Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia
Mkakati wa Kitaifa wa Kisomo na Elimu kwa Umma (MTaKEU) 2020/2021 - 2024/2025
Januari, 2020
ii
Yaliyomo
DIBAJI ���������������������������������������������������������������������������������������������������������������������� iv
SHUKURANI ������������������������������������������������������������������������������������������������������������ vi
ORODHA YA VIFUPISHO ���������������������������������������������������������������������������������������� vii
MUHTASARI ����������������������������������������������������������������������������������������������������������� viii
SURA YA KWANZA �������������������������������������������������������������������������������������������������� 1
UTANGULIZI ������������������������������������������������������������������������������������������������������������� 1
1.1 Usuli ........................................................................................................................ 1
1.2 Madhumuni ya MTaKEU ...................................................................................... 4
1.3 Hatua za Uandaaji wa MTaKEU ....................................................................... 4
SURA YA PILI ������������������������������������������������������������������������������������������������������������ 5
UPEMBUZI YAKINIFU WA MAZINGIRA �������������������������������������������������������������������� 5
2.1 Maendeleo ya Kisomo na Elimu kwa Umma Tanzania ................................. 5
2.2 Mifumo ya Kisera Inayozingatiwa katika MTaKEU ...................................... 7
SURA YA TATU ������������������������������������������������������������������������������������������������������� 10
UCHANGANUZI WA UWEZO, UDHAIFU, FURSA NA CHANGAMOTO ������������������ 10
3.1 Muhtasari wa Uchanganuzi ............................................................................10
3.2 Tathmini ya Mazingira ya Ndani ....................................................................10
SURA YA NNE ��������������������������������������������������������������������������������������������������������� 14
DIRA, DHIMA NA MALENGO YA KIMKAKATI ������������������������������������������������������� 14
4.1 Dira .......................................................................................................................14
4.2 Dhima ...................................................................................................................14
4.3 Malengo ya Kimkakati ....................................................................................14
4.4 Malengo ya Kimkakati, Mikakati, Shabaha na Viashiria vya Utendaji.15
iii
SURA YA TANO ����������������������������������������������������������������������������������������������������� 30
MFUMO WA USHIRIKIANO KITAASISI KATIKA KUTEKELEZA MTaKEU ���������������� 30
5.1 Wahusika wa MTaKEU ......................................................................................30
5.2 Mfumo wa Kitaasisi katika Kutekeleza MTaKEU .........................................31
SURA YA SITA ��������������������������������������������������������������������������������������������������������� 42
UFUATILIAJI, TATHMINI NA MFUMO WA UTOAJI TAARIFA ��������������������������������� 42
6.1 Maelezo ya Jumla ............................................................................................42
6.2 Ufuatiliaji na Tathmini ya utekelezaji wa MTaKEU .....................................42
SURA YA SABA ������������������������������������������������������������������������������������������������������� 44
UWEZESHWAJI WA KIFEDHA NA UENDELEVU WA MKAKATI ������������������������������� 44
7.1 Uwezeshwaji wa Kifedha wa MTaKEU ..........................................................44
7.2 Mikakati ya Kupata Fedha ..............................................................................41
7.3 Makadirio ya Gharama za MTaKEU kwa kipindi cha 2020/2021- 2024/2025 .......................................................................................................45
7.4 Uendelevu katika Utekelezaji wa MTaKEU .................................................49
KIAMBATISHO �������������������������������������������������������������������������������������������������������� 50
iv
DIBAJI
Upatikanaji wa stadi za kisomo na elimu kwa umma ni jambo la
muhimu katika kuwasaidia wanaume na wanawake wa Tanzania
kuyatawala mazingira yao. Kutokana na umuhimu wa stadi za kisomo
katika kumwezesha mtu kuwa raia mwema, kisomo kimekuwa ni sehemu
ya programu za elimu ya watu wazima nchini. Kwa hiyo, mkakati huu
unalenga kuleta mabadiliko kwa vijana na watu wazima nchini Tanzania,
ambao wanakabiliwa na changamoto zinazotokana na kutokuwa na stadi
za kisomo katika maisha yao ya kila siku. Madhumuni ya mkakati huu
ni kubuni, kuendeleza na kuandaa programu bora za kisomo na elimu
kwa umma zinazowafikia watanzania wengi. Vilevile, umejikita katika
kuhakikisha umahiri unaopatikana unaendelezwa kwa kuimarisha huduma
saidizi za kisomo. Mkakati umebuniwa baada ya kufanya upembuzi
yakinifu wa hali ya kisomo na elimu kwa umma na kwa kuhusisha
watekelezaji mbalimbali wa programu za kisomo na elimu kwa umma
nchini. Mkakati huu unatanabahisha masuala muhimu yaliyobainishwa
na wadau wakuu wa kisomo na elimu kwa umma kama njia ya kusaidia
kushughulikia changamoto za kisomo na elimu kwa umma nchini Tanzania.
Watekelezaji mbalimbali wa shughuli za kisomo na elimu kwa umma kama
vile Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia (WyEST), Tawala za Mikoa na
Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima, Wizara,
Idara na Wakala za Umma, mamlaka za serikali za mitaa, asasi za kiraia,
wadau wa maendeleo, vyuo vikuu, Bodi ya Huduma za Maktaba Tanzania,
na Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi ni washirika wakubwa katika
kubuni na kutekeleza Mkakati wa Kitaifa wa Kisomo na Elimu kwa Umma
(MTaKEU). Hivyo, unahitajika ushirikiano madhubuti kati na baina ya
wizara na taasisi mbalimbali za serikali katika kuhakikisha utekelezaji
sawia na wenye kuleta tija. Kwa mantiki hiyo, serikali itaendeleza juhudi
v
zake ili kuhakikisha kwamba kunakuwepo na jamii ya watu walioelimika
na wenye uwezo wa kupata taarifa sahihi ili kuwa na maisha bora na
maendeleo endelevu. Serikali inatambua pia ukweli kwamba ukosefu wa
stadi za kisomo kwa vijana na watu wazima ni kikwazo katika jitihada
za kutimiza agenda za maendeleo ya taifa na malengo ya maendeleo
endelevu kufikia mwaka 2030, ambayo Tanzania imeridhia kuyatimiza
kikamilifu. Kwa hali yoyote ile, Serikali kupitia WyEST itaendelea kuweka
mazingira mazuri yatakayoruhusu wadau mbalimbali kushiriki kikamilifu
katika kutekeleza mkakati huu.
……………………………
Dkt� Lyabwene M� Mtahabwa
Kamishna wa Elimu
vi
SHUKURANI
Mkakati wa Kitaifa wa Kisomo na Elimu kwa Umma (MTaKEU) ni matokeo
ya juhudi na michango mbalimbali kutoka kwa watu binafsi, mashirika na
wizara za serikali. Taasisi ya Elimu ya Watu wa Wazima (TEWW) inatoa
shukurani za dhati kwa wadau wote ambao wamefanikisha maandalizi ya
mkakati huu. Kwa nafasi ya pekee, TEWW inaishukuru Wizara ya Elimu,
Sayansi na Teknolojia (WyEST) kwa kuongoza maandalizi ya mkakati
huu. Maelekezo na msaada ambao umeendelea kutolewa na WyEST
umefanikisha kuandikwa kwa mkakati huu. TEWW inatoa shukurani pia
kwa wataalamu wa ndani ya TEWW, WyEST, na Ofisi ya Raisi - Tawala
za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI) kwa mchango na ushauri
wao wa dhahiri ambao umefanikisha andiko hili.
Vivyo hivyo, TEWW inatoa shukurani kwa mashirika mengine na wadau
mbalimbali walioshiriki kwa mchango wao mkubwa mpaka kukamilika kwa
mkakati huu. Pia, Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima inatambua mchango
kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Chuo Kikuu Huria cha Tanzania,
Taasisi ya Elimu Tanzania, Baraza la Mitihani la Tanzania na Mamlaka ya
Elimu na Mafunzo ya Ufundi. Mashirika mengine ni pamoja na Bodi ya
Huduma za Maktaba Tanzania, Vyuo vya Maendeleo ya Jamii, asasi za
kiraia na wadau wa maendeleo.
……………………………
Dkt� Naomi Katunzi
Mwenyekiti wa Baraza la Usimamizi TEWW
vii
ORODHA YA VIFUPISHO
CCM Chama cha Mapinduzi
MEMKWA Mpango wa Elimu ya Msingi kwa Walioikosa
MMEM Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi
MTaKEU Mkakati wa Kitaifa wa Kisomo na Elimu kwa Umma
MTEF Medium Term Expenditure Framework
MUKEJA Mpango wa Uwiano kati ya Elimu ya Watu Wazima na
Jamii
OR-TAMISEMI Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
TEWW Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima
URT United Republic of Tanzania
WyEST Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia
viii
MUHTASARI
Serikali ya Tanzania imefanya juhudi kubwa kupambana na tatizo la
kutokujua kusoma, kuandika na kuhesabu nchini. Ipo mikakati rasmi na
isiyo rasmi inayotumika katika kupambana na kutokujua kusoma, kuandika
na kuhesabu nchini Tanzania. Jitihada na mikakati hiyo inayofanywa na
serikali ya Tanzania inaendana na lengo namba 4.6 la Malengo ya
Maendeleo Endelevu ya dunia ambalo linajikita katika “kuhakikisha
kwamba vijana na watu wazima wote, wanaume na wanawake, wanafikia
kiwango cha kujua kusoma, kuandika na kuhesabu ifikapo mwaka 2030.
Lengo hili linaakisi jitihada za kiulimwengu zinazoendelea za kuzitaka
serikali zote ulimwenguni kuondoa tatizo la kutokujua kusoma, kuandika
na kuhesabu.
Licha ya jitihada zinazofanywa na nchi ya Tanzania kuendeleza fursa
za elimu na kisomo tangu uhuru, matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi
nchini Tanzania (URT, 2012) yanaonesha kwamba, vijana na watu wazima
wenye umri wa miaka 15 na zaidi wapatao milioni 5.5 (22.4% ya idadi
ya watu wote) hawajui kusoma na kuandika. Takwimu hii inatoa picha
kwamba vijana na watu wazima milioni 5.5 bado hawana haki ya msingi
ya kupata fursa za elimu na stadi za kisomo. Kutokujua kusoma na
kuandika ni kikwazo kikubwa kwa maendeleo ya mtu binafsi na jamii
kwa ujumla. Hivyo, Mkakati wa Kitaifa wa Kisomo na Elimu kwa Umma
(MTaKEU) ni programu ya miaka mitano kwa kipindi cha 2020/2021-
2024/2025 ambayo imeandaliwa kama mwitikio wa kushughulikia tatizo
hilo. Mpango huu unatambua kisomo kama haki ya msingi kwa maendeleo
ya mtu binafsi, kijamii, kiuchumi na kisiasa.
MTaKEU ni mwongozo ulioandaliwa kwa makusudi kama nyenzo ya
kuongoza wadau mbalimbali ambao wanatekeleza programu za kisomo
ix
na elimu kwa umma katika ngazi tofauti nchini. Mkakati unatambua
kwamba masuala ya kisomo na elimu kwa umma ni mtambuka na yanahitaji
kufanyiwa kazi na wadau mbalimbali wa sekta ya elimu ya watu wazima
na elimu nje ya mfumo rasmi. MTaKEU umeandaliwa kutokana na tathmini
ya mahitaji ambayo ilihusisha watu binafsi, serikali, mashiriki ya kiserikali
na yasiyokuwa ya kiserikali, taasisi za elimu na washirika wa maedeleo.
Mkakati unabainisha jitihada za taifa katika kukuza na kuendeleza
kisomo na unahusianishwa na sera, matamko na mikataba ya kitaifa na
kimataifa, kwa kuzingatia uzoefu tulioupitia katika sekta ya elimu tangu
nchi ilipopata uhuru.
Dira ya muda mrefu ya MTaKEU ni kuwa na jamii iliyoelimika na yenye
uwezo wa kupata taarifa sahihi kwa ajili ya kuwa na maisha bora na
maendeleo endelevu. Kuifanya dira hii iwe halisi, mkakati huu umeweka
malengo kadhaa ambayo ni: Kuanzisha programu za kisomo na elimu
kwa umma zilizo bora na zenye manufaa kwa jamii; Kuimarisha mifumo na
programu wezeshi za kuendeleza kisomo na elimu kwa umma; Kuboresha
mifumo ya usimamizi wa takwimu za kisomo na elimu kwa umma; Kuweka
viwango vya sifa za kitaaluma kwa ajili ya programu za kisomo na elimu
kwa umma; Kuandaa zana na vifaa bora vya kufundishia na kujifunzia
katika programu za kisomo na elimu kwa umma; Kujenga uwezo wa
wawezeshaji na waratibu wa programu za kisomo na elimu kwa umma;
Kukuza kazi za utafiti, uvumbuzi na ubunifu katika masuala ya kisomo na
elimu kwa umma. Mkakati huu umeweka pia mikakati mahsusi, shabaha
na viashiria vya utendaji kwa kila lengo.
Mkakati huu unafafanua kwa uwazi mfumo wa utekelezaji; unaonesha
jinsi ufuatiliaji na tathmini vitakavyofanyika; na unafafanua utaratibu wa
kifedha utakavyokuwa katika kufikia malengo. Wakati ambapo WyEST
inakuwa na jukumu kuu la kiuongozi katika utekelezaji wa mkakati huu
x
kwa kushirikiana na OR-TAMISEMI, wadau wengine wote wanahitaji
kuhakikisha kwamba majukumu yao yaliyobainishwa yanaingizwa
katika mipango na bajeti zao. Hivyo basi, inatarajiwa kwamba MTaKEU
utaongoza juhudi za kukuza na kuendeleza kiwango cha stadi za kisomo
miongoni mwa vijana na watu wazima nchini na kusababisha kuwa na
maisha bora na maendeleo endelevu.
1
SURA YA KWANZA
UTANGULIZI
1�1 Usuli
Kisomo ni moja kati ya nyenzo kuu za maendeleo na sehemu muhimu ya
stadi za msingi na umahiri unaohitajika kumwezesha mtu kuwa raia mwema.
Huimarisha uwezo wa watu kujishughulisha kwa uhuru na kuongeza uwezo
wao wa kutawala na kubadili maisha yao. Ukosefu wa stadi za kusoma,
kuandika na kuhesabu huwafanya watu kuwa wahanga wa umasikini,
kutengwa kijamii, na kushindwa kupata mahitaji ya msingi na kukabiliwa
na hatari ya kunyimwa haki za kibinadamu. Kwa kutambua umuhimu
mkubwa wa kisomo, tangu mwaka 1948, UNESCO imekuwa ikitazama
kisomo kama haki ya binadamu. Kwa tafsiri rahisi, kisomo humaanisha
uwezo wa kusoma, kuandika na kufanya hesabu za kawaida katika
lugha yoyote kwa kiwango kinachoridhisha. Hata hivyo, katika mkakati
huu, dhana ya kisomo haiishii tu katika uwezo wa kusoma, kuandika na
kufanya hesabu rahisi, bali pia katika kutambua matumizi yake kwenye
maingiliano ya maisha ya siku kwa siku na katika kutatua matatizo ya
maisha ya kila siku.
Tangu mwaka 1961, Tanzania ilipopata uhuru, kutokujua kusoma na
kuandika kumetambuliwa kuwa ni mojawapo ya vyanzo vikubwa vya
umasikini, maradhi, ukandamizaji na unyonyaji katika jamii. Kwa sababu
hiyo, jitihada za kuondoa tatizo la kutokujua kusoma na kuandika kwa watu
wazima zilianzishwa na serikali ya Tanzania miaka ya 1970. Ili kufikia
lengo hilo, serikali ilifanya jitihada mbalimbali zikiwemo za kukusanya
rasilimali zinazohitajika katika utekelezaji wa programu za kisomo kutoka
kwa wafadhili na wadau wengine ndani na nje ya nchi, kuweka muundo
wa usimamizi katika ngazi za chini za jamii pamoja na kutoa mafunzo kwa
2
waratibu wa elimu ya watu wazima. Walau kila halmashauri au wilaya
ilihamasisha watu wazima kujiunga katika madarasa ya kisomo kwa
ajili ya kujifunza kusoma, kuandika na kufanya hesabu rahisi. Kampeni
za kuelimisha umma ziliandaliwa, kama vile Kazi ni Uhai, Kupanga ni
Kuchagua, Uhuru na Kazi, Wakati wa Furaha, Uchaguzi ni Wako, Chakula
ni Uhai, Mtu ni Afya na Siasa ni Kilimo.
Wizara ya Elimu ya Taifa ilianzisha programu mbalimbali za kuweza
kuwasaidia wanakisomo. Kwa mfano, mtaala wa kisomo cha kujiendeleza
ulianzishwa ukiwa na hatua tatu ambazo ni hatua ya V, VI na ya VII
(baadaye majina yalibadilishwa na kuwa ngazi ya chini, ya kati na ya
juu) ili kuepusha kuzilinganisha na ngazi za shule ya msingi. Mtaala huo
ulibuniwa kwa namna ambayo inajumuisha vipengele vya nadharia na
vitendo. Kipengele cha nadharia, kwa mfano, kilihusisha masomo kama
vile Kiingereza, Kiswahili, Uchumi, Hisabati na Elimu ya Siasa, ambayo
yalifundishwa katika madarasa ya kisomo cha kujiendeleza. Kipengele
cha mafunzo kwa vitendo kilijikita sana katika programu za kazi kama
vile kilimo, maarifa ya nyumbani na ufundi stadi, ambazo zilitolewa katika
vituo maalumu vya elimu ya watu wazima na vyuo vya maendeleo ya
jamii. Kule kujumuishwa kwa kipengele cha mafunzo kwa vitendo katika
mtaala wa kisomo cha kujiendeleza kulichukuliwa kama hatua muhimu ya
kufungamanisha kisomo na uzalishaji.
Masomo ya nadharia na yale ya vitendo yaliambatanishwa katika
programu saidizi ambazo zilijumuisha matumizi ya magazeti ya vijijini,
maktaba za vijijini, programu za kielimu kwa redio na elimu kwa filamu.
Programu hizo zilizinduliwa kwa njia za hadhara ili kuwapatia wanakisomo
taarifa kuhusu elimu kwa vitendo katika kilimo, afya na kazi za ufundi wa
mikono. Lengo kubwa lilikuwa ni kujenga mazingira endelevu ya kisomo
vijijini. Ili kufanikisha hili, magazeti manane ya vijijini yalianzishwa nchini.
3
Vilevile, maktaba za vijijini zipatazo 3,170 zilianzishwa katika ngazi ya
kata, kila moja ikiwa na wastani wa vitabu 400.
Mikakati hiyo iliyotajwa ilileta mafanikio bayana mnamo miaka ya 1980.
Kwa mfano, Tanzania ilifikia rekodi ya kushuka kwa kiwango cha kutokujua
kusoma na kuandika kutoka 80% mwaka 1961 hadi kufikia 9.6% mwaka
1986. Hata hivyo, tangu kipindi hicho, nchi imeshuhudia kushuka kwa kasi
kwa kiwango cha kisomo. Sensa ya kitaifa ya mwaka 2012 ilionesha kuwa
kiwango cha kutokujua kusoma na kuandika kilifikia 28.4%, maeneo ya
vijijini yakiwa na kiwango kikubwa zaidi ambacho ni 37.7%. Katika kipindi
hicho, kulikuwa na idadi ipatayo milioni 3.5 ya watoto wenye umri wa
kwenda shule na vijana wa kati ya umri wa miaka 7 mpaka 19 waliokuwa
nje ya shule. Pia ilikadiriwa kuwa ifikapo mwaka 2015, kungekuwa na
watoto na vijana milioni 5 wenye umri wa kuwa shuleni ambao wangekuwa
nje ya shule. Tena, takwimu kutoka Basic Education Statistics of Tanzania
(BEST) ya mwaka 2017 zinaonesha kwamba wanafunzi walioacha
masomo ya elimu ya msingi kwa miaka mitano mfululizo ya 2012, 2013,
2014, 2015 na 2016 walikuwa ni 104,295; 67,037; 84,481; 85,985;
na 117,927 mtawalia. Hali hii inaweza kuchangia katika ongezeko la
kiwango cha idadi ya watu wasiojua kusoma na kuandika nchini.
Kwa kuwa kutokujua kusoma na kuandika ni moja ya vikwazo katika kuifikia
Dira ya Maendeleo ya Tanzania 2025, ambayo inalenga kuugeuza
uchumi wa Tanzania na kuufanya kuwa wa kipato cha kati na maendeleo
ya viwanda ya kiwango cha kati, programu za kisomo na elimu kwa umma
ni muhimu sana. Ni katika muktadha huu kwamba serikali, kupitia Wizara
ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, imeandaa huu Mkakati wa Kitaifa wa
Kisomo na Elimu kwa Umma (MTaKEU).
4
1�2 Madhumuni ya MTaKEU
Mkakati huu unalenga kuimarisha uendeshaji wa programu za kisomo na
elimu kwa umma nchini Tanzania. Utekelezaji wake ni wa miaka mitano
(2020/2021-2024/2025) ukiwa na lengo la muda mrefu la kufuta ujinga
ili kuinua hali ya maisha ya watu. MTaKEU umeandaliwa mahususi kama
mwongozo wa utekelezaji wa mipango na programu za kisomo na elimu
kwa umma nchini.
1�3 Hatua za Uandaaji wa MTaKEU
Mchakato wa uandaaji wa MTaKEU umehusisha watekelezaji mbalimbali
katika ngazi mbalimbali. Kwanza kabisa, Wizara ya Elimu, Sayansi na
Teknolojia iliipatia TEWW jukumu la kufanya upembuzi yakinifu ili kuandaa
rasimu ya mkakati. Upembuzi yakinifu ulifanyika, ukihusisha mikutano
ya mashauriano na wadau wakuu na kwa kuipitia mikakati ya kitaifa
na kimataifa na mipango iliyopo inayohusu kisomo na elimu kwa umma.
Mashauriano yaliyohusisha watu wenye taarifa muhimu wanaosimamia
kisomo na elimu kwa umma nchini pia yalifanyika. Rasimu iliyoandaliwa
ilipokelewa katika ngazi ya wizara kwa ajili ya kupitiwa na kushirikishana
baina ya WyEST na OR-TAMISEMI kabla ya kukamilika kwake kwa ajili
ya utekelezaji.
5
SURA YA PILI
UPEMBUZI YAKINIFU WA MAZINGIRA
2�1 Maendeleo ya Kisomo na Elimu kwa Umma Tanzania
Tangu mwaka 1961 Tanzania ilipopata uhuru, imekuwa ikifanya juhudi
mahsusi katika kukabiliana na tatizo la kutokujua kusoma na kuandika.
Katika miaka ya 1970, serikali ilizindua kampeni kubwa ya kisomo. Ili
kufanikisha hili, kisomo chenye manufaa, kisomo cha kujiendeleza pamoja
na programu saidizi za kisomo kama vile elimu kwa wafanyakazi,
elimu kwa njia ya filamu, elimu kwa njia ya redio, magazeti ya vijijini
yaliyoendana na mazingira halisi na vyuo vya maendeleo ya wananchi
vilianzishwa. Matokeo yake yalikuwa ni kupungua kwa idadi ya watu
wazima wasiojua kusoma na kuandika kutoka zaidi ya 80% mwaka 1961
hadi kufikia 9.6% mwaka 1986. Hata hivyo, tangu kipindi hicho, mafanikio
haya makubwa hayakudumu kwa muda mrefu kutokana na ugumu wa
hali ya kiuchumi nchini na matokeo ya mabadiliko kisera. Matokeo yake
sekta ndogo ya elimu ya watu wazima iliathirika kwa kiasi kikubwa, na
kusababisha kushuka kwa kasi ya kisomo kama inavyooneshwa kwenye
Mchoro 1.
Mchoro 1: Mwenendo wa Kiwango cha Kisomo 1961-2015
6
Ili kushughulika na changamoto ya kushuka kwa kasi ya kisomo, Tanzania
imefanya jitihada mbalimbali, mojawapo ikiwa ni kushiriki katika
maadhimisho ya Muongo wa Kisomo wa Umoja wa Mataifa yaliyofanywa
mwezi Desemba 2001 katika mkutano mkuu wa Umoja wa Mataifa chini
ya kauli-mbiu isemayo “Kisomo ni Uhuru”. Umuhimu wa Muongo wa Kisomo
wa Umoja wa Mataifa ulijikita katika dhana pana ya kisomo kama msingi
wa ujifunzaji endelevu katika maisha yote. Mkazo wake ulikuwa katika
kuonesha uhitaji wa kuimarisha uhusiano kati ya ujifunzaji na elimu ya
mfumo rasmi, nje ya mfumo rasmi na mfumo usio rasmi na uwekaji wa
mazingira ya kisomo kama sehemu ya mikakati ya kukuza na kuinua elimu
ya watu wazima. Tanzania ilijielekeza pia kwa dhati katika kutekeleza
makubaliano na mapendekezo ya Muongo wa Maendeleo Endelevu wa
Umoja wa Mataifa, ambayo yalilenga katika kuhuisha kasi ya kimataifa
ya ujifunzaji na elimu ya watu wazima na kuziba pengo baina ya fikira
na uhalisia wa mawazo kwa upande mmoja na ukosefu wa sera na
mazingira thabiti na ya kimfumo ya kisomo na ujifunzaji wa watu wazima
kwa upande mwingine. Tanzania pia ilikubali kutekeleza makubaliano na
mapendekezo ya CONFINTEA ambayo yalitokana na mkutano uliofanyika
Tokyo (Japani) mnamo mwaka 1972, Paris (Ufaransa) mwaka 1985 na
Humburg (Ujerumani) mwaka 1997.
Mwaka 2001 serikali ilizindua Mpango wa Maendeleo ya Elimu
ya Msingi (MMEM), kwa lengo la kuongeza, miongoni mwa mambo
mengine, utoaji wa elimu bora ulio wa haki na usawa. Utekelezaji wake
ulionesha jitihada za serikali katika kufikia malengo ya Elimu kwa Wote
na Malengo ya Maendeleo ya Milenia ya Umoja wa Mataifa. Mwaka
2002, serikali iliona umuhimu wa kuandaa Mpango wa Elimu ya Watu
Wazima na Elimu Nje ya Mfumo Rasmi ndani ya mfumo wa MMEM ili
kutoa fursa kwa kundi kubwa la watoto na vijana walio nje ya mfumo
7
rasmi wa shule kuweza kupata elimu, na kutatua tatizo la ongezeko la
wasiojua kusoma na kuandika miongoni mwa watu wazima. Mpango huo
ulizingatia changamoto kadhaa katika maeneo ya upatikanaji wa elimu,
ubora, usimamizi, uwezo, ufanisi na rasilimali. Programu muhimu kama vile
Mpango wa Elimu ya Msingi kwa Walioikosa (MEMKWA) na Mpango wa
Uwiano Kati ya Elimu ya Watu Wazima na Jamii (MUKEJA) zilianzishwa
ili kuchangia katika kutatua tatizo hilo. Mnamo mwaka 2010, Tanzania
ilianzisha mpango wa miaka mitano wa Sekta Ndogo ya Elimu ya Watu
Wazima na Elimu Nje ya Mfumo Rasmi 2010/11-2014-2015 kama
jitihada za serikali katika kufanikisha sera ya Elimu kwa Wote, Malengo
ya Maendeleo ya Milenia, Mpango Mkakati wa Kupunguza Umasikini
na Dira ya Maendeleo Tanzania 2025. Mpango huo uliweka msisitizo
katika ufikikaji na uendelezaji, kisomo cha kujiendeleza na elimu endelezi,
utolewaji wa fedha na uendelevu wa programu za elimu ya watu wazima
na elimu nje ya mfumo rasmi. Licha ya kuwepo kwa mafanikio makubwa
katika mikakati na mipango iliyotajwa, kiwango cha idadi ya wasiojua
kusoma na kuandika nchini bado kiko juu.
2�2 Mifumo ya Kisera Inayozingatiwa katika MTaKEU
Uandaaji wa mkakati huu umejengwa juu ya sera na mipango ifuatayo:
2�2�1 Malengo ya Maendeleo Endelevu 2030
Malengo ya Maendeleo Endelevu ni shabaha zilizokubaliwa miongoni
mwa serikali za dunia kuhusu maendeleo. Yanafuata baada ya Malengo
ya Mendeleo ya Milenia na yanajikita katika agenda za mwaka 2030
za Maendeleo Endelevu. Agenda hii ni mpango wa utekelezaji kwa
ajili ya watu, dunia na hatima ya mafanikio. Mpango huu unalenga
kuimarisha amani ya ulimwengu wote kwa mawanda mapana ya uhuru na
unatambua kwamba kuondoa umasikini wa aina zote ukiwemo umasikini
8
uliokithiri ni changamoto kubwa sana inayoukumba ulimwengu na ni jambo
muhimu sana linalohitajika kwa ajili ya maendeleo endelevu. Tanzania
imedhamiria kuutekeleza mpango huu kwa kushirikiana na nchi nyinginezo
na wadau mbalimbali.
Lengo la 4 ni mahsusi hasa kwa maendeleo jumuishi ya kisomo na elimu
kwa umma. Lengo la 4.6 linataka “kuhakikisha kwamba vijana na watu
wazima wote, wanaume na wanawake, wanafikia kiwango cha kujua
kusoma, kuandika na kuhesabu ifikapo mwaka 2030.”
2�2�2 Dira ya Maendeleo ya Tanzania 2025
Dira ya Maendeleo ya Tanzania 2025 inaelezea mipango ya kitaifa
ya muda mrefu ambayo Tanzania inatamani kuifikia. Pamoja na mambo
mengine, dira hii inalenga kuugeuza uchumi wa Tanzania na kuufanya kuwa
wa kipato cha kati na wa maendeleo ya viwanda ya kiwango cha kati
ifikapo mwaka 2025. Inalenga kuwafikisha watanzania wote katika hali
ya ubora wa juu wa maisha ambao unaweza kufikiwa kwa kutengeneza
jamii ya watu walioelimika vizuri na wanaojifunza, hali ambayo inaweza
kufikiwa kwa njia ya, pamoja na mambo mengine, kukomesha tatizo la
kutojua kusoma na kuandika. Programu za kisomo na elimu kwa umma
zinatoa maarifa na stadi zinazohitajika katika kutatua changamoto za
kimaendeleo kwa umahiri na kiushindani.
2�2�3 Ilani ya Uchaguzi ya CCM (2015-2020)
Ilani ya uchaguzi ya CCM imejikita katika Dira ya Maendeleo Tanzania
2025. Kwa ujumla, ilani hii (kifungu cha 51 - 52) inaelezea jitihada za
serikali katika kuimarisha uhusiano baina ya elimu rasmi, elimu nje ya
mfumo rasmi na elimu isiyo rasmi katika juhudi za kukuza na kuinua elimu
ya watu wazima kwa lengo la kuunda jamii ya watu walioelimika.
9
2�2�4 Sera ya Elimu na Mafunzo (2014)
Sera ya Elimu na Mafunzo inasisitiza kujenga jamii ya watu walioelimika
kwa kuongeza fursa za elimu na mafunzo kwa makundi mbalimbali ya
watu, na kuwasaidia walengwa kuhitimu elimu yao katika ngazi husika.
Kupitia sera hii, serikali inaonesha dhamira ya kuandaa miongozo na
mazingira yanayofaa kuhakikisha kwamba elimu na mafunzo, ikiwemo
elimu ya watu wazima, vinatolewa katika ngazi mbalimbali kwa ubora
stahiki na kwa kupitia njia mbalimbali zikiwemo ujifunzaji huria na masafa.
2�2�5 Mpango wa Maendeleo ya Sekta ya Elimu
Takwimu za hivi karibuni kutoka katika ripoti ya Mpango wa Maendeleo
ya Sekta ya Elimu wa 2016/17-2020/21 zinaonesha kwamba Tanzania
ina idadi kubwa ya watoto na vijana walio nje ya shule, na takribani robo
ya watu wazima hawajui kusoma na kuandika. Hivyo basi, kuna haja ya
kuwa na mkakati ulioandaliwa vizuri wa kukabiliana na hali hii.
2�2�6 Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa ni sehemu moja
katika mabadiliko makubwa ya sekta za umma ambayo yanasisitiza
ugatuaji wa madaraka wenye lengo la kuimarisha ushirikishwaji wa
watu walio katika ngazi za chini. Programu za elimu ya watu wazima
zinatakiwa ziendeshwe katika mifumo hii ya ugatuaji kwa kutoa elimu ya
msingi kwa watoto, vijana na watu wazima walio nje ya shule.
10
SURA YA TATU
UCHANGANUZI WA UWEZO, UDHAIFU, FURSA NA CHANGAMOTO
3�1 Muhtasari wa Uchanganuzi
Uchanganuzi wa uwezo, udhaifu, fursa na changamoto kwa mkakati huu
umejikita kwenye tathmini ya mazingira ya ndani na ya nje.
3�2 Tathmini ya Mazingira ya Ndani
Tathmini ya mazingira ya ndani imejikita katika uwezo na udhaifu kama
ifuatavyo:
(a) Uwezo
Mafanikio ambayo yanaimarisha utekelezaji wa Mpango wa
Kitaifa wa Kisomo na Elimu kwa Umma yanajumuisha:
i. Kuwepo kwa mfumo wa taasisi za serikali zenye jukumu la
kutelekeza MTaKEU;
ii. Uzoefu wa muda mrefu wa WyEST na mashirika mengine na wabia
kama vile TEWW, Bodi ya Huduma za Maktaba ya Tanzania, OR-
TAMISEMI, vyombo vya habari, vyuo vya mandeleo ya jamii na
taasisi zisizo za kiserikali katika kusimamia programu za elimu ya
watu wazima, zikiwemo programu za kisomo na elimu kwa umma;
iii. Uwepo wa taasisi za kitaaluma zinazoweza kutoa mafunzo
endelevu na kuwajengea uwezo wawezeshaji na viongozi wa
kisomo na elimu kwa umma;
iv. Utayari wa serikali na wanajamii katika kuunga mkono na
kuchangia shughuli za kisomo na elimu kwa umma nchini; na
v. Uwepo wa miongozo ya kisera inayozitaka taasisi zote za umma
kuwa vituo vya programu za kisomo.
11
b) Udhaifu
i. Uhaba wa programu zinazofaa kwa ajili ya kisomo na elimu kwa
umma;
ii. Uhaba wa mifumo saidizi na programu za kisomo katika ngazi
mbalimbali;
iii. Mfumo usio na ufanisi wa data za kisomo na elimu kwa umma;
iv. Kukosekana kwa zana na mifumo thabiti inayoratibiwa vizuri ya
namna ya kufanya upimaji wa ufundishaji na ujifunzaji wa kisomo
na elimu kwa umma;
v. Mfumo usioratibiwa vizuri wa kuandaa zana na vifaa vya
kufundishia na kujifunzia katika programu za kisomo na elimu kwa
umma;
vi. Kukosekana kwa viwango vya kitaifa vya kutambua weledi wa
wawezeshaji na waratibu wa programu za kisomo na elimu kwa
umma;
vii. Msisitizo hafifu katika kuhimiza kazi za ubunifu na uvumbuzi katika
masuala yanayohusu kisomo na elimu kwa umma;
viii. Uhaba wa tafiti za kina na zinazoratibiwa kwa ufasaha kuhusu
kisomo na elimu kwa umma nchini; na
ix. Utendaji hafifu wa kamati za elimu ya watu wazima na nje ya
mfumo rasmi katika ngazi zote.
3�3 Tathmini ya Mazingira ya Nje
Uchunguzi wa mazingira ya nje umejikita katika masuala ambayo
yanaweza kuathiri MTaKEU katika hali chanya na hasi kutokea nje. Mambo
ambayo yalitiliwa maanani katika tathmini yamejikita katika muktadha
wa kisiasa, mfumo wa sheria na kanuni, mahusiano na ushirikiano na
wadau wengine, kijamii, kiuchumi na kimazingira, ambayo yanaangukia
chini ya fursa na changamoto kama ifuatavyo:
12
a) Fursa
Utekelezaji wa MTaKEU utawezekana kwa kuzingatia fursa
zifuatazo:
i. Mifumo ya sheria na kanuni: Zipo sera, sheria na programu ambazo zinaongoza na kusaidia utekelezaji wa MTaKEU. Hizo hujumuisha Sera ya Elimu na Mafunzo (1995; 2014); Tamko la Serikali Namba 494 la 17 Disemba, 2010 lililoanzisha OR-TAMISEMI na sheria ya bunge Namba. 12 ya mwaka 1975 inayoipa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima (TEWW) jukumu la kuendesha programu za elimu endelezi, Elimu ya Watu Wazima na elimu nje ya mfumo rasmi;
ii. Uwepo wa jitihada za kimataifa na sera zinazohimiza programu za kisomo katika nchi mojamoja;
iii. Mazingira mazuri ya kisiasa yanayotamani kuwa na jamii ya wasomi kama yanavyodhihirishwa katika maamuzi ya kisiasa, hotuba na katika ilani za vyama vya siasa kama vile Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015-2020;
iv. Utayari wa wadau wengine wa ndani na wa nje ambao wanaweza kushirikishwa katika utekelezaji wa MTaKEU;
v. Uwepo wa taasisi zisizo za kiserikali, taasisi za kijamii, taasisi za kidini, vyama vya siasa na makundi mengine ya kijamii na kiuchumi ambayo yanaweza kuendeleza au kutoa majukwaa kwa ajili ya programu za kisomo;
vi. Uwepo na ongezeko la matumizi ya mitandao ya kijamii, simu za mkononi, vifaa vya huduma za maktaba zinazohamishika na kompyuta;
vii. Uwepo wa walengwa wa programu za kisomo na elimu kwa umma; na
viii. Uwepo wa wadau wenye ari ambao ni muhimu katika kutekeleza,
kuendeleza, kusaidia au kushirikiana katika kutekeleza MTaKEU.
13
b) Changamoto
Changamoto zinaweza kujumuisha yafuatayo:
i. Mazoea potofu kuhusu tafsiri ya programu za kisomo miongoni
mwa wadau mbalimbali yanaweza kurudisha nyuma utekelezaji
wa MTaKEU; na
ii. Uhaba wa fedha zinazoelekezwa katika kugharamia programu
na mipango ya elimu ya watu wazima.
14
SURA YA NNE
DIRA, DHIMA NA MALENGO YA KIMKAKATI
4�1 Dira
Dira ya huu Mkakati wa Kitaifa wa Kisomo na Elimu kwa Umma ni “kuwa
na jamii iliyoelimika na yenye uwezo wa kupata taarifa sahihi kwa ajili
ya kuwa na maisha bora na maendeleo endelevu kufikia mwaka 2025.
4�2 Dhima
Dhima ya mkakati huu ni “kubuni, kuendeleza na kuratibu programu za
kisomo na elimu kwa umma zilizo bora na zinazopatikana, na kuhakikisha
kuwa umahiri uliopatikana unakuwa endelevu kwa kuimarisha huduma
saidizi za kisomo”.
4�3 Malengo ya Kimkakati
Mkakati huu una malengo ya kimkakati saba yafuatayo:
i. Kuanzisha programu za kisomo na elimu kwa umma zilizo bora na
zenye manufaa kwa jamii;
ii. Kuimarisha mifumo na programu wezeshi za kuendeleza kisomo
na elimu kwa umma;
iii. Kuboresha mifumo ya usimamizi wa takwimu za kisomo na elimu
kwa umma;
iv. Kuweka viwango vya sifa za kitaaluma kwa ajili ya programu za
kisomo na elimu kwa umma;
v. Kuandaa zana na vifaa bora vya kufundishia na kujifunzia katika
programu za kisomo na elimu kwa umma;
vi. Kujenga uwezo wa wawezeshaji na waratibu wa programu za
kisomo na elimu kwa umma; na
vii. Kukuza kazi za tafiti, uvumbuzi na ubunifu katika masuala ya
kisomo na elimu kwa umma.
15
4�4 Malengo ya Kimkakati, Mikakati, Shabaha na Viashiria vya
Utendaji
LK 1� Kuanzisha programu za kisomo na elimu kwa umma zilizo bora
na zenye manufaa kwa jamii
Sababu
Uhaba wa programu za kisomo na elimu kwa umma unaashiria uhitaji wa hatua za muda mfupi na muda mrefu kwa kuzingatia masuala makuu mawili: ubora wa programu na jinsi zinavyokidhi mahitaji ya jamii ya kielimu. Ubora wa programu unahusu jumla ya matokeo ya uboreshaji wa uanzishwaji wa vituo vya mafunzo, mgawanyo wa rasilimali, mafunzo yatolewayo kwa wawezeshaji na wasimamizi wa programu lengwa pamoja na kuwajengea morali ya kazi. Programu zinazokidhi mahitaji ya kielimu ya jamii inahusu ubunifu unaozingatia tofauti za muktadha katika kuandaliwa kwake. Vilevile, programu zinazokidhi mahitaji ya kielimu ya jamii zinahitaji ushirikishwaji wa walengwa na wadau katika hatua mbalimbali kuanzia kipindi cha maandalizi hadi wakati wa utekelezaji na pia kuzingatia unyumbufu wa mbinu na njia za utoaji wa mafunzo. Hili linahusisha pia uwepo wa haja ya kupanua mawanda ya utoaji wa programu za kisomo ili zipatikane kwa urahisi kwa vijana na watu wazima
wanaozihitaji, hususani maskini na waliotengwa.
Mikakati
a) Kufanya upembuzi wa mahitaji kwa ajili ya kuandaa programu
bora na zinazokidhi mahitaji ya jamii;
b) Kujenga uelewa kuhusu umuhimu wa programu za kisomo na elimu
kwa umma;
c) Kuandaa miongozo ya utekelezaji wa programu za kisomo na
elimu kwa umma; na
d) Kuhamasisha wadau mbalimbali kuanzisha programu za kisomo
na elimu kwa umma.
16
Shabaha
i. Kubainishwa kwa mahitaji ya ujifunzaji kwa ajili ya kusaidia
maandalizi ya programu za kisomo na elimu kwa umma zenye
ubora na zinazokidhi mahitaji ya jamii katika wilaya zote kufikia
mwaka 2022;
ii. Kuanzishwa kwa hifadhi ya mahitaji ya kielimu kwa ajili ya
makundi mbalimbali katika kila wilaya kufikia mwaka 2022;
iii. Kuandaliwa kwa kampeni kuhusu masuala mawili ya kitaifa kufikia
mwaka 2025;
iv. Kufanyika kwa kampeni kupitia vyombo vya habari juu ya umuhimu
wa kisomo na elimu kwa umma kufikia mwaka 2025;
v. Kufanyika kwa mikutano, semina au warsha za uhamasishaji
angalau 6 katika kila kata kufikia mwaka 2022;
vi. Kuanzishwa kwa programu moja ya kisomo katika kila wilaya
kufikia mwaka 2022;
vii. Kuanzishwa kwa programu moja ya elimu kwa umma katika kila
wilaya kufikia mwaka 2022;
viii. Kuwepo na kutumika kwa miongozo ya mtaala wa kisomo na elimu
kwa umma kufikia mwaka 2025;
ix. Kuanzishwa kwa programu moja ya elimu kwa jamii kwenye kila
kata ifikapo mwaka 2023;
x. Kuhusishwa kwa wadau watatu katika kuanzisha programu za
kisomo na elimu kwa umma kwenye kila wilaya ifikapo mwaka
2025;
xi. Kuanzishwa kwa kituo kimoja cha kisomo katika kila kata ifikapo
mwaka 2025; na
xii. Kuwepo kwa walengwa milioni mbili walionufaika na programu
za kisomo ifikapo mwaka 2025.
17
Viashiria vya Mafanikio vya Msingi
i. Uwepo wa ripoti ya tathmini ya mahitaji ya kielimu;
ii. Idadi ya programu za kisomo na elimu kwa umma zilizoandaliwa
katika kila wilaya;
iii. Idadi ya programu za elimu kwa jamii zilizoanzishwa katika kila
kata;
iv. Ongezeko la asilimia ya vijana na watu wazima wanaoshiriki
katika programu za kisomo na elimu kwa umma kila mwaka;
v. Idadi ya vituo vya kisomo vilivyoanzishwa katika kila wilaya;
vi. Idadi ya walengwa walionufaika katika programu za kisomo na
elimu kwa umma;
vii. Kuwepo kwa miongozo ya kisomo na elimu kwa umma inayotumika;
na
viii. Vithibitisho vya kuboreka kwa maisha ya wanajamii.
LK 2� Kuimarisha mifumo na programu wezeshi za kuendeleza
kisomo na elimu kwa umma
Sababu
Ufanisi wa programu za kisomo na elimu kwa umma hutegemea kwa
kiasi kikubwa uwepo wa mifumo na mfululizo wa programu wezeshi zilizo
madhubuti na zenye ufanisi. Tanzania ina historia ya muda mrefu katika
kutumia mifumo wezeshi ya kisomo kama vile maktaba za vijijini, magazeti
ya vijijini na redio. Hata hivyo, mifumo wezeshi hiyo haijatumika kiasi cha
kutosha kuimarisha programu wezeshi za kisomo. Ipo haja ya kutumia
teknolojia mpya na kuendeleza mifumo iliyopo ambayo bado inakidhi
mahitaji kuhakikisha kwamba mifumo wezeshi madhubuti na yenye ufanisi
inakuwepo nchini Tanzania.
18
Mikakati
a) Kufanya upembuzi yakinifu wa mifumo na programu wezeshi za
kisomo zilizopo;
b) Kuanzisha programu na mifumo wezeshi ya kisomo katika maeneo
ya mijini na vijijini,
c) Kuanzisha maktaba zinazohama katika jamii za wafugaji ambazo
zina kiwango kikubwa cha kutojua kusoma na kuandika;
d) Kushawishi na kujenga uelewa wa jamii juu ya programu na mifumo
wezeshi ya kisomo; na
e) Kuanzisha na kuimarisha uhusiano kati ya programu za kisomo na
elimu kwa umma na vyombo vya habari.
Shabaha
i. Kufanyika kwa upembuzi yakinifu katika wilaya zote kufikia
mwaka 2022;
ii. Kufanyika kwa programu nne za kushawishi na kueneza habari
kuhusu programu na mifumo wezeshi kila mwaka;
iii. Kuwepo kwa maktaba moja ya kijiji iliyosheheni vifaa
vinavyotakiwa katika kila mkoa kufikia mwaka 2025;
iv. Kuanzishwa kwa programu moja ya kisomo kwa njia ya redio
katika kila mkoa ifikapo mwaka 2025;
v. Kuanzishwa kwa programu moja ya kitaifa ya kisomo kwa njia ya
televisheni ifikapo mwaka 2025;
vi. Kuunganishwa kwa vikundi vitatu vya kijamii na kiuchumi katika
programu za kisomo katika kila kata ifikapo mwaka 2025;
vii. Kuanzishwa kwa kituo kimoja cha kisomo cha kujiendeleza katika
kila kata ifikapo mwaka 2025;
19
viii. Kuimarishwa kwa kiwanda cha uchapaji cha Taasisi ya Elimu ya
Watu Wazima ifikapo mwaka 2025;
ix. Kutumika kwa vyuo vya maendeleo ya wananchi katika kuendeleza
kisomo na elimu kwa umma ifikapo mwaka 2025;
x. Kuanzishwa kwa maktaba moja inayohama katika kila jamii ya
wafugaji ifikapo mwaka 2025; na
xi. Kubuniwa na kutumika kwa programu ya simu za mkononi katika
mipango ya kisomo na elimu kwa umma.
Viashiria vya Mafanikio vya Msingi
i. Vithibitisho vya uwepo wa mifumo na programu wezeshi katika
kila wilaya;
ii. Idadi ya wadau wanaotambua na kudhamiria kusaidia uanzishwaji
wa huduma wezeshi za kisomo;
iii. Idadi ya miundombinu wezeshi iliyojengwa, kukarabatiwa na
kuwekewa samani kwa kuzingatia mahitaji;
iv. Idadi ya programu wezeshi za kisomo zinazofanya kazi katika
jamii;
v. Idadi na asilimia ya walengwa walionufaika na huduma wezeshi
za kisomo;
vi. Kupungua kwa idadi ya watu wanaorejea katika hali ya kutokujua
kusoma na kuandika;
vii. Idadi ya vituo na vikundi vya wanakisomo vilivyoanzishwa na
kuendelezwa kwenye makundi ambayo huwa pembezoni na
yasiyofikika kwa urahisi;
viii. Idadi ya jamii za wafugaji zilizohamasika kujiunga na programu
za kisomo na elimu kwa umma; na
ix. Ongezeko la asilimia ya jamii zinazofikiwa na programu bora za
kisomo na elimu kwa umma kupitia vyombo vya habari.
20
LK 3� Kuboresha mifumo ya usimamizi wa takwimu za kisomo na
elimu kwa umma
Sababu
Uendeshaji wa programu za kisomo na elimu kwa umma una sifa ya kuwa na unyumbufu na mawanda anuai, na unafanywa na wadau mbalimbali chini ya usimamizi wa wizara na sekta mbalimbali. Hali hii husababisha changamoto katika upatikanaji wa takwimu za uhakika na sahihi zinazoweza kusaidia kuboresha sera na kazi za utekelezaji. Mifumo iliyopo ya usimamizi wa takwimu imebuniwa kwa ajili hasa ya kushughulikia takwimu za mfumo rasmi wa elimu. Hivyo, kuna haja ya kuwa na mifumo na mikakati madhubuti ambayo inaweza kuwa na nafasi
ya kubeba pia programu za kisomo na elimu kwa umma.
Mikakati
a) Kufanya upembuzi yakinifu wa hali halisi ya mifumo ya usimamizi wa takwimu za kisomo na elimu kwa umma;
b) Kuimarisha mifumo ya usimamizi wa takwimu za kisomo na elimu kwa umma katika ngazi zote za utekelezaji; na
c) Kujumuisha takwimu za kisomo na elimu kwa umma katika mifumo
ya usimamizi wa takwimu iliyopo.
Shabaha
i. Kubainishwa kwa hali halisi ya mifumo ya usimamizi wa takwimu za kisomo na elimu kwa umma ifikapo mwaka 2021;
ii. Kuingizwa kwa viashiria vya takwimu za kisomo na elimu kwa umma katika mifumo ya BEMIS, EMIS na masijala za vijijini ifikapo mwaka 2022;
iii. Kujengewa uwezo wa kukusanya na kuchakata takwimu kwa mamlaka za serikali za mitaa ifikapo mwaka 2022; na
iv. Kusambazwa kwa takwimu za kisomo na elimu kwa umma kwa
wadau ifikapo mwaka 2023.
21
Viashiria vya Mafanikio vya Msingi
i. Kuwepo na kutumika kwa ripoti ya hali halisi ya mifumo ya
usimamizi wa takwimu;
ii. Idadi ya zana zinazotumika za kushughulikia takwimu za kisomo
na elimu kwa umma;
iii. Idadi na aina za watekelezaji waliopata mafunzo ya usimamizi
wa takwimu za kisomo na elimu kwa umma;
iv. Kuwepo kwa takwimu za kisomo na elimu kwa umma katika mifumo
ya BEMIS, EMIS, na masjala ya vijijini; na
v. Uwepo wa taarifa ya kila mwaka ya kisomo na elimu kwa umma.
LK 4� Kuweka viwango vya sifa za kitaaluma kwa ajili ya programu
za kisomo na elimu kwa umma
Sababu
Mpango wa Maendeleo wa Sekta ya Elimu unaonesha kwamba wanafunzi
katika ngazi zote za elimu wanapaswa wapate kiwango cha elimu ya
msingi kinachokubalika, inayoweza kuhawilishwa na mafunzo ya ufundi
na stadi kupitia mfumo rasmi wa elimu, ufundi, elimu ya watu wazima
pamoja na elimu katika mfumo usio rasmi. Ni dhahiri kwamba wanafunzi
wengi wanahitaji kutambuliwa, kuhalalishwa na kupewa ithibati kwa
ujifunzaji wao kuonesha thamani ya kile wanachojifunza. Tofauti na elimu
ya mfumo rasmi, programu za kisomo na elimu kwa umma zimekuwa
zikitumia mitaala na nyakati za kujifunza nyumbufu na zenye mawanda
anuwai kukidhi matakwa na mazingira ya walengwa. Muundo wake una
vigezo nyumbufu vya udahili na kuhitimu katika programu, na kudahili
tena na kuhitimu tena. Kwa hiyo, kuna uhitaji wa umakini katika kuweka
vigezo sanifu vya viwango vya sifa ili kushughulika kwa usahihi na hali hii
ya unyumbufu wa maudhui na njia za ufundishaji na ujifunzaji.
22
Mikakati
a) Kufanya upembuzi yakinifu wa hali halisi ya uendeshaji wa programu za kisomo na elimu kwa umma na waendeshaji;
b) Kuweka viwango vya sifa za kitaaluma na njia za kuendelea na elimu kwa programu za kisomo na elimu kwa umma; na
c) Kuanzisha mfumo rasmi wa upimaji na utoaji tuzo kwa programu
za kisomo na elimu kwa umma.
Shabaha
i. Kubainishwa kwa hali halisi ya uendeshaji na waendeshaji wa programu za kisomo na elimu kwa umma ifikapo mwaka 2021;
ii. Kuanzishwa kwa mfumo rasmi wa upimaji na utoaji tuzo kwa programu za kisomo na elimu kwa umma ifikapo mwaka 2022; na
iii. Kuwekwa kwa viwango vya sifa za kitaaluma na njia za kuendelea na elimu kwa programu za kisomo na elimu kwa umma ifikapo
mwaka 2022.
Viashiria vya Mafanikio vya Msingi
i. Uwepo wa ripoti ya upembuzi yakinifu inayoonesha vithibitisho vya uendeshaji na waendeshaji wa programu za kisomo na elimu kwa umma;
ii. Idadi ya programu za kisomo na elimu kwa umma pamoja na waendeshaji wa programu hizo wanaozingatia viwango vya sifa vilivyowekwa;
iii. Idadi ya wanafunzi wanaoendelea na ngazi nyingine zinazofuata za elimu;
iv. Idadi ya wahitimu wa programu za kisomo na elimu kwa umma wanaotambuliwa na mamlaka kuu za mifumo ya viwango; na
v. Idadi ya programu na waendeshaji wa programu za kisomo
na elimu kwa umma waliohalalishwa na kupewa ithibati kutoa
programu za kisomo na elimu kwa umma.
23
LK 5� Kuandaa zana na vifaa bora vya kufundishia na kujifunzia
katika program za kisomo na elimu kwa umma
Sababu
Vifaa vya kielimu kama vile vitabu, video, programu za kompyuta, na
vifaa vingine ni muhimu sana katika kuwezesha ufundishaji na ujifunzaji.
Programu za kisomo na elimu kwa umma zinahitaji vifaa vinavyoendana
na uwezo na matakwa ya walengwa wenye sifa tofauti-tofauti. Hivyo,
utayarishaji wake unatawaliwa na kanuni zinazoendana na mahitaji hayo
na kukidhi haja. Vifaa vya kufundishia na kujifunzia ambavyo vimezoeleka
kutumika katika programu za kisomo vimekuwa vile vilivyochapishwa
katika nakala ngumu, ambazo zimekuwa na gharama kubwa, ngumu
kupatikana na zisizo na mvuto mkubwa kwa wanaojifunza. Maendeleo ya
kiteknolojia ya sasa yanaweza kutoa fursa za kutumia pia vifaa ambavyo
haviko katika machapisho ya nakala ngumu.
Mikakati
a) Kuandaa zana na vifaa vya kufundishia na kujifunzia vilivyo
katika mfumo wa nakala ngumu kwa kufuata miongozo iliyopo na
mazingira halisi;
b) Kuongeza matumizi ya vifaa mbalimbali vya kihabari katika
programu za kisomo na elimu kwa umma; na
c) Kutumia vituo vya walimu kujenga uwezo wa kuandaa zana na
vifaa vya kujifunzia na kufundishia katika kisomo na elimu kwa
umma.
Shabaha
i. Kuandaliwa kwa mwongozo wa kuandaa zana na vifaa vya
kufundishia na kujifunzia kwa ajili ya programu za kisomo na
elimu kwa umma ifikapo mwaka 2022;
24
ii. Kuzalishwa kwa zana na vifaa vinavyohitajika kufundishia na
kujifunzia katika vituo vya kisomo na elimu kwa umma ifikapo
mwaka 2025;
iii. Kuandaliwa kwa zana na vifaa vya kufundishia na kujifunzia
vinavyozingatia muktadha katika kila wilaya ifikapo 2025;
iv. Kuandaliwa na kutumika kwa mwongozo wa kutumia vifaa
mbalimbali vya kihabari katika programu za kisomo na elimu kwa
umma ifikapo mwaka 2024; na
v. Kutumika kwa vituo vya walimu katika kujenga uwezo wa wadau
kuandaa zana na vifaa vya kisomo katika mazingira yao ifikapo
mwaka 2025.
Viashiria vya Mafanikio vya Msingi
i. Kuwepo na kutumika kwa mwongozo wa kuandaa zana na vifaa
vya ufundishaji na ujifunzaji;
ii. Idadi na aina za zana na vifaa vya kufundishia na kujifunzia vilivyo
bora na vinavyoendana na mahitaji ambavyo vimeandaliwa,
kuzalishwa katika nakala ngumu na kutumika;
iii. Kuwepo na kutumika kwa mwongozo wa kutumia vifaa mbalimbali
vya kihabari kufundishia na kujifunzia; na
iv. Idadi na aina ya zana na vifaa vya kisomo na elimu kwa umma
vilivyoandaliwa na kutumika katika mazingira husika.
LK 6� Kujenga uwezo wa wawezeshaji na waratibu wa kisomo na
elimu kwa umma
Sababu
Nchini Tanzania, wanafunzi walio wengi ambao wamedahiliwa katika
taasisi za mafunzo katika eneo la elimu ya watu wazima ni wale ambao
25
ni waajiriwa waliopo kazini. Baada ya kuhitimu, wanafunzi hawa hurudi
katika vituo vyao vya kazi vya awali ambavyo, kwa kiasi kikubwa, ni
katika elimu ya mfumo rasmi, huku wakiziacha programu za kisomo na
elimu kwa umma zikihudumiwa na wafanyakazi wasio na sifa stahiki.
Hali halisi iliyopo ya kwamba sekta ndogo ya elimu ya watu wazima
inakosa utambulisho dhahiri katika muundo wa ajira za utumishi wa umma
inaongeza upeo wa tatizo hili. Hivyo basi, kuna haja ya kuimarisha mfumo
wa mafunzo ya kozi za muda mfupi na za muda mrefu katika eneo la
elimu ya watu wazima na kufanya juhudi ya kutafuta kutambulika kwa
wataalamu wa eneo hili katika muundo wa ajira za utumishi wa umma.
Mikakati
a) Kuandaa programu za muda mfupi na muda mrefu za kujenga
uwezo katika maeneo ya ufundishaji, usimamizi na uaandaaji wa
zana na vifaa vya kufundishia na kujifunzia katika programu za
kisomo na elimu kwa umma;
b) Kuendesha mafunzo ya muda mfupi kwa ajili ya wawezeshaji na
waratibu wa vituo vya kisomo na elimu kwa umma; na
c) Kuweka viwango vya sifa za weledi katika eneo la kisomo na
elimu kwa umma kulingana na matakwa ya utumishi wa umma.
Shabaha
i. Kuanzishwa kwa programu mbili za mafunzo ya muda mfupi
zinazohusiana na uwezeshaji, uendeshaji na uandaaji wa zana
katika kila wilaya ifikapo 2025;
ii. Kuanzishwa kwa programu moja ya muda mrefu inayohusiana
na uwezeshaji, uendeshaji na uandaaji wa zana na vifaa vya
programu za kisomo na elimu kwa umma ifikapo 2025;
26
iii. Kupatiwa mafunzo kwa walimu watano kutoka katika kila wilaya
kila mwaka kuhusu uratibu wa programu za kisomo na elimu kwa
umma ifikapo mwaka 2025;
iv. Kupatiwa mafunzo wawezeshaji wasaidizi wawili na mwezeshaji
mtaalamu mmoja walio kwenye kila kituo ifikapo 2022; na
v. Kuandaliwa na kutambuliwa kwa viwango vya sifa za weledi kwa
ajili ya wawezeshaji na waratibu wa programu za kisomo na elimu
kwa umma ifikapo mwaka 2025.
Viashiria vya Mafanikio vya Msingi
i. Idadi ya kozi fupi-fupi na kozi za muda mrefu zilizoanzishwa;
ii. Idadi ya wawezeshaji waliohudhuria mafunzo ya muda mfupi
katika kila wilaya;
iii. Idadi ya wawezeshaji, waratibu na wadau wengine waliopatiwa
mafunzo kwa mwaka;
iv. Kutambuliwa kwa viwango vya sifa za weledi kwa wawezeshaji
wa programu za kisomo na elimu kwa umma katika muundo wa
utumishi wa umma;
v. Idadi ya waelimishaji wa kisomo na elimu kwa umma
wanaotambuliwa katika muundo wa utumihi wa umma; na
vi. Kuthibitika kwa uendeshaji wa programu za kisomo na elimu kwa
umma ulioboreshwa.
27
LK 7. Kukuza kazi za tafiti, uvumbuzi na ubunifu katika masuala ya
kisomo na elimu kwa umma
Sababu
Licha ya kuwepo kwa mabadiliko ya kiteknolojia, kijamii na ya kiuchumi
katika ulimwengu wa sasa, elimu ya watu wazima bado haijawa na
uvumbuzi na ubunifu kwa kiasi cha kutosha. Uhaba wa tafiti, uwekezaji,
maendeleo ya kiteknolojia na maendeleo duni ya ubunifu mahalia ni
miongoni mwa sababu za kuwepo kwa hali hii. Kwa hiyo, lengo hili la
kimkakati linalenga kuendeleza kazi ya utafiti, uvumbuzi na ubunifu kwa
ajili ya maendeleo na uendelevu wa programu za kisomo na elimu kwa
umma. Linahimiza kuhusu uratibu madhubuti wa kazi za utafiti na uvumbuzi
ili kuwezesha uendelezaji wa maarifa, uboreshaji wa utendaji na taarifa
za kisera katika eneo la kisomo na elimu kwa umma.
Mikakati
a) Kuweka miundo ya ushirikiano ya wadau ili kuongoza ubainishaji
wa agenda za utafiti katika kisomo na elimu kwa umma nchini;
b) Kuimarisha uwezo wa wadau mbalimbali wa kisomo na elimu kwa
umma katika kufanya tafiti na kuwasilisha matokeo;
c) Kuanzisha utaratibu wa kukuza ubunifu, uvumbuzi na tafakuri
katika eneo la kisomo na elimu kwa umma; na
d) Kuhimiza utamaduni wa ujifunzaji endelevu miongoni mwa
watendaji wa elimu ya watu wazima.
Shabaha
i. Kubainishwa kwa agenda ya kitaifa ya utafiti katika kisomo na
elimu kwa umma ifikapo mwaka 2025;
ii. Kupatiwa mafunzo ya kufanya utafiti na kuwasilisha matokeo ya
utafiti kwa watekelezaji mia moja na sitini na tisa (169) wa kisomo
na elimu kwa umma ifikapo mwaka 2025;
28
iii. Kufanyika kwa kazi moja ya utafiti kuhusiana na kisomo na elimu
kwa umma katika kila wilaya ifikapo mwaka 2025;
iv. Kuanzishwa kwa programu moja ya mafunzo elekezi kuhusu utafiti,
ubunifu na uvumbuzi katika kila wilaya ifikapo mwaka 2024;
v. Kuandaliwa na kufanyiwa majaribio programu moja ya mfano
ya kisomo na elimu kwa umma katika kila mkoa ifikapo mwaka
2025;
vi. Kujengewa uwezo wa watekelezaji katika kubuni programu na
mitaala ya kisomo na elimu kwa umma kwa kuzingatia muktadha
husika ifikapo mwaka 2025;
vii. Kuendeshwa kwa mikutano, semina, warsha na matamasha kuhusu
mahitaji mbalimbali ya watendaji wa elimu ya watu wazima
katika ngazi ya taifa, mkoa na wilaya ifikapo mwaka 2025; na
viii. Kufanyika kwa onesho moja la kitaifa kuhusiana na uzoefu wa
kazi na fikira za kiuvumbuzi kuhusu kisomo na elimu kwa umma
kila mwaka.
Viashiria vya Mafanikio vya Msingi
i. Kuwepo kwa agenda ya kitaifa ya utafiti;
ii. Idadi na aina za miongozo iliyopo ya kuboresha kazi za kisomo
na elimu kwa umma;
iii. Idadi ya watendaji waliopata mafunzo ya utafiti, ubunifu na
uvumbuzi;
iv. Idadi na aina za programu za mafunzo yaliyofanywa kuhusu
utafiti, ubunifu na uvumbuzi;
v. Kuongezeka kwa idadi ya ripoti za utafiti na machapisho
yaliyosambazwa katika ngazi mbalimbali za utekelezaji na kwa
jamii;
29
vi. Ongezeko la idadi ya uzoefu uliowasilishwa na wadau mbalimbali
kuhusu programu za kisomo na elimu kwa umma;
vii. Idadi ya mitaala na programu za kisomo na elimu kwa umma
zenye ubora na zenye kukidhi mahitaji iliyoandaliwa na watendaji
mbalimbali;
viii. Kuongezeka kwa asilimia, idadi na aina za programu za kisomo
na elimu kwa umma zinazotolewa na waendeshaji mbalimbali; na
ix. Kuongezeka kwa vithibitisho vilivyoandikwa kuhusu mchango wa
jamii kusaidia jitihada za kisomo na elimu kwa umma.
30
SURA YA TANO
MFUMO WA USHIRIKIANO KITAASISI KATIKA KUTEKELEZA MTaKEU
5�1 Wahusika wa MTaKEU
MTaKEU unatambua kwamba kisomo na elimu kwa umma ni masuala yanayohusisha sekta nyingi na yanapaswa kushughulikiwa na wadau wengi katika sekta ndogo ya elimu ya watu wa wazima na elimu nje ya mfumo rasmi. Utekelezaji wake unatakiwa kufanywa na wadau mbalimbali na katika ngazi mbalimbali. Inatakiwa kuratibiwa ikiwa ndani ya mfumo wa kitaasisi uliopo tayari ili kuwezesha mipango na mgawanyo madhubuti wa rasilimali. Utekelezaji wa mkakati huu unahusisha watendaji mbalimbali ambao wanaweza kuwa katika makundi ya watu binafsi, taasisi au
mashirika. Watekelezaji wakuu wa mkakati huu ni hawa wafuatao:
i. Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia;
ii. Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa;
iii. Wizara ya Fedha na Mipango;
iv. Wizara nyingine, Idara na Mashirika ya umma;
v. Taasisi ya Elimu ya Watu wazima;
vi. Vyuo vya maendeleo kwa wananchi;
vii. Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi;
viii. Bodi ya Huduma za Maktaba Tanzania;
ix. Vyuo vya elimu ya juu;
x. Asasi za kiraia, mashirika ya kidini na mashirika yasiyokuwa ya
kiserikali;
xi. Washirika wa maendeleo;
xii. Watoaji binafsi wa programu za kisomo na elimu kwa umma;
xiii. Wanajamii mmojammoja; na
xiv. Vikundi vya walengwa na mlengwa mmojammoja.
31
5�2 Mfumo wa Kitaasisi katika Kutekeleza MTaKEU
Utekelezaji wa shughuli za kisomo na elimu kwa umma, usimamizi, uratibu
na uendeshaji kwa jumla hufanywa kwa kuzingatia taratibu za kitaasisi
katika mgawanyo wa wajibu na majukumu kama ifuatavyo:
a) Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia (WyEST)
Majukumu na wajibu wa WyEST yatakuwa ni:
i. Kutoa mwongozo wa jumla katika kuandaa na kutekeleza MTaKEU
kwa kushirikiana na OR-TAMISEMI;
ii. Kuhakikisha utekelezaji wa MTaKEU unaendana na sera
ndogondogo za sekta zinazohusika;
iii. Kuratibu na kufuatilia utekelezaji wa MTaKEU katika ngazi ya
kitaifa;
iv. Kuweka mfumo wa uratibu na kuwa kiungo kati ya Wizara, Idara
na mashirika, asasi za kiraia, sekta binafsi, vyuo vya elimu ya juu,
na wadau wengine katika kutoa programu za kisomo na elimu
kwa umma; na
v. Kutafuta rasilimali fedha kutoka serikalini, wadau wa maendeleo,
na wadau wengine wa elimu katika kusaidia utekelezaji wa
MTaKEU.
b) Wizara ya Fedha na Mipango
Majukumu na wajibu wa Wizara ya Fedha na Mipango katika
utekelezaji wa MTaKEU yatakuwa ni:
i. Kuhakikisha programu za kisomo na elimu kwa umma zinaingizwa
katika mipango na bajeti ya serikali;
32
ii. Kuandaa mwongozo wa uwezeshwaji wa kifedha kwa shughuli za
kisomo na elimu kwa umma nchini; na
iii. Kuhakikisha fedha kwa ajili ya utekelezaji wa MTaKEU zinatolewa
kwa kila mkoa kwa wakati mwafaka.
c) Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima (TEWW)
Majukumu na wajibu wa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima katika
utekelezaji wa MTaKEU yatakuwa ni:
i. Kuandaa miongozo ya mtaala na zana na vifaa vya kufundishia
na kujifunzia katika kuwezesha utekelezaji wa pragramu za
kisomo na elimu kwa umma katika ngazi ya kitaifa;
ii. Kuanzisha na kufanya majaribio ya programu za mfano za kisomo
na elimu kwa umma;
iii. Kuandaa zana sanifu za kitaifa za kisomo za kupimia na kutahini
katika kisomo na tathmini kwa ujumla;
iv. Kuweka viwango sanifu vya upimaji na viwango vya sifa kwa
programu za kisomo nchini;
v. Kubuni na kuendesha kozi za muda mfupi na muda mrefu kwa ajili
ya waratibu, wawezeshaji, wawezeshaji-wasaidizi na watoaji wa
programu za kisomo na elimu kwa umma nchini;
vi. Kutunga na kuandaa vijitabu na vifaa vya kujifunzia kwa
wanakisomo;
vii. Kuendesha programu za kujenga uwezo kwa watekelezaji wa
MTaKEU nchini;
viii. Kutoa ushauri na huduma za kitaalamu katika masuala yanayohusu
kisomo na elimu kwa umma;
33
ix. Kufanya tafiti za kitaifa za kisomo na elimu kwa umma na
kuwasilisha matokeo kwa wadau;
x. Kufanya ufuatiliaji na tathimini ya shughuli za kisomo na elimu kwa
umma nchini;
xi. Kutoa msaada wa kitaalamu kwa watendaji na wadau;
xii. Kuratibu taratibu za upimaji na utahini na kusimamia mfumo wa
utoaji tuzo wa programu za kisomo na elimu kwa uma katika
mikoa; na
xiii. Kuanzisha na kusimamia kanzidata za kisomo nchini.
d) Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-
TAMISEMI)
Majukumu na wajibu mahususi wa OR-TAMISEMI kuhusiana na
utekelezaji wa MTaKEU yatakuwa ni:
i. Kuratibu, kufuatilia na kutathimini mipango ya kielimu ya mkoa
ambayo inajumuisha shughuli za kisomo na elimu kwa umma;
ii. Kuingiza mipango na bajeti za mikoa katika mipango ya kitaifa
ambao utakuwa msingi wa kupitisha na kuhamisha fedha kutoka
hazina kwenda katika mamlaka za serikali za mitaa;
iii. Kusimamia shughuli za utoaji wa programu za kisomo na elimu
kwa umma katika mamlaka ya serikali za mitaa;
iv. Kuhakikisha kwamba mamlaka za serikali za mitaa zinaandaa
mpango thabiti wa muda wa kati wa matumizi, mipango ya bajeti
ya kielimu ya mwaka mmoja-mmoja na ya miaka mitatu-mitatu
kwa kuzingatia mpango wa utekelezaji uliotolewa kutoka ngazi
ya kata hadi ngazi ya halmashauri kwa kulingana na malengo ya
kiserikali, sera za kielimu, na vigezo vya uthibiti ubora.
34
v. Kushirikiana na WyEST ili kusimamia, kufanya mapitio na
kutathmini mafanikio na matokeo ya programu za kisomo na elimu
kwa umma katika mamlaka ya serikali za mtaa;
vi. Kuhakikisha kwamba ripoti za robo mwaka za programu za
kisomo na elimu kwa umma na takwimu kuhusu usajili, uhifadhi na
ushiriki vinakusanywa kutoka mikoani na wilayani na kuwasilishwa
kwa usahihi kwa OR-TAMISEMI; na
vii. Kutoa miongozo na maelekezo kuhusu kutumia fedha kwa usahihi,
rasilimali watu na vifaa vingine vikiwemo kona za usomaji, maktaba
zinazohamishika, maktaba za vijijini, maktaba za kimkoa, vifaa
vya vyombo tofauti vya habari vinavyotumika, raslimali za vituo
na wawezeshaji katika maeneo husika.
e) Ngazi ya Mkoa
Ngazi ya mkoa itahusisha Katibu Tawala wa Mkoa, Afisa Elimu wa
Mkoa, wakuu wote wa idara na wakufunzi wakazi wa TEWW wa
mikoa. Wajibu na majukumu ya ngazi ya mkoa kuhusu utekelezaji
wa MTaKEU yatakuwa ni:
i. Kuratibu na kufuatilia usajili, mahudhurio na maendeleo ya vijana
na watu wazima katika vituo vya mafunzo ya kisomo katika
wilaya zote za mkoa;
ii. Kufanya shughuli za kuratibu na kufuatilia uendeshaji wa programu
za kisomo na elimu kwa umma;
iii. Kufuatilia mgawanyo wa fedha, utoaji wa fedha, malipo ya posho
na marupurupu mengine kwa wawezeshaji wa programu za kisomo
na elimu kwa umma na wasaidizi katika ngazi ya halmashauri ya
wilaya au manispaa;
35
iv. Kuunganisha mipango na bajeti za kisomo na elimu kwa umma
kimkoa na kuhakikisha kuwa shughuli za kisomo na elimu kwa umma
zinajumuishwa katika bajeti na mipango ya mwaka ya mkoa;
v. Kupanga, kuratibu na kufanya shughuli za kisomo na elimu kwa
umma wakati wa juma la elimu ya watu wazima;
vi. Kuhakikisha kwamba halmashauri za wilaya au manispaa
zinaanzisha rasilimali na kona za kusomea, maktaba
zinazohamishika, maktaba za vijiji na vituo vya vyombo mbalimbali
vya habari vya umma;
vii. Kuratibu na kusimamia kazi ya kutambua makundi yaliyotengwa
kielimu wakiwemo watu wenye ulemavu, wanawake, vijana na watu
wazima wasiojua kusoma na kuandika na kuhakikisha kwamba
wamesajiliwa na kuendelea kuhudhuria katika vituo vya mafunzo
ya programu za kisomo katika wilaya; na;
viii. Kuratibu upimaji na utahini wa wanafunzi wa kisomo na elimu kwa
umma katika mkoa.
f) Ngazi ya Halmashauri
Afisa Elimu Wilaya na wakuu wa idara wote wanaohusika watasimamia utekelezaji wa MTaKEU katika maeneo yote yaliyo katika uangalizi wao kama vile kata, vijiji/mitaa na vituo vya mafunzo ya kisomo. Wajibu na majukumu ya serikali za mitaa hizi
yatakuwa ni;
i. Kuhakikisha ufanyikaji wa usajili, mahudhurio na maendeleo ya
vijana na watu wazima katika vituo vya mafunzo ya kisomo katika
ngazi ya wilaya au manispaa;
ii. Kuandaa mpango kazi wa kisomo, bajeti na kuhakikisha malipo ya
mishahara na posho kwa wataalamu/wawezeshaji na wasaidizi
yanajumuishwa ndani ya bajeti ya mwaka ya wilaya;
36
iii. Kuhakikisha kwamba masuala ya kisomo na elimu kwa umma
yanajumuishwa kama agenda ya kudumu katika vikao na ripoti
za halmashauri za robo mwaka;
iv. Kuhakikisha kwamba data na ripoti za robo mwaka za kisomo
na elimu kwa umma zinawasilishwa kutoka katika vituo vya vijiji/
mitaa kupitia ofisi za waratibu wa elimu kata;
v. Kuanzisha vituo au kona za usomaji, maktaba zinazohamishika,
maktaba za vijiji na vituo vya habari kwa umma katika ngazi za
wilaya na za chini kwa mfano kata, vijiji/ mtaa;
vi. Kuongoza katika kuboresha utekelezaji wa kisomo na elimu kwa
umma katika wilaya;
vii. Kukusanya na kugawa rasilimali kwa ajili ya utekelezaji wa
programu za kisomo na elimu kwa umma katika halmashauri za
wilaya au manispaa;
viii. Kuhakikisha kwamba posho na marupurupu mengine yanatolewa
kwa wawezeshaji wa kisomo na wataalamu wengine katika
wilaya;
ix. Kuhamasisha na kuhimiza wadau kusaidia na kushiriki katika
utekelezaji wa shughuli za kisomo na elimu kwa umma;
x. Kufanya ufuatiliaji wa mara kwa mara wa shughuli za kisomo na
elimu kwa umma na kutoa msaada wa kiufundi kwa watendaji na
wadau;
xi. Kuwajengea uwezo waratibu elimu kata na waratibu wa vituo
katika programu za kisomo na elimu kwa umma; na
xii. Kusimamia kazi ya upimaji wa wanafunzi wa kisomo na elimu kwa
umma kulingana na miongozo iliyowekwa.
37
g) Ngazi ya Kata
Afisa Elimu Kata na maafisa wengine wanaohusika katika ngazi ya kata watatakiwa kuwa na wajibu na majukumu yafuatayo katika utekelezaji wa MTaKEU:
i. Kuhakikisha kwamba kila kijiji/mtaa kinabainisha, kusajili na kuhakikisha mahudhurio ya vijana na watu wazima katika vituo vya mafunzo;
ii. Kuratibu shughulli za vituo vya kisomo na elimu kwa umma ndani ya kata;
iii. Kuhamasisha wadau ili kuhakikisha wasaidia juhudi za upatikanaji wa rasilimali za kuwezesha shughuli za kisomo na elimu kwa umma katika ngazi ya kata;
iv. Kuhakikisha kwamba takwimu zinazohusu vijana na watu wazima walio katika programu za kisomo na elimu kwa umma katika kata zinakusanywa, kuhifadhiwa, kuhuishwa na kupelekwa katika ngazi ya wilaya; na
v. Kuanzisha zana na vifaa au kona za kujifunzia, maktaba zinazohamishika, maktaba za vijiji na vituo vya midia kwa umma
katika ngazi ya kata.
h) Ngazi ya Kijiji/ Mtaa
Jamii na uongozi wa kijiji/mtaa watakuwa na wajibu na majukumu
yafuatayo:
i. Kuhakikisha kwamba kazi za usajili, mahudhurio na ushiriki wa
vijana na watu wazima zinafanyika katika vituo vya mafunzo ya
kisomo katika ngazi ya vijiji/mtaa;
ii. Kuhakikisha kwamba rasilimali na vifaa kama vile vyumba vya
madarasa, walimu, vituo vya kisomo na viwanja vinatunzwa kwa
ajili ya kutumika kuwezesha utekelezaji wa kisomo na elimu kwa
umma;
38
iii. Kuhakikisha vijana na watu wazima wenye mahitaji maalumu au kutoka katika mazingira yaliyosahaulika wanajumuishwa katika shughuli za kisomo na elimu kwa umma;
iv. Kuhamasisha wanajamii kushiriki katika kutekeleza shughuli za kisomo na elimu kwa umma katika vijiji/mtaa;
v. Kuhamasisha vijana na watu wazima kuhusu faida za kujiunga na kushiriki katika kisomo na elimu kwa umma kwa manufaa na maendeleo yao kiuchumi na kijamii; na
vi. Kuhakikisha masuala ya kisomo ya vijana na watu wazima yanajadiliwa katika mikutano ya kijiji/mtaa.
i) Ngazi ya Vituo vya Mafunzo
Mratibu wa kituo cha mafunzo na wawezeshaji watakuwa na majukumu na wajibu ufuatao katika kuhakikisha utekelezaji wa MTaKEU katika ngazi ya vituo vya mafunzo:
i. Kusajili vijana na watu wazima katika vituo vya mafunzo ya kisomo;
ii. Kuweka mazingira bora ya ujifunzaji kwa vijana na watu wazima katika kituo;
iii. Kuhamasisha na kuhakikisha matumizi sahihi ya rasilimali katika kituo;
iv. Kushirikiana na uongozi wa kijiji/mtaa kuingiza shughuli za kituo katika mipango ya maendeleo ya mwaka ya kijiji/mtaa;
v. Kuandaa ripoti ya mara kwa mara ya utekelezaji wa shughuli za kisomo na elimu kwa umma na kuiwasilisha kwa Afisa Elimu Kata;
vi. Kuanzisha na kudumisha mahusiano ya karibu na wadau wote wa
elimu; na
vii. Kuanzisha kamati ya kituo ya kisomo na elimu kwa umma.
39
5�3 Wajibu na Majukumu ya Taasisi na Washirika Wengine
a) Mamlaka ya Mafunzo na Elimu ya Ufundi
Majukumu na wajibu wa Mamlaka ya Mafunzo na Elimu ya Ufundi
katika kutekeleza MTaKEU yatakuwa ni:
i. Kutoa msaada wa kiufundi kwa wawezeshaji wa kisomo na elimu
kwa umma katika kutoa elimu ya ufundi wa awali; na
ii. Kusaidia kufanyika mafunzo kwa vitendo ya ufundi wa awali ya
programu za kisomo na elimu kwa umma.
b) Vyuo vya Maendeleo ya Jamii
Wajibu na majukumu ya vyuo vya maendeleo ya jamii katika
kutekeleza MTaKEU yatakuwa ni:
i. Kushirikiana na TEWW katika kuhimiza programu za kisomo na
elimu kwa umma nchini;
ii. Kuhimiza kisomo na elimu kwa umma kwa kutoa maarifa na stadi
za ufundi wa awali kwa vijana na watu wazima;
iii. Kuwa vituo maalumu vya kukuza stadi za utafiti, ugunduzi na
uvumbuzi wa programu za kisomo na elimu kwa umma; na
iv. Kutoa msaada wa vifaa vya kufundishia na kujifunzia katika
kutekeleza programu za MTaKEU.
c) Taasisi za Elimu ya Juu
Katika kutekeleza MTaKEU, vyuo vikuu na taasisi nyingine za elimu
ya juu za Tanzania zitakuwa na wajibu na majukumu ya:
i. Kubuni na kujaribu programu za mfano za kisomo na elimu kwa
umma;
40
ii. Kuwajengea uwezo wafanyakazi wa ngazi mbalimbali kuhusu
stadi za kisomo na elimu kwa umma;
iii. Kufanya tafiti kuhusu kisomo na elimu kwa umma na kushirikisha
matokeo kwa wadau; na
iv. Kutoa huduma ya ushauri wa kitaalamu katika eneo la kisomo na
elimu kwa umma.
d) Asasi za Kiraia, Mashirika ya Kidini na Mashirika yasiyokuwa
ya Kiserikali
Katika utekelezaji wa MTaKEU, wajibu na majukumu ya asasi za
kiraia, mashirika ya kidini na mashirika yasiyokuwa ya kiserikali
yatakuwa ni:
i. Kuhakikisha kwamba kazi za usajili na ushiriki wa vijana na watu
wazima katika programu za kisomo zinafanyika kwa ufasaha
katika vituo vyao vya kisomo.
ii. Kutafuta rasilimali za kuwezesha utekelezaji wa MTaKEU nchini
zikiwemo jamii ambazo ni ngumu kufikiwa;
iii. Kuweka mfumo wa kuratibu kazi na mashirikiano miongoni mwa
asasi za kiraia, mashirika ya kidini na mashirika yasiyokuwa ya
kiserikali yanayoendesha programu za kisomo na elimu kwa umma
nchini;
iv. Kufanya na kusaidia tafiti katika masuala ya kisomo na elimu kwa
umma na kutoa taarifa serikalini; na
v. Kushiriki katika kukuza mtaala.
41
e) Washirika wa Maendeleo
Wajibu na majukumu ya washirika wa maendeleo katika
kutekeleza MTaKEU yatakuwa ni:
i. Kutoa rasilimali zitakazosaidia utekelezaji wa MTaKEU;
ii. Kushiriki katika kufanya mapitio na tathimini ya mipango ya
kisomo na elimu kwa umma;
iii. Kutoa msaada wa kiufundi katika kufanikisha utekelezaji wa
MTaKEU;
iv. Kuanzisha mawasiliano na mitandao; na
v. Kushirikisha mawazo na uzoefu kuhusu kisomo na elimu kwa umma.
f) Bodi ya huduma za Maktaba Tanzania
Wajibu na majukumu ya bodi ya huduma za maktaba tanzania
katika kutekeleza MTaKEU yatakuwa ni:
i. Kutoa nafasi ya kujisomea kwa vijana na watu wazima walio
katika programu za kisomo na elimu kwa umma;
ii. Kutoa vitabu na vifaa vingine vya kujisomea kwa vijana, watu
wazima na wawezeshaji wa programu za kisomo na elimu kwa
umma; na
iii. Kutoa ushauri wa kitaalamu kuhusu huduma za maktaba kuhusiana
na utekelezaji wa MTaKEU.
42
SURA YA SITA
UFUATILIAJI, TATHMINI NA MFUMO WA UTOAJI TAARIFA
6�1 Maelezo ya Jumla
Mpango wa ufuatiliaji, tathmini na uwasilishaji wa taarifa huonesha
jinsi mfumo wote wa usimamizi, tathmini na utoaji wa taarifa za kazi
za mkakati utakavyokuwa. Mpango huo hujumuisha viashiria, nani ana
wajibu wa kuvikusanya, kwa njia zipi na zana zipi zitakazotumika, na jinsi
gani mtiririko wa data utakavyokuwa katika taasisi. Ufuatiliaji, tathmini
na uwasilishaji wa taarifa unalenga kuwezesha kufuatilia utekelezaji wa
MTaKEU hatua kwa hatua kwa kutoa kwa wakati taarifa sahihi na za
uhakika kwa wadau ili kuwezesha kazi ya kufanya maamuzi.
Mpango mzima wa ufuatiliaji na tathimini umejengwa katika njia ya
mfumo wa kimantiki. Njia hii inatoa fursa ya kupitia malengo mahsusi na
kazi katika mtiririko wa kimantiki. Vilevile njia inatoa fursa ya kuunganisha
malengo, matokeo endelevu, matokeo tarajiwa na shughuli za lazima
zinazopaswa kufanikisha malengo katika namna ya kutegemeana na
katika ngazi tofauti katika mfuatano wa malengo husika.
Njia hiyo inatafsiri vipengele vya msingi vya mfumo wa ufuatiliaji na
tathmini. Inatafsiri viashiria vinavyohitajika kupima kiwango cha mafanikio,
inabainisha vyanzo vya taarifa kwa ajili ya viashiria na kutengeneza kauli
bunifu. Hata hivyo, kauli za kubuni haziwezi kujumuishwa katika ngazi
za matokeo na shughuli kwa sababu hatua hizi zipo katika uangalizi
madhubuti wa utawala wa ndani katika kutekeleza mkakati.
6�2 Ufuatiliaji na Tathmini ya utekelezaji wa MTaKEU
Katika utekelezaji wa MTaKEU ufuatiliaji utahusisha ukusanyaji wa taarifa,
uhakiki wa taarifa, uhifadhi wa taarifa na utoaji wa taarifa. Kutakuwa na
43
mfululizo wa ripoti kwa ajili ya kufuatilia mafanikio ya mkakati. Kutakuwa
na ripoti za robo mwaka zitakazotokana na zana za ndani za ufuatiliaji
kwa ajili ya kulingalisha na mpango kazi uliothibitishwa kwa kuwa na
mafanikio halisi na kubaini vikwazo na kupendekeza hatua stahiki
zinazohitajika. Pia kutakuwa na ripoti za utekelezaji wa mkakati kwa nusu
mwaka na kwa mwaka mzima. Tathmini itapima matokeo na athari za
mkakati kwa kuzingatia malengo ya kimkakati kupitia tathmini ya muda wa
kati na ya mwisho. Itapima mafanikio ya mkakati kwa kuzingatia ufanisi,
tija, matokeo na uendelevu wake. Matokeo ya ufuatiliaji na viashiria vya
tathmini yataripotiwa kwa hadhira husika kama inavyotakiwa.
44
SURA YA SABA
UWEZESHWAJI WA KIFEDHA NA UENDELEVU WA MKAKATI
7�1 Uwezeshwaji wa Kifedha wa MTaKEU
Kwa kutambua kwamba utoaji wa elimu ya watu wazima ni ajenda
shirikishi kwa wadau, fedha za utekelezaji wa MTaKEU zitatokana na
vyanzo mbalimbali. Vyanzo vikuu ni:
i. Serikali: Hiki ni chanzo kikuu cha fedha za utekelezaji wa mradi wa
MTaKEU, kupitia bajeti za kila mwaka (MTEF katika ngazi tofauti
za utekelezaji kutoka ngazi ya taifa hadi serikali za mitaa); na
ii. Wadau tofauti kama vile mashirika ya kiraia, washirika wa
maendeleo, sekta binafsi na jamii kwa ujumla.
7�2 Mikakati ya Kupata Fedha
i. Wizara, idara na mashirika ya umma yataanzisha na kuimarisha njia za uchangishaji na ukusanyaji wa fedha kutoka vyanzo mbalimbali;
ii. Wizara ya fedha na mipango itatoa fedha ya kutosha kutekeleza MTaKEU;
iii. Wizara, idara na mashirika ya umma yasisitize kuhusu kutumia mfumo wa serikali uliopo sasa na kuwajibika kwa ufanisi na kutoa ripoti ya fedha za MTaKEU;
iv. Wizara, idara na mashirika ya umma yatahakikisha miongozo iliyopo na sheria za udhibiti wa fedha ikiwemo ugavi vinatolewa katika ngazi zote ili kuongoza utekelezaji wa MTaKEU;
v. Wizara, idara na mashirika ya umma yatatenga fedha kwa
ajili ya upatikanaji wa vifaa vya kufundishia na kujifunzia kwa
ajili ya MTaKEU, posho kwa wawezeshaji na kuwajengea uwezo
watendaji wa maeneo husika; na
vi. Wizara, idara na mashirika ya umma yatashirikiana na asasi za
kiraia na sekta binafsi katika kuunga mkono MTaKEU.
45
7�3 Makadirio ya Gharama za MTaKEU kwa kipindi cha 2020/2021-
2024/2025
Makadirio ya gharama za MTaKEU yanazingatia idadi ya vipengele
vinavyoathiriwa na:
i. Idadi ya wanafunzi wa kisomo wanaotarajiwa kusajiliwa chini ya
programu za kisomo (rejea Jedwali 1); na
ii. Idadi ya wawezeshaji watakaoajiriwa, kupewa mafunzo na
kulipwa kulingana na ukubwa wa darasa (rejea Jedwali 2).
Jedwali 1: Idadi ya Wanafunzi kwa Kipindi cha 2020/2021 Hadi
2024/2025
Shughuli Idadi ya Wanafunzi kwa Kipindi cha 2020/2021 Hadi 2024/2025
2020/21 2021/2022 2022/2023 2023/2024 2024/2025 Jumla Kuu
Kisomo chenye manufaa
500,000 470,000 350,000 480,000 400,000 2,200,000
Kisomo cha Kujiendeleza
750,000 620,000 600,000 3,300,000 270,000 2,570,000
Jumla 1,250,000 1,090,000 950,000 810,000 670,000 4,770,000
Jedwali 2: Idadi ya Wawezeshaji kwa Kipindi cha 2020/2021 Hadi
2024/2025
Shughuli Idadi ya Wawezeshaji kwa Kipindi cha 2020/2021 Hadi 2024/2025
2020/21 2021/2022 2022/2023 2023/2024 2024/2025 Jumla Kuu
Kisomo chenye manufaa
5,570 5,000 6,000 4,500 5,070 26,140
Kisomo cha Kujiendeleza
5,200 4,535 3,537 3,535 2,535 19,342
Jumla 10,770 9,535 9,537 8,035 7,605 45,482
46
Ukubwa wa darasa la vijana na watu wazima linakadiriwa kuwa na
wanafunzi 30 kama ilivyoelekezwa katika miongozo ya usajili wa elimu
ya watu wazima; na linasimamiwa na mwezeshaji mmoja na wawezeshaji-
wasaidizi wawili.
Kwa kila mwanafunzi mtu mzima aliye katika programu ya kisomo na
kisomo cha kujiendeleza, makadirio ya gharama ya TZS. 6,500 (US $ 3)
kwa kila mtu zimetengwa kwa ajili ya vitabu na shajara kwa muda wote
wa mafunzo. Programu za kisomo katika ngazi za vituo zitawezeshwa
na wawezeshaji na wawezeshaji wasaidizi. Wakati wa uwezeshaji,
watapewa posho ili kuwapa motisha.
Wawezeshaji katika madarasa ya kisomo na kisomo cha kujiendeleza
watapewa posho ya TZS. 50,000 kwa mwezi kwa kadirio la juu la miezi
10. Makadirio ya gharama kwa wawezeshaji ni malipo yatakayolipwa
kwa wale ambao tayari wapo katika mfumo wa malipo ya serikali kwa
kazi hii ya kufundisha madarasa haya kama awamu ya pili. Wawezeshaji
ambao ni wasaidizi watalipwa kiwango cha TZS. 50,000 pia kwa kadirio
la juu kwa miezi 10 kwa mwaka.
Jumla ya gharama za MTaKEU itakuwa takribani TZS bilioni 42.6 kwa
kipindi cha miaka mitano. Mgawanyo wa fedha umeoneshwa kwa kifupi
katika Jedwali la 3.
47
Jedw
ali 3
:
Muh
tasa
ri w
a M
akad
irio
ya G
hara
ma
za S
hugh
uli z
a M
TaKE
U 2
020/
2021
-202
4/20
25
Shug
huli
Muh
tasa
ri w
a G
hara
ma
za M
kaka
ti kw
a K
ipin
di c
ha 2
020/
2021
Had
i 202
4/20
25
2020
/202
120
21/2
022
2022
/202
320
23/2
024
2024
/202
5Ju
mla
Kuu
Kiso
mo
chen
ye
man
ufaa
3,25
0,00
0,00
03,
055,
000,
000
2,27
5,00
0,00
03,
120,
000,
000
2,60
0,00
0,00
014
,300
,000
,000
Kiso
mo
cha
kujie
ndel
eza
4,87
5,00
0,00
04,
030,
000,
000
3,90
0,00
0,00
02,
145,
000,
000
1,75
5,00
0,00
016
,705
,000
,000
Ufu
ndish
aji
538,
500,
0000
476,
750,
000
476,
850,
000
351,
750,
000
380,
250,
000
2,22
4,10
0,00
0
Kuje
nga
uwez
o, ta
thm
ini
ya m
ahita
ji,
usim
amiz
i
wa
data
,
kusim
amia
viw
ango
na
upim
aji
na
tath
min
i
5,73
5,00
0,00
028
0,00
0,00
032
1,10
0,00
011
0,12
1,00
013
0,00
0,00
09,
466,
121,
000
Jum
la k
uu14
,398
,500
,000
7,84
1,75
0,00
09,
862,
850,
000
5,72
6,87
1,00
04,
865,
250,
000
42,6
95,2
21,0
00
47
48
7�4 Uendelevu katika Utekelezaji wa MTaKEU
Katika kuhakikisha uendelevu wa utekelezaji wa MTaKEU, Serikali itaweka
mazingira mazuri kwa wadau mbalimbali kushiriki katika programu za
kisomo na elimu kwa umma; na kwa upekee:
i. Wizara, Idara na Mashirika ya umma yatatoa msaada wa kiufundi kwa mamlaka za serikali za mitaa katika kupanga na kujumuisha MTaKEU katika mipango yao ya maendeleo;
ii. Wizara, Idara na Mashirika ya umma na mamlaka za serikali za mitaa zitatumia vizuri fursa tofauti zilizopo, ikiwemo Maadhimisho ya Mwaka ya Elimu ya Watu Wazima na Elimu kwa Wote;
iii. Wizara, Idara na Mashirika ya umma na mamlaka za serikali za mitaa watatafuta fedha za kuwezesha utekelezaji wa shughuli za MTaKEU;
iv. Wizara, Idara na Mashirika ya umma pamoja na vyombo vya habari watafanya kampeni katika vyombo vya habari ili kuhamasisha na kuwaweka pamoja wadau wengine kuchukua jukumu la kuwa mstari wa mbele katika kuunga mkono MTaKEU;
v. Wizara, Idara na Mashirika ya umma na mamlaka za serikali za mitaa watatumia kikamilifu kamati za elimu ya watu wazima na elimu nje ya mfumo rasmi zilizoundwa katika ngazi zote katika kufuatilia na kutathmini shughuli za MTaKEU;
vi. Wizara, Idara na Mashirika ya umma na mamlaka za serikali za mitaa watahakikisha kunakuwa na uwazi katika kukusanya rasilimali na mgawanyo wake kupitia mifumo ya uwajibikaji iliyopo;
vii. Wizara, Idara na Mashirika ya umma watajenga uwezo kuhusu utendaji thabiti katika utekelezaji wa MTaKEU; na
viii. MTaKEU itafanyiwa mapitio baada ya miaka mitano.
49
KIA
MBA
TISH
O
Mal
engo
ya
Kim
kaka
ti, V
iash
iria
vya
Maf
anik
io, S
haba
ha, M
zung
uko
wa
Uku
sany
aji w
a D
ata,
Mhu
sika
na M
uda
wa
Ute
kele
zaji
Na�
Leng
o la
K
imka
kati
Via
shiri
a vy
a M
afan
ikio
Shab
aha
Mzu
nguk
o w
a ku
kusa
nya
da
ta
Mhu
sika
Mud
a w
a U
teke
leza
ji
1.Ku
anzi
sha
prog
ram
u za
ki
som
o na
elim
u kw
a um
ma
ziliz
o bo
ra n
a ze
nye
man
ufaa
kw
a ja
mii.
i. Id
adi y
a vi
tuo
vya
kiso
mo
viliv
yoan
zish
wa
katik
a ki
la w
ilaya
.
ii. id
adi y
a wa
leng
wa
walio
nufa
ika
katik
a
prog
ram
u za
kiso
mo
na e
limu
kwa
umm
a.
i. Ku
anzi
shwa
kwa
kitu
o ki
moj
a ch
a
kiso
mo
katik
a ki
la
kata
ifika
po m
waka
2025
.
ii. K
uwep
o kw
a
wale
ngwa
mili
oni
mbi
li wa
lionu
faik
a
na p
rogr
amu
za
kiso
mo
ifika
po
mwa
ka 2
025.
Robo
m
wak
a
Mw
aka
Mud
a w
a ka
ti
TEW
W,
WyE
ST, O
R-
TAM
ISEM
I,
Serik
ali z
a
mita
a, A
ZISE
,
VET
A, S
IDO
2021
-202
5
49
50
Na�
Leng
o la
K
imka
kati
Via
shiri
a vy
a M
afan
ikio
Shab
aha
Mzu
nguk
o w
a ku
kusa
nya
da
ta
Mhu
sika
Mud
a w
a U
teke
leza
ji
2.Ku
imar
isha
mifu
mo
na
prog
ram
u w
ezes
hi z
a ku
ende
leza
ki
som
o na
elim
u kw
a um
ma
i. Id
adi y
a pr
ogra
mu
wez
eshi
za
kiso
mo
zina
zofa
nya
kazi
ka
tika
jam
ii.
ii.
Ong
ezek
o la
asil
imia
ya
jam
ii zi
nazo
fikiw
a na
pro
gram
u bo
ra z
a ki
som
o na
elim
u kw
a um
ma
kupi
tia v
yom
bo
vya
haba
ri
i. Ku
anzi
shwa
kwa
prog
ram
u m
oja
ya k
isom
o kw
a
njia
ya
redi
o
katik
a ki
la m
koa
ifika
po m
waka
2025
.
ii. K
uanz
ishwa
kwa
kitu
o ki
moj
a
cha
kiso
mo
cha
kujie
ndel
eza
katik
a ki
la k
ata
ifika
po m
waka
2025
.
Robo
mw
aka
Mw
aka
Mud
a w
a ka
ti
TEW
W,
WyE
ST, O
R-
TAM
ISEM
I,
Serik
ali z
a
mita
a, A
ZISE
,
Was
hirik
a w
a
mae
ndel
eo,
Vyuo
vik
uu,
Bodi
ya
Mak
taba
,
SID
O
2021
-202
5
50
51
5150
Na�
Leng
o la
K
imka
kati
Via
shiri
a vy
a M
afan
ikio
Shab
aha
Mzu
nguk
o w
a ku
kusa
nya
da
ta
Mhu
sika
Mud
a w
a U
teke
leza
ji
3.Ku
bore
sha
mifu
mo
ya
usim
amiz
i wa
takw
imu
za
kiso
mo
na e
limu
kwa
umm
a
i. Ku
wep
o kw
a ta
kwim
u za
kiso
mo
na e
limu
kwa
umm
a ka
tika
mifu
mo
ya B
EMIS
, EM
IS, n
a m
asja
la y
a vi
jijin
i
ii.
Idad
i na
aina
za
wat
ekel
ezaj
i wa
liopa
ta m
afun
zo
usim
amiz
i wa
takw
imu
za k
isom
o na
elim
u kw
a um
ma
i. Ku
ingi
zwa
kwa
vias
hiria
vya
takw
imu
za
kiso
mo
na e
limu
kwa
umm
a ka
tika
mifu
mo
ya B
EMIS
,
EMIS
na
mas
ijala
za v
ijijin
i ifik
apo
mwa
ka 2
022
ii. K
ujen
gewa
uw
ezo
wa k
ukus
anya
na k
ucha
kata
takw
imu
kwa
mam
laka
za
serik
ali z
a m
itaa
ifika
po m
waka
2022
Robo
mw
aka
Mw
aka
Mud
a w
a ka
ti
TEW
W,
WyE
ST, O
R-
TAM
ISEM
I,
Serik
ali z
a
mita
a,
2020
-202
5
52
Na�
Leng
o la
K
imka
kati
Via
shiri
a vy
a M
afan
ikio
Shab
aha
Mzu
nguk
o w
a ku
kusa
nya
da
ta
Mhu
sika
Mud
a w
a U
teke
leza
ji
4.Ku
wek
a vi
wan
go
vya
sifa
za
kita
alum
a kw
a aj
ili y
a pr
ogra
mu
za
kiso
mo
na e
limu
kwa
umm
a
i. Id
adi y
a pr
ogra
mu
za k
isom
o na
elim
u
kwa
umm
a pa
moj
a
na w
aend
esha
ji
wa p
rogr
amu
hizo
wana
ozin
gatia
viw
ango
vya
sifa
viliv
yow
ekwa
.
ii.
Idad
i ya
wana
funz
i wa
naoe
ndel
ea
na n
gazi
nyi
ngin
e zi
nazo
fuat
a za
elim
u.
iii.
Idad
i ya
wahi
timu
wa
prog
ram
u za
kiso
mo
na e
limu
kwa
umm
a wa
naot
ambu
liwa
na m
amla
ka k
uu z
a m
ifum
o ya
viw
ango
i. Ku
anzi
shwa
kwa
m
fum
o ra
smi
wa u
pim
aji n
a ut
oaji
tuzo
kwa
pr
ogra
mu
za
kiso
mo
na e
limu
kwa
umm
a ifi
kapo
mwa
ka
2022
.
ii. K
uwek
wa k
wa
viwa
ngo
vya
sifa
za k
itaal
uma
na
njia
za
kuen
dele
a na
elim
u kw
a pr
ogra
mu
za
kiso
mo
na e
limu
kwa
umm
a ifi
kapo
m
waka
202
2
Robo
mw
aka
Mw
aka
TEW
W,
WyE
ST, O
R-
TAM
ISEM
I,
Serik
ali z
a
mita
a
2020
-202
2
52
53
5352
Na�
Leng
o la
K
imka
kati
Via
shiri
a vy
a M
afan
ikio
Shab
aha
Mzu
nguk
o w
a ku
kusa
nya
da
ta
Mhu
sika
Mud
a w
a U
teke
leza
ji
5.Ku
anda
a za
na
na v
ifaa
bora
vy
a ku
fund
ishia
na
kuj
ifunz
ia
katik
a pr
ogra
mu
za
kiso
mo
na e
limu
kwa
umm
a.
i. Id
adi n
a ai
na z
a za
na n
a vi
faa
vya
kufu
ndish
ia n
a ku
jifun
zia
viliv
yo b
ora
na v
inav
yoen
dana
na
mah
itaji
amba
vyo
vim
eand
aliw
a,
kuza
lishw
a ka
tika
naka
la n
gum
u na
ku
tum
ika.
i. Ku
zalis
hwa
kwa
zana
na
vifa
a vi
navy
ohita
jika
kufu
ndish
ia n
a ku
jifun
zia
katik
a vi
tuo
vya
kiso
mo
na e
limu
kwa
umm
a ifi
kapo
m
waka
202
5.
ii. K
utum
ika
kwa
vitu
o vy
ote
vya
walim
u vi
livyo
hai
ka
tika
kuje
nga
uwez
o wa
wad
au
kuan
daa
zana
na
vifa
a vy
a ki
som
o ka
tika
maz
ingi
ra
yao
ifika
po
mwa
ka 2
025.
Robo
mw
aka
Mw
aka
Mud
a w
a ka
ti
TEW
W,
WyE
ST, O
R-
TAM
ISEM
I,
Serik
ali z
a
mita
a, A
ZISE
,
Bodi
ya
Mak
taba
,
2020
-202
5
54
Na�
Leng
o la
K
imka
kati
Via
shiri
a vy
a M
afan
ikio
Shab
aha
Mzu
nguk
o w
a ku
kusa
nya
da
ta
Mhu
sika
Mud
a w
a U
teke
leza
ji
6.Ku
jeng
a uw
ezo
wa
waw
ezes
haji
na w
arat
ibu
wa
kiso
mo
na e
limu
kwa
umm
a
i. Id
adi y
a ko
zi fu
pi-
fupi
na
kozi
za
mud
a m
refu
zili
zoan
zish
wa
ii.
Kuta
mbu
liwa
kwa
vi
wang
o vy
a sif
a za
wel
edi k
wa
waw
ezes
haji
wa
prog
ram
u za
kiso
mo
na e
limu
kwa
umm
a ka
tika
muu
ndo
wa
utum
ishi w
a um
ma
i. Ku
anzi
shwa
kw
a pr
ogra
mu
2 za
maf
unzo
ya
mud
a m
fupi
zi
nazo
husia
na
na u
wez
esha
ji,
uend
esha
ji na
ua
ndaa
ji wa
za
na k
atik
a ki
la
wila
ya ifi
kapo
20
25ii.
Kua
ndal
iwa
na
kuta
mbu
liwa
kwa
viwa
ngo
vya
sifa
za
wel
edi k
wa a
jili
ya w
awez
esha
ji na
war
atib
u wa
pro
gram
za
kiso
mo
na e
limu
kwa
umm
a ifi
kapo
m
waka
202
5
Robo
mw
aka
Mw
aka
Mud
a w
a ka
ti
TEW
W,
WyE
ST, O
R-
TAM
ISEM
I,
Serik
ali z
a
mita
a, A
ZISE
,
Vyuo
vik
uu,
Bodi
ya
Mak
taba
,
SID
O
2021
-202
5
54
55
54
55
Na�
Leng
o la
K
imka
kati
Via
shiri
a vy
a M
afan
ikio
Shab
aha
Mzu
nguk
o w
a ku
kusa
nya
da
ta
Mhu
sika
Mud
a w
a U
teke
leza
ji
7.Ku
kuza
kaz
i za
tafit
i, uv
umbu
zi
na u
buni
fu
katik
a m
asua
la
ya k
isom
o na
el
imu
kwa
umm
a.
i. Id
adi y
a wa
tend
aji
walio
pata
maf
unzo
ya
uta
fiti,
ubun
ifu n
a uv
umbu
zi.
ii.
Idad
i ya
mita
ala
na
prog
ram
u za
kiso
mo
na e
limu
kwa
umm
a ze
nye
ubor
a na
ze
nye
kuki
dhi m
ahita
ji ili
yoan
daliw
a na
wa
tend
aji m
balim
bali.
i. Ku
patiw
a m
afun
zo y
a ku
fany
a ut
afiti
na k
uwas
ilish
a m
atok
eo
ya u
tafit
i wa
teke
leza
ji m
ia
moj
a na
sitin
i na
tisa
(169
) wa
kiso
mo
na
elim
u kw
a um
ma
ifika
po m
waka
20
25.
ii. K
ujen
gewa
uw
ezo
wa w
atek
elez
aji
katik
a ku
buni
pr
ogra
mu
na
mita
ala
ya
kiso
mo
na e
limu
kwa
umm
a kw
a ku
zing
atia
m
ukta
dha
husik
a ifi
kapo
mwa
ka
2025
.
Robo
mw
aka
Mw
aka
Mud
a w
a ka
ti
TEW
W,
WyE
ST, O
R-
TAM
ISEM
I,
Serik
ali z
a
mita
a, A
ZISE
,
Was
hirik
a w
a
mae
ndel
eo,
Vyuo
vik
uu,
Bodi
ya
Mak
taba
,
SID
O, V
ETA
2021
-202
5
56
57