Upload
others
View
4
Download
0
Embed Size (px)
Citation preview
2019 -2029
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA
YA KUVUNA
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Wizara ya Kilimo
2019 -2029
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA
YA KUVUNA
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Wizara ya Kilimo
2019 -2029
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA
YA KUVUNA
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Wizara ya Kilimo
2019 -2029
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA
YA KUVUNA
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Wizara ya Kilimo
2019 -2029
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA
YA KUVUNA
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Wizara ya Kilimo
2019 -2029
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA
YA KUVUNA
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Wizara ya Kilimo
2019 -2029
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA
YA KUVUNA
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Wizara ya Kilimo
2019 -2029
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA
YA KUVUNA
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Wizara ya Kilimo
2019 -2029
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA
YA KUVUNA
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Wizara ya Kilimo
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-20292
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
Wizara ya Kilimo
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA
2019-2029
Dodoma, TanzaniaAgosti, 2019
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-20294
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-2029 i
YALIYOMO
ORODHA YA VIFUPISHO ........................................................................ iii
Dibaji .............................................................................................. vii
Shukrani ............................................................................................... ix
1. Utangulizi .............................................................................................11.1 Usuli............................................................................................1
1.2 Sera, Mikakati na Programu za Kitaifa ........................................3
1.3 Dhana ya kuwa na mkakati wa taifa wa usimamizi wa
mazao baada ya kuvuna .............................................................4
1.4 Methodolojia iliyotumika kuandaa mkakati ................................5
1.5 Mawanda ....................................................................................6
2. Hali halisi ..............................................................................................72.1 Hali ilivyo sasa ya upotevu wa Mazao baada ya kuvuna
Tanzania ......................................................................................7
2.2 Athari zinazotokana na hifadhi na usimamizi hafifu wa mazao ya chakula .....................................................................14
2.3 Vyanzo vya upotevu wa mazao baada ya kuvuna nchini ..........15
2.4 Athari za upotevu wa mazao kwenye usalama wa chakula
na lishe. ....................................................................................18
2.5 Juhudi za kukabiliana na upotevu wa mazao baada ya kuvuna nchini. ..........................................................................20
2.6 Masuala Muhimu katika Usimamizi wa Mazao baada ya Kuvuna .....................................................................................26
3. Mkakati wa Usimamizi wa Mazao baada ya Kuvuna ........................263.1 Dira na Dhima ..........................................................................273.2 Malengo Mkakati ......................................................................27
Lengo Mkakati A: Kujenga uelewa kuhusu usimamizi wa mazao baada ya kuvuna ili kuboresha ufanisi na kupunguza upotevu wa mazao katika mnyororo wa thamani .....................27Lengo Mkakati B: Kuhamasisha upatikanaji, ufikiaji, unafuu na utumiaji wa teknolojia na mbinu zilizothibitishwa kupunguza upotevu wa mazao baada ya kuvuna. ....................28
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-2029ii
Lengo Mkakati C: Kuwezesha mifumo ya masoko ya kilimo, ili kuboresha upatikanaji wa soko na kupunguza upotevu wa mazao baada ya kuvuna. ........................................................29Lengo Mkakati D: Kuhamasisha tatifi na uvumbuzi wa teknolojia mpya inayoendana na mazingira yetu pamoja na mbinu za kupunguza upotevu wa mazao .................................30Lengo Mkakati E: Kupitia na kuweka sheria mpya ili kuhakikisha kuwa viwango vya ubora vinazingatiwa kwa mujibu wa sheria ili kupunguza upotevu baada ya kuvuna. .....31Lengo Mkakati F: Kuimarisha uwezo wa taasisi, uratibu, ushirikiano, ubia na ushiriki wa wadau wa usimamizi wa upotevu baada ya kuvuna katika kuimarisha utekelezaji malengo ya kimkakati ...............................................................31Lengo Mkakati G: Kutengeneza mifumo ya usimamizi wa mazao baada ya kuvuna ili kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi. .........................................................33Lengo Mkakati H: Kukabiliana na upungufu wa fedha katika kugharamia Usimamizi wa Mazao baada ya Kuvuna. ...............34Lengo Mkakati I: Kuwa na mbinu za kiwango kinachokubalika za kukusanya taarifa za upotevu wa mazao baada ya kuvuna nchini. .......................................................................................25
4. Mipango ya Utekelezaji .....................................................................364.1. Wadau muhimu katika utekelezaji ............................................424.2. Mpango wa uendeshaji – Mpango kazi na bajeti .....................424.3 Fedha za kutekeleza Mkakati ...................................................434.4 Ufuatiliaji na Tathmini ...............................................................444.5 Utaratibu wa utoaji taarifa ........................................................45
MAREJEO ..............................................................................................47ORODHA YA VIAMBATISHO .................................................................49KIAMBATISHO 1: Muundo wa utekelezaji Malengo Mkakati .................49KIAMBATISHO NAMBA 2: MUUNDO WA TAARIFA YA ROBO MWAKA ..........................................65KIAMBATISHO NAMBA 3: MUUNDO WA TAARIFA YA ROBO MWAKA ..........................................66KIAMBATISHO NAMBA 5: ORODHA YA WAJUMBE WA KIKOSI KAZI ............................................67
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-2029 iii
ORODHA YA VIFUPISHO
ADB African Development BankAEZ Agro-Ecological ZoneAFB1 Aflatoxin B1 (Sumu Kuvu B1)AGRA Alliance for a Green Revolution in AfricaANSAF Agricultural Non State Actors ForumAPA Agricultural Produce ActARI Agriculture Research InstitutesASDP Agricultural Sector Development Programme ASDS Agricultural Sector Development Strategy ASLMS Agriculture Sector Lead MinistriesAU African UnionAZISE Asasi Zisizo za SerikaliBMI Body Mass IndexBRN Big Results NowCAADP Comprehensive African Agricultural Development Program CAMARTECCentre for Agricultural Mechanisation and Rural Technology CBOs Community-Based OrganizationsCFS Committee on World Food SecurityCMEW Crop Monitoring and Early Warning CMT Coordination and Management TeamCOSTECH Tanzania Commission for Science and Technology COWABAMA Collective Warehouse Based Marketing schemesCVC Commodity Value ChainDADPs District Agriculture Development PlansDAICO District Agricultural, Irrigation and Cooperative OfficerDASIP District Agriculture Sector Investment PlanDCP District CVC Platform DEDs District Executive DirectorsDNFS Division of National Food Security
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-2029iv
DPs Development Partners (DPs) EAC East African CommunityFAO Food and Agriculture Organization of the United NationsFFS Farmers Field SchoolFPs Focal PersonsFSAS Food Security Assistance Scheme. FSC Food Supply ChainFSD Food Security DepartmentGDP Gross Domestic ProductGMP Good Manufacturing PracticeGPLP Grain Postharvest Loss Prevention ProjectHACCP Hazard Analysis Critical Control PointsHSI HELVETAS Swiss Interco-operation.ICT Information and Communication TechnologiesJSR Joint Sector ReviewLGAs Local Government AuthoritiesLGB Larger Grain BorerLTPP Long-Term Perspective PlanM & E Monitoring and EvaluationMOA Ministry of Agriculture MATIs Ministry of Agriculture Training InstitutesMDAs Ministries, Departments, and AgenciesMIS Market Information SystemsMITI Ministry of Industries Trade and InvestmentMIVARF Marketing Infrastructure Value Addition and Rural Finance ProgrammeMoFP Ministry of Finance and PlanningMT Metric TonnesNASSM National Agricultural Sector Stakeholders MeetingNEPAD New Partnership for Africa’s DevelopmentNFS National Food SecurityNGOs Non-Governmental Organizations
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-2029 v
NMC National Milling CorporationNPHMS National Post-Harvest Management StrategyNSAs Non-State ActorsPH Post-HarvestPHL Pots-Harvest LossesPHM Post-Harvest ManagementPHM-TWG Post-Harvest Management Services-Technical Working GroupPHTs Post-Harvest TechnologiesPMO Prime Minister’s OfficePO-RALG President ‘s Office - Regional Administration and Local GovernmentPPP Public Private PartnershipPS MOA Permanent Secretary Ministry of Agriculture RAS Regional Administrative SecretariatREA Rural Energy AgencyREPOA Research on Poverty AlleviationRS Regional SecretariatSACCOS Savings and Credit Cooperative SocietySADC Southern Africa Development CommunitySAGCOT Southern Agriculture Growth Corridor of TanzaniaSC Steering CommitteeSDC Swiss Agency for Development and Cooperation. SDG Sustainable Development Goals.SGR Strategic Grain ReserveSIDO Small Industries Development OrganisationSMEs Small and Medium EnterprisesSO Strategic Objective SSA Sub-Saharan AfricaTAFSIP Tanzania Agriculture and Food Security Investment PlanTBS Tanzania Bureau of Standards TCD Technical Committee of Directors
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-2029vi
TDV Tanzania Development VisionTEMDO Tanzania Engineering and Manufacturing Design OrganisationTF Task Force.TFDA Tanzania Food and Drug AuthorityTIRDO Tanzania Industrial Research and Development OrganisationTMA Tanzania Meteorological AgencyTPMP Tanzania Post-harvest Management Platform. TV TelevisionTWG Thematic/Technical Working Groups (TWG) UN United NationsUNDP United Nations Development ProgrammeUNGA United Nations General AssemblyUSD US DollarsVICOBAs Village Community BanksWRC Ward Resource CentreWRRB Warehouse Receipts Regulatory Board
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-2029 vii
DibajiUzalishaji wa chakula nchini Tanzania, unatosheleza mahitaji ya taifa. Hata hivyo, baadhi ya mikoa huathirika kwa uhaba wa chakula kutokana na mifumo hafifu ya kuhifadhi mazao baada ya kuvuna, hali inayosababisha upungufu wa mazao na kupanda kwa bei. Hali hiyo inatokana na upotevu wa mazao baada ya kuvuna unaokadiriwa kuwa kati ya asilimia 30 na 40 kwa mazao ya nafaka na asilimia kubwa zaidi kwa mazao yanayoharibika haraka. Hali ya upotevu wa mazao baada ya kuvuna nchini imeifanya Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali kuandaa Mkakati wa Taifa wa Usimamizi Mazao baada ya Kuvuna. Mkakati huu utatekelezwa kwa kipindi cha miaka kumi na utahusisha mazao ya aina mbalimbali yakiwemo mazao ya nafaka, jamii ya mikunde, matunda, mboga, mizizi pamoja na mazao ya mbegu za mafuta. Aidha, mkakati umeainisha afua mkakati zitakazowezesha kupunguza upotevu wa mazao baada ya kuvuna na hatimae kuimarisha usalama wa chakula na lishe hapa nchini. Kudhibiti upotevu wa mazao baada ya kuvuna kutasaidia jamii kuwa na uhakika wa chakula na lishe bora na kuongeza kipato bila kutumia rasilimali za ziada.
Inatambulika duniani kote kuwa kudhibiti upotevu wa mazao unaotokea wakati wa kuvuna mpaka chakula kinapofika mezani kunatoa fursa kubwa ya kupunguza baa la njaa na kuchochea ukuaji wa viwanda. Hivyo, juhudi zinapaswa zielekezwe kwenye uzalishaji wa mazao kulingana na mahitaji pamoja na kuongeza thamani na matumizi ya bidhaa za mazao.
Mkakati huu unalenga kuwawezesha na kuwajengea uwezo wadau wa usimamizi wa kupunguza upotevu wa mazao baada ya kuvuna kwa lengo la kuongeza kipato na uhakika wa chakula na lishe. Aidha, mkakati utachangia kutekeleza Sera ya Taifa ya Kilimo, inayotekelezwa kupitia Programu ya Kuendeleza Sekta ya Kilimo Awamu ya Pili. Program hii inalenga kuleta mageuzi katika sekta ya kilimo, ili kuongeza uzalishaji na tija, kufanya kilimo kiwe cha kibiashara na kuongeza pato la wakulima wadogo kwa ajili ya kuboresha maisha yao, uhakika wa usalama wa chakula na lishe, kuongeza upatikanaji wa malighafi kwa ajili ya maendeleo ya viwanda na kuchangia pato la taifa. Pia, mkakati huu
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-2029viii
unalenga kuwezesha ufikiaji wa Malengo ya Kimataifa ya kupunguza upotevu wa mazao baada ya kuvuna kwa asilimia 50 ifikapo 2025 kama ilivyoainishwa katika Azimio la Malabo chini ya Umoja wa Afrika, na lengo namba 12.3 katika Malengo ya Maendeleo Endelevu ya Umoja wa Mataifa ifikapo mwaka 2030.
Maandalizi ya Mkakati huu yameshirikisha wadau mbalimbali wakiwemo wataalam wa serikali, wahadhiri kutoka vyuo vikuu, jukwaa la wadau wa usimamizi wa mazao baada ya kuvuna, asasi zisizokuwa za kiserikali na mashirika ya kimataifa yanayojishughulisha na kilimo. Matumaini yangu ni kuwa, utekelezaji wa mkakati huu utapunguza upotevu wa mazao baada ya kuvuna na kuchangia ipasavyo uhakika wa usalama wa chakula na lishe na kuongezeka kwa kipato cha mkulima na pato la taifa kwa ujumla.
Mhandisi Mathew J. Mtigumwe
Katibu Mkuu
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-2029 ix
Shukrani
Wizara inapenda kutoa shukrani za dhati kwa wadau mbalimbali waliopo kwenye mnyororo wa usimamizi wa mazao baada ya kuvuna ambao ni pamoja na sekta za umma, binafsi, taasisi zisizo za kiserikali, taasisi za elimu na utafiti kwa kushiriki vyema katika hatua mbalimbali za kuandaa mkakati huu.
Kwa namna ya pekee, Wizara inapenda kukishukuru kikosi kazi kilichojumuisha wataalam kutoka Wizara ya Kilimo, Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Ofisi ya Waziri Mkuu, Jukwaa Lisilo la Kiserikali la Wadau wa Kilimo-ANSAF na Shirika la Maendeleo na Ushirikiano la Uswisi-HELVETAS kwa kazi kubwa ya kuandaa mkakati huu.
Aidha, Wizara inatoa shukrani za pekee kwa Shirika la Maendeleo na Ushirikiano la Uswisi (SDC), Umoja wa Mapinduzi ya Kijani Afrika -AGRA, na Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa-FAO kwa msaada wao mkubwa wa kifedha, kitaalamu na kiufundi katika uandaaji wa mkakati huu.
Mwisho shukrani za dhati ziwafikie wadau wote waliofanikisha kwa hali na mali uandaaji wa Mkakati huu wa Taifa wa Usimamizi Mazao baada ya Kuvuna.
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-2029x
UTANGULIZI
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-2029 1
1. Utangulizi 1.1 Usuli Uhaba wa chakula duniani ni moja ya changamoto inayofahamika ambapo kulingana na tafiti mbalimbali inakadiriwa kuwa ifikapo mwaka 2050 kutakuwa na walaji wapatao bilioni tisa (9) (Parfitt, Barthel na Macnaughton, 2010). Hivyo, mahitaji ya chakula yanakadiriwa kuwa asilimia 60 zaidi ya ilivyo sasa. Katika kukabiliana na changamoto hiyo, Umoja wa Mataifa umedhamiria kutokomeza baa la njaa, kuhakikisha usalama wa chakula na lishe, na kukuza kilimo endelevu kama lengo lake la pili kati ya malengo yake kumi na saba ya Maendeleo Endelevu ifikapo mwaka 2030. Kadhalika, mkazo utawekwa katika kuongeza uzalishaji wa mazao ya chakula kati ya asillimia 50-70 ili kufikia malengo hayo. Udhibiti wa upotevu wa mazao ya chakula ni suala muhimu na la kipekee ambalo linapaswa kupewa kipaumbele ili kufikia malengo hayo. Shabaha ya tatu katika lengo hili (shabaha ya 12.3) inahamasisha kupunguza kwa asilimia 50 upotevu wa chakula kwa kila mtu duniani katika ngazi za uuzaji na ulaji kwa kupunguza upotevu wa chakula kwenye mnyororo wa uzalishaji na usambazaji (ikihusisha upotevu wa mazao baada ya kuvuna) ifikapo 2030. Njia zote hizo mbili ni muhimu kwa upatikanaji wa chakula na kuondokana na baa la njaa. Kutokana na kuongezeka kwa bei za vyakula duniani kuanzia mwaka 2006, uhakika wa upatikanaji wa chakula umekuwa ni changamoto. Kwa nchi zenye kipato kidogo kama Tanzania, tatizo la uhaba wa chakula limekuwa likijitokeza katika baadhi ya maeneo kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo uzalishaji mdogo, ukosefu wa mikakati ya kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi, bei kubwa za vyakula na ukosefu wa mikopo. Hata hivyo, upotevu wa mazao baada ya kuvuna umekuwa ukisahaulika kama sababu muhimu ya upungufu wa chakula na kipato hasa kwa wakulima wadogo. Upotevu wa mazao baada ya kuvuna unajitokeza katika mipango mbalimbali duniani kama vile Mwongozo Kabambe wa Vitendo uliotolewa mwaka 2009 na Kikosi Maalumu cha Ngazi ya Juu cha
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-20292
Umoja wa Mataifa kinachoshughulikia Masuala ya Usalama wa Chakula na Lishe kutokana na uhaba wa chakula duniani, Mpango wa Dunia wa Kilimo ambao uliridhiwa na Benki ya Dunia (2010) pamoja na Kamati ya Usalama wa Chakula Duniani. Aidha, Umoja wa Afrika kupitia Mpango kabambe wa Maendelo ya Kilimo Afrika umeainisha kuwa, upunguzaji wa upotevu wa mazao baada ya kuvuna ni moja ya kipaumbele kwa mataifa ya Afrika. Pamoja na hatua mbalimbali zilizochukuliwa, Mkutano Mkuu wa Umoja wa Afrika uliofanyika Malabo mwaka 2014, uliazimia kutokomeza baa la njaa kwa kupunguza upotevu wa mazao baada ya kuvuna kwa asilimia 50 ifikapo mwaka 2025.
Upunguzaji wa Upotevu wa Mazao baada ya Kuvuna duniani, ni njia mojawapo muhimu ya kuhakikisha usalama wa chakula na lishe. Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa na Benki ya Dunia wamebaini kuwa, theluthi moja ya chakula kinachozalishwa duniani hupotea au kuharibika. Upotevu huo ni sawa na tani bilioni 1.3 za chakula kwa mwaka duniani ambapo zaidi ya watu milioni 870 hukumbwa na baa la njaa. Taarifa ya Benki ya Dunia (2011), ilibainisha kuwa, kiasi kikubwa cha mazao ya nafaka yenye thamani ya Dola za Kimarekani bilioni 4 hupotea katika nchi za Afrika zilizo Kusini mwa Jangwa la Sahara. Taarifa hiyo, pia imeonesha kuwa, upotevu huo ni mkubwa kuliko thamani yote ya misaada yote ya chakula iliyotolewa kwa nchi za Afrika zilizo Kusini mwa Jangwa la Sahara katika kipindi cha muongo mmoja uliopita au kulinganishwa na thamani ya kiasi chote cha nafaka zinazoingizwa katika nchi hizo. Kadhalika, upotevu huo unakadiriwa kuwa ni sawa na mahitaji ya nishati (kilo kalori) yanayotosheleza watu milioni 48 kwa mwaka.
Aidha, FAO pamoja na Benki ya Dunia wamekadiria kiasi cha dola za Kimarekani 940 kinahitajika kutokomeza baa la njaa katika nchi za Afrika zilizo Kusini mwa Janga la Sahara ifikapo mwaka 2050. Kwa mukhtadha huo, kupunguza upotevu wa chakula ni njia muhimu ya kuhakikisha upatikanaji wa chakula na lishe pamoja na kupunguza umasikini. Hata hivyo, Mkakati wa upunguzaji upotevu
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-2029 3
wa mazao baada ya kuvuna, una matokeo chanya kwa mazingira na mabadiliko ya tabia nchi kwa kuwezesha uzalishaji katika ngazi ya shamba na kuokoa rasilimali za uzalishaji au upatikanaji wa mazingira bora ya uzalishaji yatakayowezesha uzalishaji wa chakula kinachopotea au kutoliwa. Matumizi ya rasilimali adimu kama vile ardhi, maji, nishati na rasilimali nyinginezo kuzalisha bidhaa ambazo matumizi yake ni kidogo huathiri utekelezaji wa mipango endelevu ya kilimo.
1.2 Sera, Mikakati na Programu za Kitaifa Kumekuwa na mabadiliko mbalimbali ya kisera na miongozo ya Kitaifa inayotokana na utekelezaji wa Dira ya Maendeleo ya Taifa 2025, na Mpango wa Maendeleo wa Muda Mrefu na Mpango (2010-2021) na mpango wa Pili wa Miaka Mitano wa Maendeleo (2016-2021). Miongozo na Sera za Kisekta zinatoa kipaumbele katika jitihada za kuhakikisha usalama wa chakula na lishe nchini. Kwa mantiki hiyo, serikali imeandaa sera, mikakati na programu mahususi kuhusu upotevu wa mazao ya chakula baada kuvuna. Hii ni pamoja na Sera ya Taifa ya Kilimo (2013) na Sera ya Masoko ya Kilimo (2008), ambazo kwa ujumla wake, zimezingatia masuala yanayohusu upotevu wa mazao baada ya kuvuna ambayo ni tishio kwa usalama wa chakula na lishe nchini. Katika kutekeleza sera hizo, kumekuwa na maazimio na mipango mbalimbali ya kitaifa na kikanda ikiwa ni pamoja na KILIMO KWANZA, Mpango wa Uwekezaji wa Kilimo na Chakula wa Tanzania, Mpango wa Kukuza Kilimo Ukanda wa Kusini mwa Tanzania, Programu kabambe ya kuendeleza sekta ya kilimo Afrika, na Mpango wa Umoja wa Afrika wa kuhamasisha Maendeleo ya Kilimo. Mipango hiyo yote ambayo inahamasisha maendeleo ya sekta ya kilimo nchini inatekelezwa kupitia Programu ya Kuendeleza Sekta ya Kilimo.
Pamoja na jitihada mbalimbali za serikali za kuendeleza sekta ya kilimo, bado kuna changamoto za kukabiliana na upotevu wa mazao baada ya kuvuna. Changamoto hizo ni pamoja na upatikanaji wa teknolojia za kuhifadhi mazao baada ya kuvuna, uelewa mdogo wa wadau katika kukabiliana na upotevu wa mazao na uhaba wa miundombinu ya masoko. Hivyo, mkakati huo utakuwa mwongozo
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-20294
kwa sekta za umma na binafsi katika kukabiliana na changamoto ya upotevu wa mazao baada ya kuvuna. Aidha, mkakati huo umezingatia mabadiliko yanayoendelea ya kitaasisi na kisera.
1.3 Dhana ya kuwa na mkakati wa taifa wa usimamizi wa mazao baada ya kuvuna
Sera ya Taifa ya Kilimo (2013) inatambua kuwa, mojawapo ya changamoto za sekta ya kilimo ni upotevu wa mazao kabla na baada ya kuvuna unaokadiriwa kuwa kati ya asimia 30-40 kwa mwaka. Upotevu mkubwa unatokea kwenye mazao ya matunda, mboga na mazao jamii ya mizizi. Upotevu huo husababishwa na kukosekana kwa miundombinu sahihi ya uhifadhi wa mazao hayo. Upotevu wa Mazao baada ya kuvuna, unawaathiri wadau mbalimbali katika mnyororo mzima kuanzia ngazi ya uzalishaji hadi mlaji. Tija ya kilimo kwa mkulima haitakuwa na faida iwapo masuala ya upotevu wa mazao baada ya kuvuna hayatapewa kipaumbele kinachostahili kupitia programu na mikakati mbalimbali. Hii itaathiri usalama wa chakula, lishe, ukuaji wa uchumi na pato la taifa.
Aidha, Sera ya Masoko ya Kilimo (2008) inatambua kuwa, soko la mazao ya kilimo linaathirika kutokana na uhaba wa miundombinu ya masoko, ukosefu wa mipango ya masoko, uhusiano duni wa wadau katika masoko, uwekezaji mdogo katika usindikaji, hifadhi na uongezaji thamani katika mazao. Changamoto hizo husababisha upotevu mkubwa wa mazao kabla na baada ya kuvuna. Lengo kuu la sera hiyo ni kuhakikisha kuwa, miundombinu ya masoko ya bidhaa za kilimo inaimarishwa na kuendelezwa ili kupunguza upotevu wa mazao baada ya kuvuna. Hivyo, jitihada zinazoelekezwa katika kupunguza upotevu, zitatoa fursa mbalimbali za kuimarisha upatikanaji endelevu wa chakula na hivyo kudumisha usalama wa chakula na lishe nchini.
Mazingira ya kisera yaliyopo kwa sasa yamezingatia umuhimu wa kukabiliana na upotevu wa mazao baada ya kuvuna. Hata hivyo, mikakati ya kuendeleza kilimo iliyopo haijatoa kipaumbele katika
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-2029 5
masuala ya upotevu wa mazao baada ya kuvuna kama juhudi za kuimarisha usalama wa chakula, lishe na kipato. Aidha, bado kuna uelewa mdogo wa wadau kuhusu masuala ya upotevu wa mazao kabla na baada ya kuvuna jambo ambalo huleta athari za kiuchumi na kimazingira. Ni kwa minajili hiyo upotevu wa mazao baada ya kuvuna unaendelea kuwa tatizo kubwa na tishio kwa usalama wa chakula. Hivyo, mkakati huu utasaidia utekelezaji wa mipango mbalimbali inayoendelea katika ngazi za kisekta, kitaifa, kikanda na kimataifa ikiwemo maazimio ya Malabo ya kupunguza upotevu wa mazao baada ya kuvuna kwa asilimia 50 ifikapo 2025.
1.4 Methodolojia iliyotumika kuandaa Mkakati Mchakato wa uandaaji wa mkakati huu umeshirikisha wadau mbalimbali ili kuibua masuala na changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta ndogo ya usimamizi wa mazao kabla na baada ya kuvuna nchini. Mchakato ulianza kwa kuunda kikosi kazi kilichojumuisha wataalam 11 kutoka Wizara ya Kilimo, Wizara ya Viwanda Biashara na Uwekezaji, Ofisi ya Waziri Mkuu, Jukwaa la Taasisi zisizo za Kiserikali la Wadau wa Kilimo, na asasi isiyo ya kiserikali ya Kiswizi HELVETAS. Orodha ya walioandaa mkakati imeambatishwa kwenye kiambatisho Na.5. Kikosi kazi hiki kilifanya kazi kwa karibu na watalaam wa wanataaluma wa kilimo kutoka Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine-SUA na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam-UDSM
Aidha, ili kupanua wigo wa maoni, kikosi kazi kiliandaa warsha na makongamano ya wadau mbalimbali wa mnyororo wa thamani wa mazao yaliyofanyika katika kanda mbalimbali hapa nchini ambapo maoni na taarifa za kuboresha mkakati huu zilikusanywa. Rasimu ya kwanza ya mkakati iliyotokana na maoni ya wadau iliwasilishwa katika kongamano la jukwaa la wadau wa masuala ya kupunguza upotevu wa mazao baada ya kuvuna ili kupata maoni na mapendekezo ya kuboresha rasimu ya mkakati. Kadhalika, rasimu hiyo ya mkakati iliwasilishwa kwenye menejimenti ya Wizara ya Kilimo kwa ajili ya maoni na uboreshaji.
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-20296
1.5 MawandaUtekelezaji wa mkakati huu utakuwa katika kipindi cha miaka 10 (2019-2029) na ni mahsusi kwa ajili ya mazao ya chakula hususan nafaka, jamii ya mikunde, matunda na mboga, mizizi na mbegu za mafuta ya kula. Aidha, utekelezaji wa mkakati huu utahusisha wadau waliopo kwenye mnyororo wa thamani kuanzia hatua ya kuvuna hadi ulaji.
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-2029 7
2. Hali halisi 2.1 Hali ilivyo sasa ya upotevu wa Mazao baada ya kuvuna
Tanzania“Upotevu wa Mazao baada ya Kuvuna” unamaanisha upotevu wa kiasi, ubora na thamani ya mazao kutokana na sababu mbalimbali wakati na baada ya kuvuna. Tafiti zinaonesha kuwa upotevu huo unaweza kupimika na kuthaminishwa kutokana na vigezo vya kiuchumi katika sehemu husika (de Lucia and Assennato, 1994). Mfumo wa upotevu unahusisha muunganiko wa shughuli mbalimbali kuanzia muda wa uvunaji, usindikaji, uuzaji, uhifadhi hadi ulaji.
Upotevu wa mazao baada ya kuvuna umewekwa katika makundi makuu matatu ambayo ni upotevu wa kiasi cha mazao, upotevu wa ubora na upotevu wa kiuchumi au kibiashara (Suleiman and Rosentrater, 2015). Watafiti wengine wanaainisha upotevu huu kama upotevu wa moja kwa moja na upotevu usio wa moja kwa moja. Upotevu wa kiasi cha mazao huhusisha upungufu wa uzito na huwa rahisi sana kujua thamani yake na kiasi kilichopotea. Mfano, kiasi cha nafaka kilicholiwa na wadudu au kupotea wakati wa usafirishaji kinaweza kuhesabika na kuthaminishwa haraka.
Upotevu wa kiasi cha mazao ni wa aina nyingi na mara nyingi huhusisha sifa za nje za zao husika, umbo, ukubwa, rangi na ladha, ambavyo huathiri ukubalikaji wake kwa walaji, na kupungua ubora kilishe. Mambo yanayosababisha upotevu huu yanahusisha tamaduni mbalimbali zinazochangia tabia za ulaji wa chakula, kuchangayika kwa nafaka safi na chafu, mabaki mbalimbali ya mimea, michanga, mawe na vipande vya plastiki na glasi. Baadhi ya uchafu ni mgumu kuuondoa na ni hatari zaidi kwa afya za walaji. Kwa mfano; mabaki ya uchafu wa dawa za kuua wadudu unaoyeyuka, mafuta, dawa za kuua wadudu waharibifu, wadudu na vimelea wanaosababisha magonjwa na wanaosambazwa na wanyama waharibifu na sumu ya fangasi. Uwepo wa uchafu usiotakiwa unaweza kuharibu uhalisia wa uzito wa mzigo wa mazao unaouzwa hivyo kuharibu ubora wake na thamani ya soko la mazao husika.
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-20298
Tafiti mbalimbali zinaonesha kuwa, hasara za kiuchumi zinapatikana pale thamani ya kifedha ya mazao inapopungua kutokana na kupoteza thamani au kiasi. Hivyo, makundi ya upotevu yanaweza kupimwa kwa njia mbalimbali na matokeo yake huwa na mahusiano ya moja kwa moja. Kwa mfano, upungufu mkubwa wa uzito na ubora unaashiria upungufu wa virutubisho na thamani ya bidhaa hiyo.
Upotevu wa moja kwa moja hutokea pale mazao yanapopungua kwa kumwagika kwa mfano, mazao yanapopungua baada ya mfuko kupasuka au kuliwa na viumbe waharibifu (wanyama, wadudu ndege), wakati upotevu usio wa moja kwa moja unasababishwa na upungufu wa ubora wa mazao pale walaji wanaposita kununua kutokana na sababu mbalimbali kama vile kuwepo kwa kiwango cha juu cha masalia ya viuatilifu na sumukuvu.
Hata hivyo upungufu wa uzito haumaanishi kuwa ni lazima uwe umesababishwa na upotevu wa mazao bali inawezekana ni upungufu wa unyevu wakati wa kukausha mazao. Kwa upande mwingine, uzito mkubwa wa mazao yaliyohifadhiwa katika sehemu zilizowazi yanaponyonya unyevu unaotokana na mvua kunyesha, huharibu mazao na kusababisha upotevu mkubwa.
2.1.1 Ukubwa wa upotevu wa uzito na maumbileUkubwa na aina ya upotevu wa mazao baada ya kuvuna hutofautiana kati ya nchi moja na nyingine kulingana na ngazi ya maendeleo ya nchi husika. Taarifa mbalimbali zinaonesha kuwa nchi zenye uchumi mkubwa na wa kati, upotevu mkubwa hutokea katika hatua za mwanzo za mnyororo wa thamani wa chakula na katika ngazi ya mlaji (United Nations, 2011). Katika nchi zenye uchumi mdogo upotevu wa mazao hutokea katika hatua za mwanzo na kati katika mnyororo wa thamani na kiasi kidogo sana hupotea katika ngazi ya mlaji. Uhaba wa chakula katika nchi zinazoendelea ni matokeo ya “upotevu usiokusudiwa” kutokana na mapungufu kwenye mnyororo wa thamani wa nchi hizo (Kielelezo namba 1).
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-2029 9
Kielelezo Na 1: Upotevu wa mazao hutofautiana katika ngazi mbalimbali
Kuna changamoto mbalimbali katika mfumo wa huduma za mazao baada ya kuvuna ambazo huchangia katika upotevu wa mazao kabla na baada ya kuvuna. Baadhi ya changamoto hizo ni; kuvuna kabla ya mazao kukomaa, vifaa duni vya kuhifadhia mazao, ukosefu wa miundombinu ya hifadhi na ukosefu wa teknolojia na vifaa vya kusindika. Changamoto za kiufundi baada ya kuvuna husabishwa na mtaji mdogo, ujuzi mdogo wa ubebaji mazao pamoja na matatizo ya masoko na sera. Mikakati ya kutatua matatizo ya upotevu wa mazao baada ya kuvuna inahitaji uchunguzi na uchambuzi wa mapungufu ya kitaalam na changamoto za kijamii na kiuchumi. Matokeo ya tafiti za FAO yanaonesha kuwa, wakulima wa Tanzania hupoteza hadi asilimia 40 ya mazao baada ya kuvuna (hii inategemea aina ya zao na eneo la kijiografia). Hali hiyo inaathiri kipato, maisha na uzalishaji kwa mkulima. Hata hivyo, kuna uhaba wa takwimu zinazohusu masula ya upotevu wa mazao ya chakula nchini. Takwimu zilizopo ni za muda mrefu na haziakisi hali halisi ya sasa.
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-202910
Katika nchi zinazoendelea makadirio ya upotevu wa mazao unaonesha viwango tofauti vya upotevu katika mazao kama vile katika mazao ya nyanya ambayo ni kati ya asilimia 20 na 50, viazi vikuu kati ya asilimia 10 na 60, ndizi kati ya asilimia 20 na 80 na mapapai kati ya asilimia 10 na 40. Aidha, utafiti uliofanywa na FAO mwaka 2011 kuhusu nafaka, umeonesha makadirio ya upotevu katika nchi za Mashariki na Kusini mwa Afrika ni asilimia 13.5. Matokeo hayo yanafanana na yale yaliyofanywa na Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine mwaka 2012 ambayo yanaonesha upotevu wa mazao makuu ya nafaka kama ifuatayo: Mahindi asilimia 15.5, Mpunga asilimia 10.7 na Mtama asilimia 12.5. Tofauti ya makadirio ya upotevu wa mazao ya chakula kati ya nchi moja na nyingine unaweza kusababishwa na mabadiliko ya mahitaji ya chakula katika ngazi mbalimbali kutegemea kipato. Tafiti zinaonesha kuwa mabadiliko ya kipato katika ngazi ya kaya duniani kote husababisha mabadiliko ya uhitaji wa chakula (Regmi, et al, 2001). Walaji wenye vipato vikubwa wanapendelea bidhaa zenye ubora wa hali ya juu. Katika kukabiliana na hali hiyo, wauzaji na wasambazaji wa vyakula wameweka taratibu za viwango mbalimbali vikiwemo vigezo vya ubora na utaratibu wa utoaji vibali. Bidhaa zinazoshindwa kukidhi mahitaji haya, hata kama zina virutubishi na ni salama kwa matumizi ya binadamu, huachwa hivyo, kuchangia upotevu wa vyakula.
Upotevu wa mazao ni mkubwa kwa nchi zinazoendelea ikilinganishwa na nchi zilizoendelea. Hiyo inatokana na sababu kuwa bajeti ya maendeleo ya kilimo katika nchi zinazoendelea ni ndogo. Aidha, matumizi ya teknolojia za kisasa katika nchi zilizoendelea katika hatua mbalimbali kama vile utumiaji wa mashine wakati wa kuvuna, kusafirisha, kukausha na kuhifadhi zimeonesha ufanisi mkubwa ikilinganishwa na teknolojia duni za asili zinazotumika katika nchi zinazoendelea (Kielelezo Na 2).
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-2029 11
Chanzo: Hodges, Buzby na Bennett, 2011.
Kielelezo Na 2: Ufanisi kati ya njia za asili na za kisasa
2.1.2 Upotevu wa mazao kiuchumiUpotevu wa mazao kiuchumi unaotokea baada ya kuvuna ni tishio kwa usalama wa chakula, kipato na maisha ya familia nyingi katika nchi za Afrika zilizo Kusini mwa Jangwa la Sahara. Upotevu wa mazao ya nafaka hususan kwa mtama pekee unakadiriwa kuwa zaidi ya dola za Kimarekani bilioni 4 kwa mwaka. Kulingana na takwimu za uzalishaji wa mazao ya chakula, kwa wastani Tanzania inajitosheleza kwa zaidi ya asilimia 100. Hata hivyo, kaya nyingi kutokana na tofauti za kiikolojia, baadhi ya maeneo ya nchi yamekuwa yakikumbwa na upungufu wa chakula.
Upotevu wa thamani ya mazao ya nafaka hutokea kwenye mnyororo wa thamani katika hatua za uzalishaji, uvunaji, uhifadhi, usafirishaji na usindikaji. Changamoto kubwa hutokea katika nchi zinazoendelea kutokana na ukweli kwamba kilimo kimehodhiwa na wakulima wadogo na wenye mitaji midogo ya kuwekeza kwenye kilimo. Wakulima hao, hutumia teknolojia duni katika uzalishaji, uvunaji, usafirishaji, uhifadhi na usindikaji. Aidha, athari zinazotokana na majanga ya asili, hali ya hewa na mabadiliko ya tabia nchi huathiri mwenendo wa kiuchumi.
Pamoja na ongezeko la uzalishaji katika ngazi ya kitaifa linalokadiriwa wastani wa tani 9,455,000 kwa mwaka, teknolojia zinazotumika kabla, wakati na baada ya kuvuna bado ni duni. Suala hilo husababisha upotevu wa wastani wa tani 3,782,000
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-202912
kwa mwaka. Hii inamaanisha kuwa asilimia 40 ya kiasi cha nafaka kinachozalishwa hupotea kwa sababu ya matumizi ya teknolojia kama inavyoonekana kwenye (Kielelezola 2).
Katika ukanda wa Afrika Mashariki, upotevu wa mazao ya chakula baada ya kuvuna unakadiriwa kuwa kati ya asilimia 20 na 60 kutegemea aina ya mazao, jambo ambalo huchangia kuathiri hali ya usalama wa chakula na lishe katika ukanda huo. Upotevu huo wa kiwango na ubora unadhihirisha hasara kiuchumi ambayo ina athari za moja kwa moja kwa pato la mkulima na taifa kwa ujumla.
Wadau mbalimbali katika mnyororo wa thamani kwa mazao ya nafaka hukumbana na changamoto mbalimbali kulingana na majukumu yao. Wakulima wadogo hukabiliwa na changamoto za miundombinu na upatikanaji wa masoko. Vilevile, wafanyabiashara, hukabiliwa na upotevu wa bidhaa kutokana na teknolojia duni za utunzaji na uhifadhi ambao huchangia ongezeko la bei kutokana na upungufu wa chakula katika soko.
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-2029 13
Chanzo: REPOA, 2014 na WK, 2015
Kielelezo Na 3: Mwenendo wa Upotevu baada ya Kuvuna kwa Mazao yaliyochaguliwa
Thamani ya nafaka kifedha hushuka kutokana na kupungua kwa ubora na kiasi cha nafaka kilichozalishwa. Nchini Tanzania, thamani ya mahindi inakadiriwa kuwa Shilingi za Kitanzania bilioni 3.92 (sawa na Dola milioni 1.8) ambapo takriban Sh.milioni 600 (sawa na Dola 273,000) zinapotea kwenye mnyororo wa thamani, mtama Sh. milioni 767 (sawa na Dola 349,000) ukiwa na makadirio ya upotevu wa mazao baada ya kuvuna ya Sh. milioni 95 (sawa na Dola 43,200), Mchele Sh. bilioni 2.58 (sawa na Dola bilioni 1.2) na upotevu wake ukikadiriwa kufikia milioni 276 (sawa na Dola 125,500) (Jedwali 1).
Mavuno Mavuno Mavuno MavunoUpotevu Upotevu Upotevu Upotevu
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-202914
Jedwali Na. 1: Wastani wa upotevu kiuchumi baada ya kuvuna kwa mazao makuu ya chakula katika kipindi cha mwaka 2012-2016
Mazao Wastani (Tani 000’)
Wastani wa thamani Kifedha TZS (000’)
Uzalishaji Hasara Thamani iliyobaki
Iliyopotea
Mahindi 6,046 937 3,920 601
Mtama 793 99 767 95
Mchele 1,780 190 2,580 276
Chanzo: REPOA, 2014; WK, 2015
Wakulima wadogo hulazimika mara kwa mara kuuza bidhaa zao kwa bei ambayo hailingani na bei ya soko. Hali hiyo siyo ina madhara kwa mkulima mmoja mmoja tu, bali inaathiri pia uchumi wa taifa. Upotevu wa mazao baada ya kuvuna unachangia kuongezeka kwa umaskini hususan kwa wananchi waishio vijijini kwa vile hupunguza kipato chao katika mlolongo wa mnyororo wa thamani wa chakula. Aidha upotevu wa mazao huathiri ubora wa bidhaa na kusababisha bei ya mazao kushuka katika soko na hatimaye kuongezeka kwa bei ya vyakula katika soko. Mwenendo wa upotevu wa mazao baada ya kuvuna huwakatisha tamaa wakulima kuwekeza kwenye sekta ya kilimo kwa sababu vipato na maisha yao kwa ujumla huathirika kwa kiasi kikubwa.
2.2 Athari zinazotokana na hifadhi na usimamizi hafifu wa mazao ya chakula
Hifadhi na usimamizi usioridhisha wa mazao ya chakula kabla, wakati na baada ya kuvuna ni chanzo cha vimelea vinavyosababisha sumu kuvu za aina mbalimbali kama vile aflatoksini. Tafiti mbalimbali zimedhihirisha kuwa mazao makuu ya chakula hususan mahindi na muhogo yamekuwa yakiathirika kutokana na hifadhi na utunzaji duni. Suala la uchafuzi wa sumu kuvu katika mazao ya chakula lina athari za moja kwa moja katika afya na biashara. Tafiti zilizofanywa
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-2029 15
na iliyokuwa Mamlaka ya Chakula na Dawa-kwa kushirikiana na kampuni ya Abt (2012) zimebaini kuwepo kwa uchafuzi mkubwa wa sumu kuvu aina ya AFB1 kwenye mazao ya chakula katika baadhi ya mikoa ya Tanzania. AFB1 ni miongoni mwa sumu kuvu ambayo ni tishio kwa afya ya binadamu. Sumu hiyo inasadikiwa kuwa ni kisababishi cha ugonjwa wa saratani ya ini. Kutokana na hali hiyo, Mamlaka imetoa angalizo kuwa uchafuzi wa sumu kuvu katika vyakula ni moja ya tatizo linalotishia afya ya binadamu. Aidha, tatizo hilo lina madhara ya kiuchumi hivyo, kuwa kikwazo katika biashara ya mazao ya chakula ndani na nje nchi.
2.3 Vyanzo vya upotevu wa mazao baada ya kuvuna nchiniVyanzo ambavyo huchangia upotevu wa mazao baada ya kuvuna hujumuisha uvunaji, usindikaji, hali ya hewa, mbinu za uzalishaji, usafirishaji, upangaji madaraja, miundombinu, utashi wa walaji na upatikanaji wa mikopo. Katika siku za hivi karibuni imebainika kuwa, mabadiliko ya tabia nchi yanaongeza tatizo la upotevu wa mazao baada ya kuvuna hususan wakati wa kuvuna na kukausha, udhibiti wa visumbufu vya mimea shambani na wakati wa kuhifadhi. Tazama Kielelezo Na. 4.
Chanzo: Abasset et al, 2014
Kielelezo Na. 4: Sifa za upotevu wa mazao baada ya kuvuna katika mnyororo wa thamani
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-202916
Kulingana na Kielelezo Na. 4 hapo juu, upotevu wa mazao baada ya kuvuna hujumuisha hatua za usafirishaji wa mazao kutoka shambani hadi kumfikia mlaji. Upungufu unaotokea katika kila hatua hutofautiana kulingana na taasisi na hatua zilizotumika katika mnyororo wa thamani wa chakula. Aidha, kwa nchi zinazoendelea mlolongo wa uzalishaji hutumia zana bora kwa kiwango kidogo hivyo husababisha upotevu mkubwa kutokea katika hatua mbalimbali kama vile wakati wa kukausha, kuhifadhi, kuchakata na kusafirisha.
Upotevu wa mazao baada ya kuvuna nchini Tanzania husababishwa na vyanzo mbalimbali ambavyo hutofautiana kutokana na asili yake na kiwango cha madhara kinachoweza kusababishwa (Kielelezo Na. 4). Vyanzo hivyo vya upotevu ni pamoja na wadudu na wanyama waharibifu, miundombinu duni ya hifadhi na usafirishaji, huduma duni za utunzaji, teknolojia duni za uvunaji na ukaushaji, ukosefu wa vifungashio na huduma sahihi za vipimo, masoko yasiyotabirika na uelewa mdogo wa wakulima kuhusu huduma sahihi za utunzaji na uhifadhi wa mazao kwenye mnyororo wa thamani. Hata hivyo, matokeo ya tafiti mbalimbali yanaonesha kuwa, wakulima wana uelewa kuhusu vyanzo vya upotevu wa mazao baada ya kuvuna lakini hawana uwezo wa kukabiliana navyo kutokana na uwezo mdogo wa kifedha (Jedwali Na. 2).
Jedwali la 2: Mitazamo ya wakulima kuhusu sababu za upotevu mazao baada ya kuvunaSababu ya Upotevu baada ya kuvuna
Mitazamo ya Mkulima
Uharibifu wa panya na wadudu Unatambuliwa na asilimia 35
Uharibifu wakati wa Usafirishaji hadi utunzaji
Unatambuliwa na asilimia 16
Upimaji na upakiaji mbovu Unatambuliwa na asilimia 12
Ukaushaji usiofaa Unatambuliwa na asilimia 9
Kutotabirika kwa masoko (kuchelewesha mauzo)
Unatambuliwa chini ya asilimia 5
Upotevu kipindi cha usindikaji Unatambuliwa chini ya asilimia 5
Kukatika kwa nafaka (hasa mchele)
Unatambuliwa chini ya asilimia 5
Chanzo: REPOA, 2014.
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-2029 17
Kwa ujumla, vyanzo vya upotevu na uharibifu wa chakula katika nchi za kipato cha chini unahusishwa na masuala ya kifedha, uratibu na uhaba wa teknolojia zinazotumika katika uvunaji, uhifadhi na usafirishaji katika mazingira tofauti. Aidha, teknolojia duni ya vifungashio na mifumo ya masoko huchangia kwa kiasi kikubwa upotevu wa mazao baada ya kuvuna. Vilevile, tafiti zimebainisha kuwa, upotevu baada ya kuvuna hutofautiana kutokana na bidhaa katika hatua mbalimbali.
Kwa kuwa mfumo wa uvunaji wa mazao unajumuisha hatua mbalimbali za kuondoa au kupunguza vikwazo ikijumuisha matatizo yote utafanyika kwa kutazama mfumo wa chakula unaoangalia maeneo ambayo udhibiti wa upotevu unaoweza kupatikana na kutoa motisha kwa maeneo ambayo yana mabadiliko ya tabia nchi kwa hatua mbalimbali
Mkakati wa usimamizi baada ya kuvuna unajumuisha michakato mingi, hatua za kuondokana na tatizo hili jumuishi zitafanyika kwa suluhisho jumuishi zitakazozingatia mnyororo mzima wa chakula ili kugundua ni sehemu gani inaweza kudhibiti upotevu na kutoa motisha za kutatua tatizo kwa njia ya kubadili tabia katika ngazi mbalimbali.
Jedwali la 3: Utofauti wa upotevu mazao katika mnyororo wa thamaniBidhaa Hatua ya Mnyororo wa Thamani Upotevu%)Mahindi Kuvuna 1-4.5
Kuhifadhi 2.8-17Maharage Kuhifadhi 14.7-17.5Viazi Vitamu
Kuvuna 4Usafirishaji 16Thamani ya soko kwa sababu ya kuharibika 11-37
Mihogo Kuhifadhi vipande vipande vilivyokaushwa 4.5Thamani ya soko kwa sababu ya ubora duni wa vipande
15-45
Nyanya Kuvuna 2.6Usafirishaji 2
Maembe Kuvuna 2.6Kusafirisha kwenda kwenye masoko 10.6Kuuza jumla 30.6
Chanzo: REPOA, 2014.
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-202918
Kwa ujumla, wakulima wana uelewa mzuri wa matatizo yanayosababisha upotevu wa mazao baada ya kuvuna. Hata hivyo, siyo vyema kuhusisha masuala ya upotevu wa mazao baada ya kuvuna na hifadhi duni peke yake. Hivyo, kutoa teknolojia ya kuhifadhi hakuwezi kuwa ufumbuzi endelevu wa upotevu wa mazao baada ya kuvuna. Upotevu wa mazao huanzia shambani hadi mezani na pia maamuzi yanayofanyika kabla ya kuvuna huathiri kwa kiwango kikubwa hatua ya upotevu wa kuvuna hapo baadaye.
Aidha, mkazo zaidi uwekwe katika njia za pamoja za kushughulikia upotevu wa mazao baada ya kuvuna. Hivyo, njia jumuishi zinahitajika ili kuongeza ufanisi ikiwa ni pamoja na uwepo wa mfumo sahihi wa uzalishaji utakaopunguza upotevu kwenye mnyororo mzima wa uzalishaji, uhifadhi, usafirishaji na usindikaji.
2.4 Athari za upotevu wa mazao katika usalama wa chakula na lishe.
2.4.1 Athari za Upotevu wa mazao katika usalama wa chakula. Zaidi ya asilimia 70 ya idadi ya watu wanaoishi Kusini mwa Jangwa la Sahara hutegemea kilimo kujipatia kipato na chakula. Hivyo, ili kuondoa umaskini uliokithiri na njaa barani Afrika, ni muhimu kukuza uzalishaji na kuongeza tija kwenye kilimo. Hata hivyo, tija kwenye uzalishaji na thamani ya bidhaa za kilimo kwenye ukanda wa Jangwa la Sahara ni ndogo kuliko maeneo mengine duniani. Licha ya tija kuwa ndogo kwenye kilimo, upotevu baada ya kuvuna pia uko juu.
Tanzania hukabiliwa na uhaba wa chakula wa mara kwa mara katika baadhi ya maeneo, hususan baadhi ya sehemu za mikoa ya kanda ya Pwani, kanda ya Kati na Kaskazini-magharibi. Sababu mojawapo ya uhaba huo ni upotevu wa mazao unaotokana na mifumo hafifu ya usimamizi baada ya kuvuna, hali inayosababisha upungufu wa bidhaa sokoni na hatimaye kupanda kwa bei.
Ingawa ukubwa na madhara ya upotevu wa mazao baada ya kuvuna unajulikana, juhudi za kupunguza tatizo hilo bado hajizafanikiwa kwa kiasi kikubwa. Hii ni kwa sababu suala hili ni mtambuka na huhusisha wadau mbalimbali katika hatua tofauti za upotevu. Aidha, wadau hawa wanafanya kazi katika muktadha wa kijamii, kisiasa, kiuchumi na kimazingira, ambao mara nyingi haueleweki vya kutosha. Kupunguza upotevu baada ya kuvuna ni njia fanisi na
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-2029 19
endelevu ya kuongeza usalama wa chakula na lishe. Pia, uongezaji wa thamani katika mazao ya kilimo yaliyopo katika minyororo ya thamani ya chakula, utatoa fursa za ajira na kuongeza kipato hivyo kukabiliana na umaskini na njaa vijijini. 2.4.2 Madhara ya Upotevu wa mazao katika LisheLishe duni ni mojawapo ya kikwazo kikubwa zaidi kwa maendeleo ya binadamu na ukuaji wa uchumi. Magonjwa yanayotokana na lishe duni huathiri ufanisi wa binadamu na huchangia kupunguza pato la taifa kwa asilimia mbili hadi tatu. Utafiti wa Afya ya watu 2010, ulionesha kuwa, asilimia 35 ya watoto wameathiriwa na udumavu; asilimia nne (4) wana ukondefu na asilimia 15 wana uzito pungufu. Ukosefu mkubwa wa virutubishi hujitokeza katika madini chuma, vitamini A na upungufu wa madini joto (iodine). Tatizo la lishe duni kwa watoto limekithiri zaidi katika maeneo ya vijijini kuliko mijini na hasa katika kaya maskini. Hii husababishwa na lishe duni kwa wanawake walio katika umri wa kuzaa, ulaji wa chakula kisichotosheleza mahitaji ya mwili na magonjwa ya kuambukiza. Asilimia 11 ya wanawake walio katika umri wa kuzaa wana uzito pungufu wa mwili chini ya 18.5kg /m2, na asilimia 53 ya wanawake wajawazito wana tatizo la upungufu wa damu, vyote hivi vikiwa ni vihatarishi vya kupata watoto wenye uzito mdogo.
Upotevu wa mazao baada ya kuvuna unahusisha pia upotevu wa virutubishi, hali ambayo huathiri kwa kiasi kikubwa ubora wa lishe. Chakula tunachokula huipa miili yetu virutubishi kwa ajili ya ukuaji, maendeleo na uwezo wa kufanya kazi ipasavyo. Kuna aina kuu mbili za virutubishi vinavyopatikana kwenye vyakula ambavyo ni virutubishi vinavyohitajika kwa wingi na vinavyohitajika kwa kiasi kidogo. Virutubishi vinavyohitajika kwa kiasi kidogo vina umuhimu mkubwa katika mwili, hasa kutoa kinga dhidi ya magonjwa mbalimbali. Vyakula katika kundi hili ni pamoja na matunda na mboga. Hata hivyo, mazao ya mboga na matunda yana kiwango kikubwa cha upotevu ikilinganishwa na aina nyingine kama vile nafaka. Inakadiriwa kuwa zaidi ya asilimia 50 ya mazao haya hupotea baada ya kuvuna katika ukanda wa Kusini mwa Jangwa la Sahara. Matunda na mboga ni vyanzo vya kuzalisha virutubishi ambavyo husaidia ufyonzaji wa virutubishi vingine vinavyopatikana katika mazao mengine kama nafaka, mbegui za mafuta na jamii ya mikunde. Kupunguza upotevu wa mazao haya na mengine baada ya kuvuna kutaboresha hali ya lishe kwa kuokoa virutubishi ambavyo vingepotea hivyo kuongeza upatikanaji wa mlo kamili kwa kupanua wigo wa upatikanaji wa vyakula mbalimbali na kwa bei nafuu.
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-202920
Lishe pia inaathiriwa na upotevu wa ubora wa mazao baada ya kuvuna, hususan kupitia uharibifu unaoweza kusababishwa na sumu kuvu au vitu vingine vinavyoweza kuathiri afya ya mwili. Tafiti zinaonesha kuna uhusiano kati ya saratani inayosababishwa na sumu kuvu na ukuaji wa watoto (Suleiman, 2015). Pia, ulaji wa sumu kuvu unaweza kuathiri mfumo wa kinga ya mwili, au kupunguza ufyonzwaji/umeng’enywaji wa virutubishi mwilini.
2.5 Juhudi za kukabiliana na upotevu wa mazao baada ya kuvuna nchini.
Masuala ya upotevu wa mazao baada ya kuvuna hapa nchini yalianza kupewa kipaumbele miaka ya 1980 baada ya kutokea mdudu anayejulikana kwa jina la dumuzi na kusababisha upotevu mkubwa wa nafaka na kuhatarisha usalama wa chakula nchini. Wakati huo, mabadiliko ya sera katika sekta ya kilimo, hususan kupunguza upotevu baada ya kuvuna yalifanyika, na serikali ikaanza kusaidia wakulima kudhibiti upotevu wa mazao baada ya kuvuna.
2.5.1 Kuanzishwa kwa Idara ya Usalama wa Chakula Kabla ya kuanzishwa kwa idara ya Usalama wa Chakula, nguvu nyingi za kuhakikisha usalama wa chakula zilielekezwa kwenye kuongeza uzalishaji na tija. Katika kipindi hicho, juhudi mbalimbali zilifanyika, zikiwemo kutekeleza programu mbalimbali na kutunga sera na sheria mbalimbali za usalama wa chakula. Hiyo ilijumuisha sheria ya mazao ya kilimo ya mwaka 1962, Mpango wa Kusaidia Usalama wa Chakula (1976) ambao ulilenga kupunguza uagizaji wa chakula toka nje ya nchi uliojitokeza miaka ya 1971/72, ambao pia ulisababisha kuanzishwa kwa hifadhi ya Chakula ya Taifa chini ya Shirika la Usagishaji la Taifa na Kitengo cha Usalama wa Chakula cha Wizara ya Kilimo. Sheria ya Usalama wa Chakula ya mwaka 1991 ilihamisha majukumu yaliyohusu mazao ya chakula kutoka shirika la usagishaji la taifa kwenda Idara ya Usalama wa Chakula ya iliyokuwa Wizara ya Kilimo na Ushirika. Idara ilianza rasmi kufanya kazi mwaka 2001 ambapo vitengo viwili vya Usimamizi wa Mazao ya Chakula na Tahadhari ya Njaa na Huduma za Hifadhi na Usindikaji wa Mazao vilianzishwa na kupewa majukumu yake. Hivyo, Sehemu ya Huduma za Hifadhi na Usindikaji wa Mazao ilipewa jukumu la kusimamia masuala yote yanayohusu huduma za mazao baada ya kuvuna nchini kwa kupitia muundo huo.
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-2029 21
2.5.2 Kuundwa kwa Jukwaa la wadau wa Usimamizi wa Mazao baada ya Kuvuna Tanzania (TPMP)
Wazo la kuanzisha Jukwaa la Usimamizi baada ya Kuvuna Tanzania lilitokana na mwamko na dhamira ya wadau katika kudhibiti upotevu mkubwa wa mazao baada ya kuvuna. Pamoja na upotevu mkubwa wa mazao nchini, kuna sera, sheria na kanuni chache za kukabiliana na tatizo hilo. Jukwaa lilianzishwa rasmi mwaka 2014, likiwa na lengo la kuunganisha nguvu za wadau wa usimamizi wa mazao baada ya kuvuna, hasa kwenye masuala ya kisera, sheria na kanuni. Jukwaa ili linaundwa na wadau mbalimbali katika mnyororo wa usimamizi wa upotevu wa mazao baada ya kuvuna. Miongoni mwa malengo ya jukwaa ni kuishauri Serikali kuwa na Sera, Sheria na mikakati mbalimbali ya kupunguza upotevu wa mazao wakati na baada ya kuvuna. Aidha, Jukwaa lina jukumu la kuwajengea uwezo wadau juu ya kukabiliana na changamoto za upotevu wa mazao.
2.5.3 Kuanzishwa kwa taasisi zinazojihusisha na Teknolojia za Kupunguza Upotevu wa mazao baada ya kuvuna
Kuna taasisi nyingi zenye majukumu ya kufanya tafiti, kubuni, kutangaza na kusambaza teknolojia sahihi za kilimo nchini. Pia, taasisi hizi zimekuwa zikitoa mafunzo na kusambaza teknolojia mbalimbali za kuzuia upotevu baada ya kuvuna, kwa wakulima wadogo. Teknolojia hizi ni pamoja na hifadhi ya mazao kwa kutumia njia isiyoruhusu hewa (hemetic bags, Plastic Barrels na metal silos). Matumizi ya teknolojia hizi yamesaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza upotevu wa mazao hivyo kuhakikisha usalama wa chakula na kuongeza kipato cha wakulima.
Miongoni mwa taasisi hizi ni pamoja na; Shirika la Maendeleo ya Viwanda Vidogo, Kituo cha Zana za Kilimo na Teknolojia Vijijini, Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine SUA na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Teknolojia za kuhifadhi kwa kutumia vifaa visivyopitisha hewa na matumizi ya msongamano mkubwa wa Polithilini, zimesaidia sana kupunguza upotevu na kuongeza uhakika wa usalama wa chakula na lishe na kuongeza pato la kaya. Pia, Wakulima wamekuwa wakitumia mbinu za asili kuhifadhi mazao yao. Njia hizo ni pamoja na kutumia kinyesi cha ng’ombe, majani maalum ya mimea, majivu ya mimea, pumba za mpunga na nishati ya jua.
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-202922
2.5.4 Juhudi za Serikali kwa Kushirikiana na Wadau Wengine Kusimamia Upotevu wa Mazao
Serikali kwa kushirikiana na Shirika la Chakula na Kilimo na Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa waliwawezesha wakulima kwa kuwajengea maghala ya kuhifadhi mazao ili kukabiliana na mashambulizi ya mdudu dumuzi na upotevu mkubwa wa mazao ya nafaka baada ya kuvuna miaka ya 1980. Uwepo wa dumuzi ulihatarisha usalama wa chakula nchini. Msaada huo ulihusisha ujenzi na/au ukarabati wa maghala katika ngazi ya jamii yenye uwezo wa kuhifadhi kati ya tani 200 na 400. Maghala haya yalijengwa kwa usimamizi wa Vyama vya Msingi vya Ushirika kwa dhana ya kuwa wakulima wangeendelea kuuza mazao yao kupitia vyama vya ushirika.Pia, iliyokuwa Wizara ya Kilimo Usalama wa Chakula na Masoko kwa kushirikiana na Sasakawa Global 2000, walitekeleza mradi wa kupunguza upotevu wa kuvuna kwa kutumia mbinu shirikishi za kupunguza upotevu baada ya kuvuna. Maghala 1,260 yalijengwa chini ya mradi huo. Hata hivyo, maghala hayo yalikuwa machache ikilinganishwa na mahitaji ya vijiji 11,000 kwa nchi nzima kwa wakati huo.
Aidha, kutoka mwanzoni mwa mwaka 2000, kumekuwepo na jitihada za kuboresha usimamizi wa mazao baada ya kuvuna zilizofanywa na serikali. Juhudi zililenga zaidi katika ujenzi na ukarabati wa maghala ya kuhifadhi mazao pamoja na mafunzo kwa wakulima kuhusu uhifadhi bora wa mazao. Kufuatia uchunguzi uliofanywa na Wizara ya Viwanda na Biashara mwaka 2013, Tanzania ina maghala 2081 yenye uwezo tofauti tofauti wa kuhifadhi mazao. Maghala hayo yanajumuisha maghala makubwa na madogo. Maghala ni nyenzo muhimu katika kupunguza upotevu wa mazao baada ya kuvuna kwani yanasaidia kupunguza mashambulizi ya wadudu waharibifu, panya na unyevu. Wadau mbalimbali kama vile HELVETAS kupitia ufadhili wa Shirika la Maendeleo na Ushirikiano la Uswisi-SDC wanatekeleza Mradi wa Kuzuia upotevu wa Mazao ya nafaka baada ya kuvuna unaolenga kuongeza usalama wa chakula na kipato kwa kaya za wakulima pamoja na kutengeneza ajira vijijini kupitia teknolojia sahihi, na kuwajengea uwezo na sera wezeshi. Kwa msaada wa Mfuko wa Hisani wa Rockefeller, AGRA inatekeleza mradi wa mazao ya mahindi ujulikanao kwa Kiingereza kama YieldWise Maize project (2015-2019) ili kupunguza upotevu wa mazao baada ya kuvuna nchini Tanzania. Mradi unalenga kuongeza kipato cha wakulima wadogo kwa asilimia 25 kwa kupunguza upotevu wa kuvuna kwa zao la mahindi kwa asilimia 50.
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-2029 23
2.5.5 Programu ya kuendeleza sekta ya kilimoSerikali imekuwa ikitekeleza programu ya kuendeleza sekta ya kilimo katika awamu mbalimbali ili kuendeleza sekta ya kilimo na kuboresha maisha ya wakulima wadogo. Mpango wa kwanza ulitekelezwa kipindi cha 2006/2007 hadi 2013/2014. Mpango wa pili wa maendeleo ya kilimo umeanza kutekelezwa 2017/2018 hadi 2027/2028 kwa vipindi viwili vya miaka mitano mitano. Mpango huu ni nyenzo ya kutekeleza Dira ya Maendeleo ya Taifa ya 2025 na Mkakati wa Kuendeleza Sekta ya Kilimo (2015). Programu ya Maendeleo ya Kilimo huipatia serikali mifumo ya kisekta katika kusimamia taasisi, matumizi na maendeleo ya uwekezaji wa sekta ya kilimo. Afua za mfumo wa masoko ya kilimo na miundombinu yake zinazofanywa na Programu ya Maendeleo ya Kilimo zimesaidia kuboresha ukarabati na ujenzi wa maghala 450 nchini kote. Uwezo wa maghala hayo kuhifadhi mazao ulikuwa ukitofautiana kutoka tani 200 hadi 500. Uwekezaji katika maghala kupitia Mpango wa Maendeleo ya Kilimo Wilaya unatarajia kuwa na mafanikio makubwa katika mfumo wa kubadilishana bidhaa na kwa sasa msisitizo unawekwa katika makubaliano ya pamoja ya wakulima kupitia vifaa vya ukusanyaji na uhifadhi wa pamoja wa mazao yanayotokana na kilimo. Pia itasaidia kupungua kwa upotevu wa mazao baada ya kuvuna. Mpango huu pia ulisaidia kuwajengea uwezo wakulima kuhusu taratibu za ulimaji mzuri wa mazao na utumiaji wa teknolojia sahihi ikiwa ni pamoja na usimamizi wake baada ya kuvuna. Aidha, Mpango wa Wilaya wa Uwekezaji katika Sekta ya Kilimo uliimarisha utekelezaji wa Programu ya Maendeleo ya Kilimo ambapo vituo 73 vya kuhifadhia mazao vilijengwa.
Pamoja na jitihada hizi, uwezo wa sekta na malengo yake ya ukuaji bado havijafikiwa kikamilifu. Fursa za kuongeza thamani kwenye mazao ya kilimo kwa kiasi kikubwa hazijafanyiwa kazi. Hii ni pamoja na ukubwa wa upotevu wa mazao baada ya kuvuna kutokana na kuwa na miundombinu duni ya hifadhi, hasa katika maeneo ya vijijini. Kutokana na tatizo hilo, Serikali kwa kushirikiana na miradi na programu mbalimbali imekuwa ikifanya jitihada za kujenga maghala ili kuboresha usimamizi wa mazao baada ya kuvuna kama ilivyooneshwa katika Jedwali Namba 4
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-202924
Jedwali la 4: Idadi ya Maghala na Uwezo wa Kuhifadhi Mazao
Programu/Miradi Idadi ya maghala
yaliyojengwa
Uwezo(katika tani)
Programu ya Maendeleo ya Kilimo 429 Tani 250 hadi 500
Sasakawa Global 2000 1260 -
DADP 450 -
DASIP 73 Tani 200 hadi 500
Mingine (LCGD, FAO and NMC) 1652 Tani 100 hadi 21,000
Chanzo; Utafiti wa Wizara ya Viwanda na Biashara 2013.
Hata hivyo, maghala hayo ni machache sana ikilinganishwa na mahitaji yake nchini hali ambayo imesababisha kuchangia katika upotevu baada ya kuvuna unaotokana na uhifadhi duni, wanyama na wadudu waharibifu, unaokadiriwa kuwa kati ya asilimia 30 na 40. Aidha, kulingana na utafiti wa Wizara ya Viwanda na Biashara wa mwaka 2013, kuna mashine 6,995 za usindikaji mazao zinazomilikiwa na wasindikaji wadogo. Jedwali la 5 linaonesha idadi na aina mbalimbali za mashine.
Jedwali la 5: Idadi ya Mashine za Usindikaji wa Bidhaa za Kilimo 2013S/No Aina ya Sekta Idadi ya vifaa vya
usindikaji
1 Mashine za kusindika mafuta 622
2 Mashine za kuchakata mihogo 313
3 Mashine za kusaga 6,043
4 Mashine za kusindika matunda 17
Jumla 6,995Chanzo; Utafiti wa Wizara ya Viwanda na Biashara 2013.
Kama nchi, tunahitaji kupanua wigo wa shughuli za usindikaji wa mazao ya kilimo, hasa katika maeneo ya vijijini ikiwa ni pamoja na kuongeza ubora wa mazao yanayotokana na kilimo ili kudhibiti upotevu baada ya kuvuna na kuongeza thamani ya soko la bidhaa.
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-2029 25
2.5.6 Programu ya Miundombinu ya Masoko Uongezaji wa Thamani na Huduma za Kifedha Vijijini
Katika kukabiliana na uhaba wa miundombinu ya kuhifadhi mazao na barabara zinazoelekea mashambani ikiwa ni pamoja na miundombinu ya masoko, Serikali imechukua hatua kadhaa ikiwa ni pamoja na utekelezaji wa Programu ya Miundombinu ya Masoko, Uongezaji wa Thamani na Huduma za Kifedha Vijijini kwa lengo la kuimarisha kipato na usalama wa chakula. Programu hii inasaidia ujenzi na ukarabati endelevu wa miundombinu bora ya masoko. Pia, inasaidia utoaji wa mafunzo ya usimamizi wa mazao baada ya kuvuna. Aidha kupitia programu hii huduma za kitaalam zimetolewa kwa taasisi, wakulima na vikundi vya usindikaji wa mazao, ambavyo kwa pamoja yalikuwa na lengo la kupunguza upotevu wa mazao baada ya kuvuna. Vilevile, programu hii imesaidia ukarabati na ujenzi wa barabara za mashambani ili kurahisisha usafirishaji wa mazao kutoka mashambani na hivyo kupunguza upotevu.
2.5.7 Mfumo wa Kimasoko wa Hifadhi ya Pamoja Wakulima wadogo nchini wanakabiliwa na vikwazo kadhaa vinavyopunguza uwezo wao wa kushiriki katika soko kwa faida na kuongeza thamani ya mazao yao. Kwa kutambua hilo, Serikali kupitia mpango wa Matokeo Makubwa Sasa wa mwaka 2013 ilianza kukarabati na kujenga maghala ya mahindi na mpunga kupitia Mfumo wa Kimasoko wa Pamoja.
Madhumuni ya mfumo wa masoko wa pamoja yalikuwa ni kuwaunganisha wakulima ili waweze kuhifadhi na kuuza kwa pamoja ili waweze kupata bei nzuri ya mazao yao. Kupitia mpango huu jumla ya maghala 123 yalikarabatiwa na kuwekewa vifaa muhimu kwa ajili ya hifadhi bora ya mazao inayolenga kupunguza upotevu wa mazao baada ya kuvuna. Lengo la kupunguza upotevu wa mazao baada ya kuvuna na kuongeza uwezo wa kuyahifadhi ni takwa la msingi ili kuhakikisha kuwepo kwa usalama wa chakula na maendeleo endelevu.
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-202926
2.6 Masuala Muhimu katika Usimamizi wa Mazao baada ya Kuvuna
Kutokana na uchambuzi wa hali halisi ya sasa ya usimamizi wa mazao baada ya kuvuna, masuala tisa ya kimkakati yameainishwa ambayo yanapaswa kushughulikiwa. Masuala hayo ni;
i. Uelewa mdogo kuhusu upotevu wa mazao baada ya kuvuna ikiwa ni pamoja na vyanzo vyake, athari zake na ufumbuzi wake kwa wahusika katika mnyororo wa thamani
ii. Upatikanaji mdogo wa teknolojia fanisi na za gharama nafuu za usimamizi wa mazao baada ya kuvuna.
iii. Mifumo duni na isiyotosheleza ya kimasoko na miundombinu ya mazao ya chakula.
iv. Tafiti chache na ubunifu mdogo katika masuala ya usimamizi wa mazao baada ya kuvuna
v. Usimamizi duni wa kanuni na miongozo ya usimamizi wa mazao baada ya kuvuna .
vi. Uwezo mdogo wa kitaasisi, uratibu usiotosheleza na ushiriki mdogo wa wadau wengine katika usimamizi wa mazao baada ya kuvuna.
vii. Uwezo mdogo wa kutambua na kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi juu ya usimamizi wa mazao baada ya kuvuna.
viii. Uwekezaji mdogo wa kifedha kwenye shughuli za usimamizi wa mazao baada ya kuvuna
ix. Ukosefu wa takwimu na taarifa sahihi za upotevu wa mazao baada ya kuvuna
3. Mkakati wa Usimamizi wa Mazao baada ya Kuvuna Mkakati wa Usimamizi wa Mazao baada ya Kuvuna unabainisha na kuchambua vikwazo vinavyosababisha upotevu wa mazao ya chakula na kusababisha kutokuwa na chakula cha kutosha kwa kaya na taifa kwa ujumla, hatimaye kupoteza mapato kwa wahusika katika mnyororo wa thamani. Mkakati huu unapendekeza Malengo Mkakati ya Usimamizi wa Mipango ambayo itawezesha taifa kukabiliana na tatizo hilo. Mkakati wa Usimamizi wa Upotevu baada ya Kuvuna umeundwa na dira (ambayo Tanzania inatarajia kuifikia ndani ya miaka 10 ijayo); dhima (mkakati mkubwa wa kufikia matarajio); Mpango Mkakati (mwongozo wa kusudi /mwelekeo) na Afua za Usimamizi (mikakati mahsusi ya kufikia malengo yaliyokusudiwa). Hivyo, Afua za Usimamizi zinabeba malengo, shughuli za kutekeleza, mgawanyo wa majukumu na vigezo vya upimaji.
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-2029 27
3.1 Dira na Dhima
3.1.1 DiraKupungua kwa upotevu wa mazao baada ya kuvuna katika minyororo ya thamani ya bidhaa, inayowanufaisha wadau na kuchangia usalama wa chakula, lishe na ukuaji wa uchumi.
3.1.2 DhimaKuboresha usimamizi wa mazao baada ya kuvuna kwa kuhakikisha uwepo wa mbinu na teknolojia za kupunguza upotevu na kuongeza thamani ya mazao baada ya kuvuna, kutoa motisha kwa uwekezaji katika mifumo ya masoko, pamoja na kuboresha uwezo na uratibu wa afua za mkakati
3.2 Malengo MkakatiMkakati umeainisha masuala tisa ya kimkakati ambayo yanapaswa kushughulikiwa ili kuboresha usimamizi wa mazao baada ya kuvuna nchini. Kipengele hiki kinaelezea malengo mkakati, dhana na afua muhimu zitakazo saidia kufikia malengo tarajiwa ndani ya kipindi cha 2019 - 2029. Kufika mwaka wa 2029, miongozo mingine ya maendeleo katika ngazi ya kitaifa kama vile Dira ya Maendeleo ya Taifa 2025, LTPP 2026 na Program ya Pili ya Maendeleo ya Kilimo 2027, itakuwa imefikia kikomo. Hali hii inatoa fursa ya kupitia/kurekebisha mkakati huu. Aidha, ili kuwa na mtiririko mzuri, maelezo kuhusu afua za usimamizi, malengo, shughuli, majukumu, viashiria vya utekelezaji na matokeo tarajiwa vimewekwa kwenye Kiambatisho Na. 1
Lengo Mkakati A: Kujenga uelewa kuhusu usimamizi wa mazao baada ya kuvuna ili kuboresha ufanisi na kupunguza upotevu wa mazao katika mnyororo wa thamani
Dhana: Upotevu mkubwa wa mazao baada ya kuvuna hutokea katika matunda, mboga na mizizi. Hali hii husababishwa na uasili wa bidhaa hizo ambazo huharibika haraka. Njia duni zinazotumika kutunza na kusafirisha bidhaa za namna hiyo katika mnyororo wa thamani huchangia zaidi upotevu wa mazao baada ya kuvuna. Vilevile, upotevu wa mazao mengine kama vile nafaka,mazao ya mikunde, mbegu za mafuta, na viungo, hutokea kwa sababu ya kutumia teknolojia duni za utunzaji na usindikaji (kupura, kubangua, kupepeta na kukausha), kukusanya na kusafirisha, kuhifadhi na kufuatilia hali ya soko, uuzaji na usindikaji. Wahusika wa mchakato huo hawana maarifa kuhusu sababu, athari na ufumbuzi sahihi wa matatizo hayo. Njia ya kujenga uelewa ni fanisi na ina gharama
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-202928
nafuu katika kupunguza upotevu wa mazao baada ya kuvuna. Kwa hiyo, lengo mkakati huu una shabaha ya kuongeza uelewa wa wadau husika katika Usimamizi wa Mazao baada kuvuna ili kupunguza upotevu.
Afua ya Usimamizi 1: Kutekeleza mikakati ya mawasiliano na habari ili kukuza ufahamu kuhusu upotevu wa mazao, sababu na athari zake.Lengo: Kutayarisha angalau vifurushi vitatu (3) vya mikakati ya mawasiliano kuhusu ufahamu wa vyanzo, athari na ufumbuzi wa upotevu wa mazao baada ya kuvuna na kuvifikisha kwa wahusika katika mnyororo wa thamani na kwa watumiaji bidhaa hizo ifikapo 2022.Lengo: Kuwepo angalau njia tano (5) tofauti za kutoa habari kuhusu usimamizi wa mazao baada ya kuvuna ifikapo 2024.
Afua ya Usimamizi 2: Kuwajengea uwezo wadau wanajihusisha na masuala ya upotevu wa mazao baada ya kuvuna na kuimarisha majukwaa ya mawasiliano.Lengo: Kujengea uwezo angalau asilimia 80 ya wadau wa kupunguza upotevu mazao baada ya kuvuna ifikapo 2028
Afua ya Usimamizi 3: Kuhamasisha matumizi ya mbinu bora za usimamizi wa mazao baada ya kuvuna kwe mnyororo wa thamani.Lengo: Angalau asilimia 50 ya wadau wawe wanatumia mbinu bora za hifadhi ya mazao ifikapo mwaka 2024
Afua ya Usimamizi 4: Kuongeza uelewa kwa wadau na walaji kuhusu mbinu na mifumo ya usimamizi inayozuia na kudhibiti sumu kuvu katika mnyororo wa thamani.Lengo: Asilimia 30 ya watumiaji watambue umuhimu wa kushughulikia upotevu wa mazao baada ya kuvuna, upotevu wa chakula na hatari za kula chakula kilicho na sumukuvu
Lengo Mkakati B: Kuhamasisha upatikanaji, ufikiaji, unafuu na utumiaji wa teknolojia na mbinu zilizothibitishwa kupunguza upotevu wa mazao baada ya kuvuna.Dhana: Tafiti nyingi zinaonesha kuwa teknolojia duni ni moja ya sababu inayochangia upotevu wa mazao baada ya kuvuna miongoni mwa wakulima wadogo. Baadhi ya teknolojia za usimamizi wa kuvuna zinapatikana hapa nchini lakini ni vigumu kufikiwa na wakulima au gharama zake ni za juu na matumizi yake kwa wakulima ni ya kiwango cha chini sana.Teknolojia chache
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-2029 29
za baada ya kuvuna kutoka nje ya nchi zinawafikia na kutumiwa na wakulima zikiwa ama hazina ufanisi katika utendaji kazi au si rafiki katika mazingira husika. Vilevile, kuna haja ya kuhamasisha mbinu na njia mbalimbali za kudhibiti upotevu baada ya kuvuna. Hivyo, ni muhimu kusaidia kuhamasisha upatikaaji na matumizi ya teknolojia na mbinu ambazo zimethibitishwa ili kupunguza upotevu wa mazao baada ya kuvuna.
Afua ya Usimamizi 1: Kukuza uelewa wa wadau na matumizi ya teknolojia za usimamizi wa mazao baada kuvuna.Lengo: Wadau wasiopungua asilimia 80 waelewe na watumie teknolojia za usimamizi wa kuvuna ifikapo mwaka 2029.
Afua ya Usimamizi 2: Kuhamasisha usindikaji wa bidhaa za kilimo katika mnyororo wa thamani.Lengo: Uwekezaji katika usindikaji wa bidhaa za kilimo uwe umeongezeka kwa asilimia 30 ifikapo mwaka 2029
Lengo Mkakati C: Kuwezesha mifumo ya masoko ya kilimo, ili kuboresha upatikanaji wa soko na kupunguza upotevu wa mazao baada ya kuvuna.
Dhana: Masoko ya mazao ya chakula nchini Tanzania yanakabiliwa na changamoto za miundombinu duni hasa maeneo ya vijijini kama vile maghala na mifumo ya kuhifadhi mazao yanayoharibika kwa haraka ili kusaidia wadau kufanya kazi kwa ufanisi na tija katika masoko ya kilimo. Pia kuna ukosefu wa mifumo mizuri ya masoko, mahusiano hafifu kati ya wadau wa ngazi mbalimbali kutokana na mpangilio usiyo rasmi wa masoko unaozuia upatikanaji wa taarifa za masoko na kusababisha upotevu mkubwa wa mazao baada ya kuvuna .
Pia, taarifa za tafiti nchini zinaonesha kuwa wakulima wadogo takribani asilimia 95 hawana vifaa sahihi vya kuhifadhia mazao yao na mazao yanayozalishwa huhifadhiwa majumbani mwao na wengi wao huuza mazao yao kupitia mifumo isiyo rasmi. Inakadiriwa kuwa asilimia tano (5) ya wakulima ndio wanaohifadhi mazao yao katika vifaa vinavyofaa na zaidi ya asilimia 80 ya nafaka huuzwa katika mfumo wa biashara usiyo rasmi. Aidha, ripoti ya Wizara ya Kilimo, 2016 inaonesha kuwa uwezo wa kuhifadhi mazao kitaifa ulikuwa karibu mita za ujazo 2,042,559 wakati uzalishaji wa mwaka 2015/2016 ulikuwa mita za ujazo 16,172,841. Hii ina maana kuwa ili kuendana na ongezeko la uzalishaji kuna haja ya kuboresha miundombinu ya masoko.
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-202930
Afua ya Usimamizi 1: Kuboresha na kurasimisha upatikanaji wa masoko ili kupunguza upotevu baada ya kuvuna.Lengo: Asilimia 80 ya bidhaa za kilimo ziuzwe katika mifumo rasmi ya masoko ifikapo 2024.
Afua ya Usimamizi 2: Kuhakikisha uwepo wa rasilimali watu waliobobea katika usimamizi wa miundombinu ya masoko.Lengo: Kuwepo idadi ya kutosha ya rasilimali watu waliobobea katika usimamizi wa miundombinu ya masoko ifikapo 2029.
Lengo Mkakati D: Kuhamasisha tatifi na uvumbuzi wa teknolojia mpya inayoendana na mazingira yetu pamoja na mbinu za kupunguza upotevu wa mazao
Dhana: Tanzania ina teknolojia anuwai na mbinu mbalimbali zinazotumika katika kupunguza upotevu wa mazao baada ya kuvuna. Hata hivyo, baadhi yake hazina ufanisi/tija katika kukabiliana na upotevu wa mazao. Wakati mwingine, teknolojia zinazoweza kukabiliana na upotevu wa mazao vipuri vyake hupatikana kwa gharama kubwa na maarifa ya utumiaji teknolojia hizo miongoni mwa walengwa huwa ni kikwazo katika kudhibiti upotevu. Vilevile, taarifa za teknolojia hizo zimetawanyika na wakati mwingine hazijulikani kwa wale ambao si miongoni mwa makundi yanayotumia teknolojia husika. Hivyo, ni vema taarifa hizo ziwekwe katika kanzidata moja ili kuwawezesha watumiaji kuzipata kiurahisi pale wanapozihitaji ili kusadia uhakika wa usalama wa chakula na masuala ya maendeleo kwa ujumla. Aidha, ni muhimu kuhakikisha kuwa nguvu zinawekwa katika kujua idadi ya teknolojia zilizopo ikiwa ni pamoja na teknolojia mpya zinazoingia sokoni, kujaribu ufanisi wake na kusambaza teknolojia zenye ufanisi kwa wazalishaji, wasindikaji na watendaji husika walio katika mnyororo wa thamani wa mazao. Jambo hili linahitaji uanzishaji wa kanzidata ya mkakati wa usimamizi wa masuala ya upotevu baada ya kuvuna katika nchi, kufanya tafiti ili kutambulisha teknolojia mpya ikiwa ni pamoja na kufanya zoezi la kufanya uhakiki wa teknolojia zilizopo.
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-2029 31
Afua ya Usimamizi 1: Kuhakikisha usimamizi wa upotevu wa mazao baada ya kuvuna yanaingizwa katika mada za tafiti za kilimo.Lengo: Masuala yote ya upotevu baada ya kuvuna yanaingizwa katika mada za tafiti za kilimo.
Afua ya Usimamizi 2: Kuanzisha kanzidata ya usimamizi wa upotevu wa mazao baada ya kuvuna.Lengo: Kufikia mwaka 2021 kuwepo na kanzidata ya upotevu wa mazao ya chakula.
Afua ya Usimamizi 3: Kuanzisha teknolojia zenye ubunifu na kufanya uhakiki wa teknolojia zilizopo na zinazotengenezwa ili kupunguza upotevu baada ya kuvuna.Lengo: Asilimia 80 ya teknolojia za kusaidia kupunguza upotevu baada ya kuvuna ziwe zimehakikiwa na kupitishwa ifikapo 2029.
Lengo Mkakati E: Kupitia na kuweka sheria mpya ili kuhakikisha kuwa viwango vya ubora vinazingatiwa kwa mujibu wa sheria ili kupunguza upotevu baada ya kuvuna.
Dhana: Tangu miaka ya 1980, serikali imekuwa ikisaidia wakulima kupunguza upotevu wa mazao baada ya kuvuna. Hata hivyo, kuna miongozo na kanuni zisizotosheleza usimamizi wa mazao baada ya kuvuna kwa baadhi ya mazao, na katika baadhi ya maeneo hakuna miongozo na kanuni hizo kwa ajili ya kutumiwa na wadau husika. Aidha, kuna mapungufu katika utekelezaji wa miongozo na kanuni hizo zikiwemo zile zilizotungwa na serikali za mitaa. Matokeo yake ni kwamba kumekuwa na mafanikio madogo katika masuala mazima ya viwango vinavyohitajika kwa mazao ya chakula na kushindwa kupunguza upotevu wa mazao. Katika kutekeleza Mkakati wa usimamizi wa upotevu baada ya kuvuna kwa ufanisi ni muhimu kuwepo miongozo na kanuni na zitekelezwe ipasavyo.
Afua ya Usimamizi 1: Kuhakikisha kuwa masuala yote yanayohusu upotevu baada ya kuvuna yanaingizwa katika sheria zilizopo.Lengo: Sheria zilizopo ziwe zimepitiwa upya kufikia mwaka 2024.
Lengo Mkakati F: Kuimarisha uwezo wa taasisi, uratibu, ushirikiano, ubia na ushiriki wa wadau wa usimamizi wa upotevu baada ya kuvuna katika kuimarisha utekelezaji malengo ya kimkakati
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-202932
Dhana: Jitihada za Usimamizi wa mazao baada ya kuvuna zinakabiliwa na uratibu dhaifu miongoni mwa serikali na taasisi zisizo za kiserikali. Kurundikana kwa juhudi zinazohusu usimamizi wa upotevu baada ya kuvuna zinazofanana katika baadhi ya maeneo limekuwa ni jambo la kawaida katika maeneo mengi nchini huku maeneo mengine yanayohitaji kupewa kipaumbele yakionekana kutengwa. Hali hiyo imekuwa kikwazo katika utekelezaji wa mipango, ugawanyaji wa rasilimali na ni mapungufu katika kukabiliana na upotevu baada ya kuvuna. Hivyo, mkakati huu umeandaliwa ili kujumuisha mipango yote ya aina hii na kuratibu juhudi mbalimbali zinazofanywa na sekta mbalimbali kuhusiana na mnyororo wa thamani wa mazao baada ya kuvuna. Mikakati inahitajika katika kuimarisha uratibu na ubia miongoni wa sekta zote zinazohusika na mambo ya usimamizi wa mazao baada ya kuvuna ili kuhakikisha utekelezaji wake unakuwa wenye tija na ufanisi kuhusu hatua zilizokubaliwa katika kupunguza upotevu wa mazao baada ya kuvuna.
Kwa sasa kuna sekta nyingi zinazohusiana na mnyororo wa thamani baada ya kuvuna; ni muhimu kuhakikisha kuwa vinara wa usimamizi wa upotevu baada ya kuvuna wanabainishwa na kuwezeshwa kulingana na mahitaji yao ili kuratibu na kusimamia kikamilifu mkakati wa usimamizi wa upotevu baada ya kuvuna. Taasisi inayoongoza mpango huu ambao kwa mujibu wa mpango wa sasa ni Idara ya Taifa ya Usalama wa Chakula chini ya Wizara ya Kilimo, inapaswa kuimarishwa ili kutimiza majukumu yake ipasavyo. Taasisi na mashirika mengine pia yanahitaji kuimarishwa ili kusaidia au kuunga mkono juhudi za chini ya Wizara ya Kilimo. Juhudi za kuimarisha taasisi hizo zinajumuisha uwepo wa rasilimali watu, kurekebisha na kutathmini uwepo wa rasilimali ya kutosha katika kutekeleza shughuli za usimamizi na uratibu kama zilivyoanishwa. Lengo mkakati litafanikiwa tu iwapo utekelezaji wa afua za mkakati uliotajwa hapa chini utafanyika kulingana na malengo yaliyowekwa.
Afua ya Usimamizi 1: Kuwezesha uratibu katika ngazi zote ili kuongeza ushiriki wa wadau muhimu katika masuala ya usimamizi wa mazao baada ya kuvuna.Lengo: Mbinu za uratibu ziwe zimewezeshwa katika ngazi ya kitaifa, mkoa na za serikali za mitaa.
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-2029 33
Afua ya Usimamizi 2: Kupendekeza motisha mbalimbali za uwekezaji ili kuongeza ushiriki wa sekta binafsi.Lengo 1: Vifurushi vya motisha vya uwekezaji viandaliwe na kutekelezwa fikapo mwaka 2024.Lengo 2: Thamani ya uwekezaji wa sekta binafsi kwa usimamizi wa upotevu wa mazao baada ya kuvuna iongezeke angalau kwa asilimia 50 ifikapo 2029.
Afua ya Usimamizi 3: Kuimarisha rasilimali watu ili kushughulikia suala la upotevu wa mazao baada ya kuvuna nchini. Lengo: Kujenga msingi wa rasilimali watu kwa asilimia 80 ifikapo 2025.
Afua ya Usimamizi 4: Kuwezesha utoaji na upatikanaji wa huduma za ugani kuhusu upotevu katika mnyororo wa thamani wa mazao.
Lengo Mkakati G: Kutengeneza mifumo ya usimamizi wa mazao baada ya kuvuna ili kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi.
Dhana: Usimamizi wa mazao mengi baada ya kuvuna nchini unaathiriwa sana na mabadiliko ya hali ya hewa yenye uhusiano wa moja kwa moja na unyevu na kuenea kwa wadudu waharibifu pamoja na magonjwa ya mimea. Mabadiliko ya tabia nchi huathiri pia ufanisi wa teknolojia zitumikazo uvunaji, ukaushaji, udhibiti wa wadudu waharibifu na magonjwa, na hifadhi. Kwa mfano, mabadiliko ya tabia nchi yanachangia uwepo wa sumu kuvu kutokana na kuongezeka kwa joto na mvua zisizotarajiwa. Pia, katika hali ya ukame, mazao huzalisha vimelea vya fangasi ambayo husababisha sumu kuvu. Vivyo hivyo, kuhifadhi nafaka kwenye kiwango kikubwa cha unyevu huweza kusababisha kuongezeka kwa fangasi inayozalisha sumu kuvu. Matokeo yake ni kuziweka kaya na taifa kwa ujumla katika hatari ya uchafuzi wa chakula kutokana na sumu kuvu inayoathiri afya ya walaji na atimae kupunguza nguvu kazi ya taifa.
Katika kukabiliana na athari za mabadiliko ya hali ya hewa hatua zenye ufanisi na za kimkakati zinahitajika ili kujenga jamii inayotambua athari za mabadiliko ya tabia nchi ikiwa ni pamoja kutoa kipaumbele kwa huduma za hali ya hewa katika ajenda za maendeleo. Hii itawezesha maamuzi kuhusu hali ya hewa katika ngazi zote na kupunguza vihatarishi na gharama. Mafanikio ya kukabiliana na athari za mabadiliko ya hali ya hewa hutegemea ufanyaji kazi wa mifumo bunifu ya kilimo, hasa katika hatua za uzalishaji na hifadhi ya mazao.
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-202934
Afua ya Mkakati 1: Kuhakikisha upatikanaji wa habari muhimu za tabia nchi zinazohusiana na Upotevu wa Mazao baada ya Kuvuna na mifumo ya tahadhari mapema.Lengo: Taarifa zote muhimu za tahadhari zilizotambuliwa na zinazohusu hatari ya mabadiliko ya tabia nchi katika mnyororo wa thamani ziandaliwe na kusambazwa ifikapo 2029
Afua ya Usimamizi 2: Kuanzisha teknolojia na miundombinu bunifu ya baada ya kuvuna na inayostahimili tabia nchiLengo: Kufikia 2029 asilimia 80 ya teknolojia za kupunguza upotevu baada ya kuvuna na zinastahimili mabadiliko ya tabia nchi ziwe zimeingizwa katika mifumoLengo: Asilimia 80 ya wasambazaji na wanufaika wa teknolojia baada ya kuvuna wawe wamejengewa uwezo wa kutumia teknolojia hizoifikapo 2029
Lengo Mkakati H: Kukabiliana na upungufu wa fedha katika kugharamia Usimamizi wa Mazao baada ya Kuvuna.
Dhana: Hivi sasa, taasisi zinazoratibu usimamizi wa upotevu wa mazao baada ya kuvuna zinakabiliwa na uwekezaji mdogo wa kifedha zaidi ikilinganishwa na sekta nyingine.Aidha, sekta hii ndogo inakabiliwa na upatikanaji mdogo wa mikopo na fedha za kugharamia programu muhimu. Hivi sasa nakadiriwa kuwa takribani asilimia 10 pekee ya mikopo ndiyo imeelekezwa kwenye sekta ya kilimo ijapokuwa mchango wake kwa pato la Taifa ni kati ya asilimia 25 na 30. Vilevile taarifa mbalimbali zinabainisha kuwa kati ya hiyo asilimia 10 ya mikopo inayoelekezwa kwenye sekta ya kilimo ni sehemu ndogo sana inayowekezwa kwenye shughuli za kukabiliana na upotevu baada ya kuvuna.
Ili kukabiliana na suala hili la uwekezaji mdogo katika kilimo, mkakati huu umeainisha mbinu madhubuti za kuwekeza katika kilimo na kuimarisha mikakati iliyopo ya uwekezaji katika kilimo. Mkakati huu pia umeweka mikakati ya kupunguza viatarishi katika mnyororo wa thamani wa hifadhi ya mazao ikiwa ni pamoja na kuimarisha sera na mifumo ya bima katika sekta ya kilimo. Aidha matumizi ya TEHAMA katika mifumo ya kibenki ni muhimu katika kufanikisha suala hili badala ya mifumo iliyozoeleka ambayo haikidhi haja. Hivyo mkakati huu umelenga kushughulikia mahitaji ya kifedha ya wadau katika mnyororo wa thamani wa hifadhi ya mazao ikiwa ni pamoja na hatua za usindikaji, usafirishaji na katika teknojia za kupunguza upotevu wa mazao. Suala hili litaenda sambamba na kuimarisha uwezo wa taasisi za kifedha kama benki ya Maendeleo
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-2029 35
ya Kilimo Tanzania (TADB), VICOBA na SACCOS zinazojihusisha na masuala ya hifadhi na usindikaji wa mazao.
Afua za Usimamizi 1: Kuanzisha utaratibu bunifu wa kuhamasisha uwekezaji wa kifedha katika Nyanja za usambazaji na matumizi ya teknolojia za kisasa baada ya kuvuna.Lengo: Ukopeshaji wa wawekezaji, wakulima na taasisi ndogo na za kati zinazojishughulisha na teknolojia za usimamizi wa mazao baada ya kuvuna uongezeke kwa asilimia 50 ifikapo mwaka 2024.
Afua za Usimamizi 2: Kuanzisha utaratibu wakupunguza madhara na athari zinazotokana na majanga katika kilimo na kuwa na mifumo mbalimbali ya kufadhili shughuli za kilimo.Lengo: Kuimarisha jitihada zakufadhili shughuli za kukabiliana na upotevu hususan teknolojia ambazo zimekuwa zinafanywa na serikali kwa kushirikiana na wabia wa maendeleo ifikapo 2024.Lengo: Kuanzisha utaratibu wa kupunguza athari za kifedha zinazotokana na usimamizi duni wa mazao ifikapo 2024.
Afua za Usimamizi 3: Kuhakikisha upatikanaji wa rasilimali fedha za kutosha na kwa wakati kusaidia shughuli za usimamizi wa mazao baada ya kuvuna.Lengo: Rasilimali fedha za kutosha kuwezesha shughuli za usimamizi wa mazao baada ya kuvuna zipatikane ifikapo mwaka 2025.
Lengo Mkakati I: Kuwa na mbinu za kiwango kinachokubalika za kukusanya taarifa za upotevu wa mazao baada ya kuvuna nchini.Dhana: Kuna tafiti mbalimbali zinazofanyika kuhusu upotevu wa mazao baada ya kuvuna hapa nchini. Taarifa zilizopo zinatofautiana kulingana na aina ya zao katika mnyororo wa thamani. Hata hivyo, taarifa hizo hazioneshi upotevu uliopo kwa mazao yote na nyingine zimepitwa na wakati ukilinganisha miaka zilipotayarishwa pamoja na jitihada mbalimbali zilizokwishafanyika. Aidha njia mbalimbali zimekuwa zikitumika kutathmini upotevu wa mazao baada kuvuna na hakuna mbinu moja iliyopitishwa na kukubalika katika kufanya tathmini hizi, hivyo kusababisha kuwa na takwimu tofauti tofauti nchini na zisizokuwa na uhakika.
Afua ya Usimamizi 1: Kupitia, kuboresha na kulinganisha mbinu zilizopo za kutathmini upotevu wa Mazao baada ya Kuvuna.Lengo: Kuwa na mbinu moja na yenye kukubalika ambayo itatumika nchini kutathmini upotevu wa mazao baada ya kuvuna ifikapo 2020
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-202936
4. Mipango ya Utekelezaji
Sura hii inaonyesha wadau muhimu kwenye utekelezaji wa mkakati. Pia imeweka njia mbalimbali za kutafuta rasilimali kwa ajili ya kutekeleza afua mbalimbali zilizobainishwa. Wafadhili muhimu wa afua za kimkakati zimeorodheshwa ili kuraisisha utekelezaji wake. Kwenye sura hii, umuhimu wa uratibu na ushirikiano wenye ufanisi umesisitizwa kama ilivyosisitizwa kwenye lengo mkakati F ambalo ni hatua za kuimarisha uratibu, ushirikiano na ushiriki wa wadau katika kusimamia masuala ya hifadhi ya mazao baada ya kuvuna.
4.1. Wadau muhimu katika utekelezaji Mkakati wa Taifa wa Usimamizi wa Mazao baada ya Kuvuna unajumuisha na unahitaji ushiriki wa wadau mbalimbali wakiwemo: Sekta Binafsi, Asasi za Kiraia, Taasisi za Kijamii, Taasisi zisizo za Kiserikali na Wabia wa Maendeleo ili kufikia dira kuu. Mkakati utatekelezwa kwa kipindi cha miaka 1O ukitilia mkazo mazao ya chakula hususan nafaka, jamii ya mikunde, matunda, mboga, mizizi na mbegu za mafuta. Wajibu wa wadau na mipaka ya ushirikiano inayotarajiwa ni kama ifuatavyo:
4.1.1. Wizara ya KilimoMasuala ya kupunguza upotevu wa mazao baada ya kuvuna ni mtambuka na hivyo mkakati wa kukabiliana na suala hilo unahusisha wadau mbalimbali ambao wanahitaji kuratibiwa ili kutekeleza shughuli hizo kwa ufanisi. Kwa ujumla uratibu wa mkakati huu utakuwa chini ya dhamana ya Wizara inayosimamia masuala ya kilimo nchini. Wizara hii itakuwa na jukumu la kuratibu utekelezaji wa mkakati huu kama inavyofanyika katika program ya maendeleo ya kilimo. Hata hivyo, kwa vile utekelezaji wa mkakati huu ni sehemu ya utekelezaji wa program hii hautakuwa na Kamati ya Taifa ya Utendaji wa Mkakati. Hivyo, Kamati ya utendaji ya program ya maendeleo ya kilimo itatumika kuratibu mkakati huu.
Miundo mingine ya Utekelezaji wa program ya maendeleo ya kilimo, ambayo inaweza kutumika katika utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Usimamizi wa Upotevu wa Mazao baada ya Kuvuna ni: (i) Mkutano wa Kitaifa wa Wadau wa Sekta ya Kilimo; (ii) Mapitio ya Pamoja ya Sekta; (iii) Kamati ya Wakurugenzi Wataalam; (iv) Vikundi Kazi vya Wataalam; na (v) Timu ya Uratibu na Usimamizi. Kama inavyoonekana Mkakati utakuwa na Vikundi kazi vya kitaalam na Timu ya Uratibu na Usimamizi.
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-2029 37
Katika utekelezaji wa mkakati huuMajukwaa ya Usimamizi Mazao baada ya Kuvuna yataongozwa na Mwenyekiti ambaye ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo na wajumbe watakaochaguliwa kutoka kwenye Wizara na Idara za kisekta, Washirika wa Maendeleo, Sekta Binafsi na Asasi Zisizo za Serikali (AZISE) zinazojihusisha na masuala ya mazao baada ya kuvuna. Hivyo, Sekraterieti ya Mkakati itakuwa ni Idara ya Usalama wa Chakula iliyo chini ya Wizara ya Kilimo. Mikutano ya Wadau wa Mkakati itaainishwa katika mpango kazi. Aidha, Katika utekelezaji wa shughuli hii, Wizara ya Kilimo itasaidiwa na Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kama ilivyobainishwa kwenye Programu ya Pili ya Maendeleo ya Kilimo. Majukumu mengine ya Wizara ya Kilimo yatahusisha utafutaji wa rasilimali, kuandaa bajeti, mipango na kusimamia matumizi na manunuzi.
4.1.2. Wizara ya Viwanda Biashara na Uwekezaji Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji inafanikisha biashara ya kikanda na kimataifa na kuendeleza masoko ya mazao na bidhaa za kilimo. Wizara hii inalenga kuhamasisha fursa za uwekezaji kwenye maendeleo ya viwanda na sekta nyingine kwa kuwezesha na kuimarisha mahusiano ya biashara na nchi za nje na kutengeneza mwongozo wa sera husika.
4.1.3. Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI)Ofisi hii itaratibu utekelezaji wa afua zote zinazotekelezwa kwenye ngazi za Mikoa na Wilaya na kuwasiliana na Wizara za kisekta kulingana afua husika. Katika ngazi ya Mkoa, Sekretarieti ya Mkoa, kupitia Wawakilishi wa Mikoa husika. itawezesha uratibu wa wadau muhimu (wakiwemo sekta binafsi, wadau wasio wa kiserikali na wengine) katika kutekeleza mipango ya shughuli za mazao baada ya kuvuna katika mkoa, wakati shughuli kama hizo katika ngazi ya Wilaya zitaratibiwa na Mkurugenzi wa Wilaya akisaidiwa na Mwakilishi wa Wilaya husika.
4.1.4 Wabunifu na Waendelezaji wa TeknolojiaTIRDO ni taasisi mtambuka ya utafiti na maendeleo iliyoanzishwa mwaka 1979. Mamlaka yake ni kuisaidia sekta ya viwanda Tanzania kwa kutoa huduma za kitaalam na usaidizi, ili kuboresha teknolojia zinazotumika. Tafiti maalum za teknolojia za mazao baada ya kuvuna hufanywa pamoja na kuendeleza utaalam ili kuboresha usindikaji wa mazao ya kilimo kwa kuzingatia hatua muhimu katika usindikaji ili kutengeneza bidhaa zilizo bora zaidi.
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-202938
TEMDO inajihusisha na usanifu, ubunifu na utohoaji wa teknolojia pamoja na kutengeneza mashine na vifaa na kukuza uzalishaji wa kibiashara wa mashine na matumizi yake. TEMDO pia, inajihusisha na uhawilishaji wa teknolojia kwenda kwa wajasiriamali wadogo na wa kati, na kutoa huduma za mafunzo na ushauri wa kiutaalam viwandani inajihusisha na uendelezaji wa viwanda vidogo ikijikita kuanzia utungaji sera hadi uanzishaji wa viwanda vidogo vijijini na mijini. inajihusisha na ubunifu, utengenezaji na uhawilishaji wa teknolojia ya zana za kilimo na maendeleo vijijini inatengeneza na kusambaza zana za kilimo kama mashine za kupigia haro, kupandia, kukamulia mafuta, matoroli, mikokoteni, matanki ya kuhifadhia maji na mashine za kufyatulia matofali pamoja na vipuli vyake.
4.1.5 Mamlaka za Usimamizi
4.1.5.1 Mamlaka ya Mzani na Vipimo Mamlaka ya Mizani na Vipimo inajihusisha na udhibiti wa mifumo ya kupima uzito na ujazo pamoja na kusimamia udhibiti wa kanuni na sheria zaa uzito na ujazo. Mamlaka ya Uzani na Vipimo humlinda mnunuzi na mlaji kwa kuhakikisha vipimo vya uzani na ujazo ni sahihi kisheria. Mamlaka pia hutoa vibali vya matumizi ya vifaa vya uzani na ujazo kwa kukagua, kurekebisha (kusanidi) na kuhakiki pamoja na kufanya ukaguzi wa mara kwa mara wa mizani katika maduka na viwanda vinavyotumia mifumo ya kupima uzito ili kuhakikisha kuwa wakulima na watumiaji wengine wanapata haki za vipimo. Wakala pia hutoa ushauri kwa wazalishaji na wateja kuhusu matumizi bora, utunzaji na uhifadhi bora wa vifaa vya uzani na vipimo.
4.1.5.2 Bodi ya usimamizi wa stakabadhi za ghalaBodi hii ina majukumu ya kuratibu na kuendeleza Mfumo wa Stakabadhi Ghalani unaohakikisha upatikanaji wa mikopo endelevu na yenye masharti nafuu pamoja na mifumo ya uuzaji wa bidhaa. Bodi itatimiza wajibu wake kwa kutoa vibali vya biashara ya maghala, waendeshaji na wakaguzi kwa kuusimamia mfumo. Pia, bodi inawajibika kuwaunganisha wazalishaji kwenye mfumo rasmi wa Stakabadhi Ghalani wenye ufanisi na uhakika.
4.1.5.3 Mamlaka ya Chakula na Dawa Mamlaka hii inajihusisha na kudhibiti na kuhakiki ubora na usalama wa vyakula, madawa, vipodozi na vifaa tiba. inadhibiti taarifa za uhamasishaji wa bidhaa na vifaa hivyo, inafanya utafiti na michanganuo ya kimaabara pamoja na kudhibiti uingizaji na uuzaji
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-2029 39
wa bidhaa vifaa hivyo ndani na nje ya nchi. Pia, inawajibu wa kutoa vibali na leseni kwenye sekta hizi.Katika mkakati huu itashiriki katika kusimamia na kudhibiti masuala ya ubora na usalama wa vyakula katika mnyororo wa thamani.
4.1.5.4 Shirika la Viwango Tanzania Shirika la viwango lina mamlaka ya kuandaa, kutoa na kusimamia viwango vya ubora vya bidhaa nchini. Majukumu ya shirika ili katika mkakati huu ni kuandaa, kutoa na kusimamia viwango vya ubora katika mnyororo mzima wa thamani ya mazo baada ya kuvuna.
4.1.5.5 Wakala wa Umeme Vijijini Inajihusisha na usambazaji na upatikanaji wa nishati ya umeme ya uhakika na ya bei nafuu vijijini pamoja na kukuza ufanisi wa utumiaji wa nishati hiyo ili kusaidia viwanda vya kusindika mazao.
4.1.5.6 Taasisi za Elimu na UtafitiTaasisi nyingi za elimu na utafiti zinachangia Usimamizi wa Mazao baada ya kuvuna kwa kutoa mafunzo na kufanya tafiti husika. Taasisi hizi ni pamoja na taasisi za utafiti wa kilimo, taasisi za mafunzo ya kilimo, TIRDO, CAMARTEC, COSTECH, TEMDO, Chuo kikuu cha Kilimo SUA na vinginevyo. Wajibu wao mkubwa ni pamoja na kutoa mafunzo ya muda mfupi au mrefu zikiwemo kozi maalumu ili kutimiza mahitaji ya kitaalam. Pia zinafanya utafiti, kusambaza matokeo ya utafiti na kutoa ushauri kwa Serikali na Sekta Binafsi kupitia ushauri elekezi na njia nyingine.
4.1.5.7 Wabia wa Maendeleo
Kwa utekelezaji bora wa mkakati huu, Wabia wa Maendeleo ni wadau muhimu katika utoaji wa huduma za kitaalam na rasilimali fedha. Wabia wa Maendeleo pia ni sehemu muhimu ya mikutano kati ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo pamoja na vikundi kazi vya kitaalam. Kwa kuuwezesha mkakati huu, Wabia wa Maendeleo watasaidia utekelezaji wa lengo kuu la kupunguza umaskini na kuchangia ukuaji wa uchumi pamoja na usalama wa chakula na lishe wa taifa.
4.1.5.8 Sekta BinafsiSekta binafsi hususan watengezaji, wasambazaji, wasindikaji, wasafirishaji, wauza pembejeo za kilimo, wakulima, wafanyabiashara na watoa huduma ni muhimu sana katika utekelezaji wa mkakati huu kwenye ngazi mbalimbali.
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-202940
4.1.5.9 Watendaji Wasio wa KiserikaliWatendaji Wasio wa Kiserikali na wadau wengine ni muhimu pia katika kufanikisha utekelezaji wa Mkakati na uhamasishaji wa rasilimali zinazohitajika. Hivyo, watajumuishwa katika Vikundi kazi vya kitalaam, watafuatilia na kutathmini pamoja na kusaidia kitalaam. Ili kufanikisha utekelezaji wa mkakati huu, kutahitajika kuongeza ushirikiano uliopo kati ya Wizara ya Kilimo na Watendaji Wasio wa Kiserikali.
4.1.5.10 Vyama vya UshirikaVyama vya ushirika ni muhimu katika Usimamizi wa Mazao baada ya kuvuna kwa kutokana na majukumu yake la msingi la kuwaunganisha wakulima katika hatua mbalimbali za mchakato wa hifadhi kama vile ukusanyaji, uchambuaji, upangaji madaraja, uhifadhi, usafirishaji, usambazaji na masoko. Ukitilia maanani kuanziishwa kwa Soko la Bidhaa hapa nchini, Vyama vya Ushirika vitatumika kuongezea nguvu katika sekta binafisi. Misaada kwa Vyama vya Ushirika itatoa vipaumbele kwa sehemu dhaifu za mnyororo wa thamani wa mazao baada ya kuvuna ikiwa ni pamoja na maeneo yasiyofikika kwa urahisi na kuongeza uwezo wa kuhifadhi mazao.
4.1.5.11 Watoa Huduma KifedhaUtekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Usimamizi wa Upotevu wa Mazao baada ya Kuvuna unahitaji kuhusisha taasisi zinazotoa huduma za kifedha kama vile mabenki, zisizo za kibenki, bima, vyama vya kuweka na kukopa na mifumo ya kijamii ya kuweka akiba (VICOBA, HISA n.k.) ili kukabiliana na changamoto za kifedha zinazoukabili mnyororo wa thamani wa mazao baada ya kuvuna, ikiwemo kutoa fedha kwa vyama vya ushirika na usimamizi wa dhima. Taasisi hizo zitahitajika kutayarisha huduma maalum za kifedha kwa ajili ya kuwawezesha wadau wa teknolojia baada ya kuvuna kama watengenezaji, wasambazaji, wasindikaji, wasafirishaji, wakusanyaji, wakulima, wauza pembejeo za kilimo, wafanyabishara na watoa huduma, kama vile vyama vya ushirika.
4.1.5.12 Vikundi Kazi vya KitaalamVikundi kazi vya Kitaalam vya usimamizi mazao baada ya kuvuna vitakuwepo kufanya kazi zikiwemo zile za Kikundi kazi cha Programu ya Pili ya Maendeleo ya Kilimo. Pia, kutahitajika vikundi kazi maalum vya kitaalam kwa ajili ya kutoa ushauri kwa Wizara ya Kilimo kwenye masuala maalum.
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-2029 41
Wajibu wa Vikundi Kazi vya kitaalam vya Usimamizi wa Upotevu wa Mazao baada ya kuvuna katika kutekeleza mkakati utakuwa kutoa ushauri wa kiufundi na kitaalam katika masuala maalum. Kikundi kitaundwa na wataalam kutoka katika makundi ya wadau mbalimbali wa mkakati.
Vikundi vitakavyoundwa vitatokana na ngazi mbalimbali katika mnyororo wa mazao baada ya kuvuna na umuhimu wa hiyo sekta ndogo. Kwa kuzingatia hayo, vifuatavyo vitakuwa vikundi kazi vya awali: Kikundi cha Teknolojia za Mazao baada ya kuvuna, Kikundi cha Masoko na Miundombinu ya Uhifadhi, Kikundi cha kujenga uwezo, kikundi cha fedha na manunuzi pamoja na kikundi cha ufuatiliaji na tathmini. Vikundi hivi vitafanya kazi zao kwa kufuata miongozo maalumu ya Wizara ya Kilimo na Hadidu zao za rejea zitaboreshwa kwenye ngazi za uandaaji Mpango Kazi wa Mkakati. Mpango wa Utekelezaji ni kama ulivyooneshwa kwenye Kielelezo namba 5.7
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-202942
Kielelezo 5 : Mpango wa Utekelezaji
Katika ngazi ya Wilaya na Mkoa kutakuwepo na mratibu wa masuala ya usimamizi wa mazao baada ya kuvuna ambaye atateuliwa na mamlaka husika katika ngazi hizo. Mratibu huyu atakuwa na jukumu la kusimamia utekelezaji wa afua zote katika eneo husika na kuwasilisha taarifa za utekelezaji wa mkakati katika ngazi husika. Taarifa hizi zitakusanywa na kuwasilishwa katika sekretariet ya uratibu ngazi ya Taifa.
4.2. Mpango wa uendeshaji – Mpango kazi na bajetiMkakati wa Kitaifa wa Usimamizi wa Mazao baada ya Kuvuna utatekelezwa kwa kipindi cha miaka 10 ambapo utekelezaji wa mkakati na miongozo mingine ya kisera na kitaifa kama vile Dira ya Maendeleo ya Taifa - 2025 , LTPP 2026, na Programu ya pili ya Maendeleo ya Kilimo 2026 utafanyika. Hii itaruhusu mwendelezo wa Mkakati wa Usimamizi wa Upotevu wa Mazao baada ya Kuvuna ikizingatia muelekeo wa kisera wa mwendelezo wa mikakati ya Dira ya Maendeleo ya Tanzania ya 2025, LTPP 2026, na Programu ya pili ya Maendeleo ya Kilimo.
Ili kutekeleza mkakati wa Usimamizi wa Upotevu wa Mazao baada ya Kuvuna katika kipindi hiki, mkakati umetambua kuwa, shughuli ya kwanza ya mkakati ni kuandaa mpango kazi wa kina na gharama za shughuli muhimu, kupanga majukumu na wajibu maalum, pamoja na kuweka malengo ya muda mfupi ya kati na ya muda mrefu.
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-2029 43
Idara ya Usalama wa Chakula kwa kushirikiana na watendaji wengine, itaandaa mpango wa uendeshaji, utakaoainisha shughuli, muda wa utekelezaji na bajeti.
4.3 Fedha za kutekeleza Mkakati Usimamizi wa Upotevu wa Mazao baada ya Kuvuna kwa kiasi kikubwa utategemea fedha kutoka bajeti za Serikali, Sekta binafsi, Jumuiya ya Kimataifa pamoja na michango ya watu binafsi. Hata hivyo, mtazamo jumuishi na mfumo wa kuratibu kazi pamoja unahitajika kuhakikisha kuwa fedha kwa ajili ya masuala ya mazao baada ya kuvuna zinatumika ipasavyo ili kufikia malengo yaliyoainishwa kwenye mkakati
Ili kuwa na mwelekeo thabiti wa utekelezaji wa mkakati huu, uhamasishaji na ukusanyaji wa fedha kwa ajili ya kutekeleza afua za Mkakati wa Usimamizi wa Mazao baada ya Kuvuna kutoka kwa wafadhlili mbalimbali utasimamiwa kwa utaratibu maalum kama ule wa Programu ya Pili ya Maendeleo ya Kilimo. Kama italazimika, utaratibu wa fedha utahitaji kusaini Randama ya Makubaliano kati ya Serikali ya Tanzania na Wadau wa Maendeleo watakaokubaliana na taratibu za utendaji kazi wa mfuko wa fedha za pamoja wa serikali wa ugawaji fedha na ugavi wa pembejeo.
Fedha za miradi kutoka kwa wabia wengine wa maendeleo zitawasilishwa tofauti kwenye mawasilisho ya bajeti na Hazina itatoa ushauri ipasavyo. Matumizi ya mwaka pendekezwa yatakuwa ni msingi wa kupanga matumizi ya Mkakati wa Kitaifa wa Usimamizi wa Mazao baada ya Kuvuna yatakayowekwa kwenye bajeti zitakazowasilishwa. Fedha za shughuli za Usimamizi wa upotevu wa mazao baada ya kuvuna, zitaratibiwa na Wizara ya Kilimo kwa kushirikiana na Wizara za Kisekta pamoja na wadau wengine.
Kutokana na uzoefu uliopo, vyanzo vya fedha vinaweza kuwa hivi vifuatavyo:
Fedha za Kitaifa: Chanzo kikubwa cha fedha za Taifa ni zile za mapato yatokanayo na ukusanyaji wa kodi. Wizara, idara na wakala mbalimbali pamoja na Mamlaka za Serikali za Mitaa hupewa fedha hizi kupitia Mwongozo wao wa Matumizi utakaoainishwa kwenye bajeti za matumizi ya kawaida na za maendeleo. Utoaji fedha kwa ajili ya afua za usimamizi wa mazao baada ya kuvuna kwenye Wizara, Idara, Wakala na Serikali za Mitaa zinaweza kupatikana kwa kupitia mpango huu. Vyanzo vingine vya fedha za ndani ni
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-202944
fedha zinazopatikana kwa ushirikiano wa Serikali na sekta binafsi na zile zinazotoka kwenye asasi zisizo za kiserikali. Fedha hizi zinaweza kutumika kwa ajili ya shughuli zilizopangwa kwa kufuata mipango iliyowekwa kwa ajili ya matumizi ya fedha hizo.
Fedha za Kimataifa: Fedha za Kimataifa kwa ajili ya Usimamizi wa Mazao baada ya Kuvuna kama vile Benki ya Dunia, Benki ya Maendeleo Afrika na fedha za makubaliano kati ya nchi inayofadhili na nchi inayofadhiliwa. Fedha za makubaliano kati ya nchi mbili hizo huingizwa nchini kupitia taasisi maalumu za ufadhili kutoka nchi wahisani. Msaada rasmi wa nyongeza huingizwa kupitia mashirika mbalimbali ya Kimataifa na taasisi zisizo za Kiserikali za Kimataifa. Baadhi ya Wafadhili huelekeza misaada kwenye kanda na wengine kwenye mitandao ya kikanda- kwa mfano SADC, EAC na AU. Matakwa ya baadhi ya wafadhili huelekezwa kwenye masuala maalum ya Upotevu wa Mazao baada ya Kuvuna.
Fedha za Mikataba ya Kimataifa: Fedha hizi zinahusiana na utekelezaji wa Miongozo na makubaliano ya Umoja wa Mataifa katika kusaidia utekelezaji wa shughuli za usimamizi wa mazao baada ya kuvuna.
4.4 Ufuatiliaji na Tathmini Mfumo wa Ufuatiliaji na Tathmini ya Mkakati wa Usimamizi wa Upotevu wa Mazao baada ya Kuvuna una majukumu ya kufanya ufuatiliaji na tathmini kwa kazi zote zilizopangwa na kuchukua hatua stahiki kwa changamoto zitakazojitokeza wakati wa utekelezaji wa mkakati pale itakapohitajika. Ingawa, uratibu wa zoezi la ufuatiliaji na tathmini ya mkakati utafanywa kwa kiasi kikubwa na Wizara ya Kilimo. Ni dhahiri kuwa kazi za ufuatiliaji na tathmini zinatakiwa kutekelezwa kwa ushirikiano wa wadau mbalimbali ili kuongeza usahihi wa matokeo ya ufuatiliaji na tathmini kwenye mnyororo mzima wa thamani. Zoezi la Ufuatiliaji na Tathmini ya ndani na nje utafanyika ipasavyo. Kutakuwa na Ufuaitiliaji na Tathmini shirikishi katikati na mwisho wa kipindi cha utekelezaji wa mkakati.
Shughuli za Ufuatiliaji zinahusisha ukusanyaji wa taarifa, uchambuzi, mchanganuo na uwasilishaji wa matokeo kwenye Kamati Kuu ya Utendaji ya mkakati pamoja na kwenye Majukwaa na Wadau husika. Lengo ni kulinganisha malengo yaliyopangwa na matokeo yake. Ufuatiliaji na Tathmini ni chombo muhimu kitakachowawezesha wadau kugundua tofauti zozote kutoka kwenye malengo yaliyopangwa kwa wakati na kufanya marekebisho stahiki.
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-2029 45
Lengo kuu la tathmini ni kujifunza kutoka uzoefu uliopatikana wakati wa utekelezaji wa afua za usimamizi na kuziwasilisha Wizara ya Kilimo na wadau wengine ili kupima kasi na uzito wa matokeo ya kupunguza upotevu wa mazao ya chakula baada ya kuvuna katika kipindi cha utekelezaji kama ilivyotarajiwa.
Zoezi la Ufuatiliaji na Tathmini litahusisha yafuatayo: -
i. Kutathmini iwapo shabaha zilizopangwa kwenye Mkakati ni sahihi
ii. Kutathmini iwapo utekelezaji wa Mkakati unafikia matokeo yaliyotarajiwa
iii. Kutathmini iwapo rasilimali za kutosha watu na fedha) zinahamasishwa ili kutekeleza Mkakati.
iv. Kutathmini Ufanisi wa matumizi ya rasilimali zilizopov. Kutathmini sababu zilizofanya/zilizosababisha kutotekeleza
baadhi ya kazi zilizokubaliwavi. Kutathmini ufanisi wa Wizara ya Kilimo katika kuongoza
utekelezaji wa Mkakati.
Mfumo wa Ufuatiliaji na Tathmini utarejewa kila mwaka ili kubaini vipengele vinavyohitaji marekebisho au kuondolewa.
Kwa kuwa Mkakati wa Usimamizi wa Upotevu wa Mazao baada ya kuvuna umepangwa kwa miaka 10, kutakuwa na tathmini ya mkakati kila miaka mitatu kwa kutumia mthamini wa nje asiyehusika na mkakati ili kubaini mabadiliko yanayoweza kuathiri ufanisi wa Mkakati kwa kipindi kinachobaki cha utekelezaji. Katika utekelezaji wa mkakati huu, Ufuatliaji na tathmini utatumia malengo na viashiria vya Azimio la Malabo.
4.5 Utaratibu wa utoaji taarifaMfumo wa kutoa taarifa utafuata utaratibu serikali ambapo kwenye ngazi ya mamlaka ya serikali za mitaa ambapo taarifa za utekelezaji zitaandaliwa na kuwasilishwa katika Sekretariet ya Mkoa. Taarifa za kutoka wilayani na mkoani zitajumuishwa na kuwasilishwa kwenye ngazi ya Taifa.
Kwa kuwa masuala ya usimamizi wa upotevu wa mazao baada ya kuvuna yapo chini ya Sekta ya Kilimo na Programu ya Pili ya Maendeleo ya Kilimo ndio mwongozo wa kutekeleza mipango ya kuendeleza sekta ya kilimo nchini, taarifa za utekelezaji wa Mkakati wa Usimamizi wa Mazao baada ya Kuvuna zitaripotiwa chini ya
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-202946
Sekretariet ya Program ya Pili ya Maendeleo ya Kilimo. Taarifa zitawasilishwa kwa kila robo muhula na kwa mwaka na zitahusisha:
i. Muhtasari wa maendeleo ya utekelezaji wa mpango kazi, yakiwemo mapitio ya changamoto zozote zilizojitokeza;
ii. Muhtasari wa matumizi ya rasilimali fedha yanayohusiana na malengo ya miradi;
Muhtasari wa matokeo yaliyopatikana, ikiwemo nakala ya mwongozo wa matokeo unaoonesha malengo ya utendaji na ufanisi wake. Malengo ya utendaji hayatarajiwi kubadilika kwenye taarifa za kila robo muhula. Hata hivyo, timu ya utekelezaji inatarajiwa kutayarisha muhtasari wa maendeleo ya ufuatiliaji utendaji na kuainisha changamoto zinazoweza kuathiri mafanikio ya malengo ya miradi.
Katika ngazi ya Wilaya, mwakilishi wa wilaya husika katika utekelezaji wa Usimamizi a Upotevu wa Mazao baada ya kuvuna chini ya usimamizi wa Afisa Kilimo wa Wilaya atakuwa na jukumu la kuandaa ripoti za Usimamizi wa Mazao baada ya Kuvuna katika ngazi ya Wilaya na kuziwasilisha ngazi ya mkoa. Kwenye ngazi ya Mkoa, mwakilishi wa mkoa husika katika utekelezaji wa usimamizi wa Mazao baada ya Kuvuna atachambua na kuandaa taarifa za Wilaya zote katika Mkoa wake na kuziwasilisha kwenye Wizara husika, ambayo ni Ofisi ya Rais-TAMISEMI na nakala kuwasilishwa Wizara ya Kilimo.
Kwenye ngazi ya taifa, kitengo cha Usimamizi wa Upotevu wa Mazao baada ya Kuvuna chini ya Wizara ya Kilimo kitakuwa na jukumu la kuandaa na kuchambua taarifa zote za mikoa. Masuala yaliyotambuliwa yatawasilishwa kwa kikundi kazi husika kwa ajili ya utekelezaji. Masuala yanayohitaji maamuzi ya ngazi za juu, yatapelekwa kwenye Kamati ya Juu ya Utendaji kwa utekelezaji.Taarifa zitazingatia kwa makini upatikanaji wa rasilimali zinazohitajika kutekeleza Mkakati wa Usimamizi wa Mazao baada ya Kuvuna, mafanikio ya shabaha lengwa, vikwazo vinavyozuia utekelezaji wa shughuli zilizopangwa na hatua zitakazofuatia.
Kitengo husika cha Wizara ya Kilimo kitapewa jukumu la kuandaa taarifa za mkakati kwa kina, kwa kutia mkazo malengo na mafanikio mahsusi, vikwazo vilivyojitokeza wakati wa utekelezaji, hatua zilizochukuliwa kutatua vikwazo hivyo na kupendekeza hatua muhimu za kufuata.
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-2029 47
MAREJEO
Abass, A.B., Ndunguru, G., Mamiro, P., Alenkhe, B., Mlingi, N., and Bekunda, M. (2014): Post- harvest food losses in a maize-based farming system of a semi-arid savannah area of Tanzania. Journal of Stored Products Research 57: 49-57
De Lucia, M., and Assennato, D. (1994): Agricultural engineering in development. Post-harvest operations and management of food grains. FAO Agricultural Service Bulletin No. 93.
FAO (2011): Global Food Losses and Food Waste: Extent, Causes and Prevention. Rome, Italy. FAO and World Bank (2010): FAO/World Bank Workshop onReducing Post-Harvest Losses in Grain Supply Chains in Africa; Lessons Learned and Practical Guidelines. Rome, Italy
FARA, (2006). Framework for African Agricultural Productivity. Retrieved from http://faraafrica.org/wp-content/uploads/2015/04/FAAP_English.pdf.
Hodges, Buzby, and Bennett, (2011). Postharvest losses and waste in developed and less developed countries: opportunities to improve resource use. Retrieved from http://ucanr.edu/datastoreFiles/234-2203.pdf.
Kimanya M.E, De Meulenaer B, Roberfroid D, Lachat C, Kolsteren P. (2010). Fumonisin exposure through maize in complementary foods is inversely associ-ated with linear growth of infants in Tanzania. Mol Nutr Food Res 54:1659–1667; doi:10.1002/mnfr.200900483.
Mutungi, C. & Affognon, H, (2013). Fighting food losses in Tanzania: The way forward for postharvest research and innovations.
Mittal, A. et al, (2007). Effect of maternal factors on nutritional status of 1-5-year- old children in urban slum population
Parfitt, J., Barthel, M., and Macnaughton, S. (2010). Food waste within food supply chains: quantification and potential for change to 2050. Retrieved from http://rstb.royalsocietypublishing.org/content/royptb/365/1554/3065.full.pdf.
Regmi, A., Deepak, M.S., James, L., Seale Jr., Bearnstein, J.et (2001). Cross-country analysis of food consumption patterns. Retrieved fromhttps://www.researchgate.net/publication/281582351_Crosscountry_analysiof_food_consumption_patterns.
REPOA, (2014). Annual report. Retrieved fromhttp://www.repoa.or.tz/documents_storage/REPOA_2014_Annual_Report.pdf.
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-202948
Suleiman, R., Rosentrater, K. A., & Bern, C. J. (2015). Evaluation of maize weevils Sitophilus zeamais Motschulsky infestation on seven varieties of maize. Journal of Stored Products Research, 64, 97-102.
Tefera, T. (2012). Post-harvest losses in African maize in the face of increasing food shortage. Food Security , 4(2), 267-277.
TFDA, (2012). Guidelines for application for registration of pre-packaged food in Tanzania. Retrieved from https://tanzania.go.tz/egov_uploads/documents/2012-9-17_guidelines_registration_of_pre-packaged_foods_sw.pdf.
United Nations, (2011). Human Development Report. Sustainability and Equity: A better Future for All. Retrived from http://hdr.undp.org/sites/default/files/reports/271/hdr_2011_en_complete.pdf.
URT (1962). Agricultural Produce Act no. 56 of 1962.
URT (1991). The Food Security Act N0. 4 of 1991. Retrieved fromhttp://www.kilimo.go.tz/uploads/regulations/The_Food_Security_Act__1991.pdf
URT (2008). Agricultural Marketing Policy, Ministry of Industry, Trade and Marketing, Governemnt Printer, Dar es Salaam
URT (2010). Tanzania Demographic Health Survey. National Bureau of Statistics, Retrievedfromhttps://dhsprogram.com/pubs/pdf/FR243/FR243[24June2011].pdf.
URT (2013). National Agriculture Policy, Ministry of Agriculture Food Security and Cooperatives, Governemnt Printer, Dar es Salaam.
World Bank, (2010). Annual report. Retrieved from http://siteresource.worldbank.org/EXTANNREP2010/Resources/WorldBank-AnnualReport2010.pdf.
World Bank (2011): Missing Food: the Case of Post-harvest Grain Losses in Sub-Saharan Africa, Report No. 60371-AFR.
World Bank et al., 2011). Health, Nutrition and Population (HNP) Discussion Paper Chronic Emergency: Why NCDs Matter. Retrieved from https://openknowledge.worldbank.org/bitstream/handle/10986/13591/639270WP0Chron0Box 0361533B00PUBLIC0.pdf sequence=1.
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-2029 49
ORO
DH
A Y
A V
IAM
BATI
SHO
KIA
MBA
TISH
O 1
: Muu
ndo
wa
utek
elez
aji M
alen
go M
kaka
ti
Leng
o M
kaka
ti A
: Kuj
enga
uel
ewa
kuhu
su u
beba
ji bo
ra il
i kuo
ngez
a uf
anis
i na
kupu
nguz
a up
otev
u w
a m
azao
ka
tika
mny
oror
o w
a th
aman
i.Na
.Af
ua za
Us
imam
iziSh
abah
aSh
ughu
liM
ajuku
mu
Vias
hiria
vya
Utek
eleza
jiM
atok
eo
Tara
jiwa
1K
utek
elez
a M
kaka
ti w
a M
awas
ilian
o ili
ku
utaa
rifu
umm
a
kuhu
su u
pote
vu
wa
chak
ula,
sa
babu
na
mad
hara
yak
e
Ang
alau
ain
a ta
tu
za m
awas
ilian
o
kuhu
su s
abab
u,
mad
hara
na h
atua
za
kudh
ibiti
upo
tevu
zi
we
zim
eand
aliw
a na
kuk
abid
hiw
a kw
a w
aten
daji
kwen
ye m
nyor
oro
wa
tham
ani i
fikap
o m
wak
a 20
22.
Ang
alau
ain
a 5
za
maw
asili
ano
ziw
e zi
met
umik
a ifi
kapo
20
22
Kuk
usan
ya, k
uand
aa n
a ku
tafs
iri ta
arifa
ili z
itum
ike
kwa
urah
isi.
Kua
ndaa
na
kuta
ngaz
a pr
ogra
mu
mba
limba
li ku
pitia
vy
ombo
vya
hab
ari (
Kam
a Re
dio,
TV,
mac
hapi
sho,
ru
ning
a, m
itand
ao y
a ki
jam
ii,
Vitu
o vy
a M
aarif
a vy
a K
ata,
M
aone
sho
ya K
itaifa
na
Kim
atai
fa y
a K
ibia
shar
a na
M
aone
sho
maa
lum
ya
Kili
mo)
Kut
afsi
ri ta
arifa
zili
zoku
sany
wa
na k
uziw
eka
katik
a ka
tika
mfu
mo
mzu
ri w
a ut
umia
ji.
Kuw
ezes
ha v
ituo
vya
Maa
rifa
vya
Kat
a na
Elim
u ya
Vite
ndo
kwa
Wak
ulim
a ka
ma
njia
za
ku
pata
taar
ifa z
a U
sim
amiz
i w
a U
pote
vu M
azao
baa
da y
a ku
vuna
Wiz
ara
ya
Kili
mo
ikis
hirik
iana
na
wad
au
mba
limba
li
Idad
i ya
wat
enda
ji w
alio
pata
ta
arifa
hus
ika
kuhu
suU
sim
amiz
i wa
M
azao
Baa
da y
a K
uvun
a
Kup
ungu
za
upot
evu
baad
a ya
K
uvun
a.
Maa
muz
i sah
ihi
na ta
arifa
kuh
usu
Upo
tevu
wa
M
azao
baa
da
ya k
uvun
a na
Te
knol
ojia
za
baad
a ya
Kuv
una
katik
a ng
azi z
ote.
Kuw
a na
mip
ango
bo
ra k
wa
ajili
ya
kut
ekel
eza
shug
huli
za
Upo
tevu
m
azao
baa
da
na T
ekno
lojia
za
baad
a ya
Kuv
una.
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-202950
2K
uwaj
enge
a uw
ezo
wat
enda
ji w
ote
wa
Usi
mam
izi
wa
Upo
tevu
baa
da
ya k
uvun
a
Ang
alau
as
ilim
ia 8
0 ya
w
aten
daji
waw
e
wam
ewez
eshw
a ku
husu
Usi
mam
izi
baad
a ya
kuv
una
ifika
po 2
029
Kua
ndaa
na
kuoa
nish
a vi
tini
kwa
ajili
ya
maf
unzo
ya
Usi
mam
izi b
aada
ya
kuvu
na
Kuf
anya
maf
unzo
kw
a w
aten
daji
wot
e w
a U
sim
amm
izi b
aada
ya
Kuv
una
kwen
ye m
nyor
oro
wa
tham
ani.
Kut
oa v
ifaa
vya
kufa
nyia
kaz
i kw
a M
aafis
a U
gani
.
Wiz
ara
ya K
ilim
o ik
ishi
rikia
na
na w
adau
w
engi
ne
wah
usik
a.
Idad
i ya
wat
enda
ji w
alio
wez
eshw
a ku
husu
U
sim
amiz
i wa
Maz
ao b
aada
ya
kuvu
na
Kia
si k
ikub
wa
cha
upot
evu
maz
ao
baad
a ya
kuv
una
ki
mep
uguz
wa
Mip
ango
ya
utek
elez
aji
wa
mas
uala
ya
Usi
mam
izi
baad
a ya
kuv
una
imeb
ores
hwa
3K
ubor
esha
mbi
nu
za u
beba
ji m
azao
kw
a w
aten
daji
maa
lum
kw
enye
m
nyor
oro
wa
tham
ani
Ang
alau
asi
limia
50
ya
wat
enda
ji w
akub
ali
mbi
nu
bora
za
ubeb
aji
maz
ao ifi
kapo
m
wak
a20
24
Kuf
anya
maf
unzo
ya
mbi
nu
bora
za
ubeb
aji m
azao
kw
a w
aten
daji
wot
e kw
enye
m
nyor
oro
wa
tham
ani
Kuu
elim
isha
um
ma
kuh
usu
ub
ebaj
i maz
ao m
zuri
kulik
o w
ote,
ili k
uhak
ikis
ha u
bora
na
usal
ama
kwen
ye m
nyor
oro
wa
tham
ani w
a m
azao
.
Wiz
ara
ya K
ilim
o ik
ishi
rikia
na
nata
asis
i m
aalu
mu.
Idad
i ya
wat
enda
ji w
alio
kuba
li ku
tum
ia n
jia
mak
husu
si n
a nz
uri k
ulik
o zo
te z
a ub
ebaj
i m
azao
.
Kia
si c
ha a
silim
ia
ya u
pote
vu
kim
epun
guzw
a
Ubo
ra w
a bi
dhaa
za
ndan
i zi
lizoo
ngez
wa
tham
ani
umeo
ngez
wa
Ubo
ra n
a us
alam
a w
a m
azao
um
eong
ezw
a.
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-2029 51
4K
uong
eza
uwez
o w
a w
aten
gene
zaji
wa
Usi
mam
izi
baad
a ya
Kuv
una
ili k
uzui
a na
ku
dhib
iti s
ibik
o la
maz
ao. M
f. su
mu
kuvu
, sum
u/vi
uatil
ifu v
ya
kuua
wad
udu
wah
arib
ifu n
a m
abak
i men
gine
ya
kem
ikal
i
Tatiz
o la
su
mu
kuvu
lim
epun
guzw
a
hadi
kufi
kia
10µg
/kg
kw
a S
umu
kuvu
yot
e n
a 5
µg/k
g k
wa
AFB
1
Kuf
anya
uta
fiti w
a ki
na il
i ku
bain
i sab
abu,
uku
bwa
na
usam
baaj
i wa
sum
u ku
vu,
viua
tilifu
vya
kuu
a w
adud
u w
ahar
ibifu
/ na
sib
iko
la
mab
aki y
a ke
mik
ali n
ying
ine
Kuf
anya
uta
fiti w
a ki
na il
i ku
bain
i sab
abu,
uku
bwa
na
usam
baaj
i wa
Sum
u K
uvu,
da
wa
za k
uuw
a w
adud
u/ n
a si
bik
o la
mab
aki y
a ke
mik
ali
nyin
gin
e
Kuk
uza
hat
ua s
ahih
i za
afua
za
kup
ungu
za s
ibik
o la
sum
u ku
vu
Wiz
ara
ya K
ilim
o ik
ishi
rikia
na
na t
aasi
si
maa
lum
u
Kiw
ango
cha
si
biko
la m
abak
i ya
sum
u ku
vu
imep
ungu
a
Sibi
ko la
su
mu
kuvu
lim
epun
guzw
a.
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-202952
Leng
o M
kaka
ti B:
Kuk
uza
Uw
epo,
Upa
tikan
aji n
a U
kuba
likaj
i wa
Tekn
oloj
ia Z
ilizo
fany
iwa
Mar
ekeb
isho
ili
Kud
hibi
ti U
pote
vu w
a M
azao
baa
da y
a K
uvun
a.
NaAf
ua za
Us
imam
iziSh
abah
aSh
ughu
liM
ajuku
mu
Vias
hiria
vya
Uten
daji
Mat
okeo
Ta
rajiw
a
1K
uwez
esha
W
aten
daj
i ku
husu
ufa
ham
u na
utu
mia
ji w
a
tekn
oloj
ia z
a b
aad
a ya
kuv
una
ziliz
ojar
ibiw
a
Ang
alau
asi
limia
80
ya
Wat
enda
ji w
anaj
ua
na k
utum
ia
tekn
oloj
ia b
aada
ya
kuv
una
ifika
po m
wak
a 20
29
Kuw
ahim
iza
na
kuw
ashi
rikis
ha
Wat
enda
ji ku
husu
mat
umiz
i sa
hihi
ya
tekn
oloj
ia
za b
aada
ya
kuvu
na
Kus
amba
za ta
arifa
za
tekn
oloj
ia z
ilizo
po.
Kuu
nga
mko
no n
a ku
wez
esha
utu
mia
ji w
a te
knol
ojia
zi
lizoj
arib
iwa
Wiz
ara
ya K
ilim
o ik
ishi
rikia
na
na ta
asis
i ny
ingi
ne
maa
lum
.
Idad
i ya
wat
enda
ji w
anao
faha
mu
na k
utum
ia
tekn
oloj
ia
ziliz
obor
eshw
a.
Upo
tevu
wa
maz
ao b
aada
ya
kuv
una
umep
ungu
zwa
kwa
kias
i kik
ubw
a
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-2029 53
Leng
o M
kaka
ti C:
Kuw
ezes
ha M
fum
o w
a M
asok
o, ik
iwa
ni p
amoj
a na
Miu
ndom
binu
na
vifa
a vy
a ku
tunz
ia il
i m
azao
yas
ihar
ibik
e m
apem
a na
kup
ungu
za u
pote
vu b
aada
ya
kuvu
na.
NaAf
ua za
Us
imam
iziSh
abah
aSh
ughu
liM
ajuku
mu
Vias
hiria
vya
Uten
daji
Mat
okeo
Tara
jiwa
1K
uong
eza
upat
ikan
aji
wa
mas
oko
ili
kupu
nguz
a up
otev
u ba
ada
ya
kuvu
na
Upa
tikan
aji
wa
mas
oko
umeo
ngez
eka
ifika
po 2
024
Uta
ratib
u w
a ku
dhib
iti n
a w
a ki
utaw
ala
ili k
uong
eza
upat
ikan
aji w
a m
asok
o ifi
kapo
2024
um
eele
zwa
Kua
nzis
ha n
a ku
imar
isha
mfu
mo
ulio
po w
a ub
ebaj
i (m
f. U
safir
isha
ji na
utu
nzaj
i) ka
tika
ngaz
i zot
e, m
agha
la
ya k
upak
ia, v
yum
ba
barid
i, m
agha
la y
a ku
tunz
ia n
a m
asilo
)K
uanz
isha
mfu
mo
wa
utoa
ji ta
arifa
wa
mas
oko
Kuu
nga
mko
no
utar
atib
u w
a m
asok
o ya
leta
yo
mae
ndel
eo,
Mf.
WRS
na
muu
ngan
iko
wak
e kw
a m
fum
o w
a ku
badi
li bi
dhaa
Wiz
ara
ya E
limu
na M
amla
ka z
a Se
rikal
i za
mita
a zi
kish
iriki
ana
na
wad
au h
usik
a
Idad
i ya
sher
ia
na ta
ratib
u za
ki
utaw
ala
kuhu
su
kupa
ta m
asok
o zi
meb
ores
hwa
Upa
tikan
aji w
a m
asok
o na
bei
bo
ra z
imep
atik
ana
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-202954
2U
pat
ikan
aji
wa
rasi
limal
i w
atu
wal
iob
obea
ku
sim
amia
m
ifum
o ya
so
ko n
a m
iund
o m
binu
yak
e
Idad
i bor
a ya
ra
silim
ali w
atu
wal
iobo
bea
kupa
tikan
a ifi
kapo
202
9
Kuf
undi
sha
au
kuaj
iri w
ataa
lam
u w
enye
uju
zi
maa
lum
u
Wiz
ara
ya K
ilim
o na
Mam
laka
za
Serik
ali z
a M
itaa
ziki
shiri
kian
a na
ta
asis
i maa
lum
u
Idad
i ya
wat
u w
alio
bobe
a ka
tika
PH
M
imep
atik
a
Kun
a ub
ora
wa
maz
ao k
atik
a m
nyor
oro
wa
maz
ao w
a nd
ani
3K
uwez
esha
M
fum
o w
a U
toaj
i ta
arifa
wa
Mas
oko
Maz
ao y
ote
mak
uu/b
idha
a zi
mei
ngiz
wa
katik
a M
fum
o w
a Te
ham
a ul
ioha
kiki
wa
Kui
mar
isha
Mfu
mo
wa
kuto
a ta
arifa
wa
mas
oko
Kuu
ngan
isha
m
azao
mak
uu
katik
a m
fum
o w
a ku
badi
lisha
na
maz
ao
Wiz
ara
ya K
ilim
o na
Mam
laka
za
Serik
ali z
a M
itaa
kwa
kush
iriki
ana
na
Taas
isi M
uhim
u
Mfu
mo
wa
Uto
aji T
aarif
a w
a M
asok
o U
mea
nzis
hwa
Upa
tikan
aji
wa
mas
oko
na
bei z
inaz
ofaa
vi
mep
atik
ana
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-2029 55
Leng
o M
kaka
ti D
: Kuk
uza
utafi
ti na
uvu
mbu
zi w
a te
knol
ojia
na
njia
mpy
a na
zin
azof
aa il
i kup
ungu
za u
pote
vu
wa
maz
ao
Na.
Afua
za
usim
amizi
Male
ngo
Shug
huli
Maju
kum
uVi
ashir
ia vy
a Ut
enda
jiM
atok
eo
Tara
jiwa
1K
uhak
ikis
ha
uwep
o w
a m
asul
a ya
U
sim
amiz
i b
aad
a ya
ku
vuna
kat
ika
tafit
i za
kilim
o
Mas
uala
ya
PH
M
yam
ehus
ishw
a ka
tika
mau
dhui
za
tafit
i za
kilim
o
Kup
itia
upya
na
kuin
giz
a m
asua
la y
a U
sim
amiz
i wa
Up
otev
u w
a M
azao
baa
da
ya k
uvun
a ka
tika
taas
isi
zina
zojih
usis
ha n
a ut
afiti
wa
kilim
o
Wiz
ara
ya K
ilim
o ik
ishi
rikia
na
na ta
asis
i za
maf
unzo
na
tafit
i za
kilim
o
Kia
si c
ha
tafit
i juu
ya
mas
uala
ya
Usi
mam
izi w
a U
pote
vu w
a M
azao
baa
da
ya k
uvun
a zi
mef
anyw
a
2K
uanz
isha
m
fum
o w
a ut
unza
ji ta
arifa
za
Mka
kati
wa
Usi
mam
izi w
a U
pot
evu
wa
Maz
ao b
aad
a ya
kuv
una
Mfu
mo
wa
kutu
nza
taar
ifa z
a us
imam
izi w
a up
otev
u w
a m
azao
baa
da
ya k
uvun
a kw
a m
azao
ya
kili
mo
umea
nzis
hwa
ifika
po 2
020
Kua
nzis
ha k
anzi
data
Kuf
anya
tafit
i kw
a un
dani
ili
kuju
a ha
li ha
lisi y
a up
otev
u nc
hini
, uki
wem
o ut
afiti
kuhu
su
ukub
wa
wa
upot
evu
baa
da
ya
kuvu
naK
ukus
anya
taar
ifa z
a ki
la s
iku
ili k
uwa
na ta
arifa
za
upot
evu
baad
a ya
kuv
una
na p
iaK
ufan
ya ta
fiti z
a vi
tend
o/ze
nye
mre
ngo
wa
soko
kuh
usu
mas
uala
ya
usim
amizi
wa
upot
evu
wa
maz
ao b
aada
ya
kuvu
na
Wiz
ara
ya K
ilim
o ik
ishi
rikan
a na
wad
au
husi
ka
Utu
nzaj
i na
taar
ifa z
a U
sim
amiz
i wa
upot
evu
wa
maz
ao b
aada
ya
kuv
una
unaf
anyi
ka
Utu
nzaj
i wa
maz
ao b
aad
a ya
kuv
una
umep
ung
uzw
a
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-202956
Leng
o M
kaka
ti E:
Kup
itia
upya
na
kuw
eka
mio
ngoz
o m
ipya
na
sher
ia k
uwez
esha
viw
ango
na
vite
ndo
vita
kavy
opun
guza
upo
tevu
baa
da y
a ku
vuna
.
Na.
Afua
za u
simam
iziM
aleng
oSh
ughu
liM
ajuku
mu
Vias
hiria
M
atok
eo Ta
rajiw
a
1K
uing
iza
mam
bo
ya U
sim
amiz
i wa
Upo
tevu
wa
Maz
ao
baad
a ya
kuv
una
ka
tika
sher
ia
ziliz
opo
Sher
ia
ziliz
opo
zim
epiti
wa
upya
ifika
po
2024
.
Kuz
itam
bua
na
kuzi
pitia
she
ria
husi
ka z
a ba
ada
ya k
uvun
a
Wiz
ara
ya K
ilim
o ik
ishi
rikia
na
na w
adau
hu
sika
Mas
uala
ya
usim
amiz
i ba
ada
ya
kuvu
na
yam
eing
izw
a ka
tika
sher
ia
ziliz
opo
Ute
ndaj
i wa
PHM
um
ebor
eshw
a
Kut
ambu
a na
ku
pitia
upy
a m
iong
ozo
Wiz
ara
ya K
ilim
o ik
ishi
rikia
na
na w
adau
hu
sika
Ute
ndaj
i wa
PHM
um
ebor
eshw
a
Kut
oa e
limu
kwa
wad
au
maa
lum
juu
ya s
heria
na
mio
ngoz
o ili
yopi
tiwa
Wiz
ara
ya K
ilim
o ik
ishi
rikia
na
na w
adau
hu
sika
Ute
ndaj
i wa
PHM
um
ebor
eshw
a
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-2029 57
Leng
o M
kaka
ti F:
Kui
mar
isha
ura
tibu,
ush
iriki
ano
na u
husi
shw
aji w
a w
adau
ili k
uwez
esha
ute
kele
zaji
wa
mka
kati
Na.
Afua
za u
simam
iziM
aleng
oSh
ughu
liM
ajuku
mu
1K
uhak
ikis
ha
urat
ibu
unaf
anyi
ka
katik
a ng
azi z
ote
ili k
uong
eza
ushi
rikis
hwaj
i wa
wat
enda
ji m
uhim
u ka
tika
mas
ula
ya u
sim
amiz
i wa
upot
evu
wa
maz
ao
baad
a ya
kuv
una
Uta
ratib
u w
a ku
ratib
u ka
tika
ngaz
i za
Taifa
, Mik
oa
na M
amla
ka
za S
erik
ali
za M
itaa
umeb
ores
hwa
ifika
po 2
020.
Kut
ambu
a na
kuw
eka
kum
buku
mbu
za
taas
isi
zina
zojis
hugh
ulis
ha n
a m
asua
la y
a us
imam
izi w
a m
azao
baa
da y
akuv
una
Kuh
amas
isha
na
kuel
imis
ha ta
asis
i zi
nazo
fany
a m
aam
uzi
Wiz
ara
ya K
ilim
o ik
ishi
rikia
na
na w
adau
hu
sika
Mfu
mo
wa
urat
ibu
hai
Kite
ngo
cha
urat
ibu
kim
eim
aris
wa
Upo
tevu
ba
ada
ya
kuvu
na
umep
ung
uaU
linzi
wa
chak
ula
umeo
ngez
eka
Kui
mar
isha
maj
ukw
aa y
a us
imam
izi w
a up
otev
u nc
hini
Tan
zani
a K
uim
aris
ha k
iteng
o ch
a ur
atib
u ki
taifa
kilic
hopo
w
izara
niK
uten
geza
TWG
na
kute
ua
mhu
sika
mku
u ka
tika
ngaz
i ya
Sek
retr
ieti
-TA
MIS
EMI
Kut
oa v
itend
ea k
azi v
ya
kuto
sha
kwa
kite
ngo
cha
urat
ibu
kita
ifa.
Kuu
nga
mko
no u
tend
aji
wa
kite
ngo
cha
utat
ibu
kita
ifa.
Sekr
etar
ieti
imea
nzis
hwa
Wah
usik
a w
akuu
Se
kret
arie
ti ya
TA
MIS
EMI
wam
epat
ikan
aB
ajet
i im
eong
ezek
aK
iasi
cha
vi
tend
ea k
azi
kim
epat
ikan
aId
adi y
a m
ikut
ano
imef
anyw
a
Ufa
nisi
wa
uten
daji
umeb
ores
hwa
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-202958
2 K
uanz
isha
na
kus
imam
ia
vifu
rush
i vya
m
otis
ha y
a uw
ekez
aji i
li ku
onge
za u
shiri
ki
wa
kise
kta
Vifu
rush
i vy
a m
otis
ha
vim
eand
aliw
a na
ku
teke
lezw
a ifi
kapo
202
2.
Kut
ambu
a na
kut
atua
vi
kazo
vya
uw
ekez
aji
katik
a us
imam
izi b
aad
a ya
ku
vuna
Kut
enge
neza
vifu
rush
i vya
uw
ekez
aji k
atik
a m
nyor
oro
wa
tham
ani w
a ba
ada
ya
kuvu
na
Wiz
ara
ya K
ilim
o na
wad
au
wen
gin
e hu
sika
Kia
si fu
lani
ch
a vi
furu
shi
vya
mot
isha
vi
mea
nzis
hwa
na
kute
kele
zwa
Upo
tevu
ba
ada
ya
kuvu
na
umep
ungu
zwa
Ulin
zi w
a ch
akul
a na
lish
e um
eong
ezw
a3
Kui
mar
isha
msi
ngi
wa
rasi
limal
i w
atu
kwa
taas
isi
zina
zoon
goza
ka
tika
upot
evu
baad
a ya
kuv
una
Asi
limia
80
ya m
sing
i wa
rasi
limal
i wat
u in
apat
ikan
a ku
tatu
a m
atat
izo
ya u
pote
vu
maz
ao b
aada
ya
kuv
una
ifika
po 2
025
Kua
jiri w
afan
yaka
zi
Kuk
uza
uwez
o na
m
aend
eleo
ya
rasi
limal
i w
atu
kuhu
su u
sim
amiz
i wa
upot
evu
baad
a ya
kuv
una
Kut
oa v
itend
ea k
azi n
a ku
haki
kish
a m
azin
gira
bo
ra
Wiz
ara
ya K
ilim
o na
wad
au
wen
gine
hu
sika
Kia
si c
ha m
sing
i w
a ra
silim
ali w
atu
kipo
Ufa
nisi
ut
enda
ji um
epat
ikan
a
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-2029 59
Leng
o M
kaka
ti G
: K
uim
aris
ha M
kaka
ti w
a U
sim
amiz
i m
azao
baa
da y
a ku
vuna
na
kupu
nguz
a m
adha
ra y
a m
abad
iliko
ya
tabi
a nc
hi
Na.
Afu
a za
U
sim
amiz
i M
alen
goSh
ughu
liM
ajuk
umu
Via
shiri
a vy
a U
tend
aji
Mat
okeo
tara
jiwa
1 K
uhak
ikis
ha
upat
ikan
aji w
a ta
arifa
za
tab
ianc
hi
zina
zohu
sian
ana
up
otev
u b
aad
a ya
ku
vuna
,m
ifum
o ya
ut
oaji
taar
ifa
map
ema
Taha
dhar
i zot
e kw
a ha
tari
husi
ka
zita
tam
buliw
a m
apem
a
Mab
adili
ko y
a ta
bia
nchi
kw
enye
m
nyor
oro
wa
tham
ani w
a us
imam
izi
wa
upot
evu
wa
maz
aoba
ada
ya
kuvu
na
unaz
indu
liwa
ifika
po 2
029
Kuw
aelim
isha
wak
ulim
a na
w
adau
wen
gine
kuh
usu
mad
hara
ya
tabi
a nc
hi
kwa
usim
amiz
i wa
upot
evu
wa
maz
ao b
aada
ya
kuvu
naK
uwae
limis
ha w
akul
ima
juu
ya u
patik
anaj
i wa
maz
aom
balim
bali
yana
yost
ahim
ilim
adha
ra y
a ta
bia
nchi
K
uim
aris
ha u
husi
ano
na m
tiriri
ko w
a ta
rifa
za
maz
ao y
a ki
limo
na h
ali
ya h
ewa
nchi
ni T
anza
nia
Mita
zam
o ya
Mam
laka
ya
Hal
i ya
Hew
a, k
uhus
u ta
bia
nchi
za
msi
mu
na
za m
wez
i
Wiz
ara
ya K
ilim
o ik
ishi
rikia
na
na w
adau
m
balim
bali
Vifu
rush
i vya
ta
arifa
m
balim
bali
maa
lum
u kw
a us
imam
izi w
a up
otev
u w
a m
azao
baa
da
ya k
uvun
a zi
met
olew
a
Taar
ifa m
balim
bali
ku
husu
ong
ezek
o la
hu
dum
a m
balim
bali
za
mic
haka
to y
a m
ipan
go
na b
ajet
i ya
PHM
Ong
ezek
o la
Ufa
nisi
ka
tika
shug
huli
za P
HM
Kup
itish
a PH
M
inay
ooen
dana
na
tabi
a nc
hi
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-202960
Kua
nzis
ha
tekn
oloj
ia n
a m
iund
ombi
nu
imar
a zi
nazo
husu
sh
ughu
li ba
ada
ya k
uvun
a
Uku
balik
aji
kwa
asili
mia
80
wa
tekn
oloj
ia
imar
a ba
ada
ya k
uvun
a na
zi
nazo
him
ili
mab
adili
ko
ya ta
bia
nchi
ifi
kapo
202
9.
Asi
limia
80
ya
kuje
nga
uwez
o kw
a w
auza
ji na
w
atej
a ku
husu
ua
nzis
haji
na
uend
esha
jii
wa
tekn
oloj
ia
baad
a ku
vuna
zin
azos
tahi
mili
m
abad
iliko
ya
tabi
a nc
hi u
we
umef
anyi
ka
ifika
po
2029
Kuj
enga
na
kuka
raba
ti m
agha
la/ v
ifaa
vya
uhifa
dhi,
sehe
mu
za
kupa
kia
maz
ao, n
a vi
faa
vya
uhifa
dhi
vye
nye
ubar
idi
Kug
awa
na k
ufun
ga v
ifaa
vya
kusin
dika
maz
ao
Kus
aidi
a na
mna
ya
utum
iaji
wa
vifa
a bo
ra
vya
uhifa
dhi,
mf m
asilo
ya
chu
ma
Kup
itish
a nj
ia b
ora
za u
hifa
hi z
ikiw
emo
tekn
oloj
ia z
enye
kia
si
kido
go c
ha k
abon
i
Wiz
ara
ya K
ilim
o na
wad
au
wen
gine
hu
sika
Viw
ango
vya
uk
ubal
ikaj
i na
uto
faut
i ili
kupe
ndek
eza
aina
m
balim
bali
za te
knol
ojia
ba
ada
kuvu
na
Kia
si c
ha
wau
zaji
na
wan
ufai
ka
waw
e w
amek
ubal
iut
umia
ji w
a te
knol
ojia
im
ara
baad
a ya
ku
vuna
Uw
ezo
wa
ujuz
i na
tekn
oloj
ia, p
amoj
a na
upa
tikan
aji w
a te
knol
ojia
imar
a ba
ada
ya k
uvun
a na
zi
nazo
enda
na n
a ta
bia
nchi
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-2029 61
Leng
o M
kaka
ti H
: Kus
hugh
ulik
ia U
pung
ufu
wa
fedh
a kw
a aj
ili y
a sh
ughu
li ba
ada
ya k
uvun
a
Na.
Afua
za
Usim
amizi
M
aleng
oSh
ughu
liM
ajuku
mu
Vias
hiria
vya
Uten
daji
Mat
okeo
tara
jiwa
1.K
uanz
isha
ub
unifu
wa
upat
ikan
aji
fedh
a ili
kus
aidi
a uw
ekez
aji,
kuta
ngaz
a,
kusa
mba
za
na k
utum
ia
tekn
oloj
ia b
aada
ku
vuna
Uto
aji w
a ta
arifa
za
uko
pesh
aji k
wa
wat
enda
ji, ta
asis
i nd
ogo
ndog
o na
wak
ulim
a ili
waw
ekez
aji
kwen
ye
tekn
oloj
ia b
aad
a ku
vuna
uw
e um
eong
ezek
a kw
a as
ilim
ia 5
0 ifi
kapo
20
22.
Kuw
aelim
isha
wak
ulim
a na
w
adau
wen
gine
kuh
usu
mad
hara
ya
tabi
a nc
hi
kwa
usim
amiz
i wa
upot
evu
wa
maz
ao b
aada
ya
kuvu
na.
Kuw
aelim
isha
w
akul
ima
kuhu
su
upat
ikan
aji w
a m
azao
mba
limba
li ya
nayo
stah
imili
mad
hara
ya
tabi
a nc
hi
Kui
mar
isha
uhu
sian
o na
mtir
iriko
wa
taar
ifa
za m
azao
ya
kilim
o na
ha
li ya
hew
a nc
hini
Ta
nzan
iaM
itaza
mo
ya M
amla
ka
ya H
ali y
a H
ewa,
ku
husu
tabi
a nc
hi z
a m
sim
u na
za
mw
ezi
Wiz
ara
ya K
ilim
o ik
ishi
rikia
na
na w
adau
m
balim
bali
Vifu
rush
i vya
ta
arifa
m
balim
bali
maa
lum
kw
a us
imam
izi w
a up
otev
u w
a m
azao
baa
da
ya k
uvun
a zi
met
olew
a
Taar
ifa m
balim
bali
ku
husu
ong
ezek
o la
hud
uma
mba
limba
li za
m
icha
kato
ya
mip
ango
na
baje
ti ya
PH
M
Ong
ezek
o la
U
fani
si k
atik
a sh
ughu
liza
za P
HM
Kup
itish
a PH
M
inay
ooen
dana
na
Ta
bia
nchi
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-202962
2.K
uanz
isha
tekn
oloj
ia n
am
iund
ombi
nu
imar
azi
nazo
husu
sh
ughu
liba
ada
ya
kuvu
na
Uku
balik
aji k
wa
asili
mia
80w
a te
knol
ojia
imar
a ba
ada
ya k
uvun
a na
zin
azoh
imili
m
abad
iliko
ya
tabi
a nc
hi ifi
kap
2029
.
Asi
limia
80
ya
kuje
nga
uwez
o kw
a w
auza
ji na
w
atej
a ku
husu
ua
nzish
aji n
a ue
ndes
hajii
w
a te
knol
ojia
zin
azos
tahi
mili
m
abad
iliko
ya
tabi
a nc
hi b
aada
ya
kuv
una
uwe
umef
anyi
ka
ifika
po
2027
.
Kuj
enga
na
kuka
raba
ti m
agha
la/ v
ifaa
vya
uhifa
dhi,
sehe
mu
za
kupa
kia
maz
ao, n
a vi
faa
vya
uhifa
dhi
vy
enye
ub
arid
i
Kug
awa
na k
ufun
ga
vifa
a vy
a ku
sindi
ka
maz
ao
Kus
aidi
a na
mna
ya
utum
iaji
wa
vifa
a bo
ra
vya
uhifa
dhi,
mfa
no,
mas
ilo y
a ch
uma
Kup
itish
a nj
ia b
ora
za u
hifa
dhi z
ikiw
emo
tekn
oloj
ia z
enye
kia
si
kido
go c
ha k
abon
i
Wiz
ara
ya
Kili
mo
na w
adau
w
engi
ne h
usik
a
Viw
ango
vya
uk
ubal
ikaj
i na
uto
faut
i ili
kupe
ndek
eza
aina
mba
limba
li za
tekn
oloj
ia
baad
a ku
vuna
Kia
si c
ha
wau
zaji
na
wan
ufai
ka w
awe
wam
ekub
ali
utum
iaji
wa
tekn
oloj
ia
imar
a ba
ada
ya
kuvu
na
Uw
ezo
wa
ujuz
i na
tekn
oloj
ia, p
amoj
a na
upa
tikan
aji w
a te
knol
ojia
baa
da
kuvu
na im
ara
na
zina
zoen
dana
tabi
a nc
hi u
mep
atik
ana
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-2029 63
3K
uhak
ikis
ha
upat
ikan
aji w
a ra
silim
ali w
atu
katik
a ta
asis
i za
mst
ari w
a m
bel
e zi
nazo
jis
hug
hulis
ha
na u
pot
evu
baa
da
ya
kuvu
na
Kia
si c
ha fe
dha
cha
kuto
sha
kusa
idia
shu
ghul
i za
upo
tevu
ba
ada
ya k
uvun
a zi
napa
tikan
a ifi
kapo
mw
aka
2025
Kut
etea
upa
tikan
aji
wa
fedh
a kw
a aj
ili y
a m
ipan
go y
a up
otev
u ba
ada
ya k
uvun
a kw
enye
nga
zi z
ote
za
waf
anya
maa
muz
i.
Kuo
mba
fedh
a kw
a aj
ili y
a sh
ughu
li za
up
otev
u ba
ada
ya
kuvu
na k
utok
a kw
a w
adau
wot
e w
a se
kta
za u
mm
a na
bin
afsi
Kui
ngiz
a us
imam
izi
wa
upot
evu
wa
maz
ao
baad
a ya
kuv
una
katik
a pr
ogra
mu
na
mira
di m
ingi
illiy
opo
ya
kim
koa
na k
itaifa
.K
uand
aa m
pang
o w
a ue
ndes
haji
na b
ajet
i kw
a aj
ili y
a ku
ekel
eza
mka
kati
Wiiz
ara
ya
Kili
mo
na
wad
au w
engi
ne
husi
ka
Kia
si c
ha fe
dha
ki
licho
eten
gw
a kw
a aj
ili y
a sh
ughu
li za
up
otev
u b
aad
a ya
kuv
una
Ufa
nisi
wa
uten
daj
i um
eong
ezw
a
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-202964
Leng
o M
kaka
ti I:
Kua
ndaa
njia
bor
a za
Uku
sany
aji t
aarif
a na
Uka
diria
ji U
pote
vu w
a M
azao
baa
da y
a ku
vuna
nc
hini
NaAf
ua za
us
imam
iziM
aleng
oSh
ughu
liM
ajuku
mu
Vias
hiria
vya
Uten
daji
Mat
okeo
Tara
jiwa
1K
upiti
a na
ku
unga
nish
a nj
ia z
a ku
tath
min
i U
pote
vu w
a M
azao
baa
da
ya k
uvun
a zi
lizop
o
Njia
za
kaw
aida
za
FA
O n
a FL
AM
zik
ubal
ike
zipi
tishw
e na
ku
kuba
lika
kwa
kias
i kik
ubw
a kw
a aj
ili y
a ta
thm
ini
ya u
pot
evu
baa
da
ya k
uvun
a
Kut
ambu
a nj
ia z
a ku
tath
min
i upo
tevu
ba
ada
ya k
uvun
a zi
lizop
o
Kup
itia
na
kupe
ndek
eza
njia
bo
ra z
a ku
tath
min
i up
otev
u w
a M
azao
ba
ada
ya k
uvun
a
Kui
ngiz
a nj
ia z
a ku
tath
min
i upo
tevu
ba
ada
ya k
uvun
a zi
lizok
ubal
ika
katik
a m
taal
a w
a ta
asis
i za
kuto
a m
afun
zo
Wiz
ara
ya K
ilim
o na
wad
au
wen
gine
hu
sika
Njia
bor
a za
ku
tath
min
i up
otev
u ba
ada
ya k
uvun
a
Njia
sah
ihi z
a ku
kusa
nya
upot
evu
baa
da
ya k
uvun
a zi
lizob
ores
hwa
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-2029 65
KIAMBATISHO NAMBA 2: MUUNDO WA TAARIFA YA ROBO MWAKA
Idara/Kitengo kinachotoa
taarifa:…………………………………………………..
KIPINDI: Kutoka:
Hadi:
Idara/Kitengo Shughuli Zilizopangwa
Maelezo Mafanikio
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-202966
KIAMBATISHO NAMBA 3: MUUNDO WA TAARIFA YA ROBO MWAKA
Idara/Kitengo kinachotoa taarifa:……………………………………………. KIPINDI: Kutoka: Hadi: Lengo Makakati
Lengo lililopangwa
Shughuli zilizopangwa
Mafanikio ya Shughuli
Bajeti iliyopangwa
Matumizi Halisi
Maelezo yanayoelezea tofauti kati ya utendaji halisi na tarajiwa na mapendekezo ya kukabiliana na changamoto kuu
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-2029 67
KIAMBATISHO NAMBA 5: ORODHA YA WAJUMBE WA KIKOSI KAZI
S/n Jina Nafasi Taasisi
1 Mr. Clepin Josephat Mwenyekiti Ministry of Agriculture
2 Mr. Honest Mseri Katibu Agricultural Non-State Actors Forum (ANSAF)
3 Ms. Magreth Natai Mjumbe Ministry of Agriculture
4 Ms. Josephine Amolo Mjumbe Ministry of Agriculture
5 Mr. Daktari Hango Mjumbe Ministry of Agriculture
6 Mr. James Ngwira Mjumbe Ministry of Agriculture
7 Mr. Sadoti Makwaruzi Mjumbe Ministry of Agriculture
8 Ms. Zakia Lamwala Mjumbe Ministry of Agriculture
9 Mr. John Chassama Mjumbe Ministry of Industry and Trade
10 Ms Shamim Daudi Mjumbe HELVETAS Swiss Intercooperation
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-202968
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA YA KUVUNA | 2019-2029 69
2019 -2029
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA
YA KUVUNA
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Wizara ya Kilimo
2019 -2029
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA
YA KUVUNA
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Wizara ya Kilimo
2019 -2029
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA
YA KUVUNA
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Wizara ya Kilimo
2019 -2029
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA
YA KUVUNA
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Wizara ya Kilimo
2019 -2029
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA
YA KUVUNA
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Wizara ya Kilimo
2019 -2029
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA
YA KUVUNA
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Wizara ya Kilimo
2019 -2029
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA
YA KUVUNA
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Wizara ya Kilimo
2019 -2029
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA
YA KUVUNA
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Wizara ya Kilimo
2019 -2029
MKAKATI WA TAIFA WA USIMAMIZI WA MAZAO BAADA
YA KUVUNA
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Wizara ya Kilimo
Kwa Maelezo ya kina kuhusu Mkakati wa Kitaifa wa Kupunguza Upotevu wa Mazao baada ya Kuvuna:
Wasilianana
Katibu MKuuWizara ya Kilimo
Simu: +255 262321407/2320035 | Nukushi: +255 262320037Barua pepe: [email protected]
Au tembelea tovuti: www. kilimo.go.tz