 4,017 2 2,008 1 1,004 0 0 0 0

62

Chinga 0 0 2 2,008 4 4,017 0 0 0 0 0 0

Mvundo 1 1,004 1 1,004 4 4,017 1 1,004 0 0 0 0

Mhunsa 2 2,008 0 0 4 4,017 0 0 0 0 0 0

Mfulofulo 0 0 0 0 1 1,004 0 0 0 0 0 0

Kabumbu 4 4,017 15 15,063 21 21,089 4 4,017 2 2,008 1 1,004

Mhongolo 1 1,004 5 5,021 12 12,051 11 11,047 1 1,004 2 2,008

Kasemele 1 1,004 0 0 1 1,004 0 0 0 0 0 0

Kolwe 0 0 0 0 16 16,068 2 2,008 0 0 0 0

Mfulu 0 0 1 1,004 0 0 0 0 0 0 0 0

Mgagala 0 0 3 3,013 2 2,008 0 0 0 0 0 0

Kabolobolo 0 0 1 1,004 0 0 1 1,004 0 0 0 0

Mpogopogo 1 1,004 2 2,008 3 3,013 2 2,008 0 0 0 0

Mpogolo 0 0 7 7,030 4 4,017 0 0 0 0 0 0

Mkalakate 1 1,004 1 1,004 15 15,063 5 5,021 0 0 0 0

Simpogo 0 0 1 1,004 2 2,008 1 1,004 0 0 0 0

63

Mtungulu 0 0 1 1,004 0 0 2 2,008 0 0 0 0

Mbangubangu 0 0 0 0 0 0 1 1,004 0 0 0 0

Nankungu 0 0 1 1,004 6 6,025 0 0 0 0 0 0

Mkolwa 0 0 4 4,017 8 8,034 3 3,013 0 0 0 0

Mtofu 0 0 0 0 1 1,004 0 0 0 0 0 0

Tulu 0 0 0 0 3 3,013 0 0 0 0 0 0

Mzamba 0 0 0 0 1 1,004 0 0 0 0 0 0

Mpapaipori 0 0 0 0 1 1,004 2 2,008 0 0 0 0

Mlyapombo 0 0 0 0 1 1,004 3 3,013 0 0 0 0

Mbuluu 1 1,004 1 1,004 0 0 0 0 0 0 0 0

Mbombo 0 0 0 0 1 1,004 0 0 1 1,004 0 0

Mfumbe 0 0 3 3,013 2 2,008 0 0 0 0 0 0

Kalyalya 0 0 0 0 2 2,008 0 0 0 0 0 0

Kankundu 0 0 2 2,008 0 0 1 1,004 0 0 0 0

Msakasaka 0 0 1 1,004 0 0 0 0 0 0 0 0

Mketya 2 2,008 7 7,030 3 3,013 2 2,008 0 0 0 0

64

Mpangala 0 0 1 1,004 0 0 0 0 0 0 0 0

Kalumilumi 0 0 0 0 1 1,004 0 0 0 0 0 0

Mpapa 0 0 0 0 1 1,004 4 4,017 0 0 0 0

Mputuka 1 1,004 1 1,004 3 3,013 0 0 0 0 0 0

Tembwe 7 7,030 21 21,089 28 28,118 1 1,004 0 0 0 0

Mpakakofi 0 0 0 0 0 0 3 3,013 0 0 0 0

Mrabuka 0 0 0 0 1 1,004 1 1,004 0 0 0 0

Msogoro 0 0 0 0 1 1,004 0 0 0 0 0 0

Mda 0 0 0 0 1 1,004 0 0 0 0 0 0

Buketya 1 1,004 0 0 2 2,008 0 0 0 0 0 0

Mlyapombo 0 0 0 0 0 0 1 1,004 0 0 0 0

Kasanda 0 0 0 0 2 2,008 0 0 0 0 0 0

Bugogolo 0 0 1 1,004 0 0 0 0 0 0 0 0

Mlumbulu 0 0 0 0 0 0 2 2,008 1 1,004 0 0

Mlyansole 0 0 1 1,004 1 1,004 1 1,004 0 0 0 0

Nawowo 0 0 2 2,008 0 0 0 0 0 0 0 0

Kamshweke 0 0 2 2,008 2 2,008 0 0 0 0 0 0

sifunfwe 17 17,072 59 59,250 102 102,432 24 24,102 0 0 0 0

65

Mkoma 0 0 0 0 2 2,008 1 1,004 0 0 0 0

Mpapa 0 0 0 0 1 1,004 4 4,017 0 0 0 0

Mlangalanga 0 0 1 1,004 2 2,008 1 1,004 0 0 0 0

Simanzi 0 0 1 1,004 2 2,008 0 0 0

0

Total in FMU other spp 57 57,241 255 256,079 487 489,060 158 158,668 12 12,051 3 3,013

Average other spp 22

98 187

61 5

1

total in FMU important

spp 51,085

354,755 590,513

265,357 96,493

46,195

Average important spp

19.57

135.87

226.16

101.63

36.96

17.69

All spp combined 108,326

610,834 1,079,573

424,025 108,544

49,208

Average all spp

combined

41.49

233.95

413.47

162.40

41.57

18.85

Na

JINA LA MTI

IDADI YA MITI

KATIKA EDU

IDADI YA MITI VUNWA KWA

MIAKA 5

2016/2017-2020/2021

IDADI YA MITI

VUNWA KILA

MWAKA

1 Msawala 43,969 394 78

2 Mkola 39,466 58 12

3 Mninga 35,187 68 14

66

4 Kabamba 372,313 6110 121

5 Masaka 43,983 106 21

6 Mjovu

7 Mkurungu 6,335 88 14

JUMLA KUU