Upload
others
View
62
Download
0
Embed Size (px)
Citation preview
SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR
HOTUBA YA WAZIRI WA ELIMU NA
MAFUNZO YA AMALI
MHESHIMIWA
RIZIKI PEMBE JUMA (MBM)
KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA
MATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA
WA FEDHA 2019/2020
Mei, 2019
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 ii
YALIYOMO
UTANGULIZI.......................................................................... 1
MIRADI YA SEKTA YA ELIMU…………………………. 4
MAFANIKIO YA UTEKELEZAJI WA VIPAUMBELE
VYA MWAKA WA FEDHA WA 2018/19…………………… 4
UTEKELEZAJI WA KAZI ZA WIZARA KWA MWAKA
2018/19………………………………………………………….
6
MUUNDO WA PROGRAMU………………………………. 6
MAELEZO YA UTEKELEZAJI WA PROGRAMU…….. 6
PROGRAMU YA KWANZA: ELIMU YA MAANDALIZI
NA MSINGI…………………………………………………..
7
PROGRAMU YA PILI: ELIMU YA SEKONDARI………. 10
PROGRAMU YA TATU: ELIMU YA JUU ……… 14
Programu ndogo ya Mafunzo ya Ualimu……………………… 14
Huduma ya Elimu ya Juu, Ushauri na Utafiti………………… 16
Huduma ya Sayansi na Teknolojia……………………………. 18
Huduma ya Mikopo ya Elimu ya Juu…………………………. 19
Huduma ya Uratibu wa Elimu ya Juu………………………… 21
PROGRAMU YA NNE: ELIMU MBADALA NA
MAFUNZO YA AMALI…………………………………….
23
Programu ndogo ya Mafunzo ya Amali………………………….. 23
Programu ndogo ya Elimu Mbadala na Watu Wazima………….. 26
PROGRAMU YA TANO: UBORA WA ELIMU…………….. 29
Huduma ya Mitaala na Vifaa vya Kufundishia…….…………….. 30
Huduma ya Upimaji na Tathmini ya Elimu……………………… 31
Huduma ya Ukaguzi wa Elimu………………………………...... 34
Huduma za Maktaba…………………………………………....... 34
Huduma ya Urajisi wa Elimu……………………………………. 37
Programu ndogo ya Elimu Mjumuisho na Stadi za Maisha…...... 40
Programu ndogo ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano katika
Elimu……………………………………………………………..
43
Programu ndogo ya Michezo na Utamaduni katika Skuli……….. 44
PROGRAMU YA SITA: UTAWALA NA UONGOZI …........ 46
Programu ndogo ya Uongozi Kiujumla………………………….. 47
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 iii
Programu ndogo ya Uratibu wa Shughuli za Mipango, Sera na
Utafiti …………………………………………………………
48
Programu ndogo ya Uratibu wa Shughuli za Elimu
Pemba…………………………………………………………….
50
MPANGO WA UTEKELEZAJI KWA MWAKA 2019/20
KATIKA MFUMO WA PROGRAMU………………………..
51
Vipaumbele………………………………………………………. 51
Miradi mitano ya Sekta ya Elimu………………………………... 54
Programu za Wizara ya Elimu…………………………………… 54
MAELEZO YA PROGRAMU ZA ELIMU……………………... 54
PROGRAMU YA KWANZA: ELIMU YA MAANDALIZI
NA MSINGI……………………………………………….…….
54
PROGRAMU YA PILI: ELIMU YA SEKONDARI………… 55
PROGRAMU YA TATU: ELIMU YA JUU ………………… 56
Programu ndogo ya Mafunzo ya Ualimu……………………....... 56
Huduma ya Elimu ya Juu, Ushauri na Utafiti……………………. 57
Huduma ya Sayansi na Teknolojia……………………………..... 58
Huduma ya Mikopo ya Elimu ya Juu…………………………..... 58
Huduma ya Uratibu wa Elimu ya Juu……………………………. 59
PROGRAMU YA NNE: ELIMU MBADALA NA
MAFUNZO YA AMALI………………………………………..
60
Programu ndogo ya Mafunzo ya Amali………………………….. 60
Programu ndogo ya Elimu Mbadala na Watu Wazima………….. 61
PROGRAMU YA TANO: UBORA WA ELIMU 61
Huduma ya Mitaala na Vifaa vya Kufundishia………………….. 62
Huduma ya Upimaji na Tathmini ya Elimu…………………....... 62
Huduma ya Ukaguzi wa Elimu………………………………...... 63
Huduma za Maktaba…………………………………………….. 63
Huduma ya Urajisi wa Elimu…………………………………… 64
Programu ndogo ya Elimu Mjumuisho na Stadi za Maisha…….. 65
Programu ndogo ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano katika
Elimu…………………………………………………..................
65
Programu ndogo ya Michezo na Utamaduni katika Skuli………. 66
PROGRAMU YA SITA: UTAWALA NA UONGOZI ……… 66
Programu ndogo ya Uongozi Kiujumla……………………….. 67
Programu ndogo ya Uratibu wa Shughuli za Mipango, Sera na
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 iv
Utafiti…………………………………………………………….. 67
Programu ndogo ya kuratibu shughuli za elimu Pemba………..... 68
MGAWANYO WA FEDHA KWA PROGRAMU…………… 68
PROGRAMU YA KWANZA: ELIMU YA MAANDALIZI
NA MSINGI……………………………………………………...
PROGRAMU YA PILI: ELIMU YA SEKONDARI ………
68
69
PROGRAMU YA TATU: ELIMU YA JUU………………… 69
PROGRAMU YA NNE: ELIMU MBADALA NA
MAFUNZO YA AMALI………………………………………
69
PROGRAMU YA TANO: UBORA WA ELIMU…………… 70
PROGRAMU YA SITA: UTAWALA NA UONGOZI …….. 70
JUMLA YA GHARAMA ZA WIZARA YA ELIMU NA
MAFUNZO YA AMALI………………………………………..
71
SHUKURANI……………………………………………………. 71
KIAMBATISHO…………………………………………………. 73
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 1
HOTUBA YA WAZIRI WA ELIMU NA MAFUNZO YA
AMALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO KWA
MWAKA WA FEDHA 2019/2020
UTANGULIZI
1. Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja kwa Baraza lako
Tukufu liingie katika Kamati ili niweze kutoa maelezo ya
makadirio ya mapato na matumizi ya Fedha ya Wizara ya
Elimu na Mafunzo ya Amali kwa mwaka 2019/2020.
2. Mheshimiwa Spika, Kwanza kabisa, napenda kumshukuru
Mwenyezi Mungu kwa Rehma zake kwetu na akatujaalia
uhai, uzima na siha njema. Vile vile akatuwezesha tukakutana
katika kikao hiki cha Bajeti katika kipindi cha Awamu ya pili
ya Kiongozi wetu mahiri Mheshimiwa Rais wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Ali Mohammed
Shein. Namuomba Mwenyezi Mungu atuzidishie Kheri katika
Neema zake na anipe uwezo na uwasilishaji fasaha wa hotuba
hii ya makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara yangu. Pia
namuomba Mwenyezi Mungu atujaalie wasaa wajumbe wote
wa kuichangia vizuri na hatimaye Baraza lako tukufu liweze
kuipitisha kwa kauli moja Bajeti ya Wizara yangu.
3. Mheshimiwa Spika, pili, nachukua nafasi hii kumpongeza
kwa dhati Mheshimiwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein kwa uongozi
wake imara, wenye busara na moyo thabiti katika kusimamia
uimarishaji wa huduma za jamii kwa wananchi wake ikiwemo
huduma ya elimu. Pongezi za pekee kwa kutimiza miaka tisa
ya Uongozi wake iliyoleta maendeleo makubwa katika Sekta
ya Elimu nchini. Maendeleo yaliyotokana na juhudi zake za
kuhakikisha changamoto zote zinazowakabili watoto na vijana
wote kupata elimu anapambana nazo. Hii imetokana na
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 2
kuiwezesha Wizara kufidia gharama za elimu baada ya kufuta
michango ya lazima inayotolewa na wazee katika ngazi ya
elimu ya lazima. Uongozi wa Wizara unatoa shukrani za dhati
kwa Mheshimiwa Rais wetu kwa ushauri na miongozo
anayoitoa yenye lengo la kuiendeleza sekta yetu ya elimu. Pia
tunampongeza Mheshimiwa kwa kutimiza miaka 71 ya umri
wake. Mwenyezi Mungu amzidishie umri wenye kheri, afya
njema na maarifa zaidi ili aendelee kuiongoza na kuiendeleza
nchi yetu. Vile vile, napenda kutoa pongezi na shukurani za
dhati kwa Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar,
Mheshimiwa Balozi Seif Ali Iddi, kwa utendaji wake mzuri,
wenye kukuza mashirikiano ya Taasisi yetu na wadau
mbalimbali wa elimu wa ndani na nje ya nchi pamoja na
michango yake binafsi katika kuiendeleza sekta ya elimu.
4. Mheshimiwa Spika, Vilevile, nachukua fursa hii
kukupongeza wewe binafsi, Naibu Spika pamoja na
Mwenyekiti wa Chombo hichi adhimu cha kujadili na
kupitisha maamuzi ya nchi yetu kwa mashirikiano yenu na
miongozo mizuri mnayotupatia inayopelekea kupata ufanisi
katika utendaji wa majukumu yetu unaochangia katika kuleta
maendeleo ya Taifa letu. Namuomba Mwenyezi Mungu
akuzidishieni busara, hekima, umahiri na uadilifu katika
kuliongoza Baraza hili tukufu.
5. Mheshimiwa Spika, Naomba pia Shukurani za dhati
nizifikishe kwa wajumbe wote wa Baraza hili Tukufu na hasa
Wajumbe wa Kamati ya Ustawi wa Jamii chini ya uongozi
mahiri wa Mwenyekiti wake Mheshimiwa Mwanaasha
Khamis Juma kwa ushauri na maelekezo ya kimaendeleo
wanayotupatia katika utekelezaji wa shughuli zetu mbalimbali
wanapopata muda wa kuwa nasi katika taasisi za Wizara ya
Elimu na Mafunzo ya Amali.
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 3
6. Mheshimiwa Spika, Nachukua fursa hii ya pekee
kumpongeza aliyekuwa Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo
ya Amali Mheshimiwa Mmanga Mjengo Mjawiri kwa
kuchaguliwa kuwa Waziri wa Kilimo, Mali Asili, Mifugo na
Uvuvi kutokana na mashirikiano makubwa aliyonipa na
utendaji wake mzuri uliyopelekea kupanda juu zaidi. Ni imani
yangu kwamba tutaendelea kukuza mashirikiano yetu katika
utekelezaji wa majukumu yetu. Pia, napenda kutoa pongezi
zangu za dhati kwa Mheshimiwa Mohammed Ramia
Abdulwawa kwa kuchaguliwa kuwa Waziri wa Fedha na
Mipango
7. Mheshimiwa Spika, Kwa dhati kabisa, nampongeza
Mheshimiwa Simai Mohammed Said wa Jimbo la Tunguu
kwa kuteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya
Amali na kwa jitihada kubwa anazozionyesha kwa kipindi
kifupi katika kuhakikisha kuwa sekta ya elimu na mafunzo ya
amali inapiga hatua kubwa zaidi ya maendeleo. Ingawa ni
kipindi kifupi tangu kuteuliwa kwake lakini juhudi na
mashirikiano yake yananipa faraja na imani ya kufikia
malengo ya sekta yetu. Namuomba Mwenyezi Mungu
atuzidishie mashirikiano, uadilifu, imani, ujasiri na maarifa
mazuri zaidi katika kuyakabili majukumu yetu na kuliongoza
Taifa letu kupata maendeleo endelevu. Aidha, nawapongeza
watendaji wote wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali
wakiwemo Katibu Mkuu, Manaibu Katibu Wakuu,
Wakurugenzi, Maafisa wa ngazi mbalimbali wa Wizara,
Viongozi na watendaji mbalimbali wa Ofisi ya Rais, Tawala
za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalumu za Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar bila kuzisahau Kamati zetu za Skuli
ambazo kwa pamoja zinashiriki katika kuleta maendeleo ya
elimu. Pia, nazipongeza Bodi za Mashirika na Taasisi za
Elimu kwa michango na ushauri mbali mbali wanaotupatia.
Aidha, nawashukuru sana walimu, wazazi, wanafunzi na
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 4
washirika wote wa elimu wa ndani na nje kwa kushiriki
kikamilifu katika kusaidia harakati za utoaji na upatikanaji wa
huduma ya elimu iliyo bora kwa watoto, vijana na wazee wetu
waliokosa fursa hiyo. Mola awazidishie moyo wa imani na
upendo ili michango yao iendelee kuwapatia elimu wahitaji
wote kwa kiwango chenye ubora.
8. Mheshimiwa Spika, Mwisho nawashukuru sana watendaji
wa Wizara ya Fedha na Mipango kwa ushirikiano wao ambao
umechangia katika kuimarisha huduma za elimu katika
mwaka 2018/19. Ni matumaini yetu kuwa ushirikiano huo
utaimarika katika utekelezaji wa shughuli za Sekta ya Elimu
kwa lengo la kuimarisha upatikanaji wa huduma ya elimu
katika Taifa letu kwa kupitia kauli mbiu ya Wizara yetu ya
“Elimu Bora Kwanza”.
9. Mheshimiwa Spika, sasa naomba nitoe maelezo ya
utekelezaji wa kazi kwa mwaka wa fedha wa 2018/19.
MIRADI YA SEKTA YA ELIMU
10. Mheshimiwa Spika, kwa mwaka wa fedha 2018/2019,
Wizara ilitekeleza kazi zake kupitia miradi mikuu mitano,
ifuatayo: -
1. Uimarishaji wa Elimu ya Maandalizi
2. Uimarishaji wa Elimu ya Msingi
3. Uimarishaji wa Elimu ya Lazima
4. Uimarishaji wa Elimu Mbadala na Amali
5. Miundombinu katika elimu
MAFANIKIO YA UTEKELEZAJI WA VIPAUMBELE
VYA WIZARA KWA MWAKA WA FEDHA WA 2018/19
11. Mheshimiwa Spika, kwa mwaka wa fedha wa 2018/19,
mafanikio mbalimbali yalipatikana katika utekelezaji wa sekta
ya elimu yakiwemo: -
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 5
• Kuongezeka kwa idadi na asilimia ya uandikishaji
kwa wanafunzi katika ngazi za maandalizi na msingi.
Jumla ya wanafunzi 85,974 sawa na asilimia 81.4
wameandikishwa katika madarasa ya maandalizi kwa
mwaka 2019. Hii ni ongezeko la asilimia 17.3
ikilinganishwa na wanafunzi 72,151 sawa na asilimia
69.4 walioandikishwa mwaka 2018.
• Matokeo ya mitihani ya Darasa la Sita, Kidato cha
Pili na Kidato cha Nne yameimarika kwa kiasi katika
mwaka 2018 ikilinganishwa na matokeo ya mwaka
2017.
• Jumla ya TSh. 2,105,351,985 za ruzuku zimetolewa
kwa skuli 204 za sekondari za Serikali kwa ajili ya
uendeshaji baada ya kufutwa michango ya lazima
kutoka kwa wazee.
• Jumla ya katuni 5,000 za chaki kwa skuli za
sekondari na mabuku 3,831,400 yamenunuliwa. Kati
ya hayo, 2,537,500 yamegaiwa kwa wanafunzi wa
sekondari na 1,293,980 ya wanafunzi wa maandalizi
na msingi.
• Jumla ya wanafunzi 41 wanaendelea na masomo ya
Udaktari wa Mifugo nchini China. Kati ya hao,
wanafunzi 10 watarejea Nchini. Watano wanahitimu
masomo yao na watano wanakuja kwa “field work”
ya kumalizia masomo yao.
• Jumla ya vikalio 44,620 (viti na meza) vimenunuliwa
na kusambazwa katika skuli mbalimbali za sekondari
Unguja na Pemba.
• Ujenzi wa skuli 9 za sekondari, Ujenzi wa skuli ya
Msingi ya Fuoni Mambosasa Unguja na Ngadu
iliyopo Mkumbuu Pemba umekamilika. Aidha,
ujenzi wa Skuli ya Sekondari ya Kibuteni unaendelea
na unatarajiwa kukamilika mwezi Septemba, 2019.
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 6
• Ujenzi wa Vituo vya Mafunzo ya Amali unaendelea
kwa asilimia 42 Makunduchi na 52 kwa Daya.
• Matayarisho ya mapitio ya Mitaala ya Elimu ya
Maandalizi ili uendane na hali halisi ya mahitaji
yameanza.
• Walimu 451 wenye sifa za kufundisha ngazi ya
elimu ya Msingi na Sekondari wameajiriwa.
UTEKELEZAJI WA KAZI ZA WIZARA KWA
MWAKA 2018/19
12. Mheshimiwa Spika, sasa naomba kuwasilisha utekelezaji wa
mpango wa maendeleo ya elimu kwa mwaka wa fedha wa
2018/19 kwa kupitia programu sita za Wizara yangu.
MUUNDO WA PROGRAMU
13. Mheshimiwa Spika, programu kuu za Wizara ya Elimu na
Mafunzo ya Amali ni hizi zifuatazo: -
Programu ya 1: Elimu ya Msingi
Programu ya 2: Elimu ya Sekondari.
Programu ya 3: Elimu ya Juu
Programu ya 4: Elimu Mbadala na Mafunzo ya Amali
Programu ya 5: Ubora wa Elimu
Programu ya 6: Uongozi na Utawala
MAELEZO YA UTEKELEZAJI KWA PROGRAMU
14. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2018/19 Wizara
ilitekeleza kazi zake kupitia Programu nilizoziainisha kwa
kuzingatia makubaliano ya maendeleo ya elimu ya Kitaifa na
Kimataifa ikiwemo Dira ya Taifa ya Maendeleo ya Zanzibar
ya mwaka 2020, Lengo la MKUZA III la kuzingatia usawa
katika kutoa elimu bora, vipaumbele vya Sekta yangu pamoja
na lengo la nne la Maendeleo Endelevu Duniani.
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 7
15. Mheshimiwa Spika, Programu hizo zilitekelezwa kwa
mashirikiano ya karibu sana kati ya Serikali, Jamii na
Washirika wa Maendeleo wa ndani na nje ya Zanzibar.
Programu zote hizo zilitengewa jumla ya TSh.
179,605,900,000. Kati ya fedha hizo, TSh. 96,164,299,000
zilitengwa kwa matumizi ya kazi za kawaida na TSh.
83,441,600,000 kwa kazi za maendeleo. Kati ya fedha hizi za
maendeleo, TSh. 5,890,000,000 ni mchango wa SMZ na TSh.
77,551, 600,000 ni mchango wa wahisani zikiwemo fedha za
mkopo kutoka Benki ya Kiarabu ya Afrika (Badea), Benki ya
Maendeleo ya Afrika (ADB) na Benki ya Dunia.
16. Mheshimiwa Spika, hadi kufikia Aprili, 2019, jumla ya TSh.
131,300,891,146 sawa na asilimia 73 ya makadirio
zilipatikana. Kati ya fedha hizo, TSh. 83,801,880,907 za SMZ
kwa matumizi ya kawaida pamoja na ruzuku ambazo ni sawa
na asilimia 87.14 zilipatikana. Kwa upande wa fedha za
maendeleo, jumla ya TSh. 47,499,010,239 zilipatikana, kati ya
hizo TSh. 44,738,005,239 kutoka kwa wahisani ambazo ni
sawa na asilimia 58 ya makadirio ya fedha za wahisani na
TSh. 2,761,005,000 za Serikali sawa na asilimia 47.
Kiambatisho namba 49 kinatoa ufafanuzi zaidi.
17. Mheshimiwa Spika, Utekelezaji halisi wa Programu za
Wizara yangu ni kama ifuatavyo: -
PROGRAMU YA KWANZA:
ELIMU YA MAANDALIZI NA MSINGI
18. Mheshimiwa Spika, Programu hii inahusika na uimarishaji
na utoaji wa elimu ya maandalizi na msingi kwa wanafunzi
wenye umri kati ya miaka minne na kumi na mbili. Programu
hii inatekelezwa kupitia mfumo wa Ugatuzi. Hivyo, kazi za
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 8
kawaida za Programu hii zimegatuliwa rasmi na
zinatekelezwa na Wizara ya Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za
Mikoa na Idara Maalumu za Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar kwa mashirikiano ya karibu sana na Wizara yangu.
Katika utekelezaji wa programu hii kitaifa, Wizara
inashirikiana na washirika wa maendeleo wa ndani na wa nje
wakiwemo Ofisi ya Mufti na Jumuiya ya Zanzibar Madrasa
Early Childhood Program (ZMECP) katika kusimamia
Madrasa na Vyuo vya Kur-ani ambavyo kimsingi vinatoa
elimu ya awali kwa watoto wetu, Serikali ya Jamhuri ya Watu
wa China, Global Partnership for Education (GPE), Table for
Two (TfT) ya Japan, Good Neighbors tawi la Tanzania na
Shirika la Maendeleo ya Watoto Duniani (UNICEF).
19. Mheshimiwa Spika, Kwa upande wa miradi ya maendeleo ya
Programu hii ambayo inatekelezwa na Wizara ya Elimu na
Mafunzo ya Amali ilitengewa jumla ya TSh. 10,092,100,000
kwa kazi za maendeleo kutoka kwa wahisani. Hadi kufikia
Aprili, 2019, jumla ya TSh. 6,154,072,258 sawa na asilimia
56.6 zilipatikana.
20. Mheshimiwa Spika, Utekelezaji halisi wa programu hii ni
kama hivi ifuatavyo: -
i). Ujenzi wa Skuli ya Msingi ya Fuoni Mambosasa na
Ngadu iliyopo Mkumbuu umekamilika. Aidha, jumla
ya madarasa 187 kati ya 200 yaliyoanzishwa kwa
nguvu za wananchi yamekamilika kwa kiwango cha
uezekaji na kupiga plasta, hatua ya kupaka rangi
inaendelea. Wizara inaendelea na kazi za kuezeka
madarasa 6 katika skuli za Mgenihaji na Chunga. Pia,
ujenzi huu unajumuisha vyumba 23 vikiwemo vyumba
vya walimu, maabara, vyumba vya kompyuta na vyoo.
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 9
ii). Awamu ya kwanza ya ujenzi wa Skuli ya Msingi ya
Kwarara chini ya ufadhili wa Good Neighbor ya Korea
unatarajiwa kumalizika mwezi wa Juni, 2019.
iii). Huduma ya chakula kwa skuli 27 za msingi
imeendelea kutolewa kwa Unguja na Pemba. Huduma
hii inatolewa kwa mashirikiano kati ya Wizara, Shirika
la Maendeleo ya Watoto “Partnership for Child
Development” (PCD) la Uingereza na “Table for Two”
(TfT) la Japan.
iv). Jumla ya madaftari 1,293,980 ya kuandikia wanafunzi
yakiwemo yenye mistari, yasiyo na mistari na yenye
vyumba yamenunuliwa na kukakabidhiwa Wizara ya
Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa, Serikali za
Mitaa na Idara Maalumu za SMZ kwa kugaiwa katika
skuli za maandalizi na msingi.
Matokeo ya Muda Mfupi;
i. Jumla ya wanafunzi 308,616 wameandikishwa katika
vyuo 2,773 vya Kur-ani Unguja na Pemba vyenye
jumla ya walimu 11,616.
ii. Jumla ya watoto 85,974 ambao ni sawa na asilimia
81.4 wameandikishwa katika ngazi ya elimu ya
maandalizi, wakiwemo wanawake 43,643 na wanaume
42,331 katika mwaka 2019. Hii ni sawa na ongezeko la
asilimia 17.3 ikilinganishwa na asilimia 69.4 ya
uandikishaji ya mwaka 2018. Jadweli namba 13(a),
(b) na (c) yanatoa ufafanuzi zaidi.
iii. Jumla ya wanafunzi 56,259 wapya wameandikishwa
kuanza darasa la kwanza kwa mwaka 2019. Kati yao,
wanawake 27,872 na wanaume 28,387. Aidha, jumla
ya watoto 37,680 waliopata elimu ya maandalizi
ambao ni sawa na asilimia 66.9 ya walioandikishwa
kuanza Darasa la Kwanza katika mwaka wa 2019.
Jadweli namba 15(a) na (b) yanatoa ufafanuzi zaidi.
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 10
iv. Jumla ya wanafunzi 290,510 wameandikishwa katika
ngazi ya elimu ya msingi kwa mwaka 2019 ambao ni
sawa na asilimia 118.1 Kati yao, wanawake ni 144,174
sawa na asilimia 49.6 na wanaume ni 146,336 sawa na
asilimia 50.4 Jadweli namba 14 linatoa ufafanuzi zaidi.
PROGRAMU YA PILI: ELIMU YA SEKONDARI.
21. Mheshimiwa Spika, Programu hii inalenga kutoa na
kuimarisha elimu ya sekondari. Kwa mwaka 2018/19
programu hii imetekelezwa kwa pamoja kati ya SMZ na
wafadhili wa ndani na nje ya nchi. Jumla ya TSh.
95,587,550,000 zilipangwa kutumika. Kati ya fedha hizo,
TSh. 40,415,050,000 ni kwa kazi za kawaida na TSh.
55,172,500,000 kwa miradi ya maendeleo zikiwemo
3,100,000,000 za SMZ na TSh. 52,072,500,000 za wahisani.
Hadi kufikia Aprili, 2019, jumla ya TSh. 75,533,172,197
zilipatikana sawa na asilimia 79. Kati ya fedha hizo, TSh.
34,183,454,635 sawa na asilimia 60 kwa kazi za maendeleo.
Kati ya fedha hizo, TSh. 32,130,999,635 za wafadhili kutoka
BADEA, Mfuko wa OPEC, Benki ya Dunia na Good
Neighbour sawa na asilimia 62 na TSh. 2,052,455,000 kutoka
Serikalini sawa na asilimia 66.2 zilipatikana.
22. Mheshimiwa Spika, Utekelezaji kwa programu hii ni kama
ifuatavyo: -
i). Jumla ya viti na meza 44,620 vimenunuliwa kutoka
China. Vikalio 21,767 vimeshasambazwa katika
baadhi ya skuli za sekondari za Unguja na Pemba.
Kazi ya usambazaji inaendelea. Jadweli namba 12 (f)
linaonyesha orodha wa mgao huo.
ii). Jumla ya TSh. 744,900,000/= zimetumika kwa kulipia
gharama za Mitihani ya Taifa kwa watahiniwa 14,898
wa Kidato cha Nne waliofanya mitihani Novemba,
2018. Aidha, jumla ya shilingi 82,700,000/=
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 11
zimelipwa kwa ajili ya kuwalipia wanafuzi 1,652
waliofanya mtihani ya kumalizia Kidato cha Sita
mwezi wa Mei, 2019.
iii). Mwanafunzi mmoja wa skuli ya Sekondari ya
Kiembesamaki “A” amepatiwa kifaa cha kusaidia
kusikia wakati wa kujifunza. Kifaa hicho kimegharimu
TSh. 710,000 na jumla ya wanafunzi 27 wanaotoka
maeneo ya vijijini wanaosoma Skuli ya Sekondari ya
SUZA wamelipiwa gharama ya kuwasaidia huduma ya
Chakula.
iv). Jumla ya kompyuta 23 zimenunuliwa na kusambazwa
katika skuli za sekondari ambazo zimepata idadi ndogo
ya fedha za ruzuku kutokana na idadi ndogo ya
wanafunzi katika skuli hizo. Skuli husika ni
Pongwemwera, Bandamaji, Kidimni, Ukongoroni,
Charawe, Kibuyuni, Ubago, Kibondeni, Mtende,
Ghana, Mbuyutende, Kiyongwe, Miwani, Umbuji,
Muungoni, Mgambo, na Kilombero kwa Unguja na
Skuli ya Bwagamoyo, Maziwani,Kijumbani,Mtangani,
Chwaka na Mgelema kwa Pemba. Aidha, Kompyuta
15 zilinunuliwa na kusambazwa katika skuli za
mchepuo wa biashara katika skuli ya Biashara
Mombasa kwa Unguja na Skuli ya Chasasa kwa
Pemba. Pia, Idara imepokea Kompyuta 10 zilizotolewa
na Mwakilishi wa Viti Maalum wa CCM Mkoa wa
Magharibi Kichama. Kompyuta hizo zimegaiwa
sawasawa kwa Skuli ya Sekondari ya Mbuzini na
Kisauni.
v). Vifaa vya maabara na kemikali kwa ajili ya Mitihani
ya Taifa vimenunuliwa na kusambazwa katika skuli za
sekondari 164 zenye madarasa ya kidato cha nne na 13
zenye kidato cha sita kwa Unguja na Pemba. Aidha,
TSh. 3,014,000 zimetumika kufanya matengenezo ya
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 12
chumba cha kufundushia fani ya umeme katika Skuli
ya Sekondari ya Ufundi Mikunguni.
vi). Jumla ya madaftari 2,537,500 ya wanafunzi wa
sekondari na katuni 5,000 za chaki zimenunuliwa na
kusambazwa katika skuli zote za sekondari Unguja na
Pemba. Aidha, wanafunzi 1,571 wa Unguja na Pemba
wanaoishi dakhalia wamelipiwa jumla ya TSh.
460,224,450 kwa ajili ya gharama za huduma ya
chakula.
vii). Jumla ya walimu 179 waajiriwa wapya wakiwemo 141
wa Sayansi na 38 wa Sanaa wamepatiwa mafunzo
elekezi na kupangiwa kazi ya kufundisha katika skuli
za sekondari za Mikoa mitatu ya Unguja na walimu 96
kwa upande wa Pemba. Aidha, wakutubi 41
wameajiriwa na wamepangiwa kazi ya ukutubi katika
skuli 41 za sekondari zenye maktaba.
viii). Jumla ya wanafunzi 10, walimu watano na Mratibu
mmoja walishiriki katika mashindano ya Young
Scientist yaliyofanyika Tanzania Bara. Wanafunzi hao
walitoka katika Skuli za Tumekuja, Kiembesamaki
Islamic na Benbella kwa Unguja na Skuli ya Uweleni
na Maendeleo Ngwachani kwa Pemba. Skuli ya
Tumekuja ilipata ushindi na kuzawadiwa fedha taslimu
TSh. 2,846,000.
ix). Wanafunzi 40 na walimu watano walishiriki katika
mafunzo ya TEHAMA ya wasichana yaliofanyika Dar
es salaam. Mashindano hayo yaliendelea Dodoma
ambapo mwanafunzi Haitham Idrissa Omar kutoka
mchepuo wa Kiislamu katika Chuo cha Kiislamu
Pemba alichaguliwa kuiwakilisha Zanzibar katika siku
ya Kitaifa ya TEHAMA nchini Ethiopia tarehe
24/4/2019.
x). Jumla ya wanafunzi 12,106 wamefaulu mtihani wa
Kidato cha Nne uliofanyika Novemba, 2018.
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 13
Wanafunzi 3,235 wataendelea na Kidato cha Tano
katika skuli mbalimbali za Serikali za Unguja na
Pemba. Kati ya wanafunzi hao, wanafunzi 1,244
watasomea fani ya Sanaa wakiwemo wanawake 875 na
wanaume 369. Wanafunzi 1,891 wa sayansi
wakiwemo wanawake 867 na wanaume 1,024 na
wanafunzi 100 wa fani ya biashara na kompyuta
wakiwemo wanawake 40 na 60 wanaume.
xi). Jumla ya wanafunzi 1,995 wamefanya mitihani ya
kumalizia kidato cha sita iliyoanza tarehe 06/05/2019
hadi 23/05/2019. Wanafunzi 1,672 kutoka skuli za
Serikali na 323 kutoka skuli binafsi.
xii). Jumla ya washiriki 541 walipatiwa mafunzo ya athari
za utoro wa wanafunzi, lengo la mafunzo haya ni
kuweza kuihamasisha jamii ili kupunguza au
kuondosha kabisa tatizo la utoro katika skuli zetu.
xiii). Jumla ya wanafunzi watatu (wawili wa Unguja na
mmoja kutoka Pemba) wamechanguliwa kujiunga na
masomo ya Kidato cha Kwanza katika Skuli za Mama
Salma Kikwetwe za Mkoa wa Pwani Wilaya ya Rufiji.
Matokeo ya muda mfupi;
i. Ngazi ya Elimu ya Sekondari ya awali (kidato 1 – 4)
ina jumla ya wanafunzi 130,711 sawa na asilimia 87.2
kati yao, wanafunzi 72,119 wa kidato cha kwanza na
pili (wanaume ni 33,862 na wanawake ni 38,257)
Kidato cha tatu na nne kina jumla ya wanafunzi
58,592 wakiwemo wanawake 34,497 na wanaume
24,095.
ii. Jumla ya wanafunzi 4,808 wameandikishwa katika
ngazi ya sekondari ya juu kati yao wanafunzi 2,745 ni
wa kidato cha tano wakiwemo wanawake 1,340 na
wanaume 1,405 na wanafunzi 2016 wa kidato cha sita
kati yao wanawake ni 1,027 na wanaume ni 1,036.
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 14
PROGRAMU YA TATU: ELIMU YA JUU
23. Mheshimiwa Spika, Madhumuni ya programu hii ni kutoa
elimu itakayomuwezesha muhitimu kujiajiri au kuajiriwa.
Programu hii ina programu ndogo moja ambayo ni mafunzo
ya ualimu na maeneo manne ya huduma, ikiwemo Huduma ya
Uratibu wa Elimu ya Juu, Huduma ya Mikopo ya Elimu ya
Juu, Huduma ya Sayansi na Teknolojia na Huduma ya Elimu
ya Juu, Ushauri na Utafiti. Utekelezaji wa programu hii ni
kama ifuatavyo: -
Programu ndogo ya Mafunzo ya Ualimu
24. Mheshimiwa Spika, programu hii ndogo ilitengewa jumla ya
TSh. 1,396,183,000 za SMZ kwa kuendelea kutoa mafunzo ya
ualimu katika ngazi ya Stashahada na kutoa mafunzo ya
Ualimu kazini. Hadi kufikia Aprili, 2019, jumla ya TSh.
686,314,839 sawa na asilimia 49 zilipatikana.
25. Mheshimiwa Spika, utekelezaji halisi wa programu hii ndogo
ni kama hivi ifuatavyo: -
i). Jumla ya Moduli 600 za masomo ya Jiografia na
TEHAMA zimechapishwa na kutolewa mafunzo kwa
walimu 308 wanaosomesha masomo hayo darasa la
tano na la sita ili kumudu ufundishaji sahihi wa
masomo hayo kwa wanafunzi wao.
ii). Jumla ya walimu 392 (Wanawake 132 na Wanaume
260) wa skuli za sekondari wamepatiwa mafunzo ya
ufundishaji wa mada zinazowapa tabu katika
kuzifundisha kwa masomo ya Jiografia, Historia
Kiingereza na Hisabati. Vile vile walimu hawa
wamepatiwa taaluma na mbinu za namna ya
kuwafundisha wanafunzi njia bora za kujibu maswali
ambayo hayajibiwi vizuri katika mitihani ya Taifa.
iii). Jumla ya walimu 639 wa Sanaa wanaofundisha
masomo ya Sayansi na Hisabati Kidato cha Kwanza na
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 15
cha Pili wanaendelea na mafunzo kazini ya
kuwawezesha kufundisha masomo hayo kwa umahiri
katika vituo vya walimu vya Unguja na Pemba.
Walimu hao watakapohitimu watasaidia kupunguza
tatizo la uhaba wa walimu wa Sayansi na Hisabati
katika skuli zetu za sekondari. Pia, walimu hawa
wanapatiwa mafunzo ya lugha ya Kiingereza ili
waweze kuitumia vizuri lugha hiyo katika kufundisha
masomo husika. Walimu hawa walifanyiwa mitihani
ili kupima maendeleo yao na uwezo wao katika
kumudu kufundisha masomo ya Sayansi na Hisabati
ambapo ufaulu wao unaashiria mafanikio ya malengo
ya mpango huu. Aidha, walimu 600 wanaosomesha
Sayansi, Hisabati na Kiingereza katika darasa la tano
na sita wanapatiwa mafunzo ya utumiaji wa mbinu
mbalimbali za ufundishaji wa masomo haya katika
vituo vya walimu Unguja na Pemba. Mafunzo yote
haya yanaendeshwa na Chuo Kikuu cha Taifa cha
Zanzibar (SUZA).
iv). Mtaala wa Stashahada ya Ualimu Msingi unaendelea
kupitiwa ambapo kwa sasa zana za kukusanyia taarifa
katika kufanya utafiti na kukusanya maoni kwa wadau
tofauti zimeshatayarishwa ikiwemo dodoso na
muongozo wa usaili.
v). Jumla ya ziara 75 za ufuatiliaji wa walimu katika skuli
za maandalizi Msingi na Sekondari zimefanyika.
Ufuatiliaji huo umebaini walimu wanaowajibika zaidi
ni wale walimu wanaofundisha madarasa ya mitihani
ambapo hutumia juhudi zote kuhakikisha wanafunzi
wanafaulu. Aidha, jumla ya skuli 50 za msingi
zilifuatiliwa na wanafunzi 2,500 wa madarasa ya
kwanza na ya pili wamepimwa uwezo wa kusoma
maandishi ya Lugha ya Kiswahili. Matokeo ya
ufuatiliaji huo yameonyesha kwamba wanafunzi 1,002
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 16
wameweza kusoma vizuri, 600 kusoma kwa kudodosa
na wanafunzi 898 hawajui kusoma kabisa. Wanafunzi
waliosoma kwa kudodosa na walishindwa kusoma
kabisa wamegaiwa kwa walimu wa skuli husika na
wamepangiwa muda maalumu wa kuwasaidia
kujifunza. Lengo ni kuhakikisha watoto wote wanapata
fursa ya kujifunza na kuelewa wanachofundishwa.
vi). Wakufunzi 55 wa masomo ya Sayansi na Hisabati (29
Unguja na 26 Pemba) walipatiwa mafunzo ya
matumizi ya mbinu sahihi za kufundishia masomo
hayo kwa vitendo zaidi kwa lengo la kuwajengea
umahiri. Katika mafunzo hayo walishiriki washauri wa
masomo ya Sayansi na Hisabati na walimu wasaidizi.
Matokeo ya muda mfupi
Jumla ya wanafunzi 947 wanasomea Ualimu kwa ngazi ya
Cheti cha Maandalizi, Stashahada ya Dini na Kiarabu,
Stashahada ya Sayansi Jamii, Stashahada ya Elimu ya Msingi
kwa Unguja na Pemba na Cheti cha Elimu Mjumuisho kwa
Unguja. Kati yao, wanafunzi 664 wakiwemo wanaume 144 na
wanawake 520 wanasomea Ualimu katika Chuo cha Kiislamu
Mazizini Unguja. Aidha, wanafunzi 283 wakiwemo wanaume
94 na wanawake 193 katika Chuo cha Kiislamu Kiuyu.
Huduma ya Elimu ya Juu, Ushauri na Utafiti
26. Mheshimiwa Spika, Huduma ya Elimu ya Juu, Ushauri na
Utafiti ina lengo la kuwaandaa wanafunzi kuingia katika fani
za kitaalamu na ajira. Huduma hii inatolewa katika Vyuo
vikuu vitatu vilivyopo Zanzibar ambavyo ni Chuo Kikuu cha
Taifa cha Zanzibar (SUZA), Chuo cha Kumbukumbu ya
Abdulrahman Al-Sumait cha Chukwani na Chuo Kikuu cha
Zanzibar Tunguu.
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 17
27. Mheshimiwa Spika, ngazi hii ya elimu ina jumla ya
wanafunzi 7,067 wanaosoma katika vyuo vikuu hivi vitatu.
Kati ya wanafunzi hao, wanawake 4,040 na wanaume 3,027
Kwa mwaka wa fedha wa 2018/19, Chuo Kikuu cha Taifa cha
Zanzibar (SUZA) kilitengewa ruzuku ya TSh.
11,060,200,000/=. Hadi kufikia Aprili, 2019, jumla ya TSh.
9,133,231,850 zimepatikana, ambazo ni sawa na asilimia 80.
28. Mheshimiwa Spika, utekelezaji halisi wa huduma hii ni kama
hivi ifuatavyo: -
i). Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar kwa kushirikiana
na Chuo Kikuu cha Copenhagen cha Denmark
kimeendelea kufanya utafiti wa kuangalia mabadiliko
ya mazingira ya baharini pamoja na kuangalia
usalama wa vyakula vya baharini.
ii). Ujenzi wa ukumbi wa mkutano wa Dkt. Ali
Mohamed Shein katika Kampasi ya Tunguu
umekamilika na umetumika rasmi katika mahafali ya
12 yaliyofanyika tarehe 23/04/2019. Ukumbi huu wa
kisasa upo katika eneo la Kampasi ya Tunguu na una
uwezo wa kuchukua watu 3,000 kwa wakati mmoja.
Vilevile, Chuo kinaendelea na ukarabati wa majengo
ya Kampasi ya Vuga na ukarabati wa nyumba za
walimu katika Kampasi ya Mbweni.
iii). Jumla ya wafanyakazi 15 wa fani za Udaktari,
Uendeshaji na Uhudumu wameajiriwa. Aidha, Chuo
kimeendelea kuwalipia ada za masomo wafanyakazi
wake 77 ambao wapo masomoni, kwenye ngazi za
Shahada ya Uzamivu 39, Shahada ya Uzamili 29,
Shahada ya Kwanza wanane na mmoja wa
Stashahada.
iv). Jumla ya Programu 54 zinafundishwa katika ngazi za
Shahada ya Uzamivu, Shahada ya Uzamili, Shahada
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 18
ya Kwanza, Stashahada na Cheti. Jadweli namba
26(a) – (f) yanatoa ufafanuzi zaidi.
Matokeo ya muda mfupi;
i. Jumla ya wanafunzi 3,620 wameandikishwa katika
Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA). Kati
yao, wanawake ni 1,997 na wanaume ni 1,623.
ii. Jumla ya wanafunzi 861 (321 wanaume na 540
wanawake) wamehitimu SUZA na kutunukiwa
Stashahada, shahada, shahada ya uzamili na shahada
ya uzamivu katika mahafali ya 12 yaliyofanyika
tarehe 23/04/2019 katika Kampasi ya Tunguu.
iii. Jumla ya wanafunzi 841 wakiwemo 491 wanawake na
wanaume 350 wameandikishwa katika Chuo cha
Kumbukumbu ya Abdulrahman Al-Sumait cha
Chukwani. Jadweli namba 27 linatoa ufafanuzi zaidi.
iv. Jumla ya wanafunzi 2,334 wameandikishwa katika
Chuo Kikuu cha Zanzibar Tunguu, kati yao
wanawake ni 1,367 na 967 wanaume. Jadweli namba
28 linatoa ufafanuzi zaidi.
Huduma ya Sayansi na Teknolojia
29. Mheshimiwa Spika, Huduma ya Sayansi na Teknolojia ina
madhumuni ya kuimarisha elimu ya sayansi na teknolojia.
Shughuli za huduma hii zinatekelezwa na Taasisi ya Karume
ya Sayansi na Teknolojia. Kwa mwaka 2018/19, Taasisi hii
ilitengewa ruzuku ya TSh. 1,631,500,000. Hadi kufikia Aprili,
2019, jumla ya TSh. 1,266,017,370 za SMZ zilipatikana
ambazo ni sawa na asilimia 70
30. Mheshimiwa Spika, Utekelezaji halisi wa huduma hii kwa
mwaka 2018/19 ni kama hivi ifuatavyo: -
i). Jumla ya wanafunzi wapya 858, wanaume 638 na
wanawake 220 kwa fani zote za Taasisi.
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 19
ii). Wafanyakazi wapya 12, kati yao tisa kada ya
wakufunzi na watatu kada za uendeshaji
wameajiriwa.
iii). Mafunzo ya ngazi ya stashahada hadi shahada ya
kwanza yameendelezwa kwa ufanisi wa hali ya juu.
iv). Vifaa vya kisasa vya kusomeshea na kufundishia
vimenunuliwa.
v). Mafunzo mapya ya kuiendeleza Taasisi na yale ya
kuisaidia jamii kwa kutumia Sayansi na Teknolojia
yameanzishwa.
vi). Taasisi imepanua mashirikiano na Taasisi za ndani
na nje ya nchi. Miongoni mwa Taasisi hizo ni
Netherland University na Arusha Technical College.
Mashirikiano yamesaidia katika kubadilishana
uzoefu na yameongeza umahiri wa kutatua
changamoto za kitaaluma na uendeshaji zinazoikabili
Taasisi.
Matokeo ya muda Mfupi
Jumla ya wanafunzi 1,471 wakiwemo wanawake 367 na
wanaume 1,104 wanaendelea na masomo katika fani
mbalimbali zikiwemo, Shahada ya urubani na uhandisi wa
ndege, Stashahada za uhandisi, Stashahada ya teknolojia ya
habari mawasiliano na biashara, Stashahada ya Mafunzo ya
Hisabati na Sayansi kwa Skuli za Msingi, Stashahada
mafunzo ya Ualimu (VTA), Stashahada ya usimamizi wa
maabara na Cheti kwa mafunzo ya Amali (VETA).
Huduma ya Mikopo ya Elimu Juu
31. Mheshimiwa Spika, Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu
Zanzibar inatoa huduma ya Mikopo ya Elimu ya Juu yenye
dhamana ya kuwapatia mikopo kwa wanafunzi wanaojiunga
na wanaoendelea na masomo ya elimu ya juu katika fani
mbalimbali. Kwa mwaka wa fedha 2018/2019, jumla ya TSh.
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 20
11,775,900,000 za ruzuku kutoka Serikalini zilitengwa kwa
ajili ya kutoa mikopo kwa wanafunzi wapya 1,720 na 1,799
wanaoendelea na masomo ya Elimu ya Juu. Hadi kufikia
Aprili 2019, jumla ya TSh. 8,620,441,405 zilipatikana ambazo
ni sawa na asilimia 70 ya makadirio.
32. Mheshimiwa Spika, Utekelezaji halisi wa programu hii ni
kama ifuatavyo: -
i) Jumla ya wanafunzi 3,519 wamepatiwa mikopo ya
elimu ya juu wakiwemo wanafunzi wapya 1,720 na
1,799 wanaoendelea na masomo. Idadi hii
imeongezeka kwa asilimia 36 ukilinganisha na mwaka
2017/2018. Hali hiyo, inatokana na ongezeko la
ruzuku kutoka Shilingi bilioni 10.2 kwa mwaka
2017/18 hadi bilioni 11.7 kwa mwaka 2018/19. Hadi
kufikia Aprili, 2019 jumla ya TSh. 7.5 bilioni
zimetumika kuwalipia wanafunzi hawa.
ii) Wanafunzi 66 wamepatiwa nafasi za ufadhili wa
masomo nje ya nchi zilizotolewa na washirika wa
maendeleo mbalimbali wakiwemo Serikali ya Jamhuri
ya Watu wa China (16), Serikali ya Falme ya Oman
(5), Falme ya Ras Al-Khaimah (3), Benki ya
Maendeleo ya Kiislamu – IsDB (4), Shirika la
Munadhamat (16) na Chuo Kikuu cha Shimla cha
India (22)
iii) Serikali imeendelea na utaratibu wa kutoa scholaships
ikiwa ni zawadi kwa wanafunzi bora waliofaulu vizuri
zaidi kwa daraja la kwanza katika mitihani ya Taifa ya
kidato cha sita katika masomo ya sayansi, biashara na
sanaa. Wanafunzi 49 wanaendelea kufaidika na
utaratibu huu. Hadi mwezi Machi 2019 jumla ya
Shilingi milioni 85.2 zimetumika kuwalipia
wanafunzi hawa.
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 21
iv) Jumla ya wanafunzi wapya 72 wamepatiwa ufadhili
wa masomo wakiwemo 58 kupitia taasisi za Darul
Imaan katika Chuo Kikuu cha Zanzibar kilichopo
Tunguu na 14 kupitia Shirika la “Direct Aid” lililotoa
ufadhili wa masomo kwa wanafunzi wa Chuo Kikuu
cha Abdulrahman Al-Sumait cha Chukwani.
v) Jumla ya wanafunzi 767 wakiwemo wanafunzi 554
wanaosoma vyuo vya Zanzibar, 160 katika vyuo vya
Tanzania Bara na 53 wa vyuo ya nje ya Tanzania
wanatarajiwa kuhitimu masomo yao katika ngazi
mbalimbali.
33. Mheshimiwa Spika, Juhudi mbalimbali zinachukuliwa na
Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu Zanzibar ili kuhakikisha
wadaiwa wote wanarejesha mikopo yao kwa wakati.
Matarajio yalikuwa ni kukusanya Shilingi billioni 2.3 ifikapo
mwezi wa Juni, 2019. Hadi kufikia mwezi Aprili, 2019, jumla
ya Shilingi bilioni 1.7 zimerejeshwa sawa na asilimia 74 ya
lengo lililowekwa kutoka kwa wadaiwa 2,806.
Huduma ya Uratibu wa Elimu ya Juu
34. Mheshimiwa Spika, Huduma ya Uratibu wa Elimu ya Juu ina
jukumu la kusimamia na kutathmini maendeleo ya elimu ya
juu. Huduma hii inatekelezwa na Kitengo cha Uratibu wa
Elimu ya Juu. Kwa mwaka 2018/19 Kitengo kilitengewa
ruzuku ya TSh. 40,000,000 kutoka Serikalini. Utekelezaji
halisi wa huduma hii ni kama ifuatavyo: -
i) Nafasi za masomo kwa ufadhili wa nchi za China,
Queen Elizabeth, Australia, Hungary, Qatar, Nigeria,
Jumuiya ya Madola, Alexandria, Indonesia,
Mauritius, Uturuki, Marekani, Korea, Belgium, na
Thailand zimetangazwa. Nafasi hizo zilijumuisha fani
mbalimbali zikiwemo; Udaktari, Uchumi, Ukandarasi,
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 22
Uuguzi na Sayansi ya Mazingira, Usimamizi wa
Biashara na Utawala kwa viwango vya Shahada ya
Kwanza, ya Pili na ya Tatu. Jumla ya waombaji 126
wakiwemo wanaume 106 na wanawake 20
waliwasilisha maombi yao. Majibu ya maombi hayo
hayajatolewa na Taasisi husika.
ii) Kitengo kiliendelea na kazi zake za kuratibu Elimu ya
Juu kwa kuzifuatilia na kuzitathmini Taasisi 50 za
Elimu ya Juu zinazotoa huduma ya elimu ya juu kwa
Unguja na Pemba.
iii) Mkutano na wajumbe wa Baraza la Taifa la Elimu ya
Ufundi na wakuu wa Vyuo Vikuu umefanyika.
Mkutano huo umejadili changamoto, mafanikio na
muelekeo katika kutoa Elimu na Miongozo kwa
walimu na wanafunzi wa Sekondari kiwilaya zote za
Unguja na Pemba ili waweze kuchagua fani za Vyuo
Vikuu zinazoendana na uwezo wao kitaaluma.
iv) Pia, Kitengo kimetoa elimu na miongozo kwa walimu
na wanafunzi 122 wa sekondari kwa Wilaya zote za
Unguja na Pemba ili waweze kuchagua fani za Vyuo
Vikuu zinazoendana na masomo yao na mahitaji ya
Taifa.
v) Kitengo kimeandaa na kurikodi vipindi viwili (kimoja
cha redio na kimoja cha televisheni) vya kutoa elimu
kwa wanafunzi na jamii kuhusiana na taratibu za
kujiunga na Vyuo Vikuu pamoja na kujua vigezo
vinavyostahiki, kutambua vyuo vilivyosajiliwa na
ambavyo havisajiliwa.
Matokeo ya muda mfupi;
i. Jumla ya wahitimu saba waliripoti kutoka masomoni
wakiwemo wanaume watano na wanawake wawili ili
kupatiwa barua ya kupeleka Tume ya Utumishi
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 23
Serikalini. Pia wameelekezwa utaratibu wa kufuata ili
waweze kuajiriwa
ii. Muombaji mmoja alifanikiwa kupata nafasi ya
masomo Chuo cha Alexandria nchini Misri.
PROGRAMU YA NNE: ELIMU MBADALA NA
MAFUNZO YA AMALI
35. Mheshimiwa Spika, Programu hii ina madhumuni ya kutoa
elimu ya mafunzo ya amali na elimu mbadala kwa wanafunzi
kulingana na mahitaji ya soko la ajira. Programu hii ina
programu ndogo mbili; Mafunzo ya Amali na Elimu Mbadala
na Watu Wazima. Programu hii inatekelezwa kwa pamoja kati
ya Idara ya Elimu Mbadala na Watu Wazima na Mamlaka ya
Mafunzo ya Amali. Programu hii ilipangiwa jumla ya TSh.
24,540,026,000. Kati ya fedha hizo TSh. 7,553,026,000 kwa
kazi za kawaida na TSh. 16,987,000,000 kwa kazi za
maendeleo. Kati ya fedha hizo TSh. 15,387,000,000 ni kutoka
kwa mhisani Benki ya Maendeleo ya Afrika na TSh.
1,600,000,000 ni za Serikali.
Programu ndogo ya Mafunzo ya Amali
36. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2018/19, programu hii
ndogo ilikuwa na madhumuni ya kutoa elimu
itakayowawezesha vijana kujiajiri ili kujikwamua na
umasikini ilitengewa ruzuku ya TSh. 6,621,600,000 kwa kazi
za kawaida. Hadi kufikia Aprili, 2019, jumla ya TSh.
4,591,651,992 kutoka Serikalini zilipatikana ambazo ni sawa
na asilimia 60.
37. Mheshimiwa Spika, Utekelezaji halisi kwa programu hii ni
kama hivi ifuatavyo: -
i) Ujenzi wa jengo jipya la Taasisi ya Karume ya
Sayansi na Teknolojia lenye madarasa 18, maabara na
karakana nne umekamilika. Kukamilika kwa jengo
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 24
hili jipya kumepunguza tatizo la uhaba wa madarasa,
ofisi na karakana. Samani kwa matumizi ya darasani
na ofisini zimenunuliwa na kusambazwa katika jingo
hilo jipya.
ii) Vifaa vya kufundishia na kujifunzia kwa fani
zinazotolewa katika vituo vitatu vya Mafunzo ya
Amali vya serikali; Mwanakwerekwe, Mkokotoni na
Vitongoji vimenunuliwa na kusambazwa. Vifaa hivyo
ni vitambaa, gesi, saruji, nondo, mbao, rangi pamoja
na mashine ya “On Board Diagnostic Scan” ya
kuangalia gari. Pia, viti na meza 158 kwa Kituo cha
Mwanakwerekwe na Mkokotoni vimenunuliwa.
iii) Ujenzi wa uzio kwa awamu ya pili katika Kituo cha
Vitongoji na ujenzi wa karakana mbili ya ushoni na
useremala katika Kituo cha Mkokotoni umekamilika.
Aidha, ukarabati wa vyarahani 60 vya vituo vitatu
umefanyika. Pia, ujenzi wa madarasa manne mapya
na ujenzi wa uzio katika kituo cha Mkokotoni
unaendelea.
iv) Michoro kwa ajili ya ujenzi wa madarasa na karakana
katika kituo cha Mwanakwerekwe, dakhalia na
nyumba za walimu kwa kituo cha Mkokotoni na
Vitongoji imekamilika na imewasilishwa kwa
wasanifu na watathmini majengo.
v) Vifaa vya kufundishia fani ya Mpira wa Miguu
(Sports Academy) na mafunzo ya Mtandao wa
CISCO vimenunuliwa ikiwa ni maandalizi ya kutoa
mafunzo hayo kwa vitendo. Aidha, mafunzo ya
CISCO kwa walimu wa Kompyuta wa vituo vya
mafunzo ya amali yataanza kutolewa Juni, 2019.
vi) Mamlaka imekuza mashirikiano yake na vituo vinne
vya binafsi kwa kufadhili miradi ya maendeleo ya
vituo hivyo kwa kuvipatia vifaa vya kufundishia fani
11 vyenye thamani ya TSh. 111,219,000. Pia
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 25
Mamlaka imejitangaza katika vyombo vya habari vya
Serikali na vya binafsi vikiwemo redio, televisheni na
magazeti ya Zanzibar na Tanzania Bara.
vii) Mamlaka kwa kushirikiana na wataalamu kutoka
VETA inaendelea na zoezi la kupitia upya mitaala ya
Mafunzo ya Amali. Kwa sasa uchambuzi wa data kwa
ajili ya kufanya utafiti wa soko la ajira unaendelea.
viii) Jumla ya vikundi 13 (11 vya Unguja na viwili vya
Pemba) vimepatiwa mkopo wenye thamani ya TSh.
65,366,000. Mkopo huu unalenga kuwawezesha
vijana kujiajiri. Aidha, mafunzo juu ya kuongeza
masoko na udhibiti mzuri wa fedha yametolewa.
ix) Mamlaka imesimamia ufanyaji wa Mtihani wa Taifa
wa MMA kwa wanafunzi wa vituo 10 vikiwemo
vitatu vya Serikali na saba vya binafsi ambapo jumla
ya wanafunzi 1,239 (789 wanaume na wanawake 450)
walishiriki katika mitihani hiyo.
x) Jumla ya vituo 26 vya binafsi vinavyotowa mafunzo
ya amali vimefanyiwa ukaguzi wa kawaida kwa lengo
la kuangalia kiwango pamoja na kutoa maelekezo ya
njia nzuri za utoaji wa mafunzo ya fani husika. Aidha,
vituo 15 vimefanyiwa ukaguzi wa usajili na vituo
vinane vimepatiwa usajili wa muda. Vituo hivyo ni
pamoja na ICPS Vocational Training Centre, Zanzibar
Technical Centre, Stone Town Youth Centre, Capital
Technology Centre, Al Riayat Computer Training
Centre, Adult Training Centre, Al Hidayat Computer
Training Centre na Samael Vocational Training
Centre.
xi) Mamlaka imewalipia wafanyakazi wake wanane
masomo ya muda mrefu wakiwemo watano
wanaoendelea na masomo na watatu wapya. Pia
imewapatia udhamini wa masomo ya muda mfupi
watano wanaosomea mafunzo maalum ya kuchoma
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 26
kwa kutumia gesi (Gas Welding) katika chuo cha
ufundi stadi VETA Chang’ombe. Taaluma hiyo
inalenga kutolewa katika vituo vya MMA vya
Zanzibar.
xii) Jumla ya wanafunzi 411 wanaoishi dakhalia ya
Mkokotoni na Vitongoji wanaendelea kupatiwa
huduma ya chakula ya milo mitatu kwa siku.
Matokeo ya muda mfupi;
i. Jumla ya vijana 1,309 wamejiunga na vituo vya
Mamlaka ya Mafunzo ya Amali mwanzoni mwa
mwaka 2019.
ii. Jumla ya TSh. 21,472,050 zimerejeshwa na vikundi
vya vijana vilivyopatiwa mkopo wa kuweza kujiajiri.
iii. Jumla ya vijana 807 (wanawake 379 na wanaume
428) sawa na asilimia 65.13 kati ya 1,239
waliotahiniwa wamefaulu mitihani yao.
iv. Jumla ya vijana 276 (wanawake 115 na wanaume
161) kwa fani 15 zinazotolewa katika vituo vitatu vya
Serikali; Mwanakwerekwe, Mkokotoni na Vitongoji
wamehitimu mafunzo yao.
Programu ndogo ya Elimu Mbadala na Watu Wazima
38. Mheshimiwa Spika, Programu hii inatekelezwa na Idara ya
Elimu Mbadala na Watu Wazima na ina lengo la kupunguza
kiwango cha wasiojua kusoma, kuandika na kuhesabu
miongoni mwa wanajamii. Kwa mwaka wa fedha 2018/19,
programu hii ilitengewa jumla ya TSh. 17,855,167,000. Kati
ya hizo, TSh. 868,167,000 ni kwa kazi za kawaida na TSh.
16,987,000,000 ni kwa kazi za maendeleo. Kati ya fedha za
maendeleo TSh. 1,600,000,000 ni mchango wa SMZ na
15,387,000,000/= ni kutoka kwa wahisani. Hadi kufikia
Aprili, 2019, jumla ya TSh. 7,534,726,843 kwa kazi za
maendeleo ambazo ni sawa na asilimia 40 zilipatikana
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 27
zikiwemo TSh. 82,005,000 za Serikali sawa na asilimia 5 na
TSh 7,452,721,843 sawa na asilimia 48 za wahisani. Aidha,
jumla ya TSh. 573,988,698 kwa matumizi ya kawaida sawa na
asilimia 60 zimepatikana.
39. Mheshimiwa Spika, Utekelezaji halisi wa shughuli za
programu hii ni kama ifuatavyo: -
i) Madarasa 40 mapya ya kisomo kwa Unguja na Pemba
yamefunguliwa. Idadi ya madarasa ya kisomo imefikia
521 mwaka 2019 kutoka 481 mwaka 2018. Aidha, jumla
ya wanakisomo 6,883 wa kisomo cha Watu Wazima
wamefanyiwa Upimaji katika hatua zote nne za kisomo.
Wanafunzi 520 wa hatua ya nne wamekombolewa
kupitia upimaji huo.
ii) Wanakisomo 825 wamefanyiwa uchunguzi wa macho
Unguja na Pemba na wanakisomo 709 kati ya
waliopimwa walipatiwa miwani na wengine walipatiwa
huduma baada ya kugunduliwa na tatizo.
iii) Maadhimisho ya Juma la Elimu ya Watu Wazima
yamefanyika. Uzinduzi wa Juma hilo ulifanyika Wilaya
ya Kaskazini ‘A’ Unguja katika Kituo cha Mafunzo ya
Amali Mkokotoni na kilele kilifanyika Wilaya ya
Micheweni katika Kituo cha Elimu Mbadala Wingwi
Mtemani.
iv) Jumla ya vikundi 128 (83 Unguja 45 Pemba) vikiwemo
vipya 14 vyenye jumla ya wanachama 2,863
vimeendelezwa kwa lengo la kuwapunguzia utegemezi
wanawake na umasikini wa kipato.
v) Mafunzo ya ufugaji nyuki kwa awamu ya pili kwa
wanafunzi 25 wa Elimu Mbadala yalifanyika Mgonjoni.
vi) Jengo kuu la Idara la Forodhani limefanyiwa
matengenezo ya kupakwa rangi katika baadhi ya sehemu
zake za ndani, na baadhi ya vyumba kuwekwa
marumaru (tiles).
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 28
vii) Jumla ya wanafunzi 1,575 (wanaume 853 na wanawake
722) wamesajiliwa katika vituo vya kujiendeleza kwa
Unguja na Pemba. Aidha, wanafunzi 55 (wanawake 50
na wanaume 5) walioshindwa kuendelea na masomo yao
baada ya mtihani wa Kidato cha Pili na cha Nne
wameandikishwa katika Kituo cha Sayansi Kimu
Forodhani kusomea fani ya Upishi, Ushoni, Kudarizi na
Kufuma.
viii) Mafunzo kwa walimu 25 wa Sayansi Kimu na programu
ya Youth Empowerment Life Program (YELP)
yametolewa. Aidha, mikutano kwa walimu 100 wa vituo
vya Elimu ya kujiendeleza Unguja imefanyika na
mikutano na wadau juu ya utafiti wa Costal Area Drop
Out (CADO) kwa mikoa mitatu ya Unguja imefanyika.
ix) Mafunzo ya kuwapatia taaluma ya kupambana na
majanga ya moto yametolewa kwa wafanyakazi 90
unguja wa Kituo cha Elimu Mbadala na Ofisi kuu ya
Idara Forodhani.
x) Mafunzo ya kuwajengea uwezo walimu wa Vituo vya
Elimu Mbadala yametolewa kwa walimu 60 wa Unguja
na Pemba. Aidha, uhamasishaji wa kitambua programu
ya Elimu Mbadala ulifanyika kwa wazazi 100 na vijana
100 kwa Unguja na Pemba kupitia mradi wa
“Alternative Learning Skills Development II”.
xi) Vipindi 15 vya Elimu Mbadala na Watu Wazima
viliandaliwa na kurushwa hewani kupitia Shirika la
Utangazaji la Zanzibar kwa ajili ya kuielimisha jamii
juu ya umuhimu wa programu zinazotolewa na Idara ya
Elimu Mbadala na Watu Wazima zenye lengo la
kuhamasisha uandikishaji wa wanafunzi katika vituo ili
wapate elimu itakayowakomboa na changamoto
zinazowakabili katika jamii na za kiuchumi.
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 29
Matokeo ya muda mfupi;
i. Jumla ya wanakisomo 8,899 wameandikishwa
wakiwemo wanawake 7,845 na wanaume 1,054.
ii. Jumla ya wanafunzi 791 wenye umri wa miaka 9 hadi
14 waliokuwa nje ya mfumo rasmi wa skuli
wameandikishwa katika madarasa ya Elimu Mbadala.
Kati ya hao, wanafunzi 500 wameandikishwa Unguja na
291 kwa Pemba wakiwemo wanawake 222 na wanaume
569.
iii. Jumla ya wanafunzi 351 wenye umri kati ya miaka 15
hadi 22 wameandikishwa katika Kituo cha Elimu
Mbadala Rahaleo Unguja na Kituo cha Wingwi
Mtemani Pemba. Kati yao, wanawake 113 na wanaume
238. Vijana hawa wanasomea fani mbalimbali zikiwemo
Umeme, Ushoni, Upishi, Useremala, Udobi, Mafunzo
ya Kompyuta na Utunzaji Nyumba pamoja na masomo
ya kawaida ili kuwajengea uwezo wa kujua kusoma,
kuandika na kuhesabu.
iv. Jumla ya wanafunzi 4,432 wamefanya mtihani wa
faragha wa Kidato cha Nne. Kati ya hao, wanafunzi
2,183 sawa na asilimia 49.26 ya watahiniwa wote
wamefaulu. Aidha, wanafunzi 184 kati ya
257(wanawake 110 na wanaume 147) waliofanya
mtihani wa faragha wa Kidato cha Sita Mei, 2018 kwa
Unguja na Pemba ambao ni sawa na asilimia 71.59
wamefaulu.
v. Jumla ya wahitimu 71 (wanawake 62 na wanaume 9) wa
Kituo cha Sayansi Kimu wamejiajiri katika fani za
ushoni na upishi na wengine wameajiriwa mahotelini.
PROGRAMU YA TANO: UBORA WA ELIMU
40. Mheshimiwa Spika, Programu hii ina lengo la kutoa elimu
bora kwa ngazi zote za elimu, ina jumla ya programu ndogo
tatu na maeneo matano ya kutoa huduma kama yafuatayo: -
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 30
Huduma ya Mitaala na Vifaa vya Kufundishia
41. Mheshimiwa Spika, Huduma hii ina madhumuni ya
kutayarisha mitaala ya elimu na kuratibu upatikanaji wa vifaa
vya kufundishia na kujifunzia kwa ngazi za elimu ya
maandalizi, msingi, sekondari na mafunzo ya
Ualimu. Shughuli za utoaji wa huduma hii zinatekelezwa na
Taasisi ya Elimu Zanzibar iliyoanzishwa rasmi kwa Sheria
namba 4 ya mwaka 2016. Kwa mwaka wa fedha 2018/19,
Taasisi ilitengewa ruzuku ya TSh. 329,200,000 kwa kazi za
kawaida. Hadi kufikia Aprili, 2019, jumla ya TSh.
284,895,390 sawa na asilimia 80 zilipatikana. Utekelezaji
halisi wa programu hii ni kama ifuatavyo:-
i) Rasimu ya muundo wa Paneli za mitaala za kitaifa kwa
ngazi ya Elimu ya Maandalizi, Msingi na Sekondari kwa
vituo 10 vya walimu (vituo sita Unguja na vinne Pemba)
imeandaliwa.
ii) Kanuni za Sheria ya Taasisi ya Elimu ya Zanzibar
zimeandaliwa.
iii) Miswada minne ya vitabu vya kufundishia somo la Dini
ya Kiislamu kwa Darasa la Kwanza hadi la Nne
imetayarishwa. Aidha, miswada minne ya vitabu vya
wanakisomo ya somo la Kiswahili na Hisabati kwa
juzuu ya kwanza na ya pili imehaririwa.
iv) Taasisi kwa kushirikiana na Mshauri Mwelekezi inapitia
Mitaala ya Elimu ya Maandalizi na Msingi. Kazi hiyo
ipo katika hatua ya awali ya kukusanya maoni ya wadau
mbalimbali kwa lengo la kuandaa mfumo wa Mtaala.
v) Mafunzo ya miongozo ya kufundishia kwa watendaji
274 wakiwemo maafisa wa Taasisi ya Elimu, wakaguzi,
waratibu TCs, washauri wa masomo na walimu wa
taaluma wa skuli za Serikali na binafsi yametolewa
Unguja na Pemba. Miongozo hiyo imehusisha muundo
wa Azimio la Kazi, Andalio la somo, Uwekaji wa
kumbukumbu za ufundishaji kwa kila kipindi cha
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 31
mwalimu pamoja na daftari la kumbukumbu za
maendeleo ya wanafunzi.
vi) Mkataba wa huduma kwa wateja, Muundo wa Taasisi ya
Elimu ya Zanzibar na kufanya utafiti wa kuchunguza
uwezo wa kusoma, kuandika na kuhesabu kwa
wanafunzi wa Darasa la Kwanza na la Nne
umetayarishwa. Jumla ya skuli 33 (21- Unguja, 12-
Pemba) zimeshiriki.
Huduma ya Upimaji na Tathmini ya Elimu
42. Mheshimiwa Spika, Programu hii ina madhumuni ya kupima
na kutathmini utekelezaji wa utoaji wa elimu. Shughuli za
huduma hii zinatekelezwa na Baraza la Mitihani la Zanzibar.
Kwa mwaka wa 2018/19 huduma ya Upimaji na Tathmini
ilitengewa ruzuku na Serikali ya TSh. 4,672,500,000. Hadi
kufikia Aprili, 2019, jumla ya TSh. 4,445,728,791 ambazo ni
sawa na asilimia 95.1 zilipatikana. Utekelezaji halisi wa
shughuli za huduma ya Upimaji na Tathmini ni kama
ifuatavyo: -
i) Matayarisho ya kumpata Mshauri elekezi wa
kuimarisha mfumo wa Upimaji na Tathimini wa
Baraza la Mitihani kupitia Mradi wa Benki ya Dunia
unaolenga kuimarisha mfumo wa mitihani Zanzibar
yanaendelea.
ii) Jumla ya wanafunzi 47,979 (wanawake 23,402 na
wanaume 24,577 wa darasa la nne walisajiliwa
kufanya mtihani wa kuwapima maendeleo yao
kitaaluma katika ngazi ya elimu ya msingi chini
(darasa la kwanza hadi la nne) na uwezo wa kuendelea
na darasa la elimu ya msingi juu (darasa la tano).
Wanafunzi halisi waliofanya mtihani huu ni 44,471
sawa na asilimia 92.7 ya walioandikishwa wakiwemo
wanawake 22,447 na wanaume 22,025
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 32
iii) Jumla ya wanafunzi 34,822 wa darasa la sita ambao ni
sawa na asilimia 94.85 ya waliosajiliwa walifanya
mtihani wa kumalizia elimu ya msingi. Kati ya
wanafunzi hao wanawake walikuwa ni 18,418 na
wanaume walikuwa ni 16,404. Kati ya watahiniwa
hao, 33,519 ambao ni sawa na asilimia 96 walifaulu.
iv) Jumla ya wanafunzi 32,636 sawa na asilimia 93.7 kati
ya wanafunzi 34,846 waliosajiliwa walifanya mtihani
wa kumaliza Kidato cha Pili, wakiwemo wanawake
17,425 na wanaume ni 15,211. Jumla ya wanafunzi
23,907 wamefaulu na kuendelea na masomo ya Kidato
cha Tatu ambao ni sawa na asilimia 73.
v) Serikali imesikitishwa sana na kuvuja kwa mtihani wa
Kidato cha Pili ya 2018 hali iliyopelekea mitihani hiyo
kufutwa na kuiingizia Serikali hasara kubwa. Baada ya
uchunguzi wa awali kufanyika, watu wanaotuhumiwa
kuhusika na uvujaji huo wamepatikana na tayari hatua
za kisheria zimeanza kuchukuliwa dhidi yao.
Wafanyakazi wote wa Serikali wanaotuhumiwa
wameshasimamishwa kazi ili kupisha uchunguzi zaidi
na ikithibitika watachukuliwa hatua kwa mujibu wa
sheria. Kwa walio nje ya utumishi wa umma kesi zao
zimeshawasilishwa katika vyombo husika kwa
kuchukuliwa hatua. Serikali inaendelea kusisitiza
kwamba wahusika wote wa kadhia hii watachukuliwa
hatua kali kwa mujibu wa sharia ili kuhakikisha kuwa
tukio kama hili halitokei tena.
vi) Jumla ya walimu wanafunzi 139 walisajiliwa kufanya
mitihani ya kumalizia masomo yao ya Cheti cha
Ualimu wa Maandalizi na Msingi chini katika Vyuo
vya Kiislamu. Kati yao, 87 Mazizini Unguja na 52
Kiuyu Pemba wakiwemo 125 wanawake na 14
wanaume. Asilimia 100 ya walimu walioandikishwa
walifanya mitihani hiyo mwezi wa Novemba, 2018.
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 33
vii) Jumla ya walimu wanafunzi 331 (196 Unguja na 135
Pemba) watakaofanya mitihani ya kumalizia masomo
yao ya Stashahada ya Ualimu wa ngazi ya Msingi na
ngazi ya Sekondari katika Vyuo vya Kiislamu vya
Mazizini wamesajiliwa. Kati ya hao, 259 ni wanawake
na 72 ni wanaume. Miongoni mwao 129 wa
Stashahada ya Msingi na 32 wa Stashahada ya
Sekondari. Mitihani hiyo itafanyika mwishoni mwa
mwezi wa Mei, 2019.
viii) Ripoti ya tathmini ya mitihani na uchambuzi wa taarifa
unaendelea kutayarishwa. Taarifa hiyo itawasilishwa
kwa wadau wa elimu kupitia Wilaya zao ili
kuzifahamu changamoto zinazowakabili watoto katika
kujibu mitihani na mafanikio yaliyopatikana.
Matokeo ya Muda mfupi;
i. Jumla ya wanafunzi waliofaulu mtihani wa Darasa la
Nne ni 31,317 sawa na asilimia 70.4 Kati ya hao,
wanawake ni17,477 sawa na asilimia 39.3 na wanaume
ni 13,840 sawa na asilimia 31.1 ya watahiniwa wote.
ii. Wanafunzi waliofaulu mtihani wa kumaliza Darasa la
sita ni 33,519 sawa na asilimia 96.3 (wanawake ni
18,160 sawa na asilimia 52.2 na wanaume ni 15,359
sawa na asilimia 44.1) ya watahiniwa wote.
iii. Wanafunzi 23,907 kati ya waliofanya mtihani wa
kumaliza Kidato cha Pili ambao ni sawa na asilimia
73.25 wamefaulu kuendelea na masomo yao ya Kidato
cha tatu (wanawake ni 13,986 na wanaume ni 9,921)
iv. Walimu wanafunzi 127 sawa na asilimia 91.37
wakiwemo wanawake ni 114 (asilimia 82.01) na
wanaume ni 13 (asilimia 9.36) ya watahiniwa wote
wamefaulu mtihani wa kumaliza mafunzo ya Ualimu ya
Cheti cha Maandalizi na Msingi Chini uliofanyika
Novemba, 2018.
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 34
Huduma ya Ukaguzi wa Elimu
43. Mheshimiwa Spika, utoaji wa huduma hii una madhumuni ya
kusimamia ubora wa elimu itolewayo kwa kuhakikisha kuwa
elimu hiyo inafuata sera, sheria, miongozo na taratibu za
Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali zilizoelekezwa
kufuatwa na taasisi inayotoa elimu. Shughuli za huduma hii
zinatekelezwa na Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Elimu. Kwa
mwaka wa fedha 201819, programu hii imepangiwa ruzuku ya
TSh. 428,700,000. Hadi kufikia Aprili, 2019, jumla ya TSh.
537,426,345 zilipatikana ambazo ni sawa na asilimia 120.
Utekelezaji halisi ni kama ifuatavyo: -
i) Sheria ya kuanzishwa kwa Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa
Elimu imeshapitishwa na Mfumo Mpya wa Ukaguzi
umeanza kutumika.
ii) Jumla ya skuli 622 za Unguja na Pemba sawa na
asilimia 84.2% ya makadirio ya skuli zilizopangwa
kukaguliwa zimekaguliwa. Aidha, skuli 26
zimekaguliwa kwa ajili ya kupatiwa usajili.
iii) Jumla ya walimu 1,503 wamekaguliwa na kupewa
ushauri kulingana na masomo wanayofundisha, Unguja
na Pemba.
Huduma za Maktaba
44. Mheshimiwa Spika, Programu hii ina madhumuni ya kutoa
fursa ya kutumia vitabu na nyenzo nyengine za taaluma kwa
watoto, wanafunzi wa ngazi zote na watu wote. Shughuli za
huduma hii zinatekelezwa na Shirika la Huduma za Maktaba
Zanzibar kwa mashirikiano na mashirika ya “Books for
Africa, Book Aid International, Sida, GPE na Children
International”. Kwa mwaka wa fedha 2018/19, programu hii
ilipangiwa kutumia ruzuku ya TSh. 845,100,000 kwa kazi za
kawaida. Hadi kufikia Aprili, 2019 jumla ya TSh.
624,518,970 sawa na asilimia 70 zilipatikana. Utekelezaji
halisi wa shughuli za Programu hii ni kama ifuatavyo: -
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 35
i) Jumla ya vitabu 36,413 kutoka Shirika la Book Aid
International” la Uingereza vimepokelewa na
kusambazwa katika taasisi sita za Mkoa wa Mjini
Magharibi, moja ya Mkoa wa Kusini Unguja, 13 za
Mkoa wa Kusini Pemba na sita za Mkoa wa Kaskazini
Pemba. Aidha, vitabu 3,945 vimegaiwa katika taasisi 26
za elimu ya juu zikiwemo Chuo Kikuu cha Taifa cha
Zanzibar (SUZA) iliyopatiwa maboksi 32 na maboksi
42 yalipelekwa Chuo cha Kumbukumbu ya
Abdulrahman Al-Sumait Chukwani. Skuli 10 za msingi
zimepatiwa vitabu 1,230, skuli 16 za sekondari
zimepatiwa vitabu 2,505 na Kituo cha Elimu Mbadala
cha Rahaleo kimepatiwa vitabu 210.
ii) Programu 101 za watoto zilizowashirikisha watoto
5,644 zimefanyika. Miongoni mwa programu hizo,
programu 82 zilifanyika ndani ya Maktaba Kuu na
programu 19 zilifanyika nje ya Maktaba.
iii) Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya kujua kusoma na
kuandika (International Literacy Day) yaliyoshirikisha
watu 443 (348 Unguja na 95 Pemba) wakiwemo
wanafunzi, walimu, wazazi, waandishi wa vitabu na
viongozi mbalimbali yalifanyika katika viwanja vya
Maktaba Kuu Maisara kwa Unguja na Maktaba ya
Chakechake kwa Pemba.
iv) Mdahalo wenye mada ya “Nini kifanyike ili idadi ya
watumiaji wa huduma za maktaba iongezeke”
ulifanyika. Jumla ya washiriki 170 walitoa maoni yao
juu ya kuimarisha huduma za maktaba nchini. Mdahalo
huo ulifanyika katika Maktaba Kuu za Unguja na
Pemba. Aidha katika midahalo hiyo, tovuti ya Shirika la
Huduma za Maktaba (www.zls.go.tz) ilizinduliwa rasmi.
v) Programu za “Youth English Corner” zinaendeshwa
kwa kushirikiana na Jumuiya isiyo ya kiserikali ya
“Youth Empowerment and Change”. Jumla ya programu
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 36
18 (9 za nje na 9 za ndani) za Kiingereza kwa vijana
zimefanyika na kuwashirikisha vijana 1,000. Aidha,
mafunzo kwa walimu wa hisabati kuhusu mbinu bora za
kufundishia somo la hisabati yalitolewa kwa walimu 33
na mafunzo ya Kiingereza kwa walimu wanaosomesha
masomo yanayotumia lugha ya Kiingereza yametolewa
kwa walimu 127 na kati yao walimu 87 walimaliza na
kupata vyeti.
vi) Programu mbalimbali za kijamii kupitia Kitengo cha
“American Corner” zinaendeshwa kwa mashirikiano na
Shirika la Huduma za Maktaba na Ubalozi wa
Marekani. Jumla ya wanajamii 10,894 walipatiwa
huduma kupitia kitengo hicho. Watu 6,308 (1856
wanawake na 4452 wanaume) walipatiwa huduma za
kompyuta, 625 (551 wanawake na 74 wanaume)
walishiriki katika programu na 2,978 (1,272 wanawake
na 1,706 wanaume) walipatiwa huduma za kusoma
vitabu.
vii) Huduma za maktaba kwa njia ya shamiana ilitolewa
katika viwanja vya Skuli ya Mikindani kwa Unguja na
Skuli ya Mkanyageni, Pemba. Jumla ya wananchi 250
walishiriki na kupata fursa ya kusoma vitabu na
kupatiwa maelezo yanayohusu shughuli zinazofanywa
na maktaba zetu.
viii) Mafunzo yaliyolenga kuwaongezea uwezo
wanyakazi na kuwawezesha kukabiliana na ukuaji wa
teknolojia ya habari na mawasiliano kwa wakutubi wa
maktaba za umma na maktaba za skuli yalitolewa.
Mafunzo hayo yalijadili mada za masuala ya ubunifu na
mabadiliko (innovation and transformation), namna
nzuri ya kuhudumia mteja (customer care) na huduma
kwa kutumia mtandao (search 4 life). Jumla ya wakutubi
70 walishiriki katika mafunzo hayo.
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 37
Matokeo ya Muda Mfupi
i. Jumla ya wanachama wapya 599 walisajiliwa katika
Maktaba za Shirika. Kati ya hao, wanachama 411 kwa
Unguja wakiwemo wanaume 170, wanawake 204 na
37 ni watoto. Pia wanachama 188 kwa Pemba
walisajiliwa wakiwemo 46 wanaume, 69 wanawake
na watoto 34.
ii. Idadi ya watumiaji wa maktaba imefikia 48,043. Kati
yao, 18,069 wakiwemo wanawake 6,327, wanaume
3,424 na watoto ni 8,318 kwa Unguja na watu 29,974
wakiwemo 7,831 wanawake na 11,290 wanaume na
10,853 ni watoto kwa Pemba.
Huduma ya Urajisi wa Elimu
45. Mheshimiwa Spika, Programu hii ina madhumuni ya
kuhakikisha Sheria, Sera na taratibu za Wizara zinafuatwa
katika skuli za Serikali na za binafsi. Huduma hii pia inatoa
leseni kwa walimu na kuzisajili skuli za Serikali na za binafsi.
Shughuli za huduma hii zinatekelezwa na Ofisi ya Mrajisi wa
Elimu. Kwa mwaka wa fedha 2018/19, programu hii
ilipangiwa kutumia jumla ya TSh. 190,400,000 kwa kazi za
kawaida. Hadi kufikia Aprili, 2019, jumla ya TSh.
170,528,455 ambazo ni sawa na asilimia 80 zilipatikana.
46. Mheshimiwa Spika, Utekelezaji halisi wa huduma hii ni
kama hivi ifuatavyo: -
i) Ofisi ya Urajis wa Elimu Zanzibar inaendelea na
utayarishaji wa rasimu ya Sheria ya Elimu kwa
kuifanyia mapitio Sheria inayotumika. Rasimu hiyo
imewasilishwa kwa wadau kwa kupata maoni yao kabla
ya kuwasilishwa katika Kamati ya Uongozi ya Wizara
ya Elimu na kufuata taratibu zote za ukamilishaji wake.
ii) Jumla ya skuli 286 (195 Unguja na 81 Pemba) za ngazi
ya elimu ya maandalizi, msingi na sekondari za Serikali
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 38
na za binafsi zimehakikiwa uhalali wake wa kiutendaji
na wafanyakazi wake.
iii) Jumla ya vikao vitatu vya kuiwasilisha na kuijadili
Ripoti ya Uhakiki mkuu wa usajili wa skuli za Serikali
na za binafsi, leseni za walimu, uwepo na matumizi ya
Sera na Sheria za uendeshaji wa skuli uliofanyika 2017
vimefanyika. Kikao kimoja kilifanyika Unguja, kimoja
Pemba na kikao kimoja na Uongozi wa Wizara ya
Elimu. Vikao hivyo viliwawezesha wadau wakuu wa
elimu kutoa mapendekezo yao juu ya masuala
mbalimbali ili kuimarisha na kupunguza changamoto
katika utoaji na upatikanaji wa elimu nchini pamoja na
kuleta ustawi mzuri wa wanafunzi.
iv) Kesi 18 za udhalilishaji zimeripotiwa kwa Unguja na
Pemba zikiwemo ubakaji na ulawiti. Kati ya hizo, kesi
nne kwa wanafunzi wa skuli za sekondari na kesi tisa
kwa wanafunzi wanaosoma skuli za msingi. Aidha, kesi
17 za ujauzito zilizopokelewa kwa Unguja na Pemba na
zimeripotiwa kwa Kamanda wa Polisi wa Mikoa husika.
Kati ya hizo, kesi tatu zimejadiliwa katika ofisi ya
Mrajis wa Elimu na kwa mujibu wa Sheria namba 4
(2005) ya Kuwalinda Wari na Mtoto wa Mzazi Mmoja
imewapa fursa wanafunzi hawa wanne kuendelea na
masomo yao.
v) Kesi nane za ndoa (moja Unguja na saba kwa Pemba)
zimeripotiwa. Kwa mujibu wa Sheria ya Elimu Namba 6
ya mwaka 1982 kifungu cha 20(3) mwanafunzi hao
hawaruhusiwi kuendelea na masomo yao kwa vile bado
wapo katika ngazi ya Elimu ya Lazima.
Matokeo ya muda mfupi;
i. Jumla ya walimu wapya 819 wakiwemo wa Cheti cha
Ualimu, Stashahada, Shahada ya Kwanza na ya Pili
walipatiwa leseni za kufundishia za muda wa miaka
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 39
mitano (LTT). Kati ya hao, walimu 419 ambao
hawajasomea ualimu wamepatiwa leseni za
kufundishia za muda wa mwaka mmoja (LUT) na
wametakiwa kujiunga katika vyuo vya Ualimu
vilivyosajiliwa na kutambuliwa na Serikali ili kusomea
kazi ya Ualimu.
ii. Jumla ya kesi tano za udhalilishaji zimesikilizwa,
kujadiliwa na kuripotiwa kwa Kamanda wa Polisi wa
Mikoa husika. Wanafunzi wanaohusika na kesi hizo
wamepatiwa ushauri nasaha na wanaendelea na
masomo yao.
iii. Jumla ya skuli 36 za Serikali zimepatiwa usajili
zikiwemo skuli moja ya maandalizi, 10 za maandalizi
na msingi, sita za msingi na 19 za sekondari kwa
Unguja na Pemba.
iv. Kati ya maombi 37 ya usajili wa muda yalipokelewa
kutoka skuli za binafsi zikiwemo 28 za maandalizi,
skuli tano za maandalizi na msingi, skuli moja ya
maandalizi, msingi na sekondari na skuli tatu za
sekondari ni maombi ya skuli 11 tu ndio yamepatiwa
usajili wa muda. Aidha, kati ya maombi matano ya
usajili wa kudumu yaliwasilishwa kwa Unguja na
Pemba ni skuli mbili tu zimepatiwa usajili wa kudumu.
Skuli ambazo zimejitokeza kasoro wakati wa ukaguzi
hazijasajiliwa na zimetakiwa kuzifanyia kazi kasoro
zilizojitokeza na wakikamilisha watapatiwa usajili
kulingana na maombi husika.
v. Vyuo vinne vya binafsi vimesajiliwa vikiwemo Chuo
kimoja kinachotoa mafunzo ya ualimu ngazi ya Cheti
cha Maandalizi na cheti cha Ualimu wa msingi, Chuo
chengine kinatoa mafunzo ya Ualimu kwa ngazi Cheti
cha Maandalizi, Cheti cha Ualimu wa msingi na
Stashahada ya Sanaa na kimoja kinatoa mafunzo ya
Cheti cha Maandalizi na Stashahada ya Ualimu wa
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 40
Maandalizi. Vyuo hivyo ni Sumait Teacher Education,
Zanzibar Teacher College, Madrassa Early Childhood
Center Unguja na Madrassa Early Childhood Center
Pemba.
Programu ndogo ya Elimu Mjumuisho na Stadi za Maisha
47. Mheshimiwa Spika, Programu hii ina jukumu la kuhakikisha
upatikanaji wa elimu kwa watoto wote wakiwemo wenye
mahitaji maalum. Programu hii inatekelezwa na Kitengo cha
Elimu Mjumuisho na Stadi za Maisha. Kwa mwaka 2018/19
programu hii ilitengewa TSh. 75,000,000. Hadi kufikia Aprili,
2019 jumla ya TSh. 40,224,450 sawa na ailimia 54
zilipatikana. Utekelezaji halisi wa shughuli za programu hii
ndogo ni kama ifuatavyo: -
i). Moduli saba kwa ajili ya mafunzo ya Elimu Mjumuisho
kazini zimekamilika. Moduli hizi zitatumiwa na Washauri
wa Vituo vya Walimu Unguja na Pemba kwa kutoa
mafunzo ya Elimu Mjumuisho katika skuli za zoni zao.
Kukamilika kwa moduli hizi kutaimarisha ufundishaji na
kutumia mbinu shirikishi zinazolenga wanafunzi wote
katika tendo la kujifunza.
ii). Wanafunzi watoro 99 (59 wanaume na 40 wanawake) wa
skuli 8 za majaribio ya elimu mjumuisho ya awamu ya
pili wamerejeshwa skuli. Mafanikio haya yametokana na
ushirikiano nzuri uliojengeka kati ya kamati za elimu
mjumuisho, washirika wa elimu na wanajamii. Aidha,
mazingira ya upatikanaji wa elimu katika skuli 50
yameimarishwa kwa kujengewa rampu na kuwafanya
wanafunzi wenye mahitaji maalumu kuyafikia maeneo
husika bila ya changamoto kubwa. Pia, vyoo vya skuli za
elimu mjumuisho vimetengenezwa na kuendana na
mahitaji ya wanafunzi wenye ulemavu. Mazingira haya
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 41
yanachangia sana katika kuimarisha ubora wa elimu
inayotolewa.
iii). Mafunzo ya lugha ya alama yalitolewa kwa ajili ya
kuimarisha matumizi ya lugha ya alama katika
ufundishaji na kujifunza kwa mwanafunzi ili kuimarisha
ufahamu wa wanafunzi viziwi. Mafunzo hayo
yaliwajumuisha wanafunzi wenye ulemavu wa usikivu
(viziwi), marafiki zao pamoja na walimu wao kutoka
Skuli za Mwanakwerekwe ‘A’, ‘F’ na ‘H’, Kiembesamaki
‘A’ Sekondari, Mkunazini Msingi na Mfenesini. Mafunzo
hayo yalitolewa kwa awamu mbili. Awamu ya kwanza ya
mafunzo hayo yalihudhuriwa na washiriki 127 wakiwemo
wanafunzi walengwa 36 (wanawake 24 na wanaume 12)
marafiki zao 56 (wanawake 40 na wanaume 16) na
walimu 35 (wanawake 29 na 6 wanaume). Awamu ya pili
yalihudhuriwa na washiriki 133. Kati yao, wanafunzi
viziwi 49 (wanawake 24 na wanaume 25), marafiki zao
32 (wanawake 19 na wanaume 13) na walimu 52
(wanawake 46 na wanaume sita).
iv). Uhamasishaji kwa jamii kuhusu athari na madhara ya
udhalilishaji kwa wanafunzi na walimu umefanyika
kupitia vipindi vya redio vilivyoandaliwa na kurushwa
hewani. Vipindi hivyo pia vilikusanya maoni ya jamii
kuhusiana na kadhia hiyo ili kulielewa tatizo na hatua za
kuchukuliwa kwa njia ya simu. Kwa ujumla, wanajamii
wa ndani na nje ya Zanzibar walitoa maoni yao na
waliunga mkono ufundishwaji wa elimu ya afya ya uzazi
kwa wanafunzi kulingana na umri wao kama njia moja ya
kupambana na vitendo hivyo.
v). Kufuatia mafunzo ya Nidhamu Endelevu (Positive
discipline) yaliyotolewa mwaka 2017/18 na Shirika la
Save the Children kwa walimu 1,539 wa Wilaya Kusini
na Kaskazini “A” Unguja. Wizara ilifanya ufuatiliaji
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 42
katika skuli 18 ili kujiridhisha kwa kiwango gani mafunzo
hayo yamefanyiwa kazi pamoja na kuendelea kushajiisha
walimu kuyafanyia kazi mafunzo hayo. Kwa ujumla
imeonekana kwamba idadi kubwa ya walimu wameanza
kubadili mitazamo yao kwa kutumia mbinu mbadala za
namna bora ya kuwalea na kuwaadabisha wanafunzi bila
ya kutumia adhabu dhalilishi kama vile bakora nyingi na
nzito, kuwafinya wanafunzi, lugha za matusi na kashfa
ambayo hatimaye huleta mahusiano mabaya baina ya
walimu na wanafunzi na hata kwa wazazi wa wanafunzi.
vi). Ufuatiliaji wa utekelezaji wa mafunzo ya Afya ya Uzazi
na Stadi za Maisha kwa ujumla katika skuli nne za
Unguja ulifanyika kwa kushirikiana na ZAPHA+ ambapo
taarifa zilikusanywa kutoka kwa wanafunzi moja kwa
moja ili kujua nini wamefundishwa na athari gani chanya
imepatikana kutokana na mafunzo hayo. Ripoti kamili ya
ufuatiliaji huo inapatikana na wanafunzi waliopata athari
wanapatiwa huduma za afya.
vii). Kongamano kwa wanafunzi 250 kutoka skuli 11 za
sekondari linalohusu Muongozo wa Ajira (Career
Guidance) lilifanyika ili kuwasaidia wanafunzi kuweka
malengo katika uchaguzi wa kazi kwa kuzingatia masomo
yatakayoendana na malengo yao baada ya kumaliza
masomo yao. Katika kongamano hilo wanafunzi pia
walipata muongozo ambao utawasaidia wakati wa kutaka
kudahiliwa katika vyuo mbalimbali, muongozo huo
ulijikita katika sifa na vigezo vya msingi katika udahili
wa vyuo mbali mbali.
viii). Kongamano la kuadhimisha siku ya mtoto wa kike
duniani lilifanyika Pemba. Kongamano hilo lilihudhuriwa
na wanafunzi 200 (wanawake 147 na wanaume 53).
Kongamano hilo lilizungumzia umuhimu wa mtoto wa
kike kujiunga na vyuo vya mafunzo ya amali ili kupata
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 43
ujuzi na taaluma itakayowawezesha kujiendesha kimaisha
baada ya kuhitimu.
Programu ndogo ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
katika Elimu
48. Mheshimiwa Spika, Programu hii ina madhumuni ya
kuifanya teknolojia ya habari na mawasiliano itumike katika
ngazi ya utawala, kujifunza na kufundishia, kuimarisha
huduma ya mawasiliano, kutunza usalama wa taarifa na katika
maisha ya kila siku. Shughuli za programu hii zinatekelezwa
na Idara ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano katika
Elimu. Kwa mwaka 2018/19, programu hii ilipangiwa
kutumia jumla ya TSh. 532,686,000 kwa kazi za kawaida.
Hadi kufikia Aprili, 2019, jumla ya TSh. 333,835,372
zilipatikana ambazo ni sawa na asilimia 60.
49. Mheshimiwa Spika, maelezo ya utekelezaji halisi wa
programu hii ya TEHAMA ni kama hivi ifuatavyo: -
i). Rasimu ya Sera ya TEHAMA imetayarishwa na ipo
katika hatua ya kuwasilishwa katika kikao cha
Makatibu Wakuu.
ii). Kuendelea kutayarisha na kurusha hewani vipindi vya
sayansi kwa ngazi ya msingi kwa darasa la tano na
sita. Jumla ya vipindi saba vimeshakamilika katika
kipindi hiki na kukamilisha jumla ya vipindi 21
ambavyo vinaendelea kurushwa na hewani na shirika
la ZBC kwa upande wa televisheni. Lengo la programu
hizi ni kuwasaidia walimu na wanafunzi katika
kurahisisha ufundishaji na kupunguza changamoto za
mada ngumu katika kuwafundisha wanafunzi wa ngazi
ya msingi.
iii). Kuendelea kutoa mafunzo ya tasnia ya habari kupitia
studio zetu za TV na Radio kwa wanafunzi 30 wa
sekondari. Wanafunzi hawa wanapatia mafunzo ya
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 44
uandishi wa makala, matumizi ya vifaa vya televisheni
na radio. Katika kipindi hiki, miongoni mwa
wanafunzi hao wa sekondari wanafunzi wanne na
mwalimu mmoja walipata nafasi ya kuongeza ujuzi
wao katika tasnia hiyo ya habari nchini Korea ya
Kusini kwa muda wa wiki tatu.
iv). Idara ya TEHAMA ilifanya zoezi ukaguzi wa Taasisi
mbali mbali za Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali
kuangalia hali halisi ya matumizi TEHAMA ndani ya
taasisi hizo na kuangalia weledi wa watendaji katika
matumizi ya TEHAMA, Uwepo wa vifaa
vinavyotumika na vile vilivyochakaa. Katika zoezi hilo
jumla ya skuli 374 zilikaguliwa pamoja na Idara na
Taasisi 15 za Wizara ya Elimu.
v). Kuendelea kuimarisha miundombinu ya TEHAMA
ikiwemo ujenzi wa kibanda cha kutunzia umeme
hakaiba unaotokana na nguvu za jua, ununuzi wa
mitambo ya uendeshaji na usimamizi wa mtandao na
utunzaji wa taarifa. Aidha, tovuti ya izara
imeimarishwa pamoja na kuwajengea uwezo watendaji
12 kwa kupatiwa mafunzo ya uandishi na uhakiki wa
taarifa na kuziweka katika tovuti hiyo. Jumla ya taasisi
nane za WEMA zimeshaunganishwa na mkonga wa
Taifa.
Matokeo ya muda mfupi;
Jumla ya walimu 208 kutoka katika skuli 23 za sekondari
zilizoteuliwa kwa hatua ya majaribio wamepatiwa mafunzo ya
TEHAMA na matumizi ya mfumo wa Infoskuli. Mfumo huu
unarahisisha upatikanaji wa alama za maendeleo ya wanafunzi
kitaaluma (continuos assessment). Taarifa zinazopatikana
katika mfumo huo ni za mahudhurio, tathmini, utendaji wa
kazi za walimu, uwekaji wa kumbukumbu za taarifa za
wanafunzi kwa masomo kwa uhakika, kwa muda mrefu na ni
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 45
njia salama zaidi. Aidha, mfumo huu unamuwezesha mzazi
kupata taarifa hizo za maendeleo ya mtoto wake wakati
wowote na pahali popote alipo nchini kupitia simu yake ya
mkononi.
Programu ndogo ya Michezo na Utamaduni katika Skuli
50. Mheshimiwa Spika, Programu hii ina madhumuni ya
kumuandaa mwanafunzi kimwili, kiafya na kiakili katika
kujifunza kwa kupitia michezo. Shughuli za programu hii
zinatekelezwa na Idara ya Michezo na Utamaduni katika
elimu. Kwa mwaka wa fedha 2018/19, programu hii
imepangiwa kutumia jumla ya TSh. 650,043,000 kwa kazi za
kawaida. Hadi kufikia Aprili, 2019, jumla ya TSh. 454,
574,130 sawa na asilimia 60 zilipatikana.
51. Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa programu hii ni kama
ifuatavyo: -
i). Mpango mkakati wa ‘Nchi yetu ni Urithi wetu’
unaolenga ushajihishaji wa uzalendo, nidhamu na
kuwajenga wanafunzi katika maadili mema pamoja na
kuwafahamisha historia ya nchi yetu umezinduliwa na
kuanza kufanyiwa kazi katika skuli zote.
ii). Skuli 168 zimepatiwa vifaa vya michezo kupitia
mpango wa Sport 55, vifaa hivyo ni vya michezo ya
riadha, mpira wa miguu, mpira wa kikapu na mpira wa
pete. Aidha, walimu 475 wamepatiwa mafunzo ya
uendeshaji na usimamizi wa mpira wa miguu, riadha,
mpira wa kikapu, mpira wa wavu, mpira wa mikono na
mpira wa pete.
iii). Wanafunzi 200 kutoka skuli za msingi na sekondari
wameshiriki katika kuandaa na kuwasilisha kazi za
sanaa katika Tamasha la Utamaduni wa Mzanzibari
lililoratibiwa na Wizara ya Habari, Utalii, Utamaduni
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 46
na Michezo pamoja na kushiriki mashindano maalumu
ya uibuaji vipaji ngazi za mikoa Unguja na Pemba.
iv). Mafunzo maalumu ya huduma ya kwanza na tiba
michezoni yametolewa kwa walimu 40 kwa awamu ya
kwanza.
v). Mashindano ya michezo na sanaa ya Tamasha la Elimu
bila Malipo kuanzia ngazi ya skuli, wilaya, mkoa hadi
Taifa yamefanyika kwa ufanisi na kuongeza hamasa na
ushiriki wa wanafunzi katika michezo.
vi). Mashindano ya mchezo wa mbio za nyika
yamefanyika katika ngazi za wilaya na kuibua vipaji
vipya vya wanafunzi katika mchezo huo. Aidha,
mashindano ya mchezo wa mpira wa miguu kwa
mikoa mitano ya Zanzibar yamefanyika kwa
mashirikiano na kampuni ya ZAT.
vii). Matamasha ya michezo ya wanafunzi wenye ulemavu
wa akili, kusikia na viungo yamefanyika katika
viwanja vya Amani, Maisara na Kariakoo na
wanafunzi wameonesha uwezo na vipaji vyao.
viii). Maandalizi ya kuadhimisha miaka 107 ya shughuli za
Skauti yanayojulikana “Zanzibar Skauti Jamboree”
yamekamilika. Shughuli hiyo itafanyika Juni, 2019 na
mialiko ya kushiriki shughuli hiyo imetolewa kwa
mikoa yote ya Tanzania.
PROGRAMU YA SITA: UTAWALA NA UONGOZI
52. Mheshimiwa Spika, programu hii madhumuni yake
makubwa ni kuhakikisha nyenzo zilizo bora zinapatikana na
zinatumika kwa lengo la kuimarisha utoaji na upatikanaji wa
huduma ya elimu nchini. Programu hii ina programu ndogo
tatu; Programu ya Uongozi Kiujumla, Programu ya Uratibu
wa Shughuli za Mipango, Sera na Utafiti na Programu ya
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 47
Uratibu wa Shughuli za Elimu Pemba. Utekelezaji wa
programu ya Utawala na Uongozi ni kama ifuatavyo: -
Programu ndogo ya Uongozi Kiujumla
53. Mheshimiwa Spika, programu hii ina madhumuni ya kutoa
ufanisi wa Uongozi na utawala wa rasilimali za Wizara.
Shughuli za programu hii ndogo zinatekelezwa na Idara ya
Utumishi na Uendeshaji. Kwa mwaka wa fedha 2018/19,
programu hii ilipangiwa jumla ya TSh. 7,241,104,000. Hadi
kufikia Aprili, 2019, jumla ya TSh. 4,743,209,582
zimepatikana ambazo ni sawa na asilimia 66. Utekelezaji wa
kazi za programu hii ni kama ifuatavyo: -
i) Jumla ya walimu 451 (238 Unguja na 213 Pemba) na 92
nje ya kada ya ualimu waliajiriwa baada ya kupata kibali
cha uajiri kutoka Tume ya Utumishi Serikalini. Kati yao,
kwa upande wa Unguja walimu 56 ni wa Shahada ya
Kwanza Sayansi, 49 Shahada ya Sanaa, 67 Stashahada ya
Sayansi, 25 Stashahada ya Sanaa, 41 Cheti cha daraja la
IIIA na 70 nje ya kada ya ualimu. Kwa upande wa
Pemba, waliajiriwa walimu 39 wa Shahada ya Kwanza
Sayansi, 48 Shahada ya Kwanza Sanaa, 33 Stashahada
Sayansi, 33 Stashahada ya Sanaa, 60 Cheti cha daraja la
IIIA na 22 wa nje ya kada ya ualimu.
ii) Jumla ya wafanyakazi 1,020 Unguja na 434 Pemba
waliopewa likizo walilipwa posho la likizo la jumla ya
TSh. 154,900,000.
iii) Idara hii imeendelea kutoa fursa zaidi kwa walimu na
wafanyakazi wa Uendeshaji ili waweze kujiendeleza
kimasomo kwa lengo la kuimarisha utendaji wa kazi zao,
kuimarisha Mfumo wa uwekaji kumbukumbu (database)
la wafanyakazi kwa mujibu wa muundo wa utumishi na
kuwapatia huduma bora na vitendea kazi wafanyakazi ili
kuimarisha utendaji kazi.
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 48
iv) Jumla ya wafanyakazi 25 (21 Unguja na 4 Pemba)
walipatiwa fursa ya kujiunga na masomo katika vyuo
mbali mbali vya ndani na nje ya nchi katika ngazi tofauti
baada ya kukamilisha masharti ya kiutumishi na ya vyuo.
Kati yao, wafanyakazi wanane wamepatiwa mafunzo ya
muda mfupi na 17 (wanane wanaume na tisa wanawake)
ni wa mafunzo ya muda mrefu.
v) Jumla ya wafanyakazi 199 walistaafu kazi kwa mujibu wa
sharia. Wafanyakazi 23 walifariki dunia, Mwenyezi
Mungu awalaze mahali pema peponi Amin. Aidha
Wafanyakazi tisa wamepewa uhamisho kwenda
kuendelea na kazi katika Wizara na Taasisi mbalimbali za
Serikali, wafanyakazi wanne wamechukua likizo bila ya
malipo na wafanyakazi tisa wameacha kazi kwa hiari.
vi) Wafanyakazi 350 Unguja na 259 Pemba wamedhaminiwa
kupata mikopo ya Benki na Saccos mbalimbali nchini.
Wafanyakazi hao kupata mikopo ya fedha taslim, vifaa
vya ujenzi, vipando na vifaa vya matumizi ya nyumbani.
Mikopo iliyotolewa ina thamani ya TSh.1,227,284,338
kwa Unguja na TSh 136,326,4310 kwa Pemba.
Matokeo ya muda mfupi;
Jumla ya wafanyakazi 6,185 wameajiriwa katika Wizara ya
Elimu na Mafunzo ya Amali. Kati yao, 3,403 ni wanawake na
2,782 wanaume. Wafanyakazi 4,560 wapo Unguja 2,793
wanawake na 1,767 wanaume) kwa upande wa Pemba wapo
wafanyakazi 1,625 (wanawake 610 na wanaume ni 1015.
Kati ya wafanyakazi wote hawa 5,551 ni wa kada ya ualimu
na 634 ni wafanyakazi wasiokuwa wa kada ya ualimu.
Programu ndogo ya Uratibu wa Shughuli za Mipango,
Sera na Utafiti
54. Mheshimiwa Spika, programu hii ina madhumuni ya
kufanikisha na kuratibu Mipango, Sera na Utafiti katika
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 49
Wizara. Programu hii ndogo inatekelezwa na Idara ya
Mipango, Sera na Utafiti. Kwa mwaka 2018/19 ilipangiwa
kutumia jumla ya TSh. 4,048,980,000. Kati ya fedha hizo,
TSh. 400,000,000 kwa kazi za maendeleo na TSh.
3,648,980,000 kwa kazi za kawaida. Hadi kufikia Aprili,
2019, jumla ya TSh. 3,358, 054,176 kwa kazi za kawaida
zilipatikana ambazo ni sawa na asilimia 82.9.
55. Mheshimiwa Spika, utekelezaji halisi wa programu hii ni
kama hivi ifuatavyo: -
i. Mapitio ya Sera ya elimu (2006) na Sheria ya Elimu
(1982) ili ziendane na Mpango Mkuu wa Elimu
(2017/18 – 21/22), Dira ya 2020, MKUZA III na
Mipango mbalimbali ya maendeleo Dunia yapo katika
hatua za mwisho kukamilika.
ii. Mpango Mkuu wa Elimu wa miaka mitano unafanyiwa
mapitio ya muda wa kati ili kuingiza mikakati ya
maendeleo ya Kitaifa inayosimamiwa na Sekta
nyengine za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
iii. Ufuatiliaji na uandaaji wa ripoti za kila robo mwaka
umefanyika. Ripoti hizo zinasaidia sana katika kufanya
maamuzi na kupunguza changamoto za kiutendaji
katika sekta ya elimu.
iv. Zoezi la utafiti wa SEACMEQ V limeanza kwa hatua
ya kutayarisha na kuhariri dodoso za kukusanyia data.
Aidha, Idara imefanya utafiti wa kuangalia upatikanaji
na matumizi ya vifaa vya kufundishia na kujifunzia
kwa Skuli 160 za Sekondari zikiwemo 96 za Unguja
na 64 za Pemba. Uchambuzi wa taarifa za utafiti huu
unaendelea.
v. Mfumo wa kielektroniki wa kukusanya taarifa za skuli
umeanza kutumika. Mfumo huu umesaidia kuinua
usimamizi wa skuli zetu katika utoaji na upatikanaji
wa elimu.
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 50
vi. Mkutano mkuu unaowashirikisha wadau wa elimu wa
ndani na nje ya Zanzibar wakiwemo wafadhili
umefanyika. Mkutano huo uliwashirikisha wadau 150
na ulifanyika kwa siku tatu tarehe 26 - 28/02/2019
katika ukumbi wa Ngalawa Beach Resort.
Programu ndogo ya kuratibu shughuli za elimu Pemba
56. Mheshimiwa Spika, Programu hii ina madhumuni ya
kuratibu na kusimamia shughuli zote za elimu kwa upande
wa Pemba. Msimamizi Mkuu wa shughuli za programu hii ni
Afisa Mdhamini wa Wizara yangu kupitia katika Divisheni
ya Idara ya Uendeshaji na Utumishi Pemba. Programu hii
ndogo ilipangiwa jumla ya TSh. 2,611,928,000 kwa kazi za
kawaida. Hadi kufikia Aprili, 2019, jumla ya TSh.
2,041,301,190 zilipatikana sawa na asilimia 77 ambazo
zilitumika katika kusimamia na kufuatilia shughuli na
programu za elimu Pemba. Uhaba wa walimu imeendelea
kuwa ni miongoni mwa changamoto zinazoikabili sekta ya
elimu hasa kwa upande wa Pemba. Hata hivyo, Wizara kwa
kushirikiana na Taasisi husika inaendelea kuchukua hatua
mbalimbali za kutatua changamoto hii kwa maendeleo ya
elimu hapa Visiwani.
MPANGO WA UTEKELEZAJI KWA MWAKA
2019/2020 KWA MFUMO WA PROGRAMU
57. Mheshimiwa Spika, baada ya taarifa hiyo ya utekelezaji wa
bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali kwa mwaka
wa fedha 2018/19 naomba sasa niwasilishe vipaumbele vya
Wizara yangu na kisha makadirio ya mapato na matumizi
kwa mwaka 2019/2020.
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 51
Vipaumbele
58. Mheshimiwa Spika, kwa mwaka wa fedha 2019/2020
vipaumbele vya Sekta ya Elimu ni hivi vifuatavyo: -
i. Kutoa ruzuku kwa skuli 875 za Maandalizi (za Jamii,
za Serikali na vituo vya TuTu).
ii. Kuanzisha vituo 20 vya madarasa ya TuTu na
madarasa 10 mapya ya Maandalizi.
iii. Kukamilisha na kufanya ukarabati wa madarasa 400
ya Maandalizi na Vituo vya TuTu.
iv. Kutoa mafunzo ya lugha ya Kiingereza kwa walimu
wa darasa la 3 na 4 na kuandika vitabu mbalimbali
vya kujifunza kusoma kwa wanafunzi wa darasa la 3
na 4.
v. Kuendelea na ujenzi wa skuli mbili za sekondari
Mwanakwerekwe na Wingi na ujenzi wa madarasa
48, maabara na Maktaba katika Skuli 22 za Sekondari
Unguja na Pemba.
vi. Kukamilisha madarasa 50 ya sekondari
yaliyoanzishwa na wananchi Unguja na Pemba.
vii. Kujenga Maabara katika skuli 15 za sekondari za
Unguja na Pemba.
viii. Kukamilisha ujenzi wa vyoo 100 katika skuli za
msingi na sekondari.
ix. Kuzizawadia skuli 300 zitakazoongeza asilimia ya
ufaulu katika mitihani ya Taifa ya darasa la 6, Kidato
cha Pili na Kidato cha Nne.
x. Kufanya matengenezo makubwa katika Skuli ya
Sekondari ya Benbella na Skuli ya Msingi ya
Madungu.
xi. Kutoa mafunzo kazini kwa walimu 639 wa sanaa
wanaosomesha masomo ya Sayansi, Hisabati na
Kiingereza ngazi ya sekondari.
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 52
xii. Kutoa mafunzo kwa walimu 1,500 wa madarasa ya 5
na 6 na Kidato cha Pili ya namna ya kuwasaidia
wanafunzi wenye ufahamu mdogo katika kujifunza.
xiii. Kukamilisha ujenzi na kununua samani kwa Vituo
vya Mafunzo ya Amali vya Daya na Makunduchi.
xiv. Kuipitia na kuifanyia marekebisho Mitaala ya
mafunzo ya walimu wa ngazi ya maandalizi pamoja
na mtaala wa wanafunzi wa maandalizi.
xv. Kujenga Maktaba moja ya Wilaya ya Kaskazini B
xvi. Kuziunga na Mkonga wa Taifa taasisi tano za elimu
zikiwemo vituo vya walimu na Ofisi za Elimu za
Wilaya.
xvii. Kuendelea na zoezi la kuupitia na kuandaa mfumo
mpya wa ukaguzi wa elimu na kujenga ofisi moja ya
ukaguzi wa elimu katika Mkoa wa Kaskazini Unguja.
xviii. Kuimarisha shughuli za tafiti, machapisho na ushauri
wa kitaaluma pamoja na kuunganisha kampasi zote na
mtandao wa Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar.
xix. Kuanza hatua za ujenzi wa majengo ya dakhalia, kituo
cha wanafunzi pamoja na ukaratabi wa Skuli ya
Kilimo Kizimbani.
59. Mheshimiwa Spika, Naomba sasa, kuwasilisha mpango wa
maendeleo ya elimu kwa mwaka wa fedha wa 2019/2020 kwa
mfumo wa programu kama hivi ifuatavyo: -
60. Mheshimiwa Spika, Kwa mwaka wa fedha wa 2019/2020
Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali itaendelea kutekeleza
malengo yake yaliyozingatia Dira 2020, MKUZA III, Sera ya
Elimu, Mpango Mkuu wa Elimu (2017 – 2021), vipaumbele
vya Wizara kwa mwaka 2019/20 pamoja na mikakati
mengine ya Kitaifa na Kimataifa yenye lengo la kuimarisha
upatikanaji wa huduma ya elimu nchini. Wizara pia,
itaendelea kushirikiana na sekta nyengine zinazotoa huduma
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 53
za jamii na kuimarisha uchumi ikiwemo Wizara ya Afya,
Wizara ya Ardhi, Maji, Nishati na Mazingira, Wizara ya
Kazi, Uwezeshaji, Maendeleo ya Wazee, Wanawake na
Watoto, Wizara ya Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa,
Serikali za Mitaa na Idara Maalumu, washirika mbalimbali
wa maendeleo, mashirika yasiyo ya Serikali na wananchi.
61. Mheshimiwa Spika, Katika mwaka wa fedha wa 2019/2020,
Wizara yangu itatekeleza miradi mitano ya maendeleo kupitia
programu zake sita. Programu ya Maandalizi na Msingi
inatekelezwa kwa pamoja kati ya Wizara yangu na Wizara ya
Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na
Idara Maalum za SMZ kupitia mfumo wa Ugatuzi.
62. Mheshimiwa Spika, Programu sita za Wizara zitaendelea
kutekelezwa kwa mashirikiano kati ya Serikali ya Mapinduzi
ya Zanzibar na washirika wa maendeleo wa ndani na nje ya
nchi. Jumla ya TSh. 178,917,149,000 zitahitajika, kati ya hizo
TSh. 111,343,101,000 ni za SMZ ambapo TSh.
5,800,000,000 ni za miradi ya maendeleo na TSh. 67,574,
048,000 ni kutoka kwa wahisani. Kati ya fedha za wahisani,
TSh. 8,469,702,000 ni ruzuku kutoka GPE, UNICEF,
USAID, Table for Two (TfT), Shirika la “Good Neighbour”
la Korea, Jamhuri ya Watu wa China, NORAD na “Milele
Zanzibar Foundation” na TSh. 59,104,346,000 ni mkopo
kutoka Benki ya Dunia, Benki ya Kiarabu kwa Maendeleo ya
Afrika (BADEA), Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) na
Mfuko wa OPEC. Jadweli Nam. 49 linatoa ufafanuzi zaidi.
Mheshimiwa Spika, Miradi na Programu zitakazotekelezwa
na Wizara yangu ni kama ifuatavyo: -
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 54
Miradi mitano ya Sekta ya Elimu
i). Mradi wa Uimarishaji wa Elimu ya Maandalizi
ii). Mradi wa Uimarishaji wa Elimu ya Msingi
iii). Mradi wa Uimarishaji wa Elimu ya Lazima
iv). Mradi wa Uimarishaji wa Elimu Mbadala na Amali.
v). Mradi wa Uimarishaji wa Miundombinu katika elimu
Programu Sita za Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali
Programu ya 1: Elimu ya Maandalizi na Msingi.
Programu ya 2: Elimu ya Sekondari.
Programu ya 3: Elimu ya Juu.
Programu ya 4: Elimu Mbadala na Mafunzo ya Amali.
Programu ya 5: Ubora wa Elimu.
Programu ya 6: Uongozi na Utawala.
MAELEZO YA PROGRAMU ZA ELIMU
63. Mheshimiwa Spika, yafuatayo ni maelezo ya programu za
Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali yanayohusisha
Madhumuni, Matokeo ya muda mfupi, Viashiria na Shabaha
za utekelezaji kwa kila programu.
PROGRAMU YA KWANZA:
ELIMU YA MAANDALIZI NA MSINGI
64. Mheshimiwa Spika, Programu hii ina madhumuni ya
kumuandaa mtoto kimwili na kiakili kwa ajili ya kupata
elimu ya maandalizi na msingi na kumuwezesha mwanafunzi
kujua kusoma, kuandika na kuhesabu na kumtayarisha kwa
elimu ya sekondari.
Matokeo ya muda mfupi;
• Kumtayarisha mtoto kwa ajili ya elimu ya msingi.
• Kutoa elimu ya msingi
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 55
Viashiria vya matokeo;
• Uwiano wa uandikishaji wa wanafunzi katika ngazi ya
maandalizi na msingi.
• Uwiano wa idadi ya walimu kwa wanafunzi.
• Uwiano wa wanafunzi kwa darasa.
• Uwiano wa ufaulu wa wanafunzi.
Shabaha za utekelezaji;
• Kuongeza kiwango halisi cha uandikishaji wanafunzi
wa maandalizi kutoka asilimia 48.8 katika mwaka 2018
hadi kufikia asilimia 60.5 ifikapo mwaka 2020.
• Kuongeza kiwango cha halisi uandikishaji wa
wanafunzi wa elimu ya msingi kutoka asilimia 89.3 ya
2018 hadi kufikia asilimia 95.0 mwaka 2020.
65. Mheshimiwa Spika, Shughuli za programu hii zinatekelezwa
na Idara ya Maandalizi na Msingi. Kwa mwaka wa fedha
2019/2020, programu hii imepangiwa jumla ya TSh.
9,010,580,000.
PROGRAMU YA PILI: ELIMU YA SEKONDARI
66. Mheshimiwa Spika, Programu ya Elimu ya Sekondari
madhumuni yake makubwa ni kumtayarisha mwanafunzi
aweze kuendelea na masomo katika ngazi za juu zaidi.
Matokeo ya muda mfupi;
• Kutoa Elimu ya Sekondari.
Viashiria vya matokeo;
• Uwiano wa wanafunzi wanaomaliza elimu ya lazima,
• Uwiano halisi wa uandikishaji wa wanafunzi katika
ngazi ya kidato cha nne na cha sita,
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 56
• Uwiano wa idadi ya walimu kwa nyumba za
wafanyakazi katika maeneo yasiyofikika kirahisi
• Uwiano wa wanafunzi kwa madarasa.
Shabaha za utekelezaji;
• Kuongeza kiwango halisi cha uandikishaji wanafunzi
wa sekondari ya awali (Kidato cha 1 – 4) kutoka
asilimia 85.6 katika mwaka 2018 hadi kufikia asilimia
89 ifikapo mwaka 2020.
• Kiwango cha mpito kutoka kidato cha pili kwenda cha
tatu kuongezeka kutoka asilimia 73.3 mwaka 2018 hadi
kufikia asilimia 75.5 ifikapo mwaka 2020.
• Kiwango cha mpito kutoka kidato cha nne kwenda cha
tano kuongezeka kutoka asilimia 68.1 mwaka 2018 hadi
asilimia 70.5 ifikapo mwaka 2020.
• Kiwango cha mpito kutoka kidato cha sita kuendelea na
elimu ya juu kuongezeka kutoka asilimia 98.2 mwaka
2018/19 hadi asilimia 98.9 ifikapo mwaka 2019/20.
67. Mheshimiwa Spika, Shughuli za programu hii zinatekelezwa
na Idara ya Elimu ya Sekondari. Kwa mwaka wa fedha
2019/2020, programu hii imepangiwa TSh. 104,591,382,000.
PROGRAMU YA TATU: ELIMU YA JUU
68. Mheshimiwa Spika, programu hii madhumuni yake ni kutoa
elimu itakayomuwezesha muhitimu kujiajiri au kuajiriwa.
Programu hii ina programu ndogo moja na maeneo madogo
manne ambayo ni: -
Programu ndogo ya Mafunzo ya Ualimu
69. Mheshimiwa Spika, programu hii ina madhumuni ya
kuwawezesha wanafunzi kuwa wabunifu, wataalamu na
wenye uwezo wa kuongoza ili kukuza ubora wa elimu.
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 57
Matokeo ya muda mfupi;
• Elimu ya Diploma ya Ualimu kutolewa
Viashiria vya matokeo;
• Idadi ya wanafunzi wote walioandikishwa vyuo vya
ualimu.
Shabaha za Utekelezaji;
• Kuongeza kiwango cha asilimia ya walimu wenye sifa
kutoka 99.2 mwaka 2018 hadi kufikia asilimia 99.6
mwaka 2020
70. Mheshimiwa Spika, Shughuli za programu hii zinatekelezwa
na Idara ya Mafunzo ya Ualimu. Kwa mwaka wa fedha
2019/2020, programu hii imepangiwa TSh. 1,719,367,000.
Huduma ya Elimu ya Juu, Ushauri na Utafiti
71. Mheshimiwa Spika, Huduma hii ina madhumuni ya
kumtayarisha mwanafunzi kuingia katika fani za kitaalamu na
ajira.
Matokeo ya muda mfupi;
• Kiwango cha elimu ya Stashahada, Shahada ya kwanza,
Shahada ya pili na Shahada ya tatu kutolewa.
Viashiria vya matokeo;
• Idadi ya wanafunzi wanaomaliza ngazi ya Astashahada
na Stashahada.
• Idadi ya wanafunzi wanaomaliza ngazi ya Shahada ya
kwanza ya Uzamili na ya Uzamivu.
• Idadi ya tafiti zinazofanywa.
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 58
Shabaha za Utekelezaji;
• Kuongeza idadi ya wanafunzi wa Chuo Kikuu kutoka
4,037 mwaka 2018/19 hadi kufikia 4,537 mwaka
2019/2020
72. Mheshimiwa Spika, Shughuli za huduma hii zinatekelezwa
na Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA). Kwa mwaka
wa fedha 2019/20, huduma hii imepangiwa ruzuku ya TSh.
12,539,100,000.
Huduma ya Elimu ya Sayansi na Teknolojia
73. Mheshimiwa Spika, Huduma hii ina madhumuni ya
kuimarisha elimu ya sayansi na teknolojia.
Matokeo ya muda mfupi;
• Kuimarisha ufundishaji na kujifunza Sayansi, Hisabati
na Teknolojia
• Elimu ya Ufundi kuimarishwa.
Viashiria vya matokeo;
• Idadi ya wanafunzi wahitimu katika Taasisi,
• Uwiyano wa wanafunzi kwa madarasa.
74. Mheshimiwa Spika, Shughuli za huduma hii zinatekelezwa
na Taasisi ya Karume ya Sayansi na Teknolojia. Kwa mwaka
wa fedha 2019/20, programu hii imepangiwa ruzuku ya TSh.
1,626,000,000.
Huduma ya Mikopo ya Elimu ya Juu
75. Mheshimiwa Spika, Huduma hii ina madhumuni ya kutoa
mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya Juu.
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 59
Matokeo ya muda mfupi;
• Mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu kutolewa.
• Fedha zilizokopeshwa kwa wanafunzi kurejeshwa.
Viashiria vya matokeo;
• Idadi ya wanafunzi wanaopokea mikopo
• Idadi ya wanafunzi wanaorudisha mikopo.
Shabaha za Utekelezaji;
• Kuongeza utoaji wa mikopo kwa wanafunzi kutoka
asilimia 36 ya waombaji mwaka 2018/19 hadi kufikia
asilimia 45 ifikapo mwaka 2020.
• Kuongeza makusanyo ya marejesho ya mikopo kutoka
TSh. 1,500,000,000 ya mwaka 2018/19 na kufikia TSh.
2,300,000,000 mwaka 2019/20.
76. Mheshimiwa Spika, Shughuli za huduma hii zinatekelezwa
na Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu. Kwa mwaka wa fedha
2019/20, programu hii imepangiwa ruzuku ya TSh.
10,298,600,000 kutoka Serikalini.
Huduma ya Uratibu wa Elimu ya Juu
77. Mheshimiwa Spika, Huduma hii ina madhumuni ya
usimamizi na tathmini ya elimu ya juu.
Matokeo ya muda mfupi;
• Tathmini katika vyuo vinavyotoa elimu ya juu
kufanyika.
• Wahitimu waliomaliza masomo ya elimu ya juu
kuratibiwa.
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 60
Viashiria vya matokeo;
• Idadi ya wanafunzi wanaoendelea na masomo ya elimu
ya juu kijinsia.
• Idadi ya wahitimu wa elimu ya juu kijinsia.
78. Mheshimiwa Spika, Shughuli za huduma hii zinatekelezwa
na Kitengo cha Uratibu wa Elimu ya Juu. Kwa mwaka wa
fedha 2019/20, Huduma hii imepangiwa jumla ya TSh.
50,000,000.
PROGRAMU YA NNE: ELIMU MBADALA NA
MAFUNZO YA AMALI
79. Mheshimiwa Spika, Programu hii madhumuni yake ni kutoa
elimu ya mafunzo ya amali kwa mwanafuzi kulingana na
mahitaji ya soko la ajira. Programu hii ina programu ndogo
ndogo mbili kama ifuatavyo;
Programu ndogo ya Mafunzo ya Amali
80. Mheshimiwa Spika, Programu hii ina madhumuni ya kutoa
elimu itakayowawezesha vijana kujiajiri ili kujikwamua na
umasikini.
Matokeo ya muda mfupi;
• Mafunzo ya Amali na ufundi kutolewa.
Viashiria vya matokeo;
• Ukosefu wa ajira kwa vijana kupungua
• Idadi ya wanafunzi wanaomaliza mafunzo ya amali
kuongezeka.
81. Mheshimiwa Spika, shughuli za programu hii zinatekelezwa
na Mamlaka ya Mafunzo ya Amali. Kwa mwaka wa fedha
2019/20, Mamlaka imetengewa ruzuku ya TSh.
7,761,200,000.
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 61
Programu ndogo ya Elimu Mbadala na Watu Wazima
82. Mheshimiwa Spika, Programu hii ina madhumuni ya
kupunguza kiwango cha kutojua kusoma, kuandika na
kuhesabu miongoni mwa wanajamii.
Matokeo ya muda mfupi;
• Elimu mbadala na ya watu wazima kutolewa.
Viashiria vya matokeo;
• Kiwango cha kujua kusoma, kuandika na kuhesabu kwa
watu wazima,
• Idadi ya watu wazima wanaoshiriki katika madarasa ya
wanakisomo,
• Idadi ya vijana waliojiunga na madarasa na vituo vya
elimu mbadala,
• Idadi ya wanakisomo walioanzisha vikundi vya ushirika
Shabaha za Utekelezaji;
• Kuongeza kiwango cha kujua kusoma na kuandika
kutoka asilimia 84 mwaka 2012 hadi kufikia asilimia 90
ifikapo mwaka 2020.
83. Mheshimiwa Spika, Shughuli za programu hii zinatekelezwa
na Idara ya Elimu Mbadala na Watu Wazima. Kwa mwaka
wa fedha 2019/20, programu hii imetengewa jumla ya TSh.
8,974,245,000.
PROGRAMU YA TANO: UBORA WA ELIMU
84. Mheshimiwa Spika, Programu hii ina madhumuni ya kutoa
elimu bora kwa ngazi zote za elimu. Ina programu ndogo tatu
na maeneo matano ya kutoa huduma kama yafuatayo;
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 62
Huduma ya Mitaala na Vifaa vya Kufundishia
85. Mheshimiwa Spika, Huduma hii ina madhumuni ya
kutayarisha mitaala ya elimu na vifaa vya kufundishia na
kujifunzia kwa ngazi za elimu ya maandalizi, msingi,
sekondari na mafunzo ya Ualimu.
Matokeo ya muda mfupi;
• Mitaala ya Elimu na vifaa vya kufundishia na kujifunzia
kwa ngazi zote kutayarishwa.
Viashiria vya matokeo;
• Idadi ya Mitaala na vifaa vya kufundishia na kujifunzia
vilivyotayarishwa na kusambazwa katika skuli.
86. Mheshimiwa Spika, Shughuli za utowaji wa huduma hii
zinatekelezwa na Taasisi ya Elimu Zanzibar. Kwa mwaka wa
fedha 2019/20, Taasisi imetengewa ruzuku ya TSh.
573,100,000.
Huduma ya Upimaji na Tathmini ya Elimu
87. Mheshimiwa Spika, Programu hii ina madhumuni ya
kupima na kutathmini utekelezaji wa utoaji wa elimu.
Matokeo ya muda mfupi;
• Malengo ya elimu kupimwa.
Viashiria vya matokeo;
• Asilimia ya wanafunzi na kiwango cha mpito katika
ngazi za darasa la nne, darasa la sita, kidato cha pili,
kidato cha nne na cha sita.
• Asilimia ya ufaulu wa walimu wanafunzi waliofaulu
88. Mheshimiwa Spika, Shughuli za programu hii zinatekelezwa
na Baraza la Mitihani la Zanzibar. Kwa mwaka wa fedha
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 63
2019/20, programu hii imepangiwa ruzuku ya TSh.
4,941,800,000.
Huduma ya Ukaguzi wa Elimu
89. Mheshimiwa Spika, utoaji wa huduma hii una madhumuni
ya kusimamia utoaji wa elimu unaofuata mtaala na
kuhakikisha ufanisi na ubora wa elimu inayotolewa.
Viashiria vya matokeo;
• Idadi ya skuli zilizokaguliwa
• Idadi ya ripoti za ukaguzi zilizowasilishwa
90. Mheshimiwa Spika, Shughuli za huduma hii zinatekelezwa
na Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Elimu. Kwa mwaka wa fedha
2019/20, programu hii imepangiwa ruzuku ya TSh.
1,090,500,000.
Huduma za Maktaba
91. Mheshimiwa Spika, Programu hii ina madhumuni ya kutoa
fursa ya kutumia vitabu na vyanzo vyengine vya taaluma kwa
wananchi.
Matokeo ya muda mfupi;
• Kutoa nafasi kwa wanafunzi na watu wengine ya kupata
taarifa mbalimbali kupitia maktaba.
Viashiria vya matokeo;
• Idadi ya watu wanaotumia maktaba
• Idadi ya vitabu, CDs, magazeti na majarida yaliyopo
katika maktaba.
• Idadi ya skuli zenye maktaba kamili.
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 64
92. Mheshimiwa Spika, Shughuli za huduma hii zinatekelezwa
na Shirika la Huduma za Maktaba Zanzibar. Kwa mwaka wa
fedha 2019/20, programu hii imepangiwa kutumia ruzuku ya
TSh. 886,200,000.
Huduma ya Urajisi wa Elimu
93. Mheshimiwa Spika, Programu hii ina madhumuni ya
kuhakikisha Sheria, Sera na taratibu za Wizara zinafuatwa.
Pia kutoa leseni kwa walimu na kusajili skuli za Serikali na
za binafsi.
Matokeo ya muda mfupi;
• Skuli za Serikali na binafsi zenye viwango bora
kusajiliwa
• Leseni za walimu kutolewa.
Viashiria vya matokeo;
• Idadi ya leseni za walimu zilizotolewa.
• Idadi ya skuli zilizosajiliwa.
• Sheria ya Elimu iliyopitiwa na kurekebishwa.
• Idadi ya wanafunzi waliopata ujauzito na kurejea
masomoni baada ya kujifungua.
• Idadi ya kesi za ndoa kwa wanafunzi zilizofuatiliwa na
kutolewa uamuzi.
94. Mheshimiwa Spika, Shughuli za utowaji wa huduma hii
zinatekelezwa na Ofisi ya Mrajisi wa Elimu. Kwa mwaka wa
fedha 2019/20, programu hii imepangiwa kutumia jumla ya
TSh. 249,600,000.
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 65
Programu ndogo ya Elimu Mjumuisho na Stadi za
Maisha
95. Mheshimiwa Spika, Programu hii ina madhumuni ya kutoa
elimu kwa wote wakiwemo watoto wenye mahitaji maalum.
Matokeo ya muda mfupi;
• Vifaa vya kufundishia na kujifunzia kwa watoto wenye
mahitaji maalum kutolewa
Viashiria vya matokeo;
• Idadi ya wanafunzi na walimu katika Elimu Mjumuisho.
96. Mheshimiwa Spika, Shughuli za programu hii zinatekelezwa
na Kitengo cha Elimu Mjumuisho na Stadi za Maisha. Kwa
mwaka wa fedha 2019/20, Kitengo kimepangiwa kutumia
jumla ya TSh. 77,610,000.
Programu ndogo ya Teknolojia ya Habari na
Mawasiliano (TEHAMA)
97. Mheshimiwa Spika, Programu hii ina madhumuni ya
kuifanya teknolojia ya habari na mawasiliano itumike katika
kujifunza, kufundisha, ngazi ya utawala na katika maisha ya
kila siku.
Matokeo ya muda mfupi;
• Walimu na wanafunzi wanapatiwa mafunzo juu ya
matumizi ya Teknolojia ya kisasa.
Viashiria vya utekelezaji;
• Idadi ya walimu wenye ujuzi wa Teknolojia ya Habari
na Mawasiliano,
• Idadi ya vifaa vya Teknolojia ya Habari na mawasiliano
katika skuli na Wizara
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 66
• Idadi ya Taasisi za elimu zilizounganishwa na mkonga
wa Taifa.
• Mafunzo ya matumizi ya kompyuta kutolewa kuanzia
katika skuli za msingi.
98. Mheshimiwa Spika, Shughuli za programu hii zinatekelezwa
na Idara ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano Katika
Elimu. Katika mwaka wa fedha 2019/20, programu hii
imepangiwa kutumia jumla ya TSh. 526,393,000.
Programu ndogo ya Michezo na Utamaduni katika Skuli
99. Mheshimiwa Spika, Programu hii ina madhumuni ya
kumuandaa mwanafunzi kimwili, kiafya na kiakili katika
kujifunza kwa kupitia michezo.
Matokeo ya muda mfupi;
• Kuinua taaluma ya michezo katika skuli.
Viashiria vya matokeo;
• Idadi ya walimu wenye taaluma ya michezo
• Idadi ya skuli zenye viwanja vya michezo
• Idadi ya skuli zenye vifaa vya michezo
• Idadi ya wanafunzi wenye vipaji vya michezo
100. Mheshimiwa Spika, Shughuli za programu hii zinatekelezwa
na Idara ya Michezo na Utamaduni katika Elimu. Kwa
mwaka wa fedha wa 2019/20, programu hii imepangiwa
kutumia jumla ya TSh. 752,271,000.
PROGRAMU YA SITA: UTAWALA NA UONGOZI
101. Mheshimiwa Spika, Programu hii madhumuni yake
makubwa ni kuhakikisha nyenzo zilizo bora zinapatikana na
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 67
zinatumika kwa kuimarisha utoaji wa elimu. Programu hii ina
programu ndogo tatu kama zifuatavyo: -
Programu ndogo ya Uongozi kiujumla
102. Mheshimiwa Spika, programu hii ina madhumuni ya kutoa
ufanisi wa Uongozi na Utawala wa rasilimali za Wizara.
Matokeo ya muda mfupi;
• Kupatikana kwa ufanisi katika utoaji wa huduma,
uongozi na utawala wa rasilimali za Wizara.
Viashiria vya matokeo;
• Idadi ya wafanyakazi wanaoajiriwa na kustaafu,
• Mafunzo yanayotolewa kwa wafanyakazi.
Shabaha za Utekelezaji;
• Kuongeza ufanisi katika kutoa huduma kwa
wafanyakazi na upatikanaji wa nyenzo za kufanyia kazi.
103. Mheshimiwa Spika, Shughuli za programu hii zinatekelezwa
na Idara ya Utumishi na Uendeshaji. Kwa mwaka wa fedha
2019/20, programu hii imepangiwa kutumia jumla ya TSh.
6,091,971,000.
Programu ndogo ya Uratibu wa Shughuli za Mipango,
Sera na Utafiti
104. Mheshimiwa Spika, programu hii ina madhumuni ya
kufanikisha na kuratibu Mipango, Sera na Utafiti katika
Wizara.
Matokeo ya muda mfupi;
Kupatikana kwa sera na mipango ya Wizara, kufanya utafiti
na kufanya ufuatiliaji na tathmini.
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 68
Viashiria vya matokeo;
• Idadi za tafiti zilizofanywa
• Ripoti za utekelezaji na ripoti za tathmini.
105. Mheshimiwa Spika, Shughuli za programu hii zinatekelezwa
na Idara ya Mipango, Sera na Utafiti. Kwa mwaka wa fedha
2019/20, programu hii imepangiwa kutumia jumla ya TSh.
5,233,552,000.
Programu ndogo ya kuratibu shughuli za Elimu Pemba
106. Mheshimiwa Spika, programu hii ina madhumuni ya
kuratibu na kusimamia shughuli zote za elimu kwa upande
wa Pemba. Matokeo ya muda mfupi na shabaha za
utekelezaji zinazotumika ni kama zile zilizoelezwa katika
programu za Uongozi kiujumla na Uratibu wa shughuli za
Mipango, Sera na Utafiti.
107. Mheshimiwa Spika, msimamizi wa shughuli za programu hii
ni Afisa Mdhamini wa Wizara yangu kupitia katika Divisheni
ya Idara ya Uendeshaji na Utumishi Pemba.
108. Mheshimiwa Spika, kwa mwaka wa fedha 2019/20,
programu hii imepangiwa kutumia TSh. 3,273,678,000.
MGAWANYO WA FEDHA KWA PROGRAMU
109. Mheshimiwa Spika, Sehemu hii inaonesha mgawanyo wa
fedha kwa Programu za Wizara ya Elimu na Mafunzo ya
Amali yenye kuzingatia gharama za Idara/Vitengo/Taasisi
zilizomo katika programu husika.
PROGRAMU YA KWANZA:
ELIMU YA MAANDALIZI NA MSINGI
Idara Husika: Idara ya Elimu ya Maandalizi na Msingi
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 69
110. Gharama za Programu: Jumla ya TSh. 9,010,580,000
zimepangwa kwa ajili ya kufanikisha programu hii. Kati ya
fedha hizo, TSh. 540,878,000 kwa kazi za kawaida na TSh.
8,469,702,000 kwa kazi za maendeleo.
PROGRAMU YA PILI: ELIMU YA SEKONDARI
Idara Husika: Idara ya Elimu ya Sekondari
111. Gharama za Programu: Jumla ya TSh. 104,591,382,000
zimepangwa kwa ajili ya kufanikisha programu hii. Kati ya
hizo TSh. 49,187,036,000 kwa kazi za kawaida na TSh.
55,404,346,000.
PROGRAMU YA TATU: ELIMU YA JUU
Taasisi Husika: Idara ya Mafunzo ya Ualimu, Chuo Kikuu
cha Taifa cha Zanzibar, Taasisi ya Karume ya Sayansi na
Teknolojia, Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu na Kitengo cha
Uratibu wa Elimu wa Juu.
Gharama za Programu: Jumla ya TSh. 24,883,067,000
zimepangwa kwa kufanikisha programu hii kwa kazi za
kawaida.
PROGRAMU YA NNE: ELIMU MBADALA NA
MAFUNZO YA AMALI
Idara Husika: Mamlaka ya Mafunzo ya Amali pamoja na
Idara ya Elimu Mbadala na Watu Wazima.
Gharama za Programu: Jumla ya TSh. 16,735,445,000
zimepangwa kwa ajili ya kufanikisha programu hii. Kati ya
fedha hizo, TSh. 8,735,445,000 ni kwa kazi za kawaida na
TSh. 8,000,000,000 kwa kazi za maendeleo.
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 70
PROGRAMU YA TANO: UBORA WA ELIMU
Idara Husika: Taasisi ya Elimu ya Zanzibar, Baraza la
Mitihani la Zanzibar, Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Elimu,
Kitengo cha Elimu Mjumuisho na Stadi za Maisha, Shirika la
Huduma za Maktaba Zanzibar, Idara ya Teknolojia ya Habari
na Mawasiliano Katika Elimu, Ofisi ya Mrajisi wa Elimu,
Idara ya Michezo na Utamaduni Katika Skuli.
Gharama za Programu: Jumla ya TSh. 9,097,474,000
zimepangwa kwa ajili ya kufanikisha programu hii kwa kazi
za kawaida.
PROGRAMU YA SITA: UONGOZI NA UTAWALA
Idara Husika: Idara ya Utumishi na Uendeshaji, Idara ya
Mipango, Sera na Utafiti na Ofisi ya Elimu Pemba.
Gharama za Programu: Jumla ya TSh. 14,599,201,000
zimepangwa kwa ajili ya kufanikisha programu hii kwa kazi
za kawaida. Kati ya fedha hizo, TSh. 1,500,000,000 kwa kazi
za maendeleo.
112. Mheshimiwa Spika, kwa mwaka wa fedha 2018/19 Wizara
ya Elimu na Mafunzo ya Amali ilikadiriwa kukusanya
mapato ya jumla ya TSh. 104,095,000. Hadi kufikia Aprili,
2019 Wizara yangu imefanikiwa kukusanya jumla ya TSh.
82,185,628 sawa na asilimia 78 ambazo zimewasilishwa
hazina. Fedha hizo ni makusanyo ya malipo ya leseni za
walimu na ada za usajili wa skuli za binafsi zinazotoa
huduma ya Elimu katika ngazi ya Maandalizi, Msingi na
Sekondari.
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 71
JUMLA YA GHARAMA ZA WIZARA YA ELIMU NA
MAFUNZO YA AMALI
113. Mheshimiwa Spika, gharama kwa programu zote sita za
Wizara ni TSh. 178,917,149,000 sawa na bajeti yote ya
Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali inayotumia programu
iliyoainishwa Barazani. Kati ya fedha hizo, TSh.
105,543,101,000 zimetengwa kwa kazi za kawaida na TSh.
73,374,048,000 kwa kazi za maendeleo. Kati ya fedha za
maendeleo, TSh. 5,800,000,000 ni mchango wa SMZ na TSh.
67,574,048,000 ni mchango wa Wahisani.
SHUKURANI
114. Mheshimiwa Spika, napenda kuchukua fursa hii kutoa
shukurani za dhati kwa washirika wote wa sekta ya elimu
wakiwemo wananchi, washirika wa maendeleo na mashirika
ya misaada ya kimataifa kwa kutuunga mkono katika
jitihada zetu za kuendeleza elimu. Tunatoa shukurani zetu
za pekee kwa Serikali ya Sweden, Marekani, Oman na
Serikali ya Watu wa China, Serikali ya India na Iran. Pia,
napenda kuyashukuru mashirika mbalimbali ya kimataifa
yakiwemo, Sida, USAID, KOICA, UNESCO, UNICEF,
ILO, VSO, OPEC Fund, GPE, Good Neighbours, Table for
Two na Patnership for Child Development. Shukurani zetu
za dhati kwa Aga Khan Foundation, Benki ya Dunia, Benki
ya Kiarabu kwa Maendeleo ya Afrika na Benki ya
Maendeleo ya Afrika. Napenda pia, kuyashukuru mashirika
yasio ya kiserikali yakiwemo Milele Zanzibar Foundation,
Jumuiya ya Madrasa Early Childhood Education Program,
NFU, FAWE, Save the Children Fund, “Book Aid
International” na ZAPDD. Vile Vile napenda kuyashukuru
makampuni na mashirika mbalimbali ya kifedha ya kiwemo
ZTE, Benki ya watu wa Zanzibar, CRDB, Barclays, NBC,
NMB, Postal Bank Tanzania, ZANTEL, kampuni ya SHA
chini ya Mheshimiwa Ahmada Abdulwakil na Bakhresa.
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 72
SACCOSS mbalimbali na Tigo kwa misaada yao katika
sekta yetu ya elimu na kwa wafanyakazi kwa ujumla.
Shukurani za pekee ziziendee Kamati zetu za Skuli na
Halmashauri zetu za Wilaya kwa kazi kubwa wanayoifanya
katika kuchangia maendeleo ya elimu Zanzibar.
115. Mwisho, napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa
viongozi wenzangu kuanzia wewe Mheshimiwa Spika na
wajumbe wa Baraza lako Tukufu kwa ushirikiano mkubwa
walionipa na kwa namna watakavyoichangia hotuba yangu
hii. Nasema ahsanteni sana.
116. Mheshimiwa Spika, sasa naliomba Baraza lako Tukufu
liidhinishe makadirio ya matumizi ya Wizara ya Elimu na
Mafunzo ya Amali ya jumla ya TSh. 178,917,149,000 kwa
mwaka wa fedha 2019/20, ili kuiwezesha Wizara yangu
kutekeleza majukumu yake.
Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja.
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 73
KIAMBATISHO
(Takwimu za Maendeleo ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali
Kwa Kipindi cha 2014/15- 2018/19 na Hali Halisi ya Elimu na
Mafunzo ya Amali kwa Mwaka 2018/19)
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 74
JADWELI NAM. 1
2015 SERIKALI BINAFSI JUMLA
SKULI ZA MAANDALIZI 277 289 328 347 30 352 382
SKULI ZA MSINGI (DAR I - VII) 260 285 299 357 266 115 381
SKULI ZA MSINGI/KATI 'A' (DAR I - KID 2) 49 46 41 38 19 10 29
SKULI ZA MSINGI/KATI 'B' (DAR I - KID 4) 57 61 67 54 2 57 59
SKULI ZA MSINGI/SEKOND.(DAR I - KID 6) 4 2 5 9 0 9 9
SKULI ZA KATI 'A' FORM 1 - FORM 2 4 2 3 3 7 0 7
SKULI ZA SEKOND. FORM 1 - FORM 4 122 134 117 135 127 9 136
SKULI ZA SEKOND. YA JUU (FORM 1 - 6) 11 21 13 11 24 2 26
SKULI ZA MCHEPUO WA KIFARANSA 1 1 1 1 1 0 1
SKULI ZA MCHEPUO WA UFUNDI 3 3 2 2 2 0 2
SKULI ZA MCHEPUO WA BIASHARA 1 2 1 1 2 0 2
SKULI ZA MCHEPUO WA KIISLAMU 2 2 1 2 2 0 2
SKULI ZA MCHEPUO WA SAYANSI JAMII 3 6 2 1 2 0 2
SKULI ZA MCHEPUO WA SAYANSI 4 9 10 7 8 0 8
SKULI ZA MCHEPUO WA KOMPYUTA 1 1 1 1 3 0 3
SKULI ZA MCHEPUO WA MICHEZO 0 0 0 2 0 0 0
VITUO VYA MAFUNZO YA AMALI 3 3 3 2 2 0 2
VYUO VYA UALIMU 3 3 2 2 2 0 2
TAASISI YA SAYANSI NA TEKNOLOJIA 1 1 1 1 1 0 1
CHUO KIKUU CHA TAIFA Z'BAR (SUZA) 1 1 1 1 1 0 1
CHUO KIKUU CHA SUMAIT - CHUKWANI 1 1 1 1 0 1 1
CHUO KIKUU CHA ZANZIBAR 1 1 1 1 0 1 1
JUMLA 809 874 900 979 501 556 1057
2019
UKUAJI WA IDADI NA AINA ZA VITUO VYA ELIMU VILIVYOSAJILIWA, 2015 - 2019
AINA ZA VITUO 20172016 2018
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 75
JADWELI NAM. 2(a)
*ONGEZEKO
KWA
MWAKA %
95,818 94,848 103,950 105,653
4 - 5(Ulezi) 4 - 5(Ulezi) 4 - 5(Ulezi) 4 - 5(Ulezi)
241,718 239,284 237,634 246,069
6 - 11(Msingi) 6 - 11(Msingi) 6 - 11(Msingi) 6 - 11(Msingi)
85,744 84,871 76,060 76,483
12 - 13(Kid 1-2) 12 - 13(Kid 1-2) 12 - 13(Kid 1-2) 12 - 13(Kid 1-2)
327,462 324,155 313,694 326,209
6 - 13(Dar1-Kid2) 6 - 13(Dar1-Kid2) 6 - 13(Dar1-Kid2) 6 - 13(Dar1-Kid2)
69,369 68,666 66,780 73,487
14 - 15 (Kid 3 - 4) 14 - 15 (Kid 3 - 4) 14 - 15 (Kid 3 - 4) 14 - 15 (Kid 3 - 4)
396,831 392,821 369,993 399,696
6 - 15 (Dar1-Kid4) 6 - 15 (Dar1-Kid4) 6 - 15 (Dar1-Kid4) 6 - 15 (Dar1-Kid4)
* Kuanzia mwaka 2016 umri wa watoto wa kwenda skuli katika ngazi tafauti za elimu umefuata sera mpya ya elimu ya mwaka 2006 ilivyoagiza
0.1
-5.7
7 - 13 (Msingi)
14 - 15 (KIidato 1 - Kidato 2)
135,965
265,591 -1.6
1.0
-0.7
60,184
398,506
7 - 15 (Darasa 1-Kidato 2)
16 - 17 (Kidato 3 - 4)
3.6
7 - 17 (Msingi/Kati "B")(Darasa 1-Kidato 4)
72,731
338,322
UKUAJI WA IDADI YA WATOTO WA UMRI WA KWENDA SKULI KWA MWAKA, 2015 - 2019
UMRI WA NGAZI YA ELIMU 2015 2016* 2017* 2018* 2019*
4 - 6 (Ulezi)
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 76
JADWELI NAM. 2(b)
SERIKALI BINAFSI JUMLA
Maandalizi 41,687 55,731 62,720 72,151 38,370 47,604 85,974 19.84
Msingi (Darasa I - VI/VII) 261,212 249,143 256,048 276,858 257,453 33,057 290,510 2.69
Kati 'A' (Kidato 1 - 2 Bila ya Mchepuo) 52,876 80,423 81,246 67,657 63,683 5,864 69,547 7.09
Kati 'B' (Kidato 3 - 4 Bila ya Mchepuo) 26,392 28,656 31,828 49,024 49,736 6,268 56,004 20.69
Sekondari ya Juu (Kidato 5 - 6) 2,640 3,848 3,643 4,590 4,076 732 4,808 16.17
Vipawa vya Juu (Kidato 1 - 4) 1,049 1,027 563 585 559 - 559 -14.56
Mchepuo wa Sayansi (Kidato 1 - 4) 1,086 1,464 1,580 2,033 2,305 - 2,305 20.70
Mchepuo wa Ufundi (Kidato 1 - 4) 375 361 362 378 403 - 403 1.82
Mchepuo wa Kifaransa (Kidato 1 - 4) 153 190 189 197 211 - 211 8.37
Mchepuo wa Kiislamu (Kidato 1 - 4) 367 428 409 414 455 - 455 5.52
Mchepuo wa Biashara (Kidato 1 - 4) 503 361 585 568 572 - 572 3.27
Mchepuo wa Kompyuta (Kidato1 - 4) 548 470 452 447 382 - 382 -8.63
Mchepuo wa Sayansi Jamii (Kidato 1 - 4) 936 870 591 435 196 77 273 -26.51
Mchepuo wa Wanawake (Kidato 1- 4) 640 915 715 - - - - N/A
Ufundi Sanifu 315 308 545 522 649 - 649 19.81
Ualimu (Benjamin Mkapa) Diploma 228 123 - - - - - N/A
Ualimu (Kiislamu) Diploma - Kiuyu + Mazizini 556 809 395 841 1,224 - 1,224 21.81
Chuo Kikuu Cha Taifa Zanzibar - SUZA 2,538 2,925 2,952 4,465 3,892 - 3,892 11.28
Chuo Kikuu Cha SUMAIT - Chukwani 1,917 1,684 1,506 969 - 841 841 -18.62
Chuo Kikuu Cha Zanzibar 1,915 2,719 2,579 3,094 - 2,334 2,334 5.07
Jumla 397,933 432,455 448,908 485,228 424,166 96,777 520,943 6.97
UKUAJI WA UANDIKISHAJI WA WANAFUNZI KATIKA NGAZI MBALI MBALI, 2015 - 2019
NGAZI YA ELIMU
2019
2015 2016
ONGEZEKO
KWA
MWAKA %2017 2018
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 77
JADWELI NAM. 2(c)
UMRI WA NGAZI YA ELIMU 2015 2016 2017 2018 2019
Maandalizi 30.7 58.2 66.1 69.4 81.4
Msingi 98.4 103.1 106.9 116.5 118.1
Kati 'A' (Kid 1 - Kid 2)* 76.3 97.6 98.6 92.1 94.3
Kati 'B' (Kidato 3 - 4)* 47.7 45.6 50.5 64.3 74.5
Msingi na Kati 'A' (Dar.I - Kid.2)* 93.6 101.6 104.7 110.6 112.4
Msingi na Kati 'B' (Dar.I - Kid.4)* 86.5 91.9 95.3 90.2 96.0
*Pamoja na Michepuo
ASILIMIA YA UANDIKISHAJI (GROSS LEVEL ENROLMENT RATIO)
KATIKA NGAZI MBALI MBALI ZA ELIMU, 2015 - 2019
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 78
JADWELI NAM. 3
WAS J'LA WAS J'LA WAS J'LA WAS J'LA WAS J'LA WAS J'LA WAS J'LA WAS J'LA
Darasa I 21728 44189 25510 52587 25218 51389 29167 60040 25844 53389 3775 7503 29619 60892 8.05 8.35
Darasa II 20364 41316 21337 43313 23931 48708 24304 49341 23710 48403 3453 6738 27163 55141 7.47 7.48
Darasa III 20083 40134 20547 41499 20945 42157 24065 48364 20938 42928 3012 6033 23950 48961 4.50 5.10
Darasa IV 19139 38218 19726 39391 19869 40055 21370 43267 23182 46941 2572 5059 25754 52000 7.70 8.00
Darasa V 18273 36093 19326 38523 19629 39030 19513 38736 18516 36636 2098 4159 20614 40795 3.06 3.11
Darasa VI 15795 29793 17310 33491 18165 34709 19199 37110 15266 29156 1808 3565 17074 32721 1.97 2.37
Darasa VII 15844 31469 178 339 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 N/A N/A
Kid. I (Michepuo) 678 1296 999 1587 593 948 812 1345 765 1225 19 19 784 1244 3.70 -1.02
Kid I (Wengine) 14783 28555 28886 55642 17624 34711 17595 33702 17138 32876 1620 3105 18758 35981 6.13 5.95
Kid.2 (Michepuo) 654 1351 894 1698 964 1566 628 1035 784 1306 22 22 806 1328 5.36 -0.43
Kid. 2 (Wengine) 13211 24321 13175 24781 25462 46535 17637 33955 16397 30807 1512 2759 17909 33566 7.90 8.39
Kid. 3 (Michepuo) 588 1259 768 1499 803 1568 1146 1825 678 1114 21 21 699 1135 4.42 -2.56
Kid. 3 (Wengine) 7519 13534 9091 15749 9577 16652 19574 33275 14153 25115 1844 3352 15997 28467 20.77 20.43
Kid. 4 (Michepuo) 553 1037 712 1489 693 1364 745 1437 899 1438 15 15 914 1453 13.38 8.80
Kid. 4 (Wengine) 7357 12858 7335 12907 8903 15176 9167 15749 15299 24621 1588 2916 16887 27537 23.09 20.97
Kid 5 na NTA 4 1112 2064 892 2007 1267 2370 1437 2951 1245 2622 208 397 1453 3019 6.92 9.97
NTA 5 16 83 31 96 98 142 86 196 66 156 0 0 66 156 42.51 17.09
Kid 6 na NTA 6 408 815 999 2053 821 1666 1044 2063 934 1923 180 335 1114 2258 28.55 29.02
Jumla 178105 348385 187716 368651 194562 378746 207489 404391 195814 380656 23747 45998 219561 426654 5.37 5.20
UKUAJI WA IDADI YA WANAFUNZI KATIKA MADARASA, 2015 - 2019
MADARASASERIKALI BINAFSI2015 2017
ONGEZEKOKWA MWAKA (%)
20192016 JUMLA2018
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 79
JADWELI NAM. 4
WALIOSOMEA WASIOSOMEA JUMLA % WASIOSOMEA WALIOSOMEA WASIOSOMEA JUMLA %WASIOSOMEA WALIOSOMEA WASIOSOMEA JUMLA %WASIOSOMEA
2015 9942 89 10031 0.9 1441 354 1795 19.7 11383 443 11826 3.7
2016 9857 93 9950 0.9 1638 405 2043 19.8 11495 498 11993 4.2
2017 10187 87 10274 0.8 1865 401 2266 17.7 12052 488 12540 3.9
2018 10674 59 10733 0.5 2108 319 2427 13.1 12782 378 13160 2.9
2019 11420 52 11472 0.5 2584 374 2958 12.6 14004 426 14430 3.0
Takwimu hizi hazijumuishi Walimu wa Chuo cha Karume na Skuli za Maandalizi
UKUAJI WA IDADI YA WALIMU KATIKA NGAZI YA MSINGI NA SEKONDARI
JUMLA
(DARASA LA 1 - KIDATO 6) 2015 - 2019 SKULI ZA SERIKALI NA BINAFSI
MWAKA
SKULI ZA BINAFSISKULI ZA SERIKALI
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 80
JADWELI NAM. 5
IDADI YA IDADI YA W'FUNZI KWA IDADI YA IDADI YA W'FUNZI KWA IDADI YA IDADI YA W'FUNZI KWA
WANAFUNZI WALIMU WALIMU WANAFUNZI WALIMU WALIMU WANAFUNZI WALIMU WALIMU
2015 318,955 10,031 28 29,226 1,795 14 305,121 11,593 26
2016 335,080 9,950 34 33,226 2,043 16 368,306 11,993 31
2017 341,870 10,274 33 35,970 2,266 16 377,840 12,540 30
2018 361,631 10,733 34 42,251 2,427 17 403,882 13,160 31
2019 379,845 11472 33 46,038 2958 16 425,883 14,430 30
UKUAJI WA WANAFUNZI NA WALIMU (PUPIL TEACHER RATIO)
KATIKA NGAZI YA MSINGI NA KATI (DAR. 1 - KID. 6) 2015 - 2019
SKULI ZA SERIKALI NA BINAFSI
MWAKA
SKULI ZA SERIKALI SKULI ZA BINAFSI JUMLA
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 81
JADWELI NAM. 6a(i)
WAV WAS JUMLA WAV WAS JUMLA WAV WAS JUMLA
2014 10119 11825 21944 6373 8011 14384 63.0 67.7 65.5
2015 10820 13231 24051 6950 9794 16744 64.2 74.0 69.6
2016 11673 13414 25087 7497 10084 17581 64.2 75.2 70.1
2017 20514 26056 46570 13670 20791 34461 66.6 79.8 74.0
2018 15211 17425 32636 9921 13986 23907 65.2 80.3 73.3
MATOKEO YA MITIHANI WA KIDATO CHA 2, 2014- 2018
MWAKA
WATAHINIWA WALIOFAULU KIMA CHA KUFAULU (%)
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 82
JADWELI NAM. 6a(ii)
STD VI STD VII
1 Madungu A Sek Madungu A Fidel Castro Fidel Castro Fidel Castro Lumumba
2 Chambani Mauwani Lumumba Lumumba Lumumba Fidel Castro
3 Kisiwani Mahonda Madungu "B" Tumekuja S.O.S Hermann Moh'd Juma Pindua
4 Jendele Shengejuu Zanzibar Ccommercial Tumekuja Chasasa 'B' Feza
5 Makangale Pandani Mikunguni Ben-bella Laureat International Mikindani Dole
6 Jongowe Kangani Ben-bella Mikunguni Mahad Istiqama Zanzibar Commercial
7 Muyuni Uroa Chasasa Kiembesamaki Islamic Ben-bella Chasasa 'B'
8 Vikunguni Hurumzi Tumekuja Mahad Istiqama Sunni Madressa Ben-bella
9 Cheju Mfenesini S.O.S Hermann Zanzibar Commercial Francis Maria Brilliant Academy
10 Mfurumatonga Maendeleo High-view International Chasasa 'B' J.K.U Mikunguni
2018
NAFASI ZA SKULI KUMI BORA KATIKA MATOKEO YA MTIHANI
WA KIDATO CHA PILI (2014 - 2018)
2017201620152014NAFASI
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 83
JADWELI NAM. 6(b)(i)
JUMLA JUMLA
DIV.I-IV DIV. I-IV
2014 5267 57 326 614 2170 3167 1.1 6.2 11.7 41.2 60.1
2015 5188 46 260 697 2839 3842 0.9 5.0 13.4 54.7 74.1
2016 6207 145 450 891 2954 4440 2.3 7.2 14.4 47.6 71.5
2017 6905 85 433 849 3429 4796 1.2 6.3 12.3 49.7 69.5
2018 7444 112 463 1054 3478 5070 1.5 6.2 14.2 46.7 68.1
DIV. II DIV. III DIV. IV
MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA 4, 2014- 2018 WAVULANA
MWAKA WATAHINIWA
WALIOFAULU KIMA CHA KUFAULU (%)
DIV. I DIV. II DIV. III DIV. IV DIV. I
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 84
JADWELI NAM. 6(b)(ii)
JUMLA JUMLA
DIV. I-IV DIV. I - IV
2014 7545 52 301 681 3512 4546 0.7 4.0 9.0 46.5 60.3
2015 7020 14 185 658 4191 5048 0.2 2.6 9.4 59.7 71.9
2016 7835 97 411 995 4150 5653 1.2 5.2 12.7 53.0 72.2
2017 9541 70 370 907 4930 6277 0.7 3.9 9.5 51.7 65.8
2018 9824 73 422 1151 5273 6861 0.7 4.3 11.7 53.7 69.8
DIV. II DIV. III DIV. IV
MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA 4, 2014 - 2018 WASICHANA
MWAKA WATAHINIWA
WALIOFAULU KIMA CHA KUFAULU (%)
DIV.I DIV.II DIV.III DIV.IV DIV. I
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 85
JADWELI NAM. 6(b)(iii)
JUMLA JUMLA
DIV. I - IV DIV. I - IV
2014 12812 109 627 1295 5682 7713 0.851 4.894 10.11 44.35 60.201
2015 12208 60 445 1355 7030 8890 1.054 6.658 16.85 75.44 72.821
2016 14042 242 861 1886 7104 10093 1.723 6.132 13.43 50.59 71.877
2017 16446 155 803 1756 8359 11073 1.471 4.883 10.68 50.83 67.329
2018 17268 185 885 2205 8751 12026 1.401 5.125 12.77 50.68 69.643
DIV. I DIV. II DIV. III DIV. IV
MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA 4, 2014 - 2018
JUMLA YA WAVULANA NA WASICHANA
MWAKA WATAHINIWA
WALIOFAULU KIMA CHA KUFAULU (%)
DIV.I DIV.II DIV. III DIV. IV
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 86
JADWELI NAM. 6(c)(i)
JUMLA JUMLA
DIV. I - IV DIV. I - IV
2013/14 586 26 98 295 129 548 4.4 16.7 50.3 22.0 93.5
2014/15 358 41 98 164 41 344 11.5 27.4 45.8 11.5 96.1
2015/16 985 33 213 515 130 891 3.4 21.6 52.3 13.2 90.5
2016/17 777 43 188 370 79 680 5.5 24.2 47.6 10.2 87.5
2017/18 871 77 256 476 41 850 8.8 29.4 54.6 4.7 97.6
MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA 6, 2013/14 - 2017/18 WAVULANA
MWAKA WATAHINIWA
WALIOFAULU KIMA CHA KUFAULU (%)
DIV.I DIV. II DIV. III DIV.IV DIV.I DIV. II DIV. III DIV. IV
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 87
JADWELI NAM. 6(c)(ii)
JUMLA JUMLA
DIV. I - IV DIV. I - IV
2013/14 573 25 96 334 104 559 4.4 16.8 58.3 18.2 97.6
2014/15 315 58 95 126 33 312 18.4 30.2 40.0 10.5 99.0
2015/16 978 17 164 612 128 921 1.7 16.8 62.6 13.1 94.2
2016/17 727 45 167 425 78 715 6.2 23.0 58.5 10.7 98.3
2017/18 938 48 251 576 51 926 5.1 26.8 61.4 5.4 98.7
MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA 6, 2013/14 - 2017/18 WASICHANA
WALIOFAULU KIMA CHA KUFAULU (%)
MWAKA WATAHINIWA DIV. I DIV. II DIV. III DIV. IVDIV. IV DIV. I DIV. II DIV. III
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 88
JADWELI NAM. 6(c)(iii)
JUMLA JUMLA
DIV. I - IV DIV. I - IV
2013/14 1159 51 194 629 233 1107 4.4 16.7 54.3 20.1 95.5
2014/15 673 99 193 290 74 656 14.7 28.7 43.1 11.0 97.5
2015/16 1963 50 377 1127 258 1812 2.5 19.2 57.4 13.1 92.3
2016/17 1504 88 355 795 157 1395 5.9 23.6 52.9 10.4 92.8
2017/18 1809 125 507 1052 92 1776 6.9 28.0 58.2 5.1 98.2
MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA 6, 2013/14 - 2017/18
WALIOFAULU KIMA CHA KUFAULU (%)
JUMLA YA WAVULANA NA WASICHANA
MWAKA WATAHINIWA DIV. I DIV. II DIV. III DIV. IVDIV. III DIV.IV DIV.I DIV. II
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 89
JADWELI NAM. 6(d)
WAS JUMLA WAS JUMLA WAS JUMLA WAS JUMLA
20 8217 11
213 276161 219
(85.0%) (13.4%) (75.6%) (79.4%)
2014/15 21 9320 59
208 264185 236
(95.2%) (63.4%) (88.9%) (89.4%)
27 91 254 321
(84.4%) (82.7%) (81.1%) (82.3%)
32 80 144 175
(84.2%) (76.9%) (70.9%) (71.4%)
38 118 102 129
(97.4%) (92.2%) (71.8%) (73.3%)
2017/18 39 128 142 176
2013/14
UALIMU DIPLOMA
MATOKEO YA MITIHANI MINGINE YA TAIFA YA TANZANIA 2013/14 - 2017/18
MWAKA WATAHINIWA
FTC / DIPLOMA YA UFUNDI NTA 6
WALIOFAULU WALIOFAULUWATAHINIWA
2015/16 32 110 313 390
2016/17 38 104 203 245
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 90
JADWELI NAM. 7
W'FANYA W'FAULU % W'FANYA W'FAULU % W'FANYA W'FAULU % W'FANYA W'FAULU % W'FANYA W'FAULU %
MJINI 1321 517 39.1 1155 443 38.4 1017 392 38.5 1111 618 55.6 1339 552 41.2
MAGHARIBI 'A' & 'B' 1127 475 42.1 1355 685 50.6 1071 559 52.2 1198 736 61.4 1291 698 54.1
KASKAZINI 'A' 405 177 43.7 299 128 42.8 210 74 35.2 199 110 55.3 202 72 35.6
KASKAZINI 'B' 129 48 37.2 157 80 51.0 111 46 41.4 95 53 55.8 136 51 37.5
KATI 370 142 38.4 477 230 48.2 337 170 50.4 387 220 56.8 399 178 44.6
KUSINI 142 61 43.0 142 72 50.7 118 57 48.3 139 61 43.9 140 75 53.6
MICHEWENI 185 72 38.9 101 21 20.8 121 39 32.2 97 43 44.3 96 40 41.7
WETE 470 210 44.7 260 99 38.1 374 141 37.7 303 159 52.5 335 167 49.9
CHAKE CHAKE 337 121 35.9 278 118 42.4 299 123 41.1 273 168 61.5 341 207 60.7
MKOANI 172 68 39.5 163 64 39.3 129 65 50.4 98 70 71.4 145 80 55.2
ZANZIBAR 4658 1891 40.6 4387 1940 44.2 3787 1666 44.0 3900 2238 57.4 4424 2120 47.9
WILAYA2016 2017 20182014 2015
MATOKEO YA MTIHANI KWA WATAHINIWA WA FARAGHA KIDATO CHA 4 VITUO VYA ZANZIBAR, 2014- 2018
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 91
JADWELI NAM. 8
MATOKEO YA MTIHANI KWA WATAHINIWA WA FARAGHA,
KIDATO CHA 6, VITUO VYA ZANZIBAR, 2013/2014 - 2017/2018
JUMLA YA WAVULANA NA WASICHANA
2017/20182013/2014 2016/20172014/2015 2015/2016
KITUO
Lumumba 108 43 39.81 56 31 55.36 57 30 52.63 82 41 50.00 52 27 51.92
F/Castro 8 4 50.00 8 3 37.50 - - - 14 3 21.43 7 2 28.57
Ben-Bella 113 23 20.35 19 17 89.47 19 16 84.21 44 35 79.55 21 12 57.14
Zanzibar Comm. 15 5 33.33 5 2 40.00 5 2 40.00 12 9 75.00 5 5 100.00
Utaani 32 13 40.63 2 1 50.00 2 1 50.00 13 11 84.62 9 9 100.00
Shamiani 41 11 26.83 14 13 92.86 14 13 92.86 17 17 100.00 11 11 100.00
Pemba Islamic 17 16 94.12 2 2 100.00 2 2 100.00 7 7 100.00 2 1 50.00
Hamamni 14 4 28.57 0 0 - - - - 26 19 73.08 6 6 100.00
Uweleni 23 6 26.09 0 0 - - - - 5 5 100.00 5 5 100.00
CCK 33 8 24.24 0 0 - - - - - - 0.00 - - -
WALIOFAULU
WATAHINIWA
WALIOFAULU
WALIOFAULU
KIMA CHA KUFAULU (%
)
KIMA CHA KUFAULU (%
)
WATAHINIWA
WALIOFAULU
WALIOFAULU
KIMA CHA KUFAULU (%
)
KIMA CHA KUFAULU (%
)
KIMA CHA KUFAULU (%
)
WATAHINIWA
WATAHINIWAKITUO
WATAHINIWA
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 92
JADWELI NAM.8 Iinaendelea
Kiponda 31 11 35.48 13 13 100.00 13 13 100.00 35 30 85.71 13 12 92.31
Al - Falah 14 8 57.14 0 0 0.00 - - - - - 0.00 - - -
Nyuki JWTZ 12 7 58.33 0 0 0.00 - - - 28 26 92.86 10 0 0.00
Mbarali 14 1 7.14 0 0 0.00 - - - - - 0.00 - - -
Mkwajuni 25 5 20.00 8 7 87.50 8 7 87.50 - - 0.00 3 2 66.67
M/kwe 'C' 55 17 30.91 24 21 87.50 25 21 84.00 37 25 67.57 37 32 86.49
Philter F.School 0 0 0.00 0 0 0.00 - - - - - 0.00 - - -
AL HARAMAIN 45 24 53.33 0 0 0.00 - - - 74 59 79.73 - - -
Haile Selassie 33 11 33.33 6 5 83.33 7 5 71.43 - - 0.00 - - -
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 93
JADWELI NAM.8 Iinaendelea
Mchangamdogo 0 0 0.00 11 7 0.00 11 7 63.64 37 33 89.19 15 13 86.67
K/Samaki 24 8 33.33 21 11 52.38 21 11 52.38 24 17 70.83 26 20 76.92
HIGH VIEW 0 0 0.00 0 0 0.00 - - - - - 0.00 - - -
Tumekuja - - 0.00 - - 0.00 - - - 17 9 52.94 11 7 63.64
Mazizini Islamic - - 0.00 - - 0.00 - - - 11 5 45.45 - - -
Azania - - 0.00 - - 0.00 - - - 38 25 65.79 - - -
Jabal Hiraa - - 0.00 - - 0.00 - - - 82 75 91.46 - - -
Chasasa - - - - - - - - - 15 7 46.67 6 3 50.00
Faraja - - - - - - - - - - - - 18 17 94.44
Jumla 644 220 34.16 644 220 34.16 184 128 69.57 618 458 74.11 257 184 71.5953
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 94
JADWELI NAM. 9
(TSH.000,000)
PATO LA
TAIFA KAWAIDA MAENDELEO JUMLA KAWAIDA MAENDELEO JUMLA PLT SERIKALI
2014/15 2,133,500 431,404 51,880 483,284 96,827 2,900 99,727 4.7 20.6
2015/16 2,308,000 446,490 65,000 511,490 98,990 1,550 100,540 4.4 19.7
2016/17 2,628,000 382,330 43,790 426,120 78,444 13,750 92,194 3.5 21.6
2017/18 3,101,000 457,104 219,759 676,863 116,106 19,996 136,102 4.4 20.1
2018/19 3,663,000 594,425 85,625 680,050 125,051 4,314 129,365 3.5 19.0Chanzo Cha Takwimu za Pato la Taifa na Matumizi ya Maendeleo ya Serikali 2018.
Hotuba ya Waziri wa Fedha na Uchumi, Kuhusu Mpango wa Maendeleo na Makadiro ya Mapato na
Matumizi ya Serikali kwa mwaka 2018/2019 , Mei 2019
MATUMIZI YA ELIMU KWA ULINGANISHO NA MATUMIZI
YA SERIKALI NA PATO LA TAIFA 2014/15 - 2018/19
MWAKA
MATUMIZI YA SERIKALI MATUMIZI YA ELIMU MGAO WA ELIMU (%) KWA
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 95
JADWELI NAM. 10 (a)
RUZUKU MKOPO RUZUKU MKOPO
0000P001 Uimarishaji wa Elimu ya
Maandalizi na Msingi 790,000 10,092,100 10,882,100 626,545 5,527,527 6,154,072 55 79
0000P002 Uimarishaji wa Elimu ya Lazima
3,100,000 52,072,500 55,172,500 2,052,455 32,130,999 34,183,454 62 66
0000P003 Uimarishaji wa Elimu Mbadala
na Amali 1,600,000 15,387,000 16,987,000 82,005 7,452,722 7,534,727 48 5
0000P004 Kupanga na kusimamia kazi za
Wizara 400,000 400,000 - -
JUMLA 5,890,000 10,092,100 67,459,500 83,441,600 2,761,005 5,527,527 39,583,721 47,872,253 58 47
UPATIKANAJI WA FEDHA ZA MIRADI YA MAENDELEO KWA SERIKALI NA WAHISANI KWA MWAKA WA FEDHA 2018/2019
KASMA MRADI
MAKAMDIRIO KWA MWAKA KILICHOPATIKANA JULAI - APRIL
MCHANGO WA
SMZ
MAKADIRIO YA MISADAJUMLA
MCHANGO
WA SMZ
MAKADIRIO YA MISADA
JUMLASMZ
%
RUZUKU/
MIKOPO
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 96
JADWELI NAM. 10 (b)
KASMA PROGRAMU BAJETI KILICHOPATIKANA %
ELIMU YA MAANDALIZI NA MSINGI
Matumizi ya kawaida
Mshahara
Maendeleo (SMZ) 790,000,000 626,545,000 79
Maendeleo - (Muhisani) 10,092,100,000 5,527,527,258 55
Jumla ndogo 10,882,100,000 6,154,072,258 57
Matumizi ya kawaida 7,593,453,000 7,099,834,337 93
Mshahara 32,821,597,000 34,249,883,225 104
Maendeleo (SMZ) 3,100,000,000 2,052,455,000 66
ELIMU YA SEKONDARI
WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA AMALI
RIPOTI YA UPATIKANAJI WA FEDHA KWA PROGRAMU NA PROGRAMU
NDOGO KWA KIPINDI CHA JULAI 2018 HADI APRILI 2019
P01/S01
P02/S01
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 97
Maendeleo - (Muhisani) 52,072,500,000 32,130,999,635 62
Jumla ndogo 95,587,550,000 75,533,172,197 79
Matumizi ya kawaida 371,772,000 265,545,859 71
Mshahara 1,024,411,000 420,768,980 41
Matumizi ya kawaida 600,000,000 300,000,000 50
Mshahara 10,460,200,000 8,833,231,850 84
Ruzuku 415,000,000 262,830,800 63
Mshahara 1,216,500,000 1,003,186,570 82
Ruzuku 11,555,700,000 8,366,104,775 72
Mshahara 220,200,000 254,336,630 116
Ruzuku 50,000,000 37,500,000 75
Mshahara 1,006,800,000 508,369,340 50
Jumla ndogo
Jadweli nam. (10b) linaendelea
P03/S01
ELIMU YA JUU
MAFUNZO YA UALIMU
CHUO KIKUU CHA TAIFA
TAASISI YA KARUME YA SAYANSI NA TEKNOLOJIA
LOAN BOARD
CHUO CHA KIISLAMU
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 98
Matumizi ya kawaida 444,943,000 282,155,338 63
Mshahara 486,483,000 291,833,360 60
Maendeleo (SMZ) 1,600,000,000 82,005,000 5
Maendeleo - (Muhisani) 15,387,000,000 7,452,721,843 48
Ruzuku 5,371,500,000 3,538,278,487 66
Mshahara 1,250,100,000 1,053,373,505 84
Jumla ndogo 24,540,026,000 12,700,367,533 52
P05/S01
TAASISI YA ELIMU
Matumizi ya kawaida 95,900,000 72,246,875 75
Ruzuku 233,300,000 212,648,515 91
Jadweli nam. (10b) linaendelea
P04/S01
P04/S02
ELIMU MBADALA
VOCATIONAL TRAINING
UBORA WA ELIMU
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 99
BARAZA LA MITIHANI
Ruzuku 4,261,300,000 4,095,492,661 96
Mshahara 411,200,000 350,236,130 85
OFISI YA MKAGUZI MKUU WA ELIMU
Ruzuku 126,000,000 84,748,000 67
Mshahara 302,700,000 452,678,345 150
Ruzuku 455,441,000 300,572,060 66
Mshahara 194,602,000 154,002,070 79
BARAZA LA ELIMU
Ruzuku 100,100,000 70,981,250 71
Mshahara 90,300,000 99,547,205 110
HUDUMA ZA MAKTABA
Ruzuku 450,000,000 308,506,400 69
Mshahara 395,100,000 316,012,570 80
Ruzuku 289,278,000 167,348,992 58
Mshahara 243,408,000 166,486,380 68
Elimu Mjumuisho 75,000,000 40,224,450 54
Jumla ndogo 7,723,629,000 6,891,731,903 89
Matumizi ya kawaida 2,443,910,000 1,539,363,890 63
Mshahara 4,797,194,000 3,203,845,692 67
Jumla ndogo 7,241,104,000 4,743,209,582 66
Jadweli nam. (10b) linaendelea
P05/S01
P06/S01
UTUMISHI NA UENDESHAJI
MICHEZO NA UTAMADUNI MASKULINI
TEKNOLOJIA YA HABARI NA MAWASILIANO
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 100
Ruzuku 233,300,000 212,648,515 91
BARAZA LA MITIHANI 0
Ruzuku 4,261,300,000 4,095,492,661 96
Mshahara 411,200,000 350,236,130 85
OFISI YA MKAGUZI MKUU WA ELIMU 0
Ruzuku 126,000,000 84,748,000 67
Mshahara 302,700,000 452,678,345 150
Ruzuku 455,441,000 300,572,060 66
Mshahara 194,602,000 154,002,070 79
BARAZA LA ELIMU 0
Ruzuku 100,100,000 70,981,250 71
Mshahara 90,300,000 99,547,205 110
HUDUMA ZA MAKTABA 0
Ruzuku 450,000,000 308,506,400 69
Mshahara 395,100,000 316,012,570 80
Ruzuku 289,278,000 167,348,992 58
Mshahara 243,408,000 166,486,380 68
Elimu Mjumuisho 75,000,000 40,224,450 54
Jumla ndogo 7,723,629,000 6,891,731,903 89
Matumizi ya kawaida 2,443,910,000 1,539,363,890 63
Mshahara 4,797,194,000 3,203,845,692 67
Jumla ndogo 7,241,104,000 4,743,209,582 66
P05/S01
P06/S01
UTUMISHI NA UENDESHAJI
MICHEZO NA UTAMADUNI MASKULINI
TEKNOLOJIA YA HABARI NA MAWASILIANO
Jadweli nam. (10b) linaendelea
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 101
Matumizi ya kawaida 3,138,335,000 2,929,936,676 93
Mshahara 510,645,000 428,468,500 84
Maendeleo (SMZ) 400,000,000 - -
Jumla ndogo 4,048,980,000 3,358,405,176 83
Matumizi ya kawaida 1,091,569,000 775,013,990 71
Mshahara 1,520,359,000 1,216,287,200 80
Ruzuku 50,000,000 50,000,000 100
Jumla ndogo 2,661,928,000 2,041,301,190 77
Jumla kuu 179,605,900,000 131,674,134,642 73
Jumla ya Mishara 41,598,699,000 40,131,575,407 96
Jumla ya Ruzuku ya Mishahara 15,586,400,000 13,083,620,660 84
Jumla ya Matumizi ya Kawaida 15,903,701,000 13,399,995,592 84
Jumola ya Ruzuku 23,075,500,000 17,186,689,248 74
Jumla ya Maendeleo (SMZ) 5,890,000,000 2,761,005,000 47
Jumla ya Maendeleo (WAHISANI) 77,551,600,000 45,111,248,735 58
Jumla Kuu 179,605,900,000 131,674,134,642 73
Jadweli nam. (10b) linaendelea
P06/S03
KURATIBU SHUGHULI ZA ELIMU PEMBA
P06/S02
MIPANGO, SERA NA UTAFITI
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 102
JADWELI NAM. 11(a)
NA SKULI MADARASA AFISI GHALA MENGINEYO MFADHILI
1 Mbuzini 2 1 0 0 Wananchi/SMZ
JUMLA 2 1 0
1 Tomondo 2 0 0 0 Wananchi/SMZ
2 Kilimahewa 3 0 0 0 Wananchi/SMZ
JUMLA 5 0 0
1 Kinyasini Msingi 3 0 0 0 Wananchi/SMZ
2 Gamba 5 0 0 2 Wananchi/SMZ
3 Kigunda 3 1 0 0 Wananchi/SMZ
4 Kandwi 4 0 0 0 Wananchi/SMZ
5 Kidoti 4 0 0 0 Wananchi/SMZ
JUMLA 19 1 0 2
MADARASA YALIYOKAMILIKA
WILAYA YA MAGHARIBI 'A'
WILAYA YA MAGHARIBI 'B'
WILAYA YA KASKAZINI 'A'
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 103
Jadweli 11(a) linaendelea
1 Fujoni 2 0 0 0 Qatar
JUMLA 2 0 0
1 Bambi 2 2 0 0 Wananchi/SMZ
2 PongwePwani 4 2 0 1 Wananchi/SMZ
3 Kidimni 2 1 0 0 Wananchi/SMZ
4 Chwaka 4 0 0 1 Wananchi/SMZ
JUMLA 12 5 0 2
1 Ukongoroni 3 0 0 0 Wananchi/SMZ
2 Uzi Ng'ambwa 2 0 0 0 Wananchi/SMZ
3 Charawe 5 2 0 3 Wananchi/SMZ
JUMLA 10 2 0 3
WILAYA YA KASKAZINI 'B'
WILAYA YA KATI
WILAYA YA KUSINI
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 104
Jadweli 11(a) linaendelea
1 Tumbe Sec 8 1 0 Wananchi, SMZ na
Nyota
2 Msuka Sec 5 1 1 Ukumbi na Chumba
Chamabara
Wananchi na SMZ
3 Shengejuu Sec 4 1 0 Wananchi na SMZ
JUMLA: 17 3 1 -
-
JUMLA
1 Kengeja Sec 6 - - Ukumbi Wanachi na SMZ
JUMLA: 6 - -
WILAYA YA CHAKE:
1 Wawi Msng 3 1 1 Vyoo 2 SMZ
2 Furaha Msng 4 0 0 SMZ
3 ch'wiri Sec 2 0 0 Vyoo 6 Wananchi na SMZ
4 Chambani 4 1 Wananchi na SMZ
JUMLA: 9 1 1
JUMLA KUU 87 4 0 5
WILAYA YA MICHWENI
WILAYA YA MKOANI
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 105
Jadweli 11(b)
SKULI MADARASA AFISI GHALA MENGINEYO MFADHILI
1 Kilimahewa 1 SMZJUMLA 1 0 0 0
1 Matemwe 0 0 0
Chumba cha
MaabaraWananchi
JUMLA 1 0 0 0
WILAYA YA MKOANI:
1 Uweleni Sec 2 1 1
Ukumbi na
Vyoo 5 Wananchi na SMZ
2 Mwambe Sec 0 1 1 Wananchi
JUMLA: 2 2 2
WILAYA YA CHAKE:
1 Uwandani Sec 7 0 0 Vyoo 3 Wananchi na SMZ
JUMLA: 7 0 0
JUMLA KUU 11 2 2
WILAYA YAMJINI
WILAYA YA KASKAZINI 'A'
MADARASA YALIYOKWISHA EZEKWA LAKINI KAZI ZA UPIGAJI
PLASTA NA SAKAFU HAZIJAKAMILIKA
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 106
Jadweli 11(c)
SKULI MADARASA AFISI GHALA MENGINEYO MFADHILI
1 Jang'ombe 2 0 0 0 Wananchi
JUMLA 2 0 0 0
1 Fuoni Kibondeni 2 0 0 0 Wananchi
2 Tomondo 2 0 0 0 Wananchi
JUMLA 4 0 0 0
1 Kihinani 2 1 0 0 Wananchi
2 Chuini 2 1 0 0 Wananchi
3 Mbuzini 2 0 0 0 Wananchi
JUMLA 6 2 0 0
2 Mkwajuni Msingi 2 1 0 0 Wananchi
3 Mkwajuni Sekondari 4 2 0 Ukumbi Wananchi
4 Bwereu 5 1 0 0 Wananchi
5 Nungwi 4 0 0 0 Wananchi
JUMLA 15 4 0 0
1 Kidimni 3 0 0 0 Wananchi
2Ndijani Msewni Muhibu
Msngi3 1 1 0 Wananchi
JUMLA 6 1 1
WILAYA YA KATI
MADARASA YALIYOFIKIA HATUA YA KUEZEKWA
WILAYA YA MAGHARIBI 'A'
WILAYA YA KASKAZINI A
WILAYA YA MJINI
WILAYA YA MAGHARIBI 'B'
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 107
Jadweli 11(c) linaendelea
1 Kibele 0 1 0 0 Wananchi
JUMLA 0 1 0 0
WILAYA YA WETE
1 Gando Sek. 0 1 5 - Wananchi/SMZ
2 Kangagani Sec 5 0 0 Wananchi/SMZ
Mitiulaya Sek 0 0 0 Ukumbi Wananchi/SMZ
5 Uondwe Sec 4 0 0 Wananchi/SMZ
JUMLA 9 1 5 0
WILAYA YA MKOANI
8 Kangani Sec 4 0 0 - Wananchi/SMZ
9 Chambani 0 0 0 Ukumbi Wananchi/SMZ
10 K/panza 4 1 - - Wananchi/SMZ
Makongwe Sec Maktaba na Chumba
cha mabara Wananchi/SMZ
JUMLA: 8 1 0
WILAYA YA CHAKE:
1 Nga'mbwa Sec 2 0 0 Chumba cha Walimu Wananchi/SMZ
2 Uwandani Sec 1 1 0 Chumba cha Walimu Wananchi/SMZ
3 Ndagoni Sec 2 0 0 Wananchi/SMZ
4 Chambani 0 0 1 Wananchi/SMZ
JUMLA: 5 1 0
JUMLA KUU 55 11 6
WILAYA YA KUSINI
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 108
Jadweli 11(d)i
SKULI MADARASA AFISI GHALA MENGINEYO MFADHILI
1Ndijani Mseweni Muhibu
Msingi3 0 0 0 Wananchi
2 Kiboje Msingi 4 2 0 Wananchi
JUMLA 7 2 0 0
1 Kidagoni 4 1 0 0 Wananchi
2 Kilindi 2 1 1 0 Wananchi
3 Matemwe 0 0 0 Maktaba Wananchi
4 Kibeni 5 0 0 0 Wananchi
JUMLA 11 2 1 0
WILAYA YA WETE
1 Uwondwe Sekondari 3 - - - Wananchi/SMZ
3 Jadida 13 2 1 Vyoo 12 Wananchi/SMZ
4 Minungwini 3 - -
5 Limbani 4 - - Chumba cha Kompyuta,
labrary, Maabara.
Wananchi/SMZ
6 Piki 6 - - - Wananchi/SMZ
JUMLA: 29 2 1
WILAYA YA MICHEWENI
1 Simai 4 - 0 - Wananchi/SMZ
JUMLA: 20 1 1 -
WILAYA YA MKOANI:
5 Wambaa Sek. 4 - - - SMZ/ Wananchi
9 Mkanyageni Sek 5 - - - SMZ Wananchi
10 Mizingani 2 0 0 Ukumbi SMZ Wananchi
11 Michenzani Sek 3 1 - Chumba cha Walimu SMZ/ Wananchi
JUMLA: 14 1 15
JUMLA KUU 81 8 18
WILAYA YA KATI
KASKAZINI 'A'
MADARASA AMBAYO YAMO KATIKA HATUA ZA UJENZI WA KUTA NA NGUZO
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 109
No SKULI MFADHILI
1 Mwanakwerekwe WB
2 Bububu OPEC (ZATEP) UNGUJA
3 Chumbuni OPEC (ZATEP) UNGUJA
4 Fuoni OPEC (ZATEP) UNGUJA
5 Mwemeshauri OPEC (ZATEP) UNGUJA
6 Kinuni OPEC (ZATEP) UNGUJA
7 Wara OPEC (ZATEP) PEMBA
8 Kizimbani OPEC (ZATEP) PEMBA
9 Mwambe OPEC (ZATEP) PEMBA
10 Micheweni OPEC (ZATEP) PEMBA
11 Pangeni WANANCHI/SMZ
12 Mlilile SMZ
13 Mbuyumaji SMZ
14 Fuoni Pangawe CNQC
15 Uroa WB
16 Wingwi WB
17 Bwefum BAKHRESA
18 Kwarara Msingi GOOD NEIGHBOURS
Jadweli 11(d)ii
UJENZI WA VYUO/SKULI MPYA
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 110
No SKULI MFADHILI
1 KISAUNI WB
2 JANG'OMBE WB
3 REGEZA MWENDO WB
4 UNGUJA UKUU WB
5 BWEJUU WB
6 TUMBATU WB
7 KIJINI WB
8 MKWAJUNI WB
9 MAHONDA WB
10 KITOPE WB
11 KIJINI WB
12 MTONI KIGOMENI WB
13 FUNDO WB
14 KOJANI WB
15 PUJINI WB
16 KILINDI WB
17 KIUYU WB
18 MAKANGALE WB
19 LIMBANI WB
20 KISIWA PANZA WB
Jadweli 11(d)iii
UJENZI MPYA WA UPANUZI WA SKULI/MAABARA
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 111
Jadweli 12(a)
SKULI MADARASA AFISI GHALA MENGINEYO MFADHILI
WILAYA YA MJINI
1 Jang'ombe SMZ
2 Kidogngo Chekundu Msingi 13 0 0 0 SMZ
JUMLA 13 0 0 0
1 Langoni Msingi 3 1 0 0 SMZ
JUMLA 3 1 0
1 Pale 4 0 0 0 SMZ
JUMLA 4 0 0
1 Ukongoroni 5 0 0 0 SMZ
WILAYA YA WETE
1 Kinyasini Sec 5 SMZ
2 Daya 4 SMZ
3 Chasasa Miundombinu ya
umeme
SMZ
4 Chwale 1 1 Chumba cha walimu SMZ
JUMLA 9 1 1
1 Konde Sec 0 0 0 Miundombinu ya
Umeme
SMZ
JUMLA 0 0 0
1 Chokocho 5 1 1 Chumba cha maabara SMZ
2 Chokocho Mandalizi 2 1 Vyoo 3 SMZ
3 Makoongwe 4
4 Makombeni Chumba cha maabara SMZ
5 Tironi 10 1 1 SMZ
JUMLA: 21 3 2
1 Oles Sec 4 0 0 0 SMZ
2 Madungu Sec 12 2 2 Vyoo 12 na Mabara SMZ
JUMLA 16 2 2
WILAYA YA MKOANI
WILAYA YA CHAKE.
SKULI AMBAZO UKARABATI UMEFANYIKA
WILAYA YA MAGHARIBI 'A'
WILAYA YA KASKAZINI A
WILAYA YA KASKAZINI A
WILAYA YA MICHEWENI
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 112
SKULI AMBAZO UKARABATI UNAENDELEA
SKULI MADARASA AFISI GHALA MENGINEYO MFADHILI
WILAYA YA MJINI
1 Faraja 0 0 0 1 SMZ
2 Kidongochekundu Sekondari 10 0 0 0 SMZ
JUMLA 10 0 0 1
WILAYA YA MAGHARIBI 'A'
1 Langoni 4 SMZ
JUMLA 4 0 0 0
WILAYA YA KASKAZINI B
1 Pwani Mchangani 0 1 0 1 SMZ
JUMLA 0 1 0 1
WILAYA YA CHAKE:
1 Madungu Msingi 5 1 1
Chumba cha
walimu na Vyoo SMZ
Jadweli 12(b)
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 113
SKULI MADARASA AFISI GHALA MENGINEYO MAELEZO
1 Mikunguni 3 0 0 0
Paa, apron, rangi, palasta,
sakafu na dari
Hailesalasie
20 0 0 0
Paa, rangi, madirisha,
milangu, dari, sakafu na
mashimo ya vyoo
2 Benbella
1 Fukuchani 4 1 kuta,paa na dari
1 Kilombero 4 1 1 Paa na dari
WILAYA YAMICHEWENI:
Konde Msingi 3 0 0 0 Kuta, rangi na Paa
1 Wambaa 4 0 0 0 Kuta,rangi na Paa
WILAYA YA MKOANI:
Jadweli 12(c)
SKULI AMBAZO UKARABATI UKO KATIKA HATUA ZA MAANDALIZI
WILAYA YA MJINI
WILAYA YA KASKAZINI 'A'
WILAYA YA KASKAZINI 'B'
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 114
NAM SKULI IDADI HATUA ILIYOFIKIWA MFADHILI
1 Kihinani 14 Umemaliza UNICEF
2 Mbuzini 13 Umemaliza UNICEF
1 Chunga 10 Umemaliza UNICEF
2 Kwerekwe D&G 17 Umemaliza UNICEF
3 Welezo 12 Umemaliza UNICEF
4 Mtoni kidatu 12 Umemaliza UNICEF
2 Mkokotoni 8 Unaedela UNICEF
3 Kibeni 10 Unaedela UNICEF
1 Pangeni 10 Umemaliza SMZ
1 Koani 11 Umemaliza SMZ
2 Uzi Ng'ambwa 11 Umemaliza SMZ
1 Mchangani 11 Umemaliza SMZ
2 Unguja Ukuu 11 Umemaliza SMZ
1 Micheweni 14 Umemaliza UNICEF
2 Haroun 9 Umemaliza UNICEF
3 Simai 9 Umemaliza UNICEF
4 Shumba 9 Umemaliza UNICEF
5 Kinowe 11 Umemaliza UNICEF
WILAYA YA KUSINI
WILAYA YA MICHEWENI
WILAYA YA MAGHARIBI 'A'
Jadweli 12(d)
SKULI AMBAZO UJENZI WA VYOO KWA AJILI YA
WALIMU NA WANAFUNZI UMEKAMILIKA
WILAYA YA MAGHARIBI 'B'
WILAYA YA KASKAZINI 'A'
WILAYA YA KASKAZINI 'B'
WILAYA YA KATI
Jadweli 12(d) Linaendelea
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 115
SKULI IDADI MFADHILI
1 Kidongochekundu Msingi A 4 GPE
2 Kidongochekundu Msingi B 6 GPE
3 Kidongochekundu Sekondari 4 GPE
4 Shauri Moyo Msingi 6 GPE
5 Mwembeladu Sekondari 6 GPE
6 Jang'ombe Sekondari 3 GPE
7 Jang'ombe Msingi A & B 9 GPE
8 Jang'ombe Msingi A 8 GPE
JUMLA 46
1 Mfenesini Msingi 5 GPE
JUMLA 5
Jadweli 12(e)
SKULI AMBAZO ZINAJENGEWA RAMPU
WILAYA YA MJINI
WILAYA YA MAGHARIBI 'A'
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 116
1 Kijito Upele Msingi A 7 GPE
2 Kijito Upele Msingi B 5 GPE
3 Mtopepo Msingi 6 GPE
4 Mtopepo Sekondari 1 GPE
5 Mfenesini Msingi 5 GPE
JUMLA 24
1 Chaani Sekondari 7 GPE
2 Pale Sekondari 4 GPE
3 Kikombweni 6 GPE
JUMLA 17
WILAYA YA MAGHARIBI 'B'
WILAYA YA KASKAZINI 'A'
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 117
Jadweli nam. 12(e) linaendelea
1 Mahonda Sekondari 4 GPE
2 Kitope Msingi 3 GPE
3 Kilombero Msingi 4 GPE
4 Kiwengwa Msingi 6 GPE
5 Kiwengwa Sekondari 2 GPE
JUMLA 19
1 Jumbi Msingi 3 GPE
2 Uroa Msingi 3 GPE
3 Uroa Sekondari 3 GPE
4 Pagali Msingi 3 GPE
5 Mpapa Msingi 7 GPE
JUMLA 19
WILAYA YA KASKAZINI 'B'
WILAYA YA KATI
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 118
Jadweli nam. 12(e) linaendelea
Kiongoni Msingi 8 GPE
Muyuni Msingi 7 GPE
Paje Msingi 3 GPE
Paje Sekondari 3 GPE
JUMLA 21
1 Mchanga Mdogo Kambi 5 GPE
2 Chwale 6 GPE
3 Mabatini 5 GPE
4 Ukunjwi 6 GPE
Daya 5 GPE
Kisiwani 5 GPE
JUMLA 32
WILAYA YA KUSINI
WILAYA YA WETE
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 119
Jadweli nam. 12(e) linaendelea
Michenzani Sekondari 5 GPE
Mkanyageni Sekondari 5 GPE
Michenzani Msingi 5 GPE
JUMLA 15
1 Mbuzini Msingi 5 GPE
2 Mbuzini Sekondari 6 GPE
3 Kwale Msingi 5 GPE
4 Uwandani Msingi 3 GPE
5 Pujini 5 GPE
6Ng'ambwa Sekondari 5
GPE
7Ng'ambwa Msingi 5
GPE
8Chanjaani 3
GPE
9Ng'amgwa Msingi 5
GPE
JUMLA 42
WILAYA YA CHAKECHAKE
WILAYA YA MKOANI
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 120
Jadweli nam. 12(e) linaendelea
Karume 5GPE
Maziwa Ng'ombe 5GPE
JUMLA 10
WILAYA YA MICHEWENI
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 121
NAM SKULI MEZA VITI MFADHILI
1 Haileselassie 500 500 SMZ
2 Mikunguni 80 80 SMZ
3 Forodhani 145 145 SMZ
4 Lumumba 380 380 SMZ
5 Kwamtipura 650 650 SMZ
6 Nyerere 410 410 SMZ
7 Jang'ombe 150 150 SMZ
8 Tumekuja 473 473 SMZ
9 Hamamni 273 273 SMZ
10 Mpendae 253 253 SMZ
11 Faraja 274 274 SMZ
12 Kidongo Chekundu 600 600 SMZ
4188 4188
1 Bububu Sekondari 800 800 SMZ
2 Mtopepo 694 694 SMZ
3 Mbuzini 400 400 SMZ
4 Mfenesini 324 324 SMZ
5 Mtoni Kigomeni 850 850 SMZ
6 Mtoni Kidatu 200 200 SMZ
7 Chuini 337 337 SMZ
8 kama 250 250 SMZ
9 Mwenge 186 186 SMZ
10 Mikindani 78 78 SMZ
11 Langoni 147 147 SMZ
12 Rgeza Mwendo 280 280 SMZ
JUMLA: 4546 4546
SKULI ZILIZOPATIWA MADAWATI, VITI NA MEZA
Jadweli 12(f)
WILAYA YA MJINI
JUMLA
WILAYA YA MAGAHRIB 'A'
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 122
1 Maungani 30 30 SMZ
2 Kwarara 373 373 SMZ
3 Mwanakwerekwe 'B' 350 350 SMZ
4 Biashara 200 200 SMZ
5 Chukwani 137 137 SMZ
6 Fuoni 333 333 SMZ
7 Kibondeni 120 120 SMZ
8 Kinuni 401 401 SMZ
9 Mwanakwerekwe 'A' 245 245 SMZ
10 Kisauni 200 200 SMZ
11 Kombeni 150 150 SMZ
12 Kiembe Samaki 700 700 SMZ
13 Mwanakwerekwe 'C' 350 350 SMZ
3589 3589
1 Mapinduzi 110 110 SMZ
2 Chaani 360 360 SMZ
3 Jongowe 100 100 SMZ
4 Tumbatu 436 436 SMZ
5 Potoa 300 300 SMZ
6 Mkwajuni 560 560 SMZ
7 Mlimani 32 32 SMZ
8 Kidoti 250 250 SMZ
Jadweli nam 12(f) linaendelea
WILAYA YAMAGHARIB 'B'
WILAYA YA KASKAZINI 'A'
JUMLA
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 123
8 Kidoti 250 250 SMZ
9 Mbuyu Tende 229 229 SMZ
10 Kijini 69 69 SMZ
11 Kigunda 60 60 SMZ
12 Kilindi 150 150 SMZ
13 Nungwi 100 100 SMZ
14 Banda Maji 130 130 SMZ
15 Matemwe 254 254 SMZ
16 Kibeni 265 265 SMZ
17 Gamba 283 283 SMZ
18 Kandwi 120 120 SMZ
19 Kidagoni 50 50 SMZ
20 Kinyasini 350 350 SMZ
21 Pale 200 200 SMZ
22 Fukuchani 50 50 SMZ
23 Kibuyuni 200 200 SMZ
24 Kiwengwa 150 150 SMZ
25 Upenja 121 121 SMZ
4929 4929
Jadweli nam 12(f) linaendelea
JUMLA
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 124
1 Pwani Mchangani 150 150 SMZ
2 Kilombero 130 130 SMZ
3 Bumbwini 300 300 SMZ
4 Donge 140 140 SMZ
5 Fujoni 300 300 SMZ
6 Mahonda 200 200 SMZ
7 Kitope 183 183 SMZ
8 Mwanda 120 120 SMZ
9 Kiongwe 45 45 SMZ
10 Mgambo 200 200 SMZ
11 Makoba 250 250 SMZ
JUMLA 2018 2018
1 Marumbi 55 55 SMZ
2 Chwaka 61 61 SMZ
3 Mpapa 101 101 SMZ
4 Umbuji 185 185 SMZ
5 Kidimni 119 119 SMZ
6 Mwera 515 515 SMZ
7 Uroa 107 107 SMZ
8 Pongwe Pwani 24 24 SMZ
9 Jumbi 205 205 SMZ
Jadweli nam 12(f) linaendelea
WILAYA YA KASKAZINI 'B'
WILAYA YA KATI
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 125
10 Ndijani 150 150 SMZ
11 UngujaUkuu 150 150 SMZ
12 Uzi 65 65 SMZ
13 Kikungwi 40 40 SMZ
14 Ubago 163 163 SMZ
15 Kibele 450 450 SMZ
16 Machui 55 55 SMZ
17 Jendele 90 90 SMZ
18 Michanvi 32 32 SMZ
19 Tunguu 345 345 SMZ
20 Dunga 326 326 SMZ21 Bambi 170 170 SMZ22 Charawe 186 186 SMZ
23 Mwera Pongwe 271 271 SMZ
24 Umoja Uzini 371 371 SMZ
4236 4236
1 Jambiani 20 20 SMZ
2 Kizimkazi Dimbani 50 50 SMZ
3 Pete 50 50 SMZ
4 Kizimkazi 246 246 SMZ
5 Makunduchi 290 290 SMZ
6 Kusini 30 30 SMZ
7 Muungoni 164 164 SMZ
8 Mtende 20 20 SMZ
9 Paje 116 116 SMZ
10 Bwejuu 440 440 SMZ
11 Muyuni 66 66 SMZ
JUMLA 1492 1492
WILAYA YA KUSINI
JUMLA
Jadweli nam 12(f) linaendelea
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 126
1 Mbuzini 339 339 SMZ
2 Ndagoni 45 45 SMZ
3 Kilimndi 126 126 SMZ
4 Wesha 20 20 SMZ
5 Shamiani 57 57 SMZ
6 Madungu 142 142 SMZ
7 Ole 126 126 SMZ
8 Ziwani 148 148 SMZ
9 Furaha 164 164 SMZ
10 Dr. Omari 274 274 SMZ
11 Nga'mbwa 200 200 SMZ
12 Cha'wiri 180 180 SMZ
13 Fidelcastro 130 130 SMZ
14 Kwale 349 349 SMZ
15 Uwanadani 6 6 SMZ
16 Vitongoji 401 401 SMZ
17 Vikunguni 1 1 SMZ
JUMLA 2708 2708
WILAYA YA CHAKE CHAKE
Jadweli nam 12(f) linaendelea
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 127
WILAYA YA MKOANI
1 Kengeja Sec 66 66 SMZ
2 Mizingani 36 36 SMZ3 Wambaa 136 136 SMZ
4 Mwambe 160 160 SMZ
5 Chokocho 101 101 SMZ
6 Mkanyageni 261 261 SMZ
7 Pindua 378 378 SMZ
8 Kangani 143 143 SMZ
9 Ukutini 27 27 SMZ
10 Maendeleo 91 91 SMZ
11 K/panza 71 71 SMZ
12 Chambani 225 225 SMZ
13 Chwaka 198 198 SMZ
14 Makongwe 300 300 SMZ
15 Uweleni 470 470 SMZ
JUMLA 2663 2663
WILAYA YA WETE
1 Pandani 152 152 SMZ
2 Kangagani 62 62 SMZ
3 Minungwini 521 521 SMZ
Jadweli nam 12(f) linaendelea
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 128
4 Chasasa 300 300 SMZ
5 Mzambarautakao 48 48 SMZ
6 Ukunjwi 18 18 SMZ
7 Mabatini 24 24 SMZ
8 Kizimbani 400 400 SMZ
9 Limbani 360 360 SMZ
10 Mitiulaya 387 387 SMZ
11 Mchangamdogo 350 350 SMZ
JUMLA 2622 2622
WILAYA YA MICHEWENI
1 Micheweni 385 385 SMZ
2 Kiuyu 255 255 SMZ
3 Shumba 42 42 SMZ
4 Kinowe 238 238 SMZ
5 Chuo cha Kislam 306 306 SMZ
6 Konde 451 451 SMZ
7 Makangale 160 160 SMZ
8 Msuka 127 127 SMZ
9 Wingwi 300 300 SMZ
JUMLA 2264 2264
JUMLA KUU 35255 35255
Jadweli nam 12(f) linaendelea
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 129
JADWELI NAM. 13 (a)
WAV WAS JUMLA WAV WAS JUMLA WAV WAS JUMLA WAV WAS JUMLA WAV WAS JUMLA
Mjini 6,904 6,927 13831 2056 1972 4028 3154 3418 6572 5210 5390 10600 75.5 77.8 76.6
Magharibi 'A' 6,487 6,320 12807 2304 2460 4764 3058 3218 6276 5362 5678 11040 82.7 89.8 86.2
Magharibi 'B' 7,753 7,554 15307 1936 1958 3894 4916 4836 9752 6852 6794 13646 88.4 89.9 89.1
Kaskazini 'A' 3,891 3,905 7796 2239 2336 4575 1930 2100 4030 4169 4436 8605 107.1 113.6 110.4
Kaskazini 'B' 3,168 3,040 6208 858 876 1734 1404 1448 2852 2262 2324 4586 71.4 76.4 73.9
Kati 2,697 2,617 5314 1913 1828 3741 1021 1090 2111 2934 2918 5852 108.8 111.5 110.1
Kusini 1,223 1,240 2463 587 589 1176 705 822 1527 1292 1411 2703 105.6 113.8 109.7
Micheweni 5,547 5,411 10958 1259 1333 2592 2810 3001 5811 4069 4334 8403 73.4 80.1 76.7
Wete 5,287 5,246 10533 2218 2242 4460 990 1021 2011 3208 3263 6471 60.7 62.2 61.4
Chake Chake 4,958 4,962 9920 1943 1945 3888 1455 1550 3005 3398 3495 6893 68.5 70.4 69.5
Mkoani 5,344 5,172 10516 1771 1747 3518 1804 1853 3657 3575 3600 7175 66.9 69.6 68.2
Jumla 53259 52394 105653 19084 19286 38370 23247 24357 47604 42331 43643 85974 79.5 83.3 81.4
ASILIMIA YA UANDIKISHAJI WA WATOTO KATIKA SKULI ZA MAANDALIZI, MACHI - 2019
WILAYA
WATOTO WENYE UMRI WA
SKULI ZA SERIKALI SKULI ZA BINAFSI
JUMLA SKULI ZA KIMA CHA
MIAKA 4 - 5 SERIKALI NA BINAFSI UANDIKISHAJI (%)
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 130
JADWELI NAM. 13 (b)
WAV WAS JUMLA WAV WAS JUMLA WAV WAS JUMLA
MJINI 4 959 919 1878 17 1097 1053 2150 0 0 0 0
MAGHARIBI 'A' 1 121 109 230 22 2089 2214 4303 1 94 137 231
MAGHARIBI 'B' 0 0 0 0 23 1865 1886 3751 1 71 72 143
KASKAZINI 'A' 5 723 771 1494 24 1226 1248 2474 5 290 317 607
KASKAZINI 'B' 1 72 77 149 15 585 615 1200 4 201 184 385
KATI 5 380 354 734 24 1483 1411 2894 2 50 63 113
KUSINI 4 313 309 622 5 230 232 462 1 44 48 92
MICHEWENI 4 561 619 1180 20 698 714 1412 0 0 0 0
WETE 2 217 250 467 34 2001 1992 3993 0 0 0 0
CHAKE 2 347 343 690 25 1572 1577 3149 1 24 25 49
MKOANI 2 154 175 329 31 1500 1486 2986 2 117 86 203
JUMLA 30 3847 3926 7773 240 14346 14428 28774 17 891 932 1823
UANDIKISHAJI WA WATOTO WA MAANDALIZI WANAOSOMA KATIKA SKULI
ZA SERIKALI ZA MAANDALIZI, MSINGI NA MSINGI NA KATI, KIWILAYA MACHI - 2019
WILAYA
MAANDALIZI MSINGI MSINGI NA KATI
IDADI
YA
SKULI
IDADI YA WANAFUNZI IDADI
YA
SKULI
IDADI YA WANAFUNZI IDADI
YA
SKULI
IDADI YA WANAFUNZI
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 131
JADWELI NAM 13 ( c )
WAVULANA WASICHANA JUMLA WAVULANA WASICHANA JUMLA
MJINI 71 3154 3418 6572 0 0 0 0
MAGHARIBI 'A' 65 2495 2635 5130 17 563 583 1146
MAGHARIBI 'B' 100 4531 4431 8962 10 385 405 790
KASKAZINI 'A' 13 522 539 1061 82 1408 1561 2969
KASKAZINI 'B' 13 595 595 1190 48 809 853 1662
KATI 26 1021 1090 2111 0 0 0 0
KUSINI 20 705 822 1527 0 0 0 0
MICHEWENI 10 420 419 839 92 2390 2582 4972
WETE 18 868 914 1782 5 122 107 229
CHAKE CHAKE 16 748 791 1539 30 707 759 1466
MKOANI 10 409 396 805 58 1395 1457 2852
JUMLA 362 15468 16050 31518 342 7779 8307 16086
Angalia: RISE - Radio Instruction to Strengthen Education
UANDIKISHAJI WA WANAFUNZI NGAZI YA MAANDALIZI KATIKA
VITUO/SKULI ZA BINAFSI, KIWILAYA MACHI - 2019
WILAYA
SKULI VITUO (RISE)
IDADI YA
SKULI
IDADI YA WANAFUNZI IDADI
YA
VITUO
IDADI YA WANAFUNZI
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 132
JADWELI NAM. 14
WAV WAS JUMLA WAV WAS JUMLA WAV WAS JUMLA WAV WAS JUMLA WAV WAS JUMLA
Mjini 17,558 17,775 35,333 11,884 12,221 24,105 3,847 3,939 7,786 15,731 16,160 31,891 89.6 90.9 90.3
Magharibi 'A' 15,858 15,779 31,637 17,615 18,283 35,898 2,621 2,848 5,469 20,236 21,131 41,367 127.6 133.9 130.8
Magharibi 'B' 19,038 19,166 38,204 17,145 17,115 34,260 6,650 6,881 13,531 23,795 23,996 47,791 125.0 125.2 125.1
Kaskazini 'A' 10,276 10,118 20,394 11,645 11,730 23,375 265 267 532 11,910 11,997 23,907 115.9 118.6 117.2
Kaskazini 'B' 7,820 7,941 15,761 6,797 6,751 13,548 340 369 709 7,137 7,120 14,257 91.3 89.7 90.5
Kati 6,908 6,825 13,733 8,710 8,391 17,101 541 578 1,119 9,251 8,969 18,220 133.9 131.4 132.7
Kusini 3,335 3,073 6,408 3,700 3,414 7,114 253 256 509 3,953 3,670 7,623 118.5 119.4 119.0
Micheweni 11,977 11,485 23,462 11,558 11,237 22,795 262 236 498 11,820 11,473 23,293 98.7 99.9 99.3
Wete 9,526 9,622 19,148 14,333 13,358 27,691 365 268 633 14,698 13,626 28,324 154.3 141.6 147.9
Chake Chake 10,210 10,518 20,728 12,415 12,029 24,444 930 864 1,794 13,345 12,893 26,238 130.7 122.6 126.6
Mkoani 10,793 10,468 21,261 14,195 12,927 27,122 265 212 477 14,460 13,139 27,599 134.0 125.5 129.8
Jumla 123,299 122,770 246,069 129,997 127,456 257,453 16,339 16,718 33,057 146,336 144,174 290,510 118.7 117.4 118.1
ASILIMIA YA UANDIKISHAJI KATIKA NGAZI YA MSINGI (DARASA LA I - VI), MACHI - 2019
WILAYA
WATOTO WENYE UMRI WA UANDIKISHAJI KATIKA NGAZI YA MSINGI ASILIMIA YA
MIAKA 6 - 11 SERIKALI BINAFSI JUMLA UANDIKISHAJI
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 133
JADWELI NAM. 15(a)
WAV WAS JUMLA WAV WAS JUMLA WAV WAS JUMLA WAV WAS JUMLA
Mjini 1281 1408 2689 595 619 1214 1876 2027 3903 68.3 69.5 68.9
Magharibi 'A' 1965 1911 3876 1540 1598 3138 3505 3509 7014 56.1 54.5 55.3
Magharibi 'B' 1982 1977 3959 1064 1086 2150 3046 3063 6109 65.1 64.5 64.8
Kaskazini 'A' 1347 1304 2651 1169 1243 2412 2516 2547 5063 53.5 51.2 52.4
Kaskazini 'B' 820 837 1657 492 494 986 1312 1331 2643 62.5 62.9 62.7
Kati 1441 1430 2871 292 212 504 1733 1642 3375 83.2 87.1 85.1
Kusini 557 533 1090 25 26 51 582 559 1141 95.7 95.3 95.5
Micheweni 1421 1524 2945 875 851 1726 2296 2375 4671 61.9 64.2 63.0
Wete 1777 1743 3520 1247 947 2194 3024 2690 5714 58.8 64.8 61.6
Chake Chake 1456 1419 2875 1023 897 1920 2479 2316 4795 58.7 61.3 60.0
Mkoani 1594 1507 3101 1105 966 2071 2699 2473 5172 59.1 60.9 60.0
Jumla 15641 15593 31234 9427 8939 18366 25068 24532 49600 62.4 63.6 63.0
WALIOPITIA MAANDALIZI WASIOPITIA MAANDALIZI JUMLA
UANDIKISHAJI WA WANAFUNZI KATIKA DARASA LA KWANZA, SKULI ZA SERIKALI - 2019
WILAYA
WATOTO WALIOANDIKISHWA
% YA WALIOPITIA MAANDALIZI
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 134
JADWELI NAM. 15(b)
WAV WAS JUMLA WAV WAS JUMLA WAV WAS JUMLA WAV WAS JUMLA
Mjini 700 722 1422 27 39 66 727 761 1488 96.3 94.9 95.6
Magharibi 'A' 543 553 1096 6 9 15 549 562 1111 98.9 98.4 98.6
Magharibi 'B' 1393 1412 2805 47 34 81 1440 1446 2886 96.7 97.6 97.2
Kaskazini 'A' 81 76 157 0 0 0 81 76 157 100.0 100.0 100.0
Kaskazini 'B' 33 44 77 0 0 0 33 44 77 100.0 100.0 100.0
Kati 92 74 166 0 0 0 92 74 166 100.0 100.0 100.0
Kusini 55 55 110 1 0 1 56 55 111 98.2 100.0 99.1
Micheweni 46 40 86 1 3 4 47 43 90 97.9 93.0 95.6
Wete 62 70 132 0 0 0 62 70 132 100.0 100.0 100.0
Chake Chake 154 146 300 0 0 0 154 146 300 100.0 100.0 100.0
Mkoani 51 44 95 27 19 46 78 63 141 65.4 69.8 67.4
Jumla 3210 3236 6446 109 104 213 3319 3340 6659 96.7 96.9 96.8
UANDIKISHAJI WA WANAFUNZI KATIKA DARASA LA KWANZA, SKULI ZA BINAFSI - 2019
WILAYA
WATOTO WALIOANDIKISHWA
% YA WALIOPITIA MAANDALIZI
WALIOPITIA MAANDALIZI WASIOPITIA MAANDALIZI JUMLA
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 135
Jadweli Nam. 15(c) JADWELI NAM. 51
Na Jina la Skuli Wilaya
1 Mfurumatonga Kaskazini A
2 Mbuyutende Kaskazini A
3 Kigunda Kaskazini A
4 Kidagoni Kaskazini A
5 Bwereu Kaskazini A
6 Kijini Kaskazini A
7 Mto wa Pwani Kaskazini A
8 Panga tupu Kaskazini B
9 Mgonjoni Kaskazini B
10 Kiyongwe Kaskazini B
11 Upenja Kaskazini B
12 Charawe Kati
13 Ukongoroni Kati
14 Bambi Kati
15 Kibuteni Kusini
16 Michamvi Kusini
17 Kinowe Micheweni
18 Mkia Ng’ombe Micheweni
19 Mgogoni Micheweni
20 Makangale Micheweni
21 Kipangani Micheweni
22 Maziwani Wete
23 Mjini Kiuyu Wete
24 Tasini Mkoani
25 Tironi Mkoani
26 Mtuhaliwa Mkoani
27 Kunguni Mkoani
Skuli za msingi zilizo ndani ya Mpango wa utoaji
wa chakula kwa wanafunzi – (HOME GROWN
SCHOOL FEEDING PROGRAMME) (HGSFP)
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 136
JADWELI NAM. 16
WAV WAS JUMLA WAV WAS JUMLA WAV WAS JUMLA WAV WAS JUMLA WAV WAS JUMLA
Mjini 5,784 5,759 11543 4897 5443 10340 415 497 912 5312 5940 11252 91.8 103.1 97.5
Magharibi 'A' 4,703 4,788 9491 4175 4622 8797 505 493 998 4680 5115 9795 99.5 106.8 103.2
Magharibi 'B' 5,566 5,883 11449 4208 4715 8923 1196 1569 2765 5404 6284 11688 97.1 106.8 102.1
Kaskazini 'A' 3,045 3,125 6170 2256 3069 5325 0 0 0 2256 3069 5325 74.1 98.2 86.3
Kaskazini 'B' 2,391 2,248 4639 1521 1576 3097 39 28 67 1560 1604 3164 65.2 71.4 68.2
Kati 2,018 1,941 3959 2355 2480 4835 139 126 265 2494 2606 5100 123.6 134.3 128.8
Kusini 967 861 1828 1102 1006 2108 46 46 92 1148 1052 2200 118.7 122.2 120.4
Micheweni 3,545 3,387 6932 2016 2403 4419 23 26 49 2039 2429 4468 57.5 71.7 64.5
Wete 3,659 3,595 7254 3198 3534 6732 100 85 185 3298 3619 6917 90.1 100.7 95.4
Chake-Chake 3,346 3,295 6641 2675 3095 5770 259 291 550 2934 3386 6320 87.7 102.8 95.2
Mkoani 3,445 3,132 6577 2727 3141 5868 10 12 22 2737 3153 5890 79.4 100.7 89.6
Jumla 38469 38014 76483 31130 35084 66214 2732 3173 5905 33862 38257 72119 88.0 100.6 94.3
ASILIMIA YA UANDIKISHAJI KATIKA NGAZI YA KATI (KIDATO 1 - 2), MACHI - 2019
WILAYA
WATOTO WENYE UMRI WA UANDIKISHAJI KATIKA NGAZI YA KATI (KIDATO 1 - 2) ASILIMIA YA
MIAKA 12 - 13 SERIKALI BINAFSI JUMLA UANDIKISHAJI
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 137
JADWELI NAM. 17
WILAYA
IDADI YA
SKULI
WAV WAS JUMLA WAV WAS JUMLA WAV WAS JUMLA
Mjini 13 2071 2529 4600 1779 2920 4699 3850 5449 9299
Magharibi 'A' 12 1323 1807 3130 1089 1678 2767 2412 3485 5897
Magharibi 'B' 13 1669 2000 3669 1199 1941 3140 2868 3941 6809
Kaskazini 'A' 15 937 1385 2322 885 1398 2283 1822 2783 4605
Kaskazini 'B' 8 382 672 1054 304 720 1024 686 1392 2078
Kati 21 692 970 1662 665 1186 1851 1357 2156 3513
Kusini 9 480 595 1075 306 457 763 786 1052 1838
Micheweni 10 566 666 1232 756 964 1720 1322 1630 2952
Wete 24 1033 1267 2300 992 1692 2684 2025 2959 4984
Chake-chake 18 1056 1244 2300 604 1140 1744 1660 2384 4044
Mkoani 21 753 1018 1771 743 1203 1946 1496 2221 3717
JUMLA 164 10962 14153 25115 9322 15299 24621 20284 29452 49736
UANDIKISHAJI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA 3 NA 4 WA MIKONDO YA KAWAIDA
KIDATO 3 KIDATO 4 JUMLA KUU
(ISIYOKUWA MICHEPUO) KIWILAYA KATIKA SKULI ZA SERIKALI MACHI - 2019
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 138
JADWELI NAM. 18
WAV WAS JUMLA WAV WAS JUMLA WAV WAS JUMLA
ENGLISH SPEAKING INTERNATIONAL 18 21 39 16 30 46 34 51 85
BILAL ISLAMIC SEMINARY 29 51 80 32 61 93 61 112 173
SUNCITY SCHOOL 17 2 19 32 22 54 49 24 73
AL-RIYAMI ACADEMY 25 18 43 13 16 29 38 34 72
GLORIOUS ACADEMY 52 81 133 73 87 160 125 168 293
STONE TOWN INTERNATIONAL 4 9 13 6 4 10 10 13 23
SUNNI MADRESSA 44 87 131 23 46 69 67 133 200
MAD HUDA 13 17 30 12 11 23 25 28 53
ST MONICA 7 11 18 6 9 15 13 20 33
MUNAA 10 2 12 32 20 52 42 22 64
KARIBU INTERNATIONAL SCHOOL 11 9 20 7 6 13 18 15 33
UANDIKISHAJI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA 3 NA 4 WA MIKONDO YA KAWAIDA SKULI ZA BINAFSI,
2019
SKULI
KIDATO 3 KIDATO 4 JUMLA KUU
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 139
Jadweli nam. 18 linaendelea
ROYAL INTERNATIONAL SCHOOL 2 2 4 11 4 15 13 6 19
BEIT EL RAAS SCHOOL 61 91 152 29 52 81 90 143 233
MWERA SUPER SCHOOL 5 9 14 3 9 12 8 18 26
BRILLIANT ACADEMY SCHOOL 17 23 40 13 19 32 30 42 72
SHAMUSLEY ACADEMY 6 5 11 7 3 10 13 8 21
MOUNTAIN HILL 9 4 13 5 3 8 14 7 21
JKU SECONDARY SCHOOL 151 145 296 119 131 250 270 276 546
ALHARAMAYN 10 19 29 0 0 0 10 19 29
RAUDHA 40 68 108 31 19 50 71 87 158
ALHIDAYA ISLAMIC 0 0 0 0 0 0 0 0 0
SUFA 16 30 46 14 24 38 30 54 84
AL MUBARAK ISLAMIC 22 8 30 11 0 11 33 8 41
FARUK AKTAS MUSLIM 24 29 53 24 28 52 48 57 105
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 140
Jadweli nam. 18 linaendelea
LAUREATE INT. SCHOOL 52 103 155 23 55 78 75 158 233
INTERNATIONAL SCHOOLOF ZNZ 2 6 8 7 4 11 9 10 19
ZANZIBAR PROGRESSIVE 18 23 41 23 17 40 41 40 81
AL-FALAAH 47 61 108 41 50 91 88 111 199
AL-QUWIYY ISLAMIC SCHOOL 9 14 23 7 12 19 16 26 42
PHILTER FEDERAL 15 7 22 17 21 38 32 28 60
MNEMONIC 31 19 50 82 81 163 113 100 213
SOS 43 60 103 41 63 104 84 123 207
WILLEY 12 20 32 11 9 20 23 29 52
JUBA 8 10 18 4 18 22 12 28 40
SSP 13 18 31 22 30 52 35 48 83
HIFADHI 13 17 30 17 19 36 30 36 66
FRANCIS MARIA 34 42 76 22 39 61 56 81 137
HIGH PERFORMANCE 7 7 14 17 17 34 24 24 48
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 141
Jadweli nam. 18 linaendelea
FEZA 36 32 68 16 13 29 52 45 97
HIGH VIEW 31 43 74 23 37 60 54 80 134
MOMBASA CENTRAL 15 14 29 38 18 56 53 32 85
TRIFONIA 35 42 77 39 47 86 74 89 163
MBARALI 21 31 52 31 42 73 52 73 125
AL - IHSAN 0 77 77 0 40 40 0 117 117
NYUKI 45 46 91 50 48 98 95 94 189
SUN WAY 5 4 9 0 0 0 5 4 9
MEMON 32 47 79 13 16 29 45 63 108
UNIQUE LEARNING SCHOOL 14 9 23 9 10 19 23 19 42
MAAHAD ISTIQAMA 35 54 89 36 40 76 71 94 165
MAARIF SEC SCHOOL 22 3 25 15 12 27 37 15 52
AL-HARAMAIN SEC SCHOOL 23 27 50 46 42 88 69 69 138
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 142
Jadweli nam. 18 linaendelea
CHARITY BWEJUU 28 23 51 9 11 20 37 34 71
ASSALAM 13 19 32 0 0 0 13 19 32
UFUNDI DODEANI 4 0 4 16 0 16 20 0 20
WETE ISLAMIC 29 30 59 19 23 42 48 53 101
AMBASHA ISLAMIC HIGH SCHOOL 30 36 66 18 23 41 48 59 107
FARAHEDY 24 18 42 19 29 48 43 47 90
CONNECTING 45 33 78 34 35 69 79 68 147
ISTIQAMA MKANJUNI 15 31 46 8 12 20 23 43 66
AMIN ISLAMIC 43 23 66 12 15 27 55 38 93
ALIKHAMIS CAMP 66 54 120 24 36 60 90 90 180
JUMLA 1508 1844 3352 1328 1588 2916 2836 3432 6268
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 143
JADWELI NAM. 19
WAS J'LA WAS J'LA WAS J'LA WAS J'LA WAS J'LA
Kiembesamaki 21 62 39 54 28 60 47 102 135 278
Kiuyu 26 46 11 37 19 37 35 57 91 177
47 108 50 91 47 97 82 159 226 455
Kifaransa Kiponda 28 53 28 45 33 63 39 50 128 211
Maarifa ya nyumbani Ben Bella 53 53 48 48 58 58 37 37 196 196
Skuli ya Biashara 48 62 34 53 24 48 27 43 133 206
Kiembesamaki 0 0 0 0 0 0 34 76 34 76
Chasasa 17 38 18 25 12 17 8 20 55 100
65 100 52 78 36 65 69 139 222 382
Skuli ya Biashara 34 59 45 51 25 38 46 86 150 234
Ben Bella 50 50 48 48 62 62 73 73 233 233
Chasasa 26 42 11 29 8 16 4 18 49 105
110 151 104 128 95 116 123 177 432 572
Jumla Ndogo
Kiislam
Jumla Ndogo
Jumla Ndogo
Biashara
Kompyuta
UANDIKISHAJI KATIKA AINA MBALI MBALI ZA MICHEPUO - 2019
MCHEPUO
KIDATO 1 KIDATO 2 KIDATO 3 KIDATO 4 JUMLA KUU
SKULI
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 144
Mikunguni 23 79 24 68 32 61 26 37 105 245
Kengeja 19 38 13 56 6 32 25 32 63 158
42 117 37 124 38 93 51 69 168 403
Lumumba 42 69 75 115 35 60 76 154 228 398
F/Castro 32 49 19 50 16 25 10 37 77 161
74 118 94 165 51 85 86 191 305 559
Utaani 45 45 33 33 25 25 55 55 158 158
Madungu 39 54 34 49 36 61 46 80 155 244
Chasasa 23 37 0 0 20 33 26 54 69 124
Moh'd Juma Pindua 23 58 73 147 34 61 0 0 130 266
F/Castro 0 0 34 68 19 45 72 102 125 215
Mikindani 55 106 40 72 42 84 50 73 187 335
Ben Bella 50 50 57 57 62 62 59 59 228 228
Kiembesamaki 35 49 53 82 28 64 20 42 136 237
Tumekuja 76 126 47 119 54 102 84 151 261 498
346 525 371 627 320 537 412 616 1449 2305
765 1225 784 1306 678 1114 899 1438 3126 5083
Sayansi ya jamii Al -Ihsani 19 19 22 22 21 21 15 15 77 77
19 19 22 22 21 21 15 15 77 77
784 1244 806 1328 699 1135 914 1453 3203 5160JUMLA KUU
JUMLA (BINAFSI)
JUMLA (SERIKALI)
Jumla Ndogo
Jumla Ndogo
Vipawa vya juu
Jumla Ndogo
Ufundi
Sayansi
Jadweli nam. 19 linaendelea
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 145
JADWELI NAM. 20
WAV WAS JUMLA WAV WAS JUMLA WAV WAS JUMLA
1. SKULI ZA SERIKALI
KIDATO CHA 1 15738 17138 32876 460 765 1225 16198 17903 34101
KIDATO CHA 2 14410 16397 30807 522 784 1306 14932 17181 32113
KIDATO CHA 3 10962 14153 25115 436 678 1114 11398 14831 26229
KIDATO CHA 4 9322 15299 24621 539 899 1438 9861 16198 26059
JUMLA 50432 62987 113419 1957 3126 5083 52389 66113 118502
2. SKULI ZA BINAFSI
KIDATO CHA 1 1485 1620 3105 0 19 19 1485 1639 3124
KIDATO CHA 2 1247 1512 2759 0 22 22 1247 1534 2781
KIDATO CHA 3 1508 1844 3352 0 21 21 1508 1865 3373
KIDATO CHA 4 1328 1588 2916 0 15 15 1328 1603 2931
JUMLA 5568 6564 12132 0 77 77 5568 6641 12209
JUMLA KUU 56000 69551 125551 1957 3203 5160 57957 72754 130711
UANDIKISHAJI KATIKA NGAZI YA SEKONDARI (KIDATO 1 - 4), MACHI - 2019
ELIMU YA KATI ELIMU YA MICHEPUO JUMLA
DARASA
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 146
JADWELI NAM. 21
WAV WAS JUMLA WAV WAS JUMLA WAV WAS JUMLA WAV WAS JUMLA WAV WAS JUMLA
Mjini 11335 11698 23033 9046 11622 20668 879 1102 1981 9925 12724 22649 87.6 108.8 98.3
Magharibi 'A' 8956 9221 18177 6652 8199 14851 961 1008 1969 7613 9207 16820 85.0 99.8 92.5
Magharibi 'B' 10743 11559 22302 7356 8935 16291 2456 3269 5725 9812 12204 22016 91.3 105.6 98.7
Kaskazini 'A' 5926 6194 12120 4078 5852 9930 0 0 0 4078 5852 9930 68.8 94.5 81.9
Kaskazini 'B' 4564 4504 9068 2207 2968 5175 62 47 109 2269 3015 5284 49.7 66.9 58.3
Kati 3973 3840 7813 3712 4636 8348 316 304 620 4028 4940 8968 101.4 128.6 114.8
Kusini 1850 1724 3574 1888 2058 3946 83 80 163 1971 2138 4109 106.5 124.0 115.0
Micheweni 7126 6767 13893 3378 4087 7465 56 45 101 3434 4132 7566 48.2 61.1 54.5
Wete 7269 6870 14139 5303 6651 11954 196 197 393 5499 6848 12347 75.7 99.7 87.3
Chake-Chake 6451 6468 12919 4486 5678 10164 549 577 1126 5035 6255 11290 78.0 96.7 87.4
Mkoani 6692 6240 12932 4283 5427 9710 10 12 22 4293 5439 9732 64.2 87.2 75.3
Jumla 74885 75085 149970 52389 66113 118502 5568 6641 12209 57957 72754 130711 77.4 96.9 87.2
BINAFSI JUMLA
ASILIMIA YA UANDIKISHAJI KATIKA NGAZI YA SEKONDARI ( KIDATO 1 - 4) MACHI - 2019
WILAYA
WATOTO WENYE UMRI ASILIMIA YA
WA MIAKA 12 - 15 SERIKALI UANDIKISHAJI
UANDIKISHAJI KATIKA NGAZI YA SEKONDARI (KIDATO 1-4)
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 147
JADWELI NAM. 22
WAS JUMLA WAS JUMLA WAS JUMLA
Lumumba 69 187 67 170 136 357
Ben - Bella 117 117 44 44 161 161
Hamamni 145 265 100 156 245 421
Kiembe Samaki 'A' Islamic 79 158 38 89 117 247
Biashara Mombasa 25 67 39 83 64 150
Mwanakwerekwe 'C' 95 205 49 79 144 284
Mpendae 53 130 71 141 124 271
Tumekuja 86 249 93 195 179 444
Kiponda 39 79 13 60 52 139
Haile Selassie 36 53 48 96 84 149
Faraja 84 174 27 77 111 251
Jang'ombe 71 106 29 46 100 152
Chuo cha Kiislamu (Pemba) 17 59 13 55 30 114
Madungu 32 88 70 106 102 194
Shamiani 59 114 16 54 75 168
UANDIKISHAJI KATIKA NGAZI YA ELIMU YA SEKONDARI YA JUU 2019
SKULI
KIDATO CHA 5 KIDATO CHA 6 JUMLA
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 148
Fidel-Castro 41 109 50 118 91 227
Chasasa 18 93 29 94 47 187
Utaani 'A' 32 0 24 0 56 0
Uweleni 13 25 7 17 20 42
Moh'd J. Pindua 9 36 10 27 19 63
M/Mdogo 12 34 10 21 22 55
JUMLA SERIKALI 1132 2348 847 1728 1979 4076
SUZA 28 71 14 39 42 110
SOS 54 117 33 87 87 204
Al Ihsaan 47 47 34 34 81 81
Nyuki 0 0 9 19 9 19
Philter 4 12 19 31 23 43
Al-Haramayn 18 29 17 36 35 65
Feza 18 28 29 49 47 77
Mnemonic 2 17 0 0 2 17
SSP 10 19 18 25 28 44
High View 23 45 7 15 30 60
International school 4 12 0 0 4 12
JUMLA BINAFSI 208 397 180 335 388 732
JUMLA KUU 1340 2745 1027 2063 2367 4808
JADWELI NAM. 22 linaendelea
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 149
JADWELI NAM. 23
WAV WAS JUMLA WAV WAS JUMLA WAV WAS JUMLA WAV WAS JUMLA WAV WAS JUMLA
Mjini 23342 23534 46876 16781 17664 34445 4262 4436 8698 21043 22100 43143 90.2 93.9 92.0
Magharibi 'A' 20561 20567 41128 21790 22905 44695 3126 3341 6467 24916 26246 51162 121.2 127.6 124.4
Magharibi 'B' 24604 25049 49653 21353 21830 43183 7846 8450 16296 29199 30280 59479 118.7 120.9 119.8
Kaskazini 'A' 13321 13243 26564 13901 14799 28700 265 267 532 14166 15066 29232 106.3 113.8 110.0
Kaskazini 'B' 10211 10189 20400 8318 8327 16645 379 397 776 8697 8724 17421 85.2 85.6 85.4
Kati 8926 8766 17692 11065 10871 21936 680 704 1384 11745 11575 23320 131.6 132.0 131.8
Kusini 4302 3934 8236 4802 4420 9222 299 302 601 5101 4722 9823 118.6 120.0 119.3
Micheweni 15522 14872 30394 13574 13640 27214 285 262 547 13859 13902 27761 89.3 93.5 91.3
Wete 13185 13217 26402 17531 16892 34423 465 353 818 17996 17245 35241 136.5 130.5 133.5
Chake-Chake 13556 13813 27369 15090 15124 30214 1189 1155 2344 16279 16279 32558 120.1 117.9 119.0
Mkoani 14238 13600 27838 16922 16068 32990 275 224 499 17197 16292 33489 120.8 119.8 120.3
Jumla 161768 160784 322552 161127 162540 323667 19071 19891 38962 180198 182431 362629 111.4 113.5 112.4
ASILIMIA YA UANDIKISHAJI KATIKA NGAZI YA MSINGI NA KATI (DARASA I - KIDATO 2) - 2019
WILAYA
WATOTO WENYE UMRI UANDIKISHAJI KATIKA NGAZI YA MSINGI NA KATI (DARASA LA 1 - KIDATO 2) ASILIMIA YA
WA MIAKA 6 - 13 SERIKALI BINAFSI JUMLA UANDIKISHAJI
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 150
JADWELI NAM. 24
DAKHALIA WAVULANA WASICHANA JUMLA
1 Mbweni A - 100 100
2 Mbweni B 124 - 124
3 Mazizini - 176 176
4 Fidel-Castro 177 200 377
5 Utaani 109 252 361
6 Kengeja Ufundi 93 64 157
7 C.C.K (Kiuyu) 86 92 178
8 Pindua 157 161 318
9 Chuo cha Ufundi - Mkokotoni 102 94 196
10 Chuo cha Ufundi - Vitongoji 140 52 192
Jumla 988 1191 2179
IDADI YA WANAFUNZI WANAOKAA DAKHALIA, 2019
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 151
JADWELI NAM. 25(a)
M F T M F T M F TVYUO VYA TANZANIA BARA
1 Aga Khan University - 2 2 - 1 1 - 3 3
2 Ardhi University 3 9 12 9 5 14 12 14 26
3 Arusha Technical College 2 2 4 - - - 2 2 4
4 Catholic University of Health and Allied 4 2 6 1 3 4 5 5 10
5 Centre for Foreign Relations 5 4 9 4 1 5 9 5 14 6 College of Business Education - Dar es salaam 7 10 17 8 1 9 15 11 26
7 College of Business Education - Dodoma - - - 1 - 1 1 - 1
8 Community Development Training Institute - - - 1 - 1 1 - 1
9 Dar es Salaam Institute of Technology 21 7 28 13 7 20 34 14 48
10 Dar es Salaam Maritime Institute (DMI) 6 1 7 13 2 15 19 3 22
11 Dar es Salaam University College of Education - - - 2 - 2 2 - 2
12 Eastern Africa Statistical Training Centre 3 2 5 3 3 6 6 5 11
13 Hubert Kairuki Memorial University 2 13 15 11 9 20 13 22 35
14 Institute of Accountancy Arusha 3 1 4 4 - 4 7 1 8
WANAFUNZI WALIOKO MASOMONI CHINI YA UDHAMINI ZHELB KATIKA VYUO MBALI MBALI
TANZANIA NA NJE YA TANAZANIA MWAKA 2017-2018
JINA LA CHUO
IDADI YA
WANAFUNZI
WANAONDELEA NA
MASOMO
IDADI YA
WANAFUNZI WAPYAJUMLA KUU
Na.
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 152
Jadweli nam. 25a linaendelea
15 Institute of Finance Management 6 13 19 15 5 20 21 18 39
16 Institute of Procurement and supply - 2 2 - - - - 2 2
17 Institute of Rural Development Planning 7 4 11 11 6 17 18 10 28
18 Institute of Social Work - - - 1 - 1 1 - 1
19 Institute of Tax Administration 1 3 4 2 2 1 5 6
20 Kampala International University - Tanzania 15 22 37 4 3 7 19 25 44
21 Kilimanjaro Christian Medical University College 2 3 5 1 - 1 3 3 6
22 Mbeya University of Science and Technology 10 6 16 6 2 8 16 8 24
23 Mkwawa Univrsity College of Education MUCE) 1 - 1 3 - 3 4 - 4
24 Muhimbili University of Health and Allied 3 2 5 9 2 11 12 4 16
25 Muslimu University of Morogoro 1 3 4 4 8 12 5 11 16
26 Mwalimu Nyerere Memorial Academy 5 3 8 7 - 7 12 3 15
27 Moshi Cooperative University (MoCU) - - - 1 - 1 1 - 1
28 Mzumbe University 10 4 14 13 3 16 23 7 30
29 National Institute of Transport 13 5 18 15 5 20 28 10 38
30 Nelson Mandela African Institute of Science and - - - 1 - 1 1 - 1
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 153
Jadweli nam. 25a linaendelea
31 Ruaha Catholic University (RUCU) 1 - 1 - - - 1 - 1
32 Sebastian Kolowa Memorial University 1 1 2 - - - 1 1 2
33 Sokoine University of Agriculture 4 4 8 9 10 19 13 14 27
34 St. Augustine University of Tanzania 1 1 2 8 - 8 9 1 10
35 St. Jordan University College (JUCO) - 1 1 4 2 6 4 3 7
36 St Johns University of Tanzania (SJUT) 3 3 6 - 2 2 3 5 8
37 St. Joseph College of Engineering and 2 - 2 - 1 1 2 1 3
38 St. Joseph College of Health and Allied 8 1 9 5 7 12 13 8 21
39 Stefano Moshi Memorial University College - 1 1 - - - - 1 1
40 Tanzania Institute of Accountancy - Dar es 13 6 19 13 3 16 26 9 35
41 Tanzania Institute of Accountancy - Mbeya - 2 2 - - - - 2 2
42 Teofilo Kisanji University (TEKU) - 1 1 - - - - 1 1
43 Tumaini University Dar es Salaam College - 1 1 - 2 2 - 3 3
44 Tumaini University Makumira (TUMA) - 1 1 1 1 2 1 2 3
45 Unique Academy - - - - 1 1 - 1 1
46 University of Arusha - 1 1 - - - - 1 1
47 University of Dar es Salaam 25 8 33 21 15 36 46 23 69
48 University of Dodoma 27 10 37 35 16 51 62 26 88
49 University of Iringa 1 1 2 2 - 2 3 1 4
JUMLA NDOGO 216 166 382 259 128 387 475 294 769
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 154
Jadweli nam. 25a linaendelea
VYUO VYA ZANZIBAR
50 Abdulrahman Al-Sumait University 35 49 84 66 98 164 101 147 248
51 Institute of Public Administration 28 28 56 4 6 10 32 34 66
52 Karume Istitute of Science and Technology 10 1 11 5 2 7 15 3 18
53 The Mwalimu Nyerere Memorial Academy 26 35 61 55 86 141 81 121 202
54 The Open University of Tanzania 11 2 13 41 24 65 52 26 78
55 The State University of Zanzibar 196 270 466 224 244 468 420 514 934
56 Zanzibar University 200 291 491 90 117 207 290 408 698
JUMLA NDOGO 506 676 1,182 485 577 1,062 991 1,253 2,244
SMZ SCHOLARSHIPS
1 Ardhi University (ARU) - 2 2 3 1 4 3 3 6
2 Catholic University of Health and Allied - - - 1 1 1 - 1
3 Hubert Kairuki Memorial University (HKMU) 1 2 3 1 1 1 3 4
4 Institute of Rural Development Planning (IRDP) - 1 1 - - 1 1
5 Karume Institute of Science and Technology - - - 1 1 1 - 1
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 155
Jadweli nam. 25a linaendelea
6 Kilimanjaro Christian Medical University Cllege 1 - 1 1 1 1 1 2
7 Muhimbili University of Health and Allied - - - 1 1 2 1 1 2
8 National Institute of Transport (NIT) 1 - 1 - - - 1 - 1
9 St. John's University of Tanzania (SJUIT) - 1 1 - - - - 1 1
10 Tanzania Institute of Accountancy (TIA) - Dar es - - - - 1 1 - 1 1
11 The Institute of Finance Management (IFM) - - - 1 - 1 1 - 1
12 The State University of Zanzibar (SUZA) 3 - 3 - 2 2 3 2 5
13 University of Dar es Salaam (UDM) 4 3 7 7 6 13 11 9 20
14 University of Dodoma (UDOM) - - - 2 - 2 2 - 2
15 Zanzibar University (ZU) - - - - 1 1 - 1 1
JUMLA NDOGO 10 9 19 16 14 30 26 23 49
JUMLA KUU (WANAFUNZI VYUO VYA NDANI) 732 851 1,583 760 719 1,479 1,492 1,570 3,062
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 156
Jadweli nam. 25a linaendelea
CHINA
1 Anhui Medical University - - - - 1 1 - 1 1
2 Beijing University of Civil Engineering and - - - 1 1 1 - 1
3 Capital University of Economics and Business - - - 1 1 1 - 1
4 Central South China - - - 1 1 - 1 1
5 Changsha Medical University 1 1 - 1 - 1
6 Chengdu University of Traditional Chinese - - - 1 - 1 1 - 1
7 Chefang Medical University - 1 1 - - - 1 1
8 China Pharmaceutical University 2 2 4 - - 2 2 4
9 China University of Mining - 1 1 - - - 1 1
10 Communication University of China - - - 1 - 1 1 - 1
11 East China Normal University - - - - 1 1 - 1 1
12 Fujian Medical College 4 2 6 - - 4 2 6
13 He University - - - 1 - 1 1 - 1
14 Hebei University - - - 1 - 1 1 - 1
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 157
Jadweli nam. 25a linaendelea
15 Hebei North University - 2 2 - - - - 2 2
16 Henan University of Science and Technology 1 - 1 - - 1 - 1
17 Huazhong University of Science and 1 1 2 2 1 3 3 2 5
18 Hubei University - - - - 2 2 - 2 2
19 Hubei University of Arts nd Science - - - 2 3 5 2 3 5
20 International Education College (Liaoning Shihua - - - 1 1 1 - 1
21 Jinggangshan University 1 - 1 - 2 2 1 2 3
22 Jinzhou Medical University - - - - 2 2 - 2 2
23 Liaoning University of Peroleum and Chemical - - - - 1 1 - 1 1
24 Liaocheng University - - - - 1 1 - 1 1
25 Shandong Jiaotong University - - - 1 - 1 1 - 1
26 Shenyang Medical University 1 - 1 3 3 1 3 4
27 Sichuan University of Science and Engineering - - - 2 - 2 2 - 2
28 Suzhou University of Science and Technology - - - 1 1 - 1 1
29 University of Electronic Science and 1 - 1 1 - 1
30 University of International Business and - - - - 1 1 - 1 1
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 158
Jadweli nam. 25a linaendelea
31 Weifang University - - - - 1 1 - 1 1
32 Wenzhou Medical University - 1 1 1 1 1 1 2
33 Wuhan University - 1 1 1 1 - 2 2
34 Xi'an Shiyou University - - - 2 1 3 2 1 3
35 Yichun University 8 16 24 7 13 20 15 29 44
36 Zhejiang Chinese Medical University - - - - 1 1 - 1 1
37 Zhejiang Normal University 1 1 - - 1 - 1
38 Zhejiang OceanUniversity - - - 1 - 1 1 - 1
39 Zhejiang Sci-Tech University - - - 1 - 1 1 - 1
40 Zhejiang University of Technology - - - 2 - 2 2 - 2
41 Zhengzhou University - - - 2 1 3 2 1 3
42 Communication University of Zhejiang (Zhejiang 10 21 31 1 5 6 11 26 37
43 Zunyi Normal College 5 9 14 - - - 5 9 14
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 159
Jadweli nam. 25a linaendelea
CYPRUS - - - - - - - - -
44 Cyprus International University - - - 1 - 1 1 - 1
45 Eastern Mediterranean University - - - 1 2 3 1 2 3
EGYPT - - - - - - - - -
46 Alexandria University - - - 1 - 1 1 - 1
INDIA - - - - - - - - -
47 Aditya Bangalore Institute of Pharmacy - - - 2 5 7 2 5 7
48 AP Goyal Shimla University - - - 12 10 22 12 10 22
49 CT University - - - 2 4 6 2 4 6
50 JSS Academy of Higher Education and - - - 1 - 1 1 - 1
51 Rajiv Ghandi Institute of Technology - - - 1 - 1 1 - 1
52 Sharda University - - - 1 - 1 1 - 1
53 Tilak Maharashtra Vidyapeeth - - - - 1 1 - 1 1
IRAN - - - - - - - - -
54 Kerman University of Medical Services - - - 1 - 1 1 - 1
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 160
Jadweli nam. 25a linaendelea
KENYA - - - - - - - - -
55 Mount Kenya University - - - - 1 1 - 1 1
MALAYSIA - - - - - - - - -
56 Asia Pacific University - - - 1 - 1 1 - 1
57 UCSI University - - - 1 - 1 1 - 1
58 Universiti Teknolojia Malaysia - - - 1 - 1 1 - 1
59 University Tun Abdulrazak 1 - 1 - - - 1 - 1
60 University Putra Malaysia 1 1 2 - - - 1 1 2
ROMANIA - - - - - - - - -
61 Constanta Maritime Univeristy 2 - 2 - - - 2 - 2
RUSSIA - - - - - - - - -
62 Tambov State University 1 - 1 - - - 1 - 1
63 Kalashnikov Izhensk State University - 1 1 - - - - 1 1
SULTANATE OF OMAN - - - - - - - - -
64 Modern College of Business and Science - - - - 1 1 - 1 1
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 161
Jadweli nam. 25a linaendelea
SUDAN - - - - - - - - -
65 International University of Africa 50 46 96 8 8 16 58 54 112
66 University of Arab States - - - 1 - 1 1 - 1
UGANDA - - - - - - - - -
67 Bugema University - - - 1 23 24 1 23 24
68 Cavendish University - - - 5 7 12 5 7 12
69 Institute of Petroleum Studies-Kampala - - - 1 - 1 1 - 1
70 Islamic University in Uganda 1 1 1 1 2 2 1 3
71 Kampala International University - Uganda 2 2 4 2 2 4 4 4 8
72 Kampala University - Uganda 1 - 1 12 6 18 13 6 19
73 Ernest Cook Ultrasound Research and 7 - 7 4 2 6 11 2 13
74 Makerere University 1 - 1 3 - 3 4 - 4
75 Mbarara University of Science and Technology - - - 1 - 1 1 - 1
76 Uganda Institute of Allied Heath and 1 - 1 2 7 9 3 7 10
77 University of Kisubi - - - 1 1 - 1 1
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 162
Jadweli nam. 25a linaendelea
UKRAINE - - - - - - - - -
78 Horbachevsky Ternopil State University 1 - 1 - - - 1 - 1
79 Kharkiv National Medical University - 1 1 - - - - 1 1
80 Sumy State University 2 1 3 2 1 3 4 2 6
UNITED ARAB EMIRATES - - - - - - - - -
81 RAK College of Medical and Health Sciences - - - - 1 1 - 1 1
UNITED KINGDOM - - - - - - - - -
82 Coventry University - - - 1 - 1 1 - 1
UNITED STATES OF AMERICA - - - - - - - - -
83 Duke University - Sanford School of Public - - - 1 - 1 1 - 1
84 University of Missouri - - - 1 - 1 1 - 1
IDB SCHOLARSHIPS - - - 1 3 4 1 3 4
OMAN SCHOLARSHIPS - - - 3 2 5 3 2 5
RAK GAS SCHOLARSHIPS - - - 3 3 3 - 3
JUMLA YA WANAFUNZI WA VYUO VYA NJE 107 109 216 110 131 241 217 240 457
JUMLA KUU YA WANAFUNZI WA VYUO VYA
NDANI NA NJE YA NCHI 839 960 1,799 870 850 1,720 1,709 1,810 3,519
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 163
NCHI W'ME W'KE JUMLA
1 UKRAINE 1 0 1
2 SCOTLAND 0 1 1
3 MALAYSIA 1 0 1
4 CHINA 17 5 22
5 UGANDA 18 12 30
6 INDIA 2 1 3
9 INDONESIA 2 0 2
11 QATAR 1 1 2
12 UTURUKI 2 0 2
13 SUDAN 4 5 9
14 NORWAY 1 0 1
15 MISRI 1 0 1
16 ITALY 0 1 1
JUMLA 50 26 76
WANAFUNZI WALIOKO MASOMONI KATIKA VYUO
MBALI MBALI NJE YA TANZANIA MWAKA 2018/2019
JADWELI NAM. 25(b)
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 164
JADWELI NAM. 26(a)
M’me W’ke M’me W’ke M’me W’ke M’me W’ke M’me W’ke W'ke Jumla
Shahada ya Uzamivu - Kiswahili 3 4 8 9 0 0 0 0 0 0 13 24
Shahada ya Uzamili - Kiswahili 4 2 0 0 0 0 1 1 0 0 3 8
Shahada ya Uzamili – Kemia 2 2 0 0 3 2 4 7 0 0 11 20
Shahada ya Uzamili – Sayansi ya
Mazingira 9 3 0 0 0 0 4 1 0 0 4 17
Shahada ya Uzamili - Mabadiliko
Tabianchi 5 3 12 12 0 0 0 0 0 0 15 32
Shahada ya Uzamili - Elimu ya Vijana,
Jinsia ana Utawala 11 6 6 11 0 0 0 0 0 0 17 34
Shahada ya Uzamili - Elimu ya
Kiswahili kwa Wageni 3 3 4 12 0 0 0 0 0 0 15 22
Shahada ya Ualimu - Sayansi 38 57 56 64 15 15 - - - - 136 245
Shahada ya Ualimu – Sanaa 37 76 27 58 54 76 - - - - 210 328
Shahada ya Ualimu- IT 0 0 0 0 0 12 - - - - 12 12
Shahada ya Sayansi – Kompyuta 16 8 11 3 18 3 - - - - 14 59
Shahada ya Habari na Mawasiliano 31 30 28 20 31 20 - - - - 70 160
Shahada ya Sanaa- Jografia na Mazingira 17 32 21 10 10 15 - - - - 57 105
UANDIKISHAJI ELIMU YA JUU MACHI, 2019
CHUO KIKUU CHA TAIFA ZANZIBAR (SUZA)-MAIN CAMPUS
JUMLAMWAKA 5
AINA YA PROGARAMU
MWAKA 1 MWAKA 2 MWAKA 3 MWAKA 4
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 165
Jadweli nam. 26(a) linaendelea
Shahada ya Sanaa- Historia 9 3 0 0 0 0 3 12
Shahada ya Lugha- Kiswahili 0 0 3 4 1 27 31 35
Stashahada ya Sanaa- Elimu 7 10 11 8 - - - - - - 18 36
Stashahada ya Lugha- Elimu 3 24 6 38 - - - - - - 62 71
Stashahada ya Sayansi- Elimu 25 21 9 13 - - - - - - 34 68
Stashahada ya Kazi za Jamii 4 9 3 18 - - - - - - 27 34
Stashahada ya Elimu – Michezo 6 3 2 5 - - - - - - 8 16
Stashahada ya IT 26 13 22 11 - - - - - - 24 72
Stashahada ya Sayansi ya Kompyuta 11 5 7 3 - - - - - - 8 26
Stashahada ya Ukutubi 0 10 0 0 - - - - - - 10 10
Stashahada ya Elimu Mjumuisho 11 21 6 37 - - - - - - 58 75
Stashahada ya Elimu ya Awali 0 6 0 30 - - - - - - 36 36
Cheti cha Teknolojia ya Kompyuta 0 0 - - - - - - - -
Pre - Diploma Science 22 47 24 30 30 46 - - - - 123 199
JUMLA 300 398 266 396 162 216 9 9 - - 1,019 1,756
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 166
JADWELI NAM. 26(b)
NCHI WALIZOTOKA WANAFUNZI WAVULANA WASICHANA JUMLA
Uingereza - 2 2
Marekani 7 28 35
Ujerumani 3 6 9
Sudan 5 0 5
Sweden - 1 1
Kenya - 1 1
MALVIS ISLAND 1 0 1
Japan 0 1 1
Nigeria 2 0 2
Qatar 1 0 1
Switzerland - 1 1
Denmark - 1 1
China 1 0 1
Australia 1 1 2
Algeria 1 0 1
Saudi Arabia 1 0 1
Ufaransa 0 3 3
JUMLA 23 45 68
UANDIKISHAJI WA WANAFUNZI WA KIGENI KATIKA SKULI
YA KISWAHILI NA LUGHA ZA KIGENI - MACHI, 2019
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 167
JADWELI NAM. 26(c)
M’me W’ke M’me W’ke M’me W’ke M’me W’ke M’me W’ke M’me W’ke
Shahada ya Sayansi ya Afya na Mazingira 12 16 11 15 14 12 - - - - 37 43 80
Shahada ya Udaktari 18 13 15 15 7 9 31 25 22 28 93 90 183
Stashahada ya Uuguzi na Ukunga 8 33 8 51 24 54 - - - - 40 138 178
Stashahada ya Sayansi ya Afya ya Mazingira 11 14 13 10 11 5 - - - - 35 29 64
stashahada ya Sayansi ya Mabaara 19 27 29 24 44 25 - - - - 92 76 168
Stashahada ya Sayansi ya Famasia 26 33 22 39 31 34 - - - - 79 106 185
Stashahada ya Afya Kinywa na Meno 11 7 13 4 10 7 - - - - 34 18 52
Stashahada ya Afya ya Tabibu 18 27 33 34 41 39 - - - - 92 100 192
Stashahada ya Fisiotherapia 5 13 6 20 11 6 - - - - 22 39 61
JUMLA 128 183 150 212 193 191 31 25 22 28 524 639 1163
UANDIKISHAJI ELIMU YA JUU MACHI, 2019
SCHOOL OF HEALTH AND MEDICAL STUDIES
AINA YA PROGARAMU
MWAKA 1 MWAKA 2 MWAKA 3 JUMLA
JUMLA
MWAKA 4 MWAKA 5
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 168
M’me W’ke M’me W’ke M’me W’ke M’me W’ke
Shahada ya Uongozi wa Fedha na Uhasibu 28 48 24 34 15 27 67 109 176
Shahada ya Manunuzi na Ugamvi 4 2 1 5 7 14 12 21 33
Shahada ya Tehama na Uhasibu 31 28 22 18 20 17 73 63 136
Shahada Banki na Fedha 5 7 6 10 1 15 12 32 44
Stashahada Manunuzi na Ugavi 2 7 2 4 - - 4 11 15
Stashahada ya Tehama na Uhasibu 15 16 29 24 - - 44 40 84
Stashahada ya Uongozi wa Fedha 17 38 38 50 - - 55 88 143
Cheti cha Uongozi Fedha 48 35 - - - - 48 35 83
JUMLA 150 181 122 145 43 73 315 399 714
JADWELI NAM. 26(d)
UANDIKISHAJI ELIMU YA JUU MACHI, 2019
SCHOOL OF BUSINESS
AINA YA PROGARAMU
MWAKA 1 MWAKA 2 MWAKA 3 JUMLA
JUMLA
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 169
JADWELI NAM. 26(e)
M’me W’ke M’me W’ke M’me W’ke M’me W’ke
Shahada ya Sanaa – Utalii 20 19 0 0 22 19 42 38 80
Stashshada ya Utalii na Urithi 6 1 7 10 - - 13 11 24
Stashahada ya Ukarimu na Uongozi wa Utalii 4 4 8 7 - - 12 11 23
Stashahada ya Teknologia ya Habari na
Uhasibu 0 0 2 6 - - 2 6 8
Cheti cha Ukaribishaji Wageni 4 6 - - - - 4 6 10
Cheti cha Huduma ya Chakula na Vinywaji 3 1 - - - - 3 1 4
Cheti cha Upishi 8 4 - - - - 8 4 12
Cheti cha Utunzaji Hotel 0 0 - - - - 0 0 0
Cheti cha Uongozaji Watalii 27 3 - - - - 27 3 30
JUMLA 72 38 17 23 22 19 111 80 191
UANDIKISHAJI ELIMU YA JUU MACHI, 2019
INSTITUTE OF TOURISM DEVELOPMENT
AINA YA PROGARAMU
MWAKA 1 MWAKA 2 MWAKA 3 JUMLA
JUMLA
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 170
JADWELI NAM. 26(f)
SUZA Main Campus 737 1019 1756
School of Kiswahili and Foreign Language 23 45 68
School of Health and Medical Science 524 639 1163
School of Business 315 399 714
Institute of Tourism 111 80 191
JUMLA 1710 2182 3892
W'ME W'KE
MUHTASARI WA UANDIKISHAJI CHUO KIKUU CHA TAIFA CHA ZANZIBAR
(SUZA), 2019
JUMLATAASISI
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 171
JADWELI NAM. 27
CHUO KIKUU CHA SUMAIT - CHUKWANI
W'me W'ke W'me W'ke W'me W'ke W'me W'ke
Shahada ya Sayansi ya Ualimu 66 73 26 15 13 9 105 97 202
Shahada ya Sanaa ya Ualimu 28 89 36 33 42 108 106 230 336
Shahada ya Sayansi ya Komputa 0 0 0 0 4 0 4 0 4
Shahada ya Sanaa ya Ushauri nasaha 0 0 0 0 9 27 9 27 36
Shahada ya Teknolojia ya Habari na mawasiliano 7 15 4 7 10 8 21 30 51
Stashahada ya Sayansi ya Ualimu 12 8 6 3 0 0 18 11 29
Stashahada ya Sanaa ya Ualimu 17 10 9 11 0 0 26 21 47
Stashahada ya Teknolojia ya Habari na mawasiliano 20 13 29 14 0 0 49 27 76
Cheti cha Ualimu 0 17 0 0 0 0 0 17 17
Cheti cha Teknolojia ya Habari na mawasiliano 12 31 0 0 0 0 12 31 43
JUMLA 162 256 110 83 78 152 350 491 841
JUMLA
KUU
UANDIKISHAJI ELIMU YA JUU MACHI, 2019
JUMLA
AINA YA PROGRAMU
Mwaka 1 Mwaka 2 Mwaka 3
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 172
JADWELI NAM. 28
W'me W'ke W'me W'ke W'me W'ke W'me W'ke W'me W'ke
CERTIFICATE IN BUSINESS ADMINISTRATION 18 38 - - - - - - 18 38 56
CERTIFICATE IN COMMUNITY DEVELOPMENT 21 37 - - - - - - 21 37 58
CERTIFICATE IN CIT 22 15 - - - - - - 22 15 37
CERTIFICATE IN PROCUREMENT AND SUPPLY 5 14 - - - - - - 5 14 19
DIPLOMA IN BUSINESS ADMINISTRATION 28 32 35 38 - - - - 63 70 133
DIPLOMA IN COMMUNITY DEVELOPMENT 19 27 23 41 - - - - 42 68 110
DIPLOMA IN CIT 32 26 20 14 - - - - 52 40 92
DIPLOMA IN NURSING AND MIDWIFERY 19 50 34 97 13 40 - - 66 187 253
DIPLOMA IN ISLAMIC BANKING 0 0 7 14 0 0 - - 7 14 21
DIPLOMA IN LAW AND SHARIAH 0 0 17 19 0 0 - - 17 19 36
BACHELOR OF ACCOUNTING AND FINANCE 41 51 26 27 31 51 - - 98 129 227
BACHELOR OF ACCOUNTING AND FINANCE - PEMBA 0 0 0 0 6 5 - - 6 5 11
BACHELOR OF ECONOMICS 8 10 6 20 21 28 - - 35 58 93
BACHELOR OF ECONOMICS - PEMBA 0 0 0 0 9 7 - - 9 7 16
UANDIKISHAJI ELIMU YA JUU MACHI, 2019
CHUO KIKUU CHA ZANZIBAR
AINA YA PROGRAMU
Mwaka 1 Mwaka 2 Mwaka 3 Mwaka 4 JUMLA JUMLA
KUU
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 173
BACHELOR OF MARKETING 2 1 2 14 2 11 - - 6 26 32
BACHELOR OF NURSING 0 0 6 13 18 40 12 28 36 81 117
BACHELOR OF PUBLIC ADMINISTRATION 17 24 0 0 4 2 - - 21 26 47
BACHELOR OF TELECOMMUNICATION
ENGINEERING 2 2 1 0 9 4 10 3 22 9 31BACHELOR OF BUSINESS INFORMATION
TECHNOLOGY 0 0 19 12 38 21 - - 57 33 90
BACHELOR OF COMPUTER ENGINEERING 0 0 1 1 4 3 8 2 13 6 19
BACHELOR OF INFORMATION SCIENCE 0 0 4 17 13 42 - - 17 59 76
BACHELOR OF INTERNATIONAL RELATION 0 0 26 12 60 39 - - 86 51 137
BACHELOR OF IT WITH EDUCATION (BIOLOGY) 0 0 9 2 8 21 - - 17 23 40
BACHELOR OF IT WITH EDUCATION (MATHEMATICS) 0 0 2 3 2 13 - - 4 16 20
BACHELOR OF IT WITH EDUCATION (GEOGRAPHY) 0 0 0 0 9 10 - - 9 10 19
BACHELOR OF LANGUAGES (ENGLISH - SWAHILI) 0 0 8 10 8 31 - - 16 41 57
BACHELOR OF LANGUAGES (ARABIC - SWAHILI) 0 0 0 0 6 13 - - 6 13 19
BACHELOR OF LAW AND SHARIAH 0 0 9 5 25 19 8 10 42 34 76
BACHELOR OF PROCUREMENT AND LOGISTICS 0 0 9 23 32 47 - - 41 70 111
BACHELOR OF SOCIAL WORK 0 0 5 18 18 60 - - 23 78 101
BACHELOR OF ISLAMIC BANKING - - 0 0 7 8 - - 7 8 15
MASTERS OF BUSINESS ADMINISTRATION 15 12 13 16 - - - - 28 28 56
MASTERS OF PUBLIC ADMINISTRATION 13 8 10 13 - - - - 23 21 44
MASTERS OF LAW 3 4 2 2 - - - - 5 6 11
MASTERS OF ECONOMICS AND FINANCE 9 18 18 9 - - - - 27 27 54
JUMLA 274 369 312 440 343 515 38 43 967 1367 2,334
Jadweli nam. 28 linaendelea
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 174
JADWELI NAM. 29
FANI WANAUME WANAWAKE JUMLA
Civil Engineering and Transportation NTA - 4 31 16 47
Civil Engineering and Transportation NTA - 5 20 4 24
Civil Engineering and Transportation NTA - 6 20 9 29
Mechanical Engineering NTA - 4 2 1 3
Mechanical Engineering NTA - 5 4 0 4
Mechanical Engineering NTA - 6 6 2 8
Automotive Engineering NTA - 4 6 0 6
Automotive Engineering NTA - 5 3 0 3
Automotive Engineering NTA - 6 4 0 4
Mechanical with Oil and Gas Engineering NTA - 4 26 4 30
Mechanical with Oil and Gas Engineering NTA - 5 5 1 6
Mechanical with Oil and Gas Engineering NTA - 6 0 0 0
Electrical Engineering NTA - 4 17 0 17
UANDIKISHAJI KATIKA TAASISI YA KARUME YA SAYANSI NA TEKNOLOJIA
MACHI - 2019
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 175
Electrical Engineering NTA - 5 12 0 12
Electrical Engineering NTA - 6 26 9 35
Electrical with Renewable Energy Engineering NTA - 4 11 5 16
Electrical with Renewable Energy Engineering NTA - 5 9 5 14
Electrical with Renewable Energy Engineering NTA - 6 0 0 0
Telecommunication and Electronic Engineering NTA - 4 8 2 10
Telecommunication and Electronic Engineering NTA - 5 11 1 12
Telecommunication and Electronic Engineering NTA - 6 9 10 19
Computer engineering - NTA - 4 6 0 6
Computer engineering - NTA - 5 2 4 6
Computer engineering- NTA - 6 6 4 10
ICT Certificate-NTA- 4 28 12 40
ICT Diploma I-NTA- 5 13 8 21
Jadweli nam. 29 linaendelea
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 176
ICT Diploma II-NTA- 6 12 6 18
Vocational Technical Teacher (VTT)-NTA-4 0 0 0
Vocational Technical Teacher (VTT)-NTA-5 0 0 0
Vocational Technical Teacher (VTT)-NTA-6 15 17 32
Teacher for Primary Education-NTA-4 2 54 56
Teacher for Primary Education-NTA-5 4 36 40
Teacher for Primary Education-NTA-6 6 21 27
Laboratory Engineering - NTA - 4 24 19 43
Laboratory Engineering - NTA - 5 7 7 14
Laboratory Engineering NTA - 6 4 9 13
JUMLA NTA 4 161 113 274
JUMLA NTA 5 90 66 156
JUMLA NTA 6 108 87 195
Bachelor Degree in Aircraft Maintanance Engineering and Pilot Studies
NTA 7, 1 yr 8 3 11
Bachelor Degree in Aircraft Maintanance Engineering and Pilot Studies
NTA 7, 3 yr 12 1 13
DEGREE 20 4 24
JUMLA KUU 379 270 649
Angalia:
NTA = National Technical Award
Jadweli nam. 29 linaendelea
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 177
JADWELI NAM. 30(a)
W'ME W'KE W'ME W'KE W'ME W'KE
Stashahada ya Ualimu-Sayansi Msingi 40 139 49 80 89 219 308
Stashahada ya Ualimu-Sanaa Msingi 6 40 6 42 12 82 94
Stashahada ya Ualimu-Masomo ya Kiislamu - - 5 14 5 14 19
Stashahada ya Ualimu-Sekondari 7 15 - - 7 15 22
ECD 8 91 - - 8 91 99
Pre-Diploma 23 99 - - 23 99 122
Jumla 84 384 60 136 144 520 664
JUMLA KUUDARAJA ZA MASOMO
IDADI YA WANAFUNZI KATIKA CHUO CHA KIISLAMU MAZIZINI UNGUJA, MACHI - 2019
MWAKA WA KWANZA MWAKA WA PILI JUMLA
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 178
JADWELI NAM. 30(b)
DARAJA ZA MASOMO WANAUME WANAWAKE JUMLA
Wanafunzi wa Kidato cha 1 20 26 46
Wanafunzi wa Kidato cha 2 26 11 37
Wanafunzi wa Kidato cha 3 18 19 37
Wanafunzi wa Kidato cha 4 17 26 43
Wanafunzi wa Kidato cha 5 42 17 59
Wanafunzi wa Kidato cha 6 42 13 55
Cheti 8 34 42
Stashahada ya Ualimu (Mwaka 1) 33 72 105
Stashahada ya Ualimu (Mwaka 2) 49 87 136
Jumla 255 305 560
IDADI YA WANAFUNZI KATIKA CHUO CHA KIISLAMU KIUYU PEMBA, MACHI - 2019
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 179
JADWELI NAM. 31
WAVULANA WASICHANA JUMLA WAVULANA WASICHANA JUMLA WAVULANA WASICHANA JUMLA
Mjini 1911 1991 3902 1828 1962 3790 95.7 98.5 97.1
Magharibi 'A' 2096 2506 4602 1954 2478 4432 93.2 98.9 96.3
Magharibi 'B' 2117 2430 4547 1967 2395 4362 92.9 98.6 95.9
Kaskazini 'A' 1200 1513 2713 1096 1476 2572 91.3 97.6 94.8
Kaskazini 'B' 788 770 1558 693 758 1451 87.9 98.4 93.1
Kati 1043 1103 2146 920 1086 2006 88.2 98.5 93.5
Kusini 543 501 1044 472 488 960 86.9 97.4 92.0
Micheweni 1176 1341 2517 1144 1319 2463 97.3 98.4 97.9
Wete 1620 1799 3419 1528 1763 3291 94.3 98.0 96.3
Chake-Chake 1225 1435 2660 1149 1428 2577 93.8 99.5 96.9
Mkoani 1265 1511 2776 1194 1491 2685 94.4 98.7 96.7
Skuli za Binafsi 1420 1518 2938 1414 1516 2930 99.6 99.9 99.7
Jumla 16404 18418 34822 15359 18160 33519 93.6 98.6 96.3
MATOKEO YA MTIHANI WA DARASA LA VI KWA 2018 NA
WALIOTEULIWA KUENDELEA NA MASOMO - 2019
WILAYA
WALIOFANYA MTIHANI WALIOTEULIWA KUENDELEA ASILIMIA YA WANAOENDELEA
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 180
JADWELI NAM. 32
WAVULANA WASICHANA JUMLA WAVULANA WASICHANA JUMLA WAVULANA WASICHANA JUMLA
Mjini 2535 2780 5315 1593 2302 3895 62.8 82.8 73.3
Magharibi 'A' 1646 1990 3636 948 1514 2462 57.6 76.1 67.7
Magharibi 'B' 1975 2026 4001 1306 1672 2978 66.1 82.5 74.4
Kaskazini 'A' 1053 1497 2550 764 1172 1936 72.6 78.3 75.9
Kaskazini 'B' 747 900 1647 337 652 989 45.1 72.4 60.0
Kati 633 625 1258 383 474 857 60.5 75.8 68.1
Kusini 1123 1170 2293 515 839 1354 45.9 71.7 59.0
Micheweni 1048 1265 2313 648 933 1581 61.8 73.8 68.4
Wete 1172 1260 2432 768 1041 1809 65.5 82.6 74.4
Chake-Chake 1248 1494 2742 879 1207 2086 70.4 80.8 76.1
Mkoani 731 896 1627 523 672 1195 71.5 75.0 73.4
Skuli za Binafsi 1300 1522 2822 1257 1508 2765 96.7 99.1 98.0
Jumla 15211 17425 32636 9921 13986 23907 65.2 80.3 73.3
MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA PILI - 2018 NA
WILAYA
WALIOFANYA MTIHANI WALIOTEULIWA KUENDELEA ASILIMIA YA WANAOENDELEA
WALIOTEULIWA KUENDELEA NA MASOMO - 2019
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 181
JADWELI NAM. 33(a)i
WAS JUMLA WAS JUMLA WAS JUMLA WAS JUMLA WAS JUMLA WAS JUMLA WAS JUMLA TZ ZNZ
WILAYA YA MJINI
1 Lumumba 50 112 17 53 29 52 4 7 0 0 50 112 100.0 100.0 71 1
2 Mikunguni 23 48 2 6 5 16 8 14 7 11 22 47 95.7 97.9 328 7
3 Kiponda 27 35 0 0 4 7 15 19 8 9 27 35 100.0 100.0 180 15*
4 Tumekuja 56 122 7 11 31 71 17 36 1 4 56 122 100.0 100.0 218 3
5 Jang'ombe 104 186 0 0 1 4 6 11 58 94 65 109 62.5 58.6 3321 99
6 Haileselassie 156 253 0 0 0 2 4 11 84 132 88 145 56.4 57.3 3398 116
7 Vikokotoni 82 195 0 5 1 11 29 77 51 95 81 188 98.8 96.4 727 24
8 Faraja 175 278 0 0 1 1 4 10 108 166 113 177 64.6 63.7 3334 102
9 Forordhani 75 103 0 0 0 0 2 5 47 73 49 78 65.3 75.7 3367 109
10 Ben-Bella 145 145 2 2 39 39 62 62 41 41 144 144 99.3 99.3 471 14
MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE, SKULI ZA SERIKALI - 2018/19
KIMA CHA UFAULU NATIJAWATAHINIWA JUMLA
SKULI
DIV. I DIV. II DIV. III DIV. IV
Nam.
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 182
Jadweli Nam. 33(a)i Linaendelea
11 Kidongo Chekundu 169 284 0 0 0 2 11 27 113 169 124 198 73.4 69.7 3060 56
12 Kwamtipura 165 305 0 0 0 1 6 15 86 152 92 168 55.8 55.1 3394 114
13 Hurumzi 65 136 0 0 1 3 9 18 44 82 54 103 83.1 75.7 2679 41
14 Hamamni 104 441 0 0 0 0 3 4 40 65 43 69 41.3 15.6 3474 135
15 Mpendae 136 249 0 0 0 2 16 30 81 137 97 169 71.3 67.9 2358 36
16 Chumbuni 109 198 0 0 0 0 3 10 58 92 61 102 56.0 51.5 3429 125
17 Nyerere 173 262 0 0 0 2 12 24 15 70 27 96 15.6 36.6 3013 54
18 Mwembeladu 176 299 0 0 1 2 8 21 113 196 122 219 69.3 73.2 3051 56
Jumla 1990 3651 28 77 113 215 219 401 955 1588 1315 2281 66.1 62.5
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 183
Jadweli Nam. 33(a)i Linaendelea
WILAYA YA MAGHARIBI 'A'
1 Mtoni Kigomeni 71 125 0 0 0 1 5 8 46 85 51 94 71.8 75.2 3041 55
2 Mfenesini 95 153 0 0 1 2 7 9 67 97 75 108 78.9 70.6 3132 64
3 Bububu 287 477 0 0 0 1 4 17 150 241 154 259 53.7 54.3 3391 113
4 Langoni 46 79 0 0 0 0 2 4 37 54 39 58 84.8 73.4 3164 69
5 Regeza Mwendo 100 167 0 0 1 1 8 12 50 80 59 93 59.0 55.7 3335 103
6 Mtopepo 210 360 0 0 0 0 4 15 136 208 140 223 66.7 61.9 3353 105
7 Chuini 109 177 0 1 1 1 6 9 71 104 78 115 71.6 65.0 3173 71
8 Mwenge 36 63 0 0 0 0 0 1 17 34 17 35 47.2 55.6 3415 120
9 Mikindani Dole 31 52 0 1 4 9 18 30 9 12 31 52 100.0 100.0 499 16
10 Mtoni Kidatu 24 38 0 0 0 0 0 0 16 28 16 28 66.7 73.7 1287 44*
11 Kianga 53 74 0 0 0 0 3 5 33 45 36 50 67.9 67.6
Jumla 1062 1765 0 2 7 15 57 110 632 988 696 1115 65.5 63.2 3116 60
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 184
Jadweli Nam. 33(a)i Linaendelea
1 Mwanakwerekwe 'A' 111 182 0 0 2 8 12 28 80 122 94 158 84.7 86.8 1997 33
2 Kiembe Samaki 'A' Islamic 104 194 0 1 17 36 62 107 25 40 104 184 100.0 94.8 526 17
3 Chukwani 51 67 0 1 0 3 5 8 32 37 37 49 72.5 73.1 2153 35
4 Kinuni 131 184 0 0 0 1 5 11 76 97 81 109 61.8 59.2 3354 106
5 Kisauni 48 72 0 0 0 0 3 5 31 44 34 49 70.8 68.1 3134 65
6 Fuoni 128 208 0 0 1 2 1 10 78 123 80 135 62.5 64.9 3289 90
7 Mwanakwerekwe 'C' 293 474 0 0 0 0 26 36 190 290 216 326 73.7 68.8 3169 70
8 Zanzibar commercial 42 101 0 3 8 29 25 45 9 24 42 101 100.0 100.0 438 11
9 Maungani 25 39 0 0 2 2 0 0 18 28 20 30 80.0 76.9 1161 33*
10 Kwarara 30 56 0 0 0 0 2 6 25 40 27 46 90.0 82.1 2794
11 Kiembesamaki 141 247 0 0 2 3 11 20 99 166 112 189 79.4 76.5 2874 45
12 Kombeni 41 63 0 0 0 0 3 3 19 34 22 37 53.7 58.7 3395 115
13 Bwefum 15 21 0 0 0 0 0 1 8 12 8 13 53.3 61.9 1294 47*
Jumla 1160 1908 0 5 32 84 155 280 690 1057 877 1426 75.6 74.7
WALAYA YA MAGHARIBI 'B'
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 185
WILAYA YA KASKAZINI 'A'
1 Tumbatu 58 113 0 0 0 4 1 13 35 61 36 78 62.1 69.0 2857 44
2 Mkwajuni 149 215 0 0 1 1 3 10 56 85 60 96 40.3 44.7 3412 119
3 Fukuchani 24 38 0 0 0 0 0 0 17 29 17 29 70.8 76.3 1228 37*
4 Jongowe 44 87 0 0 0 1 4 10 36 69 40 80 90.9 92.0 2231 36
5 Potoa 64 87 0 0 0 0 0 1 50 69 50 70 78.1 80.5 3033
6 Kidoti 59 93 0 0 2 6 7 17 46 65 55 88 93.2 94.6 1362 28
7 Mapinduzi 83 127 0 0 0 3 6 8 56 87 62 98 74.7 77.2 2991
8 Pale 36 60 0 0 1 1 4 7 24 37 29 45 80.6 75.0 3000 52
9 Kinyasini 70 118 0 0 0 1 2 5 21 43 23 49 32.9 41.5 3362 107
10 Gamba 37 73 0 0 0 1 2 3 27 45 29 49 78.4 67.1 3201 75
11 Pwani Mchangani 30 60 0 0 0 0 0 1 5 13 5 14 16.7 23.3 3488 141
12 Mlimani Matemwe 21 45 0 0 0 1 0 1 14 25 14 27 66.7 60.0 3371 111
13 Kijini 32 55 0 0 0 0 0 0 21 34 21 34 65.6 61.8 3483 137
14 Nungwi 47 97 0 0 0 1 5 16 38 69 43 86 91.5 88.7 2051 34
15 Matemwe 14 22 0 0 0 0 0 0 4 8 4 8 28.6 36.4 1368 52*
JUMLA 768 1290 0 0 4 20 34 92 450 739 488 851 63.5 66.0
Jadweli Nam. 33(a)i Linaendelea
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 186
1 Donge 89 124 0 0 0 0 40 64 47 58 87 122 97.8 98.4 3461 131
2 Mahonda 69 101 0 0 1 1 4 5 35 58 40 64 58.0 63.4 3257 84
3 Fujoni 39 60 0 0 0 1 23 31 15 27 38 59 97.4 98.3 3439 126
4 Bumbwini 47 82 0 0 0 0 26 46 21 35 47 81 100.0 98.8 3445 127
5 Makoba 54 70 0 0 0 0 0 0 35 47 35 47 64.8 67.1 3406 117
6 Mwanda 35 60 0 0 0 0 0 1 25 37 25 38 71.4 63.3 3418 122
7 Upenja 23 37 0 0 0 0 0 0 14 20 14 20 60.9 54.1 1347
8 Kitope 56 102 0 0 0 5 2 33 37 47 39 85 69.6 83.3 3098 59
JUMLA 412 636 0 0 1 7 95 180 229 329 325 516 78.9 81.1
Jadweli Nam. 33(a)i Linaendelea
WILAYA YA KASKAZINI 'B'
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 187
Jadweli Nam. 33(a)i Linaendelea
1 Mpapa 33 50 0 0 0 0 3 3 24 41 27 44 81.8 88.0 2915 48
2 Uroa 30 58 0 0 0 2 0 2 22 39 22 43 73.3 74.1 3085 58
3 Ndijani 43 64 0 0 0 1 2 2 22 39 24 42 55.8 65.6 3215 76
4 Mwera 70 121 0 0 1 2 5 7 42 72 48 81 68.6 66.9 3184 72
5 Dunga 43 71 0 0 0 1 2 6 30 45 32 52 74.4 73.2 2901 46
6 Unguja Ukuu 31 45 0 0 0 0 0 2 20 29 20 31 64.5 68.9 3300 94
7 Ukongoroni 5 15 0 0 0 0 0 3 5 12 5 15 100.0 100.0 695 23*
8 Kiboje 49 75 0 0 0 0 4 8 19 30 23 38 46.9 50.7 3365 108
9 Bambi 27 52 0 0 1 1 0 1 20 32 21 34 77.8 65.4 3258 85
10 Machui 32 55 0 0 0 1 1 5 18 31 19 37 59.4 67.3 3122 61
11 Charawe 7 16 0 0 0 0 0 0 6 12 6 12 85.7 75.0 1264 41*
12 Jendele 28 45 0 0 0 0 1 3 16 31 17 34 60.7 75.6 3123 62
13 Uzi 30 40 0 0 0 0 1 1 18 24 19 25 63.3 62.5 3386 112
14 Kibele 43 68 0 0 0 0 4 4 21 39 25 43 58.1 63.2 3298 93
15 Jumbi 46 73 0 0 0 2 4 5 32 49 36 56 78.3 76.7 2987 51
16 Umbuji 9 15 0 0 0 0 0 0 7 13 7 13 77.8 86.7 1160 32*
17 Chwaka 19 47 0 0 0 0 0 1 15 33 15 34 78.9 72.3 3320 98
18 Umoja Uzini 67 109 0 0 2 2 3 6 38 55 43 63 64.2 57.8 3329 101
JUMLA 612 1019 0 0 4 12 30 59 375 626 366 634 59.8 62.2
WILAYA YA KATI
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 188
Jadweli Nam. 33(a)i Linaendelea
1 Paje 19 34 0 0 0 0 3 7 12 21 15 28 78.9 82.4 939 28*
2 Makunduchi 56 104 0 0 0 2 1 6 23 48 24 56 42.9 53.8 3368 110
3 Mtule 19 36 0 0 2 2 9 10 0 12 11 24 57.9 66.7 1225 36*
4 Jambiani 29 57 0 0 0 3 1 3 8 17 9 23 31.0 40.4 3218 78
5 Kusini 35 67 0 0 0 0 2 4 14 31 16 35 45.7 52.2 3424 124
6 K/Dimbani 17 25 0 0 0 0 0 1 7 8 7 9 41.2 36.0 1365 51*
7 Bwejuu 35 61 0 0 0 0 0 3 13 25 13 28 37.1 45.9 3457 129
8 Kizimkazi 19 28 0 0 0 0 3 3 8 13 11 16 57.9 57.1 1281 43*
9 Muyuni 17 25 0 0 0 0 2 3 14 21 16 24 94.1 96.0 1001 30*
JUMLA 246 437 0 0 2 7 21 40 99 196 122 243 49.6 55.6
WILAYA YA KUSINI
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 189
Jadweli Nam. 33(a)i Linaendelea
1 Pemba Islamic 14 30 0 2 3 7 8 14 3 7 14 30 100.0 100.0 118 8*
2 Tumbe 33 66 0 0 0 0 3 9 26 46 29 55 87.9 83.3 2677 40
3 Wingwi 52 109 0 0 1 2 3 9 30 66 34 77 65.4 36.0 3125 63
4 Shumba 26 51 0 0 0 0 1 1 18 36 19 37 73.1 72.5 3303 95
5 Konde 74 119 0 1 0 0 0 2 45 64 45 67 60.8 56.3 3428 93
6 Micheweni 38 71 0 1 0 1 3 10 26 48 29 60 76.3 84.5 2533 37
7 Msuka 23 35 0 0 0 0 1 1 12 23 13 24 56.5 68.6 1291 46*
8 Chwaka Tumbe 26 53 0 0 0 0 0 3 18 34 18 37 69.2 69.8 3266 86
9 Makangale 27 52 0 0 0 2 0 0 19 26 19 28 70.4 53.8 2967
10 Kiuyu 15 37 0 0 0 0 0 5 10 20 10 25 66.7 67.6 1194 34*
11 Kinowe 40 64 0 0 0 0 0 1 22 30 22 31 55.0 48.4 3458 130
JUMLA 368 687 0 4 4 12 19 55 229 400 252 471 68.5 68.6
WILAYA YA MICHEWENI
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 190
Jadweli Nam. 33(a)i Linaendelea
1 Utaani 107 107 1 1 3 3 22 22 62 62 88 88 82.2 82.2 1926 32
2 M/Mdogo 80 157 0 0 0 1 4 9 43 82 47 92 58.8 58.6 3348 104
3 Chasasa 40 153 0 0 7 26 14 46 18 76 39 148 97.5 96.7 696 22
4 Minungwini 43 92 0 0 1 1 1 7 28 53 30 61 69.8 66.3 3253 82
5 Pandani 34 60 0 0 0 3 2 6 23 34 25 43 73.5 71.7 2896 46
6 Wete Secondary 29 60 0 5 7 27 4 7 16 19 27 58 93.1 96.7 379 9
7 Piki 27 37 0 0 1 1 1 3 14 19 16 23 59.3 62.2 1239 38*
8 Kangagani 34 50 0 0 0 0 1 2 13 17 14 19 41.2 38.0 3473 134
9 Kinyasini 18 28 0 0 0 1 0 1 8 15 8 17 44.4 60.7 1247 39*
10 Gando 43 67 0 0 0 1 0 2 26 39 26 42 60.5 62.7 3268 87
WILAYA YA WETE
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 191
Jadweli Nam. 33(a)i Linaendelea
11 Kojani 16 31 0 0 0 2 1 2 12 22 13 26 81.3 83.9 976 29*
12 Makongeni 9 15 0 0 0 0 0 1 3 4 3 5 33.3 33.3 1342 49*
13 Uondwe 23 51 0 0 0 0 0 2 13 28 13 30 56.5 58.8 3417 121
14 Shengejuu 29 67 0 0 0 1 1 6 13 33 14 40 48.3 59.7 3297 92
15 Kizimbani 50 111 0 1 0 1 4 9 39 75 43 86 86.0 77.5 2851 43
16 Limbani 37 73 0 0 0 1 1 5 19 38 20 44 54.1 60.3 3287 89
17 Mitiulaya 48 93 0 0 0 0 11 17 34 54 45 71 93.8 76.3 3296 91
18 Fundo 4 6 0 0 0 0 0 0 3 5 3 5 75.0 83.3 1202 35*
19 M/Takao 19 38 0 0 0 0 0 0 13 27 13 27 68.4 71.1 1217 36*
20 Chwale 22 38 1 1 0 3 1 3 14 23 16 30 72.7 78.9 847 26*
21 Ukunjwi 6 15 0 1 0 0 0 0 6 10 6 11 100.0 73.3 1107 31*
22 Kijumbani 9 14 0 0 0 0 0 0 5 6 5 6 55.6 42.9 1364 50*
JUMLA 727 1363 2 9 19 72 68 150 425 741 514 972 70.7 71.3
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 192
Jadweli Nam. 33(a)i Linaendelea
1 F/Castro 29 67 6 20 11 28 12 19 0 0 29 67 100.0 100.0 146 3
2 Shamiani 94 146 0 0 0 0 10 19 50 75 60 94 63.8 64.4 3145 66
3 Ch/Mjawiri 44 58 0 0 0 0 4 6 25 36 29 42 65.9 72.4 2939 49
4 Vitongoji 59 93 0 0 1 2 4 7 37 61 42 70 71.2 75.3 2809 41
5 Dr Omar Ali Juma 78 140 0 0 0 0 1 5 56 99 57 104 73.1 74.3 3197 74
6 Pujini 37 65 0 0 0 0 2 6 27 47 29 53 78.4 81.5 2969 50
7 Wesha 25 44 0 0 1 1 3 4 15 22 19 27 76.0 61.4 3151 68
8 Kilindi 52 77 0 0 0 0 2 7 18 29 20 36 38.5 46.8 3410 118
9 Furaha 112 208 0 0 1 2 4 16 59 105 64 123 57.1 59.1 3250 81
WILAYA YA CHAKE
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 193
Jadweli Nam. 33(a)i Linaendelea
10 Ziwani 36 76 0 0 1 4 1 10 17 37 19 51 52.8 67.1 2612 38
11 Ole 43 69 0 0 0 0 2 3 27 42 29 45 67.4 65.2 3317 96
12 Kwale 15 27 0 0 0 0 0 6 13 19 13 25 86.7 92.6 733 25*
13 Pondeani 32 76 0 0 0 3 2 6 23 42 25 51 78.1 67.1 3077 57
14 Ng'mbwa 50 101 0 0 0 0 0 1 20 40 20 41 40.0 40.6 3477 136
15 Uwandani 16 37 0 0 1 3 1 1 7 13 9 17 56.3 45.9 1289 45*
16 Madungu 66 98 2 5 16 24 25 36 20 29 63 94 95.5 95.9 441 12
17 Mbuzini 27 54 0 0 1 2 1 2 20 34 22 38 81.5 70.4 3150 67
Vikunguni 20 41 0 0 0 0 2 2 13 27 15 29 75.0 70.7 3238 79
JUMLA 835 1477 8 25 33 69 76 156 447 757 564 1007 67.5 68.2
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 194
Jadweli Nam. 33(a)i Linaendelea
1 Kengeja Tech. 5 33 0 0 1 9 2 14 2 10 5 33 100.0 100.0 167 12*
2 Kiwani 33 56 0 0 0 0 0 1 21 36 21 37 63.6 66.1 3271 88
3 Mkanyageni 22 50 0 0 0 0 1 4 13 23 14 27 63.6 54.0 3413 139
4 M/Ngwachani 52 88 0 0 0 0 1 2 30 51 31 53 59.6 60.2 3423 123
5 Kangani 53 88 0 0 1 1 1 4 43 67 45 72 84.9 81.8 3002 53
6 Uweleni 83 133 0 0 0 0 3 5 56 77 59 82 71.1 61.7 3319 97
7 Kengeja Sec. 51 80 0 0 0 0 0 1 21 37 21 38 41.2 47.5 3465 132
8 Kisiwa Panza 23 34 0 0 0 0 0 0 6 7 6 7 26.1 20.6 1721 53*
9 Mtambile 40 71 0 0 0 0 4 5 32 57 36 62 90.0 87.3 2614 39
10 Wambaa 28 56 0 0 0 0 0 1 13 21 13 22 46.4 39.3 3469 133
WILAYA YA MKOANI
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 195
Jadweli Nam. 33(a)i Linaendelea
11 Mizingani 20 40 0 0 0 0 1 1 11 26 12 27 60.0 67.5 3328 100
12 Mwambe 23 72 0 0 0 0 2 7 18 51 20 58 87.0 80.6 2913 47
13 Makombeni 16 35 0 0 0 0 3 4 8 18 11 22 68.8 62.9 1251 40*
14 Mauwani 20 42 0 0 2 2 5 10 13 30 20 42 100.0 100.0 1220 27
15 Mtangani 10 19 0 0 0 0 0 0 7 13 7 13 70.0 68.4 1296 48*
16 Chokocho 13 41 0 0 0 2 1 6 4 12 5 20 38.5 48.8 3190 73
17 Ukutini 31 51 0 0 0 0 0 0 4 14 4 14 12.9 27.5 3487 138
18 Moh'd Juma Pindua 26 37 0 0 12 17 14 17 0 2 26 36 100.0 97.3 77 5*
19 Michenzani 46 76 0 0 0 1 2 8 21 37 23 46 50.0 60.5 3241 80
20 Chambani 29 66 0 0 0 0 1 3 13 29 6 32 20.7 48.5 3454 128
JUMLA 624 1168 0 0 16 32 41 93 336 618 379 711 60.7 60.9
JUMLA KUU 8804 15401 38 122 235 545 815 1616 4867 8039 5898 10227 67.0 66.4
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 196
JADWELI NAM. 33a (ii)
WAS JUMLA WAS JUMLA WAS JUMLA WAS JUMLA WAS JUMLA WAS JUMLA WAS JUMLA TZ ZNZ
WILAYA YA MAGHARIBI 'A'
1 Sunni Madressa 40 76 0 2 7 14 14 23 19 37 40 76 100.0 100.0 611 20
2 Sun City 34 99 0 0 0 0 4 5 22 57 26 62 76.5 62.6 3216 77
3 Glorious 40 72 1 1 14 33 15 26 10 12 40 72 100.0 100.0 339 8
4 Bilali 33 49 0 1 10 13 13 21 9 13 32 48 97.0 98.0 452 14
7 High Perfomance 20 41 0 0 1 2 3 8 15 24 19 34 95.0 82.9 1486 30
8 Stone Town 5 11 2 2 1 4 2 3 0 1 5 10 100.0 90.9
9 Ndame 6 13 0 0 0 0 0 0 5 10 5 10 83.3 76.9 1266 42*
10 Al Riyami 17 30 0 0 3 7 11 18 2 4 16 29 94.1 96.7 110 7*
Jumla 195 391 3 6 36 73 62 104 82 144 183 327 93.8 83.6
WILAYA YA MAGHARIBI 'A'
1 Beit el ras 27 41 3 3 6 9 8 12 10 17 27 41 100.0 100.0 527 18
2 Royal 8 15 0 0 0 1 2 3 1 3 3 7 37.5 46.7 84 6*
3 JKU 68 131 2 7 17 42 28 46 20 35 67 130 98.5 99.2 403 10
Jumla 103 187 5 10 23 52 38 61 31 55 97 178 94.2 95.2
MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE, SKULI ZA BINAFSI - 2018
SKULI
WATAHINIWA DIV. I DIV. II DIV. III DIV. IV JUMLA KIMA CHA UFAULU NATIJA
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 197
Jadweli Nam. 33(a)ii Linaendelea
1 Laureate 29 48 7 14 9 17 11 15 2 2 29 48 100.0 100.0 161 2
2 Francis Maria 12 36 0 3 6 16 5 16 1 1 11 36 91.7 100.0 53 2*
3 SOS 32 52 6 8 10 20 13 21 3 3 32 52 100.0 100.0 226 4
4 Al Ihsaan 60 60 3 3 14 14 24 24 18 18 59 59 98.3 98.3 445 13
5 High View 32 57 2 4 11 19 14 26 3 6 30 55 93.8 96.5 299 5
6 Al Falah 36 69 0 0 3 5 8 20 24 41 35 66 97.2 95.7 1063 25
7 Alharamyn 28 55 0 0 8 10 14 25 6 19 28 54 100.0 98.2 567 19
8 Mnemonic 65 130 0 0 1 3 22 37 40 85 63 125 96.9 96.2 1084 26
9 Memon Academy 17 30 0 0 3 4 10 18 4 8 17 30 100.0 100.0 201 16*
10 Al Huda 24 41 0 0 3 7 8 13 13 21 24 41 100.0 100.0 641 21
11 SSP 24 54 0 0 0 0 5 11 17 36 22 47 91.7 87.0 1709 31
12 Filter Fideral 22 48 0 0 0 1 4 7 16 34 20 42 90.9 87.5 1820 32
WALAYA YA MAGHARIBI 'B'
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 198
Jadweli Nam. 33(a)ii Linaendelea
13 Mbarali Preparatory 27 50 0 0 1 1 6 15 17 27 24 43 88.9 86.0 1438 29
14 Zanzibar Feza 12 34 1 2 7 8 3 9 1 3 12 22 100.0 64.7 46 1*
15 Trifonia 19 35 0 1 6 10 7 16 3 5 16 32 84.2 91.4 63 3*
16 Hifadhi 17 21 0 0 5 6 9 10 3 5 17 21 100.0 100.0 140 9*
17 Al mubarak 19 29 0 0 2 3 3 6 14 20 19 29 100.0 100.0 433 21*
18 Zanzibar Progressive 14 23 0 0 3 6 7 11 4 6 14 23 100.0 100.0 161 11*
19 Mombasa Central 23 39 0 0 1 2 7 11 12 19 20 32 87.0 82.1 329 21
20 St . Monica 4 7 0 0 1 2 1 2 2 3 4 7 100.0 100.0 179 14*
21 Al- Quwwiyyi 10 18 0 0 1 1 5 6 4 11 10 18 100.0 100.0 408 20*
22 Juba 4 7 0 0 0 1 0 0 3 5 3 6 75.0 85.7 908 27*
23 Nyuki 33 58 0 1 0 0 4 8 21 36 25 45 75.8 77.6 19*
24 Willey 11 17 0 0 1 1 1 6 9 10 11 17 100.0 100.0 344 18*
25 Sufa 22 28 2 2 6 6 8 12 6 8 22 28 100.0 100.0 143 10*
Jumla 596 1046 21 38 102 163 199 345 246 432 567 978 95.1 93.5
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 199
Jadweli Nam. 33(a)ii Linaendelea
WILAYA YA KASKAZINI 'B'
1 Unique Learning 9 17 0 0 0 0 1 3 7 11 8 14 88.9 82.4 116 8
JUMLA 9 17 0 0 0 0 1 3 7 11 8 14 88.9 82.4
1 Mahad Istiqama 24 46 5 6 9 13 9 20 1 7 24 46 100.0 100.0 306 6
JUMLA 24 46 5 6 9 13 9 20 1 7 24 46 100.0 100.0
1 Bwejuu Charity 7 18 0 0 0 1 2 3 5 12 7 16 100.0 88.9 727 24*
JUMLA 7 18 0 0 0 1 2 3 5 12 7 16 100.0 88.9
1 Wete Islamic 21 35 0 0 2 4 4 9 7 8 13 21 61.9 60.0 249 17*
JUMLA 21 35 0 0 2 4 4 9 7 8 13 21 61.9 60.0
1 Connecting Continents 28 54 0 1 5 13 11 23 12 16 28 53 100.0 98.1 476 15
2 Alkhamis Camp 8 20 0 0 5 10 3 9 0 1 8 20 100.0 100.0 67 4*
3 Amini 8 18 0 0 1 6 4 6 3 6 8 18 100.0 100.0 178 13*
4 Istiqama Mkanjuni 10 14 0 0 3 3 2 2 5 9 10 14 100.0 100.0 375 19*
5 Farahedy 11 21 1 2 1 2 1 4 7 11 10 19 90.9 90.5 853 25
JUMLA 65 127 1 3 15 34 21 44 27 43 64 124 98.5 97.6
JUMLA KUU 1020 1867 35 63 187 340 336 589 406 712 963 1704 94.4 91.3
WILAYA YA KATI
WILAYA YA KUSINI
WILAYA YA WETE
WILAYA YA CHAKE
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 200
JADWELI NAM. 33(b)i
WAS JUMLA WAS JUMLA WAS JUMLA WAS JUMLA WAS JUMLA WAS JUMLA WAS JUMLA
1 Lumumba 50 112 50 112 100.0 100.0 50 112 0 0 50 112 100.0 100.0
2 Mikunguni 23 48 22 47 95.7 97.9 0 0 15 36 15 36 68.2 76.6
3 Kiponda 27 35 27 35 100.0 100.0 19 26 0 0 19 26 70.4 74.3
4 Tumekuja 56 122 56 122 100.0 100.0 55 118 0 0 55 118 98.2 96.7
5 Jang'ombe 104 186 65 109 62.5 58.6 7 15 0 0 7 15 10.8 13.8
6 Haile Selassie 156 253 88 145 56.4 57.3 4 11 0 0 4 11 4.5 7.6
7 Vikokotoni 82 195 81 188 98.8 96.4 30 93 0 0 30 93 37.0 49.5
8 Faraja 175 278 112 177 64.0 63.7 5 11 0 0 5 11 4.5 6.2
MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE, SKULI ZA SERIKALI - 2018/19
IDADI YA WANAOENDELEA NA MASOMO
FTCMTIHANI KUFAULU (%) CHA 5 KIDATO CHA 5 + FTC KUENDELEA
KIDATO JUMLA YA ASILIMIA YA
SKULI
WALIOFANYA
WALIOFAULU
KIMA CHA
WILAYA YA MJINI
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 201
9 Forodhani 75 103 49 78 65.3 75.7 2 5 0 0 2 5 4.1 6.4
10 Benbella 145 145 144 144 99.3 99.3 103 103 0 0 103 103 71.5 71.5
11 Kidongochekundu 169 284 124 198 73.4 69.7 29 124 0 0 29 124 23.4 62.6
12 Kwamtipura 165 305 92 168 55.8 55.1 6 16 0 0 6 16 6.5 9.5
13 Hurumzi 65 136 54 103 83.1 75.7 10 21 0 0 10 21 18.5 20.4
14 Hamamni 104 441 43 69 41.3 15.6 3 4 0 0 3 4 7.0 5.8
15 Mpendae 136 249 97 169 71.3 67.9 16 32 0 0 16 32 16.5 18.9
16 Chumbuni 109 198 61 102 56.0 51.5 3 10 0 0 3 10 4.9 9.8
17 Nyerere 173 262 27 96 15.6 36.6 12 24 0 0 12 26 44.4 27.1
18 Mwembeladu 176 299 122 219 69.3 73.2 9 23 0 0 9 23 7.4 10.5
JUMLA 1990 3651 1314 2281 66.0 62.5 363 748 15 36 363 724 27.6 31.7
Jadweli Nam. 33(b)i Linaendelea
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 202
1 Mtoni Kigomeni 71 125 51 94 71.8 75.2 5 9 0 0 5 9 9.8 9.6
2 Mfenesini 95 153 75 108 78.9 70.6 2 8 0 0 2 8 2.7 7.4
3 Bububu 287 477 154 259 53.7 54.3 4 18 0 0 4 18 2.6 6.9
4 Langoni 46 79 39 58 84.8 73.4 2 4 0 0 2 4 5.1 6.9
5 Regeza Mwendo 100 167 59 93 59.0 55.7 9 13 0 0 9 13 15.3 14.0
6 Mtopepo 210 360 140 223 66.7 61.9 4 15 0 0 4 15 2.9 6.7
7 Chuini 109 177 78 115 71.6 65.0 7 11 0 0 7 11 9.0 9.6
8 Mwenge 36 63 17 35 47.2 55.6 0 1 0 0 0 1 0.0 2.9
9 Mikindani Dole 31 52 31 52 100.0 100.0 22 40 0 0 22 40 71.0 76.9
10 Mtoni Kidatu 24 38 16 28 66.7 73.7 0 0 0 0 0 0.0 0.0
11 Kianga 53 74 36 50 67.9 67.6 3 5 0 0 3 5 8.3 10.0
JUMLA 1062 1765 696 1115 65.5 63.2 58 124 0 0 58 124 8.3 11.1
Jadweli Nam. 33(b)i Linaendelea
WILAYA YA MAGHARIBI 'A'
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 203
1 Mwanakwerekwe 'A' 111 182 94 158 84.7 86.8 14 36 0 0 14 36 14.9 22.8
2 Kiembe Samaki "A" Islamic 104 194 104 184 100.0 94.8 79 144 0 0 79 144 76.0 78.3
3 Chukwani 51 67 37 49 72.5 73.1 5 11 0 0 5 11 13.5 22.4
4 Kinuni 131 184 81 109 61.8 59.2 5 12 0 0 5 12 6.2 11.0
5 Kisauni 48 72 34 49 70.8 68.1 3 5 0 0 3 5 8.8 10.2
6 Fuoni 128 208 80 135 62.5 64.9 2 12 0 0 2 12 2.5 8.9
7 Mwanakwerekwe 'C' 293 474 216 326 73.7 68.8 26 36 0 0 26 36 12.0 11.0
8 Zanzibar commercial 42 101 42 101 100.0 100.0 33 77 0 0 33 77 78.6 76.2
9 Maungani 25 39 20 30 80.0 76.9 2 2 0 0 2 2 10.0 6.7
10 Kwarara 30 56 27 46 90.0 82.1 2 6 0 0 2 6 7.4 13.0
11 Kiembesamaki 141 247 112 189 79.4 76.5 13 23 0 0 13 23 11.6 12.2
12 Kombeni 41 63 22 37 53.7 58.7 3 3 0 0 3 3 13.6 8.1
13 Bwefum 15 21 8 13 53.3 61.9 0 1 0 0 0 1 0.0 7.7
Jumla 1160 1908 877 1426 30.0 74.7 187 368 0 0 187 368 21.3 25.8
Jadweli Nam. 33(b)i Linaendelea
WALAYA YA MAGHARIBI 'B'
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 204
WILAYA YA KASKAZINI 'A'
1 Tumbatu 58 113 36 78 62.1 69.0 1 17 0 0 1 17 2.8 21.8
2 Mkwajuni 149 215 60 96 40.3 44.7 4 11 0 0 4 11 6.7 11.5
3 Fukuchani 24 38 17 29 70.8 76.3 0 0 0 0 0 0 0.0 0.0
4 Jongowe 44 87 40 80 90.9 92.0 4 11 0 0 4 11 10.0 13.8
5 Potoa 64 87 50 70 78.1 80.5 0 1 0 0 0 1 0.0 1.4
6 Kidoti 59 93 55 88 93.2 94.6 7 23 0 0 7 23 12.7 26.1
7 Mapinduzi 83 127 62 98 74.7 77.2 6 11 0 0 6 11 9.7 11.2
8 Pale 36 60 29 45 80.6 75.0 5 8 0 0 5 8 17.2 17.8
9 Kinyasini 70 118 23 49 32.9 41.5 2 6 0 0 2 6 8.7 12.2
10 Gamba 37 73 29 49 78.4 67.1 2 4 0 0 2 4 6.9 8.2
11 Pwani Mchangani 30 60 5 14 16.7 23.3 0 1 0 0 0 0 0.0 7.1
12 Mlimani Matemwe 21 45 14 27 66.7 60.0 0 2 0 0 0 2 0.0 7.4
13 Kijini 32 55 21 34 65.6 61.8 0 0 0 0 0 0 0.0 0.0
14 Nungwi 47 97 43 86 91.5 88.7 5 17 0 0 5 17 11.6 19.8
15 Matemwe 14 22 4 8 28.6 36.4 0 0 0 0 0 0 0.0 0.0
JUMLA 768 1290 488 851 63.5 66.0 32 101 0 0 36 111 7.4 13.0
Jadweli Nam. 33(b)i Linaendelea
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 205
1 Donge 89 124 87 122 97.8 98.4 40 64 0 0 40 64 46.0 52.5
2 Mahonda 69 101 40 64 58.0 63.4 5 6 0 0 5 6 12.5 9.4
3 Fujoni 39 60 38 59 97.4 98.3 23 32 0 0 23 32 60.5 54.2
4 Bumbwini 47 82 47 81 100.0 98.8 26 46 0 0 26 46 55.3 56.8
5 Makoba 54 70 35 47 64.8 67.1 0 0 0 0 0 0 0.0 0.0
6 Mwanda 35 60 25 38 71.4 63.3 0 1 0 0 0 1 0.0 2.6
7 Upenja 23 37 14 20 60.9 54.1 0 0 0 0 0 0 0.0 0.0
8 Kitope 56 102 39 85 69.6 83.3 2 38 0 0 2 38 5.1 44.7
JUMLA 412 636 325 516 78.9 81.1 94 187 0 0 96 187 29.5 36.2
Jadweli Nam. 33(b)i Linaendelea
WILAYA KASKAZINI 'B'
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 206
1 Mpapa 33 50 27 44 81.8 88.0 3 3 0 0 3 3 11.1 6.8
2 Uroa 30 58 22 43 73.3 74.1 0 4 0 0 0 4 0.0 9.3
3 Ndijani 43 64 24 42 55.8 65.6 2 3 0 0 2 3 8.3 7.1
4 Mwera 70 121 48 81 68.6 66.9 6 9 0 0 6 9 12.5 11.1
5 Dunga 43 71 32 52 74.4 73.2 2 7 0 0 2 7 6.3 13.5
6 Unguja Ukuu 31 45 20 31 64.5 68.9 0 2 0 0 0 2 0.0 6.5
7 Ukongoroni 5 15 5 15 100.0 100.0 0 3 0 0 0 3 0.0 20.0
8 Kiboje 49 75 23 38 46.9 50.7 4 8 0 0 4 8 17.4 21.1
9 Bambi 27 52 21 34 77.8 65.4 1 3 0 0 1 3 4.8 8.8
WILAYA YA KATI
Jadweli Nam. 33(b)i Linaendelea
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 207
10 Machui 32 55 19 37 59.4 67.3 1 6 0 0 1 6 5.3 16.2
11 Charawe 7 16 6 12 0.0 75.0 0 0 0 0 0 0 0.0 0.0
12 Jendele 28 45 17 34 60.7 75.6 1 3 0 0 1 3 5.9 8.8
13 Uzi 30 40 19 25 63.3 62.5 1 1 0 0 1 1 5.3 4.0
14 Kibele 43 68 25 43 58.1 63.2 4 4 0 0 4 4 16.0 9.3
15 Jumbi 46 73 36 56 78.3 76.7 4 7 0 0 4 7 11.1 12.5
16 Umbuji 9 15 7 13 77.8 86.7 0 0 0 0 0 0 0.0 0.0
17 Chwaka 19 47 15 34 78.9 72.3 0 1 0 0 0 1 0.0 2.9
18 Umoja Uzini 67 109 43 63 64.2 57.8 5 8 0 0 5 8 11.6 12.7
JUMLA 612 1019 409 697 66.8 68.4 29 72 0 0 34 72 8.3 10.3
Jadweli Nam. 33(b)i Linaendelea
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 208
1 Paje 19 34 15 28 78.9 82.4 3 7 0 0 3 7 20.0 25.0
2 Makunduchi 56 104 24 56 42.9 53.8 3 8 0 0 3 8 12.5 14.3
3 Mtule 19 36 11 24 57.9 66.7 11 12 0 0 11 12 100.0 50.0
4 Jambiani 29 57 9 23 31.0 40.4 1 6 0 0 1 6 11.1 26.1
5 Kusini 35 67 16 35 45.7 52.2 2 4 0 0 0 6 12.5 11.4
6 K/Dimbani 17 25 7 9 41.2 36.0 0 1 0 0 1 1 0.0 11.1
7 Bwejuu 35 61 13 28 37.1 45.9 0 3 0 0 0 3 0.0 10.7
8 Kizimkazi 19 28 11 16 57.9 57.1 3 3 0 0 3 3 27.3 18.8
9 Muyuni 17 25 16 24 94.1 96.0 2 3 0 0 5 3 12.5 12.5
JUMLA 246 437 122 243 49.6 55.6 25 47 0 0 27 49 22.1 20.2
WILAYA YA KUSINI
Jadweli Nam. 33(b)i Linaendelea
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 209
1 Pemba Islamic 14 30 14 30 100.0 100.0 11 24 0 0 11 24 78.6 80.0
2 Tumbe 33 66 29 55 87.9 83.3 3 9 0 0 3 9 10.3 16.4
3 Wingwi 52 109 34 77 65.4 70.6 4 11 0 0 4 11 11.8 14.3
4 Shumba 26 51 19 37 73.1 72.5 1 1 0 0 1 1 5.3 2.7
5 Konde 74 119 45 67 60.8 56.3 0 3 0 0 0 3 0.0 4.5
6 Micheweni 38 71 29 60 76.3 84.5 3 12 0 0 3 12 10.3 20.0
7 Msuka 23 35 12 24 52.2 68.6 1 1 0 0 1 1 8.3 4.2
8 Chwaka Tumbe 26 53 18 37 69.2 69.8 0 3 0 0 0 3 0.0 8.1
9 Makangale 27 52 19 28 70.4 53.8 0 2 0 0 0 2 0.0 7.1
10 Kiuyu 15 37 10 25 66.7 67.6 0 5 0 0 0 5 0.0 20.0
11 Kinowe 40 64 22 31 55.0 48.4 0 1 0 0 0 1 0.0 3.2
JUMLA 368 687 251 471 68.2 68.6 23 72 0 0 23 72 9.2 15.3
WILAYA YA MICHEWENI
Jadweli Nam. 33(b)i Linaendelea
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 210
1 Utaani 107 107 88 88 82.2 82.2 26 26 0 0 26 26 29.5 29.5
2 M/Mdogo 80 157 47 92 58.8 58.6 4 10 0 0 4 10 8.5 10.9
3 Chasasa 40 153 39 148 97.5 96.7 21 72 0 0 21 72 53.8 48.6
4 Minungwini 43 92 30 61 69.8 66.3 2 8 0 0 2 8 6.7 13.1
5 Pandani 34 60 25 43 73.5 71.7 2 9 0 0 2 9 8.0 20.9
6 Wete Secondary 29 60 27 58 93.1 96.7 11 39 0 0 11 39 40.7 67.2
7 Piki 27 37 16 23 59.3 62.2 2 4 0 0 2 4 12.5 17.4
8 Kangagani 34 50 14 19 41.2 38.0 1 2 0 0 1 2 7.1 10.5
9 Kinyasini 18 28 8 17 44.4 60.7 0 2 0 0 0 2 0.0 11.8
10 Gando 43 67 26 42 60.5 62.7 0 3 0 0 0 3 0.0 7.1
11 Kojani 16 31 13 26 81.3 83.9 1 4 0 0 1 4 7.7 15.4
WILAYA YA WETE
Jadweli Nam. 33(b)i Linaendelea
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 211
12 Makongeni 9 15 3 5 33.3 33.3 0 1 0 0 0 1 0.0 20.0
13 Uondwe 23 51 13 30 56.5 58.8 0 2 0 0 0 2 0.0 6.7
14 Shengejuu 29 67 14 40 48.3 59.7 1 7 0 0 1 7 7.1 17.5
15 Kizimbani 50 111 43 86 86.0 77.5 4 11 0 0 4 11 9.3 12.8
16 Limbani 37 73 20 44 54.1 60.3 1 6 0 0 1 6 5.0 13.6
17 Mitiulaya 48 93 45 71 93.8 76.3 11 17 0 0 11 17 24.4 23.9
18 Fundo 4 6 3 5 75.0 83.3 0 0 0 0 0 0 0.0 0.0
19 M/Takao 19 38 13 27 68.4 71.1 0 1 0 0 0 1 0.0 3.7
20 Chwale 22 38 16 30 72.7 78.9 2 7 0 0 2 7 12.5 23.3
21 Ukunjwi 6 15 6 11 100.0 73.3 0 1 0 0 0 1 0.0 9.1
22 Kijumbani 9 14 5 6 55.6 42.9 0 0 0 0 0 0 0.0 0.0
JUMLA 727 1363 514 972 70.7 71.3 67 228 0 0 89 232 17.3 23.9
Jadweli Nam. 33(b)i Linaendelea
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 212
1 F/Castro 29 67 29 67 100.0 100.0 29 67 0 0 29 67 100.0 100.0
2 Shamiani 94 146 60 94 63.8 64.4 10 19 0 0 10 19 16.7 20.2
3 Ch/Mjawiri 44 58 29 42 65.9 72.4 4 6 0 0 4 6 13.8 14.3
4 Vitongoji 59 93 42 70 71.2 75.3 5 9 0 0 5 9 11.9 12.9
5 Dr Omar Ali Juma 78 140 57 104 73.1 74.3 1 5 0 0 6 5 10.5 4.8
6 Pujini 37 65 29 53 78.4 81.5 2 6 0 0 2 6 6.9 11.3
7 Wesha 25 44 19 27 76.0 61.4 4 5 0 0 4 5 21.1 18.5
8 Kilindi 52 77 20 36 38.5 46.8 2 7 0 0 2 7 10.0 19.4
WILAYA YA CHAKE
Jadweli Nam. 33(b)i Linaendelea
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 213
9 Furaha 112 208 64 123 57.1 59.1 5 18 0 0 5 18 7.8 14.6
10 Ziwani 36 76 19 51 52.8 67.1 2 14 0 0 2 14 10.5 27.5
11 Ole 43 69 29 45 67.4 65.2 2 3 0 0 2 3 6.9 6.7
12 Kwale 15 27 13 25 86.7 92.6 0 6 0 0 0 6 0.0 24.0
13 Pondeani 32 76 25 51 78.1 67.1 2 9 0 0 2 9 8.0 17.6
14 Ng'mbwa 50 101 20 41 40.0 40.6 0 1 0 0 0 1 0.0 2.4
15 Uwandani 16 37 9 17 56.3 45.9 2 4 0 0 2 4 22.2 23.5
16 Madungu 66 98 63 94 95.5 95.9 43 65 0 0 43 65 68.3 69.1
17 Mbuzini 27 54 22 38 81.5 70.4 2 4 0 0 2 4 9.1 10.5
18 Vikunguni 20 41 15 29 75.0 70.7 2 2 0 0 2 2 13.3 6.9
JUMLA 835 1477 564 1007 67.5 68.2 111 229 0 0 116 250 20.6 24.8
Jadweli Nam. 33(b)i Linaendelea
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 214
JADWELI NAM. 34
WAS J'LA WAS J'LA WAS J'LA WAS J'LA WAS J'LA WAS J'LA
BEN BELLA 102 102 0 0 13 13 74 74 13 13 100 100
KIPONDA 16 48 1 1 7 16 8 30 0 1 16 48
SUZA 28 54 8 14 14 29 6 11 0 0 28 54
PEMBA ISLAMIC 14 43 0 1 6 19 7 19 1 4 14 43
UTAANI 14 35 0 0 6 16 12 18 0 0 18 34
ZNZ. FEZA 28 50 5 16 10 15 10 13 0 3 25 47
MADUNGU 29 65 2 5 3 13 22 44 2 2 29 64
SOS 36 52 14 24 17 22 4 5 0 0 35 51
TUMEKUJA 28 110 0 1 1 13 23 84 4 11 28 109
FIDEL CASTRO 56 117 2 11 21 34 27 52 2 9 52 106
ZNZ. COMMERCIAL* 13 39 7 15 1 10 5 13 0 0 13 38
JANG'OMBE 26 41 0 0 0 1 21 34 5 6 26 41
AL-IHSAN 34 34 0 0 21 21 13 13 0 0 34 34
WALIOFAULU
WATAHINIWASKULI
MATOKEO YA MTIHANI WA TAIFA WA KIDATO CHA 6
(A - LEVEL), MWAKA 2017/2018
JUMLADIV. IVDIV. IIIDIV. IIDIV. I
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 215
Jadweli nam 34
FILTER FEDERAL 7 19 0 1 1 5 4 9 1 3 6 18
SHAMIANI 34 59 2 4 10 19 21 34 1 2 34 59
FARAJA 84 174 0 1 19 56 61 112 4 4 84 173
NYUKI 2 18 0 1 1 11 1 6 0 0 2 18
HAMAMNI 110 152 0 2 37 49 70 97 3 4 110 152
CHASASA 40 93 3 6 9 18 22 58 4 6 38 88
M/MDOGO 2 24 0 2 0 8 2 12 0 1 2 23
MWANAKWEREKWE 'C' 99 135 0 0 17 27 82 107 0 1 99 135
UWELENI 15 32 0 0 0 3 11 24 4 5 15 32
MPENDAE 41 103 0 1 9 23 28 70 3 7 40 101
KIEMBE SAMAKI 40 99 0 2 8 17 26 68 4 10 38 97
LUMUMBA 40 111 4 17 20 49 16 45 0 0 40 111
JUMLA 938 1809 48 125 251 507 576 1052 51 92 926 1776
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 216
JADWELI NO. 35
W'KE J'LA W'KE J'LA W'KE J'LA W'KE J'LA W'KE J'LA W'KE J'LA W'KE J'LA
MJINI 22 21 22 359 437 192 226 14 130 31 45 32 38 269 439
MAGHARIBI 'A' 25 19 25 311 326 182 187 62 66 39 40 10 10 293 303
MAGHARIBI 'B' 18 14 18 290 315 86 102 119 123 50 55 35 35 290 315
KASKAZINI ' A' 122 77 122 2057 2258 795 877 581 638 342 382 87 98 1805 1995
KASKAZINI ' B' 61 36 61 764 910 335 418 228 258 153 181 60 79 776 936
KATI 25 18 25 249 319 76 106 74 94 58 69 42 50 250 319
KUSINI 5 2 5 69 74 9 11 10 12 13 14 14 14 46 51
MICHEWENI 65 45 65 1348 1532 567 637 291 330 185 210 54 65 1097 1242
WETE 64 53 64 1255 1353 542 580 326 351 206 218 107 117 1181 1266
CHAKE-CHAKE 37 26 37 641 739 200 225 178 199 108 122 60 65 546 611
MKOANI 61 43 61 1124 1368 428 525 313 361 220 254 125 157 1086 1297
JUMLA 505 354 505 8467 9631 3412 3894 2196 2562 1405 1590 626 728 7639 8774
UANDIKISHAJI WA WANAKISOMO KIWILAYA, MACHI -2019
IDADI YA WALIMU
IDADI YA WANAKISOMO
WA KUJIANDIKISHA
WILAYA MADARASA
WANAKISOMO WALIOMO MADARASANI
JUMLAHATUA I HATUA II HATUA III HATUA IV
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 217
JADWELI NAM. 36
JINA LA
KITUO W'ME W'KE J'LA MAD W'KE J'LA MAD W'KE J'LA MAD W'KE J'LA MAD W'KE J'LA MAD W'KE J'LA MAD W'KE J'LA
FARAJA - 6 6 - - - - - - 1 11 47 - - - - - - 1 11 47
MIKUNGUNI - 15 15 - - - 1 14 33 1 23 42 - - - - - - 2 37 75
MWEMBELADU 3 10 13 - - - - - - 1 25 43 - - - - - - 1 25 43
HAILESELASSIE 8 2 10 - - - - - - 1 12 20 - - - - - - 1 12 20
LUMUMBA - 16 16 - - - 1 16 44 2 33 64 - - - - - - 3 49 108
HAMAMNI 8 5 13 - - - - - - 1 18 40 - - - - - - 1 18 40
KIJANGWANI - 6 6 - - - - - - 1 8 20 - - - - - - 1 8 20
KWALAMSHA - 4 4 - - - - - - 2 42 80 - - - - - - 2 42 80
HAMAMNI - LUMUMBA 0 4 4 - - - - - - 1 10 18 - - - - - - 1 10 18
KAJIFICHENI 1 1 2 - - - - - - 1 3 6 - - - - - - 1 3 6
LUMUMBA 'A' LEVEL - 4 4 - - - - - - - - - - - - 1 8 14 1 8 14
MBADALA RAHALEO 3 2 5 - - - - - - - - - 1 6 23 - - - 1 6 23
JUMLA 23 75 98 0 0 0 2 30 77 12 185 380 1 6 23 1 8 14 16 229 494
YELP
UANDIKISHAJI KATIKA VITUO VYA KUJIENDELEZA KWA MWEZI, MACHI - 2019
WALIMU UFUNDI Q - TEST FORM IV JUMLAFORM VI
WILAYA YA MJINI
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 218
Jadweli 36 inaendelea
WILAYA YA MAGH. 'A'
J.K.U - 5 5 - - - - - - 1 4 25 - - - - - - 1 4 25
REGEZAMWENDO 3 6 - - - - - - 1 11 24 - - - - - - 1 11 24
BUBUBU 4 8 12 - - - 1 10 25 1 8 28 - - - - - - 2 18 53
JUMLA 7 19 17 - - - 1 10 25 3 23 77 - - - - - - 4 33 102
BIASHARA 0 10 10 - - - - - - 1 31 49 - - - - - - 1 31 49
NYUKI 1 12 13 - - - - - - 1 20 48 - - - - - - 1 20 48
FUONI 2 3 5 - - - 1 1 2 1 5 21 - - - - - - 2 6 23
KIEMBESAMAKI 1 10 11 - - - - - - 1 12 28 - - - - - - 1 12 28
JUMLA 4 35 39 0 0 0 1 1 2 4 68 146 - - - - - - 5 69 148
KINYASINI 1 4 5 - - - - - - 1 6 13 - - - - - - 1 6 13
JONGOWE 0 6 6 - - - - - - 1 4 11 - - - - - -
JUMLA 1 4 5 0 0 0 0 0 0 1 6 13 0 0 0 0 0 0 1 6 13
FUJONI 5 2 7 - - - 1 7 7 1 7 15 - - - - - - 2 14 22
MAKOBA 0 2 2 - - - 1 - 2 1 1 4 - - - - - - 2 1 6
JUMLA 5 4 9 0 0 0 2 7 9 2 8 19 0 0 0 0 0 0 4 15 28
WILAYA YA MAGH. 'B'
WILAYA YA KASK.'A'
WILAYA YA KASK.'B'
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 219
Jadweli 36 inaendelea
UBAGO 0 8 8 - - - 1 8 15 1 20 40 - - - - - - 2 28 55
CHWAKA 1 1 2 - - - 1 5 12 - - - - - - 1 5 12
KIBELE 3 3 - - - 1 3 5 - - - - - - - - - 1 3 5
UZI 0 3 3 - - - - - - - - 7 - - - - - - - - 7
JUMLA 1 15 16 0 0 0 2 11 20 2 25 59 0 0 0 0 0 0 4 36 79
MAKUNDUCHI 2 8 10 1 6 16 1 5 21 2 11 37
JUMLA 2 8 10 0 0 0 1 6 16 1 5 21 0 0 0 0 0 0 2 11 37
WINGWI 2 7 9 - - - - - - 1 2 4 - - - - - - 1 2 4
MICHEWENI 1 11 12 - - - - - - 1 2 8 - - - - - - 1 2 8
C.C.K 0 12 12 - - - - - - 1 25 37 - - - - - - 1 25 37
KIUYU 2 5 7 - - - - - - 1 2 2 - - - - - - 1 2 2
MTEMANI 1 4 5 - - - - - - - - - 1 13 41 - - - 1 13 41
JUMLA 6 39 45 0 0 0 0 0 0 4 31 51 1 13 41 0 0 0 5 44 92
WILAYA YA MICHEWENI
WILAYA YA KATI
WILAYA YA KUSINI
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 220
UTAANI 1 9 10 - - - 1 20 41 - - - - - - - - - 1 20 41
MCHANGAMDOGO 1 4 5 - - - 2 32 61 1 3 15 - - - - - - 3 35 76
CHASASA 3 6 9 - - - 1 34 54 1 3 12 - - - - - - 2 37 66
KIZIMBANI 5 7 12 - - - 1 0 2 1 0 4 - - - - - - 2 - 6
GANDO 0 4 4 - - - - - - 1 1 6 - - - - - - 1 1 6
JUMLA 10 30 40 0 0 0 5 86 158 4 7 37 0 0 0 0 0 0 9 93 195
SHAMIANI 5 3 8 - - - - - - 1 4 8 - - - - - - 1 4 8
FIDEL-CASTRO 2 11 13 - - - - - - 1 25 37 - - - - - - 1 25 37
KILINDI 2 5 7 - - - - - - 1 2 2 - - - - - - 1 2 2
JUMLA 9 19 28 0 0 0 0 0 0 3 31 47 0 0 0 0 0 0 3 31 47
UWELENI 0 6 6 - - - - - - 1 8 19 - - - - - - 1 8 19
WAMBAA 3 3 6 - - - - - - 1 1 3 - - - - - - 1 1 3
CHOKOCHO 1 4 5 - - - - - - 1 - 2 - - - - - - 1 - 2
JUMLA 4 13 17 0 0 0 0 0 0 3 9 24 0 0 0 0 0 0 3 9 24
JUMLA LA KUU 72 261 324 - - - 14 151 307 39 398 874 2 19 64 1 8 14 56 576 1,259
WILAYA YA WETE
WILAYA YA CHAKE
WILAYA YA MKOANI
Jadweli 36 inaendelea
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 221
JADWELI NAM. 37(a)
IDADI % IDADI %
WILAYA YA MJINI
1 LUMUMBA 192 2 1.04 104 54.17
2 TUMEKUJA 20 0 0.00 12 60.00
3 BENBELLA 16 0 0.00 4 25.00
4 MIKUNGUNU 66 0 0.00 16 24.24
5 HAMAMNI 45 0 0.00 18 40.00
6 HAILESELASSIE 40 1 2.50 18 45.00
7 K/CHEKUNDU 21 0 0.00 9 42.86
8 KIPONDA 19 0 0.00 15 78.95
9 JANG'OMGE 29 0 0.00 12 41.38
10 FARAJA 46 3 6.52 17 36.96
11 BILALI- ISLAMIC 107 1 0.93 55 51.40
12 CHUMBUNI 13 0 0.00 8 61.54
13 MWEMBELADU 34 1 2.94 5 14.71
14 MEMON 3 0 0.00 3 100.00
15 SUNCITY 11 0 0.00 8 72.73
16 NYERERE 16 0 0.00 11 68.75
JUMLA 678 8 1.18 315 46.46
MATOKEO YA MTIHANI KWA WATAHINIWA WA FARAGHA, KIDATO
WALIOFAULU CREDITS
CHA 4 VITUO VYA ZANZIBAR- 2019, WAVULANA TU
NAM. KITUO
WALIOFANYA WOTE WALIOFAULU"3" AU ZAIDI
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 222
Jadweli 37(a) inaendelea
WILAYA YA MAGHARIBI 'A'
1 BUBUBU 27 0 0.00 10 37.04
2 LANGONI 14 0 0.00 2 14.29
3 MTOPEPO 17 0 0.00 8 47.06
4 REGEZAMWENDO 27 0 0.00 10 37.04
5 MWENGE 4 0 0.00 4 100.00
6 CHUINI 13 0 0.00 7 53.85
7 ROYAL SEC. SCHOOL 3 0 0.00 2 66.67
8 J.K.U 37 1 2.70 22 59.46
9 MIKINDANI 3 0 0.00 2 66.67
10 MTONI KIGOMENI 2 0 0.00 2 100.00
JUMLA 147 1 2.7 69 46.94
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 223
Jadweli 37(a) inaendelea
1 AL - IHSANI 0 0 0.00 0 0.00
2 NYUKI J.W.T.Z 59 1 1.69 29 49.15
3 M/KWEREKWE 'A' 17 0 0.00 11 64.71
4 M/KWEREKWE 'C' 10 0 0.00 4 40.00
5 FUONI 33 0 0.00 17 51.52
6 CHUKWANI 25 0 0.00 12 48.00
7 KOMBENI 16 0 0.00 7 43.75
8 KISAUNI 7 0 0.00 1 14.29
9 Z'BAR COMMERCIAL 74 0 0.00 41 55.41
10 Z'BAR PROGRESSIVE 4 0 0.00 2 50.00
11 AL - FALAH 72 0 0.00 55 76.39
12 KINUNI 5 0 0.00 3 60.00
13 PHILTER FIDERAL 15 0 0.00 3 20.00
14 MBARARI PREPARATION 30 0 0.00 13 43.33
15 S.S.P HIGH SCHOOL 53 0 0.00 37 69.81
16 RAUDHA 12 0 0.00 10 83.33
17 KIEMBESAMAKI 42 1 2.38 10 23.81
JUMLA 474 2 0.42 255 53.80
WILAYA YA MAGHARIBI 'B'
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 224
WILAYA YA KASKAZINI 'A'
1 MKWAJUNI 8 0 0.00 2 25.00
2 TUMBATU 7 0 0.00 3 42.86
3 JONGOWE 9 0 0.00 2 22.22
4 CHAANI 16 0 0.00 4 25.00
5 KIDOTI 5 0 0.00 1 20.00
6 KINYASINI 24 1 4.17 8 33.33
7 PALE 4 0 0.00 1 25.00
8 POTOA 11 0 0.00 5 45.45
9 GAMBA 4 0 0.00 3 75.00
10 MATEMWE 3 0 0.00 1 33.33
11 FUKUCHANI 1 0 0.00 0 0.00
JUMLA 92 1 1.09 30 32.61
WILAYA YA KASKAZINI 'B'
1 DONGE 1 0 0.00 0 0.00
2 MAHONDA 4 0 0.00 2 50.00
3 MFENESINI 12 0 0.00 6 50.00
4 FUJONI 12 0 0.00 2 0.00
5 BUMBWINI 7 0 0.00 3 42.86
6 KITOPE 15 0 0.00 7 46.67
7 MAKOBA 2 0 0.00 1 50.00
8 MUANDA 7 0 0.00 2 28.57
JUMLA 60 0 0.00 23 38.33
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 225
Jadweli 37(a) inaendelea
WILAYA YA KATI
1 NDIJANI 2 0 0.00 0 0.00
2 UROA 8 0 0.00 3 37.50
3 UNGUJA UKUU 2 1 50.00 1 50.00
4 DUNGA 36 0 0.00 16 44.44
5 MWERA 42 0 0.00 27 64.29
6 BAMBI 8 1 12.50 6 75.00
7 CHWAKA 19 0 0.00 5 26.32
8 KIBELE 30 0 0.00 11 36.67
9 MACHUI 7 0 0.00 5 71.43
10 JENDELE 4 0 0.00 3 75.00
11 UBAGO 47 0 0.00 16 34.04
12 KIBOJE 2 0 0.00 2 100.00
UZINI 207 2 0.97 95 45.89
WILAYA YA KUSINI
1 MAKUNDUCHI 24 0 0.00 17 70.83
2 KITOGANI 6 0 0.00 6 100.00
3 JAMBIANI 0 0 0.00 0 0.00
4 CHARAWE 4 0 0.00 1 25.00
5 MUYUNI 8 0 0.00 5 62.50
6 KUSINI 17 0 0.00 6 35.29
7 BWEJUU CHARITY 6 0 0.00 2 33.33
8 UKONGORONI 20 0 0.00 9 45.00
JUMLA 85 0 0.00 46 54.12
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 226
Jadweli 37(a) inaendelea
WILAYA YA MICHEWENI
1 KONDE 5 0 0.00 3 60.00
2 WINGWI 8 0 0.00 3 37.50
3 MICHEWENI 14 0 0.00 7 50.00
4 TUMBE 16 0 0.00 11 68.75
5 SHUMBA VYAMBONI 23 0 0.00 3 13.04
6 KINOWE 2 0 0.00 1 50.00
7 KOJANI 8 0 0.00 2 25.00
JUMLA 76 0 0.00 30 39.47
1 UTAANI 5 0 0.00 3 60.00
2 MCHANGA MDOGO 24 0 0.00 17 70.83
3 PANDANI 8 0 0.00 5 62.50
4 PEMBA ISLAMIC 16 1 0.00 13 0.00
5 MINUNGWINI 10 0 0.00 3 30.00
6 UONDWE 9 0 0.00 2 22.22
7 SHENGEJUU 2 0 0.00 0 0.00
8 KINYASINI PEMBA 2 0 0.00 0 0.00
9 KIZIMBANI PEMBA 5 0 0.00 3 60.00
10 MITIULAYA 10 0 0.00 4 40.00
11 KIUYU 11 0 0.00 4 36.36
12 MZAMBARAU TAKAO 15 0 0.00 11 73.33
13 CHASASA 20 0 0.00 10 50.00
14 KANGAGANI 3 0 0.00 1 33.33
15 GANDO 8 0 0.00 1 12.50
16 WETE 13 0 0.00 7 53.85
JUMLA 161 1 0.62 84 52.17
WILAYA YA WETE
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 227
Jadweli 37(a) inaendelea
WILAYA YA CHAKE-CHAKE
1 FIDEL - CASTRO 58 0 0.00 48.00 82.76
2 SHAMIANI 16 0 0.00 10.00 62.50
3 CHANJAMJAWILI 10 0 0.00 8.00 80.00
4 NGWACHANI 2 0 0.00 0.00 0.00
5 PIKI 2 0 0.00 1.00 50.00
6 KILINDI 9 0 0.00 5.00 55.56
7 WESHA 12 0 0.00 5.00 41.67
8 FURAHA 6 0 0.00 2.00 33.33
9 ZIWANI 3 0 0.00 1.00 33.33
10 MBUZINI 11 0 0.00 7.00 63.64
11 NG'AMBWA 1 0 0.00 1.00 100.00
12 DR. OMAR ALI JUMA 13 0 0.00 6.00 46.15
13 MADUNGU 30 0 0.00 16.00 53.33
JUMLA 173 0 0.00 110 63.58
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 228
Jadweli 37(a) inaendelea
WILAYA YA MKOANI
1 KANGANI 5 0 0.00 4.00 80.00
2 UWELENI 28 0 0.00 10.00 35.71
3 KENGEJA TECHNICAL 7 0 0.00 4.00 57.14
4 MKANYAGENI 8 0 0.00 3.00 37.50
5 MTAMBILE 11 0 0.00 8.00 72.73
6 WAMBAA 11 0 0.00 6.00 0.00
7 MWAMBE 9 0 0.00 4.00 44.44
8 MAKOMBENI 1 0 0.00 1.00 100.00
9 CHAMBANI 7 0 0.00 1.00 14.29
JUMLA 87 0 0.00 41 47.13
JUMLA KUU 2240 15 0.67 1098 49.02
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 229
JADWELI NAM. 37(b)
IDADI % IDADI %
1 LUMUMBA 189 1 0.53 103 54.50
2 TUMEKUJA 13 0 0.00 9 69.23
3 BENBELLA 67 0 0.00 35 52.24
4 MIKUNGUNU 47 0 0.00 10 21.28
5 HAMAMNI 28 0 0.00 5 17.86
6 HAILESELASSIE 49 0 0.00 12 24.49
7 K/CHEKUNDU 10 0 0.00 4 40.00
8 KIPONDA 18 0 0.00 8 44.44
9 JANG'OMGE 14 0 0.00 3 21.43
10 FARAJA 57 0 0.00 25 43.86
11 BILALI- ISLAMIC 109 1 0.92 0.00
12 CHUMBUNI 22 0 0.00 13 59.09
13 MWEMBELADU 15 0 0.00 1 6.67
14 MEMON 1 0 0.00 0 0.00
15 SUNCITY 9 0 0.00 5 55.56
16 NYERERE 13 0 0.00 4 30.77
JUMLA 661 2 0.30 237 35.85
MATOKEO YA MTIHANI KWA WATAHINIWA WA FARAGHA, KIDATO
WALIOFAULU CREDITS
NAM. KITUO
WALIOFANYA WOTE WALIOFAULU"3" AU ZAIDI
CHA 4 VITUO VYA ZANZIBAR- 2017, WASICHANA TU
WILAYA YA MJINI
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 230
Jadweli 37(b) inaendelea
1 BUBUBU 58 0 0.00 25 43.10
2 LANGONI 2 0 0.00 2 100.00
3 MTOPEPO 11 0 0.00 6 54.55
4 REGEZAMWENDO 16 0 0.00 12 75.00
5 MWENGE 0 0 0.00 0 0.00
6 CHUINI 17 0 0.00 9 52.94
7 ROYAL SEC. SCHOOL 3 0 0.00 1 33.33
8 J.K.U 59 1 1.69 41 69.49
9 MIKINDANI 3 0 0.00 1 33.33
10 MTONI KIGOMENI 2 0 0.00 1 50.00
JUMLA 171 1 0.58 98 57.31
WILAYA YA MAGHARIBI 'A'
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 231
Jadweli 37(b) inaendelea
1 AL - IHSANI 57 0 0.00 33 57.89
2 NYUKI J.W.T.Z 49 0 0.00 31 63.27
3 M/KWEREKWE 'A' 16 1 6.25 10 62.50
4 M/KWEREKWE 'C' 24 0 0.00 14 58.33
5 FUONI 33 0 0.00 17 51.52
6 CHUKWANI 10 0 0.00 5 50.00
7 KOMBENI 20 0 0.00 7 35.00
8 KISAUNI 6 0 0.00 2 33.33
9 Z'BAR COMMERCIAL 44 0 0.00 23 52.27
10 Z'BAR PROGRESSIVE 7 0 0.00 5 71.43
11 AL - FALAH 73 0 0.00 55 75.34
12 KINUNI 11 0 0.00 4 36.36
13 PHILTER FIDERAL 15 0 0.00 5 33.33
14 MBARARI PREPARATION 40 0 0.00 21 52.50
15 S.S.P HIGH SCHOOL 51 0 0.00 25 49.02
16 RAUDHA 14 0 0.00 10 71.43
17 KIEMBESAMAKI 29 0 0.00 9 31.03
JUMLA 499 1 0.20 276 55.31
WILAYA YA MAGHARIBI 'B'
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 232
Jadweli 37(b) inaendelea
1 MKWAJUNI 6 0 0.00 3 50.00
2 TUMBATU 3 0 0.00 2 66.67
3 JONGOWE 12 0 0.00 6 50.00
4 CHAANI 19 0 0.00 11 57.89
5 KIDOTI 15 0 0.00 5 33.33
6 KINYASINI 32 0 0.00 7 21.88
7 PALE 10 0 0.00 2 0.00
8 POTOA 2 0 0.00 1 50.00
9 GAMBA 2 0 0.00 1 50.00
10 MATEMWE 3 0 0.00 0 0.00
11 FUKUCHANI 6 0 0.00 4 66.67
JUMLA 110 0 0.00 42 38.18
1 DONGE 3 0 0.00 1 33.33
2 MAHONDA 10 0 0.00 1 10.00
3 MFENESINI 11 0 0.00 6 54.55
4 FUJONI 21 0 0.00 9 0.00
5 BUMBWINI 9 0 0.00 4 0.00
6 KITOPE 16 0 0.00 7 43.75
7 MAKOBA 3 0 0.00 0 0.00
8 MUANDA 3 0 0.00 0 0.00
JUMLA 76 0 0.00 28 36.84
WILAYA YA KASKAZINI 'A'
WILAYA YA KASKAZINI 'B'
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 233
Jadweli 37(b) inaendelea
1 NDIJANI 6 0 0.00 2 33.33
2 UROA 10 0 0.00 4 40.00
3 UNGUJA UKUU 5 0 0.00 4 80.00
4 DUNGA 40 0 0.00 18 45.00
5 MWERA 21 0 0.00 12 57.14
6 BAMBI 4 0 0.00 2 0.00
7 CHWAKA 34 0 0.00 12 35.29
8 KIBELE 30 1 3.33 13 43.33
9 MACHUI 8 0.00 3 37.50
10 JENDELE 1 0 0.00 0 0.00
11 UBAGO 26 0 0.00 11 42.31
12 KIBOJE 4 0 0.00 3 75.00
13 UZINI 7 0 0.00 2 28.57
JUMLA 196 1 0.51 86 43.88
WILAYA YA KATI
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 234
Jadweli 37(b) inaendelea
WILAYA YA KUSINI
1 MAKUNDUCHI 6 0 0.00 4 66.67
2 KITOGANI 2 0 0.00 1 50.00
3 JAMBIANI 6 0 0.00 5 83.33
4 CHARAWE 5 0 0.00 3 60.00
5 MUYUNI 5 0 0.00 3 60.00
6 KUSINI 3 0 0.00 1 33.33
7 BWEJUU CHARITY 9 0 0.00 6 66.67
8 UKONGORONI 19 0 0.00 6 31.58
JUMLA 55 0 0.00 29 52.73
1 KONDE 2 0 0.00 0 0.00
2 WINGWI 4 0 0.00 1 25.00
3 MICHEWENI 5 0 0.00 3 60.00
4 TUMBE 2 0 0.00 1 0.00
5 SHUMBA VYAMBONI 3 0 0.00 3 100.00
6 KINOWE 1 0 0.00 0 0.00
7 KOJANI 3 0 0.00 2 66.67
JUMLA 20 0 0.00 10 50.00
WILAYA YA MICHEWENI
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 235
Jadweli 37(b) inaendelea
1 UTAANI 26 0 0.00 12 46.15
2 MCHANGA MDOGO 30 0 0.00 18 60.00
3 PANDANI 9 0 0.00 1 11.11
4 PEMBA ISLAMIC 26 1 3.85 22 84.62
5 MINUNGWINI 3 0 0.00 1 33.33
6 UONDWE 3 0 0.00 2 0.00
7 SHENGEJUU 5 0 0.00 3 60.00
8 KINYASINI PEMBA 1 0 0.00 0 0.00
9 KIZIMBANI PEMBA 6 0 0.00 2 0.00
10 MITIULAYA 4 0 0.00 0 0.00
11 KIUYU 12 0 0.00 1 8.33
12 MZAMBARAU TAKAO 9 0 0.00 3 33.33
13 CHASASA 10 0 0.00 6 60.00
14 KANGAGANI 7 0 0.00 2 28.57
15 GANDO 12 0 0.00 4 33.33
16 WETE 11 0 0.00 6 54.55
JUMLA 174 1 0.57 83 47.70
WILAYA YA WETE
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 236
Jadweli 37(b) inaendelea
1 FIDEL - CASTRO 65 1 1.54 45 69.23
2 SHAMIANI 16 0 0.00 8 50.00
3 CHANJAMJAWILI 3 0 0.00 3 100.00
4 NGWACHANI 3 0 0.00 0 0.00
5 PIKI 2 0 0.00 1 50.00
6 KILINDI 0 0 0.00 0 0.00
7 WESHA 12 0 0.00 9 75.00
8 FURAHA 2 0 0.00 0 0.00
9 ZIWANI 0 0 0.00 0 0.00
10 MBUZINI 9 0 0.00 8 88.89
11 NG'AMBWA 6 0 0.00 1 0.00
12 DR. OMAR ALI JUMA 6 0 0.00 3 50.00
13 MADUNGU 44 0 0.00 19 43.18
JUMLA 168 1 0.60 97 57.74
WILAYA YA CHAKE-CHAKE
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 237
Jadweli 37(b) inaendelea
1 KANGANI 9 0 0.00 6 66.67
2 UWELENI 16 0 0.00 12 75.00
3 KENGEJA TECHNICAL 0 0 0.00 0 0.00
4 MKANYAGENI 3 0 0.00 2 66.67
5 MTAMBILE 13 0 0.00 9 69.23
6 WAMBAA 3 0 0.00 2 66.67
7 MWAMBE 11 0 0.00 7 63.64
8 MAKOMBENI 1 0 0.00 0 0.00
9 CHAMBANI 2 0 0.00 1 50.00
JUMLA 58 0 0.00 39 67.24
JUMLA KUU 2188 7 0.32 1025 46.85
WILAYA YA MKOANI
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 238
JADWELI NAM. 37(c)
IDADI % IDADI %
1 LUMUMBA 381 3 0.79 207 54.33
2 TUMEKUJA 33 0 0.00 21 63.64
3 BENBELLA 83 0 0.00 39 46.99
4 MIKUNGUNU 113 0 0.00 26 23.01
5 HAMAMNI 73 0 0.00 23 31.51
6 HAILESELASSIE 89 1 1.12 30 33.71
7 K/CHEKUNDU 31 0 0.00 13 41.94
8 KIPONDA 37 0 0.00 23 62.16
9 JANG'OMGE 43 0 0.00 15 34.88
10 FARAJA 103 3 2.91 42 40.78
11 BILALI- ISLAMIC 216 2 0.93 55 25.46
12 CHUMBUNI 35 0 0.00 21 60.00
13 MWEMBELADU 49 1 2.04 6 12.24
14 MEMON 4 0 0.00 3 75.00
15 SUNCITY 20 0 0.00 13 65.00
16 NYERERE 29 0 0.00 15 51.72
JUMLA 1339 10 0.75 552 41.22
WILAYA YA MJINI
MATOKEO YA MTIHANI KWA WATAHINIWA WA FARAGHA, KIDATO
WALIOFAULU CREDITS
NAM. KITUO
WALIOFANYA WOTE WALIOFAULU"3" AU ZAIDI
CHA 4 VITUO VYA ZANZIBAR- 2017, WAVULANA NA WASICHANA
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 239
Jadweli 37(c) inaendelea
1 BUBUBU 85 0 0.00 35 41.18
2 LANGONI 16 0 0.00 4 25.00
3 MTOPEPO 28 0 0.00 14 50.00
4 REGEZAMWENDO 43 0 0.00 22 51.16
5 MWENGE 4 0 0.00 4 100.00
6 CHUINI 30 0 0.00 16 53.33
7 ROYAL SEC. SCHOOL 6 0 0.00 3 50.00
8 J.K.U 96 2 2.08 63 65.63
9 MIKINDANI 6 0 0.00 3 50.00
10 MTONI KIGOMENI 4 0 0.00 3 75.00
JUMLA 318 2 2.1 167 52.52
WILAYA YA MAGHARIBI 'A'
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 240
Jadweli 37(c) inaendelea
1 AL - IHSANI 57 0 0.00 33 57.89
2 NYUKI J.W.T.Z 108 1 0.93 60 55.56
3 M/KWEREKWE 'A' 33 1 3.03 21 63.64
4 M/KWEREKWE 'C' 34 0 0.00 18 52.94
5 FUONI 66 0 0.00 34 51.52
6 CHUKWANI 35 0 0.00 17 48.57
7 KOMBENI 36 0 0.00 14 38.89
8 KISAUNI 13 0 0.00 3 23.08
9 Z'BAR COMMERCIAL 118 0 0.00 64 54.24
10 Z'BAR PROGRESSIVE 11 0 0.00 7 63.64
11 AL - FALAH 145 0 0.00 110 75.86
12 KINUNI 16 0 0.00 7 43.75
13 PHILTER FIDERAL 30 0 0.00 8 26.67
14 MBARARI PREPARATION 70 0 0.00 34 48.57
15 S.S.P HIGH SCHOOL 104 0 0.00 62 59.62
16 RAUDHA 26 0 0.00 20 76.92
17 KIEMBESAMAKI 71 1 1.41 19 26.76
JUMLA 973 3 0.31 531 54.57
WILAYA YA MAGHARIBI 'B'
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 241
Jadweli 37(c) inaendelea
1 MKWAJUNI 14 0 0.00 5 35.71
2 TUMBATU 10 0 0.00 5 50.00
3 JONGOWE 21 0 0.00 8 38.10
4 CHAANI 35 0 0.00 15 42.86
5 KIDOTI 20 0 0.00 6 30.00
6 KINYASINI 56 1 1.79 15 26.79
7 PALE 14 0 0.00 3 0.00
8 POTOA 13 0 0.00 6 46.15
9 GAMBA 6 0 0.00 4 66.67
10 MATEMWE 6 0 0.00 1 0.00
11 FUKUCHANI 7 0 0.00 4 57.14
JUMLA 202 1 0.50 72 35.64
1 DONGE 4 0 0.00 1 25.00
2 MAHONDA 14 0 0.00 3 21.43
3 MFENESINI 23 0 0.00 12 52.17
4 FUJONI 33 0 0.00 11 0.00
5 BUMBWINI 16 0 0.00 7 0.00
6 KITOPE 31 0 0.00 14 45.16
7 MAKOBA 5 0 0.00 1 0.00
8 MUANDA 10 0 0.00 2 20.00
JUMLA 136 0 0.00 51 37.50
WILAYA YA KASKAZINI 'A'
WILAYA YA KASKAZINI 'B'
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 242
Jadweli 37(c) inaendelea
1 NDIJANI 8 0 0.00 2 25.00
2 UROA 18 0 0.00 7 38.89
3 UNGUJA UKUU 7 1 14.29 5 71.43
4 DUNGA 76 0 0.00 34 44.74
5 MWERA 63 0 0.00 39 61.90
6 BAMBI 12 1 0.00 8 0.00
7 CHWAKA 53 0 0.00 17 32.08
8 KIBELE 60 1 1.67 24 40.00
9 MACHUI 15 0 0.00 8 53.33
10 JENDELE 5 0 0.00 3 60.00
11 UBAGO 73 0 0.00 27 36.99
12 KIBOJE 9 0 0.00 4 44.44
JUMLA 399 3 0.75 178 44.61
WILAYA YA KATI
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 243
Jadweli 37(c) inaendelea
1 MAKUNDUCHI 30 0 0.00 21 70.00
2 KITOGANI 8 0 0.00 7 87.50
3 JAMBIANI 6 0 0.00 5 83.33
4 CHARAWE 9 0 0.00 4 44.44
5 MUYUNI 13 0 0.00 8 61.54
6 KUSINI 20 0 0.00 7 35.00
7 BWEJUU CHARITY 15 0 0.00 8 53.33
8 UKONGORONI 39 0 0.00 15 38.46
JUMLA 140 0 0.00 75 53.57
1 KONDE 7 0 0.00 3 42.86
2 WINGWI 12 0 0.00 4 33.33
3 MICHEWENI 19 0 0.00 10 52.63
4 TUMBE 18 0 0.00 12 0.00
5 SHUMBA VYAMBONI 26 0 0.00 6 23.08
6 KINOWE 3 0 0.00 1 33.33
7 KOJANI 11 0 0.00 4 36.36
JUMLA 96 0 0.00 40 41.67
WILAYA YA KUSINI
WILAYA YA MICHEWENI
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 244
Jadweli 37(c) inaendelea
1 UTAANI 31 0 0.00 15 48.39
2 MCHANGA MDOGO 54 0 0.00 35 64.81
3 PANDANI 17 0 0.00 6 35.29
4 PEMBA ISLAMIC 42 2 4.76 35 83.33
5 MINUNGWINI 13 0 0.00 4 30.77
6 UONDWE 12 0 0.00 4 0.00
7 SHENGEJUU 7 0 0.00 3 42.86
8 KINYASINI PEMBA 3 0 0.00 0 0.00
9 KIZIMBANI PEMBA 11 0 0.00 5 0.00
10 MITIULAYA 14 0 0.00 4 28.57
11 KIUYU 23 0 0.00 5 21.74
12 MZAMBARAU TAKAO 24 0 0.00 14 58.33
13 CHASASA 30 0 0.00 16 53.33
14 KANGAGANI 10 0 0.00 3 30.00
15 GANDO 20 0 0.00 5 25.00
16 WETE 24 0 0.00 13 54.17
JUMLA 335 2 0.60 167 49.85
WILAYA YA WETE
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 245
Jadweli 37(c) inaendelea
1 FIDEL - CASTRO 123 1 0.81 93 75.61
2 SHAMIANI 32 0 0.00 18 56.25
3 CHANJAMJAWILI 13 0 0.00 11 84.62
4 NGWACHANI 5 0 0.00 0 0.00
5 PIKI 4 0 0.00 2 50.00
6 KILINDI 9 0 0.00 5 55.56
7 WESHA 24 0 0.00 14 58.33
8 FURAHA 8 0 0.00 2 25.00
9 ZIWANI 3 0 0.00 1 33.33
10 MBUZINI 20 0 0.00 15 75.00
11 NG'AMBWA 7 0 0.00 2 0.00
12 DR. OMAR ALI JUMA 19 0 0.00 9 47.37
13 MADUNGU 74 0 0.00 35 47.30
JUMLA 341 1 0.29 207 60.70
WILAYA YA CHAKE-CHAKE
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 246
Jadweli 37(c) inaendelea
1 KANGANI 14 0 0.00 10 71.43
2 UWELENI 44 0 0.00 22 50.00
3 KENGEJA TECHNICAL 7 0 0.00 4 57.14
4 MKANYAGENI 11 0 0.00 5 45.45
5 MTAMBILE 24 0 0.00 17 70.83
6 WAMBAA 14 0 0.00 8 57.14
7 MWAMBE 20 0 0.00 11 55.00
8 MAKOMBENI 2 0 0.00 1 50.00
9 CHAMBANI 9 0 0.00 2 22.22
JUMLA 145 0 0.00 80 55.17
JUMLA KUU 4424 22 0.50 2120 47.92
WILAYA YA MKOANI
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 247
JADWELI NAM. 38(a)
IDADI % IDADI %
LUMUMBA 36 0 0.00 14 38.89
BENBELLA 9 1 11.11 7 77.78
HAMAMNI 5 1 20.00 5 100.00
KIPONDA 11 0 0.00 10 90.91
Z'BAR COMMERCIAL 2 0 0.00 2 100.00
KIEMBESAMAKI 18 1 5.56 15 83.33
M/KWEREKWE 'C' 14 0 0.00 11 78.57
TUMEKUJA 6 0 0.00 3 50.00
FARAJA 12 1 8.33 12 100.00
MKWAJUNI 0 0 0 0 0
NYUKI J.W.T.Z 6 0 0.00 0 0.00
FIDEL - CASTRO 5 0 0.00 2 40.00
CHASASA 2 - 0.00 1 50.00
UTAANI 3 0 0.00 3 100.00
SHAMIANI 4 1 25.00 4 100.00
MCHANGA MDOGO 9 1 11.11 7 77.78
UWELENI 3 0 0.00 3 100.00
PEMBA ISLAMIC 2 0 0.00 1 50.00
Jumla 147 6 4.08 100 68.03
MATOKEO YA MTIHANI KWA WANAFUNZI WA FARAGHA KIDATO
CHA 6 VITUO VYA ZANZIBAR - 2017/2018 - WAVULANA TU
WATAHINIWAKITUO
WALIOFAULU
P2 + S1 AU ZAIDI
WOTE
WALIOFAULU
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 248
JADWELI NAM. 38(b)
IDADI % IDADI %
LUMUMBA 16 0 0.00 13 81.25
BENBELLA 12 0 0.00 5 41.67
HAMAMNI 1 0 0.00 1 100.00
KIPONDA 2 0 0.00 2 100.00
Z'BAR COMMERCIAL 3 1 33.33 3 100.00
KIEMBESAMAKI 8 0 0.00 5 62.50
M/KWEREKWE 'C' 23 0 0.00 21 91.30
TUMEKUJA 5 0 0.00 4 80.00
FARAJA 6 0 0.00 5 83.33
MKWAJUNI 3 0 0.00 2 66.67
NYUKI J.W.T.Z 4 0 0.00 0 0.00
FIDEL - CASTRO 2 0 0.00 0 0.00
CHASASA 4 - 0.00 2 50.00
UTAANI 6 0 0.00 6 100.00
SHAMIANI 7 0 0.00 7 0.00
MCHANGA MDOGO 6 0 0.00 6 100.00
UWELENI 2 0 0.00 2 100.00
PEMBA ISLAMIC 0 0 0 0 0
Jumla 110 1 0.91 84 76.36
MATOKEO YA MTIHANI KWA WANAFUNZI WA FARAGHA KIDATO
CHA 6 VITUO VYA ZANZIBAR - 2017/2018 - WASICHANA TU
KITUO WATAHINIWA
WALIOFAULU WOTE
P2 + S1 AU ZAIDI WALIOFAULU
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 249
JADWELI NAM. 38(c)
IDADI % IDADI %
LUMUMBA 52 0 0.00 27 51.92
BENBELLA 21 1 4.76 12 57.14
HAMAMNI 6 1 16.67 6 100.00
KIPONDA 13 0 0.00 12 92.31
Z'BAR COMMERCIAL 5 1 20.00 5 100.00
KIEMBESAMAKI 26 1 3.85 20 76.92
M/KWEREKWE 'C' 37 0 0.00 32 86.49
TUMEKUJA 11 0 0.00 7 63.64
FARAJA 18 1 5.56 17 94.44
MKWAJUNI 3 0 0.00 2 66.67
NYUKI J.W.T.Z 10 0 0.00 0 0.00
FIDEL - CASTRO 7 0 0.00 2 28.57
CHASASA 6 0 0.00 3 50.00
UTAANI 9 0 0.00 9 100.00
SHAMIANI 11 1 0.00 11 0.00
MCHANGA MDOGO 15 1 6.67 13 86.67
UWELENI 5 0 0.00 5 100.00
PEMBA ISLAMIC 2 0 0.00 1 50.00
Jumla 257 7 2.72 184 71.60
MATOKEO YA MTIHANI KWA WANAFUNZI WA FARAGHA KIDATO
WALIOFAULU WOTE
CHA 6 VITUO VYA ZANZIBAR - 2017/2018 - WAVULANA NA WASICHANA
KITUO WATAHINIWA
P2 + S1 AU ZAIDI WALIOFAULU
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 250
JADWELI NAM. 39a
WAS JUMLA WAS JUMLA WAS JUMLA WAS JUMLA WAS JUMLA WAS JUMLA
CHUMBUNI 0 0 6 10 2 8 0 0 1 1 9 19
M/SHAURI 3 20 0 0 0 0 0 0 0 0 3 20
MUUNGANO 0 0 1 3 3 5 1 2 0 0 5 10
NYERERE 1 2 0 1 1 1 0 2 0 1 2 7
K/CHEKUNDU “B” 0 0 9 21 0 0 0 0 0 0 9 21
DARAJANI 1 1 1 4 1 4 2 3 0 0 5 12
KILIMAHEWA 0 0 1 2 0 5 0 0 0 0 1 7
FUONI 0 2 3 9 0 1 1 1 0 1 4 14
K/SAMAKI 1 1 0 0 0 0 0 0 0 0 1 1
MTOPEPO ‘B’ 2 5 2 3 0 0 0 0 0 2 4 10
M/KWEREKWE ‘B’ 0 0 0 0 0 0 0 0 1 1 1 1
KINDUNI 0 0 0 0 2 4 0 3 0 0 2 7
KINYASINI 2 5 3 9 1 11 0 2 0 0 6 27
MKWAJUNI 0 0 0 4 0 11 0 0 0 0 0 15
KIBENI 0 2 0 1 0 5 0 1 0 0 0 9
JUMLA 10 38 26 67 10 55 4 14 2 6 52 180
KITUO
IDADI YA WANAFUNZI WALIOFAULU ELIMU MBADALA NA
KUJIUNGA KATIKA MADARASA YA KAWAIDA, UNGUJA - 2019
JUMLA
E/MBADALA
RAHALEOIII IV V VI
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 251
JADWELI NAM. 39b
WAS JUMLA WAS JUMLA WAS JUMLA WAS JUMLA WAS JUMLA WAS JUMLA WAS JUMLA
NG’OMBENI 0 0 1 3 0 3 0 0 0 0 0 0 1 6
KENGEJA 4 6 1 2 1 3 0 3 1 1 0 0 7 15
SH/MUAMBE 0 0 0 3 3 15 2 5 0 0 0 0 5 23
PUJINI MSINGI 0 0 11 18 0 10 0 2 0 0 0 0 11 30
UWANDANI 0 1 3 4 2 2 0 1 1 2 0 0 6 10
MATALE MSINGI 0 0 0 0 0 0 0 9 0 10 0 0 0 19
GOMBANI 0 0 6 10 1 2 0 0 0 0 0 0 7 12
MTONI 3 9 5 13 0 0 0 0 0 0 0 0 8 22
SHUMBA MJINI 0 0 1 2 2 6 0 0 0 0 0 0 3 8
MICHEWENI 11 30 12 20 0 0 0 0 0 0 0 0 23 50
JUMLA 18 46 40 75 9 41 2 20 2 13 0 0 71 195
IDADI YA WANAFUNZI WALIOFAULU ELIMU MBADALA NA
KUJIUNGA KATIKA MADARASA YA KAWAIDA, PEMBA - 2019
JUMLA
KITUO
II III IV V VI
E/MBADALA
WINGWI
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 252
W'ME W'KE W'ME W'KE W'ME W'KE W'ME W'KE W'ME W'KE W'ME W'KE W'ME W'KE W'ME W'KE W'ME W'KE
1Useremala 10 0 5 0 1 0 0 0 0 0 0 0 20 0 20 0 11 0
2Ushoni 2 32 2 30 0 19 4 25 3 18 1 18 2 44 6 13 0 19
3Uchoraji/Uandishi 7 3 2 7 0 4 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
4Mafriji 18 0 23 0 5 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
5Electronics 5 0 9 0 2 0 0 0 0 0 0 0 25 0 10 2 0 0
6Uwashi 11 0 3 0 0 0 17 2 6 0 21 0 0 0 0 0 0 0
7Ufundi bomba 15 0 21 0 3 1 43 4 14 0 28 7 0 0 0 0 0 0
8Magari 34 0 18 0 3 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
9Uhunzi 7 0 5 1 5 0 13 0 18 0 3 0 0 0 0 0 0 0
10Upishi 15 18 10 14 3 3 9 8 7 5 2 1 0 0 0 0 0 0
11Kilimo 1 8 0 6 0 3 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
12 Teknolojia mawasiliano 6 13 8 2 0 0 0 0 0 0 0 0 20 24 21 12 0 0
13Huduma za mahoteli 5 5 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
14Ufundi wa umeme wa
magari
34 1 18 0 3 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
15Umeme wa Majumbani 48 2 36 1 5 0 58 6 0 0 47 5 32 4 19 1 12 0
JUMLA 218 82 160 61 30 30 144 45 48 23 102 31 99 72 76 28 23 19
MWAKA II I
MWANAKWEREKWE
JADWELI NAM. 40(a)
MKOKOTONI
MWAKA I MWAKA II MWAKA II I
IDADI YA WANAFUNZI KATIKA VITUO VYA AMALI, MACHI - 2019
Nam FANI
MWAKA I MWAKA II MWAKA II I
VITONGOJI
MWAKA I MWAKA II
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 253
IDADI YA JUMLA YA
VITUO WANAKISOMO
Mjini Sayansi Kimu 9 167 169
Magharibi 'A' Sayansi Kimu 9 178 182
Magharibi 'B' Sayansi Kimu 8 154 162
Sayansi Kimu 13 266 266
Uchongaji 1 - 16
Kaskazini 'B' Sayansi Kimu 15 326 331
Kati Sayansi Kimu 4 187 187
Kusini Sayansi Kimu 2 163 163
Micheweni Sayansi Kimu - - -
Wete Sayansi Kimu 1 10 10
Chake-Chake Sayansi Kimu - - -
Mkoani Sayansi Kimu 1 20 20
63 1471 1506
JADWELI NAM. 40(b)
Kaskazini 'A'
JUMLA
WANAWAKE
VITUO VYA KAZI ZA AMALI, 2019
WILAYA AINA YA KITUO
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 254
JADWELI 41
W'ME W'KE W'ME W'KE W'ME W'KE W'ME W'KE
Ufundi wa Magari 0 38 0 25 0 10 0 73 73
Majokufu na vipoza hewa 0 18 0 23 0 5 0 46 46
Ushoni 32 2 30 2 19 0 81 4 85
Uchoraji na Mapambo 3 7 7 2 4 0 14 9 23
Welding 0 7 1 5 0 5 1 17 18
Useremala 0 10 0 5 0 1 0 16 16
Upishi 18 15 14 10 3 3 35 28 63
Huduma za chakula. 5 5 0 0 0 0 5 5 10
Uashi 0 11 0 3 0 0 0 14 14
Electronics 0 5 0 9 0 2 0 16 16
Umeme wa magari 1 34 0 18 0 3 1 55 56
Kilimo 8 1 6 0 3 0 17 1 18
Ufundi bomba 0 15 0 21 1 3 1 39 40
ICT 13 6 2 8 0 0 15 14 29
Umeme wa majumbani 2 48 1 36 0 5 3 89 92
JUMLA 82 222 61 167 30 37 173 426 599
MKO
KOTO
NI
WALIOJIUNGA NA VYUO VYA MAMLAKA YA MAFUNZO YA AMALI 2018 -2019
KITU
OFANI
LEVEL I LEVEL II LEVEL III JUMLA JUMLA
KUU
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 255
Umeme 6 58 0 0 5 47 11 105 116
Ushoni 25 4 18 3 18 1 61 8 69
Ufundi bomba 4 43 0 14 7 28 11 85 96
upishi 8 9 5 7 2 1 15 17 32
Uashi 2 17 0 6 0 21 2 44 46
Welding 0 13 0 18 0 3 0 34 34
JUMLA 45 144 23 48 32 101 100 293 393
Ushoni 44 2 13 6 19 0 76 8 84
Electronics 0 25 2 10 0 0 2 35 37
ICT 24 20 12 21 0 0 36 41 77
Useremala 0 20 0 20 0 11 0 51 51
Umeme 4 32 1 19 0 12 5 63 68
JUMLA 72 99 28 76 19 23 119 198 317
JUMLA KUU 199 465 112 291 81 161 392 917 1309
VIT
ON
GO
JIM
/KW
ER
EK
WE
Jadweli nam. 41
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 256
JADWELI NAM. 42
Mjini 4 71 75 20 21 41 0 11 11 18 0 18 42 103 145
Magharibi 'A' 1 65 66 22 33 55 1 9 10 14 1 15 38 108 146
Magharibi 'B' 0 33 33 23 34 57 1 35 36 14 3 17 38 105 143
Kaskazini 'A' 5 13 18 31 4 35 5 0 5 24 0 24 65 17 82
Kaskazini 'B' 1 5 6 19 6 25 4 1 5 8 1 9 32 13 45
Kati 5 26 31 32 4 36 4 2 6 25 1 26 66 33 99
Kusini 4 20 24 8 2 10 3 2 5 9 0 9 24 24 48
Micheweni 4 8 12 20 1 21 0 1 1 11 1 12 35 11 46
Wete 2 16 18 34 3 37 0 2 2 26 1 27 62 22 84
Chake-Chake 2 9 11 25 4 29 1 3 4 19 3 22 47 19 66
Mkoani 2 8 10 31 1 32 2 1 3 20 0 20 55 10 65
Jumla 30 274 304 265 113 378 21 67 88 188 11 199 504 465 969
SEKONDARI TU
SERIKALI BINAFSI JUMLAJUMLA BINAFSIJUMLA
IDADI YA SKULI ZA MAANDALIZI, MSINGI, MSINGI NA KATI
NA SEKONDARI ZILIZOSAJILIWA KIWILAYA, MACHI - 2019
MAANDALIZI MSINGI TU MSINGI NA KATI JUMLA
WILAYA SERIKALIBINAFSISERIKALI JUMLABINAFSI SERIKALI SERIKALIBINAFSI JUMLA
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 257
JADWELI NAM. 43(a)
W'KE J'LA W'KE J'LA W'KE J'LA W'KE J'LA W'KE J'LA W'KE J'LA W'KE J'LA
Mjini 4 4 410 442 3 5 0 0 545 680 548 853 1510 1984
Magharibi 'A' 2 3 227 254 6 7 5 11 524 603 410 563 1174 1441
Magharibi 'B' 5 5 348 386 2 3 1 1 538 633 414 589 1308 1617
Kaskazini 'A' 2 2 164 266 5 10 13 13 260 429 171 389 615 1109
Kaskazini 'B' 1 1 167 227 3 3 0 0 178 259 117 230 466 720
Kati 0 1 178 269 10 17 5 6 290 437 184 373 667 1103
Kusini 0 0 95 151 0 1 0 0 76 145 40 113 211 410
Micheweni 5 7 46 81 0 5 1 1 126 228 49 203 227 525
Wete 5 9 146 209 2 15 0 5 210 334 130 315 493 887
Chake-Chake 1 1 197 242 4 7 1 2 214 296 169 321 586 869
Mkoani 5 7 122 195 3 9 0 1 161 299 88 244 379 755
Jumla 30 40 2100 2722 38 82 26 40 3122 4343 2320 4193 7636 11420
IDADI NA AINA MBALI MBALI ZA WALIMU WA MSINGI NA
SEKONDARI ( DAR. I - KID. 6 ) WALIOSOMEA KWA UCHAMBUZI WA KIWILAYA
KATIKA SKULI ZA SERIKALI, MACHI - 2019
DIGRII NA ZAIDI JUMLAKID. 6 DIPLOMAFTC
WILAYA
CHINI YA KID 4 KID. 4
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 258
JADWELI NAM. 43b)
W'KE J'LA W'KE J'LA W'KE J'LA W'KE J'LA W'KE J'LA W'KE J'LA W'KE J'LA
Mjini 0 0 1 1 0 0 0 2 0 0 4 11 5 14
Magharibi 'A' 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Magharibi 'B' 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 7 0 7
Kaskazini 'A' 0 0 0 3 0 0 0 1 0 2 0 1 0 7
Kaskazini 'B' 0 0 2 4 1 3 0 0 0 0 0 0 3 7
Kati 0 1 0 0 0 0 0 2 0 0 0 1 0 4
Kusini 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Micheweni 1 1 0 0 0 0 0 1 0 0 0 0 1 2
Wete 0 0 0 0 0 1 1 1 0 0 0 0 1 2
Chake-Chake 0 2 0 2 0 1 0 0 0 1 0 2 0 8
Mkoani 0 0 0 0 1 1 0 0 0 0 0 0 1 1
Jumla 1 4 3 10 2 6 1 7 0 3 4 22 11 52
IDADI NA AINA MBALI MBALI ZA WALIMU WA MSINGI NA
SEKONDARI ( DAR. I - KID. 6 ) WASIOSOMEA KWA UCHAMBUZI WA KIWILAYA
KATIKA SKULI ZA SERIKALI, MACHI - 2019
CHINI YA KID 4 KID. 4 FTC DIPLOMA DIGRII NA ZAIDIKID.6 JUMLA
WILAYA
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 259
JADWELI NAM. 43(c)
W'KE J'LA W'KE J'LA W'KE J'LA W'KE J"LA W'KE J'LA W'KE J'LA W'KE J'LA
Mjini 4 4 411 443 3 5 0 2 545 680 552 864 1515 1998
Magharibi 'A' 2 3 227 254 6 7 5 11 524 603 410 563 1174 1441
Magharibi 'B' 5 5 348 386 2 3 1 1 538 633 414 596 1308 1624
Kaskazini 'A' 2 2 164 269 5 10 13 14 260 431 171 390 615 1116
Kaskazini 'B' 1 1 169 231 4 6 0 0 178 259 117 230 469 727
Kati 0 2 178 269 10 17 5 8 290 437 184 374 667 1107
Kusini 0 0 95 151 0 1 0 0 76 145 40 113 211 410
Micheweni 6 8 46 81 0 5 1 2 126 228 49 203 228 527
Wete 5 9 146 209 2 16 1 6 210 334 130 315 494 889
Chake-Chake 1 3 197 244 4 8 1 2 214 297 169 323 586 877
Mkoani 5 7 122 195 4 10 0 1 161 299 88 244 380 756
Jumla 31 44 2103 2732 40 88 27 47 3122 4346 2324 4215 7647 11472
KID. 4 KID. 6
IDADI NA AINA MBALI MBALI ZA WALIMU WOTE WA MSINGI NA
SEKONDARI, ( DARASA 1 - KIDATO 6 ) WASIOSOMEA NA WALIOSOMEA KWA
UCHAMBUZI WA KIWILAYA KATIKA SKULI ZA SERIKALI, MACHI - 2019
JUMLAFTC DIPLOMA
WILAYA
DIGRII NA ZAIDICHINI YA KID.4
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 260
JADWELI NAM. 43 d
W'KE J'LA W'KE J'LA W'KE J'LA W'KE J'LA W'KE J'LA W'KE J'LA W'KE J'LA
Mjini 100 100 100 100 100 100 0 0 100 100 99 99 100 99
Magharibi 'A' 100 100 100 100 100 100 100 100 100 100 100 100 100 100
Magharibi 'B' 100 100 100 100 100 100 100 100 100 100 100 99 100 100
Kaskazini 'A' 100 100 100 99 100 100 100 93 100 100 100 100 100 99
Kaskazini 'B' 100 100 99 98 75 50 0 0 100 100 100 100 99 99
Kati 0 50 100 100 100 100 100 75 100 100 100 100 100 100
Kusini 0 0 100 100 0 100 0 0 100 100 100 100 100 100
Micheweni 83 88 100 100 0 100 100 50 100 100 100 100 100 100
Wete 100 100 100 100 100 94 0 83 100 100 100 100 100 100
Chake-Chake 100 33 100 99 100 88 100 100 100 100 100 99 100 99
Mkoani 100 100 100 100 75 90 0 100 100 100 100 100 100 100
Jumla 97 91 100 100 95 93 96 85 100 100 100 99 100 100
JUMLA
( DAR. 1 - KID. 6 ) WALIOSOMEA KATI YA WALIMU WOTE WA SKULI
ASILIMIA ZA WALIMU MBALI MBALI WA MSINGI NA SEKONDARI
WILAYA
CHINI YA KID 4 KID. 4 KID. 6 FTC
ZA SERIKALI, KIWILAYA, MACHI - 2019
DIGRII NA ZAIDIDIPLOMA
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 261
JADWELI NAM. 44a)
MADARASA WANAFUNZI WANAFUNZI WASTANI WA
(VYUMBA VYA KWA CHUMBA KWA MKONDO SHIFTI ZA
(DAR.I - KID. 4) KUSOMEA) KIMOJA MM0JA MASOMO
Mjini 54540 864 1155 63 47 1.34
Magharibi 'A' 58187 810 885 72 66 1.09
Magharibi 'B' 69807 1219 1271 57 55 1.04
Kaskazini 'A' 33837 712 658 48 51 0.92
Kaskazini 'B' 19541 335 633 58 31 1.89
Kati 27188 580 608 47 45 1.05
Kusini 11732 264 259 44 45 0.98
Micheweni 30859 351 501 88 62 1.43
Wete 40671 594 738 68 55 1.24
Chake-Chake 37528 531 699 71 54 1.32
Mkoani 37331 415 651 90 57 1.57
Jumla 421221 6675 8058 63 52 1.21
UWIANO WA WANAFUNZI, MADARASA NA MIKONDO KATIKA NGAZI YA MSINGI NA KATI
(DAR 1 - KID. 4) KWA UCHAMBUZI WA KIWILAYA: SKULI ZA SERIKALI NA BINAFSI, MACHI - 2019
UANDIKISHAJI
MIKONDOWILAYA
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 262
JADWELI NAM. 44(b)
MADARASA WANAFUNZI WANAFUNZI WASTANI WA
(VYUMBA VYA KWA CHUMBA KWA MKONDO SHIFTI ZA
(DAR 1 - KIDATO.4) KUSOMEA) KIMOJA MMOJA MASOMO
Mjini 44773 505 796 89 56 1.58
Magharibi 'A' 50749 494 593 103 86 1.20
Magharibi 'B' 50551 500 406 101 125 0.81
Kaskazini 'A' 33305 684 639 49 52 0.93
Kaskazini 'B' 18723 304 603 62 31 1.98
Kati 25449 515 544 49 47 1.06
Kusini 11060 238 233 46 47 0.98
Micheweni 30260 334 483 91 63 1.45
Wete 39645 561 710 71 56 1.27
Chake-Chake 34608 432 619 80 56 1.43
Mkoani 36832 402 638 92 58 1.59
Jumla 375955 4969 6264 76 60 1.26
UWIANO WA WANAFUNZI, MADARASA NA MIKONDO KATIKA NGAZI YA MSINGI NA KATI
(DAR I - KID 4) KWA UCHAMBUZI WA KIWILAYA: SKULI ZA SERIKALI, MACHI - 2019
WILAYA
UANDIKISHAJI
MIKONDO
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 263
JADWELI NAM. 44(c)
MADARASA WANAFUNZI WANAFUNZI WASTANI WA
(VYUMBA VYA KWA CHUMBA KWA MKONDO SHIFTI ZA
(DAR 1 -KIDATO.4) KUSOMEA) KIMOJA MMOJA MASOMO
Mjini 9767 359 359 27 27 1.00
Magharibi 'A' 7438 316 292 24 25 0.92
Magharibi 'B' 19256 719 865 27 22 1.20
Kaskazini 'A' 532 28 19 19 28 0.68
Kaskazini 'B' 818 31 30 26 27 0.97
Kati 1739 65 64 27 27 0.98
Kusini 672 26 26 26 26 1.00
Micheweni 599 17 18 35 33 1.06
Wete 1026 33 28 31 37 0.85
Chake-Chake 2920 99 80 29 37 0.81
Mkoani 499 13 13 38 38 1.00
Jumla 45266 1706 1794 27 25 1.05
WILAYA
UANDIKISHAJI
MIKONDO
UWIANO WA WANAFUNZI, MADARASA NA MIKONDO KATIKA NGAZI YA MSINGI
NA KATI KWA UCHAMBUZI WA KIWILAYA: SKULI ZA BINAFSI, MACHI - 2019
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 264
JADWELI NAM. 45(a)
UANDIKISHAJI
WA WANAFUNZI
(DAR I - KID 6) WALIOSOMEA WASIOSOMEA JUMLA ALIYESOMEA ASIYESOMEA JUMLA
Mjini 56560 2513 80 2593 23 707 22
Magharibi 'B' 58297 1907 43 1950 31 1356 30
Magharibi 'A' 71145 2690 202 2892 26 352 25
Kaskazini 'A' 33837 1182 13 1195 29 2603 28
Kaskazini 'B' 19541 770 14 784 25 1396 25
Kati 27279 1215 9 1224 22 3031 22
Kusini 11732 448 13 461 26 902 25
Micheweni 30973 538 14 552 58 2212 56
Wete 40969 943 7 950 43 5853 43
Chake-Chake 38114 1014 30 1044 38 1270 37
Mkoani 37436 784 1 785 48 37436 48
Jumla 403882 14004 426 14430 29 948 28
UWIANO WA WANAFUNZI NA WALIMU KATIKA NGAZI YA MSINGI NA KATI (DAR.1 - KID 6)
KWA UCHAMBUZI WA KIWILAYA KATIKA SKULI ZA SERIKALI NA BINAFSI - MACHI, 2019
IDADI YA WANAFUNZI
KWA MWALIMU MMOJA
WILAYA
IDADI YA WALIMU
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 265
JADWELI NAM. 45b)
UANDIKISHAJI WA
WANAFUNZI
(DAR I - KID 6) WALIOSOMEA WASIOSOMEA JUMLA ALIYESOMEA ASIYESOMEA JUMLA
Mjini 46728 1984 14 1998 24 3338 23
Magharibi 'A' 50859 1441 0 1441 35 0 35
Magharibi 'B' 51273 1617 7 1624 32 7325 32
Kaskazini 'A' 33305 1109 7 1116 30 4758 30
Kaskazini 'B' 18723 720 7 727 26 2675 26
Kati 25449 1103 4 1107 23 6362 23
Kusini 11060 410 0 410 27 0 27
Micheweni 30374 525 2 527 58 15187 58
Wete 39943 887 2 889 45 19972 45
Chake-Chake 35194 869 8 877 40 4399 40
Mkoani 36937 755 1 756 49 36937 49
Jumla 379845 11420 52 11472 33 7305 33
IDADI YA WANAFUNZI KWA
UWIANO WA WANAFUNZI NA WALIMU KATIKA NGAZI YA MSINGI NA KATI (DAR.1 - KID 6)
KWA UCHAMBUZI WA KIWILAYA KATIKA SKULI ZA SERIKALI - MACHI, 2019
WILAYA
IDADI YA WALIMU MWALIMU MMOJA
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 266
JADWELI NAM. 45(c)
UANDIKISHAJI
WA WANAFUNZI
(DAR I - KID 6) WALIOSOMEA WASIOSOMEA JUMLA ALIYESOMEA ASIYESOMEA JUMLA
Mjini 9832 529 66 595 19 149 17
Magharibi 'A' 7438 466 43 509 16 173 15
Magharibi 'B' 19872 1073 195 1268 19 102 16
Kaskazini 'A' 532 73 6 79 7 89 7
Kaskazini 'B' 818 50 7 57 16 117 14
Kati 1830 112 5 117 16 366 16
Kusini 672 38 13 51 18 52 13
Micheweni 599 13 12 25 46 50 24
Wete 1026 56 5 61 18 205 17
Chake-Chake 2920 145 22 167 20 133 17
Mkoani 499 29 0 29 17 0 17
Jumla 46038 2584 374 2958 18 123 16
KWA MWALIMU MMOJAIDADI YA WALIMU
UWIANO WA WANAFUNZI NA WALIMU KATIKA NGAZI YA MSINGI NA KATI (DAR.1 - KID 6)
KWA UCHAMBUZI WA KIWILAYA KATIKA SKULI ZA BINAFSI - MACHI, 2019
WILAYA
IDADI YA WANAFUNZI
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 267
W'KE J'LA W'KE J'LA W'KE J'LA W'KE J'LA W'KE J'LA W'KE J'LA W'KE J'LA
Mjini 4 4 72 72 1 1 0 0 30 30 3 3 110 110
Magharibi 'A' 3 3 70 71 3 3 0 0 25 25 0 1 101 103
Magharibi 'B' 0 0 60 61 0 2 0 0 34 34 3 3 97 100
Kaskazini 'A' 0 0 77 81 1 1 4 4 21 21 0 0 103 107
Kaskazini 'B' 1 1 43 43 1 1 0 0 7 7 0 0 52 52
Kati 2 3 89 91 0 0 1 1 21 22 1 1 114 118
Kusini 1 1 42 42 0 0 0 0 4 4 1 1 48 48
Micheweni 0 0 19 22 0 0 0 0 13 14 0 0 32 36
Wete 7 8 43 48 1 3 0 0 6 6 0 0 57 65
Chake-Chake 3 3 48 49 0 0 0 0 3 3 0 0 54 55
Mkoani 2 2 46 50 1 1 0 0 9 10 0 0 58 63
Jumla 23 25 609 630 8 12 5 5 173 176 8 9 826 857
JUMLA
IDADI NA AINA MBALI MBALI ZA WALIMU WA
MAANDALIZI WALIOSOMEA KWA UCHAMBUZI WA KIWILAYA
KATIKA SKULI ZA SERIKALI, MACHI - 2019
Jadweli nam. 46a
WILAYACHINI YA KID 4 KID. 4 KID.6 FTC DIPLOMA DIGRII NA ZAIDI
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 268
W'KE J'LA W'KE J'LA W'KE J'LA W'KE J'LA W'KE J'LA W'KE J'LA W'KE J'LA
Mjini 2 2 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 2 2
Magharibi 'A' 2 2 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 2 2
Magharibi 'B' 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Kaskazini 'A' 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Kaskazini 'B' 0 0 1 1 0 0 0 0 0 0 0 0 1 1
Kati 0 0 2 2 0 0 0 0 0 0 0 0 2 2
Kusini 0 0 2 2 0 0 0 0 0 0 0 0 2 2
Micheweni 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Wete 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Chake-Chake 0 0 1 1 0 0 0 0 0 0 0 0 1 1
Mkoani 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Jumla 4 4 6 6 0 0 0 0 0 0 0 0 10 10
Jadweli nam. 46b
JUMLA
IDADI NA AINA MBALI MBALI ZA WALIMU WA
MAANDALIZI WASIOSOMEA KWA UCHAMBUZI WA KIWILAYA
KATIKA SKULI ZA SERIKALI, MACHI - 2019
WILAYACHINI YA KID 4 KID. 4 KID.6 FTC DIPLOMA DIGRII NA ZAIDI
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 269
ME KE ME KE ME KE ME KE ME KE ME KE ME KE
Mjini 0 4 24 396 0 2 0 0 68 378 13 49 105 829 934
Magharibi 'A' 0 1 23 226 0 6 5 4 38 432 16 91 82 760 842
Magharibi 'B' 0 5 36 336 0 1 0 0 38 406 10 73 84 821 905
Kaskazini 'A' 0 2 86 159 5 4 0 13 95 215 26 52 212 445 657
Kaskazini 'B' 0 1 55 166 0 3 0 0 53 146 8 39 116 355 471
Kati 0 0 78 176 4 10 1 5 68 250 17 45 168 486 654
Kusini 0 0 48 93 0 0 0 0 24 62 7 8 79 163 242
Micheweni 2 5 33 46 2 0 0 0 80 108 16 18 133 177 310
Wete 4 5 61 146 13 2 5 0 79 175 14 32 176 360 536
Chake-Chake 0 1 44 195 0 4 0 0 49 188 9 40 102 428 530
Mkoani 2 5 71 121 6 3 0 0 63 119 9 20 151 268 419
Jumla 8 29 559 2060 30 35 11 22 655 2479 145 467 1408 5092 6500
Jadweli nam. 46c
JUMLA
KUU
JUMLA
IDADI NA AINA MBALI MBALI ZA WALIMU WA
MSINGI ( DAR. I - VI ) WALIOSOMEA KWA UCHAMBUZI WA KIWILAYA
KATIKA SKULI ZA SERIKALI, MACHI - 2019
WILAYACHINI YA KID 4 KID. 4 KID. 6 FTC DIPLOMA DIGRII NA ZAIDI
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 270
ME KE ME KE ME KE ME KE ME KE ME KE ME KE
Mjini 0 0 0 1 0 0 0 0 0 0 0 0 0 1 1
Magharibi 'A' 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Magharibi 'B' 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Kaskazini 'A' 0 0 2 0 0 0 0 0 0 0 0 0 2 0 2
Kaskazini 'B' 0 0 2 2 0 0 0 0 0 0 0 0 2 2 4
Kati 1 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 1 0 1
Kusini 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Micheweni 0 1 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 1 1
Wete 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Chake-Chake 2 0 2 0 1 0 0 0 0 0 0 0 5 0 5
Mkoani 0 0 0 0 0 1 0 0 0 0 0 0 0 1 1
Jumla 3 1 6 3 1 1 0 0 0 0 0 0 10 5 15
Jadweli nam. 46d
JUMLA
KUU
JUMLA
IDADI NA AINA MBALI MBALI ZA WALIMU WA
MSINGI ( DAR. I - VI ) WASIOSOMEA KWA UCHAMBUZI WA KIWILAYA
KATIKA SKULI ZA SERIKALI, MACHI - 2019
WILAYACHINI YA KID 4 KID. 4 KID. 6 FTC DIPLOMA DIGRII NA ZAIDI
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 271
JUMLA
ME KE ME KE ME KE ME KE ME KE ME KE ME KE KUU
Mjini 0 0 8 14 2 1 0 0 67 167 292 499 369 681 1050
Magharibi 'A' 1 1 4 1 1 0 1 1 41 92 137 319 185 414 599
Magharibi 'B' 0 0 2 12 1 1 0 1 57 132 165 341 225 487 712
Kaskazini 'A' 0 0 16 5 0 1 0 0 74 45 192 119 282 170 452
Kaskazini 'B' 0 0 5 1 0 0 0 0 28 32 105 78 138 111 249
Kati 1 0 13 2 3 0 0 0 79 40 172 139 268 181 449
Kusini 0 0 8 2 1 0 0 0 45 14 66 32 120 48 168
Micheweni 0 0 2 0 3 0 0 1 22 18 138 31 165 50 215
Wete 0 0 2 0 0 0 0 0 45 35 171 98 218 133 351
Chake-Chake 0 0 1 2 3 0 1 1 33 26 143 129 181 158 339
Mkoani 0 0 2 1 0 0 1 0 75 42 147 68 225 111 336
Jumla 2 1 63 40 14 3 3 4 566 643 1728 1853 2376 2544 4920
Jadweli nam. 46e
JUMLA
IDADI NA AINA MBALI MBALI ZA WALIMU WA SEKONDARI
(KIDATO 1 - 6) WALIOSOMEA KWA UCHAMBUZI WA KIWILAYA
KATIKA SKULI ZA SERIKALI, MACHI - 2019
WILAYACHINI YA KID 4 KID. 4 KID. 6 FTC DIPLOMA DIGRII NA ZAIDI
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 272
JUMLA
ME KE ME KE ME KE ME KE ME KE ME KE ME KE KUU
Mjini 0 0 0 0 0 0 2 0 0 0 7 4 9 4 13
Magharibi 'A' 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Magharibi 'B' 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 7 0 7 0 7
Kaskazini 'A' 0 0 1 0 0 0 1 0 2 0 1 0 5 0 5
Kaskazini 'B' 0 0 0 0 2 1 0 0 0 0 0 0 2 1 3
Kati 0 0 0 0 0 0 2 0 0 0 1 0 3 0 3
Kusini 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Micheweni 0 0 0 0 0 0 1 0 0 0 0 0 1 0 1
Wete 0 0 0 0 1 0 0 1 0 0 0 0 1 1 2
Chake-Chake 0 0 0 0 0 0 0 0 1 0 2 0 3 0 3
Mkoani 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Jumla 0 0 1 0 3 1 6 1 3 0 18 4 31 6 37
Jadweli nam. 46f
JUMLA
IDADI NA AINA MBALI MBALI ZA WALIMU WA SEKONDARI
( KIDATO 1 - 6 ) WASIOSOMEA KWA UCHAMBUZI WA KIWILAYA
KATIKA SKULI ZA SERIKALI, MACHI - 2019
WILAYACHINI YA KID 4 KID. 4 KID. 6 FTC DIPLOMA DIGRII NA ZAIDI
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 273
MCHANGO WA
SMZ RUZUKU MKOPO
0000P001 Uimarishaji wa Elimu ya Maandalizi 8,469,702,000 8,469,702,000
0000P002 Uimarishaji wa Elimu ya Lazima 3,300,000,000 52,104,346,000 55,404,346,000
0000P003 Uimarishaji wa Elimu Mbadala na Amali 1,000,000,000 7,000,000,000 8,000,000,000
00000P004 Kupanga na Kusimamia kazi za Wizara 1,500,000,000 1,500,000,000
JUMLA 5,800,000,000 8,469,702,000 59,104,346,000 73,374,048,000
JADWELI NAM.47
MAKADIRIO NA MATUMIZI YA FEDHA ZA MIRADI YA MAENDELEO KWA MWAKA WA FEDHA 2019/2020
MAKAMDIRIO KWA MWAKA
MRADIKASMA MAKADIRIO YA MISAADAJUMLA
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 274
JADWELI NAM. 48
KIFUNGU MAELEZO MAKISIO YA
MAPATO
KILICHOPATIKANA JULAI
2018 - APRILI 2019%
0401/142201 LESENI ZA WALIMU 55,000,000.00 55,635,882.00 101.16%
0401/142202 LESENI ZA USAJILI SKULI BINAFSI 49,095,000.00 26,549,746.00 54.08%
JUMLA 104,095,000.00 82,185,628.00 78.95%
FEDHA ZA MAPATO ZILIZOKUSANYWA KWA KIPINDI CHA JULAI 2018 - APRILI 2019
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 275
JADWELI NAM. 49
KASMA MAELEZO MAKISIO YA
MAPATO
1422001 LESENI ZA USAJILI WA SKULI BINAFSI 96,828,000.00
1422002 LESENI ZA WALIMU 98,827,000.00
JUMLA 195,655,000.00
MAKISIO YA MAPATO KIKASMA KWA MWAKA 2019/2020
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwaka 2019/2020 276
SMZ WAHISANI JUMLA
1 Maandalizi na Msingi 383,709,000 157,169,000 - 8,469,702,000 8,469,702,000 9,010,580,000
2 Elimu ya Sekondari 42,362,596,000 6,824,440,000 3,300,000,000 52,104,346,000 55,404,346,000 104,591,382,000
Mafunzo ya Ualimu 585,136,000 428,531,000 - - - 1,013,667,000
Chuo Kikuu cha Taifa 10,739,100,000 500,000,000 - - - 11,239,100,000
Karume 1,205,900,000 420,100,000 - - - 1,626,000,000
Bodi ya Mkopo 298,600,000 10,000,000,000 - - - 10,298,600,000
Chuo cha Kiislamu 599,700,000 106,000,000 - - - 705,700,000
Jumla ndogo 13,428,436,000 11,454,631,000 - - - 24,883,067,000
Elimu Mbadala - -
Elimu Mbadala 438,941,000 535,304,000 1,000,000,000 7,000,000,000 8,000,000,000 8,974,245,000
Elimu ya Amali 1,261,200,000 6,500,000,000 - - - 7,761,200,000
Jumla ndogo 1,700,141,000 7,035,304,000 1,000,000,000 7,000,000,000 8,000,000,000 16,735,445,000
Taasisi ya Elimu 271,500,000 301,600,000 - - - 573,100,000
Baraza la Mitihani 424,800,000 4,517,000,000 - - - 4,941,800,000
Ukaguzi wa Elimu 756,900,000 333,600,000 - - - 1,090,500,000
Michezo katika Elimu 172,660,000 579,611,000 - - - 752,271,000
Baraza la Elimu 149,400,000 100,200,000 - - - 249,600,000
Huduma za Maktaba 393,100,000 493,100,000 - - - 886,200,000
Teknolojia ya Habari na Mawasiliano 248,334,000 278,059,000 - - - 526,393,000
Elimu Mjumuisho - 77,610,000 - - - 77,610,000
Jumla ndogo 2,416,694,000 6,680,780,000 - - - 9,097,474,000
Utawala na Uendeshaji 2,460,139,000 3,631,832,000 - - - 6,091,971,000
Mipango, Sera na Utafiti 495,453,000 3,238,099,000 1,500,000,000 - 1,500,000,000 5,233,552,000
Uratibu wa shughuli za Elimu Pemba 2,570,433,000 703,245,000 - - - 3,273,678,000
Jumla ndogo 5,526,025,000 7,573,176,000 1,500,000,000 - 1,500,000,000 14,599,201,000
Jumla kuu 65,817,601,000 39,725,500,000 5,800,000,000 67,574,048,000 73,374,048,000 178,917,149,000
JADWELI NAM. 50
MAKISIO YA MATUMIZI YA WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA AMALI
KWA PROGRAMU MWAKA 2019/2020
NAM. PROGRAMU MSHAHARAMATUMIZI YA
KAWAIDA
BAJETI YA MAENDELEO JUMLA KWA
PROGRAM
3 Elimu ya Juu
4
5 Ubora wa Elimu
6 Uratibu wa shughuli za Wizara