81
SERIKALI YA MAPINDUZI ZANZIBAR OFISI YA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI ZANZIBAR RIPOTI YA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI KWA MASHIRIKA NA TAASISI ZA SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR KWA MWAKA WA FEDHA 2015/2016

SERIKALI YA MAPINDUZI ZANZIBAR - OCAGZ1 RIPOTI YA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI KWA MASHIRIKA NA TAASISI ZA SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR - KWA MWAKA WA FEDHA

  • Upload
    others

  • View
    19

  • Download
    0

Embed Size (px)

Citation preview

  • SERIKALI YA MAPINDUZI ZANZIBAR

    OFISI YA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA

    HESABU ZA SERIKALI ZANZIBAR

    RIPOTI YA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA

    HESABU ZA SERIKALI

    KWA MASHIRIKA NA TAASISI ZA SERIKALI

    YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR

    KWA MWAKA WA FEDHA 2015/2016

  • ii

    YALIYOMO

    SURA YA KWANZA…………………………………………………………………………………..……1

    1.0 UTANGULIZI ...................................................................................................... 1

    2.0 MAJUKUMU YA OFISI YA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI . 1

    3.0 UPEO NA MADHUMUNI YA RIPOTI YA UKAGUZI ................................................... 2

    4.0 NJIA ZILIZOTUMIKA KATIKA UKAGUZI ................................................................. 3

    5.0 MAJUKUMU YA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI ............... 5

    6.0 UMUHIMU WA KUFANYA UKAGUZI ....................................................................... 5

    7.0 SHUKURANI ....................................................................................................... 6

    SURA YA PILI……………………………………………………..………………………………………..7

    8.0 MATOKEO YA UKAGUZI KWA MWAKA 2015/2016 .................................................. 7

    9.0 UTEKELEZAJI WA HOJA ZA UKAGUZI ULIOPITA WA MWAKA WA FEDHA 2014/2015 7

    10.0 UWASILISHAJI WA HESABU ZA MWISHO WA MWAKA 2015/2016 KWA AJILI YA UKAGUZI ...................................................................................................................... 7

    11.0 AINA YA HATI ZA UKAGUZI ............................................................................... 10

    SURA YA TATU………………………………………………………………………………………….…13

    12.0 MAMBO YALIYOBAINIKA KATIKA UKAGUZI WA MASHIRIKA NA TAASISI ZA SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR ........................................................................ 13

    13.0 UKAGUZI WA HESABU ZA MWISHO WA MWAKA 2015/2016 ................................. 13

    14.0 SHIRIKA LA MAGAZETI ..................................................................................... 13

    15.0 SHIRIKA LA UTANGAZAJI ZANZIBAR (ZBC) ......................................................... 20

    16.0 CHUO CHA KILIMO –KIZIMBANI ........................................................................ 25

    17.0 MAMLAKA YA MAJI ZANZIBAR (ZAWA) ............................................................... 29

    18.0 MAMLAKA YA VITEGA UCHUMI ZANZIBAR (ZIPA) ................................................ 37

    19.0 CHUO CHA UTAWALA WA UMMA -IPA ................................................................ 42

    20.0 CHUO CHA MAENDELEO YA UTALII ZANZIBAR (ZITOD) ...................................... 47

    21.0 CHUO CHA UANDISHI WA HABARI. .................................................................... 52

    22.0 CHUO CHA SAYANSI ZA AFYA ZANZIBAR ............................................................ 57

    23.0 CHUO KIKUU CHA TAIFA ZANZIBAR (SUZA) ....................................................... 61

  • iii

    24.0 SHIRIKA LA MELI NA UWAKALA ......................................................................... 65

    25.0 MAMLAKA YA UVUVI WA BAHARI KUU ............................................................... 70

    26.0 SHIRIKA LA BANDARI ZANZIBAR ....................................................................... 74

  • 1

    RIPOTI YA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA

    SERIKALI KWA MASHIRIKA NA TAASISI ZA SERIKALI YA

    MAPINDUZI YA ZANZIBAR - KWA MWAKA WA FEDHA

    2015/2016

    SURA YA KWANZA

    1.0 UTANGULIZI

    Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali anawajibika kukagua mahesabu

    yote ya Serikali, Mashirika ya Umma ,Taasisi za umma pamoja na Miradi mbali mbali

    ya maendeleo na baadae kutoa taarifa za ukaguzi huo kila mwaka. Taarifa hiyo

    itaeleza udhibiti na uhifadhi wa fedha na mali za Umma.

    Kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 kifungu 112(5) Mdhibiti na

    Mkaguzi Mkuu wa Hesabu anawajibika kuwasilisha kila taarifa ya ukaguzi wa

    mahesabu atakayoitoa kwa mujibu wa masharti ya kifungu cha 112(3) cha Katiba.

    Kutokana na mabadiliko ya kazi za ukaguzi kumekuwa na mafanikio makubwa

    katika utendaji na uwajibikaji katika sekta za umma kwenye matumizi ya rasilimali

    za umma. Aidha, kuimarika kwa mfumo wa fedha pamoja na utekelezaji wa sheria

    za fedha na manunuzi za umma kumechangia kwa kuimarika kwa uwazi na

    uwajibikaji katika taasisi za Serikali pamoja na utekelezaji wa miradi mbali mbali ya

    maendeleo na kuleta tija kwa wananchi.

    2.0 MAJUKUMU YA OFISI YA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU

    ZA SERIKALI

    Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali anawajibika kikatiba kukagua

    mahesabu ya Taasisi za Serikali na baadae kutoa taarifa zake za ukaguzi huo kila

    mwaka. Taarifa hizo zitaelezea hali halisi za mapato na matumizi ya fedha kutoka

    Mfuko Mkuu wa Hazina ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar pamoja na utekelezaji

    wa sheria mbali mbali zikiwemo sheria za fedha, sheria za manunuzi na sheria

    nyenginezo.

    Kwa mujibu wa kifungu 112 (3) cha Katiba ya Zanzibar 1984,Mdhibiti na Mkaguzi

    Mkuu wa Hesabu anawajibika kufanya yafuatayo:-

  • 2

    “a) Kuhakikisha kwamba fedha zote zinazokusudiwa kutolewa kutoka Mfuko Mkuu

    wa Hazina ya Serikali ya Zanzibar, matumizi yake yameidhinishwa na iwapo

    nitatosheka kwamba masharti hayo yatatekelezwa ipasavyo basi nitaidhinisha fedha

    hizo zitolewe

    b) Kuhakikisha kwamba fedha zote ambazo matumizi yake yameidhinishwa

    yanatokana na fedha zilizomo katika Mfuko Mkuu wa Hazina ya Serikali ya Mapinduzi

    au fedha ambazo matumizi yake yameidhinishwa na sheria iliyotungwa na Baraza la

    Wawakilishi, na ambazo zimetumika kwa ajili ya shughuli zilizohusika na matumizi ya

    fedha hizo na kwamba matumizi yamefanywa kwa kufuata idhini iliyotolewa kuhusu

    matumizi hayo; na

    c) Angalau mara moja kwa mwaka kufanya ukaguzi na kutoa taarifa juu ya ukaguzi

    wa hesabu za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, hesabu zinazosimamiwa na

    watumishi wote wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, hesabu za Mahkama zote za

    Zanzibar, hesabu za Tume au vyombo vyengine vinavyohusika na Baraza la

    Wawakilishi ”.

    Ukaguzi wa mahesabu umefanywa kwa kuzingatia miongozo na vigezo mbali mbali

    vya ukaguzi ili kukidhi matarajio ya wadau wetu na wananchi kwa ujumla. Ofisi ya

    Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali inaendelea kufanya uchambuzi wa

    njia bora zaidi kwa kufanya ukaguzi utakaoleta tija na kuongeza wigo na maeneo

    yanayokaguliwa kwa lengo la kuimarisha utendaji na uwajibikaji katika sekta za

    umma.

    3.0 UPEO NA MADHUMUNI YA RIPOTI YA UKAGUZI

    Ripoti hii imekusanya taarifa za ukaguzi wa mahesabu ya Serikali ya Mapinduzi ya

    Zanzibar yakiwemo Mashirika ya Umma na Taasisi mbali mbali za Serikali kwa

    kuzingatia taarifa za mapato na matumizi ambazo zimeelezwa kwenye taarifa za

    ukaguzi zilizotumwa kwa Taasisi husika.

    Ukaguzi ulifanyika kwa mujibu wa viwango vya kimataifa vya taasisi kuu za ukaguzi

    (ISSAIs) ili kutoa uhakika kama taarifa za fedha zinaonyesha sura halisi. Taratibu za

    ukaguzi zinajumuisha uchambuzi na kumbukumbu za taarifa mbali mbali, mifumo ya

    udhibiti wa ndani, mifumo ya taarifa za kisheria zinazosimamia uendeshaji wa taasisi

    zilizokaguliwa.

  • 3

    Taarifa hizo zinaonesha kwa muhtasari matokeo ya ukaguzi uliofanyika kwa misingi

    ya sampuli, kwa hivyo matokeo ya ukaguzi kwa kiasi kikubwa yalitegemea

    kumbukumbu za taarifa na nyaraka tulizoziomba na kuwasilishwa kwa ajili ya

    kufanya ukaguzi.

    Taarifa hizo zilijumuisha mahesabu ya mwisho wa mwaka ambapo ziliandaliwa kwa

    mujibu wa viwango vya kitaifa na kimataifa vya uhasibu kwa sekta ya umma.

    Taarifa hizo ni kama zifuatazo: -

    I. Mizani ya Hesabu

    II. Taarifa ya Mapato na Matumizi

    III. Taarifa kuhusu mabadiliko ya mtaji

    IV. Taarifa ya mtiririko wa fedha

    V. Taarifa ya uwiano wa bajeti na kiasi halisi cha matumizi

    VI. Sera za uhasibu na maelezo ya taarifa za fedha

    4.0 NJIA ZILIZOTUMIKA KATIKA UKAGUZI

    Katika kufanya ukaguzi wa Hesabu kwa Mashirika ya Umma na Taasisi za Serikali

    tulizingatia taratibu za ukaguzi zifuatazo: -

    i. Kutoa barua za kushiriki ukaguzi kwa taasisi inayokaguliwa kabla ya kuanza kazi

    za ukaguzi inayoeleza madhumuni na upeo wa ukaguzi, maeneo yanayotarajiwa

    kufanya ukaguzi na kuelezea majukumu ya ukaguzi kwa mkaguzi (Engagement

    Letter).

    ii. Kuandaa mkakati na ujumla wa ukaguzi unaonesha muelekeo mzima wa ukaguzi,

    vigezo vitakavyotumika katika hatua za mwanzo za kutathmini Mashirika ya

    Umma na Taasisi za Serikali zinazokaguliwa.

    iii. Kufanya kikao cha kuanza kazi za ukaguzi (Entrance Meeting) ambapo katika

    kikao hicho uongozi wa Mashirika ya Umma na Taasisi za Serikali zinazokaguliwa

    kwa lengo la kupata uelewa kabla ya kuanza kazi za ukaguzi.

    iv. Kujadiliana na uongozi wa Mashirika ya Umma na Taasisi za Serikali kuhusu

    utekelezaji na utendaji kwa kipindi cha mwaka husika.

    v. Kupitia na kuhakiki nyaraka mbalimbali kwa ajili ya kupata uelewa wa shughuli za

    Mashirika ya Umma na Taasisi za Serikali.

  • 4

    vi. Kutumia njia na mbinu nyingine za ukaguzi kama ilivyoainishwa kwenye

    muongozo wa ukaguzi (Regularity Audit Manual).

    vii. Kutoa ripoti ya ukaguzi mawazo kwa uongozi ambayo itakuwa inaonyesha

    kilichobainika wakati wa ukaguzi na kutoa nafasi kwa uongozi kutoa maelezo

    kuhusu ripoti hiyo.

    viii. Kutoa rasimu ya ripoti ya ukaguzi kwa uongozi inayoeleza hoja za ukaguzi

    zilizobainishwa na kutoa muda kwa uongozi kuweza kujibu hoja hizo.

    ix. Kufanya kikao cha mwisho (Exit Meeting) na mkaguliwa baada ya kumaliza

    ukaguzi ambapo katika kikao hicho hupitia kwa pamoja hoja zilizojitokeza wakati

    wa ukaguzi.

    x. Kutoa ripoti ya mwisho kwa uongozi wa Mashirika ya Umma na Taasisi za Serikali

    inayoonesha matokeo ya ukaguzi ikiwemo hoja za ukaguzi na kutoa nafasi kwa

    uongozi na mkaguliwa kuweza kujibu hoja hizo.

    xi. Kutoa ripoti ya ukaguzi kwa uongozi inayoonesha hati ya ukaguzi aliyopata

    mkaguliwa kuhusiana na taarifa za fedha.

    Aidha mbinu za kuangalia viashiria vya maeneo hatarishi katika Mashirika ya Umma

    na Taasisi za Serikali zilizokaguliwa zilitumika katika ukaguzi ambapo mbinu hizi za

    ukaguzi zinasisitiza haja ya kuelewa kwa kina mazingira ya taasisi inayokaguliwa

    ikiwemo mfumo wa udhibiti wa ndani, kutathmini vihatarishi na kubaini viashiria

    vitakavyoathiri udhibiti wa ndani.

    Mbinu za ukaguzi zinatekelezwa kwa kutumia muongozo na utaratibu wa ukaguzi, ili

    kuhakikisha kwamba mbinu za ukaguzi zinaenda na wakati ambapo Ofisi inafanya

    mapitio ya muongozo wa utaratibu na ukaguzi kila mwaka kwa kuimarisha ukaguzi

    na kuhakikisha kwamba mabadiliko yoyote muhimu yanajitokeza katika fani ya

    ukaguzi na uhasibu pamoja na mabadiliko ya mifumo ya sheria yanazingatiwa

    ipasavyo.

    Aidha utendaji wa mashirika ya umma na taasisi za Serikali zilizokaguliwa

    umeangaliwa na kuonesha viwango vya kiutendaji kifedha na kiuendeshaji. Utendaji

    wa kifedha umepimwa kwa kuangalia faida au hasara iliyopatikana kwa kipindi cha

    mwaka husika. Utendaji wa kiuendeshaji umepimwa kwa kuangalia ni kwa kiasi gani

    taasisi imeweza kufikia malengo yake ya msingi.

  • 5

    5.0 MAJUKUMU YA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA

    SERIKALI

    Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali anawajibika kikatiba kukagua

    mahesabu ya Mashirika ya Serikali pamoja na Taasisi za Serikali kama ilivyoainishwa

    katika Katiba ya Zanzibar,1984 na sheria nyenginezo na baadae kutoa taarifa zake

    za ukaguzi huo kila mwaka. Taarifa hizo zitaelezea hali halisi za mapato na

    matumizi ya fedha pamoja na utekelezaji wa sheria mbali mbali zikiwemo sheria za

    fedha, sheria za manunuzi na sheria nyenginezo.

    Baada ya kumaliza ukaguzi Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali

    anawajibika kutoa maoni juu ya mahesabu hayo na kuonesha hali halisi ya taarifa za

    hesabu iwapo zinatoa sura sahihi na halisi kwa kipindi kilichokaguliwa. Maoni hayo

    yatahusiana na mambo yafuatayo: -

    i. Kutoa ushauri juu ya mambo yanayohitaji kufanyiwa marekebisho kuhusiana

    na shughuli za Taasisi zinazokaguliwa.

    ii. Kuzuia na kupunguza matumizi ya Fedha za umma yasiyokua na tija

    iii. Kuongeza makusanyo na kuzuia upotevu wa fedha na rasilimali za umma.

    iv. Kuzuia hasara au kutoa tahadhari juu ya hasara inayoweza kutokea kwa

    uzembe, upotevu,kukosa uaminifu,udanganyifu au rushwa kuhusiana na

    fedha au rasilimali za umma.

    v. Kuongeza uchumi, tija na ufanisi katika kutumia fedha za umma.

    6.0 UMUHIMU WA KUFANYA UKAGUZI

    Lengo kuu la kufanya ukaguzi ni kumuwezesha Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa

    Hesabu za Serikali kutoa maoni ya ukaguzi huru kuhusiana na hesabu za Taasisi

    zilizokaguliwa ikiwemo Wizara, Idara, Wakala na Serikali pamoja na Mamlaka mbali

    mbali za Serikali. Vile vile kubaini kwamba hesabu hizo kama zinatayarishwa kwa

    kuzingatia viwango vya kitaifa na kimataifa vya Uhasibu katika sekta ya umma au

    kwa viwango vya kimatifa vya taarifa za fedha. Ufanisi wa ukaguzi unategemea

    mawasiliano mazuri na uongozi wa taasisi inayokaguliwa.

    Aidha tunahakikisha kwamba ukaguzi tunaofanya unalenga kutoa kipaumbele katika

    maeneo muhimu ili kuchangia maendeleo katika sekta za umma na hatimae

    kuimarisha maendeleo ya wananchi kwa ujumla.

  • 6

    Ni imani yangu kwamba kuimarika kwa kazi za ukaguzi kutaongeza na kuimarisha

    uwazi na uwajibikaji katika mapato na matumizi ya fedha na rasilimali za umma na

    tunategemea ufanisi na tija vinapatikana kwa kila rasilimali itakayotumika kwa ajili

    ya maendeleo ya wananchi na taifa kwa jumla.

    7.0 SHUKURANI

    Napenda kutoa shukurani kwa wote waliochangia kwa namna moja au nyengine

    kuanzia kazi za ukaguzi, ufuatiliaji maeneo mbali mbali yaliyokaguliwa hadi

    kukamilika kwa ripoti hii ya ukaguzi ya mwaka 2015/2016.

    Aidha, natoa shukrani zangu za dhati kwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa

    jitihada mbali mbali zinazochukuliwa katika kuimarisha Ofisi hii kiutendaji na

    watendaji kwa ujumla. Vile vile napenda kuwapongeza na kuwashukuru

    wafanyakazi wote wa Ofisi hii kwa juhudi zao wanazochukuwa hadi kufanikisha

    kukamilika kwa ripoti hii kwa wakati.

    Hali kadhalika, ninawashukuru viongozi na watendaji wakuu wa Serikali ya

    Mapinduzi ya Zanzibar na watendaji wa taasisi mbali mbali za Serikali kwa

    mashirikiano mazuri wanayotupa wakati wa kutekeleza kazi zetu za ukaguzi.

    Mwisho, ninapenda kuishukuru Kamati ya Kuchunguza Hesabu za Serikali (PAC) na

    Kamati ya Kusimamia Ofisi za Viongozi Wakuu wa Kitaifa za Baraza la Wawakilishi

    na wengineo kwa ujumla wao wamechangia maendeleo makubwa yaliyopatikana

    katika Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali.

    ………………………………...

    FATMA MOHAMED SAID

    MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI

    ZANZIBAR

  • 7

    SURA YA PILI

    8.0 MATOKEO YA UKAGUZI KWA MWAKA 2015/2016

    Katika ukaguzi wa mahesabu ya mwaka 2015/2016 imebainika kwamba uwekaji wa

    kumbukumbu na taarifa mbali mbali za mahesabu ikiwemo fedha na rasilimali za umma

    pamoja na udhibiti wa ndani umeimarika.

    9.0 UTEKELEZAJI WA HOJA ZA UKAGUZI ULIOPITA WA MWAKA WA FEDHA

    2014/2015

    Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu imekuwa ikitoa ripoti zenye ushauri na

    mapendekezo mbalimbali katika usimamizi wa matumizi ya rasilimali za umma kwa

    lengo la kuwa na utawala bora unaoheshimu sheria za fedha na manunuzi na sheria

    nyenginezo.

    Kufuatia tathmini ya utekelezaji wa mapendekezo yaliyotolewa tumebaini kwamba

    mapendekezo yaliyotolewa katika ripoti za ukaguzi za mwaka uliopita 2014/2015

    yamefanyiwa kazi na kuonesha matumaini ya kuimarika kwa nidhamu ya matumizi ya

    fedha na rasilimali za umma.

    Tunapongeza juhudi zinazochukuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika

    kusimamia nidhamu ya matumizi ya fedha na rasilimali za umma na kupelekea

    kuimarika kwa utendaji na uwajibikaji katika Mashirika na Taasisi za umma.

    Hata hivyo kumejitokeza dosari za usimamizi wa fedha na ukiukwaji wa sheria za fedha

    na manunuzi ya umma kwa baadhi ya Mashirika na Taasisi na kupelekea mapungufu

    katika hesabu za mwisho wa mwaka.

    10.0 UWASILISHAJI WA HESABU ZA MWISHO WA MWAKA 2015/2016 KWA

    AJILI YA UKAGUZI

    Kwa mujibu wa kifungu namba 24(2) cha sheria ya fedha No. 12, 2005, inazitaka

    Taasisi zote za Serikali zitayarishe na kuwasilishwa kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa

    Hesabu za Serikali, hesabu za mwaka, zinazojumuisha Mapato na matumizi ya Taasisi

    husika. Aidha kifungu No.8 cha sheria hiyo, kinawataka wasimamizi wa fedha katika

    Taasisi za Serikali kuwasilisha kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali,

    hesabu zao za mwisho wa mwaka ndani ya miezi mitatu baada ya kukamilika kipindi cha

    mwaka.

  • 8

    Tunatoa pongezi kwa Mashirika na Taasisi mbali mbali za Serikali kwa jitihada

    walizochukuwa za kuwasilisha hesabu za mwisho wa mwaka kwa mujibu wa sheria.

    Uwasilishwaji wa hesabu za mwisho wa mwaka kwa ajili ya ukaguzi kutoka kwa

    Mashirika na Taasisi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ni kama ifuatavyo: -

    Nam Fungu Shirika/Taasisi Tarehe iliyowasilishwa kwa

    ukaguzi

    2014/2015 2015/2016

    1. Ruzuku Shirika la Magazeti 01/10/2015 30/09/2016

    2. Ruzuku Shirika la Utangazaji

    Zanzibar

    29/09/2015 26/07/2016

    3. Ruzuku Chuo cha Kilimo

    Kizimbani

    28/09/2015 27/09/2016

    4. Ruzuku Mamlaka ya Maji (ZAWA) 29/09/2015 29/09/2016

    5. Ruzuku Mamlaka ya Vitega

    Uchumi Zanzibar(ZIPA)

    10/09/2015 30/09/2016

    6. Ruzuku Chuo cha Utawala wa

    Umma

    29/09/2015 30/09/2016

    7. Ruzuku Chuo cha Maendeleo ya

    Utalii

    30/09/2015 30/09/2016

    8. Ruzuku Chuo cha Uandishi wa

    Habari

    30/09/2015 30/09/2016

    9. Ruzuku Chuo cha Sayansi za Afya

    Zanzibar

    23/10/2015 09/11/2016

    10. Ruzuku Chuo Kikuu cha Taifa

    (SUZA)

    23/09/2015 27/09/2016

    11. Ruzuku Mamlaka ya Uvuvi wa

    Bahari Kuu

    29/09/2015 29/09/2016

  • 9

    12. Linajitegemea Shirika la Bandari 28/09/2015 09/09/2016

    13. Ruzuku Shirika la Meli na

    Uwakala

    23/09/2015 27/09/2016

    14. Linajitegemea Shirika la Biashara la

    Taifa (ZSTC)

    Haikuwasilishwa

    kwa wakati

    Haikuwasilishwa

    kwa wakati

  • 10

    11.0 AINA YA HATI ZA UKAGUZI

    Hati za ukaguzi zinatolewa kutokana na matokeo ya ukaguzi ambapo hati hizo huonesha

    aina ya hati inayotolewa kulingana na taarifa za mahesabu yaliyokaguliwa yenye

    kuonyesha hali halisi ya mahesabu hayo.

    Aina tofauti ya hati za ukaguzi zinatolewa kwa mazingira tofauti kulingana na usahihi wa

    hesabu zilizokaguliwa. Hati zenyewe ni kama zifuatazo:-

    Hati inayoridhisha, Hati isiyoridhisha, Hati yenye mashaka na Hati mbaya.

    11.1 Hati inayoridhisha

    Hati ya aina hii inatolewa pale ambapo ukaguzi umejiridhisha kutokana na kukidhi

    viwango vilivyotumika katika uaandaji wa mahesabu, usahihi wa taarifa pamoja na

    ushahidi uliopatikana wakati wa ukaguzi, na kupelekea kutoa sura sahihi na halisi ya

    mahesabu hayo.

    11.2 Hati isiyoridhisha

    Hati ya aina hii inatolewa pale ambapo ukaguzi umejiridhisha kwamba taarifa za

    mahesabu zilizoandaliwa imebainika kuwa zina dosari kubwa na za umuhimu, dosari

    ambazo zinaweza kusababisha taarifa za hesabu kupoteza uhalisia wake na hivyo

    kutoaminiwa na kupelekea kutokuonyesha sura sahihi na halisi ya mahesabu hayo.

    11.3 Hati yenye shaka

    Hati ya aina hii hutolewa baada ya Ukaguzi kujiridhisha kuwa, kulingana na ushahidi wa

    kiukaguzi mambo yafuatayo yamejitokeza.

    Taarifa za fedha zilizoandaliwa zina dosari kubwa ambazo zinaweza kuathiri

    mahesabu endapo zikichukuliwa aidha moja baada ya moja au kwa ujumla wake

    kwenye taarifa hizo haitoweza kuleta sura sahihi na halisi za mahesabu hayo.

    Pale ambapo Ukaguzi umeshindwa kupata taarifa, nyaraka na vielelezo vya kutosha

    vitakavyosaidia kufanya ukaguzi na kuweza kutoa maoni ya ukaguzi kwa mahesabu

    hayo.

    Kuwepo kwa kiasi kikubwa cha mapato na matumizi yasiyokua na nyaraka muhimu

    na kufanya matumizi bila ya kuwa na kibali halali au matumizi ya mapato ambayo

    hayakuidhinishwa kutumika.

  • 11

    Kutozingatiwa kwa Sheria na kanuni mbalimbali ambapo kunapelekea madhara

    makubwa ambayo yanaweza kusababisha kutokutoa sura sahihi na halisi ya

    mahesabu hayo kwa mfano, kuwa na vitu ambavyo vilitakiwa kuripotiwa kwenye

    taarifa za mahesabu lakini havikuripotiwa na manunuzi ya vifaa hayakufuata Sheria

    na kanuni za manunuzi.

    Kufanya matumizi ambayo hayakuleta tija kwa Taasisi husika.

    Kutofanyika kwa usuluhisho wa benki hali inayopelekea kushindwa kupata usahihi

    wa salio la fedha mwishoni mwa mwaka wa fedha.

    11.4 Hati mbaya

    Hati hii hutolewa pale ambapo ukaguzi umeshindwa kupata nyaraka na vielelezo vya

    kutosha wakati wa ukaguzi ili kuweza kutoa maoni ya ukaguzi kutokana na mapungufu

    yaliyojitokeza na kushindwa kugundua mambo ambayo yanaweza kusababisha madhara

    makubwa katika Mashirika na Taasisi.

    Hati zilizotolewa ni kama ifuatavyo: -

    Nam Fungu Shirika/Taasisi Aina ya Hati

    iliyotolewa

    2015/2016

    1. Ruzuku Shirika la Magazeti Hati inayoridhisha

    2. Ruzuku Shirika la Utangazaji Zanzibar Hati inayoridhisha

    3. Ruzuku Chuo cha Kilimo Kizimbani Hati inayoridhisha

    4. Ruzuku Mamlaka ya Maji (ZAWA) Hati inayoridhisha

    5. Ruzuku Mamlaka ya Vitega Uchumi

    Zanzibar(ZIPA)

    Hati inayoridhisha

    6. Ruzuku Chuo cha Utawala wa Umma Hati inayoridhisha

    7. Ruzuku Chuo cha Maendeleo ya Utalii Hati inayoridhisha

    8. Ruzuku Chuo cha Uandishi wa Habari Hati inayoridhisha

  • 12

    9. Ruzuku Chuo cha Sayansi za Afya

    Zanzibar

    Hati inayoridhisha

    10. Ruzuku Chuo Kikuu cha Taifa (SUZA) Hati inayoridhisha

    11. Ruzuku Mamlaka ya Uvuvi wa Bahari Kuu Hati inayoridhisha

    12. Linajitegemea Shirika la Bandari Hati inayoridhisha

    13. Ruzuku Shirika la Meli na Uwakala Hati inayoridhisha

  • 13

    SURA YA TATU

    12.0 MAMBO YALIYOBAINIKA KATIKA UKAGUZI WA MASHIRIKA NA

    TAASISI ZA SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR

    Ukaguzi uliofanyika katika Mashirika na Taasisi mbali mbali za Serikali ya Mapinduzi ya

    Zanzibar imebainika kujitokeza kwa kasoro za kiutendaji kwa baadhi ya Mashirika na

    Taasisi hizo ambapo hoja mbali mbali za ukaguzi ziliainishwa katika ripoti za ukaguzi

    zilizotolewa kwa Mashirika na Taasisi hizo na baadhi ya hoja hizo zilipatiwa maelezo na

    vielelezo vilivyokosekana wakati wa ukaguzi.

    13.0 UKAGUZI WA HESABU ZA MWISHO WA MWAKA 2015/2016

    Ukaguzi wa hesabu za mwisho wa mwaka 2015/2016 umebaini kwamba kumekuwa na

    mabadiliko makubwa katika uwekaji wa kumbukumbu za mahesabu pamoja na udhibiti

    mzuri wa rasilimali za umma na kupelekea mafanikio katika ufungaji wa hesabu za

    mwisho wa mwaka kwa Mashirika na Taasisi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

    Matokeo ya ukaguzi wa hesabu hizo kwa Mashirika na Taasisi za Serikali pamoja na

    maoni ya ukaguzi wa hesabu hizo ni kama ifuatavyo: -

    14.0 SHIRIKA LA MAGAZETI

    14.1 TAARIFA YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA 2015/2016

    Taarifa ya Mapato

    Mapato ya Shirika la Magazeti yameonekana kupanda kutoka shilingi 1,233,854,256 kwa

    mwaka 2014/2015 hadi kufikia shilingi 1,369,924,774 kwa mwaka 2015/2016 kukiwa na

    ongezeko la shilingi 136,070,518 sawa na asilimia 11 ya ongezeko.

    Taarifa ya Matumizi

    Matumizi ya Shirika la Magazeti yameonekana kupungua kutoka shilingi 684,011,998

    kwa mwaka 2014/2015 hadi kufikia shilingi 616,889,381 kwa mwaka 2015/2016 kukiwa

    na upungufu wa shilingi 67,122,617 sawa na asilimia 10 ya mapungufu.

  • 14

    14.2 HESABU ZA MWISHO WA MWAKA 2015/2016.

    THE CORPORATION OF GOVERNMENT NEWSPAPER (CGN)

    AS AT 30TH JUNE 2016

    STATEMENT OF FINANCIAL POSITION

    Assets Notes 2015/16 2014/15

  • 15

    Uchambuzi wa hesabu za mwisho wa mwaka.

    Uwiano wa mali za Mpito ukilinganisha na Dhima za Mpito kwa mujibu wa hesabu za

    mwisho wa mwaka ni kama ifuatavyo: -

    Uchambuzi wa hapo juu unaonesha uwiano wa mali za mpito ni mkubwa ukilinganisha

    na dhima za mpito. Hata hivyo uwezo wa Shirika wa kulipa dhima zake za mpito

    umepungua ukilinganisha na mwaka 2014/2015. Katika mwaka wa fedha 2015/2016

    uwezo wa Shirika la Magazeti kuweza kulipa dhima zake za mpito ni mdogo

    ukilinganisha na vigezo vya kiuhasibu juu ya uwiano wa mali za mpito na dhima za

    mpito ambapo kwa mwaka huu Shirika lingeweza kulipa dhima za mpito na kubakisha

    kiwango kidogo cha mali za mpito hivyo kuashiria kuwepo kwa hali isioridhisha ya

    mwenendo wa Shirika hilo.

    2015/2016 2014/2015

    Mali za mpito (current assets) 600,362,509 843,630,958

    Dhima za mpito (current liabilities) 362,473,034 629,404,553

    Uwiano wa mali za mpito na dhima

    za mpito (current ratio)

    = current assets/current liabilities

    1.6:1 1.3:1

  • 16

    THE CORPORATION OF GOVERNMENT NEWSPAPER (CGN)

    AS AT 30TH JUNE 2016

    STATEMENT OF COMPREHENSIVE INCOME

  • 17

    Uchambuzi wa hesabu za mwisho wa mwaka.

    Hesabu za hapo juu zinaonyesha kwamba Shirika la Magazeti limepata faida ya shilingi

    3,810,751.00 kwa mwaka 2015/2016. Ambapo kwa mwaka wa fedha 2014/2015 Shirika

    lilipata hasara ya shilingi 215,198,816.00. Ukaguzi umebaini kwamba faida hiyo inaweza

    kuongezeka iwapo hatua za kuongeza mauzo na kupunguza gharama za uendeshaji

    zitachukuliwa.

    14.3 MATOKEO YA UKAGUZI

    UCHAMBUZI WA KIFEDHA KATIKA UTENDAJI WA SHIRIKA

    14.3.1 Uwezo wa Shirika katika upatikanaji wa mapato

    Own source revenue to total revenue = Own source /Total Revenue

    30 /06/2016 30/06/2015

    Owne source

    revenue to total

    revenue

    Mapato ya ndani /

    Mapato kwa jumla

    883,221,624 720,388,256

    1,369,924,774 1,233,854,256

    64.5 58.4

    Uchambuzi wa kifedha hapo juu unaonyesha kuwa hali ya Shirika kujitegemea kupitia

    vyanzo vyake vya ndani vya mapato inaonekana kuimarika na kufikia asilimia 64.5 kwa

    mwaka wa fedha 2016 ukilinganisha na asilimia 58.4 kwa mwaka wa fedha 2015.

  • 18

    14.3.2 Uwezo wa Shirika kujiendesha kiufanisi pasipo kutegemea Ruzuku

    kutoka Serikali kuu

    Operating Self- Sufficiency = Business Revenue / Total Expenses

    30 /06/2016 30/06/2015

    Mapato ya ndani

    Jumla ya gharama

    za uendeshaji

    883,221,624 720,388,256

    1,366,114,230 1,449,053,072

    0.65 0.50

    Uchambuzi wa hapo juu unaonyesha kwamba uwezo wa Shirika kukidhi gharama za

    uendeshaji kupitia vyanzo vyake vya ndani unaonekana kuimarika na kufikia asilimia

    0.65 kwa mwaka wa fedha wa 2015/2016 ukilinganisha na asilimia 0.50 kwa mwaka wa

    fedha wa 2014/2015. Hata hivyo bado uwezo wa Shirika kukidhi gharama za uendeshaji

    kupitia vyanzo vyake vya ndani vya mapato ni mdogo.

    14.3.3 Hali ya Ukwasi katika Shirika

    Uwezo wa Shirika kuweza kumudu kulipa dhima za Mpito

    Current Ratio = Current Assts / Current Liability

    Uwiano wa mali za

    mpito na dhima za

    mpito

    30 /06/2016 30/06/2015

    Mali za mpito 600,362,509 843,630,958

    Dhima za Mpito 362,473,036 629,404,553

    Uwezo wa kulipa

    dhima za mpito

    1.66:1 1.34:1

    Uchambuzi wa hesabu hapo juu unaonyesha kuwa uwezo wa Shirika kuweza kumudu

    kulipa dhima za mpito ni mkubwa hali inayoonesha kuimarika kwa Shirika na kufikia

    uwiano wa 1.66:1 kwa mwaka wa fedha 2016 ukilinganisha na uwiano wa 1.34:1 kwa

    mwaka wa fedha 2015.

  • 19

    3.4.4 Uwezo wa Shirika kujiendesha kwa Faida

    Gharama za Uendeshaji ukilinganisha na Mapato.

    30 /06/2016 30/06/2015

    Mapato 1,369,924,774 1,233,854,256

    Matumizi 1,366,114,023 1,449,053,072

    3,810,751 (215,198,816)

    Uchambuzi wa hesabu hapo juu unaonyesha kuwa Shirika la Magazeti limeendelea

    kuimarika kwa kujiendesha kwa faida na kufikia Shilingi 3,810,751 kwa mwaka 2016

    ukilinganisha na hasara ya Shilingi 215,198,816 iliyopatikana katika kipindi cha mwaka

    2015. Kuimarika huko kutokana na kuongezeka kwa kasi ya ukusanyaji mapato pamoja

    na kupungua kwa gharama za uendeshaji.

    Maoni ya Ukaguzi

    Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za mahesabu kwa

    mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Shirika la Magazeti kwa mwaka wa

    fedha unaoishia 30 Juni, 2016 zinaonesha sura sahihi na halisi kufuatana na vigezo

    vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.

    Kwa hali hiyo Shirika la Magazeti limepata hati inayoridhisha kwa mwaka wa fedha

    unaoishia 30 Juni, 2016.

  • 20

    15.0 SHIRIKA LA UTANGAZAJI ZANZIBAR (ZBC)

    15.1 TAARIFA YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA 2015/2016

    Taarifa ya Mapato

    Mapato ya Shirika la Utangazaji Zanzibar yameonekana kuongezeka kutoka shilingi

    1,975,771,397 kwa mwaka 2014/2015 hadi kufikia shilingi 2,262,200,453 kwa mwaka

    2015/2016 kutokana na ongezeko la shilingi 286,429,056 sawa na ongezeko la asilimia

    14.5.

    Taarifa ya Matumizi

    Matumizi ya Shirika la Utangazaji yameonekana kuongezeka kutoka shilingi 652,636,529

    kwa mwaka 2014/2015 hadi kufikia shilingi 655,058,367 kwa mwaka 2015/2016 kukiwa

    na ongezeko la shilingi 2,421,838 sawa na asilimia 0.4.

  • 21

    15.2 HESABU ZA MWISHO WA MWAKA 2015/2016

  • 22

    Uchambuzi wa hesabu za mwisho wa mwaka.

    Uwiano wa mali za Mpito Ukilinganisha na Dhima za Mpito kwa mujibu wa hesabu za

    mwisho wa mwaka ni kama ifuatavyo: -

    2015/2016 2014/2015

    Mali za Mpito (current assets) 543,642,228 336,736,829

    Dhima za mpito (current liabilities) 990,265,055 780,256,306

    Uwiano wa mali za mpito na dhima

    za mpito (current ratio)

    = current assets/current liabilities 0.5:1 0.43:1

    Uchambuzi wa hapo juu unaonesha uwiano wa Mali za mpito ni mdogo ukilinganisha na

    dhima za mpito, hata hivyo uwezo wa shirika kumudu kulipa dhima za mpito bado upo

    chini mbali ya kuongezeka kwa mwaka 2015/2016 ukilinganisha na mwaka 2014/2015.

    Shirika la Utangazaji halina uwezo wa kuweza kulipa dhima zake zote za mpito kutokana

    na kuwepo kwa kiwango kikubwa cha dhima hizo.

  • 23

    Uchambuzi wa hesabu za mwisho wa mwaka

  • 24

    Uwiano wa Mapato yanayokusanywa na Shirika (Own Revenue) na Mapato yote (Total

    Income) kwa mujibu wa hesabu za mwisho wa mwaka ni kama ifuatavyo: -

    2015/2016 2014/2015

    Mapato yanayokusanywa na Shirika (Own

    Revenue) 552,545,818 533,671,743

    Mapato yote (Total Income) 2,262,200,453 1,888,935,963

    Asilimia ya mapato yanayokusanywa

    na shirika kwa mapato yote 24.42% 28.25%

    Uchambuzi wa mapato ya Shirika unaonyesha kuwa Shirika linategemea sana ruzuku

    kutoka Serikalini ambayo ni sawa na asilimia 75.57 ya mapato yake yote kwa mwaka wa

    fedha 2015/2016. Hivyo Shirika bado halijaweza kuendesha shughuli zake kwa

    kutegemea mapato yake wenyewe bila ya kutegemea ruzuku kutoka Serikalini.

    Aidha, uchambuzi unaonesha kwamba Shirika limepata hasara ya shilingi 270,179,901

    kwa mwaka 2015/2016 ukilinganisha na hasara ya shilingi 151,841,502 iliyopatikana

    kwa mwaka 2014/2015. Ikiwa ni ongezeko la shilingi 118,338,399 ambapo ni sawa na

    asilimia 0.78 ya hasara ya mwaka uliopita.

    Mwenendo wa hesabu za shirika unaonesha kuna uwezekano wa kupungua kwa hasara

    iwapo juhudi zaidi zitachukuliwa katika ukusanyaji wa mapato sambamba na kupunguza

    gharama za uwendeshaji.

    Maoni ya Ukaguzi

    Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za mahesabu kwa

    mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Shirika la Utangazaji Zanzibar kwa

    mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2016 zinaonesha sura halisi na sahihi kufuatana na

    vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.

    Kwa hali hiyo Shirika la Utangazaji Zanzibar limepata hati inayoridhisha kwa mwaka wa

    fedha unaoishia 30 Juni, 2016.

  • 25

    16.0 CHUO CHA KILIMO –KIZIMBANI

    16.1 TAARIFA YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA 2015/2016

    Taarifa ya Mapato

    Mapato ya Chuo cha Kilimo yameonekana kupanda kutoka shilingi 681,015,093 kwa

    mwaka 2014/2015 hadi kufikia shilingi 965,613,430 kwa mwaka 2015/2016 kukiwa na

    ongezeko la shilingi 284,598,337 sawa na asilimia 29.

    Taarifa ya Matumizi

    Matumizi ya Chuo cha Kilimo yameonekana kuongezeka kutoka shilingi 879,336,974

    Kwa mwaka 2014/2015 hadi kufikia shilingi 1,030,647,506 kwa mwaka 2015/2016

    kukiwa na ongezeko la shilingi 151,310,532 sawa na asilimia 17.

  • 26

    16.2 HESABU ZA MWISHO WA MWAKA 2015/2016

    KIZIMBANI AGRICULTURAL TRAINING INSTITUTE

  • 27

    Uchambuzi wa hesabu za mwisho wa mwaka.

    Uchambuzi wa hesabu za Chuo zinaonesha kwamba, Chuo hakina dhima za mpito

    kutokana na kukosekana kwa madeni.

    2015/2016 2014/2015

    Mali za Mpito (current assets) 182,751,612 195,976,580

    Dhima za mpito (current liabilities) NIL NIL

    Uwiano wa mali za mpito na dhima

    za mpito (current ratio)

    = current assets/current liabilities

    NIL NIL

  • 28

  • 29

    Ukaguzi umebaini kwamba Chuo cha Kilimo Kizimbani kinaendelea kupata hasara

    ambapo kwa mwaka 2015/2016 Chuo kimepata hasara ya shilingi 111,138,282

    ukilinganisha na mwaka wa fedha 2014/2015 ambapo chuo kilipata hasara ya shilingi

    199,321,881.

    Maoni ya Ukaguzi

    Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za mahesabu kwa

    mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Chuo cha Kilimo Kizimbani kwa

    mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2016 zinaonesha sura sahihi na halisi kufuatana na

    vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.

    Kwa hali hiyo Chuo cha Kilimo Kizimbani kimepata hati inayoridhisha kwa mwaka wa

    fedha unaoishia 30 Juni, 2016.

    17.0 MAMLAKA YA MAJI ZANZIBAR (ZAWA)

    17.1 TAARIFA YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA 2015/2016

    Taarifa ya Mapato

    Mapato ya Mamlaka ya Maji yameonekana kuongezeka kutoka shilingi

    14,634,315,587.52 kwa mwaka 2014/2015 hadi kufikia shilingi 15,707,554,021 kwa

    mwaka 2015/2016 kukiwa na ongezeko la shilingi 1,073,238,423 sawa na asilimia 7 ya

    ongezeko.

    Taarifa ya Matumizi

    Matumizi ya Mamlaka ya Maji yameonekana kupungua kutoka shilingi

    15,482,116,196.87 kwa mwaka 2014/2015 hadi kufikia shilingi 10,092,122,038 kwa

    mwaka 2015/2016 kukiwa na upungufu wa shilingi 5,389,994,159 sawa na asilimia 35

    ya upungufu.

  • 30

    17.2 HESABU ZA MWISHO WA MWAKA 2015/2016

  • 31

    Uchambuzi wa hesabu za mwisho wa mwaka.

    Uwiano wa mali za Mpito Ukilinganisha na Dhima za Mpito kwa mujibu wa hesabu za

    mwisho wa mwaka ni kama ifuatavyo: -

    2015/2016 2014/2015

    Mali za Mpito (current assets) 9,130,415,580.46 8,374,551,891.33

    Dhima za mpito (current liabilities) 2,275,908,879 2,037,884,357.00

    Uwiano wa mali za mpito na dhima

    za mpito (current ratio)

    = current assets/current liabilities

    4:1 4:1

    Uchambuzi wa hapo juu unaonesha kwamba uwiano wa mali za mpito na dhima za

    mpito wa Mamlaka ya Maji kwa mwaka wa fedha 2015/2016 unaonesha mali za mpito

    ni kubwa ukilinganisha na dhima za mpito. Hali hii imechangiwa na kuongezeka kwa

    mali za mpito ikiwemo kiwango kikubwa cha wadaiwa kwa mwaka 2015/2016.

    Aidha imebainika udhaifu katika ufuatiliaji na ukusanyaji wa mapato na kupelekea

    wadaiwa wengi kushindwa kulipa madeni yao kwa wakati na hatimae kufutwa kwa

    madeni ya wadaiwa hao. Mamlaka inashauriwa kuchukua jitihada za makusudi katika

    ufuatiliaji na ukusanyaji wa mapato kutoka kwa wadaiwa.

  • 32

  • 33

    Uchambuzi unaonyesha kwamba Mamlaka inaendelea kupata hasara ambapo kwa

    mwaka wa fedha 2015/2016 ilipata hasara ya shilingi 524, 845, 759.89 na mwaka wa

    2014/2015 ilipata hasara ya shilingi 847,800,609. Hasara hiyo inaonekana imepungua

    kwa shilingi 322,954,849.46 . Hata hivyo bado jitihada za makusudi zinahitajika

    kuchukuliwa na Mamlaka kupunguza gharama za uendeshaji pamoja na gharama

    kubwa za uchakavu zinazotokana na uchakavu wa visima, mahodhi ya kuhifadhia maji

    na mashine.

    Aidha, mwenendo wa hesabu za Mamlaka unaonesha kuwepo na uwezekano wa

    kupunguza hasara hiyo iwapo juhudi zaidi zitachukuliwa katika ukusanyaji wa mapato

    sambamba na kupunguza gharama za uendeshaji.

    UWIANO WA MAPATO YA MAMLAKA

    Uwiano wa mapato yanayokusanywa na Mamlaka (Own Revenue) na mapato yote

    (Total Income) kwa mujibu wa hesabu za mwisho wa mwaka ni kama ifuatavyo: -

    2015/2016 2014/2015

    Makusanyo ya Mamlaka (Own

    Revenue) 6,025,274,270.66 5,806,519,774.34

    Mapato mengineyo 9,682,279,750.17 8,827,795,813.18

    Mapato yote (Total Income) 15,707,554,020.83 14,634,315,587.52

    Asilimia ya mapato

    yanayokusanywa na Mamlaka

    kwa mapato yote 38.4 39.7

    Asilimia ya mapato mengineo 61.6 60.3

    Uchambuzi wa mapato ya Mamlaka unaonyesha kuwa Mamlaka inategemea sana

    ruzuku kutoka Serikalini na Washirika wa maendeleo ambayo ni sawa na asilimia 61.6

    ya mapato yake yote kwa mwaka wa fedha 2015/2016. Hivyo Mamlaka inashauriwa

    kuongeza jitihada katika ukusanyaji wa mapato yake yenyewe ili kupunguza utegemezi

    kutoka Serikalini na Washirika wa maendeleo.

  • 34

    Mapato ya Mamlaka yanatokana na vianzio mbalimbali ni kama ifuatavyo: -

    Mapato yanayokusanywa na Mamlaka: -

  • 35

    17.3 MATOKEO YA UKAGUZI

    17.3.1 Visima vilivyochimbwa na mradi wa Ras - Al- Khaimah

    Ukaguzi umebaini kwamba kuna visima vimechimbwa kupitia mradi wa Ras al Khaimah

    kwa ajili ya kuendeleza upatikanaji wa maji mijini na vijijini. Ujenzi huo ulifanyika kwa

    awamu tatu ambapo awamu ya kwanza ilikuwa visima 50, awamu ya pili 50 na awamu

    ya tatu 50. Ujenzi ambao ulianza tangu mwaka 2013 hadi kufikia 2016.Hadi ukaguzi

    unamalizika visima vilivyokamilika na kutumika ni 22, Pemba 12 na Unguja 10 idadi

    ambayo ndogo ukilinganisha na hali ya mahitaji ya huduma hio.

    17.3.2 Kutokupata taarifa za ukodishwaji wa vibanda vya kuuzia maji

    Katika kupanua wigo wa ukusanyaji mapato, Mamlaka ya Maji Zanzibar imeingia katika

    mikataba ya uuzaji maji na watu mbali mbali katika vituo vyake vikuu vikiwemo Kiosk

    cha Msikiti Mabuluu, Kiosk cha Kijito Upele na Kiosk cha Chaani kwa kipindi cha mwaka

    mmoja kuanzia tarehe 8/12/2014 hadi tarehe 7/12/2015, lakini ukaguzi umeshindwa

    kupata taarifa sahihi kutoka kwa wahusika wa uuzaji wa maji hayo ikiwemo:

    Idadi ya maji ya nayouzwa kila siku

    Idadi ya fedha zinazokusanywa kila siku

    Ripoti ya kila mwezi ya uuzaji wa maji

    Ripoti ya mwaka na tathmini halisi ya maji na mauzo husika.

    Aidha ukaguzi umebaini kwamba mikataba hiyo ya ukodishwaji imeshamaliza muda

    wake hadi ukaguzi unakamilika Mamlaka imeshindwa kuwapa mikataba mipya wahusika

    na wanaendelea na uuzaji wa maji hadi tunakamilisha ukaguzi huu pasipo kuwa na

    mikataba mipya.

    MAMLAKA YA MAJI PEMBA

    17.3.3 Malipo yasiyokuwa na vielelezo (nyaraka pungufu) shilingi 9,150,000

    Ukaguzi umebaini kuwa jumla ya shilingi 9,150,000 zimekosa vielelezo husika kinyume

    na kanuni ya 94 (4) ya kanuni ya fedha ya Zanzibar ya mwaka 2005. Kwa hali hiyo,

    uhalali wa malipo hayo haukuweza kuthibitishwa.

  • 36

    Baadhi ya malipo hayo ni kama ifuatavyo:-

    Hati namba Hundi

    namba

    Fedha

    zilizolipwa

    Aliyelipwa Maelezo

    5/7

    14/7/2015

    000610 5,120,000 Moharash

    Restaurent

    Malipo ya fedha

    kwa ajili ya

    kugharamia

    futari kwa

    wafanyakazi wa

    mamlaka

    Pemba kwa ajili

    ya mwezi

    mtukufu wa

    ramadhani.

    22/8

    17/8/2015

    2,520,000 Alhabna

    Restaurent

    Malipo ya fedha

    kwa ajili ya

    kugharamia

    chakula cha

    wageni wa ADB

    na viongozi wa

    mamlaka ya

    maji.

    38/6

    27/6/2016

    001019 1,510,000 Mamlaka ya

    maji

    Malipo ya fedha

    za tende

    wanazolipwa

    wafanyakazi wa

    mamlaka ya

    maji Pemba kwa

    ajili ya mwezi

    mtukufu wa

    ramadhani.

  • 37

    17.3.4 Deni la fidia shilingi 387,895,000

    Ukaguzi umebaini kuwa jumla ya shilingi 387,895,000 zinadaiwa na wananchi mbali

    mbali kwa ajili ya kukatwa kwa vipando vyao ili kupisha upitishaji umeme na ulazaji wa

    bomba za maji safi. Deni hili ni la mda mrefu.

    Deni la fidia kwa upitishaji umeme.

    Namba Wilaya inayohusika Kiwango

    1 Chake Chake 58,589,000

    2 Wete 96,852,000

    3 Mkoani 60,842,000

    4 Mkoani 171,612,000

    Jumla 387,895,000

    Maoni ya Ukaguzi

    Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za mahesabu kwa

    mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Mamlaka ya Maji Zanzibar, kwa

    mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2016 zinaonesha sura halisi na sahihi kufuatana na

    vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.

    Kwa hali hiyo Mamlaka ya Maji imepata hati inayoridhisha kwa mwaka wa fedha

    unaoishia 30 Juni, 2016.

    18.0 MAMLAKA YA VITEGA UCHUMI ZANZIBAR (ZIPA)

    18.1 TAARIFA YA MAPATO NA MATUMIZI

    Taarifa ya Mapato

    Mapato ya Mamlaka ya Vitega Uchumi yanaonyesha kupungua kutoka shilingi

    2,020,717,904 kwa mwaka 2014/2015 hadi kufikia shilingi 1,992,907,960 kwa mwaka

    2015/2016 kukiwa na upungufu wa shilingi 21,955,973 sawa na asilimia 1.1 ya

    upungufu.

  • 38

    Matumizi

    Matumizi ya Mamlaka ya Vitega Uchumi yameonekana kupungua kutoka shilingi

    2,290,497,499 kwa mwaka 2014/2015 hadi kufikia shilingi 1,708,343,740 kwa mwaka

    2015/2016 kukiwa na upungufu wa shilingi 582,153,759 sawa na asilimia 25 ya

    upungufu.

  • 39

  • 40

    Uchambuzi wa hesabu za mwisho wa mwaka.

    Uwiano wa mali za mpito Ukilinganisha na Dhima za Mpito kwa mujibu wa hesabu za

    mwisho wa mwaka ni kama ifuatavyo: -

    2015/2016 2014/2015

    Mali za Mpito (current assets) 1,840,099,869.12 1,620,845,442.99

    Dhima za mpito (current liabilities) 389,004,614.00 297,006,214.00

    Uwiano wa mali za mpito na dhima

    za mpito (current ratio)

    = current assets/current liabilities

    4.7:1 5.5:1

    Uchambuzi wa hapo juu unaonesha uwiano wa Mali za mpito ni mkubwa ukilinganisha

    na dhima za mpito, hata hivyo uwezo wa Mamlaka ya Vitega Uchumi kumudu kulipa

    dhima za mpito umepungua kwa mwaka 2015/2016 ukilinganisha na mwaka

    2014/2015. Mamlaka ya Vitega Uchumi ina uwezo wa kukidhi dhima zake zote za mpito

    kutokana na kuwepo kwa kiwango kikubwa cha dhima hizo.

  • 41

  • 42

    Uchambuzi wa hesabu za mwisho wa mwaka.

    Uchambuzi wa hesabu unaonyesha kwamba Mamlaka ya Vitega Uchumi inaendelea

    kupata hasara ambapo kwa mwaka wa fedha 2015/2016 imepata hasara ya shilingi

    201,080,568.68 na mwaka wa 2014/2015 imepata hasara ya shilingi 248,923,686.81.

    Hasara hiyo inaonekana imepungua kwa shilingi ni 47,843,118.13 sawa na asilimia 23.8

    ya upungufu. Hata hivyo bado jitihada za makusudi zinahitajika kuchukuliwa na

    Mamlaka ili kupunguza gharama za uendeshaji.

    Aidha, mwenendo wa hesabu za Mamlaka unaonesha kuwepo na uwezekano wa

    kupunguza hasara hiyo iwapo juhudi zaidi zitachukuliwa katika ukusanyaji wa mapato

    sambamba na kupunguza gharama za uendeshaji.

    Maoni ya ukaguzi

    Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za mahesabu kwa

    mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Mamlaka ya Vitega Uchumi kwa

    mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2016 zinaonesha sura halisi na sahihi kufuatana na

    vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.

    Kwa hali hiyo Mamlaka ya Vitega Uchumi imepata hati inayoridhisha kwa mwaka wa

    fedha unaoishia 30 Juni, 2016.

    19.0 CHUO CHA UTAWALA WA UMMA -IPA

    19.1 TAARIFA YA MAPATO NA MATUMIZI

    Taarifa ya Mapato

    Mapato ya Chuo cha Utawala wa Umma yanaonyesha kupungua kutoka shilingi

    2,656,374,870 kwa mwaka 2014/2015 hadi kufikia shilingi 2,273,296,195 kwa mwaka

    2015/2016 kukiwa na upungufu wa shilingi 383,078,675 ambapo ni sawa na asilimia

    0.14 ya upungufu.

    Matumizi

    Matumizi ya chuo cha Utawala wa Umma yameonekana kupungua kutoka shilingi

    2,386,042,878 kwa mwaka 2014/2015 hadi kufikia shilingi 2,078,772,856 kwa mwaka

    2015/2016 kukiwa na upungufu wa shilingi 68,053,248 ambapo ni sawa na asilimia

    0.03 ya upungufu.

  • 43

    HESABU ZA MWISHO WA MWAKA 2015/2016

  • 44

    Uchambuzi wa hesabu za mwisho wa mwaka.

    Uwiano wa mali za Mpito Ukilinganisha na Dhima za Mpito kwa mujibu wa hesabu za

    mwisho wa mwaka ni kama ifuatavyo: -

    2015/2016 2014/2015

    Mali za Mpito (current assets) 674,772,056 1,212,838,077.48

    Dhima za mpito (current liabilities) 475,696,457 50,000

    Uwiano wa mali za mpito na dhima

    za mpito (current ratio)

    = current assets/current liabilities 1.4 : 1 24256 : 1

    Uchambuzi wa hapo juu unaonesha uwiano wa Mali za mpito ni mdogo ukilinganisha na

    dhima za mpito, hata hivyo uwezo wa chuo kumudu kulipa dhima za mpito bado upo

    chini mbali ya kuongezeka kwa mwaka 2015/2016 ukilinganisha na mwaka 2014/2015.

    Chuo cha Utawala wa Umma hakina uwezo wa kuweza kulipa dhima zake zote za mpito

    kutokana na kuwepo kwa kiwango kikubwa cha dhima hizo.

  • 45

  • 46

    Takwimu zinaonyesha kwamba Chuo cha Utawala wa Umma kimepata faida ya shilingi

    51,121,918.65 kwa mwaka wa fedha 2015/2016 ambapo kwa mwaka wa fedha

    2014/2015 faida ya chuo ilikuwa ni shilingi 312,353,563.20 ikiwa ni upungufu wa shilingi

    261,231,644.55 sawa na asilimia 83.6 ya upungufu. Kupungua kwa faida kumetokana

    na ongezeko la gharama za uendeshaji.

    19.2 MATOKEO YA UKAGUZI

    19.2.1 Kasoro katika ukusanyaji wa mapato

    Ukaguzi umebaini kwamba kuna kasoro zenye jumla ya shilingi 5,777,000 katika

    ukusanyaji wa Ada za malipo kwa wanafunzi mbali mbali, baada ya kufanya mahojiano

    na wanafunzi imebainika kuwa wanafunzi hao walikua wakipewa stakabadhi za malipo

    ambazo zinasemekana kuwa sio sahihi ukilinganisha na stakabadhi za malipo

    zinazotolewa na Benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ).

    Fedha hizo zililipwa kwa stakabadhi zifuatazo:

    S/N Jina la mwanafunzi Kozi Stakabadhi

    namba

    Tarehe Shs.

    1 NOURDIN ALI MMANGA DPA IV 496421 25/8/2015 490,000

    2 SABRINA KEIS MWINYI DRM IV 496423 25/8/2015 490,000

    3 WARDA MOHD RASHID DRM IV 496424 25/8/2015 490,000

    4 SALUM ALI NASSOR CHRM II 496485 26/8/2015 490,000

    5 ALLY MBARUKU FENESI DBIT II 496429 26/8/2015 515,000

    6 SALHA YUSSUF MBARUK DRM IV 496442 26/8/2015 490,000

    7 TABIA KHAMIS MJUMBE DRM IV 496443 26/8/2015 490,000

    8 MOHD ALI JUMA CHRM II 496486 26/8/2015 490,000

  • 47

    9 BADRU HAJI SETI DIR III 496928 26/8/2015 220,000

    10 BILAL AMOUR AMEIR DIR III 496453 27/8/2015 490,000

    11 SAID MOHD KHAMIS DRM IV 496422 27/8/2015 490,000

    12 SAIRA HAFIDH KHAMIS CRM II 496444 27/9/2015 490,000

    13 NASSRA HASSAN IDDI CPR II 496484 28/8/2015

    142,500

    Jumla 5,777,500

    Maoni ya Ukaguzi

    Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za mahesabu kwa

    mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Chuo Cha Utawala wa Umma kwa

    mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2016 zinaonesha sura halisi na sahihi kufuatana na

    vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.

    Kwa hali hiyo Chuo Cha Utawala wa Umma kimepata hati inayoridhisha kwa mwaka wa

    fedha unaoishia 30 Juni, 2016.

    20.0 CHUO CHA MAENDELEO YA UTALII ZANZIBAR (ZITOD)

    Taarifa ya Mapato

    Mapato ya Chuo cha Maendeleo ya Utalii Zanzibar yanaonekana kupungua kutoka

    shilingi 849,902,817 kwa mwaka 2014/2015 hadi kufikia shilingi 654,848,400 kwa

    mwaka 2015/2016kukiwa na upungufu wa shilingi 195,054,417 ambapo ni sawa na

    asilimia 23 ya upungufu.

    Taarifa ya Matumizi

    Matumizi ya Chuo cha Maendeleo ya utalii Zanzibar yameonekana kupungua kutoka

    Shilingi 896,579,628 kwa mwaka 2014/2015 hadi kufikia Shilingi 749,543,835 kwa

    mwaka 2015/2016 kukiwa na upungufu wa shilingi 147,035,793 ambapo ni sawa na

    asilimia 15.62 ya upungufu.

  • 48

    20.1 HESABU ZA MWISHO WA MWAKA 2015/2016

  • 49

    Uchambuzi wa hesabu za mwisho wa mwaka.

    Uwiano wa mali za Mpito Ukilinganisha na Dhima za Mpito kwa mujibu wa hesabu za

    mwisho wa mwaka ni kama ifuatavyo: -

    2015/2016 2014/2015

    Mali za Mpito (current assets) 206,472,788 348,157,874

    Dhima za mpito (current liabilities) 40,622,738 32,548,098

    Uwiano wa mali za mpito na dhima

    za mpito (current ratio)

    = current assets/current liabilities

    5.08:1 10.7:1

    Uchambuzi wa hapo juu unaonyesha uwiano wa mali za mpito ni mkubwa ukilinganisha

    na dhima za mpito. Hali hii inaonesha Chuo cha Maendeleo ya Utalii kina uwezo wa

    kuhimili na kukidhi madeni yake.

  • 50

  • 51

    Uchambuzi wa hesabu za mwisho wa mwaka.

    Uchambuzi unaonyesha kwamba Chuo cha Maendeleo ya Utalii kinaendelea kupata

    hasara ambapo kwa mwaka wa fedha 2015/2016 ilipata hasara ya shilingi 62,062,832

    na mwaka wa 2014/2015 ilipata hasara ya shilingi 44,120,951 Hasara hiyo inaonekana

    imeongezeka kwa shilingi 18,431,122 sawa na asilimia 42.24.

    Jitihada za makusudi zinahitajika kuchukuliwa na Chuo cha Maendeleo ya Utalii

    kupunguza gharama za uendeshaji

    Aidha,mwenendo wa hesabu za Chuo cha Maendeleo ya Utalii unaonesha kuwepo na

    uwezekano wa kuongezeka kwa hasara hiyo iwapo juhudi zaidi hazitochukuliwa katika

    ukusanyaji wa mapato sambamba na kupunguza gharama za uendeshaji.

    UCHAMBUZI WA KIFEDHA (FINANCIAL ANALYSIS)

    Katika ukaguzi na uchambuzi wa kifedha uliofanyika kwenye taarifa za fedha za mwaka

    2015/2016 za Chuo cha Uandishi wa Habari yafuatayo yalibainika:-

    Uwezo wa Chuo katika ukusanyaji wa mapato

    Owne source revenue to total revenue = Own source /Total Revenue

    30/06/2016 30/06/2015

    Owne source

    revenue to total

    revenue

    Mapato ya ndani /

    Mapato kwa jumla

    349,718,280 466,718,616

    780,882,180 852,947,917

    44.8 54.7

    Uchambuzi wa kifedha hapo juu unaonyesha kuwa bado Chuo kinategemea Ruzuku

    kutoka Serikali kuu kwa kiwango kikubwa ikiwa ni chanzo kikuu cha mapato kutokana

    na kwamba uwezo wa kukusanya mapato kupitia vyanzo nyake vya ndani ni

    mdogo.Uwezo wa Chuo katika ukusanyaji wa mapato kupitia vyanzo vyake vya ndani

    umepungua na kufikia asilimia 44.8 kwa mwaka wa fedha wa unaoishia Juni 2016

    ukilinganisha na uwiano wa asilimia 54.7 katika kipindi cha mwaka wa fedha ulioishia

    Juni 2015. Kutokana na uchambuzi uliofanyika bado uwezo wa katika ukusanyaji wa

    mapato kupitia vyanzo vyake wenyewe ni mdogo.

  • 52

    Uwezo wa Chuo kujiendesha kiufanisi pasipo kutegemea Ruzuku kutoka

    Serikali kuu

    Operating Self- sufficiency = Business Revenue / Total Expenses

    30 /06/2016 30/06/2015

    Mapato ya ndani

    Jumla ya gharama

    za uendeshaji

    349,718,280 466,718,616

    842,945,012 896,579,628

    0.41 0.52

    Uchambuzi wa hapo juu unaonyesha kwamba uwezo wa Chuo kukidhi gharama za

    uendeshaji kupitia vyanzo vyake vya ndani umepungua na kufikia asilimia 0.41 kwa

    mwaka wa fedha 2015/2016 ukilinganisha na asilimia 0.52 kwa mwaka wa fedha

    2014/2015. Hata hivyo bado uwezo wa chuo kukidhi gharama za uendeshaji kupitia

    vyanzo vyake vya ndani vya mapato ni mdogo.

    Maoni ya ukaguzi

    Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za mahesabu kwa

    mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Chuo cha Maendeleo ya Utalii

    Zanzibar kwa mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2016 zinaonesha sura halisi na sahihi

    kufuatana na vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.

    Kwa hali hiyo Chuo cha Maendeleo ya Utalii Zanzibar kimepata hati inayoridhisha kwa

    mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2016.

    21.0 CHUO CHA UANDISHI WA HABARI.

    Taarifa ya Mapato

    Mapato ya Chuo cha Uandishi wa Habari yameonekana kuongezeka kutoka shilingi

    430,521,925 kwa mwaka 2014/2015 hadi kufikia shilingi 491,586,700 kwa mwaka

    2015/2016 kukiwa na ongezeko la shilingi 61,064,775 sawa na asilimia 14 ya ongezeko.

    Taarifa ya Matumizi

    Matumizi ya Chuo Cha Uandishi wa Habari yameonekana kuongezeka kutoka shilingi

    438,207,002 kwa mwaka 2014/2015 hadi kufikia shilingi 445,440,319.40 kwa mwaka

    2015/2016 kukiwa na ongezeko la shilingi 9,266,683 sawa na asilimia 21 ya ongezeko.

  • 53

    HESABU ZA MWISHO WA MWAKA 2015/2016

  • 54

    Uchambuzi wa hesabu za mwisho wa mwaka.

    Uwiano wa mali za Mpito Ukilinganisha na Dhima za Mpito kwa mujibu wa hesabu za

    mwisho wa mwaka ni kama ifuatavyo: -

    2015/2016 2014/2015

    Mali za Mpito (current assets) 41,711,083.10 12,511,072.50

    Dhima za mpito (current liabilities) 18,883,890 23,221,600.00

    Uwiano wa mali za mpito na dhima

    za mpito (current ratio) = current

    assets/current liabilities

    2.2:1 0.54:1

    Uchambuzi wa hapo juu unaonyesha uwiano wa mali za mpito ni mkubwa ukilinganisha

    na dhima za mpito. Hali hii inaonesha Chuo cha Uandishi wa Habari kina uwezo wa

    kukidhi dhima za mpito.

  • 55

  • 56

    Uchambuzi unaonyesha kwamba Chuo cha Uandishi wa Habari kimepata faida ya

    shillingi 19,955,768.35 kwa mwaka wa fedha 2015/2016. Faida hiyo inaweza

    kuongezeka iwapo jitihada za makusudi zitachukuliwa ikiwemo kupunguza gharama za

    uendeshaji, pamoja na udhibiti mzuri wa ukusanyaji wa mapato.

    UCHAMBUZI WA KIFEDHA (FINANCIAL ANALYSIS)

    Katika ukaguzi na uchambuzi wa kifedha uliofanyika kwenye taarifa za fedha za mwaka

    2015/2016 za Chuo cha Uandishi wa Habari yafuatayo yalibainika:-

    Uwezo wa Chuo katika ukusanyaji wa mapato

    Own source revenue to total revenue = Own source /Total Revenue.

    30 /06/2016 30/06/2015

    Own source

    revenue to total

    revenue

    Mapato ya ndani /

    Mapato kwa jumla

    173,339,500 137,014,800

    491,586,700 430,521,925

    35.3 31.8

    Uchambuzi wa kifedha hapo juu unaonyesha kuwa bado Chuo kinategemea Ruzuku

    kutoka Serikali kuu kwa kiwango kikubwa ikiwa ni chanzo kikuu cha mapato kutokana

    na kwamba uwezo wa kukusanya mapato kupitia vyanzo nyake vya ndani ni mdogo.

    Uwezo wa Chuo umeongezeka na kufikia asilimia 35.3 kwa mwaka wa fedha unaoishia

    Juni 2016 ukilinganisha na uwiano wa asilimia 31.8 katika kipindi cha mwaka wa fedha

    ulioishia Juni 2015. Pamoja na ongezeko hilo bado uwezo wa ukusanyaji wa mapato

    kupitia vyanzo vyake wenyewe ni mdogo.

  • 57

    Uwezo wa Chuo kujiendesha kiufanisi pasipo kutegemea Ruzuku kutoka

    Serikali kuu Operating Self- sufficiency = Business Revenue / Total Expenses

    30 /06/ 2016 30/ 06/ 2015

    Mapato ya ndani

    Jumla ya gharama

    za uendeshaji

    173,339,500 137,014,800

    471,630,931.65 450,621,312.5

    0.37 0.30

    Uchambuzi wa hapo juu unaonyesha kwamba uwezo wa Chuo kukidhi gharama za

    uendeshaji kupitia vyanzo vyake vya ndani umeongezeka na kufikia asilimia 0.37 kwa

    mwaka wa fedha 2015/2016 ukilinganisha na asilimia 0.30 kwa mwaka wa fedha

    2014/2015. Hata hivyo bado uwezo wa Chuo kukidhi gharama za uendeshaji kupitia

    vyanzo vyake vya ndani vya mapato ni mdogo.

    Maoni ya ukaguzi

    Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za mahesabu kwa

    mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Chuo Cha Uandishi wa Habari kwa

    mwaka wa fedha unaoishia Juni 2016 zinaonesha sura sahihi na halisi kufuatana na

    vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.

    Kwa hali hiyo Chuo cha Uandishi wa Habari kimepata hati inayoridhisha kwa mwaka wa

    fedha unaoishia 30 Juni, 2016.

    22.0 CHUO CHA SAYANSI ZA AFYA ZANZIBAR

    Taarifa ya Mapato

    Chuo cha Sayansi za Afya kwa mwaka wa fedha 2015/2016 kimekadiria kukusanya

    jumla ya shilingi 1,470,505,000 ambapo hadi kufikia tarehe 30 Juni 2016 jumla ya

    shilingi 1,179,863,350 zimekusanywa sawa na asilimia 80.2 ya makadirio.

    Taarifa ya Matumizi

    Kwa mwaka wa fedha 2015/2016 Chuo cha Sayansi za Afya kimekadiria kutumia jumla

    ya shilingi 1,470,505,000 ambapo hadi kufikia tarehe 30 Juni 2016 jumla ya shilingi

    1,118,962,741 zimetumika sawa na asilimia 76.1 ya makadirio.

  • 58

  • 59

    Uchambuzi wa hesabu za mwisho wa mwaka.

    Uwiano wa mali za Mpito ukilinganisha na Dhima za Mpito kwa mujibu wa hesabu za

    mwisho wa mwaka ni kama ifuatavyo: -

    2015/2016 2014/2015

    Mali za Mpito (current assets) 98,949,975 25,953,365

    Dhima za mpito (current liabilities) 32,464,240 72,875,379

    Uwiano wa mali za mpito na

    dhima za mpito (current ratio)

    = current assets/current

    liabilities

    3:1

    0.4:1

    Uchambuzi wa hapo juu unaonyesha uwiano wa mali za mpito ni mkubwa ukilinganisha

    na dhima za mpito. Hali hii inaonesha Chuo cha Sayansi za Afya kina uwezo mzuri wa

    kukidhi dhima za mpito.

  • 60

  • 61

    Uchambuzi wa hapo juu unaonesha kwamba Chuo cha Sayansi za Afya kimepata ziada

    ya shilingi 79,623,975 kwa mwaka 2015/2016.

    Maoni ya ukaguzi

    Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za mahesabu kwa

    mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Chuo cha Sayansi za Afya kwa

    mwaka wa fedha unaoishia Juni 2016 zinaonesha sura sahihi na halisi kufuatana na

    vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.

    Kwa hali hiyo Chuo cha Sayansi za Afya kimepata hati inayoridhisha kwa mwaka wa

    fedha 2015/2016.

    23.0 CHUO KIKUU CHA TAIFA ZANZIBAR (SUZA)

    Taarifa ya Mapato

    Mapato ya Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar (SUZA) yameonekana kupungua kutoka

    shilingi 12,566,712,308 kwa mwaka 2014/2015 hadi kufikia shilingi 10,955,608,931 kwa

    mwaka 2015/2016 kukiwa na upungufu wa shilingi 1,611,103,377 sawa na asilimia

    12.82 ya upungufu.

    Taarifa ya Matumizi

    Kwa mwaka wa fedha 2015/2016 Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar (SUZA) kimekadiria

    kutumia jumla ya shilingi 14,756,438,319 ambapo hadi kufikia tarehe 30 Juni 2016

    jumla ya shilingi 11,102,420,135 zimetumika sawa na asilimia 75.23 ya makadirio.

  • 62

    HESABU ZA MWISHO WA MWAKA 2015/2016

  • 63

    Uchambuzi wa hesabu za mwisho wa mwaka.

    Uwiano wa mali za Mpito ukilinganisha na Dhima za Mpito kwa mujibu wa hesbu za

    mwisho wa mwaka ni kama ifuatavyo: -

    Uchambuzi wa hapo juu unaonyesha uwiano wa mali za mpito ni mkubwa ukilinganisha

    na dhima za mpito kwa mwaka 2015/2016 umeongezeka ukilinganisha na mwaka

    2014/2015. Hali hii inaonesha Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar kina uwezo wa kuhimili na

    kukidhi dhima za mpito.

    2015/2016 2014/2015

    Mali za Mpito (current assets) 3,279,746,078 3,241,466,096

    Dhima za mpito (current liabilities) 218,321,692 243,943,395

    Uwiano wa mali za mpito na dhima

    za mpito (current ratio)

    = current assets/current liabilities 15.02 : 1 13.3:1

  • 64

  • 65

    Uchambuzi wa hapo juu unaonyesha kwamba mapato ya Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar

    kwa mwaka wa fedha 2015/2016 yamepungua kufikia shilingi 10,955,608,931

    ukilinganisha na shilingi 12,566,712,308 kwa mwaka 2014/2015. Aidha, ukaguzi

    umebaini kwamba matumizi ya Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar yameongezeka kufikia

    shilingi 11,102,420,135 ukilinganisha na shilingi 10,056,040,950 kwa mwaka

    2014/2015.

    Ukaguzi umebaini kwamba upungufu wa mapato hayo umechangiwa zaidi na kupungua

    kwa misaada ya fedha kutoka kwa wahisani wa maendeleo kutoka shilingi

    3,187,770,101 kwa mwaka wa fedha 2014/2015 hadi kufikia shilingi 1,054,736,308 kwa

    mwaka wa fedha 2015/2016. Aidha upungufu huo umechangiwa na mapato mengineyo

    kutoka shilingi 192,994,549 kwa mwaka wa fedha 2014/2015 hadi kufikia shilingi

    133,385,782 kwa mwaka wa fedha 2015/2016.

    Maoni ya Ukaguzi

    Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za mahesabu kwa

    mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar kwa

    mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2016 zinaonesha sura sahihi na halisi kufuatana na

    vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.

    Kwa hali hiyo Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar kimepata hati inayoridhisha kwa mwaka

    wa fedha unaoishia 30 Juni, 2016.

    24.0 SHIRIKA LA MELI NA UWAKALA

    Taarifa ya Mapato

    Mapato ya Shirika la Meli Zanzibar yameonekana kuongezeka kutoka shilingi

    7,540,478,026.71 kwa mwaka 2014/2015 hadi kufikia shilingi 8,721,602,539.62 kwa

    mwaka 2015/2016 ikiwa ni ongezeko la shilingi 1,181,124,514 sawa na asilimia 15.5.

    Taarifa ya Matumizi

    Matumizi ya Shirika la Meli Zanzibar yameonekana kuongezeka kutoka shilingi

    6,342,649,518.15 kwa mwaka 2014/2015 hadi kufikia shilingi 10,959,437,155.20 kwa

    mwaka 2015/2016 kukiwa na ongezeko la shilingi 4,626,787,637.10 sawa na asilimia 73

    ya ongezeko.

  • 66

  • 67

    Uchambuzi wa hesabu za mwisho wa mwaka.

    Uwiano wa mali za Mpito Ukilinganisha na Dhima za Mpito kwa mujibu wa hesbu za

    mwisho wa mwaka ni kama ifuatavyo: -

    Uchambuzi wa hapo juu unaonyesha uwiano wa mali za mpito ni mdogo ukilinganisha

    na dhima za mpito kwa mwaka 2015/2016. Hali hii inaonesha shirika la meli na uwakala

    halina uwezo wa kuhimili na kukidhi dhima za mpito.

    2015/2016 2014/2015

    Mali za Mpito (current assets) 513,957,790.27 863,739,670.31

    Dhima za mpito (current liabilities) 2,154,703,649.31 2,053,778,383

    Uwiano wa mali za mpito na dhima

    za mpito (current ratio)

    = current assets/current liabilities 0.2:1 0.4:1

  • 68

  • 69

    Uchambuzi unaonyesha kwamba Shirika la Meli na Uwakala limepata hasara ya shilingi

    552,967,502.85 kwa mwaka wa fedha 2015/2016. Hasara hiyo inaweza kupungua

    iwapo jitihada za makusudi zitachukuliwa ikiwemo kupunguza gharama za uendeshaji,

    pamoja na udhibiti mzuri wa ukusanyaji wa mapato.

    MATOKEO YA UKAGUZI

    Kukosekana kwa mikataba ya utoaji wa huduma za uwakala

    Shirika la Meli na Uwakala hutoa huduma mbalimbali za uwakala kwa meli mbali mbali

    za kigeni ambazo hazina usajili hapa Zanzibar.

    Ukaguzi umebaini kwamba hakuna mikataba ya makubaliano baina ya Shirika la Meli na

    wamiliki wa meli. Kufanya hivyo ni kwenda kinyume na Sheria ya Fedha ya Zanzibar

    namba 12 ya mwaka 2005 pamoja na kanuni zake.

    Wamiliki wenyewe wa meli (Shipping Liners) ni kama hawa wafuatao:-

    CMA CGM

    EMIRATE (WILHELMSEN)

    PIL

    UAFL

    MSK

    MSC

    Maoni ya ukaguzi

    Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za mahesabu kwa

    mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Shirika la Meli na Uwakala kwa

    mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2016 zinaonesha sura sahihi na halisi kufuatana na

    vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.

    Kwa hali hiyo Shirika la Meli na Uwakala limepata hati inayoridhisha kwa mwaka wa

    fedha unaoishia 30 Juni, 2016.

  • 70

    25.0 MAMLAKA YA UVUVI WA BAHARI KUU

    Taarifa ya Mapato

    Mamlaka ya Uvuvi wa Bahari Kuu kwa mwaka wa fedha 2015/2016 imekusanya jumla

    ya shilingi 2,913,640,961.51 ambapo kwa mwaka wa fedha 2014/2015 imekusanya

    jumla ya shilingi 1,917,891,250 kukiwa na ongezeko la shilingi 1,095,749,711.51 sawa

    na asilimia 60.28

    Taarifa ya Matumizi

    Kwa mwaka wa fedha 2015/2016 Mamlaka ya Uvuvi wa Bahari Kuu imetumia jumla ya

    shilingi 1,758,591,435.12 ambapo kwa mwaka wa fedha 2014/2015 imetumia jumla ya

    shilingi 1,755,598,234.16 kukiwa na ongezeko la shilingi 2,993,200.96 sawa na asilimia

    0.17 ya ongezeko.

  • 71

    HESABU ZA MWISHO WA MWAKA 2015/2016

    DEEP SEA FISHING AUTHORITY

    BALANCE SHEET AS AT 30TH JUNE 2016

    Assets Notes 2015/16 2014/15

  • 72

    Uchambuzi wa hesabu za mwisho wa mwaka.

    Uwiano wa mali za Mpito Ukilinganisha na Dhima za Mpito kwa mujibu wa hesbu za

    mwisho wa mwaka ni kama ifuatavyo: -

    Uchambuzi wa hesabu za Mali za Mpito za Mamlaka ya Uvuvi wa Bahari Kuu

    zinaonekana kuongezeka kutoka shilingi 3,603,205,347.87 kwa mwaka wa fedha

    2014/2015 hadi kufikia shilingi 4,401,230,258.05 kwa mwaka wa fedha 2015/2016.

    Aidha dhima za mpito zinaonekana kupungua kutoka shilingi 369,905,014 kwa mwaka

    wa fedha 2014/2015 hadi kufikia shilingi 8,984,500 kwa mwaka wa fedha 2015/2016.

    2015/2016 2014/2015

    Mali za Mpito (current assets) 4,401,230,258.05 3,603,205,347.87

    Dhima za mpito (current liabilities) 8,984,500 369,905,014

  • 73

    Uchambuzi unaonyesha kwamba Mamlaka ya Uvuvi wa Bahari Kuu imepata ongezeko la

    shilingi 1,155,049,526.40 kwa mwaka wa fedha 2015/2016 ukilinganisha na shilingi

    62,293,015.85 kwa mwaka wa fedha 2014/2015.

    Ziada hiyo inaweza kuongezeka zaidi iwapo jitihada za makusudi zitachukuliwa ikiwemo

    kupunguza gharama za uendeshaji pamoja na udhibiti mzuri wa ukusanyaji wa mapato.

    Maoni ya ukaguzi

    Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za mahesabu kwa

    mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Mamlaka ya Uvuvi wa Bahari Kuu

    kwa mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2016 zinaonesha sura sahihi na halisi

    kufuatana na vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.

    Kwa hali hiyo Mamlaka ya Uvuvi wa Bahari Kuu limepata hati inayoridhisha kwa mwaka

    wa fedha unaoishia 30 Juni, 2016.

  • 74

    26.0 SHIRIKA LA BANDARI ZANZIBAR

    Taarifa ya Mapato

    Shirika la Bandari Zanzibar kwa mwaka wa fedha 2015/2016 imekusanya jumla ya

    shilingi 29,916,824,568.20 ambapo kwa mwaka wa fedha 2014/2015 imekusanya jumla

    ya shilingi 25,543,319,987.20 kukiwa na ongezeko la shilingi 4,373,504,581 sawa na

    asilimia 17

    Taarifa ya Matumizi

    Kwa mwaka wa fedha 2015/2016 Shirika la Bandari Zanzibar limetumia jumla ya shilingi

    23,886,625,020.50 ambapo kwa mwaka wa fedha 2014/2015 imetumia jumla ya shilingi

    21,858,491,535.80 kukiwa na ongezeko la shilingi 2,028,133,484.70 sawa na asilimia

    9.3 ya ongezeko.

  • 75

    HESABU ZA MWISHO WA MWAKA 2015/2016

  • 76

    Uchambuzi wa hesabu za mwisho wa mwaka.

    Uwiano wa mali za Mpito Ukilinganisha na Dhima za Mpito kwa mujibu wa hesbu za

    mwisho wa mwaka ni kama ifuatavyo: -

    Uchambuzi wa hapo juu unaonyesha uwiano wa mali za mpito ni mkubwa ukilinganisha

    na dhima za mpito kwa mwaka 2015/2016. Hali hii inaonesha Shirika la Bandari

    Zanzibar lina uwezo wa kuhimili na kukidhi dhima za mpito.

    2015/2016 2014/2015

    Mali za Mpito (current assets) 18,045,555,484.92 19,840,101,259.35

    Dhima za mpito (current liabilities) 4,949,873,792.70 6,434,625,586.66

    Uwiano wa mali za mpito na dhima

    za mpito (current ratio)

    = current assets/current liabilities

    3.6:1 3.08:1

  • 77

  • 78

    Uchambuzi unaonyesha kwamba Shirika la Bandari Zanzibar limepata faida ya shilingi

    4,620,772,945.52 kwa mwaka wa fedha 2015/2016 ukilinganisha na shilingi

    4,166,260,540.68 kwa mwaka wa fedha 2014/2015. Faida hiyo inaweza kuongezeka

    zaidi iwapo jitihada za makusudi zitachukuliwa ikiwemo kupunguza gharama za

    uendeshaji pamoja na udhibiti mzuri wa ukusanyaji wa mapato.

    Maoni ya ukaguzi

    Kutokana na ukaguzi uliofanyika kupitia vitabu na kumbukumbu za mahesabu kwa

    mujibu wa sheria na kanuni za ukaguzi, hesabu za Shirika la Bandari Zanzibar kwa

    mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni, 2016 zinaonesha sura sahihi na halisi kufuatana na

    vigezo vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.

    Kwa hali hiyo Shirika la Bandari Zanzibar limepata hati inayoridhisha kwa mwaka wa

    fedha unaoishia 30 Juni, 2016.

    1.0 UTANGULIZI2.0 MAJUKUMU YA OFISI YA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI3.0 UPEO NA MADHUMUNI YA RIPOTI YA UKAGUZI4.0 NJIA ZILIZOTUMIKA KATIKA UKAGUZI5.0 MAJUKUMU YA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI6.0 UMUHIMU WA KUFANYA UKAGUZI7.0 SHUKURANI8.0 MATOKEO YA UKAGUZI KWA MWAKA 2015/20169.0 UTEKELEZAJI WA HOJA ZA UKAGUZI ULIOPITA WA MWAKA WA FEDHA 2014/201510.0 UWASILISHAJI WA HESABU ZA MWISHO WA MWAKA 2015/2016 KWA AJILI YA UKAGUZI11.0 AINA YA HATI ZA UKAGUZI11.1 Hati inayoridhisha11.2 Hati isiyoridhisha11.3 Hati yenye shaka11.4 Hati mbaya

    12.0 MAMBO YALIYOBAINIKA KATIKA UKAGUZI WA MASHIRIKA NA TAASISI ZA SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR13.0 UKAGUZI WA HESABU ZA MWISHO WA MWAKA 2015/201614.0 SHIRIKA LA MAGAZETI14.1 TAARIFA YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA 2015/201614.2 HESABU ZA MWISHO WA MWAKA 2015/2016.14.3 MATOKEO YA UKAGUZI14.3.1 Uwezo wa Shirika katika upatikanaji wa mapato14.3.2 Uwezo wa Shirika kujiendesha kiufanisi pasipo kutegemea Ruzuku kutoka Serikali kuu14.3.3 Hali ya Ukwasi katika Shirika

    15.0 SHIRIKA LA UTANGAZAJI ZANZIBAR (ZBC)15.1 TAARIFA YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA 2015/201615.2 HESABU ZA MWISHO WA MWAKA 2015/2016

    16.0 CHUO CHA KILIMO –KIZIMBANI16.1 TAARIFA YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA 2015/201616.2 HESABU ZA MWISHO WA MWAKA 2015/2016

    17.0 MAMLAKA YA MAJI ZANZIBAR (ZAWA)17.1 TAARIFA YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA 2015/201617.2 HESABU ZA MWISHO WA MWAKA 2015/201617.3 MATOKEO YA UKAGUZI17.3.1 Visima vilivyochimbwa na mradi wa Ras - Al- Khaimah17.3.2 Kutokupata taarifa za ukodishwaji wa vibanda vya kuuzia maji17.3.3 Malipo yasiyokuwa na vielelezo (nyaraka pungufu) shilingi 9,150,00017.3.4 Deni la fidia shilingi 387,895,000

    18.0 MAMLAKA YA VITEGA UCHUMI ZANZIBAR (ZIPA)18.1 TAARIFA YA MAPATO NA MATUMIZI

    19.0 CHUO CHA UTAWALA WA UMMA -IPA19.1 TAARIFA YA MAPATO NA MATUMIZI19.2 MATOKEO YA UKAGUZI19.2.1 Kasoro katika ukusanyaji wa mapato

    20.0 CHUO CHA MAENDELEO YA UTALII ZANZIBAR (ZITOD)20.1 HESABU ZA MWISHO WA MWAKA 2015/2016

    21.0 CHUO CHA UANDISHI WA HABARI.UCHAMBUZI WA KIFEDHA (FINANCIAL ANALYSIS)

    22.0 CHUO CHA SAYANSI ZA AFYA ZANZIBAR23.0 CHUO KIKUU CHA TAIFA ZANZIBAR (SUZA)24.0 SHIRIKA LA MELI NA UWAKALA25.0 MAMLAKA YA UVUVI WA BAHARI KUU26.0 SHIRIKA LA BANDARI ZANZIBAR