28
1 JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI TAARIFA YA UTENDAJI YA SHIRIKA LA UTAFITI NA MAENDELEO YA VIWANDA TANZANIA (TIRDO) KWA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA VIWANDA, BIASHARA NA MAZINGIRA 8 MACHI 2017

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA …tirdo.or.tz/documents/KAMATI YA BUNGE 2017.pdfViwanda, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, P.O. Box 601, Zanzibar 7. Bi. Christina Kilindu

  • Upload
    others

  • View
    10

  • Download
    0

Embed Size (px)

Citation preview

Page 1: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA …tirdo.or.tz/documents/KAMATI YA BUNGE 2017.pdfViwanda, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, P.O. Box 601, Zanzibar 7. Bi. Christina Kilindu

1

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI

TAARIFA YA UTENDAJI YA SHIRIKA LA UTAFITI NA

MAENDELEO YA VIWANDA TANZANIA (TIRDO) KWA KAMATI YA

KUDUMU YA BUNGE YA VIWANDA, BIASHARA NA MAZINGIRA

8 MACHI 2017

Page 2: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA …tirdo.or.tz/documents/KAMATI YA BUNGE 2017.pdfViwanda, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, P.O. Box 601, Zanzibar 7. Bi. Christina Kilindu

2

TAARIFA KUHUSU UTENDAJI WA SHIRIKA LA UTAFITI NA

MAENDELEO YA VIWANDA TANZANIA (TIRDO) KWA KAMATI YA

KUDUMU YA BUNGE YA VIWANDA, BIASHARA NA MAZINGIRA

1.0 UTANGULIZI

Shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) lilianzishwa kwa Sheria

ya Bunge namba 5 ya mwaka 1979 na kuanza kazi zake rasmi tarehe 1 Aprili, 1979.

Sheria hii ilipitiwa na kutangazwa tena na gazeti la Serikali mwaka 2002 (CAP 159 of

2002). Shirika liliundwa ili kufanya utafiti na kutoa huduma za kitaalam ili

kuendeleza viwanda nchini.

2.0 DIRA, DHAMIRA NA MADHUMUNI

2.1 DIRA (VISION)

Shirika la utafiti unaohitajika na wadau, lenye matokeo bora yasiyoharibu mazingira yatakayowezesha ushindani wa viwanda

2.2 DHAMIRA (MISSION)

Kuendeleza utafiti, huduma za kitaalamu na uzalishaji wa bidhaa viwandani kwa kutumia malighafi za hapa nchini na kwa kushirikisha viwanda

2.3 DHUMUNI KUU:

Ni kufanya utafiti (Applied Research), kutoa huduma za kitaalamu viwandani, kukusanya na kusambaza taarifa zinazohusu utaalamu wa viwanda kwa ajili ya kuimarisha na kuongeza uzalishaji bora viwandani.

Aidha, Shirika pia lina dhumuni la kufanya utafiti unaolenga kuongeza thamani ya malighafi inayopatikana nchini na kuzalishwa na viwanda vya ndani kwa malengo ya kuuza nje ya nchi.

3.0 MAJUKUMU YA SHIRIKA

Majukumu ya Shirika ni kama ifuatavyo:-

3.1 Kufanya utafiti wa teknolojia zinazotoka nje ya nchi na za hapa

nchini kwa ajili ya matumizi ya viwanda.

3.2 Kuendeleza na kutoa mafunzo yenye kuwezesha kufanya utafiti wa

kisayansi na kiteknolojia unaoendeleza viwanda.

Page 3: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA …tirdo.or.tz/documents/KAMATI YA BUNGE 2017.pdfViwanda, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, P.O. Box 601, Zanzibar 7. Bi. Christina Kilindu

3

3.3 Kusimamia na kusambaza matokeo ya utafiti unaofanywa hapa

nchini au mahali pengine popote kwa manufaa ya Serikali ya

Tanzania na kutoa tathmini ya utafiti huo katika viwanda.

3.4 Kuanzisha mfumo wa kusajili matokeo ya utafiti unaofanywa nchini

na kuendeleza matokeo ya utafiti huo katika viwanda vyetu.

3.5 Kuanzisha na kuendesha mfumo wa kutunza taarifa za kitaalamu na

kusambaza matokeo ya utafiti wa aina yoyote unaofanywa hapa

nchini kwa niaba ya Serikali.

3.6 Kutoa huduma na ushauri wa kitaalamu Serikalini na katika

mashirika yanayohusika na uzalishaji viwandani, ili kuendeleza

shughuli za viwanda na matumizi ya teknolojia mpya.

3.7 Kushauri na kusaidia Serikali na viwanda kuanzisha mfumo wa

kudhibiti na kuwianisha shughuli za viwandani na kuepusha ama

kupunguza vyanzo vya uchafu wa mazingira wakati wa uzalishaji

viwandani kwa kutumia teknolojia zinazofaa na zinazoongeza

uzalishaji.

4.0 UONGOZI WA SHIRIKA

4.1 Baraza la Shirika:-

Shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania linasimamiwa na Baraza la Shirika ambalo limeundwa kwa mujibu wa Sheria. Baraza lina majukumu ya kusimamia utekelezaji wa majukumu ya Shirika, na kusimamia shughuli zinazofanywa na Menejimenti ya Shirika. Baraza linaongozwa na Mwenyekiti anayeteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Wajumbe wa Baraza wanateuliwa na Waziri mwenye dhamana ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji. Mkurugenzi Mkuu ndiye Mtendaji Mkuu wa Shirika na Katibu wa Baraza. Baraza lina wajumbe kumi kutoka Serikalini Taasisi za Umma, na sekta binafsi. Wajumbe wa Baraza waliopo sasa waliteuliwa 1 Novemba 2015 kwa kipindi cha miaka mitatu.

Page 4: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA …tirdo.or.tz/documents/KAMATI YA BUNGE 2017.pdfViwanda, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, P.O. Box 601, Zanzibar 7. Bi. Christina Kilindu

4

JEDWALI 1: WAJUMBE WA BARAZA LA TIRDO

Na. Jina Wadhifa Mahali alipotoka

1. Prof. Idrissa Bilali Mshoro Mwenyekiti Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ardhi

2. Prof. Evelyne Mbede Mjumbe Mkurugenzi wa Sayansi na Teknolojia Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia

3. Dkt. Hassan Mshinda Mjumbe Mkurugenzi Mkuu, Tume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH)

4. Bi. E.N. Pallangyo Mjumbe Mkurugenzi Msaidizi wa Viwanda Wizara ya Viwanda na Biashara

5. Bw. Bernard Mchomvu Mjumbe FAC Chairperson, P.O. Box 22703, Dar es Salaam

6. Bw. Salehe Selemani Hamadi Mjumbe Mkurugenzi wa Masoko na Biashara za Viwanda, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, P.O. Box 601, Zanzibar

7. Bi. Christina Kilindu Mjumbe Private Sector

8. Ms. Kulthum Mansoor Mjumbe Mchumi, Idara ya Sera na Mipango, TAKUKURU Makao Makuu, P.O. Box 486, Dar es Salaam

9. Bw. Fadhili J. Manongi Mjumbe Mkurugenzi Mkuu, CDE Consulting Ltd. P.O. Box 33025 Dar es Salaam

10 Bi. Fatuma Oloo Mjumbe Mhasibu Mkuu, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

11 Prof. Mkumbukwa M. Mtambo Katibu Mkurugenzi Mkuu, TIRDO

4.2 Mfumo wa Menejimenti ya Shirika

4.2.1 Muundo uliopo hapa shirikani ulianza kutumika katika kipindi cha 2007/2008.

(Ona Kiambatanisho A).

4.2.2 Mkurugenzi Mkuu anaongoza kurugenzi ambazo ni:-

a) Utafiti Viwandani

b) Maendeleo ya Uhandisi

c) Elektroniki na tekinolojia ya habari

d) Rasilimali watu na miliki

e) Fedha

4.2.3 Chini ya kurugenzi hizi kuna vitengo vifuatavyo:-

Page 5: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA …tirdo.or.tz/documents/KAMATI YA BUNGE 2017.pdfViwanda, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, P.O. Box 601, Zanzibar 7. Bi. Christina Kilindu

5

(a) Teknolojia ya Kilimo na Kemia ya Viwandani (Agrotechnology and industrial

Chemistry)

(b) Chakula na Teknolojia ya Baiolojia (Food and Biotechnology)

(c) Mazingira na usalama mahali pa kazi (Environmental Technology and

occupational safety)

(d) Teknolojia ya Vifaa vya Kihandisi (Materials Science and Technology)

(e) Teknolojia ya Nishati (Energy Technologies)

(f) Teknolojia ya Nyuzi na Ngozi (Fibre and Leather technologies)

(g) Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Information and Communication

Technologies)

(h) Ufundi wa Vifaa vya Elektroniki (Electronics and Instrumentation

Technologies)

(i) Maendeleo ya Teknolojia na Viwanda vya Mfano (Technology Development

and Pilot plant))

(j) Ushirikishwaji Wadau kutoa huduma (Corporate Services)

(k) Utumishi na Rasilimali Watu (Human Resources)

(l) Miliki na Ukarabati (Estate and Maintenance)

(m) Utawala

5.0 UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA SHIRIKA LA TIRDO

5.1 UTANGULIZI:-

Kwa muda mrefu tangu kuanzishwa kwake shirika la TIRDO kama mashirika

mengine yanayotegemea ruzuku kutoka Serikalini ili kuendesha shughuli zake

Shirika limepambana na changamoto nyingi hasa kutokana na ukosefu wa

fedha. Aidha ukosefu wa fedha pia umesababisha kutokamilika kwa baadhi ya

majengo ambayo yangetumika kama maabara za kufanya utafiti na upimaji

ubora na usalama wa malighafi na bidhaa zinazozalishwa viwandani ili kutoa

ushauri wa kitaalamu kwa wazalishaji.

Pamoja na matatizo hayo, kwa mwaka 2016/17 Shirika limeweza kufanya tafiti

mbalimbali na kutoa huduma za kitaalamu viwandani kwa kutumia fedha za

Page 6: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA …tirdo.or.tz/documents/KAMATI YA BUNGE 2017.pdfViwanda, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, P.O. Box 601, Zanzibar 7. Bi. Christina Kilindu

6

wahisani na fedha za ndani. Baadhi ya Tafiti zinazoendelea ni kama ifuatavyo;

1. Mfumo wa kijani wa usindikaji zao la muhogo usiozalisha taka kwa ajili ya

kuimarisha masoko kwa ajili ya wazalishaji wadogo na wakati, (Greener

cassava processing system leading to zero waste for enhanced

market access by small and medium entrepreneurs). Mradi

unafadhiliwa na USAID ambapo unahusisha kukausha muhogo kwa kutumia

kaushio la jua na kutumia mabaki ya maganda ya muhogo kuzalisha gesi

ambayo inatumika pia katika kaushio nyakati za usiku ama wakati wa mvua.

Mradi wa ukaushaji muhogo na uzalishaji gesi kwa kutumia maganda ya mihogo

2. Mradi wa kuongeza thamani katika taka ngumu za ngozi na kuzalisha bidhaa

mbalimbali za ngozi (Value addition on solid leather waste to produce

leather boards). Mradi ulianzishwa kwa Fedha za Utafiti chini ya COSTECH

na sasa umeingizwa katika bajeti ya Maendeleo ya Serikali.

3. Kujenga uwezo wa kuzalisha kwa biashara uyoga wa kawaida na ule

unaotumika kama dawa (Capacity building for commercial production

of Edible and Medicinal Mushrooms in Tanzania) Mradi unatekelezwa

kwa kushirikiana na chuo cha Hubert Kairuki chini kwa kupitia Fedha za utafiti

chini ya COSTECH.

4. Kutathmini hali halisi ya sekta ya ngozi na nguo nchini (Status of leather

and textile sector in Tanzania). Utafiti huu ulifanyika katika kitengo cha

Page 7: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA …tirdo.or.tz/documents/KAMATI YA BUNGE 2017.pdfViwanda, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, P.O. Box 601, Zanzibar 7. Bi. Christina Kilindu

7

Nguo na Ngozi hapa Shirikani na kuweza kutoa andiko katika majarida ya

kimataifa (Pulication) na pia kuwasilishwa katika mikutano na wadau wa ngozi

nchini.

5. Kutumia mabaki ya mbegu za mafuta katika kutengeneza chakula chenye

protein nyingi (Utilization of Tanzanian oilseed meals to develop high

protein foods and wellness ingrediantes). Utafiti huu unafanyika kwa

kushirikiana na kituo cha Utafiti nchini India – CSIR

6. Kutathmini taka ngumu zitokanazo na usindikaji wa mafuta ya kula kwa ajili

ya kuboresha uzalishaji biogesi itokanayo na kinyesi cha ng’ombe

(Characterization of spent bleaching earth and improvement of

biogas through supplementation of manure). Utafiti huu unafanyika kwa

kushirikiana na CSIR India na umetokana na mahitaji ya viwanda katika

kuongeza thamani katika mabaki yatokanayo na usindikaji mafuta na

kutumika katika kuzalisha bidhaa nyingine na vilevile kutunza mazingira.

7. Uzalishaji wa Citric Acid kutokana na aina mbili za viazi visivyoliwa

(Production of Citric Acid from two Non-Edible yam species) Utafiti

unatekelezwa chini ya makubaliano na Taasisi ya Utafiti nchini India -CSIR

8. Utengenezaji wa mbinu za gharama nafuu za kibiolojia za kutathimini uchafuzi

wa maji katika mito ya nchi za joto za kiafrika (Development of cost

effective biomonitoring methods for assessing water pollution in

tropical Africa rivers, (Julius, Doctoral study)

9. Tathimini ya uchafuzi wa hewa unaosababishwa na ndege katika uwanja wa

kimataifa wa ndege wa Mwalimu Julius Kambarage Nyeyere (Assessment of

Aviation Emisions at Julius Nyerere International Airport JNIA in

Tanzania and their effects on Air Quality of neighboring community

(Jacqueline Mwenda, Doctoral study).

10. Uchunguzi wa madhara ya mabaki ya viuatilifu katika mazao ya mbogamboga

kwa walaji wa mkoa wa Arusha (Investigating Human Exposure of

Page 8: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA …tirdo.or.tz/documents/KAMATI YA BUNGE 2017.pdfViwanda, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, P.O. Box 601, Zanzibar 7. Bi. Christina Kilindu

8

Pesticides residue through vegetable consumption in Arusha region

(Purificator Andrew, Doctoral study).

Mtambo wa kuchakata taka ngumu za ngozi

Aidha Shirika limetoa na linaendelea kutoa huduma za kitaalamu za Upimaji

ubora wa majaa ya mawe (Coal Quality Testing), Matumizi bora ya Nishati

(Energy Auditing), Mazingira (Environmental Auditing), Upimaji wa

Kihandisi bila kuharibu vifaa (Non Destructive Testing) kwenye mabomba

ya gesi, maji, mabwela (Boilers) na upimaji wa ubora wa vyakula.

Vilevile katika kipindi cha 2016/17 Shirika kwa kutumia wataalamu wake wa

ndani limeweza kutengeneza na kufufua vifaa vya maabara (scientific

equipment) na hivyo kuweza kuokoa Fedha nyingi ambazo zingetuka aidha

kununua vifaa vingine ama kuleta wataalamu kutoka nje ya nchi kufanya

matengenezo. Utaalamu huu ukiendelezwa utaweza kusaidia taasisi nyingine

nyingi za Serikali na hata viwanda kuweza kufufua vifaa na mitambo iliyokufa

na hivyo kuokoa gharama kubwa na muda. Vifaa hivyo ni kama

inavyoonekana katika jedwali;

Na: Kifaa Kitengo

1 Water Bath Chakula na bioteknolojia

2 Distiller Chakula na bioteknolojia

3 Nuve Incubator Chakula na bioteknolojia

4 Stomacher Chakula na

Page 9: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA …tirdo.or.tz/documents/KAMATI YA BUNGE 2017.pdfViwanda, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, P.O. Box 601, Zanzibar 7. Bi. Christina Kilindu

9

bioteknolojia

5 GerhardtKjedahl Kemia ya Viwanda

6 Oxford XRF Mazingira

7. Eltra CHS Analyser Nishati

5.2 MAANDIKO YA MIRADI

Katika kipindi 2016/17 Shirika limefanya juhudi kubwa ya kuandika miradi mbalimbali

ya utafiti, na miradi ya kujenga uwezo (capacity building projects) kwa ajili ya

kutafuta fedha za utafiti na kujenga uwezo wa taasisi. Miradi hiyo iliwasilishwa

Wizara ya Fedha, UNIDO, DANIDA, JICA, WB, USAID, HDIF n.k. Miradi hii imelenga

sekta za Mafuta na Gesi, Makaa ya Mawe, Chuma, Usindikaji vyakula

(agroprocessing), ngozi na TEHAMA. Katika miradi hiyo, DANIDA iliweza

kufadhili mradi wa kutathmini tekinolojia na ubunifu mbalimbali ambao unastahili

kuibuliwa na kuendelezwa kutokana na miradi ya kitafiti iliyofadhiliwa na Danida

Tanzania. Vilevile, miradi mbalimbali ya kutoa huduma za kitaalamu pamoja na

ukaguzi wa viwanda iliandikwa kwa viwanda mbalimbali .

6.0 HUDUMA KWA VIWANDA NA WADAU WENGINE

6.1 UKAGUZI WA VIWANDA VILIVYOKUFA KWA LENGO LA KUSHAURI

SERIKALI

TIRDO kupitia Msajili wa Hazina ilifanya ukaguzi wa viwanda viwili

vilivyofungwa ikiwa ni pamoja na kiwanda cha chai Mponde (Mponde Tea

Factory) na kiwanda cha ngozi Mwanza (Mwanza Tanneries ltd). Ukaguzi huo

ulihusisha pia tathmini ya mitambo na teknolojia zilizopo ili kuweza kushauri

serikali juu ya ufufuaji wa viwanda husika.

Pia, TIRDO kwa kushirikiana na NDC, ilifanya ukaguzi katika kiwanda cha

matairi (General tyre) cha Arusha na TIRDO ina uwakilishi katika kamati ya

Kitaifa ya kushauri kuhusu ufufuaji wa kiwanda hicho.

6.2 UPEMBUZI YAKINIFU KWA UANZISHWAJI WA VIWANDA

(FEASIBILITY STUDIES FOR START UP INDUSTRIES)

TIRDO imefanya upembuzi yakinifu (feasibility study) wa uanzishwaji wa

kiwanda cha kuzalisha viuatilifu (pesticides) Bajuta Arusha, kiwanda cha

Page 10: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA …tirdo.or.tz/documents/KAMATI YA BUNGE 2017.pdfViwanda, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, P.O. Box 601, Zanzibar 7. Bi. Christina Kilindu

10

nyama Sumbawanga na uanzishwaji wa viwanda vya madawa Simiyu. Vilevile

Shirika linategemea kushiriki katika kufanya upembuzi yakinifu katika

uanzishwaji wa kiwanda kikubwa cha chaki Maswa Mkoani Simiyu, kiwanda

cha kusindika nyanya (Tomato paste) mkoani Morogoro na viwanda vingine

vinavyoanzishwa na mifuko ya hifadhi za jamii pamoja na majeshi ya ulinzi na

usalama.

6.3 KUANZISHWA KWA VIWANDA VIWILI VYA MADAWA MKOANI

SIMIYU

TIRDO kwa kushirikiana na Taasisi nyingine nane zimeandaa andiko la

kitaalamu kuhusu uanzishwaji wa viwanda viwili kimoja cha bidhaa za pamba

za mahospitalini na kingine cha kuzalisha dripu mkoani Simiyu. Tayari andiko

limekwisha wasilishwa kwa Makamu wa Rais Mh. Samia Suluhu na kupatiwa

Baraka zote. Inategemewa kuanza kwa upembuzi yakinifu baada ya

kukamilisha taratibu za kifedha na kisheria kati ya NHIF na TIB. Taasisi

nyingine ni pamoja na NDC, TFDA, TBS, TEMDO, NEMC na MSD.

6.4 UPIMWAJI WA UBORA WA MAKAA YA MAWE YANAYOPATIKANA

TANZANIA

Shirika kupitia maabara yake ya makaa ya mawe limeweza kutoa taarifa sahihi

kuhusu ubora wa makaa ya mawe ya Tanzania na hivyo kuweza kutatua

mgogoro uliookuwepo kati ya kiwanda cha simenti cha Dangote na Serikali.

Maabara hii imeweza kusaidia kuepuka hasara kwa Serikali kwa viwanda

kuacha kuagiza makaa ya mawe nje ya nchi na badala yake kutumia makaa

ya mawe ya Tanzania. Maabara inakwenda sambamba na kufanya utafiti wa

nishati mbadala na kubuni tekinolojia za matumizi bora ya makaa ya mawe

viwandani na majumbani. Tayari Wizara ya nishati na madini imekwisha kutoa

agizo la kutaka TIRDO kwa Kushiriana na GST kupima ubora wa makaa ya

mawe nchini, vilevile katika bajeti ya maendeleo ya mwaka 2016/17 lipo

fungu kwa ajili ya kufanya utafiti na kuboresha ‘coal briquettes’ zinazozalishwa

na wajasiriamali wa Tanzania.

Page 11: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA …tirdo.or.tz/documents/KAMATI YA BUNGE 2017.pdfViwanda, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, P.O. Box 601, Zanzibar 7. Bi. Christina Kilindu

11

Maabara ya kupima ubora wa makaa ya mawe TIRDO

6.5 UKAGUZI WA MATUMIZI YA NISHATI VIWANDANI NA MAJENGO YA

SERIKALI (ENERGY AUDITING)

TIRDO inatoa huduma za kitaalamu viwandani amabazo zinalenga kupunguza

gharama za nishati kati ya Asilimia 10 hadi 20. TIRDO imetoa huduma hizo

kwenye viwanda takribani vitano katika mwaka 2016/17.

Ukaguzi wa matumizi ya nishati katika moja ya kiwanda

6.6 UKAGUZI NA USHAURI WA KUZUIA UCHAFUZI WA MAZINGIRA

VIWANDANI (ENVIRONMENTAL AUDITING)

Shirika katika mkakati wa kupunguza uharibifu wa mazingira katika viwanda

vinavyozalisha bidhaa mbalimbali limetoa huduma za upimaji wa viwango vya

hewa zinazochafua mazingira, viwango vya kelele vinavyozidi katika sehemu

mbalimbali ndani ya viwanda na viwango vya vumbi litolewalo wakati wa

Page 12: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA …tirdo.or.tz/documents/KAMATI YA BUNGE 2017.pdfViwanda, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, P.O. Box 601, Zanzibar 7. Bi. Christina Kilindu

12

uzalishaji ndani ya viwanda. Lengo ni kuhamasisha uzalishaji wa bidhaa bora

bila kuchafua mazingira katika viwanda. Huduma zilitolewa katika viwanda vya

sigara, vinywaji baridi, bia, simenti, makaratasi, mbao na mtambo wa kuzalisha

umeme wa Ubungo (Gas Power Plant).

6.7 UPIMAJI UBORA WA VIFAA NA MAJENGO BILA KUHARIBU VIFAA

(NON-DESTRUCTIVE TESTING)

Shirika kwa kushirikiana na kampuni binafsi liliandaa andiko la kufanya kazi ya

uhakiki wa maungio katika bomba la gesi la kutoka Tanga hadi Uganda lakini

halikufanikiwa kukidhi ushindani. Vilevile Shirika kwa kushirikiana na kampuni

ya TASA linaendesha mafunzo ya kitaalamu ya NDT yatakayowezesha wazawa

kushiriki katika sekta ya mafuta na gesi. Kwasasa wafanyakazi watano wa

TIRDO wanaendelea na mafunzo hayo ambapo watakapo hitimu watapatiwa

vyeti vya umahiri hivyo kuweza kutambulika kimataifa.

Kwa mwaka 2016/17 Shirika limehakiki maungio ya kivuko cha MV Njombe

Pamoja na kufanya ukaguzi katika mtambo wa kuzalisha mafuta wilayani Chato.

Uhakiki wa maungio katika kivuko cha MV Njombe kwa kutumia XRay

Page 13: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA …tirdo.or.tz/documents/KAMATI YA BUNGE 2017.pdfViwanda, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, P.O. Box 601, Zanzibar 7. Bi. Christina Kilindu

13

6.8 USALAMA WA VYAKULA MAHOTELINI

Katika kuhakikisha ubora na usalama wa bidhaa za chakula ili kumlinda mteja

shirika limepima sampuli mbalimbali za vyakula na maji ili kuangalia ubora

wake na kuona kama vinakidhi matakwa ya viwango vya kimataifa

vinavyokubalika katika vyakula. Pia wataalamu wametoa huduma za ushauri

kuhusu ubora na usalama wa chakula kwa wasindikaji, na watoa huduma za

hoteli.

6.9 UHAKIKI WA MAABARA (LABORATORY ACCREDITATION)

Ili kuweza kutoa huduma zinazokubalika kimataifa kwa wazalishaji viwandani

Shirika liko katika mkakati wa kupanua wigo wa uhakiki wa maabara yake ya

chakula ili iweze kutoa huduma katika maeneo ya upimaji maji, samaki, asali

na nyama katika viwango vya kimataifa. Maabara hii ya chakula ndiyo pekee

iliyohakikiwa kimataifa kwa TIRDO. Aidha Maabara ya mazingira imekwisha

omba usajili (SADCAS) na kuanza hatua za mwanzo za kufanya ushindani wa

kimaabara (profiency testing) ambao unahitajika katika hatua za kuhakiki.

Inategemewa kwamba maabara hii iweze kuhakikiwa katika upimaji wa maji

safi na maji taka kwa kuanzia na kisha baadae kupanua wigo wa uhakiki.

Maabara iliyohakikiwa ya Chakula

6.10 KUTANGAZA SHUGHULI ZA SHIRIKA (MARKETING)

Katika hatua za kutafuta masoko, Shirika limeshiriki katika maonyesho

mbalimbali ili kujulisha umma juu ya shughuli za Shirika. Maonesho hayo ni

pamoja na maonesho ya Kimataifa ya Biashara Dar es Salaam, maonesho ya

wakulima “Nanenane” na maonesho ya kwanza ya Viwanda Dar es Salaam.

Page 14: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA …tirdo.or.tz/documents/KAMATI YA BUNGE 2017.pdfViwanda, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, P.O. Box 601, Zanzibar 7. Bi. Christina Kilindu

14

Shirika pia limetoa makala zaidi ya saba katika magazeti mbalimbali nchini

ikiwa ni hatua za kueleza umma wa Watanzania juu ya Shughuli mbalimbali za

Shirika. Aidha Shirika linatafuta fedha ili kuweza kujitangaza zaidi ili Wadau

wote wafahamu shughuli zinazofanywa na shirika.

7.0 UTAWALA

Katika kuboresha huduma za Shirika, Shirika liko katika hatua mbalimbali za

kukamilisha yafuatayo:-

i) Kanuni za Utumishi na Motisha (Staff Regulations and Incentive

Scheme)

ii) Muundo wa Utumishi (Scheme of Service).

iii) Kupitia upya sheria ya Shirika (Review of TIRDO Act)

vi) Kanuni za Fedha (Financial Regulation)

vii) “Land use, feasibility and Business plan”

viii) Muundo wa urishwaji madaraka (Staff succession plan)

Katika kuendeleza watafiti, Shirika liliwapeleka kusoma kozi fupi na za muda

mrefu ndani na nje ya nchi wafanyakazi wake. Wafanyakazi wanne wa Shirika

wanafanya masomo ya Shahada ya uzamivu (PhD) na mfanyakazi mmoja

anafanya mafunzo ya muda mfupi nchini India.

8.0 CHANGAMOTO

Katika kutekeleza majukumu yake Shirika linakabiliana na changamoto

mbalimbali kama vile:-

8.1 Kupata ruzuku ndogo toka Serikalini ambayo:-

i. kuathiri shughuli za utafiti hivyo kutegemea wafadhili tu.

ii. Kushindwa kuboresha na kuhakiki Maabara kuwa na viwango vya

kimataifa

iii. Kushindwa kujenga uwezo wa kutosha kwa wataalamu katika kozi za

utaalamu za muda mfupi (professional training) na mafunzo ya elimu

ya juu (M.Sc. na PhD).

iv. Kushindwa kumalizia majengo yaliyokusudiwa kutumika kwa kazi za

utafiti yakiwemo jengo la teknolojia ya habari na karakana za uhandisi.

Page 15: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA …tirdo.or.tz/documents/KAMATI YA BUNGE 2017.pdfViwanda, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, P.O. Box 601, Zanzibar 7. Bi. Christina Kilindu

15

8.2 Viwango vidogo vya mishahara kwa watumishi ukilinganisha na sekta

nyingine.

8.3 Viwanda vinavyomilikiwa na makampuni ya Kimataifa hutaka kufanyiwa kazi

na mashirika/asasi ambazo huduma zake hutambulika Kimataifa na ziko nje

ya nchi.

9.0 MIKAKATI YA UFUMBUZI WA CHANGAMOTO

9.1 JUHUDI ZA UTATUZI WA CHANGAMOTO ZA TIRDO

Juhudi za utatuzi wa changamoto zilizopo ni kama ifuatavyo:-

9.1.1 Shirika limendaa maandiko ya Miradi mbalimbali kwa Serikali ili kujenga

uwezo kwenye maabara za metallurgy, kwa ajili ya chuma, energy kwa ajili

ya makaa ya mawe na gesi, na agro-processing kwa ajili ya vyakula (value

addition) kwas asa huduma hizi wadau wanazipata toka nje ya nchi na

kuigharimu nchi kiasi kikubwa cha fedha za kigeni. Kwa kufanya hivyo

mapato yataifanya TIRDO kupunguza kuitegemea Serikali.

9.1.2 Sehemu ya mapato ya Shirika kutokana na huduma kwa wateja hutumika

kuwaendeleza wataalam. Pia shirika kwa kushirikiana na taasisi zingine za

utafiti zinaendelea na juhudi za kuishawishi Serikali iweze kutoa pesa za

kufanyia utafiti ambazo sasa zinatolewa kupitia COSTECH.

9.1.3 Shirika linatekeleza mkakati wa mipango ya maendeleo ‘Corporate

Strategic Plan’. eneo moja ambalo limelenga kulikwamua shirika kifedha ni

mpango wa muda mfupi wa kati na muda mrefu wa matumizi bora ya

ardhi yote ya TIRDO (land use plan, feasibility study and Business plan).

Mpango huo tayari umeanza kutekelezwa kwa kutafuta wadau mbali mbali

kuja kuwekeza katika maeneo mbalimbali ya uwekezaji.

9.1.4 Kuimarisha uwezo wa kutoa huduma zake kufikia kiwango

kinachotambulika kimataifa kwa kuhakiki maabara.

9.1.5 Juhudi za upatikanaji wa Hati Miliki kwa viwanja viwili ambavyo vina kesi

Mahakamani zinaendelea.

9.1.6 Shirika kuimarisha mashirikiano na taasisi zingine za ndani na nje ya nchi.

Page 16: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA …tirdo.or.tz/documents/KAMATI YA BUNGE 2017.pdfViwanda, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, P.O. Box 601, Zanzibar 7. Bi. Christina Kilindu

16

9.1.7 Kuwaongezea watafiti uwezo (Skills) katika kuandika maandiko ya miradi

(competitive proposal writing).

9.1.8 Shirika kujitangaza kwa wadau wake.

10.0 TIRDO NA MIKAKATI YA AWAMU YA UCHUMI WA VIWANDA

10.1 UTANGULIZI:

Shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) limejipanga ili

kuweza kutoa mchango wake katika mikakati ya kukuza uchumi wa viwanda

Tanzania kama inavyoelekezwa na Serikali ya Awamu ya tano. Katika

kutekeleza maelekezo mbalimbali ya serilkali ya Awamu ya Tano yanayolenga

kuwa na uchumi wa Viwanda kwa kuhakikisha kuwa ifikapo mwaka 2020,

Viwanda vimechangia kwa zaidi ya Asilimia 40% ya ajira Tanzania na pia

Mchango wa Viwanda kwenye Pato la Taifa kuongezeka toka Asilimia 9.9 hadi

Asilimia 15, Shirika limebuni mikakati kadhaa ambayo ikitekelezwa itatoa

matokea chanya na kuchangia kwa kiasi kikubwa maendeleo ya viwanda

Tanzania.

TIRDO imejipanga na imebuni Miradi inayolenga Sekta ya Gesi na Mafuta,

Makaa ya Mawe, Chuma, Usindikaji wa Vyakula, Ngozi na TEHAMA. Miradi

iliyobuniwa ni ile inayolenga kuongeza Pato la taifa, kuongeza ajira na

kuendeleza teknolojia.

Ili kutekeleza hayo, Shirika la Utafiti wa Maendeleo ya Viwanda Tanzania

(TIRDO) limepanga kufanya yafuatayo kwa kipindi cha 2016 – 2020/21 kama

litawezeshwa.

10.1.1 Mchango wa Pato la Taifa kutokana na viwanda kupanda

toka 9.9% hadi 15% ifikapo mwaka 2020.

Katika hili TIRDO imeandaa miradi 21 ambayo katika utekelezaji wake utaleta

tija kwa viwanda na hivyo kuchangia katika ongezeko la pato la Taifa hadi

kufikia 15% mwaka 2020. Miradi hiyo inalenga sekta ya kilimo

(Agroprocessing), sekta ya Ngozi (leather goods), sekta ya mafuta na gesi (oil

Page 17: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA …tirdo.or.tz/documents/KAMATI YA BUNGE 2017.pdfViwanda, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, P.O. Box 601, Zanzibar 7. Bi. Christina Kilindu

17

and gas) na Makaa ya Mawe na Chuma. Miradi hiyo iliwakilishwa Wizarani ili

kuingizwa kwenye Mpango wa Maendeleo wa Miaka mitano.

10.1.2 Sekta ya Viwanda kuongeza ajira kufikia asilimia 40 ya ajira

zote ifikapo 2020

TIRDO kwa kushirikiana na Serikali itaweka kipaumbele kwenye tafiti na

huduma za kitaalamu kwenye viwanda vinavyotumia malighafi zinazozalishwa

hapa nchini kama vile kilimo, mifugo, uvuvi na maliasili; Viwanda hivyo ni

pamoja na viwanda vya nguo, sabuni korosho, matunda n.k

10.1.3 Mikakati ya kuhamasisha sekta binafsi kuanzisha viwanda

vikubwa na vya kati na kuweka utaratibu wa kuvilinda dhidi

ya viwanda vya nje

Kwa kutumia wataalam wake, TIRDO itatoa huduma za kitaalam za ushauri

(Feasibility studies) kwa wawekezaji wa viwanda. TIRDO inao uzoefu wa

kutosha na imekuwa ikitumika na Benki ya Rasilimali (TIB) kutoa ushauri kwa

wateja wanaokopa kwa ajili ya kuanzisha viwanda. Hivyo TIRDO itatoa

mchango mkubwa wa kuishauri Serikali na wawekezaji juu ya uanzishwaji wa

viwanda na kuvilinda dhidi ya viwanda vya nje kwa kuhakikisha ubora wa

bidhaa zake ambazo zinazalishwa kwa gharama nafuu.

10.1.4 Kujenga mazingira rafiki yatakayowezesha kupunguza

gharama za uwekezaji na uendeshaji wa viwanda

TIRDO inatoa huduma za kitaalam za matumizi ya nishati na kuweza kusaidia

kupungua gharama za matumizi ya nishati viwandani kati ya asilimia 10 hadi

30. TIRDO imetoa ushauri huo wa kitaalam kwa viwanda na majengo ya

Serikali. Hivyo TIRDO itajitangaza ili kufikia wadau wengi zaidi ili kuhakikisha

viwanda vinazalisha bidhaa kwa gharama nafuu ya Nishati.

TIRDO pia hutoa huduma za kitaalam juu ya kupunguza athari za uchafuzi wa

mazingira ili kupunguza athari ya mazingira zinazotokana na viwanda lakini pia

Page 18: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA …tirdo.or.tz/documents/KAMATI YA BUNGE 2017.pdfViwanda, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, P.O. Box 601, Zanzibar 7. Bi. Christina Kilindu

18

kusaidia viwanda visisimamishe shughuli zake kwa sababu ya uchafu wa

mazingira wanapokaguliwa na wadhibiti wa mazingira kama (NEMC). TIRDO

itajitahidi pia kwenye eneo hili ili wadau wengi waendeshe viwanda bila

kuathiri mazingira na shughuli za uzalishaji.

10.1.5 Kuanzisha viwanda vya msingi vinavyotumia malighafi ya

chuma katika maeneo ya Liganga na Mchuchuma

Katika miradi iliyobuniwa na TIRDO ni ule wa Metallajia (Metallurgy) ambao

unalenga kupima ubora wa malighafi na bidhaa za chuma. Mradi huu

utasaidia wenye viwanda vinavyotumia malighafi ya chuma kuweza kupata

aina ya chuma bora ambazo zinaweza kukidhi ubora wa kimataifa hivyo

kuweza kuongeza soko na kipato. Hii itasaidia kuongeza pato la taifa pia ajira.

Pamoja na hayo, maabara hiyo pia itasaidia sana kuhakikisha kuwa chuma

kinachotumia kwenye nondo za ujenzi wa majumba ya ghorofa zinakuwa bora

na kupunguza athari ya majengo kubomoka hovyo.

10.1.6 Sekta ya viwanda kuongeza fursa za masoko hususan yenye

upendeleo wa ushuru wa forodha

TIRDO ina maabara ya chakula iliyohakikiwa kimataifa ambayo husaidia

kupima ubora wa bidhaa za chakula. Kwa hivyo TIRDO itasaidia sana kuweza

kusaidia katika kuongeza thamani kwa bidhaa na kuweza kupata masoko

mazuri kimataifa. Iwapo itaongezewa uwezo maabara hiyo itapima ubora wa

Bidhaa kama Asali, Maziwa, Nyama, Samaki, Maji n.k. Vipimo ambavyo

vinatambuliwa kimataifa.

10.1.7 Kuendeleza kazi ya ujenzi wa viwanda vidogo na vya kati hasa vinavyosindika mazao

Maabara ya chakula itasaidia pia kuongeza thamani za bidhaa kwenye

viwanda vodogo na vya kati. Pamoja na hilo, TIRDO itaendelea kubuni

mitambo mbalimbali nafuu kwa wawekezaji wadogo na wa kati

wanaojishughulisha na usindikaji wa mazao (Agroprocessing).

Page 19: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA …tirdo.or.tz/documents/KAMATI YA BUNGE 2017.pdfViwanda, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, P.O. Box 601, Zanzibar 7. Bi. Christina Kilindu

19

10.1.8 Benki ya Rasilimali (TIB) kupanua wigo wa Dirisha Maalumu ili liweze kutoa huduma zake kwenye maeneo yote nchini ikiwemo Tanzania Zanzibar

TIRDO ina mahusiano ya karibu na Benki ya Rasilmali (TIB) na ina

makubaliano (MOU) ya kushirikiana katika kufanya tathmini za viwanda kwa

wale wanaochukua mikopo kwa ajili ya uanzishaji wa viwanda. Kwa hiyo,

TIRDO itakuwa na nafasi nzuri pia kuweza kuishauri Benki na wawekezaji wa

Zanzibar juu ya uanzishwaji wa viwanda. Pamoja na hayo, TIRDO pia ina

mahusiano mazuri ya kikazi na Wizara ya Viwanda na Biashara ya Zanzibar na

Zanzibar State Trading Corporation.

10.1.9 Kuhakikisha kuwa viwanda vilivyopo vinafanya kazi

Ili kuhakikisha kuwa viwanda vilivyopo vinafanya kazi kwa kiwango

kinachokubalika, tathmini ya uwezo wa uzalishaji na teknolojia haina budi

kufanyika. TIRDO kwa kushirikia na taasisi nyingine imejipanga kufanya

tathmini hizo pindi itakapowezeshwa.

10.1.10 Msajili wa Hazina kushughulikia viwanda ambavyo vimeshindwa kufanya kazi.

Ili kuhakikisha kuwa viwanda vilivyokufa wanapewa wawekezaji wenye uwezo,

tathmini ya uwezo wa uzalishaji na teknolojia haina budi kufanyika. TIRDO

ilishawasiliana na Wizara na Msajili wa Hazina kuwa iko tayari kufanya hizo

tathmini kwa kusaidiana na taasisi nyingine za serikali kwani ina utaalam wa

kutosha na imeshawahi kufanya shughuli kama hizo.

11.0 HITIMISHO

Shirika likiwezeshwa kwenye utafiti na kupewa msukumo unaostahili, Shirika

litapiga hatua katika kutatua matatizo yanayovikabili viwanda vyetu kuongeza

uzalishaji na ubora wa bidhaa hivyo kukuza uchumi wa nchi kwani nchi

zilizoendelea pato lake kubwa hutokana na viwanda.

Page 20: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA …tirdo.or.tz/documents/KAMATI YA BUNGE 2017.pdfViwanda, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, P.O. Box 601, Zanzibar 7. Bi. Christina Kilindu

20

MUUNDO WA SHIRIKA

Kiamb. ‘A’

Page 21: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA …tirdo.or.tz/documents/KAMATI YA BUNGE 2017.pdfViwanda, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, P.O. Box 601, Zanzibar 7. Bi. Christina Kilindu

21

KIAMBATISHO B TAFITI ZILIZO FANYIKA TIRDO

1. Kuzalisha “Sodium Alginate” kutokana na kaoli

2. Kuzalisha “Caustic Soda” na kutokana na Magadi

3. Uzalishwaji wa furfural na furane resins kutoka katika mabaki ya pentosan

4. Utengenezaji wa “essential oil” kutokana na majani kama michungwa, michachai

5. Utunzaji wa bidhaa za mbao kwa kutumia gundi iliyozalishwa kutokana na mafuta ya

maganda ya korosho, gundi hiyo pia ilitumika katika utengenezaji wa ‘plywood’ na

‘chipboard’

6. Kuondoa sumu ya Ocharatoxin A katika kahawa. Mradi huu ulifadhiliwa na Jumuiya ya

ulaya, na kutekelezwa katika mikoa ya Kilimanjaro na Arusha

7. Kuboresha uyoga kwa kuzalisha uyoga wenye madini joto na uyoga wa dawa (medicinal

mushroom)

8. Kuboresha unga wa muhogo uliochachushwa (fermented cassava flour) unaozalishwa

kwa njia za asili lengo likiwa ni kuongeza ubora wa bidhaa hiyo, kuongeza udumu (shelf

life) na usafi wa bidhaa, kwa kuondoa sumu aina ya cyanide – uliopelekea

kutengenezwa kwa mashine ya kuchakata muhogo (cassava grating machine). Mashine

hizi zilibuniwa na kutengeneaw kwa ushirikiano kati ya TIRDO na Intermech Engineering

Ltd, na kusambazwa na TIRDO katika mikoa ya Pwani, Lindi, Mtwara na Ruvuma na

baada sehemu mbambali ndani na nje ya nchi (e.g. Malawi)

9. TIRDO kwa kushirikiana na “Tropical Pesticide Research Institute” ilifanya utafiti wa jinsi

ya kutunza bidhaa ya mbao kwa kutumia mimea “plant preservative” ambayo

inapatikana hapa hapa nchini ili kulinda bidhaa za mbao kutokana na wadudu na ukungu

(fungus) ambao wanaharibu na kusababisha mbao kulika .

10. Mfumo wa ufuatiliaji wa bidhaa za chakula ambapo ulipelekea kuanzishwa kwa GSI

Tanzania ambayo ni kampuni inayota namba za mstari ‘Bar code’ nchini Tanzania.

11. Kuongeza thamani kwenye taka ngumu zitokanazo na uzalishwaji katika viwanda vya

ngozi (Value addition in leather solid wastes to produce leather boards).

12. Kutumia mazao ya kilimo na mabaki ili kupata nishati mbadala (Industrial Bioconversion

of selected Tanzania crops and residues into value added products using Biotechnology)

13. Makaushio yanayotumia nishati ya Jua Tunnel solar dryer)

Page 22: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA …tirdo.or.tz/documents/KAMATI YA BUNGE 2017.pdfViwanda, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, P.O. Box 601, Zanzibar 7. Bi. Christina Kilindu

22

14. Uboreshaji wa machine za kusaga nafaka kwa kuondoa chembechembe za chuma

zinazochanganyika na unga.

15. Usalama wa mtandao (Cyber Security) kwa mazingira ya Tanzania iliyopelea kuanzishwa

kwa maabara ya ‘Cyber security’ TIRDO.

16. Uzalishaji wa bioethanol kutoka katika mimea ya Dioscorea sansibarensis na Pyrecantha

kaurabasana.

17. Uzalishaji wa biogesi kutokana na taka zitokanazo na usindikaji wa mafuta ya kula

(spent bleaching earth) na kinyesi cha ng’ombe (cow dung manure)

18. Utengenezaji wa mashine ya kukamulia juice ya machungwa iliyofungwa Wilaya ya

Muheza, Tanga.

19. Kutathimini viwanda vinavyoanzishwa na wateja wanaokopa pesa (mtaji) kutoka katika

Benki ya TIB Thathimin imeshafanyika Rombo, Kilimanjaro, Bukoba, Kagera, Pwani,

Arusha, Sumbawanga, Mahonda, Zanzibar, Bunju, Kigamboni, DSM, Kibaha Pwani.

20. Mradi wa kuwasaidia wajasiriamali wa mashamba ya chumvi kuongeza thamani ya zao

la chumvi huko Wawi Pemba, Zanzibar.

21. Mradi wa kutengeneza na kufundisha ukaushaji wa mazao ya kilimo, Mikoa ya Lindi na

Mtwara kwa ushirikiano na FAO.

22. Ufundishaji, utengenezaji na usambazaji wa makaushio ya jua katika mkoa wa Pwani na

shirika la Kibelijiji linalo hudumia wakulima wadogowadogo vijini (VECO).

23. Mradi wa kutengeneza, makaushio ya wajasiriamali wa zao la pilipili, Mikumi, Morogoro

kwa ajili ya kuzuia Tembo waharibifu na kuongeza thamani ya zao hili kwa kushirikana

na ‘World Animal Protection’ ya Nairobi, Kenya.

KIAMBATISHO D

HUDUMA VIWANDANI

1. Upembuzi yakinifu na kutayarisha mpango wa ufufuaji wa kiwanda cha ngozi Mwanza na chai

Mponde Tanga (Mwanza Tanneries na Mponde tea factory)

2. Kupunguza uharibifu wa mazingira katika viwanda vinavyozalisha bidhaa mbalimbali kwa kutoa

huduma za upimaji wa viwango vya hewa zinazochafua mazingira, viwango vya kelele katika

sehemu mbalimbali viwandani na viwango vya vumbi litolewalo wakati wa uzalishaji viwandani

3. Kupima sampuli mbalimbali za vyakula na maji ili kuangalia ubora wake na kuona kama vinakidhi

matakwa ya viwango vya kimataifa vinavyokubalika katika vyakula

Page 23: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA …tirdo.or.tz/documents/KAMATI YA BUNGE 2017.pdfViwanda, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, P.O. Box 601, Zanzibar 7. Bi. Christina Kilindu

23

4. TIRDO imeshiriki katika mradi wa gesi huko MnaziBay Mtwara mpaka Msimbati kwa kuhakiki

ubora wa bomba linalosafirisha gesi hiyo kwa kupima pasipo kuharibu maungio yote ya bomba

hilo ili kuepusha madhara kwa mazingira na kwa wakazi wa maeneo mbalimbali ambapo bomba

hilo limepita. Bomba hilo lilikuwa lenye urefu wa kilometa 26.

5. Shirika limetoa mafunzo kwa wajasiriamali katika maeneo ya uchomeleaji na pia teknolojia za

uboreshaji chuma viwandani

6. Shirika lilitoa huduma ya ukaguzi wa vifaa vya kihandisi ikiwa ni pamoja na matanki ya mafuta,

vivuko (pantoon), mitambo ya kuzalisha umeme

7. Upimaji wa ufanisi wa majiko ya mkaa na yale yanayotumia mafuta ya mbegu kutoka vikundi

mbalimbali ili kupata matumizi bora ya nishati

8. Matumizi bora ya nishati katika viwanda, majengo ya ofisi na makazi (energy auditing)

9. Mafunzo ya ‘Good manufacturing practices (GMP)’, ‘Good hygine practices (GHP) na ‘Hazard

analysis critical control point’ (HACCP) kwa viwanda vya chakula na wajasiriamali

10. Kufanya upembuzi yakinifu (feasibility study and evaluation) katika viwanda vipya na viwanda

vinavyoongeza uzalishaji chini ya Benki ya Uwekezaji (Tanzania investment Bank)

Page 24: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA …tirdo.or.tz/documents/KAMATI YA BUNGE 2017.pdfViwanda, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, P.O. Box 601, Zanzibar 7. Bi. Christina Kilindu

24

KIAMBATISHO E

TIRDO PROJECTS TO SUPPORT INDUSTRIALIZATION DRIVE

1. TIRDO Industrial Park

Establishment of industrial park at TIRDO facility for incubation and transfer of industrial and agro

technologies

Incubation of entrepreneurs for various agro processing and industrial technologies is necessary to effective

technology transfer. Facility for technology incubation is currently lacking at TIRDO

OBJECTIVE

Industrial park established at TIRDO by 2018

Reverse engineered products for industries and agro-processing

Industrial incubates graduate by 2020 Increased Investment in agro-processing

Increased job creation

Increased government revenue through new investment in agro-processing

2. Petro-Chemical Industries

Petrochemical laboratory at TIRDO

There is no specialized laboratory for the petrochemical industry in Tanzania. Most of the petrochemical

products e.g. fertilizers need tailored quality assurance services to ensure quality products to meet both

national and internal standard requirements

OBJECTIVE

Establish an accredited petrochemical laboratory at TIRDO

Establish database for nutrient requirement in each agricultural zones

Establish quality assurance systems in petrochemical factories

3. Agro-industries

Reducing Chromium in tanneries effluent waste through unit process recycling in Leather Industries

(TIRDO)

A lot of Chromium is disposed in tanneries waste water Leather Industries and is difficult to recover from

tanneries effluent.

This is environmental hazard and adds more expenses in waste water treatment

OBJECTIVE

Determination of residue Chromium in tanneries effluent

Training on Chromium recycling process to tanneries SMMES

Recycling within the tanning processing area

4 Market access of Tanzania Agro- products through accredited testing services (TIRDO)

In adequate accredited laboratory services to support the agro-industry in Tanzania

Most testing services such as residue analysis in honey, meat and milk are sourced outside the country.

These services are expensive and make the Agro-industry in Tanzania less competitive

No single laboratory catering for seafood in all the coastal zone in Tanzania

The Tanzania coast is more endowed with fish than other countries sharing the Indian ocean coast because

of adverse weather (warm and cold current from Mombasa and Mozambique respectively, however this vast

resource is under exploited because of lack of support services

OBJECTIVE

Extend accredited capacity of TIRDO (equipment and human capacity) to include residue analysis,

pesticides residues and mycotoxins analysis

Page 25: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA …tirdo.or.tz/documents/KAMATI YA BUNGE 2017.pdfViwanda, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, P.O. Box 601, Zanzibar 7. Bi. Christina Kilindu

25

Accreditation of food analysis, agro-chemistry environment and health safety laboratories through SADCAS

Establish and accredited a seafood laboratory using the space and expertise available at TIRDO

5 Innovative technologies for reduction of post harvest losses and efficient utilization of resources in the

agro-industry sector (TIRDO)

Post-harvest losses in cereals e.g. rice is about 40% attributed to brokenness, storage pests and

inappropriate technology.

Valuable resources such as rice brand oil and nutraceutical molecules in brand and husk are not tapped due

to lack of appropriate technology.

Increasing rise of people living in cities more rice is being consumed than ever before. Because rice starch is

generally of high glycemic index (GI) , the city dwellers are at risk of health problems associated with high

GI foods including diabetes and cardiovascular diseases

Lack of appropriate processing technologies for small grains such as millet, sorghum and finger millet is

disincentive to cultivate and processing of these draught resistant and highly nutritious cereals

OBJECTIVE

Pilot appropriate handling, drying and di-husking rice to reduce brokenness

Employ molecular techniques to classify Tanzania rice varieties into high and low GI and develop tailored

products for infants and elderly

Develop process for extraction of rice bran oil and blending with conventions oils to produce functional

cooking oils

Extraction and characterization of nutraceutical compounds for rice husk and bran and develop various

nutraceutical products

Develop appropriate technology for processing small grains and develop various products form them

Establish process for biofuel and biofertiliser production from cereal processing waste to result to zero

waste

6 Value Addition on Tanzania vegetable tanned leather using Kaolin from Tanzania (TIRDO)

There is Low quality of hides and skins and poor value addition locally. Vegetable tanned leather

exhibits lower shrinkage temperature. Chrome tanning is associated with environmental degradation

OBJECTIVE

Replacement of traditional tanning by introducing mimosa and aluminium sulphate from kaolin (semi-

metal tanning)

Skills development to SMMEs

Utilization of locally available raw materials to tanning in replacement of imported ones

7 Establishment of accredited leather testing laboratory (TIRDO)

Absence of accredited leather testing laboratory leads to use of health hazardous chemicals in leather

processing. There is also lack of quality assurance practices for exported leather and leather goods.

Rejection or down grading of leather and leather goods in external market is common coupled with lack of

enforcement to tanners to improve quality of their products. Utilization of leather goods with harmful

chemicals to human health is also common in Tanzania

OBJECTIVE

Building and accrediting special leather testing laboratory

Testing and certifying leather and leather goods for internal and external market

Advising tanners about the quality of their leather and ways to improve based on found results after

testing of leather properties

8 Value addition on leather solid wastes to produce leather boards at TIRDO

High production of leather solid wastes in tanneries. It is also Difficult disposing of leather solid wastes as

they contain chromium (hazardous chemical)

OBJECTIVE

Recycling of leather solid wastes to produce leather goods

Page 26: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA …tirdo.or.tz/documents/KAMATI YA BUNGE 2017.pdfViwanda, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, P.O. Box 601, Zanzibar 7. Bi. Christina Kilindu

26

9 Production of fine chemicals and allied products from Cashewnut Shells

Huge amount of cashewnut shells are produced and they are environmental concern. Cashewnut shells are

important resource for industrial chemicals but little is utilized in Tanzania. Fluctuating price of cashew

does not take on board the value of the shells and hence loss to the farmers

OBJECTIVE

Production of cashewnut shell liquid for fibreboard industries

Production of Arcadic acids for chemical industries

Compaction of cashewnut shell for solid waste for bio-energy

10 Coal for Industries and Households

Rural Electrification through Decentralized Small to Medium Scale Electricity Generation Facilities

Using Locally Available Coal and Biomass (TIRDO)

Rural electrification is less than 5%. There is also Poor (electrified) services for health, schools and

water supply leading to Poor economic activities, Rampant diseases from use of fuel wood and

Environmental degradation from intensive use of fuel wood

OBJECTIVE

Provision of clean energy technologies for electricity generation

Utilization of locally available coal and biomass materials

Development and dissemination of local technologies for electricity generation

11 Use of carbonized coal briquettes to substitute charcoal and firewood as cooking fuel in Tanzania

(TIRDO)

Rampant diseases from use of fuel wood. Environmental degradation from intensive use of fuel wood.

Also, there drudgery of women in search of fuel wood

OBJECTIVE

Development of carbonized coal briquettes in substitution of fuel wood and charcoal for household

cooking

Utilization of locally available coal and biomass materials

Development and dissemination of local technologies for household cooking

12 Comprehensive assessment of Tanzania coal quality using accredited laboratory (TIRDO)

Despite the abundant coal deposits, less is on their quality. There is a Danger of utilizing quality

(coking) coal for thermal applications. Technology development is impaired in absence of coal quality

information

OBJECTIVE

Establishment of coal quality databank for Tanzania

Undertaking a detailed sampling and analysis of Tanzania coal

13 Iron and Steel

Development of iron and steel technologies from locally available ore deposits (TIRDO)

Existing ore deposit under-utilized and there is Overdependence on scrap metal for iron and steel

industry. There are also low technological capacity in iron and steel industry, Low quality of iron and

steel products, Low iron and steel per capital consumption and hence low GDP

OBJECTIVE

Capacity development to the TIRDO accredited metallurgical laboratory

Carrying out evaluation of raw materials for iron & steel and other related industries.

Characterization and optimization of raw materials and direct reduction (DR) process parameters for

production of high-grade sponge iron from e.g. Liganga and Maganga Matitu iron ores

Develop appropriate iron and steel technologies for SMEs

Transfer the technology of sponge iron as metallic feedstock in rolling mills and foundries to replace

Page 27: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA …tirdo.or.tz/documents/KAMATI YA BUNGE 2017.pdfViwanda, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, P.O. Box 601, Zanzibar 7. Bi. Christina Kilindu

27

conventional scrap metal

Assist local industries to produce high quality iron & steel products e.g. high strength steel

reinforcement bars

14 Oil and Gas

Enhancing Local Content through skills Development in Welding, Inspection, Fabrication for SMEs

to participate in the emerging oil and gas industry (TIRDO)

Welding and inspection skills are low. Participation of local technicians and entrepreneurs in the oil and

gas industry is low. Almost all services in oil and gas are done by foreign companies. There are no

certification services to local practitioners

OBJECTIVE

Welding and inspection skills development to local technicians and entrepreneurs through accredited

welding services

Establishment of certification programs

15 Industrial services

Provision of Professional Coal Analytical Services for Supporting Industrial Coal Users (Cement,

Paper Mills and Others) and the Proposed Thermal Power Plants (Kiwira, Mchuchuma, and Ngaka)

(TIRDO)

Tanzania coal is analyzed abroad. Results of coal analysis from foreign laboratories is skeptical and is

associated with delays. Also, Tanzania coal quality is less known which poses for cheating in coal export

deals. There is also rampant revenue loss due to adulterated coal quality

OBJECTIVE

Strengthening the technical capacity to the coal accredited laboratory at TIRDO

Dedicating the TIRDO coal laboratory into a reference coal laboratory

16 Improving competitiveness to industries through energy management (TIRDO)

Energy cost to industries consumes up to 40% of total revenue. The high energy cost makes industries not

attractive . The high energy cost makes products not competitive regionally and internationally

OBJECTIVE

Introduce energy management practices to industries

Train the industries to adopt the practices and energy efficient technologies

Energy management skills development to industrialists

17 Revival of privatized industries (TIRDO)

Majority of the privatized industries are said to be marginally contributing to the development agenda. Less

is known on their status and some are said to have shifted their basic role

OBJECTIVE

Undertake an industrial audit to establish the status of the privatized industries

Undertake the needs assessment

Establish a prioritized strategy by taking into consideration of employment, GDP contribution and

contribution to socio-economic development

18 Automatic water Quality Monitoring and Reporting in Aquaculture (TIRDO)

There is inadequate supply of fish to the existing fish processing industries. This is due to the lack of

modern technology in aquaculture. There is a need of establishing automatic monitoring and reporting

systems of aquaculture industry in Tanzania and identification of baseline conditions suitable for

aquatic life.

OBJECTIVE

Establishment of automatic monitoring and reporting system in Tanzania

identification of baseline conditions suitable for aquatic life Environmental impact assessment

Page 28: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA …tirdo.or.tz/documents/KAMATI YA BUNGE 2017.pdfViwanda, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, P.O. Box 601, Zanzibar 7. Bi. Christina Kilindu

28

19 Deployment of Wireless Sensor Networks for Industrial Environmental Monitoring

There is great emission of pollutant gases in manufacturing industries. Currently rudimentary technologies

are employed to monitor industrial pollutants. These technologies are inaccurate and unsafe to users

OBJECTIVE

Establish innovate industrial environmental pollutant gases (CO, O2, CO2, CO, SO2, H2S, NO, NO2, HC

and PM10(Lead)) monitoring base on sensor technology

Awareness creation in the use sensor technology to monitor industrial processors

Transfer of sensor industrial process monitoring technology to SMMES

20 Advanced Cyber Security Training Services (TIRDO)

Critical infrastructure security in Tanzania is insufficient. Media used in banking transaction for industrial

business is not safe. There is lack of awareness of cyber security threats

OBJECTIVE

Training on cyber security issues to raise awareness

To establish security measures in Tanzania industrial firms (major automated industrial)

Development of Industrial application software.

21 Environment

Auditing and valorization of Municipal waste for generation of electricity (TIRDO)

Disposal of municipal waste in most of the big cities in Tanzania is a challenge due to lack of appropriate

systems yet the municipal waste is great bioresource which can be converted to biofuels and biofertiliser

OBJECTIVE

To introduce an innovative system for collection, sorting and classifying municipal waste in organic and

non-organic waste

Building an innovative biogas plant for each municipal Dar-es salaam, Arusha, Mwanza, Tanga, Iringa,

Mbeya, Morogoro

Characterize, pre-treat and produce biogas from the organic fraction of municipal waste

The biogas to used to generate electricity to be fed into the national grid

The biogas slurry to be evaluated for biofertiliser to boot peri-urban vegetable production