Upload
youthkingdomministries
View
104
Download
4
Embed Size (px)
Citation preview
YOUTH KINGDOM
MINISTRIES
MKAKATI WA KUJENGA
MSINGI
WA HUDUMA YA YKM
1
UTANGULIZI
Huu ni mpango mkakati wa kujenga na kuimarisha msingi wa huduma ya YKM ndani
ya mwaka 2015. Mpango mkakati huu umegusa kwa sehemu kubwa namna ya
kujenga uwezo wa ndani wa huduma katika kufanya kazi zake za kila siku, na hivyo
basi kiini cha mkakati huu ni kujenga uwezo wa ndani wa YKM. Ili kufanikisha
kujengwa kwa uwezo wa ndani na kisha kuimarisha msingi wa huduma, vipengele
muhimu vimegusiwa,vipengele hivyo ni; Vipao mbele vya huduma, Katiba, sera na
ofisi zilizopo ndani ya YKM, usimamizi wa rasirimali na usuluhishi , uanachama rasmi,
matukio, vyanzo vya fedha, matumizi ya teknolojia, miundo Mbinu, mpango wa muda
mrefu.
Mkakati huu unachambua namna ya utekelezaji wa shughuli za kimkakati kwa kila
hatua. Ni imani ya kwamba mkakati huu utatumika kama dira ya kufanikisha huduma
kutimiza wajibu wake katika maisha ya vijana na taifa la Tanzania.
2
UWEZO WA NDANI (internal ability)
Uwezo wa ndani
Msingi mkuu wa taasisi yoyote kufanikiwa ni uwezo wake wa ndani wa
kupanga na kutekeleza shughuli zenye tija. Kwa kuwa taasisi ina
wafanyakazi ambao ni watu, basi msingi mkuu wa maendeleo ya taasisi
ni watu wenye uweledi wa kupanga na kutekeleza shughuli zenye tija
kwa ajili ya maendeleo ya watu. Kwa kuwa wafanya kazi wa YKM ni
vijana na wanafanya kazi na vijana kwa ajili ya faida ya vijana katika
kutimiza kusudi la uwepo wa huduma, YKM ita andaa mtaala rasmi wa
kuwajengea uwezo watenda kazi ambao ni viongozi.
3
Maeneo ambayo viongozi wata jengewauwezo kwa mwaka 2015 ni:
ENEO SABABU
Uongozi wa
kimkakati(Strategic
leadership)
Viongozi wakiwa na mbinu za kuongoza kimkakati, itarahisisha
kufikia vitu tarajiwa ndani ya muda uliopangwa na kwa ufanisi.
Ushauri(Counseling) Utoaji wa ushauri ni jambo la msingi kwa kipindi tulichonacho haswa
ukizingata huduma ina kutana na vijana walio na historia tofauti za
kimaisha (background). Kwa kuwa utoaji wa ushauri siyo sawa na
mazungumzo ya kawaida ni vyema viongozi waka jengewa uwezo
wa kushauri vijana katika masuala tatanishi yanayo wasibu vijana
katika maisha.
Stadi msingi za
teknohama(Basics
skills of IT)
Kwa kuwa teknolojia inakuwa ni vyema viongozi wakapatiwa stadi
msingi za teknohama, ili waweze kufanya kazi kwa ufanisi na ndani
ya muda uliopangwa.
4
Kwa kuwa viongozi wa kitaifa wapo katika mikoa tofauti, ni vyema
viongozi hawa wakawa wanakutana mara moja kwa mwezi kwa ajili ya;
Kupata mafunzo ya kujengewa uwezo katika maeno tajwa hapo juu.
Kutathmini hali ya utendaji kazi wa masuala muhimu yaliyojadiliwa katika
vikao vilivyopita.
Kujadili, kufanya maamuzi na kutekeleza makubaliano. Makubaliano
yote yatapaswa kuandikwa katika karatasi (Tazama kiambatanisho cha
kwanza).
5
Kwa kuwa katibu mkuu ndiyo mtendaji wa kazi za kila siku za
huduma, ofisi hiyo itateua ofisi tatu ndani ya YKM kuandaa mtaala
wa mafunzo wa maeneo matatu yaliyotajwa katika jedwali hapo
juu.Uteuzi huo unapaswa kufanywa tarehe 12 Aprili 2015. Ofisi ya
katibu itatoa muda usiozidi wiki tatu kwa ajili ya kazi hiyo.
Mara baada ya kazi hiyo kukamilika, nakala itawasilishwa ofisi ya
katibu mkuu na ofisi hiyo itaitisha kikao cha kamati kuu tendaji ya
huduma kwa lengo la kujadili na kuboresha maeneo ya uwezeshaji
kabla ya kuanzwa kwa utekelezaji.
6
Vikao vyote vya viongozi vitaratibiwa na ofisi ya katibu mkuu.
Kwa kuzingatia changamoto ya umbali kati ya kiongozi mmoja na
mwingine, tarehe 20 Aprili 2015 ofisi ya katibu itatangaza rasmi ya
kwamba mikutano mikubwa miwili ambayo ni;
Mkutano mkuu wa mwaka wa huduma.(Mwezi Julai, kila mwaka)
Mkutano wa mwezi februari. (Mwezi februari, Kila mwaka)
Itakuwa ni mikutano rasmi ya kuwajengea uwezo viongozi wa kitaifa.
Hivyo basi mkakati unapendekeza ya kwamba kuwepo na vipindi
ambavyo washiriki wake watakuwa viongozi wa kitaifa tu. Ofisi ya
mipango, ofisi ya ukusanyaji rasirimali, ofisi ya mhazini mkuu zitakuwa
ni ofisi kuu katika kutengeneza mpango wa uendeshwaji wa mikutano
hiyo. Mpango huo unapaswa uwe umekamilika miezi mitatu kabla ya
tarehe ya mkutano husika.
7
Vipao mbele vya huduma
Mkakati unapendekeza ofisi ya mkurugenzi mkuu iainishe vipao
mbele vya huduma kwa miaka miwili mfululizo (2015-2016). Ili
kufanikisha suala hilo, ni vyema ofisi ya katibu mkuu ikaitisha kikao
cha kujadili vipao mbele vya huduma, iwapo kikao hakitafanikiwa
kufanyika ofisi ya katibu itapaswa kukasimu madaraka ya
kuainisha vipao mbele kwa moja ya ofisi au ofisi zaidi ya moja.
Vipao mbele vinapaswa kuwa tayari kabla ya tarehe 20 Aprili 2015.
8
Katiba, sera na ofisi zilizopo ndani
ya YKM.
Mkakati unapendekeza kabla ya tarehe 12 Aprili 2015, ofisi ya
katibu mkuu itume katiba ya YKM kwa kila ofisi ndani ya YKM. Ofisi
zote zitapaswa kuandaa sera na taratibu za ufanyaji wa kazi kwa
kufuata msingi wa katiba ya YKM, kazi hiyo inapaswa kufanywa
kabla ya tarehe 30 juni 2015.
9
Usimamizi wa rasirimali na
usuluhishi
Kwa kuwa ofisi ya ukusanyaji rasilimali ndiyo chombo husika katika
usimamizi wa rasirimali za YKM.mkakati unapendekeza ofisi hiyo
itengeneze sera rasmi ya kuratibu usimamizi wa mali zote zilizomo
mikononi wa viongozi wa YKM. Sera hiyo inapaswa kuwa tayari
kabla ya tarehe 12 Aprili 2015, na iwasilishwe ofisi ya katibu mkuu,
siku saba baada ya ofisi ya katibu kupokea, ofisi hiyo itapaswa
kutuma sera hiyo kwa walezi wa mikoa ya YKM, walezi wa mikoa
watapaswa kusoma sera na kuielewa na kisha kuwatumia
wakurugenzi wa mikoa ya YKM.
10
Kuhusu usuluhishi; Iwapo kutatokea kutoelewana katika utendaji wa kazi,
ufanyaji wa maamuzi na ugawanywaji wa rasirimali (Resources allocation).
Mkakati utashauri viongozi kuwa makini katika utendaji wa kazi.
Wafilipi 2:3-4
“3 Msitende neno lo lote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa
unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa bora kuliko nafsi yake.
4 Kila mtu asiangalie mambo yake mwenyewe, bali kila mtu aangalie mambo
ya wengine.”
11
Uanachama rasmi
Kwa kuwa huduma ina uanachama, basi mkakati unapendekeza
wanachama wote wa andikishwe upya kwa kujaza fomu ya
maombi ya uanachama (Tazama kiambatanisho cha pili), pia
mkakati unapendekeza ofisi ya katibu na ofisi ya mipango zipitie
katiba ya YKM na kuangalia kipengele kinachohusiana na
uanachama.
12
Matukio (events)
Ili kuongeza ufanisi wa uandwaaji na ufanyikaji wa matukio, YKM itakuwa na
matukio kwa mkoa wa Dodoma tu kwa kipindi cha mwaka 2015.
Matukio yatakayo fanyika Dodoma ni;
“Kingdom Transformer Leadership Gathering”-Tukio litakuwa likifanyika kila
juma pili ya mwisho wa mwezi.
Matukio ya huduma za YKM mfano “Kingdom inspiration”, “Kingdom ladies”
Kwa kuwa mkoa wa Dodoma utahusika katika matukio hayo, mkakati
unapendekeza mlezi wa mkoa aandae utaratibu maalumu wa kuwajengea
uwezo viongozi wa mkoa husika ili waweze kuandaa matukio katika ubora wa
hali ya juu.
13
Mfumo utakao tumika kuwajengea uwezo viongozi wa Dodoma,
utakuwa ni mfumo mfano (Model system) katika kuwajengea uwezo
viongozi wa mikao mingine ya YKM, hivyo basi mkakati unashauri mlezi
wa mkoa wa Dodoma afanye mawasiliano na ofisi ya mipango katika
kufanikisha suala hili. Ofisi ya mipango inapendekeza “event
guidelines” zitumike. Kwa maelezo zaidi, tazama kiambatanisho namba
tatu(Event guidelines)
Mkakati unapendekeza ofisi ya ukusanyaji wa rasirimali, ofisi ya miradi
na ofisi ya habari ifanye tathmini ya mapungufu yaliyojitokeza katika
matukio ya mwaka 2012 mpaka mwaka 2014, ofisi ya ukusanyaji
rasirimali,ofisi ya miradi na ofisi ya habari zinapaswa kuanza kazi hiyo
tarehe 12 aprili 2015 mpaka tarehe 2 Mei 2015.Tathimini itapaswa
kuzingatia maeneo yafuatayo;
14
Uandwa aji wa matukio
Uendeshwaji wa matukio
Changamoto ya uuzaji wa bidhaa katika matukio.
Yatokanayo na matukio(out comes)
Changamoto kuu za matukio
Mapendekezo juu ya suluhu (solutions) stahiki zinazopaswa kutekelezwa
katika uanda aji wa matukio.
Mapendekezo ya kupunguza au kuongeza matukio,kwa ajili ya kufanikisha
kusudi la huduma
Ripoti itapaswa kupigwa chapa (printing) na kufungwa (binding).
Tarehe 7 Mei 2015, tathmini itakabidhiwa kwa ofisi ya katibu mkuu na katibu
mkuu ataiwasilisha ofisi ya mkurugenzi mkuu wa taifa. Ofisi ya mkurugenzi
mkuu itachukuwa hatua zinazopaswa kuchukuliwa baada ya kuisoma ripoti,kwa lengo la kuboresha matukio yatakayo fuata.
15
Vyanzo vya fedha Kwa muda mrefu huduma imekuwa ikitegemea kupata fedha kwa
njia ya michango ya hiari kutoka kwa wadau mbali mbali, hali hii
imepelekea kuwepo changamoto katika utendaji. Mkakati
unashauri kuwepo upembuzi yakinifu (analysis) ni kwa jinsi gani
huduma inaweza ikapata fedha za kuendesha shughuli zake.
Mkakati unapendekeza ofisi ya ukusanyanyi rasilimali, ofisi ya
miradi, ofisi ya hazina kuu ya huduma na ofisi ya habari, zifanye
kazi hiyo ya upembuzi yakinifu na kuja na mapendekezo
yatakayoweza kutekelezwa kwa ajili ya kuongeza upatikanaji wa
fedha katika huduma. Kazi hiyo inapaswa kufanyika kuanzia tarehe
12 April 2015 mpaka 10 July 2015. (Tazama kiambatanisho cha nne,
mkakati unashauri hatua zilizo ainishwa katika kiambatanisho hicho
zifuatwe)
16
Kwa kuwa kuna ofisi za hazina katika mikoa ya YKM, mkakati
unashauri ofisi ya hazina kuu na ofisi ya miradi, ziandae utaratibu
maalumu wa kusimamia fedha zilizopo katika mikoa husikana
uuzwaji wa bidhaa za YKM, utaratibu huo unapaswa uwe tayari
kabla ya tarehe 4 Mei 2015 na usambazwe kwa walezi wa mikoa ili
walezi wausambaze utaratibu huo kwa viongozi wao wa mikoa.
17
Matumizi ya teknolojia
Mkakati una pendekeza makundi yote ya “WhatsApp” yatumike
kama nyenzo muhimu katika kusuma mbele maendeleo ya YKM. Ni
vyema maudhui (content) ya kila kundi yakafanyika msaada kwa
kila mtu aliyepo ndani ya kundi. Kwa kuwa wamiliki wa “WhatsApp”
hawatengenezi content bali “content” hutengenezwa na watu
waliopo ndani ya kundi husika, hivyo basi ni busara kila mwana
kundi akatuma jumbe zilizo na maadili, kuelemisha na zenye kutoa
msaada.
18
Msaada wa namna gani?
Kwa kuwa asilimia kubwa ya washiriki katika makundi ya
“WhatsApp” ni vijana waliopo chuoni na baadhi yao ni vijana
waliopo nje ya chuo, mkakati unapendekeza “content” iwe katika
maeneo ambayo yana wagusa vijana kwa sehemu kubwa,
maeneo hayo ni;
19
Ajira- Baada ya kumaliza chuo kijana atajiajiri au ata ajiriwa. Ni
vyema waliopo kwenye kundi waka wana pashana habari
zinahohusu namna gani kijana anaweza akajiajiri au vitu gani
kijana anapaswa kuvifuata ili aweze kuajiriwa na kupata ajira
yenye tija kwa maisha yake binafsi. Matangazo ya kazi
hayataruhusiwa kuwekwa, kwani matangazo yaliyo mengi ni
marefu, mkakati ushauri badala ya kuweka tangazo mtoa post
aweke “link” ya tangazo ili mtu atakaye penda kusoma zaidi
kuhusu tangazo la ajira afuate “link” husika.
Suala la kuwa na kipato ni suala la msingi sana katika kipindi hiki,
mkakati unapendekeza siku ya juma tatu iwe ni siku rasmi kwa
majadiliano yanayohusu ni namna gani mtu binafsi unaweza
ukajiongezea kipato na masuala ya maendeleo ya mtu. Mjadala
utafungwa saa tano usiku na Mbeba maono wa huduma ya YKM,
Raphael J. Lyela.
20
Mahusiano- Mahusiano ni moja kati ya mambo ambayo
yanajadiliwa sana na vijana kila mahali, kwani wengi wao huwa
katika kipindi cha kutafuta wenzi wao wa maisha. Licha ya mjadala
kuwa mkubwa, bado vijana wanafanya makosa mengi ya
kimahusiano na hivyo kuathiri hatma ya maisha yao. Mkakati
unapendekeza siku ya juma nne iwe siku rasmi ya kujadili
mahusiao, wanaojadili wanapaswa wawe wa angalifu sana na
wenye hekima, na hivyo basi mchangiaji atapaswa kuchangia ki
uadilifu, kwa uangalifu, umakini ili mchango wake uwe mchango
wenye mantiki na si kwa ajili ya mzaha, katika majadiliano hayo
hairuhusiwi kutuma picha zisizo na maadili. Mkakati unashauri kila
kijana aliyepo kwenye kundi husika ajishibishe maarifa juu ya
mahusiano pasipo kwenda kinyume na Mungu.
21
“Spiritual growth”- Vijana katika kila kundi husika watapaswa
kupata mafundisho juu ya “personal spiritual growth” Kwa
kuzingatia neno la Mungu. Aidha wachangiaji wanashauriwa wawe
na uelewa juu ya wanacho changia ili kuondoa upotoshaji,
wachangajia wasichangie kwa lengo la kushinda bali kwa lengo la
kuelimishina. Mkakati unapendekeza siku ya juma tano iwe siku ya
mafundisho na majadilino.
22
Kwa kuwa siku ya jumatatu mpaka jumatano zitakuwa na shughuli
zilizo ainishwa hapo juu. Mkakati unapendekeza siku ya alhamisi,
iwe siku maalumu ya kufundishwa somo maalumu kutoka kwa
Mbeba maono wa huduma. Raphael J. Lyela watu watapata muda
wa kuuliza maswali juu somo husika na kisha kujibiwa maswali. Siku
ya ijumaa itakuwa siku ya maombi, ofisi ya kuu ya maombi katika
huduma itasimamia utaratibu rasmi wa kuratibu maombi kwa
kushikirikiana na ofisi nyingine ndani ya YKM. Siku ya juma mosi ni
siku ya mawasiliano baina ya mtu mmoja na mwingine ndani ya
YKM. Siku ya juma pili ni siku ya kushirikishana namna ya
kukabiliana na kuzishinda changamoto za maisha.
23
Mkakati unapendekeza makundi ya “WhatsApp” yasiwe mahali pa
kukutana, bali pawe ni mahali pa kukuzana katika Nyanja muhimu za
maisha, hivyo basi ni muhimu kwa mtu kabla ya kutuma ujumbe
wake afikiria kwa umakini na kufanya maamuzi sahihi, kwa manufaa
ya wengine
Ufanyaji kazi kupitia “WhatsApp”. Mkakati unapendekeza makundi
ya viongozi yawe ni mahali pa kupashana habari zinazohusu kazi na
si mazungumzo binafsi.
Kwa kuwa kuna makundi kadhaa ya YKM, mkakati unapendekeza
kila kundi liwe na msimamizi maalumu wa kundi husika, na kila
msimamizi atawajibika kwa ofisi kuu ya habari. Ofisi kuu ya habari
itafanya mabadiliko wakati wowote kuhusiana na uendeshwaji wa
makundi kwa lengo la kuongeza ufanisi katika uwajibikaji.
24
Miundo Mbinu.
Ili kuweza kufanikisha kuwaleta vijana pamoja, YKM ita kuwa na
mpango rasmi wa kujenga kituo cha mafunzo ya uongozi kwa
vijana, kituo kitaiwa “Leadership Garden”. Kituo kitatumika kama
nyenzo muhimu katika kutimiza kusudi la uwepo wa YKM. Mkakati
unapendekeza ofisi ya mkurugenzi mkuu ipitie pendekezo la
kuanzishwa kwa kituo hicho na kulifanyia maamuzi kabla ya tarehe
20 July 2015. Ili kupata taarifa zaidi juu ya “Leadership Garden”
tazama kiambatanisho namba tano.
25
Mpango wa muda mrefu
Kutakuwa na ujenzi wa chuo kitakacho itwa “KingdomTransformer leadership Institute”. Mkakati unashaurihatua za awali zifanyike kabla ya 30 disemba 2015.Hatua hizo ni pamoja na.
Uandikwaji wa andiko la uanzishwaji wa taasisi(Proposal)
Uandwa aji wa mtaala wa mafunzo yatayotolewa(Curriculum).Mkakati unapendekeza chuo kianze namitaala miwili, ambayo ni;-
Mtaala wa mafunzo ya teknolojia ya habari na
mawasiliano (information and communication
technology), ngazi ya cheti
26
Mtaala wa mafunzo ya usimamizi wa biashara(Business
management),ngazi ya cheti
Kufuata taratibu za kuanzishwa chuo chini ya VETA(Tazama
kiambatanisho cha sita)
Kujua taratibu za kupata usajili wa NACTE(Tazama kiambatanisho
cha saba)
27
Mkakati unashauri upembuzi yakinifu ufanyike katika eneo la kujua
gharama halisi ya kuendesha chuo kwa faida ya kipato na utoaji
wa elimu bora. ofisi ya mkurugenzi mkuu wa taifa inapaswa
kukasimu kazi hii kwa ofisi zaidi ya mbili ndani ya YKM kabla ya
tarehe 20 Aprili 2015, kwa mantiki hiyo ofisi ya mkurugenzi wa taifa
itakuwa msimamizi mkuu wa mradi huu.
28
Utekelezaji wa mkakati
Kwa kuwa utekelezaji wa mikakati huathiriwa na sababu
mbalimbali na changamoto zinazowakumba watekelezaji wa
mkakati, ili kuhakikisha utekelezwaji wa mkakati huu ofisi ya
mkurugenzi mkuu na ofisi ya katibu mkuu zita kuwa ofisi
zinazosimamia na kufuatilia utekelezaji wa mkakati mpaka 30
Disemba 2015.
Utekelezaji uta anza rasmi tarehe 12 Aprili 2015 na utakuwa una
tathminiwa kila tarehe 12 ya kila mwezi katika mwaka 2015, baada
ya tamko kutoka ofisi ya mkurugenzi mkuu.
29
Hatua za kufuata kabla ya kutoa tamka la utekelezwaji wa mkakati
huu.
Ofisi ya mkurugenzi itapaswa kuitisha kikao kupitia ofisi ya katibu
mkuu.
Kazi ya kikao itakuwa ni kujadili mkakati huu, ku ufanyia
marekebisho na kukubaliana namna bora zaidi ya kuutekeleza.
Baada ya makubaliano, ofisi ya mkurugenzi mkuu itatoa rasmi
tamko.
Mkakati utatekelezwa mpaka tarehe 30 Disemba 2015.
Hitimisho
Tathmini kuu ya mkakati itafanyika tarehe 5 Januari 2016.
30